Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Umetuahidi Edna anazagamuliwa ila umetuacha solemba
Hukumuelewa vizuri mwandishi.

Najua kiu yako na ya wengine ni kushuhudia Edna anavyonyanduliwa na mfalme. Hivi hujasoma pale mfalme alipowekewa ngumu kula kitumbua na queen?

Edna alitoa hadi machozi baada ya kuiona ile bed kubwa ya kunyanduana sevensome, na hicho ndicho kilio alichomaanisha mwandishi 😂

Je hujaelewa tu ?
 
Mkuu Singano naomba sababu ya kubaki nyumbani jpili hii. Tupia chakula ya ubongo.
Whatsapp kwangu mimi tutakutana kwa simulizi ijayo utakapomaliza hii mpaka mwisho.
 
SEHEMU YA 477.
Roma alijihisi roho yake inataka kumtoka ni kama vile yupo kwenye uwanja mkubwa huku mbele yake kukiwa na giza totoro na kukosa uelekeo.
“Hey! unawezaje kukata tamaa kirahisi hivyo?” Sauti ilijipenyeza kwenye ubongo wake, ilikuwa ni sauti iliosikika vyema kiasi kwamba ni kama kuna mtu anamwongelesha kutoka nje.
Alijitahidi kunyanyua mdomo kuongea lakini mdomo ulikuwa mzito kutokana na kukosa nguvu kabisa , hakuweza hata kufumbua macho yake angewezaje kuongea.
“Nafsi ya binadamu ipo kati ya ulimwengu wa roho na ulimwengu unaonekana , muunganiko ambao hurahisisha mawasiliano , mtu yoyote anaejaribu kujifuza mbinu za uvunaji wa nishati za urejesho kati ya mbingu na ardhi anatakiwa kuwa na nguvu kubwa ambayo inemuwezesha kutimiza malengo yake, Dhana ni kichekesho na upuuzi kwani pia zinapata uwezo wake kwa kufyonza nishati ya mbingu na ardhi, kwanini wewe mwenyewe usijibadilishe na kuwa dhana? , nikuambie leo hii nguvu zinatofautiana, mbingu ina nguvu kubwa lakini ndio chanzo cha ukweli wa mambo yote….”Sauti iliendelea kumuongelesha kwenye ubongo wake , ilikuwa ni kama inamuelekeza na kumfanya Roma akili yake kuwa kwenye tafakari nzito.
Kwa kiasi flani kwa muda huo hakuweza kushangazwa na sauti hio lakini pia alishindwa kujali hali aliokuwa nayo , ilikuwa sio mara yake ya kwanza kuongeleshwa na sauti , mara ya mwisho ilikuwa ni China na sauti hio na ile zilikuwa zikifanana kwa kiasi kikubwa.
“Nishati na nguvu?”
Wazo lilipita kwenye akili yake lakini hata hivyo alishindwa kuelewa nini maana ya nyuma kati ya maneno ya Nishati na Nguvu.
“Ngoja nikusaidie maana hujiwezi kwa sasa , hayo mengine utayagundua kwa muda wako” Sauti iliendelea kumuongelesha.
Ni Magdalena ambaye alifanikisha kumdaka Roma na kisha kwenda kumlaza chini ya majani.
Kila mmoja alijawa na huzuni pamoja na kukata tamaa mara baada ya kuona hali aliokuwa nayo, ni kama sio Roma tena.
Mage na Neema Luwazo walishindwa kujizuia na kuanza kutoa vilio wakimlilia Roma .
Roma amepoteza pambano kwa Yan Buwen ndio mawazo ya wanajeshi wote akiwemo Afande Tozo na yeye alikisubiri kifo kutoka kwa Yan Buwen.
Mjumbe kutoka miliki ya kijini ya Hongmeng na Roma wote wamedhibitiwa na Yan Buwen.
Mstaafu Kigombola hakuamini mambo yamekuwa marahisi hivyo na hakuweza kuamini kama kweli Roma amekwisha kupoteza maisha.
“Pluto gani mdhaifu hivyo , mwanaume wa ukweli hatakiwi kujitengenezea udhiafu ,, nilichokifanya ni kukutishia tu kuhusu wanawake wako na kupandwa na jazba na sasa upo kwenye hali kama hio”Aliongea Yan Buwen kwa kejeli
“Wewe mjinga usijifanyishe umeshinda, hujapambana kama mwanaume bali umetutumia sisi kuweza kushinda”Aliongea Neema Luwazo kwa hasira , alitamani kumtukana Yan buwen kwa matusi yote anayoyafahamu lakini alishindwa kufanya hivyo.
“Foolish woman , ningekuacha uishi kama ungeamua kumfuata mzee pale , lakini sasa hivi nikueleze tu sitaki maneno yako hasi juu yangu”Aliongea Yan Buwen na palepale aliinua mkono na kutengeneza mpita mwingine wa nguvu ya ant-matter , huku akinuia kwenye akili yake hilo ndio pigo lake la mwisho kumaliza kazi kabisa.
Muda ule ule Roma ambaye alikuwa amelala usingizi wa pono kama maiti alishituka kama vile mtu ambaye alikuwa kwenye ndoto na kugundua alikuwa kwenye mapaja ya Magdalena ambaye alikuwa akimwangalia huku akitoa machozi.
Alijitoa kwake huku akionekana kutokuwa na nguvu na alijitahidi kusimama , alijikokota kama mlevi lakini alifanikiwa kusimama na kumwangalia Yan Buwen ambaye alikuwa akijiandaa kuachia pigo.
“Oh! You can still stand up? Interesting , I could always kill you again anyways”
“Oh naona umeweza kusimama tena , inavutia , ninakwenda hata hivyo kukua tena”Aliongea Yan Buwen kwa lugha ya kingereza na palepale aliachia pigo la nguvu ya ant-matter kuelekea aliposimama Rom.
“Hapanaa…!!”Magdalena alihamaki kwani aliamini kama pigo lile lingeweza kumpiga Roma na hali aliokuwa nayo angekufa moja kwa moja hivyo Magdalena hakujiuliza mara mbili mbili alienda kusimama mbele ya Roma kumkinga, hakujali kufa kwa wakati huo na akili yake ilimwambia amuokoe hata kama ingekuwa ni kifo chake baada ya hapo.
Alifumba macho yake kwa ajili ya kupokea pigo huku machozi yakiwa yanamtoka mfululizo.
Afande Tobwe alishangazwa na kitendo cha Magdalena baada ya kuona anataka kumuokoa Roma kwa kujitoa kafara , aliijikuta akili yake ikifanya kazi haraka na kuanza kugundua kitu ambacho siku nyingi alikuwa akikipotezea.
Wakati ule kila mtu aliamini pigo lile lingekwenda kumuua Magdalena lakini kitu cha kushangaza kilitokea.
Miale ile yenye mionzi ilipotea ghafla kabla haijamfikia Magdalena, ilikuwa ni kama kuna kitu ambacho hakionekani kimeimeza yote.
Magdalena alikuwa ashajiandaa kufa kwa ajili ya Roma lakini hakuna kilichomtokea , alijikuta akifumbua macho yake na kugeuka ili kuangalia ni nani ambaye amemuokoa.
Yan Buwen mwenyewe alijikuta akishangaa naada ya kuona mabadiliko ambayo ni kama hakuyategemea kwa wakati kama huo.
“Ant-matter energy?” Aliongea Roma huku akitoa tabasamu ambalo ilikuwa ni ngumu kujua ni nini anafikiria na ilikuwa kama sio yeye vile kwa namna ambavyo anaonekana.
“Njia zote ndani ya dunia hii zina mwisho unaofanana, hio nguvu unayotumia hata kama haitokei kwenye dunia hii lakini uhakika ni kwamba itakuwa ipo kwenye anga , unapata wapi uthubutu wa kujiona shujaa na mwenye kiburi kwasababu ya njia ulioichagua , Upuuzi kabisa?”Aliongea Roma kwa sauti nzito sana na kumfanya Yan Buwen kukunja sura.
“Acha kujiona kijogoo , unahisi ninaweza kukuogopa kwasababu ya hotuba yako , Kutana na ghadhabu yangu”Aliongea Yan Buwen kwa hasira na palepale aliita kiasi kikubwa cha mionzi ya ant-matter na mwanga uliokuwa kama kitenesi ulitokea kwenye mikono yake kwa zaidi ya mara tatu.
Upande wa Roma muda uleule aliita nguvu ya Kimaandiko ya urejesho na kisha akajiponyesha kwa haraka sana pasipo kujali watu waliokuwa wakimwangalia ka mshangao.
“Siwezi kukupa nafasi ya kujiponyesha tena , ninataka kukua moja kwa moja na kupotea kwenye uso huu wa dunia”Aliongea Yan Buwen huku misuli ikionekana kwenye uso wake uliokuwa mwekundu , ilionekana alitumia nguvu nyingi sana mpaka muda huo,
Roma hakujalishwa na maneno ya Yan Buwen kwanza kabisa alifumba macho yake kama mtu ambaye anausikilizia upepo wa baharini.Kitendo kile kilizidi kumuuzi Yan Buwen na kuona kama amedharauliwa pakubwa.
“Kufaa..!!”Aliongea na palepale mwanga kama wa kimondo ulimsogelea Roma kwa kasi kubwa.
Kila mmoja alikuwa na wasiwasi juu ya Roma lakini wasiwasi wao uligeuka kuwa mshituko baada ya matokeo.
Ule mwanga wa mionzi baada ya kumfikia Roma, baadala ya kumwathiri ulianza kumzunguka na kuanza kubadilika rangi kutoka kuwa nyeupe na kuwa kama rangi ya zambarau isiokolea , huku ukicheza cheza kama mwanga wa radi kwa kuangalia kwa ukaribu zaidi ni kama vile ulikuwa ukimuogopa Roma.
“Viumbe vyote kwenye ulimwengu huu vilitokana na chanzo , Unajisikiaje kuona mashambulizi yako yakigeuka na kuwa nyoka umeme”Aliongea Roma kwa sauti nzito.
BOOM.
Mwanga ule uliokuwa ukimzunguka Roma ulitoka na kumfuata Yan Buwen kwa spidi kubwa , ilikuwa ni kama nyoka wale wa baharini wanaozalisha umeme, ndio mwanga ulivyoonekana na Yan Buwen kabla hajachukua hatua alishachelewa kwani mlipuko wa shoti kubwa ulitokea na mwanga mkali kumfunika palepale mzimamzima.
Yan Buwen alifanikiwa kuzuia lakini kiasi kikubwa kilimjeruhi na kuanza kuungua na aliweza kuhisi harufu ya ngozi yake ikiungua kama vile nyama iliopo kwenye moto.
“Arrggh..!!”
Maumivu aliohisi ni jambo ambalo kwenye maisha yake hajawahi kupitia na kama sio nguvu ya anti matter kuponyesha mwili wake kwa haraka basi huenda angeshakufa palepale.
Kila mmoja alishangazwa maana sio tu kwamba alizuia pigo a Yan Buwen , lakini aligeuza pigo lake na kuwa siraha.
“Your ant- matter energy might be pure but it’s weak , let me show what I have prepared for you..”
“Nguvu yako ya Anti matter inaweza kuwa safi lakini bado ni dhaifu , ngoja nikuonyeshe kile nilichokuandalia..”Aliongea Roma.
Ghafla mawingu ambayo yalikuwa yametanda angani kuonyesha dalili ya mvua yalianza kuzunguka kwa kasi mno kama vile yalikuwa chini ya udhibiti wa Roma.
Kadri yalivyokuwa yakizunguka ndio yalianza kutengeneza radi kwani msuguano wa atomu za hewa ulikuwa ni mkubwa mno , ngurumo ziligonga kwa nguvu kiasi kwmaba ni kama anga lote linataka kushika chini.
Yan Buwen alijikuta akiangalia juu angani kwa wasiwasi asijue nini kinachokwenda kutokea .
“Wapi unaangalia huko?”Aliongea Roma na palepale Yan Buwen aligeuza macho yake na kuangalia aliposimama Roma na alijikuta akishangaa kuona moto kama lava, ukijitengeneza kwenye mkono wa Roma kwa umbo la nyoka, ulikuwa ni moto wa njano uliokuwa ukitoa cheche, ni sahihi kusema nyoka wa moto, licha ya kwamba ulikuwa ukiwaka kutoka kwenye kiganja cha Roma lakini hakuonyesha ishara yoyote ya maumivu kama alikuwa akiungua.
“Kila kitu ndani ya dunia hii kinafuata sheria kuu ya chanya na hasi , mchanga , maji , upepo ,ngurumo , radi na moto. Moto wa rangi nyekundu unaweza usiwe mkali zaidi ya moto wa bluu lakini moto wa njano unaweza kutosha kuyeyusha chuma na unatosha kabisa kukudhibiti”Aliongea Roma na palepale ule moto wa kichawi uliokuwa kwenye umbo la nyoka ulitoka kwenye kiganja chake na kumsogelea Yan Buwen kwa kasi na kadri ulivyokuwa ukisogea ulizidi kuwa mkubwa na kuwa na muundo kama wa dragoni.
Ya Buwen alitaka kukwepa lakini alikuwa akienda kulia unamfuata huko huko na kuona hakuna namna ya kuukwepa zaidi ya kuuzuia na palepale alijizingira na kiasi kikubwa cha nguvu ya ant-matter kama vile anajiwekea ngao lakini ajabu ni kwamba nguvu yake haikufua dafu kwa moto ule kwani wote uliweza kumfunika na kujihisi maumivu makali ya ngozi yake kuungua.
Kwa waliokuwa wakiangalia kwa mbali ni kama vile wanaona dhoruba ya radi , kwani muda ule ngurumo kubwa ilipiga kisawasawa na kwa mgonjwa wa presha huenda angepoteza fahamu au kupata shambulio la moyo kwani ilikuwa kama anga limechanika katikati.
“Argh!..”Yan Buwen alijikuta akitoa ukulele wa maumivu na alichoweza kugundua ni kwamba kilichokuwa kikimuunguza sio moto tu bali kuna zaidi ya nguvu ambayo ilikuwa ikimuunguza.
“Nguvu ya nishati kati ya mbingu na ardhi haina ukomo , unapata wapi uthubutu wa kulinganisha nguvu yako na ya kwangu”Aliongea Roma kwa sauti nzito, sauti yake ilikuwa imebadilika na ilionyesha huenda ni dhahiri hakuwa yeye.
“Usijifanye kijogoo, siwezi kupoteza hili pambano”Aliongea Yan Buwen kwa kiburi mara baada ya maumivu kupungua. Jiwe la kimungu ambalo lilikuwa kwenye kifua chake lilianza kutoa miale mingi ambayo ilizingira kipenyo kikubwa cha duara.
“Unapoteza nguvu zako bure”Aliongea Roma huku akitoa sonyo na palepale kwenye mkono wake wa kulia ulitengeneza kitenesi cha umeme rangi nyeupe na palepale kilitoka kwenye kiganja cha mikono yake kwa spidi na kupaa kwenda juu na kupotelea kwenye wingu sehemu iliokuwa na mzunguko mkubwa wa mawingu.
“BOOM!”
Kabla Yan Buwen hajapona vizuri mara baada tu ya kitenesi kile cha umeme kupotelea kwenye wingu ilipiga radi ya mwanga mweupe uliokuwa kwenye fungu kama vile mizizi ya mti na ilimpiga Yan Buwen mfululizo.
Ilikuwa kama vile Roma alivyonaswa na mapigo ya Radi kwenye bahari ya kusini ya China ndio kilichotokea kwa Yan Buwen na haikueleweka Roma aliwezaje kusababisha radi ile na isimfuate yeye zaidi ya kwenda kwa Yan Buwen , ni sahihi kusema Yan Buwen ameingia kwenye levo ya dhiki lakini ki uhalisia ni kwamba alikuwa akipata pigo.
Alijaribu kusogea kuikwepa lakini ilimfuata na alijikuta akikata tamaa baada ya kugundua ile radi ilichokuwa ikifuata ni lile jiwe la kimungu na hakuwa na uwezo wa kulitoa kwani angefanya hivyo kingekuwa ndio kifo chake, mbaya zaidi ile radi ilikuwa ni kama inameza nguvu yote ya anti- matter na kutengeneza ‘annihilation’ ni sahihi kusema Matter na Ant-matter zinavutana.
Huenda Christen na Poseidon angekuwepo angekuwa kwenye mshangao , kwani mara nyingi radi kama hizo hutokea pale wavunaji wa nishati ya mbingu na ardhi kukasirisha anga , ni hakika wangejiuliza imekuwaje Yan Buwen na yeye kupitia dhiki kama ilivyomtokea Roma kwani kanuni za Yan Buwen ni tofauti kabisa na nguvu za kijini.
Radi ilipiga kwa nguvu mno na ilikuwa kali mno kama ile iliogonga jengo la world trade centre jijini New York, iliweza kusababisha mwili wa Yan Buwen kuanza kugeuka na kuwa majivu na kilichoweza kubakia ni jiwe la kimungu tu ambalo lilimezwa lote na radi na palepale ilikoma mara moja.
Ukawa mwisho wa Yan Buwen baada ya kipitishwa kwenye Dhiki na Roma kwa kushushiwa radi.
Kwa Yan Buywen haikuhitajika mapigo tisa ya radi , lilikuwa pigo moja tu la mwanga mweupe wa radi ndio uliommaliza kabisa na kuyeyukia hewani na jiwe la kimungu lilivutwa angani na kupotea na palepale Radi zilikoma mara moja na wingu likanza kutawanyika.
Magdalena ambaye alijificha mbali kuangalia kile kinachotokea alijikuta akitoa kilio cha shangwe mara baada ya kushuhudia mwisho wa Yan Buwen , wengine wote walijikuta wakishangalia bila ya kupenda.
Hata Queen ambaye alikuwa na penzi nzito na Yan Buwen alijikuta akishangalia kwa matokeo yale.
Roma alirudi chini na ile anakanyanga tu ardhi alidondoka chini na kupoteza fahamu na kuwafanya watu wote kumkimbilia na kumzingira.
“Asante kwa kuniazimisha mwili wako Roma , naendelea kusubiria kwa hamu siku nitakayo weza kuutawala mwili wako kabisa na kuishi kama binadamu wa kawaida, naamini umejifunza kitu leo nini maana ya nguvu ya kimaandiko ya urejesho”Sauti kwa mara ya pili ilisikika kwenye akili ya Roma , ijapokuwa alikuwa kama amepoteza fahamu lakini akili yake ni kama ilikuwa ikiwasiliana na nafsi yake ya ndani.
“Romaa..”Sauti ilimwita kwa nguvu na alijikuta akishituka haraka kama vile alikuwa kwenye ndoto na kuangalia watu waliokuwa wamemzunguka , alisimama haraka.
“Nipo sawa”Aliongea na kuwafanya wote kuvuta pumzi za ahueni..
Mage, Magdalena na Neema waliangaliana na kujikuta wakiachia tabasamu zito.
Tukio la leo huenda limewafanya kuwa karibu zaidi na kutengeneza mazoea ni tukio ambalo pia lingedumu kwenye fikra zao , lakini hata hivyo kila mtu alipatwa na ahueni mara baada ya Yan Buwen kudhibitiwa.
“Heaven and Earth , Power….”Alibwabwaja Roma huku akiwa amesimama akifikiria na kuwafanya wasielewe anajaribu kuongea nini.
“Roma unaongea nini?”
“Huyu mpuuzi kwanini hajanielekeza kila kitu, ila sio mbaya lazima nielewe fumbo hili mimi mwenyewe…”Aliongea Roma ka mara ya pili, akili yake ilionekana kuwa mbali lakini ile anakuja kurudi katika uhalisia alishangaa Mage alikuwa amemkumbatia huku akitoa machozi, alimwangalia na kutabasamu.
“Mage unanukia vizuri”Aliongea Roma huku akito atabasamu ambalo limezoeleka na ucheshi wake kurudi, Mage alijihisi aibu maana watu wazima walikuwa wakimwangalia.
“Acha kuigiza ,unaonekana upo sawa nakuwa na wasiwasi bure”Aliongea Mage huku akimsukuma na kujitoa kwake.
“Njooni mnipe kumbatio la ushindi”Aliongea Roma akiwaongelesha kwa ishara huku akiwa amechanua mikono yake na wote waliangaliana na kuonyesha kusita sita lakini Neema alikuwa ndio wa kwanza kwenda , Mage kuona vile na yeye akaunga , Magdalena na yeye hakutaka kubakia nyuma alikumbatia upande wake , Donyi nae hivyo hivyo.
Warembo wote walimzingira Roma na kumkumbatia kwa furaha , Omari aliekuwa bado kwenye maumivu ya mionzi ya Thanatos alimwangalia Queen na kujikuta akitabasamu kwa furaha.
Afande Tozo na Afande Tobwe wote walijikuta wakitabasamu na kisha waligeukia wanajeshi waliobaki na kutoa ishara na palepale walimzingira raisi Kigombola ambaye alikuwa akiangalia namna ya kukimbia.
“Roma nadhani tumalize kabisa, tunasubiri maamuzi yako juu ya mstaafu” Aliongea Afande Tobwe na Afande Tozo na yeye alimwangalia.
Wote walimuachia Roma na kumpa nafasi ,Roma alimwangalia Raisi kigombola na wafuasi wake waliokuwa wakimwangalia kwa woga mno kama vile hawaamini ni yeye kwa kile walichoshuhudia kwa dakika kadhaa zilizopita.
“Yan Buwen ashakufa tayari na sipo kwenye nafasi ya kufanya maamuzi , mnaweza kufanya mnachoona kinafaa kwa mstaafu na wafuasi wake”Aliongea Roma.
Hakutaka kumuua Kigombola kwani alikuwa baba yake Donyi na kama angefanya hivyo ingemuathiri sana , alijua damu ni nzito kuliko maji hivyo kama akichukua hatua basi huenda uhusiano wake na Neema pia ukayumba, hivyo alitaka sheria ichukue mkondo wake, hata hivyo ushahidi wa makosa ya Kigombola ulikuwa wazi.
Mstaafu kigombola sura ilimshhuka kwa kiasi kikubwa , hakuamini kama Roma angeweza kumshinda Yan Buwen na ni mpaka aliposhuhudia mwenyewe ndio alipomkubali.
“Baba..!!!”Donyi alisimama huku akimwangalia baba yake na machozi yakiwa yanamtoka na kumfanya Neema Luwazo kumuonea mtoto wake huruma na kumsogelea na kumkumbatia kwa nyuma.
“Usiniangalie kwa kunionea huruma Donyi mwanangu , kwenye maisha unatakiwa kuelewa kufeli na kufanikiwa ni matokeo ya aina mbili ambayo hayana budi kutokea , nimeishi kwa muda mrefu na nimegundua kufeli kwangu ndio mwanzo wa mafanikio yenu, hata kama nimefeli leo naamini nilichokianzisha hakiwezi kupotea”Aliongea na kisha akamgeukia Roma.
“Wewe mtoto , hata kama umefanikiwa kumshinda Yan Buwen bado hutoweza kumshinda bosi wake , siku moja utatambua kwamba juhudi zako zote hazikuwa na maana”Aliongea lakini Roma hakuwa na cha kuongea hivyo alipotezea maneno yake, hata hivo alikuwa akiishi kwasababu ya Donyi tu la sivyo angekuwa maiti muda huo.
Roma hakutaka kujihusisha nae kabisa na hakutaka kumsikiliza maana alijiambia akizidi kumsikiliza anaweza kukasirika na kumuua hapo hapo , hivyo alimsogelea Omari kwa ajili ya kumuondolea mionzi ya Thanatosi kwenye mwili wake.
“Bro ulivyodonoka nilijua tayari ndio mwisho wetu kabisa, ila ulichokifanya mpaka sasa nashindwa kuelewa ni nguvu ya aina gani unamiliki?”
“Aliefanya vile sio mimi” Aliongea Roma
“Sio wewe! , Unamaanisha nini?”
Roma alishindwa kujibu maana alikosa maelezo ya kutosha kueleweka kwa kila mmoja , ukweli kilichofanyika haikuwa akili yake , ni kama mwili wake ulikuwa ukitawaliwa na kiumbe wa ziada ambaye anaishi ndani yake , ilikuwa ni kama alikuwa na nafsi mbili , nafsi ya Roma na nafsi ambayo haikuwa akiifahamu.
Roma aliweza kumponyesha Omari kwa kufyonza ile mionzi na hatimae maumivu aliokuwa akiyasikia yalipungua kwa kiasi kikubwa na sasa ilibidi kidonda chake kipona kiasili lakini kwa spidi kutokana na nguvu zake za kijini.
“Queen naamini sasa huna sababu ya kunikataa tena, najua tayari unanipenda acha kuficha”Aliongea Omari mara baada ya kuhisi maumivu yake yashapona na Roma alijiambia kama angejua hayo ndio matokeo asingemponyesha.
Queen hakutegemea Omari angemchumbia hapo hapo mara baada ya tukio.
“Acha basi , huu sio muda mzuri na wewe”
“Nani anajali , hakuna ninachothamini kwenye maisha yangu zaidi yako”Aliongea kwa sauti na kufanya watu wote kumgeukia..
“Wewe mpuuzi , huu sio muda wa kufanya ujinga wako”Aliongea Afande Tozo akimkaripia
“Nakutafutia mkwe baba tulia uone , sijali muda na mahali kufanya ninaloona ni sahihi”Aliongea na kisha alimshika Queen mkono.
“Queen wewe ndio msichana ambaye nilipenda na nitaendelea kupenda kwa maisha yangu yote, Will you marry me?” Kauli ya Omari na kutokosa aibu iliwashangaza watu na kufanya wawaangalie, Queen alishindwa kujibu ukizingatia alikuwa na tumbo kubwa la mimba ya mwanaume mwingine.
“Mimi ni mwanamke mpumbavu ambaye nilijidanganya mwenyewe kwa kujiaminisha napendwa kumbe natumiwa , mimi sio mrembo na sina manufaa kuzidi wanawake wengine, Wewe ni mrithi wa mali za familia yako na una nguvu naamini wapo wasichana wazuri na warembo kuzidi mimi ambao watakupenda , usipoteze muda na nguvu zako kwa mtu asie na thamani kama mimi, maamuzi unayotaka kuyafanya muda huu ni ya haraka na utakapokaa chini na kutulia utaona maamuzi yako hayakuwa sahihi, Omari siwezi kukubalia , sitaki kuja kukuumiza huko mbeleni”Aliongea huku akitoa machozi.
Watu watu wote walihisi huzuni baada ya kusikiliza maneno ya Queen , ilikua ngumu kwake na alimuonea huruma Omari kwani angeenda kulea kiumbe ambacho sio cha kwake na huenda huko mbeleni mtoto wake kuja kuonekana mzigo na mbaya zaidi alijua mtoto ambaye anakwenda kuzaa atakuwa na mwonekano tofauti kabisa kwasababu baba yake alikuwa mchina.
Upande wa Roma hakuwa na huzuni ila alimuona Omari kama mtu jasiri sana ambaye hakujali mazingira kuweka hisia zake wazi, alipenda watu wa aina hio maana hata yeye yupo hivyo.
“Kila siku unasema hauna thamani ya kuolewa na mimi kama ni hivyo kwanini unanikataa kila mara , nimekuomba lakini umenikataa ,sawa mwanzo nilikubali lakini leo nimeyaokoa maisha yako , kwanini usinilipe kwa kuwa mke wangu”Aliongea Omari.
“Wewe…!,Kwanini unaongea hivyo?”Aliongea huku akikosa utulivu na kuhisi aibu kwasababu kila mtu alikuwa akimwangalia
“Queen sema ndio , kuwa wangu kwa maisha yako yote na naapia sitokusumbua tena kwenye maisha yako yote hata baada ya kifo , nakuahidi utaishi kwa kuoga mvua ya mahaba kwa maisha yako yote na nitaishi maisha marefu kuzidi wewe ili kutumiza ahadi yangu”
“Lakini .. Omari mimi tayari nina mimba?”
“Nasema sijali, nakupenda hivyo hivyo wewe pamoja na mimba yako hata kama sio yangu “Aliongea Omari akiwa siriasi.
“Huyu ni chizi , jamani huyu ni chizi , nina mtoto chizi..”Aliongea Afande Tozo akishindwa kuamini kile anachokiona lakini hata hivyo hakuwa na cha kufanya , alikuwa akielewa mapenzi ya mwanae kwa Queen yaikuwa ni ya muda mrefu sana.Lakini kilichokuwa kikimtekenya ni kwamba wanakwenda kulea mtoto wa Yan Buwen na watu wangewanyooshea vidole kwani mtoto ambaye angezaliwa angekuwa tofauti sana na Omari , yaani angekuwa mzungu.
“Queen nishafanya kila kitu kukuonyesha ni kiasi gani nakupenda na sasa sina namna tena ya kukushawishi na kama utanikataa ni bora nife tu”Aliongea huku akiinua kiganja cha mkono wake na kuanza kujipiga vibao mashavuni kama mwehu.
“Hapana “ Queen aishindwa kujizuia na kumshika mikono yake huku machozi yakimtoka.
“Ukifa nani anakwenda kunininulia Ice cream ..”Aliongea kwa sauti tamu huku akiweka tabasamu na kumfanya Omari kumwangalia na kisha kulipukwa na furaha, mapenzi yao walipokuwa watoto yalianza kwa Omarri kumnunulia ueen Ice cream za koni.
“Hahaha.. Queen natafsiri maneno yako kama ‘ndio’”Aliongea Omari na kisha akamvutia Queen kwake na kukumbatiana kwa furaha na ndio ikawa Queen alivyoweza kufungua moyo wake kwa Omari kwa mara nyingine.
NB: Wanaume tuwe na subira tule mbivu(Jokes).




SEHEMU YA 478.
NORTH POLE (NCHA YA KASKAZINI YA DUNIA)
Wakati wingu kubwa lililotanda angani jijini Dar es salaam likitawanyika mambo yalikuwa tofauti kabisa kaskazini mwa ncha ya dunia.
Hakukuwa na dalili yoyote ya maisha ndani ya eneo hilo kutokana na mazingira yake kutosapoti maisha kutokana na hari ya ubaridi sana wa barafu.
Chini ya mfuniko wa barafu kulikuwa na chombo kikubwa mno mfano wa manuari ya kijeshi iliojengwa kwa chuma , sasa ndani yake kulikuwepo na maabara ya kisasa mno ambayo imejaa vifaa vingi vya kieletorniki ambavyo vilikuwa vikitoa signal ambazo hazikuwa zikieleweka kwa uharaka, kwenye skrini zilizofungwa ukutani kulionekana maandishi na data ambazo pia hazikutafsrika lakini pia picha mbalimbali zilionekana kwenye skrini nyingine
Skrini zile zilionyesha kulikuwa na vyumba vingine , kwani zilionyesha upande mwingine wa chumba katikati kulikuwa na masanduku kama ‘tube’ ambayo yamejaa virutubisho vilivokuwa kwenye mfumo wa majimaji mazito ,masanduku yalikuwa yametengenezwa kwa kioo hivyo ilikuwa rahisi kuona kile kilichokuwepo ndani yake.
Moja wapo ya sanduku kimiminika chake kilianza kutikisika kwa nguvu na palepale alionekana mwanaume mwenye nywele ndefu akishituka kutoka kwenye usingizi wa pono na kufungua macho yake baada kutoa kichwa nje kimiminika kwani sanduku lile likuwa na uwazi usiojaa kwa juu.
Na pale pale ni kama vile kuna kitu kiliwashwa kwenye akili yake kwani macho yake yalianza kuonyesha hasira na chuki kubwa , alikunja ngumi ndani ya kimiminika kile na ndani ya dakika chache mbeleni alinyanyua mkono na kufikia kitufe kilichokuwa kimetenengezwa kwa ndani na kisha akakibonyeza, ilikuwa ni kama switch kwani palepale kile kimiminika kilianza kufonzwa na mirija iliounganishwa kwenye lile sanduku ambalo lilikuwa kama Tube na dakika nyingine mbele baada ya ule ujiuji wote kuisha mlango wa juu ulifunguka wenyewe na kisha akajinyanyua kivivu na kutoka nje kwa kudondokea chini sakafuni , alionekana alikuwa dhaifu mno.
Upande mwingine mbele yake kwenye meza ya chumba kulikuwa na boksi dogo la mraba la kioo ambalo ndani yake lilikuwa na kitu kama kitenesi cha kung’aa sana na kutoa mwanga mkali huku kikizunguka hewani kwa namna ya kuelea pasipo kugusana na kioo.
“Hades ulifikiria unaweza kuniua kirahisi , siku zote ninaishi nikiwa na mbinu mbadala , nitakuja kukuua tu kadri jiwe la kimungu litakavyoendelea kuwa chini ya umiliki wangu “Aliongea huku akiweka tabasamu la kifedhuli , alikuwa uchi wa mnyama.
Alikuwa ni Yan Buwen , alijitahidi kusimama lakini alikosa balansi na kudondoka chini na alijilaza chali kivivu huku akipumua kama mbwa aliekimbia maili nyingi.
Muda ule ule skrini zilionyesha mlango wa chumba wa kuingilia kwenye chumba kile ukifunguliwa kwa kuslide(kuteleza) kwenda pembeni kama lift huku ukitoa mlio kama wa kengele , vilevile kama lift inavyojifunga na kufunguka na palepale mwanamke alietangulizana na wanaume wawili aliingia.
Mwanamke alikuwa amevalia gauni fupi lililoishia juu ya magoti , lenye maua maua lakini ambalo lilichora vyema umbo lake na kuzidi kuwa mrembo , hakuwa mzungu wala mweupe bali ni sahihi kusema alikuwa ni ‘black Beuty’ na alikuwa akivutia haswa kingono(Sexy).
Mwanaume mwingine alikuwa amevalia kombati za jeshi la Tanzania na mwingine alikuwa amevaa gauni, mavazi maalumu ya wagonjwa na alionekana kuwa na mguu bandia wa chuma.
Licha ya kwamba ncha ya kaskazini ya dunia kuwepo kwa baridi ambalo binadamu hawezi kuvumilia lakini watu hao walionekana kuwa sawa kabisa bila shida yoyote.
Yan Buwen ambaye alikuwa amelala chali aliinua shingo yake kidogo na kuwaangalia watu waliongia hapo ndani na baada ya kuwafahamu alikunja sura na kuonyesha tabasamu la kejeli.
“Nyie watu kwanini mmerudi , si niliwaambia mkaishi kwanza nchini kwenu Tanzania mpaka nitakapowaita?”Aliuliza.
Naam watu watatu ambao waikuwa wakimwangalia walikuwa ni Kizwe , Lekcha na Denisi Senga na haikueleweka kwanini walikuwepo hapo au wamefika lini hususanni kwa Lekcha.
“Hakukua na sababu ya sisi kwenda Tanzania , tuliona tukusubirie hapa hapa na tuliweza kupokea taarifa kutoka Tanzania kwamba umeuliwa na yule mpuuzi, lakini mtu kama wewe kwa ukubwa wako ni sahihi kuona ulikuwa na mpango mbadala”Aliongea Denisi.
“Mhmh! Kwanini? Mbona kama mlikuwa mkiniombea kifo?”
“Hapana bwana”Aliongea Kizwe na kisha akamsogelea na kumnyanyua na kumkarisha kwenye kiti na kisha akamwambia.
“Tungekuwa tushakufa muda mrefu kama isingekuwa wewe kutusaidia , tunakutegemea sana wewe kuua maadui zetu”
“Watu weusi mna akili za kimasikini sana, kama sio mimi wote nyie mngekuwa mnaoza kwenye makabuli”Aliongea huku akitabasamu kwa jeuri , watu waliokuwa mbele yake ni kama walikuwa kituko.
“Master umewezaje kujifufua mwenyewe, unaweza angalau kunielewesha maana inashangaza sana na inanifanya niwe na shauku ya kufahamu japo kidogo”Aliongea Lekcha kwa kunyenyekea na Yan Buwen alimwangalia kwa kiburi.
“Mwili wako licha ya kwamba nimeanza kuutengeneza lakini upo kwenye hatua za mwanzo hivyo huwezi kuwa kama Denisi au Kizwe , kwangu wewe utaendelea kuwa kilema mwokota makopo, Hehe.. hayo ndio yatakuwa maisha yako milele”Aliongea na kumfanya Lekcha kutetemeka
“Ila sijali sana kukuelezea kile unachotaka kujua lakini unaweza usielewe , nilichokifanya ni ku ‘clone’ mwili wangu na nikakopi kumbukumbu zangu zote kwenye biochip”Aliongea harafu akaendelea.
“I sync it and set a password on it and if my original body was destroyed the biochip will be activated and my memories would be pasted over into the new body and so on , The so called scientists of this world would not be able to utilize this technology, I doubt they would be abe to achieve this even in the next century”
“Na kisha kuzilandanisha na kuziwekea nywira na kama mwili wangu wa mwanzo ungeharibika biochip ingejiwasha na kumbukumbu zangu zingejihamisha kwa kuingia kwenye mwili wangu mpya na kuendelea , hao wanaojiita wanasayansi wa ulimwengu huu hawawezi kutumia hii teknolokia , nina mashaka huenda wasiweze kufanikisha hata kwenye kare ijayo”Aliongea kwa majigambo ni kama alijiona yeye pekee ndani ya dunia ndio mwenye uwezo wa kutumia teknolojia ilioendelea.
Lakini muda huo bado alionekana kuwa na wasiwasi kwasababu siku zote alikuwa akimtumia Kigombola kama chanzo cha pesa kwenye kujiendesha lakini kwasababu muda huo kuwa chini ya sheria basi alifikiria anapaswa kutafuta mtu mwingine wa kumfadhili.
Lekcha alioneyaha kuwa kwenye mshangao mno baada ya kusikia maelezo ya Yan Buwen.
Sikujua kama ndio inavyofanya kazi , hakika Master Yan Buwen wewe ni jiniasi”Aliongea huku akijirahidi kuwa chawa
“Hahaha… upo vizuri kwenye uchawa , nimependa”Aliongea Yan Buwen.
“Hapana sio uchawa bali maneno yangu yanatoka kwenye uvungu wa moyo wangu kabisa”
“Sio mbaya . nimependa”Aliongea Yan Buwen na kuwafanya Denisi na Kizwe kuangaliana na kutoa tabasamu ambao lilikuwa na zaidi ya maana , ni kama walikuwa wakimkebehi Yan Buwen.
“Master unajisikia vibaya , mbona kama unaonekana kuwa mgonjwa hivi?”Aliuliza Lekcha ambaye ndie aliekuwa amevlia gauni la mavazi ya wagonjwa,
“Nipo sawa nitapona baada ya kutumia Jiwe la Kimungu kwenye huu mwili na baada ya hapo nitaenda tena kukiamsha Tanzania”Aliongea huku aking’ata meno yake kwa hasira na kumfanya Lecka kuangalia kiboksi ambacho ndani yake kulikuwa na kijiwe cha kung’aa.
“Kwahio hilo ndio jiwe la kimungu , ndio mara yangu ya kwanza kushuhudia kwa macho?”
“Linaonekana kua dogo si ndio , linaweza kuwa kama kipande cha kajiwe lakini nina mbinu za kuweza kulikuza na kutoa nguvu isiokuwa ya kawaida , The anti-matter energy can be expanded through self absorption”Aliongea na kumfanya Lekcha kuwa kwenye shauku kubwa,
“Maste ngoja nikakuletee angalau mavazi ya kuvaa” Aliongea Lekcha na kumfanya Yan Buwen kuangalia mwili wake ambao ulikuwa uchi , ijapokuwa hakujali kuwa uchi lakini alitingisha kichwa kukubali.
“Yan Buwen inaonekana huyu kilema anakupenda sana na kukujali”Aliongea Kizwe huku akianza kumpapasa Yan Buwen kama wale makahaba wanaofanya kazi kwenye macasino.
Yan Buwen mwili wake ulianza kumsisimka kutokana na ulaini wa mikono ya Kizwe na alianza kuugulia utamu kwa kutoa sauti.Denisi aliangalia bila ya kuwa na wasiwasi.
Kizwe alimpuliza Yan Buwen kwenye masikio kwa staili ya kimahaba , alikuwa akifanya kazi kwa uzoefu mkubwa kama vile alikuwa emefanya kazi kwenye makasino.
“How’s this, am I still a bitch?”
“Unaonaje, bado unanichukulia kama kahaba?”
Yan Buwen aliishia kuguna kutokana na msisimko , ijapokuwa bado hakuwa na nguvu ya kutembea , lakini mikono yake ilikuwa na nguvu hivyo aliishia kumvuta Kizwe na kumuweka kwenye mapaja yake , ni kama alikuwa akimwambia afanye kazi.
Kizwe na yeye alielewa somo na kuinamisha uso wake na kuanza kunyonya koni na kuiingiza yote mdomoni kiasi cha kufikia kwenye koo.
Yan Buwen alijikuta akigugumia utamu alijikuta akitiginsha kichwa huku akifurahia huduma anayopewa.
Muda huio huo , Lecka alisharudi akiwa ameshikilia nguo mfano wa joho , macho yake yaliongezeka ukubwa mara baada ya kushuhudia Kizwe akipiga blow job lakini alijitahidi kujizuia na kujiweka sawa ili asishitukiwe.
“Master naomba uniruhusu nikuvalishe “Aliongea na Yan Buwen alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kutokana na joto la mdomo wa Kizwe na aliishia kutingisha kichwa akimpa ishara ya kumvalisha.
Kizwe muda ule ule aliinua macho yake juu huku akiendelea kuitafuna mashine ya Yan Buwen na ulimi na Lekcha alimpa ishara flani na palepale Kizwe aling’ata dudu ya Yan Buwen kama kipande cha nyama
“Argh..!!!”
Yan Buwen alijihisi kama mnyama amefungua kifua chake kwa maumivu alioweza kusikia na yaliweza kufika kwenye ubongo wake , lakini kabla hajafanikisha kumsukuma Kizwe kuachia dudu yake, Lekcha alichomoa kisu palepale kutoka kwenye vazi alilokuja nalo na kumchinja kwenye shingo kwa kulengesha mshipa mkubwa wa damu.
Ali’chikita’ kwa nguvu kama anachinja kuku kiasi kwamba kisu kilikata misuli yote ya shingo na kikalemea upande mmoja na damu mfululizo ziliruka kama bomba la maji ya Dawasa na damu zilimrukia Lekcha na Kizwe.
Kizwe na yeye aling’ata kabisa dudu yake yote na kipande kilibakia mdomoni na alifanya kukitema chini baada ya Yan Buwen kudondoka chini na kuanza kutetema akikata roho kama Kuku alielekezwa Kibra.Denisi alipiga makofi ya shangwe.
“Vyema sana , vizuri sana , Welldone mmefanya kazi nzuri bila kuhiraji msaada wangu”Aliongea na Lekcha ambaye ameloana damu usoni alitupa kisu chini mara baada ya kumalizia kutenganisha shingo ya Yan Buwen na kiwiliwili kikatili mno na kulamba baadhi ya damu zilizokuwa kwenye lipsi ya midomo yake.
“Dumbass . how dare you to act so arrogant in front of us when you have not recoverd , everything you owned now belongs to me , Hahahaha… Hades wait fo me”
“Mpumbavu , Unapata wapi uthubutu wa kuleta kiburi mbele yetu wakati hujapona ,sasa kila kitu chako kimekuwa changu , Hahaa,, Hades nisubirie nakuja”Aliongea huku akianza kucheka na kutembea kulisogelea jiwe la Kimungu na baada ya kulifikia aliinua kile kiboksi kwa mikono yote miwili na kuanza kucheka tena zaidi ya sana huku akilikodolea macho na jiwe lile lilitoa mng’ao wa aina yake na kufanya chumba chote kubadilila rangi.
“Hatimae funguo ya kulipiza kisasi changu ipo mikononi , Hades ulinifanya kuwa kilema na bahati mbaya hukunikumbuka na nitakulipa zaidi ya mara mia maumivu ulionisababishia”Aliongea Lekcha kwa hasira.
Wakati Roma akijua ashamaliza kazi ndio kwanza inaanza.
Huku Kizwe katikati Lekcha kule Denisi wote wanachuki na Roma na wamepata jiwe la Kimungu , unadhani nini kitatokea.
Lekcha amefikaje North pole , Aliwezaje kufanywa kilema na Roma ,Athena yupo wapi Aisee ni motoo
 
SEHEMU YA 479.
Uhai na kifo ni kitu kimoja kama ilivyo mto na bahari kuwa kitu kimoja , Yan Buwen licha ya kuwa na nguvu kwa kiasi kikubwa lakini hakuwahi kuwaza kifo chake ni baada ya kuhamisha kumbukumbu zake kwenye mwili mpya.
Upande mwingine nae Roma akijua kwamba amemuua Yan Buwen hakujua kwamba mwenzake alikuwa hai na aliweza kuuliwa na watu dhaifu kama Kizwe na Lekcha.
Lekcha alitemea mate maiti ya Yan buwena kana kwamba anautangazia ulimwengu mwanasayansi nguli kutoka taifa la China ameweza kufa kikatili.
“Una uhakika unaweza kutumia teknolojia zake?”Aliuliza Denisi.
“Ushasahau alichoongea , amesema kuna kitu ametumia ku syncronize memori zake kwenye mwili wake mpya”
“Lekcha unamaanisha Biochip?”Aliuliza Kizwe.
“Upo sahihi , tunachotakiwa kufanya ni kupasua ubongo wake na kuitoa na tunaweza kupata kila taarifa na baada ya hapo tutakuwa na uwezo wa kupata nguvu , nina uhakika kama hatutamshambulia Roma ana kwa ana kama huyu mjinga tunaweza kumshinda huku sisi tukiwa nyuma ya pazia”Aliongea Lekcha akimaanisha kwamba kwasababu Yan Buwen ameshindwa kumdhibiti Roma basi uwezekano wao wa kumshinda kwa kupigana nae ana kwa ana unaweza usifanikiwe , hivyo njia pekee ya kumzidi ni kumshambulia kwa njia isiokuwa ya moja kwa moja.
“Kama ni hivyo basi nipo tayari , nitahakikisha mahitaji yote unapata ya kiuendeshaji”Aiongea Denisi.
“Licha ya kwamba baba yako ni raisi lakini kupata kiasi kikubwa cha pesa kusapoti uendeshaji wa hili eneo sidhani kama utakuwa nao”Aliongea Kizwe.
“Hilo lisikupe shida , mimi ni mtoto pendwa kutoka kwa baba yangu hawezi kushindwa kunifanyia uchochoro wa kukwapua bilioni kadhaa za watanzania”Aliongea na Kizwe na Lekcha waliangaliana na kutabasamu.
*******
Upande wa Tanzania ilikuwa ni kizaa zaa mara baada ya raisi Kigombola kujipiga mwenyewe risasi ya kichwa , Roma kama angeamua kumuokoa angefanikisha lakini hakutaka kufanya hivyo.
Watu wote walishangazwa na maamuzi yake , lakini hakuna ambaye alimlaumu kwa maamuzi alioyachukua kutokana na makosa ambayo amefanya na kama sheria ingechukua mkondo wake huenda angehukumiwa jera miaka isiopungua therathini kisheria hivyo ingekuwa moja kwa moja maisha yake yote angeyamalizia gerezani na huenda ndio sababu alioona inafaa kujimaliza mwenyewe .
Neema licha ya kwamba alimchukia alijikuta akilia mno na sio yeye Donyi pia alimlilia baba yake , kila mmoja alieweza kushuhudia kile kilichotokea aliweza kulia na kushikwa na huzuni.
Licha ya kigombola kujiua , lakini huku nyuma alikuwa ameacha kiasi kikubwa cha utajiri na kutokana na mali zake alivyokuwa akizimiliki basi hata kama serikali itachukua hatua ya kuzifuatilia ingekuwa ngumu kuzitaifisha , kwani nyingi zilikuwa kwa majina bandia.
Athari kubwa ambayo inatarajiwa kutokea kwasababu ya kifo chake ni ile nguvu aliokuwa nayo serikalini kupotea , watoto wake ndio walikuwa wanasiasa lakini walikuwa na nguvu kutokana na kwamba baba yao ndio aliekuwa akiendesha usukani, sasa dereva amekufa gari halina budu kuyumba na hatimae kupoteza mwelekeo.
Kifo cha Kigombola watu ambao wanakwenda kunufaika kwa kiasi kikubwa ni familia ya Afande Kweka, mathalani kwa raisi mwenyewe Senga, kwani tokea ayachukue madaraka kuna maamuzi ambayo alikuwa akishindwa kuyachukua kutokana na namna ambavyo Kigombola alikuwa akiingilia uongozi wake , hivyo kifo chake ni kama angeenda sasa kuwa raisi kamili na mwenye ushawishi kwenye maeneo karibia yote ndani ya taifa.
Huenda baada ya habari kuzisikia kutoka Marekani alipokuwepo kikazi atakuwa anashangilia kwa shangwe.licha ya kwamba yeye sio aliefanikisha kifo chake bali msababishaji mkuu ni mtoto wake Roma ambaye siku zote hakutaka kumtambua.
Baada ya taratibu zote hapo ndani kumalizika za kuondoa mwili wa marehemu kwa ajili ya kupeleka hospitalini kuhifadhia , Roma alikadiria muda ambao Edna angefika Tanzania na kwa haraka haraka aliamini kama ni kufika Dar es salaam ingekuwa ni usiku sana , hivyo hakuwa na haja ya kurudi nyumbani kwani angeenda kuwa mwenyewe.
Alichokifanya ni kuondoka na Neema Luwazo pamoja na Donyi ambao wote walikuwa kwenye majonzi ya kifo cha Kigombola , aliona akae nao karibu kwa ajili ya kuwafariji.
Neema mara baada ya kurudi kwenye jumba lake wageni waliokuwa wakimpa salamu za pole walikuwa wengi mno , maana habari za kifo cha mheshimiwa zilikuwa zishawafikia watu wengi.
Roma aliwasiliana na Ron kuulizia kama Edna amekwisha kuondoka Visiwa vya wafu na Rona alimwambia Edna anatarajia kuondoka asubuhi ya saa tano mchana kwani na Blandina na Bi Wema wote hawakuona haja ya kuendelea kubakia kwenye hivyo visiwa ilihali hakuna ambae walikuwa wakiwafahamu.
Roma baada ya kusikia hivyo aliamini mpaka muda ambao watakuja kutua nchini Tanzania ni siku inayofuata sasa, muda wa asubuhi siku hivyo alimpigia simu Diego na kumtaarufu amerudi na Edna angerudi siku inayoafuata hivyo wanapaswa kuwa makini na usalama wake atakapofika.
*******
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa , Roma aliamkia ndani ya nyumba ya Neema Luwazo kama vile yeye ndio mwenye nyumba, baada ya kupata kifungua kinywa aliamua kuwasindikiza mpaka msibani ambako alikaa kwa masaa kama matano hivi.
Baadhi ya watu walikuwa wakimwangalia kwa chuki lakini hakujali , kwanza sio yeye ambaye alimuua Kigombola bali alijiua mwenyewe, hakuhisi hatia ya kile kilichotokea.
Wakati Roma anatoka msibani kurejea mjini ilikuwa ni saa nane kwenda saa tisa , wakati alipokuwa kwenye gari alikuwa akijaribu kufanya mawasiliano kwa kumpigia Edna simu lakini ajabu ni kwamba simu yake haikuwa ikipatikana, alishangaa kwani kwa muda huo atakuwa tayari ashafika Tanzania kama kweli walitoka saa tano , sasa alijiuliza imekuwaje simu yake isiwe hewani, alijua Edna anaweza kuwa na hasira na yeye lakini hawezi kuzima simu ili asipatikane hewani kwa makusudi , alichokifanya ni kumpigia simu mama yake mzazi.
Na ndipo alipoambiwa Edna aliondoka nyumbani mara baada ya kurudi tu na kuaga anaelekea kazini.
“Roma nenda huko huko ofisini kwake ,mkayamalize maana alikuwa amenuna njia nzima mpaka tunafika Tanzania , msipo yamaliza mapema hali inaweza kuwa mbaya zaidi mbeleni , umekosea mwenyewe kumuacha mwenzio wakati ulikuwa usiku wake wa kwanza baada ya ndoa,Mnunulie na chakula umpelekee”Aliongea Blandina kwenye simu na Roma alimwambia anaelekea huko na asiwe na wasiwasi atayamaliza.
Ilionekana Blandina mara baada ya kutoka Visiwa vya wafu alikwenda kuishi tena nyumbani kwa mwanae .
Roma baada ya kufika Posta aliingia kwenye mgahawa wa vyakula vya haraka (Fastfood) na kununua chakula ambacho aliamini Edna atakipenda , aliotea kwamba muda huo Edna atakuwa hajala chochote kutokana na kuwa na hasira pamoja na mawazo ndio maana alichukua maamuzi ya kufanya hivyo
Dakika kumi na tano mbele aliweza kufika ndani ya jengo la kampuni ya Vexto na alishuka na kisha aliingia kwenye lift na kupandisha moja kwa moja mpaka kwenye floor ambayo ofisi ya Edna inapatikana.
Roma baada ya kufika kwenye meza ya sekretari aliweza kumuona Recho akutokea ndani ya ofisi ya Edna.
Alikuwa amevaa suti ya rangi nyeusi na viatu vya visigino virefu huku mkononi akiwa ameshikilia mafaili , Roma alijiambia Recho anazidi kupendeza siku hadi siku na hivi karibuni alionekana kuonesha mabadiliko makubwa zaidi , kwanza alionekana kuwa na furaha.
“Roma umerudi? Umechelewa kuja maana naona bosi hayupo kwenye mudi nzuri”Aliongea Recho kwa heshima huku akitabasamu.
“Ndio maana nimekuja kumuona , huenda naweza kumfanya kuwa na furaha”Aliongea Roma na kumfanya Recho kutabasamu.
“Yupo kwenye ofisi yake lakini ana mgeni”.
“Mgeni?”Roma alishangaa kwani kwa alivyokua akielewa taarifa za Edna kuwa likizo zilikuwa ni rasmi , hivyo ilikuwa ngumu kwa mgeni kuja ofisini kwake kwa siku kama hio ambayo ndio kwanza tu amerudi kutokea Mediterranian.
“Ni nani?, au ni mtu ambaye namfahamu?”
“Sina uhakika kama unamfahamu, kwa majina yake ni Hanson , ni mzungu na inaonekana wanafahamiana sana na bosi”Aliongea Recho na kumfanya Roma sura yake kujikunja .
“Asante , unaweza kuendelea na kazi zako”
Recho alitaka kuongea neno lakini alishindwa kuongea lolote , kwa namna ambavyo Edna alionekana tokea asubuhi , kama mwanamke alijua tu kulikuwa na tatizo kati yake na Roma , hata hivyo alikuwa na taarifa zote kwamba Edna alikuwa amesafairi kwa ajili ya kwenda kufanya sherehe ya harusi na hata yeye mwenyewe alishangazwa na kurudi kwake kwa ghafla.
Roma alivuta pumzi na kisha aligonga mlango.
“Come in”Sauti nyororo ya Edna kutokea ndani ilijibu na Roma alisukuma mlango na kisha akaingia ndani huku mkononi akiwa na mfuko wake wa vyakula.
Edna hakuwa amekaa kwenye kiti chake cha kufanyia kazi , bali alikuwa amekaa kwenye sofa , alionekana kupauka kidogo lakini kauzu zaidi , hisia mbalimbali zilipita kwenye moyo wake mara baada ya kumuona Roma.
Roma macho yake yote yalikuwa kwa mwanaume wa kizungu ambaye alikuwa amekaa upande wa kushoto kwenye sofa.
Alikuwa ni Hanson , yule yule wa miezi kadhaa iliopita baada ya kukutana nae mara ya kwanza kwenye kusanyiko la wahitimu wa chuo cha oxford ,wanadarasa wa Edna.
Hanson baada ya kumuona Roma ndio ameingia alisimama kwa haraka na kisha alimwinamia kwa ishara ya kumsalimia.
“Mr Roma nice to meet you again”Aliongea Hanson lakini Roma hakujibu salamu yake zaidi ya kwenda kuweka ule mfuko juu ya meza.
“Mama kanipigia simu na kuniambia nikuchukulie chakula kwa waswasi hujala chochote mchana”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu hafifu akimpotezea Hanson mzungu.
Edna aliangalia ule mfuko kwa dakika kadhaa na kisha akarudisha macho yake chini.
“Haina haja, nishakula tayari”Aliongea Edna kwa sauti kavu
“Ndio usijali Mr Roma nilimshawishi muda wa mchana tukapate chakula mara baada ya kugundua hajakula chochote tokea asubuhi”Aliongea Hanson
“Kwahio unasema mlipata chakula cha mchana pamoja?”Aliuliza Roma huku akianza kupandwa na hasira pamoja na wivu.
Edna ambaye alikuwa akiangalia sakafu alihisi Roma kuwa katika hasira hivyo aliinua shingo yake na kumwangalia.
“Ndio tumekula pamoja, nimefahamiana nae kwa muda mrefu sikuona kuna tatizo kama nitakula nae chakula cha mchana”Aliongea na kumfanya Roma amwangalie Hanson kwa macho makali na alimfanya mwenzake kuhisi ubaridi wa woga kusambaa mgongoni.
“Kwanza kwanini upo hapa?”Aliuliza swali Roma kwenda kwa Hanson
“Mr Roma tafadhari usifikirie vibaya , nadhani unajua nimechaguliwa kuwa mwakilishi wa kampuni ya magari ya BMW ndani ya Afrika ili kupanua soko hivyo kampuni imeamua kufungua tawi ndani ya Afrika mashariki na nimeichagua Tanzania, nimeona nifanye ushirikiano wa kibiashara na Edna”Aliongea.
“Nenda kwenye idara husika sio hapa, halafu siku nyingine ukikutana na mke wangu sitaki umwite kwa jina lake unaweza kumuita kama Mrs Roma au CEO Edna”Aliongea kibabe na kumfanya mzungu wa watu kupauka uso kwa woga.
“Romaa!” Edna alikunja sura kwa hasira na kisha akasimama.
“Nani kakupa ruhusa ya kumkaripia mgenni wangu na kumpa maagizo utavyo?,Kwanini unaingilia kazi yangu?”Aliongea kwa kufoka.
“Mpaka sasa unatakiwa kuelewa nimejitahidi kuwa mpole la sivyo angekuwa marehemu tayari”Aliongea Roma huku akimwangalia Hanson kwa macho makali mno na kumfanya kutetemeka.
“Ndio kwanza umerudi nchini, tena kabla hata likizo yako haijaisha lakini ameweza kufahamu umerudi na kuja moja kwa moja ofisini kwako na kuanza kuzungumzia maswala ya kazi , nani mwenye akili timamu anaweza kuamini hakuna ajenda nyingine anapanga kwenye kichwa chake?,Unataka uniambie amekuja ofisini na kubahatika kukutana na wewe?”
“Unamaanisha nini wewe?”
“Unaniuliza namaanisha nini tena?”Aliongea Roma huku akicheka kwa kicheko cha hasira huku akimwangalia.
“Kama amekuja hapa akifahamu upo ofisini basi ninaweza kusema sio bahati mbaya bali kuna uwezekano nyie wawili mna mahusiano au mnawasiliana kwa siri, au nadanganya?”Aliuliza Roma.
“Mr Roma nadhani unanifikiria vibaya , niliweza kupata taarifa Edna asharudi hapa nchini na imetokea na mimi sijaondoka hivyo nikaona sio mbaya kuja kuonana nae ili kujadili kuhusu mipango yangu ya kibiashara”.
“Unafikiria ninaweza kukuamini?” Aliongea na kumfanya Hanson kukaa kimya huku akitetemeka.
Upande wa Edna alijikuta machozi yakianza kujitengeza kwenye macho yake , ilionyesha muda wowote angetoa kilio.
“Roma unanishuku...?”
“Nimeona kwa macho yangu na kusikia pia kwa masikio yangu, kwaninni useme nakushuku wakati ushahidi upo?”
“Tulikula chakula pamoja huku tukizungumzia maswala ya biashara , kwanini unakuwa na uwezo mdogo wa kufikiria?”
“Unaniambia nina uwezo mdogo wa kufikiria ?”Aliongea Roma huku akitingicha kichwa chake kwa hasira.
“Unajiona upo sahihi kumwambia ana uwezo mdogo wa kufikiria mbele ya huyu mwanaume , ujasiri huo unautoa wapi?”
“Bora hata yeye hawezi kuingia kwenye ofisi ya watu na kuanza kutoa vitisho bila kuelewa ukweli wote”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma kwa macho makali.
Roma alijikuta kichwa chake kutaka kumpasuka kutokana na hasira alizokuwa nazo kwa Edna kumjibisha ujinga na kumlinganisha na Hanson.
Haikueleweka Hanson kawezaje kupata taarifa ya kurudi kwa Edna nchini , lakini ujio wake ndani ya ofisi ni kutaka kujenga ukaribu wa kibiashara na Edna, hakuwa na mawazo ya kumfanya mwanamke wake wala mchepuko bali alichokuwa akilenga ni kutaka kuwa na ukaribu na Roma pia kupitia kwake ili aweze kufanikisha maswala yake ya uwekezaji na wazo hilo alipewa na Tajiri Azizi kwamba ili arahisishe maswala yake ya uwekezaji nchini basi anapaswa kuwa na urafiki na Roma.
Lakini tatizo kwa mtu yoyote lazima angefikiria kama Roma kwa hali ilivyokuwa , Edna alikuwa amesafiri na likizo yake ilikuwa ikifahamika kiofisi na mara baada ya kukatisha likizo yake tu na kurudi ofisini Roma anamkuta yupo na Hanson , ukizingatia urembo wa Edna lakini pia umaarufu wake kama mwanamke tajiri ni sahihi kwa mwanaume huyo kuona anammendea au wana mawasiliano.
Hanson hakuelewa kama kuna ugomvi kati yao na mbaya zaidi ni kama alijiingiza na kuwa katikati ya ugomvi.
“Mr Roma and CEO Edna , I shall take my leave , Please calm down”Aliongea Hanson lakini kutokana na macho makali ya Roma alishindwa kujua aondoke au abaki.
“Mr Hanson unaweza kuondoka hatokufanya chochote”Aliongea Edna na kumfanya Hanson kujisikia ahueni na kisha aliondoka huku akiwa mwekundu na jasho kumtoka, alikuwa akizisikia habari za Roma ndio maana alikuwa akimhofia na mbaya zaidi alikuwa kwenye nchi ambayo sio yake.
Edna alimwangalia Roma usoni kwa dakika kadhaa na kisha akarudi kwenye meza yake ya kufanyia kazi.
“Ameondoka sasa, umeridhika?”
“Kwahio ulidhania nilishindwa kutomfanyia chochote?” Aliongea Roma huku bado akionekana kuwa na hasira na kumwangalia.
“Unataka kufanya nini tena, si yashaisha?”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu.
“Tokea siku ambayo tumeweza kukutana nilifanya kila kitu ambacho ulitaka nifanye , nilikuacha pia ufanye vile utakavyo na nilijitahidi sana kukufarahisha, nakubali nimefanya mambo mengi ya kukukasirisha na kwa hilo naelewa sana na ndio maana sikutaka kukulazimisha kunifanyia chochote”Alivuta pumzi na kuendelea.
“Sikuweza kuwa makini kwenye usiku wa ndoa na kukukasirisha na hilo nakubali na najua nimefanya makosa kuondoka lakini nikuambie kwamba sijutii kabisa maamuzi yangu , sijutii kwani maamuzi nilioyafanya yalisaidia kuokoa maisha ya watu , Haijalishi una hasira kiasi gani lakini angalau jaribu kuelewa wapi natokea na mimi ni nani , najua wewe ni mgumu sana kujishusha mpaka kufanya maamuzi ya kurudi mapema nje ya makubaliano hilo pia kwangu ni sawa kwani nakufahamu ulivyo , lakini nimekuja hapa kwa ajili ya kuyamaliza..”Aliongea Roma na hasira zilianza kujitengeneza kwenye macho ya Edna.
“Kwahio hicho ndio kimekuleata hapa , kwamba nikushukuru kwa kipindi chote mabacho umenivumilia na kuniaacha nikifanye nikavyo?”
“Hapana, ninachokuelezea ni kwamba kuna baadhi ya mambo napaswa kufanya bila hata ya kukutaarifu, Unajua unanifanya muda mwingine niwe na shauku ya kujua nini kipo ndani ya moyo wako , Kwanini unakosa huruma?’Aliongea Roma huku akijitahidi kujiruliza.
“Unamaanisha nini mimi kukosa huruma?”Aliongea huku akionyesha kutoridhishwa na kauli yake.
“Edna hivi unafikiri ninaweza kuvumilia tabia yako, au niache kila kitu kinachonihusu kwa ajili yako , ninaweza kuvumilia kisirani chako, ninaweza kukuvumilia kwa kunikataa kwenye usiku wetu wa ndoa , ninaweza kukuvumilia kwa kurudi bila hata ya kutaka ruhusa yangu au kutotaka kunisikiliza ….Lakini swezi kukuvumilia kukutana na mwanaume yoyote yule bila mimi kufahamu, hususani mwanaume kama yule au unafikiri nina moyo mkubwa wa kukuruhusu unisaliti , unadhani ninaweza kukunyenyekea na kukuruhusu kukutana na mtu yoyote unavyojisikia kwasababu na mimi nina wanawake nje?”
“Naomba usiendelee kuongea” Aliongea Edna huku akitetemeka na machozi kumtoka.
“Huwezi kuniongelesha hivyo mimi”
“Hahaha,,, kwanini nisiweze , Edna hivi unajiona wewe ni keki au mungu mtu na kukuacha ufanye utakavyo , ngoja nikuambie kwangu wewe ni muhimu na nakiri nakupenda lakini ukithubutu kunikasirisha na kutaka kua juu yangu sishindwi kukutembeza uchi kwenye hio mitaa ya jiji huko nje , usitumie mapenzi yangu kama siraha ya kutaka kunipanda kichwani , huna thamani yoyote bila mimi wewe…”
“Wewe..”
Edna alishindwa kuongea lakini hakuwa tayari kusikia maneno yake tena , alijihisi kukosewa sana , alikuwa na hasira kiasi kwamba alinyanyua mkono wake kutaka kumpiga Roma kibao , lakini Roma hakutaka kumpa nafasi aliushika mkono wake kwa kuudaka.
“Unataka kunipiga, unafikiri kama nitaamua kupigana na wewe unaweza hata kunigusa.?”
“Wewe…wewe mwanaharamu nakuchukia..”Aliongea na kuanza kulia kwa kwikwi lakini machozi yake hayakumyumbisha Roma.
“Sasa hivi nimekuja kugundua kukujali kwangu sana imenifanya kuwa kipofu na unaanza kunichukulia poa..”Aliongea Roma na kisha alimsukumia kwenye meza.
Alibananishwa kwenye meza kiasi kwamba aliweza kuhisi pumzi za Roma kumpuliza usoni..
Walijikuta wakiangaliana usoni kama makondoo huku wakiachana nafasi kwa umbali wa sentimita moja, Edna alianza kupaniki lakini upande wa Roma aliachia tabasamu flani hivi kama vile aliekuwa mbele yake ni adui, lilikuwa tabasamu la kifedhuli.
“Edna siwezi kuwaacha wanawake wote ambao nawapenda , wanastahidili ulinzi wangu haijalishi ni Rose ,Amina au Nasra , kwanini niwaache wakati wapo tayari kufanya chochote kwa ajili yangu au unafikiri kwamba wao ni tofauti na sio warembo na wasingeweza kupata mwanaume bora zaidi yangu? , ngoja nikuambie Neema alikuwa tayari kufa na mimi licha ya kwamba alikuwa na nafasi ya kuachana na mimi na kuyaokoa maisha yake , kwanini unajiona kama wewe ndio pekee ambaye unaweza kuwa mke wangu na wao hawawezi?”
“Kama unawaona bora zaidi acha kupoteza muda wako na mimi na chukua mmoja wapo umuoe”Aliongea Edna kwa kiburi.
“Unaongea nini wewe, nikuache wakati hatujamalizana”Aliongea Roma na kisha alianza kuyalamba masikio ya Edna kwa spidi..
Edna damu zilianza kumchemka huku akishindwa kujua Roma anataka kufanya nini , lakini kwa jinsi Roma alivyomkaribia hakuwa mjinga kufahamu ni nini kinafuatia.
NB: kipande kinachofuatia kina mambo ya ki utu uzima kama wewe ni mtoto ishia hapa tukutane next season.




SEHEMU YA 480.
Roma macho yake yalichanua huku akijihisi msisimko usioelezeka, upande wa Edna alishindwa kufanya chochote.
“Nilijitahidi sana kuvumilia kwa zaidi ya miezi tisa, lakini sasa hivi tushafunga ndoa rasmi nadhani ni muda sahihi wa kukamilisha ndoa yetu”
“Roma …Romaa..”
“Nini .. au wewe sio mke wangu?”
“Roma najua haupo hivyo … subiri tusifanyie hapa ofisni”Edna alibembeleza lakini maneno yake hayakuwa na athari kwa mbogo ambayo ishaamua lake kichwani na alijihisi mwichi kugusana na mapaja yake.
Ijapokuwa lilikuwa ndani ya suruali lakini aliweza kuhisi joto lake na namna ambavyo limetuna alizidi kuona aibu za kike , Roma hakujali , alianza kumbusu kwenye paji la uso akaenda kwenye mashavu , mdomoni na kisha akanyanyua kidevu chake juu na kuanza kulamba shingo.Mtekenyo wa ulimi ulimfanya kuanza kuhema kwa shida
“Roma…”
“Unanukia vizuri sana mke wangu”
Harufu nzuri Roma aliokuwa akiinusa kwenye mwili wa mrembo Edna ilimfanya mashetani yake kucharuka maradufu na hakukuwa na uwezo wa kuyashusha kwa muda huo.
Alimwangalia usoni huku akitabasamu na kisha akapitisha mkono wake kwenye kiuno chake na kumminyia kwake na hakuishia hapo tu mkono mwingine aliupandisha mpaka kwenye nyonyo zake zilizosimama , mkono wa kushoto haukuishia kwenye kiuno tu bali uliendelea kusafiri mpaka kwenye makalio na kuyaminya minya kama embe.
Koti lake la suti alilovaa liliachia lenyewe na kumfanya iwe rahisi kuanza kufungua vifungo vya shati lake na kuchomoa nyonyo na kulipima na kiganja chake cha mkono na aliona linaenelea vyema na kuanza kuminya minya.Yalikuwa malaini kiasi cha kushindwa kufanannisha na kitu chochote.
Edna aliweza kuhisi mwili ukimtetemeka kila muda ambapo alikuwa akisungua chuchu zake, ilionyesha ndio eneo ambalo lilikuwa likiamsha muwasha washa na kumfanya kuanza kushindwa kuvumilia na kugugumia kwa kutoa kilio ambacho kilizidi kumfanya Roma kuchanganyikiwa , Macho ya Roma yalivyolegea ilionyesha kama mtu ambaye alikuwa na kiu na mbele yake ni mto na hakuna namna anaweza kuvuka upande wa pili pasipo kukata kiu yake.
Edna alijikuta akihisi kusisimkwa na mwili sana kila saa anayoguswa na alijikuta akiacha kukamaa mwili na kulegea mwenyewe ili kuruhusu utamu usambae kila kona ya mwili wake.
Alifumba macho kwa utamu huku machozi yakianza kumtirika, sio kwa kuchukia kile anachofanyiwa bali alishindwa kuyazuia kutokana na kiwango kikubwa cha hisia, ni msisimko ambao ndio mara yake ya kwanza kuhisi.
Alijikuta hata akiona aibu baada ya kuhisi mchuzi ukianza kutoka sehemu zake za siri na ilikuwa ni kama eneo limekuwa wazi na upepo kuingia hivyo kuhitaji kitu chochote cha kuongezea ili kuziba upepo usiingie.
Alijiambia huyu mwanaume alianza kumkasirisha na kumfokea lakini bado tu amefanikiwa kumnyegesha na sasa amejilegeza na kuacha afanye kile anachotaka.
Edna alikuwa na wasiwasi kwasababu wapo ndani ya ofisi lakini alishindwa hata kuinua mdomo na kusema Roma usiendelee, ni zaidi ya miezi nane tokea waishi pamoja na huenda alitakiwa kumruhusu kumfanyia hivyo mapema , lakini kwa muda huo ni kipi angeweza kufanya , hata hivyo ni mume wake.
Alijiambia labda maisha yake yote ataishi kwa kukasirishwa na kuchokozwa na huyu mwanaume lakini mwisho wa siku angejilegeza kwake.
Edna akili ilimtoka mara baada ya Roma kushusha suruali yake ya suti chini kwa kuikusanya na nguo ya ndani na kisha kupeleka mkono kwenye mbususu yake, alijikuta akikosa uvumilivu na kutoa mguno wa mahaba lakini Roma hakutaka apige kelele alimshika kidevu chake na kuanza kumpa kiss na aliweza kupokea kwa hiari yake kwa pupa huku miguu yake ikikosa balansi maana alianza kutetema kama Mayele lakini Roma alikuwa imara kumshikili.
Alijikuta akihisi kitu kama mkojo ukimtoka na alishindwa kujizuia na kuruhusu utoke , lakini aliishia kuona aibu na kuanza kulia, huku akishindwa kuelewa kwanini mwili wake unamwaibisha na kuanza kujikojolea.
“Sijategemea mke wangu kuwa hisia kali kiasi hichi , sio kwa maporomoko haya ya maji”Aliongea Roma kwa kutania lakini Edna alishindwa kuongea zaidi ya kuguna na Roma alimbusu shavuni kwa upole.
“Wakati tunafanya kwa mara yetu ya kwanza ulikuwa umelewa , lakini sasa hivi upo na akili yako timamu nataka ujue kwamba itakuwa inauma lakini tamu na ole wako siku nyingine unichokoze mwendo ni huu huu…”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kuelewa anamaanisha nini kwani alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa.
Roma na yeye hakujali sana , alichokifanya ni kumalizia kutoa nguo zake zote zilizobakia mwilini na kumuacha akiwa mtupu kabisa na kisha akapeleka mdomo kwenye manyonyo na kuanza kunyonya na kumfanya Edna kuweka mkono yake mdomoni akijiuzia asitoe sauti kubwa kwa kuhofia huenda Recho yupo nje.
Roma hakujali aliendelea na kazi pasipo ya kujali mtetemo wa Edna na baada ya kuridhika alivua suruali yake na kuishusha chini na mtambo ukafyatujka kwa nje huku ukiwa na hasira.
Roma alimshika kiuno na kisha alimnyanyua na kumpandisha kwenye meza huku akiendelea kumpiga Denda kwa dakika kadhaa na huku chombo yake ikiisuguanisha karibu na mlango wa kuingilia ndani , Edna alizidi kutoa unyevu nyevu mtelezo kwa wingi.
“Hubby …naogopa” Aliongea Edna kwa sauti ndogo ya kubembeleza lakini ya kuvutia.
Roma muda huo alikuwa kama amechangayikiwa na hakuwa na mpango wa kuacha kile alichokipanga .
“Nishakuambia itakuwa inauma lakini muda huo huo itakuwa tamu”Aliongea Roma kwa sauti nzito lakini yenye kubembeleza na Edna kabla hajaitikia alishitukia tu mwichi ukizama ndani na kumsababishia ubaridi wa aina yake uliosafiri kuanzia kichwani kupitia mgongoni na kwenda kutua kwenye mbususu.
“Oh…”
“Ah.!”
Wakati Roma akihisi utamu , upande wa Edna alihisi maumivu na machozi yalianza kumtoka, ijapokuwa alikuwa ashawahi kufanya lakini kutokana na kukaa muda mrefu sehemu yake ni kama imerudi kuwa ya msichana tena.
Roma alifurahia mno mchezo maana alikuwa akibanwa vizuri mno na aliweza kuhisi hisia za aina yake , ni hisia ambazo zilikuwa za tofauti mno na zile alizokuwa akipata wakati akifanya mapenzi na wanawake wake wengine.
Mpaka hapo sasa tunaweza kusema ndoa yao imekamilika maana ndoa hukamilishwa na tendo la ndoa na hicho ndio ambacho kilikuwa kikifanyika , ijapokuwa ilikuwa ni ofisini lakini maana ni ileile tu kwamba hilo nalo ni tendo la ndoa linalofanyikia ofisini.
Zilipita kama dakika kumi na tano wakati Roma akiendelea kupeleka mbele na nyuma kama anacheza amapiano alijihisi naniliu yake uvutwa kwa ndani kwa staili ya kukabwa , alishindwa kuamini anachofanyiwa na Edna na aliishia kumwangalia usoni na kutabasamu.
“Edna mke wangu , sikujua kama una mbinu zako za siri, umefanya kwa kudhamiria nini , unaonekana kama mzoefu umewezaje kuifinyia kwa ndani”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kujibu chochote zaidi ya uangalia pembeni kwa kuona aibu kumwangalia usoni hata hivyo alishindwa kumuelewa anamaanisha nini kusema kufinyia kwa ndani.
Roma alijiua Edna hakuwa akifanya makusudi kuifinyia kwa ndani ila ni namna ya asili ya mwili wake ulivyo, hata hivyo licha ya kwamba Edna hakuwa na udhoefu lakini alitokea kumpagawisha na kumfanya ajihisi kama yupo juu kileleni mawinguni.
Alikuwa amekutana na wanawake wengi na kuwa mdhoefu lakini hisia alizokuwa akipata zilikuwa za aina yake, Edna na yeye ni kama alikuwa akianza kuishiwa na pumzi maana ni zaidi ya magori ambayo amefunga.
“Arrgh…Romaa …taratibu ..inauma ..oooh!”Alijikuta akilalamika lakini Roma alikuwa kama kiziwi na kuendelea kuongeza spidi na ilifikia muda akaona staili ya kimeza meza haimtoshi hivyo alimgeuza na kumshikisha mikono kwenye meza huku akiwa ameinama na kufanya msambwanda wote kurudi nyuma na Roma aliingiza tena na kuendelea kusukuma songombile yake.
Alihisi maumivu kidogo lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea alizidi kupata raha na sehemu zake ni kama sasa zishaanza kuzoea ukubwa wa mwichi wa mume wake na shoti za utamu alizokuwa akisikia zilimfanya kujihisi yupo mbingu ya saba.
Edna baada ya kuona dudu ya Roma ilikuwa ikiyasugua makalio yakekwakupita na kumwingia kwenye kitumbua chake alihisi aibu , lakini hata hivyo alishindwa kuacha kumuangalia Roma usoni.
Alijihisi utamu kwa jinsi Roma alivyokuwa akimwangalia kwa upole na kuridhika , hata hivyo ilikuwa ni kama mara yao ya kwanza kufanya mapenzi.
Edna alishindwa kuongea chochote na kuona aibu karibia muda wote tendo linafanyika na aliishia kutii maagizo kila staili ambayo alikuwa akiambiwa akae.
Mchezo uliendelea kwa zaidi ya lisaa limoja na walianzia kwenye meza na kisha wakahamia kwenye sofa, lakini Roma akaona haitoshi na kwenda kumshikisha mikono kwenye vioo vya madirisha na kumfanya Edna aliangalie jiji huku akiendelea kuhisi utamu usio na kipimo ambao ulianzia kwenye vidole vya miguu na kusambaa mwili mzima na kumwingia ubongoni.
Huenda kama kuna mtu angekuwa na darubini jengo la pili yake angeona kile ambacho kilikuwa kikifanyika , lakini Roma hakufanya mambo bila ya kuwa makini aliweza kutumia uwezo wake kuchunguza maeneo ya mbali ili isije ikatokea mtu anawaangalia.
Roma aliendelea na shughuli yake kwa muda mrefu na kufanya sauti kama za watu wanaopiga makofi kusikika ndani ya ofisi nzima.
Paah! ..Paah!!
Ilifikia kipindi Edna hakutaka kuendelea na kutaka kupumzika kwani alipiga magori mengi na kujikojolea kiasi kwamba alikosa idadi na sasa mwili wake ulikuwa umechoka mno.
“Huby inatosha .. tupumzike .. niche nipumzike kidog…”Aliongea Edna huku akihema kama mbwa ambaye amekimbia maili nyingi.
“Ni saa limoja tu lakini unaonyesha kuchoka , tufanye angalau yawe mawili , babe sikujua kumbe unatembea na Dhana ya kimaajabu kwenye mwili wako”Aliongea Roma lakini Edna alikuwa akielekea kwenye kuzimia kwani hakusikia tena utamu lakini ilionyesha kuzidi kumfurahisha Roma , huenda ni kwasababu alishaanza kuvimba sehemu zake kwa ndani hivyo eneo kuzidi kuwa dogo.
“Tafadhari Hubby … siwezi kuendelea ..naomba unionee huruma..”Aliongea na kuanza kulia kama mtoto na kumfanya Roma amwangalie namna ambavyo amelegea , hakuamini ndio yule mke wake aliekuwa akijifanyisha kauzu , muda huo alikuwa kama mtoto mchanga.
“Huwataki wanawake wangu wengine… lakini huwezi kudumu kwa zaidi hata ya lisaa kwa staili hii unakwenda kushindana nao vipi”?”
“Wewe…! kwanini uzungumzie wanawake wengine kwenye muda kama huu?” Aliongea na kumfanya Roma amlambe kibao cha kalio la kulia.
“Sihitaji ruhusa yako ninapotaka kuwazungumzia , nilichoongea ni kweli, sijatoa bao hata moja lakini bado unaonekana umechoka ,utawezaje kunizalia mtoto kwa namna hii?”Aliongea Roma na kumfanya Edna ashindwe kujibu , hakujua kama kosa lilikuwa lake kuchoka haraka au ni la mtu mwingine.
Roma ilibidi amuonee huruma na alimbeba na kumkalisha kwenye sofa ili apumzike.
“Hata hivyo mke wangu umefanya kazi nzuri angalau umenifanya nijisikie vizuri kuliko mwanamke yoyote yule”Aliongea Roma huku akimfinya mashavu lakini Edna alishia kutojibu kwani alikuwa akihema kwa tabu , alishukuru tu ameachiwa maana hakujua nini kingeendelea kama Roma angeng’ang’nia mpaka atakapotoa bao.
“Nisikilize kwa umakini siku nyingine usije ukanichokoza na kunikasirisha , wewe ni mwanamke wangu na siwezi kukuruhusu kukutana na wanaume waliokaa kihuni huni , ninaweza kuonekana sina sababu za msingi lakini unapaswa kunisikiliza mimi tu kwasababu wewe ni wa kwangu milele , unaweza usikubali lakini hakuna mtu yoyote anaweza akaja kukusaidia kama nitaamua kukuadhibu , hata hivyo kama utataka tena lazima uniombe…., Hahaa..Kaone sasa kanavyotia huruma, haina haja ya kuniangalia kwa macho lawama umeyataka mwenyewe…”Aliongea na kumfanya Edna atamani kulia.
“Mwanaume mdhalimu wewe”
“Hehe ..niiite vyovyote unavyotaka , nilifikira mambo mengi usiku wote wa jana na nimegundua hata kama nijizuie kutokufanyia chochote bado wewe ni mke wangu , hata nikiamua kukufosi pia wewe ni mke wangu ya nini kujiumiza wakati upo”Aliongea Roma na kisha alimshika kidevu na kupitisha kidole chake kwenye lipsi zake kwa kusugua sugua.
Edna alionekana kuwa na adabu sasa, hakuleta ubishi na alikuwa kama piritoni,ule ubosi kwisha habari yake.
“Pumzika bibi harusi wangu , tutaendelea tena angalau kwa lisaa lingine, unifanye agalau nimwage bao moja”Aliongea Roma.
“Lakini sitosikia chochote tukifanya tena, nahisi kumevimba..”Aliongea huku akionekana kutia huruma lakini Roma hakuwa kwenye nafasi ya kumuonea huruma maana bado hata dudu yake haijalala.
“Nitakuponyesha, kaa vizuri niingize na nitakuonyesha kwanini naitwa mfalme Pluto” Aliongea Roma na kabla Edna hajajibu alishangaa ashawekwa sawa na yote ikazama.
“Ah..!”Alijikuta akihisi damu kumcheka huku Roma akiwa amemuweka kifo pendwa cha yule mdudu msumbufu usiku anaeogpwa na wadada , wakati akidhania angehisi maumivu Roma alikusanya nguvu ya kimaandiko na kuipeleka kwenye dudu yake na Edna alihisi mtekenyo wa aina yake na aliishia kutoa mdomo kama kabanwa na mlango.
Lisaa lingine mbele alijihisi uji uji mzito ukimwagika ndani ya sehemu zake za uzazi , ulikuwa wa moto kiasi kwamba alihisi raha ya ajabu na alijikuta akikakamaaa mwili na yeye kufunga goli ambalo haikueleweka lilikuwa la ngapi na aliishia kuhema huku akimwangalia Roma usoni na alijikuta akiachia tabasamu huku akiwa amelembua na kuangalia pembeni kwa aibu.
Naam hivyo ndivyo ilivyokuwa……..
MWISHO WA SEASON 16.
WWTSAPP 0687151346 NICHEKI KUOATA MWENDELEZO , SIMULIZI NDIO INAANZA
 
SEHEMU YA 479.
Uhai na kifo ni kitu kimoja kama ilivyo mto na bahari kuwa kitu kimoja , Yan Buwen licha ya kuwa na nguvu kwa kiasi kikubwa lakini hakuwahi kuwaza kifo chake ni baada ya kuhamisha kumbukumbu zake kwenye mwili mpya.
Upande mwingine nae Roma akijua kwamba amemuua Yan Buwen hakujua kwamba mwenzake alikuwa hai na aliweza kuuliwa na watu dhaifu kama Kizwe na Lekcha.
Lekcha alitemea mate maiti ya Yan buwena kana kwamba anautangazia ulimwengu mwanasayansi nguli kutoka taifa la China ameweza kufa kikatili.
“Una uhakika unaweza kutumia teknolojia zake?”Aliuliza Denisi.
“Ushasahau alichoongea , amesema kuna kitu ametumia ku syncronize memori zake kwenye mwili wake mpya”
“Lekcha unamaanisha Biochip?”Aliuliza Kizwe.
“Upo sahihi , tunachotakiwa kufanya ni kupasua ubongo wake na kuitoa na tunaweza kupata kila taarifa na baada ya hapo tutakuwa na uwezo wa kupata nguvu , nina uhakika kama hatutamshambulia Roma ana kwa ana kama huyu mjinga tunaweza kumshinda huku sisi tukiwa nyuma ya pazia”Aliongea Lekcha akimaanisha kwamba kwasababu Yan Buwen ameshindwa kumdhibiti Roma basi uwezekano wao wa kumshinda kwa kupigana nae ana kwa ana unaweza usifanikiwe , hivyo njia pekee ya kumzidi ni kumshambulia kwa njia isiokuwa ya moja kwa moja.
“Kama ni hivyo basi nipo tayari , nitahakikisha mahitaji yote unapata ya kiuendeshaji”Aiongea Denisi.
“Licha ya kwamba baba yako ni raisi lakini kupata kiasi kikubwa cha pesa kusapoti uendeshaji wa hili eneo sidhani kama utakuwa nao”Aliongea Kizwe.
“Hilo lisikupe shida , mimi ni mtoto pendwa kutoka kwa baba yangu hawezi kushindwa kunifanyia uchochoro wa kukwapua bilioni kadhaa za watanzania”Aliongea na Kizwe na Lekcha waliangaliana na kutabasamu.
*******
Upande wa Tanzania ilikuwa ni kizaa zaa mara baada ya raisi Kigombola kujipiga mwenyewe risasi ya kichwa , Roma kama angeamua kumuokoa angefanikisha lakini hakutaka kufanya hivyo.
Watu wote walishangazwa na maamuzi yake , lakini hakuna ambaye alimlaumu kwa maamuzi alioyachukua kutokana na makosa ambayo amefanya na kama sheria ingechukua mkondo wake huenda angehukumiwa jera miaka isiopungua therathini kisheria hivyo ingekuwa moja kwa moja maisha yake yote angeyamalizia gerezani na huenda ndio sababu alioona inafaa kujimaliza mwenyewe .
Neema licha ya kwamba alimchukia alijikuta akilia mno na sio yeye Donyi pia alimlilia baba yake , kila mmoja alieweza kushuhudia kile kilichotokea aliweza kulia na kushikwa na huzuni.
Licha ya kigombola kujiua , lakini huku nyuma alikuwa ameacha kiasi kikubwa cha utajiri na kutokana na mali zake alivyokuwa akizimiliki basi hata kama serikali itachukua hatua ya kuzifuatilia ingekuwa ngumu kuzitaifisha , kwani nyingi zilikuwa kwa majina bandia.
Athari kubwa ambayo inatarajiwa kutokea kwasababu ya kifo chake ni ile nguvu aliokuwa nayo serikalini kupotea , watoto wake ndio walikuwa wanasiasa lakini walikuwa na nguvu kutokana na kwamba baba yao ndio aliekuwa akiendesha usukani, sasa dereva amekufa gari halina budu kuyumba na hatimae kupoteza mwelekeo.
Kifo cha Kigombola watu ambao wanakwenda kunufaika kwa kiasi kikubwa ni familia ya Afande Kweka, mathalani kwa raisi mwenyewe Senga, kwani tokea ayachukue madaraka kuna maamuzi ambayo alikuwa akishindwa kuyachukua kutokana na namna ambavyo Kigombola alikuwa akiingilia uongozi wake , hivyo kifo chake ni kama angeenda sasa kuwa raisi kamili na mwenye ushawishi kwenye maeneo karibia yote ndani ya taifa.
Huenda baada ya habari kuzisikia kutoka Marekani alipokuwepo kikazi atakuwa anashangilia kwa shangwe.licha ya kwamba yeye sio aliefanikisha kifo chake bali msababishaji mkuu ni mtoto wake Roma ambaye siku zote hakutaka kumtambua.
Baada ya taratibu zote hapo ndani kumalizika za kuondoa mwili wa marehemu kwa ajili ya kupeleka hospitalini kuhifadhia , Roma alikadiria muda ambao Edna angefika Tanzania na kwa haraka haraka aliamini kama ni kufika Dar es salaam ingekuwa ni usiku sana , hivyo hakuwa na haja ya kurudi nyumbani kwani angeenda kuwa mwenyewe.
Alichokifanya ni kuondoka na Neema Luwazo pamoja na Donyi ambao wote walikuwa kwenye majonzi ya kifo cha Kigombola , aliona akae nao karibu kwa ajili ya kuwafariji.
Neema mara baada ya kurudi kwenye jumba lake wageni waliokuwa wakimpa salamu za pole walikuwa wengi mno , maana habari za kifo cha mheshimiwa zilikuwa zishawafikia watu wengi.
Roma aliwasiliana na Ron kuulizia kama Edna amekwisha kuondoka Visiwa vya wafu na Rona alimwambia Edna anatarajia kuondoka asubuhi ya saa tano mchana kwani na Blandina na Bi Wema wote hawakuona haja ya kuendelea kubakia kwenye hivyo visiwa ilihali hakuna ambae walikuwa wakiwafahamu.
Roma baada ya kusikia hivyo aliamini mpaka muda ambao watakuja kutua nchini Tanzania ni siku inayofuata sasa, muda wa asubuhi siku hivyo alimpigia simu Diego na kumtaarufu amerudi na Edna angerudi siku inayoafuata hivyo wanapaswa kuwa makini na usalama wake atakapofika.
*******
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa , Roma aliamkia ndani ya nyumba ya Neema Luwazo kama vile yeye ndio mwenye nyumba, baada ya kupata kifungua kinywa aliamua kuwasindikiza mpaka msibani ambako alikaa kwa masaa kama matano hivi.
Baadhi ya watu walikuwa wakimwangalia kwa chuki lakini hakujali , kwanza sio yeye ambaye alimuua Kigombola bali alijiua mwenyewe, hakuhisi hatia ya kile kilichotokea.
Wakati Roma anatoka msibani kurejea mjini ilikuwa ni saa nane kwenda saa tisa , wakati alipokuwa kwenye gari alikuwa akijaribu kufanya mawasiliano kwa kumpigia Edna simu lakini ajabu ni kwamba simu yake haikuwa ikipatikana, alishangaa kwani kwa muda huo atakuwa tayari ashafika Tanzania kama kweli walitoka saa tano , sasa alijiuliza imekuwaje simu yake isiwe hewani, alijua Edna anaweza kuwa na hasira na yeye lakini hawezi kuzima simu ili asipatikane hewani kwa makusudi , alichokifanya ni kumpigia simu mama yake mzazi.
Na ndipo alipoambiwa Edna aliondoka nyumbani mara baada ya kurudi tu na kuaga anaelekea kazini.
“Roma nenda huko huko ofisini kwake ,mkayamalize maana alikuwa amenuna njia nzima mpaka tunafika Tanzania , msipo yamaliza mapema hali inaweza kuwa mbaya zaidi mbeleni , umekosea mwenyewe kumuacha mwenzio wakati ulikuwa usiku wake wa kwanza baada ya ndoa,Mnunulie na chakula umpelekee”Aliongea Blandina kwenye simu na Roma alimwambia anaelekea huko na asiwe na wasiwasi atayamaliza.
Ilionekana Blandina mara baada ya kutoka Visiwa vya wafu alikwenda kuishi tena nyumbani kwa mwanae .
Roma baada ya kufika Posta aliingia kwenye mgahawa wa vyakula vya haraka (Fastfood) na kununua chakula ambacho aliamini Edna atakipenda , aliotea kwamba muda huo Edna atakuwa hajala chochote kutokana na kuwa na hasira pamoja na mawazo ndio maana alichukua maamuzi ya kufanya hivyo
Dakika kumi na tano mbele aliweza kufika ndani ya jengo la kampuni ya Vexto na alishuka na kisha aliingia kwenye lift na kupandisha moja kwa moja mpaka kwenye floor ambayo ofisi ya Edna inapatikana.
Roma baada ya kufika kwenye meza ya sekretari aliweza kumuona Recho akutokea ndani ya ofisi ya Edna.
Alikuwa amevaa suti ya rangi nyeusi na viatu vya visigino virefu huku mkononi akiwa ameshikilia mafaili , Roma alijiambia Recho anazidi kupendeza siku hadi siku na hivi karibuni alionekana kuonesha mabadiliko makubwa zaidi , kwanza alionekana kuwa na furaha.
“Roma umerudi? Umechelewa kuja maana naona bosi hayupo kwenye mudi nzuri”Aliongea Recho kwa heshima huku akitabasamu.
“Ndio maana nimekuja kumuona , huenda naweza kumfanya kuwa na furaha”Aliongea Roma na kumfanya Recho kutabasamu.
“Yupo kwenye ofisi yake lakini ana mgeni”.
“Mgeni?”Roma alishangaa kwani kwa alivyokua akielewa taarifa za Edna kuwa likizo zilikuwa ni rasmi , hivyo ilikuwa ngumu kwa mgeni kuja ofisini kwake kwa siku kama hio ambayo ndio kwanza tu amerudi kutokea Mediterranian.
“Ni nani?, au ni mtu ambaye namfahamu?”
“Sina uhakika kama unamfahamu, kwa majina yake ni Hanson , ni mzungu na inaonekana wanafahamiana sana na bosi”Aliongea Recho na kumfanya Roma sura yake kujikunja .
“Asante , unaweza kuendelea na kazi zako”
Recho alitaka kuongea neno lakini alishindwa kuongea lolote , kwa namna ambavyo Edna alionekana tokea asubuhi , kama mwanamke alijua tu kulikuwa na tatizo kati yake na Roma , hata hivyo alikuwa na taarifa zote kwamba Edna alikuwa amesafairi kwa ajili ya kwenda kufanya sherehe ya harusi na hata yeye mwenyewe alishangazwa na kurudi kwake kwa ghafla.
Roma alivuta pumzi na kisha aligonga mlango.
“Come in”Sauti nyororo ya Edna kutokea ndani ilijibu na Roma alisukuma mlango na kisha akaingia ndani huku mkononi akiwa na mfuko wake wa vyakula.
Edna hakuwa amekaa kwenye kiti chake cha kufanyia kazi , bali alikuwa amekaa kwenye sofa , alionekana kupauka kidogo lakini kauzu zaidi , hisia mbalimbali zilipita kwenye moyo wake mara baada ya kumuona Roma.
Roma macho yake yote yalikuwa kwa mwanaume wa kizungu ambaye alikuwa amekaa upande wa kushoto kwenye sofa.
Alikuwa ni Hanson , yule yule wa miezi kadhaa iliopita baada ya kukutana nae mara ya kwanza kwenye kusanyiko la wahitimu wa chuo cha oxford ,wanadarasa wa Edna.
Hanson baada ya kumuona Roma ndio ameingia alisimama kwa haraka na kisha alimwinamia kwa ishara ya kumsalimia.
“Mr Roma nice to meet you again”Aliongea Hanson lakini Roma hakujibu salamu yake zaidi ya kwenda kuweka ule mfuko juu ya meza.
“Mama kanipigia simu na kuniambia nikuchukulie chakula kwa waswasi hujala chochote mchana”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu hafifu akimpotezea Hanson mzungu.
Edna aliangalia ule mfuko kwa dakika kadhaa na kisha akarudisha macho yake chini.
“Haina haja, nishakula tayari”Aliongea Edna kwa sauti kavu
“Ndio usijali Mr Roma nilimshawishi muda wa mchana tukapate chakula mara baada ya kugundua hajakula chochote tokea asubuhi”Aliongea Hanson
“Kwahio unasema mlipata chakula cha mchana pamoja?”Aliuliza Roma huku akianza kupandwa na hasira pamoja na wivu.
Edna ambaye alikuwa akiangalia sakafu alihisi Roma kuwa katika hasira hivyo aliinua shingo yake na kumwangalia.
“Ndio tumekula pamoja, nimefahamiana nae kwa muda mrefu sikuona kuna tatizo kama nitakula nae chakula cha mchana”Aliongea na kumfanya Roma amwangalie Hanson kwa macho makali na alimfanya mwenzake kuhisi ubaridi wa woga kusambaa mgongoni.
“Kwanza kwanini upo hapa?”Aliuliza swali Roma kwenda kwa Hanson
“Mr Roma tafadhari usifikirie vibaya , nadhani unajua nimechaguliwa kuwa mwakilishi wa kampuni ya magari ya BMW ndani ya Afrika ili kupanua soko hivyo kampuni imeamua kufungua tawi ndani ya Afrika mashariki na nimeichagua Tanzania, nimeona nifanye ushirikiano wa kibiashara na Edna”Aliongea.
“Nenda kwenye idara husika sio hapa, halafu siku nyingine ukikutana na mke wangu sitaki umwite kwa jina lake unaweza kumuita kama Mrs Roma au CEO Edna”Aliongea kibabe na kumfanya mzungu wa watu kupauka uso kwa woga.
“Romaa!” Edna alikunja sura kwa hasira na kisha akasimama.
“Nani kakupa ruhusa ya kumkaripia mgenni wangu na kumpa maagizo utavyo?,Kwanini unaingilia kazi yangu?”Aliongea kwa kufoka.
“Mpaka sasa unatakiwa kuelewa nimejitahidi kuwa mpole la sivyo angekuwa marehemu tayari”Aliongea Roma huku akimwangalia Hanson kwa macho makali mno na kumfanya kutetemeka.
“Ndio kwanza umerudi nchini, tena kabla hata likizo yako haijaisha lakini ameweza kufahamu umerudi na kuja moja kwa moja ofisini kwako na kuanza kuzungumzia maswala ya kazi , nani mwenye akili timamu anaweza kuamini hakuna ajenda nyingine anapanga kwenye kichwa chake?,Unataka uniambie amekuja ofisini na kubahatika kukutana na wewe?”
“Unamaanisha nini wewe?”
“Unaniuliza namaanisha nini tena?”Aliongea Roma huku akicheka kwa kicheko cha hasira huku akimwangalia.
“Kama amekuja hapa akifahamu upo ofisini basi ninaweza kusema sio bahati mbaya bali kuna uwezekano nyie wawili mna mahusiano au mnawasiliana kwa siri, au nadanganya?”Aliuliza Roma.
“Mr Roma nadhani unanifikiria vibaya , niliweza kupata taarifa Edna asharudi hapa nchini na imetokea na mimi sijaondoka hivyo nikaona sio mbaya kuja kuonana nae ili kujadili kuhusu mipango yangu ya kibiashara”.
“Unafikiria ninaweza kukuamini?” Aliongea na kumfanya Hanson kukaa kimya huku akitetemeka.
Upande wa Edna alijikuta machozi yakianza kujitengeza kwenye macho yake , ilionyesha muda wowote angetoa kilio.
“Roma unanishuku...?”
“Nimeona kwa macho yangu na kusikia pia kwa masikio yangu, kwaninni useme nakushuku wakati ushahidi upo?”
“Tulikula chakula pamoja huku tukizungumzia maswala ya biashara , kwanini unakuwa na uwezo mdogo wa kufikiria?”
“Unaniambia nina uwezo mdogo wa kufikiria ?”Aliongea Roma huku akitingicha kichwa chake kwa hasira.
“Unajiona upo sahihi kumwambia ana uwezo mdogo wa kufikiria mbele ya huyu mwanaume , ujasiri huo unautoa wapi?”
“Bora hata yeye hawezi kuingia kwenye ofisi ya watu na kuanza kutoa vitisho bila kuelewa ukweli wote”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma kwa macho makali.
Roma alijikuta kichwa chake kutaka kumpasuka kutokana na hasira alizokuwa nazo kwa Edna kumjibisha ujinga na kumlinganisha na Hanson.
Haikueleweka Hanson kawezaje kupata taarifa ya kurudi kwa Edna nchini , lakini ujio wake ndani ya ofisi ni kutaka kujenga ukaribu wa kibiashara na Edna, hakuwa na mawazo ya kumfanya mwanamke wake wala mchepuko bali alichokuwa akilenga ni kutaka kuwa na ukaribu na Roma pia kupitia kwake ili aweze kufanikisha maswala yake ya uwekezaji na wazo hilo alipewa na Tajiri Azizi kwamba ili arahisishe maswala yake ya uwekezaji nchini basi anapaswa kuwa na urafiki na Roma.
Lakini tatizo kwa mtu yoyote lazima angefikiria kama Roma kwa hali ilivyokuwa , Edna alikuwa amesafiri na likizo yake ilikuwa ikifahamika kiofisi na mara baada ya kukatisha likizo yake tu na kurudi ofisini Roma anamkuta yupo na Hanson , ukizingatia urembo wa Edna lakini pia umaarufu wake kama mwanamke tajiri ni sahihi kwa mwanaume huyo kuona anammendea au wana mawasiliano.
Hanson hakuelewa kama kuna ugomvi kati yao na mbaya zaidi ni kama alijiingiza na kuwa katikati ya ugomvi.
“Mr Roma and CEO Edna , I shall take my leave , Please calm down”Aliongea Hanson lakini kutokana na macho makali ya Roma alishindwa kujua aondoke au abaki.
“Mr Hanson unaweza kuondoka hatokufanya chochote”Aliongea Edna na kumfanya Hanson kujisikia ahueni na kisha aliondoka huku akiwa mwekundu na jasho kumtoka, alikuwa akizisikia habari za Roma ndio maana alikuwa akimhofia na mbaya zaidi alikuwa kwenye nchi ambayo sio yake.
Edna alimwangalia Roma usoni kwa dakika kadhaa na kisha akarudi kwenye meza yake ya kufanyia kazi.
“Ameondoka sasa, umeridhika?”
“Kwahio ulidhania nilishindwa kutomfanyia chochote?” Aliongea Roma huku bado akionekana kuwa na hasira na kumwangalia.
“Unataka kufanya nini tena, si yashaisha?”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu.
“Tokea siku ambayo tumeweza kukutana nilifanya kila kitu ambacho ulitaka nifanye , nilikuacha pia ufanye vile utakavyo na nilijitahidi sana kukufarahisha, nakubali nimefanya mambo mengi ya kukukasirisha na kwa hilo naelewa sana na ndio maana sikutaka kukulazimisha kunifanyia chochote”Alivuta pumzi na kuendelea.
“Sikuweza kuwa makini kwenye usiku wa ndoa na kukukasirisha na hilo nakubali na najua nimefanya makosa kuondoka lakini nikuambie kwamba sijutii kabisa maamuzi yangu , sijutii kwani maamuzi nilioyafanya yalisaidia kuokoa maisha ya watu , Haijalishi una hasira kiasi gani lakini angalau jaribu kuelewa wapi natokea na mimi ni nani , najua wewe ni mgumu sana kujishusha mpaka kufanya maamuzi ya kurudi mapema nje ya makubaliano hilo pia kwangu ni sawa kwani nakufahamu ulivyo , lakini nimekuja hapa kwa ajili ya kuyamaliza..”Aliongea Roma na hasira zilianza kujitengeneza kwenye macho ya Edna.
“Kwahio hicho ndio kimekuleata hapa , kwamba nikushukuru kwa kipindi chote mabacho umenivumilia na kuniaacha nikifanye nikavyo?”
“Hapana, ninachokuelezea ni kwamba kuna baadhi ya mambo napaswa kufanya bila hata ya kukutaarifu, Unajua unanifanya muda mwingine niwe na shauku ya kujua nini kipo ndani ya moyo wako , Kwanini unakosa huruma?’Aliongea Roma huku akijitahidi kujiruliza.
“Unamaanisha nini mimi kukosa huruma?”Aliongea huku akionyesha kutoridhishwa na kauli yake.
“Edna hivi unafikiri ninaweza kuvumilia tabia yako, au niache kila kitu kinachonihusu kwa ajili yako , ninaweza kuvumilia kisirani chako, ninaweza kukuvumilia kwa kunikataa kwenye usiku wetu wa ndoa , ninaweza kukuvumilia kwa kurudi bila hata ya kutaka ruhusa yangu au kutotaka kunisikiliza ….Lakini swezi kukuvumilia kukutana na mwanaume yoyote yule bila mimi kufahamu, hususani mwanaume kama yule au unafikiri nina moyo mkubwa wa kukuruhusu unisaliti , unadhani ninaweza kukunyenyekea na kukuruhusu kukutana na mtu yoyote unavyojisikia kwasababu na mimi nina wanawake nje?”
“Naomba usiendelee kuongea” Aliongea Edna huku akitetemeka na machozi kumtoka.
“Huwezi kuniongelesha hivyo mimi”
“Hahaha,,, kwanini nisiweze , Edna hivi unajiona wewe ni keki au mungu mtu na kukuacha ufanye utakavyo , ngoja nikuambie kwangu wewe ni muhimu na nakiri nakupenda lakini ukithubutu kunikasirisha na kutaka kua juu yangu sishindwi kukutembeza uchi kwenye hio mitaa ya jiji huko nje , usitumie mapenzi yangu kama siraha ya kutaka kunipanda kichwani , huna thamani yoyote bila mimi wewe…”
“Wewe..”
Edna alishindwa kuongea lakini hakuwa tayari kusikia maneno yake tena , alijihisi kukosewa sana , alikuwa na hasira kiasi kwamba alinyanyua mkono wake kutaka kumpiga Roma kibao , lakini Roma hakutaka kumpa nafasi aliushika mkono wake kwa kuudaka.
“Unataka kunipiga, unafikiri kama nitaamua kupigana na wewe unaweza hata kunigusa.?”
“Wewe…wewe mwanaharamu nakuchukia..”Aliongea na kuanza kulia kwa kwikwi lakini machozi yake hayakumyumbisha Roma.
“Sasa hivi nimekuja kugundua kukujali kwangu sana imenifanya kuwa kipofu na unaanza kunichukulia poa..”Aliongea Roma na kisha alimsukumia kwenye meza.
Alibananishwa kwenye meza kiasi kwamba aliweza kuhisi pumzi za Roma kumpuliza usoni..
Walijikuta wakiangaliana usoni kama makondoo huku wakiachana nafasi kwa umbali wa sentimita moja, Edna alianza kupaniki lakini upande wa Roma aliachia tabasamu flani hivi kama vile aliekuwa mbele yake ni adui, lilikuwa tabasamu la kifedhuli.
“Edna siwezi kuwaacha wanawake wote ambao nawapenda , wanastahidili ulinzi wangu haijalishi ni Rose ,Amina au Nasra , kwanini niwaache wakati wapo tayari kufanya chochote kwa ajili yangu au unafikiri kwamba wao ni tofauti na sio warembo na wasingeweza kupata mwanaume bora zaidi yangu? , ngoja nikuambie Neema alikuwa tayari kufa na mimi licha ya kwamba alikuwa na nafasi ya kuachana na mimi na kuyaokoa maisha yake , kwanini unajiona kama wewe ndio pekee ambaye unaweza kuwa mke wangu na wao hawawezi?”
“Kama unawaona bora zaidi acha kupoteza muda wako na mimi na chukua mmoja wapo umuoe”Aliongea Edna kwa kiburi.
“Unaongea nini wewe, nikuache wakati hatujamalizana”Aliongea Roma na kisha alianza kuyalamba masikio ya Edna kwa spidi..
Edna damu zilianza kumchemka huku akishindwa kujua Roma anataka kufanya nini , lakini kwa jinsi Roma alivyomkaribia hakuwa mjinga kufahamu ni nini kinafuatia.
NB: kipande kinachofuatia kina mambo ya ki utu uzima kama wewe ni mtoto ishia hapa tukutane next season.




SEHEMU YA 480.
Roma macho yake yalichanua huku akijihisi msisimko usioelezeka, upande wa Edna alishindwa kufanya chochote.
“Nilijitahidi sana kuvumilia kwa zaidi ya miezi tisa, lakini sasa hivi tushafunga ndoa rasmi nadhani ni muda sahihi wa kukamilisha ndoa yetu”
“Roma …Romaa..”
“Nini .. au wewe sio mke wangu?”
“Roma najua haupo hivyo … subiri tusifanyie hapa ofisni”Edna alibembeleza lakini maneno yake hayakuwa na athari kwa mbogo ambayo ishaamua lake kichwani na alijihisi mwichi kugusana na mapaja yake.
Ijapokuwa lilikuwa ndani ya suruali lakini aliweza kuhisi joto lake na namna ambavyo limetuna alizidi kuona aibu za kike , Roma hakujali , alianza kumbusu kwenye paji la uso akaenda kwenye mashavu , mdomoni na kisha akanyanyua kidevu chake juu na kuanza kulamba shingo.Mtekenyo wa ulimi ulimfanya kuanza kuhema kwa shida
“Roma…”
“Unanukia vizuri sana mke wangu”
Harufu nzuri Roma aliokuwa akiinusa kwenye mwili wa mrembo Edna ilimfanya mashetani yake kucharuka maradufu na hakukuwa na uwezo wa kuyashusha kwa muda huo.
Alimwangalia usoni huku akitabasamu na kisha akapitisha mkono wake kwenye kiuno chake na kumminyia kwake na hakuishia hapo tu mkono mwingine aliupandisha mpaka kwenye nyonyo zake zilizosimama , mkono wa kushoto haukuishia kwenye kiuno tu bali uliendelea kusafiri mpaka kwenye makalio na kuyaminya minya kama embe.
Koti lake la suti alilovaa liliachia lenyewe na kumfanya iwe rahisi kuanza kufungua vifungo vya shati lake na kuchomoa nyonyo na kulipima na kiganja chake cha mkono na aliona linaenelea vyema na kuanza kuminya minya.Yalikuwa malaini kiasi cha kushindwa kufanannisha na kitu chochote.
Edna aliweza kuhisi mwili ukimtetemeka kila muda ambapo alikuwa akisungua chuchu zake, ilionyesha ndio eneo ambalo lilikuwa likiamsha muwasha washa na kumfanya kuanza kushindwa kuvumilia na kugugumia kwa kutoa kilio ambacho kilizidi kumfanya Roma kuchanganyikiwa , Macho ya Roma yalivyolegea ilionyesha kama mtu ambaye alikuwa na kiu na mbele yake ni mto na hakuna namna anaweza kuvuka upande wa pili pasipo kukata kiu yake.
Edna alijikuta akihisi kusisimkwa na mwili sana kila saa anayoguswa na alijikuta akiacha kukamaa mwili na kulegea mwenyewe ili kuruhusu utamu usambae kila kona ya mwili wake.
Alifumba macho kwa utamu huku machozi yakianza kumtirika, sio kwa kuchukia kile anachofanyiwa bali alishindwa kuyazuia kutokana na kiwango kikubwa cha hisia, ni msisimko ambao ndio mara yake ya kwanza kuhisi.
Alijikuta hata akiona aibu baada ya kuhisi mchuzi ukianza kutoka sehemu zake za siri na ilikuwa ni kama eneo limekuwa wazi na upepo kuingia hivyo kuhitaji kitu chochote cha kuongezea ili kuziba upepo usiingie.
Alijiambia huyu mwanaume alianza kumkasirisha na kumfokea lakini bado tu amefanikiwa kumnyegesha na sasa amejilegeza na kuacha afanye kile anachotaka.
Edna alikuwa na wasiwasi kwasababu wapo ndani ya ofisi lakini alishindwa hata kuinua mdomo na kusema Roma usiendelee, ni zaidi ya miezi nane tokea waishi pamoja na huenda alitakiwa kumruhusu kumfanyia hivyo mapema , lakini kwa muda huo ni kipi angeweza kufanya , hata hivyo ni mume wake.
Alijiambia labda maisha yake yote ataishi kwa kukasirishwa na kuchokozwa na huyu mwanaume lakini mwisho wa siku angejilegeza kwake.
Edna akili ilimtoka mara baada ya Roma kushusha suruali yake ya suti chini kwa kuikusanya na nguo ya ndani na kisha kupeleka mkono kwenye mbususu yake, alijikuta akikosa uvumilivu na kutoa mguno wa mahaba lakini Roma hakutaka apige kelele alimshika kidevu chake na kuanza kumpa kiss na aliweza kupokea kwa hiari yake kwa pupa huku miguu yake ikikosa balansi maana alianza kutetema kama Mayele lakini Roma alikuwa imara kumshikili.
Alijikuta akihisi kitu kama mkojo ukimtoka na alishindwa kujizuia na kuruhusu utoke , lakini aliishia kuona aibu na kuanza kulia, huku akishindwa kuelewa kwanini mwili wake unamwaibisha na kuanza kujikojolea.
“Sijategemea mke wangu kuwa hisia kali kiasi hichi , sio kwa maporomoko haya ya maji”Aliongea Roma kwa kutania lakini Edna alishindwa kuongea zaidi ya kuguna na Roma alimbusu shavuni kwa upole.
“Wakati tunafanya kwa mara yetu ya kwanza ulikuwa umelewa , lakini sasa hivi upo na akili yako timamu nataka ujue kwamba itakuwa inauma lakini tamu na ole wako siku nyingine unichokoze mwendo ni huu huu…”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kuelewa anamaanisha nini kwani alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa.
Roma na yeye hakujali sana , alichokifanya ni kumalizia kutoa nguo zake zote zilizobakia mwilini na kumuacha akiwa mtupu kabisa na kisha akapeleka mdomo kwenye manyonyo na kuanza kunyonya na kumfanya Edna kuweka mkono yake mdomoni akijiuzia asitoe sauti kubwa kwa kuhofia huenda Recho yupo nje.
Roma hakujali aliendelea na kazi pasipo ya kujali mtetemo wa Edna na baada ya kuridhika alivua suruali yake na kuishusha chini na mtambo ukafyatujka kwa nje huku ukiwa na hasira.
Roma alimshika kiuno na kisha alimnyanyua na kumpandisha kwenye meza huku akiendelea kumpiga Denda kwa dakika kadhaa na huku chombo yake ikiisuguanisha karibu na mlango wa kuingilia ndani , Edna alizidi kutoa unyevu nyevu mtelezo kwa wingi.
“Hubby …naogopa” Aliongea Edna kwa sauti ndogo ya kubembeleza lakini ya kuvutia.
Roma muda huo alikuwa kama amechangayikiwa na hakuwa na mpango wa kuacha kile alichokipanga .
“Nishakuambia itakuwa inauma lakini muda huo huo itakuwa tamu”Aliongea Roma kwa sauti nzito lakini yenye kubembeleza na Edna kabla hajaitikia alishitukia tu mwichi ukizama ndani na kumsababishia ubaridi wa aina yake uliosafiri kuanzia kichwani kupitia mgongoni na kwenda kutua kwenye mbususu.
“Oh…”
“Ah.!”
Wakati Roma akihisi utamu , upande wa Edna alihisi maumivu na machozi yalianza kumtoka, ijapokuwa alikuwa ashawahi kufanya lakini kutokana na kukaa muda mrefu sehemu yake ni kama imerudi kuwa ya msichana tena.
Roma alifurahia mno mchezo maana alikuwa akibanwa vizuri mno na aliweza kuhisi hisia za aina yake , ni hisia ambazo zilikuwa za tofauti mno na zile alizokuwa akipata wakati akifanya mapenzi na wanawake wake wengine.
Mpaka hapo sasa tunaweza kusema ndoa yao imekamilika maana ndoa hukamilishwa na tendo la ndoa na hicho ndio ambacho kilikuwa kikifanyika , ijapokuwa ilikuwa ni ofisini lakini maana ni ileile tu kwamba hilo nalo ni tendo la ndoa linalofanyikia ofisini.
Zilipita kama dakika kumi na tano wakati Roma akiendelea kupeleka mbele na nyuma kama anacheza amapiano alijihisi naniliu yake uvutwa kwa ndani kwa staili ya kukabwa , alishindwa kuamini anachofanyiwa na Edna na aliishia kumwangalia usoni na kutabasamu.
“Edna mke wangu , sikujua kama una mbinu zako za siri, umefanya kwa kudhamiria nini , unaonekana kama mzoefu umewezaje kuifinyia kwa ndani”Aliongea Roma lakini Edna alishindwa kujibu chochote zaidi ya uangalia pembeni kwa kuona aibu kumwangalia usoni hata hivyo alishindwa kumuelewa anamaanisha nini kusema kufinyia kwa ndani.
Roma alijiua Edna hakuwa akifanya makusudi kuifinyia kwa ndani ila ni namna ya asili ya mwili wake ulivyo, hata hivyo licha ya kwamba Edna hakuwa na udhoefu lakini alitokea kumpagawisha na kumfanya ajihisi kama yupo juu kileleni mawinguni.
Alikuwa amekutana na wanawake wengi na kuwa mdhoefu lakini hisia alizokuwa akipata zilikuwa za aina yake, Edna na yeye ni kama alikuwa akianza kuishiwa na pumzi maana ni zaidi ya magori ambayo amefunga.
“Arrgh…Romaa …taratibu ..inauma ..oooh!”Alijikuta akilalamika lakini Roma alikuwa kama kiziwi na kuendelea kuongeza spidi na ilifikia muda akaona staili ya kimeza meza haimtoshi hivyo alimgeuza na kumshikisha mikono kwenye meza huku akiwa ameinama na kufanya msambwanda wote kurudi nyuma na Roma aliingiza tena na kuendelea kusukuma songombile yake.
Alihisi maumivu kidogo lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea alizidi kupata raha na sehemu zake ni kama sasa zishaanza kuzoea ukubwa wa mwichi wa mume wake na shoti za utamu alizokuwa akisikia zilimfanya kujihisi yupo mbingu ya saba.
Edna baada ya kuona dudu ya Roma ilikuwa ikiyasugua makalio yakekwakupita na kumwingia kwenye kitumbua chake alihisi aibu , lakini hata hivyo alishindwa kuacha kumuangalia Roma usoni.
Alijihisi utamu kwa jinsi Roma alivyokuwa akimwangalia kwa upole na kuridhika , hata hivyo ilikuwa ni kama mara yao ya kwanza kufanya mapenzi.
Edna alishindwa kuongea chochote na kuona aibu karibia muda wote tendo linafanyika na aliishia kutii maagizo kila staili ambayo alikuwa akiambiwa akae.
Mchezo uliendelea kwa zaidi ya lisaa limoja na walianzia kwenye meza na kisha wakahamia kwenye sofa, lakini Roma akaona haitoshi na kwenda kumshikisha mikono kwenye vioo vya madirisha na kumfanya Edna aliangalie jiji huku akiendelea kuhisi utamu usio na kipimo ambao ulianzia kwenye vidole vya miguu na kusambaa mwili mzima na kumwingia ubongoni.
Huenda kama kuna mtu angekuwa na darubini jengo la pili yake angeona kile ambacho kilikuwa kikifanyika , lakini Roma hakufanya mambo bila ya kuwa makini aliweza kutumia uwezo wake kuchunguza maeneo ya mbali ili isije ikatokea mtu anawaangalia.
Roma aliendelea na shughuli yake kwa muda mrefu na kufanya sauti kama za watu wanaopiga makofi kusikika ndani ya ofisi nzima.
Paah! ..Paah!!
Ilifikia kipindi Edna hakutaka kuendelea na kutaka kupumzika kwani alipiga magori mengi na kujikojolea kiasi kwamba alikosa idadi na sasa mwili wake ulikuwa umechoka mno.
“Huby inatosha .. tupumzike .. niche nipumzike kidog…”Aliongea Edna huku akihema kama mbwa ambaye amekimbia maili nyingi.
“Ni saa limoja tu lakini unaonyesha kuchoka , tufanye angalau yawe mawili , babe sikujua kumbe unatembea na Dhana ya kimaajabu kwenye mwili wako”Aliongea Roma lakini Edna alikuwa akielekea kwenye kuzimia kwani hakusikia tena utamu lakini ilionyesha kuzidi kumfurahisha Roma , huenda ni kwasababu alishaanza kuvimba sehemu zake kwa ndani hivyo eneo kuzidi kuwa dogo.
“Tafadhari Hubby … siwezi kuendelea ..naomba unionee huruma..”Aliongea na kuanza kulia kama mtoto na kumfanya Roma amwangalie namna ambavyo amelegea , hakuamini ndio yule mke wake aliekuwa akijifanyisha kauzu , muda huo alikuwa kama mtoto mchanga.
“Huwataki wanawake wangu wengine… lakini huwezi kudumu kwa zaidi hata ya lisaa kwa staili hii unakwenda kushindana nao vipi”?”
“Wewe…! kwanini uzungumzie wanawake wengine kwenye muda kama huu?” Aliongea na kumfanya Roma amlambe kibao cha kalio la kulia.
“Sihitaji ruhusa yako ninapotaka kuwazungumzia , nilichoongea ni kweli, sijatoa bao hata moja lakini bado unaonekana umechoka ,utawezaje kunizalia mtoto kwa namna hii?”Aliongea Roma na kumfanya Edna ashindwe kujibu , hakujua kama kosa lilikuwa lake kuchoka haraka au ni la mtu mwingine.
Roma ilibidi amuonee huruma na alimbeba na kumkalisha kwenye sofa ili apumzike.
“Hata hivyo mke wangu umefanya kazi nzuri angalau umenifanya nijisikie vizuri kuliko mwanamke yoyote yule”Aliongea Roma huku akimfinya mashavu lakini Edna alishia kutojibu kwani alikuwa akihema kwa tabu , alishukuru tu ameachiwa maana hakujua nini kingeendelea kama Roma angeng’ang’nia mpaka atakapotoa bao.
“Nisikilize kwa umakini siku nyingine usije ukanichokoza na kunikasirisha , wewe ni mwanamke wangu na siwezi kukuruhusu kukutana na wanaume waliokaa kihuni huni , ninaweza kuonekana sina sababu za msingi lakini unapaswa kunisikiliza mimi tu kwasababu wewe ni wa kwangu milele , unaweza usikubali lakini hakuna mtu yoyote anaweza akaja kukusaidia kama nitaamua kukuadhibu , hata hivyo kama utataka tena lazima uniombe…., Hahaa..Kaone sasa kanavyotia huruma, haina haja ya kuniangalia kwa macho lawama umeyataka mwenyewe…”Aliongea na kumfanya Edna atamani kulia.
“Mwanaume mdhalimu wewe”
“Hehe ..niiite vyovyote unavyotaka , nilifikira mambo mengi usiku wote wa jana na nimegundua hata kama nijizuie kutokufanyia chochote bado wewe ni mke wangu , hata nikiamua kukufosi pia wewe ni mke wangu ya nini kujiumiza wakati upo”Aliongea Roma na kisha alimshika kidevu na kupitisha kidole chake kwenye lipsi zake kwa kusugua sugua.
Edna alionekana kuwa na adabu sasa, hakuleta ubishi na alikuwa kama piritoni,ule ubosi kwisha habari yake.
“Pumzika bibi harusi wangu , tutaendelea tena angalau kwa lisaa lingine, unifanye agalau nimwage bao moja”Aliongea Roma.
“Lakini sitosikia chochote tukifanya tena, nahisi kumevimba..”Aliongea huku akionekana kutia huruma lakini Roma hakuwa kwenye nafasi ya kumuonea huruma maana bado hata dudu yake haijalala.
“Nitakuponyesha, kaa vizuri niingize na nitakuonyesha kwanini naitwa mfalme Pluto” Aliongea Roma na kabla Edna hajajibu alishangaa ashawekwa sawa na yote ikazama.
“Ah..!”Alijikuta akihisi damu kumcheka huku Roma akiwa amemuweka kifo pendwa cha yule mdudu msumbufu usiku anaeogpwa na wadada , wakati akidhania angehisi maumivu Roma alikusanya nguvu ya kimaandiko na kuipeleka kwenye dudu yake na Edna alihisi mtekenyo wa aina yake na aliishia kutoa mdomo kama kabanwa na mlango.
Lisaa lingine mbele alijihisi uji uji mzito ukimwagika ndani ya sehemu zake za uzazi , ulikuwa wa moto kiasi kwamba alihisi raha ya ajabu na alijikuta akikakamaaa mwili na yeye kufunga goli ambalo haikueleweka lilikuwa la ngapi na aliishia kuhema huku akimwangalia Roma usoni na alijikuta akiachia tabasamu huku akiwa amelembua na kuangalia pembeni kwa aibu.
Naam hivyo ndivyo ilivyokuwa……..
MWISHO WA SEASON 16.
WWTSAPP 0687151346 NICHEKI KUOATA MWENDELEZO , SIMULIZI NDIO INAANZA
Bro singanojr ...u have made my weekend
Kati ya scene ambazo nilizokuwa nasibir ni mfalme Pluto kumla Edina [emoji23]
Ila jamaa kaanza kuwa serious Sasa
 
Back
Top Bottom