Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE
SONGA NAYO................
Achana na kitu kinaitwa pesa bwana! Walisema wahenga, pesa inanunua nafsi na mioyo ya watu, pesa zinawabadilisha watu, pesa inafanya watu wanakuwa na tamaa na ushetani ndani yao ila Lucas aliona kwamba kwake anafanya kitu sahihi. Yale maisha ambayo aliyaishi huko nyuma bado yalikuwa yametawala kwenye kichwa chake, alihitaji jina lake liimbwe kila mtaa na kila kona ya nchi, licha ya wakati huo kuwa na pesa nyingi lakini hazikumfanya kuimbwa kwa sababu ni wachache walikuwa wakilitaja jina lake mara kwa mara na lengo lake kubwa lilikuwa ni kujulikana kila pembe ya nchi na Afrika kwa ujumla ndiyo maana akahitaji kutawala biashara nzima ya bosi wake.

Ndani ya mitaa ya Peenuga walikuwa wanamuogopa Lucas, Lucas ndiye alikuwa mkono wa kulia wa mtu ambaye alikuwa msambazaji mkuu wa madawa hilo eneo na ndiye ambaye alikuwa akiwalipa watu hao pesa nyingi hivyo kama wangecheza vibaya na Lucas basi ingekula kwao. Alihakikisha hawamuogipi tu bali kumheshimu, hilo alilitambua mapema hivyo alikuwa anaishi nao vizuri na kuwapa misaada mikubwa kiasi kwamba wakampenda. Lucas alianza kuhamisha pesa nyingi ambazo zilikuwa zimefichwa kwenye mataifa mbalimbali duniani kuzileta Tanzania kwa siri, akaunti nyingi mpya za benki zilikuwa kwa jina lake hivyo hizo hazikuwa shida kwake kabisa kuziweka chini ya mikono yake.
Alijua kabisa kwamba jambo hilo linaweza kuja kumletea shida sana hapo baadae hivyo ni mapema alikuwa amemshauri Gustavo wafungue kampuni kubwa ya madini ili serikali isije ikaanza kuhoji siku siku moja kuhusu uhalali wa hizo pesa zao ambazo zilikuwa nyingi mno. Gustavo bila kujua lengo la kijana wake aliona kwamba ni pointi ya msingi kwani aliamini hata siku moja angekuja kukamatwa bado pesa zake zingekuwa salama kwa sababu zingeonekana kumilikiwa kihalali ndani ya nchi ya Tanzania na Lucas ambazo baadae zingekuja kumsaidia kumtoa gerezani hata kwa kuhonga.
Gustavo alijisahaulisha sehemu moja kwamba wanadamu hawaaminiki linapokuja suala zima la pesa, zile noti huwa ni mbaya sana mtu anapokuwa nazo kwenye mkono wake halafu anajua baada ya muda anatakiwa kuzipeleka kwa mtu mwingine, kwahiyo anafanyaje? Hapo yupo tayari kufanya lolote ili ziendelee kuwa zake tu mwenyewe. Gustavo akawekwa kwenye kikaango ili aweze kuuawa sasa mchezo ukabaki kwamba anauawaje? Kumbuka Gustavo alikuwa ni mtu mzito na alikuwa anajulikana kila pembe ya dunia na wauzaji wenzake wa madawa ya kulevya hivyo hata kifo chake kingeleta mjadala mrefu, Lucas alilijua hilo mapema.
Mauaji ya Gustavo yalipangwa kufanyika ndani ya Sinaloa, kwenye taifa lake mwenyewe. Watu ambao walitakiwa kumuua ni DEA agents ambao walikuwa wanamtafuta kwa muda mrefu yaani Drug Enforcement Administaration agents lakini alitumika mtu mmoja tu kumuua, agent Rakeem. Mwanaume huyo alikuwa ameshirikishwa na Lucas mwenyewe ambaye alimlipa pesa nyingi mno ili kuhakikisha kwamba anafanikiwa kumuua Gustavo kwa namna yoyote ile kwa sababu jambo hilo lingempa sifa kubwa kwa serikali yake ya Marekani kufanikiwa kumuondoa gwiji huyo wa madawa ya kulevya ambaye walimsaka kwa miaka mingi bila mafanikio.
Siku zote hatari ipo kwenye udhaifu wa mtu na ndicho ambacho kilikuwa kinafanyika, Gustavo kila awapo kwenye viunga vya Mexico alikuwa akienda sehemu moja ambayo alikuwa anaishi mwanamke mrembo sana Latina, huyo alikuwa mwanamke wake wa muda mrefu na kila awapo huko mara nyingi alikuwa akijiachia na mwanamke huyo kula raha na kupata mahaba ila hakujua kama hatari yake ilikuwa hapo. Kwa sababu alikuwa akienda kwa siri sana eneo hilo hakuhitaji kuwa na ulinzi huko kwa sababu ingejulikana uwepo wake hivyo alikuwa akiingia mwenyewe na gari yake sehemu ambayo alikuwa anaishi mwanamke huyo ili asigundulike na mtu yeyote yule.
Hiyo ndiyo nafasi pekee ambayo aliitumia Rakeem kuweza kumuua bwana huyo kwa kumpiga risasi nyingi kichwani. Taarifa hiyo iliushtua umma na dunia kwa ujumla lakini ilimpa umaarufu Rakeem kwa kumfanya awe shujaa wa kufanikisha kazi ambayo iliwachukua muda mrefu kupambana nayo. Biashara nyingi za dawa za kulevya Mexico zilisimama kwa muda kwa sababu maajenti walitapakaa kila sehemu kuhitaji kuujua mfumo mzima wa Gustavo lakini hawakuweza kwa sababu mhusika alikuwa amekufa na Rakeem hakuwa akimjua mtu ambaye alimpa kazi, yeye alimpatia pesa tu na kudai anampa msaada wa kumpata mtu huyo ambaye alikuwa akiangamiza kizazi kwa dawa za kulevya ila katu hakuwahi kujitambulisha kabla.
Gustavo alikufa ghafla hivyo mali zake zote kwa wakati huo zilikuwa zinaelea kwenye mikono ya Lucas ambaye alishikilia kila kitu, mwanaume huyo kila biashara na pesa ambayo ilikuwa ya Gustavo ikabaki kuwa ya kwake yeye ndipo akarudi Tanzania haraka kwa watu wake wa mitaa ya Peenuga. Kusikia kifo cha Gustavo ilikuwa habari mbaya kwa wengi kwa sababu ndiye ambaye kwa kiwango kikubwa alikuwa anawahakikishia kuishi vizuri hivyo kutokuwepo kwake ilikuwa ni hatari ya kukosa mlo kwa wengi tumaini lao la pekee likabaki kwa Lucas mwanaume ambaye alichagua kuwa fala kwa miaka kadhaa akiwa anautengeneza ulimwengu wake.
Lucas aliwahakikishia watu wake kwamba kila kitu kitaenda sawa hata zaidi ya mara ya kwanza, aliwaahidi watu hao wataishi vizuri bila shida na maisha yatakuwa mazuri zaidi ya mwanzo. Lucas alikuwa amejitengenezea heshima kubwa tangu mwanzo kwa sababu aliishi nao vizuri watu hao, kuwahakikishia maisha mazuri kwao hawakuwa na muda wa kuhoji tena juu ya kilicho tokea kwa sababu Gustavo ilionekana kwamba kilicho muua ni tamaa zake mwenyewe ndipo Lucas akasimama rasmi kama kiongozi wa watu hao akiwa na pesa nyingi mkononi huku hata huko Mexico biashara ikiwa inategemea mzunguko wake yeye maana soko zima lilikuwa kwenye mikono ya Gustavo hivyo kama wangecheza naye vibaya basi ingekula kwao.
Lucas alitengeneza ulinzi mkali wa kila sehemu ambayo alikuwa anaenda, Lucas akaanza kuonyesha jeuri yake ya pesa hadharani. Kwa makadirio ni kwamba kwa wakati huo alikuwa na pesa za kimarekani zaidi ya bilioni hamsini ambazo kwa bara zima la Afrika alidaiwa kuwa ndiye tajiri namba moja kuwahi kutokea ndani ya bara lililo barikiwa kila kitu pamoja na watu wajuaji wa kila kitu. Pesa za Lucas ndizo ambazo zilifanya aanze kuimbwa kila mtaa, kila kijiji, mji, nchi na hata nje ya mipaka ya Tanzania. hali hiyo ilifanya mamlaka kuanza kumtolea jicho la karibu kwa sababu hapo kunakuwa na ulaji lakini kujua uhalali wa mtu kumiliki pesa zote hizo.
Kulikuwa na stori kuhusu biashara yake ya madawa ya kulevya lakini hakuna ambaye alikuwa ana uwezo wa kuithibitisha hadharani, waligundua kwamba ana kampuni kubwa ya madini na ndiyo ambayo ilikuwa ikimpatia pesa nyingi bwana Lucas. Mitaa ilimpenda sana kwa sababu alisaidia mno jamii ya watu maskini huku pesa zikiwa zinaingia mabilioni kila siku mpaka alipo amua kuibadilisha mitaa hiyo ya Penuuga na kujenga LUCAS VILLA, mji wake mwenyewe.


**************
LUCAS VILLA
Biashara yake ilizidi kushamiri kila kulipokucha, Lucas alikuwa na utajiri ambao ulianza kuwatisha mpaka wanasiasa nchini, akawa anaogopwa kuliko hata raisi wa nchi hivyo hatari ikaonekana mbele lakini nani angejali zinapotumika pesa? Hakuna muda alikuwa na muda na mambo mengine, wanasiasa wakawa wanakwapua pesa zake na kuwa chini yake, wakawa watumwa wake, kukawa hakuna sheria ambayo inaweza kukinzana na Lucas tena, mwanaume huyo akaitia nchi kwenye mkono wake ndipo akaamua kuujenga mji wake ili kuweka heshima na kuacha kumbukumbu hata siku asipo kuwepo.
Mji haukujengwa mbali bali ile ile mitaa ya Peenuga ambayo ndiyo ilimpa jina na pesa ndiyo aliamua kuibadilisha na kuifanya kuwa jiji la kifahari kuwahi kutokea nchini Tanzania. Peenuga ilifumuliwa upya, mitaa yote ilivunjwa yakaanza kushushwa majengo ya kifahari ndani ya ile sehemu chini ya usimamizi wa Lucas. Peenuga haikuwa mitaa michafu na ya kukera tena, peenuga ikabadilika na kuwa mji wa kisasa na wa kuvutia, ulipo kamilika ukaitwa LUCAS VILLA. Ukawa ni mji wake yeye, watu waliishi kwa sheria zake yeye, ukawa mji wa kifahari ndani ya Afrika ambapo kila mtu akawa anatamani kuweza kufika na kula maisha huko lakini hakuna mtu alikuwa anaruhusiwa kuingia bila ruhusa yake yeye mwanaume yule kutoka Tanga.
Wananchi wa mitaa ile ambao aliwakuta aliwapa maisha bora, akawapa pesa za bure wakawa wanaishi kama wapo peponi, hakuna mtu alikuwa anataka kusikia mtu akimuongelea vibaya Lucas, wangekuua kabla hujafika hata hatua mbili kwa sababu walikuwa wakimtukuza, ni yeye ambaye aliwapa maisha bora na kubadilisha maisha yao hivyo hawakuwa tayari kumpoteza ili warudi kwenye maisha ya mwanzo hususani wakiwa wanaelewa kabisa kwamba serikali haikuwa na muda nao kabisa.
Mji huo ukapambwa kwa kila aina ya maisha safi, ni wanasiasa wachache tu ambao walikuwa na ruhusa yake ndio ambao walikuwa wanaruhusiwa kwenda huko kula maisha. Lucas akawa gumzo lakini kwenye moyo wake bado alikuwa ana mawazo, hakuwa amewahi kusahau kule ambako alitoka zamani kwenye maisha magumu. Kila alipokuwa anawaza kuhusu yale maisha basi kumbukumbu zilikuwa zinampeleka mpaka pale kwenye mto ambapo siku ya mwisho alifanya maamuzi magumu ya kumtosa mwanamke aliye mpenda sana kwa sababu tu hakuwa na pesa.
Moyo wake bado haukuwa umefanya maamuzi ya kumpenda mwanamke mwingine, alikuwa akitembea na picha ya mwanamke yule Linda kila sehemu ambayo alikwenda lakini kwenye nafsi yake aliapa kutokuja kutaka kukutana na mwanamke huyo tena kwenye maisha yake yote. Alijua kabisa kukutana naye kungezalisha mambo mengine na asingekubali kumuona akiwa na damu ya mwanaume mwingine kitu ambacho kingemuuma sana, nadhiri yake ikawa ni kutokutana naye tena mpaka siku anatoweka duniani. Alijua kabisa kwa mali ambazo alikuwa nazo angehitaji kuwa na mke lakini hakuelewa angempata wapi mke kwa sababu wanawake wote walikuwa wanazitamani mali zake tu na yeye alihitaji kupata mwanamke ambaye angekuwa mama watoto wake ambaye hatafahamika hata kwa walimwengu.
Akiwa kwenye mawazo hayo Lucas, siku isiyo na jina alipata ugeni kwenye mji wake, ugeni kutoka ngazi za juu serikalini. Waziri mkuu alikuwa amemtembelea bwana huyo kwa mwaliko wake mwenyewe ambapo alihitaji kuzungumza mambo kadhaa na waziri mkuu huyo ili aweze kutoa sehemu ya utajiri wake kuwasaidia watanzania. Waziri mkuu wakati anaenda huko aliongozana na mtoto wake wa kike Glady. Glady alikuwa ni mwanamke mrembo sana asiye mwongeaji, ni muda mchache tu alikuwa amerudi kutoka masomoni baada ya kumaliza, hakuonekana kuwa mtu mwenye furaha ndiyo maana baba yake aliongozana naye kwenda kwenye hilo eneo ili angalau mwanae aweze kuchangamsha akili na kubadili mawazo yake.

Ishirini na nne inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO
SONGA NAYO................
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwenye maisha yao kukutana, Lucas na Glady ila ndiyo yale huwa wanasema mapenzi sehemu ya kwanza. Kila mmoja baada ya kumuona mwenzake walijua kabisa kwamba wao wanatakiwa kutengeneza familia moja, hakuna ambaye alimwambia mwenzake moja kwa moja ila nafsi zao na macho yao yalikuwa yanaongea kwa hisia kali. Waziri mkuu alifanya kikao cha masaa mawili na bwana Lucas na kumpa maamuzi ya serikali kwamba serikali haipo tayari kuruhusu yeye kufanya yale hadharani kwa sababu wanahisi pesa zake ni za madawa ya kulevya hivyo serikali iliridhia yeye kufanya jambo hilo lakini asitumie njia ya wazi moja kwa moja kutoa hiyo misaada yake.
Hakuwa na kipingamizi Lucas kwa sababu alikuwa anatamani kuisaidia jamii na alijua kabisa jamii ilikuwa na watu wengi ambao walikuwa na uhitaji mkubwa na msaada wake. Waziri mkuu baada ya kumaliza mkutano wake alizungushwa kwenye maeneo ya mhimu ndani ya ule mji ambayo yalikuwa yakivutia mno hali ambayo ilimfurahisha hasa baada ya kumuona mwanae akianza kutabasamu bila shaka aliyapenda yale mazingira. Glady alimtaka baba yake arudi tu yeye angebaki kule kwa muda ili aweze kufurahia mazingira, baba yake alionekana kusita kufanya maamuzi ya kumruhusu na alikuwa sahihi, sio rahisi kumuacha mwanao wa pekee kwenye mikono ya muuza madawa ya kulevya tena mwenye utajiri wa kutisha namna ile, lazima angekuwa na maadui wengi.
Lakini Lucas alimhakikishia usalama wa binti yake kwa asilimia miamoja, waziri mkuu hakuwa na kipingamizi kwa sababu alijali zaidi furaha ya mwanae na ndipo akamruhusu binti yake wa pekee Glady kubaki ndani ya lile eneo ili afurahi. Ujio wa waziri mkuu ndani ya lile eneo na mwanae Glady, ule ndio ulikuwa mwanzo wa historia mpya ya maisha ya Lucas, ule ndio ulikuwa mwanzo wa safari mpya ya maisha ya Gavin Luca. Wawili wale taratibu walianza kuwa karibu sana, wawili wale bila shaka iliandikwa kwamba ni lazima wangekuja kuwa pamoja na kufanya makubwa wakiwa karibu, wawili wale taratibu walianza kuzama kwenye mapenzi mazito, wawili wale wakaikamilisha asili kwa kuamua kuwa mwili mmoja.
Mapenzi yao yalileta furaha mpya kwenye uso wa Lucas, hakuwa mtu wa kuishi kwa mawazo tena kwa sababu aliamini siku chache mbeleni angeenda kuwa na familia yenye furaha kubwa hivyo hata yeye alitakiwa kuwa mwenye furaha. Lucas na Glady alipendana sana kiasi kwamba taarifa zikamfikia waziri mkuu kuhusu mwanae na yule bwana muuza madawa ya kulevya, licha ya Lucas kuwa na utajiri mkubwa kiasi kwamba kila mtu alitamani mwanae apate bahati ya kuolewa naye lakini waziri mkuu alikuwa anasita kufanya maamuzi. Aliipenda furaha ya mwanae ile mtu ambaye alikuwa anahitaji kuwa naye alikuwa ni mtu hatari sana, mamlaka zilikuwa zimeaanza kumfuatilia kwa ukaribu, alijua kabisa ingekuja kufika wakati ambao mtu huyo angekuja kuingia kwenye mikono ya serikali akaishia kuuawa ama kupoteza kila kitu hali ambayo ingemfanya mwanae kuingia kwenye matatizo mazito ama kubaki mjane, hilo likamtisha.
Nani wa kulizuia penzi likichipua? Hakuwa na uwezo wa kumzuia mwanae kuwa na mtu ambaye anamtaka, huo ndio ulikuwa msimamo wa Glady, alikuwa tayari kufa lakini sio kuishi mbali na Lucas. Mwanamke huyo aliteseka kwa muda mrefu kuisaka furaha, alikuja kuipata halafu baba yake anataka kuwa kikwazo tena? Hakuwa tayari Glady hivyo baba yake akapewa chaguo, akubali ama ampoteze mwanae ndipo kwa mara ya kwanza waziri mkuu akatoa baraka wawili hao kuweza kuoana kwa sharti. Alijua kabisa kwamba yeye alikuwa ndiye mratibu mkuu wa serikali, kuonekana kwamba aliruhusu mwanae kuolewa na muuzaji wa dawa za kulevya ambaye huenda yeye ndiye alitakiwa kumshughulikia ingemletea sifa mbaya sana kwa jamii kiasi kwamba hata ile nafasi yake angeipoteza, akawataka watu hao waoane kwa siri yaani asije akajua mtu yeyote yule kutoka nje kwamba wawili hao ni mume na mke.
Hilo halikuwa shida sana kwao, wawili hao wakaoana kwa siri wakawa mume na mke huku ulimwengu ukiwa haulewi lolote ambalo lilikuwa linaendelea. Glady alijua kabisa aina ya mwanaume ambaye aliolewa naye ila hakujali, alichojali yeye ni kwamba alimpenda bwana huyo ambaye naye alionyesha kumjali na kumpenda isivyo kawaida, hayo mengine hayakumhusu. Ukurasa mpya ukafunguka kwa Lucas kama kiongozi wa familia yake mwenyewe, Lucas alifanya mambo makubwa ya kutisha, kuna watu ambao walikuwa wanaingia kwenye njia yake aliwaua ili kuweka mfano kwa wengine, wanasiasa ambao walikuwa wanahitaji kumpoteza kwenye ile nafasi yake aliwaua ikafikia hatua akawa anaogopwa mpaka na wanyama ambao walifundishwa uelewa kama mbwa mtaani.
Jina lake lilikuwa zaidi ya lile jina la Osama Bin Laden, lilikuwa likisikika mahali basi watu watakosa amani lakini watu wake walimpenda mno, aliwapa kila walicho kitaka hata wananchi wa Tanzania waliliimba jina lake kama shujaa wa nchi kwa sababu aliwasaidia kila walipo mhitaji, bwana yule akaendelea kuwa na utajiri wa kutisha mpaka ilipofikia hatua ikasemekana kwamba ana utajiri wa dola za kimarekani zaidi ya bilioni miamoja. Ni pesa ambazo hata kama angesema aache kufanya kazi ale maisha yake yote, wangekula mpaka wajukuu zake na bado wasingeweza kuzimaliza.
Mtandao wake wa dawa za kulevya uliendelea kuwa mkubwa, serikali haikuwa tayari kuendelea kumfumbia macho tena mwanaume yule wakaanza kumuweka kwenye ramani ili waje watembee na kichwa chake kama sio yeye mwenyewe wakati huo mkewe alikuwa mjamzito. Lucas alijua kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea kuhusu yeye kutafutiwa mazingira ya kupotezwa hivyo naye akawa makini isivyokuwa kawaida kwa kila ambacho alikuwa anakifanya na kila hatua ambayo alikuwa anaipiga.


TANZANIA INVESTIGATORY GROUP OF INTELLIGENCE (TIGI)
Hili ni shirika letu la kijasusi nchini, shirika hili kipindi Lucas anaingia kwenye utawala wa kuwa tajiri namba moja Afrika lilikuwa limepoteza mvuto wake tayari, lilipoteza mvuto kabisa kwa sababu lilionekana kwamba lipo kwa ajili ya kuwalinda wanasiasa na maslahi yao. Halikuwa pale kwa ajili ya maslahi ya wananchi na taifa, bali lilikuwa kwa ajili ya kuwalinda wanasiasa, vyama vyao na matumbo yao. Watu walikuwa wakipiga kelele na kulitaka lifutwe tu kwa sababu halikuwa na maana yoyote kuendelea kuwepo lakini baadhi ya ambao walionekana kupigia kelele zaidi suala hilo walitafutwa na kuuawa huku wengine wakiishia kufungwa kwenye magereza ya siri kama haya ambayo sisi tupo.
Jambo hilo lilileta ukakasi kwa wananchi, kama unavyojua taarifa huwa hazipotei lazima zitakuwepo tu hata kama wakifanya siri hivyo wananchi wakaanza kuishi kwa mashaka na kuwaogopa watu ambao walikuwa ndani ya shirika hilo kama ugonjwa na njaa kali kama sio umaskini. Lilikuja kupotea kabisa baada ya mtoto wa kigogo mmoja serikalini kumbaka mwanafunzi hadharani watu wakiona lakini shirika hilo lilikanusha kwamba kijana huyo hakufanya tukio hilo, jambo hilo lilipoteza imani hata ile ndogo ambayo ilibakia kwa wananchi kiasi kwamba wakawa wanalidharau sana mpaka wakalipotezea kama halipo wakawaacha watu hao wafanye kile ambacho wanakitaka wao.
Wananchi wakidharau na kukisusia kitu maana yake hakina umuhimu tena wa kuwepo, walipoteza mvuto vibaya mpaka raisi ambaye alikuwa madarakani kipindi kile alipo maliza mhula wake ndipo akaingia raisi mpya ambaye alihitaji kubadili mtazamo wa shirika hilo ili apate imani kwa wananchi kwani aliona ndiyo sehemu pekee ya kuweza kuwashika wakampa imani zao zote. Alicho kifanya ni kufumua fumua uongozi kwenye shirika hilo na kumteua mkurugenzi mpya bwana Jaali Chitundu, kuna nadharia huwa zinasema kwamba bwana huyu alitengenezwa ili akampoteze kabisa Lucas, sasa kwanini?
Raisi wa kipindi kile Natron Vinza inadaiwa kwamba baada ya kuchaguliwa tu alifanya kikao cha siri na kigumu na bwana Lucas, raisi huyo alimtaka mwanaume huyo ampatie robo ya utajiri wake ili aweze kumlinda kutoka kwa mtu yeyote yule, yaani ofisi ya Ikulu itumike kama ofisi ya ziada ya Lucas lakini mwanaume huyo aligoma kabisa kuhusu jambo hilo na kudai kwamba hakuwa tayari kabisa kuweza kutoa mali zake ili kumpatia mtu huyo. Mtafaruko wao ulipelekea wawili hao kupishana kauli kiasi kwamba wakaanza mpaka kutishiana kuhusu maisha jambo ambalo lilipelekea Lucas kumpa onyo raisi huyo kwamba kama angeendelea kumpa hivyo vitisho basi angemtoa Ikulu kwa kumuua, Natron kwake suala lile alichukulia kama dharau, akaondoka akiwa na kinyongo kikali moyoni ndiyo sababu kubwa akahitaji kulitumia shirika lile kuweza kumdondosha na kumpoteza kabisa Lucas.

Majasusi kadhaa walipandikizwa kwenye mfumo wa biashara wa Lucas bila yeye mwenyewe kujua kwa sababu hakuwa akiwafahamu, waliingia kama watu ambao walikuwa wanausaka utajiri kwa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya. Watu hao waliifanya kazi yao kwa ukubwa mpaka wakakamilisha taarifa nyingi sana juu ya mtu huyo na waliona kwamba ilikuwa ni nafasi kubwa kwao kuweza kuirudisha heshima ya shirika lao kama wangefanikiwa kumdondosha mwanaume huyo. Jina la Lucas lilianza kutiwa dosari, raisi akawa anatumia watu wasio julikana kuwaweka wazi wananchi kuhusu ushetani na mambo ya nyuma ya pazia ya Lucas na jinsi anavyo husika kwa kiasi kikubwa kuteketeza kizazi cha watanzania.
Ishirini na tano inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA
SONGA NAYO................
Ilikuwa imebakia hatua ndogo sana kufanikiwa kumdondosha kabisa Lucas pale alipokuwepo lakini ilishindikana baada ya jambo kubwa kuukumba Ulimwengu. Dunia iliingia kwenye vita baridi, vita vikaathiri uchumi kuanzia soko la dunia na kila sehemu, hali ikaanza kuwa mbaya na miongoni mwa nchi ambazo ziliathirika sana ilikuwa ni Tanzania kwa sababu inategemea zaidi kuagiza kuliko kutoa vitu vyake nje. Vitu vilikuwa ghali sana kuvipata, ikapelekea benki ya nchi kuanguka vibaya, hali ikawa ngumu, wananchi wakaanza kulalamika kila upande wa nchi, ni matajiri tu ambao walikuwa wana uwezo wa kuzimudu gharama za maisha.
Vilio vilitanda kila kona, kila mtaa, kila wilaya na kila mkoa, watu walimlilia raisi aweze kuwasaidia, hakuwa na huo uwezo wa kuwasaidia mamilioni ya watu wakati hata akiba ya benki kuu ilikuwa ya kusua sua. Licha ya kubana matumizi lakini bado haikutosha kuifanya hali iwe kawaida kama mwanzo, sasa nchi ikawa inaingia kwenye njaa kali mno na hali mbaya, hakuna aliyejali kuhusu mipango miji tena. Watu walijisaidia popote pale, takataka zingezagaa kila sehemu, watu wakaanza kuuana kugombania mikate na kazi, wababe ndio ambao walikuwa na nafasi ya kuweza kuwa na uhakika wa kujaza matumbo yao kwa wanyonge ikawa ni tatizo jipya.
Wananchi wakawa hawaelewi ni nani angewapa msaada na huko kwenye soko la dunia vitu vikawa vinazidi kupanda kila kuitwapo leo, hata zile nchi ambazo zilikuwa zinategemewa kwamba ni watoa misaada wakuu kwa Tanzania zikapotea. Ni kama nao walikuwa wanapambana na hali zao ama waliamua kuaacha watanzania wapate somo la kujitegemea, wasitegemee misaada kila siku na kutia tia huruma, wajifunze namna ya kuishi wakiwa wenyewe. Raisi angefanya nini na yeye ndiye ambaye alikuwa anategemewa kutatua tatizo? Hakuna na njia nyingine zaidi ya njia moja ambayo kwake ilikuwa ni ngumu kuipita.
Alitakiwa kwenda kuomba msaada kwa Lucas aweze kulisaidia taifa, kwake ilikuwa ni ngumu kwa sababu alikuwa na kisasi naye moyoni, ni yeye ambaye alikuwa anataka kumpoteza mwanaume huyo lakini kwa wakati huo ni Lucas ambaye alikuwa ameshika kisu chenye makali. Hakuwa na namna ya kufanya, misaada yote ya nje ilikatwa na hakuna kiongozi wa taifa kubwa hata mmoja ambaye alikuwa anapokea simu zake ndipo akakubali yaishe, akaamua kwenda kumuomba msaada Lucas aweze kumsaidia. Wakati haya yanafanyika wewe ulikuwa mpuuzi tu mmoja Medrick na sina uhakika kama ulikuwa umeanza hata mazoezi yako ya kwanza.
Ilikuwa ni aibu lakini pia ndiyo ilikuwa njia pekee ya yeye kama raisi kuweza kuwajibika kulisaidia taifa lake, vyombo vya habari vilihitajika ikiwa ni kama takwa la Lucas, kwa sababu raisi huyo aliwahi kumuonyeshea kiburi na dharau alimtaka apige magoti na kuomba msaada mbele ya watanzania wote wamuone. Haikuwa kwa sababu ya kiburi tu lakini hao wawili walikuwa na mambo yao binafsi kumbuka kwamba raisi huyo alikuwa anapambana sana kuweza kumpoteza kabisa Lucas hivyo hata yeye alipopata nafasi ya kumnyoosha, alitaka kumuonyesha ni nani bosi wa kweli kati yao.
Raisi huyo alipiga magoti mbele ya vyombo vya habari akiomba msaada kwa Lucas tena alilazimika kusafiri mpaka kule Lucas Villa. Jambo hilo lilimpatia kisasi kizito mno kwenye moyo wake, raisi kupigishwa magoti na mwananchi ambaye hata hata nafasi yoyote ile? Kwake ilikuwa ni moja kati ya jambo la aibu kuwahi kumkuta lakini hata hivyo ilisaidia pakubwa kwa sababu Lucas alikubali kutoa pesa za kimarekani dola bilioni kumi kwa ajili ya kuingizwa kwenye bajeti ya taifa kuanza kuandaa mazingira ya kuwasaidia wananchi kwa muda mrefu.
Hakuishia hapo tu lakini pia ili aingize pesa hizo kwenye akaunti ya benki alimtaka raisi huyo aweze kujiuzulu kwenye nafasi yake, yalikuwa ni maamuzi magumu lakini ilikuwa ni lazima yafanyike kwa ajili ya usalama wa taifa zima. Hadharani kwenye vyombo vya habari raisi wa nchi alitangaza kuweza kujiuzulu nafasi yake tena kwa aibu ya kumpigia magoti mtu. Baada ya pale ndipo pesa ilidhinishwa na kwenda kuleta mabadiliko makubwa ndani ya taifa kwa ujumla.
Natron Vinza baada ya kukumbana na ile aibu kubwa alishindwa kuishi mbele ya macho ya watu, alipotea kabisa kwenye masikio ya watu na baada ya miezi sita kupita bwana yule alidaiwa kwamba alikutwa amekufa kwa kujiua mwenyewe baada ya kuzidisha madawa ya kuongeza nguvu kwenye mwili wake. Ile hadithi mbaya ikawa imeishia pale baada ya kifo chake lakini sio kweli kwamba hadithi ile iliishia pale bali ule ulikuwa ni mwanzo wa hadithi mpya ya kutisha" maelezo ya mzee Hasheem ya muda mrefu yalimchanganya Medrick Savato ambaye alikuwa makini muda wote kusikiliza kwa usahihi kabisa. Ulikuwa ni muda mrefu kidogo tangu akae hapo kuweza kusimuliwa historia nzima ya maisha ya Gavin Luca ila kwa wakati huo aliona kabisa kwamba kulikuwa na haja kubwa ya kuweza kuuliza.
"Mzee wangu umeniacha kidogo hapo, umesema kwamba aliyekuwa raisi wa wakati alikufa kitu ambacho ni sahihi kabisa kwa sababu ilikuwa ni taarifa kubwa kwa taifa zima ila unapo sema kwamba ule ulikuwa ni mwanzo ya hadithi ya kutisha unamaanisha nini?" mzee Hasheem alitabasamu akiwa anamwangalia mkuu wa majeshi ambaye bila shaka alikuwa amenogewa na simulizi ile.
"Kijana wangu dunia yetu ina kila aina ya viumbe, kuna vile ambavyo vinaishi kama ambavyo maisha yanataka viishi na kuna vile ambavyo vinaipinga asili yaani hivi vinaishi kutokana na sheria zao vyenyewe. Isingekuwa bahati mbaya mtu alikuwa raisi halafu kirahisi tu ajiue kwa vidonge wakati ana uhasama na mtu, wewe unaona hilo linakuingia akilini kweli?" swali la mzee huyo lilimuacha mkuu wa majeshi akiwa ametumbua macho, kiuhalisia hakuelewa hapo angeongeza kitu gani.
"Hapana bwana, yule bwana hakufa kama ambavyo aliuaminisha uma bali alimuua mtu mwingine akamfanyia plastic surgery akamuweka kwenye nafasi yake hivyo yule mtu ambaye alikufa hakuwa yeye"
"Unamaanisha nini mzee?"
"Mpaka hii leo Natron Vinza ni mzima"
"Whaaaaaat?"
"Yeah ni mzima na ndiye bosi wako wewe hapo"
"Bila shaka mzee umeshaanza kuchoka"
"Kijana wangu tatizo mnaendeshwa na mihemko akili zenu mnazitumia kukaangia mayai tu na kuwavimbia watu mtaani, watu kama wewe wanatumika kwenye maeneo mengi sana na watu wenye akili kwa sababu anajua wewe unapenda maujiko anakupa nafasi ili uweze kutekeleza mambo yake kisha akaiona huna faida anakuua. Nina uhakika wewe mwenyewe unajua kabisa kwamba una uwezo mdogo mno haukutakiwa kuwa hata kwenye hiyo nafasi ambayo upo ndiyo maana licha ya upuuzi wako wote bado raisi huwa anakulinda. Unaijua sababu ya msingi ya wewe kuwekwa hapo?" Medrick alibaki ametumbua macho asielewe kile embacho kilikuwa kinaendelea ni kama alikuwa ndotoni halafu mtu akamuamusha ghafla na kumtaka aelezee jambo fulani kwa ufasaha, asingeweza kufanya hivyo bila akili yake kutulia kwanza.
"Unamaanisha Natron Vinza bado anaishi?"
"Yeah ni mzima wa afya kabisa"
"Unaweza ukanieleza sehemu ya kumpatia tafadhali?"
"Hilo sio jukumu langu, mtu ambaye amekupa taarifa za wewe kunipata mimi huku ndiye unapaswa kwenda kumuuliza atakujibu kila kitu kwa sababu anajua mambo yote haya" bwana Savato alibaki anacheka kwa hasira na uchungu mkubwa. Taarifa ambazo alikuwa nazo juu ya hiyo kazi alijiona kwamba anazo nyingi sana ila baadae aligundua kwamba hakuwa na taarifa zozote za mhimu ambazo alikuwa anazijua, sasa kwanini afichwe miaka yote hiyo huku akiwa ni mmoja wa watu ambao waliwafanyia watu hao kazi kwa moyo mmoja? Hakuwa na jibu, alijiona kama takataka asiye na thamani mkuu wa majeshi.
"Unaweza ukaniambia kuhusu maisha ya Lucas na mkewe mjamzito baada ya pale?"
"Mhhhhhh una haraka sana CDF, wakati haya mambo yanatokea ya raisi kuigiza kifo chake mwenyewe tayari mke wa Lucas alikuwa amejifungua. Hapa ndipo kuna siri kubwa ambayo iliuchanganya ulimwengu mzima na ni watu wachache ambao tulikuwa na taarifa hizi, Glady alijifungua watoto wawili wa kiume mapacha ila ambaye ulimwengu ulikuja kumjua ni mmoja tu pekee mmoja hakuwahi kujulikana na hapa ndipo inaanzia historia ya maisha ya hicho kiumbe ambacho wewe uliamini kwamba umekiua"
"Unamaanisha miongoni mwa hao watoto wawili mmoja wao ndiye Gavin Luca?"
"Siwezi kukujibu hilo swali Medrick"
"Mzee wangu sipo hapa kwa ajili ya kukubembeleza" Medrick aliongea kwa hasira huku akiwa anaitoa bastola yake, alifika sehemu ambayo binafsi alikuwa anahitaji zaidi kupata taarifa zake, ilikuwa ndiyo sehemu sahihi ya kuanza kumtambua Gavin Luca.
"Weka bastola pembeni, mimi ndiye mtu pekee ambaye naweza kukupatia taarifa ambazo unazihitaji hivyo unanihitaji zaidi nikiwa mzima wa afya na sina tatizo lolote lile. Natambua ahadi yako ni ya uongo kusema kwamba utaniua mimi pekee na wafungwa wengine utawaacha hivyo ninacho kitaka mimi nahitaji kutoka hapa nikiwa hai, nahitaji kuonana na Gavin Luca kabla sijafa hivyo ua wengine kisha utoke na mimi nikiwa mzima na unipeleke sehemu nzuri nikaishi kwa raha" maada ilibadilika kabisa kutoka kwenye kinywa cha mzee huyo kiasi kwamba hata Medrick mwenyewe alibaki ameduwaa kama haamini kile ambacho kilikuwa kinatokea ndani ya eneo hilo. Aliishia kucheka kwa hasira.

Ishirini na sita inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
SONGA NAYO................


"Unahisi wewe ni nani mzee labda?"
"Medrick muda mwingine tumia akili ili upunguze majuto ya baadae huko, kwa taarifa yako ni kwamba hata yule waziri mkuu ambaye alikuwa ni baba yake na Glady bado mpaka leo yupo hai" CDF alichoka, aliwaita vijana wake na huwataka wamtoe mzee huyo kisha waue watu wote waliokuwa humo ndani mpaka walinzi, hakuna ushahidi ambao ulitakiwa kuachwa huko. Ndicho ambacho kilitokea, walinzi wake waliuawa watu wote pamoja na wafungwa ambao walichinjwa vibaya kisha ikaanza safari ya kurudi ndani ya bandari ya Salama huku huko nyuma lile gereza la siri likiwa limeteketezwa ila jambo moja ambalo alilifanya CDF ni kumtunza huyo mzee sehemu ya siri sana ambayo haikutakiwa mtu yeyote kuja kufahamu kwamba yupo ama bado anaishi.


****************
Usiku upepo ulikuwa unapuliza kutengeneza baridi kali, anga lilitulia kuashiria uwepo wa amani ya kutosha ndani ya eneo hilo, walimwengu walikuwa wamejipumzisha na matatizo mengi ya dunia. Ilikuwa ni tofauti kwa Sarah Martin, kwake hali haikuwa tulivu, licha ya uwepo wa ile baridi kali hakuwa hata anaisikia kwenye mwili wake, akili haikuwa hapo, ilikuwa inawaza mbali na mambo mengi ambayo hakuyaona kuwa ya kawaida kwa upande wake.
Hakuelewa kwamba ni kwanini mambo yale yalikuwa yanamtokea yeye tena kwa kasi namna hiyo, usiku huo alikuwa amevaa traki na koti ambalo lilikuwa linaendana na traki yake huku chini akiwa amevaa raba za adidas. mikononi alikuwa na gloves na kichwani alivaa mzura huku mkono wake mmoja ukiwa umeishika sigara ambayo alikuwa anaipuliza kwa mbali na kwa hisia nzito kidogo kupunguza mawazo yake ambayo yalikuwa mengi kichwani. Moyo ulianza kumuenda mbio isivyokuwa kawaida na mwili ulimsisimka pale ambapo alikuwa amekaa, aligundua kwamba mazingira ya kwake hapo palikuwa na hatari.
Aliruka kwa kujifyatua pale ambapo alikuwa amekaa baada ya kuhisi kuna kivuli kinaelekea hapo alipokuwepo, alipishana na buti zito ambalo lilitua na kuvunja kile kiti ambacho alikuwa amekikalia. Akiwa anashangaa alipishana na ngumi kwenye shingo hata hivyo mtu ambaye alikuwa amemvamia aliikunjua ile ngumi na kumkita na kiganja kikali shingoni kikamfanya ayumbe kidogo na kusimama vizuri. Alimwangalia bwana yule ambaye alikuwa mbele yake, sura ilikuwa ngeni, hakuwahi kumuona mahali popote pale, hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kabisa kumuona.
Mwanaume huyo alimpa ishara ya kiganja akiwa anamuita kwa dharau, alikunja ndita zake kwa hasira Sarah kwa sababu aliona kama watu hao walikuwa wanaelekea kumzoea sasa hivyo huyo mmoja alitakiwa kuwa somo kwa wengine. Alihesabu hatua zake kadhaa akageuka kwa sarakasi ya mbele ambapo mguu wake ulitua kwenye bega la bwana huyo aliye ukunjua mkono wake na kumdaka Sarah kwenye ziwa moja kisha akamsogeza karibu yake na kumpiga denda mdomoni kisha akamuachia ghafla.
Sarah alipatwa na hasira kali, alimsogelea mtu huyo kwa jazba, alizunguka na double kick ikatua kwenye mikono ya mwanaume yule ambaye alikuwa amesimama pale, alimtandika Sarah na kofi moja kali shavuni lililo mfanya aanze kuona dunia inzunguka mara sita sita. Akiwa anajiandaa kuipanga mikono yake tena mwanaume huyo alimuonyesha kitambulisho ambacho kiliashiria kwenye yeye ni mwanajeshi ambaye anatokea ndani ya special force.
"Bado una mifupa laini, hautakiwi kupigana na mtu kama mimi kwa sababu kama ningeamua kukupiga hata ngumi yangu moja tu basi ungepata kilema cha maisha"
"Ndiyo maana umekuja kunidhalilisha hapa kwa sababu unajua unaweza kunishinda?"
"Hilo busu halihusiani na kilicho nileta hapa, nimetumwa na mamlaka za juu kuja kukuuliza baadhi ya maswali"
"Mamlaka zipi wakati nilishatoa taarifa za kile ambacho nakifahamu?"
"Wote tunajua kwamba haiwezi kuwa rahisi namna hiyo, wanajeshi waliokufa ni wengi tena wengine walikuwa ni makomando, nadhani hukuambiwa hilo hivyo nchi imepata hasara kubwa maana yake wewe utakuwa unatoa taarifa pale ambapo kutakuwa na ulazima wa wewe kufanya hivyo"
"Kwanini usije kistaarabu nyumbani kukikucha mpaka univamie muda huu?"
"Hakuna sehemu imendikwa kwamba natakiwa kuja kwa namna ambayo unaitaka wewe. Hili ni jambo nyeti na taarifa hizi zinahitajika muda huu kwahiyo nina imani kwamba utanipa maelekezo na ushirikiano wa kutosha ambao utasaidia kwa ukubwa"
"Unataka kujua nini labda! Kwa sababu ninacho kijua nilishakueleza"
"Nipo kwenye hii kazi kabla hata jina lako halijaingizwa kwenye listi ya jeshi, haiwezi kuwa bahati mbaya, nina uhakika stori ambayo umeitoa ni ya uongo"
"Una uhakika gani juu ya hilo?"
"Nina uhakika kwamba ulionana na Gavin Luca lakini kitu ambacho sikijui ni kwamba kwanini alikuacha wewe hai na kwanini unatumia nguvu kubwa sana kumlinda kiasi kwamba unasahau hata miiko ya kazi yako kwamba inatakaje?"
"Hizo ni nadharia ambazo unazitunga wewe kwa sababu haukuwepo na hujui ni kipi kilitokea, kwahiyo unatakiwa kuniamini kwa kile ambacho nakueleza mimi"
"Sikuwepo ndiyo maana ni rahisi kuhitaji kunidanganya lakini ukumbuke kitu kimoja, unavyo endelea kutudanganya ndivyo unazidi kuiweka familia yako kwenye hatari kubwa"
"Una maswali mengine?"
"Sarah Martin kwanini unamlinda Gavin Luca? Alikutishia maisha yako na familia yako! Unampenda? Pointi ya msingi iko wapi? Huyo ni mtuhumiwa wa taifa anatakiwa kupatikana kwa namna yoyote ile tujue yule ambaye alikufa alikuwa nani hasa kwa sababu wakati ile nyumba inateketea mwili wake baadae haukukutwa eneo la tukio maana yake mtu ambaye wewe ulimuona ama kuongea naye ndiye ambaye aliupoteza huo mwili. Naongea kistaarabu sana na wewe, nisaidie kumpata Gavin Luca"
"Sielewi unacho kiongea, Gavin tulimuua kuhusu yule ambaye alituvamia mimi sijui lolote kwa sababu alivaa maski usoni, hata mimi hakuniacha kama ambavyo unadai wewe bali alihisi ameniua" mwanaume yule ambaye alikuwa pale alicheka kwa sauti, hakuwa mwingine alikuwa ni kijana wa CDF, Bashiri Aden. Alijua kabisa Sarah ni muongo kwa sababu hata yeye mwenyewe alikuwa ni muuaji wa kutisha hivyo alikuwa anaelewa vyema kwamba wauaji huwa hawafanyi makosa ya kipuuzi namna hiyo. Alisimama na kumzunguka binti huyo akiwa anamwangalia kwa umakini, kama sio kukatazwa na CDF angemfanya binti huyo kitu kibaya kiasi kwamba asinge msahau kwenye maisha yake yote.
"Alikuacha kwa bahati mbaya sio? Wote tunajua huo ni uongo, muuaji wa namna ile hawezi kufanya kosa la kipuuzi namna hiyo Sarah" Sarah kauli hiyo ilimshtua na kuanza kuhisi kwamba huenda mwanaume huyo hakuwa special force kama alivyokuwa anajitambulisha, hizo habari za wauaji kuwa hivyo alizifahamia wapi? Kidogo moyo wake ulianza kukosa amani na kuhisi huenda familia yake ilikuwa kwenye hatari nzito dhidi ya bwana huyo na hakuwa na uhakika kama eneo hilo alikuwa mwenyewe au alikuwa na watu wengine.
"Kwani na wewe ni muuaji wa namna ile mpaka ujue kwamba wauaji hawafanyi makosa?" swali lilimfanya bwana huyo kukunja ndita, hakulipenda japo hakuwa na namna ya kuweza kufanya.
"Tutaonana wakati mwingine Sarah Martin ila hiki unacho kitengeneza kama familia yako itapata matatizo basi hakikisha hautafuti mtu wa kuweza kumtupia lawama, utakuwa ni wewe mwenyewe umeiua kwa mkono wako" bwana huyo hakusubiri jibu alitoweka na kutokomea zake kusiko julikana majira ya usiku huo.

Sarah ile hali hakuichukulia kawaida kwake, lilikuwa ni onyo la hatari lile na aliona kuendelea kukaa kungoja hatima yake kungemletea matatizo. Alihitaji kurudi kazini haraka ili aanze uchunguzi wake juu ya jambo hilo lakini kabla ya kufanya huo uamuzi alihitaji kukutana na Nick angalau ndiye mtu ambaye alikuwa anamwamini na ni yeye ambaye mara moja aligundua kwamba Sarah alikuwa anawadanganya lakini akampa nafasi kwamba atakapokuwa tayari basi amshirikishe ili aweze kumsaidia kwa namna moja ama nyingine. Sarah aliitoa simu yake kumpigia mwanaume huyo ambaye kwa wakati huo alikuwa ndani ya jiji la watalii (Arusha) akimpa taarifa kwamba alihitaji waonane muda huo hivyo alikuwa anaenda huko huko usiku huo huo.
Sehemu ya ishirini na saba inafikia mwisho hapa.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE
SONGA NAYO................

TANZANIA MILITARY ACADEMY
Alitumia masaa mawili kutoka Moshi mpaka kufika kilipo Chuo Cha Mafunzo ya Jeshi Monduli. Huko alienda kwa ajili ya kukutana na Nick, Licha ya Nick kuwa mwanajeshi lakini pia alikuwa ni moja kati ya wakufunzi ndani ya chuo hicho hivyo muda mwingi alikuwa anashinda na kulala karibu kabisa na eneo hilo. Sarah alifika na kupokelewa na Nick ambaye bado alikuwa na wasiwasi, alihisi mwanamke huyo alikuwa kwenye matatizo hivyo alimkaribisha kwenye nyumba ambayo alikuwa anaishi akiwa ndani ya eneo hilo.
Kitu cha kwanza ambacho walianza nacho ni kumtajia jina la mwanaume ambaye alikuja nyumbani kwake akijitanabaisha kama special Force, jina la mtu huyo halikuonekana sehemu yoyote ile hivyo alidanganya, kama alidanganya maana yake hakuwa mtu wa jeshi sasa alikuwa ni nani? Walibaki wanaangaliana.
"Nick nahisi kabisa familia yangu haipo salama na jambo hilo linako elekea linaweza kunileta matatizo makubwa sana huko mbeleni kwa kuiponza familia yangu"
"Ni uamuzi gani umeamua kuuchukua Sarah?"
"Nataka nikwambie ukweli kwa sababu wewe ni mtu wangu ambaye ninakuamini sana na baada ya hapo unaweza ukaona namna sahihi ya kunishauri nini cha kufanya kwa sababu naona kabisa akili yangu imefika kwenye ukomo wa kufikiri, sielewi tena ni kitu gani nifanye" Nick alimpatia bilauri la maji apooze koo lake, alikuwa anaongea kwa mashaka mno kisha naye akakaa kando yake ili kumsikiliza.
"Ni kweli yule mtu hakunisahau kule mimi kwa bahati mbaya bali alikuwa ana uwezo wa kuniua lakini aliniacha hai, mpaka sasa ukiniuliza mimi sababu ya msingi ya kuachwa hai siijui kabisa lakini yeye binafsi aliniambia kwamba sio muda wangu wa kufa"
"Ulimuona nani?"
"Gavin Luca"
"Ambaye mlimuua muda mfupi ambao ulipita?"
"Ndiyo"
"Kwahiyo ni kweli kwamba huyo mtu hakufa?"
"Sijui ilikuwaje ila ukweli ni kwamba kweli kabisa hajafa, bado yupo hai na mzima wa afya kabisa"
"Inawezekanaje?"
"Hata mimi mpaka sasa najiuliza swali kama hilo ila nimeshindwa kuweza kulipatia majibu yake"
"Kwahiyo kilitokea nini?"
"Baada ya kuua watu karibia wote pale sikuwa hata na uwezo wa kusimama tena, nilibaki nimeganda kama nimekufa ndipo akaitoa ile maski yake usoni. Nilitamani kufa kwa sababu niliona sura ya mtu ambaye aliuawa muda mfupi uliokuwa umepita, aliniambia kwamba yeye ni mzima kabisa ila kwa yote ambayo yalitokea pale IDAIWE MAITI YAKE hivyo yeye hayupo hai kama ambavyo wengi wanaamini kwamba amekufa basi hata mimi nilitakiwa kumhesabia kwamba ni mfu vile vile.
"Baadae alinitajia jina lake kwamba yeye ndiye GAVIN LUCA, akanipiga mpaka nikazimia, hapo sikuelewa kilicho tokea tena mpaka baadae nilipokuja kushtuka na kupiga simu kuomba msaada"
"Kuna kingine labda ambacho kiliendelea baadae Sarah?"
"Ndiyo, alikuja nyumbani akaacha begi na ujumbe huku akiahidi kwamba ipo siku tutakuja kuonana kwenye maisha mengine"
"Umesema begi?"
"Ndiyo"
"Lilikuwa na nini?"
"Lilijaa pesa"
"Mlishawahi kujuana kabla ya sasa au kuwa karibu?"
"Hapana"
"Mtu anakupaje pesa kirahisi namna hiyo tena ambazo zipo kwenye begi?"
"Mpaka sasa sielewi, aliandika tu kwamba ni zawadi kwa mama yangu"
"Maana yake hakutaka wewe ufe au uendelee kuteseka, hiyo ina maana mbili huenda anakufahamu au anamfahamu mama yako kwenye maisha ya huko nyuma au anakutaka wewe ukiwa mzima wa afya, maana yake ana kazi na wewe huko mbeleni hivyo lazima atakutafuta wakati ambao atakuhitaji"
"Awe na kazi na mimi kivipi? Sioni kama naweza kuwa na matumizi yoyote kwa mwanadamu wa namna ile"
"Watu wenye akili huwa wanaona hata vitu vidogo Sarah, hili jambo kama likifahamika ngazi za juu itakuwa hatari kwa upande wako hivyo unatakiwa kuusimamia ule msimamo wako wa kwanza, yaani usiubadili hata kidogo kwa namna yoyote ile. Kama utabadilisha stori basi watajua kwamba wewe ni msaliti na hakikisha hakuna mtu anakuja kukuhoji bila kibali maalumu kwa sababu kuna watu watatumika kuhitaji kuzipata taarifa hizi. Muda wowote kama ukihitaji jambo lolote nipo hapa kwa ajili yako" Sarah alifurahi angalau kupata mtu ambaye aliweza kumueleza shida zake akamuelewa. Wawili hao walibaki wanatazamana huku wanatabasamu, macho yalianza kuwaza ujinga wakashindwa kujizuia kabisa, walijikuta wanaegamiana taratibu na kuanza kubadilishana juisi safi za midomoni, walipokuja kushtuka walikuwa uchi kitandani, wakayaachia mashuka historia nzito kwenye kitanda hicho.




**********
NORA HASSAN
Lilikuwa jina la askari polisi wa kike ambaye alikuwa anafanyia kazi Singida Mjini. Mwanamke ambaye alikuwa mrembo sana lakini alikuwa na misimamo mikali kiasi kwamba ni watu wachache ambao walikuwa na uwezo wa kumzoea. Baba yake alikuwa mtanzania lakini mama yake alikuwa ni Mhabeshi, Ethipioa ndiko lilikuwa chimbuko la mama yake mzazi huenda ndiyo maana alikuwa mrembo sana kwa sababu kwenye taifa hilo ndiko ambako wanatoka wanawake warembo zaidi ndani ya bara zima la Afrika.
Mwanamke huyo alikuwa anafanya kazi hiyo lakini pia alibahatika kuwa kwenye ndoa ambayo ilimpatia mtoto mmoja wa kike mrembo kama yeye alivyokuwa ambaye alimpenda isivyokuwa kawaida. Kitu kimoja ambacho kilikuwa kinamchanganya mwanamke huyo ni kuhusu maisha ya mumewe, mumewe hakuwa mtu mwenye kazi za kueleweka lakini hakuwahi kuonekana kuishiwa wala kupata taabu ya aina yoyote ile kwenye maisha yake kwa sababu angemuona tu anasafiri na kurudi nyumbani bila shida.
Alikuwa ni mume bora kwa upande wake na baba bora kwa mwanae, mumewe amewahi kumuonyesha biashara zake kadhaa ambazo alikuwa anazifahamu lakini ratiba ya mumewe ilikuwa inamshtua kiasi kwamba kuna muda akawa kama ana wasiwasi na aina ya mtu ambaye alikuwa ameolewa naye. Mumewe alikuwa mtu wa swala tano, alikuwa mwanaume mstaarabu mno isivyokuwa kawaida kiasi kwamba ilikuwa ni ngumu hata kumkuta akiwa anakoromeana na mtu yeyote yule. Mbali na hilo mwanaume huyo alikuwa na mwili ambao ulijengeka kwa mazoezi makali sana, mwili huo kwa mara ya kwanza binafsi aliupenda kwa sababu mumewe alimsisitizia kwamba alikuwa akipenda kunyanyua vyuma ndiyo ilikuwa siri ya kuupata mwili huo lakini kadri siku zilivyokuwa zinazidi kwenda alihisi kuna kitu hakikuwa sawa kuanzia siku ya kwanza wanaonana.
Kazi yake ilikuwa inamuweka busy muda mwingi kiasi kwamba nyumbani mumewe ndiye ambaye alikuwa akishinda hivyo hakuwa akipata muda mwingi wa kushinda naye kila wakati na hakuona sababu ya kumuingilia kwa kila kitu kwa sababu alikuwa akimuamini kuliko kitu chochote kile. Norah kuna matukio kadhaa ambayo alianza kuyawekea mashaka japo mara ya kwanza hakuwahi kabisa kuyatiilia maanani, ni kwamba kila mumewe alipokuwa anaaga kwamba anasafiri kibiashara ilikuwa ni lazima taifa lingepata tukio la kutisha.

Sehemu ya ishirini na nane inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA
SONGA NAYO................

Alianza kumhisi mumewe vibaya lakini nafsi yake ilikataa kabisa, mumewe alikuwa mtu safi tena wa dini aliyependa kutoa misaada kwa watu wote ambao hawakuwa na uwezo sasa iweje aanze kumhisi vibaya? Aliona kama anamuonea ila kuna nafsi ilikuwa inamgomea kupingana na ukweli ambao alikuwa anauwaza kichwani mwake. Wakati hayo yote yanatokea alikuwa juu ya balkoni akiwa na glass ya wine mkononi akiangalia uoto wa asili ulivyokuwa umekubali kwa jitihada za mumewe, mawazo yake yalikuja ikiwa ni siku chache tu tangu mumewe arudi kutoka Dar es salaam na wakati akiwa huko kuna matukio mengi yalitokea ya kutisha ndani ya jiji hilo pamoja na Zanzibar kwa vifo vya watu wazito serikalini kutokea.
Alijiona mjinga kuwa na hayo mawazo, yaani mumewe na baba mtoto wake ndiye amuue kiongozi kama makamu wa raisi ambaye ana ulinzi mkali namna ile? Aliishia kucheka na kujiona ni mjinga kwa sababu alikuwa anawaza upuuzi ila hakuwa na amani na safari za kutotabirika za mumewe wa ndoa tena akiwa hajui hizo safari zote za biashara kwanini hajawahi kumualika hata moja. Mawazo mengi yalikuja kichwani baada ya mumewe kumuomba ruhusa ya kuweza kuondoka, mwanaume huyo alidai kwamba ana safari ya kwenda ndani ya taifa la Botswana kusaka fursa mpya za biashara. Ilikuwa ni safari ya kushtukiza kwa upande wake na hakujiandaa, alihitaji kutumia muda na familia lakini wakati huo mumewe alimuahidi kwamba alitakiwa kuondoka mapema iwezekanavyo.

Norah akiwa kwenye balkoni yake alikumbuka mbali sana, mbali kwa mara ya kwanza alipo fanikiwa kukutana na mumewe MIKE TORES. Watu hao wawili walikutania kwenye basi, safari ambayo ilikuwa na machungu mengi kwa mwanamke huyo ambaye muda wote alikuwa akilia kwenye safari hiyo. Siti ya pembeni yake alikuwa amekaa mwanaume mmoja ambaye alikuwa amevaa kanzu safi nyeupe na ndevu zake zilishamiri vyema, hakuonekana kuwa mtu mwenye njaa sana ya maisha bwana huyo japo hakutaka mazoea na watu ndani ya basi hilo.
Hali ya mwanamke huyo jirani yake ndiyo ilimpa umakini, alihitaji kujua ni tatizo gani lilikuwa linamsumbua lakini mwanadada huyo hakuwa tayari kuongea na bwana huyo ambapo ilibidi amuache kama alivyo japo aligundua kwamba hakuwa sawa, alihitaji msaada. Walipokaribia kufika Singida mjini mwanadada huyo aliomba kushuka kwenye basi hilo akiwa amejitanda baibui kwenye uso wake, hakutaka kabisa kuwa kero kwa watu wengine moyo wake ulikuwa unamuuma kwa uchungu mkubwa mno. Kushuka kwake kwa shari namna ile kulimpa taarifa bwana yule kwamba hapakuwa pema hivyo naye alishuka na kuliacha basi liende jambo ambalo lilimshangaza hata yule mwanamke.
Bwana yule alijitambulisha kwa jina la Mike na mrembo yule alijitambulisha kama Norah na huo ndio ukawa mwanzo wao wa kufahamiana. Norah alipata sehemu ya kumalizia uchungu wake ndipo akamwambia bwana huyo kuhusu kilichokuwa kimemsibu mpaka kufikia hatua ya kuwa kwenye ile hali na wakati ule alikuwa anahitaji kwenda kujiua kwani maisha yake hakuyaona kama yana thamani tena jambo ambalo lilimshtua bwana yule. Norah alizaliwa kwenye familia ya bwana jela, bwana jela huyo hakuwa na elimu hivyo alikuwa analipwa ujira mdogo ambao hata yeye mwenyewe binafsi ulikuwa haukudhi mahitaji yake lakini ndiye alikuwa baba yake.
Kwenye ujana wake baba yake aliwahi kutembea kidogo mpaka ambapo alikuja kukutana na mama yake Norah, mwanamke ambaye alizamia Tanzania kutafuta maisha hususani baada ya familia yake kumfukuza baada ya mama na baba yake kufariki na mali zao zote kuchukuliwa na ndugu zake. Maisha ya Tanzania hayakuwa rahisi kwake kwa sababu alikuwa mgeni na hakujua anaanzia wapi, hakuwa tayari kuuza utu wake kwa kuanza kuuza utupu wake hivyo aliamua kupambana na jiji mpaka alipokutana na baba yake Norah.
Bwana huyo alimuoa mwanamke huyo licha ya maisha yake kutoeleweka na alifanya hivyo baada ya mwanamke huyo kumpa mkasa mzima wa maisha yake. Maisha hayakuwa mazuri lakini walipendana ziku zote mpaka wakabahatika kupata binti ambaye ndiye Norah mwenyewe. Lakini kipindi cha ukuaji wake baba yake alikuja kupata maradhi kwa sababu ya kufanya kazi kwenye mazingira mabovu akapoteza maisha hivyo uwepo wake ukawa msalaba kwa mama yake. Mama huyo alijitahidi sana kumlea mwanae japo kwa ugumu mpaka akafanikiwa kumaliza elimu ya msingi na baada ya hapo safari ya elimu yake ikawa imeishia hapo. Wakaanza maisha ya kuhangaika mtaani, mama yake alimkuza vyema binti yake, isingejalisha ni magumu mangapi anayapitia ila kamwe hakutakiwa kabisa kuutoa mwili wake kwa ajili ya kupewa pesa, alitakiwa kujilinda mpaka siku ambayo angefanikiwa kuolewa aje ampe mumewe zawadi ya bikra yake naye hayo maneno yalimkaa vyema kichwani.
Mama yake alimpambania mwanae mpaka akampeleka kwenye mafunzo ya uaskari ili aweze siku moja kuwa msaada kwake, alijitahidi kila shilingi ambayo alikuwa anaipata kuiwekeza kwa binti yake mpaka alipofanikiwa kumaliza mafunzo hayo japo kwa shida kubwa huku akiwa anaombwa sana rushwa ya ngono lakini haikuwa sehemu ya maisha yake na hakuwa tayari kwa hilo. Baada ya kumaliza alikaa nyumbani mwaka mzima akiwa anahangaika na mama yake kutafuta kazi lakini hakuipata. Sio kwamba kazi hazikuwepo, lahasha! Kazi zilikuwa nyingi kila sehemu lakini alielewa kwamba yupo kwenye dunia ambayo ili upate kitu basi lazima na wewe upate kitu na hakuwa tayari kutoa mwili wake ili apate kazi akaendelea kupigika mtaani.
Mama yake hakuchukua muda, alipoteza maisha kwa mshtuko akabaki mwenyewe bila msaada wowote ule. Ulikuwa ni wakati mgumu na mbaya sana kwake Norah, alitamani kujifanyia kitu kibaya ila alikumbuka kwamba ni yeye ambaye anatakiwa kumpumzisha mama yake kwa heshima ndipo angekuja kufanya maamuzi mengine kwenye maisha yake. Binti huyo hakuona kama ni ustaarabu kumzika mama yake kwenye ardhi isiyokuwa yake, yeye Tanzania palikuwa nyumbani ila sio mama yake hivyo akaandika barua kwa ubalozi wa Ethipia Tanzania kuweza kuomba msaada wa kuusafirisha mwili wa mama yake na ndiyo ikawa mara yake ya kwanza kufika huko Ethiopia tangu azaliwe.
Ulikuwa ni wakati ambao alikutana na ndugu zake wa huko kwa msaada mkubwa wa Ubalozi wao lakini hapakuwa pema. Ndugu zake hawakuwa wakimtambua yeye bali walimtambua mama yake hivyo baada ya mazishi tu walimtaka arudi haraka alikokuwa ametoka, hawakuwa na uhitaji naye wala kutaka kumuona. Rambirambi chache za msiba na Ubalozi ndio ambao walimsaidia kurudi kwa mara nyingine tena Tanzania kwenye ardhi ya wapenda amani na wajuaji kuliko hata Google. Wakati anakutana na Mike ndiyo kwanza alikuwa ametua Dar es salaam kutoka Ethiopia hivyo akachukua gari kuweza kurudi Tabora ambako ndiko yalikuwa makazi yake na mama yake.
Kwenye gari uvumilivu ulimshinda, aliona kabisa kwenda kwenye ile sehemu ingemkumbushia machungu makali mno ndiyo maana akaamua kushukia hapo Singida ili ikiwezekana ajiulie hapo ndipo alitokea malaika kusiko julikana akataka kujua yaliyo msibu mwanamke huyo. Ile simulizi ya maisha ya Norah ilimgusa mno bwana yule Mike, alimtaka mwanamke huyo aachane na mawazo yale ya kuuchukua uhai wake yeye angemsaidia na hata kama angehitaji kuishi naye basi alikuwa tayari kumuoa ili amlinde, kukosa mtu wa kumsimamia ndilo lilionekana kuwa tatizo lake kubwa Norah. Hakuamini kwanza mtu kukatisha safari zake na kuamua kupambana na tatizo lake ilikuwa ni habari mpya na njema kwake, hakujua kama kuna watu wenye mioyo ya hivyo bado wapo na wanaendelea kuishi.
Ule ukawa mwanzo wa kufahamiana kwao, ule ukawa mwanzo wa wao kuishi Singida hata ile safari ya kwenda Tabora ilifia pale. Wawili hao waliishi pamoja na baada ya kujuana vya kutosha wakaamua kufunga kabisa ndoa na kuishi kama mume na mke kwa furaha kubwa hata lile tabasamu ambalo lilipotea kwenye uso wa Norah lilirudi kwa mara nyingine tena. Norah alipewa simulizi ya maisha ya Mike akaridhika nayo kwa sababu bwana huyo naye hakuwa na ndugu kabisa alikuwa kama alivyo japo yeye alifanikiwa kusimamisha biashara zake kadhaa mjini na baadhi ya mikoa.
Alipenda kuwa askari Norah, aliliweka hilo wazi kwa mumewe naye hakuwa na kipingamizi nalo hivyo alimuuliza sehemu ambayo alitaka kufanyia kazi, hakutaka kuwa mbali na familia yake akachagua hapo hapo Singida ambapo aliamini kwamba wangeishi wote lakini mumewe aligoma kabisa kuishi mjini. Alimuahidi mkewe kwamba yeye angepatiwa kazi hapo mjini kisha wao wangejenga kijijini ambako angekuwa anaenda kila wikiendi, mwanzoni mkewe hakumuelewa mumewe anamaanisha nini lakini tangu aseme anataka kufanya kazi hapo mjini ilichukua msaa kumi tu akapigiwa simu kwamba kesho alitakiwa kuripoti kuanza kazi.
Alijitahidi sana kumuuliza mumewe ili ajue kile ambacho alikifanya lakini bwana huyo alimwambia alienda kumuombea tu hakukuwa na changamoto kubwa na ndio ukawa mwanzo wa wao kuishi hivyo kwenye hayo maisha yake japo hakujua kipi kilimfanya mumewe ahitaji wasiishi pamoja mjini. Norah kumbukumbu hizo zilikuwa zimejirudia kwenye kichwa chake akikumbuka mwanaume huyo aliko mtoa, hakuona sawa kumuwazia mabaya japo kuna nafsi ilianza kuwa na tamaa ya kutaka kumchunguza mumewe huenda kuna vitu hakuwa anavifahamu sana kwa sababu muda mwingi alikuwa anashinda kazini na huenda kulikuwa na sababu ya mumewe kuhitaji muda mwingi waishi mbali. Hilo halikuizuia safari ya kwenda Botswana lakini haikuwa Botswana kweli bali mwanaume huyo alisafiri kwenda ndani ya jiji la Johannesburg wao wanaliita JOZI.

Sehemu ya ishirini na tisa imefika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwa wale watu wa kutaka kuimaliza kwa siku moja..... 3000 yako tu inatosha kumalizia yote mpaka 105 [emoji871]



0621567672 (HALOPESA)

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

36316279 (LIPA NAMBA (M-PESA) inapokea mitandao yote)

FEBIANI BABUYA

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom