Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA MWISHO
COUNT-DOWN PART 5
nilikatwa uume wangu. Nataka ujuwe mimi ni nani".
Nuru akabaki ameduwaa. Alitamani kupiga kelele lakini sauti ilikuwa kama iliyouhama mwili wake.
"Vua nguo zako zote".
Bado Nuru alikuwa ameduwaa.
"Nasema vua nguo zako. Au utapenda nizivue mimi? Usitegemee kuvuliwa nguo kistaarabu", Proper alisema akimsogelea Nuru pole pole. Macho yake yalidhihirisha kila dalili ya unyama na yalimfanya Nuru ashikwe na hofu kubwa hivyo akabaki amekodoa macho.
"Utavua au nikuvue?" Proper alihoji tena mikono yake ikiliendea koo la Nuru na kuanza kuliminya.
"Hatazivua na wala hatavua nguo", ilisema sauti nyepesi kutoka nyuma yao. Wote wakagauka kutazama. Msemaji alikuwa akitokea bafuni, akawasogelea taratibu sigala ikiwa mkono mmoja, bastola mkono wa pili. Aliwaangalia akitabasamu.
"Heko Bi. Nuru, U msichana shujaa kuliko nilivyotegemea. Umenifurahisha sana kwa kutobabaishwa kwako na huyu mwehu. Poa moyo. Hataweza kufanya lolote la kinyama tena kwako".
Sauti haikuwa ngeni masikioni mwa Nuru. Ilikuwa sauti ambayo aliizowea sana. Sauti ambayo aliondokea kuihusudu hata akaipenda. Lakini sura na umbile lilikuwa la mtu mwingine asiyemfahamu kabisa. Umbo zuri lenye dalili zote za afya na sura ya kuvutia yenye kila dalili ya ushujaa. Sura ambayo ilioana sana na sauti yake. Kwa Nuru hii ilikuwa enzi yake ya miujiza. Hivyo, kwa kuzingatia alivyoifahamu sauti hiyo alisema pole pole, "Wewe ni Duncan".
Mgeni huyo akacheka. U msichana shujaa na mwenye hekima sana. Umewezaje kunifahamu kwa urahisi kiasi hicho? Kisha akamgeukia Proper na kusema: "Hata hivyo rafiki yangu huyu ananifahamu kwa jina lingine kabisa. Nililazimika kujigeuza sura na umbile kuwa Duncan ili kumthibitishia jamaa huyu kuwa utaalamu wa binadamu kujibadili si jambo geni katika nchi hii. Kila mtu anaweza. Au sivyo Proper, ambaye wakati mwingine ulijiita Profesa Kimara".
Proper alijikuta katika wakati mgumu mno katika maisha yake. Mshangao aliokuwa nao ulikuwa mkubwa kiasi cha kutawala hofu na hasira ambayo ilikuwa imeanza kujitokeza. Proper hakupenda kuyaamini macho yake, kuwa
COUNT-DOWN PART 5
nilikatwa uume wangu. Nataka ujuwe mimi ni nani".
Nuru akabaki ameduwaa. Alitamani kupiga kelele lakini sauti ilikuwa kama iliyouhama mwili wake.
"Vua nguo zako zote".
Bado Nuru alikuwa ameduwaa.
"Nasema vua nguo zako. Au utapenda nizivue mimi? Usitegemee kuvuliwa nguo kistaarabu", Proper alisema akimsogelea Nuru pole pole. Macho yake yalidhihirisha kila dalili ya unyama na yalimfanya Nuru ashikwe na hofu kubwa hivyo akabaki amekodoa macho.
"Utavua au nikuvue?" Proper alihoji tena mikono yake ikiliendea koo la Nuru na kuanza kuliminya.
"Hatazivua na wala hatavua nguo", ilisema sauti nyepesi kutoka nyuma yao. Wote wakagauka kutazama. Msemaji alikuwa akitokea bafuni, akawasogelea taratibu sigala ikiwa mkono mmoja, bastola mkono wa pili. Aliwaangalia akitabasamu.
"Heko Bi. Nuru, U msichana shujaa kuliko nilivyotegemea. Umenifurahisha sana kwa kutobabaishwa kwako na huyu mwehu. Poa moyo. Hataweza kufanya lolote la kinyama tena kwako".
Sauti haikuwa ngeni masikioni mwa Nuru. Ilikuwa sauti ambayo aliizowea sana. Sauti ambayo aliondokea kuihusudu hata akaipenda. Lakini sura na umbile lilikuwa la mtu mwingine asiyemfahamu kabisa. Umbo zuri lenye dalili zote za afya na sura ya kuvutia yenye kila dalili ya ushujaa. Sura ambayo ilioana sana na sauti yake. Kwa Nuru hii ilikuwa enzi yake ya miujiza. Hivyo, kwa kuzingatia alivyoifahamu sauti hiyo alisema pole pole, "Wewe ni Duncan".
Mgeni huyo akacheka. U msichana shujaa na mwenye hekima sana. Umewezaje kunifahamu kwa urahisi kiasi hicho? Kisha akamgeukia Proper na kusema: "Hata hivyo rafiki yangu huyu ananifahamu kwa jina lingine kabisa. Nililazimika kujigeuza sura na umbile kuwa Duncan ili kumthibitishia jamaa huyu kuwa utaalamu wa binadamu kujibadili si jambo geni katika nchi hii. Kila mtu anaweza. Au sivyo Proper, ambaye wakati mwingine ulijiita Profesa Kimara".
Proper alijikuta katika wakati mgumu mno katika maisha yake. Mshangao aliokuwa nao ulikuwa mkubwa kiasi cha kutawala hofu na hasira ambayo ilikuwa imeanza kujitokeza. Proper hakupenda kuyaamini macho yake, kuwa