Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 51
“Mlijua kwamba nitakuja hapa?”
“Yeah”
“Kivipi?”
“Tulikuwa tunabeti tu kama ikitokea mtu huyo akahojiwa basi akuelekeza wewe hivyo ili uje tukukamatie huku na huko ulikotoka watu wako wanauawa bila wewe kuwepo kisha unapewa kesi na kutangazwa kama gaidi na baada ya hapo utakuwa hauna kazi tena tunakuua”
“Hahahah hahahaha” Max alicheka kwa hasira sana kwa sababu alikuwa amechezewa mchezo wa kitoto sana.
“Unamaanisha Brandina hayupo huku?”
“Huyo yupo lakini kwa bahati mbaya hauwezi kumpata” mwanaume huyo aliongea huku akiwa anaichomoa bastola na kulenga tenki la mafuta la gari ambapo gari la Max lililipuka hivyo ikawa hakuna njia ya kumfanya yeye kurudi haraka ndani ya Dar es salaam.
“Ulitakiwa kuniua ukiwa na nafasi bado, umefanya kosa kubwa sana kuniacha hai wakati ambao ulikuwa unanishambulia”
“Hata mimi nilitamani sana kukuua ni kwa sababu tu siruhusiwi kukuua ndiyo maana mpaka sasa upo hai” wakati mwanaume huyo anamalizia kuongea Max alinyanyua buti lake na kuanza kuja kwa kasi kali mno. Alijirusha chini ya mchanga na wakati ananyanyuka hapo kasi ambayo alisimama nayo akiwa ameirusha michanga juu ilikuwa ngumu sana kwa mwanaume yule kuweza kuihimili hivyo akajikuta anapiga hewa na mwanaume alizunguka nyuma yake na kuliachia shoka lake kwa nguvu huku akiwa ameshikilia kwenye mpini.
Shoka hilo lilitua kwenye mgongo wa huyo mwanaume na kuupasua vibaya mno, alivutwa kisha shoka hilo likawekwa shingoni, alichinjwa mithili ya kuku wa pasaka. Aliachiwa chini akiwa mfu kama wa miaka mia nane iliyokwisha kupita. Max akiwa amesimama hapo alishangaa kuona geti likiwa linafunguliwa kama alama ya kumkaribisha aingie ndani, alishangaa sana na kuangalia pembezoni mwa geti hilo ndipo aligundua kwamba kulikuwa na kamera kila mahali kumaanisha kwamba watu ambao walikuwa ndani ya jengo hilo na pengine ambao walikuwa wapo nje ya jengo hilo walikuwa wanaangalia kile ambacho kilikuwa kinaendelea moja kwa moja.
Aliingia akiwa makini sana kuweza kuangalia mazingira ya ndani jinsi yalivyokuwa, ndani ya jengo hilo alikutana na sura ngumu saba za wanaume ambao walionekana kwamba walikuwa wanamsubiri kwa hamu kubwa sana. Akiwa anawahesabu kwa umakini wanaume hao alisikia sauti ya mtu akiwa anapiga makofi juu ya ghorofa, kwenye balcony alikuwa amesimama Brandina akiwa amevaa bikini huku nyuma yake akiwa amefunikwa na gauni ambayo mbele ilikuwa wazi na kuvifanya viungo vyake vilivyo nona sana kuonekana kwa usahihi.
“Wewe ni moja kati ya wanaume wajinga sana, you were too smart sikufikiria kama unaweza kuingia kwenye mtego wa kitoto ule kisa uchi wa mwanamke. Uchi umekufanya umewasaliti wenzako kwa kuiweka wazi mipango ambayo inaenda kuwateketeza wote kwa pamoja”
“Umeniangusha sana, kwenye nyumba yako ulikuwa unajifanya kwamba ulikuwa makini sana hasa kwenye kufanya maongezi yako lakini ulishindwa kutambua kwamba nilikuwa nimeweka vifaa vya mawasiliano kila sehemu hivyo kila ambacho ulikuwa unakiongea na kila ambacho kilikuwa kinaendelea mle nilikuwa nasikia lakini sio mimi tu na watu wengine wengi walikuwa wanasikia kirahisi sana ndiyo maana iliturahisishia kuweza kuzisoma alama zenu ambazo zilikuwa zinafuata” “Mpaka unafika hapa najua Philipo huenda umemuua kwa hasira na sijali kuhusu yeye hata kama ndiye mwanaume ambaye amenifikisha hapa ila huwa najali maslahi yangu binafsi tu. Kuna muda sikulaumu sana kwa sababu niliwahi kufundwa kabisa kuhusu kitanda ndio maana mwanaume yeyote ambaye anauona uchi wangu na kunipanda kamwe hawezi kuniacha ila kwa wewe, you were too smart for that sijajua kama ni ushamba wako wa mapenzi ambayo hata hauyajui ndo umekufanya ukawa zuzu kiasi hiki? Hebu fikiria kama taifa lilikuwa limekutuma kufanya kazi nyeti nje ya nchi si ndo ungekuwa umesha liingiza taifa hasara wewe? Na ukumbuke kwamba huko nje ya nchi kuna wanawake warembo na wanawake watamu sana hata zaidi yangu, hahahahah hahahaha”
“Kosa ambalo umelifanya ni kukurupuka kuja huku bila kupiga hesabu kwamba ukishakuja huku ni kipi ambacho kinabaki kinatokea huko ulikotoka, unajua kinacho endelea? Ulipaswa kwanza kujiuliza kwamba Karistus yuko wapi ambaye wewe umemzoea kwa jina la Dax. Hapo unaona kosa la kwanza ambalo umelifanya kukurupuka? Dax alikuwa pale pale Ikulu kwenye ofisi ya katibu akiwa amejificha kwa sababu yule katibu pia ni kijana wetu, maskini raisi wa watu changundoa yule hana msaada wowote kwa sasa”
“Umekuja hapa ukiwa umemuacha raisi wako anakufa bila msaada wala kutoa wosia wake wa mwisho kwako na kwa wenzako pia, hii ni mbaya sana kwa upande wako lazima. Lakini pia hao vijana wa DRAGON BOYS ambao bila shaka ulihisi watakuwa msaada mkubwa sana kwako, kule kwa Madilu wametengenezewa mtego wanaenda ni kufa tu na hakuna hata mmoja ambaye anaweza kutoka akiwa hai”
“Inanisikitisha sana, wewe upo kwenye wakati mgumu sana namna hii, wewe unakamatwa saivi kusubiria muda wako wa kuuawa ufike, raisi wako muda wowote kuanzia sasa anakufa lakini hata wale vijana watatu ambao unawategemea kwa sasa nao wanaweza kufa kuanzia wakati huu. Unahisi utafanya nini maskini?” Brandina alikuwa anampa somo Max namna walivyokuwa wameicheza michezo yao huku akiwa anamskitikia kinafiki sana mwanaume huyo ambaye alikuwa anamsikiliza mwanamke huyo kwa umakini sana wakati huo.
“Unataka kujua baada ya haya kutokea kitafuata nini? Unataka kujua kipi kitafuata baada ya raisi kufa, baada ya wenzako watatu kufa na wewe kuwa hai? Kiukweli ni kwamba nilikuwa nataka nikuue huku huku ni basi tu unatakiwa kufika kule ukiwa mzima wa afya. Sababu ya wewe kuwa hai ni kwamba raisi akifa utakamatwa ukiwa haujadhurika kabisa ili kuwe na ushahidi kwa watu kuhusu wewe kumuua raisi na picha nyingi sana zitapigwa ukiwa karibu na mwili wa raisi lakini baada ya hapo wewe utauawa na taarifa zitachapishwa kwamba umeuawa ukiwa unataka kuwashambulia makomando ambao walikuwa eneo la tukio kukudhibiti Max. unataka kujua tena nini kitafuata baada ya wewe kufa?”
“Huenda hii ndiyo sehemu mbaya zaidi ambayo hautaipenda kwa sababu naenda kuwa waziri mkuu wa nchi hii kwa kazi kubwa ambayo nimeifanya lakini waziri mkuu atarudishwa nchini kisha wananchi watatungiwa uongo mwingine wa kupewa, unataka kusikia huu uongo utakuwaje Max?”
“Magazeti yataandikwa kwa ukubwa kwamba Gaidi namba moja aliye muua raisi auawa eneo la tukio na kuwapongeza mshujaa ambao wamelifanikisha hilo. Kisha Denis Kijazo atasimama kwenye vyombo vya habari na kukanusha habari ile mbaya ambayo raisi aliisema kwamba yeye ndiye mbaya wa nchi ni kwa sababu tu raisi huyo alikuwa na mipango miovu sana juu ya taifa hili na Denis Kijazo alisimama ili kupingana naye ndipo akaanza kumchafua na kumtishia kifo huku wewe ukionekana kama mtu ambaye ndiye ulikuwa unatumwa na raisi Teodensia Mpanzi kufanya shughuli zake haramu na baada ya kufanya kazi zake nyingi alitaka kukuua ili kulinda siri zake ila kwa bahati mbaya sana ukamuwahi na kumuua”
“Nadhani hii itakuwa habari mbaya sana pale ambapo kila mtu atajua kamba wewe na raisi pamoja na kundi lako mlikuwa magaidi. Kuhusu wananchi wao huwa wamwamini kiongozi muongo zaidi na anayewapa uongo ambao unawafurahisha kisha wataahidiwa kushushiwa kodi kidogo na kupatiwa malipo kwa usumbufu wa vitisho ambavyo walivipata na vinguo kidogo na watasahau kila kitu ambacho kilitokea na wakati huo unajua wewe na wenzako mtakuwa wapi?”
“Mtakuwa mmekufa, watu ambao mlijitoa kulipigania taifa hili kwa hali na jasho, historia itawaandika kama magaidi na watu wataishi wakiwa wanawachukia sana wakiamini nyie ndio watu ambao kwa kiasi kikubwa mlichangia kuimomonyoa amani ya taifa hili. Waziri mkuu atatangazwa kuwa raisi rasmi wa Tanzania na nchi itarudi kwa Denis Kijazo and we don’t give a https://jamii.app/JFUserGuide Max kwamba who is the owner kikubwa sisi tunaangalia maslahi yetu tu basi mengine hayatuhusu.”
“Nadhani kwa sasa umetambua kwamba ni nani mwenye karata ya ushindi. Unahisi utaweza kujisaidia na kuwasaidia wengine ambao umewaacha huko Dar es salaam? Upo nje ya muda, labda jaribu bahari yako kwani ninajua kwamba wewe ni mtu hatari sana ila pia unatakiwa kutambua kwamba najua uhatari wako ndiyo maana nimekuandalia hawa wanaume ambao ni zaidi yako. Mimi naenda kusikiliza muziki ndani, good luck DONNY” Alipewa shule haswa mwanaume na kila ambacho aliambiwa kilikuwa kinamuingia moja kwa moja kwenye moyo wake mpaka alijihisi kwamba alizingua sana, B aliiangalia saa yake na kutabasamu kisha akaingia ndani na kuwaachia wanaume uwanja waweze kufanya yale ambayo yalikuwa yanawahusu.
Mwanaume mmoja alimrushia pingu na kumtaka ajifunge mwenyewe bila kuumizwa ili wawahi kutoweka ndani ya hilo eneo, mwanaume aliona kama hiyo ilikuwa ni dharau kubwa sana ukizingatia alikuwa kwenye hasira kubwa sana. Alimsogelea mwanaume huyo ambaye alimrushia hiyo pingu akiwa ameiokota na kuishika mkononi, mwanaume huyo naye alimsogelea pale alipokuwepo akiwa anazikunja ngumi zake maana hakuwa akiruhusiwa kuweza kutumia silaha ambayo ingeweza kuyatoa maisha ya Max.
Kusogea kwake alikutana na pingu ambayo ilirushwa kwa nguvu sana ikiwa inakuja upande wake, alijaribu kuinama ili asipate madhara lakini alishindwa kutokana na ukaribu sana ambao walikuwepo hivyo ilimpasua kwenye pua yake hali ambayo ilimfanya afumbe macho yake na wakati anafumbua alikuwa amechelewa sana. Shoka lilipitishwa kwenye uso wake na kuuchana chana uso wake vibaya mno hali ambayo iliwafanya wenzake kuja kwa kasi sana maana waliona kumchukulia kimzaha mwanaume huyo ingewaletea madhara makubwa sana isivyo kawaida.
Walikuwa wanakuja kwa kujizungusha maana walikuwa wengi, Max alijaribu kurudi nyuma kwa nguvu ili kuweza kupishana nao wote lakini asingeweza kuzikwepa ngumi kumi na mbili kwa pamoja. Alipigwa mabuti na ngumi kali sana japo hata yeye alifanikiwa kuwapiga wanaume wawili, kipigo kizito ambacho kilitua kwenye mwili wake kilimbeba kwa umbali kidogo na kumfanya ajivute huku akilichomweka shoka chini ambalo lilimpa balansi ya kutulia vizuri. Alisimama kwa nguvu kupitia shoka lake kisha akadunda kwenye mpini ambapo aliruka sarakasi na kulirudia shoka lake ambalo lilikuwa chini na wakati anafanikiwa kunyanyuka aliachia shoka hilo kuelekea kwa wale wanaume huku yeye mwenyewe akiwa anakuja kwa kasi mno.
Shoka lilitua kwa mwanaume mmoja kwenye kiuno chake, hali ambayo ilimfanya kupiga kelele kwa nguvu sana maana alipata maumivu makali lakini wakati huo huo mwanaume alikuwa amefika akiwa anachomoa visu viwili kwenye kiuno chake. Alijirusha kwa sarakasi ya hatua ndefu ambapo alipishana nao wakiwa wanamfuata maana yeye aliruka kwa juu na kutua karibu na mwanaume ambaye alikuwa mwishoni.
Alimdaka mwanaume huyo kwenye kola ya shati yake na kumguzia kwake, hakuwa na hadhithi za kumsimulia zaidi ya kuzamisha visu vyake kwenye shingo na kuichana chana huku akiwa anamsukumia mwanaume huyo pembeni maana hakufaa kabisa kuwepo ulingoni tena. Wanaume hao walianza kuingiwa na wasiwasi sana maana walikuwa saba lakini mpaka wakati huo wanne tu ndio walikuwa wamesimama mbele yake akiwa anawaangalia kwa hasira sana. Aliangalia saa yake mkononi, muda haukuwa rafiki kabisa kwake kwani aliambiwa kwamba alitakiwa kuwahi Dar es salaam kwa ajili ya kuwaokoa wenzake akiwemo mheshimiwa raisi ambaye alikuwa kwenye hatari kubwa sana.
Alivizungusha visu vyake akiwa anawasogelea ambapo walikuwa wamesimama, alidunda kwa buti moja kwa sarakasi ya mbele kisha akajivuta nyuma, wanaume wawili walidanganyika na ile sarakasi hivyo wakawa wamemfuata kwa pupa pale ambapo alikuwepo lakini kujivuta kwake kuliwafanya wakutane na hewa tupu huku yeye wakiwa wamemkosa. Baada ya kumkosa aliwasogelea mwenyewe ambapo mmoja alimpiga na kiganja eneo la sikio lake akaacha kabisa kusikia na mwingine alizamisha kisu kwenye moyo wake na kukishindilia kwa ngumi nzito sana kisha kwa kasi akamgeukia yule ambaye alikuwa bado anazunguka kwa maumivu ambayo aliyapokea kwenye sikio lake.
51 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 51
“Mlijua kwamba nitakuja hapa?”
“Yeah”
“Kivipi?”
“Tulikuwa tunabeti tu kama ikitokea mtu huyo akahojiwa basi akuelekeza wewe hivyo ili uje tukukamatie huku na huko ulikotoka watu wako wanauawa bila wewe kuwepo kisha unapewa kesi na kutangazwa kama gaidi na baada ya hapo utakuwa hauna kazi tena tunakuua”
“Hahahah hahahaha” Max alicheka kwa hasira sana kwa sababu alikuwa amechezewa mchezo wa kitoto sana.
“Unamaanisha Brandina hayupo huku?”
“Huyo yupo lakini kwa bahati mbaya hauwezi kumpata” mwanaume huyo aliongea huku akiwa anaichomoa bastola na kulenga tenki la mafuta la gari ambapo gari la Max lililipuka hivyo ikawa hakuna njia ya kumfanya yeye kurudi haraka ndani ya Dar es salaam.
“Ulitakiwa kuniua ukiwa na nafasi bado, umefanya kosa kubwa sana kuniacha hai wakati ambao ulikuwa unanishambulia”
“Hata mimi nilitamani sana kukuua ni kwa sababu tu siruhusiwi kukuua ndiyo maana mpaka sasa upo hai” wakati mwanaume huyo anamalizia kuongea Max alinyanyua buti lake na kuanza kuja kwa kasi kali mno. Alijirusha chini ya mchanga na wakati ananyanyuka hapo kasi ambayo alisimama nayo akiwa ameirusha michanga juu ilikuwa ngumu sana kwa mwanaume yule kuweza kuihimili hivyo akajikuta anapiga hewa na mwanaume alizunguka nyuma yake na kuliachia shoka lake kwa nguvu huku akiwa ameshikilia kwenye mpini.
Shoka hilo lilitua kwenye mgongo wa huyo mwanaume na kuupasua vibaya mno, alivutwa kisha shoka hilo likawekwa shingoni, alichinjwa mithili ya kuku wa pasaka. Aliachiwa chini akiwa mfu kama wa miaka mia nane iliyokwisha kupita. Max akiwa amesimama hapo alishangaa kuona geti likiwa linafunguliwa kama alama ya kumkaribisha aingie ndani, alishangaa sana na kuangalia pembezoni mwa geti hilo ndipo aligundua kwamba kulikuwa na kamera kila mahali kumaanisha kwamba watu ambao walikuwa ndani ya jengo hilo na pengine ambao walikuwa wapo nje ya jengo hilo walikuwa wanaangalia kile ambacho kilikuwa kinaendelea moja kwa moja.
Aliingia akiwa makini sana kuweza kuangalia mazingira ya ndani jinsi yalivyokuwa, ndani ya jengo hilo alikutana na sura ngumu saba za wanaume ambao walionekana kwamba walikuwa wanamsubiri kwa hamu kubwa sana. Akiwa anawahesabu kwa umakini wanaume hao alisikia sauti ya mtu akiwa anapiga makofi juu ya ghorofa, kwenye balcony alikuwa amesimama Brandina akiwa amevaa bikini huku nyuma yake akiwa amefunikwa na gauni ambayo mbele ilikuwa wazi na kuvifanya viungo vyake vilivyo nona sana kuonekana kwa usahihi.
“Wewe ni moja kati ya wanaume wajinga sana, you were too smart sikufikiria kama unaweza kuingia kwenye mtego wa kitoto ule kisa uchi wa mwanamke. Uchi umekufanya umewasaliti wenzako kwa kuiweka wazi mipango ambayo inaenda kuwateketeza wote kwa pamoja”
“Umeniangusha sana, kwenye nyumba yako ulikuwa unajifanya kwamba ulikuwa makini sana hasa kwenye kufanya maongezi yako lakini ulishindwa kutambua kwamba nilikuwa nimeweka vifaa vya mawasiliano kila sehemu hivyo kila ambacho ulikuwa unakiongea na kila ambacho kilikuwa kinaendelea mle nilikuwa nasikia lakini sio mimi tu na watu wengine wengi walikuwa wanasikia kirahisi sana ndiyo maana iliturahisishia kuweza kuzisoma alama zenu ambazo zilikuwa zinafuata” “Mpaka unafika hapa najua Philipo huenda umemuua kwa hasira na sijali kuhusu yeye hata kama ndiye mwanaume ambaye amenifikisha hapa ila huwa najali maslahi yangu binafsi tu. Kuna muda sikulaumu sana kwa sababu niliwahi kufundwa kabisa kuhusu kitanda ndio maana mwanaume yeyote ambaye anauona uchi wangu na kunipanda kamwe hawezi kuniacha ila kwa wewe, you were too smart for that sijajua kama ni ushamba wako wa mapenzi ambayo hata hauyajui ndo umekufanya ukawa zuzu kiasi hiki? Hebu fikiria kama taifa lilikuwa limekutuma kufanya kazi nyeti nje ya nchi si ndo ungekuwa umesha liingiza taifa hasara wewe? Na ukumbuke kwamba huko nje ya nchi kuna wanawake warembo na wanawake watamu sana hata zaidi yangu, hahahahah hahahaha”
“Kosa ambalo umelifanya ni kukurupuka kuja huku bila kupiga hesabu kwamba ukishakuja huku ni kipi ambacho kinabaki kinatokea huko ulikotoka, unajua kinacho endelea? Ulipaswa kwanza kujiuliza kwamba Karistus yuko wapi ambaye wewe umemzoea kwa jina la Dax. Hapo unaona kosa la kwanza ambalo umelifanya kukurupuka? Dax alikuwa pale pale Ikulu kwenye ofisi ya katibu akiwa amejificha kwa sababu yule katibu pia ni kijana wetu, maskini raisi wa watu changundoa yule hana msaada wowote kwa sasa”
“Umekuja hapa ukiwa umemuacha raisi wako anakufa bila msaada wala kutoa wosia wake wa mwisho kwako na kwa wenzako pia, hii ni mbaya sana kwa upande wako lazima. Lakini pia hao vijana wa DRAGON BOYS ambao bila shaka ulihisi watakuwa msaada mkubwa sana kwako, kule kwa Madilu wametengenezewa mtego wanaenda ni kufa tu na hakuna hata mmoja ambaye anaweza kutoka akiwa hai”
“Inanisikitisha sana, wewe upo kwenye wakati mgumu sana namna hii, wewe unakamatwa saivi kusubiria muda wako wa kuuawa ufike, raisi wako muda wowote kuanzia sasa anakufa lakini hata wale vijana watatu ambao unawategemea kwa sasa nao wanaweza kufa kuanzia wakati huu. Unahisi utafanya nini maskini?” Brandina alikuwa anampa somo Max namna walivyokuwa wameicheza michezo yao huku akiwa anamskitikia kinafiki sana mwanaume huyo ambaye alikuwa anamsikiliza mwanamke huyo kwa umakini sana wakati huo.
“Unataka kujua baada ya haya kutokea kitafuata nini? Unataka kujua kipi kitafuata baada ya raisi kufa, baada ya wenzako watatu kufa na wewe kuwa hai? Kiukweli ni kwamba nilikuwa nataka nikuue huku huku ni basi tu unatakiwa kufika kule ukiwa mzima wa afya. Sababu ya wewe kuwa hai ni kwamba raisi akifa utakamatwa ukiwa haujadhurika kabisa ili kuwe na ushahidi kwa watu kuhusu wewe kumuua raisi na picha nyingi sana zitapigwa ukiwa karibu na mwili wa raisi lakini baada ya hapo wewe utauawa na taarifa zitachapishwa kwamba umeuawa ukiwa unataka kuwashambulia makomando ambao walikuwa eneo la tukio kukudhibiti Max. unataka kujua tena nini kitafuata baada ya wewe kufa?”
“Huenda hii ndiyo sehemu mbaya zaidi ambayo hautaipenda kwa sababu naenda kuwa waziri mkuu wa nchi hii kwa kazi kubwa ambayo nimeifanya lakini waziri mkuu atarudishwa nchini kisha wananchi watatungiwa uongo mwingine wa kupewa, unataka kusikia huu uongo utakuwaje Max?”
“Magazeti yataandikwa kwa ukubwa kwamba Gaidi namba moja aliye muua raisi auawa eneo la tukio na kuwapongeza mshujaa ambao wamelifanikisha hilo. Kisha Denis Kijazo atasimama kwenye vyombo vya habari na kukanusha habari ile mbaya ambayo raisi aliisema kwamba yeye ndiye mbaya wa nchi ni kwa sababu tu raisi huyo alikuwa na mipango miovu sana juu ya taifa hili na Denis Kijazo alisimama ili kupingana naye ndipo akaanza kumchafua na kumtishia kifo huku wewe ukionekana kama mtu ambaye ndiye ulikuwa unatumwa na raisi Teodensia Mpanzi kufanya shughuli zake haramu na baada ya kufanya kazi zake nyingi alitaka kukuua ili kulinda siri zake ila kwa bahati mbaya sana ukamuwahi na kumuua”
“Nadhani hii itakuwa habari mbaya sana pale ambapo kila mtu atajua kamba wewe na raisi pamoja na kundi lako mlikuwa magaidi. Kuhusu wananchi wao huwa wamwamini kiongozi muongo zaidi na anayewapa uongo ambao unawafurahisha kisha wataahidiwa kushushiwa kodi kidogo na kupatiwa malipo kwa usumbufu wa vitisho ambavyo walivipata na vinguo kidogo na watasahau kila kitu ambacho kilitokea na wakati huo unajua wewe na wenzako mtakuwa wapi?”
“Mtakuwa mmekufa, watu ambao mlijitoa kulipigania taifa hili kwa hali na jasho, historia itawaandika kama magaidi na watu wataishi wakiwa wanawachukia sana wakiamini nyie ndio watu ambao kwa kiasi kikubwa mlichangia kuimomonyoa amani ya taifa hili. Waziri mkuu atatangazwa kuwa raisi rasmi wa Tanzania na nchi itarudi kwa Denis Kijazo and we don’t give a JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala Max kwamba who is the owner kikubwa sisi tunaangalia maslahi yetu tu basi mengine hayatuhusu.”
“Nadhani kwa sasa umetambua kwamba ni nani mwenye karata ya ushindi. Unahisi utaweza kujisaidia na kuwasaidia wengine ambao umewaacha huko Dar es salaam? Upo nje ya muda, labda jaribu bahari yako kwani ninajua kwamba wewe ni mtu hatari sana ila pia unatakiwa kutambua kwamba najua uhatari wako ndiyo maana nimekuandalia hawa wanaume ambao ni zaidi yako. Mimi naenda kusikiliza muziki ndani, good luck DONNY” Alipewa shule haswa mwanaume na kila ambacho aliambiwa kilikuwa kinamuingia moja kwa moja kwenye moyo wake mpaka alijihisi kwamba alizingua sana, B aliiangalia saa yake na kutabasamu kisha akaingia ndani na kuwaachia wanaume uwanja waweze kufanya yale ambayo yalikuwa yanawahusu.
Mwanaume mmoja alimrushia pingu na kumtaka ajifunge mwenyewe bila kuumizwa ili wawahi kutoweka ndani ya hilo eneo, mwanaume aliona kama hiyo ilikuwa ni dharau kubwa sana ukizingatia alikuwa kwenye hasira kubwa sana. Alimsogelea mwanaume huyo ambaye alimrushia hiyo pingu akiwa ameiokota na kuishika mkononi, mwanaume huyo naye alimsogelea pale alipokuwepo akiwa anazikunja ngumi zake maana hakuwa akiruhusiwa kuweza kutumia silaha ambayo ingeweza kuyatoa maisha ya Max.
Kusogea kwake alikutana na pingu ambayo ilirushwa kwa nguvu sana ikiwa inakuja upande wake, alijaribu kuinama ili asipate madhara lakini alishindwa kutokana na ukaribu sana ambao walikuwepo hivyo ilimpasua kwenye pua yake hali ambayo ilimfanya afumbe macho yake na wakati anafumbua alikuwa amechelewa sana. Shoka lilipitishwa kwenye uso wake na kuuchana chana uso wake vibaya mno hali ambayo iliwafanya wenzake kuja kwa kasi sana maana waliona kumchukulia kimzaha mwanaume huyo ingewaletea madhara makubwa sana isivyo kawaida.
Walikuwa wanakuja kwa kujizungusha maana walikuwa wengi, Max alijaribu kurudi nyuma kwa nguvu ili kuweza kupishana nao wote lakini asingeweza kuzikwepa ngumi kumi na mbili kwa pamoja. Alipigwa mabuti na ngumi kali sana japo hata yeye alifanikiwa kuwapiga wanaume wawili, kipigo kizito ambacho kilitua kwenye mwili wake kilimbeba kwa umbali kidogo na kumfanya ajivute huku akilichomweka shoka chini ambalo lilimpa balansi ya kutulia vizuri. Alisimama kwa nguvu kupitia shoka lake kisha akadunda kwenye mpini ambapo aliruka sarakasi na kulirudia shoka lake ambalo lilikuwa chini na wakati anafanikiwa kunyanyuka aliachia shoka hilo kuelekea kwa wale wanaume huku yeye mwenyewe akiwa anakuja kwa kasi mno.
Shoka lilitua kwa mwanaume mmoja kwenye kiuno chake, hali ambayo ilimfanya kupiga kelele kwa nguvu sana maana alipata maumivu makali lakini wakati huo huo mwanaume alikuwa amefika akiwa anachomoa visu viwili kwenye kiuno chake. Alijirusha kwa sarakasi ya hatua ndefu ambapo alipishana nao wakiwa wanamfuata maana yeye aliruka kwa juu na kutua karibu na mwanaume ambaye alikuwa mwishoni.
Alimdaka mwanaume huyo kwenye kola ya shati yake na kumguzia kwake, hakuwa na hadhithi za kumsimulia zaidi ya kuzamisha visu vyake kwenye shingo na kuichana chana huku akiwa anamsukumia mwanaume huyo pembeni maana hakufaa kabisa kuwepo ulingoni tena. Wanaume hao walianza kuingiwa na wasiwasi sana maana walikuwa saba lakini mpaka wakati huo wanne tu ndio walikuwa wamesimama mbele yake akiwa anawaangalia kwa hasira sana. Aliangalia saa yake mkononi, muda haukuwa rafiki kabisa kwake kwani aliambiwa kwamba alitakiwa kuwahi Dar es salaam kwa ajili ya kuwaokoa wenzake akiwemo mheshimiwa raisi ambaye alikuwa kwenye hatari kubwa sana.
Alivizungusha visu vyake akiwa anawasogelea ambapo walikuwa wamesimama, alidunda kwa buti moja kwa sarakasi ya mbele kisha akajivuta nyuma, wanaume wawili walidanganyika na ile sarakasi hivyo wakawa wamemfuata kwa pupa pale ambapo alikuwepo lakini kujivuta kwake kuliwafanya wakutane na hewa tupu huku yeye wakiwa wamemkosa. Baada ya kumkosa aliwasogelea mwenyewe ambapo mmoja alimpiga na kiganja eneo la sikio lake akaacha kabisa kusikia na mwingine alizamisha kisu kwenye moyo wake na kukishindilia kwa ngumi nzito sana kisha kwa kasi akamgeukia yule ambaye alikuwa bado anazunguka kwa maumivu ambayo aliyapokea kwenye sikio lake.
51 inafika mwisho.
mbona rais anatia huruma jamani
 
Mkuu [mention]FEBIANI BABUYA [/mention] jana hatujalala kusubiria hizo episode 5, jitahid leo tuwekee
Poleni na mnisamehe sana.

Majukumu yalinikaba nikasahau hata kuingia huku tena.

Naziweka muda huu [emoji996]
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 52
Hakuwa na stori naye maana alizamisha kisu kwenye jicho lake na kukichomoa kwa nguvu kisha akakizamisha kwenye shingo na kukisukumizia kwa kasi ambapo kilizama mpaka kikatokezea upande wa pili habari yake ikaishia hapo huku mwanaume akiwa amebakia mikono mitupu na hakutaka kabisa kutumia silaha yoyote kwa wakati huo. Aliwaita wale wawili ambao walikuwa wamebaki kwa mkono ili waje na waache kuwa waoga, wanaume hao licha ya kuwa na miili ya kutisha sana walikuwa wanaogopa mno hivyo walianza kusogea wakiwa na wasiwasi mkubwa sana.
Mwanauume mmoja alijirusha kwa nguvu na double kick ambapo Max alibendi chini kuikwepa, wakati mwanaume huyo anashusha miguu chini alikutana na buti kwenye mguu ambao ulitangulia kutua chini. Alishtukizwa mno hivyo akawa anashuka chini bila balansi lakini alikutanishwa na buti la kifua na wakati anataka kudondokea kwingine Max alimdaka na kuizungusha shingo yake huku akipiga ngumi nyingi sana kifuani ambapo kifua hicho kilivunjwa vibaya sana na kubaki kinanesa nesa kama bembea. Alipokuja kumuachia mtu huyo alikuwa kama alikufa miaka mingi sana.
Mmoja alikuwa anaangalia sehemu ambayo ni kama alitaka kukimbilia
“Unaenda wapi mtoto wa kiume, njoo uniue?” mwanaume aliongea kwa sauti ambayo ilimtisha sana yule mwanaume wa kazi, alikuwa kama amependwa na wazimu na kwa namna alivyo ona anawaua wenzake alikuwa ameanza kumuogopa sana lakini Max alikuwa anamsogelea pale alipo.
“Nipige, nipige” alitamka kwa sauti kali akiwa anampa ishara mtu huyo ampige ambapo alianza kufanya hivyo na kumfanya Max kutoka damu mdomoni na puani.
“Acha kupiga kama mtoto mdogo, piga ngumi za kiume mshenzi wewe” alitamka kwa msisitizo kiasi kwamba mwanaume huyo alirusha ngumi nzito sana, Max hakukwepesha naye alirusha ngumi nzito ambayo ilikutana na ngumi na mwanaume huyo. mkono wake ulivunjwa vibaya sana kwani uzito wa ngumi yake ulishindwa kuendana na kasi ambayo max alikuwa ameirushia ngumu yake hali ambayo ilimfanya mwanaume huyo kupiga makelele kama mtoto mdogo.
Max alimuita tena kwa mkono wake ambapo alikuja kwa spidi na mkono mmoja ambao ulikuwa umebaki, Max alimuacha mtu huyo ampige na ngumi hiyo lakini naye wakati anakaa sawa alipigwa mtama wa nguvu na wakati anadondoka mwanaume alimdaka na kumgeuza kwa nguvu kisha akamshushia kwenye goti lake ambapo aliuvunja uti wa mgongo kama utani lakini mwanaume huyo akawa ameumaliza mwendo kikatili sana.
Alikuwa amebakia mmoja ambaye alipigwa shoka la kiuno, mwanaume alisogea na kuliokota shoka lake akiwa anamsogelea mwanaume yule ambaye alikuwa anafanya juhudi za kuweza kujivuta nyuma lakini haikuwa ikiwezekana kabisa kufanya hilo jambo. Mwanaume hakutaka kupiga naye stori nyingi sana alinyanyua shoka lake na kukipasua kifua chake vibaya sana kisha akaitoa bastola moja na kupandisha nayo ghorofani mkononi akiwa na shoka lake.
Baada ya kufika kwenye mlango wa humo ndani aliukanyaga kwa nguvu sana na baada ya kufika ndani alimkuta Brandina akiwa anakatika huku kwenye mkono wake akiwa na bastola ambayo aliigeuzia haraka sana kwa Max maana ni kama hakuamini kama mtu huyo alikuwa amepona kwa sababu alijua moja kwa moja kwamba wanaume ambao walikuwa chini wangeweza kumdhibiti, licha ya kuwa na mziki wa sauti ya juu humo ndani bado ule mvunjiko wa mlango aliusikia vizuri sana.
“Usifanya ujinga wowote nitakupiga risasi Max”
“Unajua kabisa nipo fasta kuliko wewe, unavyo nitishia bastola kumbuka hata mimi ninayo mkononi na kama tukipiga risasi kwa pamoja unajua kabisa kwamba risasi yangu itakupata lazima na wewe haujui kama mimi utanipata au utanikosa”
“What do you want Max?”
“Unauliza nini nataka saivi?”
“Ndiyo”
“Kukuua wewe na washenzi wenzako wote”
“Kumbuka huwezi kuniua mimi kwa sababu unanipenda sana”
“Acha maneno binti, weka bastola yako chini ujitetee kwa mikono yako sitaki nikuue haraka sana kwa risasi ila kama ukilazimisha nitafanya hivyo”
“Siwezi kukuamini”
“Wakati unakata viuno hapo kama ningetaka kukuua ningekupiga risasi hivyo sitaki kukuua kama yatima, nataka ufe ukiwa unayapambania maisha yako ili ujue kauli zako kama zinaweza kukurudia mwenyewe” Brandina hakuwa na namna akiwa anatetemeka aliirushia bastola yake pembeni kwa sababu alijua kabisa kwamba hawezi kuendena na kasi ya Max angekufa kama angejaribu kufanya urushaji wa risasi hivyo akaamua kubeti maisha yake kwa kuyapigania na kuyatetea kwa mkono japo alikuwa anazisikia hadithi za mwanaume huyo ambaye alikuwa mbele yake kwamba kwenye dunia ya mapigano hakuwa levo yake kabisa na jambo ambalo lilikuwa linamtisha sana ni baada ya mwanaume huyo kufanikiwa kuwaua wanaaume ambao aliwakuta nje ambao Brandina aliamini kwamba wangemkamata kirahisi sana maana alihakikishiwa kwamba walikuwa wana uwezo kuliko Max lakini mambo yalikuwa yanaenda nje na matarajio na wakati huo alikuwa mwenyewe akiwa anatakiwa kuyatetea maisha yake.
Max pia alirusha bastola yake pembeni na kuliachia shoka kuelekea alipokuwepo Brandina ambapo aliinama na shoka hilo likaenda kukita ukutani. Mwanaume alidunda kwenye sofa akiwa anamfuata Brandina kwa haraka mno maana hakutakiwa kukaa sana hapo, mrembo huyo aliyaona mateke ambayo yalikuwa yanakuja hivyo akawa ametumia mikono yake kuyapangua lakini mikono ilikuwa laini sana mbele ya mguu wa mwanaume wa kazi kama huyo hivyo licha ya kuyazuia lakini bado yalimbeba mbaka ukutani ambapo alijibamiza na kusimama huku gauni lake likiwa limetoka mwilini hivyo akawa amebakiwa na bikini tu pekee.
Alirudi kwa sarakasi kuhitaji kumshambulia Max lakini wakati anamkaribia Max alijivuta nyuma kisha akalivuta kwa nguvu kapeti ambalo lilikuwa chini ya sakafu. Brandina alitua vibaya baada ya kapeti hilo kuvutwa tofauti na alivyokuwa amekusudia yeye hivyo alidondoka vibaya sana na kujigongesha kwenye meza ya kioo ambayo ilikuwa pembeni na kumfanya achanike kwenye mbavu yake. Alisimama akiwa na maumivu na wakati huo Max alikuwa anamsogelea akiwa anamwangalia binti huyo kwa macho ambayo yalikuwa yanawaka moto kwani ndiye ambaye alikuwa chanzo cha kila kitu mpaka mipango yao inaharibika.
Brandina alirusha ngumi zake ambazo zilikuwa kama karatasi tu mbele ya mwili wa Max, mwanaume alimdaka mwanamke huyo na kumpiga ngumi moja nzito sana ya kifua ambayo ilimfanya ateme damu ghafla lakini hakumuachia aliendelea kumkita na ngumi hapo kwenye kifua huku akiwa anamwangalia machoni na alipokuja kumuachia Brandina alikuwa hoi sana. Mwanaume alisogea mpaka pale ukutani na kulichomoa shoka lake kisha akawa anarudi alipokuwa mrembo huyo na wakati ule Brandina alikuwa anafanya jitihada za kuweza kuisogelea bastola alipokuwa ameirushia akiwa anajivuta lakini ule mkono ambao ulikuwa umeikaribia bastola hiyo ulikatwa na shoka na kumfanya abaki ameduwaa kwa muda asiamini kile ambacho alikuwa anakiona.
Mshtuko ulipoisha alitoa kilio kikali sana cha maumivu, kwa mwanamke mrembo kama yeye kuanza kukosa baadhi ya viungo kwneye mwili wake lilikuwa ni tatizo kubwa sana na ni kitu ambacho kingemfanya awe na picha ya tofauti sana popote ambapo alikuwa anapita. Max alimsogelea pale ambapo alikuwa amelala akiwa anageuka geuka kwa maumivu.
“Ulikuwa sahihi kusema kwamba mimi ni mwanaume mshamba sana, mwanaume mjinga sana kwa sababu ya uchi wako nikakuamini na kukupa taarifa ambazo haukutakiwa kabisa kuzipata na ni jambo ambalo nakubali kulaumiwa kwa sababu kuingia kwako kwenye maisha yangu kumefanya nimeyahatarisha maisha ya raisi na watu ambao huenda taifa hili lilikuwa linawahitaji sana kuliko kitu chochote kile. Hilo ni jambo ambalo nitalibeba mpaka siku naingia kaburini”
“Nakumbuka Bilali alinishauri sana nisimwamini mtu yeyote hata yule ambaye nahisi napaswa kumuamini sana lakini alinipa ushuri kwa kuchelewa sana hivyo hakuna kitu ambacho ningeweza kukibadilisha kwa wakati ule na niliamua kuyaficha yote nikijua kwamba nitakuwa nakulinda wewe lakini kwa bahati mbaya sana nilikuwa nafanya jambo la kipuuzi sana bila mimi mwenyewe kujua ona sasa tumefikia huku. Kwanini B uliamua kufanya haya?”
“Huwezi kuelewa Max, naomba uniue tafadhali sana mimi siwezi kuishi nikiwa hivi”
“Unahisi kwamba nakuuliza kwa kukubembeleza au?”
“Kila mtu huwa anachagua njia zake kwenye maisha Max ila haya mambo yatakuwa na mwisho mbaya sana”
“Hilo nalijua ndiyo maana nipo hapa, nataka uniambie kwamba kwanini uliamua kuyafanya haya na kwanini wewe uwe mpenzi wa Philipo Tibaigana?”
“Hahaha haahhaah hahaha unaumia kuona kwamba nilikuwa nampa uchi wangu mwanaume mwenzako ambaye sio w…….” Brandina hakuweza kuendelea na taarabu zake kwani aliishia kwenye maumivu na kilio kikali sana baada ya shoka kupita kwenye kiganja cha mguu wake na kumfanya kuwa kilema wa maisha. Aliuangalia mguu wake na kulia sana maana hakuwa akiamini kama mrembo kama yeye kuna siku atakuja kufikia kuwa kwenye hatua mbaya kama hiyo ambayo itamfanya asiweze hata kujiamini kusimama mbele ya mwanaume yeyote atakaye katiza mbele yake.
“Huenda ulikuwa unanijua kama Max ambaye ulimfanya kuwa fala kwako ila nakuhakikishia kwamba upande wangu wa pili wa shilingi haunijui zaidi ya kusikia tu watu wakiwa wanauongelea. Usinifanye nikakuuliza mara mbili mbili maana utapoteza viungo vyako vyote mwilini”
“Kwa sababu ya pesa Max, tafadhali sana naomba uniue”
“Mimi siwezi kukuua kirahisi sana namna hii bibie. Kwahiyo pesa ndiyo ilikufanya uisaliti nchi yako na raisi wako?”
“Ndiyo”
“Ni mpango gani ambao unafuata kwa sasa?”
“Yote nimeshakwambia Max na unavyo endelea kukaa hapa utakuta watu wako wote wameisha hata na huyo raisi ambaye unajisifia kwamba ni wako”
“Nakuahidi B hawa mahawala wenzako nitawaua wote tena nitawaua kikatili sana na ndiyo maana nitakuacha ukiwa hai ili kazi ikiisha nije nikuchukue na kwenda kukuonyesha walipo. Nakuhakikishia kwamba kwenye taifa hili hakuna mtu hata mmoja ambaye atazaliwa na kuweza kutishia amani ya nchi yetu labda kama nitakuwa sipo hai. Kwa sasa nahitaji unionyeshe usafiri wa dharura humu ndani uko wapi?”
“Siwezi kufanya hivyo na hakuna kitu ambacho utakiokoa”
“Bado unaniletea jeuri sio?”
“Go and https://jamii.app/JFUserGuide yourself Max” mwanaume hakubonga sana alisogea pembeni akaiokota bastola yake na kumiminia risasi tatu kwenye goti la Brandina. Mrembo huyo alipiga sana kelele za maumivu tena kwa sauti kubwa mno lakini hakuna ambacho kiliweza kumsaidia. Max alilishika shoka na kuukata mguu huo kuanzia kwenye goti.
“Bado huwezi kusema?”
52 inafika tamati.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 53
“Nasema nasema tafadhali usinifanyie haya yote Max mimi kweli nilikupenda kutoka moyoni ni kazi za watu tu zilinifanya nikafikia hapa”
“Nakusikiliza”
“Nyuma ya nyumba hii kuna mlango wa chuma na huko unatumia kuhifadhia magari na pikipiki. Namba ya siri ya kufungulia ni namba yako ya utambulisho”
“Why?”
“Sijui ila inesemekana kwamba kama usingezingua haya yote wewe ndo ungekuja kuwa kiongozi wetu ndiyo maana walianza kuandaa mazingira mapema sana”
“Goodbye bitch” Max aliongea akiwa analipitisha shoka mara mbili kwenye uso wa Brandina na kuchora X. hakuzamisha kiasi kwamba angemuua mwanamke huyo bali alipitisha kuacha alama ambazo zilichimba chimba sana uso wa mwanamke huyo na kufanya sura yake kuharibika sana. Mwanaume alianza kutoka haraka sana humo ndani ili aweze kufanikiwa kurudi ndani ya jiji la Dar es salaam maana ulikuwa ni usiku wa kutosha tayari.
“Niue tafadhali Max, nakuomba usiniache hivi niue” sauti yake ni kama alikuwa anampigia mbuzi gitaa kwani mwanaume huyo alikuwa ameshatoweka na kwenda huko nyuma ambako alitoka na pikipiki moja kubwa ya bei ghali sana na kutoweka kwa kasi ya ajabu mno ndani ya hilo eneo. Brandina baada ya kubaki pekeyake, alijivuta kwa tabu sana maana hali yake ilikuwa ni mbaya mno hivyo alitumia muda mrefu sana mpaka kuifikia bastola yake ambayo aliirushia hapo yeye mwenyewe na baada ya kufika hapo alijipiga risasi ili apumzike maana mateso ambayo alikuwa anayapitia yalikuwa ni makali sana.


Mambo yote ambayo yalikuwa yanatokea kule Bagamoyo yalikuwa yanaonekana moja kwa moja kwa Denis Kijazo. Alikuwa amekaa kwake akiwa analishuhudia tukio hilo moja kwa moja na alijua kabisa kwamba lazima ingekuwa hivyo kwahiyo mpango wake bado ulikuwa unafanya kazi kwa usahihi sana. Aliinyanyua simu yake na kuipiga Ikulu moja kwa moja bila wasiwasi ambako alijua kwamba itakuwa safari ya kwanza kabisa ya Max kufika ili kuhakikisha usalama wa mheshimiwa raisi.
“Ndiyo Bosi” mwanaume ambaye aliipokea simu hiyo alikuwa ni kijana mtiifu sana kwake, kijana ambaye alikuwa anautafuta umaarufu kwa nguvu sana ili kuweza kuhakikisha anapata jina kubwa na nafasi kubwa ambayo itamfanya awe anakula meza moja na wakubwa. Karistus Dickson ambaye jina lake la kifupi alikuwa anaitwa KD huku namba yake ya utambulisho ikiwa ni 002 lakini kiongozi wake alimpatia jina feki ambalo alikuwa analitumia kwenye mikakati ya siri kwa jina la Dax ndiye ambaye alikuwa hewani kwenye simu wakati huo.
“Asijue mtu yeyote kwamba mkurugenzi wa usalama wa taifa amekufa mpaka akiapishwa raisi mwingine ambaye atamchagua mkurugenzi mwingine. Max anarudi saivi na lazima moja kwa moja atakuja hapo Ikulu hivyo nahitaji uandae mazingira mapema kabisa ya kufanya hivyo lakini pia hakikisha kijana yeyote ambaye unahisi kwamba hayupo upande wetu mnamuua haraka sana na hilo jambo lifanyike kimya kimya, kuna watu wangu wengine ambao nawatuma hapo kuja kuhakikisha Ikulu inakuwa salama na wakati Max anaingia hapo asizuiliwe akiingia ndani ndipo mchezo unatakiwa kuanzia hapo.
“Sawa bosi, na raisi nimfanye nini?”
“Mfanye unacho jisikia wewe ila hakikisha anakufa kwa kuchomwa visu ili huyo mpuuzi anapofika hapo uwe umemaliza kazi tayari. Mimi nitakuwa na waandishi wa habari kuanzia sasa ambao walikuwa wanataka kunihoji kwa muda mrefu sana na nimewakaribisha nyumbani hivyo tukio hili litakuwa moja kwa moja kwenye mitandao kwahiyo hata huyo malaya akifa mimi nitakuwa nje kabisa ya hatia na kila mtu atajua huo muda nitakuwa na waandishi wa habari na baada ya kuhakikisha mmemkamata Max nipigie simu nikiwa kwenye mkutano wa habari ili nitangaze moja kwa moja kuhusu kifo cha raisi kwa mshtuko sana ambao utafanya watu waamini kwamba nilikuwa nampenda sana raisi huyo na itaaminika kwamba sikuhusika kwa namna moja ama nyingine kuhusu kufa kwake”
“Na vipi kuhusu makamu wa raisi?”
“Makamu wa raisi nimemuua hivyo hawezi kua raisi tena, jaji mkuu nimempa nafasi ya kukaa mbali na haya maana naye alitaka kunizunguka na spika ni kijana wangu hivyo mtu pekee ambaye anabakia kwenye hii nafasi ni waziri mkuu ambaye nimempigia simu amerudi ila yupo airport bado kwenye ndege kama ikitokea kuna tatizo basi atatoweka haraka sana lakini kama kazi ikienda vizuri basi nakuhakikishia waziri mkuu anakuja kuapishwa na mambo yetu mengine yataanzia hapo kama zamani tu”
“Sawa kiongozi” maelekezo yalikuwa yanajitosheleza sana na baada ya kumalizana na hilo simu ilikatwa na Dax akawa anatakiwa kutekeleza kile ambacho aliambiwa. Mwanaume hakuwa na wasiwasi kabisa kwani alijua kwamba ndani ya Ikulu hiyo asilimia zaidi ya tisini walikuwa ni watu wa Denis Kijazo ambao wengi aliwapata kwa kuzitisha familia zao kuzifanyia mauaji hivyo dakika za mwisho sana walijikuta wanamkataa raisi wao na kumfuata mtu huyo ambaye ndiye alionekana kuwa na kisu kikali wakati huo wa vita.
Kwa wale watu ambao hawakuwa upande wa mheshimiwa Denis Kijazo walikuwa wanauawa kwa kuchukuliwa mmoja mmoja na mpaka hatua ya mwisho kabisa mwanaume alikuwa amemaliza kuisafisha kazi yake na kuelekea moja kwa moja kwenye ofisi ya raisi huku kila mtu akiwa anampa heshima kwani alikuwa ni mtu wa kuaminika sana kwa kiongozi wake. Alifika kwenye ofisi ya katibu wa raisi, mwanamke huyo alimkimbilia mwanaume huyo na kumyonya mate kwa furaha sana. Hilo huenda ni jambo ambalo hata raisi mwenyewe hakuwahi kabisa kulijua kwamba alikuwa amezungukwa na mamluki kila sehemu ambayo alikuwepo hivyo akawa anajijengea kaburi lake mwenyewe bila kujua.
“Baby nenda nyumbani ili hii kesi usije ukahusishwa kabisa kwani itaonekana kwamba muda wa kazi ulikuwa umepita hivyo kwa wewe haukuwepo kabisa hapa”
“I love you babe” mwanamke huyo hakuwa mbishi maana alikuwa anaujua mchezo mzima hivyo alibeba kimkoba chake na kutoweka ndani ya hilo eneo akiwa hana hata wasiwasi kwenye uso wake kabisa. Dax alisimama na kuvua shati yake kiasi kwamba alibakia na vesti tu pekee huku akiwa anahema kwa nguvu sana na wakati huo alikuwa anausogelea mlango wa ofisi ya raisi kwenda kutekeleza kila ambacho aliagizwa na bosi wake.

Teodensia mpanzi, raisi wa taifa la Tanzania alikuwa ndani ya ofisi yake usiku huo akiwa anasubiri ripoti ya Max lakini pia ripoti kutoka kwa Bilali ili kujua kwamba walikuwa wamefikia hatua gani juu ya kile ambacho walikuwa wanakifanya. Alisubiri kwa muda sana lakini hakupata simu wala majibu kutoka kwa watu hao juu ya nini ambacho kilikuwa kinaendelea kitu ambacho kilianza kumpa hofu sana maana hao wawili ndio ambao alikuwa anawaegemea sana kuweza kuyakamilisha majukumu ambayo yalikuwa mbele yake.
Hofu yake uilimfanya kusogea kwenye droo yake moja ya hapo ofisini kwake na kuichukua simu yake ili aweze kuwapigia watu hao lakini alishtuka baada ya kuona kwamba simu haikuwa ikitoka. Alishangaa sana maana haikuwa kawaida kwenye ofisi yake kukutana na jambo la aibu kama hilo hivyo alijaribu tena lakini ni vile vile hakuna kitu ambacho kilibadilika hali ambayo ilianza kumpa mashaka na alipo angalia vizuri aligundua kwamba hakukuwa na mtandao.
Alisogea kwenye kamera ili kujua kwamba ni kipi ambacho kilikuwa kinaendelea humo ndani ila kwa bahati mbaya sana kwenye kamera kilikuwa kinaonekana kiza tu. Alianza kuhisi kwamba hakuwa kwenye mazingira salama kwa wakati huo hivyo alisogea haraka kwenye mlango ili kuweza kuupiga loki, lakini kwa bahati mbya sana alikuwa amechelewa kufanya maamuzi kwani wakati anafika hapo mlangoni ni wakati ambao mlango huo ulikuwa unasukumwa kwa nguvu sana mpaka ukawa umemgonga kwenye uso wake na kumrushia kwenye sofa.
Aliyekuwa ameingia hapo hakuwa mwingine bali Dax akiwa na wanaume ambao walikuwa kwenye mavazi ya suti huku yeye akiwa na vesti tu pekee kifuani.
“Dax”
“Nakusikia”
“Unafanya nini kwa raisi wako mpuuzi mkubwa wewe?”
“Raisi wangu? Unahisi mimi ni mjinga sana mpaka kuwa na raisi changudoa?”
“Angalia sana mdomo wako, hili ni jambo ambalo utalijutia kwenye maisha yako yote”
“Badala upige magoti bado unaendelea kunitishia kuhusu nafasi ambayo hata hauna mpaka sasa?”
“Unahitaji nini Dax na kwanini unakubali kutumika kuisaliti nchi yako?”
“Unajua wapi ulipokosea Teo?” mwanaume alimuita jina lake kabisa tena kwa kulifupisha badala ya kumpa heshima yake kama raisi wake kisha akaendelea
“Ulikosea pale ambapo ulikuwa unajua kwamba sipo upande wako halafu bado ukawa unaniangalia tu kwa kujifanya kwamba wewe ni smart sana lakini je ni kweli kwamba wewe ni smart sana? Jibu ni hapana kwa sababu uliwaamini watu ambao hawakutakiwa kuaminika. Max alifanya kosa sana kushawishika na urembo wa Brandina na kuingia kwenye ule mtego pale ndipo tulipo tumia kujua hatua zenu zote ambazo mlikuwa mnataka kuzipiga na wakati anakuja kushtuka alikuwa ameshachelewa tayari na huo wakati ambao nyie mnajipanga sisi tulikuwa tunautumia kuhakikisha tunawamiliki watu karibia wote ndani ya Ikulu”
“Unamaanisha kwamba Ikulu nzima wamenisaliti?”
“Kama wangekuwa na wewe unahisi mimi ningefanikiwa kufika humu ndani ya ofisi yako? Ikulu ndiyo sehemu inayolindwa zaidi ndani ya nchi hivyo ukiona kwamba nimefanikiwa kufika hapa basi ujue kabisa kwamba hakuna mtu ambaye yupo upande wako kwa sababu kama wangekuwa upande wako basi wangekuwa wameniua au kunikamata kwa muda mrefu sana”
“Umefanikiwa vipi kuwafanya hawa wazalendo walisaliti taifa lao?”
“Unatumia neno uzalendo? Toa kabisa hilo neno kwenye kinywa chako, hakuna mtu mzalendo ni basi tu watu wanakuwa hawajazipata nafasi ila siku wakiliona tobo nakuhakikishia hata baba yako mzazi anaweza akakukataa kabisa”
“Unajua kabisa kwamba taifa halitakusamehe kwa hii dhambi na hata Max na Bilali hawatakuacha hai kwa hili ambalo unataka kulifanya, huyo Denis Kijazo atakuwa hana huo uwezo wa kukulinda kama wewe unavyohisi. Nakusihi sana ninayo nafasi ya kuweza kukusamehe kwa huu ujinga ambao unaufanya hapa na nikakusamehe kana kwamba hakuna kitu ambacho kimetokea ila acha mara moja” raisi aliongea kwa sauti ya mamlaka lakini mwanaume huyo aliishia kucheka tu akiwa anamsogelea raisi huyo pale ambapo alikuwepo
“Hao unao waongelea sidhani kama unajua ambacho kinaenda kutokea kwao, Bilali kwa sasa kama bado atakuwa hai basi ana Mungu wake sana maana alijulikana kama anaenda kwa Madilu Mpagazi hivyo mpango uliandaliwa vizuri sana kwamba habari yao na wenzake inaishia kule kule hivyo hataweza kurudi tena wala hautamuona tena kwenye maisha yako yote machache ambayo yamesalia lakini pia huyo Max” mwanaume alisikitika sana akiwa anamuelezea Max.
“Huyo anaenda kuwa gaidi namba moja nchini ndani ya muda mfupi ujao kwa sababu ni yeye ambaye anaenda kupewa kesi ya kuhusika na mauaji yako kisha baada ya hapo naye tutamuua na waziri mkuu anakuwa raisi wa taifa hili maana hata makamu amekufa hivyo nchi inarudi kwenye mikono yetu. Huyo Denis Kijazo licha ya kwamba ulikuwa ukimpanulia miguu yako ila haukuwahi kumjua kiundani na jinsi alivyo huenda usingejaribu hata kushindana naye ila kwa bahati mbaya sana kwa sasa hana nafasi ya msamaha kabisa kwako maana yeye anataka taarifa za kwamba umekufa hivyo hapa ni mimi na wewe lakini kabla ya kukuua kuna kitu kwanza nataka nikionje”

53 inafika tamati.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 54
“Nimesikia sifa zako wa wanaume ambao waliwahi kupita katikati ya miguu yako kwamba wewe ni mwanamke mtamu sana tena isivyo kawaida hivyo na mimi nataka niweze kujionea huo utamu namna ulivyo nisipitwe sana kwahiyo kabla ya kukuua nakubaka kwanza”
“Dax usifanye hivyo” maneno yake yalifuatiwa na vitendo baada ya mwanaume huyo kumdaka na kuchana chana nguo za raisi huyo na kumuacha uchi kabisa ambapo alianza kumbaka kwa pupa sana pale kwenye sofa huku akiwa anainjoi sana kufanikiwa kumwingilia kimwili raisi wa taifa kubwa kama Tanzania. Dax licha ya kusikia kelele za kuomba msaada kwa raisi huyo lakini hakumuachia katu wala kumuonea huruma mpaka pale ambapo aliona ametosheka.
Alimbeba mwanamke huyo ambaye alikuwa amekata tamaa huku machozi tu pekee yakiwa yanamtoka akiwa anayakumbuka maisha yake ya nyuma na matukio mbalimbali ambayo aliwahi kukutana nayo kwenye maisha yake. Alikuwa anajiona kabisa anakufa kifo kibaya sana ambacho kilimfanya ahisi kwamba huenda familia yake ilikuwa na laana na kwa bahati mbaya sana alifanya uzembe mkubwa wa kutokuacha hata mtoto mmoja ili iwe kumbukumbu nzuri ya uwepo wake duniani siku atakayo kufa.
Alikuwa amelazwa kwenye sakafu akiwa uchi kabisa huku mawazo yakiwa mbali sana na chozi likiendelea kumshuka taratibu tena kwa hisia nzito sana. Dax alisogea mpaka pale na kumkalia juu kisha kama utani akakizamisha kisu tumboni taratibu sana, Teodensia Mpanzi alikuwa analia tu kimya kimya huku akiukunja mdomo wake kwa maumivu makali mpaka pale ambapo mwanaume huyo alianza kukizamisha kisu kwa nguvu sana ndipo mwanamke huyo alipoanza kulia kwa sauti.
Alichomwa chomwa vibaya sana na kumfanya hali yake kuwa mbaya mno akiwa anahema kwa nguvu na kwa taabu kubwa mno. Dax alimpiga denda mdomoni huku akiwa anakizamisha kisu sehemu ulipokuwepo Moyo. Busu ambalo alimpiga mdomoni lilimfanya ashindwe kuhema vizuri na wakati huo mwanaume alikuwa anakinyonganyonga kisu ambacho kilikuwa kwenye moyo na kumfanya mwanamke huyo kuyatoa macho sana huku akiwa anaikata pumzi taratibu tena kimya kimya kama vile hakuna kitu ambacho kilikuwa kinatokea.
Teodensia Mpanzi, raisi wa Tanzania alikuwa ameikata kauli, raisi wa nchi alikuwa amepoteza maisha yake kwenye mikono ya moja kati ya walinzi wake ambaye walijua kwamba alitoweka Ikulu kutokana na taarifa ambazo zilikuwa zimeletwa mezani lakini kitu cha ajabu ni kwamba mwanaume huyo alikuwepo hapo hapo Ikulu na ndiye ambaye aliyatoa maisha ya raisi huyo.

Max alikuwa barabarani na pikipiki ambayo ilikuwa kwenye mwendo mkali sana kiasi kwamba kama ingetokea mtu akarusha hata jiwe basi angepata ajali ambayo asiwengeweza kupona. Mwanaume alikuwa na wasiwasi sana kuwaza kama angefanikiwa kumuwahi raisi ili ahakikishe anakuwa salama ila kila akikumbuka kwamba alipewa muda mfupi tu kwamba kazi hiyo ingekuwa imeisha basi alijikuta anachoka sana na kuongeza mwendo zaidi maana hayo yote yalikuwa yanatokea kwa sababu ya uzembe wake mkubwa wa kuweza kumwamini mwanamke haraka kwa sababu tu walikuwa wanafanya kazi pamoja.
Baada ya muda mefu kidogo kupita mwanaume alikuwa anaingia kwenye malango ya Ikulu. Aliitupa pikipiki yake na kusogea getini ambapo aliweka kitambulisho chake kwenye mashine kwa ajili ya kuscan na baada ya kumaliza geti lilifunguka moja kwa moja akatokezea kwenye chumba ambacho kila ambaye alikuwa anaingia hapo ilikuwa ni lazima akaguliwe. Wanaume ambao aliwakuta hapo walitoa ishara ya heshima kwake kwa sababu alikuwa na cheo kikubwa kuwazidi na mwanaume hakuwa na muda nao kabisa alipita akiwa anakimbia kwa kasi sana kuelekea kwa raisi.
Kwa namna mazingira yalivyokuwa hakukuonekana kuwa na tatizo lolote ndani ya sehemu hiyo lakini kila ambaye alikuwa anamuona alikuwa akimshangaa mwanaume huyo maana alikuwa kwenye mavazi ya kutisha sana huku akiwa na matone ya damu ya kutosha kwenye mwili wake lakini hakujali aliendelea kuzama ndani mpaka alipofika kwenye lango la kuelekea ilipo ofisi ya raisi ndipo alizuiliwa. Kwa mavazi ambayo alikuwa nayo watu hao walilazimika kumfanyia ukaguzi maana hakuonekana kuwa salama, baada ya ukaguzi walichukua shoka lake, wakachomoa visu kiunoni pamoja na bastola kisha wakamruhusu aingia ndani.
Watu hao ambao walimfanyia ukaguzi hapo sura zilikuwa ngeni sana kwake kwani hakuwa na kumbukumbu kama aliwahi kuwaona watu wa namna hiyo ndani ya Ikulu huku wakiwa kimya bila kumuuliza jambo lolote lile kitu ambacho kilianza kumpa sana hofu mwanaume hivyo akawa anatembea kwa tahadhari sana. Alifika mpaka ndani ya chumba cha katibu wa raisi ila kwa bahati mbaya palikuwa patupu bila mtu hali ambayo ilimfanya moja kwa moja anyooshe kuelekea ilipokuwa ofisi ya mkuu wa nchi, kwenye nafsi yake akiwa na wasiwasi sana akiwa anaombea jambo lolote baya lisiwe limetokea maana asingeweza kujisamehe kabisa na yeye ndiye angekuwa amesababisha yote hayo.
Mlango ulikuwa umeegeshwa tu na hakukuwa na walinzi eneo hilo, alitazama kamera ambazo zilikuwa karibu na eneo hilo, alishtuka baada ya kugundua kwamba kamera hizo zilikuwa zimegeuzwa na kuelekezewa juu maana ambako hazikuwa na uwezo wowote wa kurekodi kile ambacho kilikuwa kinaendelea hapo. Aliusukuma mlango huo kwa nguvu sana akiwa amekitoa kisu chake ambacho alikiweka kwenye buti lake.
Alichokutana nacho ndani ya chumba hicho kilimtisha na kumpa wasiwasi mkubwa sana. Mwili wa raisi wake ulikuwa upo sakafuni ukiwa unavuja damu ambayo ilionekana kuwa mbichi tu bado, alikimbilia sehemu hiyo na kumpiga goti huku akiuinua mwili huo ambao ambapo aligundua kwamba kiongozi huyo tayari alikuwa ameuliwa ndipo akashtuka na kugundua kwamba huo ulikuwa ni mtego na ndiyo maana hakuzuiliwa kuweza kuingia humo ndani ila alishtukia mtego huo akiwa amechelewa sana.
Aligeuka na kuangalia mlangoni akiwa na kisu mkononi huku akiwa ameushika mwili wa raisi na kwenye koti lake akiwa na damu ambayo aliipata Bagamoyo kwa watu ambao alikuwa anawaua kwa kutumia shoka lake. Mlangoni alimuona Dax akiwa na wanaume wengine nane ambao waliingia humo ndani huku wote wakiwa na bastola kwenye mikono yao lakini haikuwa hivyo tu bali kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa anapiga picha nyingi sana Max akiwa ameushika mwili wa raisi ambao ulitapakaa damu huku ukiwa umeveshwa kinguo chepesi sana na kwa namna alivyokuwa anaonekana Max hakuna mtu angeamini kwamba yeye sio muuaji. Kwa mazingira yaliyokuwepo na kwa jinsi yalivyokuwa yeye ndiye alikuwa muuaji halali kabisa wa raisi wa taifa la Tanzania.
“Welcome back Max the DONNY” Dax alitamka akiwa anacheka sana tena sana maana mtu ambaye alikuwa anamtamani kwa kipindi kirefu sana alikuwa mbele yake tena akiwa amejileta kirahisi sana.
“Dax umefanya kosa kubwa sana kuweza kumuu raisi”
“Kosa kumuua? Nafikiri ungeanza na kosa langu la kumbaka kwanza kabla hata sijamuua lakini unajua nini Max hayo yote yanaenda kuwa yako. Mitandao inaenda kuchapishwa kila sehemu, watu wote wanaenda kujua kwamba wewe ni mtu ambaye umemuua raisi wa nchi yako. Najua kwamba kuna watu wataanza kuhojhi inakuwaje raisi anauawa wakati ana ulinzi mkali? Unajua jibu lake litakuwa ni lipi?”
“Lawama mtabebeshwa watu wawili Max, wewe na mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi kwamba raisi ameuawa na mlinzi wake ambaye alikuwa anamuamini sana na kumpatia siri zake na kumtumia kwenye mambo yake maovu ila kwa bahati mbaya hakujua kama mlinzi wake alikuwa na ajenda zake za siri ndani ya moyo wake na baada ya kuona kwamba raisi anaenda kinyume na yale matakwa yake basi akaamua kufanya maamuzi ya kumuua. Kuhusu kwamba alimuuaje jibu ni rahisi tu kwamba huyo ndiye mtu pekee ambaye mheshimiwa raisi alikuwa anamuamini sana hivyo ndiye pekee ambaye raisi alimpatia mpaka ruhusa ya kuweza kuingia ofisini kwake akiwa na mavazi yoyote yale na kwa wakati wowote ule ila kumbe alimwamini mtu ambaye walikuwa wamepishana kwenye maslahi” Dax alikuwa anatoa hayo maelezo mithili ya mtu ambaye alikuwa anaisimulia tamthiliya fulani kwa furaha sana.
“Halafu baada ya hapo tutahamia kwa mkurugenzi sasa, huyu atalaumiwa kwa kosa la kuweza kukuamini wewe kiasi kwamba akakuchagua kuwa kwenye listi ya watu wa kumlinda raisi wakati alijua kabisa kwamba ni mtu ambaye haukuwa unafaa kwa hii kazi hivyo mzigo huu utawaangukia nyie wawili lakini inatasaidia nini Max? haitasaidia kitu kwa sababu utakuwa umeshakufa lakini pia mkurugenzi alishakufa hivyo mamlaka za ulinzi zitatoa msisitizo kwamba unatakiwa kutengenezwa ulinzi mkubwa sana na umakini mkubwa sana kwa vijana ambao wanachaguliwa kwenda kuwalinda viongozi wakubwa wa taifa. Nadhani umenielewa ila utakuwa haujaelewa juu yangu mimi kwamba itakuwaje Max”
“Mimi nitaibuka kama shujaa ambaye ndiye nilikukamata na timu yangu baada ya mheshimiwa kufanikiwa kupiga alamu ya kuomba msaada na mimi nikaja haraka sana ila sikufanikiwa kuingia moja kwa moja mpaka pale ambapo niliuvunja mlango ambao una ulinzi maalumu mpaka mtu ufanikiwe kuingia ndani kisha baada ya hapo nitajitetea kwamba nilikushambulia kwa risasi baada ya kuwa na kisu mkononi ukawa unakuja na upande wangu ili uweze kuniua kama ulivyo muua raisi. Watu wote wananipongeza sana mimi kwa kumuua gaidi, historia zitaandikwa kwenye vitabu na vipeperushi mbali mbali ambavyo vitaishi miaka na miaka watu wengi wakiliimba jina langu kama shujaa wa taifa hili huku wewe ukionekana kuwa msaliti wa hili taifa”
“Wakati mataifa mengine yakiwa yanahoji kuhusu hili yakiwepo mashirika makubwa kama umoja wa mataifa, itahitajika awepo mtu ambaye alilishuhudia tukio na hapo ndipo ambapo mimi nitaitwa kila sehemu kuhojiwa. Mahojiano yangu huenda yatakuwa mahojiano ambayo yatafuatiliwa sana duniani kwa miaka kama kumi ijayo kwa mwanaume ambaye nitaimbwa kama jasusi ambaye niliibuka kidedea kuipigania bendera ya nchi yangu baada ya gaidi kumuua raisi na kuhitaji kuipindua serikali. Haya ndiyo yatatokea na hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa Max au unaonaje juu ya hili?” mwanaume huyo alikuwa ameiandaa vizuri sana hadithi yake ya kusisimua hiyo ambayo ilikuwa mbaya sana kwenye masikio ya Max maana ilikuwa inaenda kumfanya yeye kuwa binadamu mbaya sana kwenye masikio na macho ya wengi ila angefanya nini Max? hakuwa na cha kufanya zaidi ya kukubaliana na hali ambayo ilikuwa inaenda kutokea kwa wakati huo.
“How dare you Dax? Kipi kinakufanya mtu kama wewe ambaye nilikuchukulia kama kaka kwangu, mwanaume ambaye tumehangaika pamoja kwenye nchi nyingi sana kuja kuhakikisha kwamba taifa letu linaenda kuwa salama kwa muda ambao tutakuwa hai kukengeuka namna hii KD?”
“Umeniuliza swali zuri sana lakini jibu lake linaweza kuwa rahisi sana, sitaki kuwa sehemu ambayo hakuna mtu anaona ninacho kifanya, nataka kuwepo sehemu ambayo nikifanya jambo zuri napigiwa makofi, sehemu ambayo watu wananishangilia na kuniheshimu, nataka kuwepo sehemu ambayo dunia nzima itajua kwamba mimi ni nani na nipewe heshima yangu”
“Kwahiyo shida yako kubwa ni pesa na umaarufu?”
“Sio hivyo tu Max, nataka heshima kubwa sana, nataka niheshimiwe sana kama simenti na maji vinavyo heshimiwa na mjenzi au kama pesa na muda vinavyo heshimiwa na mpambanaji wa kimaskini. Nakumbuka kauli yako siku ile ulisema kama nataka kucheza mchezo wako wa last card basi niingie niucheze, au sio wewe ambaye uliniambia hivyo? Nakuhakikishia kwamba mimi niliamua kuingia kwa miguu yangu yote miwili ili kuucheza mchezo huu safi kabisa”

54 inafika tamati.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 55
“Utakuwa na mwisho mbaya sana KD, haya mambo hayapo kama unavyo yadhania wewe, hii mifumo ipo na itatoweka. Umefanya kosa kubwa sana tena sana kwenye maisha yako na siwezi kukusamehe katika hili kwa namna yoyote ile”
“Unataka kuniambia kwamba unafikiria kuniua? Au unadhani hao wenzako watakusaidia katika hili? Hapana hakuna kitu ambacho watakiweza kwa sababu tulijua mipango yenu yote hivyo hata wakati huu ambao sisi tunaongea nadhani watakuwa wamekufa wote na akama sio kufa basi watakuwa kwenye mateso makali sana. Jambo ambalo litakuwa baya sana kwako ni kwamba unaenda kuwa miongoni mwa wanaume mafala sana kuwahi kuzaliwa kwa sababu mwanaume wa kazi kama wewe unaiuza nchi yako kwa kudanganyika na uchi Max? uchi wa mwanamke ambao unaweza kwenda kasino na laki moja tu ukapata mwanamke wa kulala naye usiku mzima na ukamtumia kwa namna ambayo unaitaka wewe? Hilo ni jambo ambalo limenifanya nikudharau sana na kukuona wewe ni looser tu huna lolote” Dax alikuwa anaongea akiwa anaangalia wanaume wa kazi walivyokuwa wanautoboa toboa mlango ili akisimulia kwamba aliuvunja mlango huo dunia iweze kumuamini kabisa.
Max matusi yalimzidia sana aliona kabisa kwamba asingeweza kuyahimili hivyo alinyanyuka kama mzimu na kusogelea pale ambapo alikuwepo Dax akijigeuza kwa nguvu sana hali ambayo iliwafanya watu wote washangae sana humo ndani ila kwa bahati mbaya sana hakufanikiwa kumfikia mwanaume huyo baada ya kutandikwa risasi mbili kwenye kifua chake ambazo zilimpeleka chini akiwa anauma meno kwa hasira sana.
Mwanaume hakuwa mrembo, alikuwa mwanaume wa kazi haswa hivyo alikuwa anataka kusimama kutoka hapo alipokuwa ili apambane na watu hao lakini hakuwa na huo uwezo maana aliposimama tu akiwa anayumba yumba Dax alimuongeza risasi za mbavu na tumboni na kumfanya jumla kuwa na risasi sita kwenye mwili wake na hali yake ilianza kuwa mbaya sana akawa amepiga magoti ameinama na kuvuja damu akiwa hana la kufanya.
“Dax niue ukiwa bado una nafasi ila kumbuka kwamba mimi nitarudi kwa ajili yako na hao watu wako, nakuahidi NITARUDI” Dax alimshika kidevu na kumpiga kwa nguvu sana na kitako cha bunduki kwenye uso wake na kumpasua juu ya jicho.
“Unaahidi kwamba utarudi kwa ajili yangu? Si ulikuwa unajifanya wewe ndo mwanaume wa shoka sana kwenye mapigano, si ulikuwa unajifanya kwamba wewe ndiyo wewe kwenye ulimwengu wa watu wa kutisha sana? Unataka nikuue saivi? Unahisi naamini kwamba hizo risasi sita pekee zitakuua? Najua hauwezi kufa kirahisi sana namna hiyo kwa sababu mwili wako ni mgumu sana hivyo una kinga za ziada na mimi siwezi kukuua kirahisi sana namna hii ndiyo maana nilikuwa nazingatia sana maeneo ambayo nilikuwa nakupiga risasi Max” ilikuwa zamu yake Dax kutamba sasa maana mwanaume huyo hakuwa na uwezo wa kufanya jammbo lolote kutokana na hali yake ya wakati huo ilivyokuwa.
“Lazima kwanza uteseke, unatakiwa ujutie kuwahi kukutana na sisi kwenye maisha yako na hapo ndipo naweza kukuua lakini pia unatakiwa kwanza ukutane na kiongozi akuage kwanza na amalize hasira zake kwanza kwani ujio wako ulianza kumuingiza matatizoni na kisha baada ya hapo tutamalizana mimi na wewe” Dax aliongea akiwa analichana chana koti la Max lakini pia alikata tshirt yake na kisu ambapo alizamisha kisu kwenye kifua na kukata sehemu hiyo kisha akatoa kitu kama alamu hivi kidogo sana.
“Siku umesalimiana na waziri mkuu wakati anakuja kwenye mkutano nadhani kwa baadae mlikuja kushtuka kwamba huenda aliwauza kitu ambacho kilikuwa cha kweli kabisa na baada ya kuwafanyia hivyo aliwaachia hivi vifaa vya mawasiliano ambavyo vingetufanya tujue kila seehmu ambayo mngekuwepo hivyo wakati mnaruka ruka sana kujifanya wasiri na mnafanya mambo yenu kwa makini tulikuwa tunamuona kila mmoja wenu alipo ila tulisubiri mjae tu kwenye kumi na nane ndipo tufanye maamuzi ya mwisho kitu ambacho kweli kimekuwa kama tulivyokuwa tumepanga sisi. Kwa sasa nakitoa kwa sababu hatutakuwa na kazi na wewe tena maana unaenda kufa” baada ya kumaliza maongezi hayo Dax aliitoa simu yake mfukoni na kupiga simu kwa bosi wake kumpa taarifa ya kazi na sehemu ambayo alikuwa amefikia.
“Nipe ripoti”
“Kazi meisha tayari, raisi amekufa na Max nipo naye hapa tayari ana risasi sita kwenye mwili wake ila ni mzima asiye na madhara na nasubiria amri yako tu kisha nifanye maamuzi ya kuweza kumuua au kukukutanisha naye kama utakuwa na lolote la mwisho kwake”
“Nimemaliza mkutano na waandishi wa habari na wameshtuka sana baada ya mimi kuwaambia kwamba nimepata taarifa kwamba Ikulu kuna shida kubwa sana hivyo nakuja sasa hivi huko ila hakikisha kwamba unamuonyesha kile ambacho kimetokea kwa wenzake kupitia video ambayo imerekodiwa kule ili afe akiwa na maumivu sana kwenye nafsi yake kwa ujinga ambao alikuwa ameufanya.
“Sawa mkuu” mwanaume aliikata simu hiyo na ujiko ulikuwa wake, waheshimiwa wangeanza kumzingatia sana kama kijana wa mhimu mno kwa upande wao. Aliwapa ishara vijana wake waweze kumbeba Max na kumeleka kwenye moja kati ya vyumba vikubwa sana ambavyo vilikuwa vina runinga ndani yake na ndicho ambacho watu hao waliweza kukifanya.
Mwanaume alibebwa mpaka kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa na vyuma vingi sana na kilikuwa na viti viwili tu basi na runinga kubwa sana ukutani. Kwa mazingira yalivyokuwa ilionyesha kwamba vilikuwa moja ya vyumba vya mipango mikali sana hususani zinapokuwa zinaongelewa siri kubwa sana za nchi. Max alikuwa kwenye hali mbaya sana ila hakuwa na sehemu ya kuweza kudeka wala kusema kwamba kuna mtu angeweza kumuonea huruma juu ya yale ambayo yalikuwa yanaendelea hapo.
Runinga hiyo iliwashwa na alijua kabisa kwamba lazima kulikuwa na kitu kibaya sana ambacho kingemuumiza moyo na ndiyo maana watu hao waliamua kumuonyesha hivyo licha ya kuwa kwenye hali mbaya na kutokuwa tayari kwa hilo bado hakuwa na namna zaidi ya kuangalia na alicho kiona kilimshtua sana. Ulikuwa ni ujio wa DRAGON BOYS kwenye jumba la kifahari la Madilu Mpagazi ambalo lilikuwa pembezoni kabisa mwa bahari eneo la Kawe na hapo alianza kujionea kile ambacho kilikuwa kinatokea huko.


KAWE, DAR ES SALAAM.
Muda mchache ambao ulikuwa umepita ndani ya Kawe wanaume watatu walikuwa wanaingia eneo hilo. DRAGON BOYS ndio ambao walikuwa kwenye huo msafara wao wa kuelekea huko na huko hawakuwa wanakwenda kupoteza muda wao bali kwenda kufanya mauaji kwa Madilu Mpagazi na baada ya kumalizana naye ingekuwa ni vita ya Denis Kijazo ambaye ndio ulikuwa mpango wao mkubwa lakini waliamua kuanza na matawi yake kwanza ili asije akapata msaada kwa watu hao ambao walikuwa wanampa kiburi cha kuendelea kuyafanya yale ambayo alikuwa anajisikia kuyafanya bila kujali usalama wa watu wengine.
Ila jambo baya ambalo Bilali na wenzake walishindwa kulitambua mapema ni kwamba kila hatua ambayo walikuwa wanaipiga kuna watu walikuwa wanajua kwamba watu hao wangekuwepo eneo hilo na walikuwa wanawaona na kuwafuatilia pia. Madilu Mpagazi hakuwa na wasiwasi kabisa kwa sababu alijua kwamba hao watu wake wangefika ndani ya eneo hilo hivyo aliamini kwamba angekuwa salama maana mpango mzima Denis Kijazo alimwambia pamoja na kumpa maelekezo kwamba wanaume ambao walikuwa wanaenda hapo walikuwa wanamlinda na hakuna mtu hata mmoja ambaye angefanya jambo lolote baya kwake mbele ya wanaume hao.
Ujinga wake alimwamini moja kwa moja mtu ambaye aliamini kwamba alikuwa kiongozi wake kwenye hizo mbio za kuweza kuipigana hiyo vita lakini naye jambo moja ambalo hakujua ni kwamba Denis Kijazo alipanga kumuua hadi yeye na hakutaka kabisa mtu yeyote yule kubakia upande wake kwani watu hao kwa dalili aliona kama baadae wanaweza wakaja kumgeuka baada ya kuzijua siri zake nyingi sana. Kwahiyo wakati anajiachia na kufurahia majukumu ambayo yalikuwa yanaendelea hakujua kabisa kwamba alitakiwa kufa.
Bilali na wenzake waliingia ndani ya jumba hilo kikazi sana maana waliwaua vibaya sana walinzi wote ambao walikuwa ndani ya eneo hilo. Walifanikiwa kufika mpaka ndani ambako walimkuta Mpagazi Madilu akiwa anastarehe na mwanamke akinywa kwa nguvu zote na ndipo aliposhtuka baada ya kuwaona watu hao wakiwa eneo hilo. Bilali hakuwa na huruma naye alimchinja vibaya sana na kumuacha mwanamke ambaye alikuwa naye hapo akitoka nje lakini Bilali alishtuka sana baada ya kufika nje na kukuta mwanamke huyo akiwa amepigwa risasi ya kichwa hapo aligundua kwamba kulikuwa na ugeni ambao haukuwa wa kawaida ukiacha wao ndani ya hilo eneo.
Bilali aliwaangalia wenzake kwa umakini sana na kusogelea ile sehemu ambayo mwanamke yule alidondokea, aliitoa ile risasi kwenye paji ya uso la mwanamke yule na kuiangalia, aliishia kutikisa kichwa akionekana kabisa kwamba amekata tamaa.
“Kuna nini kiongozi?”
“Hapana hatuwezi kupona hivyo anatakiwa mmoja wetu aishi”
“Whaaaat?”
“Hizi risasi ni tofauti kabisa na za kwetu ni zile risasi ambazo zimetoka kwenye silaha ambazo ziliibiwa miaka kadhaa nyuma na zilikuwa chache sana kwa sababu zilitengenezwa maalumu kwa ajili ya makomando na baada ya kuibiwa kwa silaha zile hakuna mtu ambaye aliruhusiwa na serikali kuzimiliki tena hivyo kama zimeonekana hapa ni kwamba huyu monster amerudi kwa sababu yeye na mabaniditi wenzake ndio waliziiba silaha zile na risasi hizi”
“Unamzungumzia nani?”
“Ted”
“Oooh shiiit” wote walisikitika sana kwa sababu walikuwa wanamjua sana mwanaume huyo.
“Tunafanyaje kiongozi?”
“James unatakiwa kuishi” alimgekia mwanaume ambaye alikuwa ni mtaalamu sana wa komputa pamoja na kumiliki saa ambayo ilikuwa na ncha kali sana.
“Kiongozi siwezi kuondoka na kuwaacha kwenye hali kama hii”
“Sikuombi ila hii ni amri. Haitakiwi wote tufe hapa kwa sababu kuna nafsi inaniambia kwamba Max anaweza kulifanikisha hili hata kama sio leo basi siku moja, maana yake kama itakuwa hivyo basi lazima mmoja wetu aishi ili aje kusaidiana naye kukamilisha hili jambo. Hapa hauondoki kwa sababu unatusaliti James ila kwa sababu unataka kuilinda nchi ambayo unaipenda sana” Bilali aliongea kwa uchungu sana akiwa anameza mate na kuendelea.
“Najua mpaka hawa watu wanakuja huku ni lazima raisi amekufa na kama wamefanikiwa kumuua raisi basi moja kwa moja wamefanikiwa kumkamata Max maana kama sio kumkamata basi muda huu angekuwa hapa. Kwa maana hiyo nataka ukabahatishe kitu kimoja James, kama ukifanikiwa kutoka hapa ukiwa hai hakikisha unautumia uwezo wako wote wa kucheza na mitandao kumpata Max. Nina imani kwamba zile simu ndogo za mawasiliano hata kama wakimkamata bado anaweza kuwa nayo kwenye mwili wake hivyo jitahidi na kama utafanikiwa kumpata akiwa hai basi hakikisha unaondoka naye ndani ya huu mji kwanza mpaka pale mambo yatakapokuja kutulia na watu hawa wakajitangazia ushindi na kusahau kama kuna mtu alibaki wala kuiishi. Lakini pia kuna yule mwanamke wa Max Ariana, hakikisha unampata pia maana kama yule akiendelea kuwepo muda wowote atakamatwa na anaweza kuuawa kitu ambacho sitakipenda kitokee kama nilikubali kumlinda Max basi natakiwa kumlinda kila ambaye yupo naye karibu. Chukua na hii frashi kama utabahatika kumpata Max akiwa bado hai basi mpatie aipitie atajua cha kufanya na kama ikitokea hautampata Max basi ipitie wewe mwenyewe ila hakikisha kwanza umeshindwa kumpata ndipo uipitie na kama ikitokea umeshindwa kabisa kumpata mwanaume huyo basi ondoka na uende mbali sana katengeneze watu wapya, katengeneze timu ya watu wazalendo siku moja uje kulikomboa taifa letu” mwanaume aliongea kiasi kwamba kijana wake huyo alibaki anashusha machozi.

55 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 56
Hao watatu walikuwa ni zaidi ya familia na ndiyo maana mambo mengi walikuwa wakiyafanya pamoja hivyo wenzake kuanza kumuaga aliona kama amepoteza kitu kikubwa sana kwenye maisha yake. Alishusha chozi kuwakimbia watu ambao walikuwa kama mapacha, alipiga saluti ya heshima na kuwakumbatia wanaume hao kisha akakimbia kuelekea nyuma ya jumba hilo ambako alitakiwa kuhakikisha kwamba anatoka salama. Bilali na mwenzake walifumba macho na kutamka kwa sauti kali sana tena ya kizalendo mno.
“MUNGU ibariki Tanzania, Mungu ibariki nchi yetu” huo ulikuwa utamaduni wao siku zote pale ambapo walikuwa wanaingia kwenye majukumu mazito sana ambayo walikuwa wanahisi kwamba kuna uwezekano yakaondoka na maisha yao.
Baada ya kumaliza hilo waliyafumbua macho yao na kutoa visu vikali sana ambavyo walikuwa navyo viunoni, silaha za moto hazikufaa hapo kwani hawakujua watu hao wapo wapi na wapi na walikuwa ni wanaume ambao walikuwa wanaupenda sana mkono kuliko kitu chochote kile hivyo kwa risasi walijua kama watu hao wangeamua kuwaua huenda wangewaua kwa muda mrefu sana ndiyo maana walichagua silaha ambazo zilihitaji mikono ili zitumike kwa ufasaha bila kuparuana na bastola au silaha za wadunguaji ambao waliamini lazima wangekuwepo eneo hilo.
Mbele yao juu ya paa la nyumba ya mlinzi ambayo ilikuwa pembezoni kidogo mwa geti la hapo alionekana mwanaume mmoja ambaye Bilali alikuwa anamjua sana huenda kuliko watu wote ndani ya taifa la Tanzania. Mwanaume huyo hakuwa na wasiwasi kabisa huku akiendelea kupata fegi taratibu bila wasiwasi na moshi mwingi sana ukimtoka. Hakuwa mwingine bali Ted akiwa anawaangalia vijana hao wawili kwa hamu kubwa sana lakini chini kabisa walikuwepo wanaume wanne ambao walikuwa wanaongozwa na Kenedy kijana ambaye kwenye mkono wake alikuwa na shoka moja kali sana ambalo alikuwa analizungusha kiwepesi sana kuonyesha kwamba halikuwa zito kabisa kulingana na kilo nyingi ambazo alikuwa nazo kwenye mkono wake. Kazi ilikuwa mbele yao Bilali na mwenzake wakiwa wawili tu basi mbele ya wanaume hao wa kazi tena wa kutisha sana.
Kenedy alisogea pembeni na kuwaacha vijana hao watatu ambao walikuwa nae waende kwa watu hao wawili, ilikuwa kama fungulia mbwa kwa namna walivyoenda kwa kasi kubwa sana kusogelea sehemu ambayo walikuwepo hao wanaume kila mtu kwenye mkono wake akiwa na kisu. Bilali aliitoa cheni yake ambayo ilikuwa inakunjwa na kuwa na alama ya B13, B ikiwa ni kifupisho (Bilali) lakini 13 ilikuwa ni namba ya mchezaji wa mpira ambaye alikuwa anamhusudu sana ambaye alikuwa ni Nesta.
Wanaume wawili walikuwa wamemlenga Bilali huku mwanaume mmoja akiwa anapambana na mwenzake mmoja. Wanaume ambao walikuwa kwa Bilali walikuwa na kasi kubwa sana kiasi kwamba wote walifanikiwa kuzamisha mabuti yao kwenye mbavu zake ambapo alirushwa mbali lakini mwanaume alitua kwenye ngazi za kupandishia kwenye nyumba hiyo na aliponyanyuka hapo kasi yake ilikuwa mithili ya mzimu. Alikuja kwa kasi akiwa anajizungusha kwa kuuachia mwili wake na alipowakaribia alijigeuza kwa sarakasi kali sana na kutua nyuma yao, wa nyuma kabisa wakati anageuka shingo yake ilichanwa vibaya mno na mwenzake wakati anakuja kwa kasi baada ya kuona mwenzake kauliwa alisukumiziwa mwili wa mwenzake na baada ya kugongana na mwenzake aliyumba sana na ndio wakati ambao Bilali alikuwa amefika ambapo alimchukua mtama mkali akaruka kwa juu na kuanza kushuka chini ila kwa bahati mbaya sana hakufanikiwa kufika chini kwani alikatwa katwa na kisu pamoja na ile cheni na wakati anatua chini sehemu ya moyo wake ilikuwa haifai kwani iliharibika vibaya sana.
Kijana wa Bilali naye hakuwa mnyonge, yeye aliitoa shilingi kwenye mkono wake na kuirusha kwa nguvu sana kuelekea kwa mwenzake baada ya mapigano ya muda mfupi na wakati mwenzake anahangaika kuikwepa alikituma kisu naye akiwa anafuata nyuma. Kisu kilizama tumboni kwa mwanaume yule na wakati anahangaika kukitoa mwanaume alikuwa amefika na kurusha ngumi kali sana kuelekea kilipo kisu ambapo kilizama sana mpaka ndani akabaki anahangaika nacho hali ikiwa mbaya, shingo yake ilipokea ngumi nne ambazo zilitosha kuipindisha akadondoka akiwa anatoa udenda tu mdomoni.
Ndani ya dakika chache sana za kuhesabu walikuwa wamebaki wanaume wawili tu pekee huku Ted akiwa hana wasiwasi anashuhudia mpambano huo akiwa anavuta sigara yake kama mwanzo tu lakini hata Kenedy pia alikuwa amelishika shoka lake akiangalia wenzake walivyokuwa wanauawa ndani ya eneo hilo. Tedy alikurusha kipisi cha sigara hewani kisha alizunguka kwa nguvu sana na buti lake ambapo alikikosa kidogo tu kipisi hicho lakini kutokana na hali kali ya upepo ambayo ilitoka kwenye buti hilo alifanikiwa kuuzima moto ambao ulikuwa kwenye kipisi hicho cha sigara kisha mwanaume alitua chini kama alikuwepo tangu mwanzo.
“Sikuwahi kujua kwamba ndani ya nchi hii kuna watu wana uwezo mkubwa wa mapigano kiasi hiki na wanaishi kwa kujificha. Ngumi ni kipaji na ukiwa nacho hautakiwi kabisa kukificha ndugu yangu kwani kuna watu wanalipwa kwa sababu hiyo ila kwa bahati mbaya sana huwa wanaishia pabaya kama sio kuwa na maisha mafupi. Kwa namna nilivyokuona unapigana hapa basi moja kwa moja nimetambua kwamba ni wewe ambaye uliwahi kuwa unakuja kwenye ulingo kule na utambulisho feki, hivyo bila shaka ulikuwa unafanya ni uchunguzi wa kuweza kuikamilisha hii kazi ambayo unahisi leo umeijia hapa sio? Lakini kwa bahati mbaya sana hautafanikiwa hata kuliona jua la asubuhi na hapa ndipo huwa pananifanya nijihisi hatia sana ya kupambana na watu ambao wana uwezo wa chini sana mbele yangu kama nyie” Ted aliongea akiwa anasogea pale ambapo wanaume hao walikuwepo.
Walikuwa wanamjua vizuri sana mwanaume huyo ndiyo maana walikuwa wamekata kabisa hata tamaa ya kuweza kuishi kwani uwezo wake haukuwa wa kawaida.
“Kwanini uliamua kuisaliti nchi yako?” Bilali aliuliza huku wakiwa wanazungukana na Kennedy alikuwa anasogea taratibu kwa yule mwanaume mwingine.
“Nimepitia faili lako ni lazima utakuwa unajua ni kipi ambacho kilitokea huko nyuma hivyo usijizime data kuniambia kwamba niliisaliti nchi wakati nchi ndiyo ilinisaliti na hawa wajinga ambao mimi nilikuwa silali kwa ajili ya kuwalinda wakawa wananicheka na kunitukana na wenzangu kwamba hatuwafai na ikiwezekana tuuawe lakini kuna mtu mmoja tu ndiye aliamua kuja kurudishia tumaini letu bado unataka kusema nakosea kufanya kazi chini yake?”
“Jukumu lako la kwanza kabisa ni kuilinda nchi kuhusu wananchi mara nyingi huwa wanasikiliza upande ambao una mdanganyaji bora hivyo isingekuwa sababu pekee ya kuamua kulisaliti taifa zima kwa sababu wewe ndiye ambaye unaweza kufanya watu wasio na maisha bora wakayapata lakini wewe ndiye unaweza kufanya haya mambo yote kama ukiamua”
“Kwahiyo unanishawishi nimuue bosi wangu?”
“Hiyo ndiyo njia pekee Ted ya kulifanya taifa liwe salama”
“Sasa kama ndiyo plani umekuja nayo, nakupa nafasi ya mwisho ya kuishi. Kubali kufanya kazi chini yetu na uachane na hayo ambayo unayafanya, wewe na wenzako mtaishi tena na mtapata kila kitu kweye haya maisha” Ted aliongea kama utani lakini alikuwa anamaanisha sana kwa maelezo ambayo alikuwa anayatoa wakati huo.
“Unahisi sisi tunanunulika kama wewe?”
“Hata mke wa Madilu amenifanya niiue familia yake yote kabla ya nyie kuja hapa kwa sababu ya kauli zake za majivuno. Nilikuwa namshauri kwamba mumewe anafanya umalaya na wanawake wengine hivyo yeye hatuna haja kabisa ya kuweza kumuua hivyo akubali kufanya kazi chini yangu lakini kwa bahati mbaya nahisi ni moja ya wale ambao hawakulelewa kwenye malezi bora ya namna ya kuishi na watu wengine hivyo akajikuta anajipoteza yeye na familia yake yote na shukrani kwako umerahisisha kazi kwa kumuua mumewe. Hilo ndilo ambalo linaenda kutokea na kwako kwa kuonekana umeipuuza ofa yangu ambayo siitoagi kwa mtu ni leo tu bahati ilikudondokea wewe hapo” aliongea kwa hisia sana akiwa anamwangalia Kenedy kwa macho yenye hasira mno.
“Kill him” ni amri ambayo aliitoa kwa kijana wake Kenedy kwamba yule kijana ambaye alikuwa na Bilali alitakiwa kufa haraka sana huku yeye akimalizana na Bilali. Mwanaume huyo aliruka kwa kasi ya ajabu huku akilizungusha koti lake kwa nguvu ambalo ndani yake lilikuwa na visu vingi sana. Bilali alikuwa anaerudi nyuma akiwa anajaribu kwenda na kasi ya mwanaume yule na kufanikiwa kupangua ngumi kumi mpaka alibaki anashangaa huyo mtu alirushaje ngumi kumi kwa haraa sana namna hiyo.
Licha ya kufanikiwa kupangua ngumi hizo bado alibakia na maumivu makali sana kwani ngumi hizo zilikuwa nzito sana kuliko uwezo wake wa kuweza kuendana nazo. Alikuwa amepiga goti moja chini akiwa anamwangalia Ted ambaye alitabasamu kidogo uso wake ukiwa umekunjika mno, Bilali alijivutia mbele na kumsogelea mwanaume huyo kwa nguvu ambapo alitishia kama anapiga kisha akajirusha pembeni na kumtwisha Ted ngumi ya mbavu ambayo ilionekana kumuingia maana aliukunja uso wake lakini wakati anapigwa ngumi hiyo pia aligeuka na teke kali sana ambalo lilimkosa Bilali na kutua chini ambapo mpaka zege ili bomoka kidogo na sehemu hiyo ilitoa mtetemo kiasi kwa nguvu ambayo ilikuwa mguuni.
Kazi ya Bilali ilikuwa ni kupangua na kukimbia kimbia akiwa anashambulia kwa mahesabu makali kwani alijua kama akikosea hatua hata moja tu alikuwa anapoteza maisha. Kwenye kushambulia kwake alibahatika kuzamisha kisu kwenye mwili wa mwanaume huyo eneo la kifua lakini Ted hakutetereka kwa hilo ambapo hasira zake zilimfanya kuwa binadamu wa tofauti sana. Alirusha ngumi kwa mkupuo na mateke ambayo yalikuwa yana kasi kubwa sana, ngumi tano zilizama kwenye kifua cha Bilali mpaka akawa anahisi kama kuna mtu alikuwa anachoma moto ndani yake kwa maumivu makali sana ambayo alikuwa anayapata wakati huo.
Alipigwa na goti kwenye mbavu yake moja kisha alikutwa na ugoko kwenye uso wake mpaka akawa anaona nyota sita sita mbele yake akiwa anayumba. Alijitahidi sana kukaa sawa na wakati anafanikiwa kukaa sawa ni wakati ambao aliona kijana wake akiwa anachomekwa shoka la shingo na mwanaume ambaye hakuwa na huruma kabisa kwenye maisha yake. Hilo ni jambo ambalo lilimmaliza sana nguvu Bilali kumshuhudia mwanaume ambaye kwake alikuwa kama ndugu akifa mbele yake huku naye akiwa hana hata msaada wa kuweza kumsaidia.
Alinyanyuka kwa hasira sana na kukusanya nguvu zake kwenda kwa kasi sana eneo ambalo alikuwepo Ted lakini wakati anakaribia hapo alihisi kama kuna mvumo wa upepo ulikuwa unaelekea kilipo kichwa chake hali ambayo ilimfanya atulie kwa muda kujua ni nini. Aligeuka na kukutana na shoka likiwa linakuja upande wake ambao alikuwepo, kusimama kwake kwa ajili ya kulikwepa shoka hilo ambalo alifanikiwa kulikwepa ulikuwa mwisho mbaya wa maisha yake kwani wakati anageuka alikutanishwa na kisu ambacho kilizama kwenye shingo yake.
Bilali alitamani kujitoa kweye mikono ya mwanaume fedhuli huyo lakini hakuweza maana alishikwa vyema mno, alikatwa katwa vibaya sana mpaka kichwa kilipo jichomoa kwenye kiwili wili chake ndipo alidondoka chini nafsi ikiwa imeacha mwili hapo hapo.
Upande wa nyuma ambako James alipitia ili kuweza kutokea kiasi kwamba alitakiwa kutoka akiwa hai alikutana na mwanaume mmoja ikiwa ni kwenye ile idadi ya wanaume watano ambao Ted alienda nao Dar es salaam kwa sababu upande wa mbele walikuwa wanne pamoja na Tedy mwenyewe hivyo hakukutana na ule urahisi wa kutoka kiwepesi kama alivyokuwa anahisi kwamba huenda upande huo haukuwa na mtu ambaye alikuwepo.
Mkononi mwake alikuwa na bastola ambayo aliitoa na kupiga risasi lakini aligundua kwamba zilikuwa zimeisha hivyo mkono wake pekee ndio ambao ulikuwa unamsaida sana hapo kutoka au kuweza kufia ndani ya eneo hilo hilo ambalo alikuwepo. Alihema kwa nguvu sana na kumfuata mwanaume ambaye alikuwa na upanga ambao ulikuwa unang’aa sana mbele yake huku yeye akiwa mikono mitupu.

56 inafika mwisho.
 
Hii imenisikitisha umewaua weng ambao nlidhan wangepona
 
Hii imenisikitisha umewaua weng ambao nlidhan wangepona
Hivyo ndivyo inavyo takiwa. Kazi ikiwa predictable sana Haina maana.

Unatakiwa kukutana na surprise ambazo hukuzitegemea.

Huo ulikuwa Moja ya mpango wangu wakati naiandaa. Nilijua kabisa kwamba kuna watu ambao mngetegemea wangemaliza mpaka mwisho lakini matarajio yanakuwa tofauti unavyozidi kwenda mbele.
 
Hivyo ndivyo inavyo takiwa. Kazi ikiwa predictable sana Haina maana.

Unatakiwa kukutana na surprise ambazo hukuzitegemea.

Huo ulikuwa Moja ya mpango wangu wakati naiandaa. Nilijua kabisa kwamba kuna watu ambao mngetegemea wangemaliza mpaka mwisho lakini matarajio yanakuwa tofauti unavyozidi kwenda mbele.
[emoji91][emoji91] simulizi inaupekee wake
 
Hivyo ndivyo inavyo takiwa. Kazi ikiwa predictable sana Haina maana.

Unatakiwa kukutana na surprise ambazo hukuzitegemea.

Huo ulikuwa Moja ya mpango wangu wakati naiandaa. Nilijua kabisa kwamba kuna watu ambao mngetegemea wangemaliza mpaka mwisho lakini matarajio yanakuwa tofauti unavyozidi kwenda mbele.
Nouma sana
 
Hivyo ndivyo inavyo takiwa. Kazi ikiwa predictable sana Haina maana.

Unatakiwa kukutana na surprise ambazo hukuzitegemea.

Huo ulikuwa Moja ya mpango wangu wakati naiandaa. Nilijua kabisa kwamba kuna watu ambao mngetegemea wangemaliza mpaka mwisho lakini matarajio yanakuwa tofauti unavyozidi kwenda mbele.
It's so sad to a president
 
Back
Top Bottom