SEHEMU YA 570.
Jerry alidhani alikuwa akiota , mlango huo ulikuwa ni wa chuma kigumu sana , imewezekanaje ukabobolewa kirahisi namna hio.
Muda huo ni shoti pekee za umeme ambazo zilikuwa zikisikika ndani ya eneo hilo na Roma wala hakujali kabisa aliingia kama vile ni mnyama.
Nyuma yake kulikuwepo na damu nyingi ambazo zilikuwa zimetengeneza mfereji mkubwa wa damu kuingia ndani mara baada ya mlango kuvunjika.
Zilikwa ni damu za walinzi ambao walikuwa walilinda katika hilo eneo na ilionekana dhahiri kabisa Roma aliwapasua pasua viungo vyao pasipo huruma.
Roma mara baada ya kugundua eneo ni lenyewe , alitolea hasira zake zote za kutafuta usiku kucha kwa walinzi hao na aliwaua vifo vibaya sana, huenda ni aina ya vifo ambavyo havijawahi kutekelezwa hapa duniani , vilikuwa ni vya ukatili wa hali ya juu sana.
“Clark!!”Aliita mara baada ya kumuona Clark aliekuwa yupo chini sakafutni akitetema kama mgonjwa mwenye kifafa na palepale alimkimbilia na kumkalisha.
“Nini kimetokea ?Umepewa sumu?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi mkubwa na hakuacha kujaribu kumchunguza kwa kumuingizia nguvu za kimaandiko.
“I… I knew it ..you.. would save me ..just like ten years ago..”Aliongea kwa tabu sana akisema kwamba alijua tu atakuja kumuokoa kama miaka kumi iliopita.
Roma macho yake yalianza kuwa mekundu hakuwa na uwezo wa kujua ni aina gani ya sumu ambayo ipo kwenye mwili wa Clark , alikuwa na uwezo wa kuhisia sumu iliokuwa kwenye mwili wake ilikuwa ikinyong’onyesha saa utendaji kazi wa mwili.
Lakini alishindwa kumponyesha kwani sumu iliokuwa kwenye mwili wake iliionekana tayari ishaingia kwenye mfumo wa damu moja kwa moja na wakati akiwa amemshikilia palepale alitema damu nyingi nje mara baada ya Roma kujaribu kumponyesha.
“Ni sumu ya aina gani hii , niambie namna ya kukuponyesha”Aliongea Roma akijaribu kumtingisha lakini Clark aliishia kutingisha kichwa chake akimuonyesha ishara kwamba hakuna namna ya kumponyesha.
“Ni sumu ambayo niliiandaa dakika ya mwisho kabisa na ili kuhakikisha hawawezi kuniponyesha nilitumia mbinu ya kipekee ambayo inafanya viungo vya mwili kutofanya kazi sawasawa .. kwasasa haiwezekani kitu”Aliongea kwa tabu na kumfanya Roma palepale kumgeukia Jerry ambaye alikuwa amemsahau kwa muda.
“Wewe mnyama , yote haya ni kwasababu yako , kama utafanikisha kumponyesha mwalimu wako nitakuua lakini mwili wako sitouharibu”Aliongea Roma kimkwara huku akisambaza msisimko wa hali ya juu wa nguvu za kijini ili kumuogopesha Jerry.
Muda huo Jerry alikuwa ameshikwa na ubaridi wa aina yake hasa baada ya kuona damu nyingi zikiingia ndani kutokea nje , lakini licha ya hivyo chuki yake zidi ya Roma ziliifunika hofu yake na kaunza kucheka kama kichaa.
“Wewe shetani ijapokuwa sijui namna ulivyoipata hii sehemu lakini nakuambia hivi hakuna namna ya kumuokoa , sumu ambayo Clark ametengeneza anaweza kutengenza dawa yeye mwenyewe , inatia huruma kwamba anakufa kwenye mikono yako ukiwa huwezi kumsaidia “
“Unakiomba kifo wewe..”Aliongea Roma huku akitaka kumshambulia lakini Jerry alimzuia kwa kumpigia makelele.
“Usinisogelee, ukinigusa tu hii maabara yote italipuka na zile FURY mbili zitalipuka, madhara hayatakuwa kwako tu lakini kwa ukanda wote wa eneo la Bavaria, Ujerumani yote itageuka na kuwa toharani ya dunia, Je upo tayari kutoa kafara mamilioni ya watu kwa ajili ya kuniua mimi?”Aliongea na kumfanya Roma kunasa neno FURY.
“FURY siraha aliotaja je ndio sababu ambayo imewafanya wakuteke?”Alimuuliza Clark.
“Ndio .. niliipatia jila hilo ikimaanisha neno kisasi”Aliongea .
“Inahusiana na nini?”
“Ni aina ya siraha ya nyuklia ambayo teknolojia yake imeboreshwa zaidi … risasi yake moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hydrojeni”
“Nini..!!”
Roma alishangaa kwa uhatari wa siraha hio , kama kweli risasi moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hyrdrojeni si ni hatari hio , maana kama siraha hio ikatumika basi mionzi yake isingeathiri tu Ujerumani huenda na nchi za karibu.
Alijiuliza inakuwaje watu wa North Buyeo na kundi la kigaidi kutafuta teknolojia ya namna hio, ni kipi ambacho wanalenga?.
“Hehe.. sasa nadhani tayari ushajua ukuu wake, ninataka kuona kama utathubutu kuniua …Wewe shetani utapata maumivu makubwa sana baada ya mwanamke unaempenda akifa mbele yako …Hahaa, nimesubiria hii sku kwa muda mrefu sana , na unastahili kwa kila kitu , unapaswa kwenda jehanamu”Aliongea kwa hasira .
Roma alikuwa katika kiwango cha juu cha hasira na alitamani kumfanya kitu kibaya , lakini hakuweza kuthubutu kufanya maamuzi ya haraka kwani maisha ya watu zaidi ya mamilioni yalikuwa hatarini.
“Nini tatizo , Umekosa ujasiri tena?, Umejileta mwenyewe hata hivyo , ninakwenda kulipiza kisasi cha vifo vya familia yangu , baba yangu , mama yangu na dada yangu ambaye alikuwa na miaka mitatu tu”
“Kisasi? Ni kipi nimekufanyia mpaka kutaka kulipiza kisasi?”
“Bila shaka hukumbuki , umeua watu wengi sana unawezaje kuwakumbuka wote , umesahau ulichokifanya miaka mitano iliopita pale Simbokrog nchini Belarus kwenye kijiji cha Wozic si ndio?”
“Kijiji cha Wozic ?”Aliongea Roma huku akikunja sura , hakuwa akikumbuka kabisa kama kuna sehem kama hio na isitoshe kulikuwa na maeneo mengi madogo madogo aliopita ambayo hakuyakumbuka na kote hhuko huenda aliua.
“Unaonekana hukumbuki , Kijiji chetu kilikuwa na watu 186, kati yao therathini walikuwa ni watoto na wakati huo ni mimi pekee ambaye sikuwepo nyumbani kutokana na kwamba nilienda shuleni kwenye mji mwingine wa pembeni , lakini wewe ukaja na kufyeka kila mtu uliemkuta kijijini bila kujali wana hatia au hawana kwasababu tu adui yako alikuja kwenye kijiji chetu , kwanini usingeacha hata maisha ya watoto wadogo ambao walikuwa hawana hatia , kwanini ulivyomaliza ukawachoma na moto…”Aliongea Jerry kwa hasira kubwa na kauli yake ilimfanya Roma sasa kukumbuka lakini hakuwa akikimbuka vizuri sana , kipindi anafanya hivyo alikuwa katika hali ya ukichaa na ugonjwa wake ulikuwa ndio unaitawala akili yake.
Alikumbuka kabisa kitendo cha kuua watu wa kijiji kile ndio kilichosababisha Seventeen kumkimbia na mwisho wa siku akaingia kwenye mikono ya maadui na kumuua akiwa na ujauzito tumboni mbele ya macho yake.
Roma alishindwa kujizuia kusikia uchungu kutokana na maelezo ya Jerry , haikujalisha alikuwa akitamani kuwa na maisha ya amani , lakini mambo ambayo ameyafanya miaka iliopita yalimfanya kutengeneza maadui wengi ambao muda wowote watataka kulipza kisasi na aliona hata kwa Jerry ni mwanzo tu.
Lakini licha ya hayo yote , kipindi hicho akili yake ni kama ilikuwa ikiendeshwa kwa rimoti , ugonjwa wake ulikuwa mkubwa kiasi kwamba alikuwa ni kama shetani na bila kumwaga damu kwa siku hakuweza kutulia.
“Naona sasa unakumbuka ..?”Aliongea Jeryy huku akifuta machozi .
“Unapaswa kuadhibiwa pia , mwanzoni wakubwa waliniahidi watanisaidai katika kulipiza kisasi , na nikaamua kuishi na chuki na kuvumilia mpaka leo hii , lakini kwa leo kwasababu umepajua hapa sina mpango wa kuondoka hapa nikiwa hai”
“Unapanga kufanya nini , je unafikiri kulipua hilo bomu la FURY na kuniua kutakufanya ulipize kisasi cha ndugu zako , sahau kabisa hizo ni ndoto za kufikirika utaua watu wengi kuliko mimi”
“Inanihusu nini , ni matendo yako ya kishetani ndiio ambayo yamenifanya kuwa katika hali hii , usijaribu kunidanganya, hata kaam nitaondoka leo utanitafuta na kuniua , ni kheri niende na mamia ya watu katika kaburi langu , maisha ya hawa watu yatakuwa yametolewa kafara kwa sababu yako hahahaa..”
Baaada ya kuongea huku akicheka kwa kejeli palepale alisogea upande wa kulia wa kile kioo cha kuzuia mionzi na kukipiga ngumi kwa nguvu kubwa.
“Twiii , Twi, Twiit”
Ilionekana ndio namna maabara ilivyotengenezwa ili kuilipua njia ya mkato ya kuwasha bomu ni kupiga ngumi kioo na hicho ndio ambacho kilikuwa kikienda kutokea , hata hivyo maabara nyingi za kufanya majaribio ya siraha hutegeshewa bomu la kuiharibu kabisa pale panapotokea tatizo.
Muda uleule alivyoopiga ngumi kile kioo sauti kutoka kwenye tarakishi humo ndani ilisikika ikiwatahadharisha.
“Destruction Mode has been turned on , the labaratory will be exploding after the countdown , thirty .. twenty nine…”
“Ni mwisho haha , hatimae imekuwa mwisho”Aliongea Jeryy.
Roma alishangaa , hakutaka kumuua Jerry kwasababbu aliogopa siraha hio ya FURY ingelipuka , lakini sasa hivi maabara yote inakwenda kulipika , ilikuwa haiwezekani kwa yeye kuzuia kutokulipuka kwa bomu hilo la nyuklia.
Roma aligeuza macho yake na kumwangalia Clark aiekuwa kwenye mikono yake ambaye afya yake inaelekea ukingoni alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira
Baada ya kuona hana uwezo wa kuzuia mlipuko wa maabara hio pamoja na mlipuko wa FURY kitu pekee ambacho aliona angeweza kufanya ni kujiuoko yeye na Clark kuondoka katika hilo eneo.
Kufumba na kufumbua alikuwa ashatoka nae na kwenda kutua mbali kabisa na eneo hilo katika mlima na msitu usiokaliwa na watu, Kusini mwa nchi ya Austria.
Alikadiria kwa umbali huo hata kama bomu hilo la nyuklia litalipuka upande wa Ujerumani halitowaathiri kwa muda kupitia mionzi yake.
Baada ya kutafuta sehemu yenye majani makavu aliamua kumuweka Clark chini na kuanza kumfanyia uchunguzi wa mwili wake.
Haikuleta maana kwake kuomba msaada kwa muda huo , kwani aliona asingepata msaada huo ndani ya muda , hivyo kitu pekee ambacho alitaka kujaribu kufamnya ni kumpontysha yeye.
Mapigo ya moyo ya Clark yalikua ya chini mno na yalikuwa yakiendelea kuwa ya chini na muda wowote yangeacha kabisa kudunda na kupelekea kifo chake.
Roma alijikuta akijikatia tamaa mara baada ya kumungizia nishati ya mbingu na Ardhi kwa kuunganisha na ya Urejesho lakini bado alishindwa kumponyesha.
Mwili wake ulikuwa ni kama vile seli zake zinaoza ndani kwa ndani na hiko ndio kilichomuogopesha zaidi , kwani aliona dakika yoyote Clark angeweza kufa kwenye mikono yake maana tayari alishaanza kuwa wa baridi.
“Damn it … Clark , jarobu hata kuongea kidogo , ninaweza vipi kukuokoa?”Roma ujasiri wake wote ulimwishia na aliishia kuukumbatia mwili wa Clark huku akishindwa kuzuia machozi yaliochanganyika na hofu.
Ni mwanamke huyo ambaye hakulala usiku na mchana kwa ajili tu ya kumtengenezea dawa, na katika kipindi chote ambacho alihisi kuwa mpweke ni yeye pekee ambaye alifanya kila liwezekanalo kumsaidai , lakini sasa mwanamke huyo anafia kwenye mikono yake bila ya kuwa na msaada kwake.
Aliogopa kwamba bado hakuwa amelipa fadhila zake zote kwa yale aliomfanyia , alijilaumu na kuona yatakuwa makosa yake kuruhusu akifariki kwenye mikono yake kwani itamaanisha kwamba alishindwa kumlinda na maadui ambao aliwatengeneza yeye mwenyewe.
Clark alijitahidi kuamsha kinyonge sana mkono wake akimfuta machozi roma ,Roma hakujua hata alikuwa akilia alihisi maji yanaririka katika mashavu yake , lakini hakujua kama ni machozi yake .
“Ni sawa … wewe .. usilie tena .. nina furaha , mtu wa mwisho ninaemuona .. ni wewe”Aliongea Clark kwa kukata kata maneno.
Alishindwa kujizuia zaidi na zaidi mara baada ya mwanamke huyo kuongea kauli hio na alizidi kutoa machozi na kulia kwa kwikwi.
“Huwezi kuondoka hivi … utakuwa umenikatili sana ,,,, siwezi kujisamehe tena , umeniokoa mara nyingi sana na umefanya mambo mengi kwa ajili yangu ,, lakini mimi nashindwa kukukoa ,, sina thamani kabisa kwako , mimi ni mjinga”Aliongea huku akiinua mkono wake na kujipiga kibao kwa nguvu na kutokana kutumia nguvu za kijini ilisababisha mpaka majani ya miti kuanza kudondoka lakini bado aliendelea kujipiga vibao mara nyingi zaidi na kumfanya Clark azidi kutoa machozi ya kumuonea huruma na huzuni kwa wakati mmoja.
“Usi.. usi , fanye hivyo”Alijitahidi kuongea.
“Clark naomba usife , naomba usife tafadhari , siwezi kufikiria nitakuwa na maisha ya namna gani ukishaniach…”Alianza kulia kama mtoto huku akimwangalia mwanamke huyo kwa kuomba.
“Na.. naomba,, nikuulize swali na unijibu kabla sijafa?”
“Niulize chochote na nitakujibu”Aliongea haraka haraka.
“Roma … nataka tu .. kujua kama .., je .. unanipenda?”
“Ndio , Nakupenda , siku zote nilikuwa nikikupenda sana ,… wewe ni moja wapo ya wanawake ninaowapenda sana..”Roma aliongea bila kujiuma uma , hayo ni maneno ambayo hakupanga kumwambia mwanamke huyo katika maisha yake.
Zamani hakutaka kabisa kumsogelea mwanamke huyo kutokana na madhambi ya umwagaji damu alioyafanya, lakini baada ya kurudi Tanzania na kujipatia mke ndio kabisa hakutaka kumfanya mwanamke huyo mchepuko kwa kuamini alistahili kitu kikubwa zaidi.
Roma hakuwa na mashaka kabisa juu ya mapenzi yake kwa Clark, ni mapenzi ambayo hayakuanza jana wala leo , ni tokea alivyokuwa mdogo na kadri mrembo huyo alivyokuwa anakuwa alizidi kumpenda.
Mapenzi yake kwa mwanamke huyo yalikuwa sio ya kawaida ambayo yanaweza kueleweka kirahisi kwa binadamu.
Pengine katika dunia kuna wanawake wengi ambao aliwapenda na wao pia kumpenda na kumpa kila kitu na yeye kufanya kila kitu kushinda magumu yote kwa ajili yao lakini mapenzi yake ya kweli katika kumbukumbu zake yapo kwa Seventeen na katika uhalisia yapo kwa Edna na mpenzi anaemuona kama ndoto ni Clark.
“Kweli!?”Aliuliza Clark akiwa kama haamini na alijitahidi kufumbua macho yake ..
“Ni kweli , nilichokwisha kukisema ni ukweli , na unapaswa kuniamini , sijawahi kukuweka wazi kwasababu tu niliona hustahili kuwa na mtu kama mimi , … samahani sikukuambia hili mapema”Macho ya Clark yalionyesha kabisa kufurahishwa na kauli yake na tabasamu la furaha lilifunika uso wake .
“Honey … I knew it , you loved me..”Aliongea.
Roma alikuwa akilia hivyo hakuwa akiongea zaidi ya kutingisha kichwa tu kumwaminisha ni namna gani anamkubali huyo mwanamke.
Clark alipanua mdomo wake huku akiinamisha kichwa chini na alionekana kama anataka kung’ata kitu flani..”
Roma aliweza kuona lakini hakujua Clark anataka kufanya nini na alimwangalia kwa kuchanganikiwa.
“Collar …”Aliongea Clark kwa sauti dhaifu akimaanisha Kola ya koti lake.
Roma palepale alielewa sasa anataka kung’ata nini na alifanya haraka na kumsaidia kumpelekea karibu Kola ya koti ili kuweza kugusanisha na lipsi zake.
“Clark unafanya nini, kwanini unamg’ata Kola ya koti, ni kwa ajili ya nini?”Aliuliza lakini Clark hakuongea neno na muda huo alikuwa kama mtoto anaetafuna nguo kwani alifyonza kwa nguvu ule ukola wa koti mpaka ukaanza kujaa mate.
Ni muda huo huo aliweza kuona Ukola ule wa shati ukibadilika rangi na kuwa wa bluu ambayo haijakolea sana na kama sio kwa kuloana basi isingetokea
Wakati akishangaa palepale aliweza kushangaa mara baada ya Clark kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha baada ya kuonekana kumaliza alichokuwa akifanya na kadri dakika zilivyokuwa zikisogea ndio ambavyo alizidi kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Unashangaa nini mpenzi? , sijafufuka ni kwamba tu sijafa”Aliongea huku akitabasamu.
“Wewe , umewezaje kufanya hivyo.. nini..?”
“Unataka kuuliza nimewezaje kurudi katika hali ya kawaida si ndio , basi ni kwasababu nimejiponyesha mwenyewe”Aliongea huku akijaribu kukusanya nguvu na kukaa mwenyewe chini.
Roma aliangalia ile Kola ya koti kwa mara nyingine jinsi ilivyokuwa na doa la rangi ya bluu na kisha akamgeukia Clark aliekuwa na uso wa furaha .
“Ulinidanganya?”
“Nani kakuambia udanganyike kizembe , mimi ni nani , mimi ni Profesa Clark, mwalimu wa mwanafunzi mjinga kama Jerry , hivi unadhani naweza kuzidiwa akili na mwanafunzi niliemfundisha mimi?”
Roma alikosa cha kusema, alimwangalia mwanamke huyo namna ambavyo aliweza kurudi katika hali yake ya kawaida kwa haraka sana na alijikuta akichoka kabisa na kujikalia chini.
“Huu ulikuwa ni mpango wako?”Aliuliza Roma.
“Ndio , hivi unafikiri ungeweza kunipata kwa kubahatisha , wakati nilipokuwa nikitumia tarakishi zao nilituma Link kwa siri katika satilaiti yenu , kama mwalimu nilimjua Jerry hakuwa vizuri kwenye maswala ya Compyuta hivyo hakuweza kujua ninachokifanya kabisa , nilijua tu kama mtafika maeneo ya karibu na nilipo basi mngehisi mawasiliano ni kama yameingiliwa kutoka ndani”Aliongea na kumfanya Roma asipinge kwani ndio alivyoweza kumpata.
“Kama ni hivyo vipi kuhusu Sumu ni nini kile?”
“Ile ni sumu kweli , niliweza kuchanganya aina mpya ya sumu nilioitengeneza pale, ni sumu ambayo inavilegeza viungo vya mwili na kukufanya uonekakane kama umekufa na kama hutachukua dawa yake basi utakuwa wa baridi kwa masaa ishirini na nne na ikiisha makali yake mwili utarudiwa na joto lake na utaweza kuamka , nilipanga kama wataniona nimekufa watatafuta sehemu ya kunizika au kunipatia matibabu na ndio nitajua namna ya kutoroka ,lakini hio ilikuwa ni mpango wangu wa mwisho kabisa kwani sikuwa na uhakika kama hawatachoma mwili wangu lakini nilipanga kama hakuna ambae atakuja kuniokoa basi moja kwa moja nitadanganya nimekufa ili kuepuka wasinidhuru, lakini bahati nzuri umeweza kuja ndani ya muda hivyo nikatumia mpango B”Aliongea na kisha akashika Kola ya koti lake.
“Nililoanisha hii Kola na dawa maalumu ya sumu ,ilihitajika tu mimi kunyonya na ndani ya lisaa limoja ninarudi kuwa sawa tena”
“Kama ni hivyo kwanini ulinichezea hila hata mimi , hivi ulijua ni kwa kiasi gani moyo wangu uliuma?”Aliongea Roma huku akisimama na palepale mrembo huyo alisimama na kupitisha mikono yake yote mwili katika shingo ya Roma na kumbusu kwenye paji la uso..
“Kama nisingetumia fursa hii , usingeweza kuniambia nilichotoka kusikia kutoka kwako kwa muda mrefu”Aliongea na wakati Roma anataka kuongea neno alizuiwa na lipsi laini za mwanamke huyo.
Baada ya busu jepesi , Clark alionyesha uso wa kuomba huku macho yake yakionyesha hali ya kutia huruma.
“Honey usinikasirikie , nilitaka tu kuwa na wewe kama mpenzi wako , nilijua kama hutoniambia nitakuwa na huzuni milele”
Roma alijiambia ile siku ambayo alikuwa akiiepuka kwa miaka mingi hatimae imewadia na hakujua anakwenda vipi kumwelezea mke wake kwa maneno marahisi na kumuelewa.
“Umeandaa mpango wako , ili kunifanya niingie katika mtego na ukanifanya nilie kama mtoto , aisee inatia aibu Daah”Aliongea Roma huku akitabasamu kwa uchungu na kumfanya Clark amwangalie kwa macho ya utani huku akimtolea ulimi nje kama anamcheka.
“Nilikuwa nikienda na hali inavyoruhusu , Jerry alinitishia kwenda kuwaua wale watoto wsio na hatia , sikuwa na chaguo lingine..”Baada ya kusikia hivyo alijikuta akikumbuka kitu alichosahau.
“Oh nimesahau kuhusu FURY Ujerumani ndio kwaheri”Aliongea.
“Haha.. nilikuambia kila kitu nilipanga mimi , unadhani ninaweza kutengeneza kitu hatari namna hio”
“Kwahio ulichotengeneza ni nini , ni feki pia?”
“Hebu fikiria , unadhani ninaweza kuhatarisha maisha ya mamilioni ya watu kwasababu ya watoto , hata kama niwe kwenye hali gani siwezi kwenda mbali kiasi hivyo , teknolojia ya FURY kwasasa ipo katika nadharia tu , inawezekana vipi kuitengeneza ndani ya siku mbili au moja? , kutengeneza tu elementi ya mwisho inayokamilisha kanuni inahitajika mchanganyo wa kikemia ambao unaweza kuchukua mwaka mzima kutoa matokeo”
“Kwahio unasema sasa hivi Jerry atakuwa na hasira sana mara baada ya kuona umemdanganya?”
“Labdal , Ujerumani naamini watashughulika na tatizo hilo , kwasasa ninafuraha ya nilichoweza kutimiza baada ya muda mrefu , Roma naomba unibusu japo kidogo tu”
“Nini!”
“Umesema unanipenda hivyo unapaswa kunifidia kwa miaka yote nilioteseka kwa ajili yako”Baada ya kuongea alifumba macho na kunyanyua kichwa chake juu kuweka mdomo vizuri ubusiwe.
Roma aliangalia Lips zake zilizokuwa nyekundu kutokana na weupe wake wa kizungu na kisha palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kumshika kiuno kisha akamvutia kwake.
Clark mpaka hapo alijua kabisa alikuwa amefanya kosa kwa kujirahisisha mbele ya mwanaume ambaye alikuwa kama Simba mwenye njaa.
Dakika moja mbele wote walikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa ulioitwa Busu, inasemekana wazungu wapo vizuri sana kwenye Kubusu na hicho ndio kilichompagawisha Roma.
MWISHO WA SEASON YA 19
SEHEMU YA 571.
Katika jiji la Palermo giza tayari lilikuwa lishatawala na katika uwanja wa kivita uliokuwa ukifanyia mashindano , ulikuwa mtupu kwa wakati huo ikimaanisha kwamba mashindano kwa siku hio yamesha mpaka siku inayofuata.
Katika siku hio ya kwanza hakukua na maajabu makubwa kwani wale wanajeshi kutoka mashindano yaliopita wote kwa pamoja wameweza kuingia raundi inayofuata na kwa wale wahudhuriaji wenyewe wanasema mapigano yenyewe yanaanza siku inayofuata katika raundi ya pili.
Katika Moja ya Balkonni ya hoteli ya Cassano , mwanaume wa makamo mzungu alievalia mavazi ya upishi meupe alionekana akiwa bize kucharanga samaki aina ya Salmoni kwa haraka sana na kwa ufanisi mkubwa.
Kila kipande cha samaki kilikuwa kikilingana na kingine ni hivyo tu kwamba vilikuwa na ukubwa kidogo ambao unamuwezesha mlaji kutafuna kipande kimoja chote kwa wakati mmoja.
Mbali kidogo na alipokuwa anafanyia kazi mwanaume huyo kulikuwa na meza kubwa ambayo wahudumu wawili walionekana wakiwa bize kumsaidia kuhudumia kila anachokamilisha kupika na kuweka mezani.
Katika meza Christen alinyanyua Glasi yake ya Champagne na kumnyooshea Rose kugonga zao Cheers ambaye alikuwa karibu yake.
“Aphrodite, unaonekana kutokuwa kabisa na wasiwasi , vipi kuhusu hiko kinywaji?”Ares ambaye alikuwa ameegamia kwenye kiti kivivu aliongea kwa kuonyesha sura ya dhihaka.
“Wasiwasi wa nini , nipo hapa kwa ajili ya burudani sio kuteseka”Baada ya kusema hivyo alimgeukia Poseidon ambaye alikuwa akikomaa na upishi.
“Poseidon vipi hiko chakula bado tu? Nina njaa mimi”
“Hakuna mtu kugusa chakula kabla sijamaliza ,atakae fanya hivyo nitahakikisha hali chakula nilichopika mimi”
Upande wa Magdalena aliekuwa kimya alikuwa kwenye mshangao , bila shaka alikuwa akimjua Poseiodon ni mpishi maarufu duniani aliefahamika kwa jina la Mr Kelphin lakini hakuwahi kuwaza mtu huyo huyo kuwa mwanajeshi wa jeshi la Marekani upande wa majini.
“Christen kuna haja gani ya kusubiria amalize kila kitu , kwanini tusianze kula?”Aliuliza Magdalena ambaye alikuwa na njaa.
“Ndio sheria ya Poseidon hio kama atajitolea kupika chakula basi hataki mtu akiguse mpaka aridhike kimekamilika , anajali sana mlo kamilifu kuliko kitu kingine chochote”
“Kwa maneno marahisi Miss Magdalena ni kwamba bwana huyo ni mpishi Mbishi sana kwahi kutokea”Aliongezea Stern na Rose na Magdalena waliishia kushangaa tu.
Dakika chache mbele Poseidon aliweza kukamilisha sahani za Sashimi na kuwekwa kwenye meza hio kubwa , katika meza hio kilichoonekana ni aina mbalimbali ya vitoweo vya baharini ambavyo vimepikwa katika ubora wa hali ya juu.
Na kabla ya kuwaruhusu kula aliwaambia wasiguse kwanza chakula chake mpaka apige Selfie na palepale alitoa simu yake ya I Phone Toleo la juu na kupiga picha mbalimbali ya chakula chake na kisha kupost mtandaoni kwenye akaunti yakeiliokuwa ikifuatiliwa na watu zaidi ya milioni.
Baada ya kutaniwa na ndugu zake kutoka sayari nyingine , hatimae aliweza kukaa sasa na kuwaambia wale wahudumu waondoke.
Ukweli Magdalena na Rose walipata fursa ya kushiriki kwasababu ya heshima ya Roma pekee , lakini chakula hicho cha usiku ni kama vile kimeandaliwa kwa ajili ya ndugu hao ambao ni mara chache sana hukusanyika pamoja kama hivyo.
“Hermes tayari upo ndani ya hoteli , kwanini usivue hilo lisuti lako , huoni kwamba ni wewe tu hapa ulievaa suti na joto lote hili?”Aliongea Christen huku akimwangalia Raphaeli aliekuwa amekaa pembeni yake.
“Kuwa na amani sisi Vampire miili yetu ni ya baridi”
“Mwacheni nani anajali kama anahisi baridi au Joto , kwanza unaweza kunywa damu na ukaishi , kuna haja gani ya kula na sisi?”
“It’s recognition to Poseidon ‘s Culinary arts”Alijibu.
“Haina haja , chakula changu kipo Perfect”Aliongea Poseidon akijigamba.
Rose na Magdalena waliishia kuangaliana pasipo kuongea chochote , na walijiambia Poseidon na yeye ni kama Roma tu hana aibu kabisa kwa matendo yake.
Chakula kilichokuwa mbele ya Ares kilipotea kwa haraka sana na baada ya kumaliza kila kitu alisimama na kuelekea upande wa Balkoni.
“Ares unaenda wapi?”Aliuliza Stern.
“Hilo nalo ni swali gani?”
“Sio muda sahihi wa kuwatafuta, au unadhania unaweza kuwashinda?”
“Sina muda wa kupoteza kula na nyie mpaka usiku wa manane mimi wala sitamani kuangalia mapigano ya kibinadamu ya Caesar Conference nipo hapa kwa ajili ya kupigana nao”
“Hey Bro unataka kuzaliwa upya katika mwili mwingine labda?”
“So what , nevet try never know , I am not interested in their conspiracies , I dare to go if you don’t”(“Kwani vipi , usipo jaribu huwezi kujua , sina matamanio ya uzushi wao , ninathubutu kwenda kama wewe huwezi”Aliongea na kumfanya Stern na Alcie kukunja sura zao kutokana na ukichaa wa Ares.
Muda huo huo Rose na Magdalena waliweza kuhisi msisimko maalumu ambayo ni kama vile ni mawasiliano yao na Roma na walijikuta wote wakiangalia upande wa nje na waliweza kumuona Roma akiwasogelea kwa kasi na walijikuta wakiwa na furaha.
Kufumba na kufumbua Roma aliweza kutua katika Balkoni huku akiwa na tabasamu pana.
“The Annoying Hades , you finally came back , we thought you run away in fear”Aliongea Christen akimtania kama walidhania amekimbia kutokana na uoga.
Roma aliangalia kila mmoja aliekuwepo na alionekana kuridhika kupitia macho yake.
“Naona kila mmoja ameweza kufika , hakuna chochote kilichotokea wakati nilipokuwa sipo, nilienda Scotland ndio maana nimchelewa kuja”Aliongea.
Alikuwa amempeleka Clark Scotland kwani walikuwa na jukumu la kushiriki katika sherehe za Summer Bank Holliday , yeye na mama yake.
“Kwasasa bado lakini ni swala la muda tu”Aliiongea Stern huku akimwangalia Ares.
Baada ya hapo Roma aliongea na wanawake wake na kuwatoa hofu kwamba tayari alifanikiwa kumpata Clark na kumrudisha nyumbani.
Baada ya kuelezea kwa ufupi kwa upande wake na yeye alimuuliza Christen kile kilichotokea wakati ambao hakuwepo na alielezewa kila kitu kwa ufupi na namna ambavyo Ares anapanga kutoka hapo na kwenda kuwatafuta akiwa peke yake.
Upande wa Roma hakuwa na msingi mzuri wa historia nzuri juu ya hadithi ya miungu ya kigiriki hivyo hakuwa na uelewa mkubwa na licha ya kusikia stori zinazohusiana na majitu hakuwahi kuamini kama kweli walikuwepo.
“Nakushauri usiende kwanza mpaka ufahamu mbinu zao zote”Alishauri Roma.
“Acha kunidharau , Hades usijifanye wewe una nguvu kunishinda mimi kwasababu tu mara ya mwisho ulinishinda , kipindi kile sikuwa makini na nilikudharau na mbinu zako za kichawi”
“Kama unajiamini basi hakuna wa kukuzuia kufanya kile unachotaka, ni sawa kama unataka kufa lakini haitakuwa vizuri kwasisi kuja kuulizwa baadae”Aliongea Roma na kisha akajifanyisha kufikiria.
“Unaonaje ikawa hivi , kwasababu una uhitaji wa mtu wa kupigana nae , kwanini usipigane na Raphaeli”
“Damn it Hades , unanitania , nani anataka kupigana nae?”Alijitetea Hermes.
Ares baada ya kuambiwa pigane na Raphaeli alionyesha kuwa katika hali ya furaha mno , ukweli ni kwamba mikono yake ilikuwa ikimuwasha muda wote , hakujali kama angeweza kushinda au kushindwa alitaka kupigana tu.
“Hehe.. Hermes wewe ndio ulijifanyisha kuwa Farid kule Tanzania si ndio?”
“Farid !!, yupi huyo?”
“Haishagazi kwa mtu kama wewe kukosa makando kando na haina haja ya kujifanyisha hujui ninachomaanisha, ijapokuwa sijui kwanini ulileta mkanda wa kichawi feki Tanzania lakini haitokei tu ukaamua kunichokoza mimi peke yangu”
“Unamaanisha nini? , Hermes ule mkanda wangu feki ulionekana Tanzania wewe ndio uliehusika na kuzusha habari hizo?”Aliuliza Christen kwa mshangao.
“Aphrodite unaamini vipi anachoongea , kwanini nifanye kitu cha namna hio kwa faida ipi kwa mfano?”
“Acha kongea ujinga , Hades hawezi kuongea bila kuwa na ushahidi na zaidi ya yote Hermes tumejuana kwa muda mrefu tokea katika syari yetu, siku zote ukidanganya unakuwa na utulivu wa hali ya juu mno”
“Wewe..”Alitaka kuongea lakini aliishia kimwangalia Poseidon na wengine wanavyochukulia swala hilo.
“Mnaonaje na nyie , mnadhani ni mimi niliefanya kitendo hiko , mnamuamini Hades anachoongea tofauti na mimi , nitapata faida gani nikifanya hivyo kwanza?”Alijitetea. na Stern na Alice hawakuongea chochote na kuweka sura za maigizo.
“Hermes your skills in deception is not as good as your illusions”Aliongea Poseidon akimwambia uwezo wake wa kudanganya ni mdogo kuliko uwezo wake wa kutengeneza udanganyifu.
“Poa, nakubali kwamba wote nyie mnanijua vizuri , na nakubali nilifanya mimi , lakini sababu kubwa ni kwamba nilikuwa ninajisikia vibaya hivyo nikaona nikamchokoze Hades , kuna ttatizo juu ya hilo?”Aliongea kinafiki alikuwa akijua anadanganya.
“Hehe.. Hermes sijali sana kuhusua mambo yako ya kishenzi unayoyafanya , kama kweli umekasirika sasa hivi kwanini usitolee hasira zako kwangu kwa kujaribbu kunipiga”Aliongea Ares.
“Pumbavu , nina hasira kweli , lazima nikufundishe adabu wewe mshenzi”Aliongea kwa hasira huku akisimama na alimwangalia Roma kwa dakika kadhaa na kisha alisogelea Balkoni na kupotea nje na mabawa yake kama vile ni Makerubi akimfukuzia Ares.
“Aphrodite , Hermes ndio aliezusha uzushi juu ya mkanda wako wa kichawi , huna mpango wa kwenda kuungana na Ares kumshikisha adabu Hermes?”Aliuliza Alice akitania.
“Hapana, uwezekano wa sisi kushinda au wa Hermes kutushinda ni asilimia hamsini kwa hamsini, nilikuwa nikijaribu kukaa upande wa Hades tu hapa , sijali kati yenu anaetumia jina langu kwa mambo yenu”
“Vyovote vile , lakini kumuacha Hermes kwenda kushindana na yule kichaa ili tu kutoa hasira zake ni sawa na kupigana na yale Majitu tu”Aliongezea Stern huku akicheka.
“Ni wazi kabisa wametuleta hapa kwa makusudi , vinginevyo wasingeenda ndani ya hoteli ambayo ulipanga kukaa Hades , inaonekana wanasubiria wote tuwe sehemu moja ndio watushambulia , hivyo kwa muda kama huu kama tutakuwa na haraka na kukosa mpango lazima tutaingia kwenye mtego wao , hivyo tunapaswa kusubiri kuona ni nini wanatuandalia , isitoshe Athena hayupo hapa na hatuwezi kujihakikishia ushindi wa moja kwa moja”Aliongea Poseidon.
“Mbona unamuamini sana Athena?”Aliuliza Roma.
“Tayari nasikia umekutana nae na kuona uwezo wake , je sipaswi kujiamini?”Aliuliza na kumfanya Roma kushindwa kuongea chochote , ukweli ni kwamba katika nyakati zoe ambazo aliweza kukutana na Athena hakuweza kufanya chochote mbele yake , tukio la Korea kusini halikuwa limefutika katika akili yake na kila siku alikuwa akifikiria ni kwa namna gani anaweza kuwa katika levo za juu kumpita Athena.
Lakini kwa wakati mmoja alishindwa kuelewa ni kwa namna gani hao watu wenye asili ya Ujitu wametoa wapi hali ya kujiamini mpaka kujitokeza na kuanza kuwachokoza makusudi.
****
Siku nyingine ya mashindano iliwadia katika jiji la Palermo , watu wengi walikuwa wakitarajia kwanzia siku hio mashindano yangekuwa ya moto sana kwani makundi makubwa makubwa ndio ambayo yalikuwa yakikutana.
Kila mmoja aliekuwa akimfahamu Roma alifurahi kwamba amerudi na alikuwa akishiriki , Kwa Sauron alonekana kama vile amezeeka tu ndani ya siku mbili zilizopita lakini mara baada ya kumfuata Roma hotelini asubuhi kidogo hali yake ya utulivu ilimrejea.
Roma hakuwazuia wasiendelee na uchunguzi, alihitaji kujua zaidi kuhusu tukio lile , alitaka kujua kuhusu kundi la kigaidi ambalo limemteka Clark na kutaka kuunda siraha ya kimaangamizi ya teknolojjia ya FURY.
Kwa wakati huo uchunguzi ulikuwa ni rahisi kutokana na kwamba Umoja wa Norh Buyeo kutoka Korea ulikuwa ukijihusisiha , hivyo Roma alimpa kazi Makedon na wengine kujaribu kutafuta nguvu ambayo ipo nyuma yao na pamoja na mipango yao yote.
Wakati mashindano yanaanza Roma alikuwa eneo la VIP huku kulia na kushoto akiwa na Mage na Magdalena.
Upande wa Magdalena alikuwa na aibu sana asubuhi hio kumwangalia Roma usoni , pengine huenda ni kwasababu ya kile kilichotokea usiku kucha.
Ukweli ni kwamba baada ya chakula cha usiku Rose yeye alichukuana na Christen na kusingizia wanaenda kufanya Shopping , ilikuwa ni usiku ndio kakini maduka katika jiji la Palermo yalifanya kazi masaa ishirini na nne na watu ambao walikua ni maarufu maarufu wanaofika katika jiji hilo walikuwa wakifanya Shopping usiku ili kuepuka macho ya wengi.
Sasa kilichotokea ni kama kuna mpango ambao Rose na Magdalena walikuwa wamepanga , kwani wakati Rose alivyotaka kwenda kufanya Shopping Magdalena yeye alisema amechoka na alitaka kulala, upande wa Roma na yeye alikuwa amechoka kwa kutolala siku mbili mfululizo hivyo alitaka kupumzika.
………….
Kutokana na wote kupewa chumba kimoja basi ilitokea , Roma na Magdalena wakalala kitanda kimoja.
“Magdalena vinauma?”Ni sauri ya mwanaume iliosikika usiku wa jana katika chumba cha hadhi ya juu alichokuwa akilala mfalme Pluto.
Licha ya mwanaume kuuliza swali la namna hio , hakukuwa na majibu kutoka kwa mwanamke mrembo aliekuwa amelaliwa kwa juu na mwanaume aliejengeka mwili kimazoezi, upande wa yule mwanamke alionekana kuwa katika raha ya ajabu kiasi kwamba alitumia miguu yake na kuipitisha katika kiuno cha mwanaume yule.
“Arggh..”Mwanamke alitoa mguno huku akiachama kama vile kabanwa na mlango , alionekana alikuwa akipitia hali ya maumivu na raha kwa wakati mmoja
“Samahani , lakini inaonekana kubanwa sana ndio maana unasikia maumivu”Aliongea mwanaume kwa sauti ya kunong’ona, ilionekana kwa upande wa mwanamke kinachoendelea kwake kilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanyiwa.
“Ni sawa tu , nitapona kwa haraka , isitoshe na mimi pia sio wa kawaida”Ilisikika sauti nyororo ya mwanamke.
“Kama ni hivyo basi nitaanza kuchezesha kiuno”
“Sawa , usije kunifanya niijutie hii siku”
“Usijali , nitahakikisha hii siku unaikumbuka katika maisha yako yote”Aliongea yule mwanaume kwa besi na kisha makalio yake yalionekana kubonyea chini.
“Argh…!!”
…………….
Naam hayo ndio maongezi yaliosikika nje ya mlango wa chumba cha mfalme Pluto usiku wa jana.
Sasa wakati wakisubiria pambano lianze , ndio Roma alimuuliza mrembo Rose namna usiku wake wa Shopping ulivyokuwa na mrembo huyo alimwelezea kwa ufupi.
“Hakuna kikubwa kilichotokea”Alijibu Rose.
“Pengine anaona aibu , jana kanunua nguo za ndani kibao ambazo zimekaa kiuchokozi uchokozi”Aliongea Christen bila aibu na kumfanya Rose amkazie macho na alijikuta akiona aibu, Bahati tu waliokuwepo karibu yao ni Stern na Alice , angejisikia aibu sana kama Ron na Sauron wangekuwepo hapo.
Christen hakujali namna Rose alivyokuwa akimwangalia na alitoa ulimi kumtania na kisha akageuza shingo yake mbele.
“Kama ni hivyo , hakikisha unanunua za kutosha”Aliongea Roma akiwa na uso uliokaa kifisi.
“Haikuwa hivyo..Usimsikilize Christen”
“Najua , mimi natoa maoni yangu tu , ila usisahau usiku wa leo nataka kuona namna utakavyopendez… sawa Babe?”
………………
Wakati wakiendelea kuongea hatimae ilifikia zamu ya The Eagles , washindani wao ilikuwa ni kundi la Kimasenari lifahamikalo kwa jina la Odin Mercenary Corp, walikuwa na makazi yao Kaskazini mwa ncha ya dunia.
Rose na Magdalena mara baada ya kuona ni watu wa Roma waliweza kuongeza umakini , lakini upande wa Roma alionekana kabisa kutopenda sana kuangalia maishindano ya aina hio kwani yalikuwa ya kawaida sana kwake.
Lakini licha ya hivyo alifurahi kuona wanajeshi wake walikuwa wameimarika sana , hususani Maninja upande wa New Zero kwani walionyesha uwezo mkubwa katika kupambana na wapiganaji wa kundi la Odin, mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa The Eagles waliibuka washndi na kuigia katika hatua inayofuatia.
Roma ndio aliekuwa wa kwanza kuondoka na hakuwa na mpango kabisa wa kurudi tena, upande wa Rose mara baada ya kuona Roma kaondoka katika hilo eneo na yeye alifuata nyuma nyuma lakini kwa Magdalena yeye alisema ataangalia mashindano hayo mpaka mwisho
Ukweli ni kwamba alitaka kuendelea kuangalia , ila tu kumpa nafasi na Rose kuwa karibu na Roma kwani usiku wa jana kama sio Rose basi huenda asingeweza kuonja dunia ya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake, alikuwa na raha na akili yake yote ilikuwa ikiwaza usiku wa jana wote aliofanya mapenzi na Roma.
Hakuwaza rena kama Roma alikuwa mpenzi wa pacha mwenzake au mume wa rafiki yake wa utotoni Edna , bali muda huo alijiambia amefanya maamuzi sahihi kufata kile moyo wake unachotaka.
Wakati Roma na Rose wanakaribia hotelini waliweza kukutana na mwanaume wa Kijapani , Rose alionekana kumfahamu mwanaume huyo na upande wa Roma pia alikuwa akikumbuka sura ya mwanaume huyo, alikumbika kipindi alichosafiri kwenda Japani akiwa na Dorisi aliweza kukutana na huyo mwaname katika kambi ya jeshi wakati akienda kumpatia mateso Kapteni Kisu Mvunjiko na alishangaa kumuona akiwa hapo kwani alikuwa na cheo kikubwa mno serikalini.
Roma ilibidi kwanza amhoji Rose inakuwaje akawa anamfahamu huyo Mjapani na ndipo alipomuelezea kwamba alikutana nae usiku wa jana akiwa na Christen na huyo mwanaume ndio aliewasogelea na kuwachombeza kwa ajili ya kwenda kumpa huduma usiku kucha kwa malipo ya hela , lakini Christen akamjibu kwa kumwambia yeye atamlipa kwa kila pigo atakalompiga na ndio akaondoka na kuwaacha.
Roma mara baada ya kusikia hivyo aliguna , aliona sio jambo la kawaida kigogo wa serikali kutoka Japani ghafla tu kumsogelea Christen na Rose na kuwataka wampatie huduma.
Baada ya kuingiwa na wasiwasi ya uwepo wa mwanaume huyo hapo Sicilly haraka sana alimpigia simu Sauron na kumpa maelekezo ya kumfanyia uchunguzi , hisia zake zilimwambia huenda alikuwa akihusika na wale watu wa mavazi meupe au kundi la Cyclops.
*****
Ikiwa ni muda wa jioni kabisa wakati Roma akiwa ameuchapa usingizi mara baada ya kazi nzito alioifanya na Rose mlango wa chumba chao ulifunguliwa na Magdalena.
Mara baada ya kuona namna Rose na Roma walivyolala wakiwa hawana nguo mwilini alijikuta akiona aibu , lakini alijitahidi kujikaza na kwenda kumuamsha Roma.
Roma mara baada ya kuamka hakuona aibu licha ya kwamba alikuwa uchi yeye na Rose na alienda mbali kumtania Magdalena na kumwambia ajiunge na yeye lakini Magdalena aligoma na kumwambia kwamba amekuja hapo kumpa taarifa kwamba wenzake wanamuhitaji katika eneo lileile la siku ya jana kwa ajili ya maongezi.
Roma mara baada ya kupewa taarifa hio hakuwa na muda wa kupoteza , alikuwa na hamu kubwa ya kuwajua kiundani watu alioambiwa wana aasii ya Ujitu ndani yake hivyo ndani ya dakika chache tu alikuwa tayari amekwisha kujiandaa na kutoka.
Roma mara baada ya kufika aliweza kukuta kila mmoja alikuwa amekaa katika nafasi yake na yeye pia alisogelea kiti na kuketi , lakini wakati huo akiangalia barua iliokuwa juu ya meza.
“Nini kinaendelea hapa , hio ni nini?”Aliuliza Roma na kumfanya Christen aliekuwa akimwangalia Roma muda wote katika eneo la chini ya kiuno chake palivyotuna kuvuta mdomo na kisha kuchukua ile barua na kumpatia.
“Je ungependa kujifunza lugha yetu?”Aliuliza na kumfanya Roma kuangalia ile barua ilioandikwa kwa herufi zisizoeleweka na kumrudishia Christen.
“Haina haja , ninajua lugha nyingi sitaki kuongeza nyingine kwenye kichwa changu , niambie barua hii inahusu nini”
“Ni rahisi tu , ni kwamba kiongozi wa Cyclops anaefahaika kwa jina la Brontes ametutumia mwaliko , anatualika sisi wote kwenda kupata chakula cha mchana katika mgahawa siku ya kesho baada ya awamu ya kwanza ya mashindano ya asubuhi”Aliongea Poseidon.
“Kwanini wanataka kukutana na sisi? , hawajawahi kututafuta hapo kabla”Aliuliza Roma.
“Hata sisi imetushagnaza pia , wanaonekana kama hawatafuti kulipiza kisasi na wanajaribu kutualika namna hii , wanajaribu kufanya nini?”Aliongea Stern.
“Kwanini tujali wanachotaka , huenda wametualika kwa ajili ya kumaliza tofauti zetu , lakini kama wanataka kupigana na sisi tutapigana na kama wanataka amani tutawaacha waendelee kuishi”Aliongea Ares na kufanya wote wamwangalie kwa mshangao kidogo lakini haa hivyo washazoea Ares amekaa kifujo fujo.
“Hivi wasiwasi wenu ni kwamba tunaweza tusiweze kupambana nao?”Aliuliza Roma baada ya kimya cha muda mfupi.
“Kama tungekua kwenye sayari yetu , wasingethubutu hata kutusogelea na ningewapiga mimi mwenyewe, lakinii sasa hivi mambo ni tofuati bila ya Athena na Zeus tunaweza tusifanikiwe kuwashinda ijapokuwa tutakuwa na uwezo wa kujilinda”Aliongea Hermes.
“Mimi nipo , yupo pia Rose na Magdalena ambao wote wapo katika levo ya Nafsi , je bado tu haitoshi , kwanini tuwaogope?”Aliuliza Roma.
“Hades unawachukulia poa hawa majitu , ngoja nikuambie Cyclops na Hecatoncheires wanao uwezo mkubwa kuliko jamii zote za majini na hawaathiriki na nguvu za mbingu na ardhi kwasababu wana damu ya kizazi chetu , Damu ya Titan”Aliongea Artemis.
“Damu ya Titan!!?”Aliuliza Roma kwa mshangao.
“Ndio …”Alice aliwaangalia wenzake kuona kama kuna ambaye anajaribu kumzuia na baada ya kuona wapo kimya aliendelea.
“Damu ya Titan ndio asili yetu kamili na sisi ni mwendelezo wa kizazi cha damu yake , ndio chanzo kikubwa cha nguvu zetu wakati tulipokuwa kwenye sayari yetu m sababu ambayo imetufanya uwezo wetu kushuka kufikia asilimia therathini ni kwasababu tulikosa miili yetu yenye asili ya damu ya Titan , hawa Majitu wenyewe ni sehemu ya uzao wetu hivyo wana asili ya damu ya Titan na kama tulivyosema mwanzo, wao walikuja duniani na wakaweza kuishi kwa miili yao lakini sisi ikashindikana, Mpaka sasa hivi damu yetu ipo Sealed”
“Hebu subiri kwanza , nilikuwa nataka siku zote kuuliza ilikuwaje miungu mkapoteza uwezo wenu kwa kiasi kikubwa , kama kweli hii damu ya Titan ndio chanzo cha nguvu zenu , kwanini ipo ‘Sealed’ mpaka sasa , je swala hili lina uhusiano na moyo wa Gaia?”Aliuliza Roma.
“Kuhusu hilo..”Alice alitaka kuongea lakini alisita lakini palepale Christen na yeye aliingilia.
“Usiulize maswali Hades , kwetu kumbukumbu hizo ni maumivu makali kila zinapojirudia .. nitaendelea kukuelezea kwa niaba ya Alice, hawa majitu wanao uwezo mkubwa kutokana na kuwa na damu ya Titan na ndio maana hawaogopi kabisa watu wanaovuna nishati za mbingu na ardhi , kwasababu ni nishati ya muunganiko wa dunia hii , Damu ya Titan unaweza kusema ina nguvu ya Kiroho kama mnavyopenda kuita hapa duniani , sasa unatakiwa kujua ni Zeus pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kutumia mwanga kuifubaza nguvu za damu hio na kuwafanya wawe dhaifu , hivyo hakuna mtu ambaye anaweza kuwashinda hata Athena mwenyewe hakuwa na uwezo huo”
“Kwa maelezo yenu mnaamaanisha kwamba tunapaswa kufa kwenye mikono yao si ndio?”Aliuliza Roma huku akitabasamu kwa uchungu
“Hatuwezi kwenda mbali hivyo , kwasasa hatujui ni ipi mipango yao na isitoshe una nafasi kubwa , angalau unaweza kutumia kanuni za anga pamoja na nguvu za nishati ya mbingu na ardhi , lakini hata hivyo inatia huzuni kwasababu haupo kwenye levo ya juu zaidi ya kuweza kudhibiti Radi kama Majinni tuliokutana nayo kipindi tunafika la sivyo ungekuwa tishio kwao”Aliongea Poseidon.
Roma alijiambia hata kama hakuwa katika levo za juu kama watu waliowakuta miaka hio , lakini yeye alikuwa na chungu cha maafa hivyo alijiambia kwamba mwisho wa kila kitu bado haujulikani kama watapambana.
Hao watu kilichomuudhi sana ni kwamba ni wasiri sana kuhusu hio damu ya Titan na alijua kabisa ameelezwa nusu na ni kitu ambacho kinahusiana na moyo wa Gaia
Baada ya mazungumzo ya muda mfupi Poseion alimtaka Hermes kunagalia Ulingo kama haujawekwa mtego ili kuwa salama na haikuwa tatizo kwa Hermes kulingana na spidi yake
******
Siku ya tatu hatimae iliweza kuwadia na makundi therathini na mbili yalikuuwa ndo yamebakia , wawakilishi mbalimbali kutoka serikalini walikuwepo.
Kama kawaida Poseidon , Hermes na Ares walikuwa katika eneo lao la sku zote na Roma , Magdalena , Rose Alice , Stern na Christine wlaikuwa wamekaa katika eneo moja.
Kabla ya mashindano kuanza Roma aliweza kupokea ripoti kutoka kwa Makedoni juu ya baadhi ya chunguzi alizomwambia Sauron afanyie kazi.
Na kwa maelezo yake ni kwamba mwanaume wa Kijapani aliemuona katika hoteli ya Cassano alikuwa akifahamika kwa jina laKagawa Chusho na ni waziri wa ulinzi wa Japani na hana uhusiano wowote na kundi la watu wa mavazi meupe , lakini alimwambia kwamba wakati ambao alimuona hotelini ilionekana kulikuwa na kikao kilichokwisha kufanyika hivyo hawakuwa na uelelwa nini kilitokea au kilizungumzwa katika kikao hicho ndani ya hoteli ya Cassano.
Roma kuna hisia ambazo zilimwambia kabisa huenda serikali ya Japani ilikuwa ikihusika kabisa na uwepo wa hawa Majitu hapo Sicilly lakini hakuwa na namna ya kuthibtisha dukuduku lake kutokana na kwamba alijua fika kikao ambacho kilifanyika ndio kilikuwa na taarifa kamili lakini kwa bahati mbaya walichelewa kugundua mapema..
Wakati ambao Roma alikuwa katika mawazo alikuja kushituliwa na Sauron aliekuwa anakuja mbio mbio kwake .
“Your Majesty Pluto something is wrong”Aliongea Sauron akimwambia kuna tatizo.
“What are you saying?”(Unaongea nini?”);
‘Hapa , hebu angalia wahusika ambao wanakwenda kushiriki katika mecho inayofuatia”Aliongea Sauron na kushika Kishikwambi alichokuwa ameshikilia Sauron.
“Mechi inayofuata ni The Eagles na Deicide?”Aliongea Roma kwa mshangao akimaanisha kwamba mechi inayokwneda kuanza ni kati ya Majitu wanaojiita godkiller na wanajeshi wake wa The Eagles.
“Nini kimetokea , nilijua wanakwenda kukutana katika nusu fainali tu?”Aliuliza Roma huku akiwa na wasiwasi na kuanza kupitia orodha ya wanajeshi wake ambao wanakwenda kushindana katika mechi inayofuata.
“Kuna mtu ambaye amebadilisha na meneja anasema ni makosa tu yaliofanyika , nadhani ni makusudi kabisa wanataka tukutane kwanza na hao wauaji ili watudhalilishe kututoa katika mashindano mapema“Aliongea Sauron kwa hasira.
Lakini licha ya hivyo ni kama washachelewa , kwani tayari wanajeshi wa The Eagles walionekana wakiingia kwenye ulingo na walionekan kuwa na mchecheto mara baada ya kusikia wanakwenda kupambana na kundi la Deicide watu waliowaonyeshea kiburi katika hoteli ya Federico.
Wakati Nasri na wenzake wakiwa na shauku ya kulipiza kisasi kwa kuwashikisha adabu watu hao, upande wa Roma alikuwa na wasiwasi kwa kile kinachokwenda kutoktea kwa kuamini kwamba wanajeshi wake hao hawana uwezo wa kushinda na kwa mara ya kwanza jeshi lake linakwenda kudhalilishwa.
Makofi ya shangwe na vifijo yalisikika pande zote baada ya wanajeshi wa mavazi meupe kuingia kwa mbwembwe zote na baada ya kufika katikati waligeuka upande ambao wamekaa Poseidon , Roma na ndugu zake na kuwaangalia , ijapokuwa sura zao hazikuwa zikioneana kwa kuvaa Mask lakini likuwa ni kama vile walikuwa na sura za kejeli.
ITAENDELEA WIKIEND NJOO WATSAPP TUPIGE STORI NAMBA 0687151346