Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simpingi Singanojr. Ni mwandishi aliyebobea na pengine simulizi ya kwake imeishinda ya kwangu. Mimi mwenyewe nilianza kusoma simulizi hii ya Roma kitambo sana. KALI!!!Lakini ikizingatiwa utashinda siku nzima, wiki nzima ukiangalia kama ameposti. Niliudhika na huu unyama.Unakuwa addicted na kitu lakini unakatiziwa, hupewi.
Sasa ukaona ulete ya kwako hapa??????????

wewe post tu huko kwingine kadiri itakavyokuwa inasomwa na watu ambao tumewafollow ndo itakapokuwa inatufikia na sisi automatically tutaisoma kama inavutia tunasubscribe kama ni chai tunaignore.

hapa ni Kwa Roma na Edina tu. usije ukarudia tena hata kupost comment yenye maneno meeengi.
 
Simpingi Singanojr. Ni mwandishi aliyebobea na pengine simulizi ya kwake imeishinda ya kwangu. Mimi mwenyewe nilianza kusoma simulizi hii ya Roma kitambo sana. KALI!!!Lakini ikizingatiwa utashinda siku nzima, wiki nzima ukiangalia kama ameposti. Niliudhika na huu unyama.Unakuwa addicted na kitu lakini unakatiziwa, hupewi.
Dogo huku kulilialilia story za watu kama mwanamke alokuwa desparate kwa issue za mumewe haipendezi.

Halafu mbaya zaidi unatuletea stories za watu ambazo tushapita nazo too way back tena bila consent yao.
Kama umekuwa addicted sana na hizi mambo, anza mdomdo kutunga thereafter utaregain na kuwa nguli.
 
SEHEMU YA TAT U.

Siku tatu zilikuwa zimepita pasipo ya Roma kuonana na Najma , jambo ambalo halikumshangaza kwani alikuwa akikumbuka vyema kuwa Najma alimuona mwanamke kahaba alielala nae siku mbili zilizopita , hivyo alijua fika kuwa mrembo huyo atakuwa na hasira kali sana juu yake , kwani alikuwa akijua sana kwamba alikuwa akimpenda , hivyo hata yeye hakutaka kujishugulisha sana juu ya Najma , kwanza aliona ni jambo zuri kwani angejiweka mbali na Najma.

Upande wa Juma pia jambo hilo lilimfurahisha sana , kwani aliamini kwa jambo ambalo Roma amefanya litamfanya dada yake kutomfikiria kabisa Roma na kuendelea na maisha yake huku akimtafutia mpango wa kueoelwa na mwanamke mwenye pesa zake na ili kuhakikisha Najma hafikiriii kabisa kuendelea kumpenda Roma alifanya kila njia kuhakikisha taarifa za Roma kulala na kahaba mpaka asubuhi zinasambaa ndani ya wapangaji pamoja na majirani.

“Mh! Roma kabisa … siku zote nilikuwa namuona kama anamatatizo flani hivi kumbe anaonekana na yeye anapenda wanawake . lakini alishindwa nini kumchuku Najma mwanamke mrembo mpaka kwenda kuchukua mwanamke kahaba mtaani”

“Heheee… huenda Najma kuna kitu anakosa katika mwili wake ambacho hakimvutii Roma” Hao walikuwa ni wapangaji waliokuwa wakiongea kishambenga wakiwa wanasukana , na yote hio ilikuwa ni kumuumiza Najma ambae alikuwa akiingia kutoka kazini , na Najma aliwasikia vizuri tu na kuzidi kumchukia Roma kwa kitendo cha kuleta kahaba kwenye nyumba yao.

Najma alionekana ni mwenye mawazo , mengi mno , lakini licha ya hayo yote ambayo yalikuwa yakiendlea kwa wapangaji , moyo wake ni kama umegawanyika vipande viwili , kwani kuna upande ulikuwa bado ukimpenda sana Roma na hakuwa tayari kumuacha , lakini pia kuna upande ambao ulikuwa ukimchukia sana Roma, Pande zote mbili zilionekana kushindana vikali sana , huku upande unaompenda Roma ukichukua ushindi kila baada ya pambano., baada ya upande huo kushinda kila mara , hamu ya kutaka kumuona Roma ilizidi kujaa katika moyo wake , alikuwa amemkumbuka sana na alipanga usiku wa leo kumuona kwa namna yoyote ile.

Muda nao haukukawia sana kwani ulienda kwa haraka haraka , kwani ile Najma anakuja kushituka kutoka usingizini ilikuwa ni saa kumi na mbili , alinyanyuka haraka haraka na kisha alielekea gengeni kununua mboga za usiku , na siku hio alipanga kupika wali na Choroko , hivyo alinunua choroki na kuzichemsha na kuanza kuandaa chakula cha usiku.

“Noja leo nipike kingi , nitamuwekea Roma wangu katika chumba Chake akirudi ale”Alijiongelesha mwenyewe wakati huo akichambua mchele.

“Vipi mwenzetu mbona leo unaonekana ni mwenye furaha hivyo”Aliuliza mama Debora moja ya wapangaji , huku akimwangalia Najma usoni, Mama Debora ndio mpangaji pekee ambaye hakuwa na umbea mwingi na alikuwa ni Mlokole katika kanisa flani lililokuwa mita chache kutoka nyumbani kwa Najma na pia ndio mpangaji pekee aliekaa kwa muda mrefu mno , kwani yeye pamoja na mume wake walianza kupanga hapo kwao tokea wakianza kuona na mpaka sasa ambapo walikuwa na mtoto mkubwa tuambaye alikuwa chekechea anaefahamika kwa jina la Debora ,Mama Debora hakuwa mtu wa Nyumbani sana kwani alikuwa akifundisha shule ya msingi Ikwiriri , sehemu ambayo ilikuwa mbali na kumfanya kudamka sana asubhi na kurudi jioni , hivyo hakuwa akijua maswala yoyote yaliokuwa yakimuhusu Roma kuingiza kahaba.

“Hakuna jipya mama Debo , ni ile tu leo nimejikuta kuwa ni mwenye furaha”Aliongea Najma na kumfanya Mama Debo atabasamu.

“Hehehe .. acha kunificha Roma kakutamkia anakupenda nini?” Najma aliona aibu kwa sentensi hio na kuzidisha tabasamu .

“Nilijua tu , unaonekana kumpenda sana Roma Najma”

“Hhaha .. ndio”

“Muone sasa anavyoona aibu … nimekuja kuweka umeme mimi”Aliongea Mama Debo huku akimpita Najma na kuingia ndani kwa ajili ya kuweka umeme kwani Luku ilikuwa kwa ndani.

Najma alidumu sebuleni kwao kwa muda mrefu sana huku akiwasubiria kaka yake na Roma kurudi kazini licha ya kwamba alikuwa na usingizi mzito uliokuwa ukimnyemelea , lakini hamu yake ya kutaka kumuna Roma iliushinda usingizi na kuendelea kusubiri , siku hii ya leo si kama siku zingine kwani walichelewa kurudi mno , kwani mpaka inafika saa tano na nusu kaka yake hakuwa amerudi , baada ya kusubiri kwa takribani dakika ishirini hatimae mlango uligongwa na Najma haraka haraka alikwenda kufungua mlango.

“Najma hujalala tu , leo mbona umekua kunifungulia wewe”Aliongea Juma huku akiwa ni mwenye kumshangaa dada yake ,kwani siku mbili za nyuma alionekana sio mwenye kujali kuwafungulia yeye na Roma.Kwa Najma licha ya swali hilo , hakujali kabisa kwani alichokuwa akitaka kuona ni Roma Tu , lakini kilichomshangaza ni kwamba siku hio alimuona kaka yake pekee jambo ambalo lilimshangaza.

“Roma yuko wapi kaka , mbona haingii”

“Nilijua tu unataka kumuona Roma”Aliongea Juma huku akiweka uso wa hasira na kumpita baada ya kufunga mlango , lakini Najma hakuridhika alifungua mlango na kuangalia nje lakini Roma hakuonekana , jambo ambalo lilimfanya kuwa katika hali ya maswali , alifunga mlango na kukimbilia ndani.

“Kaka Roma yuko wapi , mbona hujaja nae”.

“Bwana eeh usiniulize maswali yako mimi , kwani umeona natembea nae mfukoni”Aliongea Juma na alikerwa sana na maswali ya mdogo wake , na aliona kabisa si kama alivyofikiria kuwa Najma alikuwa ashaachana na Roma baada ya kumuingiza kahaba geto kwake, alikula chakula alichowekewa na mdogo wake huku akitabasamu kwa kuona kuwa mdogo wake anajua kupika na baada ya kushiba aliignia kwenye chumba chake na kujilaza.

“Najma akiolewa na mimi naoa , nyumba yote inakuwa yangu na ili hili litimie sitaki Najma aolewe na Roma maana nina uhakika kwa maisha ya Roma atataka aishi na Najma hapa hapa”Alijiongelesha huku akiwa amejilaza na kukodolea macho taa mpaka pale alipopitiwa na usingizi pasipo ya kuzima taa.

Upande wa Najma yeye hakuweza kupata usingizi kabisa , muda wote masikio yake yalikuwa kwenye geti tu , ili asikie geti likigongwa ili akamfungulie Roma , lakini muda ulizidi kwenda , lakini alichokuwa akitegemea hakikuweza kutokea kabisa, baada ya kuona atasinzia alienda kusbiria Sebleni mpaka pale alipokuja kupotelea usingizini , na alikuja kushituka kukiwa kumekucha kabisa na hii ni baada ya kaka yake kumkuta Najma akiwa Sebleni, alijikuta hasira zikimpanda baada ya kuona dada yake kalala hapo sebleni na kung`atwa na mbu huku akimsubiria fukara Roma arudi.

“Huyu mpuuzi akirudi leo na mfukuza akapange kwingine , kwa hali hii Najma hawezi kuoelewa”Aliongea Juma na kisha alitoka mpaka vyumba vya nje vya wapangaji na kwenda kwenye chumba cha Roma na kukifungua na kuingia , ndani na kitu cha kwanza alichoona ni mabakuri mawili makubwa ambayo alikuwa akiyafahamu yakiwa kwenye kijimeza , aliyasogelea na kisha kufungua bakuli la kwanza na hapo nipo alipotoa macho huku sura yake ikianza kujikunja.

“Yaani huyu mpuuzi anamuwekea Roma mapaja ya kuku halafu mimi kaka yake ananiwekea wali na Choroko, hii haiwezi kuendelea hivi”Aliongea Juma kwa hasira huku akinyanyua yale mabakuli na kutoka nayo nje huku akipishana na Najma ambaye alimkata jicho , baada ya dakika chache Juma alitoka akiwa na kufuri lingine na kisha alifunga mlango wa Roma na kisha kurudi ndani na kupasha kiporo kile na kula.

Wakati yote hayo yakiendelea Najma ambaye alikuwa kwenye hali ya wasiwasi , alikuwa akimwangalia kaka yake tu , huku akiogopa hata ya kumuuliza chochote kuhusu Roma alipo , baada ya kusimama nje kwa dakika kadhaa , Juma alitoka nje huku akionekana safari ya kwenda kazini kwake ikiw aimewaidia.

“Kaka najua umekasirika lakini naomba uniambie Roma yuko wapi”.

“Usiniulize maswali ya kupuuzi na , kwa upendo wako wa kijinga jinga Roma kwanzia leo akirudi anaenda kutafuta chumba kwingine na nisikie fyoko fyoko uone”Aliongea Juma huku akiweka kibakrashia chake vizuri na kutoka huku mlango wa geti ukiipigiza kwa nguvu.

“Halafu huyu Mpuuzi kaenda wapi , tokea jana mchana sijamuona tena alipofuatwa na yule mtu mwenye suti”

****

JANA YAKE SAA SABA MCHANA

Roma mpaka kufikia muda wa Saa saba mchana alikuwa amepiga kazi kubwa sana ya kuteremsha mizigo ya Cement , kwenye Duka kubwa la vifaa vya ujenzi la Bozi , yeye pamoja na wenzake walikuwa wamechafuka mno kiasi kwamba hawakuwa wakitamanika , lakini wala hawakujali sana , kwani kwao pesa ilikuwa ndio kila kitu.

Njaa nayo haikuwaacha salama , na baada ya kupewa ujira wao , Juma aliwaongoza wenzake kuelekea upande wa pili wa barabara ili kwenda kujipatia chakula cha mchana kwa Mama Joshua. Kama ilivyokuwa desturi yao.

Baada ya dakika kadhaa tu Roma alikuwa ndio alikuwa mtu wa mwisho kunawa mikono , alianza kunawa uso ili kutoa vumbi la Cement na kisha alimalizia mikono , lakini ile anamaliza tu mita kadhaa kwenye barabara kuu , ilisimama gari aina ya V8 nyeupe , gari ambayo iliwafanya baadhi ya watu kuikodolea macho .

Baada ya gari hii kusimama , alitoka mwanadada mmoja aliekuwa amevalia suti ya rangi ya bluu na viatu vya rangi ya Pink , mwanadada huyu alitoa picha kwenye mkoba wake na kisha aliangaza kulia na kushoto huku akitoa simu yake iliokuwa ikiita na kisha kuiweka sikio mara baada ya kuipokea na baada ya maongezi machache alikodolea upande wa kimgahawa cha Mama Joshua huku akikagua mtu mmoja mmoja na baada ya kuona kile alichokuwa akitafuta alisogea kuelekea upande huo wa mgahawa ,. Huku baadhi ya watu wakishangazwa na urembo na shepu ya mwanamke huyo , lakini hakuna aliekuwa ni mwenye kujali.

“Habari yako kaka”Aliongea mwanamke huyu kwa sauti ya kujiamini kabisa na kuwafanya wakina Juma na wenzake kushangazwa na kitendo hicho , kwani mtu aliekuwa akisalimiwa alikuwa ni Roma.

“Salama”Aliitikia Roma pasipo kujali uzuri wa mwanamke aliekuwa mbele yake na kusogelea meza ya plastiki ya rangi ya bluu na kuketi kwenye kiti huku mrembo huyu kuonesha kuchukizwa na kitendo cha Roma kutokumuangalia usoni , licha ya kumsemesha , kwake alitafsiri kama dharau kubwa ambayo ameonyeshwa kwa mwaka huo , yaani katika maisha yake na urembo wake , hakuwahi kudharauiwa na mwanaume wa aina yoyote ile , lakini kwa Roma ilikuwa tofauti na hio aliingiza katika Top Ten ya dharau alizowahi kuonyeshwa katika maisha yake, lakini licha ya hivyo , mwanadada huyu bado alionekana kuwa ni mwenye shida ya kuongea na Roma kwani alisogea mpaka kwenye meza aliokuwa amekaa Roma na kumwangalia kwa kumshusha kwa mavazi yake ya kimasikini na uchafu uliomjaa.

“Mama Joshua nipe ugali mkubwa na Samaki “Aliongea Roma na kuwafanya marafiki zake wazidi kumshangaa Roma kwa kitendo hicho cha kutokujali , licha ya kuongeleshwa na mwanamke mrembo kama huyo ambaye kwao , ilikuwa ni kama ndoto kupata bahati ya kuongeleshwa na mrembo kama huyo.

“kaka nimekusalimia”

“Ooh !,, sorry sister , nilikuwa bize kidogo , kumbe ulikuwa ukiniongelesha mimi”.

“Ulifikiri na muongelesha nani , au dharau tu kaka yangu , sio vizuri”Aliongea mwanadada huyu kwa sauti yake ya kuvutia huku akionekana amekereka kweli kwa kitendo cha Roma kujifanya hakumsikia wakati wote huo aliokuwa anamsalimia , na kilichomkera Zaidi mwanadada huyu ni kutokana na watu waliokuwa wakimwangalia , alichokuwa ametegemea mwanamke huyu ni Roma kumnyenyekea , lakini swala hilo likawa nje ya mategemeo yake na kumfanya yeye ndio aonekane mwanamke mwenye shobo na katika baadhi ya watu waliamini huenda huyo mwanadada alikuwa ni demu wake.

“Ulikuwa unasemaje sista”.

“Wewe si ndio Roma”

“Ndio ni mimi”

“Basi naomba utangulizane na mimi kuna mtu muhimu sana anataka kuonana na wewe”Aliongea mwanadada huyu na kuwafanya watu wote waliokuwa hapo mgahawani kushangazwa na maneno hayo , ila kwa Roma hakuonekana ni mwenye kushangaa sana , kwani alipokea chakula chake na kuanza kula.

“Sister naomba ukae , kwanza unisubirie nimalize nipige msosi ndio tuongee maswala ya mtu Muhimu .. maana hii ni moja ya starehe yangu na mara nyingi ni kila sipendaki kusumbuliwa”Aliongea Roma kwa kujiamini huku akianza kumega bonge la tonge na kulichovya kwenye mchuzi na kisha kulimeza lote , kitendo ambacho kilimshangaza sana huyu mrembo , na kumkera kwa wakati mmoja.

“Nitasubiri kwenye gari , ukimaliza naomba tufutatishane kama nilivyokuambia”Aliongea ule mwanadada pasipo kusubiri jibu , na kisha kuondoka .

“Halafu we Ms**nge unapenda kuifanyisha matawi ya juu , mtoto mkali kama yule anakuongelesha unajifanya unaongea kama hutaki kama vile Mondi , vile au unatuoshea tu washikaji zako hapa”Aliongea Yusuph huku akiungwa mkono na wenzake.

“Ila jamaa nimemkubali sana , ile pia ni heshima”:Aliongea jamaa mmoja ambaye yeye hakuwa muongeaji sana , ila siku hio alionekana kuchangia.

“Hahaha .. Mhando hata wewe leo umechangia mada , inaonekana pia umeguswa sana na jambo hili”Aliongea Juma na kuwafanya wengine wacheke maana ni kwa mara ya kwanza kwa Mhando kuchangia mada , yeye alikuwa ni mkimya wa hali ya juu

Baada ya Zaidi ya nusu saa ya Roma kumaliza msosi wake , alipiga maji kwenye kikombe , na kisha alijishika tumbo lake na kujiona kushiba vyema na kutoka mgahawani na moja kwa moja alielekea kweye gari , na kugonga mlango wa kioo ulioshushwa.

“Ingia kwenye gari”Aliongea mwanadada huyu kwa sauti iliojaa machukizo na kwa Roma wala hakujali , baada ya kuingia kwenye gari , ilitolewa nduki kuelekea upande wa Kongonwe na kuja kugeuzwa na kurudi upande wa kuelekea kariakoo.

“Unanipeleka wapi Mrembo”Aliongea Roma lakini hakujibiwa , Zaidi ya kusonywa na Roma aliamua kutulia kwenye kiti chake , huku akifurahia kiyoyozi kilichokuwa kwenye gari hilo, na kutokana na uchomvu aliokuwa nao , alipitiwa na usingizi na hata pale alipokuja kushituka alijishangaa akiwa mbele ya jengo refu mno maeneo ya Mawasiliano Sehemu ambayo alijua haraka kwani alikuwa ni mwenyeji wa maeneo hayo , baada gari hii kusimama kwenye jengo hili Geti lilifunguliwa na gari ile iliingizwa mpaka ndani na kuegeshwa na kisha mwanamke yule mrembo alishuka .

“Karibuni Grand palace hoteli wateja wetu”Ilisikika sauti ya muhudumu iliowakaribisha kwa tabasamu na ucheshi wa hali ya juu ,Roma alimwagalia mwanamke huyo aliekuwa amevalia sare ya hoteli hio na kisha alimkonyeza kitendo ambacho yule mwanadada aliekuja na Roma kukiona na kubetua midomo , lakini kwa muhudumu alirudisha kwa tabasamu la kuita.

“Watu wenye pesa wanakula maisha sio poa”Aliongea Roma baada ya kuingia kwenye lift huku akiwa si mwenye kuacha kumkonyeza mrembo huyu ambaye amenuna kama muuza sumu.

Baada ya lift kufunguka katika Floor namba kumi na nane , Roma alifuata nyuma nyuma mpaka walipofika kwenye mlango wa chumba namba 708 na kisha huyu mrembo aligonga mlango na ndani ya dakika kadhaa mlango ulifunguliwa na mwanaume alievalia suti.

“Karibu Suzzane”Aliongea mwanaume huyu alievalia suti huku akiwa ni mwenye tabasamu lakini pia macho yake hayakuwa mbali na uso wa mwanaume aliekuwa nyuma ya Suzzane , mwanaume ambaye kwa macho ya haraka haraka alionekana kama Fukara.

“Bossi nisharudi na nimemleta”Aliongea mrembo Suzzane kikakamavu huku akimwangalia mwanamke aliegeukia dirishani , akionekana kuangalia nje akiwa amewapa watu wote katika chumba hiko mgongo.

Mwanamke huyu alikuwa amependeza mno kwa vazi lake la suti alilokuwa amevaa ,suti ya rangi nyeupe

“Asante Suzzane , mnaweza kuondoka mpaka pale nitakapowaita”

“Boss!!”Aliongea Suzzane kwa hali ya wasiwasi .

“Fanya kama nilivyosema Suzzane”Aliongea mwanadada huyo kwa sauti ya Amri na kumfanya Suzzane amkate jicho Roma ambaye alikuwa akikagua uzuri na ufahari wa chumba hiko.

Licha ya Roma kushangazwa na ufahari wa chumba hicho , lakini pia sauti ya mwanadada aliekuwa mita kadhaa mbele yake aliempa mgongo ilikuwa ikimsisimua mno , ilionekana kama inamkumbusha mbali sana.

Baada ya Suzzane na mwanaume yule kutoka nje , mwanadada yule aligeuka na kumwangalia Roma , kitendo ambacho kilimfanya Roma atoe mshangao na kutamka:

“Kahabaaa…!!!”

ITAENDELEA SIKU YA KESHO JIONI..
Story nzuri unajua kueleza
 
SITAPOSTI TENA!!!! Kuja kwenye uzi wangu usome simulizi hiyo huku ukimngoja Roma aangushwe huku pale ambapo mtadhaminiwa na watu wa grupu!!!!
Yes mkuu asante kwa kuelewa , hapa Ni mwendo wa Roma tu

BAADAE TUNAENDELEA
 
SEHEMU YA 305.

Ilionekana Dhahiri kwamba watu wote waliokuwa juu ya meli hio ya kifahari walikuwa wakionekana kwA ukaribu kabisa kutoka kwenye meli ya kivita iliokuwa ikiongozwa na Makedoni, kwani baada ya Khalifa kuonyesha Tatoo iliokuwa kwenye mgongo wake kulitokea kimya cha takribani dakika kama mbili hivi mpaka sauti ya Kapteni Makedoni kusikika tena.

Watu waliokuwa ni wageni ndani ya hili eneo hawakuwa na uelewa wa aina yoyote ile juu ya alama aliokuwa akiongelea Tajiri Khalifa, lakini pia hawakuwa wakielewa alikuwa akimaanisha nini kuhusu jina la Hades , hata kwa upande wa Amina mwenyewe hakuwa akimfahamu Roma kwamba ndio Hades, alietambua hilo jina alikuwa ni Mheshimiwa Kigombola na Tajiri Khalifa peke yao , wageni wote hawakuwa na ufahamu na jina la Hades na hata kwa Khatibu ambaye alikuwa mshukiwa wa kwanza kumkasirisha Roma alikuwa hafahamu chochote kuhusu Hades , yeye alichokuwa akijua kuhusu Roma Ramoni ni kwamba bwana huyo alikuwa ni mbeba mizigo ndani ya soko la Mbagala Rangi tatu na aliacha kazi yake hio baada ya kupata shavu la kuona na mwanamke mrembo Tajiri ,Edna Adebayo, ni Dhahiri kabisa kwamba hata Fayezi mwenyewe licha ya kumtambua Roma kama Hades hakuwa na faili lote la utambulisho linalohusiana na Hades na laiti kama angekuwa nalo basi asingefanya vitu vya kumchokoza, ama kuingizwa kwenye mtego na Jasoni Pamoja na kundi la Takamagahara.

Watu wote sasa tumaini lao ilikuwa ni kwa Tajiri Khalifa pekeee , waliomba tatoo iliokuwa kwenye bega lake iwe na msaada kwao na Imani zao zilikuwa juu kidogo kutokana na ukweli kwamba Khalifa alikuwa ni muislamu haswa wa swala tano na alikuwa akifuatisha taratibu zote za uislamu, na sheria kubwa ya uislamu haikuwa ikiruhusu michoro ya tatoo kwenye miili, sasa kitendo cha Tajiri Khalifa kuwa na tatoo hio licha ya miiko ya dini waliamini kabisa kuna maana kubwa kwenye mchoro huo.

“Rafiki yangu ameona alama unayozungumzia na ameitambua . lakini licha ya hivyo anasema kuwepo kwa alama hio kwenye mwili wako hakubadilishi jambo lolote”Ilisikika sauti ya Makedoni na kufanya Tajiri Khalifa akiwa myonge na kukaa kwenye kiti.

Haiwezekani , nafurahi kwamba ameitambua na hili linanitibitihsia kwamba ndio mtu niliekuwa nikimsubiri kwa muda mrefu , lakini kwanini anakataa kutoa msamaha kwangu na watu waliopo kwenye meli hii”Aliwaza Tajiri Khalifa.

“Upande wa meli ya kivita Roma alikuwa kwenye chumba maalumu, kikubwa ambacho kilionekana kama ofisi , kutokana na uwepo wa mpangilio wa viti na masofa , pembeni yake walikuwa wamesimama wanajeshi kama kumi hivi wakiwa wamemzunguka , Roma alieonekana kutokuwa mtu mwenye wasiwasi kabisa , kwanza kabisa alikuwa ameweka miguu juu ya meza huku akigida Wine ya Cheval Blanc iliohifadhiwa tokea mwaka 1948 ikioezeshwa tu , ilikuwa ni wine ya bei mbaya mno na kwa mahesabu ya haraka haraka chupa yake inagharimu Zaidi ya Dollar za kimarekani laki tatu sawa na milioni mia saba za kitanzania.

Yaani kwa jinsi alivyoonekana ni tofauti na maneno ya Makedoni , kwani alisema kwamba rafiki yake huyo alikuwa kwenye makasiriko ya hali ya juu sana , lakini haikuwa kweli kwani Roma alikuwa akiburudika na Wine huku akiwa amezungukwa na wanajeshi walio kwenye sare tofauti tofauti, alionekana kama mfalme kamili na jambo la kushangza Zaidi ni kwamba wanajeshi waliomzunguka walionekana kuwa wenye umri mkubwa kuliko yeye ambaye umri wake ulikuwa miaka ishirini na nane tu.

Roma alikuwa akiona kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwenye meli ya kifahari kwa kupitia runinga iliokuwa imefungwa ndani ya meli hio ya kivita ya Hatakaze.

Makedoni yeye hakuwa hapo kwenye hiko chumba , ilionyesha alikuwa upande wa chumba cha kuendeshea meli hio kwani yeye mwenyewe alikuwa ndio Kapteni wa meli, lakini kila alichokuwa akiongea Makedoni Roma alikuwa akikisikia na mbele yake kwenye meza kulikuwa na simu ambayo alikuwa akiwasiliana moja kwa moja na Makedoni akimpa maelekezo, hata baada ya kusikia maneno ya Tajiri Khalifa Pamoja na kuona alama iliokuwa kwenye bega lake alishangaa kidogo na kukunja uso kwa sekunde , ilikuwa ni mara yake ya pili kuona mtu ambaye hakuwa akiishi ndani ya visiwa vya wafu kuwa na alama hio , mtu wa kwanza alikuwa ni mwanamke ambaye alikuwa akimuona kama mpumbavu tu kutokana na ndoto zake za kuiangusha Marekani , mwanamke aliekuwa akiitwa Mellisa, ukweli Roma licha ya kwamba Tajiri Khalifa alisema alama hio kaipata kutoka kwa Hades wa zamani , yeye hakuwa ni mwenye kujua sababu gani ya Hades wa zamani kuwachora alama hio ambayo ilikuwa ni kama kitambulisho cha uraia, kwa wananchi wake kutoka Visiwa cha wafu.

Roma licha ya kuona alama hio haikuwa na sababu ya kutaka kuacha kile kilichopo kwenye kichwa chake , ni kweli kabisa alikuwa akijihisi moyo wake kubadilika na kujihisi kama Mlokole, lakini alivyomshudia Khatibu mpwa wa Fayezi na kukumbuka Kejeli zake kipindi akiwa kwenye tukio la mnada , aliamini hio roho ambayo ilikuwa ikimwambia asiue , alijiambia hawezi kuitii sana kwani inavunja moja ya sheria zake na aliamini namna nzuri ya kuikomesha sauti hio yenye upole ndani yake ni kuhakikisha anaenda nayo kinyume kwa namna yoyote , na mpango wa kwanza ni kushuhudia kifo cha Khatibu.

Roma alichukua kifaa cha mawasiliano na kuwasiliana na Makedoni na kumpa maelekezo juu ya msimamo wake.

Dakika kadhaa tu , yaani kama dakika tatu hivi baada ya tajili Khalifa kukosa tumaini licha ya kujigamba kwamba alikuwa rafiki na Hades wa zamani na pia kuwa na uthibitisho wa Tatoo , alijikuta akirejewa na tumaini tena , yeye Pamoja na wageni wake wote na hio ni mara baada ya Makedoni kutoa msimamo wa rafiki yake.

“Kama nilivyosema kwamba rafiki yangu kaitambua hio alama , lakini licha ya hivyo hawezi kutoa msamaha kwa alama ambayo kwake haina maana hata kidogo na haiwezi kupunguza kile anachojisikia moyoni , hivyo basi anasema kwamba anajisikia angalau kutoa msamaha kwa familia nya Khalifa Pamoja na wageni wote , ila kwa sharti moja tu,Khatibu Omary atupiwe baharini , pili hataki ugomvi wowote na familia ya Khalifa licha ya kwamba anapanga kumuua mtoto wenu Fayezi kutokana na makosa yake, hivyo kama mnakubaliana na uamuzi wake Tajiri Khalifa utaongoza adhabu ya kifo kwa Katibu Omary.”

Maneno ya Makedoni licha ya kuwa na tumaini kwa wageni , lakini kwa upande wa mama mzazi wa Fayezi ilikuwa ni kilio kikubwa mno, hakuwa tayari kwa mtoto wake Fayezi kufa, alijua alikosa na alitaka mtoto asamehewe na kabla hata ya Tajiri Khalifa kutaka kutoa tamko kwa kile alichoamua , mzazi huyo alimkwapua kipaza sauti na kuongea.

“Tafadhari naomba mwanangu asamehewe , naomba Fayezi asife jamani nipo tayari kufanya lolote hata kufa kwa niaba yak… hiii… jamani naomba..”

“Tajiri Khalifa tunachotaka kuona ni agizo kutekelezwa sio kusikia kilio kutoka kwa mke wako , maamuzi ni ya kwako , ‘ofcourse’ kuna mbadala , kama utakubali tulipue meli yenu na kufuta kila uhai wa mtu alieopo kwenye hio meli basi utachagua na mtoto wenu Fayezi ataachwa hai”Yalisikika maneno ya Makedoni aliongea kwa niaba ya Roma Ramoni a.k.a Hades.

Tajiri Khalifa alijikuta akifumba macho kwa muda mrefu kidogo na kufanya kila mtu kumwangalia , hata kwa Raisi Kigombola hakuweza kumsoma Tajiri huyo atachukua maamuzi gani , ni kweli mpaka muda huo licha ya Makedoni kuongea , lakini hawakuweza kusikia sauti ya Hades mwenyewe , hivyo hata Kigombola kuwa katika hali ambayo ina mashaka ndani yake , jana yake alionyeshwa pucha za Hades akiwa mfu , leo hii wanavamiwa na meli ya kivita na mtu anaejitambulisha kwa jina la Makedoni , huku akiongea kwa niaba ya Hades , aliona huenda Hades mwenyewe alikuwa maiti na Makedoni anataka kulipiza kisasi , lakini hata hivyo pia alikuwa akikumbuka na maneno ya Yan Buwen juu ya kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kumuua Hades Zaidi yake mwenyewe , hivyo pande zote mbili zilikuwa zikipigana vita katika akili yake , ubongo wa kulia ulikuwa ukimwambia Hades yupo hai na anapaswa kuamini maneno ya Yan Buwen kwamba hakuna mtu anaeweza kumuua Zaidi yake na upande wa kushoto alikuwa akikumbuka picha alizoonyeshwa na Fayezi , lakini pia upande huo ukiwa na sababu nyigine ya kusapoti kutokana na kwamba sauti ya Hades yenyewe haijasikika Zaidi ya mtu aliejitambulisha kwao kama rafiki yake.

“Kigombola unahisi ni maamuzi gani napaswa kuchukua? , nimwache Mwanagu Feyezi kufa kama adhabu ya makosa yake , au niruhusu kundi hili la wageni wote kufa Pamoja na mimi na kuacha Fayezi awe hai?”Aliuliza Khalifa na mheshimiwa Kigombola aliona swali hilo ni kama la mtego..

Upande wa meli Roma akiwa anaendelea kuburudika na mvinyo wake mara macho yake yalitua kwa Mheshimiwa Kigombola, kwanza kabisa hakushangazwa na uwepo wake hapo, kwani alikua akijua machache kwamba mheshimiwa huyo mstaafu alikuwa na ukaribu na familia ya Khalifa , hivyo kualikwa halikuwa jambo la kushangaza , kilichomfanya Roma kumwangalia kwa namna ya udadisi ni kutokana na taarifa ambayo aliipata muda huo kutoka kwa kundi la Yamata Sect kupitia kiongozi wao , Tanya.

“Boss Mheshimiwa Kigombola ndio mtu wa mwisho kuongea na Fayezi ndani ya hoteli ya El-Fadhi na kwa maelezo ya shushu wetu kaeleza kwamba kilichokuwa kikizungumziwa ni juu ya kifo chako , baada ya mazungumzo hayo mheshimiwa alioongea na simu ambayo tumefatilia na kujua imepigwa Kwenda Tanzania na ameongea na mtu alieopo ndani ya hoteli ya Serena na bado hatujaweza kufahamu ni mtu gani aliekuwa akiwasiliana nae , kwani namba yake Special”Aliongea Tanya na kumfanya Roma kufikiria kwa dakika kadhaa.

Sasa kabla hata hajamjibu Tanya simu nyingine iliingia kutoka Tanzania kwa njia ya satilaiti yake , licha namba hio kutokuwa na jina lakini kodi zake zilimfanya kujua kabisa alikuwa akipigiwa simu na The Eagles na alipokea haraka haraka na kuweka sikioni na hapo ndipo alipojikukuta akivuta pumzi nyingi , mtu aliekuwa akiwasiliana nae ni Diego kutoka Tanzania na alimpasha Habari ya uvamizi uliotokea nyumbani kwake.

“Diego nimeumia kusikia kifo cha Chiara na pia kuumia kwa John , wasiliana na Sauroni ili kupata utaratibu wote wa kusafirishwa kwa Chiara mpaka visiwa vya wafu kwa ajili ya maziko, taratibu zote za fidia kwa familia zitapangwa na Sauroni kutokana na sheria za wanajeshi wetu”Aliongea Roma huku akionekana hata mudi yake ya kunywa bia ikimtoka, na hata mawazo aliokuwa nayo juu ya mheshimiwa Kigombola aliyaacha kwa muda.

Roma alimshukuru Aphrodite kumsaidia kuiokoa familia yake , kwani kama sio yeye huenda ingekuwa huzuni zana kwa upande wake na angepoteza watu anaowapenda kwa mara nyingine, lakini hata hivyo aliamini lazima kuna malipo , kwani alikuwa akimuelewa sana Christine anapopata msaada wake , lakini hilo hakutaka kulipa kipaumbele sana, aliamini chochote atakachoongea Christine ni lazima atakitimiza kwani jambo alilofanya kwake ni kubwa sana, lakini pia wakati huo huo alikuwa akijiuliza ilikuwaje Christine akafika nyumbani kwake ndani ya muda na kuokoa familia yake.







SEHEMU YA 306.

Kabla hata ya mheshimiwa Kigombola kujibu wanaume wawili ambao walikuwa ni wageni wa kualikwa walimkamata Khatibu ambaye alionekana kutafuta namna ya kutoroka , na wanaume hao walionekana kuungwa mkono na kila mgeni , walikuwa tayari kumtoa Khatibu kama sharti walilolopewa na hawakuata kuyaweka Maisha yao mikononi mwa Khalifa na Kigombola ndio maana walaiona kufanya maamuzi wenyewe ndio busara iliokuwepo kwa muda huo.

Kitendo cha Khatibu kukamatwa kilimfanya kuloa mwili mzima , huku akianza kujikojolea, sasa ukumbuke walikuwa juu kabisa ya meli hii , hivyo Wanaume wale wawili walimsogeza Katibu mpaka kwenye ukingo wa meli ile kwa ajili ya kumtupia majini, huku wakisaidiwa na baadhi ya walinzi.

“Mtupee…!!”Zilikuwa ni kelele za watu wote na Khatibu kuna sauti alijikuta akisikia kwa upande wa kulia kwake na hakutaka kuamini kama sauti hio ni ya mtu anaeyemfahamu na kumjali sana, alijikuta akigeuza kichwa chake na hapo nipo alipoamini kwamba sauti ile ilikuwa ikitoka kwa mtu ambaye anamfahamu , mpenzi wake Hadija ni mojaya watu waliokuwa wakikemea kwa juu kuhusu kutupwa kwake majini , Khatibu moyo wake uliuma Zaidi ya kile kitendo ambacho kitatokea dakika kadhaa mbele , kwake aliamini ni afadhari kutupiwa majini kuliko kusalitiwa na mwanamke ambaye alikuwa akimpenda kwa moyo wote, hakuamini mwanamke Hadija aliekuwa amejtolea kumpenda Zaidi na Zaidi ndio huyoo ambaye anaungana na wageni wengine kuruhusu kifo chake, Khatibu aliangalia upande mwingine na kuangalia ndugu zake wengine na kila mmoja alionekana kutojali kifo chake , mtu pekee ambaye alikuwa na huzuni alikuwa ni mama yake Fayezi na huzuni yake sio kwa ajili ya kifo ambacho kinataka kumkumba bali ni juu ya mtoto wake Fayezi na mama huyo alikuwa akimwangalia Khatibu na katika moyo wake ni kama alikuwa akisema anatamani kifo cha Khatibu kiponye kifo cha mwanae , yaani kwa maneno marahisi mama huyo alikuwa akitamani kwamba kufa kwa Khatibu kuwe mbadilisihano wa uhai wa Fayezi.

Sasa baada ya Khatibu kuona kila mtu alikuwa akitamani kifo chake , hakutaka hata kusikia na mjomba wake Khalifa atasema nini , alijua kabisa mjomba wake huyo lazima ataruhusu kifo chake na kwanza kabisa alishaonyesha nia ya kutoumizwa na kifo chake.

“Chubwii..!!!!” Khatibu hakutaka kufa kwa kusukumwa , baada ya kuona hakuna mtu ambaye alikuwa akihuzunishwa na kifo chake , hata kwa wale aliokuwa anawapenda , aliona ni bora kufa kishujaa kuliko fedheha ambayo inataka kumkumba , maumivu aliokuwa akisikia kwenye moyo wake alijiambia ni bora kujirusha majini.

Katika maji ya katikati ya bahari hio , hatimae Khatibu kifo chake kinadhihirika kwa wengi , hakuna mtu ambaye anaweza kuamini kama Khatibu anaweza kupona kwenye maji hayo mengi , hivyo moja kwa moja alihesabika kama mfu na jambo hilo liliwafanya watu wote kuvuta pumzi ya ahueni.

Dakika nne baada ya kupita hatime chopa ilitua kwenye meli hio , chopa ambayo haikuwa na nembo yoyote , ilikuwa ikiendeshwa na wazungu wawili wote wakiwa wakike waliovalia mavazi ya uniform. Za kijeshi.



“Miss Amina na Baba yako mnapaswa kupanda kwenye hio Hawk , hayo ni maelekezo kutoka kwa rafiki yangu “Aliongea Makedoni na kuwafanya watu wote kumwangalia Amina na baba yake Kanan ambao walikuwa hapo ndani .

Kanani baada a kusikia maneno hayo alijiambia hawezi kupanda , kwani alikuwa akikiendea kifo chake , Mzee huyu licha ya kusikia baadhi ya maelezo , lakini hakuwa akimfahamu huyo rafiki ambaye Khalifa alimtaja kama Hades , aliamini kupanda chopa hio ni kukiendea kifo chake.

Wakati akiwa anafikiria cha kufanya, Amina ndio aliekuwa wa kwanza kupanda upande wa juu kabisa wa meli hio kwa ajili ya kupanda chopa hio.

“No ..Amina mwanngu usipande , watu wale ni wabaya kwetu na huenda tunajiingiza Zaidi kwenye matatizo ni heri kufa tukiwa wengi”Aliongea Mzee Kanani kwa wasiwasi na Amina alimgeukia baba yake.

“Baba yangu mpendwa , unaamini kubakia hapa ndio utakuwa salama , lakini unajuaje huko tuendako tunakwenda kufa , huenda mtu alietuita anataka kuongea na sisi tu na kisha atatuachia”Aliongea Amina na kisha kupewa mkono na mzungu mwanajeshi kwa ajili yakupanda juu ya chopa.

Sasa kwakuwa lile ni agizo kutoka kwa Makeodni basi wageni wote walimwangalia Kanani kwa macho ya kumtaka kutii maagizo na mzee huyo baada ya kukumbuka kilichomtokea khatibu hakuwa na ajizi kwani alipanda kinyonge kwenye ndege hio na ajabu mara baada ya kuipanda wanajeshi hao hawakuwaangalia kwa macho ya chuki zaidi ya kuwapa heshima na kisha chopa kuondoshwa.

Na kutoka na wa wanajeshi hao walivokuwa wakimpa heshima alianza kujiuliza maswali ni mtu gani ambaye anaitwa Hades ambaye anataka kuonana nae , yeye Pamoja na mwanae , mwanaume huyu mpenda pesa , hakuwa na uelewa kwamba mtu ambaye anakwenda kukutana nae ndio yule ambaye alimtoa bikra mtoto wake Amina , mwanaume ambaye alimsahau siku ileile na kuendelea na mipango ya ndoa kwa Binti yake na Fayezi.

Baada ya Chopa kuondoka hatimae meli iliwashwa na kufanya wageni wote kushangaa kwani dakika kadhaa zilizopita walikuwa na taarifa kwamba meli hio ilikuwa haina kapteni.

“I’m very satisfied with each of your cooperation. Everyone is safe now, while the countdown on our missile launcher has stopped. The cruise will arrive at the port in an hour’s time, I hope everyone to have a happy journey…”

“Nimeridhishwa sana na ushirikiano kutoka kwa kila mtu , kwasasa kila mmoja yupo salama , bomu letu tumelizima na meli yenu itafika bandarini ndani ya lisaa limoja baadae , natumaini kila mmoja atakuwa na safari iliojaa furaha”Aliongea Makedoni na watu wote walishangilia mara baada ya kusikia kwamba wamepona, wengi walishasahau kabisa jambo ambalo ilikuwa limewaleta hapo ndani wengi wao hawakumkumbuka Khatibu na Fayezi , wala hali za machungu waliokuwa nayo wanafamilia wao , akiwemo mama yake mzazi wa Fayezi, Tajiri Khalifa na yeye pia licha ya kuwa kwenye majonzi , ila hakuwa na jinsi kabisa na hakutaka kabisa ugomvi na Hades , kwani kuna baadhi ya meneno kutoka kwa rafiki yake Hades wa zamani aliokuwa akiyakumbuka na aliamini kifo cha Fayezi ni kwa ajili ya kusudio kubwa Zaidi na hakijatokea bure , hakuwa na maneno ya faraja ambayo alitakiwa kumpatia mke wake kwa wakati huo Zaidi ya kuwapa maagizo wasaidizi kumchukua na Kwenda kumpumzisha , upande pia wa Wake zake wengine wlaikuwa wakichekelea kwani siku zote hawakuwa wakimpenda Fayezi kutokana na kupendelewa na baba yake na mpaka muda huo ni kwamba Khalifa hana mrithi wa kiume tena kwani Watoto wake wengine waliobakia ni wanawake.

Upande wa kwenye meli ye kivita ya Hatakaze , hatimae chopa ile ilitua na wa kwanza kushuka alikuwa ni Amina ambaye alishangazwa na uwepo wa wanajeshi waliokuwa wapo kwenye meli hio wakiwa katika mavazi ya kijeshi ambayo yana rangi tofauti tofauti.

Makedoni , mwanaume mzungu mwenye ndevu nyingi alievalia kombati za jeshi pia alionekana kutoka kwenye chumba cha Kapteni na sasa alikuwa amesimama akiwa na wanajeshi wengine kwa ajili ya kumpokea mrembo Amina,yaani kwa jinsi Amina alivyokuwa akisubiriwa ni kama vile ni mtu mkubwa sana , kumbe ni mchepuko tu wa Roma Ramoni ndio maana alikuwa akipewa heshima kubwa ya namna hio.

Amina mara baada ya kumuona babe wake Roma Ramoni alisahau kila kitu na kumkimbilia na Kwenda kumkumbatia kwa fuaraha mno , hakuamini Roma alikuwa na uwezo wa aina hio , yaani kwa ajili tu ya kuzuia ndoa yake isifanikiewa kaleta meli ya kivita.

“Babe Amina angalia pembeni”Aliongea Roma na kumfanya Amina kuangalia pembeni na hapo ndipo alipogundua macho ya wanajeshi wote yalikuwa kwake na kumfanya kuona aibu.

Mzee Kanani sasa macho yake ni kama yalikuwa yakimdanganya , mtu aliekuwa akimchukulia kama kapuku kumbe ndio alikuja kufanya uchafuzi wa hali ya hewa wa namna hio , hakuwa akiamini kama mwanaume yule alieitoa bikra ya mtoto wake ndio huyo alievuruga ndoa na kuonyesha nguvu kubwa sana, alishindwa hata kuongea lolote Zaidi ya kumwangalia mtoto wake aliening’inia kwa mwanaume huyo.

“Kama ni hivi basi nilikosea kuchagua upande , kuna fursa hapa”Aliwaza Mzee Kanani huku akikagua wanajeshi wote hao , licha ya kwamba alikuwa kwenye misukosuko dakika kadhaa zlizopiita , lakini kuona mmeli huo wa kivita Pamoja na wanajeshi walivyokuwa wakimuheshimu Roma , aliona fursa , yaani kwake fursa ndio kila kitu mpaka kwa wakati huo.

“Babe sikufahamu unaweza kuja na meli kwa ajili tu ya kuzuia ndoa yangu , umenifurahisaha mno , lakini sikudhania kama una uwezo wa kua na meli kama hii ambayo mara nyingi naiona kwenye muvi”Aliongea amina kwa kingereza na kumfanya Roma kutabasamu.

“Hehe.. hii meli yenyewe sio yangu tumeiazima kutoka jeshi la Japani , si nilikuambia nilitakakufanya ndoa yako kuwa ya kipekee , huu ndio upekee wenyewee, mimi babe wako Roma Ramoni nakuja kukuokoa na meli ya kivita inakaaje hio , si Romantic?”Amina alishangaa , hakuamini maneno ya Roma.

“Unao uwezo wa kuazima meli ya kivita kutoka jeshi la Japani?”

“Ndio babe , Waziri mkuu wa Japani nilikuwa nikimdai hivyo nilipomwambia anilipe kwa kunikodisha meli ya kivita kwa masaa mawili hakusita kufanya hivyo.”

Roma aliamza kumtabulisha Amina kwa wanajeshi wake wote , akiwemo Makedoni na sasa Amina aliweza kupata kumjua aliekuwa akiongea kwa rafudhi ya kizungu.

Kazi ya kumuokoa Amina ikawa imekwisha kwa namna hio , kifo cha Fayezi kilitekelezwa na kundi la Yamata Sect kutoka kwa maagizo ya Roma.

“Mr Roma najua kuna mahali nilikukosea kwenye siku hizi za karibuni na siku ile nilikutolea maneno ya kejeli , hivyo naomba unisamehe mimi , na kwanzia leo hii nipo tayari mwanangu Amina umchukue kama mkeo?’Aliongea Tajiri Kanani huku akionekanna kumaanisha kile anchoongea na kumfanya hata Amina kushangaa baba yake kwa namna anavyobadlika badilika.

“Mzee msamaha nimekupatia kwasababu Amina ni mtoto wako , kuhusu kumchukua Amina kama mke wangu hilo sijalifikiria , kwani nina mke tayari na siwezi kuoa mwanamke mwingine Zaidi na niliekuwa naye”

“Hapana .. sijamaanisa umuache mkeo , ninachomaanisha umuoe kama mke wa pili , sisi katika Imani yetu tunaruhusiwa kuoa wanawake mpaka wa nne”Aliongea Kanani.

“Sasa kama nikifuata Imani yako ya kuoa wanawake mpaka wanne inaamana kwamba kuna baadhi ya wanawake wangu wengine watakosa nafasi”Aliongea Roma na alichoongea ni sahihi , kama kweli atafatisha sheria za Imani ya Mzee Kanani ni kwamba wanawake wake watakosa nafasi kwani mpaka muda huo walikuwa wamezidi wanne tayari.

“Mzee licha ya kwamba sitomua mtoto wako kwa ndoa, lakini naweza kukuhakikishia kwamba Amina ni mwanamke wangu kuanzia sasa na nilioyafanya haya yote na ninayotarajia kuyafanya juu yake ni kumhakikishia kwamba ana nafasi sawa na cheo cha mke, hivyo usiwe na wasiwasi na uhakikishe siku zinazokuja haufanyi jambo ambalo litanisabibishia kukasirika”Aliongea Roma kwa usuriasi na Mzee Kanani alitingisha kichwa kwa heshima kubwa , alikuwa yupo tayari kuwa upande mzuri na Roma kwa namna yoyote ile ili atumie fursa ya kupanua biashara zake.

“Babe kumbe una wanawake wengine tofauti na mke wako?”Aliuliza Amina kwa kulalama.

“Hehe… ndio ukimuacha mke wangu wewe ni mwanamke wangu wa nne”Aliongea Roma kwa kujiamini na kumfanya Amina kumwangalia Roma usoni kama asieamini na aliishia kucheka na kumfanya Roma atabasamu na kupendezwa na urembo wa Amina kwa jinsi alivyokuwa akicheka.

“Nikifika Tanzania lazima nijitambulishe kwao wote ili wanitambue kama moja ya mwanamke wako”

“Babe unauhakika na unayoongea?”

“Niko siriasi , kubwa Zaidi nitajitahidi kumfurahisha mkeo ili asije akanichukia, siko tayari kukukosa Darling”Aliongea Amina na kumfanya Roma kutabasamu na kisha kumfinya Amina mashavu yako.

Ni baada ya masaa kama manne kupita Roma alikuwa kwenye ndege binafsi ya Yamata Sect akirejea Tanzania akiwa na Amina , ndani ya ndege hio kilichokuwa kikifanyika hakikuwa kikielezeka , kwani kila staili ya mapenzi ilifanyika , hata zile ambazo hazina majina zilifanywa na mtaalamu Roma, kiasi kwamba Amina kuwa mwekundu mno kutokana na rangi yake.

Jambo ambalo lilimfurahisha Roma ni kwamba katika wanawake wake wote , Amina pekee ndio mwanamke ambaye alikuwa yupo Romantic kuliko wanawake wote na alikuwa mvumilivu mno, kwani aliweza kuhimili Kwenda mizunguko miwili kwa wakati mmoja jambo ambalo lilikuwa tofauti kwa wanawake wake wengine kama Rose , Roma akienda mzunguko mmoja tu Rose atakuwa amechoka na hana hamu tena ya kuendelea , lakini kwa Amina alikuwa na joto kiasi kwamba mpaka mizunguko miwili alikuwa akienda na angalau kumfanya Roma kupunguza moto uliokuwa ndani ya mwili wake,sasa Roma mwenyewe kutokanana mwili wake, ili hamu ya kufanya mapenzi iishe ni lazima Kwenda mizunguko tisa kitu mabcho ni ngumu sana kutekelezeka kwa wanawake wake wote , yaani kama ataamua Kwenda nao mizunguko yote nay eye kuridhika basi watakufa.

Saa moja kamili za usiku ndio muda ambao Roma aliweza kufika Tanzania na kuachana na Amina ambaye alienda kulala nyumbani kwao , Amina hakuwa amesafiri na baba yake , kwani mzee huyo alibakia Japani na kuwaruhusu kitu na mpenzi wake kusafiri Pamoja.

Mzee Kanani alifanya hivyo kwa kuona kwamba ni wakati wa kumuacha Roma na Amina kuwa na ukaribu mzuri ili Roma azidi kudata kwa binti yake , huku yeye akitafuta namna ya kutumia ‘Ukwe’ kujiendeleza kibiashara Zaidi, aliamini Roma alikuwa mtu mzito sana , kwani aliweza hata kusikia Roma akisema meli ile ya Hatakaze alipewa na jeshi la Japani kwa kuiomba tu kwa masaa , sasa hakuwa mjjinga wa kutoelewa kwamba hakuna nchi ambayo ilikuwa na uwezo wa kumuazimisha meli ya kivita mtu bila kuleta shida , aliamini Roma ni mtu mzito sana na mpango wake kwanzia muda huo ni kuchimba taarifa za Roma na kumfahanu ni nani , na akishaelewa ndio aanze kuangalia atanufaika vipi.

“Allah ananiepusha na hili na ananileta kwenye jambo kubwa Zaidi , nadhani ananikusudia mtoto wake nitengeneneze pesa nyingi sana”Aliwaza Mzee Kanani mara baada ya kumpigia mtu wake ambaye humtumia mara nyingi anapokuwa anataka taarifa za mtu Fulani , hivyo mtu huyo alimpa kazi ya kumfuatilia Roma ni nani haswa, muda huo alikuwa hotelini jijini Tokyo akiwa amepumzika.

“Babe I am Back….”Roma aliongea mara baada ya kuingia ndani ya jumba ambalo ni mali ya mke wake , sasa ile anaingia mtu wa kwanza kukutana nae ni Edna aliekuwa akitoka jikoni na alionekana alikuwa akipika

“Mwaaa.,,, Welcome home Babe” Roma hakutarahia ukaribisho wa aina hio kabisa na macho yake yote yalikuwa kodo akiangalia mbele.



ITAENDELEA…..

Summary ya simulizi tulipotoka

Mpaka sasa nadhani tumeweza kuona chimbuko la Hades kwanzia mwanzo wa simulizi hii , tumeweza kumfahamu licha ya kwamba ni sehemu ya miungu kumi na mbili ya kipagani(Greek Olympian Gods) lakini yeye ni wa tofauti na wenzake.

Hades yeye kwa jinsi utlivyoona ni kwamba ni sehemu ya miungu ambaye sifa yake kubwa ni kwamba yeye ni ROHO HURU yaan hana muunganiko wowote na miungu mingine.

Tumeweza pia kuona misheni ya Athena ambaye anafahamika kwama The Don ndani ya ulimwengu wa wahalifu(Underwold) lakini pia kama Minerva ndani ya tamaduni za Kiroma.

Tumeshuhudia pia misheni kubwa ambayo Athena anayo ni kutaka kurudisha hai Roho za ndugu zake zilizomezwa na binadamu , roho ambazo zimetokea Pamoja na yeye katika sayari ya Utopia mara baada ya maangamizo na Mungu.

Sasa kama misheni yake itafanikiwa kutokana na maelezo ya Hades wa Zamani kupitia mawakala wake kama vile mtoto wa Profesa Banosi , mchungaji, lakini pia Shekh Assad ni kwamba dunia itabadilika kwa kiasi kikubwa sana na huenda hata ile amani ambayo ipo kwa sasa kutoweka na ikumbukwe kwamba chanzo cha maangamizo ya sayari ya Utopia ni kutokana na kumkaidi Mungu mara baada ya kuona wanao uwezo wa kufanya mambo makubwa Zaidi ya Mungu kupitia sayansi.

Athena pia anaelezea nia yake ya kutaka kuunda dini moja na kushawishi binadamu kuacha kumtumikia Mungu ambaye haonekani na kumtumikia Mugu ambaye atakuwa anaonekana , mungu ambaye atakuwa tayari kufanya miujiza yote huku akionekana , sasa kama tulivyo ona , ili mipango yake kuweza kufanikiwa mambo makuu mawili lazima yatimie kwanza lazima awapate wanachama wote wa Illuminat ambao anaamini wanachama hao wamebeba roho za ndugu zake , lakini baada ya hapo apate jiwe la Kimungu ambalo hajalipata bado , jiwe ambalo ndani yake kuna Roho ya Gaia(Mother of earth) , Roho ambayo itampa uwezo wa kutawala nafsi za miungu yote mingine na yeye pia na miungu hio kuweza kupata nguvu zao zote ambazo walipoteza mara walivyofika kwenye uso wa dunia, unafikiri atafanikiwa katika mipango yake.

Upande wa Edna pia anaonekana kutokufahamu kuwa alizaliwa na pacha ake , pacha ambaye anafahamika kwa jina la Seventeen , lakini pia anashindwa kufahamu kwmaba mama yake kifo chake sio cha kuitwa na Mungu bali kilisabishwa na First Lady mke wa baba yake mzazi ambaye bado hakuwa akimfahamu,

Edna anaendelea kutafuta siri iliopo juu ya kisasi ambacho mama yake alitaka kutimiza , kisasi ambacho mpaka muda huo hakufahamu kinahusiana na nini , mrembo Edna pia tunamuona hisia zake za mapenzi zikiibuka kwa mume wake wa mkataba Roma Ramoni licha ya udhaifu aliokuwa nayo mathalani kwa kupenda sana ngono na anaamua kuingia nae dili la kutokusumbua na michekupuko yake huku akitaka kuishi na Lanlan ambaye hafahamu kama ni mtoto wa Roma wa damu na pacha wake , yaani Seventeen.

Sasa unafikiri juu ya yote hayo nini kitaendelea , basi nikwambie tu simulizi ni ndefu sana na mimi SinganoJr nimejitolea kuhakikisha maswali yako yote nilioorodhesha na yale ambayo sijaorodhesha mwisho wa stori hii yanajibika kwa urahisi.
 
SEHEMU YA 307

Wakati Edna akishangaa kurudi kwa ghafla kwa Roma , Christine ambaye alikuwa amejilaza kwenye sofa alikuwa alishahisi uwepo wa Hades tokea muda mrefu sana tu na ndio maana baada ya kusikia kauli ya Roma kwamba amerudi alinyanyuka haraka haraka na Kwenda kumkumbatia Roma pasipo kumjali mke wake na kitendo hicho ndio kilichomduwaza Roma , kwani hakukitegemea na aliishia kumwangalia Edna.

Wanafamlia wote waliokuwa nyumbani kasoro Yezi, walitoka kuja kumlaki Roma Ramoni ,licha ya kwamba alikuwa ameondoka kwa takribani siku nne ila kwa yale ambayo yametokea ilikuwa ni Zaidi ya mwezi mzima kwao.

Bi Wema alifurahi , Blandina pia alifurahi kumuona mwanae karudi salama , upande wa Sophia na yeye alijisikia Faraja kumuona Roma , Upande wa Edna yeye alikuwa na furaha na makasiriko kwa wakati mmoja , kitendo cha Roma kuwaacha na Kwenda Japani tena yeye mwenyewe akihusika katika mchakato wa kupata tiketi kumbe anaenda kumpambania mchepuko wake kilimuuzi sana na alishindwa kuweka wazi hasira zake ila ndani kwa ndani alikuwa akiumia.

“Ankoo…..!!!”Lanlan aliekuwa akishuka kutoka juu mara baada ya kumuona Roma alimkimbilia kama mshale na Kwenda kumrukia na kufanya kila mmoja kushangazwa na kitendo hiko , huku kwa Qiang aliekuwa akijua ukweli juu ya Lanlan na Roma kuwa kitu na baba yake hatia ilimtekenya ndani kwa ndani ,kwani Lanlani licha ya kwamba alikuwa na furaha , lakini kitendo cha kumuita Roma Anko na sio baba ndio kilimfanya kuwa katika hatia.

Roma pia alifurahishwa na namna ambayo Lanlan alimlaki , alijikuta akijisikia vizuri kwa wakati mmoja , ijapokuwa sio yeye aliependekeza kumlea Lanlan , lakini uwepo wake ulimfanya kiasi flani kuhisi kama ameshakuwa baba kwa muda huo.

“Anko umemletea Lanlan zawaidi gani?”Aliuliza Lanlan na kumfanya Roma kufikiria namna ya kujibu swali hilo , maana hakuwa na zawadi ya aina yoyote ambayo aliibeba..

“Chubi Zawaidi yako utaipata asubuhi”Aliongea Roma na Lanlan mara baada ya kusikia jina la Chubi alikunja sura.

“Lanlan hadanganyiki na Lanlan sio chubi”Aliongea Lanlan huku akijitoa kwenye mikono ya Roma na Kwenda kusimama kwa Edna ambaye anamtambua kama mama yake.

Wakati hayo yote yakiendelea Christine alikuwa pembeni akiangalia kinachoendelea na alijikuta akishangazwa mno , hakuamini Hades anaemfahamu kwa kuwa mpweke leo hii ana wanafamilia wengi ambao wanamlaki, alimuona kama mtu mwenye bahati sana tofauti na yeye ambaye hata mtoto wa kusingiziwa wala ndugu hakuwa nae.

“Edna mkaribishe mumeo karudi”Aliongea Blandiina akimtaka Edna asimwangalie Roma tu bali amkaribishe kwa heshima , sasa kauli hio ilimfanya hata Roma kumwangalia Edna na macho yao yakakutana na Roma kwa kumwangalia Edna tu aligundua kuna jambo ambalo haliko sawa.

Sasa Edna hakutaka kuwa mtukutu mbele ya mama mkwe.

“Karibu”Aliongea Edna na pasipo hata ya kusubiri jibu kutoka kwa Roma aligeuka na kurudi jikoni.

“Hahaha… Hades inabidi uwe na maelezo ya kutosa kwa mkeo nishamdokezea ulichoenda kufanya Japani”Aliongea Christine tena hakutumia jina la Roma Zaidi ya kutumia la Hades lenyewe na sasa hapo ndio Roma alijua nini kinaendelea na lawama zote alizielekeza kwa Christine.

“Nilijua tu uwepo wako ndani ya familia yangu haujengi Zaidi ya kubomoa”Aliongea Roma huku akimpita Christine.

“Hehe.. Hades unanifahamu vizuri kwamba siku zote siwezi kusema uongo na pia nina tabia ya kuropoka ropoka”Aliongea Christine huku akimfatisha Roma kwa nyuma , Roma alitamani azichape na Aphrodite palepale licha ya kwamba alimsaidia kuokoa familia yake.

“Sawa mrembo Ropo Ropo, mwenye familia nisharudi ni muda sasa muafaka wa kuondoka maana kadri utakavyokuwa hapa ndio mambo yatazidi kuharibika”

“Hades… kwa hio unanifukuza licha ya kukusaidia kuilinda familia yako ,naona hunifahamu ngoja nikamwambie mkeo siri nyingine ambazo sijamweleza”Aliongea Christine huku akijifanya kujinunisha na Kwenda upande wa jikoni na kabla hata hajafika Roma alimzuia kwa mbele.

“Hahahaha….. Masikini Hades…. umebadilika sana ,,”Aliongea Christine huku akimcheka Roma kutokana na namna alivyomzuia , ukweli ni kwamba aliokuwa akifanya yote hayo ni kumpima Roma ni kiasi gani alikuwa akiogopa mke wake kujua baadhi ya siri zake , sasa kitendo cha Roma kumzuia kilimpa picha halisi namna Roma anavyomjali Edna na mpaka hapo aliamini Roma kapenda kweli tena Zaidi ya alivyokuwa akimpenda Seventeen , kwani katika kichwa chake alikuwa akikumbuka licha ya kwamba Seventeen na Hades walikuwa na mahusiano , lakini Roma hakuwa akimuogopa hata kidogo , alikuwa akitembea hata na warembo mbele ya Seventeen na mwanamke huyo wala asikasirike wala kujishughulisha , lakini sasa kitendo cha Roma kuficha mambo yake ya nyuma kilimfurahisha sana na kuona Roma kabadilika sana.

Sasa wakati hayo yakiendelea wanafamilai wote walikuwa wakiwaangalia kwa macho ya kiulizo , sio kwa Sophie , sio kwa Qiang wala kwa Blandina , kwa jinsi walivyoona Christine alivyokuwa akiongea na Roma , waliamini walifahamina kwa muda mrefu sana, huenda Zaidi ya wanavyofahamu.Christine alionekana kujiachia sana mbele ya Roma kuliko mtu yoyote yule.

Licha ya kwamba s Ceiling body iliharibiwa , lakini ilikuwa isharekebishwa haraka sana , hivyo wanafamilia waliendelea na matumizi ya sebule ya chini.

Roma baada ya kupumzika kwa dakika kadhaa na kupata chakula cha usiku , hatimae alimuomba Christine kuongea, Roma alikuwa na mambo kadhaa alitaka kuyathibitisha kutoka kwa mwanamke huyo na alikuwa akiyafikiria tokea akiwa njiani.

Upande wa Blandina na yeye alitaka kukaa na Roma na kutaka kujua kwanini alikuwa na jina lingine la Hades, jina ambalo hakuwa akilifahamu , hakutaka kusikia kutoka kwa Christine bali alitaka kusikia kwa Roma mwenyewe, na jambo lingine sasa liliongezeka katika kichwa chak, alitaka pia kujua Roma alikuwa akifanya nini Japani kitendo ambacho mpaka kinamfanya mke wake Edna kuwa katika hali isio na furaha, yote hayo alipanga kuongea na mtoto wake , lakini sio kwa muda huo.

Chrisitne na Roma walitoka mpaka eneo la nje ya bustani na kuketi sehemu maalumu ambayo imejengwa kwa ajili ya mapumziko kwa nyakati zote yaani usiku na mchana.

Wakati Roma na Christine wakiongea upande wa juu Edna alikuwa kwenye Balconi akiwaangalia kwa chini.

Ukweli ni kwamba tokea ujio wa Christine ndani ya familia hio , Edna alikosa utulivu kabisa na hio yote huenda ilichangiwa na uzuri wa Chrisinte lakini pia umaarufu wake , sasa Edna alikuwa akipata hisia ambazo zilikuwa zikimfanya kuogopa Roma anaweza kumuacha yeye na kuzama na mwanamke huyo , ijapokuwa mwenyewe aliona anawaza ujinga lakini aliruhusu hisia zake kumuendesha na kutotumia akili kwenye kufikiria.

“Hades mkeo ana wivu wa kisiri siri”Aliongea Chrisitne kwa Kingereza na Roma alitabasamu, ukweli walikuwa washamuona Edna akiwa juu ya Balconi , yaani hawakuwa na haja ya kugeuka kujua kwamba wanaangalia bali hisia zao zilikuwa zikitambua kila kitu hapo ndani.

“Unaniharibia kwa mke wangu kwa umbea wako , kuna haja gani ya kumueleza kama nilikuwa Japani kwa ajili ya mwanamke?”Aliongea Roma na Christine akatabasamu.

“Kwahio ulitaka nidanganye , sina fani hio Hades napenda kuongea ukweli”Aliongea Chrisinte na kumfanya Roma kutabasamu kwa uchungu.

“Okey kama kweli unapenda kuongea ukweli basi unieleze ulijuaje familia yangu ipo hatarini , ijapokuwa nashukuru sana kwa msaada wako , lakini uwepo wako hapa Tanzania kabla ya muda tuliopanga unanifanya niamini kwamba haupo Tanzania kwa ajili ya swala kuwa jaji pekee”Aliongea Roma, hakupenda sana kuzunguka zunguka na Christine kwanza alishamuharibia kwa Edna na sasa anapaswa kumaliza mazugumzo na kujua ni namna gani ya kumfanya Edna kumchangamkia.

“Nadhani kabla ya kukueleza kwanini nipo Tanzania unieleze namna ulivyopoteza Godstone kwa Athena”Aliongea Aphrodite na kumfanya Roma kushangaa.

“Umejuaje nimepoteza Godstone kwa Athena?”Aliuliza Roma na Christine akatabasamu.

“Wote sisi tulikuwa tukilinda jiwe hilo lisitue kwenye mikono ya Athena na siku ambayo alikuzidi ujanja na kulichukua tuliweza kufahamu kupitia uwezo wetu, Hades unatakiwa kuelewa kwamba sisi miungu wote tofauti na wewe tuna muunganiko wa moja kwa moja na jiwe hilo na mara nyingi nguvu yake inapoachiliwa huwa tunao uwezo wa kutambua”Aliongea Christine na jambo hilo lilikuwa jipya kwa Roma ,kwani hakuwa akifahamu.

“Ni kweli Athena alinizidi nguvu , lakini ninachoamini ni kwamba jiwe hilo silihitaji kwani halina msaada wowote kwangu zaid ya kuniweka katika wakati wa kuandamwa na watu wengi wanaolihitaji”Aliongea Roma na Christine alivuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Umeongea kweli kwa maneno yako , kwani kati ya miungu yote kumi na moja ni wewe pekee ambaye una nguvu kubwa kutuzidi, hata Athena kakuzidi mbinu chache sana kwasababu ulikataa kujifunza mambo ya anga na akili yako yote ukaielekezea kwenye mafunzo ya kijini kutoka China”

“Unamaanisha kwamba kama ningejifunza namna ya kutumia ‘Space laws’ ningekuwa na uwezo kama wa Athena?”Aliuliza Roma kwa mshangao , ukweli ni kwamba tokea mwanzo hakuwa akiamini kabisa juu ya kanuni za za anga kama zinaweza kumpa nguvu kubwa sana , lakini siku za hivi karibuni alianza kuhisi huenda kanuni za anga zinanguvu kubwa sana kuliko mbinu za kijini alizofundishwa na Master Chi.

Unachotakiwa kuelewa ni kwamba licha ya kwamba Roma mwili wake una sayansi inayotokana na ‘Devine Light ‘, lakini haikuwa ikimaanisha kwamba ategemee uwezo wake huo tu , Kumulikwa na mwanga wa Jiwe la Kimungu(Godstone) ilikuwa ni hatua ya kwanza tn na hatua zingine zilikuwa zikitegemea uwezo wa kipekee kwa mtu mwenyewe wa kujifunza mapigano Pamoja na kuvuna nishati ya asili ya dunia(Cultivation of natural energy).

Sasa Roma licha ya kwamba mwanzoni alishauriwa kujifunza Zaidi kanuni za anga yeye akajikita katika upande wa pili ,kujifunza mbinu ambazo zilikuwa zikitumiwa sana na viumbe visivyoonekana , yaani majini na jamii nyingine , mbinu hizi licha ya kwamba kuwa kama uchawi lakini jina lake maarufu zinafahamika kwa jina la ‘Cultiuvation of Natural Energy’ , ni mbinu ambayo mara nyingi huwezekana mtu kuipata kwa kufanya Tahajudi.

Sasa inasemekana kwamba ukifanya Tahajudi na kufikia levo za juu kabisa mwili wako unajiunganisha moja kwa moja na vyanzo vya nishati asili na nguvu ambavyo vipo katika uso wa dunia na kanuni kubwa ambayo inatumika katika kuweza kubobea mbinu hizo ni kutoka kwenye msingi wa kanuni ya Ying And Yang(Mbingu na Ardhi), sasa hio ni njia ambayo Roma aliichagua kuitumia baada ya kushawishiwa na Master Chi kujifunza , lakini upande wa Zeros hawakupenda Roma kujifunza mbinu hio na hata siku ambayo Zeros waligundua eneo la siri(Gobi-Desert) ambalo Roma anafundishwa namna ya kutumia nguvu hizo ambazo kwao walizitafsiri kama za kichawi kutokana na kutozielewa kwa mtazano wa kisayansi ndipo ulikuwa mwanzo wa Wa Zeros kuwanza kumuwinda Master Chi.

Sasa Sababu ya kifo cha Master Chi ilikuwa ni kutokana na kumfundisha Roma mbinu ambazo Zeros hawakuzitaka , Zeros walitaka Roma kujifunza ‘Space Laws’ mbinu ambayo inaeleweka kisayansi.

“Ndio , ungekuwa na uelewa kidogo tu wa namna ya kutumia siri ya nguvu iliojificha kwenye ‘Space Laws’ , huenda ungekuwa na uwezo hata kumzidi Athena kwa sasa”Aliongea Christine na kumfanya Roma sasa kujua kwanini Athena alimuona kuwa na uwezo wa ajabu kumbe siri yote ipo kwenye ‘Space Laws’ , lakini hata hivyo aliamini njia alioichagua ilikuwa sahihi Zaidi ya hio ya kutumia ‘Space Laws’ na kama atazidi kupanda levo za juu Zaidi , basi anaweza kumzidi Athena.

“Kama ni kweli kuna nguvu kubwa kwenye utumiaji wa ‘Space Laws’ , kwanini mnazidiwa na Athena?”

“Sio kweli kama tunazidiwa na Athena , unachotakiwa kuelewa ni kwamba kati yetu wote kumi na mbili Athena ndio ambaye ana akili nyingi sana kutuzidi , hivyo uwezo wake wa kugundua kanuni za anga na kuzitumia ni mkubwa mno kuliko sisi wote , kwa maneno marahisi katika kuweza kutumia siri ya nguvu iliopo kwenye kanuni za anga ni kutokana na uwezo wa akili wa mtu , tunatofautishwa uwezo wetu kutokana na akili zetu zinavyoweza kung’amua”

“Ndio maana sikutaka kuichagua hio njia , kwani kama uwezo wenyewe unatofautishwa na akili za mtu basi siku zote ningekuwa wa chini sana katika levo za mapambano”Aliongea Roma na kumfanya Chrisine kutabasamu m alionekana kuelewa Roma alichokuwa akimaanisha.

“Acha kujidharau Hades , unao uwezo mkubwa sana kuliko binadamu yoyote yule ndio maana Old Hades alikuchagua”

Ni kweli kabisa , Athena moja ya zawadi kubwa ambayo amependelewa basi ni uwezo wake wa akili , hata katika historia ya miungu hii ya kipagani enzi hizo Athena alitambulika kama sehemu ya miungu ambae anatumia akili nyingi sana na kwasababu hio amekuwa tishio kubwa sana katika mampambano.

Na inasemekeana hata Athena alivyombana na Zeus ambaye anaaminika kwa kuwa mbabe katika kuzipiga waliishia suruhu , kwani hakukuwa na mbabe kati yao.

“Hades kitendo cha kupoteza jiwe l kimungu kwa Athena unatuweka kwenye hatari kubwa sana”Aliongea Christine na kumfanya Roma kushangaa kwani ni kama hakuwa amemuelewa na siku zote Roma anapokuwa na Christine anajikuta kama mwananfuzi kwani ni mengi sana ya kujifunza kutoka kwake , kwani alikuwa akifahamu kwamba Christine alikuwa ameishi miaka mingi sana , miaka Zaidi ya mia tano.

“Unamanisha nini kuwaweka kwenye hatari?”

“Subiri siku utakapoona hatari yenyewe ndio nitakuelezea ,kwasasa hata nikuelezee unaweza usielewe”Aliongea na kumfanya Roma kukuna kichwa.

“Watu ambao walishambulia familia yako ni watu ambao walishakufa na wakafufuliwa”Aliongea na kumfanya Roma kutoa macho.

“Unamaanisha kitu gani?”

“Ushawahi kusikia juu ya Teknolojia ya ‘Resurrection Fluid?’”

“Ndio nishawahi kuisikia na sijawahi kuthibitisha kama teknolojia hio ni ya kweli, unataka kumaanisha kwamba teknolojia hio ni ya kweli na inafanya kazi?”

“Ndio teknolojia hio ni ya kweli kabisa na watu ambao waliweza kuigundua ni kutoka kundi la ‘Darkparliament’ katika tafiti zao za kuifanya miili yao ya kivampire kuishi milele kwani tunajua kwamba licha ya Vampire kuishi miaka mingi lakini mwisho wa siku wanakufa, sasa tafiti zao ndio zilikuja kuvumbua hii teknolojia ya waliipa jina la ‘Resurrection Fluid’ , kutokana na uwezo wa teknolojia hio, mpaka sasa wanaamini hata Yesu baada ya kifo chake kimiminika hiko ndio kilitumika kwenye mwili wake ndio maana alifufuka”Aliongea Aphrodite na kumfanya Roma kujua jambo moja lingine kwa siku hio , lakini hata hivyo bado alikuwa na maswali.

“Sasa ilikuwaje watu hao wakashambulia familia yangu baada ya kufufuliwa na hicho kimiminika?”

“Mwanasayansi ambaye aligundua teknolojia hii ya ‘Ressurection Fluid’ alikufa miaka mitano mbele baada ya majaribio kuonekana ni ya kuridhisha na kwa taarifa ambazo zipo mpaka sasa inasemekana mtu aliemuua ni Athena na kukwapua teknolojia yote , Pamoja na vimiminika ambavyo vilitengenezwa na wanasayansi hao, jambo la kushangaza ni kwamba miaka kadhaa nyuma tulibaini matumizi ya kimiminika hiko kwa baadhi ya watu na taarifa zote zinaonyesha majaribio ya kimiminika hayo yalisimamiwa na kampuni yangu ya INNOVA pasipo kuwa na uelewa na kile kinachoendelea na hili ndio swala ambalo lilinifanya nifike Tanzania kwani swala hili linaweza kutufanya kuwa katika mgogoro jambo ambalo sitaki litokee”Aliongea Christine na kumchanganya Zaidi Roma.

“Unamaanisha nini kusema mgogoro mimi na wewe , najua kampuni ya Innova imekuwa kubwa kiasi kwamba imekuwa nje ya uwezo wako kuongoza kila mwanasyansi na wanafanya mambo mengi kwa mitazamo yao na hilo nalifahamu fika , lakini kwanini unasema kwamba tunaweza kuingia kwenye migogoro?”Aliongea Roma hakumuelewa Aphrodite anataka kumaanisha nini.

“Kama nilivyosema kwamba kimiminika hiki cha kufufua watu kilitumika miaka kadhaa nyuma , huku majaribio hayo yakifanyika chini ya kampuni yangu ya INNOVA , na majaribio hayo hayakua na mafanikio kwani watu waliofanyiwa majaribio hayo waliishia kupatwa na shida za kiafya tofauti tofauti”

“Lakini umesema teknolojjia hii inatumika kwenye watu waliokufa tu pekee , kwanini unasema imesababishia watu matatizo?”

“Wanasayansi walikuwa wakifanya majaribio kujua kitatokea nini kama mtu atapewa kiminika hiko akiwa hai , hivyo majaribio hayakuwa kufufua watu bali kuangalia nini kitatokea , Hades moja ya watu ambao wapo kwenye orodha ya kufanyiwa majaribio hayo ni Rahel Adebayo mama yake na Edna”Aliongea Aphrodite na kumfanya Roma kutoa macho.











SEHEMU YA 308.

Jnnova ni kampuni ya utafiti ilioanzishwa nchini Italy mwaka 1920 , ikiwa ni mwaka mmoja na siku kadhaa mara baada ya vita ya kwanza ya Dunia , kampuni hii ilianzishwa na mwanamama Sienna Alessandro , mwanasayansi nguli, kampuni hii kutoka kuanzishwa kwake ilijikita katika tafiti mbalimbali na ilijozolea umaarufu mkubwa sana ndani ya Italy na nje ya Italy.

Mpaka inakuja kufikia mwaka 2002 ndio kampuni hii ikawa chini ya Christine Stewart msanii mrembo kutoka Marekani , unaweza ukashangaa iliwezekanaje kwa kampuni hii kuwa chini ya Christine , jibu ni rahisi sana Aphrodite kabla ya kuhamia kwenye mwili wa msanii chipukizi Christine , Sienna Alesandro ni mfululizo wa binadamu ambao walivaa roho au nafsi ya Aphrodite, hivyo ni rahisi kusema kwamba alienzishha kampuni ya Innova alikuwa ni Aphrodite au Christine, sasa katika miili yote ambayo Aphrodite alipitia , wanawake wote walikuwa warembo , Sienna Alesandro ilikuwa ni mwanamke maarufu sana na mrembo ndani ya Italy na alishawahi kuhusishwa kutoka kimapenzi na Benito Musolini japo taarifa hizo hazikuwahi kuthibitishwa.

Sasa basi kampuni ya Innova ilikuwa kiasi kwamba ilikuwa na matawi mengi na moja ya sheria ya Aphrodite kwenye taasisi hio ni kuiacha kuwa huru , yaani wanasayansi wengi walipewa uhuru wa kufanya tafiti zao kwa kutumia jina la la taasisi pasipo kuingiliwa na hili nadhani ndio lilikuwa kosa kubwa kwa Chrisitne kwani baada ya taasisi hii kuwa kubwa hatimae wanasaynasi wengi walianza kufanya mambo nje ya utaratibu wa kampuni.

Sasa kwa maelezo ya Aphrodite Kwenda kwa Roma ni kwama miaka kadhaa nyuma katika utafiti shirikishi , kati ya kampuni ya kitafiti ya Maya tawi la Canada na ya Innova walifanya majaribio ya teknolojia ya Resurrection Fluid ambayo ilikuwa ikiaminika kwamba inafufua watu , sasa majaribio hayo hayakuwa upande wa ufufuzi wa watu bali kujua ni nini kitetokea kama teknolojia iliopo ndani ya kimiminika hiko itaingizwa kwenye watu ambao wako hai.

Utafiti huo ulifanyika na kufeli kwa asilimia tisini na tisa , kwani watu karibia wote walioweza kupatiwa kimiminika hiko walipatwa na shida mbalimbali za kiafya , kuna waliopatwa na mishituko ya moyo na kuna waliopatwa na kufeli kwa figo na kuna wale ambao pia walipatwa na shida za kuchanganyikiwa.

Christine anashindwa kuelewa ilikuwaje kati ya orodha ya watu waliochaguliwa kufanyiwa majaribio hayo mmoja wapo akawa ni Raheli Adebayo.

Roma alikuwa kwenye mshangao juu ya maelezo hayo , kwani mpaka hapo sasa anafahamu kwamba kifo cha mama yake Edna hakikuwa cha kuitwa na Mungu bali kimesababishwa na watu kwa kupewa kimiminika ambacho yeye alikiona ni kama sumu tu kutokana na kwamba hakikuweza kufanya kazi mwilini, kimiminika chenye jina la Ressurection Fluid.

“Umesema kwamba teknolojia hii ilikuwa kwenye mikono ya Athena , sasa kwanini ikafaikia wanasayansi wa Innova na wakashirikiana na kampuni ya Maya?”Aliuliza Roma.

“Hades hizo ni taarifa ambazo namimi nazitafutia ufumbuzi kwasasa , wanasayansi wote ambao walihusika kwenye majaribiio hayo walishakufa wote akiwemo dokta ambaye aliekuwa akimtibu Baba yake na Edna , hizo ni taarifa fupi ambazo nipo nazo mpaka sasa na nilikuwa nikifanya uchunguzi na naendelea kufanya uchunguzi mpaka sasa kujua kila kitu , kwanini teknolojia ambayo iliaminika imepotea kuwa ndani ya kampuni yangu Pamoja na Maya na kufanyiwa tafiti na baada ya hapo mafaili yote ya majaribio kuharibiwa na baada ya miaka mingine watu wanaoaminika miili yao kutumia kimiminika hiki kupatikana tena”

“Unamaanisha hio miaka kadhaa inahusiana na hawa watu ambao wamekuja kuishambulia familia yangu?”

“Hades mwaka jana nchini China watafiti kutoka taasisi ya kiutafiti wa kibailoji ndani ya Wuhan ndio walioweza kufanikiwa kugundua matumizi ya Resurrection Fluid kwenye mwili wa ‘Assasin’ alietumwa kumuua raisi mstaafu wa China”

Ndio mwaka mmoja nyuma ilitokea kashfa ya raisi wa China kushambuliwa na muuaji ambaye alionekana kuwa kama Roboti au msukule , taarifa hii licha ya kwamba ilikuwa ya siri , lakini ilifanyiwa uchunguzi wa kina sana baada ya muuaji huyo kushindwa kutekelezeka , majaribio ya kimauaji ya raisi mstaafu Cheng Li, sasa katika uchunguzi uliofanyika ndio walikuja kugundua kuwa muuaji siku kadhaa nyuma kifo chake kiliripotiwa ndani ya hospitali moja ndani ya jiji la Beijing , yaani kwa maneno marahisi ni kwamba raisi alishambuliwa na mtu ambaye alikua ameaminikika kufariki , sasa jambo hili ndio liliibua wanasayansi kutoka Wuhan kuanza kufanya tafiti na hapo ndipo walipokuja kugundua matumizi ya Resurrection Fluid ndani ya mwili wa muuaji na taarifa hii ndio ikamfikia Christine.

Sasa kwa maelezo ya Christine ni kwmaba baada ya kupatikana kwa maiti hio iliofufuka ambayo ilimshambulia raisi mtaafu wa china ,idara za usalama zilingiwa na wasiwasi na kuamini huenda kukawa na watu wa namna hio wengi ambao wamefufuliwa hivyo kuweka hatarini usalama wa raia , kutokana na wasiwasi huo ndio msako ulianza kufanyika kwa muda mrefu sana , lakini hakukuwa na majibu chanya kabisa , lakini hata hivyo vyombo vya usalama vya China kushirikiana na taasisi nyingine waliendeleza msako huo kimya kimya , lakini pia wakitafuta taasisi ambayo inatumia Ressurection Fluid kufufua maiti, lakini pia juhudi zao ziligonga mwamba mpaka baada ya mwaka kuisha na siku ambayo wanakuja kugundua watu hao ni ndani ya ndege iliokuwa ikisafiri kutoka China Kwenda taifa la Tanzania.

Sasa wasichokuwa wakijua ni kwamba wakati wao wanahaingaika mtaalamu Yan Buwen ndio aliekuwa nyuma ya kila kitu , huku teknolojia hio akiwa amepatiwa na Athena.

Na lengo la kuleta misukule yake hapa Tanzania ilikuwa ni kwa ajili yakuendelea kuifanyia majaribio ndani ya maabara ya kitafiti iliokuwa ikitumiwa na Profesa Shelukindo.

Sasa siku ambayo tunamuona Salah akifufuliwa na Yan Buwen , ndani ya vyumba vingine kulikuwa na maiti nyingine ambazo zilikuwa zimeshafufuliwa tayari na kimiminika.

Sasa watu wale wote ambao walifika nyumbani kwa Edna usiku ule , walikuwa wamepelekwa na mtaalamu Yan Buwen , sasa haikueleweka kwanini Yan Buwen akaamua kupeleka misukule yake yote Kwenda kuifyeka familia ya Roma , lakini tunaweza kudhania jambo moja , Yan Buwen alimuongezea nguvu Salah , lakini sasa kuitumia hio misukule lilikuwa kosa kubwa kwani muda mrefu ilikuwa ikifuatiliwa tokea inatoka China na kuingia Tanzania.

Sasa ujio wa Christine ndani ya muda na kuisaidia familia ya Roma haikutokea bahati mbaya , Christine alikuwa na taarifa na misukule hio , lakini jambo ambalo hafahamu ni juu ya misukule hio kumilikiwa na Yan Buwen.

“Kwa maelezo yako naweza kuhitimisha kwamba kuna mtu ambaye anashirikiana na Athena na mtu huyo ndio kapatiwa Resurrection Fluid?”Aliongea Roma huku akianza kuunganisha matukio , kwanza aliona jambo hilo lilifanyika mara baada yeye kusafiri Kwenda Japani na kwa mantiki hio mtu ambaye kaagiza misukule hio kuja kuishambbulia familia yake ni Dhahiri kabisa alikuwa akifahamu uwezo wake na anamfatilia kwa kila hatua , lakini pia alifikiria kama ni kweli kwanini mtu huyo kulenga familia yake , mambo mbalimbali yalipita kwenye kichwa chake na hapo ndipo alipoyafikiria maneno yote ya Christine hususani kwenye kifo cha mama yake Edna.

Roma aliona kwa kurahisisha zaidi ni kufikia muafaka kwamba mama yake Edna aliuliwa na kampuni ya Maya na wanasayansi waliopo chini ya INNOVA , lakini swali bado linaibuka kwenye kichwa chake , je uongozi wa juu wa kampuni ya Maya ulikuwa ukihusika? na kwanini Rahel kutoka Tanzania akawa chaguo juu ya majaribio hayo.

Swala hilo aliona asimwachie Aphrodite kulifanyia kazi , aliona yeye ndio ambaye anapswa kulifanyia kazi ili kufahamu ukweli wote , kwani kwa mantiki hio mpaka wakati huo alishaelewa kwamba Edna alikuwa kwenye sintofahamu na swala hilo , na kabla halijamfikia lazima yeye afahamu kwanza.

“Hades siamini kama Athena ndio katoa maagizo ya Raheli kuwa chaguo la majaribio, kama unavyoelewa kwenye kampuni yangu nimekuwa wa kutoa msaada wa kifeza kwa tafiti nyingi, na mengi ambayo yanafanyika nje ya jengo la kampnni muda mwingi sina taarifa nayo”

“Hata mimi nina uhakika Athena hawezi kuitageti familia yangu na kumchagua Raheli kuwa sehemu ya majaribio naamini swala hili ni kubwa kuliko isivyokuwa kawaida”

Wakati Roma akiendelea kuongea na Christine , upande wa ndani Edna na yeye alikuwa akiumia ndani kwa ndani , hakuwa akisikia Christine na Roma walikuwa wakiongea nini na alitamani kusikia , lakini hakuwa na uwezo wa kimungu wa kuweza kusikia maongezi yao kwani walikuwa mbali.

Sasa alikuwa kila akikaa kaa kwa dakika kadhaa anaamka na Kwenda kuchungulia na aliishia kukita miguu chini kwa hasira na kurudi kitandani na muda huu Lanlan alikuwa ashalala tayari.

“Wameoondoka?”Aliongea Edna mara baada ya kuchungulia kwa mara ya mwisho na kugundua kuwa wametoka kwenye bustani na alijitahidi kuangalia kila kona ya eneo hilo kuona uelekeo wao , lakini hakuambulia kitu.

“Wameenda wapi tena?”Aliongea kwa sauti lakini alijikuta akikodoa macho mara baada ya kukumbatiwa kwa nyuma.

“Babe Wife kumbe unamwoneaga mumeo wivu kiasi hiki”Aliongea Roma na kufanya pumzi yake iguse shingo ya Edna na mrembo huyu alijikuta akipata msisimko.

Mpaka hapo alikuwa amekamatika , kwani Aliamini Roma alimuona akichungulia nje , sasa asichokijua Edna ni kwamba kila alichokuwa akikifanya Roma alikuwa akiona kwa jicho lake la tatu la kiuungu na jambo hilo lilimfurahisha na ndio maana akaamua kumfanyia Surprise ya kuingia kwenye chumba cha mke wake kwa kimya kimya ili amkamate vizuri.
 
SEHEMU YA 309

Edna alitaka kuleta upinzani mbele ya Roma , lakini Hades ni kama alikuwa ashatarajia kuletewa upinzani, alichokifanya ni kumgeuza Edna na kumwangalia usoni na walijikuta macho yao yakigongana na wote kwa pamoja waliangaliana na kadri sekunde zilivyokuwa zikihesabu ndio sura zao zilivyokuwa zikisogeleana.

Edna mwenyewe alishindwa kujielewa ni kweli alikuwa na hasira na Roma , lakini kwa jinsi alivyokuwa akijisikia alishindwa kujizuia na walijikuta midomo yao ikinasa na kilichoendelea ni kupeana busu nyevu kwa muda mrefu kidogo, huku Edna akiwa amefumba macho na Roma akiwa amekodoa macho , lakini akiwa ulimwengu mwingine.

Roma hisia alizokuwa akizipata wanapokuwa kwenye hali kama hio zilikuwa za tofauti sana na za wanawake wake wengine.

Walirudi kinyume nyume na wote kwa Pamoja wakajikuta wakitia kwenye sofa ambalo lipo humo chumbani na kuendelea kubusiana, Roma hakutaka kuishia kwenye busu tu.

Edna alikuwa amevaa gauni la kulalia(Night Dress) hivyo ilimfanya Roma kupata urahisi wakupenyeza mkono katikati ya mapaja ya mrembo Edna na hapo ni kama alikuwa amegusa penyewe kwani Edna alijihisi shoti za umeme zikisambaa mwili mzima , kiasi cha kupelekea ua lake kujawa na unyevu mwingi.

Edna licha ya kwamba hisia zake zilikuwa mbali na akili yake, lakini mwisho wa dakika kadhaa aliweza kurejewa na akili yake na kumzuia Roma kutokuendelea.

“Nataka nilale”Aliongea Edna huku akijitoa kwenye mwili wa Roma kibabe na kupanda kitandani.

Sasa namna ambavyo Edna alijinasua kwa Roma ilikuwa ni kibabe sana kiasi kwamba Roma alishangaa mwenyewe.

Roma aliweza kujisemea kwamba licha ya Edna na Seventeen kuwa mapacha lakini walikuwa wakitofautiana sana tabia,Seventeen licha ya kwamba hakuwa Romantic lakini akipandishwa hisia zake hawezi kumuacha njiani wala kujinasua kama ilivyo kwa Edna , yaani kwa maneno marahisi ni kwamba Edna alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuzitawala hisia zake kuliko ilivyokuwa kwa Seventeen.

“Wife haujaniuliza mumeo safari ya Japani ilikuwaje?”

“Sina haja ya kujua imekuwaje, najua huna cha maana ulichokuwa unakifanya huko Japani”Aliongea Edna na alionekana kukumbuka swala hilo tena na hasira palepale zlimpanda na alichokifanya ni kuvuta shuka na kujifunika gubi gubi.

Roma aliangalia matendo ya Edna na kusogea karibu ya kitanda.

“Edna mke wangu , hivi unajua ni kiasi gani nakupenda….”

“Anko unamsumbua Lanlan amelala”Roma kabla hajamaliza sentensi yake ilikatishwa na sauti ya Lanlani, sasa hakueleweka Lanlan alikuwa macho muda gani , bali aliongea huku akiwa amefumba macho , yaani hakufumbua macho wakati akiongea na baada ya kuongea kauli hio aliendelea kuuchapa usingizi huku akitafuna tafuna yaani ilikuwa ni kama anaota.

Roma ilimbidi kuondoka ndani ya chumba hiko pasipo kuongea maneno ambayo alikusudia kutaka kuyatamka ,alitamani kumlegeza Edna kidogo na maneno matamu ,lakini Lanlan aliingilia kati.

****

Ni siku nyingine asubuhi Roma alikuwa mezani na wanafamilia wote wakijipatia kifungua kinywa akiwemo Christine.

Edna alikuwa ndio mkimya kuliko wanafamilia wote , wenzake licha ya kwamba walikuwa wakipiga stori za hapa na pale , lakini kwa Edna yeye hakuchangia Zaidi ya kunywa chai taratibu huku pembeni yake akiwepo Lanlan.

“Anko Roma ,kwanini unaitwa Hades?”Swali hilo lilitoka kwa Yezi na kumfanya Roma kumwangalia Yezi na kisha akainua macho yake na kumgeukia Christine na mwanadada huyo aliishia kutingisha mabega.

“Sio Hades tu ana majina mengi , kuna lingine anaitwa mfalme Pluto , Edna unajua kwanini unaitwa Persephone basi jibu ni kwamba Persephone ni mke wa Hades hapo zamani , hivyo wewe kuolewa na Hades umepewa cheo cha Persephone”Alibwabwaja Christine bila ya kumjali Roma aliekuwa akimwangalia kwa macho yasioeleweka yanaashiria nini ndani yake.

“Kwahio Miss Christine, Anko Roma jina lake halisi ni lipi?”

“Jina lake halisi ni Hades au Mfalme Pluto… Oooh! Yes ,najua hajawaeleza kuwa yeye ni mfalme si ndio?”

“Mfalme..!!! wan chi gani?”Sophia alihamaki na haikuwa kwake tu ,hatakwa Blandina mama yake Roma na wanafamilia wengine walijikuta wakiwa kwenye mshangao.

“Christine ukimaliza kupata hiki kifungua kinywa nakupa amri uondoke mara moja nyumbani kwangu, sikutaki ukiwa karibu na familia yangu”

“Malkia Persephone napaswa kufanya nini mfalme Hades ananifukuza nyumbani kwake?”Aliongea Christine kwa kujihurumisha na kumfanya hata Bi Wema asiekuwa akielewa kitu kutabasamu kwa maongezi hayo.

“Miss Christine tueleze Habari za mfalme Pluto tafadhari tunaomba….”Aliongea tena Sophia kwa kubembeleza lakini Christine alimwangalia Roma na hapo ndipo alipokatwa jicho na Roma.

“Jamani niseme nimependa sana familia hii ya mfalme Pluto na natamani kuongeza siku….Hades naamini utaieleza familia yako juu ya majina yako halisi , wanapaswa kujua kwani wote wanaonekana kukujali”Aliongea Christine na kisha akanyanyuka.

“Miss Christine malizia kunywa chai kwanza”Aliongea Bi Wema.

“Nimeshiba jamani asanteni sana”Aliongea Christine.

Ssa unachotakiwa kuelewa ni kwamba Chrisitne alikuwa akitumia lugha ya Kiswahili katika kuwasiliana , mwanzoni hata Edna na wanafamilia wengine walishangazwa na Mzungu huyo kuongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha kwani hata kwenye matamasha yake yote ya uimbaji hakuwahi hata kuonekana akizungumza lugha ya Kiswahili na wanafamilia hawa juzi yake walivyomuliza Christine, alijibu kwamba aliipenda lugha ya Kiswahili ndio maana akajifunza , lakini huo sio ukweli, kwani Christine alidanganya , ukweli ni kwamba Christine alikuwa na uwezo wa kuzungumza lugha nyingi Zaidi takribani ya lugha zote maarufu duniani alikuwa akifahamu kuzizungumza na hilo liliwezekana kutokana na kwamba aliishi miaka mingi Sana hapa Duniani kwa sura tofauti tofauti.

“Roma ni kweli alichosema Miss Christine tunapaswa kujua kwanini una majina mengi na pia kwanini unafahamiana sana na watu wengi”Aliongea Bandina kwa sauti ya chini kidogo na kumfanya Roma ambaye alikuwa akila kwa spidi zote wakishindana na Lanlani kupunguza spidi na kumwangalia mama yake.

“Kuna stori ndefu sana kuhusu mimi na hata niwaambie hapa mambo mengine mtayaona hayawezekani na ni kama hadithi, siku ikifika nitawaeleza mkiwa mnaangalia na Ushahidi”Aliongea Roma na jibu lake lilionekana kueleweka kwa wote , lakini hawakuridhika , lakini kwasababu Roma ashasema ni Habari ndefu basi hawakutaka kulazimisha na Edna mwenyewe alipumua kwa ahueni mara baada ya Roma kuongea maneno hayo.

Ukweli upande wa Edna licha ya kwamba alitamani kuijua historia ya Roma ya Maisha yake ya nyuma , lakini upande mwingine ulikuwa na hofi kujua yote , yaani alitamani aishi hivyo hivyo na asijue kitu , lakini pia upande mwingine ulikuwa ukimwambia kwamba anapaswa kujua kila kitu.

Roma ndio aliebeba jukumu la kuondoka na Christine asubuhi hio , huku Christine akiaga kwamba anaelekea hotelini kwake ambako alipaswa kufikia wakati anakuja hapa Tanzania kwani wasaidizi wake wlaikuwa washafanya maandalizi tayari

“Aphrodite hili swala ambalo tumeongea jana nitalifanyia kazi kwa kushirikiana na The Eagles nataka uwape nafasi ya kufanya uchunguzi ndani ya kampuni yako”Aliongea Roma.

“Hades usiniambie huniamini katika uchunguzi wangu ninaondelea nao?”

“Sio kwamba sikuamini , ila hili swala lishagusa familia yangu moja kwa moja, nataka kuuchimba ukweli kwa haraka na kufahamu kila kitu kabla ya mke wangu kugundua swala hili kwani linaweza kumuathiri”

“Hades naona kila unachokifanya siku hizi lazima mkeo ahusike, umebadilika sana nadhani ulijifunza kwa makosa yako ulioyafanya kwa Seventeen”Aliongea Christine.

“Sitaki kukumbuka mara kwa mara habari za Seventeen , alishakuwa jua lililozama kwenye Maisha yangu na ataishi pekee kwenye kumbukumbu zangu”

“Hades hivi unaamini Seventeen alikufa kweli?”Aliuliza Christine na kumfanya Roma kupunguza mwendo wa gari.

“Kwanini unauliza swali la namna hio , wakati unaelewa kila kitu”

“Nashindwa kuamini kwa uwezo aliokuwa nao Seventeen kufa kifo cha namna ile”Aliongea na kumfanya Roma kufikitia kidogo , ni kweli Seventeen alikuwa na uwezo wa ajabu sana na walikuwa wamepishana sana kimbinu likija swala la ‘martial Art’ , pamoja na mbinu za kijeshi , lakini Roma kwa alivyoweza kujihisi kwamba kama yeye mwenyewe anaweza kufa hivyo pia aliamini pia kwa Seventeen anaweza kufa , pia jambo ambalo lilimfanya kuamini kifo cha Seventeen ni uhusikaji wa kundi la Dhoruba nyekundu.

Roma alimfikisha Christine hotelini , huku wakiwa wamekubaliana Roma kuanza uchunguzi wa namna ilivyotokea mpaka Raheli Adebayo akahusishwa kwenye majaribio yaliokuwa yakihusiana na Kimiminika ambacho kiliaminika kufufua maiti.

Baada ya kumshusha hotelini hapo , maeneo ya Serena Hoteli , moja kwa moja aliendesha gari lake kuelekea Kivukoni kwa ajili ya kuvuka upande wa pili, huku kwenye akili yake akidhamiria Kwenda kuonana na kikosi chake cha The Eagles , kwani muda huo aliamini walikuwa kwenye majonzi ya kufiwa na mwenzao , hivyo ilikuwa jukumu lake Kwenda kuwapa pole.

Wakati akiendelea na safari simu yake ilianza kuita mfululizo na kumfanya kuendesha gari na mkono moja na kuipokea.

“Roma usiniambie hutaki kunitembelea babu yako kabisa na kumleta mkeo nyumbani?”Ilisikika sauti upande wa pili ya mtu mzima.

“Wewe mzee unanilazimisha sana nije nyumbani kwako , licha ya mimi kutokuona sababu ya kufanya hivyo , nitakuja ukiwa unakaribia kufa”Aliongea Roma kwa kejeli.

“Mjinga sana wewe mtoto, najua unauwezo mkubwa na unaweza kujitegemea kwa kila kitu , lakini huwezi kuikimbia Asili yako ,Anyway kama hutaki kuja kunitembelea kwa hiari yako nitakufanya uje mwenyewe”Aliongea Mzee Kweka.

“Mzee una mbinu gani ambayo unaamini unaweza kunishawishi?”

“Mr Roma Hongera kwa kuingia level namba tisa ya mafunzo yetu ya kimapigano ya kijini…”Ilisikika sauti ya mwanamke na hapo hapo Roma alimtambua huyo mwanamke , alikuwa ni Zenzhei mwanamke jamii ya majini kutoka koo za Hongmeng China.

Sasa kitendo cha Zenzhei kumpa Roma hongera ya kuingia levo namba tisa , alichanganyikiwa kwani hajakutana na Zenzhei na swali likaibuka , amefahamu vipi kama ameingia levo namba tisa.

“Umefahamu vipi nimeingia levo namba tisa, sidhani kama tushawahi kukutana , lakini pia sifikirii kwamba una uwezo wa kuangalia uwezo wangu nikiwa mbali”

“Mr Roma kuna siri kubwa sana kuhusu namna ya kutumia Nishati na nguvu za asili za ‘Heavean and Earth’ ambazo sisi majini hutumia mara nyingi, napanga kukueleza kama utakubaliana na masharti ya Camilius”Aliongea Zenzhei.

“Vipi Hades bado hutaki kuja kunisalimia babu yako?”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kwanza kuangalia mbele , kwani alikuwaakiendesha gari muda huo na alikuwa akikaribia eneo la kivukoni , sehemu ya kulipia ushuru.

“Tuseme umeshinda mzee , nitakuja”

“Hahahaha….. halafu sitaki uje mwenyewe nataka uje Pamoja na Edna , halafu pia nimesikia mnaishi na katoto kadogo hivi kazuri mnakotarajia kukalea ,kabla hamjafanya maamuzi nataka pia kuonana nae”Aliongea Afande Kweka kwa bashasha huku akijihisi mshindi na Roma alifikiria kidogo na kuanza kumkumbuka Lanlan na kwa masharti hayo aliona sio magumu kwanza hata hivyo Afande kweka ni familia yake na mwisho wa siku hawezi kuikimbia asili.

“Okey kwasababu nahitaji kuongea na Zenzhei nitafika , lakini siku nyingine usifikirie kama utaweza kuniwekea mtego na nikaingia wewe mzee”

“Sawa Hades , nakukumbusha tu mimi ndio babu yako Camilius Kweka”

“Sawa Mzee wa kujivunia , ninakata simu naendesha gari”Aliongea Roma na palepale akakata simu.

Baada ya madakika kadhaa tu Roma alikuwa ashafika Kigamboni wanapoishi The Eeagles na ile anakaribia aliona gari nyingine ikiingia ndani ya geti la jumba hilo na aliitambua mara moja.

“Hubby!!”Roma alikumbatiwa na mchepuko wake Rose mara baada ya kushuka kwenye gari.

ALUTA CONTINUARA
WATSAPP NICHEKI 0687151346 NIKUPE MUONGOZO
 
SEHEMU YA 309

Edna alitaka kuleta upinzani mbele ya Roma , lakini Hades ni kama alikuwa ashatarajia kuletewa upinzani, alichokifanya ni kumgeuza Edna na kumwangalia usoni na walijikuta macho yao yakigongana na wote kwa pamoja waliangaliana na kadri sekunde zilivyokuwa zikihesabu ndio sura zao zilivyokuwa zikisogeleana.

Edna mwenyewe alishindwa kujielewa ni kweli alikuwa na hasira na Roma , lakini kwa jinsi alivyokuwa akijisikia alishindwa kujizuia na walijikuta midomo yao ikinasa na kilichoendelea ni kupeana busu nyevu kwa muda mrefu kidogo, huku Edna akiwa amefumba macho na Roma akiwa amekodoa macho , lakini akiwa ulimwengu mwingine.

Roma hisia alizokuwa akizipata wanapokuwa kwenye hali kama hio zilikuwa za tofauti sana na za wanawake wake wengine.

Walirudi kinyume nyume na wote kwa Pamoja wakajikuta wakitia kwenye sofa ambalo lipo humo chumbani na kuendelea kubusiana, Roma hakutaka kuishia kwenye busu tu.

Edna alikuwa amevaa gauni la kulalia(Night Dress) hivyo ilimfanya Roma kupata urahisi wakupenyeza mkono katikati ya mapaja ya mrembo Edna na hapo ni kama alikuwa amegusa penyewe kwani Edna alijihisi shoti za umeme zikisambaa mwili mzima , kiasi cha kupelekea ua lake kujawa na unyevu mwingi.

Edna licha ya kwamba hisia zake zilikuwa mbali na akili yake, lakini mwisho wa dakika kadhaa aliweza kurejewa na akili yake na kumzuia Roma kutokuendelea.

“Nataka nilale”Aliongea Edna huku akijitoa kwenye mwili wa Roma kibabe na kupanda kitandani.

Sasa namna ambavyo Edna alijinasua kwa Roma ilikuwa ni kibabe sana kiasi kwamba Roma alishangaa mwenyewe.

Roma aliweza kujisemea kwamba licha ya Edna na Seventeen kuwa mapacha lakini walikuwa wakitofautiana sana tabia,Seventeen licha ya kwamba hakuwa Romantic lakini akipandishwa hisia zake hawezi kumuacha njiani wala kujinasua kama ilivyo kwa Edna , yaani kwa maneno marahisi ni kwamba Edna alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuzitawala hisia zake kuliko ilivyokuwa kwa Seventeen.

“Wife haujaniuliza mumeo safari ya Japani ilikuwaje?”

“Sina haja ya kujua imekuwaje, najua huna cha maana ulichokuwa unakifanya huko Japani”Aliongea Edna na alionekana kukumbuka swala hilo tena na hasira palepale zlimpanda na alichokifanya ni kuvuta shuka na kujifunika gubi gubi.

Roma aliangalia matendo ya Edna na kusogea karibu ya kitanda.

“Edna mke wangu , hivi unajua ni kiasi gani nakupenda….”

“Anko unamsumbua Lanlan amelala”Roma kabla hajamaliza sentensi yake ilikatishwa na sauti ya Lanlani, sasa hakueleweka Lanlan alikuwa macho muda gani , bali aliongea huku akiwa amefumba macho , yaani hakufumbua macho wakati akiongea na baada ya kuongea kauli hio aliendelea kuuchapa usingizi huku akitafuna tafuna yaani ilikuwa ni kama anaota.

Roma ilimbidi kuondoka ndani ya chumba hiko pasipo kuongea maneno ambayo alikusudia kutaka kuyatamka ,alitamani kumlegeza Edna kidogo na maneno matamu ,lakini Lanlan aliingilia kati.

****

Ni siku nyingine asubuhi Roma alikuwa mezani na wanafamilia wote wakijipatia kifungua kinywa akiwemo Christine.

Edna alikuwa ndio mkimya kuliko wanafamilia wote , wenzake licha ya kwamba walikuwa wakipiga stori za hapa na pale , lakini kwa Edna yeye hakuchangia Zaidi ya kunywa chai taratibu huku pembeni yake akiwepo Lanlan.

“Anko Roma ,kwanini unaitwa Hades?”Swali hilo lilitoka kwa Yezi na kumfanya Roma kumwangalia Yezi na kisha akainua macho yake na kumgeukia Christine na mwanadada huyo aliishia kutingisha mabega.

“Sio Hades tu ana majina mengi , kuna lingine anaitwa mfalme Pluto , Edna unajua kwanini unaitwa Persephone basi jibu ni kwamba Persephone ni mke wa Hades hapo zamani , hivyo wewe kuolewa na Hades umepewa cheo cha Persephone”Alibwabwaja Christine bila ya kumjali Roma aliekuwa akimwangalia kwa macho yasioeleweka yanaashiria nini ndani yake.

“Kwahio Miss Christine, Anko Roma jina lake halisi ni lipi?”

“Jina lake halisi ni Hades au Mfalme Pluto… Oooh! Yes ,najua hajawaeleza kuwa yeye ni mfalme si ndio?”

“Mfalme..!!! wan chi gani?”Sophia alihamaki na haikuwa kwake tu ,hatakwa Blandina mama yake Roma na wanafamilia wengine walijikuta wakiwa kwenye mshangao.

“Christine ukimaliza kupata hiki kifungua kinywa nakupa amri uondoke mara moja nyumbani kwangu, sikutaki ukiwa karibu na familia yangu”

“Malkia Persephone napaswa kufanya nini mfalme Hades ananifukuza nyumbani kwake?”Aliongea Christine kwa kujihurumisha na kumfanya hata Bi Wema asiekuwa akielewa kitu kutabasamu kwa maongezi hayo.

“Miss Christine tueleze Habari za mfalme Pluto tafadhari tunaomba….”Aliongea tena Sophia kwa kubembeleza lakini Christine alimwangalia Roma na hapo ndipo alipokatwa jicho na Roma.

“Jamani niseme nimependa sana familia hii ya mfalme Pluto na natamani kuongeza siku….Hades naamini utaieleza familia yako juu ya majina yako halisi , wanapaswa kujua kwani wote wanaonekana kukujali”Aliongea Christine na kisha akanyanyuka.

“Miss Christine malizia kunywa chai kwanza”Aliongea Bi Wema.

“Nimeshiba jamani asanteni sana”Aliongea Christine.

Ssa unachotakiwa kuelewa ni kwamba Chrisitne alikuwa akitumia lugha ya Kiswahili katika kuwasiliana , mwanzoni hata Edna na wanafamilia wengine walishangazwa na Mzungu huyo kuongea lugha ya Kiswahili kwa ufasaha kwani hata kwenye matamasha yake yote ya uimbaji hakuwahi hata kuonekana akizungumza lugha ya Kiswahili na wanafamilia hawa juzi yake walivyomuliza Christine, alijibu kwamba aliipenda lugha ya Kiswahili ndio maana akajifunza , lakini huo sio ukweli, kwani Christine alidanganya , ukweli ni kwamba Christine alikuwa na uwezo wa kuzungumza lugha nyingi Zaidi takribani ya lugha zote maarufu duniani alikuwa akifahamu kuzizungumza na hilo liliwezekana kutokana na kwamba aliishi miaka mingi Sana hapa Duniani kwa sura tofauti tofauti.

“Roma ni kweli alichosema Miss Christine tunapaswa kujua kwanini una majina mengi na pia kwanini unafahamiana sana na watu wengi”Aliongea Bandina kwa sauti ya chini kidogo na kumfanya Roma ambaye alikuwa akila kwa spidi zote wakishindana na Lanlani kupunguza spidi na kumwangalia mama yake.

“Kuna stori ndefu sana kuhusu mimi na hata niwaambie hapa mambo mengine mtayaona hayawezekani na ni kama hadithi, siku ikifika nitawaeleza mkiwa mnaangalia na Ushahidi”Aliongea Roma na jibu lake lilionekana kueleweka kwa wote , lakini hawakuridhika , lakini kwasababu Roma ashasema ni Habari ndefu basi hawakutaka kulazimisha na Edna mwenyewe alipumua kwa ahueni mara baada ya Roma kuongea maneno hayo.

Ukweli upande wa Edna licha ya kwamba alitamani kuijua historia ya Roma ya Maisha yake ya nyuma , lakini upande mwingine ulikuwa na hofi kujua yote , yaani alitamani aishi hivyo hivyo na asijue kitu , lakini pia upande mwingine ulikuwa ukimwambia kwamba anapaswa kujua kila kitu.

Roma ndio aliebeba jukumu la kuondoka na Christine asubuhi hio , huku Christine akiaga kwamba anaelekea hotelini kwake ambako alipaswa kufikia wakati anakuja hapa Tanzania kwani wasaidizi wake wlaikuwa washafanya maandalizi tayari

“Aphrodite hili swala ambalo tumeongea jana nitalifanyia kazi kwa kushirikiana na The Eagles nataka uwape nafasi ya kufanya uchunguzi ndani ya kampuni yako”Aliongea Roma.

“Hades usiniambie huniamini katika uchunguzi wangu ninaondelea nao?”

“Sio kwamba sikuamini , ila hili swala lishagusa familia yangu moja kwa moja, nataka kuuchimba ukweli kwa haraka na kufahamu kila kitu kabla ya mke wangu kugundua swala hili kwani linaweza kumuathiri”

“Hades naona kila unachokifanya siku hizi lazima mkeo ahusike, umebadilika sana nadhani ulijifunza kwa makosa yako ulioyafanya kwa Seventeen”Aliongea Christine.

“Sitaki kukumbuka mara kwa mara habari za Seventeen , alishakuwa jua lililozama kwenye Maisha yangu na ataishi pekee kwenye kumbukumbu zangu”

“Hades hivi unaamini Seventeen alikufa kweli?”Aliuliza Christine na kumfanya Roma kupunguza mwendo wa gari.

“Kwanini unauliza swali la namna hio , wakati unaelewa kila kitu”

“Nashindwa kuamini kwa uwezo aliokuwa nao Seventeen kufa kifo cha namna ile”Aliongea na kumfanya Roma kufikitia kidogo , ni kweli Seventeen alikuwa na uwezo wa ajabu sana na walikuwa wamepishana sana kimbinu likija swala la ‘martial Art’ , pamoja na mbinu za kijeshi , lakini Roma kwa alivyoweza kujihisi kwamba kama yeye mwenyewe anaweza kufa hivyo pia aliamini pia kwa Seventeen anaweza kufa , pia jambo ambalo lilimfanya kuamini kifo cha Seventeen ni uhusikaji wa kundi la Dhoruba nyekundu.

Roma alimfikisha Christine hotelini , huku wakiwa wamekubaliana Roma kuanza uchunguzi wa namna ilivyotokea mpaka Raheli Adebayo akahusishwa kwenye majaribio yaliokuwa yakihusiana na Kimiminika ambacho kiliaminika kufufua maiti.

Baada ya kumshusha hotelini hapo , maeneo ya Serena Hoteli , moja kwa moja aliendesha gari lake kuelekea Kivukoni kwa ajili ya kuvuka upande wa pili, huku kwenye akili yake akidhamiria Kwenda kuonana na kikosi chake cha The Eagles , kwani muda huo aliamini walikuwa kwenye majonzi ya kufiwa na mwenzao , hivyo ilikuwa jukumu lake Kwenda kuwapa pole.

Wakati akiendelea na safari simu yake ilianza kuita mfululizo na kumfanya kuendesha gari na mkono moja na kuipokea.

“Roma usiniambie hutaki kunitembelea babu yako kabisa na kumleta mkeo nyumbani?”Ilisikika sauti upande wa pili ya mtu mzima.

“Wewe mzee unanilazimisha sana nije nyumbani kwako , licha ya mimi kutokuona sababu ya kufanya hivyo , nitakuja ukiwa unakaribia kufa”Aliongea Roma kwa kejeli.

“Mjinga sana wewe mtoto, najua unauwezo mkubwa na unaweza kujitegemea kwa kila kitu , lakini huwezi kuikimbia Asili yako ,Anyway kama hutaki kuja kunitembelea kwa hiari yako nitakufanya uje mwenyewe”Aliongea Mzee Kweka.

“Mzee una mbinu gani ambayo unaamini unaweza kunishawishi?”

“Mr Roma Hongera kwa kuingia level namba tisa ya mafunzo yetu ya kimapigano ya kijini…”Ilisikika sauti ya mwanamke na hapo hapo Roma alimtambua huyo mwanamke , alikuwa ni Zenzhei mwanamke jamii ya majini kutoka koo za Hongmeng China.

Sasa kitendo cha Zenzhei kumpa Roma hongera ya kuingia levo namba tisa , alichanganyikiwa kwani hajakutana na Zenzhei na swali likaibuka , amefahamu vipi kama ameingia levo namba tisa.

“Umefahamu vipi nimeingia levo namba tisa, sidhani kama tushawahi kukutana , lakini pia sifikirii kwamba una uwezo wa kuangalia uwezo wangu nikiwa mbali”

“Mr Roma kuna siri kubwa sana kuhusu namna ya kutumia Nishati na nguvu za asili za ‘Heavean and Earth’ ambazo sisi majini hutumia mara nyingi, napanga kukueleza kama utakubaliana na masharti ya Camilius”Aliongea Zenzhei.

“Vipi Hades bado hutaki kuja kunisalimia babu yako?”Aliongea Afande Kweka na kumfanya Roma kwanza kuangalia mbele , kwani alikuwaakiendesha gari muda huo na alikuwa akikaribia eneo la kivukoni , sehemu ya kulipia ushuru.

“Tuseme umeshinda mzee , nitakuja”

“Hahahaha….. halafu sitaki uje mwenyewe nataka uje Pamoja na Edna , halafu pia nimesikia mnaishi na katoto kadogo hivi kazuri mnakotarajia kukalea ,kabla hamjafanya maamuzi nataka pia kuonana nae”Aliongea Afande Kweka kwa bashasha huku akijihisi mshindi na Roma alifikiria kidogo na kuanza kumkumbuka Lanlan na kwa masharti hayo aliona sio magumu kwanza hata hivyo Afande kweka ni familia yake na mwisho wa siku hawezi kuikimbia asili.

“Okey kwasababu nahitaji kuongea na Zenzhei nitafika , lakini siku nyingine usifikirie kama utaweza kuniwekea mtego na nikaingia wewe mzee”

“Sawa Hades , nakukumbusha tu mimi ndio babu yako Camilius Kweka”

“Sawa Mzee wa kujivunia , ninakata simu naendesha gari”Aliongea Roma na palepale akakata simu.

Baada ya madakika kadhaa tu Roma alikuwa ashafika Kigamboni wanapoishi The Eeagles na ile anakaribia aliona gari nyingine ikiingia ndani ya geti la jumba hilo na aliitambua mara moja.

“Hubby!!”Roma alikumbatiwa na mchepuko wake Rose mara baada ya kushuka kwenye gari.

ALUTA CONTINUARA
WATSAPP NICHEKI 0687151346 NIKUPE MUONGOZO
Shukrani sana Mkuu
 
mambo yanazidi kuwa mtamu! mambo ni moto mambo ni fire. kama inaisha vile kumbe ndio inaanza. Big up Sir Singanojr. tunakufuatilia mnooo usiache hata nukta ktk simulizi.
 
Back
Top Bottom