FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #161
Tuhifadhi manenoItakuwa Max. Lakin nae ameumaliza mwendo mapema kisheria
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tuhifadhi manenoItakuwa Max. Lakin nae ameumaliza mwendo mapema kisheria
Si inasemekana kafa? 🤔
Inasadikika. Mkuu. 001 is going to dieeTuhifadhi maneno
Hongera mkuu kazi nzuriHADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 10
Aliyekuwa mbele alipigwa kwenye shingo na kiganja alikata moto hapo hapo hakuweza kuongea tena alidondoka chini, buti la mwanaume wa pili lilikuwa linakuja kwenye shingo yake alibendi kwa nyuma huku visigino vyake pekee ndivyo vilikuwa chini. Kwa namna alivyo jizungusha ilikuwa ni ngumu kwa mtu wa kawaida kubaki amesimama zaidi ya kudondoka vibaya lakini kwa mwanaume huyo lilikuwa zoezi rahisi sana wakati anasimama vyema alirudi na ngumi mbili ambazo zilitua kwa mwanaume mmoja lakini na yeye pia alipokea mateke ya mbavu mawili kutoka kwa mwanaume mmoja ambaye alitokea pembeni akateleza chini kwa miguu yake na kusimama kisha na yule mwanaume ambaye alikuwa amedondokea mbele yake akiwa ananyanyuka na kudondoka tena kwa ngumi ambazo zilikuwa zimetua kwenye kifua chake lakini alifanikiwa kusimama vyema.
Mwanaume huyo baada ya kuona watu hao wanazidi kumchukulia muda wake alijiviringisha kwa chini na kuinukia pale walipokuwepo huku kwenye mkono wake akiwa na cheni ambayo ilikuwa imeandikwa B13 na cheni hiyo alikuwa akiikunjua kinakuwa kisu kikali sana hivyo wakati anasimama hapo mguu wa mwanaume mmoja ambaye alikuwa anahitaji kumtwisha nao hapo alipokuwepo aliudaka na kuzamisha cheni hiyo ambayo ilitoboa toboa vibaya sana hilo buti hali ambayo ilimfanya mwanaume huyo ajivute nyuma ili asije akapata madhara ya cheni hiyo lakini kurudi kwake nyuma kulimfanya mwanaume ambaye alikuwa kwenye hayo manguo ya magunia kuinamia kwa mbele kisha akampiga mwanaume mwenzake vibaya sana na kisigino cha mdomoni ambacho kilimtoa damu nyingi sana na kumfanya arudi nyuma akiwa anaguna kwa maumivu.
Mwenzake alikuwa anakuja kwa haraka sana lakini hatua zake hazikuendana na mtu ambaye alikuwa anashindana naye mpaka aliposhtukia cheni ipo kwenye shingo yake, mwanaume huyo alihitaji kuifungua cheni hiyo ili kuipoteza shingo ya mtu huyo ila alighairisha zoezi lake baada ya kusikia mlio wa gari ukifika hilo eneo kwa kasi sana.
“Stop” ni sauti ambayo ilisikika kutoka kwa mzee ambaye alikuwa anashuka ndani ya gari hiyo ambapo mwanaume huyo alimzunguka mwenzake kwa nguvu na kumpiga mtama mkali kisha akamkita na goti kwenye kifua chake ambapo alienda kudondokea kwenye miguu ya yule mze ambaye alikuwa ameshuka akiwa na walinzi wawili.
“Bosi?” mwanaume huyo ambaye alikuwa amevamiwa hilo eneo akiwa kwenye hayo manguo yake aliita kwa mshangao huku akiwa anainama kutoa heshima kwa kiongozi wake huyo.
“Ni vizuri haujamuua hata mmoja maana kama ningechelewa kidogo ningewapoteza vijana hawa ambao hawana hatia yoyote ile”
“Sikujua kama ni wewe uliwatuma hapa ila washukuru sijataka kuwaua haraka maana nilitaka niwajue kwanza kwamba ni akina nani ila bila hivyo ningewaua muda mrefu sana”
“Panda kwenye gari” mzee huyo alitoa amri moja tu kisha gari hiyo ikatolewa hapo kwa kasi sana huku wale wanaume watatu ambao walikuwa wamevamia hapo wakikokotana na kutoweka haraka sana hilo eneo kwani maagizo ambayo walikuwa wamepewa na kiongozi wao walikuwa wameyatakeleza vizuri. Gari hiyo ilienda kusimamishwa maeneo ya mzambarauni pembezoni mwa reli ya treni na mzee huyo akawataka walinzi wake wawili watoke ndani ya hiyo gari alihitaji kubaki na kijana wake tu pekee na taa zote zikazimwa pakawa kimya sana ndani ya hilo eneo.
“Bilali nadhani unatakiwa kuwa makini sana, usipende sana kuitoa toa cheni yako hiyo kwa sababu ina utambulisho wa kifupisho cha jina lako, kuna watu ambao ni wataalamu sana wa kuunganisha doti hivyo inaweza kupelekea wewe ukajulikana haraka sana sehemu ambayo unakuwa upo mwisho wa siku ukaja kupotea kizembe sana. Kwenye kikosi cha DRAGON BOYS kumbuka wenzako wawili wanakutazama wewe hapo hivyo hautakiwi kufanya ujinga wowote ule ambao unaweza ukafanya wenzako wakaingia kwenye hatari”
“Nimekuelewa bosi, naomba unisamehe sana kwa hilo”
“Hayo yameisha nipe ripoti kamili”
“Hawa watu nimewafuatilia kwa umakini sana lakini kiufupi ni kwamba mheshimiwa raisi yupo kwenye hatari kubwa sana ya kuweza kuuawa”
“Hilo nalijua, nahitaji unipe taarifa kamili kwamba ni nani yupo upande wetu na ni nani hayupo upande wetu na nahitaji kujua sana kwamba ni akina nani ambao Denis anawaamini sana na kuwatumia sana kwenye hizi kazi zake”
“Watu wengi ambao wapo kwenye mfumo wa serikali ni wake na wanamtii yeye, kuanzia jaji mkuu wa serikali, mwanasheria mkuu wa serikali, spika wa bunge, waziri mkuu ambaye mpaka sasa hajatolewa, makamu wa raisi ambaye amemaliza naye utawala na watu wengi sana Ikulu wapo upande wake lakini jambo la hatari zaidi hata mkurugenzi wa shirika letu la kijasusi ni mtu wake wa karibu sana na kila habari nyeti huwa anampatia”
“Whaaaat?”
“Ndiyo bosi iko hivyo lakini pia kuna watu wachache sana ambao hawapo upande wake”
“Ni akina nani hao?”
“Kuna kiongozi mmoja wa upinzani lakini kwa wale ambao wapo ndani ya chama chake kuna DCI na IGP, hawa tunaweza kuwatumia kama silaha kwetu”
“Kwa namna ipi?”
“Kwa sasa mheshimiwa raisi anatakiwa kumteua waziri mkuu ambaye anamwamini sana kwa sababu tutamhitaji sana hapo baadae lakini pia anatakiwa kumpata makamu wa raisi ambaye ataweza kumuamini sana ndiye ampe hii nafasi na kwenye baadhi ya vitengo vikubwa tuwapenyeze wapelelezi wetu wa kuaminika ambao watakuwa wanakusanya taarifa za watu hao na kutupatia na hapa inatakiwa tuwapate watu ambao wapo nje ya mfumo ndio itakuwa rahisi zaidi kuweza kuwamudu kwenye kuwaendesha ila asimtoea mkurugenzi wa taasisi ya kijasusi”
“Kwanini asitolewe?”
“Huyu atatusaidia sana kwenye ukamilisho wa kuzipata taarifa za ndani sana za watu hao”
“Mtu ambaye hayupo upande wetu anatupaje taarifa za watu hao?”
“Nadhani unajua kuhusu yeye kumpa mheshimiwa raisi wale walinzi wawili na unajua kabisa kwamba wamelekwa pale kwa kazi maalumu?”
“Hilo nalijua, endelea”
“Sasa kwa wale vijana wawili ambao wamepewa ile kazi kuna walakini kwamba mmoja ni mzalendo na mwingine ni mtu wao ambaye wamemtuma kwa kazi maalumu pale Ikulu ndiyo maana nasema kwamba maisha ya raisi yapo hatarini muda wote kwa sababu muuaji yupo naye anamlinda muda wote vipi kama akipewa maagizo ya kuweza kumuua? Ni suala la dakika moja tu kutekeleza amri ya kiongozi wake ila sisi tutaitumia hii nafasi kuwaingiza wao kwenye shimo” mwanaume huyo ambaye alijulikaan kama Bilali alikohoa kidogo kujiweka sawa ili ampe mheshimiwa mpango mzima juu ya kile ambacho walitakiwa kukifanya hapo kuwatia watu hao kwenye mifuko yao.
“Nimefuatilia kwa undani sana taarifa za wale vijana tangu wanaanza kupatiwa mafunzo hapa Tanzania mpaka wanafikia hatua ya kumlinda mheshimiwa raisi ila mmoja wao kuna tatizo kidogo kwenye rekodi zake ndiyo maana ndiye ambaye naweza kusema kwamba ni msaliti na anafanya kazi zao wale watu. Anaitwa Karistus Dickson ni mzaliwa wa jiji la Mwanza huko, huyu kwenye rekodi zake alikuwa ni mtu ambaye kila baada ya siku kadhaa alikuwa akipotea kwenye kambi na baada ya muda kama wa dakika kumi angeonekana anarudi na kujumuika na wenzake na kwa huo muda ambao aluikuwa anapotea inaonekana alikuwa anafanya mawasiliano kwenye simu na baadhi ya watu jambo ambalo kiitifaki halikutakiwa kufanyika hivyo hilo limeleta uwalakini kwamba lazima alikuwa anaendelea kufanya kazi yake hata akiwa mafunzoni ya kuripoti kila ambacho kilikuwa kinaendelea kwa viongozi wake hivyo huyu ndiye hatari kubwa zaidi ambayo ipo kwa upande wa raisi na haitakiwi huu mpango ubadilike haraka sana namna hii maana inaweza kuwa hatari huyu anatakiwa kuendelea kuwepo pale ili kutimiza kazi yetu kwa usahihi”
“Lakini huyu mwingine ambaye anaitwa Donald Daniel, yeye ni kijana ambaye sina uhakika ila anaonekana ni mzalendo sana na ndiye ambaye tunatakiwa kumpata haraka sana kwa namna yoyote ile maana jina lake ni safi zaidi hata ya Obama kwa sababu hana historia yoyote ile mbaya wala kukutwa na tatizo au dosari yoyote ile kwenye maisha yake hata alipokuwa huko kwenye mafunzo lakini pia ni mwanaume wa shoka sana. Rekodi zake zinaonyesha kwamba alikuwa amepata alama za juu sana za mapigano na upelelezi kwenye kila sehemu ambayo alikuwa amepita hivyo naweza kusema anatufaa moja kwa moja”
“Na huyo kijana tunampataje?” mzee huyo aliingilia meongezi hayo baada ya kuonekana kwamba alikuwa amemuelewa sana kijana wake.
“Mtu pekee ambaye anatakiwa kufanya naye haya mazungumzo ni mheshimiwa raisi bosi”
“Hilo ni jambo gumu sana, tunaweza kujiingiza kwenye shimo sisi wenyewe, vipi kama akimmwagia hizo siri halafu akawa tofauti na unavyo mdhania huoni kama raisi atakuwa amejiteketeza yeye mwenyewe?”
“Bosi hii ndiyo njia ngumu lakini ndiyo njia pekee. Nina uhakika na taarifa zangu hivyo kwa asilimia sabini nina imani nipo sahihi na kama sipo sahihi basi ni kwa asilimia thelathini tu ambazo haziwezi kuathiri mpango wetu na kama tukimpata huyu tayari tutakuwa na mtu wa mhimu wa kumwamini kwenye mkono wetu ambaye anaweza kutusaidia sana kutekeleza majukumu haya ya mhimu”
“Na baada ya kumpata mpango wako ni upi?”
“Huyu atatusaidia kumchunguza kwa ukaribu sana mkurugenzi wa taasisi ya kijasusi kwa sababu yeye anaweza kukutana naye muda wowote ule hivyo kupitia yeye tutaweza kupata taarifa nyingi na kumbuka ukimtoa raisi yule ndiye mtu mhimu zaidi ndani ya taifa kwa sababu ana taarifa za siri ambazo zinaweza kuliteketeza taifa au kulikomboa taifa”
“Mpango wako mwingine ni upi?”
“Wakati kazi hiyo inafanyika ndio muda ambao raisi anatakiwa kuufungia ukumbi ule kama tulivyokuwa tumekubaliana mwanzo na muda huo mimi nitakuwa nimeingia kwenye upelelezi ili kuweza kuwajuia washirika wake wengine wa siri ambao huenda wanampa nguvu kuliko hawa wanasiasa maana lazima kuna wawekezaji wakubwa ambao wapo nyuma yake sasa tunatakiwa kuwapata hao na kama tutafanikiwa kuwapoteza ndipo tunaweza kumfuata yeye moja kwa moja itakuwa kazi sio ngumu sana kuliko kumfuata yeye bila kuwajua ambao wapo nyuma yake hapo hakuna jambo la maana ambalo tutakuwa tumelifanya zaidi ya kupoteza muda tu”
“Good, umefanya kazi nzuri sana lakini kuna jambo lingine ambalo ulisema kwamba ulikuwa unahitaji sana kuniambia kwa haraka mno”
“Ndiyo bosi ndiyo maana nikataka tuonane moja kwa moja”
“Lipi hilo”
“Unamkumbuka Laurenti Mande?”
“Ndiyo, aliwahi kuwa rafiki yangu kwa kipindi fulani, huyo si gavana ambaye alipoteaga kwenye mazingira ya kutatanisha na mpaka sasa inaaminika kwamba alifia baharini?”
Naweka nukta sehemu ya 10 panapo majaaliwa tukutane tena wakati ujao.
Tchao.
Hiyo umepeyana ni flashback ya Miaka 12 ilopita, ngoma inogileSi inasemekana kafa? 🤔
Niko apa mjengoni mkuuInasadikika. Mkuu. 001 is going to diee
Respect 👏Have my sincere appreciation.
Acha tuone kama ni ya kweli hayaInasadikika. Mkuu. 001 is going to diee
Shukrani sana mkuuHongera mkuu kazi nzuri
😅😅😅👋Hiyo umepeyana ni flashback ya Miaka 12 ilopita, ngoma inogile
😎🤏M Niko apa mjengoni mkuu
001. Apone aendelee kuokoa taifaHADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 60
“Hahahah hahaha namhitaji” mheshimiwa alicheka sana akiwa anasogea kwenye kiti na kukaa
“Lakini hii sio garantii mheshimiwa kwa sababu ni Kamari tu hivyo tunatakiwa kuendelea na mipango mingine tukiwa tunasubiria kama hili litafanikiwa”
“Nalijua hilo na nahitaji nchi hii ilipe gharama zangu zote, waziri mkuu anatakiwa kukopa pesa nyingi sana nje na kusaini mikataba ya pesa nyingi sana kupitia jina langu ili nirudishe hasara yangu na kama isipopatikana hii pesa basi kuna watu lazima nitawaua na watakao umia sana ni wananchi na sio mimi kama walivyokuwa wanadhani kwamba watanikomoa. Kwa sasa nataka nitafutiwe malaya mrembo kuzidi wote nchi hii nadhani unajua ni wapi pa kumpeleta nitakaa naye kwa siku kadhaa”
“Sawa bosi” maagizo yalikuwa yanajitosheleza hivyo mwanaume alitoka nje kwenda kuanza kuyakamilisha.
James, mmoja wa memba wa kundi hatari la DRAGON BOYS alifanikiwa kutoroka na kutoka akiwa mzima wa afya kabisa lakini ilikuwa tofauti kwa wenzake wawili ambao walipoteza maisha yao pale pale sehemu ambayo walikuwa wanapambana na Ted na Kenedy. Mwanaume huyo kuishi kwake alikuwa anatakiwa kuhakikisha kwamba Max anaishi tena na kuwa hai na ndiyo majukumu ambayo aliachiwa na kiongzi wake Bilali Rikardo.
Baada ya kufanikiwa kutoka pale alienda moja kwa moja mpaka ndani ya jumba lao ambalo lilikuwa karibu kabisa na shirika la msalaba mwekundu na kuingia ndani ya chumba kimoja ambacho kilikuwa na mashine moja ya mionzi na mashine moja iliyokuwa na makali mithili ya sindano. Aliingia kwenye mashine hizo ambazo zilikuwa zimeunganishwa, ile mionzi iliwashwa kuelekea ulipokuwa mwili wake na baada ya sekunde kadhaa alikuwa anapiga makelele sana kwa maumivu makali ambayo alikuwa ameyapata.
Baada ya dakika moja tu mashine ambayo ilikuwa na sindano kali na kubwa ilichana sehemu ya mwili wake na kutoa kitu ambacho kilikuwa kama laini ya simu lakini kilikuwa kidogo sana. Kilikuwa ni kifaa cha mawasiliano ambacho kilikuwa kimepandikizwa kwenye mwili wake na alijua kwamba hicho kingemfanya yeye akamatwe kirahisi sana. Mwanaume alipitia maumivu makali sana kiasi kwamba alidondoka kabisa chini huku mashine hizo zikijizima zenyewe baada ya kazi hiyo kuisha. Alikaa hapo kwa dakika kama tano akiwa nahema kwa nguvu sana maana ile mionzi ilikuwa na nguvu kubwa mno na mwili wake haukuwa bado umetulia vizuri lakini hakuwa na muda wa kupoteza.
Akiwa kifua wazi alisimama kwa kusaidiwa na ukuta akaanza kujivuta kuelekea kwenye chumba kingine ambacho kilikuwa na komputa nyingi sana, aliziwasha na kutaka kubahatisha jambo moja japo kwenye nafsi yake hakuwa na imani kama jambo hilo lingeweza kufanikiwa ila aliamua kuziamini hisia zake na kukisia hivyo hivyo. Wakati wanafanya mawasiliano ya mwisho na Max alikuwa na simu kwenye mwili wake, hata wakati anakamatwa na Dax mwanaume alitolewa shati na koti tu pekee, suruali yake nzito ya kazi ilikuwa kwenye mwili wake na hata buti lake ilikuwa hivyo lakini moja kati ya makosa ambayo waliyafanya ni kushindwa kumkagua mtu huyo kwenye mifuko yake kwa sababu walijua ni siku yake ya mwisho hivyo hawakuwa na huo umakini zaidi ya kutoa kifaa cha mawasiliano tu kwenye mwili wake.
Hiyo ndiyo simu ambayo ilikuwa kwenye mifuko ya Donny ndiyo James alikuwa anahitaji kuitumia ili kujua kama mwanaume huyo alikuwa wapi majira hayo ya usiku ili kama atakuwa hai awahi kuweza kumsaidia. Ilikuwa ni kama bahati nasibu tu kwa mdukuzi hatari sana huyo ambaye alikuwa anategemewa sana na kundi lake kwa hiyo kazi. Alikaa kwenye komputa hizo na kubonyeza kwa muda kidogo ambapo simu hiyo aliipata tena ikiwa hewani na location yake ilikuwa inasoma Ikulu.
Alisubiri kuona kama inaweza kupotea hapo na kweli baada ya muda aliona inaanza kusogea na kuonekana inatoka kabisa ndani ya hilo eneo. Mwanaume alisogea kwenye kabati moja na kutoa vidonge akiwa anayumba yumba kwa sababu bado mwili wake ulikuwa na maumivu makali sana. Vidonge alivyotumia vilikuwa ni hatari sana kwa uhai wa seli kwa sababu vilikuwa vinaupa mwili nguvu kwa lazima hivyo ilikuwa ni hatari kwa upande wa afya yake ila hakuwa na namna kazi ambayo ilikuwa mbele yake kuliokoa taifa ilikuwa ni mhimu sana kuliko hata maisha yake.
Baada ya kunywa dawa hizo alilia kama mtoto mdogo akiwa ameshika kichwa maana zilimletea maumivu makali sana na baada ya dakika tatu alitulia kwa dakika moja kisha akaamka akiwa sawa kabisa mwili ukiwa umelowa kwa jasho.
“Max wewe ndiye pekee ambaye unaweza kuja kulisaidia taifa hili tafadhali sana naomba usife, nakuja kwa ajili yako” aliongea kwa msisitizo sana akichukua nguo zake za kazi na bastola kwenye kiuno chake kisha akatoweka kwa gari ndani ya hilo eneo.
Simu hiyo ilikuwa inamuelekeza wapi pa kwenda kulingana na namna ilivyokuwa inahama, alitembea akiwa umbali kidogo baada ya kuziona gari ambazo zilionyesha kwamba ndimo simu hiyo ilimokuwemo. Hakuwa na uhakika kama simu hiyo alikuwa nayo bado Max ila hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya pekee kabisa maana hakuona tobo lingine la kuweza kufanya hivyo. Safari ya wanaume hao iliishia msituni ambapo hata yeye mwenyewe alisimama na kuligeuza gari lake na kulipenyeza ndani ya miti baada ya kuona watu hao wanamtoa mtu kwenye gari na kuanza kuelekea naye ndani msituni huku wengine wakiwa wameshika majembe na koleo kadhaa wakiwa na haraka sana mvua ikiwa inaendelea kushuka.
Mwanaume aliwafuatilia kwa umakini sana mpaka walipofika pale na kuanza kuchimba kaburi ambapo walichimba na kisha kwa muda mfupi mwanaume huyo alirushiwa ndani ya kaburi hilo na kuanza kufukiwa. James kwa hali ambayo alikuwa ameiona alikuwa amekata tamaa kabisa kwamba mtu huyo mpaka anazikwa maana yake ni kwamba alikuwa ameshauawa hivyo alikata kabisa tamaa lakini kuna kitu kimoja ambacho kilimshtua na kuhisi kwamba kuna kitu huenda hakikuwa sawa kabisa. Ni baada ya kumsikia Dax akiwa anamkumbushia mwanaume huyo kwamba sura yake ndicho kitu cha mwisho kabisa yeye kuweza kukiona kisha utafuata mchanga na giza halafu pumzi itaanza kukata na baada ya hapo utakufa vibaya sana.
Tambo za Dax ndizo ambazo zilimhakikishia kwamba mwanaume huyo alikuwa mzima bado ila huenda kuna kitu kibaya alifanyiwa. Hayo yote alikuwa anayashuhudia akiwa amejibanza sehemu kwenye mti mmoja mkubwa ambao ulikuwa na matawi mengi sana. Aliwashuhudia wanaume hao wakifukia kaburi hilo mpaka walipomaliza kisha Dax akalishindilia vizuri na kuanza kuondoka lakini kitu ambacho walikosea ni baada ya kuona vifaa vyao vina tope sana waliamua kuvitupia porini na kuvitelekeza huko huko.
James alikuwa makini sana kuwaangalia watu wale walivyokuwa wanatokomea mpaka kufika kwenye magari yao na kuanza kuondoka. Mwanaume alisogea hiyo sehemu akiwa na wasiwasi sana, alishika koleo moja na kuanza kufukua kwa kasi ya ajabu mno kwenye kaburi hilo ambalo lilimchukua muda mfupi sana kuweza kuukuta mwili wa mwanaume huyo wa kazi tena ukiwa kifua wazi kabisa. Alimtoa nje na kumgusa puani, mwanaume hakuwa akitoa pumzi yoyote ile, alimgusa kwenye moyo palikuwa kimya sana na mwisho akagusa shingo, hakuhisi kitu chochote kile kama mtu yule alikuwa hai.
“Hapana Max huwezi kufa kwa staili hii, hii nchi inakuhitaji sana” aliongea akiwa na wasiwasi sana, alimjazia pumzi sana kwenye mdomo lakini wapi hakuona chochote, alimbeba akiwa anakimbia na kuelekea alipokuwa amepaki gari yake kwa kasi mno kisha aliitoa hapo kama vile ana kichaa kuwahi kwenye makazi yake akaangalie kama anaweza kumsaidia mtu huyo maana nafsi yake ilikuwa inagoma kabisa kuamini kwamba mtu huyo alikuwa amekufa.
Akiwa anapita njiani kwa kasi alikutana na ule msafara wa akina Dax, wao hawakuwa wamemuona maana aliwapita kasi sana ila alifanikiwa kumuona mwanaume huyo kupitia dirishani akiwa anajipongeza kwa pombe kali, alimwangalia kwa hasira sana lakini hakuwa na cha kufanya muda huo ulikuwa ni wakati wa kujaribu bahati yake kama anaweza kumsaidia huyo mwanaume ambaye aliambiwa kwamba ndipo tumaini la nchi lilipokuwa.
Alifanikiwa kurudi nyumbani, ambapo yalikuwa ni makao makuu ya DRAGON BOYS na kumuweka Max kitandani akiwa bado ana tope kwenye mwili wake, alimsafisha vizuri kisha akajaribu kupampu moyo na mashine lakini hakuona chochote. Alijitahidi sana kumuwekea mpaka vifaa vya kupumulia lakini bado ilikuwa kama ni kazi bure na dalili za kuamini kwamba mtu huyo hakuwa hai na alikuwa amekufa zilikuwa zinaanza kuja hasa baada ya kumsafisha na kuona kwamba mwanaume huyo alikuwa na risasi za kutosha kwenye mwili wake.
James alisogea kwenye komputa yake na kuingia kwenye mtandao wa madaktari, alikuwa anahitaji kumpata daktari wa kukodisha kwa muda. Alitengeneza jina feki ili liweze kumsaidia kwenye kuaminina na akafanikiwa kumkuta daktari mmoja ambaye alikuwa anajulikana kama daktari hodari sana lakini alikuwa ni mtu mpenda rushwa sana kwenye huduma yake hiyo. Aliwasiliana naye na kumuahidi kiasi kikubwa sana cha pesa ila kikubwa yeye alikuwa anataka tu mtu wake aweze kupona na daktari huyo hakuwa na tatizo kikubwa ambacho yeye alikuwa anajali ni pesa kuingia kwenye akaunti yake tu.
Dakatri huyo alifika ndani ya dakika arobaini tu usiku huo huo wa manane maana dau ambalo aliwekewa mezani lilimfanya hata usingizi wake kuisha baada ya kupokea simu. Kukutana na James alimkuta mwanaume huyo akiwa na wasiwasi mkali sana hivyo akajua kabisa kwamba hapakuwa pema. Bila kuongea walipeana mikono na mwanaume huyo akamuongoza daktari huyo ambaye alikuwa anawaza pesa tu kwenye kichwa chake mpaka ndani ya chumba ambacho alikuwa amelazwa Max. alishtuka sana baada ya kuiona sura hiyo kwa sababu kila sehemu ya nchi zilikuwa zimesambazwa taarifa kwamba mwanaume huyo alikuwa ni gaidi na alikuwa amekufa, sasa ilikuwaje awe hapo na awe hai? Alihisi hakuwa salama.
“Huyu si gaidi?”
“Vyombo vya habari ndo vinasema hivyo”
“Unataka mimi nimtibu mtu aliye muua raisi wa nchi? Unataka mimi nimtibu mtu ambaye dunia nzima inajua kwamba ni msaliti kwa taifa lake? Unahisi kitanikuta nini watu wakijua kwamba mimi ndiye niliyaokoa maisha yake?”
“Hakuna atakaye jua kuhusu hili”
“Unajuaje kwamba itakuwa hivyo?”
“Kwa sababu hakuna namna ya wewe kuweza kuongea” kauli za James daktari alishindwa kabisa kuzielewa ila kama angezielewa huenda angetafuta mapema njia ya kuweza kuyaokoa maisha yake.
“Hata kama ni hivyo bado siwezi kumtibu mimi”
“Nakulipa bilioni moja kwa kazi ya usiku mmoja tu. Pesa ambayo huenda haujawahi kuishika mkononi hapo hapo na huenda hautakuja kuishika milele mpaka unakufa, wewe ni mtu smart sana dokta usitake kuikataa hii ofa ambayo ninaweza kumpatia daktari yeyote yule na akaja muda huu” dau lilikuwa ni kubwa mpaka yeye mwenyewe anavyotajiwa alishtuka sana maana hakutegemea huko, aliishia kuguna na kuiweka tai yake sawa huku akilitua begi lake la kazi mezani. Hiyo ilikuwa ni ishara ya kukubali kazi.
“Huyu mtu ni nani hasa kwako mpaka unaweka pesa nyingi sana kiasi hicho kwa ajili yake?”
60 inafika mwisho.