SEHEMU YA 549.
Edna alijikuta akimeza maneno yake aliotaka kuongea kutokana na namna Roma alivyomwangalia.
Maneno yale aliongea Roma ni kama yaligeuka na kuwa jiwe ambalo limetua moja kwa moja kugonga katika moyo wake uliokuwa kama barafu.
Alimwangalia machoni kwa muda mrefu kabla ya kuvuta pumzi na kuzitoa na kisha akalamba lipsi za midmo yake na kuongea.
“Wewe ni mbinafsi sana”
“Nakubali mimi ni mninafsi , ndio maana sitokubali sisi kutalakiana . siwezi kukuruhusu ukaondoka kwenye maisha yangu ,siwezi kupiga magoti pia na kukuomba tena wala sitoomba msamaha , unayo kila haki yakubakia hapa lakini wewe ni wangu na hilo haliwezi kubadilika”
“Unaongea mambo ambayo hayana sababu ya msingi”Aliongea huku akishikilia kwa nguvu nguo yake ya kulalia.
“Nataka uone uhalisia ulivyo , wewe unadhani mama amekukera sana kwa kualika wale wanawake nyumbani , unafikiria sisi wote tulikuwa tukikuchokoza kwa kukushuku , mbona unakuwa mwenye kutukandamiza , unaweza kuwa na kisirani chako kwangu utakavyo na naweza kuvumilia lakini hasira zako za haraka zilifanya kila mtu kukosa furaha , je unadhani wewe ndio unaepaswa kufanya tu hivyo , kwanini unataka kushindana na mimi? , mimi ni mume wako na uyle ni mama mkwe wako na sisi ni wanafamilia , kwanini unataka kutuletea tabu”
“Wewe… nilijua tu hujawahi kunionea huruma”
“Naongea ukweli”
“Inaniuma kwasababu kila kitu ulichoongea ni ukweli”Baada ya kumaliza kauli hio aliingia ndani na kufunga mlango wa balkoni na Roma aliishia kumwangalia lakini hakuwa na sababu ya kumsogelea tena kuingia ndani , aliamua zake kupotea na kurudi nje.
Alijikuta akisimama nje kwa muda akivuta upepo mkali unaotoka baharini na baada ya dakika tano aliingia kwenye gari , lakini ile anataka tkuliwasha simu yake ilianza kuita na aliekuwa akimpigia ni Neema Luwazo.
“Kipenzi changu , uko wapi?”Sauti ya kichokozi ya kumnyanyua nyoka pangoni ilisikika kwenye ngoma zake za masikio.
“Sauti yako inaonyesha kama unajua kinachoendelea”
“Wewe hujui wafanyabiashara mtaji wetu ni taarifa na isitoshe ni swala linalokuhusu , nasikia umekosana na mkeo na amehama kabisa nyumbani?”
“Umesikia wapi , Nasra ndio kakuambia?”
“Ah..,! Nasra sio mtu wa kuongea ongea umbea nadhani hata wengine hajawaambia , nilienda nyumbani kwenu nikakuta hakuna mtu ndio nilipofanya maamzui ya kumpigia Bi Wema na akaniambia kinachondelea , kwanini unajaribu kutuficha , haujui mtu kama mimi ambaye siku zote nina ajenda za siri nilikuwa nikisubiria hii siku itimie kwa hamu zote , namchukulia Edna kama mshindani wangu hata hivyo”Aliongea huku akicheka na kumfanya na Roma pia kucheka kutokana na utani wake.
“Inakupasa usubiri muda mrefu, kwani kisheria haturuhusiwi kupeana talaka angalau tuwe tumeishi pamoja miaka miwili”
“Haha.. Naamini atarudi tu ndani ya siku chache zijazo , nadhani sina haja ya kuendela na mpango wangu , unaonaje ukinisindikiza twende Shopping, hutujaonana muda mrefu”
“Si kwasababu muda wote unasema upo bize wewe , uko wapi nije sasa hivi kukuchukua”
“Nipo nyumbani kwangu , Donyi kaondoka leo asubuhi kulekea Los Angels na mchumba wake Kasimu nipo mpweke mno”
Baada ya kuambiwa hivyo moja kwa moja aliendesha gari kurudi uelekeo wa nyumbani kwa ajili ya kumfuata Neema.
Ndani ya madakika kadhaa Roma aliweza kufika na kusimamisha gari nje ya geti na Neema Luwazo alikuwa ashatoka nje na kumpokea kwa kumbatio , alionekana ashajiandaa tyaari kwa ajili ya kuondoka, aikuwa amevalia blauzi na suruali ya jeans ambayo ilimpendeza na kuchora umbo lake namba nane.
“Unaangalia nini , ingia kwenye gari tuondoke”Aliongea kwani Roma alikua akiangalia mtetemno kwa nyuma huku akiwa ameweka tabasamu a kifedhuli , aliishia kucheka na kungia ndani ya gari.
“Mh! Jamani mbona hili gari linanuka sigara”Aliuliza lakini Roma hakujibu zaidi ya kuguna na kumfanya Neema kumwangalia.
“Kwahio mawazo yamekuwa mengi , sijawahi kukuona ukivuta sigara , nilidhani mwanaume wangu ni wa kipekee lakini inaonekana kumbe hauko imara kudhibiti mawazo yako”Aliongea huku akivuta mdomo na kumfanya Roma kucheka.
“Okey kwanzia leo nitaacha, Wapi unataka kwenda?”
“Mimani City , tunaweza pia kula huko huko chakula cha mchana , unaonaje?”Aliuliza na Roma hakubisha kwanza hata hivyo asingerudi nyumbani na kukaa peke yake wikiend yote hio , hivyo aliona huenda ingekuwa afadhali.
Baada ya kufika Mlimani walianza kupita kwenye kila duka kwasababu Neema hakuwa na kitu kichwani anachotaka kununua hivyo alijaribisha kila kitu kilichomfurahisha , lakini mwisho wake hakuridhika na wakaishia kwenda kwenye Brand maarufu za Balenciarga , Dr Martens, Luis Vuiton na lancome.
Roma aliishia kumsindikiza maana wafanyakazi walikuwa wakimsaidia kushika kila ambacho anachagua , lakini Roma kwenye upande wa nguo hakuona kwanini Neema anachagua aina hizo za nguo kwani hazikuwa zikimvutia.
“Hey , kama unataka kununua nguo nadhani ulizopita kule nyuma ndio zinakufaa zaidi , hizi nguo nadhani ni kwa ajili ya maonyesho ya fasheni, hakuna maana kuziangalia”Aliongea Roma.
“Wewe mwanaume huelewi kama nisipovaa nguo ambazo ni za brand kubwa nikienda kwenye vikao wataniona kituko , sisi wanawake siku hizi tunajali sana kile ambacho tunavaa kuendana na wakati”
“Kuna haja gani ya kujali watu wanasemanini , kwani hakuna anaeweza kuipima thamani yako kupitia mavazi”.
“Hehe ndio dunia inavyoenda , kama sio hivyo unadhani makampuni kama haya yangekuwa maarufu , kampuni ya mkeo ukiachana na upande wa kampuni zake ndogo ndogo za ujenzi na mambo ya mafuta lakini pia upande wa fasheni umemuinua sana kiuchumi”
“Inaonekaa hufatilii sana kile ambacho kinaendelea kwenye kampuni , hivi majuzi tu aliweza kuingia ubia wa kibiashara na kampuni zenye majina makubwa makubwa kuomba haki ya kusambaza bidhaa zinazotokana na malighafi mpya , kampuni alizoingia nazo mkataba ni kama Prada , Hermes na Burberry , faida alizopata kwenye ubia na kampini hizo ni mara mbili yake anayopata kwenye kampuni zake za ujenzi ukiachana na mafuta pamoja na viwanda vya utengenezaji wa bidhaa za ndani”
“Ana kipaji cha kufanya biashara , lakini nadhani anapaswa kujifunza namna ya kuwa mke bora”Aliongea lakini Neema alicheka.
“Mbona unacheka?”
“Ni hivyo uliposema ana kipaji cha biashara lakini kwa mtazamo wangu naamini ni kinyume chake , ameweza kufanikisha yote hayo kutokana na ukweli kwamba baba yake ni mtu mzito na ana ushawishi mkubwa kwa Raisi Senga na nchi zote za Afrika ya mashariki na kati
“Unamaanisha nini?”
“Wafanyabiashara kama sisi siku zote tunapaswa kufanya vitu kwa wakati sahihi , sehemu sahihi na watu sahihi , kuwa na watu sahihi sio kitu kigumu kwasababu unachotakiwa ni kuwa na ushawishi tu na maipo mazuri , kuhusu sehemu sahihi inategemeana na bahati yako katika biashara , kama sio kampuni ya Vexto kuchagua maeneo sahihi katika kufanya biashara basi siamini ingeweza kuwa na mafanikio makubwa kwa nchi kama hii ya kwetu ambayo ndio kwanza inaendelea , kitu kigumu katika biashara ni kufanya vitu kwa wakati sahihi kwasababu kikawaida inategemnea sana na sera za nchi , kadri utakavyofanya vitu ndani ya sera za serikali basi huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu fursa za kibiashara , kama sera haiendani na biashara yako hata uwe na mtaji mkubwa kiasi gani huwezi kufanikiwa na ndio maana wawekezaji wanapoenda kuwekeza kufanya biashara katika mataifa ya nje wanachoangalia ni Sera”
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba Raisi Jeremy alikuwa akimsaidia Edna katika maswala ya sera ndio maana kampuni yake inafanya vizuri?”
“Ndio maana nakushauri kuwa makini na Raisi Jeremy , ijapokuwa hakuwahi kumtambua Edna waziwazi kama mtoto wake, lakini amesaidia sana kampuni ya Vexto kufikia pale ilipo, huenda kama atakuja kumwambia Edna mambo ambayo amefanya Edna moja kwa moja ataguswa”Aliongea Neema na kumfanya Roma kukumbuka kuna siku Edna ashawahi kumwambia kuhusu mtu anaefahamika kwa jina la the Protector ni kama maneno ya Neema yamemkumbusha kuhusu hilo jina kwani alikuwa amesahau kwa muda mrefu.
“Kwanini unaniambia haya ghafla tu, unadhani kwanini Jeremy anaushawishi mkubwa ndani ya Afrika mashariki na kati?”
“Kuna kitu sikukuambia kwasababu nilikuwa bize na kazi , lakini katika moja ya vitu ambavyo niliweza kugundua katika baadhi ya nyaraka alizoacha mstaafu Kigombola ni juu ya raisi Jeremy na siri zake”
“Siri zake!”
“Ukweli kama ningeona taarifa hizo miaka ya nyuma kabla ya kukutana na wewe nisingezielewa wala kuamini , lakini kwa kipindi ambacho tumekutana na nikajua mengi ambayo hayaonekani katika huu ulimwengu ndio maana nimefanikiwa kuelewa kile alichoandika”
“Umegundua nini?”
“Kwa maelezo ya Kigombola ni kwmaba Raisi Jeremy ana nguvu kubwa nyuma yake ambayo inamlinda na inahusiana na viumbe wasioonekana(majini) , katika nyaraka nilizoweza kupata kusoma jamii hio inafahamjka kwa jina la Panas kama sikosei”Roma alishangaa maneno ya Neema.
“Amejuaje kuhusu hii jamii kuwa nyuma ya Jeremy , mwenyewe nilianza kufikiria hili swala mara baada ya kuona watu wawili kutoka Panas ambao tayari wapo katika levo ya Nafsi wakimsindikiza kama mabodigadi”
“Nini!!, kwahio nilichosoma ni kweli jamii hio ipo, kama ndio hivyo inamaanisha kwamba wametoka katika maficho yao sasa wanataka kuingilia amswala ya kawaida ya dunia?”Aliongea Neema Luwazo kwa mshangao.
“Siwezi kujua, lakini uwepo wao hapa nchini ulinipa maswali mengi ambayo sijayapatia majibu bado na kama uliosema ni kweli basi naanza kupata picha lakini pia shauku yangu kuzidi kuongezeka , je hakuna kitu kingine ambacho uliweza kupata katika maelezo uliosoma?”
“Maelezo niliosoma ni hayo pekee na ndio nguvu kubwa ya Raisi Jeremy nchini Rwanda , ilionekana Kigombola bado hakuwa na majibu ya kutosha na hata alichokiandika hakikuwa na ushahidi , lakini baada ya wewe kusema wameonekana hapa Tanzania sasa naamini maneno yake”Roma alifikiria kidogo na kuona huenda kuna sababu ambayo watu wa Panas wakaamua kuja upande wa duniani , lakini kama ni hivyo kwanini Aphrodite na wenzake hawakumweleza kuhusu hii jamii maana kama na wao walikuwa wakitumia nguvu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi basi wangewalaetea mtafaruku wakati walipokuja duniani.
“Kama ni hivyo je unadhani swala hili linaweza kumuhusu Edna?”
“Lazima liwe linamuhusu , nadhani mpaka sasa huna taarifa, ukweli ni kwamba mpaka sasa mtoto wa pekee wa Raisi Jeremy hafahamiki alipo , ijapokuwa taarifa hio ni ya siri lakini hawezi kuificha kwa watu kama sisi ambao tunahusiano wa moja kwa moja na serikali, kama hisia zangu zitakuwa sahihi basi naamini anataka kumfanya Edna kuwa mrithi wake”Aliongea na kumfanya sasa Roma kuelewa kitu.
“Nadhani ndio maana alionekana kuwa na haraka ya kumtaka Edna kumtambua kama baba”
“Unamaanisha alishaanza kuongea na Edna?”
“Siku ambayo niliwaona hao watu kutoka Panas ndio wakati ambao alifika nyumbani kwetu kwa ajili ya kuongea nae , lakini inaonyesha Edna hakuwa tayari kukubali”
“Wasiwasi wangu ni kwamba ataishia kukubali na kama hilo litatokea mkeo anaweza akakuingiza kwenye mtego , mpaka sasa naamini Hongmeng ni maadui zako na hata jamii hio ya Panas sidhani kama wanakuchukulia kama rafiki au adui, Jeremy ndio mtu pekee ambaye atafanya kila kitu kwa faida yake na mawazo yake yote ni kuona Rwanda inakuwa kimaendeleo kwa kunyonya rasimali za nchi zinazomzunguka kupitia njia za kijasusi”Roma alijikuta akianza kuwa na wasiwasi, alijua msimamo wa Edna ulivyo likija swala la familia.
“Lakini sidhani Edna anaweza kuwa mwepesi namna hio”Aliongea Roma.
“Hata mimi natumaini asiwe mwepesi wa kukubali kila kitu”
“Okey, nimekuja kurelex sio kuongea mazungumzo haya , hebu tuendelee na kilichotuleta”Aliongea Roma na kisha waliendelea kufanya shoping.
Ni muda wa saa saba wakati wakiwa kwenye mgahawa wakipata chakula cha mchana Roma aliweza kupata msisimko wa kuongezeka kwa mtu mwenye nguvu za kijini na kujikuta kugeuza shingo yake kuangalia upande wa kulia na palepale aliweza kumuona Omari Tozo akiingia eneo hilo.
Omari alikuwa amevalia mavazi ya suti na kwa mwonekano wake ni kama vile amekuja hapo ndani kwa ajili ya kuonana na mtu , baana ya kukagua baadhi ya watu palepale aligeukia upande wa aliposimama Roma na kisha akatabasamu na kupiga hatua kumsogelea.
Tokea siku ambayo waliweza kuhudhuria harusi yake hawakuwahi kuonana tena.
“Madam Neema nadhani hutonilaumu kwa kuingilia muda huu mzuri kwenu wa chakula cha mchana nikimchukua kwa dakika huyu kiumbe , si ndio?”Aliongea Omari huku akiweka tabasamu.
Kwa muonekano wa Omari alivyo alijua tu kuna kitu anahitaji kuongea nae.
“Nadhani ndoa tamu , naona una mabadiliko makubwa ya kiafya”Aliongea Neema kwa utani na kumfanya Omari kutoa cheko kama kawaida yake.
“Nadekezwa mwenzenu , nashindwaje kunenepa sasa”Aliongea na kisha wakasogea meza ya pembeni kwa ajili ya kuongea,.
“Kwa muonekano wako nadhani hatujakutana hapa kwa bahati mbaya si ndio?”
“Upo sahihi , nipo hapa kwa niaba ya serikali chini ya TSS kukuuliza maswali kadhaa ya kiusalama”
“Maswala ya kiusalama , tangu lini serikali ikaniuliza maswala ya kiusalama wakati mimi ni rais mwema?”Aliuliza Roma kwa mshangao.
SEHEMU YA 550.
Roma alijua sio rahisi kwa Omari kumtafuta na kutaka kuongea nae maswala ya kiusalama , lazima kutakuwa na kitu ambacho kinaendelea ambacho yeye hakifahamu , imepita wiki kama tatu tokea The Eagles kuondoka Tanzania na kurudi visiwa vya Mediterranian hivyo hakuwa na chanzo sahihi cha taarifa.
Aliwaondoa kwasababu ya kwamba tishio la kiusalama lilishaisha kutokana na kumuua Yan Buwen na washirika wake akiwemo Mzee Longoli.
“Kwa muonekano wako naamini huna taarifa ya makundi ya watu waliongia Tanzania hivi majuzi?”
“Ndio sina taarifa nadhani mnafahamu The Eagles project yao hapa Tanzania imesitishwa na kurudi, kwasasa nipo mwenyewe tu hapa Dar es salaam”
“Ndio maana hujaweza kupata taarifa”
“Kuna nini kinachoendelea?”
“Intellijensia ya usalama wa taifa imeweza kubaini kikosi cha giza cha Siraha Kwenye Jiwe(SIS) kutoka Scotland ,Bunge la Kiza likijumuisha wanachama wao wa kundi la Camarilla na Sabbat wapo hapa nchini , kuna pia baadhi ya makundi madogo ya watu wanaotumia nguvu za giza pia wamefika”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa.
“Wamekuja hapa Tanzania , kwasabau gani , kama ni jiwe la Kimungu nadhani wanajua halipo chini ya umiliki wangu?”
“Nadhani hawajaja kwa ajili yako na isitoshe sidhani kama wana uwezo wakupigana na wewe”
“Kama sio hivyo kwanini wamefika?”
“Intellijensia tulioweza kuvujishiwa kutoka nje ya nchi ni kwamba wapo hapa kwa ajili ya siraha ya kichawi ifahamikayo kwa jina la Magical Girdle”Aliongea Omari na kumfanya Roma kushangaa kwani neno la Magical Girdle ashawahi kusikia.
“Unamaanisha siraha iliopo kwenye hadithi za miungu ya kigiriki ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Aphrodite?”
Katika hadithi za miungu ya kigiriki na kiroma , mungu wa urembo aliefahamika kwa jina la Venus kwa kirumi au Aphrodite kwa kigiriki alikuwa na siraha ya mvuto ya mshipi wa kichawi wa dhahabu ambao uliwafanya miungu mingine kuvutiwa nae sana kimapenzi.
Inasemekana alitumia siraha hio kuwapumbaza miungu na kutawala akili zao kihisia , alifikia hatua ya kushindana na Athena pamoja na Hera katika kujiongezea mvuto kwa kutumia siraha hio na alifanya miungu yote kumchagua yeye kama mrembo zaidi.
Lakini hata hivyo ni hadithi tu , kitu ambacho kilitungwa na binadamu wakiwa wamedhibiitwa kiakili ili kufanya binadamu wengine kuwaabudu viumbe hao waliovamia dunia na kuona Binadamu ni kiumbe dhaifu.
Sasa Roma hakuwahi kusikia kutoka kwa Christen kama kweli alishawahi kuwa na siraha hio ya kichawi ifahamikayo kwa jina a magical Girdle lakini kama ilivyokuwa kwa Hades wa zamani kutokumuambia kuhusu siraha yake ya Helmeti of Invisibility(Helmet la kutokuonekana) wakati alivyomuachia urithi basi aliona huenda ni sawa kwa Christen pia.
Siraha za aina hio hata hivyo hazikuwa na maana sana kwa viumbe hawa wa sayari nyingine ambao wameishi hapa duniani kwa muda mrefu , kutokana na kwamba wanakosa miili yao halisi.
Na Roma aliona kama Christen kweli alikuwa na huo mshipi kwa alivyokuwa akimtamani huenda angeshaidhibiti akili yake na kumfanya alale nae au kufanya zaidi ya hivyo na hana uhakika kama angeweza pia kutawala akili ya Zeus na wengine.
“Kama ni hivyo unamaanisha wanatafuta huo mshipi hapa Dar es salaam ,unamaanisha mshipi huo umeonaka hapa Tanzania?”
“Hata sisi hatuna uhakika pia , na tumeshindwa kuweza kujua taarifa kamili”
“Kama ni hivyo wamejuaje kama Mshipi huu wa kichawi upo hapa Tanzania?”
“Kuna mtu ambaye ametumia Mshipi huo wa kichawi kuwadhibiti wanajeshi wa kitengo maalumu na aliweza kuonekana kwenye Rekodi ya Vidio , hio Vidio ndio ambayo imesambazwa kwa Kundi la SIS , Bunge la Kiza na baadhi ya makundi madogo madogo, Eneo ambalo limeonekana kwenye Vidio hio ni katika kambi yetu ya kijeshi ya Ruvu”
“Kama unayo hio vidio unaweza kunionyesha?”Aliuliza Roma huku akianza kuwa siriasi na Omari alionekana alishajiandaa kabla ya kufika hapo na alitoa simu yake na kuchezesha kicha akamkabidhi Roma.
“Kwenye Vidio hio ilionyesha kivuli cha mtu mwenye ngozi nyeusi yaani muafrika akijaribu kutawala akili za wanajeshi waliokuwa katika Demo ya mazoezi ya siraha na kwa kutumia Mshipi wa Dhahabu palepale wale wanajeshi waligeukana wao wenyewe na kupigana risasi.
“Ni Vidio fupi sana , tukio hili mpaka sasa ni siri ya serikali na limetokea wiki iliopita , baada ya uchunguzi wa kina kufanyika na kivuli cha mtu kinachoonekana kwenye hio Vidio kutotambulika Serikali ilipanga kikao kuzima swala hili ili kubakia siri , lakini ajabu ni kwamba hio Vidio ilisambaa nje ya nchi kwa makundi hayo ya watumiaji wa nguvu za giza”
“Inasemekena pia mtu ambaye anatumia hio Dhana ametangaza kwamba ameipata kwabahati mbaya na anashindwa kufahamu namna ya kuitumia hivyo anapanga kuiachia kwa watu wengine wenye uwezo na ameificha ndani ya jiji la Dar es salaam na mtu ambaye atabahatika kuipata ndio atakuwa mmiliki”Roma alijikuta akiwaza kidogo kusharabu maneno hayo.
“Nadhani sio sawa ,kama kweli hio dhana ni yenyewe sidhani Aphrodite angeshindwa kuinasa kihisia, lakini mpaka sasa hakuna hatua aliochukua na isitoshe siraha hio haiwezi kutumiwa na mtu yoyote kwani inahitajika kuwa na nguvu ya kiuungu ndani yake, Kwahio hamjatambua kabisa hiko kivuli cha mtu ni nani na nia yake ya kufanya hivyo?”
“Bado hatujaweza kufahamu , ni swala ambalo ucunguzi wake unaendelea kwani mpaka sasa linaumiza vichwa vya wakuu wa majeshi , maana tukio la kupigana risasi wanajeshi kwa wanajeshi ni la kuogofya sana kwa usalama wa nchi”Aliongea na kumfanya Roma aanze kufikiri.
Kuna kipindi wakati alipokuwa Ufaransa watu walikusanyika kwa ajili tu ya kutaka kuipata siraha ya Thanatos , lakini sio hivyo tu hapa Dar es salaam ni kama tukio hilo linajirudia , kwani mara ya kwanza Dhana ya Holly Grail ilionekana Tanzania na makunndi ya nguvu za giza na za Nuru walifika na kuanza kupigana kuipata.
Roma mara baada ya kuwaza aliishia kucheka , alijua hata kama inaweza kuwa halisi , hakuna uwezekano kwamba wanaweza kuitumia kupumbaza watu kwani ni siraha inayomjua mmiliki.
“Lakini kwanini hili swala naona kama ni mtego , nadhani nyie watu msijisumbue , ngoja wafanye wanachoweza kufanya na sisi tuone”Aishauri Roma,
“Bro unapaswa kutusaidia katika hili , hawa watu kama itatokea wakahatarisha usalama wa nchi vikosi vyetu vya idara ya uchawi sidhani kama wanaweza kufanikisha kuwadhibiti na isitoshe wewe pi ni mtoto wa raisi na familia yenu imeweka mizizi katika usaama wa taifa”
“Ohoo!, siwezi hata kumdhibiti mke wangu mwenyewe, halafu nijihusishe katika haya mambo . kwanini niingilie?”Aliongea Roma akijaribu kukataa.
“Kama huwezi kuingilia tunalo ombi moja kwa sasa , wewe unafahamiana na miungu wenzako mathalani Aphrodite mungu wa urembo, kama kutakuwa na uwezekano wa kujitokeza na kutusaidia , maana kama watu hao wataanzisha vurugu mambo yanaweza kuwa nje ya uwezo wetu”Roma alifikiria kidogo.
“Okey nitampigia simu baadae”
“Mpigie sasa hivi Bro wakuu wanasubiri majibu muda huu”Aliongea kwa msisitizo na kumfanya Roma kukosa neno la kuongea na palepale aliamua kutoa simu yake na kutafuta namba ya Christen na kupiga na iliita kwa muda mrefu kidogo lakini Roma hakukata tamaa kwani alijua muda huo Los Angeles itakuwa ni usiku kukikaribia kupambazuka.
“Hades , are you calling to ask me about Magical Girdle too?”Aliuliza akimaanisha kwamba je anampigia kwa ajili ya kuulizia mshipi wa kichawi pia.
“Ndio”Alijibu Roma.
“Mshipi wangu wa thamani kubwa haujaibiwa , ninao siku zote hivyo naomba usiulizie tafadhari , Mshipi ambao umeonekana kwenye vidio unafanana sana na wa kwangu lakini ni feki , kuna wachawi wengi wa kiroho dunia hii, kwa mfano kundi la kichawi la Siraha kwenye Jiwe wanaweza kutengeneza udanganyifu , hivyo kwanini iwe dhana yangu ya Mshipi wa dhahabu”Aliongea kwa namna ya kujitetea na kukereka kwa wakati mmoja na kumfanyaRoma kukunja sura.
“Kwanini sasa unaonekana kuwa na hasira , miimi nimepiga simu kwa niaba ya jeshi la Tanzania kitengo cha wachawi kwani hawana uwezo wa kukuuliza moja kwa moja na isitoshe nilijua usingeshindwa kunasa kihisia pale mtu anapotumia dhana yako”
“Tatizo mnanisumbua , muda si mrefu Poseidon ,Hermes na Artemis wamenipigia na kuniamsha kwenye usingizi , naomba usijihusishe , waache watafute kama wanavyoamani lakini kama utagundua muhusika wa kuzusha uongo huo ni nani niambie nitahakikisha namchuna ngozi akiwa hai”
“Sawa lakini kwa nilivyosikia kundi la Sabbat pia lipo hapa nchini , nadhani chuki zako uzielekezee kwa Raphael kwani ndio kiongozi wa kundi hilo ambae ameagiza watu wake kuja hapa nchini na wakafatia kundi la Camarilla”
Raphaeli ndio kiongozi wa kunti la Tzimisce ambaye anatumia mwili wa Vampire , ni kiumbe kutoka sayari nyingine ambaye alifanya watu duniani wamuabudu kwa kumuita Hermes mchunga kondoo.
“Hermes ni mtu wa ajabu na sipendi kuongea nae, nadhani amefanya hivyo kutokana na kuficha uhusika wake, mpaka sasa hakuna Vampire anaemfahamu kwa jina la Hermes, Hades nitakuw amkweli kwako kila dhana ambayo tulikuja nayo imeunganishwa na roho zetu kuna zile zilizopotea na tulizobakiwa nazo , ndio maana hata Artemis aliweza kuhisia uwepo wa Selene nchini Korea kusini licha ya kwamba alikuwa umbali wa takribani nusu ya dunia, mpaka sasa dhana pekee ambayo imepotea na na imeshindikana kufahamika imepotelea wapi ni Helmeti la kutokuonekana ambalo ni siraha yako , kama hujui, Helmet hilo ni kama taji na nitofauti sana na dhana tulizokuja nazo kwani teknolojia yake ilikuwa ni ya hali ya juu sana na Hades wa dhamani kwasababu alikuwa ni mwanasayansi ndio anajua siri yake”
“Ndio maana Hades wa zamanni sikuwahi kumuona nalo , kumbe ni dhana ambayo haionekani”
“Nadhani umeelewa sasa narudi zangu kulala , kama utakuwa na muda naomba uniangalizie nani kaanzisha huo uvumi , niambie na nitakuja kumuua mwenyewe , anadhani kujificha Tanzania siwezi kumpata na kumuua”
“Kuhusu hilo usijali nitakusaidia ,lakini na mimi utanisaidia kujibu maswali yangu yote ya kile kilichotokea Korea kusini bila kunificha kitu”Aliongea Roma na kauli yake ilimfanya Christen kuwa kimya.
“Nilishakujibu tokea muda mrefu hukuzingatia ndio maana , mimi nalala”Aliongea na kisha akakata simu na kumfanya Roma kukuna kichwa chake na kujiambia atajua tu ukweli wote kuliko mambo nusu nusu wanayomwambia.
Roma ilibidi amwelezee Omari juu ya alichoweza kupata na wote walijikuta wakiwa na ahueni na aliwathibitisha hakuna mgogoro unaoweza kutokea baina ya wageni hao kama tu Mshipi huo hautakuwa halisi.
“Asante sana Bro , nadhani napaswa kuondoka sasa nikuache na shemeji, tutakutaarifu tukimpata muhusika”
“Haina haja ya kunifahamisha , hilo ni swala ambalo halinihusu”Aliongea na Omari aliaga na kuondoka.
Neema hakumuuuliza sana maswali Roma juu ya kile ambacho alikuwa akiongea na Denisi , kwani mara baada ya kurudi kwenye meza walikula chakula kama wapenzi huku wakishushia na mvinyo.
Wikiend nzima Roma alimalizia kwa Neema Luwazo na walipika na kupakua na alimsaidia pia kwenye kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Siku ya jumatatu mara baada ya kuamka mawazo ya Edna yalianza kukisumbua kichwa chake na wakati alipokuwa akipata kifungua kinywa kilichoandaliwa na Neema alimkumbuka na alijiambia kutokana na anavyo mjua Edna muda huo atakuwa hajapata chochote , hivyo alimwambia Neema amwandalie vitu vya kuondoka navyo kwani anampelekea mke wake, aliongea bila ya kupindisha kauli.
Neema baada ya kuambiwa hivyo alimuonea wivu Edna lakini aliishia kuandaa kwani alijua yeye ni mchepuko tu na ili aendeee kufurahia penzi na kijana huyo mdogo basi ni kuhakikisha anamfurahisha na kumsapoti kwa kila kitu na isitoshe anapata faida kubwa ya kuvuna nishati kitu kitakachompeekea kuwa mrembo muda mrefu.
Roma asubuhi hio mara baada ya kufika nje ya ofisi ya Edna aliweza kukutana na Recho ambaye alikuwa akitoka katika ofisi ya Edna na kwa haraka haraka alijua huenda alikuwa akisafisha na kuweka mazingira sawa lakini aligundua sio hivyo mara baada ya kuona amebeba mabakuli na juisi kwenye mfuko wa plastiki.
Hakuwa amemuona Recho kwa muda mrefu kidogo ni kama zaidi ya miezi mwili , lakini alionekan hakuwa amebadilika sana zaidi ya kwamba kipindi hiko alionekana ni mwanamke mwenye kujiamini sana kuliko alivyokuwa mwanzo na ni kama urembo wake umeongezeka zaidi.
“Ni wewe .,… nikajua Boss ndio amefika”Aliongea huku kidogo akionyesha hofu.
Tokea kitendo kilichotokea miezi kadhaa iliopita ilifanya wao kujihisi vibaya kila pale wanapokutana .
“Edna yuko wapi , bado hajafika kazini?”Aliuliza Roma na kumfanya Recho kushangaa kidogo.
“Kuna chochote kilichotokea kati yako na Boss? Kwanini amehamia Msasani?”
“Nadhani haina haja ya kuongelea hilo kwasasa”Aliongea Roma maana hakutaka kutanganza matatizo ya ndoa yake hadharani.
“Ulichobeba ni kifungua kinywa kwa ajili ya Edna?”Aliulizia Roma kupotezea mada.
“Ndio , amenipigia simu nimwandalie ..”Aliongea Sekretari Recho huku macho yake yote akiwa ameyaelekeza chini , alikuwa na aibu za kike kwani alishindwa kumwangalia Roma usoni.
Ukweli ni kwamba Recho licha ya kwamba alikuwa na maisha mazuri na kule kukataliwa na wanaume kuisha , lakini akili yake haikufuta tukio la kufanya mapenzi na Roma , ni tukio ambalo muda mwingine hujirudia hata wakati anapofanya mapenzi na mpenzi wake mpya na kadri siku zinavyozidi kuendelea ndio ambavyo tukio lilizidi kutawala akili yake lakini hakupata ujasiri wa kumsogelea Roma tena kwani ni mke wa bosi wake na aliogopa ikija kugundulika , kwani maisha yake wakati huo na familia yake yalikuwa mazurri kutokana na mshahara mnono pamoja na posho anazopata kutoka kwa Edna.
Muda huo ambao hawakuwa wakijua ni topiki gani waendelee nayo kuongea wakimsubiria Bosi hatimae Edna alitokea kwenye lift na kuingia eneo hilo na alijikuta akipatwa na ubaridi mara baada ya kumuona Roma mbele yake.
Jicho moja tu kwa Recho ni kama aliona lazima kuna kitu kilichotokea kati ya Roma na sekretari wake na hapo hapo alizidi kuongeza ukauzu wake.
“Boss karibu kazini , nimekuandalia ulichoniagiza”Aliongea Recho kwa mtindo wa heshima kwa bosi huku akiwa na afadhali.
Edna alimpita Roma kama hamjui na kisha alimsogelea Recho na kuchukua mfuko alioshikilia mkononi na kisha akatingisha kichwa kama ishara ya kushukuru na kupiga hatua kuingia ofisini kuingia kwake , lakini kabla hajafikia mlango Roma alianzisha maongezi.
“Edna na mimi nimekuletea kifungua kinywa mke wangu, niliju tu muda huu utakuwa hujapata chochote”Aliongea huku akimwonyeshea mfuko alioshikilia na Edna alijikuta akitoa kicheko hafifu cha kukera.
“Una uhakika umeleta kwa ajili yangu?”
SEHEMU YS 551.
Upande mwingine nyumbani kwa Afande Kweka mara baada ya Lanlan kufika nyumbani hapo akiwa ametangulizana na Qiang , aliweza kupokelewa kwa furaha na wazee wawili ngozi tofauti ,mmoja akiwa ni Mzee Kweka mwenyewe na mwingine alikuwa ni Pastor Cohen.
Pastor Cohen mara baada ya kumuona Lanan alimwangalia Afande Kweka kwa tabasamu kubwa na kutingisha kichwa kuonyesha ishara ya kukubali jambo.
Ukiachana na maswala mengi ambayo Afande Kweka na Pastor Cohen waliweza kuzungumza lakini kubwa zaidi ni swala la Lanlan kuwa mtoto wa Seventeen pacha wa Edna ambaye aichanganywa na Roma kwenye mpango LADO.
Pastor Cohen na Afande Kweka ndio watu ambao walioratibu mchakato wa kumuingiza Roma na Seventeen katika mpango LADO na moja wapo ya matokeo hayo ni uwepo wa Lanlan duniani.
“Komredi nikiri hapa hakuna ubishi , lakini nashindwa kuelewa inakuaje Roma kushindwa kumfahamu binti yake mwenyewe”
“Komredi hilo ni swali gumu kwangu , najua nilihusika kuwaingiza kwenye mpango LADO lakini uendelevu wake sikuhusika”
“Sio wewe tu ambaye hukuhusika , wote hatukuhusika, mpango LADO kumbuka ulikuwa chini ya Zeros organisation na sisi tulichokifanya ni kufuata maagizo ya kuchomeka watu ambao hawakuwa katika mpango ili kutengeneza mafanikio”Aliongea na Afande Kweka alionekan kutopinga.
“Nadhani imekuwa ngumu kutokumfahamu mtoto wake kutokana na kilichomtokea Seventeen”
“Nakuunga mkono , lakini bado kuna kitu nashindwa bado kuelewa , kama wewe umeweza kumfahamu mjukuu wako kwanini yeye baba ameshindwa hilo”
“Ukiniuliza hilo nitasema ni uzoefu lakini nikikujibu kwa niaba yake nitasema licha ya mengi ambayo yametokea lakini bado mtoto wake ameweza kurudi nyumbani kumfuata , damu ni nzito kuliko maji”
“Ningetamani kujua kila kilichotokea , nadhani mzee mwenzangu una shauku ya kujua pia nini kilitokea baada ya kupotea kwa ile ndege , kwani mpaka sasa ni mpango wa siri ambao ni watu wachache sana duniani wanaoufahamu”
“Ninatamani sana , lakini kwa uzee huu nadhani naweza kuangulie mbele za haki bila kujua kile kilichotokea”Aliongea na kumfanya Pastor Cohen kutingisha kichwa.
“Wewe ni mimi Komredi hatuna haja ya kuwa na huzuni ilimradi tulichokifanya kinakwenda kuisaidia dunia , kwasasa nadhani shauku yangu imetimia sasa , nimemwona kitukuu chako, nadhani ni muda wa mimi kuondoka , lakini kabla ya yote nataka kukueezea kile kinachoendelea ndani ya umoja”
“Nakusikiliza Komredi”
“Kwasasa ndani ya kundi , kuna ‘interval’ kubwa ya tarehe katika kalenda kwa kile ambacho wanachana wanapaswa kufanya”
“Unamaanisha nini Komredi?”
“Ukiachana na taratibu za kawaida ambazo zinaendelezwa kufanywa na wanachama kwa sasa kinachosubiriwa ni siku ya kwanza ya mvua ya theluji kwa bara la Afrika”Aliongea na kumfanya Afande Kweka kushangaa.
“Mvua ya kwanza ya Theluji katika bara la Afrika , unamaanisha Tanzania Mvua ya Theluji itawezekana kunyesha?”
“Hakika , ndio ishara kubwa inayosubiriwa “
“Ishara hii inamaanisha nini?”
“Katika umoja wetu ishara hii inamaanisha ule wakati uliosubiriwa umetimia ni kama unabii umetimia , kwa upande wa Illuminat na Allien kwao ni ishara ya utawala wao duniani kuanza”
“Nini kitatokea baada ya hapo?”
“Kwasasa hakuna majibu sahihi ,mpaka itakapojulikana ni kipi kingine kinapaswa kufanyika kulingana na Kalenda , lakini mpaka sasa tunaweza kufanya makisio, nadhani unajua nini kinasababisha Theluji?”
“Najua ni Baridi?”
“Sahihi kabisa, makisio ni kwamba kuna uwezekano joto la dunia kushuka katika viwango vya chini sana kiasi cha kupelekea bara la Afrika kuweza kupitia vipindi vya majira ya mvua ya Theluji”Aliongea na kumfanya Afande Kweka kushika kidevu , ijapokuwa hakuonyesha mshangao wake waziwazi lakini ilikuwa dhahiri taarifa hio ilikuwa ya kumshangaza.
*****
Roma alijikuta akishangazwa na swali la mke wake kwani hakuwa amemulewa kabisa , alimbebea yeye kifungua kinywa lakini tena anatilia mashana nia yake ya kumletea.
“Edna unamaanisha nini?”
“Nadhani Recho hajapata kifungua kinywa bado , usipoteze hela zako kwa mtu kama mimi , nitajifanya sijaona chochote”Aliongea na Roma palepale aliweza kuelewa anachomaanisha na kushindwa kuzuia hasira zake .
“Edna hata kama unataka kuonyesha hasira zako hupaswi kwenda mbali hivyo , ndio nimefika sasa hivi na kukutana na Recho hapa , hata kama unadhani sina jema lakini huwezi kuongea hivyo kwa kumsingizia msaidizi wako”
“Nimeonyesha wapi hasira? , au umeelewa vipi kauli yangu , kwanini unajishtukia kama huna hatia?”Aliongea na kumfanya Roma kuwa katika mtego wa maneno.
Alikuwa na hasira na kauli ya Edna lakini alishindwa kukataa wala kukubali , kwani ni kweli kuna dhambi ambayo alishawahi kufanya na Recho.Aliona kama angekataa asingeweza kuituliza roho yake yenye dhamira ya kuhukumu.
“Madam , tafadhari naomba usituelewe vibava Mr Roma amenikuta hapa na amekuletea kifungua kinywa , hakuna chochote kinachoendelea baina yetu naomba usifikirie hivyo tafadhari”Aliongea kwa uwoga huku akiangalia chini.
Roma baada ya kumuona namna ambavyo Recho anajitetea ilimfanya amuonee huruma , kwani alikuwa kwenye hali ya taharuki mno , alikuwa kama mtu ambaye amekamatika katika jambo na sasa anahofia kibarua chake kuota nyasi.
“Recho wewe unaweza kutumia hiki kifungua , kama mtu hataki haina haja ya kumlazimisha ilihali wahitaji wapo”Aliongea Roma na kuweka kwenye miguu ya Recho ule mfuko na kisha aliondoka hilo eneo na kuzisogelea lift.
Recho mara baada ya kuona ameachiwa msala alitamani kupiga magoti , lakini palepale aliushika ule mfuko kwenye sakafu na kisha akamnyoshea Edna aupokee.
“Madam naomba usimfikirie vibaya , Mr Roma kakuletea hiki kifungua kinywa kwa ajili yangu naomba ukichukue..”
Edna aliangalia ule mfuko aliopewa na Recho ulivyotuna na kisha alimsogelea Recho na kuuweka chini.
“Unaweza kuchukua na hiki pia , sina hamu ya kula chochote leo”Baada ya kusema hivyo aliingia ofisini kwake.
Recho aliona siku hio imeanza vibaya sana kwake , alijikuta akiangalia ile mifuko yote miwili , alioleta Roma na alioleta yeye mwenyewe na kujikuta akikosa cha kufanya kwani aliishia kusimama katika sehemu moja bila ya kusogea.
**********
Upande mwingine katika ofisi ya Raisi Senga asubuhi hio , Raisi wa nchi ya Tanzania akiwa ofisini kwake akiendelea na majuku yake , aliweza kufika Kabwe nje ya ofisini huku ameshikilia faili mkononi na baada ya kuruhusiwa kuingia ndani moja kwa moja alimsalimia Mheshimiwa.
“Vipi kuna jipya , kuna chochote ambacho mmefanikiwa kupata?”Aliuliza Raisi Senga kwa shauku.
“Mheshimiwa mpaka sasa hatujapata mwanga wowote wa kumpata Denisi , lakini vijana wamejjitahidi kutafuta taarifa ambazo kwa kiasi flani zinatupa tafsiri ya kile kinachoendelea”Aliongea Kabwe.
“Nipe taarifa”
“Kuna baadhi ya watu hapa nchini tuliweza kuwahoji , mmoja wapo ni Abubakari Hamadi mtoto wa Mzee Alex mmiliki wa kampuni ya JR na mwingine ni Elvis Temba mtoto wa Mkuu wa mkoa wa Dodoma”
“Na mlichogundua ni kitu gani?”
“Nadhani Denisi alikuwa na mpango anaoendeleza yeye na Yan Buween kwa siri hapa nchini kwani kwa maelezo tuliokusanya ni kwamba aliwaambia marafiki zake wote kwamba kuna kitu ambacho wanapanga kumfanyia Roma”
“Lakini Yan Buwen si ameshakufa?”
“Hili ni tukio ambalo limetokea miezi takribani mitano nyuma Mheshimiwa kabla hata ya mheshimiwa Kigombola na Yan Buwen kufariki”
“Kama usemayo ni sahihi basi hayapingani na taarifa tulioweza kupata ya Denisi kuwa na uwezo wa ajabu si ndio?”
“Ndio Mheshimiwa”
“Kama ni hivyo kapotelea wapi?, mwezi wa pii na nusu huu haonekani nyumbani na mbaya zaidi kakomba hela zangu zote zilizokuwa chini ya jina lake katika visiwa vya Shelishei , kapeleka wapi pesa zote hizo?”
“Mheshimiwa nadhani swala hili linahusiana na kinachoendelea nchini Rwanda kwani kati ya marafiki wa karibu wa Denisi ni Desmond mtoto wa Raisi Jeremy”
“Nimejaribbu kumuhoji Jeremy lakini anakuwa mgumu wa kufunguka , lakini chanzo kinaanzia katika kifo cha mke wake, sijui nini ananificha kwasasa inanipa wasiwasi kuhusu Denisi mahali alipo kama yupo salama”
“Mheshimiwa kwanini usifanye kama ambavyo Madam anapendekeza , nadhani Mr Roma atakuwa na majibu sahihi zaidi”Alipendekeza Kabwe na kumfanya Raisi Senga kusimama akitoka kwenye kiti chake.
Ukweli ni kwamba Raisi Jeremy familia yake haikuwa na amanni hata kidogo na yote hayo ni juu ya swala la kupotea kwa Denisi , lakini vile vile kuwa na uwezo wa ajabu ambao alikuwa na uhakika ni uwezo ambao amepewa na Yan Buwen.
Mama yake Denisi yaani Damasi alikuwa na mawazo sana na muda wote ni mwenye kumbebesha Lawama mume wake kwa kutokuwa makini na mtoto mpaka kufikia katika hatua ya kupotea.
Ilikuwa ni miezi miwlii imepita sasa , tokea Denisi alivyopotea ghafla mara baada ya kuweza kukwapua kiasi kikubwa cha pesa cha baba yake alichokificha katika visiwa vya Shelisheli.
Hofu ya Damasi ni kwamba alijua fika kuna uwezekano kuna jambo baya ambalo Denisi analiandaa na hilo linaweza kumuweka katika hatari ya kuuliwa na Roma kwani kwa muda mrefu alishaweza kufahamu kinyongo cha Denisi kwenda kwa kaka yake , hivyo hofu yake ilikuwa ni kubwa mno huku akimlazimisha mume wake kuchukua hatua za haraka kuweza kunusuru hali hio kabla kubwa zaidi halijatokea.
Kilichomshangaza zaidi Senga ni kwamba tukio ambalo linamtokea yeye mwenyewe ni kama linalomtokea rafiki yake Jeremy raisi wa Rwanda, kwani wote watoto wao wa kiume ambao wanaamini kuwa warithi wao hawaonekani walipo na kila dalili inaonyesha hawawezi kuwa sawa tena.
Ilikuwa ni afadhali kwa Raisi Senga kwani alikuwa na Ashley ambaye ni mkubwa na angemrithisha kila kitu chake , lakini bado sheria za ukoo wako zinampa nafasi kubwa mtoto wa kiume.
“Kabwe nadhani kwasasa sina jinsi , ni muda sahihi wa kumkubali Den.. namaanisha Roma kama mtoto wangu”Aliongea Raisi Senga na kumfanya Kabwe kidogo kutoa macho ya mshangao.
“Mheshimiwa unataka nifanye nini?”
“Blandina aliniomba nimsaidie yule msichana Najma nafasi serikalini kama hatua ya kwanza ya kujenga uhusiano wangu na Roma nadhani kwanza nitekeleze hilo”
“Ndio mheshimiwa nitakuletea faili lake”
“Haina haja, fanya utaratibu wa kuangalia nafasi gani itaweza kumfaa katika Wizara ya elimu”
“Sawa mheshimiwa”
“Kingine nitaenda nyumbani kuonana na mzee jioni ya leo na nitapata chakula cha usiku huko huko”
“Sawa mheshimiwa nitaandaa itifaki?”Aliongea na kisha akampa ruhusa ya kuondoka na kumfanya Raisi Senga kuonekana kuwa katika mawazo.
“Huenda uamuzi wangu ukawa sahihi , nikirudisha ukaribu na Roma na kuzuia hatari yoyote kumtokea Denisi nitaweza kupata faida nyingine , naweza kuushinda udhaifu walionitengenezea Freemason na naweza kurudi kwenye mstali kama kiongozi wa taifa hili”Aliwaza mheshimiwa Senga lakini muda ule ule katibu Muhtasi aligonga mlango na kumshtua katika mawazo na aimruhusu kuingia.
SEHEMU YA 552.
Ilikuwa ni saa moja za jioni , haikueleweka Roma alishinda wapi lakini muda huo alionekana ndio kwanza anarudi kuelekea Ununio nyumbani, alikuwa na haraka kwani alikuwa na miadi na Rufi siku hio kwenda kula chakula cha usiku nyumbani kwa Bi Wema , kwani tokea Bi Wema anunue nyumba ambayo anaishi na Rufi mtoto wake wa kike hakuwahi kufika.
Sasa wakati akiwa Tegeta aliweza kupokea ujumbe wa meseji ambao ulimfanya atabasamu kifedhuli ulikuwa ni ujumbe unaotoka kwa namba ambayo hajaisajili kwenye simu yake lakini kutokana na kilichotokea dakika chache zilizopita alijua nani katuma ujumbe huo na alishangaa kwa kuona kwamba mtu huyo hakuwa amekata tamaa , kwani ilikuwa ni kama mwezi mmoja umepita huenda na zaidi tokea akutane nae.
Dakika chache nyuma wakati akiwa anatokea Mbagala akiwa anapita uwanja wa taifa aliweza kugundua kuna gari inamfuatilia nyuma na licha ya kugundua hilo hakutaka kwanza kumchezea mchezo mtu aliekuwa akimfuatilia , kwani aliendesha gari kusonga mbele bila wasiwasi lakini alipokuja kupita katika daraja la Kijazi interchange Ubungo ndio alipanga namna ya kumpotezea mtu ambaye alikuwa akimfatilia nyuma nyuma.
Mtu aliekuwa anemfuatilia alikuwa ashamtambua na ilionekana pia hata mtu huyo ashajua kama ashajulikana kutokana na kwamba alikuwa akisambaza nguvu za kijini na kwa kufahamu uwezo wa Roma alijuwa atakuwa amehisi uwepo wake, lakini haikumkatisha tamaa kutimiza dhamira yake.
Roma mara baada ya kuingia katika barabara ya Sam Nujoma sehemu pekee ambaye aliamini anaweza kumpoteza mtu anaemfatilia ni eneo la Mwenge Mataa na kweli aliweza kufanikisha hilo kwani alihakikisha alikuwa mbele kabisa anagalau mbele ya magari mawili kutoka kwa mtu anaemfatilia na hio alilifanikisha na wakati tu ambao anakaribia Mwenge taa za kijani zilimruhusu kupita lakini kitendo cha kupita tu taa za rangi nyekundu ziliwaka na kuzuia magari yaliokuwa nyuma yake kupita.
Ilikuwa ni tukio la kushangaza kwani ilionekana kwa wale wanaoendesha magari kama taa hizo zilikosea kimahesabu katika kupitisha magari kwani taa iliwaka kwa sekunde sita tu na kuzima na kisha ikawaka nyekundu.
Mtu aliekuwa akimfatilia Roma katika gari aina ya Toyota Camry alitoa tusi kwa lugha ya kichina huku akigonga usukani kwa hasira na kujiapiza.
Sasa Roma alipokuwa katika eneo la Mbuyuni akikaribia Tegeta aliweza kupokea ujumbe kutoka kwa namba ambayo hakuwahi kuisevu lakini alikuwa akiikumbuka ilikuwa ikimtumia meseji za ajabu ajabu.
Roma licha ya kwamba aliweza kumpoteza mtu huyo lakini wasiwasi wake ni kwa Rufi kwani aliamini kama mtu huyo ataendeea kumfuatiia na kujua anapoishi na kuja mara kwa mara basi nafasi ya kumuona Rufi ingekuwa kubwa.
Ndio alikuwa ni msichana wa kichina afahamikae kwa jina la Xiao Xiao ambaye kwa maelezo ya Rufi alikuwa anatokea katika familia ya wakwe zake katika ulimwengu wa jamii za watu wasionekana za kichina.
Roma alipotezea kwanza swala hilo na kuwa na umakini katika kuendesha gari kwani muda umeenda, ndani ya dakika chache tu aliwea kufika nyumbani kwake na laishangaa kumkuta mtu akiwa amesimama nje ya geti na alipoangalia kwa umakini alikuwa ni Rufi na ilionyesha alishindwa kuingia ndani kwani alikuwa amefunga geti kabisa wakati wa kutoka.
“Rufi kwanini umenisubiri hapa, ungekaa nyumbani kwenu tu ningekukuta”Aliongea Roma mara baada ya kusimamisha gari.
“Ni sawa tu , nilikuwa nikipata hewa safi ya bahari”
“Msichana mjinga , huwezi kuvuna nishati za mbingu na ardhi na mishipa yako ya damu ni myembaba kwasasbu ya kiwango kikubwa cha nishati ya Yin, unatakiwa ujali afya yako upepo kama huu unakuumiza”
“Kweli?”
“Ndio”
“Nilipatwa na wasiwasi maana sikukuona siku zaidi ya tatu zote , nilikuwa na shauku kubwa ulivyosema utakuja kuungana na sisi kwa ajili ya chakula cha usiku, niishindwa kuvumilia ndani ndio maana nikaja kukusubiri hapa”Aliongea na kumfanya Roma kuguswa na matedo yake na kumwambia aingie kwenye gari waelekee nyumbani kwao , kwani ilikuwa ni upande wa pili.
Baada ya kufika na kuingiza gari ndani Roma alishuka na kumfugulia Rufi mlango na kisha alimshika mkono na kumfanya mrembo huyo kutoa tabasamu na kuona aibu kwa wakati mmoja.
Bi Wema alikuwa amenunua nyumba nzuri , ijapokuwa haikuwa kubwa kama ya kwao , lakini ilitosha familia ya watu saba na mazingira yake yalikuwa mazuri pia kufanya watu wanaoishi hapo kuonekana wa kipato cha juu , lakini ajabu kwake ni kwamba hakuwahi kuingia ndani , licha ya kwamba alipafahamu.
Baada ya kuingia ndani aliweza kuona ubunifu wa mapambo ya ndani haukuwa na utofauti na nyumbani kwake , kitu kidogo kiichotofatiana ni kwamba nyumba hio haikuwa na mapambo mengi eneo la sebuleni , ubunifu wake ulikuwa ni ule wanaoitwa Simple enterior design.
Bi Wema alitoka akiwa ameshikilia mabakuli akionekana alikuwa jikoni akiandaa chakula.
“Sir ushafika , karibu sana ndio naandaa chakula na kuna vitu vichache naendelea navyo muda si mrefu chakula kitakuwa tayari , karibu uketi”Aliongea Bi Wema kwa ukarimu.
Ukwei Bi Wema hapo alikuwa akimchukulia Roma kama Mkwe wake sio kwa Edna bali kwa mtoto wake wa kike Rufi.
“Halafu nimesahau kwenye gari nimenunu samaki , ngoja nikawalete”Aliongea Roma akitaka kutoka lakini Bi Wema alimzuia na kumpa kazi hio Rufi aifanye na Roma alitingisha kichwa kukubali na kumwachia Rufi ufunguo.
Muda wa saa mbili wakati Roma aipojikaribisha Mezani kwa ajili ya kushambulia chakula mlango wa kuingiia ulifunguliwa na kumfanya Roma ageuke na kumwangalia mgeni aliefika.
“Aisee, kunanukia vizuri jamani , naona nimechelewa , Bi Wema , Rufi nimekuja tena”Ilikuwa ni sauti ya Amina na kiswahili chake kisichonyooka na alijikuta akishangaa baada ya kumuona Roma pia yupo kwenye meza.
“Mpenzi kwanini uko hapa , na wewe umekuja kwa ajili ya chakula cha usiku?”Aliuliza kwa kingereza.
“Kwannini inaonekana kama vile unakuja mara kwa mara?”Aliuliza Roma huku akiwa ameupamba uso wake na tabasamu kwa furaha ya kumuona huyo mrembo na alishangazwa siku hio kumuona Amina akiwa amevalia Shungi kichwanni na kumfanya kupendeza zaidi.
“Anasema hajisikii kula peke yake , lakini pia anapenda mapishi ya Mama , amekuwa bize kwenye siku hizi chache hatujaonana kwa muda”Aliongea Rufi.
Amina kutokana na baba yake kusafiri kwenda nje ya nchi kimatibabu kwa mara nyingine alijikuta akiishi peke yake , kutokana na kwamba hakuwa na uzoefu na maswala ya biashara za baba yake ilimchukua muda mrefu kukaa kazini na kukamilisha majukumu yake.
“Mr unaweza ukawa hujui , ukweli ni kwamba Amina na Rufi ni marafikii wakubwa na kipidi ulipokuwa nnje ya nchi walikuwa wakitoka mara nyingi pamoja kufanya shopping na aimfundisha pia namna ya kujiremba”Aliongea Bi Wema.
“Yeah mimi sio kama nakula bure nafanya juhudi pia”Aliongea Amina na kisha aliweka chini mifuko aliokuja nayo na kusogea mezani.
Roma aligundua hakuwa makini na hawa wanawake, hakuwa na uelewa kwamba Rufi na Amina wamekuwa marafiki kama iivyokuwa kwa Dorisi na Rose kuwa marafiki, lakini ilileta maana , ukiachana na kwamba wote hawakuwa wakielewa vizuri kiswahili lakini pia walikuwa na tabia zinazoendana.
Muda wote wa chakula Amina alikuwa akipiga stori na Rufi ambazo hazikuwa na miguu wala kichwa na Roma hakutaka kuingilia zaidi ya kuweka umakini wake kwenye kula.
“Halafu sikukuona wiki nzima , ulikuwa umeenda wapi?”Aliuiza Rufi na kumfanya Amina kushika shingo yake kuizungusha kuonyesha ishara ya kuchoka.
“Nimekuja kugundua kuongoza kampuni sio mchezo , tokea nirithi nafasi ya baba yaani mambo ndani ya kampuni ni mengi , wakurugenzi wa bodi kazi yao ni kunilalamikia hili halipo sawa lile halipo sawa khaa”
“Nini kimetokea kwani?”
“Washindani wetu wa kibiashara wanahati hati ya kupata tenda ya kufunga mitambo ya gesi kwenye baadhi ya hoteli na majumbani hio ni mara baada ya kupata uwekezaji mkubwa kutoka nje ya nchi , nadhani unajua tunajihusisha zaidi katika uwekezaji wa nishati , sasa kama zabuni hio tukikosa hisa za kampuni zitaporomoka maana washindani wetu wanasapoti kubwa serikalini”Aliongea huku akitia huruma.
“Lakini kampuni yenu si ilifanya Merge na baadhi ya biashara zilizokuwa chini ya Tajiri Khalifa Tanzania , bado kuna kampuni inayoweza kuwaletea ushindani?”
“Hakika ipo , mambo kwasasa yanabadilika sana tena kwa haraka sana , ni rahisi kujenga kampuni yenye msingi mzuri wa kibiashara kadri utakavyokuwa na rasilimali watu wenye talanta kubwa ya ubunifu lakini pia wenye ushawishi wa juu , Washindani wetu inapokea sapoti kubwa kutoka serikaini hivyo kazi lazima ifanyike kwa umakini katika kudili nao , najihisi muda mwingine kuzimia nikiwa ofisini”
“Hubby tafadhari msaidie Amina anatia huruma , wewe si una hela nyingi kwanini usinunue hio kampuni?”Aliongea Rufi.
“Ujinga , kwanini nifanye hivyo wakati hawajafanya hila yoyote , wameonyesha ushindani wa haki na kama nitaingilia kwasababu tu mimi tajiri itanifanya nionekane muhun na sina maadilii, hata kama nikifanikiwa kununua vipi kuhusu makampuni mengine lazima na yenyewe niyanunue ili kumuondolea ushindani, haina haja ya kuwa na wasiwasi , Amina hata kama kampuni yako ikifilisika nitakuwa na pesa za kuwatunza wote”
“Okey nimeelewa , lakini sipendi kuona akipoteza kampuni ambayo ndio kwanza amepewa kuongoza”
“Nilishawahi kujiambia kuongoza kampuni sio jambo gumu sana lakini tokea nilivyopewa majukumu yote na baba , niligundua ni kazi ngumu mno , kuna baadhi ya vitu najikuta kwenye Dilemma hata kuvitolea maamuzi , nimejikuta nikimkubali Dada Edna , Ameweza kuwa CEO wa kampuni katika umri mdogo lakini anazidi kung’ara tu”Aliongea kwa kulalamika , lakini mara baada ya kmtaja Edna moyo wa Roma ulishituka tena na hata hamu ya chakula ikapungua palepale.
“Sir sijawahi kukuuliza , Je ulienda kumtafuta Edna nakuongea nae kwenye siku hizi mbli , amekubali kurudi nyumbani?”Aliuliza Bi Wema mara baada ya kusikia jina la Edna, kwa wakati huo Bi Wema alikuwa akijua kingeereza licha ya kwamba alikuwa na ugumu kwenye kuongea lakini aliweza kusikia baadhi ya maneno na alijifunza kwa ajili ya Rufi.
Amina na Rufi walimwangalia Roma wakitaka kusikia jibu kutoka kwake kuhusu Edna, lakini swali hilo lilimfanya Roma kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Bi Wema nafikiri Edna hatorudi nyumbani hivi karibuni?”
“Kwanini unaongea hivyo , nini kimetokea?”Aliliza Bi Wema kwa wasiwasi na Roma hakuona haja ya kuwaficha na aliwaeleza mambo alioyafanya katika siku zote alizoenda kuongea na Edna na kuchomolewa.
“Bi Wema nashindwa kujua ni namna gani naweza kumaliza tatizo , nilimpelekea kifungua kinywa kwasababu nilikuwa nikimuwazia lakini badala ya kunipoktea alinishuku na Recho ambaye nilimkuta ofisini akiwa yeye hajafika kazini, kwanini akaanza kupandisha jazba na kutaka ugomvi?”Aliongea kwa kulalamika na kumfanya Rufi na Amina kiumwangalia kwa huzuni na walishindwa kuongea chochote.
“Mr Najua umekasirika namna ambavyo Edna anakufanyia lakini naamini anajua unafanya hayo yote kumbembeleza , lakini muda mwingine wanawake wanapofikiria kitu hawazingatii kipi ni sahihi na kipi sio sahihi wala kujali nani anatakiwa kuwajibika “
“Kwahio anataka nini sasa?”
“Mtazamo wako”
“Mtazamo wangu?”
“Ndio wanawake wanajali sana mtazamo wa mwanaume kwao , inaweza ikaonekena labda napindisha lakini hata kama amefanya makosa kukufanyia hivyo , mtazamo wako ndio tatizo , kwa mfano ulienda anapoishi kuomba msamaha lakini hukumtaarifu kwamba unaenda na ulienda kama vile atakusikiliza na kukusamehe hapohapo, nadhani hicho kimemfanya ajisikie vibaya zaidi , Edna anatabia ngumu sana kuzoeleka lakini ni mtu mkarimu na mwenye moyo mzuri, angekusamehe kama ungeongea nae vizuri , kuhusu kifungua kinywa cha leo nadhani usingemjibu wala kuonyesha kukasirika , alikuwa anajaribu kutafuta sababu tu ya kukukasirikia , sidhani kama alifikiria kweli kuna kitu kinaendelea kati yako na Recho”Aliongea Bi Wema na Roma aliona ni sahihi , alikuwa akijiamini sana mambo yangekuwa marahisi kwake kusamehewa , ijapokuwa aliomba msamaha kwa dhati lakini hakuonyesha uhatari wa kuona kwamba hatosamehewa alionyesha mwonekano ambao ni kama vile ni haki yake Edna kumsamehe na hapo ndio alipoona amekosea..
“Bi Wema upo sahihi , lakini bado naweza kusema mpaka sasa hatua ambayo tumefikia sidhani mambo yatakuwa marahisi na sioni sababu yake ni hasira zake juu yangu kumshuku au kuna mengine , sina mpango wa kumtafuta kwa sasa”Aliongea Roma.
“Unaonaje mimi nikienda na kuongea nae?”Amina aliongea na kumfanya Roma kucheka.
“Amina humuogopi Edna ?”
“Namuogopa ndio lakini sidhani kama atakataa kuonana na mimi , kwasababu siku zote ananichukulia mimi ni mwepesi kwake .. ninaweza kwenda na kumuuliza baadhi ya mbinu za kibiashara pia”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria.
Ijapokuwa aliona sio wazo zuri kwani lingemkasirisha zaidi Edna , ila aliona ni kheri Amina na yeye kwenda kujaribu maana yeye amekwama.
ITAENDELEA - MAWASILIANO 0687151346
Watsapp tunaelekea mwishoni mwishoni mwa hii simulizi... tunaelekea sehemu ya 700 wiki hii nicheki kama unahitaji mwendelezo