Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA MWISHO
COUNT-DOWN PART 13
alipokitoa kidani hakuzungumza chochote akipeleleza juu yangu au juu ya kidani hiki?".
Nuru hakukumbuka kitu hicho. Alichokumbuka ni kwamba katika maongezi ya jana sauti ya Duncan ilikuwa ya kawaida bila dalili yoyote ya kujua mengi juu ya mkufu huo.
Mgeni aliyasoma hayo katika uso wa Nuru. Akaridhika. "Wala hakukuonya usikivae tena?", aliuliza.
"Aliniambia nikurudishie. Kwa hiyo chukua uondoke. Nataka kulala mapema", Nuru alifoka.
"Kweli", mgeni huyo aliunga mkono. Akacheka kidogo kabla ya kusema. Bi. Nuru tafadhali yasahau yote yaliyopita kati yetu. Ulikuwa mzaha tu. Nadhani utanisamehe nikikupa hii? Alitia mkono wake mfukoni na kuutoa. Ulikuwa umeshikilia kitita cha pesa. Hazikuwa chini la laki mbili. "Tafadhali pokea".
Pesa ni pesa. Zina nguvu na starehe yake. Zinashawishi. Lakini hizi zilimtisha Nuru. Kuzipokea ilikuwa kama kupokea nauli ya kuelekea kuzimu. "Mara ngapi niseme kuwa sihitaji chochote kutoka kwako?, Nuru alifoka tena. "Ondoka na pesa zako. Zinanuka".
"Zipokee. Kama hupendi ni juu yako. Lakini hizo sikupi bure. Ni malipo kwa kazi ndogo ambayo lazima utaifanya kesho mkutanoni". Akaingiza tena mkono wake mfukoni na kutoa kopo la poda ambalo lilikuwa limefungwa katika mfuko wa nailoni. Hii ni zawadi yako nyingine. Poda ya aina yake. Wewe utakuwa mtu wa pili katika nchi hii kuitumia. Hata hivyo utalazimika kuitumia kwa uangalifu sana ukifuata maelekezo yangu. Unanisikia?".
Nuru alitikisa kichwa kukubaliana na mgeni wake.
"Nisikilize kwa makini. Kesho utakwenda na poda hii kazini, ikiwa ndani ya pochi yako. Utakapowadiwa wakati wa kuwapatia wageni vinywaji ndipo utakapokwenda bafuni na kufungua poda hii. jipake ya kutosha usoni na mikononi. Kisha utarudi na kuanza kuwahudumia hao waheshimiwa. Hakikisha mikono yako inagusa karibu kila kikombe. Sawa?".
COUNT-DOWN PART 13
alipokitoa kidani hakuzungumza chochote akipeleleza juu yangu au juu ya kidani hiki?".
Nuru hakukumbuka kitu hicho. Alichokumbuka ni kwamba katika maongezi ya jana sauti ya Duncan ilikuwa ya kawaida bila dalili yoyote ya kujua mengi juu ya mkufu huo.
Mgeni aliyasoma hayo katika uso wa Nuru. Akaridhika. "Wala hakukuonya usikivae tena?", aliuliza.
"Aliniambia nikurudishie. Kwa hiyo chukua uondoke. Nataka kulala mapema", Nuru alifoka.
"Kweli", mgeni huyo aliunga mkono. Akacheka kidogo kabla ya kusema. Bi. Nuru tafadhali yasahau yote yaliyopita kati yetu. Ulikuwa mzaha tu. Nadhani utanisamehe nikikupa hii? Alitia mkono wake mfukoni na kuutoa. Ulikuwa umeshikilia kitita cha pesa. Hazikuwa chini la laki mbili. "Tafadhali pokea".
Pesa ni pesa. Zina nguvu na starehe yake. Zinashawishi. Lakini hizi zilimtisha Nuru. Kuzipokea ilikuwa kama kupokea nauli ya kuelekea kuzimu. "Mara ngapi niseme kuwa sihitaji chochote kutoka kwako?, Nuru alifoka tena. "Ondoka na pesa zako. Zinanuka".
"Zipokee. Kama hupendi ni juu yako. Lakini hizo sikupi bure. Ni malipo kwa kazi ndogo ambayo lazima utaifanya kesho mkutanoni". Akaingiza tena mkono wake mfukoni na kutoa kopo la poda ambalo lilikuwa limefungwa katika mfuko wa nailoni. Hii ni zawadi yako nyingine. Poda ya aina yake. Wewe utakuwa mtu wa pili katika nchi hii kuitumia. Hata hivyo utalazimika kuitumia kwa uangalifu sana ukifuata maelekezo yangu. Unanisikia?".
Nuru alitikisa kichwa kukubaliana na mgeni wake.
"Nisikilize kwa makini. Kesho utakwenda na poda hii kazini, ikiwa ndani ya pochi yako. Utakapowadiwa wakati wa kuwapatia wageni vinywaji ndipo utakapokwenda bafuni na kufungua poda hii. jipake ya kutosha usoni na mikononi. Kisha utarudi na kuanza kuwahudumia hao waheshimiwa. Hakikisha mikono yako inagusa karibu kila kikombe. Sawa?".