FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #41
STORY: DOCUMENT NUMBER 72
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
EPISODE 7.
Mita chache kutoka eneo lilipokuwepo bunge la nchi ya Tanzania, mji ulio fahamika kama DOGMA TULIPO, kwenye chumba kimoja cha mapumziko walionekana vijana wawili wakiwa ndani ya suti huku wakiwa wanabadilishana mazungumzo ambayo yalionekana kutokuwa na maelewano makubwa.
"Ndugu yangu ujue mimi sikuelewi mpaka sasa lengo lako kubwa hasa ni lipi mpaka unataka kuyafanya haya yote?"
"Hauwezi kunielewa kwa sababu unaishi kama bendera fuata upepo tu hujui hata kesho kipi kinatakiwa kufanyika ndani ya nchi yako mwenyewe, sasa sijui huo ubunge wananchi wako walikupa vipi mwanaume muoga kama wewe ambaye huwezi hata kuwasemea kabisa changamoto zao zikatatuliwa" mwanaume aliye Julikana kama Isaya Ndango, aliongea kwa jeuri kwa mbunge mwenzake huku yeye akijinasibu kwamba alikuwa shababi hivyo hakuwa akiogopa chochote kile.
"Muda mwingine kukurupuka kwa mtu kuropoka huwa hakutoi maana ya moja kwa moja kwamba yeye ni mpenda haki na anatumia akili kwa kile anacho kifanya. Jambo ambalo unalifanya linaenda kuigawanyisha nchi kabisa na kufanya watu waanze kuichukia serikali yao, sasa huoni kama unaiingiza nchi kwenye machafuko makubwa?
Tumia akili ndugu yangu sio kuhitaji kutafuta umaarufu na sifa za muda mfupi ambazo zinaweza kukuletea matatizo na kuiweka nchi kwenye machafuko yasiyo na ulazima kwa tamaa za watu wachache" mbunge huyo alimsihi sana Isaya ndango kusitisha hicho alichokuwa anahitaji kukifanya.
Isaya alicheka kwa muda kwanza akiwa anamwangalia mwenzake huyo usoni kwake huku akifunga vizuri kifungo cha juu kwenye koti la suti.
"Nina uhakika mpaka hapo ulipo wewe mwenyewe haujui unataka nini ndiyo maana unakosa misimamo kwa kuhisi mimi natafuta sifa. Nakukumbusha jambo moja tu, unahisi ni kwanini mimi ndiye mwanasiasa pendwa zaidi nchini kwa sasa? Unahisi ni mwanini wananchi kila siku wanaliimba jina langu kwamba siku moja natakiwa kuingia Ikulu? vipi unahisi haya mambo yanakuja kwa bahati mbaya?" Isaya Ndango alimuuliza mbunge mwenza huyo kisha akaendelea;
"Mambo siyo rahisi kama unavyo yaona wewe kwenye macho yako yanafanyika, kila ambacho unakiona kwenye macho yako basi ujue walikaa watu wenye akili wakakipanga na namna ya kukimaliza wanajua. Sasa ukija na uoga wako hapa na kuanza kuhubiri kwamba natafuta sifa basi wewe ndiye utakuwa hauna akili kabisa na unategemea akili za watu wachache ili uweze kufanya mambo yako" alitulia na kuendelea tena;
"Hii nchi, ni nchi iliyo barikiwa sana kwa kila kitu, kuanzia rasilimali zake, watu wenye uwezo mkubwa kiakili na kiuongozi ambao kwa tamaa za watu wachache wenye nia ovu hawapewi nafasi kwa sababu watu hao wanaogopa kwamba nafasi zao zitabebwa na hao watu"
"Hawa watu wenye uwezo mkubwa ndio ambao wanapaswa kuiongoza serikali hii ambayo imejaa udhalimu, ukatili wa kila namna, watu wanauawa kila siku, watu wanalia ajira kila kuitwapo leo huku viongozi wakubwa wakiwa wanawaajiri ndugu zao ambao hawafai hata kuwa viongozi sehemu yoyote ile"
"Nchi inapelekwa mputa kwa maslahi ya watu wachache, hivyo mtu kama mimi siwezi kukubali kuona nchi yangu inateketea kwa kumuogopa mtu yeyote yule na ndiyo sababu ambayo imefanya nimepigania hili mpaka leo bunge limeitishwa rasmi ili tuweze kuzungumza kwa kina kuhusu hili jambo na mwafaka wake utakuwaje mbeleni.
Hivyo kwa leo wabunge na viongozi wengine ambao watafika leo nitajua ndio hao ambao tupo nao pamoja kwenye safari hii ya kwenda kupata nchi mpya yenye kila lililo jema" alimaliza kuongea huku akiwa anaangalia saa yake. Mbunge mwenzake ni kama hakumuelewa ilimlazimu kumuuliza.
"Usiniambie kwamba ulipita kwa kila mbunge kuweza kumshawishi kuhakikisha unatekeleza mipango yako?" Aliuliza kwa mshangao lakini Isaya Ndango alitabasamu tu,
"Nisikilize rafiki yangu, mimi na wewe tumeanza siasa pamoja tukiwa sekondari lakini wewe ni muoga sana, kwa sasa mimi ndiye mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa zaidi nchini hivyo kuwashawishi watu kwangu ni kazi ndogo sana na ndicho nilicho anza nacho, najua kwamba kama wabunge wengi wakiwa upande wangu basi kazi inaenda kuwa rahisi sana kwa upande wangu"
"Isaya unamaanisha nini kusema hivyo?"
"Hili ni jaribio langu la kwanza kwenda kuharibu kila kitu ambacho unakiona, na baada ya hapa nadhani karibia kila mbunge atakuwa upande wangu pale ambapo watasikia kile ambacho nitakiongea bungeni"
"Hey! hey! Suburi kidogo, unaamisha kwamba unataka......!?" mwenzake huyo akiwa anaongea kwa kigugumizi, mbunge Isaya alimsaidia kulisema hilo jambo.
"Tunataka kuipindua serikali madarakani"
"No, no, no Isaya. Umepatwa na nini ndugu yangu mpaka unawaza mambo mazito ya kigaidi namna hiyo? Ni tamaa ya madaraka au ni kipi kimekufanya ghafla sana umebadilika namna hiyo" rafiki yake alishangazwa sana na namna mwenzake huyo alivyokuwa anawaza mambo mazito sana namna hiyo.
"Haupaswi kuniuliza mimi hilo swali bali unatakiwa kuwauliza hao viongozi wako kwamba wanafeli wapi? Mpaka mbunge wa kawaida kama mimi nataka kuwatoa madarakani!"
"Hili jambo haliwezekani Isaya"
"Unajua kwanini sikutaka hata kukushirikisha?"
"Hapana"
"Sababu ndiyo hiyo, wewe ni mbinafsi sana kwa sababu huwa unajiwazia wewe tu na sio vinginevyo, mimi nina watu wengi ambao wapo upande wangu hivyo usije ukahisi kwamba nafanya haya mambo kwa kukurupuka kama unavyohisi wewe. Yule raisi hafai kuiongoza nchi hii tena kuanzia sasa, ana mambo mengi sana ya kutisha nyuma ya pazia ambayo wananchi wakiyajua basi siku hiyo hiyo watahitaji wamtoe hata kwa nguvu pale Ikulu"
"Ndo uwaze kumtoa raisi madarakani ndugu yangu? Kipi kinakupa hiyo jeuri namna hiyo?" Mbunge huyo baada ya kuuliza, Isaya alitabasamu tu na kuangalia saa yake na ghafla mlango wa hicho chumba walicho kuwepo ukawa unafunguliwa.
Mtu aliye ingia humo ndani alimuacha mdomo wazi mbunge huyo lakini kwa Isaya Ndango ilikuwa ni tofauti maana hata kauli ambayo aliitamka ilizidi kumchanganya mwenzake huyo.
"Mr President karibu sana" mbunge huyo alishangazwa na mambo makubwa mawili. Aliyekuwa ameingia hapo alikuwa ni waziri mkuu wa nchi ya Tanzania, wakati akiwa anajiuliza kwamba vipi waziri mkuu naye anahusika? Ndipo aliposhangazwa zaidi na maneno ya Isaya ndango baada ya kumuita waziri mkuu huyo, Mr president.
Kichwa chake kwa haraka sana kiliweza kuelewa kwamba ina maana kama huo mpango wa kumpindua mheshimiwa raisi pamoja na serikali yake ukikamiloka basi waziri mkuu ndiye ambaye alikuwa anategemewa kukalia kiti hicho, sasa alielewa kwamba ni kwanini Isaya Ndango alikuwa na jeuri ya kusema kwamba ana watu wazito sana upande wake.
Kama mpaka mtendaji mkuu huyo wa serikali alikuwa yupo upande wake basi ilionyesha walikuwa na mengi makubwa ambayo walitaka kuyafanya hata hivyo aliona kwamba ni jambo la hatari sana ambalo walikuwa wanalifanya vipi kama ingejulikana moja kwa moja na alisema siku hiyo anaenda kumwaga mboga mbele ya bunge ambalo huwa linarushwa moja kwa moja mubashara kabisa na watu wanaangalia kinacho endelea?.
Moyoni mwake alikiri kwamba hakuwa tayari kabisa kushiriki kwenye hilo jambo, kwa maana hakuelewa raisi huyo alikosea wapi kwa maana alikuwa anamuona kama mtu safi ambaye alikuwa anaiendesha nchi kwenye misingi safi kabisa na demokrasia ya wazi ambayo kila mwananchi alikuwa anaifurahia, vipi leo aambiwe kwamba kiongozi huyo alikuwa ana mambo ya ajabu ambayo kama wananchi wakiyajua wanaweza kumtoa madarakani hata siku hiyo hiyo, alichoka maana hakuwa na majibu ya moja kwa moja.
Swali la mwisho ambalo alishindwa kulipatia majibu yake, ni kuhusu huyo rafiki yake, ni kwanini alikuwa amemficha kwa kipindi chote hicho? Alikuwa hamuamini? na kama anataka kumtoa raisi madarakani maana yake yeye ndiye anaye itaka hiyo nafasi kwa sababu wananchi wanamkubali sana kwa siasa zake zenye mitazamo ya mbali mno, iweje aweze kumpatia hiyo nafasi waziri mkuu ndiye aingie Ikulu?
Kama waziri mkuu akiingia Ikulu, yeye atakuwa nani? na ana mpango upi hasa wa siri ambao unamfanya azisukume kete zake kwa kujiamini sana namna hiyo mpaka kuwaza mambo makubwa kiasi hicho?. Akiwa kwenye hayo mawazo ndipo waziri mkuu alipo msogelea.
"Heshima yako mheshimiwa!" alimsalimia kiongozi huyo mkubwa kwa heshima. Jina lake alikuwa anajulikana kama William Ivan Msoka, hilo ndilo lilikuwa jina la kisheria la mheshimiwa waziri mkuu huyo wa nchi ya Tanzania.
Alimpa mkono mbunge huyo ambaye alikuwa ana wasiwasi mno, macho yake yakiwa yanamuangalia Isaya na kumuuliza.
"Mbona huyu kijana ana wasiwasi sana, hauoni hatari kuingiza watu waoga kama hawa kwenye mpango kama huu?" waziri mkuu aliuliza huku akigeukia upande wa mbunge yule na kumkazia macho
"Hapana mheshimiwa, huyo ni kijana wangu tangu tunakua ndiyo maana hata safari yetu inafanana kwa kila kitu hata majimbo yetu ni jirani ila nadhani kwamba hakutegemea kukuona hapa ndiyo maana ana wasiwasi sana kiasi hicho maana sikumwambia kwamba unakuja" Isaya Ndango ilimbidi amtetee mwenzake maana hakuwa na namna nyingine huenda angeingia kwenye matatizo.
Waziri huyo alimuangalia vizuri sana huyo mbunge na kutamka;
"Nadhani ni muda mwafaka tuelekee kulutekeleza jambo letu maana ni dakika ishirini tu zijazo bunge linaanza ila kuna kitu kimoja naona kama hakipo sawa!" alimgeukia mbunge Isaya akiwa amehamaki kwa mshtuko,
"Spika wa bunge hatakuwepo leo"
"Whaaat? Kivipi?" Isaya Ndango alishtukizwa na hayo maelezo ya ghafla ambayo hakuyategemea kabisa.
"Ameitwa na raisi muda sio mrefu na kudai kwamba wana kikao cha dharura"
"Unamaanisha kwamba mheshimiwa raisi anajua juu ya huu mpango wetu?"
"Sina uhakika sana na hilo ila kahakikishe unaongea kila kitu mle, hivyo hata kama atakuwa amejua, atashtuka akiwa amesha chelewa, hivyo kwa leo bunge litaongozwa na naibu spika. Ni muda wa kwenda kuanza rasmi mapinduzi kwa kuwafahamisha wananchi yale ambayo hawayajui" Mr William Msoka aliongea kwa kujiamini na kutoka humo ndani kwani hakutakiwa kuongozana na vijana hao.
Isaya alimsogelea mbunge mwenzake na kumpiga piga mgongoni
"Ninayo karata yangu ya mhimu sana ambayo ipo mahali nimeiweka, sina wasiwasi ile nitaitumia kama plan B pale mambo yatakapokukuwa mabaya kwangu, usijali huu mchezo nauchezesha mimi" aliongea kwa tabasamu huku akitaka mwenzake huyo amfuate nyuma. Mbunge huyo hakumfuata kama Isaya alivyo hitaji bali alichepuka na kutokea mlango mwingine, aliondoka kahisa eneo hilo, yeye hakutaka kuwa mmoja wa waasi wa nchi yake mwenyewe.
Unahisi kuna mapinduzi ya nini? Raisi kweli ana mambo yake ya siri au ni tamaa zao za madaraka? Hiyo karata ambayo inampa kiburi zaidi ni ipi? Watafanikiwa mipango yao?
Episode ya 7 inafika tamati.
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
EPISODE 7.
Mita chache kutoka eneo lilipokuwepo bunge la nchi ya Tanzania, mji ulio fahamika kama DOGMA TULIPO, kwenye chumba kimoja cha mapumziko walionekana vijana wawili wakiwa ndani ya suti huku wakiwa wanabadilishana mazungumzo ambayo yalionekana kutokuwa na maelewano makubwa.
"Ndugu yangu ujue mimi sikuelewi mpaka sasa lengo lako kubwa hasa ni lipi mpaka unataka kuyafanya haya yote?"
"Hauwezi kunielewa kwa sababu unaishi kama bendera fuata upepo tu hujui hata kesho kipi kinatakiwa kufanyika ndani ya nchi yako mwenyewe, sasa sijui huo ubunge wananchi wako walikupa vipi mwanaume muoga kama wewe ambaye huwezi hata kuwasemea kabisa changamoto zao zikatatuliwa" mwanaume aliye Julikana kama Isaya Ndango, aliongea kwa jeuri kwa mbunge mwenzake huku yeye akijinasibu kwamba alikuwa shababi hivyo hakuwa akiogopa chochote kile.
"Muda mwingine kukurupuka kwa mtu kuropoka huwa hakutoi maana ya moja kwa moja kwamba yeye ni mpenda haki na anatumia akili kwa kile anacho kifanya. Jambo ambalo unalifanya linaenda kuigawanyisha nchi kabisa na kufanya watu waanze kuichukia serikali yao, sasa huoni kama unaiingiza nchi kwenye machafuko makubwa?
Tumia akili ndugu yangu sio kuhitaji kutafuta umaarufu na sifa za muda mfupi ambazo zinaweza kukuletea matatizo na kuiweka nchi kwenye machafuko yasiyo na ulazima kwa tamaa za watu wachache" mbunge huyo alimsihi sana Isaya ndango kusitisha hicho alichokuwa anahitaji kukifanya.
Isaya alicheka kwa muda kwanza akiwa anamwangalia mwenzake huyo usoni kwake huku akifunga vizuri kifungo cha juu kwenye koti la suti.
"Nina uhakika mpaka hapo ulipo wewe mwenyewe haujui unataka nini ndiyo maana unakosa misimamo kwa kuhisi mimi natafuta sifa. Nakukumbusha jambo moja tu, unahisi ni kwanini mimi ndiye mwanasiasa pendwa zaidi nchini kwa sasa? Unahisi ni mwanini wananchi kila siku wanaliimba jina langu kwamba siku moja natakiwa kuingia Ikulu? vipi unahisi haya mambo yanakuja kwa bahati mbaya?" Isaya Ndango alimuuliza mbunge mwenza huyo kisha akaendelea;
"Mambo siyo rahisi kama unavyo yaona wewe kwenye macho yako yanafanyika, kila ambacho unakiona kwenye macho yako basi ujue walikaa watu wenye akili wakakipanga na namna ya kukimaliza wanajua. Sasa ukija na uoga wako hapa na kuanza kuhubiri kwamba natafuta sifa basi wewe ndiye utakuwa hauna akili kabisa na unategemea akili za watu wachache ili uweze kufanya mambo yako" alitulia na kuendelea tena;
"Hii nchi, ni nchi iliyo barikiwa sana kwa kila kitu, kuanzia rasilimali zake, watu wenye uwezo mkubwa kiakili na kiuongozi ambao kwa tamaa za watu wachache wenye nia ovu hawapewi nafasi kwa sababu watu hao wanaogopa kwamba nafasi zao zitabebwa na hao watu"
"Hawa watu wenye uwezo mkubwa ndio ambao wanapaswa kuiongoza serikali hii ambayo imejaa udhalimu, ukatili wa kila namna, watu wanauawa kila siku, watu wanalia ajira kila kuitwapo leo huku viongozi wakubwa wakiwa wanawaajiri ndugu zao ambao hawafai hata kuwa viongozi sehemu yoyote ile"
"Nchi inapelekwa mputa kwa maslahi ya watu wachache, hivyo mtu kama mimi siwezi kukubali kuona nchi yangu inateketea kwa kumuogopa mtu yeyote yule na ndiyo sababu ambayo imefanya nimepigania hili mpaka leo bunge limeitishwa rasmi ili tuweze kuzungumza kwa kina kuhusu hili jambo na mwafaka wake utakuwaje mbeleni.
Hivyo kwa leo wabunge na viongozi wengine ambao watafika leo nitajua ndio hao ambao tupo nao pamoja kwenye safari hii ya kwenda kupata nchi mpya yenye kila lililo jema" alimaliza kuongea huku akiwa anaangalia saa yake. Mbunge mwenzake ni kama hakumuelewa ilimlazimu kumuuliza.
"Usiniambie kwamba ulipita kwa kila mbunge kuweza kumshawishi kuhakikisha unatekeleza mipango yako?" Aliuliza kwa mshangao lakini Isaya Ndango alitabasamu tu,
"Nisikilize rafiki yangu, mimi na wewe tumeanza siasa pamoja tukiwa sekondari lakini wewe ni muoga sana, kwa sasa mimi ndiye mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa zaidi nchini hivyo kuwashawishi watu kwangu ni kazi ndogo sana na ndicho nilicho anza nacho, najua kwamba kama wabunge wengi wakiwa upande wangu basi kazi inaenda kuwa rahisi sana kwa upande wangu"
"Isaya unamaanisha nini kusema hivyo?"
"Hili ni jaribio langu la kwanza kwenda kuharibu kila kitu ambacho unakiona, na baada ya hapa nadhani karibia kila mbunge atakuwa upande wangu pale ambapo watasikia kile ambacho nitakiongea bungeni"
"Hey! hey! Suburi kidogo, unaamisha kwamba unataka......!?" mwenzake huyo akiwa anaongea kwa kigugumizi, mbunge Isaya alimsaidia kulisema hilo jambo.
"Tunataka kuipindua serikali madarakani"
"No, no, no Isaya. Umepatwa na nini ndugu yangu mpaka unawaza mambo mazito ya kigaidi namna hiyo? Ni tamaa ya madaraka au ni kipi kimekufanya ghafla sana umebadilika namna hiyo" rafiki yake alishangazwa sana na namna mwenzake huyo alivyokuwa anawaza mambo mazito sana namna hiyo.
"Haupaswi kuniuliza mimi hilo swali bali unatakiwa kuwauliza hao viongozi wako kwamba wanafeli wapi? Mpaka mbunge wa kawaida kama mimi nataka kuwatoa madarakani!"
"Hili jambo haliwezekani Isaya"
"Unajua kwanini sikutaka hata kukushirikisha?"
"Hapana"
"Sababu ndiyo hiyo, wewe ni mbinafsi sana kwa sababu huwa unajiwazia wewe tu na sio vinginevyo, mimi nina watu wengi ambao wapo upande wangu hivyo usije ukahisi kwamba nafanya haya mambo kwa kukurupuka kama unavyohisi wewe. Yule raisi hafai kuiongoza nchi hii tena kuanzia sasa, ana mambo mengi sana ya kutisha nyuma ya pazia ambayo wananchi wakiyajua basi siku hiyo hiyo watahitaji wamtoe hata kwa nguvu pale Ikulu"
"Ndo uwaze kumtoa raisi madarakani ndugu yangu? Kipi kinakupa hiyo jeuri namna hiyo?" Mbunge huyo baada ya kuuliza, Isaya alitabasamu tu na kuangalia saa yake na ghafla mlango wa hicho chumba walicho kuwepo ukawa unafunguliwa.
Mtu aliye ingia humo ndani alimuacha mdomo wazi mbunge huyo lakini kwa Isaya Ndango ilikuwa ni tofauti maana hata kauli ambayo aliitamka ilizidi kumchanganya mwenzake huyo.
"Mr President karibu sana" mbunge huyo alishangazwa na mambo makubwa mawili. Aliyekuwa ameingia hapo alikuwa ni waziri mkuu wa nchi ya Tanzania, wakati akiwa anajiuliza kwamba vipi waziri mkuu naye anahusika? Ndipo aliposhangazwa zaidi na maneno ya Isaya ndango baada ya kumuita waziri mkuu huyo, Mr president.
Kichwa chake kwa haraka sana kiliweza kuelewa kwamba ina maana kama huo mpango wa kumpindua mheshimiwa raisi pamoja na serikali yake ukikamiloka basi waziri mkuu ndiye ambaye alikuwa anategemewa kukalia kiti hicho, sasa alielewa kwamba ni kwanini Isaya Ndango alikuwa na jeuri ya kusema kwamba ana watu wazito sana upande wake.
Kama mpaka mtendaji mkuu huyo wa serikali alikuwa yupo upande wake basi ilionyesha walikuwa na mengi makubwa ambayo walitaka kuyafanya hata hivyo aliona kwamba ni jambo la hatari sana ambalo walikuwa wanalifanya vipi kama ingejulikana moja kwa moja na alisema siku hiyo anaenda kumwaga mboga mbele ya bunge ambalo huwa linarushwa moja kwa moja mubashara kabisa na watu wanaangalia kinacho endelea?.
Moyoni mwake alikiri kwamba hakuwa tayari kabisa kushiriki kwenye hilo jambo, kwa maana hakuelewa raisi huyo alikosea wapi kwa maana alikuwa anamuona kama mtu safi ambaye alikuwa anaiendesha nchi kwenye misingi safi kabisa na demokrasia ya wazi ambayo kila mwananchi alikuwa anaifurahia, vipi leo aambiwe kwamba kiongozi huyo alikuwa ana mambo ya ajabu ambayo kama wananchi wakiyajua wanaweza kumtoa madarakani hata siku hiyo hiyo, alichoka maana hakuwa na majibu ya moja kwa moja.
Swali la mwisho ambalo alishindwa kulipatia majibu yake, ni kuhusu huyo rafiki yake, ni kwanini alikuwa amemficha kwa kipindi chote hicho? Alikuwa hamuamini? na kama anataka kumtoa raisi madarakani maana yake yeye ndiye anaye itaka hiyo nafasi kwa sababu wananchi wanamkubali sana kwa siasa zake zenye mitazamo ya mbali mno, iweje aweze kumpatia hiyo nafasi waziri mkuu ndiye aingie Ikulu?
Kama waziri mkuu akiingia Ikulu, yeye atakuwa nani? na ana mpango upi hasa wa siri ambao unamfanya azisukume kete zake kwa kujiamini sana namna hiyo mpaka kuwaza mambo makubwa kiasi hicho?. Akiwa kwenye hayo mawazo ndipo waziri mkuu alipo msogelea.
"Heshima yako mheshimiwa!" alimsalimia kiongozi huyo mkubwa kwa heshima. Jina lake alikuwa anajulikana kama William Ivan Msoka, hilo ndilo lilikuwa jina la kisheria la mheshimiwa waziri mkuu huyo wa nchi ya Tanzania.
Alimpa mkono mbunge huyo ambaye alikuwa ana wasiwasi mno, macho yake yakiwa yanamuangalia Isaya na kumuuliza.
"Mbona huyu kijana ana wasiwasi sana, hauoni hatari kuingiza watu waoga kama hawa kwenye mpango kama huu?" waziri mkuu aliuliza huku akigeukia upande wa mbunge yule na kumkazia macho
"Hapana mheshimiwa, huyo ni kijana wangu tangu tunakua ndiyo maana hata safari yetu inafanana kwa kila kitu hata majimbo yetu ni jirani ila nadhani kwamba hakutegemea kukuona hapa ndiyo maana ana wasiwasi sana kiasi hicho maana sikumwambia kwamba unakuja" Isaya Ndango ilimbidi amtetee mwenzake maana hakuwa na namna nyingine huenda angeingia kwenye matatizo.
Waziri huyo alimuangalia vizuri sana huyo mbunge na kutamka;
"Nadhani ni muda mwafaka tuelekee kulutekeleza jambo letu maana ni dakika ishirini tu zijazo bunge linaanza ila kuna kitu kimoja naona kama hakipo sawa!" alimgeukia mbunge Isaya akiwa amehamaki kwa mshtuko,
"Spika wa bunge hatakuwepo leo"
"Whaaat? Kivipi?" Isaya Ndango alishtukizwa na hayo maelezo ya ghafla ambayo hakuyategemea kabisa.
"Ameitwa na raisi muda sio mrefu na kudai kwamba wana kikao cha dharura"
"Unamaanisha kwamba mheshimiwa raisi anajua juu ya huu mpango wetu?"
"Sina uhakika sana na hilo ila kahakikishe unaongea kila kitu mle, hivyo hata kama atakuwa amejua, atashtuka akiwa amesha chelewa, hivyo kwa leo bunge litaongozwa na naibu spika. Ni muda wa kwenda kuanza rasmi mapinduzi kwa kuwafahamisha wananchi yale ambayo hawayajui" Mr William Msoka aliongea kwa kujiamini na kutoka humo ndani kwani hakutakiwa kuongozana na vijana hao.
Isaya alimsogelea mbunge mwenzake na kumpiga piga mgongoni
"Ninayo karata yangu ya mhimu sana ambayo ipo mahali nimeiweka, sina wasiwasi ile nitaitumia kama plan B pale mambo yatakapokukuwa mabaya kwangu, usijali huu mchezo nauchezesha mimi" aliongea kwa tabasamu huku akitaka mwenzake huyo amfuate nyuma. Mbunge huyo hakumfuata kama Isaya alivyo hitaji bali alichepuka na kutokea mlango mwingine, aliondoka kahisa eneo hilo, yeye hakutaka kuwa mmoja wa waasi wa nchi yake mwenyewe.
Unahisi kuna mapinduzi ya nini? Raisi kweli ana mambo yake ya siri au ni tamaa zao za madaraka? Hiyo karata ambayo inampa kiburi zaidi ni ipi? Watafanikiwa mipango yao?
Episode ya 7 inafika tamati.
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app