Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Unamalizia 2500 tu nakupa ilipo ishia mpaka mwisho...


WhatsApp au kawaida

0621567672
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA TATU
SONGA NAYO................

Swali la msingi linaweza kuwa ni kwa namna gani Gavin alishindwa kumlinda ndugu yake? Wakati ndugu yake anakufa alifanyiwa mchezo mbaya kwa sababu kuna mtu ambaye alisambaza habari kwamba familia imevamiwa na inaonekana kwamba ni mtu ambaye alikuwa karibu na familia hivyo Gavin alisafiri kwenda haraka ilipokuwepo familia yake lakini baada ya kufika huko alikuta familia ipo salama kabisa hivyo alishtuka hapo akagundua kwamba lazima hesabu zilikuwa kwa ndugu yake na wakati anafika kwa ndugu yake biashara ilikuwa imeisha tayari, alikutana na maiti. Kuna baadhi ya watu ambao waliwahi kuwa karibu na familia hiyo wanadai ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa mwanaume huyo kuweza kutoa machozi na kulia kama mtoto mdogo baada ya kumpoteza kaka yake wakati alikuwa ana uwezo wa kumlinda.
Sasa wakati ameenda sehemu ambako kaka yake alihifadhiwa huko nyuma tena yalitokea mabalaa mengine kwani kuna watu walienda kwenye ule mji wa baba yake na kuteketeza familia nzima. Yalikuwa ni mauaji ya kikatili isivyokuwa kawaida, Gavin alibaki amechanganyikiwa akiwa haelewi kitu kilicho mtokea, yalikuwa ni maluwe luwe yanamtokea kwa muda mfupi, ilikuwa ni ngumu watu wale kufanya jitihada za kuua familia bila uhusika wa watu wa karibu wa familia hiyo hivyo mpaka hapo alijua kabisa kwamba usaliti mkubwa ulianzia ndani lakini swali la msingi lilikuwa ni nani ambaye alikuwa anamtaka baba yake afe kwa gharama yoyote namna hiyo kiasi kwamba akateketeza familia nzima?
Mama yake mzazi ambaye alikuwa anaitwa Glady, baba yake, kaka yake na baadhi ya watu wao wa karibu wote waliuawa siku ile. Ni siku ambayo ilikuwa ni pigo kubwa mno kwake lakini kitu kibaya ni kwamba hakutakiwa kujulikana kama yupo hai. Inadaiwa kwamba usiku wa siku ile aliua watu miambili na hamsini ndani ya ule mji ambao alihisi kwamba walihusika kuusuka mpango huo lakini hakupata ukweli juu wa wahusika, Gavin alikuwa kama amechanganyikiwa hivyo ikatakiwa mama yake mlezi aondoke naye kwa muda na kwenda kumfungia mahali kwa sababu kuendelea kuwepo mtaani angeua watu wengi wasio na hatia na alikuwa ana nguvu za ajabu ambazo zinadaiwa alizipatia huko ambako alikuwa anaizungukia dunia kipindi hicho.

Alimaliza mwaka mmoja akiwa hana uwezo wa kuzimudu zile nguvu ambazo alikuwa nazo kutokana na kuwa mtu mwenye hasira muda wote, ndio wakati ambao kanali alikuwa amestaafu kazi na ndiye ambaye aliondoka na mwanaume huyo na kwenda kumfungia mahali ambako inadaiwa kwamba ni yeye tu pekee ndiye ambaye alikuwa anapajua na ndiye pekee ambaye alikuwa anaweza kuonana na Gavin akiwa anaishi kwenye minyororo. Lengo la kumfungia huko ilikuwa ni kumfanya aweze kuzituliza nguvu zake ambazo ulihitajika mwaka mzima ili kuziweka sawa na kuzipunguza nguvu aweze kurejea kwenye hali ya kawaida ndipo wangejua ni kitu gani kilitakiwa kufuata baada ya hapo kwa sababu kama angeendelea kuwepo mtaani basi huenda angeua watu wengi na jambo hilo lingekuwa ni la hatari isivyokuwa kawaida.
Ule mwaka mmoja ulipoisha ndipo alirudi tena Gavin Luca na mwanamama yule ila kwa bahati mbaya wakati wanarudi mama yule alikutana na pigo kubwa, mumewe na mwanae waliuawa pembezoni mwa fukwe ya bahari. Hakujua ni nani alifanya hivyo ila alikuwa ana uhakika kwamba lazima kulikuwa na muunganiko mkubwa wa kuwa karibu na familia ya Lucas na vile vifo. Lile lilikuwa pigo kubwa mno kwa upande wake kiasi kwamba lilimfanya akaishi na maumivu mazito moyoni na inadaiwa kwamba tangu kipindi kile lile tukio litokee, huwa anaenda kila siku ambayo lile tukio lilitokea kwenye lile eneo siku ambayo mumewe na mwanae waliuawa pale kwa ajili ya kumbukumbu yao.
Lile tukio lilimfanya Gavin ajisikie vibaya kwa sababu aliamini kwamba huenda yeye ndiye alikuwa sababu ya yale yote kutokea, hivyo baada ya tukio lile hakutaka binadamu yeyote aliye hai aje kumgusa yule mama kwa namna yoyote ile na ambaye angekaidi hilo basi hakuwa na muda wa kuweza kuishi tena. Mama huyo alikuja kuigiza kuwa na ugonjwa wa akili baada ya hapo, alijifanya ana maisha magumu na hali ya chini kwa kufilisika baada ya mumewe kufa na ndiyo sababu akaamua kustaafu na kuhitaji kwenda uswahilini huko ambako mpaka sasa ndiko umetoka wewe kudai kwamba ulienda kuongea naye na ndiko huko ambako raisi alituma watu wake waweze kumuua kama sio kuondoka naye” mzee huyo alikuwa anaidadavua historia ambayo ilionekana kuwa ndefu huenda tofauti hata ambavyo mheshimiwa alikuwa anaifikiria.
“Mhhhhh historia yake sio nzuri sana japo kuna baadhi ya maeneo nayajua kwa sababu mimi mwenyewe nilihusika kwa namna fulani ila bado sijaelewa kuhusu historia ya Gavin Luca, aliwezaje kuishi kwa siri bila kufahamika? Hizo nguvu ambazo unazisema wewe alizipatia wapi? Wakati ambao alikuwa anaishi nje alikuwa anaishi na nani? Na ilikuwaje mpaka akatuaminisha amekufa, baadae likaibuka hilo jina lakini hatukujua kama ni mtoto wa yule muuza madawa ya kulevya lakini pia nataka kujua kwamba ugomvi wa Aurelia na Valeria mke wa raisi ulianzia wapi maana kwenye maeneo yote hayo sijaona sehemu ambayo inazungumzia jambo hilo”
“Wewe ni mkuu wa majeshi ambaye unatakiwa kutafuta baadhi ya taarifa kwa sababu sio kila taarifa utegemee mimi nitakupa, hapa nimekupa historia yake fupi tena kwa kuruka ruka na siwezi kukumalizia yote kwa leo kwa sababu ya usalama wangu labda mpaka siku ambayo nitakuwa na uhakika kwa asilimia miamoja kwamba nitakuwa salama ndipo nitakunyooshea kila kitu kuhusu huyu bwana mdogo ambaye wewe unamtafuta”
“Kwahiyo unahisi kwamba bado naweza kukuua?”
“Kwenye historia yako tu hukuwahi kuwa mtu mwaminifu sana mpaka muda huu umemsaliti bosi wako ambaye amekuagiza kwangu unataka mimi ndiye nikuamini kirahisi tu bwana Savato?”
“Naona unafika mbali mzee wangu”
“Sio mbali, huu ndio uhalisia wenyewe na kama unaona sipo sawa unaruhusiwa kunikosoa kama utakuwa na hoja za kufanya hivyo”

“Nina maswali mengi sana juu yako, natakiwa kujua uhusika wa raisi wa zamani uliishia wapi kwenye hili, nataka kujua kuhusu maisha ya nyuma ya mtu ambaye amenituma kwako maana anadai yeye anafahamiana vizuri na Gavin na waliwahi kukutana akamuachia makovu ya maisha ambayo yamemfanya mpaka sasa hawezi hata kujitokeza hadharani kuishi na watu wengine lakini haya yote sijayasikia kabisa kwenye historia ambayo ulikuwa unanipa juu ya mtu huyo. Ukiacha hilo nataka kujua yule waziri mkuu wa zamani ambaye umedai ni babu yake na Gavin yuko wapi na yeye alihusika vipi kwenye hili jambo maana hujamtaja licha ya kudai kwamba mtoto wake ambaye ni Glady aliuawa na watu hao wanao jiita THE IMMORTALS ambao ndo kwanza nawasikia na kwa maelezo yako mimi naonekana kabisa kuwa mmoja wao.” Mkuu wa majeshi alimeza mate kidogo na kuendelea

“Kuhusu kuingia na uhusika wangu kwenye jambo hili naujua vizuri hivyo hauna haja ya kuniambia, ila usisahau nataka kukujua wewe ni nani kwenye hii historia na ilikuwaje ukawa na taarifa nyingi za ile familia? Yaani wewe ni nani hasa kwao lakini kwa sababu umesema kwamba kuna mambo ni ngumu kuyaongelea hapa leo basi nataka kujua Aurelia na Valeria vita yao ilianzia wapi kiasi kwamba mtu ahitaji mke wa raisi afe kwa gharama yoyote ile?” mkuu wa majeshi bado alikuwa na mengi ya kuyajua na kujifunza lakini mtu huyo alikuwa anazitumia taarifa hizo kuyalinda maisha yake.
“Una watoto wangapi?” mkuu wa majeshi alishtuka baada ya kuulizwa swali hilo
“Mambo ya familia yangu yanakuhusu nini?”
“Yanaweza kuwa yananihusu bwana mkubwa”
“Kwanini”
“Ifiche familia yako sehemu ambayo hakuna mtu ataweza kufika ingali bado una muda bwana Savato”
“Whaaaaat?”
“Kuna kitu kimoja sikukwambia siku ile kwa sababu sikuwa nakifahamu bado kwa kukaa ndani kule kwa muda mrefu ila nimekigundua baada ya kuja huku uraiani. THE IMMORTALS wana taarifa zako zote wewe maana yake kama ni hivyo hata yule bwana mdogo Yosef Biton alikuwa na taarifa zako wewe. Nadhani unajua kwamba amekufa tayari kwa kukutwa ameuawa huko Jozi na mtu ambaye bila shaka amehusika kwenye mauaji yake ni Gavin hivyo kama amekutana naye maana yake ni lazima jina lako limetajwa tu kwa namna yoyote ile na kama iko hivyo basi ni suala la muda tu kukutembelea mheshimiwa”
“Unahisi Gavin hana akili aje kumvamia mkuu wa majeshi?”
“Kwani wenzako walio uawa hawakuwa na ulinzi?”
“Huwezi ukafananisha na mimi hapa”

“Hivi unajisikia hata unacho kiongea? Unahisi kile kiumbe huwa kinajali kwamba wewe ni nani kinapo kujia? Itoe familia yako kwa sababu huwa ana hasira kila akikumbuka namna familia yake ilivyo uawa hivyo kuna mtu familia yake itakuja kulipa kwa hilo kumbuka kwamba kwenye hili jambo kuna orodha ya watu wengi ambao walitia mkono na watu hao wote ambao walihusika ni lazima wafe hivyo anamtumia mmoja mmoja kuwapata wengine na hatari inazidi kuja mbele kadri wanavyo julikana vigogo”
“Nimekusikia kwa ushauri wako ambao nina uhakika hata haujali lolote kuhusu mimi, hivyo endelea na nilicho kuuliza”
“Ukweli ni kwamba mimi sijali kabisa lolote kuhusu wewe ila najali kuhusu familia yako, hata kama wewe ni mshenzi ila sidhani kama watoto wako wanatakiwa kulipa kwa kile ulicho kifanya wewe” mr Savato hakumjibu mzee Hasheem bali alimtaka ampe chanzo cha ugomvi kati ya Aurelia na Valeria.






******
Wote mle ndani walikuwa kimya, walikuwa wametulia kumsikiliza princess Dayana kwa sababu alikuwa na machache ya kuweza kuwafunulia kuhusu Gavin Luca wakawa hawana namna huku mkurugenzi akiwa haamini wala kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
“Wale watoto baada ya kuzaliwa wawili, ni mmoja tu ndiye alijulikana kuwa mtoto wa Luca hata hivyo ni taarifa ambazo zilizagaa tu nje lakini hakuna mtu ambaye alikuwa na majibu ya moja kwa moja kuhusu mtoto huyo kwa sababu hakuwahi kuonyeshwa na kutambulishwa hadharani. Sasa mmoja ndiye alikabidhiwa kwa mtu mwingine ili amlee kama mtoto wake wa kumzaa na baadae mtoto huyo akaja kuchukuliwa na kuondoshwa kabisa nchini kila kitu akiwa anakisimamia huyo mlezi wake kwa sababu baba yake hakutaka kujihusisha sana na huyo mtoto kwani kama angeingia moja kwa moja kama baba watu wengekuja kujua na ingekuwa ni kama kuwatoa sadaka watoto wake wote tena kwa wakati mmoja”
“Mtoto mmoja alitumia muda mwingi kusoma lakini mtoto mwingine anadaiwa kwamba muda mwingi wa maisha yake umetumika kumtengeneza ambaye ndiye huyu Gavin Luca mwenyewe ambaye sisi tunamtafuta. Huyu ndiye alilelewa na mtu wa pembeni na sio wazazi wake ambao walikuwa na ratiba maalumu ya kumuona na kukutana naye hivyo muda mwingi zaidi ameutumia nje ya Tanzania akiishi kwenye maeneo mengi hapa duniani lakini eneo ambalo ameishi kwa muda mrefu sana ni china na inadaiwa kwamba hata nguvu zake wanazo dai ni za ajabu amezipatia huko”

Sehemu ya arobaini na tatu inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA NNE
SONGA NAYO................


“Kwahiyo mtu huyu anadaiwa kwamba alipotea na baada ya kurudi alianza kumtafuta mmoja mmoja ambaye alihusika na mauaji ya familia yake, haijalishi alihusika moja kwa moja au alitoa hata kipande cha taarifa tu ila ni lazima wote ahakikishe anawaua ndipo anaweza kuja kuacha kulifanya jambo hili. Hawa wanaokufa hawafi kwa bahati mbaya bali ni watu ambao wanajua ni kitu gani kilitokea miaka ya huko nyuma na kuna majina kadhaa ambayo ninayo kwenye mkono wangu yanaweza kuwa na msaada mkubwa kama ambavyo nilielekeza mwanzo japo ni pagumu tunapo elekea” Dayana alikuwa anashusha maelezo taratibu huku wenzake wakiwa wanamsikiliza kwa umakini mkubwa.
“Majina ya nani na nani?” mkurugenzi aliuliza wakati huu akiwa anasimama kutoka pale ambapo alikuwa ameketi.
“Kuna majina mengi na mengine ni yale ambayo huenda sisi tunapaswa kuyalinda”
“Taja tu”
“Wa kwanza ni mama yale mlezi”
“Unamjua alipo?”
“Sio alipo nalijua mpaka jina lake”
“Anaitwa nani?”
“Aurelia Vicent” Dayana alipo litaja tu hilo jina likatokea kwenye runinga kubwa mbele yao, ilikuwa picha ya mwanamama mmoja ambaye alikuwa ametabasamu kwenye hiyo picha
“Huyu ni kanali mstaafu wa jeshi” mkurugenzi aliongea kwa mshangao
“Huyu ndiye ana taarifa zote za Gavin kwa sababu ndiye alimlea kwa niaba ya wazazi wake na ndiye mtu pekee ambaye Gavin anamsikiliza kuliko binadamu yeyote hapa duniani”
“Ilikuwaje huyu ndiye akawa mlezi wake?”
“Sina taarifa zake kiundani zaidi”
“Hili jambo mbona linanichanganya! Huyu mama mara ya mwisho alistaafu kwa sababu alikuwa na matatizo ya kiafya na baadae akapata ugonjwa wa akili sasa inawezekana vipi awe na uhusiano wa moja kwa moja na Gavin?”
“Sijajua bosi huenda alifanya hivyo makusudi kuhakikisha kwamba hakuna ambaye anamfuatilia.
“Huyu tunatakiwa kumpata haraka sana, nipe majina mengine”
“Majina mengine, moja ni la rafiki yako, mengine ni mkuu wa majeshi pamoja na raisi kama nilivyotaja kule juu”
“Dayana una uhakika na hizi habari?”
“Raisi naye anadaiwa kwamba haya mambo yote anayajua kwa kila sentensi”
“Son of a bitch, huyu mpuuzi ndiyo maana hajali lolote hata nilipo enda kumpa hizi habari hakuonekana kujali maana yake hakuna msaada wowote ambao tunaweza kuupata kwake na kwa sasa tunatakiwa kuzifanya hizi kazi kwa usiri mkubwa kwa sababu kama watajua lolote kuhusu sisi basi hakuna jambo ambalo tutafanikiwa kulifanya, ni sisi ambao taifa linatuangalia, hatuwezi kuruhusu taifa kuteketea kwa namna yoyote hata kama tutamwaga damu yetu. Kwa sasa naenda kukutana na rafiki yangu wa zamani nyie endeleeni na kikao hapa na muangalie ni wapi mnaweza kuanzia” mkurugenzi aliishia njiani na kuwashangaza vijana wake, alidai kwamba alihitaji kwenda kukutana na huyo rafiki yake wa zamani ambaye alidaiwa kuwa babu yake na Gavin Luca, aliamini mzee huyo angeweza kumsaidia kuweza kutuliza hali hiyo japo hakuwa na uhakika.

**
Micho Othman aliwaacha vijana wake na kwenda kupigania hatima ya jambo hilo ambalo lililikuwa linaendelea nchini, alihitaji sana kukutana na rafiki yake huyo wa zamani hasa baada ya kugundua kwamba ndiye alikuwa babu wa mwanaume aliyedaiwa kuwa hatari ndani ya taifa. Ilikuwa ni kwa mara ya kwanza anaendesha gari yeye mwenyewe, hakutaka kabisa kuondoka na mtu yeyote yule ndani ya sehemu hiyo kwa sababu hakutaka kabisa ajulikane kwamba anaenda wapi. Safari yake ilikuwa ni kwenda Tandika lilipo soko kuu la ndizi pamoja na kuku, alishuka kwenye gari yake aina ya V8 nyeusi na kuiacha pembezoni mwa barabara. Kiongozi huyo alikuwa ni mtu wa siri mno hivyo hakuna mtu ambaye alikuwa anaweza kumtambua mtaani japo wahuni wengi hususani wale wapigaji wa mtaani walikuwa wanajua kabisa wangempiga pesa mtu huyo kwa mwonekano wake ulivyokuwa ila hakuonekana kabisa kuwajali.
Aliingia kwenye soko hilo na kotokezea kwa mbele ambako kulikuwa na mabanda ya kuku mpaka alipofika kwenye banda moja ambalo liliandikwa chizo. Vijana wengi walimshambulia wakisifia biashara zao ila yeye alimtaka kijana ambaye alikuwa na hilo jina, alikuja akiwa anakimbia akijua pesa zimejileta ila baada ya kufika hapo alishtuka sana huenda hakutegemea kumuona mtu huyo maeneo hayo ambaye yeye alionekana kumfahamu kama sio kuwa na taarifa zake kiasi cha kumshtua.
“Karibu sana kiongozi” aliongea akiwa anajichekesha huku akiongoza ndani sehemu ambayo haikuwa na mtu.
“Nahitaji kuonana na O.M.B muda huu”
“Sikutarajia kama ungekuwa hapa mheshimiwa maana imekuwa ghafla sana”
“Kwamba wakati nakuja ilitakiwa nikupe taarifa?”
“Hapana kiongozi” kijana huyo alijibu akiwa anaandika kitu kwenye katarasi yake
“Yupo mwembe yanga, na hili ndilo jina la duka lake ni maarufu sana pale ukifika utampata” kijana huyo aliongea kwa heshima kubwa, ni wazi alikuwa akimheshimu mtu mtu huyo. Mkurugenzi aliingiza mkono kwenye mfuko wake na kutoa bunda zima la pesa ambazo alimuachia kijana huyo na kuondoka hiyo sehemu.

Aliwasha gari yake kwa spidi kubwa alienda kufunga breki nje ya duka hilo na kushusha kioo. Ndani ya hilo duka alioneakana mwanaume mmoja ambaye mwilini alikuwa na vesti nyeupe, mwili wake haukuwa haba, ulishiba kwa mazoezi ya kutosha kama sio vyuma ambavyo vilikubali. Lilikuwa ni duka kubwa la vifaa vya magari na pikipiki, kijana yule aliiona ile gari pale nje na moja kwa moja akatoka na kulifuata akazunguka upande wa pili na kuingia ndani.
“Heshima yako kiongozi”
“Nataka kukutana na Hassan muda huu”
“Lakini si unalijua sharti lake?”
“Nakumbuka kwenye barua ya mwisho aliniambia kwamba kama kutakuja kuwa na ulazima sana wa kukutana basi tutakutana mara moja tu kwenye maisha yetu ya baadae hivyo sitakuja kumuona tena. Kwahiyo nipo tayari kukutana naye kwa mara ya mwisho” kijana huyo hakuongeza neno alishuka kwenye gari, aliingia kwenye lile duka na baada ya dakika moja alirudi akiwa na simu mkononi akamkabidhi mkurugenzi na kumtakia safari njema ya huko ambako alikuwa anahitaji kwenda wakati huo.

Aliibeba simu na kuondoa gari yake hapo, akiwa anaendelea kuendesha aliiwasha hiyo simu ndogo ambayo ndani yake alikutana na namba moja tu pekee hivyo akapiga. Simu ilipokelewa upande wa pili lakini mtu huyo hakuongea neno lolote akisubiri mkurugenzi ajitambulishe.
“Micho Othman, mkurugenzi wa shirika la kijasusi la TIGI. Nahitaji kuonana na Hasssan” alipo maliza kutamka tu simu hiyo ikakatwa kisha ukaingia ujumbe kwenye simu yake kumpa maelekezo sehemu ya kwenda. Alienda mpaka uwanja wa taifa wa mpira na kushuka kwenye gari yake akisubiri wahusika waje kumbeba.
Akiwa hapo ilikuwa ni majira ya alasiri tayari, kwenye simu yake alipata ujumbe wa taarifa ambayo haikuwa nzuri kabisa, taarifa ya kifo cha mke wa raisi. Alihisi kama kichwa kinataka kupasuka akabaki ameganda, hakuelewa hilo tukio lilitokeaje na mhusika wake alikuwa nani na alifanya hayo yote kwa sababu zipi za msingi. Ni yeye ambaye alijua atalaumiwa licha ya kwamba halikuwa jukumu lake kuweza kumlinda mke wa raisi, alimuelewa raisi huyo alivyokuwa anapenda kutafuta sehemu ya kuangushia mizigo ya lawama na siku hiyo hiyo alitoka kuipata taarifa kwamba raisi huyo alikuwa miongoni mwa wahusika ambao walidaiwa kuhusika na kujua historia ya mambo ambayo yaliwahi kutokea huko nyuma.

Akiwa anaendelea kuwaza na kufikiria kitu cha kufanya kwa mbele yake kidogo kuna gari aina ya cadillac Escalade ikikuja ikapaki, kuna mwanaume mmoja ambaye alivaa suti yake safi alishuka na kufungua mlango ikiwa ni ishara ya kumsubiri mheshimiwa kuweza kwenda kuingia. Akiwa anaanza kuinyanyua hatua yake moja akagundua kwamba simu yake ilikuwa inaita, aliyekuwa anapiga alikuwa ni raisi, maamuzi yalikuwa kwenye mkono wake apokee simu ya raisi kisha arudi kupambana na kesi ya mke wa raisi ama ampotezee raisi amtafute swahiba wake akapate majibu ambayo alitumia muda mrefu kuyawazia bila kuelewa kilichokuwa nyuma yake. Aliizima simu hiyo na kuiweka kwenye mfuko wake kisha akaongoza kuingia kwenye ile gari ya kifahari kisha baada ya hapo akafungwa kitambaa usoni gari ikatolewa baada ya kuzungushwa mara mbili asijue walikuwa wanaelekea wapi.

Mkurugenzi akiwa ndani ya gari, mawazo yake yalienda mbali sana, alikumbuka nyuma maisha yake kabla ya kuwa hapo, maisha ambayo yalikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na kule ambako yeye alikuwa anaelekea wakati huo. Historia ya maisha yao inaanzisha pembezoni mwa ziwa Tanganyika huko, ndani ya mkoa wa Kigoma. Huko ndiko kulikuwa nyumbani kwao, hiyo ndiyo sehemu ambayo wawili hao walizaliwa.
Walizaliwa maeneo ya karibu kwenye familia za wavuvi ndiyo maana wakawa marafiki walio shibana kwa sababu kila kitu walikuwa wanakifanya pamoja hata kwenda shule walikuwa pamoja, kucheza ungewakuta pamoja. Vijana wadogo ambao walikuwa na ndoto za kufanya makubwa, hiyo ilisababishwa na maisha ambayo wao walitokea, hawakuwahi kuyapenda hata siku moja ndiyo maana walipanga kuja kuleta utofauti kwenye familia zao japo wanaume hao walikuwa wakipishana kwenye suala zima la mitazamo hususani njia za kuzitumia kuyafikia maisha ya ndoto zao japo walikubaliana kwamba kwa namna yoyote ile wasingeweza kuja kutupana abadani hivyo kila mmoja alitakiwa kuwa na mwenzake bega kwa bega kuyatafuta maisha.
Walitokea kwenye zile familia za kimaskini sana hivyo njia pekee ya wao kuzifikia ndoto zao ulikuwa ni mstari mwembamba wa elimu, waliamini kwamba elimu ndicho kilikuwa kitu cha pekee cha kuwafikisha kule ambako walihitaji kufika hivyo walifanya yote lakini hawakuwahi kuiacha elimu hata siku moja. Hali hiyo iliwafanya kusoma kwa nguvu kubwa isivyo kawaida, walisoma sana mpaka wakafanikiwa kuondoka Kigoma na kusafiri kwa sababu ya elimu, mabwana hao wawili hawakuwahi kuachana baada ya hapo.
Mmoja alikuwa na akili zaidi darasani lakini mmoja alimzidi mwenzake maarifa ya mtaani hivyo kwa kuyajumlisha pamoja walijikuta wanatengeneza kitu kimoja kikubwa ambacho kiliwafanya wasione kizuizi chochote kwenye kuzipigania hizo ndoto zao. Walifanikiwa kuingia ndani ya jiji la Dar es salaam wakiwa wanapambania elimu yao ambapo mmoja alitamani kuwa mwanasiasa mkubwa na mmoja alipenda kufanya kazi ya kizalendo kulitumikia jeshi kwa ajili ya kuhakikisha anailinda amani ya taifa lake.

Sehemu ya arobaini na nne inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO
SONGA NAYO................

Wakiwa wanasomea elimu ya juu mmoja aliamua kuingia rasmi kwenye siasa na mmoja akajiingiza jeshini. Msomi alifanikiwa kwenda kusoma mpaka nje ya chi na yule wa jeshi baada ya kumaliza elimu yake ya juu aliingia huko na kwa sababu alikuwa na elimu kubwa ilimsaidia kumbeba mpaka kufika mbali. Mwenzake baada ya kurudi kutoka masomoni alipata kazi kama mwanasiasa ambapo kadri muda ulivyokuwa unazidi kwenda alizidi kula vitengo na baada ya kufikisha karibia nusu ya ndoto zake alifanikiwa kumuingiza mwenzake ndani shirika la kijasusi la nchi na baada ya kuwa waziri mkuu na ndiye alimsaidia pakubwa kuhakikisha anafahamika kwa wakubwa jambo ambalo lilimpa msaasa mkubwa mno kiasi kwamba akaishia kuja kuwa ndiye mkurugenzi mkuu wa shirika la kijasusi la taifa.

Huyo mtu ambaye alisaidiwa alikuwa ni othman Micho mwenyewe na yule mtu ambaye alimsaidia yeye alikuwa ni Mr Hassan ambaye ndiye alikuwa babu yake Gavin. Huyo ndiye mwanaume ambaye yeye alikuwa amejitoa siku hiyo kwenda kukutana naye baada ya kutambua siri ambayo waziri mkuu aliishi nayo kwenye moyo wake bila hata kumwambia rafiki yake wa karibu, alijisikia vibaya sana bwana othman kwa hilo ila hakuwa na namna alitakiwa kukutana naye kwanza kwa sababu walikuwa na mengi ambayo walitakiwa kuyaongea pamoja.
Mawazo yake yalikatika baada ya kugundua kwamba walikuwa wamefika kule ambako walikuwa wanaenda kwa sababu gari ilikuwa imesimama kwa dakika kumi na hata mlinzi ambaye alikuwa anamuamsha hakumsikia kabisa hivyo walimuacha amalizane na mawazo yake ambapo wakati anashtuka aligundua kwamba alikuwa ametolewa kile kitambaa ni yeye tu ndiye alikuwa ameyafumba macho yake. Alishuka kwenye hiyo gari akiwa anaangaza kujua eneo ambalo alikuwepo, alitabasamu baada ya kugundua kwamba alikuwa ndani ya uwanja mkubwa ambao ulizungushiwa fensi nzito. Lilikuwa ni jumba la kifahari mno mbele yake ambalo alikuwa akitazamana nalo.

Mlinzi mmoja alihitaji kiongozi huyo amfuate kwani alikuwa akisubiriwa na mwenyeji wake, baada ya kuzunguka mpaka nyuma ya jumba hilo waliingia sehemu moja ambayo ilikuwa ya kisasa na huko ndani kulikuwa na bwawa la kuogelea ambalo lilijengwa ndani ya nyumba sehemu kubwa tu. Alimuona mwanaume mmoja akiwa amevaa nguo za kutumia kuogelea akiwa na miwani yake usoni, alitabasamu kwa sababu alikuwa ni yule swahiba wake wa kitambo hicho, mwanaume ambaye waliyapanga maisha pamoja lakini ndiye ambaye alimsaidia yeye mpaka kutimiza ndoto zake kubwa na huenda kama sio yeye bado yeye angeishia kuwa mwanajeshi wa kawaida tu.
“Unazeeka vibaya sana kaka” mkurugenzi alitamka huku akicheka na kwenda kumkumbatia mwanaume huyo ambaye umri wake kidogo ulikuwa umeenda, alikuwa ni mtu mnene ambaye bila shaka maisha safi yalikuwa upande wake, hakuwa na papara na maisha yake kabisa.
“Sikutegemea kama tungekutana wakati kama huu Othman, ni muda mrefu umepita, bila shaka maisha ya jiji na hiyo nafasi yako yanakupendeza isivyokuwa kawaida” Othman alitabsaamu akiwa anabadilisha nguo zake kwa sababu lengo la kwenda huko kwenye bwawa ilikuwa ni kukumbushia yale maisha yao ya enzi zile wakiwa wanaogelea ndani ya ziwa Tanganyika. Marafiki wawili wa muda mrefu wakikutana huwa wanakumbushia maisha yao ambayo yamepita kuna muda kumbukumbu ndizo ambazo huwa zinaleta matukio bora ya maisha ambayo watu wanayapitia. Kila mmoja alifurahi kumuona mwenzie lakini kila mmoja alijua huenda mazungumzo yao yasiishe vizuri kwa sababu mmoja alikuwa hapo kwa ajili ya kulilinda taifa lake na kupata uhakika kama ambacho aliambiwa ni cha kweli au la! Lakini mwingine alikuwa hapo kwa ajili ya kuilinda familia yake kwa gharama yoyote ile.

“Maisha yanaenda kasi sana kaka, japo nilijisikia vibaya kwa jinsi ulivyo ondoka. Baada ya yale matukio kutokea hukutaka hata kuniona tena, hukutaka hata nije kuhudhuria msiba wa Glady ikafika hatua ukanificha kuhusu kifo chake. Nilijisikia vibaya sana”
“Othaman kwenye haya maisha wanaume tunaishi kwa sababu kubwa moja tu, familia. Mambo yote ambayo unaona tunayafanya, mipango yote thabiti ya maisha ambayo tunayo lengo kubwa ni kwa ajili ya kuhakikisha familia zetu zinaishi vizuri na kuhakikisha haziteseki kama ambavyo sisi tuliteseka miaka ile kwa sababu umaskini ni kitu kibaya sana ndugu yangu. Ukiona mwanaume anaukimbia hata uhalisia wake basi ujue kabisa kwamba nyuma yake sababu kubwa kama hajafanya uhalifu wa kuhatarisha maisha yake ni kwa ajili ya familia yake na ndicho ambacho mimi nilikifanya”

“Kumbuka tulikotoka mimi na wewe, hata kama ulifanya kwa ajili ya familia, nilipaswa kujua angalau hata ungeniaga kwa heshima mimi sio wa kuniachia barua Hassan”
“Nafasi yako uliyo nayo na kazi yako hairuhusu mimi na wewe kukaa meza moja Othman na unajua hilo. Sikutaka siku moja ije ifike mimi naanza kutafutana na wewe na kutishiana maisha ndiyo maana nilihitaji kukaa mbali na wewe kwenye maisha yangu yote. Najua unaelewa kwamba mimi siku zote ni mtu ambaye huwa naishi kwenye maneno yangu, kama ni hivyo kwenye haya maisha tulifanya makubaliano ya kuja kukutana mara moja tu na baada ya hapo hautakuja kunipata tena. Nina uhakika haujaja hapa kunipa salamu au kwa sababu unanikumbuka sana, nambie ni kipi kimekuleta hapa Othman” mzee huyo aliamua kunyoosha maelezo baada ya kuona kama mwenzake anasita kumuuliza kile ambacho kilimpeleka hilo eneo.

“Upo sahihi kabisa na siwezi kukuficha kwenye hilo, mpaka nimekubali kuonana na wewe kwa mara ya mwisho basi ni jambo ambalo lipo nje ya uwezo wangu na huenda nakuhitaji wewe ili niweze kulimaliza ama kujua ni wapi natakiwa kuanzia”
“Nakusikiliza”
“Umajua Gavin Luca?”
“Ni swali la mtego au?”
“Nimekuuliza swali rahisi sana kaka”
“Ndiyo”
“Unamfahamuje?”
“Ni jina maarufu kila kona ya mitandao na sidhani kama ni mimi tu ndiye namfahamu, kila mtanzania ana hilo jina”
“Hakuna mahusiano yako mengine na Gavin?”
“Kama yapi labda?”
“Damu”
“Othman naona kama unazunguka sana, unataka nini kwangu?”
“Hayo maswali ambayo nakuuliza ndiyo yanaweza kuwa na majibu ya kitu ninacho kitaka”
“Okay, nambie hicho unacho kiwaza kwenye akili yako”
“Miaka kadhaa nyuma hili jina lilianza kutokeza kwenye rada za shirika letu lakini tukazuiwa kabisa kulifuatilia kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi. Kabla ya mimi kuingia hapa shirika lilikuwa na taswira mbaya kwa jamii hivyo walitumia sababu ya kumuua mfanya biashara yule wa madawa ya kulevya bwana Lucas Antony wakaja kuunganisha na uhusika wa shirika hili ambapo lilipata kidogo imani kutoka kwa wananchi baada ya propaganda za muda mrefu za kumchafua bwana yule”
“Ubaya ni kwamba kwenye tukio hilo halikuyabeba maisha yake tu bali maisha ya watu wengi ambao wangine walionekana kutokuwa na hatia lakini haikuondoa ukweli kwamba nao walikuwa wamekufa. Jina lile lilisumbua ila kesi ilitua kwenye mikono ya mkuu wa majeshi ambaye alidai kwamba angeimaliza haraka iwezekanavyo. Ilitoka taarifa kwamba mhalifu Gavin ameweza kuuawa lakini baadae tena zikaja taarifa kwamba bwana huyo alikuwa mzima wa afya kabisa hakufa kama taarifa za mwanzo zilivyotoka”
“Kuishi kwake ukawa mwanzo wa mambo ambayo nina uhakika hata wewe unajua kwamba yanatokea ndani ya taifa hili mpaka sasa na huenda wewe ndiye mtu wa pekee ambaye unaweza kuzuia haya yote kwa sababu sio salama kwa taifa letu” maelezo ya Othman mheshimiwa yule aliyasikia vizuri akiwa ameketi kwa umakini mkononi mwake akiwa na Cigar kibosile huyo wa kitambo.
“Mimi nawezaje kukusaidia mtu ambaye una kila aina ya rasilimali kwenye kupambana na mtu kama huyo?”
“Najua kila kitu kuhusu wewe na Gavin Hassan, hauna haja ya kuendelea kuigiza”
“Unazungumzia kuhusu nini labda?”
“Najua kwamba huyu ni mjukuu wako, naelewa kwamba huyu ni mtoto wa damu wa Glady hivyo naomba msaada wako tafadhali” mzee huyo alivuta moshi mwingi na kuuachia nje kisha akakohoa kidogo kuusikilizia kwa namna ulivyokuwa umepenya kwa umaridadi mkubwa.
“Sijajua aliyekupatia hizi taarifa kwamba mimi ndiye babu wa huyo mtoto lakini hizi habari sina taarifa nazo na sio za kweli”
“Comon Hassan, huwezi kunikataa mimi namna hiyo”
“Kama ningekuwa nafahamu ningekwambia Othman, kama ni hilo tu ambalo limekuleta hapa nadhani tumemaliza na unaweza kwenda” mzee huyo aliongea huku akisimama ili aanze kuondoka eneo hilo.
“Kama huwezi kunisaidia kumpata basi jua kwamba watamuua” hiyo ndiyo kauli ambayo ilimfanya mzee huyo kusimama, aliuma meno kwa hasira kali akageuka kurudi pale ambapo alikuwepo rafiki yake wa zamani.
“Naona saivi umeanza kujiona mkubwa sana kiasi kwamba unakuja kunitisha Othman, vipi ni hicho cheo ndicho kinakupa jeuri ya kuhisi unaweza kuja kunitishia hapa?”
“Ameua waziri wa mambo ya ndani, amemuua makamu wa raisi wa zamani, amemuua mtoto wa watu huko Zanzibar, jaji mkuu wa zamani amekufa naye tunahisi anahusika, kwa sasa ametoka Afrika ya kusini ambako ameua watu usiku wa jana na kesi inaendelea huko kiasi kwamba ninaweza kuvujisha taarifa zake akaanza kutafutwa. Nakuja hapa kukuomba msaada ambao utamsaidia hata yeye unaona kama mimi nakutisha Hassan?”

“Labda nikuulize swali, hawa watu ambao unaonekana kuwa na uchungu nao sana naweza kujua kwamba ni akina nani kwako? Unaonekana umekosa kabisa utulivu kwa habari za watu hao, una jazba kali, wamekupa nini Othman. Taifa limejaa matapeli ambao wewe unawalinda, Ikulu raisi kila siku anaingiza mahawara wake mle ndio wanaenda kukalia viti ambavyo vinatakiwa kutumika kujadilia mipango ya baadae ya taifa hili na upo tu hujawahi kukemea hata siku moja. Taifa kila siku linazalisha mafisadi upo upo tu kuwasifia viongozi wako leo vifo vya hao watu ndo vinakutoa jasho namna hiyo? Unaweza ukaniambia ni lini wamekununua wewe na shingapi wanakulipa?” aliongea kwa jazba mzee huyo, hakuna mwanaume duniani ambaye huwa anakubali mtu aitishie familia yake, hiyo inakuwa ni kesi nyingine ambayo ni nzito mno.
“Usinikosee heshima Hassan, mimi sio mtu wa kununulika kama unavyo taka kujiaminisha hapa, nimekuja hapa kwa wema”
“Kwa wema ndo umekuja kunitisha?”
“Sioni kama kuna mahali nimekutisha”
“Othman mtu wa mwisho kuongea kauli ya kitisho kuhusu familia yangu nakumbuka nilimuua siku ile ile kwahiyo tafadhali usije ukanifanya nikaishia kuwa muuaji kwa mtu ambaye nilimchukulia kama ndugu wa damu”

Sehemu ya arobaini na tano inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA
SONGA NAYO................


“Kwahiyo umekubali kwamba Gavin ni mjukuu wako wa damu”
“Yes, ni mjukuu wangu vipi una tatizo juu ya hilo?”
“Kwanini umenifanyia hivi ndugu yangu kwa sababu taarifa hii nilitakiwa kuipata kwenye kinywa chako na sio kuzipata kwa watu wengine”
“Ulitaka kuzipata hizi taarifa halafu uzifanyie nini Othman? Uanze kumuwinda mjukuu wangu naye umuue kama mlivyo sababisha wazazi wake kufa? Hivi unaelewa kwamba nilimpoteza mwanangu, mkwe wangu na mjukuu wangu mmoja? Hivi unaelewa kwamba Gavin ndiye pekee ambaye nimebaki naye kama familia? Jitahidi sana usije ukanitisha tena kuhusu mjukuu wangu kwa sababu nitakuua”

“Hassan naelewa jinsi unavyo jisikia ndiyo maana nipo hapa, nataka kutoa msaada ili asije kuishia kufa kama wengine” mzee huyo alimwangalia mkurugenzi akatabasamu kwa uchungu na kumsogelea pale ambapo alikuwepo.
“Umesema umekuja hapa kuhitaji uonane na Gavin ili umzuie, saivi unadai unataka kumsaidia. Othman nisikilize kwa umakini kwanza unatakiwa uelewe kwamba mimi niliamua kupotea kwenye macho ya watu kwa ajili ya familia yangu, lakini pia nilifanya hili kwa ajili ya kuwalinda baadhi ya watu kama wewe, kama ningeendelea kuishi uraiani mtu kama wewe ungekuwa umekufa ndugu yangu. Wewe hauna haja ya kumtafuta Gavin, kama itafika siku atakuwa na umuhimu wa kukutafuta wewe basi atakuja mwenyewe halafu uje uongee haya maneno ambayo unaniongelea hapa. Gavin hujawahi kukutana naye ndiyo maana hapa unajisifia kwamba unataka kutoa msaada ila kama ungekuwa umekutana naye basi ungegudua kwamba wewe ndiye unaye uhitaji msaada kutoka kwake”

“Othman maisha yanabadilika na mambo yanaenda mbio kila siku, maisha yanabadilika na watu wanabadilika, naomba isije ikafika siku mimi nikaanza kumtafuta rafiki yangu wa damu kwa ajili ya kumuua. Nampenda mjukuu wangu kuliko kitu chochote kile kwenye maisha yangu lakini haiwezi kuwa sababu ya kumzuia yeye kulipa kisasi kwa wale wote ambao waliharibu maisha ya familia yake yote. Kwa ushauri wangu kama rafiki kwako nakusihi kaa naye mbali kwa sababu siku unakutana naye nina imani sitakuwa karibu kwa ajili ya kukulinda, serikali mlishindwa kutenda haki hivyo muache afanye kazi yake akimaliza ataondoka mwenyewe kwa sababu hana shida na mtu mwingine yeyote zaidi ya hao watu wake ambao anawatafuta”
“Unategemea kama mkurugenzi natakiwa kukaa pembeni na kuangalia haya mambo ambayo yanaharibu amani ya nchi yatokee tu halafu niwe kama vile sioni lolote?”
“Kama ndiyo njia sahihi kwanini usifanye hivyo Othman?”
“Wote tunajua kwamba hilo haliwezekani Hassan”
“Basi kafanye kile ambacho unakitaka wewe kwa sababu nina imani huu ndio mwisho wetu kuweza kuonana dear old friend”
“Nina maswali mawili kwako Hassan kabla sijaondoka”
“Nakusikiliza”
“Hawa vijana wake ambao anawatumia kufanya mauaji aliwapata wapi?”
“Hilo swali lihifadhi ili uje umuulize siku ambayo utafanikiwa kukutana naye”
“Swali la pili, anazikuta wapi pesa za kufanya mambo yote haya? Kumiliki watu na kuendesha shughuli kama hizi zinamtaka mtu ambaye ana kipato kikubwa”
“Mhhhhhh Othman acha kuwa mjinga namna hiyo, yule baba yake alikuwa ndiye mtu tajiri zaidi ndani ya bara la Afrika leo unauliza anazitoa wapi pesa?”
“Pesa za baba yake zilidaiwa kupotea karibia zote baada ya kufa, kuna pesa zilidaiwa kuingia kwenye makundi mengine ya wauzaji wa dawa za kulevya na zingine serikali ilizibeba”
“Na wewe uliziamini hizo propaganda?”
“Kwahiyo zile pesa zote zipo kwenye mikono yake?”
“Othaman ulikuwa ni wakati mwema mimi kufahamiana na wewe kwenye haya maisha, nina uhakika hakuna nafasi ya mimi na wewe kuja kukutana tena, jiangalie sana ndugu yangu” mzee huyo aliongea kama utani ila alikuwa amemeliza kikao na kiongozi huyo. Kama ambavyo alitegemea kwamba maongezi yao yasingekuwa na mwisho mwema na ndicho ambacho kilitokea.

Marafiki wawili wa zamani ambao walishibana enzi zao, ambao walikula kiapo kusaidiana kwa namna yoyote yale walikuja kutangaziana uhasama uzeeni mmoja akiyatekeleza majukumu yake lakini mweingine akiwa kwa ajili ya kuilinda familia yake. Wahenga walisema nenda mashariki, nenda magharibi lakini nyumbani ndiyo sehemu bora zaidi. Waliingia wanaume kadhaa humo ndani na kumfunga uso asijue alikuwa wapi, walimuongoza mpaka kwenye gari kisha wakatoweka naye kumrudisha kule ambako walikuwa wamemtoa.



*****
Majasusi wa TIGI walibaki wenyewe baada ya kuiongozi wao kuweza kuondoka kwenda kukutana na rafiki yake wa zamani hivyo ikawalazimu kuendea na kikao wenyewe ili kuweza kujua hatua ambazo walitakiwa kwenda nazo kwenye harakati za kumtafuta Gavin kwani walikuwa wamepata taarifa mpya kutoka kwa mwenzao Dayana ambaye muda aliokuwa amewekwa pembeni hakuutumia kufanya mambo ya ajabu bali kufanya utafiti juu ya mtu ambaye walikuwa wanamtafuta kwa wakati huo.
“Kwahiyo tunaanzia wapi kuwatafuta watu hawa?” Tigana aliuliza akiwa kama mtu ambaye alikuwa anaelekea kukata tamaa.
“Bariki anatakiwa kwenda kwa yule mama yake mlezi kwa sababu anajulikana ni wapi anaishi lakini kuwa makini usije ukafanya jambo lolote la ajabu ukiwa huko”
“Roger that”
“Kwa wengine ambao tunabaki tuna kazi moja kubwa, kwa sababu hawa watu wake hatuna uwezo wa kuwapata maana yake tunatakiwa kutumia plan B”
“Ambayo ni ipi?”
“Mnakumbuka kwamba tulishindwa kupata mwendelezo wa vifo vya hawa watu wote ambao mlikuwa mnawachunguza?”
“Ndiyo”
“Majibu yetu yapo kwa hawa watu”
“Kivipi?”
“Huyu tu anaenda nao kwa hatua, maana yake kuna orodha ya majina ambayo anayo na ndiyo anaitumia kwenda nao kuwateketeza hawa watu hivyo hata sisi tunatakiwa kuipata hiyo orodha angalau ya mtu hata mmoja ambaye atafuatia kwa kuamini kwamba tunaweza kukutana naye eneo la tukio tukamkamata. Kutokana na hilo kuwa gumu kwetu sisi binafsi basi inatakiwa Ismail Mhammed apatikane”
“Unamaanisha baba yake na Zara?”
“Ndiyo”
“Naona kabisa hii haitakuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu”
“Kwanini?”
“Kwa sababu yule ni mfiwa na kwa sasa hatakiwi kusumbuliwa jambo ambalo linaweza kumfanya akafungua mashtaka dhidi yetu. Bosi ameenda kukutana na rafiki yake na kama hilo likiwezekana basi anaweza kurudi na taarifa nzuri ambazo zitatusaidia kwenye hili”
“Jaden umewahi kuwa na familia sio?”
“Ndiyo mke na mtoto”
“Unaweza ukakubali kumuuza mtoto wako?”
“Hapana bora nife mimi”
“Sasa bosi ameenda kukutana na mtu ambaye ndiye babu yake na Gavin, una imani kabisa kwamba anaweza kumuuza mjukuu wake tena wa pekee kwa sababu tu ya rafiki yake ambaye walikutana kwenye maisha tu haya?”
“Kwa hili itakuwa ni ngumu”
“Ndiyo maana inatakiwa tumpate Ismail”
“How?”
“Kazi ni yako Slyvanos, wewe ndiye ulienda Zanzibar kwa mara ya kwanza hivyo ni kazi yako kwenda kulimaliza jukumu lako”
“Unamaanisha natakiwa kumteka?”
“Ndiyo njia pekee na hili halitakiwi kulala kwa sababu hatujui ni nani anaenda kufa tena huenda tunavyozidi kuchelewa kuna mtu maisha yake yanaendelea kuingia hatarini”
“Nimekupata bosi lady” Slyvanos baada ya kutamka wote walimgeukia na kumwangalia Dayana kujua atasema nini ila aliishia kucheka tu, walikuwa wakiishi zaidi hata ya familia. Wengine ambao walibakia walipewa majukumu ya kutembelea sehemu za mhimu ndani ya jiji kwa ajili ya kusaka taarifa juu ya bwana huyo ambaye alikuwa ni adimu zaidi ya pesa muda wa masika huku wakisubiri taarifa kutoka kwa bosi wao kama kuna jambo angekuwa amelifanikisha.


Baada ya kumaliza kikao hicho kifupi, Tigana alimsogelea Dayana na kuhitaji waongee pembeni wawili tu kwa sababu alikuwa na mambo binafsi ya kuongea naye.
“Nakuheshimu sana kama kiongozi wangu lakini kwenye hili jambo nina mtazamo tofauti kabisa na wengine”
“Unamaanisha nini Tigan?”
“Hili taifa limejaa ushenzi kwa muda mrefu sasa, viongozi hawajali kwa lolote ambalo linetokea wanajaza matumbo yao tu na muda wote wanakomaa kuwadanganya raia kwanini anapotokea mtu mmoja kama huyu anahitaji kuwapunguza wapuuzi kama hawa tena ambao wanaonekana walimfanyia ushenzi kwanini itumike nguvu kubwa namna hii kumtafuta?”
“Tigan sisi tunafuata amri na sheria inavyotaka tufanye”
“Unazungumzia sheria ya kuwalinda mafisadi? Dayana ebu lifikirie hili jambo kwa umakini”
“Tigana hivi ukikuta kwamba hata raisi anahusika kwa hili utafanya nini? Kwamba utampeleka mahakamani? Utaenda kumshtaki raisi wa nchi?”
Sehemu ya arobaini na sita inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
SONGA NAYO................

“Sina maana hiyo”
“Ila”
“Gavina anaweza kuwa anatumia njia ambayo sio sahihi lakini binafsi nahisi anafanya kitu sahihi kwa maslahi ya wengi ambao hawawezi kufanya”
“Kwahiyo unataka tumwangalie afanye hiki anacho kifanya?”
“Dayana Comon, taifa linawahitaji watu kama hawa”
“Mbona umekuwa mlaini siku hizi Tigan nini kinaendelea kwako?”
“Nisikilize vizuri, huyu mtu inatumika nguvu kubwa kumpoteza kwa sababu anayagusa moja kwa moja maslahi ya watu fulani. Hili sio jambo la kuwa na ulaini ila ni kufanya kile ambacho ni sahihi”
“Unalijua jukumu lako ambalo lilikufanya ukala kiapo?”
“Ndiyo”
“Ni lipi?”
“Kuilinda nchi yangu pamoja na raia wake kwa gharama yoyote ile hata kuyatoa sadaka maisha yangu, amani ndiyo inapaswa kuwa kipaumbele namba moja”
“Kwa haya ambayo yanaendelea unaona yanaleta amani?”
“Hapana”
“Kwa sababu hiyo tunakubaliana kwamba Gavin anatakiwa kupatikana kwa gharama yoyote ile hivyo sitategemea kupata mawazo ya namna yako tena na kwa sasa huo mjadala unatakiwa kufa. Gavin lazima apatikane, awe amekufa au yupo hai, haiwezekani kila siku watu wakose amani kwa sababu ya kufanya mauaji ya hadharani. Japo inadaiwa kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kupigana naye ila nina uhakika hatakuwa na uwezo wa kuikimbia risasi hata kama atakuwa na uwezo wa ajabu namna gani na kama italazimu tufike huko basi nitamuua mimi mwenyewe kwa mkono wangu”
Dayana aliongea kwa msisitizo kuonyesha kwamba alikuwa anamaanisha kile alichokuwa anakizungumza, Tigana hakuongeza neno tena japo aliona kabisa bwana huyo alichokuwa anakifanya alikuwa sahihi ila ni wao ambao walikuwa wakijaribu kumfanaya aonekane ni mkosaji ama anafanya kitu kibaya.



*********
THE ERA OF GAVIN LucA
Wakati dunia inalalamika kukutana na mambo ya kutisha hususani ndani ya taifa la Tanzania, kwenye chumba kimoja alionekana mwanaume mmoja akiwa ameyafumba macho yake akiwa anafanya sala. Alikuwa amekaa chini ya zulia moja safi kwenye chumba ambacho kilikuwa kitupu zaidi ya kuzungukwa na silaha za kutosha ukutani, alitumia nusu saa nzima akiwa amefumba macho yake, alipokuja kuyafumbua yalikuwa mekundu na katikati ya mboni zake moto ulikuwa unawaka. Alikuwa anauangalia mshumaa ambao ulikuwa mbele yake mithili ya mtu ambaye alikuwa anafanya tahajudi na baada ya muda mfupi macho yalirudi kwenye hali yake.

Mwanaume yule alikuwa ni Gavin Luca mwenyewe ndiye ambaye alikuwa kwenye hicho chumba, kwenye mwili wake alikuwa amevaa suruali nyepesi tu na kujifunga kitambaa kichwani, sehemu zingine za mwili zilikuwa wazi kabisa bila kufunikwa na kitu chochote kile. Baada ya kukamilisha salamu yake alisimama, mwili ulikuwa unavutia kuuangalia lakini ulikuwa unatisha kama ni mtu ambaye ungeingia naye kwenye matatizo kwa namna ulivyokuwa umejigawa kwenye mapande mapande. Mwili haukuwa mkubwa sana ila ulijengwa vyema na mhusika, ulipangiliwa kiasi kwamba ukawa ni wa kuvutia.
Baada ya kusimama alisogea kwenye ukuta na kufungua kisanduku kidogo ambapo alitoa sarafu moja ya shilingi na kuirusha juu, aliidaka na kuirushia ukutani sehemu ambayo ilikuwa na kitufe cha kubonyeza. Shilingi iligonga sehemu ile milango ikafunguka, kwenye vile vyumba vidogo zilikuwa zinahifadhiwa roboti ambazo yeye alikuwa anazitumia kufanyia mazoezi. Zilitoka zikiwa na mapanga kwenye mikono ya chuma na kuanza kumshambulia kwa nguvu Gavin, alirudi nyuma na kuzunguka hewani na kuzifanya zipishane.

Zilikuwa zinamjia kwa kasi mno kwa sababu zenyewe zilikuwa zikitumia umeme yeye damu ila alionekana kuwa na kasi zaidi hata ya zile roboti, aliona kwa jicho lake upanga ukiwa unakuja kwenye shingo yake, aliizungushia pembeni na kujivuta, aliituma ngumi yake iliyotua kwenye moyo wa chuma wa roboti moja likapelekewa mbali huku lingine likiwa linakuja kwa kuzunguka kila sehemu ili kumshambulia, mwanaume huyo alibendi mpaka chini kisha alinyanyuka kwa nguvu za ajabu kama anataka kupaa juu, alijigeuza hewani na kuzungusha mguu wake uliokuwa peku, ulitua kwenye kichwa cha lile roboti mpaka kikameguka wakati ule alitua karibu kabisa na ukuta, aligusa kwa kidole ukutani pakafunguka, aliutoa upanga mmoja kwa nguvu kutoka kwenye ala yake.

Hakutazama nyuma bali aliutuma ule upanga bila hata kuangalia, wakati anautuma yeye mwenyewe alikuwa anaujia kwa nguvu, ulikita kwenye tumbo la roboti na kuzama kidogo wakati roboti lile linahangaika kuutoa alikuwa amelifikia ambapo alilitwisha ngumi nyingi za kifua mpaka likadondoka chini na kuzima kama limeisha chaji. Lile moja lilisogea kwa nguvu alipokuwepo Gavin, alisikika akipiga kelele ambapo aliikunja ngumi yake macho yake yakiwa kama yanawaka moto, alipoikutanisha ngumi hiyo kwenye mwili wa wa chuma wa lile roboto, lilimeguka vipande vipande yeye akibaki anahema na jasho linamtoka mwilini. Alionekana kuwa na nguvu za ziada kwenye mwili wake, hazikuwa salama sana kwa wanadamu wa kawaida.

Alitikisa kichwa chake kwa masikitiko kwa sababu alitakiwa kuzitumia nguvu hizo kwa ajili ya kuulia watu, ni jambo ambalo hakulipenda lakini kwa wakati huo hakuwa na chaguo lingine. Akiwa amesimama hapo kuyaangalia yale maroboti ambapo moja lilikuwa chini na lingine lilimeguka, ulifunguka mlango mmoja mkubwa wa kioo humo ndani akaingia mwanaume mmoja ambaye alionekana mara ya mwisho Kariakoo akifanya mambo ya kutisha, Othman chunga ndiye alipenya humo ndani.
“Boss mama anahitaji kuonana na wewe” Othman aliongea akiwa na tablet lake mkononi huku mwilini akiwa amevaa vesti tu pekee.
“Yuko wapi?”
“Kwenye chumba cha picha” hakumjibu tena Othman zaidi ya kutoka humo ndani akimuacha Othman anayaweka sawa yale maroboti.

Mwanaume alienda kuoga kisha akavaa nguo safi na kwenda moja kwa moja kwenye eneo ambalo alikuwa ameagizwa. Ndani ya eneo hilo alionekana yule mwanamama Bi Aisha waweza kumuita Aurelia, ndiye yule kanali wa zamani wa jeshi, mwanamama huyo macho yake yalikuwa ukutani. Ndani ya chumba hicho walikuwa wanaruhusiwa kuingia wao wawili tu basi kwa sababu ilikuwa ni sehemu ya kuhifadhia picha za familia ambazo zilibandikwa kila kona ya ukuta na kujengewa vizuri.
“Nakumbuka ukiwa mdogo ulikuwa msumbufu lakini tabasamu lako lilikuwa likimvutia kila mtu, kwa mwonekano tu ulionekana kabisa umeandikiwa kuja kufanya makubwa kwenye huu ulimwengu. Siku ambayo ulitakiwa kwenda mbali na mimi nilijisikia vibaya sana kwa sababu wewe na Adam mlikuwa kama mapacha kwangu, mlikuwa kila kitu ambacho niliomba kuwa nacho kwenye haya maisha na jambo ambalo lilinipa furaha zaidi ni baba yako na mama yako kuniamini mimi kuwa mama kwako, hilo ndilo jambo bora zaidi kuwahi kunitokea kwenye maisha yangu” mama huyo aliongea akiwa anazigusa picha za watoto wawili wadogo huku akimwaga machozi.

“Ukiwa mama moyo wako wote unakuwa kwa watoto wako, kama mtoto wako akipata shida yoyote hata ndogo hata chakula huwezi kula wala kufanya jambo lolote la maana, watoto wanaibeba sehemu kubwa ya moyo wako ndiyo maana huwa unaona mama yeyote hata kama mtoto wake ni mwizi au ana tabia mbaya za kuwa chukizo kwa watu wengine lakini mama yake hawezi kumchoka, atampenda mwanae kama ambavyo anawapenda wanae wengine. Nakumbuka siku moja wakati unanyonya na mwenzako, ulikuja ukatulia ghafla kiasi kwamba ukawa hauhemi vizuri, ile ndiyo siku ambayo moyo wangu uliniuma na kunifanya nilie kama mtoto, nilihisi nimekupoteza kwenye maisha yangu”

“Ukiacha mawazo ambayo nilikuwa nayo juu ya nini nitawaambia wazazi wako juu ya lile jambo ila mimi mwenyewe kwenye moyo wangu nilitamani hata kujiua kama ningekupoteza, niliwapenda na kuwazoea wote wawili ndiyo maana hata baada ya kuondoka kwenye mikono yangu bado ni mimi pekee ambaye niliruhusiwa kuja popote ulipo duniani kwa sababu ulikuwa ukihitaji upendo wa mama. Kwa bahati iliyokuwa nzuri daktari wa familia alikuwa karibu, alikushtua baada ya dakika kumi ukaanza kulia, kile kilio kilinifanya na mimi nilie kwa furaha, kuna vilio vingine vya watoto huwa ni furaha kwa mzazi kwa sababu anakuwa na uhakika kwamba mwanae yupo salama kabisa”

“Tangu wazazi wako wakukabidhi kwangu mpaka leo binafsi huwa najua nina watoto mapacha, mwenzako kwa sasa hayupo lakini namshukuru Mungu kwa uwepo wako wewe kwa sababu bado najihisi nimekamilika kwa kila kitu. Naelewa namna mama yako alivyo pitia kipindi kigumu kwenye maisha yake baada ya baba yako kumwambia ukweli kwamba wewe ulitakiwa kulelewa na mwanamke mwingine, mama yako alikuwa mtu wa kilio kila nilipokuwa namuona, kama nilivyokwambia hakuna kitu kinamuumiza mama kama kumuona mwanae yupo kwenye matatizo au anawekwa naye mbali, kila mama anahitaji kuwa na mwanae au wanae karibu wawe wanamsumbua, vile kila muda wanavyo mwita mama, mama huwa inaleta msisimko mkubwa moyoni japo machoni anaweza kuonyesha ukawaida tu”

“Kutokana na ile hali ilifanya mimi na mama yako tukawa marafiki wakubwa, tulishibana na kuna muda nilikuwa nakupeleka kwake kwa siri ili tu atumie muda wa pamoja na wewe kwa sababu nilikuwa najua jinsi ambavyo alikuwa akijisikia kuishi mbali na wewe. Mama yako alikuwa akiwapenda mno, siku zote akikubeba kwenye mikono yake ungemkuta anaimba nyimbo nzuri za zamani, muda wote ulikuwa ukicheka na kufurahi. Alikuwa anawaweka pamoja wewe na kaka yako ambaye Mungu alimbeba, mlikuwa mnafanana kwa kila kitu na kama sio kuwekwa mbali basi nina uhakika hata yeye angepata taabu kubwa kuwatofautisha. Mlikuwa mkifanana mpaka matendo yenu ambayo mlikuwa mnayafanya, ile ilikuwa ni zawadi kubwa ambayo Mungu aliipatia familia hali ambayo ilitufanya tuishi kwa furaha kubwa kwa sababu kila kitu kilikuwepo”

“Kama ambavyo ulimwengu unajieleza mwanangu, dunia kuna wakati sio sehemu salama sana kwa ajili ya kuishi, dunia imekuwa sehemu hatari zaidi kwa maisha ya binadamu. Ile furaha ndani ya muda mfupi iligeuzwa kuwa karaha ambayo imeacha vidonda vikali kweye maisha yetu. Wale watu hawakujali tena kuhusu furaha ya ile familia, hawakujali lolote juu ya majeraha ambayo wangeyaacha kwa baadhi wa wanadamu wakaamua kuyafanya yale ambayo walihisi wanaweza kuyafanya wakiwa na nguvu. Leo hawa wapendwa wetu tunaishia kuwaangalia kwenye picha badala ya kukaa nao sehemu moja kufurahi, nazikumbuka zile nyakati zangu za upendo, nayakumbuka mapenzi ya zile familia huwa naishia kutoa machozi”

Sehemu ya arobaini na saba inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
Unamalizia kwa 2500 tu nakupa ilipo ishia mpaka mwisho...

WhatsApp au kawaida

0621567672
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
SONGA NAYO................

“Sina maana hiyo”
“Ila”
“Gavina anaweza kuwa anatumia njia ambayo sio sahihi lakini binafsi nahisi anafanya kitu sahihi kwa maslahi ya wengi ambao hawawezi kufanya”
“Kwahiyo unataka tumwangalie afanye hiki anacho kifanya?”
“Dayana Comon, taifa linawahitaji watu kama hawa”
“Mbona umekuwa mlaini siku hizi Tigan nini kinaendelea kwako?”
“Nisikilize vizuri, huyu mtu inatumika nguvu kubwa kumpoteza kwa sababu anayagusa moja kwa moja maslahi ya watu fulani. Hili sio jambo la kuwa na ulaini ila ni kufanya kile ambacho ni sahihi”
“Unalijua jukumu lako ambalo lilikufanya ukala kiapo?”
“Ndiyo”
“Ni lipi?”
“Kuilinda nchi yangu pamoja na raia wake kwa gharama yoyote ile hata kuyatoa sadaka maisha yangu, amani ndiyo inapaswa kuwa kipaumbele namba moja”
“Kwa haya ambayo yanaendelea unaona yanaleta amani?”
“Hapana”
“Kwa sababu hiyo tunakubaliana kwamba Gavin anatakiwa kupatikana kwa gharama yoyote ile hivyo sitategemea kupata mawazo ya namna yako tena na kwa sasa huo mjadala unatakiwa kufa. Gavin lazima apatikane, awe amekufa au yupo hai, haiwezekani kila siku watu wakose amani kwa sababu ya kufanya mauaji ya hadharani. Japo inadaiwa kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kupigana naye ila nina uhakika hatakuwa na uwezo wa kuikimbia risasi hata kama atakuwa na uwezo wa ajabu namna gani na kama italazimu tufike huko basi nitamuua mimi mwenyewe kwa mkono wangu”
Dayana aliongea kwa msisitizo kuonyesha kwamba alikuwa anamaanisha kile alichokuwa anakizungumza, Tigana hakuongeza neno tena japo aliona kabisa bwana huyo alichokuwa anakifanya alikuwa sahihi ila ni wao ambao walikuwa wakijaribu kumfanaya aonekane ni mkosaji ama anafanya kitu kibaya.



*********
THE ERA OF GAVIN LucA
Wakati dunia inalalamika kukutana na mambo ya kutisha hususani ndani ya taifa la Tanzania, kwenye chumba kimoja alionekana mwanaume mmoja akiwa ameyafumba macho yake akiwa anafanya sala. Alikuwa amekaa chini ya zulia moja safi kwenye chumba ambacho kilikuwa kitupu zaidi ya kuzungukwa na silaha za kutosha ukutani, alitumia nusu saa nzima akiwa amefumba macho yake, alipokuja kuyafumbua yalikuwa mekundu na katikati ya mboni zake moto ulikuwa unawaka. Alikuwa anauangalia mshumaa ambao ulikuwa mbele yake mithili ya mtu ambaye alikuwa anafanya tahajudi na baada ya muda mfupi macho yalirudi kwenye hali yake.

Mwanaume yule alikuwa ni Gavin Luca mwenyewe ndiye ambaye alikuwa kwenye hicho chumba, kwenye mwili wake alikuwa amevaa suruali nyepesi tu na kujifunga kitambaa kichwani, sehemu zingine za mwili zilikuwa wazi kabisa bila kufunikwa na kitu chochote kile. Baada ya kukamilisha salamu yake alisimama, mwili ulikuwa unavutia kuuangalia lakini ulikuwa unatisha kama ni mtu ambaye ungeingia naye kwenye matatizo kwa namna ulivyokuwa umejigawa kwenye mapande mapande. Mwili haukuwa mkubwa sana ila ulijengwa vyema na mhusika, ulipangiliwa kiasi kwamba ukawa ni wa kuvutia.
Baada ya kusimama alisogea kwenye ukuta na kufungua kisanduku kidogo ambapo alitoa sarafu moja ya shilingi na kuirusha juu, aliidaka na kuirushia ukutani sehemu ambayo ilikuwa na kitufe cha kubonyeza. Shilingi iligonga sehemu ile milango ikafunguka, kwenye vile vyumba vidogo zilikuwa zinahifadhiwa roboti ambazo yeye alikuwa anazitumia kufanyia mazoezi. Zilitoka zikiwa na mapanga kwenye mikono ya chuma na kuanza kumshambulia kwa nguvu Gavin, alirudi nyuma na kuzunguka hewani na kuzifanya zipishane.

Zilikuwa zinamjia kwa kasi mno kwa sababu zenyewe zilikuwa zikitumia umeme yeye damu ila alionekana kuwa na kasi zaidi hata ya zile roboti, aliona kwa jicho lake upanga ukiwa unakuja kwenye shingo yake, aliizungushia pembeni na kujivuta, aliituma ngumi yake iliyotua kwenye moyo wa chuma wa roboti moja likapelekewa mbali huku lingine likiwa linakuja kwa kuzunguka kila sehemu ili kumshambulia, mwanaume huyo alibendi mpaka chini kisha alinyanyuka kwa nguvu za ajabu kama anataka kupaa juu, alijigeuza hewani na kuzungusha mguu wake uliokuwa peku, ulitua kwenye kichwa cha lile roboti mpaka kikameguka wakati ule alitua karibu kabisa na ukuta, aligusa kwa kidole ukutani pakafunguka, aliutoa upanga mmoja kwa nguvu kutoka kwenye ala yake.

Hakutazama nyuma bali aliutuma ule upanga bila hata kuangalia, wakati anautuma yeye mwenyewe alikuwa anaujia kwa nguvu, ulikita kwenye tumbo la roboti na kuzama kidogo wakati roboti lile linahangaika kuutoa alikuwa amelifikia ambapo alilitwisha ngumi nyingi za kifua mpaka likadondoka chini na kuzima kama limeisha chaji. Lile moja lilisogea kwa nguvu alipokuwepo Gavin, alisikika akipiga kelele ambapo aliikunja ngumi yake macho yake yakiwa kama yanawaka moto, alipoikutanisha ngumi hiyo kwenye mwili wa wa chuma wa lile roboto, lilimeguka vipande vipande yeye akibaki anahema na jasho linamtoka mwilini. Alionekana kuwa na nguvu za ziada kwenye mwili wake, hazikuwa salama sana kwa wanadamu wa kawaida.

Alitikisa kichwa chake kwa masikitiko kwa sababu alitakiwa kuzitumia nguvu hizo kwa ajili ya kuulia watu, ni jambo ambalo hakulipenda lakini kwa wakati huo hakuwa na chaguo lingine. Akiwa amesimama hapo kuyaangalia yale maroboti ambapo moja lilikuwa chini na lingine lilimeguka, ulifunguka mlango mmoja mkubwa wa kioo humo ndani akaingia mwanaume mmoja ambaye alionekana mara ya mwisho Kariakoo akifanya mambo ya kutisha, Othman chunga ndiye alipenya humo ndani.
“Boss mama anahitaji kuonana na wewe” Othman aliongea akiwa na tablet lake mkononi huku mwilini akiwa amevaa vesti tu pekee.
“Yuko wapi?”
“Kwenye chumba cha picha” hakumjibu tena Othman zaidi ya kutoka humo ndani akimuacha Othman anayaweka sawa yale maroboti.

Mwanaume alienda kuoga kisha akavaa nguo safi na kwenda moja kwa moja kwenye eneo ambalo alikuwa ameagizwa. Ndani ya eneo hilo alionekana yule mwanamama Bi Aisha waweza kumuita Aurelia, ndiye yule kanali wa zamani wa jeshi, mwanamama huyo macho yake yalikuwa ukutani. Ndani ya chumba hicho walikuwa wanaruhusiwa kuingia wao wawili tu basi kwa sababu ilikuwa ni sehemu ya kuhifadhia picha za familia ambazo zilibandikwa kila kona ya ukuta na kujengewa vizuri.
“Nakumbuka ukiwa mdogo ulikuwa msumbufu lakini tabasamu lako lilikuwa likimvutia kila mtu, kwa mwonekano tu ulionekana kabisa umeandikiwa kuja kufanya makubwa kwenye huu ulimwengu. Siku ambayo ulitakiwa kwenda mbali na mimi nilijisikia vibaya sana kwa sababu wewe na Adam mlikuwa kama mapacha kwangu, mlikuwa kila kitu ambacho niliomba kuwa nacho kwenye haya maisha na jambo ambalo lilinipa furaha zaidi ni baba yako na mama yako kuniamini mimi kuwa mama kwako, hilo ndilo jambo bora zaidi kuwahi kunitokea kwenye maisha yangu” mama huyo aliongea akiwa anazigusa picha za watoto wawili wadogo huku akimwaga machozi.

“Ukiwa mama moyo wako wote unakuwa kwa watoto wako, kama mtoto wako akipata shida yoyote hata ndogo hata chakula huwezi kula wala kufanya jambo lolote la maana, watoto wanaibeba sehemu kubwa ya moyo wako ndiyo maana huwa unaona mama yeyote hata kama mtoto wake ni mwizi au ana tabia mbaya za kuwa chukizo kwa watu wengine lakini mama yake hawezi kumchoka, atampenda mwanae kama ambavyo anawapenda wanae wengine. Nakumbuka siku moja wakati unanyonya na mwenzako, ulikuja ukatulia ghafla kiasi kwamba ukawa hauhemi vizuri, ile ndiyo siku ambayo moyo wangu uliniuma na kunifanya nilie kama mtoto, nilihisi nimekupoteza kwenye maisha yangu”

“Ukiacha mawazo ambayo nilikuwa nayo juu ya nini nitawaambia wazazi wako juu ya lile jambo ila mimi mwenyewe kwenye moyo wangu nilitamani hata kujiua kama ningekupoteza, niliwapenda na kuwazoea wote wawili ndiyo maana hata baada ya kuondoka kwenye mikono yangu bado ni mimi pekee ambaye niliruhusiwa kuja popote ulipo duniani kwa sababu ulikuwa ukihitaji upendo wa mama. Kwa bahati iliyokuwa nzuri daktari wa familia alikuwa karibu, alikushtua baada ya dakika kumi ukaanza kulia, kile kilio kilinifanya na mimi nilie kwa furaha, kuna vilio vingine vya watoto huwa ni furaha kwa mzazi kwa sababu anakuwa na uhakika kwamba mwanae yupo salama kabisa”

“Tangu wazazi wako wakukabidhi kwangu mpaka leo binafsi huwa najua nina watoto mapacha, mwenzako kwa sasa hayupo lakini namshukuru Mungu kwa uwepo wako wewe kwa sababu bado najihisi nimekamilika kwa kila kitu. Naelewa namna mama yako alivyo pitia kipindi kigumu kwenye maisha yake baada ya baba yako kumwambia ukweli kwamba wewe ulitakiwa kulelewa na mwanamke mwingine, mama yako alikuwa mtu wa kilio kila nilipokuwa namuona, kama nilivyokwambia hakuna kitu kinamuumiza mama kama kumuona mwanae yupo kwenye matatizo au anawekwa naye mbali, kila mama anahitaji kuwa na mwanae au wanae karibu wawe wanamsumbua, vile kila muda wanavyo mwita mama, mama huwa inaleta msisimko mkubwa moyoni japo machoni anaweza kuonyesha ukawaida tu”

“Kutokana na ile hali ilifanya mimi na mama yako tukawa marafiki wakubwa, tulishibana na kuna muda nilikuwa nakupeleka kwake kwa siri ili tu atumie muda wa pamoja na wewe kwa sababu nilikuwa najua jinsi ambavyo alikuwa akijisikia kuishi mbali na wewe. Mama yako alikuwa akiwapenda mno, siku zote akikubeba kwenye mikono yake ungemkuta anaimba nyimbo nzuri za zamani, muda wote ulikuwa ukicheka na kufurahi. Alikuwa anawaweka pamoja wewe na kaka yako ambaye Mungu alimbeba, mlikuwa mnafanana kwa kila kitu na kama sio kuwekwa mbali basi nina uhakika hata yeye angepata taabu kubwa kuwatofautisha. Mlikuwa mkifanana mpaka matendo yenu ambayo mlikuwa mnayafanya, ile ilikuwa ni zawadi kubwa ambayo Mungu aliipatia familia hali ambayo ilitufanya tuishi kwa furaha kubwa kwa sababu kila kitu kilikuwepo”

“Kama ambavyo ulimwengu unajieleza mwanangu, dunia kuna wakati sio sehemu salama sana kwa ajili ya kuishi, dunia imekuwa sehemu hatari zaidi kwa maisha ya binadamu. Ile furaha ndani ya muda mfupi iligeuzwa kuwa karaha ambayo imeacha vidonda vikali kweye maisha yetu. Wale watu hawakujali tena kuhusu furaha ya ile familia, hawakujali lolote juu ya majeraha ambayo wangeyaacha kwa baadhi wa wanadamu wakaamua kuyafanya yale ambayo walihisi wanaweza kuyafanya wakiwa na nguvu. Leo hawa wapendwa wetu tunaishia kuwaangalia kwenye picha badala ya kukaa nao sehemu moja kufurahi, nazikumbuka zile nyakati zangu za upendo, nayakumbuka mapenzi ya zile familia huwa naishia kutoa machozi”

Sehemu ya arobaini na saba inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
🪑🍜
 
Back
Top Bottom