IBILISI RUDISHA AKILI YA MKE WANGU
MTUNZI: DR SINGANOJR .
‘Your self-worth is not determined by your relationship status’-unknown
SEHEMU YA 07.
Mkataba wa Mpenzi wa Kukodi.
“Kifungu cha kwanza cha mkataba wa kukodisha mpenzi ,Mhusika A ana haki ya kumtafuta mhusika B wakati wowote ndani ya masaa 24, Mhusika B ana wajibu wa kuhakikisha simu yake muda wote ipo wazi , pili muhusika B ana wajibu wa kushirikiana kikamilifu na maombi yote ya Mhusika A maadamu maombi hayo hayavunji sheria za nchi au mkataba , tatu Mguso wowote wa kimwili lazima uruhusiwe na Mhusika A kabla ya kufanyika… nne ,,, tano …”
Ndani ya chumba cha kifahari cha hoteli ya Dosam V alionekana mwanamke mrembo akiwa amekaa kwenye sofa upande wa dirishani . alikuwa mrembo mno na siku hio mavazi yake yalizidi kumfanya kuwa mrembo zaidi.
Alikuwa amevalia mwenyewe gauni la light blue huku akiwa nywele zake amezirudisha nyuma mara baada ya kutoa ile kofia ya Hat na mkononi alikuwa ameshikilia karatasi ya mkataba akimsomea Hamza.
Macho ya mwanamke huyo yalikuwa mazuri na angavu kama vile ni maji ya vuli , nyusi zilizopindwa , kope zake ndefu na midomo yake myekundu na minene vilimfanya kuvutia zaidi ,bila kusahau uumbwaji wa uso wake ulioendana na haiba yake , alikuwa kama vile ni mchoro wa sanaa uliotoka kwa mchoraji maridadi.
Hamza alikuwa ameketi mbele ya mwanamke huyo mrembo akimwangalia na kumsikiliza kwa umakini mkubwa.
Ki ufupi umakini wake haukuwa kwenye mkataba bali ulikuwa kwenye uzuri wa huyo mwanamke , kwake ni kama vile yupo ndotoni.
Kusomewa mkataba huo ilikuwa ikimaanisha alikuwa amepita kwenye usaili na sasa alikuwa akipewa mashari ya kuanza kazi.
Ukweli ni kwamba huyo mwanamke baada ya kumwangalia Hamza kwa sekunde kadhaa alionekana kuridhika nae na alienda moja kwa moja kwenye mkataba.
Upande wa Hamza kwa namna ambavyo alikuwa akitingisha kichwa kila mara baada ya mwanamke huyo alipokuwa akisoma ni kama vile aliogopa mwanamke huyo angebadilisha mawazo na kushindwa kusaini mkataba wa kazi.
Alijiambia ni kheri hata kuigiza kuwa mpezi tu wa kukodi na hio yenyewe ingetosha kumletea heshima.
“Sahihi ya mkataba kipengele A , Regina Wilson Dosam., kipengele B Hamza Mzee.. ni muda wa kusaini…”Aliongea mwanadada mrembo ambae anafahamika kwa jina la Regina na kuweka mkataba ule juu ya meza kwa ajili ya kusaini mara baada ya kusoma vipengele.
Regina alijikuta akivuta pumzi ya ahueni huku akimwangalia Hamza ambaye ndio amekutana nae kwa mara ya kwanza siku hio na alionekana kuridhika nae.
Alikuwa na uhakika kuhusu macho yake kulingana na muonekano wa Hamza na taarifa ambazo amempatia alikuwa na uwezo wa kuona kwamba alikuwa ni mtu muamiifu na muwazi.
Zaidi ya yote mrembo Regina aliona muonekano wa Hamza sio mbaya sana , ijapokuwa mavazi yake hayajamkaa vizuri lakini kama atamvalisha na kupata matunzo kidogo atafanikisha kuwadanganya watu kuwa ni mpenzi wake halisi kumbe ni feki.
Wasiwasi wake kwa muda huo ni ugonjwa wake tu, lakini kulingana na vipengele vya mkataba huo aliamini Hamza kila atakachokiona kwake kwa bahati mbaya basi itakuwa ni siri.
“The contract is roughly like this , first I’ll rent it for three months, then we‘ll see how it goes , do you have any objections?”Aliongea kwa kingereza kitamu makusudi kabisa akitaka kumpima Hamza uwezo wake wa kuongea kingereza.
Hamza alitoa tabasamu , kadri mrembo huyo anavyoongea ndio alivyokuwa akipata hali ya kujiamini na kumzoea na palepale alishika mkataba ule na kupitia kwa haraka haraka kabla ya kusaini.
“Miss Regina , I have a few questions that I need to confirm first”Aliongea akimaanisha kwamba anayo maswali kadhaa ya kuuliza kujihakikishia kwanza.
“Unaweza kuuliza?”
“Vipi kama itatokea nipo kwenye kipindi na siwezi kuja kwako mara baada ya kunipigia simu na nikapoteza muda?”
“Upo makini , inaonekana pia ni mwanafunzi mtiifu”
“Nishatoa ada hivyo nataka kuitumia vizuri”Aliongea na kumfanya Regina kuonyesha ishara ya kuridhika, hakujali kuhusu Hamza bado kuendelea na masomo , alichojali alionekana kuwa siriasi, na yeye alikuwa akitafuta mtu siriasi.
“Usijali siwezi kukusumbua wakati wa masomo yako , utanipa ratiba ya vipindi na kama kuna dharula utaniambia”
“Hapo vizuri , naona na wewe pia ni mtu muwajibikaji” Aliongea huku akiwa na tabasamu na muda uleule simu yake ilianza kuita na kujikuta akilaani kimoyo moyo , Regina s alimpa ishara ya kuipokea na Hamza mara baada ya kuangalia jina la mtu anaepiga ni Iryn.
“Huyu ni mwanafunzi wangu namfundisha masomo ya jioni twisheni , yupo form six anapiga maana jioni ya leo nina kipindi nae”aliongea Hamza.
“Hakuna shida unaweza kupokea na kumsikiliza sina haraka” Aliongea Regina na palepale Hamza alipokea.
“Ticha nadhani hujasahau leo tuna kipindi?”
“Najua lakini si niliwasiliana na mama yako na kumwambia tutaanza wiki ijayo?, kwasasa nina kazi nyingine hivyo nitakuwa bize tutaanza wiki inayokuja kulingana na nilivyokubaliana na mzazi wako”
“Oh! , Mama hajaniambia kuhusu hili”Sauti nzuri ya kike ilisikika.
“Unaweza kumuuliza tu “
“Basi sawa nadhani tutaonana wiki ijayo”Aliongea huyo mwanamke na palepale simu ilikatwa na kwa sauti ya Iryn alijua tu lazima amekasirika.
Ukweli ni kwamba Hamza katika kujitafutia kipato alikuwa akifanya kazi za aina mbalimbali ,miezi kadhaa iliopita wakati akifanya kazi ya kibarua chini ya kampuni ya mazingira ya Tata ndio aliweza kukutana na Mama Iryn nyumbani kwake kwa mara ya kwanza na hapo ndio mwanamama huyo alimfahamu Hamza ni mwanachuo kutoka FEMU ,
Sasa katika kuongea ndio mama huyo alisema ana binti yake kutoka shule ya sekondari ya Alpha na anachukua masomo ya EGM na alimuomba kama ingewezekana kwa Hamza kumfundisha twisheni kwa malipo na Hamza alikuwa na uhitaji wa pesa hivyo hakukataa.
Tatizo lilianza mara baada ya kufanya vipindi kadhaa na Iryn alianza kumtega Hamza na kumtaka kimapenzi,, Hamza alikuwa hana mwanamke ndio lakini hakuwa tayari kutoka na mwanafunzi na hio yote ni kutokana na mama yake Iryn kuweka imani kubwa kwake hivyo kutokana na dalili hizo Hamza alikuwa akimkwepa Iryn kiaina.
Ki ufupi Hamza ni mtu wa harakati na aliishi kwa kuchakalika , hakuchagua kazi ili mradi ilikuwa na pesa, lakini kwa Iryn ilikuwa ngumu licha ya kazi hio ilikuwa na malipo mazuri kutokana na mama yake Iryn kutokea kumpenda Hamza.
Kitu kingine sio kwamba Hamza alishindwa kumuonya lakini ukweli ni kwamba Iryn alikuwa binti mrembo sana ambaye kwa mwanaume rijali yoyote yule ni rahisi kuingia kwenye mtego wake ndio maana alikuwa akiona ugumu.
“Samahani Miss Regina kwa kukuchelewesha wakati naongea na simu”Aliijibu Hamza.
“Hakuna shida , kama huna pingamizi lolote unaweza kusaini mkataba”Aliongea.
Ijapokuwa sauti yake ilikuwa ya kirafiki lakini alionekana kuwa kauzu mno na hata Hamza mwenyewe alijiambia hajawahi kuona mwanamke Kauzu kama huyo halafu mrembo , lakini alichopenda ni kwamba hakuona aina yoyote ya Dharau,
Hamza alitia sahihi yake kama vile ana saini mkataba wa mabilioni kwa niaba ya nchi , sahihi yake ilikuwa nzuri mno na kumfanya hata Regina kushangaa kidogo, ilionekana Hamza alikuwa na mwandiko mzuri sana kwa kuangalia sahihi yake tu.
Baada ya kutia sahihi yake na Leilani kutia sahihi yake palepale alifungua mkoba wake na kutoa bahasha na kumpatia.
“Haya ni malipo ya utangulizi kama mkataba unavyosema ni milioni tano , unaweza kuhesabu kujihakikishia, lakini hela zipo katika mfumo wa dollar hivyo utazibadili”Aliongea na Hamza alipokea ile bahasha .
“Haina haja ya kuhesabu uzito wa bill ya dollar mia ni sawa na gramu 1.51 na humu ndani kuna dollar elfu mbili hivyo uzito wake ni sawa na gramu 30.2, hivyo kwa kuzingatia uzito huu basi hesabu zipo sawa”
Leilani macho yake mazuri yalichanua , hakuamini kama mtu anaweza kuhesabu hela kwa kuzingatia uzito wake tu , moja kwa moja ilimwambia mtu ambaye yupo mbele yake anapenda sana hela na hilo lilimuongezea pointi.
Upande wa Hamza alifanya makusudi tokea jana yake alikuwa akipanga namna ya kukubalika na kushinda usaili na alikuwa na mbinu nyingi lakini hata hivyo mbinu zake hakuwa ameziandaa na kutokana na kuamini kichwa chake kilivyo chepesi basi angetunga hapo hapo.
Sasa mara baada ya kupewa kibunda alitaka kumhakikishia Regina kwamba yeye anajali sana pesa kuliko kitu chochote kile.
Unajua bwana watu wanaopenda hela ni rahisi kuwakontrol na kuwaambia hiki na kile na wakatii kuliko watu ambao hawapendi sana hela mara nyingi wanakuwa sio watiifu hio ni kanuni ambayo Hamza aliizingatia.
Regina aliona na hicho ni kigezo pia ambacho alikuwa akitafuta , alitaka pia mtu ambaye anakwenda kuigiza kama mpenzi wake awe anapenda pesa ili iwe rahisi kumuendesha.
Regina mara baada ya kuzuia mshangao wake aliingiza mkono wake kwenye mkoba na kisha akaibuka na bahasha nyingine na kumpatia Hamza.
“Katika hii nyaraka kuna taarifa ambazo zinahusiana kuhusu wewe na mimi namna ambavyo tumekutana na tulivyoanza kuwa pamoja , nenda nayo na ukaisome uilewe lakini hakikisha hakuna mtu ambaye ataiona.”
Hamza hakuamini mwanamke huyo kuwa profesheno kwenye kazi yake namna hio na alitoa tabasamu na kuchukua ile bahasha.
“Nitaisoma kwa umakini nikisharudi”
“Kesho asubuhi saa nne kamili tukutane Dosam Tower kwenye parking B2, hakikisha hauchelewi”Baada ya kuongea kauli hio alisimama akitaka kuondoka.
“Ms Regina usiwe na wasiwasi , mimi najali sana muda”
“That is for the best”Aliongea na Hamza aliangalia glasi ya juisi ambayo ilikuwa mbele ya mwanamke huyo , alichukua ya kwake kwanza na kuinywa na kisha akamwangalia.
“Ms Regina bado umebakisha nusu ya juisi yako”
“Siitaki tena”Aliongea.
“Utakuwa ni uharibifu sana kwa alieitengeneza”Aliongea Hamza na palepale aliinua ile glasi na kisha akainywa yote kwa mkupuo mmoja.
Mrembo Regina alitaka kumzuia lakini aliona aibu kwa kitendo chake na mawazo yake ya kijinga yalimwambia anachokifanya Hamza ni kubusiana nae kwa njia isio ya moja kwa moja.
Hamza na Regina walitoka pamoja na sasa rasmi Hamza alikuwa ni mpenzi feki wa mrembo Regina , Hamza ijapokuwa alikuwa hapo kwa kazi lakini alijiambia atahakikisha huyo mrembo anampenda mwenyewe.
Baada ya kutoka nje ya mlango alimwambia mlinzi wake kwenda nyumbani na kuanzia hapo ataendesha gari yake mwenyewe , mwanadada yule mlinzi alitaka kugoma lakini alikubali na aliishia kumwangalia bosi wake na Hamza wakitokomea kwenye lift akiwa katika hali ya wasiwasi.
Haikueleweka Prisila alikuwa ameenda wapi na Hamza alitamani kumuona mara ya mwisho , kwake ni kama alikuwa ameokota embe kwenye mnazi.
Baada ya kutoka kwenye lift watu waliokuwa eneo la mapokezi walikuwa wakimwangalia mrembo Regina kwa macho ya mshangao na matamanio lakini alionyesha kutojali na moja kwa moja alitoka nje na kwenda upande wa magari yalipoegeshwa na kusogelea gari moja ya kifaharai aina ya Maserati Gran Gabrio.
Uzuri wa lile gari ulimfanya Hamza kumwangalia kwa macho yaliokuwa na matamanio ilikuwa ni gari ambayo inaendana na muonekano wake,
“Hivi ulisema upo mwaka wa ingapi chuo?”
“Nipo mwaka wa tatu , kuna tatizo?”Aliuliza Hamza kiwasiwasi.
“Hakuna”
Aliongea na palepale kimadaha aliingia upande wa mbele ya gari na kuliwasha.
Regina alijihisi kujiamini na kuona sio mbaya mwanafunzi wa digrii ya uchumi mwaka wa tatu anamfaa sana.
SEHEMU YA 08.
Hamza alihisi siku hio ni kama vile muda wowote ataamka kutoka ndondoni , ndoto ambayo ilianzia tokea siku ambayo aliweza kusoma Tangazo la ajira ya mchumba feki katika mtandao wa JamiiForum mpaka siku hio ambayo ameweza kupata kazi hio.
Wakati anatoka katika hoteli ya Dosam V alitamani kuonana na mrembo Prisca lakini kwa bahati mbaya hakumuona na alijua pengine amekwisha kuondoka hivyo hakutaka hata kujisumbua kumtafuta na kutoka zake katika hio hoteli na kuelekea nje.
Alikuja kwa usafiri wa mwendokasi hivyo kama ni kurudi nyumbani alipaswa kuondoka kwa mwendokasi.
Wakati akiwa anapita eneo la Posta ya Zamani akitembea huku kichwa chake kikiwa katika mawazo mbalimbali alijikuta akisimama kwa muda na palepale ilionekan kuna wazo lilimuingia , wazo hilo lilimwambia huo sio wakati wa kurudi moja kwa moja geto kwake bali anapaswa kutafuta mahali kukaa na kupunga upepo na mahali alipoona panamfaa ni maeneo ya Kivukoni.
Ukweli ni kwamba wazo hilo lilimjia kutokana na kutaka kukaa chini na kuanza kutafakari mambo ya kimaajabu ambayo yamemtokea siku hio ndio maana.
Hamza maisha yake yalikuwa ni yenye maajabu tokea alivyokuwa mdogo mpaka kufikia wakati huo na msururu wa maajabu huo ulionekana kutokukoma katika maisha yake.
Maisha ni msururu wa mshangao , mzuri na mbaya na hatujui ni kipi kipo katika dakika nne zinazofuatia na hichi ndio kinafanya maisha yawe ni yenye msisimko mkubwa na muda ambao maisha yanapokutupia mshangao chukua muda wako kutathimini yale ambayo hayakuwa ndani ya matarajo na hicho ndio ambacho aliona.
Hamza alitumia zaidi ya lisaa kufikiria kile ambacho kimetokea siku hio , licha ya kwamba alikuwa na mambo mengi ya kuwazia lakini ambalo limetokea siku hio alilipa kipaumbele.
Ukweli ni kwamba hakujua kitakacho kwenda kutokea kwanzia siku zitakazofuatia lakini aliamini chochote kile ambacho kitamtokea kitakuwa ni jambo lenye msisimko mkubwa.
Alikuja kushitushwa na simu yake ambayo ilianza kuita mfululizo na mara baada ya kuotoa na kuangalia aliekuwa akimpigia ni Mama mmoja ambaye alishawahi kwenda kufanya kazi kwake kwa kutengeneza AC(Air Conditioner) yake ilipoharibika na alishangaa mama huyo kumpigia lakini moja kwa moja alijua lazima atakuwa na kazi hivyo alipokea kwa furaha zote.
Ijapokuwa alikuwa na pesa nyingi mfukoni ambazo zingemtosha katika matumizi ya takribani mwezi mmoja kabla ya kupokea mshahara wake wa kwanza lakini bado hakutaka kudharau kazi ambazo zimemsukuma na kumfikisha leo hio.
“Kijana habari yako?”
Sauti ya mwanamama mtu mzima iliweza kusikika upande wa pili ya simu.
“Salama mama habari za masiku?”
“Ni nzuri tu , bado unapatikana hapa Dar sik hizi?”
“Ndio Mama nipo”
“Oh! basi vizuri, kuna jirani yangu nae kapatwa na shida kama ileile ya kwangu , je unaweza kufiika kumsaidia kumtengenezea?”
“Mama mimi kama malipo yapo ninaweza kuja hata muda huu?”
“Asante sana baba yangu , mimi nipo kazini kwasasa lakini yeye pia atakuwa ndio anatoka kazini nitakupatia namba yake uwasiliane nae ukifika”
“Sawa mama Asante kwa kuniunganisha na hii kazi?”Aliongea Hamza na mara baada ya simu kukatwa alitoa tabasamu na kuangalia saa yake na kuona ilikuwa imetimu saa tisa hivi.
Ukweli muda huo alikuwa akijichukulia kama mwajiriwa lakini kwasababu kwake pesa ilikuwa kipaumbele hakuona haja ya kukataa kazi , hata hivyo licha ya kwamba chuoni alikuwa akisomea maswala ya uhumi na uhasibu lakini ukweli alikuwa akipendasana kazi ya ufundi , ni kama alikuwa na kipaji hicho kwani kazi ambazo nyingi alikuwa akifanya zilikuwa ni za ufundi, kusoma uhasibu ilikuwa ni sehemu ya maagizo ya Mzee.
Shukrani kwa mtandao wa The Job uliweza kumuunganisha na watu wengi ndani ya jiji la Dar es salaam ambao wana shida na maswala ya ufundi na ndio katika mtandao huo ambapo aliweza kupata kazi kwa mama huyo.
Eneo la kazi ilikuwa ni Kigamboni na kwasababu alikuwa kivukoni ilikuwa rahisi kusafiri kutoka hapo kuelekea huko lakini alikuja kugundua kwamba hakuwa na vitu muhimu vya kumsaidia kutengeneza lakini kutokana na kuwa na hela kidogo mfukoni aliona atapitia dukani na kununua vifaa.
Kazi yenyewe ilikuwa ni kurekebisha AC hivyo licha ya kwamba mama huyo kamwambia tatizo lilikuwa kama la kwake matatizo ya AC hayafanani hivyo kwanza alipaswa kuona tatizo na hapo ndio atajua namna ya kudili na tatizo.
Dakika chache Hamza alikuwa ashafika katika Apartment za Lotus , jambo moja ambalo Hamza alipenda kwenye hizo Apartment ni kwamba zilikuwa zikikaa wanawake tupu tena wale ambao hawajaolewa.
Unaweza ukashangaa lakini inasemekeana ndio utaratibu uliowekwa na mmiliki wa Apartment hizo ambazo asilimia kubwa ya wanaoshi hapo ni wafanyakazi a kampuni ya Dosam Global.
Sio kwamba kampuni hio ilikuwa ikipendelea wanawake, hapana bali ukweli ni kwamba ilikuwa imejenga majengo hayo kwa kulingana na stutus, yaani kama mwanamke ameolewa basi haruhusiwi kukaa ndani ya Apartment hizo.
Ni sehemu maarufu sana ndani ya jiji la Dar es salaam kwa kuwa na warembo wa viwango , yaani hakuna pisi mbovu ambazo zilikuwa zikishi ndani ya jengo hilo na hio yote ni kutokana na aina yao ya kazi , asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Dosam wa kike aidha ni wafanyakazi ndani ya hoteli, Shopping Mall, Wahudumu wa ndege na Benki.
Yaani kwa haraka sana ni kwamba kampuni ya Dosam inajihusisha na biashara za miamala(Dosam Bank ) , Usafiri wa Anga (Dosam Air) ,Mahoteli(Dosam hotels and hospitality) na maduka(Dosam Distributions&Department store).
Sasa aina ya kampuni hizo ni kwamba zinahitaji sana wafanyakazi ambao wana mvuto wa kipekee kimuonekano iwe ni mwaname au mwanamke , kwa mfano mhudumu wa Hoteli hawezi kuwa na sura ngumu lazima awe na sura ambayo akitabasamu mgeni palepale anavutik, bila shaka hicho sio kigezo pekee cha kuajiriwa ndani ya kampuni hio kikubwa ni ujuzi na taaluma, moenekano ni sifa ya ziada tu.
Sasa asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Dosam walikuwa wakiishi katika Apartment za kampuni kwa wale ambao hawana makazi ,sio sheria kuishi katika Apartment hizo lakini asilimia kubwa ya wafanyakazi walikuwa wakiishi katika Apartment hizo kutokana na kwamba walikuwa wakilipia gharama nusu halafu mazingira ni Premium.
Yaani kama nyumba kwa mwezi ni milioni moja basi mfanyakazi hulipia laki tano, huo ni mfano tu na sio gharama husika..
Sasa nyumba hizo mara nyingi ni kama zimetengwa japo si sheria, kuna Apartment ambayo inachukua tu wanaume ambao ni mabachela na kuna Apartment ambayo ilikuwa ikichukua wanawake ambao ni mabachela na kuna nyingine ambayo ilikuwa ikipangisha wale ambao wameoa au kuolewa , yaani familia.
Sasa katika Apartment zote ambazo zinakaliwa na wafanyakazi wa kampuni ni hio ya Lotus Flower Apartment, hio Apartent ilikuwa na warembo sio mchezo , ilikwa ikiendana na jina lake, wanaume wengi mabachela walikuwa wakitembelea hapo kujaribu bahati zao.
Ukitaka kuthibitisha hilo ni nje ya eneo la apartment hio kulikuwa na Dustibin kubwa ambayo ilikuwa na maua mengi sana pamoja na kadi , yote hayo ni wanaume ambao walikuwa wakitembelea mji huo kwa ajili ya kujaribu bahati zao na pale ambapo wanakataliwa wanaishia kutupa maua yao pamoja na kadi zao kwenye Dustibin hizo na kuondoka.
Hamza alikuwa akisikia habari za Apartment hii lakini ukweli ni kwamba siku ambayo alikuja kufanya kazi ilikuwa ni muda wa mchana muda wa kazi hivyo hakukutana na warembo wengi.
Ilikuwa ni muda ambao Hamza anakaribia kufika ndani ya Aparttn hizo , mita kadhaa kabla ya lilipo geti aliweza kuona gari mbili zilikiwa zimesimama, moja ilikuwa ni gari aina ya Aud na nyingine ilikuwa ni gari aina ya Noah.
Kwa macho yake ambayo yanaona mbali aliweza kushuhudia mwanamke ambaye alikuwa amezingirwa na wanaume na ilionekana ni kama vile wanaume wale walikuwa wakibishana hivi na yule msichana kwa kumzonga zonga.
Hamza jambo lile lilimtia shauku na kuongeza mwendo ili kujua kililichokuwa kikiendelea , ukweli ni kwamba hata kama asingetaka kujua angejua tu kwani watu hao walikuwa wamesimama njiani kuingia katika Apartment hizo.
“Eliza nimechoshwa na majibu yako ya kis**nge , ninachotaka leo hii ni pesa zangu na si vinginevyo”Mzee mmoja mwenye mwili ambao ulikuwa umetuna kidogo aliongea.
“Mzee Amosi nilishakuambia nivumilie , hela unayonidai ni nyingi na sasa hivi sina uwezo wa kupata mkopo tena, unafikiri kiasi chote hicho nitatoa wapi , isitoshe hela ambazo nimekupatia ni kiasi kikubwa mno kuliko hata ulichonikopesha, unachonidai hapa ni riba”
“Sitaki maelezo yako Eliza yashanichosha na kila siku unatoa kauli zinazofanana , hivyo leo una chaguzi mbili aidha ukubaliane na sharti ambalo nakuambia kila siku na tuondoke pamoja urudi kesho au unipate pesa yangu leo hii, kama hela huna na sharti langu hukubaliani nalo basi vijana niliokuja nao watafanya kazi yao”Aliongea kwa kufoka.
Hamza ambaye ndio sasa amekaribia karibu alikuwa akisikia kila kitu na kwa haraka haraka aliweza kuelewa kinachoendelea, kwanza ilionekana watu hao walimkinga mwanadada huyo kupitisha gari kuingia ndani na ilionekana walikuwa wakimdai pesa.
Kadri mzozo huo ulivyokuwa ukiongezeka wanawake baadhi ambao walikuwa wakiishi ndani ya hilo eneo walikuwa wanajikusanya huku wakionyesha hofu ya kuamulia ule ugomvi , ni kama walikuwa wakimjua huyo mzee ambaye anaonyesha yupo kifujo fujo hata kama anadai pesa yake.
“Mzee Amosi naomba usinifanyie hivyo , kwanini unakosa utu?”
“Haha,… leo ndio unasema sina utu , wakati nakupatia pesa yangu nani alimbembeleza mwenzake, kama nisingekuwa na utu nisingekupatia kiasi chote kile cha pesa , sasa mama yako amekwisha kupona lakini unashindwa kulipa pesa yangu , kingine unasema unalipa riba kwani makubaliano yetu yapoje wakati unachukua mkopo?, hebu acha kupoteza muda , nimekupa njia nyepesi kabisa lakini unaleta maringo , kwani mimi ni mbaya sana mpaka ushindwe kutii sharti langu dogo namna hio?”
Hamza ambaye mara baada ya kusikia kauli hio alijua kabisa hapo huyo mwanaume sio kama alikuwa na shida sana ya pesa au huyo mwanadada mrembo alikuwa ameshindwa kulipa ila ilionekana analazimisha kulipwa pesa yake hapo hapo akijua huyo mwanadada atashindwa kuitoa ili akubaliane na sharti lingine ambalo kwa haraka haraka alijua ni ngono.
Hamza alifikiria kidogo mwanamke aliekuwa akizongwa alionekana kuwa mrembo mno, lakini kwasababu watu walikuwa wakiongezeka kukusanyika ndani ya eneo hilo hakuona haja ya kuendelea kusimama kwani muda ulikuwa ukisogea kwa kasi hivyo palepale alitoa simu yake na kutafuta namba ambayo alitumiwa na kisha akaipiga.
Akiwa amesogea pembeni ya barabara aliweza kusikia simu ile ilikuwa ikiita pasipo ya kupokelewa na iliita mpaka ikakatika , akarudia kupiga na ikaita mpaka ikakatika mara baada ya kurudia mara ya nne akijiambia isipopokelewa anaondoka palepale simu ilipokelewa.
“Sikia Eliza sitaki kukudhalilisha na isitoshe mimi na wewe tumetoka mbali , kama huna hela kwanini tusiwe wote wastaarabu,ongozana na mimi na kuondoka mbele ya macho haya ya watu?”
“Helloo..!!!”
Hamza alianza kuongea lakini sauti ambayo ameweza kusikia ni ya mwanaume ambae anamdai Eliza , palepale aligeuza sura yake na kuangalia upande wa ugomvi unapoendelea na alikuwa haoni vizuri kutokana na kuzibiwa na watu na ilimfanya kusogea karibu zaidi.
“Boss amepokea simu..?”
“Kijana ambaye alikuwa karibu na yule mzee alieitwa Amosi aliongea na kauli ile ilimfanya Amosi kumwangalia Eliza mkononni mwake na palepale alimpokonya ile simu.
“Umetutegeshea simu sio , Eliza kwanini unaenda mbali hivi?”Aliongea huku hasira zikionekana zaidi na zaidi katika macho yake huku akiwa tayari ashakata ile simu.
Upande wa Hamza mara baada ya simu ile kukatwa palepale alijua mtu ambaye anapaswa kuja kumfanyia kazi ni huyo mrembo ambaye anadhalilishwa na wadeni wake.
“Nakuuliza ulikuwa ukiongea na nani?”Amosi alipatwa na mashaka na palepale alimshikilia mkono na kummnya Eliza kwenye gari.
“Puuh!!!”
Haikueleweka imekuwaje lakini Amosi alijikuta akidondoka kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu kama vile amevutwa.
Kitendo kile kilishangaza waliokuwa wakiangaliana na hapo hapo ndipo sasa waligundua Amosi alikuwa amevutwa kurudi nyuma na kijana ambaye alikuwa amefika hapo muda huo.
Hata Eliza hakujua namna ambavyo Amosi alitoka mbele yake na alijikuta akiinua uso wake ambao alikuwa amefumba macho kwa kile ambacho alitegemea kufanyiwa na hapo ndipo alipoweza kushuhudia sura ya kijana ambaye amesimama mbele yake.
“Dogo unakitafuta kifo sio?”Mzee Amosi mara baada ya akili yake kufanya kazi alionyesha kukasirika mno kwa kile alichofanyiwa.
“Mzee hebu tuliza kwanza jazba najua una shida na huyu mwanadada lakini vilevile na mimi nina shida nae”Aliongea Hamza kwa sauti iliojaa upole , ni kama alikuwa akitania hivi na kufanya watu kumshangaa , hata Eliza mwenyewe alionekana kushangaa na kujiuliza huyo kijana ni nani kwanini anajiingiza kwenye mgogoro wake na kusababisha matatizo zaidi.
“Chongolo mnashangaa nini , hebu mshikisheni kwanza adabu ndio tuongee nae vizuri na kumjua ni nani”Aliongea Amosi kwa hasira , hakutaka kusikia ngonjera za kijana huyo.
Chongolo mara baada ya akili yake kurudishwa kwenye uhalisia ni kama alishituka na palepale pamoja na wenzake wawili walimsogelea Hamza kwa ajili ya kumdhibiti.
“Mamaa…!!!”
Kijana mmoja ambae alikuwa kimbelembele mara baada ya kumsogelea Hamza alijikuta akipigwa teke la kigoti na kumfanya atoe ukulele huku akichuchumaa chini kutokana na maumivu.
Kitendo kile kilishangazwa wengi kwani kilitokea kwa spidi ya hali ya juu sana kutoka kwa Hamza , ilikuwa ni kama vile alikuwa na uzoefu wa hali ya juu kwenye kudili na watu wa namna hio.
Wale wengine mara baada ya kuona kiilichomtokea wenzao ni kama hawakuaini amini kama shamblizi hilo lilitoka kwa kijana wasiemjua na moja kwa moja hasira zao ziliongezeka mara mbili na kusogelea Hamza kwa kasi.
Puuh! , Bam!!!”
Chongolo mara baada ya kumsogelea Hamza kwa ajili ya kurusha ngumi mkono wake ulidakwa ukiwa hewani na kuvutwa mbele , wakati huo huo yule mwenzake aliekuwa nyuma akipigwa teke la makagari na kumfanya adondoke kama furushi huku Chongolo akisukumiziwa kwenye kiooo cha mbele cha gari ya Noah kiasi cha kutengeneza ufa.
“Sikutaka kwenda mbali hivi ila nachukia kupotezewa muda, Mzee unaonaje ukirudi siku nyingine kudai pesa yako, nahitaji kumalizana na huyu mrembo mapema nirudi kwenye shughuli zangu nyingine”Aliongea Hamza huku akimwangalia Mzee Amosi ambae alionekana kuwa katika kiwewe asiamini vijana wake watatu aliokuwa akiwaamini kupambana na watu ndani ya dakika moja tu wamedhibitiwa na wote wanaugulia maumivu.
Alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa ya kawaida kama kwamba alikuwa akimtathimini.
Mzee Amosi alionekana kutafakari kwa muda , kwa jinsi alivyomuona Hamza akifanya mashambulizi na kupitia uzoefu wake wa miaka mingi kuna kitu alikiona haraka haraka na hakutaka kuendelea kuuliza ni nani.
“Chongolo tuondokeni tutarudi , Eliza jiandae siku nitakayorudi sitokuwa na huruma tena , ni kheri upige simu mapema kabla ya kukutafuta”Aliongea Mzee yule huku akimwangalia Eliza kwa macho makali na kisha alipangua watu na kuingia ndani ya gari.
Hamza mara baada ya kuona mzee huyo amekuwa mtiifu kwake alijikuta akivuta pumzi za ahueni maana hakutaka kwenda mbali sana.
Wakati akiona amefanya jambo la kawaida upande wa watu waliokuwa ndani ya eneo hilo walionekana kuwa katika mshangao, kila mtu alikuwa na lake kichwani na kuna wale walioamini huenda Hamza ni mwanajeshi licha ya kwamba muonekano wake haukuwa ukisanifu kile alichokifanya.
Mrembo Eliza alikuwa ni kama haamini alikuwa amesalimika na aliemsaidia ni kijana aliekuwa mbele yake ambaye ndio mara yake ya kwanza kukutana nae, maswali kibao yalichipua katika akili yake lakini alishindwa kuuliza zaidi ya kumwangalia Hamza bila ya neno.
Hamza ni kama sasa alikuwa akimthaminisha mrembo huyo , wakati anafanya maamuzi ya kumsaidia mwanamke huyo hakufikiria sana kwa sababau aliamini akifukuza watu wale kazi yake iliomleta hapo itaisha haraka na kupata ujira wake , lakini mara baada ya kukutanisha macho na msichana huyo aliekuwa katika hali ya mshangao ni kama sasa alikuwa akipata wazo la pili.
“Kwanini ndani ya hizi siku chache nimekuwa nikikutana na wanawake warembo namna hii , hii ni ishara nzuri kwangu au mbaya?”Hamza alijiuliza swali hilo.
Alikumbuka wakati alipokuwa katika Apartment za Dosam Homes alikutana na mwanamke aliefahamika kwa jina la Tresha Noah, akaja kukutana na mrembo aliempelekea chungu , hatimae Prisca , Mrembo Regita ambae ndio alimshangaza zaidi na hatimae leo hio anakutana na msichana aliefahamika kwa jina la Eliza.
Kama angewapangilia warembo hao kulingana na uzuri wao basi Regina angeshika namba moja , Prisca namba mbili , huyo Eliza namba tatu , Anitha namba nne na kisha Tresha Noah namba tano.
Ukweli Tresha Noah alikuwa akifikiana uzuri na huyo Eliza lakini alikosa vigezo katika macho ya Hamza mara baada ya Amiri kumwambia uzuri wake ni wa kutengeneza.
“Kaka upo vizuri kwa kweli , ni mara ya kwanza kuona mtu mwenye uwezo wa kuwashinda wale Vibaka ,Wewe ni mwanajeshi au polisi , Vipi Eliza ni mpenzi wako?”Kundi lile la wanawake waliokuwa wakiangalia tukio hilo walimzunguka Hamza wakitaka kusikia neno kutoka kwake.
“Eliza kumbe una mpenzi mwanajeshi na husemi jirani?”Aliongea wanamama mwingine na kumfanya Eliza kushangazwa na swali hilo na kuishia kumwangalia Hamza.
“Jamani mimi sina mahusiano na huyu dada , mimi ni fundi na nimekuja kutengeneza AC , kama kuna yoyote mwenye shida inayohitaji fundi nipo hapa natengeneza kila kitu”
Kauli ya Hamza iliwashangaza wanawake waliokuwa wamemsikia , ila kauli ile ni kama haijamfurahisha Eliza ni kama vile alitamani Hamza akubali na aseme niwapenzi hata yeye mwenyewe alijishangaa kuwa na mawazo ya namna hio , pengine ni kutokana na kuwa single kwa muda mrefu..
“Handsome , upo siriasi unatengeneza kila kitu?, unaonaje ukatengeneza na moyo wangu ulioumizwa”Aliongea mrembo mmoja ambae alikuwa ametumia Make up nyingi mno huku akiwa na kikuku mguuni.
“Recho..!!!”Aliongea Eliza ambae ni kama vile ameamka sasa kutoka kwenye mshangao na kumsogelea Hamza.
“Kaka tunaweza kwenda ukaanganlie shida ya Ac yangu”Aliongea Eliza na kwasababu alikuwa na aibu za kutosha kuendelea kukaa katika eneo hilo kwa yale yaliomsibu alimchukua Hamza na wakaingia ndani huku wakimwacha mwanadada aliefahamika kwa jina la Recho akivuta mdomo.
Hamza alikuwa kimya kimya na mwanamke huyo mpaka wanaingia kwenye lift, ilikuwa ni kama vile amerudi kwenye upole wake.
Ukweli ni kwamba Hamza kimuonekano alikuwa mpole sana lakini matendo yake yalikuwa tofauti na yeye alivyo , haikueleweka ana historia gani ya maisha yake ya yuma lakini ni rahisi kuotea maisha yake hayakuwa ya kawaida.
Eliza na yeye ilikuwa mara yake ya kwanza kusaidiwa na mwanaume , tena mbele ya wale waliokuwa wakimdai.
“Asante kaka kwa kunisaidia”Aliongea Eliza kwa kukosa kujiamini na kumshitua Hamza aliekuwa akijiwazia mambo ya ajabu na yote hayo ni kutokana na kumtamani mrembo huyo Eliza.
“Hii tabia ya kuwazia kile mwanamke inatokana na kukosa mchezo muda mrefu nini?”Alijiwazia Hamza.
“Hakuna shida ya kunishukuru Eliza , kama nilivyosema nimekusaidia ili kumaliza kazi yangu kwa haraka”Aliongea Hamza huku akijiona kidume na kauli ile ilimfanya Eliza kumwangalia Hamza kwa macho ya kidadisi, ni kama vile alikuwa amejawa na hamu ya kumjua vizuri Hamza.
Kwa mtu yoyote pengine siku hio angevutiwa na Hamza hususani kwa muonekao wake na kwa kile abacho amefanya dakika chache zilizopita.
Hamza hakuwa amebadili mavazi yake ambayo yalikuwa mapya na mtindo wa nywele ulikuwa umempendeza sasa ukijumlisha na ngozi yake yenye mchanganyo wa kizungu ilimfanya kuwa mtanashati kupindukia na hakika mwanamke yoyote angempenda na kuvutiwa nae , siku hio hakuwa akionekana kama fundi kabisa , kwa kumlinganisha na mrembo Eliza moja kwa moja kwa tu asie na uelewa atasema wawili hao ni wapenzi kwa namna wanavyoendana.
“Ding..!!!”
Lift ilifunguka katika Ghorofa ya kumi na tano ambayo ndio mwisho kabisa , mazingira ya Jengo hilo yalikuwa yakvutia mno , yamejaa ufahari wa macho , Ijapokuwa haikuwa kama apartment za Dosam Homes lakini ni mazingira ambayo yanatosha kuhifadhi watu wa vipato vya kati na juu.
“Karibu kaka”
“Asante , unaweza kuniita Hamza”Aliongea Hamza huku akijitahidi kuonekana mpole mbele ya mwanamke huyo , ni kama alikuwa akijitahidi kumpangawisha Eliza.
“Oh karibu sana Hamza fundi”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu, alitamani aendelee kuisikia sauti ya Eliza kwani ni kama ilikuwa ikibembeleza.
Kama alivyotegemea nyumba hio ilikuwa safi mno na mpangilio wake ulikuwa ni wa kiwango cha juu , kulingana na uzoefu wa Hamza hata apartment ya Mellisa mwanamke wa Amiri haikuwa na mpangilio safi kama huo , ijapokuwa hakuona chumbani kulivyo lakini eneo la sebuleni lilimpa picha.
Wazungu wanasema ‘A house is a mirror to its owner’ hivyo mazingira ya eneo hilo yalimpa picha kamili Eliza ni mwanamke wa namna gani.
“Hamza sijui nikukaribishe kwanza kinywaji au uanze kazi moja kwa moja nikikuandalia chochote”Aliongea Eliza ambae alionekana kukosa kujiamini kwa namna flani hivi , pengine ilikuwa ni kwasababu ya kile kilichomtokea dakika kadhaa ilizopita mpaka Hamza kuingilia kati.
“Kwa leo naomba niende moja kwa moja kwenye ufundi , itakuwa vizuri baada ya ufundi kupata hata juisi tu itatosha kutia baraka”Aliongea Hamza akijiamini .
*****
Upande mwingine ikiwa ni dakika kadhaa tokea kuondoka kwa Amosi na kundi lake , ikiwa ni kilomita kadhaa kutoka eneo hilo la Apartment walienda kusimamisha gari katika moja ya mgahawa na kabla ya Amosi kushuka aliwaangalia vijana wake waliokuwa hawajiamini kwa kile kilichotokea na kisha akavuta pumzi.
“Chongolo nadhani unajua hii kazi hainihusu mimi moja kwa moja bali ni bosi, kama atasikie kile ambacho kimetokea leo hii nadhani kuna swala lolote ambalo litatokea , nani anajua anachokiwaza bosi sasa hivi?”Aliongea Amosi.
“Mkuu tunapaswa kufanya nini?”
“Inamaana bado tu hamjaelewa ninachomaanisha , mbona mnakuwa na vichwa vidogo namna hii”Aliongea Amosi huku akionyesha kukasirika , ni kama aliongea kauli tatanishi ili mradi wasielewe ili tu awafokee kupunguza hasira zake.
“Sikieni kuhusu Eliza hili swala nitaongea na bosi mwenyewe , ninachotaka ni kumfatilia yule mpuuzi alievuruga mipango yetu, kazi hii inaanza sasa hivi mtaondoka na gari”Aliongea Amosi na palepale akashuka kwenye gari na kisha akaingia katika Mgahawa huo.
Hazikupita dakika kadhaa Chongolo na wenzake waliondosha gari hio ya Noah na kutokomea upande waliotokea.
Amosi alitembea kiwasiwasi kuingia ndani ya Mgahawa huo wa kisasa , kulikuwa na watu wachache sana lakini hao wachache walionyesha ni wale wenye uwezo mkubwa wa kifedha.
“Unavyonifanyia sio vizuri , unajua kabisa nakupenda lakini kwanini leo unataka kukatisha mahusiano yetu , kwanini unanifanyia hivi Chriss”
“Anitha unaenda mbali na nadhani akili yako haifanyi kazi vizuri , mimi na wewe nani alitaka mahusiano , ulinifuata mwenyewe ukitaka niwe Boyfriend wako kwa muda kuwaringishia wenzako lakini kwa huruma zangu tumefikisha mwezi huu , unataka nini kutoka kwangu , leo ndio mwisho maana nina mtu tayari ninaempenda , naomba uondoke nina mazungumzo muhimu na Amosi”Aliongea mwanaume mmoja mtanashati sana aliekuwa amekaa kwenye Kona ya mgahawa huo huku mbele yake akiwa ni msichana mrembo ambae alionyesha hali ya kutaka kulia katika macho yake,
Kwa kauli mbili tu ambazo Amosi aliweza kusikia alijua fika kile kinachoendelea , ila hakutaka kuongea neno kwanza bosi wake amalizane na mlimbwende huyo.
Mwanamke huyo aliefahamika kwa jina la Anitha alionekana kuwa na hasira mno na mwanaume aliefahamika kwa jina la Chriss , kwa kile kilichokuwa kikionekana hapo ni kama msichana huyo anafosi penzi kwa kijana huyo.
“Anitha nimesema naomba uondoke , mkataba wangu na wewe umeisha leo hii”Alirudia Chriss kuongea na msichana mrembo wa haja alimwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliojaa hasira na kisha akasimama na kuchukua mkoba wake.
“Siku moja utakuja kujua mimi ndio mtu ninaekupenda kwa dhati na sio pesa zako Chriss na utakuwa umechelewa”Aliongea na kisha palepale akageuka na kuondoka.
Amosi ambae alikuwa amesimama pembeni ya meza hio aliishia kugeuza shingo kumtathimini mwanamke ambae analilia penzi , na aliishia kuona wivu kwani msichana huyo alikuwa amebarikiwa kila kitu , alikuwa ni mrembo haswa kuliko maelezo , pengine katika maisha yake na uzee huo hajawahi kuwa na mwanamke wa urembo huo , hata kuota kuwa na mwanamke wa namna hio hajawahi , sasa kijana aliekuwa mbele yake alikuwa na uwezo wa kuacha mwanamke mrembo huyo ambae analilia penzi , aliona wivu na kujiambia katika maisha pengine sio pesa tu na muonekano pia huvutia zaidi wanawake.
“Chriss huyu binti ni mrembo sana , lakini kuna haja gani ya kumuacha namna hii ni bora ungemdanganya na kuendelea nae pale unapomhitaji”AliongeaAmosi huku akikaa kwenye kile kiti.
“Nina sababu za kuachana nae ambazo hata wewe ukizijua hutonilaumu”Aliongea na kumfanya Amosi kutabasamu..
“Wewe na mzee wako mna tabia zinazofanana , tatizo mnapenda sana wanawake lakini kudumu nao hamuwezi”
“Haha .. Siwezi kufanana na yule mzee mimi , ni muhuni kupindukia, sidhani kuna mwanamke mrembo ambae ashawahi kumvutia akashindwa kumpata”Aliongea Chriss na kumfanya Amosi kutabasamu na kujiambia kwa wakati mmoja Chriss hakuwa akimfahammu baba yake vizuri , sio kila mwanamke anaemtaka ashawahi kumpata, kwani ni mwaka wa pili huo alikuwa akihaha kutaka kumuweka Eliza kwenye himaya yake lakini imeshindikana.
“Nimeitikia wito bosi wangu , simu kama hizi hunipa hamasa kwani naamini kuna malipo”Aliongea Amosi huku akiweka tabasamu.
“Haha.. Amosi mimi napenda watu wanaopenda pesa kama wewe , ndio maana kila inapokuja swala linalohitaji juhudi na uharaka wa utimilifu jina lako hujitokeza”
“Hii ndio kazi inayoniweka mjini , ijapokuwa pesa ni kipaumbele lakini matokeo mazuri nazingatia sana , kuna wanaopenda pesa zaidi kiasi cha kutumbukia kwenye utapeli, matokeo ndio kila kitu baada ya malipo”
“Haha.. Ijapokuwa unaniita bosi lakini wewe ni mtu mzima sana kwangu , si shaka kuwa na busara na nidhamu katika kazi yako , anyway tokea nikujue kupitia baba nimekuwa na shauku sana kuyajua maisha yako lakini maswali hayo nitayaweka kapuni kwa leo na niende moja kwa moja kwa kilichonifanya nikutafute”Aliongea lakini kwa sauti yake ilimfanya Amosi kuona hali ya kusita sita katika macho ya Chriss.
“Kuna mwanamke nataka unisaidie kumtafuta”Hatimae Chriss aliongea na kumfanya Amosi kushangaa kidogo.
“Mwanamke!!!?”
“Ndio mwanamke , kuhusu taarifa zake faili lake utaletewa kesho ofisini kwako, Mzee Amosi nimekuita tuongee swala hili ili kuonyesha ni kwa namna gani ni swala muhimu, hii inaweza kuwa kazi kubwa kuwahi kuipata tokea kuanza kwako kazi ya maswala ya kijasusi..”Alisita kidogo na kisha akaendelea kuongea.
“Kuna watu nyuma yangu juu ya hii kazi , mimi ni kama Freelancer , ijapokuwa sitowataja ni wakina nani kwa ajili ya usalama wako na wangu lakini wapo tayari kulipa kiasi chochote cha pesa , cha msingi ni matokeo ya kuridhisha”Aliongea na kwa namna Amosi alivyokuwa akimuona Chriss alihisi uzito wa kazi yenyewe maana bwana huyo mara nyingi alionekana kutokuwa siriasi lakini kwa namna flani ni kama hofu ilianza kumvaa.
“Kwa muonekano inaonekana sio kazi ya kawaida na inahitaji rasilimali za ki uwezeshaji?”
“Haha.. Amosi unaonekana kuwa na uelewa wa haraka , ndio maana Mzee anakuita jasusi nje ya mfumo,, kama ulivyosema mimi ni kama Freelancer katika hii kazi hivyo nipo tayari kuwekeza kiasi cha pesa kwako kwa ajili ya uwezeshaji wa ukamilishaji wa hii kazi, tutaanza na milioni mia moja”Aliongea Chriss.
“Milioni mia moja!!?”Amosi alishangaa mno.
“Kama ni milioni mia moja kama rasilimali uwezeshaji inamaana…..”
“Ndio Amosi , kazi hii ni ya mabilioni ya pesa , wenye uhitaji wa kukamilisha kazi hii wanataka ifanikiwe kwa haraka na kwa ufanisi lakini wapo Desparate, ukubwa wa pesa unaendana na ukubwa wa kazi yenyewe hivyo usishangae”Aliongea Chirss na kumfanya Amosi kumeza mate mengi.
“Nipo tayari juu ya kazi hii”Aliongea Amosi bila ya kufikiria , ukweli kilichomfanya kutoa jibu la haraka haraka sio ukubwa wa kiasi cha pesa bali ni shauku juu ya kazi yenyewe , kama anataka matokeo ya kazi hio anataka kutoa mapesa mengi kiasi hicho basi jambo hilo linaweza kumshangaza.
“Safi Amosi, unaonekana kuwa na shauku , hata mimi nilipokea kazi hii kutokana na shauku, nadhani tutazungumza zaidi baada ya kupokea faili, kumbuka usiri mkubwa unahitajika katika kazi hii na tahadhari zote zimechukuliwa, katika faili kutaambatana na fomu ya makubalianao ya kufanya jambo hili kuwa siri”Aliongea na Amosi alitingisha kichwa.
****
Dakika chache mbele mara baada ya Hamza kuelezewa tatizo la AC aliweza kuijua shida yake kabla hata hajafanya uchunguzi , ilionekana kulikuwa na shida ya kipima joto cha AC hivyo kufanya Ac kushindwa kukadiria kiwango flani cha ubaridi ndani ya nyumba hio.
Hamza hilo halikuwa tatizo kubwa kwake na aliweza kurekebisha haraka haraka na kumaliza lakini hakuishia hapo tu alijaribbu kuagalia na shida nyingine na aligundua kulikuwa na vumbi jingi upande wa Evaporator Coill hivyo alijaribub kurekebisha, mpaka anakuja kumaliza kazi yake ni kama nusu saa imepita na alijihisi njaa.
Kilichomfanya kuhisi njaa ni harufu ya chakula iliokuwa ikisambaa ndani ya nyumba hio ikimaanisha mrembo Eliza alikuwa jikoni.
“Inaonekana huyu mwanamke amekamilika kila idara , sio kwa kunukiza huku”Alijiwazia Hamza huku akijifuta vumbi kwenye mikono yake na Hangerchief , shati ambalo alikuwa amevaa lilikuwa limechafuka kutokana na kuparamia ukuta wakati wakusafisha Ac hio.
Inaweza ikawa kazi nyepesi kwa Hamza kutokana na uzoefu lakini kwa mtu mwingine ingekuwa kazi ngumu mno , kwani kwanza ilimhitaji kuchungulia upande wa nje wa jengo hilo , jambo ambalo lilikuwa likiogopesha kutokana na urefu wa jengo.
“Nishamaliza kazi yako , kulikuwa na shida ya setting tu na nimerekebisha”Aliogea Hamza huku akimwangalia Eliza ambae alionekana kutokea upande wa jikoni kuja eneo la sebulenni, alikuwa amependeza kwa mavazi ya kinyumbani zaidi na kumfanya kuonekana wife material.
“Oh!, Asante kaka yangu , naona pia namna ulivyochafuka”
“Yeah, wakati mama ananipigia kuja nnilikuwa nimetoka mahali na kuona nisiende nyumbani moja kwa moja”
“Na maamuzi yako yemeishia kuniokoa siku ya leo , nashindwa hata kuelezea tukio hili , linanifanya niwe na aibu mbele yako”Aliongea Eliza huku sauti yake ikionekana ni ya kusita sita na hakukutanisha macho kumwangalia Hamza .
“Ni swala la kawaida ambalo linaweza kumtokea yoyote , watu wa aina ile hawana mipaka na ni vizuri kutojihusisha nao”
“Asante sana , Hamza sijui nakushukuru vipi lakini naamini kile ulichokifanya ni kwa ajili ya kuninsaidia , kila mtu alikuwa akifurahia kudhalilika kwangu, ni swala la kawaida kwa binadamu , nadhani dunia sio mbaya kama nilivokuwa nikifiiria , umekuwa mtu wa kwanza kusimama upande wangu..”Aliongea Eliza huku hali yake ya kihisia ilionekana kubadilika mara moja jambo ambalo lilimshangaza Hamza , ilikuwa ni kama ashasoma Eliza ni mwanamke ambae alikuwa amepitia changamoto za kimaisha na kutokana hali ile ya kubadilika alishindwa kujua ni hatua gani achukue.
“Eh! , jamani naunguza..!!!”Aliongea Eliza akiwa kama ameshituka na kukimbilia jikoni na kumfanya Hamza atabasamu na kukaa kwenye sofa akimsubiria achukue pesa yake na aondoke maana muda ulikuwa umeenda.
“Samahani kwa kukuchelewesha mwaya , naandaa chakula cha kupeleka hospitalini , muda naona umeenda , unaonaje ukipata kabisa chakula cha usiku?”Aliongea Eliza huku akionekana kutokujiamini.
“Pole kwa kuuguza”
“Asante , nimeshapoa”Aliongea.
“Sasa mimi nisikucheleweshe , kwasababu kazi ilionileta ni ufundi na nishaimaliza ngoja nikuache uendelee na ratiba zingine”
“Malipo yatakuwa kiasi gani?”
“Nipatie elfu kumi tu inatosha “Aliongea Hamza , ijapokuwa mwanamke huyo alikuwa akimfanya amwambe nimetengeneza bure lakini aliona ni udhaifu hivyo anapaswa kuchukua chake.
Eliza palepale aliingia chumbani na kutoka na noti mbili za elfu kumi na kisha kumpatia Hamza.
“Sidhani ni sawa nikikuita fundi au Hamza wewe ni mwokozi wangu leo hii na angalau nilipaswa kukupa chochote kuweka baraka zaidi ya hii juisi, hii ya ufundi na hii naomba utumie kama nauli”
“Wewe unaweza kuniita fundi , namba yangu inayo ukiwa na tatizo unaweza kuniambia muda wowote nitafika”Aliongea Hamza na kupokea ile hela , hakutaka kukataa malipo ya elfu ishirini , ijapokuwa alijua mwanamke huyo alikuwa na matatizo lakini kama atakataa angeonekana kama alikuwa na ajenda zaidi ya moja.
Baada ya hela kama kawaida alipewa juisi na Korosho lakini Hamza kutokana na haraka na kutomfanya mwanamke huyo kuwa na wasiwasi ,korosho aliweka kwenye koti na juisi akainywa kama maji na kisha akaaga na kuondoka.
*******
Saa mbili kamili za usiku ndani ya mgahawa wa Golden Fork mbezi Beach ilisimama gari nzuri ya thamani aina ya BMW 14Oi ya rangi ya blue metallic.
Ilikuwa gari nzuri kweli iliofanya watu baadhi waliokwa wamekaa upande wa madirisha yanayoangaliana na maegesho kukaza macho kwa mtu anaeshuka katika gari hio.
Dakika kama moja kupita aliweza kutoka mtu katika gari hio ,ijapokuwa ilikuwa usiku na taa hazikuwa kali sana lakini ilitosha kuwafanya watu kukaza macho zaidi, kwani mwanamke alietoka katika gari hio hakuwa wa kawaida,alikuwa mrembo haswa japo kwa macho ya Hamza ambae ameshakutana na mrembo Regina angemuweka pengine nafasi ya tatu au ya pili mwanamke huyo.
Akiwa si mwenye kujali macho yanayomwangalia alizipiga hatua kuingia ndani ya mgahawa huo huku waliokuwa wakimtathimini wakitaka kujua yupo peke yake au kuna mtu amefika hapo kwa ajili ya kukutana nae.
Mwanamke huyo alievalia suruali ya rangi nyeupe na blazia ya rangi ya bluu alitembea kwa kuchezesha miguu yake na viatu vyake vya high heels mpaka upande wa kulia wa mgahawa huo huku nyuma akiacha usumbufu wa marashi yake.
“Alex!, umefika muda mrefu sana?”Aliongea yule mwanamke baada ya kumfikia mwanaume aliekuwa ameketi kwenye meza peke yake upande wa kulia wa mgahawa huo ,sehemu ambayo ni kama imejitenga.
“Wakati na kutumia meseji ndio nilikuwa nikikaribia , ni kama dakika ishirini zilizopita, kwanza sijategemea kama ungewahi maana najua wanawake na tabia zenu”Aliongea Alex kwa namna flani hivi ya kukosa amani kutokana na uzuri wa mwanamke huyo.
“Wewe mwenyewe ndio ulitaka usumbufu wa kukutana , malipo yangeweza kufanyika kwa njia ya mtandao kwanini unataka Cash?”
“Nadhani ushajua sababu ya mimi kutaka Cash Frida , nataka kuongea na wewe maana kuna mambo mengi bado sijayaelewa , mimi ndio ambae nilikuwa nikikuletea mzigo na hakuna kosa la aina yoyote limetokea , Frida kama ni lile swala la kuzielezea hisia zangu kwako naomba usahau , chukulia kama halijatokea na kazi iendelee”Aliongea Alex akiwa katika hali ya kulalamika hivi mbele ya mwanamke huyo , kwa macho ya haraka ilikuwa ni sawa na kusema alikuwa akimpenda huyo mwanamke lakini ilionekana mwanamke alikuwa amemkataa.
Mwanamke aliefahamika kwa jina la Frida alitoa tabasamu huku akimwangalia Hamza bila ya kujibu akimpa nafasi muhudumu kuweka juisi alioagiza kisha aendelee kuongea.
“Tatizo lako Alex unakosa focus, wewe ni mfanyabiashara lakini unakuwa kama vile ni mwajiriwa”
“Unamaanisha nini kusema hivyo??”
“Namaanisha utaendelea kutii kile ambacho ninahitaji kama mteja wako na si vingineyvyo,kuhusu sababu ulizoelezea kwangu huwa sizipi kipaummbele sana, wewe sio wa kwanza hata hivyo,anyway nimekuja hapa kwa maswala mawili tu, la kwanza ni kukupatia mzigo wako na hii ni mara ya mwisho sisi kuonana moja kwa moja , malipo yote yatafanyika kwa njia za kawaida , pili Alex acha kuuliza maswali mengi , wewe fanya biashara na kidhi mahitaji ya mteja wako , maswali mengi huua uaminifu, Nadhani kuna sheria na vigezo umepatiwa na Binamu mpaka kukidhi kuendesha biashara zao”Aliongea Frida huku akinywa juisi ile kimapozi.
“Lazima awe Hamza , Frida kuna ajenda gani, yeye ana nini mpaka ndio awe mwenye kukuletea mzigo?”
“Lazima awe Hamza ndio na si vingineyo , nadhani unashindwa kuelewa nilichokuambia , hizi ni hela zako natumaini mahitaji yangu katika mtazamo wa kibiashara yatashughulikiwa ipasavyo , Alex nakuambia mara nyingine acha kuuliza sana maswali , fanya biashara”Aliongea Frida na kisha alitoa bahasha na kuiweka mezani na kisha akamwinamia Alex na kumbusu shavuni la kwaheri ya kuoanana.
Busu lile lilimfanya Alex mwili wake wote kusisimka lakini kwa Frida ilionekana ni kitendo cha kuficha kile kilichokuwa kikiendele kati yao , ijapokuwa walikuwa wamejitenga lakini eneo hilo lilikuwa wazi kufanya watu wawaone.
Alex aliishia kumwangalia mrembo Frida akitokomea kwenye macho yake , hata ile hamu ya kuendelea kukaa hapo ilikuwa imempotea , mwanamke huyo alikuwa akimvutia kimapenzi mno.
Alex kama mfanyabiashara maarufu wa vyungu jijini Dar es salaam alikuwa akifanya biashara na wateja wengi ambao sio wa kutafuta bali ni wale wa oda , yaani ki ufupi ni kwamba biashara yake haikuwa ya kujitangaza kama zilivyo biashara nyingi , alikuwa kama mfanyabiashara ambae ameridhika na wateja aliokuwa nao lakni ukweli ni kwamba sio kama kile kilichokuwa kikionekana , wateja wake alikuwa akiwatafuta kwa namna za upekee sana na mathalani sio yeye ambae anawatafuta , wapo watu wa kazi hio.
Sasa kati ya wateja ambao anafanya nao kazi ni mwanamke mrembo , Frida , ijapokuwa mwanamke huyu hakuwa mrembo sana kuliko wanawake wote aliokuwa akifanya nao biashara lakini Frida ni aina ya wanawake ambao walianza kumvutia kingono kwa mara ya kwanza tu kuonana nae , pengine ni ile tabia ya mwanamke huyo ya kizungu ndio iliomfanya kumvutia kingono , mwanzoni ulikuwa ni mvuto wa kupenda kufanya nae ngono na Alex aliamini kwa namna yoyote ile lazima mwanamke huyo angeingia kwenye kumi na nane zake kama wanawake wengi ambao amepita nao , ‘hakuna mkate mgumu mbele ya chai’ ndio falsafa yake ya siku zote kila anapomtongoza mwanamke , hivyo aliamini falsafa hio hio ingefanya kazi kwa Frida lakini kinyume chake mwanamke huyo mlimbwende wa haja hakuwa na haraka nae , ki ufupi licha ya kwamba alikuwa mwanamke wa kujiachia achia lakini alionekana ni wanawake ambao si rahisi kumvua nguo moja tu ambayo mara nyingi Alex ndio humkuta nayo kila alipokuwa akipeleka mzigo wa chungu.
Mara nyingi mwanamke huyo angemkuta akiwa na nguo za kuogelea tu akipunga upepo na kusitiri manyonyo na kitumbua pekee huku akiacha kila kitu wazi , tabia ambayo ilizidi kumpagawisha mno Alex , ule ugumu wa mwanamke huyo ulimfanya kuanza kutengeneza chembechembe za kihisia na hapo ndipo ambao alipojihisi kupenda.
Kitu pekee ambacho kilianza kumchanganya Alex ni siku kadhaa nyuma mara baada ya Frida kumwambia anahitaji mwanaume aliefahamika kwa jina la Hamza Mzee kumletea mzigo wake kila siku.
Alex alishangaa , ndio alishangaa kwani Hamza alikuwa ni mtu wa kawaida mno kufahamika kwa Frida na hata yeye aliona pengine Frida anamaanisha Hamza mwingine , lakini kwa msisitizo Frida alimwambia ni Hamza huyo huyo anaemfikiria.
Japo swala hili lilimshangaza lakini lilimpa shauku na maswali mengi kichwani, akijiuliza inakuwaje Frida mwanamke mrembo anaemsumbua kumfahamu Hamza na kwanini anataka yeye ndio amletee delivery.
Kama kawaida ya Frida alikuwa ni mtu wa kuongea mara moja na atakachotaka ni vitendo ndio ambavyo alimpa Alex namna ya kupinga maamuzi yake.
Alex alikuwa na maswali , lakini biashara yake ilipaswa kuendelea na tokea amekabidhiwa biashara hio kulikuwa na misingi ya sheria ambayo alitakiwa kuifuata , kwanza hakupaswa kuwa na maswali mengi kwa wateja na anapaswa kuwasikiliza kwa chochote wanachohitaji na ikitokea amevunja kanuni hizo basi ilitosha kuhamishwa kikazi au kuachishwa kabisa.
Hivyo akiwa na wasiwasi wake na shauku aliamua kutii takwa la mteja wake na kumfuata Hamza kwa ajili ya kazi hio , bila shaka alikuwa na matumaini makubwa Hamza hawezi kukataa kazi ya donge nono hilo ,alijiambia ni rahisi kumchimba Hamza zaidi kuliko ilivyo kwa Frida ambae alionekana kama mwanamke msiri.
Dakika chache mara baada ya kupokea simu kutoka kwa Frida juu ya mzigo kufika , huku mwanamke huyo akionyesha furaha yake ya kuletewa na mzigo na Hamza ilimfanya Alex kutaka kumhoji Frida ana kwa ana ndio maana akawekeana miadi nae kwa kisingizo kwamba anahitaji pesa yake cash, wazo zima ilikuwa ni kutaka kujua au Frida alikuwa na hisia za kimapenzi na Hamza ,au Hamza alishawahi kufahamiana na Frida lakini kulingana na Hamza ilionekana ni kama wawili hao hawafahamiani kabisa.
Sasa anapata nafasi ya kumhoji Frida mrembo lakini bado anashindwa kupata majibu anayotaka.
“Kuna kitu kinaendelea kuhusu huyu Frida , nina uhakika sio swala la kimapenzi , Hamza ni nani kwanini mwanamke kama huyu mrembo mwenye pesa anataka kuweka ukaribu na Hamza kupitia delivery ya vyungu”Kichwa cha Alex kilicheza , alijua lazima Frida alikuwa akilenga kujenga ukaribu na Hamza.
Zikiwa ni dakika chache baada ya Frida kutoa gari yake katika mgahawa wa Golden Fork , akiwa anaendesha katika barabara ya Bagamoyo uelekeo wa Jogoo, heads up display(HUD) ya gari yake ilionyesha ujumbe ambao ulikuwa kama vile ni kodi.
“Board to Alamos!!
Ujumbe huo ulisomeka hivyo na Frida bila ya kubadili uelekeo alikanyaga pedeli zaidi akiongeza spidi.
SEHEMU YA 09.
Saa mbili za usiku Hamza alionekana katika pikipiki ambayo ilienda kusimama kando kando ya barabara ndani ya Kijichi.
Hamza mara baada ya kushuka katika bodaboda hio aliangaza kulia na kushoto na kisha alianza kupiga hatua kwa kuvuka barabara upande wa pili akiachana na ile iliokuwa ikinyoosha moja kwa moja kuelekea uelekeo wa Vikunai kwenda Kibada.
Mtaa huo ulikuwa ndio mtaa wa kifahari kwa wilaya ya Temeke ndani ya jiji la Dar es salaam , kulikuwa na utulivu wa hali ya juu na mazingira yake yalikuwa safi na hata Hamza aliyapenda.
Baada ya kutembea umbali mfupi alikuja kukunja kulia kwake na kuingia katika moja ya mgahawa mkubwa uliokuwa ukipatikana ndani ya eneo hilo , uliofahamika kwa jina la Dina Tea House & Restaurant.
Ulikuwa ni mgahawa wa kifahari mno na wa kipekee ambao unapatikana ndani ya jiji la Dar e salaam , upekee wake ulitokana na kwamba ndio mgahawa pekee ambao umejipambanua kwa kuuza vinywaji aina ya chai pekee na chakula cha aina zote ambacho kinaendana na aina ya chai husika.
Kwa mfano chai aina ya Kombucha lazima iendane na chakula chake na aina hii ya huduma iliufanya mgahawa huo kuwa maarufu kati ya watu matajiri..
Ndio ulikuwa ni mgahawa wa kifahari kwani unaambiwa kikombe kimoja cha chai kinaweza kuuzwa si chini ya thamani za shilingi elfu kumi za kitanzania na kuna zaidi ya hapo, kwa mfano chai ya Gisaeng kutoka Korea tu ilikuwa ikiuzwa zaidi ya shilingi laki moja.
Ndani ya maegesho kulikuwa na magari mengi ya kifahari , hakukwa na gari la chini ya milioni therathini ndani ya magahawa huo.
Hamza alishazoea na alijua aina ya wateja ambao huhudumiwa na mgahawa huo lakini siku hio kidogo magari yalikuwa mengi kuliko siku zote ambazo alikuwa amefika ndani ya eneo hilo.
Hamza alijiambia pengine kutofika kwake hapo zaidi ya mwezi mmoja kunamfanya kuona mabadiliko makubwa.
“Bro Hamza leo naona umefika , karibu sana Madam anakusubiria ndani”Aliongea kijana mmoja huku akitoa tabasamu akimkaribisha Hamza.
“Lau nishakuambia mara nyingi haina haja ya kutoka kunipokea kama hivi”Aliongea Hamza akiwa na muonekano ambao haukuwa umebadilika sana.
“Bro unakuja mara chache sana hili eneo , hivyo sidhani kama nitapata usumbufu wa kutoka mara kwa mara na kuja kukupokea kila ninapokuona”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.
“Naona hali ya hewa siku hizi ni ya joto sana ndani ya hili jiji , kazi zimekuwa nyingi kwangu na kunifanya kuwa bize ndio maana sikupata muda wa kufika kuwasalimia”
“Ndio ndio , nakujua wewe ni mtu ambae upo bize sana”.
“Naona baisikeli yangu hamjaitoa bado ipo palepale”Aliongea Hamza huku akishangaa kidogo na kutaka kucheka kwa wakati mmoja baada kati ya usafiri wa hali ya chini uliokuwa ndani ya maegesho hayo ilikuwa baiskeli yake ambayo mara ya mwisho alifika nayo hapo na aliiacha kwasababu iliharibika mara ya mwisho.
“Nimeitoa na kuirudisha , madam alinipa kazi ya kuipeleka kwa fundi na imetengenezwa , si unaona sasa hivi inamuonekao mzuri”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa kidogo kwa kukubali na kisha kuanza kuzipiga hatua kuelekea mlango wa nyuma.
“Bro naomba usitumie mlango wa nyuma , Madam akijua hili ataniletea shida”Aliongea kwa kubembeleza bwana aliefahamika kwa jina la Lawrence au Lau wengi wanavyomuita.
“Hebu kwanza angalia nguo zangu namna zilivyochafuka , sidhani hao mabosi waliopo hapa ndani wataniangalia vizuri nikipita mlango wa mbele, nashusha hadhi ya huu mgahawa pia”
“Braza haina haja ya kuongea hivyo , Madam sio mtu wa namna hio , hawezi kujali na ititoshe unadhani kuna yoyote ndani ya hili eneo mwenye kutosha umuhimu wako kwa Madam?”
Hamza mara baada ya kuona Lau yupo ni mwenye kubembeleza sana aliona asikatae ukarimu huo hivyo aliamua kupita mlango wa mbele na kwa bahati nzuri katika Korido ya mgahawa huo hakukuwa na watu wengi , staili ya mgahawa huo ilijengwa kwa namna ya vyumba kama Kabini tokea mwanzo , ijapokuwa kulikuwa na sehemu ambayo ni kama watu wote waliweza kukaa lakini kwa wale ambao walikuwa wakihitaji kufanya maongezi ya muhimu walikuwa wakitumia vyumba hivyo kukutania , hii ni moja wapo ya faida ya mgahawa huo.,
Hamza alinyoosha mpaka katika moja ya chumba cha mwisho kabisa binafsi ambacho aliekuja kumsalimia ilikuwa ni kama ofisi yake na kisha alishika komeo na kusukuma mlango.
Sekunde ambayo mlango alifungua visu vitatu vilirushwa kuelekea alipo vikilenga eneo la moyo na tumbo kwa spidi ya mwanga.
“Damn!!”
Hamza alijikuta akimaka kwa mshangao lakini wepesi wake ulimfanya kusogea pembeni na visu hivyo vilipita inchi chache sana kutoka kwenye mwili wake .
“Tuk ! , Tuk , tuk!!!”
Vile visu vitatu vilikuwa vimefungwa na vishada(Tassels) vya rangi ya Violet , vilikuwa vyembamba mno na vyenye makali kama viwembe na viligonga katika ukuta na kudondoka chini.
Hamza mwanzoni alidhani huo ndio mwisho lakini dakika ileile ilitokea mianga kama flash aina tatu na kumsogelea kwa kasi kubwa.
Lakini Hamza alionekana kuwa mwepesi na shambulizi hilo lingine na palepale aliinua mkono wake juu na vile visu vyote vitatu vilinasa katiki ya vidole vyake, ilikuwa ni utaalamu wa hali ya juu mno.
“Dina , kuna haja ya haya mambo , kwani lazima uone utumbo wangu ndio uridhike?”Aliongea Hamza huku akitoa kicheko.
“Nilitaka kuona kama uwezo wako umeusahau kama ulivyonisahau na mimi, miezi miwili inapita bila ya kunitembelea”Aliongea mwanamke mrembo .
Alikuwa ni mrembo haswa , akiwa amevalia gauni jeupe lenye maua maua ya rangi nyekundu ambalo limefungwa na mkanda kiunoni na kuufanya mwili wake kugawanyika vizuri kati ya kiuno na juu , alikuwa na sura ya kuchongoka kama yai na lips pana ambazo zimepakwa rangi nyekundu.
Muonekano wake ulikuwa sio wa kawaida kabisa , pengine licha ya kwamba alikuwa akivutia sana lakini ni ngumu sana kwa mwanamke wa kawaida kuwa na mapozi ya aina hio.
“Sio muda mrefu sana tokea nifike , mimi naona ni juzi tu”Aliongea Hamza huku akiokota vile visu vilivyokuwa vimedondoka chini na kuweka mezani.
“Miezi miwili bado tu unasema sio muda mrefu , wanaume wengi wenye pesa zao na maarufu hufika hapa kila siku kwa ajili ya kuniona mimi Dina , kiasi cha kunifanya kushindwa kutoka lakini wewe mkorofi umekosa hata nafasi moja katika mwezi kuja kunitembelea?”
“Distance makes the heart grow fonder , Kama tukionana kila siku haitaleta raha tena , kwangu mimi naona ni vizuri zaidi kukuona mara moja kwa uda mrefu , inannifanya nikuone kama malaika alieshushwa kutokana na urembo wako”Aliongea Hamza.
Kwa namna ambavyo alikuwa akiongea ni kama vile amebadilika mbele ya mwanamke huyo , hakuwa na muonekano wa kipole bali ulikuwa ni muonekano wa kicheshi uliojaa utu uzima.
“Eti malaika alieshushwa , kwaho mimi ni mzuri sana mpaka kuitwa malaika?”
“Nadhani unanijua vizuri mimi ni msema kweli “Aliongea Hamza , lakini ukweli ni kwamba katika moyo wake mwanamke ambae amekutana nae muda wa mchana hakuwa wa kawaida kabisa , mrembo Regina kwake alikuwa mzuri zaidi ya Dina , faida kubwa ya Dina ni mvuto aliokuwa nao kutokana na mapozi yake ya kike na mazoezi.
Upande wa mrembo huyo aliefahamika kwa jina la Dina , ambae hatujui wanafahamiana vipi na Hamza mpaka kuanza kurushiana visu alionyesha tabasamu katika uso wake lililomfanya kuvutia zaidi na yote hayo ni ile raha ya kusifiwa kama mwanamke mzuri.
“Nimekusamehe siku ya leo , nina njaa ya usiku , hebu kaa na wewe ule , vyakula vyote unavyopenda vipo hapa”Aliongea.
Hamza alikuwa na njaa mno na harufu ya chakula hicho tokea anaingia ilimfanya njaa izidi kuuma , alisogea na kisha alivuta kiti na kukaa na mara baada ya kufunua chakula ambacho kilikuwa kimefunikwa alijikuta akivuta pumzi nyingi.
“Unasemaje hiki ni chakula ninachokipenda ilihali siwezi kabisa kukilipia .. ugali wa hizi Abaloni za ki’Australia nadhani nikianza kula nitatokwa na damu puani”Aliongea Hamza na kisha alisogelea bakuli ambao lilikuwa na pilau ndani yake na kisha alijisevia kwenye sahani na akachukua na nyama wa kukaanga pamoja na mchuzi wa samaki na kuweka kwenye sahani yake na kuanza kula chapu chapu , ndani ya dakika chache tu asilimia sabini ya pilau yote ilikuwa imeisha.
“Dina dada yangu mbona umeacha kula?”Aliuliza Hamza mara baada ya kuona Dina hakuwa akifanya chochote zaidi ya kumwangalia tu .
“Nishamaliza kula tayari , pili nnimeanza diet hivi karibuni,nakula kidogo sana”
“Kuna haja gani ya kufanya diet ilihali mwili wako huo huo unakupendeza?”
“Wewe ni mwanaume na huwezi kuelewa , ‘diet’ ni ‘life carear’ ya mwanamke , sitaki kuongeza uzito mimi .. kwanza hebu niambie, unapendelea mwanamke wa aina gani , mwembamba mwenye nyama au mnene?”
“Napenda wale wanawake ambao ni wembamba na wana kalio lainiii ukiliminya”Aiongea Hamza huku akitabasamu kifedhuli , alikuwa mtu mwingine kabisa kwa kile alichokuwa akikifanya.
“Wewe muhuni , yaani huna hata aibu nitakukata mimi?”Aliongea Dina na palepale kutaka kumrushia tena Hamza vile visu.
“Dina inatosha bwana , haina haja ya kutaka kunitumia kama kifaa cha majaribio ya mbinu zako za kininja””Aliongea na kumfanya Dina kutulia.
“Hamza hebu niambie kwanza ukweli , unadhani nitachukua miaka mingapi ya mazoezi mpaka kufanikiwa kukupiga na mashambulizi yangu?”
“Miaka..!, hehe , labda arobaini au hamsini hivi”
“Kwanini usiseme tu maisha yangu yote”Aliongea huku akiwa siriasi.
“Haha.,. haina haja ya kuwa siriasi hivyo , ukiachana na mbinu za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi, siku zote mtu anapaswa kuangalia kipaji chake kwanza kabla ya bidii, ule msemo wa kusema Bidii hushinda kipaji ni uongo, ni msemo ambao watu hutumia kujifariji tu”Aliongea Hamza.
“Halafu Dina hii supu ya kuku ina radha flani hivi, ni kama kuna chembe chembe za vinyama nyama ,umeweka Sea Cucumber nini?”
“Oh! , kumbe umeona, kuhusu hilo ni nyama ya kusaga ya mkia wa Kangaruu , nimenunua bei sana na ni kwa ajili yako kukupa virutubisho”Aliongea Dina huku akiwa na tabasamu flani la kichokozi.
“Mkia wa Kangaruu!!!”
“Unaonaje? , imekuwaje kwanza ukagundua utofauti wa harufu maana unasagwa na kuwa kama vumbi la nyama na kisha huweka kama viungo kwenye supu na harufu yake hupotea kabisa, inafanyika hivyo ili iwe rahisi kufanya kazi mwilini”Aliongea.
Mkia wa Kangaruu ni sawa na mtu anapotumia Viagra au Mkongo , mara nyingi hutumiwa sana na matajiri tena kwa siri kuwekwa kwenye vinywaji kama Mvinyo na baadhi ya dawa za kuongeza hamu ya tendo.
“Dah , sasa kwanini ukanifanya ninywe supu yenye huu mchanganyiko ,unataka nitokwe na damu puani?”Aliongea Hamza mara baada ya kuhisi presha ya damu kuongezeka kwa kasi.
Unaambiwa vumbi la vinyama vya mkia wa Kangaruu kidogo tu inaweza kumfanya mwanaume kupatwa na uchizi na ni ngumu sana kuepuka mtego wa mwanamke ukiwa katika athari ya dawa hio.,
“Unadhani kwanini nimefanya hivi?” Aliongea Dina na alisimama kutoka alipokuwa amekaa na kumsogelea Hamza na kisha alimwinamia shingoni na kufanya marashi yake yaliochanganyika na pumzi kumsisimua Hamza shingoni.
Kutokana na Athari ya dawa hio , mwanamke ambae alikuwa mbele yake urembo wake ni kama umeongezeka mara kumi , lakini kwa uwezo wake wote alijizuia kutoruhusu akili kumpotea na kumgusa kwa namna yoyote ile.
Alikuwa akijua kabisa kufanya mapenzi na Dina kila kitu kisingekuwa sawa tena , tokea arudi nchini Tanzania na kuanza chuo huku akiishi maisha ya kawaida ni kama ilimfanya kupata amani ambayo alikuwa akiiota hivyo hakutaka hali hio kubadilika.
Dakika ileile muonekano wa Hamza ulianza kubadilika na chumba kilizidi kuwa cha baridi huku msisimko ndani ya eneo hilo ukiwa ni ule wa kuogofya,Hamza alikuwa ni mtu mwingine kabisa na hakuwa na ishara yoyote ya utani katika macho yake.
“Dina usiendelee..!”Aliongea Hamza kwa sauti iliokuwa na mikwaruzo lakini kwa namna flani ya kuhamasisha.
Mabadiliko ya Hamza yalimfanya mwanamke huyo kushikwa na hali ya uchungu mno kwenye macho yake na ishara za hasira lakini dakika hio hio alibadilisha muonekano wake na tabasamu bandia na kujiondoa kwake.
“Hebu muone sasa uoga ulivyokushika , unadhani mimi Dina nataka kukumeza mpaka kunibadilikia hivyo , haya sitaki tena hata kuchokozana na wewe mimi”Aliongea akijitahidi kurudisha hali ya utani ili kuonoa hali hio isiokuwa ya kawaida katika uso wa Hamza.
“Tena umekuja wakati muafaka , nimepokea mzigo wangu wa majani ya chai kutoka nje ambayo nahitaji ujuzi wako kuyachunguza, nione kama sijapigwa maana ni hela nyingi nimetumia”Aliongea.
Dakika hio Hamza hatimae alikuwa amerudi katika ule muonekano wake wa kizembe na kuangalia chai ambayo ilikuwa ikimiminwa kutoka kwenye jagi.
“Hakuna shaka , ni wakati wa kufurahia chai ya kimatawi ya mrembo Dina kwamara nyingine”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu , spidi yao ya kubadilika haikuwa ya kawaida kabisa , pengine watu wa kawaida kwa kile kilichotokea dakika chache zilizopita wasingerudi katika hali hio.
Dina kama bosi wa mgahawa huo ambao umaarufu wake ni kutokana na kuhudumia aina mbalimbali ya ‘premium tea’ alikuwa makini sana kwa kila mzigo ambao anaagiza.
Dina upande wake alionekana kuwa siriasi na hakutaka kuendelea kuongea matani na alianza kuonyesha umahili wake katika kufanya mchanganyiko wa viungo vya chai , pamoja na kuweka majani flani katika kikombe na kuyaloanisha na maji ya moto. Na baada ya hapo ndipo alipompatia kikombe Hamza ajaribu.
“Hii ni chai ya mmea wa jamii ya Camellia Sinensis , ambayo hutengeneza chai maarufu ya Hui , majani haya yamefika jana kutoka China, hebu jaribu kuonja na uniambie ni gredi ya ngapi?”Aliongea Dina kwa kirefu wakati wa kumpatia kikombe Hamza.
Hamza kabla ya kunywa kwanza aliangalia majani hayo , yalikuwa majaini kama majani ambayo hayajasagwa na ilishangaza kwa namna ambavyo yalionekana mabichi licha ya kusafirishwa umbali mrefu.
“Hili jani limenyooka na ni zito , ukiangalia veini zake kidogo ni nyeusi kuliko jani , hii ni jamii moja ya majani ya Camellia kama ulivyosema , mmea wa chai ya kijani , unaofahamika kwa jina maarufu la kichina, Taipeng”
“Sio mbaya hebu jaribu radha yake kwanza”Aliongea na Hamza alionja pamoja na kunusa harufu ya chai ile.
“Mh! , hii ni chai nzuri sana , radha yake unaipata baada ya kumeza , sio chungu hata kidogo”
“Hio ndio maana yake , la sivyo isingenigharimu zaidi ya kiasi cha shilingi laki moja kwa kilo tu , ninachouliza ni gredi ya ngapi?”Aliongea na kumfanya Hamza kunywa tena na alionekana ni kama alikuwa akiichezesha kwenye ulimi na kisha akameza.
“Harufu na ‘Aftertaste’ inatosha kusema imeingia gredi namba tatu , lakini kuhusu utamu usioisha haraka naweza kusema hii ni Grade A”Aliongea Hamza.
“Kwa maneno yako , ni sahihi kusema kwamba Lawrence bado hana uelewa wa kutosha kuhusu sayansi ya chai, licha ya kusoma food science”Aliongea.
“Uzoefu unahitajika sana likija swala la chai za tamaduni mbalimbali , ni rahisi kufanya makosa kwa mtu ambae hajatembea sana na kuonja kila aina ya chai”Aliongea Hamza.
“Unaonaje ukifanya kazi hapa , utapata faida ya sehemu ya kuishi na chakula, lakini pia malipo mazuri, kuliko kule uswahilii unakoiishi”Aliongea.
“Ah! Hapana, napenda aina ya maisha yangu bwana , yananitosheleza”Aliongea Hamza huku akijiambia wakati huo hakuhitaji kazi nyingine kabisa ya uboifried wa maigizo inamtosha.
“Unaongea kama vile nitakuingilia kwenye mambo yako, nataka kukuona mara kwa mara ndio nia yangu”
Mara baada ya mwanamke huyo kuongea kwa sauti hio ya kubembeleza ilimfanya Hamza moyo wake kulainika na kwa mvuto wa huyo mwanamke alijiambia anapaswa kuondoka la sivyo anaweza kushindwa kuvumilia.
“Dina muda umeenda , ngoja niondoke”
“Mbona haraka , hivyo kwanini usikae kidogo tukipiga stori , inachosha sana kukaa mwenyewe”
“Hahaha… kaa na Lawrence mpige stori , kwaheri , haina haja ya kunisindikiza”Aliongea Hamza na kisha alitoka.
“Mjinga sana wewe, mpuuzi sana wewe Hamza, unanuka, umeniona sivutii ndio maana unanikwepa kila siku?”Mrembo huyo alilaani huku macho yake yakitawaliwa na upweke.
Upande wa Hamza mara baada ya kutoka nje ya mgahawa huo alijikuta akipatwa na ahueni kwa kupumua kwa nguvu , maana alikuwa akijitahidi kujizuia mno na alikosa amani kwa kuona kwamba ataishia kufanya kitu ambacho hakikuwa kwenye mpango wake , ukweli ni kwamba ijapokuwa alikuwa akimkwepa huyo mwanamke lakini alifika hapo kutokana na kwamba alikuwa amemmisi.
“Bro vipi unaondoka na baiskeli yako?”Aliuliza Lau.
“Nitaiacha usiku mkubwa huu nitaondoka na pikipiki, ihifadhi vizuri”
“Sawa broo”
“Halafu hivi unamjua mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Amosi , mzee flani hivi ambae ni kama mkopeshaji?”
“Unamzungumia Jasusi mstaafu , ni maarufu sana katika maeneo haya mpaka Kigamboni yote , yupo chini ya tajiri Hamdu mfadhili mkuu wa mgombea wa uraisi kupitia chama tawala.. anajitapa sana kwa kuamini jeshi lote la polisi lipo mikonoi mwake , anaweza kufungwa leo kwa uhalifu na kesho asubuhi ashatoka … vipi amekuletea tatizo lolote?, kwanini unamuulizia?, kama unataka nikamshikishe adabu niambie , nitahakikisha asubuhi anaitwsa hayati”
“Ah! , sijamaanisha hivyo , huyo bwana kuna mwanamke anamdai na anatumia deni kumtaka kingono , nataka angalau apatiwe vitisho ila usiende mbali”Aiongea Hamza.
“Nimekuelewa braza”Aliongea na kisha Hamza alimshika Lau Bega na kisha alizichapa raba kuelekea barabarani kutafuta bajaji au boda kwenda nyumbani , alitaka akakae chini kwanza asome karatasi ambayo alipewa na mrembo Regina kwa ajili ya kujiandaa na ajira yake kuanzia siku inayofuata.
“Madam !!”Aliita Lau mara baada ya kumuona bosi wake amesimama mlangoni akimwangalia Hamza akitokomea.
“Alikuwa akikuambia nini?”
“Inaonekana Braza Hamza amekosana na Amosi , Jasusi mstaafu , vipi tumuue?”Aliuliza Lau huku akiwa na muonekano tofauti na ambao alikuwa nao wakati wa kuongea na Hamza, alikuwa siriasi mno kama vile ni ninja.
“Haina haja tutaamsha matatizo mengine tu , hakikisha mnampa vitisho na onyo , pia fuatilia umfahamu mwanamke ambae Hamza anajaribu kumlinda , nataka kuona picha yake”
“Sawa Madam , halafu Zedi , Mbunge wa Ukonga amepiga simu ,anaulizia kama upo free kesho kwa ajili ya chakula cha usiku?”
“Mwambie siko free”Aliongea Dina kikauzu na Lau alitingisha kichwa na kutoka.