Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI
SONGA NAYO................
JOHANNESBURG, AFRIKA KUSINI.
JOZI ndilo jiji kubwa zaidi ndani ya nchi ya Afrika ya kusini, ni jiji la kale sana ambalo linadaiwa kugunduliwa mnao mwaka wa 1886. Kinacho lipa zaidi umaarufu jiji hilo ni biashara ya dhahabu pamoja na mzunguko mkubwa wa fedha kiasi kwamba likapewa jina la JIJI LA DHAHABU (GOLDEN CITY).
Jozi ni ndilo jiji kubwa zaidi ndani ya nchi hiyo lakini pia ndilo jiji tajiri zaidi, utajiri wake unapambwa zaidi na biashara kubwa ya madini ambao ndio msingi mkuu wa kuendelea na kufanikiwa kwake. Taifa hilo limefikia hatua linaanza kupoteza ile ladha ya kuitwa Afrika kwa sababu ya mchanganyiko wa rangi zilizopo ndani ya taifa hilo. Ni taifa kubwa kibiashara duniani hivyo huvutia watu wengi ndani yake kiasi kwamba hata wale wazawa wanaanza kupoteza nguvu kubwa ambayo inachukuliwa na wazungu, waasia, na wamarekani kwa kiwango kikubwa.
Kuvutia kwake watu wengi kumefanya pia ndani ya nchi hiyo hususani kwenye hilo jiji kuwepo kwa matukio mengi ya kutisha hususani mauaji, watoto wa mama hawahitajiki kwenda kuishi huko kwa sababu wanahitajika wanaume zaidi. Hali hiyo imefanya sehemu hiyo kuwa kivutio kwa watu wengi ambao wanajishughulisha na shughuli haramu pia kujiingiza huko kwani wanaamini kuna fursa nyingi za maisha. Kuna watu huko huwa wanabahatika kufanikiwa lakini wengine huishia kufanyiwa unyanyasaji na hata kuuawa.

O.R. Tambo International Airport ambao ndio uwanja mkubwa zaidi wa ndege ndani ya hilo jiji, usiku ulipokea ugeni wa msafiri kutoka Tanzania. Bwana huyo uso wake ulipo onekana kutoka nje ya uwanja wa ndege, alikuwa ni bwana Mike Tores ambaye alimuaga mkewe Singida kwamba anaenda kibiashara Botswana. Uso wake ulikuwa umejaa ndevu, mwili wake ulifunikwa na kanzu safi ya kumtoa mashakani kutoka kwa mtu yeyote ambaye angemtazama. Kichwani alikuwa na barakashea ya kukamilisha mtazamo wa imani yake, mtu wa maana kabisa.
Bwana huyo aliingia kwenye nchi hiyo kama mfanya biashara wa madini na alikuwa na vibali vyote halali kabisa ndiyo maana hakupata pingamizi yoyote wakati anafanyiwa ukaguzi ndani ya uwanja wa ndege. Alifikia kwenye hoteli ambayo ilikuwa umbali mfupi tu kutoka ulipo uwanja wa ndege huo, Airport Inn and Suits Isando. Hakuwa anabahatisha kila kitu chake kilikuwa kinaenda kwa mahesabu makali.
Hakwenda Afrika ya kusini kuuza sura au kupoteza muda, hakwenda Afrika ya kusini kushangaa namna jiji la Jozi lilivyo bali alikwenda huko kumtafuta mtu wake, kuna mtu alikuwa ana shida naye kwa muda mrefu kwenye maisha yake, mtu huyo alikuwa ana historia naye mbaya isivyokuwa kawaida. Ilipita miaka mingi akiwa anamtafuta bila mafanikio, kwa mara ya kwanza alipata kuzijua habari za anapo patikana bwana huyo, asingemuacha aende kirahisi, alikuwa na mengi ya kuongea naye mezani kama wanaume lakini alijua kabisa sio rahisi kumpata mtu kwenye jiji kubwa kama hilo ambalo unakuwa hujui uanzie wapi ila kwake alijua ni sehemu zipi anatakiwa kupita. Ilikuwa ni lazima ampate bwana mkubwa Master G.S.

Mitaa ya Jozi imechangamka kwa masaa ishirini na manne ya siku, hilo likawa faida kwake Mike. Alijua muda wowote angeenda popote kufanya kile ambacho anakihitaji lakini haikuwa rahisi kama ambavyo alikuwa anahisi yeye, mwanaume ambaye alikuwa anaenda kudili naye wakati huo hakuwa wa kawaida. Ulikuwa msimu wa baridi, majira ya usiku huwa kunakuwa na baridi maeneo hayo hivyo mwanaume huyo alijua kabisa muda kama huo magenge mengi mtaani huutumia kwa ajili ya kutumia vitu vizito kama madawa ili kuipa miili joto, kazi yake ingeanzia hapo.
Alibeba mabunda kadhaa ya pesa na kutoka ndani ya hoteli ambayo alifikia, walimsihi kwamba wamsaidie na usafiri wa hoteli kwa sababu kwa mgeni kama yeye usiku angepata changamoto mtaani lakini aliishia kutabasamu tu na kuhitaji kuelekezwa tu ilipo club ndani ya hilo eneo, kazi yake ilikuwa inaenda kuanzia huko.

CHEEKY TIGER
Ni moja kati ya night clubs maarufu sana jijini hapo ambazo zipo wazi kwa masaa ishirini na manne, ni club ambayo ilikuwa maarufu hususani kwa upatikanaji wake wa wanawake ambao wanafanya biashara ya kuuza miili yao na kutoa burudani, wao wanawaita striper kwa kiswahili unaweza kusema tu malaya au wanawake ambao huwa wananengua kwenye steji wakiwa nusu uchi kwa ajili ya kuwavutia wanaume ambao wanawaangalia kwa lengo la kujipatia pesa.
Umaarufu wa club hiyo na yale ambayo yalikuwa yanaendelea ndani yake kilitumika kama kivutio kikubwa kwa vijana wengi na watu wengi hivyo kufanya eneo hilo kujaa watu wa kila namna, baada ya kupata taarifa za Club hiyo Mike aliamua kutembelea eneo hilo ambalo aliamini kwamba angeweza kupata Abc za kile ambacho kilimpeleka ndani ya hilo jiji. Mitaa ilikuwa tulivu, ulikuwa usiku wa manane, ni jiji tu lilikuwa linavutia kwa namna lilivyokuwa linawaka na kuonyesha umaridadi wake kila kona.
Alijongea mpaka ndani ya eneo hilo ambapo mara ya kwanza aligomewa kwa sababu alikuwa mgeni lakini haikuwa shida, pesa alikuwa nayo. Alimpatia mlinzi randi 1000 akaruhusiwa kuingia tena kwa heshima kubwa, pesa inaongea watu hawataki maneno mengi. Ndani kulikuwa kumechangamka isivyokuwa kawaida, watu walikuwa wakila maisha na kuzisahau shida zao wote kwa muda, humo ndani hakuna mtu alikuwa anazikumbuka shida zake tena bali ni raha tu zilitawala huku wakiamini matatizo huwa yanajileta yenyewe.
Kulikuwa na jukwaa upande wa mbele, lilikuwa kubwa ambalo lilinakishiwa vyema likawa linavutia kwa mbadilishano wa taa mbalimbali ambazo zilikuwa zinawaka eneo hilo, kuvutia kwake hakukuchagizwa tu na zile taa, lahasha! Bali maua mazuri ambayo yalikuwa yakionekana kwenye zile taa, wanawake walikuwa wamevaa vibikini tu, wengine matiti yakiwa nje kuupa ulimwengu maraha, watu walikuwa wanaweuka kila wanawake wale warembo walipokuwa wanayakata mauno.
"Sawubona mngani!" Mike alishtuka baada ya kusikia hayo maneno, ni baada ya kupamiana na mtu, alimaanisha hello rafiki huku akiwa anacheka.
"Sawubona mngani, ngiyisihambi lapha (safi rafiki mimi mgeni hapa)"
"Hahaha ngiyakubona nje (Hahaha nimekuona tu). Uphuma kuphi? (unatokea wapi?)"
"Ngivela eKenya (natokea Kenya)
"Wenzani lapha"
"Ngidla ubumnandi"
"Ake ngihambe ngiyokukhombisa lapho kukhona ubumnandi"

Mike hakuonekana kuwa mgeni ndani ya ardhi ya Mandela, alipamiana na mtu ambaye alikuwa anamuongelesha Kizulu naye alikuwa anajibu bila papara lakini hakuonekana kuwa mzulu kwa sababu hao watu lafudhi yao inaendana na hata asili yao inaendana ndiyo maana alidanganya kwamba anatokea Kenya. Bwana huyo alimuuliza kama ameenda kufanya nini ndani ya nchi hiyo akadai kwamba ameenda kura maraha ndipo akamtaka amfuate ili amuonyeshe raha zilipo.
Licha ya sauti kubwa ya mziki na kelele ambazo zilikuwepo humo ndani lakini bado walielewana vizuri, bwana huyo alitangulia akimtaka Mkenya amfuate sehemu ambayo aliahidi kwamba angepata maraha ya kutosha. Walipita eneo lile mpaka walipofika kwenye korido moja kubwa, huko kulikuwa na bar nyingine kubwa, walikaa watu na warembo wakila raha wengine wakiendelea kutumia madawa ilimradi kila mtu kile ambacho kilikuwa burudani kwake.
Upande wa mbele kulikuwa na mlango mkubwa, waliingia humo, eneo hilo lilikuwa limepambwa kuliko nje, kulikuwa na sofa kubwa mbili na kitanda ambacho kilizungukwa na maua. Kitandani alikuwepo mwanamke mmoja mrembo sana akiwa uchi kabisa. Bwana yule alimuahidi Mike kwamba angerudi muda mfupi ambao ungefuata akimuacha ale raha ambazo alikuwa anazitaka. Baada ya kutoka mrembo yule alimsogelea Mike na kuanza kukatika akiwa hana nguo hata moja lakini mwanaume huyo alimzuia, alimtolea bunda la pesa na kumtaka akae chini kwani alizihitaji taarifa na kama mwanamke huyo angezitoa basi bunda zima la pesa ambazo angezipata kwa mwaka mzima alikuwa anazipata ndani ya dakika kadhaa tu.
"Sipo hapa kwa ajili ya kufanya mapenzi na wewe bibie, nipa hapa kuna mtu namtafuta" aliamua kutumia kiingereza ambacho alijua wote wataelewana vizuri. Mwanamke yule alionekana kusita sita ikabidi atembee mpaka mlangoni akaurudishia, hakuwa tayari kuliacha bunda la pesa kama lile liende ambalo alikuwa anatakiwa kukusanya pesa za mwaka mzima ndipo alipate. Alimwangalia Mike kwa umakini akachukua shuka na kujifunika.

Sehemu ya thelathini inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA
SONGA NAYO................
"Yule ambaye amekuleta humu ndani unafahamiana naye?" lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa mwanamke huyo.
"Hapana"
"Naitwa Nandi, nipo kwenye hii biashara ya kuuza mwili wangu kwa miaka mitano sasa japo sioni mwelekeo wa maisha yangu. Sipo hapa kwa sababu napenda ninacho kifanya ila kwa sababu sina namna ya kufanya, kuwa hapa kumenifanya niyajue na kushuhudia mambo mengi mabaya, yule ambaye amekuleta humu wanamuita Bongani. Huyu hajakutana na wewe kwa bahati mbaya, mara nyingi akiona sura ngeni humu ndani huwa anajifanya kama ameipamia kwa bahati mbaya na anamleta mtu humu ambapo nitampa anacho kitaka, atalipia lakini kabla hajaondoka atajifanya anamkarimu sana na kutaka kumpeleka eneo lililo tulivu zaidi hapo utakutwa unavamiwa na watu wake ni wanaweza kukuua na kama ukibahatika basi watakupora kila ulicho nacho kisha wanakwambia uondoke Jozi vinginevyo wanakuua"
"Kwahiyo huyu kijana ni mhuni na mporaji pia?"
"Ndiyo"
"Kwa maana hiyo anaweza kuwa anawajua watu wengi ndani ya hili jiji hususani ambao wanafanya shughuli haramu?"
"Ndiyo kwa sababu watu wengi huwa wanamtumia yeye na muda mwingine huwa anatutumia sisi pia kwenye kazi za kusafirisha madawa kutoka jiji moja kwenda jingine"
"Kuna mtu anaitwa Master G.S, unamfahamu?"
"Master G au G.S"
"Wewe unamfahamu yupi?"
"Hakuna ninaye mjua ila hilo jina sio geni, nimewahi kusikia mtu akilitaja ila yeye alisema Mater G humu humu ndani ndiko niliwahi kusikia likitajwa"
"Unaweza ukajua alipo huyo Master G?"
"Hapana ila Bongani anaweza kuwa na taarifa za huyo mtu kwa asilimia kubwa na kama yeye hana basi watu wake lazima watakuwa nazo"
"Kama nahitaji kukutana na hao watu wake nawapataje?"
"Unaweza ukafa lakini njia rahisi ilikuwa ni kufuata maelekezo yake kama anavyo hitaji kwa sababu lazima watakuja kukuvamia ili kukupora na hivi alishajua una pesa na unaonekana kuwa wa kuja hili eneo lakini hii njia ni hatari mno kwako nafasi ya kupona ni ndogo"
"Asante kwa taarifa yako Nandi, wao ndio wanapaswa kuogopa kukutana na mimi. Unaonekana ni binti mzuri hivyo kuanzia leo uachane na hii kazi kabisa, katafute biashara ya kufanya ufanye na utafute mume mzuri mpate familia kwa sababu haya unayo yafanya mwisho ake utakuwa mbaya kwako na utaishia kujuta tu kwa muda ambao umeupoteza bila kufanya mambo ya maana yenye manufaa makubwa kwa maisha yako" mwanaume alichomoa bunda lingine yakawa mabunda mawili akamkabidhi binti huyo kwa sababu alimkarimu na kuonyesha kuwa mtu mwema ila ni maisha tu yalimfanya kuishia ndani ya hilo eneo.
Alipewa maagizo ya kumuita mtu wake huyo Bongani ambapo ndani ya muda mfupi alifika hapo akiwa amechangamka isivyo kawaida.

“Nina imani utakuwa haujaujutia muda wako?” Bongani aliongea akiwa anajichekesha macho yake yakiwa hayatulii kabisa lakini wakati huu hakujihangaisha kuongea Kizulu tena bali kiingereza ambacho kilinyooka vizuri kabisa.
“Najuta kwanini sikuwahi kuijua hii sehemu mapema” Mike alijibu
“Huu ni mwanzo tu usiku wa leo utakula raha ambazo umeishia kuziona kwenye tamthiliya za magharibi tu ndugu yangu. Karibu Jozi” alijihisi amepata ndiyo maana alikuwa akimkaribisha kwa mbwembwe zote.
“Hakika nitakupatia malipo mazuri mno kwa kunifanya nijisikie amani japo kwa siku moja. Kuna sehemu nyingine ya kwenda ambayo naweza kupata raha zaidi ya hizi?”
“Upo na mimi hakuna kitu utakosa ndani ya huu mji, nifuate” Aliongea na kuanza kuongoza huku macho yake yakiwa hayatulii kabisa, yule binti alimkonyeza Mike wakaagana.

Safari ya wawili hao ilienda kuishia nje kabisa ya jengo hilo kwa kupitia milango ambayo ilikuwa ya dharura, ni ishara kwamba Bongani alikuwa mwenyeji wa hilo eneo ndiyo maana kila kona alikuwa akizijua kwa usahihi.
“Mbona hatufiki?” Mike aliuliza lakini kulikuwa na ukimya, walikuwa wametokezea kwa nyuma eneo ambalo usiku huo palikuwa kimya. Hakujibiwa zaidi mwanaume huyo alitembea kidogo akasimama, ilisikika sauti ya mtu akibamiza mlango na Mike alipogeuka aligundua kwamba kwa nyuma kundi la watu limeongezea na mmoja alifunga ule mlango. Alitabasamu.
“Kijana unatakiwa kutupatia kila ulicho nacho tunaweza kufikiria kukuacha hai” aliropoka mwanaume mmoja ambaye mdomo wake ulionekana kabisa ulibadilika rangi kutokana na uvutaji wa bangi. Wanaume hao walikuwa na mapanga mkononi, mmoja ambaye alikuwa anaongea kwa jeuri hivyo alikuwa na bastola kwenye kiuno ambayo ilikuwa inaonekana kwa kuionyesha kwa makusudi.
“Bongani kwamba umeniuza rafiki yangu?” Bongani alishtuka kwa sababu kwa kumbukumbu zake ni kwamba hakumtajia huyo mtu jina lake.
“Umelifahamu vipi jina langu wewe?” aling’aka kwa jazba.
“Ulitaka tufahamiane vizuri kama kumbukumbu zangu zitakuwa sawa”
“Sijakutajia jina langu” alizidi kuwa na hofu huku akiwa anamsogelea Mike kwa jazba, wenzake hawakuwa mbali. Wakati anakaribia alipokuwepo Mike alihisi kama ameona kivuli kikija pale ambapo yeye alikuwepo hivyo alishtuka, hakikukuwa kivuli ni Mike alikuwa amemfikia kijana yule wa mjini.
Alipigwa ngumi ya shingo akashuka chini taratibu, ilikuwa ni ghafla, hawakutarajia kukutana na jambo kama lile wakati ule, kijana mmoja alikuwa karibu na upanga wake mkononi alijisogeza pale kurusha ule upanga kwa nguvu, ulipiga kwenye hewa wakati Mike anarudi nyuma kuukwepa, alimsogelea kijana yule akiwa anajiandaa kuurusha tena, aliudaka mkono wake na kuuvunja kwa mkono wake mmoja. Zilisikika kelele tu kijana yule hakuw ana uwezo wa kuushikilia upanga tena hivyo aliuachia ukaenda chini.
Haukufika chini kwa sababu ulitua kwenye mikono ya Mike, aliuzunguka na kuikita kwenye paja ya kijana huyo ambapo baada ya kuuchomoa aliuachia kwa nguvu kwenda kwa yule mwanaume ambaye alikuwa na bastola kwenye kiuno chake na wakati huo alikuwa anajiandaa kuweza kupiga risasi. Upanga ule ulitua kwenye bega lake ukatokezea mpaka nyuma. Alipiga kelele huku bastola yake ikienda chini. Mike alikimbia kwa kasi ya ajabu kumuwahi kijana mmoja ambaye aliirukia ile bastola, wakati anaifikia alikutana na buti la uso ambalo lilimbeba mpaka ukutani ambako alijibamiza na kupoteza fahamu.
Alikuwa anaangaliana na vijana watatu wakiwa na mapanga kwenye mikono yao, walienda kwa pamoja ili kuweza kushindana naye lakini kilicho wapata ni majuto. Aliwatia vibao vijana hao vya nguvu mpaka wakawa wanatoka damu kwenye mashavu yao, aliwataka waondoke ndani ya eneo hilo kabla ya kufanya maamuzi ya kuweza kuwaua, kwake walionekana kuwa viumbe wadhaifu mno ndiyo maana hakutaka kuwafanyia jambo lolote baya.

Baada ya kuona amemalizana nao na wengine wakiwa wanakimbia hususani yule ambaye mara ya kwanza alionekana kuwa na bastola kiunoni bila kujali damu ambayo ilikuwa inamtoka kwenye mwili wake, Mike alisogea mpaka pale ambapo alikuwa amelala Bongani, alimgusa kwenye mishipa ya shingo kijana huyo akakurupuka mithili ya mtu ambaye alikuwa amefumaniwa na hajui ni wapi angetokea.
“Nipo wapi, nipo wapi?” alifoka kwa kiingereza akitaka kujua mahali ambapo alikuwepo lakini alitulizwa na kofi kali usoni ambalo lilimfanya abaki anatoka udenda huku akiwa analia kwa kwikwi, alijuta kuingia kwenye mikono ya bwana huyo ambaye hakuwa akimjua.
“Bwana mdogo sio kila king’aacho ni dhahabu, acha kucheza na maisha yako kipuuzi namna hii utakuja kufa vibaya”
“Wewe ni nani?” aliuliza akiwa anahema kwa mashaka akiangaza kila upande lakini hakuona msaada wa karibu zaidi ya mwenzake mmoja ambaye alikuwa pembeni amelala bila shaka alipoteza fahamu.
“Hautakiwi kunijua kitu pekee ambacho unatakiwa kukifanya kwangu ni kunipa taarifa ambazo nazihitaji ili niweze kukuacha ukiwa hai”
“Najua huwezi kuniua kwa sababu unajua kabisa kwamba hili eneo lina kamera”
“Wewe ndiye umeniongoza huku ili uje uniibie na wenzako, usingeweza kuiniibia kwenye eneo lenye kamera kwa sababu ungekamatwa. Mpaka unanileta hii sehemu maana yake ni kwamba huku kamera hakuna ndiyo maana nimefanya haya yote kwa sababu najua hakuna mtu ananifahamu na hakuna mtu atajua kilicho tokea hapa”
“Nandi ameiona sura yako hivyo anaweza kuwa msaada kwa polisi kwani kule mbele kuna kamera lazima imenasa sura yako”
“Kwa bahati mbaya Nandi ndiye ambaye amenipa maelekezo namna ya kukupata na baada ya hapa usije ukamtafuta kumfanyia jambo lolote lile kwa sababu nitakutafuta kwa nanma yoyote ile”
“Kipi unataka kukijua?”
“Nahitaji kuonana na Master G” Bongani alionekana kushtuka na kuogopa baada ya kulisikia hilo jina kwenye masikio yake.
“Sijawahi kulisikia hilo jina kwenye maisha yangu yote” alidanganya hadharani macho yake yakiwa na mashaka. Mike alitoa kisu kutoka kwenye kiuno chake, kisu kilikuwa kinang’aa, bila shaka ni muda mrefu ulikuwa umepita hakikuwa kimetumika kumuulia mtu yeyote yule. Alimeza mate Bongani.
“Kijana bila shaka haunifahamu mimi ni nani na usilazimishe uweze kunifahamu kwa sasa kwa sababu hautakuwa na hiyo nafasi ya kuishi kwa mara ya pili”
“Hilo jina huwa hatulitamki hovyo”

Sehemu ya 31 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI
SONGA NAYO................

“Kwanini?”
“Huyo ni mtu hatari sana”
“Nampatia wapi?”
“Kwa huku mtaani sisi hatujui makazi yake yanapatikana wapi, huwa tunamuona mara moja kwa miezi sita”
“Kwahiyo hujui naweza kumpata vipi?”
“Ndiyo”
“Ila unajua mtu ambaye anaweza kunisaidia kumpata si ndiyo?”
“Ndiyo”
“Nipe taarifa zake”
“Dumisani Raymond”
“Nipe taarifa zake”
“Huyu anamiliki gereji kubwa zaidi ndani ya Jozi lakini gereji yake huwa inatumika kama kituo cha kusambazia madawa ya kulevya cha master G na huyu ndiye kijana wake anaye muamini zaidi kuliko mtu yeyote yule” Kijana huyo alitoa address ya mahali ambako anapatikana Dumisani Raymond. Mike alimrushia bunda la pesa na kuamua kumuacha.
“Kama hii taarifa ukiifikisha kwa hao watu basi nitarudi kukuua na hakikisha unawaziba midomo hata wale vijana wako haraka” Aliondoka kuelekea kwa huyo Dumisani, asingeweza kulala usiku huo kwa sababu kesho alitakiwa kuondoka Jozi baada ya kukamilisha kilicho mpeleka huko. Master G alikuwa ni Douglas Shenzi, mtu huyo yeye binafsi hakuwahi kukutana naye kwenye maisha yake yote lakini alikuwa na shida naye kubwa kwa sababu alimuachia kidonda kibaya kwenye moyo wake na muda wake wa kukilipia ulikuwa umewadia.


D.R. GARAGE
Ilikuwa ni miongoni mwa gereji kubwa zaidi ndani ya jiji la Jozi, DR kilikuwa ni kifupi cha Dumisani Raymond. Gereji hiyo ilikuwa inatoa huduma masaa ishirini na manne kwa wiki nzima, hakuna muda ambao ilikuwa ikifungwa, kila wakati ilionekana kuwa busy ikitoa huduma hata usiku wa manane huku watu kadhaa wakiwa wanapishana wakiwa wanaingia na kutoka ndani ya eneo hilo.
Haikuwa tu gereji kama wengi walivyokuwa wanadhani, eneo hilo lilikuwa likitumika kama sehemu kubwa ya kuendeshea biashara ya madawa ya kulevya na lile neno gereji lilikuwa linatumika tu kwa ajili ya kuwalinda watu hao. Usiku wa manane huo walikuwa humo ndani wakiendelea na kazi zao za kawaida mpaka walipo ona kuna gari ndogo inaingia ikiwa imebonyea kwa mbele.
Walimpokea mgeni wao ambaye alikuwa ni Mike, hakuonekana kuwa mwenyeji wa eneo hilo kwa sababu kwenye mwili wake alivaa kanzu ndefu nyeupe na sando huku kichwani akiwa amejifunga kilemba, kwa kumwangalia kwa haraka haraka basi karibia kila mtu anegejua kwamba bwana huyo alikuwa ametokea Dubai bila shaka na gari yake huenda alikodi kwa matumizi ya kila siku ndani ya Jozi.
“Karibu mheshimiwa”
“Asante sana, gari yangu imepata hitilafu kidogo hivyo nahitaji muweze kunirekebishia”
“Ni usiku sana saivi halafu kuna kazi nyingi, naomba uiache kisha uijie asubuhi”
“Hiyo gari ni mhimu kuliko unavyo fikiri siwezi kuondoka bila kuwa nayo na nimeambiwa kwamba nyie ndio mabingwa ndani ya hili jiji hivyo nina imani nitaondoka nayo”
“Kama kuna ulazima wa kuwa na gari basi unaweza kuacha vitambulisho vyako ukapewa gari ya ofisi”
“Sio kirahisi namna hiyo, niruhusu niongee na bosi wako”
“Umesema?”
“Niruhusu niongee na Dumisani Raymond” kijana ambaye alikuwa anafanya mazungumzo yaliyokosa maelewano na Mike alishangazwa na kushtuka baada ya kusikia jina hilo likitajwa.
“Wewe ni nani?”
“Mbona umeshtuka namna hiyo?”
“Hakuna mtu wa mbali ambaye analijua hilo jina kwa kirefu kwa usahihi namna hiyo, pia hakuna mtu ambaye anajua kama ni yeye anamiliki hii gereji”
“Basi huenda ni siku yangu ya bahati leo”
“Sio kirahisi namna hiyo, who are you?” sauti ilibadilika kwa bwana huyo ambaye alihisi mtu wake hakuja hapo kwa ajili ya gari bali alikuwa na mambo yake mengine. Mike aligeukia ukutani, kulikuwa na kamera ambayo ilikuwa inamtazama eneo hilo, alitabasamu.

Alipogeuka kumtazama tena kijana yule ambaye alianza kumletea upinzani kabla hata hajafika ndani, hakumpa hiyo nafasi, aliigusa shingo yake kwa nguvu na kuizungusha, alimnyonga bila huruma baada ya kuona mkono wake unagusa kwenye kiuno chake. Akiwa hapo alinyoosha mikono yake juu baada ya kuona wanaume kadhaa wamekuja na silaha hapo, walimuongoza mpaka ndani ya godauni ambalo lilikuwa na vyuma vya kutosha.
Baada ya kufika huko aliona kuna mwanaume mmoja akiwa amempa mgongo, bwana huyo alikuwa amevaa jeans nzito pamoja na koti jeusi mkononi alionekana kuwa na sigara ambayo alikuwa anaivuta kwa mkupuo. Aligeuka kumwangalia Mike, usoni alikuwa na alama kama ya kisu karibu na jicho lake, kwa kazi yake hiyo haikuwa ajabu kuwa namna hiyo.
“Bila shaka utakuwa mgeni wangu ila kwanini umeamua kuua mtu wangu? Huku kwetu hiyo huwa haiendi bure ni labda ufe au uchague nipunguze kiungo chako kimoja kama kutakuwa na haja ya kukuacha hai.
“Ni kweli mimi ni mgeni wako ila niliona kabisa kwamba hatuwezi kusikilizana hivyo nikahitaji umakini wako na kuupata ilitakiwa nitumie njia kama hiyo”
“Tunafahamiana kabla?”
“Hapana na haina umuhimu wa mimi na wewe kufahamiana, inaweza kuwa mwisho wa kuonana kwa sababu hakutakuwa na ulazima kama tu utafanya ninacho kitaka”
“Umesema nikifanya?”
“Ninacho kitaka”
“Mimi hapa ndo nifanye unacho kitaka wewe?”
“Ndiyo”
“Hahahaha hahaha, una uhakika upo timamu?” aliongea Dumisani mwenyewe akiwa anaikoki vizuri bastola yake na kumnyooshea Mike.
“Bastola hiyo haitakusaidia kwa lolote hapa, nataka unipeleke alipo Master G ila mimi namfahamu kama Douglas Shenzi” gudauni zima lilibaki kimya, kila mtu alibaki anamshangaa mtu huyo mgeni hata Dumisani mwenyewe alibaki ameduwaa akiwa ameishikilia bastola yake.
“Umechanganyikiwa, unakuja hapa kuulizia majina ya kufikirika ndiyo sababu unaua hadi mtu wangu?”
“Dumisani wote tunajua kwamba hili sio jina la kufikirika, ni jina la mtu ambaye naishi japo kwa kujificha ila mimi nina historia naye ndefu kuna deni langu anatakiwa kulilipa na sidhani kama ni busara ukajiingiza kwenye hilo jambo kwa sababu wewe halikuhusu kabisa”
“Kill him” ndiyo kauli ambayo ilitoka kwenye mdomo wa Dumisani akiwa anaishusha bastola yake, hakutaka kumuua mtu huyo kwa uharaka, alitakiwa kuteseka kwanza. Aligeuka akiwa anatukana ila haikusaidia lolote lile.

Kijeba mmoja alisogea akitaka kumbeba Mike juu ila huenda hakujua aina ya mtu ambaye alikuwa ansogeleana naye, mkono wake ulitangulizwa mbele, ulidakwa kwenye viganja akavutwa kwa nguvu bila kutegemea, mkono wa Mike ulizama kwenye kifua cha kijeba huyo na kuirarua sehemu ya moyo pakabaki shimo. Wote walibaki wanashangaa, alikuwa kijeba ambaye alijaza kwa mazoezi makali lakini alikufa ndani ya sekunde kadhaa tu mwili wake ukatupwa. Kishindo cha kudondoka kwake ndicho kilimshtua Dumisani kugeuka wakati anageuka alikutana na kijana wake mwingine akiwa ameshikilia shingo, koromeo lilinyofolewa.
Mtu ambaye walimchukulia kimzaha alikuwa anayabeba maisha yao, Mike alikuwa anatembea kwa kasi kama umeme. Wanaume wawili waliruka hewani kumsogelea, alijigeuza kwa sarakasi za haraka haraka, alitua kwenye shingo ya mmoja na kushuka naye ambapo goti lilitua kwenye shingo ya mwanaume huyo ikavunjwa vibaya. Yule mmoja ambaye alimkosa alikuwa amepitiliza, wakati anageuka alidakwa kwenye mbavu zake, mbavu zilivutwa kwa nguvu ikasikika tu sauti “Kha kha kha” zilivunjika, akashindiliwa na nguvu ya uti wa mgongo, hakutikisika tena akadondoka pale pale.

Dumisani alinyoosha bastola ili apige risasi, kiganja chake kilikufa ganzi, ni shilingi ilikuwa ikiharibu vibaya ambayo ilitambaa kwenye bastola na kutua kwenye mkono wake. Ilisikika mlio wa kelele tu akiwa anaitupa bastola mbali na yeye akidondokea nyuma kuweza kuuguza mkono wake. Vijana wake ambao hata hawakuwo humo ndani walianza kumiminika kwa wingi, kijana mmoja ambaye alijifanya kuwa na jazba zaidi alikimbia akipiga makelele ila kwa bahati mbaya ilichomolewa nondo moja ikazamishwa kwenye mdomo na kutokezea nyuma, alikufa akiwa anapiga maakelele yake. Mike alibadilika macho yake yakawa mekundu sana.

Alikunjuka kwa mbio ambapo alimzunguka kijana mmoja aliyejawa na hofu, wakati kijana huyo anageuka alipigwa ngumi ya kwenye moyo, hakutikisika tena alibaki amesimama hivyo hivyo. Vijana wengine wakati wanamsogelea aliokota ile bastola na kuwatandika risasi kwa sababu walikuwa wanampotezea muda wake tu.
Dumisani kiganja kilikuwa kimeharibika vibaya, baada ya kuona vijana wake wameisha alijitahidi kukimbia ili aweze kupona kwenye huo msala ila kwa bahati mbaya nondo ilirushwa na kuzama kwenye mguu wake akadondoka. Mike alichomoa bastola yake kiunoni na kumsogelea Dumisani akiwa anajivuta, alisogea kwenye sakafu ambapo bwana yule alilala akiwa anajitahidi kunyanyuka ila mguu ukawa unamhukumu kwa maumivu makali ambayo alikuwa akiyapata.
“Jina langu naitwa GAVIN LucA, mimi ni mtanzania na Douglas kuna wakati amewahi kuishi ndani ya ardhi ya nyumbani kwangu ila wakati anaishi huko kuna tukio la mauaji aliyafanya kwa kuiua damu yangu hivyo siwezi kumuacha akiwa hai na anatakiwa kuniambia ni nani alimpa amri ya kufanya vile. Ungenijibu kistaarabu hata tusingefika huku ndugu yangu Dumisani, ningekuacha na maisha yako”

32 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI
SONGA NAYO................

“Kwanini?”
“Huyo ni mtu hatari sana”
“Nampatia wapi?”
“Kwa huku mtaani sisi hatujui makazi yake yanapatikana wapi, huwa tunamuona mara moja kwa miezi sita”
“Kwahiyo hujui naweza kumpata vipi?”
“Ndiyo”
“Ila unajua mtu ambaye anaweza kunisaidia kumpata si ndiyo?”
“Ndiyo”
“Nipe taarifa zake”
“Dumisani Raymond”
“Nipe taarifa zake”
“Huyu anamiliki gereji kubwa zaidi ndani ya Jozi lakini gereji yake huwa inatumika kama kituo cha kusambazia madawa ya kulevya cha master G na huyu ndiye kijana wake anaye muamini zaidi kuliko mtu yeyote yule” Kijana huyo alitoa address ya mahali ambako anapatikana Dumisani Raymond. Mike alimrushia bunda la pesa na kuamua kumuacha.
“Kama hii taarifa ukiifikisha kwa hao watu basi nitarudi kukuua na hakikisha unawaziba midomo hata wale vijana wako haraka” Aliondoka kuelekea kwa huyo Dumisani, asingeweza kulala usiku huo kwa sababu kesho alitakiwa kuondoka Jozi baada ya kukamilisha kilicho mpeleka huko. Master G alikuwa ni Douglas Shenzi, mtu huyo yeye binafsi hakuwahi kukutana naye kwenye maisha yake yote lakini alikuwa na shida naye kubwa kwa sababu alimuachia kidonda kibaya kwenye moyo wake na muda wake wa kukilipia ulikuwa umewadia.


D.R. GARAGE
Ilikuwa ni miongoni mwa gereji kubwa zaidi ndani ya jiji la Jozi, DR kilikuwa ni kifupi cha Dumisani Raymond. Gereji hiyo ilikuwa inatoa huduma masaa ishirini na manne kwa wiki nzima, hakuna muda ambao ilikuwa ikifungwa, kila wakati ilionekana kuwa busy ikitoa huduma hata usiku wa manane huku watu kadhaa wakiwa wanapishana wakiwa wanaingia na kutoka ndani ya eneo hilo.
Haikuwa tu gereji kama wengi walivyokuwa wanadhani, eneo hilo lilikuwa likitumika kama sehemu kubwa ya kuendeshea biashara ya madawa ya kulevya na lile neno gereji lilikuwa linatumika tu kwa ajili ya kuwalinda watu hao. Usiku wa manane huo walikuwa humo ndani wakiendelea na kazi zao za kawaida mpaka walipo ona kuna gari ndogo inaingia ikiwa imebonyea kwa mbele.
Walimpokea mgeni wao ambaye alikuwa ni Mike, hakuonekana kuwa mwenyeji wa eneo hilo kwa sababu kwenye mwili wake alivaa kanzu ndefu nyeupe na sando huku kichwani akiwa amejifunga kilemba, kwa kumwangalia kwa haraka haraka basi karibia kila mtu anegejua kwamba bwana huyo alikuwa ametokea Dubai bila shaka na gari yake huenda alikodi kwa matumizi ya kila siku ndani ya Jozi.
“Karibu mheshimiwa”
“Asante sana, gari yangu imepata hitilafu kidogo hivyo nahitaji muweze kunirekebishia”
“Ni usiku sana saivi halafu kuna kazi nyingi, naomba uiache kisha uijie asubuhi”
“Hiyo gari ni mhimu kuliko unavyo fikiri siwezi kuondoka bila kuwa nayo na nimeambiwa kwamba nyie ndio mabingwa ndani ya hili jiji hivyo nina imani nitaondoka nayo”
“Kama kuna ulazima wa kuwa na gari basi unaweza kuacha vitambulisho vyako ukapewa gari ya ofisi”
“Sio kirahisi namna hiyo, niruhusu niongee na bosi wako”
“Umesema?”
“Niruhusu niongee na Dumisani Raymond” kijana ambaye alikuwa anafanya mazungumzo yaliyokosa maelewano na Mike alishangazwa na kushtuka baada ya kusikia jina hilo likitajwa.
“Wewe ni nani?”
“Mbona umeshtuka namna hiyo?”
“Hakuna mtu wa mbali ambaye analijua hilo jina kwa kirefu kwa usahihi namna hiyo, pia hakuna mtu ambaye anajua kama ni yeye anamiliki hii gereji”
“Basi huenda ni siku yangu ya bahati leo”
“Sio kirahisi namna hiyo, who are you?” sauti ilibadilika kwa bwana huyo ambaye alihisi mtu wake hakuja hapo kwa ajili ya gari bali alikuwa na mambo yake mengine. Mike aligeukia ukutani, kulikuwa na kamera ambayo ilikuwa inamtazama eneo hilo, alitabasamu.

Alipogeuka kumtazama tena kijana yule ambaye alianza kumletea upinzani kabla hata hajafika ndani, hakumpa hiyo nafasi, aliigusa shingo yake kwa nguvu na kuizungusha, alimnyonga bila huruma baada ya kuona mkono wake unagusa kwenye kiuno chake. Akiwa hapo alinyoosha mikono yake juu baada ya kuona wanaume kadhaa wamekuja na silaha hapo, walimuongoza mpaka ndani ya godauni ambalo lilikuwa na vyuma vya kutosha.
Baada ya kufika huko aliona kuna mwanaume mmoja akiwa amempa mgongo, bwana huyo alikuwa amevaa jeans nzito pamoja na koti jeusi mkononi alionekana kuwa na sigara ambayo alikuwa anaivuta kwa mkupuo. Aligeuka kumwangalia Mike, usoni alikuwa na alama kama ya kisu karibu na jicho lake, kwa kazi yake hiyo haikuwa ajabu kuwa namna hiyo.
“Bila shaka utakuwa mgeni wangu ila kwanini umeamua kuua mtu wangu? Huku kwetu hiyo huwa haiendi bure ni labda ufe au uchague nipunguze kiungo chako kimoja kama kutakuwa na haja ya kukuacha hai.
“Ni kweli mimi ni mgeni wako ila niliona kabisa kwamba hatuwezi kusikilizana hivyo nikahitaji umakini wako na kuupata ilitakiwa nitumie njia kama hiyo”
“Tunafahamiana kabla?”
“Hapana na haina umuhimu wa mimi na wewe kufahamiana, inaweza kuwa mwisho wa kuonana kwa sababu hakutakuwa na ulazima kama tu utafanya ninacho kitaka”
“Umesema nikifanya?”
“Ninacho kitaka”
“Mimi hapa ndo nifanye unacho kitaka wewe?”
“Ndiyo”
“Hahahaha hahaha, una uhakika upo timamu?” aliongea Dumisani mwenyewe akiwa anaikoki vizuri bastola yake na kumnyooshea Mike.
“Bastola hiyo haitakusaidia kwa lolote hapa, nataka unipeleke alipo Master G ila mimi namfahamu kama Douglas Shenzi” gudauni zima lilibaki kimya, kila mtu alibaki anamshangaa mtu huyo mgeni hata Dumisani mwenyewe alibaki ameduwaa akiwa ameishikilia bastola yake.
“Umechanganyikiwa, unakuja hapa kuulizia majina ya kufikirika ndiyo sababu unaua hadi mtu wangu?”
“Dumisani wote tunajua kwamba hili sio jina la kufikirika, ni jina la mtu ambaye naishi japo kwa kujificha ila mimi nina historia naye ndefu kuna deni langu anatakiwa kulilipa na sidhani kama ni busara ukajiingiza kwenye hilo jambo kwa sababu wewe halikuhusu kabisa”
“Kill him” ndiyo kauli ambayo ilitoka kwenye mdomo wa Dumisani akiwa anaishusha bastola yake, hakutaka kumuua mtu huyo kwa uharaka, alitakiwa kuteseka kwanza. Aligeuka akiwa anatukana ila haikusaidia lolote lile.

Kijeba mmoja alisogea akitaka kumbeba Mike juu ila huenda hakujua aina ya mtu ambaye alikuwa ansogeleana naye, mkono wake ulitangulizwa mbele, ulidakwa kwenye viganja akavutwa kwa nguvu bila kutegemea, mkono wa Mike ulizama kwenye kifua cha kijeba huyo na kuirarua sehemu ya moyo pakabaki shimo. Wote walibaki wanashangaa, alikuwa kijeba ambaye alijaza kwa mazoezi makali lakini alikufa ndani ya sekunde kadhaa tu mwili wake ukatupwa. Kishindo cha kudondoka kwake ndicho kilimshtua Dumisani kugeuka wakati anageuka alikutana na kijana wake mwingine akiwa ameshikilia shingo, koromeo lilinyofolewa.
Mtu ambaye walimchukulia kimzaha alikuwa anayabeba maisha yao, Mike alikuwa anatembea kwa kasi kama umeme. Wanaume wawili waliruka hewani kumsogelea, alijigeuza kwa sarakasi za haraka haraka, alitua kwenye shingo ya mmoja na kushuka naye ambapo goti lilitua kwenye shingo ya mwanaume huyo ikavunjwa vibaya. Yule mmoja ambaye alimkosa alikuwa amepitiliza, wakati anageuka alidakwa kwenye mbavu zake, mbavu zilivutwa kwa nguvu ikasikika tu sauti “Kha kha kha” zilivunjika, akashindiliwa na nguvu ya uti wa mgongo, hakutikisika tena akadondoka pale pale.

Dumisani alinyoosha bastola ili apige risasi, kiganja chake kilikufa ganzi, ni shilingi ilikuwa ikiharibu vibaya ambayo ilitambaa kwenye bastola na kutua kwenye mkono wake. Ilisikika mlio wa kelele tu akiwa anaitupa bastola mbali na yeye akidondokea nyuma kuweza kuuguza mkono wake. Vijana wake ambao hata hawakuwo humo ndani walianza kumiminika kwa wingi, kijana mmoja ambaye alijifanya kuwa na jazba zaidi alikimbia akipiga makelele ila kwa bahati mbaya ilichomolewa nondo moja ikazamishwa kwenye mdomo na kutokezea nyuma, alikufa akiwa anapiga maakelele yake. Mike alibadilika macho yake yakawa mekundu sana.

Alikunjuka kwa mbio ambapo alimzunguka kijana mmoja aliyejawa na hofu, wakati kijana huyo anageuka alipigwa ngumi ya kwenye moyo, hakutikisika tena alibaki amesimama hivyo hivyo. Vijana wengine wakati wanamsogelea aliokota ile bastola na kuwatandika risasi kwa sababu walikuwa wanampotezea muda wake tu.
Dumisani kiganja kilikuwa kimeharibika vibaya, baada ya kuona vijana wake wameisha alijitahidi kukimbia ili aweze kupona kwenye huo msala ila kwa bahati mbaya nondo ilirushwa na kuzama kwenye mguu wake akadondoka. Mike alichomoa bastola yake kiunoni na kumsogelea Dumisani akiwa anajivuta, alisogea kwenye sakafu ambapo bwana yule alilala akiwa anajitahidi kunyanyuka ila mguu ukawa unamhukumu kwa maumivu makali ambayo alikuwa akiyapata.
“Jina langu naitwa GAVIN LucA, mimi ni mtanzania na Douglas kuna wakati amewahi kuishi ndani ya ardhi ya nyumbani kwangu ila wakati anaishi huko kuna tukio la mauaji aliyafanya kwa kuiua damu yangu hivyo siwezi kumuacha akiwa hai na anatakiwa kuniambia ni nani alimpa amri ya kufanya vile. Ungenijibu kistaarabu hata tusingefika huku ndugu yangu Dumisani, ningekuacha na maisha yako”

32 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Duuh
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
SONGA NAYO................

“Go https://jamii.app/JFUserGuide yoursel……” alikatishwa kwa kupigwa risasi kwenye goti mpaka kwenye paja karibu na kiunoni.
“Nitakwambia nakwambia alipo muda huu” alijibu akitokwa jasho kwa wingi, machozi yalikuwa yanashuka kama maji, maumivu ya risasi hayakuwa yakivumilika kabisa kwenye moyo wake. Alihema kwa nguvu huku akiangalia kule nyuma, vijana wake wote walikuwa wameuawa vibaya.
“Huyo mtu ni komando wa zamani kutoka Israeli, alikuwa komando wa Special Force huko kwao na jina lake halisi anaitwa Yosef Biton. Sijajua kuhusu maisha yake ya Tanzania ila alikuja hapa Jozi kama muwekezaji na kwa wakati ule mitaa mingi ilikuwa yangu hivyo alinitafuta ili tufanye kazi lakini amekuwa mtu wa kuishi maisha ya siri na ndiye akaja kuwa bosi wangu kwa sababu ni mtu mwenye pesa nyingi lakini pia ni mtu mkatili na mwenye uwezo wa ajabu sana”
“Umesema ni komando wa Israeli?”
“Ndiyo wa zamani”
“Na huku anatafuta nini?”
“Inaonekana kwamba kuna kitu kibaya alikifanya hivyo akafukuzwa na kuambiwa aondoke Israeli vinginevyo wangemuua ndipo akaamua kukimbilia Tanzania ambako kwa mujibu wake ni kwamba mazingira hayakuwa rafiki ndiyo sababu akaamua kuja kuishi Afrika ya Kusini”
“Mlipanga kuonana lini?”
“Huwa kila siku usiku lazima tuonane”
“Unamaanisha nini?”
“Huwa napeleka hesabu za siku nzima”
“Kwa maana hiyo bado haujaenda?”
“Ndiyo, nilikuwa kwenye maandalizi ya kuonana naye”
“Mnakutania wapi?” mwanaume huyo alionekana kusita sita kutaja sehemu ambayo ilikuwa ni lazima wakutanie huko.
“New millenia tattoo center”
“Ni wapi huko?” mwanaume huyo alitoa karatasi kwenye mfuko wake ambayo ilikuwa na maelezo ya sehemu hiyo akampatia Mike.
“Hiyo sehemu ni yake pia?”
“Ndiyo, ndiko huwa tunakutania na kila tukikutana huwa anaongeza tatoo mpya kwenye mwili wake”
“Nionyeshe picha yake” hakuwa mbishi aliitoa simu na kumuonyesha, lilikuwa pande la mtu ambalo lilijaza, hapo aliyaelewa maelezo ya Dumisani aliposema kwamba mtu huyo alikuwa ni komando.
“Ilitakiwa nikuche hai lakini haiwezekani tena kwa sababu umesha ujua utambulisho wangu na hii haitakuwa nzuri kwa upande wangu binafsi”
“Hapana, siwezi kumwambia mtu yey……” hakuna mtu anapaswa kukiamini kiumbe kinaitwa mwanadamu bwana, hawatabiriki hawa. Alipigwa risasi ya kichwa ili afe na siri yake moyoni” Mike alihakikisha anabeba mikanda ya video ili sura yake isije kuonekana kisha akategesha shoti kwenye sehemu hiyo ili kuua kila ushahidi, alijua baada ya muda fulani kupita hiyo sehemu ingeteketea kwa moto kuwakosesha askari kupata mwanya wa kujua kilicho fanyika.


*************
Ilikuwa inasoma saa tisa na nusu usiku kipindi ambacho Mike, mwanaume aliye jitambulisha kama Gavin Luca akiwa anaelekea kukutana na mtu ambaye ndiye alidaiwa alipiga risasi, haikueleweka kwamba hiyo risasi alimpiga nani na kwa sababu zipi bila shaka ilikuwa inamhusu mtu wake wa karibu mno.
Alikuwa anaendesha gari kwa kasi ili aweze kuwahi kuho kwani ilionekana kuwa mhimu kwake kukutana na bwana huyo Master G. Kwenye eneo moja ambalo lilijengwa vyema kwa ghorofa moja ya vioo ndipo address yake ilipokuwa inamuelekeza kuwepo. Kwa juu aliona jina kwa herufi kubwa la ile sehemu huku pembeni yake kukiwa na picha kubwa ya mwanaume na mwanamke wakiwa nusu uchi mwanaume akimchora mwanamke tattoo kwenye sehemu zake za siri.
Haikuwa hiyo tu bali jengo karibia lote lilikuwa na picha nyingi za mvuto ambazo zilikuwa zinavuta ashki ya mapenzi. Nje kulikuwa na walinzi wawili tu mlangoni wakati ndani ulikuwa ukisikika mziki mkali na taa nyekundu na blue ndizo zilikuwa zikiangaza kwenye vioo. Hakuwa na kanzu tena kwenye mwili wake Gavin, alivaa shati ya mikono mifupi ambayo iliinyosha muisuli yake barabara.
Baada ya kushuka kwenye gari alisogea kwenye lango la kuingilia mle ndani lakini alizuiliwa na wale wanaume wawili pale nje ambao nao hawakuwa haba.
“Njoo kesho, hapa kwa sasa pamefungwa”
“Bila shaka mhusika yupo hapa na nina shida ya kuchorwa tattoo muda huu”
“Umeambiwa hakuna huduma muda huu uje kesho” alidakia mwanaume mwingine ambaye alikuwa ni mbavu zaidi. Alisogea na kuhitaji kumsukuma Gavin ila alicho kutana nacho hata mwenzake hakuelewa, alibaki ameduwaa tu baada ya kumuona mwenzake akianza kukakamaa mwenyewe na kudondoka.
Ile kumsukuma Gavin kwa mikono yake aliacha shingo wazi, mwanaume alipachika sindano ndogo kwenye ile shingo ndiyo ambayo ilimfanya akakamae namna ile. Alishtuka akiwa amechelewa kwani wakati anajipanga alipishana na kisu kidogo ambacho kilizama kwenye shingo yake, alibaki ameshikilia shingo damu ikiwa inamtoka kwa wingi wakati huo Gavin hakuhangaika naye tena bali alipitiliza ndani kukutana na mdau wake kwa mara ya kwanza.

Ndani ya jengo hilo kulikuwa na mwanaume mmoja ambaye alikuwa anachorwa tattoo kwenye mguu wake na mwanamke mrembo sana huku mwanamke mmoja akiwa amemkalia kiunoni anaendelea kufanya naye mapenzi. Wote watatu walikuwa wapo uchi kabisa wa nyama bila nguo yoyote. Dunia ni tamu ukiwa na pesa, walikuwa wanajirusha kwa furaha kwa sababu maisha mazuri yalikuwa yapo upande wao.
“Nikiwa na umri mdogo wa miaka nane niliwahi kushuhudia maiti kadhaa zikiwa zimerundikana mtaani, siku ile niliogopa sana kuona maiti hadharani lakini nikiwa sijakaa sawa nikashuhudia mtoto wa miaka kumi akimuua mwanaume aliyekuwa na umri usio pungua miaka thelathini. Mpaka pale nilijiuliza kuna sababu gani ya msingi ambayo inafanya mpaka mtoto mdogo kama yule kuwa muuaji?”
“Baadae niligundua kwamba watu wote huwa wanazaliwa wakiwa wema kabisa ila dunia ndiyo ambayo huwa inawatengeneza baadae kuwa watu wabaya”
“Niligundua hilo siku ambayo hata mimi nilitakiwa kuua kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu. Damu ya mtu ni mbaya sana kwa sababu ukishaiweka kwenye mikono yako basi milele haitaondoka, kila siku itakuwa inataka uendelee kuua tu watu wengine, nasikitika hata mimi najiona kabisa nitaacha kuua siku ambayo nitaingia kaburini. Mimi sikuzaliwa kuwa muuaji Yosef ila watu kama wewe ndio mmenifanya mimi kuwa mkatili namna hii”

Ilikuwa ni sauti ya mshtuko kwa wote ambao walikuwa humo ndani baada ya mziki kuzima ghafla bila matarajio, wakati wote wanashangaa ni nani kazima mziki huo kuwaharibia starehe yao ndipo walisikia maneno hayo kutoka kwa mtu mbaye hawakuwa wakimjua kabisa. Kwenye mkono wake bwana Gavin alikuwa na picha ya sura yake mwenyewe ila kwenye hiyo sura ilikuwa ni tofauti na yake ya sasa kwa sababu ya wakati huo ilikuwa na ndevu chache ila ya sasa ilifunikwa na ndevu nyingi kiasi kwamba alihitajika mtu ambaye anamjua kiundani ili kuweza kumtambua kwamba ni yeye.
“Unalijua jina langu, maana yake umekutana na Raymond. Yuko wapi kijana wangu?” ilikuwa sauti ya mmlaka kutoka kwa mwanaume huyo akiwa anamtoa yule mrembo pale juu ya mapaja yake, hakuna ambaye alionekana kujali uwepo wa Gavin hapo ndani ila Master G mwenyewe.
“Nasikitika kwamba hataweza kuonana na wewe tena”
“You killed him!”
“If you say so”
“Hilo ni moja kati ya makosa ambayo haukutakiwa kuyafanya na bila shaka wewe ni mgeni wa hili jiji hauelewi jinsi linavyo endeshwa”
“Ndiyo maana nipo hapa ili tulimalize hilo Yosef”
“Mpaka umesafiri kuja ndani ya jiji hili, ukaua watu wangu, ukaua walinzi wangu na kisu chako, ukafanikiwa kulijua jina langu; maana yake unanifahamu na kuna kitu unakihitaji kutoka kwangu”
“Kweli nakufahamu ila sikujui, sababu ambayo imenileta hapa ni kukuua Yosef”
“Hahahah hahahaha wewe hapo ndo umekuja kuniua mimi?”
“Ndiyo”
“Hajazaliwa mtu wa kuweza kuniua kwenye haya maisha bado” Gavin alitabasamu kwa hasira huku akimgeuzia picha bwana Yosef
“Oooooh waooooooo, wewe ni nani yake?”
“Kwahiyo ni kweli wewe ndiye ulimuua?”
“Inategemea na anaye uliza, wewe ni nani?”
“Aliteseka sana wakati anakufa?” Gavin aliuliza macho yakiwa mekundu.
“Lazima ateseke, sijawahi kumuua mtu kwa hali ya kawaida kiasi kwamba afe kwa am…….”
“Stop” Gavin aliongea kwa hasira akiwa anakirusha kisu kile ambacho kilikuwa na damu, kilimkosa mwanamke mmoja na kwenda kukita ukutani. Aliwataka warembo hao watoke humo ndani haraka iwezekanavyo. Waliona kabisa hali ya mtu huyo hawakukaa tena, walikimbia huku maungo yao yakiwa yanatikisika kwa nyuma.
“Kijana umeniharibia starehe yangu na hilo ni kosa ambalo siwezi kukusamahe. Huyu mpuuzi nakumbuka nilimuulia Tanzania, ana uhusiano gani na wewe” Gavin alitembea mpaka dirishani akiwa anazibeba hizo kejeli kwa maumivu makali.
“Una mtu anaye kutegemea kwenye maisha yako?” Douglas aliwasha sigara na kuivuta kwa mikwara.
“Malaya wengi wananitegemea mimi ili waishi vizuri na wahuni wa mitaani huko. Wewe ni nani kwa huyo bwana mdogo wa kwenye hiyo picha?”
“Mimi ni kaka yake?”
“Rudia tena umesema?”
“Mimi ni kaka yake na huyu binadamu ambaye hakuwa na hatia, ulimuua kaka yangu na nimekutafuta kwa muda mrefu bila mafanikio Douglas Shenzi”

33 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA NNE
SONGA NAYO................

“Mhhhhh huyo bwana mdogo alizaliwa pekeyake kwao”
“Sio kweli aliyekupa hizi taarifa hakuwa akiujua ukweli. Walikwambia nipo mwenyewe lakini kipindi cha miaka mitano wametumia muda kumtafuta mtu ambaye wewe ulipewa kazi uweze kumuua ndipo wakahisi wamempata juzi hapo ambapo napo waliamini wamemuua lakini mimi bado nipo hai Yosef”
“Whaaaaat”
“Mimi ndiye”
“Gavin Luca?”
“Yes”
“Nooooooooo Gavin Luca nilimuua mwenyewe kwa mkono wangu”
“Ulifanya makosa makubwa kwa sababu ambaye ulimua hakuwa Gavin bali ulimuua pacha wangu”
“Hili haliwezekani” Yosef alibaki ameduwaa akiwa haelewi kile alichokuwa anaambiwa.
“Sisi tulizaliwa wawili mapacha ila dunia ilimtambua mmoja tu ambaye ni kaka yangu. Wakati wewe umetumwa kuja kuniua uliye muua sikuwa mimi alikuwa ni kaka yangu hivyo mimi nimesababisha kaka yangu kufa na wewe hapo ndiye ulipiga risasi Yosef, unategemea nitakufanya nini ikiwa nimekutafuta kwa miaka mingi namna hii?”
“Sikuwahi kujua kama mko wawili, aliye itunza hii siri anastahili pongezi kwa sababu kama ningelijua hilo basi hata wewe ulitakiwa kufa zamani”
“Nahitaji kumjua kiongozi wenu ni nani Yosef, nani ambaye alikupa wewe hiyo kazi ya kumuua kaka yangu?”
“Hahahaha Gavin Gavin, walisema wewe ni beast lakini kaka yako alikuwa mdhaifu mpaka nikabaki najiuliza maswali mengi ila kama leo nimekutana na wewe basi nahitaji kukufahamu kwa hiyo hatari ambayo wengi huwa wanakuimba kwamba unayo”
“Haukutakiwa kukutana na mimi tena kwenye maisha yako yote Yosef kwa sababu unaenda kuwa miongoni mwa wanadamu ambao nitawaua vibaya sana”
“Comon boy” aliita kwa dharau Yosef akiwa anamuonyesha mkono tena akiwa uchi kabisa kwenye mwili wake. Gavin alidunda kwenye kioo alirudi akiwa amelala wima ambapo alimkosa mwanaume huyo baada ya kuruka juu kwa miguu yake Gavin akapita katikati na kutua kwa kushika meza ambayo ilikuwa chini, sehemu ambayo alishika na mkono wake meza hiyo ilibonyea kabisa jambo ambalo hata Yosef lilianza kumshtua, nguvu za kwenye hiyo mikono hazikuwa za kawaida ila hakuwa na wasiwasi.

Yosef alizunguka kwa mikono yake ambapo mkono mmoja ulitua kwenye bega la Gavin akayumba kidogo ila wakati anakaa sawa alikuwa amejizungusha kwa haraka mno kiasi kwamba hata Yosef hakutarajia, alikutana na teke kwenye mishipa yake ya shingo na kama sio kuikaza shingo hiyo huenda ingepinda. Alirudi nyuma akiwa amejipinda kusikilizia maumivu ila aliuma meno yake kwa hasira akaupanga mkono wake.

Alikipiga kiti kidogo na mguu kuelekea alipokuwepo Gavin, kiliishia kwenye mikono yake kikavunjika, wakati huo Yosef alikuwa amerusha mguu wake ambao ulishia kwenye mbao, alipigwa ngumi ya unyao na kutua pembeni ambapo alizunguka na kutua kwa miguu badala ya mgongo. Aliinuka kwa kasi na kumfuata Gavin akiwa ana jaziba, alikuwa anarusha ngumi kama alikuwa vitani ila kwa bahati mbaya ngumi hizo ziliishia kupanguliwa tu, alitishiwa usoni akafumba macho, alihisi utumbo wake unapasuka baada ya kukutana na mgandamizo mkali kwenye tumbo lake.

Alisogezwa nyuma kwa kiganja kisha akapokea vidole kwenye kifua, vidole hivyo vilinyofoa nyama ya kifuani kwake na kama sio kujivuta nyuma kidogo basi vingezama zaidi ndani ya mwili wake na kumletea madhara makubwa. Yosef aliona kabisa mtu ambaye alikuwa mbele yake hakuwa levo yake kabisa hivyo alirukia kwenye kitanda kidogo ambacho alikuwa anakitumia kufanyiwa masaji, alirusha godoro mbali na kuchomoa upanga mmoja mrefu ambao ulikuwa unang’aa sana.
Aliuzungusha upanga huo kwa nguvu akiwa anakuja kwa kuzunguka kuelekea pale ambapo alikuwepo Gavin, wakati anautuma upanga kwa umbali ambao alihisi ungempata Gavin alihisi kama anakutana na hewa, kivuli kilipiga karibu yake akagundua alipishana na bwana huyo ambaye kasi yake hata yeye ilianza kumtisha. Gavin alimzunguka haraka bwana huyo na kunyofoa sikio lake, aliurudisha upanga wake kwa nguvu kule nyuma lakini haikuwa bahati kwake kwa sababu bado alishindana na hewa.

Sikio lake la kulia lilikuwa limenyofolewa, Gavin alikuwa mbele yake anamwangalia bwana huyo alivyokuwa akilaani kuhusu hali hiyo, alitukana tusi huku akiurusha upanga huo kwa nguvu kubwa na yeye mwenyewe akiwa anakuja kwa nyuma damu ikiwa inashuka taratibu kwenye mwili wake ambao haukuwa na nguo hata moja. Ule upanga ulimkosa Gavin kwenye shingo baada ya kuukwepa, kabla haujafika mbali alinyoosha mkono wake wa kulia haraka akaudaka ule upanga kwenye mpini.
Wakati Yosef anafika hakumgusa mwilini bali aligusana moja kwa moja na ule upanga ambao ulizama kwenye bega lake la mkono wa kulia. Yosef waweza kumuita Douglas shenzi aliushika upanga huo kwenye makali kwa maumivu ili usizidi kuiingia zaidi kitu kilicho fanya mkono wake nao kuanza kuvuja damu kwa wingi. Ulivutwa kwa lazima akayumba kidogo, ukazamishwa kwenye paja lake na kuchomolewa, Douglas alikutana na mguu mzito wa uso ambao ulimbeba mpaka kwenye kioo. Alijibamiza hapo mpaka kioo kikaonyesha mpasuko mdogo.
Akiwa kwenye hayo maamivu makali, alitaka kugeuka haraka, ila wakati anafanya hivyo alikutana na sura ya Gavin ikiwa karibu. Alihema kwa hofu moyo wake ukiwa unaenda mbio. Alirusha mkono wake kwa nguvu, kilimkuta kitu kibaya Yosef, kiganja chake kilishuka chini kisha upanga ukasokomezwa kweye jicho lake na kutolewa. Alipiga kelele kumtaka mtu huyo amuache waweze kuzungumza, Gavin alikuwa ni mkatili kama hakuzaliwa na mwanamke.
“Nambie Gavin unataka kujua nini kutoka kwangu?” mwanaume huyo alijieleza akiwa anajivuta nyuma huku Gavin akiwa anamsogelea taratibu. Alimfikia na kukipunguza kidole kimoja kwenye mguu wa kulia wa Yosef, alijikojolea pale pale na hilo lilikuwa rahisi tu kwake kwa sababu hakuwa amevaa nguo ya kuzuia.
“Nani alikupa kazi ya kumuua kaka yangu?”
“Mavamba Davoc, ndilo jina ambalo alijitambulisha kwangu”
“Unamfahamje huyu mtu?”
“Kiukweli nilikutana naye mara moja tu, hili lilikuwa moja ya masharti ya mimi kuweza kupewa uraia Tanzania. Walinipa kazi ya kukuua na kama ningekamilisha uraia na baadae kweli ikawa hivyo ila niliona kule nitachelewa kutengeneza pesa nyingi ndiyo maana nikaamua kukimbia na kuja Afrika ya Kusini kwa makubaliano kwamba wangekuwa wanakuja kuniita pale ambapo kungekuwa na kazi ya mimi kuifanya huko”
“Nampatia wapi?”
“Anakopatikana sikujui ila kuna mtu anaweza kukupa msaada huo”
“Nani”
“Medric Savato”
“Unamaanisha mkuu wa majeshi?”
“Ndiyo”
“Yupoje huyo mtu ambaye alikupa kazi?”
“Ana makovu mengi kwenye mwili wake, ni wazi aliwahi kupitia mengi huko nyuma na anaonekana kabisa kwamba sio mtu wa kuonekana sana”
“Umesema ana makovu mengi kwenye mwili wake”
“Ndiyo ndiyo”
“Hicho ndicho kilifanya ukubali kufanya kazi ya kumuua kaka yangu Yosef?”
“Hapana hapana, nafanya hizi kazi ili niishi Gavin”
“Kaka yangu alistahili kuishi pia, siwezi kukuacha hai kwa sababu hata yeye huko aliko atanishangaa mimi”
“Hapana, tafadhani, naweza kuwa msaada kwako Gav” mwanaume alizamisha upanga kwenye lile jicho lingine nalo likatoboka vibaya. Yosef akiwa anapiga kelele mwanaume huyo aliukata uume wake pamoja na korodani zake zote zikadondoka chini. Yosef waweza kumuita Douglas alipiga mayowe kama mtoto mdogo ambaye amezaliwa siku hiyo, mkono uliokuwa salama ulikuwa mmoja, alikuwa anatamani kujipapasa kila sehemu lakini hakuweza kwa sababu ya maumivu makali. Kile kiganja kingine cha mkono ambao ulikuwa umebaki nacho kilikatwa pamoja na ulimi wake akabaki hana hata uwezo wa kutoa sauti. Gavin alimuacha kwenye hiyo hali ya maumivu ili afe kwa mateso kama malipo ya kumuua kaka yake kipenzi wa damu. Aliacha shilingi lile eneo kabla ya kutoka pale.

Muda mfupi tangu aondoke Gavin kuna watu waliingia humo ndani wakiwa na nguo nyeusi, walionekana kabisa kuwa watanzania ila huenda walifika kwa kuchelewa. Watu hao walionekana kushtuka kwa aina ya kifo ambacho Yesef alikufa, wengi walimjua kama Douglas Shenzi huku Jozi wakimjua kama Master G ikiwa ili kuweza kuficha uhalisia wake mwanaume huyo. mwanaume mmoja aliitoa simu yake na kupiga mahali, iliita kwa muda mfupi na kupokelewa.
“Amewahi kabla yetu, amemuua tayari”
“Ndiyo bosi ni yeye mwenyewe”
“Sawa” Maelezo yalikuwa mafupi, aliwapa ishara wenzake waweze kutoweka ndani ya hilo eneo kwa sababu walichelewa na kuendelea kukaa hapo ingekuwa ni hatari. Walitoka baada ya kubeba baadhi ya nyaraka ambazo zilikuwa kwenye safe ya siri ndani ya jengo hilo la Tattoo.


***********
Tanzania ilikuwa inazidi kuingia kwenye sintofahamu ambayo ilizidi kuwaumiza vichwa vyombo vya usalama. Ni baada ya kupokea taarifa nyingine ya kushtua ya kidogo juu ya kifo cha mwanamama ambaye aliwahi kuwa mwanasheria mkuu pamoja na jaji mkuu wa Tanzania Emilia clark. Zilikuwa ni taarifa za kushtua na lawama zikaongezeka kwa vyombo vya usalama japo kesi hiyo ilikuwa ni ya tofauti kidogo kwani mwanamama huyo alidaiwa kujiua mwenyewe huku sababu ikiwa haijulikani ilikuwa ni ipi.

Ilitoka amri juu kwamba mwili wake usafirishwe mpaka Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi zaidi lakini mwili huo ulipofika Dar es salaam uliwekewa zuio la kutofanyiwa uchunguzi tena amri hiyo ikitoka moja kwa moja Ikulu jambo ambalo lilikuwa la kushangaza. Vijana wa Micho Othman walikuwa wakiutaka mwili huo kwa ajili ya kuufanyia kazi, lawama zilikuwa zinaenda kwao kwa kudai kwamba walikuwa wazembe na kazi iliwashinda lakini ni baadhi ya wakubwa ndio ambao walikuwa wanakwamisha kazi hiyo.
Siku hiyo walikuwa wamekutana na kiongozi wao kumpa taarifa za kila ambacho kilitokea kwa sababu aliwapa hayo majukumu kwa kuwagawa, taarifa wakati zinarudi ndipo waliamka na hiyo taarifa mbaya ya kifo cha jaji mkuu mstaafu Emilia clark. Walikuwa ndani ya chumba cha mikutano lakini ni ukimya ulitawala humo ndani wakiwa wanamsubiri mkurugenzi aanze kuzungumza maana alikuwa amekaa kimya.
“Nina ima….” hakumalizia sentensi yake asubuhi hiyo ya mapema kwenye skrini kubwa ambayo ilikuwa inaonyesha taarifa ya habari pembeni kuna taarifa ambayo ilikuja mbele yao kutoka Afrika ya kusini. Bariki Dumba ndiye ambaye alikuwa ameyatupa macho yake kwenye runinga baada ya kuona kama hoja ina mashiko akampa ishara kiongozi wake aangalie upande huo kisha yeye akanyanyuka na kwenda kuongeza sauti ili wasikie vizuri.

Kwenye taifa la Mandela hususani kwenye jiji la Jozi yalifanyika mauaji ya kutisha ndani ya usiku mmoja kwa watu wawili ambao kwa muda mrefu walikuwa wakisakwa na serikali ya nchi hiyo kwa kujihusisha na biashara haramu. Watu hao wawili walionekana kuuawa na mtu wa aina moja baada ya sehemu zote mbili kukutwa shilingi ya zamani huku mmoja wa wanaume hao kukutwa amekufa kwa risasi na kisha sehemu yake kuchomwa moto. Licha ya watu hao kuwa wahalifu lakini muuaji wa watu hao alitakiwa kupatikana ndiyo maana asubuhi hiyo walizua safari zote za ndege kasoro ndege moja tu ambayo iliondoka mapema kwenda Tanzania na ndege hiyo iliondoka kabla ya kugundua kuna tatizo.

Tigana baada ya kuona taarifa hiyo aliishia kucheka kiasi kwamba wote wakabaki wanamshangaa.

Sijajua bado huyu bwana ni kitu gani kimemfanya awe kwenye hiyo hali. Thelathini nan ne sina la kukuongezea mpaka hapa.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
SONGA NAYO................

“Kuna namna naona inatakiwa tuachane na mawazo ya kumtafuta huyu mtu kwanza bali tujue sababu za msingi ambazo zinamfanya ayafanye haya yote”
“Unahisi ni yeye kafanya haya?”
“Shilingi ndio utambulisho wake inaonekana hivyo ni yeye”
“Ni yeye ambaye alitakiwa kuwa amehusika na mauaji ya jaji mkuu mstaafu, inakuwaje ndani ya usiku mmoja yeye mwenyewe awe afrika ya kusini?”
“Kuhusu jaji mkuu nina uhakika sio yeye”
“Umelijuaje hilo Tigana?”
“Kwa sababu tangu nianze kuona mauaji yake, hakuna sehemu anaruhusu mtu wake ajiue mwenyewe hivyo huyo mama ameuawa na watu wake mwenyewe” kila mtu alimpa umakini Tigana kujua anacho kimaanisha kwa sababu alikuwa na hisia kali mno.
“Unataka kusemaje?”
“Kama ameenda Afrika ya kusini maana yake alihitaji kumjua mtu fulani ambaye huenda angemuongoza mpaka kwa Emilia. Kuna uwezekano mkubwa Emilia anawajua watu kadhaa ambao Gavin anawatafuta hivyo ingekuwa hatari kwao na kuimaliza hatari hiyo wakaamua kumuua ili akirudi amkose”
“Una uhakika na hili?”
“Hisia zangu zinanituma hivyo, kuna mnyororo wa watu wengi wakubwa wanaonekana wanatafutwa na huyu bwana”
“Kwahiyo unashauri nini Tigana?”
“Kwa hili ambalo limetokea maana yake kwa sasa atakuwa kwenye ndege ambayo inatua muda sio mrefu JNIA hivyo tunatakiwa kusimamisha kila kitu tukajaribu bahati yetu kama tunaweza kumpata. Kama tukifanikiwa kumkamata basi huenda haya yatafika mwisho na tutajua sababu ya yeye kuwa hivi kwa wakati huu”
“Are you sure?”
“Hisia zangu zinaniambia hivyo kiongozi” Walikuwa wanamwamini sana Tigana hivyo walipewa amri ya kuwahi mara moja uwanja wa ndege kumkamata Gavin ambaye waliamini wakati huo alikuwa kwenye ndege kurudi Tanzania baada ya kufanya mauaji hayo ya kutisha huko Afrika ya kusini. Je ni kweli alikuwa kwenye ndege na walikuwa wanaweza kumpata Gavin?





**********
SOUTH AFRIcAN AIRWAYS.
Ndiyo ndege ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu na majasusi kutoka ndani ya shirika la kijasusi la TIGI la Tanzania, ndege hiyo ilikuwa imeondoka masaa mawili yaliyokuwa yamepita ndani ya jiji la Jozi wakati wao wanapata taarifa juu ya mauaji ambayo yalifanya ndani ya jiji hilo. Baada ya kuipata taarifa hiyo walighairi kila kitu na kuamua kufanya zoezi la kubahatisha kwenda kumkamata Gavin kwa sababu walijua ni lazima alisafiri na ndege hiyo.

Wanaume hao watano walikuwa wamejipanga kwenye maeneo tofauti wakijifanya wapo hapo kwa ajili ya kupokea wageni wao huku wengine wakiwa wanajifanya kama walinzi wa eneo hilo kuhakikisha kila ambaye anapita hapo wanamuona na kama wangemuona mtu wao basi hawakutakiwa kupoteza muda zaidi ya kuondoka naye japo walijua zoezi hilo halikuwa rahisi kama ambavyo lilikuwa limeandikwa kwenye makaratasi ndiyo maana walibebwa wote watano ili kukiwa na ulazima wa kutumia nguvu za zaida isije kula kwao mtu mwenyewe alikuwa anaishi kama mzimu.

Zilikuwa ni dakika kumi na tano zimebakia ili ndege hiyo ambayo ilikuwa inatumia masaa yasiyo pungua matatu kutoka Jozi kufika Dar es salaam ili iweze kutua, muda huo hao wanaume walikuwa ndani ya uwanja huo wa ndege mkubwa tayari wakiwa makini kwa kila kitu kilichokuwa kinaendelea ndani ya hilo eneo bila kuwashtua watu au kuleta mtafaruko ama tafurani ya aina yoyote ile kwenye hilo eneo.
Hatimaye ndege ilitua na baada ya muda watu walianza kupita wakipishana huku na huko, wenyeji walikuwa wanashangilia wageni wao kufika huku wakiwapokea kwa bashasha na furaha ila wao walikuwa makini kupiga kila hatua kuhakikisha mtu wao haondoki ndani ya hilo eneo bila kupatikana. Watu walizidi kuwa wengi ila muda ulivyokuwa unazidi kwenda ndivyo walikuwa wakizidi kupungua taratibu mpaka walipo isha wote wakabaki wachache ambao walienda migahawani kupata chakula na wapendwa wao. Jambo la kushangaza ni kwamba mpaka abiria wanaisha hapo hawakumuona mtu wao huku kila mtu akiwa na picha yake mkononi.

“Nini kimetokea hapa?” Aliongea Tigana akiwa anaangaza kila upande baada ya kukutana na wenzake.
“Huenda hajasafiri” aliongea Jaden Mrisho
“Hapana, alijua kabisa kwamba kungekuwa na tatizo kama hili lazima kungekuwa na kizuizi kwenye viwanja vya ndege na washukiwa wa kwanza wangekuwa wageni maana yake hata yeye angekuwa hatarini kuweza kugundulika hivyo lazima amekuja na hii ndege ya mapema baada tu ya kufanya mauaji” Alieleza crispin Mkono.

“Kwa maana hiyo ni lazima alifika na kuchukua chumba karibu kabisa na uwanja wa ndege ili awahi kuondoka. Sina imani kama huyu bwana ni binadamu kama sisi” Sylvanos aliongea akiwa anasikitika.
“Hapana, ni mahesabu tu watu wa hivi wapo duniani ila ni wachache ndiyo maana wakifanya vitu huwa vinaonekana kuwa vya ajabu na wengine wakiamini kwamba haviwezekani. Swali la msingi ni kwamba kama alikuwepo hapa kapitaje? Na kama kapita tupo hapa maana yake yeye anatufahamu vizuri tu” Bariki baada ya kuongea hivyo ni kama kuna kitu kilipiga kwenye kichwa chake, alihisi kwamba aligongana na abiria mmoja wakati anageuka kumuangalia mtu huyo alitabasamu na kuweka mkono wake mmoja kifuani kama ishara ya heshima ila hakuelewa kama alikuwa ni yeye au siyo.

Alikimbia mpaka nje lakini hakuna ambacho alikiona wenzake wakiwa wanamshangaa bwana huyo
“Nahisi nimepishana naye” Aliongea Bariki
“Umejuaje?”
“Twendeni kwenye chumba cha kamera haraka” walikuwa na kibali cha mkurugenzi hivyo kwao kila kitu kilikuwa rahisi tu, waliingia ndani ya chumba hicho na kuanza kurudisha matukio yote nyuma ili waone kama mtu huyo alifanikiwa kutoka nje na alitokaje. Bariki alibaki anacheka kwa alicho kiona huku akiwa anatikisa kichwa
Kwenye ile video ya kwenye kamera, alipishana na shekhe mmoja ambye alikuwa amevaa kwa heshima mno, ndevu zilitengenezwa vizuri lakini ziliwekwa za kizee kidogo hivyo shekhe huyo alikuwa anaonekana kama mzee kiasi. Kwenye mkono wake mmoja alikuwa na fimbo ya kutembelea huku mkono mwingine ukiwa na begi jeusi la mkononi. Kichwani alikuwa na balakashea na miwani, alionekana kuwa mtu safi.
Huyo ndiye ambaye yeye Bariki aligongana naye na mtu huyo akaonyesha ishara ya kuomba msamaha huku akitabasamu kisha akaenda zake lakini kwenye mkono wake alikuwa na kitu kama kadi, haikuwa kadi bali kilikuwa kitambulisho cha Bariki. Baada ya kupishana pale yule bwana alitokomea zake kwenye gari ambayo haikuwa na namba hata moja ya usajili na bila shaka kuna mtu ambaye alikuwa kwenye ile gari akimsubiri kwani yeye baada ya kuingia kwenye ile gari hakukaa mbele bali nyuma hivyo kuna mtu ambaye alikuwa anamuendesha. Bariki alitabasamu ila moyoni alikuwa na hasira sana.

Tigana Mdachi alisogea kwenye skrini hiyo na kuirudisha nyuma ile video wakati mtu yule akipishana na Bariki, alitaka kuona ni kwa namna gani mtu huyo alifanikiwa kumuibia kitambulisho mwanaume huyo wa kazi bila hata yeye mwenyewe kushtuka! Alicho kiona yeye kilimtisha, vidole viwili ndivyo vilifanya ile kazi, kasi ambayo ilitumika kukibeba kile kitambulisho ilimfanya kuhisi hilo tukio lilihusiana na njia za giza.
“Binadamu gani ana uwezo wa kuwa na kasi ya namna hii?” alikuwa anaongea huku akiwa anairudia mara mbili mbili.

“Dunia inatuhakikishia kwamba bado tuna mengi ya kujifunza Tigana, kuna watu ukikutana nao unaweza kuona ni heri hata ukafa tu dunia uwaachie wenyewe. Watu wanaofanya haya matukio usiombe ukutane naye kwenye mazingira mabaya halafu ukawa mwenyewe, anakuua na hakuna mtu atakuja kujua kwamba uliwahi kuishi. Kama ameweza kumuibia Bariki bila hata yeye kujua kwa muda mfupi namna ile maana yake uwezo wake huyu umevuka kwenye ile hali ya ubinadamu, hii ni hatari kwa mwanadamu wa kawaida kuwa na nguvu za namna hii, anatakiwa kuzuiliwa mapema kabla hajawa hatari zaidi kwa watu wengine” Jaden Mrisho aliongea huku akiwa anaangalia dirishani kuona namna dunia ilivyokuwa inaenda kasi.
“Kwa hapa tulipo fikia tunamhitaji Princess sana na bosi anatakiwa kulijua hili”
“Ni ngumu kumrudisha kazini, amesimamishwa kazi kwa miaka miwili”
“Nina uhakika akiwa kiongozi wetu tulifanya makubwa sana ni wakati wetu wa kumpigania aweze kurudi kazini, ni mwanamke ndiyo lakini uwezo wake hapa sisi wote hatuna kwenye upande wa akili na sasa nguvu hazina msaada mkubwa zaidi ya akili ndizo ambazo zinahitajika zaidi”

“Upo sahihi Tigana, nadhani hilo linatakiwa kufika ofisini mara moja wakati huu”
“Lakini binafsi kuna jambo limenishangaza, kama amebeba kitambulisho maana yake ni kwamba hatujui ila ametuhisi ndiyo maana amekibeba ili akapate uhakika” Bariki aliongea jambo hili akiwa anamaanisha kabisa
“So, una shauri nini?”
“Kwa sasa turudi ofisini, tukae na kuandaa huu mpango upya kwa kuunganisha matukio yote ambayo tumeyapata huko tulikokuwa kufanya kazi hii halafu Malkia wetu arudishwe tuingie kazini mpaka huyu mtu apatikane na naahidi kwamba nitamtia mkononi na siku ambayo nitakutana naye nina imani atajuta” Bariki aliongea jambo la maana na kujisifia
“Bariki chunga ulimi wako ndugu yangu” Bariki hakumjibu Mrisho zaidi ya kuondoka hilo eneo kwani hawakuwa na jambo lingine la kufanya baada ya kumkosa mtu wao aliyekuwa amewapelekea hapo.
Sehemu ya thelathini na tano inafika tamati hapa.

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom