UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,753
- 12,932
Kana Umusaghane wegero kwetu Hayi wasera sikochino?Murisya
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kana Umusaghane wegero kwetu Hayi wasera sikochino?Murisya
Aseeeh[emoji119]SEASON 04
SEHEMU YA 91
Roma baada ya kusoma kikaratasi kilichokuwa kimeachwa na kundi la Kijapani lililokuwa likifahamika kama Yamata Sect , alin`gata meno kwa hasira.
Alietembea uelekeo wa chumba cha mazoezi na baada tu ya kufika alifungua sehemu ambayo alikuwa ameficha kiboksi alichokuwa ametoka nacho kutoka Mbagala na baada ya kukitoa , alikifungua ndani na akatoa kijiwe flani hivi ambacho kilikuwa na ukubwa wa Goroli , ni jiwe ambalo kwa kuliangalia tu halikuwa lakawaida kabisa , kwani mara baada ya Roma analitoa kwenye kile kiboksi na kupigwa na mwanga wa jua lililotoa mg`ao Flani wa bluu , mg`ao ambao ulikuwa ukiumiza macho.
Roma aliweka kile kijiwe mfukoni na akatoka ndani ya nyumba hii baada ya kufunga vizuri na alianza safari ya kutafuta Mabwepande kama alivyokuwa ameelekezwa ,kutokana na spidi yake ya kuendesha alitumia Zaidi ya dakika arobaini hivi , aliingia ndani ya msitu wa Mabwepande.
Aliegesha gari yake na kisha akasonga mbele kwa mguu kutokana na kwamba barabara ilikuwa imefikia ukomo , alipita nyumba kadhaa chache zilizokuwa ndani ya haya maneo na kutokomea juu kabisa msituni na ile anatembea kwa dakika kama kumi hivi aliweza kuwaoona watu aliokuwa akiwatafuta, walikuwa wapo watatu na wote walikuwa wajapani , wakwanza alikuwa ni Tanya , kulikuwa na Tanuki ambaye Roma alikuwa akimfahamu na mwingine alikuwa akifahamika kwa jina la Tengu,Tanya alionekana akiwa ameketi kwenye gogo huku akiangalia kucha zake.
“Yuko wapi Edna na Bi Wema?”Aliuliza Roma mara baada ya kuwafikia kwa mita kadhaa.
““Your Majesty Pluto, don’t get impatient. If you want to see them, we have to see God’s Stone.”
“God’s Stone is in the pocket of my pants, but I want to ensure the safety of the hostages”(Jiwe la Kimungu lipo kwenye mfuko wangu , nataka kuwaona kwanza ili kuhakiki kama wako salama)
“Hehe”Alicheka Tanuki
“The mighty ‘Beheading of Ten Thousand People’ is indeed worthy of its title. The Death God Hades who has slain countless lives unexpectedly came to negotiate for the life of an ordinary woman using God’s Stone.”
“Mtu mwenye uwezo wa kuua watu Zaidi ya elfu moja,Mungu wa wafu ambaye amechinja na kuua watu wasiohesabika leo hii amekuja kumuokoa mwanamke wa kawaida kwa kutumia Jiwe la kimungu”Aliongea Tanuki kwa kejeli. Na leo alikuwa akitumia kingereza tu.
“Your Majesty Pluto, I really got a bit jealous as a woman myself”
“Mfalme Pluto najukuta mwenyewe kuona wivu kama mwanamke”Aliongea Tanya huku akitabasamu
“Acheni kuongea upuuzi , sijaja kuokoa maisha ya mtu mmoja , mmeteka watu wawili,halafu sio mwanamke wa kawaida kama mnavyodhania”Aliongea Roma huku hasira zikionekana kwenye macho yake
“Usiwe na wasiwasi kama utatupatia Jiwe la kimungu tutakurudishia mwanamke yule mzee, na baada ya kuturuhusu kukimbia kwa umbali wa kilomita moja bila ya kutufukuzia tutakuambia ni wapi mkeo alipo kwa kutumia njia zetu maalumu za kuwasiliana , na usije ukathubutu kutudanganya au kufanya jambo lolote la kijinga , ukifanya hivyo tutahakikisha humuoni mkeo mrembo”Aliongea Tanuki.
“Kwahio mnanitishia?”Aliuliza Roma kwa hasira.
“Mfalme Pluto tunajua kwamba hupendi kutishiwa kwenye maisha yako , tunachokuambia ni jambo jepesi sana , tupatie jiwe umpate mkeo na mpaka sasa muda unaenda na zikipita dakika chache huenda mkeo akapatwa na shida”
Roma alijikuta akipandwa na jaziba sana , aliingiza mkono wake kwenye mfuko , aliona hakuwa na jinsi Zaidi ya kuwapatia kile walichokuwa wanataka , ili amuokoe mke wake
Baada ya kutoa kile kijiwe alichokuja nacho , Tanya , Tengu na Tanuki walijikua wakitoa macho kwa furaha , ukweli ni kwamba licha ya kwamba walikuwa wakisikia kuhusu jiwe la kimungu , lakini hawakuwahi kuliona laivu.
“Mfalme Pluto umekuja nalo kweli .. hahaha tupatie sasa chapu”
“Nataka kumuona kwanza Bi Wema kama yupo salama ndio niwapatie”
“We swear upon the dignity of the warriors in Japan, as long as you give us God’s Stone, we’ll definitely give the two hostages back to you safely”
Tunaapia kwa hadhi ya miungu ya kivita ya kijapani , kama utatupatia hilo jiwe ni uhakika lazima tukurudishie familia yako ikiwa salama”aliongea Tengu.
“Huna haja ya kutaja hadhi ya Miungu ya Japani , sidhani kama mnaijua hata maana ya hio hadhi”Aliongea Roma huku akijiandaa kuwarushia jiwe upande wa Tanuki, lakini wakati ule ule uliskika mvumo wa visu kumpita Roma kwa spidi kuelekea upande wa wale wajapani na , wale wajapani wakavikwepa.
“Wewe ni nani?”Aliongea Tanya kwa sauti na kufanya sauti yake ijirudie rudie kwenye huu msitu na muda huo huo alitokea Ajenti flamingo aliekuwa akihema , alionekana amekuja hapo kwa spidi kweli.
“Ajenti flamingo umekuja kufanya nini?”Aliuliza Roma.
“Nimekuja kukupatia taarifa , Jenerali wa jeshi ameniagiza , usije ukatoa hilo jiwe”
“Wewe na huyo Jenerali wenu hamuwezi kunifanyia maamuzi , jiwe ni la kwangu na nina uhuru wa kufanya maamuzi ninayotaka”Aliongea Roma.
“Ndio Ajenti Flamingo , tunakujua sana kabla ya kuja hapa Tanzania ,na unatakiwa kufikiria vizuri , tunachoongea hapa ni dili la Maisha ya mke wake Hades na Jiwe la Kimungu ni bora ukakaa kimya”Aliongea Tanuki.
“Acha kuongea , unatakiwa uelewe hapa ni Tanzania na sio kama hatuna uwezo wa kuwafanya chochote, Mpo kwenye ardhi yetu msijifanye vijogoo”aliongea Magdalena huku hasira ikionekana kwenye macho yake.
“Unaongea sana mrembo , lakini sidhani kama wewe unamaamuzi , sisi tunaongea na Pluto hapa na yeye ndio atafanya maamuzi ya kuacha familia yake ife au atupatie jiwe la kimungu”Aliongea Tanya na Flamingo akaachana nao na kumuangalia Roma kwa macho ya huruma.
“Hades tulikuwa tunataarifa ya juu ya uwepo wa hilo jiwe hapa nchini na uhatari wake likifikiwa watu mashetani kama hao na tulikuwa tukiamini kwamba hautowapa watu wabaya ,hivyo tunaomba usifanye hivyo , jeshi la Tanzania lina jukumu la kulinda hilo jiwe”
“Magdalena licha ya wewe kuwa mwanajeshi , Edna ni rafiki yako , kwanini unaweka maslahi mbele zidi ya maisha ya mtu”Aliongea Roma
“Naelewa na pia najisikia vibaya , lakini naheshimu sheria za jeshi, na jambo unalotaka kulifanya linahatarisha usalama wa dunia kwa wakati mmoja,Na pia Jenerali Mstaafu Athumani kaniagiza jiwe hilo lisitolewe kwa namna yoyote ile”
Unajua baada ya General Yang kuja Tanzania na kuomba kuundwe kikosi ambacho kitakuwa na kazi ya kulinda jiwe la kimungu ambalo lilikuwa kwenye mikono ya Roma , kikundi hiko kiliundwa na mkuu wa kikundi hiko alikuwa ni jenerali mstaafu Athumani babu yake Edna.
“Hahahaha…Acha kunichekesha ,huyo mzee kwa maelezo ya Edna ni kwamba anataka Edna amuite babu , lakini leo hii anasahau kuwa Edna ni mjukuu wake na anataka kumuacha afe kwa ajili ya kijwe kama hiki ambacho kwanza sio cha kwake na hata hajui kilipotoka”
“Hades Jenerali anafanya haya mambo kwa ajili ya usalama wa raia wa dunia yote , kwanini unashindwa kuona hili , mtu yupo tayari kutoa mjukuu wake kwa ajili ya usalama wa watu wengi”
“Hayo ni juu yenu , mimi Hades siwezi kutoa kafara familia yangu kwa kajiwe kama haka , tena mke wangu , hapana yaani nina uwezo hata kwa kuuza dunia nzima kwa ajili ya kuokoa familia yangu , nyie mnaojiita jeshi kama mnaona ni sawa kwa kutoa familia zenu kwa ajili ya kulinda taifa na usalama wa raia ,sidhani mpaka miaka ijayo mtakuwa na familia, huwezi ukajiita unalinda nchi huku ukishindwa kulinda familia yako , nchi inaanzia kwenye familia , ukiwa na mtu unaempenda utapata hamasa ya kulinda taifa, kwani usalama wa raia unahusisha na familia yako , sasa mnachoongea ninyi ni upuuzi”
“Vyovyote vile Hades nimetuwa hapa kuhakikisha hilo jiwe haulitoi , wanajeshi wetu wanakuja na hawa watu hawatafanikiwa kuondoka”
“A living entrepreneur is far more useless than a dead person to the country,I can’t afford to risk Edna life. I won’t complain to trade this stone for my wife’s life.”Aliongea Roma na kisha akarusha jiwe kwenda kwa Tanuki.
“Hahaha ..Hades wewe unabusara sana”Aliongea Tanuki kwa furaha baada ya jiwe la kimungu kutua kwenye mikono yake.
Ajenti flamingo machozi yalianza kumtoka hakuelewa ni kipi anaenda kueleza wakuu wake juu ya jambo ambalo Roma alikuwa amelifanya.
“Roma kwanini umefanya jambo la kijinga namna hio , ni kweli umewapa hilo jiwe?”
“Magdalena tafahdari naomba usinipigie kelele juu ya hilo jiwe mimi kwangu halina thamani”
“Kwa hio unamaanisha Edna ni muhimu kwako kuliko maisha ya watu wa dunia hii?”Aliongea huku machozi yakimtoka ,alionekana kuwa mwanamke ambaye alikuwa na machozi ya karibu.
“Magdalena ngoja nikwambie , sio Edna tu mwanamke wangu yoyote yule ambaye unamjua wewe ana umuhimu mkubwa kuliko hako kajiwe”
“Hehe….Sikujua Mfalme Pluto unapenda warembo kiasi hiki,Watu unaowatafuta wapo kwenye hii karatasi”Aliongea Tanuki huku akitoa karatasi na kuipuliza na mdomo wake na ikamsogelea Roma na kuidaka.
Na palepale Tanya na Wenzake walitoweka , Magdalena alitaka awkimnbize lakini alishindwa kabisa , aliishia kumwangalia Roma kwa hasira.
Roma baada ya kuangalia ile karatasi alijikuta akitoa matusi , watu ambao alikuwa akiwatafuta walikuwa wapo kulekule kigamboni.
“Hades jenaral atasikitishwa sana na hili jambo , nasema kwamba kwenye jambo la kijinga ulilolifanya ni hii leo , sijui kwanini hata unaitwa Pluto”aliongea Magdalena.
“Acha kunipigia kelele Magdalena na ukiendelea kunisumbua nitakwenda kumuua huyo Jeneral unaenipigia nae kelele”Aliongea Roma na kuondoka.
Roma aliamua kupiga simu kwa The Eagles na kuwapa maelekezo ya sehemu ambapo Edna na Bi Wema walipo ,maana alijua hatopata muda wa kuwafikia kama atataka kuwaokoa yeye mwenyewe.
Chiara na John baada ya kupata maekekezo kutoka kwa Mfalme Pluto waliondoka haraka sana kwenda eneo husika.
Ilikuwa sio mbali sana na eneo la Mbutu , wale wajapani walionekana kukodi kabisa nyumba na walioekana walikuwa hapo kwa muda mrefu kidogo , kwani ndio sehemu ambayo walikuwa wamewaweka Edna na Bi Wema na jambo la kusikitisha ni kwamba walikuwa wamewafunga kwenye Swimming Pool , ambayo haikuwa na maji na wakaachia maji yanayoingia kidogokidogo na kujaa , na kama Roma angechelewa kidogo kuwaifikia Yamata Sect , basi huenda Edna na Bi Wema wangezama kwani mpaka The Eagles wanafika maji yalikuwa yamewafikia kwenye kifua.
Edna baada ya kumuona Mzungu mwanadada, alijikuta moyo wake ukitulia sasa kwani alikuwa na wasiwasi mwingi na mtu aliekuwa akimuonea huruma ni Bi Wema , kwani miguu ishaanza kumvimba tayari kwa ubaridi wa maji.
“Malkia Persephone , Tusamehe kwa kufanya haya yakufikie ni uzembe wetu katika kazi , Mfalme Pluto katuagiza tuje kukuokoa”
Aliongea Chiara kwa heshima na kumchanganya Edna hakujua kwanini anamwita Malkia na hakuelewa huyo mfalme ni nani , na pia hakutaka kuuliza , licha ya kwamba hakuwa na maelezo ya kutosha juu ya Roma kuwa na hawa wazungu ambao walionekana kumfanyia kazi , kwa muda huo alihitaji kutolewa kwenye maji kwanza.
Kilio ha Nasra hata hakinistui, furaha ilioje leo Edna na Roma wanalala room moja na kitanda kimoja[emoji3][emoji3]SEHEMU YA 352.
“Ningependa niseme licha ya kwamba nilikuwa nikitamani kuja Tanzania , nchi hii ambayo imebarikiwa na vitu vingi vya kvutia macho , lakini sikuweza kujua ni siku gani ambayo natakiwa kufanya maamuzi ya kufanya safari mpaka nilipopata mualiko maalumu kutoka kwa rafiki yangu Mr Roma Ramoni”Aliongea Christen na kisha akamsogelea Roma na kumshika mkono na kufanya watu wote kushangazwa na maneno ya Christen juu ya Roma kumwalika Christen Tanzania , watu walianza kunong’ona na kujiuliza Roma ni nani haswa mpaka kuwa na urafiki na msanii mkubwa kama Christen, kwani hata maraisi wengi ndani ya ukanda wa Afrika washawahi kuonekana hadharani wakimualika mrembo huyu kutembelea kwenye nchi zao , lakini Christen hakuwahi kutii mualiko kutokana na ubize , lakini mtu aliekuwa akionekana wa kawaida sana kaweza kumfanya mwanamke huyo kuja Tanzania.
Ukweli Roma hakupenda sana Christen kuongea vile kwani aliona anamfanya kuwa maarufu na yeye hakuwa akipenda umaarufu na hio yote ni kutokana na jina lake , lakini pia historia iliokuwa nyuma ya Maisha yake, lakini hata hivyo hakuwa na uwezo wa kumzuia.
Sasa watu wanafahamu kwamba ujio wa Christen Tanzania uliwezekana kutokana na Roma kumwalika kuja Tanzania , lakini pia wanajua kwamba Roma ni mtu muhimu kwa Christen , lakini jambo moja ambalo wanashindwa kufahamu ni ukaribu ambao upo kati ya malkia wa biashara, Edna na Roma mpaka Chrsiten kuwatambulisha kama watu muhimu kwake.
Ukumbuke ndani ya tukio hili walikuwepo watu wakubwa sana , wakiwemo wafanyabiashara , wasanii wakubwa ndani ya Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla , lakini vile vile walikuwemo wanasiasa wakubwa , lilikuwa tukio kubwa hivyo kila ambaye alikuwa na uwezo wa kulipia kiingilio kuhudhuria aliweza kufika ,tofauti na wale ambao walikuwa na mwaliko maalumu.
“Najua kuna maswali mengi kwanini nimesema watu waliokuwa mbele yenu ni muhimu sana , licha ya alienialika Tanzania ni Mr Roma Ramoni ningeomba Miss Edna kunisaidia , Karibu Miss Edna”Aliongea Christen huku akiweka Tabasamu na kisha akamkabidhi Edna maiki huku akimwinamia sikioni.
“Prove them you are Queen Persephone”Aliongea kwa sauti ya chini aliweza kuisikia Edna na Christine alitoka kwa madaha na kurudi kwenye nafasi yake.
Kusema ukweli Christen ndio ulikuwa mpango wake haikueleweka kwanini alikuwa akifanya hivyo , ila yeye ndio aliweka utaratibu wa Edna kufunga mashindano hayo kama CEO wa kampuni na hata maneno yake ya kumwambia Edna aweke wazi kwanini Roma na yeye ni watu muhimu ulikuwa ni mtego, Christen alikuwa akielewa haikuwa ikifahamika kwa watu wengi kama Edna kaolewa na alitaka kumfanya mwanamke huyo atamke hadharani sasa haikueleweaka kwanini anataka Edna afanye hivyo kwani yeye ni kama wanawake wengine tu ambao walikuwa wakimtaka Roma, ilionekana alikuwa na sababu yake.
“Ladies and Gentlemen , it’s my great pleasure to acknowledge Miss Christen as our guest of honor, who has made significant impact on this project…… ,as you all may know , Miss Christen is a great artist with a busy schedule , but she made the effort and came to Tanzania for the first time , Her presence here is not only a benefit for our company but it also shows her love and commitment to all her fans worldwide ,on behalf of all Tanzanian Fans ,Miss Christen we love and appreciate you very much for coming to Tanzania”
“Mabibi na mabwana , ni furaha kwangu kumtambua Miss Christen kama mgeni wetu wa heshima ambaye ameweza kuleta matokeo chanya kwenye projecti hii, kama mjuavyo Christen ni msanii mkubwa ambaye ana ratiba ya kubana lakini amejitoa na kuja Tanzania kwa mara ya kwanza , uwepo wake hapa sio kwa manufaa ya kampuni tu bali pia ni namna ya kuonyesha mapenzi aliokuwa nayo kwa mashabiki zake wote dunia nzima, Miss Christen tunakupenda na tunashukuru ujio wako hapa Tanzania”Aliongea Edna na makofi mengi yakapigwa na kisha Edna akaendele.
“And also I would like to take a moment to specifically recognize and thank the director of Vexto Media , Mr. Roma Ramoni, his leadership have been instrumental in the success of this event, this is a first successful project of our new branch Company and all appreciation’s goes to all who participated in it”
“Na pia ningependa kuchukua nafasi kumtambua na kumshukuru mkurugenzi wa Vexto Media , Mr Roma Ramoni.. uongozi wake uliotukuka ndio sababu ya mafanikio ya tukio hili.., hii ni projekti ya kwanza ya mafanikio iliofanywa na kampuni tawi letu jipya la kampuni na shukrani ziende kwa wote ambao wamehusika”Aliondelea Edna kuongea , alimshukuru pia mwanadada YoonHe kwa kufika Tanzania , lakini pia kwa wafanyakazi wote pamoja na majaji waliofanikisha mashindano yote, lakini sasa moja ya jambo ambalo liliwaaacha watu kwenye mshangoa ni namna Edna alviyomaliza.
“Mwisho kabisa licha ya kupendelea kuyafanya maisha yangu kuwa binafsi sana , lakini naomba nitumie nafasi hii pia kuweka wazi, Mr Roma Ramoni na mimi ni familia , ni Zaidi ya miezi sita mpaka sasa tokea tufunge ndoa yetu, hivyo kuendeleza alichokisema Miss Christen , ni kweli sisi ni muhimu kwake kama familia, Miss Christen tunakukaribisha muda wowote kwenye familia yetu kwani wewe ni muhimu kwetu sana na Tanzania kwa ujumla”Aliongea Edna na makofi yalipigwa huku watu wasiokuwa wakifahamu kile kinachoendelea kushangazwa na kauli ya Edna na sio watu wa kawaida tu lakini pia mpaka kwa wafanyakazi wa kampuni ya Vexto.
Upande wa Roma kauli hio ilimshangaza sana , kwani hakutegemea kama Edna anaweza kupata ujasiri wa kuweka uhusiano wao wazi mbele ya kadamnasi ya watu wengi namna hio, Roma alimgeukia Edna na kumwangalia usoni na Edna alimwangalia kwa tabasamu na kisha akaendelea na ratiba inayofuata ya ugawaji wa zawadi kwa Sophia.
Edna alimtambulisha pia Sophia kama mdogo wake , jambo ambalo pia liliwashangaza wengi , kwani hakukuwa na ambaye alikuwa akifahamu, ila Edna alitoa sababu kwamba alijaribu kuweka siri ili isionekanae kama Sophia anapendelewa na kampuni katika mashindano hayo.
Baada ya ratiba za ugawaji zawadi kwa mshindi wa kwanza kuisha hatimae washiriki wote tano bora waliweza kusainishwa mkataba na kampuni ya Vexto Media kama wasanii rasmi na kazi zao zote ambao watahitaji kufanya zitakuwa chini ya udhamini wa kampuni ya Vexto Media , kila mtu alipendezwa sana na tukio hilo.
*********
“Mama naomba unisamehe”Ilikuwa ni kauli ya Nasra Kwenda kwa mama yake akimuomba msamaha.
Mama yake na Nasra alijukuta akipagawa mara baada ya kusikia Roma ni mume wa mtu , hakutaka kuamini kama mtoto wake alikuwa akitoka kimapenzi na mume wa mtu , moyo wake ulijikuta ukiuma na kilichomuuma Zaidi ni kwamba Roma hakuwa mume wa mtu tu, bali Roma alikuwa ni mume wa Edna , ambaye wazazi wake ndio walikuwa na mchango mkubwa kwa Maisha ya kimasomo ya mtoto wake Nasra.
Mama Nasra alijikuta akipandwa na Jazba kweli , hakuamini kama Nasra anaweza kumfanyia mwanamke mwenzake kwa kuiba mume wake , alijikuta akijawa na uchungu na alijiambia anakwenda vipi kutoa shukrani kwa familia ya Edna , ilihali mtoto wake amekosa shukrani .
“Nasra licha ya kwamba sijabahatika kukulea kwenye makuzi yako yote , lakini jambo hili siwezi kulikubali kabisa , Nasra hauwezi kumfanyia hivi Edna , familia yake imekusaidia na leo hii una Maisha mazuri kuliko familia yoyote kule kijijjini , kwanini Nasra , kwanini mume wa Edna mbona wanaume wapo wengi sana ndani ya jiji hili, kwanini usichague hao na ukamchagua mume wa mtu?”
“Mama nisamehe , ni kweli nimefanya kosa lakini nampenda sana Roma …”
“Nasra nyamaza , nakuambia nyamaza na sitaki kusikia maneno yako yasio na shukrani sijakulea hivyo mimi na unapaswa kujua ni dhambi”
“Lakini mam..”
“Nasra nisikilize kwa makini , tena nisikilize unielewe , kwanzia leo hii sitaki ujihusishe kabisa na Roma kimapenzi, Nasra Sitaki ujihusishe na mume wa mtu kabisa na ikitokea ukaendelea nae mimi sio mama yako mzazi na umtafute aliekuzaa”Aliongea Mama Nasra , alionekana kuwa na Hasira sana , kwani alikuwa amejaa kwa Jazba.
Nasra alishangazwa na maneno ya mama yake , hakuwahi kumuona mama yake akiwa na hasira hio kwenye Maisha yake yote aliomfahamu , swala la kusema kwamba asimfahamu kama mama kama atakubali kuendelea na Roma ni maneno ambayo hakuwa ameyategemea kama mama yake angeongea.
“Naomba upunguze Jazba mama yangu, ni kweli nimekosea lakini..”
“Nasra nishakueleza , ijapokuwa sijasoma kama wewe lakini najua ulichokifanya sio haki kwa Edna kabisa na unapaswa kumuomba msamaha na kuachana na mume wake , kama haupo Tayari kufanya hivyo nitaenda mimi na kupiga magoti kwa ajili yako , lakini sipo tayari kukuona ukiendelea na mume wa mtu Nasra , nilimkubali Roma kule kijijini kwakua niliamini hakuwa ameoa… Nasraa..”Mama huyu alijikuta akihema kwa nguvu na kukaa kwenye sofa, hasira zilionekana kumzidia.
“Mama naomba unisamehe, naomba unisamehe mama yangu”
“Nasra nitakusemehe kama utaachana na Roma huo ndio msimamo wangu , kama utaniambia haupo tayari kuachana nae kesho nitarudi kijijini na sitoendelea kukutambua kama mwanangu , Nasra chagua moja kabla ya kesho asubuhi”Aliongea Mama Nasra huku akijitahidi kuzuia hasira zake , kwani alisindwa kupumua vizuri.
Nasra alijikuta akiwa kwenye wakati mgumu sana , hakuamini kama mama yake angekuwa hivyo juu ya swala lake na Roma ,siku zote aliamini mama yake angemuelewa kwa maamuzi yake ya kuwa na mahusiano na Roma licha ya kuwa mume wa mtu , lakini sasa anajikuta yupo kwenye mtihani wa kumchagua mama yake au Roma.
Nasra alijikuta alikaa kwenye sofa na kuinamisha kichwa chini na kuanza kulia , lakini hata hivyo kilio chake kwa Mama Nasra hakikumpa shida alichokifanya ni kulala kabisa kwenye sofa, mwanamama huyo hakutaka kabisa kumuona mwanae Nasra anaendelea kuwa na mahusiano na Roma.
Mama Nasra katika Maisha yake alitamani kumuona Nasra akiolewa kwa harusi na mwanaume wa kueleweka na sio kutoka na mume wa mtu na kuwa mchepuko tu na kukosa nafasi ya kuwa mke , Aliona kabisa Nasra anapotea , hivyo hakuwa tayari na aliona asipo simama yeye kama mama basi Nasra hawezi kumsikiliza.
“Wewe lia unavyolia , lakini kama mimi nitaendelea kuwa mama yako sitotaka kukuona ukiendelza mahusiano na mume wa Edna , Nasra sisi ni waislamu na tunafunzwa kuwa na shukrani kwa wale wanaotutendea mema , lakini unachokifanya wewe sio shuktani kabisa , unafikiri Mungu anatuoanaje , siwezi kukubali hili likiendelea , achana na Roma mara moja na kwa uzuri wako naamini utapata mwanaume atakae kupenda na kuanzisha familia”Aliongea na kisha alielekea chumbani akimwacha Nasra sebuleni, akiwa kwenye wakati mgumu.
Unafikiri Nasra atamuacha Roma?”
Ile jumapili ndio leoITAENDELEA JUMAPIL , RAMADAN MUBARAK- MKO NYUMA SANA MBELE KWA MOTO HAYA NITAFUTE WATSAPP 0687151346.
YeapIle jumapili ndio leo
Honde mura Nemaha nkire hakeKana Umusaghane wegero kwetu Hayi wasera sikochino?
Siku hizi Ni once per weekIle jumapili ndio leo
Naona sasa hiv imeshaanza kuwa kipengele
Za asubuh mkuu singanojr ? We lipua tu mkuu! Paragraph sijui herufi kubwa na ndogo! Tutapanga wenyewe huku! Asiejua kukonekti dot apite hivi ===>Nakuwa tu na mizunguko mingi , naweza post kwa simu lakini haijiweki kwa mfumo wa Aya inashonana na inaboa kusoma tusubirie nitaweka mwendelezo
wewe post kaka hayo mengine tuachie sisi.Nakuwa tu na mizunguko mingi , naweza post kwa simu lakini haijiweki kwa mfumo wa Aya inashonana na inaboa kusoma tusubirie nitaweka mwendelezo
tutapambna ivo ivo tuwewe post kaka hayo mengine tuachie sisi.