HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 64
Baada ya kijana huyo kutoka humo ndani alipasua pasua meza yake kwa hasira kali ambazo alikuwa nazo baada ya kuambiwa mambo ambayo kwake hayakuwa mema kabisa, ilikuwa ni ishara mbaya sana. Aliifungua tai yake na kuitupa kisha akamimina pombe kali sana na kuigida yote, akaketi kwenye meza ambayo ilikuwa na simu hapo, aliipigia namba moja kwenye simu hiyo ikawa inaita lakini wakati anasubiri simu hiyo iweze kupokelewa upande wa pili simu yake ya mkononi ilianza kuita na namba ambayo ilikuwa inapiga ilionekana kutokea Marekani ila alijua kwamba anahezewa tu. Aliipokea kwa wasiwasi sana
“Hello bwana Denis Kijazo” ilisikika sauti nzito sana kutoka upande wa pili.
“Nani wewe?”
“Usiwe na haraka sana mzee wangu, nina maelekezo mafupi sana kwako”
“Yapi?”
“Jiue mwenyewe kabla sijakukamata au nenda kwneye vyombo vya habari ueleze kila ambacho umekifanya tangu uingie kwenye siasa, ukifanya hivyo mimi nitakuacha na maisha yako na sitakugusa kabisa ila kama itakuwa ni ngumu sana kuchagua moja kati ya haya machaguo mawili basi mimi nitakusaidia kuweza kuyachagua” mwanaume huyo ambaye hakujulikana hakuwa na haraka kabisa wakati wa kuyatoa maelezo hayo, alitulia kusikiliza jibu la mheshimiwa huyo.
“Hahah hahaha hahahah nadhani bado wewe ni mgeni ndani ya hili jiji”
“Hata wewe hili jiji ulilidandia tu bwana kijazo na ukataka kuligeuza lionekane lako kwa nguvu, au nakosea?”
“Wewe ni nani?”
“Muda sio mrefu sana utanijua”
“Wanaume huwa wanakutana uso kwa uso wanapofanya mazungumzo kama haya, unajisifia huku umejificha nyuma ya simu? Jitokeze nikufahamu kama wewe mwanaume kweli”
“Ni bahati kwako tunaongea kwenye simu kwani kama tungeonana kama unavyotaka wewe basi ungerudi kwako ukiwa na mkono mmoja na mguu mmoja tu pekee hivyo wewe ndiye unatakiwa kushukuru kwa hili la kuongea na mimi kwenye simu na sio ana kwa ana. Nadhani umenielewa kile ambacho nilikwambia hivyo unatakiwa kuanza kukifanyia kazi wakati huu na nakupa masaa ishirini na manne tu uwe umefanya maamuzi yako ya mwisho” simu ilikatwa baada ya kupewa hayo maelekezo. Hayakuwa ya muda mrefu sana lakini yalikuwa yanaeleweka vizuri, alishangaa sana mtu ambaye alikuwa anatoa amri kila siku eti naye alikuwa anatishiwa kwenye simu.
“Max, hahahahahah hahahaha kama ulifanikiwa kuishi kwa kuzikwa, saivi nitakutia kwenye mafuta ya moto nishuhudie ukiwa unaungua kwa macho yangu halafu kama utapona tena basi nitakuacha uendelee na maisha yako” mzee huyo alitamka kwa hasira sana akiwa anatoka eneo hilo ambapo walinzi walikuwa makini sana kuhakikisha anakuwa salama wakati wote.
Mwanaume ambaye alimvamia Dax hakuwa mbali na lile eneo wakati umeme unarudi na Dax anajikuta yupo mwenyewe pale. Mwanaume huyo hakuwa mwingine, mawazo ya Dax yalikuwa sahihi kabisa, kipindi hicho mvua ikiwa inayesha kwa kasi sana maeneo hayo Max alikuwa juu ya paa moja la nyumba akiwa amesimama na begi mkono mmoja na mkono mwingine alikuwa amelishika shoka jipya kabisa.
Alikuwa hapo akiwa anamtazama mwanaume mwenzake jinsi alivyokuwa akihangaika pale chini tena akiwa mwingi wa wasiwasi sana na ile karatasi ambayo alikuwa anaisoma. Dax aliondoka kwa kukimbia kwa kasi sana na kila ambacho alikuuwa anakifanya DONNY alikuwa akimshuhudia na wakati huo alikuwa ameitoa mask yake usoni, uso ulikuwa wazi unanyeshewa na mvua. Baada ya kukamilisha kitu ambacho kilimpeleka ndani ya hilo eneo alitoweka haraka sana na kwenda mahali ambako hakuna aliyekuwa anajua.
“Kiongozi” ilikuwa sauti ya mwanaume ambaye alienda kumpokea Max wakati anaingia ndani ya jumba moja la ghorofa tatu. Mtu huyo alionekana kuwa mkubwa sana kwake ila alionyesha hali ya kumheshimu sana mtu huyo.
Walikuwa ndani ya Mbezi Beach karibu kabisa na ufukwe wa bahari, huko ndiko walikokuwa wanaishi watu hao. Mwanaume baada ya kupokelewa mzigo huo, waliondoka wakiwa wameongozana kuelekeaa kwenye lifti ambayo iliwapeleka mpaka vyumba vya chini kabisa. Aliyekuwa amempokea Max alikuwa ni mwanaume wa kazi James masalia ya DRAGON BOYS na ndiye ambaye alimuokoa Max na kumfanya aendelee kuipata pumzi ya bure kabisa.
“Nimemuacha hai”
“Kwanini”
“Kwa sababu yeye kuwa hai sisi tunapiga hatua ya mbali zaidi, kama ningeamua kumuua basi ningepata mzigo lakini kile ambacho nimekidhamiria nisingeweza kukifanikisha”
“Unataka kuniambia una mpango upi mwingine?”
“Nilitaka huyu afikishe taarifa kwao kwamba mimi nipo hai na bado ninaishi”
“Kwahiyo umejitambulisha kwake?”
“Hapana, kuna ujumbe nimeuacha na nina imani ameelewa umetoka kwa nani kwa sababu ameondoka pale akiwa anatetemeka sana na ile kauli niliyo iandika pale ni yeye pekee ndiye ambaye aliwahi kuisikia kutoka kwenye kimywa changu”
“Nadhani umekosea sana kufanya hawa watu watambue kwamba bado upo hai”
“Hicho ndicho nilikuwa nakitaka, nataka watu hawa wapate mshtuko mkubwa sana na hilo litakuwa moja kati ya anguko lao kubwa mno na hizi nyaraka zipo kwenye mikono yetu kwa sasa hivyo kazi itakuwa rahisi kuimaliza. Kuchanganyikiwa kwao kutafanya waanze kufanya mambo kwa presha sana na hatutawapa nafasi nyingine ya kuweza kujiandaa mpaka presha yao ije kuisha kazi imesha isha kisha sitataka tena kukaa ndani ya nchi hii. Nitaondoka moja kwa moja”
“Sawa kiongozi lakini umeumia”
“Usijali ni jeraha dogo sana hili James”
“Kwahiyo kwa sasa unafuata mpango gani?”
“Tutazipitia hizo nyaraka zote na baada ya hapo anaanza kufa mmoja mmoja kila ambaye anahusika nazo”
“Hata raisi?”
“Yeah, lazima nimuue”
“Huoni kama itaibua mambo mengine ambayo yanaweza kuleta wasiwasi kwa wananchi?”
“Ni bora wapate shida kwa muda mfupi kuliko kuwa watumwa kwa maisha yao yote”
“Jifute damu hizo na ubadilishe hayo mavazi haraka” James aliongea kama ishara ya kumwambia kwamba alitakia kujiweka vizuri kwani kulikuwa na ugeni ndani ya nyumba hiyo. Max alimwangalia sana mwanaume huyo.
“Whaaaaaat? James, Noo” aliongea akiwa anamsogelea na kumkaba shingo yake kwa nguvu na hasira kubwa sana.
“I’m sorry boss” mwanaume huyo alitamka kuomba samahani kwa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.
“Kwanini umeruhusu familia yangu ije huku?”
“Sio mimi ni mkeo ndiye kataka hivyo kwa sababu mwanao alikuwa anagoma hata kwenda shule bila kukuona wewe”
“This is one of the biggest mistake James”
“Nadhani unapaswa kuongea na mkeo kuhusu hili” mwanaume aliiondoka hapo kichwa kikiwa kimepata moto sana, alivaa vizuri na kujiweka kwenye hali ya usafi kisha akapanda juu sebuleni ambapo baada ya kufika tu alipokelewa na sauti ndogo na laini sana yenye furaha tele.
“Dady” ni binti yake ambaye alikuwa anaitwa Naima ndiye ambaye alimkimbilia kwa furaha sana na kumkumbatia baba yake. Alimpokea mwanae kwa furaha sana na kumbeba huku akiwa anamzungusha hewani kwani alikuwa anampenda isivyo kawaida na hakuwa tayari kuona kitu chochote kinasogea katikati ya mwanae na mkewe.
Akiwa amembeba mwanae na kucheka nae kwa furaha sana kwenye kona moja alimuona mwanamke mrembo sana akiwa ameegamia kona hiyo na kumtazama mwanaume huyo kwa furaha kubwa sana isiyo isha hamu. Alikuwa anainjoi kumuona baba na mwana wakiwa kwenye furaha kubwa furaha ambayo yeye hakuipata huko nyuma lakini kwa wakati huo alikuwa anaipata kupitia mumewe na mwanae. Ilikuwa inamkumbusha mwanamke huyo mrembo kwamba duniani hata kama utakuwa na nini ila hakuna kitu bora kuizidi familia, familia ndiyo kila kitu na familia ndipo zilipo baraka za furaha kwa mwanadamu yeyote yule.
Mwanaume baada ya kuinua macho yake na kumwangalia mwanamke huyo alitabasamu, mkewe alikuwa anazidi kuwa mrembo kila siku moja ilivyokuwa inasogea mbele. Alimwachia mwanae na kumwambia akacheze mezani angeenda kumchukua tena na wakati huo alisogea sehemu ambayo alikuwepo mkewe na kumbeba kwa furaha sana huku wakipigana mabusu ya kuonyesha jinsi walivyokuwa wamekumbukana sana.
Alimbeba mkewe mpaka chumbani ambapo alihakikisha anampatia haki yake kama mume na baada ya hapo alihitaji waweze kuongea na kujua sababu ambayo imemfanya mwanamke huyo kumfuata maana alimkataza kabisa kufanya jambo kama hilo na ingekuja kuwa hatari kubwa sana kwa familia yake ndiyo maana alitaka wabaki kuishi huko huko nje ya nchi.
“Kwanini mmekuja Tanzania tena?”
“Ni kwa sababu nakupenda sana mume wangu, mimi sikuwa tayari kuishi maisha ya upweke tena kwenye maisha yangu. Hii miaka kumi na mbili ambayo nimekuwa karibu yako ndiyo miaka yangu bora zaidi kuwahi kuishi na kujihisi kama mwanadamu, kila siku nimekuwa nahitaji kuwa karibu na mume wangu tangu siku ya kwanza nimegundua kwamba nafsi yangu inakuhitaji siku zote sasa unahisi ningewezaje kuishi mwenyewe? Mwanao kila akiamka asubuhi alikuwa amezoea kukuona na angekuita kwa furaha sana ndipo aende shule kitu ambacho kimekuwa tofauti sana kwa huu mwezi mzima, kila akiamka swali la kwanza ni yuko wapi baba, amegoma hata kwenda shule muda wote analia anataka kukuona baba yake, unahisi mimi ningefanya nini mume wangu? Nakupenda sana” mwanamke ambaye alikuwa anayaongea hayo maneno alikuwa ni Ariana, dada yake Siza ambaye Max aliachiwa majukumu ya kuweza kumlinda.
Huyo ndiye alikuwa mkewe na alimzawadia mtoto mmoja wa kike Naima ambaye mpaka wakati huo aliikamilisha furaha ya wao kuwa na familia ambayo walitamani sana kuiita familia bora lakini mbele yao kulikuwa na mambo makubwa sana na ya kutisha mno ndiyo maana Max aliogopa sana baada ya kujua kwamba familia yake ilikuwa imerudi tena ndani ya nchi. Mwanaume hakuongea jambo lolote tena zaidi ya kumkumbatia mkewe kwani aliyo yaongea yalikuwa ya kweli na aliyaongea kwa uchungu mkubwa isivyo kawaida.
64 inafika mwisho.