Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 39
“Max na Bilali wanakutana lini na mpango unatakiwa kuanza lini mheshimiwa” waziri mkuu aliuliza akionekana kabisa kuwa na hamu kubwa sana ya kuweza kulijua jambo hilo.
“Nitawapa taarifa kuhusu hilo lakini na nyie kwa sasa kila mtu anatakiwa kuanza kuifanya kazi ikiwa ni kukusanya taarifa zote za mtu huyu na watu wake maana naamini kwamba mna vijana wenye uwezo mkubwa sana na kama mtapungukiwa vijana basi mtanipa taarifa niweze kuwaongezea”

“Sawa mheshimiwa, lakini huyu mtu ni mkubwa sana huoni kama kifo chake kinaweza kuleta utata na kutuchafua kama taifa?”
“Hilo nalijua vyema na mniachie mimi, siku ya mwisho nitamhitaji akiwa hai kabisa mzima wa afya ili afe kifo ambacho hakuna mtu hata mmoja ambaye ataweza kuhisi chochote zaidi ya kuamini kwamba amekufa kihalali”

“Nchi ilikuwa inasubiri kwa hamu kubwa sana kuweza kumpata raisi wa aina yako na kwa hili najua Tanzania itakuwa kwenye mikono salama sana”

“Hatutakiwi kuanza kujipongeza mapema sana namna hii kwa sababu hii ni vita ambayo yeyote anaweza kufa kati yetu, kumbuka huyu mtu anaijua serikali hii kuliko sisi wote hapa kwa sababu ameiendesha kwa miaka kumi akiwa kama kiongozi mkuu hivyo usije ukaona ukimya wake ukajua amekata tamaa, huko aliko naye pia anajiandaa na kutuundia mipango mizito sana. Kwahiyo jambo la mhimu sana ni kuutanguliza uzalendo mbele kwanza kabla ya jambo lolote lile, Mungu atulinde tuweze kuikamilisha kazi hii”

“Mungu ibariki Tanzania” waliitikia kwa pamoja kisha raisi akawaruhusu wanaume hao waweze kuondoka Ikuku. Baada ya kufika nje ya ofisi hiyo waziri mkuu akigeuka na kutamka;
“Tumia imani ya mtu ili kumfanya akuamini, kufanikisha hilo unatakiwa kuhakikisha yeye anakuamini kwanza kisha unaitawala akili yake. Rahisi sana” waziri mkuu aliongea kwa msisitizo sana huku akiwa anatabasamu na kutoweka hilo eneo.


Saa saba na dakika ishirini na tano usiku, Max alikuwa anatembea taratibu ndani ya mitaa ya Kariakoo. Alikuwa anategemea kutumiwa location ya mheshimiwa raisi lakini mpaka zinabakia dakika tano tu za kuweza kukutana na mtu ambaye aliambiwa akakutane naye hakuwa ametumiwa hiyo location na wakati huo alikuwa ameishika barabara ya Mnazi mmoja kuelekea kwenye makutano ya barabara ya Mnazi mmoja, gerezani, Karume na Msimbazi.

Alikuwa ameishika simu yake akiwa anaingalia kwa umakini wakati anakaribia kufika kwenye hayo makutano, alisimama baada ya kuhisi kwamba simu yake haikuwa sawa, simu ilikuwa nzito sana tofauti na alivyokuwa ameizoea siku zote. Hali hiyo ilifanya taa nyekundu kuwaka kwenye kichwa chake baada ya kujua kwamba hapakuwa na usalama sana ndani ya hilo eneo. Aliiangalia vizuri sana aligundua kwamba dakika kumi zilizokuwa zimepita simu hiyo ilikuwa imehakiwa bila yeye kujua, alitabasamu na kusikitika maana alikuwa mzembe sana siku hiyo kitu ambacho kilikuwa kosa kubwa sana anapokuwa mazingira hatari sana kama hayo.

Aliirudisha simu yake mfukoni na kusimama pembezoni mwa duka moja akiwa ameegamia nguzo na kufumba macho, masikio yake yalikuwa makini sana kusikiliza kile ambacho kilikuwa kinakuja eneo hilo. Mwili ulisisimka sana na kumfanya asimame na kuhema kwa nguvu baada ya kuhisi kama kuna upepo ulikuwa unakuja kwa kasi sana ndani ya sehemu ambayo alikuwepo, alijivuta pembeni kidogo ulisikika mlio mkali wa kitu kikigonga kwenye nguzo ya umeme. Aliangalia kwa umakini na kugundua kwamba kilikuwa ni kitu kama saa lakini pembezoni kilikuwa na vitu vyenye ncha kali sana kiasi kwamba kama vingezama kwenye mwili wake ingekuwa hatari sana.

Akiwa anashangaa kutaka kujua kwamba ni nani ambaye alikuwa amefika ndani ya hilo eneo umeme ulikatika ghafla sana, alishangaa sana eneo hilo kutowepo kwa mlinzi hata mmoja hiyo ilikuwa ni ishara kwamba wenyewe walifika mapema hata kabla yake na kuweza kusafisha eneo hilo hivyo hata yeye wakati anafika walimuona vizuri sana.

Akiwa anaendelea kujiuliza alipokea maumivu makali kwenye bega lake bila kuelewa kwamba mtu ambaye alikuwa anamshambulia alikuwa anatokea wapi, kabla hajatua chini alipigwa na buti lingine kali sana ambalo lilimzoa mpaka katikati ya barabara ambapo alitua kwa mkono mmoja na kuzunguka kwa nguvu sana kisha akakaa sawa akiwa kwenye mavazi meusi. Mwanaume alisimama vizuri na kujinyoosha pale ambapo alikuwa ameguswa na mwanaume huyo huku akizizungusha koti lake kubwa na kutoa shoka ambalo aliliweka pembeni kwani alipewa maagizo kwamba anatakiwa kuongea na mhusika hivyo hakuona sababu ya msingi ya yeye kuweza kutumia shoka maana ingekuwa ni kufanya mauaji.

Umeme ulirudi tena ghafla sana hiyo sehemu tu ambayo walikuwepo ndipo alipo muona mwanaume mmoja akiwa na simu yake anaibonyeza na bila shaka huyo ndiye ambaye alikuwa anacheza michezo yote hiyo ya kuhaki simu na kukata kata umeme. Walikuwa ni wanaume wawili ambao walikuwa wanamtazama kwa hasira sana.

“Aliye watuma yuko wapi?” aliuliza swali rahisi sana lakini nani angemjibu hilo swali lake? Hawakutakiwa kuwa na maneno ya kwenye kanga sana bali walipaswa kujibizana kiume. Aligundua kitu ambacho kilikuwa kinahitajika hapo hivyo aliurudisha mguu wake mmoja nyuma na kuuweka vizuri kuwapokea wanaume ambao walikuwa wanakuja kwa pamoja wakiwa wanazunguka kwa kasi kubwa sana ambayo ilimfanya arudi nyuma.

Mwanaume mmoja alikuwa anakuja kwa kasi akiwa anazunguka chini huku mmoja akiwa juu, alijigeuza kutaka kupita katikati yao lakini hakufanikiwa baada ya kupigwa na ngumi tatu za nguvu lakini hata yeye hakutua kinyonge baada ya kugeuka kwa kasi na kumtandika mwanaume mmoja na mabuti mawili wa kifua ambayo yalimtupa mbali sana. Aliyekuwa na saa ya chuma kwenye mkono wake aliirudisha kwa nguvu na kuanza kumfuata Max lakini saa hiyo ilidakwa na kurudishwa kwake hali ambayo ilimfanya aache kushambulia kwanza na kuamua kujilinda na kuikwepa saa yake mwenyewe ambayo ilimbaraza kwenye shavu lake ila kwa bahati mbaya sana wakati anageuka baada ya kuikwepa saa yake alichotwa na mtama bila kutarajia wakati anashuka chini alipigwa na buti baya sana la uso ambalo lilimburuza kwa hatua kadhaa akabaki chini anagugumia kwa maumivu.

Aliyekuwa kando yake alizunguka na double kick ya hatari ambapo teke moja Max lilimkosa na lingine likatua kwenye mbavu yake na lilionekana kumuingia vyema kwa namna alivyo itikia ila naye alirudisha ngumi nyingi sana za kifua ambazo zilimfanya mwanaume huyo kuhema na kupiga goti huku akiwa anatapika damu maana ngumi ambazo zlitandikwa zilionekana kuwa nzito sana kuliko hata hali yake ilivyokuwa inaweza kuhimili. Max alikuwa anamsogelea taratibu mwanaume huyo hali ambayo ilionyesha hatari ya yeye kuimaliza kazi haraka sana.

“Mwache bwana mdogo huyo, mimi ndo nina shida na wewe. Sogea ujaribu habati yako kwa dakika tatu na kama ukishindwa kuzihimili basi nakuua”
“Wewe hapo ndo unanipa mimi muda wa kujilinda, hahaha hahaha hahahah” max alicheka sana akiwa anamsogelea Bilali kwa mahesabu makali sana, huyo ndiye mwanaume ambaye alikuwa amefika hapo na huo ulikuwa ni muda wao mzuri zaidi wa kuweza kupimana mabavu.

Hatua zao wote ziliwakutanisha katikati ya barabara ambapo wote walizunguka na mateke makali ambayo yalitua kwenye shingo zao na kila mmoja akaonekana kuyasikilizia maumivu haswa maana walikuwa wamekutana wanaume wawili ambao walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kimapigano. Bilali alidunda chini huku akiwa kama anaruka sarakasi ya mbele ila ilikuwa danganya toto tu maana hakwenda bali alisimama ila kwa bahati mbaya sana Max akawa ameingia kwenye huo mtego ambapo aliishia kupiga hewa alikutanishwa na buti la taya na kumfanya arudi nyuma lakini hakurudi kijinga bali aliudaka mkono wa Bilali ambapo alimvutia upande wake na kulipitisha goti kali sana kwenye kifua cha mwanaume huyo na kila mtu akadondokea upande wake huku akiwa anajishika kwa nguvu.

Wote walichomoa visu vikali sana kwenye viuno vyao huku vijana wa Bilali wakiwa wamekaa pembeni kila mtu akiwa anasikilizia maumivu makali wakiangalia wazee wa kazi wanavyo itendea haki sanaa ya mapigano huku wao wakionekana kama waliingilia sherehe ambayo hakikuwa yao. Namna watu hao walivyokuwa wanavizungusha visu vyao ilikuwa ni ngumu sana kuweza kuamini kwamba kuna mmoja angepona hapo.

Ilichukua dakika kumi na tano wakiwa bado wanapigana vibaya sana bila kupumzika, kila mtu alikuwa na maumivu kwenye sehemu ya mwili wake mpaka pale ambapo Max alifanikiwa kukifikisha kisu kwenye shingo ya Bilali lakini naye mwanaume huyo kwa mkono wake wa kushoto alikuwa amekiweka kisu chake kwenye sehemu ya siri ya Max. waliangaliana kwa dakika nzima kisha kila mtu akaitoa silaha yake wakasogea pambezoni mwa barabara ili wazungumze sasa baada ya kupokeana na kuweza kutambuana kwa uzuri kabisa.

“Kuna sababu gani ambayo imekufanya wewe uhitaji kuniona hapa?”
“Hutaki hata tutambuane japo kwa majina ndugu yangu?”

“Max”
“Bilali”
“Nakusikiliza”

“Unaonekana ni mtu ambaye hupendi kupoteza kabisa muda wako”
“Namchukia sana mtu ambaye anautumia vibaya muda wangu na msaliti. Hao ndio adui zangu wakubwa wawili kwenye maisha yangu”

“Unaonekana kuwa makini lakini mbona unakuwa mzembe sana kiasi hicho, huoni kama unaweza kufa kirahisi sana namna hii?”
“Mhhhh inawezekana ila huyo wa kuja kuniua alitakiwa awe amejipanga sana kwa sababu atawatoa sadaka watu wengi sana”

“Wakija watu wawili wenye uwezo kama wangu si wanakuua vizuri sana?” Bilali alitamka huku akiwa anatoa kinywaji kwenye koti lake na kukinywa kidogo kisha akamrushia na Max.

“Mhhhh sio rahisi sana namna hii, kama unataka kuniua linakuwa suala la kuishi na kufa hivyo siwezi kupigana kirahisi sana namna hii. Kama ningekuwa na lile shoka kwenye mkono wangu wale vijana wako wawili wote walikuwa wanakufa kwa dakika mbili tu kwa namna walivyo wazito lakini pia hata wewe sidhani kama ungekuwa umekaa kwa amani sana mpaka sasa ila nikiri kwamba wewe ni miongoni mwa watu hatari sana ambao mimi nimewahi kukutana nao”

39 inafika mwisho.
Much thanks
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 40
“Kuna watu wana uwezo zaidi yangu na miongoni mwao ni watu ambao tunaenda kupambana nao”
“Unamaanisha nini?”
“Hii ndiyo sababu ya kukutana na wewe kwa sababu wote tupo kwenye safari moja ya kuweza kumpoteza Denis Kijazo”

“Sasa nimekuelewa vizuri, umejipangaje juu ya jambo hili?”
“Kwa hesabu za haraka haraka ni kwamba wengi hatutaweza kuishi bali tutakufa hivyo huu mlima nadhani unaweza kuupanda pekeyako”

“Kila mtu ananiambia habari za kufa kwani mmejuaje kwamba mtakufa? Ni jambo ambalo niliogopa sana baada ya kulisikia kwa raisi mwenyewe hata yeye akiwa hana uhakika wa maisha”
“Unataka kuniambia hata mwanaume wa kazi kama wewe unaogopa kufa pia?”

“Hakuna binadamu ambaye haogopi kufa hasa pale ambapo unajua kabisa kwamba kila nafsi lazima ilambe mchanga. Kuna muda huwa nakifikiria aina ya kifo ambacho nitakufa basi najikuta naogopa sana”

“Kuna muda uoga huwa ni mhimu sana kwa sababu unakusaidia kwenye kuchukua hatua stahiki na kuweza kujihami kwa kila hali ambayo inaweza kuja mbele yako. Nadhani mheshimiwa raisi alikwambia kila kitu kuhusu kiongozi na muasisi wa harakati hizi lakini pia alikupatia taarifa juu ya jambo hili hivyo ilikuwa imebaki mimi na wewe tu kuweza kuonana ndipo tuanze rasmi kazi ila jambo hili ni nyeti sana na hautakiwi kumhusisha mtu yeyote yule hata kama unamwamini kiasi gani” Max alitaka kuongea kitu ila alimezea baada ya kugundua kwamba alikuwa amesha ropoka kwa Brandina. Alijua kama akikiri hilo jambo wazi basi huenda watu hao wangeweza kumuua mrembo huyo hivyo alitakiwa kutafuta muda mzuri zaidi wa kuweza kuliteketeza hilo.

“Nalielewa hilo ila nadhani kuna watu ambao inabidi tuanze nao kwanza”
“Nani na nani?”

“Gavana wa benki kuu bil kumsahau Madilu Mpagazi ambaye ni moja kati ya wafanya biashara wakubwa sana hapa nchini”
“Hao wanahusikaje na haya?”

“Ndio watu ambao ni wawekezaji wakubwa sana kwa Denis Kijazo na ndio ambao wanaonekana kuwa watu wake wa karibu zaidi”
“Umewezaje kuyajua haya?”

“Siku ile wakati mnakuja kule kwenye ule ukumbi ambao mlikoswa koswa kufa ndiko ambako nilifanikiwa kuyajua haya yote baada ya kumhoji mlinzi mmoja pale getini”

“Huyu mjinga ndiyo maana ana kiburi sana kwa sababu anajua kamba ana watu wengi ambao wanamzunguka nyuma yake. Kwahiyo tunaanza na nani?”

“Tuanze na gavana wa benki kuu kwa sababu huyu atatusaidia sana kuzipata pesa za Denis ambazo zipo hapa Tanzania kirahisi sana”
“Wazo zuri na baada ya hapo kitaendelea nini?”

“Huyo tunatakiwa kuhakikisha anapotea kimya kimya bila kuacha ushahidi wowote na moja kati ya kazi ambazo atatusaidia ni kujua alipo gavana mwenzake ambaye amepita” Maelezo ya max yalimshtua sana Bilali.
“Unajua kuhusu gavana kuwa hai?”

“Unapokuwa kwenye kazi kama yangu unakuwa mtu ambaye una taarifa nyingi sana karibia nchi nzima. Utofauti wangu mimi na wewe ni kwamba wewe ni komando na kazi yako kubwa ni kuweka ulinzi tu lakini tofauti na mimi ambaye nipo kwenye shirika la kijasusi kwa sababu kazi yangu ya kwanza ni kuweza kukusanya taarifa hivyo hautakiwi kabisa kushangaa mimi kuwa na hizi taarifa”

“Huyo mtu mpaka anakupa hizo tarifa mlikuwa mnafahamiana? Haiwezekani adui akupe taarifa zote hizo bila kuwa na sababu nyuma yake”
“Kuna kitu aliomba nimsaidie akifa”
“Nini hicho”

“Kumlinda dada yake ambaye anabaki”
“Una uhakika utalifanikisha hilo?”
“Ndiyo”

“Kama utahitaji msaada wangu utawasiliana na mimi kwa namna ambayo itakufaa”
“Shukrani sana kwa hiyo heshima”
“Kwahiyo kazi inaanza kufanyika lini na inafanyikaje?”

“Kesho mimi nitaenda kumtafuta huyu mwanamke ambaye niliahidi kumlinda kwa sababu naona kama naye yupo kwenye hatari kubwa sana ya kuweza kuuliwa na hawa tu. Lakini wakati ambao mimi nitakuwa huko ndio muda ambao nyie mtautumia kumkamata gavana na siku moja baada ya nyie kumkamata mimi nitakuja na mheshimiwa raisi ili tufanye kikao cha pamoja”

“Kwenye kikao hicho kutakuwa na watu wengine?”
“Inawezekana ikawa hivyo maana sijajua mipango ya mheshimiwa ipoje”

“Tunatakiwa kutumia eneo ambalo ni bandia ili kupima imani ya hao watu ambao atakuwa nao maana kuanza kumuamini kila mtu mapema sana hivi itakuwa hatari kubwa sana kwetu. Hivyo nitakutumia eneo ambao mtakuja na tukiwa hapo tutafanya mazungumzo ya pamoja na kumweleza raisi mipango yote ili tujue tunaanzia wapi na kuishia wapi”

“Hilo nimekuelewa, kuna jambo lingine ambalo labda ulitaka kuniambia?”
“Mheshimiwa amekufa akiwa ameacha familia japo ni kwa siri kubwa sana ila tunapaswaa kuilinda na hili naona ni jukumu ambalo mimi nimeachiwa binafsi”
“Una uhakika hauhitaji msaada?”

“Yeah kwa sababu wewe kwa sasa una kazi kubwa tatu, kwanza kumlinda raisi, pili kumlinda huyo mwanamke ambaye unaonekana hata haumfahamu lakini ya tatu ni kujilinda wewe mwenyewe kwa sababu wewe ni mhimu sana hivyo kwa namna yoyote ile hakikisha unakuwa salama na ukihitaji msaada muda wowote ule basi nambie”

“Nimekuelewa ila nikikuangalia ni kama bado una jambo unataka kuniambia” Bilali alikuwa ameanza kunyanyuka lakini maneno hayo yalimfanya arudi tena chini kukaa.
“Ni kweli”
“Lipi hilo?”

“Kuna mtu mwingine ambaye yupo ndani ya huu mpango ila ni mtu wa siri sana lakini naye pia tunatakiwa kukutana naye kwa sababu bosi kwa maelezo ambayo aliyaacha ni kwamba mtu huyo ana maelezo ya mhimu sana ya kuweza kutupa ambayo yanaweza kutusaidia sana kwenye hili ila ni mtu ambaye utambulisho wake hautakiwi kujulikana kabisa hata baada ya kutupa taarifa hiyo inatakiwa tufanye kama hatukuwahi kukutana naye, ndivyo maelezo yanavyosema”

“Ni nani huyo?”
“Maelezo yananitaka niende huko Mkuranga”
“Ndiko anakoishi au?”

“Hapana inatakiwa nienda huko ili niweze kumfahamu mtu huyo kisha nirudi huku mjini kumtafuta”
“Nahisi bado sijakuelewa vizuri”

“Kuna alama ambazo nilipewa, kupitia alama hizo nitafanikiwa kumpata mhusika. Inasemekana kwamba kuna mzee mmoja ambaye anatumia alama ya kunguru kama utambulisho wa kwake na ni maarufu sana huko. Huyo ni mtu ambaye amewahi kuwa rafiki mkubwa sana wa bosi hivyo kupitia yeye ndiye atatufanya tukutane na huyo mtu ambaye naye pia maelezo yake yanahitajika sana kuweza kuikamilisha hii kazi”
“Raisi anajua hili?”

“Hapana kuna mambo sijamwambia bado ila nimekwambia wewe kwa sababu sikupata nae muda wa kutosha na naamini kwamba siku ya kikao tutaongea kila kitu tukiwa pamoja”

“Huko unaenda lini?”
“Tupo nyuma ya muda sana inatakiwa niende saivi” mwanaume huyo aliongea akiwa ananyanyuka na hata Max alinyanyuka wanaume hao wakapeana mikono na kutakiana heri kisha kila mtu akawa ameingia upande wake.

Mkuranga.
Kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa ya kifahari eneo hilo kwa sababu ilikuwa tofauti sana na nyumba zingine ambazo zilikuwa zimezunguka eneo hilo. Kwenye nyumba hiyo alikuwa anaishi mzee mmoja ambaye alikuwa anaitwa Awesu Hasheem lakini jina lake la umaarufu sana lilikuwa ni mr Eagle ikiwa na maana ya Tai. Mzee huyo alifahamika sana kwa jina hilo kwa sababu kwenye miaka yake ya utafutaji alikuwa mtu ambaye hakuwahi kabisa kuchezea fursa hata moja yaani kila fursa ambayo ilikuwa inakatiza mbele yake basi alikuwa anapita nayo kama ilivyokuwa inatakiwa.

40 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 41
Kutokana na jambo hilo watu wengi walianza kumfananisha sana na ndege aina ya Tai kutokana na kwamba ndege huyo hakuwa akiacha mzoga wowote ule popote ambapo angepita hivyo maisha yake yalifanana sana na jamii hiyo ya ndege na ndipo jina lake lilipo zaliwa na kutokana na kuwa maarufu sana watu waliamua kumbatiza jina hilo na yeye hakuwa na namna zaidi ya kuweza kulikubali na kuendelea kulitumia.

Eneo hilo alikuwa anaishi na familia yake pamoja na walinzi wake kwa sababu alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wamedumu ndani ya jeshi kwa muda mrefu sana hivyo serikali ilikuwa inamgharamia kwa kila kitu juu ya ulinzi wake. Akiwa ndani kwake amelala alihisi kama amesikia milio ya mbwa wakibweka ila kukawa kimya hivyo akapotezea lakini kama angejua basi alitakiwa kuchukua tahadhari mapema sana kabla hajachelewa.

Nje kulikuwa na wanaume wawili ambao walikuwa wanaingia ndani ya hilo eneo kwa kuruka ukuta, walitumia dakika mbili tu kuweza kuwaua walinzi wote kisha wakawarushia mbwa gesi kwenye banda lao ambayo iliwafanya kubweka kidogo tu na kupoteza maisha. Wanaume hao walivunja mlango wa nyumba hiyo na kuiteka familia nzima wakiwa na silaha za moto mkononi, kitu ambacho walikitaka kutoka kwa mzee huyo ilikuwa ni kuwatajia huyo mtu wa siri ambaye alionekana kuwa na dili sana na alipo jaribu kukataa juu ya hilo walimuonyesha mfano kwa kumuua mkewe kwa risasi nyingi sana kichwai kisha wakatoa onyo kwamba wangefuata watoto.

Hakuwa na namna zaidi ya kuwaambia ukweli watu hao na kila ambacho alikuwa anakijua ili kuweza kuilinda familia yake, lakini licha ya kuweza kuongea ukweli ambao alikuwa anaujua bado watu hao waliiua familia yake yote pamoja na yeye mwenyewe ambapo walimchoma visu vingi sana na kumuacha akiwa anahangaika huku wakiwa na uhakika kwamba kwa namna yoyote ile kwa maeneo ambayo walikuwa wamemchoma hata angefanyaje basi asingeweza kabisa kupona.

Ilimchukua saa moja tu pekee Bilali kuweza kufika ndani ya eneo hilo, alikuwa kwenye gari kwa mwendo wa kasi sana akiwa mwenyewe ila alipunguza kasi ya gari hiyo baada ya kupishana na gari ambazo zilitokea uelekeo ambao alikuwa anakwenda tena zikiwa kwenye kasi kubwa sana. Alishtuka sana na jambo hilo lilikuwa ni ishara mbaya sana kwamba huenda alikokuwa anakwenda hakukuwa kwema kabisa.

Mwanaume baada ya kufika getini alishangaa kukuta geti lipo wazi, alichomoa bastola kiunoni na kuingia kwa mahesabu makali sana lakini kwa bahati iliyokuwa mbaya sana walinzi walikuwa wamechinjwa vibaya mno. Alikimbilia mpaka ndani ambapo alimkuta mzee Awesu akiwa anahangaika sana.

“Umechelewa saaaaaan kuu…j” mzee huyo alikuwa anatoa maneno kwa mateso sana huku maneno yakiwa yanagoma kabisa kutoka.
“Mzee unaweza kunitajia jina?”
“Dokta”
“Dokta yupi?” Bilali alikuwa anamtikisa ili asije akapoteza maisha kabla hajamtajia jina.

“D…k.. t.. ar..i mk…..uuuuu” alitamka kwa shida sana maneno yake na muda huo huo nafsi iliacha mwili. Bilali alibaki akiwa ameganda sana akiwa anawaza ni daktari mkuu yupi huyo maana nchi ilikuwa na madaktari wakuu wengi sana. Kumbukumbu zake zilimpeleka mpaka siku za nyuma wakati ambao bosi wake alikuwa hai, mkuu wa majeshi licha ya kuwa na daktari wake lakini alikuwa akipenda sana kwenda kutibiwa mhimbili. Baada ya kuunganisha hizo doti zake aligundua kwamba mtu ambaye alikuwa anatajwa hapo alikuwa ni daktari mkuu wa mhimbili.

“Ooooh shiiiit” alitamkakwa sauti akiwa anaangalia saa yake, muda haukuwa rafiki sana kwake. Aliitoa simu yake mfukoni na kuitafuta namba ambayo alikuwa ameificha sana, simu hiyo iliita na kupokelewa na mtu ambaye alikuwa ametoka usingizini.
“Max uko wapi?”
“Nyumbani”

“Nenda nyumbani kwa daktari mkuu wa mhimbili haraka sana kuna watu wanahitaji kumuua muda huu. Nipo mbali ila nitajitahidi kuwahi, wewe wahi haraka sana huko unaweza ukayaokoa maisha yake”
“Kinaendelea nini?”
“Max wahi haraka sana tupo nje ya muda nakuja huko nitakueleza kila kitu”

“Roger that” simu ilikatwa, mwanaume alivaa ndani ya sekunde kama thelathini tu akawa tayari na kutoka humo ndani. Aliingia kwenye gari yake na kutoweka kwake haraka sana kuelekea nyumbani kwa daktari huyo ambaye alikuwa maarufu sana hivyo hata kwake kulikuwa kunafahamika sana na watu wengi.

Akiwa kwenye gari alikuwa na mawazo mengi sana, hakuwa akielewa kile ambacho kilikuwa kimeendelea au kutokea kule ambako Bilali alikuwepo mpaka kujua kwamba daktari mkuu alikuwa hatiani kuuawa. Mwanaume alitembea na gari kwa kasi ya ajabu ambapo alitumia dakika kumi na tano tu pekee kufika sehemu ambayo ilikuwa ni nyumbani kwa daktari huyo wa hospitali kubwa zaidi ya nchi. Alipaki gari yake mbali sana na kuifunga vizuri, mwanaume alisogea kwa kasi sana na kuuparamia ukuta ambapo alirukia ndani na kutua kama paka bila kupiga kelele huku kwenye mkono wake akiwa ameishika bastola vyema sana.

Alishangaa baada ya kugundua kwamba humo ndani walinzi wengi sana walikuwa wamepigwa risasi lakini pia alishangazwa na namna daktari huyo alivyokuwa analindwa na watu wengi sana. Alikimbilia ndani haraka sana lakini alicho kiona kilikuwa kinatisha, daktari huyo alikuwa ameuliwa na binti zake wawili lakini mabinti wote walikuwa uchi na ilionekana kwamba muda mfupi tu walitoka kubakwa. Max alisikitika sana na kuwafunika na shuka ambalo aliliona pembeni yao, aliitoa simu yao na kuipigia namba ya Bilali.

“Umefanikiwa kuwapata?”
“Too late brother, wameua familia nzima”
“Ndani ya hizi dakika zisizozidi ishirini?”
“Yeah”
“Nakuja sasa hivi hapo” Bilali aliongea kinyonge sana akiwa anaikata simu.

Ndani ya dakika ishirini zingine ambazo zilikuwa zinafuatia mwanaume alikuwa anaingia ndani ya eneo hilo kwa kasi ya ajabu. Aliruka kwenye gari bila hata kuizima na kuwahi ndani lakini hakuna ambacho angeweza kukiokoa muda huo.
“Nini kinaendelea na huyu daktari ni nani?”

“Wakati nafika kule nimepishana na gari ambayo ilikuwa imetoka kwa yule mzee na baada ya kuingia ndani nimekuta hali yake ni mbaya sana huku yeye akiwa kwenye hatua za mwisho kabisa za kuyapigania maisha yake ndipo akafanikiwa kuniambia kwamba daktari huyu ndiye mhusika mwenyewe ambaye mimi nilitakiwa kukutana naye kisha akafariki. Nilishtuka kwa sababu nilipishana na watu wakiondoka na gari kwa kasi sana ndani ya eneo lile hivyo nikaamini kwamba lazima safari yao ingekuwa ni kuja kwa huyu mzee ndiyo maana nilitaka uwahi”

“Kama ni hivyo basi walikuwa ni wengi ila waligawana majukumu, hakuna namna dakika ishirini zitoshe kufika hapa kutoka Mkuranga hivyo ni lazima kuna watu ambao walikuwa huku na ndio ambao wametekeleza haya”

“Ndiyo maana nilikwambia Max hawa watu ni hatari sana na wana watu kila mahali”
“Wao walijuaje kama wewe utakuwa Mkuranga?”
“Ina maanisha kwamba kuna mtu alikuwa anatusikiliza maongezi yetu Max”
“Unamaanisha nini kusema kwamba kuna mtu alikuwa anatusikiliza?”

“Kwa sababu hili jambo hakuna mwanadamu ambaye alikuwa analijua zaidi yangu mimi na leo hii nimekwambia wewe tu sasa unahisi wamejuaje?” hiyo kauli ilimshtua sana Max, mwanaume alivuta kumbukumbu zake vyema sana baada ya kutoka kuongea na Bilali hakwenda sehemu yoyote ile zaidi ya kwake ambako alimkuta Brandina akiwa amelala kama kawaida maana walikuwa wameanza kuishi wote na hakutaka kumsumbua mwanamke wake.

Aliichukua simu yake na kwenda chooni ambako alifanikiwa kumpigia mheshimiwa raisi;
“Hello mheshimiwa”
“Ndiyo Max ni usiku sana umekutana na mwenzako?”
“Ndiyo tumefahamiana bila shida ila kuna kitu kingine kimejitokeza bosi”
“Nakusikiliza”
“Kuna mtu ambaye ameongezeka kwenye hili na Bilali ameenda kuongea nae”
“Nani huyo?”

“Nasikia anatumia alama ya kunguru anapatikana huko Mkuranga nadhani kesho nitakuwa na taarifa zote”
“Sawa kuwa makini sana kama kutakuwa na jambo lingine utanijulisha”
“Sawa mheshimiwa” mwanaume aliikata simu hiyo na kurudi kitandani kulala ambapo aliweka earphone kwenye sikio lake, hiyo ilikuwa ni kama alamu kwake pale ambapo mtu angepiga na hakutaka Brandina ajue lolote usiku huo. Alivyokuwa anafikiria yeye haikuwa hivyo Brandina hakuwa amelala bali alikuwa macho kabisa anaangalia kila ambacho kilikuwa kinafanyika humo ndani.

Max nyumba yake haikuwa salama kama alivyokuwa anahisi yeye, kumuamini mtu kupitia uchi wake kulikuwa kunaenda kuwaponza vibaya sana. Nyumba ilikuwa imetegwa vinasa sauti kila kona kiasi kwamba kila sehemu ya mhimu ambayo angeitumia kufanyia mazungumzo kilikuwepo kifaa kimoja hivyo hata wakati anatoka kwenda chooni Brandina alisikia kila kitu lakini kuna watu ambao walikuwepo upande wa pili nao walikuwa wakisikia kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea.

41 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 42
Baada ya kulitambua hilo watu hao ambao walikuwa wamesambazana kila kona waliwahi huko na kutekeleza mauaji hayo kama ambavyo Bilali aliikuta hali huko. Hata wakati ambao Bilali alimpigia simu Max kwamba awahi nyumbani kwa huyo daktari Brandina na watu wake walikuwa wakisikia kila kitu na baada ya Max kuondoka mwanamke huyo aliinyanyua simu yake na kupiga.
“The man is on his way, finish that task immediately ASAP (As-Soon-As-Possible) this man is very very dangerous, never play on his way” ilikuwa ni sentensi ya msisitizo sana kutoka kwa Brandina kwenda kwa hao watu akiwapa tahadhari juu ya huyo mwanaume wake kwa sababu hakutakiwa kabisa kuwakuta maana hakuna ambaye angetoka huko.
Kosa kubwa la Max ilikuwa ni kupiga simu kwa raisi usiku huo na kumpa hiyo siri ambayo ilitakuwa kubakia yao wao wenyewe na Bilali mpaka pale ambapo kulikuwa na ulazima wa raisi kuijua.
“https://jamii.app/JFUserGuide” Max alitamka kwa hasira sana baada ya kutoka kwenye kumbukumbu zake hizo, mawazo yake makubwa haikuwa kwa Brandina kabisa na wala hakufikiria kumuwazia huyo mwanamke jambo baya ila alihisi kwamba huenda ile simu yake ambayo alikuwa anaipiga kuna watu walikuwa wameihaki na ndio hao ambao waliweza kumsikia japo hakutaka kuliweka hilo wazi.
“Huyu kwetu angekuwa ni mtu wa mhimu sana ila nimefanikiwa kuipata cctv kamera nyumbani kwa yule mzee hivyo tutawajua tu walioenda pale maana ile nyumba ilivyokaa ni ngumu sana kujua kama kuna kamera kwa sababu zimewekwa ndani ya taa za umeme hivyo nahisi hata wao baada ya kufika pale hawakulijua hilo ila kwa hapa hatuwezi kuzipata maana ni nyumba ambayo inajulikana kuwa na ulinzi mkubwa hivyo ni lazima wangekuwa makini sana” Bilali alitamka maneno hayo akiwa anaukagua mwili wa daktari huyo.
“Kipi kinafuata kwa sasa?”
“Hatuna namna zaidi ya kutumia kile tulicho nacho ila nina imani kama tukiwapata hawa ambao walienda kwa yule mzee basi tunaweza kupata chochote chenye muunganiko na hili”
“Nadhani kesho una kazi ya kwenda kumteka gavana wa benki na wenzako hivyo hili jambo niachie mimi” Max aliongea akiwa anahitaji mkanda huo wa kamera.
“Kazi utaifanya wewe lakini nitakutumia picha na majina na taarifa zao, nina mtaalamu sana wa mitandao pale nataka nikawapekue vizuri hawa watu niwajue kiundani kisha kesho ukamalizane nao wakati naenda kwa gavana wa benki kuu” wanaume walipeana mikono kila mtu akaingia kwenye gari yake na kutoweka maana kulikokuwa kunaendelea ilikuwa ni kesi ya polisi hiyo na ingekuwa ni hatari sana kama wangekutwa eneo hilo ila mpango wa kwanza wakiwa pamoja ulikuwa umefeli vibaya sana.

Max safari yake mpaka kufika nyumbani kwake tayari kulikuwa kumeanza kupambazuka hivyo wakati anaingia ndani kwake hakumkuta Brandina zaidi ya mwanamke huyo kuacha ujumbe kwamba alikuwa amewahi kazini hivyo haikumuumiza sana kichwa ila alikaa chini na kuanza kufikiria kwa namna lile jambo lilivyokuwa limefanyika hata yeye alianza kupoteza kabisa imani na kuamini kwamba hakuna mahali ambapo palikuwa salama ndani ya nchi bali ilikuwa inahitajika kuchukua tahadhari kubwa sana kila sehemu maana watu ambao walikuwa wanawategemea kwamba wangejitokeza hadharani baada ya wao kufanya hayo matukio hawakufanya hivyo ila wao walijikuta ndio wanajulikana na kuanza kuonekana hadharani jambo ambalo lingekuwa ni hatari kubwa sana kwao.
Hakukaa sana aliamua kwenda kazini na kuomba ruhusa moja kwa moja kwa mheshimiwa raisi ili akamtafute Ariana kama alivyokuwa ameahidi kwa Siza kabla ya kifo chake. Huo ulikuwa ni moja ya mpango wa kazi yao hivyo hata raisi alikuwa anaelewa na hakuwa na ugumu wowote ule kumpa hiyo ruhusa. Hivyo mwanaume siku hiyo alipotea kazini mapema sana kwenda huko Salasala kumtafuta huyo mwanamke ambaye kaka yake alimuomba kwamba kama inawezekana basi amuoe kabisa akiamini kwamba labda mtu huyo angemlinda kwa uhakika zaidi lakini pia kwa Max hakuelewa sababu ambayo hasa ilimfanya mwanaume huyo amshauri yeye kumuoa mrembo huyo ambaye hakuwa akimfahamu.
Hakuchukua muda mrefu sana kufanikiwa kufika ndani ya nyumba ambayo alikuwa ameelekezwa ambayo ilikuwa ni namba 100 kikiwa ni kinyume cha namba yake yeye. Alikaa kwa mbali akiwa analisoma vizuri eneo hilo maana alisikia kwamba mwanamke huyo alikuwa na walinzi, alijiangalia kwenye mwili wake alikuwa amevaa kawaida sana. Jinzi na hood kisha raba chini kumfanya kuwa na mwonekano wa kiraia tu. Baada ya kusubiri kwa nusu saa nzima ndipo aliona gari ndogo inatoka ndani ya jengo lile kubwa na kuanza kutoweka mazingira yale.
Aliwasha gari yake na kuanza kuifuatilia gari ile ilikokuwa inaenda. Ilikuwa taratibu sana ila hakuwa na namna, ilitokezea mpaka mwenge akiwa nayo taratibu kisha ilienda kushika njia ya Sinza, baada ya dakika kadhaa ilienda kusimama karibu na saluni moja kubwa sana ya kike kisha akashuka mwanamke ambaye macho yake ni kama hayakuwa yakimuona vizuri akiwa na walinzi wawili ambao baada ya kushuka mmoja alienda kusimama ng’ambo na kuagiza kinywaji akiwa kama mpitaji tu kisha mmoja alipotea na gari na haikujulikana kwamba alienda wapi wakati mwanamke yule anaingia ndani. Macho yake yalibaki yameduwaa kumwangalia yule mwanamke akiingia ndani.
“Namaanisha umuoe kabisa” ile sauti kwenye kichwa chake ambayo aliambiwa na Siza siku ile ilikuwa inajirudia vizuri sana, alikumbuka mwanaume yule alimsisitiza sana yeye kumuoa mdogo wake na swali lake alikuwa anajiuliza kwanini? Wakati macho yake yanaendelea kutazama kitu ambacho alikishuhudia mbele yake hakuwa na maswali tena baada ya kumshuhudia mwanamke mrembo sana.
Urefu wa wastani, shingo ndefu kidogo ambayo haikuwa inaboa kuitazama. Alikuwa ana shepu kama kuna mtu alikuwa analipanga kwa mita na ile rangi yake ya chocolate ndiyo ilimfanya Max abaki anatabsamu tu, lilikuwa ni tukio la muda mfupi sana lakini alilifurahia mno, alitamani sana kama jambo hilo lisingeisha lakini hakuwa na namna kwa sababu mwanamke huyo alikuwa ameingia saluni tayari na bila shaka alijua kwamba ile ilikuwa ni saluni yake. Moyoni alimpongeza sana Siza kwa kumtengenezea mdogo wake mazingira mapema sana ambayo yangemfanya kutoteseka hata yeye asipokuwepo.
Alishuka kwenye gari yake taratibu akiwa ameishusha hood yake ambayo ilimfunika usoni, mwanaume ambaye alikuwa ng’ambo ya barabara alikuwa akimwangalia kwa umakini sana na wakati huo hata yule mwingine ambaye aliondoka na gari alikuwa amesharudi tayari. Hakujali akaingia ndani ya saluni ile kiasi kwamba wanawake ambao walikuwa wanafanya kazi mle walikuwa wanamshangaa maana ilikuwa ni saluni ya kike ila mwanaume hakujali.
“Samahani naweza kuongea na meneja?” alimuuliza mwanamke mmoja ambaye alionekana kukaa sehemu ambayo ilikuwa kama mapokezi. Kutokana na eneo hilo kuwa kubwa sana kulikuwa na ofisi ya bosi humo humo ndani pia hivyo hakukuwa na namna mwanaume aliruhusiwa kuingia maana alidai kwamba alikuwa pale kwa sababu ya maongezi ya kibiashara.
“Karibu” sauti nyororo ilipenya kwenye masikio yake vizuri kabisa
“Asante, bila shaka wewe ndo Ariana?”
“Mwenyewe, nikusaidie nini?”
“Wafanyakazi wako wanajua kwamba nipo hapa kwa sababu ya kibiashara ila sio hivyo kwa sababu sio biashara imenileta hapa na huwa sipendi kupoteza muda wangu hivyo nataka nikwambie ambacho kimenileta hapa lakini mazingira haya sio rafiki kabisa”
“Unamaanisha nini?”
“Nina mazungumzo nyeti sana na wewe”
“Unavyo niona unaona ni mwanamke mrahisi sana kiasi hicho?” Ariana aliongea akiwa anamwangalia mwanaume huyo usoni ambaye aliishia kusikitika tu.
“Ni haki yako kusema hivyo kwa sababu mimi ni mgeni na hatujuani ila sijaja hapa kwa sababu ya mapenzi ni maagizo kutoka kwa mtu wako wa mhimu sana”
“Unamjua mtu wangu wa mhimu sana?”
“Ndiyo maana nimekwambia kwamba hili eneo sio sahihi kwa haya mazungumzo”
“Hapa najihisi amani na kuwa salama zaidi hivyo unaweza kuongea maana hata upige kelele vipi ndani ya hiki chumba hakuna mtu wan je ambaye anaweza kukusikia”
“Ni maagizo kutoka kwa kaka yako”
“Whaaaat?”
“Siza”
“Umemfahamu vipi Siza?”
“Sisi ni wanaume kufahamiana ni jambo dogo sana nadhani ulipaswa kuwa na hamu ya kuyasikia maagizo yake na sio kutaka kujua kwamba tulijuanaje”
“Haujanijibu swali langu”
“Kwa sababu nilitumwa kumuua” mwanaume aliongea bila kupepesa macho kitu ambacho kilimfanya mremb huyo kuanza kutetemeka aliishika simu yake ya mezani baada ya kuhisi hatari mbele yake lakini mwanaume huyo alinyofoa waya za simu hiyo na kumpa ishara ya kutulia mwanamke huyo
“Shiiiiiiiiiiiiiii”
“Umemfanya nini kaka yangu shetani wewe?”
“Sidhani kama ulipaswa kufika huko japo naelewa kwa sababu ni ndugu yako na mnaonekana mlikuwa mnapendana sana”
“Yuko wapi kaka yangu?”
“Nisikilize kwanza, unajua kazi ambayo alikuwa anaifanya kaka yako?”
“Hiahusiani na haya, naomba uniambie kwamba kaka yangu ni mzima”
“Natamani kukwambia hivyo ila unatakiwa unisikilize kwa sababu nimebakiwa na dakika chache sana za kuweza kukaa hapa na vinginevyo hautapata hii nafasi tena ya kujua kwamba ni kitu gani kimetokea na ni maagizo gani ambayo amenipa” mwanaume alihema kwa nguvu wakati huo mrembo huyo machozi yalikuwa yanashuka taratibu kwenye mashavu yake maana alianza kuona kila dalili ya kupewa habari mbaya sana.
“Kaka yako nadhani utakuwa unajua kwamba alikuwa ni komando ambaye alikuwa amelitumikia taifa hili kwa moyo na uzalendo mkubwa sana lakini kuna wanadamu ambao walikuja kumbadilisha na kumfanya kuwa mashine ya mauaji kuhakikisha wanayatimiza yale ambayo wao wanayataka. Siza alinipa historia ya vitu ambavyo vilimfanya abadilike sana mpaka nilishikwa na huruma, kazi ambayo alipewa kuifanya hakuifanya kwa sababu aliipenda hapana bali kwa sababu ya mtu ambaye alimpenda sana. Kwenye huu ulimwengu watu wengi huwa wanatawaliwa kupitia udhaifu wao au kupitia watu ambao wanawapenda sana, hawa watu walijua kwamba Siza kitu pekee alicho nacho na anacho kipenda sana ni wewe hapo mdogo wake hivyo walikuwa wanakutafuta sana lakini hawakufanikiwa kukupata kwa sababu alikuwa analijua hilo mapema hivyo akakuweka mbali kabisa na maisha yake usije ukajulikana hata siku moja”
“Lakini alijua kabisa kwamba jambo hilo lingefanyika kwa muda tu na watu hao wangekuja kukupata siku moja kama angegoma kufanya nao kazi hivyo ili kuwafanya waache kabisa kukutafuta aliamua kukubali kufanya yale ambayo waliyataka wao ili kukulinda wewe hapo na rasmi akawa muuaji na kufanya kazi kinyume na serikali ilivyo mtaka awe kwa sababu yako japo hakupenda na maisha yake yakawa huko. Kwa sababu nimeamua kukwambia uhalisia wa kila kitu basi nitakwambia hata mimi ni nani pia lakini hili linatakiwa kubakia kwenye nafsi yako na kifuani kwako tu kwani kama ukija kutaja jina langu sehemu yoyote ile basi huenda hiyo itakuwa ndiyo siku yako ya mwisho kuishi kwani utapatikana kirahisi sana hivyo unatakiwa kuishi kama haunijui wala kunifahamu kabisa mimi” mwanaume alimeza mate na kuendelea maana alikuwa anamuonea huruma sana mwanamke huyo ambaye alionekana kukata tamaa sana kwa sababu stori hiyo haikuonekana kuwa na mwisho mwema huko mbele.

42 inafika mwisho.
 
Mwisho kabisa ni 88.

Ukitaka vyote kwa pamoja, unachangia 1500 tu.

0621567672 (HALOPESA)..... WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA


See you [emoji102]
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 43
“Donald Daniel ndilo jina langu, mimi nafanya kazi kwenye shirika la kijasusi la nchi hii lakini mimi na kaka yako tulikuwa ni watu wawili tofauti kiutendaji kwa sababu yeye alikuwa ni komando jeshini na mimi nipo ndani ya shirika la kijasusi. Kazi ambayo mimi nilikuwa natakiwa kuitekeleza ilikuwa ni kuanza kuwaondoa hawa watu wote ambao alikuwa anafanya nao kazi Siza kwa sababu ndio ambao wanaleta matatizo kwenye taifa hili na ndio ambao ni chanzo cha kila hali ngumu ya maisha kwenye taifa la Tanzania”
“Nilipewa kazi ya kwanza kwenda kufanya kazi hiyo kwa kuuteketeza ule ukumbi wa ALEXIOUS ARENA ambao bila shaka uliona taarifa yake kwamba ulilipuka na lile tukio mimi ndiye ambaye nililifanya la kuuteketeza ule ukumbi” maelezo yake yalikuwa ya kutisha sana hususani kwa mtoto wa kike, alimuona Ariana akiwa anameza mate kwa shida sana na kwa hofu kubwa ambayo ilionekana kuingia ndani yake.
“Wakati naenda kwenye ukumbi ule nilikutana na walinzi sita lakini mlinzi wa kwanza ambaye alikuwa getini alikuwa ni kaka yako Siza, mwanaume ambaye alikuwa pale kuhakikisha kwamba hakuna mtu ambaye anavuka na kuingia ndani ya jengo lile hi……”
“Naomba usiniambie kwamba ulimuua kaka angu tafadhali”
“Unapaswa unisikilize tena kwa umakini mkubwa sana ili ufanikiwe kujua kwamba ni kitu gani kiliweza kutokea mpaka leo nipo hapa. Kaka yako alikuwa ni mwanaume haswa maana nilivyofika pale tulikuwa tunapigana kila mtu akitaka kuwa mshindi wa kuweza kuikamilisha kazi. Mapigano yale yalitufikisha sehemu mbaya sana baada ya mimi kuukata mguu wake na kuanza kumhoji, nilitaka kujua idadi ya watu waliokuwepo pale na sababu ya ukumbi kuwa kimya ila yeye alinipa tahadhari kwamba nikimbie kwa sababu nisingeweza kutoka nikiwa hai na hapo ndipo nikataka kujua sababu ni ipi?”
“Ndio ulikuwa mwanzo wa mimi kujuana na Siza japo kwa muda mfupi tu kwani aliniambia hata yeye alitamani sana kulitumikia taifa kama mimi lakini angehatarisha maisha yako wewe hivyo aliamua kukubali kuwa msaliti wa taifa ili kukulinda wewe hapo. Siza aliniomba kama nikifanikiwa kutoka salama basi nihakikishe nakulinda wewe na k…….” mwanaume alitaka kuongea jambo lakini alisita akiwa anamwangalia mwanamke huyo kwa huruma sana.
“Sema alicho kwambia”
“Alitaka nikuoe ili niweze kukulinda japo usiliwazie sana hili maana siwezi kufanya jambo ambalo halipo kwenye moyo wako nadhani yeye aliona ni njia sahihi zaidi ya wewe kuwa salama kutoka kwa hao watu. Mimi niligoma kabisa kufanya hayo kwa sababu nilimuahidi kwamba ningemsaidia ili aje ayatimize mwenyewe ila alisisitiza sana kwamba hatuwezi kupona wote wawili ila mimi nilitakiwa kuishi kuja kukusaidia. Alinisimulia kwa namna bosi wake alivyomkata vibaya na kisu kwenye uso wake na kumtengenezea alama kubwa ambayo alikufa nayo. Hakutaka jambo kama hilo litokee kwako, akaninisitiza tena kwamba nikuoe na kuhakikisha upo salama, na jambo la mwisho kulitamka mbele yangu alitaka ujue kwamba anakupenda sana” hiyo ni kauli ambayo ilimfanya Ariana kuangua kilio, kaka yake alikuwa ndiye kila kitu kwenye maisha yake, ni mwanaume ambaye alichukua jukumu la wazazi wao kumlea tangu wazazi wao walipokufa wakiwa wadogo na ndiye huyo mwanaume ambaye alikuwa anasisitiza kwamba alikuwa anampenda sana mdogo wake.
“Kilitokea nini?”
“Wenzake walimuua” mwanaume aliingiza mkono kwenye mfuko wake na kutoa kidani ambacho alikichukua shingoni kwa Siza kwa sababu aliamini kwamba huenda mwanamke huyo asimuamini ndiyo maana alikibeba, hata yeye alikuwa nacho kwenye shingo yake, baada ya kukiona cha kaka yake alilia sana Ariana ikamlazimu Max kuanza kumbembeleza.
“Pole sana na naomba unisamehe sana mimi kwa sababu huenda kwenda pale ndiyo ilikuwa sababu yay eye kupoteza maisha lakini sikuwa na namna kwa sababu yalikuwa ni maagizo ya bosi wangu kuhakikisha tunaisafisha nchi ila naweza kukiri kwamba kaka yako ni miongoni mwa watu wachache sana duniani ambao wanatoa kila walicho nacho kwa sababu ya kuwalinda wanao wapenda, ulikuwa umepata kaka bora sana”
“Sidhani kama maisha yangu yana thamani tena, yule ndiye pekee alikuwa tumaini langu mimi, kaka yangu ndiye mtu ambaye alikuwa kwa ajili yangu wakati wowote ule ambao mimi ningemhitaji, nitamuita nani tena, nani atakuwa upande wangu tena? Tulizaliwa wawili tu pekee, yule ndiye alikuwa ndugu kwangu, yule ndiye alikuwa kila kitu kwangu? Kwanini ulishindwa hata kumsaidia kaka yangu nikamuona kwa mara ya mwisho akaniaga mdogo wake? Kwanini?” Aliongea kwa hasira sana Ariana akiwa anampiga piga Max kifuani kitu ambacho kilimfanya mwanaume ajisikie vibaya sana. Alijihisi kwamba yeye ndiye ambaye alikuwa chanzo cha hayo yote ambayo yalikuwa yanatokea.
Alichukua muda mrefu sana kumbembeleza mwanamke huyo mpaka kumuweka kwenye hali ya kawaida ambayo ingewafanya wasikilizane.
“Mimi kwa sasa nitakuwa hapa kwa ajili yako, muda wowote ambao unanihitaji unaweza ukapiga kwa hiyo namba ambayo nimekuwekea mezani nitakuja muda huo huo popote pale ulipo. Najua kwamba siwezi kuwa kaka yako wala siwezi kuiziba nafasi ya kaka yako ila angalau utakuwa na mtu wa kumpatia bega lako pale unapihisi kulia. Ila kitu cha kuzingatia hiyo namba asije akaiona mtu yeyote kwa sababu sio namba ambazo wanatumia raia wa kawaida na hata simu ya kupigia hiyo namba ni hii hapa” mwanaume alimpa simu ndogo ambayo ilikuwa ni mpya kabisa.
“Ni simu ambayo imetengezwa maalumu tofauti na zingine na ndiyo yenye uwezo wa kupiga hizo namba hivyo unatakiwa kuhakikisha kila wakati unayo lakini asije akajua mtu yeyote yule hata ambaye unahisi unamwamini sana. Kingine usimwamini mtu hata walinzi wako maana hawa watu wapo kila sehemu na hawatakiwi kujua umekutana na nani na kwanini kwa sababu wanaweza wakawa wanakuuliza sana kwa ajili ya maswali ya kujifanya wanajali usalama wako lakini kila mtu ana mahesabu yake kwenye haya maisha na wewe ukishindwa kuyapiga vyema ya kwako kuna watu watakupigia na itakuwa hatari sana kwako”
“Kwanini unahitaji niishi kwa maisha ya kukosa uhuru sana namna hiyo na sina cha kupoteza?”
“Maisha yako kuna siku utakuja kuelewa kwamba yana umuhimu kiasi gani. Unaweza ukashangaa kwamba kwanini nakupa hii tahadhari kubwa sana namna hii, unataka kujua ni nani ambaye yupo nyuma ya haya yote?”
“Ndiyo”
“Denis Kijazo”
“Unamaanisha raisi mstaafu?”
“Ndiye huyo”
“How?”
“Hauwezi kuelewa mpaka uwe ndani huko, raia wengi wameathiriwa sana na ujinga wa mitandao kwahiyo viongozi wanaitumia njia hiyo kuwapumbaza wanavyotaka wao ila mambo ambayo yanaendelea huko yanatisha sana. Nimekupa hii taarifa kwa sababu najua itakupa hofu ya kuyalinda maisha yako ili uelewe kwamba maisha yana umuhimu kiasi gani”
“Kwanini usimuue kama ni yeye?”
“Unaelewa namna ya kumfikia?”
“Hapana”
“Yule ndiye mtu mwenye nguvu zaidi ndani ya taifa hili hivyo kuweka naye mashindano ni kubeti maisha yako ila hakuna namna tumeamua kulifanya hili na tutalitekeleza kwa namna yoyote ile hata kwa kuyatoa sadaka maisha yetu”
“Wewe unafanya kazi na nani?”
“Unataka kumfahamu?”
“Ndiyo”
“Raisi wa Tanzania”
“Ndiye bosi wako?”
“Ndiyo”
“Hapana”
“Unahisi wewe unajua zaidi yangu?”
“Sijamaanisha hivyo”
“Ndiyo maana nimekwambia kwamba kuna siku utakuja kugundua kwamba maisha yako ni ya thamani sana”
“Nashukuru sana kwa kila kitu”
“Kuna jambo moja ambalo inabidi uliweke kichwani kwako”
“Lipi?”
“Haya mazungumzo leo mimi na wewe hayajawahi kufanyika na hii siku haijawahi kutokea. Hili ndilo jambo la mhimu zaidi”
“Haijawahi kutokea kwa namna gani wakati mimi na wewe tupo hapa saivi?”
“Unaweza ukachelewa kunielewa ila unatakiwa kujua hivyo, tuliyo yaongea leo fanya kama hatujawahi kuyaongea kwa ajili ya usalama wako na hakuna mtu zaidi yako ambaye anatakiwa kujua kwamba kaka yako amekufa. Haijalishi hili jambo litakuumiza kiasi gani ila hakuna mtu anatakiwa kabisa kujua hili wala kuwa na taarifa juu ya hili na hautakiwi kuonyesha utofauti wowote ule hata mimi nitakapotoka hapa yaani wewe kuwa kawaida tu kama siku zingine kabla ya hii siku”
“Bado sikuelewi mbona unaniacha njiapanda?”
“Ariana kuna kazi ya mhimu sana ambayo natakiwa kuifanya muda huu hivyo mimi naondoka ila zingatia sana niliyokwambia na kama ukihitaji msaada wangu wowote nadhani nimekwelekeza namna ya kunipata” mwanaume alikuwa akiongea huku akiwa amefika mlangoni.
“Subiri kwanza” hakuna kilicho msimamisha, alitoweka hilo eneo huku walinzi wakiwa makini sana lakini hakuna walicho fanikiwa kukiona au kukijua zaidi ya kuona hood tu kichwani. Baada ya kuondoka mfanyakazi wa Ariana aliwahi kwenye ofisi ya bosi wake kujua kama kuna usalama na bosi wake alimhakikishia kwamba kulikuwa salama ni mazungumzo ya biashara tu yalikuwa yanafanyika japo mwanamke huyo hakuonekana kuwa salama kama alivyokuwa anadai yeye. Aliambiwa mambo makubwa sana ambayo yaliacha kovu na maumivu makali sana kwenye moyo wake lakini alitakiwa kuishi kana kwamba hakuna kitu ambacho kilitokea, kweli alikua na akayaona.

43 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 44
Usiku ambao daktari mkuu wa mhimbili aliuawa ndio usiku ambao wanaume sita kutoka Arusha walikuwa wanaingia ndani ya jiji la Dar es salaam. Wanaume hao walipandia ndege kutoka KIA na kutua ndani ya JNIA majira ya usiku, wote walikuwa kwenye mavazi ya kutisha sana na ya kazi haswa kitu ambacho kiliwafanya wahudumu wa ndege kuwa na maswali mengi sana kuhusu watu hao lakini walidai kwamba walikuwa ni wafanya biashara wa madini na kwa sababu walitoka kazini moja kwa moja ndiyo maana walikuwa kwenye hali kama hiyo ila haikuwa ikihusiana na jambo lolote lile na wao kuwa na shida hapo ambapo walikuwa wamefika.
Hakukuwa na shida sana kwa sababu walikuwa na vithibitisho vyote hivyo rasmi wakawa wameingia ndani ya jiji, walikuwa wakiongozwa na mwanaume ambaye alikuwa anaitwa Ted na ndiye alikuwa kiongozi wao.
Wanaume hao safari yao moja kwa moja ilikuwa ni kuelekea kwa bosi wao ambaye ndiye alikuwa kila kitu na kuwafanya waishi maisha ambayo walikuwa wanayataka wao. Saa zima liliwafanya wafike ndani ya jengo kubwa la kifahari la Denis Kijazo ambaye aliwapokea kwa furaha sana kwa sababu alikuwa akimuamini sana mwanaume huyo Ted ndiyo maana baada ya kuona kwamba kuna mambo hayakuwa yakienda vizuri aliamua kumuita mwenyewe aje kumaliza kazi bila shaka.
“That’s my boy” aliongea kwa kicheko akiwa anamkumbatia Ted kwa furaha na kuwasalimia vijana wengine ambapo kwenye hilo kundi pia Kenedy alikuwepo. Baada ya kuwaona vijana wote ambao walikuwa ni watu wa kazi haswa alihitaji kubaki na kijana wake ambaye alikuwa anamuamini sana kuliko mtu yeyote yule.
“Biashara inaendaje huko?”
“Kila kitu kipo sawa bosi kama kilivyokuwa kimepangwa”
“Vipi uzalishaji wa sumu unaongezeka? Maana ile ni sumu ambayo inauzwa bei ghali sana hivyo inatakiwa tuwe na mzigo wa kutosha”
“Rasilimali zake ni adimu sana lakini yule mwanasayansi anafanya kazi kubwa sana hivyo naweza kusema kwamba kila kitu kinaenda vizuri”
“Safi, sasa mambo huku yameharibika kiasi fulani, mambo yanaenda kwa namna ambayo sipendi mpaka imefika hatua washirika wangu hawaniamini tena jambo ambalo ni la hatari sana maana ukifikia sehemu ya kuanza kuwakwaza watu ambao wanatakiwa kukulinda na kuwa na wewe hasa unapokuwa kwenye matatizo basi hiyo ni ishara ya mwelekezo mbaya mno kwenye haya maisha yetu ambayo tunayaishi. Watu wananisaliti Ted, hata wale ambao niliwaamini na kuamini kwamba nitawamudu wamegeuka kuwa mbogo kwangu jambo ambalo limenipa hasira sana na kilichokuwa kinaniumiza ni kutojua kwamba ni nani na nani ambao walikuwa wapo upande wetu na wapi walikuwa kwao na ndiyo maana jambo hili limechukua muda mrefu sana kuweza kufanyika hivyo nimekuita wewe ili kila kitu ukiweke sawa haraka sana kabla haya mambo hayafika mbali”
“Nakuelewa kiongozi, unataka nienze na kazi gani?” mheshimiwa akiwa anajiandaa kumjibu Ted swali lake, simu yake ilianza kuita kwa fujo sana, baada ya kuangalia simu hiyo aliona mpigaji ni mkurugenzi Philipo Tibaigana hivyo akaipokea.
“Hello mheshimiwa”
“Nakusikiliza”
“Tumeipata kete nyingine ambayo inatufanya tuutawale mchezo”
“Malizia maelezo yako”
“Kuna mzee Mkuranga huko ambaye ana taarifa za siri kuhusu mtu mwingine ambaye mheshimiwa Francis Mboye alikuwa amemuandaa lakini hajulikani hivyo kupitia mzee huyo tunaweza kumjua mtu huyo mwingine ambaye anatakiwa kupatikana haraka sana kabla wao hawajampata”
“Good, si unaweza kulishughulikia?”
“Hapana tupo nje ya muda kwenye hili cha kufanya tuma watu ambao upo nao kule hata ambao wapo wilayani wakaikamilishe kazi ya kumhoji haraka sana kisha wamuue na kutoweka eneo la tukio kwani kuna mtu anawahi huko hivyo hatakiwi kufika kabla ya wao kumaliza kazi na kama wakifanikiwa kumjua huyo mhusika mwingine basi wapige simu haraka sana kuweza kuripoti anapatikana ili ambao wapo karibu pia waweze kulishughulikia hili. Baada ya hapo mimi kuna vijana ambao nitawatuma maeneo yote kwa ajili ya kwenda kufuta ushahidi wote”
“Good job Philipo” mheshimiwa alipokea taarifa ambao ilionekana kumfurahisha sana kisha akaikata simu hiyo na kutabasamu. Simu ilipigwa haraka sana kwa watu husika na ndio wale ambao walienda kutekeleza matukio kama ambavyo watu hao waliyapanga kwenye simu.
“Kazi yako wewe ni kuwatafuta hawa watu ambao aliwaacha Francis Mboye, inasemekana kwamba wapo watatu tu na kundi lao linaitwa DRAGON BOYS. Hawa wakifa nadhani atakuwa hana msaada mwingine na wakati huo huo tunamuua makamu wa raisi baada ya hapo raisi anakufa na kesi anabebeshwa bwana mdogo kisha naye anauawa na kesi inaishia hapo. Halafu yule mwandishi ataandika makala ya kuusifia utawala wangu ambao umepita na kumchafua huyu changudoa kitu ambacho kitafanya wananchi waniamini na kunisikiliza kwa kila kitu wakati ambao waziri mkuu atakaimu madaraka kwa muda lakini ndiye atakuwa raisi wa moja kwa moja kwa sababu mimi ndiye nitakuwa mtoa maoni wa kuaminika. Hiyo makala piga simu kesho ianze kuandikwa haraka sana”
“Sawa mkuu, watu hao mna taarifa zao zozote?”
“Hawajulikani sana lakini kuna mmoja tuna picha yake, nadhani utakuwa mwanzo mzuri”
“Hilo lipo chini yangu kuanzia sasa na sio muda litakuwa limeisha mheshimiwa”
“Nakuamini Ted, go and make me proud”
“Absolutely sir” mwanaume alitoa heshima kwa kiongozi wake na kutoweka hapo maana maagizo alikuwa kayapata na kilichokuwa kimebaki ni utekelezaji tu wa kile ambacho aliambiwa na bosi wake.

Usiku ulipo ingia Max aliamua kupotea kimya kimya kwa mara nyingine na safari yake ilikuwa ni kuelekea SUPERDOME Masaki ambao ulikuwa ni ukumbi mkubwa na wa kisasa sana kwa ajili ya matukio na sherehe mbalimbali zilikuwa zikifanyika hapo. Alienda huko kwa sababu alipewa taarifa kwamba ndiyo sehemu ambayo alikuwa anaweza kuwapata watu wake kwani kulikuwa na sherehe na walikuwa ni watu ambao walikuwa wanaihusudu sana starehe. Taarifa za watu hao ambao alikuwa anawafuata huko alikuwa amepewa na Bilali baada ya kwenda kuzipitia video za marejeo ambazo alifanikiwa kuzipata Mkuranga.
Alikuwa na picha zao ambapo walikuwa ni wanaume watatu na taarifa ambazo alipatiwa ni kwamba usiku huo walikuwa ushuani huko kuponda raha kwani hawakuwa na shida ndogo ndogo kwenye maisha yao. Aliingia ndani bila kutambulika na mtu yeyote yule baada ya kumpatia pesa mlinzi mlangoni. Mwanaume alikuwa anaangaza kila sehemu ndani ya sehemu hiyo mpaka alipofanikiwa kuwaona watu hao wakiwa wamejihifadhi kwenye moja ya kona wakiwa watatu vile vile lakini pia wakiwa na warembo ambao walikuwa wanaburudika nao. Alitoa picha ambazo alikuwa nazo na kuwaangalia kwa umakini sana, alijiridhisha kwamba walikuwa ni wenyewe na hakufanya makosa kwenye hilo.
Alikaa maeneo ya karibu kidogo na walipokuwepo kisha akaagiza kinywaji na kuendelea kuangalia namna watu walivyokuwa na heka heka nyingi mle ndani. Baada ya muda kidogo kupita alimuona mwanaume mmoja akiwa anajikokota kwenda chooni, ile kwake ilikuwa ni nafasi ya dhahabu na hakutakiwa kabisa kucheza nayo. Baada tu ya mwanaume yule kuingia eneo ambalo lilikuwa linaelekea chooni hata yeye alinyanyuka na kuanza kutembea kwa kuyumba yumba kuelekea chooni.
Kwa namna alivyokuwa anatembea ilikuwa ni ngumu sana kwa mtu wa kawaida kumtengenezea hisisa mbaya maana alionekana kuwa mlevi haswa, alienda kudondokea kwenye meza ya wale wanaume ambao waliishia kumcheka naye akatabasamu na kuendelea kuyumba yumba kwenda chooni. Baada ya kuvuka ile sehemu alisimama akiwa vizuri kabisa kisha akaingia chooni na baada ya kuona mwanaume yule yupo mwenyewe akafunga mlango.
“Unafanya nini?” aliuliza yule mwanaume akigeuka kwa hasira baada ya kuona kuna mtu kaingia na kufunga mlango. Hakujibiwa chochote zaidi ya Max kuanza kumsogelea karibu na alipokuwepo.
“Kuna kitu gani ambacho mmekigundua jana kilichofanya mpaka Denis Kijazo akawa anaogopa sisi kumuwahi yule mzee?”
“Ndo wewe kumbe? Tumeahidiwa pesa nyingi sana tukipeleka hata kichwa chako” mwanaume huyo aliongea kwa kubwatuka huku akishika kwenye kiuno chake kuitoa bastola akihisi huyo ndiye alikuwa kijana wa Francis Mboye bila kujua kwamba huyo walikuwa wanamhitaji akiwa hai bado. Akiwa anataka kulitekeleza zoezi lake hilo alipishana na kisu ambacho kilizungushwa kwa nguvu na wakati anakaa sawa mwanaume alikuwa ameshamfikia kwa chini.
Alimnyanyua kwa mabuti makali ambayo alisimama nayo, yalimrushia mwanaume yule kwenye masinki wakati anataka kunyanyuka alipokea risasi za miguu akabaki anagala gala tu chini.
“Unaweza ukanijibu nikupe nafasi ya kuishi”
“Go and fu**k your self” kauli yake ilimponza baada ya kumiminiwa risasi mbili za paja.
“Sina ambacho nakijua lakini moja kati ya watu ambao unawaamini sana sio mmoja wenu?”
“Ipo hivyo, mmoja kati ya watu wenu sio mtu wenu ni msaliti na huenda ni moja kati ya watu ambao unawaamini sana”
“Nambie ni nani?” alimuuliza kwa ghadhabu mtu huyo lakini kwa bahati ambayo haikuwa yake ni kwamba mwanaume huyo alianza kutokwa na povu mdomoni baada ya kumeza kidonge ambacho kilikuwa kwenye ulimi wake.
“https://jamii.app/JFUserGuide” alitamka akiwa anasimama na kuzunguka humo ndani, ilibidi atoke haraka sana kuwawahi wale ambao aliwakuta pale nje wasije kupotea kwenye macho yake lakini baada ya kukaribia alikutana na jambo ambalo lilimshangaza sana. Watu walikuwa wanakimbia kila sehemu hovyo huku wengine wakiwa wanaomba msaada kitu ambacho kilimlazimu yeye kuchungulia walipokuwa wamekaa wale wanaume. Wote walikuwa wamekufa kwa kupigwa risasi, jibu rahisi ni kwamba walikuwa wanafuatiliwa na watu wao wenyewe ili wasije kuropoka siri zao popote pale.
Akiwa ameduwaa kwa mbali aliona kuna mwanaume akiwa kaunta amevaa mavazi meusi, alikuwa anamlenga alipo, alilazimika kujivuta haraka sana alipishana narisasi ambazo zilikuwa zimerushwa mfululizo. Alirukia upande wa pili akiwa anapiga risasi kwenye mita ambayo aliiona juu kabisa ya ukuta na umeme ukakatika humo ndani, hakutaka kuzubaa alitoka na watu ambao walikuwa humo ndani kwa sababu hakujua kwamba watu hao walikuwa wangapi hivyo hata angesimama kusema anataka kupambana nao angekuwa anahatarisha maisha yake bila sababu za msingi.

44 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 45
Baada ya kutoka Masaki usiku wa mapema na kuacha matatizo makubwa ambayo yaliwafanya polisi kufika ndani ya eneo hilo na habari hiyo kuanza kusambaa sana kwenye mitandao ya kijamii, usiku huo huo pembezoni mwa bahari ndiko ambako walikutana kwa ajili ya kikao. Kikao ambacho kilikuwa kinaongozwa na mheshimiwa raisi mwenyewe na alikuwa ameongozana na Brandina kabisa pamoja na walinzi wengine kuhakikisha mheshimiwa anakuwa salama wakati wote.
Eneo la kukutania watu hao lilipangwa na Bilali kama alivyokuwa ameahidi kwa sababu aliamini kwamba kulikuwa na watu ambao walikuwa ni wasaliti ndiyo maana alihitaji kuicheza kadi yake ya mwisho ili kuhakikisha kama mawazo yake yapo sahihi au vipi. Ni kikao ambacho kilikuwa ni mjumuiko wa watu wengi kidogo akiwepo makamu wa raisi, waziri mkuu, Max mwenyewe, DRAGON BOYS Pamoja na mheshimiwa raisi Teodensia Mpanzi na mlinzi wake mkuu Brandina Elkana.
“Max unaweza kutueleza kwamba umefikia wapi kwenye kazi ambayo ulienda kuifanya?” raisi alifungua mazungumzo ambayo yalitakiwa kufanyika hapo.
“Kwa bahati mbaya sana kuna watu wamewaua kabla sijawatia mikononi”
“Watu wamewaua?”
“Ndiyo mheshimiwa habari hiyo imesambaa sana kwenye mitandao”
“Umefanikiwa kuwajua watu hao?”
“Hapana ilikuwa ni gjhafla sana na sikujua walikuwa wangapi hivi niliwahi kutoka lile eneo”
“Kwamba kuna mtu alikuwa anajua kwamba wewe utaenda huko?”
“Sijajua mheshimiwa”
“Ok, nipeni taarifa ya huko Mkuranga”
“Kila kitu kimeharibika kwani kuna watu ambao waliwahi eneo la tukio na kuua familia zote mbili”
“Unamaanisha kwamba hawa watu ambao umewakosa leo ndio ambao ulikuwa mhimili mkubwa kuweza kuyajua haya?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Makamu wa raisi unaweza ukawa na la kuchangia juu ya hili?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Uwanja ni wako” raisi alikuwa anaongea huku macho yake yakiwa kwa Bilali. Alikuwa anamkadiria sana mwanaume huyo na hammalizi.
“Familia yangu imepotea mheshimiwa”
“Whaaaaat?”
“Ndiyo, leo jioni wakati narudi sijamkuta mtu nyumbani”
“Si ulisema kwamba umeihamishia sehemu salama?”
“Mimi nilidhani hivyo mheshimiwa lakini sikuwa sahihi”
“Kwahiyo nini kinaendelea mpaka sasa?”
“Nimepigiwa simu ya vitisho”
“Aliyekupigia amesemaje?”
“Anataka nitoke hadharani kukupinga wewe”
“Na usipofanya hivyo?”
“Sitaiona familia yangu”
“Na wewe umeamua nini?”
“Naumia sana lakini nimeshindwa kukusaliti mheshimiwa” umri ulikuwa umeenda kidogo lakini alikuwa anatoa machozi kiasi kwamba kila mtu alikuwa anamuonea huruma ndani ya chumba hicho.
“Umefanya jambo la maana sana, familia yako itapatikana mimi kesho nitaenda kuongea na Denis Kijazo mwenyewe”
“Mheshimiwa ni hatari sana”
“Hawezi kuniua nikiwa kwenye mazingira yake kwa sababu damu itakuwa kwenye mikono yake hivyo kwenda kwake ndiyo sehemu salama zaidi kwangu”
“Unahisi ni jambo sahihi hilo kulifanya?”
“Ndiyo, viandaliwe vyombo vya habari na zisambazwe taarifa kwamba kesho naenda kumtembelea mtangulizi wangu na nadhani wananchi wataipenda hiyo”
“Sawa mheshimiwa tutafanya vile unataka wewe”
“Makamu bado haujanipa mchango wako juu ya hili”
“Nadhani ni muda wa kumuua huyu shetani” Bilali alitikisa kichwa kuonyesha ishara ya kukataa, mzee huyo hakutakiwa kuendelea kuongea kwa sababu alikuwa kwenye simanzi nzito sana wakati huo angeishia kuongea vitu kwa mihemko tu. Raisi alimgeukia waziri mkuu ambaye muda wote alikuwa anawasikiliza kwa umakini sana akiwa ametulia.
“Mimi nadhani kwamba kabla hata ya kumuua yeye tunatakiwa kujua sababu kubwa zaidi ambayo inamsukuma yeye kufanya haya mambo hapo ingekuwa ni kazi ndogo sana kuja kumalizana naye”
“Hilo linaweza kufanyika vipi?”
“Tulitakiwa kuwa na mtu ambaye yupo naye karibu na huyo ndiye mtu ambaye angetumika kuweza kumdhoofisha kwa kutupatia kile ambacho tunakihitaji kisha sisi tungemaliza kirahisi sana”
“Hili jambo nikikukabidhi mwenyewe nitakuwa nimekosea?”
“Hapana mheshimiwa itakuwa heshima kubwa sana kwangu”
“Basi lifanyie kazi haraka sana kisha unipe majibu bila kuchelewa”
“Sawa mheshimiwa” waziri mkuu aliongea jambo fupi lakini lilionekana kuwa na umuhimu mkubwa sana.
“Kama hamtajali naombeni waziri mkuu na makamu wa raisi mkapumzike na asanteni sana kwa ushirikiano wenu mkubwa ila kwa sasa ni muda wa kumpa majibu ya maswali juu ya kazi ambayo alitupa na haya ni mambo binafsi hivyo tunaomba chumba viongozi wangu” makamu wa raisi hakuwa na shida aliaga maana hakuwa sawa ila raisi alisisitiza kwamba mtu huyo aongezewe ulinzi lakini waziri mkuu alichukia sana na kumwangalia Bilali kwa macho makali sana ambapo watu hao macho yao yaligongana. Aliwapa wote mikono kisha alitoka mpaka nje ambapo alikuwa amesimama Brandina, alimkonyeza na kutabasamu kisha akaondoka.
“Unaweza ukanipa sababu ya kufanya haya yote?” raisi aliuliza
“Tunaishi na msaliti miongoni mwetu mheshimiwa na nadhani tumefanya makosa makubwa sana kuwaamini hawa watu mapema sana namna hii” Bilali alijibu akiwa anazunguka.
“Lakini ni watu safi sana hata mzee aliwapendekeza hawa” raisi aliongeza
“Kuwapendekeza sio tatizo lakini watu wanabadilika mheshimiwa”
“Ok, unaweza kutueleza hicho ambacho ulikuwa umeshindwa kukiongea?”
“Tumempata gavana wa benki kuu”
“Unamaanisha?”
“Nipo nae humu humu ndani”
“Are you serious?”
“Yes, ila sikutaka hawa watu wajue juu ya hili”
“Why?”
“Kuna kitu nataka nihakikishe. Muda huu tuhame nyumba haraka kisha walinzi wako wote wakaguliwe na hakuna hata mmoja ambaye anatakiwa kuruhusiwa kuwa na simu ndipo utaamini kile ambacho nakwambia”
“Bilali bado sikuelewi unataka kuniaminisha nini?”
“Bosi Bilali anacho kiongea ni ukweli hata mimi kusema kwamba kule sijakutana na wale watu nimedanganya tu”
“What are you talking about?”
“Ni kwamba nimewakuta wale watu na kukutana na mmoja ambaye nilimbana sana akanipa ukweli kwamba miongoni mwetu kuna mtu ni msaliti, nilimbana sana aweze kunitajia jina la huyo msaliti lakini nilishindwa kwa sababu alikuwa na kidonge cha sumu ambacho alikimeza akapoteza maisha. Wakati natoka pale nikadili na wale wengine nimekuta wameuawa kwa risasi na muuaji baada ya kuniona akaanza kunishambulia ndipo nikatoweka pale maana ingekuwa ni hatari sana kama ningeonekana”
“Ohhh shiiit, kamera hazijaipata sura yako?”
“Hapana wakati naingia pale nilizima kamera zote hivyo wasingeweza kunipata”
“Huyu atakuwa ni nani?”
“Mheshimiwa tuondoke kisha utayathibitisha maneno yangu”
“Na huyo mpuuzi umemficha wapi?”
“Huyu amezimishwa yupo nje kwenye buti ya gari”
“Ok twendeni huko ambako mnahisi ni sahihi kuwepo kwa sasa” baada ya maelezo hayo walitoweka hapo na kwenda umbali wa dakika kumi tu ambapo kulikuwa na jumba lingine la kifahari ambalo Bilali alikiri kwamba lilikuwa jumba lake. Waliingia humo ndani na kuketi wote kwenye chumba kikubwa mbele kukiwa na skrini kubwa sana. Nje ya jumba hilo Brandina alikuwa akihangaika sana kuangalia saa yake lakini hakuwa na cha kufanya maana vifaa vyote vya mawasiliano walikabidhi wakati wanatoka walikokuwa mara ya kwanza ikiwa ni amri ya raisi na hakuwa na cha kufanya ila alionekana kama mtu ambaye alikuwa anataka kutoa taarifa mahali juu ya kile ambacho kilikuwa kinaendelea.
Wakiwa hapo walikuwa wanaangalia moja kwa moja kwenye ile nyumba ambako walikuwa wametoka kwani nyumba ile Bilali alitega kamera kila mahali. Zilipita dakika tano kukiwa kimya lakini baada ya muda mfupi tu kuna wanaume wa kazi wakiwa kumi na tano waliingia lile eneo kwa kasi sana. Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake raisi alikuwa anaangalia moja kwa moja jinsi ambavyo watu wa kazi huwa wanafanya kazi hizo hususani wanapokuwa wanavamia mahali, alijikuta anaogopa sana.

45 inafika mwisho.
 
Mwisho kabisa ni 88.

Ukitaka vyote kwa pamoja, unachangia 1500 tu.

0621567672 (HALOPESA)..... WhatsApp

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

FEBIANI BABUYA

See you [emoji102]
 
Jumamosi jioni au jumapili asubuhi sana mzigo huu unaachiwa kwa softcopy.
FB_IMG_1716481144225.jpg
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: +18

UTANGULIZI................

SURA YA 1.
MIMI NI NANI?


MZIZIMA,
Mvua zilizokuwa zimeambatana na upepo mkali zilikuwa zikiendelea kulisumbua jiji la bandari ya Salama, jiji la kale ambalo watu wa zamani walilijua kama mzizima. Mvua hizo ziliwafanya Tanesco wapate kisingizio kizuri kabisa cha kuweza kuukata umeme ambao ulikuwa unaimulika mitaa mbali mbali na kuonyesha umaridadi wake.

Kwenye chumba kimoja maeneo ya Kigogo Mwisho alionekana ndani mwanaume mmoja, kuonekana kwake kulidhihirisha wasiwasi na hofu ambayo ilikuwa imeugubika uso wake na simanzi ikauzidisha upole wa ile sura yake ambayo haikuwa ikionekana vyema huenda kwa sababu ya kukosekana kwa mwanga. Uso wake ulitoa taarifa ya kwamba maisha yake hayakuwa salama ndiyo maana alikuwa hana amani wala kuwa na utulivu wa kutosha, alikuwa ameketi kwenye mkeka ambao ulikuwa umetandikwa chini kwenye chumba kidogo cha hovyo ambacho kiligubikwa na joto kali kwa kukosa nyenzo mhimu za kupambana na joto. Sanjari na hilo udogo wa chumba nao ulichangia kwa kiasi kikubwa.
Mwanaume yule alijizoa kutoka kwenye ule mkeka na kusimama, alijisogeza kwenye dirisha dogo ambalo lilifunikwa kwa tambala kuu kuu lilolokuwa chafu, alifunua kidogo pazia hilo ili kujua kama nje kulikuwa na chochote lakini hakufanikiwa kuona jambo lolote lile zaidi ya radi ambazo zilikuwa inamulika kila wakati kwenye kiza totoro kilicho lifanya jiji hilo kuwa na utulivu ambao sio kawaida yake. Alirudi tena kwenye mkeka wake akiwa anatweta kwa jasho kutokana na joto kali huku akiwa anajifuta jasho hilo kwa kutumia shati lake ambalo lilikuwa mwilini.

Akiwa anaendelea kuhema kwa hesabu maalumu ambazo alizijua yeye na nafsi yake, alihisi kama kuna kitu kinamtekenya kwenye mfuko wake wa suruali, hapo ndipo akakumbuka kwamba kwenye mfuko huo alikuwa amehifadhi kisimu kidogo ambacho alikuwa amekifunga funga kutokana na uchakavu ambao kilikuwa nao. Aliipokea haraka simu hiyo ambayo namba yake haikuwa na jina na kuiweka kwenye sikio lake.
"Ondoka haraka kwenye hilo eneo, una dakika kumi na tano tu za kuyaokoa maisha yako, vinginevyo unakufa" sauti ya upande wa pili iliongea kwa msisitizo kisha simu ikakatwa. Alibaki kwenye mshangao mithili ya mtoto ambaye alikuwa ametelekezwa na mama yake mzazi huku akiamini kwamba alikuwa na usalama wa kutosha kwa sababu mama yake alikuwa karibu.

Alijizoa kivivu huku moyo wake ukiwa unamuenda mbio, alisogea kwenye ule mkeka na kuukunja upande wa juu ambapo eneo hilo kulikuwa na udongo ambao ulijazwa, aliufukua haraka haraka na kukitoa kimfuko cha plastiki. Alikifungua na ndani yake kulikuwa na pesa za kigeni maarufu kama dola huku pembeni yake kukiwa na bastola moja pamoja na kisu kimoja. Alizoa pesa haraka haraka na kuzitupia kwenye mfuko wake, bastola akaipachika kwenye kiuno chake huku kisu akikishika mkononi.
Alipafukia kama alivyokuwa amepakuta mwanzo na kuurudishia ule mkeka kwa mara nyingine tena kisha akanyanyuka na kuanza kutoka nje. Baada ya kufika mlangoni alikuwa amepoteza dakika tatu tayari, aliufungua mlango taratibu kisha akaangaza kila upande ili kuona kama angefanikiwa kuona kile ambacho alikuwa ameambiwa kinaenda kutokea lakini hali ilikuwa shwari kabisa hivyo akajitosa kwenye maji ya mvua na kuanza kutembea haraka haraka ili kuelekea kilipokuwepo kituo cha magari.
Alikunja kona ya kwanza akiwa anapishana na sauti ya kudondoka kwa maji, akakutana na uwazi ambao ulikuwa na mita kama kumi na tano, sehemu ambayo ilimshtua kidogo kwa sababu moyo wake ulimuenda mbio isivyokuwa kawaida. Alitembea haraka haraka ili aweze kulivuka eneo hilo salama huku kwenye mkono wake kisu akiwa amekishikilia vyema, ila hakupiga hatua hata kumi akahisi kabisa kulikuwa na harufu ya mtu ndani ya eneo hilo hali ambayo ilimfanya kupunguza mwendo na kumfanya aanze kutembea taratibu.

Aligeuka kuangalia nyuma yake, hakuona kitu zaidi ya anga ambalo lilikuwa linamcheka hivyo akahitaji kuendelea na safari yake tena lakini nafsi iligoma kabisa, moyo wake ulikuwa mzito na hakuwa mtu wa kuupuuzia huo mlango wake wa sita ambao ulikuwa wa hisia. Alishuka chini kama anajilaza kifudi fudi lakini hakufika chini kwa sababu ule mkono wenye kisu ndio ambao ulitangulizwa kisu ndicho kikafika chini na hata baada ya kufika pale chini kwa mkono wake hakuzubaa, alijigeuza kwa sarakasi kwa kuuviringisha mwili wake hali ambayo ilimfanya atue pembeni.

Mahesabu yake yalikuwa sahihi kwa sababu wakati anashuka pale chini, juu yake kilipitishwa kisu kutoka kwenye mikono ambayo ilionekana kuwa na nguvu kubwa na lengo la mtu huyo halikuonekana kuwa kumzimisha tu bali alikuwa anahitaji kuondoka na nafsi yake moja kwa moja. Hata baada ya kutua pale chini hakuzubaa kwa sababu alijua huenda akampa adui nafasi nzuri ya kuweza kufanikisha jambo lake kitu ambacho hakutaka kiweze kutokea kwake yeye ndiyo maana alijiviringisha kwa sarakasi na kutua pembeni. Kujiviringisha kwake kulimfanya kulikwepa buti zito la ngozi ambalo lilikuwa limeshushwa na mwanaume ambaye alionyesha kuwa na uhasama naye mkubwa mithili ya mtu ambaye alimuibia mkewe, buti hilo kama lingefanikiwa kutua kwenye mgongo wake basi asingefanikiwa kutembea tena kwenye maisha yake yote.

Kiza kinene kilimfanya mwanaume huyo ashindwe kumtambua mwanaume ambaye alikuwa amekuja mbele yake ila mwanga wa radi ulimumulika mtu huyo ambaye bila shaka alikuwa ni mweusi usoni akiwa kwenye ghadhabu isiyo pimika. Aliukunjua mkono wake ambao ulikuwa na kisu kwa sababu alijua kwamba anatakiwa kufa wakati huo asipo yatetea maisha yake, hakupata muda wa kutosha wa kupiga tathmini juu ya uwezekano kama alikuwa anamfahamu mwanaume huyo kwa sababu alikuwa anamjia kwa kasi pale alipokuwepo huku mabuti yake yakiwa yanapiga piga kwa nguvu kwenye maji ambayo yalikuwa yametuama chini.
Miguu yenye nguvu miwili ilikuwa inakuja kwenye uso wake, kama bahati tu, tope lililokuwa chini lilimsaidia kuteleza kidogo na kurudi nyuma hali ambayo iliifanya miguu hiyo kumkosa na badala yake akarushiwa maji machafu usoni ambayo yalimuingia kwenye macho. Mtetemo wa ardhi aliusikia vyema baada ya ile miguu ambayo ilimkosa kutua chini na kukita kwa nguvu. Aliyafumbua macho yake haraka ili kujilinda, alichelewa kwenye mahesabu, ngumi ilizama kifuani na kumfanya ahisi kama kuna mtu alimpasua na shoka.

Ndiyo kwanza kabisa tunaufungua utangulizi wa simulizi hii mpya ya NAFSI ZILIZO TELEKEZWA. Hii ni simulizi bora zaidi kati ya simulizi zangu tisa za kijasusi ambazo nimeziandika.
Ndani yake utakutana na stori kali zilizo simama, utakutana na watu kutoka mataifa makubwa na mashirika makubwa ja kijasusi duniani hususani IRINA ESPANOVICH, mwanamama kutoka ndani ya KGB ambayo alikuja akaiweka Tanzania kwa mkono wake baada ya kutoroka nchini mwake akiwa anatafutwa kwa nguvu na Moja ya mashirika makubwa duniani, shirika la kijasusi la Uruai KGB kwa kuwasaliti wenzake na kufanya Umoja wa nchi za kisovieti kudondoka mwaka 1991.

Kutoroka kwake ukawa mwanzo wa kuanzisha jamii ya hatari ndani ya TANZANIA ambayo ilifahamika kama LUNATIC SOCIETY. IRINA alifanikiwa vipi kuwakimbia watu wa kutisha hao wa KGB kwa kuwasaliti mbele ya CIA halafu akafanikiwa kufika Tanzania?
Hiyo jamii ambayo aliianzisha ilikuwa inajishughulisha na nini hasa na mwisho wake ulikuwaje?
IRINA ni nani hasa na alifanya usaliti wa namna gani mpaka KGB wamsakame kila kona ya ulimwengu huku yeye akipotelea Tanzania?

Hizo NAFSI ZILIZO TELEKEZWA Zina maana ipi na ni NAFSI za nani na nani?

Maswali ni mengi lakini ungana NAMI wakati huu uweze kusoma simulizi yangu bora kuliko zote ambazo nimeziandika. Ipo tayari kuanzia muda huu.

Bei yake ni shilingi 6000 tu za kitanzania unajipatia nakala yako kwa mfumo wa softcopy (pdf) kwa kulipia kwa namba hizi hapa.

0621567672 (HALOPESA)..... WHATSAPP

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

Zote jina ni FEBIANI BABUYA
IMG-20240526-WA0009.jpg
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 46
Wanaume hao walikuwa na silaha kali sana, wakiwa wamefunika sura zao. Walikagua kila eneo kwenye jumba hilo lakini hawakuona chochote kile mwisho wa siku wakaamua kutoka baada ya kumpigia simu kiongozi wao kwamba kwenye nyumba hiyo hakukuwa na mtu yeyote yule. Wakati wanaume wale wanatoka mle ndani, kiongzoi wao alikitupa kitambaa ambacho kilikuwa usoni kwake na uso wake ulionekana moja kwa moja.
“Oooh https://jamii.app/JFUserGuide” Bilali aliongea kwa sauti kubwa yenye mshangao sana ndani yake huku akiwa anaigandisha video hiyo kwenye picha ya huyo mwanaume ili kumwangalia vizuri.
“Unamfahamu?”
“Zaidi ya sana”
“Who is this man?”
“Bilali alisikitika na kurudi kukaa kwenye kiti”
“Kama wana huyu mtu basi tupo kwenye hatari kubwa sana”
“Ni nani huyu mtu?”
“Inadaiwa kwamba taifa hili halikuwahi kumtengeneza mtu hatari kama huyu kwa miaka ya hapo nyuma na ilikuwa inajulikana kwamba alishakufa muda mrefu sana, leo nashangaa kumuona”
“Amekufa?”
“Ndiyo, hawa ni watu ambao walilipigania sana taifa hili lakini serikali haikuziona juhudi zao zaidi ya kuja kuwakataa baadae na ndipo huyu akaanza kuwakusanya wenzake wakaunda kundi la mabanditi wa milimani ambako walikuwa wanatoka na kwenda mjini kupora mali na silaha ili kuja kuilipa serikali tena kwa baadae. Wakiwa kwenye huo mpango kuna taarifa zilivuja kwamba serikali ilijua hilo na ilituma watu wakawaua wote. Ni taarifa ambazo zilikuwa na utata mwingi sana lakini kuna watu wachache walikuwa mpaka na ushahidi wa mwili wake ambao ulikuwa ulishakufa hivyo ikathibitishwa kwamba kweli alikufa japo haikuwekwa wazi kwamba alikufaje”
“Baada ya hapo hakukuwa na taarifa yoyote kwa miaka mingi sana hali ambayo hata sisi ilituaminisha kwamba alishakufa. Maana yake kama yupo hai basi huu mchezo aliucheza Denis Kijazo wakati ule serikali imewatupa yeye aliwatafuta na kuwapa maslahi makubwa kisha akadanganya kuhusu kifo cha huyu mtu na baadae akaanza kumtumia kwenye kazi zake”
“Anaitwa nani jina lake”
“Atupakisye Mwashoni. Asili yake ni mtu wa Mbeya Tukuyu huko, dunia ilimpatia jina la Ted Bundy moja kati ya mwanaume mmoja muuaji wa kutisha na mkatili sana kuwahi kuishi duniani. Walimpa jina hilo kwa sababu walikuwa wanaendana sana tabia hivyo mpaka sasa anajulikana kama Ted Bundy, ni mtu mkatili sana lakini pia ana uwezo mkubwa sana kwenye tasnia ya mapigano na rekodi zake ni kwamba tangu azaliwe hajawahi kupoteza pambano lake hata moja na alianza kuua akiwa na miaka saba tu” historia fupi ya mtu huyo ilikuwa inatisha sana kiasi kwamba kila mtu humo ndani alibaki anahema kwa nguvu sana na hofu kubwa moyoni.
“Msaliti ni nani na tunatakiwa kufanya nini?” raisi aliuliza kwa hasira sana.
“Hesabu za kwanza zinatakiwa kuwa kwa waziri mkuu ambaye hisia zangu zinaniambia hivyo lakini pia anaweza asiwe pekeyake hivyo tunatakiwa kuwa makini sana na kujilinda kila hatua maana naona hawa watu wamesha ingia tena ndani yetu”
“Hivi waziri mkuu amelalamika japo hata kidogo kuhusu familia yake?”
“Hapana”
“Huyu mjinga nadhani ni kweli anaweza kuwa anahusika kwa namna moja ama nyingine, basi kama ni kweli nitamfanyia jambo ambalo atanikumbuka kwenye vizazi vyake vyote” raisi aliendelea kufoka huku akiwa anairudia video ile maana yake kama wangebaki pale Denis Kijazo alikuwa anaua ndege wote kwa jiwe moja tu kisha angetengeneza tukio kwa taifa kuhusu kifo cha raisi ambaye alikuwa madarakani.
“Sio hilo tu pia nina mashaka sana na jambo lingine”
“Lipi?”
“Kuhusu huyo mlinzi wako wa kike”
“Amefanyaje?”
“Nina uwezo wa kumsoma mtu haraka sana kwa kumwangalia machoni, ni mjanja janja sana. Unatakiwa kumchunguza kwa umakini ili ujiridhishe ila naona kama hatupo naye na anaweza kuwa ni miongoni mwa wauzaji wa taarifa za kila kitu ambacho unakifanya. Sina uhakika na hilo jambo lakini ninahisi hivyo” maelezo ya Bilali yalimshtua sana raisi lakini moyoni Max ndiye ambaye alishtuka zaidi maana lilikuwa ni jambo siriasi sana. Aliwaza namna taarifa ambayo aliongea na raisi ilivyo vuja kirahisi sana, alianza kuhisi huenda kweli mwanamke huyo alikuwa na ajenda zake maana hata penzi lao lilikuwa la haraka sana bila sababu za msingi. Alianza kujiona ni fala sana kumuamini mtu ambaye hakumjua kiundani sana kisa tu alikuwa anamvulia nguo na kuanzia siku hiyo alikuwa anatakiwa kuanza kumchunguza kwa ukaribu sana mwanamke.
“Kama nikijiridhisha na hili, huyu malaya namuua kwa mkono wangu mwenyewe” raisi alikuwa anatoa sauti ya kukata tamaa na hilo hakuna mtu ambaye alikuwa anamuingilia bali alitakiwa kulifanyia maamuzi mwenyewe. Bilali alimweleza kila kitu juu ya kile ambacho kilikuwa ndani ya frashi na raisi huyo alitakiwa kukifahamu.
“Kipi kinatakiwa kufanyika?”
“Tukamhoji gavana lakini pia tuzichukue pesa zote za watu hawa kisha tutamuua na rasmi kesho ukitoka kuongea na Denis Kijazo kama itatokea basi jioni yake tunatakiwa kumuua mtu mwingine kwa sababu hata wao wataanza kutufanyia msako mkali hivyo tunatakiwa kuwawahi mapema na kwa ambao watabakia tutajua namna sahihi ya kumalizana nao ila kesho mkurugenzi wa shirika la kijasusi muite ofisini, akifika tu mvue nafasi yake na akamatwe, mpeleke Max akamhoji kisha baada ya hapo auawe.”
“Bilali are you sure?”
“Hiyo ndiyo njia ngumu na huenda ni njia pekee kwa sababu mtu huyu kuendelea kuwepo anakuwa ni kirusi kipya kwa sababu ndiye kiunganishi chao. Akifa hautakiwi kumteua mwingine mpaka tumalize hii kazi, watu wake wataanza kuhangaika sana na hapo tutaanza kumpoteza mmoja mmoja” makubaliano yalifikiwa lakini Max alikuwa mbali sana, bado mawazo yake yalikuwa kama yanagoma kukubaliana na ukweli kwa sababu kama kazi hiyo ingeharibiwa na jambo la Brandina kuwa msaliti lingekuwa la kweli basi chanzo angekuwa ni yeye kuharibika kwa kazi hiyo na hilo ndilo jambo ambalo lilikuwa linamfanya ajisikie viaya sana.
Vijana wawili wa Bilali waliingia humo ndani wakiwa na gavana wa benki kuu akiwa amepoteza fahamu zake bado. Alimwagiwa maji ya baridi na kushtuka maana alionekana kwamba alizimishwa kabla ya kuletwa hapo, alikurupuka kutoka kwenye huo usingizi na baada ya akili yake kurudi vizuri alishangaa anamuona raisi mbele yake, alishtuka mno maana hakutarajia jambo kama hilo.
“Mheshimiwa!”
“Una muda gani tangu uanze kuyafanya haya?”
“Unamaanisha nini mheshimiwa?”
“Umeanza lini kufanya kazi na Denis Kijazo?”
“Sijawahi kufanya kazi pamoja na mtu huyo” mwanaume huyo alikana kabisa hayo mashtaka, Bilali alisikitika sana huku akiwa anachomoa bastola mbili kwenye kiuno chake na kuhakikisha kama zina risasi full kisha akamsogelea gavana huyo.
“Vipi unatuona kama tumekuja kuuza sura hapa labda?”
“Hapana”
“Unaweza kujibu kwa amani?”
“Kweli mimi sina uhusiano wowote na huyo mtu na nashangaa umeniteka na kunileta hapa, unaweza ukaniambia familia yangu ipo wapi mpuuzi wew…….” Alianza kuleta ujeuri kitu ambacho kilimponza, Bilali alimpiga risazi kuanzia kwenye unyayo mpaka kwenye paja, mguu huo ambao ulipokea hizo risasi uliacha hata kufanya kazi huku mhusika akiwa analia kwa sauti kali ya uchungu lakini alipigwa na kofi kali sana la uso na Bilali mwenyewe.
“Hakuna mkeo wa kukubembeleza hapa, ungejibu kistaarabu tu haya mambo yangekuwa yameisha muda mrefu sana. Vipi unajibu au tuendelee?”
“Hapana usinifanyie hivi ndugu yangu, nasema ukweli nasema ukweli”
“Mwangalie raisi kisha umwambie hayo ambayo unayajua”
“Ni miaka kumi sasa tangu nianze kufanya naye kazi”
“Ni shingapi ambazo mmezipoteza benki kwa hiyo miaka?”
“Zaidi ya tirioni kumi”
“Whaaaaat the https://jamii.app/JFUserGuide?” Bilali aliropoka kwa hasira sana baada ya kusikia kiasi cha pesa ambacho watu hao walikuwa wamezipoteza kwenye mfumo na kujimilikisha wenyewe. Zilikuwa ni pesa nyingi mno tena sana ambazo zingesaidia kuweza kubadilisha nchi kwenye maeneo mengi sana na nchi ikawa mfano wa kuigwa kwa mataifa mengine.
“Ziko wapi hizo pesa?”
“Kuna baadhi ya pesa zipo kwenye akaunti za siri lakini zingine tumegawana na zingine huwa zinatumika kulipa na kuwanunua watu wengi sana ambao wanafanya kazi chini yetu”
“Ooooh Mungu wangu, na mlikuwa mnafanyaje mpaka serikali inashindwa kushtuka juu ya hilo?”
“Serikali ingeshtuka wapi wakati raisi alikuwa ni Denis Kijazo mwenyewe? Hiyo ni moja kati ya sababu kubwa ya kutaka kuendelea kuwaweka watu wake Ikulu ili wasije kumpigia kelele lakini pia tulikuwa tunapandisha riba za watu ambao wanahifadhi pesa benki hivyo kuna pesa walikuwa wanairudisha wateja wenyewe bila wao kujua wala kushtuka” alikuwa anatoboa siri kwasababu hakuwa na namna ila ni siri ambazo zilikuwa zinatisha sana, ni siri ambazo zilikuwa zinalifanya taifa kurudi nyuma sana kwenye suala zima la maendeleo.
“Nazihitaji hizo pesa sasa hivi” raisi alitamka kwa hasira sana
“Siwezi kufanya hicho kitu”
“Unahisi labda una chaguo lingine?”
“Hata kama angekuwa nani nisingeweza kumpatia hizo pesa, mtakufa vibaya sana wapuuzi nyie” alifoka huku akiwa anacheka gavana lakini laiti kama angejua aina ya watu ambao alikuwa anadili nao hapo basi alitakiwa kufanya kama wanavyotaka. Bilali hakuwa mtu wa kubonga sana, alitoa ishara tu kwa vijana wake, mmoja akatoka na kurudi na chuma ambacho kilikuwa kimechomwa sana huku akiwa na upanga mkononi.
Vitu hivyo alimkabidhi Bilali kila mtu akiwa hajui mtu huyo alikuwa anataka kufanya nini, alisogea pembeni na kumkabidhi Max kisha akampiga piga mgongoni, Max alikuwa kama vile ameshtuka kutoka kwenye mawazo maana muda mwingi alikuwa anawaza sana kuhusu Brandina.

46 inafika tamati.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 47
“Sipo kwenye mood ya kufanya haya ndugu yangu unaweza ukasema mapema tu” Max alimwelekeza mtu huyo lakini aliishia kumtemea mate tu kwa jeuri ambayo alikuwa nayo japo alikuwa na risasi za kutosha kwenye mwili wake.
“Umechagua njia mbaya sana” alitamka huku akiwa anaupitisha upanga kwenye kiganja cha mguu ambao ulikuwa salama kisha akawa anapitisha kile chuma cha moto kwenye damu sehemu ambazo alikuwa amemkata. Kiongozi huyo maumivu alishindwa kuyavumilia akaishia kujikojolea.
“Nitafanya hivyo, nitafanya hivyo” jasho lilikuwa linamtoka mwili mzima huku akiwa anatetemeka, alikuwa tayari kufanya kama walivyokuwa wanataka wao lakini alikuwa amechelewa sana kujibu kwani hata mhusika hakuwa na muda wa kumsikiliza tena.
“Ulikuwa na hilo chaguo mapema, it’s too late” mwanaume aliongea huku akianza kuucharanga mguu wa mwanaume huyo vibaya sana na upanga huku akizamisha chuma hicho kila sehemu ambayo alikuwa anaikata mpaka wenzake walibaki wanamshangaa maana mtu huyo alikubali kufanya walicho kitaka lakini hakumuacha, ilifikia hatua mpaka gavana akawa anambembeleza raisi aweze kumpa amri kijana wake aache hicho alichokuwa anakifanya. Mwanaume baada ya kuifanya shughuli hiyo kwa haraka sana, alikinyanyua chuma na kukilengesha kwenye macho ya gavana huyo ambapo zilibakia sentimita chache sana chuma kiweze kuzama kwenye jicho huku jicho likiakisi ile miale mikali ya moto. Gavana alikuwa anatetemeka mpaka moyo ukawa unapiga kwa nguvu isivyo kawaida hata kama mtu angekuwa mbali basi angeweza kuishuhudia hali hiyo.
“Muda mwingine ukija kupata tena nafasi, usije ukacheza na mimi utishia pabaya sana” laptop ililetwa alitakiwa kuhamisha kiwango kikubwa sana cha pesa ambacho kilikuwa kwenye akaunti za watu hao na kuziingiza kwenye akaunti mpya ya raisi kwa sababu pesa hizo yeye ndiye ambaye alikuwa anazitunza kupitia mgongo wa benki kuu ambapo zilikuwa salama sana.
Zilitumika dakika kumi mpaka kufanikisha kuhamisha pesa hizo lakini mtu huyo alisisitiza sana kwamba kulikuwa na pesa zingine nje ya nchi ambazo zilikuwa kwenye akaunti za watu hao hivyo hiyo ilikuwa ni sehemu tu ya hizo pesa. Raisi aliwaonyesha vijana wake hao wawili akaunti hiyo na namba za siri kabisa na kuhakikisha kila mu ameishika vyema kwa sababu vita ambayo ilikuwa mbele yao yeyote angeweza kufa muda wowote hivyo kwa ambaye angebaki alitakiwa kuja kuzitumia kwa usahihi kwa ajili ya taifa.
“Sasa naomba ututajie mtu ambaye ni msaliti kati yetu sisi”
“Sidhani kama mpo tayari kulisikia hili”
“Ndiyo maana tumekuuliza”
“Waziri mkuu”
“Ohhhh shiiit, nilijua tu” Bilali aliongea huku akiwa anamsogelea kwa ukaribu zaidi mwanaume huyo.
“Kuna mambo mawili ya mwisho hapa unatakiwa kuyatolea ufafanuzi”
“Kisha baada ya hapo mnaniua sio?”
“Hilo halikuhusu kwa sasa. Nataka kujua sehemu ambayo amefichwa gavana mstaafu lakini pia nataka kujua sehemu ya mhimu zaidi ya Denis Kijazo iko wapi?”
“Mhhhhh maswali yako ni magumu sana kujibika kwa sababu hata sisi hakuna mtu ambaye anajua vizuri labda kwa kukuelekeza tu. Huyu gavana najua utakuwa na taarifa kwamba yupo Morogoro ila kwamba yupo wapi hata mimi sijui ila ni nje ya mji milimali huko kuna sehemu ambayo ilitengenezwa chini ya ardhi kisha ikaunganishwa mpaka kwenye mti na hapo ndipo upo mlango lakini panalindwa sana na mabanditi. Hizo ni taarifa ambazo mimi nilizipata baada ya kufanya uchunguzi wangu maana nilitaka kujua udhaifu wake ili siku akija kunisaliti niwe najua naanzia wapi kuweza kujilinda. Lakini kuhusu sehemu yake ya mhimu zaidi?” alitulia kwanza gavana kisha akaendelea.
“Hii ipo Arusha japo sijui ni sehemu gani ipo ila inadaiwa kwamba hapo ndipo ulipo moyo wake kutokana na mambo ambayo yanaendelea huko na ndiyo sehemu ambayo inamuingizia pesa nyingi sana”
“Kuna kipi hasa mpaka apate pesa nyingi sana kupitia sehemu hiyo?”
“Anatengeneza sumu za hatari sana ambazo zinauzwa kwa bei kubwa sana kwenye masoko ya kimataifa huko lakini pia anatengeneza madawa ya kulevya sehemu hiyo ambayo kila wiki anasafirisha kwenda nje ya nchi. Bila kusahau sehemu hiyo ndiko ambako anawahifadhi watu wake wa kutisha sana na hivi tunavyo ongea kiongozi wa kikosi hicho amesha ingia Dar es salaam kuja kuwaua nyie wote”
“So, anajua kuhusu sisi wote?”
“Alikuwa hajui ila amejua kupitia watu wenu wenyewe kwa sababu inaonekana kwamba kuna pandikizi lake lingine ukiacha waziri mkuu”
“Ni nani huyo?”
“Huyo hata mimi simjui hivyo kwa sasa anajua kila kitu chenu, anajua idadi yenu na kila kitu kwani hicho ndicho kilimchelewesha yeye kukuua wewe mheshimiwa kwa sababu alikuwa anataka kujua kwamba ni nani alikuwa nyuma yako ila kwa sasa ameshajua kila kitu basi ni suala la muda tu kuja kukuua wewe na watu wako wote na sidhani kama mtakuwa na sehemu ya kukimbilia”
“Tunatakiwa kufanya nini?” raisi aliwageukia Max na Bilali akiwa anawauliza swali hilo.
“It’s too late” ndiyo ilikuwa kauli ya Max.
“Unamaanisha nini?”
“We are fucked, kilicho bakia sasa ni kupigana vita ya moja kwa moja. Mpigie simu mkurugenzi simu asubuhi hii kwamba unampa maagizo ya kazi na akifika kama alivyosema Bilali anakamtwa na naenda kumhoji kisha baada ya hapo anauawa na wewe unatangaza hadharani kumpindua kwenye nafasi yake lakini lazima huyu mjinga naye ataanza kutumia vyombo vya habari kukuchafua kabla ya kutaka kukuua na huenda kuanzia usiku wa kesho hata sisi tutakuwa kwenye mstari mbaya sana wa kifo hivyo kila mtu anatakiwa kujilinda kwa uangalifu sana hii sio vita ya kujificha tena. Na huenda kuna mmoja wetu mpaka sasa atakuwa hayupo” Max alisikitika wakati anatoa maelezo hayo.
“Nani?”
“Tumefanya kosa kumuacha makamu wa raisi kuondoka pale tena akiwa sambamba na mtu ambaye ni msaliti lazima wanaweza kuwa wamemteka” raisi alikuwa kama ameshtuka, aliichukua simu yake na kuipiga hiyo simu ya makamu wa raisi lakini aliambiwa namba hiyo haikuwa ikipatikana labda angeacha ujumbe wa sauti.
“So what now?” raisi aliuliza akionekana kabisa kwamba alikata tamaa.
“Action”
“Huyu mjinga tunamfanya nini?”
“Kill him”
“Hapaa msini…….” Alipigwa risasi nyingi sana za kichwa gavana.
“Vipi kuhusu familia yake?”
“Niliwaacha hai kwa sababu hawana hatia”
“Na huyu Brandina tunamfanyaje?”
“Huyo bado hatujajua kama ni kweli anatusaliti hivyo tuna jambo moja tu la kuhakikisha, kwa sasa muite umpe kazi ya kuubeba huu mwili na kuupeleka kwa Denis Kijazo. Kama akifanikiwa kuupeleka mwili na kurudi akiwa mzima basi moja kwa moja tutakuwa na uhakika kwamba ni mtu wao ila kama sio mtu wao lazima watamshika mateka tu. Lakini hilo likishindikana asubuhi mkurugenzi atatupa majibu sahihi maana huyu ni kijana wake hivyo yeye lazima anamjua kiundani sana na kuhusu wewe kwenda kwa Denis Kijazo, unatakiwa kuifuta hiyo ratiba hakuna umuhimu tena” Bilali alikuwa anapiga maesabu marefu mno.
“Una imani kwamba atasema?”
“Kalisome vizuri file la Max kwa mara ya pili ndipo utajua kwamba mkurugenzi hatakuwa na chaguo lingine zaidi ya kufanya hivyo” mazungumzo hayo yalifuatiwa na vitendo baada Brandina kuitwa na kuambiwa kwamba alitakiwa kwenda kuupeleka mwili wa gavana nyumbani kwa Denis Kijazo auache huko. Alishtuka sana lakini hakuwa na namna maana ilikuwa ni kauli ya bosi wake, aligeuka kumwangalia Max, mwanaume alikuwa amemkazia sana macho, nafsi ya Brandina ilimpe tahadhari kabisa kwamba watu hao walikuwa wamesha mtambua tayari hivyo alimbeba mtu huyo haraka haraka sana huku akiomba Mungu aweze kutoka ndani ya eneo hilo akiwa salama.
Baada ya hilo kuisha raisi aliomba kubaki na Bilali ili wazungumze mambo yao binafsi, ilikuwa ni siku ya kulikumbushia penzi lao la muda mrefu, penzi ambalo lilikuja ghafla na kuweza kupotea miaka kumi iliyokuwa imepita. Watu hao wawili walizama kwenye hilo penzi kuzifurahisha nafsi zao ambalo huenda lilikuwa penzi la kuagana kwa ajili ya maisha mengine kwani hakuna ambaye alikuwa anajua kwamba anaweza kuishi na nani alikuwa anaweza kupona, walikuwa kwenye mstari mbaya sana wa kifo na maisha.
Justin Mtadei ambaye alikuwa ni waziri mkuu baada ya kutoka pale kwenye kikao cha siri ambacho hata hivyo yeye na makamu walitolewa aliitoa simu yake mfukoni na kuipiga kwa Denis Kijazo.
“Hello mheshimiwa”
“Ndiyo waziri mkuu kuna nini mpaka unanipigia simu na usiku wote huu”
“Kikao kinaendelea saivi kama nilivyokuwa nimekwambia na watu hawa wanaonekana tayari wameshatujua wote”
“Kivipi?”
“Kwa sababu wameongea mambo ya kawaida tu lakini umefika muda wa kuweza kuongelea mambo ya mhimu ghafla wametutoa lakini mwenzangu nadhani wamemtoa baada ya kuonekana kutokuwa sawa kwa sababu familia yake imepotea nadhani hili unalijua?”
“Ndiyo familia yake ipo kwenye mkono wangu”
“Nadhani kama vijana wapo karibu kwa sababu walikuwa wananifuatilia na kifaa changu cha mawasiliano wanaweza kwenda pale”
“Nakurudia baada ya muda mfupi lakini hakikisha kwamba huyo makamu wa raisi hafiki mbali unamleta kwenye mkono wangu”
“Sawa mheshimiwa wapo watu wa kufanya hiyo kazi” simu ilikatwa na ndio muda ambao Ted na kundi lake walikuwa wanaingia pale ina maana wahusika walikuwa wana taarifa za ujio wa watu hao. Ndani ya dakika kumi na sita zilizo fuata Denis Kijazo alimpigia tena simu waziri mkuu.
“Walikuwa wanajua kila kitu”
“Haiwezekani, mimi nimetoka sio muda hapo nimewaacha wapo pale”
47 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 48
“Ulikuwa sahihi kusema kwamba wamekushtukia na muda wowote huenda wamekuweka kwenye mtego na wanaweza kukukamata kuanzia sasa kwa sababu tayari wameshakuwa na uhakika kwamba wewe sio mwenzao tena”
“Kwahiyo natakiwa kufanya nini?”
“Makamu wa raisi umempata?”
“Ndiyo”
“Vijana wanakupeleka uwanja wa ndege saivi ambapo utakutana na familia yako maana kuna vijana wengine pia nimewatuma wakaichukue familia yako, ukifika pale kuna ndege binafsi ambayo itakusafirisha wewe na familia yako mpaka Kenya. Huko utakaa mpaka nitakapo kupigia simu ya kukutaka urudi kwani siwezi kuruhusu ukaingia kwenye matatizo kwa sababu baada ya hili nataka nikufanye uwe raisi”
“Mheshimiwa una uhakika na hili? Naona kama inaweza kuwa hatari zaidi”
“Fanya kama navyo kuelekeza kwani kila kitu kipo ndai ya mipango yangu”
“Sawa mheshimiwa” waziri mkuu alihema kwa nguvu baada ya kuikata simu hiyo, mpango ulikuwa ni kwamba yeye alitakiwa kuishi na sio kufa kwa sababu alikuwa anahitajika sana kwa hapo baadae. Aliingia kwenye gari na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ilianzia pale.
Asubuhi na mapema sana mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Tanzania, mheshimiwa Philipo Tibaigana alipigiwa simu yake na raisi kwamba afike ofisini kwake kwani alikuwa na maagizo yake ya mhimu sana. Taarifa hiyo ilikuwa ni ghafla sana na ilimshtua kwa kiasi kikubwa sana kiongozi huyo wa usalama hivyo baada ya simu hiyo kukatwa alimpigia Denis Kijazo kumpa taarifa hiyo ili aone kama kulikuwa na umuhimu wa kwenda au asiende.
“Mheshimiwa nahisi kabisa huko sio salama kwenda”
“Kwahiyo unataka kujionyesha hadharani kwamba rasmi unamgeuka raisi? Yule anasikilizwa na kila mtu anaweza kuandaa mkutano wa vyombo vya habari akatangaza kwamba umeiasi nchi unahisi sisi tutakua kwenye hali gani?”
“Kwahiyo nifanye nini mheshimiwa?”
“Nenda kamsikilize”
“Mheshimiwa”
“Fanya nilivyokwambia halafu huyu binti amekuja kwangu muda sio mrefu sana”
“Brandina?”
“Ndiyo”
“Kwa sababu gani?”
“Gavana ameuawa”
“How?”
“Wameshajua kila kitu na sisi tumejua kila kitu hivyo kilicho baki na kutafuta nafasi ya kumuua raisi tu”
“Brandina yupo salama?”
“Hapana”
“Kwanini?”
“Nina uhakika huu utakuwa ni mtego kumtuma yeye kuleta mwili kwangu, nadhani walitaka kujua kama yupo kwao au yupo kwangu”
“Watajuaje?”
“Kama binti akirudi akiwa mzima watajua ni mmoja wetu”
“Usiniambie kwamba umepanga kumuua?”
“Hapana, hilo lipo juu yako wewe, nimemuacha aende”
“https://jamii.app/JFUserGuide”
“Nenda kamsikilize huyo changudoa kisha ukitoka nambie kilicho endelea, mpango wote unafanyika leo usiku”
“Una uhakika gani?”
“Huwa naishi mbele ya mu dasana”
“Unamaanisha nini?”
“Yule bwana mdogo Bilali ambaye alikuwa anajifanya anaishi kwa kificho sana leo usiku anakufa na wenzake hivyo raisi anabaki na kijana mmoja tu Max ambaye baada ya kifo cha raisi anapewa kesi ya kifo kisha na yeye anakufa”
“Utawapata vipi watu ambao hata hawajulikani walipo?”
“Kuna kifaa amewekewa kwenye mwili wake wakati anasalimiana na waziri mkuu, nijua sehemu yoyote ile atakayokuwa na wenzake”
“Naomba hili liishe haraka sana mheshimiwa kabla mambo hayajaharibika sana”
“Go” mheshimiwa aliikata simu hiyo baada a kuhakikisha kwamba amemaliza maagizo yake kwa mkurugenzi huyo. philipo Tibaigana alikuwa na hofu sana kitu ambacho kilifanya apige simu kwa pupa sana kwa Brandina na simu hiyo ilipokelewa baada ya muda mfupi tu.
“B upo salama?”
“Sijui”
“Upo wapi kwa sasa?”
“Nawaza kama nirudi Ikulu au niende wapi maana watu hao wameshanijua”
“Sasa nisikilize kwa makini, nenda safe house kule kisha usiku majira ya saa sita nitakuja kukutoa nikusafirishe kwenda nje ya nchi. Hiyo simu itupe saivi kwa sababu huenda sio salama na usimwamini mtu yeyote kwamba upo wapi hata hiyo gari iache hapo hapo ulipo na uondoke haraka sana”
“Sawa naomba usiniache kwenye hili bosi”
“Nipo kwa ajili yako siku zote. Fanya nilivyo kuelekeza utakuwa salama mpenzi, siwezi kuruhusu kukupoteza nikalikosa lile penzi ambalo sijawahi kulipata kwingine kolote” Brandina alikata simu akiwa anacheka kicheko cha hofu lakini chenye imani ndani yake baada ya mtu ambaye alikuwa anamtegemea kuonekana kwamba hakuwa tayari kumsaliti hata wakati wa shida bado angekuwa naye sambamba na jambo hilo wangelimaliza pamoja.
Lakini simu hiyo ilikuwa inasikilizwa upande wa pili, Bilali na Max walikuwa Ikulu kwenye chumba cha mawasiliano wakiwa wanasikiliza watu hao ambao moja kwa moja walikuwa ni wapenzi.
“Pole sana ndugu yangu” Bilali aliongea akiwa anakunywa kahawa kidogo
“Pole ya nini?”
“Najua kila kitu kuhusu wewe na huyo binti. Mimi nikitaka kufanya kazi na mtu huwa namfuatilia hadi namna anavyo ishi, nadhani haukutegemea mwanamke ambaye ulikuwa umeanza kumpenda sana anaweza kuwa msaliti na alikuja kwako kwa kazi ambayo mpaka sasa amefanikiwa kwa asilimia tisini”
“Nimefanya kosa kubwa sana ambalo limetuingiza wote mpaka sasa kwenye matatizo mazito sana”
“Unatakiwa kukosea ili ujifunze kwenye haya maisha bila hivyo ni ngumu sana kufanya mambo sahihi. Kitu cha mhimu ni kuhakikisha kwamba hautarudia tena kosa la namna hiyo kwenye maisha yako na usiku wa leo huo muda wewe ndiye unatakiwa ukakutane na huyo binti na hakikisha sura yako ndiyo inakuwa sura yake ya mwisho kuiona kwenye maisha yake. Twende naona mtu wetu amefika kwenye kamera hapo” hakumtuhumu vibaya bali alimpatia ushauri na siku nyingine namna ya kuchukua tahadhari hususani kwenye matukio ya hatari kama hayo kisha akamtaka waende sasa kukutana na mkurugenzi.
Philipo Tibaigana alikuwa anaingia Ikulu akiwa ndani ya suti kali sana, moyoni mwake alikuwa na hofu kubwa sana isivyokuwa kawaida. Alitembea taratibu mpaka kwa katibu wa raisi ambaye alikuwa ofisi ya nje, alikaa hapo akiwa na mawazo sana kiasi kwamba alisahau hata kusalimia mpaka alipokuja kushtuliwa kwamba raisi alikuwa akimsubiri ndani, aliiweka tai yake vizuri na kuhema kisha akaingia ndani ya ofisi kubwa na mhimu zaidi nchini.
“Karibu sana mheshimiwa Tibaigana”
“Asante mheshimiwa, ni heshima kubwa sana kuitwa na wewe hapa”’
“Unajisikiaje kuwa kwenye nafasi kubwa kama hiyo?”
“Najisikia fahari kubwa sana kuwa moja ya sehemu ya watu ambao wanahakikisha taifa hili linakuwa salama”
“Una uhakika taifa lipo salama kweli?”
“Nahisi hivyo mheshimiwa”
“Lakini kumbuka kwamba kuna matatizo mengi sana yanatokea, kuna mauaji yanatokea kila siku na wananchi wanahitaji majibu ila kwa bahati mbaya haujawahi kuniletea ripoti hata moja hapa”
“Mheshimi……”
“Hata usijali, haya nitawajibu wananchi mwenyewe kwa sababu walinichagua mimi na sio wewe hivyo naona hili halikuhusu”
“Bado sijakuelewa mheshimiwa”
“Usijali utanielewa tu muda sio mrefu, hapo mezani kuna laptop ambayo nadhani umeiona, hilo ni shirika lako ambalo nahitaji taarifa zake uziweke wazi kwa kutoa hizo codes za kufungulia kwenye mafaili ya siri ambayo mimi siyajui na nywila wewe ndo unazo’’
“Hili ni jambo la hatari sana”
“Ni hatari kwa raisi kulijua kuliko watu ambao hawahusiki kulijua?”
“Sijamaanisha hivyo”
“Unahisi labda nakuomba?”
“Hapana mheshimiwa”
“Basi fanya hivyo” hakuwa na namna zaidi ya kufungua akaunti za siri za shirika hilo na raisi alikuwa makini sana kumwangalia kwa kila ambacho alikuwa anakifanya.
“Siku nyingine hautakiwi kuwa mbishi sana bwana hasa unapo ongea na mtu ambaye amekufanya umeendelea kuwepo kwenye hiyo nafasi”
“Mheshimiwa kuna jambo lingine labda?”
“Ndiyo, ndiyo lipo hata usiwe na haraka, nadhani unamfahamu vizuri sana Denis Kijazo”
48 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 48
“Ulikuwa sahihi kusema kwamba wamekushtukia na muda wowote huenda wamekuweka kwenye mtego na wanaweza kukukamata kuanzia sasa kwa sababu tayari wameshakuwa na uhakika kwamba wewe sio mwenzao tena”
“Kwahiyo natakiwa kufanya nini?”
“Makamu wa raisi umempata?”
“Ndiyo”
“Vijana wanakupeleka uwanja wa ndege saivi ambapo utakutana na familia yako maana kuna vijana wengine pia nimewatuma wakaichukue familia yako, ukifika pale kuna ndege binafsi ambayo itakusafirisha wewe na familia yako mpaka Kenya. Huko utakaa mpaka nitakapo kupigia simu ya kukutaka urudi kwani siwezi kuruhusu ukaingia kwenye matatizo kwa sababu baada ya hili nataka nikufanye uwe raisi”
“Mheshimiwa una uhakika na hili? Naona kama inaweza kuwa hatari zaidi”
“Fanya kama navyo kuelekeza kwani kila kitu kipo ndai ya mipango yangu”
“Sawa mheshimiwa” waziri mkuu alihema kwa nguvu baada ya kuikata simu hiyo, mpango ulikuwa ni kwamba yeye alitakiwa kuishi na sio kufa kwa sababu alikuwa anahitajika sana kwa hapo baadae. Aliingia kwenye gari na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ilianzia pale.
Asubuhi na mapema sana mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Tanzania, mheshimiwa Philipo Tibaigana alipigiwa simu yake na raisi kwamba afike ofisini kwake kwani alikuwa na maagizo yake ya mhimu sana. Taarifa hiyo ilikuwa ni ghafla sana na ilimshtua kwa kiasi kikubwa sana kiongozi huyo wa usalama hivyo baada ya simu hiyo kukatwa alimpigia Denis Kijazo kumpa taarifa hiyo ili aone kama kulikuwa na umuhimu wa kwenda au asiende.
“Mheshimiwa nahisi kabisa huko sio salama kwenda”
“Kwahiyo unataka kujionyesha hadharani kwamba rasmi unamgeuka raisi? Yule anasikilizwa na kila mtu anaweza kuandaa mkutano wa vyombo vya habari akatangaza kwamba umeiasi nchi unahisi sisi tutakua kwenye hali gani?”
“Kwahiyo nifanye nini mheshimiwa?”
“Nenda kamsikilize”
“Mheshimiwa”
“Fanya nilivyokwambia halafu huyu binti amekuja kwangu muda sio mrefu sana”
“Brandina?”
“Ndiyo”
“Kwa sababu gani?”
“Gavana ameuawa”
“How?”
“Wameshajua kila kitu na sisi tumejua kila kitu hivyo kilicho baki na kutafuta nafasi ya kumuua raisi tu”
“Brandina yupo salama?”
“Hapana”
“Kwanini?”
“Nina uhakika huu utakuwa ni mtego kumtuma yeye kuleta mwili kwangu, nadhani walitaka kujua kama yupo kwao au yupo kwangu”
“Watajuaje?”
“Kama binti akirudi akiwa mzima watajua ni mmoja wetu”
“Usiniambie kwamba umepanga kumuua?”
“Hapana, hilo lipo juu yako wewe, nimemuacha aende”
Where We Dare To Talk Openly
“Nenda kamsikilize huyo changudoa kisha ukitoka nambie kilicho endelea, mpango wote unafanyika leo usiku”
“Una uhakika gani?”
“Huwa naishi mbele ya mu dasana”
“Unamaanisha nini?”
“Yule bwana mdogo Bilali ambaye alikuwa anajifanya anaishi kwa kificho sana leo usiku anakufa na wenzake hivyo raisi anabaki na kijana mmoja tu Max ambaye baada ya kifo cha raisi anapewa kesi ya kifo kisha na yeye anakufa”
“Utawapata vipi watu ambao hata hawajulikani walipo?”
“Kuna kifaa amewekewa kwenye mwili wake wakati anasalimiana na waziri mkuu, nijua sehemu yoyote ile atakayokuwa na wenzake”
“Naomba hili liishe haraka sana mheshimiwa kabla mambo hayajaharibika sana”
“Go” mheshimiwa aliikata simu hiyo baada a kuhakikisha kwamba amemaliza maagizo yake kwa mkurugenzi huyo. philipo Tibaigana alikuwa na hofu sana kitu ambacho kilifanya apige simu kwa pupa sana kwa Brandina na simu hiyo ilipokelewa baada ya muda mfupi tu.
“B upo salama?”
“Sijui”
“Upo wapi kwa sasa?”
“Nawaza kama nirudi Ikulu au niende wapi maana watu hao wameshanijua”
“Sasa nisikilize kwa makini, nenda safe house kule kisha usiku majira ya saa sita nitakuja kukutoa nikusafirishe kwenda nje ya nchi. Hiyo simu itupe saivi kwa sababu huenda sio salama na usimwamini mtu yeyote kwamba upo wapi hata hiyo gari iache hapo hapo ulipo na uondoke haraka sana”
“Sawa naomba usiniache kwenye hili bosi”
“Nipo kwa ajili yako siku zote. Fanya nilivyo kuelekeza utakuwa salama mpenzi, siwezi kuruhusu kukupoteza nikalikosa lile penzi ambalo sijawahi kulipata kwingine kolote” Brandina alikata simu akiwa anacheka kicheko cha hofu lakini chenye imani ndani yake baada ya mtu ambaye alikuwa anamtegemea kuonekana kwamba hakuwa tayari kumsaliti hata wakati wa shida bado angekuwa naye sambamba na jambo hilo wangelimaliza pamoja.
Lakini simu hiyo ilikuwa inasikilizwa upande wa pili, Bilali na Max walikuwa Ikulu kwenye chumba cha mawasiliano wakiwa wanasikiliza watu hao ambao moja kwa moja walikuwa ni wapenzi.
“Pole sana ndugu yangu” Bilali aliongea akiwa anakunywa kahawa kidogo
“Pole ya nini?”
“Najua kila kitu kuhusu wewe na huyo binti. Mimi nikitaka kufanya kazi na mtu huwa namfuatilia hadi namna anavyo ishi, nadhani haukutegemea mwanamke ambaye ulikuwa umeanza kumpenda sana anaweza kuwa msaliti na alikuja kwako kwa kazi ambayo mpaka sasa amefanikiwa kwa asilimia tisini”
“Nimefanya kosa kubwa sana ambalo limetuingiza wote mpaka sasa kwenye matatizo mazito sana”
“Unatakiwa kukosea ili ujifunze kwenye haya maisha bila hivyo ni ngumu sana kufanya mambo sahihi. Kitu cha mhimu ni kuhakikisha kwamba hautarudia tena kosa la namna hiyo kwenye maisha yako na usiku wa leo huo muda wewe ndiye unatakiwa ukakutane na huyo binti na hakikisha sura yako ndiyo inakuwa sura yake ya mwisho kuiona kwenye maisha yake. Twende naona mtu wetu amefika kwenye kamera hapo” hakumtuhumu vibaya bali alimpatia ushauri na siku nyingine namna ya kuchukua tahadhari hususani kwenye matukio ya hatari kama hayo kisha akamtaka waende sasa kukutana na mkurugenzi.
Philipo Tibaigana alikuwa anaingia Ikulu akiwa ndani ya suti kali sana, moyoni mwake alikuwa na hofu kubwa sana isivyokuwa kawaida. Alitembea taratibu mpaka kwa katibu wa raisi ambaye alikuwa ofisi ya nje, alikaa hapo akiwa na mawazo sana kiasi kwamba alisahau hata kusalimia mpaka alipokuja kushtuliwa kwamba raisi alikuwa akimsubiri ndani, aliiweka tai yake vizuri na kuhema kisha akaingia ndani ya ofisi kubwa na mhimu zaidi nchini.
“Karibu sana mheshimiwa Tibaigana”
“Asante mheshimiwa, ni heshima kubwa sana kuitwa na wewe hapa”’
“Unajisikiaje kuwa kwenye nafasi kubwa kama hiyo?”
“Najisikia fahari kubwa sana kuwa moja ya sehemu ya watu ambao wanahakikisha taifa hili linakuwa salama”
“Una uhakika taifa lipo salama kweli?”
“Nahisi hivyo mheshimiwa”
“Lakini kumbuka kwamba kuna matatizo mengi sana yanatokea, kuna mauaji yanatokea kila siku na wananchi wanahitaji majibu ila kwa bahati mbaya haujawahi kuniletea ripoti hata moja hapa”
“Mheshimi……”
“Hata usijali, haya nitawajibu wananchi mwenyewe kwa sababu walinichagua mimi na sio wewe hivyo naona hili halikuhusu”
“Bado sijakuelewa mheshimiwa”
“Usijali utanielewa tu muda sio mrefu, hapo mezani kuna laptop ambayo nadhani umeiona, hilo ni shirika lako ambalo nahitaji taarifa zake uziweke wazi kwa kutoa hizo codes za kufungulia kwenye mafaili ya siri ambayo mimi siyajui na nywila wewe ndo unazo’’
“Hili ni jambo la hatari sana”
“Ni hatari kwa raisi kulijua kuliko watu ambao hawahusiki kulijua?”
“Sijamaanisha hivyo”
“Unahisi labda nakuomba?”
“Hapana mheshimiwa”
“Basi fanya hivyo” hakuwa na namna zaidi ya kufungua akaunti za siri za shirika hilo na raisi alikuwa makini sana kumwangalia kwa kila ambacho alikuwa anakifanya.
“Siku nyingine hautakiwi kuwa mbishi sana bwana hasa unapo ongea na mtu ambaye amekufanya umeendelea kuwepo kwenye hiyo nafasi”
“Mheshimiwa kuna jambo lingine labda?”
“Ndiyo, ndiyo lipo hata usiwe na haraka, nadhani unamfahamu vizuri sana Denis Kijazo”
48 inafika mwisho.
kazi nzuri. mkuu
 
mpaka ukutani ambako kilisikika kishindo kikali sana na sauti ya mtu mara moja tu ikiwa inapiga
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 48
“Ulikuwa sahihi kusema kwamba wamekushtukia na muda wowote huenda wamekuweka kwenye mtego na wanaweza kukukamata kuanzia sasa kwa sababu tayari wameshakuwa na uhakika kwamba wewe sio mwenzao tena”
“Kwahiyo natakiwa kufanya nini?”
“Makamu wa raisi umempata?”
“Ndiyo”
“Vijana wanakupeleka uwanja wa ndege saivi ambapo utakutana na familia yako maana kuna vijana wengine pia nimewatuma wakaichukue familia yako, ukifika pale kuna ndege binafsi ambayo itakusafirisha wewe na familia yako mpaka Kenya. Huko utakaa mpaka nitakapo kupigia simu ya kukutaka urudi kwani siwezi kuruhusu ukaingia kwenye matatizo kwa sababu baada ya hili nataka nikufanye uwe raisi”
“Mheshimiwa una uhakika na hili? Naona kama inaweza kuwa hatari zaidi”
“Fanya kama navyo kuelekeza kwani kila kitu kipo ndai ya mipango yangu”
“Sawa mheshimiwa” waziri mkuu alihema kwa nguvu baada ya kuikata simu hiyo, mpango ulikuwa ni kwamba yeye alitakiwa kuishi na sio kufa kwa sababu alikuwa anahitajika sana kwa hapo baadae. Aliingia kwenye gari na safari ya kuelekea uwanja wa ndege ilianzia pale.
Asubuhi na mapema sana mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Tanzania, mheshimiwa Philipo Tibaigana alipigiwa simu yake na raisi kwamba afike ofisini kwake kwani alikuwa na maagizo yake ya mhimu sana. Taarifa hiyo ilikuwa ni ghafla sana na ilimshtua kwa kiasi kikubwa sana kiongozi huyo wa usalama hivyo baada ya simu hiyo kukatwa alimpigia Denis Kijazo kumpa taarifa hiyo ili aone kama kulikuwa na umuhimu wa kwenda au asiende.
“Mheshimiwa nahisi kabisa huko sio salama kwenda”
“Kwahiyo unataka kujionyesha hadharani kwamba rasmi unamgeuka raisi? Yule anasikilizwa na kila mtu anaweza kuandaa mkutano wa vyombo vya habari akatangaza kwamba umeiasi nchi unahisi sisi tutakua kwenye hali gani?”
“Kwahiyo nifanye nini mheshimiwa?”
“Nenda kamsikilize”
“Mheshimiwa”
“Fanya nilivyokwambia halafu huyu binti amekuja kwangu muda sio mrefu sana”
“Brandina?”
“Ndiyo”
“Kwa sababu gani?”
“Gavana ameuawa”
“How?”
“Wameshajua kila kitu na sisi tumejua kila kitu hivyo kilicho baki na kutafuta nafasi ya kumuua raisi tu”
“Brandina yupo salama?”
“Hapana”
“Kwanini?”
“Nina uhakika huu utakuwa ni mtego kumtuma yeye kuleta mwili kwangu, nadhani walitaka kujua kama yupo kwao au yupo kwangu”
“Watajuaje?”
“Kama binti akirudi akiwa mzima watajua ni mmoja wetu”
“Usiniambie kwamba umepanga kumuua?”
“Hapana, hilo lipo juu yako wewe, nimemuacha aende”
Where We Dare To Talk Openly
“Nenda kamsikilize huyo changudoa kisha ukitoka nambie kilicho endelea, mpango wote unafanyika leo usiku”
“Una uhakika gani?”
“Huwa naishi mbele ya mu dasana”
“Unamaanisha nini?”
“Yule bwana mdogo Bilali ambaye alikuwa anajifanya anaishi kwa kificho sana leo usiku anakufa na wenzake hivyo raisi anabaki na kijana mmoja tu Max ambaye baada ya kifo cha raisi anapewa kesi ya kifo kisha na yeye anakufa”
“Utawapata vipi watu ambao hata hawajulikani walipo?”
“Kuna kifaa amewekewa kwenye mwili wake wakati anasalimiana na waziri mkuu, nijua sehemu yoyote ile atakayokuwa na wenzake”
“Naomba hili liishe haraka sana mheshimiwa kabla mambo hayajaharibika sana”
“Go” mheshimiwa aliikata simu hiyo baada a kuhakikisha kwamba amemaliza maagizo yake kwa mkurugenzi huyo. philipo Tibaigana alikuwa na hofu sana kitu ambacho kilifanya apige simu kwa pupa sana kwa Brandina na simu hiyo ilipokelewa baada ya muda mfupi tu.
“B upo salama?”
“Sijui”
“Upo wapi kwa sasa?”
“Nawaza kama nirudi Ikulu au niende wapi maana watu hao wameshanijua”
“Sasa nisikilize kwa makini, nenda safe house kule kisha usiku majira ya saa sita nitakuja kukutoa nikusafirishe kwenda nje ya nchi. Hiyo simu itupe saivi kwa sababu huenda sio salama na usimwamini mtu yeyote kwamba upo wapi hata hiyo gari iache hapo hapo ulipo na uondoke haraka sana”
“Sawa naomba usiniache kwenye hili bosi”
“Nipo kwa ajili yako siku zote. Fanya nilivyo kuelekeza utakuwa salama mpenzi, siwezi kuruhusu kukupoteza nikalikosa lile penzi ambalo sijawahi kulipata kwingine kolote” Brandina alikata simu akiwa anacheka kicheko cha hofu lakini chenye imani ndani yake baada ya mtu ambaye alikuwa anamtegemea kuonekana kwamba hakuwa tayari kumsaliti hata wakati wa shida bado angekuwa naye sambamba na jambo hilo wangelimaliza pamoja.
Lakini simu hiyo ilikuwa inasikilizwa upande wa pili, Bilali na Max walikuwa Ikulu kwenye chumba cha mawasiliano wakiwa wanasikiliza watu hao ambao moja kwa moja walikuwa ni wapenzi.
“Pole sana ndugu yangu” Bilali aliongea akiwa anakunywa kahawa kidogo
“Pole ya nini?”
“Najua kila kitu kuhusu wewe na huyo binti. Mimi nikitaka kufanya kazi na mtu huwa namfuatilia hadi namna anavyo ishi, nadhani haukutegemea mwanamke ambaye ulikuwa umeanza kumpenda sana anaweza kuwa msaliti na alikuja kwako kwa kazi ambayo mpaka sasa amefanikiwa kwa asilimia tisini”
“Nimefanya kosa kubwa sana ambalo limetuingiza wote mpaka sasa kwenye matatizo mazito sana”
“Unatakiwa kukosea ili ujifunze kwenye haya maisha bila hivyo ni ngumu sana kufanya mambo sahihi. Kitu cha mhimu ni kuhakikisha kwamba hautarudia tena kosa la namna hiyo kwenye maisha yako na usiku wa leo huo muda wewe ndiye unatakiwa ukakutane na huyo binti na hakikisha sura yako ndiyo inakuwa sura yake ya mwisho kuiona kwenye maisha yake. Twende naona mtu wetu amefika kwenye kamera hapo” hakumtuhumu vibaya bali alimpatia ushauri na siku nyingine namna ya kuchukua tahadhari hususani kwenye matukio ya hatari kama hayo kisha akamtaka waende sasa kukutana na mkurugenzi.
Philipo Tibaigana alikuwa anaingia Ikulu akiwa ndani ya suti kali sana, moyoni mwake alikuwa na hofu kubwa sana isivyokuwa kawaida. Alitembea taratibu mpaka kwa katibu wa raisi ambaye alikuwa ofisi ya nje, alikaa hapo akiwa na mawazo sana kiasi kwamba alisahau hata kusalimia mpaka alipokuja kushtuliwa kwamba raisi alikuwa akimsubiri ndani, aliiweka tai yake vizuri na kuhema kisha akaingia ndani ya ofisi kubwa na mhimu zaidi nchini.
“Karibu sana mheshimiwa Tibaigana”
“Asante mheshimiwa, ni heshima kubwa sana kuitwa na wewe hapa”’
“Unajisikiaje kuwa kwenye nafasi kubwa kama hiyo?”
“Najisikia fahari kubwa sana kuwa moja ya sehemu ya watu ambao wanahakikisha taifa hili linakuwa salama”
“Una uhakika taifa lipo salama kweli?”
“Nahisi hivyo mheshimiwa”
“Lakini kumbuka kwamba kuna matatizo mengi sana yanatokea, kuna mauaji yanatokea kila siku na wananchi wanahitaji majibu ila kwa bahati mbaya haujawahi kuniletea ripoti hata moja hapa”
“Mheshimi……”
“Hata usijali, haya nitawajibu wananchi mwenyewe kwa sababu walinichagua mimi na sio wewe hivyo naona hili halikuhusu”
“Bado sijakuelewa mheshimiwa”
“Usijali utanielewa tu muda sio mrefu, hapo mezani kuna laptop ambayo nadhani umeiona, hilo ni shirika lako ambalo nahitaji taarifa zake uziweke wazi kwa kutoa hizo codes za kufungulia kwenye mafaili ya siri ambayo mimi siyajui na nywila wewe ndo unazo’’
“Hili ni jambo la hatari sana”
“Ni hatari kwa raisi kulijua kuliko watu ambao hawahusiki kulijua?”
“Sijamaanisha hivyo”
“Unahisi labda nakuomba?”
“Hapana mheshimiwa”
“Basi fanya hivyo” hakuwa na namna zaidi ya kufungua akaunti za siri za shirika hilo na raisi alikuwa makini sana kumwangalia kwa kila ambacho alikuwa anakifanya.
“Siku nyingine hautakiwi kuwa mbishi sana bwana hasa unapo ongea na mtu ambaye amekufanya umeendelea kuwepo kwenye hiyo nafasi”
“Mheshimiwa kuna jambo lingine labda?”
“Ndiyo, ndiyo lipo hata usiwe na haraka, nadhani unamfahamu vizuri sana Denis Kijazo”
48 inafika mwisho.
Kwahiyo ndo tuje WhatsApp
 
NINI SIRI YA NAFSI ZILIZO TELEKEZWA?

Inahusu nini, inamhusu nani, kipi kipo nyuma yake? Ungana nami kwenye mtiririko huu uweze kuelewa NAFSI ZILIZO TELEKEZWA inahusu nini.

Mwaka 1991, ni mwaka ambao umoja wa nchi za Kisovieti ulidondoka baada ya kushindwa kwenye vita baridi dhidi ya watu wa Magharibi hususani Marekani. Baada ya vita hiyo kuisha kulikuwa na sababu nyingi sana zilizo wafanya washindwe ikiwemo utaifa na mchango wa nchi za magharibi.

Kwa madhara makubwa ambayo yalipatikana, nchi ya Urusi ilikaa chini kufanya tathmini ili kujua ni wapi walifanya makosa mpaka jambo hilo likatokea nchini mwao. Moja kati ya sababu kubwa ambazo walizipata ni kufeli kwa shirika lao la kijasusi la KGB kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kiusalama kwa asilimia miamoja, waliamini kwamba huenda kama shirika hilo lingekuwa imara mapema na kutekeleza majukumu yake kwa usahihi basi wangeishinda vita hiyo.

Sasa mjadala ukawekwa mezani, walishindwaje? Ndipo ikanukia harufu ya usaliti ndani yao, iligundulika kwamba ndani ya shirika lao kuna watu ambao walikuwa wasaliti na usaliti wao ndio ambao ulifanya shirika hilo kuyumba na kufeli. Sasa wasaliti walikuwa nani na nani? Jina ambalo lilitokezea kwenye makablasha yao ni jina la mwanamke wa miaka ishirini na mitano (IRINA ESPANOVICH). Sasa IRINA ni nani na alitokea vipi kwenye hiyo orodha ya wasaliti?

IRINA ESPANOVICH alikuwa ni jasusi mbobevu ndani ya shirika hilo, Moja kati ya wapelelezi ambao waliaminika mno kiasi kwamba akapata bahati ya kuolewa na moja kati ya maafisa wakubwa ndani ya shirika hilo la KGB. Kuolewa kwake na kiongozi mkubwa wa shirika hilo ikawa nafasi ya yeye kupata taarifa nyingi na za siri za shirika hilo kwa njia ya kawaida ama kuziiba kwa sababu huyo mwanaume alikuwa akiishi naye nyumba moja. Sasa kwenye ule mchakato wa kuwatafuta wasaliti, waligundua kwamba kuna akaunti ndani ya Urusi ilipokea mabilioni ya fedha kutoka ndani ya nchi ya Marekani na walipo jaribu kuichunguza akaunti hiyo ili wajue sababu ya msingi ya pesa nyingi kiasi hicho kutumwa kwa mtu ambaye taifa lake lilikuwa vitani na nchi hiyo ni ipi! Ndipo wakagundua kwamba akaunti hiyo ilikuwa inamilikiwa kwa siri na mwanamke huyo IRINA ESPANOVICH.

Baada ya kuunganisha doti, wakagundua kwamba hizo pesa zilitoka ndani ya shirika la kijasusi la Marekani CIA ambalo wengi huwa wanaamini kwamba ndilo shirika namba Moja kwa ubora zaidi duniani kutokana na kuwa na bajeti kubwa ya uendeshwaji wake. IRINA alipokea pesa nyingi ambazo hata angefanya kazi miaka mia-moja asingeweza kuzipata, CIA wamtumie pesa kama nani? Ikahitimishwa kwamba huyo ndiye msaliti ambaye alikuwa akiwauza kwa CIA ndiyo maana walifeli hivyo ikatolewa amri kwamba asakwe popote alipo, akamatwe, ateswe kisha auawe mrembo huyo.

Bahati ikawa upande wake, mlinzi mkuu wa mumewe akampatia taarifa kwa simu kwamba Maam you are to be killed (unatakiwa kuuawa) hawa watu wanajua kila kitu hivyo KIMBIA (RUN). Alikuwa hatarini hivyo hakuwa na muda wa kupoteza akapotea haraka, KGB hawakumpata mwanamke huyo hivyo ukaanza msako wa kimya kimya kwa sababu waliogopa kuziweka taarifa hizo wazi kwani zingewavua nguo kwa kuonekana ni wazembe mpaka yote hayo yanatokea na hawana taarifa! Hawakutaka aibu wakaamua kuifanya siri kumtafuta huyo DOUBLE AGENT IRINA ESPANOVICH.

Kupotea kwake Urusi mikononi mwa KGB ambao walimpachika jina la LUNATIC GIRL, ukawa mwanzo wake wa kuingia ndani ya nchi ya Tanzania. Kwanini iwe Tanzania? IRINA alipiga hesabu zake akagundua kwamba kama angeenda nchi kubwa hususani ambazo zina usambaaji wa taarifa haraka wangekuja kumpata tu siku moja hivyo alihitaji kuishi sehemu ambayo hata KGB wenyewe wasingeidhania kwamba anaweza kuwepo na ile amani ambayo imetawala Tanzania ikamvutia kuishi hapa kwani ingekuwa ni ngumu kuja kujulikana kwamba yupo hapa. Yes, mpango ulikuwa sahihi sasa Tanzania angeishije na angeweza vipi kujilinda? Ukawa mwanzo wa kuanzisha jamii ya Siri ambayo aliiita LUNATIC SOCIETY, jina ambalo alipewa na KGB kwa usaliti wake. Kumbuka alikuwa mgeni hivyo asingeweza kuianzisha jamii hiyo mwenyewe ikamlazimu kumtafuta mtu.

Macho yake yakadondokea kwa Novack Nyangasa, mdogo wa raisi wa Tanzania ambaye aliamini angekuwa na nguvu ya kumpeleka anapo pataka yeye. Alimshawishi mwanaume huyo kwa urembo wake na kumpa mpango mzima juu ya utajiri ambao wangeenda kuutengeza, Novack akatokwa na mate ya uchu, akakubali. Jamii hiyo ikaanzishwa kwa nguvu ya mdogo wa raisi ambapo waliwasajili watu wakubwa; wanasiasa wakubwa, maprofesa, wanafalsafa, madaktari bingwa, wafanya biashara wakubwa na kila ambaye walimuona anafaa. Baadae raisi akazipata habari, akachukia sana na kumuita mdogo wake IKULU.

Akamtaka aifute jamii hiyo kwa mwezi mmoja tu pekee, huo mwezi ukatumika kummaliza yeye, raisi akawekwa kati akatakiwa kufa ili jamii hiyo iwepo. Moja kati ya mipango mikakati ambayo waliiweka ili kujilinda ni kuanzisha chuo cha kuwatengeneza vijana hatari kwa ajili ya ulinzi na kufanya kazi yao kwa nguvu pale ambapo ingebidi, zoezi hilo likatua mikononi mwa jasusi wa zamani wa Tanzania ambaye aliachana na kazi hiyo baada ya kuhusika na mauaji ya watu wengi sana, NIKOLAI GIBSON. Mwanaume huyo kwenye moja ya mazao yake alifanikiwa kumtengeneza kijana wa kuitwa YOHANI MAWENGE, bwana mdogo ambaye alimuokota Tandale kwa Tumbo akililia mapenzi na kutaka kujiua kisa uchi wa mwanamke.

Alimfunza namna ya kuwa mwanaume akampa begi la pesa akale maisha kwa mwezi mzima, alale na wanawake warembo ambao aliishia kuwaona kwenye runinga ili ushamba umtoke kisha baada ya hapo alikuwa na kazi naye. Alitengenezwa kikawa kiumbe cha kutisha na Kazi yake ya kwanza ikawa kwenda kumuua mcheza KAMARI mmoja huko BAMBALI Senegal na alitakiwa kurudi na bilioni 30 zilizokuwa mkononi mwa bwana huyo..... Huyu tuna mengi ya kuyasoma kwake ni mhimu sana.

Ukawa mwanzo wa mwanamke huyo wa KGB kuitawala Tanzania kwa miaka takribani thelathini. Lakini baadae Moja kati ya makosa makubwa ambayo waliyafanya ni kumuua mwanasayansi aliyedaiwa kuwa binadamu mwenye akili zaidi nchini.

NAFSI ZILIZO TELEKEZWA ni zipi na za nani?
Kulikuwa na utata wa maisha ya mwanaume Edison, bwana ambaye hakuwa na kumbukumbu na kwenye mfuko wake alikuwa anatembea na picha ambayo walidai ni ya mkewe, bwana huyu alikuwa akishangaa kwa sababu yeye binafsi hakuwa na kumbukumbu yeyote kama aliwahi kuwa na mke au familia. Kitu cha kushangaza kwa EDISON ni kwamba alikuwa anatafutwa ili auawe kuliko hata pesa inavyo tafutwa na maskini mpaka yeye mwenyewe akawa anashangaa.

Hali hiyo ilimlazimu kwenda kuishi maisha ya chini sana huko Kigogo Mwisho ili awe salama kwani hakuna ambaye angempata kirahisi akiwa kwenye maisha ya kifukara huko lakini usiku mmoja mvua ikiwa inanyesha akiwa ndani ya kijumba kibovu kwenye mkeka, anapokea simu ambayo ilimtaka atoweke eneo hilo kwa dakika kumi na tano vinginevyo angekufa. Aliduwaa ila hakuwa na namna aliondoka haraka ila kabla hajafika mbali akavamiwa na wanaume wa kutisha ambapo alimuua mmoja akafanikiwa kutoroka.

Safari yake ikawa ni kwenda kwa mlezi wake ambaye ndiye alimpa taarifa hiyo na ndiye alimtaka akaishi huko Kigogo mapaka mambo yakae sawa ili akampe ukweli wa kwanini anatafutwa sana? Kufika kwa huyo mlezi wake ambaye alikuwa ni mchungaji wa KKKT pale Mabibo Mwisho karibu na hosteli za wanafunzi wa NIT, alimkuta mtu huyo yupo kwenye hatua za mwisho za uhai wake. Hakumwambia kitu zaidi ya kumtaka aende nyumbani kwake kwenye banda la mbwa akachukue kitabu ambacho kingemfunulia ukweli kwamba yeye ni nani, kwanini hana kumbukumbu, maisha yake kabla yalikuwaje na kwanini anatafutwa sana na watu ambao yeye alidai hawajui!

EDISON alishangaa baada ya kuambiwa kwamba anatafutwa kwa kuhusika na mauaji ya makomando TISA wa kikosi maamulu cha KOM (KILL ON MISSION).akabaki ameduwaaaa!!!!!!!

Ilishawahi kukukuta kwenye maisha yako ukatakiwa kumuua mama yako mzazi kwa mkono wako mwenyewe? Hilo ni jambo baya na gumu lakini Yes, kuna mwanaume alitakiwa kumuua mama yake aliye mzaa ili nchi iwe salama. Je huyu naye hatima yake ilikuwaje?

Kuna uhusiano gani kati ya hizo NAFSI ZILIZO TELEKEZWA, IRINA ESPANOVICH na EDISON?

Unataka kumjua zaidi IRINA ESPANOVICH? Unataka kuijua kiundani LUNATIC SOCIETY? Unataka kujua uhalisia wa maisha ya EDISON kabla na baada ya hapo? Hizo nafsi ZILIZO TELEKEZWA ndizo hizo za makomando TISA (9) ambao alidaiwa kuwaua au kuna mengine nyuma ya mlango wa siri? Ungana nami kwenye simulizi yangu bora zaidi kuwahi kuiandika kwa mkono wangu.

1. Storyline yake ni kali sana
2. Dialogue (majibizano) yake ni kali sana.
3.Haitabiriki kabisa (huwezi kutabiri kinacho tokea baadae)
4.Lakini pia ina actions kali mno.

Simulizi hii imetoka tayari na unaweza kuipata kwa shilingi ELFU SITA (6000 tu za kitanzania). Unaweza ukalipia 6000 yako kwa namba hizi ili uipate muda huo huo. Inapatikana kwa Softcopy.

0621567672 (HALOPESA)..... WhatsApp.
0745982347 (M-PESA)
0714581046 (TIGO-PESA)
0689440143 (AIRTEL MONEY)

FEBIANI BABUYA

Lipia muamala wako Kisha nicheki nikutumie yote, ama unaweza ukanicheki WhatsApp, ukatuma sms ama ukapiga cm kama utakuwa na swali lolote.

CIAO.
FB_IMG_1716969749372.jpg
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 49
“Ndiyo mheshimiwa”
“Nataka kujua taarifa zake zote za maisha yake tangu anazaliwa, ushenzi alio ufanya na mpaka leo pale alipo”
“Yule alikuwa raisi hakuna mtu ambaye alikuwa anaruhusiwa kumchunguza mheshimiwa”
“Mhhhh una uhakika?”
“Ndiyo”
“Mbona mimi mlikuwa mnanichunguza?”
“Utakuwa umenielewa vibaya mheshimiwa”
“Kweli?”
“Ndiyo”
“Brandina yuko wapi?”
“Sijajua mheshimiwa kwa sababu mara ya mwisho alikuwa hapa kuhakikisha anakulinda”
“Na Dax?”
“Wote walikuwa hapa mheshimiwa”
“Wapo kunilinda au wapo kuyalinda maslahi yako na marafiki zako?”
“Mheshimiwa unaongea nini?”
“Kwamba natumia lugha ngeni sana?”
“Hapana ila nashindwa kuelewa unamaanisha nini”
“Ok, ngoja ukaongee na watu ambao wanaweza kukuelewesha zaidi” Tibaigana alibaki amepigwa na butwaa asielewe kwamba kiongozi wake alikuwa anamaanisha nini hasa lakini akiwa kwenye hiyo taharuki kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa ndani ya ofisi hiyo walitoka wanaume wawili Max na Bilali.
“Habari bosi” Max alimsalimia kiongozi wake
“Max?”
“Nakusikiliza”
“Kuna mchezo gani mnaucheza?”
“Usijali mheshimiwa, naitwa Bilali, nadhani umehangaika sana kunipata”
“Whaat?”
“Take him” kauli ya Bilali ilifuatiwa na wanaume wa kazi kuingia humo ndani ambapo walimchukua na kuondoka naye kwenda kumhifadhi kwenye chumba cha mateso.
“Kill this motherf**ker” Bilali alimwambia Max akiwa anampiga piga mgongoni na mwanaume aliondoka kuelekea kwenye hicho chumba.
“Haya mambo yanaenda kuwa na mwisho mbaya sana kwa hili taifa” raisi aliongea akiwa anakaa kwenye kiti chake na kuwasha skrini ambayo ilikuwa mbele yake ili kuweza kuangalia wakati mtu huyo akiwa anateswa.
“Ukiona sehemu fulani kuna mafanikio au maendeleo basi ujue kuna watu waliamua kujitoa sadaka nyuma yake. Ndicho kitu ambacho sisi tumeamua kukifanya bila kujali kama watu watakuja kujali juu ya hili au hawatajali ila nina imani kwamba tunafanya kitu sahihi ambacho tunatakiwa kukifanya”
“Ngoja tuone”
“Kiongozi, nasikitika sana mimi kuwa mtu ambaye natakiwa kukuhoji wewe kwa sababu mambo mengi umenifunza wewe mwenyewe maana nina imani haya mazungumzo yataishia sehemu mbaya sana”
“Kwa muda gani umejiingiza kwenye haya?”
“Kwa muda mrefu sana bosi”
“Unajua nini kuhusu haya?”
“Najua kila kitu”
“Kuhusu mimi?”
“Ndiyo”
“Hahha hahaha hapana hakuna unalo lijua”
“Tuna muda kidogo wa kuongea vizuri mimi na wewe hivyo usijali utaniambia hayo ambayo unasema sikuwa nayajua”
“Mtoto mpumbavu sana wewe”
“Huenda ni kweli ila nataka kujau kwamba mpango wenu mnataka kuutimiza lini?”
“Mpango gani?”
“Usinipe ugumu kiongozi wa kukufanyia kitu kibaya”
“Bwana mdogo utayajutia sana maamuzi ya hovyo ambayo umeyafanya”
“Sawa” Max alitoa ishara kwa wanaume wawili ambao walikuwa karibu, walimletea box la chuma. Aliwapa ishara waweze kuondoka humo ndani kisha akakisogeza kiti na kukaa karibu na mheshimiwa huyo.
“Usipange kudanganya lolote kwa sababu tunakujua muda mrefu sana kwamba wewe ni kijana mtiifu sana kwa Denis Kijazo, sasa mzee wangu unaanza vipi kusema mimi ndo nakurupuka?”
“Una imani huyo changudoa atakulinda 001?”
“Hakuna mtu mwenye uwezo wa kunilinda mimi, muda wangu wa kufa ukifika nitakufa tu”
“Utaijutia sana hii siku”
“Tuache kelele nijibu kistaarabu tu”
“Go and https://jamii.app/JFUserGuide your president” Max alicheka tu na kutoa nondo kali sana kwenye box ambalo lilikuwa karibu yake na mkasi. Aliizamisha nondo hiyo kwenye goti la mheshimiwa ambalo lilimletea maumivu ya kushtukiza, alipiga kelele. Akiwa anaendelea na harakati za kufurukuta hapo mkasi ulitumika kukikata kidole chake cha mguu taratibu kisha Max akachukua kitambaa na kujifuta damu ambayo ilimrukia taratibu bila wasiwasi.
“Should i go and https://jamii.app/JFUserGuide my president?”
“Max usifanye hivi”
“Unanipotezea muda”
“What dou you want to know?”
“Nimekuuliza mpango wenu unaanza kutimia lini?”
“Leo usiku kila kitu kinaisha”
“Whaaaaat?”
“Nyie wote mnakufa leo usiku kasoro wewe huenda ukafika hata kesho?”
“How?
“Sijui ila wewe watakuacha hai”
“Why?”
“Kuna kazi ambayo wataikamilisha kupitia wewe raisi akifa”
“Kazi gani?”
“Nadhani wanataka kukutengenezea kesi ya kumuua raisi”
“Oooh https://jamii.app/JFUserGuide. Wanajua vipi kwamba sisi tutakuwa maeneo fulani?”
“Hawana muda na wewe kabisa sema wa kuwawazia ni hao wenzako wawili raisi na huyo kijana wa Francis Mboye na wenzake”
“Unamaanisha kwamba wanatujua kiasi hicho?”
“Yeah, wanajua hadi hatua ambazo mtazipiga hapo baadae”
“Nani amefanya hili?”
“Mmefanya kosa kubwa sana kumuita waziri mkuu kwenye kikao chenu ameshawauza muda mrefu sana”
“Kivipi?”
“Kila mmoja wenu ameachiwa kifaa cha mawasiliano kwenye mwili wake hivyo watajua kila sehemu ambayo mtakuwepo” Max alishtuka na kuingiza mkono wake mfukoni haraka sana ambapo alikutana na kitu kama kipepeo kidogo sana.
“Hiyo ni mashine ambayo inatumika kupandikiza vifaa vya mawasiliano, ukiona unaweza kuhisi ni kipepeo ila ukweli ni kwamba sio, kinacho fanyika hicho kinakung’ata kidogo kiasi kwamba ni ngumu sana kushtuka na kukung’ata huko kunafanya damu yako watu hao wanaipata kirahisi sana kupitia DNA lakini kinakuwa kimekuachia Visalia vya vifaa mwilini ambapo wanaweza kujua mahali popote ulipo hivyo hakuna sehemu mnaweza kwenda”
“Shiiit! Na kama tukihitaji kufanya oparesheni?”
“Mtu mmoja anatakiwa kufanyiwa oparesheni ya masaa sita ili kuweza kutoa kila kitu sasa mpaka muishe wote? Hamna muda wa kufanya hayo yote kwa sababu mtakuwa mnapoteza ni muda tu”
“Waziri mkuu yuko wapi?”
“Sijajua ila ameikimbia nchi muda ule ule alivyotoka kukutana na nyie na ndiye raisi ajae”
“Kwanini ulikuwa unafanya haya yote?”
“Huwezi kuelewa ila siku moja utakuja kunielewa”
“Nipo hapa ndiyo maana nataka kujua”
“Bwana mdogo kuna watu wametokea maisha ya kawaida sana hivyo hata taifa kuja kuwakumbuka inakuwa ni ngumu sana hata wakijitoa vipi wanakuwa kama walikuwa wanapoteza muda tu lakini kuna wapuuzi hawajafanya la maana lolote na wanaimbwa kila siku huoni kama ni jambo la kijinga sana hilo? Mimi niliamua kuchagua watu ambao wanaweza wakanifanya jina langu likaja kusomwa na kuimbwa na kila mtu ndiyo maana nilikuwa upande wa mafanikio”
“Ndiyo sababu pekee ambayo ilikufanya ukaisaliti nchi yako”
49 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 50
“Yeah”
“Brandina yupo kwenye nyumba ipi?”
“Nyumba?”
“Nimekusikia ukiwa unafanya mazungumzo yako yote na yule malaya”
“Mhhhhhh basi ninazeeka vibaya sana mpaka nafuatiliwa kiasi hicho na nashindwa kabisa kujua, hili ni jambo la hatari sana lakini wewe ni miongoni mwa vijana wapumbavu sana ulitegeka kirahisi sana kwa sababu ya mapezi hahahaaha hahaha” mheshimiwa alianza kumcheka mwanaume na ni kweli alikuwa ni fala sana kukubali kuandeshwa na mapenzi lakini kicheko chake kiligeuka kuwa karaha baada ya nondo kuchomolewa mguuni na kuzamishwa kwa nguvu kwenye bega lake kisha ikavutwa na kulichana chana bega lake vibaya sana.
“Yupo safe house. Nyumba ya siri ya shirika la kijasusi ila niliamua kuigeuza kuwa yangu kwa sababu ilijengwa chini yangu” aliongea kwa lazima huku akiwa anahema kwa kasi sana.
“Iko wapi”
“Unataka kumuua Brandina?”
“Ukinijibu mapema atakamatwa tu na kuhukumiwa kisheria lakini kama ukileta uhuni nitamuua hata wewe mwenyewe hautakufa ila nitakacho kufanyia utatamani ni bora ungekufa”
“Najua huwezi kumuacha hai Donald Daniel ila kumbuka tu kwamba hakuna hata mmoja ambaye ataishi kati yenu. Nyumba namba 001 ipo Bagamoyo pembezoni mwa bahari”
“Kwani umeipa hiyo namba 001?”
“Kwa sababu wakati nakutengeneza wewe ndiye ulitokea kuwa kijana ambaye nilikutegemea sana na nilijua kwamba kuna siku kwa miaka ya baadae ungekuja kuikaimu nafasi yangu kwa sababu kama ningeitwa kumpendekeza mkurugenzi wa kuja kwenye hii nafasi yangu basi kwa miaka ya baadae wewe ndiye ambaye niliona unafaa sana ila kwa bahati mbaya sana umeamua kuchagua njia ambayo itayafanya maisha yako yawe mafupi sana”
“Hilo ndilo kosa ambalo umelifanya kuwamini sana hao watu wako ukihisi sisi ni wadhaifu sana, nakuhakikishia hakuna atakaye kufa kati yetu na hao watu wako wote hakuna atakaye pona”
“Haujui unacho kisema bwana mdogo”
“Una neno lolote la mwisho”
“Acha kupoteza muda niue tu” hakukuwa na la ziada, nondo ilichomekwa kwenye shingo yake ikatokezea nyuma na habari yake ikawa imeishia hapo.
Tukio hilo lilimfanya mpaka raisi kufumba macho yake maana lilikuwa la kikatili sana.
“Sidhani kama kuna mtu atapona kati yetu kama ni kweli yule mshenzi ametufanyia hivi”
“Usikate tamaa mapema sana kiasi hicho mheshimiwa bado tunayo nafasi” Bilali alimwambia raisi wake ila hata yeye alijua kwamba jambo hilo halikuwa likiwezekana kabisa kutimia.
“Unahisi kwanini waziri mkuu ametoroka?”
“Nina uhakika kwamba lazima wanataka kumfanya kuwa raisi mpango wao ukikamilika”
“Leo naiona hofu ya kifo mbele yangu na sijui kwamba ni kipi ambacho nitakifanya wala kukiamua” raisi alikuwa amekata tamaa sana na wakati huo Max alikuwa anaingia hapo ndani.
“What is next?” Bilali aliuliza akiwa anamwangalia Max
“Hatuna namna zaidi ya kuwaface moja kwa moja. Jioni ya leo mimi nitaenda Bagamoyo kumalizana na huyu malaya kisha baada ya hapo nitarudi haraka sana. Wakati huo Bilali na vijana wako mtatakiwa kwenda Kwa Madilu Mpagazi kumuangamiza, najua mkiwa kule watu hawa watahitaji kuja kule moja kwa moja ila wakati wanakuja nina imani utakuwa usiku na ni muda ambao mimi nitakuwa nimesharudi tayari hivyo hakutakuwa msalia mtume zaidi ya kuua kila ambaye atakuja mbele yetu na usiku huo huo tunatakiwa kumuua Denis Kijazo huku raisi yeye akiwa Ikulu kwa ajili ya usalama wake”
“Max hilo ni jambo la hatari sana”
“Una njia nyingine bora zaidi?” Bilali alihema tu maana hakuwa na namna nyingine zaidi ya kukubaliana na hali hiyo ambayo kiuhalisia ilikuwa inaenda kuyahatarisha sana maisha yao.
“Na mheshimiwa safari ya kwenda kwa Denis Kijazo inatakiwa ife, hauna haja ya kukutana naye tena kwa sababu ya usalama wako na muda huu unatakiwa kuitisha mkutano ukaseme ukweli kuhusu hawa waasi wa taifa hili lakini pia utangaze kuitengua nafasi ya waziri mkuu, makamu wa raisi pamoja na mkurugenzi wa usalama wa taifa”
“Na Madilu?”
“Yule usilitaje jina lake kwa sababu usiku wa leo anatakiwa kufa, kama ukilitaja jina lake utampa tahadhari na anaweza kukimbia nchi tukapata kazi nyingine kubwa ya kuanza kuhangaika kumtafuta tena”
“Na Dax yuko wapi?”
“Nimepata taarifa kwa walinzi kwamba mara ya mwisho alionekana akitoweka ndani ya eneo la Ikulu”
“Huyu mshenzi lazima atakuwa ameenda kujiunga na watu wake hivyo nina imani wakati tunaenda kule tutamkuta usiku na kama hajapatikana basi mimi nitamsaka ndani na nje ya nchi hii na nikimkatama nitamfanyia unyama ambao hakuwahi kukutana nao kwenye maisha yake yote” waliipanga mipango yao vizuri huku Max akiwa ndiye kiongozi wa mipango hiyo na kuweka kila kitu sawa kwa makubaliano ya siku hiyo usiku kuimaliza kazi kama ambavyo maadui zao walikuwa wamepanga nao. Hakukuwa na namna ya kuweza kuwakimbia zaidi ya kukumbana nao tu na kukubaliana nao.
Mheshimiwa raisi alitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu uharamia ambao ulikuwa unaendelea nchini, alielezea namna raisi mstaafu alivyokuwa na genge lake la hatari ambalo lilikuwa linahitaji kujimilikisha nchi. Raisi huyo alieleza kwamba huenda asiwe na uhakika wa kuishi kwa muda mrefu baada ya jambo hilo ila watu walitakiwa kujua kuhusu Denis Kijazo kwamba ndiye alikuwa kirusi hatari sana cha taifa hilo na haya mambo yote mabaya ya kutisha kwenye taifa hilo yalikuwa yamesababishwa na yeye. Raisi alitumia pia nafasi hiyo kutengua nafasi za watu wakubwa serikalini kama ambavyo walikuwa wamekubaliana huku akiahidi kwamba angetoa majina ya watu wapya kwenye nafasi hizo.
Taarifa ambayo mheshimiwa aliweza kuitoa kwenye vyombo vya habari iliacha gumzo kubwa, hofu na maswali mengi sana kwa wananchi kiasi kwamba walianza kuandamana kuweza kujua utata wa hizo kauli za mheshimiwa raisi. Kwa maelezo ya raisi wao ni kwamba hata yeye hakuwa salama hata kidogo na alikuwa na muda mfupi sana tangu aingie kwenye hiyo nafasi yake. Kundi la watu ambao walikuwa wameamua kujimilikisha nchi ndio ambao alidai kwamba walikuwa wanahitaji kuyachukua maisha yake.
Kama raisi wa nchi hakuwa na uhakika wa maisha yake sasa ni nani mwingine ambaye angejihisi salama ndani ya nchi? Watu walikuwa wanataka raisi awaeleze kwa kina lakini wengine walikuwa wanahitaji raisi mstaafu Denis Kijazo ajitokeze hadharani kuweza kujibu tuhuma hizo za kila ambacho kilikuwa kinaendelea lakini kwa bahati mbaya sana hakuna jambo lolote ambalo lilifanyika zaidi ya wananchi kuendelea kuzua taharuki kuandamana ambapo waliishia kuchezea vipigo tu kutoka kwa maaskari ambao walilazimika kutumia nguvu ili kuhakikisha watu wanarudi majumbani kwao.
Raisi baada ya kutoka kwenye chumba cha mikutano, alitembea akiwa na mawazo mengi sana na kuelekea mpaka ndani ya chumba ambacho alikuwa analala. Aliifungua droo yake na kuitoa picha yake ya tangu zamani sana akiwa binti na sasa alikuwa mtu mzima, aliiangalia kwa muda kidogo huku machozi yakiwa yanamtoka usoni kwake. Hakuwa akielewa namna mambo yalivyokuwa yanaenda kwa kasi sana lakini pia hakujua hatima ya mambo hayo ingekuwa nini kwani mambo yalikuwa yanazidi kuwa mabaya na kama raisi alionekana kabisa kushindwa kuifanya kazi yake kwa usahihi huku tegemeo lake pekee likibakia kwa Max pamoja na DRAGON BOYS ambao walikuwa wanaongozwa na Bilali.
Alizunguka kwa muda sana ndani ya chumba chake hicho akiwa ana imani kwamba huenda hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya mwisho kabisa kuweza kukaa Ikulu na huenda ndiyo ilikuwa siku yake ya mwisho kabisa ya yeye kuwa hai. Alicheka kwa nguvu kisha akatamka.
“Perharps this is not an end of the beginning; it is the beginning of an end” alitamka kwa msisitizo sana huku akimeza vidoge vya usingizi na kujilaza ili apumzike.


Saa kumi na mbili ya jioni ilimkutia Max akiwa anaishika Bagamoyo road kuelekea Bagamoyo ambako alielekezwa kwamba alikuwepo mrembo Brandina amejificha huko kwa taarifa ambayo ilitolewa na mkurugenzi wa shirika la kijasusi. Alikuwa na usongo sana na mwanamke huyo kwa sababu kuingia kwenye maisha yake kulileta matatizo makubwa sana kwa wenzake kiasi kwamba mipango mingi sana ilianza kuvuja na kuwafanya kushindwa kutekeleza yale ambayo walikuwa wanayatarajia tangu mwanzo kabisa hivyo aliona kwamba mwanamke huyo alitakiwa kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kuweza kuyalipa hayo.
Alikuwa anaendesha gari kwa kasi sana kwa sababu alitakiwa kufika huko na kuimaliza kazi haraka sana kisha ageuke usiku na kufika kwa Madilu ili akaifanye hiyo kazi pamoja na DRAGON BOYS. Kiza kikiwa kinaanza kutawala alikuwa anaingia ndani ya eneo ambalo alikuwa ameelekezwa kwamba angefanikiwa kumkuta mwanamke huyo. Aliliona jumba moja kwa mbali kidogo ambalo lilikuwa ufukweni kabisa mwa bahari, taa zake zilikuwa zinawaka sana kiasi kwamba mtu ambaye alikuwa ndani ya sehemu ile alikuwa amejiachia isivyokuwa kawaida.
Hakuwa fala sana kwenda kichwa kichwa kwa sababu aliamini kwamba eneo hilo lazima lilikuwa na ulinzi mkali sana, mwilini mwake alikuwa amejihami vya kutosha akiwa amejiandaa na kazi. Bastola nne zilikuwa kiunoni na visu vikali sana vitatu lakini kwenye mkono wake alikuwa na shoka lake ambalo alikuwa analiamini sana. Alikuwa na hasira sana na mwanamke huyo kiasi kwamba hakutaka kabisa kuufunika uso wake, alihitaji waonane ana kwa ana ili aweze kumjibu maswali ambayo aliona yanafaa kupatiwa majibu.
Gari yake aliizima kabisa na kusogea hatua kadhaa mbele ila alihisi kama kuna ishara ya watu karibu na alipokuepo. Alingaza pembeni palikuwa na bustani safi sana kabla ya kuingia ndani ya jumba hilo, alitembea kwa spidi sana kuelekea kwenye bustani ambayo ilikuwa karibu na ukuta. Alilala chini baada ya mvumo wa upepo kuzidi kusogea alipokuwepo yeye, kisu kikali sana kilipita na kwenda kukita ukutani.
Alishangaa baada ya kuona kuna mwanaume alikuwa anamjia kwa nguvu sana huku akiwa anachota chota mchanga wa ufukweni kwa mabuti yake, aliona mchanga ukiwa unamjia machoni hali ambayo ilimfanya ajifunike usoni na hilo likawa kosa. Alipigwa ngumi za tumbo wakati anataka kujihami alipokea kiganja cha shingo ambacho kilimpeleka pembeni akiwa anayumba yumba lakini bado hakupewa kabisa nafasi ya kupumua vizuri alipigwa na goti la kifua ambalo lilimbeba mpaka ukutani.
Mshambuliaji alitabasamu baada ya kumpatia mvamiaji kwa usahihi sana akihisi kwamba alikuwa amejigongesha vibaya ukutani lakini baada ya kuangalia vizuri alishangaa kumuona mwanaume huyo akiwa anabembea kwenye huo ukuta hali ambayo ilimshanmgaza sana. Max alikuwa amelichomeka shoka lake ukutani kisha miguu miwili akawa ameikanyagia ukutani na shoka ndo linampa balansi, alishuka na kusimama akiwa anayasikilizia maumivu makali na kujinyoosha.
50 inafika mwisho.
 
Back
Top Bottom