Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SIMULIZI ZANGU ZILIZOKAMILIKA AMBAZO ZIPO FULL NI
  1. WARAKA WA RAISI KABLA YA KIFO
  2. BOOK OF ALL NAMES
UNAWEZA KUPATA SIMULIZI ZANGU ZOTE KWA 3000 TU LIPIA KWA NAMBA HIZO HAPO JUU
SIMULIZI ZINAZOENDELEA KWENYE GRUPU NI
  1. MASAA MAWILI YA KUMBUKUMBU
  2. MY FREEDOM(UHURU WANGU)
  3. NILIEMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
Hizo zote zinaendelea kwenye grupAu ukichangia kuanzia 2000 kuendelea utatumiwa zote
Boss unajua mno, lazima nilipie hizo simulizi maana ni zaidi ya burudani.
 
Anaejua ratiba ya hii simulizi anisaidie ili nisije mlaumu muhusika anajidai na hadithi yake kumbe ana siku zake
 
Ndugu zangu huyu ni tapeli,mwenye riwaya zote hizo anaitwa Patrick Ck ukitaka riwaya yoyote wasiliana nae kwa namba 0764294499
Maelezo hayajajitosheleza na inawezekana hata hii namba ni ya tapeli tu.
 
Maelezo hayajajitosheleza na inawezekana hata hii namba ni ya tapeli tu.
Isitishe inaonekana na wewe unasoma za humu jamii sio kuwaunga mkono wanaotunga kwa kununua,mpenzi wa riwaya anazo namba za watunzi kina Patrick,bahati mamba,bishop na wengineo
 
Mkuu ,Asante kwa kutupigania aisee , ukinunua simulizi kwa muhisika inatia hamasa na mwandishi anajituma zaidi
Kweli kaka,kuna vilaza wanataka kunufaika kupitia migongo yenu,hawajui mnatumia muda wenu mwingi kutunga,na ukichelewa kuleta humu wengine wanakutukana na kukukashifu!
 
SEHEMU YA 172

PARIS CHARLES DE GAULLE AIRPORT

Kutoka Tanzania Dar Es salaam mpaka Paris ni masaa tisa kama na nusu tu hivi , hapakuwa mbali sana ukilinganisha na teknolojia ya sasa ya ndege na saa kumi kasoro Roma na Edna ndio muda ambao waliweza kufika ndani ya Paris ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Parisi Charles De Gaulle.

Tanzania na Paris tumeachana lisaa limoja , yaani kama Tanzania itakuwa saa sita na dakika kumi basi jua Ufaransa Parisi itakuwa ni saa tano na Dakika kumi hivyo kama utatoka Dar saa moja kamili utafika Paris saa tisa kasoro au kumi kutokana na kwamba unavyenda Parisi unapunguza muda.

Tabasamu alilokuwa nalo Roma lilipotea mara baada tu ya kukanyaga Ardhi ya Taifa hili kubwa ndani ya Ulaya , alijikuta kumbukumbu mbalimbali zikipita ndani ya kichwa chake.

Edna aliebeba mkoba wake , aliona mabadiliko ya Roma ila hakutaka kuuliza sana , Roma tofauti na wasafiri wengine ni kwamba yeye hakuwa amebeba chochote Zaidi ya simu yake ndogo ya Tecno ambayo ilionekana kama ya urithi na hakujali kabisa kutumia aina hio ya simu. Edna kwa muonekano wa Roma aliona kabisa huyu ndio Roma mwenyewe na yule wa kufanya mambo ya kimatani ni feki,

“Unafikiria nini?”aliuliza Edna baada ya kuingia kwenye jengo hili la wanaofika , Edna hakuwa abeba nguo nyingi kutokana pia alikuwa na kampuni ndani ya jiji hilo la Paris.

“Aaa,,, mambo yasio kuwa ya msingi tu , ila yote ni mambo ya zamani”Aliongea Roma na Edna aliona asiulize maswali Zaidi na hio ni kawaida ya wasomi, hawanaga maswali mengi kwenye mabadiliko ya hali ya mtu kama hio.

“Halafu nimesahau ni nani anakuja kutupokea?”Aliuliza Roma.

“Director wa kampuni yangu ya Athena ndio atakuja kutupokea , anaitwa Goodman , mara nyingi nimezoea kumuita Chibu ni jina la utani tulilokuwa tukimuita ulivyokuwa chuo Oxford”

“Ni mwanamke au mwanaume?”

“Ni mwanaume bhna ana asili mbili ya Kijapan na ulaya , lakini pia ni sehemu ya asili ya familia za kifalme(Royal Families) mama yake alikuwa akifahamiana sana na Mama ndio maana akaaminiwa kupewa kampuni”Aliongea Edna huku wakitoka nje kabisa wakipishana na jamii nyingi ndani ya uwanja huu.

Matafa yaliondelea kama Ufaransa wasafiri walikuwani wengi sana masalani kwenye uwanja wa kimataifa mkubwa kama huu wa De Gaullie , kulikuwa na kila aina ya Ngozi , Afrikan , Arabs , Indian na wengine wengi.

Roma baada ya kusikia jina la Chibu alikumbuka kipindi mke wake ashawahi kumsikia akiongea na simu na akitaja jina la Chibu , kumbe ndio huyu aliekuwa akiongoza kampuni Ufaransa.

“Ni kabila mchanganyiko na pia ni rafiki yako ulivyokuwa chuo , Bebi Edna na yeye ni Handsome na msumbufu kama Elvice?”Aliuliza Roma na Edna kubetua midomo.

“Goodman sio kama Elvice , kwanza hana tamaa na pesa na mara nyingi anajali sana damu yake ya kifalme na pia anajua kujali mno , nimekutana nae mara mbili tokea nilivvyokuwa CEO na sikupata tabu nilivyokuja kwenye maswala ya kibiashara”Aliongea Edna.

“Ushasema baada ya kumaliza chuo , ulikutana nae mara mbili tu , ukute kashabadilika”

“Naelewa watu kwa haraka sana kasoro wewe..”Aliongea Edna huku akitangulia mbele na kumfanya Roma atabasamu na kumsogelea huku akiangalia mtetemo wa Ardhi , alijiambia kama Edna angekuwa mwanamke kama kahaba angelishikilia pale pale mbele ya watu.

Baada ya kutembea kwa dakika kama kumi na tano hatimae walifika nje kabisa na kukutana na kundi kubwa la watu waliokuwa wamekuja kupogea wageni wao na Roma na Edna waliweza kuona bango kubwa lililokuwa na maandishi ya VEXTO INTERNATIONAL.

Alieshikilia bango alikuwa ni mwanaume mmoja wa kizungu ambaye alikuwa na nywele nyeusi alievalia suti nyeusi ilimpendeza vyema , alikuwa mrefu kidogo kuliko Roma , mwenye macho yake yenye kiini cha bluu.

Baada ya mwanaume huyu anaefamika kwa jina la Goodman kumuona Edna mbele yake mita kadhaa , alijikuta akitoa tabasamu mwanana kabisa na kuweka bango lake chini na kupanua mikono huku akiwasogelea kwa kuoneysha haja ya kutaka kumkumbatia Edna na Edna hakutaka kukataa kwani alikuwa akielewa tamaduni za kizungu kukumbatia na mabusu ni jambo la kawaida hivyo na yeye alipanga kumkumbatia huku akimsogelea.

“Haha, it’s great to see you. Let’s have a hug.”

Edna alijikuta akishangaa , kwani kabla hajakumbatiana na Goodman Roma alikuwa ashamuwahi na kukumbatiana nae na hata Goodman hakutegemea , kwani alishitukia tu mtu aliemkumbatia alikuwa ni Roma sio Edna, na Roma alikuwa akimgonga gonga Goodman mgongoni kama vile ni marafiki ambao hawajaonana muda mrefu.

“Wh…who are you?Aliongea Goodman kwa kubabaika.

“Anaitwa Roma Ramoni ni Director wa Kampuni ya Vexto Entartaiment ninayokaribia kuifungua”Aliongea Edna kwa Kingereza huku akitamani kucheka ,unajua hakujua ni kwa namna gani Roma aliweza kumpita nyuma yake na kukumbatiana na Goodman , sasa alichekeshwa nakubabaika kwa Goodman.

Baada ya kusikia utambulisho huo , aliona apotezee na kumuona Roma kama mtu ambaye alikuwa na mambo ya kitoto.

“Mr Roma, I’ve heard of your name before. You must be extraordinary to become a director at such a young age. I’m Goodman, it’s great to see you. I’ll definitely serve you well in France. Please ask if you require anything”

“Mr Roma nishawahi kulisikia jina lako , utakuwa na uwezo mkubwa sana mpaka kuaminiwa na kuwa Director kwa umri mdogo uliokuwa nao naitwa Goodman , nimefurahi kukutana na wewe , nitahakikisha unaishi kwa huduma bora utakapokua hapa Ufaransa”

“Unaonekana kuwa mpole sana Mr Goodman , nimekukubali , unaonaje tukikumbatiana kwa mara nyingine”

“Hehe, Mr Roma is indeed humorous. Let’s go out now and chat in the car. I haven’t met Edna in a very long time. We need to catch up nicely.”Aliongea akimaanisha kwamba waende sasa wakaongelee kwenye gari , kwani hakuwa amekutana na Edna kwa muda mrefu hivyo wanayo mengi ya kuongea.

Roma kwa kumwangalia tu Goodman aliona kabisa walikuwa na ukaribu mkubwa sana na Edna na pia kwa muonekano wa Goodman aliona alikuwa akimpenda Edna , lakini pia alipojaribu kufikiria na maelezo ya Edna kuwa Goodman alikuwa akimjali sana , alipata ukakasi.

Waliendelea kutembea huku wakifuata upande uliokuwa na magari , huku Goodman akiendelea kumuongelesha Edna kwa kumuuliza namna safari ilivyokuwa na kumpa pole na mambo mengine ambayo Roma aliona ni Blah Blah.

“I wonder what Mr Roma used to work as. Was your position high as well? I bet you have a lot of working experience”(Najiuliza Roma ulikuwa ukifanya kazi ganni hapo nyuma , kazi yako ilikuwa pia ni kubwa na una uzoefu wa kutosha?”)

“Kabla ya hapo nilikuwa nikibeba mizigo ndani ya soko moja huko Dar”Aliongea Roma na kumfanya Goodman kushangaa na Edna alijifanya hajasikia chochote na kupiga hatua mbele.

Ilikuwani gari ndegu ambayo Goodman alikuwa ameandaa kwa ajili ya Edna , ilikuwa ni Bentley Limuisine gari ya milango mingi , ilikuwa ni gari ambayo watu wanaipa jina la utani kama Hoteli inayotembea kutokanana ufahari wake.

Wote kwa Pamoja waliingia ndani ya gari hio na Goodman alimwambia Dereva aendeshe kuelekea Sofirel Hoteli , hoteli moja kubwa ndani ya jiji la Parisi , hoteli ya nyota tano.

“Nimeandaa magari manne ya kutusindikiza yote yana walinzi wenye silaha kwa ajili ya ulinzi , kuna tishio la ugaidi ndani ya Parisi siku ya leo na baadhi ya matajiri wametekwa Nyara ndio maana nikakodi walinzi”Aliongea Goodman na kumfanya Edna ashangae na kuishia kutingisha kichwa.

“You’re indeed as careful as ever”Aliongea Edna huku akitabasamu na baada ya kusikia walinzi alimgeukia Roma na kumwangalia na Roma muda huu tayari alikuwa bize kwani alishatoa chupa kubwa ya bia iliokuwa imehifadhiwa kwenye friji ya hili gari la kifahali na alikuwa anafungua kwa ajili ya kujihudumia , hakuwa na wasiwasi ni kama mtu aliekuwa ameambiwa jisikie huru.

“Sina haja ya kuogopa magaidi , Roma yupo”Aliwaza Edna huku akikumbuka baadhi ya matukio ya Roma.

Wakati huo huo Roma baada ya kuangalia Chupa ya wine iliokuwa kwenye mikono yake , aligeuza macho na kuangalia tena sehemu aliotoa hio chupa ya Wine na kutoa tabasamu.

“Bingo…!”Aliongea Roma baada ya kuvuta chupa nyingine ya Wine na kumfanya Goodman amwangalie.

“It’s great that Mr Roma likes it. This margarita was made in 1982. There are less than ten bottles in the entire Paris. Even the rich would find themselves hard pressed to get their hands on one of these bottles without connections”

“Ni vyema kama Mr Roma ameipenda , Hii Margarita ilitengenezwa mwaka 1982, kuna chupa sizizo zidi kumi ndani ya jiji lote la Parisi na hata matajiri wenyewe inakuwa ngumu kwao kupata Wine kama hio bila ya kuwa na koneksheni”

Kabla hata Goodman hajamaliza kuongea Roma alikuwa ashaifungua na kufanya gari lote kujaa harufu ya Grape ilikuwa ni harufu nzuri kiasi kwamba ilimfanya hata Edna kutamani kuonja aina hio ya Wine, lakini jambo ambalo lilimuacha hoi ni pale aliposhuhudia sauti

“Kud,,Kud ..Kud”Koo la Roma lililikuwa likipishana na hii ni baada ya kupeleka chupa yote mdomoni na kuanza kunywa kama anakunywa maji ya uhai , ikumbukwe bia hio inathamani kubwa sana ya pesa .
 
SEHEMU YA 173

Edna alijikuta akikasirishwa na jambo hilo na sio kwamba labda ni kwasababu Roma hakumkumbuka , ila ukweli ni kwamba namna ambavyo Roma alikuwa anakunywa hio Wine haikuwa kistaarabu.

Goodman hakuamini Wine ambayo alikuwa ameitafuta kwa tabu na kutoa Zaidi ya Milioni arobaini za Kitanzania ni hio ambayo Rom alikuwa akiishusha kama Maji na kumfanya hata Edna amwangalie mzungu wa watu kwa macho ya huruma.

“I’m sorry, Goodman. Roma has always behaved this way. He isn’t intentionally messing with you”

“Samahani Goodman, Roma ndio tabia yake hio , sio kama anakufanyia makusudi kukukasirisha”Aliongea Edna akimtetea Roma.

““It’s fine, as long as Mr Roma likes it. There are two more bottles here. Edna, I’ll open another one for you”

“Usijali kabisa kama Roma ameipenda , kuna Chupa mbili nyingine hapa , Edna nitakufngulia moja kwa ajili yako”Aliongea Goodman na Edna alitingisha kichwa kukubali.

“Hehe, I’m sorry. I didn’t know it was this expensive. How about letting me pour some of it for you guys as well? Sharing is caring”

“Hehe..Mnisamehe , sikujua kuwa ni gharama kiasi hiko , mnaonaje mkichukua Glass niwamiminie kiasi , ‘Sharing is caring’”

“Usijali Mr Roma unaweza kuendelea”Aliongea Goodman huku akifungua kijjifriji na kutoa chupa nyingine kama alioshikilia Roma.

“Nafikiri haina haja ya kufungua chupa nyingine , bali uangalie uelekeo wa gari inakoenda , mbona naona sio uelekeo wa Sofitel Hotel”Aliongea Roma huku akiangalia nje na kumfanya na Goodman aangalie nje kwa haraka akiacha alichokuwa akifanya.

“Haha..Mr Roma huna haja ya kuwa wasiwasi , ijapokuwa dereva anaetuendesha sijamchagua mwenyewe , lakini madereva wote wa kampuni wanauelewa sana huu mji hatupaswi kuwa na wasiwasi “Aliongea Goodman

“Kweli! Nafikiri uangalie kwa umakini nje , mimi naona tunaenda upande mwingine kabisa na ilipo hoteli ya Sofitel”Aliongea Roma lakini Goodman alianza kukasirika , alimuona Roma anamuona kama mpumbavu yaani mtu anaebeba mizigo aanze kumuelekeza yeye kuhusu jiji la Paris ambalo anajua chocho zote. , hakutaka kabisa hata kuzingatia kuwa yeye na Roma wanakwenda kuwa na nafasi sawa ndani ya kampuni kama Director, lakini pia kuweza kusafiri na mwanamke mrembo kama Edna alijiambia

“The low-class will always stay that way. What does he even know?”Aliwaza akianisha kuwa mtu wa daraja la chini siku zote atakuwa wa daraja la chini.

“Mr Roma, forgive me for asking, but have you come to Paris before? Do you know where Hotel Sofitel is? Do you how our traffic works?”

“Mr Rom samahani kwa kuuliza , ushawahi kufika Parisi , unajua namna magari ya Parisi yanayoongozwa katika barabara”Roma alimwangalia Goodman na kisha akatabasmu.,

“15 rue Boissy d'Anglas, ai-je raison ?” Aliongea Roma kwa Kifaransa akimaanisha kwamba hoteli ya Sofitel inapatikana katika mtaa unaofahamika kwa jina la 15 Boissy d`Anglas na hii ilimfanya bwana huyu kushangaa hatari kwa namna ambavyo Roma ameongea kifaransa , kwanni aliongea kama Mzawa lakini pia eneo ambalo ametaja ni sahihi kabisa katika masikio ya Goodman.

Edna alikuwa akiangalia tu kinachoendelea hakushangaa Zaidi kwani alikuwa akijua mambo mengi kuhusu Roma , lakini yapo pia mambo ambayo hakuwa akiyafahamu na alitegemea muda si mrefu atayafahamu.

Goodman aliangalia nje na kuona ni kweli maelezo ya Roma yapo sahihi hawakuwa wakielekea upande ambao ulikuwa ni wa hoteli , ila uelekeo hakuwa hata akiufahamu , kwa wakati huo.

“Nini kinatokea?”Aliongea Goodman , unachotakiwa kuelewa nni kwamba magari haya ya Limuisine Bentley yalikuwa yametanganishwa kabisa na Dereva na hii yote ni kwa ajili ya ‘Privacy’ na yalikuwa na Soundproof

Edna baada ya kuona hali haikuwa sawa , alimgeukia Roma ili kuelezea nni nini kinaendelea.

“Mimi sijui chochote kinachoendelea, ninachojua ni kwamba upande tunaoelekea sio”Aliongea Roma na Goodman ilimbidi kubonyeza kifaa ambacho inatumika kuwasiliana na Dereva.

“Spiel! What are you doing?! You’re going the wrong way! Do you hear me?!”

“Spiel unafanya nini , unaenda upande ambao sio , unanisikia” lakini hakukua na jibu lolote upande wa dereva Zaidi ya gari kusonga mbele , ten ani kama dereva aliambiwa aongeze spidi.

“Acha kupiga kelele haisaidii kitu , unatakiwa kujua kuwa Merecenz benz iliokuwa nyuma yetu ishapotea muda mrefu na kwa hali ninayoona hapa madereva walibadilishwa ulivyokuwa mbali na magari , ni bahati mbaya simfahamu dereva wako ningekuambia kama ni jambazi au sio jambazi”Aliongea Roma na kumalizia Wine yake yake , hakuwa na wasiwasi , lakini kwa Goodman alikuwa akitaka kujikojolea , aliamini huenda kile kilichokuwa kikitanganzwa kwenye taarifa za Habari ndio kinachokwenda kumtokea., kitendo cha watu matajiri na wenye uhusiano moja kwa moja na familia za kifalme kutekwa na kuepelekwa kusiko julikana.

“Ngoja niwapigie polisi …”Aliongea baada ya kugeuka nyuma na kuona kweli gari aliokuwa amekuja nayo ya Mercedenz ilikuwa imepotea na alijua mpaka hao wapo kwenye hatari.

“Acha kujisumbua lazima kutakuwa na kifaa cha kuzuia mawasiliano ndani ya hili gari , unafikiri ni wapumbavu wakuachie upige simu “Aliongea Roma huku akiweka tabasamu la kejeli kwenye uso wake akimwangaia Goodman aliekuwa bize kuhangaika , kwani siti ilikuwa ya moto.

“Bahati mbaya kweli kweli, Goodman umetuambia kuwa kuna ujambazi unaondelea ndani ya Paris , lakini tushatekwa mpaka sasa hivi muda tu baada ya kutua”

“Roma acha kumtisha mwenzio na matani yako , jaribu kutafuta namna ya sisi kujinasua”Aliongea Edna , hakuonekana kuwa na hofu kama ilivyokuwa kwa Goodman , lakini aliona sio kitendo kizuri kwa Roma kumtishia mwenzake , Edna aliona hana haja ya kuwa na hofu kwani yupo na Roma.

“Mr Roma, judging from how calm you are, you must have a plan, don’t you? My safety isn’t important. But Edna is the core pillar of Vexto. Without her, Vexto International will collapse, not to mention she’s a lady. Nothing bad shall happen to her.”Aliongea Goodman , hakujua kwanini anaongea hivyo , ila aliamini kwa namna ambavyo Roma hakuonyesha hofu , lakini pia kwa namna ambavyo Edna pia hakuonyesha wasiwasi , aliamini huenda Roma akawa na kaujuzi , isitoshe dakika chache nyuma aliongea Kifaransa.

Roma baada ya Goodman kuongea hayo maneno kwanza , alifikiria kidogo na kuanza kuangaza macho yake na bahati macho yakatua kwenye sigara kubwa iliokuwa pembeni yake , ni zile sigara za bei ghali zinazotengenezwa na kampuni ya Chancellor Tobbacco , sigara iliokuwa ikifahamika kwa jila la Trasaurer Alluminiaum Gold , sigara moja ilikuwa ikiuzwa laki na ishirini za Kitanzania , Roma aliichukua na kiberiti cha gesi kilichokuwa pembeni na kisha akaiwasha , Edna alitaka kumzuia lakini Roma alimkwepa na alivuta kidogo na kutoa moshi hewani na kumfanya Edna akohoe kidogo kutokana na moshi ule wa Sigara.

Ila kwa Goodman hakujali kabisa , muda huo alikuwa akiwaza mbinu tu za kutoka ndani ya hilo gari , na kukimbia watekaji na alikuwa kitegemea neno kutoka kwa Roma , alimuona Roma wakati huo kama mwokozi.

“Njia ya kutoka ipo ….”Aliongea Roma huku akivuta tena na kufanya Edna na Goodman wapatwe na tumaini.

“Lakini njia yenyewe hata siijui”Aliongea Roma na kuwafanya washangae Zaidi na kuzidi kumuongezea wasiwasi Goodman.
 
SHEMU YA 174

Goodman alijikuta uso ukimshuka , alijua Roma alikuwa kweli ana njia kumbe alikuwa hana , alijikuta akijiegemeza kwenye kiti kama mtu aliekosa tumaini na ndani ya dakika chache mbele gari ilizidi kuyoyoma na ilikuwa kwenye spidi kali kweli .

“Roma Go to Hell”Aliongea Edna huku akimfinya Roma kwenye paja la Mguu baada ya kuona Roma anafanya utani kwenye hali ya kifo kama hio , ila Roma hakutikisika Zaidi ya kuchukua chupa nyingine ya wine na kunywa kidogo huku akiendelea kuvuta sigara.

Gari ilisonga mbele na dereva hakuonekana kabisa kusimamisha na Waliokuwa ndani ya gari walioweza tu kushuhudia baadi ya mabango yaliokuwa yamewekwa barabrani ,lisaa la kwanza likapita la pili mpaka yakatimia manne gari ilikuwa kwenye mwendo na mbaya Zaidi hawakuona tena mbango na gari ilikuwaikihama hama kwenye barababara na hali ilizidi kuwa mbaya kwa Goodman kwani alipoteza fahamu na kujilaza na kumfanya Roma atoe tabasamu la kifedhuli.

“Nilijiua yuko imara kumbe ni dhaifu kiasi hiki”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna na mpaka muda huo Roma alikuwa ashamaliza chupa mbili za bia.

“Roma umefanya makusudi si ndio?”

“Nini..?”

“Najua ulikuwa na uwezo wa kutoka kwenye hili gari , ila hujataka tu kufanya hivyo”Aliongea Edna na kumfanya Roma atabasamu.

“Kweli wewe unasifa zote za kuwa mke wangu”Aliongea Roma huku akimshika Edna mashavu , lakni Edna alimpiga na mkono.

“Nataka kujua ni wapi wanatupeleka na nia yao ni nini ndio maana”Aliongea Roma ,

“Kwa ninavyokujua , nilikuwa nishafahamu tu unafanya makusudi, ila usije ukafanya mambo ambayo yatafanya nichelewe kutimiza majukumu yangu yalionileta Paris”

“Usijali mke wangu , kwanza kabisa bado hatujafanyana , toke tuoane , siwezi kuruhusu tufe kabla ya hiko kitendo”

“Romaa…”Aliongea Edna huku akimkodolea macho huku akimwangalia Goodman kuhakikisha kama amelala, maana maneno ya Roma aliyaona kama mazito , maana yalimfanya aone hata aibu.

Baada ya safari ya muda mrefu wasiokuwa wakijua uelekeo wake , hatimae Gari ile ilipunguza mwendo na kukata kulia ikiacha barabara kuu , ndani ya msitu na mtingishiko wa gari ulimfanya hata Goodman kushituka.

“Tuko wapi?”Aliuliza Goodman na kumfanya Edna amwangalie Goodman kwa kumkatia tamaa , alijiambia licha ya Goodman kuwa na damu ya kifalme , lakini hakuwa imara.

“Haieleweki mpaka sasa hivi ni wapi tulipo , kwani hii wametuzungusha kwenye barabara nyingi ili tukose uelekeo , hatujui ni wapi hapa”Aliongea Edna.

“Edna hatuwezi kufa?”Aliuliza Goodman kwa wasiwasi

“Sidhani kama nia yao ilikuwa kutuaa nadhani tungekuwa tuashakufa mpaka sasa hivi”

“Mimi nina mawazo tofauti , nahisi wanataka kwanza kuhakikisha tunatoa pesa nyingi kutoka kwetu na baada ya hapo ndio watatuua”Aliongea Roma na kumfanya Goodman kuzidi kutoa macho na kutetemeka.

“Roma acha bwana kumuongoepesa , yaani haupo siriasis kila sehemu”Aliongea Edna na Roma alitabasamu na kuona atulie na muda huo huo gari ilisimamishwa baada ya kutembea kilomita kadhaa na milango ikafunguliwa na walionekana wanaume wanne waliokuwa na siraha za bunduki wakiwa wameshikilia pia Tochi kubwa.

Walianza kuwakagua mmoja mmoja na muda huu wote waikuwa hawaonekani sura kwanni walikuwa wamevalia ma helmet makubwa , baada ya kuwakagua kwa dakika , walimmulika Goodman na kutulia kwa dakika na mmoja wao muda ule ule akakodi siraha yake

“Kacha Kacha”

*******

Upande wa Tanzania ndani ya nyumba ya mrembo Nadia , baada ya safari ya Roma na Edna kuelekea Ufaransa kuanza , mrembo huyu alionekana nje ya Balconi , kwenye chumba chake cha kulalia huku akiwa amevalia Bukta ndogo yenye maua maua , akiwa na sweta la mikono mirefu rangi nyeupe , huku , mkononi akiwa na simu upande wa kulia na upande wa kushoto akiwa na Glass yenye mvinyo ,Alionekana kuongea na mtu mrembo huyu kwenye simu.

“Nadia umefikia wapi?”

“Boss bado naandaa mpango wa kuhakikisha wanaachana naomba uwe mvumilivu”Aliongea Nadia, lakini alihisi kusikia pumzi ndefu upande wa pili.

“Hauko siriasi Nadia , narudia Hauko Siriasi muda unaenda na hakuna majibu ya kuridhisha, ni mpango gani huo unaandaa?”

“Boss…”

“Sikia Nadia mpaka sasa umeshindwa kazi , na leo nasikia Hades na Edna watafika Ufaransa”Ilisikika sauti hio nzito na kumfanya Nadia Glass ile imponyoke na kutua chini.

“Boss umewezaje kujua juu ya swala hili , naomba usimdhuru Roma tafadhali , nipe wiki mbili ,,, Hapana wiki moja kila kitu kitakuwa tayari”.

“Nadia sijakupigia hapa kusikiliza ngonjera zako,, na mpaka sasa misheni yako imefeli kwa asilimia mia moja na ukae mbali na mimi la sivyo na wewe kifo kitakuhusu , nina watu wangu kila kona ya dunia”Ilisikika sauti hio na muda huo mtu aliekuwa akiongea nae alikuwa akiongea kwa lugha ya Kingereza na simu pale pale ikakatwa na kumfanya Nadia wasiwasi uonekane kwenye macho yake na kugeuka kwa ajili ya kupiga hatua kurudi ndani

“Arrgh..!”Alijikuta akitoa mlio wa kuumia na ni baada ya kukatwa na kipande cha Glasi iliokuwa imedondoka chini na kupasuka.

******

Upande mwingine nchini Kenya , hali kwa mheshimiwa haikuwa nzuri hata kidogo na hii yote ni baada ya kusikia taarifa kutoka kwa mtu wao aliekuwa ndani ya ikulu Tanzanis , taarifa iliokuwa ikihusiana juu ya Blandina.

“Mheshimiwa anapanga kuonana na baba Yake Mzee Kweka kwa ajili ya kumwambia juu ya uwepo wa Blandina”Hio ndio taarifa iliokuwa imemfikia Mheshimiwa Kamau Kamau na kujikuta akichanganyikiwa.

Ukweli bwana huyu hakuwa tayari kuona ukweli unatoka mapema kiasi hicho na ndio maana alikuwa akifanya kila linalowezekana kuzuia jambo hilo na ni jana yake tu pia aliweza kusaini nyaraka zinazohusiana na mpango TASAC mpango ambao ulikuwa ukihusiana na taifa la Urusi na hiyo yote ni katika kuzuia siri yake aliokuwa nayo kwa muda mwingi isifahamike.

“Noo..!Hapana hili swala lazima lisifanikiwe kwa namna yoyote”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kisha alivuta simu yake aina ya Google Pixel , Siku zote ukimuona Mheshimiwa Kamau akishika hio simu , jua tu kuna jambo ambalo ni baya sana linakwenda kutokea.

“Andaa mazingira , Someone has to be Terminated”Aliongea Mheshimiwa akisema kwamba mazingira yaandaliwe kuna mtu anapaswa kufa.

“Name please”

“Senga Kweka”Aliongea Mheshimiwa Kamau.

“Copy that”Ilisikika sauti upande wa pili na simu ikakatwa.

“Gumilaaaa…!!!”Aliongea mheshimiwa kwa sauti kubwa kidogo akiwa ndani ya hii ofisi yake ya ikulu yenye ulinzi mkubwa sana na baada ya kuongea tu hilo neno Gumilaa ,,, mara muda huo huo kama mwanga wa Radi , ulipiga kwenye Ofisi yake na akashuka mtu kutoka juu pasipo kueleweka ametokea wapi , lakini mtu huyu akiwa mjapani kabisa , tena Ninja aliekuwa kwenye mavazi meusi , huku akiwa ameshikilia panga lake refu , alikuwa na sura ngumu hatari na macho yake ni kama yalikuwa yakitoa damu , lakini ajabu ni kwamba Raisi huyu hakumuongopa hata kidogo huyo mtu.

“ Noriko Gumila nataka kujua spidi ya kuua ndani ya kundi la Yamaguchi , inachukua dakika ngapi?”Aliuliza kwa lugha ya Kingereza.

“Inategemea na aina ya kifo”Ilisikika suati nzito.

“Kisichokuwa cha kumwanga damu , Mshituko wa moyo, but very Discretly”

“That is ten second”

“Noriko najua kabisa sheria moja ya The Doni inakuhitaji kunilinda masaa ishirini na nne , kwasababu umekuwa ukinilinda kila siku tokea nikiwa kiongozi wa ikulu hii , nataka unifanyie jambo moja”Aliongea Mheshimiwa na Gumila alikuwa haeleweki sura yake ilikuwa ikiashiria nini , ilikuwa ni ngumu kumsoma kabisa , na ikumbukwe kwamba moja ya maneno ya Yan Buwen wakati akiongea na Scorpion ni kwamba kila nchi ina angalau Ninja Mia moja ambao wapo karibu na watu wenye nguvu kwa kila taifa , ambao muda wowote wakiambiwa kuua wanaua , sasa halikuwa jambo la kushangaza kwa uwepo wa Noriko Gumila ndani ya ikulu hii ya Kenya , akitoa ulinzi kwa Tageti yake , akiwa chini ya maelekezo ya The Doni.

“Sheria zinaniruhusu kutii ombi lako moja tu mheshimiwa kwenye Maisha yangu yote, lakini nikutahadharishe mheshimiwa ningekuacha hai kama tu ningeagizwa kufanya hivyo na ukafanya ombi hilo , lakini kwasababu unataka ombi hili kwa ajili ya kumuua mtu nipo tayari , lakini uelewe kwamba hauna ombi lingine unaweza kufanya kwangu”Aliongea Gumila na kumfanya Mheshimiwa kamau afikirie.

“Gumila nipo tayari , nifanyie ombi langu hilo moja na baada ya hapo nitaishi Maisha yangu yote kumtii The Doni na kuhakikisha hatokuwa na sababu ya kukupa maagizo ya kuniua Zaidi ya kuhakikisha ulinzi wangu”Aliongea Mheshimiwa na Gumila palepale alinyanyua mikono yake juu kama vile anasali na kisha akapiga magoti chini na kugusisha kichwa chake chini kama vile mtu anesujudu kwa dakika kadhaa na kisha akanyanyuka , bwana huyu ukimangalia utadhani ni wale waigizaji wa filamu za kale za kijapani , hakuw hana utofauti wa aina yoyote

“Nipo tayari kupokea ombi lako la kwanza na la mwisho”Aliongea kwa sauti yenye kitetemeshi.

“Anaitwa Raisi Senga Kweka ni raisi wa Tanzania , nahitaji afe ndani ya masaa mawili kwanzia sasa”Aliongea Mheshimiwa kwa sauti ndogo sana na Gumila aliinamisha kichwa chake chini kama ishara ya kukubali na hapo hapo kama Radi alipotea kwenye macho yake.

“Nisamehe Senga , wewe ni rafiki yangu , ila ili nchi zetu ziendelee kuwa na urafiki lazima mmoja wetu atoweke kwenye huu uso wa dunia”Aliwaza mheshimiwa na kuanza kupiga Simu kwa mtu aliempigia dakika chache zilizopita na ilionyesha alikuwa akimwabia muda halisi wa ‘Target kuwa terminated’
 
SEHEMU YA 175

“Kabwe nitaenda kumtembelea baba leo , Weka utaratibu wa kutoka baadae”Aliongea Mheshimiwa Senga mara baada ya kutoka ofisini akielekea upande anakoishi na familia yake na muda huo ilikuwa ni saa kumi za jioni na ni baada ya kumaliza kikao na muwekezaji kutoka Dubai.

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Kabwe msaidizi wa karibu wa mheshimiwa.

“Sitaki msafara wa watu wengi gari tatu zinatosha”Aliongea Mheshimiwa na kisha akAendelea kupiga hatua kukata Kona ndani ya jumba hili na Kabwe alievalia suti yake aliishia kuitikia kwa heshima na kisha akageuka, licha ya kwamba ameambiwa na mheshimiwa Baadae watatoka , ila hakujua ni muda gani safari itaanza , ila alikuwa ashazoea baadae ya Mheshimiwa mara nyingi ilikuwa ni saa moja.

“Wife leo nitaelekea kumsalimia baba”Aliongea Mheshimiwa mara baada ya kukumbatiana na mke wake Damasi , aliekuwa amevalia gauni la maua maua.

“Lakini siku zote amekua akija hapa ikulu akitaka kuonana na wewe kwanini leo anataka uende?”

“Sijui mke wangu , ila ukiona hivyo labda kuna jambo kubwa ambalo anataka kunieleza , napaswa Kwenda”

“Nitakusindikiza”

“Haina haja Mpenzi , juzi tu umetoka huko”Aliongea mwanamama huyu , aliekuwa na urembo wa ajabu , licha ya kwamba umri wake umeenda , lakini uzuri wake wa asili haukuwa umepotea kabisa, ni mwanamama ambaye amebahatika kupata watoto wawili yaani Ashley Pamoja na Denisi.

“Mume wangu najua una majukumu mazito sana ndani ya taifa hili lakini hizi wiki chache umebadilika sana , unaonekana kuwa na mawazo, nini tatizo?”Aliongea Damasi huku akimalizia kumvua mheshimiwa Senga Shati na kulitupia kwenye kikapu(Hamper) cha kuhifadhia nguo chafu na Senga alimwangalia mke wake kwa sekunde na kisha akamvuta kwake na kumbusu kwenye paji la uso.

“Ni majukumu tu ya kikazi Mama Ashley , Nothing Much”

“Noo.. Senga you look so Troubled, nina wasiwasi juu yako , chochote unachopitia Senga hakikisha unakumbuka kuwa licha ya wewe kuwa raisi wa wa Tanzania lakini pia ni baba wa Watoto wangu”Aliongea Damasi au Mama Ashley na kumfanya Senga atabasamu na kuvua suruali mwenyewe na kumpatia mke wake na kisha akatingisha kichwa kumuelewa.

“Denisi amekupigia?” Aliuliza Senga na kumfanya Mama Ashley kukosa utulivu kwenye macho yako.

“Denisi ananitia wasiwasi sana Senga , licha ya kwamba sasa ni mtu mkubwa lakini tabia yake inaniweka kwenye wakati mgumu”

“Kwahio hajakupigia?”

“Ndio tokea aseme anaelekea China hajanipigia kabisa na nimejaribu kuwasiliana nae lakini simpati..”Aliongea Kinyonge huku akikaa kitandani.

“Usiwe na wasiwasi mke wangu , He will be fine”

“Najua Senga lakini moyo wangu umekuwa mzito kweli siku hizi chache nahisi kuna jambo baya linaweza kumtokea”

“Mother Intuition..!?”Aliongea Senga huku akitabasamu na Damasi alimwangalia na kutingisha kichwa.

“Nitajaribu kuwapa kazi vijana wangu wamfatilie”Aliongea na kisha akchukua taulo na kuelekea bafuni.

*******

“Ah! Don’t kill me” Goodman alijikuta akikurupuka mara baada ya kuwekea Bunduki usawa wake kiasi kwamba kidogo amuumize Edna lakini Roma alikuwa na kasi kweli kwani alimvutia kwake kumkwepesha na Goodman.

Na kitendo chake kiliwafanya wale majambazi kucheka kwa sauti, walifurahishwa na uoga aliokuwa nao Goodman.

Roma yeye alianza kukagua watu waliokuwa mbele yake , ijapokuwa kulikuwa na giza lakini aliweza kuwaona vyema kutokana na mwanga ,kwa mavazi yao hawa majambazi walikuwa wamevalia nguo za kijeshi za kimasenari*Marecenary black Military Uniform) Roma aliweza kuangalia kwa ukaribu ili kupata kuona jina la jeshi watu hawa wanatokea.

“Sun Gold Totem!!”Roma aliweza kusoma maneno hayo kutoka kwenye Kombati zao za sehemu ya kifuani,

“Inawezekana vipi sijawahi kusikia hili kundi?”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake , ukweli alishindwa kujua kundi hilo la kijeshi linalojiita Sun Gold Totem, aliweza kufikiria makundi yote ya kijeshi , lakini pia mashirika ya Kimamluki yanayotumia nguvu za giza na alishindwa kupata jina la Sun Gold Totem Army.

“Labda ni kundi jipya lililojitokeza baada ya mimi kurudi Tanzania?”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake.

Baada ya hawa wanajeshi kumaliza kucheka walimsogelea Goodman aliekuwa amejificha kwenye gari na kumvuta nje na kisha mwingine akataka kumvuta na Roma.

“Nitatoka mwenyewe”Aliongea Roma kwa usiriasi huku akitoka kwenye gari na mwanajeshi mwingine akampa ishara na Edna kwa kutumia bunduki lake na yeye atoke.

Edna licha ya mwanzoni hakuwa na wasiwasi , lakini baada ya kuona watu waliokuwa mbele yake ni wanajeshi alianza kupatwa na wasiwasi , kwani muda wote alitegemea ni majambazi yaliowateka , lakini sasa alijua ni jeshi ndio maana wasiwasi ulianza kumjaa.

Baada ya kutolewa wote kwenye Gari waliongozwa njia na mwanajeshi mmoja huku watatu wakiwa nyuma na wakazunguka upande wa kulia ndani ya msitu huu , sehemu iliokuwa na mwinuko kama mlima na mbele yao lilionekana shimo kubwa na kwa haraka haraka Roma alitambua ni Handaki kutokana na lilivyojengewa kwa nje.

Mlango wa chuma ulifunguliwa na Mwanajeshi wa mbele na kisha wote wakaingizwa ndani ,Sehemu ambayo ilikuwa na ubaridi wa aina yake na kumfanya Roma amuonee huruma Edna na kutaka kutoa Koti , lakini aliamini akifanya hivyo wanajeshi hao wanaweza kumuona anataka kuleta madhara ndio maana aliacha kwanza waingie kabisa.

Dakika chache walifika ndani kabisa , Sehemu iliokuwa na giza totoro na ukafunguliwa mlango mwingine kulia na wote wakasukumiwa ndani na mlango wa ukafungwa kwa nje.

Goodman alidongoka mkuku mkuku kwa kukosa balansi na alijikuta akila mchanga , huku harufu ya uozo ikisumbua pua zake.

“Wh….where’s this place?”Aliropoka kwa woga , kwani hakuweza kuwaona wenzake na alijihisi yuko peke yake.

“It’s a warehouse,”Ilisikika sauti ya kiume ambayo haikuwa nzito sana ndani ya eneo hilo hilo walilokuwepo na kumfanya Edna woga umjae na kumkumbaitia Roma,Huku Goodman akirudi kinyume nyume na kujigonga kwenye Mlango wa Nondo kwa woga.

“Argh!!.”

“Usiogope , hakuna kibaya kitakachokutokea”Aliongea Roma huku akivua koti lake la Suti na kumvalisha Edna , Ukweli ni kwamba Roma alikuwa akiona kila kitu na aliweza kuona watu wawili waliokuwa kwenye kona ya chumba hiki ambacho kilikuwa kama Gereza la karne zilizopita.

Roma aliingiza mkono wake kwenye mfuko na kutoa simu yake ndogo na kisha akawasha Tochi na kufanya mwanga uonekane eneo lote na kuwafanya Edna na Goodman waweze kuona mazingira waliyopo , Roma aliwasogelea watu wawili waliokuwa wamejibanza kwenye kona na kuwamulika usoni ili awatambue.

“Inaonekana nina bahati sana , Sikutegemea kama ninaweza kukutana na nyie hapa”Aliongea Roma huku akitabasamu na alionekana watu hao walikuwa akiwajua , walikuwa ni mwanaume na mwanamke wamekumbatiana na , kwa jinsi walivyokuwa wakionekana ilidhihirisha kuwa walikuwa wapenzi , wote wakionekana kuwa katika rika sawa huku mwanaume akiwa na nywele nyeupe na mwanamke akiwa na nywele zilizppakwa rangi ya Zambarau na kumfanya kuonekana mrembo sana na macho yake yenye kiini cha Rangi ya Blue.

Edna baada ya kuwaangalia hao wazungu na mkao wao alguna huku akigeuza macho yake pembeni na Roma alimwangalia huku akitabasamu.

“Bebi japo huyu mwanamke ni mrembo ila hakuzidi , nimependa tu staili ya nywele zake maana sio za kawaida”Aliongea Roma

“Sijakuuliza mimi usijitetee , unaweza kumkodolea tu macho utakavyo”Aliongea Edna.

Usichokijua ni kwamba huyo mwanamke alikuwa amevaa kigauni kifupi , lakini wakati huo huo akiwa amekipandisha juu na kumruhusu mwanaume huyu wa kizungu kuingiza mkono kwenye nguo ya ndani , sasa haikueleweka anatafuta nini , ila alikuwa akifukunyua huku mwanamke akihemea kifuani na hawakujali kabisa uwepo wa watu waliongezeka, walikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa , ulimwengu wa mahaba , yaani licha ya kwamba walionekana kama mateka , ila wao ni kama wapo kwenye chumba cha hoteli cha hadhi ya nyota tano.

““You guys… Aren’t you guys… the siblings Stern and Alice from the Cromwell clan?!”

“Nyie….! ,Nyie si dada na kaka ,Stern na Alice kutoka ukoo wa Cromwell?”Aliongea Goodman na hata yeye alionekana kuwatambua hao watu , baada ya kuwasogelea na baada ya kuitwa majina yao waliinua vichwa vyao na kuwaangalia sasa Edna na Roma , Pamoja na Goodman , walionekana akili zao kurudi kutoka walipokuwepo.

“I’m sorry Sir, I don’t know you. Are you a British?”

“Samahani Mkuu , sikutambui, wewe ni Muingereza?”Aliuliza Stern huku akimwangalia Goodman.

“Oh… No, no, it’s totally reasonable that you don’t know me. I’m the director of Athena Trading company , Vexto International branch ,I am called Goodman. I only remember you two because I was lucky enough to have seen you in the London Fashion Week a few years ago”

“Oh.. No , no ,nisahihi kabisa huwezi kunitambua ,Mimi ni director kutoka Athena, Tawi la kimataifa la Kampuni ya Vexto nafahamika kwa jina la Goodman , Nimeweza kuwakumbuka kwasababu nilibahatika kuwaona London miaka michache iliopita kwenye maonyesho ya wiki ya Fasheni”Aliongea Goodman huku akijiweka sawa na kusimama wima.

“Huyu hapa ni Bosi wa kampuni yangu Mama anaitwa Edna na huyu hapa ni Mr Roma , wamekuja hapa Parisi kibiashara,Aisee sikuweza kudhania naweza kukutana na watu wazito kama nyie hapa”Aliongea Goodman akimtambulisha Edna na Roma kwa Heshima , kama vile watu waliokuwa mbele yake walikuwa ni maraisi.

RATIBA NI JUMMANE , ALHAMISI , JUMAMOSI VIPANDE VINNE MPAKA VITANO , SIKU NYINGINE NITAWAPENDELEA
NICHEKI WATSAPP 0687151346 HUKU TUPO SEHEMU YA 235
 
Back
Top Bottom