Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

Simulizi ya kipelelezi: Jiji la kamari (gambling city)

HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 65
“Nitawalinda kwa gharama yoyote ile” aliongea akiwa anamuacha mkewe apumzike baada ya kupitiwa na usingizi na ndipo akarudi kwa James.
“Kwa muda gani ulijua kwamba watarudi?”
“Siku mbili”
“Kwanini haukuniambia?”
“Alinisisitiza sana kwamba kama ningekwambia basi asingenisamehe kamwe kwenye maisha yangu maana ningekuwa nahatarisha hali ya mtoto”
“James unajua mpaka hivi ninavyozungumza kuna watu huenda wana picha za mwanangu na mke wangu?”
“Unahisi wanaweza wakawa wamehisi kwamba kuna mtu mgeni amefika ndani ya nchi?”
“Denis Kijazo kila taarifa za nchi hii anaweza kuzipata kwa dakika kumi tu pekee unahisi mke wangu wakati anaingia pale uwanja wa ndege hakuna kitu ambacho watakipata kutoka kwake?”
“Niliangalia sana usalama wa kamera pale sidhani kama inawezekana kuna tatizo lolote”
“Mimi nilifanya kazi ndani ya shirika letu la kijasusi, najua una uwezo mkubwa sana kwenye mitandao ila ninacho kizungumzia hapa ni kitu tofauti kabisa. Sehemu kama zile huwa zina kamera za siri sana ambazo ili kuzifungia ni mpaka ujue kwamba zipo na najua haukuwa ukijua kuhusu jambo hilo je una imani bado kwamba kutakuwa na uhakika wa usalama wao na wako pia?”
“Nisamehe sana kiongozi”
“Huu sio muda wa kuombana msamaha ila ni muda wa kujua kwamba ni kitu gani tunatakiwa kukifanya baada ya hapa. Nina imani kwamba picha zao, mke wangu na mwanangu mpaka sasa kuna watu wanazo kitu ambacho litakuwa suala la muda tu kufanikiwa kutufikia hivyo tunatakiwa kuifanya kazi hii kabla ya wao hawajafanya lolote lakini kuna ombi moja ambalo ninalo kwako”
“Nahitaji kuimaliza kazi hii na nashukuru sana kwa mchango wako mkubwa mpaka sasa tupo wote ila kwa sasa naomba uilinde familia yangu.”
“Hii tayari ishakuwa familia yangu hivyo hakuna mtu hata mmoja ambaye atafanikiwa kuigusa kama mimi bado nipo hai na kama mtu huyo atataka kufanya hivyo basi anatakiwa kuhakikisha kwamba mimi nakufa kwanza” wanaume hao walikumbatiana kisha kila mtu akaingia kwenye majukumu yake ya kawaida japo Max alikuwa ni mtu mwenye wasiwasi sana.
Kurudi kwa Max ilikuwa ni habari mbaya sana kwa Denis Kijazo lakini habari mbaya zaidi ni kwamba kijana wake alipoteza mzigo wa mhimu sana ambao kwa maelezo yake alidai kwamba ungeweza ukampoteza kabisa duniani. Nyaraka ambazo ziliibiwa zilikuwa ni mhimu sana kwake na ndiyo maana alimpa Dax masaa ishirini na manne tu awe amefanikiwa kuzipata vinginevyo angedili naye mwenyewe. Alikuwa yupo kwenye gari yake anaelekea Ikulu ambako alionekana kuwa na mazungumzo ya mhimu sana na mheshimiwa raisi wa taifa la Tanzania.
Akiwa kwenye gari aliichukua simu yake na kujiweka sawa kisha akaipiga kwa kijana wake ambaye alikuwa anamwamini sana. Simu hiyo ilikuwa inaelekea Ngarenaro ya chini Jengo la saba sehemu ambako ilikuwepo ngome yake ya siri ambayo ilikuwa inamuingizia mabilioni ya fedha. Simu ilimkuta Ted akiwa amekaa na vijana wake wakiwa wanafunga mahesabu ya pesa, aliipokea haraka sana na kusogea pembeni ili kuweza kumsikiliza bosi wake.
“Mzigo ambao Max alienda kuuchukua kwa yule mzee umepotea na upo kwenye mikono ya Max”
“Hilo haliwezekani bosi, huyo mtu alikufa miaka kumi na mbili iliyopita”
“Hata mimi nilijua hivyo ila kwa sasa kinachotakiwa ni mzigo kupatikana kisha ndo tuanze kujua kwamba huyu mtu aliponaje wakati alizikwa. Nadhani unajua ni kipi ambacho unatakiwa kukifanya lakini kabla haujafanya jambo lolote pitia kamera zote za uwanja mkubwa wa ndege ambao unapokea watu kutoka pande zote za dunia kisha kama kutakuwa na kitu utakipata utanipa taarifa”
“Sawa mkuu” Ted alikata simu na kuhema kwa nguvu sana, hiyo kazi haikuonekana kwamba itakuwa nyepesi sana japo haikuwa inampa mashaka maana alizoea sana kufanya kazi za namna hiyo. Alirudi kwa vijana wake na kumuita Kenedy pembeni ambaye naye alikuwa akimwamini sana.
“Mimi leo natakiwa kwenda Dar es salaam kuna tatizo kubwa sana limetokea. Nyaraka za mhimu sana za bosi ambazo zinaweza kumpoteza zimepotea hivyo natakiwa kwenda kuhakikisha zinapatikana na hii sehemu naiacha kwenye mikono yako ila na wewe unatakiwa kuja Dar es salaama haraka sana hesabu zikikamilika”
“Unajua ni nani amezichukua?”
“Yeap, ni Max”
“Unamaanisha yule mlinzi wa zamani wa raisi Teodensia Mpanzi ambaye alizikwa”
“Kuhusu kuzikwa unasema wewe ila yupo hai na tunatakiwa kujua kwamba ni wapi yupo, anataka kufanya nini na alikuwa wapi mpaka ajitokeze baada ya miaka hii kumi na miwili?” Maelezo ya Ted yalimchanganya sana Kenedy, ni kama alikuwa anasimuliwa simulizi za zamani ambazo zisingekuwa kweli ila kwa bahati mbaya sana alitakiwa kukubaliana na huo ukweli ambao alikuwa anapewa wakati huo.
“Kwahiyo ni kipi kinafuata kwa sasa?”
“Tunatakiwa kuangalia marejeo ya video za pale uwanja wa ndege kwa miezi kadhaa nyuma ila nataka za kuanzia leo kisha zingine zifuate” ilikuwa ni amri ambayo mara moja ilianza kutekelezwa hapo. Walisogea kwenye chumba cha kazi ambacho kilikuwa na komputa nyingi sana na kuna vijana ambao walikuwa hapo wakiwa makini sana kucheza na komputa hizo.
Walikuwa makini sana kwenye kukagua kila hatua na kila mtu ambaye alikuwa anapita eneo hilo taarifa zake zote zilikuwa zinajitokeza kwenye komputa hizo kitu ambacho kiliwarahisishia sana kazi wanaume hao. Walizipitia kwa muda mrefu sana na mara ghafla walimuona mwanamke mmoja mrembo sana akiwa na mtoto.
Ted ambaye alikuwa ameanza kusinzia kutokana na kukaa muda mrefu alishtuka sana baada ya kumuona mwanamke huyo akahitaji watu hao wasimamishe hapo kwanza.
“Stop” aliongea akimpa ishara mwanaume mmoja kuweza kuirudia video hiyo na kuikuza picha ya mwanamke huyo pamoja na mwanae. Jina lake lilikuwa linasoma mrs Howartson kutokea ndani ya nchi ya Marekani, kwake jina halikuwa na shida sana ila kitu ambacho kilimshtua ni mtoto ambaye alikuwa na mwanamke huyo, mtoto alikuwa anafanana sana na mtu ambaye aliamini kwamba alikuwa anamfahamu sana.
Mwanaume alisogea mwenyewe kwenye komputa nyingine ambayo ilikuwa pembeni yake na kuandika jina la Max. zilikuja taarifa za mtu huyo kwa sababu alikuwa maarufu sana na alidaiwa kuwa ndiye gaidi hatari zaidi wa taifa la Tanzania kwa kumuua raisi miaka kadhaa ambayo ilipita. Aliikuza picha ya mwanaume huyo akaikuza na ya mtoto kisha akawa anaangalia kwa zamu zamu kama kufananisha kitu. Baba na mtoto walikuwa wanafanana vitu vingi sana kama ungewaangalia kwa umakini mkubwa na ndiyo sababu ambayo ilimshtua sana baada ya kumuona mtoto huyo akiwa na mama yake.
“Yes, nimekupata Max”
“Mkuu unamaanisha nini?”
“Hii ni familia yake, huyo mwanamke mrembo ni mkewe na huyo binti mrembo ni mwanae wa damu. Mchezo huu unaenda kuwa mrahisi sana na mimi siku zote ndiye huwa nazichanga karata kwenye huu mchezo”
“Unataka kufanya nini?”
“Binadamu yeyote yule duniani hata kama atakuwa mgumu au katili kiasi gani, udhaifu wake mkubwa huwa ni familia. Mbele ya familia hata watu wa kutisha huwa wanapiga magoti wakiomba watu wao wanao wapenda waachiwe. Kama tukiipata familia yake basi niamini mimi atakuja yeye mwenyewe popote ambapo nitahitaji aje na kwa sasa nataka nishuhudie anavyokuja kufufuka tena kwenye mikono yangu” Ted aliongea kwa furaha sana akiwa anaangalia mpaka mwanamke huyo anavyotoka ambapo alienda kupokelewa na mwanaume mmoja ambaye alikuwa anamsubiria kwenye gari moja ya kifahari sana.
Alimpokea mwanamke huyo kwa heshima na kumpandisha kwenye gari hiyo na mtoto kisha akaondoka eneo hilo akionekana kuwa makini sana huku mbele yake kukiwa na gari moja na nyuma yake kukiwa na gari nyingine na hao wote walikuwa ni walinzi ambao walitakiwa kumlinda mwanamke huyo na mtoto.
Ted alibaki anamtazama huyo mwanaume kwa umakini mkubwa sana ambaye alikuwa anamlinda mke wa max akifahamaika kwa jina la mrs Howartson. Aliikuza na picha ya mwanaume huyo akiwa kama anaifananisha pia na alikuwa ana uhakika kwamba aliwahi kuiona mahali japo ni zamani sana. Kumbukumbu zake zilimrejesha ule usiku ambao walikuwa kwenye nyumba ya Madilu Mpagazi walipokutana na DRAGON BOYS, huyo ndiye pekee ambaye alifanikiwa kuishi na alimdharau sana kwa kipindi kile lakini ndiye alikuwa chanzo cha mambo yaote hayo kutokea.
“Ooooh shiiit! Nilifanya kosa kubwa sana kumuacha hai huyu mjinga na nahisi kwamba yeye ndiye ambaye alimsaidia Max kutoka kwenye kifo hivyo natakiwa kurudi Dar es salaam haraka sana na kama kuna kitu mtagundua basi mtatakiwa kunitaarifu haraka sana hawa watu natakiwa kuwaweka kwenye mkono wangu kwa muda mchache sana ujao”
“Sawa mkuu” wate waliitikia wakati huo mwanaume huyo alikuwa anatoka ndani humo na vijana kadhaa ili kuweza kusafiri mpaka ndani ya jiji la Dar kwenda kuikamilisha kazi ambayo alikuwa ameianza na bosi wake alihitaji yeye aimalize mapema sana.


IKULU
Bado ilikuwa ipo chini ya Justin Mtadei, mwanaume ambaye aliingizwa hapo baada ya kifo cha Teo akiwa kama ameikaimu nafasi yake na miaka ile ya kwanza haikuhesabika kama yake ndiyo maana mpaka wakati huo alikuwa kwenye hicho kiti akiwa anaimalizia miaka yake ya kula mema ya nchi. Siku hiyo alitembelewa na bosi wake ambaye ndiye alimuweka kwenye hicho kiti ili kuweza kulinda maslahi yao kwa ujumla na kuhakikisha kwamba mambo yao yanaenda vyema na kuhusu watanzania hawakuona kama ni biashara ambayo ilikuwa inawahusu.
“Karibu sana kiongozi, imekuwa ni muda mrefu sana tangu uweze kunitembelea hapa”
“Huwa sioni sababu ya msingi kuzunguka kwenye hili eneo kama mambo yangu yanaenda vizuri hivyo ukiniona nakuja hapa basi ujue kwamba kuna sehemu mambo hayapo sawa”
“Nini shida kiongozi?”
“Max bado anaishi”
“Nambie unanitania bosi” raisi aliongea kwa wasiwasi hata lile tabasamu lake lilipotea kabisa kwenye uso wake.

65 inafika mwisho.
🪑
 
Poleni sana kwa ukimya wa kupotea hizi siku mbili. Baadae tunaendelea

See you all.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 66
“Mimi na wewe hatukuwahi kuwa watani kabla hivyo sioni sababu ya mimi kuanza kukutania juu ya jambo kama hili”
“Uliniambia kwamba amekufa na ndiyo maana ulinirudisha nchini, sasa inakuwaje tena uniambie kwamba anaishi?”
“Hata mimi nilijua hivyo ila nadhani kuna kosa moja kubwa sana lilifanyika. Kuna kijana mmoja kati ya wale watatu aliishi na baada ya kuona kwamba yupo mbali na haya mambo tuliamua kumpotezea ila kumuacha hai lilikuwa ni kosa la maisha ambalo natakiwa kulifuta kabla haya mambo hayajafika kwa wananchi”
“Unamaanisha nini kusema kabla hayajafika kwa wananchi?”
“Zile nyaraka za siri ambazo zina taarifa zetu zote zipo kwenye mikono yake kwa sasa”
“Whaaaaaaaaaat?” aliuliza akiwa ananyanyuka na kushika kichwa chake.
“Zimepotea kwenye mikono ya Dax, inatakiwa mpaka kesho ziwe zimepatikana”
“Naona kabisa mwisho wetu unaanza kuwa mbaya sana”
“Raisi mzima wa nchi unaanza kukata tamaa kwa vitu vidogo kama hivi?”
“Unaona vitu vidogo? Vipi kama taarifa hizi zikiwafikia wananchi?”
“Ndiyo maana hatutakiwi kuruhusu ziwafikie kwa namna yoyote ile tunatakiwa kuhakikisha jambo hili linaishia huku huku. Kilicho nileta hapa leo ni kutaka kukutahadharisha kwamba hakikisha familia yako unaiweka mahali salama na ulinzi wa kutosha wakati sisi tunaendelea kumtafuta na kujua kwamba yuko wapi kwani hatujui kwa sasa ataanza na nani na hatujui dhumuni lake kubwa ni lipi na hatujui yupo na nani. Nahitaji muda kidogo kuweza kulishughulikia jambo hili haraka sana na muda huu kamwambie mkurugenzi wa shirika la kijasusi kwamba namhitaji nyumbani leo usiku pamoja na mkuu wa majeshi na wote wafike saa sita kamili”
“Na mimi nitatakiwa kuwepo?”
“Ungekuwa unatakiwa kuwepo basi nisingekuja hapa muda huu”
“Bosi sijawahi kukuona ukiwa na wasiwasi sana namna hii kiasi kwamba ufikie mpaka hatua ya kunionya familia yangu niifiche na kuipa ulinzi mkubwa sana namna hiyo. Naweza kuuliza kwamba ni kitu gani hasa ambacho kwa wakati huu kinakupa sana hofu kubwa namna hiyo?”
“Kwenye maisha yangu yote tangu siku ya kwanza kabisa mimi kujiunga kwenye siasa nikiwa bado kijana mdogo sana, baada ya kuyapata mamlaka sikuwahi kabisa kufikiria kumuogopa yeyote yule wala kuhofia jambo lolote lile lakini imekuwa tofauti sana kwa wakati huu. Sijajua kama hatima yangu itakuwaje ila kila nikifikiria najiona na mimi siku moja nikiwa nabembeleza mtu aweze kuyaacha maisha yangu, yaani mimi nitakuwa naomba kuishi inanisikitisha sana”
“Nimeua watu wengi sana kwenye maisha yangu, nimeua watu ambao walikuwa wakiomba niweze kuyasamehe maisha yao yaani kuishi kwao inakuwa sio mipango ya Mungu tena bali mipango yangu mimi, leo nimeota ndoto mbaya sana nikiwa naona kabisa watu wananiita huko waliko kwa nguvu sana na huenda ndiyo sababu ya mimi kuanza kuogopa sana na kuona kabisa kwamba maisha yangu yanaweza kuwa kwenye wakati mgumu sana. Sio kwamba naogopa kwa sababu sina uwezo wa kuyafanya mambo mazito hapana bali nadhani ni kwa sababu wakati huu napambana na mtu ambaye aliwahi kukionja kifo na baadae akaja kupona tena na kurudi kuwa mtu wa kawaida kama sisi na ndiye huyu amerudi tena”
“Mheshimiwa lakini kumbuka sisi tuna kila kitu kwenye nchi hii kuanzia watu, ulinzi mkali lakini tuna mali nyingi sana na kila mtu anasikiliza kile ambacho mimi nakisema na kila mtu anatii kile ambacho mimi nakiamuru, sasa kwanini uwe na wasiwasi na haya mambo ambayo nina imani wewe ndiye nguzo yangu kubwa?”
“Nimekuja hapa sio kukupa moyo wala kukwambia kwamba mimi namuogopa mtu yeyote yule bali huu ni uhalisia. Unajua neno kifo ni rahisi sana kulitaja ukiwa upo sehemu ambayo haikaribiani na uhalisia wa neno hilo lakini unapokuwa kwenye mazingira ambayo unakuwa karibu na uhalisia wake basi hilo neno linatisha sana na sio rahisi sana kama ambavyo huwa unasikia watu wakilitaja. Kifo ni kitu kibaya sana kwa sababu unayaacha maisha ambayo uliyazoea na kuyapenda kisha unaelekea mahali ambapo hata haujui nini kitafuata baada ya hapo, yaani unakuwa sehemu ambayo huwezi hata kujua kama huu ni usiku au mchana au ni kipi kitafuata kwenye maisha yako baada ya hilo kupita sasa unaanzaje kuwa na amani linapokatiza neno kifo mbele yako? Mimi naenda ila ufanyie kazi ushauri wangu kwa sabbau nafsi yangu inasita sana kuna mambo mabaya sana yanaweza kutokea na natakiwa kulizuia hili mapema sana kabla mambo hayajawa mabaya zaidi.” Mheshimiwa Denis Kijazo aliongea mambo mazito sana mbele ya raisi wa Tanzania.
Justin Mtadei ambaye ndiye alikuwa raisi, hiyo ilikuwa siku ya kwanza yeye kuanza kupata wasiwasi moyoni kwa mara ya kwanza tangu apewe madaraka hayo. Mtu ambaye yeye alikuwa anamtegemea sana kama ngao yake ndiye ambaye alikuwa anaonekana kukata tamaa kabisa wakati huo sasa yeye angeutoa wapi ujasiri wa kuwa na uhakika wa kila kitu? Ni jambo ambalo halikuwa linawezekana kabisa. Akiwa bado amezama kwenye dimbwi hilo la mawazo kuingia kwenye vita mbaya ambayo walikuwa wanaongozwa moja bila, Denis Kijazo aligeuka na kumwangalia sana raisi huyo kisha akamtamkia.
“Sio kila mmiliki shule nyingi basi watoto wake au yeye atafanikiwa sana kimasomo. Maana yangu ni kwamba kuna watu wamekufa kwenye hiyo nafasi na walikuwa na nguvu kuliko hata wewe, unahisi hawakuwa na ulinzi ambao unausema? Hata hao walinzi ni wanadamu kama wewe vipi kama wakikutana na mtu mwenye ushawishi kwao zaidi yako? Habari yako inakuwa inaishia hapo na watu hao huwa wanafanya kazi kama mimi hakutani na watu wote bali wanakutana na mtu ambaye watu hao wanamsiliza na huyo kama akitoa amri wewe utoke hapo Ikulu unaweza ukatolewa ndani ya dakika tano tu na ukatengenezwa mchezo kama ule ambao tulimtengenezea Teo. Hivyo usikae hapo kuuamini ulinzi tu pekee, kitu ambacho kinafanya uweze kuishika sehemu au kuishi sehemu fulani kwa muda mrefu ukiwa salama hakikisha una vitu vikubwa viwili. Kitu cha kwanza uwe na akili sana lakini kitu kingine hakikisha unaujua udhafu wa watu, kupitia udhaifu unaweza ukamuendesha mtu yeyote yule ndiyo maana ukiwa na mihemko basi watu wasijue maana ukikutana na watu wenye akili sana wanaitumia mihemko yako mwenyewe kukutawala na unakuwa hauna cha kukifanya” mheshimiwa aliweza kuongeza maneno mengine ya msisitizo sana kisha akatoka kwenye hiyo ofisi ambayo alikuwa anaingia muda wowote akijisikia kama palikuwa kwake vile.


Mkurugenzi mpya wa shirika la kijasusi la nchi ya Tanzania WTIS alikuwa mtu wa kwanza kabisa kufika ndani ya kikao ambacho waliagizwa na Denis Kijazo kwamba waweze kufika hapo. Mwanamama huyo alikuwa anajulikana kwa jila la Chuki Steward akiwa ni mwanamke ambaye alikuwa na roho mbaya sana na watu ambao walikuwa wakimfahamu walikuwa wakimuogopa isivyokuwa kawaida lakini baada ya mucha mchache kupita pia aliingia mwanaume mwingine ambaye umri wake ulikuwa umekwenda kiasi mwilini akiwa na vazi la kijeshi lililokuwa na nyota za kutosha.
Mwanaume huyo mgeni alikuwa ni CDF Steven Mwilonga mkuu wa majeshi wa nchi ya Tanzania ambaye aliichukua nafasi iliyokuwa imeachwa na Francis Mboye aliyekuwa mwanzilishi wa kundi la DRAGON BOYS.
“Za siku nyingi mheshimiwa CDF” mwanamke huyo alimsalimia mkuu wa majeshi akiwa anampa mkono.
“Imekuwa ni muda mrefu kidogo hatujaonana kabisa Chuki, nadhani ni kwa sababu ya kutingwa na majukumu ya kitaifa”
“Huenda ni kweli ila sina uhakika kama jambo hilo ni la kweli”
“Unamaanisha nini Chuki?”
“Kila mtu naona anapambana kujenga tumbo lake lakini hapa unataka kuniaminisha kwamba watu wapo kulipambania taifa kitu ambacho sio kweli na huenda hakiwezi kuwa kweli kamwe”
“Kwahiyo unataka kusemaje”
“Nawaza sana kwamba ni kwanini raisi mstaafu anahitaji kukutana na mimi na wewe wakati huu, ni jambo la ajabu sana sema nimekuja kwa sababu ya heshima yake tu”
“Ni vyema uungalie mdomo wako sana pindi akifika hapa, nakujua Chuki kwa sababu huwa unapenda sana ujiko na sifa za muda mfupi ambazo hazina umuhimu wowote na nakuhakikishia mambo hayo yatakuja kukuponza siku moja”
“Kufanikiwa kuitoa bikra yangu isiwe sababu ya kuhisi unanijua sana mimi”
“Nasema hivyo kwa sababu bado nakupenda na sitaki kuona ukipotea kwa sababu za kijinga”
“Ulikuwa unanipanda pale ukiwa na hamu tu leo unajifanya kunipenda na kunitakia mema kwenye maisha yangu?”
“Mimi nilikuwa nasema tu”
“Unataka kuniambia kwamba natakiwa kufanya kila ambacho huyu mzee atakiongea?”
“Ni jambo zuri zaidi kwako”
“Kwenye hii nafasi hajaniweka yeye”
“Unahisi ni raisi ndo kakuweka? Nenda kamuulize halafu utaona utaishia wapi” viongozi hao wakubwa walionekana kujuana sana huko nyuma kabla hata ya kuwa kwenye hizo nafasi zao. Waliacha kuendelea kuongea baada ya mzee huyo kuingia hapo ndani kisha akaketi kwa dakika mbili akiwa anawaangalia watu hao kwa umakini sana.
“Mnajua kwanini mpo hapa?”
“Hapana mheshimiwa” Chuki alijibu kijasiri sana
“Kwa sababu nataka niwape kazi ya kuua?”
“Mheshimiwa unamaanisha nini?” Chuki ndiye alionekana kuwa mdadisi sana
“Kipi ambacho huelewi kwenye neno kuua?”
“Haujaniweka wewe kwenye hii nafasi hivyo huezi kunituma popote pale”
“Binti hivi unahisi nipo hapa kukubembeleza?”
“Ila unaongea kama nani?”
“Nadhani utakuwa unajifanya ni mgeni au unajitoa ufahamu. Nisikilize bibie una watoto wawili ambao unawapenda sana lakini hata mumeo anafundisha pale chuo kikuu cha taifa hivyo usitake ndani ya siku kadhaa uanze kuwa na misiba isiyo isha kwako, unatakiwa ukae kimya unisikilize na huwa sipendi kabisa mtu kunikatisha katisha nikiwa naongea na hii ya leo nitakusamehe kwa kuhesabia kama bahati mbaya tu”
“Unanitisha kwa kuitaja familia yangu?”
“Una kichwa kigumu sana sio?”
66 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 67
“Siwezi kukubali kufanya kazi yako mheshimiwa utanisamehe sana kwa hilo. Mimi namsikiliza mtu mmoja tu ambaye ni raisi na kuhusu familia yangu usije ukathubutu hata kutia mkono wako kwa sababu nitakufanya kitu kibaya sana na familia yako nzima” Chuki aliongea kwa mihemko sana huku akianza kupiga hatua kuondoka ndani ya eneo hilo baada ya kushindwa kuelewana na mtu ambaye alikuwa amewaita hapo.
“Bibie piga simu kwako uone kama hiyo familia ambayo inakufanya unipatie mgongo wako na kuondoka bila ruhusa yangu hapa kama ipo salama” Chuki alishtuka sana baada ya kusikia kauli kama hiyo, alipiga simu nyumbani na simu hiyo haikuwa ikipokelewa kabisa, alipiga mpaka kwa walinzi lakini hakuna ambaye alikuwa akipokea hali ambayo ilifanya arudi kwa hasira sana sehemu ambayo alikuwepo Denis Kijazo lakini CDF alimdaka na kumpa ishara ya kutulia kabla hajaleta matatizo makubwa zaidi.
“Kama kuna kitu kitawakuta wanangu, nakuapia nitakuua kwa mkono wangu mwenyewe’’ aliongea kwa hasira sana
“Kwa akili zako labda unajihisi kwamba wewe ndiye mtu wa kwanza kuwepo kwenye hiyo nafasi ambayo upo unasahau kwamba waliwahi kuwepo watu bora zaidi yako lakini leo hawapo. Nina uhakika hauna hata wazo kujua kwamba ni nani amekuweka kwenye hiyo nafasi, sikutaka tufike huku ila unaonekana kuwa mtu mwenye kichwa kigumu sana. Naweza nikaua familia yako yote na hauna kitu unaweza kukifanya hivyo unatakiwa kunisikiliza kwa umakini mkubwa sana? mzee huyo alisimama na kumsogelea mwanamke huyo karibu.
“Kuna bwana mdogo anaitwa Max ila jina lake halisi ni Donald Daniel. Miaka kumi na miwili ambayo imepita alituhumiwa kumuua raisi wa wakati ule Teodensia Mpanzi na kuuawa akiwa anapambana na walinzi ili kuweza kukimbia, sasa huyo mtu bado yupo na anaishi” mwanaume huyo aliongea na kutulia kuuangalia mshtuko mkubwa sana kwenye uso wa Chuki.
“How, na ulitangaza mwenyewe kwamba mtu huyo amekufa’’
“Siasa ina mambo mengi sana na kuna mambo hautakaa ukayajua kamwe hivyo huyu kijana nahitaji apatikane haraka sana kwa sababu kuna mzigo wangu anao ambao unanifanya niishi kwa mawazo sana. Vijana wangu wanaingia kazini kumtafuta lakini nina imani kufanya kazi kwa ukaribu na wewe itakuwa rahisi kuweza kudili na jambo hili hivyo kitu ambacho unatakiwa kukifanya ni kuunda kikosi cha wanaume ambao unawaamini sana uwape kazi ya kwenda kufanya upepelezi wa maisha yote ya mwanaume huyo ambayo ameyaishi kwa hii miaka kumi na miwili na kama kuna mahali utakwama basi utawasiliana na CDF ambaye naye anatakiwa kuandaa kikosi cha makomando ambao anawaamini waweze kumtafuta mtu huyu na anatakiwa kupatikana haraka sana ila watu wake wote wanao mzunguka wanatakiwa kufa kabla yake” mzee huyo alimaliza maongezi yake na kusogea mlangoni.
“Watoto wako ndani ya dakika kumi watakuwa wameachiwa ila nakuonya usije ukarudia tena tabia ya kishenzi kama uliyo ionyesha leo kwa sababu utapoteza kila kitu ndani ya siku moja tu. Hiyo nafasi ambayo leo upo ni mimi ndiye nilipendekeza jina lako kwa sababu nilijua kwamba nitakuwa na kazi na wewe kwa baadae ila pia naweza kukutoa hata muda huu iwe kwa kukuua au kukuacha hai ukijutia au kuipoteza familia yako” lilikuwa ni onyo kali sana kwa mkurugenzi kisha mzee huyo akatokomea zake wakiwa wamebaki wawili ndani humo wanaangaliana tu.
“Hivi hii ni amri au ombi?”
“Mpaka leo bado haujui tofauti ya mtu anaye omba na kutoa amri?”
“Huyu mzee anajiona kama nani labda?”
“Chuki achana na hicho unacho kiwaza kwenye akili yako kwa sababu majivuno yako yatakufanya upoteze familia yako na kilakitu ndani ya masaa ishirini na manne tu kisha baadae ukaanza kujutia bure”
“Hivi ndivyo anavyo iendesha nchi hii?”
“Yeah, raisi pale ni kivuli tu ila yeye ndiye anaiendesha hii nchi na ni miongoni mwa watu makatili sana, shukuru Mungu ameiacha familia yako salama maana alikuwa anaweza kuua wote na bado ukaifanya kazi yake” mwanamke huyu alimeza mate kwa taabu sana hakuwahi kuyashuhudia mambo kama hayo na hiyo kwake ilikuwa mara ya kwanza.
“Hakuwahi kuniita kama hivi kabla wala kuongea na mimi kuhusu mambo kama haya kwanini iwe sasa?”
“Huyo bwana huwa anajitahidi sana kuwajua watu wengi kwa kuwa na imani kwamba ipo siku atawahitaji kwenye maisha yake hivyo kama hakuna ulazima wa yeye kufanya kazi na wewe basi hauwezi ukamuona kwenye maisha yako kamwe ila kama kutakuwa na kazi ambayo inakuhusu wewe moja kwa moja kuwa naye karibu basi usishangae akija kukugongea hata kwenye mlango wa nyumbani kwako. Tangu tukio hilo liweze kutokea hakuna jambo lolote lile baya ambalo limewahi kujitokeza ndiyo maana hukuwahi kuona kama anakuhitaji wewe’
“Kwahiyo haya wewe unayajua kwa muda mrefu tu?”
“Yeah, ulitaka nifanye nini?”
“Ukakubali tu kufanya hizi kazi?”
“Mpaka siku ambayo utaletewa maiti ya mwanao mlangoni kwako ndipo akili itakurudi na utaelewa kwamba hawa watu hawana muda wa kucheka na mtu”
“kwanini tusiungane kuweza kuwatoa? Huoni kama ni hatari sana kwa taifa kuwa na watu kama hawa wakiwa ndo viongozi wakubwa?”
“Nadhani umechoka sana, kalifanyie kazi jambo ambalo amekwambia hapa tena ulifanyie kazi leo leo mpaka kesho asubuhi uwe na majibu yake”
“Hii kesi ya huyu kijana ambaye aliwahi kuwa maarufu sana na ikathibitishwa kwamba amekufa ilikuwaje?”
“Huyo bwana mdogo ndiye ambaye alitakiwa kumlinda Teodensia Mpanzi na wenzake hivyo waliamua kumuua raisi halafu kesi hiyo wakamsingizia huyo bwana mdogo ambaye alikuwa ni mlinzi wake na baada ya hapo wakamuua sasa hata mimi sijaelewa anavyosema kwamba mtu huyo amepona bado sijajua aliponaje”
“Kwahiyo Denis Kijazo ndiye ambaye alimuua raisi?”
“Ndiyo”
“Inamaanisha kwamba kuna kitu hakikuwa sawa na lazima mwanamke yule alitaka kumtoa kabisa kwenye mfumo kama sio kumuua?”
“Yes, hata wewe naona unataka kufanya hilo, sasa kama alimuua raisi wa nchi tena ndani ya Ikulu sasa wewe mkurugenzi unahisi itampa ugumu gani kukupoteza? Unatakiwa kufikiria mara mbili kabla ya kufanya uamuzi wa kijinga ambao yatakufanya uweze kujutia maisha yako yote” CDF alitamka na kuanza kuondoka humo ndani lakini alisimama baada ya kusikia swali kutoka kwa Chuki.
“Ni kitu gani ambacho huyo kijana anacho kiasi kwamba kimemtisha sana kiasi hicho?”
“Mpaka amepaniki kiasi kile basi huenda ni kitu ambacho kinaweza kuyasambaratisha maisha yake” CDF aliondoka bila kugeuka baada ya kulijibu swali hilo na mwanamke huyo akatabasamu na kutoweka kwenye chumba hicho cha mikutano ya siri ambacho kilikuwa nyumbani kwa Denis Kijazo.


PHOENI* ARIZONA MAREKANI
Hiyo ndiyo sehemu ambayo DONNY na James waliishi kwa miaka mingi sana wakiwa wanaipambania afya ya Donald. Ule usiku baada ya matatizo kutokea ndani ya Tanzania, ndiyo siku ambayo James alimwambia Ariana kwamba walitakiwa kuhama kwa muda mpaka pale ambapo mwanaume huyo angekuja kupona kwani kwa hali ambayo alikuwa nayo ilikuwa ni ngumu sana kuishi ndani ya Tanzania kwani wangekuja kukamatwa kirahisi sana hivyo alihitaji wakaishi mbali huko na wangekuja kurudi baadae sana.
Usiku mwanaume alikuwa amefanya maandalizi ya kila kitu na baada ya kumaliza kila kitu, aliishika simu yake na kupiga mahali ambapo alikuwa ana uhakika kwamba wangesaidiwa. Simu hiyo iliita kwa muda mrefu ikakata lakini hakukata tamaa akaipiga tena ambapo ilipokelewa na mtu ambaye alionekana kwamba alitoka kwenye sauti ya usingizi mkali.
“Hello” mwanaume aliongea akiwa anahema kwa nguvu
“Baba Rafael?”
“Yeah mwenyewe”
“Uko wapi saivi”
“Nahitaji msaada wako”
“Umenipigia simu nikajua unarudi nyumbani ajabu unataka msaada tena?”
“Ndiyo na ni wa haraka sana”
“Kuna tatizo gani?”
“Nahitaji kusafiri muda huu na ndege binafsi kwenda Marekani. Tupo watatu ila mmoja ni mgonjwa sana na hayupo kwenye fahamu zake hivyo naomba msaada wako wa haraka sana ili tusipate tatizo lolote hapo uwanja wa ndege” mwanaume huyo mwanamke ambaye alikuwa anaongea nae alikuwa ni mkewe na mama mtoto wake. James mkewe alikuwa ni meneja wa mamlaka ya usafiri wa anga ndani ya uwanja wa JNIA hivyo alijua kupitia mkewe safari yao ingekuwa rahisi sana.
“Hivi unafikiria kabisa kuhusu mtoto?”
“Tutatafuta wakati sahihi wa kuyaongelea haya nipo nje ya muda kadri tunavyozidi kupoteza muda ndivyo kunakuwa na hatari kubwa sana ya sisi kufa wote. Sasa utaamua wewe kama utahitaji mwanangu abakie yatima au tukutane muda huu uwanja wa ndege na kila kitu nikute kimekamilika” mwanaume hakuona kama ulikuwa ni wakati sahihi wa kuanza kubembelezana kwa sababu alikuwa nje ya muda.
Mkewe alikubali kishingo upande kwa sababu huyo ndiye alikuwa mumewe na baba mtoto wake na alimpenda sana na jambo ambalo aliombwa lilikuwa ndani ya uwezo wake. Mwanaume baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa, alimpakia Donny kwenye gari na Ariana akapanda kisha safari ikaanza kuelekea huko kwa kasi kubwa sana maana ilikuwa ni hatari mno kama wangejulikana kwamba bado wapo na ukizingatia taifa lilikuwa kwenye msiba mzito wa raisi Teodensia Mpanzi hivyo polisi walitapakaa sana kila sehemu.
Japo uwepo wa polisi wengi sana barabarani ulishamiri lakini mwanaume gari yake haikuwa ikikaguliwa kutokana na kuweka plate number ya kijeshi ndani ya hiyo gari ya gharama sana. Alifika uwanja wa ndege majira ya saa nane kamili usiku na aliyeenda kuipokea gari hiyo alikuwa ni mkewe mwenyewe hivyo haikukaguliwa na mtu yeyote yule na mwanamke huyo aliwaongoza mpaka ilipokuwa ndege hiyo binafsi kubwa ikiwa na rubani wake tayari kwa safari ya watu hao.
“Huyu mtu ni nani?”
“Siwezi kukwambia kwamba huyu ni nani ila ni mtu mhimu sana ndani ya taifa hili na siku tukifanikiwa kurudi nitakujibu kwamba huyu ni nani”
“Kwahiyo siku hizi hata mkeo humuamini tena”
67 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 68
“Kama ningekuwa sikuamini unahisi ningekutafuta?”
“Umenitafuta kwa sababu unahitaji msaada tu”
“Kweli siku zote nimekuwa baba mbaya sana na huenda nimekuwa mume mbaya sana kwa upande wako ila leo nahitaji uweze kuijua kazi yangu mimi ni ipi maana nimekudanganya kwa miaka mingi sana” mwanamke huyo alimsogelea mwanaume wake huyo ambaye kila siku alikuwa ameishi akiwa anamdanganya kwamba yeye ni mfanya biashara wa madini ila kiuhalisia haikuwahi kuwa kweli hata siku moja na siku hiyo alidai kwamba alikuwa tayari kuweza kumwambia ukweli.
“Mimi ni komando wa Tanzania”
“Unasema?”
“Najua umesikia, mimi ni komando wa taifa na mkuu wa majeshi ambaye alikufa siku kadhaa hapo nyuma ndiye alikuwa bosi wangu na ndiye mtu ambaye alinitengeneza mimi. Kulikuwa na mpango wa kuweza kuwamaliza watu wote ambao wanalifanya taifa hili liingie kwenye matatizo makubwa sana lakini kwa bahati mbaya watu hao wakaweza kutujua mapema hivyo wakaua kila ambaye tulikuwa naye kuanzia mkuu wa majeshi mpaka mheshimiwa raisi Teodensia Mpanzi kisha wakamtangaza kama muasi wa taifa pamoja na mlinzi wake ambaye wamedai kwamba ndiye amemuua raisi huyo. wenzangu wote wamekufa ila namshukuru Mungu mimi nimeishi na kuishi kwangu ndipo yalipo matumaini mapya ya taifa hili” mwanamke huyo alikaa hini kwanza maana hata hizo nguvu za kuendelea kusimama hakuwa nazo.
“Tangu lini umeyaishi haya maisha?”
“Ni miaka mingi sana”
“Kwahiyo kila kitu kilikuwa uongo kwangu na kwa mwanangu?”
“Hapana ila uhalisia wa maisha yangu ndio ulikuwa uongo, sikuwa tayari kuiingiza familia yangu kwenye matatizo hivyo nilikubali kubeba lawama hata ikinilazimu kufa ila sikuwa tayari kuwapoteza nyie hapo maana kama watu wangejua kwamba wewe ni mke wangu basi maisha yako yangekuwa hatarini sana”
“Sisi tulikuwa tunakuhitaji, sisi tunakuhitaji bado, haijalishi ulikuwa unatafutwa na nani unahisi mimi naogopa kufa? Kuna kipi tena unataka kunidanganya leo?”
“Siwezi kukudaganya ila pia sitaki kukuahidi lolote, jitahidi sana asije akajua mtu yeyote kwamba unanifahamu mimi kwa sababu utakuwa umeyaweka hatarini sana maisha ya mwanangu na wewe hapo kitu hiki hakitakiwi kutokea”
“Ila wewe kufa unaona sawa tu?”
“Mama Rafael nisikilize, hatuna muda wa kuanza kubishana hapa saivi, kama kuna mtu yeyote atakuuliza kuhusu mimi basi mshangae na kuonyesha haujawahi kumsikia mtu kama mimi kwani sifahamiki sana kwa kila mtu kwa sababu tulikuwa watu wa siri sana. Shika hii kadi ya benki ndani yake kuna milioni miatano, nina imani itakuwa msaada mkubwa kwenu pindi nitakapokuwa sipo”
“Unamaanisha nini?”
“Hatutawasiliana tena mpaka siku ambayo nitakutafuta tena hivyo unaweza kuyaanza maisha mapya ya bila mimi. Usikae kumsubiri mtu ambaye asilimia zake za kurudi ni kidogo kuliko za kufa. Kama mwanangu akikuuliza kuhusu baba yake basi mwambie anisamehe sana kwa mimi kuwa baba mbaya sana kwake lakini huenda nafanya haya ili kuyalinda maisha ya watu wengi sana wa Tanzania” mwanaume aliongea na kuanza kuondoka, mwanamke huyo alimfuata na kumkumbatia kwa nyuma.
“Mimi nitakusubiri” alitamka mahozi yakiwa yanamshuka kwa huruma sana lakini mwanaume hakuweza kusimama wala kugeuka na huo ukawa ni mwisho wa kuonana kwa usiku huyo.
“Anaonekana kuwa mwanamke mwenye uvumilivu sana” Ariana alimwambia James wakati huo mwanaume alikuwa anaangalia pale hini ambapo mkewe alikuwa amekaa na kumuonea huruma sana.
“Mwanamke kama yeye anastahili kupata mwanaume anaye eleweka na anaweza kutulia na familia. Nimemshauri sana aweze kuanzisha familia yake na mtu mwingine lakini amekuwa mgumu sana kuelewa kitu hiki kinanifanya nijihisi kuwa na hatia kubwa sana kwenye maisha yangu”
“Mwanamke akipenda huwa ni kazi ngumu sana kuweza kuyapindua mawazo yake na ndilo linalo mkuta, jitahidi sana hata siku moja uje uwepo kwenye maisha yake”
“Kazi yangu hainiruuhusu mimi kufanya hivyo, sisi ni watu ambao leo tunaweza kuamka hai na kesho hiyo hiyo unaletewa maiti nyumbani kwamba mtu wako kafia kazini. Hata usipokufa kukuona tu inapita muda mrefu sana hivyo hakuna siku ataweza kuwa na furaha kama ataendelea kuhitaji uwepo wangu”
“Basi unatakiwa siku moja utenge muda kwa ajili yake pia”
“Pengine”


Huo ndio ulikuwa mwanzo wao wa kwenda kuishi ndani ya Marekani, James aliamua kwenda ndani ya taifa hilo kwa sababu alikuwa na rafiki yake mmoja mwenye asili ya Marekani ambaye waliwahi kupata mafunzo kwa pamoja ya kikomando ndani ya taifa hilo miaka hiyo wakiwa wanafuliwa na meja jenerali Mboye. Na mtu huyo ambaye alikuwa ni rafiki yake alikuwa ni kiongozi mkubwa sana ndani ya jeshi la Marekani hivyo kupitia yeye aliomba msaada wa kusaidiwa kwenda kuishi huko lakini pia kupatiwa ulinzi na msaada wa kuweza kuingia kwenye taifa hilo bila tataizo lolote.
Hiyo ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya James ahitaji waende ndani ya taifa hilo na baada ya kufika huko walifanikiwa kupata msaada mkubwa sana na Donny akafanikiwa kupata matibabu ya hali ya juu sana ambapo baada ya mwaka mmoja mwanaume alifanikiwa kurudisha fahamu zake taratibu hali ambayo ilileta matuamini makubwa sana baina yao kwa kuamini kwamba mtu huyo ndani ya muda mfupi angeweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida.
Miaka minne ilipopita mwanaume alifanikiwa kurudi kwenye fahamu zake za kawaida kama mwanzo ila hakuwa na uwezo wa kusimama wala kutembea hali ambayo ilimfanya ajisikie vibaya sana lakini James na Ariana siku zote walikuwa pale kwa ajili yake. Mwanaume alimshukuru sana James kwa kuweza kumuokoa mwnamke huyo na kumfanya kuwa salama lakini alihitaji kujua kila kilikuwa kinaendelea na baada ya kuambiwa na kuonyeshwa kila kitu aliumia sana lakini hakuwa na namna zaidi ya kusubiri wakati mwafaka uweze kufika ndipo aweze kufanya maamuzi ya juu ya nini alitakiwa kukifanya.
Miaka sita ilipoisha mwanaume alifanikiwa kusimama kwa mara nyingine kwenye maisha yake na kuanza kutembea taratibu hali ambayo ilileta furaha kubwa sana miongoni mwao. Alitafutiwa wataalamu wa mapambano ya ngumi ili kuweza kuurudisha uwezo wake kama alivyokuwa mwanzo na wakati wote huo Ariana alikuwa karibu naye sana kwani alikuwa amesha mpenda sana mwanaume huyo hali ambayo ilikuja kuzalisha penzi zito sana baina ya watu hao wawili hali iliyopelekea kuoana kabisa wakiwa huko huko marekani.
Ilipita miaka tisa mwanaume huyo akiwa amakamilika na kurudi kwneye hali ya mwanzo na wakati huo alikuwa na mke na mtoto kabisa huku James akiwa karibu sana muda wote ambao alimhitaji. Maisha ya Marekani yaliwafanya kupata ari mpya na nguvu mpya kiasi kwamba walikuwa kama wamezaliwa upya kwani watu hao wawili walikuwa wanafanya mazoezi ya hatari na makali sana wakiwa huko wakiamini kwamba walikuwa na kazi nzito sana ya kuifanya mbele yao.
Baada ya kuhakikisha kila kitu kimekuwa sawa, sasa walihitaji kuanza taratibu kuunda mipango mikali ya namna ya kuweza kurudi upya ndani ya taifa la Tanzania. Donny alihitaji warudi haraka sana lakini alizuiwa na daktari wake kwani kuna sehemu kwenye mwili wake haikuwa sawa bado hivyo kama angekutana na hatari eneo hilo basi ingempelekea kupooza maisha yake yote lakini kama alihitaji miaka mingine ya kupona basi walimhakikishia kwamba ndani ya miaka miwili na nusu akiwa anafanya mazoezi na kutibiwa angepona kabisa na angekuwa kama yule wa mwanzo hivyo safari ya kwanza ikawa imefeli.
Baada ya miaka kumi na moja na miezi kumi kuweza kupita wanaume hao walikuwa tayari tena kurudi ndani ya taifa la Tanzania. Walikuwa tayari kurudi na kulisafisha taifa sehemu ambayo waliona kwamba haikuwa sawa na ni wakati ambao walitakiwa kuiandaa mipango yao thabiti namna ya kuweza kurudi. Pesa haikuwa tatizo sana kwao kwa sababu kabla ya kufa Teo aliwahi kuwaonyesha Bilali na Donny akaunti namba na namba za siri za akaunti ya benki ambayo waliibeba kutoka kwa gavana wa benki kuu ambaye walimuua kwa kuwa na ushirikiano wa karibu na Denis Kijazo hivyo kwa wakati huo mabilioni yote hayo yalikuwa ya Donny ndiyo maana kwao pesa kilikuwa ni kitu kidogo sana.
Kwa ajili ya usalama wa familia yake Donny alimhitaji mkewe na mwanae wabaki huko huko Marekani mpaka pale ambapo angefanikiwa kuweza kuwafuata yeye mwenyewe au kwenda kuishi huko yeye hivyo walisafiri wao tu wawili ambapo yeye alijitengeneza kama mzee wa makamo sana ambaye umri wake ulikuwa umekwenda na James ndiye alikuwa mlinzi wake naye akiwa na mwonekano wa tofauti sana. Donny alikuwa amerudi ndani ya taifa kama mwekezaji ambaye alikuwa anaenda kufungua fursa nyingi sana za vijana hivyo kupitia kuwa na nyaraka feki alifanikiwa tena kurudi ndani ya Tanzania sehemu ambayo walikuwa wamezaliwa huku wakiwa na kazi kubwa na nzito sana mbele yao.
Tangu wafike walitumia miezi miwili kuweza kutafiti kila hatua ambayo ilikuwa imepigwa na watu ambao walikuwa wanatakiwa kuwapoteza, walimtafuta kila mmoja ili kuweza kumjua kiundani zaidi na hatua zote ambazo walitakiwa kuzifuata lakini watu hao pia waliitembelea familia ya Mboye huku wakijinadi kwamba wao ni wafanya biashara wakubwa sana ambao walikuwa wanahitaji kuwekeza kwenye familia hiyo hali ambayo iliwafanya kuipatia familia hiyo pesa nyingi sana kama msaada lakini familia hiyo haikuwahi kujua kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na nini.
Ilikuwa imetimia miaka kumi na miwili kamili tangu yatokee yale matatizo ya zamani sana na sasa walikuwa na taarifa za kutosha mezani, ulikuwa ni muda wa kuanza kuifanya kazi ambayo waliijia Tanzania kwa wakati huo. James alipewa kazi ya kutafuta vijana wa kuaminika kutoka jeshini kumi, hao wangekuja kuwa msaada mkubwa sana kwa hapo baadae na kwa sababu alikuwa anawajua vijana wengi sana alifanikiwa kuwatafuta huku kila mtu akiwa anashangaa kumuona komando huyo ambaye alikuwa ni adimu sana kuweza kupatikana kwenye maisha yake.
Baada ya zoezi hilo kukamilika mtu ambaye aliwekwa mezani alikuwa ni Karistus, ambaye alikuwa ni mtu wake wa karibu sana miaka ya nyuma huko wakiwa wanapata mafunzo ya kijasusi kwenye mataifa mbali mbali ila kwa sababu ya tamaa za maslahi walijikuta wanakuwa maadui wakubwa sana kila mtu akienda upande wake na mmoja alikuwa anajua mwenzake alikufa miaka mingi sana ambayo ilikwaisha kupita hivyo hakuwa na muda kabisa naye lakini mwenzake huo ulikuwa ni wakati ambao yeye alikuwa amerudi upya na alikuwa anamfuatilia kwa umakini sana mwenzake.
Alikuwa amefanikiwa kujua ratiba nzima ya Karistus na namna mwanaume huyo alivyokuwa mpenda starehe kwani alikuwa na pesa nyingi sana wakati huo hivyo alikuwa anaishi kwa namna ambayo angetaka yeye na mara nyingi sana alikuwa anatumika kuweza kufanya mauaji pale ambapo angehitajika.
68 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 69
Kwenye kumfuatilia kwa undani sana Karistus waligundua kwamba alikuwa amepewa kazi maalumu na Denis Kijazo ya kwenda sehemu kuzibeba nyaraka zake na kisha alitakiwa kuhakikisha anazifikisha zikiwa salama kabisa kwa bosi wake huyo. Mwanaume huyo hakujua nyaraka hizo ni za nini maana alisisitizwa sana kwamba haruhusiwi kabisa kuziona bali anatakiwa kuzifikisha kama zilivyo na kuna sehemu ambayo alitakiwa kwenda kuzifuata.
Nyaraka hizo za siri zilikuwa zimehifadhiwa Maktaba ya taifa na ndiyo sehemu ambayo Karistus alikuwa anatakiwa kuzifuata siku hiyo na kuzirejesha kwenye mikono ya Denis Kijazo. Sasa zilifikaje maktaba ya taifa? Miaka kadhaa iliyokuwa imepita wakati Philipo Tibaigana akiwa mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Tanzania aliwatuma majasusi watano kwenda kukusanya taarifa za siri sana kwenye mataifa ambayo aliona kwamba yalikuwa yanakinzana na Tanzania.
Majasusi hao walifanikisha kazi yao vizuri sana lakini kati ya hao wote ambao walirudi wanne Philipo Tibaigana aliwaua kwa mkono wake mwenyewe kwani wengi walirudi wakiwa na jibu moja kwamba msababishaji wa hayo yote alikuwa ni Denis Kijazo na kila aliyerudi na taarifa hizo za siri zilikuwa zinamlenga kiongozi huyo ambaye kwa kipindi hiko yeye ndo alikuwa raisi, kitu hiko kilikuwa kinaleta tafsiri mbaya sana kama taarifa hizo zingeweza kuvuja na ndipo akaamua kufanya huo uamuzi wa kuwaua ili kumlinda mheshimiwa raisi.
Ila kwa bahati mbaya sana miongoni kwa hao majasusi watano mmoja alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha sana tena akidaiwa kuwa na taarifa za siri sana za kiongozi huyo mkubwa. Mwanaume huyo alitafutwa sana kila mahali kwa siri kubwa sana lakini hakuwahi kabisa kuonekana kwamba alipoteleaga wapi na baada ya miaka kadhaa kuweza kupita alizituma kopi kwa Denis Kijazo ili aone nyaraka ambazo zilikuwa na siri za maisha yake yote ambayo aliwahi kuyaishi huko nyuma na mpaka wakati huo mambo yote ambayo alikuwa ameyafanya mpaka mali zake zote ambazo alikuwa nazo.
Baada ya kuziona aliogopa sana maana kama ushahidi huo ungeweza kufika kwenye mikono ya raia ingekuwa ni hatari kubwa sana kwenye nafasi ambayo ilikuwepo kitu hiki kilimfanya kukodi watu wa siri sana kuweza kumfanyia msako kijana huyo ambaye alikuwa anajifanya kuwa mjuaji kwa kuzibeba kizembe taarifa za watu wakubwa kama hao. Asad ndilo lilikuwa jina lake jasusi huyo ambaye kwa kipindi hiki alikuwa akiishi Kisarawe wakati wote ambao walikuwa wakimtafuta kwa siri sana kila pande ya jiji la Dar es salaam na mikoa ya jirani.
Asad maisha yake yalikuwa ya mashaka makubwa sana kwa sababu alikuwa amebeba bomu ambalo lingemlipukia muda wowote ule na ingekuwa hatari kubwa sana kwake hivyo aliangalia namna nzuri ya kuweza kuuhifadhi ushahidi huo na ndipo hesabu zake zilipogota maktaba ya taifa kwani eneo hilo ni salama sana na halifanyiwi ukaguzi mkubwa na mtu yeyote yule kwa kuwa ni miongoni mwa sehemu zinazo heshimika sana. Kwenye makataba hiyo kulikuwa na mzee mmoja ambaye alikuwa kiongozi wa hapo na kiongozi huyo aliwahi kuwa rafiki mkubwa sana wa baba yake hivyo alikuwa akimjua vyema na kumheshimu sana na ndiyo sababu aliona kwamba pale palikuwa mahali sahihi zaidi kwa kwenda kufanya hivyo.
Alifanya maamuzi ya kwenda kumweleza ukweli mzee huyo juu ya udhalimu wa raisi wao na kuomba nyaraka hizo zihifadhiwe ndani ya makataba kwakuwa alihisi ndiyo sehemu sahihi zaidi mpaka pale ambapo wangekuja kupata watu sahihi wa kufanya nao kazi ya kuweza kumdondosha raisi huyo basi wangezitumia kama silaha kwa ajili ya kazi hiyo. Mzee huyo alimshauri sana kijana huyo kupotezea hayo mawazo kwani alikuwa anafanya jambo la hatari sana lakini hata hivyo Asad alidai kwamba alidhamiria kufanya hivyo kutoka moyoni kwani hata kama asingefanya hivyo bado watu hao walikuwa wanamuua vile vile angalau kama angefanya hivyo kuna siku taifa lingekuja kumkumbuka kama shujaa ambaye aliyatoa maisha yake sadaka ili kulikomboa taifa.
Asad baada ya kuzihifadhi nyaraka hizo haikupita hata wiki moja alikutwa akiwa amekufa baada ya kujulikana anapoishi na wanaume kumi walitumwa kwenda kumfuata huko Kisarawe na baada ya kumpata haikuwa rahisi kuondoka naye kwani alifanikiwa kuwaua wanaume watatu huku yeye mwenyewe akimeza kidonge na kufa hapo hapo. Aliona ni bora kufanya hivyo kuliko kuingia kwenye mikono ya hao watu maana alijua kabisa kile angekipata hakutaka kuruhusu huo ujinga na ndiyo sababu akaamua kuyatoa maisha yake sadaka.

Mzee Bariadi ambaye ndiye alikuwa amepewa nyaraka hizo alisikitishwa pakubwa sana na Asad kufa hivyo kwa heshima ya kijana huyo akaamua kuzihifadhi sehemu salama sana nyaraka hizo ambapo zilitafutwa sana na hazikuwahi kupatikana mpaka pale Denis Kijazo alipo amua kuzipotezea baada ya mhusika mwenyewe kuwa amekufa tayari hivyo hakukuwa na mtu mwingine ambaye angekuja kujua kuhusu siri hiyo lakini haikuwa kweli.
Mzee Bariadi alikaa na siri hiyo ya kuwa na nyaraka za mheshimiwa kwa miaka mingi sana mpaka Denis Kijazo anatoka madarakani bado mzee huyo aliendelea kuzitunza tu mpaka siku moja ambapo alianza kuumwa ikiwa imepita miaka mingi sana. Hali yake haikuwa nzuri sana na alijua huenda ipo siku angekuja kufa wakati hajazifanyia kazi yoyote ile nyaraka hizo na ndipo alitamani sana kuzikabidhi kwa mtu ambaye angemwamini sana.
Akiwa ndani ya maktaba hiyo ambayo aliisimamia kwa miaka mingi sana kuna kijana ambaye alikuwa anamuamini sana kutokana na kufanya naye kazi kwa uaminifu na kwa muda mrefu huku kijana huyo akiwa ndiye msaidizi wake. Hali yake ilipo tengamaa kidogo na kurudi tena ofisini alimkalisha kijana huyo na kumpatia siri ambayo alikaa nayo kwenye moyo wake kwa muda mrefu sana, alimsisitiza kijana huyo kuzitunza sana nyaraka hizo pindi yeye atakapokufa mpaka siku ambayo atapatikana mtu sahihi wa kuzimiliki hizo nyaraka kwa ajili ya kazi maalumu kwa hao mafisadi.
Alisahau kitu kimoja mhimu sana kwamba Imani ndiyo inakufanya unakufa haraka sana. Baada ya kijana huyo kupewa taarifa hizo mhimu sana aliaga anaenda nyumbani kupumzika lakini baada ya kufanikiwa kufika nyumbani alipiga simu mahali na kuelezea yote ambayo alikuwa ameambiwa na kuwataka watu wa upande wa pili kwenda kuzibeba siku hiyo hiyo maana hakuwa anamwamini sana yule mzee angeweza hata kubadilisha maamuzi na kumkabidhi mtu mwingine. Na hiyo ndiyo siku ambayo baada ya Denis Kijazo kuzipata taarifa hizo alimuagiza Karistus kwenda kumuua mzee huyo na kisha kuondoka na nyaraka hizo kuzipeleka kwake.
Huo mpango mzima Donny na James walikuwa nao mezani hivyo walijua kwamba siku hiyo ni kitu gani kingefanyika na wao walipaswa kufanya nini. James alibakia kwenye komputa ili kuhakikisha kamera za jiji haziipati sura ya Donny na mwanaume huyo akaenda kukutana kwa mara ya kwanza tangu apotee na hasimu wake wa miaka hiyo Karistus Dikson (KD).
Hivyo wakati Karistus anaenda makataba ya taifa kubeba nyaraka hizo Donny alikuwa karibu sana na mitaa hiyo akimfuatilia kwa ukaribu sana. Mwanaume huyo alifika hapo na kuua watu wote ambao aliwakuta humo ndani na kwa sababu taarifa zote alikuwa nazo alifanikiwa kubeba begi la nyaraka hizo na kuwez akutoweka nalo akiwa ameua kila mtu lakini haikupita muda sana kuna wanaume walifika eneo hilo na kuanza kusafisha kiasi kwamba mtu kama angefika kesho yake asingeweza kabisa kujua na kuamini kwamba eneo hilo lilikuwa limevamiwa wala mauaji kutokea.
Baada ya Karistus kufika katikati ya jiji ndio wakati ambao Donny aliweza kumtokea na kumpa kipigo kizito sana kisha akatoweka na begi hilo ambapo wakati Karistus anaondoka alikuwa juu ya paa la jengo moja refu akiwa anamwangalia mwanaume huyo akihangaika maana James alikata umeme ghafla sana na wakati umeme unarudi Karistus alijikuta mwenyewe akinyeshewa na mvua pamoja na ujumbe ambao alikuwa ameuona wenye maandishi ya damu yaliyo mtisha na kumfanya akimbie sana kutoka eneo hilo ambalo alikuwepo.

Dax usiku alikuwa kula starehe akiwa anajiandaa na kazi nzito sana ambayo ilikuwa mbele yake ya kuweza kulikabili upya zimwi ambalo lilikuwa limerudi mjini kwa mara nyingine hali ambayo ilimfanya ajihisi kukosa amani sana na kutuliza akili yake, alitakiwa kuigeuza starehe kuwa upande wake yeye. Alikuwa na wakati mgumu sana kwa sababu bosi wake alikuwa amempa muda mchache sana wa kuhakikisha anazirudisha nyaraka ambazo alizipoteza kizembe sana lakini haikuwa kizembe sana kama ambavyo watu hao walikuwa wanafikiria kwenye akili zao. Alikuwa ametoka kufanya kufuru ya pesa na wanawake majira hayo ya usiku mpaka pale alipofanikiwa kurudi nyumbani kwake Magomeni alipokuwa anaishi.
Akiwa na walinzi wake wakati anafika getini alishuka kwenye gari yake ya kifahari akiwa hana hata wasiwasi lakini alihisi kama kuna kitu amekiona kwa macho yake lakini macho yake ni kama hayakuwa na uhakika kwa sababu kilikuwa kama kivuli tu kimepita. Ni kivuli cha mtu alikiona kikikatiza kwenye ukingo wa geti lake hilo kitu ambacho kilimfanya asimame kuangalia eneo lile kwa muda
"Bosi kuna tatizo?"Vijana wake waliuliza wakiwa wanamsogelea kiongozi wao kwani hakuonekana kuwa sawa kabisa
"Hili eneo nahisi tumevamiwa"
"Bosi nadhani utakuwa umechoka sana nadhani ungewahi ndani ukapumzike" aligeuka na kumwangalia kijana wake huyo kisha akampiga piga mgongoni na kuingia ndani lakini mwili uligoma kabisa kukubaliana na hali hiyo kwani mwili ulikuwa ukimsisimka sana. Alisimama na kuangalia pande zote lakini palikuwa kimya sana hali ambayo ilimfanya kusogea taratibu kwenye mlango wa ndani akiwa anajivuta mithili ya mtu ambaye alilazimishwa kufanya jambo hilo.
Akiwa anasogea mbele taratibu alihisi kitu hivyo aligeuka nyuma, alishangaa baada ya kuona mlinzi mmoja ambaye alibaki nje hakuwa ameingia bado na huyo ndiye alitakiwa kuingia na gari ndani hali hiyo ilimshtua hivyo akatoka haraka sana kwenda nje ili kuweza kushuhudia kile ambacho kilikuwa kinaendelea hapo. Walicho kiona kilikuwa kinatisha sana, kijana huyo alikuwa amevunjwa uti wa mgongo na kitu chenye ncha kali sana hali ambayo ilileta mshtuko kwa walinzi wake watatu ambao walikuwa wamemzunguka bosi wao kuhakikisha kwamba yupo salama.
"Max" alitamka baada ya kugundua kwamba mlinzi wake huyo alikuwa amekatwa na shoka eneo hilo. alinyanyuka akiwa na wasiwasi sana hata pombe ilikata kabisa, aliangaza huku na huko lakini hakuona mtu yeyote hivyo akachomoa bastola na kiunoni kwake akiwa anahema kwa nguvu sana maana alikuwa anamjua mwanaume huyo ambaye alivamia hapo tangu wanapata mafunzo hakuwahi kumshinda kwa jambo lolote lile na hata mara ya mwisho wanakutana alikuwa na uwezo wa kumuua lakini alimuacha hai huku yeye mwenyewe akiwa hajui kwamba ni kwanini aliweza kuachwa akiwa hai bado.
Aliikoki bastola yake na kurudi ndani haraka sana na walinzi wake watatu akiwa anataka kuwahi ndani lakini alihisi mchakacho nyuma hali ambayo ilimfanya kugeuka haraka sana akiwa ameshika bastola kwenye mkono wake, alishtuka sana kumuona mtu karibu na geti akiwa amesimama. Mavazi yake moja kwa moja yalimpa taarifa kwamba huyo alikuwa ni yule yule ambaye alikutana naye usiku na bila shaka alikuwa ni Max mwenyewe.
"Nilishangaa sana kwanini ulipata nafasi ya kuniua na ukaniacha, niliwaza sana lakini nilikosa jibu kabisa mpaka nikaahidi kwamba siku ambayo nitakuona tena nitakuuliza ili unipe jibu sahihi kwamba ni kipi kinaendelea"
"Ile siku ulivyopata nafasi ya kuweza kuishi haukutakiwa kabisa kurudi tena kwenye dunia yangu maana ilikuwa ni nafasi yako ya kwanza na ya mwisho kuipata kwenye maisha yako ila jeuri yako naona inakuponza na kujifanya una nafasi nyingi sana za kuishi. leo nimekuja kuimaliza hadithi yangu mimi na wewe ambayo nimeisubiri kwa miaka kumi na miwili nikiwa naishi mbali ambapo niliondoka nikiwa kijana mdogo na leo nimerudi nikiwa mwanaume mtu mzima"
"Max wewe ndiye ambaye ulitakiwa kuitumia ile nafasi ambayo uliipata nadhani hautakuja kuipata tena kwa sababu leo nakuua" mwanaume aliongea kwa hasira sana huku akitaka kufyatua risasi lakini ghafla sana umeme ulikatika kwenye nyumba yake hiyo. Alishtuka sana asijue kwamba mtu huyo alikuwa amefanya nini hata hivyo bado aliachia risasi hivyo hivyo sehemu ambapo alikuwa na uhakika kwamba Max alikuwepo.

69 inafika tamati.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 70
Hakujali hata uwepo wa walinzi wake hilo eneo aliendelea kumimina risasi kwa hasira sana na alipokuja kushtuka alikuwa ameua walinzi wake wawili tayari huku mlinzi wake mmoja akiwa anazunguka zunguka na bastola mkononi asijue ashambulie wapi au amshambulie nani. Umeme ulirudi ghafla sana, Max alikuwa amesimama nyuma ya yule mlinzi ambaye alikuwa amebakia, alimgusa begani mwanaume huyo akageuka kwa pupa sana alikutanishwa na kisu cha shingo ambapo shingo hiyo ilichanwa chanwa vibaya sana. Alishuka chini akiwa amekufa muda mrefu tu sasa wakawa wamebaki wawili tu wakiwa wanaangaliana.
Dax alijaribu kupiga risasi lakini aligundua kwamba zilikuwa zimeisha na alikuwa amebakiwa na kisu tu pekee. Kazi ya kuweza kukata umeme ilikuwa inafanywa na James ambaye alikuwa kwenye gari ambayo haikuwa mbali sana na eneo hilo akiwa anaangalia kila kinacho endelea kwenye kamera na alikuwa hapo kutoa msaada pale ambapo angehitajika. Dax hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuyapambania maisha yake mwenyewe maana msaada wake walikuwa ni walinzi ambao walikuwa hawapo tena hivyo alikuwa ni yeye wa kuyatetea maisha yake kwa mara ya pili tena akiwa anakutana na mtu huyo ambaye alipotea miaka kumi na miwili.
Alijigusa kwenye kiuno akiwa anahesabu hatua zake kwa kasi ya ajabu, alichomoa bisu kubwa sana ambalo alikuwa amelilenga kwenye shingo ya Max. alimfikia lakini kisu hicho kilipita pembeni kidogo baada ya Max kukikwepa hata hivyo Dax alijigeuza kwa mateke matano mfululizo ambapo matatu yalizama kwenye kifua cha Max na baada ya kumpata alisogea nyuma kidogo ambapo alikuwa anajibamiza ukutani lakini alichomEka shoka ukutani likampa balansi ya kuweza kusimama vyema kisha akajiweka sawa wakati huo Dax alikuwa amekirusha kisu hicho kwa nguvu sana kuja kwa mwanaume huyo akiwa bado yupo ukutani.
Kisu kilienda kuchimba kwenye ukuta baada ya Max kuinama lakini hata wakati yeye mwenyewe anainama aliliachia shoka lake ambalo Dax alishtuka linaikaribia shingo yake hivyo aliruka sarakasi kwenda pembeni, alihEma kwa nguvu sana kwani lilikuwa linaondoka na shingo yake moja kwa moja. Wakati anasimama hapo alipokuwa amedondokea alishangaa buti linakuja kwenye uso wake hivyo alijivuta nyuma na kujigeuza kwa sarakasi kwa mkono mmoja na kusimama.
Buti lile ambalo lilimkosa, lilichimba chimba chini vibaya sana kiasi kwamba zege ilipasuka kiasi fulani, alimeza sana mate kwani kama lingetua kwenye mwili wake basi hali ingekuwa mbaya sana. Wanaume walikutana kwa mikono yao sasa ambapo ngumi zilikuwa zinarushwa kwa nguvu na kwa spidi ya ajabu sana ambapo kasi yao haikuwa ya kawaida. Dax alikuwa anajilinda zaidi maana mwenzake alikuwa anarusha ngumi kwa kasi na nguvu ya ajabu sana, ngumi zake mbili aliziachia kwa pamoja kama anapiga pushup, Max aliziacha ngumi hizo zipenye kwake lakini yeye mwenyewe wakati huo huo aliziachia zake na wote ngumi zilitua kwenye vifua vyao.
Max ngumi zake ziliwahi kufika kwenye kifua cha Dax hali ambayo ilifanya zake zifike zikiwa zina kasi ndogo sana maana alipunguzwa kasi kwa kiasi kikubwa sana na ngumi mithili ya chuma ambazo zilikuwa zimekita kwenye kifua chake. Dax alirudi nyuma akiwa anakohoa damu, kifua kilikuwa kinawaka moto sana lakini alikuwa kwenye vita hakukuwa na mtu wa kumbembeleza alijikaza na kuikaza mifupa yake lakini kwa maumivu makali mno maana mwili ulikuwa unawaka moto sana.
Alimkimbilia Max na kuhitaji kumzoa lakini mwanaume huyo aliinama kwa kasi sana na kuachia kisigino chake ambacho kilienda kukita kwenye paji la uso la Dax hali iliyo mfanya kuyumba yumba sana na kurudi nyuma. Wakati anayumba yumba Max alimjia kwa kasi na kumgonga na viganja kwa nguvu sana kwenye masikio yake na kumfanya kusikia sauti za milio mikali sana kama mtu anapiga mluzi kisha alivutwa kwa kasi na kupigwa na ngumi sita za haraka tumboni na kifuani.
Zilimpeleka mbali sana lakini haikuwa sababu ya yeye kuachwa Max alijibetua na kutua kwenye mguu wa Dax ambao ulivunjwa hapo hapo akawa anashuka chini akiwa anaguna kwa maumivu ila kushuka kwake alikutanishwa na buti la uso ambalo lilimbamiza vibaya sana ukutani na kumfanya akae kinyonge akiwa ameegamia ukuta anatokwa damu sehemu nyingi sana za mwili wake. Max alisogea lilipokuwa shoka lake akaliokota na kuichomoa bastola yake kisha akaenda kukaa mbele ya Dax wakawa wanaangaliana.
"Kuna watu wataanza kuniogopa sana kama wakijua historia nzima ya maisha yangu, kuna muda unafika hata mimi najiogopa sana ndugu yangu. Sio rahisi mtu unazikwa halafu baada ya miaka kadhaa unarudi ukiwa hai tena, inahitaji moyo wa kipekee sana mtu kuamini na kukubali tena kuwa karibu na mtu kama mimi. Kwenye maisha yangu sikuwahi kukata tamaa kabla lakini siku ile ukiwa unanifukia kwenye lile shimo la futi sita nilijikuta naanza kuogopa sana, niliiona hofu halisi ya mwanadamu na mimi nikajua kabisa kwamba sikuwahi kuwa roboti bali ni mwanadamu wa kawaida tu ambaye naye anakufa pia"
"Kabla ya siku ile kuna namna sikuwahi kuwaza kuhusu kifo hali ambayo ilinifanya nikawa nampotezea sana Mungu ila siku ile niliamini kwamba wanadamu huwa tunakuwa na jeuri pale ambapo tuna kila kitu kwenye maisha na furaha ipo upande wetu ila hayo mambo yanapokuwa nje ya uwezo wako na hauna ulicho bakia nacho kwenye maisha yako basi niamini mimi utaamini kwamba Mungu yupo na huenda utalia sana na kujuta ukiwa unaomba Mungu akusamehe sana huku ukiwa hujui kwamba ukifa utaenda wapi kwake au kwa wale ambao inadaiwa wapo motoni. Hii ni hofu ambayo naiona kwako saivi pia ukiwa unahema kwa kukosa matumaini hapo, basi hiyo hofu mimi siku ile niliipata kutoka kwa mtu ambaye mara ya kwanza niliwahi kuamini kwamba ni mtu wangu wa karibu sana ila nilikuwa najidanganya sana mwanzo."
"Ujue Karistus, kwenye maisha yangu mimi sikuwahi kuwa na furaha kabisa, mimi sikuwahi kuwa mmoja wa wale watu ambao waliishi kwa tabasamu hata siku moja ila nikushukuru wewe kwa kuwa sababu ya mimi kupata tabasamu upya tena kwenye maisha yangu. Kunifanyia lile jambo siku ile kulinifanya nikawa karibu na mwanamke ambaye amekuwa kila kitu kwangu kwa sasa, mwanamke ambaye amenipatia familia bora sana na kwa upande wangu naweza kusema kwamba hilo ndilo jambo ambalo linanipa furaha sana kila ninapo waona wale wawili wakiwa wanacheka" mwanaume alisikitika sana akiwa anampa mwenzake huyo hisia zake ambazo alikuwa nazo kwenye moyo wake.
"Uliponaje siku ile Donald?"
"Hilo ni swali ambalo hata mimi baada ya kuamka nilikuwa nahitaji sana majibu yake, swali ambalo lilikuwa ni gumu sana kulijibu kwa sababu kwa mara ya mwisho nilijiona kabisa kwamba mimi nakufa lakini nimekuja kushtuka nipo kitandani tena watu wakifurahia mimi kuamka tena. Nadhani kuna mkosa makubwa sana ambayo yalifanyika siku ile wakati DRAGON BOYS wanauawa kwa sababu mmoja wao aliishi na kufanikiwa kutoroka na wewe hapo na wenzako mlifanya kosa la kipumbavu sana kushindwa kunikagua kwenye mwili wangu ambapo mngeikuta simu ambayo nilikuwa naitumia kuweza kuwasiliana na wale watu"
"Uzembe wako ndio umefanya mpaka leo nipo hapa kwa sababu kupitia simu ile alifanikiwa kunipata na wakati ule ambao wewe ulkuwa unaenda kunizika nikiwa hai mwanaume yule alikuwa anaufuatilia msafara wako na kila ambacho ulikuwa unakifanya alikuwa anakiona ndiyo maana ikawa rahisi sana kuweza kunifikua pale baada ya nyie kuondoka japo hakuwa na matumaini kama anaweza kunikuta nikiwa bado hai lakini Mungu ametenda miujiza yake baada ya miaka mingi sana ya kulala kitandani leo nipo tena hapa na tumeweza kukutana kwa mara nyingine Karistus" mwanaume alikuwa anampa mipango ambayo ilifanyika mpaka yeye kuweza kupona na wakati wanaongea wakati huo walikuwa wanayatumia majina ya halisi kabisa.
"Hahaha hahaha kwahiyo na mimi nilifanya kosa la kipumbavu kama ulivyofanya wewe"
"Hapana, kosa lako lilikuwa dogo sana ukifananisha na langu, ujinga wangu wa kumwamini yule malaya umeliingiza taifa hili kwenye tatizo kubwa sana. Nina imani kama sio kumwamini Brandina mpaka leo hii basi huenda haya yote yangeisha wakati ule ule lakini ujinga wangu uliyaondoa maisha ya raisi, uliyaondoka maisha ya Bilali na kijana wake lakini watu wengi walibaki wanateseka kwa sababu ya kosa langu moja tu ndiyo maana nimerudi kuhakikisha kwamba kosa langu ambalo nililifanya haliji kujirudia tena"
"Huenda upo sahihi Donald lakini kumbuka kwa sasa unaweza usifanye kosa ila tayari una udhaifu, kuwa karibu na familia ni kosa kubwa sana unapo ingia kwenye vita na watu kama hawa hivyo bado huenda mchezo huu utakuwa mgumu sana kwa upande wako. Yule mtu ana pesa sana, ana watu wa hatari sana bado unahisi kwamba unaweza kushinda vita hii ambayo ipo mbele yako?"
"Unawaza kuhusu pesa? nina pesa nyingi sana ambazo hata nikisema nichukue watu miamoja nianze kuwaleta wasifanye kazi kwa miaka mingine miamoja ijayo hawatazimaliza, sidhani kama suala la mhimu ni pesa kwa sasa ila suala la mhimu ni uhai"
"Umezipata wapi hizo pesa?"
"Nadhani unakumbuka kwamba niliwahi kuwa na gavana kwenye mkono wangu, sidhani kama kuna haja ya kuendelea kuuliza kwamba nilizipataje pesa"
"Max una uhakika na hili unalo lifanya kwamba utashinda?"
"Unatakiwa kuyahofia kwanza maisha yako kabla ya kuanza kuwawazia watu wengine Karistus. Nina maswali machache sana ambayo nataka unijibu hapa saivi maana hatutakuwa na namna tena ya kuweza kuja kuongea tena baada ya leo. Ni kipi kilikufanya ukaisaliti nchi yako?"
"Pesa"
"Pesa tu?"
"Yeah, maisha haya ni mafupi sana kuna muda unajito sana kupigania maslahi ya wengi lakini hakuna anaye ona wala hakuna anayejali kabisa sasa kuna maana gani kuweza kuendelea kuwapigania watu ambao hawawezi hata kuona thamani ya unacho kifanya? siku zote nilikuwa nataka kuwepo sehemu ambayo nitakuwa naheshimiwa, sehemu ambayo nitakuwa napewa kile ambacho nastahili na hicho ndicho nilikifanya kwa sasa. Hii miaka kumi na miwili nimeishi maisha mazuri sana, maisha ya kifahari sana kwa kadri nilivyokuwa nataka mwenyewe na hakukuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaweza kuja mbele yangu na kuwa kama tishio kwangu na hiki ndicho ambacho mimi nilikuwa nakihitaji kwa miaka ambayo nilikuwa naishi duniani"
"Lakini bado ulikuwa mtumwa"
"Hiyo sio biashara yangu kwa sababu hainihusu kikubwa nimeishi vile nilivyotaka mimi"
"Sawa, kuna neno lolote lile la mwisho kwa familia yako?"
"Whaaat?"
"Sio muda umetoka kutishia kuhusu kuwa na udhaifu wangu ambao ni familia yangu lakini wewe upande wako mbona unashtuka sana? Najua kwamba baada ya lile kutokea ulikuwa umempa mimba yule mwanamke ambaye alikuwa katibu wa raisi na baadae ukawa unaishi naye lakini ukaamua kukaa naye mbali baada ya yeye kupata mtoto ukihofia kwamba watu wakijua wanaweza kuja kumvamia na kumuua mwanao"
"Max usije ukathu......"
"Naona unaogopa sana, mtoto siwezi kumuua kwa sababu hahusiki kwa lolote na hajui kama baba yake ni mtu wa hovyo sana namna hii hivyo ataishi lakini vipi kuhusu mama yake karistus? mtu ambaye alihusika kumteketeza raisi wa nchi unataka naye aendelee kuishi au kuwa hai? huoni kama nitakuwa nawakosea heshima Watanzania na wapiganaji wenzangu ambao wametangulia kaburini?"

70 inafika mwisho.
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 70
Hakujali hata uwepo wa walinzi wake hilo eneo aliendelea kumimina risasi kwa hasira sana na alipokuja kushtuka alikuwa ameua walinzi wake wawili tayari huku mlinzi wake mmoja akiwa anazunguka zunguka na bastola mkononi asijue ashambulie wapi au amshambulie nani. Umeme ulirudi ghafla sana, Max alikuwa amesimama nyuma ya yule mlinzi ambaye alikuwa amebakia, alimgusa begani mwanaume huyo akageuka kwa pupa sana alikutanishwa na kisu cha shingo ambapo shingo hiyo ilichanwa chanwa vibaya sana. Alishuka chini akiwa amekufa muda mrefu tu sasa wakawa wamebaki wawili tu wakiwa wanaangaliana.
Dax alijaribu kupiga risasi lakini aligundua kwamba zilikuwa zimeisha na alikuwa amebakiwa na kisu tu pekee. Kazi ya kuweza kukata umeme ilikuwa inafanywa na James ambaye alikuwa kwenye gari ambayo haikuwa mbali sana na eneo hilo akiwa anaangalia kila kinacho endelea kwenye kamera na alikuwa hapo kutoa msaada pale ambapo angehitajika. Dax hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuyapambania maisha yake mwenyewe maana msaada wake walikuwa ni walinzi ambao walikuwa hawapo tena hivyo alikuwa ni yeye wa kuyatetea maisha yake kwa mara ya pili tena akiwa anakutana na mtu huyo ambaye alipotea miaka kumi na miwili.
Alijigusa kwenye kiuno akiwa anahesabu hatua zake kwa kasi ya ajabu, alichomoa bisu kubwa sana ambalo alikuwa amelilenga kwenye shingo ya Max. alimfikia lakini kisu hicho kilipita pembeni kidogo baada ya Max kukikwepa hata hivyo Dax alijigeuza kwa mateke matano mfululizo ambapo matatu yalizama kwenye kifua cha Max na baada ya kumpata alisogea nyuma kidogo ambapo alikuwa anajibamiza ukutani lakini alichomEka shoka ukutani likampa balansi ya kuweza kusimama vyema kisha akajiweka sawa wakati huo Dax alikuwa amekirusha kisu hicho kwa nguvu sana kuja kwa mwanaume huyo akiwa bado yupo ukutani.
Kisu kilienda kuchimba kwenye ukuta baada ya Max kuinama lakini hata wakati yeye mwenyewe anainama aliliachia shoka lake ambalo Dax alishtuka linaikaribia shingo yake hivyo aliruka sarakasi kwenda pembeni, alihEma kwa nguvu sana kwani lilikuwa linaondoka na shingo yake moja kwa moja. Wakati anasimama hapo alipokuwa amedondokea alishangaa buti linakuja kwenye uso wake hivyo alijivuta nyuma na kujigeuza kwa sarakasi kwa mkono mmoja na kusimama.
Buti lile ambalo lilimkosa, lilichimba chimba chini vibaya sana kiasi kwamba zege ilipasuka kiasi fulani, alimeza sana mate kwani kama lingetua kwenye mwili wake basi hali ingekuwa mbaya sana. Wanaume walikutana kwa mikono yao sasa ambapo ngumi zilikuwa zinarushwa kwa nguvu na kwa spidi ya ajabu sana ambapo kasi yao haikuwa ya kawaida. Dax alikuwa anajilinda zaidi maana mwenzake alikuwa anarusha ngumi kwa kasi na nguvu ya ajabu sana, ngumi zake mbili aliziachia kwa pamoja kama anapiga pushup, Max aliziacha ngumi hizo zipenye kwake lakini yeye mwenyewe wakati huo huo aliziachia zake na wote ngumi zilitua kwenye vifua vyao.
Max ngumi zake ziliwahi kufika kwenye kifua cha Dax hali ambayo ilifanya zake zifike zikiwa zina kasi ndogo sana maana alipunguzwa kasi kwa kiasi kikubwa sana na ngumi mithili ya chuma ambazo zilikuwa zimekita kwenye kifua chake. Dax alirudi nyuma akiwa anakohoa damu, kifua kilikuwa kinawaka moto sana lakini alikuwa kwenye vita hakukuwa na mtu wa kumbembeleza alijikaza na kuikaza mifupa yake lakini kwa maumivu makali mno maana mwili ulikuwa unawaka moto sana.
Alimkimbilia Max na kuhitaji kumzoa lakini mwanaume huyo aliinama kwa kasi sana na kuachia kisigino chake ambacho kilienda kukita kwenye paji la uso la Dax hali iliyo mfanya kuyumba yumba sana na kurudi nyuma. Wakati anayumba yumba Max alimjia kwa kasi na kumgonga na viganja kwa nguvu sana kwenye masikio yake na kumfanya kusikia sauti za milio mikali sana kama mtu anapiga mluzi kisha alivutwa kwa kasi na kupigwa na ngumi sita za haraka tumboni na kifuani.
Zilimpeleka mbali sana lakini haikuwa sababu ya yeye kuachwa Max alijibetua na kutua kwenye mguu wa Dax ambao ulivunjwa hapo hapo akawa anashuka chini akiwa anaguna kwa maumivu ila kushuka kwake alikutanishwa na buti la uso ambalo lilimbamiza vibaya sana ukutani na kumfanya akae kinyonge akiwa ameegamia ukuta anatokwa damu sehemu nyingi sana za mwili wake. Max alisogea lilipokuwa shoka lake akaliokota na kuichomoa bastola yake kisha akaenda kukaa mbele ya Dax wakawa wanaangaliana.
"Kuna watu wataanza kuniogopa sana kama wakijua historia nzima ya maisha yangu, kuna muda unafika hata mimi najiogopa sana ndugu yangu. Sio rahisi mtu unazikwa halafu baada ya miaka kadhaa unarudi ukiwa hai tena, inahitaji moyo wa kipekee sana mtu kuamini na kukubali tena kuwa karibu na mtu kama mimi. Kwenye maisha yangu sikuwahi kukata tamaa kabla lakini siku ile ukiwa unanifukia kwenye lile shimo la futi sita nilijikuta naanza kuogopa sana, niliiona hofu halisi ya mwanadamu na mimi nikajua kabisa kwamba sikuwahi kuwa roboti bali ni mwanadamu wa kawaida tu ambaye naye anakufa pia"
"Kabla ya siku ile kuna namna sikuwahi kuwaza kuhusu kifo hali ambayo ilinifanya nikawa nampotezea sana Mungu ila siku ile niliamini kwamba wanadamu huwa tunakuwa na jeuri pale ambapo tuna kila kitu kwenye maisha na furaha ipo upande wetu ila hayo mambo yanapokuwa nje ya uwezo wako na hauna ulicho bakia nacho kwenye maisha yako basi niamini mimi utaamini kwamba Mungu yupo na huenda utalia sana na kujuta ukiwa unaomba Mungu akusamehe sana huku ukiwa hujui kwamba ukifa utaenda wapi kwake au kwa wale ambao inadaiwa wapo motoni. Hii ni hofu ambayo naiona kwako saivi pia ukiwa unahema kwa kukosa matumaini hapo, basi hiyo hofu mimi siku ile niliipata kutoka kwa mtu ambaye mara ya kwanza niliwahi kuamini kwamba ni mtu wangu wa karibu sana ila nilikuwa najidanganya sana mwanzo."
"Ujue Karistus, kwenye maisha yangu mimi sikuwahi kuwa na furaha kabisa, mimi sikuwahi kuwa mmoja wa wale watu ambao waliishi kwa tabasamu hata siku moja ila nikushukuru wewe kwa kuwa sababu ya mimi kupata tabasamu upya tena kwenye maisha yangu. Kunifanyia lile jambo siku ile kulinifanya nikawa karibu na mwanamke ambaye amekuwa kila kitu kwangu kwa sasa, mwanamke ambaye amenipatia familia bora sana na kwa upande wangu naweza kusema kwamba hilo ndilo jambo ambalo linanipa furaha sana kila ninapo waona wale wawili wakiwa wanacheka" mwanaume alisikitika sana akiwa anampa mwenzake huyo hisia zake ambazo alikuwa nazo kwenye moyo wake.
"Uliponaje siku ile Donald?"
"Hilo ni swali ambalo hata mimi baada ya kuamka nilikuwa nahitaji sana majibu yake, swali ambalo lilikuwa ni gumu sana kulijibu kwa sababu kwa mara ya mwisho nilijiona kabisa kwamba mimi nakufa lakini nimekuja kushtuka nipo kitandani tena watu wakifurahia mimi kuamka tena. Nadhani kuna mkosa makubwa sana ambayo yalifanyika siku ile wakati DRAGON BOYS wanauawa kwa sababu mmoja wao aliishi na kufanikiwa kutoroka na wewe hapo na wenzako mlifanya kosa la kipumbavu sana kushindwa kunikagua kwenye mwili wangu ambapo mngeikuta simu ambayo nilikuwa naitumia kuweza kuwasiliana na wale watu"
"Uzembe wako ndio umefanya mpaka leo nipo hapa kwa sababu kupitia simu ile alifanikiwa kunipata na wakati ule ambao wewe ulkuwa unaenda kunizika nikiwa hai mwanaume yule alikuwa anaufuatilia msafara wako na kila ambacho ulikuwa unakifanya alikuwa anakiona ndiyo maana ikawa rahisi sana kuweza kunifikua pale baada ya nyie kuondoka japo hakuwa na matumaini kama anaweza kunikuta nikiwa bado hai lakini Mungu ametenda miujiza yake baada ya miaka mingi sana ya kulala kitandani leo nipo tena hapa na tumeweza kukutana kwa mara nyingine Karistus" mwanaume alikuwa anampa mipango ambayo ilifanyika mpaka yeye kuweza kupona na wakati wanaongea wakati huo walikuwa wanayatumia majina ya halisi kabisa.
"Hahaha hahaha kwahiyo na mimi nilifanya kosa la kipumbavu kama ulivyofanya wewe"
"Hapana, kosa lako lilikuwa dogo sana ukifananisha na langu, ujinga wangu wa kumwamini yule malaya umeliingiza taifa hili kwenye tatizo kubwa sana. Nina imani kama sio kumwamini Brandina mpaka leo hii basi huenda haya yote yangeisha wakati ule ule lakini ujinga wangu uliyaondoa maisha ya raisi, uliyaondoka maisha ya Bilali na kijana wake lakini watu wengi walibaki wanateseka kwa sababu ya kosa langu moja tu ndiyo maana nimerudi kuhakikisha kwamba kosa langu ambalo nililifanya haliji kujirudia tena"
"Huenda upo sahihi Donald lakini kumbuka kwa sasa unaweza usifanye kosa ila tayari una udhaifu, kuwa karibu na familia ni kosa kubwa sana unapo ingia kwenye vita na watu kama hawa hivyo bado huenda mchezo huu utakuwa mgumu sana kwa upande wako. Yule mtu ana pesa sana, ana watu wa hatari sana bado unahisi kwamba unaweza kushinda vita hii ambayo ipo mbele yako?"
"Unawaza kuhusu pesa? nina pesa nyingi sana ambazo hata nikisema nichukue watu miamoja nianze kuwaleta wasifanye kazi kwa miaka mingine miamoja ijayo hawatazimaliza, sidhani kama suala la mhimu ni pesa kwa sasa ila suala la mhimu ni uhai"
"Umezipata wapi hizo pesa?"
"Nadhani unakumbuka kwamba niliwahi kuwa na gavana kwenye mkono wangu, sidhani kama kuna haja ya kuendelea kuuliza kwamba nilizipataje pesa"
"Max una uhakika na hili unalo lifanya kwamba utashinda?"
"Unatakiwa kuyahofia kwanza maisha yako kabla ya kuanza kuwawazia watu wengine Karistus. Nina maswali machache sana ambayo nataka unijibu hapa saivi maana hatutakuwa na namna tena ya kuweza kuja kuongea tena baada ya leo. Ni kipi kilikufanya ukaisaliti nchi yako?"
"Pesa"
"Pesa tu?"
"Yeah, maisha haya ni mafupi sana kuna muda unajito sana kupigania maslahi ya wengi lakini hakuna anaye ona wala hakuna anayejali kabisa sasa kuna maana gani kuweza kuendelea kuwapigania watu ambao hawawezi hata kuona thamani ya unacho kifanya? siku zote nilikuwa nataka kuwepo sehemu ambayo nitakuwa naheshimiwa, sehemu ambayo nitakuwa napewa kile ambacho nastahili na hicho ndicho nilikifanya kwa sasa. Hii miaka kumi na miwili nimeishi maisha mazuri sana, maisha ya kifahari sana kwa kadri nilivyokuwa nataka mwenyewe na hakukuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaweza kuja mbele yangu na kuwa kama tishio kwangu na hiki ndicho ambacho mimi nilikuwa nakihitaji kwa miaka ambayo nilikuwa naishi duniani"
"Lakini bado ulikuwa mtumwa"
"Hiyo sio biashara yangu kwa sababu hainihusu kikubwa nimeishi vile nilivyotaka mimi"
"Sawa, kuna neno lolote lile la mwisho kwa familia yako?"
"Whaaat?"
"Sio muda umetoka kutishia kuhusu kuwa na udhaifu wangu ambao ni familia yangu lakini wewe upande wako mbona unashtuka sana? Najua kwamba baada ya lile kutokea ulikuwa umempa mimba yule mwanamke ambaye alikuwa katibu wa raisi na baadae ukawa unaishi naye lakini ukaamua kukaa naye mbali baada ya yeye kupata mtoto ukihofia kwamba watu wakijua wanaweza kuja kumvamia na kumuua mwanao"
"Max usije ukathu......"
"Naona unaogopa sana, mtoto siwezi kumuua kwa sababu hahusiki kwa lolote na hajui kama baba yake ni mtu wa hovyo sana namna hii hivyo ataishi lakini vipi kuhusu mama yake karistus? mtu ambaye alihusika kumteketeza raisi wa nchi unataka naye aendelee kuishi au kuwa hai? huoni kama nitakuwa nawakosea heshima Watanzania na wapiganaji wenzangu ambao wametangulia kaburini?"

70 inafika mwisho.
Thanks ur Bro...!![emoji1545]
 
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+

Episode 70
Hakujali hata uwepo wa walinzi wake hilo eneo aliendelea kumimina risasi kwa hasira sana na alipokuja kushtuka alikuwa ameua walinzi wake wawili tayari huku mlinzi wake mmoja akiwa anazunguka zunguka na bastola mkononi asijue ashambulie wapi au amshambulie nani. Umeme ulirudi ghafla sana, Max alikuwa amesimama nyuma ya yule mlinzi ambaye alikuwa amebakia, alimgusa begani mwanaume huyo akageuka kwa pupa sana alikutanishwa na kisu cha shingo ambapo shingo hiyo ilichanwa chanwa vibaya sana. Alishuka chini akiwa amekufa muda mrefu tu sasa wakawa wamebaki wawili tu wakiwa wanaangaliana.
Dax alijaribu kupiga risasi lakini aligundua kwamba zilikuwa zimeisha na alikuwa amebakiwa na kisu tu pekee. Kazi ya kuweza kukata umeme ilikuwa inafanywa na James ambaye alikuwa kwenye gari ambayo haikuwa mbali sana na eneo hilo akiwa anaangalia kila kinacho endelea kwenye kamera na alikuwa hapo kutoa msaada pale ambapo angehitajika. Dax hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuyapambania maisha yake mwenyewe maana msaada wake walikuwa ni walinzi ambao walikuwa hawapo tena hivyo alikuwa ni yeye wa kuyatetea maisha yake kwa mara ya pili tena akiwa anakutana na mtu huyo ambaye alipotea miaka kumi na miwili.
Alijigusa kwenye kiuno akiwa anahesabu hatua zake kwa kasi ya ajabu, alichomoa bisu kubwa sana ambalo alikuwa amelilenga kwenye shingo ya Max. alimfikia lakini kisu hicho kilipita pembeni kidogo baada ya Max kukikwepa hata hivyo Dax alijigeuza kwa mateke matano mfululizo ambapo matatu yalizama kwenye kifua cha Max na baada ya kumpata alisogea nyuma kidogo ambapo alikuwa anajibamiza ukutani lakini alichomEka shoka ukutani likampa balansi ya kuweza kusimama vyema kisha akajiweka sawa wakati huo Dax alikuwa amekirusha kisu hicho kwa nguvu sana kuja kwa mwanaume huyo akiwa bado yupo ukutani.
Kisu kilienda kuchimba kwenye ukuta baada ya Max kuinama lakini hata wakati yeye mwenyewe anainama aliliachia shoka lake ambalo Dax alishtuka linaikaribia shingo yake hivyo aliruka sarakasi kwenda pembeni, alihEma kwa nguvu sana kwani lilikuwa linaondoka na shingo yake moja kwa moja. Wakati anasimama hapo alipokuwa amedondokea alishangaa buti linakuja kwenye uso wake hivyo alijivuta nyuma na kujigeuza kwa sarakasi kwa mkono mmoja na kusimama.
Buti lile ambalo lilimkosa, lilichimba chimba chini vibaya sana kiasi kwamba zege ilipasuka kiasi fulani, alimeza sana mate kwani kama lingetua kwenye mwili wake basi hali ingekuwa mbaya sana. Wanaume walikutana kwa mikono yao sasa ambapo ngumi zilikuwa zinarushwa kwa nguvu na kwa spidi ya ajabu sana ambapo kasi yao haikuwa ya kawaida. Dax alikuwa anajilinda zaidi maana mwenzake alikuwa anarusha ngumi kwa kasi na nguvu ya ajabu sana, ngumi zake mbili aliziachia kwa pamoja kama anapiga pushup, Max aliziacha ngumi hizo zipenye kwake lakini yeye mwenyewe wakati huo huo aliziachia zake na wote ngumi zilitua kwenye vifua vyao.
Max ngumi zake ziliwahi kufika kwenye kifua cha Dax hali ambayo ilifanya zake zifike zikiwa zina kasi ndogo sana maana alipunguzwa kasi kwa kiasi kikubwa sana na ngumi mithili ya chuma ambazo zilikuwa zimekita kwenye kifua chake. Dax alirudi nyuma akiwa anakohoa damu, kifua kilikuwa kinawaka moto sana lakini alikuwa kwenye vita hakukuwa na mtu wa kumbembeleza alijikaza na kuikaza mifupa yake lakini kwa maumivu makali mno maana mwili ulikuwa unawaka moto sana.
Alimkimbilia Max na kuhitaji kumzoa lakini mwanaume huyo aliinama kwa kasi sana na kuachia kisigino chake ambacho kilienda kukita kwenye paji la uso la Dax hali iliyo mfanya kuyumba yumba sana na kurudi nyuma. Wakati anayumba yumba Max alimjia kwa kasi na kumgonga na viganja kwa nguvu sana kwenye masikio yake na kumfanya kusikia sauti za milio mikali sana kama mtu anapiga mluzi kisha alivutwa kwa kasi na kupigwa na ngumi sita za haraka tumboni na kifuani.
Zilimpeleka mbali sana lakini haikuwa sababu ya yeye kuachwa Max alijibetua na kutua kwenye mguu wa Dax ambao ulivunjwa hapo hapo akawa anashuka chini akiwa anaguna kwa maumivu ila kushuka kwake alikutanishwa na buti la uso ambalo lilimbamiza vibaya sana ukutani na kumfanya akae kinyonge akiwa ameegamia ukuta anatokwa damu sehemu nyingi sana za mwili wake. Max alisogea lilipokuwa shoka lake akaliokota na kuichomoa bastola yake kisha akaenda kukaa mbele ya Dax wakawa wanaangaliana.
"Kuna watu wataanza kuniogopa sana kama wakijua historia nzima ya maisha yangu, kuna muda unafika hata mimi najiogopa sana ndugu yangu. Sio rahisi mtu unazikwa halafu baada ya miaka kadhaa unarudi ukiwa hai tena, inahitaji moyo wa kipekee sana mtu kuamini na kukubali tena kuwa karibu na mtu kama mimi. Kwenye maisha yangu sikuwahi kukata tamaa kabla lakini siku ile ukiwa unanifukia kwenye lile shimo la futi sita nilijikuta naanza kuogopa sana, niliiona hofu halisi ya mwanadamu na mimi nikajua kabisa kwamba sikuwahi kuwa roboti bali ni mwanadamu wa kawaida tu ambaye naye anakufa pia"
"Kabla ya siku ile kuna namna sikuwahi kuwaza kuhusu kifo hali ambayo ilinifanya nikawa nampotezea sana Mungu ila siku ile niliamini kwamba wanadamu huwa tunakuwa na jeuri pale ambapo tuna kila kitu kwenye maisha na furaha ipo upande wetu ila hayo mambo yanapokuwa nje ya uwezo wako na hauna ulicho bakia nacho kwenye maisha yako basi niamini mimi utaamini kwamba Mungu yupo na huenda utalia sana na kujuta ukiwa unaomba Mungu akusamehe sana huku ukiwa hujui kwamba ukifa utaenda wapi kwake au kwa wale ambao inadaiwa wapo motoni. Hii ni hofu ambayo naiona kwako saivi pia ukiwa unahema kwa kukosa matumaini hapo, basi hiyo hofu mimi siku ile niliipata kutoka kwa mtu ambaye mara ya kwanza niliwahi kuamini kwamba ni mtu wangu wa karibu sana ila nilikuwa najidanganya sana mwanzo."
"Ujue Karistus, kwenye maisha yangu mimi sikuwahi kuwa na furaha kabisa, mimi sikuwahi kuwa mmoja wa wale watu ambao waliishi kwa tabasamu hata siku moja ila nikushukuru wewe kwa kuwa sababu ya mimi kupata tabasamu upya tena kwenye maisha yangu. Kunifanyia lile jambo siku ile kulinifanya nikawa karibu na mwanamke ambaye amekuwa kila kitu kwangu kwa sasa, mwanamke ambaye amenipatia familia bora sana na kwa upande wangu naweza kusema kwamba hilo ndilo jambo ambalo linanipa furaha sana kila ninapo waona wale wawili wakiwa wanacheka" mwanaume alisikitika sana akiwa anampa mwenzake huyo hisia zake ambazo alikuwa nazo kwenye moyo wake.
"Uliponaje siku ile Donald?"
"Hilo ni swali ambalo hata mimi baada ya kuamka nilikuwa nahitaji sana majibu yake, swali ambalo lilikuwa ni gumu sana kulijibu kwa sababu kwa mara ya mwisho nilijiona kabisa kwamba mimi nakufa lakini nimekuja kushtuka nipo kitandani tena watu wakifurahia mimi kuamka tena. Nadhani kuna mkosa makubwa sana ambayo yalifanyika siku ile wakati DRAGON BOYS wanauawa kwa sababu mmoja wao aliishi na kufanikiwa kutoroka na wewe hapo na wenzako mlifanya kosa la kipumbavu sana kushindwa kunikagua kwenye mwili wangu ambapo mngeikuta simu ambayo nilikuwa naitumia kuweza kuwasiliana na wale watu"
"Uzembe wako ndio umefanya mpaka leo nipo hapa kwa sababu kupitia simu ile alifanikiwa kunipata na wakati ule ambao wewe ulkuwa unaenda kunizika nikiwa hai mwanaume yule alikuwa anaufuatilia msafara wako na kila ambacho ulikuwa unakifanya alikuwa anakiona ndiyo maana ikawa rahisi sana kuweza kunifikua pale baada ya nyie kuondoka japo hakuwa na matumaini kama anaweza kunikuta nikiwa bado hai lakini Mungu ametenda miujiza yake baada ya miaka mingi sana ya kulala kitandani leo nipo tena hapa na tumeweza kukutana kwa mara nyingine Karistus" mwanaume alikuwa anampa mipango ambayo ilifanyika mpaka yeye kuweza kupona na wakati wanaongea wakati huo walikuwa wanayatumia majina ya halisi kabisa.
"Hahaha hahaha kwahiyo na mimi nilifanya kosa la kipumbavu kama ulivyofanya wewe"
"Hapana, kosa lako lilikuwa dogo sana ukifananisha na langu, ujinga wangu wa kumwamini yule malaya umeliingiza taifa hili kwenye tatizo kubwa sana. Nina imani kama sio kumwamini Brandina mpaka leo hii basi huenda haya yote yangeisha wakati ule ule lakini ujinga wangu uliyaondoa maisha ya raisi, uliyaondoka maisha ya Bilali na kijana wake lakini watu wengi walibaki wanateseka kwa sababu ya kosa langu moja tu ndiyo maana nimerudi kuhakikisha kwamba kosa langu ambalo nililifanya haliji kujirudia tena"
"Huenda upo sahihi Donald lakini kumbuka kwa sasa unaweza usifanye kosa ila tayari una udhaifu, kuwa karibu na familia ni kosa kubwa sana unapo ingia kwenye vita na watu kama hawa hivyo bado huenda mchezo huu utakuwa mgumu sana kwa upande wako. Yule mtu ana pesa sana, ana watu wa hatari sana bado unahisi kwamba unaweza kushinda vita hii ambayo ipo mbele yako?"
"Unawaza kuhusu pesa? nina pesa nyingi sana ambazo hata nikisema nichukue watu miamoja nianze kuwaleta wasifanye kazi kwa miaka mingine miamoja ijayo hawatazimaliza, sidhani kama suala la mhimu ni pesa kwa sasa ila suala la mhimu ni uhai"
"Umezipata wapi hizo pesa?"
"Nadhani unakumbuka kwamba niliwahi kuwa na gavana kwenye mkono wangu, sidhani kama kuna haja ya kuendelea kuuliza kwamba nilizipataje pesa"
"Max una uhakika na hili unalo lifanya kwamba utashinda?"
"Unatakiwa kuyahofia kwanza maisha yako kabla ya kuanza kuwawazia watu wengine Karistus. Nina maswali machache sana ambayo nataka unijibu hapa saivi maana hatutakuwa na namna tena ya kuweza kuja kuongea tena baada ya leo. Ni kipi kilikufanya ukaisaliti nchi yako?"
"Pesa"
"Pesa tu?"
"Yeah, maisha haya ni mafupi sana kuna muda unajito sana kupigania maslahi ya wengi lakini hakuna anaye ona wala hakuna anayejali kabisa sasa kuna maana gani kuweza kuendelea kuwapigania watu ambao hawawezi hata kuona thamani ya unacho kifanya? siku zote nilikuwa nataka kuwepo sehemu ambayo nitakuwa naheshimiwa, sehemu ambayo nitakuwa napewa kile ambacho nastahili na hicho ndicho nilikifanya kwa sasa. Hii miaka kumi na miwili nimeishi maisha mazuri sana, maisha ya kifahari sana kwa kadri nilivyokuwa nataka mwenyewe na hakukuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa anaweza kuja mbele yangu na kuwa kama tishio kwangu na hiki ndicho ambacho mimi nilikuwa nakihitaji kwa miaka ambayo nilikuwa naishi duniani"
"Lakini bado ulikuwa mtumwa"
"Hiyo sio biashara yangu kwa sababu hainihusu kikubwa nimeishi vile nilivyotaka mimi"
"Sawa, kuna neno lolote lile la mwisho kwa familia yako?"
"Whaaat?"
"Sio muda umetoka kutishia kuhusu kuwa na udhaifu wangu ambao ni familia yangu lakini wewe upande wako mbona unashtuka sana? Najua kwamba baada ya lile kutokea ulikuwa umempa mimba yule mwanamke ambaye alikuwa katibu wa raisi na baadae ukawa unaishi naye lakini ukaamua kukaa naye mbali baada ya yeye kupata mtoto ukihofia kwamba watu wakijua wanaweza kuja kumvamia na kumuua mwanao"
"Max usije ukathu......"
"Naona unaogopa sana, mtoto siwezi kumuua kwa sababu hahusiki kwa lolote na hajui kama baba yake ni mtu wa hovyo sana namna hii hivyo ataishi lakini vipi kuhusu mama yake karistus? mtu ambaye alihusika kumteketeza raisi wa nchi unataka naye aendelee kuishi au kuwa hai? huoni kama nitakuwa nawakosea heshima Watanzania na wapiganaji wenzangu ambao wametangulia kaburini?"

70 inafika mwisho.
Daaah!! "huoni kama nitakuwa nawakosea heshima Watanzania na wapiganaji wenzangu ambao wametangulia kaburini?" Script hatar
 
Back
Top Bottom