Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 454.

Mwanaume yule alitoa tabasamu huku akimwangalia Denisi ,lilikuwa tabasamu ambalo liliashilia kuridhika nae.

“Umebadilika sana , Yan Buwen amekufunza vizuri”Aliongea kwa lugha ya kingereza, lakini Denisi maneno yale aliyachukulia kama tusi kwani palepale alimsogelea kwa spidi na kumkwida tai kwa namna ya kumminya.

“Acha kufanya maigizo mbele yangu ,mimi ni tofauti na wewe , nina jitegemea kwenye mambo mengi mwenyewe na kwako wewe…. Unaishi kwasababu ya baba yak”Aliongea Denisi huku akiweka sura yenye usiriasi kwenye macho yake.

“Usiwe mwepesi wakukasirika ,wote tunatambua kama sio kwa Master wetu Yan Buwen , tusingekuwa hai mpaka muda huu”Aliongea huku akionyesha hana hasira na Denisi , licha ya kwamba alikuwa amemkwida kwenye shingo.

“Wanachama wawili kutoka kundi la Camarilla watafika hapa muda si mrefu , Nadhani unafahamu Yan Buwen amekupa maagizo usionyeshe uwezo wako mpaka muda utakapowadia”

“Una uhakika utaweza kuwadhibiti ukiwa peke yako?”Aliuliza Denisi akionyesha wasiwasi kidogo na uwezo wa mwenzake na kumfanya yule bwana Vampire kupiga mwayo huku akimwangalia.

“Ingekuwa ni Zamani ningewahofia , lakini sasa hivi hata waungane na wazazi wao , hakuna ambaye anaweza kunizidi”Aliongea kwa majigambo na palepale Denisi alipotea kwa spidi na sekunde chache alionekana akifungua mlango wa gari yake aina ya V8 na kuondoka kwenye nyumba hio.

Muda huo huo wakati akitokomea , Lilith na Lefayette waliweza kutua ndani ya nyumba hio kwenye eneo la sebuleni sehemu ile ile aliokuwa amesimama Denisi mwanzoni.

“Karibuni sana , Ni kitambo kidogo bila ya kuonana na wewe mrembo Lilith pamoja na Marquess Lefayette”Aliongea na kumfanya Lefayette kumwambagalia kwa hasira.

“Nilijua tu ni wewe Drogba , upumbavu wako umepitiliza na awamu hii hakuna ambaye anaweza kujitokeza kukuokoa”

“Don’t be such a buzzkill , Shouldn’t we just sit and enjoy the view ? its rare for two of us to meet , The gracefull princess of the Venture clan, the mighty heir of the Brujah Clan and I , a minion of the sabbbat from the Tzimisce clan , Care for glass of blood?”

Aliongea huku akiweka tabasamu lake ambalo lilikuwa likiashria unafiki, akiwakaribisha huku akiwaambia kama watajali kupata angalau glass moja ya damu.

Sasa hapa unatakiwa kuelewa kimiminika cha rangi nyekundu kilichokuwepo kwenye glasi ilikuwa ni damu.

“Hatuna haja ya kuungana na wewe kwenye kijisherehe chako cha kuua mtu , nadhani ingekuwa kipaumbele chako kukimbia”Aliongea Lilith.

“Unafahamu ni kwanini Vampire ilipotea kwenye uso wa dunia kwa kuangamaizwa na binadamu?”Aliuliza Drogba na kumfanya Lilith na Lefayette kuangaliana ikionyesha hawakuwa na majibu.

“Ni kwasababu ya mitazamo yao ya kiburi kwa binadamu ndio ilikuwa anguko lao , nyie wawili mnaonekana kuwa wapole mno na hamfahamu mambo mengi,hivi mnadhania nimekaa hapa kuwasubiria kwasababu nawaogopa?”

“Unaongea ujinga na leo ndio mwisho wako”Aliongea Lilith na palepale ulionekana upanga wa kung’aa kwenye mikono yake maarufu kama Massace Blade au upanga wa maafa.

Drogba aliweka glasi ya damu kwenye meza na kuanza kunyoosha mabega yake kwa mbwembwe.

“Niliwauliza kama mnapenda mandhari ya hapa , lakni ukimya wenu huenda ndio jibu “

“Vizuri sana , unaonekana kuwa na nguvu nyingi ambazo zinakufanya ujihisi ni mwenye kujiamini , naamini awamu hii utajitahidi angalau hata kunipiga ngumi moja na isiwe kila siku mimi ndio ninakubutua”Aliongea Lefayette na palepale na yeye mkono wake ulionekana kushikilia siraha ya kichawi ambayo ipo muundo wa shoka lenye makali pande zote huku ikiwa na mpini wa mita kama moja na nusu hivi.

“Hio siraha yako inavutia sana kwa macho ,lakini kwa bahati mbaya sasa hivi haina athari kwangu”

“Unaweza kujaribu tuone kama haina athari”Aliongea na palepale alimsogela kwa kasi na kutaka kumpiga nayo lakini Drogba alikuwa mwepesi kwani sekunde tu alikuwa nje eneo la bustani na wote kwa pamoja walitoka nje huku Lefayette akiwa na hasira kwani alipelekea mashambulizi kwa kasi akidhamiria kumdhuru Drogba lakini adui yake alionekana kuwa na spidi isio na kifani.

Kwa spidi ambayo walikuwa wakitumia binadamu huenda macho yake yasingeweza kuona kile kinachoendelea na labda kuhisi eneo kuwa na upepeo usiokuwa wa kawaida peke yaeke..

Namna Lefayette alivyokuwa akishambulia ilikuwa tofauti kabisa na namna ambavyo Lilith na yeye anashambulia , lakini matokeo yalikuwa sio haba , kwani walimpelekesha Drogba kwa kiasi chake.

“Imekuawaje akabadilika kwa muda mfupi spidi yake sio tulioizoea”aliongea Lefayete kwa hamaki mara baada ya kugundua kila pigo analopeleka linapita hewani licha ya kwamba alijaribu kutumia spidi kubwa.

“Haijalishi unaspidi kiasi gani lakini nakuhakikishia siku ya leo huwezi kuondoka hapa ukiwa hai”Aliongea Lilith na muda ule ule Lefayette alipiga chini shoka lake na kukusanya upepo usiokuwa wa kawaida ambao ulikuwa kama kimbunga na kwa spidi kali sana alimsogelea nao Drogba.

Drogba licha ya kwamba alikuwa na spidi lakini alikuwa amechelewa kwani spidi ya kimbunga ilikuwa ni kali kuliko ya kwake na palepale ilimvaa , lakini hakutaka kuzembea , alichokifanya nikujiokoa kwa kutaka kuruka kwenda juu , lakini Lilith alikuja kwa spidi ya ajabu akiwa na panga lake na kushambulia , na kwasababu spidi ya ya Lilith ilikuwa kubwa kuliko ya Lefayette ilimuwia vigumu Drogba kukwepa pigo lake na kumkata Drogba mkono kuanzia begani na Drogba alitoa ukulele huku akidondoka pembeni, Lefayyete hakutaka kumpa nafasi nyingine alimsogelea na kumcharanga na lile shoka lake eneo la tumboni na kusababisha damu na nyama nyama kusambaa eneo zima.

Mpaka hapo aliamini ndio mwisho wa Drogba na walijikuta wakivuta pumzi za ahueni kwani mwanzo walihofia spidi yake.

Lakini sasa palepale walijikuta wakishangaa mabadiliko yalioanza kutokea kwenye mwiliwa Drogba , kila tone la damu na nyama zilizosambaa zilianza kujikusanya kwa spidi kubwa huku zikivutwa eneo moja kwa nguvu isiokuwa ya kwaida na kilikuwa ni kitendo cha dakika tu Drogba alirudi kwenye uhai wake.

“Play time is over , Time to get serious”Aliongea

“How… How can this be possible”Lilith alijawa na mshangao na hofu isiokuwa na kifani kwani ni mara yake ya kwanza kushuhudia tukio la namna hio.

“Ilitakiwa mpaka sasa awe ameshakufa kutokana na laana iliokuwa kwenye mwili wake, lakini kwanini akaweza kujirudisha hai”Lefayette nae aliongea huku akimwangalia Lilith.

“Nishawaambia ukiburi na ukale ndio anguko la jamii ya Vampire , ndio maana haijatokea hata siku moja mkapiga hatua kwenye kujikomboa na kujiweka huru , not only you guys but even the maing god will also face the true Rangarok”

“Unaongea ujjinga , usifikirie ndio tumekushindwa”Aliongea Lilith huku akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kusababisha kifua chake kupanda na kushuka.

“Naona hamtaki kuelewa sasa ni muda wa kuweza kuonja radha kamili ya ghadhabu yangu”Aliongea na palepale alipotea na ile anakuja kuibuka alikuwa mbele ya Lefayette na alimramnba ngumi yenye uzito wa tani eneo la shavuni na Lefayette alipeperushwa kama mpira na kwenda kuvaa mnara wa tanki la maji ambao ulipondeka palepale na kufanya tanki kumdondokea na maji yote kumwagika.

Lilith baada ya kuona vile alijiandaa kwa ajili ya kujilinda , lakini ilikuwa amechelewa kwani alijikuta akipokea mateke mawili mazito ambayo yalimrusha na kwenda kujipiza kwenye ukuta .

Lilith hakutaka kushindwa palepale alisimama na kupaa juu huku akitema mate na kumsogelea Drogba kwa kasi ya kutaka kumshambulia na panga lake la Maafa , lakini alikuwa amecheelewa kwani Drogba kwa kasi ya upepo alimvaa Lilith na kupaaa nae na ile anafika juu alimpiga ngumi yenye uzito watani mbili na kumfanya apepesuke na kwenda kutua kwenye maji ya bahari.

Akiacha hewani matone ya damu kama mvua yakidondoka chini kwenye mchanga wa fukwe.

Lefayette alipigika lakini haikumaanisha alishindwa .hivyo kushuhudia mchumba wake Llith akishambuliwa kwa namna ambayo ilimfanya kudhania amepoteza maisha alipandwa na jazba kwa kiasi kikubwa na palepale aliamka kwa spidi na kumfuata Drogba kwa kumshambulia na shoka lake.

“Blood Avalanche”

Aliongea kwa sauti kubwa akiita nguvu za kichawi na palepale wingu kama la moshi unaozunguka kwa spidi ulimsogelea Drogba kwa spidi kubwa huku akifuatia Lefayette kwa nyuma

“Inatia aibu dhana hio ya kichawi ikipotelea kwenye mikono yako”Aliongea Drogba na palepale alinyanyua mikono yake na kuzuia pigo lile la kichawi kwa kunyumbulisha Anga kutengeneza wigo.

Lefayette alishangazwa na tukio lile na kuhofia kwa wakati mmoja na kujiuliza inawezekana vipi Dogba kuwa na uwezo wa kutumia kanuni za anga ,mpaka hapo alijua kabisa kuna utofauti mkubwa kati yake na yeye , mwili wa Drogba umepitia mabadiliko makubwa yasiotamithilika.

Lakini hakutaka kukata tamaa , alifyatua shoka lake kuelekewa kwa Drogba , huku akiwa na asilimia chache za kufanikiwa na Drogba alitoa tabasau la kejeli.

“Dhaifu sanaa”

Aliongea na kumsogelea Lefayette kwa kasi na kumpiga ngumi nzito kwenye eneo la kifuati ambayo ilichangua mbavu zake na kumsababishia kushindwa kupumua palepale kutokana na kifua kujaa damu, hakuwa amekufa kwani moyo wake haukuwa umeathrika lakini hakuwa na nguvu za kuendelea kupambana zaidi ya kumwangalia Drogba kwa kumlaani, lakini kilichomfanya kuwa na wasiwasi na kukiona kifo chake ni kwamba mwili wake ulishindwa kujiponyesha wenyewe kama ilivyo kwa Vampire na kuna nguvu iliokuwa ikizuia kitendo hicho kutokea.

“Hii ni nguvu nguvu .. gani , Wewe bado ni Vampire kweli?” Aliuliza kinyonge lakini Drogba hakumjali zaidi ya kugeukia bahari na kumwangalia lilith ambaye alishatoka kwenye maji huku akiwa amepiga magoti akihema kama mbwa huku maji yaliolawanisha nywele zake pamoja na nguo yakitiririka kwenye mchanga.

“Lilith unajua kwamaba nilikuwa nikikupenda sana na mpaka sasa bado na kupenda , hivyo nipo tayari kukupa dili , kama utakubali kuwa kijakazi wangu nitakuacha uendelee kuwa hai”Aliongea Drogba.

“Ukoo wa Tzimsce licha ya kuwa kwenye umoja wa kishetani wa Sabbat na wanachama wake kuwa wenye roho mbaya , lakini bado wewe ni Vampire , Drogba wewe ni mjinga kweli kuitelekeza nafasi yako kama mrithi na kuamua kuruhusu mwili wako kutumika kama siraha ya kibailojjia”Aliongea Lilith.

“Mwanamke usipoteze pumzi yako kunijali mimi , nani anajali kuhusu urithi, uwezo na nguvu ndio urithi pekee , sio wewe tu hata wazazi wako hawana uwezo wa kuweza kushindana na mimi , nikitoka hapa naenda kuwaua wote na kuchukua mamlaka yote , ninakwenda kuwa mfalme na sio kupata urithi wa kipuuzi”Aliongea huku akianza kucheka.

“Usifanyishe kijogoo unaweza kweli umenishindwa mimi lakini kuna mtu huna uwezo wa kupambana nae maana umemkosea pia na huyo ndio atakuwa ni mwenye kutoa hukumu yako”Aliongea

“Oh you are saying the ever great Pluto ,Mr Roma Ramoni?”Aliongea bila hofu na kumfanya Lilith kuwa na wasiwasi , alikuwa akiamini mpaka muda huo mtu pekee ambaye anaweza kumshinda Drogba ni Roma pekee lakini kwa namna alivyokuwa akijiamini alijawa na wasiwasi.

“Lilith unaonaje tukishambulia wote , mpaka sasa anaonekana kutumia kiasi kiukubwa cha nguvu zake”Aliongea Lefayeytte aliekuwa akijitahidi kusimama.

“Usiwe mjinga wewe mrithi kutoka ukoo wa Brujah , kama kweli una nguvu za kushindana na mimi anza kunishambulia tuone utatumia dakika ngapi kuhimili”Aliongea na kumfanya Lefayette kuwa ni mwenye hasira kali mno na alijaribu kukusanya nguvu zake kusogea lakini aliishia kudondoka , muda huo huo breki za gari zilisikika mita kadhaa kutoka walipo.

Lilith ndio aliekuwa wa kwanza kuangalia ni mtu gani kaweza kufika na alijikuta akipata ahueni mara baada ya kuona ni Roma akiwa kwenye gari aina ya Lexus.

“Haha… nadhani nimekuwa na bahati kufika ndani ya muda muafaka , msongamano wa magari Kivukoni ndio umenipa changamoto”Aliongea Roma huku akimwangalia Drogba na kumfanya Lilith kutoa tabasamu hafifu.



.









SEHEMU YA 455.

Lefayette licha ya kumuona mwokozi wake alionyesha kutofurahishwa na ujio wake , aliamini huenda Lilith ndio alifanya mawasiliano na Roma na kumwambia eneo walipo, hivyo aliona kabisa Lilith alikuwa akidharau uwezo wake wa kupigana.

“Pluto nilikuwa nikikusubiria sana”Aliongea Drogba.

Roma hakumjali sana Drogba zaidi ya kumsogelea Lefayette aliekuwa akihema kwa tabu .

“Bado hujafa tu?”Aliuliza Roma.

“Usinisogelee kama kweli una uwezo pigana nae na ushinde”Aliongea .

“Ineonyesha bado una nguvu kiasi za kupigana , unaonaje nikiyakatisha maumivu yako?”Aliongea Roma na palepale aliinua mkono wake na kumpiga karate ya kichwa na kilichotokea Lefayette kichwa chake kilichanguka kama tikiti maji na Roma alitumia uchawi wake na palepale alianza kuungua kwa kasi ya ajabu mno na mwili wake kupukutika kama majivu.

“Why!!?”Lilith alijikuta akitoa macho ya mshangao kwa kitendo alichokifanya Roma.

“Mfalme Pluto kwnaini umemuua Lefayette , Adui wetu ni Drogba kutoka ukoo wa Tzimsce?”

“Lefayette amevunja sheria yangu kubwa , hua sipendi kutishiwa kwenye maisha yangu kama nakumbuka vizuri alisema angevunja shingo yangu na nilijizuia muda ule kwasababu mke wangu alikuwa amenilalia la sivyo asingefika hata hapa”Aliongea Roma na kumfanya Lilith kutetemeka , hakuamini kauli tu inaweza kupelekea mtu kuuliwa.

Lakini sio hivyo tu Roma na Camarila hawakuwa na ugomvi, hata kama hawakuwa na ushirika lakini washawahi kushirikiana kule Ufaransa , lakini Roma hakujali kabisa kama Lefayette alikuwa ni mwanachama wa Camarila lakini wakati huo huo akiutokea kwenye koo yenye nguvu ya Brujah.

“Anatokea ukoo wa Brujah na ni mtoto wa mfalme , Ulichofanya mfalme Pluto kinaweza kuku,,”

“Sijali anatokea wapi , kama familia yake inataka kulipa kisasi nipo hapa Tanzania , lakini kama wana akili ya kuchanganua mambo nadhani ni bora wapotezee”Aliongea na kumgeukia Dtogba.

“Haishangazi kwa ukoo wa Tzimsce kupenda kutumia miili ya wengine , mwili wako unatisha na ulivyo ungua ungua , Kwanini usingemuomba Yan Buwen angalau akakuchagulia mwili mzuri wakati anakufanyia majaribio?”

“Sipendi unachoongea , lakini nimependezwa na ulichomfanyia Lefayette”Aijibu Drogba.

“Kama unaonyesha humfahamu Yan Buwen , vipi kuhusu Denisi hakuwepo hapa kwa ajili ya kukupa msaada?”

“Denisi ndio nani, simjui mtu huyo mim”

“Unaonekana kweli unakitafuta kifo , unadhani nguvu aliokupa Yan Buwen inaweza kukuokoa muda huu?’

“Hapana m sifikirii kabisa kupambana na wewe kama Clone aliotuma Yan Buwen ilionyesha kushindwa kwanini mimi nishinde , nilishaandaa mpango wa kujiokoa muda mrefu tu”Aliongea kwa kujiamini na kumfanya Roma kumsogelea.

“Ilinichukua mapigo manne kuipiga na kuiua Clone , vipi kuhusu wewe ni mapigo mangapi utaweza kuhimili?”

“Mfalme Pluto kabla hatujaendelea , unaonaje kwanza ukipiga simu nyumbani luona kama wapo salama”Aliongea na kumfanya Roma kushituka baada ya kusikia neno nyumbani , alikuwa ashatuma wanajeshi wa The Eagles kutoa ulinzi sasa alijiuliza nini hakijaenda sawa.

“Ni juu yako kunishambulia, lakini naomba nikwambie kwamba inaweza kugharimu maisha ya wanafamilia wako?” Aliongea na kumfanya Roma kusita , hata hivyo alijiambia kwamba Drogba hawezi kumponyoka kwa namna yoyote ile , hivyo alitoa simu yake kujaribu kupiga nyumbani.

“Hello !”Sauti ya Blandina mama yake ilisikika lakini haikuwa sawa ni kama alikuwa akitetemeka.

“Mama kuna nini kimetokea?”

“Roma kuna mwanaume amekuja nyumbani akiwa amebeba wanaume wawili wa kizungu ambao hawana fahamu na ametuzuia tusiondoke hapa nyumbani , imekuwa bahati Sophia kaondoka mapema”Aliongea Blandina kwa wasiwasi na kumfanya Roma kupagawa na kujiuliza je ni kazi ya Yan Buwen.

Hata hivyo kusikia wazungu wawili wamepoteza fahamu alielewa kabisa ni The Eagles ambao amewatuma kwa ajili ya kuipa ulinzi familia yake.

Roma wasiwasi umemjaa na kuhisi huenda Yan Buwen akawa ameunda jeshi la watu wenye miili isio kawaida pamoja na nguvu za kucheza na kanuni za anga..

“Mama mpe simu aongee na mimi”

“Your Majesty Pluto , bado unakumbuka sauti yangu”Ilisika sauti upande wa pili na Roma kutoa macho.

“Mourihno?”Aliongea Roma na sasa kuanza kuelewa fumbo ambalo alikuwa akijaribu kulifumbua tokea siku ya jana .

“Ndio ni mimi , shukrani zikuendee ewe mfalme Pluto kwa kunisaidia kujiokoa kutoka kwa Lilith na Lefayette na kuja kuingia kwenye nyumba yako na sasa ipo chini yangu”

“Kwahio unasema ulikuwa na ushirikiano na Drogba muda wote?”

“Bingoo.. Mfalme Pluto unaonaje ujuzi wangu wa kuigiza, nadhani naweza kushinda tuzo ya Oscar , nilivyoona umeweza kununua maneno yangu nilitaka hata kucheka lakini niliishia kujizuia”

“Mfallme Pluto , Mourihno si ndio Peasant ambaye ulitaka sisi tumuachie pindi tutakapo mkamata , nini kimeenda kombo?”Aliuliza Lilith mara baada ya kusikia jina la Mourihno.

“Ngoja nikuambie miim kilichomkuta mfalme wako”

“Roma aliweza kudanganywa na Mourihno kwa kuambiwa na Mouihno alitaka kulipiza kisasi kwa kifo cha mpenzi wake wakati alipomkamata lakini huo sio ukweli, Dina alikuwa ni mpenzi wa Mourihno lakini alijifanyisha mjanja kwa kutaka kutoa siri kwenda kwa Nessa juu ya sababu ya kifo cha mama yake, nakiri Mourihno alikuwa mpumbavu kumwambia Dina siri zote , lakini hata hivyo Dina hakuwa na pakwenda kwani wakati anataka kuweka ukaribu na Nessa kwa kumwambia siri iliofukiwa miaka mingi aliweza kumzuia , Lilith mwanaume unaejisifia kumwita Mfalme hana lolote na ameweza kudanganyika kirahisi”Aliongea Drogba huku akainza kucheka.

Ujio wa Nessa Nchini Tanzania haukuwa wa bahati mbaya hata kidogo, ni kweli msanii wa kimaifa Nessa alikuwa kwenye Tour dunia nzima , lakini ratiba yake haikuwa ikimwambia kwamba angeweza kufika nchini Tanzania , maamuzi ya kuja Tanzania akitokea nchini China aliweza kuyafanya mara baada ya kupokea ujumbe kutoka kwa mtu asiojulikana unaosema kwamba alikuwa na siri nzito iliokuwa ikihusiana na kifo cha mama yake mzazi Ms Doleres.

Mpaka leo hii kifo cha Ms Doleres kutoka Ireland kilikuwa kina utata mwingi licha ya taarifa iliotolewa kuonyesha alijizamisha kwenye swimming Pool akiwa hotelini kutokana na tatizo la Sonono.

Kama ijulikanayvo kundi la Cranberries ilikuwa ni Band maarufu ambayo ilikuwa ikipigania sana haki za raia kupitia nyimbo zao , ni kama hata Tanzania uwafananishe na msanii Roma Mkatoliki ambaye hana uwoga kuwaponda wanasiasa, basi ndivyo ilivyokuwa kwa Ms Doleres, haikueleweka ni siri gani ambayo ilifasababisha kifo chake lakini ni dhahiri kwamba aliuliwa na wahusika wakuu ni jamii ya watu wanaojiita Vampire.

Ikumbukwe kwamba mume wa Ms Doleres pia alikuwa ni Vampire hivyo pia kwa mtoto wao Nessa ambaye ni msanii.

Sasa Dina aliweza kupata ubuyu wote kutoka kwa Mourihno juu ya sababu ya kifo cha Ms Doleres na baada ya kupata siri hio aliona nikama kadi muhimu sana ya kuicheza kama tu atataka kuwa na ukaribu na msanii mkubwa duniani ,ni rahisi kusema kwamba Dina msukumo wake ulikuwa ni kutokana na kuogopa kufunikwa na kimuziki na Sophia , hivyo alitaka kumtumia Nessa ambaye alikuwa tishio kubwa kwenye mziki kwa kutumia siri aliopata kwa Mourihno , lakini asichokifahamu ni kwamba mchezo wake uligundulika mapema tu mara baada ya taarifa kumfikia Mourihno baada ya ujio wa Nessa nchini Tanzania, hivyo kuuliwa kabla hajaweza kutoa siri,

Hivyo hitimisho tamaa ndio iliomuua msanii Dina na hivyo kujibu maswali ya Roma kwamba kama kweli Dina alikuwa akibadilishwa kuwa Vampire kwanii Vampire hao hao wamuue.

Lilith alijikuta akishangaa mara baada ya kusikia habari hio kwamba Roma aliweza kuchezewa akili na Mourihno.

Upande wa Roma alijikua akikunja ngumi yake kwa hasira, ilikuwa ni sahihi kwake kufikiria kwamba The Eagles wameweza kuzibitiwa kirahisi kutokana na kwmaba Vampire ni viumbe ambavyo vina uwezo mkubwa wa kumlewesha binadamu na kumuamuru kufanya watakvyo.

Lakini kitu kingine ambacho Roma kilimkasirisha zaidi ni namna ambavyo alidanganywa na kuingizwa kwenye mtego bila ya yeye mwenyewe kujua na kumuachia mhusika kundoka bila ya yeye mwenyewe kufahamu.

“Vipi naweza sasa kuondoka.?, Naamini kabisa mfalme Pluto huwezi kuhatarisha maisha ya wanafamilia wako kwasababu tu unahitaji kuniua”Aliongea Drogbs

Mpango wao ulikuwa mwepesi sana , Drogba alifahamu kwamba hana uwezo wa kushindana na Roma hivyo walipanga kwanza kuiteka familia ili Drogba atakapotoweka na Mourihno angeiteka familia ya Roma na kukimbia nayo mpaka msaada wa Yan Buwen utakapo wafikia na hapo ndipo Lilith atakuwa hana uwezo wa kuwanasa na kifaa chake na wataweza kucheza na Roma kupitia udhaifu wa familia.

“Mfalme Pluto kwanini tusimuache tu akaondoka, sio kosa lako , ni tabia yake kuwa mjanja , familia yako kwasasa tuiweke kipaumbele”Aliongea Lilith lakini Roma bado hakujibu , alionekana kuwa kwenye tafakari

“Mfalme Pluto nakushauri uzingatie hili , Drogba ni mtoto wa Prince Raphaeli kutoka koo ya Tzimsce , ukimuua inamaanisha kwamba unatangaza vita na ukoo wetu hawapo kwenye ushirikiano mzuri na kundi la Sabbat na baba sikuzote amesema hatupaswi kumchokoza Prince Raphaeli kutokana na uwezo wake mkubwa wa mapambano”Aliendelea kuongea Lilith.

“Lilith asante kwa maneno yako , lakini niseme tu kwamba siku hizi mbili nilisahau kwamba viumbe hivi damu yao ni ya baridi tofauti na binadamu ndio maana nikadanganyika kirahisi”Aliongea Roma na kumfanya Lilith kuguna lakini Roma alitabasamu kifedhuli.

“Unajua ni kosa gani kubwa ambalo umeweza kufanya?”Alimuuliza Drogba ambaye aliishia kushangaa.

“Kosa gani?”Aliuliza kwa hofu.

“Vizuri , siwezi sana kukulaumu kwa kutokufahamu , na nimekuja hapa kwa kutumia usafiri kwa kuogopa malipizi”Aliongea na kumfanya Drogba asielewe

“Acha majigambo na kujifanyisha, huna lolote la kunifanya , ukijaribu kunishambulia Mourihno ataweza kugundua mapema kwani kuna kifaa maalumu ambacho kitafanya kuona nguvu zangu zikiniishia na hapo hapo atachukua hatua ya kummaliza mama yako , sina muda wa kucheza mchezo na wewe mim”Aliongea.

“Hili sio mchezo” Aliongea Roma na palepale alipotea na kumfanya Drogba kuchanganyikiwa , lakini kabla hajaelewa kinachoendelea Roma huyu hapa na alitumia staili ile ile aliomshambulia Lefayette lakini awamu hii aliongeza nguvu kidogo na kufanya kichwa cha Drogba kuvunjika palepale na kugeukia mgongoni.

Kitendo kile kilimuacha na hamaki Lilith kwa kudhania kwamba Mourihno angeua familia ya Roma, lakini ile anaangalia vizuri , Roma hakuonekana tena mbele yake akawa amepotea mara baada ya kumpiga Drogba.

Upande mwingine ndani ya sekunde ile ile upande wa Ununio , mkono mrefu ambao haukujulikana umetokea wapi , ulitokezea kwenye hewa na kuishika shingo ya Morihno kwa nguvu wakati akijiandaa kumcharanga Blandina kwa panga.

Hata yeye alishangaa nguvu ya ajabu ikimvuta , lakini alichelewa kwani mkono ule ulikuwa na nguvu sana na ulienda moja kwa moja eneo la moyo na kubomoa kifua na kuunyofoa moyo wote nje na ikawa mwisho wa maisha ya Mourihno.

Blandina na Bi Wema walitoa ukulele kwa tukio lile kwani walishangaa midamu ikiwarukia pasipo ya kuelewa nini kimetokea.

Upande wa huku Kigamboni wakati Drogba alipojirudisha hai kwa mara nyingine palepale Roma alijitokeza mbele yake tena na Drogba alishindwa kujilinda kwani ilitokea ghafla sana na sekunde ya pili ni kwamba moyo wake uliachana na mwili wake palepale na kuwa kwenye mikono ya Roma,

Lilith kitendo kile kilimfanya apige magoti pasipo ya kuelewa mwenyewe huku mdomo ukiwa wazi akishindwa kuamini namna hali ilivyogeuka na kuanza kumuogopa Roma palepale.

Drogba bado hakuwa amekufa , licha ya moyo wake kutolewa lakini ilimaanisha kwamba hana dakika nyingi angepoteza maisha kama moyo wake usingerudishwa kwenye kifua chake, hivyo aliishia kumwangalia Roma kwa macho ya kumwambia anaomba moyo wake tafadhari.

“Niambie Yan Buwen yuko wapi, unadakika moja tu kabla moyo wako haujapoteza uwezo wake?”Aliuliza Roma huku akitishia kuuyeyusha moyo wa Drogba.

Alitaka kujua alipo Yan Buwen kutokana na kwamba watu wake waliweza kutafuta kona zote za dunia pasipo ya kupata taarifa ya mahali alip.

“Hahaha… Hahahaa….”

Alichena na kisha alidondoka chini na kupiga magoti huku akitema damu , hakua na uwezo wa kujiponyesha tena kwasababu mwili wake hauna moyo na ni nguvu ya jiwe la kimungu pekee ambalo lilimpa uwezo wa kuongea kwa dakika chache.

“Kabla sijakufa naomba nikuambie hivi , Hades huna uwezo wa kumzidi Yan Buwen kwa namna yoyote na siku atakayorudi ndio itakuwa mwisho wako , sijutii kufa kwa ajili yake kwani naamini kisasi changu atakilipi… za.”Aliongea na palepale alidondoka chini akionyesha hayupo tayari kutaja mahali Yan Buwen alipo.

“Huwe….wezi, kumpata … Yan Buwen mpaka siku atakayokutafuta ,, ye ..ye mwenye,,, kwa ajili ya kuku.. kuku..”Alishindwa kumalizia kauli na palepale ikawa ndio mwisho wa uhai wwake

Roma hakuona haja ya kuendela kushikilia moyo wake zaidi ya kutumia nguvu ya kimaandiko kuuyeyusha pale pale na kisha akamkausha na Drogba palepale na kuwa majivu pasipo kuacha ushaihidi wa aina yoyote.

Lilith kuona namna Drogba alivyomalizwa na kuwa majivu ,alijihisi kukosa pumzi, alikuwa akijua uwezo wa Roma kuwa mkubwa lakini namna alivyodhibiti watu wawili waliopo sehemu mbili tofauti kwa wakati mmoja ilikuwa ni jambo la kushangaza

Ukumbuke sasa hapa Roma macho yake yalikuwa ni ya njano kama jua licha ya kwamba mwili wake haukubadilika kama ilivyokuwa miezi kadhaa nyuma kabla hajapitia steji za kupanda levo za nguvu ya kimaandiko za kijini.

Lilith hisia zake alizokuwa nazo juu ya Roma zilikata palepale kwa kumugopa na alijiambia ni kheri akawa na urafiki wa kawaida tu na sio wa kimapenzi alikuwa ashashuhudia watu wenye uwezo wa ajabu lakini kwa Roma alijawa a hofu hata ya kumsogelea tena.

…………………….

Baada ya Mourihnno na Drogba kudhibitiwa ilibidi Mage kwa kushirikiana na jeshi la polisi watengeneze ushahidi ambao ulithibitisha kwamba Recho hakuhusika na mauaji ya msanii Dina.

Wanasema hata kama vyombo vya habari viwe na ukubwa gani lakini mwisho wa siku vipo kwenye mikono ya serikali , hivyo ushahidi feki uliotolewa ulisambazwa kwa kasi mno na ndani ya muda mfupi swala la Recho kumuua msanii Dina lilipotelea hewani.

Lilith alimuaga Roma na kusema atarudi nyumbani na kuhakikisha kwamba hakuna kitu kitatokea kwa kuhusika na kifo cha Lefayette na Roma hakujali sana alimwambi aafanye vile atakavyoona inafaa.

“Nguvu alizoniachia Hades nilidhani hazitofanya kazi , lakini inaonyesha uwezo wa kucheza na kaununi za anga pia ninao, nilihofia muda mrefu kuzitumia nahisi ni wakati wa kujifunza kutumia mbinu zote”Aliwaza Roma wakati akiendesha gari kuelekea nyumbani kwake.

Ndio Roma alishawahi kuachiwa nusu ya nguvu za kunyumbulisha kanuni za anga na Hades wa Zamani lakini hakuwahi kuzitumia kutokana na kwamba alihisi zisingefanya kazi kwa upande wake.

Kitendo cha kumshambuliaMourihno na Drogba kwa wakati mmoja licha ya kwamba walikuwa sehemu mbili tofauti ilikuwa ni kutokana na kucheza na kanuni za anga na ku’fold space’ hivyo kumpelekea kuwa sehemu moja kwa wakati mmoja lakini kuwa kwenye maeneo tofauti , ulikuwa ni uwezo wa ajabu sana lakini jaribio lake lilimfumbuliajambo jipya kuhusu kanuni za anga.

Lakini licha ya hivyo mbinu zake zilikuwa za chini mno kufananisha na zile ambazo anatumia Athena..

Roma kutokana na kusikia habari za Yan Buwen alizidi kuhimiza watu wake kuongeza kasi ya kumtafuta , lakini wakati huo huo akiongeza wanajeshi ndani ya Tanzania kwa ajili ya ulinzi.

Hatimae mwezi mmoja ulipita tokea tukio la kifo cha Dina na Vampire Drogba na Mourihno.

Lanlan aliweza kuandikishwa shule ndani ya mwezi huo huo mmoja , shule ambayo ilikuwa maarufu kwa watoto wa vigogo wengu kusoma hapo na wale wa matajiri , iliokuwa ikitumia mtaala wa Cambridge, ilimchukua siku chache tu kwa Lanlan kuzoea mazingira ya shule na hatimae kuweza kupata rafiki.

Lakini licha ya hivyo Lanlan alileta gumzo na mshangao kwa wengi kwani licha ya umri mdogo aliokuwa nao alionyesha uwezo mkubwa mno wa akili , jambo ambalo liliwafanya Roma na Edna kufika shuleni kwa majadiliano na walimu na makubaliano yalifanyika Lanlan asianzie chekechea bali aanze darasa la kwanza kabisa.

Kitendo cha Lanlan kupata rafiki ndio mwanzo wa mwanafunzi mmoja kupigwa mpaka kuzimia.

Itaendelea siku kesho tumalize tukio la kumuona mshrika mkuu waAthena then twende sasa Korea Kusini.

Nawakumbusha Kuna jiwe moja ambalo lina Roho ya Gaia halijapatkana lakini pia kuna kisa kilichopelekea Athena kumuua Hades wa Zamani.

Najma anaendeleaje huko alipo Aluta Continuara kesho mapema , vipande vitatu.
 
SEHEMU YA 456.

Ni mwezi mmoja sasa umepita hakuna kubwa ambalo lilitoke, Rose alikuwa tayari ashaanza kujifunza mafunzo ya kijini na alionekana kuwa na matokeo mazuri kwa kutumia mbinu ambayo Roma aliweza kuelekeza.

Upande wa wanawake wengine Roma aliweza kumuelekeza mmoja mmoja namna ya kufanya ‘Meditation’ ili kuweza kupata ‘Reveletion’ au ufunuo juu ya mbinu za kuvuna nishati kati ya mbingu na ardhi.

Ni Edna pekee ambaye alikuwa hajaanza bado na yote hio ni kutokana na Roma kuona mwili wa Edna haukuwa tayari kuhimili hivyo ilimbidi aendelee kufanya mazoezi, alikuwa na wasiwasi kuzidiwa na wenzake lakini kwasababu Roma alimwambia hakuwa tayari ilibidi amsikilize.

Sophia na yeye umaarufu ulizidi kuongezeka mara baada ya kutoa albamu yake ya kwanza ambayo ilikuwa na nyimbo zilizofanya vizuri sana na wale waliomtabiria mema kuridhishwa na matokeo , lakini hata hivyo wanasema siku zote matarajio ni mazuri kuliko matokeo hivyo kuna wale ambao pia hawakuridhishwa kwa aina yake , lakini mzani uliegamia upande wa walioridhika.

Naam ilikuwa ni siku ya Jumamosi ya tarehe ishirini ya mwezi wa pili , siku hio kulikuwa na hafla fupi ya kumpongeza Sophia kwa mafanikio yake ya kimuziki lakini kubwa zaidi siku hio pia ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa , hivyo nyumbani kwa Edna na Roma kulikuwa na sherehe ambayo ilijumuisha watu wachache sana ,mathalani ndugu wa kifamilia ambao walijumuika kwa chakula cha cha mchana.

Ni muda wa saa saba kamili ndani ye aneo la bustani walionekana watu mbalimbali waliokuwa wameketi huku wakiongea kwa vicheko, alikuwepo Neema Luwazo na mtoto wake Donyi , Nasra ,Tajiri Azizi na mke wake pamoja na Kassimu mtoto wa Tajiri Azizi wengine waliokuwepo ni Roma Edna , Bi Wema bila ya kumsahau Lanlan ambaye alikuwa kivutio zaidi.

Baada ya nusu saa kupita alifika Omari Tozo ambaye alikuwa ameambatana na Queen ambaye tumbo lake lilikuwa lishaanza kujitokeza kutokana na ujauzito.

Roma ilikuwa mara yake ya pili kukutana na Queen , mara ya kwanza ilikuwa ni ndani ya hospitali ya Aghakani na ilikuwa kipindi ambacho alikuwa akiongea na Sauroni juu ya mwanamke anaefahamika kwa jina la Zoe Kovac , hivyo baada ya kumuona mrembo yule ndio mwanamke aliekuwa akimsumbua Omari , lakini mwanamke pia ambaye alikuwa na mimba ya Yan Buwen alishangaa , lakini kubwa zaidi alishangaa mara baada ya kufahamu Queen ni mtoto wa Mzee Alex.

Upande wa Queen pia alimkumbuka Roma , lakini awamu hii alionyesha aibu kidogo kuliko kipindi kile na huenda ni kutokana na ujauzito wake.

Omari alionekana kuwa na furaha , ijapokuwa Queen hakuwa amemkubali Omari kwa ajili ya ndoa , lakini walikubaliana kuwa marafiki na Omari alionekana kufa kuoza kwa mrembo Queen hivyo licha ya kwamba Queen alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine , lakini alitaka kumuoa hivyo hivyo na kutaka mimba hio iwe ya kwake lakini Queen bado alikuwa na tumaini kwamba Yan Buwen wake angekuja kumrudia.

Blandina alifurahi sana mara baada ya kujua Omari alikuwa rafiki yake Roma , hakujua namna walivyokutana lakini alipenda urafiki wao isitoshe Omari alikuwa mtoto wa familia ya mkuu wa majeshi hivyo ilikuwa faida kwa Roma kuzungukwa na marafiki ambao wanaweza kumsaidia hata Tajiri Azizi alionyesha kufurahishwa na ukaribu wa Roma na Omari.

Edna mwenyewe alishangazwa na ukaribu wa hao wawili, ijapkuwa alitaka kujua namna walivyokutana , lakini alijiambia Omari na Roma hawana utofauti mkubwa , kwanza wote hawakuwa na aibu na ni waongeaji sana na mawazo ya Edna yalikuwa kama wa wengine tu walimuona Omari kutokuwa na aibu kama ilivyokuwa kwa Roma na alichekesha kila alipokuwa akiongea na ni kama alitawala maongezi , huku asilimia kubwa akimsifia Queen kuwa mrembo kuliko ya Edna.

Ilikuwa ni familia kamili hivyo kwa Sophia alifurahi uwepo wa kila mmoja aliefika kwa ajili yake ,ijapokuwa familia yake ilikuwa nchini Japani lakini alihisi watu waliokuwa wakimzunguka kwake ni familia tosha kabisa.

Stori mbalimbali ziliingiziwa, Donyi na Kassimu walionyesha walikuwa kwenye penzi moto moto hivyo ilikuwa ni jambo ambalo lilizungumziwa pia na ukizingatia Jestina na Tajiri Azizi walikuwepo, pamoja na Neema Luwazo ambaye muda si mrefu angekuwa na undugu utakaounganishwa na ndoa

Ilikuwa rahisi kwa tajiri Azizi kumkumbali Donyi katika familia , kwanza kabisa Kassimu ndio angekuwa mrithi wa familia , lakini pia upande wa Donyi alikuwa mrithi wa mali za mama yake hivyo walilandana kwa kiasi kikubwa kwa kuzingatia kwamba siku zote mtoto wa tajiri anamuoa mtoto wa tajiri mwenzake na ni mara chache tajiri kuolewa na masikini ni ukweli mchungu lakini ndio ilivyo.

Asilimia kubwa ya maongezi pia zilikuwa sifa kwenda kwa Edna

Wakati Stori zikiendelea geti lilifunguliwa na ikaingia gari aina ya V8 ya rangi nyeusi na alishuka Denisi kwenye gari hio huku akiwa ameshikilia furushi la mua Waridi ya rangi tofauti tofauti , ilioneysha alikuwa na taarifa ya kilichokuwa kikiendelea hapo ndani.

Ujio wake ambao haukuwa na mwaliko ulifanya watu kuwa kimya lakini hata hivyo Denisi hakuonyesha hali ya kutokujiamini zaidi ya kuwasogelea na kusaliamiana na kila mmoja na mwisho kabisa akamsogelea Sophia na kumkabidhi yale maua aina ya Roses fresh plant, Sophia hakupenda ila alipokea hivyo hivyo.

“Denisi hayo ni maua mengi sana umeweza kununua nadhani ni pesa nyingi umetumia nilitamani na mimi kumnunulia mpenzi wangu Queen kama zawadi lakini hela sina”Aiongea Omari.

“Bwana Omari unasema kwamba unashindwa kununua maua kama hayo , mbona thamani yake ni ndogo sana”Aliongea Tajiri Azizi

“Mzee nadhani hujaulizia bei ya haya maua hivi karibuni yamekuwa ghari mno na wenye bustani wengi wamekuwa wakiyasafarisha kwenda nje ya nchi kutokana na uhitaji wake kuwa mkubwa”

“Hilo naelewa kuna mmoja wa rafiki yangu ni kweli hivi karibuni aliongea kwamba maua ya Waridi yamepanda bei sana sehemu nyingi za dunia , hivyo uhitaji wake kuwa mkubwa na thamani kupanda , lakini hata hivyo sio lazima kumzawadia unaempenda na maua ya Waridi kwani kuna aina yingi za maua ambazo zinawakilisha upendo pia”Aliongea

“Imekuwa ngumu kwa hapa Tanzania kuweza kuhifadhi maua na Watanzania wengi hawajachangamka juu ya uthamani wa maua , kuna siku nilipotembelea Thailland na Singapore nilishangazwa na mashamba makubwa ya maua ya Roses , ilinitamanisha na kampuni yangu ya Maple kuwa na shamba moja lakini Watanzania wengi sio wenye kuzingatia kupeana zawadi za maua”Aliongea Neema , ilikuwa sawa kuongea hivyo kwani alikuwa mfanya biashara na siku zote wafanyabiashara kila kinachomzunguka anakiangalia kwa namna ya fursa.

Lakini ilikuwa ukweli kwamba ni mara chache sana watanzania kupeana zawadi za maua kama Zawadi, wanawake wengi wa Afrika wanachopenda zaidi ni pesa , pesa na pesa tena au vitu vya thamani kubwa maua watakwambia waachie Nyuki , yaani una mpenzi wako yupo Manzese ndani ndani huko umbebee zawadi ya maua unaachwa siku hio hio.

Kwa wenzetu ni tofauti sana lakini hata hapa Tanzania ustaarabu huo upo lakini kwa watu wachache sana , ndio maana ukitembelea majiji makubwa kama Paris , Guanzhou au Seoul utakuta bustani zipo kila kona katikati ya jiji na uzaji wa maua ni biashara nzuri tu.

Chakula kiliandaliwa na wahudumu waliopewa tenda ya kazi hio ,walikuwa ni wafanyakazi kutoka moja ya hoteli ambayo ilikuwa chini ya umiliki wa Edna.

Baada ya kufurahia chakula pamoja mpaka kumaliza , Denisi alisimama na kisha akamsogelea Sophia.

“Sophia nimekuletea zawadi nyingine , hizi siku chache sitokuwepo Tanzania kwa ajili ya misheni maalumu hivyo naomba nikupatie leo hii hii katika siku yako maalumu ya kuzaliwa”Aliongea Denisi bila ya aibu mbele ya watu wote na kufanya kimya kitawale.

Kilikuwa ni kiboksi cha rangi nyeusi ambacho kwa haraka haraka mtu angegundua ndani yake kulikuwa na nini.

“Asante sana kwa zawadi , lakini siwezi kuipokea”Aliongea Sophia huku akiangalia kiboksi ambacho ndani yake kama hakikuwa na mkufu wa dhahabu basi ni saa au Pete.

Watu wote walikuwa kimya kuangalia namna tukio hilo linavyochukua nafasi yake , lakini hata hivyo walishangazwa na namna ya Denisi asivyokuwa na aibu , lakini kwa wakati mmoja walishangazwa na namna Sophia alivyokataa zawadi ile.

“Denisi unaboa sana ,inaonyesha kwenye maswala ya wanawake upo kama mimi tu na Roma hapa anatushinda kwenye vitu vingi..”Aliongea Omari kama kawaida yake ya kuvunja ukimya.

Denisi mara baada ya kusikia maneno yale alimgeukia Roma na kumwangalia kwa muda mfupi kisha akamgeukia Sophia kwa mara nyingine.

“Sophia sijui ni sababu gani ambayo inakufanya unikatae tumejuana kwa muda mrefu sana na tumepitia mengi na hata ulivyonikataa kipindi kile niliona labda ni kwasababu haukuwa tayari , lakini vipi kuhusu sasa huna sababbu yoyote ya kunikataa kwani hata mpenzi huna, nini kinakuzuia kufanya maamuzi”Aliongea Denisi bila kujali kuna watu wazima waliokuwa wamezunguka.

Ukweli ni kwamba Sophia alimkataa mara nyingi Denisi na sio mara mooja tu ni zaidi ya mara mbili , kilichokuwa kikimuuma sana Denisi ni kwamba Sophia sababu kubwa iliokuwa ikimpelekea kumkataa ni Roma.

Ikumbukwe Denisi na Sophia walishawahi kufanya mafunzo pamoja na Kung Fu Nchini China katika moja ya Temple maarufu na huko ndipo walipofahamiana na hata Denisi kuweka hisia zake wazi kwa mara ya kwanza na ndio mara ya kwanza ambayo Sophia alimkataa Denisi.

Sophia alikuwa na hasira kwani aliona ni kama Denisi anamdhalilisha mbele ya kundi la watu.

“Sababu kubwa ni kwamba sikupendi Denisi”Aliongea Sophia na kauli yake ilikuwa ikionyesha kukasirika na Edna alijikuta na yeye kuona Denisi anavuka mipaka na aliona aingilie.

“Denisi huwezi kumlazimisha Sophia akupende , hivyo usimsumbue tena”Aliongea Edna.

“Denisi nadhani alichoongea Shemeji yako ni sahihi , Sophia hakupendi na huwezi kumlazimisha na hata hivyo ana ndoto nyingi za kutimiza hivyo nadhani ni sababu pia ya kutotaka kujihusha na mapenzi”Aliongea Blandina.

“Mimi siamini hio ndio sababu kubwa”Aliongea Denisi na kufanya watu kumwangalia kwa shauku , huku wengi wao wakisisimkwa na mwili kwani hali haikuwa ya kawaida na walishangazwa na ukiburi na kujiamini kwa Denisi.

“Naamini Sophia kuna mtu anampenda ndio maana hataki kunikubalia”Aliongea Denisi huku akimwangalia Roma.

Ndio Denisi anajua Sophia anampenda Roma na Sophia mwenyewe ndio aliemwmabia hivyo , na ilionekana hata ujio wake siku hio ulikuwa ni kutaka kumchokoza Roma mbele ya Edna mke wake , lakini pia mbele ya wazazi wa Roma.

Denisi alikuwa akijua fika Sophia hakuwa na uhusiano wa kindugu na Edna licha ya kwamba watu waliwachukulia kama dada na mdogo wake , mwanzoni ingeweza kufahamika Edna ni dada kamili wa damu kwa Sophia lakini mara baada ya Marehemu Adebayo kujulikana hakuwa na uwezo wakumzalisha mwanamke hivyo moja kwa moja ni kwamba Edna na Sophia ni wa damu tofauti na kama ni udada basi ni ule wa hiari ,sasa yote hayo Dennisi alikuwa akiyajua na aliamini huenda Sophia mapenzi yake juu ya Roma ni ya siri na Edna hayafahamu , hivyo kufahamu kuna kajisherehe aliona yes ndio nafasi nzuri ya kumfanya Sophia aweke wazi kile anachojaribu kuficha.

Sasa kitendo cha Denisi kuongea vile halafu akamwangalia Roma ni kama alikuwa akitoa majibu.

Watu wote walimwangalia Roma na kisha wakamgeukia Sophia wakisubiria jibu .

“Hapana! Msisikilize kwani sina mwanaume ninaempenda kwa sasa nikwamba tu sitaki kuwa na mahusiano na Denisi kwani hana vigezo ninavyovitaka”Aliongea Sophia ili kutuliza ile hali.

Edna alimwangalia Sophia kwa namna ya kumchunguza na kisha akamgeukia Roma aliekuwa kimya na kumwangalia

“Hii topic na tuachane nayo na Sophia usimzingatie sana Denisi na akiendelea na ujinga nitahakikisha anamwaga damu hapa ndani kabla ya kuondoka , Denisi usinichokoze kwasababu unahisi siwezi kukufanya chochote kwasababu kuna wazazi hapa”Aliongea Roma akiwa siriasi

“Roma usiongee hivyo Denisi ni mdogo wako?”Aliongea Blandina

“Jamani jamani mbona tulikuwa tukicheka hapa na kufurahi nadhani tuachane na habari za kuuana kwa sasa”Aliongea Jestina mke wa tajiri Azizi na Roma alibakia kimya lakini Omari alijikuta akipata msisimko kwa mtifuano wa Roma na Denisi ndugu wa damu.

Kasimu yeye alionekana kuwa na wasiwasi na alimpa ishara baba yake kuongea neno ili kutuliza hali ilioanza kubadilika.

Lakini Tajiri Azizi hakutaka kusimama upande wowote na hio yote ni kutokana na kwamba alikuwa akifahamika kama tajri lakini yote hio ni kutokana na kuweza kuoa katika familia ya Mzee Atanasi ambaye alikuwa na utajiri mkubwa ni rahisi kusema kwamba nusu ya mali alizokuwa akiendesha ni za Blandina na nusu ni za mke wake na familia , hivyo hakutaka kujiingiza kwenye ugomvi wa Denisi na Roma kwani pia alikuwa akijua siku zote Denisi ni chaguo la baba yake Raisi Senga kuliko Roma ambaye alikuwa chaguo la babu yake Afande Camillius Kweka.

Denis alifungua kile kiboksi na kuonyesha kilichokuwepo ndani na pete mbili za madini ya Platinum zilionekana ziking’aa sana zikiashiria ni za bei ghali.

“Sophia nataka uniambie sababu ambayo inakupelekea kunikataa”Aliongea Denisi kwa mara nyingine lakini muda ule ule chupa ilirushwa kuelekea upande wake kupiga kile kiboksi lakini Denisi alikuwa mwepesi kwani palepale aliizuia na ikadondoka chini na kupasuka.

Alierusha hakuwa mwingine bali ni Roma Ramoni na alionekana kuanza kukosa uvumilivu uwepo wa Denisi.

“Denisi ondoka nyumbani kwangu la sivyo nitakutoa kwa nguvu”Aliongea Roma kwa amri kali na kufanya watu kuingiwa na ubaridi

“Usiniharakishe na nitaondoka kama unavyotaka lakini lazima nithibitishe jambo moja”Aliongea na kisha palepale alimwinamia Sophia aliekuwa ameketi.

“Sophia sitokulazimisha tena nikitoka hapa lakini nataka uapie kwa mbingu na Ardhi mbele ya kila mmoja kama humpendi Roma”Aliongea kwa sauti na kila mmoja aliweza kusikia na kuwafanya kuvuta pumzi na kumwangalia Sophia kwa jibu ambalo anakwenda kutoa.













SEHEMU YA 457

Kwenye watu waliokuwa na wasiwasi muda huo alikuwa ni Blandina , ni kama alikuwa akitabiri kuna jambo baya sana linakwenda kutokea hapo ndani ,alitamani amwambie Denisi aondoke lakini hakuwa na uwezo huo , lakini pia aliogopa hasira aliokuwa nayo Roma kwani ilidhihirika kwa kila mmoja.

Uzuri ni kwamba muda huu Lanlan alikuwa upande mwingine akicheza na Qiang Xi kwa kutumia Drone yake hivyo hakuona kinachoendelea hapo.

Lakini wengine wote walionyesha wasiwasi , Neema licha ya kwamba alikuwa akimpenda Roma lakini hakuwahi kumuona akiwa na hasira namna hio na sio kwake tu kwa wengine wote walitulia kimya huku wakiomba Roma asichukue hatua yoyote.

Upande wa Sophia sura ilishabadilika na kuwa nyekundu , ni kweli alikuwa akimpenda sana Roma hivyo alishindwa kutamka kama hakuwa akimpenda Roma waziwazi , kila alipokuwa akijaribu kuongea alikosa nguvu na alijua kabisa Denisi siku hio alipanga kumkomesha.

Nikijibu simpendi si itamaanisha lazima niachane nae kabisa na kujikatia tamaa , lakini hata hivyo sio kama naweza kupata nafasi ya kumfungukia kama nampenda , kwanini nashindwa kujielezea mbele yake kwamba simpendi na hali hii ikaisha?”Maswali yalipita kwenye kichwa cha Sophia, tokea siku anafika kuishi na Roma mpango ulikuwa ni kuwa mke wa pili na si vinginevyo na mapenzi yake aliyaficha kwa kumchukulia Roma kama kaka yake , lakini ukwelia alikuwa akimpenda mno

Ukimya wa Sophia na mwonekano wake ulifanya kila mmoja kujua kile kilichokuwa kikiendelea ndani ya moyo wake , lakini hata hivyo ilikuwa kawaida kwa Roma kupendwa na wanawake wengi na sio jambo jipya na hata muda huo alikuwa amezungukwana wachumba , lakini swala la Sophia lilikuwa na utofauti kwani Edna na Sophia walitambulika kama dada na kaka na ndio maana hali ya hewa ilikuwa yenye ubaridi licha ya kwamba jiji la Dar es salaam lilikuwa na joto.

Edna mapigo ya moyo wake yalikuwa yanadunda kwa kasi , kwenye moyo wake alishajiapiza siku Roma akitoka kimahusiano na Sophia hatoangalia nyuma na wataachana kwa namna yoyote ile.

Ukweli ni kwamba alikuwa ni mwanamke mvumilivu lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea hapo ndani kama nimwanamke ambaye anaendeshwa na hisia asingeweza kuendelea kukubali yanayoendelea kwani ni kama udhalilishaji, alimchukia hata Denisi alieanzisha hio mada ghafla.

Edna sio kwamba hakujua kama Sophia hampendi Roma alikuwa akijua sana tu tokea siku aliogundua Sophia na Roma walimdanganya ka kujifanyisha ni ndugu lakini vile vile mara baada ya kusikia habari za ndoa kutoka kwa mama yake Sophia , lakini aliamini kwa kumchukulia Sophia kama mdogo wake ingemfanya Sophia kutojihusisha kabisa kimapenzi na Roma, huo ndio mtazamo wake na ni kweli Sophia alijitahidi kyaficha mahaba yake kwa Roma ili asilete mgogoro na Edna.

Edna alijikuta akipunguza wasiwasi mara baada ya kuhisi mkono wake umeshikwa chini ya meza na aligundua ni Roma aliekuwa amemshika na aliinua macho na kumwangalia na Roma alitumia ishara ya kumwambia kwamba asiwe na wasiwasi.

Edna alijua Roma alikuwa akijaribu kumfariji lakini haikuwa ikisaidia kwani wote walikuwa wakihitaji kusikia majibu kutoka kwa Sophia, lakini kubwa zaidi alijua kwamba alikuwa akiujua ukweli na alishindwa kumlaumu Sophia katika hilo kwani swala lakumpenda mtu ni swala ambalo lipo nje ya uwezo wa mtu.

“Sophia nadhani kimya chako ni jibu tosha ila nashindwa kuwaelewa nyie wanawake mnampendea nini huyu mtu kwanza kabisa sio muaminifu na amezungukwa na michepuko kibao lakini bado tu mnampenda”

“Huna haja ya kumsema vibaya Bro Roma na kingine sio lazima nikujibu kwa kila unachouliza kwani wewe sio msemaji wa maisha yangu na jibu nishakupa kwamba sipo tayari kuwa kwenye mahusiano na wewe”Aliongea Sophia kwa hasira.

“Hahaha… au nipo kizamanni inashangaza sana wanawake kumg’ang’ania mtu ambaye sio mwaminifu na kuacha yule anaewapenda kweli”

Aliongea, wakati wengine wakitaka kujua mwisho wa mazungumzo hayo Edna na Neema wenyewe walijiuliza kwanini wametokea kumpenda Roma licha ya kwamba alikuwa sio mwaminifu maana maeneno ya Denisi yalikuwa ya kweli ni kwamba tu aliyazungumza wakati ambao sio sahihi.

Roma aliamua kupunguza hasira zake kwanza na kukaa kimya huku akionyesha kufikiria namna ya kutatua hali hio.

“Denisi hivyo ndio mahusiano yalivyo na pia ndivyo wanawake walivyo na hupaswi kuwaelewa sana , inaonyesha ulikuwa na ukaribu na Sophia wa muda mrefu lakini hio isikupe sababu ya kwamba akupende licha ya kwamba wewe unampenda”

“Kaa kimya wewe chongo unajua ninni kwanza”Aliongea Denisi

“Ndio sijui kitu kwasababu hata mwanamke ninaempenda ananikataa licha ya kwamba nimekamilika na familia yangu ni kubwa pia , lakini naelewa sababu kwanini Sophia hakupendi”Aliongea

“Oh! Hebu nieleweshe”

“Ni rahisi sana , hutakiwi kumfosi licha ya kwamba alikukataa , kama kweli unampenda furaha yake ingekuwa kipaumbele, ni kama mimi tu ijapokuwa Queen amekuwa akinikataa lakini sikumlazimisha zaidi ya kwamba nilitamani aendeelee kuwa na furaha , sijui Roma ana wanawake wangapi na ni mwaminifu kwa kiasi gani lakini naamini kwa tabia yako ya kulazimisha vitu hata visivyokupenda hakuna mwanamke ambaye anaweza kukuvumilia”Aliongea Omari.

“Kaa kimya na acha kuwa mnafiki , unaongea hivyo kwasababu Roma ni rafiki yako”

“Haha.. wewe ni nani wa kuniambia ninyamaze unajifanyisha mjuaji lakini kichwani huna kitu”Aliongea Omari.

“Unaongea kishari unataka ngumi sio?”

“Acha ukijogoo Denisi , wewe ni mtoto sana kwangu”Aliongea

“Haha.. Omari usijifanyishe kwasababu baba yako ana cheo serikalini uone kwamba siwezi kufundisha adabu , Wewe huna cha kunitishia mimi”

“Jamani mnisamehe ninakwenda kuharibu wakati huu mzuri lakini hili lipuuzi siwezi kulivumilia tena”Aliongea Omari huku akionyesha kupandwa na hasira.

Mpaka hapo ugomvi ulihama kutoka kwa Roma kwenda kwa Omari na walianza kutunishiana misuli , Omari alisimama vile vile Denisi alimsogelea huku wote wakionyesha kuwa na hasira.

Omari hakumpenda Denisi kutoka na ukaribu wake na yan Buwen ambaye alikuwa ni adui yake namba moja na Denisi hakumpenda Omari kutokana na kuwa na ukaribu na Roma ambaye ni adui yake namba moja.

Omari alikuwa na nguvu za kijini levo ya Nafsi lakini Denisi vilevile mwili wake ulikuwa umefanyiwa sayansi na Yan Buwen hivyo kama ni kupigana ingekuwa ngumu kutabiri mshindi.

Omari akikasirishwa anakuwa mtu mwingine kabisa na alijiambia siku hio hamuachi salama Denisi na palepale alimpiga Denisi ngumi ya kifua na kumrudisha nyuma.

Kitendo kile kiliwafanya watu wote kusimama na kurudi nyuma huku macho yakimwangalia Roma na Tajiri Azizi pamoja na Kasimu waamue ugomvi kwani ndio waliokuwa wanaume , lakini Roma alikuwa amekaa ametulia akiangalia kwa hamu kile kinachokwenda kutokea , upande wa tajiri Azizi hakuwa na nguvu za kuamulia na Kassimu hivyo hivyo hakutaka kununua ugomvi wa watu wazima.

Denisi baada ya kurudi nyuma mara baada ya kupigwa ngumi ambayo haikuwa na madhara kwake , Omari hakutaka kumchelewesha alikuja na teke la hewani akidhamiria kumpiga Denisi kwenye mbavu lakini Denisi alikuwa ametarajia pigo lake kwani alidaka mguu wake na mkono mmoja huku akitabasamu kifedhuli.

“Unapata wapi ujasiri wa kupambana na mimi na vinguvu vyako vya kijini ulivyokuwa navyo”Aliongea Denisi na palepale kwa mkono wa kushoto alimfyatua Omari kwa kumrusha juu kupitia mguu wake aliokuwa ameushikilia.

Lakini Omari alitua salama kwani alitumia uwezo wa kijini kujikontrol , lakini hata hivyo alihamaki kwani uwezo wa Denisi ulikuwa mkubwa.

“Naona matokeo ya Yan Buwen kuufanyia mwili wako majaribio imekufanya kuimarika sana”Aliongea Omari kwa kebehi.

“Ushaanza kujitetea sasa”Aliongea Denisi huku akimpa ishara Omari kuja tena na pigo lingine , ilionekana ni kama amekuja sehemu hio kuamsha ugomvi kwani alionyesha mchecheto mno.

Queen alikuwa na wasiwasi mno kwa kile kinachoendelea na kujiuliza Denisi ana uhusiano gani na Yan Buwen na haikuwa kwake tu kila mmoja hakudhania mambo yangebadilika mpaka kufikia hapo na yote hayo ni ujio wa Denisi ndio uliovuruga kila kitu.

“Roma famya kuwaamulia bwana sio vizuri kuangalia watu wazima wakipigana mbele yetu”Aliongea Tajiri Azizi.

“Denisi acheni mnachokifanya mara moja huoni mnajidhalilisha nyie ni watu wazima”Aliongea Blandina lakini Denisi alionyesha hakuwa tayari kuliacha hilo lipite , hata hivyo ujio wake hapo ndani ulikuwa ni kutafuta ugomvi ili amkomeshe Roma ,lakini kwasabau Omari ameamua kujiingiza alijiambia ni kheri aanze nae kwanza hata hivyo Yan Buwen alikuwa akifahamu Omari ni zao la Hongmen na yupo uraini kwa misheni ya kumfatilia hivyo Denisi alijiambia akimuua huyu atajiongezea credit mbele ya Yan Buwen.

“Vipi umeufyata mkia?”Aliuliza Denisi kwa dharau na kumfanya Omari kupandwa na jaziba zaidi kwani kwenye maisha yake hakupenda dharau lakini pia Denisi alikuwa mtoto mdogo sana kwake.

“Nitakuonyesha mbwa wewe”Aliongea Omari na palepale alishika jicho lake la kushoto kwa namna ya kuliziba na alipotoa mkono jicho lilikuwa mkononi.

Kitendo kile kilimuogofya mno Queen lakini pia wengine wote walishangazwa na tukio lile ,ijappokuwa watu wengi walikuwa wakijiuliza ni kwa namna gani Omari aliweza kupona jicho lake kabisa lakini kulitoa ilikuwa tukio la ajabu mno.

Roma alijikuta mwili ukimsisimka , alikuwa akijua nini maana ya Omari kufanya vile.

Omari uwezo wake uliongezeka mara mbili yake na upande wa Denisi ni kama na yeye alifunguliwa uwezo wake wote na muda huo huo walianza kushambuliana kwa kasi kiasi kwamba ni Roma pekee aliekuwa na uwezo wa kuona namna wanavyo pambana ila wengine wote macho yao yalikuwa ya kibinadamu hivyo spidi waliokuwa wakitumia iliwafanya kuona vivuli tu na upepo ukipeperusha maua.

Omari alirusha ngumi wa haraka sana kumlenga Denisi maeneo mbalimbali ya mwili , alikuwa akitumia spidi kubwa sana lakini Denisi na yeye hakuwa vibaya kwenye kupangua.

Wanafamilia waijikuta wakiwa kwenye mshituko kwa mabadiliko hayo , ijapokuwa walishindwa kujua nani atashinda kutokana na kutoweza kuona namna ngumi zinavyotembea lakini namna walivyokuwa wakipambana ilichanganya.

“Roma waamulie bwana, mwisho wao utakuwa mbaya na mmoja anaweza kuumia na ikawa shida nyingine”Aliongea Tajiri Azizi kwa namna ya kumuamrisha Roma.

“Unafikiri nani atapoteza pambanno”Aliongea Roma kwa namna ya kuonyesha kwamba alikuwa akifurahia kinachoendelea hata hivyo matukio ya aina hio kwake yalikuwa yakawaida sana.

“Mdogo wako anaweza kuwa kwenye hatari , Omari ni kama jini”Aliongea Tajiri Azizi.

“Sio kweli Omari ndio atazidiwa”Alijibu na kuwafanya kushangaa , walikaa upande wa Denisi kutokana na namna Omari alivyotoa jicho lake kwa namna ya kimazingara hivyo walimuona Omari kama kiumbe cha ajabu.

Kitendo kile kilimfanya hata Queen kuzidi kutokumpenda Omari na kuanza kumuogopa alijiambia kheri yake Yan Buwen baba wa mtoto wake ambaye yupo tumboni.

Muda ule ule Omari alipigwa ngumi nzito ambayo ilimpata kifuani karibu na bega na kumfanya kwenda kudondoka mita kadhaa kutoka ilipo Swimming pool na hapo ndipo walipoona shati alilovaa Omari lilikwisha kuchanika upande mmoja.

Pigo lile lilimfanya sasa Roma aone uwezo halisi wa Denisi maana Omari alionyesha kushindwa kumhimili licha ya kwamba uwezo wake wa nguvu za kijini ulikuwa mkubwa.

Omari alijinyanyua kwa kujilazimisha na kusimama wima huku akitema damu , pigo alilipigwa na Denisi lilionyesha kupelekea viongo vya ndani kuathirika.

“Bado unataka kuendelea?”Aliuliza Denisi.

“Sikuwa makini ndio maana nikashindwa kukwepa ngumi yako , nisogelee tena kama unajihisi una uwezo mkubwa”Aliongea Omari huku akionyesha hali ya kutotaka kushindwa.

“Nadhani unakitafuta kifo kabisa ngoja nikumalizie kabisa nisibakiwe na deni”Aliongea huku akionyesha hali ya kuwa na hasira mno.

“Jamani inatosha sasa mtaumizana zaidi mkiendelea hivyo”Aliongea Blandina huku sauti yake ikiwa ya kitetetemshi alionyesha wasiwasi usiokuwa na kifani na alitaka Roma awazuie wasiendelee.

“Bro Roma wazuie wasiendelee”Aliongea Sophia ambaye sasa alianza kujawa na wasiwasi.

Upande wa tajiri Azizi na mke wake walijikuta hata wakijutia kuja kwenye hafla hio kwani waliamini kama kuna jambo lolote baya litakalotokea lazima wangetakiwa kutoa maelezo.

“Roma Omari ni rafiki yako , kwanini usimsaidie”Aliongea Tajiri Azizi, ukweli hakuwa na uwezo wa kumlazimisha Roma kwani alikuwa akijua hakuwa mtu wa kawiada na vile vile alikuwa akisikia habari kwmaba Omari pia hakuwa mtu wa kawaida na ndio maana hata mabadiliko hayo hakushangaa sana lakini alihofia matokeo.

“Naweza nikaingilia hapa , lakini ikanipelekea kumuumiza kabisa Denisi na wote hapa mnaweza kunilaumu kwa kusema nimempiga mdogo wangu mimi lawama sitaki”Aliongea Roma

“Roma waamulie sitojali kitakachotokea una sapoti yote kutoka kwangu”Aliongea Blandina na kumfanya Roma atabasamu ndio alichokuwa akitaka hivho , alipanga muda wote kama ni kumuua Denisi angalau apate sapoti kwa mama yake mzazi.

“Mama lakini naweza kumuaa kabisa kutokana na nguvu zake ambazo sio za kawaida”Aliongea Roma na Blandina alitaka kuongea kitu lakini mdogo wake alimzuia.

“Dada kwa mwonekano wa Denisi sidhani ni wakati wa kumuonea huruma, inaonekana hata akili sio yake tena , angalia alivyo”Aliongea mke wa tajiri Azizi.

“Najua lakini Denisi na Roma ni ndugu ..”

Mapigano sasa yalibadilika na ilikuwa ni Roma na Denisi sasa na Omari ilibidi atulie pembenni akiugulia maumivu , purukushani hizi zilimfanya hata Lanlan na Qiang Xi kufika eneo la tukio na Lanlan alisogea mbele kabisa huku akiwa amekodoa macho akishuhudia mtanange

Lanlan ndio aliekuwa akiona kabisa kile kilichokuwa kikiendelea , alikuwa na macho ambayo hayakuwa ya kwaida hivyo aliweza kuona namna baba yake anavyopigana na baba yake mdogo na alionyesha kufurahishwa na tukio hilo na kumfanya Edna kuwa na wasiwasi.

Roma alishangazwa na kitu kimoja kuhusu Denisi , ilionysha ni kama hakuwa kwenye akili yake timamu ni kama miezi kadhaa alioweza kumuadhibu akiwa na maambukizi ya kirusi cha Wolverine, alitafsiri kama athari zilizotokea kwa sayansi iliofanywa ndani ya mwili wake na Yan Buwen au alihisi huenda akili yake ilikuwa ikitawalia na Yan Buwen kwani Denisi alikuwa hana huruma kabisa kwenye macho yake na alimwangalia Roma kama Simba aliekuwa mbele ya kitoeo.

Inaawezekana kabisa kwa Yan Buwen kufanya hivyo, teknolojia ilikuwa kubwa sana na mtu kufanyiwa upasuaji na kuwekewa Chip ndani ya ubongo haikuhitaji utaalamu mkubwa na ni mchakato unachokua mwezi tu kukamilika.

Roma alijiambia lazima Yan Buwen alichukua tahadhari kila anapotengeneza mwanajeshi kwa kuwawekea sayansi ambayo ingemuewezesha kuwaendesha atakavyo na hicho ndicho kilichoonekana kwa Denisi.

Mpaka hapa Roma alijiambia hana namna zaidi ya kumuua Denisi kwani asipofanya hivyo anaweza kuwa hatari zaidi kwa usalama wa familia yake maana sasa Denisi hakuwa binadamu bali alikuwa ni kama Drone ya kijeshi inayoendeshwa kwa ajili ya kushambulia

“Roma kama usingekuja kunisaidia nilikuwa na mpango wa kuchapa Raba”Aliongea Omari akikubali kushindwa.

“Niliamini ungepambana mpaka pumzi yako ya mwisho?”

“Wewe hayo ni maamuzi ya watu wapumbavu , ninapenda maisha yangu na isitoshe Queen sijamuoa bado”Aliongea Omari.

Denisi alimsogelea Roma kwa kasi na Roma hakutaka kumpa nafasi yakumfikia na yeye alimsogelea na alipomkaribia aliachia teke ambalo lilimpiga Denisi kwenye tumbo.

Ijapokuwa Denisi alikuwa na uwezo mkubwa kutokana na uwezo aliopewa na Yan Buwen lakini hakuwa akimfikia Roma hata kwa Robo ya uwezo wake..

Teke lile lilimrusha mbali na kwenda kutua kwenye ukuta , lakini hakutaka kukata tamaa aliamka tena na kumsogeleaRoma kwa kasi huku nguvu ya ajabu ikianza kumzingira Denisi na palepale Roma alihisi kitu kisichokuwa cha kawaida ilikuwa ni nguvu ambayo hata Yan Buwen alitumia katika kupambana.

Nguvu inayotokea kwenye Godstone , ni nguvu ambayo Drogba alikuwa nayo na Clone ilikuwa nayo pia lakini kwa Denisi ilikuwa kubwa zaidi.

Roma baada ya kuona nguvu ya Denisi imejiongeza maradufu hakutaka kuzembea na yeye aliita nguvu ya kijini ya kimaandiko na kisha alitengeneza ngao kama kioo na kuisukumia aliposimama Denisi, upande wa Denisi alifanya hivyo hivyo aliachia pigo ambalo ni kama mwanga wa Radi kuelekea upande wa Roma hivyo ngao ya Roma ilikutana na shambulizi la Denisi.

Roma hakutaka kumchelewesha alikusanya nguvu ya kijini na kutengeneza shambulizo ambalo lilikuwa kama kimbunga cha mvuke na kusukumiza upande wa Denisi.

Ile ngao ilizuia pigo la Denisi na ikaruhusu shambulizi la Roma kumsogelea Denisi kwa kasi na alionekana kuchelewa kulizuia kwanni palepale upepo ambao ulikuwa kama mvuke ulimzingira kwa kasi na akawa katikati, Denisi alijikuta akitoa kelele akiashiria kuhisi maumivu makali ya kuungua , lakini licha ya hivyo Roma hakumuonea huruma na kadri nafsi yake ilivyokuwa ikinuia ndio maumivu yalivyokuwa yakizidi kumuathiri Denisi.

Ilishangaza kwa waliokuwa wakiangalia kwani hakuna walichoweza kuona zaidi ya kumuona Denisi akililia huku akitoa machozi makali ya kuhisi maumivu.

“Roma naomba umuache….”Blandina alijikuta akitoa machozi kwa tukio lile aliamini lolote litakalomtokea Denisi angewajibika na kila kitu kingebadilik.

Roma alijiambia hana haja ya kuacha na hakutaka kumuacha Denisi hai , aliamini kufanya hivyo ndio kujiweka hatari zaidi kwa Yan Buwen kuzidi kuwa na nguvu.

Watu wote walishangazwa na tukio lile na kujikuta wakitamani Roma aache anachokifanya lakini Lanlan alipiga makofi ya Shangwe huku akimwigiza Roma kwa kila alichokuwa akifanya, akizungusha mikono alikuwa akifanya hivyo hivyo kwake haikuwa hofu bali fursa ya kujifunza.

Edna baada ya kuona kitendo kile alimsogelea Lanlan kwa namna ya kutaka kumzuia asiige kinachofanyika lakini aligusa hewa kwani Lanlan alimkimbia na kwenda kusimama upande mwingine na Edna alipotaka kumfuata Sophia alimzuia na kumwambia amuache.

Denisi mara baada ya kuona hawezi kusogea kutokana na nguvu isiokuwa ya kawaida kumshika miguu huku akijihisi kuungua alijikuta bila ya kupenda akipiga magoti huku akitoa machozi ya maumivu na Roma alitabasamu kifedhuli kwani ndio alichotaka

Lakini sasa muda ule ule Denisi alisimama kwa mara nyingine na upande wa Roma kila alipojaribu kuitwa nguvu za kijini alishindwa kabisa hivyo hata kile kimbunga cha kijini cha mvuke kiliacha kumzunguka Denisi.

Muda ule ule wakati akijaribu kuita nguvu za kijini alishindwa kabisa na aliweza kushuhudia Denisi akitoka aliposimama na kumsogelea Blandina mama yake kwa spidi ya ajabu na kumlenga na ngumi kali kifuani eneo la sehemu unapokaa moyo na ngumi ile kuchangua kifua na damu kusambaa huku Blandina akitupwa mbali.

“Mamaa..!!”Roma alijikuta akitoa ukulele mara baada ya kushuhudia Denisi akimuua mama yake mbele yake huku yeye akishindwa kufanya chochote.











SEHEMU YA 458.

Ukweli ni kwamba alichokuwa akikiona Roma sio uhalisia kwamba kilikuwa kikitendeka , watu wote walishangaa kwanini alikuwa vile , Denisi hata yeye alishangazwa na mabadiliko ya Roma lakini hakutaka kujiuliza mara mbilimbili kwani alitoweka palepale baada ya kupata mwanya.

Wakati Denisi alivyokimbia Roma hakuweza hata kutambua nini kinatokea , lakini kile alichokuwa akiona sio uhalisia na alikuwa akiongea mwenyewe kama vile mtu aliechanganyikiwa ghafla.

“Roma unafanya nini?”Omari alikosa uvumilivu na kumsogelea Roma lakini Roma hakujibu zaidi ya kuendelea kuwa kimya na kuongea mwenyewe huku maneno yake yasisikike.

Watu wote walijikuta wakianza kujawa na wasiwasi kwa kile kinachomtokea Roma kwani Denisi ashakimbia lakini Roma alibakia kama amechanganyikiwa.

Roma aliendelea kumuona mama yake akiwa amepoteza maisha kwenye akili yake huku akiwa amelala chini na Denisi kupotea.

“Mama…!”Aliita huku akisogea mbele akitaka kumshika mama yake lakini palepale alipotaka kumkaribia tu kwa kumgusa alitoweka na kujikuta akishika ukuta na hapo hapo akili yake ilirudi kwenye uhalisia na baada ya kugeuka aliposimama mama yake alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akijidharau na aliweza kugundua ilikuwa ni ‘Illusion’ na alichokuwa akiona ni uhalisia mdanganyifu.

Edna na Lanlan ndio waliokuwa wa kwanza kumkimbilia na kumshika na Roma aligeuza macho yake na kuwaaangali.

“Hubby nini kimekutokea?”Edna aliuliza huku akimwangalia Roma huku machozi yakianza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake.

Roma alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kumshika Lanlan kwenye kichwa.

“Nipo sawa kuna kitu kimenitokea ila nimekuwa sawa”Aliongea .

Roma maumivu aliosikia aliposhuhudia Blandina mama yake akipoteza maisha mbele yake yalikuwa yasio ya mfano na mpaka hapo alijua ni kwa kiasi gani alikuwa akimpenda mama yake.

Kila mmoja alivuta pumzi ya ahuenni mara baada ya kuona hakuna aliekufa hapo ndani kwani ingekuwa tatizo lingine kabisa , Roma aliangalia juu angani kwa dakika kadhaa na kisha akawageukia.

“Nitarudi muda si mrefu kuna mtu napaswa kuonana nae mnaweza kusahau kilichotokea hapa na kuendelea kama kawaida”Aliongea Roma na hakusubiri jibu palepale alipotea na kumfanya Lanlan kutoa macho.

Dakika chache mbele Roma alikuja kuonekana Bagamoyo nyuma ya kituo cha afya na alitembea kwenye tifutifu ya mchanga kwenda mbele akikatisha eneo la shule ya msingikwa mbele na alikuja kusimama mara baada ya kuona mzungu mwanaume aliekuwa ameweka Headphone masikioni akiwa amechutama mbele ya bwawa la samaki ambalo limezingirwa na magugu.

Alikuwa ni mwanaume alievalia suti ya rangi nyeusi na tai nyekundu huku akiwa na nywele zake nyeupe (Blonde hair).

Kwa mwonekano wake ilionyesha dhahiri hakuwa mtu wa hilo eneo na ni mgeni ambaye alionekana kama kuvutiwa na mazingira na alikuwa amempa Roma mgongo huku akionyesha kuburudika na mziki uliokuwa ukisikika kwenye Headphone kutokana na namna alivyokuwa akitingisha kichwa.

Roma alimsogelea yule mwanaume wa kizungu taratibu na alipomfikia alimvua zile Headphone .

“Hey..!”Yule mwanaume aligeuka nyuma huku akionyesha kukasirishwa na kitendo cha kuvuliwa Headphone zake

“Nani kakwambia unaweza kunivua Headphone zangu kabla ya mziki haujamalizika?”Aliongea kwa Kijerumani.

Roma hakumjali zaidi ya kuzivaa zile Headphone ili kusikiliza mziki wenyewe na alitumia kama dakika moja na kisha alizivua huku yule mwanaume akimwangalia kwa namna ya kumchunguza kwanzia juu mpaka chini.

“Toccata and Fugue in D Minor by Bach”Aliongea Roma nakumfanya yule mzungu kushangaa.

“You know this piece?”Aliuliza akimaanisha kwamba anaufahamu huo wimbo.

“Ndio”Alijibu Roma

“Sio mbaya mtu yoyote anaelewa huo wimbo lazima aelewe maana halisi ya uhai”Aliongea kwa Kijerumanni.

“Sijasema na uelewa”

“Lakini inaonyesha unaupenda”Aliongea lakini Roma hakumjali zaidi.

“Naona una uwezo usiokuwa wa kawaida mpaka kufanikiwa kunitengenezea ‘Illusion’ ya kifo cha mama yangu kwa kuitawala akili yangu”Aliongea Roma akionyesha kwamba kitendo kilichomtokea dakika kadhaa zilizopita kilisababishwa na huyo mzungu.

“It wasn’t illusion”Aliongea huku sauti yake ikibadilika na kuwa nzito zaidi kuliko mwanzo akimaanisha kwamba alichokiona Roma haikuwa mazingira danganyifu.

“Oh! What’s that then?”Aliuliza kama sio mazingira danganyifu nini.

“Ni ndoto ambayo imetokea kwenye fahamu zako”

“Ndoto . Huh!. inaonyesha upo sahihi”Aliongea Roma

“Inaonyesha tayari umekwisha kunifahamu?”Aliuliza kwa kingereza.

“Haikuwa ngumu kwangu kukufahamu kutokana na Aura yako , licha ya kwamba ni mara yetu ya kwanza kuonana, lakini inashangaza kwanini mmoja wapo wa miungu kumi na mbili, Hermes(Mercury) akawa Vampire na isitoshe wewe ndio mwenye akili kuliko wenzako wote”

Roma pia alionyesha kushangaa na kujiuliza kuna sababu gani ya Hermes kujitokeza kwake tena kwa kipindi hicho.

Athena anaweza kuaminika kwa busara zake lakini kwa Hermes alisifika kama mchunga kondoo(sheepherd) na aliaminika kwa kuwa na mitego mingi.

Hermes katika historia ya miungu ya kigirika alifahamika kama mungu wa biashara , msafiri , mwizi , mhuni, tapeli na mpenda michezo lakini pia alifahamika kama mjumbe kati ya binadamu na miungu ya ugiriki kwasababu ya kupenda kusafiri kusafiri , kwa mfano anaweza kufika Tanzania watu wakataka kutuma salamu kwenda kwa Athena basi angewaambia kwamba wamlipe kiasi flani cha pesa na angefikisha maombi yao lakini moyoni hakuwa na mpango wa kufikisha maombi bali alifanya utapeli tu ni kama baadhi ya wachungaji wanavyowadanganya waumini walipe sadaka ili wapate magari, alikuwa pia akifahamika kwa kuupenda mziki ,ukisikia the first Song katika historia ni kutoka kwa Hermes

Roma ilikuwa mara yake ya kwanza kumfahamu na aliweza kumtambua kutokana na Aura yake na hata kuja hapo alifuata harufu(Scent).

“Nilishawahi kusikia kwamba unao uwezo wa kudhibiti miungu yote kupitia ndoto inaonyesha una uwezo mkubwa kuliko nilivyotegemea , sikuamini kwamba ungeweza kuniathiri kwa kiasi kikubwa”Aliongea Roma.

“Ni rahisi sana kila kiumbe chenye uhai lazima kiwe na mawazo na ukishakuwa na mawazo lazima uweze kuota ndoto ,hivyo ninao uwezo hata wa kutawala akili za mnyama kwa kutumia ndoto”Aliongea,

“Upo sahihi penye mawazo hapakosi ndoto”Aliongea Roma na yule mzungu alitabasamu.

“Now that we know that we’re on the same side can I have my headphones back , the newly appointed Hades”

“Sasa ushajua tupo upande mmoja nirudishie Headphone zangu , Hades mpya uliechaguliwa”Aliongea awamu hii kwa kingereza lakini Roma aliamua kukaa kwenye gogo pembeni yake na Hermes alitaka kumpokonya Roma zile Headphone lakini Roma alikwepesha mkono.

“Unafanya nini nirudishie mali yangu”

“Mpaka uniambie kwanini umemsaidia Denisi kutoroka?”Aliuliza Roma akitaka kujua kwanini huyo mzungu kaharibu mpango wake wa kumuua Denisi.

“Unataka kuujua ukwel?”Aliuliza na Roma alitingisha kichwa kukubali.

“Kama upo tayari kuniambia, nataka kuufahamu ukweli”

“Hauwezi kuniamini hata nikikuambia hata hivyo mimi ni mungu wa wezi na muongo”

“Nina akili zangu hivyo nitajua ukweli mwenyewe”Aliongea na Hermes ilibidi amwinamie sikioni na kumnong’oneza na Roma alijikuta akitoa macho huku sura yake kubadilika.

“Siku nyingine ukinichokoza siwezi kukuachia kirahisi kwa sababu zako kipuuzi”Aliongea Roma huku akisimama

“Nilijua tu hutoamini?”Aliongea lakini Roma hakujali zaidi ya kuondoka akimwacha amesimama asiamini macho yake Headphone zake za thamani kubwa zinaondoka na Roma.

“Hey! Hades are you a robber?”Aliuliza kwamba Roma ni mwizi.

“Umenichokoza mwenyewe kwa kuruhusu adui yangu kunitoroka hii ni kama fidia na sababbu yako najua ni ya uongo hivyo kama unazitaka njoo uzichukue kwenye mikono yangu”Aliongea na kumfanya Hermes kumwangalia kwamshangao

“Una uhakika gani nimedanganya?’Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli huku akimwangalia kwa namna isioelezeka anafikiria nini kwenye kichwa chake.

Mwanaume aliekuwa akiongea na Roma ni yule yule tuliemuona nchini Ujerumani akiitana na Athena kaka na dada , lakini ni yule yule ambaye alikuwa akiongea ndani ya kanisa na Snejder.

Jina lake halisi ni Prince Raphaeli na Count Dogba alieuliwa na Roma ni mtoto wake, na yeye ni Vampire.

Unafikiri kaja kulipiza kisasi

Itaendelea . Nicheki watsapp 0687151346
 
SEHEMU YA 456.

Ni mwezi mmoja sasa umepita hakuna kubwa ambalo lilitoke, Rose alikuwa tayari ashaanza kujifunza mafunzo ya kijini na alionekana kuwa na matokeo mazuri kwa kutumia mbinu ambayo Roma aliweza kuelekeza.

Upande wa wanawake wengine Roma aliweza kumuelekeza mmoja mmoja namna ya kufanya ‘Meditation’ ili kuweza kupata ‘Reveletion’ au ufunuo juu ya mbinu za kuvuna nishati kati ya mbingu na ardhi.

Ni Edna pekee ambaye alikuwa hajaanza bado na yote hio ni kutokana na Roma kuona mwili wa Edna haukuwa tayari kuhimili hivyo ilimbidi aendelee kufanya mazoezi, alikuwa na wasiwasi kuzidiwa na wenzake lakini kwasababu Roma alimwambia hakuwa tayari ilibidi amsikilize.

Sophia na yeye umaarufu ulizidi kuongezeka mara baada ya kutoa albamu yake ya kwanza ambayo ilikuwa na nyimbo zilizofanya vizuri sana na wale waliomtabiria mema kuridhishwa na matokeo , lakini hata hivyo wanasema siku zote matarajio ni mazuri kuliko matokeo hivyo kuna wale ambao pia hawakuridhishwa kwa aina yake , lakini mzani uliegamia upande wa walioridhika.

Naam ilikuwa ni siku ya Jumamosi ya tarehe ishirini ya mwezi wa pili , siku hio kulikuwa na hafla fupi ya kumpongeza Sophia kwa mafanikio yake ya kimuziki lakini kubwa zaidi siku hio pia ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa , hivyo nyumbani kwa Edna na Roma kulikuwa na sherehe ambayo ilijumuisha watu wachache sana ,mathalani ndugu wa kifamilia ambao walijumuika kwa chakula cha cha mchana.

Ni muda wa saa saba kamili ndani ye aneo la bustani walionekana watu mbalimbali waliokuwa wameketi huku wakiongea kwa vicheko, alikuwepo Neema Luwazo na mtoto wake Donyi , Nasra ,Tajiri Azizi na mke wake pamoja na Kassimu mtoto wa Tajiri Azizi wengine waliokuwepo ni Roma Edna , Bi Wema bila ya kumsahau Lanlan ambaye alikuwa kivutio zaidi.

Baada ya nusu saa kupita alifika Omari Tozo ambaye alikuwa ameambatana na Queen ambaye tumbo lake lilikuwa lishaanza kujitokeza kutokana na ujauzito.

Roma ilikuwa mara yake ya pili kukutana na Queen , mara ya kwanza ilikuwa ni ndani ya hospitali ya Aghakani na ilikuwa kipindi ambacho alikuwa akiongea na Sauroni juu ya mwanamke anaefahamika kwa jina la Zoe Kovac , hivyo baada ya kumuona mrembo yule ndio mwanamke aliekuwa akimsumbua Omari , lakini mwanamke pia ambaye alikuwa na mimba ya Yan Buwen alishangaa , lakini kubwa zaidi alishangaa mara baada ya kufahamu Queen ni mtoto wa Mzee Alex.

Upande wa Queen pia alimkumbuka Roma , lakini awamu hii alionyesha aibu kidogo kuliko kipindi kile na huenda ni kutokana na ujauzito wake.

Omari alionekana kuwa na furaha , ijapokuwa Queen hakuwa amemkubali Omari kwa ajili ya ndoa , lakini walikubaliana kuwa marafiki na Omari alionekana kufa kuoza kwa mrembo Queen hivyo licha ya kwamba Queen alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine , lakini alitaka kumuoa hivyo hivyo na kutaka mimba hio iwe ya kwake lakini Queen bado alikuwa na tumaini kwamba Yan Buwen wake angekuja kumrudia.

Blandina alifurahi sana mara baada ya kujua Omari alikuwa rafiki yake Roma , hakujua namna walivyokutana lakini alipenda urafiki wao isitoshe Omari alikuwa mtoto wa familia ya mkuu wa majeshi hivyo ilikuwa faida kwa Roma kuzungukwa na marafiki ambao wanaweza kumsaidia hata Tajiri Azizi alionyesha kufurahishwa na ukaribu wa Roma na Omari.

Edna mwenyewe alishangazwa na ukaribu wa hao wawili, ijapkuwa alitaka kujua namna walivyokutana , lakini alijiambia Omari na Roma hawana utofauti mkubwa , kwanza wote hawakuwa na aibu na ni waongeaji sana na mawazo ya Edna yalikuwa kama wa wengine tu walimuona Omari kutokuwa na aibu kama ilivyokuwa kwa Roma na alichekesha kila alipokuwa akiongea na ni kama alitawala maongezi , huku asilimia kubwa akimsifia Queen kuwa mrembo kuliko ya Edna.

Ilikuwa ni familia kamili hivyo kwa Sophia alifurahi uwepo wa kila mmoja aliefika kwa ajili yake ,ijapokuwa familia yake ilikuwa nchini Japani lakini alihisi watu waliokuwa wakimzunguka kwake ni familia tosha kabisa.

Stori mbalimbali ziliingiziwa, Donyi na Kassimu walionyesha walikuwa kwenye penzi moto moto hivyo ilikuwa ni jambo ambalo lilizungumziwa pia na ukizingatia Jestina na Tajiri Azizi walikuwepo, pamoja na Neema Luwazo ambaye muda si mrefu angekuwa na undugu utakaounganishwa na ndoa

Ilikuwa rahisi kwa tajiri Azizi kumkumbali Donyi katika familia , kwanza kabisa Kassimu ndio angekuwa mrithi wa familia , lakini pia upande wa Donyi alikuwa mrithi wa mali za mama yake hivyo walilandana kwa kiasi kikubwa kwa kuzingatia kwamba siku zote mtoto wa tajiri anamuoa mtoto wa tajiri mwenzake na ni mara chache tajiri kuolewa na masikini ni ukweli mchungu lakini ndio ilivyo.

Asilimia kubwa ya maongezi pia zilikuwa sifa kwenda kwa Edna

Wakati Stori zikiendelea geti lilifunguliwa na ikaingia gari aina ya V8 ya rangi nyeusi na alishuka Denisi kwenye gari hio huku akiwa ameshikilia furushi la mua Waridi ya rangi tofauti tofauti , ilioneysha alikuwa na taarifa ya kilichokuwa kikiendelea hapo ndani.

Ujio wake ambao haukuwa na mwaliko ulifanya watu kuwa kimya lakini hata hivyo Denisi hakuonyesha hali ya kutokujiamini zaidi ya kuwasogelea na kusaliamiana na kila mmoja na mwisho kabisa akamsogelea Sophia na kumkabidhi yale maua aina ya Roses fresh plant, Sophia hakupenda ila alipokea hivyo hivyo.

“Denisi hayo ni maua mengi sana umeweza kununua nadhani ni pesa nyingi umetumia nilitamani na mimi kumnunulia mpenzi wangu Queen kama zawadi lakini hela sina”Aiongea Omari.

“Bwana Omari unasema kwamba unashindwa kununua maua kama hayo , mbona thamani yake ni ndogo sana”Aliongea Tajiri Azizi

“Mzee nadhani hujaulizia bei ya haya maua hivi karibuni yamekuwa ghari mno na wenye bustani wengi wamekuwa wakiyasafarisha kwenda nje ya nchi kutokana na uhitaji wake kuwa mkubwa”

“Hilo naelewa kuna mmoja wa rafiki yangu ni kweli hivi karibuni aliongea kwamba maua ya Waridi yamepanda bei sana sehemu nyingi za dunia , hivyo uhitaji wake kuwa mkubwa na thamani kupanda , lakini hata hivyo sio lazima kumzawadia unaempenda na maua ya Waridi kwani kuna aina yingi za maua ambazo zinawakilisha upendo pia”Aliongea

“Imekuwa ngumu kwa hapa Tanzania kuweza kuhifadhi maua na Watanzania wengi hawajachangamka juu ya uthamani wa maua , kuna siku nilipotembelea Thailland na Singapore nilishangazwa na mashamba makubwa ya maua ya Roses , ilinitamanisha na kampuni yangu ya Maple kuwa na shamba moja lakini Watanzania wengi sio wenye kuzingatia kupeana zawadi za maua”Aliongea Neema , ilikuwa sawa kuongea hivyo kwani alikuwa mfanya biashara na siku zote wafanyabiashara kila kinachomzunguka anakiangalia kwa namna ya fursa.

Lakini ilikuwa ukweli kwamba ni mara chache sana watanzania kupeana zawadi za maua kama Zawadi, wanawake wengi wa Afrika wanachopenda zaidi ni pesa , pesa na pesa tena au vitu vya thamani kubwa maua watakwambia waachie Nyuki , yaani una mpenzi wako yupo Manzese ndani ndani huko umbebee zawadi ya maua unaachwa siku hio hio.

Kwa wenzetu ni tofauti sana lakini hata hapa Tanzania ustaarabu huo upo lakini kwa watu wachache sana , ndio maana ukitembelea majiji makubwa kama Paris , Guanzhou au Seoul utakuta bustani zipo kila kona katikati ya jiji na uzaji wa maua ni biashara nzuri tu.

Chakula kiliandaliwa na wahudumu waliopewa tenda ya kazi hio ,walikuwa ni wafanyakazi kutoka moja ya hoteli ambayo ilikuwa chini ya umiliki wa Edna.

Baada ya kufurahia chakula pamoja mpaka kumaliza , Denisi alisimama na kisha akamsogelea Sophia.

“Sophia nimekuletea zawadi nyingine , hizi siku chache sitokuwepo Tanzania kwa ajili ya misheni maalumu hivyo naomba nikupatie leo hii hii katika siku yako maalumu ya kuzaliwa”Aliongea Denisi bila ya aibu mbele ya watu wote na kufanya kimya kitawale.

Kilikuwa ni kiboksi cha rangi nyeusi ambacho kwa haraka haraka mtu angegundua ndani yake kulikuwa na nini.

“Asante sana kwa zawadi , lakini siwezi kuipokea”Aliongea Sophia huku akiangalia kiboksi ambacho ndani yake kama hakikuwa na mkufu wa dhahabu basi ni saa au Pete.

Watu wote walikuwa kimya kuangalia namna tukio hilo linavyochukua nafasi yake , lakini hata hivyo walishangazwa na namna ya Denisi asivyokuwa na aibu , lakini kwa wakati mmoja walishangazwa na namna Sophia alivyokataa zawadi ile.

“Denisi unaboa sana ,inaonyesha kwenye maswala ya wanawake upo kama mimi tu na Roma hapa anatushinda kwenye vitu vingi..”Aliongea Omari kama kawaida yake ya kuvunja ukimya.

Denisi mara baada ya kusikia maneno yale alimgeukia Roma na kumwangalia kwa muda mfupi kisha akamgeukia Sophia kwa mara nyingine.

“Sophia sijui ni sababu gani ambayo inakufanya unikatae tumejuana kwa muda mrefu sana na tumepitia mengi na hata ulivyonikataa kipindi kile niliona labda ni kwasababu haukuwa tayari , lakini vipi kuhusu sasa huna sababbu yoyote ya kunikataa kwani hata mpenzi huna, nini kinakuzuia kufanya maamuzi”Aliongea Denisi bila kujali kuna watu wazima waliokuwa wamezunguka.

Ukweli ni kwamba Sophia alimkataa mara nyingi Denisi na sio mara mooja tu ni zaidi ya mara mbili , kilichokuwa kikimuuma sana Denisi ni kwamba Sophia sababu kubwa iliokuwa ikimpelekea kumkataa ni Roma.

Ikumbukwe Denisi na Sophia walishawahi kufanya mafunzo pamoja na Kung Fu Nchini China katika moja ya Temple maarufu na huko ndipo walipofahamiana na hata Denisi kuweka hisia zake wazi kwa mara ya kwanza na ndio mara ya kwanza ambayo Sophia alimkataa Denisi.

Sophia alikuwa na hasira kwani aliona ni kama Denisi anamdhalilisha mbele ya kundi la watu.

“Sababu kubwa ni kwamba sikupendi Denisi”Aliongea Sophia na kauli yake ilikuwa ikionyesha kukasirika na Edna alijikuta na yeye kuona Denisi anavuka mipaka na aliona aingilie.

“Denisi huwezi kumlazimisha Sophia akupende , hivyo usimsumbue tena”Aliongea Edna.

“Denisi nadhani alichoongea Shemeji yako ni sahihi , Sophia hakupendi na huwezi kumlazimisha na hata hivyo ana ndoto nyingi za kutimiza hivyo nadhani ni sababu pia ya kutotaka kujihusha na mapenzi”Aliongea Blandina.

“Mimi siamini hio ndio sababu kubwa”Aliongea Denisi na kufanya watu kumwangalia kwa shauku , huku wengi wao wakisisimkwa na mwili kwani hali haikuwa ya kawaida na walishangazwa na ukiburi na kujiamini kwa Denisi.

“Naamini Sophia kuna mtu anampenda ndio maana hataki kunikubalia”Aliongea Denisi huku akimwangalia Roma.

Ndio Denisi anajua Sophia anampenda Roma na Sophia mwenyewe ndio aliemwmabia hivyo , na ilionekana hata ujio wake siku hio ulikuwa ni kutaka kumchokoza Roma mbele ya Edna mke wake , lakini pia mbele ya wazazi wa Roma.

Denisi alikuwa akijua fika Sophia hakuwa na uhusiano wa kindugu na Edna licha ya kwamba watu waliwachukulia kama dada na mdogo wake , mwanzoni ingeweza kufahamika Edna ni dada kamili wa damu kwa Sophia lakini mara baada ya Marehemu Adebayo kujulikana hakuwa na uwezo wakumzalisha mwanamke hivyo moja kwa moja ni kwamba Edna na Sophia ni wa damu tofauti na kama ni udada basi ni ule wa hiari ,sasa yote hayo Dennisi alikuwa akiyajua na aliamini huenda Sophia mapenzi yake juu ya Roma ni ya siri na Edna hayafahamu , hivyo kufahamu kuna kajisherehe aliona yes ndio nafasi nzuri ya kumfanya Sophia aweke wazi kile anachojaribu kuficha.

Sasa kitendo cha Denisi kuongea vile halafu akamwangalia Roma ni kama alikuwa akitoa majibu.

Watu wote walimwangalia Roma na kisha wakamgeukia Sophia wakisubiria jibu .

“Hapana! Msisikilize kwani sina mwanaume ninaempenda kwa sasa nikwamba tu sitaki kuwa na mahusiano na Denisi kwani hana vigezo ninavyovitaka”Aliongea Sophia ili kutuliza ile hali.

Edna alimwangalia Sophia kwa namna ya kumchunguza na kisha akamgeukia Roma aliekuwa kimya na kumwangalia

“Hii topic na tuachane nayo na Sophia usimzingatie sana Denisi na akiendelea na ujinga nitahakikisha anamwaga damu hapa ndani kabla ya kuondoka , Denisi usinichokoze kwasababu unahisi siwezi kukufanya chochote kwasababu kuna wazazi hapa”Aliongea Roma akiwa siriasi

“Roma usiongee hivyo Denisi ni mdogo wako?”Aliongea Blandina

“Jamani jamani mbona tulikuwa tukicheka hapa na kufurahi nadhani tuachane na habari za kuuana kwa sasa”Aliongea Jestina mke wa tajiri Azizi na Roma alibakia kimya lakini Omari alijikuta akipata msisimko kwa mtifuano wa Roma na Denisi ndugu wa damu.

Kasimu yeye alionekana kuwa na wasiwasi na alimpa ishara baba yake kuongea neno ili kutuliza hali ilioanza kubadilika.

Lakini Tajiri Azizi hakutaka kusimama upande wowote na hio yote ni kutokana na kwamba alikuwa akifahamika kama tajri lakini yote hio ni kutokana na kuweza kuoa katika familia ya Mzee Atanasi ambaye alikuwa na utajiri mkubwa ni rahisi kusema kwamba nusu ya mali alizokuwa akiendesha ni za Blandina na nusu ni za mke wake na familia , hivyo hakutaka kujiingiza kwenye ugomvi wa Denisi na Roma kwani pia alikuwa akijua siku zote Denisi ni chaguo la baba yake Raisi Senga kuliko Roma ambaye alikuwa chaguo la babu yake Afande Camillius Kweka.

Denis alifungua kile kiboksi na kuonyesha kilichokuwepo ndani na pete mbili za madini ya Platinum zilionekana ziking’aa sana zikiashiria ni za bei ghali.

“Sophia nataka uniambie sababu ambayo inakupelekea kunikataa”Aliongea Denisi kwa mara nyingine lakini muda ule ule chupa ilirushwa kuelekea upande wake kupiga kile kiboksi lakini Denisi alikuwa mwepesi kwani palepale aliizuia na ikadondoka chini na kupasuka.

Alierusha hakuwa mwingine bali ni Roma Ramoni na alionekana kuanza kukosa uvumilivu uwepo wa Denisi.

“Denisi ondoka nyumbani kwangu la sivyo nitakutoa kwa nguvu”Aliongea Roma kwa amri kali na kufanya watu kuingiwa na ubaridi

“Usiniharakishe na nitaondoka kama unavyotaka lakini lazima nithibitishe jambo moja”Aliongea na kisha palepale alimwinamia Sophia aliekuwa ameketi.

“Sophia sitokulazimisha tena nikitoka hapa lakini nataka uapie kwa mbingu na Ardhi mbele ya kila mmoja kama humpendi Roma”Aliongea kwa sauti na kila mmoja aliweza kusikia na kuwafanya kuvuta pumzi na kumwangalia Sophia kwa jibu ambalo anakwenda kutoa.













SEHEMU YA 457

Kwenye watu waliokuwa na wasiwasi muda huo alikuwa ni Blandina , ni kama alikuwa akitabiri kuna jambo baya sana linakwenda kutokea hapo ndani ,alitamani amwambie Denisi aondoke lakini hakuwa na uwezo huo , lakini pia aliogopa hasira aliokuwa nayo Roma kwani ilidhihirika kwa kila mmoja.

Uzuri ni kwamba muda huu Lanlan alikuwa upande mwingine akicheza na Qiang Xi kwa kutumia Drone yake hivyo hakuona kinachoendelea hapo.

Lakini wengine wote walionyesha wasiwasi , Neema licha ya kwamba alikuwa akimpenda Roma lakini hakuwahi kumuona akiwa na hasira namna hio na sio kwake tu kwa wengine wote walitulia kimya huku wakiomba Roma asichukue hatua yoyote.

Upande wa Sophia sura ilishabadilika na kuwa nyekundu , ni kweli alikuwa akimpenda sana Roma hivyo alishindwa kutamka kama hakuwa akimpenda Roma waziwazi , kila alipokuwa akijaribu kuongea alikosa nguvu na alijua kabisa Denisi siku hio alipanga kumkomesha.

Nikijibu simpendi si itamaanisha lazima niachane nae kabisa na kujikatia tamaa , lakini hata hivyo sio kama naweza kupata nafasi ya kumfungukia kama nampenda , kwanini nashindwa kujielezea mbele yake kwamba simpendi na hali hii ikaisha?”Maswali yalipita kwenye kichwa cha Sophia, tokea siku anafika kuishi na Roma mpango ulikuwa ni kuwa mke wa pili na si vinginevyo na mapenzi yake aliyaficha kwa kumchukulia Roma kama kaka yake , lakini ukwelia alikuwa akimpenda mno

Ukimya wa Sophia na mwonekano wake ulifanya kila mmoja kujua kile kilichokuwa kikiendelea ndani ya moyo wake , lakini hata hivyo ilikuwa kawaida kwa Roma kupendwa na wanawake wengi na sio jambo jipya na hata muda huo alikuwa amezungukwana wachumba , lakini swala la Sophia lilikuwa na utofauti kwani Edna na Sophia walitambulika kama dada na kaka na ndio maana hali ya hewa ilikuwa yenye ubaridi licha ya kwamba jiji la Dar es salaam lilikuwa na joto.

Edna mapigo ya moyo wake yalikuwa yanadunda kwa kasi , kwenye moyo wake alishajiapiza siku Roma akitoka kimahusiano na Sophia hatoangalia nyuma na wataachana kwa namna yoyote ile.

Ukweli ni kwamba alikuwa ni mwanamke mvumilivu lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea hapo ndani kama nimwanamke ambaye anaendeshwa na hisia asingeweza kuendelea kukubali yanayoendelea kwani ni kama udhalilishaji, alimchukia hata Denisi alieanzisha hio mada ghafla.

Edna sio kwamba hakujua kama Sophia hampendi Roma alikuwa akijua sana tu tokea siku aliogundua Sophia na Roma walimdanganya ka kujifanyisha ni ndugu lakini vile vile mara baada ya kusikia habari za ndoa kutoka kwa mama yake Sophia , lakini aliamini kwa kumchukulia Sophia kama mdogo wake ingemfanya Sophia kutojihusisha kabisa kimapenzi na Roma, huo ndio mtazamo wake na ni kweli Sophia alijitahidi kyaficha mahaba yake kwa Roma ili asilete mgogoro na Edna.

Edna alijikuta akipunguza wasiwasi mara baada ya kuhisi mkono wake umeshikwa chini ya meza na aligundua ni Roma aliekuwa amemshika na aliinua macho na kumwangalia na Roma alitumia ishara ya kumwambia kwamba asiwe na wasiwasi.

Edna alijua Roma alikuwa akijaribu kumfariji lakini haikuwa ikisaidia kwani wote walikuwa wakihitaji kusikia majibu kutoka kwa Sophia, lakini kubwa zaidi alijua kwamba alikuwa akiujua ukweli na alishindwa kumlaumu Sophia katika hilo kwani swala lakumpenda mtu ni swala ambalo lipo nje ya uwezo wa mtu.

“Sophia nadhani kimya chako ni jibu tosha ila nashindwa kuwaelewa nyie wanawake mnampendea nini huyu mtu kwanza kabisa sio muaminifu na amezungukwa na michepuko kibao lakini bado tu mnampenda”

“Huna haja ya kumsema vibaya Bro Roma na kingine sio lazima nikujibu kwa kila unachouliza kwani wewe sio msemaji wa maisha yangu na jibu nishakupa kwamba sipo tayari kuwa kwenye mahusiano na wewe”Aliongea Sophia kwa hasira.

“Hahaha… au nipo kizamanni inashangaza sana wanawake kumg’ang’ania mtu ambaye sio mwaminifu na kuacha yule anaewapenda kweli”

Aliongea, wakati wengine wakitaka kujua mwisho wa mazungumzo hayo Edna na Neema wenyewe walijiuliza kwanini wametokea kumpenda Roma licha ya kwamba alikuwa sio mwaminifu maana maeneno ya Denisi yalikuwa ya kweli ni kwamba tu aliyazungumza wakati ambao sio sahihi.

Roma aliamua kupunguza hasira zake kwanza na kukaa kimya huku akionyesha kufikiria namna ya kutatua hali hio.

“Denisi hivyo ndio mahusiano yalivyo na pia ndivyo wanawake walivyo na hupaswi kuwaelewa sana , inaonyesha ulikuwa na ukaribu na Sophia wa muda mrefu lakini hio isikupe sababu ya kwamba akupende licha ya kwamba wewe unampenda”

“Kaa kimya wewe chongo unajua ninni kwanza”Aliongea Denisi

“Ndio sijui kitu kwasababu hata mwanamke ninaempenda ananikataa licha ya kwamba nimekamilika na familia yangu ni kubwa pia , lakini naelewa sababu kwanini Sophia hakupendi”Aliongea

“Oh! Hebu nieleweshe”

“Ni rahisi sana , hutakiwi kumfosi licha ya kwamba alikukataa , kama kweli unampenda furaha yake ingekuwa kipaumbele, ni kama mimi tu ijapokuwa Queen amekuwa akinikataa lakini sikumlazimisha zaidi ya kwamba nilitamani aendeelee kuwa na furaha , sijui Roma ana wanawake wangapi na ni mwaminifu kwa kiasi gani lakini naamini kwa tabia yako ya kulazimisha vitu hata visivyokupenda hakuna mwanamke ambaye anaweza kukuvumilia”Aliongea Omari.

“Kaa kimya na acha kuwa mnafiki , unaongea hivyo kwasababu Roma ni rafiki yako”

“Haha.. wewe ni nani wa kuniambia ninyamaze unajifanyisha mjuaji lakini kichwani huna kitu”Aliongea Omari.

“Unaongea kishari unataka ngumi sio?”

“Acha ukijogoo Denisi , wewe ni mtoto sana kwangu”Aliongea

“Haha.. Omari usijifanyishe kwasababu baba yako ana cheo serikalini uone kwamba siwezi kufundisha adabu , Wewe huna cha kunitishia mimi”

“Jamani mnisamehe ninakwenda kuharibu wakati huu mzuri lakini hili lipuuzi siwezi kulivumilia tena”Aliongea Omari huku akionyesha kupandwa na hasira.

Mpaka hapo ugomvi ulihama kutoka kwa Roma kwenda kwa Omari na walianza kutunishiana misuli , Omari alisimama vile vile Denisi alimsogelea huku wote wakionyesha kuwa na hasira.

Omari hakumpenda Denisi kutoka na ukaribu wake na yan Buwen ambaye alikuwa ni adui yake namba moja na Denisi hakumpenda Omari kutokana na kuwa na ukaribu na Roma ambaye ni adui yake namba moja.

Omari alikuwa na nguvu za kijini levo ya Nafsi lakini Denisi vilevile mwili wake ulikuwa umefanyiwa sayansi na Yan Buwen hivyo kama ni kupigana ingekuwa ngumu kutabiri mshindi.

Omari akikasirishwa anakuwa mtu mwingine kabisa na alijiambia siku hio hamuachi salama Denisi na palepale alimpiga Denisi ngumi ya kifua na kumrudisha nyuma.

Kitendo kile kiliwafanya watu wote kusimama na kurudi nyuma huku macho yakimwangalia Roma na Tajiri Azizi pamoja na Kasimu waamue ugomvi kwani ndio waliokuwa wanaume , lakini Roma alikuwa amekaa ametulia akiangalia kwa hamu kile kinachokwenda kutokea , upande wa tajiri Azizi hakuwa na nguvu za kuamulia na Kassimu hivyo hivyo hakutaka kununua ugomvi wa watu wazima.

Denisi baada ya kurudi nyuma mara baada ya kupigwa ngumi ambayo haikuwa na madhara kwake , Omari hakutaka kumchelewesha alikuja na teke la hewani akidhamiria kumpiga Denisi kwenye mbavu lakini Denisi alikuwa ametarajia pigo lake kwani alidaka mguu wake na mkono mmoja huku akitabasamu kifedhuli.

“Unapata wapi ujasiri wa kupambana na mimi na vinguvu vyako vya kijini ulivyokuwa navyo”Aliongea Denisi na palepale kwa mkono wa kushoto alimfyatua Omari kwa kumrusha juu kupitia mguu wake aliokuwa ameushikilia.

Lakini Omari alitua salama kwani alitumia uwezo wa kijini kujikontrol , lakini hata hivyo alihamaki kwani uwezo wa Denisi ulikuwa mkubwa.

“Naona matokeo ya Yan Buwen kuufanyia mwili wako majaribio imekufanya kuimarika sana”Aliongea Omari kwa kebehi.

“Ushaanza kujitetea sasa”Aliongea Denisi huku akimpa ishara Omari kuja tena na pigo lingine , ilionekana ni kama amekuja sehemu hio kuamsha ugomvi kwani alionyesha mchecheto mno.

Queen alikuwa na wasiwasi mno kwa kile kinachoendelea na kujiuliza Denisi ana uhusiano gani na Yan Buwen na haikuwa kwake tu kila mmoja hakudhania mambo yangebadilika mpaka kufikia hapo na yote hayo ni ujio wa Denisi ndio uliovuruga kila kitu.

“Roma famya kuwaamulia bwana sio vizuri kuangalia watu wazima wakipigana mbele yetu”Aliongea Tajiri Azizi.

“Denisi acheni mnachokifanya mara moja huoni mnajidhalilisha nyie ni watu wazima”Aliongea Blandina lakini Denisi alionyesha hakuwa tayari kuliacha hilo lipite , hata hivyo ujio wake hapo ndani ulikuwa ni kutafuta ugomvi ili amkomeshe Roma ,lakini kwasabau Omari ameamua kujiingiza alijiambia ni kheri aanze nae kwanza hata hivyo Yan Buwen alikuwa akifahamu Omari ni zao la Hongmen na yupo uraini kwa misheni ya kumfatilia hivyo Denisi alijiambia akimuua huyu atajiongezea credit mbele ya Yan Buwen.

“Vipi umeufyata mkia?”Aliuliza Denisi kwa dharau na kumfanya Omari kupandwa na jaziba zaidi kwani kwenye maisha yake hakupenda dharau lakini pia Denisi alikuwa mtoto mdogo sana kwake.

“Nitakuonyesha mbwa wewe”Aliongea Omari na palepale alishika jicho lake la kushoto kwa namna ya kuliziba na alipotoa mkono jicho lilikuwa mkononi.

Kitendo kile kilimuogofya mno Queen lakini pia wengine wote walishangazwa na tukio lile ,ijappokuwa watu wengi walikuwa wakijiuliza ni kwa namna gani Omari aliweza kupona jicho lake kabisa lakini kulitoa ilikuwa tukio la ajabu mno.

Roma alijikuta mwili ukimsisimka , alikuwa akijua nini maana ya Omari kufanya vile.

Omari uwezo wake uliongezeka mara mbili yake na upande wa Denisi ni kama na yeye alifunguliwa uwezo wake wote na muda huo huo walianza kushambuliana kwa kasi kiasi kwamba ni Roma pekee aliekuwa na uwezo wa kuona namna wanavyo pambana ila wengine wote macho yao yalikuwa ya kibinadamu hivyo spidi waliokuwa wakitumia iliwafanya kuona vivuli tu na upepo ukipeperusha maua.

Omari alirusha ngumi wa haraka sana kumlenga Denisi maeneo mbalimbali ya mwili , alikuwa akitumia spidi kubwa sana lakini Denisi na yeye hakuwa vibaya kwenye kupangua.

Wanafamilia waijikuta wakiwa kwenye mshituko kwa mabadiliko hayo , ijapokuwa walishindwa kujua nani atashinda kutokana na kutoweza kuona namna ngumi zinavyotembea lakini namna walivyokuwa wakipambana ilichanganya.

“Roma waamulie bwana, mwisho wao utakuwa mbaya na mmoja anaweza kuumia na ikawa shida nyingine”Aliongea Tajiri Azizi kwa namna ya kumuamrisha Roma.

“Unafikiri nani atapoteza pambanno”Aliongea Roma kwa namna ya kuonyesha kwamba alikuwa akifurahia kinachoendelea hata hivyo matukio ya aina hio kwake yalikuwa yakawaida sana.

“Mdogo wako anaweza kuwa kwenye hatari , Omari ni kama jini”Aliongea Tajiri Azizi.

“Sio kweli Omari ndio atazidiwa”Alijibu na kuwafanya kushangaa , walikaa upande wa Denisi kutokana na namna Omari alivyotoa jicho lake kwa namna ya kimazingara hivyo walimuona Omari kama kiumbe cha ajabu.

Kitendo kile kilimfanya hata Queen kuzidi kutokumpenda Omari na kuanza kumuogopa alijiambia kheri yake Yan Buwen baba wa mtoto wake ambaye yupo tumboni.

Muda ule ule Omari alipigwa ngumi nzito ambayo ilimpata kifuani karibu na bega na kumfanya kwenda kudondoka mita kadhaa kutoka ilipo Swimming pool na hapo ndipo walipoona shati alilovaa Omari lilikwisha kuchanika upande mmoja.

Pigo lile lilimfanya sasa Roma aone uwezo halisi wa Denisi maana Omari alionyesha kushindwa kumhimili licha ya kwamba uwezo wake wa nguvu za kijini ulikuwa mkubwa.

Omari alijinyanyua kwa kujilazimisha na kusimama wima huku akitema damu , pigo alilipigwa na Denisi lilionyesha kupelekea viongo vya ndani kuathirika.

“Bado unataka kuendelea?”Aliuliza Denisi.

“Sikuwa makini ndio maana nikashindwa kukwepa ngumi yako , nisogelee tena kama unajihisi una uwezo mkubwa”Aliongea Omari huku akionyesha hali ya kutotaka kushindwa.

“Nadhani unakitafuta kifo kabisa ngoja nikumalizie kabisa nisibakiwe na deni”Aliongea huku akionyesha hali ya kuwa na hasira mno.

“Jamani inatosha sasa mtaumizana zaidi mkiendelea hivyo”Aliongea Blandina huku sauti yake ikiwa ya kitetetemshi alionyesha wasiwasi usiokuwa na kifani na alitaka Roma awazuie wasiendelee.

“Bro Roma wazuie wasiendelee”Aliongea Sophia ambaye sasa alianza kujawa na wasiwasi.

Upande wa tajiri Azizi na mke wake walijikuta hata wakijutia kuja kwenye hafla hio kwani waliamini kama kuna jambo lolote baya litakalotokea lazima wangetakiwa kutoa maelezo.

“Roma Omari ni rafiki yako , kwanini usimsaidie”Aliongea Tajiri Azizi, ukweli hakuwa na uwezo wa kumlazimisha Roma kwani alikuwa akijua hakuwa mtu wa kawiada na vile vile alikuwa akisikia habari kwmaba Omari pia hakuwa mtu wa kawaida na ndio maana hata mabadiliko hayo hakushangaa sana lakini alihofia matokeo.

“Naweza nikaingilia hapa , lakini ikanipelekea kumuumiza kabisa Denisi na wote hapa mnaweza kunilaumu kwa kusema nimempiga mdogo wangu mimi lawama sitaki”Aliongea Roma

“Roma waamulie sitojali kitakachotokea una sapoti yote kutoka kwangu”Aliongea Blandina na kumfanya Roma atabasamu ndio alichokuwa akitaka hivho , alipanga muda wote kama ni kumuua Denisi angalau apate sapoti kwa mama yake mzazi.

“Mama lakini naweza kumuaa kabisa kutokana na nguvu zake ambazo sio za kawaida”Aliongea Roma na Blandina alitaka kuongea kitu lakini mdogo wake alimzuia.

“Dada kwa mwonekano wa Denisi sidhani ni wakati wa kumuonea huruma, inaonekana hata akili sio yake tena , angalia alivyo”Aliongea mke wa tajiri Azizi.

“Najua lakini Denisi na Roma ni ndugu ..”

Mapigano sasa yalibadilika na ilikuwa ni Roma na Denisi sasa na Omari ilibidi atulie pembenni akiugulia maumivu , purukushani hizi zilimfanya hata Lanlan na Qiang Xi kufika eneo la tukio na Lanlan alisogea mbele kabisa huku akiwa amekodoa macho akishuhudia mtanange

Lanlan ndio aliekuwa akiona kabisa kile kilichokuwa kikiendelea , alikuwa na macho ambayo hayakuwa ya kwaida hivyo aliweza kuona namna baba yake anavyopigana na baba yake mdogo na alionyesha kufurahishwa na tukio hilo na kumfanya Edna kuwa na wasiwasi.

Roma alishangazwa na kitu kimoja kuhusu Denisi , ilionysha ni kama hakuwa kwenye akili yake timamu ni kama miezi kadhaa alioweza kumuadhibu akiwa na maambukizi ya kirusi cha Wolverine, alitafsiri kama athari zilizotokea kwa sayansi iliofanywa ndani ya mwili wake na Yan Buwen au alihisi huenda akili yake ilikuwa ikitawalia na Yan Buwen kwani Denisi alikuwa hana huruma kabisa kwenye macho yake na alimwangalia Roma kama Simba aliekuwa mbele ya kitoeo.

Inaawezekana kabisa kwa Yan Buwen kufanya hivyo, teknolojia ilikuwa kubwa sana na mtu kufanyiwa upasuaji na kuwekewa Chip ndani ya ubongo haikuhitaji utaalamu mkubwa na ni mchakato unachokua mwezi tu kukamilika.

Roma alijiambia lazima Yan Buwen alichukua tahadhari kila anapotengeneza mwanajeshi kwa kuwawekea sayansi ambayo ingemuewezesha kuwaendesha atakavyo na hicho ndicho kilichoonekana kwa Denisi.

Mpaka hapa Roma alijiambia hana namna zaidi ya kumuua Denisi kwani asipofanya hivyo anaweza kuwa hatari zaidi kwa usalama wa familia yake maana sasa Denisi hakuwa binadamu bali alikuwa ni kama Drone ya kijeshi inayoendeshwa kwa ajili ya kushambulia

“Roma kama usingekuja kunisaidia nilikuwa na mpango wa kuchapa Raba”Aliongea Omari akikubali kushindwa.

“Niliamini ungepambana mpaka pumzi yako ya mwisho?”

“Wewe hayo ni maamuzi ya watu wapumbavu , ninapenda maisha yangu na isitoshe Queen sijamuoa bado”Aliongea Omari.

Denisi alimsogelea Roma kwa kasi na Roma hakutaka kumpa nafasi yakumfikia na yeye alimsogelea na alipomkaribia aliachia teke ambalo lilimpiga Denisi kwenye tumbo.

Ijapokuwa Denisi alikuwa na uwezo mkubwa kutokana na uwezo aliopewa na Yan Buwen lakini hakuwa akimfikia Roma hata kwa Robo ya uwezo wake..

Teke lile lilimrusha mbali na kwenda kutua kwenye ukuta , lakini hakutaka kukata tamaa aliamka tena na kumsogeleaRoma kwa kasi huku nguvu ya ajabu ikianza kumzingira Denisi na palepale Roma alihisi kitu kisichokuwa cha kawaida ilikuwa ni nguvu ambayo hata Yan Buwen alitumia katika kupambana.

Nguvu inayotokea kwenye Godstone , ni nguvu ambayo Drogba alikuwa nayo na Clone ilikuwa nayo pia lakini kwa Denisi ilikuwa kubwa zaidi.

Roma baada ya kuona nguvu ya Denisi imejiongeza maradufu hakutaka kuzembea na yeye aliita nguvu ya kijini ya kimaandiko na kisha alitengeneza ngao kama kioo na kuisukumia aliposimama Denisi, upande wa Denisi alifanya hivyo hivyo aliachia pigo ambalo ni kama mwanga wa Radi kuelekea upande wa Roma hivyo ngao ya Roma ilikutana na shambulizi la Denisi.

Roma hakutaka kumchelewesha alikusanya nguvu ya kijini na kutengeneza shambulizo ambalo lilikuwa kama kimbunga cha mvuke na kusukumiza upande wa Denisi.

Ile ngao ilizuia pigo la Denisi na ikaruhusu shambulizi la Roma kumsogelea Denisi kwa kasi na alionekana kuchelewa kulizuia kwanni palepale upepo ambao ulikuwa kama mvuke ulimzingira kwa kasi na akawa katikati, Denisi alijikuta akitoa kelele akiashiria kuhisi maumivu makali ya kuungua , lakini licha ya hivyo Roma hakumuonea huruma na kadri nafsi yake ilivyokuwa ikinuia ndio maumivu yalivyokuwa yakizidi kumuathiri Denisi.

Ilishangaza kwa waliokuwa wakiangalia kwani hakuna walichoweza kuona zaidi ya kumuona Denisi akililia huku akitoa machozi makali ya kuhisi maumivu.

“Roma naomba umuache….”Blandina alijikuta akitoa machozi kwa tukio lile aliamini lolote litakalomtokea Denisi angewajibika na kila kitu kingebadilik.

Roma alijiambia hana haja ya kuacha na hakutaka kumuacha Denisi hai , aliamini kufanya hivyo ndio kujiweka hatari zaidi kwa Yan Buwen kuzidi kuwa na nguvu.

Watu wote walishangazwa na tukio lile na kujikuta wakitamani Roma aache anachokifanya lakini Lanlan alipiga makofi ya Shangwe huku akimwigiza Roma kwa kila alichokuwa akifanya, akizungusha mikono alikuwa akifanya hivyo hivyo kwake haikuwa hofu bali fursa ya kujifunza.

Edna baada ya kuona kitendo kile alimsogelea Lanlan kwa namna ya kutaka kumzuia asiige kinachofanyika lakini aligusa hewa kwani Lanlan alimkimbia na kwenda kusimama upande mwingine na Edna alipotaka kumfuata Sophia alimzuia na kumwambia amuache.

Denisi mara baada ya kuona hawezi kusogea kutokana na nguvu isiokuwa ya kawaida kumshika miguu huku akijihisi kuungua alijikuta bila ya kupenda akipiga magoti huku akitoa machozi ya maumivu na Roma alitabasamu kifedhuli kwani ndio alichotaka

Lakini sasa muda ule ule Denisi alisimama kwa mara nyingine na upande wa Roma kila alipojaribu kuitwa nguvu za kijini alishindwa kabisa hivyo hata kile kimbunga cha kijini cha mvuke kiliacha kumzunguka Denisi.

Muda ule ule wakati akijaribu kuita nguvu za kijini alishindwa kabisa na aliweza kushuhudia Denisi akitoka aliposimama na kumsogelea Blandina mama yake kwa spidi ya ajabu na kumlenga na ngumi kali kifuani eneo la sehemu unapokaa moyo na ngumi ile kuchangua kifua na damu kusambaa huku Blandina akitupwa mbali.

“Mamaa..!!”Roma alijikuta akitoa ukulele mara baada ya kushuhudia Denisi akimuua mama yake mbele yake huku yeye akishindwa kufanya chochote.











SEHEMU YA 458.

Ukweli ni kwamba alichokuwa akikiona Roma sio uhalisia kwamba kilikuwa kikitendeka , watu wote walishangaa kwanini alikuwa vile , Denisi hata yeye alishangazwa na mabadiliko ya Roma lakini hakutaka kujiuliza mara mbilimbili kwani alitoweka palepale baada ya kupata mwanya.

Wakati Denisi alivyokimbia Roma hakuweza hata kutambua nini kinatokea , lakini kile alichokuwa akiona sio uhalisia na alikuwa akiongea mwenyewe kama vile mtu aliechanganyikiwa ghafla.

“Roma unafanya nini?”Omari alikosa uvumilivu na kumsogelea Roma lakini Roma hakujibu zaidi ya kuendelea kuwa kimya na kuongea mwenyewe huku maneno yake yasisikike.

Watu wote walijikuta wakianza kujawa na wasiwasi kwa kile kinachomtokea Roma kwani Denisi ashakimbia lakini Roma alibakia kama amechanganyikiwa.

Roma aliendelea kumuona mama yake akiwa amepoteza maisha kwenye akili yake huku akiwa amelala chini na Denisi kupotea.

“Mama…!”Aliita huku akisogea mbele akitaka kumshika mama yake lakini palepale alipotaka kumkaribia tu kwa kumgusa alitoweka na kujikuta akishika ukuta na hapo hapo akili yake ilirudi kwenye uhalisia na baada ya kugeuka aliposimama mama yake alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akijidharau na aliweza kugundua ilikuwa ni ‘Illusion’ na alichokuwa akiona ni uhalisia mdanganyifu.

Edna na Lanlan ndio waliokuwa wa kwanza kumkimbilia na kumshika na Roma aligeuza macho yake na kuwaaangali.

“Hubby nini kimekutokea?”Edna aliuliza huku akimwangalia Roma huku machozi yakianza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake.

Roma alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kumshika Lanlan kwenye kichwa.

“Nipo sawa kuna kitu kimenitokea ila nimekuwa sawa”Aliongea .

Roma maumivu aliosikia aliposhuhudia Blandina mama yake akipoteza maisha mbele yake yalikuwa yasio ya mfano na mpaka hapo alijua ni kwa kiasi gani alikuwa akimpenda mama yake.

Kila mmoja alivuta pumzi ya ahuenni mara baada ya kuona hakuna aliekufa hapo ndani kwani ingekuwa tatizo lingine kabisa , Roma aliangalia juu angani kwa dakika kadhaa na kisha akawageukia.

“Nitarudi muda si mrefu kuna mtu napaswa kuonana nae mnaweza kusahau kilichotokea hapa na kuendelea kama kawaida”Aliongea Roma na hakusubiri jibu palepale alipotea na kumfanya Lanlan kutoa macho.

Dakika chache mbele Roma alikuja kuonekana Bagamoyo nyuma ya kituo cha afya na alitembea kwenye tifutifu ya mchanga kwenda mbele akikatisha eneo la shule ya msingikwa mbele na alikuja kusimama mara baada ya kuona mzungu mwanaume aliekuwa ameweka Headphone masikioni akiwa amechutama mbele ya bwawa la samaki ambalo limezingirwa na magugu.

Alikuwa ni mwanaume alievalia suti ya rangi nyeusi na tai nyekundu huku akiwa na nywele zake nyeupe (Blonde hair).

Kwa mwonekano wake ilionyesha dhahiri hakuwa mtu wa hilo eneo na ni mgeni ambaye alionekana kama kuvutiwa na mazingira na alikuwa amempa Roma mgongo huku akionyesha kuburudika na mziki uliokuwa ukisikika kwenye Headphone kutokana na namna alivyokuwa akitingisha kichwa.

Roma alimsogelea yule mwanaume wa kizungu taratibu na alipomfikia alimvua zile Headphone .

“Hey..!”Yule mwanaume aligeuka nyuma huku akionyesha kukasirishwa na kitendo cha kuvuliwa Headphone zake

“Nani kakwambia unaweza kunivua Headphone zangu kabla ya mziki haujamalizika?”Aliongea kwa Kijerumani.

Roma hakumjali zaidi ya kuzivaa zile Headphone ili kusikiliza mziki wenyewe na alitumia kama dakika moja na kisha alizivua huku yule mwanaume akimwangalia kwa namna ya kumchunguza kwanzia juu mpaka chini.

“Toccata and Fugue in D Minor by Bach”Aliongea Roma nakumfanya yule mzungu kushangaa.

“You know this piece?”Aliuliza akimaanisha kwamba anaufahamu huo wimbo.

“Ndio”Alijibu Roma

“Sio mbaya mtu yoyote anaelewa huo wimbo lazima aelewe maana halisi ya uhai”Aliongea kwa Kijerumanni.

“Sijasema na uelewa”

“Lakini inaonyesha unaupenda”Aliongea lakini Roma hakumjali zaidi.

“Naona una uwezo usiokuwa wa kawaida mpaka kufanikiwa kunitengenezea ‘Illusion’ ya kifo cha mama yangu kwa kuitawala akili yangu”Aliongea Roma akionyesha kwamba kitendo kilichomtokea dakika kadhaa zilizopita kilisababishwa na huyo mzungu.

“It wasn’t illusion”Aliongea huku sauti yake ikibadilika na kuwa nzito zaidi kuliko mwanzo akimaanisha kwamba alichokiona Roma haikuwa mazingira danganyifu.

“Oh! What’s that then?”Aliuliza kama sio mazingira danganyifu nini.

“Ni ndoto ambayo imetokea kwenye fahamu zako”

“Ndoto . Huh!. inaonyesha upo sahihi”Aliongea Roma

“Inaonyesha tayari umekwisha kunifahamu?”Aliuliza kwa kingereza.

“Haikuwa ngumu kwangu kukufahamu kutokana na Aura yako , licha ya kwamba ni mara yetu ya kwanza kuonana, lakini inashangaza kwanini mmoja wapo wa miungu kumi na mbili, Hermes(Mercury) akawa Vampire na isitoshe wewe ndio mwenye akili kuliko wenzako wote”

Roma pia alionyesha kushangaa na kujiuliza kuna sababu gani ya Hermes kujitokeza kwake tena kwa kipindi hicho.

Athena anaweza kuaminika kwa busara zake lakini kwa Hermes alisifika kama mchunga kondoo(sheepherd) na aliaminika kwa kuwa na mitego mingi.

Hermes katika historia ya miungu ya kigirika alifahamika kama mungu wa biashara , msafiri , mwizi , mhuni, tapeli na mpenda michezo lakini pia alifahamika kama mjumbe kati ya binadamu na miungu ya ugiriki kwasababu ya kupenda kusafiri kusafiri , kwa mfano anaweza kufika Tanzania watu wakataka kutuma salamu kwenda kwa Athena basi angewaambia kwamba wamlipe kiasi flani cha pesa na angefikisha maombi yao lakini moyoni hakuwa na mpango wa kufikisha maombi bali alifanya utapeli tu ni kama baadhi ya wachungaji wanavyowadanganya waumini walipe sadaka ili wapate magari, alikuwa pia akifahamika kwa kuupenda mziki ,ukisikia the first Song katika historia ni kutoka kwa Hermes

Roma ilikuwa mara yake ya kwanza kumfahamu na aliweza kumtambua kutokana na Aura yake na hata kuja hapo alifuata harufu(Scent).

“Nilishawahi kusikia kwamba unao uwezo wa kudhibiti miungu yote kupitia ndoto inaonyesha una uwezo mkubwa kuliko nilivyotegemea , sikuamini kwamba ungeweza kuniathiri kwa kiasi kikubwa”Aliongea Roma.

“Ni rahisi sana kila kiumbe chenye uhai lazima kiwe na mawazo na ukishakuwa na mawazo lazima uweze kuota ndoto ,hivyo ninao uwezo hata wa kutawala akili za mnyama kwa kutumia ndoto”Aliongea,

“Upo sahihi penye mawazo hapakosi ndoto”Aliongea Roma na yule mzungu alitabasamu.

“Now that we know that we’re on the same side can I have my headphones back , the newly appointed Hades”

“Sasa ushajua tupo upande mmoja nirudishie Headphone zangu , Hades mpya uliechaguliwa”Aliongea awamu hii kwa kingereza lakini Roma aliamua kukaa kwenye gogo pembeni yake na Hermes alitaka kumpokonya Roma zile Headphone lakini Roma alikwepesha mkono.

“Unafanya nini nirudishie mali yangu”

“Mpaka uniambie kwanini umemsaidia Denisi kutoroka?”Aliuliza Roma akitaka kujua kwanini huyo mzungu kaharibu mpango wake wa kumuua Denisi.

“Unataka kuujua ukwel?”Aliuliza na Roma alitingisha kichwa kukubali.

“Kama upo tayari kuniambia, nataka kuufahamu ukweli”

“Hauwezi kuniamini hata nikikuambia hata hivyo mimi ni mungu wa wezi na muongo”

“Nina akili zangu hivyo nitajua ukweli mwenyewe”Aliongea na Hermes ilibidi amwinamie sikioni na kumnong’oneza na Roma alijikuta akitoa macho huku sura yake kubadilika.

“Siku nyingine ukinichokoza siwezi kukuachia kirahisi kwa sababu zako kipuuzi”Aliongea Roma huku akisimama

“Nilijua tu hutoamini?”Aliongea lakini Roma hakujali zaidi ya kuondoka akimwacha amesimama asiamini macho yake Headphone zake za thamani kubwa zinaondoka na Roma.

“Hey! Hades are you a robber?”Aliuliza kwamba Roma ni mwizi.

“Umenichokoza mwenyewe kwa kuruhusu adui yangu kunitoroka hii ni kama fidia na sababbu yako najua ni ya uongo hivyo kama unazitaka njoo uzichukue kwenye mikono yangu”Aliongea na kumfanya Hermes kumwangalia kwamshangao

“Una uhakika gani nimedanganya?’Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli huku akimwangalia kwa namna isioelezeka anafikiria nini kwenye kichwa chake.

Mwanaume aliekuwa akiongea na Roma ni yule yule tuliemuona nchini Ujerumani akiitana na Athena kaka na dada , lakini ni yule yule ambaye alikuwa akiongea ndani ya kanisa na Snejder.

Jina lake halisi ni Prince Raphaeli na Count Dogba alieuliwa na Roma ni mtoto wake, na yeye ni Vampire.

Unafikiri kaja kulipiza kisasi

Itaendelea . Nicheki watsapp 0687151346
Mmmh.
 
SEHEMU YA 456.

Ni mwezi mmoja sasa umepita hakuna kubwa ambalo lilitoke, Rose alikuwa tayari ashaanza kujifunza mafunzo ya kijini na alionekana kuwa na matokeo mazuri kwa kutumia mbinu ambayo Roma aliweza kuelekeza.

Upande wa wanawake wengine Roma aliweza kumuelekeza mmoja mmoja namna ya kufanya ‘Meditation’ ili kuweza kupata ‘Reveletion’ au ufunuo juu ya mbinu za kuvuna nishati kati ya mbingu na ardhi.

Ni Edna pekee ambaye alikuwa hajaanza bado na yote hio ni kutokana na Roma kuona mwili wa Edna haukuwa tayari kuhimili hivyo ilimbidi aendelee kufanya mazoezi, alikuwa na wasiwasi kuzidiwa na wenzake lakini kwasababu Roma alimwambia hakuwa tayari ilibidi amsikilize.

Sophia na yeye umaarufu ulizidi kuongezeka mara baada ya kutoa albamu yake ya kwanza ambayo ilikuwa na nyimbo zilizofanya vizuri sana na wale waliomtabiria mema kuridhishwa na matokeo , lakini hata hivyo wanasema siku zote matarajio ni mazuri kuliko matokeo hivyo kuna wale ambao pia hawakuridhishwa kwa aina yake , lakini mzani uliegamia upande wa walioridhika.

Naam ilikuwa ni siku ya Jumamosi ya tarehe ishirini ya mwezi wa pili , siku hio kulikuwa na hafla fupi ya kumpongeza Sophia kwa mafanikio yake ya kimuziki lakini kubwa zaidi siku hio pia ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa , hivyo nyumbani kwa Edna na Roma kulikuwa na sherehe ambayo ilijumuisha watu wachache sana ,mathalani ndugu wa kifamilia ambao walijumuika kwa chakula cha cha mchana.

Ni muda wa saa saba kamili ndani ye aneo la bustani walionekana watu mbalimbali waliokuwa wameketi huku wakiongea kwa vicheko, alikuwepo Neema Luwazo na mtoto wake Donyi , Nasra ,Tajiri Azizi na mke wake pamoja na Kassimu mtoto wa Tajiri Azizi wengine waliokuwepo ni Roma Edna , Bi Wema bila ya kumsahau Lanlan ambaye alikuwa kivutio zaidi.

Baada ya nusu saa kupita alifika Omari Tozo ambaye alikuwa ameambatana na Queen ambaye tumbo lake lilikuwa lishaanza kujitokeza kutokana na ujauzito.

Roma ilikuwa mara yake ya pili kukutana na Queen , mara ya kwanza ilikuwa ni ndani ya hospitali ya Aghakani na ilikuwa kipindi ambacho alikuwa akiongea na Sauroni juu ya mwanamke anaefahamika kwa jina la Zoe Kovac , hivyo baada ya kumuona mrembo yule ndio mwanamke aliekuwa akimsumbua Omari , lakini mwanamke pia ambaye alikuwa na mimba ya Yan Buwen alishangaa , lakini kubwa zaidi alishangaa mara baada ya kufahamu Queen ni mtoto wa Mzee Alex.

Upande wa Queen pia alimkumbuka Roma , lakini awamu hii alionyesha aibu kidogo kuliko kipindi kile na huenda ni kutokana na ujauzito wake.

Omari alionekana kuwa na furaha , ijapokuwa Queen hakuwa amemkubali Omari kwa ajili ya ndoa , lakini walikubaliana kuwa marafiki na Omari alionekana kufa kuoza kwa mrembo Queen hivyo licha ya kwamba Queen alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine , lakini alitaka kumuoa hivyo hivyo na kutaka mimba hio iwe ya kwake lakini Queen bado alikuwa na tumaini kwamba Yan Buwen wake angekuja kumrudia.

Blandina alifurahi sana mara baada ya kujua Omari alikuwa rafiki yake Roma , hakujua namna walivyokutana lakini alipenda urafiki wao isitoshe Omari alikuwa mtoto wa familia ya mkuu wa majeshi hivyo ilikuwa faida kwa Roma kuzungukwa na marafiki ambao wanaweza kumsaidia hata Tajiri Azizi alionyesha kufurahishwa na ukaribu wa Roma na Omari.

Edna mwenyewe alishangazwa na ukaribu wa hao wawili, ijapkuwa alitaka kujua namna walivyokutana , lakini alijiambia Omari na Roma hawana utofauti mkubwa , kwanza wote hawakuwa na aibu na ni waongeaji sana na mawazo ya Edna yalikuwa kama wa wengine tu walimuona Omari kutokuwa na aibu kama ilivyokuwa kwa Roma na alichekesha kila alipokuwa akiongea na ni kama alitawala maongezi , huku asilimia kubwa akimsifia Queen kuwa mrembo kuliko ya Edna.

Ilikuwa ni familia kamili hivyo kwa Sophia alifurahi uwepo wa kila mmoja aliefika kwa ajili yake ,ijapokuwa familia yake ilikuwa nchini Japani lakini alihisi watu waliokuwa wakimzunguka kwake ni familia tosha kabisa.

Stori mbalimbali ziliingiziwa, Donyi na Kassimu walionyesha walikuwa kwenye penzi moto moto hivyo ilikuwa ni jambo ambalo lilizungumziwa pia na ukizingatia Jestina na Tajiri Azizi walikuwepo, pamoja na Neema Luwazo ambaye muda si mrefu angekuwa na undugu utakaounganishwa na ndoa

Ilikuwa rahisi kwa tajiri Azizi kumkumbali Donyi katika familia , kwanza kabisa Kassimu ndio angekuwa mrithi wa familia , lakini pia upande wa Donyi alikuwa mrithi wa mali za mama yake hivyo walilandana kwa kiasi kikubwa kwa kuzingatia kwamba siku zote mtoto wa tajiri anamuoa mtoto wa tajiri mwenzake na ni mara chache tajiri kuolewa na masikini ni ukweli mchungu lakini ndio ilivyo.

Asilimia kubwa ya maongezi pia zilikuwa sifa kwenda kwa Edna

Wakati Stori zikiendelea geti lilifunguliwa na ikaingia gari aina ya V8 ya rangi nyeusi na alishuka Denisi kwenye gari hio huku akiwa ameshikilia furushi la mua Waridi ya rangi tofauti tofauti , ilioneysha alikuwa na taarifa ya kilichokuwa kikiendelea hapo ndani.

Ujio wake ambao haukuwa na mwaliko ulifanya watu kuwa kimya lakini hata hivyo Denisi hakuonyesha hali ya kutokujiamini zaidi ya kuwasogelea na kusaliamiana na kila mmoja na mwisho kabisa akamsogelea Sophia na kumkabidhi yale maua aina ya Roses fresh plant, Sophia hakupenda ila alipokea hivyo hivyo.

“Denisi hayo ni maua mengi sana umeweza kununua nadhani ni pesa nyingi umetumia nilitamani na mimi kumnunulia mpenzi wangu Queen kama zawadi lakini hela sina”Aiongea Omari.

“Bwana Omari unasema kwamba unashindwa kununua maua kama hayo , mbona thamani yake ni ndogo sana”Aliongea Tajiri Azizi

“Mzee nadhani hujaulizia bei ya haya maua hivi karibuni yamekuwa ghari mno na wenye bustani wengi wamekuwa wakiyasafarisha kwenda nje ya nchi kutokana na uhitaji wake kuwa mkubwa”

“Hilo naelewa kuna mmoja wa rafiki yangu ni kweli hivi karibuni aliongea kwamba maua ya Waridi yamepanda bei sana sehemu nyingi za dunia , hivyo uhitaji wake kuwa mkubwa na thamani kupanda , lakini hata hivyo sio lazima kumzawadia unaempenda na maua ya Waridi kwani kuna aina yingi za maua ambazo zinawakilisha upendo pia”Aliongea

“Imekuwa ngumu kwa hapa Tanzania kuweza kuhifadhi maua na Watanzania wengi hawajachangamka juu ya uthamani wa maua , kuna siku nilipotembelea Thailland na Singapore nilishangazwa na mashamba makubwa ya maua ya Roses , ilinitamanisha na kampuni yangu ya Maple kuwa na shamba moja lakini Watanzania wengi sio wenye kuzingatia kupeana zawadi za maua”Aliongea Neema , ilikuwa sawa kuongea hivyo kwani alikuwa mfanya biashara na siku zote wafanyabiashara kila kinachomzunguka anakiangalia kwa namna ya fursa.

Lakini ilikuwa ukweli kwamba ni mara chache sana watanzania kupeana zawadi za maua kama Zawadi, wanawake wengi wa Afrika wanachopenda zaidi ni pesa , pesa na pesa tena au vitu vya thamani kubwa maua watakwambia waachie Nyuki , yaani una mpenzi wako yupo Manzese ndani ndani huko umbebee zawadi ya maua unaachwa siku hio hio.

Kwa wenzetu ni tofauti sana lakini hata hapa Tanzania ustaarabu huo upo lakini kwa watu wachache sana , ndio maana ukitembelea majiji makubwa kama Paris , Guanzhou au Seoul utakuta bustani zipo kila kona katikati ya jiji na uzaji wa maua ni biashara nzuri tu.

Chakula kiliandaliwa na wahudumu waliopewa tenda ya kazi hio ,walikuwa ni wafanyakazi kutoka moja ya hoteli ambayo ilikuwa chini ya umiliki wa Edna.

Baada ya kufurahia chakula pamoja mpaka kumaliza , Denisi alisimama na kisha akamsogelea Sophia.

“Sophia nimekuletea zawadi nyingine , hizi siku chache sitokuwepo Tanzania kwa ajili ya misheni maalumu hivyo naomba nikupatie leo hii hii katika siku yako maalumu ya kuzaliwa”Aliongea Denisi bila ya aibu mbele ya watu wote na kufanya kimya kitawale.

Kilikuwa ni kiboksi cha rangi nyeusi ambacho kwa haraka haraka mtu angegundua ndani yake kulikuwa na nini.

“Asante sana kwa zawadi , lakini siwezi kuipokea”Aliongea Sophia huku akiangalia kiboksi ambacho ndani yake kama hakikuwa na mkufu wa dhahabu basi ni saa au Pete.

Watu wote walikuwa kimya kuangalia namna tukio hilo linavyochukua nafasi yake , lakini hata hivyo walishangazwa na namna ya Denisi asivyokuwa na aibu , lakini kwa wakati mmoja walishangazwa na namna Sophia alivyokataa zawadi ile.

“Denisi unaboa sana ,inaonyesha kwenye maswala ya wanawake upo kama mimi tu na Roma hapa anatushinda kwenye vitu vingi..”Aliongea Omari kama kawaida yake ya kuvunja ukimya.

Denisi mara baada ya kusikia maneno yale alimgeukia Roma na kumwangalia kwa muda mfupi kisha akamgeukia Sophia kwa mara nyingine.

“Sophia sijui ni sababu gani ambayo inakufanya unikatae tumejuana kwa muda mrefu sana na tumepitia mengi na hata ulivyonikataa kipindi kile niliona labda ni kwasababu haukuwa tayari , lakini vipi kuhusu sasa huna sababbu yoyote ya kunikataa kwani hata mpenzi huna, nini kinakuzuia kufanya maamuzi”Aliongea Denisi bila kujali kuna watu wazima waliokuwa wamezunguka.

Ukweli ni kwamba Sophia alimkataa mara nyingi Denisi na sio mara mooja tu ni zaidi ya mara mbili , kilichokuwa kikimuuma sana Denisi ni kwamba Sophia sababu kubwa iliokuwa ikimpelekea kumkataa ni Roma.

Ikumbukwe Denisi na Sophia walishawahi kufanya mafunzo pamoja na Kung Fu Nchini China katika moja ya Temple maarufu na huko ndipo walipofahamiana na hata Denisi kuweka hisia zake wazi kwa mara ya kwanza na ndio mara ya kwanza ambayo Sophia alimkataa Denisi.

Sophia alikuwa na hasira kwani aliona ni kama Denisi anamdhalilisha mbele ya kundi la watu.

“Sababu kubwa ni kwamba sikupendi Denisi”Aliongea Sophia na kauli yake ilikuwa ikionyesha kukasirika na Edna alijikuta na yeye kuona Denisi anavuka mipaka na aliona aingilie.

“Denisi huwezi kumlazimisha Sophia akupende , hivyo usimsumbue tena”Aliongea Edna.

“Denisi nadhani alichoongea Shemeji yako ni sahihi , Sophia hakupendi na huwezi kumlazimisha na hata hivyo ana ndoto nyingi za kutimiza hivyo nadhani ni sababu pia ya kutotaka kujihusha na mapenzi”Aliongea Blandina.

“Mimi siamini hio ndio sababu kubwa”Aliongea Denisi na kufanya watu kumwangalia kwa shauku , huku wengi wao wakisisimkwa na mwili kwani hali haikuwa ya kawaida na walishangazwa na ukiburi na kujiamini kwa Denisi.

“Naamini Sophia kuna mtu anampenda ndio maana hataki kunikubalia”Aliongea Denisi huku akimwangalia Roma.

Ndio Denisi anajua Sophia anampenda Roma na Sophia mwenyewe ndio aliemwmabia hivyo , na ilionekana hata ujio wake siku hio ulikuwa ni kutaka kumchokoza Roma mbele ya Edna mke wake , lakini pia mbele ya wazazi wa Roma.

Denisi alikuwa akijua fika Sophia hakuwa na uhusiano wa kindugu na Edna licha ya kwamba watu waliwachukulia kama dada na mdogo wake , mwanzoni ingeweza kufahamika Edna ni dada kamili wa damu kwa Sophia lakini mara baada ya Marehemu Adebayo kujulikana hakuwa na uwezo wakumzalisha mwanamke hivyo moja kwa moja ni kwamba Edna na Sophia ni wa damu tofauti na kama ni udada basi ni ule wa hiari ,sasa yote hayo Dennisi alikuwa akiyajua na aliamini huenda Sophia mapenzi yake juu ya Roma ni ya siri na Edna hayafahamu , hivyo kufahamu kuna kajisherehe aliona yes ndio nafasi nzuri ya kumfanya Sophia aweke wazi kile anachojaribu kuficha.

Sasa kitendo cha Denisi kuongea vile halafu akamwangalia Roma ni kama alikuwa akitoa majibu.

Watu wote walimwangalia Roma na kisha wakamgeukia Sophia wakisubiria jibu .

“Hapana! Msisikilize kwani sina mwanaume ninaempenda kwa sasa nikwamba tu sitaki kuwa na mahusiano na Denisi kwani hana vigezo ninavyovitaka”Aliongea Sophia ili kutuliza ile hali.

Edna alimwangalia Sophia kwa namna ya kumchunguza na kisha akamgeukia Roma aliekuwa kimya na kumwangalia

“Hii topic na tuachane nayo na Sophia usimzingatie sana Denisi na akiendelea na ujinga nitahakikisha anamwaga damu hapa ndani kabla ya kuondoka , Denisi usinichokoze kwasababu unahisi siwezi kukufanya chochote kwasababu kuna wazazi hapa”Aliongea Roma akiwa siriasi

“Roma usiongee hivyo Denisi ni mdogo wako?”Aliongea Blandina

“Jamani jamani mbona tulikuwa tukicheka hapa na kufurahi nadhani tuachane na habari za kuuana kwa sasa”Aliongea Jestina mke wa tajiri Azizi na Roma alibakia kimya lakini Omari alijikuta akipata msisimko kwa mtifuano wa Roma na Denisi ndugu wa damu.

Kasimu yeye alionekana kuwa na wasiwasi na alimpa ishara baba yake kuongea neno ili kutuliza hali ilioanza kubadilika.

Lakini Tajiri Azizi hakutaka kusimama upande wowote na hio yote ni kutokana na kwamba alikuwa akifahamika kama tajri lakini yote hio ni kutokana na kuweza kuoa katika familia ya Mzee Atanasi ambaye alikuwa na utajiri mkubwa ni rahisi kusema kwamba nusu ya mali alizokuwa akiendesha ni za Blandina na nusu ni za mke wake na familia , hivyo hakutaka kujiingiza kwenye ugomvi wa Denisi na Roma kwani pia alikuwa akijua siku zote Denisi ni chaguo la baba yake Raisi Senga kuliko Roma ambaye alikuwa chaguo la babu yake Afande Camillius Kweka.

Denis alifungua kile kiboksi na kuonyesha kilichokuwepo ndani na pete mbili za madini ya Platinum zilionekana ziking’aa sana zikiashiria ni za bei ghali.

“Sophia nataka uniambie sababu ambayo inakupelekea kunikataa”Aliongea Denisi kwa mara nyingine lakini muda ule ule chupa ilirushwa kuelekea upande wake kupiga kile kiboksi lakini Denisi alikuwa mwepesi kwani palepale aliizuia na ikadondoka chini na kupasuka.

Alierusha hakuwa mwingine bali ni Roma Ramoni na alionekana kuanza kukosa uvumilivu uwepo wa Denisi.

“Denisi ondoka nyumbani kwangu la sivyo nitakutoa kwa nguvu”Aliongea Roma kwa amri kali na kufanya watu kuingiwa na ubaridi

“Usiniharakishe na nitaondoka kama unavyotaka lakini lazima nithibitishe jambo moja”Aliongea na kisha palepale alimwinamia Sophia aliekuwa ameketi.

“Sophia sitokulazimisha tena nikitoka hapa lakini nataka uapie kwa mbingu na Ardhi mbele ya kila mmoja kama humpendi Roma”Aliongea kwa sauti na kila mmoja aliweza kusikia na kuwafanya kuvuta pumzi na kumwangalia Sophia kwa jibu ambalo anakwenda kutoa.













SEHEMU YA 457

Kwenye watu waliokuwa na wasiwasi muda huo alikuwa ni Blandina , ni kama alikuwa akitabiri kuna jambo baya sana linakwenda kutokea hapo ndani ,alitamani amwambie Denisi aondoke lakini hakuwa na uwezo huo , lakini pia aliogopa hasira aliokuwa nayo Roma kwani ilidhihirika kwa kila mmoja.

Uzuri ni kwamba muda huu Lanlan alikuwa upande mwingine akicheza na Qiang Xi kwa kutumia Drone yake hivyo hakuona kinachoendelea hapo.

Lakini wengine wote walionyesha wasiwasi , Neema licha ya kwamba alikuwa akimpenda Roma lakini hakuwahi kumuona akiwa na hasira namna hio na sio kwake tu kwa wengine wote walitulia kimya huku wakiomba Roma asichukue hatua yoyote.

Upande wa Sophia sura ilishabadilika na kuwa nyekundu , ni kweli alikuwa akimpenda sana Roma hivyo alishindwa kutamka kama hakuwa akimpenda Roma waziwazi , kila alipokuwa akijaribu kuongea alikosa nguvu na alijua kabisa Denisi siku hio alipanga kumkomesha.

Nikijibu simpendi si itamaanisha lazima niachane nae kabisa na kujikatia tamaa , lakini hata hivyo sio kama naweza kupata nafasi ya kumfungukia kama nampenda , kwanini nashindwa kujielezea mbele yake kwamba simpendi na hali hii ikaisha?”Maswali yalipita kwenye kichwa cha Sophia, tokea siku anafika kuishi na Roma mpango ulikuwa ni kuwa mke wa pili na si vinginevyo na mapenzi yake aliyaficha kwa kumchukulia Roma kama kaka yake , lakini ukwelia alikuwa akimpenda mno

Ukimya wa Sophia na mwonekano wake ulifanya kila mmoja kujua kile kilichokuwa kikiendelea ndani ya moyo wake , lakini hata hivyo ilikuwa kawaida kwa Roma kupendwa na wanawake wengi na sio jambo jipya na hata muda huo alikuwa amezungukwana wachumba , lakini swala la Sophia lilikuwa na utofauti kwani Edna na Sophia walitambulika kama dada na kaka na ndio maana hali ya hewa ilikuwa yenye ubaridi licha ya kwamba jiji la Dar es salaam lilikuwa na joto.

Edna mapigo ya moyo wake yalikuwa yanadunda kwa kasi , kwenye moyo wake alishajiapiza siku Roma akitoka kimahusiano na Sophia hatoangalia nyuma na wataachana kwa namna yoyote ile.

Ukweli ni kwamba alikuwa ni mwanamke mvumilivu lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea hapo ndani kama nimwanamke ambaye anaendeshwa na hisia asingeweza kuendelea kukubali yanayoendelea kwani ni kama udhalilishaji, alimchukia hata Denisi alieanzisha hio mada ghafla.

Edna sio kwamba hakujua kama Sophia hampendi Roma alikuwa akijua sana tu tokea siku aliogundua Sophia na Roma walimdanganya ka kujifanyisha ni ndugu lakini vile vile mara baada ya kusikia habari za ndoa kutoka kwa mama yake Sophia , lakini aliamini kwa kumchukulia Sophia kama mdogo wake ingemfanya Sophia kutojihusisha kabisa kimapenzi na Roma, huo ndio mtazamo wake na ni kweli Sophia alijitahidi kyaficha mahaba yake kwa Roma ili asilete mgogoro na Edna.

Edna alijikuta akipunguza wasiwasi mara baada ya kuhisi mkono wake umeshikwa chini ya meza na aligundua ni Roma aliekuwa amemshika na aliinua macho na kumwangalia na Roma alitumia ishara ya kumwambia kwamba asiwe na wasiwasi.

Edna alijua Roma alikuwa akijaribu kumfariji lakini haikuwa ikisaidia kwani wote walikuwa wakihitaji kusikia majibu kutoka kwa Sophia, lakini kubwa zaidi alijua kwamba alikuwa akiujua ukweli na alishindwa kumlaumu Sophia katika hilo kwani swala lakumpenda mtu ni swala ambalo lipo nje ya uwezo wa mtu.

“Sophia nadhani kimya chako ni jibu tosha ila nashindwa kuwaelewa nyie wanawake mnampendea nini huyu mtu kwanza kabisa sio muaminifu na amezungukwa na michepuko kibao lakini bado tu mnampenda”

“Huna haja ya kumsema vibaya Bro Roma na kingine sio lazima nikujibu kwa kila unachouliza kwani wewe sio msemaji wa maisha yangu na jibu nishakupa kwamba sipo tayari kuwa kwenye mahusiano na wewe”Aliongea Sophia kwa hasira.

“Hahaha… au nipo kizamanni inashangaza sana wanawake kumg’ang’ania mtu ambaye sio mwaminifu na kuacha yule anaewapenda kweli”

Aliongea, wakati wengine wakitaka kujua mwisho wa mazungumzo hayo Edna na Neema wenyewe walijiuliza kwanini wametokea kumpenda Roma licha ya kwamba alikuwa sio mwaminifu maana maeneno ya Denisi yalikuwa ya kweli ni kwamba tu aliyazungumza wakati ambao sio sahihi.

Roma aliamua kupunguza hasira zake kwanza na kukaa kimya huku akionyesha kufikiria namna ya kutatua hali hio.

“Denisi hivyo ndio mahusiano yalivyo na pia ndivyo wanawake walivyo na hupaswi kuwaelewa sana , inaonyesha ulikuwa na ukaribu na Sophia wa muda mrefu lakini hio isikupe sababu ya kwamba akupende licha ya kwamba wewe unampenda”

“Kaa kimya wewe chongo unajua ninni kwanza”Aliongea Denisi

“Ndio sijui kitu kwasababu hata mwanamke ninaempenda ananikataa licha ya kwamba nimekamilika na familia yangu ni kubwa pia , lakini naelewa sababu kwanini Sophia hakupendi”Aliongea

“Oh! Hebu nieleweshe”

“Ni rahisi sana , hutakiwi kumfosi licha ya kwamba alikukataa , kama kweli unampenda furaha yake ingekuwa kipaumbele, ni kama mimi tu ijapokuwa Queen amekuwa akinikataa lakini sikumlazimisha zaidi ya kwamba nilitamani aendeelee kuwa na furaha , sijui Roma ana wanawake wangapi na ni mwaminifu kwa kiasi gani lakini naamini kwa tabia yako ya kulazimisha vitu hata visivyokupenda hakuna mwanamke ambaye anaweza kukuvumilia”Aliongea Omari.

“Kaa kimya na acha kuwa mnafiki , unaongea hivyo kwasababu Roma ni rafiki yako”

“Haha.. wewe ni nani wa kuniambia ninyamaze unajifanyisha mjuaji lakini kichwani huna kitu”Aliongea Omari.

“Unaongea kishari unataka ngumi sio?”

“Acha ukijogoo Denisi , wewe ni mtoto sana kwangu”Aliongea

“Haha.. Omari usijifanyishe kwasababu baba yako ana cheo serikalini uone kwamba siwezi kufundisha adabu , Wewe huna cha kunitishia mimi”

“Jamani mnisamehe ninakwenda kuharibu wakati huu mzuri lakini hili lipuuzi siwezi kulivumilia tena”Aliongea Omari huku akionyesha kupandwa na hasira.

Mpaka hapo ugomvi ulihama kutoka kwa Roma kwenda kwa Omari na walianza kutunishiana misuli , Omari alisimama vile vile Denisi alimsogelea huku wote wakionyesha kuwa na hasira.

Omari hakumpenda Denisi kutoka na ukaribu wake na yan Buwen ambaye alikuwa ni adui yake namba moja na Denisi hakumpenda Omari kutokana na kuwa na ukaribu na Roma ambaye ni adui yake namba moja.

Omari alikuwa na nguvu za kijini levo ya Nafsi lakini Denisi vilevile mwili wake ulikuwa umefanyiwa sayansi na Yan Buwen hivyo kama ni kupigana ingekuwa ngumu kutabiri mshindi.

Omari akikasirishwa anakuwa mtu mwingine kabisa na alijiambia siku hio hamuachi salama Denisi na palepale alimpiga Denisi ngumi ya kifua na kumrudisha nyuma.

Kitendo kile kiliwafanya watu wote kusimama na kurudi nyuma huku macho yakimwangalia Roma na Tajiri Azizi pamoja na Kasimu waamue ugomvi kwani ndio waliokuwa wanaume , lakini Roma alikuwa amekaa ametulia akiangalia kwa hamu kile kinachokwenda kutokea , upande wa tajiri Azizi hakuwa na nguvu za kuamulia na Kassimu hivyo hivyo hakutaka kununua ugomvi wa watu wazima.

Denisi baada ya kurudi nyuma mara baada ya kupigwa ngumi ambayo haikuwa na madhara kwake , Omari hakutaka kumchelewesha alikuja na teke la hewani akidhamiria kumpiga Denisi kwenye mbavu lakini Denisi alikuwa ametarajia pigo lake kwani alidaka mguu wake na mkono mmoja huku akitabasamu kifedhuli.

“Unapata wapi ujasiri wa kupambana na mimi na vinguvu vyako vya kijini ulivyokuwa navyo”Aliongea Denisi na palepale kwa mkono wa kushoto alimfyatua Omari kwa kumrusha juu kupitia mguu wake aliokuwa ameushikilia.

Lakini Omari alitua salama kwani alitumia uwezo wa kijini kujikontrol , lakini hata hivyo alihamaki kwani uwezo wa Denisi ulikuwa mkubwa.

“Naona matokeo ya Yan Buwen kuufanyia mwili wako majaribio imekufanya kuimarika sana”Aliongea Omari kwa kebehi.

“Ushaanza kujitetea sasa”Aliongea Denisi huku akimpa ishara Omari kuja tena na pigo lingine , ilionekana ni kama amekuja sehemu hio kuamsha ugomvi kwani alionyesha mchecheto mno.

Queen alikuwa na wasiwasi mno kwa kile kinachoendelea na kujiuliza Denisi ana uhusiano gani na Yan Buwen na haikuwa kwake tu kila mmoja hakudhania mambo yangebadilika mpaka kufikia hapo na yote hayo ni ujio wa Denisi ndio uliovuruga kila kitu.

“Roma famya kuwaamulia bwana sio vizuri kuangalia watu wazima wakipigana mbele yetu”Aliongea Tajiri Azizi.

“Denisi acheni mnachokifanya mara moja huoni mnajidhalilisha nyie ni watu wazima”Aliongea Blandina lakini Denisi alionyesha hakuwa tayari kuliacha hilo lipite , hata hivyo ujio wake hapo ndani ulikuwa ni kutafuta ugomvi ili amkomeshe Roma ,lakini kwasabau Omari ameamua kujiingiza alijiambia ni kheri aanze nae kwanza hata hivyo Yan Buwen alikuwa akifahamu Omari ni zao la Hongmen na yupo uraini kwa misheni ya kumfatilia hivyo Denisi alijiambia akimuua huyu atajiongezea credit mbele ya Yan Buwen.

“Vipi umeufyata mkia?”Aliuliza Denisi kwa dharau na kumfanya Omari kupandwa na jaziba zaidi kwani kwenye maisha yake hakupenda dharau lakini pia Denisi alikuwa mtoto mdogo sana kwake.

“Nitakuonyesha mbwa wewe”Aliongea Omari na palepale alishika jicho lake la kushoto kwa namna ya kuliziba na alipotoa mkono jicho lilikuwa mkononi.

Kitendo kile kilimuogofya mno Queen lakini pia wengine wote walishangazwa na tukio lile ,ijappokuwa watu wengi walikuwa wakijiuliza ni kwa namna gani Omari aliweza kupona jicho lake kabisa lakini kulitoa ilikuwa tukio la ajabu mno.

Roma alijikuta mwili ukimsisimka , alikuwa akijua nini maana ya Omari kufanya vile.

Omari uwezo wake uliongezeka mara mbili yake na upande wa Denisi ni kama na yeye alifunguliwa uwezo wake wote na muda huo huo walianza kushambuliana kwa kasi kiasi kwamba ni Roma pekee aliekuwa na uwezo wa kuona namna wanavyo pambana ila wengine wote macho yao yalikuwa ya kibinadamu hivyo spidi waliokuwa wakitumia iliwafanya kuona vivuli tu na upepo ukipeperusha maua.

Omari alirusha ngumi wa haraka sana kumlenga Denisi maeneo mbalimbali ya mwili , alikuwa akitumia spidi kubwa sana lakini Denisi na yeye hakuwa vibaya kwenye kupangua.

Wanafamilia waijikuta wakiwa kwenye mshituko kwa mabadiliko hayo , ijapokuwa walishindwa kujua nani atashinda kutokana na kutoweza kuona namna ngumi zinavyotembea lakini namna walivyokuwa wakipambana ilichanganya.

“Roma waamulie bwana, mwisho wao utakuwa mbaya na mmoja anaweza kuumia na ikawa shida nyingine”Aliongea Tajiri Azizi kwa namna ya kumuamrisha Roma.

“Unafikiri nani atapoteza pambanno”Aliongea Roma kwa namna ya kuonyesha kwamba alikuwa akifurahia kinachoendelea hata hivyo matukio ya aina hio kwake yalikuwa yakawaida sana.

“Mdogo wako anaweza kuwa kwenye hatari , Omari ni kama jini”Aliongea Tajiri Azizi.

“Sio kweli Omari ndio atazidiwa”Alijibu na kuwafanya kushangaa , walikaa upande wa Denisi kutokana na namna Omari alivyotoa jicho lake kwa namna ya kimazingara hivyo walimuona Omari kama kiumbe cha ajabu.

Kitendo kile kilimfanya hata Queen kuzidi kutokumpenda Omari na kuanza kumuogopa alijiambia kheri yake Yan Buwen baba wa mtoto wake ambaye yupo tumboni.

Muda ule ule Omari alipigwa ngumi nzito ambayo ilimpata kifuani karibu na bega na kumfanya kwenda kudondoka mita kadhaa kutoka ilipo Swimming pool na hapo ndipo walipoona shati alilovaa Omari lilikwisha kuchanika upande mmoja.

Pigo lile lilimfanya sasa Roma aone uwezo halisi wa Denisi maana Omari alionyesha kushindwa kumhimili licha ya kwamba uwezo wake wa nguvu za kijini ulikuwa mkubwa.

Omari alijinyanyua kwa kujilazimisha na kusimama wima huku akitema damu , pigo alilipigwa na Denisi lilionyesha kupelekea viongo vya ndani kuathirika.

“Bado unataka kuendelea?”Aliuliza Denisi.

“Sikuwa makini ndio maana nikashindwa kukwepa ngumi yako , nisogelee tena kama unajihisi una uwezo mkubwa”Aliongea Omari huku akionyesha hali ya kutotaka kushindwa.

“Nadhani unakitafuta kifo kabisa ngoja nikumalizie kabisa nisibakiwe na deni”Aliongea huku akionyesha hali ya kuwa na hasira mno.

“Jamani inatosha sasa mtaumizana zaidi mkiendelea hivyo”Aliongea Blandina huku sauti yake ikiwa ya kitetetemshi alionyesha wasiwasi usiokuwa na kifani na alitaka Roma awazuie wasiendelee.

“Bro Roma wazuie wasiendelee”Aliongea Sophia ambaye sasa alianza kujawa na wasiwasi.

Upande wa tajiri Azizi na mke wake walijikuta hata wakijutia kuja kwenye hafla hio kwani waliamini kama kuna jambo lolote baya litakalotokea lazima wangetakiwa kutoa maelezo.

“Roma Omari ni rafiki yako , kwanini usimsaidie”Aliongea Tajiri Azizi, ukweli hakuwa na uwezo wa kumlazimisha Roma kwani alikuwa akijua hakuwa mtu wa kawiada na vile vile alikuwa akisikia habari kwmaba Omari pia hakuwa mtu wa kawaida na ndio maana hata mabadiliko hayo hakushangaa sana lakini alihofia matokeo.

“Naweza nikaingilia hapa , lakini ikanipelekea kumuumiza kabisa Denisi na wote hapa mnaweza kunilaumu kwa kusema nimempiga mdogo wangu mimi lawama sitaki”Aliongea Roma

“Roma waamulie sitojali kitakachotokea una sapoti yote kutoka kwangu”Aliongea Blandina na kumfanya Roma atabasamu ndio alichokuwa akitaka hivho , alipanga muda wote kama ni kumuua Denisi angalau apate sapoti kwa mama yake mzazi.

“Mama lakini naweza kumuaa kabisa kutokana na nguvu zake ambazo sio za kawaida”Aliongea Roma na Blandina alitaka kuongea kitu lakini mdogo wake alimzuia.

“Dada kwa mwonekano wa Denisi sidhani ni wakati wa kumuonea huruma, inaonekana hata akili sio yake tena , angalia alivyo”Aliongea mke wa tajiri Azizi.

“Najua lakini Denisi na Roma ni ndugu ..”

Mapigano sasa yalibadilika na ilikuwa ni Roma na Denisi sasa na Omari ilibidi atulie pembenni akiugulia maumivu , purukushani hizi zilimfanya hata Lanlan na Qiang Xi kufika eneo la tukio na Lanlan alisogea mbele kabisa huku akiwa amekodoa macho akishuhudia mtanange

Lanlan ndio aliekuwa akiona kabisa kile kilichokuwa kikiendelea , alikuwa na macho ambayo hayakuwa ya kwaida hivyo aliweza kuona namna baba yake anavyopigana na baba yake mdogo na alionyesha kufurahishwa na tukio hilo na kumfanya Edna kuwa na wasiwasi.

Roma alishangazwa na kitu kimoja kuhusu Denisi , ilionysha ni kama hakuwa kwenye akili yake timamu ni kama miezi kadhaa alioweza kumuadhibu akiwa na maambukizi ya kirusi cha Wolverine, alitafsiri kama athari zilizotokea kwa sayansi iliofanywa ndani ya mwili wake na Yan Buwen au alihisi huenda akili yake ilikuwa ikitawalia na Yan Buwen kwani Denisi alikuwa hana huruma kabisa kwenye macho yake na alimwangalia Roma kama Simba aliekuwa mbele ya kitoeo.

Inaawezekana kabisa kwa Yan Buwen kufanya hivyo, teknolojia ilikuwa kubwa sana na mtu kufanyiwa upasuaji na kuwekewa Chip ndani ya ubongo haikuhitaji utaalamu mkubwa na ni mchakato unachokua mwezi tu kukamilika.

Roma alijiambia lazima Yan Buwen alichukua tahadhari kila anapotengeneza mwanajeshi kwa kuwawekea sayansi ambayo ingemuewezesha kuwaendesha atakavyo na hicho ndicho kilichoonekana kwa Denisi.

Mpaka hapa Roma alijiambia hana namna zaidi ya kumuua Denisi kwani asipofanya hivyo anaweza kuwa hatari zaidi kwa usalama wa familia yake maana sasa Denisi hakuwa binadamu bali alikuwa ni kama Drone ya kijeshi inayoendeshwa kwa ajili ya kushambulia

“Roma kama usingekuja kunisaidia nilikuwa na mpango wa kuchapa Raba”Aliongea Omari akikubali kushindwa.

“Niliamini ungepambana mpaka pumzi yako ya mwisho?”

“Wewe hayo ni maamuzi ya watu wapumbavu , ninapenda maisha yangu na isitoshe Queen sijamuoa bado”Aliongea Omari.

Denisi alimsogelea Roma kwa kasi na Roma hakutaka kumpa nafasi yakumfikia na yeye alimsogelea na alipomkaribia aliachia teke ambalo lilimpiga Denisi kwenye tumbo.

Ijapokuwa Denisi alikuwa na uwezo mkubwa kutokana na uwezo aliopewa na Yan Buwen lakini hakuwa akimfikia Roma hata kwa Robo ya uwezo wake..

Teke lile lilimrusha mbali na kwenda kutua kwenye ukuta , lakini hakutaka kukata tamaa aliamka tena na kumsogeleaRoma kwa kasi huku nguvu ya ajabu ikianza kumzingira Denisi na palepale Roma alihisi kitu kisichokuwa cha kawaida ilikuwa ni nguvu ambayo hata Yan Buwen alitumia katika kupambana.

Nguvu inayotokea kwenye Godstone , ni nguvu ambayo Drogba alikuwa nayo na Clone ilikuwa nayo pia lakini kwa Denisi ilikuwa kubwa zaidi.

Roma baada ya kuona nguvu ya Denisi imejiongeza maradufu hakutaka kuzembea na yeye aliita nguvu ya kijini ya kimaandiko na kisha alitengeneza ngao kama kioo na kuisukumia aliposimama Denisi, upande wa Denisi alifanya hivyo hivyo aliachia pigo ambalo ni kama mwanga wa Radi kuelekea upande wa Roma hivyo ngao ya Roma ilikutana na shambulizi la Denisi.

Roma hakutaka kumchelewesha alikusanya nguvu ya kijini na kutengeneza shambulizo ambalo lilikuwa kama kimbunga cha mvuke na kusukumiza upande wa Denisi.

Ile ngao ilizuia pigo la Denisi na ikaruhusu shambulizi la Roma kumsogelea Denisi kwa kasi na alionekana kuchelewa kulizuia kwanni palepale upepo ambao ulikuwa kama mvuke ulimzingira kwa kasi na akawa katikati, Denisi alijikuta akitoa kelele akiashiria kuhisi maumivu makali ya kuungua , lakini licha ya hivyo Roma hakumuonea huruma na kadri nafsi yake ilivyokuwa ikinuia ndio maumivu yalivyokuwa yakizidi kumuathiri Denisi.

Ilishangaza kwa waliokuwa wakiangalia kwani hakuna walichoweza kuona zaidi ya kumuona Denisi akililia huku akitoa machozi makali ya kuhisi maumivu.

“Roma naomba umuache….”Blandina alijikuta akitoa machozi kwa tukio lile aliamini lolote litakalomtokea Denisi angewajibika na kila kitu kingebadilik.

Roma alijiambia hana haja ya kuacha na hakutaka kumuacha Denisi hai , aliamini kufanya hivyo ndio kujiweka hatari zaidi kwa Yan Buwen kuzidi kuwa na nguvu.

Watu wote walishangazwa na tukio lile na kujikuta wakitamani Roma aache anachokifanya lakini Lanlan alipiga makofi ya Shangwe huku akimwigiza Roma kwa kila alichokuwa akifanya, akizungusha mikono alikuwa akifanya hivyo hivyo kwake haikuwa hofu bali fursa ya kujifunza.

Edna baada ya kuona kitendo kile alimsogelea Lanlan kwa namna ya kutaka kumzuia asiige kinachofanyika lakini aligusa hewa kwani Lanlan alimkimbia na kwenda kusimama upande mwingine na Edna alipotaka kumfuata Sophia alimzuia na kumwambia amuache.

Denisi mara baada ya kuona hawezi kusogea kutokana na nguvu isiokuwa ya kawaida kumshika miguu huku akijihisi kuungua alijikuta bila ya kupenda akipiga magoti huku akitoa machozi ya maumivu na Roma alitabasamu kifedhuli kwani ndio alichotaka

Lakini sasa muda ule ule Denisi alisimama kwa mara nyingine na upande wa Roma kila alipojaribu kuitwa nguvu za kijini alishindwa kabisa hivyo hata kile kimbunga cha kijini cha mvuke kiliacha kumzunguka Denisi.

Muda ule ule wakati akijaribu kuita nguvu za kijini alishindwa kabisa na aliweza kushuhudia Denisi akitoka aliposimama na kumsogelea Blandina mama yake kwa spidi ya ajabu na kumlenga na ngumi kali kifuani eneo la sehemu unapokaa moyo na ngumi ile kuchangua kifua na damu kusambaa huku Blandina akitupwa mbali.

“Mamaa..!!”Roma alijikuta akitoa ukulele mara baada ya kushuhudia Denisi akimuua mama yake mbele yake huku yeye akishindwa kufanya chochote.











SEHEMU YA 458.

Ukweli ni kwamba alichokuwa akikiona Roma sio uhalisia kwamba kilikuwa kikitendeka , watu wote walishangaa kwanini alikuwa vile , Denisi hata yeye alishangazwa na mabadiliko ya Roma lakini hakutaka kujiuliza mara mbilimbili kwani alitoweka palepale baada ya kupata mwanya.

Wakati Denisi alivyokimbia Roma hakuweza hata kutambua nini kinatokea , lakini kile alichokuwa akiona sio uhalisia na alikuwa akiongea mwenyewe kama vile mtu aliechanganyikiwa ghafla.

“Roma unafanya nini?”Omari alikosa uvumilivu na kumsogelea Roma lakini Roma hakujibu zaidi ya kuendelea kuwa kimya na kuongea mwenyewe huku maneno yake yasisikike.

Watu wote walijikuta wakianza kujawa na wasiwasi kwa kile kinachomtokea Roma kwani Denisi ashakimbia lakini Roma alibakia kama amechanganyikiwa.

Roma aliendelea kumuona mama yake akiwa amepoteza maisha kwenye akili yake huku akiwa amelala chini na Denisi kupotea.

“Mama…!”Aliita huku akisogea mbele akitaka kumshika mama yake lakini palepale alipotaka kumkaribia tu kwa kumgusa alitoweka na kujikuta akishika ukuta na hapo hapo akili yake ilirudi kwenye uhalisia na baada ya kugeuka aliposimama mama yake alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akijidharau na aliweza kugundua ilikuwa ni ‘Illusion’ na alichokuwa akiona ni uhalisia mdanganyifu.

Edna na Lanlan ndio waliokuwa wa kwanza kumkimbilia na kumshika na Roma aligeuza macho yake na kuwaaangali.

“Hubby nini kimekutokea?”Edna aliuliza huku akimwangalia Roma huku machozi yakianza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake.

Roma alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kumshika Lanlan kwenye kichwa.

“Nipo sawa kuna kitu kimenitokea ila nimekuwa sawa”Aliongea .

Roma maumivu aliosikia aliposhuhudia Blandina mama yake akipoteza maisha mbele yake yalikuwa yasio ya mfano na mpaka hapo alijua ni kwa kiasi gani alikuwa akimpenda mama yake.

Kila mmoja alivuta pumzi ya ahuenni mara baada ya kuona hakuna aliekufa hapo ndani kwani ingekuwa tatizo lingine kabisa , Roma aliangalia juu angani kwa dakika kadhaa na kisha akawageukia.

“Nitarudi muda si mrefu kuna mtu napaswa kuonana nae mnaweza kusahau kilichotokea hapa na kuendelea kama kawaida”Aliongea Roma na hakusubiri jibu palepale alipotea na kumfanya Lanlan kutoa macho.

Dakika chache mbele Roma alikuja kuonekana Bagamoyo nyuma ya kituo cha afya na alitembea kwenye tifutifu ya mchanga kwenda mbele akikatisha eneo la shule ya msingikwa mbele na alikuja kusimama mara baada ya kuona mzungu mwanaume aliekuwa ameweka Headphone masikioni akiwa amechutama mbele ya bwawa la samaki ambalo limezingirwa na magugu.

Alikuwa ni mwanaume alievalia suti ya rangi nyeusi na tai nyekundu huku akiwa na nywele zake nyeupe (Blonde hair).

Kwa mwonekano wake ilionyesha dhahiri hakuwa mtu wa hilo eneo na ni mgeni ambaye alionekana kama kuvutiwa na mazingira na alikuwa amempa Roma mgongo huku akionyesha kuburudika na mziki uliokuwa ukisikika kwenye Headphone kutokana na namna alivyokuwa akitingisha kichwa.

Roma alimsogelea yule mwanaume wa kizungu taratibu na alipomfikia alimvua zile Headphone .

“Hey..!”Yule mwanaume aligeuka nyuma huku akionyesha kukasirishwa na kitendo cha kuvuliwa Headphone zake

“Nani kakwambia unaweza kunivua Headphone zangu kabla ya mziki haujamalizika?”Aliongea kwa Kijerumani.

Roma hakumjali zaidi ya kuzivaa zile Headphone ili kusikiliza mziki wenyewe na alitumia kama dakika moja na kisha alizivua huku yule mwanaume akimwangalia kwa namna ya kumchunguza kwanzia juu mpaka chini.

“Toccata and Fugue in D Minor by Bach”Aliongea Roma nakumfanya yule mzungu kushangaa.

“You know this piece?”Aliuliza akimaanisha kwamba anaufahamu huo wimbo.

“Ndio”Alijibu Roma

“Sio mbaya mtu yoyote anaelewa huo wimbo lazima aelewe maana halisi ya uhai”Aliongea kwa Kijerumanni.

“Sijasema na uelewa”

“Lakini inaonyesha unaupenda”Aliongea lakini Roma hakumjali zaidi.

“Naona una uwezo usiokuwa wa kawaida mpaka kufanikiwa kunitengenezea ‘Illusion’ ya kifo cha mama yangu kwa kuitawala akili yangu”Aliongea Roma akionyesha kwamba kitendo kilichomtokea dakika kadhaa zilizopita kilisababishwa na huyo mzungu.

“It wasn’t illusion”Aliongea huku sauti yake ikibadilika na kuwa nzito zaidi kuliko mwanzo akimaanisha kwamba alichokiona Roma haikuwa mazingira danganyifu.

“Oh! What’s that then?”Aliuliza kama sio mazingira danganyifu nini.

“Ni ndoto ambayo imetokea kwenye fahamu zako”

“Ndoto . Huh!. inaonyesha upo sahihi”Aliongea Roma

“Inaonyesha tayari umekwisha kunifahamu?”Aliuliza kwa kingereza.

“Haikuwa ngumu kwangu kukufahamu kutokana na Aura yako , licha ya kwamba ni mara yetu ya kwanza kuonana, lakini inashangaza kwanini mmoja wapo wa miungu kumi na mbili, Hermes(Mercury) akawa Vampire na isitoshe wewe ndio mwenye akili kuliko wenzako wote”

Roma pia alionyesha kushangaa na kujiuliza kuna sababu gani ya Hermes kujitokeza kwake tena kwa kipindi hicho.

Athena anaweza kuaminika kwa busara zake lakini kwa Hermes alisifika kama mchunga kondoo(sheepherd) na aliaminika kwa kuwa na mitego mingi.

Hermes katika historia ya miungu ya kigirika alifahamika kama mungu wa biashara , msafiri , mwizi , mhuni, tapeli na mpenda michezo lakini pia alifahamika kama mjumbe kati ya binadamu na miungu ya ugiriki kwasababu ya kupenda kusafiri kusafiri , kwa mfano anaweza kufika Tanzania watu wakataka kutuma salamu kwenda kwa Athena basi angewaambia kwamba wamlipe kiasi flani cha pesa na angefikisha maombi yao lakini moyoni hakuwa na mpango wa kufikisha maombi bali alifanya utapeli tu ni kama baadhi ya wachungaji wanavyowadanganya waumini walipe sadaka ili wapate magari, alikuwa pia akifahamika kwa kuupenda mziki ,ukisikia the first Song katika historia ni kutoka kwa Hermes

Roma ilikuwa mara yake ya kwanza kumfahamu na aliweza kumtambua kutokana na Aura yake na hata kuja hapo alifuata harufu(Scent).

“Nilishawahi kusikia kwamba unao uwezo wa kudhibiti miungu yote kupitia ndoto inaonyesha una uwezo mkubwa kuliko nilivyotegemea , sikuamini kwamba ungeweza kuniathiri kwa kiasi kikubwa”Aliongea Roma.

“Ni rahisi sana kila kiumbe chenye uhai lazima kiwe na mawazo na ukishakuwa na mawazo lazima uweze kuota ndoto ,hivyo ninao uwezo hata wa kutawala akili za mnyama kwa kutumia ndoto”Aliongea,

“Upo sahihi penye mawazo hapakosi ndoto”Aliongea Roma na yule mzungu alitabasamu.

“Now that we know that we’re on the same side can I have my headphones back , the newly appointed Hades”

“Sasa ushajua tupo upande mmoja nirudishie Headphone zangu , Hades mpya uliechaguliwa”Aliongea awamu hii kwa kingereza lakini Roma aliamua kukaa kwenye gogo pembeni yake na Hermes alitaka kumpokonya Roma zile Headphone lakini Roma alikwepesha mkono.

“Unafanya nini nirudishie mali yangu”

“Mpaka uniambie kwanini umemsaidia Denisi kutoroka?”Aliuliza Roma akitaka kujua kwanini huyo mzungu kaharibu mpango wake wa kumuua Denisi.

“Unataka kuujua ukwel?”Aliuliza na Roma alitingisha kichwa kukubali.

“Kama upo tayari kuniambia, nataka kuufahamu ukweli”

“Hauwezi kuniamini hata nikikuambia hata hivyo mimi ni mungu wa wezi na muongo”

“Nina akili zangu hivyo nitajua ukweli mwenyewe”Aliongea na Hermes ilibidi amwinamie sikioni na kumnong’oneza na Roma alijikuta akitoa macho huku sura yake kubadilika.

“Siku nyingine ukinichokoza siwezi kukuachia kirahisi kwa sababu zako kipuuzi”Aliongea Roma huku akisimama

“Nilijua tu hutoamini?”Aliongea lakini Roma hakujali zaidi ya kuondoka akimwacha amesimama asiamini macho yake Headphone zake za thamani kubwa zinaondoka na Roma.

“Hey! Hades are you a robber?”Aliuliza kwamba Roma ni mwizi.

“Umenichokoza mwenyewe kwa kuruhusu adui yangu kunitoroka hii ni kama fidia na sababbu yako najua ni ya uongo hivyo kama unazitaka njoo uzichukue kwenye mikono yangu”Aliongea na kumfanya Hermes kumwangalia kwamshangao

“Una uhakika gani nimedanganya?’Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli huku akimwangalia kwa namna isioelezeka anafikiria nini kwenye kichwa chake.

Mwanaume aliekuwa akiongea na Roma ni yule yule tuliemuona nchini Ujerumani akiitana na Athena kaka na dada , lakini ni yule yule ambaye alikuwa akiongea ndani ya kanisa na Snejder.

Jina lake halisi ni Prince Raphaeli na Count Dogba alieuliwa na Roma ni mtoto wake, na yeye ni Vampire.

Unafikiri kaja kulipiza kisasi

Itaendelea . Nicheki watsapp 0687151346
Safari hii umetupunja KAMANDA SAURONI
 
Walisema subira huvuta heri. Wewe mwandishi unatuumiza matumbo. Wiki inapita bila post. Haya makubwa; eti nimebanwa.
 
Walisema subira huvuta heri. Wewe mwandishi unatuumiza matumbo. Wiki inapita bila post. Haya makubwa; eti nimebanwa.
ni kweli subira yavuta kheri , tutaendelea kesho wikiend
 
Akiendelea kukaa kimya hivi ntawapostia yote hapa maana kwenye group lake amepost sehemu ndefu subirieni
Achana nae atawasumbua wengine ndivyo tulivyo waafrika tunapenda sana kupigiwa magoti kwa vitu vidogo mwanzoni hakuwa bize ila sasa baada ya fan base kuwa kubwa kawa bize sikatai kabisa kuwa ni haki yake kupata kile ambacho kinastahili anapokosea anawapa ahadi za uongo pia mara atarudia siyo poa.

Singano ni mwandishi mzuri sana nakubali ila rekebisha hayo hii dunia tulipofika wasio bize naamini wachache.
 
SEHEMU YA 459.

Roma alisimama mara baada ya Hermes kumwambia ana uhakika gani alichomwambia alikuwa akidanganya.

“Mpaka sasa nipo kwenye mshangao , Aphrodite aliniambia ukiachana na Zeus na Athena , Poseidon ndio mwenye nguvu zaidi anaefuatia lakini nikikuangalia naona unao uwezo mkubwa kuliko wa Poseidon mathalani kwenye mbinu yako ya kuweza kumdhibiti mtu kupitia ndoto, hio ni zaidi ya kanuni za anga na nina wasiwasi kama tukipigana hapa nitaweza kukushinda na kama pia ungeamua kunikimbia nisingeweza kukukamata kwani wewe ni Vampire na mnasifika kwa mbinu mbinu nyingi likija swala la kujificha.

“Kwa hio huo ndio mchanganuo wako?”Aliuliza Hermes.

“Kuna zaidi ya nilichosema?”

“Bila shaka , Hao wazee muda mwingi wanajichukulia kama ndio wenye nguvu kuzidi wengine lakini nikwambie wana nguvu kwasababu binadamu wanawaogopa , Vampire wana uwezo mkubwa zaidi kuliko kiumbe chochote , nilikuwa ndani ya huu mwili kwa miaka elfu moja, wakati wao wakizaliwa upya kwenye miili mingine mimi bado nilikuwa nikiendelea kuishi , unaweza kusema pia nilikuwa dhaifu lakini nilipokuja kuwa Vampire nguvu zangu zilikuwa maradufu zaidi kuliko Poseidon”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa kwani tofauti na wengine wote walikuwa wakivaa miili tofauti tofauti ya binadamu kila pale unapozeeka na kuhamia mwingine , lakini kwa Hermes alimaaisha kwamba yeye mwili wake ni huo huo na hajaubadilisha kwa milenia moja kwasababu alikuwa ni Vampire.

“Kama kweli umeweza kuishi kwa kuwa Vampire naweza kuamini kwamba una cheo kubwa katika jamii yako , lakini kwanini sijawahi kukusiakia hapo kabla?”Aliuliza Roma.

“Nadhani ushawahi kunisikia , jina langu la kibinadamu ni Raphaeli”Aliongea na Roma sasa kuelewa lakini alijikuta akishangaa.

“Raphaeli ! Unamaanisha kiongozi mkuu wa kundi la Tzimsce ?’

“Upo sahihi , siku nyingi nilikuwa nikiishi kwa kuficha ubini wangu kwa wengine kwani niliona haina maana , hivyo maisha yangu yamekuwa ya siri , Drogba ni mtoto wangu niliemzaa miaka zaidi ya mia mbili iliopita”Aliongea

Roma alishangaa kwani miaka kadhaa iliopita alishawahi kukutana na mtoto wa Christen afahamikae kwa jina la Judy hivyo ikawa mara yake ya kwanza kushuhudia mtoto wa miungu , lakini kusikia Drogba alikuwa mtoto wa mojawapo ya miungu ilimshangaza.

Judy ni mtoto wa Christen na Hades wa Zamani na kipindi cha nyuma wakati Roma akiwa bado ni Agent code 13 alimuua baada ya kuingia kwenye kumi nane zake , ilikuwa ni taarifa ya kusikitisha kwa Christen na Hades lakini kwasababu mwenye makosa wakati huo alikuwa ni Judy Roma hakulaumiwa.

Roma pia ashawahi kusikia kwamba ukoo wa Tzimsce ulikuwa mkubwa likija jamii za Vampire au wanywa damu na hata Prince Sergeras baba yake Lilith alikuwa akiogopa sana ukoo huo , lakini Roma hakuwahi kujua aliekuwa akiogopwa ni Hermes , ilikuwa ikiletea maana sasa.

“Kwahio umekuja Tanzania kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa kile nilichomfanyia mtoto wako?”

“Huyo ashakufa tayari kuna haja gani ya mimi kulipiza kisasi , alikuwa akinichukiza na tamaa yake ya madaraka na ndio maana nilimfukuza kwenye ukoo”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu.

“Lakini ukweli ni kwamba hata kama ningejaribu kupigana na wewe nina wasiwasi naweza nisikushinde lakini naamini usingeweza kuniua pia na mimi nisingeweza kukua hivyo haileti maana kupigana na wewe, Hivyo Mr Roma Ramoni nirudishie Headphone zangu”Aliongea.

“Hizi Headphone siwezi kukupatia na kingine usije ukaingilia mambo yangu tena kama ulivyofanya leo”Alitoa onyo

“Lakini hizo ndio chaguo langu la muda wote huwezi kuzichukua”

“Ninaondoka”Aliongea Roma na Hermes alimkimblia akitaka kumpokonya lakini Roma aliita nguvu za kijini na kuzigeuza siraha kisha akampiga nayo Hermes tumboni na kuishia kuugulia maumivu , lakini Hermes na yeye palepale aliita uwezo wake na kisha kuanza kucheza na kanuni za anga na kutengeneza matabaka ya anga msambo na kisha alirudishwa nyuma kwa spidi , Roma alijikuta akishangazwa na kitendo kile kwani kutumia kanuni za anga ni nguvu kubwa iliohitajika lakini kwa Hermes ilionyesha rahisi kwake.

“Damn it Hades, are you seriously doing this?”Aliuliza kwa kuchuki.

“I’m not interested playing games”Aliongea Roma akimaansiha havutiwi na michezo michezo.

“Okey tufanye umeshinda , Headphone zangu hizo ni za gharama sana hivyo ninakupatia kama zawadi, nimekuja kukupa tahadhari lakini naona haunichukulii siriasi , kwa heri”Aliongea na palepale aliita mabawa yake maarufu kama Sandals Talaria na kupaa huku akionekana angani kama malaika wa mabawa mawili.

Roma alijua kabisa kama angepambana na Hermes huenda ingemchukua muda mwingi kushinda kwani alikuwa na mbinu nyingi za kutoroka ukizingatia na uwezo wake wa anga lakini pia uwezo wake wa kujitengenezea mabawa lakini pia kuwa Vampire.

Roma hakutaka kukaa eneo hilo kwa dakika nyingi zaidi , kwani alijua familia yake ingekuwa kwenye wasiwasi , hivyo alipotea na kutokezea nje ya geti na kisha akaingia ndani.

“Mjomba ulienda wapi kila mmoja alikuwa na wasiwasi”Aliongea Donyi baada ya kufungua geti.

“Si nilisema naenda kukutana na mtu?”Aliongea Roma na kupita na kisha alisogea mpaka kwenye meza na kuweka zile Headphone juu yake.

“Mnaonaje hizo ni nzuri?”Aliuliza akiwafanya wote kuangalia zile Headphone

“Hizi si Headphone..?”Aliongea Sophia kwa namna ya kushangaa.

“Sophia mbona umeshangaa hivyo , ni Headphone ndio?”Alijibu Donyi

“Ah.. ninachotaka kumaanisha ni kwamba hizi ni za utofauti sana , hata ninazotumia sio kama hizi , inaonyesha hizi ni gharama kubwa”

“Uko vizuri Sophia inaonyesha fani yako ya mziki inakufanya kutofautisha baadhi ya vitu, hizi ni ‘electrostatic headphone’ kutoka Ujerumani zinazofahamika kwa jina la Sennheiser’s Orpheus , zipo jumla ya 300 dunia nzima ambazo zimewahi kutengenezwa , Ninakupatia kama zawadi yangu kwako”Aliongea Roma.

“Brother kwa hio hizi ndio Orpheus nishawahi kuzisikia kutoka kwa rafiki yangu nilipokuwa masomoni nje ya nchi inasemekana moja thamani yake ni zaidi ya milioni mia moja na nusu za kitanzania”Aliongea Kasimu na kumfanya Sophia kutetemeka na kuziweka chini na kumpatia Roma.

“Bro kwanini usizitumie wewe , ni ghali sana kwangu”Aliongea

“Usijali mimi na dada yako Edna hatusikilizi sana mziki hivyo zinakufaa wewe msanii , Edna ndio ambaye siku zote amekuwa akikupatia zawadi lazima na mimi angalau nitoe zawadi kama shemeji yako?’Aliongea Roma.

Ni kweli Sophia aliweza kuzawadiwa gari na Edna yenye thamani kubwa kampuni ya Bentley. ni aina ya gari ambazo ni chache sana ndani ya Tanzania hivyo Roma aliona itakuwa sawa na yeye kutoa zawadi.

Sophia alijikuta moyo wake ukipiga kwa nguvu mara baada ya kusikia neno Shemeji , ilikuwa mara yae ya kwanza Roma kuongea hivyo na ilikuwa ni kama anaweka mpaka kati yake na yeye.

Watu wote walielewa maeneno ya Roma na kuishia kumuonea huruma Sophia , hata Edna aliona maneno yake yamekaa kikatili lakini aliona ni afadhali kwani hakujua angejisikiaje kama Sophia akiwa mpenzi wa Roma.

Kama Sophia angekubali zawadi hio inamaana angehesabika kwanzia siko hio kama shemeji rasmi na kuachana hata na jina la Bro.

“Bro kwahio unataka nikuite shemeji kwa kunipa hizi Headphone pekee?”Aliuliza Sophia na kufanya hali ya hewa kubadilika , lakini hakujali zaidi ya kuzichukua na kuzikumbatia.

“Asante kwa zawadi lakini hazitoshi kama zawadi kutoka kwa Shemeji , unatakiwa kuelewa mimi ni mtu maarufu mwenye hadhi hivyo nategemea kitu kikubwa zaidi”Aliongea huku akiweka tabasamu kuonyesha kwamba amekubali na kila mtu alivuta pumzi ya ahueni.

Na ndio hivyo Sophia ukawa mwanzo wa kumuita Roma Shemeji kutoka kwenye jina la Bro Roma.

Baada ya kuongea ongea kwa muda mfupi kidogo ilikuwa ni saa kumi hivyo kila mmoja aliaga na kuondoka na wa mwisho kabisa alikuwa ni Omari Tozo.

“Nipigie muda wowote ukiwa na shida,, hata mrembo Queen hapa akikusumbua niambie tu nitakusaidia”.

“Una uhakika utanisaidia katika hilo?”

“Ndio nitahakikisha nakufariji”

“Aah.. Nikajua unasema utanisaidia kumrudisha kwangu”

“Hio sio kazi yangu ukiachwa umeachwa na mimi kama rafiki yako nitahakikisha nakusaidia lesso ya kufutia machozi”Aliongea Roma na Omari alionekana kutopenda maneno yake na kufungua gari lake mlango.

“Shemeji Edna nitakupigia wa kwanza kukutaarifu siku ya harusi yangu na Queen”Aliongea Omari.

“Nitarufahi nikiwa wa kwanza”Aliongea Edna akipunga mkono na kisha akamgeukia Roma na kumwangalia kwa dakika kadhaa na kisha akaingia kwenye gari lake na kuondoka.

Roma alitambua kitendo cha Omari kupigana na Denisi ilikuwa ni kumsaidia maana wakati ule hata yeye hakujua namna ya kumchukulia Denisi hatua lakini ni shukrani kwa Omari aliweza kutatua tatizo kwa kumshugjulikia kisawa sawa Denisi , ijapokuwa alikuwa ametoroka lakini aliamini ilikuwa ni adhabu ya kutosha kwake.

Siku iliofuata Sophia alihamia rasmi katika nyumba ya kigamboni, upande wa Blandina na yeye baba yake afya yake haikuwa sawa hivyo ilimbidi kuondoka kwenda kumhudumia kwa muda, hivyo familia ikabakia watu wachache sana , lakini hata hivyo haikupoa kwasababu ya uwepo wa Lanlan.

Ilikuwa siku ya jumapili Roma , Edna na mtoto wao Lanlan walitoka kwenda matembezini , sehemu walioichagua siku hio ilikuwa ni kwenye hoteli moja iliokuwepo Kigamboni ambayo ilikuwa na Zoo ya wanyama, walichagua sehemu hio kutokana na Lanlan kutaka kwenda kuona wanyama.

Safari yao ilianza asubuhi, ilikuwa siku nzuri sana kwa Edna kutoka kama hivyo akiwa yupo na Roma pamoja na mtoto wao wa kumlea.

Ktuokana na mazingira ya hoteli hii maarufu kuwa tulivu sana na ya kuridhisha ilimfanya Edna kuwa na utulivu wa akili wa hali ya juu sana na kufurahia mazingira , walifanya mambo mengi ya kufarahisha na kuwa kivutio kwa wageni kadhaa waliokuwa wapo pia katika maeneo hayo.

Jambo ambalo liliwafanya watu wengi kushangaa ni pale Lanlan alipokataa kupanda na Roma kuendesha farasi akitaka yeye kuendesha mwenyewe.

“Lanlan anataka kuendesha mwenyewe farasi”

“Lanlan utadondoka , panda na baba yako”

“Lanlan hawezi kudondoka na babu aliniacha nikapanda mwenyewe”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kumwangalia Roma , walijua jina la babu lilikuwa likitokea wapi , walijua lazima angekuwa ni Afande Kweka.

Edna ilibidi amuangalie Roma kuona anasemaje na Roma alimwambia amuache afanye anavyotaka , Edna alikuwa na wasiwasi lakini Roma hakuwa na wasiwasi , kwanza alikuwa akijua Lanlan hakuwa mtoto wa kawaida.

Lanlan ilionyesha kweli alikuwa na uwezo wa kuendesha farasi , kilichoashangaza watu hata yule ambaye anawahudumia wanyama na kuongoza wageni katika Zoo ni namna pekee ya Lanlan kuamrisha Farasi kutembea kwa namna ya tofauti kabisa , hata Roma mwenyewe alishangazwa na kitendo hicho, ijapokuwa halikuwa jambo jipya kuliona kwenye maisha yake lakini kwa umri wa Lanlan kuweza kuwasiliana na wanyama lilimfanya kujiuliza maswali, aliamini huenda ndio maana muda mwingi Lanlan alikuwa akipenda kuona wanyama kuliko kitu kingine.

“Lanlan nani kakufundisha kuongea na wanyama?”Aliuliza Roma

“Ni mama yake Lanlan” Alijibu kwa Kingereza huku akimshika Edna akionyesha kufurahia sana kuja eneo hilo kwa siku hio.

Sasa muda huo huo wakati wakipata chakula cha mchana, upande mwingine ndani ya hoteli hio hio Rufi alikuwepo akiwa ameambatana na Mika na walikuwa wamekaa upande mwingine , muda wote ambao Roma alikuwa akimsaidia Edna kupanda kwenye Farasi alikuwa akiona kila kitu.

Wakati wakiwa wamemaliza kula ,Edna alipokea simu kutoka kwa Rufi na haikujulikana alikuwa akiongea nae nini , lakini Roma alijua Edna anaongea na Rufi na ile anamaliza kuongea alirudisha simu chini.

“Alikuwa anaongea nini?”Aliuliza Roma kwa shauku ya kujua mke wake alikuwa akiongea nini na Rufi.

“Aliniambia kuna kitu anataka kuniambia , ambacho alipaswa kuniambia siku ile ile niliokutana nae”Aliongea na kumfanya Roma moyo wake kupiga Paah.

“Edna yule msichana sio mtu mzuri na anakutumia tu”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia Romakwa mshangao.

“Unamaanisha nini kusema ananitumia?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kujilaumu na kuona ametumia kauli ambayo hakupaswa kuongea , lakini hata hivyo alikuwa na hofu kama Rufi ataongea ukweli kabla yake..

“Edna kuna kitu sijakuambia kuhusu Rufi… , najua unaweza kukasirika lakini nilishawahi kukutana nae L.A Marekani”Aliongea Roma kwa upole sana kama sio yeye vile , ijapokuwa alifahamu hakupaswa kuliongelea jambo hilo kwa muda kama huo ambao wamekuja kufurahi ,lakini aliona ni kheri Edna kufahamu mapema kuliko Rufi kumwambia.

Kauli ya Roma ni kama ilitafisirka kwa namna ya tofauti kwenye kichwa cha Edna , kwa mwonekano wa kirembo wa Rufi aliamini kama kweli Roma aliweza kukutana na Rufi basi ni lazima ilikuwa zaidi ya kukutana.

“Edna nilipaswa kukuambia pale hospitalini lakini ukweli alikudanganya alijifanyisha kugongwa na gari ili kujenga ukaribu na wewe”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumkata jicho na palepale alichukua simu yake kwenye meza na kumpigia Rufi.

“Sitojali kama ulijifanyisha kugongwa na gari yangu kwa makusudi , lakini nipe jibu moja ni uhusiano gani unao na mume wangu?”Aliuliza Edna baada ya simu kupokelewa.

“I… we,,,we met in LA”Rufi alisikika akijing’ata ng’ata meneno akimaanisha kwamba wamekutana Loss Angeles.

“Ilikuwa ni lini?”

“Miezi miwili na wiki tatu zilizopita”Alijibu na kumfanya Edna akili yake kufanya kazi kama mashine , alikumbuka mara ya mwisho Roma kwenda Marekani ni miezi miwili iliopita.

“Na mlifanya nini mlivyokutana?”Aliuliza Edna kwa kingereza.

“We…we.. did that..”Aliongea na kumfanya Edna kukunja sura .

“That!?”Alijuliza na kufikiria kwa muda na alijikua akielewa alichomaanisha.

“Miss Edna naomba unisamehe kwa kutokukuambia , lakini .. lakini nampenda sana Roma, tulipiga hata picha tukiwa kitandani, ninaweza kukutumia uzione”Sauti ya Rufi ilisikika , ilionyesha alidhamiria kwa asilimia mia moja kumharibia Roma kwa mke wake , sasa haikueleweka ni wivu alioupata alivyowaona wakiwa wapo pamoja au alipanga kuongea ukweli , baada ya simu kukatwa picha zilitumwa palepale na Edna alifungua moja moja na alipojaribu kuchunguza mazingira aligundua kabisa ni picha zilizokuwa zimepigwa hotelini.

Mpaka hapo Roma aliamini kabisa Rufi alikuwa akimfanyia makusudi lakini muda huo hakuwa na namna ya kuchukulia swala hilo hatua, Edna aliona picha na Rufi hakutuma vidio yenyewe lakini hata hivyo ulikuwa ushahidi wa kutosha kabisa ambao hata hivyo Roma alikiri mwenyewe kwamba amekutana nae LA.

Edna alijikuta akiinua macho yake na kumwangalia Roma na chozi hakuelewa hata machozi yalimtoka wapi , lakini yalianza kujitengeneza na kutiririka kama mto.

Hakuamini mwanaume anaefahamika kwa jina la mume wake ndio huyo ambaye yupo uchi kwenye picha akiwa kitandani na msichana Rufi.





SEHEMU YA 460

Roma alijikuta akiumia kumuona Edna kutoa machozi namna hio , alishukuru Lanlan alikuwa akicheza upande mwingine hivyo hakusikia hayo mazungumzo.

“Kwanini hukuniambia tokea mwanzo kama alikuwa na yeye ni mwanamke wako , unao wanawake wengi na umekuwa hata na ujasiri wa kuwakaribisha mpaka nyumbani umeshindwaje kuniambia na huyu ni wa kwako au kwasababu unao wengi sana kiasi cha kusahau mahesabu si ndio”Aliongea Edna huku sauti yake ilikuwa kavu mno akimfokea mfalme Pluto.

Roma alifumba macho yake na kuvuta pumzi nyingi , hata hivyo ndio alienzisha hayo maongezi hivyo alitakiwa kujitetea na kumtuliza.

“Edna ni kweli nilikutana nae Marekani na kwangu nilimchukulia kama ‘Onenight stand’ lakini nakuapia sina hisia zozote na yeye, unaweza kusema ni ajali , huwezi kusema ni mpenzi wangu .. alichokuambia ni kujaribu kunisingizia tu”

“Kimyaa!!”

“Rufi ni msichana wa kawaida unawezaje kusema anakusingizia ukijumlisha na uwezo usio wa kawaida uliokuwa nao , unanifanya mimi ni mtoto mdogo si ndio?”Aliuliza na kumfanya Roma kukosa jibu , ukweli ni kwamba siku aliokutana na Rufi alijua uwepo wa zile Kamera za siri ,lakini kwasababbu alijua asingeweza kukutana na Rufi tena ndio maana hakuchukua hatua yoyote..

“I’m sorry”Aliongea .

“Unaomba msamaha tena , unasaidia nini kwenye hali kama hii , kama hili lingetokea zamani ningekubali lakini ni juzi hapo tu , kama huna mpango wa kuachana na tabia yako kwanini unataka kufunga ndoa na mimi?”Aliongea huku machozi yakiwa yanamtoka lakini Roma alishindwa kujjitetea.

“Nina weza kupotezea swala la wewe kuwa na wanawake wengine ambao unawapenda kupitiliza lakini siwezi kuvumilia kitendo chako cha kunidanganya, umenidanganya umeenda Loss Angeles kumsaidia Christen kumbe ulimfuata mwanamke”

“Edna .. najua umekasirika na lilishatokea tayari lakini Rufi ni mwanamke hatari na nilitaka kukuambia mapema”

“Wewe ndio hatari zaidi kwangu , siku zote unaniambia kwamba utakuwa muwazi kwangu kwa kila kitu lakini kumbe maneno yako ni tofuati na vitendo, Wewe ni muongo Romaa”.

Uzuri wa hoteli hii ni kwamba kila nyumba ilikuwa ikijitegemea na ilikuwa imejitenga na nyumba zingine hivyo hakuna ambaye alikuwa akiona ugomvi huo kwani ni hoteli iliokuwa ikipokea wageni wa kifamilia.

Edna alishindwa kuongea zaidi na alichukua mkoba wake na kutoka akimuacha Roma ,mpango ulikuwa ni kuamkia ndani ya hoteli hio lakini hakuwa na uwezo wa kumvumilia Roma ambaye muda huo alihisi kumchukia.

Alijifuta machozi na kutoka nje kuelekea eneo la maegesho ya magari, wakati akiwa anafungua mlango wa gari waliokuja nalo alijikuta akikumbatiwa miguuni na alipogeuka alijikuta akimwangalia Lanlan ambaye alikuwa akitoa machozi na alichuchuma chini na kisha akamkumbatia huku akijiona mkosaji kumsahau kwasababu ya hasira zake.

Hasira zake zilimfanya kumsahau Lanlan na alijiuliza kama Lanlan aliweza kusikia ugomvi wao na Roma.Dakika chache mbele Edna aliondoka na Lanlan ndani ya hoteli hio, na siku yake ilioanza vizuri ikawa imeingia doa..

Roma akili yake ilikuwa ikizunguka na alijikuta hata akijilaumu kumwambia mke wake ukweli , aliona huenda angemdhibiti Rufi kabla hata hawajakutana na mke wake , huenda ingekuwa afadhali lakini kwasababu ambazo yeye mwenyewe hakuwa akizijua aliamua kuchukua maamuzi ya kumwambia.

Alijilaumu kwa kutochukua tahadhari siku ile ile pale hospitalini lakini kwa stori ya Rufi kutaka kumtafuta mzazi wake nchini Tanznai ndio iliomfanya kusita kutokuchukua hatua.

Wakati akiendelea kuwaza mlango ulifunguliwa na aligeuka kwa kudhania ni Edna karudi lakini bahati mbaya ile sura ya mtu aliemuharibia na mke wake ilitokeza mbele yake.

Roma alijjikuta akimwangalia Rufi huku akishindwa hata kujielewa , alijikuta hata yeye akijidharau na kujiuliza kwanini maisha yake yamebadilika kiasi hicho na kuendeshwa na mwanamke, ilikuwa kama sio yeye , lakini alijua kabisa yeye ni binadamu licha ya kwamba alikuwa akifahamika kwa jina la Hades na matatizo yanayomtokea ni kwasababu aliamua kuishi kama binadamu wa kawaida , huenda angeishi kama Hades angeweza kuchukua tahadhari na kuendelea kumfurahisha mke wake hata kama ni kwa kumficha baadhi ya vitu kwa kutumia uwezo wake.

“Umeridhika ? Ndio ulichotaka?”Aliuliza Roma , hakutaka kujua Rufi kafikaje hapo ndani wala ndani ya hoteli hio.

“Ndio! tokea mara ya mwisho tulivyoachana pale hotelini ulionyesha kutonipenda tena , nilidhania ungenitafuta ila ukaamua kunipotezea moja kwa moja na kunifanya niishi kama mgonjwa , hivyo nimeamua kuyafanya maisha yako kuwa magumu”Aliongea kwa Kingereza.

“Tulikubaliana nini , kwanini ukaamua kuvunja ahadi yako?”

“Unachekesha, nani kavunja makubalino?, wewe ndio umeamua kumwambia mkeo ukweli na akanipigia simu kuulizia kuuthibitisha ulitaka mimi nifanyeje”Aliongea kwa Kingereza.

Ijapokuwa ni kweli Rufi alimwambia Edna kuna kitu anapaswa kumwambia , lakini haikumaanisha kwamba ni mahusiano yake na Roma , huenda alitaka kumwambia kitu kingine.

Ukweli ni kwamba Rufi mara baada ya kuona Edna na Roma wanafurahi huku wakiwa na mtoto ambaye alijuwa kabisa ni mtoto wao , alijikuta akijawa na wivu mkali sana , kubwa zaidi ni kitendo cha Roma kumpotezea kabisa tokea walivyo achana.

Kitendo cha kumpigia Edna kwamba kuna kitu anahitaji kumwambia, ulikuwa ni mtego, alijua Edna amepokea simu mbele ya mume wake , hivyo alijua lazima Roma angeweza kuhisi moja kwa moja kile ambacho anakwenda kumwambia hivyo angechukua nafasi ya kumtafuta kabla hajaonana nae.

Yaanni kwa lugha nyepesi Rufi alitaka atumie siri ya kukutana na Roma Marekani kama udhaifu wa kumwendesha Roma , lakini matokeo yake yakawa tofauti , Roma akaweka wazi kila kitu jambo ambalo hakuwa amelitegemea wala kutaka litokee, hivyo baada ya Edna kumpigia simu na kumuuliza swali la uhusiano wake na Roma alishangaa na kuona aliharibu na Roma ameshindwa kuingia kwenye mtego wake hivyo ilibidi kuweka ukweli wazi.

Roma hata yeye alijua Rufi anajaribu kumuigiza mtegoni na ndio maana aliamua kumwambia Edna palepale lakini ndio hivyo ukweli ulikuwa mchungu kwa Edna na kuishia kugombana, lakini alijiambia ni swala ambalo angemalizana na Edna , kwani aliamini hata kama asingemwambia Edna ukweli ungekuja kujulikana tu.

“What will you get out of this?”Aliuliza Roma kwamba angefadika nini.

“Nothing”Alijibu Rufi.

“You’re Crazy woman”Aliongea Roma akimwabia Rufi kwamba ni kichaa.

“Ndio unachosema ni kweli mimi ni Chizi”

“Huogopi nitakuua muda huu?”

“Nilikupatia mwili wangu ukanitoa bikra yangu , unafikiri ninaogopa nini kukupa na maisha yangu?”Aliongea Rufi huku akicheka kwa kejeli.

“Usicheke”Aliongea Roma na palepale alimsogelea kwa spidi na kumshika shingo na kuanza kuiminya , alikuwa na hasira mno lakini alijitahidi kujizuia kwani angeongeza nguvu kuiminya zaidi basi angeivunja palepale.

Rufi alijikuta akianza kukosa hewa na macho yalimtoka huku kile kiini chake cheusi kilianza kupungua ukubwa kwa namna kama kilikuwa kinapotea ndani, Roma alijikuta akimwachia palepale , alishangazwa na kile alichokiona kwenye macho ya Rufi na kujiuliza kwanini amekuwa hivyo ghafla.

“Kwanini umeshindwa kuniua?”Aliuliza Rufi huku akitoa tabasamu la kejeli.

“Nimesema usitabasamu”

“Nataka kutabasamu kwanini unizuie”

“Unaweza kulia ila sio kutabasamu”Aliongea Roma huku akijikuta hasira zikishuka.

“Naomba uniue , siwezi kutabasamu kama nitakuwa nimekufa”Aliongea huku akiwa ametoa tabasamu vilevile lakini wakati huo huo machozi yakimtoka.

Ni ngumu binadamu kutoa machozi huku akionyesha tabasamu na akifanya hivyo ujue ni kwamba tabasamu limeambatana na maumivu makali.

“Wewe mwanamke hukiogopi kifo?”

“Kifo..!!”Aliongea na kuanza kucheka sana kwa zaidi ya dakika moja nzima

“Nimekufa zaidi ya mara elfu moja , kipi kinakufanya uamini naweza kuogopa kifo”Aliongea na kumfanya Roma kuvuta pumzi na kumwangalia.

Ni kweli alijua Rufi hakuwa akiogopa kifo , ukizingatia na maisha yake, kwa sumu iliokuwa ndani ya mwili wake kipindi anakutana nae ilikuwa ni miujiza mikubwa akawa anaendelea kuishi.

“Hutaki kuniua?”

“Sijui kwanini umeamua kuja Tanzania na kuvuruga maisha yangu lakini sitaki kukuona tena , Uhai kwako ni zaidi ya Adhabu kuliko hata ya kifo”Aliongea Roma na kisha alichukua kila kitu chake na kutoka hapo ndani

“Umesema unataka kuniua , lakini ukashindwa kufanya hivyo , umesema huna hisia na mimi lakini ulivyoona mwonekano wangu wakati wakunikaba hasira zako zikaisha … Looh! Wanaume ndio mlivyo siku zote ni waongo sana”Aliongea wakati akiwa ameugeukia mlango

Roma hakutaka kukaa kabisa hapo ndani kwenye hio hoteli , ijapokuwa alikuja na gari akiwa na mke wake na mtoto wake , lakini alikuwa akiondoka peke yake tena kwa mguu , ilihuzunisha lakini hakuwa na jinsi kwa muda huo.

Hakujali sana nini Rufi angefanya zaidi ya hapo lakini hakutaka kujihusha nae tena na alijiambia kwake Rufi ni mwanamke aliejipigia mbususu na kusepa tu na asingeeweza kuwa na mahusiano yoyote.

Huku nyuma muda ule ule Mika alimfuata Rufi akiwa ni mwenye wasiwasi sana .

“Hajakuua?”Aliuliza huku akivuta pumzi nyingi za ahueni na Rufi aliachia tabasamu pana la ushindi.

“Nilikuambia asingeweza kuniua na hukuniamini , tuondoke sitaki kuendelea kubakia hapa”Aliongea na kisha alipiga hatua kueleka upande wa maegesho ya magari na kumfanya Mika kusimama huku akimwangalia Rufi kwa nyuma.

Ijapokuwa Rufi alikuwa na baba mchina lakin umbo halikuwa la kichina , umbo lilikuwa la kitanzania kabisa , hakuwa na umbo kubwa lakini Shepu yake ilijitengeneza vizuri mno , Rufi urembo wake ulikuwa ni wa kipekee , ule ambao haukuwa ukikinasha mbele ya mwanaume rijali.

Mika alimwangalia Rufi na kujikuta akitingisha kichwa na kutabasamu kwa wakati mmoja , alikumbuka na nyumbani kwao baba yake alivyokuwa akimlazimisha Benadetha kuhakikisha anakuwa hata mchepuko wa Roma.

“Baba siwezi kuwa mahusiano na Roma kwani ni mume wa bosi wangu”

“Benadetha naomba unisikilize mimi baba yako , sijali Roma anaweza kukuoa au hatokuoa lakini nataka uwe sehemu ya wanawake zake ikibidi umzalie hata mtoto”

“Baba Benadetha kwanini unamlazimisha mtoto kuwa na mahusinao na mwanaume alieoa?”

“Mke wangu huwezi kunielewa mara moja hata nikikuelezea kila kitu hapa , lakini Roma ni zaidi ya binadamu ambaye mimi Samweli Nguluma lazima nimfanye kuwa ndugu yangu kama ninayahitaji mafanikio”

“Lakini Benadetha hawezi kuwa na mwanaume ambaye hampendi?”

“Hahaha.. mke wangu hebu muulize , akiniambia hampendi Roma nipo tayari kupokea mahali ya mwanaume yoyote”

“Benadetha anayo ongea baba yako ni kweli?”

“Mamaa..!”

“Nipe majibu kama unampenda au humpendi huyo Roma?”

“Mama hata kama nampenda inasaidia nini, kwani mtu mwenyewe siwezi kuwa nae kwenye mahusiano , hii mada sitaki iendelee”Alijibu na kukimbilia ngazi na kwenda chumbani kwake.

“Mke wangu unaona sasa?, Mika hakikisha dada yako anakuwa na mahusiano na Roma”

“Sawa baba”

“Yaani hata siwaelewi , huyu Roma ana nini mpaka mnataka mwanangu awe mchepuko”

“Tunamsaidia Benadetha , kaa nae uongee vizuri la sivyo atazeekea hapa nyumbani bila kuleta mwanaume”

Mika alijikuta akirudi kutoka kwenye mawazo ya mazungumzo ya mama yake na baba yake, ni kweli alikuwa akijua Roma hakuwa mtu wa kawaida kutokana kushuhudia yeye mwenyewe uwezo wake , lakini hakujua kwanini kila mwanamke anamtaka.

Roma hakuchukua hata taksi , alitembea kwenye barabara inayotoka eneo hilo kwa mguu huku akionyesha ni mwenye kuwaza , ilikuwa ni saa kumi za jioni lakini hakuwa na hamu ya kurudi nyumbani kuonana na Edna kwani alijua asingeweza kupata namna ya kumtuliza.

Alitoa simu yake mfukoni na kumpigia Diego na kumpa maagizo ya kuhakikisha Edna anakuwa salama kwa kufuatiliwa kwa ukaribu.

Baaada ya kuwaza namna ya kuimaliza siku hio , alijikuta akijipiga kibao na kukumbuka jambo moja ambalo ni kama amelisahau , wiki iliiopita Clark alimtaarifu amerudi Tanzania lakini hakuwa amemtafuta.

Roma alitafuta usafiri haraka na kuanza safari ya kuelekea Makongo juu na ndani ya dakika chache tu Taksi iliweza kumfikisha na alifunguliwa mlango na mlizi na kisha akaingia ndani.

Baada ya kufika eneo la sebuleni nyumba ilionekana kuwa tulivu kama haikuwa na mtu , lakini mezani aliweza kuona chupa ya maji iliofunguliwa nusu na kuona Clark yupo , alinyoosha moja kwa moja kwenda chini ya maabara na slishangaa kukutana milango ya kwenda chini ya maabara hio ilikuwa wazi.

Wakati anakarribia kufika ndani kabisa ya maabara hio ambayo hakuweza kupata kizuizi cha aina yoyote , alisikia sauti za kudondoka kwa vitu mfululizo zikitokea ndani ya maabara na kumfanya moyo wake kushituka na kuogopa jambo baya kumkuta Clark.

********

Edna mara baada ya kuondoka na Lanlan alienda kusimamisha gari kwenye fukwe maarufu iliokuwa ndani ya Kigamboni , alikuw a na mawazo hivyo hakutaka kuendesha gari mpaka nyumbani akiwa kwenye hali hio.

Eneo lilichangamka kwasababu alikuwa ni Weekend , lakini Edna hakuenda moja kwa moja upande wa mikusanyiko ya watu wengi bali alichagua upande wa hotelini.

Lanlan alifurahi kufika Beach na Edna alimzuia asijichanganye na watu hivyo alisimama akiwa amemshikilia mkono , ilikuwa ahueni, zile hasira zimepungua kutokana na uwepo wa Lanlan lakini mawazo yalikuwa yakimwendesha.

Alitamani kumpotezea moja kwa moja Roma , lakini alivyokuwa akijihisi kwenye moyo wake ni kama hakuwa na uwezo wa kuachana na Roma kabisa , hakuelewa hata yeye imekuwaje akawa hivyo kwani mwaka mmoja uliopita hakuwa ni mwenye kujali kuhusu wanaume zaidi ya kampuni.

Lanlan aliona mama yake alikuwa kwenye mawazo hivyo na yeye alisimama pembeni yake pasipo ya kuongea , alionyesha hali ya kuwa mtiifu.

Wanaume waliokuwepo kwenye hilo eneo waliishia kumwangalia Edna kwa macho ya kimatamanio kuna waliokuwa wakimfahamu na kuna ambao hawakuwa wakimfahamu , gauni la rangi nyeupe na nyeusi lililokuwa na muundo kama wa Dera halikuficha uzuri wake na umbo lake, Lanlan pia uzuri wake aliorithi kwa mama , ulifanya pia wanawake waliokuwa eneo hilo kumwangalia kwa macho ya kumuonea wivu.

Na kuna wale walioenda mbali kwa kumlaumu Mungu kumbariki Edna kwa kila kitu , hela alikuwa nazo , uzuri alikuwa nao na mtoto alikuwa nae mzuri tu.

Licha ya Edna kuangaliwa sana ni kama hakuweza kufahamu kwani alikuwa kwenye mawazo na hakujua pia kwamba uwepo wake hapo ndani uliwafanya watu kukosa amani.

Roma kitendo cha kutoa maagizo ya Edna kulindwa kwa ukaribu kiliwafanya Molin, Adeline na Fanny kuweka umbali wa mita chache na yeye , mbaya zaidi siku hii wote walivalia suti nyeusi na kila mtu alikuwa amekaa upande wake huku wakiwa na Earpices masikioni.

Uwepo wa wazungu eneo hili wakiwa wapo na umakini wa hali ya juu kumlinda Edna ndio uliofanya watu kukosa amani na utulivu na hata baadhi ya watu Edna aliokuwa akiwakaribia walimpisha kwa tahadhari.

Ilikuwa ni tukio la kuvutia na la kushangaza kuona mwaftika kupewa ulinzi na wazungu , ijapokuwa watu hawakushangaa sana kutokana na kwamba Edna alikuwa mwanamke tajiri , lakini swala la wazungu lilikuwa sio la kawaida.

Kwa wale waliokuwa wakifuatilia baadhi ya maswala ya walinzi kwa ukaribu huenda mwafrika alionekana hadharani akilindwa kwa ukaribu na wazungu ni Raisi wa Afrika ya Kati.

Sasa Edna akiwa haelewi kile kilichokuwa kikiendelea hapo ufukweni ghafla tu alishikwa na kizunguzungu kikali sana kilichoambatana na maumivu ya kichwa na alijikuta akikosa balansi na palepale alishuka chini mzima mzima na kupoteza fahamu.

Kitendo kile kiliwafanya Walinzi kumsogelea kwa kasi lakini lilikuwa kosa kubwa ambalo wamelifanya kwani Lanlan aliwachukulia kama maadui na ndio waliomfanya mama yao kudondoka.
 
Back
Top Bottom