Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Mkuu Singano jr wewe jamaa unajua sana hizi habari hasa character ya Roma Ramoni nimekutana nazo kwenye historia ya miungu ya Kigiriki. Ushahidi huo hapo chini [emoji2][emoji122][emoji122][emoji122]

Titans walikuwa ni miungu mikubwa ya kizamani ya kigiriki ambayo enzi hizi waliamini wao ndo miungu pekee ya kuitawala hii dunia na waligawana maeneo mbalimbali ya dunia ili warahisishe katika utawala wao ,sasa ilitokeaga vita ya wenyewe kwa wenyewe ambapo mungu mkuu wa titans ambaye ndo alizaaa watoto wengi akiwemo zeus poseidon ,aedes ,athena na wengine wengi alishambuliwa vikali na watoto zake ambao walitaka kumpindua ili wajitawale wenyewe kwa wenyewe na walifanikiwa kumpindua baba yao ambapo zeus alikuwa mstari wa mbele kwa hyo akapewa cheo cha mungu na wengine wakapewa vyeo vya miungu ya bahari,uzuri ,vita,njaa,anga na mengine mengi ,,ila zeus ni mungu mkuu wa vyote hivi na mwenye kutoa mamlaka kwa wote hao wadogo zake ambao aliwapa vyeo hivyo

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Singano jr wewe jamaa unajua sana hizi habari hasa character ya Roma Ramoni nimekutana nazo kwenye historia ya miungu ya Kigiriki. Ushahidi huo hapo chini [emoji2][emoji122][emoji122][emoji122]

Titans walikuwa ni miungu mikubwa ya kizamani ya kigiriki ambayo enzi hizi waliamini wao ndo miungu pekee ya kuitawala hii dunia na waligawana maeneo mbalimbali ya dunia ili warahisishe katika utawala wao ,sasa ilitokeaga vita ya wenyewe kwa wenyewe ambapo mungu mkuu wa titans ambaye ndo alizaaa watoto wengi akiwemo zeus poseidon ,aedes ,athena na wengine wengi alishambuliwa vikali na watoto zake ambao walitaka kumpindua ili wajitawale wenyewe kwa wenyewe na walifanikiwa kumpindua baba yao ambapo zeus alikuwa mstari wa mbele kwa hyo akapewa cheo cha mungu na wengine wakapewa vyeo vya miungu ya bahari,uzuri ,vita,njaa,anga na mengine mengi ,,ila zeus ni mungu mkuu wa vyote hivi na mwenye kutoa mamlaka kwa wote hao wadogo zake ambao aliwapa vyeo hivyo

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
Umetisha sana , Asante kwa kuongezea nyama nyama ni sahihi kabisa
 
SEHEMU YA 218.

Haikueleweka Roma alikuwa wapi muda wote wa mchana ila muda wa usiku alikuwa ndani ya Upepo Beach Garden akijipatia Sea Food kutoka kwa mgahawa wa Mzee Chino , kwa jinsi alivyokuwa akifurahia msosi ni kama hakuna kilichotokea mchana.

Wakati akiendelea kufurahia na msosi wake , alijikuta akifumbwa macho na mikono milaini ya mtoto wa kike na kujikuta akiweka kijiko chini.

“Bebi Neema usiniambie Mzee Chino kakuambia nipo hapa”Aliongea Roma na mrembo yule akamuachia na ni kweli alikuwa ni Neema Luwazo , Naibu Waziri wa Sanaa na utamaduni.

“Sikutarajia kama nitakukuta hapa?”Aliongea Neema huku akiweka mkoba wake pembeni na kukaa kwenye kiti cha mbele yake Roma.

“Nikajua yule mzee ndio kakuambia nipo hapa”

“Hapana .. ila kwa nilivyokumisi nilitamani kukukipigia simu muda wowote, sikuwa sawa kimawazo tokea nimetoka bungeni”Aliongea Neema kwa sauti chini na kumfanya amwangalie mrembo huyu , licha ya kuonekana mtu mzima , ila alikuwa anaita na kuvutia balaa.

“Nadhani leo tunahitajiana kufarijiana , nimefika hapa kwasababu sikuwa kwenye mudi nzuri”

“Mh!, nilitegemea utakuwa kwenye mudi nzuri kutokana na Kwenda na mkeo Ufaransa”Aliongea Neema na kumkumbusha Roma kuhusu Edna , alikumbuka tokea siku wanarudi hawakuongea Zaidi ya Edna kujifanyisha kuwa bize na kumkwepa muda wote.

“Bebi Neema unakumbuka mara ya mwisho hatukumaliza , leo nadhani ni siku iliopangwa maana wote hatupo kwenye mudi”Aliongea Roma huku akimkonyeza Waziri na mwanamke huyu alijikuta akicheka kicheko cha kwikwi na haikueleweka alifurahishwa na nini.

Ila ndani ya nusu saa mbele walikuwa ndani ya hoteli ya Mapple huku Neema akiwa amekodolea bahari ya Hindi huku Roma akiwa nyuma yake akicheza Boringo na kwa upande wa Neema network zilikuwa zikija na kukata.

“Hehe… hii staili ya kuiangalia bahari inafurahisha,unaonaje”

“Roma… Arggh .. miguu”

“Imefanyaje tena”.

“Inakosa..aa nguvu” Aliongea Neema Luwazo kwa kulalamika na Roma alimbeba juu juu na Kwenda kumtupia kitandani na kilichoendelea ni Neema kuyaita maji MMA”

Muda wa asubuhi saa mbili ndio Roma alifika Kigamboni kwa kutumia V8 mpyaa , yenye namba za serikali, na Roma alikuwa akiendeshwa na Dereva wa Neema Luwazo na Roma hakutaka kuingia nayo ndani na ndio maana baada ya kufika getini ilisimama na yeye akashuka.

Edna alionekana bado hakwenda kazini kwani gari yake anayoipenda kuitumia ilikuwepo , ila Roma hakujali sana alipiga hatua na Kwenda ndani na Sebule ilionekana kupoa sana, kwani hata Bi Wema hakuonekana kabisa sebuleni kama Alivyozoea , lakini Roma aliamini atakuwa amepumzika.

Roma aliingia kwenye chumba chake na kisha alivua nguo na kubadilisha zingine, alikuwa na mpango wa Kwenda kazini muda huo na ndio maana aliwahi kurudi.

Lakini baada tu ya kumaliza kuvaa koti, mlango wake ulifunguliwa bila hodi na ile anainua macho yake Edna alionekana kwenye mavazi ya kawaida kama mtu asiekuwa na mpango wa Kwenda kazini alionekana akimsogelea Roma kwa kasi na kumkumbatia Roma.

Jana yake usiku tokea Roma aondoke Edna hakulala kabisa , alikesha mpaka saa saba usiku akimsubiria Rona mpaka pale alipopotelea usingizini akiwa kwenye sofa na Bi Wema ndio aliekuja kumuamsha na kumwambia akalale chumbani.

Roma alishangazwa na kupokewa na kumbatio lililoambatana na kilio, Roma alijiambia siku zote Edna atakuwa mbabe tu mbele za watu akiwa kwenye biashara zake lakini alikuwa mdhaifu sana likija swala la mahusiano , alipewa mchunio wa siku mbili zote lakini leo hii anakumbatiwa na kilio juu.

“Wife una machozi ya karibu mno.. ndio mana unazidi kuwa M’cute”Aliongea Roma akiwangalie Edna akiwa ameshika mabegani kwa mikono miwili na Edna aliona aibu na kuangalia chini.

“Ulikuwa wapi nilikuwa na wasiwasi , na umeamua nini?”Aliuliza Edna maswali mawili kwa mpigo na Roma ilibidi amkalishe Edna kwenye kitanda kwanza.

“Nianze kukujibu swali lipi?”

“Ni jibu swali la pili?”

“Unamaanisha kuhusu yule Kikongwe asie na akili aliekuja kubwabwaja jana, nimeamua kumpotezea”Aliongea Roma kwa sauti ya kawaida , lakini kwa Edna lilionekana jibu la kuumiza , aliamini Roma anaficha kile anachojisikia moyoni kwa kuamua kupotezea.

“Roma najua unajisikia vibaya kwa muda huu na hujui cha kufanya na ndio maana unaamua kupotezea , sijui nini kilichotokea lakini katika mazungumzo yote nimezingatia sana maneno ya mwisho ya Afande Kweka”Aliongea Edna..

“Yapi hayo?”

“Kuhusu mama yako , amesema anateseka na aliteseka sana kwa ajili yako , Roma unajua nilichojisikia siku nilivyosikika baba yangu ambaye nilijua ni mzazi wangu wa damu siku nilivyopokea kifo chake..”

“Ile siku nilijutia sana kutokwenda kumtembelea na kumuona hata mara moja , licha ya kwamba hakuwahi kunipenda kwenye Maisha yangu yote , lakini iliniuma baada ya kuambiwa kafariki kabla sijamuoa kwa mara ya mwisho”

“Ninachomaanisha ni kwamba wanandoa wanaweza kupeana talaka , marafiki wanaweza wakageukana na kuwa maadui lakini upendo wa mama kwa mtoto siku zote ni wa kudumu na hakuna kitu ambacho kinaweza kumtenganisha mtoto na familia yake .. nakushauri umfikirie mama yako kwa muda huu , najua unaumia na mimi pia najisikia vibaya kwa ajili yako, Usilipotezee hili swala kama vile haujaufahamu ukweli”Aliongea Edna na maneno yalionekana kumwingina Roma vizuri na hata hivyo moja ya misheni yake ilikuwa ni kurudi Tanzania kutafuta familia yake na kuwauliza kwanini walimtelekeza na akajikuta kwenye mikono ya watu waliomtesa.

Roma aliona maneno ya Edna yana ukweli ndani yake , licha mpaka muda huo hakujua ni nini kilichotokea , lakini kama mama yake anateseka kama alivyosema Mzee Kweka aliona anasababu ya kuchukua hatua.

“Una akili sana mke wangu.. kesho nitaenda kumleta Mama Mkwe wako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kutabasamu.

Upande mwingine ndani ya familia ya Mzee Atanasi , Jestina alikuwa na furaha isiokuwa ya kawaida mara baada ya kusikia taarifa ya Mzee Kweka kumtembelea Roma.

Kile kilio chake alichokuwa nacho cha kumsaidia dada yake aliamini kinakwenda kujibiwa , hakuweza kujua ni kwa namna gani Blandina dada yake atakuwa na mshangao baada ya kumuona Roma.

*******

Blandina tokea siku aweke msimamo wake juu ya kutotaka kuvaa sura ya bandia tena , swala hili lilifanya kuwe na ugomvi mkubwa sana na mume wake Kamau Kamau.

Mwanamke huyu licha ya kwamba ni siku kadhaa tu tokea atoke Tanzania , lakini pia kujua kuwa mwanae Denis yupo hai , alionekana kukokanda ghafla , haikueleweka kinachomkondesha ni kitendo cha kamau kutomruhusu Kwenda kuonana na mwanae au kuna sababu nyingine.

Wakati Maina akiwa amejilaza chumbani kwake , chini ya ulinzi mkali wa walinzi wa ikulu , mlango wa chumbani kwake ulifunguliwa na akaingia Kamau Kamai raisi wa Kenya.

Kamau alimwangalie mke wake aliekuwa akikodolea picha zilizokuwa kwenye mikono yake na Kamau jambo lile lilimkasirisha sana na aliingia kwa pupa na kumpokonya zile picha na kisha akazichana chana na kumfanya Blandina kuanza kulia.

“Kamau kwanini lakini … nakuliza kwanini umechana picha za Denis , unajua ni kiasi gani nimemkumbika mwana…”

“Paaah!”

Kamau alikasirika maradufu kila mara alipokuwa akisikia jina la Denisi , yaani kwa jinsi alivyomuona Maina haikuwa na tofauti na miaka ishirini na tano iliopita , Blandina amerudi kuwa Blandina yule yule anaempenda mtoto wake kuliko kitu kingine na hakujali tena nafasi yake kama mke wa raisi.

Blandina licha ya kupigwa kibao , wala hakujali alimwangalia Kamau huku machozi yakimtiririka na kuchuchumaa chini na kuanza kukusanya vipande vipande vya picha za utotoni alizokuwa amepatiwa na Linda , msaidizi wa karibu wa Raisi Jeremy.

“Maina utakuwa hivi mpaka lini mke wangu?”

“Mimi sio Maina , niache Kamau…”Aliongea Blandina na kusimama na kusogela kitandani na kuanza kupanga upya picha za Denisi , kwa jinsi alivyokuwa akionekana ni kama akili zimruka kidogo , hakuonekana kama yule mama ambaye anasaidia Watoto Yatima tena.

Kamau kwa jinsi alivyomuona Mke wake aliona kabisa hawezi kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida na alipaswa kukubali ukweli kwamba muda huo Blandina alichokuwa akikiwaza kwenye kichwa chake ni Denisi tu.

Alikaa takribani dakika kumi na tano akiangalia kile ambacho Maina anakifanya na ilimchukua dakika kama tano tu hivi kwa Maina kuweza kuunganisha vipande vyote vya picha vilivyokuwa vimechanwa na Mheshimiwa Kamau na Maina alitabasamu baada ya zoezi lake kufanikiwa.

Noo.. Siwezi kukubaliana na mpango wa Mwambai , Hades kitu gani bwana akija Kenya namuua”Aliwaza Raisi Kamau na kisha alisogea mpaka kitandani na kisha akampokonya Blandina picha zile na kutoka nazo na kumuacha mwanamke huyo akitoa ukulele wa kilio ndani ya chumba, ila hakujali , na walinzi waliokuwa nje ya chumba cha Blandina First Lady waliishia kushikwa na huzuni.

“Ni mimi…”Alionekana Kamau akiongea na simu.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka ufanye mpango, kuna mwanamke analetwa hapo kambini , nataka ulinzi juu yake uimarishwe kwa masaa ishirini na nne na yoyote ataketaka kuongea nae , lazima ruhusa itoke kwangu”

“Sawa mheshimiwa , lakini tunaweza kumfahamu huyo mwanamke?”

“Hilo sio juu yako , ninachotaka ni ulinzi kwake , maswali mengi sitaki”Aliongea Mheshimiwa na kukata simu na kurudi alikotoka.

“Njiro nifuate”Aliongea Kamau na Njiro mlinzi wa First Lady alimfuatisha Kamau mpaka kwenye ofisi yake.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka mfanye utaratibu na mke wangu atapelekwa Kambi ya Moi Airbase kwa ajili ya usalama wake”Aliongea Mheshimiwa Kamau na kumfanya Njiro kushangaa.

“Kwanini mhesh..”

“Fanya utaratibu wa mke wangu kuepelekwa huko , na jambo hilo liwe siri , hakuna mtu anaeruhusiwa kumjua Blandina ndio Maina , nafikiri unajua ninchomaanisha, unaweza Kwenda”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro

“Nishaongea na mkuu wa Kambi hivyo kazi yenu ni kumfikisha tu , hakikisha unampa maelezo ya kupewa huduma nzuri”

“Sawa mheshimiwa”Aliongea Njiro na kutoka kwa ajili ya Blandina kupelekwa kambi ya Moi.

ITAEND3LEA

HAYA NIMEWAPUNGUZIA LIPENI 2000 MKUKE WATSAPP TUENDELEE TUPO 278 NICHEKI 0687151346.WATSAPP ONLY
Barikiwa mkuu
 
Haichoshi kuisoma kule kwa Bwan Denis anaamshwa huku kwa Edna Denis/Roma yupo kwenye harakati zake
 
Roma keshapoteza jiwe. Je ataendelea kuwa na uwezo wake?
 
SEHEMU YA 219

Ni siku ya asubuhi , siku nyingine baada ya Roma kumuahidi Edna kwamba ataelekea Kenya kwa ajili ya kumchukua mama yake , Asubuhi hii Roma alikuwa ashamaliza kujiandaa na ilikuwa ni saa mbili kamili akishuka kutoka juu kuelekea Sebuleni kwa ajili ya kuaga ili aondoke.

Jumla ya wanafamilia wote walikuwepo , Edna Sophia Bi Wema na Yezi walikuwepo wote mezani wakijiandaa kupata ‘Breakfast’ , Roma ilibidi aungane nao kabla ya kuanza safari yake.

“Anko ndio ushajiandaa kwa safari?”Aliuliza Yezi na kumfanya Roma amwangalie na kutabasamu na kisha alitingisha kichwa kuashiria ndio.

“Mr Roma nimefurahi sana hatimae umeweza kuifahamu familia yako, nadhani unapaswa kuwapa taarifa walezi wako”Aliongea Bi wema na kumfanya Roma akumbuke kuwa alishatoa uongo wa kulelewa Marekani na aijikuta akiangaliana na Sophia na kisha akamgeukia na Edna , lakini Edna alionekana kuwa bize na anachofanya.

“Bi wema nitawajulisha naamini watafurahi pia”Aliongea Roma huku akitabasamu.

“Kunywa chai tuwahi , nishakata tiketi”Aliongea Edna.

“ Sister na wewe unaenda?”Aliuliza Sophia.

“Ndio nitamsindikiza Roma….”

“Miss umefanya maamuzi ya busara”Aliongea Bi wema huku akitabasamu , lakini kwa upande wa Roma alishangaa , kwani mke wake hakuwa amempa taarifa kama alikuwa akimsindikiza kuelekea Kenya.

“Wife unaonekana una hamu ya kumuona mama mkwe wako kuliko hata mimi”.

“Sisi wote ni wanafamilia , tukikuacha ukienda mwenyewe ni kama tunakutenga”Aliongea Edna.

Ukweli Edna hakutaka kumuacha Roma aende mwenyewe , alijua tabia ya Roma , hivyo aliona akienda mwenyewe anaweza akajiingiza kwenye matatizo ndio maana akaona ni heri Kwenda nae ili akamchunge.

………….

Kutoka Tanzania mpaka Kenya ni lisaa moja kamili , ukijumlisha na muda wa kupaa na kutua ni takribani kama lisaa limoja na nusu, Saa nne kamili Roma na Edna walikuwa ndani ya jiji la Nairobi wakitoka nje kabisa ya uwanja wa Jomo Kenyata, Edna alikuwa amevalia suti ya rangi nyeusi na suruali pamoja na viatu vya High Heels rangi ya Zambarau, licha ya kuonekana kiofisi Zaidi lakini hakuacha kuonekana mrembo kutokana na mavazi yake na yalimfanya kuonekana mwanamke mwenye kujiamini sana.

Kwa upande wa Roma alikuwa amevaa koti la suti tisheti rangi nyeupe na suruali ya jeans rangi nyeusi na viatu vya Ngozi , licha ya kuoenekana kavaa Simple lakini mwili wake uliojengeka kimazoezi hakuacha kujionyesha kutokana na kutofunga koti la suti.

“Tunaelekea wapi?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma ajikune kichwa, Roma alikuwa amekuja Kenya ila hakuwa na mpango wowote , yeye alikuwa akifikiria Kwenda kumtoa mama yake ndani ya ikulu ya Kenya pekee , kama alivyoambiwa na Mzee Kweka na alikuwa ashajiambia kama atapata ukinzani wowote basi hatosita kubomboa ikulu yote.

“Mr Roma ..!!!”Ilisikika sauti ya mwanaume alievalia kombati za jeshi akiwa mbele yao , ndani ya eneo hili la uwanja wa ndege kabla hawajazifikia Taksi, na mwanaume huyu hakuwa amekuja peke yake , alikuwa na Escort ya magari mawili ya jeshi na gari moja aina ya V8.

Roma alimwangalia mwaname aliekuwa mbele yake , licha ya kuwa katika mavazi ya jeshi , lakini hakuwahi kumuona.

“General Wambai Rai’ ndio jina lililosomeka kwenye kombati yake ya jeshi ambayo imechafuka kwa kuwa na vyeo vingi.

“Naitwa Jenerali Wambai Rai ,Mkuu wa Majeshi”Alijitambulisha mwanaume huyu na kumfanya Edna ashangae , hakuelewa kwanini mkuu wa Majeshi alikuwa akimfahamu Roma.

“Habari General Wambai , limekuwa jambo zuri sana kwa kukutana na wewe”Aliongea Roma na Generali alitabasamu huku akionekana kumkagua Roma juu hadi chini , ni kama hakuwa akiamini mtu aliekuwa mbele yake ni Hades.

“Miss Edna karibu sana Kenya”

“Asante General”

“Nadhani wote mnamaswali mengi juu ya ujio wangu hapa uwanja wa ndege , mnaonaje tukienda kuongelea kwenye gari , maana ujio wangu hapa ni kwa ajili ya kuwapokea”Roma alitabasamu baada ya kugundua kuwa mkuu wa majeshi amekuja hadi hapo kwa ajili ya kumpokea , aliona ni jambo jema kwani dakika chache nyuma alikuwa akiumiza kichwa namna ya kuonana na mama yake.

“Edna alimwangalia Roma , ni kama alikuwa akisubiri aanze kutembea ndio afuatie na Roma alimwangalia na kutabasamu na kisha akaanza kupiga hatua kuelekea upande wa pili magari yalipokuwa yamesimama.

Wanajeshi waliokuwa wamemleta Generali Wambai walionekana kumwangalia Roma kwa mshangao, ni kama walikuwa na maswali mengi , ila Roma na Edna hawakujali macho ya wanajeshi hao.

“Mr Roma nimepata taarifa za ujio wako hapa Kenya kutoka kwa Afande Kweka , kanipa maagizo nikusaidie na kuhakikisha hakuna mikwaruzano kati ya taifa letu na wewe”Aliongea

“Unaonekana kuwa na uhusiano mzuri na yule mzee?”

“Haha.. Afande kweka ni mwalimu wangu , wakati nilipokuwa jeshini na mambo mengi nimejifunza kutoka kwake , hivyo nampa heshima yake”Aliongea

“Okey Afande nadhani mpaka sasa unajua nipo hapa Kenya kwa ajili ya kuonana na mama yangu , hivyo nadhani ili tusipoteze muda , unaonaje tukielekea Ikulu moja kwa moja maana na uwepo wako itakuwa rahisi na sisi kuingia”Aliongea Roma na Afande Wambai alitabasamu.

“Mr Roma kama nilivyosema nipo hapa kwa ajili ya kuhakikisha ujiio wako ndani ya Kenya hauleti mtafaruku baina ya Tanzania na Kenya na safari hii ni ya moja kwa moja kuelekea sehemu ambayo mama yako yupo”

“Unamaanisha sio Ikulu tena?”

“Ndio M r Roma Blandina hayupo Ikulu ila yupo kambi ya Jeshi la Anga Moi”aliongea huku gari ikizidi kusonga mbele ndani ya barabara ya OutRing .

Upande mwingine wakati Roma na Edna wakielekea Moi upande wa mheshimiwa Kamau na yeye alikuwa kwenye msafara akielekea upande wa Moi Airbase na hii yote ni baada ya kupata taarifa kutoka kwa wafanyakazi wake kuhusu ujio wa Roma nchini Kenya , alikuwa ametoa amri ya vikosi vya jeshi kuchukua hatua kali kama Roma atafosi kumchukua Blandina , lakini oda hio ilionekana kutopokelewa na wanajeshi kutokana na kupewa oda nyingine kutoka kwa mkuu wa jeshi Mwambai Rai.

Sasa mheshimiwa Kamau baada ya kuona wanajeshi hawa wanashindwa kutii amri yake , aliona afanye safari ya kuelekea Moi Aibase kwa ajili ya kumchukua Blandina na kumrudisha Ikulu.

Moi Airbase , licha ya kuwa kambi lakini pia ni sehemu yenye uwanja mkubwa wa ndege ambao unatumika kwa ajili ya kuruka na kutua kwa ndege za kivita na zile za jeshi.

Ndani ya uwanja huu , ilionekana ndege kubwa ya Jeshi ikiwa imesimama huku ikiwa tayari kwa ajili yakupaa na hii yote ni kutokana na Rubani tayari alikuwa kwenye ndege na alikuwa akisubiria amri tu ya kuipaisha.

Nje ya ndege hii alionekana Blandina aliekuwa amesimama na wanajeshi waliokuwa wakimpa ulinzi , alikuwa kwenye mavazi yake ya jana aliotoka nayo Ikulu na alionekana kuwa na shauku kubwa mno kwani macho yake yote yalikua upande wa lango la kuingilia ndani ya uwanja huu wa Ndege.

Dakika kama nne tu hivi ving`ora vya msururu wa pikipiki za wanausalama na magari vilisikika vikikaribia ndani ya eneo hili la uwanja wa ndege, Blandina baada ya kusikia milio hiyo moyo wake ulikosa amani kabisa na hata ile shauku aliokuwa nayo ilimpotea Ghafla , alikuwa ashajua nini maana ya vongora hivyo.

Na ni kweli ndani ya dakika kadhaa tu gari za Mheshimiwa Raisi Kamau Kamau ziliingia ndani ya eneo hili uwanja wa ndege na baada tu ya kusimama Mheshimiwa Kamau alifunguliwa mlango na kutoka kwenye gari na kumsogelea Blandina ambaye alikuwa akimwangalia kwa wasiwasi huku machozi yakianza kujitegeneza kwenye mboni za macho yake.

Wanajeshi waliokuwepo hapa wote walipiga saluti baada ya mkuu wa nchi kufika huku nyuso zao zikijawa na wasiwasi pia.

“Maina mke wangu , nimekuja kwa ajili ya kukurejesha Ikulu , nisamehe sana mke wangu , najua unapitia kipindi kgumu ila tunaweza kuongea na haya yote yakaisha”Aliongea Kamau baada ya kumkaribia Blandina ambaye baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Senga machozi yalianza kufunika macho yake mfululizo.

Muda huohuo kabla ya Blandina hajaongea neno , gari nyingine aina ya Mercedenz Benz iliingia uwanjani hapo na kumfanya Kamau ageuke na kuangalia gari hio na dakika chache tu baada ya gari hio kusimama alitoka mzee mmoja mkongwe sana alieshikiliwa kwenye gari na walinzi waliovalia suti na Mheshimiwa Kamau baada tu ya kumuona mtu huyo macho alijikuta akishangaa na kukosa utulivu.

Wakati mzee yule akiendelea kusindikzwa kwa kushikiliwa kuwasogela Kamau na Blandina gari ya Afande Wambai na yenyewe iliingia ndani ya uwanja huo ikitanguliwa na gari ya wanajeshi na baada ya gari hio kusimama , wa kwanza kutoka alikuwa ni Edna na wa pili alikuwa ni Roma na akafuatia Afande Wambai.

Blandina macho yake yote yalikuwa kwenye gari hio na baada ya kumuona Edna Pamoja na Roma alijikuta akishangaa huku machozi yakianza kumbubujika kwa kasi.



SEHEMU YA 220

Roma kadri alivyokuwa akisogea karibu ndivyo akili yake ilivyoanza kukumbuka sura ya mwanamke aliekuwa mbele yake , licha ya kwmaba kumbukumbu zilikuwa zikija nusunusu.

Moja ya kumbukumbu ambazo zilikuwa zikipita kwenye kichwa chake ni kipindi akiwa mtoto kabisa wa miaka sita , akiwa amevalishwa gauni la Hospitalini huku akiwa amekalishwa kwenye chumba ambacho kilikuwa hakina madirisha Zaidi ya kamera na mwanga wa taa hafifu na mbele yake alionekana mwanaume wa Kizungu alievalia suti huku akimpatia picha.

“Ajent 13 unaitambua hio picha?”Aliuliza mwanaume huyo wa kizungu aliekuwa mbele yake kwa lugha ya Kingereza na Ajenti 13 aliangalia picha hio ya mwanamke wa kiafrika aliekuwa kwenye pozi a kutabasamu na kadri alivyokuwa akivuta kumbukumbu kumfahamu mtu aliekuwa kwenye picha hakuwa akimfahamu hata kidogo na aliishia kutingisha kichwa kuwa hamfahamu na mwanaume yule alichukua picha zile na kuziweka kwenye faili alilokuwa nalo.

“Vizuri sana Ajent 13 kwa leo tutaishia hapa”Aliongea mwanaume yule na kisha akanyanyuka na kuchuua vitu vyake na kuondoka.

Ssa hizi ni kumbukumbu ambazo Roma alikuwa akizipata baada ya kumwangalia mwanamke aliekuwa amesimama mbele yake na alihisi maumivu makali ya kichwa , mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa akifanana kwa kila kitu na picha alizoonyeshwa akiwa kwenye utoto wake , lakini si hivyo tu picha ya aina hio aliiona tena alivyokuwa ndani ya kituo cha kulelea Watoto cha Son And Daughter Orphanage.

“Deniss…!!!!”Aliita Blandina huku akimsogelea Roma kwa wasiwasi kwa nanmna ya kujikokota ni kama haamini mtu aliekuwa mbele yake alikuwa Denisi, wiki kadhaa nyuma alishaonana na mwanaume aliekuwa mbele yake lakini hakuweza kumtambua kama mtoto wake , licha ya kwamba kuna hisia ambazo hazikuwa za kawaida alizipata kwa mara ya kwanza baada ya kukutana na Roma kwenye kituo cha kuelela Yatima lakini hakuweza kumtambua kama mtoto wake.

Siku ambayo anapata kupewa picha za utoto wa Denisi na Linda hisia zake juu ya Roma kuwa mtoto wake wa damu ziliongezeka maradufu, kuna Roho mbili zilikuwa zikimwambia Roma alikuwa mtoto wake na kuna Roho nyingine ilikuwa ikimwambia Roma sio Denisi lakini ambayo ilikuwa na nguvu ilikuwa ni ya Roma kutokuwa Denisi ilikuwa na nguvu kubwa.

Blandina alijiambia siku kadhaa nyuma kwamba kama Roma angekuwa ni Denisi basi angeweza kumtambua siku ileile kama ni mtoto wake hivyo hata wazo la Roma kufanana na Denisi alilipotezea , lakini muda huu sasa mawazo yake anagundua hayakuwa sawa hata kidogo na Roma ambaye hakumdhania kuwa Denisi ndio yeye mtoto wake.

“Denisi…!!!!”Aliita kwa mara ya pili Blandina huku akimsogelea Roma.

Lakini kwa upande wa Roma alishindwa kutembea Zaidi ya kusimama huku akimwangalia Blandina , lakini kama ilivyokuwa kwa watu waliokuwa hapo ndani wakiwaangalia ,kwa upande wa Roma ni kama macho yake hayakua hapo bali yalikuwa sehemu nyingine kabisa , ni kama alikuwa akikumbuka sauti hio ikimwita lakini hakuweza kufahamu ni muda gani na mwaka gani sauti hio ilikuwa ikimwita.

Mawazo yake hayakuwa uwanjani hapo kwa muda huo , lakini yalikuwa kwenye tafakari nyingine kabisa na hata Blandina alivyomfikia hakuelewa kabisa , Edna aliona mabadiliko ya Roma lakini alishindwa kuongea neno , aliishia kutokwa na machozi na kushindwa hata kujielewa kwanini na yeye alikuwa akilia ilihali swala lililokuwa mbele yake halikuwa likimuhusu.

“Denisi..mwanguuu….hiii..hii….nisamehe…”Blandina alishindwa kujiuzuia na alianza kulia kwa kwikwi na kumkumbatia Roma ambae alikuwa amesimama kama gogo.

“Kamau unapaswa kumwachia sasa Blanidna kurejeaTanzania, kilichotokea hapa ni maagizo ya wazee , tumekaa na tukafikiria na kufanya maamuzi”Aliongea Mzee ambae aliingia hapo ndani ya uwanja, na aliongea kinyonge lakini kwa msisitizo.

“Lakini mze…”

“Nishamaliza kuongea Kamau unapaswa kumwachia Maina kuondoka Kenya taratibu zote za kiusalama juu ya swala hili zishachukuliwa… hatutaki makosa mengine wewe na Blandina mnaliweka taifa hili kwenye hatari ya kiusalama, kama sisi tumeamua kuppotezea hili swala na kuchukua hatua unapaswa kufanya hivyohivyo”AliongeaMzee Gichuru na baada ya kumaliza kuongea aliwapa ishara wasaidizi wake kumrudisha mpaka kwenye gari kwa ajili ya kuondoka.

Mheshimiwa Kamau licha ya kwamba anamheshimu Mzee Gichuru kutokana na mchango wake katika safari yake ya kisiasa , lakini moyo wake haukuwa tayari kwa ajili ya kumuachia Blandina.

“Mr Roma mnapaswa kuondoka”Aliongea Afande Mwambai baada ya kumsogelea Blandina Edna na Roma waliokuwa wamesimama wakifarijiana na kauli hio ni kama ilimshtua Roma aliekuwa kwenye mawazo.

“Roma Asante sana mwanngu kwa kuja kuniona mimi mama yako , hatimae naweza kufa hata sasa kwa amani, sikutegemea kukuona ukiwa hai tena”Aliongea Blandina kwa furaha huku akifuta machozi yake na kumfanyaRoma amwangalie mwanamke anaejulikana kama mama yake aliekuwa akitoa machozi , haikueleweka Roma anahisiaa gani kwa wakati huo.

“Hupaswi kuendelea kulia Zaidi , tumekuja kukuchukua mimi na mke wangu na tutarudi Tanzania ila kama unataka kuendelea kubaki nchini Kenya sitokuzuia maamuzi ni yako”Aliongea Roma pasipo kubadili muonekano wake.

“Edna..!... asante sana mwanangu, umekuwa baraka kila iitwapo leo.. asante sana kwa kuja na Denisi nitaondoka na nyie , siwezi kubaki hapa”Aliongea Blandina huku akifuta machozi na kumshika Edna mikono na kulazimisha tabasamu la uchungu.

“Mama hupaswi tena kutoa machozi , unapaswa kufurahi umeonana na mtoto wako kwa mara nyingine , sisi wote tunafuraha juu ya jambo hili kwako na kwa Roma”Aliongea Edna.

Ukweli Edna mpaka hatua hio hakuelewa hisia zake kabisa , alikuwa na mambo mengi ya kuyafahamu kuhusu Roma mpaka ikatokea wakatengana na wazazi wake , licha ya kusikia maelezo nusu kutoka kwa Afande Kweka lakini bado hakuna alichoelewa kabisa na alitamani kupata maelezo mengine.

“Mr Roma hii ndio ndege maalumu ilioandaliwakwa ajili ya kuwarudisha Tanzania”Aliongea Afande Wambai , alionekana kuwa na wasiwasi mno na alitaka waondoke ili yeye amalizane na mheshimiwa Raisi kwa kukiuka agizo lake.Roma na yeye hakuona haja ya kubakia hapo uwanja wa ndege.

“Afande Wambai asante sana kwa maandalizi haya”Aliongea Roma na kisha alimpa ishara Edna waondoke.

Muda wote ni kama mheshimiwa Kamau haamini kile alichokuwa akiangalia muda huo ,kwanza Roma ambaye alikuwa na faili lake lililokuwa linampamba kwa sifa kibao alimuona wa kawaida sana na alishangaa kwanini watu wanamuogopa.

“Blandina ukisogea hatua nyingine tu ninamfumua ubongo mtoto wako”aliongea Mheshimiwa Kamau na haikueleweka alitoa bastora muda gani , ila alionekana kumlenga Roma Ramoni.

“Mheshimiwa naomba upunguze jazba , hili lishapita”Aliongea Afande Wabai huku akimpa ishara Afande Kamau kuacha anachotoka kufanya.

“Nyamaza wambai wewe ni mnafiki , nimetoa maagizo kama mkuu wa majeshi yote lakini ukaamua kunigeuka, nikitoka hapa ninaanza na wewe”

“Mr Roma narudia tena hatua nyingine mbele nawafumua”Aliongea Raisi Kamau .

“Kamau naomba uweke siraha chini tafadhari.. acha kuwa kama mnyama”

“Mnyama… Blandina unaniita mimi mumeo mnyama?”

“Unafikiri wewe ni nani , nimeishi miaka mingi kwa kuvumilia maumivu ya kuishi na sura ya mtu mwingine hii yote kwa ajili ya kukufurahisha nimejitoa kwa ajili yako kwa miaka yote , ni jambo gani ambalo umenifanyia Kamau mpaka kutaka kunizuia kutokuwa na mwanangu ambaye nilidhania kashakufa .. kwanini unatunyooshea Bastora , kama kweli unahisi utapata amani basi nipige risasi nife kwani sitokuwa na majuto tena kwani nishamuona mtoto wangu”Kamau alisikia vyema maneno ya Blandina na kwa hasira alizokuwa zilimpelekea mpaka kutetemeka mikono.

“Blandina hakuna kitu ambacho nilifanya kwa ajili yangu peke yangu , kila kitu ilikuwa ni kwa ajili yako na yangu , kwanini kwa Zaidi ya miaka yote ambayo tumeoana unaona haina umuhimu Zaidi ya mtoto ambaye kujamuona miaka na miaka, kwanini huthamini juhudi zangu na unataka kuniharibia wakati kama huu..”Aliongea Kamau kwa hasira , uzuri tu ni kwamba wanajeshi karibia wote walikuwa washapewa ishara ya kurudi nyuma mita kadhaa kwa ajili ya kutosikiliza kile kinachoendelea.

“Mheshimiwa kwenye Maisha yangu sitoruhusu mwanamke wangu au mama yangu kupigwa risasi kwa ajili yangu , kama umedhamiria basi inabidi ufanye haraka”Aliongea Roma huku akimrudisha Blandina nyuma.

“Roma…umeniita mama .. umenikubali kama mama yako?”Aliongea Blandina , mwanamke huyu alioenekana kuwa na hatia juu ya mtoto wake Roma.

Kila akikumbuka namna alivyokubali kumtanguliza Denisi kwenye ndege na yeye kubaki nyuma kwa ajili ya kufanya dhambi na Kamau alihisi Roma lazima amchukie juu ya swala hilo.

Roma wala hakumjali Blanidna aliekuwa akiongea , Zaidi ya kumuonea huruma kwani kwa muonekano wake alionekana hajakula chochote kwa muda mrefu na alijiambia huenda ilikuwa jambo zuri kwa kuja Kenya mapema kwani huenda angepatwa na shida kubwa Zaidi.

“Unaonekana hujala muda mrefu , inabidi tuondoke ili ukaoge , upate chakula na kisha upumzike , mke wangu ni Tajiri na nyumbani kuna msosi wa kutosha na isitoshe pia tunae Bi Wema mpishi mzuri , Edna mshikilie mtangulie mbele” Aliongea Roma.

“Okey Sawa , Kwanzia leo mimi mama yako nitakuwa ni mwenye kukusikiliza”Aliongea Blandina huku akijisikia vizuri kwa mara ya kwanza tokea siku alioamini Denisi mtoto wake kafariki.

“Nishasema hamruhusiwi kusogea , sitanii nimeshika bunduki na ninawezakuachia risasi muda wowote”

“Mheshimiwa mimi nimesimama hapa , wewe ndio umeshikilia siraha maamuzi ni yako ya kuachia risasi au lah”Aliongea Roma pasipo ya kuwa na wasiwasi na kwa upande wa Mheshimiwa Kamau hasira zilizidi kuongezeka maradufu.

“Paa.!!!”Ni mlio wa risasi uliotoka katika bunduki alioshikilia mheshimiwa Kamau.
 
SEHEMU YA 221

Blandina na Edna wote kwa Pamoja waligeuka kwa wasiwasi na kuita jina la Roma kwani walihisi Roma atakuwa amepigwa na Risasi , lakini baada ya kuangalia vizuri kwa ukaribu Roma alikuwa sawa tena alikuwa akitabasamu , jambo hili halikuwashangaza wao pekee lakini hata kwa Jenarali Wambai alishangaa mno.

Risasi iliotoka kwenye bunduki ya mheshimiwa Kamau iliishia miguuni kwa Roma na haikumgusa hata kidogo na hili jambo lilimfanya hata mheshimiwa Kamau kushangaa mno na kuanza kuamini mambo alioyasoma kwenye faili.

“Hapana .. ngoja ni jaribu tena”Aliwaza Mheshimiwa Kamau na palepale akavuta tena Triga kuelekea sehemu aliosiimama Roma , lakini kila Risasi ilivyokuwa ikimfikia Roma , ilionekana kukosa nguvu na kudondoka chini , ni kama ilikuwa ikigonga kwenye chuma.

Kila mnoja alishangazwa na jambo hilo kwa Edna alikuwa na afadhari kwani ni mengi mpaka wakati huo ashayashuhudia , lakini kwa upande wa Blandina alionekana kuwa katika mshangao na kujiuliza swala hilo linawezekana vipi kwani aliona ni kama Muvi za kihindi.

“Kwa mahesabu yangu naamini riasasi zishaisha, huwa sipendi s kutishiwa amani lakini pia kunyooshewa bunduki lakini hili nitaacha lipite kwasababu naamini umeishi na mama yangu kwa muda mrefu , lakini kwa tukio la leo deni langu mimi na wewe limeisha na ikitokea siku nyingine ukitumia siraha juu yangu basi sitojali mamlaka yako”Aliongea Roma kwa msisitizo.

“Mheshimiwa tunapasw akuondoka sasa , wazee wanakusubiri Ikulu”Aliongea Mkuu wa majeshi Wambai na Kamau kwa hasira alitupa siraha chini na kisha akamwangalia Blandina kwa macho ya huzuni na kugeuka na kurudi alikoacha gari iliomleta.

Naam dakika kumi na tano mbele ndege ya jeshi ilipaa angani kuwachukua Roma kuelekea Tanzania.

…………………

Ilikuwa ni siku ya pili yake baada ya Mama yake Roma kuungana na familia ya Edna , nyumba ilionekana kujaa sasa kiasi kwamba hata vyumba vya kulala vilikuwa vishaisha na hii ilimfanya Bi Wema kulala na Blandina.

Jana yake baada ya Blandina kufikishwa nyumbani , furaha ilitawala na ilikuwa ni kama sherehe , kwani Jestina alifika Kigamboni baada ya kupata taarifa za Dada yake kurudi Tanzania.

Na kutokana na wawili hao walivyokuwa wamekumbukana kwa muda mrefu , stori nyingi zilianza , ile hali ya upweke aliokuwa nayo Blandina ilikuwa imepotea na alionekana kurudi kwenye hali yake ya kawaida , alikuwa ashampata mtoto wake na pia ameweza kurudi kwenye taifa lake na kuungana na familia yake , hivyo alijihisi kuwa mpya na kuwa na furaha ambayo hakuwahi kuwa nayo tokea alipompoteza Denisi ambaye ni Roma.

“Miss nadhani ni muda sahihi wa kuhamia Osterbay , nyumba ya kule ni kubwa kuliko hii , lakini pia itamuwezesha Yezi kukaa karibu na chuo”Aliongea Bi Wema asubuhi hio , wakati wanafamilia wote wakiwa mezani wakipata kifungua kinywa, Edna alifikiria kidogo baada ya pendekezo hilo na aliona ni kweli nyumba ya Osterbay ilikuwa kubwa mno kuliko hii Kigamboni.

Upande wa Roma wala hakujali maongezi hayo , yeye muda wote alikuwa bize akijipatia chai nzito bila ya kuwa na wasiwasi na Blandina hata yeye hakuwa hata akisikiliza maongezi ya Bi Wema , ila macho yake yote yalikuwa ka Roma , alikuwa akijiuliza maswali mengi juu ya Roma na mpaka muda huo hakujua ilikuwaje Roma akarudi akiwa hai , kiufupi hakuwa akifahamu nini kilitokea na alitamani kujua , lakini hata pale ambapo alipomuuliza Roma kwa ajili ya kumuelezea yaliotokea , Roma alimjibu atamuelezea siku moja , hivyo ilimfanya blandika kubakia kuwa na shauku peke yake , lakini hata hivyo alijikuta moyo wake ukiwa wa moto baada ya kumuona mtoto wake kwa ukaribu akifurahia chakula , wanasema mtoto kwa mama hakui na ndio ilivyokuwa kwa Blandina , licha ya Roma kuw amtu mzima lakini Blandina bado alimuona kama mtoto..

“Bi wema , nadhani ni pendekezo zuri lakini kwakua ni katikati ya wiki inabidi tufanye utaratibu wa kuhama Wikiend”Aliongea Edna na Sophia na Yezi walitingisha kichwa kukubali.

Wakati wakiendelea kunywa chai , mara wote walinyamaza mara baada ya taarifa ya Habari ya asubuhi kutangaza taarifa iliowasitua.

“Mke wa raisi Kamau Kamau na Firsr lady wa taifa wa Kenya , Maina Kamau Kamau , ameripotiwa kufariki usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya taifa la Kenya , Taarifa za awali zinaeleza kuwa kutokuonekana kwake hadharani kwa takribani wiki tatu ilikuwa ni kwa ajili ya maradhi aliokuwa nayo ya muda mrefu.. tunaendelea kuwasiliana na msemaji wa serikali ya Kenya kwa ajili ya taarifa Zaidi”

Ni habari ambayo ilimfanya Blandina kuweka kikombe chini na kisha akageuza macho yake na kumwangalia Roma , lakini kwa upande wa Roma ni kama hajasikia taarifa hio kwani aliunganisha vipande vya mkate vitatu na kisha kuvikunja na kuvitumbukiza vyote mdomoni na akachikua na kikombe cha maziwa na kushushia.

Bi wema aliekuwa amekaa karibu na Blandina ilinidi amshike mkono na kumfariji.



*********

Upande mwingine muda huo huo wa asubuhi, mheshimiwa Senga alionekana akiwa kwenye meza akijipatia kifungua kinywa Pamoja na mke wake , huku akiwa tayari ashajiandaa kwa ajili ye kuelekea ofisini,

“Senga unampango gani?”Aliuliza Damasi mke wa Raisi Senga.

“Unamaanisha nini mke wangu?”

“Kuhusu Roma mtoto wako , nimepata taarifa jana , Blandina karudi Tanzania baada ya kufuatwa na Roma”Aliongea Damasi.

“Ninazo hizo taarifa pia , lakini ni swala ambalo mke wangu hupaswi kulifikiria kwasasa”

“Unamaanisha nini Senga , Roma ni mtoto wako wa kwanza umtambue ama usimtambue itabakia kuwa hivyo , nataka kujua msimamo wako katika hili”Aliongea Damasi na Raisi Senga ilibidi aweke uma chini na kumwangalia mke wake kwa sekunde.

“Nishamueleza baba msimamo wangu tayari na hauwezi kubadilika, Roma hawezu kuwa mtoto wangu na sitomtambua yeye na Mama yake washakufa na ajali ya ndege na hawa waliojitokeza ni feki”Aliongea Senga huku akiendela kula na kumfanya Damasi avute pumzi na kumwangalia mume wake.

“Lakini baba yako anaonekana kuwa na mipango mingi juu ya Roma , sitaki swala hili lilete migogoro kwenye familia , unaweza ukaliona swala hili kuwa dogo ila mimi ninawasiwasi Senga , unapaswa kulifanyia kazi”

“Mama Ashley umepatwa na nini usiku wa leo… mbona asubuhi yote hii unamuwaza Roma tu..”

“Sina amani kabisa kwenye moyo wangu , nahisi kuna jambo baya linakuja kutokea kati ya Denisi na Roma nimeota ndoto mbaya kweli usikuwa wa jana”

“Huo ni wasiwasi tu mke wangu ndio maana unakupelekea kupata ndoto za aina hio , hupaswi kuwaza sana , kuhusu Denisi nitahakikisha namsapoti kisiasa kwa uwezo wangu wote hilo lisikusumbue , familia yetu kwa sasa yule mzee akifa hakutakuwa na mwingine wa kuiongoza familia Zaidi yangu” Aliongea lakini kwa Damasi ni kama hakuwa akimuelewa kabisa mume wake , moyo wake ulionekana kutotulia kabisa.

“Uliniahidi utamfuatilia Denisi lakini mpaka leo sioni dalili na sidhani kama ulifanya kama ulivyoahidi…”Aliongea na kumfanya Senga afikirie kidogo.

Lakini kabla hata hajajibu simu yake ilianza kuita mfululizo na aliitoa kwenye mfuko wa suti na kuangalia jina la mpigaji na alitabasamu na kumwangalia mke wake na kumpa ishara kwamba mtu ambaye amempa kazi ndio huyo anapiga.

“Lidun Habari za huko China?”

“Salama kabisa mheshimiwa, Habari za Tanzania?”

“Huku kwema , nadhani umenipigia kwa ajili ya kazi niliokupatia”

“Ndio mheshimiwa nimeweza kumfuatilia kwa ukaribu mtoto wako Denisi Senga na ni kweli yupo hapa China”Sauti upande wa pili ilisikika mpaka kwa Damasi kwani mheshimiwa alikuwa ameweka Loudspeaker.

“Kuna taarifa nyingine ya Zaidi ya kuwa China?”

“Hakuna taarifa Zaidi mheshimiwa licha ya wiki mbili zote kutokuonekana Kambini ila mambo mengine anaonekana yupo sawa na jana yake vijana wangu wameweza kumuona akiwa na ukaribu Zaidi na Yan Buwen”.

“Hebu kwanza .. umesema kambini sijakuelewa vizuri,,,”

“Namaanisha hakuhudhuria kambini kwa muda wa wiki mbili jambo ambalo sio kawaida yake tokea ajiunge na kikosi cha mafunzo maalumu ya ukomando”

“UKOMANDOO..!!!”Raisi Senga na mke wake Damasi walijikuta wakItamka neno hilo kwa wakati mmoja , kila mmoja alishangazwa.



SEHEMU YA 222

Mheshimiwa Raisi Senga hakuwa na taarifa juu ya mtoto wake Denisi kuwa mwanajeshi na sio kwake tu hata kwa mke wake Damasi hajawahi kupata taarifa wala kufahamu Denisi kama atakuwa ni mwanajeshi na swala hilo liliwashangaza mno na walishangaa Zaidi kusikia Denisi anachukua mafunzo ya Ukomandoo nchini China , kwao ilikuwa ni Habari mpya kabisa ya kushitusha mno tofauti na vile walivyokuwa wakifahamu..

“Lidun naomba taarifa kamili ya Denis , sijawahi kupewa taarifa ya Denisi kuwa mwanajeshi , unanichanganya kusema yupo China kwa ajili ya mafunzo ya Ukomandoo?”

“Mheshimiwa na mimi nipo kwenye mshangao kama hufahamu swala hili”

“Sifahamu lolote juu ya hili na ndio maana nataka taarifa kamili unitumie baada ya masaa mawili”

“Sawa mheshimiwa nakutumia taarifa yake baada ya masaa mawili”Aliongea Lidun upande wapili na kisha Mheshimiwa Senga akakata simu na kumwangalia mke wake ambaye alikuwa kwenye mshituko wa aina yake.

“Dama…!!!”Kabla hata ya mheshimiwa hajamaliza kuongea mke wake alinyanyuka kwa hasira na kukimbilia ndani chumbani na mheshimiwa alijikuta jasho likimtoka , aliona kutokufahamu yote hayo ni kutokan ana kutokuifatilia kwa ukaribu familia yake ndio maana.

Siku zote amekuwa ni mtu wa kuhangaika na yale ambayo yalikuwa yakiendelea ndani ya Taifa la Tanzania tu, na likija swala la Watoto wake yeye aliishia kuwapa pesa za kutosha ya kufanya kile watakacho , lakini kuhusu kuwafuatilia kwa ukaribu hakuwa akifahanya hivyo.

Mheshimiwa Senga hata hamu ya kuendelea kupata kifungua kinywa ilikuwa ishaisha na alinyanyuka na kuelekea ofisini kwa ajili ya kuendelea na majukumu yake.

“Kabwe kuna lipi jipya?”aliuliza mheshimiwa Raisi mara baada ya kuingia kwenye ofisi yake.

Na huo ndio uliokuwa utaratibu wake , kila atakapofika ofisini swala la kwanza ni kupata taarifa fupi kutoka kwa Kabwe kijana ambaye alikuwa akimwaminia kwa uwezo wake wa akili ambaye alimfanya msaidizi wake aliekuwa akimwamini kwa asilimia kubwa mpaka kumpatia ukuu wa kitengo cha usalama ndani ya Ikulu.

“Mheshimiwa kuna habari kutoka Kenya….”

“Inasemaje?”

“Mke wa raisi wa Kenya Maina Kamau ameripotiwa kufariki usiku wa jana”Aliongea Kabwe na kumfanya Raisi Senga kutabasamu kifedhuli , alijua zote hizo ni janja ya Kamau kufukia swala la Blandina.

“Utampa maelekezo Msemaji wa ikulu pamoja na Meneja wa mitandao ya kijamii wa Ikulu kutoa salamu za Rambirambi”Aliongea Mheshimiwa

“Sawa mheshimiwa”

“Nieleze hilo swala lingine kama lina umuhimu …”

“Mheshimiwa ni juu ya Profesa Shelukindo?”

“Kuna nini juu ya hilo tena?”

“Jana kitendo cha mawasiliano cha Ikulu kimepokea taarifa kutoka kwa mtu ambaye hajajitambulisha jina na ametuma faili linalohusian ana kifo cha Profesa Shelukindo”Aliongea Kabwe na kumfanya Mheshimiwa amwangalie kwa shauku.

“Liko wapi hilo faili?”

“Lipo tayari kwenye mfumo wa ofisi wa Tarakishi yako mheshimiwa”aliongea Kabwe na kumfanya mheshimiwa awashe tarakishi yake kwa haraka haraka na ndani ya dakika chache alifika mpaka kwenye mafaili yaliongia kwenye mfumo wake wa kiutendaji wa kieletronics na kuanza kukagua baadhi ya mafaili na hatimae aliweza kupata faili la PDF na kulifungua.

“Yan Buwen!!”Ndio jina la kwanza ambalo aliweza kuliona kwenye Skrini , lakini pia picha mbalimbali za mtu huyo anaefahaika kwa jina la Yan Buwen zikionekana kwenye tarakishi , kuna ambazo Yan Buwen alionekana akiwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia , lakini pia kuna nyingine ambazo zilionekana Viongozi wengi wa kitaifa wakiwa Pamoja na Raisi Mstaafu Kigombla , moja ya viongozi hao alikuwemo mkuu wa Majeshi , Afande Tozo.

Mheshimiwa alijikuta akipandwa na hasira na wasiwasi juu.

“Kabwe hii linadhihirisha kabisa kwamba kitengo chetu cha ujasusi hapa ikulu hakifanyi kazi yake kwa ufasaha , inakuwaje taarifa muhimu kama hizi leo ndio nazipata tena kutoka kwa mtu ambaye hajulikani?”Aliongea mheshimiwa kwa hasira

“Mheshimiwa…!!!”

“Kabwe najua utaanza kujitetea , nishachoshwa na namna unavyoendesha mambo hapa Ikulu , nimekupatia uongozi wa kitengo hiki kutokana na uwezo wako , Stupid kabisa”Aliongea huku macho yakiwa mekundu.

“Nataka taarifa za huyu Yan Buwen ndani ya dakika chache na pili nataka mfuatilie ni nani katuma hizi taarifa hapa Ikulu na ana malengo gani, tatu hii taarifa inaelezea Yan Buwen ndio kahusika na kifo cha Profesa Shelukindo… nataka munaze uchunguzi upya wa kujua undani wa maelezo haya”.

Mheshimiwa Raisi Senga aliona kichwa chake kilikuwa kikitaka kumpasuka , aliona mambo mengi ni kama vile hayaendi , alikuwa na maumivu moyoni ya kusalitiwa na marafiki zake wa karibu , lakini pia mwanamke anaempenda lakini kabla hilo halijaisha linakuja jambo juu ya mtoto wake Denis kuwa mwanajesh, hilo nalo halijaanza kuisha linaingia swala lingine la viongozi wake anaowaamini kuanza kuonyesha ishara za kumsaliti kama mkuu wa nchi aliona mambo yalikuwa mengi sana ambayo yalikuwa yakimuhitaji yeye peke yake.

Wakati akiendelea kufikiria mlango wake uligongwa na Chief Of Staff na alimruhusu kuingia.

“Kuna nini?”

“Mheshimiwa kuona omb la wito kutoka kwa mheshimiwaMstaafu Kigombola”

“Anasemaje?”

“Anaomba kuonana na wewe kwa ajili ya mazungumzo”Aliongea Chief of Staff na kumfanya mheshimiwa kufikiria kidogo.

“Huyu mzee ningekuwa na uwezo wa kumuua ningemmaliza mara moja”Aliwaza mheshimiwa huku akingata meno yake kwa hasira.

Ni kweli licha ya kwamba Mheshimiwa Kigombola kutoka madarakani lakini hakuwa amepumzika na zaidi ni kwamba alikuwa akiendelea na kazi zake za uongozi nje ya ikulu , alikuwa na koneksheni nyingi kuanzia ikulu mpaka kwenye wizara zote jambo ambalo linamfanya Mheshimiwa Senga kuwa mnyonge katika uongozi wake , kwani kila ambacho kinaendelea ikulu ni kama kilikuwa kikimfikia moja kwa moja Mheshimiwa Kigombola na jambo lingine ni kwamba haijawahi kutokea hata siku moja kwa mheshimiwa Kigombola kuonyesha heshima ya kumuacha Senga kufanya kazi zake kama mkuu wan chi pasipo ya kumuingilia..

“Andaa taratibu za kumualika kuja ikulu kama anayo maongezi na mimi”Aliongea Mheshimiwa Kigombola na Chief Of Staff alitoka kwenye ofisi yake baada ya kutii maagizo

Mheshimiwa Kigombola baada ya kuona mlango wake umefungwa , alitoa simu yake na kupiga mahali.

“Habari za saa hizi Askofu Inuka?”

“Salama Mheshimiwa Habari za saa hizi na za majukumu?”

“Habari sio nzuri sana Askofu , mambo yamenifika shingoni kwa sasa hapa Ikulu na nahitaji nguvu za ziada”Aliongea mheshimiwa Senga na sauti ya mwanaume upande wa pili ilitulia kwa dakika kadhaa.

“Ninaweza kuhisi unayopitia mheshimiwa na mimi niko upande wako”

“Nashukuru kusikia hivyo Askofu , Nadhani ni muda muafaka sasa kwa lile swala ulilonishauri”

“Unamaanisha upo tayari mheshimiwa?”

“Kwa jinsi mambo yalivyonifikia nipo tayari Askofu kwa lolote , nipo tayari kuonana nae”

“Mheshimiwa umefanya maamuzi ya busara sana, wiki mbili zijazo natarajia Kwenda kuongeza nguvu ya upako na kuhudhuria ibada ya mpasuko wa mwezi, nadhani kabla ya siku hio nitaweka Appointment , na nitakapoanza safari inabidi twende Pamoja”

“Niko tayari Askofu Inuka juu ya hilo andaa tararibu”

“Sawa mheshimiwa nikutakie majukumu mema”

Baada ya maongezi hayo simu muda uleule ilikatwa na mheshimiwa akaiweka chini na kuvuta pumzi.

“Hapana mpaka hapa nilipofikia siwezi kuendelea kwa kutumia nguvu zangu mwenyewe , nahitaji nguvu za ziada kupambana na maadui zangu, Its Time to Shake Hand with Devil to gain power”.Aliwaza mheshimiwa , haikueleweka ni mtu gani anaenda kukutana nae kwa kutumia Koneksheni na Askofu Inuka , lakini mheshimiwa Senga alionekana kufanya maamuzi ya kukutanishwa na mtu huyo asiefahamika katika siku ya ibada ya Mpasuko wa Mwezi.

Wakari mheshimiwa akiwa kwenye mawazo simu yake ilitoa mlio na aliinua haraka na kuangaliajina la mpigaji na kuona ni Liduni.

“Mheshimiwa nimepata tayari taarifa zote zinazohusiana na Denis , na faili lake nimekutumia kwa njia ya Email”

Mheshimiwa alikata simu na kufungua barua pepe kuangalia taarifa ambayo ametumiwa na Liduni , taarifa ambazo ilikuwa ikimuhusu Denisi mtoto wake, dakika moja tu aliweza kufungua kiambatanisho kilichokuwa kimetumwa kwa njia ya barua pepe , lililkuwa ni faili ambalo lipo kwa mfumo wa Portable Document File.

Mheshimiwa Kadri alivyokuwa akisoma alijikuta akiishiwa na nguvu kabisa alijikuta akishangaa na hasra kumpanda maradufu.

“Huu wote ni mpango wa Baba Tena , huyu mzee sijui mpaka sasa ana siri ngapi ambazo bado anaendelea kuficha nina wasiwasi kabisa, na pia hili swala la yeye kutozeeka haraka nina wasiwasi nalo kwa asilimia kubwa”Aliwaza Mheshimiwa Senga kwa hasira huku akiangalia picha mbali mbali za Denisi akiwa mafunzoni jeshini
 
SEHEMU YA 223.

Naam ndani ya kampuni ya Edna mambo yalikuwa yakienda kama kawaida na Sasa Edna kidogo alikuwa amepunguza majukumu yake kwa kuyapunguza rasmi kwa CEO msaidizi Marko Ernest Komwe.

Edna alifanya hivyo kwa ajili ya kujikita zadi katika kazi zake nyingine ambazo zilikuwa zinahusiana na kujipanua Zaidi kibiashara huku akiacha maswala ya ndani ya kampuni yakiendeshwa na Ernest , lakini pia alitaka kuendelea kufanyia kazi swala ambalo alilipata kulifahamu kutoka kwa mheshimiwa Senga na hili ni swala ambalo lipo kwenye Flash aliopewa siku za nyuma na raisi , swala ambalo lilikuwa likihusiana na kisasi ambacho alikuwa nacho mama yake , kisasi ambacho hakikuweza kukamilika kutokana na kwamba mama yake alifariki mapema kabla ya jambo hilo kutimia.

Kwahio majukumu ya Edna ni kuhakikisha kisasi hiko kinatimia kwa namna yoyote ile na ili kufanikisha hilo aliamini alikuwa akihitaji muda wa kutosha kwa ajili ya kusuka mipango yake , alikuwa akiamini kuwa ana maadui wengi ambao wanamuangalia kwa kila hatua anayopitia , lakini swala hilo hakuwa tayari kulifanya lipunguze ile ari aliokuwa nayo juu ya utimilifu wa mpango wake.

Asubuhi ya leo mrembo huyu alikuwa ameketi kwenye kiti chake akiwaza hili na lile , ukweli alijiona kwamba siku kadhaa za nyuma kulikuwa na mambo mengi ambayo yamemfanya kutofikiria Maisha yake kwa ujumla na uelekeo ambao anauchukua ,lakini pia sura mpya ya biashara zake ambazo anakwenda kuanzisha.

Katika kichwa cha Edna mawazo yalikuwa mengi kwanza kabisa alikuwa akiwaza juu ya baba yake mzazi wa damu , alikuwa akiliwazia hili swala tokea siku ambayo alipata kujua kuwa Mzee Adebayo sio baba yake wa damu na alikuwa akijitahidi kujisahaulisha , lakini kadri alivykuwa akijitahidi hakuweza kusahau , alikuwa akimfahamu mama yake mzazi nje ndani , licha ya kwamba hawakuishi sana wakiwa Pamoja kutokana na mama yake kuwa bize na maswala ya kampuni lakini vilevile kwa upande wake kuwa bize na masomo mpaka pale mama yake kifo kumkuta Ghafla , lakini kwa machache ambayo alikuwa akifahamu kutoka kwa mama yake , aliamini baba yake huwenda akawa ni mtu ambaye yupo karibu yake kuliko ambavyo anafikiria kwani alimjua mama yake sio mtu wa kuokoteza okoteza wanaume , ni mwanamke ambaye alikuwa na sheria zake.

Mtu aliekuwa akijiita The Protector ni swala ambalo pia alikuwa akilifikiria katika kichwa chake , kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kabisa mtu huyo ni baba yake , lakini alijitahidi kupotezea hisia hizo , lakini licha ya hivyo hakushindwa kufikiria juu ya mtu huyo lakini pia juu ya baba yake mzazi.

Edna na Roma sasa ni takribani miezi mitatu Kwenda minne tokea wafunge ndoa yao ya mkataba na ni mambo mengi ambayo yametokea katikati yao, na mengi yalikuwa ya kuogofya sana , lakini licha ya hivyo wazo la kuachana na Roma baada ya miezi sita kuisha aliona ni gumu kutekelezeka , aliamini kama ataendelea na mpango wa kutimiliza kisasi ambacho bado hakujua kinahusiana na nini aliamini katika mchakato huo kutakuwa na maadui wakubwa ambao watajiinua zidi yake , hivyo anahitaji ulinzi na mtu pekee ambaye anapaswa kumlinda kwa hali na mali ni Roma peke yake.

Katika kufikia sehemu ya mawazo hayo mrembo huyu alijikuta akianza kukumbuka Maisha yake na Roma kuanzia mwanzo mpaka walipofikia , alihesabu meizi walioishi Pamoja , alikumbuka matukio yote kwanzia ya Tanzania mpaka yaliotokea Paris na alijikuta mwili wake ukisisimka.

“Roma kwasasa ashakuwa sehemu ya Maisha yangu , na sijui kama tunaweza kuachana hata baada ya miezi sita ya mkataba wetu kuisha , Mama yake anaonekana pia kunipenda na anaamini mimi ni mume halali wa mtoto wake, nadhani inanipaswa kumkubali sasa Roma kama mume wangu kihalali licha nina wasiwasi na wanawake wake aliokuwa nao, Lakini safari ya mapambano ambayo nimeanzisha inanihitaji kuwa nae kwa kila hatua kwa ajili yakufanikiwa lakini…..”Alijikuta akiishia kuwaza.

“Lakini siwezi kukubali aendelee kuwa na wanawake wengine , ilihali mimi ndio mke wake kihalali , kama nitampokea kama mume kamili jambo la kwanza ni kuhakikisha anaachana na wake zake na kuniangalia mimi tu”Alifikiria Edna , lakini licha ya kuwaza hivyo alionekana kukosa namna ya kulikamilisha jambo hilo.

Upande wa ofisi ya PR , Roma alionekana leo kuhudhuria kazini kama kawaida na alikuwa akicheza gemu kama ilivyokuwa kawaida yake , madhumuni ambayo alikuwa nayo kwa kuja kazini ni kutokana kutaka kuwaaga wafanyakazi wenzake kwasababu muda si mrefu angetakiwa kufanya kazi katika kampuni ambayo imefunguliwa na mke wake.

Wafanyakazi wenzake akiwemo Recho walionekana kuwa bize na kazi kama ilivyokuwa kawaida.

“Kamani leo mnaonaje tukikutana usiku kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo na kuwa Director wa kampuni mpya?”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma asubirishe gemu lake na kugeuka.

“Naunga mkono hoja”Ilisikika sauti ya Nasra ikiingia ndani ya idara hii na wote wakamwangalia na haikueleweka Nasra alikuwa hapo kufanya nini , lakini alionekana kupendeza , alimwangalia Roma na kutabasamu baada ya kumuona.

“Nani anapinga juu ya hili?”Aliuliza Benadetha na wafanyakazi wote walionekana kukubaliana na jambo hilo na aliebakia Roma kukubaliana na wengine.

“Roma kusanyiko ni kwa ajili yako , kama hukubaliani na sisi tutaghairisha”

“Nakubali gharama zitakuwa juu yangu, chagueni hoteli.”Aliongea Roma na kufanya wote wapige makofi.

“Kilimanjaro hoteli napendekeza”Aliongea Recho haraka haraka na kufanya wote waangaliane kwa pendekezo alilotoa Recho.

“Tina unasemaje , ushawahi kufika Kilimanjaro Hotel?”Aliuliza Recho kwa namna ya kumkeheli Tina.

“Sijawahi kufika .. umefurahi?”Aliongea Tina huku akivuta mdomo lakini Recho alionekana kutojali.

“Roma unasemaje , wewe ndio unakwenda kulipia?”Aliongea Benadetha akimwangalia Roma.

“Limepita kama wote mnataka twende Kilimanjaro Hoteli mimi sina tatizo”Aliongea Roma na kufanya Recho kushangilia.

“Muone wote tunajua hapa unataka ukapige picha tu za kuoshea mtandaoni”Aliongea Tina kwa kumshushua.

“Kama ninaenda kupiga picha wewe inakuuma nini fyuu.. unaongea kama hutopiga hizo picha”Aliongea Recho na kufanya hata Roma acheke kwa utani uliokuwepo kati ya Tina na Recho

……………….

Ni muda wa saa moja kamili , Roma alionekana kujiandaa tayari kwa ajili ya kuelekea sehemu ambayo alikuwa amekubaliana na wenzake kwa ajili ya Kwenda kuhudhuria kusanyiko kwa ajili ya kupongezwa kwa kupandishwa cheo.

Roma alishuka mpaka chini sebuleni kwa ajili ya kutondoka , Blandina mama yake Roma usiku huo hakuwepo kwani alikuwa ameshinda nyumbani kwa baba yake na alitegemewa kulala huko huko mpaka siku inayofuata.

“Wife natoka”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna aliekuwa ameketi kwenye masofa na Yezi na Sophia wakipiga Stori.

“Kama unaenda kwenye kusanyiko na wafanyakazi wa Idara ya PR na mimi naenda”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.

“Wife unauhakika unataka Kwenda?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Ninaenda nisubiri , labda kama hutaki nikihudhuria”Aliongea Edna huku akianza kupiga hatua kuelekea juu kujiandaa akimuacha Roma akiwa amesimama huku akimshangaa Edna, kusanyiko lilikuwa ni la wafanyakazi wa Idara ya Public Relation, hivyo asingetegemea Edna kuhudhuria kusanyiko kama hilo , lakini swala la pili ni kwamba kama ataenda na Edna inamaanisha uhusiano wao utakuwa wazi kwa wafanyakazi wenzake ndio maana Roma alishangaa.

“Yezi chuo unaanza lini?”aliuliza Roma na kukaa kwenye Sofa akimsubiria Edna.

“ Mwezi wa kumi na moja ndio tunaanza usaili Anko…”

Yezi tokea aje hapo ndani Roma hakuwa amepata nafasi ya kuongea na Yezi kabisa na kumuuliza maswala ya chuo, licha ya kujua mipango hio.

“Umefanya maamuzi mazuri kurudi chuo, inabidi ujitahidi ili baadae uje kufanya kazi , usiwe kama Sophia alieweka vyeti kwenye kabati”Aliongea Roma na kumfanya Sophia amkate Roma jicho na kuendelea kuangalia simu yake.

Ukweli Sophia siku mbili hizi tokea Roma kurudi kutoka Ufaransa alikuwa ametulia sana , hakuwa wa kuongea sana na Roma alishindwa kujua tatizo la Sophia ni nini , ila alishindwa kumuuliza.

Edna alichukua dakika kumi na tano tu kujiandaa na kumfanya Roma afurahi kwani haikuwa mategemeo yake kwa Edna kutumia muda mfupi kwa ajili ya kujiandaa.

“Wife umevaa kawaida sana , lakini ulivyopendeza kama vile umetumia lisaa kujiremba”Aliongea Roma na kumfanya Roma aone aibu na hii ni kutokana Roma alimsifia mbele ya Sophia na Yezi.

Sophia na Yezi waliishia kuangalia Roma na Edna ambao walikuwa wakitomomea nje ya mlango , walionekana ni wenye kutamani Kwenda na wao kwenye bata la usiku.

******

Ni baada ya nusu saa Edna na Roma walionekana wakiikaribia Hoteli ya Kilimanjaro , sehemu ambayo yeye na wafanyakazi wa idara yake ndio walipanga kwa ajili ya Mkusanyiko wa chakula cha usiku.

Hoteli ya Kilimanjaro ni moja ya Hoteli nzuri za nyota tano ambazo zilikuwa zikitoa huduma ya mikusanyiko midogo na mikubwa, Benadetha ndio alipewa kadi ya benki ya Roma kwa ajili ya kuandaa sehemu maalumu kwa ajili ya mkusanyiko wao huo mdogo ambao wameandaa.

Na muda ambao Roma na Edna wapo njiani Recho , Tina Benadetha na wafanyakazi wengine wawili wa kike walikuwa washafika tayari ndani ya hoteli hio na walikuwa washapata eneo maalumu binafsi ndani ya hoteli hii kwa ajili ya mkusanyiko wao.

Na walionekana wakipiga stori za hapa na pale na kufanya eneo lote kusikika sauti zao , Nasra alievalia gauni zuri la kupendeza aliingia ndani ya chumba hiko kikubwa na alionekana ndio kwanza na yeye alikuwa anafika.

“Jamani jamani siku zote nawaambiaga Nasra Mrembo , hebu muangalieni”Aliongea Recho na kufanya wenzake wote wageuze macho na kumwangalia Nasra ambaye aliona aibu kwa namna ambavyo alikuwa akisifiwa.

“Jamani najua na mimi sijaalikwa ila nimehudhuria…”Ilisikika sauti ya kiume kutoka mlangoni na kuwafanya warembo hawa waliopendeza usiku huu kugeuza macho yao na kumwangalia aneongea na kufanya kundi lote kukosa utulivu.

Alikuwa ni Ernest Komwe CEO msaidizi aliekuwa ametangulizana na Dorisi alikuwa amependeza Haswa na suti yake hata kwa Dorisi pia.

“Kuweni na amani hili ni kusanyiko kama tafrija ndogo , hivyo tusiangaliane kwa vyeo vya kazini tuweni huru , nimekuja kuungana na ninyi ili tupate kuzoeana , si eti Nasra?”Aliongea Ernest na kumfanya Nasra kutabasamu na kutingisha kichwa na Ernest alionekana kujiamini kwani alisogea na kwenda kuketi karibu na Benadetha.

Uzuri ni kwamba meza zilikuwa zimeunganishwa Pamoja na viti vilikuwa vingi kiasi kwamba hata watu ishirni wanaweza kutosha ndani ya hilo eneo.

“Hi Guys!”Ilisikika sauti nyingine kutoka mlangoni na kufanya wote wageuke na kuangalia sauti ya mwanamke mrembo aliekuwa akiingia hapo ndani , mrembo mwenyewe hakuwa mwingine bali alikuwa ni Nadia Alfonso na wote baada ya kumuona walitabasamu, Nasra alikuwa amependeza mno n ani kama amefanya makusudi kuchagua mavazi ambayo yatamfanya kupendeza kuliko wengine wote.

Kusanyiko liliandaliwa na idara ya Public Relation kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo , lakini wafanyakazi kutoka idara nyingine walihudhuria na haikueleweka taarifa wamezipata vipi.

“Msishangae hata mimi pia ni mmoja ya wafanyakazi wa Vexto hivyo naweza kusema kama ni mhusika kwenye hii tafrija ilioandaliwa kimya kimya”Aliongea Nadia , alionekena kuwa kwenye mudi nzuri mno na ni kama hakuna jambo ambalo limemtokea siku chache nyuma nchini Ufaransa.

“Jamani CEO Edna na yeye yupo njiani kuja kwenye kusanyiko hili”Aliongea Dorisi na kufanya kila mtu kushangaa.

“Dorisi unamaanisha CEO anakuja?”Aliuliza Recho kama mtu ambaye hajasikia vizuri.

“Ndio kanitumia ujumbe yupo njiani”Aliongea Dorisi pasipo kujali na kukaa

IJUMAA ASUBUHI MWENDELEZO

0687151346 nicheki watsapo tuendelee
 
SEHEMU YA 223.

Naam ndani ya kampuni ya Edna mambo yalikuwa yakienda kama kawaida na Sasa Edna kidogo alikuwa amepunguza majukumu yake kwa kuyapunguza rasmi kwa CEO msaidizi Marko Ernest Komwe.

Edna alifanya hivyo kwa ajili ya kujikita zadi katika kazi zake nyingine ambazo zilikuwa zinahusiana na kujipanua Zaidi kibiashara huku akiacha maswala ya ndani ya kampuni yakiendeshwa na Ernest , lakini pia alitaka kuendelea kufanyia kazi swala ambalo alilipata kulifahamu kutoka kwa mheshimiwa Senga na hili ni swala ambalo lipo kwenye Flash aliopewa siku za nyuma na raisi , swala ambalo lilikuwa likihusiana na kisasi ambacho alikuwa nacho mama yake , kisasi ambacho hakikuweza kukamilika kutokana na kwamba mama yake alifariki mapema kabla ya jambo hilo kutimia.

Kwahio majukumu ya Edna ni kuhakikisha kisasi hiko kinatimia kwa namna yoyote ile na ili kufanikisha hilo aliamini alikuwa akihitaji muda wa kutosha kwa ajili ya kusuka mipango yake , alikuwa akiamini kuwa ana maadui wengi ambao wanamuangalia kwa kila hatua anayopitia , lakini swala hilo hakuwa tayari kulifanya lipunguze ile ari aliokuwa nayo juu ya utimilifu wa mpango wake.

Asubuhi ya leo mrembo huyu alikuwa ameketi kwenye kiti chake akiwaza hili na lile , ukweli alijiona kwamba siku kadhaa za nyuma kulikuwa na mambo mengi ambayo yamemfanya kutofikiria Maisha yake kwa ujumla na uelekeo ambao anauchukua ,lakini pia sura mpya ya biashara zake ambazo anakwenda kuanzisha.

Katika kichwa cha Edna mawazo yalikuwa mengi kwanza kabisa alikuwa akiwaza juu ya baba yake mzazi wa damu , alikuwa akiliwazia hili swala tokea siku ambayo alipata kujua kuwa Mzee Adebayo sio baba yake wa damu na alikuwa akijitahidi kujisahaulisha , lakini kadri alivykuwa akijitahidi hakuweza kusahau , alikuwa akimfahamu mama yake mzazi nje ndani , licha ya kwamba hawakuishi sana wakiwa Pamoja kutokana na mama yake kuwa bize na maswala ya kampuni lakini vilevile kwa upande wake kuwa bize na masomo mpaka pale mama yake kifo kumkuta Ghafla , lakini kwa machache ambayo alikuwa akifahamu kutoka kwa mama yake , aliamini baba yake huwenda akawa ni mtu ambaye yupo karibu yake kuliko ambavyo anafikiria kwani alimjua mama yake sio mtu wa kuokoteza okoteza wanaume , ni mwanamke ambaye alikuwa na sheria zake.

Mtu aliekuwa akijiita The Protector ni swala ambalo pia alikuwa akilifikiria katika kichwa chake , kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kabisa mtu huyo ni baba yake , lakini alijitahidi kupotezea hisia hizo , lakini licha ya hivyo hakushindwa kufikiria juu ya mtu huyo lakini pia juu ya baba yake mzazi.

Edna na Roma sasa ni takribani miezi mitatu Kwenda minne tokea wafunge ndoa yao ya mkataba na ni mambo mengi ambayo yametokea katikati yao, na mengi yalikuwa ya kuogofya sana , lakini licha ya hivyo wazo la kuachana na Roma baada ya miezi sita kuisha aliona ni gumu kutekelezeka , aliamini kama ataendelea na mpango wa kutimiliza kisasi ambacho bado hakujua kinahusiana na nini aliamini katika mchakato huo kutakuwa na maadui wakubwa ambao watajiinua zidi yake , hivyo anahitaji ulinzi na mtu pekee ambaye anapaswa kumlinda kwa hali na mali ni Roma peke yake.

Katika kufikia sehemu ya mawazo hayo mrembo huyu alijikuta akianza kukumbuka Maisha yake na Roma kuanzia mwanzo mpaka walipofikia , alihesabu meizi walioishi Pamoja , alikumbuka matukio yote kwanzia ya Tanzania mpaka yaliotokea Paris na alijikuta mwili wake ukisisimka.

“Roma kwasasa ashakuwa sehemu ya Maisha yangu , na sijui kama tunaweza kuachana hata baada ya miezi sita ya mkataba wetu kuisha , Mama yake anaonekana pia kunipenda na anaamini mimi ni mume halali wa mtoto wake, nadhani inanipaswa kumkubali sasa Roma kama mume wangu kihalali licha nina wasiwasi na wanawake wake aliokuwa nao, Lakini safari ya mapambano ambayo nimeanzisha inanihitaji kuwa nae kwa kila hatua kwa ajili yakufanikiwa lakini…..”Alijikuta akiishia kuwaza.

“Lakini siwezi kukubali aendelee kuwa na wanawake wengine , ilihali mimi ndio mke wake kihalali , kama nitampokea kama mume kamili jambo la kwanza ni kuhakikisha anaachana na wake zake na kuniangalia mimi tu”Alifikiria Edna , lakini licha ya kuwaza hivyo alionekana kukosa namna ya kulikamilisha jambo hilo.

Upande wa ofisi ya PR , Roma alionekana leo kuhudhuria kazini kama kawaida na alikuwa akicheza gemu kama ilivyokuwa kawaida yake , madhumuni ambayo alikuwa nayo kwa kuja kazini ni kutokana kutaka kuwaaga wafanyakazi wenzake kwasababu muda si mrefu angetakiwa kufanya kazi katika kampuni ambayo imefunguliwa na mke wake.

Wafanyakazi wenzake akiwemo Recho walionekana kuwa bize na kazi kama ilivyokuwa kawaida.

“Kamani leo mnaonaje tukikutana usiku kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo na kuwa Director wa kampuni mpya?”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma asubirishe gemu lake na kugeuka.

“Naunga mkono hoja”Ilisikika sauti ya Nasra ikiingia ndani ya idara hii na wote wakamwangalia na haikueleweka Nasra alikuwa hapo kufanya nini , lakini alionekana kupendeza , alimwangalia Roma na kutabasamu baada ya kumuona.

“Nani anapinga juu ya hili?”Aliuliza Benadetha na wafanyakazi wote walionekana kukubaliana na jambo hilo na aliebakia Roma kukubaliana na wengine.

“Roma kusanyiko ni kwa ajili yako , kama hukubaliani na sisi tutaghairisha”

“Nakubali gharama zitakuwa juu yangu, chagueni hoteli.”Aliongea Roma na kufanya wote wapige makofi.

“Kilimanjaro hoteli napendekeza”Aliongea Recho haraka haraka na kufanya wote waangaliane kwa pendekezo alilotoa Recho.

“Tina unasemaje , ushawahi kufika Kilimanjaro Hotel?”Aliuliza Recho kwa namna ya kumkeheli Tina.

“Sijawahi kufika .. umefurahi?”Aliongea Tina huku akivuta mdomo lakini Recho alionekana kutojali.

“Roma unasemaje , wewe ndio unakwenda kulipia?”Aliongea Benadetha akimwangalia Roma.

“Limepita kama wote mnataka twende Kilimanjaro Hoteli mimi sina tatizo”Aliongea Roma na kufanya Recho kushangilia.

“Muone wote tunajua hapa unataka ukapige picha tu za kuoshea mtandaoni”Aliongea Tina kwa kumshushua.

“Kama ninaenda kupiga picha wewe inakuuma nini fyuu.. unaongea kama hutopiga hizo picha”Aliongea Recho na kufanya hata Roma acheke kwa utani uliokuwepo kati ya Tina na Recho

……………….

Ni muda wa saa moja kamili , Roma alionekana kujiandaa tayari kwa ajili ya kuelekea sehemu ambayo alikuwa amekubaliana na wenzake kwa ajili ya Kwenda kuhudhuria kusanyiko kwa ajili ya kupongezwa kwa kupandishwa cheo.

Roma alishuka mpaka chini sebuleni kwa ajili ya kutondoka , Blandina mama yake Roma usiku huo hakuwepo kwani alikuwa ameshinda nyumbani kwa baba yake na alitegemewa kulala huko huko mpaka siku inayofuata.

“Wife natoka”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna aliekuwa ameketi kwenye masofa na Yezi na Sophia wakipiga Stori.

“Kama unaenda kwenye kusanyiko na wafanyakazi wa Idara ya PR na mimi naenda”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.

“Wife unauhakika unataka Kwenda?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Ninaenda nisubiri , labda kama hutaki nikihudhuria”Aliongea Edna huku akianza kupiga hatua kuelekea juu kujiandaa akimuacha Roma akiwa amesimama huku akimshangaa Edna, kusanyiko lilikuwa ni la wafanyakazi wa Idara ya Public Relation, hivyo asingetegemea Edna kuhudhuria kusanyiko kama hilo , lakini swala la pili ni kwamba kama ataenda na Edna inamaanisha uhusiano wao utakuwa wazi kwa wafanyakazi wenzake ndio maana Roma alishangaa.

“Yezi chuo unaanza lini?”aliuliza Roma na kukaa kwenye Sofa akimsubiria Edna.

“ Mwezi wa kumi na moja ndio tunaanza usaili Anko…”

Yezi tokea aje hapo ndani Roma hakuwa amepata nafasi ya kuongea na Yezi kabisa na kumuuliza maswala ya chuo, licha ya kujua mipango hio.

“Umefanya maamuzi mazuri kurudi chuo, inabidi ujitahidi ili baadae uje kufanya kazi , usiwe kama Sophia alieweka vyeti kwenye kabati”Aliongea Roma na kumfanya Sophia amkate Roma jicho na kuendelea kuangalia simu yake.

Ukweli Sophia siku mbili hizi tokea Roma kurudi kutoka Ufaransa alikuwa ametulia sana , hakuwa wa kuongea sana na Roma alishindwa kujua tatizo la Sophia ni nini , ila alishindwa kumuuliza.

Edna alichukua dakika kumi na tano tu kujiandaa na kumfanya Roma afurahi kwani haikuwa mategemeo yake kwa Edna kutumia muda mfupi kwa ajili ya kujiandaa.

“Wife umevaa kawaida sana , lakini ulivyopendeza kama vile umetumia lisaa kujiremba”Aliongea Roma na kumfanya Roma aone aibu na hii ni kutokana Roma alimsifia mbele ya Sophia na Yezi.

Sophia na Yezi waliishia kuangalia Roma na Edna ambao walikuwa wakitomomea nje ya mlango , walionekana ni wenye kutamani Kwenda na wao kwenye bata la usiku.

******

Ni baada ya nusu saa Edna na Roma walionekana wakiikaribia Hoteli ya Kilimanjaro , sehemu ambayo yeye na wafanyakazi wa idara yake ndio walipanga kwa ajili ya Mkusanyiko wa chakula cha usiku.

Hoteli ya Kilimanjaro ni moja ya Hoteli nzuri za nyota tano ambazo zilikuwa zikitoa huduma ya mikusanyiko midogo na mikubwa, Benadetha ndio alipewa kadi ya benki ya Roma kwa ajili ya kuandaa sehemu maalumu kwa ajili ya mkusanyiko wao huo mdogo ambao wameandaa.

Na muda ambao Roma na Edna wapo njiani Recho , Tina Benadetha na wafanyakazi wengine wawili wa kike walikuwa washafika tayari ndani ya hoteli hio na walikuwa washapata eneo maalumu binafsi ndani ya hoteli hii kwa ajili ya mkusanyiko wao.

Na walionekana wakipiga stori za hapa na pale na kufanya eneo lote kusikika sauti zao , Nasra alievalia gauni zuri la kupendeza aliingia ndani ya chumba hiko kikubwa na alionekana ndio kwanza na yeye alikuwa anafika.

“Jamani jamani siku zote nawaambiaga Nasra Mrembo , hebu muangalieni”Aliongea Recho na kufanya wenzake wote wageuze macho na kumwangalia Nasra ambaye aliona aibu kwa namna ambavyo alikuwa akisifiwa.

“Jamani najua na mimi sijaalikwa ila nimehudhuria…”Ilisikika sauti ya kiume kutoka mlangoni na kuwafanya warembo hawa waliopendeza usiku huu kugeuza macho yao na kumwangalia aneongea na kufanya kundi lote kukosa utulivu.

Alikuwa ni Ernest Komwe CEO msaidizi aliekuwa ametangulizana na Dorisi alikuwa amependeza Haswa na suti yake hata kwa Dorisi pia.

“Kuweni na amani hili ni kusanyiko kama tafrija ndogo , hivyo tusiangaliane kwa vyeo vya kazini tuweni huru , nimekuja kuungana na ninyi ili tupate kuzoeana , si eti Nasra?”Aliongea Ernest na kumfanya Nasra kutabasamu na kutingisha kichwa na Ernest alionekana kujiamini kwani alisogea na kwenda kuketi karibu na Benadetha.

Uzuri ni kwamba meza zilikuwa zimeunganishwa Pamoja na viti vilikuwa vingi kiasi kwamba hata watu ishirni wanaweza kutosha ndani ya hilo eneo.

“Hi Guys!”Ilisikika sauti nyingine kutoka mlangoni na kufanya wote wageuke na kuangalia sauti ya mwanamke mrembo aliekuwa akiingia hapo ndani , mrembo mwenyewe hakuwa mwingine bali alikuwa ni Nadia Alfonso na wote baada ya kumuona walitabasamu, Nasra alikuwa amependeza mno n ani kama amefanya makusudi kuchagua mavazi ambayo yatamfanya kupendeza kuliko wengine wote.

Kusanyiko liliandaliwa na idara ya Public Relation kwa ajili ya kumpongeza Roma kwa kupandishwa cheo , lakini wafanyakazi kutoka idara nyingine walihudhuria na haikueleweka taarifa wamezipata vipi.

“Msishangae hata mimi pia ni mmoja ya wafanyakazi wa Vexto hivyo naweza kusema kama ni mhusika kwenye hii tafrija ilioandaliwa kimya kimya”Aliongea Nadia , alionekena kuwa kwenye mudi nzuri mno na ni kama hakuna jambo ambalo limemtokea siku chache nyuma nchini Ufaransa.

“Jamani CEO Edna na yeye yupo njiani kuja kwenye kusanyiko hili”Aliongea Dorisi na kufanya kila mtu kushangaa.

“Dorisi unamaanisha CEO anakuja?”Aliuliza Recho kama mtu ambaye hajasikia vizuri.

“Ndio kanitumia ujumbe yupo njiani”Aliongea Dorisi pasipo kujali na kukaa

IJUMAA ASUBUHI MWENDELEZO

0687151346 nicheki watsapo tuendelee
Asante sana mtunzi, nimezifurahia sana hizi scene za leo, Mungu abariki kazi ya mikono yako!
 
Back
Top Bottom