Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 84
"Kuwa mpole kwa sababu kama ukicheza vibaya hata mwanao utamkosa, wadondoshe watoto waliopo mbele yako hapo kisha unifikie mimi nione unavyotaka kuzilipiza hizo hasira zako. Usije ukafanya kosa kubwa sana la kutumia risasi nitamuua mwanao hivyo tupa hiyo bastola yako na mikono yako ifanye kazi, najua unaelewa kwamba unaweza ukanipiga risasi hata tano kwenye mwili wangu na bado nikawa hai lakini mwanao nikirusha kisu hiki kikatua kwake au kuchomoa risasi na kuirusha kwenye mwili wake basi anakufa hapo hapo. Fanya maamuzi yako kwa akili sana usitumie mihemko Donny" maneno ya kejeli kutoka kwa Ted yalimfanya mwanaume kupiga kelele kwa nguvu sana huku akiitupa bastola hiyo angani.
"Close your eyes Nai" ndiyo kauli ambayo alimtamkia binti yake huku akiwa anafumba macho, na wakati anayafumbua macho yalikuwa yanaonyesha kama yanawaka moto kwa hasira kali ambazo alikuwa nazo. Alikirusha kisu kwa nguvu ya ajabu sana huku akilitoa shoka lake begani, Kisu kilimkosa Herman kwenye moyo na kumkita kwenye mkono wake wa kushoto. Alizubaa kuweza kusikilizia maumivu makali ambayo yalimpata alishangaa shoka linakuja upande wake lakini alifanikiwa kulikwepa huku Kennedy akiwa anauchomoa upanga wake kiunoni.
Herman mkono wake mmoja haukuwa ukifanya kazi sawa sawa hivyo aliitegemea zaidi miguu, aliruka sarakasi kwa kusimama kuelekea mahali ambapo alikuwepo Max, mateke hayo yalitua sehemu ya kifua cha mwanaume huyo ambapo Herman alihisi kama anapiga ni mchanga maana alidunda tu na wakati anataka kurudi chini, alipigwa ngumi moja kwenye kisigino ambapo alitua chini vibaya sana, alipigwa buti la kichwa ambalo lilimburuza kuelekea pale alipokuwa amekaa Ted huku shoka likifuatia kwa kasi sana ambapo lilienda kutua tumboni ambapo lilipasua tumbo vibaya sana. Kijana huyo aliishia kwenye miguu ya Tedy akiwa anatoa damu kwenye mdomo wake na kuhema kwa shida sana, Ted alikizamisha kisu kwenye moyo wa kijana huyo maana hakuwa na kazi tena mahali hapo.
Kenedy alikuwa anauzungusha upanga wake kwa nguvu sana sambamba na shoka ambalo lilikuwa linaelekea kwenye bega la Max ambalo lingepasuliwa vibaya sana kama shoka hilo lingefanikiwa kutua kwenye bega hilo. Mwanaume alifanikiwa kuudaka mkono wa Kenedy ambao ulirusha shoka hilo hivyo akafanikiwa kulikwepa lakini kwa bahati mbaya ule mkono mwingine ambao ulikuwa na upanga, Kenedy aliutumia vyema baada ya kuuzamisha upanga huo kwenye tumbo la mwanaume huyo.
Max aliuma meno sana kwa maumivu makali ambayo alikuwa ameyapata, alimvutia Kenedy kwake hali ambayo ilipelekea upanga huo kuzama ndani zaidi lakini alikuwa anatafuta namna nzuri ya kumfikia kijana huyo ambapo alirusha ngumi nzito sana mbayo ilizama kwenye koromeo la Kenedy, ngumi iliyompa maumivu makali sana kiasi kwamba alidondosha shoka lake chini hata upanga hakuwa na uwezo wa kuuchomoa kutoka kwenye tumbo la Max tena.
Kenedy alirudi nyuma kwa namna ngumi hiyo ilivyokuwa kali sana ila hakupewa hiyo nafasi ya kuyasikilizia hayo maumivu yake kwani alipigwa mtama mkali sana ambao ulikuwa unampeleka chini ila kabla hajatua Max alimfunika na buti moja baya sana la kiuno ambalo lilifanya muitikio wa mifupa usikike kwa nguvu sana ikiwa inavunjika. Hicho kiuno hakikuwa na kazi tena, Kenedy alipiga makelele ya maumivu makali na kwenda kudondokea mbali na pale. Max aliuchomoa upanga kwenye tumbo lake kwa kasi sana na kuurussha kwa nguvu kuelekea pale alipokuwepo Kenedy.
Upanga ule ulikuwa unaelekea kwenye moyo wa Kennedy lakini aliutumia mkono wake kuuzuia, mkono ulichanika vibaya sana katikati na upanga huo ukapenya kidogo mpaka kutoboa kifua huku akiwa anahangaika kuuchomoa bila msaada wowote ule. Wakati anahangaika nao mwanaume alikuwa analiburuza shoka la Kenedy kuelekea pale alipokuwepo, Kenedy aligeuzia macho yake kwa Ted akiwa anaomba msaada kwa ishara maana hata sauti haikuwa ikitoka lakini alikutana na shoka la sehemu za siri ambalo lilimfanya alie kwa uchungu sana.
Akiwa kwenye dakika zake za mwisho mwanaume alimtaka ashuhudie kila ambacho kinatokea kwa kiongozi wake Ted hivyo alimuacha hivyo hivyo akiwa amezipasua sehemu zake za siri na mwili wake ulikuwa kwenye hali mbaya sana na aliamini angeweza kukaa kwa dakika kadhaa kabla ya kupoteza maisha maana alikuwa anatoa damu nyingi sana. Tedy alikuwa amebakia mwenyewe kama alivyokuwa anataka yeye lakini wakati huo alikuwa anamsogelea mtota wa max kwa kasi sana ila alikutana na kitu ambacho kilimfanya aruke sarakasi ya kasi na kudunda kwenye kiti alichokuwa ameketi mara ya kwanza na kutua upande wa pili.
Akiwa anakaribia sehemu ambayo alikuwepo Naima akiwa na kisu chake mkononi, alipishana na shoka ambalo lilikuwa linaukata mkono wake na kumfanya kuwa kilema kama angefanya kosa la kufanya maamuzi ya mapema, likiwa limerushwa na Max mwenyewe. Mtu huyo asingemuua mwanae yeye akiwa bado hai.
"Unatakiwa kuniua kwanza mimi na kama ukifanikiwa basi unaweza kumgusa mwanangu, hakuna binadamu amezaliwa kwenye dunia hii akaweza kuiua damu yangu mimi nikiwa hai. Kosa la maisha ambalo umelifanya ni kumuua mke wangu, nilikuwa naweza kukusamehe kwa yote ambayo umeyafanya ila kwa hili hakuahidi utajutia maisha yako yote hata huko unakokwenda utakiri kwamba haukuwahi kukutana na ukatili ambao naenda kukufanyia kwa hizi dakika chache ambazo utakuwa unaweza kuendelea kusimama kwa miguu yako miwili" Max aliongea akiwa anatokwa na damu mdomoni na tumboni maana alijeruhiwa vibaya sana.
"Hahaha hahaha hahaha nilitaka iwe hivyo, nilitaka kupigana na wewe ukiwa kwenye hasira kali sana namna hiyo kwa sababu nilijua nitalipata pambano bora sana na ndicho kinaenda kutokea saivi. Nadhani bado haujanifahamu vyema namna mimi nilivyo, bado haujajua kwamba ni kwanini naogopwa sana, nionyeshe huo uwezo wako ulio nao" mwanaume huyo alijigamba sana wakati huo Max alikuwa anaitoa shilingi yake mfukoni.
"Ted, ulipaswa kukimbia kabla mimi sijafika hapa. Nazijua sifa zako nyingi sana hata Bilali aliwahi kukiri hilo lakini mimi sio hao ambao uliwahi kukutana nao, mimi nilibadilika na kuwa kiumbe cha kutisha sana tangu siku ambayo nilizikwa na kuja kufufuka. Ulitakiwa kujikumbusha na kujiuliza kwamba nilikuwa nafanya nini miaka yote kumi na mbili niliyopotea na sio kuanza kujisifia muda huu. Una dakika nne za kuyaponyesha maisha yako, nakuahidi kama ukifanikiwa kuzimaliza dakika hizo hata mimi nitakuwa nimeanza kuishiwa nguvu kwa sababu nazidi kupoteza damu taratibu basi utafanikiwa kuniua kirahisi sana hata mwanangu unaweza kumuua kama unavyo hitaji ila kama ukishindwa kuzitumia vizuri hizi dakika nne basi utajuta maisha yako yote hata wakati ambao utakuwa kaburini" Mwanaume aliongea kwa sauti kali na kavu sana akiwa anaizungusha shilingi hiyo kwa nguvu sana na kuiachia ikitua chini na kuanza kuzunguka kwa kasi mno.
Wakati mambo yote hayo yanendelea mwanasayansi ambaye ndiye alikuwa anasimamia shughuli zote humo ndani alikuwa anashuhudia kila kilichokuwa kinaendelea hali ambayo ilipelekea kwenda kumfungulia mwandishi wa vitabu Dawson Nduka na kumpa taarifa mpya ya tumaini la kuweza kuishi kwa mara ya pili. Wazee hao walikuwa wamejibanza sehemu wakiwa wanamuomba Mungu kumsaidia mkombozi ambaye alikuwa ametumwa kufika sehemu hiyo.
Ted alisogea kwa kasi ambayo hata Max alishindwa kuelewa kwamba mwanaume huyo alifikaje fikaje hapo, alipigwa ngumi ya shavu mpaka akahisi mdomo umepinda, buti kali sana lilifuatia kwenye kifua chake ambalo lilimbeba na kumbamiza ukutani. Alisimama akiwa na maumivu makali mno ila mwanaume huyo alikuwa amemfikia alipokuwa ambapo aliinama kidogo na kumkutanisha Max na kisigizo chake kwenye paji la uso hali ambayo ilimfanya ayumbe yumbe sana.
Ted alikuwa amerusha mkono wake kwa nguvu sana ila max aliuona hivyo alifanikiwa kuzamisha ngumi nzito sana kwenye bega la Ted ambalo lilimfanya ayumbe na kurudi nyuma ila hata hivyo hakurudi kizembe mkono wake ulitua kwenye bega la Max na kumfanya naye apige goti maana bega hilo lilikuwa limeteguliwa vibaya sana. Mwanaume akiwa chini anahitaji kunyanyima Ted alijigeuza kwa sarakasi kali sana ambapo teke moja lilimkosa Max na kupasua chini kwenye sakafu hata hivyo teke lingine lilizama kwenye tumbo lake sehemu ambayo ilikuwa na jeraha la kukatwa na upanga.
Alidondokea mbali sana kiasi kwamba alichana chana nguo zake baada ya kulinyoosha bega lake na kubakia akiwa kifua wazi huku kwenye kiuno chake kukiwa na kisu kimoja kikali sana kilihifadhiwa hapo lakini nyuma ya kiuno alikuwa ameihifadhi bastola moja. Mwili ambao ulikuwa umeiva haswa ulikuwa unaonekana kwa mwanaume huyo, aliuma meno yake na kusimama kwa hasira sana. Alimsogelea Ted kwa double kick moja ya nguvu ambayo mwanaume huyo aliiona na kufanikiwa kuipangua na kurusha ngumi yake nzito ambayo Max naye aliiona na kuikwepa kisha aliirudisha yake ambayo ilitua kwenye paji la uso la Ted na kumfanya arudi nyuma kidogo.
Max aliiangalia shilingi ilikuwa imeanza kubendi kuonyesha muda ulikuwa unaelekea kuisha. Mwanaume aliinama na kuichana tshirt ambayo alikuwa ameivaa kwa mara ya kwanza kisha akajifunga kwenye tumbo sehemu ambayo ilikuwa inamwaga damu nyingi. Na baada ya hapo alisimama tena akiwa anajinyoosha, hilo pambano ndo kwanza lilikuwa linaanza huku akiwa amebakisha dakika mbili na sekunde kumi na tano tu kulikamilisha pambano hilo.
Ted alichomoa kisu chake baada ya kuona kwamba pambano hilo halikuwa la kushinda kirahisi kama nafsi yake ilivyokuwa inamwambia tangu mwanzo. Hata Max alikichomoa kisu chake ila wakati analikamilisha hilo mwanaume mwenzake alikuwa amemfikia pale ambapo alikuwepo, alikwepa mguu ambao ungemvunja vibaya sana na kusogea nyuma akiwa anaikaza mikoyo yake. Ngumi kumi zilirushwa zikiwa zinachanganywa na kisu kikali sana ambacho kilikuwa kwenye mkono wa Ted.
Alifanikiwa kuzikwepa ngumi zote lakini kwa bahati mbaya sana kisu kilipitishwa kwenye mbavu yake ya kulia na kumuongezea jeraha lingine ambapo alishindiliwa na ngumi nyingine ya tumbo ila wakati anarudi nyuma kwa maumivu alijigeuza kwa sarakasi ya mbele na kutua buti lake kwenye mdomo wa Ted ambao ulichanika vibaya sana na kumfanya mwanaume huyo kurudi nyuma mpaka kufikia hatua ya kukaa chini huku Max akikosa balansi na kudondoka chini. Alijitahidi kunyanyuka kwa mkono mmoja akiwa na maumivu sana, zilikuwa zimebaki sekunde kumi na tano dakika nne ziweze kutimia huku Ted naye akiwa anatikisa kichwa chake maana alihisi kinawaka moto muda mfupi alipigwa ngumi nzito sana sehemu ya paji la uso lakini muda mchache sana baadae akapigwa na buti la mdomo ambalo liliuchana chana mdomo wake vibaya sana.
Muda huo mwanasayansi na mwanasheria walimfungua Nai ambaye bado alikuwa amefumba macho yake, alikuwa akimsikiliza baba yake kuliko kitu chochote kile na wazee hao wakasogea mlangoni ili kama likitokea tatizo lolote waweze kukimbia na mtoto huyo mdogo. Ted alipiga kelele za maumivu kwa sauti kali sana akiwa anakimbia mwili wake ameukaza kuelekea pale alipokuwepo Max, mwanaume alifumba macho yake kwa hisia kali sana kumsubiria mwenzake huyo kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa nafasi ya mwisho kabisa kama angecheza vibaya alikuwa anayapoteza maisha yake na kama angecheza vyema basi alikuwa anaishinda mechi hiyo.

84 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 85
Aliyafumbua macho yake ghafla sana wakati ambao Ted alikuwa amefika hapo alipokuwepo akitoka juu ambako aliruka kwa nguvu sana, alikuwa amerusha ngumi na kisu chake ambapo Max alifanikiwa kukikwepa kisu lakini ngumi ilizama sehemu ya juu ya jicho ambapo ilipasua eneo hilo lakini hata yeye alifanikiwa kuzamisha ngumi yake moja eneo la moyo la Ted ambaye alihema kwa ngumu sana na kisha kila mtu alizamisha kisu kwenye mwili wa mwenzake kwa nguvu sana ambapo walianchiana kwa ngumi kali sana ambapo kila mtu alimpiga mwenzake ngumi nzito sana ya tumbo zikafanikiwa kuwarusha mbali sana.
Shilingi ilitulia kabisa chini kumaanisha kwamba muda ulikuwa umeisha wote wakiwa wanahema kwa taabu sana wakiwa wanaangaliana kwa macho yenye chuki vibaya mno. Wote walikuwa kwenye hali mbaya sana, Max aliangalia sehemu ambapo kisu kilikuwa kimekita, kilikuwa kimezawa karibu kabisa na shingoni na kuchimba vibaya sana eneo la bega lake. Alihema sana maana alikuwa anapata maumivu makali isivyokuwa kawaida.
Ted alijiangalia naye kujua ni sehemu gani ambayo kisu hicho kilizama, aliishia kutukana kwa hasira sana
"https://jamii.app/JFUserGuide" kisu kilikuwa kimezama sehemu mbaya sana, kwenye moyo wake kumaanisha kwamba ni muda mchache sana kuanzia dakika hiyo alikuwa anakufa. Alicheka sana Ted kwa uchungu mkubwa sana, hakuwahi kufikiria kabisa kwamba anaweza kufa kijinga sana namna hiyo. Max alinyanyuka kwa taabu sana kuelekea pale alipokuwepo Kenedy akiwa anahema kwa taabu sana, aliwaangalia wazee wale wawili ambao walikuwa na mwanae, walielewa somo wakamfumba Naima masikio, mwanaume aliachia risasi kwenda kwenye kichwa cha Kenedy kisha akalisogelea shoka lake na kulichomoa kwenye tumbo la Harman akawa anaelekea pale alipokuwa amelala Ted akiwa anatembea kwa shida sana.
"Kwanini umemuua mke wangu?" mwanaume aliongea akiwa anamwangalia Tedy kwa hasira sana, mwanaume huyo hakujibu lolote lile bali aliishia kucheka tu akiwa anatokwa na damu nyingi sana. max alishuka shoka lake kuelekea kwenye mguu wa mwanaume huyo ambao ulikatwa bila huruma na kumfanya kuanza kugugumia kwa maumivu makali sana.
Akiwa hajakaa sawa Tedy alipigwa risasi kwenye kidonda hali ambayo ilimfanya kutoa sauti kama mtoto mdogo.
"Nakuuliza haunijibu sio? ulifanya kosa kumuua mke wangu, haukutakiwa kuigusa familia yangu, umenifanya niuvuke ubinadamu wa kawaida kwenye maisha yangu" alitamka akiwa anashusha machozi Max na kuchomoa kisu begani ambacho alikizamisha kwenye jicho moja la Ted akianza kucheka kwa hasira sana
"Bado huwezi kunijibu? unajisifia kwamba wewe ndiye bonge la bwana si ndiyo, unaamini kwamba Denis kijazo anaenda kukuokoa sio? Yule atakufa kama wewe unavyokufa leo" aliongea tena kwa hasira akinyanyua shoka lake na kuikata sehemu ya paja ya Ted akiwa anacheka kwa nguvu sana Max mithili ya mtu ambaye alikuwa amechanganyikiwa.
"Mtazame mke wangu amelala pale na hataamka kwa ajili yako, unahisi naweza kukusamehe kwenye hili? naweza kukusamehe tu kama ukiweza kunirudishia mke wangu" mwanaume alikuwa anaongea kwa uchungu sana akiwa anaushuhudia mwili wa mke wake pale chini huku chozi likimshuka. Alipandwa na hasira kali sana na kulishusha shoka lake kiunoni na kuukata vibaya sana upande wa kulia wa kiuno cha Ted kama anapasua kuni vile.
"Naomba niue ndugu yangu tafadhali, nakuomba sana" maumivu makali sana yalizidi hivyo Ted aliomba mwanaume huyo aweze kumuua lakini Max aliishia kucheka tu.
"Baada ya kumuua mke wangu, baada ya kumuua Bilali na baada ya kumuua James, saivi unataka nikuue kirahisi sana namna hii? yaani ufe haraka haraka bila kuteseka kama ninavyotaka mimi? hahaha hahaha haha hapanaaaaaaaaaaaa" aliongea kwa ukali mno akiwa analikata sikio la mwanaume huyo ambaye alicha ya kuwa mwanaume ambaye alikuwa anatisha na kuogopwa sana aliishia kulia kwa uchungu mkubwa sana. Ilikuwa ni rahisi sana kuweza kuwafanyia wanadamu wengine ila kwa upande wake ilikuwa ni mbaya sana.
Ted alijutia kukutana na binadamu kama huyo kweenye hatua za mwisho kabisa za maisha yake, alikatwa katwa kwenye mikono yake na kumfanya kuwa kilema kisha mwanaume huyo alimtoboa toboa kwenye jicho lake ambalo lilikuwa limebakia vibaya sana na kumsogelea mkewe pale ulipokuwa umelala mwili wake Tedy akibaki anagala gala pale chini na kuruka ruka bila kwenda popote maana hakuwa na dalili za kuwa mzima, mikono, macho yalitobolewa alikuwa kipofu mpaka wakati huo lakini hata kiuno kilikatwa vibaya sana.
"Na" alimuita mwanae kwa nguvu sana akiwa ameukumbatia mwili wa mkewe, kwa mara ya kwanza tangu amwambie binti yake alifumbua macho yake akiwa anamwona baba yake akiwa kwenye damu nyingi sana. Alimkimbilia baba yake akiwa anatoa machozi na kwenda kumkumbatia kwa nguvu sana na kuukumbatia mwili wa mama yake mzazi ambaye alikuwa amekufa. Ilikuwa ni hali ya simanzi sana kiasi kwamba hata wale wazee walishindwa kujizuia wakakuta wanaanza kutoa machozi huku wakikumbatiana kwani kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu sana walikuwa wanaenda kuliona jua nje.
Wakiwa hapo waliingia wanaume ambao walikuwa wamevaa suti zao za bei sana, wanaume hao baada ya kufika humo ndani walionyesha ishara ya heshima kwa Max kuonyesha kwamba walikuwa wanamheshimu sana huku wazee hao wakiwa wanamshangaa sana.
"Mkurugenzi anakuhitaji Ikulu kiongozi" ni mwanaume mmoja ambaye alitamka kauli hiyo mbele ya Max akiwa anainama kutoa heshima.
"Hakikisha mwanangu anafika salama, na hao wazee tunaondoka nao lakini hii sehemu hakikisha unailipua na kila kilichopo humu ndani" mwanaume alitamka kwa msisitizo sana na kudondokea kwenye sakafu kisha akapoteza fahamu kabisa maana hali yake ilikuwa ngumu sana akiwa ametekeleza kile ambacho kilimpeleka ndani ya jiji la Arusha.







IKULU

Mkurugenzi Chuki Steward mida ya usiku wa mapema alijongea mpaka sehemu ambayo alikuwa amemhifadhi aliyekuwa raisi Justin Mtadei. Mwanaume huyo alikuwa amefungwa kwenye chumba kimoja kidogo cha adhabu ndani ya Ikulu humo akiwa anatokwa na jasho sana maana chumba hicho kilikuwa kidogo mno na hakikuwashwa feni hali ambayo ilikifanya kiwe na joto kali sana.
Mheshimiwa huyo aliingia huko akiwa na vijana wake, baada ya kuingia taa kubwa iliwashwa na feni iliwashwa hali ambayo ilimshtua hata Justin Mtadei mwenyewe maana hali kidogo ilianza kuwa angalau na baada ya kuyainua macho yake alimuona mwanamke huyo ambaye mpaka wakati huo alianza kumuogopa sana.
"Ukiwa DCI ulikuwa moja kati wa watu bora sana kwenye taifa hili, sifa zako zilikuwa zinaimbwa kila sehemu. Watu wengi walitamani kuwa kama wewe, huenda haukuwa unaambiwa ila mtaani ulikuwa una mashabiki wengi sana hata siku ambayo unateuliwa kuwa waziri mkuu watu walishangilia sana wakiamini raisi amepata mtu sahihi sana karibu yake ambaye angehakikisha kila kitu kinakwenda sawa. Ila kwa bahati mbaya sana baada ya kuingia kwenye ile nafasi ukaja kuingia kwenye kundi la wale wengi ambao huwa wanabadilika kulingana na mazingira ya kisiasa, kundi la wale ambao pesa inakuwa mhimu kwao zaidi ya maisha ya mtu na hatimae ukalisaliti taifa lako mwenyewe"
"Hivi kwa mfano kama ingekuwa familia yako ndiyo imefanyiwa yale ambayo mliwafanyia wengine ungekuwa unajisikiaje labda ukiwa kama baba watu wenye mabavu wanapo ichukua furaha yako kwa lazima? inanisikitisha sana lakini nakuahidi familia yako itaachwa hai kwa sababu hakuna kibaya ambacho wanahusika nacho baada ya kuwachunguza kwa muda hivyo wao walikuwa wanakufuta wewe kama baba"
"Unataka nini Chuki?"
"Nimekuja kukuaga kwa sababu mimi na wewe hatutaonana tena, leo ndiyo siku ya mwisho mimi kuongea na wewe. Jambo moja ambalo nakuonea huruma ni kwamba kuanzia leo usiku huenda dunia nzima ikajua yale yote ambayo umeyafanya kwenye maisha yako, nawaza familia yako itaishi maisha gani baada ya hapo, nawaza watakubali vipi kuangaliana na walimwengu wapenda maanguko ya wenzao? haya yote umeyaleta wewe huku ukifa na kuiacha aibu kubwa sana kwenye maisha yako" mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa anamzunguka mheshimiwa huyo ambaye alikuwa ameyatoa macho kama vile aliambiwa kwamba angekatwa sehemu zake za siri.
"Sidhani kama kunifanyia mimi haya utakuw aunamaliza tatizo, wewe sio mtu wa kwanza kufanya haya na nina imani sio muda utajuta sana kwa hiki ulicho kifanya Chuki"
"Wewe haupaswi kunionea mimi huruma, wewe unapaswa kujionea huruma mwenyewe kwa sababu huenda utakuwa mwanadamu ambaye utakufa kwa mateso sana kutokana na muuaji atakavyo amua kukua."
"Nani atahusika na mauaji yangu?"
"Usianze kuuliza maswali ambayo majibu yake unayo. Kinachokupa jeuri ni Denis Kijazo ila kwa bahati mbaya sana naye anakufa leo usiku huu huu pamoja na wewe"
"Whaaaat?"
"Muda sio mrefu Denis Kijazo anakuja mwenyewe hapa"
"Umejuaje?" mwanamke huyo hakuongea sana alitoa rimoti kwenye mfuko wake na kuwasha projector kubwa ukutani. Justin alishangaa anaona milima milima hakuelewa anaonyeswa nini. Haikupita hata dakika moja katikati ya mlima mmoja ulitokea mlipuko mkubwa sana na kufanya eneo hilo kutetemeka kwa zaidi ya dakika kumi ndipo hali ikaanza kutulia mlima huo mdogo ukishuka chini sehemu ambayo ililipuliwa ilibonyea kabisa.
"Hii ilikuwa ni moja kati ya sehemu ya kutegemewa sana na Denis Kijazo, lazima amehangaika sana kukutafuta hivyo kwa vyovyote atakuja Ikulu. Kama alikuwa ana mpango wa kuchelewa kuja basi akiona hii atashtuka sana huko aliko na hatavumilia tena, atajaribu kukupigia lakini hatafanikiwa kukupata hivyo kwa majivuno aliyokuwa nayo lazima aje Ikulu maana alishapageuza kama kwake vile. Akiingia ndiyo itakuwa jumla hatatoka tena humu ndani bali itakuja kutoka maiti yake"
"Whaaaaat?"

85 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 86
"Najua unashangaa sana kwa yote ambayo yanatokea lakin mtu huyu pia ana kambi huko Arusha ambayo nako muda mfupi ujao tu yanaenda kuwa majivu. Denis Kijazo kwake nimepenyeza watu wangu wengi sana maana kila mmoja wao nimemhakikishia kwamba hii vita hawezi kushinda hivyo atakaye nikataa baada ya hili namuua, hakuna mtu anapenda kuwa upande ambao unashindwa hivyo vijana wengi ambao alikuwa anawatumia atakavyo kutoka idarani nimewarejesha kwa namna hiyo huku nikiwaahidi dau nono na kuwasamehe makosa yao. Nani angeikataa hiyo ofa bwana Justin?"
"Hivi Chuki umewaza vyema kuhusu jeshi la nchi kwamba halitakuacha?"
"Mimi nawaza hatua tano mbele zaidi yako wewe hapo. Ngoja nikuonyeshe kitu Justin" mwanamke huyo aliitoa simu mfukoni ambayo ilionekana kua mpya kabisa kisha akaipiga mahali ambapo iliita kwa dakika kadhaa tu
"Hello Steven" mwanamke huyo aliongea kwa utulivu akiwa ameipiga simu hiyo kwa mkuu wa majeshi.
"Chuki?"
"Mwenyewe"
"Unapigiwa simu hupatikani muda wote, nini kinaendelea Chuki na uko wapi?"
"Ni jukumu langu kukukumbusha wewe mimi nilipo na kupatikana kwa sababu tu wewe unanihitaji?"
"Acha jeuri mimi nazungumzia usalama wa nchi unaanza kuniongelea mambo ya kijinga, hivi unanionaje?"
"Nisikilize kwa umakini we bwana, una wanajeshi wengi sana, una makomando wengi sana na ulishawahi kuniletea jeuri ukijinadi kwamba wewe ndo una watu wa mhimu sana kwenye taifa hili, sasa kipi kinakufanya kuhusu usalama wa nchi uanze kuhangaika na mimi? do your job"
"Raisi yuko wapi Chuki?"
"Mimi sio mlinzi wa raisi"
"Mlinzi wake hapatikani, raisi hapatikani mpaka sasa. Huenda ana mambo yake ya siri lakini tunahitaji kujua kama raisi yupo salama"
"Jukumu la raisi kuwa salama au kutokuwa salama lipo chini yangu, anakusikia hivi unavyo ongea huyu hapa" mwanamke huyo aliisogeza simu kwa Justin Mtadei ambaye alikuwa anahema kwa nguvu sana.
"Steven tadhali njoo unisaidie, ameichukua Iku....." kabla hajamalizia sentensi yake alipigwa na kibao kizito sana kwenye sikio ambacho kilimfanya atoe kilio kikali sana.
"We malaya unasubutu kumgusa raisi wa nchi?"
"Yeah wewe unafuata kwa sasa"
"Are you serious umeiteka Ikulu?"
"Kama unahisi nachekesha basi unaweza kuangalia katuni ili ufurahi. Kuanzia hivi ninavyo ongea Ikulu ipo chini yangu na raisi ana masaa kadhaa ya kuwa hai baada ya hapo namuua"
"Hilo ni kosa ambalo siwezi kukuacha hai, nakupa nusu saa uwe umejisalimisha Chuki, huwezi kushindana na jeshi la nchi naweza kuiteketeza hiyo sehemu ndani ya saa moja ikabaki tambarare"
"Nisikilize Steven, mimi ndiye nimekupigia simu muda huu hivyo badala ya kuleta ujuaji mwingi ulitakiwa kunisikiliza zaidi ujue nahitaji nini. Sidhani kama una taarifa zozote za umuhimu kuhusu taifa hili zaidi ya kuhitaji kutumia nguvu nyingi sehemu ambazo zinahitaji akili. Nakupa nafasi ya mwisho unatakiwa kukaa mbali na hili ukae karibu na vyombo vya habari ujue ni kitu gani ambacho ulikifanya na dunia ijue wewe ni mtu wa namna gani na baada ya hapo utaangalia namna bora zaidi ya kujitetea"
"Unanitisha sio? kwahiyo hata makomando wangu waliopotea ni wewe uliwaua?"
"Yeah niliwaua mimi mwenyewe kwa mkono wangu ila bado haujanielewa, nimekwambia nisikilize kwa umakini sana. Hivi ninavyo ongea na wewe familia yako yote ipo kwenye mkono wangu akiwepo yule mtoto wako ambaye unampenda sana kuliko hata unavyo ipenda nchi yako. Mimi sina cha kupoteza kwao na linapokuja suala la maslahi ya taifa naruhusiwa kuua mtu yeyote yule na huwa sijutii kufanya hivyo kwahiyo naweza kuua familia yako yote kama utajifanya unataka kuingilia hili jambo" mwanamke huyo alitulia akiwa anaacha maneno yaingie vyema kwa mwanaume huyo pande wa pili.
Steven Mwilonga maneno hayo yalimshtua sana akiwa makao makuu ya jeshi kwenye ofisi yake kutokana na kwamba siku hiyo mambo hayakuwa yakienda vyema. Alichukua simu nyingine hiyo ikiwa hewani na kupiga nyumbani kwake lakini simu haikuwa ikipatikana hali ambayo ilimfanya kuwasha komputa yake na kukuta wanaume wenye suti wakiwa wanaizunguka nyumba yake kupitia cctv kamera.
"Chuki nakuapia, kama ukiigusa familia yangu hata kumuumiza binti yangu japo kwa kibao tu nitakuua vibaya sana. Ugomvi ni wangu mimi na wewe hauihusu familia"
"Hauna muda wa kunitisha kwa sasa, ugomvi unaweza kuwa wangu na wewe ila ukilzamisha hata familia inahusika. Wenzako wanaumiza familia za watu umewahi kujali hilo? nadhani unawajua wavaa suti hao huwa hawana muda wa kupoteza na wananisikiliza mimi tu pekee, kama nikitoa amri tu basi ndani ya dakika moja watu wako wanageuka kuwa maiti nadhani unalielewa hilo"
"What do you want Chuki?"
"Nahitaji kama mkuu wa majeshi ukae pembeni na hili, nahitaji usifanye jambo lolote la kijinga wala kuwatumia makomando wako kuhalalisha huu ushetani ambao unafanyika. Hili jambo linatakiwa kuisha leo lakini kama ukituma watu wako tutaanza kugombana wenyewe kwa wenyewe na kuuana hali ambayo itafanya damu nyingi sana isiyo na hatia kumwagika. Baada ya hapo itafuatia kwa wananchi hususani wenye utofauti kiitikadi nao wataingia kwenye mzozo kila mtu ataenda upande wake na tutajikuta tunaliingiza taifa kwenye hatari kubwa sana ya umwagaji wa damu. Hili sio ombi ni lazima ufanye hivi kama unahitaji familia yako iwe hai na kama utafanya kitu chochote cha kipuuzi kuwatuma makomando nyumbani kwako kuiokoa familia yako utakuwa unafanya kosa la kaburi hilo maana familia pale imesha tolewa ila wale ulio waona wanailinda nyumba tu na huenda usije kuiona tena hivyo fanya kama nilivyo kwambia mimi"
"Nini hatima yangu kama nikifanya vile unavyotaka wewe chuki?"
"Dunia itajua juu ya yale yote ambayo uliyafanya na watu ambao ulikuwa unawasaidia lakini dakika ya mwisho mimi nitakupongeza hadharani kwa kuamua kuisaidia nchi yako dakika za jioni na mchango wako mkubwa utaingia kwenye historia ya nchi hii"
"Naomba usiiguse familia yangu, niahidi hili Chuki"
"Familia itakuwa salama kama tu utafanya niliyo kuagiza"
"Deal" Chuki aliikata simu baada ya mtu ambaye ndiye lilikuwa tumaini la mwisho kabisa la Justin kukubali kutolitumia jeshi kuichukua Ikulu kwa nguvu kutoka kwenye mikono ya mwanamke ambaye alikuwa mkurugenzi wa shirika la kijasusi. Justin alinyong'onyea sana baada ya hali hiyo kutokea, alijikuta anakata tamaa mno na kushindwa kujua nini ilikuwa inaenda kuwa hatima yake.
"Sasa nadhani umeelewa kwanini nilikwambia mtakuwa na mwisho mbaya sana. Denis Kijazo kama alikuwa anavumilia baada ya kuona kilicho tokea huku lazima atakuwa njiani saivi kuja na watu wake hapa, akifika ndipo rasmi anaenda kuyajutia maisha yake yote na kujuta kuzaliwa na kuingia kwenye anga zangu. sidhani kama tutaonana tena Justin, uwe na wakati mwema kwenye maisha yako mpya ya huko uendako nadhani ni vizuri zaidi kama utaanza kutubu mapema dhambi zako maana ni nyingi sana" mwanamke huyo baada ya kumaliza maneno hayo alitoka ndani humo.
Denis Kijazo akiwa kwenye harakati za kuweza kuusubiri muda ambao alipanga kwenda Ikulu usiku huo kujua ni kipi ambacho kilikuwa kinaendelea, alishtushwa na habari mbaya sana kutoka kwa mlinzi wake. Eneo la Morogoro ilipokuwa kambi yake ililipuliwa vibaya sana na ndani kulikuwa na mali nyingi sana na hata eneo hilo lilikuwa limetengenezwa kwa gharama sana.
"Andaa msafara tunaenda Ikulu muda huu"
86 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 87
"Mheshimiwa"
"Fanya yale niliyo kuagiza" halikuwa ombi bali ilikuwa ni amri hivyo ilitekelezwa haraka sana na hakukuwa na namna nyingine ya kuweza kupinga. Ndani ya saa moja kutoka nje ya mji alikokuwa anakaa alifika Ikulu ikiwa ni saa saba ya usiku. Baada ya kufika hapo walinzi walimfungulia mheshimiwa huyo baada ya kuonekana ni yeye mwenyewe ndiye alikuwa hapo hivyo baada ya kushuka alinyoosha moja kwa moja kuelekea ofisini kwa raisi lakini walinzi wake wengi walibaki nje na baada ya kuikaribia ofisi hiyo akiwa na mlinzi wake mkuu, mlinzi huyo alibaki mlangoni sehemu ambayo ilikuwa na wanaume kadhaa ambao walikuwa wamevaa suti.
Denis Kijazo alisimama na kuwaangalia kwa umakini sana walinzi hao, alishtuka maana hakuwahi kabisa kuwaona kwenye macho yake na ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza. Hata hivyo hakuwa na namna lango lilifunguliwa, aliingia akiwa na hasira kali sana lakini baada ya kuingia tu mlango ulijilock wenyewe na alicho kiona mbele yake kilimtisha sana.
Kwenye kiti ambacho alikuwa anatakiwa kukaa raisi, mkurugenzi wa shirika la kijasusi ndiye alikuwa amekaa hapo, hiyo ilikuwa ni ishara tosha kwamba Ikulu haikuwa chini ya raisi tena huku mwanamke huyo akiwa amezungukwa na wanaume wanne ambapo wawili walikuwa mbele yake na wawili walikuwa nyuma yake.
"Ni wewe ambaye upo nyuma ya kila kitu?" Denis Kijazo aliuliza akiwa anacheka kwa hasira
"Ndiyo"
"Miaka kadhaa huko nyuma wenzako waliwahi kufanya kosa kama hili wakaulipua na ukumbi wangu ambao ulikuwa unaniingizia pesa nyingi sana na wewe leo umefanya kosa lile lile. Una nafasi bado ya kuishi, piga magoti uniombe msamaha kisha uache mara moja unacho kifanya, tutaangalia namna gani unaweza kuirudisha hasara na nitachukulia kama hili halijatokea" mwanamke huyo alitabasamu na kusimama
"Mnaonekana mnaendana kwa vitu vingi sana nadhani vijana wako umewafundisha vyema sana maana hata mwenzako alikuwa anaongea hivyo hivyo ila umefikiria vizuri kabla ya kukurupuka kuja hapa ukiamini kwamba maneno yako yenye ushawishi mkubwa ndiyo yatalimaliza hili? umeaga huko ulikotoka? kwa sababu hautapata nafasi nyingine tena ya kutoka humu ndani" maneno ya mwanamke huyo yalimfanya ayageuzie macho yake kwenye skrini kubwa ambayo ilikuwa hapo kwa ajili ya raisi kuangalia habari mbali mbali. Kitu alicho kiona kilimshtua sana, walinzi wake wote ambao alikuja nao walikuwa wanachinjwa vibaya sana nje na hata yule mlinzi wake mkuu ambaye alibakia mlangoni alikatwa na panga la shingo kisha mwili wake ukabebwa na wanaume wakaondoka naye hivyo humo ndani alikuwa amebaki yeye kama yeye bila walinzi.
Alikuwa anamtazama tu mwanamke huyo ambapo alibonyeza rimoti nyingine na video ya nyumbani kwa Denis Kijazo ikawa inaonekana kwenye runinga. Kuna wanaume ambao walikuwa ndani ya nyumba yake akijua kwamba ni walinzi wa familia yake waliiweka chini ya ulinzi familia nzima ni jambo ambalo lilimshtua sana.
"Usiogope, wale hawatakufa ila huenda baada ya leo watakuwa kwenye hali mbaya sana ya maisha maana dunia nzima inaenda kuyajua yote ambayo yamejificha nyuma yako" Denis Kijazo alikuwa anatetemeka kwa hasira sana.
"We malaya unathubutuje kunifanyia mimi hivi?" aliongea akiwa anafungua begi yake kitu ambacho ilikuwa kama ishara ya kutoa silaha lakini wanaume wote wanne ambao walimzunguka walikuwa wamezishika silaha zao mkononi na kupewa amri ya kuitupa begi yake hiyo.
“Ikuku ipo chini yangu kwa sasa, mkuu wa majeshi amekubali kutoingilia hili, raisi yupo kizuizini na wewe sio muda unaingia huko na Max ndiye anakuja kuamua hatima nzima ya maisha yenu kama ataamua kuwaua au kuwaacha mkaadhibiwe na mahakama, mimi kazi yangu nitaandika ripoti tu"
"How Chuki?"
"Siku zote ukienda sehemu ambayo ina wajanja wengi sana basi muogope yule ambaye ni fala sana kuliko wote. Unajua kwanini? kwa sababu yule kama akibadilika anakuwa mtu hatari kuliko wote, yule anafanya mambo yake bila presha maana hakuna anaye mjali kabisa, yule anafanya mambo yake kwa kudharauliwa hivyo hakuna hata mmoja anachukua tahadhari juu yake maana anaonekana kuwa dhaifu tayari sasa siku ambayo akija kuamua kuwa mjanja hakuna mtu ambaye anaweza kucheza naye mechi moja maana unakuwa haujui unaanzia wapi ksuhindana naye kwani hakuna chochote ambacho unakuwa unakijua kutoka kwake"
"Sasa huyo fala ni mimi, mlifanya makosa kunipa hii nafasi kwa kuamini kwamba sijui chochote na sitajua chochote jambo ambalo ni kweli sikuwa naelewa kinacho endelea ila baada ya kuujua ukweli sikuwa tayari kuwa anguko la nchi yangu iliyo nilea mwenyewe ndiyo maana nilimtafuta Max na kukubali kuungana naye na hivi tunavyo ongea kambi yako pendwa ya Arusha inateketezwa na ndani ya saa moja lijalo utapata taarifa nzuri sana kwenye vyombo vya habari" maelezo yake yalitosha kumnyong'onyesha sana Denis Kijazo, hakuwahi kuamini kwamba anaweza kuja kuwa na mwisho mbaya na wa aibu sana namna hiyo.
Alikosa hata nguvu ya kusimama mzee huyo, alikaa chini akiwa anacheka mwenyewe kwa uchungu mkubwa sana. Kitu ambacho kilimuuma zaidi ni kuzidiwa akili na mwanamke tena ambaye anamzidi kila kitu kwenye maisha, sasa alishangaa mtu anaye mzidi kila kitu hadi dhambi ndiye anakuwa chanzo cha anguko lake.
"Nilijua kuna siku nitakuja kufeli ila sio kwa namna hii na sio kwa mwanamke kama wewe" aliongea kwa hasira sana lakini hakujibiwa kitu chochote kile. Muda ambao waliutumia kuongea hapo uliwapeleka mpaka saa nane. Chuki aliiwasha tena runinga na kwenda live kuangalia tukio ambalo lilikuwa linaruka wakati huo, tukio ambalo lilikuwa linazungumziwa sana kwenye mitandao ya kijamii kwamba lingekuwa hewani siku hiyo na hakuna binadamu aliyekuwa anatakiwa kulikosa kabisa kwani asingejisamehe mwenyewe mpaka anakufa.


THE UNTOLD
Ndicho kipindi ambacho kilikuwa live muda huo, kipindi ambacho kilikuwa kinakua kwa kasi kubwa sana ndani ya taifa la Tanzania kikiongozwa na Fabian the real ambaye ndiye alikuwa mwanzilishi wa kipindi hicho na mmiliki.

USHETANI ULIO ZUNGUMZWA KWA LUGHA SABA
Hicho ndicho kilikuwa kichwa cha habari ambayo ilikuwa inatolewa usiku huo na mwandishi huyo. Kichwa ambacho kilikuwa kinaleta msisimko sana kwa wasikilizaji na watazamaji wa kipindi hicho hali iliyowafanya kuwa na hamu kubwa sana ya kuweza kujua kwamba ni kipi kilikuwa nyuma. Kava ya kichwa hicho ilikuwa ni picha moja ya mwanaume ambaye sura yake ilikuwa ikionekana kwa mbali sana na alikuwa na sura pande zote mbili.
Upande mmoja ulionyesha tabasamu kwa mbali sana na upande huo watu walionekana wakiushangilia kwa mbali lakini upande wa pili wa sura nyingine mtu huyo alikuwa na damu mdomoni huku mguu wake ukiwa umekikanyaga chini kitabu cha sheria mkononi akiwa na kisu chenye damu na mbele yake kukiwa na raia ambao walikuwa chini wakivuja damu huku begani kwake akiwa ameliegesha vazi la polisi lenye damu nyingi sana.
Ilikuwa ni picha fikirishi sana ambayo ilimfanya kila mtanzania kutamani kuweza kuona ni kitu gani ambacho kilikuwa kinafanyika pale. Fabian the real alitokezea kwenye video na kuanza kueleza kilichokuwa kimemuweka pale akionyesha picha za moja kwa moja, video pamoja na ushahidi wa maandishi. Kichwa USHETANI ULIO ZUNGUMZWA KWA LUGHA SABA kilikuwa kinamlenga Denis Kijazo ambaye alikuwa ni raisi ambae alitawala Tanzania mpaka awamu ya saba huku akiwaweka watu wake kwenye nafasi hizo ambao aliona kwamba alikuwa anaweza kuwamudu. Kichwa kilikuwa kinaeleza vyema namna mtu huyo alivyo itumia awamu yake ya saba kuweza kutenda matendo mabaya sana, matendo ambayo yaliacha vilio kwa watu wengi sana huku akijificha kwenye kivuli cha tabasamu feki ambalo alikuwa anapenda kulitoa usoni kwake.
Kijana huyo alieleza mambo yote mabaya ya kama alivyokuwa ameahidiwa na Max, alieleza uchafu wote pamoja na watu wote ambao walikuwa ndani ya mzunguko wa Denis Kijazo pamoja na mambo yote ambayo walikuwa wameyafanya. Kwenye taarifa hiyo kijana alimpa sifa sana mwanaume ambaye alikuja kumpatia taarifa hizo mwanaume ambaye aliyatoa maisha yake kwa ajili ya kulikomboa taifa na kisha aliitakia nchi yake maisha marefu sana. Baada ya kumaliza kuitoa taarifa hiyo ambayo ilitumia masaa mawili kusimuliwa walikuja wanaume eneo hilo na kuondoka naye kwa ajili ya usalama wake.
Ni habari ambayo ilibaki inamshangaza kila mtu, habari ambayo ilianza kusambaa ndani ya ulimwengu mzima, habari ambayo kila mtu alibaki anashangaa imekuwaje hivyo kila mtu akawa anahitaji kukutana na mwandishi huyo ili kuweza kumhoji kwamba ni kipi hasa kilitokea mpaka mtu huyo akamwamini yeye na kumpa tarifa hizo nyeti.
Wakati taarifa ile inamalizika kusomwa, Denis Kijazo alikufa kwa presha mwenyewe. Dunia nzima ilikuwa imeujua ushetani wake wote ambao aliufanya, hakuwa anaweza kuimudu hofu hiyo lakini Arusha kambi yake iliripotiwa kulipuliwa, kambi ambayo ilikuwa kama mkono wake wa kulia na vijana wake wote waliuawa bila kusahau Morogoro ambako nako ililipuliwa na yote yalizungumziwa kwenye taarifa na Fabian the real.
Wakati huo huo ndio muda ambao Mkurugenzi wa usalama wa taifa alijitokeza hadharani kwenye vyombo vya habari na kueleza kwamba baada ya kuona Ikulu inaendeshwa na majangili aliamua kuiteka na kuiweka kwenye mikono yake mpaka pale hali itakapotulia kwa makubaliano maalumu na mkuu wa majeshi. Alieleza kwamba licha ya mtu huyo kuwa kundi moja na Denis Kijazo lakini dakika za mwisho alikubali kulisaidia taifa na kupelekea kufanikisha kuimaliza hiyo vita salama.
Mkurugenzi alieleza kwa undani yote ambayo yalitokea miaka kumi na mbili iliyopita na kumsafisha raisi Teodensia Mpanzi kwamba hakuwa msaliti na timu yake kama ilivyo tengenezwa bali yeye na vijana wake waliamua kupigana na hao madhalimu lakini kwa bahati mbaya sana waliuawa kabla ya kutimiza hilo. Alisisitiza kwamba yule mwanaume ambaye alisemekena kuwa gaidi kwa kumuua raisi alikuwa hai, mwanaume ambaye alizikwa akiwa hai lakini akafanikiwa kuishi tena na huyo ndiye ambaye nchi na dunia ilitakiwa kumpongeza kwa sababu ndiye ambaye alifanikiwa kulikomboa taifa kwa mkono wake na damu yake hali ambayo ilipelekea kuwapoteza watu wake wa karibu wengi ambao walikufa kwa ajili ya taifa akiwepo Francis Mboye meja jenerali, DRAGON BOYS, shemeji yake Siza, mtu wake wa karibu na raisi wake Teodensia Mpanzi baada ya kusalitiwa na watu wake wa karibu ambao kwa pamoja walikuwa walinzi wa taifa yaani Brandina Elkana ambaye alikuwa mlinzi mkuu wa raisi pamoja na Karistus Dickson yaani Dax.

87 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

FINAL EPISODE..............
Lakini kwenye kulipigania taifa mwanaume huyo alimpoteza mkewe kipenzi huku akibakia na binti yake wa pekee ambaye ilikuwa kama zawadi bora sana kutoka kwa mkewe ambaye alikufa. Alitaka watu wakaandike vitabu kuhusu shujaa huyo, jina lake liwe alama ya uzalendo kwenye taifa la Tanzania na vijana wote wakaliishi milele iwe kama chachu ya alama bora ya taifa maana bila yeye taifa lilikuwa linaangamia kwa zaidi ya miaka miamoja ijayo wananchi wangezidi kuteseka kila siku lakini pia alisisitiza kwamba alikuwa na ombi moja kwa mtu huyo ambayo angelileta hadharani kama mtu huyo angekubali kulipokea.

Mkuu wa majeshi Steven Mwilonga alikutwa akiwa amejiua ofisini kwake akiwa ameacha barua ya kuomba msamaha kwa familia yake na watanzania kwa kushindwa kuwa mzalendo na kuamua kuwatumikia watu. Alikuwa anajutia sana jambo hilo hivyo hakuona sababu ya kuweza kuishi kwa kuchangia machufuko kwenye nchi yake mwenyewe.
Mwanasayansi ambaye alikuwa anatumiwa na Denis Kijazo aliitwa mbele ya vyombo vya habari na kuelezea namna alivyokuwa anatumika kuitengeneza sumu hiyo kali kwa miaka mingi sana ambayo alifanya kazi kwa lazima chini ya mtu huyo huku akifurahia sana kuweza kurudi tena kwa mara nyingine kuungana na familia yake na alilaani sana kile ambacho alikifanya huko ila hakuwa na namna kwa sababu alifanya ili kuweza kuilinda familia yake. Alichaguliwa kuwa mwanasayansi bora wa mwaka na aliahidi kutengeneza dawa madhubuti kwa ajili ya sumu hiyo ambayo ilikuwa imesambazwa tayari kwa watu wenye pesa ili kama kuna tatizo lingekuwa kutokea basi iwe rahisi kuweza kuwatibu watu.
Dawson Nduka, mwandishi wa vitabu alielezea mambo mengi sana kwa uchungu mkubwa, alielezea sababu ambayo ilimfanya kuishia kule kwa mtu yule na kutumika kuandaa makala ambazo zilikuwa zinamfanya Denis Kijazo aandikwe kama kiongozi bora sana. Mwanaume huyo alikuwa anajutia kufanya hayo ila alifanya kwa ajili ya familia yake ambayo mkewe alikuwa anamsaliti na moja ya mlinzi wa kutegemewa na Denis Kijazo huku akijua kabisa kwamba mtu huyo ndiye ambaye alileta matatizo kwenye familia yake.
Mtu huyo hakuishia hapo tu licha ya kutoka na mkewe ambaye aliishia kupata mimba bado alitoka na mtoto wake wa damu kitu ambacho kilifanya kuzaa nao wote wawili bila wao kujua kwamba walikuwa wanachanganywa na mwanaume mmoja hali ambayo ilimuumiza na kumfanya kuishi kwa maumivu makali sana kiasi kwamba alitamani hata kujiua ila aliamua kuishia kwa sababu ya watoto wake na alidai kwamba alishamsamehe mkewe na alikuwa tayari kuwalea watoto hao wote kama wake.
Aliomba msamaha kwa familia nzima ya mwandishi wa habari ambaye alimponza baada ya kuhitaji kumtumia kukitangaza kitabu chake ambacho kingeongea ukweli wote na kusema kwamba hakuna na maana mbaya bali alitaka kuwaumbua watu hao juu ya kile ambacho walikuwa wanakifanya nchini ila kwa bahati mbaya sana akaishia kwenye mikono ya watu hao kwa miaka mingi sana. Almshukuru sana Donald Daniel kwa kuweza kuwaokoa huko Arusha na kuwafanya wazione familia zao kwa mara nyingine tena.
Mwandishi huyo rasmi alikiachia kitabu chake cha MAITI INAYO ONGEA ambacho kiliandika udhalimu ambao ulikuwa unafanywa na kiongozi. Kilichukua tuzo ya kitabu bora duniani baada ya kutafsiriwa kwa lugha la Kiingereza na kumfanya kuwa mwandishi namba moja duniani kikiuza zaidi ya kopi biliona moja na kumfanya kuwa mwandishi wa vitabu tajiri zaidi ulimwenguni Dawson Nduka akipewa na tuzo ya heshima na umoja wa mataifa.
Mkewe alijiua kwa kujiona mwenye hatia sana kwa yale ambayo alioyafanya na binti yake alibakia na sonona kubwa sana kwenye moyo wake lakini mzee huyo alikubali kuwalea watoto wa Ted kama wake.
Mmiliki wa THE UNTOLD, Fabian the real ndiye alikuwa mwandishi wa habari maarufu zaidi duniani, huku video yake ikitazamwa mara bilioni saba kwenye mtandao wake kwa muda mfupi sana kitu ambacho kilimuingizia pesa nyingi sana na kumfanya kuwa tajiri mkubwa sana akiwa na umri mdogo. Alifanya mahojiano mengi sana na vyombo vikubwa duniani huku kila mtu akiwa anataka kujua ni kwa namna gani alikutana na shujaa bora duniani Donald Daniel mpaka akamwamini yeye na kumpatia ushahidi huo na zawadi ya kiasi kikubwa sana cha pesa ambacho alisema hakupewa yeye tu bali kwa mashujaa wote ambao walipambana mwanaume huyo aliwapatia pesa hizo na kusaidia watu wengi sana wenye uhitaji nchini kote na Afrika kwa ujumla.
Gavana wa zamani Laurent Mande jina lake liliandikwa mbele ya benki kuu ya Tanzania kama heshima kwa kazi bora ambayo aliifanya baada ya taarifa kutoka kwamba alikuwepo ndani ya lile jengo la Morogoro na familia yake ilipewa maisha bora sana lakini sio yeye tu bali kwa mashujaa wote familia zao zilipewa maisha bora sana kuwaenzi watu wao kwa namna walivyo jitoa kulisaidia taifa lao.
Watu wote ambao walifahamika kwamba kwa namna moja walikuwa wanajihusisha na Denis Kijazo, wote walikamatwa na kufungwa hivyo nchi ilibaki safi kabisa. Kutokana na kufanya kazi iliyo tukuka mkurugenzi Chuki Steward aliapishwa kuwa raisi mpya wa Tanzania kwani watu waliona kwamba mwanamke huyo ndiye pekee alikuwa anaweza kuwapeleka nchi ya ahadi.
Baada ya kuapishwa na kuwa raisi alikutana na Max Ikulu wakiwa wameongozana na mwanae Naima.
"Donald sijajua ni kwa namna gani napaswa kukushukuru kwa hili, nchi inatakiwa kujivunia sana kuwa na mtu kama wewe"
"Sioni haja ya kunishukuru kwa sababu mimi nilitengenezwa kuwa hivi nadhani nilikuwa natimiza majukumu yangu kiongozi"
"Sijawahi kukutana na mtu mzalendo kama wewe, nasikia kwamba yaliyokuwa maeneo ya mke wako huko Sinza na salasala baada ya kuondoka baadae serikali ilikuja kujibinafsishia baada ya wafanyakazi kuripoti kwamba bosi wao amepotea na akaunti za benki zilizuiliwa"
"Yeah, ilichukua muda mrefu sana na aliondoka bila taarifa kwa sababu za usalama hivyo hakuwaaga wafanyakazi wake"
"Kila kitu kimerudi kwenye mikono yako na akaunti za benki zinafanya kazi nitakutumia taarifa zote nadhani ni mali sahihi kabisa kwa Naima"
"Nashukuru sana kwa hilo, itakuwa kumbukumbu bora sana ya mwanamke ambaye nilimpenda sana"
"Amekuachia zawadi ya mtoto huyo ndiye atakuwa furaha yako kwa sasa"
"Ni kweli, nadhani natakiwa kwenda kupumzika na mwanangu sasa"
"Justin umemsamehe?"
"Hapana, nimemchoma sindano ya sumu ambayo itayachukua maisha yake taratibu"
"Bora wameisha na kila kitu kinaisha ila nina ombi moja kwako Donald"
"Nakusikiliza mheshimiwa"
"Nafasi yangu ya kuwa raisi nahisi bado haijakamilika kabisa na niliwaahidi raia kwamba nina ombi kwako"
"Kwanini?"
"Najua kwa sasa utakuwa unapitia mengi sana ila nakuomba sana uwe mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi"
"Hapana mheshimiwa, kwa sasa nataka nikapumzike na mwanangu, nataka mwanangu awe na muda wa kutosha na baba yake na isitoshe naenda mbali sana na Tanzania"
"Sio amri bali ni ombi langu, hata kama utaenda kupumzika kwa miaka miwili naweza kukupa hiyo ruhusa kisha utakaporudi utaendelea na majukumu" mwanaume alitabasamu na kumwangalia mwanae ambaye alikuwa anacheka na kumpa baba yake ishara ya tano kumaanisha kila kitu kilikuwa sawa japo Kiswahili hakuwa anaelewa sana maana alizaliwa Marekani na alikuwa akikisikia kidogo tu pale walipokuwa wanaongea wazazi wake.
"Nitafanya hivyo" Mwanaume alikubali ombi hilo ambapo walikumbatiana na mheshimiwa raisi kisha akaondoka eneo hilo akiwa na ulinzi wa kutosha. Safari yake iliishia nyumbani kwa komando James ambapo baada ya kuwakuta watu hao wakiwa wamerudi kwenye furaha yao aliaga na kuondoka kabisa Tanzania kuelekea ndani ya Malaysia katika jiji la KUALA LUMPUR.

MWISHO.











Naam, tulikuwa wote ndani ya simulizi hii ya kusisimua yenye visa na mikasa ya kutosha na sasa tunafika tamati na mimi naamua kutoka ndani ya chumba ambacho nilijifungia mwenzi mzima kuandaa andiko hili.
Niseme asante sana kwa kuwa pamoja na mimi mwanzo mpaka mwisho, panapo majaaliwa tutakutana ndani ya simulizi nyingine ambayo inafuata. Sio mzuri sana wa kuahidi ila tunaweza kukutana ndani ya simulizi ya GEREZA LA HAZWA CHAPTER 2.
Langu jina naitwa FEBIANI BABUYA, wao wanapenda kuniita BUX THE STORYTELLER. Nyuma ya kalamu nilikuwa ni mimi mwenyewe till next time.
Tchao.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

FINAL EPISODE..............
Lakini kwenye kulipigania taifa mwanaume huyo alimpoteza mkewe kipenzi huku akibakia na binti yake wa pekee ambaye ilikuwa kama zawadi bora sana kutoka kwa mkewe ambaye alikufa. Alitaka watu wakaandike vitabu kuhusu shujaa huyo, jina lake liwe alama ya uzalendo kwenye taifa la Tanzania na vijana wote wakaliishi milele iwe kama chachu ya alama bora ya taifa maana bila yeye taifa lilikuwa linaangamia kwa zaidi ya miaka miamoja ijayo wananchi wangezidi kuteseka kila siku lakini pia alisisitiza kwamba alikuwa na ombi moja kwa mtu huyo ambayo angelileta hadharani kama mtu huyo angekubali kulipokea.

Mkuu wa majeshi Steven Mwilonga alikutwa akiwa amejiua ofisini kwake akiwa ameacha barua ya kuomba msamaha kwa familia yake na watanzania kwa kushindwa kuwa mzalendo na kuamua kuwatumikia watu. Alikuwa anajutia sana jambo hilo hivyo hakuona sababu ya kuweza kuishi kwa kuchangia machufuko kwenye nchi yake mwenyewe.
Mwanasayansi ambaye alikuwa anatumiwa na Denis Kijazo aliitwa mbele ya vyombo vya habari na kuelezea namna alivyokuwa anatumika kuitengeneza sumu hiyo kali kwa miaka mingi sana ambayo alifanya kazi kwa lazima chini ya mtu huyo huku akifurahia sana kuweza kurudi tena kwa mara nyingine kuungana na familia yake na alilaani sana kile ambacho alikifanya huko ila hakuwa na namna kwa sababu alifanya ili kuweza kuilinda familia yake. Alichaguliwa kuwa mwanasayansi bora wa mwaka na aliahidi kutengeneza dawa madhubuti kwa ajili ya sumu hiyo ambayo ilikuwa imesambazwa tayari kwa watu wenye pesa ili kama kuna tatizo lingekuwa kutokea basi iwe rahisi kuweza kuwatibu watu.
Dawson Nduka, mwandishi wa vitabu alielezea mambo mengi sana kwa uchungu mkubwa, alielezea sababu ambayo ilimfanya kuishia kule kwa mtu yule na kutumika kuandaa makala ambazo zilikuwa zinamfanya Denis Kijazo aandikwe kama kiongozi bora sana. Mwanaume huyo alikuwa anajutia kufanya hayo ila alifanya kwa ajili ya familia yake ambayo mkewe alikuwa anamsaliti na moja ya mlinzi wa kutegemewa na Denis Kijazo huku akijua kabisa kwamba mtu huyo ndiye ambaye alileta matatizo kwenye familia yake.
Mtu huyo hakuishia hapo tu licha ya kutoka na mkewe ambaye aliishia kupata mimba bado alitoka na mtoto wake wa damu kitu ambacho kilifanya kuzaa nao wote wawili bila wao kujua kwamba walikuwa wanachanganywa na mwanaume mmoja hali ambayo ilimuumiza na kumfanya kuishi kwa maumivu makali sana kiasi kwamba alitamani hata kujiua ila aliamua kuishia kwa sababu ya watoto wake na alidai kwamba alishamsamehe mkewe na alikuwa tayari kuwalea watoto hao wote kama wake.
Aliomba msamaha kwa familia nzima ya mwandishi wa habari ambaye alimponza baada ya kuhitaji kumtumia kukitangaza kitabu chake ambacho kingeongea ukweli wote na kusema kwamba hakuna na maana mbaya bali alitaka kuwaumbua watu hao juu ya kile ambacho walikuwa wanakifanya nchini ila kwa bahati mbaya sana akaishia kwenye mikono ya watu hao kwa miaka mingi sana. Almshukuru sana Donald Daniel kwa kuweza kuwaokoa huko Arusha na kuwafanya wazione familia zao kwa mara nyingine tena.
Mwandishi huyo rasmi alikiachia kitabu chake cha MAITI INAYO ONGEA ambacho kiliandika udhalimu ambao ulikuwa unafanywa na kiongozi. Kilichukua tuzo ya kitabu bora duniani baada ya kutafsiriwa kwa lugha la Kiingereza na kumfanya kuwa mwandishi namba moja duniani kikiuza zaidi ya kopi biliona moja na kumfanya kuwa mwandishi wa vitabu tajiri zaidi ulimwenguni Dawson Nduka akipewa na tuzo ya heshima na umoja wa mataifa.
Mkewe alijiua kwa kujiona mwenye hatia sana kwa yale ambayo alioyafanya na binti yake alibakia na sonona kubwa sana kwenye moyo wake lakini mzee huyo alikubali kuwalea watoto wa Ted kama wake.
Mmiliki wa THE UNTOLD, Fabian the real ndiye alikuwa mwandishi wa habari maarufu zaidi duniani, huku video yake ikitazamwa mara bilioni saba kwenye mtandao wake kwa muda mfupi sana kitu ambacho kilimuingizia pesa nyingi sana na kumfanya kuwa tajiri mkubwa sana akiwa na umri mdogo. Alifanya mahojiano mengi sana na vyombo vikubwa duniani huku kila mtu akiwa anataka kujua ni kwa namna gani alikutana na shujaa bora duniani Donald Daniel mpaka akamwamini yeye na kumpatia ushahidi huo na zawadi ya kiasi kikubwa sana cha pesa ambacho alisema hakupewa yeye tu bali kwa mashujaa wote ambao walipambana mwanaume huyo aliwapatia pesa hizo na kusaidia watu wengi sana wenye uhitaji nchini kote na Afrika kwa ujumla.
Gavana wa zamani Laurent Mande jina lake liliandikwa mbele ya benki kuu ya Tanzania kama heshima kwa kazi bora ambayo aliifanya baada ya taarifa kutoka kwamba alikuwepo ndani ya lile jengo la Morogoro na familia yake ilipewa maisha bora sana lakini sio yeye tu bali kwa mashujaa wote familia zao zilipewa maisha bora sana kuwaenzi watu wao kwa namna walivyo jitoa kulisaidia taifa lao.
Watu wote ambao walifahamika kwamba kwa namna moja walikuwa wanajihusisha na Denis Kijazo, wote walikamatwa na kufungwa hivyo nchi ilibaki safi kabisa. Kutokana na kufanya kazi iliyo tukuka mkurugenzi Chuki Steward aliapishwa kuwa raisi mpya wa Tanzania kwani watu waliona kwamba mwanamke huyo ndiye pekee alikuwa anaweza kuwapeleka nchi ya ahadi.
Baada ya kuapishwa na kuwa raisi alikutana na Max Ikulu wakiwa wameongozana na mwanae Naima.
"Donald sijajua ni kwa namna gani napaswa kukushukuru kwa hili, nchi inatakiwa kujivunia sana kuwa na mtu kama wewe"
"Sioni haja ya kunishukuru kwa sababu mimi nilitengenezwa kuwa hivi nadhani nilikuwa natimiza majukumu yangu kiongozi"
"Sijawahi kukutana na mtu mzalendo kama wewe, nasikia kwamba yaliyokuwa maeneo ya mke wako huko Sinza na salasala baada ya kuondoka baadae serikali ilikuja kujibinafsishia baada ya wafanyakazi kuripoti kwamba bosi wao amepotea na akaunti za benki zilizuiliwa"
"Yeah, ilichukua muda mrefu sana na aliondoka bila taarifa kwa sababu za usalama hivyo hakuwaaga wafanyakazi wake"
"Kila kitu kimerudi kwenye mikono yako na akaunti za benki zinafanya kazi nitakutumia taarifa zote nadhani ni mali sahihi kabisa kwa Naima"
"Nashukuru sana kwa hilo, itakuwa kumbukumbu bora sana ya mwanamke ambaye nilimpenda sana"
"Amekuachia zawadi ya mtoto huyo ndiye atakuwa furaha yako kwa sasa"
"Ni kweli, nadhani natakiwa kwenda kupumzika na mwanangu sasa"
"Justin umemsamehe?"
"Hapana, nimemchoma sindano ya sumu ambayo itayachukua maisha yake taratibu"
"Bora wameisha na kila kitu kinaisha ila nina ombi moja kwako Donald"
"Nakusikiliza mheshimiwa"
"Nafasi yangu ya kuwa raisi nahisi bado haijakamilika kabisa na niliwaahidi raia kwamba nina ombi kwako"
"Kwanini?"
"Najua kwa sasa utakuwa unapitia mengi sana ila nakuomba sana uwe mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi"
"Hapana mheshimiwa, kwa sasa nataka nikapumzike na mwanangu, nataka mwanangu awe na muda wa kutosha na baba yake na isitoshe naenda mbali sana na Tanzania"
"Sio amri bali ni ombi langu, hata kama utaenda kupumzika kwa miaka miwili naweza kukupa hiyo ruhusa kisha utakaporudi utaendelea na majukumu" mwanaume alitabasamu na kumwangalia mwanae ambaye alikuwa anacheka na kumpa baba yake ishara ya tano kumaanisha kila kitu kilikuwa sawa japo Kiswahili hakuwa anaelewa sana maana alizaliwa Marekani na alikuwa akikisikia kidogo tu pale walipokuwa wanaongea wazazi wake.
"Nitafanya hivyo" Mwanaume alikubali ombi hilo ambapo walikumbatiana na mheshimiwa raisi kisha akaondoka eneo hilo akiwa na ulinzi wa kutosha. Safari yake iliishia nyumbani kwa komando James ambapo baada ya kuwakuta watu hao wakiwa wamerudi kwenye furaha yao aliaga na kuondoka kabisa Tanzania kuelekea ndani ya Malaysia katika jiji la KUALA LUMPUR.

MWISHO.











Naam, tulikuwa wote ndani ya simulizi hii ya kusisimua yenye visa na mikasa ya kutosha na sasa tunafika tamati na mimi naamua kutoka ndani ya chumba ambacho nilijifungia mwenzi mzima kuandaa andiko hili.
Niseme asante sana kwa kuwa pamoja na mimi mwanzo mpaka mwisho, panapo majaaliwa tutakutana ndani ya simulizi nyingine ambayo inafuata. Sio mzuri sana wa kuahidi ila tunaweza kukutana ndani ya simulizi ya GEREZA LA HAZWA CHAPTER 2.
Langu jina naitwa FEBIANI BABUYA, wao wanapenda kuniita BUX THE STORYTELLER. Nyuma ya kalamu nilikuwa ni mimi mwenyewe till next time.
Tchao.
Barikiwa sana kaka mkubwa
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

FINAL EPISODE..............
Lakini kwenye kulipigania taifa mwanaume huyo alimpoteza mkewe kipenzi huku akibakia na binti yake wa pekee ambaye ilikuwa kama zawadi bora sana kutoka kwa mkewe ambaye alikufa. Alitaka watu wakaandike vitabu kuhusu shujaa huyo, jina lake liwe alama ya uzalendo kwenye taifa la Tanzania na vijana wote wakaliishi milele iwe kama chachu ya alama bora ya taifa maana bila yeye taifa lilikuwa linaangamia kwa zaidi ya miaka miamoja ijayo wananchi wangezidi kuteseka kila siku lakini pia alisisitiza kwamba alikuwa na ombi moja kwa mtu huyo ambayo angelileta hadharani kama mtu huyo angekubali kulipokea.

Mkuu wa majeshi Steven Mwilonga alikutwa akiwa amejiua ofisini kwake akiwa ameacha barua ya kuomba msamaha kwa familia yake na watanzania kwa kushindwa kuwa mzalendo na kuamua kuwatumikia watu. Alikuwa anajutia sana jambo hilo hivyo hakuona sababu ya kuweza kuishi kwa kuchangia machufuko kwenye nchi yake mwenyewe.
Mwanasayansi ambaye alikuwa anatumiwa na Denis Kijazo aliitwa mbele ya vyombo vya habari na kuelezea namna alivyokuwa anatumika kuitengeneza sumu hiyo kali kwa miaka mingi sana ambayo alifanya kazi kwa lazima chini ya mtu huyo huku akifurahia sana kuweza kurudi tena kwa mara nyingine kuungana na familia yake na alilaani sana kile ambacho alikifanya huko ila hakuwa na namna kwa sababu alifanya ili kuweza kuilinda familia yake. Alichaguliwa kuwa mwanasayansi bora wa mwaka na aliahidi kutengeneza dawa madhubuti kwa ajili ya sumu hiyo ambayo ilikuwa imesambazwa tayari kwa watu wenye pesa ili kama kuna tatizo lingekuwa kutokea basi iwe rahisi kuweza kuwatibu watu.
Dawson Nduka, mwandishi wa vitabu alielezea mambo mengi sana kwa uchungu mkubwa, alielezea sababu ambayo ilimfanya kuishia kule kwa mtu yule na kutumika kuandaa makala ambazo zilikuwa zinamfanya Denis Kijazo aandikwe kama kiongozi bora sana. Mwanaume huyo alikuwa anajutia kufanya hayo ila alifanya kwa ajili ya familia yake ambayo mkewe alikuwa anamsaliti na moja ya mlinzi wa kutegemewa na Denis Kijazo huku akijua kabisa kwamba mtu huyo ndiye ambaye alileta matatizo kwenye familia yake.
Mtu huyo hakuishia hapo tu licha ya kutoka na mkewe ambaye aliishia kupata mimba bado alitoka na mtoto wake wa damu kitu ambacho kilifanya kuzaa nao wote wawili bila wao kujua kwamba walikuwa wanachanganywa na mwanaume mmoja hali ambayo ilimuumiza na kumfanya kuishi kwa maumivu makali sana kiasi kwamba alitamani hata kujiua ila aliamua kuishia kwa sababu ya watoto wake na alidai kwamba alishamsamehe mkewe na alikuwa tayari kuwalea watoto hao wote kama wake.
Aliomba msamaha kwa familia nzima ya mwandishi wa habari ambaye alimponza baada ya kuhitaji kumtumia kukitangaza kitabu chake ambacho kingeongea ukweli wote na kusema kwamba hakuna na maana mbaya bali alitaka kuwaumbua watu hao juu ya kile ambacho walikuwa wanakifanya nchini ila kwa bahati mbaya sana akaishia kwenye mikono ya watu hao kwa miaka mingi sana. Almshukuru sana Donald Daniel kwa kuweza kuwaokoa huko Arusha na kuwafanya wazione familia zao kwa mara nyingine tena.
Mwandishi huyo rasmi alikiachia kitabu chake cha MAITI INAYO ONGEA ambacho kiliandika udhalimu ambao ulikuwa unafanywa na kiongozi. Kilichukua tuzo ya kitabu bora duniani baada ya kutafsiriwa kwa lugha la Kiingereza na kumfanya kuwa mwandishi namba moja duniani kikiuza zaidi ya kopi biliona moja na kumfanya kuwa mwandishi wa vitabu tajiri zaidi ulimwenguni Dawson Nduka akipewa na tuzo ya heshima na umoja wa mataifa.
Mkewe alijiua kwa kujiona mwenye hatia sana kwa yale ambayo alioyafanya na binti yake alibakia na sonona kubwa sana kwenye moyo wake lakini mzee huyo alikubali kuwalea watoto wa Ted kama wake.
Mmiliki wa THE UNTOLD, Fabian the real ndiye alikuwa mwandishi wa habari maarufu zaidi duniani, huku video yake ikitazamwa mara bilioni saba kwenye mtandao wake kwa muda mfupi sana kitu ambacho kilimuingizia pesa nyingi sana na kumfanya kuwa tajiri mkubwa sana akiwa na umri mdogo. Alifanya mahojiano mengi sana na vyombo vikubwa duniani huku kila mtu akiwa anataka kujua ni kwa namna gani alikutana na shujaa bora duniani Donald Daniel mpaka akamwamini yeye na kumpatia ushahidi huo na zawadi ya kiasi kikubwa sana cha pesa ambacho alisema hakupewa yeye tu bali kwa mashujaa wote ambao walipambana mwanaume huyo aliwapatia pesa hizo na kusaidia watu wengi sana wenye uhitaji nchini kote na Afrika kwa ujumla.
Gavana wa zamani Laurent Mande jina lake liliandikwa mbele ya benki kuu ya Tanzania kama heshima kwa kazi bora ambayo aliifanya baada ya taarifa kutoka kwamba alikuwepo ndani ya lile jengo la Morogoro na familia yake ilipewa maisha bora sana lakini sio yeye tu bali kwa mashujaa wote familia zao zilipewa maisha bora sana kuwaenzi watu wao kwa namna walivyo jitoa kulisaidia taifa lao.
Watu wote ambao walifahamika kwamba kwa namna moja walikuwa wanajihusisha na Denis Kijazo, wote walikamatwa na kufungwa hivyo nchi ilibaki safi kabisa. Kutokana na kufanya kazi iliyo tukuka mkurugenzi Chuki Steward aliapishwa kuwa raisi mpya wa Tanzania kwani watu waliona kwamba mwanamke huyo ndiye pekee alikuwa anaweza kuwapeleka nchi ya ahadi.
Baada ya kuapishwa na kuwa raisi alikutana na Max Ikulu wakiwa wameongozana na mwanae Naima.
"Donald sijajua ni kwa namna gani napaswa kukushukuru kwa hili, nchi inatakiwa kujivunia sana kuwa na mtu kama wewe"
"Sioni haja ya kunishukuru kwa sababu mimi nilitengenezwa kuwa hivi nadhani nilikuwa natimiza majukumu yangu kiongozi"
"Sijawahi kukutana na mtu mzalendo kama wewe, nasikia kwamba yaliyokuwa maeneo ya mke wako huko Sinza na salasala baada ya kuondoka baadae serikali ilikuja kujibinafsishia baada ya wafanyakazi kuripoti kwamba bosi wao amepotea na akaunti za benki zilizuiliwa"
"Yeah, ilichukua muda mrefu sana na aliondoka bila taarifa kwa sababu za usalama hivyo hakuwaaga wafanyakazi wake"
"Kila kitu kimerudi kwenye mikono yako na akaunti za benki zinafanya kazi nitakutumia taarifa zote nadhani ni mali sahihi kabisa kwa Naima"
"Nashukuru sana kwa hilo, itakuwa kumbukumbu bora sana ya mwanamke ambaye nilimpenda sana"
"Amekuachia zawadi ya mtoto huyo ndiye atakuwa furaha yako kwa sasa"
"Ni kweli, nadhani natakiwa kwenda kupumzika na mwanangu sasa"
"Justin umemsamehe?"
"Hapana, nimemchoma sindano ya sumu ambayo itayachukua maisha yake taratibu"
"Bora wameisha na kila kitu kinaisha ila nina ombi moja kwako Donald"
"Nakusikiliza mheshimiwa"
"Nafasi yangu ya kuwa raisi nahisi bado haijakamilika kabisa na niliwaahidi raia kwamba nina ombi kwako"
"Kwanini?"
"Najua kwa sasa utakuwa unapitia mengi sana ila nakuomba sana uwe mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi"
"Hapana mheshimiwa, kwa sasa nataka nikapumzike na mwanangu, nataka mwanangu awe na muda wa kutosha na baba yake na isitoshe naenda mbali sana na Tanzania"
"Sio amri bali ni ombi langu, hata kama utaenda kupumzika kwa miaka miwili naweza kukupa hiyo ruhusa kisha utakaporudi utaendelea na majukumu" mwanaume alitabasamu na kumwangalia mwanae ambaye alikuwa anacheka na kumpa baba yake ishara ya tano kumaanisha kila kitu kilikuwa sawa japo Kiswahili hakuwa anaelewa sana maana alizaliwa Marekani na alikuwa akikisikia kidogo tu pale walipokuwa wanaongea wazazi wake.
"Nitafanya hivyo" Mwanaume alikubali ombi hilo ambapo walikumbatiana na mheshimiwa raisi kisha akaondoka eneo hilo akiwa na ulinzi wa kutosha. Safari yake iliishia nyumbani kwa komando James ambapo baada ya kuwakuta watu hao wakiwa wamerudi kwenye furaha yao aliaga na kuondoka kabisa Tanzania kuelekea ndani ya Malaysia katika jiji la KUALA LUMPUR.

MWISHO.











Naam, tulikuwa wote ndani ya simulizi hii ya kusisimua yenye visa na mikasa ya kutosha na sasa tunafika tamati na mimi naamua kutoka ndani ya chumba ambacho nilijifungia mwenzi mzima kuandaa andiko hili.
Niseme asante sana kwa kuwa pamoja na mimi mwanzo mpaka mwisho, panapo majaaliwa tutakutana ndani ya simulizi nyingine ambayo inafuata. Sio mzuri sana wa kuahidi ila tunaweza kukutana ndani ya simulizi ya GEREZA LA HAZWA CHAPTER 2.
Langu jina naitwa FEBIANI BABUYA, wao wanapenda kuniita BUX THE STORYTELLER. Nyuma ya kalamu nilikuwa ni mimi mwenyewe till next time.
Tchao.
Thanks ur Bro.....!!![emoji1545][emoji1545]
........... ulikuwaa Bora wakati wote...[emoji1614]
Najivunia kuwa mmoja wanaosoma
Riwaya zako

~~ Appreciate Bro.....!!![emoji1614][emoji1614]
 
Back
Top Bottom