Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZ:SINGANOJR


SEHEMU YA 55.
USIKU WA JANA.
Hamza mara baada ya kutoka nje ya geti alisogelea moja ya gari ya Mercedenz iliokuwa imesimama mita kadhaa kutoka katika geti la nyumba yao na kisha aligonga kioo cha mbele na muda uleule kioo kile kilishushwa na ndani ya gari hio alionekana mwanaume alievalia suti, mweusi mwenye makadirio kama ya miaka therathini hivi.
“Bosi pole kwa kusubiri muda mrefu?”Aliongea Hamza kinafiki na kumfanya yule bwana kutoa tabasamu na kisha aliangalia chini.
“Umejuaje nakusubiri Bro”
“Huna haja ya kujifanya mjinga, ilihali umefanya kila hila ya kupata ‘Attention’ yangu nijue unanifuatilia”Aliongea Hamza na kumfanya yule bwana kutoa tabasamu.
“Ni kama nilivyodhania umeniona , unaonaje ukiingia ndani ya gari Bro”Aliongea na kumfanya Hamza kuzunguka upande wa pili na kuingia katika ile gari.
Kilichomfanya Hamza kujua gari hio ilikuwa ikimfuatlia ni mara baada ya kuiona zadi ya mara tatu katika safari nzima ya kutoka hospitalini mpaka kufika Kigamboni.
Wakati alipokuwa akiongea na Regina nje ya hospitalini karibu na maegesho ya magari aliweza kuiona na wakati wanasubiria Taksi kuwachukua kwenda nyumbani iliwapita , Hamza mwanzoni hakuitilia sana maanani kutokana na dereva kutoonekana kuwa na nia yote mbaya lakini mara baada ya kuona ikiwa imesimama mita kadhaa kutoka kwenye geti la nyumba yao aliona kabisa dereva wa gari hio alikuwa akifanya makusudi ili kumjulisha kwamba anamtafuta.
“Bro wewe sio wa kawaida , umeweza kuwashinda wale Maninja wa kundi la Nyoka na kisha kumuokoa Bosi Regina katika mlipuko wa gari , uwezo ulioonyesha sio wa mwanajeshi wa kawaida aliepitia mafunzo ya kikomandoo, naweza kusema wewe ni zaidi ya mwanajeshi. unaweza kuniambia mafunzo yako ni ya namna gani na uwezo wako kwa ujumla?”Aliongea yule bwana huku akiwa na hali ya urafiki katika macho yake.
“Na wewe unaweza kuniambia ni nani haswa na kwanini umefanya kila hila nikutambue?”
“Oh , Samahani bro kwa kutokujitambulisha, Naitwa Norbert Geza kutoka kitengo cha usalama wa nchi”Alongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.
“Sawa bwana Geza , je kuna sababu yoyote ya jeshi kunifuatilia?”
“Ni maswala ya Usalama wa nchi ndugu Hamza ,
tukio kama la leo tuna kila sababu ya kukufuatilia”Aliongea na kumfanya Hamza amwangalie.
“Mnapanga kufanya nini kuhusu tukio la leo , maana kama mlivyoona kuna watu wanataka kuniua mimi na bosi wangu, mpango wenu ni nini au mnapoteza muda kunifuatilia ila hakuna chochote mnachofanya”
“Tunapanga kulichukulia hatua swala hili lakini hatua ya kwanza ni hii ya kuongea na wewe , nipo hapa kwa ajili ya kukutuliza na kukutaarifu kwamba wote waliohusika hapa tutawaonya wasirudie tena kuyumbisha usalama wa nchi na raia wake”
“Haha.. mbona kama kauli yako ni ya kimaigizo na onyo kwa wakati mmoja, mimi ndio nimeshambuliwa lakini ninachoona hapa unanipa onyo nisichukue hatua kwa wale waliohusika, kama watu wameweza kukodi kundi hatari kama
hili kwa ajili ya kuhakikisha tunapoteza uhai, unadhani unachoongea hapa kinaweza kutekelezeka?”
“Kama nilivyojitambulisha Mr Hamza , kupitia vitengo vyetu ya kiusaama vya nchi tutafanya kila linalowezekana , Tanzania ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya haki na sheria , hatuwezi kumruhusu mtu kufanya anachotaka , hivyo naomba usiingilie kazi ya jeshi na kusababisha matatizo zaidi , Idara ya usalama wa nchi haiwezi kufumbia macho maswala kama haya”
“Unaongea ujinga na upuuzi , nilikuona kule hospitalini na nikakuona tena baada ya mlipuko , hii inamaanisha mlijua tukio kama hili litatokea , nyie kama kweli ni sehemu ya usalama wa nchi , kwanini hamkuzuia tukio kama hili, hii moja kwa moja inaniaminisha kwamba watu waliohusika wapo ndani ya idara zenu na walikuwa wakiangalia nini kinachokwenda kutokea , sasa kwasababu umejileta mwenyewe unaonaje ukinitajia kabisa wahusika”
“Hamza unamaanisha nini , kwahio unataka kwenda kinyume na msimamo wa idara ya usalama wa nchi?”Aliuliza yule bwana na kumfanya Hamza macho yake kuchanua na kumwangalia kwa umakini.
“Kama huna taarifa yenye maana kwangu basi naweza kusema muda umeenda na nataka kwenda kulala”Aliongea Hamza na kisha alifungua mlango na kutoka nje.
Norbert aliishia kumwangalia tu , isitoshe alikuwa akimhofia kwa kile alichokuwa amekiona leo hivyo hakuona haja ya kubembeleza.
Mara baada ya kumuona Hamza akirudi ndani aliendesha gari mpaka mita kadhaa kwenye moja ya nyumba iliokuwa geti la njano katika mtaa huo huo na mlango ulifunguliwa na wanaume wanne waliovalia mavazi ya kiraia na kisha kuingia ndani ya gari ile.
“Kapteni vipi kuhusu Hamza amekuelewa ?”
“Sina uhakika , huyu dogo inakuwa ngumu mno kujua ni kitu gani anapanga kufanya , tunapaswa kuwa makini tusiruhusu akasababisha matatizo hasa kipindi hiki cha uchaguzi”
“Haya yote ni kutokana na tamaa za mheshimiwa mstaafu na familia ya Mzee Benjamini na kuendelea kumchokoza Bosi Regina kila siku , anadhani kwasababu ya kuwa mstaafu anaweza kufanya chochote na kujimilikisha hii nchi”Aliongea mmoja ya wale watu kwa chuki kubw.
“Ni kwasababu hakuna anaeweza kumfanya chochote Mstaafu , nchi ilimwacha afanye chochote na sasa mizizi yake ipo kila kona ya nchi kwanzia kwenye uchumi mpaka kwenye siasa, Familia ya Benjamini ni sehemu ndogo sana katika Ngome yake”
“Ndio maana wanadharauliwa na huyu Hamza kwa kutumika kizembe”
“Hii ni misheni yetu ya kuhakikisha nchi inakuwa salama , sisi ni wanajeshi na lazima kila tunachofanya kinazingatia sheria na katiba ya nchi , vinginevyo hatuwezi kuwa tofauti na wahalifu”Aliongea mwingine.
“Haina haja ya kulalamika, kwasasa tokea tuanze kufatilia matukio yote yanayoendelea hatuwezi kusema usalama wa nchi upo hatarini , tunapaswa kuendelea kuwa makini na kila hatua wanazochukua , lazima tutimize kila wajibu ambao tumepewa na wakuu wetu”Aliongea Kapteni. “Ndio tumekuelewa Kapteni?”
“Ayubu vipi bado hujampata Amosi?”
“Afande Rama anaendelea na uchunguzi bado ,
Jasusi mara ya mwisho alionekana katika Mgahawa Masaki na baada ya hapo hajaonekana tena na hakuna alama alioacha nyuma inayoweza kutufanya kupiga hatua ya kujua alipo”
“Vipi ndani ya Kanisa la Wabrazili , hakuna ‘Movement’ zozote za kutilia mashaka?”
“Kuna mtu wentu ndani ya kanisa na mpaka sasa hajawasilisha taarifa yoyote , nadhani bado hakuna cha kutilia mashaka”Aliongea Ayubu na kumfanya Kapteni Norbert kufikiria kidogo.
“Kuna kitu lazima kinaendelea, nimesikia na Afande Danieli anamtafuta Amosi, Mzize wewe kwanzia kesho endelea kumfatilia Kanali Dastani kila hatua anayopiga na kisha unipe Ripoti. Fadhili wewe utaendelea kumfuatilia Hamza pamoja na washikaji zako” “Sawa Kapteni”
“Hebu waulize kwanza tujue kama Hamza bado yupo nyumbani”Aliongea na kumfanya bwana alieitwa Fadhili kutoa simu palepale na aliongea kwa dakika kadhaa na kukata.
“Bado yupo nyumbani Kapteni , hakuna Kamera inayoonyesha akitoka”
“Vizuri, kama kuna lolote litakalotokea mtanijuza naenda nyumbani”Aliongea na mabwana wale walikubali na kisha walishuka katika ile gari na kuingia ndani ya nyumba ile yenye geti na Kapteni Norbert alitoweka katika eeo hilo.
Sasa upande mwingine wakati wakijua Hamza yupo nyumbani ukweli ni kwamba alikuwa ashaondoka muda mrefu kwa kuzikwepa Kamera na hata simu yake aliacha hapo hapo nyumbani maana alijua lazima Ma ajenti hao wanafuatilia hadi simu yake.
Muda ulikuwa umeenda na kuna maeneo ndani ya mtaa huo wa Egret yalifunikwa na vivuli vya miti na ndio aliotumia kupotelea mpaka kwenda kutokea katika mtaa mwingine kabisa.
Hamza mara baada ya kuona amefika mbali kabisa na nyumbani alitoa simu ndoto ya batani na kisha alitafuta namba ya Lawrence msaidizi wa Dina.
“Bro muda umeenda sana , kuna kitu unataka nikusaidie?”
“Kundi la kininja la Black Eared Snake lipo Tanzania , nataka kujua eneo walipo?”
“Bro ! , Umejuaje wapo Tanzania na kwanini unataka kujua walipo?”Aliuliza Lau upande wa pili.
Hamza alikuwa akijua moja ya kanuni kubwa ya kundi hilo la kininja ni kusafiri kimakundi , kwa mfano ikitokea kazi ya kuua mtu katika eneo husika lazima na kiongozi wao asafiri kwenda kuweka makazi ya muda katika eneo hilo, Hamza alijua akimkamata kiongozi ndio atakavyyoweza kumpata mtu ambae anataka kumuua kwa kumsababishia ajali za mara kwa mara.
“Wewe niambie wapo wapi , kwa Network yenu lazima mtakuwa na taarifa zote”
“Lakini Madam ashalala tayari , unaonaje nikimuamsha na kumwambia kwanza?”
“Ukiendelea kuongea ujinga sitokutambua kama Bro tena , sasa chagua kuniambia au kwenda kumuamsha bosi wako”Aliongea Hamza kwa sauti ya kibabe.
Lawrence upande wa pili hakuweza kumkatalia kwani alimhofia Hamza licha ya kwamba alikuwa ni kama rafiki yake hivyo aliamua kumtajia eneo walipo.
Hamza mara baaada ya kuambiwa eneo husika aliona ni umbali mrefu mno hivyo aliona hawezi kutembea zaidi ya kupanda Taksi ya kumfikisha huko. ******
Upande mwingine ndani ya jumba la kifahari linalopatikana katika eneo la Tegeta walionekana baadhi ya watu wakiwa wameketi eneo la ukumbi.
Walikuwa ni mabosi wenye pesa nyingi na walionekana kuwa na mabodigadi waliombatana nao na kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea.
Alionekana Kanali Mstaafu Fanueli Yowe akiwa amekaa kwa kuegamia kwenye Sofa akimwangalia kwa macho ya ukauzu bwana aliekuwa amekaa mbele yake , ambae amevalia Jaketi la leather , bwana huyo alikuwa mweusi tii na amejaa makovu usoni.
“Mr Snake, umoja wetu umekuwa ukishirikiana na kundi lako la Black Eared Snake kwa miaka saba sasa , katika kipindi hicho chote tumeweza kusimamia madili mbalimbali ya siraha ambazo ziliingia nchini kwako na umeweza kujiimarisha kwa kiasi kikubwa na kuweza kufanya kundi lako kutambulika duniani kutokana na uwezo wa juu , lakini leo ndio mara ya kwanza umetuangusha na kutukatisha tamaa kabisa”Aliongea Fanueli Yowe , huyu ndio bwana ambae ni kiongozi wa kundi la watu wenye ujuzi wa sanaa ya mapigano.
Mr Snake ndio aliekuwa kiongozi wa kundi la kininja la Black Eared Snake , kutokana na kundi lake kupewa misheni ndani ya Tanzania iliokuwa na malipo mazuri ndio maana alisafiri na maninja wake kukamilisha kazi ya kumuua Hamza na Regina.
Genge la mabosi wala keki ya taifa ambao wameamua kujipa jina la kuzugia la Martial Art Association walikuwa ni washirika wakubwa na kundi hilo la kininja kwa muda mrefu ndio maana hata kazi ya kumuua Regina walipewa wao.
Unaweza kushangaa kwanini kundi hili litake kumuua Hamza na Regina, ukiachana na kwamba Master Konki ambae alikuwa mwanachama kupewa kibano na Hamza kiasi cha kuwa na chuki lakini upande mwingine kundi hili lilikuwa na sababu za kutaka kuona Regina pia anakufa.
Mwanzilishi wa kundi hili alikuwa ni Mheshimiwa Mgwenno ambae ndoto yake kubwa baada ya kuwa kiongozi mkuu wa taifa ni kutaka kuimiliki Tanzania.
Mheshimiwa Mgweno katika mbinu za kutaka kuimiliki Tanzania ndio alianzisha makundi mengi ambayo hakujihusisha moja kwa moja lakini alikuwa na nguvu ya kimaamuzi na moja wapo ni kundi hili la Umoja wa watu wanaojua Mapigano, moja ya sababu kubwa aliofanya kuunda kundi hili ni kuhakikisha katika kuendeleza kuwa na maslahi yake anakuwa upande mzuri na jeshi , isitoshe pia alikuwa mwanajeshi Komandoo kabisa kabla ya kuingia katika siasa hivyo ilikuwa rahisi kwake kushawishi wanajeshi kutengeneza kundi hilo.
Sasa kutokana na wanajeshi hao kupata pesa nyingi na pesa kuwanogea walitoka katika miiko ya kazi na kuwa wahalifu wanaojilinda katika vazi la kujiita makomandoo na jambo hilo lilimfurahisha sana Mheshimiwa Mgweno na katika kukamilisha mambo yake aliwatumia sana.
Sasa mara baada ya swala la Hamza na Regina kuletwa mezani na kiongozi wa kundi hilo Fanueli Yowe akimwakilisha mheshimiwa Mgweno moja kwa moja waliona kazi ya kumuua Hamza wawapatie washirika wao wa muda mrefu yaani Assassin wa Black Eared Snake kumaliza kazi hio, hayo yote ni kutokana na kuona uwezekano ni mdogo wa kupambana na Hamza ana kwa ana.
“Kundi letu la Nyoka Mwenye masikio meusi linahistoria ya miaka ishirini tokea kuanzishwa kwake na hatua kwa hatua tuliweza kutambulika kimataifa na ni juzi tu hapa miaka kumi iliopita tuliweza kutambuliwa na Surety International Association na kupewa cheo cha daraja C katika ulimwengu wa maninnja, uzoefu wa kazi za kuua tunazo ni kwamba tu mtu ambae mmetupa kazi ya kumuua awamu hii anaonekana kuwa na mafunzo ya juu na pengine ashawahi kuwa mwanajeshi, Afande Yowe huna haja ya kuwa na wasiwasi , kwasababu mmeshatulipa pesa nyingi juu ya hii kazi nina wahakikishia tutaimaliza haraka iwezekanavyo”
“Unaongea ujinga , tulikuambia kabisa hili ni swala ambalo linatakiwa kufanyika mara moja , lakini angalia mmefeli na kufanya mkuu wa majeshi anatupa tahadhari , kazi imekushinda tunataka urudishe malipo tuliokupatia”Aliongea bwana mmoja mwenye kitambi aliekuwa amekaa pembeni.
“Turudishe hela! Chochote ambacho sisi Noka wa Masikio meusi tunameza hatuwezi kutapika”
“Kazi imewashinda na mnataka kula pesa yetu , hamna aibu?”Aliongea yule bwana kwa hasira huku akigonga meza , alifahamika kwa jina la Afande Sucre.
Maneno ya Sucre yalionyesha kumkasilisha mmno Mr Snake huku akionyesha nia ya kutokubaliana nae kabisa.
“Mzee Sucre kaa chini ili tuweze kusikia mpango B wa Mr Snake”
Muda uleule Mr Snake alichomoa kisu chenye kifimbo chekundu , kilikuwa kidogo mno urefu wa kidole cha mkono na kilionekana chepesi na alitumia kisu kile kujikata kucha huku akiongea.
“Wote hapa ni wanajeshi lakini sijui kama mshawahi kusikia neno maarufu katika vita lifahamikalo kama Original Strike?” “Unaongea upuuzi gani ?”Aliongea Sucre kwa hasira.
“Katika ulimwengu wa kimasenari ikitokea umeshambuliwa kitu cha kwanza unachopaswa kufanya ni kutafuta chanzo cha shambulizi kwani ndio njia nzuri zaidi ya kutatua tatizo , kama hisia zangu ni sahihi huyu kijana wenu mnaemwita Hamza lazima atatafuta namna ya kututafuta ili kulipiza”
“Unamaanisha nini , kwahio unasema anaweza kuja ndani ya hili eneo?”
“Sidhanin kama ni mjinga kuja eneo hili , maana itakuwa ni kujitafutia kifo”Aliongea bwana mmoja mwwenye mwili mkakamavu.
“Mnakosea, kwa taarifa mlizonipatia makisio yangu ni sahihi , anajiona ni mpiganaji mzuri na lazima ataamini anao uwezo wa kutudhibiti , hivyo atatudharau , isitoshe wengi wenu hapa mnaonekana wazembe wazembe”Aliongea na kumfanya Afande Yowe macho yake kusinyaa, ni kweli kabisa katika mapigano licha ya kwamba wanajiita wanajeshi lakini ni wanajeshi wa kutumia siraha na sio kupigana.
“Mr Snake kama kweli Hamza akija hapa , unadhani vijana uliokuja nao watatosha kudili nae?”Aliuliza na kumfanya Mr Snake kwa kujivunia kabisa kugeuza macho yake na kuangalia wanaume waliosimama nyuma yake , walikuwa ni wanaume wenye miili iliojengeka kimazoezi huku wakiwa wamenyoa vipara, hawakuwa na ishara ya uzembe hata kidogo. “Kama akijileta ndio mtajua nini kitakachotokea?”
“F**ck you Hamza , jiafanye mjinga na ujilete hapa nitampasua na risasi moja tu”Aliongea Sucre na kitambi chake huku akikoki kwa mbwembwe bastora yake.
“Mkuu mimi sidhani kama atakuja hapa na muda umeenda , nadhani kikao kishaisha, nina miadi hivyo nitatangulia kuondoka”Aliongea Afande Sucre na kusimama akifuatiwa na mabodigadi wake.
Lakini sasa muda ambao anafikia mlango ili kuufungua ulifunguliwa kwa kishindo na mara baada ya kuangalia vizuri ni mabodigadi waliokuwa wakilinda kwa nje, walikuwa wamepoteza fahamu wakiwa wamerushiwa mlangoni.
Muda huo watu wote walikodolea macho mlango na waliweza kumuona kijana mdogo akiwa amesimama kwenye mlango huku akitafuna bublish na nyuma yake walionekana mabodigadi waliokuwa wakilinda wakiwa chini wengine wakionekana hawana fahamu na wengine walikuwa wakiugulia maumivu.
Afande Sucre alijikuta akimeza mate mengi huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi.
“Wewe ni nani?”Aliongea huku mkono ukiwa umeshafika kwenye kiuno sehemu iliopo siraha yake.
“Naitwa Hamza Mzee, mtu ambae unataka kumpiga risasi na hio bastora yako”Aliongea
Hamza akiwa na muonekano uliojaa uzembe.
Afande Yowe macho yake yalimtoka , hakuamini Hamza angefika hapo kama alivyosema Mr Snake.
Afande Sucre alijikuta akirudi nyuma kwa namna ya kujihami na kuungana na wezake.
Upande wa wanajeshi wote wa kundi hilo wanaojiita wanaojua mapigano walijikuta wakisimama kwa wasiwasi na mshangao.
“Wewe ni jasiri mno , hakika unasttahili kuitwa mwanajeshi kwa kujileta hapa”Aliongea Mr Snake akiwa na tabasamu usoni akijiambia anakwenda kuimaliza kazi muda huo huo ndani ya eneo hilo.
Ukweli ni kwamba licha ya kundi hilo kusikia habari za Hamza wengi wao hawakuwahi kuonana nae ana kwa ana zaidi ya Master Konki ambae hakuwepo kwenye kikao hicho..
“Mr Snake ulichoongea kimeonekana kuwa kweli , nipo tayari kuona kile ambacho
umeandaa”Aliongea Afande Yowe na wenzake wote walitingisha kichwa.
“Subirini kwanza?”Aliongea Hamza akinyoosha mkono.
“Unataka kuongea nini , usije ukasema unaona woga wakati umejiingiza kwenye pango la Simba”
“Sijaja hapa kupigana wala kuibua mzozo na mtu , kwa ninavyoona hapa wengi wenu mnaonekana kuwa na vyeo serikalini hivyo sitaki kujiletea matatizo”Aliongea Hamza na kuwafanya wale watu kumwangalia kwa mshangao.
“Kama hujaja hapa kupigana umekuja kufanya nini?”Aliuliza Mzee Yowe.
“Nimekuja kuwapa onyo, leo baada ya kushambuliwa na maninja wa kundi la nyoka nilijua fika kuna mkono wa mtu wenye nguvu umehusika , hivyo sitaki ugmvi na mtu yoyote na muache kushambulia watu wa karibu yangu”
“Onyo!! , Wewe ni nani wa kutupa onyo , unajua vyeo vyetu katika jeshi , kwanini mtoto mdogo kama wewe tukubali onyo lako, ukiburi umekujaa”
“Kwamaneno yako naona kabisa haupo tayari kuikumbatia hii fursa ninayokupatia , hebu jifikirie
mara mbilimbili kabla ya kuendelea kunichokoza”Aliongea .
“Wewe mtoto ni kichaa na bora umejilera mwenyewe, kama hukufunzwa adabu tutakufunza leo”Aliongea Sucre.
“Upo siriasi?”
“Unadhani natania , unadhani naweza kuogopa panya mdogo kama wewe”Aliongea.
“Mr Hamza asante kwa kufika hapa kwa ajili yangu ili niwaonyeshe ni kwa namna gani naenda kudili na mtu kama wewe”
“Na mimi nimekuja kuona unadili vipi na mimi?”Aliongea Hamza na muda uleule Mr Snake alipiga mluzi na kufumba na kufumbua kundi la watu waliovalia mavazi meusi walijitokeza na kuingia katika ukumbi huo huku wakiwa wameshikilia siraha.
Kitendo cha watu wale kutokeza kiliwafanya watu wote kushangaa akiwemo Mzee Fanueli.
“Mr Snake kumbe ulikuwa na kundi la watu wengi namna hii?”
“Nisamehee afande kwa kukutokutaarifu mapema , nilikuwa nimejiandaa kudili na huyu mtu ndio maana nimechukua kila tahadhari”
“Sidhani kuna haja ya kupoteza nguvu za vijana wetu , risasi zinamtosha”Aliongea Afande Sucre na alitoa bastora yake akifuatiwa a mabodigadi na bila ya kujiuliza mara mbilimbili walimfyatulia Hamza mfululizo mpaka bunduki zikaishwa risasi lakini kitu cha ajabu ni kwamba risasi zile ni kama zilikuwa zikipiga hewa , Hamza walikuwa wakimuona mbele yao lakini ilikuwa ni kama holograph ya Hamza , ile wanamaliza Hamza alikuwa palepale mbele yao akiwa na tabasamu.
Swala lile liliwashangaza mno wale mabwana na hofu na wasiwasi iliwavaa, walimuona Hamza kama mzimu.
“Wewe ni binadamu au Mzimu!!!”
Mr Snake alijikuta akibung’aa huku akimwangalia Hamza kwa hofu na kuna kila hali iliokuwa ikimwambia Hamza aliwafanyia kiini macho ili waamini alikuwa mbele yao lakini muda mrefu alikuwa ashapotea na amerudi baada ya kuacha kushambuliwa.
Aliona kama hisia zake ni sahihi basi njia moja tu ya kudili nae ni kushambulia ana kwa ana na sio kwa kutumia siraha kama bunduki.
“Sijaja hapa kujibu maswali , nimewapa nafasi mmeikataa”Aliongea Hamza huku akipiga hatua lakini Mr Snake alifyatuka na kumsogelea Hamza kwa spidi akiwa na kisu amekitanguliza mbele kininja kwa kumlenga eneo la shingoni.
Kitendo cha Mr Snake kumfikia Hamza usawa wa shingo mkono wake ulioshikilia kisu ulidakwa kwa spidi ya juu kiasi cha kushindwa kukwepa na kuzungushwa kwa nguvu na maumivu aliohisi alijikuta akikiachia kile kisu mwenyewe.
Hamza hakuchelewesha wakati kisu kule kinadondoka katika mikono ya Mr Snake alikidaka na mkono wa kushoto na bila ya huruma alimkita nacho Mr Snake katika paji la uso na kuzama ndani kabisa.
“Master!!!”
Maninja wawili waliokuwa karibu na bosi wao mara baada ya kuona amekitwa na kisu cha paji la uso walijikuta wakipiga yowe na kwa hasira kubwa waliinua mapanga yao na kumsogelea Hamza kwa spidi kana kwamba wanataka kumtenganisha shingo na kiwiliwili.
Wa kwanza mara baada ya kumsogelea Hamza kwa spidi kwa mtindo wa kutaka kumfyeka shingoni ,Hamza alimkwepa kuinama chini na upanga ulipita hewani na kisha palepale kwa ustadi wa hali ya juu aliachia ngumi nzito iliompiga bwana yule eneo la moyo na kilichoweza kusikika ni mbavu zake kuvunjika na alidondokea mbali huku akikodoa macho na kutema damu kisha akadondoka chini isieleweke kama amekufa au amezimia ,hakuzubaa baada ya shambulizi lile mwingine alikuwa ashamfikia akinuia kutaka kumchoma na upanga eneo la tumboni lakini Hamza alikuwa mwepesi kwani alikwepa kisu kile na kupita kwenye mbavu kiasi cha kuchana nguo aliovaa na palepale alimpiga bwana yule teke la kigoti na kumfanya kupinda na ilikuwa ni nafasi ambayo Hamza aliitaka kwani alimtandika ngumi nzito ya paji la uso iliomdondosha Ninja yule chini na kuzima palepale.
Haikuwa kwa Sucre na wenzake ama kwa kiongozi wao Afande Yowe , wote walijikuta wakipatwa na mshituko usio na kifani huku hali ya woga ikiwavaa , Afande Yowe Bastora yake ilikuwa na risasi lakini alishindwa kuchukua maamuzi ya kuitumia kutokana na kile alichoona baada a Hamza kutoathirika na risasi.
Wale maninja wengine mara baada ya kuona wenzao walivyojeruhiwa walisita kufanya mashambulizi na kumwangalia tu kwa wasiwasi , isitoshe mkuu wao alikuwa ndio mtaalamu wa hali ya juu na mabwana wawili waliozimishwa kwa ngumi moja moja tu ndio walikuwa wakifuatilia kwa uwezo sasa wanawezaje kumshambulia mtu ambae amemuua mkuu wao kwa shambulizi moja.
“Kajikundi kadogo ka daraja C wanaona wanaweza kushindana na mtu kama mimi”Aliongea Hamza mara baada ya kuona kazi yake ni njema na alipiga hatua kumsogelea Fanueli.
“Unajua kwanini tumefikia hatua hii?”Aliuliza Hamza na kumfanya Afande Fanueli kutingisha kichwa kusema hajui.
“Mmekodi watu kwa zaidi ya mara tatu sasa kwa ajili ya kuja kunishambulia na hata kutuma hawa wapuuzi mkiamini wanaweza kunishinda, lakini yote hayo yaliotokea mmeshindwa kujiuliza swali moja jepesi tu, na swali lenyewe mlipaswa kujiuliza mimi ni nani kwanza kabla ya kuchukua hatua , tokea mwanzo nilijua tu mnajitafutia matatizo kwa kunichokoza , nilitaka kuwavumila lakini inaonekana nguvu yenu hapa nchini imewapa kiburi na hamuwezi kunusa hatari”
“Mr Hamza tafadhali tunaomba usitufanyie chochote , tupo tayari kufanya chochote , najua unamahusiano makubwa na kiongozi wa mtandao wa Chatu nipo tayari kuongezea nguvu mtandao huo, tumefanya haya yote kutokana na presha kubwa kutoka kwa familia ya Mzee
Benjamini”Aliongea lakini Hamza hakumjali na muda uleule alimgeukia Afande Sucre.
“Wewe mzee njoo hapa”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Sucre kutetemeka lakini kwa hofu kubwa alimsogelea Hamza.
“Mr Hamza kama kuna chochote unataka niambie nitafanya”Aliongea kwa kunyenyekea na kufanya wenzake kumwangalia kwa macho yaliojaa dharau kwa namna alivyonywea. “Nipe hio Bastora yako”
“Eeh!”
“Hutaki kunipa?”
“Hii hapa”Aliongea Sucre kwa haraka mara baada ya kusika sita kumpatia Hamza
Hamza mara baada ya kuishika ile bastora aliangalia ndani yake kama ina risasi na ilionekana kuwa nazo tatu na kitendo cha kuiweka sawa alikuwa ashaachia risasi ambayo ilitoboa paji la uso la mzee Sucre
Sucre hata hakujua amepigwaje risasi maana mkono wa Hamza ulifyatuka kwa spidi kubwa mno lakini ndio hivyo ilikuwa mwisho wake.
Hamza hakujali maiti ile na alimgeukia Fanueli ambae alikuwa akitetemeka kwa hofu pamoja na kundi lake.
“Nilisema kabisa sijaja kupigana lakini ukaamua kunidharau”
“Mr Hamza nilikosea tafadhari naomba unisamehe hili lipi…”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake alikuwa ashachapwa lisasi mbili za kichwa na kudondoka chini.
Ndani ya dakika chache Hamza alikuwa ashamuua kiongozi wa kundi la Nyoka Mwenye masikio Meusi na Kanali Mstaafu Afande Fanueli Yowe.
“Kuna mwingine anataka kufa?”Aliuliza Hamza huku akiwaangalai waliobaki na kila mmoja alionekana kuwa katika hali ya kutetemeka huku baadhi wakitaka kujikojolea na waliishia kutingisha vichvwa vyao wakitia huruma.
Hamza hakuwa na mpango wa kumuua mtu
wakati anakuja hapo lakini uchokozi ulizidi hivyo alilazimika kutoa fundisho.
“Mimi ni kijana mpole sana tena mwanachuo , lakini naomba niwaambie tu Sipendi
Uchokozi”Aliongea Hamza na kisha alirusha ile bastora chini kisha alitoa simu yake ya batani na kuangalia saa na aliweza kuona muda ulikuwa umeenda sana.
“Nadhani taarifa zitamfikia anaewapa kiburi cha kutaka kufanya chochote ndani ya nchi hii, mwambieni ajifikirie mara mbili mbili kabla sijamchukulia hatua”Aliongea Hamza na kisha aliondoka ndani ya eneo hilo.
*****
“Wakati ulipokuwa umelela sijafanya chochote mbona?”Aliongea Hamza akiwa katika simu na Dina.
“Bado unaongea kimatani tu , asubuhi nimesikia taarifa umemuua Mzee Fanueli Yowe, mstaafu Mgweno ametoka kunipigia hapa anaomba yaishe”Aliongea Dina na kumfanya Hamza kucheka , ilionekana onyo ambalo alitoa jana limefanya kazi.
“Kuna onyo nilijaribu kutoa jana usiku na limefanya kazi , tumia nafasi hii kujiimarisha”Aliongea Hamza.
“Unajua kusababisha matatizo sana , sidhani pia kama ameomba kuyamaliza kwa nia ya dhati , kuna uchaguzi mwezi ujao ndio maana kaamua kujishusha, Mgweno ninaemjua mimi sio mtu wa kukubali yaishe kirahisi’
“Kama hajanielewa muache aje hata baada ya huo uchaguzi, mimi sipendi uchokozi ni hivyo tu basi , nitapambana kulinda amani yangu”Aliongea
Hamza na upande wa pili ulionekana kuwa kimya.
“Vipi baadae unakuja kunisalimia , sijakuona muda mrefu?”
“Muda mrefu wapi wakati ni juzi tu hapa?”
“Hata kama hakikisha unakuja usiku la sivyo nitakuja kuruka ukuta na kuingia ndani ya hilo kasri unaloishi siku hizi”Aliongea na kumfanya Hamza kuishia kukubali tu.
Hamza mara baada ya kumaliza kuongea na Dina alikata simu mara moja na muda huo ndio alikumbuka alikuwa ameghairisha mara kibao kwenda nyumbani kwa Eliza na pia kulingana na ratiba za siku hio aliona ingekuwa ngumu pia kwenda hivyo alimpigia simu na kumwelezea kuwa hatoweza kumtembelea.
Baada ya kuoga alivaa nguo na kisha alishuka chini sebuleni na aliweza kumkuta Regina akiwa bize jikoni akitengeneza Sandwich kwa kutumia kutumia Sausage.
“Regina unatengeneza Sandwichi au kitu gani?”Aliuliza Hamza.
“Sio lazima kujua ninachotengeneza”Aliongea huku akizidi kuwa bize, alionekana kujivunia kwa kile alichokuwa akifanya.
Kutokana na Shangazi kutokuwepo nyumbani aliona aingie mwenyewe jikoni.
Hamza alikumbuka Shangazi akimwambia Regina hakuwa akijua chochote kuhusu kupika hivyo alishangaa kumkuta jikoni.
Alijua Regina atatengenea utopolo wa chakula hivyo alifungua friji na kutoa mayai, tambi na nyama , vitunguu na pilipili hoho. “Unafanya nini , utachafua vyombo tu”
“Nitaviosha baadae nikirudi”
“Unadhani kula sana ndio afya , kwanini usisubiri tule hiki ninachopika?”
“Haijalishi nakula sana , sijui nitaishi kwa miaka mingapi mbeleni , mtu unapaswa kula kila unachojisikia maana hujui ni lini utashindwa kula”
“Mawazo yako yanasikitisha , kwahio unadhani kwasababu huwezi kuishi muda mrefu unachopaswa ni kula tu na sio kufanya vitu vingine ya msingi?”Aliongea huku akikunja sura lakini Hamza alikuwa mvivu kujibishana nae na alianza kusaga saga ile nyama.
Muda huo vipande viwili vya mkate vilichomoka ndani ya kibaniko.
“Aiyaa..”Regina alijikuta akishangaa huku akikunja ndita.
“Nini tatizo?” Aliuliza Hamza na huku akimgeukia na mara baada ya kuangalia kilichokuwa kikimshangaza Regina alijikuta akianza kucheka
“Haha.. Regina huo ni mkate au ni pande la mkaa?”
Vipande hivyo vya mkate vilikuwa vimegeuka kuwa vyeusi tii na sio Brown kama alivyotarajia.
“Unacheka nini sasa , nimezidisha moto ndio maana umeungua”Aliongea na kumfanya Hamza kusogea karibu na kuangalia
“Aina ya hii mikate inahitajika nyuzi tatu tu za joto kuubanika, sasa wewe umeweka sita unadhani nini kitatokea?”Aliongea na kumfanya Regina kuangalia mashine hio ya kibaniko na kuona kweli aliweka joto la juu mno.
“Nilikosea”Aliongea huku akirekebisha na kuanza kubanika upya vipande vya mikate ili ajazie na Sausage.
“Nilijua ni mzoefu wa kutumia hizo mashine za kupikia”
“Endelea na unachokifanya achana na mimi”Alimsukumia pembeni huku akiendela kuwa bize.
Baada kama ya nusu saa kila mtu alikuwa ameshamaliza kutengeneza kile alichokuwa akitengeneza , Hamza alitengeneza tambi za mayai nyama na kuweka na Regina alikuwa ametengeneza Sandwich zake za Soseji.
Baada ya kukaa mezani kila mtu alikula kile alichoandaa mwenyewe.
Sasa Regina ile anapeleka mdomoni kung’ata kipande cha mkate alijikuta akikunja sura na alitema palepale.
“Hizi Soseji nadhani zilikuwa zimeshaharibika , ni chachu mno”
“Kwahio ulipika bila ya kuangalia kama muda wake umeisha?”Aliuliza Hamza na kumfanya Regina kuwaza kwanini hakuangalia kabla.
Alijikuta akitia huruma huku akiangalia kitafunwa alichoandaa kilichokuwa kimeshachacha na kujikuta akiangalia sahani ya Hamza iliojaa tambi za mayai kama vile ni Pizza, alijikuta akimeza mate kutokana na harufu yake nzuri.
Hamza aliweza kujua mwanamke huyo alikuwa akitaka cha kwake lakini alikuwa akishindwa kuongea.
“Regina nadhani haitakuwa vizuri kuharibu chakula , unaonaje tukiambizana kumaliza hiki cha kwangu”Aliongea Hamza akimaanisha wasaidiane kula na kumfanya Regina kusafisha koo.
“Kwasababu umeniomba nikusaidie nitafanya hivyo , nitakula kidogo kukupunguzia mzigo”
“Asante kwa msaada wako bosi”Aliongea Hamza huku akimpunguzia kwenye sahani yake.
Kitendo cha Regina kuonja alijikuta macho yakimtoka na palepale alijiambia inakuwaje Hamza anajua kupika namna hio , japo tambi hizo zilionekana za kawaida kwa kupikwa na nyama pamoja na mayai lakini hakuamini zingekuwa na radha tamu kama hio.
“Hey! , hivi ushawahi kuwa mpishi?” Regina alishindwa kujizuia na kuuliza.
“Hapana”?”
“Sasa inakuwaje unajua kupika namna hi”
“Labda ni kwasababu sio rahisi kuishi, ndio maana ni vizuri kuhakikisha unajua namna ya kuridhisha tumbo lako”Aliongea Hamza lakini jibu lake ni kama halikumridhisha Regina na shauku kubwa ilimvaa.
“Regina unanisifia?”
“Kidogo tu”Aliongea Regina kwa sauti ya chini na kumfanya Hamza kutabasamu.
Baada ya kifungua kinywa walindoka kwa pamoja wakiwa na nyaraka maalumu na kuelekea Bomani kwa ajili ya kukitafuta cheti cha ndoa.
Kwasababu Lexus ilikuwa imelipuka walitumia Mercedenz Benz Maybach , ilikuwa gari nzuri ambayo haikupitisha risasi.
Kutokana na ukubwa wake katika jamii swala zima la kupata cheti halikuchuwa muda , mwanadada ambae alikuwa amesimamia swala zima alijikuta akimuonea wivu Hamza kwa kuweza kupata mwanamke mzuri kama Regina.
Mara baada ya kurudi kwenye gari , Regina alionekana kuwa na hisia mchanganyiko mara baada ya kuona picha zao katika cheti
Hamza aliishia kumuangalia kupitia kioo cha nyuma na kuona ni kwa namna gani Regina alionekana kuwa na wasiwasi.
“Vipi sasa , unahisi kuna chochote kilichobadilika?”
“Sioni chochote cha ajabu , nimefanya yote haya kwa ajili ya kumridhisha bibi tu ili anipe hisa zake”Aliongea Regina.
“Ndio unaona ipo hivyo , muda ni fumbo kubwa mno sikudhania nitajikuta katika hali kama hii , ila inanifanya niwe na furaha bila sababu ya msingi”Aliongea Hamza.
“Hiki ni cheti tu , unaweza kuoa muda wowote unaotaka , hili likipita tutafuata taratibu na kufuta hiki cheti , hakikisha mpenzi wako hajui sitaki matatizo”
“Swala la kufuta cheti ni mimi kuamua kama nakubali au lah , lakini usijali sana , muda una majibu mengi”Aliongea Hamza , lakini licha ya kuonekana ana furaha upande wa Regina hakuwa na furaha na alimtaka Hamza kuendesha gari kuelekea hospitalini ili kumuonyesha bibi yake cheti aridhie kumkabidhi hisa zote za kampuni.
Lakini sasa wakati wanafika ndani ya maegesho ya magari katika hospitali hio ni kama Hamza alikuwa akisubiriwa kwani walikuwepo Polisi wakiongozwa na Nobert.
“Mr Hamza upo chini ya ulinzi kwa makosa ya mauaji yaliotokea jana usiku”AliongeaNobert akiwa siriasi na polisi wenzake walimzingira kutaka kumfunga pingu huku wakiwa katika hali ya tahadhari na siraha zao.
Regina alijikuta akitoa macho mara baada ya kusikia kauli hio, ilikuwa ni kama hajasikia vizuri.
*****
Upande mwingine ndani ya makao makuu yya
Taasisi ya Haliz Foundation katika floor ya nne kwenda chini ya vyumba vya Ardhi, Amosi alionekana kuwa macho licha ya kwamba bado mikono yake ilikuwa imefungwa na vitu kama pingu katika kitanda na kumfanya ashindwe kusimama.
Alionekana kuwa na utulivu wa hali ya juu na alikuwa kama mtu ambae alikuwa akisubiria mtu aingie kwenye wodi hio.
Upande mwingine nyuma ya chumba alicholazwa Amosi kulikuwa na watu wanne waliovalia makoti ya kidaktari mmoja wapo akiwa ni Sister Maya Thema na mwingine alikuwa ni Frida ambae alionekana kuwa na mshangao akiangalia Skrini iliokuwa ukutani ikimuonyesha Amosi.
“Profesa kama hili lingekuwa swala ambalo jamii inapaswa kuambiwa basi katika historia Tanzania inaingia katika nchi tatu ambazo upandikizaji wa Chip kwenye ubongo wa binadamu umefanikiwa kwa asilimia mia moja”Aliongea Frida na kumfanya Dokta Maya Thema kutingisha kichwa kukubaliana nae.
“Kwasasa hii teknolojia wakuu hawataki ikitangazwa kwa jamii ya watu mpaka kukamilisha mipango yao , lakini licha ya hivyo imenipa hali ya kujivunia kufanikisha operesheni hii kwa mara ya kwanza katika Ardhi ya Afrika”Aliongea.
“Nini hatua inayofuatia baada ya hapa?”Aliuliza Frida huku akiwa na macho yaliojaa shauku.
“Sisi ni wanasayansi pekee na kazi yetu ni kukamilisha kile ambacho wafadhili wetu wanataka kufanya, hatua inayofuatia ipo chini ya Ajenti wa umoja wa Sinagogu”Aliongea.
“Profesa kwahio kwasasa pale yupo imara kiakili , hakuna athari zozote nje ya zile zilizotarajiwa zilizoweza kuonekana kupitia tabia yake?”Aliuliza Frida.
“Leo ni siku yake ya nne tokea kufanyiwa operesheni , siku ya kwanza alikuwa kwenye hali ya kawaida ya mshituko na kuikataa hali aliokuwa nayo , lakini kwa kushitua mishipa yake ya fahamu eneo la hisia tumeweza kufanikisha kumfanya kuwa katika hali ya mazoea , kuhusu tabia ambazo zipo nje ya matarajio bado hatujaona na hatuna budi kumfuatilia hata akiwa katika mazingira ya kawaida”
“Profesa hii sio operesheni ya kwanza kufanyika , mbili ziliweza kufanyika nchini Uingereza na moja nchini Marekani na mbili Israeli na ni zaidi ya miaka kadhaa imepita tokea kufanikiwa kwa operesheni hizo , kwanini tusitumie Follow up ya
data za wagonjwa waliopita?”Aliuliza Dokta John moja ya wanasayansi wa taasisi hio.
“Kila operesheni inayofanyika katika upandikizaji wa Chip katika Ubongo inabeba malengo tofauti hivyo matokeo ya kitabia kuwa tofauti pia , Katika historia ya Dunia Operesheni ya kwanza ya kupandikiza kifaa kwenye ubongo ilifanyika nchini Ujerumani chini ya Usimamizi na ufadhili wa Nazi , malengo ya upasuaji ule yalilenga kufanya wanajeshi kuwa imara zaidi katika kubuni mbinu za kumshinda adui , unachopaswa kuelewa utofauti wa operesheni ile na wa leo ni kwamba ule ulifanyika katika kufunua kichwa cha binadamu na kisha kuweka kifaa lakini huu umefanyika bila ya kufungua kichwa cha binadamu ikimaanisha dunia ilipiga hatua kutoka wakati ule , tulichelewa miaka mingi kuendeleza sayansi ya upandikizaji Chip tokea vita ya pili ya Dunia mpaka sasa kutokana na Josef Mengele kumuua Dokta Douglas kwa sumu akiwa katika maabara ambae ndio alibeba jukumu kubwa la tafiti za ubongo wa binadamu, hakuishia kumuua Dokta Douglas tu bali alichoma tafiti zake zote na kitendo kile kilirudisha dunia hatua moja nyuma katika maswala ya tafiti za kibailojia”Aliongea Dokta Maya na jibu lile kidogo lilionekana kumshangaza na Frida.
“Profesa unamaanisha Joseph Mengele huyu ambae katika historia alifahamika kama Malaika wa kifo , sijawahi kusikia jina la Dokta Douglas katika historia kwanini alimuua?”
“Hakuna ambae ashawahi kumsikia Dokta Douglas kwasababu alikuwa ni mwanasayansi ambae anapiga hatua na hakukuwa na matokeo ya wazi ya tafiti zake , mgonjwa wake wa kwanza ambae alimpandikiza kifaa katika Ubongo hakuonyesha matokeo makubwa sana kama nadharia ilivyokuwa, pengine alifanikiwa au pengine hakufanikiwa ndio maana Josef Mengele alimuua na kuchoma tafiti zake”.Aliongea Dokta Maya Thema.
“Imekuaje ukawa na taarifa ya swala hili , Profesa kwa umri wako…”
“Frida si kila kitu ndani ya dunia hii kipo wazi na sio kila mwenye umri mkubwa anafahamu kila kitu , historia ipo leo kwasababu imetunzwa , kabla ya
kuwa muumini wa Sinagogu nilikuwa mwanasayansi nchini ya Kanisa kuu”Aliongea Maya na kumfanya Frida kutingisha kichwa.
Alielewa watu wengi ambao walikuwa na historia kubwa na Kanisa kuu walikuwa wakijua mambo mengi.
Muda ule wakati wakiongea katika Floor hio aliingia bwana mmoja alievalia suti , alikuwa ni kijana ambae ana muonekano wa kidominikani au kilatini kwa lugha nyepesi, ikimaanisha kwamba alikuwa na asili ya makabila matatu yaani Mzungu kwa asilimia hamsini , Mwafrika kwa asilimia arobaini na mlatino kwa asilimia kumi.
“Ajenti Alonzo karibu sana”Aliongea Maya Thema alionekana kumfahamu yule bwana ambae tembea yake ilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa mkakamavu.
“Asante sana Profesa”Aliongea na kisha macho yake yalitua katika sura ya Frida na kumfanya ProfesaMaya kuchukua jukumu la mara moja kumtambulisha Frida na Dokta John.
“Mr Alonzo huyu ni Dokta Frida Franklin mkuu wa idara ya CST , kutana pia na Dokta John mtaalamu wa Neva”Aliongea na Ajenti Alonzo alisalimiana nao.
“Nimefurahi kukutana na wewe Frida , nimelisikia jina lako mara kadhaa na imekuwa heshima kwangu kukutana na mwanasayansi kama wewe”
“Asante sana”Aliongea huku akitoa tabasamu la ukarimu na muda uleule Ajenti Alonzo macho yake yalitua katika Skrini iliokuwa ikimuonyesha Amosi.
“Nimeambiwa kila kitu kwa upande wako kimekamilika , nipo hapa kwa ajili ya kukamilisha hatua ya pili, kwanini bado amefungwa kwenye kitanda?”Aliuliza.
“Tumeamua kuchukua tahadhari , lakini kutokana na utendaji kazi wa ubongo wake sidhani kama anaweza kuwa hatari ”Aliongea Dokta Maya.
“Operesheni hii sio kwa ajili ya kumfanya kuwa mwanajeshi mwenye uwezo bali kuwa Ajenti mtiifu na Muaminifu kwa Sinagogu ambae anaweza kutuambia kila kitu, kama kutakuwa na matumizi ya nguvu kumuweka sawa , basi mimi ni mwanajeshi”Aliongea na kumfanya Dokta Maya kukubaliana nae na aliongozwa kuelekea mpaka kwenye chumba alichokuwemo Amosi.
Ajenti Alonzo akiwa ameingia na Dokta Maya Thema kabla ya salamu aliomba Amosi afunguliwe mikono na awe huru na Dokta Maya alifanya hivyo.
“Profesa kwanzia hapa nitaendelea mwenyewe , naomba Kamera zote kuzimwa”Aliongea.
“Bila shaka Ajenti”Alijibu Profesa na kisha palepale Profesa alitoka na kumuacha Amosi na Ajenti Alonzo.






SEHEMU YA 56.
Ilimchukua dakika kama kumi tu kwa Ajenti Alonzo kujitambulisha na Amosi kumuelewa , kwa wakati huo Amosi alionekana kuwa kawaida , ki ufupi hakuwa na tofauti sana kitabia , kitu kimoja tu ambacho kilikuwa tofauti ni namna ambavyo alikuwa mtiifu kwa kile ambacho alikuwa akielezewa na Alonzo.
“Mr Amosi kwasasa utafahamika kwa jina la Ajenti Zuku ikimaanisha Askari usie na chimbuko, umenielewa?”
“Ndio Sir”Alijibu Amosi kwa utiifu akiwa ameketi kwenye kiti na kumfanya Ajenti Alonzo kuridhika.
“Kilichofanyika kwako haimaanishi kwamba jina lako katika mazingira ya kawaida linakwenda kuwa tofauti , ukitoka hapa unakwenda kuendelea na maisha yako ya kawaida”
“Ndio Sir”
“Vizuri kabisa , mpaka sasa umefahamu nini katika misheni yako juu ya Naomi Lindsey na Rosemary Macha?”Aliuliza na kumfanya Amosi kufikiria kidogo.
“Sijapata kufahamu kwa uhakika lakini hisia zangu zinaniambia Naomi na Rosemary ni mtu mmoja na kuna uwezekano Naomi alidanganya kifo chake nchini Italy na kisha akakimbilia Tanzania kwa uhusika wa Rosemary Macha”Aliongea Amosi.
Hizo ndio zilikuwa hisia zake tokea siku kadhaa apewe misheni na Chriss na katika uchunguzi wake alikuwa akitaka kuthibitisha swala hili na kisha kuliunganisha na tukio lililotokea mkoani Rukwa huko Sumbawanga.
Hio ndio ilikuwa misheni yake ambayo Chris alimpatia , misheni ya kutafuta mahusiano yaliopo katika ya Rosemary Macha na Naomi Lindsey msanii mkubwa aliefariki nchini Italy.
Ajenti Alonzo alionekana kuridhishwa na jibu la Amosi na muda ule alionekana kutoa kishikwambi katika mkoba aliokuja nao na kupangusa kwa dakika kadhaa na kisha alimwangalia Amosi.
“Unajua nini kuhusu tukio lililotokea Sumbawanga?”Aliuliza
“Sikuwa muhusika wa uchunguzi wa tukio hilo , Ajenti Sedekia Shilla ndio alieweza kufanya uchunguzi na nusu ya ripoti ilifika makao makuu na nusu nyingine haikuweza kufika kutokana na Ajenti Sedekia kutoweka, taarifa ambayo alitoa ni mwanamke ambae hakufahamika jina lake kamili zaidi ya jina la Chakwe ambalo alibatizwa na mmoja ya wanakijiji wa Kizwite aliweza kufika ndani ya kijiji hicho akiwa na watoto kumi wenye asilia ya makabila tofauti tofauti , aliishi ndani ya kijiji cha Kizwite kwa zaidi ya miezi sita na aliweza kumudu mahitaji yake na watoto kupitia kwa misaada mbalimbali ambayo wanakijiji walimpatia , siku kadhaa mara baada ya kupatiwa msaada wa eneo la kuishi ikiwa ni kipindi cha Masika kuliweza kutokea ajali ya radi na kumuua yeye na watoto wake tisa huku mmoja ambae inaaaminika alikuwa na asili ya Kizungu alitolewa eneo la tukio na mtu asiefahamika na kutoweka, Ajenti Sedekia alikusanya ushahidi kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo na aliweza kuwasilisha taarifa hio makao makuu , lakini kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja kutokana na utata wa tukio hilo kesi ilifungwa kama ajali ya asili iliomuua mama na watoto wake wote”Aliongea Amosi.
“Unadhani ni kwanini Ajenti Sedekia alipotea!?”
“Sina uhakika, lakini naamini utata wa tukio hilo ndio ulimpoteza” “Unamaanisha nini?”
“Pengine kuna kitu ambacho Ajenti Sedekia aliweza kupata kuhusu utata wa tukio hilo na kuna watu ambao walitaka kuficha taarifa hio ndio maana akapotea” “Kwanini unahisi hivyo?”
“Wakati nikiwa Ajenti nimeweza kusikia tetesi kuhitimishwa kwa kesi ile kama ajali ya kawaida ulitoka kwa Kiongozi wa juu kabisa wa nchi na kuna taarifa pia zinasema kuna nguvu ya nje ya nchi iliohusika, hisia zangu nguvu hio ndio iliompoteza Ajenti Sedekia”Aliongea Amosi kitiifu kabisa.
“Umesema wakati ukiwa Ajenti , sasa hivi wewe sio Ajenti?”Aliuliza na kumfanya Amosi kutulia kidogo na kumfanya Alonzo kumkazia macho.
“Nilikuwa Ajenti wa kitengo cha Intellijensia za kimkakati cha TISA kwasasa mimi ni Ajenti wa siri wa Kitengo cha jeshi cha kupambana na nguvu zisizoonekana kiitwacho MALIBU”Aliongea na kumfanya Ajenti Alonzo kutoa tabasamu. “Nielezee zaidi kuhusu ulichopata tokea kuanza kazi ya kuchunguza uhusiano wa Naomi Lindsey na Rosemary Macha?”Aliongea na kumfanya Amosi kufikiria kidogo.
“Katika uchunguzi wangu nimeweza kugundua watu wa kisiwa cha Binamu hawakutaka niendelee na uchunguzi sijajua kwasababu ni nini lakini kupitia kazi hio niliwekewa mtego wa kuuwawa na moja ya mkuu wangu wa kazi na kwa bahati nzuri niliweza kunusurika”
“Unadhani mkuu wako alikuwa akishirikiana na watu kutoka kisiwa cha Binamu”
“Ndio , nina uhakika ni mshirika na watu kutoka Binamu”
“Kwa ninavyojua ufanisi wa watu kutoka kisiwa
Binamu ulivyo mkubwa usingeweza kuepuka kifo , hujawahi kufikiria pengine waliamua kukuacha hai makusudi au kuna sababu nyingine ambayo wakaacha kukuwinda?”Aliuliza
Licha ya Amosi kuulizwa maswali mengi lakini alionekana kutokereka kabisa wala kuchoka , ilikuwa ni tofauti na tabia yake , pengine ni kile ambacho ubongo wake ulifanyiwa.
“Kuhusu hili nimefikiria pia , lakini mkuu wa kitengo aliniambia niendelee na uchunguzi na ameshaongea na Kitengo cha TISA kwa ajili ya Kinga”
“Kwa maelezo yako ulipokea kazi kutoka kwa Chriss sio kwasababu ya pesa , unaweza kuniambia kwanini ulipokea kazi hii licha ya kuonekana kuwa na uhatari?”
“Mwanzoni nilipokea kutokana na shauku , lakini nilipata hamasa zaidi mara baada ya kujua ni kazi ambayo inahusiana na tukio la mwaka 2002 lililomfanya Ajenti Sedekia kupotea, nimekuwa chini ya kitengo cha MALIBU kama ajenti hai kwa miaka saba, kabla ya kupewa misheni nyingine ambayo ilinifanya kuwa Undercover kwa kivuli cha kustaafu na kuanza kuwa mtumwa wa kazi za kihalifu za vigogo wa nchi”
“Misheni!, ilikuwa misheni gani?”Aliuliza Ajenti Alonzo.
Licha ya Amosi kujua kabisa anatoa siri za kitengo lakini alishindwa kujizuia kuongea.
“Nilipewa misheni ya kufuatilia tetesi za uwepo wa watu Vivuli maarufu kama ‘Night Shadows’ na kuongezeka kwa wimbi la wagonjwa wenye ‘split Personality Disorder’”Aliongea na kumfanya Alonzo kutingisha kichwa na muda ule aliangalia kishikwambi chake.
“Elezea kila kitu ulichofanya ili kufanikisha uchunguzi wa Naomi Lindsey na Rosemary Macha”
“Baada ya kunusurika kifo niliweza kuendelea na uchunguzi na kwa kumfuatilia Kanali Dastani aliekuwa mkuu wangu wa kazi niliweza kugundua kuna mfungwa ambae kuna uwezekano mkubwa
alihusika na kupotea kwa Sedekia Shilla , niliweza kupata taarifa hii kwa kufuatilia mazungumzo ya simu kati ya Dastani na moja ya aliekuwa Mkuu wa Gereza la Silo, kwa kile nilichoweza kupata kusikia ilionekana kuna watu walimtembelea huyo mfungwa Gerezani na Mkuu wa Gereza hilo aliweza kurekodi maongezi kati ya watu hao na mfungwa , kwa bahati mbaya katika harakati za kutaka kumfikia mkuu wa Gereza ili kujua walichoongea mkuu huyo wa Gereza alikumbwa na umauti na imani yangu inaniambia kifo chake kinahusiana na kitendo alichofanya cha kurekodi mazungumzo hayo”Aliongea na kumfanya Ajenti Alonzo kutingisha kichwa.
“Katika maelezo yako umesema unadhani Naomi
Lindsey ni Rosemary macha , je unadhani pia Rosemary Macha anaweza kuwa mwanamke
aliefariki katika ajali ya radi akiwa na watoto wake?”
“Wakati nikiwa Ajenti nilibahatika kuona picha ya Chakwe mhangwa wa ajali ya radi na picha yake inafanana kwa asilimia mia moja na picha ya Naomi Lindsey na Rosemary Macha , hivyo naweza kusema wote wanaweza kuwa mtu mmoja”
“Kwa hitoria ya Naomi Lindsey hajawahi kabisa kuwa na mtoto katika maisha yake na pia kulingana na umri wake ni ngumu kuwa na watoto kumi , tena wa baba tofauti tofauti , lakini pia kuna historia ya kimatibabu ambayo inaonyesha Naomi
Lindsey hawezi kubeba ujauzito kutokana na kukosa kizazi , kama unachodhania ni sahihi unadhani watoto aliokuwa nao Chakwe ni wa nani?”Aliuliza Alonzo na kumfanya Amosi akili yake kufanya kazi na sasa ni kama anapata kitu kipya na kujiambia kwanini hakuwahi kufikiria hilo.
“Nadhani Mr Amosi utakuwa na maswali kwanini nakuuliza maswali yote haya , kabla ya kujua unachokwenda kufanyia kazi nilitaka kujua unachojua kwanza, nadhani wakati unakutana na Chriss alikuelezea wewe ndio mtu sahihi katika misheni aliokupatia si ndio?”
“Ndio alisema hivyo na ilinishangaza pia kusikia hivyo?”
“Kuna sababu yoyote ambayo unadhani kwanini tulikuchagua kwa hii misheni?”
“Sijui , labda ni kwasababu nishawahi kuwa chini ya kitengo cha TISA na kuhusika kwa namna moja na kesi hio ya Radi”Aliongea Amosi na Alonzo alitingisha kichwa kukataa na palepale aliangalia tablet yake na alionekana kupangusa pangusa na kisha alimpatia Amosi.
Katika Tablet ile kulionekana picha ya watu wawili , mwanaume na mwanamke na kwa jinsi pozi lao lilivyo katika picha ni aidha watu hao walikuwa wapenzi au marafiki”Amosi alishangaa mara baada ya kuona ni picha ambayo alikuwa akiifahamu na yeye ni moja ya mhusika aliekuwa katika hio picha.
“Unaweza kuniambia huyu mwanamke pembeni yako alikuwa nani kwako?”
“Huyu ni Jasmine Mahmood niliwahi kuwa nae katika mahusiano kwa muda mfupi, alikuwa raia kutoka Botswana aliwahi kuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Aljazeera English nchini Qatar”Aliongea na kumfanya Alonzo kuchukua kile kishikwambi kwa mara nyingine na kisha alionekana kutafuta kitu na kumpatia.
Ilikuwa picha nyingine ikimuonyesha Jasmine Mahmood akiwa na Naomi Lindsey katika pozi la tabasamu na picha ile ilimshangaza mno Amosi.
ITAENDELEA.

JUMATATU , JUMA TANO NA JUMAMOSI NDIO RSTIBA ZETU KWANZIA LEO.
UKITAKA KUSOMEA WATSAPP NICHEKI 0687151346
Hamza wew
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZ:SINGANOJR


SEHEMU YA 55.
USIKU WA JANA.
Hamza mara baada ya kutoka nje ya geti alisogelea moja ya gari ya Mercedenz iliokuwa imesimama mita kadhaa kutoka katika geti la nyumba yao na kisha aligonga kioo cha mbele na muda uleule kioo kile kilishushwa na ndani ya gari hio alionekana mwanaume alievalia suti, mweusi mwenye makadirio kama ya miaka therathini hivi.
“Bosi pole kwa kusubiri muda mrefu?”Aliongea Hamza kinafiki na kumfanya yule bwana kutoa tabasamu na kisha aliangalia chini.
“Umejuaje nakusubiri Bro”
“Huna haja ya kujifanya mjinga, ilihali umefanya kila hila ya kupata ‘Attention’ yangu nijue unanifuatilia”Aliongea Hamza na kumfanya yule bwana kutoa tabasamu.
“Ni kama nilivyodhania umeniona , unaonaje ukiingia ndani ya gari Bro”Aliongea na kumfanya Hamza kuzunguka upande wa pili na kuingia katika ile gari.
Kilichomfanya Hamza kujua gari hio ilikuwa ikimfuatlia ni mara baada ya kuiona zadi ya mara tatu katika safari nzima ya kutoka hospitalini mpaka kufika Kigamboni.
Wakati alipokuwa akiongea na Regina nje ya hospitalini karibu na maegesho ya magari aliweza kuiona na wakati wanasubiria Taksi kuwachukua kwenda nyumbani iliwapita , Hamza mwanzoni hakuitilia sana maanani kutokana na dereva kutoonekana kuwa na nia yote mbaya lakini mara baada ya kuona ikiwa imesimama mita kadhaa kutoka kwenye geti la nyumba yao aliona kabisa dereva wa gari hio alikuwa akifanya makusudi ili kumjulisha kwamba anamtafuta.
“Bro wewe sio wa kawaida , umeweza kuwashinda wale Maninja wa kundi la Nyoka na kisha kumuokoa Bosi Regina katika mlipuko wa gari , uwezo ulioonyesha sio wa mwanajeshi wa kawaida aliepitia mafunzo ya kikomandoo, naweza kusema wewe ni zaidi ya mwanajeshi. unaweza kuniambia mafunzo yako ni ya namna gani na uwezo wako kwa ujumla?”Aliongea yule bwana huku akiwa na hali ya urafiki katika macho yake.
“Na wewe unaweza kuniambia ni nani haswa na kwanini umefanya kila hila nikutambue?”
“Oh , Samahani bro kwa kutokujitambulisha, Naitwa Norbert Geza kutoka kitengo cha usalama wa nchi”Alongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa.
“Sawa bwana Geza , je kuna sababu yoyote ya jeshi kunifuatilia?”
“Ni maswala ya Usalama wa nchi ndugu Hamza ,
tukio kama la leo tuna kila sababu ya kukufuatilia”Aliongea na kumfanya Hamza amwangalie.
“Mnapanga kufanya nini kuhusu tukio la leo , maana kama mlivyoona kuna watu wanataka kuniua mimi na bosi wangu, mpango wenu ni nini au mnapoteza muda kunifuatilia ila hakuna chochote mnachofanya”
“Tunapanga kulichukulia hatua swala hili lakini hatua ya kwanza ni hii ya kuongea na wewe , nipo hapa kwa ajili ya kukutuliza na kukutaarifu kwamba wote waliohusika hapa tutawaonya wasirudie tena kuyumbisha usalama wa nchi na raia wake”
“Haha.. mbona kama kauli yako ni ya kimaigizo na onyo kwa wakati mmoja, mimi ndio nimeshambuliwa lakini ninachoona hapa unanipa onyo nisichukue hatua kwa wale waliohusika, kama watu wameweza kukodi kundi hatari kama
hili kwa ajili ya kuhakikisha tunapoteza uhai, unadhani unachoongea hapa kinaweza kutekelezeka?”
“Kama nilivyojitambulisha Mr Hamza , kupitia vitengo vyetu ya kiusaama vya nchi tutafanya kila linalowezekana , Tanzania ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya haki na sheria , hatuwezi kumruhusu mtu kufanya anachotaka , hivyo naomba usiingilie kazi ya jeshi na kusababisha matatizo zaidi , Idara ya usalama wa nchi haiwezi kufumbia macho maswala kama haya”
“Unaongea ujinga na upuuzi , nilikuona kule hospitalini na nikakuona tena baada ya mlipuko , hii inamaanisha mlijua tukio kama hili litatokea , nyie kama kweli ni sehemu ya usalama wa nchi , kwanini hamkuzuia tukio kama hili, hii moja kwa moja inaniaminisha kwamba watu waliohusika wapo ndani ya idara zenu na walikuwa wakiangalia nini kinachokwenda kutokea , sasa kwasababu umejileta mwenyewe unaonaje ukinitajia kabisa wahusika”
“Hamza unamaanisha nini , kwahio unataka kwenda kinyume na msimamo wa idara ya usalama wa nchi?”Aliuliza yule bwana na kumfanya Hamza macho yake kuchanua na kumwangalia kwa umakini.
“Kama huna taarifa yenye maana kwangu basi naweza kusema muda umeenda na nataka kwenda kulala”Aliongea Hamza na kisha alifungua mlango na kutoka nje.
Norbert aliishia kumwangalia tu , isitoshe alikuwa akimhofia kwa kile alichokuwa amekiona leo hivyo hakuona haja ya kubembeleza.
Mara baada ya kumuona Hamza akirudi ndani aliendesha gari mpaka mita kadhaa kwenye moja ya nyumba iliokuwa geti la njano katika mtaa huo huo na mlango ulifunguliwa na wanaume wanne waliovalia mavazi ya kiraia na kisha kuingia ndani ya gari ile.
“Kapteni vipi kuhusu Hamza amekuelewa ?”
“Sina uhakika , huyu dogo inakuwa ngumu mno kujua ni kitu gani anapanga kufanya , tunapaswa kuwa makini tusiruhusu akasababisha matatizo hasa kipindi hiki cha uchaguzi”
“Haya yote ni kutokana na tamaa za mheshimiwa mstaafu na familia ya Mzee Benjamini na kuendelea kumchokoza Bosi Regina kila siku , anadhani kwasababu ya kuwa mstaafu anaweza kufanya chochote na kujimilikisha hii nchi”Aliongea mmoja ya wale watu kwa chuki kubw.
“Ni kwasababu hakuna anaeweza kumfanya chochote Mstaafu , nchi ilimwacha afanye chochote na sasa mizizi yake ipo kila kona ya nchi kwanzia kwenye uchumi mpaka kwenye siasa, Familia ya Benjamini ni sehemu ndogo sana katika Ngome yake”
“Ndio maana wanadharauliwa na huyu Hamza kwa kutumika kizembe”
“Hii ni misheni yetu ya kuhakikisha nchi inakuwa salama , sisi ni wanajeshi na lazima kila tunachofanya kinazingatia sheria na katiba ya nchi , vinginevyo hatuwezi kuwa tofauti na wahalifu”Aliongea mwingine.
“Haina haja ya kulalamika, kwasasa tokea tuanze kufatilia matukio yote yanayoendelea hatuwezi kusema usalama wa nchi upo hatarini , tunapaswa kuendelea kuwa makini na kila hatua wanazochukua , lazima tutimize kila wajibu ambao tumepewa na wakuu wetu”Aliongea Kapteni. “Ndio tumekuelewa Kapteni?”
“Ayubu vipi bado hujampata Amosi?”
“Afande Rama anaendelea na uchunguzi bado ,
Jasusi mara ya mwisho alionekana katika Mgahawa Masaki na baada ya hapo hajaonekana tena na hakuna alama alioacha nyuma inayoweza kutufanya kupiga hatua ya kujua alipo”
“Vipi ndani ya Kanisa la Wabrazili , hakuna ‘Movement’ zozote za kutilia mashaka?”
“Kuna mtu wentu ndani ya kanisa na mpaka sasa hajawasilisha taarifa yoyote , nadhani bado hakuna cha kutilia mashaka”Aliongea Ayubu na kumfanya Kapteni Norbert kufikiria kidogo.
“Kuna kitu lazima kinaendelea, nimesikia na Afande Danieli anamtafuta Amosi, Mzize wewe kwanzia kesho endelea kumfatilia Kanali Dastani kila hatua anayopiga na kisha unipe Ripoti. Fadhili wewe utaendelea kumfuatilia Hamza pamoja na washikaji zako” “Sawa Kapteni”
“Hebu waulize kwanza tujue kama Hamza bado yupo nyumbani”Aliongea na kumfanya bwana alieitwa Fadhili kutoa simu palepale na aliongea kwa dakika kadhaa na kukata.
“Bado yupo nyumbani Kapteni , hakuna Kamera inayoonyesha akitoka”
“Vizuri, kama kuna lolote litakalotokea mtanijuza naenda nyumbani”Aliongea na mabwana wale walikubali na kisha walishuka katika ile gari na kuingia ndani ya nyumba ile yenye geti na Kapteni Norbert alitoweka katika eeo hilo.
Sasa upande mwingine wakati wakijua Hamza yupo nyumbani ukweli ni kwamba alikuwa ashaondoka muda mrefu kwa kuzikwepa Kamera na hata simu yake aliacha hapo hapo nyumbani maana alijua lazima Ma ajenti hao wanafuatilia hadi simu yake.
Muda ulikuwa umeenda na kuna maeneo ndani ya mtaa huo wa Egret yalifunikwa na vivuli vya miti na ndio aliotumia kupotelea mpaka kwenda kutokea katika mtaa mwingine kabisa.
Hamza mara baada ya kuona amefika mbali kabisa na nyumbani alitoa simu ndoto ya batani na kisha alitafuta namba ya Lawrence msaidizi wa Dina.
“Bro muda umeenda sana , kuna kitu unataka nikusaidie?”
“Kundi la kininja la Black Eared Snake lipo Tanzania , nataka kujua eneo walipo?”
“Bro ! , Umejuaje wapo Tanzania na kwanini unataka kujua walipo?”Aliuliza Lau upande wa pili.
Hamza alikuwa akijua moja ya kanuni kubwa ya kundi hilo la kininja ni kusafiri kimakundi , kwa mfano ikitokea kazi ya kuua mtu katika eneo husika lazima na kiongozi wao asafiri kwenda kuweka makazi ya muda katika eneo hilo, Hamza alijua akimkamata kiongozi ndio atakavyyoweza kumpata mtu ambae anataka kumuua kwa kumsababishia ajali za mara kwa mara.
“Wewe niambie wapo wapi , kwa Network yenu lazima mtakuwa na taarifa zote”
“Lakini Madam ashalala tayari , unaonaje nikimuamsha na kumwambia kwanza?”
“Ukiendelea kuongea ujinga sitokutambua kama Bro tena , sasa chagua kuniambia au kwenda kumuamsha bosi wako”Aliongea Hamza kwa sauti ya kibabe.
Lawrence upande wa pili hakuweza kumkatalia kwani alimhofia Hamza licha ya kwamba alikuwa ni kama rafiki yake hivyo aliamua kumtajia eneo walipo.
Hamza mara baaada ya kuambiwa eneo husika aliona ni umbali mrefu mno hivyo aliona hawezi kutembea zaidi ya kupanda Taksi ya kumfikisha huko. ******
Upande mwingine ndani ya jumba la kifahari linalopatikana katika eneo la Tegeta walionekana baadhi ya watu wakiwa wameketi eneo la ukumbi.
Walikuwa ni mabosi wenye pesa nyingi na walionekana kuwa na mabodigadi waliombatana nao na kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea.
Alionekana Kanali Mstaafu Fanueli Yowe akiwa amekaa kwa kuegamia kwenye Sofa akimwangalia kwa macho ya ukauzu bwana aliekuwa amekaa mbele yake , ambae amevalia Jaketi la leather , bwana huyo alikuwa mweusi tii na amejaa makovu usoni.
“Mr Snake, umoja wetu umekuwa ukishirikiana na kundi lako la Black Eared Snake kwa miaka saba sasa , katika kipindi hicho chote tumeweza kusimamia madili mbalimbali ya siraha ambazo ziliingia nchini kwako na umeweza kujiimarisha kwa kiasi kikubwa na kuweza kufanya kundi lako kutambulika duniani kutokana na uwezo wa juu , lakini leo ndio mara ya kwanza umetuangusha na kutukatisha tamaa kabisa”Aliongea Fanueli Yowe , huyu ndio bwana ambae ni kiongozi wa kundi la watu wenye ujuzi wa sanaa ya mapigano.
Mr Snake ndio aliekuwa kiongozi wa kundi la kininja la Black Eared Snake , kutokana na kundi lake kupewa misheni ndani ya Tanzania iliokuwa na malipo mazuri ndio maana alisafiri na maninja wake kukamilisha kazi ya kumuua Hamza na Regina.
Genge la mabosi wala keki ya taifa ambao wameamua kujipa jina la kuzugia la Martial Art Association walikuwa ni washirika wakubwa na kundi hilo la kininja kwa muda mrefu ndio maana hata kazi ya kumuua Regina walipewa wao.
Unaweza kushangaa kwanini kundi hili litake kumuua Hamza na Regina, ukiachana na kwamba Master Konki ambae alikuwa mwanachama kupewa kibano na Hamza kiasi cha kuwa na chuki lakini upande mwingine kundi hili lilikuwa na sababu za kutaka kuona Regina pia anakufa.
Mwanzilishi wa kundi hili alikuwa ni Mheshimiwa Mgwenno ambae ndoto yake kubwa baada ya kuwa kiongozi mkuu wa taifa ni kutaka kuimiliki Tanzania.
Mheshimiwa Mgweno katika mbinu za kutaka kuimiliki Tanzania ndio alianzisha makundi mengi ambayo hakujihusisha moja kwa moja lakini alikuwa na nguvu ya kimaamuzi na moja wapo ni kundi hili la Umoja wa watu wanaojua Mapigano, moja ya sababu kubwa aliofanya kuunda kundi hili ni kuhakikisha katika kuendeleza kuwa na maslahi yake anakuwa upande mzuri na jeshi , isitoshe pia alikuwa mwanajeshi Komandoo kabisa kabla ya kuingia katika siasa hivyo ilikuwa rahisi kwake kushawishi wanajeshi kutengeneza kundi hilo.
Sasa kutokana na wanajeshi hao kupata pesa nyingi na pesa kuwanogea walitoka katika miiko ya kazi na kuwa wahalifu wanaojilinda katika vazi la kujiita makomandoo na jambo hilo lilimfurahisha sana Mheshimiwa Mgweno na katika kukamilisha mambo yake aliwatumia sana.
Sasa mara baada ya swala la Hamza na Regina kuletwa mezani na kiongozi wa kundi hilo Fanueli Yowe akimwakilisha mheshimiwa Mgweno moja kwa moja waliona kazi ya kumuua Hamza wawapatie washirika wao wa muda mrefu yaani Assassin wa Black Eared Snake kumaliza kazi hio, hayo yote ni kutokana na kuona uwezekano ni mdogo wa kupambana na Hamza ana kwa ana.
“Kundi letu la Nyoka Mwenye masikio meusi linahistoria ya miaka ishirini tokea kuanzishwa kwake na hatua kwa hatua tuliweza kutambulika kimataifa na ni juzi tu hapa miaka kumi iliopita tuliweza kutambuliwa na Surety International Association na kupewa cheo cha daraja C katika ulimwengu wa maninnja, uzoefu wa kazi za kuua tunazo ni kwamba tu mtu ambae mmetupa kazi ya kumuua awamu hii anaonekana kuwa na mafunzo ya juu na pengine ashawahi kuwa mwanajeshi, Afande Yowe huna haja ya kuwa na wasiwasi , kwasababu mmeshatulipa pesa nyingi juu ya hii kazi nina wahakikishia tutaimaliza haraka iwezekanavyo”
“Unaongea ujinga , tulikuambia kabisa hili ni swala ambalo linatakiwa kufanyika mara moja , lakini angalia mmefeli na kufanya mkuu wa majeshi anatupa tahadhari , kazi imekushinda tunataka urudishe malipo tuliokupatia”Aliongea bwana mmoja mwenye kitambi aliekuwa amekaa pembeni.
“Turudishe hela! Chochote ambacho sisi Noka wa Masikio meusi tunameza hatuwezi kutapika”
“Kazi imewashinda na mnataka kula pesa yetu , hamna aibu?”Aliongea yule bwana kwa hasira huku akigonga meza , alifahamika kwa jina la Afande Sucre.
Maneno ya Sucre yalionyesha kumkasilisha mmno Mr Snake huku akionyesha nia ya kutokubaliana nae kabisa.
“Mzee Sucre kaa chini ili tuweze kusikia mpango B wa Mr Snake”
Muda uleule Mr Snake alichomoa kisu chenye kifimbo chekundu , kilikuwa kidogo mno urefu wa kidole cha mkono na kilionekana chepesi na alitumia kisu kile kujikata kucha huku akiongea.
“Wote hapa ni wanajeshi lakini sijui kama mshawahi kusikia neno maarufu katika vita lifahamikalo kama Original Strike?” “Unaongea upuuzi gani ?”Aliongea Sucre kwa hasira.
“Katika ulimwengu wa kimasenari ikitokea umeshambuliwa kitu cha kwanza unachopaswa kufanya ni kutafuta chanzo cha shambulizi kwani ndio njia nzuri zaidi ya kutatua tatizo , kama hisia zangu ni sahihi huyu kijana wenu mnaemwita Hamza lazima atatafuta namna ya kututafuta ili kulipiza”
“Unamaanisha nini , kwahio unasema anaweza kuja ndani ya hili eneo?”
“Sidhanin kama ni mjinga kuja eneo hili , maana itakuwa ni kujitafutia kifo”Aliongea bwana mmoja mwwenye mwili mkakamavu.
“Mnakosea, kwa taarifa mlizonipatia makisio yangu ni sahihi , anajiona ni mpiganaji mzuri na lazima ataamini anao uwezo wa kutudhibiti , hivyo atatudharau , isitoshe wengi wenu hapa mnaonekana wazembe wazembe”Aliongea na kumfanya Afande Yowe macho yake kusinyaa, ni kweli kabisa katika mapigano licha ya kwamba wanajiita wanajeshi lakini ni wanajeshi wa kutumia siraha na sio kupigana.
“Mr Snake kama kweli Hamza akija hapa , unadhani vijana uliokuja nao watatosha kudili nae?”Aliuliza na kumfanya Mr Snake kwa kujivunia kabisa kugeuza macho yake na kuangalia wanaume waliosimama nyuma yake , walikuwa ni wanaume wenye miili iliojengeka kimazoezi huku wakiwa wamenyoa vipara, hawakuwa na ishara ya uzembe hata kidogo. “Kama akijileta ndio mtajua nini kitakachotokea?”
“F**ck you Hamza , jiafanye mjinga na ujilete hapa nitampasua na risasi moja tu”Aliongea Sucre na kitambi chake huku akikoki kwa mbwembwe bastora yake.
“Mkuu mimi sidhani kama atakuja hapa na muda umeenda , nadhani kikao kishaisha, nina miadi hivyo nitatangulia kuondoka”Aliongea Afande Sucre na kusimama akifuatiwa na mabodigadi wake.
Lakini sasa muda ambao anafikia mlango ili kuufungua ulifunguliwa kwa kishindo na mara baada ya kuangalia vizuri ni mabodigadi waliokuwa wakilinda kwa nje, walikuwa wamepoteza fahamu wakiwa wamerushiwa mlangoni.
Muda huo watu wote walikodolea macho mlango na waliweza kumuona kijana mdogo akiwa amesimama kwenye mlango huku akitafuna bublish na nyuma yake walionekana mabodigadi waliokuwa wakilinda wakiwa chini wengine wakionekana hawana fahamu na wengine walikuwa wakiugulia maumivu.
Afande Sucre alijikuta akimeza mate mengi huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi.
“Wewe ni nani?”Aliongea huku mkono ukiwa umeshafika kwenye kiuno sehemu iliopo siraha yake.
“Naitwa Hamza Mzee, mtu ambae unataka kumpiga risasi na hio bastora yako”Aliongea
Hamza akiwa na muonekano uliojaa uzembe.
Afande Yowe macho yake yalimtoka , hakuamini Hamza angefika hapo kama alivyosema Mr Snake.
Afande Sucre alijikuta akirudi nyuma kwa namna ya kujihami na kuungana na wezake.
Upande wa wanajeshi wote wa kundi hilo wanaojiita wanaojua mapigano walijikuta wakisimama kwa wasiwasi na mshangao.
“Wewe ni jasiri mno , hakika unasttahili kuitwa mwanajeshi kwa kujileta hapa”Aliongea Mr Snake akiwa na tabasamu usoni akijiambia anakwenda kuimaliza kazi muda huo huo ndani ya eneo hilo.
Ukweli ni kwamba licha ya kundi hilo kusikia habari za Hamza wengi wao hawakuwahi kuonana nae ana kwa ana zaidi ya Master Konki ambae hakuwepo kwenye kikao hicho..
“Mr Snake ulichoongea kimeonekana kuwa kweli , nipo tayari kuona kile ambacho
umeandaa”Aliongea Afande Yowe na wenzake wote walitingisha kichwa.
“Subirini kwanza?”Aliongea Hamza akinyoosha mkono.
“Unataka kuongea nini , usije ukasema unaona woga wakati umejiingiza kwenye pango la Simba”
“Sijaja hapa kupigana wala kuibua mzozo na mtu , kwa ninavyoona hapa wengi wenu mnaonekana kuwa na vyeo serikalini hivyo sitaki kujiletea matatizo”Aliongea Hamza na kuwafanya wale watu kumwangalia kwa mshangao.
“Kama hujaja hapa kupigana umekuja kufanya nini?”Aliuliza Mzee Yowe.
“Nimekuja kuwapa onyo, leo baada ya kushambuliwa na maninja wa kundi la nyoka nilijua fika kuna mkono wa mtu wenye nguvu umehusika , hivyo sitaki ugmvi na mtu yoyote na muache kushambulia watu wa karibu yangu”
“Onyo!! , Wewe ni nani wa kutupa onyo , unajua vyeo vyetu katika jeshi , kwanini mtoto mdogo kama wewe tukubali onyo lako, ukiburi umekujaa”
“Kwamaneno yako naona kabisa haupo tayari kuikumbatia hii fursa ninayokupatia , hebu jifikirie
mara mbilimbili kabla ya kuendelea kunichokoza”Aliongea .
“Wewe mtoto ni kichaa na bora umejilera mwenyewe, kama hukufunzwa adabu tutakufunza leo”Aliongea Sucre.
“Upo siriasi?”
“Unadhani natania , unadhani naweza kuogopa panya mdogo kama wewe”Aliongea.
“Mr Hamza asante kwa kufika hapa kwa ajili yangu ili niwaonyeshe ni kwa namna gani naenda kudili na mtu kama wewe”
“Na mimi nimekuja kuona unadili vipi na mimi?”Aliongea Hamza na muda uleule Mr Snake alipiga mluzi na kufumba na kufumbua kundi la watu waliovalia mavazi meusi walijitokeza na kuingia katika ukumbi huo huku wakiwa wameshikilia siraha.
Kitendo cha watu wale kutokeza kiliwafanya watu wote kushangaa akiwemo Mzee Fanueli.
“Mr Snake kumbe ulikuwa na kundi la watu wengi namna hii?”
“Nisamehee afande kwa kukutokutaarifu mapema , nilikuwa nimejiandaa kudili na huyu mtu ndio maana nimechukua kila tahadhari”
“Sidhani kuna haja ya kupoteza nguvu za vijana wetu , risasi zinamtosha”Aliongea Afande Sucre na alitoa bastora yake akifuatiwa a mabodigadi na bila ya kujiuliza mara mbilimbili walimfyatulia Hamza mfululizo mpaka bunduki zikaishwa risasi lakini kitu cha ajabu ni kwamba risasi zile ni kama zilikuwa zikipiga hewa , Hamza walikuwa wakimuona mbele yao lakini ilikuwa ni kama holograph ya Hamza , ile wanamaliza Hamza alikuwa palepale mbele yao akiwa na tabasamu.
Swala lile liliwashangaza mno wale mabwana na hofu na wasiwasi iliwavaa, walimuona Hamza kama mzimu.
“Wewe ni binadamu au Mzimu!!!”
Mr Snake alijikuta akibung’aa huku akimwangalia Hamza kwa hofu na kuna kila hali iliokuwa ikimwambia Hamza aliwafanyia kiini macho ili waamini alikuwa mbele yao lakini muda mrefu alikuwa ashapotea na amerudi baada ya kuacha kushambuliwa.
Aliona kama hisia zake ni sahihi basi njia moja tu ya kudili nae ni kushambulia ana kwa ana na sio kwa kutumia siraha kama bunduki.
“Sijaja hapa kujibu maswali , nimewapa nafasi mmeikataa”Aliongea Hamza huku akipiga hatua lakini Mr Snake alifyatuka na kumsogelea Hamza kwa spidi akiwa na kisu amekitanguliza mbele kininja kwa kumlenga eneo la shingoni.
Kitendo cha Mr Snake kumfikia Hamza usawa wa shingo mkono wake ulioshikilia kisu ulidakwa kwa spidi ya juu kiasi cha kushindwa kukwepa na kuzungushwa kwa nguvu na maumivu aliohisi alijikuta akikiachia kile kisu mwenyewe.
Hamza hakuchelewesha wakati kisu kule kinadondoka katika mikono ya Mr Snake alikidaka na mkono wa kushoto na bila ya huruma alimkita nacho Mr Snake katika paji la uso na kuzama ndani kabisa.
“Master!!!”
Maninja wawili waliokuwa karibu na bosi wao mara baada ya kuona amekitwa na kisu cha paji la uso walijikuta wakipiga yowe na kwa hasira kubwa waliinua mapanga yao na kumsogelea Hamza kwa spidi kana kwamba wanataka kumtenganisha shingo na kiwiliwili.
Wa kwanza mara baada ya kumsogelea Hamza kwa spidi kwa mtindo wa kutaka kumfyeka shingoni ,Hamza alimkwepa kuinama chini na upanga ulipita hewani na kisha palepale kwa ustadi wa hali ya juu aliachia ngumi nzito iliompiga bwana yule eneo la moyo na kilichoweza kusikika ni mbavu zake kuvunjika na alidondokea mbali huku akikodoa macho na kutema damu kisha akadondoka chini isieleweke kama amekufa au amezimia ,hakuzubaa baada ya shambulizi lile mwingine alikuwa ashamfikia akinuia kutaka kumchoma na upanga eneo la tumboni lakini Hamza alikuwa mwepesi kwani alikwepa kisu kile na kupita kwenye mbavu kiasi cha kuchana nguo aliovaa na palepale alimpiga bwana yule teke la kigoti na kumfanya kupinda na ilikuwa ni nafasi ambayo Hamza aliitaka kwani alimtandika ngumi nzito ya paji la uso iliomdondosha Ninja yule chini na kuzima palepale.
Haikuwa kwa Sucre na wenzake ama kwa kiongozi wao Afande Yowe , wote walijikuta wakipatwa na mshituko usio na kifani huku hali ya woga ikiwavaa , Afande Yowe Bastora yake ilikuwa na risasi lakini alishindwa kuchukua maamuzi ya kuitumia kutokana na kile alichoona baada a Hamza kutoathirika na risasi.
Wale maninja wengine mara baada ya kuona wenzao walivyojeruhiwa walisita kufanya mashambulizi na kumwangalia tu kwa wasiwasi , isitoshe mkuu wao alikuwa ndio mtaalamu wa hali ya juu na mabwana wawili waliozimishwa kwa ngumi moja moja tu ndio walikuwa wakifuatilia kwa uwezo sasa wanawezaje kumshambulia mtu ambae amemuua mkuu wao kwa shambulizi moja.
“Kajikundi kadogo ka daraja C wanaona wanaweza kushindana na mtu kama mimi”Aliongea Hamza mara baada ya kuona kazi yake ni njema na alipiga hatua kumsogelea Fanueli.
“Unajua kwanini tumefikia hatua hii?”Aliuliza Hamza na kumfanya Afande Fanueli kutingisha kichwa kusema hajui.
“Mmekodi watu kwa zaidi ya mara tatu sasa kwa ajili ya kuja kunishambulia na hata kutuma hawa wapuuzi mkiamini wanaweza kunishinda, lakini yote hayo yaliotokea mmeshindwa kujiuliza swali moja jepesi tu, na swali lenyewe mlipaswa kujiuliza mimi ni nani kwanza kabla ya kuchukua hatua , tokea mwanzo nilijua tu mnajitafutia matatizo kwa kunichokoza , nilitaka kuwavumila lakini inaonekana nguvu yenu hapa nchini imewapa kiburi na hamuwezi kunusa hatari”
“Mr Hamza tafadhali tunaomba usitufanyie chochote , tupo tayari kufanya chochote , najua unamahusiano makubwa na kiongozi wa mtandao wa Chatu nipo tayari kuongezea nguvu mtandao huo, tumefanya haya yote kutokana na presha kubwa kutoka kwa familia ya Mzee
Benjamini”Aliongea lakini Hamza hakumjali na muda uleule alimgeukia Afande Sucre.
“Wewe mzee njoo hapa”Aliongea Hamza na kumfanya Afande Sucre kutetemeka lakini kwa hofu kubwa alimsogelea Hamza.
“Mr Hamza kama kuna chochote unataka niambie nitafanya”Aliongea kwa kunyenyekea na kufanya wenzake kumwangalia kwa macho yaliojaa dharau kwa namna alivyonywea. “Nipe hio Bastora yako”
“Eeh!”
“Hutaki kunipa?”
“Hii hapa”Aliongea Sucre kwa haraka mara baada ya kusika sita kumpatia Hamza
Hamza mara baada ya kuishika ile bastora aliangalia ndani yake kama ina risasi na ilionekana kuwa nazo tatu na kitendo cha kuiweka sawa alikuwa ashaachia risasi ambayo ilitoboa paji la uso la mzee Sucre
Sucre hata hakujua amepigwaje risasi maana mkono wa Hamza ulifyatuka kwa spidi kubwa mno lakini ndio hivyo ilikuwa mwisho wake.
Hamza hakujali maiti ile na alimgeukia Fanueli ambae alikuwa akitetemeka kwa hofu pamoja na kundi lake.
“Nilisema kabisa sijaja kupigana lakini ukaamua kunidharau”
“Mr Hamza nilikosea tafadhari naomba unisamehe hili lipi…”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake alikuwa ashachapwa lisasi mbili za kichwa na kudondoka chini.
Ndani ya dakika chache Hamza alikuwa ashamuua kiongozi wa kundi la Nyoka Mwenye masikio Meusi na Kanali Mstaafu Afande Fanueli Yowe.
“Kuna mwingine anataka kufa?”Aliuliza Hamza huku akiwaangalai waliobaki na kila mmoja alionekana kuwa katika hali ya kutetemeka huku baadhi wakitaka kujikojolea na waliishia kutingisha vichvwa vyao wakitia huruma.
Hamza hakuwa na mpango wa kumuua mtu
wakati anakuja hapo lakini uchokozi ulizidi hivyo alilazimika kutoa fundisho.
“Mimi ni kijana mpole sana tena mwanachuo , lakini naomba niwaambie tu Sipendi
Uchokozi”Aliongea Hamza na kisha alirusha ile bastora chini kisha alitoa simu yake ya batani na kuangalia saa na aliweza kuona muda ulikuwa umeenda sana.
“Nadhani taarifa zitamfikia anaewapa kiburi cha kutaka kufanya chochote ndani ya nchi hii, mwambieni ajifikirie mara mbili mbili kabla sijamchukulia hatua”Aliongea Hamza na kisha aliondoka ndani ya eneo hilo.
*****
“Wakati ulipokuwa umelela sijafanya chochote mbona?”Aliongea Hamza akiwa katika simu na Dina.
“Bado unaongea kimatani tu , asubuhi nimesikia taarifa umemuua Mzee Fanueli Yowe, mstaafu Mgweno ametoka kunipigia hapa anaomba yaishe”Aliongea Dina na kumfanya Hamza kucheka , ilionekana onyo ambalo alitoa jana limefanya kazi.
“Kuna onyo nilijaribu kutoa jana usiku na limefanya kazi , tumia nafasi hii kujiimarisha”Aliongea Hamza.
“Unajua kusababisha matatizo sana , sidhani pia kama ameomba kuyamaliza kwa nia ya dhati , kuna uchaguzi mwezi ujao ndio maana kaamua kujishusha, Mgweno ninaemjua mimi sio mtu wa kukubali yaishe kirahisi’
“Kama hajanielewa muache aje hata baada ya huo uchaguzi, mimi sipendi uchokozi ni hivyo tu basi , nitapambana kulinda amani yangu”Aliongea
Hamza na upande wa pili ulionekana kuwa kimya.
“Vipi baadae unakuja kunisalimia , sijakuona muda mrefu?”
“Muda mrefu wapi wakati ni juzi tu hapa?”
“Hata kama hakikisha unakuja usiku la sivyo nitakuja kuruka ukuta na kuingia ndani ya hilo kasri unaloishi siku hizi”Aliongea na kumfanya Hamza kuishia kukubali tu.
Hamza mara baada ya kumaliza kuongea na Dina alikata simu mara moja na muda huo ndio alikumbuka alikuwa ameghairisha mara kibao kwenda nyumbani kwa Eliza na pia kulingana na ratiba za siku hio aliona ingekuwa ngumu pia kwenda hivyo alimpigia simu na kumwelezea kuwa hatoweza kumtembelea.
Baada ya kuoga alivaa nguo na kisha alishuka chini sebuleni na aliweza kumkuta Regina akiwa bize jikoni akitengeneza Sandwich kwa kutumia kutumia Sausage.
“Regina unatengeneza Sandwichi au kitu gani?”Aliuliza Hamza.
“Sio lazima kujua ninachotengeneza”Aliongea huku akizidi kuwa bize, alionekana kujivunia kwa kile alichokuwa akifanya.
Kutokana na Shangazi kutokuwepo nyumbani aliona aingie mwenyewe jikoni.
Hamza alikumbuka Shangazi akimwambia Regina hakuwa akijua chochote kuhusu kupika hivyo alishangaa kumkuta jikoni.
Alijua Regina atatengenea utopolo wa chakula hivyo alifungua friji na kutoa mayai, tambi na nyama , vitunguu na pilipili hoho. “Unafanya nini , utachafua vyombo tu”
“Nitaviosha baadae nikirudi”
“Unadhani kula sana ndio afya , kwanini usisubiri tule hiki ninachopika?”
“Haijalishi nakula sana , sijui nitaishi kwa miaka mingapi mbeleni , mtu unapaswa kula kila unachojisikia maana hujui ni lini utashindwa kula”
“Mawazo yako yanasikitisha , kwahio unadhani kwasababu huwezi kuishi muda mrefu unachopaswa ni kula tu na sio kufanya vitu vingine ya msingi?”Aliongea huku akikunja sura lakini Hamza alikuwa mvivu kujibishana nae na alianza kusaga saga ile nyama.
Muda huo vipande viwili vya mkate vilichomoka ndani ya kibaniko.
“Aiyaa..”Regina alijikuta akishangaa huku akikunja ndita.
“Nini tatizo?” Aliuliza Hamza na huku akimgeukia na mara baada ya kuangalia kilichokuwa kikimshangaza Regina alijikuta akianza kucheka
“Haha.. Regina huo ni mkate au ni pande la mkaa?”
Vipande hivyo vya mkate vilikuwa vimegeuka kuwa vyeusi tii na sio Brown kama alivyotarajia.
“Unacheka nini sasa , nimezidisha moto ndio maana umeungua”Aliongea na kumfanya Hamza kusogea karibu na kuangalia
“Aina ya hii mikate inahitajika nyuzi tatu tu za joto kuubanika, sasa wewe umeweka sita unadhani nini kitatokea?”Aliongea na kumfanya Regina kuangalia mashine hio ya kibaniko na kuona kweli aliweka joto la juu mno.
“Nilikosea”Aliongea huku akirekebisha na kuanza kubanika upya vipande vya mikate ili ajazie na Sausage.
“Nilijua ni mzoefu wa kutumia hizo mashine za kupikia”
“Endelea na unachokifanya achana na mimi”Alimsukumia pembeni huku akiendela kuwa bize.
Baada kama ya nusu saa kila mtu alikuwa ameshamaliza kutengeneza kile alichokuwa akitengeneza , Hamza alitengeneza tambi za mayai nyama na kuweka na Regina alikuwa ametengeneza Sandwich zake za Soseji.
Baada ya kukaa mezani kila mtu alikula kile alichoandaa mwenyewe.
Sasa Regina ile anapeleka mdomoni kung’ata kipande cha mkate alijikuta akikunja sura na alitema palepale.
“Hizi Soseji nadhani zilikuwa zimeshaharibika , ni chachu mno”
“Kwahio ulipika bila ya kuangalia kama muda wake umeisha?”Aliuliza Hamza na kumfanya Regina kuwaza kwanini hakuangalia kabla.
Alijikuta akitia huruma huku akiangalia kitafunwa alichoandaa kilichokuwa kimeshachacha na kujikuta akiangalia sahani ya Hamza iliojaa tambi za mayai kama vile ni Pizza, alijikuta akimeza mate kutokana na harufu yake nzuri.
Hamza aliweza kujua mwanamke huyo alikuwa akitaka cha kwake lakini alikuwa akishindwa kuongea.
“Regina nadhani haitakuwa vizuri kuharibu chakula , unaonaje tukiambizana kumaliza hiki cha kwangu”Aliongea Hamza akimaanisha wasaidiane kula na kumfanya Regina kusafisha koo.
“Kwasababu umeniomba nikusaidie nitafanya hivyo , nitakula kidogo kukupunguzia mzigo”
“Asante kwa msaada wako bosi”Aliongea Hamza huku akimpunguzia kwenye sahani yake.
Kitendo cha Regina kuonja alijikuta macho yakimtoka na palepale alijiambia inakuwaje Hamza anajua kupika namna hio , japo tambi hizo zilionekana za kawaida kwa kupikwa na nyama pamoja na mayai lakini hakuamini zingekuwa na radha tamu kama hio.
“Hey! , hivi ushawahi kuwa mpishi?” Regina alishindwa kujizuia na kuuliza.
“Hapana”?”
“Sasa inakuwaje unajua kupika namna hi”
“Labda ni kwasababu sio rahisi kuishi, ndio maana ni vizuri kuhakikisha unajua namna ya kuridhisha tumbo lako”Aliongea Hamza lakini jibu lake ni kama halikumridhisha Regina na shauku kubwa ilimvaa.
“Regina unanisifia?”
“Kidogo tu”Aliongea Regina kwa sauti ya chini na kumfanya Hamza kutabasamu.
Baada ya kifungua kinywa walindoka kwa pamoja wakiwa na nyaraka maalumu na kuelekea Bomani kwa ajili ya kukitafuta cheti cha ndoa.
Kwasababu Lexus ilikuwa imelipuka walitumia Mercedenz Benz Maybach , ilikuwa gari nzuri ambayo haikupitisha risasi.
Kutokana na ukubwa wake katika jamii swala zima la kupata cheti halikuchuwa muda , mwanadada ambae alikuwa amesimamia swala zima alijikuta akimuonea wivu Hamza kwa kuweza kupata mwanamke mzuri kama Regina.
Mara baada ya kurudi kwenye gari , Regina alionekana kuwa na hisia mchanganyiko mara baada ya kuona picha zao katika cheti
Hamza aliishia kumuangalia kupitia kioo cha nyuma na kuona ni kwa namna gani Regina alionekana kuwa na wasiwasi.
“Vipi sasa , unahisi kuna chochote kilichobadilika?”
“Sioni chochote cha ajabu , nimefanya yote haya kwa ajili ya kumridhisha bibi tu ili anipe hisa zake”Aliongea Regina.
“Ndio unaona ipo hivyo , muda ni fumbo kubwa mno sikudhania nitajikuta katika hali kama hii , ila inanifanya niwe na furaha bila sababu ya msingi”Aliongea Hamza.
“Hiki ni cheti tu , unaweza kuoa muda wowote unaotaka , hili likipita tutafuata taratibu na kufuta hiki cheti , hakikisha mpenzi wako hajui sitaki matatizo”
“Swala la kufuta cheti ni mimi kuamua kama nakubali au lah , lakini usijali sana , muda una majibu mengi”Aliongea Hamza , lakini licha ya kuonekana ana furaha upande wa Regina hakuwa na furaha na alimtaka Hamza kuendesha gari kuelekea hospitalini ili kumuonyesha bibi yake cheti aridhie kumkabidhi hisa zote za kampuni.
Lakini sasa wakati wanafika ndani ya maegesho ya magari katika hospitali hio ni kama Hamza alikuwa akisubiriwa kwani walikuwepo Polisi wakiongozwa na Nobert.
“Mr Hamza upo chini ya ulinzi kwa makosa ya mauaji yaliotokea jana usiku”AliongeaNobert akiwa siriasi na polisi wenzake walimzingira kutaka kumfunga pingu huku wakiwa katika hali ya tahadhari na siraha zao.
Regina alijikuta akitoa macho mara baada ya kusikia kauli hio, ilikuwa ni kama hajasikia vizuri.
*****
Upande mwingine ndani ya makao makuu yya
Taasisi ya Haliz Foundation katika floor ya nne kwenda chini ya vyumba vya Ardhi, Amosi alionekana kuwa macho licha ya kwamba bado mikono yake ilikuwa imefungwa na vitu kama pingu katika kitanda na kumfanya ashindwe kusimama.
Alionekana kuwa na utulivu wa hali ya juu na alikuwa kama mtu ambae alikuwa akisubiria mtu aingie kwenye wodi hio.
Upande mwingine nyuma ya chumba alicholazwa Amosi kulikuwa na watu wanne waliovalia makoti ya kidaktari mmoja wapo akiwa ni Sister Maya Thema na mwingine alikuwa ni Frida ambae alionekana kuwa na mshangao akiangalia Skrini iliokuwa ukutani ikimuonyesha Amosi.
“Profesa kama hili lingekuwa swala ambalo jamii inapaswa kuambiwa basi katika historia Tanzania inaingia katika nchi tatu ambazo upandikizaji wa Chip kwenye ubongo wa binadamu umefanikiwa kwa asilimia mia moja”Aliongea Frida na kumfanya Dokta Maya Thema kutingisha kichwa kukubaliana nae.
“Kwasasa hii teknolojia wakuu hawataki ikitangazwa kwa jamii ya watu mpaka kukamilisha mipango yao , lakini licha ya hivyo imenipa hali ya kujivunia kufanikisha operesheni hii kwa mara ya kwanza katika Ardhi ya Afrika”Aliongea.
“Nini hatua inayofuatia baada ya hapa?”Aliuliza Frida huku akiwa na macho yaliojaa shauku.
“Sisi ni wanasayansi pekee na kazi yetu ni kukamilisha kile ambacho wafadhili wetu wanataka kufanya, hatua inayofuatia ipo chini ya Ajenti wa umoja wa Sinagogu”Aliongea.
“Profesa kwahio kwasasa pale yupo imara kiakili , hakuna athari zozote nje ya zile zilizotarajiwa zilizoweza kuonekana kupitia tabia yake?”Aliuliza Frida.
“Leo ni siku yake ya nne tokea kufanyiwa operesheni , siku ya kwanza alikuwa kwenye hali ya kawaida ya mshituko na kuikataa hali aliokuwa nayo , lakini kwa kushitua mishipa yake ya fahamu eneo la hisia tumeweza kufanikisha kumfanya kuwa katika hali ya mazoea , kuhusu tabia ambazo zipo nje ya matarajio bado hatujaona na hatuna budi kumfuatilia hata akiwa katika mazingira ya kawaida”
“Profesa hii sio operesheni ya kwanza kufanyika , mbili ziliweza kufanyika nchini Uingereza na moja nchini Marekani na mbili Israeli na ni zaidi ya miaka kadhaa imepita tokea kufanikiwa kwa operesheni hizo , kwanini tusitumie Follow up ya
data za wagonjwa waliopita?”Aliuliza Dokta John moja ya wanasayansi wa taasisi hio.
“Kila operesheni inayofanyika katika upandikizaji wa Chip katika Ubongo inabeba malengo tofauti hivyo matokeo ya kitabia kuwa tofauti pia , Katika historia ya Dunia Operesheni ya kwanza ya kupandikiza kifaa kwenye ubongo ilifanyika nchini Ujerumani chini ya Usimamizi na ufadhili wa Nazi , malengo ya upasuaji ule yalilenga kufanya wanajeshi kuwa imara zaidi katika kubuni mbinu za kumshinda adui , unachopaswa kuelewa utofauti wa operesheni ile na wa leo ni kwamba ule ulifanyika katika kufunua kichwa cha binadamu na kisha kuweka kifaa lakini huu umefanyika bila ya kufungua kichwa cha binadamu ikimaanisha dunia ilipiga hatua kutoka wakati ule , tulichelewa miaka mingi kuendeleza sayansi ya upandikizaji Chip tokea vita ya pili ya Dunia mpaka sasa kutokana na Josef Mengele kumuua Dokta Douglas kwa sumu akiwa katika maabara ambae ndio alibeba jukumu kubwa la tafiti za ubongo wa binadamu, hakuishia kumuua Dokta Douglas tu bali alichoma tafiti zake zote na kitendo kile kilirudisha dunia hatua moja nyuma katika maswala ya tafiti za kibailojia”Aliongea Dokta Maya na jibu lile kidogo lilionekana kumshangaza na Frida.
“Profesa unamaanisha Joseph Mengele huyu ambae katika historia alifahamika kama Malaika wa kifo , sijawahi kusikia jina la Dokta Douglas katika historia kwanini alimuua?”
“Hakuna ambae ashawahi kumsikia Dokta Douglas kwasababu alikuwa ni mwanasayansi ambae anapiga hatua na hakukuwa na matokeo ya wazi ya tafiti zake , mgonjwa wake wa kwanza ambae alimpandikiza kifaa katika Ubongo hakuonyesha matokeo makubwa sana kama nadharia ilivyokuwa, pengine alifanikiwa au pengine hakufanikiwa ndio maana Josef Mengele alimuua na kuchoma tafiti zake”.Aliongea Dokta Maya Thema.
“Imekuaje ukawa na taarifa ya swala hili , Profesa kwa umri wako…”
“Frida si kila kitu ndani ya dunia hii kipo wazi na sio kila mwenye umri mkubwa anafahamu kila kitu , historia ipo leo kwasababu imetunzwa , kabla ya
kuwa muumini wa Sinagogu nilikuwa mwanasayansi nchini ya Kanisa kuu”Aliongea Maya na kumfanya Frida kutingisha kichwa.
Alielewa watu wengi ambao walikuwa na historia kubwa na Kanisa kuu walikuwa wakijua mambo mengi.
Muda ule wakati wakiongea katika Floor hio aliingia bwana mmoja alievalia suti , alikuwa ni kijana ambae ana muonekano wa kidominikani au kilatini kwa lugha nyepesi, ikimaanisha kwamba alikuwa na asili ya makabila matatu yaani Mzungu kwa asilimia hamsini , Mwafrika kwa asilimia arobaini na mlatino kwa asilimia kumi.
“Ajenti Alonzo karibu sana”Aliongea Maya Thema alionekana kumfahamu yule bwana ambae tembea yake ilionyesha ni kwa jinsi gani alikuwa mkakamavu.
“Asante sana Profesa”Aliongea na kisha macho yake yalitua katika sura ya Frida na kumfanya ProfesaMaya kuchukua jukumu la mara moja kumtambulisha Frida na Dokta John.
“Mr Alonzo huyu ni Dokta Frida Franklin mkuu wa idara ya CST , kutana pia na Dokta John mtaalamu wa Neva”Aliongea na Ajenti Alonzo alisalimiana nao.
“Nimefurahi kukutana na wewe Frida , nimelisikia jina lako mara kadhaa na imekuwa heshima kwangu kukutana na mwanasayansi kama wewe”
“Asante sana”Aliongea huku akitoa tabasamu la ukarimu na muda uleule Ajenti Alonzo macho yake yalitua katika Skrini iliokuwa ikimuonyesha Amosi.
“Nimeambiwa kila kitu kwa upande wako kimekamilika , nipo hapa kwa ajili ya kukamilisha hatua ya pili, kwanini bado amefungwa kwenye kitanda?”Aliuliza.
“Tumeamua kuchukua tahadhari , lakini kutokana na utendaji kazi wa ubongo wake sidhani kama anaweza kuwa hatari ”Aliongea Dokta Maya.
“Operesheni hii sio kwa ajili ya kumfanya kuwa mwanajeshi mwenye uwezo bali kuwa Ajenti mtiifu na Muaminifu kwa Sinagogu ambae anaweza kutuambia kila kitu, kama kutakuwa na matumizi ya nguvu kumuweka sawa , basi mimi ni mwanajeshi”Aliongea na kumfanya Dokta Maya kukubaliana nae na aliongozwa kuelekea mpaka kwenye chumba alichokuwemo Amosi.
Ajenti Alonzo akiwa ameingia na Dokta Maya Thema kabla ya salamu aliomba Amosi afunguliwe mikono na awe huru na Dokta Maya alifanya hivyo.
“Profesa kwanzia hapa nitaendelea mwenyewe , naomba Kamera zote kuzimwa”Aliongea.
“Bila shaka Ajenti”Alijibu Profesa na kisha palepale Profesa alitoka na kumuacha Amosi na Ajenti Alonzo.






SEHEMU YA 56.
Ilimchukua dakika kama kumi tu kwa Ajenti Alonzo kujitambulisha na Amosi kumuelewa , kwa wakati huo Amosi alionekana kuwa kawaida , ki ufupi hakuwa na tofauti sana kitabia , kitu kimoja tu ambacho kilikuwa tofauti ni namna ambavyo alikuwa mtiifu kwa kile ambacho alikuwa akielezewa na Alonzo.
“Mr Amosi kwasasa utafahamika kwa jina la Ajenti Zuku ikimaanisha Askari usie na chimbuko, umenielewa?”
“Ndio Sir”Alijibu Amosi kwa utiifu akiwa ameketi kwenye kiti na kumfanya Ajenti Alonzo kuridhika.
“Kilichofanyika kwako haimaanishi kwamba jina lako katika mazingira ya kawaida linakwenda kuwa tofauti , ukitoka hapa unakwenda kuendelea na maisha yako ya kawaida”
“Ndio Sir”
“Vizuri kabisa , mpaka sasa umefahamu nini katika misheni yako juu ya Naomi Lindsey na Rosemary Macha?”Aliuliza na kumfanya Amosi kufikiria kidogo.
“Sijapata kufahamu kwa uhakika lakini hisia zangu zinaniambia Naomi na Rosemary ni mtu mmoja na kuna uwezekano Naomi alidanganya kifo chake nchini Italy na kisha akakimbilia Tanzania kwa uhusika wa Rosemary Macha”Aliongea Amosi.
Hizo ndio zilikuwa hisia zake tokea siku kadhaa apewe misheni na Chriss na katika uchunguzi wake alikuwa akitaka kuthibitisha swala hili na kisha kuliunganisha na tukio lililotokea mkoani Rukwa huko Sumbawanga.
Hio ndio ilikuwa misheni yake ambayo Chris alimpatia , misheni ya kutafuta mahusiano yaliopo katika ya Rosemary Macha na Naomi Lindsey msanii mkubwa aliefariki nchini Italy.
Ajenti Alonzo alionekana kuridhishwa na jibu la Amosi na muda ule alionekana kutoa kishikwambi katika mkoba aliokuja nao na kupangusa kwa dakika kadhaa na kisha alimwangalia Amosi.
“Unajua nini kuhusu tukio lililotokea Sumbawanga?”Aliuliza
“Sikuwa muhusika wa uchunguzi wa tukio hilo , Ajenti Sedekia Shilla ndio alieweza kufanya uchunguzi na nusu ya ripoti ilifika makao makuu na nusu nyingine haikuweza kufika kutokana na Ajenti Sedekia kutoweka, taarifa ambayo alitoa ni mwanamke ambae hakufahamika jina lake kamili zaidi ya jina la Chakwe ambalo alibatizwa na mmoja ya wanakijiji wa Kizwite aliweza kufika ndani ya kijiji hicho akiwa na watoto kumi wenye asilia ya makabila tofauti tofauti , aliishi ndani ya kijiji cha Kizwite kwa zaidi ya miezi sita na aliweza kumudu mahitaji yake na watoto kupitia kwa misaada mbalimbali ambayo wanakijiji walimpatia , siku kadhaa mara baada ya kupatiwa msaada wa eneo la kuishi ikiwa ni kipindi cha Masika kuliweza kutokea ajali ya radi na kumuua yeye na watoto wake tisa huku mmoja ambae inaaaminika alikuwa na asili ya Kizungu alitolewa eneo la tukio na mtu asiefahamika na kutoweka, Ajenti Sedekia alikusanya ushahidi kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo na aliweza kuwasilisha taarifa hio makao makuu , lakini kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa moja kwa moja kutokana na utata wa tukio hilo kesi ilifungwa kama ajali ya asili iliomuua mama na watoto wake wote”Aliongea Amosi.
“Unadhani ni kwanini Ajenti Sedekia alipotea!?”
“Sina uhakika, lakini naamini utata wa tukio hilo ndio ulimpoteza” “Unamaanisha nini?”
“Pengine kuna kitu ambacho Ajenti Sedekia aliweza kupata kuhusu utata wa tukio hilo na kuna watu ambao walitaka kuficha taarifa hio ndio maana akapotea” “Kwanini unahisi hivyo?”
“Wakati nikiwa Ajenti nimeweza kusikia tetesi kuhitimishwa kwa kesi ile kama ajali ya kawaida ulitoka kwa Kiongozi wa juu kabisa wa nchi na kuna taarifa pia zinasema kuna nguvu ya nje ya nchi iliohusika, hisia zangu nguvu hio ndio iliompoteza Ajenti Sedekia”Aliongea Amosi kitiifu kabisa.
“Umesema wakati ukiwa Ajenti , sasa hivi wewe sio Ajenti?”Aliuliza na kumfanya Amosi kutulia kidogo na kumfanya Alonzo kumkazia macho.
“Nilikuwa Ajenti wa kitengo cha Intellijensia za kimkakati cha TISA kwasasa mimi ni Ajenti wa siri wa Kitengo cha jeshi cha kupambana na nguvu zisizoonekana kiitwacho MALIBU”Aliongea na kumfanya Ajenti Alonzo kutoa tabasamu. “Nielezee zaidi kuhusu ulichopata tokea kuanza kazi ya kuchunguza uhusiano wa Naomi Lindsey na Rosemary Macha?”Aliongea na kumfanya Amosi kufikiria kidogo.
“Katika uchunguzi wangu nimeweza kugundua watu wa kisiwa cha Binamu hawakutaka niendelee na uchunguzi sijajua kwasababu ni nini lakini kupitia kazi hio niliwekewa mtego wa kuuwawa na moja ya mkuu wangu wa kazi na kwa bahati nzuri niliweza kunusurika”
“Unadhani mkuu wako alikuwa akishirikiana na watu kutoka kisiwa cha Binamu”
“Ndio , nina uhakika ni mshirika na watu kutoka Binamu”
“Kwa ninavyojua ufanisi wa watu kutoka kisiwa
Binamu ulivyo mkubwa usingeweza kuepuka kifo , hujawahi kufikiria pengine waliamua kukuacha hai makusudi au kuna sababu nyingine ambayo wakaacha kukuwinda?”Aliuliza
Licha ya Amosi kuulizwa maswali mengi lakini alionekana kutokereka kabisa wala kuchoka , ilikuwa ni tofauti na tabia yake , pengine ni kile ambacho ubongo wake ulifanyiwa.
“Kuhusu hili nimefikiria pia , lakini mkuu wa kitengo aliniambia niendelee na uchunguzi na ameshaongea na Kitengo cha TISA kwa ajili ya Kinga”
“Kwa maelezo yako ulipokea kazi kutoka kwa Chriss sio kwasababu ya pesa , unaweza kuniambia kwanini ulipokea kazi hii licha ya kuonekana kuwa na uhatari?”
“Mwanzoni nilipokea kutokana na shauku , lakini nilipata hamasa zaidi mara baada ya kujua ni kazi ambayo inahusiana na tukio la mwaka 2002 lililomfanya Ajenti Sedekia kupotea, nimekuwa chini ya kitengo cha MALIBU kama ajenti hai kwa miaka saba, kabla ya kupewa misheni nyingine ambayo ilinifanya kuwa Undercover kwa kivuli cha kustaafu na kuanza kuwa mtumwa wa kazi za kihalifu za vigogo wa nchi”
“Misheni!, ilikuwa misheni gani?”Aliuliza Ajenti Alonzo.
Licha ya Amosi kujua kabisa anatoa siri za kitengo lakini alishindwa kujizuia kuongea.
“Nilipewa misheni ya kufuatilia tetesi za uwepo wa watu Vivuli maarufu kama ‘Night Shadows’ na kuongezeka kwa wimbi la wagonjwa wenye ‘split Personality Disorder’”Aliongea na kumfanya Alonzo kutingisha kichwa na muda ule aliangalia kishikwambi chake.
“Elezea kila kitu ulichofanya ili kufanikisha uchunguzi wa Naomi Lindsey na Rosemary Macha”
“Baada ya kunusurika kifo niliweza kuendelea na uchunguzi na kwa kumfuatilia Kanali Dastani aliekuwa mkuu wangu wa kazi niliweza kugundua kuna mfungwa ambae kuna uwezekano mkubwa
alihusika na kupotea kwa Sedekia Shilla , niliweza kupata taarifa hii kwa kufuatilia mazungumzo ya simu kati ya Dastani na moja ya aliekuwa Mkuu wa Gereza la Silo, kwa kile nilichoweza kupata kusikia ilionekana kuna watu walimtembelea huyo mfungwa Gerezani na Mkuu wa Gereza hilo aliweza kurekodi maongezi kati ya watu hao na mfungwa , kwa bahati mbaya katika harakati za kutaka kumfikia mkuu wa Gereza ili kujua walichoongea mkuu huyo wa Gereza alikumbwa na umauti na imani yangu inaniambia kifo chake kinahusiana na kitendo alichofanya cha kurekodi mazungumzo hayo”Aliongea na kumfanya Ajenti Alonzo kutingisha kichwa.
“Katika maelezo yako umesema unadhani Naomi
Lindsey ni Rosemary macha , je unadhani pia Rosemary Macha anaweza kuwa mwanamke
aliefariki katika ajali ya radi akiwa na watoto wake?”
“Wakati nikiwa Ajenti nilibahatika kuona picha ya Chakwe mhangwa wa ajali ya radi na picha yake inafanana kwa asilimia mia moja na picha ya Naomi Lindsey na Rosemary Macha , hivyo naweza kusema wote wanaweza kuwa mtu mmoja”
“Kwa hitoria ya Naomi Lindsey hajawahi kabisa kuwa na mtoto katika maisha yake na pia kulingana na umri wake ni ngumu kuwa na watoto kumi , tena wa baba tofauti tofauti , lakini pia kuna historia ya kimatibabu ambayo inaonyesha Naomi
Lindsey hawezi kubeba ujauzito kutokana na kukosa kizazi , kama unachodhania ni sahihi unadhani watoto aliokuwa nao Chakwe ni wa nani?”Aliuliza Alonzo na kumfanya Amosi akili yake kufanya kazi na sasa ni kama anapata kitu kipya na kujiambia kwanini hakuwahi kufikiria hilo.
“Nadhani Mr Amosi utakuwa na maswali kwanini nakuuliza maswali yote haya , kabla ya kujua unachokwenda kufanyia kazi nilitaka kujua unachojua kwanza, nadhani wakati unakutana na Chriss alikuelezea wewe ndio mtu sahihi katika misheni aliokupatia si ndio?”
“Ndio alisema hivyo na ilinishangaza pia kusikia hivyo?”
“Kuna sababu yoyote ambayo unadhani kwanini tulikuchagua kwa hii misheni?”
“Sijui , labda ni kwasababu nishawahi kuwa chini ya kitengo cha TISA na kuhusika kwa namna moja na kesi hio ya Radi”Aliongea Amosi na Alonzo alitingisha kichwa kukataa na palepale aliangalia tablet yake na alionekana kupangusa pangusa na kisha alimpatia Amosi.
Katika Tablet ile kulionekana picha ya watu wawili , mwanaume na mwanamke na kwa jinsi pozi lao lilivyo katika picha ni aidha watu hao walikuwa wapenzi au marafiki”Amosi alishangaa mara baada ya kuona ni picha ambayo alikuwa akiifahamu na yeye ni moja ya mhusika aliekuwa katika hio picha.
“Unaweza kuniambia huyu mwanamke pembeni yako alikuwa nani kwako?”
“Huyu ni Jasmine Mahmood niliwahi kuwa nae katika mahusiano kwa muda mfupi, alikuwa raia kutoka Botswana aliwahi kuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Aljazeera English nchini Qatar”Aliongea na kumfanya Alonzo kuchukua kile kishikwambi kwa mara nyingine na kisha alionekana kutafuta kitu na kumpatia.
Ilikuwa picha nyingine ikimuonyesha Jasmine Mahmood akiwa na Naomi Lindsey katika pozi la tabasamu na picha ile ilimshangaza mno Amosi.
ITAENDELEA.

JUMATATU , JUMA TANO NA JUMAMOSI NDIO RSTIBA ZETU KWANZIA LEO.
UKITAKA KUSOMEA WATSAPP NICHEKI 0687151346
Hivi Leo ndio jumatatu eeeh Haya nasubri EP ya Leo 😄😄
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 58
Ajenti Alonzo mara baada ya kuona Amosi alikuwa akishangaa , alijua fika kile ambacho alikuwa akikitaka kutoka kwa Amosi amekiona.
“Mr Amosi unaweza kuniambia ni lini ulikuwa na mahusiano na Jasmine Mahmood?”Aliuliza na Amosi alifikiria kidogo na kisha alitingisha kichwa.
“Ilikuwa ni mwanzoni mwaka 2002, nilikutana na
Jasmine mwezi wa kumi na moja 2001
Amsterdam nikiwa katika msafara wa mheshimiwa Raisi kama Aide , Jasmine alikuwa mwandishi wa habari aliesafiri na mheshimiwa Festos Moga na ndio urafiki wetu ulianza , mwaka 2002 wakati anafika nchini Tanzania katika maonyesho ya riadha ndio tuliingia kwenye mahusiano rasmi ambayo yalidumu kwa muda mfupi sana”Aliongea Amosi.
“Kwanini mahusiano yenu yalidumu kwa muda mfupi?”
“Sababu kubwa ilikuwa umbali lakini pia kazi yangu ilinifanya kushindwa kusafiri mara kwa mara nje ya nchi kuonana nae”
“Hii picha Jasmine aliopiga na Neema Lindsery ilikuwa ni tarahe ishirini na tano mwezi wa kumi na mbili mwaka 2001 , siku nne kabla ya kifo cha Naomi, ni picha iliopigwa na Mattia Tommaso, mara baada ya kifo cha Naomi kutokea Jasmine alionekana nchini Tanzania kama mwandishi wa habari kutoka Botswana na kama ulivyosema ndio kipindi ambacho mliingia kwenye mahusiano , si ndio?” “Ndio”Alijibu Hamza.
“Ukiachana na mahusiano yenu unakumbuka chochote kisichokuwa cha kawaida kutoka kwa Jasmine?”Aliuliza Alonzo na kumfanya Amosi kufikiria kidogo.
Ukweli ni kwamba katika kipindi hicho ni kama matukio ya nyuma alikuwa akiyakumbuka kwa urahisi mno, kwake ni kama matukio hayo yalitokea jana.
Ubongo wake ulikuwa na nguvu sana ya kukumbuka mpaka vitu ambavyo alikuwa amekwisha kuvisahau, hata vile vitu ambavyo havikuwa na msingi sana katika kipindi alichokuwa na Jasmine aliweza kukumbuka, ki ufupi ilikuwa ni kama anaangalia tamthilia ya maisha yake na Jasmine.
“Nadhani nimekumbuka kitu?”Aliongea Amosi na kumfanya Alonzo kumkazia macho.
“Umekumbuka nini?”
“Nilikuwa na mahusiano na Jasmine kwa miezi mitatu pekee kabla ya kurudi nchini kwao Botswana , katika kipindi hiki tulikuwa na furaha wakati wote ila siku moja tu alionekana kunikasirikia sana kiasi cha kubadilika na kuwa mtu mwingine”Aliongea Amosi.
“Nakusikiliza , nini sababu ya yeye kukasirika?” “Nilishika mkufu wake uliokuwa na kidani chenye muonekano wa kipekee”Aliongea Amosi na kumfanya Ajenti Alonzo midomo yake kucheza kidogo.
“Unaweza kuelezea kidogo kuhusu huo mkufu hasa kidani?”
“Kilikuwa kidani flani ambacho kilitengenezwa kwa madini meupe kama kioo kwa juu na ndani kulikuwa na rangi za ajabu zilizojikunja kunja kama wingu linalozunguka na katikati kuna kitu kama kijishimo cheusi , upande wa nje kuna duara za vitu kama nyota , na eneo ambalo mkufu ule ulishikilia kuna alama flani hivi kama sikosei ni kama zile za miungu wa Misri ya kale inayowakilisha uhai na kifo”Aliongea Amosi na kumfanya Alonzo kuridhika.
“Kuna sababu yoyote ambayo ilimfanya kukasirika , jaribu kufikiria kila kitu na uelezee katika jicho la ujasusi”Aliongea na Amosi alifikiria.
“Nakumbuka nilimwambia kwanini amekasirika ilihali nimeushika tu bila kufanya chochote ila hakunipa jibu la kueleweka , moja ya kitu ambacho ni cha ajabu mara baada ya kuona ule mkufu roho yangu ilishikwa na kiu kubwa ya kutaka niouone tena kwa mara nyingine , ilikuwa ni kama nimesahau ulivyo na nilitaka kuuona ili kuanza kuufikiria upya , wakati Jasmine anaondoka nilimsihi kuuona tena ila alinijibu kwamba haukuwa wa kwake na alirudisha kwa mwenyewe na nisahau kama nimewahi kuuona kwake”Aliongea Amosi..
“Sitilii shaka maelezo yako kabisa , kwasababu kilichofanyika katika ubongo wako ni kukuwezesha iwe rahisi kwako kukumbuka matukio yaliopita, Je uliangalia upande wa pili wa Kidani, pia je ulipata nafasi ya kuangalia kidani hicho kwa umbali kidogo?”
“Ilikuwa ni kwa sekunde kadhaa tu na Jasmine alinipokonya, sikubahatika kuangalia upande wa nyuma wala kwa umbali”Aliongea Amosi na jibu lile lilionekana kumnyong’onyesha Alonzo.
“Umejibu vizuri kabisa na nimeweza kupata kila nilichotaka, naomba nikwambie ukweli sasa , sababu ya wewe kuwa katika hali hii ni kwasababu uliona kitu ambacho ni binadamu watatu tu duniani waliowahi kuona , siwezi kukuelezea ulichoona kina maana gani ila wewe ni mtu wa tatu, hii ndio sababu ambayo tulikupa kazi ya kumfuatilia Naomi Lindsey na Rosemary Macha mara baada ya kugundua uliwahi kuwa katika mahusiano na Jasmine Mahmood katika wakati ambao ulikuwa na maswali mengi na kutufanya kuona haikuwa bahati mbaya kwenu kuwa katika mahusiano”Aliongea Alonzo na Amosi alitingisha kichwa.
“Kwanzia sasa utaendelea na misheni yako kama
kawaida , ila malengo yamebadilika , ukishafanikiwa kujua uhusiano kati ya Naomi
Lindsey na Rosemary Macha tutataka kujua wapi Jasmine alipeleka huo mkufu, taarifa za awali zinaonyesha mmiliki wa ule mkufu ni Naomi , hivyo kazi yako ni kufanya uchunguzi je Jasmine aliweza kukutana na mwanamke aliefahamika kwa jina la Rosemary nchini Tanzania na je ndio mwanamke aliefariki kwa ajali ya radi mwaka 2002 , utafuatilia na kujua kila kitu na ndipo misheni yako itaingia katika sehemu ya tatu ya malengo makuu”Aliongea Alonzo na Amosi aliitikia kukubali.
Dakika chache mbele Alonzo aliweza kuachana na
Amosi na alirudi katika ofisi ya Profesa Maya Thema.
“Profesa viongozi walikuwa na wasiwasi na mafanikio ya hii operesheni , lakini kama ulivyowaaminisha imefanikiwa kwa asilimia kubwa”Aliongea Alonzo kwa Lugha ya Kihispania na kumfanya Dokta Maya Thema kutoa tabasamu.
“Nini kimekuaminisha Ajenti?”
“Katika kipindi chote nilichokutana na wagonjwa ambao wamepitia utaratuibu maalumu wa ubongo wao kurekebishwa , wengi wao
walitofautiana katika wingi wa maswali wanayouliza
, lakini kwa Amosi hajauliza swali hata moja”Aliongea.
“Ili kupima asilimia za mafanikio mara nyingi tunaangalia wasiwasi ambao anakuwa nao mgonjwa na tabia kuu ya kuonyesha ni kwa kiasi gani yupo na wasiwasi ni wingi wa maswali anayouliza , ikitokea hajauliza swali hata moja basi tunaweza kusema tumeudhibiti ubongo wake kimawazo kwa asilimia mia moja”Aliongea Profesa na Ajenti Alonzo alitingisha kichwa.
“Nitapeleka hizi taarifa makao makuu , zitaendelea kuimarisha nafasi yako katika umoja , lakini hata hivyo katika wagonjwa wote waliopitia taratibu wengi wao ni kutaka kujua kile ambacho wanajua na wamesahau lakini kwa huyu ni tofauti hivyo Profesa ili aweze kufanikisha kazi ambayo umoja inatarajia kutoka kwake tunataka arudi katika hali yake ya kawaida kwa muda”Aliongea Alonzo na kumfanya Dokta Maya Thema kushangaa kidogo.
“Lakini ni hatari kama tutafanya hivyo , anaweza kupoteza baadhi ya kumbukumbu za maisha yake ya kawaida yaliopita”Alionge.
“Profesa haya ndio maelekezo nilioweza kupata kutoka kwa Askofu , najua njia ipo ya kumrejesha katika wakati wake wa kawaida na kusahau baadhi ya matukio yaliomtokea wakati huo huo tukimdhibiti kihisia ili isitokee akawa msaliti kwa Sinagogu”Aliongea Alonzo na kumfanya profesa Maya Thema kufikiria kwa muda.
“Nilitamani sana kuona maendeleo yake katika mazingira ya kawaida , huyu ndio mgonjwa wangu wa kwanza kuwa na matokeo chanya kwa asilimia kubwa na kuna mengi niliohitaji kujifunza kupitia tabia yake , hata hivyo kwasababu ni maagizo ya Sinagogu siwezi kupinga lakini nikufahamishe njia iliokuwepo kama itafanyika hatoweza kuishi zaidi ya miaka mitano”
“Miaka mitano ni mingi sana kwa Amosi kuweza kutimiza makusudi ya umoja wetu Profesa , nadhani unajua ninachomaanisha”Aliongea lakini licha ya Dokta Maya Thema kuonekana kukubali alionekana kuwa mzito , wito wa kidaktari ulikuwa ukimfanya kuwa na hali ya hatia.Kama Daktari alikuwa na hatia ya kumfanyia Amosi operesheni bila ridhaa yake , lakini hatia ilimshika zaidi mara baada ya kuona anakwenda kufanya procedure ambayo itaweka ukomo wa uhai wa Amosi katika muda wa miaka mitano.
“Kwasababu tunahitaji matokeo ya haraka sina budi , lakini kama Daktari nina masharti pia”Aliongea “Nakusikiliza Profesa”
“Baada ya kifo chake awekwe kwenye orodha ya mpango Genesis 210”Aliongea Profesa Maya Thema na kumfanya Ajenti Alonzo macho yake kuchanua.
“Profesa hiki ni kitu ambacho siwezi kuidhinisha na hata kama nilifikishe kwa viongozi kuna hatua kwa hatua za maamuzi na inaweza kuchukua zaidi ya miezi miwili , nadhani unafahamu ni kwa kiasi gani Mpango Genesis 210 ulivyo nyeti , hatuna muda wa kusubiri mpaka ngazi za juu kufanya maamuzi la sivyo kile kilichosimamishwa kwa miaka mingi baada ya kujitoa kwenye Kanisa kuu kitapotea”
“Huna haja ya kuongea zaidi Ajenti , nimeomba kitu ambacho kinawezekana , mkataba wangu wakati nikiingia katika maabara za shirika niliweka masharti nitalinda haki ya mgonjwa kwa namna nyingine ikitokea umoja unachonitaka kufanya kinakiuka miiko ya kazi yangu , kama Askofu alikuwa mkweli na ahadi zake basi atanikubalia katika hili”Aliongea na kumfanya Ajenti Alonzo kutoa kitambaa na kufuta jasho. “Nitafanya mawasiliano”Aliongea.
******
Saa nne kamili asubuhi ilimkuta Kanali Dastani Mpiji ndani ya Wilaya ya kibaha sehemu ambayo ndio msiba wa Afande Mchuku ulikuwa ukifanyikia.
Watu walikuwa wengi japo sio sana na Dastani hakufika na usafiri binafsi bali alifika na Taksi na hio yote ilikuwa ni kuepuka macho ya watu.
Shida ilikuwa moja tu licha ya kwamba hakutaka macho ya watu mwili wake ulikuwa mkubwa na kumfanya aonekane kama bosi , hususani kutokana na Kitambi chake.
Aliutumia uchangamfu wake kusalimiana na baadhi ya wanaume waliokuwa eneo la msiba huku akitoa pole , licha ya wengi kutomfahamu lakini walimchangamkia , isitoshe Afande Mchuku alikuwa mtu wa watu hivyo watu wengi walimfahamu.
Pembeni ya uwanja palipo wekwa maturubai kulikuwa na nyumba ambayo ilionekana haijamalizika kabisa na kwa haraka haraka fahamu zake zilimwambia lazima ndio nyumba ambayo Mchuku alikuwa akiizungumzia , aliishia kutingisha kichwa na kuona Afande Mchuku licha ya kutumia hila nyingi kujiongezea kipato lakini hela zake hakuzimaliza katika Starehe , ilikuwa nyumba kubwa mno ambayo tayari ishawekwa Grill , Milango na Plasta na kulikuwa na vitu vichache sana vya kumalizia ikiwemo madirisha ya Aluminium , kwa haraka haraka alipiga mahesabu na kujiambia kama Afande Mchuku angepata hela ambayo alitakiwa kumlipa kwa ajili ya kupata rekodi basi angeweza kumalizia jengo hilo moja kwa moja.
“Swahiba poleni na Msiba”Kijana mmoja alimsalimia Kanali Dastani , alikuwa ni bwana wa makamo kama miaka therathini hivi alievalia Kanzu na kibakrashia.
“Asante ostaz tumepoa”Aliongea Dastani na bwana yule alimpita na kuendelea kusalimiana na wazee wengine na mara baada ya kumaliza alirudi kukaa karibu na Dastani.
“Siamini Mchuku ametutoka , watu wema na tegemezi siku zote ndio wanaotangulia”Aliongea Kanali akianzisha maongezi.
“Binadamu siku ambayo anazaliwa mwisho wake umeshaandikwa, watu wote tunazaliwa tukiwa wema, dunia tu ndio inatubadilisha, mwisho wa siku tuwe wema au tuwe wabaya siku ikiwadia haichagui mwema au mtu muovu”Aliongea yule bwana huku akirekebisha kibarakashia chake.
“Nakubaliana na wewe , lakini muda mwingine katika jicho la kibinadamu tunatamani yule ambae ndio msingi wa familia kuendelea kuishi”
“Mwenyezi Mungu ni wa haki na anayajua yote ,
Anawajua Wema na waovu , anamlipa kila mtu na matendo yake , Labda Mchuku amepata kheri ya milele mbali na maumivu ya dunia hii”.
“Huzuni yangu ni kwa wale aliowaacha , alionekana mtu mwenye malengo makubwa ya kimaisha”
“Mwenyezi Mungu awape nguvu na amani katika kipindi hiki kigumu , awe faraja kwao”Aliongea yule Ostaz na kabla hata hajaingiza neno lingine la udadisi kuliibuka kilio cha mwanamke na kufanya karibia watu wote kugeuka na kutokana na kilio cha mwanamke huyo minon’gono iliibuka.
“Uwiii baba Nasra wee! , uwiii , mbona umeondoka mapema hivi mume
wanguu..”Kilikuwa kilio kilichowafanya wanawake waliokuwa wamekaa upande mwingine baadhi yao kumsogelea yule mwanamke.
Upande wa Kanali ni kama tukio lile lilimvutia , ukweli ni kwamba sio yeye tu ambae lilimvutia.
“Ostazi huyu ndio mke wa Mchuku!?”Aliuliza Kanali na kumfanya yule Ostaz kumshangaa kidogo.
“Nilijua una ukaribu na Mchuku”
“Ndio Ostaz, Mchuku ni rafiki yangu mkubwa na pia ni mfanyakazi mwenzake hatujawahi kuongea maswala yetu binafsi”Aliongea Kanali akiharakisha kujitetea.
“Inawezekana , wengi hapa ni watu ambao ni marafiki wa Mchuku , alikuwa mtu mwema, huyo ni mke wa pili ni daktari mwajiriwa huko mikoa ya Lindi”Aliongea yule Ostazi na kumfanya Dastani sasa kujibu kitu ambacho kilimvutia.
Yule mwanamke alionekana mrembo na pili ni aina ya wanawake ambao ukiangalia tu unaweza kujua hadhi yake ya kisomi. Jambo lile lilimfanya Dastani kumfikiria Mchuku kwa namna ya kumsifia, ijapokuwa hakumuona bado mke mkubwa lakini mke huyo wa pili alikuwa mrembo.
“Nasikia jamaa alimwambia mke wake mkubwa akifariki asimlilie”Moja ya Vijana waliokuwa nyuma ya Dastani walikuwa wakiongea na kauli ile ilimfanya masikio ya antena ya Kanali kunyaka mawimbi.
Aligeuka na kumwangalia Ostazi kama na yeye anasikia lakini aliweza kumuona Ostazi akiwa bize kusalimiana na mwanaume mmoja wa makamo ambae alionekana kama Shekh.
“Jamaa si alimwambia hivyo kwasababu alijua muda na saa yoyote ataondoka , licha ya huyu mwanamke kuwa mrembo lakini bado Mchuku alimpenda mke mkubwa”
“Tino wewe ndio huelewi , mchuku alimpenda huyu mwanamke lakini alishindwana nae kutokana na kutotulia , Mke mkubwa alikuwa mvumilivu na mwepesi wa kusamehe”Aliongea mwingine lakini Dastani ni kama hakuwa ameridhika hivi.
“Wadau kwani nini ilikuwa shida ya jamaa mpaka kupatwa na umauti?”
“Bro wewe ni mgeni?”Aliongea kijana mwingine na walionekana kuanza kumchangakia Dastani pengine ni kama wameona jamaa anaweza kuwapa fursa.
“Ni mgeni wa haya maeneo lakini Mchuku ni rafiki yangu wa kitambo , hatujawasiliana kwa muda mrefu na ndio nimesikia habari za kifo chake nikaona nihudhurie”Aliongea Kanali na kuwafanya wale vijana kumwelewa.
“Jamaa alikuwa na Kansa ya mapafu na alidondoka ghafla tu akiwa bar ndio ikawa hivyo”
“Ee bwana ee , sijujua kumbe jamaa alikuwa mgonjwa”Aliongea Kanali.
“Wengi hawakujua jamaa alikuwa mgonjwa , ila waliokuwa wakijua wakimkuta sehemu za starehe jamaa anawaambia anatumia siku zake vizuri za mwisho mwisho maana akhera hakuna bia’
“Jamaa alikiona kifo chake aisee”
“Ndio hivyo bro, jamaa ni kama alijua , nasikia mchana yake alienda kabisa na kumuaga mtoto wake wa kwanza shuleni”Aliongea mwingine huku zile kelele za mke wa pili hazikusikika kabisa.
“Alienda shuleni?”Aliuliza Kanali huku machale yakianza kumcheza.
“Kwa maelezo ya Abduli ndio alivyosema baba yake alimtembelea mchana”
“Dogo atakuwa ameshikwa na huzuni sana , ana miaka mingapi?”
“Ni chalii mdogo kabisa , umri wake sijui ila yupo pale St Joseph Mbagala kidato cha pili , Mchuku alikuwa akijisifia sana na Abduli kwamba ni jiniasi na amerirhi akili zake”Aliongea
“Dastani palepale akili yake ilifanya kazi na kwa haraka aliruhusu akili yake kutizama swala hilo kwa jicho la ujasusi.
“Mchuku alienda shuleni kumtembelea Abduli mtoto wake tena tarehe kumi ya huu mwezi, lazima kuna sababu ya kwenda kumtembelea Abduli katikati ya mwezi , nitaanza na Abduli lazima atanipeleka lilipo faili la sauti , lakini kwanza nijue kama kuna sheria ya kuruhusu wazazi kutembelea watoto katikati ya mwezi”Aliwaza Kanali na muda ule alitoa simu yake akiingia mtandaoni, ilikikuwa ni muda wa chakula na hata wale vijana walimpotezea kabisa na umakini wao waliweka kwenye chakula.
Dastani hakutaka kuungana na waombolezaji kwa ajili ya chakula na aliitafuta namba ya Tresha Noah na kuipiga huku akisogea pembeni nje ya maturubai.
“Huyu malaya kapotelea wapi au kasafiri na Mheshimiwa , Kama kampoteza Amosi ataibeba kesi mwenyewe”Aliwaza Kanali huku aking’ata meno yake kwa hasira kwa kitendo cha Tresha kumzimia simu tokea mara ya mwisho alivyowasiliana nae.
Wakai akiwa pembeni aliona kabisa hana chakufanya lakini hakutaka kuondoka mapema , aliona atafute namna ya kusalimiana na mke mkubwa wa Mchuku pengine anaweza kupata kitu kingine cha ziada katoka uchunguzi wake wa kusaka mahali Mchuku alipoficha rekodi ya sauti.
****
Kapteni Norbert alikuwa haelewi vijana wake wamekosea kosea vipi kushindwa kujua kama Hamza ametoka na kwenda kuua na kurudi bila ya wao kuweza kumuona kabisa wakati akitoka na kurudi.
Jambo hili licha ya kwamba liliwafanya kuona Hamza ni mtu hatari lakini vilevile waliingiwa na hofu maana kwa jinsi Kamera walivyozitega ndani ya eneo lile ilikuwa ngumu kwa mtu yoyote kuweza kuepuka kamera hizo na kupita bila ya kunaswa , kubwa zaidi ni kwamba kijana wao mtehama alikuwa ameweza kudukua Kamera zote zilizokuwa ndani ya jumba la Regina.
Wakati akijua hali ni shwari na vijana wake kumwambia kuwa jamaa alilala kumbe alikwisha kutoka na kusababisha mauaji na kuondoka kimya kimya na asubuhi akiwa katikati ya kulifurahia tendo la ndoa anaanza kufokewa na wakuu wake wa kazi kwa kutokuwa makini kupitia simu kitu kilichomfanya kughailisha kumwagiliwa ua.
Licha ya kwamba Norbert aliona ni kosa kwa vijana wake kutokumuona Hamza wakati akitoka lakini vilevile aliona ni kama wakuu zake wanamuonea bure , maana ndio hao wakuu wanaomchekea Mstaafu akiendelea kumchokoza Hamza kupitia genge lake.
Hakupatwa na huzuni yoyote ya kifo cha Kanali mstaafu Fanueli Yowe wala Afande Sucre , ukweli ni kwamba alishaachaga kuwaheshimu tokea muda mrefu japo Afande Fanueli wakati akiwa mafunzoni ndio aliekuwa mkufunzi wake.
Norbert licha ya kwamba alikuwa akitumikia mfumo ambao ulikuwa umeharibiwa na watu wenye tamaa na siasa chafu lakini bado hakusahau wajibu wake kama mwanajeshi , katika jeshi iwe ni la polisi au ulinzi kazi yake kubwa ilikuwa ni kutii maagizo lakini licha ya hivyo hakuwahi kujichukulia kama mtumwa wa maagizo machafu ya wakubwa wake.
Wakati akitoka nyumbani kwake akielekea kazini alikuwa akimshukuru Hamza kwa namna moja ama nyingine kwa kufanya kazi ambayo ilipaswa mwanajeshi kama yeye ambae anapenda haki kuifanya, lakini kwa jicho la usalama aliona alichokifanya Hamza ni kosa na anapaswa kuadhibiwa.
“Muda mwingine tunahitaji vichaa kama hawa kuendelea kutusafishia nchi”Aliwaza wakati akiagana na mke wake.
Wakati akiwa njiani mkuu wake alimwambia haina haja ya kufika kazini bali aelekee moja kwa moja kwenda kumkamata Hamza na apelekwe kituoni.
Hilo halikuwa tatizo kwake na aliitikia kwamba atafanya hivyo , lakini ilimshangaza wakati akiwa ndani ya viunga vya hospitali pamoja na timu yake wakimsubiria Hamza na Regina kufika hapo kumuona Mgonjwa ili amkamate anapokea taarifa ya pili kutoka kwa mkuu wake.
“Achana nae”
“Mkuu ni achane na nani?” Norbert aliuliza akiwa kwenye simu mara baada ya bosi wake kuwa na kauli moja tu ambayo ilikaa kiswahili sana.
“Nimekuambia achana nae , kipi huelewi Norbert , rudi na watu wako kituoni mara moja kuna kazi nyingi za kufanya”Upande wa pili simu ilikatwa na kumfanya Kapteni Norbert kushangaazwa na kauli ile na muda uleule ni kama hakutaka kuamini
kauli ya mkuu wake wa kazi na alitoa simu yake ya kawaida na kuitafuta namba.
“Umefanikiwa?”Sauti upande wa pili ilisikika.
“Nimepokea maagizo mengine , Mkuu anasema niachane nae”Aliongea.
“Kwanini!?”
“Sijajua ila nimepewa kauli moja tu na anaonekana kukasirika sana”
“Kukasirika ni lazima , Fanueli alikuwa rafiki yake wa karibu sana”
“Najuua lakini Afande hili ni swala la kisheria pia , kwanini niache kuondoka na mhalifu?”
“Norbert nadhani unapaswa kumsikiliza mkuu wako wa kazi kwasasa , kama amekuambia achana nae lazima ni maagizo kutoka juu, unatakiwa
kutii ili kulinda uhusika wako mwingine, mimi pia namuunga mkono”
“Lakini Mkuu”
“Hakuna cha mkuu Norbert fanya hivyo”
“Sawa Afande”
“Vizuri”Sauti upande wa pili ilisikika na simu ilikatwa palepale, muda huo huo ndio Norbert aliweza kuiona Mercedenz Benz Maybach ikiingia hospitalini hapo na aliweza kujua moja kwa moja lazima ni bosi Regina maana ni Watanzania wachache wa kutembelea magari ya bei ghali namna hio.
“Hata kama wakuu wanamuogopa siwezi kumuogopa, pengine bosi wake hata hajui alichofanya usiku”Alijiwazia Norbert huku akishika pingu zake na kuwapa ishara wenzake na kumsogelea Hamza na Regina , sio kwamba alikuwa akikiuka maagizo bali alitaka kumpiga mkwara Hamza na pili kuhakikisha Regina anajua kama mtu anemwita msaidizi wake ni muuaji.
Ukweli ni kwamba licha ya Norbert kuona matukio kadhaa ya Hamza akidhihirisha uwezo
wake lakini bado nafsi yake ilikuwa ikipinga kwanini dogo mzembe mzembe kama huyo anatikisa hadi watu wazito , kila akikumbuka mafunzo makali aliopitia jeshini na kupewa nishani za kila aina kutokana na ukakamavu wake alijikuta akipandwa na hasira kumuona Hamza mzembe mzembe ndio anaabudiwa, hali ya ujivuni kwa kujilinganisha na Hamza ilimvaa.
“Mr Hamza upo chini ya ulinzi kwa kosa la mauaji’Aliongea kibabe akitaka kumfunga Hamza pingu lakini Hamza hakuwa mzembe wa kukubali mikono yake ifungwe pingu kizembe.
Regina ambae alishitushwa na kauli ile ya Norbert alijikuta akirudi katika uhalisia , alikwisha kumjua Norbert ni polisi pamoja na wenzake licha ya kuvalia kiraia.
“Afande subirini kwanza”Aliongea Regina huku uso wake ukizidi kuwa na usiriasi na alimkinga Hamza kwa mbele.
“Madam unazuia jeshi la polisi kufanya kazi yake”Aliongea Norbert huku kwa namna flani akionyesha heshima mbele ya Regina , peingine uzuri wa mwanamke huyo ulimfanya kukosa kujiamini kiasi, pengine siku hio ndio mara yake ya kwanza kuona uso mzuri wa Regina kwa ukaribu hivyo, kwenye maisha ya kiraia Regina alihesabika kama mtu adimu kuonekana.
Ilikuwa ni ngumu sana kumuona Regina kutokana na kwamba akitoka kazini maegesho ya magari yapo chini ya jengo na gari lake lilikuwa na vioo visivyompa mtu nafasi kuona aliekuwa ndani.
“Kama wewe ni polisi nadhani unajua ni kosa kisheria kutaka kumkamata mtu bila kibali , isitoshe Hamza hawezi kuwa muuaji . bila Waranti hamuwezi kumkamata na hamuwezi kuongea nae chochote pasipo ya kuwepo mwanasheria wangu , hii imekuwa tabia yenu polisi kukiuka haki ya uhuru wa raia”
“Sheria hio hio inatuambia tunaweza kumkamata Muuaji bila ya kibali , mbele ya muuaji kwanini tujali uhuru wake”Aliongea Norbert huku hali ya kuanza kujiamini mbele ya mrembo Regina ikirudi upya.
Regina kabla ya kuendelea kubishana na polisi alimgeukia kwanza Hamza na kumwangalia , ukweli ni kwamba kutokana na namna ambavyo Norbert alikuwa akijiamini na vilevile siri ambazo Hamza alikuwa akimficha alijikuta akipatwa na wasiwasi kidogo na kupoteza msimamo.
“Kamuua nani , kwanini mnasingizia watu asubuhi asubuhi , mnadhani kuua ni rahisi?”Aliongea
Regina na Hamza kauli ile ilimfanya aone kama Norbert ataendelea kuropoka basi itakuwa ni taarifa kubwa kwa Regina.

“Regina tangulia kamuone bibi kwanza , nitadili na hii hali”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kukunja mikono yake na kumwangalia hamza kwa macho ya kikauzu.
“Wamesema umemuaa mtu ni kweli?”
“Sikia Regina tangulia kwanza kwenda ndani , tutaongea vizuri baadae”
“Kwanini , kama hujaua kuna haja gani ya kuongea na mimi baadae?”Aliongea Regina alikuwa na wasiwasi mno na alitaka Hamza aseme hajaua.
Ijapokuwa alimuona Hamza kama mtu ambae alikuwa na maisha yake kabla ya kukutana nae na historia yake kwa ujumla haijawa wazi lakini kitendo cha kuandikisha ndoa yao ni kama alijihisi kutaka kuwajibika kwakile ambacho kinamzunguka Hamza.
Nafsi yake ni kama ilikuwa ikimwambia hakuwa tayari kuwa karibu na mtu ambae ni mbalifu tena sio mhalifu wa kawaida bali mhalifu wa makosa ya kimauaji.
Upande wa Hamza aliona yupo katika wakati mgumu , ukweli ni kwamba tokea afike nchini amekuwa akijitahidi kujificha ili asionekane sio wa kawaida hata kujipa usumbufu na kuanza masomo ya chuo ambayo hayakuwa na faida yoyote kwake zaidi ya kupoteza muda.
Alitaka kuwa na maisha ya kawaida kabla ya kukaribia kupata kumjua mzee ni nani , historia yake ya maisha ilianzia Tanzania ndio maana alifika nchini Tanzania lakini kama mwenyewe alivyosema muda ni fumbo, saa na siku hio alikuwa kwenye mtego mwingine.
Hakuua makusudi iwe amefanya kama mfanyakazi wa Regina au kama mtu wake wa karibu yote juu ya yote hakutaka kuona mwanamke huyo akiendelea kukumbwa na hatari , alitaka kutoa onyo ambalo linaweza kueleweka kwa wale wanaomuwinda, kama amekubali kuandikisha cheti cha ndoa na mwanamke huyo na bibi yake kulazimisha swala hilo kufanikiwa basi ilikuwa pia ni jukumu lake kumalizia kila kitu na sio kufanya vitu nusu nusu , alikubali kuandikisha cheti kwa ajili ya kumlinda lakini hata kama amefanikisha hilo bado kuna hatari nyingine ambazo ni yeye ambae alipaswa kuzimaliza.
“Ndio nimemuua mtu jana”Aliongea Hamza huku muonekano wake ukitoka katika hali ya uzembe na sasa kuwa kama mtu mwingine ambae amekuwa mtu mzima ghafla , hata Aura yake ilibadilika mara moja.
Jambo lile lilimfanya Afande Norbert kushangaa na kujiuliza inakuwaje mtu anaweza kubadilika kwa dakika chache namna hio , lakini kitendo cha Hamza kukiri ilimfanya hasira kumvaa na kupata kibali cha kumkamata.
Upande wa Regina mara baada ya kusikia kauli hio ya Hamza alijikuta akipiga hatua kadhaa kurudi nyuma kana kwamba alikuwa ameona hatari mbele yake.
Kichwa chake ni kama hakikuwa kikifanya kazi vizuri na ghafla tu kilimsahaulisha na kuanza kujiuliza Hamza ni nani.





SEHEMU YA 59.
“Kwa.. kwanini?”
Regina alitaka kujua sababu ya Hamza kumuua mtu , alitaka angalau kujua sababu pengine anaweza kujishauri, tokea siku ambayo aliweza kuona Hamza akiifahamu lugha ya kifaransa vizuri , siku ambayo alijua Hamza anafahamina na mshonaji nguo mkubwa alijua fika pengine kuwa mwanachuo , fundi na mwalimu ni namna ya kuficha ubini wake , lakini licha ya hivyo ilikuwa ngumu kwake kumvumilia kama kweli amemuua mtu bila sababu licha ya kwamba hakujua uhusika wake.
“Nimewaua kwasababu walistahili kufa”Aliongea Hamza
“Kwahio unajiona Mungu?”Aliuliza kwa hasira Norbert.
“Wame… inamaana sio mmoja?”Aliuliza Regina kwa mshangao.
“Huna haja ya kuniangalia hivyo , nilichofanya ni kama mwanajeshi kumuua adui , siwezi kuhesabika muuaji kwasababu nimemmaliza adui na kurudisha ushindi nyumbani , siwezi kuua bila sababu lakini ikitokea nipo hatarinni na watu wangu wa karibu kuwa hatarini ni sababu tosha”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha mbele ya adui yangu ninachukua uhusika wa mwanajeshi na kazi ya mwanajeshi ni kuangamiza adui , hivyo sio tu jana wala kesho adui ambae ni hatari kwa usalama wangu anastahili kifo”
“Unazunguka zunguka sana na maneno mengi , au ndio sababu inayokufanya unaficha ficha mambo yako mengi”Aliuliza Regina.
“Kuna zaidi ya sababu kwa kila ninachofanya”Aliongea “Wewe ni muongo..”Regina alitaka kuongea zaidi kihasira lakini alishindwa, aliishia kuondoka mbele ya Hamza na kuingia ndani ya hospitali.
Muda uleule mara baada ya Hamza kuondoka wale mapolisi walimzingira , ni kama hali yao ya kujiamini imerudi mara baada ya bosi Regina kuondoka.
“Mr Hamza kwanza kabisa nijitambulishe vizuri ,naitwa Kapteni Norbert Geza kutoka kitendo cha usalama wa nchi , lakini vilevile nafahamika kama Jino la Fisi, matendo yako yameweka usalama wa nchi katika sintofahamu na kwa kosa hilo rasmi sasa tutakukamata”Aliongea Afande Norbert huku akijiambia potelea pote wamesema waachane nae ni wao ila yeye anamkamata akamhoji.
“Kwahio kweli unataka kunikamata?”
‘Unataka kukataa , hii ni Tanzania , hivi unajua nini kitakupata ukitaka kushindana na sisi”Aliongea Afande Gamale.
“Natamani kuona kipi kitanipata”Aliongea Hamza. “Afande Gamale acha kujibishana na huyo mhalifu mfunge pingu”Aliongea Afande Kyombo.
Gamale hakutaka kuchelewesha na alimsogelea Hamza akitaka kumvisha pingu lakini wakati akitaka kufanya vile ni kama macho yake yaliingiwa na ukungu na ashindwe kumuona Hamza mbele yake wakati akili yake inakuja kukaa sawa alishangaa yeye ndio amefungwa pingu na alijikuta akibung’aa.
“F*ck you “
Kyombo kitendo cha Gamale kuvishwa pingu na Hamza aliona ni tusi kwa jeshi la polisi na kwa hasira alifyatuka na teke akidhamiria kumpiga Hamza , lakini kabla ya kumkaribia Hamza alibadilishana nafasi na Gamale kwa kumvutia aliposimama na kutokana na Kyombo kutumia nguvu nyingi alishindwa kuzuia shambulizi lake mara baada ya kuona linaenda kumpata Gamale. “Puuh!!
Gamale alijikuta akichwapwa teke na mwenzake na kwenda chini huku akigulia maumivu. “Kyombo umekuwa kichaa , mbona unanipiga mimi”
“Unauliza ujinga ,kwani nimekupiga makusudi?”Aliongea Kyombo huku akiwa na hasira nyingi.
“Nitalipiza , huwezi kunipiga teke kubwa hivi, umefanya makusudi”Aliongea Gamale kwa hasira huku akijaribu kusimama lakini kutokana na pingu alijikuta akirudi ardhini.
“Afande Kizito mfungue Gamale hizo pingu”Aliongea Norbert mara baada ya kuona timu yake inapaluana wakiwa wamesahau adui yao ni Hamza. “Sawa kapteni”
Niobert alikuwa akiongoza vichaa wenzake , ni kama wote walikuwa wakifanana tabia , mara baada ya Gamale kuondolewa zile pingu walimzingira Hamza na kuanza kumshambulia
Lakini mbele ya Hamza aliona ni kama ngumi za wanawake wanaojaribu kuwa na hasira mbele ya mwanaume wanaempenda hivyo alizikwepa kama anacheza Amapiano.
“Wewe mpuuzi hebu acha kutukimbia , ni mwanaume kweli wewe?”.
“Kama unadhani mimi sio mwanaume kamuulize mpenzi wangu”Aliongea Hamza.
“Niachieni huyu mimi namwendea na pigo za kijetilii , tuone kama atakwepa kwepa kama anacheza rede”Aliongea Kyombo na kuanza kurusha miguu , japo alionekana kuwa na stamina na mafunzo kiasi lakini kwa Hamza ilikuwa kichekesho maana alimuacha amsogele na kisha aliudaka mguu wake na kuusukuma na kumfanya adondokee makalio yake kwa nguvu.
Baada ya kuona Kyombo ameshindwa waliobaki wote walimsogelea Hamza na kuishika mikono yake wakitaka kuikutanisha kwa ajili ya kuifunga pingu lakini licha ya wote wawili kutumia nguvu kubwa walishindwa kuikutanisha kadri walivyokuwa wakiisukuma., walihihisi ni kama wanasukuma chuma kizito.
Upande wa Kapteni Norbert alikuwa pembeni akiangalia vijana wake wanachokifanya.
Baada ya kuona wameshindwa kuuipindishahata kidogo mikono ya Hamza alijikuta akishangaa.
“Hamza kama sikosei hio ndio mbinuu maarufu inayofahamika kama Joho la Chuma”Aliongea Norbert
“Kama unaijua basi utakuwa unajua pia namna ya kuishinda , acha kutegea wenzako fanya na wewe shambulizi”Aliongea Hamza.
“Nilikuwa najiandaa”Aliongea Norbert na muda ule alianza kuizungusha mikono yake hewani kana kwamba anajaribu kukusanya nguvu ya kiroho.
Upande wa Hamza alikuwa ameshikiliwa na polisi wawili , kama vile walikuwa wakitaka bosi wao ampige Hamza shambulizi la kifuani.
Norbet mara baada ya kujikusanya kwa sekunde kadhaa alifyatuka kwa spidi kiasi kwamba alisababisha hadi upepo kama vile ni gari ambayo ilikuwa kwenye spidi kubwa na kumsogelea Hamza kwa kasi , lilikuwa ni teke la tiktaka ambalo lilienda kutua katika kifua cha Hamza.
“Bam!!
Sauti iliosikika ni kama vile mtu anafungua mlango kwa teke na mlango ukagoma kufunguka
Polisi wale walijikuta wakipatwa na wasiwasi kutokana na ukubwa wa teke lile na kuona limemsababishia Hamza matatizo.
Lakini mara baada ya kumwangalia Hamza walishangaa akiwa amesimama na hakuwa na mabadiliko yoyote hata kidogo.
“Unaonekana umejifunza funza, Precelestial Kick sio mbaya , ila umetumia hisia nyingi sana kwenye hili teke”Aliongea Hamza
Afande Norbert alijikuta akibung’aa mara baada ya kukaa sawa na kumuona Hamza yupo vilevile kama jiwe , sio kwake tu hata kwa wenzake pia.
“Vipi kuna mwingine ana shambulizi ambalo anataka kunionyesha?”Aliuliza Hamza akiwaangalia kwa zamu.
Wale polisi waliokuwa wamemshikilia Hamza walijikuta wakianza kushikwa na woga na walimuachia na kurudi nyuma.
“Hamna uwezo hata wa kunipiga halafu mnataka kunikamata , sidhani hata mna vigezo vya kuongea na mimi , poteeni wakati nikiwa na roho ya kistaarabu”Aliongea Hamza huku akianza kutoa msisimko ulioanza kumtisha Norbert kiasi kwamba mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda mbio mno.
“Hii ni Tanzania nchi ya amani huwezi…”Alitaka aendelee kujibishana lakini Hamza alimsogelea na kumpiga kofi la kifuani na kumfanya adondoke chini kama mzigo .
“Kapteni!!”
Wale polisi walijikuta wakimkimbilia mwenzao wakidhani amekufa maana sio kwa uzito wa bao lile.
Walijikuta wakipatwa na ahueni kapteni wao alikuwa hai licha ya kutema damu , lakini upande wa Norbert aliona kama Hamza angetumia nguvu kidogo kwenye mkono wake basi kifo kingemkuta palepale.
Wale polisi mara baada ya kuona Kapteni wao hali yake si nzuri walimbeba na kumrudisha kwenye gari na safari ya hospitalini ilianza mara moja. *****
Hamza mara baada ya kuingia ndani aliweza kumuona Regina akiwa ameshika kile cheti cha ndoa mbele ya bibi yake , alikuwa na furaha , ule muonekano wake wa nje ulikuwa umepotea na ilimfanya Hamza kuvuta pumzi ya ahueni.
Bibi Mirium mara baada ya kumuona Hamza alitoa tabasamu hafifu huku akimpa Hamza ishara ya kumsogelea.
“Safi sana .. wewe ni mtoto mzuri”Aliongea Bibi Mirium.
“Bibi kuna kitu unataka tena?, niambie nitakamilisha”Aliongea Hamza. “Haraka iwezekanavyo mfanye Regina apate mtoto
, ndio njia ya kuifanya nyumba yako kuchangamka”
“Bibiii!!!” Regina aliongea , aligeuka mwekundu kwa aibu kiasi kwamba hakutamani kuendelea kubakia ndani ya wodi.
“Nimekuelewa bibi nitalifanyia kazi”Aliongea Hamza akitingisha kichwa kukubaliana nae
Bibi Marium alitoa tabasamu hafifu na kisha alifunika macho yake kana kwamba amekwisha kushoshwa na dunia na yupo tayari kuondoka.
“Regina unaonaje tukitoka nje kidogo , kuna vitu nataka kukuambia”Aliongea Hamza na Regina alisita kidogo lakini aliishia kugeuka na kutangulia nje.
Mara baada ya kufika mwishonni mwa korido haikuwa na mtu yoyote hivyo ilikuwa sehemu nzuri kwao kuongea.
“Vipi kuhusu wale polisi?”
“Wameondoka”
“Kwanini hawajakuchukua?”
“Mbona kama unataka nikamatwe ?”
“Ndio, umeua na unapaswa kuadhibiwa kisheria”
“Regina mrembo , mambo hayapo ‘simple’ namna hio, haiwezekani kufupisha maisha yangu yaliopita na neno kuua”
“Basi elezea vizuri nikujue wewe ni nani na ndio nifanye maauzi kama naweza kukuamini”Aliongea Regina na kumfanya Hamza kukosa neno , aliona si vyema kumwambia chochote Regina , sio kwasababu anataka kumficha ila ni kwasababu akishamjua atakuwa hatarini.
“Ninachoweza kukuambia ni kwamba , unaweza kunijua ila sio sasa?”
“Mhh, kama hutaki kusema , vipi hiki nisichokijua kuhusu wewe, je kinahusiana na maswala ya kihalifu , kama kuua na kuteka nyara?, Aiu polisi walikuwa sahihi wewe ndio muuaji ulietangazwa kwenye vyombo vya habari?”
“Regina!!”
Hamza sauti yake ilianza kuwa siriasi kidogo.
“Unaweza kusema ndio nimemuua mtu lakini mimi sio mhalifu wala huyo muuaji muhuni muhuni . sijawahi kujihusisha hata na makundi ya kigaidi sio hivyo tu sijawahi kufanya kitu ambacho kinaifunga dhamiri yangu”
“Kwanini nikuamini kama huwezi kusema chochote?”
“Siwezi kukuambia kwasababu siri ninayoficha hapa , kama nikisema nikuambie utakuwa hatarini , nafanya haya kukulinda”
“Haina haja, hatujafahamiana muda mrefu hivyo huna haja ya kunilinda kwa staili hiii”
“Sekunde ambayo ulitia saini hiko cheti umebeba cheo cha mke wangu , unaweza usikubali lakini ni jambo siriasi kwa watu wengine”
“Unamaanisha hili karatasi , hivi unadhani kuna mwanamke duniani anaweza kukubali kuolewa na mtu asiemjua?”
Hamza alitamani kusema ndio ,isitoshe katika uzoefu wake ameshuhudia ndoa ningi zikifanyiika kwa ajili ya manufaa mbalimbali , wengine walifanya hivyo kupata uraia , wengine mali na kadhalika lakini hata hivyo aliona haitokuwa na maana mbele ya Regina.
“Hatutaachana mpaka niweze kuishikilia kampuni kwa asilimia kubwa , hivyo naomba usiambie watu chochote kuhusu ndoa yetu, una uhuru asilimia mia moja ya kutafuta mwanamke unaempenda na hata kuanza taratibu za ndoa , ikifikia muda wa ndoa nipo tayari kwenda kubatilisha hiki cheti”Aliongea Regina huku akitingisha cheti kilichokuwa kwenye mikono yake. “Regina unamaanisha nini kuongea hivyo?”
“Kipi ambacho huelewi , sina mpango wa kuwa mke wako kabisa ,haiwezi kutokea kihisia nikakubali kuwa mkeo , kitu kingine unaweza kutangulia nyumbani au kazini , nitakaa kidogo na bibi usinisubiri”
Mara baada ya kuongea hivyo aligeuka kikauzu na kisha aliingia ndani akimwacha Hamza akimwangalia kwa nyuma.
“Ningeililia ndoa kama kweli naitaka , lakini nipo kazini Regina”Aliwaza Hamza huku akitingisha kichwa , katika maisha yake pengine Regina ndio mwanamke wa kwanza kumuongelesha kwa tabia hio.
********
Upande mwingine katika moja ya hospitali ya jeshi alionekana Afande Norbert akiwa amelala kitandani huku uso wake ukiwa umepauka.
Timu yake ilikuwepo ndani ya chumba alicholazwa na walimwangalia kwa hali ya huzuni.
“Kapteni inamaana ndio tunakwenda kuachana na hii misheni?”
“Mnapaswa kuelewa sisi ni wanajeshi kabla ya kuwa polisi na yote ni kwa ajili ya kuikamilisha hii misheni , acheni kuwa kama walinzi , kuna watu wanamfatilia Hamza kwa ukaribu”Aliongea Kapteni.
“Norbert haina haja ya kuendelea kumfatilia Hamza tena”Sauti iliweza kusikika kutoka mlangoni na wote walijikuta wakikakamaa kwa mshangao wakimwangalia mwanaume aievalia gwanda za jeshi la ulinzi akiingia,alikuwa na vyeo vilivyochafuka begani mwake.
Hakuwa peke yake alikuwa ameongozana na wanajeshi wengine wawili .
“Kapteni Mdudu!!,”Aliongea Norbert kwa mshangao ni kama hakutegemea kumuona Mdudu ndani ya hilo eneo.
Afande Mdudu alikuwa ni Kapteni wa kikosi namba mbili kutoka kitengo cha uchunguzi cha
MALIBU.
Moja ya sababu kubwa ambayo ilimfanya Mdudu kuheshimika jeshini mpaka kupewa nafasi ya kukaa pamoja na wakubwa ni kutokana na kwamba ndio mwanajeshi ambae amepanda vyeo akiwa na elimu kidogo, kwa lugha nyepesi ndio mwanajeshi aliepanda vyeo bila ya kutegemea elimu zaidi ya mafanikio yake ya kijeshi.
Alionyesha uhodari wa namna yake kipindi alipokuwa katika mpango wa Umoja wa Taifa wa kulinda Amani nchini Sudani na Congo.
Mara nyingi MALIBU wanafanya uchunguzi wao kupitia jeshi la polisi , Norbert alikuwa ni mwanajeshi wa kitengo cha MALIBU ambae anaongoza timu namba moja aliepandikizwa ndani ya jeshi la polisi , hivyo alikuwa akipokea maagizo kutoka kwa mkuu wa polisi na pia vilevile alikuwa akipokea maagizo kutoka kwa mkuu wa kitengo cha MALIBU.
‘”Tumepewa maagizo ya kuja hapa , kwanzia sasa kikosi namba mbili ndio kitaongoza misheni ya kumchunguza Hamza, operesheni mlizofanya nyie kama kikosi cha kwanza hazijawaridhisha viongozi , mnaweza kuendeea na taratibu za kawaida kama polisi”
“Nini!, mbona niliwasiliana na mkuu mwenyewe na hajaniambia kuhusu hili”
“Kwahio Norbert nini ambacho huamini , angalia
hio karatasi kuna sahihi ya mkuu wa kitengo”Aliongea akimrushia karatasi kwenye kitanda na kweli kulikuwa na sahihi.
“Kwanini mnataka tuiachie hii kesi kwenu , bado hatujakamilisha kumkamata Hamza lakini vilevile hatujafanya kosa lolote”
“Norbert licha ya kwamba wakuu wanasifia uwezo wako lakini kwangu nakuona kama mjinga , kwanini hukujiuliza licha ya Afande mwenye cheo kikubwa kama Afande Yowe kuuwawa lakini bado viongozi wakakuambia uachane na Hamza , lakini angalia ulichokifanya ukajaribu kumkamata na sasa upo hapa hospitalini , viongozi hawakuridhishwa na namna yako ya kukosa utiifu na wamesikitishwa sana na hili ndio maana tumepewa jukumu la kumchunguza Hamza na kumjua kwa undani”
“Nimefanya vile kama polisi , sikuona haja ya
kumwangalia mhalifu anafanya anavyotaka”Aliongea Norbert na kumfanya Mdudu kutoa tabasamu la dharau.
“Tulichokifanya ni kujaribu uwezo wake kwa kumtishia kumkamata , timu namba mbili mnataka kuchukua crediti zetu wakati misheni inaendelea vizuri”Aliongea Kyombo.
“Norbert wewe ndio uongee , unadhani tunakuibia sifa zako?”Aliuliza Mdudu.
“Kyombo kaa kimya” Aliongea Kapteni Norbert na kumfanya Kyombo kunywea.
“Norbet una timu ina watu vilaza kweli…”Aliongea mwanajeshi aliekuwa nyuma ya Afande Mdudu lakini alizuiwa asiendelee maana angeibua ugomvi.
“Norbert uliwaambiwa viongozi kwamba hisia zako zinakuaminisha Hamza ndio muuaji anaeua wanawake ndani ya jiji la Dar es salaam , lakini kwanini umeshindwa kujiuliza swali jepesi , kwanini Bounty hunters kutoka Samar wamesafiri kutoka
Ufilipino mpaka Tanzania kwa ajili ya kumtafuta Hamza , nadhani unawajua vizuri hawa wawindaji hawatumiki sehemu ambayo haina hazina”Aliongea Mdudu.
“Ni hazina gani ambayo Hamza
anashikilia?”Aliuliza Norbert huku kidogo akiona ni kweli kuna mahali amekosea.
“Huna haja ya kuuliza maswali , tokea mwanzo ulikuwa ukitafuta kitu sehemu ambayo sio sahihi , lakini usijali mimi na timu yangu mapema tu tutaweza kujua ni kitu gani wale wawindaji wamekijia Tanzania na ndio namna tutakavyomjua Hamza kwa undani zaidi na hakuna atakaepata majeraha kama yako”
Mara baada ya Mdudu kuongea hivyo aliwapa ishara wenzake na kisha waliondoka .
******
Saa mbili kamili za usiku Hamza alikuwa ndani ya eneo la kijichi akilisogelea lango la kuingia katika mgahawa wa Dina.
Mara baada ya kuingia aliweza kuona Mercedenz s Class ikiwa imeegeshwa na Lau alionekana kuilinda gari ile.
Hamza alikuwa hapo kwa ajili ya kutii wito wa mrembo Dina mara baada ya kumpa agizo la kufika hapo bila ya kukosa.
“Bro umewahi mno , ungenipigia simu nije kukuchukua kabisa”Aliongea Lau kwa bashasha. “Mbona hii gari ipo hapa,Dina anapanga kutoka?”Aliuliza Hamza.
“Ndio , anaelekea Club”
“Club!!”
“Ndio kila mwisho wa mwezi vigogo na watu wazito wazito hukusanyika katika club moja , ni kama tukio maalumu , sio lazima kwenda lakini kutokana na kwamba wengi ya wanaohudhuria ndio wateja wetu wakubwa haina jinsi kwenda”Aliongea Lau.
Muda huo wakati wakiongea Dina aliweza kutoka akiwa amevalia amependeza.
“Nilijua utachelewa”
“Siku kwenye mudi nzuri ndio maana nimekuja, nimeambiwa unaenda Club, nitakusubiri mpaka utakaporudi”
“Nilikuambia uje leo kwasababu nataka unisindikize”Aliongea Dina.
“Lakini hujaniambia ni club ya aina gani” “Nitakuambia tukwia tunaeekea huko , ingia kwanza kwenye gari, umesema huna mudi club ndio sehemu inayokufaa”Aliongea huku akitangulia kuingia ndani.
Hamza aliishia kutingisha kichwa na paepale aliona sio mbaya kutokana na mudi yake kuwa mbaya ni kheri kidogo akapunguze mawazo huko Club.
INAENDELEA WATSAPP 0687151346
 
Back
Top Bottom