Simulizi ya Kijasusi: Salamu Kutoka Kuzimu

Simulizi ya Kijasusi: Salamu Kutoka Kuzimu

Du thanks mkuu,unanifanya nakosa hata muda wa kupiga nyagi,kesho tupia tena mkuu be blessed[emoji120]
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 25



"Mimi sijakwambia lolote ambalo nakusudia kukwambia huku huyo mwenzangu tayari amekuletea zawadi kubwa kama hii na kukuahidi kuzunguka nawe duniani".

Nuru alimkatiza Duncan kwa kicheko ambacho kilichofuata sauti yake nzuri ikisema, "Huna haja ya kuwa na hofu na mzee yule. Sina wazo naye kabisa. Zaidi ya hayo, si nimekwambia walivyomfanya? Hana madhara kwa mwanamke yeyote".

"Usiwe na kawaida ya kumwamini kila mzee kwa lolote analosema", Duncan alimtahadharisha. "Sasa tafadhali rudia tena hatua kwa hatua jinsi ilivyotokea... hata mkafahamiana na mzee huyo, na yote mliyozungumza".

Kwa mshangao kidogo Nuru alirudia hadithi hii nzima. Baada ya hadithi hiyo, Duncan aliuliza maswali mengi ambayo Nuru hakuona umuhimu wake. Ilimshangaza Nuru kuona kila jibu likimridhisha zaidi Duncan.

Hatimaye Duncan aliinuka kwenda bafuni. Aliporudi alikuwa na mkufu ule mkononi akamkabidhi Nuru huku akisema, "Naona saa yako ya kurudi kazini imewadia. Chukua zawadi yako, lakini tafadhali usiruhusu zawadi hizi zikununue. Jihadhari na wazee wa mjini".

Nuru aliupokea mkufu wake na kuinuka kutoka kwenye kochi.

Alipofika nje ya chumba alisita kidogo. Ndiyo kwanza akakumbuka kuwa Duncan hakuwa amemweleza chochote ambacho angependa kuelezwa.


"Hapa Afrika, bandari ya Salama".

"Nani mwenzangu"...

"Kigogo hapa... Napenda kujua kama lile ua bovu mmelichuma tayari au bado, na kama bado ni kwa sababu gani?".

"Bado kidogo. Mtaalamu wetu amesema bado anafanya uchunguzi wa mwisho katika kubaini mizizi yake. Mara akikamilisha huo utafiti wake litang'olewa haraka iwezekanavyo".

"Nataka ling'olewe haraka iwezekanavyo, mbegu zile ni hatari kusambaa. Unajua kesho ni siku ya mwisho? Hakikisha ua hilo linang'olewa.

"Bila shaka Kigogo. Mizizi tu ilikuwa haionekani vizuri katika darubini, hasa ilipofikiriwa kuwa mbegu zimesambaa hovyo. Sasa hali iko shwari. Mtaalamu wetu anaamini kuwa baada ya muda mfupi atakuwa tayari kalichuma".

"Alichume haraka. Alichume kikamilifu. Sitaki lichumwe na mtu mwingine, anaweza kumeza maradhi yakaleta madhara. Over".

"Off and over, Kigogo.
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 24



Chombo kilizimwa na kurejeshwa katika hifadhi yake. Msemaji alikuwa akifikiri kwa muda. Kigogo mikono yake ilikuwa ikitetemeka. Sio kazi rahisi, kupewa jukumu la kuua. Hasa kumuua mtu hatari ambaye yu macho zaidi ya Simba aliyejeruhiwa. Isitoshe, mtu huyo akiwa rafiki mkubwa, kama ndugu umpendae, mtu uliyeshirikiana pamoja katika maovu na unyama wa kila aina. Mtu kama huyo, kumwelekezea bastola na kumuua, kwa kuwa tu karopoka na kuamua jambo ambalo wakuu hawajaliamua! Aibu ilioje!.

Kwa hivyo, aliposikia habari ya kutorokea Mwanza kwa mwenzake, aliona kama bahati njema imemwangukia. Iwapo huyu aliyeamuriwa kumuua ametorokea huko na kuvuka mpaka, hatabeba jukumu la kumuua tena. Jukumu hili litawahusu wengine walioko huko aendako. Lakini mara wapelelezi wakaleta habari kwamba amerejea na yuko Arusha tayari kwa kusudio lake la kikatili. Ndipo alipowaarifu wakubwa. Nao wakamwamru kumuua. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kutekeleza amri. Akainua simu na kuzungusha namba fulani. Ilipopokelewa aliuliza, "Mmempata alipo?".

"Bado, mzee..."

"Bado! Kwa nini?" alifoka.

"Ametoweka kidogo. Nadhani amejibadili tena. Unajua anavyoipenda tabia ya kinyonga. Mara ya mwisho tulimpata alipokuwa kajifanya chongo na mguu mbovu. Sasa haonekani. Bila shaka ame..."

"Hata kama atajigeuza kinyonga kabisa, lazima apatikane haraka, sawa?".

"Sawa mzee".

"Na mara mtakapomuona niiteni mara moja. Sawa?".

"Sawa".

"Au hamuifahamu adhabu ya kushindwa kutimiza wajibu?" Alikata simu na kuliendea kasha lake la silaha. Akachunguza silaha mbalimbali zilizokuwemo; bastola aina aina, viwambo vya kuzuia sauti na mabomu kadhaa. Akaviweka katika mifuko yake ya siri.

Kisha aliiunua simu na kulipigia shirika moja la ndege za kukodi.

"Tafadhali andaa ndege itakayonifikisha Arusha mara moja", aliagiza.

"Umepata", alijibiwa. "Ungependa kuanza safari ya kuondoka saa ngapi?".

**************************
II

"Inspekta Kombora hapa naongea kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi..."

"Ndiyo, afande".

"Nifahamishe, taarifa bado ni ile ile hakuna fununu yoyote ya yule mwenda wazimu Proper?"
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 23



"Bado afande. Tumefanya kila aina ya uchunguzi. Kila hoteli na kila nyumba za wanawake malaya zimechunguzwa kwa ustadi mkubwa, hajaonekana mtu yeyote wa aina yake. Arusha nzima imepekuliwa. Bila shaka atakuwa ametorokea nje ya nchi.

Labda. Lakini sipendi kuamini kuwa katoroka. Tumewasiliana na wenzetu wa Rwanda na Burundi. Hakuna dalili ya mtu mwenye tabia kama zake. Anaweza kuwa yumo humu nchini. Na kama yumo nchini, atakuwa hapo hapo Arusha. Mmebakiwa na masaa machache sana ya kukamilisha uchunguzi. Kesho kama mnavyojua viongozi wanaanza kuwasili, lazima mhakikishe kuwa jambo lolote la kipumbavu halitokei".

"Hakuna jambo la kipumbavu litakalotokea mzee", sauti ilieleza. "Hoteli nzima imepigwa ufagio. Wageni na wafanyakazi wote wamechunguzwa kwa makini. Kuna kijana mmoja tu ambaye alielekea kututia wasiwasi. Tabia yake ya kuzungumza na kila mtu, ilitutia hofu. Ilikuwa kama anayetafuta habari fulani. Lakini baada ya kumchunguza kwa makini tumebaini kuwa hana kasoro. Tunazo hata kanda za maongezi yake kwa wafanyakazi. Kama utapenda kusikia tunaweza kukutumia".

"Msihangaike kuzituma huku. Leo nategemea kuwasili hapo Arusha wakati wowote. Anaitwa nani huyo kijana?", alihoji Kombora.

"Duncan".

"Vizuri".

Proper alikuwa juu ya kitanda katika chumba cha mojawapo ya Hoteli nyingi za Mji wa Mwanza. Mkono wake wa kulia ulikuwa ukichezea matiti ya mischana mrembo aliyelala kando yake, mkono wa kushoto ulikuwa ukipepesa kiuno cha msicha huyu. Wote walikuwa uchi na miili yao ikitokwa jasho. Jasho liliendelea kuwatoka asubuhi hii yenye baridi kali. Jasho lililotokana na juhudi za miili yao katika kuthibitisha utaalamu na uwezo wao kimahaba.

Huyo alikuwa msichana wa tano tangu Proper aingie mjini Mwanza na kufikia katika hoteli hii... Wawili waliotangulia, alikuwa amewaona wa kawaida tu. Zaidi ya uzuri wao wa sura na maumbile ya kuvutia, kitandani hawakuwa na la ziada. Hivyo aliwapa ujira wao na kuwaaga. Lakini huyu wa tatu, hakuonekana
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 22


kama alikuwa mtu wa kuagwa kwa urahisi. Sura haikuwa nzuri sana. Wala umbile lake halikuwa kama yale ambayo huwafanya madereva wa magari waroho wasababishe ajali barabarani kwa kuwatazama. Msichana huyu alikifahamu kile alichopaswa kuwatendea wanaume. Alielewa alichokusudia Muumba wake kwa kumwezesha kuwa na viungo tofauti. Kila kitendo chake kitandani alikitenda kwa ari na nia, bila uchoyo wa aina yoyote. Kila kiungo chake mwilini alikitumia kikamilifu bila hiana. Na hakuonekana mwanafunzi katika vitendo vyake vyote.

Ni hayo yaliyomfanya Proper ajisahau kwa kiasi fulani.

Ni kweli kuwa aliyoyaona Mwanza hayakuwa ya kawaida. Katika Jiji la Dar es Salaam ambako aliishi sana, kupata msichana au mwanamke wa kujiburudisha haikuwa tatizo. Ziko saa za jioni, au usiku, ambazo utajitokeza mitaani na kujipitisha. Hutavuka mtaa wa tatu kabla hujapata mtu ambaye ataivunja safari yake na kuandamana nawe hadi chumbani kitandani, ambako ataondoka alfajiri na siku ya pili. Lakini si hivyo kwa muda wa Mwanza. Hapa unachotakiwa kufanya ni kujipatia chumba chako kwanza katika moja ya hoteli nyingi zilizogaa. Kaa chumbani kwako kwa utulivu. Haitapita muda mrefu kabla hujapigiwa hodi na watoto wa kike ambao watajitia kuuliza hili na lile hadi maswali yao yatakapokufanya utoe jibu litakalowafanya waangukie kitendani.

Proper pia alitulia chumbani kwake kimya akingoja hodi yake. Haja yake haikuwa kujiburudisha tu, bali alitaka kujificha, ili aonekane kama wapangaji wengine. Kama vijana ambao waliamua kuonyesha ujana wao au wazee ambao waliifurahia fursa ya kuwaasi wake zao. Ndipo alipoanza kuwakaribisha wasichana mmoja baada ya mwingine hadi alipotokea huyu, ambaye hakuonekana kama alistahili kuondoka.

"Jina lako", Proper alimwuliza huku akihamisha mkono mmoja kutoka kiunoni na kuupeleka kichwani kwa ajili ya kuchezea nywele ndefu zilizotimuliwa kutokana na zoezi lililokuwa likiendelea kitandani hapo.

"Sofia" msichana huyu alijibu kwa sauti ya mahaba. "Na wewe?" akaendelea kuuliza.
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 21


"Bakari, ingawa rafiki zangu hupenda kuniita Beka", Proper alimlaghai.

"Kwa maana hiyo nikuite Beka siyo".

"Hapana. Niite mpenzi".

Sofia akacheka. Na kicheko chake kilikuwa cha kupendeza.

Baada ya muda, msichana huyu alipitiwa na usingizi. Kichwa akakiegemeza katika kifua cha Proper, mkono wake akauweka mahala fulani katika mwili wake, akawa amelala kwa utulivu mkubwa. Uso wa msichana huyu ulikuwa kama anacheka, kwa jinsi alivyokuwa amelala.

Proper alimtazama kwa muda. Kisha alijitoa kitandani hapo kwa uangalifu bila ya kumwamsha Sofia. Akaliendea begi lake ambalo alilifungua na kulichunguza. Sehemu za kawaida zilikuwa na mavazi yake, vitambulisho vyake bandia na vikorokocho vingine. Mifuko ya siri, ambayo kama alivyotegemea, wakaguzi wa uwanja hawakuweza kuifikia, ilikuwa na silaha zake, nyaraka zake muhimu, dawa zake maalumu, na pesa nyingi. Kila kitu kilikuwa kama kawaida. Proper akakirudia kitanda ambako alikiinua kichwa cha msichana huyo taratibu na kukirejesha kifuani kwake na mkono kuuweka kama ilivyokuwa awali. Kisha akayafumba macho yake kwa namna ya utulivu.

Lakini akilini hakuwa na utulivu wowote. Kichwa chake kilikuwa kazini kikitafakari matukio yote yaliyopita na ajali. Aliukumbuka kwa hasira mpangi wake madhubuti ambao aliuandaa kwa gharama kubwa na muda mrefu, na ulivyokaribia kumpotezea maisha. Ilimchukiza kuona kuwa waliokusudia kumwangamiza walikuwa watu wa upande wake. "Kwa ajili ya uoga", aliwaz. Uwoga usio na msingi. Uoga ule ule ambao umewafanya kwa muda mrefu watumie pesa nyingi kukamilisha mabomu ya nyuklia, lakini hadi leo hawajadhubutu kufanya majaribio walao katika nchi moja. Wapi basi haja ya kusumbua vichwa? Yeye Proper angewaonyesha. Liwalo na liwe lakini mpango wake aliouanzisha lazima atautekeleza. Peke yake na kwa mkono wake Dunia ione Ulimwengu usikie.

Proper aliyarejesha mawazo yake kwa Inspekta Kombora na jeshi lake. Walikuwa wanafanya nini alijua kwamba, kifo cha yule Padri kiliwafungulia polisi mwanya fulani. Hata hivyo alielekeza fikra zake zote kwa kazi hii ya
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 20


mwisho. Hakuna ambaye angeweza kulizuia pigo la mwisho, Pigo la kihistoria.

Proper alimtazama Sofia usoni. Akamuona alivyolala kwa utulivu. Angetokwa na kicheko kwa kumhurumia msichana huyu alivyolala kwa utulivu bila kufahamu amelala na mtu wa aina gani. Hajui kama amelala na kifo! Alinongona kimoyomoyo. Kisha alimwamsha na kumtaka wafanye tena mapenzi. Kama kawaida, msichana alikuwa tayari. Kama kawaida yalikuwa mapenzi ambayo yaliacha kumbukumbu akilini mwao.

"Wapi unaishi Sofia?" Proper aliuliza baada ya kukusanya pumzi kwa dakika kadhaa.

"Kirumba, nyuma kidogo ya Uwanja wa mpira".

"Unaishi na nani Sofia?".

"Peke yangu", Kimya kifupi kikapita. "Kwa nini unapenda kujua?".

Proper alipeleka ulimi wake kuchezea chuchu za Sofia kabla hajatoa jibu.

"Kwa sababu nyingi. Kubwa ni kwamba ni kwamba sijapata kukutana na aliyeniburudisha kama wewe. Nisingependa kutengana nawe tena, kwani nikikukosa huenda nisipate mtu wa aina yako. Hivyo, nimependa nihame hapa hotelini na kuishi kwako hadi shughuli zangu zitakapokwisha hapa Mwanza, halafu twende zetu pamoja Bujumbura. Unasemaje?"

Habari hii ilimfurahisha sana Sofia. Msichana huyu alikuwa ametoroka kwao Sengerema baada ya kupata mimba isiyokuwa na mwenyewe. Mimba hiyo iliishia chooni. Tangu siku hiyo, amekuwa mtu asiyekuwa na tumaini la kupata bwana wa kudumu. Sura yake pia, ilikuwa pingamizi kubwa. Daima mabwana aliowapata, walikuwa hawa wa 'kuokota' Mabwana waliosukumwa na uchu tu wa kuwa na mwanamke. Hali hii ilimfanya msichana huyu ajikabidhi kwa kila mwanaume bila kujali lolote, akiwatimizia kila haja bila aibu wala kinyongo. Lakini harakati zake za kuwaburudisha wanaume mara nyingi hazikumfikisha mbali. Mara kwa mara alikuwa akipewa 'kwa heri ya kuonana' na mabwana hao. Wengi waliwarudia wake zao. Wengine walikuwa wameishiwa. Na wengine walikusudia kuziponyesha pesa zao.

Ndiyo Sofia akayachukulia maombi ya 'Mzee kijana' huyu kama tunu aliyonunuliwa bila ya kutazamia. Aliyaona kama mwisho wa matatizo yake na mwanzo wa maisha mapya. Alimtazama tena Proper. Hakuona dalili yoyote ya
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 19


mzaha katika sura yake. Kama kweli mtu huyu alikuwa na tatizo lolote, pesa hazikuwa mojawapo. Angekubali mara moja. Hata hivyo alikumbuka hali ya chumba chake, mazingira yaliyostahili jina la pango. Ndipo alipomweleza Proper kwa sauti iliyonasihi.

"Ningependa sana kukukaribisha kwangu. Lakini hali ya chumba kile... kwa kweli, hakifai kwa mtu kama wewe".

Proper hakuwa mgeni kwa maisha ya wasichana wengi mjini. Alikwisha waona wengi ambao wawapo mitaani wanaonekana kama malaika kwa mavazi mazuri, lakini ukifika wanakoishi utadhani ni vijakazi. Alimsihi Sofia aondoe shaka. Alimweliezea kuhusu msingi wake wa kimaskani. Kwamba ameishi sana 'gheto' na maisha hayo anayapenda. "Nikiwa Dar hupendelea sana kutembelea sehemu za Manzese. Nikiwa Arusha makazi yangu ni Ngarenaro. Na nikiwa Moshi nastarehe zaidi nikiwa Majengo", alimhakikishia. "Sababu hiyo ndiyo iliyonifanya niishi katika hoteli hii ndogo badala ya kubwa kama Mwanza Hoteli".

Maneno hayo yalimaliza ubishi wa Sofia. Usiku uliofuata uliwakuta Kirumba katika chumba chake.

Chumba kilikuwa katika hali ambayo Proper aliitarajia. Raslimali za muhimu zilikuwa kitanda kikuukuu chenye godoro kukuukuu la sufi ambalo halikuwa na hadhi ya kuitwa godoro pia kulikuwa na sanduku, meza na sufuria mbili tatu zilizonuna kwa uchafu. Ambacho Proper hakutegemea ni ukarimu wa kunguni na mbu walikuwa huru katika chumba hicho. Walimlaki moja kwa moja bila kumpa fursa ya kujipumzisha.

Yote hayo Proper alilazimika kuyastahamili eti kwa sababu amependa, kumbe ni uhitaji tu. Alikusudia kujisetili akisubiri siku kuu ili atimize lengo lake. Hakuna askari wala mpelelezi yeyote ambaye angefikiria kumtafuta pale. Alitarajia kuwa wangeweza kumsaka katika mahoteli makubwa na kwenye vitongoji vikubwa vikubwa, siyo kwa malaya wa chini kama Sofia anayeishi maeneo yaliyosahaurika.

Siku mbili zikapita bila ya kitu chochote cha kawaida kutokea. Proper alishinda ndani akijisomea vitabu, nae Sofia alijishughulisha kutafuta vyakula
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 18


na vinywaji. Sofia alikuwa akipewa pesa zilizozidi mahitaji yake ya kawaida. Proper alikuwa amemruhusu kununua mavazi mapya. Hali hii ngeni ilimuinua Sofia, akawa anapepea mfano wa kishata. Nafasi yoyote iliyojitokeza, ilitumiwa kufanya mapenzi. Sofia alijitia kila aina ya juhudu kumridhisha Proper. Lakini hakuweza kuutambua unafiki wa Proper. Akazidi kutekwa akili na vitendo vya mtu huyu. Hata hivyo sauti nyingine ilimnong'oneza atahadhari.

Jioni ya siku ya tatu, mambo yalianza kwenda mrama. Sofia alirejea kutoka mjini na gazeti mkononi. Alimfuata Proper aliyelala chali kitandani na kumfungulia ukurasa wa tatu ambao ulikuwa na picha sita chini ya kichwa cha habari kilichosema;

"TANGAZO LA POLISI.
JIHADHARI NA MTU HUYU- MARA UMWONAPO IARIFU POLISI. ANATAFUTWA KWA MAUAJI YA WATU WENGI NA ANAWEZA KUUA WAKATI WOWOTE, KUWAMAKINI".

Proper alisoma haraka haraka. Kisha alizitazama picha hizo kwa makini. Moja ilikuwa yake halisi. Zilizosalia zilikuwa picha za kuchora. Zilikuwa zimechorwa kwa namna mbalimbali kuonyesha nywele zote; nyingine ilichorwa kuonyesha madevu mengi, nyingine kavaa miwani na kadhalika. Ni moja kati ya picha hizo ambayo ilikuwa imefanana kikamilifu na sura aliyokuwa akiitumia sasa. Alijitia utulivu na kumgeukia Sofia na kumwuliza kwa upole, "Ni hii tu uliyoiona habari ya maana katika gazeti lote".

"Hapana. Nilitaka kukuonyesha huyo mtu. Naona mmefanana naye sana".

"Tumefanana!" Proper alijitia kushangaa. "Mimi nafanana na huyo anayetafutwa kwa mauaji? Haiwezekani".

"Mmefanana sana Beka. Nadhani ni wewe".

"Usiwe mjinga Sofia, mimi siwezi kuwa muuaji".

"Kweli kabisa. Hata yule rafiki yangu aliyekuja hapa jana amesema hivyo. Labda ungesoma hapa chini uone".

Proper alianza kusoma kifungu hicho kilichoandikwa kwa herufi za mlazo.

Mtu huyu ni hatari sana, anatakiwa mapema mno. Zawadi nono ya shilingi laki nne itatolewa kwa mtu yeyote atakayewezesha kukamatwa kwake. Inasemekana kwa sasa yuko mjini Mwanza au mikoa ya jirani. Unaonywa tena kujihadhari naye...

"Ni wewe Beka?", Sofia alisisitiza huku akimkazia macho.
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 17


kama alivyotegemea. Aliifuata polepole barabara iendayo mjini. Alipofika Mabatini, alisimamisha taksi na kuingia ndani.

Dereva taksi alikuwa kijana wa Kiarabu mwenye ndevu nyingi. Alimsalimu Proper kwa adabu, kisha akamuuliza wapi anataka kwend. Proper hakumjibu kwa maneno bali kwa kitendo fulani. Aliudidimiza mkono wake katika begi lake na kutoa bastola yake. Aliigandamiza ubavuni mwa kijana huyo.

"Ukifanya ujinga utapoteza maisha. Nataka wewe na gari hii mfuate matakwa yangu. Haya endesha mpaka nitakapokwambia wapi tuelekee".

Huku akitetemeka, macho yakiwa yamemtoka, kijana huyo alilitia gari moto na kuliondoa taratibu huku mapigo ya moyo yakimwenda kasi kwa hofu.

Nuru alichelewa kufika nyumbani. yeye na wenzake Walikuwa wamechelewa kutoka kazini ili kukamilisha shughuli zote za maandalizi ya ugeni mkubwa. Ilikuwa saa mbili kasoro dakika chache alipojikuta mbele ya mlango wa nyumba yake, akiutia ufunguo katika tundu la kitasa cha mlango wa chumba chake.

Kabla ya kuanza kufungua kitasa cha mlango, alikuwa ameyatupa macho yake pande zote kwa matumaini labda ya kumwona tena yule mzee tajiri. Hakuwepo. Bila shaka alikuwa amesubiri kwa muda alipoona hatokei akaondoka zake, akadhani. Hata hivyo Nuru hakujua kama angependa kumwona tena mzee yule au la. Ingawaje Nuru alikuwa ametunukiwa zawadi ya mkufu wenye thamani kubwa, na ahadi ya kutembea duniani, lakini Nuru hakujua kama angependa kumwona tena au la.

Alichofahamu ni kwamba mashaka hayo yalikuwa yameanza pindi Duncan alipomwambia; "Unajua kidogo nina wivu... Tafadhali usiruhusu zawadi hizi zikununue ..." Hakujua kwa nini, lakini maneno hayo yalikuwa yamemburudisha zaidi ya zawadi yenyewe. Hakuna kitu alichohitaji zaidi ya kuonewa wivu na Duncan. Alihisi kama wivu huo ulikuwa mwanzo wa safari mpya, ndefu, ambayo hakujua mwisho wake. Safari ambayo aliona itakuwa ya kusisimua zaidi ya ile ya Ulaya Magharibi aliyoahidiwa na yule mzee tajiri. Alasiri nzima Nuru alishinda kwa furaha kubwa kinyume cha alivyokuwa kabla ya kuzungumza na Duncan.
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 16





"Siyo mimi". Sauti ya Proper ilikuwa ya utulivu mkubwa.

"Kwani unanionaje mimi, naweza kuwa muuaji?".

"Hapana, lakini hiyo picha inaonyesha ni wewe".

"Achana na picha hii. Huoni kama huyu amechorwa tu? Usiwe msichana mjinga Sofia. Mimi ni mtu ninayejiheshimu sana huko kwangu. Wasichana kama wewe, wazuri zaidi yako, ninao kama ishirini hivi ambao wanalipwa mshahara mzuri kutoka katika mfuko wangu. Na wanaume wengi wasiopungua mia, wote wako chini yangu, wote wananiheshimu. Au kwa vile niko nawe katika chumba hiki hafifu ndipo umefikia hatua ya kuniita mwuaji?".

"Sivyo mpenzi, ila..."

"Ila..."

"Nina mashaka yule rafiki yangu amekwenda kutoa taarifa polisi. Laki nne siyo pesa ndogo".

"Polisi. Akiwaleta hapa, wakinikuta mimi watanitia ndani kufunza adabu. Ondoa hofu. Sofia njoo kitandani, tujipumzishe nikudokeze jambo. Lete ulimi tufurahi".

Sofia alisogeza shingo. Hakutarajia radi iliyompiga ghafla. Lilikuwa pigo kali jepesi ambalo lilitua katika shingo na kulivunja kabisa. Sofia hakujua kapigwa na nini. Wala hakuona ugumu wa kufa. Alianguka chini na kupapatika kwa muda, kisha akakata roho.

Proper alifanya kazi haraka haraka. Aliuzoa mzoga wa aliyekuwa Sofia na kuulaza kitandani. Akaufunika vizuri kwa shuka. Kisha alikusanya vifaa vyake na kutoka nje. Giza lilikuwa limeanza kutanda. Hakuona haja ya kujificha
Alikuwa bado na furaha hiyo alipoingia ndani na kulipupa begi lake juu ya meza. Mkono wake wenye uzoefu ulipenya kiza na kuifikia swichi ya umeme. Akaibonyeza. Nyumba nzima ikamezwa na nuru ya rangi ya blue iliyokuwa ikitoka katika taa zake. Akavuta swichi ya kamba na kuifanya nuru hiyo ya blue itoweke na nyeupe kuchukua nafasi yake. Ni katika nuru hiyo alipoweza kumwona mgeni wake aliyekuwa ameketi kwa utulivu juu ya kochi akimtazama Nuru, uso wake ukaonekana kama wa mtu anayetabasamu.

Nuru alishtuka karibu akimbie. Hakujua ulikotokea uwezo ambao ulimfanya asite kukimbia na badala yake afoke kwa sauti ambayo ilitoka kama
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 15


mnong'ono. "Nani wewe? Na umeingiaje humu?".

Mgeni huyu alicheka kidogo. Kisha alimwuliza kwa upole, "Umenisahau mara hii? Hukumbuki jana tu tulikuwa wote humu humu ndani na tukapeana zawadi? Mkufu huo uliovaa..."

Nuru hakuyaamini macho yake. Aliyekuwa mbele yake hakuwa yule mzee wa jana. Alikuwa mtu mwingine kabisa mwenye sura nzuri, yenye dalili ya ujana. Zaidi, hakuwa na jicho moja wala mguu mbovu. Alikuwa na viungo vyake vyote, bila kovu wala dosari yoyote. Alivaa suti ya kijivu ambayo ilimkaa vyema mwilini. Haiwezekani Nuru aliwaza. Huyu hawezi kuwa yule mzee wa jana.

Mgeni huyo alikuwa akiyasoma mawazo ya Nuru. "Huniamini siyo", aliuliza. "Lazima Lazima ufahamu kuwa katika dunia hii kuna watu wa kila aina. Wako wanaoishi maisha ya kawaida, na kuna wanaoishi maisha yasiyo ya kawaida. Wengine wanalazimika kutumia sura nyingi na majina mbalimbali, ili waweze kuishi. Mimi ni mmoja wao. Jana nilikuwa mzee mkongwe, mwenye chongo, leo ni kijana mzuri anayekufaa. Au sio?" alihoji akicheka.

Ni kicheko chake ambacho kilimfanya Nuru aafikiane naye moja kwa moja. Kilikuwa kile kile cha jana, kicheko ambacho kwa namna moja au nyingine hakikuwa cha kawaida. Kilikuwa kama kinachoficha uovu na ukatili fulani. Jambo ambalo lilimfanya Nuru apatwe na hofu.

"Sasa unataka nini?" Nuru alijitahidi kuhoji akifoka. "Sidhani kama nahitaji uhusiano na watu wenye tabioa kama zako. "Chukua mkufu wako uondoke".

"Usijisumbue kuuvua", mgeni huyo alisema. "Hiyo ni zawadi yako. Bado nakuopenda", aliendelea. "Nina kazi ndogo sana yenye faida kubwa sana. Lakini kabla ya kazi hiyo nitapenda unieleze kikamilifu ni nani mliyekuwa mkizungumza naye leo hii chumbani kwake, pale hotelini?".

Nuru hakutaka kuendelea kuzungumza na mtu huyu. Aliona kama kwa namna moja ama nyingine mtu huyo angemletea madhara au maafa. Kwa nini alazimike kutumia sura za bandia? Na aliingiaje humu ndani? "Sikia", Nuru
 
SEHEMU YA MWISHO

COUNT-DOWN PART 14


alifoka tena kwa nguvu. "Sitaki kuzungumza nawe. Toka haraka kabla sijakuitia polisi".

"Naona hujanifahamu vizuri kuwa mimi ni nani", mgeni huyo alisema huku akiinuka na kumsogelea Nuru. Ndiyo kwanza Nuru akaiona bastola ambayo ilikuwa wazi mkononi mwake ikimwelekea. "Endapo utawaita polisi, watakachofanya ni kuizoa maiti yako na kuipeleka hospitali ya Maunt Meru. Sasa utayajibu maswali yangu yote kwa adabu".

Ilikuwa mara ya kwanza kwa Nuru kuelekezewa bastola. Ingawa amesoma matukio ya aina hiyo mara nyingi na kuona katika picha za sinema jinsi wasichana wenzake wanavyouawa kwa bastola, hakuona au kuamini kuwa siku ya leo ilikuwa ya mwisho katika maisha yake. Aliuona kama mchezo au mzaha wa kuchukiza. Hivyo aliruka kando na kuinua stuli ndogo ambayo aliirusha kwa nguvu kuelekea mgeni huyo. Ikamshangaza kuona mgeni huyo akiidaka kama mchezo na kuitua chini kwa utulivu. Wakati huo huo Nuru alipokea kofi zito ambalo lilimpeleka chini. Alipojaribu kusimama alirejeshwa chini kwa kofi jingine zito. Maumivu yalikuwa makali, lakini Nuru alishangaa kuona machozi yakigoma kumtoka.

"Sipendi kukuumiza bibie", mgeni huyo alisema huku akimwinua Nuru na kumkarisha juu ya kiti. "U msichana mzuri sana. Sura yako haifai kuharibiwa kwa makofi. Keti tuzungumze kama watu wenye busara". Alimazia akairudisha bastola yake kwenye mfuko wa koti na kukirudia kiti chake. "Napenda uniambie ni nani huyo kijana anayeitwa Duncan ambaye alikuchukua na kukupeleka chumbani kwake?".

"Simfahamu vizuri", Nuru alijibu.

"Anafanya kazi hapo hotelini?"

"Hapana. Ni mgeni".

"Alifika lini?"

"Ana muda mrefu kidogo".

"Alisema nini juu ya kidani hiki nilichokupa?".

"Hakusema kitu isipokuwa alikisifia tu".

"Kuna wakati mlikiondoa kidani na kukiweka kando. Mlifanya hivyo kwa ajili gani?"

Nurua akaanza kurejewa na hasira. "Kwani sina haki ya kukivua? Tulikiondoa ili tufanye mapenzi. Tuliona kinatusumbua", Nuru alisema kwa dhamira ya kumuudhi. "Kama hupendi ondoka nacho sikihitaji".

Mgeni alifikiri kidogo kabla ya kuuliza tena. "Una hakika huyo Duncan
 
Back
Top Bottom