FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #41
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA NANE
SONGA NAYO................
"Kawasalimie kuzimu mpuuzi mkubwa wewe" alipofumbua macho alichomoka pale kwa mbio kali kumuwahi mtu yule kabla hajaingia kwenye yale maduka ya jumla, ilikuwa ni ghafla na ni wakati ambao walinzi walishtuka kwamba kuna mtu anakuja ule upande wao ila kwa bahati mbaya wakati wanashtukia hilo wawili walikuwa wamepigwa risasi na yule kijana tayari hali ambayo iliwafanya wananchi wengine kuanza kukimbia hovyo huku wangine wakisahau hata maduka yao wazi, maisha yao yalikuwa mhimu zaidi. Ule muingilianao wa watu ulifanya walinzi kutopiga hovyo risasi kwani wangejikuta wanaua watu wasio na hatia.
Kijane yule aliruka mpaka juu ya gari ambapo alidunda kwa mguu wake mmoja na kutua upande wa pili kwenye shingo ya mwanaume mmoja ambaye alikufa pale pale. Walinzi wawili walikuwa wanakimbia na ile familia kuelekea kweye yale maduka, wawili ndio ambao walibakia hapo kupambana naye. Alinyanyua bastola yake kwa kasi na kuachia risasi moja ambayo ilienda kutua kwenye kichwa cha yule mwanaume wa makamo akiwa anakaribia kuzama kwenye duka mojawapo hali ambayo ilizusha kelele kwa familia yake ikabidi mwanaume mmoja aende na familia ndani mmoja ndiye akabaki pale chini akiwa anamkokota mzee yule kuelekea naye ndani pia akiwa amepigwa risasi ya kichwa anavuja damu.
Vilisikika ving'ora vya polisi vikija kwa mbali eneo hilo, kijana huyo alisonya na kuzunguka kwa kasi kiasi kwamba risasi za wa wanaume hao zilikita kwenye gari, alisubiri wapige mpaka zilipo waishia ndipo alitokezea juu ya gari kwa kujiviringisha. Alitua karibu ya mwanaume mmoja ambaye alimpokea kwa ngumi iliyotua kwenye bega lakini hakutikisika zaidi aliishika shingo ya mwanaume huyo na kuivutia kwenye kisigino chake ambapo alikutanisha mguu na kichwa, alipo muachia alitoboa shingo hiyo kwa vidole vyake na kumtupia pembeni. Yule mwenzake alikuja kwa kukimbia ila alifuatwa kule kule ambapo alikutana na ngumi nzitoa ya kifua iliyomfanya kuhema kwa nguvu na kupiga goti, akiwa pale chini alipigwa risasi tatu za kichwa kukawa kimya.
Polisi waliingia ndani ya hilo eneo ambalo lilikuwa limetapakaa damu na miili barabarani lakini muuaji hakuonekana yuko wapi. Mtaa ulikuwa kimya huku kila mwenye duka karibu akiwa amekimbia bila hata kufunga na wengine walijifungia ndani ya maduka yao. Ving'ora vya polisi ndivyo ambavyo vilimtoa mlinzi mmoja mle ndani akiwa amembeba yule mzee kwenye mkono wake na kuwataka polisi waipe ulinzi familia ipo ndani na wengine watumie gari ya polisi kumuwahisha hospitali mzee huyo kuona kama wanaweza kuyaokoa maisha yake.
Familia ilipewa ulinzi na mzee huyo akawahishwa hospitali na gari ya polisi kwa sababu ilikuwa ni ngumu kuweza kuisubiri ambulance na hali yake ilikuwa mbaya sana lakini hata kabla hawajafika huko hospitali alifia njiani hivyo walifika na maiti kule hospitali. Ni muda fupi tu tangu litokee tukio hilo afisa wa polisi kutoka Osterbay Ezra Ethan maarufu kama Double E alikuwa amefika na askari wenzake kadhaa hapo wakidai kwamba hiyo kesi wao ndio waliagizwa kuja kuisimamia kutokana na ukubwa wa mtu ambaye aliuawa hivyo wakahitaji maelezo kutoka kwa hao maaskari ambao walikuwepo eneo hilo.
Kiufupi ni kwamba mtu ambaye aliuawa hilo eneo alikuwa ni bosi wao, waziri wa mambo ya ndani ambaye idara za polisi zipo chini yake, bwana Sylivester Mboneka ndiye ambaye aliuawa hivyo hiyo kesi ilikuwa na uzito mkubwa kwa jeshi la polisi. Licha ya mtu huyo kuwa waziri lakini pia alikuwa ndiye bosi wa idara hiyo kwani ilikuwa ipo chini ya wizara yake hivyo hata msako wa mhusika ulitarajiwa kuwa mkubwa zaidi. Yalitolewa maelezo mafupi lakini mtu ambaye alikuwa na maelezo mengi zaidi ni yule bodyguard mmoja ambaye alibaki na familia ndani ya yale maduka kwa sababu mwenzake mmoja alikuwa ameenda na mheshimiwa hospitali.
Alielezea tukio zima lilivyokuwa lakini ni kama kuna sehemu walikuwa wanakosa baadhi ya matukio ya kuunganisha hivyo wakawaomba wamiliki wa yale maduka waweze kuwaonyesha video ya tukio zima kwani waliamini eneo lile lilikuwa na kamera za kutosha. Kwenye video ambayo ilionyeshwa ndani ya hizo kamera iliwasaidia kuona tukio zima namna lilivyokuwa, insipekta Ezra alishangazwa na kasi ya kijana huyo mpaka kuwa na ujasiri wa kumvamia kiongozi huyo majira ya mchana wa jua kali namna hiyo. Risasi ambayo ilipenya kwa mheshimiwa na namna ilivyopiga iliwapa tahadhari juu ya uwezo wa huyo kijana hivyo waliomba kubaki na video hiyo kwa ajili ya upelelezi zaidi maana walikuwa na kazi ya kumtafuta kijana huyo ambaye kwenye video ile alionekana kupotelea uelekeo ule ambao wao walikuwa wanatokea akiwa anakimbia kama raia ambaye alikuwa anayaponya maisha yake lakini ndiye alikuwa muuaji mwenyewe.
"Haiwezekani mtu wa kawaida tu na mwenye akili timamu aweze kufanya tukio kama hili tena mchana wa jua kali namna hii wakati anajua kabisa kwamba hili eneo la wafanya biashara kuna kamera kila sehemu" Ezra aliongea akiwa anaiangalia miili ambayo ilikuwa imefunikwa pale barabarani na barabara ilifungwa kabisa hakuna mtu aliruhusiwa kusogelea hilo eneo.
"Unahisi ni kwanini amefanya hivi labda?" aliuliza polisi mwenzake
"Bado sielewi Hassan, hainiingii akilini kabisa kwa sababu kuonyesha sura yake maana yake ni kwamba anajua kabisa atatafutwa kila kona ya nchi hii sasa kwanini afanye hivi?"
"Huenda ni moja ya makosa ambayo hata baadhi ya wahalifu huwa wanayafanya, anaweza kuwa na mipango mikali kila sehemu ila akakosea sehemu moja tu"
"Hapana, kuna watu wa kufanya makosa ya namna hiyo lakini sio mtu kama huyu, kwanza kabisa anaonekana kwamba ni mtaalamu wa mauaji, angalia ujasiri alionao kuvamia msafara wa waziri mkuu tena akiwa na walinzi saba ambao wana mafunzo ya hali ya juu, halafu muda wenyewe ni mchana? Hilo haliwezi kuniingia akilini kabisa"
"Unamaanisha kwamba amefanya hili jambo makusudi kabisa?"
"Ndiyo"
"Kwanini afanye hivyo?"
"Hiyo ndiyo kazi yetu kuweza kujua kuhusu hilo jambo, kumbuka leo asubuhi tumepokea taarifa kutoka Zanzibar kwamba kuna mauaji yametokea hotelini, siku hiyo hiyo yanatokea mauaji mengine kwa waziri wa nchi huoni kama sio jambo la kawaida hili?" Ezra wakati anaongea hilo alishtukia jambo fulani ikamlazimu kuingiza mkono wake mfukoni kuitoa simu yake ambapo moja kwa moja alienda kwenye mtandao kuangalia jambo fulani. Alishtuka kidogo na kumsogezea mwenzake simu ili aone kile ambacho kilimshtua.
"Hii picha ina uhusiano gani na hili tukio?"
"Kwenye picha hapo mmoja ni waziri ambaye amuawa hapa saivi lakini huyo mwingine ni mfanya biashara Ismail Mhammed kutoka Zanzibar. Huyo mzee ndiye ambaye mwanae amekutwa ameuawa hotelini leo, unahisi hii inaweza kuwa bahati mbaya?" mwenzake hakuwa ameligundua hilo, kidogo hata yeye alianza kupata mashaka.
"Kwamba hivi vifo vinaweza kuwa na uhusiano?"
"Ndiyo moja kwa moja kwa sababu sidhani kama kuna bahati mbaya ya namna hii, hao wazee walikuwa wanafahamiana na kama wanafahamiana maana yake muuaji alipanga haya matukio kwa ustadi mkubwa ila alicho kifanya ni kutofautisha wakati wa matukio tu"
"Sasa kwanini aue wote wawili wa kwenye hizi familia ambazo zinaonekana kuwa na uhusiano wa karibu?"
"Bado sina jibu Hassan ila huenda kuna kumuunganiko mkubwa wa matukio na hii haiwezi kuwa bahati mbaya. Muuaji anaonekana kabisa kwamba alidhamiria sisi tuweze kuona sura yake ndiyo maana akaamua kulifanya hili mchana kwa sababu kama alitaka kufanya iwe siri basi angetafuta namna nyingine ya kuweza kumfikia waziri"
"Ni mtu gani mpuuzi wa kuja kuonyesha sura yake hadharani namna hii akiwa anafanya mauaji?"
"Huenda kuna ujumbe alitaka sisi tuupate, swali la msingi ni kwamba kwanini amuue waziri na alijuaje kuhus ratiba binafsi za waziri? Maana yake huenda kuna mtu mkubwa ambaye yupo nyuma yake mwenye uwezo wa kuzipata taarifa hata za viongozi wakubwa, sema nao hawa wazee wakiambiwa wawekewe ulinzi mkubwa huwa wanakuwa wabishi sana matokeo yake ndiyo haya sasa na hapa sisi ndio ambao tunaenda kupokea lawama kwa ujinga wake mwenyewe"
"Ezra relax kwanza tuanze kazi mara moja ya kumtafuta huyu mtu kumbuka hili jambo ni kubwa ambalo linaigusa mpaka Ikulu hivyo sio muda hapa IGP ataanza kuulizia majibu ya kumpatia mheshimiwa raisi kwani wizara itatakiwa kupata mtu mwingine mapema na hilo ni jambo ambalo inabidi litekelezwe na raisi mwenyewe"
"https://jamii.app/JFUserGuide them" Ezra aliongea kwa jazba kidogo akionekana kutopendezwa na hali ambayo ilikuwa imetokea. Aliingia kwenye gari na kutuma picha za mtu huyo ofisini ili waweze kumfahamu kwamba alikuwa ni nani haswa. Ulipita muda kidogo majibu yalirudi kwamba mtu huyo hayupo kwenye mifumo rasmi ya nchi, lilikuwa jambo la kushangaza kidogo basi ikawalazimu kuomba msaada kwa shirika la kipelelezi la nchi ili liweze kuwapatia taarifa zaidi juu ya mtu huyo.
Sehemu ya nane inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA NANE
SONGA NAYO................
"Kawasalimie kuzimu mpuuzi mkubwa wewe" alipofumbua macho alichomoka pale kwa mbio kali kumuwahi mtu yule kabla hajaingia kwenye yale maduka ya jumla, ilikuwa ni ghafla na ni wakati ambao walinzi walishtuka kwamba kuna mtu anakuja ule upande wao ila kwa bahati mbaya wakati wanashtukia hilo wawili walikuwa wamepigwa risasi na yule kijana tayari hali ambayo iliwafanya wananchi wengine kuanza kukimbia hovyo huku wangine wakisahau hata maduka yao wazi, maisha yao yalikuwa mhimu zaidi. Ule muingilianao wa watu ulifanya walinzi kutopiga hovyo risasi kwani wangejikuta wanaua watu wasio na hatia.
Kijane yule aliruka mpaka juu ya gari ambapo alidunda kwa mguu wake mmoja na kutua upande wa pili kwenye shingo ya mwanaume mmoja ambaye alikufa pale pale. Walinzi wawili walikuwa wanakimbia na ile familia kuelekea kweye yale maduka, wawili ndio ambao walibakia hapo kupambana naye. Alinyanyua bastola yake kwa kasi na kuachia risasi moja ambayo ilienda kutua kwenye kichwa cha yule mwanaume wa makamo akiwa anakaribia kuzama kwenye duka mojawapo hali ambayo ilizusha kelele kwa familia yake ikabidi mwanaume mmoja aende na familia ndani mmoja ndiye akabaki pale chini akiwa anamkokota mzee yule kuelekea naye ndani pia akiwa amepigwa risasi ya kichwa anavuja damu.
Vilisikika ving'ora vya polisi vikija kwa mbali eneo hilo, kijana huyo alisonya na kuzunguka kwa kasi kiasi kwamba risasi za wa wanaume hao zilikita kwenye gari, alisubiri wapige mpaka zilipo waishia ndipo alitokezea juu ya gari kwa kujiviringisha. Alitua karibu ya mwanaume mmoja ambaye alimpokea kwa ngumi iliyotua kwenye bega lakini hakutikisika zaidi aliishika shingo ya mwanaume huyo na kuivutia kwenye kisigino chake ambapo alikutanisha mguu na kichwa, alipo muachia alitoboa shingo hiyo kwa vidole vyake na kumtupia pembeni. Yule mwenzake alikuja kwa kukimbia ila alifuatwa kule kule ambapo alikutana na ngumi nzitoa ya kifua iliyomfanya kuhema kwa nguvu na kupiga goti, akiwa pale chini alipigwa risasi tatu za kichwa kukawa kimya.
Polisi waliingia ndani ya hilo eneo ambalo lilikuwa limetapakaa damu na miili barabarani lakini muuaji hakuonekana yuko wapi. Mtaa ulikuwa kimya huku kila mwenye duka karibu akiwa amekimbia bila hata kufunga na wengine walijifungia ndani ya maduka yao. Ving'ora vya polisi ndivyo ambavyo vilimtoa mlinzi mmoja mle ndani akiwa amembeba yule mzee kwenye mkono wake na kuwataka polisi waipe ulinzi familia ipo ndani na wengine watumie gari ya polisi kumuwahisha hospitali mzee huyo kuona kama wanaweza kuyaokoa maisha yake.
Familia ilipewa ulinzi na mzee huyo akawahishwa hospitali na gari ya polisi kwa sababu ilikuwa ni ngumu kuweza kuisubiri ambulance na hali yake ilikuwa mbaya sana lakini hata kabla hawajafika huko hospitali alifia njiani hivyo walifika na maiti kule hospitali. Ni muda fupi tu tangu litokee tukio hilo afisa wa polisi kutoka Osterbay Ezra Ethan maarufu kama Double E alikuwa amefika na askari wenzake kadhaa hapo wakidai kwamba hiyo kesi wao ndio waliagizwa kuja kuisimamia kutokana na ukubwa wa mtu ambaye aliuawa hivyo wakahitaji maelezo kutoka kwa hao maaskari ambao walikuwepo eneo hilo.
Kiufupi ni kwamba mtu ambaye aliuawa hilo eneo alikuwa ni bosi wao, waziri wa mambo ya ndani ambaye idara za polisi zipo chini yake, bwana Sylivester Mboneka ndiye ambaye aliuawa hivyo hiyo kesi ilikuwa na uzito mkubwa kwa jeshi la polisi. Licha ya mtu huyo kuwa waziri lakini pia alikuwa ndiye bosi wa idara hiyo kwani ilikuwa ipo chini ya wizara yake hivyo hata msako wa mhusika ulitarajiwa kuwa mkubwa zaidi. Yalitolewa maelezo mafupi lakini mtu ambaye alikuwa na maelezo mengi zaidi ni yule bodyguard mmoja ambaye alibaki na familia ndani ya yale maduka kwa sababu mwenzake mmoja alikuwa ameenda na mheshimiwa hospitali.
Alielezea tukio zima lilivyokuwa lakini ni kama kuna sehemu walikuwa wanakosa baadhi ya matukio ya kuunganisha hivyo wakawaomba wamiliki wa yale maduka waweze kuwaonyesha video ya tukio zima kwani waliamini eneo lile lilikuwa na kamera za kutosha. Kwenye video ambayo ilionyeshwa ndani ya hizo kamera iliwasaidia kuona tukio zima namna lilivyokuwa, insipekta Ezra alishangazwa na kasi ya kijana huyo mpaka kuwa na ujasiri wa kumvamia kiongozi huyo majira ya mchana wa jua kali namna hiyo. Risasi ambayo ilipenya kwa mheshimiwa na namna ilivyopiga iliwapa tahadhari juu ya uwezo wa huyo kijana hivyo waliomba kubaki na video hiyo kwa ajili ya upelelezi zaidi maana walikuwa na kazi ya kumtafuta kijana huyo ambaye kwenye video ile alionekana kupotelea uelekeo ule ambao wao walikuwa wanatokea akiwa anakimbia kama raia ambaye alikuwa anayaponya maisha yake lakini ndiye alikuwa muuaji mwenyewe.
"Haiwezekani mtu wa kawaida tu na mwenye akili timamu aweze kufanya tukio kama hili tena mchana wa jua kali namna hii wakati anajua kabisa kwamba hili eneo la wafanya biashara kuna kamera kila sehemu" Ezra aliongea akiwa anaiangalia miili ambayo ilikuwa imefunikwa pale barabarani na barabara ilifungwa kabisa hakuna mtu aliruhusiwa kusogelea hilo eneo.
"Unahisi ni kwanini amefanya hivi labda?" aliuliza polisi mwenzake
"Bado sielewi Hassan, hainiingii akilini kabisa kwa sababu kuonyesha sura yake maana yake ni kwamba anajua kabisa atatafutwa kila kona ya nchi hii sasa kwanini afanye hivi?"
"Huenda ni moja ya makosa ambayo hata baadhi ya wahalifu huwa wanayafanya, anaweza kuwa na mipango mikali kila sehemu ila akakosea sehemu moja tu"
"Hapana, kuna watu wa kufanya makosa ya namna hiyo lakini sio mtu kama huyu, kwanza kabisa anaonekana kwamba ni mtaalamu wa mauaji, angalia ujasiri alionao kuvamia msafara wa waziri mkuu tena akiwa na walinzi saba ambao wana mafunzo ya hali ya juu, halafu muda wenyewe ni mchana? Hilo haliwezi kuniingia akilini kabisa"
"Unamaanisha kwamba amefanya hili jambo makusudi kabisa?"
"Ndiyo"
"Kwanini afanye hivyo?"
"Hiyo ndiyo kazi yetu kuweza kujua kuhusu hilo jambo, kumbuka leo asubuhi tumepokea taarifa kutoka Zanzibar kwamba kuna mauaji yametokea hotelini, siku hiyo hiyo yanatokea mauaji mengine kwa waziri wa nchi huoni kama sio jambo la kawaida hili?" Ezra wakati anaongea hilo alishtukia jambo fulani ikamlazimu kuingiza mkono wake mfukoni kuitoa simu yake ambapo moja kwa moja alienda kwenye mtandao kuangalia jambo fulani. Alishtuka kidogo na kumsogezea mwenzake simu ili aone kile ambacho kilimshtua.
"Hii picha ina uhusiano gani na hili tukio?"
"Kwenye picha hapo mmoja ni waziri ambaye amuawa hapa saivi lakini huyo mwingine ni mfanya biashara Ismail Mhammed kutoka Zanzibar. Huyo mzee ndiye ambaye mwanae amekutwa ameuawa hotelini leo, unahisi hii inaweza kuwa bahati mbaya?" mwenzake hakuwa ameligundua hilo, kidogo hata yeye alianza kupata mashaka.
"Kwamba hivi vifo vinaweza kuwa na uhusiano?"
"Ndiyo moja kwa moja kwa sababu sidhani kama kuna bahati mbaya ya namna hii, hao wazee walikuwa wanafahamiana na kama wanafahamiana maana yake muuaji alipanga haya matukio kwa ustadi mkubwa ila alicho kifanya ni kutofautisha wakati wa matukio tu"
"Sasa kwanini aue wote wawili wa kwenye hizi familia ambazo zinaonekana kuwa na uhusiano wa karibu?"
"Bado sina jibu Hassan ila huenda kuna kumuunganiko mkubwa wa matukio na hii haiwezi kuwa bahati mbaya. Muuaji anaonekana kabisa kwamba alidhamiria sisi tuweze kuona sura yake ndiyo maana akaamua kulifanya hili mchana kwa sababu kama alitaka kufanya iwe siri basi angetafuta namna nyingine ya kuweza kumfikia waziri"
"Ni mtu gani mpuuzi wa kuja kuonyesha sura yake hadharani namna hii akiwa anafanya mauaji?"
"Huenda kuna ujumbe alitaka sisi tuupate, swali la msingi ni kwamba kwanini amuue waziri na alijuaje kuhus ratiba binafsi za waziri? Maana yake huenda kuna mtu mkubwa ambaye yupo nyuma yake mwenye uwezo wa kuzipata taarifa hata za viongozi wakubwa, sema nao hawa wazee wakiambiwa wawekewe ulinzi mkubwa huwa wanakuwa wabishi sana matokeo yake ndiyo haya sasa na hapa sisi ndio ambao tunaenda kupokea lawama kwa ujinga wake mwenyewe"
"Ezra relax kwanza tuanze kazi mara moja ya kumtafuta huyu mtu kumbuka hili jambo ni kubwa ambalo linaigusa mpaka Ikulu hivyo sio muda hapa IGP ataanza kuulizia majibu ya kumpatia mheshimiwa raisi kwani wizara itatakiwa kupata mtu mwingine mapema na hilo ni jambo ambalo inabidi litekelezwe na raisi mwenyewe"
"https://jamii.app/JFUserGuide them" Ezra aliongea kwa jazba kidogo akionekana kutopendezwa na hali ambayo ilikuwa imetokea. Aliingia kwenye gari na kutuma picha za mtu huyo ofisini ili waweze kumfahamu kwamba alikuwa ni nani haswa. Ulipita muda kidogo majibu yalirudi kwamba mtu huyo hayupo kwenye mifumo rasmi ya nchi, lilikuwa jambo la kushangaza kidogo basi ikawalazimu kuomba msaada kwa shirika la kipelelezi la nchi ili liweze kuwapatia taarifa zaidi juu ya mtu huyo.
Sehemu ya nane inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA