Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbado mbadoTUPO TUNASUBIRI MKUU
Duuuuh chuma roma sasa nae zamu yake kukutana na wababe wakeSEHEMU YA 214
Athena kwa historia ya Ugiriki ya kale alikuwa ni mungu wa vita , busara na ulinzi , katika miungu yote kumi na mbili katika historia yao, Athena pekee ndie aliekuwa akiongoza kwa akili nyingi sana.
Kwa upande wa Rumi kabla ya kuja kwa Christ Yesu, Minerva pia alikuwa na sifa zinazofanana na za Athena na wagiriki na waroma walikuwa wakiwaona kama mtu mmoja.
“Minerva unataka kuongea nini?”Aliuliza Papa Adre Kleish baada ya kukaa kwenye kiti chake na Athena bila ya wasiwasi alitumia kidole kimoja kuchora alama ya Zero na baada ya kumaliza alitumia mkono wake kupitisha mkono sehemu ambayo amechora alama ile na ilionekana ni kama mkono wake unamezwa na hewa lakini alipouvuta nje aliibuka na HollyGrail.
“Mtakatifu!,kikombe cha ukumbusho alichotumia Mesiah in last Supper”Aliongea Minerva na Papa alisimama kwa kutaka kushika kile kikombe kama mtu asieamini lakini Athena alikivuta nyuma.
“Minerva that is our sacred Treasure, You stole it from us”
“Minerva hio ni hazina yetu takatifu , Uliiba kutoka kwetu?”
“Your Hollines you are mistaken , I did not Stole it but I Secured it From Dark Parliament”
“Mtukufu umekosea ,sijaiba bali nilikilinda kutoka kwenye mikono ya Bunge la Kiza”
“Minerva wewe ni mtoto wa Mungu na Bwana yupo tayari kukupokea baada ya kukutakasa Dhambi zako zote , naomba urudishe hazina ya kanisa kwetu na ahadi zake zitatimia kwako”Aliongea Andre na kumfanya Athena kutabasamu.
“Hazina hii itakaa kwenye mikono yangu mpaka nitakapo pata majibu ninayo yataka Andre”
“Majibu Gani?”
“Nahitaji kujua siri ambayo ipo nyuma ya HollyGrail na muunganiko wake na Prior of Sion”
“Why must I?”
“Because I have been the Protector of this City for Centuries , I need to know the Codes Andre , I have my own limit in Diplomatic conversation , I will be Back when you have made Decision”Aliongea Athena akimaanisha kwamba anahitaji kujua siri iliopo nyuma ya HollyGrail huku akijinasibu ya kwamba alikwa mlinzi wa Vatican kwa karne na Karne na ameshachoshwa na mazngumzo ya kidimplomasia.
Unafikiri mpango wa Athena ni nini haswa…… na siri anayoitaka ni ipi.
******
Kutokana na mwendo ambao Roma alikuwa akiutumia haikumchukua muda mrefu kufika ndani ya jiji la Dar eneo la Tegeta na baada ya takribanni dakika arobaini na tano zingine ziliweza kumfikisha Kigamboni.
Roma baada ya kufunguliwa geti moja kwa moja aliingiza gari haraka na Kwenda kuliegesha katika eneo maalumu na kutoka, kwa jinsi magari yalivyoongezeka aliona kweli kuna ugeni hapo nyumbani na hata gari ya mke wake pia ilikuwa ishafika.
Sebuleni hapakuwa na mtu , lakini ile anashangaa alimuona Edna aliejiufunga khanga akiwa amebeba kikombe cha chai akipandisha ngazi Kwenda juu.
“Njoo kwenye chumba changu cha kujisomea tunasubiriwa”Aliongea Edna baada ya kusimama na Roma alitingisha kichwa na kuanza kupiga hatua kuelekea juu , huku akishangaa ni mgeni gani ambaye kamfanya Edna kutengeneza kahawa na kujifunga khanga kiunoni kama vile mama wa nyumbani kwani muda huo Roma alijiambia mke wake angekuwa kazini akiendelea na majukumu yake , lakini sasa hivi hali aliokuwa akiona ni tofauti kabisa.
Roma baada ya kuingia kwenye chumba cha Edna cha kujisomea alionekana mzee mmoja akiwa ameketi kwenye masofa huku akiwa amekunja nne na kushikilia moja ya kitabu katika vitabu vingi vinavyomilikiwa na Edna.
Roma kwanza hakumfahamu huyo mzee kwani hakuwahi kumuona mahali popote, Edna alieshikilia kikombe alikiweka mezani na kumkaribisha mzee..
“Roma umefika!... niliomba nitegenezewe kahawa na mkwe wangu hahaha…”Aliongea Mzee huyu kwa bashasha na alionekana hakuwa na wasiwasi kama vile yupo kwake.
“Wewe ni nani mpaka ujione huru kama hapa ni kwako?”Aliuliza Roma aliesimama mlangoni na mzee yule baada ya Roma kuuliza swali la namna hio alisimama na kisha akatabasamu.
“Mimi ni babu yako Camilllis Kweka ndio maaa….”Kabla hajamaliza Sentensi yake Roma kama upepo alikuwa ashamfikia na kumshika shingo na kumning`niza hewani na Afande Kweka alianza kutapatatapa.
Edna aliekuwa amesimama akiwa katika mshangao baada ya kusikia maneno ya Afande Kweka , alishangaa Zaidi na woga kuongezeka baada ya kumuona Roma amemning`iza mzee wa watu hewani.
Edna alikuwa akijua jambo ambalo Roma analifanya ni la hatari kwani alikuwa akielewa nguvu iliokuwa nyuma ya Mzee Kweka ndani ya taifa hili , licha ya mzee huyo mtoto wake kuwa raisi , lakini pia alikuwa akiogopwa sana jeshini na maamuzi yake yalikuwa yakiheshimiwa sana.
“Romaa…”Edna alijikuta akili yake ikirudi na kumkimbilia Roma na kumshika shati aache kile ambacho anakifanya.
“Unakuja nyumbani kwangu .. halafu unajifanya ni kwako na unaanza kuongea upuuzi wa ubabu babu”Aliongea Roma kwa hasira huku akizidi kumnyonga Afande kweka na alionekana hakuwa tayari kubembeleza.
“Roma muachie tafadhari... nakuomba”Edna alikuwa akiogopa kiasi kwamba hata machozi yalianza kujitengeneza kwenye macho yake.
“Swaaaaash!!!!”
Ulikuwa ni kama upepo uliomsukuma Roma na Kwenda kutua kwenye mlango huku akimwachia Afande kweka aliedondoka chini huku akianza kukohoa mfulilizo.
“Mr Roma naomba utulie tafadhari..”Aliongea Zenzhei aliembana Roma ukutani na kwa jinsi Roma alivyoshikiliwa ilikuwa ni ngumu sana kwake kuchoropoka kwenye mikono ya Zenzhei na jambo hili lilimshangaza sana.
“You Are cultivator ?””Aliuliza Roma kwa mshangao na kumfanya Zenzhei kutabasamu na kumwachia.
“Ndio Mr Roma mimi ni Cultivator kutoka katika miliki ya kijini kutoka china ,Hongmeng”
“Hongmeng..!!!, Your From Hongmeng?”Roma alijikuta akishangaa mno hakuwahi kufikiria kama atakuja kukutana na raia wa China kutoka Hongmeng”
“Lakini kwanini unatoa ‘Aura’ kama Ninja wa kundi la Yamaguchi?”
“Mr Roma hilo ni swala ambalo mimi na wewe tutakaa na kuzungumza ila kwa sasa unapasa kumsikiliza Camilius”Aliongea Zenzhei na kumfanya Roma akumbuke kuna mtu alietaka kumuua nyuma yake , ukweli alikuwa ‘Excited’ baada ya kukutana na mtu kutoka Hongmeng.
Hongmeng katika utamaduni wa Taifa la China watu hawa hufahamika kama walinzi wakuu wa taifa, licha ya kwamba Hongmeng ni kama jina linalotambulisha utamaduni kama vile neneo Hegemony , lakini kwenye tamaduni za kichina Hongmeng maana yake ni ‘Concealment’ au Siri kwa Kiswahili chake , sasa Hongmeng ni jamii ya siri ambayo ipo China ambayo ipo kwa mfumo wa hadithi yaani ni kama hapa Tanzania mtu akuambie ziwa Tanganyika kuna njia ya kuelekea ulimwengu wa majini ndio hivyo hivyo kwa upande wa China kuna jamii(realm) ya kijini ambayo kwao wanaitambua kama Hongmeng ,sasa kilichomshangaza Roma ni kwamba watu wote wa jamii ya Hongmeng huwezi ukawakuta kwenye ‘Mundane world’, yaani ulimwengu wa kawaida wa kuchanganyika na watu ni kama hivyo hivyo kwa majini kutopenda kuchanganyika na binadamu ndio hivyohivyo kwa Hongmeng , Katika hadithi nyingi za kichina inasemekeana kundi hili la watu kutoka Hongmeng wana nguvu za kichawi ambazo sio za kawaida kabisa , sasa hapa nitakueleza kwanini majini wanatofautiana nguvu.
Edna hakuelewa kinachoendelea na alishangaa kuongezeka kwa Zenzhei hapo ndani kwa ghalfla tu , japo alishukuru kupitia mchina huyo Roma alimuachia Afande kweka lakini alikuwa na wasiwasi , lakini mrembo huyu alikuja kuchanganyikiwa Zaidi baada ya kusikia namna mchina huyo alivyokuwa akiongea.Edna alimsaidia mzee Camilius kukaa kwenye sofa na kurudi nyuma
“Mzee inabidi ujielezee vizuri la sivyo utaondoka hapa ukiwa maiti”Aliongea Roma akiweka uso wa usiriasi na ilibidi Edna amsogelee na kumwambia atulie.
Na mzee Camillius alikaa vyema na kisha kutabasamu huku akishika shingo yake inayouma na kumpa ishara Zenzhei kumsogelea.
q
WATSAPP 0687151346 NICHEKI KWA KUPATA YTARATIBU WA MWENDEKEZO
Mkuu singanojr ,huyu Raheli ni wa babati yetu hii hii ya Manyara au kuna Babati nyingine?😂.. Atakuwa mburu wa Dareda au Bashnet huyu,maana kama namkumbuka kumbuka,😂..yani sura yake kama inakuja halafu inakataa😂😂NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI:SINGANOJR KING
SEHEMU YA 206
Tukio ambalo lilitokea hapo bandarini kwa upande wa Roma alikosa maelezo mazuri ya kulielezea kabisa, jambo hilo halikuwa dogo na lilimkera sana Roma , kwani ni mara ya pili hii anakutana na mtu huyu ambaye uwezo wake ni mkubwa sana kuliko wa kwake.
Roma hakuona haja ya kubakia ndani ya hilo eneo Zaidi ya kurejea kwenye gari, Edna alikuwa vilevile kama alivyomuacha , hakuongea chochote hata pale Roma alivyorudi kwenye gari, na kutokana na Roma kutokuwa kwenye mudi nzuri kutokana na tukio la teknolojia ya siraha ya Thanatos kuchukuliwa na mtu mwenye uwezo mkubwa kuliko yeye hakutaka pia kuongea chochote Zaidi ya kuendesha gari kuelekea upande wa hoteli ya Sofiteli.
Ni madakika kadhaa tu Roma alikuwa ashafika ndani ya hoteli hio na ile anasimamisha gari tu, Edna ndio aliekuwa wa kwanza kutoka na kupiga hatua kuelekea ndani na kumfanya Roma aishie kumwangalia, pasipo kujua ni kipi kimempata Edna kwa wakati huo kwani kama ni Edna kumchunia aliona huo mchunio sio wa kawaida hata kidogo.
Upande wa ndani ya hoteli Goodman alikuwa ndani ya chumba chake akiwa anakunywa bia kwa kujipongeza kile ambacho alikuwa amekikamilisha mchana wa siku hio , alikuwa na furaha kweli kwani aliamini kwa asilimia mia moja Edna asingeweza kutoka kwenye mikono ya Apollo.
Mziki wa mahadhi ya Waltz aliokuwa ameufungulia ulimfanya bwana huyu kucheza kwa kujiachia ndani ya chumba chake cha kifahari ndani ya hoteli hii , huku akiwa amevalia taulo na mkononi akiwa ameshikilia Glass ya iliojazwa kwa kimiminika cha rangi nyekundu.
“Hahaha…Vexto inakwenda kuwa yangu,What a great Achivement!”Aliongea Goodman huku akiendelea kucheza kwa furaha akiwa amefumba macho akisikilizia mziki kutoka kwenye spika zilizokuwa zimefungwa ndani ya chumba hiko.
Wakati akiendelea kusikiliza mziki na kucheza kwa furaha, burudani yake ya kucheza Pamoja na kufurahia mvinyo ilikatishwa na mtu aliekuwa akigonga nje ya mlango.
Goodman akiwa kwenye hali ya kukereka pasipo kufikiria ni nani aliekuwa akigonga alifungua kwa jaziba na palepale macho yake yakatua kwa mtu ambaye hakutegemea kumuona mbele yake muda huo , kwani alitegemea mtu huyo kuwa mfu kwa wakati huo.
“ Mr Roma..ho…how did… how did you…”Goodman alijikuta akiwa ni mwenye kubabaika kwani hakutegemea kumuona Roma Ramoni wakati huo na kwa upande wa Roma hakujali Goodman aliekuwa ni mwenye kubabaika bali palepale kwa kutumia mguu wake wa kulia alimpiga teke Goodman na kumfanya kudondokea ndani na Roma aliingia ndani na kufunga mlango huku Goodman akitoa ukulele wa maumivu.
Ukweli Roma hakuwa na haja ya kumuuliza Nadia ilikuwaje mpaka akawa sehemu ya mateka na hii ni kwasababu alikuwa na maelezo kutoka kwa Stern na Alice ambao walimwambia Goodman ndie aliekuwa mhusika mkuu aliefika hospitalini akiwa na magaidi na kuwateka , hivyo Roma aliamini maelezo yote atayapata kupiga Goodman.
Roma baada ya kumpiga Goodman teke na kudondokea ndani , alimshika Goodma kwenye kiuno kwa kutumia mkono mmoja tu na kisha akamnyanyua juu na kumfanya Goodman kuelea hewani.
“Mr Roma uantaka kufanya nin…”Aliongea Goodman huku akiwa kwenye hali ya wasiwasi mno , lakini Roma hakuwa ni mwenye kuongea neno , alichokifanya ni kumbeba Goodman kwa staili ileile na kisha akafungua mlango uliokuwa ukimruhusu kutokezea kwenye Balconi.
Roma akiwa amemshikilia kisawasawa Goodman kwenye kiuno alijirusha kutoka juu ya Balconi na kupotea ndani ya hoteli hii ya Sofitel.
“Shwaaa…..!!!”
Ni maji yaliokuwa na mchanganyiko wa harufu mbaya ndio yalioweza kumzindua Goodman aliekuwa amepoteza fahamu.
“Hey! Wewe nguruwe mweupe naona umezinduka”Ilikiwa ni sauti ambayo Goodman hakuweza kuitambua na kutokana na ubaridi aliokuwa akihisi kwenye mwili wake aligundua hakuwa na nguo yoyote mwilini na alikuwa uchi.
“Nyie ni wakina nani na hapa nipo wapi?”Aliuliza Goodman baada ya kugundua amezungukwa na wananaume Weusi Zaidi ya wanne wakiwa wanamwangalia , huku taa za eneo hili zikiwa haififu mno na zenye rangi mbalimbali , ni kama vile alikuwa ndani ya Casino kwa muonekano wa eneo hili.
“Huna haja ya kuuliza maswali wewe nguruwe mweupe , haha… unaiona hii?”Aliongea mwanaume mwingine mweusi aliekuwa na ndevu nyingi huku akimwonyesha Goodman kiungo chake cha siri na Goodman baada ya kugundua kitu ambacho kinatarajiwa kufanyika kwake a;ijikuta akitamani hata kupoteza fahamu.
Ile furaha aliokuwa nayo dakika kadhaa nyuma ilikuwa imegeuka na kuwa majuto makuu , hakuamini kwenye Maisha yake anaweza kuwa kwenye eneo kama hilo akiwa hana msaada na huku mbele yake kukiwa na wanaume ambao wanataka kumfanyizia kitendo ambacho hakuwahi kukifikiria kwenye Maisha yake kama kitakuja kumtokea.
“Hey!Mshikilieni vizuri , nataka nianze mimi”Aliongea jamaa mmoja mwingine huku akivua bukta lake.
“Subi… subirini kwanza , nisikilizeni nitawapa pesa nying…”Goodman alianza kuweweseka , lakini palepale mlango ulifunguliwa na Roma aliekuwa ameshikilia bia aina ya Martel akiigida kwa fujo.
“Mr Roma naomba unisiadie tafadhari … nitakupa kiasi chochote cha hela unachotaka ,usinifanyie hivi , nimekosa mimi naomba unisamehe”aliongea Goodman maneno mfululizo , lakini kwa Roma hayakuwa yakimwingia hata kidogo Zaidi ya kupandwa na hasira , kila alipokuwa akikumbuka namna Edna alivyokua amemchunia alijihisi hasira zikizidi kupanda.
“Sina sababu ya kukusamehe …. Nitahakikisha hawa wanaume wanakufanya kwa zamu mpaka waliridhike na nikishamaliza nitatekeleza kifo chako”Aliongea Roma ambaye hakuhangaika na sauti za miziki zilizokuwa zikisikika kutoka nje.
Ndio sehemu ambayo Goodman alikuwa amekamatwa na kufungwa ni ndani ya ya mtaa wa Moulin Rouge upande wa Montmartre ndani ya jiji hili la Paris , hii ndio mitaa ambayo ilikuwa imechangamka sana wakati wa usiku kwa kuwa na Macasino mengi ,Bar na biashara nyingi haramu ambazo zilikuwa zikifanyika, maatufu kama Grey Business.
“Mr Roma …Pleaase….”Aliongea Goodman huku machozi yakianza kumtoka.
“Mr Goodman unaonaje kabla ya kujitetea ukaelezea tukio zima kwanza ili nielewe nia yako halisi ni ipi?”Aliongea Roma ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti cha sofa kilichokuwa pembeni ya Goodman.
Goodman baada ya kupewa nafasi hio hakuona haja ya kuficha chochote , aliona njia pekee ya kukwepa kifo na adhabu ambayo Roma alikuwa amemuandalia ni kuongea ukweli.
“Mr Roma nitakueleza kila kitu ,, naomba usiniue tafathari”Aliongea Goodman na kumfanya Roma atabasamu kifedhuli na kisha akampa ishara jamaa mmoja ambae dakika chache nyuma alitaka aanze yeye kumfanyizia Goodman, na jamaa yule baada ya kupewa ishara alimsogelea Goodman huku akiwapa ishara vijana wake wamshike vizui kwa kumuinamisha.
“Nitaongea…nitaongea”Goodman baada ya kugundua anachotaka kufanyiziwa palepale alijitetea kwa kusema ataongea ukweli na Roma aliwapa ishara kumsimamisha vizuri ili aweze kuongea.
********
Nahita , Rahel na Kizwe walikuwa ni wanachuo walioshibana sana ndani ya chuo cha Durban South Africa na urafiki wao ulitokana na kukaa chumba kimoja ndani ya hosteli za chuo hiko zilizokuwa ndani ya Campus namba moja.
Licha ya kila mmoja kuchukua kozi tofauti tofauti kati yao, hio haikuwafanya wanadada hao warembo na maarufu kutokuwa marafiki ,wakati Raheli akichukua masomo ya uhasibu, upande wa Nahita alikuwa akichukua masomo ya uongozi wa biashara, huku mwanadada mrembo Kizwe na yeye akichukua masomo ya Lugha.
Nahita alikuwa ni mjapani, huku Raheli yeye akiwa ni mtanzania na kwa upandewa Kizwe yeye akiwa ni Mrwanda, urafiki wa wadada hawa wa mataifa tofauti ulikuwa mkubwa kiasi kwamba walikuwa wakifanya mambo mengi kwa Pamoja.
Kutokana na urembo wao lakini pia namna ambavyo walikuwa wakifanya matanuzi ndani ya South Africa iliwafanya warembo hawa kuwa maarufu sana kwa wakati huo.
Mwanadada mrembo kutoka Rwanda yaani Kizwe, kwa upande wake yeye alikuwa tayari yupo kwenye ndoa na makamu wa raisi wa Rwanda mheshimiwa Jeremy Paul wakati akiwa masomoni, upande wa Nahita yeye pia alikuwa na mpenzi wake Muingereza, ila kwa upande wa Raheli bado hakuwa na mpenzi kwa wakati huo, licha ya wanaume wengi kumtakakimahusiano, na hio ni kwasababu wanaume wote walionekana kutomvutia kabisa, na hii yote ni kutokana na tabia ya Raheli kuchagua chagua wanaume.
Raheli tofauti na marafiki zake , yeye pekee ndie aliekuwa hapo chuoni kwa ufadhili maalumu wa masomo yake kutoka serikalini, hivyo unaweza kusema kwamba Raheli hakuwa mtoto wa kishua kama ilivyokuwa kwa marafiki zake Nahita na Kizwe.
Mwaka wao wa mwisho ndio Kizwe aliweza kuwatambulisha Raeli na Nahita kwa Mheshimiwa Jeremy Paul kwenye mahafali yao ya kumaliza, na pale mheshimiwa Jeremy Paul baada ya macho yake kutua kwa mrembo Rahel, alijikuta akimpenda hapo hapo(Love in first sight) na sio kwa Jeremy tu hata kwa Raheli pia baada ya macho yake kutua kwa Mheshimiwa Jeremy alijikuta akivutiwa nae mno na kutokea kumpenda, na kwa mara ya kwanza Raheli akajikuta anampenda Jeremy kwa mapenzi ya dhati pasipo kujali kuwa Jeremy alikuwa ni mume wa mtu , tena mume wa rafiki yake Kizwe.
Baada ya marafiki hao kuhitimu masomo yao kila mmoja alirejea katika taifa lake ,Nahita alitejea Japani kabla ya kuhamia uingereza baada ya kufunga ndoa na mwanaume aliekuwa akipendana nae na kwa upande wa Kizwe alirejea nchini kwao Rwanda kuendelea kuitumikia ndoa yake.
Lakini jambo ambalo Kizwe hakulifahamu, ni kwamba Raheli na Mheshimiwa Jeremy tayari walikuwa na mawasiliano ya karibu sana , mawasiliano ambayo yalipelekea mapenzi mazito ya wawili hao, na mheshimiwa Jeremy kutokana na penzi lake kwa Raheli aliamua kufadhili masomo yake ngazi ya Masters ndani ya taifa la Urusi na huko ndio sehemu ambazo mheshimiwa Jeremy alitumia sana kukutana mara kwa mara na Raheli na kufurahia penzi lao.
Upande wa Nahita mara baada ya kufunga ndoa na mzungu wake miaka miwili baadae ndipo alipopata kujifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Goodman.
Huku upande wa Raheli yeye alikuwa tayari ashamaliza masomo yake na alikuwa asharejea nchini Tanzania kuendelea na Maisha yake na wakati Nahita anajifungua ,kwa upande wa Raheli alikuwa mjamzito tayari na alikuwa ameshaolewa na Adebayo, na kwa upande wa Jeremy wakati Raheli ana ujuaito yeye ndio kwanza alikuwa akiingia madarakani kama Raisi wa Taifa la Rwanda huku Kizwe mke wake akipanda cheo na kuitwa rasmi First Lady huku jina Kizwe likikosa umaarufu .
Sasa haikueleweka ni wakati gani Kizwe aliweza kugundua mahusiano ya Jeremy na Raheli , lakini wawili hao waliendelea kuwa marafiki kwa muda mrefu sana mpaka ambapo Edna mtoto wa Raheli kufikisha umri mkubwa.
Kutokana na ushauri wa Nahita na bibi yake Edna yaani Mariaum walikubaliana na Raheli kwa Edna Kwenda kusoma ndani ya chuo cha Oxford na kipindi ambacho Edna anaanza masomo, kwa upande wa Goodman alikuwa tayari yupo chuoni na alikuwa amemtangulia Edna kwa mwaka mmoja.
Kwahio hapa tunaona kwamba Kosa alilolifanya Kizwe ni kuwatambulisha marafiki zake kwa mume wake , kwani tokea siku hio mume wake aliacha kumpenda na mapenzi yake yote yalihamia kwa mrembo Raheli kutoka Babati.
Ataliwa week ijayo viwili ila kwa mbiiiinde sana