Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

IBILISI RUDISHA AKILI YA MKE WANGU

MTUNZI: DR SINGANOJR .

‘Your self-worth is not determined by your relationship status’-unknown

SEHEMU YA 07.
Mkataba wa Mpenzi wa Kukodi.
“Kifungu cha kwanza cha mkataba wa kukodisha mpenzi ,Mhusika A ana haki ya kumtafuta mhusika B wakati wowote ndani ya masaa 24, Mhusika B ana wajibu wa kuhakikisha simu yake muda wote ipo wazi , pili muhusika B ana wajibu wa kushirikiana kikamilifu na maombi yote ya Mhusika A maadamu maombi hayo hayavunji sheria za nchi au mkataba , tatu Mguso wowote wa kimwili lazima uruhusiwe na Mhusika A kabla ya kufanyika… nne ,,, tano …”
Ndani ya chumba cha kifahari cha hoteli ya Dosam V alionekana mwanamke mrembo akiwa amekaa kwenye sofa upande wa dirishani . alikuwa mrembo mno na siku hio mavazi yake yalizidi kumfanya kuwa mrembo zaidi.
Alikuwa amevalia mwenyewe gauni la light blue huku akiwa nywele zake amezirudisha nyuma mara baada ya kutoa ile kofia ya Hat na mkononi alikuwa ameshikilia karatasi ya mkataba akimsomea Hamza.
Macho ya mwanamke huyo yalikuwa mazuri na angavu kama vile ni maji ya vuli , nyusi zilizopindwa , kope zake ndefu na midomo yake myekundu na minene vilimfanya kuvutia zaidi ,bila kusahau uumbwaji wa uso wake ulioendana na haiba yake , alikuwa kama vile ni mchoro wa sanaa uliotoka kwa mchoraji maridadi.
Hamza alikuwa ameketi mbele ya mwanamke huyo mrembo akimwangalia na kumsikiliza kwa umakini mkubwa.
Ki ufupi umakini wake haukuwa kwenye mkataba bali ulikuwa kwenye uzuri wa huyo mwanamke , kwake ni kama vile yupo ndotoni.
Kusomewa mkataba huo ilikuwa ikimaanisha alikuwa amepita kwenye usaili na sasa alikuwa akipewa mashari ya kuanza kazi.
Ukweli ni kwamba huyo mwanamke baada ya kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa alionekana kuridhika nae na alienda moja kwa moja kwenye mkataba.
Upande wa Hamza kwa namna ambavyo alikuwa akitingisha kichwa kila mara baada ya mwanamke huyo alipokuwa akisoma ni kama vile aliogopa mwanamke huyo angebadilisha mawazo na kushindwa kusaini mkataba wa kazi.
Alijiambia ni kheri hata kuigiza kuwa mpezi tu wa kukodi na hio yenyewe ingetosha kumletea heshima.
“Sahihi ya mkataba kipengele A , Regina Wilson Dosam., kipengele B Hamza Mzee.. ni muda wa kusaini…”Aliongea mwanadada mrembo ambae anafahamika kwa jina la Regina na kuweka mkataba ule juu ya meza kwa ajili ya kusaini mara baada ya kusoma vipengele.
Regina alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akimwangalia Hamza ambaye ndio amekutana nae kwa mara ya kwanza siku hio na alionekana kuridhika nae.
Alikuwa na uhakika kuhusu macho yake kulingana na muonekano wa Hamza na taarifa ambazo amempatia alikuwa na uwezo wa kuona kwamba alikuwa ni mtu muamiifu na muwazi.
Zaidi ya yote mrembo Regina aliona muonekano wa Hamza sio mbaya sana , ijapokuwa mavazi yake hayajamkaa vizuri lakini kama atamvalisha na kupata matunzo kidogo atafanikisha kuwadanganya watu kuwa ni mpenzi wake halisi kumbe ni feki.
Wasiwasi wake kwa muda huo ni ugonjwa wake tu, lakini kulingana na vipengele vya mkataba huo aliamini Hamza kila atakachokiona kwake kwa bahati mbaya basi itakuwa ni siri.
“The contract is roughly like this , first I’ll rent it for three months, then we‘ll see how it goes , do you have any objections?”Aliongea kwa kingereza kitamu makusudi kabisa akitaka kumpima Hamza uwezo wake wa kuongea kingereza.
Hamza alitoa tabasamu , kadri mrembo huyo anavyoongea ndio alivyokuwa akipata hali ya kujiamini na kumzoea na palepale alishika mkataba ule na kupitia kwa haraka haraka kabla ya kusaini.
“Miss Regina , I have a few questions that I need to confirm first”Aliongea akimaanisha kwamba anayo maswali kadhaa ya kuuliza kujihakikishia kwanza.
“Unaweza kuuliza?”
“Vipi kama itatokea nipo kwenye kipindi na siwezi kuja kwako mara baada ya kunipigia simu na nikapoteza muda?”
“Upo makini , inaonekana pia ni mwanafunzi mtiifu”
“Nishatoa ada hivyo nataka kuitumia vizuri”Aliongea na kumfanya Regina kuonyesha ishara ya kuridhika, hakujali kuhusu Hamza bado kuendelea na masomo , alichojali alionekana kuwa siriasi, na yeye alikuwa akitafuta mtu siriasi.
“Usijali siwezi kukusumbua wakati wa masomo yako , utanipa ratiba ya vipindi na kama kuna dharula utaniambia”
“Hapo vizuri , naona na wewe pia ni mtu muwajibikaji” Aliongea huku akiwa na tabasamu na muda uleule simu yake ilianza kuita na kujikuta akilaani kimoyo moyo , Regina s alimpa ishara ya kuipokea na Hamza mara baada ya kuangalia jina la mtu anaepiga ni Iryn.
“Huyu ni mwanafunzi wangu namfundisha masomo ya jioni twisheni , yupo form six anapiga maana jioni ya leo nina kipindi nae”aliongea Hamza.
“Hakuna shida unaweza kupokea na kumsikiliza sina haraka” Aliongea Regina na palepale Hamza alipokea.
“Ticha nadhani hujasahau leo tuna kipindi?”
“Najua lakini si niliwasiliana na mama yako na kumwambia tutaanza wiki ijayo?, kwasasa nina kazi nyingine hivyo nitakuwa bize tutaanza wiki inayokuja kulingana na nilivyokubaliana na mzazi wako”
“Oh! , Mama hajaniambia kuhusu hili”Sauti nzuri ya kike ilisikika.
“Unaweza kumuuliza tu “
“Basi sawa nadhani tutaonana wiki ijayo”Aliongea huyo mwanamke na palepale simu ilikatwa na kwa sauti ya Iryn alijua tu lazima amekasirika.
Ukweli ni kwamba Hamza katika kujitafutia kipato alikuwa akifanya kazi za aina mbalimbali ,miezi kadhaa iliopita wakati akifanya kazi ya kibarua chini ya kampuni ya mazingira ya Tata ndio aliweza kukutana na Mama Iryn nyumbani kwake kwa mara ya kwanza na hapo ndio mwanamama huyo alimfahamu Hamza ni mwanachuo kutoka FEMU ,
Sasa katika kuongea ndio mama huyo alisema ana binti yake kutoka shule ya sekondari ya Alpha na anachukua masomo ya EGM na alimuomba kama ingewezekana kwa Hamza kumfundisha twisheni kwa malipo na Hamza alikuwa na uhitaji wa pesa hivyo hakukataa.
Tatizo lilianza mara baada ya kufanya vipindi kadhaa na Iryn alianza kumtega Hamza na kumtaka kimapenzi,, Hamza alikuwa hana mwanamke ndio lakini hakuwa tayari kutoka na mwanafunzi na hio yote ni kutokana na mama yake Iryn kuweka imani kubwa kwake hivyo kutokana na dalili hizo Hamza alikuwa akimkwepa Iryn kiaina.
Ki ufupi Hamza ni mtu wa harakati na aliishi kwa kuchakalika , hakuchagua kazi ili mradi ilikuwa na pesa, lakini kwa Iryn ilikuwa ngumu licha ya kazi hio ilikuwa na malipo mazuri kutokana na mama yake Iryn kutokea kumpenda Hamza.
Kitu kingine sio kwamba Hamza alishindwa kumuonya lakini ukweli ni kwamba Iryn alikuwa binti mrembo sana ambaye kwa mwanaume rijali yoyote yule ni rahisi kuingia kwenye mtego wake ndio maana alikuwa akiona ugumu.
“Samahani Miss Regina kwa kukuchelewesha wakati naongea na simu”Aliijibu Hamza.
“Hakuna shida , kama huna pingamizi lolote unaweza kusaini mkataba”Aliongea.
Ijapokuwa sauti yake ilikuwa ya kirafiki lakini alionekana kuwa kauzu mno na hata Hamza mwenyewe alijiambia hajawahi kuona mwanamke Kauzu kama huyo halafu mrembo , lakini alichopenda ni kwamba hakuona aina yoyote ya Dharau,
Hamza alitia sahihi yake kama vile ana saini mkataba wa mabilioni kwa niaba ya nchi , sahihi yake ilikuwa nzuri mno na kumfanya hata Regina kushangaa kidogo, ilionekana Hamza alikuwa na mwandiko mzuri sana kwa kuangalia sahihi yake tu.
Baada ya kutia sahihi yake na Leilani kutia sahihi yake palepale alifungua mkoba wake na kutoa bahasha na kumpatia.
“Haya ni malipo ya utangulizi kama mkataba unavyosema ni milioni tano , unaweza kuhesabu kujihakikishia, lakini hela zipo katika mfumo wa dollar hivyo utazibadili”Aliongea na Hamza alipokea ile bahasha .
“Haina haja ya kuhesabu uzito wa bill ya dollar mia ni sawa na gramu 1.51 na humu ndani kuna dollar elfu mbili hivyo uzito wake ni sawa na gramu 30.2, hivyo kwa kuzingatia uzito huu basi hesabu zipo sawa”
Leilani macho yake mazuri yalichanua , hakuamini kama mtu anaweza kuhesabu hela kwa kuzingatia uzito wake tu , moja kwa moja ilimwambia mtu ambaye yupo mbele yake anapenda sana hela na hilo lilimuongezea pointi.
Upande wa Hamza alifanya makusudi tokea jana yake alikuwa akipanga namna ya kukubalika na kushinda usaili na alikuwa na mbinu nyingi lakini hata hivyo mbinu zake hakuwa ameziandaa na kutokana na kuamini kichwa chake kilivyo chepesi basi angetunga hapo hapo.
Sasa mara baada ya kupewa kibunda alitaka kumhakikishia Regina kwamba yeye anajali sana pesa kuliko kitu chochote kile.
Unajua bwana watu wanaopenda hela ni rahisi kuwakontrol na kuwaambia hiki na kile na wakatii kuliko watu ambao hawapendi sana hela mara nyingi wanakuwa sio watiifu hio ni kanuni ambayo Hamza aliizingatia.
Regina aliona na hicho ni kigezo pia ambacho alikuwa akitafuta , alitaka pia mtu ambaye anakwenda kuigiza kama mpenzi wake awe anapenda pesa ili iwe rahisi kumuendesha.
Regina mara baada ya kuzuia mshangao wake aliingiza mkono wake kwenye mkoba na kisha akaibuka na bahasha nyingine na kumpatia Hamza.
“Katika hii nyaraka kuna taarifa ambazo zinahusiana kuhusu wewe na mimi namna ambavyo tumekutana na tulivyoanza kuwa pamoja , nenda nayo na ukaisome uilewe lakini hakikisha hakuna mtu ambaye ataiona.”
Hamza hakuamini mwanamke huyo kuwa profesheno kwenye kazi yake namna hio na alitoa tabasamu na kuchukua ile bahasha.
“Nitaisoma kwa umakini nikisharudi”
“Kesho asubuhi saa nne kamili tukutane Dosam Tower kwenye parking B2, hakikisha hauchelewi”Baada ya kuongea kauli hio alisimama akitaka kuondoka.
“Ms Regina usiwe na wasiwasi , mimi najali sana muda”
“That is for the best”Aliongea na Hamza aliangalia glasi ya juisi ambayo ilikuwa mbele ya mwanamke huyo , alichukua ya kwake kwanza na kuinywa na kisha akamwangalia.
“Ms Regina bado umebakisha nusu ya juisi yako”
“Siitaki tena”Aliongea.
“Utakuwa ni uharibifu sana kwa alieitengeneza”Aliongea Hamza na palepale aliinua ile glasi na kisha akainywa yote kwa mkupuo mmoja.
Mrembo Regina alitaka kumzuia lakini aliona aibu kwa kitendo chake na mawazo yake ya kijinga yalimwambia anachokifanya Hamza ni kubusiana nae kwa njia isio ya moja kwa moja.
Hamza na Regina walitoka pamoja na sasa rasmi Hamza alikuwa ni mpenzi feki wa mrembo Regina , Hamza ijapokuwa alikuwa hapo kwa kazi lakini alijiambia atahakikisha huyo mrembo anampenda mwenyewe.
Baada ya kutoka nje ya mlango alimwambia mlinzi wake kwenda nyumbani na kuanzia hapo ataendesha gari yake mwenyewe , mwanadada yule mlinzi alitaka kugoma lakini alikubali na aliishia kumwangalia bosi wake na Hamza wakitokomea kwenye lift akiwa katika hali ya wasiwasi.
Haikueleweka Prisila alikuwa ameenda wapi na Hamza alitamani kumuona mara ya mwisho , kwake ni kama alikuwa ameokota embe kwenye mnazi.
Baada ya kutoka kwenye lift watu waliokuwa eneo la mapokezi walikuwa wakimwangalia mrembo Regina kwa macho ya mshangao na matamanio lakini alionyesha kutojali na moja kwa moja alitoka nje na kwenda upande wa magari yalipoegeshwa na kusogelea gari moja ya kifaharai aina ya Maserati Gran Gabrio.
Uzuri wa lile gari ulimfanya Hamza kumwangalia kwa macho yaliokuwa na matamanio ilikuwa ni gari ambayo inaendana na muonekano wake,
“Hivi ulisema upo mwaka wa ingapi chuo?”
“Nipo mwaka wa tatu , kuna tatizo?”Aliuliza Hamza kiwasiwasi.
“Hakuna”
Aliongea na palepale kimadaha aliingia upande wa mbele ya gari na kuliwasha.
Regina alijihisi kujiamini na kuona sio mbaya mwanafunzi wa digrii ya uchumi mwaka wa tatu anamfaa sana.












SEHEMU YA 08.
Hamza alihisi siku hio ni kama vile muda wowote ataamka kutoka ndondoni , ndoto ambayo ilianzia tokea siku ambayo aliweza kusoma Tangazo la ajira ya mchumba feki katika mtandao wa JamiiForum mpaka siku hio ambayo ameweza kupata kazi hio.
Wakati anatoka katika hoteli ya Dosam V alitamani kuonana na mrembo Prisca lakini kwa bahati mbaya hakumuona na alijua pengine amekwisha kuondoka hivyo hakutaka hata kujisumbua kumtafuta na kutoka zake katika hio hoteli na kuelekea nje.
Alikuja kwa usafiri wa mwendokasi hivyo kama ni kurudi nyumbani alipaswa kuondoka kwa mwendokasi.
Wakati akiwa anapita eneo la Posta ya Zamani akitembea huku kichwa chake kikiwa katika mawazo mbalimbali alijikuta akisimama kwa muda na palepale ilionekan kuna wazo lilimuingia , wazo hilo lilimwambia huo sio wakati wa kurudi moja kwa moja geto kwake bali anapaswa kutafuta mahali kukaa na kupunga upepo na mahali alipoona panamfaa ni maeneo ya Kivukoni.
Ukweli ni kwamba wazo hilo lilimjia kutokana na kutaka kukaa chini na kuanza kutafakari mambo ya kimaajabu ambayo yamemtokea siku hio ndio maana.
Hamza maisha yake yalikuwa ni yenye maajabu tokea alivyokuwa mdogo mpaka kufikia wakati huo na msururu wa maajabu huo ulionekana kutokukoma katika maisha yake.
Maisha ni msururu wa mshangao , mzuri na mbaya na hatujui ni kipi kipo katika dakika nne zinazofuatia na hichi ndio kinafanya maisha yawe ni yenye msisimko mkubwa na muda ambao maisha yanapokutupia mshangao chukua muda wako kutathimini yale ambayo hayakuwa ndani ya matarajo na hicho ndio ambacho aliona.
Hamza alitumia zaidi ya lisaa kufikiria kile ambacho kimetokea siku hio , licha ya kwamba alikuwa na mambo mengi ya kuwazia lakini ambalo limetokea siku hio alilipa kipaumbele.
Ukweli ni kwamba hakujua kitakacho kwenda kutokea kwanzia siku zitakazofuatia lakini aliamini chochote kile ambacho kitamtokea kitakuwa ni jambo lenye msisimko mkubwa.
Alikuja kushitushwa na simu yake ambayo ilianza kuita mfululizo na mara baada ya kuotoa na kuangalia aliekuwa akimpigia ni Mama mmoja ambaye alishawahi kwenda kufanya kazi kwake kwa kutengeneza AC(Air Conditioner) yake ilipoharibika na alishangaa mama huyo kumpigia lakini moja kwa moja alijua lazima atakuwa na kazi hivyo alipokea kwa furaha zote.
Ijapokuwa alikuwa na pesa nyingi mfukoni ambazo zingemtosha katika matumizi ya takribani mwezi mmoja kabla ya kupokea mshahara wake wa kwanza lakini bado hakutaka kudharau kazi ambazo zimemsukuma na kumfikisha leo hio.
“Kijana habari yako?”
Sauti ya mwanamama mtu mzima iliweza kusikika upande wa pili ya simu.
“Salama mama habari za masiku?”
“Ni nzuri tu , bado unapatikana hapa Dar sik hizi?”
“Ndio Mama nipo”
“Oh! basi vizuri, kuna jirani yangu nae kapatwa na shida kama ileile ya kwangu , je unaweza kufiika kumsaidia kumtengenezea?”
“Mama mimi kama malipo yapo ninaweza kuja hata muda huu?”
“Asante sana baba yangu , mimi nipo kazini kwasasa lakini yeye pia atakuwa ndio anatoka kazini nitakupatia namba yake uwasiliane nae ukifika”
“Sawa mama Asante kwa kuniunganisha na hii kazi?”Aliongea Hamza na mara baada ya simu kukatwa alitoa tabasamu na kuangalia saa yake na kuona ilikuwa imetimu saa tisa hivi.
Ukweli muda huo alikuwa akijichukulia kama mwajiriwa lakini kwasababu kwake pesa ilikuwa kipaumbele hakuona haja ya kukataa kazi , hata hivyo licha ya kwamba chuoni alikuwa akisomea maswala ya uhumi na uhasibu lakini ukweli alikuwa akipendasana kazi ya ufundi , ni kama alikuwa na kipaji hicho kwani kazi ambazo nyingi alikuwa akifanya zilikuwa ni za ufundi, kusoma uhasibu ilikuwa ni sehemu ya maagizo ya Mzee.
Shukrani kwa mtandao wa The Job uliweza kumuunganisha na watu wengi ndani ya jiji la Dar es salaam ambao wana shida na maswala ya ufundi na ndio katika mtandao huo ambapo aliweza kupata kazi kwa mama huyo.
Eneo la kazi ilikuwa ni Kigamboni na kwasababu alikuwa kivukoni ilikuwa rahisi kusafiri kutoka hapo kuelekea huko lakini alikuja kugundua kwamba hakuwa na vitu muhimu vya kumsaidia kutengeneza lakini kutokana na kuwa na hela kidogo mfukoni aliona atapitia dukani na kununua vifaa.
Kazi yenyewe ilikuwa ni kurekebisha AC hivyo licha ya kwamba mama huyo kamwambia tatizo lilikuwa kama la kwake matatizo ya AC hayafanani hivyo kwanza alipaswa kuona tatizo na hapo ndio atajua namna ya kudili na tatizo.
Dakika chache Hamza alikuwa ashafika katika Apartment za Lotus , jambo moja ambalo Hamza alipenda kwenye hizo Apartment ni kwamba zilikuwa zikikaa wanawake tupu tena wale ambao hawajaolewa.
Unaweza ukashangaa lakini inasemekeana ndio utaratibu uliowekwa na mmiliki wa Apartment hizo ambazo asilimia kubwa ya wanaoshi hapo ni wafanyakazi a kampuni ya Dosam Global.
Sio kwamba kampuni hio ilikuwa ikipendelea wanawake, hapana bali ukweli ni kwamba ilikuwa imejenga majengo hayo kwa kulingana na stutus, yaani kama mwanamke ameolewa basi haruhusiwi kukaa ndani ya Apartment hizo.
Ni sehemu maarufu sana ndani ya jiji la Dar es salaam kwa kuwa na warembo wa viwango , yaani hakuna pisi mbovu ambazo zilikuwa zikishi ndani ya jengo hilo na hio yote ni kutokana na aina yao ya kazi , asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Dosam wa kike aidha ni wafanyakazi ndani ya hoteli, Shopping Mall, Wahudumu wa ndege na Benki.
Yaani kwa haraka sana ni kwamba kampuni ya Dosam inajihusisha na biashara za miamala(Dosam Bank ) , Usafiri wa Anga (Dosam Air) ,Mahoteli(Dosam hotels and hospitality) na maduka(Dosam Distributions&Department store).
Sasa aina ya kampuni hizo ni kwamba zinahitaji sana wafanyakazi ambao wana mvuto wa kipekee kimuonekano iwe ni mwaname au mwanamke , kwa mfano mhudumu wa Hoteli hawezi kuwa na sura ngumu lazima awe na sura ambayo akitabasamu mgeni palepale anavutik, bila shaka hicho sio kigezo pekee cha kuajiriwa ndani ya kampuni hio kikubwa ni ujuzi na taaluma, moenekano ni sifa ya ziada tu.
Sasa asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Dosam walikuwa wakiishi katika Apartment za kampuni kwa wale ambao hawana makazi ,sio sheria kuishi katika Apartment hizo lakini asilimia kubwa ya wafanyakazi walikuwa wakiishi katika Apartment hizo kutokana na kwamba walikuwa wakilipia gharama nusu halafu mazingira ni Premium.
Yaani kama nyumba kwa mwezi ni milioni moja basi mfanyakazi hulipia laki tano, huo ni mfano tu na sio gharama husika..
Sasa nyumba hizo mara nyingi ni kama zimetengwa japo si sheria, kuna Apartment ambayo inachukua tu wanaume ambao ni mabachela na kuna Apartment ambayo ilikuwa ikichukua wanawake ambao ni mabachela na kuna nyingine ambayo ilikuwa ikipangisha wale ambao wameoa au kuolewa , yaani familia.
Sasa katika Apartment zote ambazo zinakaliwa na wafanyakazi wa kampuni ni hio ya Lotus Flower Apartment, hio Apartent ilikuwa na warembo sio mchezo , ilikwa ikiendana na jina lake, wanaume wengi mabachela walikuwa wakitembelea hapo kujaribu bahati zao.
Ukitaka kuthibitisha hilo ni nje ya eneo la apartment hio kulikuwa na Dustibin kubwa ambayo ilikuwa na maua mengi sana pamoja na kadi , yote hayo ni wanaume ambao walikuwa wakitembelea mji huo kwa ajili ya kujaribu bahati zao na pale ambapo wanakataliwa wanaishia kutupa maua yao pamoja na kadi zao kwenye Dustibin hizo na kuondoka.
Hamza alikuwa akisikia habari za Apartment hii lakini ukweli ni kwamba siku ambayo alikuja kufanya kazi ilikuwa ni muda wa mchana muda wa kazi hivyo hakukutana na warembo wengi.
Ilikuwa ni muda ambao Hamza anakaribia kufika ndani ya Aparttn hizo , mita kadhaa kabla ya lilipo geti aliweza kuona gari mbili zilikiwa zimesimama, moja ilikuwa ni gari aina ya Aud na nyingine ilikuwa ni gari aina ya Noah.
Kwa macho yake ambayo yanaona mbali aliweza kushuhudia mwanamke ambaye alikuwa amezingirwa na wanaume na ilionekana ni kama vile wanaume wale walikuwa wakibishana hivi na yule msichana kwa kumzonga zonga.
Hamza jambo lile lilimtia shauku na kuongeza mwendo ili kujua kililichokuwa kikiendelea , ukweli ni kwamba hata kama asingetaka kujua angejua tu kwani watu hao walikuwa wamesimama njiani kuingia katika Apartment hizo.
“Eliza nimechoshwa na majibu yako ya kis**nge , ninachotaka leo hii ni pesa zangu na si vinginevyo”Mzee mmoja mwenye mwili ambao ulikuwa umetuna kidogo aliongea.
“Mzee Amosi nilishakuambia nivumilie , hela unayonidai ni nyingi na sasa hivi sina uwezo wa kupata mkopo tena, unafikiri kiasi chote hicho nitatoa wapi , isitoshe hela ambazo nimekupatia ni kiasi kikubwa mno kuliko hata ulichonikopesha, unachonidai hapa ni riba”
“Sitaki maelezo yako Eliza yashanichosha na kila siku unatoa kauli zinazofanana , hivyo leo una chaguzi mbili aidha ukubaliane na sharti ambalo nakuambia kila siku na tuondoke pamoja urudi kesho au unipate pesa yangu leo hii, kama hela huna na sharti langu hukubaliani nalo basi vijana niliokuja nao watafanya kazi yao”Aliongea kwa kufoka.
Hamza ambaye ndio sasa amekaribia karibu alikuwa akisikia kila kitu na kwa haraka haraka aliweza kuelewa kinachoendelea, kwanza ilionekana watu hao walimkinga mwanadada huyo kupitisha gari kuingia ndani na ilionekana walikuwa wakimdai pesa.
Kadri mzozo huo ulivyokuwa ukiongezeka wanawake baadhi ambao walikuwa wakiishi ndani ya hilo eneo walikuwa wanajikusanya huku wakionyesha hofu ya kuamulia ule ugomvi , ni kama walikuwa wakimjua huyo mzee ambaye anaonyesha yupo kifujo fujo hata kama anadai pesa yake.
“Mzee Amosi naomba usinifanyie hivyo , kwanini unakosa utu?”
“Haha,… leo ndio unasema sina utu , wakati nakupatia pesa yangu nani alimbembeleza mwenzake, kama nisingekuwa na utu nisingekupatia kiasi chote kile cha pesa , sasa mama yako amekwisha kupona lakini unashindwa kulipa pesa yangu , kingine unasema unalipa riba kwani makubaliano yetu yapoje wakati unachukua mkopo?, hebu acha kupoteza muda , nimekupa njia nyepesi kabisa lakini unaleta maringo , kwani mimi ni mbaya sana mpaka ushindwe kutii sharti langu dogo namna hio?”
Hamza ambaye mara baada ya kusikia kauli hio alijua kabisa hapo huyo mwanaume sio kama alikuwa na shida sana ya pesa au huyo mwanadada mrembo alikuwa ameshindwa kulipa ila ilionekana analazimisha kulipwa pesa yake hapo hapo akijua huyo mwanadada atashindwa kuitoa ili akubaliane na sharti lingine ambalo kwa haraka haraka alijua ni ngono.
Hamza alifikiria kidogo mwanamke aliekuwa akizongwa alionekana kuwa mrembo mno, lakini kwasababu watu walikuwa wakiongezeka kukusanyika ndani ya eneo hilo hakuona haja ya kuendelea kusimama kwani muda ulikuwa ukisogea kwa kasi hivyo palepale alitoa simu yake na kutafuta namba ambayo alitumiwa na kisha akaipiga.
Akiwa amesogea pembeni ya barabara aliweza kusikia simu ile ilikuwa ikiita pasipo ya kupokelewa na iliita mpaka ikakatika , akarudia kupiga na ikaita mpaka ikakatika mara baada ya kurudia mara ya nne akijiambia isipopokelewa anaondoka palepale simu ilipokelewa.
“Sikia Eliza sitaki kukudhalilisha na isitoshe mimi na wewe tumetoka mbali , kama huna hela kwanini tusiwe wote wastaarabu,ongozana na mimi na kuondoka mbele ya macho haya ya watu?”
“Helloo..!!!”
Hamza alianza kuongea lakini sauti ambayo ameweza kusikia ni ya mwanaume ambae anamdai Eliza , palepale aligeuza sura yake na kuangalia upande wa ugomvi unapoendelea na alikuwa haoni vizuri kutokana na kuzibiwa na watu na ilimfanya kusogea karibu zaidi.
“Boss amepokea simu..?”
“Kijana ambaye alikuwa karibu na yule mzee alieitwa Amosi aliongea na kauli ile ilimfanya Amosi kumwangalia Eliza mkononni mwake na palepale alimpokonya ile simu.
“Umetutegeshea simu sio , Eliza kwanini unaenda mbali hivi?”Aliongea huku hasira zikionekana zaidi na zaidi katika macho yake huku akiwa tayari ashakata ile simu.
Upande wa Hamza mara baada ya simu ile kukatwa palepale alijua mtu ambaye anapaswa kuja kumfanyia kazi ni huyo mrembo ambaye anadhalilishwa na wadeni wake.
“Nakuuliza ulikuwa ukiongea na nani?”Amosi alipatwa na mashaka na palepale alimshikilia mkono na kummnya Eliza kwenye gari.
“Puuh!!!”
Haikueleweka imekuwaje lakini Amosi alijikuta akidondoka kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu kama vile amevutwa.
Kitendo kile kilishangaza waliokuwa wakiangaliana na hapo hapo ndipo sasa waligundua Amosi alikuwa amevutwa kurudi nyuma na kijana ambaye alikuwa amefika hapo muda huo.
Hata Eliza hakujua namna ambavyo Amosi alitoka mbele yake na alijikuta akiinua uso wake ambao alikuwa amefumba macho kwa kile ambacho alitegemea kufanyiwa na hapo ndipo alipoweza kushuhudia sura ya kijana ambaye amesimama mbele yake.
“Dogo unakitafuta kifo sio?”Mzee Amosi mara baada ya akili yake kufanya kazi alionyesha kukasirika mno kwa kile alichofanyiwa.
“Mzee hebu tuliza kwanza jazba najua una shida na huyu mwanadada lakini vilevile na mimi nina shida nae”Aliongea Hamza kwa sauti iliojaa upole , ni kama alikuwa akitania hivi na kufanya watu kumshangaa , hata Eliza mwenyewe alionekana kushangaa na kujiuliza huyo kijana ni nani kwanini anajiingiza kwenye mgogoro wake na kusababisha matatizo zaidi.
“Chongolo mnashangaa nini , hebu mshikisheni kwanza adabu ndio tuongee nae vizuri na kumjua ni nani”Aliongea Amosi kwa hasira , hakutaka kusikia ngonjera za kijana huyo.
Chongolo mara baada ya akili yake kurudishwa kwenye uhalisia ni kama alishituka na palepale pamoja na wenzake wawili walimsogelea Hamza kwa ajili ya kumdhibiti.
“Mamaa…!!!”
Kijana mmoja ambae alikuwa kimbelembele mara baada ya kumsogelea Hamza alijikuta akipigwa teke la kigoti na kumfanya atoe ukulele huku akichuchumaa chini kutokana na maumivu.
Kitendo kile kilishangazwa wengi kwani kilitokea kwa spidi ya hali ya juu sana kutoka kwa Hamza , ilikuwa ni kama vile alikuwa na uzoefu wa hali ya juu kwenye kudili na watu wa namna hio.
Wale wengine mara baada ya kuona kiilichomtokea wenzao ni kama hawakuaini amini kama shamblizi hilo lilitoka kwa kijana wasiemjua na moja kwa moja hasira zao ziliongezeka mara mbili na kusogelea Hamza kwa kasi.
Puuh! , Bam!!!”
Chongolo mara baada ya kumsogelea Hamza kwa ajili ya kurusha ngumi mkono wake ulidakwa ukiwa hewani na kuvutwa mbele , wakati huo huo yule mwenzake aliekuwa nyuma akipigwa teke la makagari na kumfanya adondoke kama furushi huku Chongolo akisukumiziwa kwenye kiooo cha mbele cha gari ya Noah kiasi cha kutengeneza ufa.
“Sikutaka kwenda mbali hivi ila nachukia kupotezewa muda, Mzee unaonaje ukirudi siku nyingine kudai pesa yako, nahitaji kumalizana na huyu mrembo mapema nirudi kwenye shughuli zangu nyingine”Aliongea Hamza huku akimwangalia Mzee Amosi ambae alionekana kuwa katika kiwewe asiamini vijana wake watatu aliokuwa akiwaamini kupambana na watu ndani ya dakika moja tu wamedhibitiwa na wote wanaugulia maumivu.
Alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa ya kawaida kama kwamba alikuwa akimtathimini.
Mzee Amosi alionekana kutafakari kwa muda , kwa jinsi alivyomuona Hamza akifanya mashambulizi na kupitia uzoefu wake wa miaka mingi kuna kitu alikiona haraka haraka na hakutaka kuendelea kuuliza ni nani.
“Chongolo tuondokeni tutarudi , Eliza jiandae siku nitakayorudi sitokuwa na huruma tena , ni kheri upige simu mapema kabla ya kukutafuta”Aliongea Mzee yule huku akimwangalia Eliza kwa macho makali na kisha alipangua watu na kuingia ndani ya gari.
Hamza mara baada ya kuona mzee huyo amekuwa mtiifu kwake alijikuta akivuta pumzi za ahueni maana hakutaka kwenda mbali sana.
Wakati akiona amefanya jambo la kawaida upande wa watu waliokuwa ndani ya eneo hilo walionekana kuwa katika mshangao, kila mtu alikuwa na lake kichwani na kuna wale walioamini huenda Hamza ni mwanajeshi licha ya kwamba muonekano wake haukuwa ukisanifu kile alichokifanya.
Mrembo Eliza alikuwa ni kama haamini alikuwa amesalimika na aliemsaidia ni kijana aliekuwa mbele yake ambaye ndio mara yake ya kwanza kukutana nae, maswali kibao yalichipua katika akili yake lakini alishindwa kuuliza zaidi ya kumwangalia Hamza bila ya neno.
Hamza ni kama sasa alikuwa akimthaminisha mrembo huyo , wakati anafanya maamuzi ya kumsaidia mwanamke huyo hakufikiria sana kwa sababau aliamini akifukuza watu wale kazi yake iliomleta hapo itaisha haraka na kupata ujira wake , lakini mara baada ya kukutanisha macho na msichana huyo aliekuwa katika hali ya mshangao ni kama sasa alikuwa akipata wazo la pili.
“Kwanini ndani ya hizi siku chache nimekuwa nikikutana na wanawake warembo namna hii , hii ni ishara nzuri kwangu au mbaya?”Hamza alijiuliza swali hilo.
Alikumbuka wakati alipokuwa katika Apartment za Dosam Homes alikutana na mwanamke aliefahamika kwa jina la Tresha Noah, akaja kukutana na mrembo aliempelekea chungu , hatimae Prisca , Mrembo Regita ambae ndio alimshangaza zaidi na hatimae leo hio anakutana na msichana aliefahamika kwa jina la Eliza.
Kama angewapangilia warembo hao kulingana na uzuri wao basi Regina angeshika namba moja , Prisca namba mbili , huyo Eliza namba tatu , Anitha namba nne na kisha Tresha Noah namba tano.
Ukweli Tresha Noah alikuwa akifikiana uzuri na huyo Eliza lakini alikosa vigezo katika macho ya Hamza mara baada ya Amiri kumwambia uzuri wake ni wa kutengeneza.
“Kaka upo vizuri kwa kweli , ni mara ya kwanza kuona mtu mwenye uwezo wa kuwashinda wale Vibaka ,Wewe ni mwanajeshi au polisi , Vipi Eliza ni mpenzi wako?”Kundi lile la wanawake waliokuwa wakiangalia tukio hilo walimzunguka Hamza wakitaka kusikia neno kutoka kwake.
“Eliza kumbe una mpenzi mwanajeshi na husemi jirani?”Aliongea wanamama mwingine na kumfanya Eliza kushangazwa na swali hilo na kuishia kumwangalia Hamza.
“Jamani mimi sina mahusiano na huyu dada , mimi ni fundi na nimekuja kutengeneza AC , kama kuna yoyote mwenye shida inayohitaji fundi nipo hapa natengeneza kila kitu”
Kauli ya Hamza iliwashangaza wanawake waliokuwa wamemsikia , ila kauli ile ni kama haijamfurahisha Eliza ni kama vile alitamani Hamza akubali na aseme niwapenzi hata yeye mwenyewe alijishangaa kuwa na mawazo ya namna hio , pengine ni kutokana na kuwa single kwa muda mrefu..
“Handsome , upo siriasi unatengeneza kila kitu?, unaonaje ukatengeneza na moyo wangu ulioumizwa”Aliongea mrembo mmoja ambae alikuwa ametumia Make up nyingi mno huku akiwa na kikuku mguuni.
“Recho..!!!”Aliongea Eliza ambae ni kama vile ameamka sasa kutoka kwenye mshangao na kumsogelea Hamza.
“Kaka tunaweza kwenda ukaanganlie shida ya Ac yangu”Aliongea Eliza na kwasababu alikuwa na aibu za kutosha kuendelea kukaa katika eneo hilo kwa yale yaliomsibu alimchukua Hamza na wakaingia ndani huku wakimwacha mwanadada aliefahamika kwa jina la Recho akivuta mdomo.
Hamza alikuwa kimya kimya na mwanamke huyo mpaka wanaingia kwenye lift, ilikuwa ni kama vile amerudi kwenye upole wake.
Ukweli ni kwamba Hamza kimuonekano alikuwa mpole sana lakini matendo yake yalikuwa tofauti na yeye alivyo , haikueleweka ana historia gani ya maisha yake ya yuma lakini ni rahisi kuotea maisha yake hayakuwa ya kawaida.
Eliza na yeye ilikuwa mara yake ya kwanza kusaidiwa na mwanaume , tena mbele ya wale waliokuwa wakimdai.
“Asante kaka kwa kunisaidia”Aliongea Eliza kwa kukosa kujiamini na kumshitua Hamza aliekuwa akijiwazia mambo ya ajabu na yote hayo ni kutokana na kumtamani mrembo huyo Eliza.
“Hii tabia ya kuwazia kile mwanamke inatokana na kukosa mchezo muda mrefu nini?”Alijiwazia Hamza.
“Hakuna shida ya kunishukuru Eliza , kama nilivyosema nimekusaidia ili kumaliza kazi yangu kwa haraka”Aliongea Hamza huku akijiona kidume na kauli ile ilimfanya Eliza kumwangalia Hamza kwa macho ya kidadisi, ni kama vile alikuwa amejawa na hamu ya kumjua vizuri Hamza.
Kwa mtu yoyote pengine siku hio angevutiwa na Hamza hususani kwa muonekao wake na kwa kile abacho amefanya dakika chache zilizopita.
Hamza hakuwa amebadili mavazi yake ambayo yalikuwa mapya na mtindo wa nywele ulikuwa umempendeza sasa ukijumlisha na ngozi yake yenye mchanganyo wa kizungu ilimfanya kuwa mtanashati kupindukia na hakika mwanamke yoyote angempenda na kuvutiwa nae , siku hio hakuwa akionekana kama fundi kabisa , kwa kumlinganisha na mrembo Eliza moja kwa moja kwa tu asie na uelewa atasema wawili hao ni wapenzi kwa namna wanavyoendana.
“Ding..!!!”
Lift ilifunguka katika Ghorofa ya kumi na tano ambayo ndio mwisho kabisa , mazingira ya Jengo hilo yalikuwa yakvutia mno , yamejaa ufahari wa macho , Ijapokuwa haikuwa kama apartment za Dosam Homes lakini ni mazingira ambayo yanatosha kuhifadhi watu wa vipato vya kati na juu.
“Karibu kaka”
“Asante , unaweza kuniita Hamza”Aliongea Hamza huku akijitahidi kuonekana mpole mbele ya mwanamke huyo , ni kama alikuwa akijitahidi kumpangawisha Eliza.
“Oh karibu sana Hamza fundi”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu, alitamani aendelee kuisikia sauti ya Eliza kwani ni kama ilikuwa ikibembeleza.
Kama alivyotegemea nyumba hio ilikuwa safi mno na mpangilio wake ulikuwa ni wa kiwango cha juu , kulingana na uzoefu wa Hamza hata apartment ya Mellisa mwanamke wa Amiri haikuwa na mpangilio safi kama huo , ijapokuwa hakuona chumbani kulivyo lakini eneo la sebuleni lilimpa picha.
Wazungu wanasema ‘A house is a mirror to its owner’ hivyo mazingira ya eneo hilo yalimpa picha kamili Eliza ni mwanamke wa namna gani.
“Hamza sijui nikukaribishe kwanza kinywaji au uanze kazi moja kwa moja nikikuandalia chochote”Aliongea Eliza ambae alionekana kukosa kujiamini kwa namna flani hivi , pengine ilikuwa ni kwasababu ya kile kilichomtokea dakika kadhaa ilizopita mpaka Hamza kuingilia kati.
“Kwa leo naomba niende moja kwa moja kwenye ufundi , itakuwa vizuri baada ya ufundi kupata hata juisi tu itatosha kutia baraka”Aliongea Hamza akijiamini .
*****
Upande mwingine ikiwa ni dakika kadhaa tokea kuondoka kwa Amosi na kundi lake , ikiwa ni kilomita kadhaa kutoka eneo hilo la Apartment walienda kusimamisha gari katika moja ya mgahawa na kabla ya Amosi kushuka aliwaangalia vijana wake waliokuwa hawajiamini kwa kile kilichotokea na kisha akavuta pumzi.
“Chongolo nadhani unajua hii kazi hainihusu mimi moja kwa moja bali ni bosi, kama atasikie kile ambacho kimetokea leo hii nadhani kuna swala lolote ambalo litatokea , nani anajua anachokiwaza bosi sasa hivi?”Aliongea Amosi.
“Mkuu tunapaswa kufanya nini?”
“Inamaana bado tu hamjaelewa ninachomaanisha , mbona mnakuwa na vichwa vidogo namna hii”Aliongea Amosi huku akionyesha kukasirika , ni kama aliongea kauli tatanishi ili mradi wasielewe ili tu awafokee kupunguza hasira zake.
“Sikieni kuhusu Eliza hili swala nitaongea na bosi mwenyewe , ninachotaka ni kumfatilia yule mpuuzi alievuruga mipango yetu, kazi hii inaanza sasa hivi mtaondoka na gari”Aliongea Amosi na palepale akashuka kwenye gari na kisha akaingia katika Mgahawa huo.
Hazikupita dakika kadhaa Chongolo na wenzake waliondosha gari hio ya Noah na kutokomea upande waliotokea.
Amosi alitembea kiwasiwasi kuingia ndani ya Mgahawa huo wa kisasa , kulikuwa na watu wachache sana lakini hao wachache walionyesha ni wale wenye uwezo mkubwa wa kifedha.
“Unavyonifanyia sio vizuri , unajua kabisa nakupenda lakini kwanini leo unataka kukatisha mahusiano yetu , kwanini unanifanyia hivi Chriss”
“Anitha unaenda mbali na nadhani akili yako haifanyi kazi vizuri , mimi na wewe nani alitaka mahusiano , ulinifuata mwenyewe ukitaka niwe Boyfriend wako kwa muda kuwaringishia wenzako lakini kwa huruma zangu tumefikisha mwezi huu , unataka nini kutoka kwangu , leo ndio mwisho maana nina mtu tayari ninaempenda , naomba uondoke nina mazungumzo muhimu na Amosi”Aliongea mwanaume mmoja mtanashati sana aliekuwa amekaa kwenye Kona ya mgahawa huo huku mbele yake akiwa ni msichana mrembo ambae alionyesha hali ya kutaka kulia katika macho yake,

Kwa kauli mbili tu ambazo Amosi aliweza kusikia alijua fika kile kinachoendelea , ila hakutaka kuongea neno kwanza bosi wake amalizane na mlimbwende huyo.
Mwanamke huyo aliefahamika kwa jina la Anitha alionekana kuwa na hasira mno na mwanaume aliefahamika kwa jina la Chriss , kwa kile kilichokuwa kikionekana hapo ni kama msichana huyo anafosi penzi kwa kijana huyo.
“Anitha nimesema naomba uondoke , mkataba wangu na wewe umeisha leo hii”Alirudia Chriss kuongea na msichana mrembo wa haja alimwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliojaa hasira na kisha akasimama na kuchukua mkoba wake.
“Siku moja utakuja kujua mimi ndio mtu ninaekupenda kwa dhati na sio pesa zako Chriss na utakuwa umechelewa”Aliongea na kisha palepale akageuka na kuondoka.
Amosi ambae alikuwa amesimama pembeni ya meza hio aliishia kugeuza shingo kumtathimini mwanamke ambae analilia penzi , na aliishia kuona wivu kwani msichana huyo alikuwa amebarikiwa kila kitu , alikuwa ni mrembo haswa kuliko maelezo , pengine katika maisha yake na uzee huo hajawahi kuwa na mwanamke wa urembo huo , hata kuota kuwa na mwanamke wa namna hio hajawahi , sasa kijana aliekuwa mbele yake alikuwa na uwezo wa kuacha mwanamke mrembo huyo ambae analilia penzi , aliona wivu na kujiambia katika maisha pengine sio pesa tu na muonekano pia huvutia zaidi wanawake.
“Chriss huyu binti ni mrembo sana , lakini kuna haja gani ya kumuacha namna hii ni bora ungemdanganya na kuendelea nae pale unapomhitaji”AliongeaAmosi huku akikaa kwenye kile kiti.
“Nina sababu za kuachana nae ambazo hata wewe ukizijua hutonilaumu”Aliongea na kumfanya Amosi kutabasamu..
“Wewe na mzee wako mna tabia zinazofanana , tatizo mnapenda sana wanawake lakini kudumu nao hamuwezi”
“Haha .. Siwezi kufanana na yule mzee mimi , ni muhuni kupindukia, sidhani kuna mwanamke mrembo ambae ashawahi kumvutia akashindwa kumpata”Aliongea Chriss na kumfanya Amosi kutabasamu na kujiambia kwa wakati mmoja Chriss hakuwa akimfahammu baba yake vizuri , sio kila mwanamke anaemtaka ashawahi kumpata, kwani ni mwaka wa pili huo alikuwa akihaha kutaka kumuweka Eliza kwenye himaya yake lakini imeshindikana.
“Nimeitikia wito bosi wangu , simu kama hizi hunipa hamasa kwani naamini kuna malipo”Aliongea Amosi huku akiweka tabasamu.
“Haha.. Amosi mimi napenda watu wanaopenda pesa kama wewe , ndio maana kila inapokuja swala linalohitaji juhudi na uharaka wa utimilifu jina lako hujitokeza”
“Hii ndio kazi inayoniweka mjini , ijapokuwa pesa ni kipaumbele lakini matokeo mazuri nazingatia sana , kuna wanaopenda pesa zaidi kiasi cha kutumbukia kwenye utapeli, matokeo ndio kila kitu baada ya malipo”
“Haha.. Ijapokuwa unaniita bosi lakini wewe ni mtu mzima sana kwangu , si shaka kuwa na busara na nidhamu katika kazi yako , anyway tokea nikujue kupitia baba nimekuwa na shauku sana kuyajua maisha yako lakini maswali hayo nitayaweka kapuni kwa leo na niende moja kwa moja kwa kilichonifanya nikutafute”Aliongea lakini kwa sauti yake ilimfanya Amosi kuona hali ya kusita sita katika macho ya Chriss.
“Kuna mwanamke nataka unisaidie kumtafuta”Hatimae Chriss aliongea na kumfanya Amosi kushangaa kidogo.
“Mwanamke!!!?”
“Ndio mwanamke , kuhusu taarifa zake faili lake utaletewa kesho ofisini kwako, Mzee Amosi nimekuita tuongee swala hili ili kuonyesha ni kwa namna gani ni swala muhimu, hii inaweza kuwa kazi kubwa kuwahi kuipata tokea kuanza kwako kazi ya maswala ya kijasusi..”Alisita kidogo na kisha akaendelea kuongea.
“Kuna watu nyuma yangu juu ya hii kazi , mimi ni kama Freelancer , ijapokuwa sitowataja ni wakina nani kwa ajili ya usalama wako na wangu lakini wapo tayari kulipa kiasi chochote cha pesa , cha msingi ni matokeo ya kuridhisha”Aliongea na kwa namna Amosi alivyokuwa akimuona Chriss alihisi uzito wa kazi yenyewe maana bwana huyo mara nyingi alionekana kutokuwa siriasi lakini kwa namna flani ni kama hofu ilianza kumvaa.
“Kwa muonekano inaonekana sio kazi ya kawaida na inahitaji rasilimali za ki uwezeshaji?”
“Haha.. Amosi unaonekana kuwa na uelewa wa haraka , ndio maana Mzee anakuita jasusi nje ya mfumo,, kama ulivyosema mimi ni kama Freelancer katika hii kazi hivyo nipo tayari kuwekeza kiasi cha pesa kwako kwa ajili ya uwezeshaji wa ukamilishaji wa hii kazi, tutaanza na milioni mia moja”Aliongea Chriss.
“Milioni mia moja!!?”Amosi alishangaa mno.
“Kama ni milioni mia moja kama rasilimali uwezeshaji inamaana…..”
“Ndio Amosi , kazi hii ni ya mabilioni ya pesa , wenye uhitaji wa kukamilisha kazi hii wanataka ifanikiwe kwa haraka na kwa ufanisi lakini wapo Desparate, ukubwa wa pesa unaendana na ukubwa wa kazi yenyewe hivyo usishangae”Aliongea Chirss na kumfanya Amosi kumeza mate mengi.
“Nipo tayari juu ya kazi hii”Aliongea Amosi bila ya kufikiria , ukweli kilichomfanya kutoa jibu la haraka haraka sio ukubwa wa kiasi cha pesa bali ni shauku juu ya kazi yenyewe , kama anataka matokeo ya kazi hio anataka kutoa mapesa mengi kiasi hicho basi jambo hilo linaweza kumshangaza.
“Safi Amosi, unaonekana kuwa na shauku , hata mimi nilipokea kazi hii kutokana na shauku, nadhani tutazungumza zaidi baada ya kupokea faili, kumbuka usiri mkubwa unahitajika katika kazi hii na tahadhari zote zimechukuliwa, katika faili kutaambatana na fomu ya makubalianao ya kufanya jambo hili kuwa siri”Aliongea na Amosi alitingisha kichwa.
****
Dakika chache mbele mara baada ya Hamza kuelezewa tatizo la AC aliweza kuijua shida yake kabla hata hajafanya uchunguzi , ilionekana kulikuwa na shida ya kipima joto cha AC hivyo kufanya Ac kushindwa kukadiria kiwango flani cha ubaridi ndani ya nyumba hio.
Hamza hilo halikuwa tatizo kubwa kwake na aliweza kurekebisha haraka haraka na kumaliza lakini hakuishia hapo tu alijaribbu kuagalia na shida nyingine na aligundua kulikuwa na vumbi jingi upande wa Evaporator Coill hivyo alijaribub kurekebisha, mpaka anakuja kumaliza kazi yake ni kama nusu saa imepita na alijihisi njaa.
Kilichomfanya kuhisi njaa ni harufu ya chakula iliokuwa ikisambaa ndani ya nyumba hio ikimaanisha mrembo Eliza alikuwa jikoni.
“Inaonekana huyu mwanamke amekamilika kila idara , sio kwa kunukiza huku”Alijiwazia Hamza huku akijifuta vumbi kwenye mikono yake na Hangerchief , shati ambalo alikuwa amevaa lilikuwa limechafuka kutokana na kuparamia ukuta wakati wakusafisha Ac hio.
Inaweza ikawa kazi nyepesi kwa Hamza kutokana na uzoefu lakini kwa mtu mwingine ingekuwa kazi ngumu mno , kwani kwanza ilimhitaji kuchungulia upande wa nje wa jengo hilo , jambo ambalo lilikuwa likiogopesha kutokana na urefu wa jengo.
“Nishamaliza kazi yako , kulikuwa na shida ya setting tu na nimerekebisha”Aliogea Hamza huku akimwangalia Eliza ambae alionekana kutokea upande wa jikoni kuja eneo la sebulenni, alikuwa amependeza kwa mavazi ya kinyumbani zaidi na kumfanya kuonekana wife material.
“Oh!, Asante kaka yangu , naona pia namna ulivyochafuka”
“Yeah, wakati mama ananipigia kuja nnilikuwa nimetoka mahali na kuona nisiende nyumbani moja kwa moja”
“Na maamuzi yako yemeishia kuniokoa siku ya leo , nashindwa hata kuelezea tukio hili , linanifanya niwe na aibu mbele yako”Aliongea Eliza huku sauti yake ikionekana ni ya kusita sita na hakukutanisha macho kumwangalia Hamza .
“Ni swala la kawaida ambalo linaweza kumtokea yoyote , watu wa aina ile hawana mipaka na ni vizuri kutojihusisha nao”
“Asante sana , Hamza sijui nakushukuru vipi lakini naamini kile ulichokifanya ni kwa ajili ya kuninsaidia , kila mtu alikuwa akifurahia kudhalilika kwangu, ni swala la kawaida kwa binadamu , nadhani dunia sio mbaya kama nilivokuwa nikifiiria , umekuwa mtu wa kwanza kusimama upande wangu..”Aliongea Eliza huku hali yake ya kihisia ilionekana kubadilika mara moja jambo ambalo lilimshangaza Hamza , ilikuwa ni kama ashasoma Eliza ni mwanamke ambae alikuwa amepitia changamoto za kimaisha na kutokana hali ile ya kubadilika alishindwa kujua ni hatua gani achukue.
“Eh! , jamani naunguza..!!!”Aliongea Eliza akiwa kama ameshituka na kukimbilia jikoni na kumfanya Hamza atabasamu na kukaa kwenye sofa akimsubiria achukue pesa yake na aondoke maana muda ulikuwa umeenda.
“Samahani kwa kukuchelewesha mwaya , naandaa chakula cha kupeleka hospitalini , muda naona umeenda , unaonaje ukipata kabisa chakula cha usiku?”Aliongea Eliza huku akionekana kutokujiamini.
“Pole kwa kuuguza”
“Asante , nimeshapoa”Aliongea.
“Sasa mimi nisikucheleweshe , kwasababu kazi ilionileta ni ufundi na nishaimaliza ngoja nikuache uendelee na ratiba zingine”
“Malipo yatakuwa kiasi gani?”
“Nipatie elfu kumi tu inatosha “Aliongea Hamza , ijapokuwa mwanamke huyo alikuwa akimfanya amwambe nimetengeneza bure lakini aliona ni udhaifu hivyo anapaswa kuchukua chake.
Eliza palepale aliingia chumbani na kutoka na noti mbili za elfu kumi na kisha kumpatia Hamza.
“Sidhani ni sawa nikikuita fundi au Hamza wewe ni mwokozi wangu leo hii na angalau nilipaswa kukupa chochote kuweka baraka zaidi ya hii juisi, hii ya ufundi na hii naomba utumie kama nauli”
“Wewe unaweza kuniita fundi , namba yangu inayo ukiwa na tatizo unaweza kuniambia muda wowote nitafika”Aliongea Hamza na kupokea ile hela , hakutaka kukataa malipo ya elfu ishirini , ijapokuwa alijua mwanamke huyo alikuwa na matatizo lakini kama atakataa angeonekana kama alikuwa na ajenda zaidi ya moja.
Baada ya hela kama kawaida alipewa juisi na Korosho lakini Hamza kutokana na haraka na kutomfanya mwanamke huyo kuwa na wasiwasi ,korosho aliweka kwenye koti na juisi akainywa kama maji na kisha akaaga na kuondoka.
*******
Saa mbili kamili za usiku ndani ya mgahawa wa Golden Fork mbezi Beach ilisimama gari nzuri ya thamani aina ya BMW 14Oi ya rangi ya blue metallic.
Ilikuwa gari nzuri kweli iliofanya watu baadhi waliokwa wamekaa upande wa madirisha yanayoangaliana na maegesho kukaza macho kwa mtu anaeshuka katika gari hio.
Dakika kama moja kupita aliweza kutoka mtu katika gari hio ,ijapokuwa ilikuwa usiku na taa hazikuwa kali sana lakini ilitosha kuwafanya watu kukaza macho zaidi, kwani mwanamke alietoka katika gari hio hakuwa wa kawaida,alikuwa mrembo haswa japo kwa macho ya Hamza ambae ameshakutana na mrembo Regina angemuweka pengine nafasi ya tatu au ya pili mwanamke huyo.
Akiwa si mwenye kujali macho yanayomwangalia alizipiga hatua kuingia ndani ya mgahawa huo huku waliokuwa wakimtathimini wakitaka kujua yupo peke yake au kuna mtu amefika hapo kwa ajili ya kukutana nae.
Mwanamke huyo alievalia suruali ya rangi nyeupe na blazia ya rangi ya bluu alitembea kwa kuchezesha miguu yake na viatu vyake vya high heels mpaka upande wa kulia wa mgahawa huo huku nyuma akiacha usumbufu wa marashi yake.
“Alex!, umefika muda mrefu sana?”Aliongea yule mwanamke baada ya kumfikia mwanaume aliekuwa ameketi kwenye meza peke yake upande wa kulia wa mgahawa huo ,sehemu ambayo ni kama imejitenga.
“Wakati na kutumia meseji ndio nilikuwa nikikaribia , ni kama dakika ishirini zilizopita, kwanza sijategemea kama ungewahi maana najua wanawake na tabia zenu”Aliongea Alex kwa namna flani hivi ya kukosa amani kutokana na uzuri wa mwanamke huyo.
“Wewe mwenyewe ndio ulitaka usumbufu wa kukutana , malipo yangeweza kufanyika kwa njia ya mtandao kwanini unataka Cash?”
“Nadhani ushajua sababu ya mimi kutaka Cash Frida , nataka kuongea na wewe maana kuna mambo mengi bado sijayaelewa , mimi ndio ambae nilikuwa nikikuletea mzigo na hakuna kosa la aina yoyote limetokea , Frida kama ni lile swala la kuzielezea hisia zangu kwako naomba usahau , chukulia kama halijatokea na kazi iendelee”Aliongea Alex akiwa katika hali ya kulalamika hivi mbele ya mwanamke huyo , kwa macho ya haraka ilikuwa ni sawa na kusema alikuwa akimpenda huyo mwanamke lakini ilionekana mwanamke alikuwa amemkataa.
Mwanamke aliefahamika kwa jina la Frida alitoa tabasamu huku akimwangalia Hamza bila ya kujibu akimpa nafasi muhudumu kuweka juisi alioagiza kisha aendelee kuongea.
“Tatizo lako Alex unakosa focus, wewe ni mfanyabiashara lakini unakuwa kama vile ni mwajiriwa”
“Unamaanisha nini kusema hivyo??”
“Namaanisha utaendelea kutii kile ambacho ninahitaji kama mteja wako na si vingineyvyo,kuhusu sababu ulizoelezea kwangu huwa sizipi kipaummbele sana, wewe sio wa kwanza hata hivyo,anyway nimekuja hapa kwa maswala mawili tu, la kwanza ni kukupatia mzigo wako na hii ni mara ya mwisho sisi kuonana moja kwa moja , malipo yote yatafanyika kwa njia za kawaida , pili Alex acha kuuliza maswali mengi , wewe fanya biashara na kidhi mahitaji ya mteja wako , maswali mengi huua uaminifu, Nadhani kuna sheria na vigezo umepatiwa na Binamu mpaka kukidhi kuendesha biashara zao”Aliongea Frida huku akinywa juisi ile kimapozi.
“Lazima awe Hamza , Frida kuna ajenda gani, yeye ana nini mpaka ndio awe mwenye kukuletea mzigo?”
“Lazima awe Hamza ndio na si vingineyo , nadhani unashindwa kuelewa nilichokuambia , hizi ni hela zako natumaini mahitaji yangu katika mtazamo wa kibiashara yatashughulikiwa ipasavyo , Alex nakuambia mara nyingine acha kuuliza sana maswali , fanya biashara”Aliongea Frida na kisha alitoa bahasha na kuiweka mezani na kisha akamwinamia Alex na kumbusu shavuni la kwaheri ya kuoanana.
Busu lile lilimfanya Alex mwili wake wote kusisimka lakini kwa Frida ilionekana ni kitendo cha kuficha kile kilichokuwa kikiendele kati yao , ijapokuwa walikuwa wamejitenga lakini eneo hilo lilikuwa wazi kufanya watu wawaone.
Alex aliishia kumwangalia mrembo Frida akitokomea kwenye macho yake , hata ile hamu ya kuendelea kukaa hapo ilikuwa imempotea , mwanamke huyo alikuwa akimvutia kimapenzi mno.
Alex kama mfanyabiashara maarufu wa vyungu jijini Dar es salaam alikuwa akifanya biashara na wateja wengi ambao sio wa kutafuta bali ni wale wa oda , yaani ki ufupi ni kwamba biashara yake haikuwa ya kujitangaza kama zilivyo biashara nyingi , alikuwa kama mfanyabiashara ambae ameridhika na wateja aliokuwa nao lakni ukweli ni kwamba sio kama kile kilichokuwa kikionekana , wateja wake alikuwa akiwatafuta kwa namna za upekee sana na mathalani sio yeye ambae anawatafuta , wapo watu wa kazi hio.
Sasa kati ya wateja ambao anafanya nao kazi ni mwanamke mrembo , Frida , ijapokuwa mwanamke huyu hakuwa mrembo sana kuliko wanawake wote aliokuwa akifanya nao biashara lakini Frida ni aina ya wanawake ambao walianza kumvutia kingono kwa mara ya kwanza tu kuonana nae , pengine ni ile tabia ya mwanamke huyo ya kizungu ndio iliomfanya kumvutia kingono , mwanzoni ulikuwa ni mvuto wa kupenda kufanya nae ngono na Alex aliamini kwa namna yoyote ile lazima mwanamke huyo angeingia kwenye kumi na nane zake kama wanawake wengi ambao amepita nao , ‘hakuna mkate mgumu mbele ya chai’ ndio falsafa yake ya siku zote kila anapomtongoza mwanamke , hivyo aliamini falsafa hio hio ingefanya kazi kwa Frida lakini kinyume chake mwanamke huyo mlimbwende wa haja hakuwa na haraka nae , ki ufupi licha ya kwamba alikuwa mwanamke wa kujiachia achia lakini alionekana ni wanawake ambao si rahisi kumvua nguo moja tu ambayo mara nyingi Alex ndio humkuta nayo kila alipokuwa akipeleka mzigo wa chungu.
Mara nyingi mwanamke huyo angemkuta akiwa na nguo za kuogelea tu akipunga upepo na kusitiri manyonyo na kitumbua pekee huku akiacha kila kitu wazi , tabia ambayo ilizidi kumpagawisha mno Alex , ule ugumu wa mwanamke huyo ulimfanya kuanza kutengeneza chembechembe za kihisia na hapo ndipo ambao alipojihisi kupenda.
Kitu pekee ambacho kilianza kumchanganya Alex ni siku kadhaa nyuma mara baada ya Frida kumwambia anahitaji mwanaume aliefahamika kwa jina la Hamza Mzee kumletea mzigo wake kila siku.
Alex alishangaa , ndio alishangaa kwani Hamza alikuwa ni mtu wa kawaida mno kufahamika kwa Frida na hata yeye aliona pengine Frida anamaanisha Hamza mwingine , lakini kwa msisitizo Frida alimwambia ni Hamza huyo huyo anaemfikiria.
Japo swala hili lilimshangaza lakini lilimpa shauku na maswali mengi kichwani, akijiuliza inakuwaje Frida mwanamke mrembo anaemsumbua kumfahamu Hamza na kwanini anataka yeye ndio amletee delivery.
Kama kawaida ya Frida alikuwa ni mtu wa kuongea mara moja na atakachotaka ni vitendo ndio ambavyo alimpa Alex namna ya kupinga maamuzi yake.
Alex alikuwa na maswali , lakini biashara yake ilipaswa kuendelea na tokea amekabidhiwa biashara hio kulikuwa na misingi ya sheria ambayo alitakiwa kuifuata , kwanza hakupaswa kuwa na maswali mengi kwa wateja na anapaswa kuwasikiliza kwa chochote wanachohitaji na ikitokea amevunja kanuni hizo basi ilitosha kuhamishwa kikazi au kuachishwa kabisa.
Hivyo akiwa na wasiwasi wake na shauku aliamua kutii takwa la mteja wake na kumfuata Hamza kwa ajili ya kazi hio , bila shaka alikuwa na matumaini makubwa Hamza hawezi kukataa kazi ya donge nono hilo ,alijiambia ni rahisi kumchimba Hamza zaidi kuliko ilivyo kwa Frida ambae alionekana kama mwanamke msiri.
Dakika chache mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Frida juu ya mzigo kufika , huku mwanamke huyo akionyesha furaha yake ya kuletewa na mzigo na Hamza ilimfanya Alex kutaka kumhoji Frida ana kwa ana ndio maana akawekeana miadi nae kwa kisingizo kwamba anahitaji pesa yake cash, wazo zima ilikuwa ni kutaka kujua au Frida alikuwa na hisia za kimapenzi na Hamza ,au Hamza alishawahi kufahamiana na Frida lakini kulingana na Hamza ilionekana ni kama wawili hao hawafahamiani kabisa.
Sasa anapata nafasi ya kumhoji Frida mrembo lakini bado anashindwa kupata majibu anayotaka.
“Kuna kitu kinaendelea kuhusu huyu Frida , nina uhakika sio swala la kimapenzi , Hamza ni nani kwanini mwanamke kama huyu mrembo mwenye pesa anataka kuweka ukaribu na Hamza kupitia delivery ya vyungu”Kichwa cha Alex kilicheza , alijua lazima Frida alikuwa akilenga kujenga ukaribu na Hamza.
Zikiwa ni dakika chache baada ya Frida kutoa gari yake katika mgahawa wa Golden Fork , akiwa anaendesha katika barabara ya Bagamoyo uelekeo wa Jogoo, heads up display(HUD) ya gari yake ilionyesha ujumbe ambao ulikuwa kama vile ni kodi.
“Board to Alamos!!
Ujumbe huo ulisomeka hivyo na Frida bila ya kubadili uelekeo alikanyaga pedeli zaidi akiongeza spidi.
SEHEMU YA 09.
Saa mbili za usiku Hamza alionekana katika pikipiki ambayo ilienda kusimama kando kando ya barabara ndani ya Kijichi.
Hamza mara baada ya kushuka katika bodaboda hio aliangaza kulia na kushoto na kisha alianza kupiga hatua kwa kuvuka barabara upande wa pili akiachana na ile iliokuwa ikinyoosha moja kwa moja kuelekea uelekeo wa Vikunai kwenda Kibada.
Mtaa huo ulikuwa ndio mtaa wa kifahari kwa wilaya ya Temeke ndani ya jiji la Dar es salaam , kulikuwa na utulivu wa hali ya juu na mazingira yake yalikuwa safi na hata Hamza aliyapenda.
Baada ya kutembea umbali mfupi alikuja kukunja kulia kwake na kuingia katika moja ya mgahawa mkubwa uliokuwa ukipatikana ndani ya eneo hilo , uliofahamika kwa jina la Dina Tea House & Restaurant.
Ulikuwa ni mgahawa wa kifahari mno na wa kipekee ambao unapatikana ndani ya jiji la Dar e salaam , upekee wake ulitokana na kwamba ndio mgahawa pekee ambao umejipambanua kwa kuuza vinywaji aina ya chai pekee na chakula cha aina zote ambacho kinaendana na aina ya chai husika.
Kwa mfano chai aina ya Kombucha lazima iendane na chakula chake na aina hii ya huduma iliufanya mgahawa huo kuwa maarufu kati ya watu matajiri..
Ndio ulikuwa ni mgahawa wa kifahari kwani unaambiwa kikombe kimoja cha chai kinaweza kuuzwa si chini ya thamani za shilingi elfu kumi za kitanzania na kuna zaidi ya hapo, kwa mfano chai ya Gisaeng kutoka Korea tu ilikuwa ikiuzwa zaidi ya shilingi laki moja.
Ndani ya maegesho kulikuwa na magari mengi ya kifahari , hakukwa na gari la chini ya milioni therathini ndani ya magahawa huo.
Hamza alishazoea na alijua aina ya wateja ambao huhudumiwa na mgahawa huo lakini siku hio kidogo magari yalikuwa mengi kuliko siku zote ambazo alikuwa amefika ndani ya eneo hilo.
Hamza alijiambia pengine kutofika kwake hapo zaidi ya mwezi mmoja kunamfanya kuona mabadiliko makubwa.
“Bro Hamza leo naona umefika , karibu sana Madam anakusubiria ndani”Aliongea kijana mmoja huku akitoa tabasamu akimkaribisha Hamza.
“Lau nishakuambia mara nyingi haina haja ya kutoka kunipokea kama hivi”Aliongea Hamza akiwa na muonekano ambao haukuwa umebadilika sana.
“Bro unakuja mara chache sana hili eneo , hivyo sidhani kama nitapata usumbufu wa kutoka mara kwa mara na kuja kukupokea kila ninapokuona”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.
“Naona hali ya hewa siku hizi ni ya joto sana ndani ya hili jiji , kazi zimekuwa nyingi kwangu na kunifanya kuwa bize ndio maana sikupata muda wa kufika kuwasalimia”
“Ndio ndio , nakujua wewe ni mtu ambae upo bize sana”.
“Naona baisikeli yangu hamjaitoa bado ipo palepale”Aliongea Hamza huku akishangaa kidogo na kutaka kucheka kwa wakati mmoja baada kati ya usafiri wa hali ya chini uliokuwa ndani ya maegesho hayo ilikuwa baiskeli yake ambayo mara ya mwisho alifika nayo hapo na aliiacha kwasababu iliharibika mara ya mwisho.
“Nimeitoa na kuirudisha , madam alinipa kazi ya kuipeleka kwa fundi na imetengenezwa , si unaona sasa hivi inamuonekao mzuri”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa kidogo kwa kukubali na kisha kuanza kuzipiga hatua kuelekea mlango wa nyuma.
“Bro naomba usitumie mlango wa nyuma , Madam akijua hili ataniletea shida”Aliongea kwa kubembeleza bwana aliefahamika kwa jina la Lawrence au Lau wengi wanavyomuita.
“Hebu kwanza angalia nguo zangu namna zilivyochafuka , sidhani hao mabosi waliopo hapa ndani wataniangalia vizuri nikipita mlango wa mbele, nashusha hadhi ya huu mgahawa pia”
“Braza haina haja ya kuongea hivyo , Madam sio mtu wa namna hio , hawezi kujali na ititoshe unadhani kuna yoyote ndani ya hili eneo mwenye kutosha umuhimu wako kwa Madam?”
Hamza mara baada ya kuona Lau yupo ni mwenye kubembeleza sana aliona asikatae ukarimu huo hivyo aliamua kupita mlango wa mbele na kwa bahati nzuri katika Korido ya mgahawa huo hakukuwa na watu wengi , staili ya mgahawa huo ilijengwa kwa namna ya vyumba kama Kabini tokea mwanzo , ijapokuwa kulikuwa na sehemu ambayo ni kama watu wote waliweza kukaa lakini kwa wale ambao walikuwa wakihitaji kufanya maongezi ya muhimu walikuwa wakitumia vyumba hivyo kukutania , hii ni moja wapo ya faida ya mgahawa huo.,
Hamza alinyoosha mpaka katika moja ya chumba cha mwisho kabisa binafsi ambacho aliekuja kumsalimia ilikuwa ni kama ofisi yake na kisha alishika komeo na kusukuma mlango.
Sekunde ambayo mlango alifungua visu vitatu vilirushwa kuelekea alipo vikilenga eneo la moyo na tumbo kwa spidi ya mwanga.
“Damn!!”
Hamza alijikuta akimaka kwa mshangao lakini wepesi wake ulimfanya kusogea pembeni na visu hivyo vilipita inchi chache sana kutoka kwenye mwili wake .
“Tuk ! , Tuk , tuk!!!”
Vile visu vitatu vilikuwa vimefungwa na vishada(Tassels) vya rangi ya Violet , vilikuwa vyembamba mno na vyenye makali kama viwembe na viligonga katika ukuta na kudondoka chini.
Hamza mwanzoni alidhani huo ndio mwisho lakini dakika ileile ilitokea mianga kama flash aina tatu na kumsogelea kwa kasi kubwa.
Lakini Hamza alionekana kuwa mwepesi na shambulizi hilo lingine na palepale aliinua mkono wake juu na vile visu vyote vitatu vilinasa katiki ya vidole vyake, ilikuwa ni utaalamu wa hali ya juu mno.
“Dina , kuna haja ya haya mambo , kwani lazima uone utumbo wangu ndio uridhike?”Aliongea Hamza huku akitoa kicheko.
“Nilitaka kuona kama uwezo wako umeusahau kama ulivyonisahau na mimi, miezi miwili inapita bila ya kunitembelea”Aliongea mwanamke mrembo .
Alikuwa ni mrembo haswa , akiwa amevalia gauni jeupe lenye maua maua ya rangi nyekundu ambalo limefungwa na mkanda kiunoni na kuufanya mwili wake kugawanyika vizuri kati ya kiuno na juu , alikuwa na sura ya kuchongoka kama yai na lips pana ambazo zimepakwa rangi nyekundu.
Muonekano wake ulikuwa sio wa kawaida kabisa , pengine licha ya kwamba alikuwa akivutia sana lakini ni ngumu sana kwa mwanamke wa kawaida kuwa na mapozi ya aina hio.
“Sio muda mrefu sana tokea nifike , mimi naona ni juzi tu”Aliongea Hamza huku akiokota vile visu vilivyokuwa vimedondoka chini na kuweka mezani.
“Miezi miwili bado tu unasema sio muda mrefu , wanaume wengi wenye pesa zao na maarufu hufika hapa kila siku kwa ajili ya kuniona mimi Dina , kiasi cha kunifanya kushindwa kutoka lakini wewe mkorofi umekosa hata nafasi moja katika mwezi kuja kunitembelea?”
“Distance makes the heart grow fonder , Kama tukionana kila siku haitaleta raha tena , kwangu mimi naona ni vizuri zaidi kukuona mara moja kwa uda mrefu , inannifanya nikuone kama malaika alieshushwa kutokana na urembo wako”Aliongea Hamza.
Kwa namna ambavyo alikuwa akiongea ni kama vile amebadilika mbele ya mwanamke huyo , hakuwa na muonekano wa kipole bali ulikuwa ni muonekano wa kicheshi uliojaa utu uzima.
“Eti malaika alieshushwa , kwaho mimi ni mzuri sana mpaka kuitwa malaika?”
“Nadhani unanijua vizuri mimi ni msema kweli “Aliongea Hamza , lakini ukweli ni kwamba katika moyo wake mwanamke ambae amekutana nae muda wa mchana hakuwa wa kawaida kabisa , mrembo Regina kwake alikuwa mzuri zaidi ya Dina , faida kubwa ya Dina ni mvuto aliokuwa nao kutokana na mapozi yake ya kike na mazoezi.
Upande wa mrembo huyo aliefahamika kwa jina la Dina , ambae hatujui wanafahamiana vipi na Hamza mpaka kuanza kurushiana visu alionyesha tabasamu katika uso wake lililomfanya kuvutia zaidi na yote hayo ni ile raha ya kusifiwa kama mwanamke mzuri.
“Nimekusamehe siku ya leo , nina njaa ya usiku , hebu kaa na wewe ule , vyakula vyote unavyopenda vipo hapa”Aliongea.
Hamza alikuwa na njaa mno na harufu ya chakula hicho tokea anaingia ilimfanya njaa izidi kuuma , alisogea na kisha alivuta kiti na kukaa na mara baada ya kufunua chakula ambacho kilikuwa kimefunikwa alijikuta akivuta pumzi nyingi.
“Unasemaje hiki ni chakula ninachokipenda ilihali siwezi kabisa kukilipia .. ugali wa hizi Abaloni za ki’Australia nadhani nikianza kula nitatokwa na damu puani”Aliongea Hamza na kisha alisogelea bakuli ambao lilikuwa na pilau ndani yake na kisha alijisevia kwenye sahani na akachukua na nyama wa kukaanga pamoja na mchuzi wa samaki na kuweka kwenye sahani yake na kuanza kula chapu chapu , ndani ya dakika chache tu asilimia sabini ya pilau yote ilikuwa imeisha.
“Dina dada yangu mbona umeacha kula?”Aliuliza Hamza mara baada ya kuona Dina hakuwa akifanya chochote zaidi ya kumwangalia tu .
“Nishamaliza kula tayari , pili nnimeanza diet hivi karibuni,nakula kidogo sana”
“Kuna haja gani ya kufanya diet ilihali mwili wako huo huo unakupendeza?”
“Wewe ni mwanaume na huwezi kuelewa , ‘diet’ ni ‘life carear’ ya mwanamke , sitaki kuongeza uzito mimi .. kwanza hebu niambie, unapendelea mwanamke wa aina gani , mwembamba mwenye nyama au mnene?”
“Napenda wale wanawake ambao ni wembamba na wana kalio lainiii ukiliminya”Aiongea Hamza huku akitabasamu kifedhuli , alikuwa mtu mwingine kabisa kwa kile alichokuwa akikifanya.
“Wewe muhuni , yaani huna hata aibu nitakukata mimi?”Aliongea Dina na palepale kutaka kumrushia tena Hamza vile visu.
“Dina inatosha bwana , haina haja ya kutaka kunitumia kama kifaa cha majaribio ya mbinu zako za kininja””Aliongea na kumfanya Dina kutulia.
“Hamza hebu niambie kwanza ukweli , unadhani nitachukua miaka mingapi ya mazoezi mpaka kufanikiwa kukupiga na mashambulizi yangu?”
“Miaka..!, hehe , labda arobaini au hamsini hivi”
“Kwanini usiseme tu maisha yangu yote”Aliongea huku akiwa siriasi.
“Haha.,. haina haja ya kuwa siriasi hivyo , ukiachana na mbinu za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi, siku zote mtu anapaswa kuangalia kipaji chake kwanza kabla ya bidii, ule msemo wa kusema Bidii hushinda kipaji ni uongo, ni msemo ambao watu hutumia kujifariji tu”Aliongea Hamza.
“Halafu Dina hii supu ya kuku ina radha flani hivi, ni kama kuna chembe chembe za vinyama nyama ,umeweka Sea Cucumber nini?”
“Oh! , kumbe umeona, kuhusu hilo ni nyama ya kusaga ya mkia wa Kangaruu , nimenunua bei sana na ni kwa ajili yako kukupa virutubisho”Aliongea Dina huku akiwa na tabasamu flani la kichokozi.
“Mkia wa Kangaruu!!!”
“Unaonaje? , imekuwaje kwanza ukagundua utofauti wa harufu maana unasagwa na kuwa kama vumbi la nyama na kisha huweka kama viungo kwenye supu na harufu yake hupotea kabisa, inafanyika hivyo ili iwe rahisi kufanya kazi mwilini”Aliongea.
Mkia wa Kangaruu ni sawa na mtu anapotumia Viagra au Mkongo , mara nyingi hutumiwa sana na matajiri tena kwa siri kuwekwa kwenye vinywaji kama Mvinyo na baadhi ya dawa za kuongeza hamu ya tendo.
“Dah , sasa kwanini ukanifanya ninywe supu yenye huu mchanganyiko ,unataka nitokwe na damu puani?”Aliongea Hamza mara baada ya kuhisi presha ya damu kuongezeka kwa kasi.
Unaambiwa vumbi la vinyama vya mkia wa Kangaruu kidogo tu inaweza kumfanya mwanaume kupatwa na uchizi na ni ngumu sana kuepuka mtego wa mwanamke ukiwa katika athari ya dawa hio.,
“Unadhani kwanini nimefanya hivi?” Aliongea Dina na alisimama kutoka alipokuwa amekaa na kumsogelea Hamza na kisha alimwinamia shingoni na kufanya marashi yake yaliochanganyika na pumzi kumsisimua Hamza shingoni.
Kutokana na Athari ya dawa hio , mwanamke ambae alikuwa mbele yake urembo wake ni kama umeongezeka mara kumi , lakini kwa uwezo wake wote alijizuia kutoruhusu akili kumpotea na kumgusa kwa namna yoyote ile.
Alikuwa akijua kabisa kufanya mapenzi na Dina kila kitu kisingekuwa sawa tena , tokea arudi nchini Tanzania na kuanza chuo huku akiishi maisha ya kawaida ni kama ilimfanya kupata amani ambayo alikuwa akiiota hivyo hakutaka hali hio kubadilika.
Dakika ileile muonekano wa Hamza ulianza kubadilika na chumba kilizidi kuwa cha baridi huku msisimko ndani ya eneo hilo ukiwa ni ule wa kuogofya,Hamza alikuwa ni mtu mwingine kabisa na hakuwa na ishara yoyote ya utani katika macho yake.
“Dina usiendelee..!”Aliongea Hamza kwa sauti iliokuwa na mikwaruzo lakini kwa namna flani ya kuhamasisha.
Mabadiliko ya Hamza yalimfanya mwanamke huyo kushikwa na hali ya uchungu mno kwenye macho yake na ishara za hasira lakini dakika hio hio alibadilisha muonekano wake na tabasamu bandia na kujiondoa kwake.
“Hebu muone sasa uoga ulivyokushika , unadhani mimi Dina nataka kukumeza mpaka kunibadilikia hivyo , haya sitaki tena hata kuchokozana na wewe mimi”Aliongea akijitahidi kurudisha hali ya utani ili kuonoa hali hio isiokuwa ya kawaida katika uso wa Hamza.
“Tena umekuja wakati muafaka , nimepokea mzigo wangu wa majani ya chai kutoka nje ambayo nahitaji ujuzi wako kuyachunguza, nione kama sijapigwa maana ni hela nyingi nimetumia”Aliongea.
Dakika hio Hamza hatimae alikuwa amerudi katika ule muonekano wake wa kizembe na kuangalia chai ambayo ilikuwa ikimiminwa kutoka kwenye jagi.
“Hakuna shaka , ni wakati wa kufurahia chai ya kimatawi ya mrembo Dina kwamara nyingine”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu , spidi yao ya kubadilika haikuwa ya kawaida kabisa , pengine watu wa kawaida kwa kile kilichotokea dakika chache zilizopita wasingerudi katika hali hio.
Dina kama bosi wa mgahawa huo ambao umaarufu wake ni kutokana na kuhudumia aina mbalimbali ya ‘premium tea’ alikuwa makini sana kwa kila mzigo ambao anaagiza.
Dina upande wake alionekana kuwa siriasi na hakutaka kuendelea kuongea matani na alianza kuonyesha umahili wake katika kufanya mchanganyiko wa viungo vya chai , pamoja na kuweka majani flani katika kikombe na kuyaloanisha na maji ya moto. Na baada ya hapo ndipo alipompatia kikombe Hamza ajaribu.
“Hii ni chai ya mmea wa jamii ya Camellia Sinensis , ambayo hutengeneza chai maarufu ya Hui , majani haya yamefika jana kutoka China, hebu jaribu kuonja na uniambie ni gredi ya ngapi?”Aliongea Dina kwa kirefu wakati wa kumpatia kikombe Hamza.
Hamza kabla ya kunywa kwanza aliangalia majani hayo , yalikuwa majaini kama majani ambayo hayajasagwa na ilishangaza kwa namna ambavyo yalionekana mabichi licha ya kusafirishwa umbali mrefu.
“Hili jani limenyooka na ni zito , ukiangalia veini zake kidogo ni nyeusi kuliko jani , hii ni jamii moja ya majani ya Camellia kama ulivyosema , mmea wa chai ya kijani , unaofahamika kwa jina maarufu la kichina, Taipeng”
“Sio mbaya hebu jaribu radha yake kwanza”Aliongea na Hamza alionja pamoja na kunusa harufu ya chai ile.
“Mh! , hii ni chai nzuri sana , radha yake unaipata baada ya kumeza , sio chungu hata kidogo”
“Hio ndio maana yake , la sivyo isingenigharimu zaidi ya kiasi cha shilingi laki moja kwa kilo tu , ninachouliza ni gredi ya ngapi?”Aliongea na kumfanya Hamza kunywa tena na alionekana ni kama alikuwa akiichezesha kwenye ulimi na kisha akameza.
“Harufu na ‘Aftertaste’ inatosha kusema imeingia gredi namba tatu , lakini kuhusu utamu usioisha haraka naweza kusema hii ni Grade A”Aliongea Hamza.
“Kwa maneno yako , ni sahihi kusema kwamba Lawrence bado hana uelewa wa kutosha kuhusu sayansi ya chai, licha ya kusoma food science”Aliongea.
“Uzoefu unahitajika sana likija swala la chai za tamaduni mbalimbali , ni rahisi kufanya makosa kwa mtu ambae hajatembea sana na kuonja kila aina ya chai”Aliongea Hamza.
“Unaonaje ukifanya kazi hapa , utapata faida ya sehemu ya kuishi na chakula, lakini pia malipo mazuri, kuliko kule uswahilii unakoiishi”Aliongea.
“Ah! Hapana, napenda aina ya maisha yangu bwana , yananitosheleza”Aliongea Hamza huku akijiambia wakati huo hakuhitaji kazi nyingine kabisa ya uboifried wa maigizo inamtosha.
“Unaongea kama vile nitakuingilia kwenye mambo yako, nataka kukuona mara kwa mara ndio nia yangu”
Mara baada ya mwanamke huyo kuongea kwa sauti hio ya kubembeleza ilimfanya Hamza moyo wake kulainika na kwa mvuto wa huyo mwanamke alijiambia anapaswa kuondoka la sivyo anaweza kushindwa kuvumilia.
“Dina muda umeenda , ngoja niondoke”
“Mbona haraka , hivyo kwanini usikae kidogo tukipiga stori , inachosha sana kukaa mwenyewe”
“Hahaha… kaa na Lawrence mpige stori , kwaheri , haina haja ya kunisindikiza”Aliongea Hamza na kisha alitoka.
“Mjinga sana wewe, mpuuzi sana wewe Hamza, unanuka, umeniona sivutii ndio maana unanikwepa kila siku?”Mrembo huyo alilaani huku macho yake yakitawaliwa na upweke.
Upande wa Hamza mara baada ya kutoka nje ya mgahawa huo alijikuta akipatwa na ahueni kwa kupumua kwa nguvu , maana alikuwa akijitahidi kujizuia mno na alikosa amani kwa kuona kwamba ataishia kufanya kitu ambacho hakikuwa kwenye mpango wake , ukweli ni kwamba ijapokuwa alikuwa akimkwepa huyo mwanamke lakini alifika hapo kutokana na kwamba alikuwa amemmisi.
“Bro vipi unaondoka na baiskeli yako?”Aliuliza Lau.
“Nitaiacha usiku mkubwa huu nitaondoka na pikipiki, ihifadhi vizuri”
“Sawa broo”
“Halafu hivi unamjua mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Amosi , mzee flani hivi ambae ni kama mkopeshaji?”
“Unamzungumia Jasusi mstaafu , ni maarufu sana katika maeneo haya mpaka Kigamboni yote , yupo chini ya tajiri Hamdu mfadhili mkuu wa mgombea wa uraisi kupitia chama tawala.. anajitapa sana kwa kuamini jeshi lote la polisi lipo mikonoi mwake , anaweza kufungwa leo kwa uhalifu na kesho asubuhi ashatoka … vipi amekuletea tatizo lolote?, kwanini unamuulizia?, kama unataka nikamshikishe adabu niambie , nitahakikisha asubuhi anaitwsa hayati”
“Ah! , sijamaanisha hivyo , huyo bwana kuna mwanamke anamdai na anatumia deni kumtaka kingono , nataka angalau apatiwe vitisho ila usiende mbali”Aiongea Hamza.
“Nimekuelewa braza”Aliongea na kisha Hamza alimshika Lau Bega na kisha alizichapa raba kuelekea barabarani kutafuta bajaji au boda kwenda nyumbani , alitaka akakae chini kwanza asome karatasi ambayo alipewa na mrembo Regina kwa ajili ya kujiandaa na ajira yake kuanzia siku inayofuata.
“Madam !!”Aliita Lau mara baada ya kumuona bosi wake amesimama mlangoni akimwangalia Hamza akitokomea.
“Alikuwa akikuambia nini?”
“Inaonekana Braza Hamza amekosana na Amosi , Jasusi mstaafu , vipi tumuue?”Aliuliza Lau huku akiwa na muonekano tofauti na ambao alikuwa nao wakati wa kuongea na Hamza, alikuwa siriasi mno kama vile ni ninja.
“Haina haja tutaamsha matatizo mengine tu , hakikisha mnampa vitisho na onyo , pia fuatilia umfahamu mwanamke ambae Hamza anajaribu kumlinda , nataka kuona picha yake”
“Sawa Madam , halafu Zedi , Mbunge wa Ukonga amepiga simu ,anaulizia kama upo free kesho kwa ajili ya chakula cha usiku?”
“Mwambie siko free”Aliongea Dina kikauzu na Lau alitingisha kichwa na kutoka.
 
Singano kule kwa Roma hatujamaliza tunaanza tena upya
 
Duu mbona kama kuna Roma mwingine hapa?? Ngoja niende Xia kwanza nikaona rudi aliokolewa then nitateleport huku kwa hamza! Hope wale washamba washamba wa hongomeni hawapo hapa
 
ungenifata dm ni mueleze mdogo wangu au unamsingizia maana yupo likizo kaenda mbinguni kujifunza jinsi ya kusuluhisha kesi za viwanja kama afanyavyo waziri jerry
 
SHETANI RUDISHA AKILI YA MKE WANGU.



MTUNZI:SINGANOJR .



ILIPOISHIA:

Upande wa Hamza mara baada ya kutoka nje ya mgahawa huo alijikuta akipatwa na ahueni kwa kupumua kwa nguvu , maana alikuwa akijitahidi kujizuia mno na alikosa amani kwa kuona kwamba ataishia kufanya kitu ambacho hakikuwa kwenye mpango wake , ukweli ni kwamba ijapokuwa alikuwa akimkwepa huyo mwanamke lakini alifika hapo kutokana na kwamba alikuwa amemmisi.

“Bro vipi unaondoka na baiskeli yako?”Aliuliza Lau.

“Nitaiacha usiku mkubwa huu nitaondoka na pikipiki, ihifadhi vizuri”

“Sawa broo”

“Halafu hivi unamjua mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Amosi , mzee flani hivi ambae ni kama mkopeshaji?”

“Unamzungumia Jasusi mstaafu , ni maarufu sana katika maeneo haya mpaka Kigamboni yote , yupo chini ya tajiri Hamdu mfadhili mkuu wa mgombea wa uraisi kupitia chama tawala.. anajitapa sana kwa kuamini jeshi lote la polisi lipo mikonoi mwake , anaweza kufungwa leo kwa uhalifu na kesho asubuhi ashatoka … vipi amekuletea tatizo lolote?, kwanini unamuulizia?, kama unataka nikamshikishe adabu niambie , nitahakikisha asubuhi anaitwsa hayati”

“Ah! , sijamaanisha hivyo , huyo bwana kuna mwanamke anamdai na anatumia deni kumtaka kingono , nataka angalau apatiwe vitisho ila usiende mbali”Aiongea Hamza.

“Nimekuelewa braza”Aliongea na kisha Hamza alimshika Lau Bega na kisha alizichapa raba kuelekea barabarani kutafuta bajaji au boda kwenda nyumbani , alitaka akakae chini kwanza asome karatasi ambayo alipewa na mrembo Regina kwa ajili ya kujiandaa na ajira yake kuanzia siku inayofuata.

“Madam !!”Aliita Lau mara baada ya kumuona bosi wake amesimama mlangoni akimwangalia Hamza akitokomea.

“Alikuwa akikuambia nini?”

“Inaonekana Braza Hamza amekosana na Amosi , Jasusi mstaafu , vipi tumuue?”Aliuliza Lau huku akiwa na muonekano tofauti na ambao alikuwa nao wakati wa kuongea na Hamza, alikuwa siriasi mno kama vile ni ninja.

“Haina haja tutaamsha matatizo mengine tu , hakikisha mnampa vitisho na onyo , pia fuatilia umfahamu mwanamke ambae Hamza anajaribu kumlinda , nataka kuona picha yake”

“Sawa Madam , halafu Zedi , Mbunge wa Ukonga amepiga simu ,anaulizia kama upo free kesho kwa ajili ya chakula cha usiku?”

“Mwambie siko free”Aliongea Dina kikauzu na Lau alitingisha kichwa na kutoka.

INAENDELEA




SEHEMU YA 10.

Hamza mara baada ya kurudi katika chumba chake alichopangisha maeneo ya uswahilini Gongo la mboto alikimbilia bafuni kuoga , maana muda huo wapangaji wote walikuwa washalala na kumaliza kuoga hivyo alikuwa huru kutumia bafu na choo.

Mara baada ya kumaliza kuoga moja kwa moja alijitupa kwenye godoro lake huku akiangalia juu kwenye ceiling board akionekana kuwaza kitu lakini ni dakika ileile alikumbuka alikuwa na karatasi ya kusoma ili kufanya vizuri katika ajira yake mpya.

Lakini kabla ya hapo aliingia katika mtandao na kutafuta jina lake na ndani ya sekunde lilionekana.

“Regina Wilson, Eldest daughter of the prestigious Dosam family in Tanzania , CEO of Dosam Group , intelligent and talented enterprenuer , the most beutifull businesswoman of the year ….”

“Kwahio kumbe huyu ndio mrembo ambae ni CEO wa makampuni ya Dosam, naona hata hii picha ni kama sio yake”Aliongea mwenyewe Hamza wakati akipitia taarifa hizo.

Ukweli ni kwamba kampuni ya Dosam ilikuwa ni maarufu sana nchini , na umaarufu wake unatokana na Brand yake , kila mahali ilikuwa ipo sio kwenye usafiri wa anga, maduka na mahoteli , hata Hamza jana yake aliweza kupendeza kutoka katika moja ya duka la Dosam.

Sasa ilimshangaza mwanamke mrembo namna ile ndio ambae alikuwa akivuma sana kwa kuwa mrembo asietaka kujionyesha lakini ambae alikuwa na akili nyingi kiasi kwamba ameiwezesha kampuni ya Dosam kutambulika kimataifa.

Hamza aliishia kupitia nyaraka ambayo alikuwa amepewa na mrembo huyo na kuanza kuisoma kwa umakini lakini ndani ya dakika tano tu alikuwa tayari ashapitiwa na usingizi.

Siku iliofuata Hamza alionekana katika moja ya mgahawa ambao alipendelea kula na alijipatia chapati zake tatu , maharage pamoja na juisi na mara baada ya kumaliza alianza safari ya kuelekea kwenye ajira yake kwa mara ya kwanza.

Hakuwa na mavazi yale ya jana , jana aliyachafua na hakufua hivyo hakujisumbua kubadilisha , mavazi yake ambayo yamemkaa vizuri lakini yamechakaa ndio aliamua kuvaa.

Kwa kutumia mwendokasi aliweza kufanikiwa kufika kituo kilichokuwa kikipakana na jengo la Dosam Tower sehemu ambayo alikuwa na miadi na mrembo Regina.

Katika jengo hilo ukiachana na kuwa na makao makuu ya baadhi ya kampuni katika floor za chini lakini chini kulikuwa na maduka makubwa ya luxury brand kama vile Chanell , Luis Vuiton na zaidi, juu kabisa kulikuwa na migahawa ya kimataifa kama vile Italian Restaurant , French Restaurant na Chiniese , ni sehemu ambazo Hamza asingeweza kutia mguu.

Saa nne kamili juu ya alama simu ya Hamza iliita na aliekuwa akipiga ni Regina na mara baada ya kumsikia Hamza amefika tayari alijikuta akipata ahueni.

Katika maegesho ya magari B2 , Hamza hakuweza kuona ile gari ya Maserati ambayo mrembo Regina alitumia jana bali kulikuwa na gari aina ya Lexus SUV.

Kama bosi wa kampuni hio kubwa sio swala la kushangaa kubadilisha badilisha magari hivyo haikumfanya Hamza kushangaa.

Mara baada ya kukaribia gari ile , kioo cha mbele kilishushwa na mwanamke mrembo sana alievalia gauni lenye kola ya bluu alionekana , gauni lililoacha mikono yake milaini wazi, huku akizidi kupendeza kwa mkufu wa madini ya dhahabu uliokuwa shingoni kwake., muonekano wake ulikuwa ni wa kitulivu mno kuliko ule wa jana.

“Goodmorning Madam, wapi tunaelekea?”Alisalimia Hamza huku akiwa na muonekano wa kizembe lakini hata hivyo hakuacha kutoa tabasamu.

“Ingia kwenye gari kwanza”Aliongea.

“Oh! , sawa boss”

Mara baada ya Hamza kuingia, Regina alimchunguza kwa dakika kadhaa , huku akijiambia huyu jana alifika akiwa amependeza lakini leo anaonekana wa kawaida , kuizoea kazi kabla hata ya kuanza.

“Vua nguo zako”

Kauli ile ilimshitua Hamza na kumwangalia mwanamke huyo kama anamaanisha , lakini hakukuonekana na utani.

“Madam!, ijapokuwa urembo wako ni wa viwango vya juu na pia tuna mahusiano ya kikazi , siwezi kuwa mrahisi namna hio , naomba ufikirie mara mbili , siamini kama wewe ni mtu mwepesi hivyo pia”Aliongea Hamza.

“Unaongea ujinga gani?” Mwanamke huyo alionekana kukunja sura na kujiambia mbona anakuwa na mawazo ya aina hio , lakini hata hivyo hakujali na alipitisha mkono nyuma ya gari na kutoa mfuko na kumpatia Hamza.

“Ninachomaanisha ni wewe kubadilisha , ndani ya hili jengo huwezi kuingia ukiwa na hayo mavazi”

“Ah , sasa si ungeongea hivyo mapema , angalau nimepata ahueni …”Aliongea Hamza huku akijifanyisha kupumua kwa nguvu , alijua sasa ndio maana alikuwa amebadilisha gari na kuja na kubwa kumbe malengo ilikuwa ni kumpa nafasi ya kubadili mavazi yake.

“Unamaanisha nini kuongea hivyo?”Aliuliza Regina huku akionekana kukosa utulivu , hata kama kitu kitatokea ndani ya hilo gari yeye ndio ambae atapata zaidi hasara kuliko Hamza , maana alijua kama mwanamke mrembo hakuna wa kumkataa , lakini ajabu yake Hamza ndio anajiona atapata hasara.

“Hamna tu , nilikuwa natania, nitabadilisha”Aliongea Hamza huku akicheka.

Hamza sio kama hakuwa akielewa ni kwamba tu alikuwa akitafuta nafasi ya kumfanya bosi wake amzoee haraka ili asiwe na wasiwasi na maigizo yao yasigundulike , hivyo kuwa mcheshi kama hivyo ilikuwa ni mbinu ya kuweka sawa mazingira yake ya kazi.

Sasa cha ajabu Hamza alivua shati lake palepale na mara baada ya Regina kuona tukio hilo aligeuka haraka kuangalia pembeni huku wakati huo akipata hisia mbaya kwa kujiambia mbona ni kama huyu mwanaume sio muwazi kama ilivyokuwa jana kwenye usaili.

Yaani Hamza wa jana alikuwa mpole na muwazi na ndio kilichomvutia , lakini wa muda huo aliionekana kama muhini fani hivi.

Lakini hata hivyo asingeweza kubadilisha mawazo , kwani kama ni mkataba umekwisha kusaini na pili hata kama atafute mtu wa kufanya maigizo asingepata mtu mwenye muonekano kama wa Hamza , muonekano wa kitanashati , alipenda sana namna ambavyo Hamza alichanganya rangi na kuona ingefaa sana kufanya maigizo.

Ndani ya dakika chache tu Hamza aliweza kumaliza kubadili mavazi yake yote ikiwemo shati na suruali , alikuwa amevalia shati la brand ya Givenchy na suruali yake , Mkanda wa ngozi brand ya Mont Blanc ulioendana na viatu vya ngozi ya Brown brand ya Ferragamo.

Mavazi yote kuanzia viatu mpaka juu iligharimu zaidi ya milioni therathini na kwa jinsi alivyokuwa amependeza iliendana vyema na ule msemo wa kizungu wa ‘Clothes make the man’ maana ndani ya dakika chache tu Hamza alikuwa ni mtu mwingine kabisa.

“Looks fine”Aliongea Regina kwa kingereza huku akijivunia kwa namna anavyojua kuchagua.

Hamza aliweka nguo zake alizokuja nazo kwenye ule mfuko na kisha akatupia nyuma.

“Miss wapi tunaelekea sasa?”

“Kukutana na wazazi wangu”Aliongea kikawaida kabisa lakini kwa Hamza alibung’aa akiwa ni kama hajasikia vizuri.

“Aisee naona mambo yanaenda haraka haraka sana , vipi napaswa kubeba zawadi au kitu chochote , naona sio vizuri kwenda kukutana na wazazi wako mikono mitupu”

“Haina haja ,,, hata hivyo unakutana nao leo tu na haijalishi kama utakutana nao siku za mbeleni , ninachotaka ni wao kujua nimepata boyfriend basi”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kumuelewa.

“Halafu usiniite madam , unaweza kuniita kivingine”

“Kama ni hivyo unaonaje nikikuita , Babe Regi , au Darling Regina , Mrs Hamza, Sweatheart..”Aliongea Hamza huku akicheka.

“Hey! Inatosha”Alibweka huku mrembo huyo akizidi kuona Hamza jana alikuwa akijifanyisha muigizaji na sio kama alivyokuwa akimdhania.

“Huyu mtu huu ni ucheshi au ni kukosa aibu , mbona jana hakuwa hivi?”Aliwaza Regina.

“Niite Regina tu inatosha”Aliongea na kisha palepale akatoka nje ya gari na kuongoza njia kuzielekea lift.

Mara baada ya kuingia kwenye lift Hamza palepale alimshika mkono Regina.

“Unafanya nini?”

Regina alionekana kutetemeka ni kama vile amepigwa na shoti , alitaka kuvuta mkono wake lakini Hamza alionekana kuushika vizuri.

“Regi nipo kazini , unadhani tutaweza kuwadanganya wazazi wako kama tusipoonyesha vitendo”

“Sawa lakini , Mkataba unakutaka kuomba ruhusa kwanza”Aliongea huku akizidi kuwa kauzu.

“Kama ni hivyo unadhani ni sawa tukiachiana?”Swali hilo lilimfanya Regina kukosa neno , alijua fika kama kweli kusipokuwa na kitendo hata cha kushikana mikono mbele ya wazazi wake itaibua wasiwasi.

“Okey , tunaweza kushikana mikono lakini…”

“Haha… Regii unaona sasa … hii ni kama unavyoingia kwenye basi kwanza na baada ya hapo ndio unapewa tiketi ..”

“Nimekuambia uniite Regina , acha kufupisha”

“Oh sawa Regi”Aliongea Hamza na dakika ambayo mrembo huyo alitaka kuongea alikosa neno.

Ndani ya lift hio walikuwa wawili tu na kumfanya Hamza kuweza kunusa harufu nzuri ya marashi.

Katika kazi ambazo amefanya hio ni moja ya Ajira ambayo aliona ni nzuri na ya kuburudisha.

“Endelea kusogeza pua zako karibu , utashitukia ngumi”Aliongea Regina mara baada ya kuona Hamza ni kama anasogeza uso wake karibu zaidi na alikosa uvumilivu.

“Regi , haina haja ya kukasirika , hii ni kazi kama kazi zingine na ili ifanyike kitaalamu unapaswa kutoa ushirikiano , hivyo kukusogelea karibu ni sehemu ya kazi , wewe unaonaje?”Aliongea Hamza , ule muonekano wa kizembe hakuwa nao tena.

“Niseme kweli tu , jana nadhani sikuwa na umakini , sikuwaza kama utaweza kubadilika ndani ya muda mfupi na kuwa mwanaume mwenye aina hii ya tabia , nikutahadharishe tu usije ukaona una uwezo wa kufanya chochote ukisingizia kazi , leo sijaja tu na bodigadi wangu la sivyo ungejutia”Mara baada ya kauli Hamza alisogea mbali kidogo.

******

Jasusi mstaafu Amosi Masekela aliingia ofisini saa nne na nusu huku akionekana ni mwenye uchomvu mkubwa huku usoni akiwa na viashiria vya michubuko na kuvimba uso.

Kwa jinsi ambavyo alikuwa akijisikia asingeweza kufika ofisini kwa namna yoyote ile , ila ilimradhimu kufika kutokana na Chriss kumsisitizia kuwepo ofisini saa tano kamili wakati bahasha ikiletwa ofisini kwake , nguvu ya pesa na shauku ya kazi ambayo anakwenda kufanya ndio ilimpa hamasa ya kujitahidi kuamka.

Wakati anaingia vijana wake walikuwa tayari wapo ndani ya eneo la kazi na hata wao pia walishangaa kumuona bosi wao akiwa na michubuko pamoja na nundu usoni.

Amosi baada ya kupita mapokezi aliwapa ishara wale vijana kumfuata kwenye ofisi yake na kisha akapita.

Amosi Masekela alikuwa akifanya kazi kama mkopeshaji , alikuwa akikopesha watu kiasi flani cha pesa na kisha kurudisha kwa riba flani ndani ya muda anaokubaliana na wateja wake , ofisi yake ilikuwa ni kama benki isio rasmi lakini iliosajiliwa kufanya biashara hio.

Alikuwa na uwezo wa kukopesha mpaka bilioni moja ndani ya ofisi hio kwa masharti nafuu kabisa.

Lakini yote hayo yanawezekana kwa kuaminika kwamba alikuwa akifanya kazi chini ya bosi mwingine , yaani ofisi hio haikuwa ya kwake kabisa bali yeye ni kama msimamizi mkuu.

Sasa aina yake ya ukopeshaji kwasababu ilikuwa ikitofautiana na wakopeshaji wengine kwa mfano kuweka dhamana ya kitu fulani alijikuta akifanya kazi ya ziada kudai pesa kwa nguvu kwa wale ambao hawakuwa wakilipa ndio maana akaajili watu wa kumsaidia kazi hio na sasa ndio vijana kama Chongolo na wenzake.

Kabla ya Masekela kuanza kazi hio iliaminika alikuwa ni mwana kitengo ambae aliachana na kazi hio na kuamua kujitegemea ndio maana alivuma sana kwa jina la Jasusi mstaafu.

Sasa iwe kweli alikuwa ni mstaafu au kuna kilichotokea mpaka kuamka kwa uvumi huo lakini ukweli ambao upo ni kwamba Amosi alikuwa akiaminiwa na watu wazito wazito serikalini katika kazi ambazo zilihitaji akili ya utafiti na ujasusi zaidi na ndio kazi ambayo ilikuwa ikimlipa kwa kiasi kikubwa na angalau kuwa na maisha mazuri,vigogo wengi walikuwa wakimwita Hunting dog.

“Bosi nini kimetokea , kwanini una michubuko na nundu usoni , tuambie ni fala gani kakufanyia hivyo tutaenda kumshikisha adabu”Aliongea Chongolo.

“Bosi tupo tayari kwenda kupambana wewe tutajie jina , ni radhi tufe tukipambana kuliko bosi wetu kuumia”Aliongea mwingine.

“Bosii…”Kijana wa tatu wa kundi hilo alitaka kuongea lakini Amosi aliinua mkono kumzuia na kisha aliangalia saa ukutani.

“Kazi niliowapa jana mmeishia wapi Chongolo?”Aliuliza huku akiwa ameegeamia kiti chake lakini swali lake ni kama liliwafanya Chongolo kuanza kukosa kujiamini.

“Bosi yule mtu ni jini , sio wa kawaida mbele ya macho yetu alitoweka”Aliongea na kumfanya Amosi kukunja sura.

“Ndio maana mshaanza kuwa chawa asubuhi asubuhi , kumbe kazi hamkumfanya inavyostahili?”

“Bosi sio hivyo , alikaa sana ndani kwa yule demu lakini wakati wa kutoka tulimuona na tulianza kumfuatilia , wakati tunafika kwa Mzee Mashimo hatukuweza kumuona tena mbele yetu”Aliongea Chongolo.

“Alikuwa akitembea?”

“Ndio bosi , alikuwa akitembea na hiki ndio kilitufanya tuchanganyikiwe na kuona ni jini , anapotea vipi mbele yetu?”Aliongea Kihedu na kumfanya Amosi kutafakari.

“Endeleeni kumfatilia Eliza kwa siri kama kawaida , picha za kila siku zinahitajika juu ya kila kitu anachokifanya”

“Lakini bosi vipi kuhusu yule jamaa?”.

“Chongolo una akili kweli wewe , kama mtu amewapotea mbele yenu mtaanzia wapi kumtafuta , kama atakuwa na mahusiano na Eliza ndio namna nyepesi ya kumuona ,hakikisheni mnafanya hili kwa siri, hakikisheni hamjitokezi mbele ya Eliza , sitaki kilichonitokea jana kijirudie sawa?”

“Ah!, Nimekuelewa bosi , lakini unamaanisha nini kilichokutokea jana?”

“Kafanyeni kazi, muda wa kuongea na nyie umeisha”Aliongea na kisha palepale alitoa bahasha kwenye mfuko wa koti lake na kurushia mezani.

Chongolo alitabasamu na kisha kwa heshima aliinua bahasha ile na kisha akaaga na wenzake wakaondoka.

Hio ndio kazi ya vijana hao, hawakuwa waajiriwa wa Masekela Credit and Loans bali walikuwa na kazi moja tu kudili na watu ambao walikuwa wagumu kulipa pamoja na baadhi ya kazi chafu ambazo Amosi hakutaka kujihusisha yeye mwenyewe kama bosi, ki ufupi Amosi kwa namna nyingine unaweza kumchukulia kama Loan Shark.

Baada ya Vijana hao kutoka , alionekana kukosa utulivu mno na kila saa alikuwa akisubiria muda ufike ili kupokea bahasha alioahidiwa na Chriss.

“Bosi kuna mzigo umefika?”

“Ulete ofisini kwangu Bertha”

“Anasema anataka upokee mwenyewe na kutia saini”Aliongea mwanamke wa mapokezi kupitia simu ya meza.

Amosi mara baada ya kuambiwa hivyo hakutaka kuchelewa , kwa taratibi hizo alijua ni kile ambacho alikuwa akisubiria hivyo kwa haraka haraka aliienda mapekezi kupokea mzigo wake.

Aliekuwa ameleta mzigo huo alikuwa ni kijana mdogo wa miaka kama ishirini na nne hivi ambae ni mfanyakazi wa Swift Courier , kampuni ambayo ilikuwa chini ya Chriss.

“Bosi nimepewa maelekezo kukufikishia huu mzigo wewe mwenyewe na kuupokea, niwe radhi kama nimekusumbua”

“Unatii maagizo , haina haja ya kukakamaa hivyo”Aliongea Amosi huku akilazimisha tabasamu na kupokea mzigo ule na kisha akasaini.

“Chriss anaonekana kuwa makini mno , sio kwa ufungashaji huu”Aliwaza Amosi wakati akiondoka mapokezi akiwa na mzigo wake.

Mara baada ya kukaa kwenye kiti , ujumbe wa meseji uliingia na aliona ni kutoka kwa Chriss na kumfanya aufungue haraka.

“Napiga baada ya dakika kumi”Meseji iliingia na Amosi alielewa alichokuwa akimaanisha Chriss.

Mzigo uliofika ulikuwa ni Limu A4 na mara baada ya kuuweka mezani alitoa ile katarasi ya juu na kisha akaanza kuchangua karatasi moja baada ya nyingine na ile anafika katikati aliweza kukutana na karatasi ambayo imechapishwa.

Amosi alikuwa na shauku , usiri wa kazi hio ulimfanya kuzidi kujawa na shauku ya kutaka kujua ni kipi ambacho Chriss anahitaji kifanyiwe kazi ambacho kina malipo makubwa hivyo.

Kabla ya kusoma karatasi ile aliendelea kuangalia vitu vingine na aliweza kuona picha ya mwanamke mrembo , ijapokuwa picha hio ilionekana kuchakaa lakini bado mwanamke aliekuwa katika picha hio alikuwa akionekana vizuri.

Picha hio ilimfanya Amosi kuiangalia kwa muda mrefu , ni kama alikuwa akijaribu kukumbuka ni mahali gani aliweza kuiona lakini licha ya kusumbua akili yake hakuweza kukumbuka mara moja.

Alihamia kwenye ile karatasi na kuanza kusoma na sasa anafahamu mtu aliekuwa kwenye picha jina lake ni Naomi Lindsey mmarekani mweusi, mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili ambae alifariki dunia mwaka 1999 kwa mshituko wa Moyo wakati akiwa katika tamasha huko jijini Milani Italia.

Mwanzo mwa taarifa hio inamshangaza Amosi na kumfanya azidi kusoma mbele , lakini anajikuta akipagawa zaidi mara baada ya kugundua ambae yupo kwenye picha anafahamika kwa majina mawili , anafahamika kwa jina la Naomi Lindsey kutoka Marekani lakini vilevile anafahamika kwa jina la Rosemary Macha raia wa Tanzania.

Amosi kabla ya kuendelea kusoma anajiuliza inamaana Rosemary na Naomi ni watu wawili wanaofanana au ni mtu mmoja mwenye majina mawili tofauti.

Amosi aliendelea kusoma karatasi ile kwa umakini mkubwa ili kujua ni kipi ambacho anapaswa kufanya na anakuja kugundua kazi iliokuwa ikihitajika ni kuunganisha historia ya Rosemary Macha na Naomi Lindsey.

“Krii.. Krii..!!”

Simu yake iliita na kwa namna ambavyo alikuwa ameweka mwito wenye nguvu ni kama alikuwa na ugonjwa wa masikio , ila mwenyewe ukimuuliza kwanini mwito wa simu wa namna hio atakwambia mwito wa simu yake ni wa fursa na kwasababu hataki kukosa fursa anakaa kimachale.

“Jasusi nadhani umesoma bahasha?”

“Ndio lakini mbona kuna mkanganyiko wa hii kazi?”

“Ndio maana nimepiga simu Jasusi , siwezi kuweka wazi kwa kila kitu lakini kazi unayotakiwa kufanya ni kumtafuta huyo Mtanzania kwanza na baada ya hapo tafuta uhusiano na Mmarekani”

“Hii taarifa haina mwelekeo wowote , kama nitaanza kutafuta tanzania nzima itachukua muda , nahitaji angalu mwanga wa uelekeo kuanza kazi yangu”Aliongea Amosi.

“Jasusi kazi hio umepewa wewe kwasababu ndio mtu pekee ambae unajua pa kuanzia , ‘hebu angalia hio picha vizuri na vuta kumbukumbu’ hio ndio kauli ambayo nimeambiwa nikufikishie kama ilivyo”

“Kwahio kazi yangu ni kumtafuta tu huyu mwannamke?”Aliongea Amosi ambae kwa namna moja hata yeye mwenyewe ni kama alikuwa katika hali ya kujiuliza , kuna kitu kilikuwa kikimwambia kabisa picha hio alishawahi kuiona mahali kama sio mtu kabisa wa kwenye picha.

Lakini kwa wakati mmoja anashanga kuona kwamba waliompatia kazi Chriss ni kama pia wanamfahamu na yeye , hali ya shauku ilizidi kuongezeka.

“Jasusi najua una maswali mengi , mimi pia nina maswali mengi lakini kwasasa ninachojali ni pesa itakayopatikana juu ya kukamilika kwa kazi hio, Narudia ninachojali ni pesa, hivyo maswali uliokuwa nayo mimi sijauliza”Aliongea Chriss na kisha simu ikakatwa.

Amosi alifikiria kidogo akiwa amekaa kwenye meza na kisha aliinua ile picha kwa mara nyingine na kuiangalia.

“Huyu mwanamke kwenye picha nishawahi kumuona , lakini ni wapi na lini?”Aliendelea kujiuliza swali hilo na kuendelea kutafakari lakini kumbukumbu zake hazikumps bahati..

Dakika chache mbele Amosi alikata shauri , hakutaka tena kuendeea kukaa ofisini na alitoka isieleweke anaelekea wapi lakini kwa muonekano wake ni lazima hakuwa akielekea nyumbani, alikuwa na karatasi zile mkononi lakini zikiwa zimehifadhiwa katika bahasha ya kaki.











SEHEMU YA 11.

Regina alijikuta akivuta pumzi ya ahueni mara baada ya kuona Hamza alikuwa muoga ndio maana kasogea mbali , alijiambia kama atashindwa kumkontrol huyo mwanaume basi ataingia kwenye kazi nyingine ya kutafuta boyfriend feki mpya.

Lift ile iliwapeleka mpaka juu kabisa kwenye moja wapo ya mgahawa uliokuwa ukipatikana floor ya mwisho , sehemu ambayo ukikaa unaona karibia jiji lote la Dar na maeneo ya mbali.

Meneja wa mgahawa huo alikuwa ni mwanaume wa makamo Mfaransa, alikuwa amevaa akapendeza na mara baada ya kumuona Regina alimtambua haraka na kumsogelea huku akiongea kwa kuchapia chapia kiswahili.

“Karibu sana Madam Regina CEO”Aliongea akiweka tabasamu lakini kwa wakati mmoja akionyesha namna ya kushangaa namna ambavyo Hamza ameshikana mkono na Regina.

Licha ya kwamba alikuwa Mfaransa ila kuishi kwake Tanzania kwa muda mrefu kumemfanya kujua vitu vingi na kati ya vitu hivyo ni urembo na ukauzu wa mwanamke Regina, CEO wa makampuni makubwa ya Dosam.

Sasa baada ya kuona mrembo huyo akiwa ameshikiliwa mkono na mwanaume aliona ni swala zito ambalo mashilawadu kama watalifahamu itakuwa habari kubwa, isitoshe Regina alikuwa ni kama kioo cha jamii ndani ya taifa .

“Wazazi wangu washafika?”Aliuliza.

“Ndio wameshafika tayari , nitawapeleka moja kwa moja walipo sasa hivi”Aliongea na kisha aliongoza njia.

Wakati wakitembea katika mgahawa huo mkubwa na wa kuvutia , Regina alijikuta bila ya kupenda akimwangalia Hamza, ni kama alikuwa na wasiwasi kwani alijua fika watu wa daraja la chini kama watafika katika eneo hilo ambalo hutembelewa na watu wa vipato vya juu watakuwa na wasiwasi.

Lakini alionekana kuridhika mara baada ya kumuona Hamza hakuwa na wasiwasi wowote na kuona hapo kweli ameajiri mtu sahihi.

Mara baada ya kuingia katika chumba binafsi kulikuwa tayari kuna watu watatu waliokuwa wamekaa kuzunguka meza.

Mmoja wapo alikuwa ni mwanaume wa hadhi wa makamo na mwingine alikuwa ni mwanamke ambae alikuwa amevalia mavazi ya thamani pamoja na mkufu wa thamani kubwa shingoni , kwa umri wake wa miaka arobaini ilionekana alikuwa akijitahidi sana kuhakikisha anaonekana kijana bado.

Kulikuwa na mwanaume pia kijana alievalia shati la kola, brand ya Ermenegildo Zegna , alikuwa ni mtanashati mno lakini pia alionyesha ni aina ya wanaume ambao wanadharau kiana hivi kutokana tu na wajihi wake.

Wote watatu walizidi kuonyesha hali ya dharau mara baada ya macho yao kutua katika sura ya Hamza akiingia hapo ameongozana na Regina.

“Regina kwanini umekuja na Bodigadi mpaka hapa ndani , huu ni mkumsanyiko wa kifamilia hatuihitaji mtu wa nje”Aliongea mwanaume yule kijana huku akimwangalia Hamza kwa kumnyali.

“James kama unalijua hilo basi na wewe hupaswi kuwepo hapa , kuhusu mwanaume niliekuja nae naomba nikutambulishe leo hii , huyu ndio Boyfriend wangu”Aliongea huku akimsogelea Hamza karibu.

Mara baada ya James macho yake kuona tukio hio alijikuta akishikwa na wovu mkali na sura yake kukunjamana..

“Acha kuongea ujinga Regina , tangu lini ukawa na boyfriend ghafla tu”

“Tumekutana kupitia njia ya mtandao zaidi ya mwaka moja uliopita , ni juzi tu hapa nilijua yupo Dar na tukaamua kuanzisha mahusiano”Aliongea Ragina, kwa namna ambavyo alikuwa amejiandaa kumtambulisha Hamza, alikuwa akijiamini na maneno yake.

Upande wa Hamza aliweza kuona hali hio ambayo haikuwa tulivu na ni mwenye kuangaliwa kwa dharau lakini hata hivyo hakujali.

“Mjomba hapo , Shangazi pale na Braza mbele hapo, salamu kwenu ….”

“Nyamaza wewe mjinga , mimi ndio mchumba halali wa Regina sio wewe bidhaa ya kuokotwa dakika za mwisho kwa ajili ya maigizo”Aliongea James kwa hasira.

“Braza .. unamaanisha mimi au , haha.. unachekesha mno”Aliongea Hamza na baada ya pale alimpotezea na kisha akamvutia kiti Regina na kisha cha kwake na kuketi chini.

“Regii , anza kukaaa”Aliongea Hamza akimpa ishara Regina kukaa na James mara baada ya kuona namna Hamza anavyomwita Regina kwa nickname uso wake ulikunjamana.

Hamza hakuona kabisa shida juu ya macho mabaya yaliokuwa yakimwangalia na alikaa mara baada ya Regina kukaa na kisha akatoa tabasamu akiulizia msosi.

“Mshaagiza tayari , nilipata chai asubuhi lakini bado najihisi njaa”Aliongea lakini kwa bahati mbaya ni kwamba hakuna ambae alimjibu.

“Regina nini unajaribu kufanya? , hivi unachukulia ndoa kama mchezo sio, James ni mwaminifu sana na amekuwa akikusubiria ufanye maamuzi zaidi ya miaka sasa , uwe na ukomo basi wa ubishi wako”Aliongea mwanamke ambae alionekana kuwa mrembo licha ya umri kuenda.

“Nyie ndio ambao mnalazimisha juu ya hii ndoa tokea mwanzo na wala sijakubali , kwasasa nishapata mwanaume ambae nataka awe mpenzi wangu , kwanini ionekane ni kama naleta ukiburi”

“Hey! Leta walinzi mara moja wamfukuze huyu mtu”Aliongea mwanaume wa makamo akiwa siriasi.

“Hakuna wa kumuondoa hapa , huyu ni mpenzi wangu , kwanini hakuna ambae anaonekana kunielewa hapa?”Aliongea Regina huku akijaribu kuonyesha ukiburi.

“Ni kweli kabisa mimi na Regi ni wapenzi na sio kuwa wapenzi tu tunapendana sana”Hamza alijitahidi kuongea huku akijiambia hii familia haipo vizuri kimahusiano na malumbano yao yatafikia hatua hawezi kupata chakula tena.

“Sijategemea hii kazi kuwa ngumu hivi , mbona hakusema kama tayari alikuwa na mchumba , kuja kwangu hapa ni kama kuibua ugomvi tu , hebu kwanza muangalie huyu anaeitwa mchumba wake , anaonekana ni mtu tajiri lakini kwa namna anavyoniangalia kwa chuki nadhani nimejipalia makaa

Ningejua tokea mwanzo mambo yanakwenda kuwa magumu hivi juu ya hii kazi,bora hata ningeomba malipo makubwa zaidi

Hamza alikuwa akijiwazia yeye mwenyewe , alikuwa akijitahidi kuendana na mazingira lakini kwa namna mazingira yenyewe yalivyo ilionekana ni kazi kubwa sana ambayo kwa mshahara aliokuwa akipewa katika ajira yake hio ulionekana mdogo.

“Regina hebu nisikilize mimi baba yako , kutaka uolewe na James ni kwa ajili ya faida yako mwenyewe , hebu acha ukiburi basi”

“Ni kwa faida yangu au ya kwenu , nadhani majibu kila mmoja anayo katika moyo wake”Aliongea Regina na kisha alimwangalia yule mwanamke, ambae jina lake anaitwa Lamla.

“Regina unaongea nini , usione unaweza kuongea chochote mbele angu kwasababu tu ni CEO wa Dosam , ijapokuwa sijakuzaa lakini mimi ndio nimekulea kwa miaka kumi , kwanini unaniona kama mtu mbaya?”Aliongea Lamla na palepale macho yake yalianza kuwa mekundu akionyesha anataka kulia.

Mzee Wilsoni mara baada ya kuona mke wake anataka kulia , haraka sana aliweka mkono wake begani na kuanza kumbembeleza.

“Aiya , Darling usikasirike , Regina hajamaanisha hivyo , usimuelewe vibaya..”

“Ni kweli hajamaanisha hivyo , Regina ni mtiifu sana na mkarimu na hiki ndio ninachokipendea kutoka kwake ndio maana nataka aje kuwa mke wangu kwa namna yoyote ile , anaweza asipende kwasababu nimewatumia nyie kumfikishia nia yangu ndio maana anagoma kufanya maamuzi”Aliongea James.

“James wewe ni kijana muelewa ambae una mfahamu vyema Regina , wewe umemsikia mwenzako namna anavyojitahidi kukuelewa , kwanini usimuombe radhi kwa kitendo chako cha kumleta mwanaume wa maigizo hapa”

“Daddy , haina haja ya kunilazimisha na kunisihi , sina mpango wa kuolewa na James mimi”Aliongea na kisha akamgeukia James .

“Jikatie tamaa tu , Dosam ni kampuni niliopewa na babu yangu kuiendesha na sipo tayari kuona inaangukia katika mikono ya mtu wa nje ya familia , huwezi kunipata na pia huwezi kuipata kampuni yangu”

“Regina , unaongea nini , sina matamanio yoyote na kampuni yako , isitoshe sina akili ya kibiashara kama wewe, macho yangu na moyo wangu unakuelekewa wewe tu siku zote , kwanini unashindwa kuona ni jinsi gani nakupenda Regina,”

“Haijalishi unaongea ukweli au uongo wewe ndio unaejua .. halafu usifikiri sijui wewe ndio unaehusika kunyanyasa wafanyakazi wa kampuni yangu”

“Regina unaongea nini , nani ananyanyasa wafanyakazi , mbona sijawahi kusikia juu ya hili?”Aliuliza mzee Wilsoni.

“Regina labda utakuwa umekosea , James hawezi kuhusika”Aliongea Lamla.

Upande wa Hamza mara baada ya kusikia kauli hio alijua pengine tukio la Eliza kunyanyaswa na wale wadeni wake lilikuwa likihusiana na swala analoongelea Regina , ila hakuwa na uhakika.

Regina hakuwa hata na mpango wa kuendelea kuzungumzia swala hilo , maana hata kama aseme hakuwa na ushahidi wa moja kwa moja.

“Kama nilivyosema , nishapata mpenzi tayari hivyo kwanzia sasa sitaki kusikia maswala ya ndoa”Aliongea

James licha ya kwamba alikuwa na tabasamu lakini uso wake ulikuwa wa kikauzu mno , ilionekana alikuwa akilazimisha furaha.

“Haha…haina shida Regina , mimi ni mtu mvumilivu, nani anajua , pengine mnaweza kuachana kesho au kesho kutwa , nadhani wakati huo utanifikiria”Aliongea James huku akitoa kicheko, na maneno yake yalionekana kuwa na zaidi ya maana.

“Wilson sitaki kumuona huyu masikini mbele yangu , hebu ita watu waje wamtoe kama unataka niendelee kubakia hapa”Aliongea Lamla.

“Akiondoka na mimi naondoka”Aliongea Regina.

“Wewe..”

“Madam usiwe na hasira , haijalishi akikaa hapa na kula chakula tulichoandaa , iwe ni familia yenu au yetu pesa sio tatizo , chukulia tu kama msaada kwa mpitaji, sidhani kama ni tatizo”

“Mh! , Kwasababu wewe ndio umeongea James basi sina jinsi na kumuacha”Alijibu Lamla..

Upande wa Regina alikuwa na wasiwasi , aliogopa James anaweza akawa na mpango kichwani usio mzuri anapanga kuufanya

Muda uleule alimwita mhudumu wa mgahawa huo wa kifaransa na kisha alibadili kutoka lugha ya kiswahili na kuongea kifaransa.

“Prenez la commande de ce monsieur , soyez pls professionel..”Aliongea akimwamlisha muhudumu kuchukua oda kutoka kwa Hamza lakini awe profesheno zaidi huku wakati uleule akimkonyeza.

Muhudumu yule wa kike ambae alikuwa akifanya kazi katika mgahawa wa matawi ya juu kama huo alikuwa akijua kuongea kifaransa na alielewa kauli ya James kwa haraka sana .

“Mmonsieur , Que desirez-vous?”.

Mhudumu huyo alikuwa ni mbongo tena mrembo aliejazia kifua , lakini licha ya hivyo aliweza kuajiriwa katika mgahawa huo wa hadhi ya juu utokana na elimu yake na Exposure , ilikuwa hivyo kwa wahudumu wote.

Upande wa Regina alikuwa ashausoma mchezo tayari , alichokuwa akitaka kufanya James ni kumuaibisha Hamza na kumchezesha shere kama mjinga.

Ni kama alikuwa akitaka kumwonyesha yeye ni wa daraja la chini , mtu ambae hakuwa akistahili kuingia katika mgahawa wa hadhi ya juu kama huo.

Regina mwenyewe hakuwa vizuri kwenye lugha ya kifaransa hivyo alitaka kuingilia kwa lugha ya kingereza akimtaka yule mhudumu kuongea kingereza.

“Waitress please speak ..”

“Le-menu s’il-vous -platue me consillez Vous?”(“Niletee menu ya mapendekezo ya vyakula nichague”)

Wakati Regina anataka kuongea , palepale alijikuta akisikia sentensi ambayo hata yeye hakuielewa ikimtoka Hamza.

Hali ya ukimya ilivaa watu wote waliouwa ndani ya chumba hich cha hoteli , Mzee Wilsoni , Lamla na James wote walikuwa katika hali ya mshituko.

Aliekuwa katika hali ya kushangaaa zaidi alikuwa ni Regina , macho yake mazuri yaliongezeka ukubwa huku akimwangalia Hamza.

Upande wa muhudumu mara baada ya kuona amejibiwa alijikuta akishangaa kidogo lakini akaupotezea mshangao wake kwa haraka.

“Sir , nitaenda kukuletea Menu haraka , nisamehe kama nimekuwa mkorofi”Aliongea yule mhudumu , alikuwa amesikia vizuri Hamza na kumuelewa kwani alikuwa ameongea kifaransa kilichonyooka , na matamshi ya Hamza kwa uzoefu wake aliona hata yeye hakuwa vizuri , hivyo hakutaka kuleta ujanja tena wa kuongea kifaransa mbele ya mtaalamu wa lugha hio.

Dakika chache tu Menu ililetwa na Hamza alitoa oda yake kwa kutumia lugha ya kifaransa na kisha akamgeukia na Regina.

“Regi, una agiza nini , nadhani uonje Oulesarinires , desert , Clafautis …. na kuhusu kinywaji nadhani itakuwa vyema kama ukitumia mvinyo wa Ubelgiji usio na kilevi , lakini nadhani hawauzi hapa , unaweza kutumia tu mvinyo mweupe..”Aliongea Hamza kama vile yeye ndio aliekuwa mwenyewe na aliowakuta ni wageni.

“Sir unao uelewa mkubwa na vyakula vya kifaransa, unapendelea kula mara kwa mara nini?”Aliuliza yule mhudumu akishangaa kidogo kwnai muonekano wa Hamza ulikuwa tofauti na matamshi yake.

“Haha.. nakuaje mara kwa mara wakati mimi masikini tu , ni kwamba tu nina mazoea ya kusoma soma vitu ndio maana..”

Baada ya kuongea hivyo ilimfanya kila mmoja sasa angalau kuelewa , huku wakijiambia hakuna uwezekano masikini kama Hamza kuwa na uelewa wa vyakula vya kifaransa.

lakini upande wa Regina yeye alikuwa tofauti , hakushawishika kabisa na maneno ya Hamza , alijiambia hata kama ni kweli anaweza kusoma kuhusu vyakula vya kifaransa katika vitabu , vipi kuhusu rafudhi yake namna anavyoongea kifaransa , swala la mtu kujifunza lugha nyingine halikuwa jepesi mno na lilihitaji muda tena wa kuishinda ni ya mazingira ya wazungumzaji wa kifaransa.

Kitu kingine ambacho kilimfanya Regine asiamini ni namna ambavyo Hamza hakuwa na wasiwasi wakati wakuingia ndani ya mgahawa huo , ilionekana ni kama vile maeneo hayo hayakuwa mageni kwake.

Kwa namna moja Regina aliona mwanaume ambae ni boyfriend wa maigizo alikuwa ni mwenye kushangaza kiana.

Baada ya kaupepo kale kupita , hatimae chakula kiliwekwa mezani na kila mtu kuanza kudili na sahani yake , lakini kwa Mzee Wilsoni alionekaa bado dukuduku lake juu ya Hamza haikuisha.

“Mr Hamza umejifunzia wapi kuongea kifaransa?”

“Ah , mimi ni mwanachuo mwaka wa mwisho , na wakati wa masomo yangu A-Level niliongeza somo la kifaransa kama la ziada , tokea hapo nimekuwa nikipendelea kuongea kifaransa”

“Kwahio kumbe wewe bado ni mwanafunzi , nilijua pengine ushahitimu kutoka vyuo vya ufaransa ndio maana rafudhi yako kuwa nzuri kumbe bado unasoma , ngoja nikuambie ukitoka hapa achana kabisa na Regina , naweza kukupatia hata kiasi kikubwa cha pesa”Aliongea Lamla.

“Mama .. sihitaji kabisa pesa zako , najua kwasasa mimi ni masikini lakini nina nguvu ya upambanaji , nitahakikisha natafuta pesa ya kumtunza Regina kwa mahitaji yake yote atakayotaka”Aliongea Hamza.

Upande wa Regina licha ya kujua Hamza alikuwa akiongea hivyo kimaigizo , lakini hakuacha kuona aibu kidogo kwani ni kama vile kauli ile ilikuwa ikimaanisha ukweli.

“Unadhani ni kiasi gani unachoweza kupata kumhudumia Regina , hivi unajua ni bilioni ngapi kampuni ya Dosam inatengeneza kwa mwaka , unamiliki nini mpaka sasa , hata ufanye kazi kwa miaka mingapi sio rahisi kufika katika daraja ambao tumefikia…”Aliongea Lamla kwa dharau.

Hamza mara baada ya kauli ile alilipiza kwa kumvuta Regina kwake na kisha akambusu kwenye shavu kwa sauti ‘Pop’.

Regina aliekuwa bize akijipatia chakula chake alishindwa kuelewa hata tukio lilivyotokea , kwani kitendo chake cha kuzubaa tayari alikuwa amepigwa busu.

“Kila kitu sio pesa , Regina ni zaidi ya pesa”Aliongea Hamza huku akicheka.

Regina alitaka kumpiga ngumi Hamza , lakini mara baada ya kukumbuka alikuwa kwenye maigizo alijikuta akivumilia kwa kile alichofanyiwa, ijapokuwa alikuwa na hasira lakini uzuri wake ulimfanya aonekane kama mwanamke ambae anaona aibu kwa kubusiwa mbele ya wazazi wake.

“Paah!!”

James aligonganisha glasi ya mvinyo kwenye meza na kisha akasimama.

“Vizuri , vizuri sana ..”Jamaa huyo mara baada ya kuona mrembo Regina akibusiwa mbele yake alikosa kabisa uvumilivu , aishindwa kumuaibisha Hamza kupitia mhudumu lakini vilevile alikuwa amesababisha mchumba wake mwenyewe kubusiwa , hivyo alishindwa kabisa kuendelea kuvumilia.

“Mzee , Madam kuna kitu napaswa kwenda kushughulikia , hivyo nitatangulia , tutaonana siku nyingine”Aliongea na baada ya hapo alizipiga hatua lakini kabla ya kutoka nje kabisa alimwangalia Hamza kwa chuki kali mno.

Regina alikuwa na hasira na Hamza lakini mara baada ya kuona sura ya hasira ya James alianza kuona wasiwasi juu ya usalama wa Hamza

Waziwazi wa Regina mara baada ya kuona kitendo cha Regina , mtoto ambae hajawahi kuwa na boyfriend maisha yake yote kukubali kubusiwa mbele yao walijua lazima ni kweli atakuwa kwenye mahusiano hivyo hakuwataka kuendelea kuongea na mara baada ya chakula waliondoka wakiwa hawana furaha.

Upande wa Hamza alimshika mkono mrembo Regina na kwa kujiamini kabisa waliingia katika lift.

Kitendo cha kuingia kwene lift tu Regina alitaka kumchapa Hamza kibao lakini Hamza alimuwahi na kuudaka mkono wake.

“Regina , unataka kufanya nini?”

“Nani kakuambia unibusu?”Aliuliza mwanamke huyo huku akionekana kama mbogo, katika maisha yake hakuwahi kufanyiwa kitendo cha namna hio na mwanaume bila ya ridhaa yake.

“Sijakubusu , nilichofanya ni kuigiza kukubusu shavuni , kuna haja gani ya kuonyesha hasira , isitoshe hii ni kazi yangu , unadhani ningewaaminisha vipi wazazi wako waliokuwa wakiniita mtu wa maigizo?”

“Mkataba unaeleza wazi kabisa , kama kuna haja ya sisi kufanya migusano ni mpaka nitoe ridhaa , kwani hukusoma vipengele?”Aliongea kwa hasira ,Ukwei Regina alikuwa akijiuliza vipi kama pela angegeuka bahati mbaya , pengine wangeishia kugusanisha lipsi na alizidi kukasirika.

“Hukuelezea kwenye mkataba wa kazi kama unamchumba tayari , umenileta hapa na kufanya watu waanze kuwa na chuki na mimi , hivi unadhani walivyokuwa wakinifanyia ni vizuri?, nilikubusu kuwakomoa pia”Aliongea.

“Wewe..”Regina aliishia kutoweza kuongea zaidi , aliona ni kama kweli lilikuwa kosa lake.

Lakini yote hayo alifanya kwasababu ya usumbufu wa James kwake kutumia wazazi wake kutaka afungishwe ndoa , ndio maana akafikia uamuzi mgumu , lakini haikuwa hivyo tu ili kutii masharti ya urithi alioachiwa na kutunza siri ya ugonjwa wake.

Moja ya sharti la urithi wa kampuni alilopewa Regina katika wosia wa babu yake ni kuolewa ndio atakuwa mrithi kamili wa kampuni ya Dosam , na kama hatokidhi kigezo hicho ndani ya miaka kumi basi baba yake angekuwa mrithi wa mali za familia.

“Unaongeaka hata wewe unamjua yule James sio mtu mzuri , nilitaka kumuaminisha wewe ni mpenzi angu , ili akuache , mtu kama yule huwezi kumkataa kwa maneno tu , kwa urembo wako kama huu hawezi kukata tamaa kirahisi labda tu umwaminishe umeolewa na si vinginevyo”

“Sidhani kama ni kweli , kuna wanawake warembo sana , anachotaka yeye ni mimi tu kwasababu kampuni yake haifanyi vizuri kwa miaka mitatu mfululizo na anashindwa kushindana na mimi likija swala la mauzo , anachotaka ni mimi niolewe nae ili kuimeza Dosam”

“Wazazi wako hawajuia juu ya hilo?”

“Sio swala jepesi kukuelezea na hupaswi kujisumbua pia juu ya hili”Aliongea na kisha alirudia ukauzu wake na ndani ya dakika chache tu walitokea katika maegesho ya magari.

“Unajua kuendesha gari?”Aliuliza Regina na kumfanya Hamza kushangaa maana alikuwa ashajidaa kuondoka zake lakini ilionekana bosi wake alikuwa na mipango mingine na yeye.

“Najua ndio ila sina leseni”

“Kuna taarifa ya kikao nataka kuindaa na nimechelewa , nisaidie kuendesha mpaka ofisini kwangu”Aliongea.

Hamza hakuwa na hiyana , hata hivyo ni kama ashajiuza kwa pesa taslimi kwa mkataba hivyo hakuona haja ya kukataa.

Hamza alitoa gari hio kwenye maegesho huku akipewa onyo asiendeshe kwa spidi kubwa na alitii , safari nzima mrembo huyo alikuwa bize na Ipad yake akionekana kufanya kazi akiwa hana habari kabisa.

Hamza alikiri mwanamke huyo alikuwa na ukauzu sio wa kawaida , pengine ndio maana hakuwa na boyfriend mpaka akatangaza ajira.

Wakati Hamza akiingia Morogoro Road macho yake yalicheza mara baada ya kugundua gari alioona wakati wakitoka kule hotelini ikiwa ipo nyuma ya na aliishia kutoa tabasamu hafifu na kujiambia tayari ashayakoroga lakini hata hivyo ni kama hakuwa na uhakika kama alikuwa akifatiliwa yeye au alikuwa akifatiliwa Regina.

Hakutaka kujali wala kuwapoteza , aliendesha gari polepole mpaka maeneo ya mawasiliano sehemu ambayo makao makuu ya kampuni ya Dosam hupatikana.

Jengo la makao makuu ya Dosam lilikuwa likivutia mno , lilijengwa kwa usanifu wa hali ya uu na ilikuwa ni fahari ya macho kwa eneo hilo, ilikuwa refu kwenda juu kwa ghorofa arobaini. Hivi na lote lilitumika kwa kampuni , ilikuwa ni kama ishara ya jinsi kampuni ya Dosam ilivyokuwa kubwa.

Hamza mara baada ya kuingiza gari hio katika maegesho kwa maelekezo ya Regina mbele yake aliona mwanamke ambae alikuwa amesimama kikakamavu katika eneo la maegesho , ilikuwa ni kama vile alikuwa akiwasubiria na huyo alikuwa tofauti na aliekutana nae kule hotelini wakati wa usaili.

Kwa macho ya haraka haraka tu , Hamza aliamini mwanamke huyo atakuwa ni bodigadi kama ambavyo Regina alisema alikuwa na bodigadi.

Mara baada ya kusimamaisha gari mwanamke yule kikakamavu kabisa alisogelea gari hio na kisha akafungua mlango wa abiria akimpa nafasi Regina kutoka.

Hamza alijikuta akiangaliwa kwa macho ya kikauzu na mwanamke yule mara baada ya kushuka kwenye gari hio , ilikuwa ni kama vile mwanamke yule anataka kummeza na hata pale alipotaka kumsogelea karibu Regina alizuiwa kwa mbele jambo ambalo lilimfanya Regina kutabasamu na kujiambia huyu mtukutu mbele ya bodigadi wake hawezi kumchukulia faida.

Kwa kumwangalia mwanamke huyo licha ya kwamba alikuwa na sura ya kirembo iliofichwa na ukakamavu wake , lakini ilioneysha alikuwa na mazoezi makali ya kijeshi.

Hamza alikuwa na uwezo wa kuona namna muunganiko wa mwili wa mwanamke huyo ulivyokuwa sahihi.

‘Yonesi Dustani’ Secirity team leader’ ndio jina ambalo lilisomeka kwenye kitambulisho chake.

“Yones hali ya Eliza ikoje?”Aliuliza Regina.

“Madam CEO , sijui nini kimetokea lakini leo amefika Amosi na kuomba msamaha kwa Eliza na kuahidi deni lake kwanzia muda huo limeisha”Aliongea Yonesi na kumfanya Regina kushangaa.

“Kwanini wabadilike wakati katika ile vidio walionyesha kumdhalilisha Eliza kiasi kile?”Aliongea Regina na kauli yake ile ni kama sasa ilimfanya Hamza kujua kinachoendelea.

“Hata mimi nimeshindwa kuelewa ,vipi tuendelee kuwachukulia hatua kama ulivyotoa maagizo?”

“Kama wameahidi kutokumsumbua tena , haina haja ya kwenda mbali , isitoshe wanaonekana kuwa na mtu nyuma yao, nitaongea na Eliza”Aliongea Regina na Yonesi alitingisha kichwa na muda uleule Regina alimgeukia Hamza.

“Utaishi nyumbani kwangu kwanzia leo hii na kuendelea , kama una mizigo nitamwagiza Yonesi kukusindikiza”Aliongea.

“Nini , unataka tuishi pamoja?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.

Hata yule mwanamke aliefahamika kwa jina la Yonesi alikuwa katika mshangao pia, hakutaka sana kujali maisha binafsi ya bosi wake lakini ilikuwa ngumu kwa mwanamke wa hadhi ya juu kama Regina anaweza kukubali kuishi na mwanaume wa kawaida kama huyo na alijiuliza ni nani.

Mara baada ya Regina kusikia neno kuishi pamoja muonekano wake ulibadilika na akavuta pumzi nyingi za masikitiko.

“Ulinzi nyumbani kwangu ni mzuri , hivyo angalau kwa muda hamia , unachokifikiria hakipo”Aliongea

Hamza mara baada ya kusikia kauli hio kavu kiasi flani alijisikia vizuri na kuona kwamba mwanamke huyo alikuwa akijali usalama wake, isitoshe alikuwa tayari ashatengeneza maadui kwa kutangazwa kama boyfriend , ijapokuwa aikuwa feki lakini watu wale walimchukulia siriasi.

“Yonesi naomba umsaidie kumpa ulinzi huyu mtu , yupo kwenye matatizo , nenda nae anapoishi na mchukue mzigo yake na kisha umpeleke nyumbani kwangu , Aunt Maliposa atajua cha kufanya”Aliongea Regine asitake kumpa nafasi Hamza kuropoka tena.

“Sawa, Madam”

Licha ya kwamba alikuwa na wasiwasi pamoja na kusita lakini alitii maagizo ya bosi wake.

Hamza aliona namna ambavyo Regina aliongea kibosi , lakini kwasababu ilikuwa ni kwa ajili yake aliona haina mbaya kuishi kwake licha yeye kama mwanaume hakutaka kuishi kwenye nyummba ya mwanamke.

“Hey ,Acha ndoto za mchana , ingia garini”Yonesi aliongea kwa kufoka.

“”Hey Mjeda , niite Hamza tu inatosha , siitwi Hey”

“Unaishi wapi ?”Aliuliza hata asimjai Hamza.

“Gongo la mboto Kivule”Aliongea Hamza na kumfanya Yonesi kumwangalia Hamza na mavazi yake ya kisasa kabisa ya bei ghali na alijikuta akikunja ndita.

“Mh , unaishi huko uswahilini kweli?”

“Yeah kunaweza kuwa uswahilini , lakini ndio ambako kodi ipo chini, nilipanga nikitoboa kimaisha naja kwenye maeneo ya kifahari, usiangalie sana mavazi yangu , Regi ndio ambae ameninunulia , sio za kwangu”AliongeaHamza akijihami.

******

Saa saba mchana Frida alionekana akiingiza gari ndani ya hospitali na taasisi ya kitafiti ya Neuroscience inayopatikana Kibaha , kilomita kadhaa kutoka ilipo hospitali ya Tumbi.

Ilikuwa ni hospitali kubwa mno na ya kisasa yenye jengo moja lililoenda hewani kwa ghorofa kumi kumi na nane hivi na kufanya kuwa jengo refu zaidi ndani ya mkoa wote wa Pwani.

Hospitali hio ilijengwa kwa msaada wa watu wa Marekani kupitia shirika na taasisi isiokuwa ya kiserikali ifahamikayo kama Haliz Neuroscience Foundation(HNF).

Taasisi ya Haliz ilisifika dunia nzima kwa kujikita zaidi katika kuutafiti ubongo na maswala ya neva kwa ujumla wake , sera ya taasisi hio ilikuwa ni kuwezesha mataifa mengi kujifunza namna mfumo wa ubongo na neva unavyofanya kazi na hii imechangia sana kufungua matawi yake mengi karibia nchi nyingi duniani.

Mashirika ya Afya ya umoja wa kimataifa yalikuwa yakiunga mkono kazi kubwa ambayo ilikuwa ikifanywa na taasisi hii kubwa ya kimarekanni isiokuwa ya faida(Non-profit organisation).

Katika miaka ya hivi karibuni maendeleo ya sayansi ya neva na ubongo yalikuwa yamepiga hatua kubwa sana , wale wagonjwa ambao walikuwa wamepoteza kumbukumbu ilikuwa rahisi kurejeshewa kumbukummbu zao ndani ya muda mfupi tu chini ya taasisi hii ya Haliz.

Haikuwa wagonjwa waliopoteza kumbukummbu tu , watu wengi ambao walionekana kusahau mambo muhimu katika maisha yao , iwe ni kubukumbu za utotini au za ukubwani taasisi ya Haliz ilikuwa na teknolojia ya tiba ya kurahisisha hayo yote.

Licha ya taasisi hio kufanikiwa lakini bado utafiti wa kuujua ubongo wa binadamu ulikuwa ukiendelea zaidi , kwani wanasayansi wanaamini ubongo uwezo wake ni mkubwa kuliko ile ambavyo inadhaniwa , hivyo wanaamini kuuwezesha ubongo kufikia uwezo wake kamili kimatumizi italeta maendeleo makubwa.

Frida alitembea kwa kujiamini kabisa ndani ya hospitali hio huku akipokelewa na harufu ya taasisi hio yenye kuzoeleka katika pua zake, kwa namna baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hio walivyokuwa wakimsalimia kwa kutingisha vichwa ilionekana alikuwa ni mfanyakazi mwenye cheo.

Aliishia kutoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa kuonyesha tabasamu kwa baadhi ya watu aliopishana nao ndani na ndani ya dakika kadhaa aliweza kuzifikia lift na kuingia ndani, lakini kabla hata ya mlango wa lift haujajifunga mwanaume mzungu wa makamo alievalia koti la kimaabara aliweza kuzuia lift hio na kuingia ndani.

Alikuwa ni mtanashati kweli aliependezeshwa na miwani ya macho , huku akiwa amepambwa na tabasamu.

“Well!. Fancy meeting you here, Frida”Aliongea yule mzungu na kumfanya Frida kutoa tabasamu.

“Una ajenda gani kukimbilia lift Blake, huu si muda wako wa kufanya Demostrations na wanafunzi?”Aliuliza Frida na kumfana Blake kutoa kicheko kama anakohoa.

“Ndio nimemaliza, kulikuwa na mabadilishano na Dr John , Vipi wewe ndio umekuja kutubariki na utaalamu wako?,nilidhani upo likizo?”

“Nipo likizo ndio , lakini haimaanishi sipaswi kufika hapa , nina biashara katika floor ya kumi na saba”

“Wow!, Wow! , Floor ya wabobevu, sina neno la kuongezea, it’s nice to see you Frida”Aliongea Dr Blake na ni muda uleule Lift ilisimama katika floor ya kumi na bwana huyo mzungu alitoka akimuacha Frida kuendelea na safari yake.

Frida aliishia kutoa tabasamu tu huku akiangalia namna ambavyo Blake anapotelea kwenye macho yake wakati lift ikijifunga.

Haikuwa kama ambavyo amesema Frida kwani mara baada ya lift kufika katika foor ya kumi na saba alitoka katika lift na kuingia katika floor hio ambayo ilikuwa na utulivu wa hali ya juu , ilikuwa ni ubaridi tu na harufu ya kuvutia , huku rangi ya taa zisizokuwa na mwanga mkali zikipendezesha eneo hilo.

Frida hakuingia ndani ya Foor hio bali alizunguka upande wa kushoto kwake na kuanza kupandisha ngazi kuelekea juu na ndani ya dakika chache tu aliweza kutokezea juu kabisa ya jengo hilo.

Licha ya kwamba alionekana kutembea kwa haraka, lakini kwa namna ambavyo alikuwa na spidi hakuonyesha hata kuchoka, alionekana kama aina ya wanawake ambao walikuwa na mazoezi makali.

Baada ya kutoka katika paa kabisa ya jengo hilo refu na kumfanya kuona mazingira ya mji wa Kibaha na baadhi ya maeneo ya Dar es salaam na Bagamoyo alivuta pumzi na kisha aliendelea kupiga hatua kusogea mbele.

Hali ya hewa haikuwa ya jua kali ,ilikuwa ni kama vile mvua ingenyesha muda wowote.

Mbele yake Frida alikuwa amesimama mwanaume alievalia suti ya rangi ya bluu akiangalia upande wa maeneo ya Dar es salaam kwa umakini mkubwa kana kwamba kuna kitu alichokuwa akitafuta.

Alikuwa ni mzungu kwa muonekao wa nywele tu na kadri Frida ambavyo alikuwa akitembea hatua zake zilionyesha hali ya kuwa dhaifu kiasi.

Kama ilivyo mwanaume yule alivyosimama ndio namna ambavyo Frida alienda kusimama katika ukingo wa jengo hilo na kuendela kuangalia upande wa mbele yake, ilikuwa ni kama vile anamwigizia yule mtu , na upande wa yule mtu hakugeuka kabisa ni kama alijua nani amefika hapo na kusimama pembeni yake.

“Any progress on KF-Target?”Aliongea yule mzungu kwa sauti nzito.

“We are almost there ,I’ve initiated a plan to bring him closer to me, his curiosity will ensure our swift entry into the next phase”Aliongea akimaanisha kwamba anakaribia kumaliza , na ameanzisha mpango wa kumuweka karibu , anasema shauku yake itawafanya waingie hatua inayofuata kwa haraka”

“Elezea”Aliongea.

“Nimemfanya anifanyie Delivery ya Viungo vya akili kutoka Binamu , uhakika ni kwamba atauliza maswali juu ya malipo makubwa yanayolipwa kwa ajili ya chungu kimoja kama njia ya usafirishaji, kwa kile nilichoona amevutiwa”

“A risky move”

“Calculated Risky Sir”Aliongea Frida kwa kingereza na jibu lake lilimridhisha.

“Vipi kuhusu wale wengine , namaanisha wanaoangalia kutoka mafichoni?”

“We are keeping eye on them , once we have what we need, they ‘ll be nothing more than loose ends”

“Endelea na kazi kwa umakini , hatuwezi kuruhusu kosa lolote”

“Umeeleweka”

“Sinagogi wanataka hii misheni kumalizika kwa haraka , siku zijazo utashughulikia na zaidi ya mtu mmoja katika tafiti yako , mategemeo makubwa yamewekwa juu ya hii sayansi mpya Frida ,natumaini kila kitu kitaenda sawa,Hatuwezi kuruhusu washindani wetu kupiga hatua kablsa yetu”

“Ili mradi malengo yanakuwa wazi , kila kitu kitaenda sawa , natumaini utakuwa vizuri kwenye kuwatoa wasiwasi”

“Kama ni hivyo tutaonana tena katika hatua inayofuata kujua maendeleo”Aliongea yule mwanaume na ilitokea kitu kama upepo tu kwani alipotea palepale na wala hali ile isimuogofye Frida ikionyesha ni jambo ambalo amezoea.
 
Back
Top Bottom