Mnachihanguuu
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 4,385
- 6,443
Unaweza kwakweli
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shukrani sana mkuuUnaweza kwakweli
Tayari mkuu.....tunasubiria📖Saa 5:00 jioni [emoji872]
Kidogo kidogo tunaokota maarifa mkuuSimulizi ni 🔥
Inatupa mafunzo kila episode 🤝🏽
Shukrani sana mtunzi 👊STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI
SONGA NAYO................
******
Sarah alikuwa kama amechanganyikiwa, ni kwa muda mfupi tu maisha mambo yalikuwa yanambadilikia. Mama yake hakuwa anamuelewa mpaka wakati huo, walikuwa kwenye mzozo baada ya mama huyo kugundua kwamba mwanae alikuwa amehusika kwenye mauaji ya mke wa raisi wa nchi, kwake jambo hilo aliliona kama baya na hatari kwa familia yake ndiyo maana hakuwa kabisa kwenye hali ya utulivu.
Alihisi mwanae huyo alikuwa akijihusisha na mambo mabaya, kama mama jambo hilo lilimfanya ajisikie vibaya kwa sababu mwisho wa familia yao ulikuwa unaonekana kabisa kuwa mbaya. Ni muda ulikuwa umepita tangu afanikishe kulitekeleza tukio hilo ambalo alilifanya kwa ajili ya familia yake lakini aliishia kupata lawama tu. Ni kawaida muda mwingine kwa mwanadamu kukubali kupokea lawama lakini jambo la mhimu zaidi ni kuhakikisha kwamba familia ipo salama na ndilo jambo ambalo yeye binafsi alikuwa akilizingatia zaidi.
Alikuwa mpweke mno, alikuwa amekaa karibu na dirisha akiwa anatazama mbalamwezi zilivyokuwa zimeupamba mlima Kilimanjaro, akiwa hapo anavuta sigara yake taratibu kupunguza mawazo ambayo yalikuwa yanamzonga kwenye jumba lake hilo umeme ulikatika ghafla na kurudi, haikuwa kawaida, hata siku moja nyumba yake haikuwahi kukutana na tatizo la namna hiyo hivyo alishtuka kidogo kisha akatulia tena na kuhisi huenda lilikuwa ni wenge lake.
Wakati amekaa tu simu yake ilianza kuita ikabidi aitoe mfukoni ndipo aligundua kwamba ilikuwa inaita, kuita kwa simu hiyo ndiko kulimpa umakini na kumshtua. Simu ilitoka kwa Nick, mwanaume ambaye walikuwa wameanzisha naye mahusiano muda mfupi uliokuwa umepita, haikuwa kawaida kabisa mtu huyo kumtafuta muda kama huo hivyo moja kwa moja aligundua kabisa kwamba hapakuwa sawa, ni lazima kulikuwa na tatizo mahali. Aliipokea simu hiyo.
“Nick kwema?”
“sina imani Sarah, unaweza ukaniambia uko wapi muda huu?”
“Leo sijatoka nipo ndani”
“Upo na familia?”
“Wao wamelala”
“Basi naomba uje unifungulie mara moja” alishtuka baada ya kugundua kwamba bwana huyo alikuwa amefika kwake majira hayo, hakuwa na kumbukumbu kabisa kama kwenye maisha yake kama aliwahi kumuelekeza kwake ni wapi, sasa alipajuaje? Akiwa anajiuliza swali hilo gumu ambalo hakuwa na jibu lake kwa wakati huo aligundua kwamba bado simu ilikuwa hewani hivyo akajichekesha na kuuliza swali.
“Nick umepajuaje nyumbani kwangu?”
“Sarah sio muda wa maswali saivi, nina dharura ya msingi ambayo imenileta hapa tafadhali na unajua kabisa kwamba nisingekuja bila ruhusa maalumu eneo hili” alisita kidogo kisha akakubali kwa sababu alikuwa akimwamini bwana huyo.
Aliiweka sawa silaha yake kiunoni na kuanza kusogea eneo ambalo lilikuwa na mlango wa kuingilia ndani ya jumba lake. Aliufungua kwa tahadhari baada ya kuwasha taa za sebule ambayo ilikuwa kubwa ya kutosha kufanyia mambo mengi ya msingi. Baada ya kuufungua mlango huo alikutana uso kwa uso na bwana yule ambaye usoni alikuwa mkavu kabisa bila wasiwasi wowote ule.
“Nick kuna nini?” aliuliza swali ambalo hakujibiwa, hakujibiwa kiasi kwamba ayeye mwenyewe alianza kupata mashaka kuhusu mtu huyo, alimkagua kuanzia juu mpaka chini, hakuwa na dalili za kwenda kirafiki hilo eneo. Moyoni alipata majibu akiwa amechelewa.
“Nick, na wewe ni miongozi mwao?” akili ilikuja kumrudi baada ya kuhisi kwamba huenda hata huyo jamaa yake alikuwa miongoni mwa wale watu ambao walimletea majanga mazito kwenye maisha yake kiasi kwamba mpaka wakati huo hakuwa na uelekeo sahihi.
“Ulikuwa ni wakati mwema kukufahamu Sarah ila naomba unisamehe kwa sababu sina namna juu ya hili, unatakiwa kufa”
“Whaaaaat?” nani alikwambia unapaswa kuweka imani yako kubwa kwa wanadamu? Itakula kwako, kuna wakati hata nafsi yako mwenyewe haupaswi kuipa imani kubwa kupitiliza. Yule mwanaume ambaye alianza kumpa imani yake na kumzawadia mwili wake, alikuwa miongoni mwa wale washenzi ambao ndio walikuwa wanamletea wakati mgumu kwenye maisha yake. Alibaki ameduwaa asiamini kile kilichokuwa kinaendelea lakini bwana yule hakuonekana kujali kwa lolote lile.
Alianza kujipapasa taratibu kwenye kiuno ili kutoa ile bastola akiwa anarudi nyuma, nani angempa nafasi kama hiyo mdunguaji hatari wa namna hiyo? Alibebwa juu na guu ambalo lilitua kwenye kiuno sehemu ambayo aliihifadhi bastola, wakati anadondokea kwenye sofa moja na bastola yake ikienda upande mwingine aligundua kwamba bwana huyo hakuwa mwenywe bali alikuja na wanaume wengine wa kutosha ndani ya hilo eneo. Walikuwa jumla wanaume sita ambao wote walionekana kuvaa nguo za jeshi.
Alisimama kupambana na mtu wake wakati huo baadhi ya wanaume waliingia kwenye vyumba vingine kufanya ukaguzi. Sarah hakuwa na namna zaidi ya kuyapambania maisha ya familia yake, alidunda kwenye sofa na kutua pale ambapo alikuwepo Nick, mateke yake mfululizo hayakufua dafu baada ya kuishia kwenye mikono ya mwanaume huyo ambaye aligeuka na buti la kichwa ambalo lilimkosa Sarah kichwa likatua kwenye shingo yake kiasi kwamba akayumba mpaka kusimamia mbali.
Wakati anakaa sawa, hakuwa na muda wa kutosha kupumzika kwa sababu mwanaume huyo alikuwa anakuja kwa kuzunguka kwa kasi mpaka alipo mfikia, alijaribu kupangua teke moja ambalo alifanikiwa lakini wakati huo mkono ulitua kwenye ziwa la kulia, alitoa sauti ya kilio kwa mbali, ulimuingia vizuri. Alirudi nyuma kwa kuyumba akaishia kushindiliwa na double kick iliyo mpeleka mpaka ukutani akapasua runinga kubwa ambayo ilikuwepo hapo.
Mwanaume huyo hakuwa na huruma kabisa, alikuwa anapigana na mtoto wa kike kama anapigana na mwanaume mwenzake. Sarah akiwa anavuja damu mdomoni na puani alisikia sauti za kelele, alikuwa mama yake na mdogo wake wakiwa wamebebwa msobe msobe kuletwa karibu na alipokuwepo yeye wakati ule. Jambo lile lilimpa hasira kuona familia yake inafanyiwa huo ukatili mbele yake, akahitaji kunyanyuka huku akiwa anapiga kelele, alikutanishwa na mguu wa uso, damu nyingi zilisambaa kila kona ya lile eneo akiwa anadondokea upande wa pili.
Mama yake alipiga makelele akiwa anaomba mwanae aachwe ila mazingira hayakuwa rafiki wakati ule, nani angemuacha Sarah? Hakuwepo wala hakuwa na msaada. Sarah alijikongoja kuegamia ukuta akiwa anamuomba mama yake msamaha kwa sababu huenda kama sio yeye basi familia hiyo ingekuwa kwenye amani lakini yeye alifanya kila kitu kuwalinda kwa sababu hata kama angegoma kufanya kazi ya watu hao mpaka muda huo familia hiyo ingekuwa imekufa muda mrefu.
“Sarah nasikitika kukwambia hili ukiwa umechelewa kuweza kulielewa, wanadamu tupo tofauti mno, wanadamu muda mwingine hatueleweki hivyo usihadaike na maneno ya mdomoni. Mimi kwako nilikuja kwa lengo maalumu ili niweze kujua kama kuna mambo ya ziada unayajua
Baada ya kujua siri ndogo ambayo ilikuwa kwenye moyo wako mimi ndiye ambaye nilipendekeza jina lako kwa mtu wa kwenda kumuua mke wa raisi kwa sababu ilikuwa ni rahisi kukumudu maana najua kila kitu kuhusu wewe
Hata kukamwatwa kwa familia yako mara ya kwanza ni mimi ambaye nilikuwa nyuma ya kila kitu, nimekuwa nikifanya kazi na hawa watu kwa muda sasa na sijutii kwa sababu napata kila ninacho kihitaji kwa wakati ambao nauhitaji mimi
Shilingi ina pande mbili Sarah, sio kila upande ni wa ushindi, mimi huwa naangalia upande ambao siku zote umeshikilia ushindi na ndiyo namna ambavyo maisha yanatufunza kuweza kuyaishi. Hawa watu wana pesa, wana nguvu kubwa, wana kila kitu hivyo hakuna mtu kwenye taifa hili ambaye anaweza kwenda kinyume nao akaweza kuishi ama kuwepo kwa muda mrefu”
“Kukufupishia maelezo ni kwamba nimekuja hapa kuhakikisha naua familia yako yote, nataka ushuhudie mama yako akifa huku unaangalia, lakini pia mdogo wako ambaye unampenda sana nataka afe ukiwa unamshuhudia pia. Wewe unaonekana kuwa hatari kwa hawa watu kwa sababu kama Gavin alifanikiwa kukuacha hai na kukupatia kiwango kikubwa cha pesa ambacho inabidi niondike nacho muda huu maana yake lazima kuna siku atakuja kukutafuta na unaweza kuja kuwa sababu ya mambo kuharibika
Sehemu ya 52 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
Karibu sanaaaaaaaShukrani sana mtunzi 👊
Ni muda wetu mkuuOn fire mwandishi [emoji120]
Tuwatag na wengine mkuu tufaidi wote maana ndo kwanza tunaanza....Its Pancho unakosa uhondo mkuu
Nimefika mkuu ndio naingia sasa naona mambo moto sanaIts Pancho unakosa uhondo mkuu