Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
SONGA NAYO................

“Kuna namna naona inatakiwa tuachane na mawazo ya kumtafuta huyu mtu kwanza bali tujue sababu za msingi ambazo zinamfanya ayafanye haya yote”
“Unahisi ni yeye kafanya haya?”
“Shilingi ndio utambulisho wake inaonekana hivyo ni yeye”
“Ni yeye ambaye alitakiwa kuwa amehusika na mauaji ya jaji mkuu mstaafu, inakuwaje ndani ya usiku mmoja yeye mwenyewe awe afrika ya kusini?”
“Kuhusu jaji mkuu nina uhakika sio yeye”
“Umelijuaje hilo Tigana?”
“Kwa sababu tangu nianze kuona mauaji yake, hakuna sehemu anaruhusu mtu wake ajiue mwenyewe hivyo huyo mama ameuawa na watu wake mwenyewe” kila mtu alimpa umakini Tigana kujua anacho kimaanisha kwa sababu alikuwa na hisia kali mno.
“Unataka kusemaje?”
“Kama ameenda Afrika ya kusini maana yake alihitaji kumjua mtu fulani ambaye huenda angemuongoza mpaka kwa Emilia. Kuna uwezekano mkubwa Emilia anawajua watu kadhaa ambao Gavin anawatafuta hivyo ingekuwa hatari kwao na kuimaliza hatari hiyo wakaamua kumuua ili akirudi amkose”
“Una uhakika na hili?”
“Hisia zangu zinanituma hivyo, kuna mnyororo wa watu wengi wakubwa wanaonekana wanatafutwa na huyu bwana”
“Kwahiyo unashauri nini Tigana?”
“Kwa hili ambalo limetokea maana yake kwa sasa atakuwa kwenye ndege ambayo inatua muda sio mrefu JNIA hivyo tunatakiwa kusimamisha kila kitu tukajaribu bahati yetu kama tunaweza kumpata. Kama tukifanikiwa kumkamata basi huenda haya yatafika mwisho na tutajua sababu ya yeye kuwa hivi kwa wakati huu”
“Are you sure?”
“Hisia zangu zinaniambia hivyo kiongozi” Walikuwa wanamwamini sana Tigana hivyo walipewa amri ya kuwahi mara moja uwanja wa ndege kumkamata Gavin ambaye waliamini wakati huo alikuwa kwenye ndege kurudi Tanzania baada ya kufanya mauaji hayo ya kutisha huko Afrika ya kusini. Je ni kweli alikuwa kwenye ndege na walikuwa wanaweza kumpata Gavin?





**********
SOUTH AFRIcAN AIRWAYS.
Ndiyo ndege ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu na majasusi kutoka ndani ya shirika la kijasusi la TIGI la Tanzania, ndege hiyo ilikuwa imeondoka masaa mawili yaliyokuwa yamepita ndani ya jiji la Jozi wakati wao wanapata taarifa juu ya mauaji ambayo yalifanya ndani ya jiji hilo. Baada ya kuipata taarifa hiyo walighairi kila kitu na kuamua kufanya zoezi la kubahatisha kwenda kumkamata Gavin kwa sababu walijua ni lazima alisafiri na ndege hiyo.

Wanaume hao watano walikuwa wamejipanga kwenye maeneo tofauti wakijifanya wapo hapo kwa ajili ya kupokea wageni wao huku wengine wakiwa wanajifanya kama walinzi wa eneo hilo kuhakikisha kila ambaye anapita hapo wanamuona na kama wangemuona mtu wao basi hawakutakiwa kupoteza muda zaidi ya kuondoka naye japo walijua zoezi hilo halikuwa rahisi kama ambavyo lilikuwa limeandikwa kwenye makaratasi ndiyo maana walibebwa wote watano ili kukiwa na ulazima wa kutumia nguvu za zaida isije kula kwao mtu mwenyewe alikuwa anaishi kama mzimu.

Zilikuwa ni dakika kumi na tano zimebakia ili ndege hiyo ambayo ilikuwa inatumia masaa yasiyo pungua matatu kutoka Jozi kufika Dar es salaam ili iweze kutua, muda huo hao wanaume walikuwa ndani ya uwanja huo wa ndege mkubwa tayari wakiwa makini kwa kila kitu kilichokuwa kinaendelea ndani ya hilo eneo bila kuwashtua watu au kuleta mtafaruko ama tafurani ya aina yoyote ile kwenye hilo eneo.
Hatimaye ndege ilitua na baada ya muda watu walianza kupita wakipishana huku na huko, wenyeji walikuwa wanashangilia wageni wao kufika huku wakiwapokea kwa bashasha na furaha ila wao walikuwa makini kupiga kila hatua kuhakikisha mtu wao haondoki ndani ya hilo eneo bila kupatikana. Watu walizidi kuwa wengi ila muda ulivyokuwa unazidi kwenda ndivyo walikuwa wakizidi kupungua taratibu mpaka walipo isha wote wakabaki wachache ambao walienda migahawani kupata chakula na wapendwa wao. Jambo la kushangaza ni kwamba mpaka abiria wanaisha hapo hawakumuona mtu wao huku kila mtu akiwa na picha yake mkononi.

“Nini kimetokea hapa?” Aliongea Tigana akiwa anaangaza kila upande baada ya kukutana na wenzake.
“Huenda hajasafiri” aliongea Jaden Mrisho
“Hapana, alijua kabisa kwamba kungekuwa na tatizo kama hili lazima kungekuwa na kizuizi kwenye viwanja vya ndege na washukiwa wa kwanza wangekuwa wageni maana yake hata yeye angekuwa hatarini kuweza kugundulika hivyo lazima amekuja na hii ndege ya mapema baada tu ya kufanya mauaji” Alieleza crispin Mkono.

“Kwa maana hiyo ni lazima alifika na kuchukua chumba karibu kabisa na uwanja wa ndege ili awahi kuondoka. Sina imani kama huyu bwana ni binadamu kama sisi” Sylvanos aliongea akiwa anasikitika.
“Hapana, ni mahesabu tu watu wa hivi wapo duniani ila ni wachache ndiyo maana wakifanya vitu huwa vinaonekana kuwa vya ajabu na wengine wakiamini kwamba haviwezekani. Swali la msingi ni kwamba kama alikuwepo hapa kapitaje? Na kama kapita tupo hapa maana yake yeye anatufahamu vizuri tu” Bariki baada ya kuongea hivyo ni kama kuna kitu kilipiga kwenye kichwa chake, alihisi kwamba aligongana na abiria mmoja wakati anageuka kumuangalia mtu huyo alitabasamu na kuweka mkono wake mmoja kifuani kama ishara ya heshima ila hakuelewa kama alikuwa ni yeye au siyo.

Alikimbia mpaka nje lakini hakuna ambacho alikiona wenzake wakiwa wanamshangaa bwana huyo
“Nahisi nimepishana naye” Aliongea Bariki
“Umejuaje?”
“Twendeni kwenye chumba cha kamera haraka” walikuwa na kibali cha mkurugenzi hivyo kwao kila kitu kilikuwa rahisi tu, waliingia ndani ya chumba hicho na kuanza kurudisha matukio yote nyuma ili waone kama mtu huyo alifanikiwa kutoka nje na alitokaje. Bariki alibaki anacheka kwa alicho kiona huku akiwa anatikisa kichwa
Kwenye ile video ya kwenye kamera, alipishana na shekhe mmoja ambye alikuwa amevaa kwa heshima mno, ndevu zilitengenezwa vizuri lakini ziliwekwa za kizee kidogo hivyo shekhe huyo alikuwa anaonekana kama mzee kiasi. Kwenye mkono wake mmoja alikuwa na fimbo ya kutembelea huku mkono mwingine ukiwa na begi jeusi la mkononi. Kichwani alikuwa na balakashea na miwani, alionekana kuwa mtu safi.
Huyo ndiye ambaye yeye Bariki aligongana naye na mtu huyo akaonyesha ishara ya kuomba msamaha huku akitabasamu kisha akaenda zake lakini kwenye mkono wake alikuwa na kitu kama kadi, haikuwa kadi bali kilikuwa kitambulisho cha Bariki. Baada ya kupishana pale yule bwana alitokomea zake kwenye gari ambayo haikuwa na namba hata moja ya usajili na bila shaka kuna mtu ambaye alikuwa kwenye ile gari akimsubiri kwani yeye baada ya kuingia kwenye ile gari hakukaa mbele bali nyuma hivyo kuna mtu ambaye alikuwa anamuendesha. Bariki alitabasamu ila moyoni alikuwa na hasira sana.

Tigana Mdachi alisogea kwenye skrini hiyo na kuirudisha nyuma ile video wakati mtu yule akipishana na Bariki, alitaka kuona ni kwa namna gani mtu huyo alifanikiwa kumuibia kitambulisho mwanaume huyo wa kazi bila hata yeye mwenyewe kushtuka! Alicho kiona yeye kilimtisha, vidole viwili ndivyo vilifanya ile kazi, kasi ambayo ilitumika kukibeba kile kitambulisho ilimfanya kuhisi hilo tukio lilihusiana na njia za giza.
“Binadamu gani ana uwezo wa kuwa na kasi ya namna hii?” alikuwa anaongea huku akiwa anairudia mara mbili mbili.

“Dunia inatuhakikishia kwamba bado tuna mengi ya kujifunza Tigana, kuna watu ukikutana nao unaweza kuona ni heri hata ukafa tu dunia uwaachie wenyewe. Watu wanaofanya haya matukio usiombe ukutane naye kwenye mazingira mabaya halafu ukawa mwenyewe, anakuua na hakuna mtu atakuja kujua kwamba uliwahi kuishi. Kama ameweza kumuibia Bariki bila hata yeye kujua kwa muda mfupi namna ile maana yake uwezo wake huyu umevuka kwenye ile hali ya ubinadamu, hii ni hatari kwa mwanadamu wa kawaida kuwa na nguvu za namna hii, anatakiwa kuzuiliwa mapema kabla hajawa hatari zaidi kwa watu wengine” Jaden Mrisho aliongea huku akiwa anaangalia dirishani kuona namna dunia ilivyokuwa inaenda kasi.
“Kwa hapa tulipo fikia tunamhitaji Princess sana na bosi anatakiwa kulijua hili”
“Ni ngumu kumrudisha kazini, amesimamishwa kazi kwa miaka miwili”
“Nina uhakika akiwa kiongozi wetu tulifanya makubwa sana ni wakati wetu wa kumpigania aweze kurudi kazini, ni mwanamke ndiyo lakini uwezo wake hapa sisi wote hatuna kwenye upande wa akili na sasa nguvu hazina msaada mkubwa zaidi ya akili ndizo ambazo zinahitajika zaidi”

“Upo sahihi Tigana, nadhani hilo linatakiwa kufika ofisini mara moja wakati huu”
“Lakini binafsi kuna jambo limenishangaza, kama amebeba kitambulisho maana yake ni kwamba hatujui ila ametuhisi ndiyo maana amekibeba ili akapate uhakika” Bariki aliongea jambo hili akiwa anamaanisha kabisa
“So, una shauri nini?”
“Kwa sasa turudi ofisini, tukae na kuandaa huu mpango upya kwa kuunganisha matukio yote ambayo tumeyapata huko tulikokuwa kufanya kazi hii halafu Malkia wetu arudishwe tuingie kazini mpaka huyu mtu apatikane na naahidi kwamba nitamtia mkononi na siku ambayo nitakutana naye nina imani atajuta” Bariki aliongea jambo la maana na kujisifia
“Bariki chunga ulimi wako ndugu yangu” Bariki hakumjibu Mrisho zaidi ya kuondoka hilo eneo kwani hawakuwa na jambo lingine la kufanya baada ya kumkosa mtu wao aliyekuwa amewapelekea hapo.
Sehemu ya thelathini na tano inafika tamati hapa.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Kongole kwa mwandishi
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA SITA
SONGA NAYO................
**********
TANZANIA INVESTIGATORY GROUP OF INTELLIGENcE (TIGI) HEAD QUARTER
Makumbusho karibu na Sayansi ndipo yalipokuwepo makao makuu ya shirika hili la kipelelezi lakini ofisi zao za siri zilikuwa zipo karibu na lilipokuwepo Baraza la Kiswahili Tanzania. Kulikuwa na mkutano kwa mara nyingine kati ya kiongozi na vijana wake, mambo ambayo yalitokea yalikuwa ni mengi lakini hawakuwa na namna, walitakiwa kuyapatia majibu mambo yote hayo kwa sababu ndiyo ilikuwa kazi yao.
Ndani ya sehemu ambayo walikutania kwenye ukumbi mkubwa ambao ulikuwa na kila aina ya vifaa vya kisasa kulikuwa na watu saba na sio sita tena. Alikuwepo Mkuregenzi mwenyewe bwana Othman lakini pia walikuwepo wanaume wale watano pamoja na yule mwanadada ambaye wao walikuwa wakimtaka arejee kwa namna yoyote ile kwa sababu ndiye alikuwa kiongozi wao na ndiye ambaye alikuwa ana akili kuwazidi wote pale hivyo kwenye hilo sakata walikiri wazi kwamba walikuwa wana uhitaji msaada wake kwa ukubwa.

Alikuwa ni mrembo mno kwa kumtazama usoni ila alikuwa ni mwanamke hatari kwenye kazi, miezi kadha nyuma alifanya makosa ya kinidhamu kwa bahati mbaya hivyo akalimwa miaka miwili ya kuwa nje ya kazi lakini kutokana na ulazima wa jambo ambalo lilikuwa mbele yao, hawakuwa na budi kumrudisha tena.
“Karibu kwa mara nyingine Princess Dayana. Mimi binafsi sikuwa na mpango wa kukurudisha kazini kwa mara nyingine ila hizi ni juhudi za vijana wako wanaonekana wanakupenda na kukuheshimu hivyo hii ni nafasi yako ya pekee kuweza kusahihisha yale makosa ambayo uliyafanya mwanzo na nina imani hakuna uzembe ambao utaufanya tena kwa sasa. Jitahidi ufanye niamini sijakosea kukurudisha kazini kwa sababu kama ukifanya upuuzi tena basi utasababisha nikifute kabisa hiki kikosi chenu cha THE INVISIBLE” Aliongea mkurugenzi kwa sauti ya mamlaka akiwa anamwangalia kwa umakini mwanamke huyo ambaye aliwageukia vijana wake na kutabasamu.
“Nitafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuhakikisha nalipambania taifa langu kwa namna yoyote ile”
“Are you sure?”
“Yes sir”
“Get the work done”
“Roger that”
“Nipeni taarifa za mlipo ishia”
“Alijua kama tutakuwa pale bosi”
“Alijuaje hilo?”
“Nadhani anaelewa vizuri kama tunamfuatilia”
“Kuna mtu hata mmoja ambaye mmempata ambaye anaweza kuwa muongozo mzuri kwenye hili?”
“Hapa ndipo tunatakiwa kuunganisha juu ya matukio yote ambayo yalitokea”
“Jaden na Mkono nyie ndio mlithibitisha kwamba mlikutana na aliyekuwa mke wa makamu wa raisi na akasema kabisa mumewe alimtajia kwamba aliyepiga risasi ni mtu anaye itwa Douglas Shenzi ambaye anaishi Afrika ya kusini. Kwahiyo ni kweli kwamba yule aliyekufa ndiye DOUGLAS SHENZI mwenyewe?”
“Ndiyo bosi”
“Hiyo risasi alimpiga nani kiasi kwamba isababishe kuua watu wengi tena kikatili namna hiyo?”
“Nadhani anaweza kuwa mmoja wa wanafamilia wake”
“Hapa ndipo tunatakiwa kuyajua maisha yake kwanza” Dayana alifungua kinywa kwa mara ya kwanza kabisa.
“Tunayajuaje maisha yake?”
“Tangu nisimamishwe kazi nimekuwa nikilifanyia kazi hili jambo” wote walibaki wameganda kumwangalia mwanamke huyo ili kujua ni kitu gani alikuwa anataka kukisema.
“Jina lake ni Gavin Luca, jina ambalo kiuhalisia halina mfanano na jina lingine lolote lile. Hapo nakiri kwamba mtu huyu alifanya mahesabu makubwa kufanikisha jambo hili lakini jina lake halisi ni Gavin Lucas, alitoa ile herufi S ili kuja kutuingiza kwenye mkanganyiko kwa sababu alijua kwamba itafika siku atakuwa anatafutwa na mamlaka kwa nguvu zote ndiyo maana akaziweka karata zake mahali sahihi. Kwa minajiri hiyo sasa huyo Lucas mwenyewe ni nani? Hapa ndipo pana majibu yote ambayo sisi tunayahitaji kwenye hii kazi” ujio wake ulikuwa kama baraka kwani alionekana kuwa na taarifa nyingi zaidi ya wenzake wote ambao walibaki wamemtumbulia macho kusubiri awape za ndani kabisa.
“Kwenye hili taifa wote tunamkumbuka mtu ambaye alipata umaarufu kama THE LIVING PABLO EScOBER. Mwanaume ambaye alilitikisa hili kwa taifa kwa biashara ya madawa ya kulevya kiasi kwamba ikapelekea kujenga mtaa wake kutoka kwenye jina la Peenuga Streets mpaka kuuita LucAS VILLA”
“Unataka kusemaje?”
“Yule ni baba yake mzazi” kauli ya Dayana iliwapa wote mshangao.
“Yule mtoto alikufa, baadae akaibuka Gavin Luca ambaye alikuwa na ajenda zake na ndiye ambaye mkuu wa majeshi alimsaka mpaka kumuua huko Kenya”
“Mtoto wa yule mzee ambaye amekufa ni mmoja tu naye hakufa kama ambavyo yeye alidai bali alitengeneza mbinu ya kuwaokoa wanae”
“Wanae?”
“Wale wawili walizaliwa wakiwa mapacha hakuzaliwa mmoja”
“Whaaaat are you talking about?”
“Huo ndio ukweli bosi, wale walizaliwa wawili na watu hawa wote ambao yeye Gavin anawaua kuna mambo mengi wanayafahamu ndiyo maana haui kila mtu bali ana kundi lake rasmi ambalo analiteketeza taratibu”
“Walizaliwaje wawili na akajulikana mmoja na mbona hainiingii akilini kuniambia kwamba huyu bwana mdogo ni mtoto wa damu wa yule mfanya biashara wa madawa ya kulevya?”
“Ndiyo maana nipo hapa bosi”
“Nakusikiliza Dayana”
“Kuna uhakika wa asilimia themanini kwamba hawa wote ambao yeye anawaua ndio walihusika na mauaji ya huyo mwenzake pamoja na familia yake”
“Kwamba mmoja amekufa na mmoja yupo hai?”

“Ndiyo yule ambaye alikuwa anaishi na wazazi wake ndiye alikuja kufa ila mmoja ambaye alilelewa na mtu wa pembeni ndiye huyu yupo hai”
“Alilelewa na mtu wa pembeni?”
“Ndiyo na kuna viongozi wanalijua hili mheshimiwa na ndio ambao wanamtaka afe”
“How?”
“Nadhani majibu mengi mkuu wa majeshi na hata raisi wanaweza kuwa nao juu ya nini kinaendelea”
“Unataka kuniambia raisi wa Tanzania naye anahusika kwenye hili jambo?”
“Ndiyo mkuu”
“Hizi taarifa umezitolea wapi?”

“Siwezi kukupa chanzo changu kwa sababu za kiusalama, ni mtu ambaye alinitafuta mwenyewe na kudai kwamba anahitaji kunipatia taarifa za mhimu ambazo yeye aliona kwamba zinaweza kuwa na msaada kwetu na kwa taifa zima. Mtu huyo ni miongoni mwa masalia ya kile kizazi”
“Unamaanisha unajua kila kitu kuhusu haya mambo?”
“Hapana, kuna taarifa nyingi ninazo ila haimaanishi kwamba najua kila kitu ila kuna watu ambao najua kwamba wana hizi taarifa zote na ndizo zinaweza kutusaidia kufika tunapo pataka ila hatutakiwi kwenda kwa njia ya kumvamia huyu mtu mmoja kwa moja kwa sababu hakuna kati yetu ambaye anaweza kupona mbele yake”
“Kivipi”
“Hakuna binadamu ambaye anaweza kusimama na Gavin akafanikiwa kuishi ndani ya dakika tano hivyo kuna njia rahisi ambayo inaweza kutusaidia kwenye hili jambo”
“Nini?”
“Tunatakiwa kuutumia udhaifu wake kukamilisha hii kazi”
“Ambao ni?”
“Ana watu wanne tu ambao anajali kuhusu uwepo wao”
“Ana familia?”
“Ndiyo. Ana mama, babu, mke na mtoto mmoja”
“Kwamba ameoa?”
“Ndiyo”
“Mke na mwanae hakuna mtu anawafahamu au kuwajua kwamba wapoje ila mama yake na babu yake wanapatikana japo hatutakiwi kwenda kinguvu”
“Babu yake ni nani?”
“Rafiki yako wa zamani” mkurugenzi alibaki ameduwaa baada ya kuambiwa hilo jambo
“Unamaanisha?”
“Mtu ambaye alikuingiza wewe kwenye mifumo ya uongozi”
“Nooooo, nooooooo Hassan?”
“Yule ndiye babu yake”
“Dayana unajua kabisa kwamba ni kosa la jinai kunidanganya mimi?”
“Najua ndiyo maana katu siwezi kudanganya mbele yako”
“Unataka kuniaminisha kwamba waziri mkuu wa zamani ndiye babu yake Gavin?”
“Ndiyo, kama unakumbuka rafiki yako alikua na binti yake mmoja mzuri sana”
“Wait, Glady?”

Sina la kuongeza tena mpaka hapa, 36 naweka nukta.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
SONGA NAYO................


“Huyo ndiyo mama mzazi wa hao watoto mapacha ila aliuawa pamoja na mumewe lakini mwili wake yeye ulitolewa ili jambo hilo lisije kujulikana kabisa” Mkurugenzi aliketi kwenye kiti akiwa amechoka, bado alihisi kama anaona haamini yale ambayo yalikuwa yanazungumzwa na malkia wa nguvu kiongozi wa THE INVISIBLE ambaye alirudishwa kazini ili kuweza kusaidia kumzuia mwanaume huyo kufanya mauaji ambayo alikuwa anaendelea nayo mjini.
“Nini kilitokea Dayana” Dayana aliliweka koo lake safi ili kuweza kuwapa kinaga ubaya nini kilisababisha mambo hayo yote kutokea na kwanini taarifa hizo hazikuwahi kujulikana kwa watu wengi zaidi ya watu wachache na wa mhimu kwa familia hiyo.



*********
Valeria George
Huyu alikuwa mke wa raisi wa Tanzania, mwanamke ambaye alipenda majivuno na matanuzi kwa sababu mumewe ndiye alikuwa kiongozi mkuu Ikulu. Alikuwa anafanya kile anakitaka kwa wakati ambao anauhitaji kwa sababu alijua hakuna mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaweza hata kumnyooshea kidole tu, alivimba, taifa lilikuwa kwenye mikono yake ungemwambia nini Valeria? Lakini hakujua kwamba kuna mtu mkubwa tu alipewa kazi ya kuweza kumuua mama huyo, hakuwa na wasiwasi kwa sababu alikuwa na ulinzi kwa masaa ishirini na manne ya wiki.

VALERIAN GENERATIVE MALLS
Zilikuwa ni malls kubwa ambazo zilikuwa zinamilikiwa na mke wa raisi Valeria katikati ya jiji. Mwanamama huyu kila wikiendi alikuwa anapenda kwenda eneo hilo mwenyewe kufanya hesabu zake na kubadilisha nguo. Alikuwa mke wa raisi lakini alipenda mauzo, alipenda kuonekana kwenye kamera, alipenda kila siku kutokea kwenye kurasa za magazeti ili kuwarusha roho wanawake wenzake. Japo mumewe alikuwa akimkanya sana na kumtaka kuipoteza tabia hiyo ukizingatia yeye ni mke wa raisi lakini siku zote sikio la kufa huwa halina dawa.

Kuishi maisha ya kawaida kwake kungemfanya aonekana wa kawaida mbele za watu, hakuwa tayari jambo hilo kutokea kwa sababu yeye ndiye alikuwa first lady wa taifa sasa angeishije kinyonge mitaa isimkome? Thubutuuuu!!! Hakuwa tayari kwa hilo. Alikuwa na msafara wa gari kumi na mbili, kodi za watanzania zilikuwa zinatumiwa vibaya sana na mwanamama huyo.
Ilikuwa wikiendi, kama kawaida kupenda kwake sifa kupita kiasi kulifanya ratiba zake kutabirika na kujulikana kirahisi likawa kosa la kwanza kwenye maisha yake kulifanya, hakutakiwa kuweka wazi ratiba zake zote kama mke wa raisi kwa sababu ilikuwa ni hatari ila alijiamini. Hakujua kwamba alikuwa kwenye mipango ya watu fulani ambao walihitaji damu yake imwagike, huo mpango alipewa mkuu wa majeshi na mwanamke ambaye yeye alimtambua kama mama yake Gavin na kufanya kwake jambo hilo huenda ndiyo ingekuwa sababu ya yeye kuendelea kuwa hai hivyo hakuwa na namna zaidi ya kufanya jambo hilo. Sasa nani ambaye alitakiwa kuhusika kwenye hayo mauaji? Alihitajika mdunguaji hatari, ambaye ni nani sasa?

Remember the name Sarah, una kumbukumbu zilizo sawa? Nimekutajia jina la Sarah Martin akiwa ndiye mwanamke pekee aliyefanikiwa kupona ndani ya msitu wa Mau? Nilikupa wasifu wake kwamba moja kati ya eneo ambalo alikuwa anaaminika sana ni kwenye udunguaji hivyo ni jina lake ambalo lilichorwa kwamba alitakiwa kumuua mwanamama huyo. Ilikuwaje na alitakiwa kumuua vipi?
Sarah baada ya kwenda Monduli kukutana na Nick, wawili hao waliishia kuzama kwenye huba zito ambalo bila shaka walikuwa wamelihifadhi kwa muda mrefu ila wakati wa kulidhihirisha ulifika. Alipewa ushauri wa nini alitakiwa kukifanya kwa wakati huo wakamalizia na usiku wao kitandani hivyo asubuhi aliondoka bila hata kumuamsha bwana huyo ilimradi awahi nyumbani kwani aliondoka usiku wa manane bila kuaga pindi ametembelewa na mtu ambaye alimtilia mashaka.

Baada ya kufika nyumbani alipigwa butwaa, alihamaki na kushika kiuno kwa hali ambayo alikutana nayo huenda hakuifikiria kabla ama hakutarajia kwamba inaweza ikamtokea yeye, alihamaki akiwa mwingi wa hofu kwenye nafsi yake nyumbani hapakuwa pema. Nyumba ilikuwa kimya kila sehemu na milango yote ilikuwa wazi nyumba nzima, haikuwa ishara nzuri kwa mazingira ya hapo kwake akalazimika kukimbilia kila sehemu kuweza kumwangalia mama yake lakini hakukuwa na ishara ya uwepo wake sehemu yoyote ile, alihisi kuchanyanyikiwa.
Alizunguka mpaka nyuma kabisa ya hiyo nyumba yake lakini nako hali ilikuwa ni ile ile hakukuwa na dalili za uwepo wa mtu yeyote. Alitamani kumpigia simu Nick ili kumpa taarifa juu ya habari ile lakini alihisi haikuwa sawa, hakuamini kwamba tukio hilo lilikuwa la bahati mbaya hivyo alitakiwa kuwa na uhakika kwanza kwa sababu kukurupuka kwake huenda kungemfanya asije kuipata familia yake tena. Aliinyanyua simu yake na kumpigia mdogo wake ambaye alikuwa anasoma chuo ila kwa bahati mbaya namba haikuwa ikipatikana, alisonya huku akiwa anakimbilia kwenye gari yake.

Safari yake ilikuwa ni kuelekea chuoni kwa mdogo wake, alikuwa ni soldier hivyo mpaka wakati huo alikuwa anajua kabisa mama yake lazima kuna watu wamembeba, hakutaka itokee na kwa mdogo wake ndiyo maana aliwahi ili kuondoka naye. Alikuwa akifahamika eneo hilo hivyo alipofika tu alipokelewa kwa heshima lakini kwa bahati mbaya aliambiwa kwamba ni dakika kumi zilizopita kuna wanaume walikuja hapo wakiwa na vitambulisho wa usalama wakidai kwamba walikuwa na mazungumzo na bwana mdogo huyo. Alihisi kuishiwa nguvu Sarah japo aliamua kujikaza na kuondoka kurudi kwenye gari yake.
Baada ya kuingia ndani ya gari, alipiga usukani kwa hasira na jazba kali akiwa anatukana bila kujua anamtukana nani, hakuwa na kitu angeweza fanya zaidi ya kusubiri wahusika wamtafute na kweli hazikuisha hata dakika tano simu yake ilianza kuita na mpigaji ilikuwa ni namba ngeni. Aliipokea kwa wasiwasi akiwa anahema kwa nguvu ila alipewa maelekezo ambayo yalimshtua na kumtisha sana Sarah Martin kwani alihisi anaota jambo hilo. Alijaribu kutaka kuijua sauti ya mtu ambaye alikuwa anaongea upande wa pili lakini hakufanikiwa kwenye hilo kwa sababu mtu wa upande wa pili alikuwa anaongea mithili ya mtu ambaye alikuwa ndani ya spika.

Maelekezo ambayo alipewa ilikuwa ni amri ya kumuua mke wa raisi, hakutakiwa kuuliza sababu ila kama angehitaji kuiona familia yake yaani mama yake na mdogo wake kwa mara nyingine alitakiwa kuifanya kazi hiyo siku ya wikiendi na baada ya kukamilisha kazi hiyo angewapata tu nyumbani kwake yaani wangerudishwa.
Aliambiwa atoe majibu ndani ya dakika tano kwa namba hiyo hiyo ili apewe maagizo na wapi ambapo angeikuta silaha ya kuweza kuitumia kwenye tukio hilo ila kama angegoma basi usiku wa siku hiyo angeelekezwa mahali pa kwenda kuzibeba maiti za mama yake na mdogo wake. Sarah alibaki anashusha machozi, hakumjua ni nani ambaye alikuwa anamuingiza kwenye game la hatari kama hilo ila kitu ambacho alikuwa anakilelewa ni kwamba alikuwa anaingizwa kwenye shimo baya ambalo hata kutoka kwake ingetumika gharama kubwa mno. Hiyo kazi ya mauaji ambayo ilikuwa mbele yake ingemfanya awe mtumwa maisha yake yote kwa sababu siku ambayo angeenda kinyume na hao watu ingekula kwake kwa kumuweka hadharani kwamba ndiye ambaye alihusika na mauaji ya mke wa raisi.

Lakini pia aligundua kwamba inaweza kuwa ni njia ya yeye kutengenezewa kesi ambayo ingeenda na maisha yake. Jambo ambalo hakuelewa ni kwamba hakuwa na baya na mtu yeyote na hata kwa kile ambacho kilitokea kule msituni hakuonekana kujua mambo mengi wala kuwa na shida na mtu yeyote sasa kwanini alikuwa anatengenezewa mazingira mabaya namna hiyo? Aliduwaa Sarah lakini alitakiwa kufanya maamuzi akatae ili familia iuawe au akubali kuifanya hiyo kazi familia irejeshwe nyumbani.
Akiwa bado kwenye mawazo simu ilianza kuita tena, aliipokea haraka haraka akiwa anauma meno yake, mdomo ulikuwa mzito kutamka ila hakuwa na namna.
“Nitaifanya” hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya pekee kuweza kuisaidia familia yake. Na hivyo ndivyo ambavyo ilipangwa mke wa raisi kuuawa siku ya wikiendi ambayo angekuwa kwenye Malls zake mjini kwa kutumia mdunguaji kwa sababu ingekuwa ni ngumu kumvamia moja kwa moja, alikuwa na ulinzi mkali sana.


VALERIAN GENERATIVE MALLS
Ilikuwa wikiendi kama kawaida yake mama wa kujivuna alikuwa anaingia kwenye biashara zake, mke wa raisi bwana, ungemwambia nini akakuelewa? Abadani asingefanya huo ujinga. Ilikuwa alasiri mama huyo alipofika na msafara wake hapo, siku ambazo anakuja ulinzi ulikuwa unakuwa mkali, wadada wengi warembo walipenda kufika hapo kupiga naye picha kwa ajili ya kwenda kutambia mitandaoni kama ilivyokuwa kawaida ya dada zetu wa mjini. Jiji lilitulia, wenye maisha yao safi walikuwa wanafaidi kwa kupata raha za kutosha lakini wenye maisha magumu hayo mambo walikuwa wakiyasikia tu kwenye mitandao ya kijamii na redioni.
Baada ya mwanamama huyo kuingia, eneo lilikuwa sawa, hakuingia ndani kama kawaida yake ilikuwa ni lazima apate picha kwanza ili kesho alindime kila kona ya vyombo vya habari hivyo alitumia muda kadhaa kukaa nje maafisa usalama wakiwa wapo makini kuhakikisha hakuna hatari yoyote inampata mama huyo.
Lakini umbali wa mita miatano kutoka ilipokuwa hiyo sehemu, upande wa dirisha la juu kwenye ghorofa moja refu alikuwa anaonekana mtu akiwa ameishika riffle. Ilikuwa ni silaha ya wadunguaji ya masaafa marefu ambayo ilikuwa ina uwezo wa kuyabeba maisha ya mtu aliye umbali wa mita miatano na zaidi. Mtu huyo hakuwa mwingine, alikuwa ni sarah Martin, alikuwa hapo kwa ajili ya kuyaokoa maisha ya familia yake huku akitakiwa kuyabeba maisha ya mtu mwingine tena mke wa raisi.
Kwenye macho yake alikuwa na miwani ya vioo ambayo ilikuwa inamfanya aone mbali kwa usahihi, dirisha hilo lilikuwa limefunguliwa vizuri upepo unapiga. Ni muda kidogo tangu mwanamke huyo aitegeshe silaha yake hapo akiwa anamsubiri mwanamama huyo aingie kwenye kumi na nane zake na wakati ulikuwa umetimia. Jicho moja lilikuwa kwenye lenzi yake ambayo alikuwa anaizoom taratibu kukuza ile taswira ya mke wa raisi. Alikuwa amejaa kwenye duara lake, alikuwa ana uhakika wa kutokumkosa kwa sababu kwenye sheria za wadunguaji kumkosa mlengwa wako kwa risasi ya kwanza unakuwa umefeli kazi yako na hata ukiendelea kumtafuta tena nafasi ya kumpata inakuwa ni ngumu.

Wakati anakumbuka sehemu ya mafunzo yake aliachia risasi yake baada ya kuhema huku akifumba jicho, wakati anafumbua aliiachia silaha hiyo na kushika kiini macho, alikuwa na uhakika kwamba hawezi kukosa shabaha yake na baada ya kuhakiki aligundua kwamba ni kweli mke wa raisi alikuwa amekufa kwa kupigwa risasi kwenye paji la uso hivyo ule ndio ungekuwa mwisho wake kuonekana hadharani kwenye maisha yake yote. Alikusanya vitu vyake na kushuka mpaka chini kabisa ya jengo hilo kupitia milango ya nyuma, baada ya kufika nje kuna gari ya taka ilikuwa inapita, alirushia begi humo gari likaenda njia yake naye akapita njia yake na kutokomea.

Ile sehemu ambayo alikuwepo mke wa raisi ilizaa taharuki mpya, ni tukio la watu kuona mke wa raisi anashuka chini pindi anapiga picha na binti mmoja. Kudondoka kwake ndiko kuliwafanya walinzi kujongea haraka pale alipokuwepo, ulikuwa ni mshangao baada ya kugundua kwamba ni risasi ilikuwa imepenya kwenye paji lake la uso. Walinzi walianza kuwasiliana kwa vifaa vyao wakitaka gari iandaliwe haraka ambayo ilikuwa ya huduma ya kwanza kwa ajili yake ila walijua kabisa hayupo hai mwanamama huyo kwa namna alivyokuwa amepigwa risasi zile.

37 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
SONGA NAYO................

Eneo hilo lilianza kutapakaa walinzi na maaskari wengi hata mitaa ikafungwa kabisa na wote ambao walikuwa pale hakuna hata mmoja ambaye alikuwa anaruhusiwa kuondoka kwa wakati huo ilikuwa ni lazima ufanyike upekuzi mkali kwa sababu aliyekuwa ameshambuliwa alikuwa ni mtu mkubwa kwa taifa kwahiyo jambo hilo lisingeisha kienyeji. Taarifa hizo ngumu na mbaya zilianza kusambaa kila pembe, mitandao ya kijamii ilianza kurusha baadhi ya picha za mara ya mwisho alipo onekana mwanamama huyo. Ilikuwa ni habari ya kushtusha mno mke wa raisi kufa tena kwa kushambuliwa kwenye halaiki akiwa kwenye matembezi yake, taarifa ile ilibebwa kwa utofauti na kukawa na hisia za kila namna kuhusu usalama wa taifa kwa ujumla.

Sarah baada ya kumaliza kazi yake hakuzubaa tena jiji Dar es salaam kwa sababu hakuna mtu wake wa karibu ambaye alitakiwa kujua kwamba yeye alikuwepo jijini hivyo aliondoka na gari yake binafsi kabla hajashtukiwa kwani alielewa kabisa kwamba baada ya muda fulani ingekuwa ni ngumu kuvuka kwenye vizuizi na kama angejulikana kwamba alikuwepo basi alitakiwa kuelezea sababu ya msingi ya kuja Dar bila ruhusa jambo ambalo lingemuingiza kwenye ushukiwa.
Usiku aliingia Moshi akiwa amechoka mno, baada ya kuingiza gari ndani kwake hakutoka, alibaki amekaa kwenye gari kwa saa zima akiwa anatafakari alichokuwa amekifanya na hatima ya hayo yote ambayo yalikuwa yanaendelea. Alijiona kuwa na hatima mbaya ya maisha yake kama asingekuwa makini, alitamani angempa taarifa hizo Nick ila hazikuwa njema na hakutakiwa kuanza kuufungua mdomo wake kwa kila mtu kwani ingemletea matatizo makubwa huko mbeleni hivyo akaamua kufa na hilo jambo moyoni.
“Nahitaji msaada wa Gavin Luca, hili jambo sina imani tena kama naweza kusimama mwenyewe na moyo wangu na nikalishinda, najiona kujiingiza kwenye shimo ambalo hata sielewi nitafanikiwa vipi kutoka” aliongea akiwa anashuka kwenye ile gari na kuingia ndani bila hata kuifunga.
“Mwanangu” Aliisikia sauti ya mama yake, alimkimbilia na kumkumbatia kwa furaha.
“Mdogo wako amelala utaongea naye kesho”
“Mpo salama mama?”
“Hata sijui kama nipo salama”
“Kuna mtu amewatesa?”
“Hapana ila nina maswali mengi sana mwanangu”
“Yapi mama?”
“Kuna kitu gani umekifanya?”
“Hamna kitu mama”
“Tulihifadhiwa sehemu tukawa tunapewa kila kitu vizuri lakini watu wale ambao mimi siwajui walinihakikishia kwamba wewe ndiye ambaye utatuweka huru mwanangu. Unaweza kuniambia umefanyaje jambo hili mpaka tukaruhusiwa kuondoka na wale watu ni akina nani?”
“Mama ni masuala ya kazi”
“Najua ni kazi mwanangu ila mpaka sasa nahisi simjui vizuri mtoto niliye mzaa mwenyewe”
“Samahani mama umesema?”
“Hiyo kazi ambayo unaisemea ni mauaji?”
“Hapana mama unajua kabisa siwezi kufanya hivyo”
“Niambie Sarah ni wewe umemuua mke wa raisi?”
“Hapana mam……” Sarah alipokea kibao kikali mno kutoka kwa mama yake.
“Wewe ni miongoni mwa wanajeshi wachache ambao wapo kwenye mkeka wa wadunguaji bora wa taifa hili, leo mke wa raisi ameuawa na baada ya yeye kufa tu sisi tukaachiwa. Unataka kuniambia hiyo ni bahati mbaya?”
“Sijui lolote mama”
“Jiangalie sana binti yangu, umeanza kuingia sehemu ambayo siyo kwenye maisha yako, mfikirie mdogo wako maisha ambayo atayaisha wewe ukipotea” mama yake aliongea kwa uchungu akiondoka hilo eneo. Alibaki analengwa lengwa na machozi Sarah akiwa hajui ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya kwa muda huo.









*********
Kifo cha mke wa raisi kilibeba tafsiri nzito na kuleta mkanganyiko mkubwa kama sio mpasuko ndani ya serikali. Kuuawa kwa viongozi wa kiserikali lilikuwa ni moja ya wimbi gumu na baya kwa serikali lakini kufa kwa mke wa mheshimiwa lilikuwa li jambo lingine ambalo lilikuwa ni gumu kulimeza isivyokuwa kawaida. Alikuwa ndiye first lady wa taifa, kifo chake ilikuwa ni lazima kije na mambo mengi. Licha ya maafisa usalama kuhitaji kuficha kilicho tokea lakini hawakuweza kabisa, dunia ipo kwenye kasi kubwa ya usambaaji wa mitandao na watu walikuwepo pale hivyo lile tukio lilianza kusambaa taratibu kila kona ya mitandao, kila chombo cha habari kikawa kinajinadi kuanza kuripoti habari hiyo mpaka ilipo tapakaa kila kona ya mtaa na taifa kwa ujumla.

Taarifa hiyo ilimkutia raisi akiwa ametoka kupata chakula, ni siku ambayo haikuonekana kuwa mbaya kwake ila ni moja ya siku ambazo zilikuja kumuishia vibaya, wakati anaipata taarifa hiyo hakuwa akiamini kabisa kuhusu jambo hilo, raisi hakuwa na imani kama ni mkewe kweli ndiye ambaye alikuwa amepigwa risasi. Raia anamuua mke wa raisi bila hata kusita mara mbili? Ni nani alikuwa na jeuri ya kumshambulia first lady tena hadharani? Mheshimiwa baada ya kuipokea taarifa hiyo alikuwa kama amechanganyikiwa, alikuwa akimpenda mno mkewe, walikuwa na historia yao ndefu ambayo ndiyo ilikuwa inamtesa halafu siku hiyo kuna mtu kirahisi tu alikuwa ameamua kupita na maisha yake, asingemsamehe abadani.
Mke wa raisi alikuwa amepelekwa kwenye hospitali ya jeshi ili apatiwe huduma chini ya ulinzi mkali, licha ya madaktari kuthibitisha kwamba mke wa raisi alikuwa mfu, ilitoka amri Ikulu kuwataka wahakikishe wanafanya jambo lolote lile kuhakikisha mke wa raisi anakuwa salama. Walifanya hivyo kumridhisha tu mheshimiwa ila hakukuwa na binadamu mwenye uwezo wa kumrejesha mtu ambaye alikuwa amekufa tayari, hiyo ni kazi ya Mungu pekee.

Msafara wa gari zipatazo hamsini ulikuwa barabarani kuelekea ndani ya hiyo hospitali ya jeshi, barabara zilifungwa, hakuna mwananchi alikuwa anaruhusiwa kuingia kwenye hiyo barabara hata kwa bahati mbaya. Mtaani walijaa polisi na wanajeshi kuhakikisha mheshimiwa hakuna kinacho mpata kibaya kwa namna yoyote ile kama kile kilicho mpata mkewe. Ndani ya dakika thelathini na tano tu mheshimiwa alikuwa anashuka kwenye gari kuingia kwenye hospitali hiyo macho yake yakiwa mekundu isivyokuwa kawaida, moyo wake ulikuwa unapasuka kwa maumivu makali kwani hakuwa tayari kumuona mkewe akiingizwa mochwari.
Hakutaka hata kusikia maneno ya madaktari alihitaji kumuona mkewe alipo, hakukuwa na namna zaidi ya kumuongoza ambako ulikuwa umehifadhiwa mwili wa first lady wa Tanzania. Alicho kiona alitamani kubishana nacho bado nafsi yake haikuwa ikikubali kwamba yule mke wake kipenzi, yule mwanamke ambaye yeye alimpenda sana alikuwa amekufa tayari, hakuwa hai tena Valeria. Alipiga kelele kwa hasira na kumkunja daktari, alichomoa bastola kutoka kwa mlinzi na kuhitaji kumpiga risasi daktari huyo lakini mlinzi wake alimuwahi na kusimama mbele ya daktari.
“Mheshimiwa tafadhali sana usifanye hili kosa kwani hizi habari zitasambaa na itakuharibia sana jina, nakuahidi tutampata mhusika kwa namna yoyote ile” mheshimiwa aliishusha silaha hiyo akiwa anahema kwa hasira mno, alitamani kuibeba damu ya mtu ila moyo wake utulie lakini mazingira hayakuwa rafiki kufanya jambo hilo zaidi angezidi kujiharibia mwenyewe tu.

“Where are you Gavin Luca? Umemuua mke wangu mshenzi mkubwa wewe, kakukosea nini yule? Nitakuua kwa mkono wangu” mheshimiwa alikuwa anaongea kwa sauti kali mpaka madaktari wakaanza kuogopa na wengine wakijificha japo kila mtu alibaki anashangaa lile jina kuhusishwa na mtu huyo ambaye ndiye alikuwa gumzo kila kona.
“Namhitaji huyu mtu akiwa hai” alimuongelea mlinzi wake akiwa anauma meno lakini wakati huo Medrick Savato alikuwa anaingia eneo hilo akiwa na walinzi wake, alipofika hapo alimkumbatia mheshimiwa na kumpiga piga mgongoni, mheshimiwa alionyesha wazi kwamba alikuwa ana uhitaji wa kuongea na mtu huyo wakiwa wenyewe wawili tu hivyo kiliandaliwa chumba haraka iwezekanavyo.

“Hata siku moja sikuwahi kutegemea kama naweza kukutana na maumivu makali namna hii, Valeria kwangu alikuwa zaidi ya mke, yule nilikuwa namuona kama mama yangu mzazi kwa sababu yupo na mimi tangu siku naanza na sina lolote mpaka sasa nimekuja kuwa raisi. Mwanamke yule aliziacha ndoto zake zote ili tu awe na mimi, alinipenda, alinijali na kunifanyia kila nilicho kihitaji mimi na mimi nilimuahidi kwamba ningemlinda siku zote za maisha yangu hata ikiwezekana kuyatoa maisha yangu lakini leo nimeshindwa kufanya hivyo. Mke wa raisi anauawa tena hadharani kwa kudhalilishwa namna ile?” raisi aliongea kwa uchungu akiwa anaibamiza chini runinga ambayo ilikuwa mbele yake.
“Mheshimiwa naelewa hali ilivyo kwa sasa, hautakiwi kujilaumu kabisa kwa sababu hata kama madam angekuwa na ulinzi mkubwa kiasi gani huyu mhusika anaonekana kabisa kwamba alikuwa anahitaji nafasi moja tu kuweza kutekeleza jambo lake. Kitu pekee ambacho alikuwa anakihitaji ni uwepo wa madam kwenye eneo lenye uwazi ndiyo maana amefanikiwa kutekeleza jambo lake”
“Unahisi ni nani amefanya haya Mr Savato zaidi ya Gavin?”
“Sina hakika sana kama atakuwa ni yeye lakini pia anaweza kuwa yeye. Kwenye mauaji yake kadhaa ambayo ameyafanya ana aina yake ya kuua na hii haionekani kuwa aina yake na kama ni yeye basi amefanya hivyo kwa sababu hana namna au kwa sababu ndiyo ilikuwa njia pekee ya yeye kufanya hivyo. Lakini mheshimiwa Gavin sidhani kama anajua lolote kuhusu wewe sasa kivipi amshambulie first lady? Kama angekuwa anajua sawa ila kwa sababu hajui ni ngumu kufanya hivyo” mkuu wa majeshi ni kama alikuwa akimsanifu mheshimiwa kwa sababu huo mpango mzima ulikuwa kwenye mkono wake, kila mtu alikuwa anajaribu kutandika karata zake vyema ili aweze kuishi na kuyatetea maisha yake.
“Tuseme labda sio yeye, sasa ni nani mwingine ambaye ana hiyo jeuri ya kwenda kumgusa mke wangu na kuyabeba maisha yake tena kirahisi namna ile?”

38 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
SONGA NAYO................

“Kwa hili vijana wanatakiwa kuingia kazini kwa masaa ishirini na manne kwa hali yoyote ile”
“Mr Savato”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Hivi yule mwanamama bado yupo hai?”
“Yupi?”
“Auleria”
“Nahisi bado ni mzima mheshimiwa, kwanini?”
“Kuna kipindi aliwahi kutoa tamko baya kumhusu mke wangu kupitia watu kadhaa nadhani unakumbuka hilo, kama yupo hai huenda kuna muunganiko wa yeye na hili labda?”
“Sidhani, ni mwanamke ambaye alishajikatia tamaa ya maisha tayari sasa inawezekana vipi afanye jambo kama hili?”
“Kumbuka yule amewahi kuwa kanali wa jeshi, ana nyenzo na ana uwezo wa kuwatafuta watu ambao wanaweza kuifanya kazi hii kwa niaba yake?”
“Mheshimiwa unahisi kuna sababu gani ya msingi ya kumfanya yeye afanye yote haya?”
“Hiyo sababu ndiyo ambayo mimi binafsi nahitaji kuifahamu kutoka kwake. Nataka kukutana na Aurelia”
“Hili sio wazo zuri mheshimiwa, kumbuka yule mama anaishi mtaani kule na huwezi kwenda ile sehemi kienyeji tu hivi”
“Hivi unajisikia unacho kiongea wewe? Tunazungumzia maisha ya mke wangu ambayo hayapo tena halafu bado unataka kuniaminisha kwamba natakiwa kutulia? Mr Savato hili jambo haliwezekani abadani”
“Nimekuelewa mkuu, unahitaji kitu gani?”
“Nahitaji Luca Gavin apatikane akiwa hai kwa sasa, kama imeshindikana kufa basi namtaka akiwa hai kabisa, nina mazungumzo naye marefu na maswali ambayo anapaswa kunijibu. Tumia mali yoyote, tumia rasilimali yoyote ile ila hakikisha huyu mtu anapatikana kwa sababu nahitaji kuja kumuua mwenyewe kwa mkono wangu”
“Sawa mheshimiwa” hakuwa na ubavu wa kumzuia tena, muda huo huo msafara uliandaliwa huku juu kukiwa na helikopta za kutosha za jeshi kudumisha ulinzi, mji ulikuwa umechafuka na kutapakaa ulinzi kila mahali huku msako mkali ukiwa unaendelea kila kona kuanzia kwenye lile jengo ambalo ndiko alikuwepo Sarah kuhakikisha muuaji wa mke wa raisi anapatikana mara moja.
Msafara wa raisi ulienda kuishia YOMBO VITUKA, eneo amblo ni uswahilini kabisa na maisha ambayo yanapatikana huko ni yale maisha ya chini. Huko hata ukiwa na miatano una uhakika wa kushiba, hukosi mihogo ya kutosha ukipata na maji basi siku yako inaisha safi kabisa. Msafara huo uligotea nje ya jumba la mwanamama Aurelia huko mtaani wengi wakimjua kama Bi Aisha. Lilikuwa ni jambo la kushangaza kwa watu wengi kuona raisi tena siku hiyo hiyo ambayo mkewe alikuwa ameuawa akiingia ndani ya eneo hilo tena kwa mwanamke ambaye muda mfupi alitoka kuwashangaza wananchi kwa kuwaonyesha kwamba yeye hakuwa kichaa bali alikuwa na akili zake timamu kabisa.
Nje ya jumba hilo walikutana na mlinzi mmoja tu akiwa na gobole mkononi ambaye hakuwaletea upinzani wowote ule, baada ya kuingia ndani ya jumba hilo walikutana na bwawa dogo la kuogelea ambalo lilikuwa kwenye hali ya usafi, mama huyo majira hayo ya jioni alikuwa ameketi pembezoni akiwa anapata kahawa bila wasiwasi hata ule ujio wa raisi haukumshtua kabisa wala kumpa papara aliendelea kunywa kahawa yake. Jambo hilo raisi alilihesabia kama dharau ila aliamua kuwa mtulivu kutaka kujua kitu kilichokuwa kinampa mwanamama huyo jeuri ya kutojali uwepo wa mtu mkubwa kama huyo kwenye taifa nyumbani kwake.

“Ni muda kidogo sijapokea taarifa zako ila mara ya mwisho nilipata habari kwamba una matatizo ya akili kiasi kwamba unazurura mtaani kama kichaa ila nimeshangaza baada ya kugundua kwamba wewe ni mzima wa afanya kabisa na hauonekani kama ni mtu mwenye shida hiyo ambayo wanadai kwamba unayo” raisi aliongea kwa hasira japo alijaribu kulizuia hilo hadharani mkuu wa majeshi akiwa pembeni yake. Raisi alimpa ishara kiongozi huyo wa jeshi awapishe kwani alikuwa na mazungumzo ya siri na mwanamama huyo.
“Nasikia mkeo amekufa alasiri ya leo, nasikitika kwa hilo lakini nikupe pole sana mheshimiwa”
“Unasikitika mke wangu kufa?”
“Ndiyo, ni mke wa raisi wa taifa langu ulitegemea nitafurahia kifo chake?”
“Kama ni wewe umeratibu hili basi lazima ufurahie” mheshimiwa alisogea kwenye kiti cha karibu akaketi alipokuwepo mwanamama huyo.
“Unahisi mimi hapa ambaye kwa sasa sina ramani yoyote ndiye ambaye naweza kuwaza huo ujinga wa kumuua mke wa raisi?”
“Huwa sipendi kuingilia ugomvi wa wanawake ila ni muda najua kwamba wewe na mke wangu hamkuwahi kuwa sawa, sijajua kuhusu historia yenu ya nyuma kwani hata mke wangu hakutaka kuniambia lolote kuhusu wewe ila inaonekana kuna mambo yenu binafsi hayakuwa sawa kwahiyo unaweza kunipa sababu ya msingi ya kunifanya nisiamini kama ni wewe ndiye umehusika kwenye hili?”
“Sina sababu ya kufanya hayo yote George”
“Unaonekana hata hauniheshimu kabisa kama raisi wa taifa hili!”
“Tangu siku ambayo nilijua kwamba wewe ni kibaraka tu ndiyo siku ambayo nilikufuta kama mtu ambaye unastahili heshima”
“Nakujua wewe Aurelia, wewe sio yule ambaye umekuwa unawaigizia watu kuwa kichaa, uliwahi kuwa kanali wa jeshi ila ghafla tu ukaja kuacha halafu baadae nikaja kusikia kwamba wewe ndiye mlezi wa Gavin habari ambazo zimekuwa zikikanushwa vikali sana. Hii ndiyo sababu una kiburi sana hata unapo niona mimi?”
“Mhhhhh mheshimiwa kwanini usiendelee kuwaongoza hao watanzania ambao wengi akili zao ni za kushikiwa? Raia hawana hata uwezo wa kuhoji, hawajui taifa lao linapelekwa wapi wapo wapo tu. Niliamua kukaa mbali na maisha hayo ambayo unayasema wewe lakini kwa sasa nimeamua kupumzika tu huku kama umekuja kuniua basi unaweza ukafanya hivyo na kuondoka kwa sababu naona kama unanipigia makelele tu hapa kwa kutafutiza sababu zisizo na msingi wowote ule” raisi alibaki anamwangalia mwanamke huyo ambaye yeye binafsi hakuwa anamuelewa vizuri.

“Kwahiyo ni kweli kwamba wewe ndiye mlezi wa Gavin?”
“Ndiyo George, yule mtoto nimemlea mimi hapa. Una tatizo juu ya hilo?”
“Naona kabisa mazungumzo yetu yanaenda kuwa marefu zaidi ya nilivyokuwa nafikiria mwanzo. Nilitaka siku moja kukutana na mlezi wake ili niyajue maisha yake yalikuwaje mpaka anajihisi kwamba anaweza kufanya kila anacho kitaka yeye? Leo nina uhakika nitayapat majibu sahihi”
“Au utafanya nini George?”
“Unajua kabisa siwezi kukuacha hai bila kupata kile ninakihitaji kwako”
“Wewe hapo ndo unataka kuniua mimi?”
“Aurelia hivi unaona kama ni maigizo sio?”
“Nisikilize George, wewe hapo Ikulu hauna lolote ambalo ni lako, kuna watu wamekuweka ili kufanikisha mambo yao na wote tunajua hilo. Kama unataka kuyajua majibu sahihi kwanini usiwaulize ambao wamekuweka hapo halafu usije siku nyingine tena nyumbani kwangu ukaanza kunitishia kuhusu kifo wewe ndiye utakuja kufa bila kujali kama ni raisi au vipi” mwanamama huyo alikuwa akijiamini mno, raisi alitoa bastola yake na kumuwekea mama huyo lakini jambo la kushangaza ni kwamba kuna mwanaume mmoja alitokea kwenye paa la nyumba hiyo na kumnyooshea raisi bastola kichwani pia hali ambayo ilipelekea walinzi wote kumnyooshea bastola mwanaume huyo pia.
“Aurelia una uhakika na hili ambalo unalifanya, unajua kijana huyu anahalalisha kuuawa kwako?”
“Mheshimiwa huyo hapo alipo hajali kuhusu kufa kwake lakini kama kuna kijana wako hata mmoja atampiga risasi tambua tu kwamba hakuna mtu hata mmoja kati yenu ambaye anaweza kutoka akiwa hai humu ndani. Wenzako wanaelewa ndiyo maana huwa wanakuja kistaarabu sio kwa sababu wewe ni raisi wa taifa basi unaweza kufanya lolote na kwa mtu yeyote yule hivyo kama hauna mazungumzo na mimi unaweza kwenda” alikuwa anazungumza na raisi wa nchi mithili ya mtu ambaye alikuwa anaongea na kibaka wa mtaani tu mwanamama huyo, raisi alibaki anacheka kwa ghadhabu lakini alimuona mkuu wa majeshi akimuonyesha ishara ya kukataa huenda yeye kuna mambo alikuwa anayajua kuhusu sehemu hiyo ndiyo maana alimpa ishara ya kutofanya kosa lolote.
“Nilijua tu kuna kitu hakipo sawa kuhusu wewe, nilijua tu lazima kuna mkono wako kwenye hili Aurelia. Naenda kufanya uchunguzi kwa sababu kama nitagundua kuna uhusika wako kwenye hili lazima ufe kwa mkono wangu”

“Jitahidi kuwa makini sana mheshimiwa raisi kwa sababu hasira siku zote huwa ni mtaji mbaya na wa hovyo wa watu wajinga na siku nyingine unapo enda kwenye nyumba za watu jitahidi kuwa mstaarabu na mkarimu ili wakupokee vizuri” alitoa elimu kwa raisi mwanamama huyo na kubeba kikombe chake kuelekea ndani, yaani mwananchi wa kawaida alikuwa anampa mgongo raisi kabla hajanyanyuka. Ile aibu na dharau ambayo aliipata kwa walinzi wake kutokana na tukio lile aliiihifadhi moyoni, asingeweza kuiacha iende hivi hivi. Alimuita mlinzi wake na kumpa maagizo ya siri kisha akahitaji waondoke eneo hilo huku akitoa maagizo ya kufanyika kwa maandalizi makubwa mno kwa ajili ya kumpumzisha mkewe kipenzi kwa heshima kubwa ili taifa lije kumkumbuka mwanamke huyo.



*********
Lile jambo la mchana halikuishia pale, raisi asingeweza kudhalilika namna ile halafu akaacha mambo yakaenda hivi hivi. Aliondoka pale huku akiwa anajua kabisa kama angefanya jambo la hovyo pale lazima kungekuwa na matatizo lakini pia hakuelewa sababu ya mwanamama yule kujiamini sana namna ile kiasi kwamba akadai hakuna mtu hata mmoja angeweza kutoka hai pale kama wangefanya jambo la kipumbavu. Alihisi kwamba huenda mwanamama yule alikuwa na watu wa siri ambao walikuwa wamelizunguka eneo lile hivyo alitakiwa kufanya mambo ambayo hakuna mtu angeweza kumshtukia.

Usiku alituma watu eneo lile, walikuwa ni wanaume maalumu ambao aliamini ila kazi lazima waifanye kwa usahihi. Alituma kikosi cha watu kumi wakiwa wanaongozwa na mlinzi wake kwa sababu alikuwa akimuamini mno, alihitaji watu hao waue kila ambaye wangemkuta kule lakini alikuwa akimtaka mwanamama yule akiwa hai na mzima wa afya kabisa kwa sababu kuna mengi ambayo alikuwa anataka kuyasikia kutoka kwake ndiyo maana amri yake ilikuwa ni kwamba mwanamama yule apelekwe kwake akiwa hai.

39 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
SONGA NAYO................

“Kwa hili vijana wanatakiwa kuingia kazini kwa masaa ishirini na manne kwa hali yoyote ile”
“Mr Savato”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Hivi yule mwanamama bado yupo hai?”
“Yupi?”
“Auleria”
“Nahisi bado ni mzima mheshimiwa, kwanini?”
“Kuna kipindi aliwahi kutoa tamko baya kumhusu mke wangu kupitia watu kadhaa nadhani unakumbuka hilo, kama yupo hai huenda kuna muunganiko wa yeye na hili labda?”
“Sidhani, ni mwanamke ambaye alishajikatia tamaa ya maisha tayari sasa inawezekana vipi afanye jambo kama hili?”
“Kumbuka yule amewahi kuwa kanali wa jeshi, ana nyenzo na ana uwezo wa kuwatafuta watu ambao wanaweza kuifanya kazi hii kwa niaba yake?”
“Mheshimiwa unahisi kuna sababu gani ya msingi ya kumfanya yeye afanye yote haya?”
“Hiyo sababu ndiyo ambayo mimi binafsi nahitaji kuifahamu kutoka kwake. Nataka kukutana na Aurelia”
“Hili sio wazo zuri mheshimiwa, kumbuka yule mama anaishi mtaani kule na huwezi kwenda ile sehemi kienyeji tu hivi”
“Hivi unajisikia unacho kiongea wewe? Tunazungumzia maisha ya mke wangu ambayo hayapo tena halafu bado unataka kuniaminisha kwamba natakiwa kutulia? Mr Savato hili jambo haliwezekani abadani”
“Nimekuelewa mkuu, unahitaji kitu gani?”
“Nahitaji Luca Gavin apatikane akiwa hai kwa sasa, kama imeshindikana kufa basi namtaka akiwa hai kabisa, nina mazungumzo naye marefu na maswali ambayo anapaswa kunijibu. Tumia mali yoyote, tumia rasilimali yoyote ile ila hakikisha huyu mtu anapatikana kwa sababu nahitaji kuja kumuua mwenyewe kwa mkono wangu”
“Sawa mheshimiwa” hakuwa na ubavu wa kumzuia tena, muda huo huo msafara uliandaliwa huku juu kukiwa na helikopta za kutosha za jeshi kudumisha ulinzi, mji ulikuwa umechafuka na kutapakaa ulinzi kila mahali huku msako mkali ukiwa unaendelea kila kona kuanzia kwenye lile jengo ambalo ndiko alikuwepo Sarah kuhakikisha muuaji wa mke wa raisi anapatikana mara moja.
Msafara wa raisi ulienda kuishia YOMBO VITUKA, eneo amblo ni uswahilini kabisa na maisha ambayo yanapatikana huko ni yale maisha ya chini. Huko hata ukiwa na miatano una uhakika wa kushiba, hukosi mihogo ya kutosha ukipata na maji basi siku yako inaisha safi kabisa. Msafara huo uligotea nje ya jumba la mwanamama Aurelia huko mtaani wengi wakimjua kama Bi Aisha. Lilikuwa ni jambo la kushangaza kwa watu wengi kuona raisi tena siku hiyo hiyo ambayo mkewe alikuwa ameuawa akiingia ndani ya eneo hilo tena kwa mwanamke ambaye muda mfupi alitoka kuwashangaza wananchi kwa kuwaonyesha kwamba yeye hakuwa kichaa bali alikuwa na akili zake timamu kabisa.
Nje ya jumba hilo walikutana na mlinzi mmoja tu akiwa na gobole mkononi ambaye hakuwaletea upinzani wowote ule, baada ya kuingia ndani ya jumba hilo walikutana na bwawa dogo la kuogelea ambalo lilikuwa kwenye hali ya usafi, mama huyo majira hayo ya jioni alikuwa ameketi pembezoni akiwa anapata kahawa bila wasiwasi hata ule ujio wa raisi haukumshtua kabisa wala kumpa papara aliendelea kunywa kahawa yake. Jambo hilo raisi alilihesabia kama dharau ila aliamua kuwa mtulivu kutaka kujua kitu kilichokuwa kinampa mwanamama huyo jeuri ya kutojali uwepo wa mtu mkubwa kama huyo kwenye taifa nyumbani kwake.

“Ni muda kidogo sijapokea taarifa zako ila mara ya mwisho nilipata habari kwamba una matatizo ya akili kiasi kwamba unazurura mtaani kama kichaa ila nimeshangaza baada ya kugundua kwamba wewe ni mzima wa afanya kabisa na hauonekani kama ni mtu mwenye shida hiyo ambayo wanadai kwamba unayo” raisi aliongea kwa hasira japo alijaribu kulizuia hilo hadharani mkuu wa majeshi akiwa pembeni yake. Raisi alimpa ishara kiongozi huyo wa jeshi awapishe kwani alikuwa na mazungumzo ya siri na mwanamama huyo.
“Nasikia mkeo amekufa alasiri ya leo, nasikitika kwa hilo lakini nikupe pole sana mheshimiwa”
“Unasikitika mke wangu kufa?”
“Ndiyo, ni mke wa raisi wa taifa langu ulitegemea nitafurahia kifo chake?”
“Kama ni wewe umeratibu hili basi lazima ufurahie” mheshimiwa alisogea kwenye kiti cha karibu akaketi alipokuwepo mwanamama huyo.
“Unahisi mimi hapa ambaye kwa sasa sina ramani yoyote ndiye ambaye naweza kuwaza huo ujinga wa kumuua mke wa raisi?”
“Huwa sipendi kuingilia ugomvi wa wanawake ila ni muda najua kwamba wewe na mke wangu hamkuwahi kuwa sawa, sijajua kuhusu historia yenu ya nyuma kwani hata mke wangu hakutaka kuniambia lolote kuhusu wewe ila inaonekana kuna mambo yenu binafsi hayakuwa sawa kwahiyo unaweza kunipa sababu ya msingi ya kunifanya nisiamini kama ni wewe ndiye umehusika kwenye hili?”
“Sina sababu ya kufanya hayo yote George”
“Unaonekana hata hauniheshimu kabisa kama raisi wa taifa hili!”
“Tangu siku ambayo nilijua kwamba wewe ni kibaraka tu ndiyo siku ambayo nilikufuta kama mtu ambaye unastahili heshima”
“Nakujua wewe Aurelia, wewe sio yule ambaye umekuwa unawaigizia watu kuwa kichaa, uliwahi kuwa kanali wa jeshi ila ghafla tu ukaja kuacha halafu baadae nikaja kusikia kwamba wewe ndiye mlezi wa Gavin habari ambazo zimekuwa zikikanushwa vikali sana. Hii ndiyo sababu una kiburi sana hata unapo niona mimi?”
“Mhhhhh mheshimiwa kwanini usiendelee kuwaongoza hao watanzania ambao wengi akili zao ni za kushikiwa? Raia hawana hata uwezo wa kuhoji, hawajui taifa lao linapelekwa wapi wapo wapo tu. Niliamua kukaa mbali na maisha hayo ambayo unayasema wewe lakini kwa sasa nimeamua kupumzika tu huku kama umekuja kuniua basi unaweza ukafanya hivyo na kuondoka kwa sababu naona kama unanipigia makelele tu hapa kwa kutafutiza sababu zisizo na msingi wowote ule” raisi alibaki anamwangalia mwanamke huyo ambaye yeye binafsi hakuwa anamuelewa vizuri.

“Kwahiyo ni kweli kwamba wewe ndiye mlezi wa Gavin?”
“Ndiyo George, yule mtoto nimemlea mimi hapa. Una tatizo juu ya hilo?”
“Naona kabisa mazungumzo yetu yanaenda kuwa marefu zaidi ya nilivyokuwa nafikiria mwanzo. Nilitaka siku moja kukutana na mlezi wake ili niyajue maisha yake yalikuwaje mpaka anajihisi kwamba anaweza kufanya kila anacho kitaka yeye? Leo nina uhakika nitayapat majibu sahihi”
“Au utafanya nini George?”
“Unajua kabisa siwezi kukuacha hai bila kupata kile ninakihitaji kwako”
“Wewe hapo ndo unataka kuniua mimi?”
“Aurelia hivi unaona kama ni maigizo sio?”
“Nisikilize George, wewe hapo Ikulu hauna lolote ambalo ni lako, kuna watu wamekuweka ili kufanikisha mambo yao na wote tunajua hilo. Kama unataka kuyajua majibu sahihi kwanini usiwaulize ambao wamekuweka hapo halafu usije siku nyingine tena nyumbani kwangu ukaanza kunitishia kuhusu kifo wewe ndiye utakuja kufa bila kujali kama ni raisi au vipi” mwanamama huyo alikuwa akijiamini mno, raisi alitoa bastola yake na kumuwekea mama huyo lakini jambo la kushangaza ni kwamba kuna mwanaume mmoja alitokea kwenye paa la nyumba hiyo na kumnyooshea raisi bastola kichwani pia hali ambayo ilipelekea walinzi wote kumnyooshea bastola mwanaume huyo pia.
“Aurelia una uhakika na hili ambalo unalifanya, unajua kijana huyu anahalalisha kuuawa kwako?”
“Mheshimiwa huyo hapo alipo hajali kuhusu kufa kwake lakini kama kuna kijana wako hata mmoja atampiga risasi tambua tu kwamba hakuna mtu hata mmoja kati yenu ambaye anaweza kutoka akiwa hai humu ndani. Wenzako wanaelewa ndiyo maana huwa wanakuja kistaarabu sio kwa sababu wewe ni raisi wa taifa basi unaweza kufanya lolote na kwa mtu yeyote yule hivyo kama hauna mazungumzo na mimi unaweza kwenda” alikuwa anazungumza na raisi wa nchi mithili ya mtu ambaye alikuwa anaongea na kibaka wa mtaani tu mwanamama huyo, raisi alibaki anacheka kwa ghadhabu lakini alimuona mkuu wa majeshi akimuonyesha ishara ya kukataa huenda yeye kuna mambo alikuwa anayajua kuhusu sehemu hiyo ndiyo maana alimpa ishara ya kutofanya kosa lolote.
“Nilijua tu kuna kitu hakipo sawa kuhusu wewe, nilijua tu lazima kuna mkono wako kwenye hili Aurelia. Naenda kufanya uchunguzi kwa sababu kama nitagundua kuna uhusika wako kwenye hili lazima ufe kwa mkono wangu”

“Jitahidi kuwa makini sana mheshimiwa raisi kwa sababu hasira siku zote huwa ni mtaji mbaya na wa hovyo wa watu wajinga na siku nyingine unapo enda kwenye nyumba za watu jitahidi kuwa mstaarabu na mkarimu ili wakupokee vizuri” alitoa elimu kwa raisi mwanamama huyo na kubeba kikombe chake kuelekea ndani, yaani mwananchi wa kawaida alikuwa anampa mgongo raisi kabla hajanyanyuka. Ile aibu na dharau ambayo aliipata kwa walinzi wake kutokana na tukio lile aliiihifadhi moyoni, asingeweza kuiacha iende hivi hivi. Alimuita mlinzi wake na kumpa maagizo ya siri kisha akahitaji waondoke eneo hilo huku akitoa maagizo ya kufanyika kwa maandalizi makubwa mno kwa ajili ya kumpumzisha mkewe kipenzi kwa heshima kubwa ili taifa lije kumkumbuka mwanamke huyo.



*********
Lile jambo la mchana halikuishia pale, raisi asingeweza kudhalilika namna ile halafu akaacha mambo yakaenda hivi hivi. Aliondoka pale huku akiwa anajua kabisa kama angefanya jambo la hovyo pale lazima kungekuwa na matatizo lakini pia hakuelewa sababu ya mwanamama yule kujiamini sana namna ile kiasi kwamba akadai hakuna mtu hata mmoja angeweza kutoka hai pale kama wangefanya jambo la kipumbavu. Alihisi kwamba huenda mwanamama yule alikuwa na watu wa siri ambao walikuwa wamelizunguka eneo lile hivyo alitakiwa kufanya mambo ambayo hakuna mtu angeweza kumshtukia.

Usiku alituma watu eneo lile, walikuwa ni wanaume maalumu ambao aliamini ila kazi lazima waifanye kwa usahihi. Alituma kikosi cha watu kumi wakiwa wanaongozwa na mlinzi wake kwa sababu alikuwa akimuamini mno, alihitaji watu hao waue kila ambaye wangemkuta kule lakini alikuwa akimtaka mwanamama yule akiwa hai na mzima wa afya kabisa kwa sababu kuna mengi ambayo alikuwa anataka kuyasikia kutoka kwake ndiyo maana amri yake ilikuwa ni kwamba mwanamama yule apelekwe kwake akiwa hai.

39 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
Salute
 
Back
Top Bottom