Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA NNE
SONGA NAYO................
Alimuita mwenzake na kumuonyesha shilingi hiyo ambayo pembeni ilikuwa na damu.
"Kuna lolote ambalo limeongelewa kuhusu shilingi?"
"Hapana, kwamba hii ni yake au watu ambao waliifuata miili ya wanajeshi waliokuwa huku?"
"Wanajeshi hawawezi kufanya hiki kitu, hii inawezekana ndiyo alama ya utambulisho wake yeye popote pale ambapo anakuwepo na kama amefanya hivi basi lazima kuna wanajeshi ambao aliacha shilingi pia kwenye miili yao" Bariki aliendelea kuongea huku akiwa anamulika pembeni ndipo aligundua uwepo wa damu ambayo ilikuwa imeganda chini kwenye nyasi ambazo zilikuwa pembezoni mwa mtu.
Alimulika mbele zaidi ndipo akaona kuna sehemu ambayo ilikuwa imekanyagwa zaidi na moja kwa moja ilionyesha kwamba kulikuwa na njia ambayo ilikuwa imeendelea basi wakalazimika kuifuata njia hiyo. Wakiwa wanaendelea kutembea Tigana mwili wake ulimsisimka kiasi kwamba mpaka akasimama na kumulika kila pembe ya hapo walipokuwepo lakini hakuona kitu wala jambo lolote lile la tofauti.
"Hili eneo hatupo pekeyetu Bariki, kuna watu wengine wapo hapa"
"Kwanini iwe hivyo na watu hao watakuwa wanatafuta nini hili eneo?"
"Sijui ila nahisi kuna watu wengine zaidi yetu hapa hivyo tuwe makini tunaweza kufa" alikuwa mtaalamu wa hayo mambo hivyo kauli yake ilikuwa ni onyo na Bariki alilijua hilo hivyo hakudharau ushauri wa mwenzake, alitakiwa kuuchukulia kwa uzito mkubwa. Walianza kutembea kwa tahadhari huku vichwani wakijua kabisa kwamba hawakuwa wenyewe ndani ya hilo eneo mpaka pale ambapo waliikuta ile sehemu ambayo ilikuwa na majivu mengi ikiwa ni ishara kwamba ndipo ilipokuwepo hiyo nyumba aliyokuwa anaishi huyo mtu aliyekuwa amefuatwa huko na wanajeshi kutoka Tanzania.
Waliizungukia hiyo sehemu, hakukuwa na vitu vya maana zaidi ya baadhi ya vifaa vichache ambavyo viliungua ungua na kubakia pamoja na chuma kimoja ambacho Tigana alikichomoa kwa nguvu wakagundua kwamba kulikuwa na shimo kwenye hilo eneo. Iliwalazimu kuchimbia hapo wakakutana na sanduku la mbao ambalo lilichimbiwa eneo hilo, hawakuamini kwamba maana yake kwa maafisa wengine ambao waliwahi kufanya uchunguzi hapo hawakugundua ishara hiyo? Wakalifungua, ndani yake walikutana na silaha nzito za kivita ambazo ziliwashangaza huku pembezoni mwa sanduku hilo kukiwa na vifaa kadhaa ambavyo bila shaka zilikuwa ni silaha za asili kutoka Japan na China.
Wanaume hao waliangaliana kama kwamba walikuwa wanaulizana maswali, wakiwa wanaendelea kusangaa ndipo wakakutana na kikaratasi kidogo ambacho kiliwekwa juu ya kitambaa. Kwenye kikaratasi hicho kulikuwa na majina ya watu wawili na tarehe pamoja na muda ambao walitakiwa kufa. Jina la kwanza lilikuwa ni la waziri wa mambo ya ndani ambaye mpaka wanafika huko tayari alikuwa ni marehemu na muda ambao uliandikwa kwenye ile karatasi ndio muda ambao aliuliwa, jina la pili ndilo liliwashangaza zaidi.
Lilikuwa jina la makamu wa raisi mstaafu wa Tanzania, alitakiwa kufa saa nane kamili usiku. Tigana aliangalia saa yake na kugundua kwamba ilikuwa saa tisa na nunu hivyo aliitafuta simu yake maalumu ambayo ilikuwa inaweza kushika mtandao popote pale alipo, aliipiga kwenda Tanzania kwa bosi wao kutaka kumpatia taarifa hiyo ili waweze kumlinda makamu huyo wa zamani wa raisi lakini wakati simu hiyo inapokelewa walikuwa wamechelewa tayari kwani waliambiwa kwamba ni muda mfupi uliokuwa umepita makamu huyo wa raisi alikuwa ameuliwa na walinzi wake wote kasoro mke na watoto tu. Walijikuta wanachoka na kukaa chini lakini Tigana bado alikuwa na ile karatasi kwenye mkono wake, taa ilimlika mwisho kabisa mwa ile karatasi na kilichokuwa kimeandikwa pale ni jina la mtu ambaye walikuwa wanamsadiki tu GAVIN LUCA.
"Inawezekana tunashindana na mzimu, binadamu gani anaweza kuyafanya mambo yote namna hii na yakaenda kama anavyo hitaji yeye?" waliona wingu zito mbele yao ndiyo maana Bariki aliongea kwa kuonyesha kabisa kwamba alinyong'onyea kwa kiasi kikubwa. Wakiwa wanafanya mazumzo hayo Bariki alimsukuma Tigana kwa nguvu kuelekea kando na kutamka
"Tumevamiwaaa" aliongea kwa sauti kali huku yeye mwenyewe akijitupa mbali naye Tigana hakulaza damu alijiviringisha na kwenda kutua mbali ambapo alikimbia kwa kasi kwenda kujificha kwenye mti ambao ulikuwa hatua kadhaa kutoka pale huku akiwa hajui Bariki naye aliingilia wapi. Bariki alimsukuma Tigana baada ya tochi kuelekea upande mmoja ambao ulikuwa na nyika ndogo akaona silaha imeelekezwa kwa mwenzake na kama angechelewa kufanya maamuzi ile risasi ingempotezea maisha Tigana.
Baada ya wao kutawanyika pale walifika wanaume wanne wakiwa kwenye silaha nzito, jambo la kushangaza ni kwamba walikuwa wamevaa mavazi ya jeshi la Tanzania.
"Hakikisheni hatoki hata mmoja"
"Lakini wale wanaonekana kuwa ni watanzania wenzetu"
"Hatakiwi kutoka hata mmoja hapa, hakikisheni wote wanakufa" aliyekuwa anayatoa hayo maelezo alionekana kuwa ndiye kiongozi wa kikosi hicho basi hawakuwa na namna ikawalazimu kugawana wawili wawili kwa sababu walijua watu hao wawili walienda sehemu tofauti. Tigana alikuwa amekishika kisu chake, silaha zao zote waliziacha pale chini walipokuwa wamekaa kwenye begi. Hatua za ujio wa watu hao wawili zilimfanya akishike kisu kile vizuri zaidi, alipohakikisha kwamba wamemkaribia alijitokeza ghafla ambapo alikata kiganja cha mwanaume mmoja ambacho kilikuwa kimeshika silaha kisha akazamisha kisu hicho kwenye moyo na kukishindilia.
Aligeuka na mguu wake ambao ulitua kwenye kichwa cha mwanaume aliyekuwa nyuma, mguu ulikuwa mzito hivyo ulimyumbisha yule bwana, alipotaka kukaa vizuri alipigwa na buti kwenye goti lake akainama chini, shingo ilidakwa na kuzungushwa mara moja, Tigana akachomoa kisu chake kwa yule mwanaume aliyekuwa chini na kukimbilia kule ambako Bariki alikuwepo. Bariki alikuwa juu ya mti akiwa anawaangalia vizuri wanaume wale na namna walivyokuwa wananyatia kuelekea hilo eneo.
Alimuona mwanaume mmoja chini lakini akasahau kabisa kumpigia hesabu yule ambaye alikuwa nyuma kwani hakumuona na yule ndiye ambaye alikuwa kiongozi wao. Alishuka kwa kuruka mpaka chini ambapo alitua nyuma, aliikutanisha mikono yake kwenye shingo ya huyo mwanaume mpaka ile shingo ikawa kama bapa, hakuwa na uhai mwanaume huyo alikuwa amekufa lakini kosa lake lilikuwa ni kusahau kwamba nyuma yake kulikuwa na mtu anakuja. Aliyekuwa nyuma alimuona vizuri hivyo alitaka kuachia risasi ndipo alishtuka na kugeuka ila silaha ilikuwa inamwangalia, aliinama ghafla chini wakati huo risasi zikawa zinasambaa hovyo kila sehemu.
Mwanaume yule alionekana kabisa kwamba alikuwa anahitaji kumhoji lakini naye alifanya upuuzi kuchelewa kwa sababu Tigana alikuwa amefika, alirusha kile kisu ambacho kilizama kwenye shingo ya mwanaume yule na ule mshtuko ndio ambao ulimfanya kurusha risasi hovyo kila sehemu ambazo zilimkosa kosa Bariki aliyeinama na kulala chini. Tigana alimsogelea mwanaume yule na kutaka kumhoji akiwa anakoroma pale chini kwa sababu kisu kilitokeza mpaka mbele ya shingo, mwanaume yule alichomoa bastola kiunoni kwake na kujipiga risasi akapoteza maisha.
Waliangaliana kwa viulizo na kuanza kumkagua, alikuwa ni mwanajeshi wa jeshi la Tanzania Hamza Malele kiasi kwamba wakabaki wamepigwa na butwaa. Waliwakagua wanaume wote wanne na kugundua wote walikuwa watanzania, sasa walikuwa wamefuata na kutafuta nini ndani ya nchi hiyo na kwenye msitu ambao ulifanyika mauaji ya ya kutisha? Hawakuwa na majibu wanaume hao wawili zaidi na wao walibaki kwenye mshangao mkubwa.


Taarifa ambazo zilikusanywa ndani ya msitu wa Mau na wale wapelelezi wawili zinatua kwenye mkono wa mkurugenzi, anastaajabishwa na taarifa hizo baada ya kugundua kwamba waliokuwa wapo huko ni wanajeshi wa Tanzania na hata walipo gundua kwamba waliokuwa wameenda huko ni watanzania bado walikuwa wanahitaji kuwaua.
Mkurugenzi ananusa jambo la hatari ambalo lipo kati yao wenyewe kwenye nafasi za juu, asubuhi alikuwa ofisini akiwa anasubiri simu ya mheshimiwa raisi ambaye baada ya kupokea taarifa za msiba wa makamu wa raisi wa zamani aliamua kuwahi kurudi nchini na asubuhi hiyo ya siku ya pili yake ndio wakati ambao alikuwa anafika. Mkurugenzi akiwa anaendelea kuwaza mambo kadhaa ambayo yalikuwa yanaendelea anapokea simu kutoka kwa raisi ambaye anamtaka wakutane kwenye nyumba yake ya siri Mbezi Beach ya chini haraka iwezekanavyo.
Yeye mwenyewe binafsi alikuwa na hamu kubwa ya kuongea na mheshimiwa kwa sababu kuna mambo mengi ambayo alionekana kufichwa hivyo kukutana na raisi aliamini angepata majibu ya maswali yake na namna mambo hayo yanatakiwa kuchukuliwa hatua kwa sababu yalikuwa yanaendelea kuharibu amani ya nchi na kuleta taharuki nzito baina ya watu na watu. Alifika nje ya jengo hilo, taarifa za ujio wake zilikuwa zinajulikana hivyo alifunguliwa moja kwa moja na kuingia mpaka ndani ya chumba cha ofisi ya raisi ambako alimkuta akiwa anamsubiri, walisalimiana na kuketi chini ili wayaanze mazungumzo yao.
"Micho pole kwa kila linalo endelea hapa nchini, naona imekuwa ni wiki ngumu kwa taifa zima lakini hii ni kazi yako kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa"

14 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA TANO
SONGA NAYO................
"Ndiyo maana nipo hapa mheshimiwa"
"Nipe ripoti nzima ya matukio yote ambayo yametokea"
"Mheshimiwa mimi na wewe tusiigize kana kwamba hatuelewi kinacho endelea nchini kwa sasa"
"Una maana gani?"
"Vifo vyote vimesababishwa na mtu mmoja na nina uhakika jina lake sio geni kwako"
"Gavin Luca"
"Ndiyo"
"Kwahiyo?"
"Kuna kitu labda unataka kuniambia kuhusu hilo mheshimiwa?"
"Kwanini unahisi kwamba kuna jambo nataka kukwambia?"
"Kwa sababu haya matukio hayatokei bahati mbaya, yana historia yake na nina imani hata wewe unaweza kuwa sehemu ya hii historia"
"Unamaanisha kwamba nahusika kwenye hili jambo?"
"Hapana ila kuna watu wa ngazi za juu nahisi wanahusika moja kwa moja"
"Kama yupi?"
"Mkuu wa majeshi"
"Kwanini?"
"Kwanza ilifanyika siri baada ya kujua mtu huyo yupo Kenya japo sijui alifahamu vipi habari hizo, baada ya hapo aliagiza mtu huyo aweze kuuawa na sio kukamatwa. Baadae wanajeshi wake wakauawa akapona mmoja tu lakini habari hiyo akaamua kuiweka siri bila kutoa taarifa sehemu yoyote ile na nilipokwenda kumhoji akanijibu jeuri. Usiku wa kuamkia leo nilikuwa nimetuma vijana wangu kwenda kufanya uchunguzi ndani ya eneo hilo ajabu ni kwamba wamevamiwa na wanajeshi wa Tanzania na walihitaji kuwaua...."
"Kwahiyo wao ndio wakawaua wanajeshi hao?"
"Yeah, nadhani unajua siwezi kuwatuma vijana walegevu huko, pointi yangu ya msingi ni kwanini watu hao wakutwe huko na walikuwa wanafanya nini kiasi kwamba wakahitaji kuwaua watanzania wenzao?"
"Ndicho hicho kimekuleta hapa Micho?"
"Mbona unaonekana kama haujali mheshimiwa"
"Kukuuliza swali ndo kumaanisha kwamba sijali?"
"Bila shaka hakuna kitu utanisaidia hapa"
"Unataka nini Micho?"
"Nataka majibu ya maswali yangu"
"Nipe muda nitakuja kukujibu"
"Watu wanaendelea kufa, inatakiwa huyu mtu apatikane na majibu yako inaweza kuwa njia nzuri ya kumkamata huyu mtu"
"Kwa taarifa zako za awali kabla sijarudi ulituma kwamba mtu huyo aliuawa, saivi unakuja na habari kwamba anafanya mauaji ya watu sasa uliwahi kusikia wapi maiti inaweza kuua watu?"
"Nina imani kwamba aliyekuwa amekufa huenda sio yeye"
"Picha na video vinaonyesha kwamba ni yeye, sasa inawezekana vipi useme sio yeye?"
"Unataka kuniambia kwenye haya matukio ya mauaji ambayo mtu huyu ameonekana kuhusika ni mtu mwingine anatumia utambulisho wake kutuchanganya?"
"Hiyo ni kazi yako wewe Micho kunipa majibu na nakupa masaa ishirini na manane tu niwe na majibu mezani, mimi ndiye napaswa kukuuliza wewe haya maswali ya usalama wa nchi na sio wewe kuniuliza mimi" Micho Othman alisikitika na kumwangalia raisi wake kwa umakini mno, hakuwa na kitu angeweza kufanya hivyo alitakiwa kuwa mpole. Hakuona haja ya kukaa hapo kwa sababu raisi alikuwa anamjibu kwa jeuri na hakuna kitu angeweza kumsaidia wakati huo hivyo aliamua kuondoka kwenda kukaa mezani upya.
Saa moja tu lilipita tangu atoke kuongea na raisi mazungumzo ambayo hayakuwa na mwafaka wa kueleweka, taarifa ilitolewa kwenye vyombo vya habari kwamba raisi anaenda kuzungumza na wananchi wake kwa ajili ya mambo yote ambayo yalikuwa yametokea nchini hususani mauaji ya viongozi wakubwa.
"Mimi Nixon George, nikiwa kama raisi wa Tanzania, nawapa pole sana wananchi wote kwa mkanganyiko huu mkubwa ambao ulikuwa unaendelea nchini baada ya mauaji kadhaa kutokea. Leo hii nimekutana na viongozi wa vyombo vyote vya usalama na wamenihakikishia kwamba tukio hili litakuwa na ukomo hivi sasa baada ya kuweka mazingira madhubuti na kuhakikisha kila ambaye alihusika anakamatwa na kuonyeshwa mfano kwa watu wengine ambao wanataka kuvuruga amani ya hili taifa tuliyo ipigania kwa miaka mingi mpaka kuwa kwenye hali kama hii hivi leo"
"Kuna jina ambalo limeibuka kwa ukubwa kwenye midomo ya watu, Gavin Luca. Hili jina ni la mtu ambaye alishakufa tayari, nadhani mhusika ambaye alikuwa anafanya haya ameamua kutumia hilo jina kwa ajili ya kutuchanganya akihisi kwamba hatapatikana ila niwahakikishieni tu kwamba mtu huyu mpaka sasa tuna taarifa zake zote na hivi sasa ninapo ongea hapa anaendelea kutafutwa kila kona ya nchi hii na nina imani baada ya muda mfupi atakuwa kwenye mikono yetu"
"Nipende kuwatoa kabisa hofu wananchi wangu, nawasihi muendelee na shughuli zenu za kila siku kwa ajili ya maendeleo na uchumi wa taifa hili. Lakini pia nichukue nafasi hii kuweza kutoa pole kwa familia ambazo zimewapoteza wapendwa wao kwa kipindi hiki, serikali itakuwa nao bega kwa bega na tutahakikisha haki ya wapendwa wao inapatikana ukizingatia walio uawa ni watu ambao wamelitendea makubwa taifa hili na walijitoa kwa nguvu zote kuweza kuipigania Tanzania mpya ambayo inazidi kukua kila iitwapo leo"
"Natoa rai pia kwa wananchi, kama ambavyo taifa letu limeundwa kwa umoja, amani na mshikamano basi iwe hivyo siku zote, hivyo vitu vitatu viwe nguzo yetu kupambana na kila aina ya ushenzi ambao unatengenezwa na watu kadhaa kwa lengo la kuivuruga hii nchi na kwa wananchi tunahitaji ushirikiano wenu wa dhati pale ambapo mnakuwa mnaona kwamba kuna mambo hayaendi sawa basi msisite kufikisha taarifa mahali husika ili kuhakikisha tunapambana na kila adui ambaye anaweza kutuharibia ramani nzima ya taifa letu. Mungu ibariki Tanzania"
Kiongozi huyo alimaliza hotuba yake fupi ambayo ilimshangaza zaidi mkurugenzi kwa sababu asilimia kubwa ya vitu ambavyo aliviongea vilikuwa ni vya uongo. Alibaki ameduwaa akishindwa kumuelewa bosi wa nchi alikuwa amepatwa na kitu gani, tangu arudi kwenye ile ziara yake alikuwa kabadilika kuanzia maongezi yake na hata maamuzi ambayo alionekana kuanza kuyafanya. Hakuonekana kujali sana kuhusu taifa lake kama ilivyokuwa mwanzo, hata vile vifo hakuonekana kwamba alivichukulia kwa uzito, kuna namna mkurugenzi alianza kuona kama hiyo vita aliachiwa yeye mwenyewe ndiye aweze kupambana nayo.


BAHARI BEACH
Pembezoni mwa bahari karibu kabisa na fukwe ya Bahari Beach kulikuwa na nyumba ambayo ilionekana kumilikiwa na mtu mwenye vyake. Ilikuwa ni nyumba binafsi ya CDF Medrick Savato na wakati huo alikuwa ndani ya eneo hilo kuweza kukutana na kijana wake ambaye alionekana kuishi nje ya nchi na wakati huo alikuwa amerejea kama ambavyo alimtaka afanye.
"Bashiri muda wa likizo umeisha sasa, unatakiwa kuingia kazini. Kazi niliwakabidhi vijana wangu baada ya kuniaminisha kwamba wanaweza kuifanya lakini imekuwa tofauti na vile nilivyokuwa nategemea hivyo unatakiwa kurudi kazini mara moja"
"Ni nani ambaye anatakiwa kupatikana bosi?"
"Mpaka sasa sijajua kwamba ni mtu gani ambaye anatakiwa kupatikana ama kufa kwa sababu mhusika namba moja alishakufa sasa inanishangaza kukutana na mtu mpya ambaye anatumia jina la Gavin Luca"
"Lakini Gavin Luca si amekufa?"
"Ndiyo amekufa ila mpaka sasa sielewei kama ni yeye kafa au ni mtu mwingine?"
"Ulinitumia video na picha na yule ni yeye mwenyewe bosi"
"Sasa huyu mwingine ni nani?"

15 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA SITA
SONGA NAYO................
"Huenda hilo nitalijua baadae, kuna kitu chochote ambacho mlikikuta eneo la tukio?"
"Ndiyo, shilingi ya zamani ndiyo ambayo aliitumia kufanyia mauaji"
"Shilingi?"
"Ndiyo, vipi una uelewa nayo?"
"Ndiyo bosi, huo uliwahi kuwa utambulisho wa Gavin Luca baada ya kujionyesha kwa mara ya kwanza ila baadae ukaja kupotea tena"
"Kwanini alikuwa anatumia shilingi kama utambulisho wake?"
"Tukipata jibu la hilo swali basi ujue kabisa tutakuwa tumejua kila kitu kuhusu yeye"
"Kwa sasa siwezi kuwatumia wanajeshi kwa sababu mkurugenzi wa wa shirika letu la upelelezi ananifuatilia inaweza kuwa tatizo na leo tena limetokea jambo lingine la kustaajabisha kwa sababu baada ya mauaji ya wanajeshi kule msituni nilipeleka vijana wengine wa kazi wanne nikiamini kwamba muuaji anaweza kurudi japo kwa bahati mbaya ili wanipe hiyo taarifa lakini habari mbaya ni kwamba nao wamekufa na hakuna alama yoyote ya mhusika ambaye amewaua zaidi tu amebeba vitambulisho vyao na kuondoka"
"Bosi kuna mtu yeyote labda ambaye unahisi kwamba anaweza kuwa amehusika na jambo hili ambaye yupo kwenye mzunguko wetu?"
"Sina imani na hili jambo lakini inawezekana ila sidhani kama kuna mtu mwenye uwezo wa kuua wale watu kikatili namna ile, inanishangaza kiasi kwamba hata mimi mpaka sasa sijui nimwamini nani na nisimwamini nani kwani huenda mtu mwenyewe nipo naye karibu ila simjui hivyo inaweza kuniletea madhara hata mimi mwenyewe"
"Kwa sasa hautakiwi kuwa na safari nyingi zisizo na umuhimu kama italazimu kuwa hivyo basi hakikisha una ulinzi wa kutosha ama mimi nipo karibu. Bado inanishangaza ni mtu yupi ambaye amejitokeza na kujitambulisha yeye kama Gavin Luca wakati mhusika amekufa au kuna jambo hatulifahamu kuhusu Gavin Luca bosi?"
"Inawezekana ikawa hivyo, ebu ichimbue historia yake kama unaweza ukaipata sehemu yoyote ile huenda kuna kitu kidogo hakipo sawa ndicho kinatuumiza akili"
"Hilo nitashughulika nalo, nakumbuka uliniambia kwamba kuna mwanajeshi wako mmoja ndiye alifanikiwa kupona kwenye lile sekeseke la msituni"
"Ndiyo, anaitwa Sarah Martin"
"Ulimhoji vizuri kwamba ni kwanini awe pekee ambaye aliachwa hai wakati wengine wote walikufa?"
"Tulimkuta ana hali mbaya huenda muuaji alihisi amemmaliza akamuacha hai"
"Hapana bosi huwa haiendi hivyo, mimi ni miongoni mwa hao wauaji ambao unawazungumzia hivyo na huwa tuna tabia ambazo zinafanana, siwezi kwenda kufanya kazi ya kuua watu halafu nikamsahau mtu kwa bahati mbaya kwa sababu huwa tunahakiki kila ambaye yupo hapo amekufa ndipo tunaondoka"
"Unajaribu kumaanisha nini?"
"Huenda aliachwa hai kwa makusudi na kama ipo hivyo basi kuna vitu aliviona ama aliongea na mhusika hivyo lazima pia atakuwa anamfahamu mhusika"
"Ni binti ambaye sina shaka naye, hali yake haikuwa nzuri hata kiakili baada ya kusimulia aliyo yashuhudia kule hivyo nilimpa ruhusa aweze kupumzika nyumbani kwake"
"Naomba maelezo yake nikamhoji"
"Usije ukafanya jambo lolote la kipuuzi ambalo litaibua hisia za watu, mauaji ya vijana wangu wote nimeamua kutoyafikisha kwenye vyombo vya habari kumaliza kelele hivyo hata hili halitakiwi kufika mahali popote pale"
"Nipo makini bosi, nataka nikamhoji tu kama mtu wa serikali nikitimiza majukumu ya itifaki za kuisalama" Alipewa maelekezo ya namna ya kumpata mwanamke huyo ili akamhoji kama alivyokuwa amesisitiza akiwa ana imani kwamba lazima kuna mambo ambayo binti huyo alikuwa anayajua vizuri kabisa.






SINGIDA
SINGIDA VIJIJINI,
KATA YA MSISI, KIJIJI CHA NTONDO.
Ni kijiji ambacho kinapatikana ndani ya kata ya Msisi, wilaya ya Singida vijijini mkoani Singida. Kijiji hicho kina maisha ya chini au tunaweza kusema yale ya kawaida sana kwa sababu ya ukosefu wa huduma mhimu za kijamii kama umeme na barabara bora ambazo zingeweza kurahisisha usafirishaji pamoja na mawasiliano. Wanakijiji wengi wanajihusisha na shughuli za kilimo kidogo kwa ajili ya chakula ndani ya eneo hilo hivyo kufanya hata maisha yao kuwa ya kawaida tu yale ya kupambana kwa ajili ya kumudu vitu vidogo vidogo.
Kutokana na hali kuwa ngumu kwenye upande wa umeme ndani ya kijiji hicho iliwalazimu wenyeji kutumia zile taa za zamani aina ya chemli kwa ajili ya kuweza kujipatia mwanga. Kwenye eneo hilo kulikuwa na nyumba nyingi za hali ya chini na zile ambazo zilikuwa angalau hazikuwa nyingi kiasi kwamba ungepata muda wa kutosha basi ungeweza kuzihesabu kwa usahihi kabisa na kupata idadi yake kamili.
Lakini ilikuwa ni tofauti kwa baadhi ya familia chache ambazo licha ya kuwa huko lakini bado maisha yao hayakuwa ya chini kihivyo, walikuwa angalau wana uhakika na kila ambacho walikuwa wanakifanya na chakula hakikuwa haba kwao. Mita miatatu kutoka ilipokuwa barabara kuu ambayo mara moja moja usafiri ulikuwa ukipita kulikuwa na nyumba ambayo ilifahamika sana kwa sababu ilikuwa inamilikiwa na askari wa polisi ambaye licha ya kufanyia kazi Singida mjini lakini huko ndiko kulikuwa kwake na familia yake.
Askari huyo alikuwa ni mwanamke mkarimu ambaye alipendwa karibia na kila mwanakijiji, roho yake nzuri iliwafanya wazidi kumuombea lakini haikuishia hapo tu bali ustaarabu na wema ambao alikuwa nao mumewe ndivyo vilizidisha kuwafanya watu hao wazidi kuwa kwenye vinywa vya wanakijiji kila wakati kwani kuishi kwao ndani ya kijiji hicho kulifanyika kuwa neema na msaada mkubwa kwa sababu walikuwa wakijitoa kwa kiasi kikubw kwa hao wanakijiji kuanzia msaada wa kifedha mpaka mawazo ya namna sahihi ya kuishi kwenye mazingira kama hayo na kuyafanya kuwa bora nyakati zote.
Wakati mkewe akiwa ni askari polisi, mumewe alikuwa ni mkulima mzuri, muda mwingi ungemkuta yupo shambani akiwa anajitahidi kuhakikisha analima matunda ya kutosha nyumbani kwake, alikuwa ana visima kadhaa vya maji ambavyo alivichimba kwa gharama kubwa ili kuhakikisha kwamba anapata uhakika wa umwagiliaji wakati wote hivyo eneo lake lilitawaliwa na ukijani. Watu wengi hawakuwahi kumjua kiundani mwanaume huyo kwa sababu hakuwa mtu wa kuonekana mara kwa mara wala kujichanganya sana na watu, alikuwa akionekana mara kadhaa akiwa anaenda kutoa misaada kwa watu wa kijiji hicho pamoja na kujitolea kwenye kazi mbali mbali ambazo zilijumuisha maendeleo ya kijiji.
Licha ya uadimu wake watu walimheshimu kwa kiwango kikubwa na kumpenda, bwana huyo alikuwa muislamu ila hakuwahi kujali sana kuhusu utofauti wa dini miongoni mwa watu, aliishi safi na kila mtu na muda mwingi ungemkuta amevaa kanzu na kofia yake kichwani, dini ilimkaa vizuri na ikampendeza lakini bado hawakuwahi kuujua ukweli wa maisha yake. Alikuwa mtu wa swala na kutenda yaliyo mema, alikuwa mtu safi kwa kila mtu naye akayaishi maisha kwa njia sahihi kama maandiko yalivyo sadiki na kusisitiza.
Kwenye familia yao hiyo walifanikiwa kupata mtoto mmoja wa kike ambaye alikuwa anasoma shule ya international ya watoto iliyokuwa Singida mjini hivyo muda mwingi kijijini alikuwa anashida yeye pekeyake kwani mkewe siku za wiki alikuwa anaishi mjini ambako alikuwa anafanyia kazi hilo kwao halikuwahi kuwa tatizo kabisa.
Mwanaume huyo siku kadhaa nyuma alimuaga mkewe kama ana safari ya kwenda ndani ya jiji la Dar es salaam ambako alimaliza wiki nzima ndipo siku ya wikiendi alipofanikiwa kurudi na mkewe ndiye aliye mpokea kwa furaha baada ya mwanaume huyo kurudi na pikipiki mpaka kwake. Alikuwa na usafiri wake wa gari lakini alitoka safarini na hakutaka kumsumbua mkewe, mkewe alimpokea kwa shangwe mumewe ambaye alimbebea zawadi nyingi yeye na mtoto ambaye naye pia alikuwa amerudi kwa ajili ya kuwa na familia yake siku za wikiendi.

16 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
SIMULIZI TUTAIMALIZA HAPA HAPA...

Ila kwa wale wa kuisoma siku moja, kuna ofa ya wikiendi hapa.....

Simulizi mwisho ni episode ya 105...... malizia kwa ofa ya wikiendi ya 3000...

Lipia 3000 yako tu nikumalizie episodes zilizo bakia au nakupa zawadi ya pdf kitabu kizima..... Ni kwa ajili ya wikiendi tu[emoji871]

0621567672 (HALOPESA)

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

36316279 (LIPA NAMBA (M-PESA) inapokea mitandao yote)

FEBIANI BABUYA
idaiwe%20Maiti3.jpg
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA SABA
SONGA NAYO................

Ilionekana kuwa familia yenye furaha kubwa ukizingatia mwanae alikuwa akimpenda mno baba yake, mwanaume huyo kwenye uso wake alikuwa amejaa ndefu ambazo zilichongwa vyema na kutunzwa kwa ustadi mkubwa. Alimtaka mkewe na mwanae watangulie ndani yeye angefuata ni baada ya kuhisi simu yake moja inaita, alitoka nje kabisa ya geti la nyumba yake na kwenda kuipokea simu hiyo ambapo alimsikiliza mtu wa upande wa pili kisha akatamka sentensi nyingine moja tu
"Kwa sasa ondoka kabisa mjini mpaka nitakaporudi nitakutafuta mwenyewe, nilitaka kuwatumia ujumbe ambao utanifanya niwapate wote" aliikata simu hiyo baada ya kauli hiyo kisha akaivunja vunja simu yenyewe na kwenda kuifukia mbali na geti la nyumba yake kisha akarejea tena ndani kuweza kujumuika kufurahia na famia yake.


TUA-NGOMA,
Ni moja ya sehemu ambazo zipo pembezoni kabisa mwa jiji la Dar es salaam. Sio kweli ila kuna watu huwa wanaamini kwamba kuna baadhi ya watu hukimbilia kuishi huko kwa sababu ya kupunguza gharama za maisha, japo kuna namna ni ukweli ila sio kweli moja kwa moja kwa sababu kuna watu wapo huko na wanaishi maisha ya gharama kushinda hata wale ambao wanaishi katikati mwa jiji la bandari ya salama.
Eneo hilo kama ilivyo kawaida kila mtu huwa anajali maisha yake tu, hakuna mtu ambaye ana muda na maisha ya mtu mwingine kwa sababu watu wanayo mengi kwenye mioyo yao ambayo yanawafanya wawe wanalia huku wanatembea, mtu wa hivyo hawezi kuwa na muda wa kufuatilia maisha ya mtu mwingine kwa sababu yeye mwenyewe binafsi anayo yake mengi ya kuyashughulikia. Kwenye mitaa ya eneo hilo kulikuwa na mwanamke maarufu ambaye alijulikana kwa kutokuwa sawa, akili zake zilionekana kuyumba kwa muda kiasi kwamba watu wakawa hawana muda naye tena.
Bi Aisha, ndilo lilikuwa jina lake maarufu, mwanamke huyo hakueleweka alitokea wapi baada ya kupatwa na hali hiyo ila mwanzoni gari za serikali zilikuwa zikifika mara kadhaa kwenye hilo eneo ila baadae baada ya miaka kadhaa zilikuja kuacha kabisa kwenda tena eneo hilo ni kama walimpotezea. Mwanamama huyo aliwai kuwa kanali wa jeshi hivyo baada ya kupatwa na matatizo mara ya kwanza wanajeshi walikuwa wakifika hapo mara kwa mara kumpatia mahitaji ya mhimu lakini pia kuna wanajeshi walikuwa wakiishi mitaa hiyo kwa ajili ya kuweza kumlinda.
Kama kawaida ya wanadamu, watakujali mwanzoni tu ila kama hauna umuhimu kwao kwa wakati huo hata serikali itakuchoka ndiyo maana waliamua kumtelekeza mama huyo na kumuacha kama alivyo, hakuna ambaye aliendelea kumjali tena kiasi kwamba wakaachana naye kabisa. Jambo kubwa kwake ni kwamba wakati serikali inamtelekeza wakati huo tayari alikuwa amejengewa nyumba nzuri tu ndani ya eneo hilo japo watu wengi waliamini kwamba ni msamaria mwema tu aliamua kumpa hifadhi ila uhalisia ni kwamba palikuwa ni kwake.
Mwanamama huyo licha ya wengi kumjua kama kichaa ambaye hakuwa akijielewa lakini kila ifikapo jumamosi saa tano usiku alikuwa anavaa vizuri, anatoka na wanaume ambao walikuwa wakifika ndani ya eneo hilo na gari za kifahari wanamchukua na kumpeleka kwenye fukwe ya bahari. Akiwa huko alikuwa akiyagusa maji kwa hisia kali, machozi yalikuwa yakimtoka kwa maumivu makali akiwa anaongea kimoyo moyo na bahari ambayo usiku huo yangesikika mawimbi tu yakitamba na taa za meli ambazo zilikuwa baharini humo zikingojea safari za kwenda mbali nje na hapo.
Ilikuwa ni miaka mingi sana imepita ila haikuwahi kupita hata jumamosi moja akakosa kwenda ndani ya eneo hilo hata kama angekuwa wapi ilikuwa ni lazima aende. Alikaa hapo kwa masaa mawili ndipo akarudi kwenye gari na kuwataka vijana wake wamrudishe nyumbnani aweze kupumzika. Mwonekano wake haukuonekana kuwa mtu ambaye hakuwa na akili timamu au kuwa na tatizo lolote la akili, alikuwa mmama mwenye afya yake na uelewa wake mzuri tu na alipendeza mno kwani hakuonekana kuwa na shida za maisha kama ambavyo wengi walikuwa wakimtazama anapokuwa mtaani.
Baada ya kurudi nyumbani kwake siku hiyo hakutaka kabisa usafiri uondoke pale kwake, alienda kulala na kuwaacha vijana wake wakiwa makini na silaha zao kuhakikisha anakuwa salama mama huyo. Kulikucha mapema ya asubuhi, mwanamama huyo alijiandaa na kupanda kwenye gari ambapo msafara wa gari nne za kifahari ulitoka ndani ya nyumba yake na kuwashangaza watu ambao walikuwa karibu na mazingira hayo. Mama huyo alitaka msafara huo usimame kwani alihitaji kutoka nje, alitoka na kwenda kumpatia pesa nyingi mwanamke mmoja ambaye alikuwa amekaa kando ya barabara akiomba msaada kwa wapita njia.
Mijadala ilianza kuzushwa na kutengenezwa watu wakiwa hawaamini kama ndiye yule mwanamke ambaye wao walimjua kama kichaa, lilikuwa ni jambo la kustaajabisha isivyokuwa kawaida ila haikuwa sababu ya kuweza kuukataa ukweli kwamba alikuwa ni yeye. Baada ya kuhakikisha kwamba wote wamemuona ndipo alirudi tena kwenye gari na kupanda kisha akautaka msafara huo uweze kuondoka eneo hilo kuelekea kule ambako yeye alihitaji kuwepo.
Safari yao ilionekana kabisa kuelekea Bunju kwenye makazi ya aliyekuwa CDF, msafara huo hakuna mtu ambaye alikuwa anautegemea ndani ya eneo hilo hivyo baada ya kufika getini alizuiliwa kwa kudaiwa kwamba hakuna mtu kama yeye ambaye kulikuwa na taarifa za kufika kwake hapo ndani. Alimtaka mlinzi huyo ampe taarifa CDF kwamba mtu ambaye yupo nje hawezi kukaa kumsubiri yeye hivyo kama ana kikao chake chochote alitakiwa kukifuta muda huo na akutane naye haraka.
Taarifa hiyo ilimshtua CDF ikamlazimu atoke mwenyewe na walinzi wake kuja kumuona mtu ambaye alikuwa analazimisha kuonana naye kwa sababu alidai wakati huo alikuwa kwenye kikao kizito cha mambo ya usalama wa nchi. Alishtuka kumuona mama huyo kwenye uso wake kiasi kwamba ule ujasiri ulimtoka kabisa akabaki ameduwaa tu
"Nasikia upo busy sana Medrick"
"Aurelia!!!!" alitamka jina la mwanamke huyo akitaka walinzi wake wamruhusu aingie humo ndani haraka. Walijongea mpaka sehemu iliyokuwa na upepo mzuri kwa ajili ya kufanya mazungumzo.
"Nini unakitaka Aurelia, nimekuacha na maisha yako na sitaki kabisa kujihusisha na wewe tena"
"Wote tunajua kwamba huwezi kulikwepa hili Medrick, una deni kubwa sana kwenye maisha yangu halafu ukaja kunifanyia ushenzi unahisi hili litapita kama unavyohisi wewe?"
"Unajua ninaweza kukuua muda wowote nikitaka Aurelia?"
"Maisha yako yanategemea uhai wangu na hilo unalifahamu, ukifanya upumbavu utakufa kijinga ukiwa unajiona na hao watu wako hata hawatakuwa na uwezo wa kukulinda"
"Kwa maana hiyo Gavin Luca yupo hai?"
"Nasikia umemua sasa unaniambiaje kwamba yupo hai?"
"Kama angekuwa amekufa usingekuwa na hiyo jeuri ya kunijia hapa kwangu na kuongea hivi"
"Wewe ni miongoni mwa watu ambao hawajulikani kwamba walihusika na hili jambo, na hakuna mtu anajua kwamba ulikuwa nyuma ya ule ushenzi ila itategemea na maamuzi yako kwa sababu huenda muda mfupi ujao ukweli unaweza kuwa wazi"
"Kwanini hukutaka kuwaambia watu mapema?"
"Kwa sababu kuna kazi nataka nikupe"
"Umpe kazi mkuu wa majeshi wa nchi?"
"Hicho cheo ni kwa hao wapumbavu wenzako sio kwangu, kumbuka wewe ulitakiwa kufa muda mrefu sana ila nikakuacha hai mpaka leo unatamba. Kila jumamosi huwa naenda baharini sehemu ambayo mume wangu na mtoto wangu walifia sio kwamba huwa nakuangalia vizuri kila nikiwakumbuka bali niliamua kukuacha ili ufanye majukumu yangu ya msingi na ipo siku ukienda tofauti na mimi kama ambavyo umefanya saivi kutaka kumuua mwanangu nitakuua kwa mkono wangu"
"Kwahiyo nipo sahihi Gavin Luca ni mzima. Kama ni hivyo yule ambaye nimemuua kule Kenya ni nani?"
"Hilo swali unatakiwa kujijibu wewe kwa sababu sicho ambacho kimenileta hapa, nimekuja kukupa kazi ya kufanya"
"Ipi"
"Nataka mke wa raisi auawe"
"Whaaaaaat?"
"Umenisikia tangu mwanzo, mke wa raisi anatakiwa kufa na hiyo kazi unatakiwa uifanye wewe kwa mkono wako na sio kutuma kijana wako. Gavin hajui kama wewe ulikuwa miongoni mwa wahusika wakuu wa yale yote ambayo yalitokea na siku akija kujua ndiyo itakuwa siku ya mwisho kuliona hili jua nadhani unalitambua hilo japo kuna mambo huyajui"

17 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA NANE
SONGA NAYO................
"Aurelia umechanganyikiwa, unataka mimi nimuue mke wa raisi wa nchi?"
"Uchaguzi ni wako Medrick ufe wewe au umuue Valeria" mama huyo aliongea akiwa mkavu sana usoni, alikuwa anamuagiza mkuu wa majeshi mithili ya mama anavyo muagiza mwanae sokoni. Mkuu wa majeshi alibaki anajichekesha kwa hasira akiwa anaukunja mkono wake.
"Usiruhusu yakutokee yale ambayo yamemkuta makamu wa raisi mstaafu na waziri wa mambo ya ndani haitapendeza kwako, bado una familia ya kuilea Medrick. Nimekupa ni msaada wa kukufanya mpaka leo upo hai kwa sababu za kiutu uzima tu ndiyo maana hii siri sijamshirikisha yeye ila nakuhakikishia siku akija kutambua kuhusu uhusika wako hata mimi sitakuwa na uwezo wa kukulinda tena"
"Gavin Luca anajifanya yeye ni nani hasa mpaka anahisi kwamba anaweza kufanya kila ambacho anakitaka yeye?"
"Kuna mambo mengi sijawahi kuongea lolote kuhusu yule mtoto, ni kama jini, kuna nguvu anazo ambazo hatakiwi kuzitumia kwa wanadamu kama sisi hapa mimi na wewe ndiyo maana nimekwambia kwamba hata mimi sitaweza kukulinda kama akitambua jambo hili. Nimemlea mwenyewe kwenye mikono yangu hivyo najua kiumbe ambacho kilitengenezwa ndani yake. Nikutakie wakati mwema" Mama huyo alimaliza na kuondoka, alikuwa ameacha maagizo ya kazi ambayo ilikuwa ni juu yake mkuu wa majeshi kuifanyia maamuzi.
Alibaki eneo hilo pekeyake akipiga kelele za hasira, mkuu wa majeshi alikuwa anatishwa na mwanamke wa kawaida mtaani na kumpa maagizo ya kumuua mke wa raisi ambaye alikuwa madarakani mpaka wakati huo kazi ambayo ilikuwa ni hatari kwa usalama mzima wa nchi na hata maisha yake yeye binafsi na nafasi yake. Aliona kabisa anahitaji msaada wakati huo, akili yake ilikuwa imefika mwisho kuwaza alipiga simu mahali na kuomba kuonana na mtu huyo wa kwenye simu ambaye aliamini angempa msaada sahihi.



***********
MLANDIZI
CDF hali ambayo alikutana nayo baada ya kukutana na mwanamke ambaye yeye alimfahamu kama Aurelia ilimchanganya na kumpa hofu, licha ya kujua kabisa kwamba alikuwa anamiliki jeshi la nchi ila alitambua aina ya mtu ambaye alikuwa anadili naye kwa wakati huo.
Kukutana na mwanamama huyo kwanza kulimhakikishia kwamba mtu ambaye yeye alihisi amemuaa alikuwa hai bado, akiwa amechanganyikiwa kuhitaji kujua kama mtu huyo alikuwa hai na yule ambaye yeye alimuua alikuwa ni nani hasa ndipo akapewa kazi ambayo ilikuwa ni kazi hatari kwa maisha yake kama taarifa zingevuja. Kumuua first lady wa nchi ilikuwa ni sawa na kuona moto unawaka mahali halafu unapeleka tenki lililojaa petroli ndani yake, ukicheza vibaya linapita na maisha yako.
Akili yake ilifika mahali ikagoma kabisa kufanya kazi na kumsaidia kufikia mwafaka ndiyo maana aliona kabisa kwamba anahitaji msaada hususani kutoka kwa mtu ambaye yeye alimhusudu na kuamini kwamba angeweza kumsaidia kutoka kwenye janga la namna hiyo. Hali hiyo ndiyo ambayo ilimfanya kufunga safari ya siri baada ya usiku kuingia kuelekea huko Mlandizi Pwani akiwa na gari tatu kwenye msafara wake ambazo ziliachana kwa umbali kadhaa ili watu wasiweze kushtuka kumuona kwa namna yoyote ile.
Medrick Savato ndilo lilikuwa jina lake kigogo huyo aliye onekana kuchanganyikiwa kwa huo muda asijue hatima yake ilikuwa ni ipi baada ya kujikuta anakuwa mnyonge mbele ya mwanamke tena raia tu ambaye alikuwa anaishi mtaani japo walionekana kuwa na historia ndefu ya pamoja watu hao. Safari yake ilipitiliza mpaka mbele kabisa baada ya kuivuka Mlandizi akiwa kama mtu ambaye aliendelea na safari ya kwenda Morogoro.
Baada ya kuivuka Mlandizi kuna eneo moja kubwa ambalo ni mashamba na eneo lililo wazi lenye umbali mrefu na mkubwa, watu wengi huwa wanatumia eneo hilo kuendeshea shughuli za kilimo na wengine maeneo mengine kuyatumia maeneo hayo kwa ajili ya ufugaji wa ndani pia. Walitembea umbali kadhaa mpaka walipofika sehemu ambayo waliikuta barabara ya vumbi imekunja kuelekea mkono wa kulia hivyo wakaiacha barabara kuu ya lami. Mbele kidogo kuliandikwa PRIVATE ESTATE ikiwa na maana kwamba eneo hilo lilikuwa limenunuliwa na mtu binafsi ambaye alikuwa anaendesha shughuli zake huko.
Kwenye hilo eneo kulikuwa kunaendeshwa shughuli za ufugaji wa samaki ndani ya uzio mrefu na mkubwa ambao ulijengwa kilomita mbili kutokea ilipo barabara kuu ya lami hivyo kwa watu wa kawaida hakuna ambaye alikuwa anajua kilichokuwa kinaendelea huko ndani. Msafara wake ulitembea kwa kilomita hizo mbili mpaka alipokutana na geti zito ambalo lilifunguliwa wakaingia kisha likafungwa. Ndani ya hilo eneo kulikuwa na vifaa vingi vya kutumika kufugia lakini mabwawa yalikuwa yakionekana huku mengine yakiwa yanatumika kufugia mamba, taa zilionyesha vyema kila kitu.
Walitembea kwa robo kilomita tena ndipo wakasimama eneo hilo na msafara huo ukaja kukaguliwa na wanaume kadhaa ambao walikuwa wamejifunika mashuka makubwa mekundu. Baada ya kukaguliwa waliruhusiwa kuingia kwenye gudauni kubwa ambalo lilikuwa limesheheni vyumba vya kutosha na ndani yake zilikuwa zinaendelea shughuli za uandaaji wa samaki kwa ajili ya kuwapeleka kwenye masoko. Walinzi wake walibaki nje yeye aliongozwa na wanaume wawili mpaka ndani ya chumba kimoja ambacho kilikuwa kama ofisi ndani, kilifunguka chini wakashuka na ngazi kisha juu pakajifunga kabisa.
Huko chini ulikuwa kama mji wa mtu, ilikuwa ni sehemu kama ngome ambayo mtu alikuwa amejiandalia kwa ajili ya maisha yake, huko hawakukutana tena na watu wenye mashuka mekundu na hata wale ambao walikuwa wakimsindikiza mheshimiwa walipotea ghafla. Huko alikutana na wanaume ambao walikuwa wamejifunika mashuka meusi wakiwa wanaendelea na sala za ajabu ambazo hakuzielewa kabisa. Alipita kwenye kona moja ndipo akaja mwanaume mmoja ambaye alimtaka avue nguo zake zote hapo hapo alipokuwepo, alivua bila shida na kupewa shuka jeupe naye akajifunika kuingia ndani kukutana na kiongozi mwenyewe wa hiyo sehemu.
Lilifunguliwa lango lingine huko ndani ambako kulikuwa ni kama ulimwengu mwingine, eneo hilo lilikuwa kama sehemu ya mashetani japo kila kitu kilipangwa kwa usahihi na kilivutia ila kilichokuwa kinaendelea ndicho kidogo kilikuwa kinaleta taharuki hata kwake mwenyewe. Kuna wanaume ambao walikuwa vifua wazi macho yakiwa mekundu sana, wale wa mashuka meusi hawakufahamika ni wapi waliishia ama kupotelea, huko wengi hawakuwa na mashuka bali walikuwa na vitu kama damu kwenye miili yao, huo ulikuwa ni utambulisho wao.
Juu ya varanda moja kubwa kulikuwa na moto mkali ambao ulikuwa unawaka na eneo hilo walionekana watu kadhaa wakiwa hapo kama wanafanya ibada, ibada hazikuwa zinaeleweka kwani mwanaume yule ambaye alionekana kufanyiwa ibada hiyo alimchinja mbwa mzima mzima na kunywa damu yake kisha akamtupia kwenye moto mkali. Juu ya sehemu hiyo kulikuwa na kichwa kikubwa cha nyoka ambaye alionekana kama bado alikuwa hai hajafa. CDF alimeza mate kwa shida ikiwa ni yeye tu ndiye alikuwa ndani ya shuka eneo hilo.
Yule aliyekuwa anafanyiwa ibada alikuwa uchi bila nguo yoyote kwenye mwili wake, mwili wake ulikuwa na alama kila sehemu na ilionekana kabisa kwamba mbavu yake ya upande wa kushoto haikuwepo. Baada ya ile sala mwanaume yule ambaye CDF alikuwa hajamsogelea bado alipita kwenye ule moto mkali sehemu ambayo alirushia yule mbwa taratibu huku wanaume wawili wakiwa wamekaa kila upande kumtandika na vyuma ambavyo navyo vilikuwa vya moto kwenye mwili wake.
Lilikuwa tukio la kutisha ambalo lilianza kumtoa jasho CDF akiwa haelewei afanye nini, alihitaji mwenyewe msaada wa hilo eneo lakini alicho kiona kilianza kumtisha na kumfanya ajutie kufika hapo wakati huo kwani alijua kabisa alikuja kwa siri eneo hilo na kosa moja tu lingeondoka na maisha yake na hakuna mtu yeyote ambaye angekuja kujua kwamba ni wapi mtu huyo aliwahi kufia. Mwanaume yule baada ya kumaliza zoezi lake alikuwa amechakaa mwilini, kwa sababu vile vyuma vilikuwa vikiacha alama kila vikimpata. Aliingia kwenye beseni kubwa ambalo lilionekana kuwa dawa, alizama humo na kuibuka baada ya dakika kumi baadae yale majeraha yakiwa yamekauka.

Baada ya kusimama CDF alikuwa amemsogelea karibu, kwenye kifua cha mtu huyo kulikuwa na tattoo ambayo ilichorwa kwa chuma na isingefutika mpaka siku anakufa, lilikuwa ni jina la mtu, GAVIN LUCA. CDF aliliona hilo ila alishtuka kwani hakutegemea kukutana na kitu kama hicho, mwanaume huyo ambaye alikuwa mbele yake usoni upande wa kulia shavu lake lilikuwa limekatwa vibaya mpaka karibu na jicho moja. Hiyo sehemu ilishonwa lakini kulikuwa na alama mbaya ya kitu chenye ncha kali ambacho kilionekana kilipitishwa mara nyingi na kwa nguvu kubwa kiasi kwamba hata angetokea daktari gani bado hiyo sehemu isingekuja kupona tena kwenye maisha yake yote.

Hiki kiumbe kimetoka wapi tena? Binafsi nimeishiwa maneno, ungana nami mwanzo mpaka mwisho. Sehemu ya kumi na nane inafika tamati.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA KUMI NA TISA
SONGA NAYO................
Tumboni pia palikuwa na alama kadhaa za vitu vyenye ncha kali kuwahi kupitishwa, halikadhalika kwenye bega lake la kulia karibu na shingo hali ilikuwa ni hiyo hiyo. Aliletewa shuka safi jeupe bwana huyo na kufunikwa nalo, alitembea taratibu mpaka kwenye kiti kimoja ambacho kilifungwa juu ya kamba karibu na kilipokuwepo kichwa cha yule nyoka. Staili ambayo aliitumia kwenda kukaa kwenye kile kiti ilimshtua CDF, alikuwa amepiga magoti wakati huo ila alitamani asimame akimbie kwa sababu mtu huyo alikuwa kama anapaa japo alijifariji kwamba huenda ni macho yake yalikuwa yameona vibaya ila huenda alitaka kushindana na ukweli wenyewe.
"Nisamehe sana kiongozi, mara ya kwanza nilihisi kwamba nimemuua huyu mtu ndiyo maana nilitanguliza hii taarifa kwako ila sio kweli inaonekana yupo hai" CDF aliongea kwa huruma akiwa ameyainua macho yake kwa yule mwanaume ambaye aliutumia mkono wake mmoja kumpapasa nyoka yule ambaye alionekana kuwa mkubwa sana, yule nyoka alirudi nyuma na kupotelea gizani akabaki yeye kama yeye, alifanya hivyo baada ya kuona CDF hali ya uoga imekuwa kubwa zaidi ya uhalisia.
"Hizo taarifa za kwamba yupo hai umezipata kwa nani?"
"Kwa Aurelia"
"Na taarifa za kuamini kwamba umemuua ulizipatia wapi?" yalikuwa maswali mfululizo kutoka kwa huyo mwanaume ambaye alikuwa na sauti nzito sana tena ya kukwaruza kiasi kwamba ungehisi una ugomvi naye kila alipokuwa anazungumza.
"Nilitumiwa video na vijana wangu pamoja na picha"
"Vijana ulio watuma kule walikuwa na uwezo gani?"
"Wengi walikuwa ni wanajeshi wenye mafunzo ya hali ya juu ila ndani yao niliwachanganya na makomando bila kuwaambia"
"Ndio hao ambao uliamini kwamba wanaweza kumuua GAVIN LUCA?" hilo swali lilimshangaza CDF
"Kiongozi kwamba ulikuwa unajua Gavin Luca yupo hai hata kabla mimi sijaja hapa?"
"Umeuliza swali la kipumbavu sana, hakuna mtu kwenye hili taifa anaweza kukiua kile kiumbe, kama ni kufa mtu pekee wa kumuua ni mimi hapa" jambo hilo liliongeza hofu kwake, hakujiona kuwa salama kwenye maisha yake kama ambavyo Valeria alimsisitiza.
"Unamaanisha nini kiongozi?"
"Unavyo niona najichora maalama kwenye mwili wangu hapa sio kwamba napenda, kila binadamu anapenda kuwa na mwonekano mzuri na wa kuvutia kwenye maisha yake. Haya yote nayafanya kwa sababu ya GAVIN LUCA"
"Bado sijakuelewa vizuri kiongozi wangu"
"Hizi alama ambazo unaona nimeshonwa kwenye mwili wangu kama ni vitu vyenye ncha kali vimepita, huu uso wangu ambao unaona umeharibika kiasi kwamba ni ngumu kutoka hata nje watu wakaniona; haya niliyapata siku ya mwisho mimi kukutana ana kwa ana na GAVIN LUCA mwenyewe" CDF alijikuta anakaa chini akiwa haamini kile ambacho alikuwa anakisikia, ni kwamba mtu huyo mwili wake uliwahi kuharibiwa na mtu ambaye yeye aliamini amemuua ndani ya huo msitu wa Mau huko kenya, alidata CDF!
"Hili linawezekanaje?"
"Umewahi kukutana naye ana kwa ana?"
"Sikumbuki ila nina uhakika sijawahi kukutana naye kiongozi ila nimemsoma sana na sioni maajabu yake ya kutisha namna hiyo"
"Basi sali usije ukakutana naye kwenye maisha yako yote mpaka siku unakufa, kwa sababu ukikutana naye basi omba siku hiyo niwe karibu niweze kukulinda bila hivyo wewe unakufa kwa sekunde mbili tu mbele yake"
"Huyu mtu kuna kitu gani hasa ambacho kipo nyuma yake kiasi kwamba inafikia hatua anaonekana kuwa tishio kwenye masikio ya baadhi ya watu?"
"Nisikilize kijana wangu CDF, kabla ya kukutana na huyu mtu niliamini hataweza kutoka kwenye mikono yangu salama lazima nimuue tena kwa namna ambayo ningeitaka mimi. Siku niliyo kutana naye hiki ndicho kilinikuta, nimetumia miaka mitano kusahau kila pigo ambalo lilikuwa linaingia kwenye mwili wangu kwa sababu hata nilipo zinduka nilikuwa naota kile kitu nikapata ugonjwa wa kutetemeka kwa miaka miwili. Niliomba aniache niishi, alikuwa na uwezo wa kuniua siku ile ila aliniacha na kunipa onyo la maisha ambapo nililipa gharama hiyo kwa kuachiwa haya makovu kwenye mwili wangu"
"Tangu siku ile mimi binafsi nimekuwa nikiishi nikiisubiri siku nije nikutane naye, baada ya kufanikiwa kupona pale nilitumia nguvu zangu zote kuanzisha ngome yangu, kutengeneza nguvu kubwa zaidi ya ile ya mwanzo, nina watu kila sehemu ya mhimu ya serikali hata huyo raisi nikitaka kumuua muda huu namuua. Nimetumia miaka yote hiyo kupona na kufanya mazoezi kwa masaa kumi na saba kila siku ili niwe imara, nisiwe na uwezo wa kupigika na mtu yeyote hata likija roboti kwa ajili tu ya siku moja kuja kumuua kwa mateso GAVIN LUCA kwa mkono wangu halafu wewe uliamini kutuma vijana wako ndiko kunaweza kumuua GAVIN LUCA?" CDF mapaka udenda ulikuwa unamtoka mdomoni, alikuwa anazidi kutishwa na maelezo ya mtu ambaye aliamini anaweza kumpa msaada wa jambo ambalo lilimleta hapo.
"Kwa maana hiyo yeye hajui kama upo hai na ndiye ambaye unayafanya haya?"
"Huenda anajua kama nipo hai ila kwa hali aliyo niacha nayo huenda anaamini nimeshakufa ama kama nipo hai basi nilisha jitenga na ulimwengu hakuna kitu nitafanya tena au kwa yale ambayo alinifanyia wakati ananiacha pale huenda anahisi kwamba huenda nilisha yachukua maisha yangu mwenyewe. Hivyo mpaka sasa naweza kusema hajui kuhusu uwepo wangu na ndipo ilipo faida yangu kubwa"
"Sasa kwanini hukuweza kumuua mapema kama ulilijua hilo?"
"Sababu ya kwanza huwa anatokea kama mzimu kwa sababu hajulikani yupo wapi na anafanya nini ila sababu kubwa ya pili ni kwamba huko nyuma sikuwa na huo uwezo ila kwa sasa ninaweza kumuua mtu yeyote yule"
"Naomba unisaidie kiongozi, mimi nitafanya lolote ambalo utahitaji nilifanye popote na kwa muda wowote ule"
"Unataka msaada gani?"
"Nataka kumuua mama yake"
"Umechanganyikiwa?"
"Kwanini kiongozi?"
"Unahisi ni kwanini mimi najua kwamba mama yake yupo na sijawahi kumgusa wakati nina huo uwezo wa kumuua hata dakika hii?"
"Hapana sijui"
"Kwenye maisha yako hakikisha kichwa chako hakiwi mzigo kwa shingo yako, mama yake amewekwa kama mtego kwa sababu GAVIN LUCA anamtafuta mtu ambaye yupo nyuma ya haya na siku mama yake akiguswa tu basi itamrahisishia kazi ya kunipata mimi muda wowote yule. Binafsi sitaki ajue uwepo wangu mpaka siku ambayo nitamfanyia suprise hivyo mama yake hatakiwi kuguswa na mtu yeyote yule na mtu ambaye atakaidi hilo basi nitaua familia yake yote"
"Nisamehe kiongozi"
"Kuna sababu gani ya msingi mpaka unataka kumuua mama yake?"
"Kwa sababu amenipa kazi ya kumuua mke wa raisi"
"Achana na mambo yote, muue huyo mke wa raisi kisha kuna kazi nataka nikupe ambayo itakuwa njia yako ya kupata majibu ya hayo yote ambayo unayahangaikia"
"Sijakuelewa kiongozi"
"Unatakiwa kwenda Tanga, Lushoto milimani. Kuna sehemu inaitwa MIZIMU INAYO ISHI. Hiyo sio sehemu tu bali ni gereza la siri ambalo huwa linatumika miaka na miaka, ni kama limeshajitenga na mifumo ya serikali ila raisi anajua uwepo wake japo nina uhakika wewe hujui. Gereza hilo linahifadhi watu ambao waliaminika kuwa na baadhi ya nguvu za ajabu halafu wakazitumia kufanyia uhalifu sasa nataka uende huko"

Unayaamini aliyo yaongea huyo bwana? Huko Tanga kweli atafanikiwa kupata kila kitu? Naweka nukta sehemu ya kumi na tisa.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI
SONGA NAYO................
"Ndani ya gereza hilo kuna mzee mmoja ndiye ambaye atakupa historia nzima ya maisha ya GAVIN LUCA na baada ya kukupa historia ya hiyo huyo mzee unatakiwa kumuua pamoja na kuua wafungwa wote wa gereza hilo kwa sababu kama akijua kwamba mzee huyo yupo hai basi anaweza kumtafuta na akimtumia litakuwa jambo baya sana kwangu"
"Huko Tanga natakiwa kwenda lini?"
"Baada ya kutoka hapa wachukue vijana wako wenye uwezo mkubwa zaidi ikiwezekana wachukue makomando ndio uende nao huko wakaifanya hiyo kazi. Utapewa maelekezo yote hivyo kwa sasa sitaki ukanyage tena kunisumbua hapa"
"Nashukuru sana kiongozi" aliinama chini kugusa ardhi kwa kichwa chake kutoa heshima kwa kiongozi huyo ambaye alimpa mwanga wa nini cha kufanya. Alivua shuka lenyewe hilo na kutoka akiwa uchi kabisa mpaka alipofika mahali ambapo zilikuwepo nguo zake. Alivaa na kupiga simu kwa makomando wake ambao alikuwa anawaamini kwa ajili ya kwenda kuifanya hiyo kazi huko Tanga usiku huo huo alitakiwa kufika na alipewa mtu wa kwenda kumpa maelekezo juu ya kitu gani ambacho alitakiwa kwenda kukifanya huko na alitakiwa kumuona nani akifika huko.


***************
MIZIMU INAYO ISHI
Amri ambayo alipewa mkuu wa majeshi ilikuwa ni kwenda Tanga ndani ya hiyo sehemu ambalo lilikuwa gereza la siri ambalo lilichimbwa mlimani, watu hawakuwahi kuwa na taarifa hiyo ila ilisemekana kwamba raisi wa nchi yeye alikuwa na hizo taarifa.
Hilo gereza lilidaiwa kwamba lilikuwa linatumika kuhifadhi watu ambao walisemekana kuwa na nguvu za ajabu ila baadae walianza kuzitumia nguvu hizo kwa ajili ya kufanya uasi na uhalifu hivyo walitafutwa kila kona na kwenda kufungiwa huko chini ya usimamizi mkali na ndiyo sehemu ambayo alitakiwa kufika CDF siku hiyo hiyo ambayo alikuwa amepewa maelekezo ya kufanya hivyo. Baada ya kutoka Mlandizi alihitaji helikopter iandaliwe haraka aweze kwenda huko Tanga.
Safari yake kwenda huko aliongozana na makomando kumi akiwa na helikopter ya jeshi ambayo ilitumia dakika thelathini tu kufika ndani ya mji wa maraha, mji wa mapenzi, sehemu ambayo inaaminika ukiingia kwa ajili ya kupata raha za mapenzi basi sahau kabisa kurudi tena ulikotoka lazima utakwamia ndani ya sehemu hiyo kwa namna yoyote ile. Baada ya kutua huko, kambi ya jeshi walienda kumpokea na magari yao safari ya kuelekea huko milimani ambako alielekezwa ikaanza mara moja kuweza kuwahi, alikuwa na hamu kubwa ya kukutana na mzee ambaye alielekezwa kwake. Angemsaidia kuijua vizuri historia ya GAVIN LUCA ukiachana na taarifa chache ambazo yeye binafsi alikuwa nazo juu ya mtu huyo.

Safari ilichukua masaa mawili kwa mwendo mkali kufika huko, njia haikuwa nzuri kabisa na miundombinu ilikuwa mibovu eneo hilo likionekana kutelekezwa kwa muda, ni gari chache zilionekana kupita ndani ya eneo hilo na hilo alilielelewa vizuri lakini hatimaye alifanikiwa kufika. Kwenye mwamba mmoja wa jiwe ndiyo sehemu ambayo ilikuwa na mlango ambao ulishonana kama jiwe.
Alifika hapo na kubonyeza kitufe kidogo ambacho kilikuwa kama jiwe pakafunguka kidogo upande wa juu, ndani alionekana mwanaume mmoja akichungulia na kutaka mtu huyo ajitambulishe. Alitoa utambulisho wake na kuonyesha kitambulisho kidogo kama ambavyo alielekezwa na baada ya hapo ndipo lango hilo likafunguliwa. CDF hakuwa akiamini kile ambacho alikuwa anakiona mbele ya macho yake, gereza la siri lilikuwa limejengwa milimani na huko ndani vyumba viliunganishwa kwenye miamba mikubwa na migumu ya mawe ni kama maisha ya watu ambao waliishi zama za mawe ila umeme haukuwa ukikatika ndani ya eneo hilo na hao watu walikuwa wakipata mahitaji yote ambayo walikuwa wanaletewa.
Kwenye vyumba ambavyo walionekana kuhifadhiwa watu hao, wengi wao hawakuwa wa kawaida, walionekana kuchoka na kuchakaa isivyokuwa kawaida. Wafungwa wote ambao walikuwa ndani ya eneo hilo walikuwa wamefungwa na minyororo kwenye miili yao wengi wakiwa na nywele nyingi mno kwenye vichwa vyao, walikuwa nje na maisha ya kawaida hata akili zao hazikuwa sawa ila hawakuwa wakiruhusiwa kuachiwa huru kutoka kwenye hiyo minyororo kwa sababu ingekuwa ni hatari ila siku hiyo walitakiwa kufa wote ili kufuta ushahidi wa kuwahi kuwepo kwao kwa sababu kuendelea kuwa hai ingekuwa ni hatari kwa baadhi ya watu.
CDF alipelekwa mpaka ndani ya sehemu ambayo bila shaka ilikuwa ni ofisi ya kiongozi wa eneo hilo ambaye alimpokea vizuri, hakuwa na kumbukumbu kama aliwahi kumuona bwana huyo kwenye maisha yake huku duniani ila aliamini alikuwa ni raia wa Tanzania.
"Karibu mheshimiwa" mwanaume huyo ambaye umri wake ulikuwa ni mkubwa kuliko wake, alimkaribisha kwa heshima kwa sababu alikuwa anajua kabisa kwamba anaongea na mkuu wa majeshi
"Mzee Hasheem nampatia wapi?" hakuitikia salamu bali alihitaji kumpata mzee huyo ambaye ndiye ilikuwa sababu ya msingi ya yeye kuwa na kimuhemuhe cha kufika ndani ya eneo hilo. Kiongozi wa eneo hilo hakuongea kitu zaidi ya kuongoza njia kutaka CDF amfuate ili aweze kumkutanisha na mtu wake, CDF aliwapa ishara makomando wake kubaki ndani ya eneo hilo ila kuna ishara nyingine aliiongeza ni wao tu ndio walimuelewa. Pindi ambapo angemalizana na mzee huyo hakuna mtu hata mmoja ambaye alitakiwa kubaki hai ndani ya hilo eneo.
Kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa mwishoni kabisa sehemu ambayo ilionekana kwamba ndipo mwamba ulikuwa unaishia ndipo ambapo alipelekwa CDF, hakutaka kuuliza kuhusu uhalali wa gereza hilo kwa sababu aliamini kwamba majibu yote angeweza kuyapata kwa mzee huyo ambaye yeye alimuulizia kama mzee Hasheem.
Ndani ya hicho chumba ambacho kilikuwa kimefungwa na mlango ambao ulikuwa ni wa nondo kubwa na ngumu, ndani yake alionekana mzee mmoja ambaye bila shaka alikuwa amekata tamaa ya maisha kama sio kuchoka na hali ambayo alikuwa nayo. Alikuwa amegeukia ukutani akiwa anachora chora kwenye kuta kubwa na nzito ambayo ilikuwa ni miamba, hakueleweka hata anachora nini kwenye ukuta huo huenda hilo alikuwa analifahamu yeye mwenyewe na akili yake. Kwenye mikono yake alikuwa amefungwa kwenye minyoror pamoja na kwenye miguu yake uso wake ukiwa umefunikwa na nywele ndefu sana.
Lango hilo lilifunguliwa na ndilo ambalo lilimfanya aache kufanya kile ambacho alikuwa anakifanya akageuka kuangalia ni nani ambaye alikuwa amefika muda huo kwani huenda haukuwa muda wa kutembelewa na wahusika wa hilo eneo ndiyo maana alijipa umakini. Kugeuka kwake kulimfanya akutane na sura ngeni ambayo ilikuwa kwenye kombati ya jeshi ambayo ilikuwa imezungukwa na nyota za kutosha. Kiongozi wa eneo hilo alitoka na kumuacha CDF pekeyake kama alivyohitaji, CDF alitembea kidogo mpaka kwenye jiwe moja ambalo lilikuwa limejitenga mfano wa kiti, akavua kofia yake na kuiweka pembeni kisha akaketi eneo hilo.
Mzee ambaye alikuwa mbele yake uso wake ulikuwa umefunikwa na nywele nyingi ambapo ilimlazimu kuzifunua na mkono ili kuona vizuri, umri wake ulikuwa umeenda mzee huyo.
"Nimesikitika kuona aina ya maisha ambayo baadhi ya watanzania mnayaishi ndani ya hili eneo, kama kiongozi mkuu wa majeshi binafsi nimejisikia vibaya sana kwa sababu hata nyie mnahitaji nafasi ya pili kwenye haya maisha. Ninaweza kuwatoa kwenye haya maisha na mkapewa nafasi ya kuishi maisha ya kawaida kama wanadamu wengine ndiyo maana nipo hapa" CDF alijieleza akiwa anamwangalia mzee huyo usoni, naye hakumkopesha alikuwa ametulia kwa usikivu akiwa amemkazia macho CDF. Alijikohoza kwa dakika nzima ndipo akakaa upande wa pili wa sehemu hiyo akiwa anajivuta kwa shida, ni wazi hata miguu yake haikuwa na nguvu tena za kutembea kama watu wengine walio vizuri kiafya.
"Kipi kimekuleta ndani ya hii sehemu?" ilikuwa ni kwa mara ya kwanza mzee huyo anafungua kinywa chake akiwa anaongea kwa shida.
"Nimesikia kwenye historia ya maisha yako licha ya kuwa na matatizo kadhaa yaliyo kufikisha hapa leo lakini ulikuwa ni mtu wa swala tano maana yake unamjua vizuri Allah, kiufupi wewe ni mtu wa dini ambaye ulikuwa tayari kuyatoa maisha yako ili kutenda yaliyo mema hivyo sina imani kama unaweza ukayatelekeza maisha ya wafungwa wenzako wote ambao wapo humu ndani kwa sababu tu ya kushindwa kunipatia kile ambacho nakitaka kwako" CDF alitulia baada ya kuongea hayo maneno mazito ambayo bila shaka hayakuwa mema machoni pa mzee huyo.
"Kitu gani hicho unakitaka kwangu kiasi kwamba unatishia maisha ya watu ambao unadai kwamba umekuja kuyaokoa?"
"Mzee wangu usininukuu vibaya, mimi sijali sana kuhusu maisha ya watu ambao wapo humu ndani kwa sababu hakuna sehemu ambayo mnajulikana kwamba mpo hai hivyo hata mkifa hakuna mtu atajua ila nimewapa nafasi nyingine ya kuishi ambayo inategemea na kile ambacho wewe utaniambia hapa leo"
"Nakusikiliza"

Anataka nini? Ungana nami tukijue wote. Ishirini sina la ziada.

FEBIANI BABUYA

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
SONGA NAYO................
"Nahitaji kuijua historia nzima ya maisha ya Gavin Luca" mzee Hasheem hakutegemea jambo hilo, baada ya kulisikia hilo jina alionekana kulegea kwa kiasi chake, ilikuwa ni ghafla kuulizwa habari za mtu huyo"
"Ni nani amekwambia kwamba mimi nazijua habari za mtu huyo?"
" Mzee tusipoteze muda kwa kuanza kuigiziana hapa, huko nje nimeawaacha makomando kumi ambao wanasubiri amri yangu tu waweze kuteketeza watu wa hilo gereza wote hivyo usitake kufa na msalaba wa kuhusika kuwaua wenzako zaidi ya hamsini ambao wapo humu ndani"
"Ni nani anaye mhitaji Gavin Luca?"
"Mimi hapa ndiye ambaye ninamhitaji"
"Wote tunajua hili haliwezi kuwa kweli, mtu dhaifu namna hiyo huwezi kuwa na uhitaji na Gavin Luca"
"Nani amekwambia mimi ni dhaifu?"
"Kila kitu kinaonyesha namna ulivyo dhaifu na mtu mjinga, unafanya vitu kwa mihemko ni wazi ulilelewa vibaya na wazazi wako"
"Mzee angalia sana mdomo wako"
"Kwamba utaniua? Hilo sio kweli kwa sababu mpaka umekuja huku maana yake unazihitaji sana taarifa hizo kwahiyo huo uwezo wa kuniua kwa sasa hauna, nataka tu nijue kwamba nakuaminije kuwa hutawaua wafungwa wote wa humu ndani baada ya mimi kukwambia unacho kihitaji?"
"Nitayachukua maisha yako na kuondoka zangu kwa sababu shida yangu kubwa ni wewe na sio watu wengine, wewe ni mtu wa dini hivyo unaelewa faida ya kufa ukiwa umeyaokoa maisha ya watu wengine" mzee huyo alitabasamu kwa mbali, alikuwa mtu wa dini sana hivyo alichokuwa anaambiwa alikuwa anakielewa vizuri kwenye kichwa chake na alitakiwa kukifanyia maamuzi haraka kwa wakati huo.

“Historia ya maisha ya huyu binadamu ambaye mnajitafutia laana za bure kumtafuta inaanzia pembezoni mwa mto mmoja uliopo kwenye moja ya vijiji vilivyopo ndani ya Tanga. Pembezoni mwa huo mtu majira ya jioni alionekana kijana mmoja akiwa amesimama mwenyewe akiwa anayaangalia maji yalivyokuwa yanaenda kwa kasi na utulivu mkubwa, tabasamu dogo lenye maumivu makali lilionekana kwenye uso wake huku akimeza mate kwa pupa kiasi kwamba aliambiwa yangekwamia kwenye shingo yake yakampalia.
Alikuwa ni kijana maskini sana na huo umaskini wake ulimfanya kudharaulika mpaka na watu wa kijijini ambao nao hawakuwa na maisha mazuri ila ya kwao angalau yalikuwa yanaongeleka. Kijana huyo maisha yake yalimchapa vilivyo kiasi kwamba hata kuishika shilingi mia tu kwake ilikuwa ni kama sherehe. Tumaini lake la pekee lilibakia kwa mwanamke mmoja ambaye ndiye alikuwa akimfanya acheke kila wakati ambapo angemuona, kwa wakati huo alikuwa na miaka kumi na tisa na mwanamke ambaye alikuwa akimfanya kutabasamu alikuwa na miaka kumi na nane.
Kwenye huo mto alikuwa amekaa akiwa anamsubiri mwanamke huyo aweze kuja kumpatia faraja, ukiachana na huyo mwanamke ni mtiririko wa maji pekee ndiyo ambao ulikuwa unampa faraja ya kuishi. Ilikuwa ni tofauti na matarajio yake ambayo alikuwa nayo kwa sababu mtu ambaye alikuwa anatakiwa kuja hapo kumpa faraja, alifika akiwa analia kuliko hata alivyokuwa akilia yeye jambo ambalo lilimshtua kidogo na kumpatia hofu. Mpenzie alifika akiwa analia kwa uchungu na kwenda kumkumbatia kijana huyo ambaye alibaki ameduwaa tu asijue ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.

Ikabidi amkalishe kitako mpenzi wake kujua ni nini kilikuwa kimempata, ndipo mrembo huyo wa kitanga, mtoto wa kidogo ambaye alikuwa mzuri wa sura mpaka tabia lakini aliishia kumpenda kijana asiye na mbele wala nyuma ampe yale ya uvunguni ili aone kama anaweza kuinama kuyapata. Kilio chake ilikuwa ni kwa sababu ya mama yake mzazi, mama yake alikuwa anaumwa na alitakiwa kufanyiwa oparesheni kubwa ambayo ilikuwa inahitaji gharama kubwa kuweza kuikamilisha. Hata alipopewa habari hiyo alibaki amekaa kimya asielewe nini cha kufanya, alitamani angekuwa mtu mwenye mafanikio aweze kumsaidia mpenzi wake lakini yeye mwenyewe hata jioni ya siku hiyo hakuwa na uhakika kama angefanikiwa kukitia kitu kwenye tumbo lake.
Alikumbuka vizuri namna wazazi wa mpenzi wake walivyo yalaani mahusiano yao na kuhitaji kumuozesha binti yao kwa wanaume wenye ukwasi ili awe msaada wa ukombozi kwa hiyo familia, alichoka kijana huyo. Hakuna na uhakika wa jambo lolote lile kwenye maisha yake na yeye ndiye ambaye mpenzi wake alikuwa akimtegemea kwenye mambo kama hayo angefanya nini tena? Alijitahidi kumtuliza mpenzi wake ila yeye ndiye ambaye alikuwa na maumivu zaidi ndani ya moyo wake akajikuta naye anashusha chozi la uchungu.
Aliulaani umaskini kwenye maisha yake, umaskini hakuna anaye upenda japo pia sio kila mtu yupo tayari kuupata utajiri kwa sababu utajiri unahitaji mtu ajitoe kweli, mtu apambane na kila hali mpaka kuufikia ila alijua kwamba kwenye maisha yake hakuna kitu kibaya kama Umaskini. Umaskini uliondoka na maisha ya wazazi wake na ndio huo huo ambao huenda ulikuwa unaenda kuyachukua maisha ya mama mkwe wake mtarajiwa ambaye hakuwa tayari kuona kijana huyo yupo na mwanae, angefanya nini kijana wa watu? Alikosa tumaini, hata lile dogo ambalo alikuwa nalo moyoni liliyeyuka, alitakiwa kumruhusu mpenzi wake aolewe na mwanaume ambaye familia ilikuwa inamtaka ili wapate msaada. Alilipata windo lakini alitakiwa kuliachia mwenyewe huku akijua kabisa kwamba ana njaa kali, aliyapata maumivu.
Alichanganyikiwa, alijua kabisa wazazi wa mwanamke yeye hawamtaki kwa sababu hakuwa akieleweka, licha ya sehemu hiyo kwa umri wake angeruhusiwa kumuoa mpenzi wake bila shida lakini haikuwa sababu, wazazi walikuwa wanajali pesa kwa ajili ya maisha yao kubadilika. Kuna sehemu kubwa aliona hakuna haja ya kuwalaumu wazazi wa binti huyo kwa sababu alijua namna umaskini ulivyokuwa mbaya. Alipaswa kufanya maamuzi ya kiume na sio kuongozwa na hisia zake, kwa maumivu makali akamruhusu mwanamke huyo aende Linda Johnson. Yale maumivu ambayo aliyapata ndiyo ulikuwa mwanzo wa mambo yote kutokea mpaka leo wewe upo hapa kutaka kujua maisha ya Gavin Luca" mzee huyo alitulia kidogo akiwa ndo kwanza anaanza kumfunulia CDF maisha halisi ya huyo binadamu wa kuitwa GAVIN LUCA.

Mapenzi yanauendesha ulimwengu, mapenzi ndiyo msingi halisi wa maisha ya mwanadamu na sababu ya mwanadamu kuishi, mapenzi ndiyo maana halisi ya maisha. Ukiwa na bahati ya kutosha ukayapata basi wewe unakuwa ndiye mwanadamu mwenye furaha zaidi duniani hata kama hauna vingi vya kujivuna navyo. Mapenzi yanaelezea maana halisi ya maisha lakini ukiyakosa ndipo utaelewa nini maana ya maumivu ya kuwa hai hususani unapokuwa unamjua mtu ambaye unampenda, unapokuwa unamjua mtu ambaye unamhitaji kwenye maisha yako lakini unaelewa kabisa kwamba hauna huo uwezo wa kumpata au wa kuja kuwa naye.
Jambo ambalo wanadamu wengi huwa linawaumiza ni kushindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba sio kila unacho kipenda utakipata, sio kila ambacho moyo wako unakitamani na ukakiridhia basi kitakuwa chako. Hilo jambo ni wanadamu wachache mno ambao wanafanikiwa kulikamilisha, wengi watakufa bila kulikamilisha jambo hilo kwa sababu halipo kwa ajili ya kila mtu. Wengi lazima wataishia kwenye maumivu makali ya kuyakosa mapenzi au vitu ambavyo wanavitaka. Lucas Antony ndilo lilikuwa jina lake kijana yule, ni moja kati ya vijana ambao walikuwa wanajua ni kitu gani wanakitaka kwenye maisha yao na kukihitaji, ni moja kati ya vijana ambao walikuwa wanaelewa kwamba ni kipi kinawafaa kwenye maisha yao ila ni miongoni mwa wachache ambao walielewa kwamba hawawezi kukipata kila ambacho wanakihitaji.
Ndiyo sababu licha ya kumpenda sana Linda alikubali kumuacha aende, alikubali kumruhusu Linda akae naye mbali na kwenda kwa mtu ambaye familia ilimchagua ili aweze kuwasaidia hususani mama yake kufanyiwa oparesheni. Zile nasaha tamu za mapenzi, zile ahadi za kuwa pamoja milele na yale matamko safi na lafudhi ambayo alipenda kuisikia kutoka kwa Linda kila muda akiitumia kama dawa ya kuweza kumponyesha majeraha, aliruhusu vyote viende siku ile. Alikuwa anasubiri kufutwa chozi la maisha yake lakini aliongezewa lundo la maumivu kwa taarifa ambayo ilikuja kwenye mikono yake ambayo ilimtaka afanye maamuzi ya kiume akiwa bado ni mvulana.
Lucas alijua kabisa kwamba maisha ambayo alikulia ndiyo yalimkomaza mapema, akiwa na miaka kumi na tisa tu alikuwa ana akili ya mtu wa miaka thelathini tayari, ukiyaelewa maisha basi kuna mengi utajifunza mapema ndiyo maana mara nyingi watu ambao wanayapitia maisha magumu tangu wakiwa wadogo huwa wanakua kabla ya wakati wao na baadae watu hao huwa wanakuwa watu hatari ama wenye mafanikio makubwa kwa sababu duniani kunakuwa hakuna kitu cha kuweza kuwayumbisha tena. Lucas ni wale vijana ambao walikomaa kichwani na mioyo kabla ya wakati wao.

Umewahi kufanya maamuzi magumu kwenye maisha yako? Umewahi kukubali kumruhusu unayempenda aende kirahisi huku ukijua utaumia? Bwana mdogo anatupatia somo la maisha. Ishirini na moja sina la ziada.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
SONGA NAYO................
Ni siku ambayo alijua Linda sio wake tena, kuendelea kumng'ang'ania mwanamke huyo kungezalisha maumivu mengine kwa sababu Linda alikuwa tayari kufanya kile ambacho Lucas angeamua hata kama angetaka wakimbie na kwenda mbali binti huyo alikuwa tayari lakini Lucas alijua dawa ya tatizo sio kulikimbia bali ni kulitatua. Kukimbia na Linda kungefanya waishi kwenye laana ya muda mrefu kwa sababu huenda wangesababisha hata kifo cha mama yake Linda, sasa kulikuwa na umuhimu gani wa mambo yote hayo kuweza kutokea? Hakuiona sababu, yeye alikuwa mwanaume na moja ya sehemu sahihi kuupima uwezo wake ilikuwa ni kwenye suala zima la kuweza kufanya maamuzi na ndicho kitu ambacho alikifanya, kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya maisha mema kwa wao wote.
Alimtaka Linda akubali kuolewa na mwanaume huyo ambaye familia ilimchagua, alikiri kwamba hakuwa tayari kumuoa Linda kwa sababu maisha yake hayakuwa sawa na alikuwa amechoka kuigiza. Linda hakuwa tayari kukubali lakini ni kauli ya mwanaume ndiyo ambayo huwa inatoa msimamo wa nini kinatakiwa kuendelea, hakutaka kuendelea kudanganya kwa ahadi za uongo kwa sababu mwisho wa siku alielewa kwamba ahadi huwa ni maneno tu. Pembezoni mwa ule mto ndiyo sehemu ambayo mahusiano yale yalivunjika rasmi na akamtaka mwanamke huyo aondoke na asije kumuwaza tena kwenye maisha yake. Kuna wahenga waliwahi kusema kwamba hakuna wakati mgumu kama kusema kwaheri kwa mtu ambaye unampenda. Lucas na Linda ule ndio ukawa mwisho wa penzi lao ambalo lilikuwa na ahadi nyingi, penzi ambalo lilitabiriwa kufika mbali na uso wa dunia ila huenda haikupangwa wawe pamoja, asili ilichagua hatima ya maisha ya kila mmoja wao.

Lucas wakati amebaki pekeyake kwenye ule mto baada ya Linda kuondoka akiwa anakimbia huku ameangua kilio, alitamani kujiua kwenye ule mto ila hakuona sababu ya kufanya hivyo. Alikuwa na sababu zake mbili za kujiacha akiwa hai, sababu ya kwanza alijua maisha yake alipewa zawadi na Mungu hivyo hakutakiwa kuyachukua kwa sheria yake ya mkononi lakini pia sababu ya pili ni kwamba ulimwengu ulimuona yeye sio kitu kwa sababu ya umaskini wake hivyo alitakiwa kuuonyesha ulimwengu kwamba yeye anaweza kufanya mambo makubwa na ulimwengu ukamhusudu.
Alihitaji siku moja watu wampigie magoti na kumuomba msamaha kwa kumcheka na kumdharau kwa sababu ya maisha yake kuwa ya hali ya chini. Lucas kwenye moyo wake alijiwekea nadhri ya kuweza kupambana na umaskini kwa gharama yoyote ile, Lucas alitaka kwenda kutengeneza pesa ambazo zisingekuwa na ukomo, alihitaji kutengeneza kizazi tajiri zaidi ndani ya nchi kupitia yeye, alihitaji jina lake liingie kwenye utajiri wa kutupwa ndani ya nchi ili aandikwe mpaka kwenye vitabu vya mashuleni kila mtu akamsome. Hiyo ikawa sababu ya kusafiri kutoka Tanga kwa kudandia roli kuja ndani ya mji wa wajuaji, mji uliojaa majungu, mji ulio jaa watu wenye roho mbaya sana, mji ambao kila kitu kipo ni pesa yako tu, mji ambao kupata ngono ni rahisi kuliko hata kupata chai lakini kichwani kwake alijua kabisa kwamba naenda kuutafuta utajiri ndani ya jiji la matajiri, jiji la DAR ES SALAAM.




**************
PEENUGA STREETS
Mitaa ambayo serikali ilikuwa kama imeipotezea, mitaa ambayo watu walikuwa wanaishi kwa sheria zao na wale wenye uwezo pekee ndio ambao walikuwa wanaishi huko. Sijamaanisha uwezo wa kifedha, namaanisha watu wenye mabavu na wasiopenda kudeka deka hata kwa vitu vidogo, kulikuwa na wanaume haswa ambao hawakuwa na muda na serikali, wao hatima ya maisha yao ilikuwa kwenye mikono yao wenyewe na waliamini wanaweza kuishi kupitia nguvu zao tu pekee na sio vitu vingine.
Mitaa hiyo watu walikuwa wakiuana kila wakati na muda mwingine ungekuta miili ya watu mtaani ila hakuna ambaye alikuwa anajali zaidi ya kuzolewa na kwenda kutupwa kama takataka, maisha ya mtu hayakuwa na thamani sana ndani ya hiyo mitaa ila pesa ndiyo ulikuwa msingi wa mitaa hiyo. Vijana waliamini zaidi kuzitafuta pesa kupitia njia yoyote ile, wengi hawakuwa na elimu hivyo njia pekee ya kuzichanga ilikuwa ni kutumia njia zilizo haramu mbele ya sheria.
Vijana wadogo walikuwa kwenye kasumba ya utumiaji wa dawa za kulevya, uporaji, uzinzi, michezo ya mapigano ya ngumi kiufupi ilikuwa ni sehemu ambayo walikuwa wanaishi watu wenye yale maisha ya chini sana lakini pia ndiyo sehemu ambayo ilikuwa inatoa matajiri wakubwa. Hiyo ndiyo mitaa ambayo kijana LUCAS alikimbilia kwenda kuishi, aliamini kwa aina ya maisha ambayo aliyasikia huko yangemsaidia kutengeneza jina la kumfanya baadae kuwa na pesa lakini zaidi kilicho mvutia ndani ya mitaa hiyo ni baada ya kusikia kwamba huko kuishi haikuhitaji uwe na elimu, ni nguvu zako tu na kujitoa kwako mhanga ndiko kungekufanya uweze kuwa hai na kuupata mkate wa kukufanya uwe hai kila siku ya MUNGU.
Hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kabisa kuweza kuingia ndani ya mitaa hiyo ambapo alikaribishwa na wenyeji kwa kipigo kikali, akavuliwa na nguo zake zote akaachwa mtaani akiwa haelewi kwa kwenda na afanye nini kitu ambacho kilimfanya kunyeshewa na mvua kwa muda mrefu. Alijuta lakini hakuwa tayari kuondoka ndani ya mitaa hiyo ambayo binafsi aliamini kwamba ndipo siri ya maisha yake ilipo kuwepo. Akiwa ndani ya mitaa hiyo aliteseka sana kuweza kwenda sawa na mazingira, alipata shida kuweza kuzoeana na watu hivyo ikamlazimu kujiingiza kwenye harakati haramu pia ambapo alianza kusambaza bangi na dawa za kulevya kwa ujira mdogo na muda mwingine alidhulumiwa ila hakuwa na sehemu ya kwenda kudeka. Alikuwa na hasira ya maisha Lucas hasa akizingatia kwamba umaskini ndio ambao ulimfanya awapoteze wazazi wake lakini pia kumpoteza mwanamke aliyempenda kwa moyo wake wote.

Kujichanganya kwake kulimfanya kuanza kufahamika ndani ya hilo eneo, alianza kukutana na watu wengi waliokuwa hapo lakini haukuwa mwisho wa mateso yake. Kila siku alikuwa anakutana na vipigo kwenye chchoro kadhaa za mitaa hiyo, mitaa ilikuwa michafu yenye kila aina ya ushenzi, uchafu ulizagaa hovyo, watu walikuwa wanafanya mapenzi hata kwenye sehemu zenye uwazi hakuna ambaye alikuwa anajali. Mateja walijaa kila kona, nani angeuliza na kila mtu anaangalia kilicho mpeleka huko? Lucas aliamua kufanya kilicho mpelekea, alizihitaji mali hivyo aliamini hilo ndilo lilikuwa shamba lake la kuweza kuzipatia mali hizo.

Mitaa ya PEENUGA ilikosa ustaarabu, hakukuwa na watu wenye busara hata wale ambao walikuwa wanaonekana kuwa watu wazima walikuwa ni wale masela ambao walizeeka. Haikuwa mitaa rahisi kuweza kupenya na kuishi kwa sababu muda wowote ule mtu angepoteza maisha yake hivyo kuishi huko ilitakiwa uwe umeyazira maisha yako moja kwa moja. Licha ya mitaa hiyo kuwa ya hovyo na ya kutisha lakini kila sehemu huwa ina starehe yake bwana, wao starehe yao ilikuwa ni ngumi. Yalikuwa ndiyo mashindano bora ndani ya eneo hilo, ngumi kwao zilikuwa ni kila kitu na ndizo hasa ambazo zilikuwa zinatumika kuleta faraja pamoja na kuwaunganisha watu hao kuwa wamoja ndani ya hilo eneo.

PEENUGA GOLDEN RING
Ulikuwa ni ulingo wa dhahabu, ndiko huko yalipokuwa yanafanyika mashindano ya mapiganio ya ngumi, hakukuwa na sheria rasmi za ngumi huko ndani. Ilikuwa ni mtu afe au asiwe na uwezo hata wa kunyanyuka ndipo angepatikana mshindi, huko hakuwa anaingia kila mtu bali wakongwe wa hilo eneo kwa malipo maalumu au kwa wale ambao walikuwa chini ya wafanya biashara maarufu hususani wa madawa ya kulevya ndani ya hilo eneo. Malipo yake yalikuwa makubwa kuingia humo ndani ndiyo maana sio kila mtu alikuwa anaweza kupata nafasi ya kuingia humo. Hayo mashindao ya ngumi kwao ilikuwa ni zaidi hata ya ile ladha ya kombe la dunia.
Baada ya kufahamika na kuanza kutumika sana na wauzaji wa dawa za kulevya ndani ya mitaa hiyo Lucas alipata nafasi ya kuingia humo ndani kwa mara ya kwanza kuona watu wanavyo pasuana na kupotezeana viungo vya mwili.


************
EMILIA CLARK
Ni mwanasheria mkongwe na mbobevu ambaye aliwahi kuhudumu kwenye nafasi mbali mbali ndani ya nchi Tanzania. Mwanamama mwenye umri wa miaka hamsini na tano akiwa na asili ya baba Mzungu na mama mtanzania, alizaliwa ndani ya Tanzania hivyo hata uraia wake ukasoma hivyo na bahati nzuri kwake ilikuwa rahisi sana kwa sababu hata asili alifuata ya mama na sio ya baba yake.
Mwanamama huyu alikuwa ni miongoni mwa magwiji wa sheria nchini ambapo baada ya kumamaliza masomo yake ndani ya chuo kikuu cha Havard nchini Marekani alipata nafasi ya kuhudumu kwenye nafasi kadhaa za sheria serikalini mpaka baadae ambapo aliteuliwa kuwa mwanasheria mkuu lakini baadae alionekana kufaa zaidi kwenye nafasi ya ujaji mkuu na ndio ambao aliufanya mpaka siku ambayo aliamua kustaafu kwa sababu za kiafya ambapo baada ya kuachana na kazi yake hii ambayo aliifanya kwa muda mrefu aliamua kwenda kupumzika kwenye jiji alilokuwa akilipenda sana, jiji la Mbeya.

Sijui alifanya kitu gani huyu mama, ishirini na mbili naweka nukta hapa tukutane sehemu ijayo.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
SONGA NAYO................
Kwenye historia yake mama huyu kuna mambo kadhaa ambayo aliwahi kuyafanya, nafasi ambazo alikuwepo zilikuwa zinamfanya kukutana na watu wengi kwa sababu za wengine kuhitaji msaada na huruma zake lakini wengine walikuwa wanadai haki zao. Dunia ni kijiji na saa ni muongozo sahihi, kila unacho kifanya unapokuwa kwenye nafasi fulani basi ujue kwamba kuna siku kitakuja kurudi kwa namna moja ama nyingine, haijalishi utakuwa tayari kwa wakati huo ama hautakuwa tayari ila lazima kirudi tu kwa wema au kwa ubaya.
Mwanamama huyo alikuwa akiishi eneo la SAI barabara ya kwenda ITUHA, alikuwa akiishi yeye na familia yake yote maeneo hayo baada ya kustaafu na ni watu wachache ambao walikuwa wanajua ni wapi anaishi mama huyo kwa sababu za kiusalama. Alikuwa na jengo lake kubwa la gharama ndani ya eneo hilo akiamini kwamba angefia huko kwa amani lakini haikuwa kweli, dunia haikuwa imesahau aliyoyafanya ule wakati wake ambao alikuwepo kwenye nafasi kubwa serikalini.
Usiku alipokea ugeni wa watu kadhaa, watu hao walifika kwake ghafla na hakuwa na kumbukumbu kama aliwahi kuwaelekeza watu hao kwamba ni wapi yeye alikuwa akipatikana hivyo hapakuwa pema sana. Baada ya kufika hiyo sehemu, mwanaume mmoja ambaye alikuwa na umri wa makamo alimtaka mama huyo akae naye nje ya nyumba hiyo alikuwa na mambo kadhaa ya kuweza kuongea naye huku ndani akiwaacha wanaume kadhaa ambao hawakuonekana kuwa wema. Mwanamama huyo alikuwa mwingi wa wasiwasi, huenda alikuwa akiwafahamu watu hao vizuri ila kwa sababu ya kuilinda familia yake alikubali kwenda kumsikiliza bwana huyo.
"Emily imekuwa kitambo sana tangu siku ya mwisho mimi na wewe tuweze kuonana, bila shaka maisha yanaenda kasi isivyokuwa kawaida. Ni zamani sana tangu mimi na wewe tukae sehemu kufanya maongezi na wakati ule bila shaka ni mimi ambaye nilikuwa nakuomba unipe msaada japo kwa kuringa sana ila ulifanya hivyo bila shaka unakumbuka miaka ile"
"Nakumbuka, unaweza kuniambia kwamba ni kipi kimekuleta kwangu bila hata kukaribishwa?"
"Emily huwa unatambua kabisa kwamba mimi sio mtu ambaye napenda kupoteza au kupotezewa muda wangu hivyo kama ukiniona sehemu basi ujue kuna jambo la mhimu limenileta, isingekuwa hivyo basi usinge niona hapa"
"Unataka nini?"
"Gavin Luca yupo hai"
"Whaaaaat?"
"Nina uhakika umenisikia vizuri"
"Utakuwa umechanganyikiwa"
"Umesikia mpaka hotuba ya raisi halafu unasema nimechanganyikiwa"
"Najua kabisa yule mpuuzi anapika taarifa zile kwa maslahi yake"
"Hii haihusiani na raisi ila nakuhakikishia kwamba Gavin Luca yupo hai"
"Yule mtoto alikufa muda mrefu"
"Hapana aliyekufa alikuwa mwingine, Gavin Luca alikuwa bado mzima wa afya ni miaka mitano ilitopita ndipo aligundulika kwamba ni mzima wa afya kabisa na baada ya hapo tulianza kumtafuta kwa nguvu. Alipatikana huko Kenya akauawa lakini jambo la ajabu ni kwamba akaonekana tena na anafanya mauaji ya kikatili mno kwa watu wetu wote wa zamani"
"Aliuawa halafu yupo hai?"
"Nadhani aliye uawa ni mtu mwingine"
"Kivipi?"
"Hilo hata mimi sina jibu lake"
"Kwa hiyo mimi nakusaidiaje sasa hiyo ni kazi yenu nyie kupambana naye"
"Hapana Emily mambo hayaendi hivyo"
"Unamaanisha nini?"
"Nahitaji ukimya wako"
"Mimi sijawahi kuongea jambo lolote sehemu yoyote ile sasa ukimya wangu unahusikaje? Hata hivyo hakuna mtu ambaye anajua kwamba mimi bado nipo Tanzania na ninaishi huku Mbeya"
"Kama ingekuwa hivyo basi hata mimi nisingekupata maana ulikimbia bila kutuaga Emily"
"Do you wanta to kill me?" mwanamama huyo aliuliza kwa mshangao baada ya kuona watu wake mwenyewe ambao aliwafanyia kazi kubwa miaka ya huko nyuma wanataka kumuua.
"Yes, Emily"
"Why?"
"Nadhani unaelewa namna kazi hizi zinavyo enda, kama ukiwa hai Gavin atakuja kukupata siku moja kwa sababu hatujui anaishi wapi mpaka sasa, kama akikupata wewe basi atajua kila kitu hata ambacho hatakiwi kukijua hivyo you need to go Emily"
"Siwezi kuruhusu huo upuuzi ufanyike kwangu, nilikubali kuharibu utu wangu kuwasaidia leo unataka kuniua mimi, Noooooooooooo"
"Utachagua wewe au familia yako, ukiamua kumalizana na mimi basi familia yako itakuwa salama lakini kama ukikaidi hilo basi nitaua familia yako yote na unawajua wale jamaa ambao tumewaacha kule ndani wanasubiri kauli yangu tu waingie kwenye kila chumba kuua kila aliye mle ndani na wanao ambao wanasoma nje ya nchi nina uhakika unajua kabisa kwamba kuwafikia ni suala la masaa tu"
"Sikutegemea mngekuwa washenzi namna hii, hili linaenda kuwa doa kubwa sana kwenu kwa sababu watu wenu watapoteza imani kwa kuamini kwamba mnaua watu wenu wenyewe"
"Sio kweli kwa sababu hakuna mtu atajua kama ni sisi tulihusika kukuua"
"Unamaanisha nini"
"Unatakiwa kujiua mwenyewe Emily kwa kujipiga risasi kichwani"
"Whaaaaaat?"
"Umenisikia vizuri" mwanaume huyo alimrushia mama huyo silaha na kumwangalia kwa umakini.
"Ilikuwa vyema kufanya kazi na wewe Emily, kama kuna maisha mengine basi tutakutana huko tukachomwe wote moto kama vitabu vya dini vilivyo andika" aliongea na kuanza kuondoka hilo eneo akimuacha mama huyo analia machozi ya uchungu mno. Watu wake ambao walimfanya afanye mabaya wakati wa utumishi wake ndio ambao walikuwa wameenda kumuua mwisho wa siku huku akiwa na chaguo la kujiua yeye ama aachwe hai ila familia yake yote ife. Majuto ni mjukuu, ulisikika mlio wa risasi nyuma wakati wanaume hao wanatoweka kwenye hilo eneo kwa ajili ya kuilinda siri isiende kwenye mikono ya Gavin Luca.


PEENUGA GOLDEN RING.
Ndani ya ule ulingo ndiko ambako Lucas aliweza kutengeneza jina, huenda unajiuliza ilikuwaje mpaka akapata jina ndani ya ile sehemu. Ushapu na ujanja wake na kutokuwa zoba ulimfanya aaminike na kuanza kutumika kuuza madawa hata akiingia mle ndani, wakati wengine wakiwa wanafurahia watu wakitoana damu na uhai yeye alikuwa akichangamkia fursa kwa kuuza sana madawa kwa watu mle ndani ambao walipenda kupata vibe jipya na kelele zinakuwa nyingi.
Kwenye mizunguko yake ya kila ambapo kulikuwa na ngumi alikuwepo mle ndani ndiko kulimkutanisha na bwana mmoja ambaye alikuwa ni mtu wa Mexico huko. Gustavo Gaviria, huyu alikuwa ni mtu kutoka Mexico ambaye kwa miaka mingi alikuwa ni msambazaji mkubwa wa dawa za kulevya ndani ya taifa la Marekani lakini baada ya muda aligundulika na serikali hiyo ikaanza kumtafuta kila kona ndipo akaamua kuhamisha njia zake za usafirishaji kwa muda mpaka pale ambapo mambo yangeenda sawa angeweza kurudi kwenye njia zake za zamani. Hapo ndipo aligundua soko jipya ndani ya Afrika kwa sababu watumiaji wa dawa za kulevya walikuwa wakiongezeka lakini alikuwa akiitumia njia ya Afrika kusafirishia dawa zake za kulevya kutokea Afrika kwenda kwenye mataifa mengine ya Afrika hususani Afrika ya kusini na nchi za bara la Asia kama China na India.
Kwa sababu ya kutafutwa kwake sana ndipo alijikuta anaishia ndani ya mitaa hiyo ya Peenuga na ndiye ambaye alikuwa anawamiliki wauzaji wengi wa dawa za kulevya ndani ya mitaa hiyo. Soko zima lilikuwa kwenye mikono yake kwa sababu Tanzania lilikuwa kama tawi lake tu ila alikuwa na masoko kila pembe ya ulimwengu. Kujituma kwa Lucas ndiko ambako kulimfanya mtu huyo amuone bwana mdogo ambaye alionekana kuwa na njaa kali ya mafanikio akiwa anazunguka ndani ya ukumbi huo wa kutisha wa mauaji na ndipo safari ya maisha ya Lucas ilipo anzia hapo.
Lucas alichukuliwa na mwanaume huyo moja kwa moja na kuanza kumtumia kwenye biashara zake taratibu, Lucas ndiye ambaye alikuja kuwa kijana wa Gustavo ambaye alianza kumuamini sana kwa sababu hakuwahi kwenda naye kinyume hata siku moja na alikuwa anamsikiliza zaidi yeye. Robert Greene kwenye kitabu chake cha 48 Laws of Power emeandikwa hizo laws zake, law ya kwanza inasema "Never outshine your master" hiyo ndiyo ilikuwa silaha kubwa ya Lucas, alimtii bosi wake na kuwa mwaminifu kwake, kadri muda ulivyokuwa unakatika ndivyo ambavyo maisha yake yalikuwa yanabadilika taratibu.
Lucas hakuwa fala, wakati wote huo alikuwa anaisoma mifumo kwa umakini sana juu ya hiyo biashara, Lucas alikuwa akiutumia muda wake mwingi kujua namna ambavyo bosi wake anafanya biashara hiyo na uaminifu wake ulifanya yeye kuanza kusimamia biashara za Gustavo ndani ya Tanzania lakini baadae mpaka Afrika nzima. Ni yeye pekee ambaye alibahatika kupata nafasi ya kusafiri na Gustavo kila pembe ya dunia mahali ambapo wangehitajika kwenda, kwanini? Haikuwa tu kwa sababu yeye ni muaminifu bali uwezo wake wa kufanya biashara na kumwingizia bwana huyo pesa nyingi.
Lucas ikawa habari nyingine, Lucas hakuwa yule maskini ambaye hakuwa na uwezo wa kulipa bili za hospitali, taratibu jina lake likaanza kupenya kwenye maskio ya watu hususani watanzania, tajiri mpya akawa ameongezeka nchini. Baada ya muda mrefu kupita Lucas akaanza kwenda mwenyewe Mexico kumuwakilisha bosi wake, biashara za Gustavo zikawa zinasimamiwa na Lucas ambaye aliaminika kuliko mtu yeyote yule. Madawa ya kulevya yalimsafirisha mpaka Kolombia ambako alikutana na magwiji wengi wa biashara hiyo, biashara hiyo ilimkutanisha na CARTELS nyingi sana za uuzaji wa dawa za kulevya huko Mexico, dawa za kulevya zilimpa watu wapya mpaka ndani ya nchi ya Pakistani ambako kulikuwa njia mpya na salama kwa biashara hiyo.
Kwa sababu Gustavo bado Marekani walikuwa wakimuandama, biashara zake nyingi zikawa zinasimamiwa na Lucas, mikataba ya pesa yote ikawa inasimamiwa na Lucas huku Gustavo akila matunda ya kukutana na kijana huyo lakini Lucas hakuwa fala. Lucas alihakikisha amesoma kila engo ya mchezo mzima jinsi unavyo chezwa, alihakikisha anaijua mifumo yote ya biashara hiyo kwa muda mrefu tangu akiwa kijana mpaka alipofikisha miaka thelathini akawa anajua kila kitu na pesa zilikuwepo za kutupa. Ndipo akaamua kuhitaji kuwa mtawala wa hizo biashara yeye mwenyewe, alihitaji kila kitu akisimamie yeye na kiwe chini ya mikono yake ndipo akapanga safari ya mauaji kwa Gustavo, bosi wake.

Mwanaume akili yake ilikuwa inawaza pesa tu, unahisi atafanikiwa kumuua kiongozi na mfanya biashara mkongwe wa madawa ya kulevya ambaye ndiye alimuonyesha njia zote? Nini hatima ya mtafutaji huyu? Ishirini na tatu niseme bye bye.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom