singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #1,801
SEHEMU YA 333
Ilipita wiki nzima pasipo ya Edna na Roma kuongeleshana, Edna alijua mambo yake na Roma hivyo hivyo alijua mambo yake.
Roma aliendelea na kazi yake katika kampuni , uwepo wa Amina ndani ya kampuni ulisaidia sana kutokana na uzoefu wa Amina , kazi hio alionekana kuipenda kweli na kilichomfurahisha Zaidi ni Projekti ya Kizazi Nyota.
Umaarufu aliokuwa nao Amina tokea akifanya kazi na kituo cha Habari cha kimataifa BBC, ulimfanya kufatiliwa sana mara baada ya Habari kufikia watu kwamba mrembo huyo anafanya kazi ndani ya kampuni mpya ya habari ya Vexto.
Hata kwa upande wa Daudi na Wendy ambao walikuwa wafanyakazi wa kampuni ya Vexto Media walishindwa kuelewa nini kilitokea mpaka mrembo kama huyu kuja kufanya kwenye kampuni ambayo inaanza , ambayo umaarufu wake bado upo chini, lakini licha ya kujiuliza maswali walikosa majibu ya moja kwa moja na jambo moja ambalo walifanyia hitimisho kwenye vichwa vyao ni kwamba Roman ni mtu mzito na mwenye koneksheni na ndio maana ameweza kumfanya mrembo kama huyu kufanya kazi kwenye kampuni yao mpya.
Naam ni siku ya jumapili sasa siku nne tokea Vexto TV(V-television) kuwa hewani kwenye ving’amuzi vyote, siku hio watu wengi ambao walikuwa ni mashabiki wa muziki walikuwa na hamu ya kushuhudia tukio la kihistoria , tukio la mahojiano ya msanii maarufu duniani yaani Christen.
“Director zimebaki dakika 10 tayari na Miss Christen hajawasili”Aliongea Daudi mara baada ya kuingia kwenye ofisi ya Roma, muda huo ilikuwa ni usiku saa mbili , muda ambao ndio’Interview’ ya Christine ilikuwa ikitarajiwa kufanyika mubashara.
Sasa zilikuwa zimebaki dakika kumi kabla ya muda wa ‘interview’ hio kuanza na Christine mlengwa mkuu wa tukio hilo bado hakuwa amewasili.
Upande wa nje ya jengo hili waandishi wa Habari walikuwa wamefurika kiasi kwamba walinzi walikuwa wakifanya kazi ya ziada kuwazuia watu hao kutokuingia ndani ya uzio.
Maswali mbalimbali yalikuwa yakiulizwa juu ya muda ambao Christine alitarajiwa kuwasili , watu wengi walikuwa na hamu ya kumuona Chrisitjne, sio kwenye runinga bali ana kwa ana na ndio maana wakajaa nje ya jengo wakitarajia ujio wa Chrisitne.
Roma alifikiria kidogo na kisha akageuza kiti chake na kuangalia mazingira ya nje na kuona watu kibao wakiwa wamejaa na kwa hali hio aliamini hata Christne akifika ndani ya eneo hilo itakuwa ngumu kupita , kwani watu walikuwa wameziba njia kila sehemu.
“Daudi huna haja ya kuwa na wasiwasi , Christene atafika hapa muda si mrefu kabla ya muda wa mahojiano kuanza”Aliongea Roma na Daudi licha ya kuwa na wasiwasi , aliitikia kwa kichwa na kisha alitoka kwenye ofisi ya Roma na ile anafunga tu mlango , Roma alijikuta akitabasamu.
“Aphrodite unaweza kujitokeza sasa , wafanyakazi wangu wana wasiwasi utachelewa”Aliongea Roma na kufumba na kufumbua mwanamke mrembo sana alionekana mbele ya Roma.Alikuwa ni Christine ambaye alionekana kupendeza kweli usiku huo.
“Hades nisifie nimependeza”Aliongea Chrisitne kwa kingereza na Roma alitabasamu nakuinuka kwenye kiti chake na kumsogelea Chrisitne karibu.
“Hakuna siku ambayo uliwahi kuniangusha kwenye swala la uvaaji , umependeza Christen”Aliongea Roma kwa tabasamu na Christine alitabasamu.
Hakukuwa na meongzi mengi kwani muda ulikuwa umewadia , Roma aliongozana na Christine kutoka kwenye ofisi yake na ile wanafika nje watu walishangazwa na ujio wa ghafla wa Christine b , jambo hilo lilimfanya hata Daudi kushangaa na kujiuliza mara moja imewezekana vipi mrembo huyo kufika ndani ya muda , tena kwa namna ya Ghalfa , lakini licha ya kuwa na maswali mengi juu ya namna Chrisitne alivyofika , hakutaka kuuliza Zaidi kwani muda huo kitu kilichokuwa kikitegemewa kufanyika ni mahojiano na muda ulikuwa ndio unakaribia na watanzania pamoja na Afrika mashariki kwa ujumla walikuwa wakisubiria kumuona Christine akihojiwa kutokea Tanzania , Vexto Television.
Upande wa Osterbay wanafamilia wote walikuwa sebuleni wakisubiria mahojiano hayo , Blandina , Bi Wema , Yezi , Sophia Lanlan, Qian Xi na Edna wote walikuwa wameketi sebuleni wakiangalia runinga.
“Ni mtangazaji gani anakwenda kuapata nafasi ya kumfanyia Christine mahojiano?”Aliuliza Sophia kwa shauku.
“Hatuwezi kujua kwasababu bado wafanyakazi wa V Tv hatuwahafamu , ila naweza kuotea watakuwa ni wafanyakazi hawa hawa waliozeoeleaka hapa Tanzani” .Aliongea Yezi akimjibu Sophia.
Saa mbili na nusu hatimae mahojiano yalianza rasmi na mtangazaji amaybe alipata nafasi ya kuongoza mahojiano hayo alikuwa ni Amina Kanani , mtangazaji maarufu kutoka shirika la Habari duniani la BBC.
Kila mmoja alishangazwa baada ya Amina kuonekana ndio mtangazaji anaemfanyia Christine mahojiano.
“Mbona mnamshangaa?”Aliuliza Blandina kwa shauku, na Sophia alimwangalia Edna kwa macho flani hivi ya kutaka kuzungumza jambo , kitendo ambacho kilimfanya na Blandina kumwangalia Edna.
“Lanlan twende ukalale , unasinzia”Aliongea Edna akimwamsha Lanlana ambaye alikuwa akisinzia , sasa haikueeweka Edna alikuwa akikimbia mahojiano hayo mara baada ya kugundua mtanganzaji alikuwa ni Amina au Lah.
Wanafamilia hao walishangazwa na Edna kutaka kuondoka hapo kabla hata ya mahojiano hayajaanza rasmi na wote kwa pamoja waligeuza macho na kumwangalia , ukweli hakuna ambae alikuwa akijua kinachoendelea kwani Edna ule uchangamfu aliokuwa nao ulikuwa umepotea kabisa na kati ya watu wote ambao waliokuwa na ufahamu na kile ambacho kimetokea alikuwa ni Sophia peke yake.
Sophia aliapata nafasi ya kuongea na Amina na alijitambulsiha kwa Sophia bila aibu kwamba yeye ni mpenzi wa Roma , jambo ambalo lilimshangaza Sophia.
“Sophia dada yako anasumbuliwa na nini , kuna chochote unafahamu?”Aliuliza Blandina na Sophia aliinua mkono wake na kunyoosha kuelekea kwenye runinga.
“Bro Roma yule ni mwanamke wake mwingine na Sister Edna anafahamu”Aliongea Sophia na kumfanya Blandina kuangalia mwanamke mwenye kupendeza aliekuwa akionekana kwenye Runinga.
“Unamaanisha Amina ana mahusiano na Roma?”Aliuliza Blandina kwa mshangao, ukweli Mama yake Roma alikuwa akimfahamu sana mrembo Amina kwani alishawahi kumuona mara kibao akitangaza taarifa ya Habari na kituo cha BBC , hivyo alikuwa akimtambua , lakini sasa swala la kwamba mwanamke huyo alikuwa akijihusisha kimapenzi na Roma , lilimshangaza kwani lilikuwa jipya kwake.
“Ndio maana Sister Edna hayupo sawa , Miss Amina anafanya kazi kama Sekretary wa Bro”Aliongea Sophia na kufanya wanafamilia hao wote kushangaa kwani lilikuwa jambo jipya kwao.
Blandina alianza kumwangalia mwanamke mrembo aliekuwa kwenye runinga na alijikuta akijiambia kimoyo moyo licha ya kwamba mambo ambayo Roma anafanya yamezidi , lakini mwanamke huyo alikuwa mrembo sana na alijikuta akishindwa kumuelewa mwanae ana kitu gani cha ziada cha kuwafanya wanawake warembo kama hao kumpenda.
Sasa ndio wanaelewa kwanini Edna alikuwa amenuna wiki nzima na hakutaka sana stori kabisa na Roma , kumbe yote yalikuwa ni makosa ya Roma kumuajili mchepuko wake kwenye kampuni , tena kampuni ya mke wake.
“Ila Bro Roma kazidi hata mimi ningekuwa kwenye nafasi ya Sister Edna ningekasirika mno, Siste Edna ni mvumilivu mno, ndio maana hata hawalalai chumba kimoja yote Bro anayasababisha”Alipigilia msumari Yezi kwa hasira na maneno yake yalionekana kuungwa mkono na kila mmoja jambo ambalo kwa upande wa Blandina lilimuumiza ndani kwa ndani kwani aliona ni kama yeye ndio mwenye makosa.
Blandina hata ile hamu ya kuendelea kuangalia rungina ilimwishia na alichokifanya ni kutoka hapo na kupandisha mpaka chumbani kwa Edna , licha ya kwamba hakua akijua namna ya kumfariji Edna kurudi kwenye hali yake ya kawaida , lakini alijiambia anaweza kufanya kitu na Edna akarudi kwenye hali yake ya kawaida.
Edna ukweli alikuwa na hasira sana na mwenyewe alikuwa akijishangaa ni kwanini alikuwa na hasira namna hio , kwani sio kwamba ilikuwa mara ya kwanza kwa Roma kuwa na mwanamke, alishindwa hata kutafsiri hasira zake zilikuwa zikisababishwa na wivu au ni kitu gani, mrembo huyu kwa mara ya kwanza alianza kuwachukia Dorisi, Rose , Neema , Amina na Nasra na wiki hio kazini Edna alikuwa ni mwendo wa amri tu na hakuwa na utani hata kidogo jambo ambalo liliwafanya warembo hao wawili kushangaa, mabadiliko ya bosi wao.
“Mama utanisamehe ila nadhani yatanishinda”Aliongea Edna mara baada ya Blandina kuingia kwenye chumba hiko cha mke mwana.
“Edna unamaanisha nini yatakushinda?”Aliuliza Blandina kwa mshangao huku akiomba kile ambacho anakiwazia kisiwe kweli.
“Kama Roma akiendelea hivi nitaachana nae kwa talaka, siwezi kuendelea nae hivi”Aliongea Edna na kuketi kwenye sofa huku macho yake yakionekana kujawa na machozi , kitendo ambacho kilimfanya Blandina amsogelea haraka haraka na kumkumbatia na Edna alianza kulia kwa kwikwi.
“Edna mwanangu usiwe hivi , nitaongea na Roma naomba uvumilie niachie swala hili mimi…”Blandina moyo wake ulikuwa ukiuma , aliona hata kama ni yeye angekuwa kwenye nafasi ya Edna basi huenda angekuwa ashakata tamaa , kwani anachokifanya Roma kilikuwa hakikubaliki kabisa kwa tamaduni za kitanzania..
Edna mwenyewe hakuwa akijielewa ni nini kinamtokea ukweli wiki kadhaa zilizipita alijiona kwamba anaweza kumvumilia Roma kuwa na wanawake wengine , lakini alivyorudi Japani alijihisi ni kama kuna mabadiliko makubwa kwenye mwili wake kiasi cha kumpelekea kutotaka kabisa kumuona Roma na mwanamke mwingine na aliweza kuhisi hali hio alivyoweza kuwafumania Amina na Roma..
Saa tano kamili za usiku ndio muda ambao Roma aliweza kurudi kutoka kazini na hio ni mara baada ya mahojiano kumalizika , Roma baada ya kushuka kwenye gari , alishangaa kuona mpaka muda huo taa za sebuleni bado zilikuwa zinawaka , alitembea mpaka sebuleni na hapo ndipo aliposhangazwa kumkuta mama yake ambaye alionekana ikuwa amesinzia kwenye sofa.
“Mama mbona hujaenda kulala mpaka muda huu ?”Aliuliza Roma akimwangalia mama yake.
“Nilikuwa nakusubiria urudi , vipi huko ushakula , ngoja nikakupashie chakula moto”Aliongea huku akinyanyuka ila Roma alimzuia.
“Nitaenda kuchukua mwenyewe mama wewe nenda ukalale sawa”Aliongea Roma huku akielekea upande wa jikoni kwa ajili yakutafuta chakula , alikuwa na njaa ndio maana kwani tokea apate chakula cha mchana akuweza kula chakula kingine.
Roma hakuwa na haja ya kupasha chakula yeye alijipakulia kama vilivyo na kutoka nacho, lakini mama yake aliemwambia kwamba aende kulala bado alikuwa hajaenda na alionekana alikuwa akimsubiri.
“Mama mbona unaonekana kuwa na wasiwasi?”Aliuliza Roma.
“Nina wasiwasi na mkeo Edna..”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa.
“Mke wangu anashida gani?”Aliuliza Roma huku akikaa kwenye kiti.
“Nilikuwa sijui kinachoendelea mpaka usiku wa leo Sophia alivyoeleza kinachoendelea..”Roma alijikuta akimwangalia Mama yake , alikuta akishangaa ni kipi kinachoendelea , ukweli swala la kufumaniwa alikuwa ashalipotezea, licha ya kwamba Edna hakuwa kiongea nae alijiambia hasira zikishuka atarudi kuwa sawa tu , kama ilivyokuwa kawaida yake.
“Edna mkeo anafikiria talaka “Aliongea Blandina kwa sauti ya upole na kumfanya Roma kuweka kijiko chini , alikuwa ni kama hajasikia vizuri.
“Mama aliesema hivyo ni Edna?”
“Roma nishakuelezea fanya mambo yako lakini usimfanye Edna akakosa uvumilivu, nimekusubiria hapa ili nipate kujua unachowaza, kama upo tayari kuachana na Edna na kuoa moja ya wanawake wako mimi sina pingamizi , ila sitaki kuona haya Maisha mnayoishi wewe na Edna yanaendelea ni bora muachane tu , wanandoa gani hamlali chumba kimoja”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kufikiria.
“Mama nitaongea kesho na Edna, kuhusu mimi kumuacha Edna na kumuoa mwanamke mwingine hicho kitu hakiwezi kutokea”Aliongea Roma na Blandina alivuta pumzi na kuzitoa kwa wakati mmoja.
“Sawa kesho hakikisha unayamaliza na amani irudi”Roma ilbidi kuitkia kwa kichwa huku akiendelea kula.
Asubuhi Roma aliamka mapema na Kwenda mpaka kwenye chumba cha mazoezi huku akili yake ikiwaza namna ya kuyamaliza na Edna , ukweli hakuelewa ni kwa namna gani anaweza kumrudisha Edna kwenye hali yake.
Roma baada ya kumaliza kuchukua mazoezi alirudi chumbani kwake na kuoga kwa ajili ya kuelekea kazini asubuhi , hio kwani ilikuwa ni jumatatu.
“Sophia Edna yuko wapi?”Aliuliza Roma mara baada ya kukuta kiti cha Edna kikiwa tupu jambo ambalo Roma hakuwa amelizoea kwani muda wa asubuhi kama huo Edna angekuwa pembeni ya Lanlan.
“Mama yake Lanlan kaenda kazini na amesema akirudi ataniletea mdoli unaofanana na Tembo”Aliongea Lanlan na kumfanya Roma kidogo kuwaza na kisha kuketi kwenye kiti, alijikuta akimwangalia Lanlan na kuishia kutabasamu , siku zote Lanlan akiwa anakula hakuwa akitaka utani kabisa yaani hakutaka hata kuongea, lakini swala ambalo linamuhusu mama yake likiongelewa atasikiliza kwa umakini.
Mashindano yalikuwa yakitarajiwa kuanza rasmi siku ya kesho , kwahio Roma alikuwa ni lazima aende kwanza kazini , lakini bado akili yake haikuwa sawa kwani bado hakuwa ameonana na Edna na wakaongea kuyamaliza , hivyo Roma aliona jambo la kwanza asubuhi hio kwanza ni Kwenda Posta kumuona Edna kwanza.
Roma baada ya kumaliza kunywa chai alimchukua Sophia na kumpeleka mpaka kwenye jengo la kampuni.
“Bro mbona haushuki?”Aliuliza Sophia baada ya kumuona Roma hashuki.
“Sophia wewe nenda kachukue mazoezi , kesho ni siku yako kuonyesha kipaji , ngoja kwanza niende kuonana na Mke wangu”.
“Eti ‘ Mke wangu’, ujitahidi sasa , maana Sister Edna anaonekana kukasirika kweli , najikuta muda mwingine namuonea huruma kama mwanamke mwenzake , anyway Goodluck”Aliongea Sophia na kisha aliondoka kuelekea ndani ya jengo huku Roma yeye akigeuza gari.
Dakika chache tu Roma aliweza kufika kwenye jengo la kampuni na baada ya kuegesha gari moja kwa moja aliingia ndani ya jengo hilo , alikuwa na wiki kadhaa hakuwa amefika kwenye hilo jengo na ilifanya wanawake wengi kumwangalia kwa macho ya husuda na Roma alitambua kwanini walikuwa wakimwangalia , ujio wa Christine ulifanya wafanyakazi wengi kujiuliza Roma aliwezaje kumualika mtu mzito kama huyo, ndio maana walionekana kujiuliza maswali , lakini kumuheshimu kwa wakati mmoja.
“Miss Airport za siku nyingi?”Alisalimia Roma mara baada ya kumfikia Sekretary wa Edna na baada ya Monica kumuona Roma alijjifanyisha yuko bize na kazi zake , yaani alikuwa nikama hakumuona, ila Roma hakujali alinyoosha moja kwa moja kuusogelea mlango wa kuingia kwenye ofisi ya Edna.
“Boss hayupo”Aliongea Monica kwa sauti kavu na kumfanya Roma kugeuka na kumwangalia.
“Kaenda wapi nina shida nae”
“Wewe jua tu hayupo acha maswali mengi”Alijibu kwa kejeli na kumfanya Roma kumsogelea.
“Kama hutaki kuniambia basi nitamsubiri ndani ya ofisi yake “Aliongea Roma huku akiurudia mlango.
“Kaenda uwanja wa ndege kuna mgeni wake muhimu amesema anakwenda kumpokea”Aliongea Monica huku akimwangalia Roma kwa macho makavu.
“Airport , yeye mwenyewe?”Aliuliza Roma , ukweli alishangaa ni mgeni gani ambaye Edna kaenda kumpokea yeye mwenyewe na sio dereva wa kampuni.
“Mbona una maswali mengi hivyo , nishakupa jibu unaweza kuondoka”Aliongea.
“Kandoka saa ngapi?”Aliuliza Roma na kumfanya Monica kumwangalia kwa mara nyingine.
“Hata dakika kumi hazijaisha tokea aondoke”Aliongea na Roma hakuendelea kusimama hapo , alipiga hatua kuondoka na kuingia kwenye lift , huku akili yake ikipata moto ni mgeni gani ambaye amemtoa Edna ofisini na Kwenda kumpokea.
Roma akili yake ilimwambia aende huko huko Airport, alijiambia kwasabau Edna alitoka ndani ya dakika Zaidi ya kumi na tano zilizopita basi ni rahisi kumkumkuta njiani.
Na ni kweli dani ya dakika therathini tu hivi baada ya kuendesha gari kwa spidi hatimae aliweza kuona Mercedenz Benz ya Edna ikisonga taratibu taratibu , Roma alitabasamu na kupunguza mwendo.
Baada ya dakika kama ishirini hatimae Roma aliweza kufika uwanja wa ndege na hio ni baada ya kama dakika tano ya Edna kufika , Sasa ile Roma anashuka kwenye gari , alimuona Edna mita kadhaa mbele yake akimkimbilia mwanaume mmoja wa kizungu na wakakumbatiana kwa furaha kubwa.
Roma ni kama hakuamini macho yake , kwani hakutegemea hata siku moja kumuona Edna kumkimbilia mwanaume na kumkumbatia kwa furaha kiasi kile.
Ilipita wiki nzima pasipo ya Edna na Roma kuongeleshana, Edna alijua mambo yake na Roma hivyo hivyo alijua mambo yake.
Roma aliendelea na kazi yake katika kampuni , uwepo wa Amina ndani ya kampuni ulisaidia sana kutokana na uzoefu wa Amina , kazi hio alionekana kuipenda kweli na kilichomfurahisha Zaidi ni Projekti ya Kizazi Nyota.
Umaarufu aliokuwa nao Amina tokea akifanya kazi na kituo cha Habari cha kimataifa BBC, ulimfanya kufatiliwa sana mara baada ya Habari kufikia watu kwamba mrembo huyo anafanya kazi ndani ya kampuni mpya ya habari ya Vexto.
Hata kwa upande wa Daudi na Wendy ambao walikuwa wafanyakazi wa kampuni ya Vexto Media walishindwa kuelewa nini kilitokea mpaka mrembo kama huyu kuja kufanya kwenye kampuni ambayo inaanza , ambayo umaarufu wake bado upo chini, lakini licha ya kujiuliza maswali walikosa majibu ya moja kwa moja na jambo moja ambalo walifanyia hitimisho kwenye vichwa vyao ni kwamba Roman ni mtu mzito na mwenye koneksheni na ndio maana ameweza kumfanya mrembo kama huyu kufanya kazi kwenye kampuni yao mpya.
Naam ni siku ya jumapili sasa siku nne tokea Vexto TV(V-television) kuwa hewani kwenye ving’amuzi vyote, siku hio watu wengi ambao walikuwa ni mashabiki wa muziki walikuwa na hamu ya kushuhudia tukio la kihistoria , tukio la mahojiano ya msanii maarufu duniani yaani Christen.
“Director zimebaki dakika 10 tayari na Miss Christen hajawasili”Aliongea Daudi mara baada ya kuingia kwenye ofisi ya Roma, muda huo ilikuwa ni usiku saa mbili , muda ambao ndio’Interview’ ya Christine ilikuwa ikitarajiwa kufanyika mubashara.
Sasa zilikuwa zimebaki dakika kumi kabla ya muda wa ‘interview’ hio kuanza na Christine mlengwa mkuu wa tukio hilo bado hakuwa amewasili.
Upande wa nje ya jengo hili waandishi wa Habari walikuwa wamefurika kiasi kwamba walinzi walikuwa wakifanya kazi ya ziada kuwazuia watu hao kutokuingia ndani ya uzio.
Maswali mbalimbali yalikuwa yakiulizwa juu ya muda ambao Christine alitarajiwa kuwasili , watu wengi walikuwa na hamu ya kumuona Chrisitjne, sio kwenye runinga bali ana kwa ana na ndio maana wakajaa nje ya jengo wakitarajia ujio wa Chrisitne.
Roma alifikiria kidogo na kisha akageuza kiti chake na kuangalia mazingira ya nje na kuona watu kibao wakiwa wamejaa na kwa hali hio aliamini hata Christne akifika ndani ya eneo hilo itakuwa ngumu kupita , kwani watu walikuwa wameziba njia kila sehemu.
“Daudi huna haja ya kuwa na wasiwasi , Christene atafika hapa muda si mrefu kabla ya muda wa mahojiano kuanza”Aliongea Roma na Daudi licha ya kuwa na wasiwasi , aliitikia kwa kichwa na kisha alitoka kwenye ofisi ya Roma na ile anafunga tu mlango , Roma alijikuta akitabasamu.
“Aphrodite unaweza kujitokeza sasa , wafanyakazi wangu wana wasiwasi utachelewa”Aliongea Roma na kufumba na kufumbua mwanamke mrembo sana alionekana mbele ya Roma.Alikuwa ni Christine ambaye alionekana kupendeza kweli usiku huo.
“Hades nisifie nimependeza”Aliongea Chrisitne kwa kingereza na Roma alitabasamu nakuinuka kwenye kiti chake na kumsogelea Chrisitne karibu.
“Hakuna siku ambayo uliwahi kuniangusha kwenye swala la uvaaji , umependeza Christen”Aliongea Roma kwa tabasamu na Christine alitabasamu.
Hakukuwa na meongzi mengi kwani muda ulikuwa umewadia , Roma aliongozana na Christine kutoka kwenye ofisi yake na ile wanafika nje watu walishangazwa na ujio wa ghafla wa Christine b , jambo hilo lilimfanya hata Daudi kushangaa na kujiuliza mara moja imewezekana vipi mrembo huyo kufika ndani ya muda , tena kwa namna ya Ghalfa , lakini licha ya kuwa na maswali mengi juu ya namna Chrisitne alivyofika , hakutaka kuuliza Zaidi kwani muda huo kitu kilichokuwa kikitegemewa kufanyika ni mahojiano na muda ulikuwa ndio unakaribia na watanzania pamoja na Afrika mashariki kwa ujumla walikuwa wakisubiria kumuona Christine akihojiwa kutokea Tanzania , Vexto Television.
Upande wa Osterbay wanafamilia wote walikuwa sebuleni wakisubiria mahojiano hayo , Blandina , Bi Wema , Yezi , Sophia Lanlan, Qian Xi na Edna wote walikuwa wameketi sebuleni wakiangalia runinga.
“Ni mtangazaji gani anakwenda kuapata nafasi ya kumfanyia Christine mahojiano?”Aliuliza Sophia kwa shauku.
“Hatuwezi kujua kwasababu bado wafanyakazi wa V Tv hatuwahafamu , ila naweza kuotea watakuwa ni wafanyakazi hawa hawa waliozeoeleaka hapa Tanzani” .Aliongea Yezi akimjibu Sophia.
Saa mbili na nusu hatimae mahojiano yalianza rasmi na mtangazaji amaybe alipata nafasi ya kuongoza mahojiano hayo alikuwa ni Amina Kanani , mtangazaji maarufu kutoka shirika la Habari duniani la BBC.
Kila mmoja alishangazwa baada ya Amina kuonekana ndio mtangazaji anaemfanyia Christine mahojiano.
“Mbona mnamshangaa?”Aliuliza Blandina kwa shauku, na Sophia alimwangalia Edna kwa macho flani hivi ya kutaka kuzungumza jambo , kitendo ambacho kilimfanya na Blandina kumwangalia Edna.
“Lanlan twende ukalale , unasinzia”Aliongea Edna akimwamsha Lanlana ambaye alikuwa akisinzia , sasa haikueeweka Edna alikuwa akikimbia mahojiano hayo mara baada ya kugundua mtanganzaji alikuwa ni Amina au Lah.
Wanafamilia hao walishangazwa na Edna kutaka kuondoka hapo kabla hata ya mahojiano hayajaanza rasmi na wote kwa pamoja waligeuza macho na kumwangalia , ukweli hakuna ambae alikuwa akijua kinachoendelea kwani Edna ule uchangamfu aliokuwa nao ulikuwa umepotea kabisa na kati ya watu wote ambao waliokuwa na ufahamu na kile ambacho kimetokea alikuwa ni Sophia peke yake.
Sophia aliapata nafasi ya kuongea na Amina na alijitambulsiha kwa Sophia bila aibu kwamba yeye ni mpenzi wa Roma , jambo ambalo lilimshangaza Sophia.
“Sophia dada yako anasumbuliwa na nini , kuna chochote unafahamu?”Aliuliza Blandina na Sophia aliinua mkono wake na kunyoosha kuelekea kwenye runinga.
“Bro Roma yule ni mwanamke wake mwingine na Sister Edna anafahamu”Aliongea Sophia na kumfanya Blandina kuangalia mwanamke mwenye kupendeza aliekuwa akionekana kwenye Runinga.
“Unamaanisha Amina ana mahusiano na Roma?”Aliuliza Blandina kwa mshangao, ukweli Mama yake Roma alikuwa akimfahamu sana mrembo Amina kwani alishawahi kumuona mara kibao akitangaza taarifa ya Habari na kituo cha BBC , hivyo alikuwa akimtambua , lakini sasa swala la kwamba mwanamke huyo alikuwa akijihusisha kimapenzi na Roma , lilimshangaza kwani lilikuwa jipya kwake.
“Ndio maana Sister Edna hayupo sawa , Miss Amina anafanya kazi kama Sekretary wa Bro”Aliongea Sophia na kufanya wanafamilia hao wote kushangaa kwani lilikuwa jambo jipya kwao.
Blandina alianza kumwangalia mwanamke mrembo aliekuwa kwenye runinga na alijikuta akijiambia kimoyo moyo licha ya kwamba mambo ambayo Roma anafanya yamezidi , lakini mwanamke huyo alikuwa mrembo sana na alijikuta akishindwa kumuelewa mwanae ana kitu gani cha ziada cha kuwafanya wanawake warembo kama hao kumpenda.
Sasa ndio wanaelewa kwanini Edna alikuwa amenuna wiki nzima na hakutaka sana stori kabisa na Roma , kumbe yote yalikuwa ni makosa ya Roma kumuajili mchepuko wake kwenye kampuni , tena kampuni ya mke wake.
“Ila Bro Roma kazidi hata mimi ningekuwa kwenye nafasi ya Sister Edna ningekasirika mno, Siste Edna ni mvumilivu mno, ndio maana hata hawalalai chumba kimoja yote Bro anayasababisha”Alipigilia msumari Yezi kwa hasira na maneno yake yalionekana kuungwa mkono na kila mmoja jambo ambalo kwa upande wa Blandina lilimuumiza ndani kwa ndani kwani aliona ni kama yeye ndio mwenye makosa.
Blandina hata ile hamu ya kuendelea kuangalia rungina ilimwishia na alichokifanya ni kutoka hapo na kupandisha mpaka chumbani kwa Edna , licha ya kwamba hakua akijua namna ya kumfariji Edna kurudi kwenye hali yake ya kawaida , lakini alijiambia anaweza kufanya kitu na Edna akarudi kwenye hali yake ya kawaida.
Edna ukweli alikuwa na hasira sana na mwenyewe alikuwa akijishangaa ni kwanini alikuwa na hasira namna hio , kwani sio kwamba ilikuwa mara ya kwanza kwa Roma kuwa na mwanamke, alishindwa hata kutafsiri hasira zake zilikuwa zikisababishwa na wivu au ni kitu gani, mrembo huyu kwa mara ya kwanza alianza kuwachukia Dorisi, Rose , Neema , Amina na Nasra na wiki hio kazini Edna alikuwa ni mwendo wa amri tu na hakuwa na utani hata kidogo jambo ambalo liliwafanya warembo hao wawili kushangaa, mabadiliko ya bosi wao.
“Mama utanisamehe ila nadhani yatanishinda”Aliongea Edna mara baada ya Blandina kuingia kwenye chumba hiko cha mke mwana.
“Edna unamaanisha nini yatakushinda?”Aliuliza Blandina kwa mshangao huku akiomba kile ambacho anakiwazia kisiwe kweli.
“Kama Roma akiendelea hivi nitaachana nae kwa talaka, siwezi kuendelea nae hivi”Aliongea Edna na kuketi kwenye sofa huku macho yake yakionekana kujawa na machozi , kitendo ambacho kilimfanya Blandina amsogelea haraka haraka na kumkumbatia na Edna alianza kulia kwa kwikwi.
“Edna mwanangu usiwe hivi , nitaongea na Roma naomba uvumilie niachie swala hili mimi…”Blandina moyo wake ulikuwa ukiuma , aliona hata kama ni yeye angekuwa kwenye nafasi ya Edna basi huenda angekuwa ashakata tamaa , kwani anachokifanya Roma kilikuwa hakikubaliki kabisa kwa tamaduni za kitanzania..
Edna mwenyewe hakuwa akijielewa ni nini kinamtokea ukweli wiki kadhaa zilizipita alijiona kwamba anaweza kumvumilia Roma kuwa na wanawake wengine , lakini alivyorudi Japani alijihisi ni kama kuna mabadiliko makubwa kwenye mwili wake kiasi cha kumpelekea kutotaka kabisa kumuona Roma na mwanamke mwingine na aliweza kuhisi hali hio alivyoweza kuwafumania Amina na Roma..
Saa tano kamili za usiku ndio muda ambao Roma aliweza kurudi kutoka kazini na hio ni mara baada ya mahojiano kumalizika , Roma baada ya kushuka kwenye gari , alishangaa kuona mpaka muda huo taa za sebuleni bado zilikuwa zinawaka , alitembea mpaka sebuleni na hapo ndipo aliposhangazwa kumkuta mama yake ambaye alionekana ikuwa amesinzia kwenye sofa.
“Mama mbona hujaenda kulala mpaka muda huu ?”Aliuliza Roma akimwangalia mama yake.
“Nilikuwa nakusubiria urudi , vipi huko ushakula , ngoja nikakupashie chakula moto”Aliongea huku akinyanyuka ila Roma alimzuia.
“Nitaenda kuchukua mwenyewe mama wewe nenda ukalale sawa”Aliongea Roma huku akielekea upande wa jikoni kwa ajili yakutafuta chakula , alikuwa na njaa ndio maana kwani tokea apate chakula cha mchana akuweza kula chakula kingine.
Roma hakuwa na haja ya kupasha chakula yeye alijipakulia kama vilivyo na kutoka nacho, lakini mama yake aliemwambia kwamba aende kulala bado alikuwa hajaenda na alionekana alikuwa akimsubiri.
“Mama mbona unaonekana kuwa na wasiwasi?”Aliuliza Roma.
“Nina wasiwasi na mkeo Edna..”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa.
“Mke wangu anashida gani?”Aliuliza Roma huku akikaa kwenye kiti.
“Nilikuwa sijui kinachoendelea mpaka usiku wa leo Sophia alivyoeleza kinachoendelea..”Roma alijikuta akimwangalia Mama yake , alikuta akishangaa ni kipi kinachoendelea , ukweli swala la kufumaniwa alikuwa ashalipotezea, licha ya kwamba Edna hakuwa kiongea nae alijiambia hasira zikishuka atarudi kuwa sawa tu , kama ilivyokuwa kawaida yake.
“Edna mkeo anafikiria talaka “Aliongea Blandina kwa sauti ya upole na kumfanya Roma kuweka kijiko chini , alikuwa ni kama hajasikia vizuri.
“Mama aliesema hivyo ni Edna?”
“Roma nishakuelezea fanya mambo yako lakini usimfanye Edna akakosa uvumilivu, nimekusubiria hapa ili nipate kujua unachowaza, kama upo tayari kuachana na Edna na kuoa moja ya wanawake wako mimi sina pingamizi , ila sitaki kuona haya Maisha mnayoishi wewe na Edna yanaendelea ni bora muachane tu , wanandoa gani hamlali chumba kimoja”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kufikiria.
“Mama nitaongea kesho na Edna, kuhusu mimi kumuacha Edna na kumuoa mwanamke mwingine hicho kitu hakiwezi kutokea”Aliongea Roma na Blandina alivuta pumzi na kuzitoa kwa wakati mmoja.
“Sawa kesho hakikisha unayamaliza na amani irudi”Roma ilbidi kuitkia kwa kichwa huku akiendelea kula.
Asubuhi Roma aliamka mapema na Kwenda mpaka kwenye chumba cha mazoezi huku akili yake ikiwaza namna ya kuyamaliza na Edna , ukweli hakuelewa ni kwa namna gani anaweza kumrudisha Edna kwenye hali yake.
Roma baada ya kumaliza kuchukua mazoezi alirudi chumbani kwake na kuoga kwa ajili ya kuelekea kazini asubuhi , hio kwani ilikuwa ni jumatatu.
“Sophia Edna yuko wapi?”Aliuliza Roma mara baada ya kukuta kiti cha Edna kikiwa tupu jambo ambalo Roma hakuwa amelizoea kwani muda wa asubuhi kama huo Edna angekuwa pembeni ya Lanlan.
“Mama yake Lanlan kaenda kazini na amesema akirudi ataniletea mdoli unaofanana na Tembo”Aliongea Lanlan na kumfanya Roma kidogo kuwaza na kisha kuketi kwenye kiti, alijikuta akimwangalia Lanlan na kuishia kutabasamu , siku zote Lanlan akiwa anakula hakuwa akitaka utani kabisa yaani hakutaka hata kuongea, lakini swala ambalo linamuhusu mama yake likiongelewa atasikiliza kwa umakini.
Mashindano yalikuwa yakitarajiwa kuanza rasmi siku ya kesho , kwahio Roma alikuwa ni lazima aende kwanza kazini , lakini bado akili yake haikuwa sawa kwani bado hakuwa ameonana na Edna na wakaongea kuyamaliza , hivyo Roma aliona jambo la kwanza asubuhi hio kwanza ni Kwenda Posta kumuona Edna kwanza.
Roma baada ya kumaliza kunywa chai alimchukua Sophia na kumpeleka mpaka kwenye jengo la kampuni.
“Bro mbona haushuki?”Aliuliza Sophia baada ya kumuona Roma hashuki.
“Sophia wewe nenda kachukue mazoezi , kesho ni siku yako kuonyesha kipaji , ngoja kwanza niende kuonana na Mke wangu”.
“Eti ‘ Mke wangu’, ujitahidi sasa , maana Sister Edna anaonekana kukasirika kweli , najikuta muda mwingine namuonea huruma kama mwanamke mwenzake , anyway Goodluck”Aliongea Sophia na kisha aliondoka kuelekea ndani ya jengo huku Roma yeye akigeuza gari.
Dakika chache tu Roma aliweza kufika kwenye jengo la kampuni na baada ya kuegesha gari moja kwa moja aliingia ndani ya jengo hilo , alikuwa na wiki kadhaa hakuwa amefika kwenye hilo jengo na ilifanya wanawake wengi kumwangalia kwa macho ya husuda na Roma alitambua kwanini walikuwa wakimwangalia , ujio wa Christine ulifanya wafanyakazi wengi kujiuliza Roma aliwezaje kumualika mtu mzito kama huyo, ndio maana walionekana kujiuliza maswali , lakini kumuheshimu kwa wakati mmoja.
“Miss Airport za siku nyingi?”Alisalimia Roma mara baada ya kumfikia Sekretary wa Edna na baada ya Monica kumuona Roma alijjifanyisha yuko bize na kazi zake , yaani alikuwa nikama hakumuona, ila Roma hakujali alinyoosha moja kwa moja kuusogelea mlango wa kuingia kwenye ofisi ya Edna.
“Boss hayupo”Aliongea Monica kwa sauti kavu na kumfanya Roma kugeuka na kumwangalia.
“Kaenda wapi nina shida nae”
“Wewe jua tu hayupo acha maswali mengi”Alijibu kwa kejeli na kumfanya Roma kumsogelea.
“Kama hutaki kuniambia basi nitamsubiri ndani ya ofisi yake “Aliongea Roma huku akiurudia mlango.
“Kaenda uwanja wa ndege kuna mgeni wake muhimu amesema anakwenda kumpokea”Aliongea Monica huku akimwangalia Roma kwa macho makavu.
“Airport , yeye mwenyewe?”Aliuliza Roma , ukweli alishangaa ni mgeni gani ambaye Edna kaenda kumpokea yeye mwenyewe na sio dereva wa kampuni.
“Mbona una maswali mengi hivyo , nishakupa jibu unaweza kuondoka”Aliongea.
“Kandoka saa ngapi?”Aliuliza Roma na kumfanya Monica kumwangalia kwa mara nyingine.
“Hata dakika kumi hazijaisha tokea aondoke”Aliongea na Roma hakuendelea kusimama hapo , alipiga hatua kuondoka na kuingia kwenye lift , huku akili yake ikipata moto ni mgeni gani ambaye amemtoa Edna ofisini na Kwenda kumpokea.
Roma akili yake ilimwambia aende huko huko Airport, alijiambia kwasabau Edna alitoka ndani ya dakika Zaidi ya kumi na tano zilizopita basi ni rahisi kumkumkuta njiani.
Na ni kweli dani ya dakika therathini tu hivi baada ya kuendesha gari kwa spidi hatimae aliweza kuona Mercedenz Benz ya Edna ikisonga taratibu taratibu , Roma alitabasamu na kupunguza mwendo.
Baada ya dakika kama ishirini hatimae Roma aliweza kufika uwanja wa ndege na hio ni baada ya kama dakika tano ya Edna kufika , Sasa ile Roma anashuka kwenye gari , alimuona Edna mita kadhaa mbele yake akimkimbilia mwanaume mmoja wa kizungu na wakakumbatiana kwa furaha kubwa.
Roma ni kama hakuamini macho yake , kwani hakutegemea hata siku moja kumuona Edna kumkimbilia mwanaume na kumkumbatia kwa furaha kiasi kile.