Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI : SINGANOJR


SEHEMU YA 75.
Katika ndoto ambayo aliota jana yake aliweza kuona mwezi wa ule ulimwengu wa ndotoni ulikuwa mwekundu ,sasa mara baada ya kupewa mchoro uliokuwa kama picha na kuona mwezi huo ni mwekundu pia,ilimfanya kushangaa.
“Kwa jinsi ulivyoshangaa nadhani tayari unajua maana yake?”Aliuliza Frida akiwa na shauku.
“Sijui maana yake lakini jana kwenye ndoto niliona mwezi mwekundu , unaweza kuniambia nini maana ya huu mwezi na kwaninni umenionyesha hii picha?”Aliuliza Hamza , mbele ya Frida aliamua kuwa mpole ili kupata kile anachokitaka.
“Inamaanisha mazingira unayoota ni sahihi”Aliongea na kumfanya Hamza kukunja ndita .
“Wewe umejuaje?”
“Nilipewa na dokta Genesha na alinimbia nikijisikia ni muda sahihi wa kukuonyesha hii picha nikupatie , mwanzoni sikumwelewa alikuwa akimaanisha nini , lakini ulivyo uliza swali nilijua nini maana ya picha hii?”Aliongea .
Ukweli ni kwamba licha ya Hamza kujihusisha na Frida hakuwa akimwamini kabisa haikuwa hivyo tu hata kwa Frida alimuona Hamza kama mtu ambae hakuwa akimwanini.
Lakini licha ya hivyo alipaswa kumfanya Hamza kumwamini kwa namna yoyote ile ili tu aweze kumshawishi kutumia mshumaa wakati wa ndoto la sivyo maisha yake yatakuwa hataini.
Hamza alionekana kufikiria kwa dakika kadhaa huku akikodolea macho ile picha , hakuwa na shaka kabisa juu ya picha hio kwani ilionyesha kitu ambacho ameota yeye, alichokuwa akiwaza je haya yote yanayomtokea ndio njia sahihi ya kumpata Mzee kama alivyosema Dokta Genesha.
“Hamza kwa ajili ya hicho unachokiwaza mshumaa ni ufunguo wako , kumbuka maneno yangu niliokuambia juu ya uwepo wa Chumba cha nuru na ni wewe pekee ambae unaweza fikia hiki chumba kwa maelekezo ya Dokta, kadri ambavyo utachelewa kufanya maamuzi ndio unazidi kujiweka katika hatari pamoja na watu wanaokuzunguka”,
“Una amini nikitumia mshumaa nitakuwa salama , sidhani inaweza kuwa hivyo , kwanzia sasa kila ninachofanya juu ya hivi vitu ndio nazidi kujiweka katika hatari”
“Watu wanaokuwinda kwasasa wanachotaka ni kitu ulichokuwa nacho , hata kama wachukue waondoke nacho hakina maana kwao, wewe pia umekishikilia kwasababu bado hujajua maana yake halisi ni nini na kinaelekeza nini , ikitokea umejua kinachoelekeza utakuwa ni wewe tu dunia nzima unaejua hilo na inabakia kuwa siri yako , hata kama ukiwapatia kujiondolea hatari kwako na kwa wapendwa wako, watakuwa wamekushikia tu lakini maana unaijua wewe tu”
“Na siri hio ikitoka inamaanisha nitazidi kuwa hatari zaidi ya mara mbili ya kuwa na kitabu?”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu lililojaa uchungu.
“Ni mpaka wakifahamu juu ya hilo lakini kwa wakati huo utakuwa umejua namna ya kujilinda na kuilinda familia yako, sidhani upo tayari kuruhusu mwanamke kama Regina kuingia katika hatari kwa ajili yako”Aliongea.
“Unajua nina mahusiano na Regina, unaonekana kunifuatilia sana”
“Wewe ni misheni yangu kutoka kwa Dokta Genesha , nipo kwa ajili ya kukuelekeza, ukifeli kwa upande wako na mimi pia nafeli kile nilichomuahidi Dokta , lazima nijue watu ambao unajihusisha nao”
“Sishangai wewe kusema hivyo ndio maana hata mimi kuleta vyungu hapa ulikuwa ni mpango wako na haikuwa bahati mbaya kwa Alex kunipa kibarua”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba akikumbuka namna ambavyo amekutana na Frida ilionekana kabisa ulikuwa ni mpango wa Frida kukutana nae.
“Siwezi kukataa na tena kuhusu Alex unapaswa kuwa nae makini?”
“Nina sababu ya kufanya hivyo?”Aliuliza Hamza .
“Alex ni shushu kutoka watu wa kisiwa cha Binamu , maisha unayomuona nayo Alex ni uwezeshwaji na mbinu ya kulinda kile ambacho anafanya”
“Unamaanisha kusambaza vyungu?”
“Hupaswi kusema ni kusambaza vyungu bali ni kusambaza teknolojia mpya ya dawa inayosisimua ubongo , nadhani unakumbuka nilikuambia natumia vile vyungu kwa ajili ya utafiti wangu?”
“Ndio nakumbuka , kwahio unamaanisha umekwisha kupata majibu?”
“Ndio majibu nimekwisha kuyapata”Aliongea na jambo lile lilimfanya Hamza mwili wake kumsisimka kwa furaha maana ndio kitu ambacho alitaka kujua tokea mwanzo.
“Mpaka sasa sijajua namna dawa hii inavyotengenezwa , lakini ni maarufu kwa jina la Stimula”
“Stimula!!” Hamza alionekana kuhangaa kidogo.
“Ushawahi kusikia?”Aliuliza na Hamza alitingishwa kichwa kukubali.
“Zipo njia nyingi za usafirishaji wa hii Stimula na haina kibali chochote duniani ni kama madawa ya Kulevya , Njia ya utumiaji wa chungu ndio maarufu kwa hapa Tanzania na maeneo mengi ya Afrika”
“Wanasafirisha vipi?”
“Ni rahisi sana , unatumia jiko la umeme na kukifanya chungu kipate moto na dawa itaungua na kudhalisha harufu mfano wa marashi , hii harufu ukiivuta inakulewesha na baada ya hapo huelewi kinachoendelea maana utakuwa ni kama mgonjwa wa akili na dalili ya kwanza utakayokuwa nayo ni uwendawazimu kama vile umetawaliwa na roho nyingine , mtu anakuwa ni kama sio yeye kwani ataanza kuonge vitu ambavyo sio vya kawaida”Aliongea Hamza na kauli hio ilimfanya kukumbuka swala la rafiki yake Amiri juu ya harufu ya marashi nyumbani kwa Mellisa huku akiongea vitu vya ajabu.
“Kwanini haya yote , kuna faida yoyote mtumaji anayopata?”
“Kwasasa hakuna jibu sahihi kama kuna faida yoyote , haijulikani ni kwa ajili ya starehe au kuna zaidi ya sababu, pengine kuna mpango unaoendelezwa ambao si ufahamu , ni ngumu kukupa majibu kwasasa”Aliongea lakini upande wa Hamza bado hakutaka kukubali kirahisi , alijua lazima kuna kitu kinaendelea juu ya hicho kitu kinachoitwa Stimula.
Alitamani kutoendelea kuchimba zaidi lakini alimkumbuka Amiri rafiki yake na alimuahidi atamsaidia , lakini kabla ya hivyo alipaswa kujua kama Mellisa alikuwa moja ya wateja wa Alex wanaonunua hivyo vyungu.
Jambo la kwanza alipaswa kujua mtu aliempa kazi ya kufuatilia lugha aliokuwa akiongea amefikia wapi, na pili ndio afanye maamuzi aidha ya kumwambia Amiri ili ajue cha kufanya ama alifuatlie yeye mwenyewe .
Maana alijua kama swala hilo Mellisa analifanya kwa siri basi ni dhahiri kuna sababu kwanini Amiri hajui.
Hamza hakuwa na haja ya kuendelea kubakia nyumbani kwa Frida , ukweli ni kwamba swala la kutumia mshumaa ama kutokutumia ilikuwa ni maamuzi yake.
Upande wa Frida alimwangalia Hamza mpaka anatokomea na zilipita kama dakika kumi tu ya Hamza kuondoka aliingia mwanaume alievalia suti ndani ya jumba hilo , alikuwa mzungu..
Frida alionekana kumjua yule mtu na hata hakumsalimia , ilikuwa ni kama vile mtu huyo anaishi ndani ya nyumba hio.
“Unaamini atautumia mshumaa kwa kumweleza alichotaka kusikia?”Aliuliza yule mtu na kisha alisogelea makaratasi yaliochanguka mezani na kuchomoa karatasi la plastiki ambalo lilikuwa chini kabisa mwa yale makaratasi na kulinyanyua juu kuliangalia huku akitoa tabasamu na palepale alilikunja na kuliweka kwenye mfuko wa koti la suti.
“Umesikia mazungumzo yetu yote, hii inatosha kuniamini juu ya kusimamia vyema utafiti wangu”Aliongea Frida akiwa siriasi.
“Hatuwezi kwenda huko haraka hivyo Frida , upo hapa sio kwasababu Sinagogu wanakuamini bali tunamwamini Dokta Genesha, ulifanya kosa kubwa kumfanya Kuhani kukutilia shaka na sasa umejitengenezea udhaifu”Alionga yule bwana huku akizunguka zunguka kana kwamba kuna kitu anatafuta kwenye hio nyumba.
“Unamaanisha nini kujitengenezea udhaifu?”
“KF ni mtu hatari sana na kadri unavyokutana nae unazidi kumdanganya, ulikuwa na ushawishi mkubwa katika maneno yako ili kumfanya akuamini ili hali kila kitu ni kinyume chake , unadhani akijua unamdaganya itakuwaje?”Aliongea na kauli ile ilimfanya Frida kujawa na ukauzu.
“Kama unalijua hilo haikuwa na haja ya kuniuliza kama ameniamini, unaongea kwa kujaribu kuniogopesha lakini unapaswa kujua kitu kimoja, hii ni kazi ambayo nilifanya maamuzi mimi mwenyewe kuifanya , hivyo vitisho vyako hapa haviwezi kufanya kazi, najua malengo ya kazi yangu”Aliongea na kumfanya yule bwana kuonyesha ishara ya kutabasamu.
“Frida kazi yangu ni kukuangalia na kukisimamia na kuhakikisha kila unachofanya ni kama ulivyomuahidi Kuhani , unapaswa kujua Kanisa halijawahi kukuamini bali tunaamini kile unachofanyia utafiti ndani ya taasisi zetu, wewe ni Wicca na kama ulivyo kwenye taasisi yetu kwa ajili ya kutumiza malengo ya ushirika wako na sisi tupo hapa kukutumia ili kutimiza malengo ya ushirika wetu, hivyo haijalishi nilichoongea unachukulia kama tishio au onyo hio ni juu yako, tutatonana tena baada ya kuona mafanikio, Frida kumbuka naona kila unachofanya”Aliongea na kisha palepale aligeuka na kutoka ndani ya nyumba ile huku akiangaliwa na macho makali ya Frida.
Bwana huyo alikuwa ni yule yule ambae alikutana na Frida juu kabisa ya jengo la Haliz Foundation na ilionekana chochote kila ambacho Frida anafanya anasimamiwa na huyo mtu na pia ilionekana mazungumzo baina ya Hamza na Frida yalifuatiliwa kupitia teknolojia ya karatasi.
*******
Lisaa limoja na nusu mbele Hamza alikuwa akitoka kituo cha Treni ya Mwendokasi ndani ya mkoa wa Morogoro na kuungana na abiri wengi ambao walikuwa wakitoka eneo hilo.
Kutokana na jua kali Hamza hakutaka kupanda pikipiki bali aliingia kwenye taksi ambazo zilipatikana ndani ya eneo hilo.
“Nipeleke Tumaini mkuu?”Aliongea Hamza.
“Tumaini ipi mkuu?”Aliuliza yule bwana na kumfanya Hamza aone hakutoa maelezo ya kutosha.
“Tumaini kituoni kwa watoto Yatima kule”Aliongea Hamza.
“Nimekusoma bosi wangu”Aliongea mwendesha taksi kwa furaha na kisha aliondoa gari kuelekea uelekeo ambao ameelezwa.
Tumaini ni moja ya vituo maarufu kongwe ambavyo hulelea watoto Yatima na wale wenye ulemavu wa ngozi.
Kutoka stendi mpaka kituoni ilikuwa ni umbali wa nusu saa kutembea na gari, eneo lote lilikuwa likimilikiwa na taasisi moja ya kimisaada kutoka Denmark lakini baadae waliacha ufadhili na kwa muda mrefu kituo hicho kipo chini ya taasisi ya FOOT(Friends of orphans Tanzania).
Hamza mara baada ya kushushwa na taksi nje geti la kuingia kituoni hapo alilipa na kisha alisogelea chumba cha mlinzi na ilionekana alikuwa akifahamika kwani hakuandika hata jina lake kwenye kitabu zaidi ya kuruhusiwa kuingia.
Ndani ya kituo hicho kulikuwa na eneo kubwa mno , ijapokuwa majengo yake hayakuwa ya kisasa sana kutokana na kujengwa zamani sana lakini mazingira yalikuwa safi na yenye utulivu wa hali ya juu.
Ilikuwa Jumamosi hivyo watoto wote wanaoishi hapo walikuwa katika shunguli za usafi.
“Mr Hamza!!”Sauti iliita kutokea upande wa kulia wa bustani na kumfanya Hamza kugeuka .
“Madam Dorisi! Habari za siku?”Alisalimia Hamza.
Mwanamke ambae alifahamika kwa jina la Dorisi alikuwa mfupi na mnene na alionyesha tabasamu kumuona Hamza.
“Ni nzuri kabisa, sijategemea kukuona leo huku?”Aliongea huku akimwangalia Hamza kwa kumchunguza mavazi yake ni kama alikuwa akishangazwa na mabadiliko ya Hamza.
“Ulitegemea kuniona lini Madam?”Aliongea Hamza na yule mwalimu ni kama alijua ameongea kitu cha kijinga na kumfanya aanze kujibaraguza.
“Nilitegemea kukuona siku yoyote kwanzia kesho ila sio leo?”
“Hayo ni maratajio au sio!?”
“Kabisa , karibu sana , kama unavyoona nawasimamia watoto kufanya usafi wao wa kimwili”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kumwelewa.
Kila mtoto alionekana kuwa bize , wengine wakifua wengine walikuwa wakiogesha watoto wadogo.
“Nipo hapa kwa ajili ya kuonana na Mkuu wa kituo nadhani sijamkosa maana nimekuja bila miadi?”
“Yupo kuna wageni wengine anawasubiria leo”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu na kisha kumuaga Madam Dorisi kuendelea na mambo yake.
Hamza alitembea kwa mwendo usio wa haraka sana na usiokuwa wa kivivu sana akielekea jengo ambalo ofisi za walezi , mkuu wa kituo na walimu zinapatikana.
Jengo la ofisi hizo lilikuwa limechakaa kidogo kutokana na stali yake ya kizamani , kwa nje usingejua kama ni jengo la Ghorofa mpaka uingie ndani.
Hamza wakati akiingia eneo la ukumbi chini kabisa ya jengo hilo aliweza kuonekana mwanaume mzee hivi kama miaka sitini kwenda therathini, hakuwa peke yake bali kulikuwa na mwanaume kijana ambae ameshika daftari kubwa na ilionekana kuna kitu ambacho walikuwa wakishaurina kwa namna walivyokuwa siraisi.
“Hamza leo naona umetukumbuka?”Aliongea yule mzee huku akionyesha hali ya kutabasamu.
“Sijawahi kukusahau mzee wangu, halafu naona hali ya hewa Morogoro kidogo ni ya ubaridi na upepo mwingi , kwa mavazi hayo huogopi kuumwa?”
“Ni kweli hali imebadilika , japo naonekana kuwa na mvi tayari lakini sijazeeka , Karibu sana”Aliongea na Hamza alionyeshwa sehemu ya kukaa huku akisalimiana na yule bwana ambae alionekana kuwa na kaunta book, kwa haraka haraka Hamza alimfahamu alikuwa ni Mgavi wa hiko kituo.
“Dean nitaenda kumalizia ili kubalansi mahesabu , ikishindikana kabisa kwa watu tunaowatarajia nifanye mawasiliano na Wizara”Aliongea yule mwanaume.
“Fanya unachoona kinafaa kwa utashi wako , hakikisha unagawa pasipo ya kubadili utaratibu licha ya kupelea kibajeti”Aliongea na yule bwana alitingisha kichwa.
Kwa namna ambavyo walikuwa wakiongea Hamza alijua tu , kituo kitakuwa kinapitia wakati mgumu kwenye maswala ya bajeti na alijiambia alifanya vizuri kuja siku hio.
“Nimesikia kutoka kwa Madam Dorisi unasubiria wageni ndio maana hujatoka leo?”Aliongea Hamza.
“Amekuambia wageni!, mimi nimemwambia kuna mtu namsubiri na sio wageni , Dorisi bwana”Aliongea huku akitabasamu na kumfanya Hamza kucheka.
“Tena una bahati kuja leo, ninaemsubiria itakuwa unamjua kama kumbukumbu za utoto wako zinafanya kazi vizuri, pengine anaweza kuwa msaada kwenye swala lako”Aliongea na kauli yake ilimfanya Hamza macho kuchanua.
“Ni moja ya watoto waliolelewa hapa!?”
“Kama una kumbukumbu nzuri, unakumbuka wakati unarejewa na fahamu kuna msichana mdogo aliekuwa pembeni yako akilia!!?”Aliuliza Dean huku alimwangalia Hamza machoni kwa matarajio.
Haikuwa ngumu kwa Hamza kuvuta kumbukumbu za kituoni hapo wakati akiwa mdogo, ukweli ni kwamba sehemu hio miaka zaidi ya ishirini iliopira ndio sehemu ambayo kwa mara ya kwanza alisikia jina la Mzee na hio ni mara baada ya kurejewa na fahamu akiwepo hapo huku akiwa hana kumbukumbu ya kilichomtokea nyuma , alijua tu alipata ajali ambayo ilimfanya kupoteza fahamu kwa kipindi cha miezi minne.
“Nadhani kweli nakumbuka , kulikuwa na mtoto kibonge aliekuwa na mashavu makubwa”Aliongea Hamza na kumfanya Dean kucheka.
“Ndio huyo,nilidhani umemsahau kabisa, ila naona umemkumbuka”Aliongea na kumfanya Hamza hamu ya kutaka kumuona huyo mtu kuongezeka.
“Mzee kwa jinsi unavyoonekana nadhani amefanya vizuri sana wakati akiwa hapa?”Aliongea Hamza na Mzee yule alitingisha kichwa kukataa.
“Hapa hakukaa kabisa na hapakuwa kwao , wakati unaondoka na yeye alichukuliwa na baba yake, amefanya vizuri sana akiwa kwa wazazi wake mpaka kupata elimu ya juu kabisa na sasa ni mwajiriwa wa kampuni kubwa hapa nchini, licha ya hivyo mpaka leo hajawahi kutusahau, amekuwa moja ya wafadhili tegemezi hapa”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kukubaliana nae.
Na wakati huo wakiongea Madam Dorisi alijiiunga nao na stori ziliendelea .
Zilipita dakika chache tu mgeni ambae alikuwa akisubiriwa aliweza kufika , Hamza alikuwa na hamu kubwa ya kumuona kweli maana hata Madam Dorisi alionekana kumsifia kama ni mrembo sana huku akimtania akimwambia aangalie asije kupagawa.
Shida ilianza pale Hamza alipo ona gari ambayo iliingia ndani ya eneo hilo,gari hio ni kama alikuwa akiitambua vizuri, kabla hata hajashuka mgeni alimtambua vizuri alikuwa ni Prisila.
Hamza hakuwa hakuamini na alihitaji uthibitisho kutoka kwa Mzee Hizza na alitingisha kichwa kwamba ni yeye huku akiwa na tabasamu. Mzee huyo mara baada ya kuona wawili wakionyesha ishara kama wanafahamina baada ya kuangaliaana kuna kitu aligundua.
Prisila alikuwa amependeza licha ya kwamba alikuwa amevalia kistaarabu sana , hakuvaa mavazi ya kumfanya aonekane wa matawi ya juu sana wala wa hali ya chini sana , alikuwa katikati.
Baada ya kumuona Hamza ndani ya hilo eneo hata yeye alishangaa maana ni kama hakuwa ametarajia kumuona.
Prisila alikumbatiana kwanza na Dorisi huku akimpatia Mzee Hizza mkono na kisha ndio alimsogelea Hamza.
“Ningejua unakuja huku nisingepanda treni , ungenipa lift tu”Aliongea Hamza huku akijifikiria kwanini kila anapomaliza kikao chake na Frida mtu anaekutana nae baada ya hapo ni Prisila , ilikuwa ni kama mara ya pili hio inatokea.
“Kumbe mnafahamiana?”Aliuliza Dorisi aliekuwa na tabasamu na mshangao.
“Nafahamina nae huyu ni mfanyakazi wetu , nimeshangaa kumkuta huku”Aliongea Prisila huku akiongea kwa macho yaliojaa wasiwasi na jambo lile hata Hamza aliliona.
“Hapa ni nyumbani, amekuja kusalimia”Aliongea Mzee Hizza na kumfanya Prisila kushangaa kidogo.
“Njooni tukae kwanza ili tujue mmekutana lini tena kwa mara ya pili mkiwa wakubwa”Aliongea akicheka na kauli ile ilimfanya Prisila kushangaa zaidi na kujawa na maswali mengi.
“Dada Dorisi ongea na Agustino, kuna oda nimeweka Msamvu dukani kwa Mzee Salum , sikutaka kununua vitu bila ya kujua kipi kimepelea”Aliongea na Dorisi aliitikia na kuondoka na kubakia Hamza na Prisila.
“Prisila yule bwana niliekuambia ni huyu na yeye anaonekana kukumbuka, Hamza huyu ndio Prisila uliesema ana mashavu makubwa akiwa mtoto”
“Dean mimi sikuwa na mashavu”Aliongea Prisila huku akionyesha kushangaa japo alikuwa na furaha lakini pia alikuwa na wasiwasi.
“Hamza kasema kitu kilichomkumbusha ni mashavu yako , ni maneno yake sio yangu”Aliongea huku akicheka.
“Mzee Hizza nadhani imepangwa tukutane tukiwa ukubwani , mimi na Prisila tunafanya kazi kampuni moja ila kumbe tulijuana tukiwa watoto?”Aliongea Hamza.
“Kila jambo lina sababu yake , kama ambavyo sikutegemea ungerudi kwenye kituo chetu kunisalimia ni kama hivi wewe na Prisila”Aliongea na kumfanya Hamza kukumbuka siku ambayo alifika Tanzania na kukutana na Mzee Hizza kama mtu wa kwanza kumjua.
Mzee Hizza alikuwa ni kama mmiliki wa hicho kituo na karibia ujana wake wote ameumalizia kukiendesha , hata kipindi ambacho wafadhili waliondoka ni yeye aliepambana kuendelea kukisimamia mpaka kuja kupata wafadhili wengine.
Kwa muda huo mzee huyo hakujua chochote juu ya Hamza kuandishika ndoa na maswala mengine, hivyo alijua pengine kukutana kwa Prisila na Hamza kutafungua milango mingine.
Stori ziliendelea ndani ya eneo hilo na kutokana na uchangamfu wa Mzee Hizza hata Prisila ambae alikuwa na wasiwasi alichangamka.
Baada ya maongezi machache Prisila yeye alienda kusalimiana na watoto na Hamza na mkuu wa kituo walibakia kuongea.
Moja ya vitu muhimu ambavyo Hamza alimuuliza ni kama kuna kitu chochote amekumbuka juu ya aliemleta kituoni hapo wakati akiwa mtoto, lakini kauli ya Mzee Hizza haikubadilika.
Kauili yake ilikuwa ni ileile ya siku zote kwamba Hamza aliachwa kituoni na mtu aliejitambulisha kwa jina la Mzee huku akitoa maelezo Hamza angekuja kuchukuliwa na mzazi wake.
Hamza alikuwa akijua kauli hio ilikuwa ikimaanisha nini, lakini alitamani kumjua mtu ambae alimuacha hapo kituoni , kuna kila hisia mtu huyo alikuwa ni Mzee anaemjua maisha yake yote lakini hakuwa na uhakika kwasababu Mzee Hizza hakumuona vizuri na mtu ambae inasadikika alimuona kwa macho kasema keshafariki muda mrefu.
Kwahio Hamza katika kipindi chote alichofika Tanzania alikuwa akitembelea kituo hicho mara kwa mara
Prisila alionekana kutokuwa na muda mrefu wa kukaa hapo hivyo aliaga na Hamza hakutaka kumuachia aondoke , isitoshe walikuwa na mengi ya kuongea hivyo aliomba lift na Prisila.
Hata Mzee Hizza licha ya kutaka Hamza abaki kwa chakula cha mchana lakini alitaka waondoke pamoja na Prisila ili wapate muda wa kuondoka.
Hamza kabla ya kuondoka alitoa cheki ya kiasi cha pesa ambacho alikipata kwa bosi Laizer na kumpatia Mzee Hizza.
Ilikuwa cheki ya hela nyingi mno hivyo ilimfanya mkuu huyo kusita kupokea, isitoshe alimuona Hamza bado hakuwa ameyapatia maisha kama Prisila , hivyo alishangaa kupewa cheki ya hela nyingi kiasi hicho.
Lakini Hamza alimwambia sio kwa ajili yake bali ni ya watoto na Mzee Hizza alipokea kwa unyenyekevu huku akimshukuru sana Hamza kwa kutatua changamoto ambayo ilikuwa ikiwasumbua, alimuona Hamza kama malaika.
Upande wa Prisila aliona tukio hilo la Hamza kutoa kiasi kikubwa cha pesa , kilikuwa kiasi kingi mno na hajawahi kutoa kiasi hicho , sio kama hakuwa na roho ya kutoa hiko kiasi ila ukweli ni kwamba uwezo wa kutoa kiasi hicho mara moja hana.
Kutokana na kitendo kile kidogo alionyesha hali ya wasiwasi kwenye macho yake kupungua.
“Prisila kuna kitu kimetokea , najua hatukufahamiana sana utotoni kiasi cha kuwa na furaha baada ya kujuana ukubwani lakini kuna hali ya wasiwasi kwenye macho yako tokea unafika hapa” Aliongea Hamza wakati wakiwa kwenye gari Hamza akiwa ameomba kuendesha.
“Ukiachana na kazi yako kama msaidizi wa Regina ni kazi gani nyingine unafanya?”Aliuliza Prisila akiwa siriasi na swali lile lilimshangaza Hamza.






SEHEMU YA 76.
“Kazi yangu nyingine , kwanini ghafla tu unaniuliza kitu kama hicho?”
“Najua utadanganya lakini nimesikia taarifa unafanya kazi chini ya mtandao wa kihalifu wa Chatu”Aliongea Prisila na pale sasa Hamza alielewa ni kipi kilikuwa kikimfanya mrembo huyo kuwa na wasiwasi.
“Unaujuaje mtandao wa Chatu?”Aliuliza Hamza.
“Niambie ukweli kama unafanya kazi kwenye mtandao huo au hapana , napatwa na wasiwasi maana mimi ndio nimekukutanisha na bosi Regina”Aliongea .
“Prisila huna haja ya kuwa na wasiwasi hivyo , sio kama unavyofikiria ni kwamba tu nina ukaribu na bosi wa huo mtandao lakini haimaanishi kama nafanya hizo kazi , lakini pia huo mtandao sio wa kihalifu kama unavyofikiria wewe”Aliongea Hamza.
“Najua habari juu za huo mtandao na imekuwa moja ya topiki kwenye kampeni za viongozi wa chama cha wapinzani, najua pia kiongozi unaemzungumzia una ukaribu nae ni Dina , mwanamke Smrembo, kwahio wewe ndio mpenzi wake ndio maana mnafanya kazi pamoja?”Aliuliza na kumfanya Hamza asijue acheke ama alie.
“Nani kakuambia hayo yote”
“Nime mfollow Instagram ana wafuasi kibao , wengi wanamjuia japo haijulikani kama ndio mmiliki wa mtandao wa Chatu, baada ya kusikia una ukaribu nae nikajua moja kwa moja mnafanya wote kazi , wasiwasi wangu sio wewe kufanya kwake kazi maana siwezi kukupangia , kama yanayozungumzwa ni sahihi basi hupaswi kuwa karibu na Bosi Regina, chochote kitakachomtokea mimi ndio nitalaumiwa kwa kutokuwa makini”Aliongea huku akionekana kuwa siraisi.
Hamza hakujua nini Prisila aliambiwa na nani lakini alijua kwa mwanamke kama huyo anajali sana kitu kinachoitwa sheria.
“Unaonaje tukifika Dar twende wote ukajionee mwenyewe na ndio utajua kwanini nashirikiana nao”Aliongea Hamza , aliona ndio namna pekee ya kuondoa wasiwasi wa Prisila na mambo mengine yaendelee.
“Wewe niamini mimi tufika twende wote?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona Prisila anasita na kutokana na msisitizo wa Hamza Prisila aliamua kukubali, hata hivyo aliona kama Hamza ni mhalifu kwanini atoe kiasi chote kile cha pesa kwa ajili ya kusaidia watoto Yatima, ukweli ni kwamba tokea aambiwe juu ya hilo swala alikuwa na wasiwasi na alitamani kumwambia Regina lakini aliona ni busara kuongea na Hamza kwanza.
Baada ya masaa mawili kupita hatimae waliweza kufika mjini Dar es salaam na Hamza alinyoosha moja kwa moja mpaka Kijichi unapopatikana mgahawa wa chai wa Dina.
Hamza mara baada ya kusimamisha gari alishuka na Prisila na kuingia ndani na mhudumu alivyomuona Hamza alitingisha kichwa kumkaribisha kwa adabu.
Muda huo waliweza kusogelewa na Lawrence ambae alionekana kuwa na haraka.
“Bro karibu sana ila Madam ameenda kwenye kikao tokea asubuhi ila naamini atawahi kurudi”Aliongea Lawrence na kumfanya Hamza kushangaa kidogo.
“Kwenye kikao?!”
“Ndio , ni juu ya lile swala la usiku ule”Aliongea Lawrence na kumfanya Hamza kuelewa.
“Hii sehemu nilikuwa napita tu , sijawahi kuelewa wanachouza hapa”
“Wanauza Chai”
“Sehemu kubwa hivi wanauza chai tu?”
“Sio chai ya kawaida Prisila, ni chai inayotumia aina nyingi ya mimea , ushawahi kusisikia Gisaeng tea?”Aliuliza Hamza akiamini Prisila atakuwa anaangalia filamu za kikorea.
“Ndio nishawahi kuona kwenye filamu wakorea wanashabikia, unasema na hapa wanauza!!?”
“Sio Gisaeng tu , hapa wanauza kila aina ya chai maarufu zote duniani ikiwemo Panda Dung kutoka China , Gyokoro , Yellow Gold na aina nyingine nyingi za chai”Aliongea na kumfanya Prisila kushangaa na alishangaa baada ya kuona kuna wateja wengi tu wakionekana kufurahia chai.
Hawakuchukua muda mrefu kuwa peke yao Dina aliweza kurejea na alishangaa kumuona Hamza akiwa na mwanamke mwingine , tena mrembo.
Upande wa Prisila pia alishangaa kumuona Dina kwa urembo wake , ijapokuwa Prisila alikuwa amemzidi Dina lakini muda huo mwonekano wa kujiamini wa Dina umemfanya kuona amezidiwa vitu vingi.
“Hamza huyu msichana mrembo ni nani , mbona hunitambulishi?”Aliongea Dina huku akiwa na wasiwasi.
“Huyu anaitwa Prisila ni mfanyakazi mwenzangu lakini vilevile nimegundua leo ni rafiki yangu wa utotoni”Aliongea Hamza na kauli ile ilimfanya Dina kujiona mdogo mbele ya Prisila maana licha ya kwamba alikuwa amevalia mavazi ya kawaida lakini alikuwa ni mrembo haswa.
“Hello ! Naitwa Dinaq , ndio bosi wa hapa”Aliongea.
“Nimefurahi kukuahamu Dina”Aliongea Prisila huku akimpatia mkono lakini alionyesha hali ya wasiwasi.
“Prisila unaonaje sasa , huyu Dina unaemuona anafanana na mtu mhalifu?”Aliuliza Hamza lakini upande wa Prisila ni kama alianza kukosa utulivu , ukweli ni kwamba alikuwa akizidi kujiuliza inakuwaje Hamza anakutana mara kwa mara na wanawake warembo warembo na wote wanaonekana kana kwamba wanampenda.
Dina mara baada ya kusikia kauli ya Hamza ni kama sasa alielewa kwanini amekuija na mrembo huyo hivyo alichukua nafasi ya kujielezea.
“Prisila , ijapokuwa kwa nje tunaweza kuonekana kama wahalifu lakini biashara zetu hazihusiani na maswala ya kihalifu, tofauti ya biashara zangu na za kawaida ni kwamba tunamalizana na wateja wetu kibiashara bila kuhusisha sheria”Aliongea.
Prisila alimwangalia Dina kwa wasiwasi , lakini tabasamu la Dina lilimfanya kushindwa kujizuia kumuamini.
“Ni kweli?”Aliuliza.
“Unadhani nakudanganya, kama kweli sisi ni wahalifu unadhani ingekuwa rahisi kwa serikali kutuangalia tu bila kuchukua hatua yoyote , ijapokuwa wapo wengi wanaotusemea mabaya kama wahalifu lakini tunacheza nafasi kubwa ya usalama ndani ya nchi hii, kama huniamini mimi unaweza kumuamini Hamza , unadhani ni mtu mbaya ukimwangalia?”Aliuliza Dina na kauli yake ilimfanya Prisila kukumbuka Hamza muda mchache uliopita alikuwa ametoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya watoto yatima, tena wakati ambao kituo hicho kilikuwa kikihitaji msaada kwa kuwa nje ya bajeti.
Walikuwepo matajiri wengi ambao walikuwa na uwezo wa kuchangia zaidi ya milioni mia tisa lakini wengi wao michango yao haizidi hata milioni mia nne , isitoshe kwa mwonekano wa Hamza alionekana kama mtu ambae anauhitaji wa hela , kama sio hivyo kwanini akubali kuajiriwa na Regina kwa ajli ya mshahara wa laki saba .
Baaada ya kufikiria hayo yote aliona wasiwasi wake ulikuw bure tu na hakupaswa kumshuku hata kidogo.
Dakika ile ile ni kama sasa ndio anaanza kumuona Hamza kama rafiki yake wa utotoni ambae alikutana nae kituoni ,ile furaha ya kumjua Hamza kama mtu aliepotezana nae ilianza kuchipua.
“Hamza Sorry kwa kukushuku , ningejua nisingemsikiliza Lea na ujinga wake, wote mnaonekana kuwa watu wazuri”Aliongea Prisila.
“Lea ndio nani na kwanini akuambie mambo yangu ?”Aliuliza Hamza akiwa amekunja sura.
“Lea ni jirani yetu na ni kama rafiki yangu wa muda mrefu , alikuja nyumbani na kuniambia alikuwa Tanganyika Club na aliwaona wewe na Dina mkiwa pamoja , amesema wewe ni mhalifu hivyo nichukue tahadhari”Aliongea na kumfanya Hamza kumgeukia Dina.
“Ile siku kulikuwa na mwanamke yoyote alieitwa Leah?”Aliuliza.
“Sijasikia jina la Leah , halafu ile siku ilikuwa ni tofauti na watu wanazopendelea kuja kuchukua mazoezi hivyo hatukutana na watu wengi”Aliongea Dina .
“Prisila nadhani umejionea mwenyewe licha ya kwamba ni kweli Chatu inachukuliwa kama mtandao wa kihalifu , sio swala la kumfanya mtu awe na aibu kama sheria zinafuatwa hivyo usiwe na wasiwasi sasa”Aliongea na kumfanya Prisila mzigo wa wasiwasi kuutua
Maana swala hilo lilikuwa likimuumiza kichwa sana , kama mwajiri aliona amemwingiza bosi wake kwenye hatari na kutafuta namna ya kumuondoa kwenye hatari lakini baada ya kuongea na Hamza na kuonyeshwa hali halisi wasiwasi ulimtoka.
“Haya yameisha sasa , Prisila unaonaje tukiwa dadaz , njoo nikuonjeshe radha ya chai tofauti tofauti”Aliongea Dina kwa furaha huku akiagiza chakula pia maana Hamza alikuwa na njaa.
Dakika chache mbele walijikuta washazoeana na kuanza kupiga soga na kucheka.
Prisila alijua vitu vingi sana kuhusu chai na faida zake mwilini na mwisho wa siku aliona ni kheri kunywa chai kama njia ya kujichangamsha kuliko mvinyo uliojaa pombe.
Dina alidhamiria kumfanya Prisila rafiki yake pengine ni kwasababu ya Hamza na ili kukazia alimwalika Prisila kwenda nae kwenye sherehe ya uzinduzi wa Albamu ya msanii maarufu , Dina alikuwa amealikwa hivyo alimchagua Prisila kwenda nae , kwasababu Prisila alikuwa akijua juu ya uzinduzi huo alikubali.
“Naona amani imerudi sasa maana ulikuwa ukiniangalia kwa wasiwasi mno?”Aliongea Hamza wakati akimsindikiza Dina kuelekea nyumbani.
“Wasiwasi wangu haukuwa wewe kufanya wapi kazi , wasiwasi wangu ulikuwa juu ya Regina na Kampuni”
“Unamjali sana Regina , sijui kama na yeye anakujali kama unavyomjali?”
“Sina mashaka kabisa na Regina , alivyosiriasi utadhania hajali lakini ukimiuona anaweka hisia zake wazi kukuonyesha kujali huwa inagusa sana , nimekuwa nae namjua vizuri”Aliongea na Hamza hata yeye alijua hilo maana hata Eliza aliongea.
“Vipi yule mtoto mwenye mashavu kule Morogoro niliekutana nae miaka zaidi ya ishirini iliopita?”Aliuliza Hamza na kumfanya Prisila kuona aibu ilionekana udhaifu wake ni kuambiwa alikuwa na mashavu makubwa akiwa mdogo.
“Wakati nikiwa mtoto nilitelekezwa na mama kule kituoni kwa Baba Hizza na sikuwahi kumuona mpaka leo”Aliongea Prisila na kauli ile ilimshangaza na kumgusa Hamza.
“Mama yako alikuacha kule kituoni , ilikuwaje?”
“Ni stori ndefu ila nikipindi ambacho baba alikuwa nje ya nchi kwenye mafunzo ya kijeshi , mama alionekana kutompenda baba , pengine ilikuwa ni kutokana na kusafiri safiri kwake ndio maana alipoteza hisia na baba mpaka akaamua kunitelekeza kituoni , Baba Hizza ni ndugu wa baba upande wa bibi , baada ya baba kurudi nchini ndio aliambiwa nipo kituoni na kuja kunichukua”
“Na mama yako sasa hivi yupo wapi?”
“Mama sijui alipo mpaka sasa , ila tetesi zinasema itakuwa anaishi nje ya nchi maana alikuwa na mahusiano ya siri na mtalii, sijui labda baba anajua anapoishi ila sijawahi kumuuliza”Aliongea na kumfanya Hamza kumuonea huruma.
Kila mwanamke aliekuwa nae alikuwa na matatizo upande wa mama lakini ilionekana Prisila alikuwa na uchungu zaidi , kutelekezwa lazima itakuwa anajihisi mama yake hakumpenda.
Hamza wakati akifikiria namna ya kumfariji muda huo wakiwa mkabala na chuo cha TIA walisimamishwa na Traffic.
Dakika hio hio baada ya Hamza kusimamisha gari pembeni, gari mbili ziliongezeka kutoka nyuma yao na mbele yao moja kati ya hizo ikiwa ni Diffenda ya kijeshi jambo ambalo lilimfanya akunje sura na kujiambia kumekucha.
Wapita njia pia walivutiwa maana ni mara chache sana kuona jeshi la ulinzi kuzingira gari mbele na nyuma kama kwamba wanakamata mhalifu maana wengi walizoea kazi hio hufanywa na jeshi la polisi.
Muda ule mlango wa gari aina ya Jeep ulifunguliwa na alitoka mwanajeshi alievalia kombati za jeshi , alikuwa ni Afande Mdudu akitanguliwa na wanajeshi wengine na wote walizingira gari ya Hamza huku wakimwamrisha atoke.
Prisila alijikuta akitetemeka mno kutokana na tukio lile na alimwangalia Hamza na kushangaa alikuwa katika hali ya utulivu.
“Hamza nini kinaendelea?” Mrembo huyo aliuliza huku akiamini pengine ni kutokana na Hamza kujihusisha na mtandao wa kihalifu.
“Prisila usiwe na wasiwasi najua wanachotaka ngoja nitoke wewe utatangulia nyumbani tutawasiliana”Aliongea Hamza lakini kauli yake haikutosha kumtoa Prisila kwenye wasiwasi na Hamza baada ya kutoka na yeye alitoka.
“Afande Mdudu nini tena tatizo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kutoka nje ya gari.
“Hamza Mzee , Naitwa Meja Mdudu , kapteni kikosi namba mbili kitengo cha usalama wa nchi , rasmi kwanzia sasa hivi upo chini ya ulinzi kwa tuhuma za mauaji , kusababisha Ghasia na Utekaji”
Baada ya kuongea hivyo alitoa nyaraka na kumuonyeshea Hamza mbele yake, ilionekana kweli ni nyaraka ya kukamawa kwake iliosainiwa na wakubwa.
Hamza macho yake yalisinyaa , ilionekana hawa wanajeshi walikuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu na hawakutaka kumkamata mbele ya Dina wakijua kuna uwezekano angemkingia kifua ndio maana wakamuwekea mtego wa kumkamatia njiani.
Japo Hamza hakupenda kukamatwa mbele ya kadamnasi ya watu na mbele ya Prisila ambae ndio kwanza anatoka kumtoa hofu ili aendelee kumuamini lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutii shuruti.
“Naona mnaniwinda sana kama mizimu”Aliongea na kumfanya Afande Mdudu kucheka kwa furaha.
“Unadhani nilikuwa nikikuogopa , kabla ya kuwa mwanajeshi mimi ni raia wa hii nchi na kabla ya kuchukua hatua lazima niwe na ushahidi wa kisheria , kwa mtu hatari kama wewe ushahidi wa uhalifu wako ninao hivyo ninakukamata”
“Kwahio unajiona raia unaetii sheria , lakini sio wewe juzi ulietaka kumfosi mwanamke kwenda kumuoa , na hio pia ni sheria ya hii nchi?”Aliuliza Hamza na kumfanya Kamanda kunywea
“Haina haja ya kubadilisha topiki , nipo hapa kikazi na sina muda wa kuongea ujinga na wewe , kama unajua kuwa mtii na tuondoke pamoja”Aliongea Kamanda Mdudu maana alijua kama Hamza akitaka kuwakimbia wanaweza wasimzuie , lakini mbele ya mwanamke kama Prisila walijua ndio njia rahisi ya kumkamata na kumfanya atii shuruti , ulikuwa ni mpango.



Hamza aliishia kutoa tabasamu la uchungu na aliona Mdudu alikuwa na akili kidogo kwa kutaka kumkamatia mbele ya Prisila.
“Hamza..!!”
Prisila alitaka kuongea neno lakini jicho alilokatwa na wanajeshi hao lilimfanya kukosa nguvu ya kujiamini.
“Sikia Prisila usiwe na wasiwasi na usifikirie mbali, nitakupigia simu hili likishaisha nakuhakikishia sijafanya kosa lolote hivyo hawatonifana chochote”
“Mhalifu hebu acha majigambo kujsafisha mbele ya mwanamke uwe umefanya au hujafanya sisi ndio tunajua”Aliongea Mdudu
Kwa jinsi wajeda hao walivyokuwa siriasi Hamza aliamua kutii amri na alimwangalia Prisila kwa macho ya wasiwasi.
“Nitakupigia simu , nakuahidi nitakupeleka kwenye sherehe aliokuwahidi Dina mimi mwenyewe”Aliongea Hamza.
“Hio ni ahadi??”
“Ndio ni ahadi , hivyo acha wasiwasi”Aliongea Hamza na kishingo upande Prisila alikubali na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
Mdudu palepale alitoa ishara kwa mwanajeshi mwenzake na Hamza alaivishwa pingu na kuingizwa ndani ya gari na kuondolewa kwa spidi kuelekea mjini”
COMING UP ON FRIDAY STAY TUNED
Hamza anagawa Wastani , kwa mnaotaka kusoma mpaka episodes ya 112 nicheki watsapp 0687151346.
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI : SINGANOJR


SEHEMU YA 75.
Katika ndoto ambayo aliota jana yake aliweza kuona mwezi wa ule ulimwengu wa ndotoni ulikuwa mwekundu ,sasa mara baada ya kupewa mchoro uliokuwa kama picha na kuona mwezi huo ni mwekundu pia,ilimfanya kushangaa.
“Kwa jinsi ulivyoshangaa nadhani tayari unajua maana yake?”Aliuliza Frida akiwa na shauku.
“Sijui maana yake lakini jana kwenye ndoto niliona mwezi mwekundu , unaweza kuniambia nini maana ya huu mwezi na kwaninni umenionyesha hii picha?”Aliuliza Hamza , mbele ya Frida aliamua kuwa mpole ili kupata kile anachokitaka.
“Inamaanisha mazingira unayoota ni sahihi”Aliongea na kumfanya Hamza kukunja ndita .
“Wewe umejuaje?”
“Nilipewa na dokta Genesha na alinimbia nikijisikia ni muda sahihi wa kukuonyesha hii picha nikupatie , mwanzoni sikumwelewa alikuwa akimaanisha nini , lakini ulivyo uliza swali nilijua nini maana ya picha hii?”Aliongea .
Ukweli ni kwamba licha ya Hamza kujihusisha na Frida hakuwa akimwamini kabisa haikuwa hivyo tu hata kwa Frida alimuona Hamza kama mtu ambae hakuwa akimwanini.
Lakini licha ya hivyo alipaswa kumfanya Hamza kumwamini kwa namna yoyote ile ili tu aweze kumshawishi kutumia mshumaa wakati wa ndoto la sivyo maisha yake yatakuwa hataini.
Hamza alionekana kufikiria kwa dakika kadhaa huku akikodolea macho ile picha , hakuwa na shaka kabisa juu ya picha hio kwani ilionyesha kitu ambacho ameota yeye, alichokuwa akiwaza je haya yote yanayomtokea ndio njia sahihi ya kumpata Mzee kama alivyosema Dokta Genesha.
“Hamza kwa ajili ya hicho unachokiwaza mshumaa ni ufunguo wako , kumbuka maneno yangu niliokuambia juu ya uwepo wa Chumba cha nuru na ni wewe pekee ambae unaweza fikia hiki chumba kwa maelekezo ya Dokta, kadri ambavyo utachelewa kufanya maamuzi ndio unazidi kujiweka katika hatari pamoja na watu wanaokuzunguka”,
“Una amini nikitumia mshumaa nitakuwa salama , sidhani inaweza kuwa hivyo , kwanzia sasa kila ninachofanya juu ya hivi vitu ndio nazidi kujiweka katika hatari”
“Watu wanaokuwinda kwasasa wanachotaka ni kitu ulichokuwa nacho , hata kama wachukue waondoke nacho hakina maana kwao, wewe pia umekishikilia kwasababu bado hujajua maana yake halisi ni nini na kinaelekeza nini , ikitokea umejua kinachoelekeza utakuwa ni wewe tu dunia nzima unaejua hilo na inabakia kuwa siri yako , hata kama ukiwapatia kujiondolea hatari kwako na kwa wapendwa wako, watakuwa wamekushikia tu lakini maana unaijua wewe tu”
“Na siri hio ikitoka inamaanisha nitazidi kuwa hatari zaidi ya mara mbili ya kuwa na kitabu?”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu lililojaa uchungu.
“Ni mpaka wakifahamu juu ya hilo lakini kwa wakati huo utakuwa umejua namna ya kujilinda na kuilinda familia yako, sidhani upo tayari kuruhusu mwanamke kama Regina kuingia katika hatari kwa ajili yako”Aliongea.
“Unajua nina mahusiano na Regina, unaonekana kunifuatilia sana”
“Wewe ni misheni yangu kutoka kwa Dokta Genesha , nipo kwa ajili ya kukuelekeza, ukifeli kwa upande wako na mimi pia nafeli kile nilichomuahidi Dokta , lazima nijue watu ambao unajihusisha nao”
“Sishangai wewe kusema hivyo ndio maana hata mimi kuleta vyungu hapa ulikuwa ni mpango wako na haikuwa bahati mbaya kwa Alex kunipa kibarua”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba akikumbuka namna ambavyo amekutana na Frida ilionekana kabisa ulikuwa ni mpango wa Frida kukutana nae.
“Siwezi kukataa na tena kuhusu Alex unapaswa kuwa nae makini?”
“Nina sababu ya kufanya hivyo?”Aliuliza Hamza .
“Alex ni shushu kutoka watu wa kisiwa cha Binamu , maisha unayomuona nayo Alex ni uwezeshwaji na mbinu ya kulinda kile ambacho anafanya”
“Unamaanisha kusambaza vyungu?”
“Hupaswi kusema ni kusambaza vyungu bali ni kusambaza teknolojia mpya ya dawa inayosisimua ubongo , nadhani unakumbuka nilikuambia natumia vile vyungu kwa ajili ya utafiti wangu?”
“Ndio nakumbuka , kwahio unamaanisha umekwisha kupata majibu?”
“Ndio majibu nimekwisha kuyapata”Aliongea na jambo lile lilimfanya Hamza mwili wake kumsisimka kwa furaha maana ndio kitu ambacho alitaka kujua tokea mwanzo.
“Mpaka sasa sijajua namna dawa hii inavyotengenezwa , lakini ni maarufu kwa jina la Stimula”
“Stimula!!” Hamza alionekana kuhangaa kidogo.
“Ushawahi kusikia?”Aliuliza na Hamza alitingishwa kichwa kukubali.
“Zipo njia nyingi za usafirishaji wa hii Stimula na haina kibali chochote duniani ni kama madawa ya Kulevya , Njia ya utumiaji wa chungu ndio maarufu kwa hapa Tanzania na maeneo mengi ya Afrika”
“Wanasafirisha vipi?”
“Ni rahisi sana , unatumia jiko la umeme na kukifanya chungu kipate moto na dawa itaungua na kudhalisha harufu mfano wa marashi , hii harufu ukiivuta inakulewesha na baada ya hapo huelewi kinachoendelea maana utakuwa ni kama mgonjwa wa akili na dalili ya kwanza utakayokuwa nayo ni uwendawazimu kama vile umetawaliwa na roho nyingine , mtu anakuwa ni kama sio yeye kwani ataanza kuonge vitu ambavyo sio vya kawaida”Aliongea Hamza na kauli hio ilimfanya kukumbuka swala la rafiki yake Amiri juu ya harufu ya marashi nyumbani kwa Mellisa huku akiongea vitu vya ajabu.
“Kwanini haya yote , kuna faida yoyote mtumaji anayopata?”
“Kwasasa hakuna jibu sahihi kama kuna faida yoyote , haijulikani ni kwa ajili ya starehe au kuna zaidi ya sababu, pengine kuna mpango unaoendelezwa ambao si ufahamu , ni ngumu kukupa majibu kwasasa”Aliongea lakini upande wa Hamza bado hakutaka kukubali kirahisi , alijua lazima kuna kitu kinaendelea juu ya hicho kitu kinachoitwa Stimula.
Alitamani kutoendelea kuchimba zaidi lakini alimkumbuka Amiri rafiki yake na alimuahidi atamsaidia , lakini kabla ya hivyo alipaswa kujua kama Mellisa alikuwa moja ya wateja wa Alex wanaonunua hivyo vyungu.
Jambo la kwanza alipaswa kujua mtu aliempa kazi ya kufuatilia lugha aliokuwa akiongea amefikia wapi, na pili ndio afanye maamuzi aidha ya kumwambia Amiri ili ajue cha kufanya ama alifuatlie yeye mwenyewe .
Maana alijua kama swala hilo Mellisa analifanya kwa siri basi ni dhahiri kuna sababu kwanini Amiri hajui.
Hamza hakuwa na haja ya kuendelea kubakia nyumbani kwa Frida , ukweli ni kwamba swala la kutumia mshumaa ama kutokutumia ilikuwa ni maamuzi yake.
Upande wa Frida alimwangalia Hamza mpaka anatokomea na zilipita kama dakika kumi tu ya Hamza kuondoka aliingia mwanaume alievalia suti ndani ya jumba hilo , alikuwa mzungu..
Frida alionekana kumjua yule mtu na hata hakumsalimia , ilikuwa ni kama vile mtu huyo anaishi ndani ya nyumba hio.
“Unaamini atautumia mshumaa kwa kumweleza alichotaka kusikia?”Aliuliza yule mtu na kisha alisogelea makaratasi yaliochanguka mezani na kuchomoa karatasi la plastiki ambalo lilikuwa chini kabisa mwa yale makaratasi na kulinyanyua juu kuliangalia huku akitoa tabasamu na palepale alilikunja na kuliweka kwenye mfuko wa koti la suti.
“Umesikia mazungumzo yetu yote, hii inatosha kuniamini juu ya kusimamia vyema utafiti wangu”Aliongea Frida akiwa siriasi.
“Hatuwezi kwenda huko haraka hivyo Frida , upo hapa sio kwasababu Sinagogu wanakuamini bali tunamwamini Dokta Genesha, ulifanya kosa kubwa kumfanya Kuhani kukutilia shaka na sasa umejitengenezea udhaifu”Alionga yule bwana huku akizunguka zunguka kana kwamba kuna kitu anatafuta kwenye hio nyumba.
“Unamaanisha nini kujitengenezea udhaifu?”
“KF ni mtu hatari sana na kadri unavyokutana nae unazidi kumdanganya, ulikuwa na ushawishi mkubwa katika maneno yako ili kumfanya akuamini ili hali kila kitu ni kinyume chake , unadhani akijua unamdaganya itakuwaje?”Aliongea na kauli ile ilimfanya Frida kujawa na ukauzu.
“Kama unalijua hilo haikuwa na haja ya kuniuliza kama ameniamini, unaongea kwa kujaribu kuniogopesha lakini unapaswa kujua kitu kimoja, hii ni kazi ambayo nilifanya maamuzi mimi mwenyewe kuifanya , hivyo vitisho vyako hapa haviwezi kufanya kazi, najua malengo ya kazi yangu”Aliongea na kumfanya yule bwana kuonyesha ishara ya kutabasamu.
“Frida kazi yangu ni kukuangalia na kukisimamia na kuhakikisha kila unachofanya ni kama ulivyomuahidi Kuhani , unapaswa kujua Kanisa halijawahi kukuamini bali tunaamini kile unachofanyia utafiti ndani ya taasisi zetu, wewe ni Wicca na kama ulivyo kwenye taasisi yetu kwa ajili ya kutumiza malengo ya ushirika wako na sisi tupo hapa kukutumia ili kutimiza malengo ya ushirika wetu, hivyo haijalishi nilichoongea unachukulia kama tishio au onyo hio ni juu yako, tutatonana tena baada ya kuona mafanikio, Frida kumbuka naona kila unachofanya”Aliongea na kisha palepale aligeuka na kutoka ndani ya nyumba ile huku akiangaliwa na macho makali ya Frida.
Bwana huyo alikuwa ni yule yule ambae alikutana na Frida juu kabisa ya jengo la Haliz Foundation na ilionekana chochote kila ambacho Frida anafanya anasimamiwa na huyo mtu na pia ilionekana mazungumzo baina ya Hamza na Frida yalifuatiliwa kupitia teknolojia ya karatasi.
*******
Lisaa limoja na nusu mbele Hamza alikuwa akitoka kituo cha Treni ya Mwendokasi ndani ya mkoa wa Morogoro na kuungana na abiri wengi ambao walikuwa wakitoka eneo hilo.
Kutokana na jua kali Hamza hakutaka kupanda pikipiki bali aliingia kwenye taksi ambazo zilipatikana ndani ya eneo hilo.
“Nipeleke Tumaini mkuu?”Aliongea Hamza.
“Tumaini ipi mkuu?”Aliuliza yule bwana na kumfanya Hamza aone hakutoa maelezo ya kutosha.
“Tumaini kituoni kwa watoto Yatima kule”Aliongea Hamza.
“Nimekusoma bosi wangu”Aliongea mwendesha taksi kwa furaha na kisha aliondoa gari kuelekea uelekeo ambao ameelezwa.
Tumaini ni moja ya vituo maarufu kongwe ambavyo hulelea watoto Yatima na wale wenye ulemavu wa ngozi.
Kutoka stendi mpaka kituoni ilikuwa ni umbali wa nusu saa kutembea na gari, eneo lote lilikuwa likimilikiwa na taasisi moja ya kimisaada kutoka Denmark lakini baadae waliacha ufadhili na kwa muda mrefu kituo hicho kipo chini ya taasisi ya FOOT(Friends of orphans Tanzania).
Hamza mara baada ya kushushwa na taksi nje geti la kuingia kituoni hapo alilipa na kisha alisogelea chumba cha mlinzi na ilionekana alikuwa akifahamika kwani hakuandika hata jina lake kwenye kitabu zaidi ya kuruhusiwa kuingia.
Ndani ya kituo hicho kulikuwa na eneo kubwa mno , ijapokuwa majengo yake hayakuwa ya kisasa sana kutokana na kujengwa zamani sana lakini mazingira yalikuwa safi na yenye utulivu wa hali ya juu.
Ilikuwa Jumamosi hivyo watoto wote wanaoishi hapo walikuwa katika shunguli za usafi.
“Mr Hamza!!”Sauti iliita kutokea upande wa kulia wa bustani na kumfanya Hamza kugeuka .
“Madam Dorisi! Habari za siku?”Alisalimia Hamza.
Mwanamke ambae alifahamika kwa jina la Dorisi alikuwa mfupi na mnene na alionyesha tabasamu kumuona Hamza.
“Ni nzuri kabisa, sijategemea kukuona leo huku?”Aliongea huku akimwangalia Hamza kwa kumchunguza mavazi yake ni kama alikuwa akishangazwa na mabadiliko ya Hamza.
“Ulitegemea kuniona lini Madam?”Aliongea Hamza na yule mwalimu ni kama alijua ameongea kitu cha kijinga na kumfanya aanze kujibaraguza.
“Nilitegemea kukuona siku yoyote kwanzia kesho ila sio leo?”
“Hayo ni maratajio au sio!?”
“Kabisa , karibu sana , kama unavyoona nawasimamia watoto kufanya usafi wao wa kimwili”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kumwelewa.
Kila mtoto alionekana kuwa bize , wengine wakifua wengine walikuwa wakiogesha watoto wadogo.
“Nipo hapa kwa ajili ya kuonana na Mkuu wa kituo nadhani sijamkosa maana nimekuja bila miadi?”
“Yupo kuna wageni wengine anawasubiria leo”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu na kisha kumuaga Madam Dorisi kuendelea na mambo yake.
Hamza alitembea kwa mwendo usio wa haraka sana na usiokuwa wa kivivu sana akielekea jengo ambalo ofisi za walezi , mkuu wa kituo na walimu zinapatikana.
Jengo la ofisi hizo lilikuwa limechakaa kidogo kutokana na stali yake ya kizamani , kwa nje usingejua kama ni jengo la Ghorofa mpaka uingie ndani.
Hamza wakati akiingia eneo la ukumbi chini kabisa ya jengo hilo aliweza kuonekana mwanaume mzee hivi kama miaka sitini kwenda therathini, hakuwa peke yake bali kulikuwa na mwanaume kijana ambae ameshika daftari kubwa na ilionekana kuna kitu ambacho walikuwa wakishaurina kwa namna walivyokuwa siraisi.
“Hamza leo naona umetukumbuka?”Aliongea yule mzee huku akionyesha hali ya kutabasamu.
“Sijawahi kukusahau mzee wangu, halafu naona hali ya hewa Morogoro kidogo ni ya ubaridi na upepo mwingi , kwa mavazi hayo huogopi kuumwa?”
“Ni kweli hali imebadilika , japo naonekana kuwa na mvi tayari lakini sijazeeka , Karibu sana”Aliongea na Hamza alionyeshwa sehemu ya kukaa huku akisalimiana na yule bwana ambae alionekana kuwa na kaunta book, kwa haraka haraka Hamza alimfahamu alikuwa ni Mgavi wa hiko kituo.
“Dean nitaenda kumalizia ili kubalansi mahesabu , ikishindikana kabisa kwa watu tunaowatarajia nifanye mawasiliano na Wizara”Aliongea yule mwanaume.
“Fanya unachoona kinafaa kwa utashi wako , hakikisha unagawa pasipo ya kubadili utaratibu licha ya kupelea kibajeti”Aliongea na yule bwana alitingisha kichwa.
Kwa namna ambavyo walikuwa wakiongea Hamza alijua tu , kituo kitakuwa kinapitia wakati mgumu kwenye maswala ya bajeti na alijiambia alifanya vizuri kuja siku hio.
“Nimesikia kutoka kwa Madam Dorisi unasubiria wageni ndio maana hujatoka leo?”Aliongea Hamza.
“Amekuambia wageni!, mimi nimemwambia kuna mtu namsubiri na sio wageni , Dorisi bwana”Aliongea huku akitabasamu na kumfanya Hamza kucheka.
“Tena una bahati kuja leo, ninaemsubiria itakuwa unamjua kama kumbukumbu za utoto wako zinafanya kazi vizuri, pengine anaweza kuwa msaada kwenye swala lako”Aliongea na kauli yake ilimfanya Hamza macho kuchanua.
“Ni moja ya watoto waliolelewa hapa!?”
“Kama una kumbukumbu nzuri, unakumbuka wakati unarejewa na fahamu kuna msichana mdogo aliekuwa pembeni yako akilia!!?”Aliuliza Dean huku alimwangalia Hamza machoni kwa matarajio.
Haikuwa ngumu kwa Hamza kuvuta kumbukumbu za kituoni hapo wakati akiwa mdogo, ukweli ni kwamba sehemu hio miaka zaidi ya ishirini iliopira ndio sehemu ambayo kwa mara ya kwanza alisikia jina la Mzee na hio ni mara baada ya kurejewa na fahamu akiwepo hapo huku akiwa hana kumbukumbu ya kilichomtokea nyuma , alijua tu alipata ajali ambayo ilimfanya kupoteza fahamu kwa kipindi cha miezi minne.
“Nadhani kweli nakumbuka , kulikuwa na mtoto kibonge aliekuwa na mashavu makubwa”Aliongea Hamza na kumfanya Dean kucheka.
“Ndio huyo,nilidhani umemsahau kabisa, ila naona umemkumbuka”Aliongea na kumfanya Hamza hamu ya kutaka kumuona huyo mtu kuongezeka.
“Mzee kwa jinsi unavyoonekana nadhani amefanya vizuri sana wakati akiwa hapa?”Aliongea Hamza na Mzee yule alitingisha kichwa kukataa.
“Hapa hakukaa kabisa na hapakuwa kwao , wakati unaondoka na yeye alichukuliwa na baba yake, amefanya vizuri sana akiwa kwa wazazi wake mpaka kupata elimu ya juu kabisa na sasa ni mwajiriwa wa kampuni kubwa hapa nchini, licha ya hivyo mpaka leo hajawahi kutusahau, amekuwa moja ya wafadhili tegemezi hapa”Aliongea na Hamza alitingisha kichwa kukubaliana nae.
Na wakati huo wakiongea Madam Dorisi alijiiunga nao na stori ziliendelea .
Zilipita dakika chache tu mgeni ambae alikuwa akisubiriwa aliweza kufika , Hamza alikuwa na hamu kubwa ya kumuona kweli maana hata Madam Dorisi alionekana kumsifia kama ni mrembo sana huku akimtania akimwambia aangalie asije kupagawa.
Shida ilianza pale Hamza alipo ona gari ambayo iliingia ndani ya eneo hilo,gari hio ni kama alikuwa akiitambua vizuri, kabla hata hajashuka mgeni alimtambua vizuri alikuwa ni Prisila.
Hamza hakuwa hakuamini na alihitaji uthibitisho kutoka kwa Mzee Hizza na alitingisha kichwa kwamba ni yeye huku akiwa na tabasamu. Mzee huyo mara baada ya kuona wawili wakionyesha ishara kama wanafahamina baada ya kuangaliaana kuna kitu aligundua.
Prisila alikuwa amependeza licha ya kwamba alikuwa amevalia kistaarabu sana , hakuvaa mavazi ya kumfanya aonekane wa matawi ya juu sana wala wa hali ya chini sana , alikuwa katikati.
Baada ya kumuona Hamza ndani ya hilo eneo hata yeye alishangaa maana ni kama hakuwa ametarajia kumuona.
Prisila alikumbatiana kwanza na Dorisi huku akimpatia Mzee Hizza mkono na kisha ndio alimsogelea Hamza.
“Ningejua unakuja huku nisingepanda treni , ungenipa lift tu”Aliongea Hamza huku akijifikiria kwanini kila anapomaliza kikao chake na Frida mtu anaekutana nae baada ya hapo ni Prisila , ilikuwa ni kama mara ya pili hio inatokea.
“Kumbe mnafahamiana?”Aliuliza Dorisi aliekuwa na tabasamu na mshangao.
“Nafahamina nae huyu ni mfanyakazi wetu , nimeshangaa kumkuta huku”Aliongea Prisila huku akiongea kwa macho yaliojaa wasiwasi na jambo lile hata Hamza aliliona.
“Hapa ni nyumbani, amekuja kusalimia”Aliongea Mzee Hizza na kumfanya Prisila kushangaa kidogo.
“Njooni tukae kwanza ili tujue mmekutana lini tena kwa mara ya pili mkiwa wakubwa”Aliongea akicheka na kauli ile ilimfanya Prisila kushangaa zaidi na kujawa na maswali mengi.
“Dada Dorisi ongea na Agustino, kuna oda nimeweka Msamvu dukani kwa Mzee Salum , sikutaka kununua vitu bila ya kujua kipi kimepelea”Aliongea na Dorisi aliitikia na kuondoka na kubakia Hamza na Prisila.
“Prisila yule bwana niliekuambia ni huyu na yeye anaonekana kukumbuka, Hamza huyu ndio Prisila uliesema ana mashavu makubwa akiwa mtoto”
“Dean mimi sikuwa na mashavu”Aliongea Prisila huku akionyesha kushangaa japo alikuwa na furaha lakini pia alikuwa na wasiwasi.
“Hamza kasema kitu kilichomkumbusha ni mashavu yako , ni maneno yake sio yangu”Aliongea huku akicheka.
“Mzee Hizza nadhani imepangwa tukutane tukiwa ukubwani , mimi na Prisila tunafanya kazi kampuni moja ila kumbe tulijuana tukiwa watoto?”Aliongea Hamza.
“Kila jambo lina sababu yake , kama ambavyo sikutegemea ungerudi kwenye kituo chetu kunisalimia ni kama hivi wewe na Prisila”Aliongea na kumfanya Hamza kukumbuka siku ambayo alifika Tanzania na kukutana na Mzee Hizza kama mtu wa kwanza kumjua.
Mzee Hizza alikuwa ni kama mmiliki wa hicho kituo na karibia ujana wake wote ameumalizia kukiendesha , hata kipindi ambacho wafadhili waliondoka ni yeye aliepambana kuendelea kukisimamia mpaka kuja kupata wafadhili wengine.
Kwa muda huo mzee huyo hakujua chochote juu ya Hamza kuandishika ndoa na maswala mengine, hivyo alijua pengine kukutana kwa Prisila na Hamza kutafungua milango mingine.
Stori ziliendelea ndani ya eneo hilo na kutokana na uchangamfu wa Mzee Hizza hata Prisila ambae alikuwa na wasiwasi alichangamka.
Baada ya maongezi machache Prisila yeye alienda kusalimiana na watoto na Hamza na mkuu wa kituo walibakia kuongea.
Moja ya vitu muhimu ambavyo Hamza alimuuliza ni kama kuna kitu chochote amekumbuka juu ya aliemleta kituoni hapo wakati akiwa mtoto, lakini kauli ya Mzee Hizza haikubadilika.
Kauili yake ilikuwa ni ileile ya siku zote kwamba Hamza aliachwa kituoni na mtu aliejitambulisha kwa jina la Mzee huku akitoa maelezo Hamza angekuja kuchukuliwa na mzazi wake.
Hamza alikuwa akijua kauli hio ilikuwa ikimaanisha nini, lakini alitamani kumjua mtu ambae alimuacha hapo kituoni , kuna kila hisia mtu huyo alikuwa ni Mzee anaemjua maisha yake yote lakini hakuwa na uhakika kwasababu Mzee Hizza hakumuona vizuri na mtu ambae inasadikika alimuona kwa macho kasema keshafariki muda mrefu.
Kwahio Hamza katika kipindi chote alichofika Tanzania alikuwa akitembelea kituo hicho mara kwa mara
Prisila alionekana kutokuwa na muda mrefu wa kukaa hapo hivyo aliaga na Hamza hakutaka kumuachia aondoke , isitoshe walikuwa na mengi ya kuongea hivyo aliomba lift na Prisila.
Hata Mzee Hizza licha ya kutaka Hamza abaki kwa chakula cha mchana lakini alitaka waondoke pamoja na Prisila ili wapate muda wa kuondoka.
Hamza kabla ya kuondoka alitoa cheki ya kiasi cha pesa ambacho alikipata kwa bosi Laizer na kumpatia Mzee Hizza.
Ilikuwa cheki ya hela nyingi mno hivyo ilimfanya mkuu huyo kusita kupokea, isitoshe alimuona Hamza bado hakuwa ameyapatia maisha kama Prisila , hivyo alishangaa kupewa cheki ya hela nyingi kiasi hicho.
Lakini Hamza alimwambia sio kwa ajili yake bali ni ya watoto na Mzee Hizza alipokea kwa unyenyekevu huku akimshukuru sana Hamza kwa kutatua changamoto ambayo ilikuwa ikiwasumbua, alimuona Hamza kama malaika.
Upande wa Prisila aliona tukio hilo la Hamza kutoa kiasi kikubwa cha pesa , kilikuwa kiasi kingi mno na hajawahi kutoa kiasi hicho , sio kama hakuwa na roho ya kutoa hiko kiasi ila ukweli ni kwamba uwezo wa kutoa kiasi hicho mara moja hana.
Kutokana na kitendo kile kidogo alionyesha hali ya wasiwasi kwenye macho yake kupungua.
“Prisila kuna kitu kimetokea , najua hatukufahamiana sana utotoni kiasi cha kuwa na furaha baada ya kujuana ukubwani lakini kuna hali ya wasiwasi kwenye macho yako tokea unafika hapa” Aliongea Hamza wakati wakiwa kwenye gari Hamza akiwa ameomba kuendesha.
“Ukiachana na kazi yako kama msaidizi wa Regina ni kazi gani nyingine unafanya?”Aliuliza Prisila akiwa siriasi na swali lile lilimshangaza Hamza.






SEHEMU YA 76.
“Kazi yangu nyingine , kwanini ghafla tu unaniuliza kitu kama hicho?”
“Najua utadanganya lakini nimesikia taarifa unafanya kazi chini ya mtandao wa kihalifu wa Chatu”Aliongea Prisila na pale sasa Hamza alielewa ni kipi kilikuwa kikimfanya mrembo huyo kuwa na wasiwasi.
“Unaujuaje mtandao wa Chatu?”Aliuliza Hamza.
“Niambie ukweli kama unafanya kazi kwenye mtandao huo au hapana , napatwa na wasiwasi maana mimi ndio nimekukutanisha na bosi Regina”Aliongea .
“Prisila huna haja ya kuwa na wasiwasi hivyo , sio kama unavyofikiria ni kwamba tu nina ukaribu na bosi wa huo mtandao lakini haimaanishi kama nafanya hizo kazi , lakini pia huo mtandao sio wa kihalifu kama unavyofikiria wewe”Aliongea Hamza.
“Najua habari juu za huo mtandao na imekuwa moja ya topiki kwenye kampeni za viongozi wa chama cha wapinzani, najua pia kiongozi unaemzungumzia una ukaribu nae ni Dina , mwanamke Smrembo, kwahio wewe ndio mpenzi wake ndio maana mnafanya kazi pamoja?”Aliuliza na kumfanya Hamza asijue acheke ama alie.
“Nani kakuambia hayo yote”
“Nime mfollow Instagram ana wafuasi kibao , wengi wanamjuia japo haijulikani kama ndio mmiliki wa mtandao wa Chatu, baada ya kusikia una ukaribu nae nikajua moja kwa moja mnafanya wote kazi , wasiwasi wangu sio wewe kufanya kwake kazi maana siwezi kukupangia , kama yanayozungumzwa ni sahihi basi hupaswi kuwa karibu na Bosi Regina, chochote kitakachomtokea mimi ndio nitalaumiwa kwa kutokuwa makini”Aliongea huku akionekana kuwa siraisi.
Hamza hakujua nini Prisila aliambiwa na nani lakini alijua kwa mwanamke kama huyo anajali sana kitu kinachoitwa sheria.
“Unaonaje tukifika Dar twende wote ukajionee mwenyewe na ndio utajua kwanini nashirikiana nao”Aliongea Hamza , aliona ndio namna pekee ya kuondoa wasiwasi wa Prisila na mambo mengine yaendelee.
“Wewe niamini mimi tufika twende wote?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona Prisila anasita na kutokana na msisitizo wa Hamza Prisila aliamua kukubali, hata hivyo aliona kama Hamza ni mhalifu kwanini atoe kiasi chote kile cha pesa kwa ajili ya kusaidia watoto Yatima, ukweli ni kwamba tokea aambiwe juu ya hilo swala alikuwa na wasiwasi na alitamani kumwambia Regina lakini aliona ni busara kuongea na Hamza kwanza.
Baada ya masaa mawili kupita hatimae waliweza kufika mjini Dar es salaam na Hamza alinyoosha moja kwa moja mpaka Kijichi unapopatikana mgahawa wa chai wa Dina.
Hamza mara baada ya kusimamisha gari alishuka na Prisila na kuingia ndani na mhudumu alivyomuona Hamza alitingisha kichwa kumkaribisha kwa adabu.
Muda huo waliweza kusogelewa na Lawrence ambae alionekana kuwa na haraka.
“Bro karibu sana ila Madam ameenda kwenye kikao tokea asubuhi ila naamini atawahi kurudi”Aliongea Lawrence na kumfanya Hamza kushangaa kidogo.
“Kwenye kikao?!”
“Ndio , ni juu ya lile swala la usiku ule”Aliongea Lawrence na kumfanya Hamza kuelewa.
“Hii sehemu nilikuwa napita tu , sijawahi kuelewa wanachouza hapa”
“Wanauza Chai”
“Sehemu kubwa hivi wanauza chai tu?”
“Sio chai ya kawaida Prisila, ni chai inayotumia aina nyingi ya mimea , ushawahi kusisikia Gisaeng tea?”Aliuliza Hamza akiamini Prisila atakuwa anaangalia filamu za kikorea.
“Ndio nishawahi kuona kwenye filamu wakorea wanashabikia, unasema na hapa wanauza!!?”
“Sio Gisaeng tu , hapa wanauza kila aina ya chai maarufu zote duniani ikiwemo Panda Dung kutoka China , Gyokoro , Yellow Gold na aina nyingine nyingi za chai”Aliongea na kumfanya Prisila kushangaa na alishangaa baada ya kuona kuna wateja wengi tu wakionekana kufurahia chai.
Hawakuchukua muda mrefu kuwa peke yao Dina aliweza kurejea na alishangaa kumuona Hamza akiwa na mwanamke mwingine , tena mrembo.
Upande wa Prisila pia alishangaa kumuona Dina kwa urembo wake , ijapokuwa Prisila alikuwa amemzidi Dina lakini muda huo mwonekano wa kujiamini wa Dina umemfanya kuona amezidiwa vitu vingi.
“Hamza huyu msichana mrembo ni nani , mbona hunitambulishi?”Aliongea Dina huku akiwa na wasiwasi.
“Huyu anaitwa Prisila ni mfanyakazi mwenzangu lakini vilevile nimegundua leo ni rafiki yangu wa utotoni”Aliongea Hamza na kauli ile ilimfanya Dina kujiona mdogo mbele ya Prisila maana licha ya kwamba alikuwa amevalia mavazi ya kawaida lakini alikuwa ni mrembo haswa.
“Hello ! Naitwa Dinaq , ndio bosi wa hapa”Aliongea.
“Nimefurahi kukuahamu Dina”Aliongea Prisila huku akimpatia mkono lakini alionyesha hali ya wasiwasi.
“Prisila unaonaje sasa , huyu Dina unaemuona anafanana na mtu mhalifu?”Aliuliza Hamza lakini upande wa Prisila ni kama alianza kukosa utulivu , ukweli ni kwamba alikuwa akizidi kujiuliza inakuwaje Hamza anakutana mara kwa mara na wanawake warembo warembo na wote wanaonekana kana kwamba wanampenda.
Dina mara baada ya kusikia kauli ya Hamza ni kama sasa alielewa kwanini amekuija na mrembo huyo hivyo alichukua nafasi ya kujielezea.
“Prisila , ijapokuwa kwa nje tunaweza kuonekana kama wahalifu lakini biashara zetu hazihusiani na maswala ya kihalifu, tofauti ya biashara zangu na za kawaida ni kwamba tunamalizana na wateja wetu kibiashara bila kuhusisha sheria”Aliongea.
Prisila alimwangalia Dina kwa wasiwasi , lakini tabasamu la Dina lilimfanya kushindwa kujizuia kumuamini.
“Ni kweli?”Aliuliza.
“Unadhani nakudanganya, kama kweli sisi ni wahalifu unadhani ingekuwa rahisi kwa serikali kutuangalia tu bila kuchukua hatua yoyote , ijapokuwa wapo wengi wanaotusemea mabaya kama wahalifu lakini tunacheza nafasi kubwa ya usalama ndani ya nchi hii, kama huniamini mimi unaweza kumuamini Hamza , unadhani ni mtu mbaya ukimwangalia?”Aliuliza Dina na kauli yake ilimfanya Prisila kukumbuka Hamza muda mchache uliopita alikuwa ametoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya watoto yatima, tena wakati ambao kituo hicho kilikuwa kikihitaji msaada kwa kuwa nje ya bajeti.
Walikuwepo matajiri wengi ambao walikuwa na uwezo wa kuchangia zaidi ya milioni mia tisa lakini wengi wao michango yao haizidi hata milioni mia nne , isitoshe kwa mwonekano wa Hamza alionekana kama mtu ambae anauhitaji wa hela , kama sio hivyo kwanini akubali kuajiriwa na Regina kwa ajli ya mshahara wa laki saba .
Baaada ya kufikiria hayo yote aliona wasiwasi wake ulikuw bure tu na hakupaswa kumshuku hata kidogo.
Dakika ile ile ni kama sasa ndio anaanza kumuona Hamza kama rafiki yake wa utotoni ambae alikutana nae kituoni ,ile furaha ya kumjua Hamza kama mtu aliepotezana nae ilianza kuchipua.
“Hamza Sorry kwa kukushuku , ningejua nisingemsikiliza Lea na ujinga wake, wote mnaonekana kuwa watu wazuri”Aliongea Prisila.
“Lea ndio nani na kwanini akuambie mambo yangu ?”Aliuliza Hamza akiwa amekunja sura.
“Lea ni jirani yetu na ni kama rafiki yangu wa muda mrefu , alikuja nyumbani na kuniambia alikuwa Tanganyika Club na aliwaona wewe na Dina mkiwa pamoja , amesema wewe ni mhalifu hivyo nichukue tahadhari”Aliongea na kumfanya Hamza kumgeukia Dina.
“Ile siku kulikuwa na mwanamke yoyote alieitwa Leah?”Aliuliza.
“Sijasikia jina la Leah , halafu ile siku ilikuwa ni tofauti na watu wanazopendelea kuja kuchukua mazoezi hivyo hatukutana na watu wengi”Aliongea Dina .
“Prisila nadhani umejionea mwenyewe licha ya kwamba ni kweli Chatu inachukuliwa kama mtandao wa kihalifu , sio swala la kumfanya mtu awe na aibu kama sheria zinafuatwa hivyo usiwe na wasiwasi sasa”Aliongea na kumfanya Prisila mzigo wa wasiwasi kuutua
Maana swala hilo lilikuwa likimuumiza kichwa sana , kama mwajiri aliona amemwingiza bosi wake kwenye hatari na kutafuta namna ya kumuondoa kwenye hatari lakini baada ya kuongea na Hamza na kuonyeshwa hali halisi wasiwasi ulimtoka.
“Haya yameisha sasa , Prisila unaonaje tukiwa dadaz , njoo nikuonjeshe radha ya chai tofauti tofauti”Aliongea Dina kwa furaha huku akiagiza chakula pia maana Hamza alikuwa na njaa.
Dakika chache mbele walijikuta washazoeana na kuanza kupiga soga na kucheka.
Prisila alijua vitu vingi sana kuhusu chai na faida zake mwilini na mwisho wa siku aliona ni kheri kunywa chai kama njia ya kujichangamsha kuliko mvinyo uliojaa pombe.
Dina alidhamiria kumfanya Prisila rafiki yake pengine ni kwasababu ya Hamza na ili kukazia alimwalika Prisila kwenda nae kwenye sherehe ya uzinduzi wa Albamu ya msanii maarufu , Dina alikuwa amealikwa hivyo alimchagua Prisila kwenda nae , kwasababu Prisila alikuwa akijua juu ya uzinduzi huo alikubali.
“Naona amani imerudi sasa maana ulikuwa ukiniangalia kwa wasiwasi mno?”Aliongea Hamza wakati akimsindikiza Dina kuelekea nyumbani.
“Wasiwasi wangu haukuwa wewe kufanya wapi kazi , wasiwasi wangu ulikuwa juu ya Regina na Kampuni”
“Unamjali sana Regina , sijui kama na yeye anakujali kama unavyomjali?”
“Sina mashaka kabisa na Regina , alivyosiriasi utadhania hajali lakini ukimiuona anaweka hisia zake wazi kukuonyesha kujali huwa inagusa sana , nimekuwa nae namjua vizuri”Aliongea na Hamza hata yeye alijua hilo maana hata Eliza aliongea.
“Vipi yule mtoto mwenye mashavu kule Morogoro niliekutana nae miaka zaidi ya ishirini iliopita?”Aliuliza Hamza na kumfanya Prisila kuona aibu ilionekana udhaifu wake ni kuambiwa alikuwa na mashavu makubwa akiwa mdogo.
“Wakati nikiwa mtoto nilitelekezwa na mama kule kituoni kwa Baba Hizza na sikuwahi kumuona mpaka leo”Aliongea Prisila na kauli ile ilimshangaza na kumgusa Hamza.
“Mama yako alikuacha kule kituoni , ilikuwaje?”
“Ni stori ndefu ila nikipindi ambacho baba alikuwa nje ya nchi kwenye mafunzo ya kijeshi , mama alionekana kutompenda baba , pengine ilikuwa ni kutokana na kusafiri safiri kwake ndio maana alipoteza hisia na baba mpaka akaamua kunitelekeza kituoni , Baba Hizza ni ndugu wa baba upande wa bibi , baada ya baba kurudi nchini ndio aliambiwa nipo kituoni na kuja kunichukua”
“Na mama yako sasa hivi yupo wapi?”
“Mama sijui alipo mpaka sasa , ila tetesi zinasema itakuwa anaishi nje ya nchi maana alikuwa na mahusiano ya siri na mtalii, sijui labda baba anajua anapoishi ila sijawahi kumuuliza”Aliongea na kumfanya Hamza kumuonea huruma.
Kila mwanamke aliekuwa nae alikuwa na matatizo upande wa mama lakini ilionekana Prisila alikuwa na uchungu zaidi , kutelekezwa lazima itakuwa anajihisi mama yake hakumpenda.
Hamza wakati akifikiria namna ya kumfariji muda huo wakiwa mkabala na chuo cha TIA walisimamishwa na Traffic.
Dakika hio hio baada ya Hamza kusimamisha gari pembeni, gari mbili ziliongezeka kutoka nyuma yao na mbele yao moja kati ya hizo ikiwa ni Diffenda ya kijeshi jambo ambalo lilimfanya akunje sura na kujiambia kumekucha.
Wapita njia pia walivutiwa maana ni mara chache sana kuona jeshi la ulinzi kuzingira gari mbele na nyuma kama kwamba wanakamata mhalifu maana wengi walizoea kazi hio hufanywa na jeshi la polisi.
Muda ule mlango wa gari aina ya Jeep ulifunguliwa na alitoka mwanajeshi alievalia kombati za jeshi , alikuwa ni Afande Mdudu akitanguliwa na wanajeshi wengine na wote walizingira gari ya Hamza huku wakimwamrisha atoke.
Prisila alijikuta akitetemeka mno kutokana na tukio lile na alimwangalia Hamza na kushangaa alikuwa katika hali ya utulivu.
“Hamza nini kinaendelea?” Mrembo huyo aliuliza huku akiamini pengine ni kutokana na Hamza kujihusisha na mtandao wa kihalifu.
“Prisila usiwe na wasiwasi najua wanachotaka ngoja nitoke wewe utatangulia nyumbani tutawasiliana”Aliongea Hamza lakini kauli yake haikutosha kumtoa Prisila kwenye wasiwasi na Hamza baada ya kutoka na yeye alitoka.
“Afande Mdudu nini tena tatizo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kutoka nje ya gari.
“Hamza Mzee , Naitwa Meja Mdudu , kapteni kikosi namba mbili kitengo cha usalama wa nchi , rasmi kwanzia sasa hivi upo chini ya ulinzi kwa tuhuma za mauaji , kusababisha Ghasia na Utekaji”
Baada ya kuongea hivyo alitoa nyaraka na kumuonyeshea Hamza mbele yake, ilionekana kweli ni nyaraka ya kukamawa kwake iliosainiwa na wakubwa.
Hamza macho yake yalisinyaa , ilionekana hawa wanajeshi walikuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu na hawakutaka kumkamata mbele ya Dina wakijua kuna uwezekano angemkingia kifua ndio maana wakamuwekea mtego wa kumkamatia njiani.
Japo Hamza hakupenda kukamatwa mbele ya kadamnasi ya watu na mbele ya Prisila ambae ndio kwanza anatoka kumtoa hofu ili aendelee kumuamini lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutii shuruti.
“Naona mnaniwinda sana kama mizimu”Aliongea na kumfanya Afande Mdudu kucheka kwa furaha.
“Unadhani nilikuwa nikikuogopa , kabla ya kuwa mwanajeshi mimi ni raia wa hii nchi na kabla ya kuchukua hatua lazima niwe na ushahidi wa kisheria , kwa mtu hatari kama wewe ushahidi wa uhalifu wako ninao hivyo ninakukamata”
“Kwahio unajiona raia unaetii sheria , lakini sio wewe juzi ulietaka kumfosi mwanamke kwenda kumuoa , na hio pia ni sheria ya hii nchi?”Aliuliza Hamza na kumfanya Kamanda kunywea
“Haina haja ya kubadilisha topiki , nipo hapa kikazi na sina muda wa kuongea ujinga na wewe , kama unajua kuwa mtii na tuondoke pamoja”Aliongea Kamanda Mdudu maana alijua kama Hamza akitaka kuwakimbia wanaweza wasimzuie , lakini mbele ya mwanamke kama Prisila walijua ndio njia rahisi ya kumkamata na kumfanya atii shuruti , ulikuwa ni mpango.



Hamza aliishia kutoa tabasamu la uchungu na aliona Mdudu alikuwa na akili kidogo kwa kutaka kumkamatia mbele ya Prisila.
“Hamza..!!”
Prisila alitaka kuongea neno lakini jicho alilokatwa na wanajeshi hao lilimfanya kukosa nguvu ya kujiamini.
“Sikia Prisila usiwe na wasiwasi na usifikirie mbali, nitakupigia simu hili likishaisha nakuhakikishia sijafanya kosa lolote hivyo hawatonifana chochote”
“Mhalifu hebu acha majigambo kujsafisha mbele ya mwanamke uwe umefanya au hujafanya sisi ndio tunajua”Aliongea Mdudu
Kwa jinsi wajeda hao walivyokuwa siriasi Hamza aliamua kutii amri na alimwangalia Prisila kwa macho ya wasiwasi.
“Nitakupigia simu , nakuahidi nitakupeleka kwenye sherehe aliokuwahidi Dina mimi mwenyewe”Aliongea Hamza.
“Hio ni ahadi??”
“Ndio ni ahadi , hivyo acha wasiwasi”Aliongea Hamza na kishingo upande Prisila alikubali na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
Mdudu palepale alitoa ishara kwa mwanajeshi mwenzake na Hamza alaivishwa pingu na kuingizwa ndani ya gari na kuondolewa kwa spidi kuelekea mjini”
COMING UP ON FRIDAY STAY TUNED
Hamza anagawa Wastani , kwa mnaotaka kusoma mpaka episodes ya 112 nicheki watsapp 0687151346.
Vipi Leo mgosi
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU



MTUNZI: SINGANOJR



SEHEMU YA 76.

Baada ya kupandishwa kwenye gari walichukua uelekeo wa kurudi Mbagala na ndani ya dakika chache tu walikunja kushoto na kuingia katika kambi ya jeshi.

Eneo hilo licha ya kuhifadhia maghala makubwa ya siraha za kijeshi lakini vilevile lilikuwa na gereza la siri ambalo hufungia wafungwa maalumu.

Ndio gereza ambalo mara nyingi lilitumiwa na kitengo cha MALIBU na TISA kwa ajili ya kuhoji na kutesa kupata taarifa.

Hamza mara baada ya kutolewa kwenye gari ndani ya eneo hilo alipelekwa mpaka kwenye nyumba ambayo ilikuwa imejengwa kwa mawe, jengo hilo lilionekana kama ngome ambayo haina madirisha.

Mara baada ya kupitishwa kwenye mlango mpana wa chuma hatimae aliingizwa kwenye chumba maalumu cha mahojiano ambacho kilikuwa kama sero.

Chumba hicho kilikuwa kimezungukwa na vioo vigumu ambavyo havipitishi risasi na hata kuhimili mlipuko wa bomu la kawaida, kulikuwa na kila aina ya ufundi uliotumika eneo hilo kuhakikisha usalama na ilimshangaza Hamza huku akijiuliza kama kuna mtu ambae ashawahi kufikishwa ndani ya eneo hilo.

Hamza alikarishwa kwenye benchi na kujikuta akigeuza macho na kugundua kulikuwa na kila tahadhari zilichochukuliwa , ilikuwa ni kama vile waliomleta hapo walikuwa wakimhofia na kujikuta kutamani kucheka.

Lakini kitendo cha kuona namna ambavyo chumba hiki kimejengwa aliamini pengine Tanzania sio nchi ya Amani kama ambavyo alitarajia,pengine kuna mambo mengi yanaendelea chini chini.

Ikumbukwe kwamba kutengeneza chumba kwa vioo ambavyo vina uwezo wa kuzuia risasi na bomu gharama yake ni kama kutumia dhahabu, sasa kama nchi imeamua kutumia kiasi chote hiko cha hela kujenga eneo hilo aliona haiwezi kuwa bure.

Haikuchukua dakika nyingi wanajeshi kadhaa waliovalia kombati za jeshi waliingia , wakiongozwa na Afande Mdudu, mmoja kati yao alikuwa amevalia kombati za jeshi la polisi zenye cheo cha Kamishina.

Afande Mdudu alikuwa na tabasamu kama lote , kitendo cha kumwingiza Hamza kwenye eneo hilo alijiona mshindi na hakuwa na wasiwasi tena.

“Hamza huyu ni Kamanda Wazo mkuu wa kitengo cha Special Crimes,huyu mwingine ni mtaalamu wa mahojiano alietumwa kutoka makao makuu ya polisi , anaitwa Afande Maningi, Hawa ndio walikuwa bize kudili na kesi yako hivyo unapaswa kutoa ushirikiano kwa kuwajibu kila watakacho kuuliza bila kupindisha”Aliongea Mdudu.

Baada ya kuwatambulisha Afande Mdudu alivuta viti viwili na kuwapa ishara wale ma’afande kukaa .

Wote walionekana kuwa na vyeo vikubwa kuliko hata Afande Mdudu, hata ambae alikuwa na sare za jeshi la polisi alionekana pia ni mwenye cheo kikubwa kutokana na vyeo vilivyokuwa kwenye sare yake.

Afande Wazo aliwapa ishara ya kuondoka wanajeshi wote waliokuwa wamefuatana nao.

“Mnaweza kuondoka , huyu mfungwa yupo kwenye selo yenye ulinzi mkali hata kama ana uwezo mkubwa hawezi kufanya chochote”Aliongea Kamanda Wazo.

“Anachomaanisha kamanda mahojiano haya yanapaswa kuwa siri hivyo mtupe nafasi ya kufanya kazi yetu”Aliogea Afande Maningi na kufanya wale makomandoo na baadhi ya wanajeshi wengine kutoka ndani ya eneo hilo na kuwaacha.

“Hili gereza lenu ni la kisasa mno mnaliitaje?”Aliuliza Hamza huku akichezesha miguu chini.

“Ukisikia Dragon lair ndio hili gereza , hakuna mtu ambae ashawahi kuingizwa hapa akatoka kwa hiari yake hata kama ana uwezo namna gani , tunao uwezo wa kukufungia hapa mpaka ukafa”Aliongea Afande Mdudu huku akicheka.

“Kwa maelezo yako hata mimi naamini hili gereza ni la hatari”Aliongea Hamza huku akitabasamu.

“Hamza huna haja ya kuwa na wasiwasi , sababu kubwa ya kukuleta hapa ni kutaka majibu juu ya maswali yetu , kama huna kosa hatuwezi kukusingizia”Aliongea Kamishina.

“Oh , maswali gani hayo afande?”

“Kwa muda mrefu kidogo tulikuwa tukifanya uchunguzi juu ya maninja wanaojiita wawindaji kutoka Samar ambao walikutwa wameuwa wilaya ya Bagamoyo , baada ya uchunguzi wetu tulibaini wewe ndio muhusika, hawa watu wametokea nchi ya Ufilipino na sio rahisi kuja Tanzania na kuuwawa hivi hivi , siku ya jana tumeweza kukamata wengine wawili ambao walijaribu kuzamia hapa nchini kama watalii na baada ya kuwafanyia mahojiano ya kina wamesema kwamba wanafuatilia siri uliokuwa nayo juu ya kitu kinachoitwa Ankh”Aliongea Kamishina Maningi na kauli yake ilimfanya Hamza kukunja sura.

Hamza alijiambia inamaana wale wapuuzi hawakukata tamaa tu au walikuja kufuatilia kwanini wenzao hawakurudi, lakini hata hivyo aliona haiwezekani, mara nyingi wawindaji hao wa binadamu wakitumwa katika misheni kuna mmoja kazi yake ni kufuatilia kisirisiri maendeleo ya misheni hio , hivyo Hamza aliamini kwa onyo alilotoa lingefika kupitia huyo mwenzao.

“Hamza hawa bounty hunters inaonekana bado hawajakata tamaa na wamerudi tena nchini na kutaka hiki kitu kinachotwa Ankh, kwa taarifa yako hivi unajua kwasababu yako nchi imeingia katika hatari huko mipakani kutokana na ongezeko kubwa la wahalifu kutaka kuingia nchini?”

“Hilo kundi ni daraja B na kwa taarifa nilzokuwa nazo kitengo chenu cha MALIBU kinahesabika kama Daraja A kwa kuwa na wataalamu wengi wenye mbinu mbalimbali za kupambana mpaka na nguvu za giza , kinachowaogopesha nini juu ya hawa Wasamar?”Aliongea Hamza.

“Hili sio swala la sisi kuogopa ama kutokuogopa , tunachotaka kujua ni mzizi wa haya yote , mpaka sasa ma Ajenti wetu wanaendelea kuwahoji hawa Wasamar lakini hatujapata majibu , tunachotaka kujua kutoka kwako hiki kitu kinachoitwa Ankh ni nini?, kwa maelezo yao wanachosema Ankh ni kama dawa ya uzima wa milele , wengine wanasema Ankh ni kitabu cha ufunuo, sasa wewe tunataka utupe majawabu ya kipi ni kweli, pili sisi kama serikali utupatie hio Ankh ili tukutunzie , vinginevyo uwepo wako hapa nchini unaweka usalama wa nchi rehani”

“Si useme tu na wewe unachotaka ni Ankh, kwa bahati mbaya hicho kitu wanachozungumzia ni uzushi tu wa kinadharia ila hakuna kitu cha namna hio”Aliongea Hamza.

“Ongea ukweli wewe”Aliongea Afande Maningi huku akipiga kofi meza.

“Hawa wazamiaji wamesema kitu ulichokuwa nacho kimetoka kwa mwanasayansi nguli wa kihistoria maarufu kama kichwa cha Tembo au Dokta Genesha na ndani ya maabara yake aliacha anuani ya uelekeo wako na ndio maana wamekupata kirahisi hapa Tanzania. Kama ni kweli unafahamiana na Dokta Genesha basi wewe sio mtu wa kawaida, taarifa tulizokuwa nazo mpaka sasa haijulikani kama kweli Dokta Genesha amekufa ama yupo hai na hata mara ya mwisho alipozushiwa kifo chake iliaminika yupo hai baada ya kuwasiliana kwa siri na wewe, kwa mantiki hio lazima utakuwa na taarifa ya siri ambayo hutaki kuongea”

“Ushasema taarifa ambayo sitaki kuongea , kwanini nikuambie sasa Afande?”Aliongea Hamza.

“Kuwa na adabu , endelea kuongea dharau uone kitakacho kupata, unajua wewe ni nani hapa ndani? , wewe ni mfungwa na ukiendelea kuongea uongo usije kulaumu tukichukua hatua nyingne kali zaidi?”

“Elezea hizo hatua kali zaidi?”Aliuliza Hamza huku mwonekano wake ukibadilika palepale.

“Tuta..”Kabla hajaongea alizuiwa na Afande Maningi.

“Hamza huna haja ya kuwa mkali juu ya hili, sisi jukumu letu kama wanajeshi ni kuhakikisha usalama wa nchi unaendelea kudumu na kwakuwa wewe ni raia wa nchi yetu tunapaswa kujua hiki kitu kinachoitwa Ankh ni nini ili tupate namna ya kukulinda bila kuathiri usalama wa nchi , ukituambia kila kitu hatutafanya mambo kuwa magumu kwako , isitoshe tunajua wewe sio mtu wa kufanya vitu ambavyo vinaweza kuumiza usalama wa nchi”Aliongea na kumfanya Hamza kuwaangalia kwa zamu.

“Kwahio ni wewe unaetaka kujua hii siri ama ni serikali inayotaka kujua?”Aliuliza.

“Sisi kujua maana yake serikali imejua , wewe weka wazi Ankh ndio nini?”Aliongea Afande Wazo.

“Kama serikali ndio inayotakiwa kujua basi itifaki ya vyeo inapaswa kuzingatiwa?”Aliongea na kauli ile ilimfanya hata Mdudu kushangaa.

“Unataka kumaanisha nini Mr Hamza ?”

“Namaanisha kwamba taarifa unayotaka kujua ni nyeti mno na inaingia katika taarifa za juu za siri za nchi , hivyo kwa cheo chako hutoshi, itifaki hapa ifuatwe nataka kuonana na kiongozi wa juu wa jeshi Daraja S?”Aliongea na kauli ile iliwafanya wote kutoa macho.

Katika nchi yoyote licha ya Raisi kuwa na madaraka makubwa ya kujua siri nyingi za nchi haimaanishi kwamba anaweza kujua kila siri ambayo anataka kuifahamu

Itifaki ya clearence ya siri za nchi huanzia dajara E ambao hawa mara nyingi ni polisi au wanajeshi wa kawaida tu kama wa doria , siri ambazo hawa wanajua ni zile ambazo mara nyingi zinahusisha matukio ya eneo husika ambazo hazina athari kubwa za ki’usalama hata zikiwa wazi, mara nyingi maelekezo ya siri hizi hutolewa kwa mdomo tu kama onyo la kutoongea chochote.

Daraja D hili ni daraja ambalo huhusisha polisi au wanajeshi pia lakini wale polisi wa vyeo vikubwa ambao wengi wao wanafanya kazi mpaka kwenye vitengo vya usalama wa taifa , hawa wanakuwa daraja D kwasababu watu wa daraja E wote huwasilisha hizi taarifa kwao na kuamua ni siri gani iweke daraja lipi.

Daraja C hili linahusisha siri zinazoendelea katika vikosi maalumu kama vile tukio la Hamza kuua Wawindaji kutoka Samar , hio operesheni inasimamiwa na vitengo maalumu vya uchunguzi na mara nyingi hapa unaweza wakuta polisi au wanajeshi mfano wa Afande Mdudu na kuendelea.

Daraja linalofuatia sasa linakuja B halafu linafuatia daraja A , Daraja A hapa anazungumziwa raisi wa nchi , Amiri jeshi mkuu na baadhi ya viongozi wenzake wa juu, mara nyingi ikitokea siri ambayo inahitaji operesheni ndani ya eneo la tukio hapa wanahusishwa watu wa Daraja B.

Daraja B anaweza kuwa mwanajeshi yoyote anaweza kuwa hata na cheo cha Ukapteni lakini akawa na Clearence ya kujua siri zote zinazoendelea katika daraja B kwa kibali maalumu kulingana na kile anachofanyia uchunguzi.

Siri zote ambazo zinatokea katika Daraja A yaani ngazi ya raisi ambazo ni nyeti hupewa hadhi ya Top Secret na hizi watu wanaopewa Clearence ya kuziona ni Daraja S.

Sasa daraja S katika itifaki hio ni daraja ambalo lijategemea kabisa na hili ndio huwa na uwezo wa kujua siri kubwa za nchi(Top Secret) siri ambazo hata kama raisi azihitaji hapewi au kama akizitaka anapaswa kuomba ruhusa kwanza kwa watu wa hili daraja.

Raisi anaweza kujua siri za daraja S lakini ni baadhi na mara nyingi siri hizo zote huwa zinatokea katika kipindi chake cha uongozi , lakini ikitokea anahitaji siri ambazo zimetokea katika uongozi uliopita ambazo zipo chini ya Daraja S ni mpaka apate kibali ambacho kinaambatana na sababu maalumu na ikitokea akikataliwa hana cha kufanya kisheria.

Bila shaka kuna baadhi ya taarifa nyeti sana ambazo baadhi ya wanajeshi wanajua siri hizo wakati wa uchunguzi lakini hata kama walihusika kwenye uchunguzi wakitaka taarifa hio hawawezi kupewa ruhusa.

Hayo madaraja ni mfano tu ila kila taifa lina itifaki zake namna ya kutoa hizo Clearence lakini zinakuwa katika mtiririko huo katika kuhakikisha usalama wa nchi unazingatiwa.

Lakini pia kuna itifaki ambayo inahusisha kujuana nani anaclearence ya daraja lipi , kwa mfano asilimia nyingi ya wanausalama ambao wana Clearence ya daraja C hawajui nani ana Clearence(Uwezo wa kufungua) ya daraja S.

Kwa mfano kuna matukio ambayo yakawa yametokea katika uongozi wa kwanza wa serikali , matukio kama haya licha ya kwamba kuna uwezekano wa kuyafuta lakini serikali kama serikali haipaswi kuyafuta kutokana na kwamba kuna siku yanaweza yakahitajika hivyo hutunzwa katika jalada la siri nyeti za nchi.

Sasa Hamza alikuwa akitaka kutoa siri yake kwa mwanausalama ambae yupo daraja la juu kabisa ambalo ni S kitu ambacho kiliwafanya Mdudu na wenzake kumuona kama ana kichaa

“Unakichaa , wewe ni nani mpaka mpaka tukutie mtu wa cheo hicho?”Aliongea Afande Mdudu huku akionyesha kutoridhishwa na Hamza kabisa.

“Hamza unapaswa kutuambia ukweli , haina haja ya kupotezena muda la sivo tutatumia njia za mateso”Aliongea Afande Wazo.

“Mimi nimekuona kama mtu ambae una akili , lakini hapa unaonekana kama mtoto mwenye kiburi uliejaa sifa kiasi cha kutaka kuonana na kiongozi wa daraja la juu”

“Mnaongea sana , ila je kuna hata mwenye fununu kati yenu juu ya hicho kitu kinachoitwa Ankh?”Aliuliza Hamza

“Kimya , kama hutaki kuongea ukweli hatuwezi kuendelea kubembelea”

“Kwahio mpo tayari kutumia nguvu kwa ajili ya hili?, kama ni hivyo msije kwenda kinyume na maneno yenu”Aliongea Hamza kwa namna ya tahadhari

Mara baada ya kuona namna ambavyo Hamza alionekana kutokuwa na hofu , wote watatu walijikuta wakisaga meno yao kwa hasira.

Kwa yale matukio machache waliokwisha kuona walijua kabisa Hamza uwezo wake sio kichekesho , lakini bado walishangaa kama alikuwa kwenye Gereza lao la Pango kwanini bado auaonyesha ukiburi.

“Kama unataka kuonana na kiongozi ambae ana Clearence daraja S , tukuambie tu kwamba hata sisi hatuwajui hawa viongozi maana majina yao ni siri , pili hata kama tunamjua mmoja wapo ni watu ambao hatuwezi kuwaambia kiwepesi wepesi lazima hatua za maombi pamoja na sababu za kueleweka zitolewe , kwahio hili ombi ambalo unataka halina mantiki, hivyo hakuna namna tunaweza kulitimiza”Aliongea Afande Maningi.

“Kwa ulichoongea ni sahihi kabisa, kwa vyeo vyenu hapa sioni kama kuna amabe atakuwa anawajua hawa watu wa usalama wenye madaraja hayo ya Clearence , mnaonaje tukifanya hivi, kwa uelewa wangu katika kila idara ya ulinzi na usalama hapa nchini wapo wawili au watatu”Aliongea Hamza na kauli yake ilimfanya Afande Mdudu na Afande Wazo kuonyesha hali ya wasiwasi maana hawakujua Hamza imekuwaje akawa na taarifa hio maana yenyewe ni siri ya daraja C.

“Kuhusu mtu ambae nataka aje hapa kama sikosei cheo chake kitakuwa ni maarufu kama Mshauri wa jeshi”Aliongea Hamza kana kwamba anajaribu kukumbuka jina lakini kauli yake iliwafanya wale wanajeshi kushituka.

“Unafaamiana na Mshauri mkuu!!?”Aliuliza Afande Mdudu maana alikuwa akifahamu mshauri mkuu ndio huyo huyo mshauri mkuu wa jeshi.

“Mdudu anazungumzia mshauri yupi?”Aliuliza Afande Maningi , sio kama hakujua ni kwasababu kulikuwa na washauri wengi na wote walikuwa wanajeshi.

“Ni Generali, Afande Himidu Siwa , unaweza kumuita mkuu wa vitengo vyote, kwanzia kitengo cha TISA, Malibu na kuendelea, hana cheo maalumu ila anafahamika kwa jina la code kama Mshauri Mkuu, kwa muda mrefu watu wanajua mshauri mkuu wa jeshi ni mkuu wa majeshi lakini yeye ndio mshauri mkuu sasa , kwa mtu ambae upo nje ya jeshi huwezi kuelewa, Afande Himidu alipaswa kuwa mkuu wa Majeshi mara mbili mfululizo lakini alikosa kigezo cha umri na kuishia kutoa ushauri wa majina ya nani awe mkuu wa majeshi huku yeye akijipachika cheo cha ushauri mkuu”Aliongea Mdudu.

Viongozi wengi wakisiasa walikuwa wakimheshimu Afande Himidu kutokana na kwamba ndio ambae alikuwa na cheo kikubwa katika utunzaji wa siri za nchi , hivyo kwa lugha nyepesi alikuwa akijua siri nyingi mno.

Kwa namna ambavyo Hamza alikuwa akiongea ni kama Afande Himidu alikuwa akimjua na hatanii katika hilo na ndio maana iliwafanya Afande Mdudu na wenzake kuwa na wasiwasi wakijiuliza amemjuaje.

“Unatuthibitishia vipi kama Afande Himidu anakufahamu na kwanini akubali kuonana na wewe?”Aliuliza Afande Wazo.

“Akigoma kuja kwa jina la Hamza, mwambie Murphy anataka kuonana na wewe”Aliongea Hamza.

“Mafiii!?”

Afande Wazo , Afande Maningi na Mdudu hawakujua jina hilo lilikuwa linamaanga gani ila limekaa kwa kingereza.

“Fanyeni haraka maana najua yupo makao makuu ya nchi , mimi nitatumia huu muda kujipumzisha kidogo mpaka akija maana mmenichosha bure tu”Aliongea Hamza na palepale alipandisha miguu kwenye benchi na kujinyoosha akiwa amejiagamiza na kufumba macho.

Ilikuwa sawa kupumzika maana kama kweli Mshauri mkuu atatoka Dodoma mpaka kufika Dar basi inaweza kuchukua angalau masaa mawili mpaka kupanda ndege na kuanza safari.

Walikuwa hawajaridhika na maelezo ya Hamza lakini Afande Wazo alikuwa makini sana na cheo chake , hakutaka kukurupuka mpaka awasilishe ripoti kwanza kwa mkuu wa kitengo chake na kisha mkuu wa kitengo chake atoe taarifa kwenda kwa Mshauri mkuu.

“Nitawasiliana na Afande Msuya na atajua namna ya kumfikishia taarifa Afande Himidu, weka watu hapa wawe wanamwangalia”Aliongea Afande Wazo huku akitoka.

Kesi hio ya Hamza ilikuwa chini ya Mkuu wa kitengo msaidizi Afande Msuya na kwa kufuata itifaki hata kama Afande Wazo alikuwa na namba ya mshauri mkuu basi asingempigia simu moja kwa moja.

“Fanya hivyo afande , huyu haina haja hata ya kumuwekewa watu wa kuangalia , hii sehemu hawezi kutoka hata kama a na uwezo kiasi gani”Aliongea Afande Maningi na wote walikubaliana nae.

*****

Mji kuu wa kiserikali licha ya kuwa na vumbi la kuchafua pamoja na jua la saa tisa mchana kwenda saa kumi kuwa kali kwa watu wenye vyeo na matajiri hawakusumbuliwa na hali hio ya karaha ya mji.

Haikuwa nyumba kubwa sana wala ndogo sana , ilikuwa ya wastani lakini yenye mazingira ya kuvutia ambayo yaliwakilisha hadhi ya mtu anaeishi ndani ya hilo eneo katika mtaa maarufu wa Mji mpya.

Upande wa eneo la bustani ndani ya nyumba hio walionekana watu wawili mwanamke na mwanaume wakiwa wamekaa katika eneo la bustani la kupumzikia pembeni ya Swimming pool.

Mwanaume alikuwa amevalia tshirt ya rangi ya ugoro , jeans na American boot , alikuwa na kipara na muonekano wake ulikuwa wa kawaida lakini macho yake yalijaa umakini ulioonyesha utulivu wa akili..

Upande wa mwanamke aliekuwa nae alikuwa mrembo haswa alievaa akapendeza , nywele zake ambazo haikufahamika ni za bandia au asili zilikuwa ndefu na nyeusi zilizomfikia mgongoni , alikuwa amevalia kana kwamba ni mgeni ambae yupo ndani ya hilo eneo kwa ajili ya kumpagawisha mwanaume aliekuwa pembeni yake.

“Ni watu wachache sana ambao wanaweza kucheza mchezo wa Chess hapa nchiin na mmoja wapo ni wewe Sophia . ijapokuwa nakwenda kushinda hii mechi lakini niseme umezidi kuimarika tokea mara ya mwisho tulivyocheza pamoja , sio mbaya licha huwezi kunishinda pengine siku zijazo utafanikiwa ukiendelea na mwendo huu huu”Aliongea yule mwanaume kwa sauti nzito na kisha alichukua chupa ya maji na kunywa kidogo huku akimsubiria yule mwanamke mrembo kucheza.

Wawili hao walikuwa makini katika kucheza mchezo maarufu wa Chess.

Mwanamke yule mrembo alionekana kukodolea ubao ule wa kuchezea kwa macho yenye hali ya kutafakari kwa kina, upande wa mwanaume simu yake ya batani iliokuwa na mkonga mkubwa ilianza kuita na aliichukua na kuipokea.

“Ongea!”Alitikia akiwa sirasi , mara nyingi akipokea simu kupitia simu hio basi ni ya kikazi ndio maana anakuwa siriasi.

“Mshauri mkuu , jina langu ni Afande Msuya..”

“Hebu acha kuzunguka nishakufahamu , nenda moja kwa moje kwenye pointi”Aliongea kwa sauti ya amri kama mtu ambae hakupendezwa kupigiwa simu hio.

“Sawa afande , ipo hivi kuna operesheni maalumu ya ki uchunguzi ambayo inaendelea hapa kitengoni chini yangu , katika operesheni hii tumeweza kumkamata mtuhumiwa anaefahamika kwa jina la Hamza Mzee , nimepokea simu kutoka kwa wanausalama wakiwa wanamfanyia mahojiano na amekataa kutupa taarifa na anataka kuonana na wewe Afande”Aliongea .

“Hamza Mzee!!”Aliongea yule bwana huku akionekana kama vile anawaza wapi amesikia hilo hina lakini hakukumbuka.

“Simfahamu mtu wa jina hilo mimi , hili swala mnaweza kudili nalo wenyewe sidhani linahitaji ushauri wangu , sitaki ripoti za namna hii kuripotiwa kwangu”Aliongea na muda ule wakati akitaka kukata simu upande wa pili uliropoka.

“Anasema Murphy anakuita”Aliongea na jina lile lilimfanya yule bwana mwenye sura ya maji ya kunde kukunja sura kiasi cha kumfanya mwanamke mrembo aliekuwa pembeni yake kumwangalia kwa wasiwasi.

“Wewe.. umesemaje hebu rudia vizuri?”

“Amesema kama humtambui kwa jina la Hamza, nikuambie Mafi…. Murphy anakuita”Sauti upande wa pili ilirudia na kumfanya yule bwana kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Waambie wanisubiri wasifanye chochote , narudia huyo mtu ambae umesema anaitwa Hamza asichokozwe , nitafika hapo ndani ya lisaa limoja au mawili yajayo kwa kutumia chopa ya jeshi”Aliongea kwa msisitizo.

“Mshauri ni kweli unafahamiana na huyu Hamza?”Upande wa pili uliuliza kwa namna ya mshangao.

“Hata mimi simjui ni nani mpaka nimuone mwenyewe”Aliongea na kisha palepale alikata simu.

“Sophia nataka kwenda Dar es salaam mara moja , nina haraka , vipi tuongozane wote?”

Mwanamke huyo mrembo alievalia nguo za rangi nyekundu aliishia kutingisha kichwa kukataa bila ya kusema neno.

“Naona kwa leo mechi yetu inaishia hapa , isitoshe sikuwezi na nakufanya usifurahie mchezo, nakuombea apatikane mtu wa kuendana na uwezo wako”Aliongea kwa namna ya kuvutia kana kwamba anamtega.

“Nadhani kuna kitu kingine tunaweza kupimana uwezo”Aliongea na kauli yake ilimfanya yule mrembo ukauzu kumvaa palepale na ghafla tu aliinua mkono wake wa kulia na kuanza kuchezesha vidole katika muundo wa ajabu na hazichukua sekunde vitu kama moshi moshi ulitawala vidole vyake.

“Upo sahihi , siku nyingine nitakuonyesha ufunuo niliopata kwenye kuvuna nishati za mbingu na ardhi”Aliongea .

“Naisubiri hio siku kwa hamu kubwa”Aliongea Afande Himidu na yule mwanamke alitingisha kichwa na kisha akasimama na kitendo cha kuinama kama mchawi alipotea palepale.

********

Masaa kama mawili mbele katika eneo la kambi ya jeshi walionekana Afande Mdudu na wenzake wakipiga saluti mbele ya Kamanda Himidu anaeshuka kwenye chopa huku wakijitahidi kupotezea wasiwasi wao na tabasamu la kulazimisha.

“Afande umetokea ghafla sana , tulikuwa tukipanga kuja kukupokea na escort”Aliongea Afande Wazo lakini upande wa Afande Himidu hakuwa na muda wa kuongea nao kwani baada ya kutoka kwenye chopa aliwapita.

“Huyo Hamza yupo wapi?”Aliuliza

“Yupo ndani ya Dragon Lair Afande”

“Nini!, yaani mmefungia ndani ya hilo gereza, vipi hakuwaletea ukinzani wowote?”Aliongea huku akionyesha mshangao kidogo.

“Afande hakuleta ukinzani pengine ameogopa wingi wetu , anaweza kutushindwa mmoja mmoja lakini kwa wingi wetu hawezi kufanya chochote”Aliongea Afande Wazo kwa majigambo.

“Una akili kweli wewe , unajua hata ninachomaanisha , nakuuliza je mpo salama?”Aliuliza lakini swali lake liliwachanganya.

“Afande unauliza nini kuhusu usalama?”Aliuliza lakini Afande Himidu hakutaka hata kuwaelezea kile anachoataka kumaanisha.

Afande huyo mara baada ya kuingia ndani na kumwangalia Hamza kupitia kioo kizito kilichokuwa mbele yake mshangao ulivaa palepale huku pumzi yake ikiwa nzito ni kama vile ameona mtu ambae hakutarajia kumuona.

“Mshauri yule ndio Hamza”Aliongea Afande Maningi.

“Nani alietoa wazo la kumfungia pale?”Aliuliza akiwa siriasi na kuwafanya Afande Wazo na Afande Maningi kuangaliana , wao sio ambao walikuwa wamemkamata Hamza Afande Mdudu ndio alifanikisha hilo na wao walipewa jukumu la kumhoji pekee.











SEHEMU YA 77.

Baada ya wote kumwangalia Afande Mdudu na Mshauri pia alimwangalia Mdudu akionekana anahitaji maelezo na kumfanya afande huyo sura yake kuzidi kuwa nyeusi.

“Afande naripoti kwako.. mimi ndio nimemkamata”

Afande Mdudu hakuona haja ya kujificha muda huo hivyo aliamua kuuvaa ujasiri na kusogea mbele.

Ukweli ni kwamba hata alipoomba ruhusa kwa mkuu wake wa misheni Afande Msuya alipewa maelekezo ikitokea ameshindwa kumkamata Hamza basi ajisalimishe kama alichukua maamuzi peke yake , ijapokuwa ilikuwa kweli Msuya alikuwa akitaka kumkamata Hamza lakini alipingana na wazo hilo kwa kuhofia kile ambacho anaweza kufanya lakini Mdudu alilazimisha.

“Afande nimemkata kwasababu mpaka sasa ameua watu wengi , tulikuwa na wasiwasi ataende…”

“Haina haja ya kuendelea kuongea”Aliongea Afande Himidu akimkatishia njiani .

"Mdudu kama niko sawa wewe ni mtoto wa pili wa Mkuu wa Majeshi aliepita Afande Mbwana?”

“Ndio afande , babu yangu pia ni waziri mkuu mstaafu”Aliongea kwa kujiamini.

“Huna haja ya kuendelea kuelezea vyeo vya wanafamilia yako , japo ni kweli familia unayotokea ni ya watu maarufu lakini haitoshi katika hali kama hii”Aliongea na kumfanya Afande Mdudu kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa.

Ukweli alikuwa akijiamini katika sehemu nyingi , sifa za jina la familia yake lilikuwa likimtangulia katika maeneo mengi , sasa alijiuliza inakuwaje jina lake hapo lisitoshe au Afande anajaribu kuongea kitu gani.




“Afande umeulizia kuhusu familia yangu , hili swala lina uhusiano?”Aliuliza.

“Unaweza kufikiria unachoweza , ila itakuwa vizuri kama ukiongea na baba yako kwanza umwelezee kilichotokea leo, pengine inaweza kukusaidia”Aliiongea lakini kauli yake ilizidi kumchanganya Mdudu kwani hakuwa akijua ni kitu gani amekosea..

Hata upande wa Afande Wazo na Maningi hawakuelewa Mshauri anachojaribu kumaanisha.

“Acha kuonyesha dalili za kuchanganyikiwa , ninachomaanisha hapa fanya kila namna kuokoa maisha ako”Aliiongea.

“Lakini Afande baso sielewi , sijui kama kuna kosa lolote nimefanya kiasi cha kutaka kunipa adhabu”

“Una uwezo mdogo wa kufikiria na sijui aliekupatia uongozi wa hii kesi alikuwa akilenga nini , ninachomaanisha yule mtu akitoka unaweza usiwe salama na akiamua kukuua sitoweza kumzuia”Aliongea na mara baada ya kusikia maelezo hayo alijikuta akitetemeka.

“Lakini Afande huyu si mfungwa , kwani tunamuachia atoke?”

“Afande anachoongea ni sahihi , sidhani kuna haja ya kumuachia huru , ana siri juu ya kitu kinachoitwa Ankh na inaonekana ni siri ya thamani kubwa mno inayofuatiliwa na watu wengi kiasi cha kuhatarisha usalama wa nchi”

“Ndio Afande Hamza yupo pale na hakuna namna anaweza kutoka kwa hiari yake labda tumuachie bila ya kujali uhalifu wake”Alikazia Afande Mdudu.

Lakini Afande Himidu hakuwa akiwasikiliza kwa maneno yao, macho yake yalikuwa yamemkazia Hamza ambae alikuwa ashasimama tayari na kusogelea kioo huku akijivuta.

Japo kwa ndani ya chumba hicho ilikuwa ngumu kuona anaengalia nyuma ya kioo lakini muda ule ni kama Hamza alikuwa akiangaliana na Afande Himidu kwani alitoa tabasamu la ishara ya salamu na kumfanya hata Afande Himidu kutabasamu pia, huku macho yake yakionyesha ishara ya heshima kwa Hamza.

“Hebu fanyeni haraka , mfungulieni atoke”Aliongea kwa sauti kubwa iliojaa ubabe.

Kundi hilo la wanajeshi waliishia kusita kupokea maagizo hayo , hawakujua wamuachie Hamza au wasimauchie , isitoshe kwao walimuona kama mhalifu na Mshauri anataka kuvunja sheria.

Lakini sasa kilichotokea baada ya hapo kiliwafanya kuganda kama vile wamegeuka mawe ya barafu.

Hamza alikuwa akipiga piga kuta za eneo hilo la ndani kana kwamba anajaribu kuona ni wapi kuna udhaifu na uimara, baada ya kuonyesha kuridhika na kugonga gonga alisogelea kioo na kuweka kiganja cha mkono huku akionekana kufumba macho.

“Anajaribu kufanya nini , au amepatwa na uchizi wa ghafla?”Mmoja aliongea kwasababu waliamini kioo alichoshika Hamza kilikuwa ni kioo kigumu mno ambacho ni kipana kiasi kwamba hakiwezi kupitisha risasi wala kupasuka kwasababbu ya mlipuko.

Afande Maningi palepale wasiwasi ulimwingia na alibonyeza kitufe ambacho kinasafirisha sauti.

“Mr Hamza tunakuomba utulie tutakuachia muda si mrefu”Aliongea , alijua kama kweli Hamza anafahamiana na Afande Himidu basi kuna uwezekano asiwe wa kawaida.

Isitoshe walikuwa ni wanajeshi wa kitengo cha kupambana na nguvu za ziada na kupitia uzoefu na stori nyingi walizosikia juu ya mafunzo mbalimbali ya maajabu walipatwa na hisia za hatari wakiamini Hamza anaweza kuwa na hayo mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi.

Hamza aliendelea kushikilia kile kioo kwa nguvu na alioekana kama mtu ambae anasali kwani midomo ilikuwa ikicheza kwa kuongea na kabla hata wale wanajeshi hawajachukua hatua ya kumfungulia eneo hilo lilianza kutetemeka kama vile ni mtikisiko wa ardhi.

Kitu kile kiliwafanya watoe macho washindwe kujua nini kinakwenda kutokea.

Wakati wakishangaa ghafla ule mtikisiko ulipotea lakini Hamza bado alikuwa ameshikilia kile kioo huku akiwa amefumba macho na kuendelea kuongea maneno.

Ghafla tu macho yaliwatoka mara baada ya kile kioo walichoamini hakiwezi kupasuka hata kwa nyundo kikianza kutengeneza nyufa taratibu kana kwamba kinapata kiwango cha juu cha moto ,hazikupita sekunde kumi kioo chote kama vile ni glasi imedondoshwa chini kwani kilipasuka vipande vipande.

Bahati ni kwamba kioo hakikuwa kimoja pekee kulikuwa na layers angalau tatu za vioo vinavyofanana.

“Afande wazo si umesema hivi vioo haviwezi kupasuka hata kama vipigwe na bomu?”Aliuliza Afande Mdudu huku akitetemeka.

“Inawezekana vipi kupasua kioo bila ya kutumia nguvu?”Afande Wazo aliekuwa kwenye bumbuwazi.

Ilikuwa ngumu kukubali maana walitumia kiasi kingi cha pesa kwa ajili ya ujenzi wa hilo eneo , lakini namna ambavyo Hamza alikuwa akividondosha sio uwezo wa kawaida.

Hamza kabla hajafikia kioo cha mwisho Afande Wazo alishikwa na hasira , alitaka kujihakikishia kama ni kweli vioo hivyo vilikuwa vigumu au kuna tatizo , hivyo mara baada ya kushika bunduki alianza kuvimiminia risasi. Lakini hakuna risasi hata moja ilioacha hata ufa kwani zilidunda tu na kudondoka chini.

“Hakuna haja ya kufanya majairibio , hakuna tatizo kabisa na ujenzi wa hili eneo, Shida ni kwamba ana uwezo mkubwa mno na wa ajabu”Aliongea Afande Himidu huku macho yake ni kama amefurahi kuona tukio kama hilo.

Hatimae vioo vyote vilipasuka chini bila ya kupigwa ngumi zaidi ya kuwekewa kiganja cha mkono tu.

“Kuna mwenye sigara kati yenu?”Aliuliza Hamza mara baada ya kutoka nje lakini kila mtu alikuwa amemkodolea macho kana kwamba wameona mnyama.

“Mnashangaa nini sasa , au hamhawahi kuona kioo kikipasuka?”Aliongea Hamza na Afande Himidu ndio aliekuwa wa kwanza kushituka.

‘”Inamaana hamjamsikia , hakuna mwenye sigara kati yenu?”Aiuliza na Afande Wazo kwa kutetemeka aliingiza mkono kwenye mfuko wake wa kombati na kuchomoka na sigara na kibiriti.

Upande wa Afande Himidu hakushangaa Hamza kuhitaji sigara , kwa mtu wa kawaida anaweza kuona Hamza hakutumia nguvu kupasua vioo hivyo lakini kwa uelewa wake alijua Hamza ametumia nguvu nyingi tu japo sio zote, kutengeneza resonance pacha kwenye kitu kigumu kama hicho haikuhitaji tu nguvu lakini matumizi makubwa ya ubongo ili kupatia hivyo hufanya akili kupata hali ambayo inaweza kuondolewa na sigara au kilevi.

“Kijana naona una mabadiliko makubwa mno , umepata mke nini?”Aliongea Hamza akimshika bega Afande Himidu huku wakiwa na tabasamu .

Kwa namna ambavyo Hamza alianzisha mazunguzo na afande wa heshima kama huyo iliwafanya Mdudu na wenzake kuzidi kushikwa na wasiwasi.

“Kama ningekuwa nimeshaoa wewe ungekuwa wa kwanza kujua , yaani nifunge ndoa bila ya kukualika mlevi kama wewe”Aliongea Afande Himidu huku akicheka,

“Haha……utaachaje kunialika na unavyopenda vitu vya mteremko , sidhani bila kutoa mchangao wangu utataka kuoa wewe”Aliongea na kumfanya Afande Himidu kujikuta akicheka mpaka mabega yanamtingishika.

Muda huo Hamza akipata muda wa kuangalia watu waliokuwa ndani ya eneo hilo na aliweza kuona kila mtu alikuwa akimwangalia kwa wasiwasi.

“Nyie watu haina haja ya kujenga upya hivyo vioo , ni kujitia hasara tu”Aliongea Hamza huku akiwa na tabasamu la kejeli lakini Afande Wazo na Afande Maningi walikuwa na wasiwasi mno.

“Ndio Afande tumekuelewa” Aliongea Afande Maningi huku hana uhakika kama kumuita Hamza afande ni sawa , alijaribu kubahatisha kwa namna yoyote ile ili kumtuliza asichukue hatua.

Muda ule Hamza macho yake yalitua kwa Afande Mdudu ambae alikuwa akijificha ficha kana kwamba anatamani kuikimbia hilo eneo.

“Afande Mdudu unajua umefanya kosa gani leo?”Aliongea Hamza na Afande Mdudu alijikuta akitetemeka kwa hofu.

“Sikupaswa kukukamata .. naomba msamaha wako”Aliongea

“Kunikamata halikuwa kosa kwasababu ulikuwa ukifuata sheria na ulikuwa na ushahidi , mtu kushurutisha watu kutii sheria sio kosa hata kidogo”

“Basi kosa langu itakuwa ni kutokukuheshimu?”Aliongea huku aking’ata meno kwa hasira , mpaka dakika hio ameshindwa kujua kabisa Hamza ni mtu wa aina gani mbona anatisha.

“Mimi sio mtu wa kukasirika kwa vitu vidogo vidogo kama hivyo , hata mimi nisingekuongelesha kwa upole, kosa lako kubwa ni ni kujaribu kunitengenezea udhaifu mbele ya mwanamke huku ukiwa na uhakika mimi ni mhalifu, umeshindwa kunikamata nikiwa Kijichi na kuniwekewa mtego njiani, mpango wako haukuwa kunikamata ila kujaribu kunidhalilisha”Aliongea Hamza huku akionyesha hali ya ukauzu na swala lile lilimfanya Afande Himidu kuingiwa na wasiwasi.

“Ni mtoto wa pili wa mkuu wa majeshi Afande Mbwana, babu yake pia alishawahi kuwa Waziri mkuu”Aliongea.

“Nishayajua hayo yote tokea muda tu , lakini kuwa mtoto wa nani haimaanishi ndio tiketi ya kuachwa afanye atakavvo”

“Unapanga kumuua?” Aliuliza. Afande Himidu akiwa na wasiwasi na Afande Mdudu kwa woga alipiga magoti mbele ya Hamza.

“Hamza naomba unisamehe , nilikosea kweli”Aliongea lakini Hamza ni kama hakuwa hata na hio hasira ya kumuua kama alivyoulizwa , alitaka kumtishia kidogo tu.

“Nikikuua mtu kama wewe nitaonekana kama mtu ambae naonea dhaifu, onyo langu kwako usije kumsumbua Yonesi tena”Aliongea Hamza na mara baada ya Mdudu kusikia kauli hio alijikuta akipatwa na ahueni huku akijiambia kwa muda huo ataacha kumsumbua Yonesi lakinin sio kama atamwacha kabisa.

“Asante sana Hamza” Aliongea huku akijifuta , licha ya kwamba alikuwa mwanajeshi lakini ukweli ni kwamba alilelewa kimayai sana kutokana na utajiri wa familia yao hivyo kumfanya kuwa mjivuni sana.

Sababu ya Hamza pia kutomfanya kitu chochote Afande Mdudu ni kwa ajili ya Afande Himidu, alikuwa ni rafiki yake hivyo hakutaka kumuingiza kwenye matatizo.

“Mnaweza kutoka nje sasa , nataka kuongea na Hamza, hakuna anaeruhusiwa kusogelea hapa”Aliongea Afande Himidu mara baada ya hali kutulia.

Wote baada ya kutoka nje Afande Himidu ghafla tu alipiga goti kwa mguu mmoja huku akiongea kwa unyenyekevu

“My Prince!!”

“Inatosha Bro , kwanini unafanya hivi kama watu wengine bwana , hatujaonana kwa zaidi ya miaka sita lakini naona bado hujasahau hizi itifaki, nakumbuka kipindi kile ukiwa kambini ulikuwa mjeuri mno lakini baada ya kuimarika ukawa humble”Aliongea Hamza.

“Hakuna mtu yoyote ndani ya Tanzania hii naweza kumpigia magoti , hata awe raisi , kwangu hii ni ishara ya kukuheshimu kama mwalimu wangu na bosi wangu”Aliongea Afande Himidu huku akiwa na tabasamu.

“Haha. Vizuri , lakini naona sasa hivi unaitwa Himidu Mshauri , jina lako la Murphy Stopphilius umelitelekeza , huwa na kukubali sana maana hubadiliki sio kama rafiki yako Mameni”Aliongea Hamza.

Kitu ambacho hawakukijua wakina Afande Wazo na wenzake ni kwamba Murphy halikuwa jina la Hamza bali ni la Afande Himidu.

“Ukweli miaka miwili iliopita niliposikia umestaafu mwanzoni sikuwaza ni wapi utaenda , lakini nikikumbuka kipindi kile ulivyokuwa ukinisumbua kufahamu kiswahili nilijua tu lazima utakuwa hapa nchini na hisia zangu zilikuwa kweli , nimefurahi kukuona sana bosi”Aliongea.

“Mwaka wa kwanza wakati nafika hapa nchini nilikuwa nikijiuliza nikutafute au nipotezee , isitoshe kati ya marafiki zangu wote wewe ndio ulikuwa mtanzania pekee, lakini mara baada ya kupata taarifa umejipenyeza kwenye jeshi la Tanzania niliona nisikusumbue , isitoshe mpango wangu ulikuwa ni kuishi maisha ya chini chini”

“Bosi hata usiwe na wasiwasi naelewa..”Aliongea huku akimwangalia Hamza kwa namna ya kumchunguza..

“Lakini bosi kwanini naona kama umebadilika sana , mbinu uliotumia kupasua vioo haifanani kabisa na ile niliokuzoea nayo?”Aliongea na kauli ile ilimfanya Hamza kucheka.

“Ndio sijatumia kabisa mbinu ya nishati za mbingu na ardhi maana nishaachana nazo?”

“Kama ni hivyo umetumia mbinu gani sasa?”Aliuliza huku akiwa anashangaa , ukweli ni kwamba hakujua kabisa ni kitu gani kinaendelea kuhusu Hamza.

“Usiwaze sana nimeachana na mbinu zote zilizozoeleka sasa hivi nipo kwenye kitu kingine kabisa”

“Boss kila siku unaonyesha wewe sio mtu wa kawaida , yaani umepata mbinu mpya na umeweza kujifunza ndani ya muda mfupi tu na sasa unaonekana kama mtu mwingine , yaani unatufanya sisi binadamu wa kawaida tukose kabisa hata tumaini”

“Hehe.. unawaza nini sasa, kama tungefanana unadhani ningekuwa bosi wenu wewe mshenzi, huna haja ya kuwaza sana labda kama unataka kunipindua”

“Hamna bosi bado najichukulia nipo chini ya himaya yako mpaka sasa. halafu sio kama nina cheo kikubwa tokea nirudi kuliko kule”

“Huko nako ndio kujihusha , ndani ya miaka saba uliorudi nchini umeweza kuingia ndani ya kitengo cha Malibu na baadae kuwa mshauri wa vitengo vyote vya usalama na ulinzi na kupanda cheo mpaka kuwa jenerali , sio kazi ndogo kulingana na umri wako”

“Mafanikio yangu ni kama kichekesho nikijaribu kulinganisha na yako , isitoshe kwa kujilinganisha na wenzangu niliowaacha sidhani napaswa kusema nina mafanikio ya juu”

Hamza aliona alichoongea kinaleta maana , isitoshe kwa kipindi kirefu walichokuwa chini yake, alikuwa kama kikwazo kwa mafanikio yao , lakini wengi baada ya kuwaachia na kurudi kwenye mataifa yao waliweza kupata mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi.

Walijikuta wakiongea kwa muda mrefu kidogo mpaka muda ambao Afande Himidu alikumbuka swala la Ankh.

“Bosi vipi kuhusu hili swala la Ankh , kwannini watu wanakufualitia nalo sana au ulikuwa mtego wa Genesha?”

“Genesha aliiniingia kwenye majaribu ni kama ananiambia hata kama nimekufa huwezi kuishi kwa amani , unadhani ni nani kajua kuhusu hii siri kama sio yeye alieisambaza , mtu ananipa kitu halafu anawapa watu taarifa ili waanze kuniwinda , huyu alichotaka ni kuona sipati amani.

Hivi unajua ndio alinirudisha hapa Tanzania , baada ya kunitumia ujumbe wa kila aina kwamba anakaribia kufa na yupo hapa hivyo nionane nae kwa mara ya mwisho , lakini sikujua kama aliacha anuani kwenye maabara yake ili ijulikane nipo Tanzania.

“Nini! , kwahio unamaanisha Dokta Genesha alifia hapa nchini, maiti yake..”

“Nilimtupia baharini , aliniambia mwenyewe niifunge maiti yake na jiwe zito na kisha nimtupe”Aliongea Hamza huku akiwasha kwa mara nyingine sigara na kuvuta moshi kidogo.

“Kama ni hivyo bosi , vipi kuhusu hii Ankh , ni siri gani , maana kwa ninavojua kama nipo sahihi Ankh maana yake ni alama ya msalaba ambayo ilikuwa ikiwakilisha uhai ndani ya Misri ya kale , si ndio?”

“Upo sahihi Ankh ni ishara ambayo alitengeneza Nekhbet mungu wa Misri ya kale kama ishara ya zawadi ya uhai kwenda kwa Farao, sababu ya dokta Genesha kuipa siri hii Ankh ni kwasababu ni siri ambayo inahusianisha na uhai wa binadamu, ushawahi kusikia mtu yoyote anasema simulizi ya njiwa juu ya mti wa Uzima?”Aliongea Hamza.

“Nakumbuka nilishawahi kusoma hiki kitu kwenye Deep web , nilichukulia kama uzushi lakini walisema kuna Dokta kagundua siri juu ya kwanini binadamu anakufa mapema?”

“Unadhani nimeanza kukuelezea juu ya Nekhbet ili ulichukulie hili swala kama hadithi za kale?”Aliuliza Hamza.

“Kwahio Bro unasema Ankh ni kitu cha enzi ya Farao au unamaanisha nini?”

“Kama nilivyokwisha kusema Ankh kama Ankh ni ishara tu ambayo imetumika kuficha siri juu ya hatua za uhai wa binadamu ulivyo , chukulia ni kama maandiko ya enzi hizo yameonekana sasa hivi kwa ligha ngumu isioweza kutafsirika”

“Kwahio bosi kama ulichoshikilia ni kanuni , si inamaanisha umeshika siri ya dunia , sidhani ni makundi ya kihalifu tu ambayo yanaweza kupigania, hata nchi zitajiingiza katika vita za kupata hiki kitu”

“Enzi ya kale watu walikuwa tayari kusafiri kwa kuvuka bahari kwa ajili ya kutafuta namna ya kurefusha maisha lakini sasa hivi sio kutafuta bali sayansi imeendelea na wanasayansi wanakaa tu maabara kufanya tafiti za kutengeneza madawa , lakini mtu yoyote ukimwambia kama kuna uwezekano maisha yakarefushwa na dawa atakuona kichaa tu”Aliongea Hamza na kumfanya Himidu kutingisha kichwa kukubaliana nae.

“Kwahio bosi kama ulichoshikiria ni kanuni juu ya siri ya uhai wa binadamu , je imewezwa kufanyiwa utafiti?”

“Hapana , Genesha alijaribu kufanyia utafiti ili kuweza kuitafsiri lakini alishindwa , kulingana na maelezo yake ana uhakika kabisa ni kitu ambacho kinaweza kubadilisha mtazamo wa binadamu juu ya uhai , lakini kutokana na msongo wa mawazo juu ya mke wake yalimshida hivyo aliniachia kila kitu na kisha akajiua , nadhani unajua nisingeweza kumzuia kama alitaka kujiua mwenyewe”

Afande Himidu alijikuta akivuta pumzi ya ahueni ,ukweli kulingana na mtazamo wake anaomba isiwe kweli , aliona kama kweli binadamu atajua namna ya kurefusha maisha , basi atakuwa kiumbe hatari zaidi kuliko hata siraha za nyuklia.

“Mimi kwangu naona hizi ni kama stori tu na uwezekano huo haupo?”Aliongea Himidu.

Hamza licha ya kuamua kumwambia ila hakutaka kumpa ukweli wote , isitoshe kuna misheni ilikuwa ikiendelea kuhusu yeye chini chini

“Ukweli ni kwamba Ankh ni ni nadharia ambayo wanasayansi wanayo tayari”Aliongea Hamza.

“Kivipi?”

“Kwanza unajua namna mwili unavyofanya kazi , mfano tu chukulia seli ambazo zinazunguka utumbo zinajigawa kila baada ya siku tatu mpaka tano na kuweka nyingine , sio hivyo tu kila baada ya miezi miwili seli za kibofu cha mkojo zinajiondoa na kuwa zingine , seli za damu zenyewe zinabadilika kila baada ya miezi minne , maana yake ni kwamba asilimia tisini na nane ya seli zote zilizopo ndani ya mwili wetu zinaondolewa na hewa na chakula kwa mwaka , kwa ligha nyepesi ni kwamba kila mwaka mmoja ukipita mwili wako umebadilika vitu vingi sana, sasa kadri mwili unavyoendelea kwa kasi kuzalisha seli mpya na kuhamisha zile zilizokufa huo mchakato unazuia mwili kuzeeka , , hivyo kama mchakato huu ni endelevu bila kupungua nyakati zote basi binadamu asingekufa mapema, ukichana na swala la kuugua na kupata ajali”

“Kama ni hivyo sasa kwanini sisi binadamu bado tunaendelea kuzeeka?”Aliuliza Afande.

“Kwasababu inafikia hatua ule mchakato wa seli kugawanyika ndani ya mwili na kutengeneza mpya hupungua kabisa , huu mchakato wote unadhibitiwa na DNA, Chukulia urefu wa uhai wako ni kama kamba ya kiatu, kadri unayotoka mwanzo wa kamba kueleleka mwisho wa kamba ndio namna unavyopunguza siku za uhai wako kutokana na seli za mwili kutojigawa na kutengeneza mpya , ukifika mwishoni mwa kamba unakutana na kile kichopoo ambacho kimeifunga kamba kuonyesha ndio mwisho, sasa pale ndio mwisho wa seli za mwili kujitengeneza upya , ukizungumzia kisayansi sasa DNA ina muundo kama wa kamba kwani mwishoni mwa urefu wake kumefungwa kitu kama kichopoo ambacho kisayansi kinaitwa Telomere.

Sasa chukulia kitendo cha kutaka kuongeza urefu wa kamba ndio kuongeza urefu wa maisha ya binadamu , utakachofanya ni kuondoa kile Kichopoo na kutafuta kamba inayofanana kwa asilimia mia moja na ulokuwa nayo kisha kutafuta namna ya kuunganisha ile kamba bila kubadili muundo wake na mwisho wa siku utafanikiwa kuiongezea urefu, ukichukulia huo mfano katika muundo wa DNA utakuwa umeongeza urefu wa maisha yako, hiki ndio kitu ambacho Genesha anaamini kipo katika siri ya Ankh”Aliongea Hamza.

Ijapokuwa hakuwa mwanabailojia lakini kwa kiasi kidogo alihisi kuelewa alichokuwa akitaka kumaanisha juu ya itu kinachoitwa Ankh.

“Inaonekana nadharia yake inaleta maana kwa kiasi flani , lakini kwasababu haikukamilika na kanunni imeshindikana kutafsirika kutokana na lugha yake si inamaanisha ni kitu ambacho hakitowezekana, kwanini akaamua kukupatia wewe hii siri ya Ankh?”

“Kwasababu anaamini kazi kubwa amekwisha ifanya , kwa maelezo yake anaamini kuna elementi moja ambayo haijagundulika bado na inaweza isigundulike kama tu kutakosekana tafsiri ya Kanuni ya Ankh , elementi hii ameitaja kama Elementi ya Nuru na kama ikipatikana basi kila kitu kitabadilika”

“Kwahio bosi Dokta Genesha anaamini fumbo la hii elementi litapatikana katika tafsiri ya kanuni hio ya Ankh?”

“Uwezekano huo upo ila sina uhakika , kuna uwezekano hii elementi isiwepo kabisa hapa duniani au hata angani katika sayari nyingine”

Ilikuwa ni siri nzito sana juu ya Ankh aliopata kuisikia Afande Himidu ,ijapokuwa aliona Hamza hakuwa ameielezea vizuri kueleweka lakini aliona pengine kuna sababu ya Dokta Genesha kumpatia Hamza, hata hivyo alijiuliza kwanini maana Hamza sio mwanasayansi.

“Bosi hiki kitu ni kama kiazi cha moto ni kheri ubakie nacho tu , sitouliza tena kuhusu hili , kuna kila sabababu ya Dokta Ganesha kutotaka tafiti zake zipotee , lakini hata hivyo swala hili likijulikana kwa watu wachache ni bora zaidi”

“Ndio maana nilitaka kuongea na wewe , ili uweze kutuliza shauku wanayoanza kuipata wanajeshi wenzio , siku zote watu wakinifuata niliishia kuwaambia simulizi ya njiwa juu ya mti wa uzima ni uzushi tu, nafanya hayo kwasababu nataka watu wasahau, vyovyote vile hata kama ikitokea kanuni yote nimeijua nitaenda nayo kaburini , sioni kama kuna faida ya binadamu kuishi muda mrefu, hivyo hakikisha uchunguzi wowote unaendelea kuhusu mimi uachwe mara moja , sio salama watu wengi kuanza kuulizia kuhusu Ankh , wakikusumbua wewe waonyeshee dole”Aliongea Hamza na kufanya Afande Himidu kucheka.

“Bosi usiwe na wasiwasi , hii ni siri yagu na wewe kwanzia sasa , hata taarifa azitake Mfalme Nyoka”

“Haha.. halafu huyu Mfalme Nyoka sijamuona kwa muda mrefu , unadhani atakuwa amenipita ki uwezo kwasasa?”

“Kama ni kipindi cha mwanzo ningeweza kusema unamuweza , lakini sasa hivi naona umeua nguvu zako zote za nishati , hivyo ni ngumu kutabiri chochote”

******

Waliongea mambo mengi mno mpaka juu ya Hamza kuoa, na Afande Himidu alitaka kujua imekuwaje kuwaje Hamza akaoa lakini Hamza alimwambia ni stori ndefu.

Alimwambia kama ni stori ndefu basi amtambulishe kwa shemeji, Hamza aliona sio mbaya kumtambulisha kwa Regina , hivyo alimwambia wakitoka hapo watafute sehemu kwa ajili ya chakula cha usiku na ampigie simu Regina kufika.

Afande Himidu alitoa maagizo kwa makamanda waachane na uchunguzi wote unaohusiana na Hamza kwanzia dakika hio na wiki inayofuatia atafika makao makuu kutoa maelekezo zaidi.

Kwasababu maneno yake ni sheria wote walikubali na kisha waliondoka huku bado wakiwa na maswali mengi , kati yao ambae hakuwa ameridhika kwa kiasi kikubwa alikuwa ni Afande Mdudu.

Baada ya Hamza kuingia kwenye V8 ya Afande Himidu ili kutafuta sehemu kwa ajili ya kupata chakua cha usiku , Hamza alitumia nafasi hio kumtafuta Regina na kumuuliza kama yupo free wakapate Dinner lakini Regina alisema yuko bize na kazi hivyo Hamza hakujishughulisha nae zaidi.

Japo Himidu alitaka kujua Hamza kashikika kwa nani lakini mara baada ya Hamza kumwambia haiwezekani kwa siku hio kukutana na shemaji yake aliamua kuridhika . Hamza hakumwambia kama ni Regina mmiliki wa makampuni ya Dosam , alitaka kuweka cheo chake pembeni na kutambulisha Regina kama Regina.

Hamza kwasababu alikataliwa na Regina kutoka wote Dinner aliona haina haja ya kwenda mjini kwa ajili ya chakula bali walichukua barabara ya kuelekea Kijichi kwa Dina.

Himidu alishangaa kuona Hamza alikuwa na mahusiano na Dina , alikuwa akimjua sana Dina kutokana na faili nyeti la mtandao wa Chatu alikuwa amekwisha kulisoma.

Kwa Hamza ilikuwa kama sherehe ya kukutana na rafiki yake na kwasababu ilikuwa wikiend walijiachia mgahawani kwa Dina na baadae wakabadilisha kijiwe na kwenda mjini zaidi.

Himidu aliamua kutumia pesa zake kuhakikisha Hamza anayafurahia maisha na Hamza hakuona shida.

Hamza upande wake hakusahau kumpigia simu Prisila na kumpa taarufa alishatoka , taarifa ambayo ilikuwa nuri kwa Prisila.

Hamza hakufanikiwa kurudi nyumbani kabisa siku hio na kuishia kulala nyumbani kwa Dina mpaka asubuhi na kulivyokucha aliendelea kukaa mpaka muda wa jioni ndio alivyoanza safari ya kurudi nyumbani.

Ilikuwa muda wa saa kumi na moja kama na nusu hivi ya jumapili ndio aliingia nyumbani na kitendo cha kuingia getini aliweza kuona gari ambayo sio ya Regina ikiwa katika maegesho ya muda mfupi.

Hamza palepale kwa kuichunguza tu hio gari aliikumbuka vizuri.

“Hii gari si ni ya Yulia hii, anafanya nini hapa nyumbani”Aliwaza Hamza huku hisia zikimwambia huyo mwanamke kamfuata mpaka hapo zikimvaa.

Unadhani Yulia kaenda nyumbani kwa Hamza kufanyaje ?



ITAENDELEA-Alhamisi

nicheki watsapp kupata mwendelezo namba ni 0687151346
 
Back
Top Bottom