Simulizi ya Kijasusi: Salamu Kutoka Kuzimu

Simulizi ya Kijasusi: Salamu Kutoka Kuzimu

TUPIA COMMENT YAKO, TUANZE NA SIMULIZI IPI... SIMULIZI IKICHAGULIWA MARA 5 TUNAANZA NAYO.

KIGUU NA NJIA [emoji736]

SALAMU KUTOKA KUZIMU[emoji736]

MIKONONI MWA NUNDA[emoji736]

MALAIKA WA SHETANI

MTAMBO WA MAUTI

ZAWADI YA USHINDI

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

NAJISIKIA KUUA TENA

ROHO YA PAKA

NOTI BANDIA
Roho ya Paka
 
View attachment 1683774


Simulizi : SALAMU KUTOKA KUZIMU
Mwandishi : BEN R. MTOBWA
Imeletwa kwenu na: PSEUDEPIGRAPHAS

SEHEMU YA 1


KIFO kaja duniani kwa kazi moja tu. Akikukuta umekwisha... Akikusalimia umekwisha... Hana mdhaha. Lakini sasa huyu anataka watu mashuhuri, watu wakubwa zaidi. Anataka kuifanya Afrika nzima iangue kilio na maombolezo ambayo hayajapata kutokea duniani. Na anataka hilo litokee siku moja, saa moja... "Bendera zote duniani zipepee nusu mlingoti", anasema huku akichekelea. "Sijawahi kushindwa..." Jasho linawatoka watu mashuhuri. Damu inamwagika kama mchezo. Inspekta Kombora machozi yanamtoka. Joram Kiango anabaki kaduwaa.

SURA YA KWANZA

"Bado nasisitiza kuwa tusithubutu wala kujaribu kufanya lolote kabla ya kuhakikisha kuwa Joram Kiango yu marehemu", ilidai sauti moja nzito.

"Naam, lazima afe", sauti nyingine iliunga mkono. "Afe kabla hatujainua mikono kufanya lolote tulilokusudia. Hakuna asiyefahamu jinsi kijana huyu alivyo hatari anusaye shari na kuingilia kati kuharibu harakati zote. Hajasahaulika alivyowakorofisha wale mashujaa waliotaka kuuangusha utawala wa nchi ya Ngoko katika tukio lile lililoitwa Dimbwi la damu. Kadhalika bado hatujasahau alivyosababisha vifo na kuharibu mipango ya majasusi waliotaka kuiharibu nchi hii katika mkasa ambao mtu mmoja aliuandikia kitabu na kuuita Najisikia kuua tena. Kwa kila hali Joram Kiango ni mtu hatari zaidi ya hatari zote zinazoweza kutokea, Hana budi kufa".

Kicheko kikavu kikasikika kidogo, kikafuatwa na sauti iliyokwaruza ikisema.

"Atakufa. Lazima afe. Na atakufa kifo cha kisayansi kabisa. Mpango huu tumeuandaa kwa uangalifu mkubwa, Na watekelezaji wake pia ni watu ambao
Umenikumbusha mbali sana. Inspekta Kombora na kachero lililokubuhu, Joram Kiango.

Kwa uandishi wa kazi hizi za Riwaya za upelelezi hapa nchini Tanzania, Ben Mtobwa anamfuatia Msiba ambaye yeye ameandika Riwaya za kachero maarufu Willy Gamba. Na ukiangalia vizuri zaidi, Mtobwa anaweza hata akamzidi Msiba kwa sababu yeye Msiba riwaya zake zinaonekana kama kuiga uandishi wa James Hardley Chase, na hivyo inaonekana kama alikuwa anamuiga Chase kwa kuandika riwaya za Kiswahili.

Nimesoma sana hivi vitabu O-level Nilikuwa na jamaa yangu tulikuwa tuko darasa moja, stream moja, alikuwa anatumia jina la Nyanda Petro (sasa hivi alishabadilisha jina). Huyu bwana alikuwa ana roho nzuri sana. Yeye alikuwa ana uwezo wa kununua vitabu hivi ila mimi sikuwa nao, lakini alikuwa kila akinunua, lazima anipe na mimi nisome. That man was a very nice. Magazeti ya Sani pia vile vile alikuwa anafanya hivyo hivyo
 
Umenikumbusha mbali sana. Inspekta Kombora na kachero lililokubuhu, Joram Kiango.

Kwa uandishi wa kazi hizi za Riwaya za upelelezi hapa nchini Tanzania, Ben Mtobwa anamfuatia Msiba ambaye yeye ameandika Riwaya za kachero maarufu Willy Gamba. Na ukiangalia vizuri zaidi, Mtobwa anaweza hata akamzidi Msiba kwa sababu yeye Msiba riwaya zake zinaonekana kama kuiga uandishi wa James Hardley Chase, na hivyo inaonekana kama alikuwa anamuiga Chase kwa kuandika riwaya za Kiswahili.

Nimesoma sana hivi vitabu O-level Nilikuwa na jamaa yangu tulikuwa tuko darasa moja, stream moja, alikuwa anatumia jina la Nyanda Petro (sasa hivi alishabadilisha jina). Huyu bwana alikuwa ana roho nzuri sana. Yeye alikuwa ana uwezo wa kununua vitabu hivi ila mimi sikuwa nao, lakini alikuwa kila akinunua, lazima anipe na mimi nisome. That man was a very nice. Magazeti ya Sani pia vile vile alikuwa anafanya hivyo hivyo

[emoji1374][emoji1374][emoji1374][emoji1374][emoji1374] asante mkuu
Mtobwa anajua sana.. Kipaji hiki hakuna mfano wake
 
Na sasa kitabu hiki kweli kilikuwa na mambo ya kuzimu... 🙂
 
Back
Top Bottom