Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

SIMULIZI RIWAYA

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2022
Posts
417
Reaction score
1,285
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(๐—ฉ๐—ถ๐˜๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐—ฎ๐˜€๐—ฎ)
๐— ๐˜๐˜‚๐—ป๐˜‡๐—ถ:๐˜€๐—ฎ๐˜‚๐—น ๐—ฑ๐—ฎ๐˜ƒ๐—ถ๐—ฑ
๐—ช๐—ต๐—ฎ๐˜๐˜€๐—ฎ๐—ฝ: 0756862047

๐—จ๐—ง๐—”๐—ก๐—š๐—จ๐—Ÿ๐—œ๐—ญ๐—œ...

"Mwanzo ilikuwa ni vita rahisi sana, vita dhidi ya ndugu yangu wa damu aliyeenda kinyume na kanuni za maisha ya utu. Sikujua kwa kufanya hivi ningeamsha vita nyingine kubwa ambayo ipo juu kabisa ya uwezo wangu na uwezo wa nchi yangu. Vita na ndugu yangu imegeuka na kuwa vita ya ulimwengu mzima. Cha ajabu ni kwamba ili kushinda vita hii haihitaji mtutu wa bunduki wala siraha yoyote. Natamani kuacha kupambana lakini siwezi kwa sababu tayari nimeshaanza. Kuendelea maana yake nimekubali kuwakabili maadui wenye rangi nyeupe ambao wamejipanga kwa zaidi ya miaka 10 kuhakikisha wanashinda.

Hatima ya Dunia yangu, Nchi yangu, Rais wangu, ndugu na familia yangu ipo mikononi mwangu. Kwa bahati mbaya ni kwamba licha ya nchi yangu kuwa na uwezo mdogo wa kupambana lakini imejikuta inatumika kama chungu cha kuandalia vita hii kali bila kujua, isitoshe tunapigana na kitu tusichokiona. Naweza kusema sasa ni wakati wa mapenzi, sayansi na teknolojia kuipeleka Dunia vile inavyotaka.

Naam kwa mara ya kwanza historia inakwenda kuandikwa, historia ya vita ambayo haijawahi kutokea popote duniani, ndio sababu nasema hii ni VITA YA KISASA (THE MODERN WAR) niite Inspekta Aron"

Huu ulikuwa ni UTANGULIZI wa simulizi hii maridhawa iliyojaa visa vingi vya kusisimua,,,
Mauaji, tamaa, mapenzi, urafiki, hila,chuki, drama, vita, usaliti, siasa, visasi, kushinda na kushindwa pamoja na mambo mengine yasiyotazamiwa na bila kusahau LOVE STORY kali ndani yake.
Like, comment and share, tuanze
 

Attachments

  • Screenshot_20220705-133238.png
    Screenshot_20220705-133238.png
    337.9 KB · Views: 125
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.........01

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

SEHEMU YA KWANZA- (KIFO CHA SHAHIDI WA MWISHO)

SASA TUANZE SIMULIZI YETU....

"Mume wangu niue mimi, muache mwanangu aishi tafadhali bado ni binti mdogo naomba usimuue"
"Mama naogopa...!"
"Usiogope mwanangu kila kitu kitakuwa sawa, usijali sawa Annah"
"Mheshimiwa, mtihani ulionipa ni mgumu sana hivi nawezaje kumuua mwanangu au mke wangu, naanzaje kumwaga damu zao"
"Kama huwezi basi acha nitakusaidia mimi mwenyewe, nimekwambia chagua moja umuue mtoto wako au mke wako"
"Mheshimiwa siwezi tafadhali nipe adhabu nyingine, waache mke wangu na mwanangu waondoke nitafanya chochote unachotaka, niko chini ya miguu yako mkuu"

Haya yalikuwa ni mazungumzo ya watu zaidi ya watano waliokuwa ndani ya jengo moja chakavu lililokuwa limetelekezwa kabla ya ujenzi kukamilika, jengo hilo lilikuwa limejitenga pembeni kidogo ya mji.

Alikuwepo Dokta Isaack Gondwe ambaye ni waziri wa afya akiwa na vijana watatu nyuma yake ambao wote walikuwa wameziba nyuso zao kwa vitambaa vyeusi. Walikuwa wamesimama mbele ya familia moja ya watu watatu yaani baba mama na binti yao mdogo mwenye umri wa miaka 22 aliitwa Annah.

"Baba Annah nimekukabidhi bastola umuue mmoja kati ya mke au mtoto wako kisha nikuache uende lakini umeshindwa, basi acha vijana wangu wafanye kazi yao" alisisitiza Dokta Gondwe huku akibinua mabega yake kwa kejeri
Kwa mara nyingi tena Baba Annah aliinua juu mkono wake wa kulia ulioshikilia bastola akaielekeza walipokuwa wamesimama mke na binti yake Annah, hali akitetemeka alivuta pumzi ndevu na kuishusha taratibu, kijasho chembamba kikawa kinamtoka mzee huyo.
Mama Annah alimkumbatia binti yake akamziba usoni na kiganja cha mkono wake hakutaka mwanae aone kinachoendelea, naye akafumba macho kwa uchungu akiwa tayari kwa lolote litakalotokea.

Mara ghafula Baba Annah aligeuka kwa kasi akabadilisha uelekeo na kuilekeza bastola yake walipokuwa wamesimama Mheshimiwa dokta Isaack Gondwe na vijana wake, bila kusita akabinya kitufe cha kufyatua risasi huku akiwa amemlenga Dokta Isaack Gondwe kichwani lakini risasi haikutoka ,akajaribu tena mara ya pili na ya tatu lakini hali ikawa ni ile ile, baba Annah akahisi kuchanganyikiwa.

"Hahahah, ha ha ha, ha ha ha haaa" Dokta Gondwe alicheka tena kwa sauti kubwa sana, kisha akaongea
"Nilijuaa...! nilijua tu wewe ni msaliti, unajifanya mjanja sio? ona sasa umeumbuka mbele ya familia yako mzee hii ni mara ya pili unanisaliti, niliwaomba msitoe ushahidi wowote mahakamani lakini mkapanga kunigeuka wewe na familia yako pamoja na kukuhonga pesa nyingi bado ukapanga kunigeuka. Sasa unanisaliti tena kwa mara ya pili unataka kuniua, bahati mbaya bastola niliyokupa haina risasi hahahaha"

"Ulaaniwe Dokta Gondwe, mungu akulaani, utakufa kifo kibaya, wewe na watu wako wote mtakufaa, hata hicho cheo ulichonacho najua ni cha dhuruma, nakwambia utakufa" Baba Annah aliishia kutoa laana kwa mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe mara baada ya kubaini kuwa hana ujanja tena.

"Acha makelele yako, laana kama hizo zilishakuja nyingi sana, hata marehemu mama yangu alinilaani tangu nikiwa tumboni lakini hadi leo hakuna laana iliyofanya kazi" alisema Dkt Gondwe huku akiinamisha kichwa chake chini kutega sikio kumsikiliza kijana wake mwingine ambaye aliingia ndani ya jengo hilo wakati anazungumza.
Kijana huyo hakuwa amefunika sura yake kama wengine, alimnong'oneza maneno kadhaa kwa takribani sekunde 30 hivi, Dokta Gondwe akaonekana kushtuka kiasi kisha akapaza sauti akifoka.

"Kwa nini, kwa nini kila siku yeye tu? hii inawezekanaje? kajuaje tuko hapa? huyu mdogo wako anataka nini? kwa nini unashindwa kumdhibiti? hivi askari ni yeye tu hakuna wengine aah!" Dkt Gondwe alifoka huku akiondoka, akapiga hatua kadhaa kisha akageuka tena.

"Unajua cha kufanya Tino, natangulia kwenye gari" alisema Dkt Gondwe kisha akatoka nje ya lile jengo.
Tino ambaye ndiye aliyeonekana kuwa na mamlaka kuliko vijana wengine wa Dkt Gondwe, alichomoa bastola iliyokuwa kiunoni kwake. Bila kuuliza alimfyatulia risasi Baba Annah, risasi iliyopenya sikio la kushoto ikatokea sikio la kulia, alifanya hivyo pia kwa Mama Annah, kisha akamalizia kumpiga risasi ya kifua Annah. wote wakaanguka chini na kupoteza maisha.
Lilikuwa ni tukio kubwa na zito, kuua watu watatu kwa wakati mmoja. Lakini kwa Tino ilikuwa ni tofauti kabisa, alifanya kwa urahisi sana kama anakunywa maji vile, ilionyesha wazi hii ilikuwa ni kazi aliyoizoea.
Baada ya kufanya hivyo Tino na wale vijana wengine waliandaa mazingira kuonyesha kuwa Baba Annah alimuua mke na mtoto wake kwa kuwapiga risasi kisha na yeye akamalizia kwa kujipiga risasi mwenyewe.
Baadae walitoka na kuingia ndani ya gari mbili zilizoegeshwa nje ya jengo hilo, wakaondoka kwa kasi kuwakimbia polisi ambao kwa mujibu wa maelezo ya Dokta Gondwe alimaanisha wapo njiani wanakuja na mmoja kati ya polisi hao ni mdogo wake na kijana wake wa kazi yaani Tino.
โญโญโญ

Ni kweli, dakika chache tu baada ya Dokta Gondwe na vijana wake kuondoka, gari za polisi zisizopungua sita zilifika na kufunga breki kali nje ya jengo hilo na punde polisi walishuka na kuanza kumiminika kwa kasi kuingia ndani ya jengo hilo huku siraha zao zikiwa mbele
Ilikuwa ni ishara tosha kuwa polisi hawa walikuwa na taarifa kamili ya kile kilichokuwa kinaendelea ndani ya jengo hilo.

Walikagua vyumba vyote vya jengo hilo, hawakupata mtu yeyote zaidi ya miili ya Baba Annah mama Annah na Annah mwenyewe, kwa haraka haraka ilionyesha wazi kuwa Baba Annah ndiye aliyetekeleza mauwaji hayo kwani mkono wake wa kulia alishika bastola iliyotumika.
Lakini hicho sicho alichokuwa akikiona na kukiwaza Inspekta Aron, kijana ambaye ni polisi mpelelezi kutoka kituo cha kati Handeni. Yeye aliyatazama mazingira ya mle ndani kwa utulivu wa hali ya juu, akaitazama ile miili mmoja baada ya mwingine huku akichukua baadhi ya vielelezo muhimu kama ilivyokuwa ada kwa polisi wengine.

"Tumempoteza shahidi mwingine" Alisema Inspekta Jada, polisi ambaye alikuwa akifanya kazi kwa ukaribu sana na Aron.
"Yah! tumechelewa kidogo sana, tungewahi tungeweza kuwaokoa pengine" alisema Aron huku akisogea pembeni pamoja na Jada wakiwaacha polisi wengine wakiendelea na kazi.

"Huenda walipata tena taarifa kama tunakuja" Alisema Jada
"Usiseme huenda, huo ndio ukweli wenyewe Inspekta Jada hii serikali ina watu wa hovyo sana" Aron alilalamika
"Usijali Aron jitihada zako zitazaa matunda siku moja, ki ufupi unajituma sana, uwe na subra siku moja tutawakamata wote"
"Inshallah iwe hivyo, lazima nitamkamata Tino"
"Mmh! unahisi kaka yako Tino kahusika kwenye hili tukio pia"
" Ndiyo lazima alikuwepo hapa, subiri uone" Alisema Inspekta Aron akachukua simu yake akaitafuta namba aliyoihifadhi kwa jina la 'Bro Tino' akapiga. Simu iliita kwa dakika kadhaa bila kupokelewa mwisho ikakata, akapiga tena.
โญโญโญ

Upande wa pili Tino na bosi wake ambaye ni Waziri wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe tayari walishafika mjini. Tino akiwa ndiye dereva alikuwa ameegesha gari pembeni ya barabara na pembeni ya gari hiyo kulikuwa na gari nyingine ya serikali V8 ilikuwa imepaki ikimsubiri Dokta Gondwe ambaye bado alikuwa na mazungumzo na kijana wake tegemezi Tino.

"Tino, kama sikosei hii ni mara ya nne kama sio ya tano nakwambia kuhusu huyu mdogo wako Inspekta Aron unaemlealea sana, hili ni bomu ambalo litakuja kutulipukia baadae" Dkt Gondwe aliongea kwa msisitizo
"Usijali bosi, huyu ni mdogo wangu najua namna ya kumdhibiti niachie mimi, kuwa na amani bosi" Tino aliongea kwa kujiamini huku akipiga jicho pembeni kuitazama simu yake iliyokuwa ikiita mpigaji akiwa ni Aron mdogo wake.

"Haya mimi nakwenda, tayari tumeshaua mashahidi wote nina hakika tutashinda kesi mahakamani na mkwe wangu Osward atakuwa huru, lakini jua vita yetu bado ni kali sana na ndio kwanza tunaanza"
"Sawa mkuu"
Dkt Isaack Gondwe alishuka kwenye gari akapiga hatua na kuingia kwenye gari nyingine ile V8 dereva akawasha gari wakaondoka.
Tino aligeuka na kuitazama simu ambayo ilikuwa ikiita kwa mara ya pili sasa, akapokea.

"Nambie dogo"
"Ulikuwa hapa Tino, ni wewe tena si ndiyo?" Inspekta Aron alisikika upande wa pili akiuliza
"Wapi mbona sikuelewi unazungumzia nini?"
"Najua unanielewa vizuri bro, sasa sikia nakuhakikisha kwamba lazima nitakukamata, nitathibitisha uchafu wako wote, mtafungwa wewe pamoja na mtandao wako mzima"
"Come down mdogo wangu, punguza vitisho huna ushahidi wowote wa kunifunga na hautokuja kufanikiwa kamwe, sahau"
"Nisikilize kwa makini kaka labda nisiwe hai, yaani kwa mikono yangu nitakupeleke je..."
"Kaa kimya Aron huna faida yoyote wewe, nahangaika usiku na mchana kutafuta mamilioni ya pesa kwa ajili ya matibabu ya mama yetu, lakini wewe unafanya nini? unahangaika kutaka kunizuia, unaakili kweli wewe?"

"Mama yangu hawezi kuendelea kutibiwa kwa pesa zako chafu kaka, hata angekuwa anajitambua ninauhakika asingekubali hili"

"Kwa hiyo unatakaje, nimuache afe?"
"Kufa au kupona kwa mama yangu ni mpango wa Mungu sio wako Tino"
"Ni mama yetu sio mama yako, kumbuka hilo" alisema tino kisha akakata simu kwa hasira

"Vipi amesemaje?" Aliuliza Inspekta Jada mara tu baada ya kukata simu.
"Kauli zake ni zile zile za kila siku, anadai anatafuta hela kwa ajili ya mama kule hospitali" Aron alijibu kinyonge.
"Pole Aron, nakuonea huruama sana, mungu akufanyie wepesi ni miezi sita mpaka sasa unapambana kwa ajili ya matibabu ya mama yako gharama ni kubwa lakini bado kaka yako naye anazidi kukuchanganya" alisema Inspekta Jada akionekana kuguswa na hali aliyokuwa akiipitia Inspekta Aron. Kabla Aron hajazunguza chochote mara kuna askari alionekana akikimbia kuwafuata, akafika na kusimama mbele yao huku akihema kwa nguvu.

"Vipi kwema?" aliuliza Aron akionekana mwenye shauku ya kujua kilichomleta, vivyo hivyo kwa Jada.
"Yu..yule binti kule nda..ndani ha..hajafa ni mzima" alisema yule askari kauli iliyowafanya Aron na Jada watazamane.

Je, nini kitafuata?
Nini hatima ya Vita kati ya ndugu hawa wawili yaani Aron na Tino?
Kwa nini Tino yupo karibu na Waziri wa afya?
Annah hajafa ni mzima huu unaweza kuwa ushahidi wa mwisho wa Inspekta Aron?
Kwa nini VITA YA KISASA?

Hii ni sehemu ya kwanza, majibu ya maswali haya utayapata ndani ya simulizi hii maridhawa iliyojaa visa vingi vya kusisimua.
Mauaji, tamaa, mapenzi, urafiki, hila,chuki, drama, vita, usaliti, siasa, visasi, mahaba, kushinda na kushindwa pamoja na mambo mengine yasiyotazamiwa bila kusahau LOVE STORY kali ndani yake.
Naam hii ndio MODERN WAR(vita ya kisasa).

WhatsApp: 0756862047

Weka comment yako chini tuendelee...
 
Mkuu itaisha nianze kusoma? Inaonekana tamu sana, naogopa kuanza na nikakumbana na arosto
 
Mkuu itaisha nianze kusoma? Inaonekana tamu sana, naogopa kuanza na nikakumbana na arosto
Be on touch, simulizi zangu huwa namaliza yote usijali,,, Angalia kuna simulizi inaitwa DO NOT SHOUT - USIPIGE KELELE karibu inafika mwisho
 
THE MODERN WAR
(vita ya kisasa)
Sehemu ya..........02
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047.

02-( KIKAO CHA SIRI)
ILIPOISHIA 01...
"Vipi kwema" aliuliza Aron akionekana mwenye shauku ya kujua kilichomleta, vivyo hivyo kwa Jada.
"Yu..yule binti kule nda..ndani , ha..hajafa ni mzima" alisema yule askari kauli iliyowafanya Aron na Jada watazamane

SASA ENDELEA....
"Nini? Unauhakika?" Aliuliza Aron
"Ndiyo afande, yule binti ni mzima hajafa"
Haraka Jada na Aron walikimbia kuelekea ndani ya lile jengo kwenda kuhakikisha ukweli wa taarifa hiyo
"Jada ita gari ya wagonjwa upesi" Alisema Aron huku akiendelea kukimbia lakini mara akasimama na kumtazama Jada ambaye tayari alishatoa simu mfukoni.

"Hapana usipige, mwite Dokta Zyunga afike hapa haraka na vifaa vyote muhimu tutampeleka hospitali kwa siri hatakiwi kujua mtu mwingine zaidi yetu" alisema Inspekta Aron, Jada akafanya kama alivyoagizwa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Nusu saa baadae Inspekta Aron mdogo wake Tino alikuwa ndani ya hospitali kubwa ya kimataifa maarufu kama MOUNTENIA HOSPITAL, Aron alikuwa amesimama nyuma ya mlango mkubwa wa kioo uliokuwa na maandishi makubwa juu yake yaliyosomeka 'MAJOR THEATER'(Chumba cha upasuaji mkubwa). Aliwatazama madaktari waliokuwa wakiendelea kupambana kuyaokowa maisha ya Annah ambaye alifikishwa hospitalini hapo kwa siri kubwa. Tayari Annah alikuwa ameshawapoteza wazazi wake wote wawili waliouwawa kikatili masaa machache yaliyopita ikiwa ni agizo la Waziri wa afya Dokta Gondwe.
Madaktari walifanikiwa kuitoa risasi iliyokuwa imezama upande wa kulia wa kifua cha Annah. Kwa bahati nzuri risasi haikuwa imeleta madhara wala kugusa viungo muhimu kama mapafu na ini, kwa sasa jitihada nyingine za kibingwa zilikuwa zikiendelea kuyanusuru maisha ya binti huyo yatima.
Inspekta Aron aliendelea kusimama pale nje huku akimuomba mungu wake ayaokoe maisha ya binti huyu muhimu sana kwake.
"You're my last hope Annah, please don't die"(wewe ndio tumaini langu la mwisho Annah tafadhali usife) Alisema Inspekta Aron huku akiwa amekutanisha mikono yake kumuomba mungu
Annah alikuwa ndiye shahidi pekee aliyehai dhidi ya kesi ngumu ya mauaji aliyofanya kijana Osward ambaye ni mkwe wa Dokta Gondwe. Kesi hiyo ilikuwa ni daraja pia la kuwatia hatiani kaka yake Tino pamoja na Waziri wa afya Dokta Gondwe ambao wamekuwa wakifanya matukio mengi ya kiharifu lakini anashindwa kuwatia nguvuni kwa sababu ya kukosa ushahidi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili ndani ya hoteli moja kubwa ya kifahari Waziri wa afya Mheshimiwa dkt Isaack Gondwe alionekana akiwa katika kikao cha siri yeye pamoja wa wazungu watatu, alikuwepo pia Rais mstaafu wa awamu ya nne mheshimiwa Profesa Cosmas Kulolwa pamoja na mkemia mkuu wa serikali bwana Andiwelo Katabi. Kilikuwa ni kikao cha siri kilichobeba ajenda nzito mno.
Wakati wakiendelea na mazungumzo mara kuna ujumbe mfupi wa maandishi uliingia kwenye simu ya Dkt Isaack Gondwe, akaufungua haraka na kuusoma.

,,,,,Yule binti Annah hajafa bado yuko hai, Inspekta Aron kamchukua kaondoka naye kwa siri hatujui alikompeleka, nitakupa taarifa zaidi naendelea kufuatilia,,,,,,,

Dkt Isaack Gondwe alikurupuka kutoka kwenye kiti akasimama ghafula kiasi cha kuwafanya watu waliokuwepo ndani ya chumba hicho wamtazame kwa pamoja.
"Aah! excuse me" (kumradhi) alisema Dkt Gondwe, akapiga hatua na kutoka nje ya kile chumba haraka.
Dokta Gondwe aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali akatoa simu yake ndogo Samsung, akaibonyeza haraka haraka akapiga namba aliyokuwa ameihifadhi kwa jina la 'SELE GEREZA' simu iliita kwa sekunde kadhaa mwisho ikapokelewa upande wa pili.

"Naam Mheshimiwa Waziri" Mkuu wa gereza la Kanondo SP Seleman alizungumza upande wa pili wa simu
"Tafadhali naomba kuongea na Osward sasa hivi kuna dharula"
"Mheshimiwa kwa sasa wafungwa wapo kantini wanakula, subiri kama dakika 15 hivi"
"Afande Sele hivi unaelewa mtu akisema ni dharula, kwanza Osward sio mfungwa yupo hapo kusubiri tarehe ya kesi yake kusikilizwa"
"Anatuhuma za mauaji ndio sababu yuko hapa, najua unaelewa taratibu zetu Mheshimiwa Waziri sipendi tubishane subiri kidogo nijaribu kukusaidia"
"Sawa nasubiri"
Simu ikakatwa, Dokta Gondwe akabaki amesimama nje ya kile chumba ambacho ndani yake kulikuwa na kikao cha siri kikiendelea. Habari za Annah kuwa hai zilimchanganya sana mbaya zaidi wakati wanafanya mauaji yeye na Tino hawakuwa wamefunika sura zao hivyo ilikuwa ni hatari kubwa kama Annah atanusurika kifo.
"Doctor, there's something wrong?"(Daktari kunakitu hakipo sawa) Dokta Gondwe alishtushwa na sauti ya mzungu mmoja aliyetoka nje kumtazama.
"Nothing wrong Mr Codrado, two minutes please am coming"(Hakuna shida bwana Codrado, dakika mbili tafadhali nakuja)
"It's you're time to talk Doctor Gondwe, let's go inside please we don't have time"(ni zamu yako kuongea Dokta Gondwe, tuingie ndani tafadhali hatuna muda) alisisitiza yule mzungu na mara hiyo simu ya Dokta Gondwe ikaita.
"Dakika moja nakuja"
"What?"(nini?)
"Moja tu moja bwana Codrado"
"What do you mean!?"(unamaanisha nini!?) aliuliza Codrado akiwa hajaelewa kiswahili
"One minute"(dakika moja) Alisema Dkt Gondwe, Codrado akarudi ndani akionekana kutofurahishwa na alichokifanya Waziri wa afya. Punde tu baada ya Codrado kuondoka dkt Gondwe akapokea simu haraka
"Baba mkwee" sauti nzito ya kiume ilisikika upande wa pili wa simu ile
"Ndiyo Osward ni mimi, tafadhali sogea sehemu salama tuzungumze jambo"
"Nimeshasogea baba hivi ni kweli mmeshindwa kufanya chochote hadi sasa nakalibia kumaliza miezi miwili huku gerezani" Osward alilalamika
"Usijali mwanangu tupo kwenye hatua za mwisho mashahidi wote tumesha wamaliza nakuhakikishia safari hii tukirudi tena mahakamani unaachiwa huru"
"Asante mkwe nikitoka tu cha kwanza nafunga ndoa na binti yako Najma"
"Sawa lakini hilo tutaongea ukitoka, kuna kitu nataka kukuliza"
"Uliza tu baba mkwe"
"Hivi wakati unafanya mauaji yule binti wa yule mzee naye alikuona?" Aliuliza dkt Gondwe akiwa na shauku ya kusikia jibu kutoka kwa Osward.
"Kale kabinti wanakaita mmm! Annah si ndiyo?"
"Ndiyo Annah huyo huyo"
Osward alibaki kimya kwa muda akijalibu kuvuta kumbukumbu siku aliyofanya mauaji.
"Kwa kweli kumbukumbu zangu hazipo sawa baba mkwe, sikumbuki kitu kuhusu Annah"
"Dah! hii ni kazi nyingine sasa"
"Kivipi mzee?"
"Tulifanikiwa kuwakamata familia nzima tukawapiga risasi wote lakini kwa bahati mbaya Annah hajafa yupo kwenye mikono ya Inspekta Aron sasa hivi"
"Aron yule mdogo wake na Tino"
"Ndiyo, jamaa anatusumbua sana yule"
"Sasa sikia baba mkwe, uweni wote, muueni huyo binti haijarishi aliniona au hakuniona muueni na huyo Inspekta Aron hapo mtakuwa mmemaliza kila kitu" Osward aliongea kwa msisitizo.

"Sawa tutafanya hivyo lakini kuhusu kumuua Inspekta Aron hilo tusubiri kwanza, baadae Osward nipo kwenye kikao muhimu nitakupigia tena" Alisema Dkt Gondwe kisha akakata simu.

Osward alibaki amesimama wima akionekana kutofurahishwa na kauli ya mwisho kutoka kwa mheshimiwa Waziri wa afya. Osward alimchukia sana Inspekta Aron huyu ndiye alikuwa chanzo cha yeye kufunguliwa tuhuma za mauaji na alikuwa akipambana kwa nguvu zote kukusanya ushahidi kuhakikisha Osward anafungwa. Osward aliamini kama Inspekta Aron atakufa basi kila kitu kitakuwa rahisi kwake.

"Wanamlealea kwa sababu ni mdogo wake na Tino si ndiyo, basi mimi siwezi kuendelea kuvumilia" Osward aliongea kwa jazba huku akibinyabinya simu ya mkuu wa gereza, akapiga namba fulani na kuweka simu sikuoni, iliita kwa muda mwisho ikapokelewa.

"Oya big! Osward hapa naongea, nakuhitaji hapa magereza chapu kwa haraka" Osward aliongea kwa kifupi kisha akakata simu, alitembea taratibu hadi pale alipomuacha mkuu wa gereza SP Seleman akamrudishia simu yake.

"Vipi rudi sasa kwa wenzako mbona umekaa tena, mfuata askari yule pale anakusubiri akusindikize" alisema SP Seleman baada ya kuona Osward anakaa badala ya kurudi kwa wafungwa wenzake.
"Kun mtu nimemwita nina mazungumzo naye muhimu"
"Sikiliza Osward, najua wewe ni mtu mkubwa unawatu huko nje baba yako mzee Matula ni tajiri mkubwa pia Waziri wa afya anakukingia kifua lakini nataka kukwambia ukiwa hapa jaribu kuwa na nidhamu, wewe hauna tofauti yoyote na wenzako waliopo humu ni lazima ufuate kanuni na taratibu zetu, kukupa simu yangu ni heshima tu kwa mheshimiwa Waziri na si vinginevyo, tabia zako tangu umeingia hapa zimekuwa ni mbovu na hazivumiliki tena naongea kama mkuu wa gereza" SP Seleman alifoka akimtazama Osward kwa macho makali. Osward hakujibu chochote, alimtazama tu SP Seleman namna alivyokuwa akifoka, akatabasamu.
"Wapi nitakutana na mgeni wangu?" Osward aliuliza akionyesha wazi kuwa maneno ya Seleman hayajamuingia hata kidogo.
SP Seleman alitoa ishara fulani kwa askari aliyekuwa karibu, askari akasogea na kumtaka Osward amfuate. Wakaongozana hadi eneo maalumu ambalo wafungwa hukutana na watu wengine kutoka nje ya gereza kama vile ndugu na jamaa zao wanaokuja kuwatembelea.
Osward alimkuta mtu aliyewasiliana naye kwenye simu dakika chache zilizopita tayari ameshafika amekaa anamsubiri. Alikuwa ni mwanume mnene, mrefu mweusi karibu kila mahali isipokuwa viganja vya mikono yake pekee. Mwili wake ulikuwa umejazia na endapo ukimuona hauna sababu ya kujiuliza mara mbili mbili kuwa huyu ni mtu wa mazoezi tena sio mazoezi tu bali mazoezi makali.

"Ooh Big' umeshafika tayari"
"Yeah, unanijua mimi mambo yangu nayaendesha kizungu"
"Hahahah kama kawaida yako"
"Vipi unatoka lini humu? kambini mambo hayaendi bila wewe mkuu" aliuliza yule bwana wa miraba minne
"Soon nitaungana na ninyi, sasa sikia kuna kazi ndogo hapa nataka nikupe"
"Ipi hiyo nambie"
"Unamjua yule askari jau ambaye ni chanzo cha mimi kuwa huku"
"Ee si yule mdogo wake Tino, anaitwa Aron"
"Yes! huyo huyo"
"Vipi tumuondoe?"
"Hayo ndio majibu, bila hivyo nitaozea humu ndani, yule jamaa jau sana wanamlealea kwa sababu ni mdogo wake Tino"
"Haina noma Osward ni hilo tu au kunalingine?"
"Ni hilo tu ila hakikisha kifo chake kisilete utata si unamjua kaka yake naye ni balaa jingine sitaki mambo mengi mimi" Osward alisisitiza

Je nini kitafuata?
Aron atakuwa salama?
Na je atafanikiwa kumlinda Annah?
Vipi kuhusu kile kikao cha Waziri wa afya na wazungu kutoka Mexico?

ITAENDELEA...

WhatsApp: 0756862047
 
MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........03
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

03- (PICHA YA CHAFU)

ILIPOISHIA...02
"Hayo ndio majibu, bila hivyo nitaozea humu ndani, yule jamaa jau sana wanamlealea kwa sababu ni mdogo wake Tino"
"Haina noma Osward ni hilo tu au kunalingine?"
"Ni hilo tu ila hakikisha kifo chake kisilete utata si unamjua kaka yake Tino naye ni balaa jingine sitaki mambo mengi mimi" Osward alisisitiza

SASA ENDELEA...

"Usijali shughuli yangu unaijua huna haja ya kunieleza sana ila nina zawadi yako hapa" Alisema Big
"Ipi tena?" Osward aliuliza na mara hiyo Big alitoa picha ndogo mfukoni kisha akamkabidhi.
Osward aliitazama ile picha huku akitabasamu. Ilikuwa ni picha ya mwanamke mmoja mrembo sana.

"Najma! Najma! malkia wangu, hahaha nitaua mtu tena kwa ajili yako, vipi anaendeleaje huko mtaani?"
"Yupo tu kama kawaida kwao geti kali, tangu arudi kutoka Nairobi baba yake Dokta Gondwe anamfungia ndani hamruhusu kudhurula hovyo"

"Hahaha! Najma kama Najma, Basi poa poa Big' asante nenda kafanya kazi tutaonana tena" alisema Osward na mwisho wakaagana na Big mwanaume wa miraba mnne aliyepewa jukumu la kumuua Inspekta Aron
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Tino alionekana akiingia ndani ya duka moja kubwa la nguo, lilikuwa ni duka lake binafsi lililoko katikati ya mji. Alimsalimia mfanyakazi wake ambaye aliitikia salamu ile kisha wakapeana ishara fulani ambayo ni wao tu ndio walikuwa wakielewa.

Tino akapiga hatua hadi kwenye kona moja ya duka hilo, akaangaza macho huku na huku, hakuna aliyekuwa akimuona, akabinya kitufe fulani kilichokuwa kimejificha nyuma ya nguo, mara ukaonekana mlango uliokuwa ukifanana na ukuta wa chumba hicho ukifunguka kuelekea ndani, Tino akaingia haraka na kuufunga.

Sasa alikuwa ndani ya chumba kingine ambacho kilikuwa ni chumba chake cha siri, kilikuwa ni chumba kikubwa sana mfano wa ofisi, huko kulikuwa na watu wengine saba wa kike na wa kiume, wote walikuwa bize na kompyuta, hakuna aliyekuwa amekaa bure kila mmoja alikuwa makini na anachokifanya.

"Karibu bosi" mmoja wa wale vijana alimkaribisha Tino.
"Asante, vipi kuna mteja?"
"Ndiyo wapo wawili, lakini wa tatu Bosco kasema umuangalie mwenyewe kwanza"
"Mmh kwa nini?"
"Sijajua lakini nahisi anasababu za muhimu" alijibu yule kijana ambaye ndiye aliyeonekana kiongozi wa wenzie katika ofisi hiyo ya siri ya Tino.

Hii ilikuwa ni ofisi ambayo ilikuwa ikimuingizia Tino kiasi kikubwa cha pesa ingawa kazi aliyokuwa akiifanya katika ofisi hii haikuwa harali.
Kabla ya kufungua ofisi hiyo Tino alizunguuka katika nyumba za wageni 'guest' mbalimbali katika mikoa tofauti tofauti, kila chumba alichoingia Tino alitegesha kamera za siri ambazo ilikuwa ni ngumu sana kuziona. Alifanya hivyo katika maeneo na nyumba za wageni tofauti tofauti na baada ya hapo akawa na mitambo maalumu ambayo kupitia kamera zile aliweza kuona kila kinachoendea ndani chumba husika.

Tino alikuwa akikusanya video za watu wengi tofauti tofauti waliokuwa wakiingia na kutoka kwenye vyumba alivyotega kamera zake. Tino aliwataka hasa wale wanaoingia na kufanya mapenzi ndani ya vile vyumba, hivyo akawa na picha/video nyingi za ngono, akishazikusanya anaanza kumfuatilia mtu mmoja baada ya mwingine mpaka anahakikisha anapata mawasiliano yake. Baada ya hapo Tino hutoa vitisho kwa muhusika akimtaka alete kiasi cha pesa atakachompangia na kama asipofanya hivyo basi atazisambaza video zake chafu mitandao.

Hivi ndivyo namna ofisi ya Tino ilivyokuwa ikifanya kazi, alijipatia pesa nyingi sana ndani ya muda mfupi. Haikuwa rahisi mtu kukubali picha au video zake za ngono zisambazwe mtandaoni, walifanya kila namna na kulipa pesa anayoihitaji Tino.

"Ukitoa taarifa polisi, au kwenda kulalamika kokote, basi utakuwa umevunja makubaliano yetu kinachofuata picha na video zako zitakuwa mtandaoni" hii ndio kauli aliyozoea kuitoa mara kwa mara kuwaziba mdomo wahusika.

Licha ya kwamba Tino alikuwa akifanya kazi chini ya Waziri wa afya Mheshimiwa dkt Isaack Gondwe lakini kazi hii ndio iliyokuwa ikimuingizia pesa kwa kiasi kikubwa. Kuwa karibu na Waziri wa afya alikuwa na sababu zake nyingine tofauti.

"Umesema kuna video ngapi leo" Tino aliuliza swali lake kwa mara nyingine.
"Ziko video za wateja wawili, lakini moja Bosco kasema uitazame kwanza"
"Sawa mmeshapata mawasiliano ya wahusika?"
"Tumepata ya mmoja, huyu wa pili bado tunaendelea kumsaka"
"Siku hizi mmepunguza kasi sijui kwa nini, kuna video ya X ipo hapa kwa zaidi ya siku tatu ila mapaka leo hamjampata muhusika na jamaa anaonekana anapesa ndefu sana"
"Ni kweli bosi ule mfumo wa serikali tulioudukua ukawa unatusaidia kupata namba za hawa watu siku hizi hatuutumii tena walibadilisha namba ya siri"
"Sawa basi tuanze na huyo mtu mliepata namba zake"

Tino na vijana wake walisogea hadi kwenye meza ya kompyuta ambayo ilionekana kuwa kubwa zaidi ya zingine wakakaa kwa kuizunguuka. Bila kuchelewa wakachukua namba za yule mtu ambae video yake ya ngono ilikuwa mikononi mwao, wakapiga simu.

Simu iliita kwa muda lakini haikupokelewa, walijaribu mara kadhaa lakini hali ikawa ni ile ile.

"Basi achana naye, mtumie baadhi ya picha WhatsApp kisha mpe vitisho akifungua atatutafuta mwenyewe" Alisema Tino na kusimama

"Bosco nimeambiwa kuna video unataka niitazama kwanza si ndiyo, ina nini kwani?"
"Aah ee..ni..ni vema ukaitazama kwanza" alijibu Bosco kijana wa Tino akionyesha kutojiamini kabisa, hali hii ilimfanya Tino kuingiwa na wร siwasi, haikuwa kawaida ya Bosco kuwa katika hali ile, alikuwa ni kijana jasiri na mzoefu wa kucheza na kompyuta, alimtegemea.

"Hebu twende tukaone" alisema Tino, wakaongozana hadi ilipo kompyuta aliyokuwa anaitumia kijana Bosco, akaifungua na kuitafuta ile video.

"Kaa utazame bosi" alisema Bosco huku akimpisha Tino akakaa kwenye kiti kisha akaicheza ile video.

Kadri muda ulivyokuwa ukienda ndivyo hali ya Tino ilizidi kubadilika, hakuamini kile anachokiona. Ilikuwa ni video ikimuonyesha mke wake wa ndoa Jesca akiwa anafanya mapenzi na mwanaume mwingine na baada ya kumuangalia mwanaume yule kwa makini alikuwa si mwingine bali bosi wake yaani mheshimiwa Dkt Isaack Gondwe Waziri wa afya.

Tino alisimama akionekana kuchanganyikiwa akaikatisha ile video, hakuweza kustahimili kuendelea kuitazama, jasho lilianza kumtoka huku mikono yake ikitetemeka. Akaicheza tena ile video kuhakikisha alichokiona, hali ilikuwa ni ile ile alichokiona mwanzo kilikuwa ni kile kile hata sasa mkewe na bosi wake Dkt Gondwe walikuwa ndani ya huba zito. Maumivu aliyoyapata moyoni hayakuwa na mfano, alimpenda mno mke wake Jesca. Wakati huo simu yake ilikuwa ikiita, alipotazama mpigaji alikuwa ni bosi wake Dkt Isaack Gondwe. Bosco alitamani kumshika bosi wake amfariji lakini aliogopa, Tino alikuwa kwenye hali mbaya sana.
Aliuma meno kwa hasira huku mikono yake ikitetemeka akajikaza na kuipokea simu ile.

"Tino kijana wangu ni nini unafanya? mbona umekuwa mzembe sana siku hizi" Dkt Gondwe alisikika upande wa pili wa simu.

Tino ambae safari hii macho yake yalikuwa yamebadilika na kuwa mekundu alipata kigugumuzi cha mdomo, akashindwa ajibu nini, picha ya mkewe akiwa amelala na mtu anaeongea naye kwenye simu wakati huu bado haikufutika kichwani kwake.

"Unanisikia lakini, mbona uko kimya kuna dharula Tino tena dharula kubwa sana naomba tukutane nyumbani kwangu baada ya nusu saa namalizia kikao hapa" alisema Dkt Gondwe.
"Sawa bosi" alijibu Tino kisha simu ikakatwa.
***********
{TANGAZO:- Epuka matapeli simulizi hii imetungwa na SAUL DAVID simu 0756862047, Tafadhali usinunue kwa mtu mwingine tofauti }
******-*-
"Iweke hii video kwenye simu yangu kisha uifute, mimi na wewe ndio tunajua kuhusu hili wengine wasijue chochote" Tino alitoa maagizo kwa kijana wake Bosco kisha akatembea haraka kuelekea ilipokuwepo bafu na choo ya ofisi hiyo ya siri.

Akiwa huko Tino alisimama mbele ya kioo kimoja kikubwa akawa anajitazama hali akiwa amekunja ngumi na kuuma meno yake kwa hasira, alionekana kuchanganyikiwa kupita kiasi.
Alifungua droo ya kabati moja iliyokuwa pembeni ya kile kioo akatoa bomba la sindano na kijichupa kidogo cha dawa, akajifunga mkono wake kisha akavuta kiasi fulani cha ile dawa na kujidunga kwenye mshipa.
Baada ya hapo Tino akavuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu kisha akaendelea kujitazama kwenye kioo huku akizungumza.

"Usijali Tino hili nalo litapita, jambo unalopigania ni kubwa mno, hauwezi kufanikiwa kirahisi, lazima upitie changamoto kama hizi" Tino alikuwa akijisemea mwenyewe huku akijitazama kwenye kioo, aliongea kwa uchungu sana kiasi cha kuifanya midomo yake itetemeke na macho kuzidi kuwa mekundu.

"Usifanye lolote Tino utapoteza muelekeo tulia kama hakujatokea chochote, najua mke anauma lakini vumilia, muda utafika utalipa kisasi, umevumilia mangapi mpaka sasa, usife moyo Tino, usijaribu kumuondoa dkt Gondwe huyo ndio njia yako kuelekea mafanikio, kama mipango yako ikikamilika nakuhakikishia utaitikisa Dunia nzima, mataifa yote kutoka pande zote za Dunia wataliita jina lako Tino Phillipo Kasebele. Pambana Tino pambana bila kurudi nyuma siku ukiupata ufalme wako hakuna atakaeweza kukuzuia, sio mmarekani wala sio mchina wote watasafiri na kuja kukupigia magoti, pambanaa..." baada ya kusema hivyo Tino alicheka kwa sauti kubwa sana, hii ilionyesha wazi kuna jambo lingine kubwa na la siri alikuwa akilifanya kijana huyu ukiacha ile kazi anayoifanya chini ya Waziri wa afya dkt Gondwe, ukiacha pia kazi anayoifanya ya kurekodi picha za ngono kwa wateja wanaoingia vyumba vya wageni alivyotegesha kamera, bado ilionyesha kuna kitu kingine kikubwa anakifanya.

Ni kitu gani hicho?
Hili ni balaa jingine ndani ya MODERN WAR...
Ukiacha ule mpango wa Osward kutaka kumuua Inspekta Aron, vipi kuhusu Tino na Waziri wa afya?
Tino atafanya nini?
Bosi katembea na mkewe...
Ni mpango gani alionao kiasi cha kuamini ataitikisa Dunia nzima?

ITAENDELEA...

WhatsApp 0756862047
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(๐—ฉ๐—œ๐—ง๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—ž๐—œ๐—ฆ๐—”๐—ฆ๐—”)

Sehemu ya...............04
Mtunzi: saul david
Email: saulstewarty@gmail.com

04-(PICHA TATU ZA X)
ILIPOISHIA...03
baada ya kusema hivyo Tino alicheka kwa sauti kubwa sana, hii ilionyesha wazi kuna jambo lingine kubwa na la siri alikuwa akilifanya kijana huyu ukiacha ile kazi anayoifanya chini ya Waziri wa afya dkt Gondwe, ukiacha pia kazi anayoifanya ya kurekodi picha za ngono kwa wateja wanaoingia vyumba vya wageni alivyotegesha kamera, bado ilionyesha kuna kitu kingine kikubwa anakifanya.

SASA ENDELEA...
Kicheko cha Tino kiliwafanya wale vijana ndani ya ofisi yake watazamane kwa macho ya kuulizana, hawakujua bosi wao kapatwa na nini isipokuwa Bosco peke yake, sekunde chache baadae Tino alitoka.
"Vipi umeshaifuta hiyo video kwenye kompyuta yako?" Tino alimuuliza kijana wake Bosco
"Ndiyo bosi nimeifuta na kuiweka kwenye simu yako kama ulivyosema" alijibu Bosco
Tino alitulia kwa muda ni kama alikuwa akitafakari jambo fulani muhimu, baada ya sekunde kadhaa akasogea na kukaa pembeni ya Bosco.

"Nisikilize Bosco, irudishe tena hiyo video kwenye kompyuta yako, mimi na wewe tunakwenda kucheza mchezo hatari hakikisha hakuna mwingine anajua, nitakuwa nakupa maelekezo nini cha kufanya sawa" alisema Tino akionekana bado ni mtu mwenye maumivu makali licha ya kujaribu kujisahaurisha lakini taswira ya mkewe akifanya mapenzi na bosi wake mheshimiwa Dkt Isaack Gondwe haikufutika kichwani kwake.

"Nimekuelewa bosi" alijibu Bosco, Tino akasimama na kumpiga piga mgongoni huku akitabasamu.
"Sasa ni wakati wako wa kucheza mziki wangu mheshimiwa Dokta Gondwe" Tino aliwaza huku akiwa bado ameachia tabasamu lenye maumivu ndani yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili katika hospitali ya Mountenia bado madaktari walikuwa wakiendelea kupambana kuyaokowa maisha ya binti Annah. Yalikuwa yamepita masaa manne mpaka sasa Inspekta Aron ambaye ni mdogo wake Tino bado hakubanduka pale mlangoni hata kidogo, alitamani kushuhudia kwa ukaribu kila kilichokuwa kinaendelea kwa binti huyo muhimu sana kwake. Mwisho oparesheni ilimalizika, mlango wa chumba cha upasuaji ukafunguliwa.

"Dokta Zyunga niambie, kazi imekwendaje? huyu mwanamke atapona?" Inspekta Aron aliuliza maswali mfurulizo mara tu baada ya daktari kutoka.

"Usijali Aron sisi tumefanya kwa upande wetu, mungu ndio ataamua hatima ya Annah, siwezi kukuahidi chochote kwa sasa tusubiri" alieleza Dokta Zyunga
"Asante daktari naamini atapona"
"Endelea kumuombea Mungu atamsaidia, Enhe! sasa taratibu za ulinzi zipoje nakumbuka umeniambia huyu mgonjwa ni wa siri anatakiwa kulindwa pia si ndiyo?"
"Ndiyo, askari wangu wako hapa, tuelekeze tu chumba atakacholazwa Annah sisi tutaweka utaratibu mzuri wa kumlinda"
"Sawa Inspekta, nifuate"

Dokta Zyunga na inspekta Aron waliongozana hadi kwenye chumba ambacho kilikuwa tayari kimeandaliwa kwa ajili ya Annah kupumzishwa mara tu atakapotolewa kwenye chumba cha upasuaji.

Licha ya kwamba inspekta Aron alimleta Annah hospitalini hapo kwa siri kubwa lakini hakutaka kujiaminisha moja kwa moja kuwa yupo salama bado aliona kuna umuhimu wa kuweka ulinzi ili kuongeza usalama. Aliwaelewa vizuri watu anaopambana nao alijua wazi kuwa mtandao unaoshirikiana na kaka yake Tino ni mkubwa tena wenye nguvu sana.
Hisia za Aron zilikuwa ni sahihi kabisa kwani mpaka sasa tayari Dokta Isaack Gondwe alikuwa ameshapata taarifa kuwa Annah yuko hai hajafa na tayari alishamwita kijana wake Tino kumkabidhi jukumu la kuhakikisha Annah anakufa.
Baada ya taratibu zote za ulinzi kukamilika Aron alitoka nje ya hospitali ya Mountenia, akaingia kwenye gari yake na kuondoka akiwaahidi askari wake watatu aliowaacha kuwa angerudi baada ya muda mfupi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Zilikuwa zimepita dakika kadhaa baada ya Dokta Gondwe na wale wazungu kutoka Mexico kumaliza kikao chao cha siri. Sasa alikuwa ameketi nje ya nyumba yake kwenye bustani nzuri ya maua akifanya mazungumzo na mmoja wa watu wake wa karibu maarufu kama Mzee Matula, tajiri mkubwa aliyekuwa amewashika masikio viongozi wakubwa serikalini Dokta Gondwe akiwa mmoja wao.

"Enh! nambie dkt Gondwe, uhakika wa kushinda kesi upo, mwanangu Osward amekaa sana mahabusu ni wakati wake wa kurudi uraiani sasa" alisema Mzee Matula
"Usijali kila kitu kipo kwenye uangalizi wangu kama nilivyokwambia awali, tayari nimesha wasambalatisha mashahidi wote, hakuna kesi tena mwanao Osward ataachiwa huru" alijibu dkt Gondwe.
"Hahaha hapo ndio huwa unanifurahisha dkt Gondwe, kwa hiyo mashahidi wote kwisha habari yao"
"Yaani wote, kasoro katoto kamoja tu ndio kamenusurika kufa, hivi nimemwita Tino yupo njiani nafikiri kufikia kesho jioni kila kitu kitakuwa sawa"
"Mmh jitahidi bwana kesi itasikilizwa baada ya siku nne tu kwanzia leo, nataka Osward abaki huru ana kazi ya kufanya"
"Usijali Matula kila kitu kipo kwenye mpango, tukikaua haka kabinti hakuna ushahidi utakaobaki kuthibitisha Osward alifanya yale mauaji, hakuna"
"Sawa nimekuelewa dkt Gondwe, enhe vipi pia kuhusu lile suala letu"
"Lipi?"
" Kuhusu ndoa ya kijana wangu Osward na binti yako Najma?"
"Aaa!! tusubiri kwanza bado hata hawajazoeana si unajua Najma tumemlazimisha tu kuolewa na Osward alikuwa hataki, tuwaache kwanza wazoeane ndio haya mengine yafuate"
"Hahahah wazoeane kitu gani dkt Gondwe sisi wazazi ndio tunajua kilichochema kwa wenetu, any way basi tusubiri hii kesi iishe kwanza kisha...ooh naona kijana wako kafika" aliongea Mzee Matula lakini akasita kuendelea mara tu baada ya kumuona Tino anakuja.
"Ni mbabe kweli kweli cheki anavyotembea" alisema Mzee Matula
"Sanaa, hanaga Mchezo na kazi, nikimwambia ua anaua chinja ana chinja kanisaidia vitu vingi mno ni mwaminifu sana" alieleza dkt Gondwe wakati huo Tino alikuwa jirani kuwafikia, macho yake alikuwa ameyakaza kumtazama mheshimiwa Dkt Isaack Gondwe bosi wake aliyemzunguuka na kulala na mke wake.
Moyo ulizidi kumuuma lakini alijikaza kisabuni akajitahidi kutoonyesha tofauti yoyote ile. Alifika na kukaa pembeni yao, baada ya salamu Mzee Matula aliaga na kuondoka akawaacha Tino na bosi wake Dkt Gondwe wazungumze
[emoji294][emoji294][emoji294]
"Annah hajafa" hii ndio iliyokuwa kauli ya kwanza kutoka kwa dkt Gondwe, Tino alionyesha mshtuko kiasi.
"Nimeambiwa hali yake sio nzuri amepelekwa hospitali kwa siri, yupo kwenye mikono ya mdogo wako Inspekta Aron" dkt Gondwe alitoa maelezo huku akimtazama Tino usoni.
"Unanielewa lakini mbona uko kimya?"
"Nakuelewa bosi"
"Eee ndio hivyo, sitaki kukulaumu sana kwa sababu najua ni kazi kidogo tu, kumuua huyu binti, tafuta ni wapi mdogo wako Aron kamficha, hakikisha unammaliza kabla hajafungua kinywa chake kuzungumza"
"Sawa bosi haina shida" Alijibu Tino na mara hiyo kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya dkt Gondwe akachukua simu yake na kuutazama, ulikuwa ni ujumbe katika mtandao wa WhatsApp, ujumbe ulioambatana na picha tatu.

Dkt Gondwe alionyesha mshtuko mkubwa mara tu baada ya kuziona zile picha. Zilikuwa ni picha zikimuonyesha akiwa mtupu yeye pamoja na mwanamke ambaye ni mke wa kijana wake aliyenaye mezani wakati huu yaani Tino.
Mapigo ya moyo ya dkt Gondwe yalibadilika yakawa yanaenda kasi huku mikono yake ikitetemeka.

"Vipi bosi uko sawa" Tino aliuliza kama vile hajui chochote lakini ukweli ni kwamba alielewa kila kitu kinachoendelea kwenye simu ya bosi wake, mipango yote hii alifanya na kijana wake Bosco.

"Aah ..ee..ni..niko sawa usijali" dkt Gondwe alijibu kwa kubabaika akilazimisha tabasamu, macho yake yakahamia kwenye ule ujumbe ulioambatana na picha zile, akausoma.

,,,, Hizo ni picha tu, nina video ya dakika 55 tangu mlipoingia hadi mlipotoka, ukifuata maelekezo yangu hakuna kitakacho haribika, ukileta ukaidi basi nitaanika huu uchafu wako mtandaoni, utakuwa gumzo Duniani kote mheshimiwa Waziri afya,,,,

Dkt Gondwe alimaliza kuusoma ujumbe huo, safari hii jasho lilikuwa likimtiririka kama maji.

"Bosi mbona kama hauko sawa nini shida" Tino aliuliza tena kwa mara nyingine, akijifanya kushangazwa na hali aliyonayo bosi wake.

Je, nini kitafuata?
Tino anataka kumfanya nini bosi wake?
Vipi kuhusu Aron atafanikiwa kumlinda Annah angali na yeye yupo hatarini kuuwawa na watu wa Osward?
BADO TUNATENGENEZA MIZIZI YA SIMULIZI HII, HAKIKISHA UNASOMA SEHEMU INAYOFUA

0756862047
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(vita ya Kisasa)
Sehemu ya...............04
Mtunzi: saul david
Email: saulstewarty@gmail.com

04-(PICHA TATU ZA X)
ILIPOISHIA...03
baada ya kusema hivyo Tino alicheka kwa sauti kubwa sana, hii ilionyesha wazi kuna jambo lingine kubwa na la siri alikuwa akilifanya kijana huyu ukiacha ile kazi anayoifanya chini ya Waziri wa afya dkt Gondwe, ukiacha pia kazi anayoifanya ya kurekodi picha za ngono kwa wateja wanaoingia vyumba vya wageni alivyotegesha kamera, bado ilionyesha kuna kitu kingine kikubwa anakifanya.

SASA ENDELEA...
Kicheko cha Tino kiliwafanya wale vijana ndani ya ofisi yake watazamane kwa macho ya kuulizana, hawakujua bosi wao kapatwa na nini isipokuwa Bosco peke yake, sekunde chache baadae Tino alitoka.
"Vipi umeshaifuta hiyo video kwenye kompyuta yako?" Tino alimuuliza kijana wake Bosco
"Ndiyo bosi nimeifuta na kuiweka kwenye simu yako kama ulivyosema" alijibu Bosco
Tino alitulia kwa muda ni kama alikuwa akitafakari jambo fulani muhimu, baada ya sekunde kadhaa akasogea na kukaa pembeni ya Bosco.

"Nisikilize Bosco, irudishe tena hiyo video kwenye kompyuta yako, mimi na wewe tunakwenda kucheza mchezo hatari hakikisha hakuna mwingine anajua, nitakuwa nakupa maelekezo nini cha kufanya sawa" alisema Tino akionekana bado ni mtu mwenye maumivu makali licha ya kujaribu kujisahaurisha lakini taswira ya mkewe akifanya mapenzi na bosi wake mheshimiwa Dkt Isaack Gondwe haikufutika kichwani kwake.

"Nimekuelewa bosi" alijibu Bosco, Tino akasimama na kumpiga piga mgongoni huku akitabasamu.
"Sasa ni wakati wako wa kucheza mziki wangu mheshimiwa Dokta Gondwe" Tino aliwaza huku akiwa bado ameachia tabasamu lenye maumivu ndani yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili katika hospitali ya Mountenia bado madaktari walikuwa wakiendelea kupambana kuyaokowa maisha ya binti Annah. Yalikuwa yamepita masaa manne mpaka sasa Inspekta Aron ambaye ni mdogo wake Tino bado hakubanduka pale mlangoni hata kidogo, alitamani kushuhudia kwa ukaribu kila kilichokuwa kinaendelea kwa binti huyo muhimu sana kwake. Mwisho oparesheni ilimalizika, mlango wa chumba cha upasuaji ukafunguliwa.

"Dokta Zyunga niambie, kazi imekwendaje? huyu mwanamke atapona?" Inspekta Aron aliuliza maswali mfurulizo mara tu baada ya daktari kutoka.

"Usijali Aron sisi tumefanya kwa upande wetu, mungu ndio ataamua hatima ya Annah, siwezi kukuahidi chochote kwa sasa tusubiri" alieleza Dokta Zyunga
"Asante daktari naamini atapona"
"Endelea kumuombea Mungu atamsaidia, Enhe! sasa taratibu za ulinzi zipoje nakumbuka umeniambia huyu mgonjwa ni wa siri anatakiwa kulindwa pia si ndiyo?"
"Ndiyo, askari wangu wako hapa, tuelekeze tu chumba atakacholazwa Annah sisi tutaweka utaratibu mzuri wa kumlinda"
"Sawa Inspekta, nifuate"

Dokta Zyunga na inspekta Aron waliongozana hadi kwenye chumba ambacho kilikuwa tayari kimeandaliwa kwa ajili ya Annah kupumzishwa mara tu atakapotolewa kwenye chumba cha upasuaji.

Licha ya kwamba inspekta Aron alimleta Annah hospitalini hapo kwa siri kubwa lakini hakutaka kujiaminisha moja kwa moja kuwa yupo salama bado aliona kuna umuhimu wa kuweka ulinzi ili kuongeza usalama. Aliwaelewa vizuri watu anaopambana nao alijua wazi kuwa mtandao unaoshirikiana na kaka yake Tino ni mkubwa tena wenye nguvu sana.
Hisia za Aron zilikuwa ni sahihi kabisa kwani mpaka sasa tayari Dokta Isaack Gondwe alikuwa ameshapata taarifa kuwa Annah yuko hai hajafa na tayari alishamwita kijana wake Tino kumkabidhi jukumu la kuhakikisha Annah anakufa.
Baada ya taratibu zote za ulinzi kukamilika Aron alitoka nje ya hospitali ya Mountenia, akaingia kwenye gari yake na kuondoka akiwaahidi askari wake watatu aliowaacha kuwa angerudi baada ya muda mfupi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Zilikuwa zimepita dakika kadhaa baada ya Dokta Gondwe na wale wazungu kutoka Mexico kumaliza kikao chao cha siri. Sasa alikuwa ameketi nje ya nyumba yake kwenye bustani nzuri ya maua akifanya mazungumzo na mmoja wa watu wake wa karibu maarufu kama Mzee Matula, tajiri mkubwa aliyekuwa amewashika masikio viongozi wakubwa serikalini Dokta Gondwe akiwa mmoja wao.

"Enh! nambie dkt Gondwe, uhakika wa kushinda kesi upo, mwanangu Osward amekaa sana mahabusu ni wakati wake wa kurudi uraiani sasa" alisema Mzee Matula
"Usijali kila kitu kipo kwenye uangalizi wangu kama nilivyokwambia awali, tayari nimesha wasambalatisha mashahidi wote, hakuna kesi tena mwanao Osward ataachiwa huru" alijibu dkt Gondwe.
"Hahaha hapo ndio huwa unanifurahisha dkt Gondwe, kwa hiyo mashahidi wote kwisha habari yao"
"Yaani wote, kasoro katoto kamoja tu ndio kamenusurika kufa, hivi nimemwita Tino yupo njiani nafikiri kufikia kesho jioni kila kitu kitakuwa sawa"
"Mmh jitahidi bwana kesi itasikilizwa baada ya siku nne tu kwanzia leo, nataka Osward abaki huru ana kazi ya kufanya"
"Usijali Matula kila kitu kipo kwenye mpango, tukikaua haka kabinti hakuna ushahidi utakaobaki kuthibitisha Osward alifanya yale mauaji, hakuna"
"Sawa nimekuelewa dkt Gondwe, enhe vipi pia kuhusu lile suala letu"
"Lipi?"
" Kuhusu ndoa ya kijana wangu Osward na binti yako Najma?"
"Aaa!! tusubiri kwanza bado hata hawajazoeana si unajua Najma tumemlazimisha tu kuolewa na Osward alikuwa hataki, tuwaache kwanza wazoeane ndio haya mengine yafuate"
"Hahahah wazoeane kitu gani dkt Gondwe sisi wazazi ndio tunajua kilichochema kwa wenetu, any way basi tusubiri hii kesi iishe kwanza kisha...ooh naona kijana wako kafika" aliongea Mzee Matula lakini akasita kuendelea mara tu baada ya kumuona Tino anakuja.
"Ni mbabe kweli kweli cheki anavyotembea" alisema Mzee Matula
"Sanaa, hanaga Mchezo na kazi, nikimwambia ua anaua chinja ana chinja kanisaidia vitu vingi mno ni mwaminifu sana" alieleza dkt Gondwe wakati huo Tino alikuwa jirani kuwafikia, macho yake alikuwa ameyakaza kumtazama mheshimiwa Dkt Isaack Gondwe bosi wake aliyemzunguuka na kulala na mke wake.
Moyo ulizidi kumuuma lakini alijikaza kisabuni akajitahidi kutoonyesha tofauti yoyote ile. Alifika na kukaa pembeni yao, baada ya salamu Mzee Matula aliaga na kuondoka akawaacha Tino na bosi wake Dkt Gondwe wazungumze
[emoji294][emoji294][emoji294]
"Annah hajafa" hii ndio iliyokuwa kauli ya kwanza kutoka kwa dkt Gondwe, Tino alionyesha mshtuko kiasi.
"Nimeambiwa hali yake sio nzuri amepelekwa hospitali kwa siri, yupo kwenye mikono ya mdogo wako Inspekta Aron" dkt Gondwe alitoa maelezo huku akimtazama Tino usoni.
"Unanielewa lakini mbona uko kimya?"
"Nakuelewa bosi"
"Eee ndio hivyo, sitaki kukulaumu sana kwa sababu najua ni kazi kidogo tu, kumuua huyu binti, tafuta ni wapi mdogo wako Aron kamficha, hakikisha unammaliza kabla hajafungua kinywa chake kuzungumza"
"Sawa bosi haina shida" Alijibu Tino na mara hiyo kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya dkt Gondwe akachukua simu yake na kuutazama, ulikuwa ni ujumbe katika mtandao wa WhatsApp, ujumbe ulioambatana na picha tatu.

Dkt Gondwe alionyesha mshtuko mkubwa mara tu baada ya kuziona zile picha. Zilikuwa ni picha zikimuonyesha akiwa mtupu yeye pamoja na mwanamke ambaye ni mke wa kijana wake aliyenaye mezani wakati huu yaani Tino.
Mapigo ya moyo ya dkt Gondwe yalibadilika yakawa yanaenda kasi huku mikono yake ikitetemeka.

"Vipi bosi uko sawa" Tino aliuliza kama vile hajui chochote lakini ukweli ni kwamba alielewa kila kitu kinachoendelea kwenye simu ya bosi wake, mipango yote hii alifanya na kijana wake Bosco.

"Aah ..ee..ni..niko sawa usijali" dkt Gondwe alijibu kwa kubabaika akilazimisha tabasamu, macho yake yakahamia kwenye ule ujumbe ulioambatana na picha zile, akausoma.

,,,, Hizo ni picha tu, nina video ya dakika 55 tangu mlipoingia hadi mlipotoka, ukifuata maelekezo yangu hakuna kitakacho haribika, ukileta ukaidi basi nitaanika huu uchafu wako mtandaoni, utakuwa gumzo Duniani kote mheshimiwa Waziri afya,,,,

Dkt Gondwe alimaliza kuusoma ujumbe huo, safari hii jasho lilikuwa likimtiririka kama maji.

"Bosi mbona kama hauko sawa nini shida" Tino aliuliza tena kwa mara nyingine, akijifanya kushangazwa na hali aliyonayo bosi wake.

Je, nini kitafuata?
Tino anataka kumfanya nini bosi wake?
Vipi kuhusu Aron atafanikiwa kumlinda Annah angali na yeye yupo hatarini kuuwawa na watu wa Osward?
BADO TUNATENGENEZA MIZIZI YA SIMULIZI HII, HAKIKISHA UNASOMA SEHEMU INAYOFUA


season 1 & 2 zipo tayari..
0756862047
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(Vita Ya Kisasa)
Sehemu ya.............05
Mtunzi: Saul David
Email saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

05-(KIGOGO BABA WA OSWARD)
ILIPOISHIA...04
,,,, Hizo ni picha tu, nina video ya dakika 55 tangu mlipoingia hadi mlipotoka, ukifuata maelekezo yangu hakuna kitakacho haribika, ukileta ukaidi basi nitaanika huu uchafu wako mtandaoni, utakuwa gumzo Duniani kote mheshimiwa Waziri afya,,,,
Dkt Gondwe alimaliza kuusoma ujumbe huo, safari hii jasho lilikuwa likimtiririka kama maji.
"Bosi mbona kama hauko sawa nini shida" Tino aliuliza tena kwa mara nyingine, akijifanya kushangazwa na hali aliyonayo bosi wake.

SASA ENDELEA...

Dokta Gondwe aliduwaa ghafula mwili wake wote ukiwa umekufa ganzi, hakuwa na uwezo wa kuongea, kusimama wala kufanya chochote kile.
Baada ya kuona Dokta Gondwe yupo kwenye hali hiyo Tino wala hakujali alisogeza kikombe cha kahawa aliyokuwa anakunywa Dokta Gondwe akaanza kunywa yeye taratibu huku akimtazama mzee huyo akiteseka na dalili zilizoonyesha wazi kuwa ni presha imepanda.
"Huu ni mwanzo tu Dokta Gondwe" aliwaza Tino huku akiendelea kunywa kawaha taratibu, wakati huo hali Dokta Gondwe ilizidi kuwa mbaya.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati hayo yakiendela Mzee Matula baba yake Osward hakuwa amefika mbali, ndio kwanza alikuwa akielekea lilipokuwa gari lake la kifahari aina ya HUMMER H3, huku nyuma hakujua timbwili aliloliacha kati ya mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe na kijana wake Tino.
Mzee Matula alifunguliwa mlango wa gari na moja kati ya walinzi wake watatu aliozoea kuongozana nao kila anapokwenda. Kabla hajaingia ndani ya gari mara alisikia sauti nzuri ya kike ikimwita.

"Najma..." Mzee Matula alisema kwa sauti ya chini huku akitabasamu taratibu akageuka, aliijua sauti hiyo ni ya nani.
Mwanamke mmoja mrembo kupindukia alionekana anakuja kuelekea pale alipo Mzee Matula, aliitwa Najma mtoto wa tatu wa mheshimiwa Waziri wa afya dkt Isaack Gondwe.

Najma alikuwa na kila sifa ya kuitwa mwanamke mrembo, alikuwa ni mrefu, umbo la wastani lililojengeka kwa kujikata vizuri kiuno kiasi cha kuzifanya hips zake nzuri kuonekana, alikuwa mzuri wa sura, macho yaliyolegea mashavu yenye vishimo yaliyofanya uzuri wake kuongezeka mara dufu, nywele zake ndevu zinazofika mgongoni. Hakika alikuwa ni mwanamke ambaye anaweza kumfanya kila mwanaume aliyekamilika kumtazama mara mbili.
Najma alikuwa amevaa suruali ya jeans, kijinguo chepesi kwa juu kilichoacha kitofu chake nje, alitembea kwa madaha kiasi cha kumfanya Mzee matula amtazame kwa macho yaliyojaa matamanio, hakumtazama kama binti anayetarajiwa kuolewa na mwanae.
Akiwa karibu kumfikia Mzee Matula mlinzi wake mmoja alisogea mbele na kunyoosha mkono wake kumzua Najma asisogee zaidi. Najma alimtazama yule mlinzi kwa macho makali na mara hiyo ikasikika sauti kutoka kwa mzee Matula.
"Muache aje"
Mlinzi akatoa mkono wake, Najma akapiga hatua kadhaa kisha akasimama mbele ya Mzee Matula huku akiwa ameweka mikono katika kiuno chake laini.
"Umependaza sana leo" alisema Mzee Matula akizidi kumtazama Najma kwa macho ya matamanio.
"Sijaja hapa kupongezwa na kizee kama wewe, nataka kujua lengo lako ni nini hasa?" Najma aliongea kwa ukali
"Kivipi Najma?"
"Hujui? Kwa hiyo baada ya wewe kunishindwa umeamua umtumie mtoto wako, yaani unamshawishi baba yangu akubali niolewe na mwanao Osward kwa faida yako wewe si ndio?" Najma alifoka

"Sikiliza Najma, pengine unaweza ukawa sahihi kama nilivyokuahidi awali nitatumia kila njia kuhakikisha nakupata" Alisema mzee Matula akionekana kujiamini.

"Ohoo! Kumbe, basi hongera zako ila kwa taarifa yako mimi kama Najma msimamo wangu uko pale pale hata kama baba yangu anakusikiliza kiasi gani lakini nakuhakikishia hakuna utakachofanikiwa"

"Hahahah, Najma unanifurahisha sana ujue, mbona tayari wewe na Osward ni wapenzi bado kidogo tu na mimi nianze kufanya yangu, nasubiri mfunge ndoa kwanza"
"Una uhakika mimi na huyu mwanao ni wapenzi? alafu nikuulize kwani Osward akinioa ndio mtakuwa mmenioa wote au?"
"Olewa kwanza atanielewa baadae" mzee Matula aliongea kwa jeuri akawa anaingia kwenye gari yake lakini mara akasita akageuka tena na kumtazama Najma kisha akaongea.

"Nashukuru pia kwa sababu haujataka kuwa shahidi mahakamani, najua ulikuwepo wakati Osward anafanya yale mauaji lakini haujasema chochote asante sana hayo ndio mapenzi, hahahah mkweee" Mzee Matula aliongea akionyesha kejeri za wazi wazi kisha akaingia kwenye gari walinzi wake wakafuata na mwisho wakaondoka.
Najma alibaki amesimama tabasamu lake likiwa limefifia usoni. Suala la Mzee Matula na mwanae Osward lilimnyima furaha kabisa, lakini angefanya nini wakati baba yake Dokta Gondwe anamshinikiza akubali kuolewa na Osward bila kujua mipango mingine aliyokuwa nayo Mzee Matula ambaye naye pia anamtaka Najma kimapenzi. Mbaya zaidi mzee huyo tajiri alikuwa akiheshimiwa sana na baba yake, kila alichokisema ilikuwa ni sheria kwa Dokta Gondwe.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Najma akiwa anarudi ndani kwa mbali alimuona Tino na baba yake wakiwa wamekaa nje katika eneo la bustani. Hakutaka kupita karibu yao kwa sababu alikuwa akimchukia Tino bila sababu, yaani ungeweza kusema hawajaendana damu. Najma akachagua kuingia ndani kupitia mlango wa nyuma. Wakati akipiga hatua aliinua macho yake akamuangalia baba yake Dokta Gondwe.
Pozi alilokuwa amekaa Dokta Gondwe kidogo lilimshangaza ni kama alikuwa ameinua mkono wake wa kulia na kuuweka shingoni kwa muda mrefu. Hakujua kuwa wakati huo baba yake alikuwa akihangaika angalau kuregeza tai ili apate hewa. Ikabidi Najma aanza kusogea taratibu, alimjua baba yake anamatatizo ya moyo, kuna wakati huwa anakauka ghafula na kupoteza fahamu.

Tino ambaye alikuwa bado anakunywa kahawa alikuwa na hisia za mbali kutokana na kazi aliyokuwa akiifanya, aliweza kubaini kuwa kuna mtu anakuja kutokea nyuma yake.

"Mzee, mzee Gondwe, mheshimiwa nini shida" Tino alikurupuka ghafula akasogea karibu na Dokta Gondwe akijifanya kama vile alikuwa hajamuona mwanzo. Kitendo hicho kilimfanya Najma aliyekuwa bado hajafika kuamini hisia zake zilikuwa sahihi haraka akaanza kukimbia kuwafuata Tino na baba yake pale walipo.

"Daddy! shida nini, eti Tino baba kapatwa na nini?" aliuliza Najma akiwa amebakiza hatua chache kuwafikia, Najma aliogopa sana.
"Sijajua nashangaa amebadilika ghafula tu" Tino alidanganya
"Hii ni presha itakuwa imepanda tena, lakini huwa haipandi bila sababu, au kuna taarifa mbaya umempa?" Najma alimtupia swali lingine Tino wakati huo akihangaika kuregeza tai na kufungua vishikizo vya shati la baba yake.

"Hapana sijampa taarifa yoyote mbaya" Tino alijitetea.
Haraka Najma aliitazama simu ya baba yake pale mezani lakini ghafula katika hali asiyotegemea baba yake Dokta Gondwe aliikwapua ile simu kwa kasi na kuiweka kwenye mfuko wa koti lake.
Hali hii ilimshangaza Najma akahisi moja kwa moja kuwa kuna kitu baba yake alikuwa anaficha na huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe licha ya dokta Gondwe kuwa katika hali mbaya lakini hakutaka kuruhusu mwanae au Tino aipekue simu yake. Ilikuwa ni hatari kubwa kwake kwani wangeweza kuziona zile picha zake chafu za ngono alizotumiwa.

"Baba nini shida, unajisikiaje?" Najma aliuliza swali.
"Ni..nipelekeni chumbani, alafu Najma nita..tafutie zile dawa zangu za presha za kuweka chi..chi..chini ya ulimi" Dokta Gondwe aliongea kwa taabu kidogo.
Haraka Najma aliwaita walinzi waliokuwa wanazunguuka zunguuka nyumbani hapo, wakasaidiana kumnyanyua dokta Gondwe wakawa wanampeleka ndani.
Wakiwa wamemfikisha mlangoni mara dokta Gondwe aliwapa ishara kuwa wasimame kwanza.

"Tino hebu sogea karibu" alisema Dokta Gondwe, Tino akosogea karibu akainama na kutega sikio karibu na mdomo wa bosi wake.

"Usijali kuhusu mimi nitakuwa sawa, nenda kafanye kazi hakikisha yule mtoto Annah anakufa leo hii, anza kumfuatilia mdogo wako Inspekta Aron kwa ukaribu yeye ndiye amemficha yule binti" dokta Gondwe alinong'ona.
"Sawa bosi" alijibu Tino kisha akawa anamsindikiza kwa macho bosi wake akiwa amebebwa juu juu na walinzi wake wakaingia naye ndani ya nyumba.

"Na bado huu ni mwanzo tu mheshimiwa Waziri, nitahakikisha unavuta pumzi ya moto ukiwa hai, huwezi kulala na mke wangu alafu ukaishi kwa amani" alisema Tino huku akitabasamu.

"Umesemaje wewe?" Tino alishitushwa na sauti ya Najma aliyekuwa amesimama nyuma yake, hakuwa amemuona.

"Aah! kwani umesikia nini?" Tino alijibu swali kwa swali akiwa hana uhakika kama Najma ameyasikia maneno yake au laa kwani aliongea kwa sauti ya chini sana.

"Nani atavuta pumzi ya moto au nimesikia vibaya?" aliuliza Najma akitaka kuhakikisha alichokisikia.

"Hapana sijasema hivyo mimi, kwa heri naondoka, muangalie mzee tafadhali" alisema Tino kisha akaondoka zake akimuacha Najma anamsindikiza kwa macho.
"Tino" Najma aliita
Tino aliyekuwa amefika umbali wa kama hatua ishirini hivi alisimama kisha akageuka.
Akawa anamtazama Najma ambaye naye alibaki anamtazama huku sura yake ikionyesha kutokuwa na hata chembe ya masihara.
Tino alinyanyua mabega yake juu ikiwa ni ishara ya kutaka kujua kwa nini amemuita. Licha ya kufanya hivyo lakini bado Najma aliendea kuwa kimya, mwisho akaongea.

"I'll be watching you from today"( nitakuwa nakuangalia kwanzia leo) Najma aliongea kauli yenye utata kisha akaondoka na kuingia ndani.
Tino alibaki amesimama wima, alijaribu kuitafakari kauli hiyo ya Najma yenye ujumbe mzito ndani yake, tayari ilionyesha wazi kuwa Najma ameshaanza kumuhisi vibaya Tino.

"Bado tuna safari ndefu sana mimi na baba yako, bado hata sijapata nachokitaka kwake, Najma ni mapema mno kuingilia utakufa bado mbichi" Tino alijiongeresha mwenyewe kisha akatabasamu na kuondoka zake.

Je nini kitafuata?
Ni kipi hasa Tino anakitafuta hadi kujiweka karibu na Waziri wa afya?
Bado anamsikiliza na kutii amri zake licha ya dkt Gondwe kulala na mke wake...
Vipi kuhusu sakata la Najma na mzee Matula?
Vipi kuhusu Aron, Annah na Big'?
. ITAENDELEA...
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............06
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047

06-(JESCA MALKIA WA NGONO)
ILIPOISHIA...05
"Bado tuna safari ndefu sana ya kwenda mimi na baba yako, bado hata sijapata nachokitaka kwake, Najma ni mapema mno kuingilia utakufa bado mbichi" Tino alijisemea mwenyewe kisha akatabasamu na kuondoka zake.
SASA ENDELEA...
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dokta Gondwe alikuwa amekaa juu ya kitanda chumbani kwake akawa anajaribu kupiga ile namba iliyomtumia picha zake chafu bila mafanikio.

"Huyu mtu kanitumia hizi picha sasa hivi inakuwaje mnasema namba haipooo...!!" Alisema Dokta Gondwe huku akiipigiza simu yake kitandani kwa nguvu.

"Baba, nini shida?" Najma aliuliza akiwa ameingia chumbani kwa baba yake bila taarifa, mkononi akiwa na kopo la dawa.
Dokta Gondwe alibaki anamtazama mwanae asijue ajibu nini, jambo lililokuwa mbele yake lilikuwa ni zito mno. Kwanza kabisa endapo akiruhusu zile picha au video zisambae mitandaoni ilikuwa ni kashfa na skendo kubwa sana ukizingatia yeye ni mtu mkubwa serikalini, Waziri wa afya. Pili mwanamke alielala naye siku hiyo alikuwa ni mke wa mtu tena mke wa kijana wake mwaminifu wa kazi zake haramu yaani Tino hii ilikuwa ni hatari kubwa, alihofu atampoteza Tino lakini pia atampoteza mke wake ambaye kwa sasa alikuwa katika mizunguuko yake nje ya nchi.
"Aibu gani hii" Dokta Gondwe aliwaza

"Haya chukua dawa zako umeze naona hata hutaki kuniambia shida ni nini umekaa kimya tu hata sikuelewi" alisema Najma akionekana kukasirika kiasi
"Sio hivyo mwanangu, hebu kaa hapa nikwambie kitu" Dokta Gondwe aliongea kwa upole akimtaka binti yake akae pembeni yake, Najma akafanya hivyo.

"Unajua nini mwanangu hebu nisikilize baba yako, ukitaka niwe salama matatizo kama haya yasinipate basi kubali kuolewa na Osward mtoto wa Mzee Matula" Dokta Gondwe aliongea kauli iliyomnyong'onyesha Najma.
"Baba una hakika hilo ndilo tatizo linalokusumbua? hakuna kitu kingine? inamaana mzee Matula anakutisha au?"
"Hilo ndio tatizo pekee mwanangu, unajua kabisa ni kiasi gani ile familia ya Mzee Matula ni muhimu kwetu, wao ndio wamenishika mkono tangu nikiwa mkuu wa mkoa mpaka sasa ni Waziri wa afya, nisipofanya kama anavyotaka nitapoteza kila kitu mwanangu, hebu fikiria uchaguzi ni mwakani tu hapa" alieleza dokta Gondwe

"Basi baba sawa nimekuelewa hata usijali, mbona nilisha kubali tangu kitambo hata leo tu naenda kumtembelea Osward kule gerezani, usiwaze baba presha yako itakutesa kama ukiwa hivyo" Najma aliongea akijaribu kumfariji baba yake akaamini suala hilo ndilo lilipelekea presha ya dokta Gondwe kupanda lakini haikuwa hivyo.
Mwisho Najma alitoka nje ya chumba cha baba yake akamuacha dokta Gondwe akihangaika tena kupiga ile namba bila mafanikio.

"Ona natuma meseji hata hazitoki, ni nani huyu unataka kucheza na akili yangu" Dokta Gondwe aliendelea kulalamika
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ndani nyumba moja kubwa iliyojengwa kisasa, nyumba ambayo awali alikuwa akiishi mwanajeshi mstaafu Jenerali Phillipo Kasebele ambaye kwa sasa marehemu.
Katika nyumba hiyo walibaki wakiishi vijana wawili watoto wa marehemu Philipo, wote walikuwa ni wa kiume. Wa kwanza aliitwa Tino na wa pili alikuwa ni Aron.
Tino na Aron waliishi kwa pamoja kama ndugu licha ya kutofautiana sana katika shughuli wanazozifanya. Tino alikuwa ni jambazi anayefanya kazi chini ya Waziri wa afya Dokta Gondwe wakati huo Aron akiwa ni polisi kitengo cha upelelezi ambaye kwa sasa anapambana kwa udi na uvumba kuhakikisha anauangusha mtandao mzima unaofanya kazi na kaka yake Tino.
Baada ya baba yao kufariki siku chache baadae mama yao maarufu kama Madam Sultana aliugua ugonjwa wa ajabu uliomlazimu kulazwa hospitali kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita akiwa hajitambua hata kupumua kwake ilikuwa ni kwa msaada wa mashine.
Gharama za matibabu ya Madam Sultana zilikuwa ni kubwa sana, walilipa si chini ya laki sita kila iitwapo leo. Licha ya serikali kutoa mamilioni ya mchango wa matibabu kwa mama huyo kama heshima ya marehemu mumewe aliyekuwa mwanajeshi lakini bado hali ilikuwa ni tete. Tino na Aron walijikuta wakitoa pesa nyingi sana kuendesha huduma za matibabu ya mama yao pale hospitali ya Mountenia.
Tino akawa anaitumia hii kama sababu ya kuharalisha uharifu wake akidai anafanya hivyo kutafuta pesa kwa ajili ya mama yake. Licha ya Inspekta Aron kumshauri kaka yake mara kadhaa kuachana na shughuli za ujambazi lakini Tino hakuacha, akazidi kufanya mauaji na matukio mengine ya kikatili.
Mwisho uvumilivu ukamshinda Inspekta Aron aliyekula kiapo kulitumikia jeshi la polisi ipasavyo akaamua kulivalia njuga suala hili. Akaweka undugu pembeni na kuanza kutafuta namna ya kumtia hatiani kaka yake Tino. Uadui kati yao ukaongezeka licha ya kuishi ndani ya nyumba moja lakini kila mmoja akawa ni adui mkubwa wa mwenzake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Mchana majira ya saa nane Inspekta Aron alisimamisha gari yake nje ya nyumba yao, alikuwa ametoka Hospitali ya Mountenia kule alikolazwa mama yake lakini pia binti mdogo Annah ambaye alikuwa akitibiwa kwa siri.
Alishuka na kuingia ndani. Ile anakanyaga tu sebureni mara ghafula alikumbatiwa kwa nguvu na mwanamke aliyekuwa anamnyatia kwa siri kutokea nyuma yake.

"Aah shem hebu acha bwana nimeshakukataza hii michezo" Aron alilalamika akionekana kutofurahishwa na kitendo alichokifanya mwanamke huyo ambaye ni mke wa kaka yake Tino aliitwa Jesca. Ndiyo ni Jesca yule yule ambaye amemsaliti mumewe kwa kulala na mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe.

"Aah! shem nae kama nimekumis siruhusiwi kukukumbatia jamani" alisema Jesca huku akilegeza sauti na kurembua macho yake.

"Sawa lakini mazoea kama haya sio mazuri, hata kaka Tino akijua hawezi kufurahia"
"Achana na kaka yako, hapa tupo mimi na wewe"
"Vipi kuna chakula nina njaa sana" Inspekta Aron akabadilisha mada makusudi. Alishamzoea shemeji yake huyo ambaye siku zote alikuwa na vijitabia vya ajabu ajabu isingekuwa msimamo wa Aron basi angelikuwa ashapitanaye.
"Yap! nishapika muda lakini mbona huniambii kama umemkamata huyo kibaka?"
"Usimwite hivyo ni mume wako kumbuka"
"Mume gani wa mchongo, nataka tu akamatwe atuachie uhuru"
"Hapana sijamkamata, ni kweli kile kifaa ulichoweka kwenye koti lake kilitusaidia kujua hadi mahali alipo, niliomba askari wa kunisindikiza kwenda kule ila wakanichelewesha makusudi pale kituoni kuna mtu anatuzunguuka, tulifika kwa kuchelewa"

"Duh! shem jamani kwa hiyo ikawaje"
"Ndio hivyo tulikuta tayari wameshafanya mauaji yaani wamemuua baba mama na mtoto wote kwa pamoja" Aron alidanganya hakutaka kuweka wazi kuwa binti Annah yupo hai.

"Huyu mwanaume laana tupu, usijali shem nipe kifaa kingine nitamuweka tena kwenye nguo yake hadi nihakikishe unamkamata"
"Kwa sasa subiri kwanza shem" alisema Aron huku akitazama simu yake iliyoingia ujumbe mfupi wa maandishi.

"Naondoka baadae"
"Mbona ghafula, alafu vipi kuhusu kula si umesema unanjaa?"
"Baadae, kuna jambo muhimu naenda kufuatilia kule gerezani alipo yule jamaa Osward" alisema Aron, akatoka nje akaingia kwenye gari yake haraka na kuondoka kwa kasi.
Wakati Inspekta Aron anatoka, getini akakutana na gari ya kaka yake akiingia ndani. Wakati magari yao yanapishana pale getini Ndugu hawa wawili walitazamana kwa macho makali kila mmoja akionyesha chuki ya wazi wazi dhidi ya mwenzake. Mwisho wakapishana kila mtu akaenda zake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Mara tu baada ya Inspekta Aron kutoka nje na gari yake, bwana mmoja aliyekuwa amesimamisha pikipiki yake umbali wa hatua kadhaa kutoka kwenye nyumba yao alianza kumfuatilia Inspekta Aron nyuma taratibu. Mtu huyu alikuwa amevalia mavazi meusi kila sehemu kuanzia viatu,suruali,gloves,koti na mzula hata rangi ya ngozi yake pia ilikuwa ni nyeusi tii. Huyu hakuwa mwingine bali BIG' yule bwana wa miraba minne aliyetumwa na Osward wakati ule gerezani kuhakikisha anamuua Inspekta Aron. Sasa alikuwa ameianza kazi yake rasmi. Mgongoni alikuwa amebeba begi kubwa lenye rangi nyeusi pia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Tino alishuka kwenye gari na kukanyaga ardhi nje ya nyumba yao. Akawa anatembea haraka haraka kuelekea ndani huku sura yake ikiwa imekunjamana kwa hasira.
Moyo wa mwanaume huyo ulikuwa umebaba hasira nzito dhidi ya mke wake baada tu ya kuishuhudia ile video ambayo mkewe alikuwa akimsaliti na bosi wake wa kazi mheshimiwa Dokta Gondwe.
Hakuwa amekutana wala kuwasiliana na Jesca mkewe, hii ndio ilikuwa mara yake ya kwanza tangu alipoitazama video ile chafu.

"Mumewangu kipenzi umeru...mamaaaaa!" Alisema Jesca lakini kabla hajamalizia sentensi yake kibao kizito kutoka kwa Tino kilitua kwenye paji lake la uso, kilikuwa ni kibao kizito mno kilichompeleka moja kwa moja sakafuni, damu zikawa zinamtoka puani.

"Una nini wewe mwanamke ni nini unakosa kwangu, kwa nini hata huwazi ikitokea mimi sipo nini kitakupata?" alisema Tino kisha akaingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake akatoa kifaa fulani kidogo cheusi akakitupa sakafuni mbele ya mkewe Jesca.

"Umeniwekea hiki kifaa kwenye koti ili kumsaidia shemeji yako Aron ajue nilipo si ndio? ili iweje? nikifungwa mimi wewe utaishije hapa nyumbani? mama kule hospitali nani atamlipia gharama? Jesca hivi hua hauwazi haya yote kabla ya kufanya upumbafu wako?" Tino aliongea kwa ukali, akaingia chumbani akabalisha koti kisha akatoka tena na kuondoka zake.

Wala hakugusia habari za ile video aliyoiona lakini kwa uzito wa lile kofi alilompiga mkewe ni kofi lililokuwa limebeba hasira zote zikiwa ni pamoja na zile za mke wake kumsaliti.

Akiwa ndani ya gari iliyokuwa ikienda kwa kasi kubwa, Tino alikunja kona na kufunga breki kali pembeni ya barabara. Alitulia kimya akihema kwa nguvu mapigo yake ya moyo yakimuenda mbio.
"Kwa nini? kwa nini umenifanyia hivi Jesca? kwa nini umenisaliti wewe mwanamke?" Tino aliongea kwa jazba akiugulia maumivu makali ya moyo huku akipiga piga usukani kwa mikono yote miwili, alionekana mwenye hasira isiyo na kipimo.

"Tulia Tino tulia, umebakiza hatua chache tu kuiweka Dunia nzima kwenye kiganja cha mkono wako" aliongea Tino akijaribu kujituliza mwenyewe.
Mwisho alituliza akili yake, akachukua simu akapiga namba aliyoihifadhi kwa jina la 'sniper K'

"Vipo mpo tayari....sawa jipangeni tukutane nje ya Hospitali ya Mountenia...leo tunamaliza kila kitu....ndiyo yule binti lazima afe leo...sawa njooni na vifaa vyote muhimu" Tino alimaliza mawasiliano kisha akakata simu, akapiga tena namba nyingine.

"Ee dogo Bosco, mtumie tena Dokta Gondwe kipande cha video yake ya X kama cha dakika moja hivi, mpe vitisho tena kisha upotee hewani kama kawaida..poa...poa" Baada ya mazungumzo hayo Tino akakata simu.
Je nini kitafuata?
Tino anataka kumuua Anna...
Tino anataka kuiweka Dunia kiganjani kwake...
Big anataka kumuua Inspekta Aron...
Inspekta Aron anataka kumlinda Annah...

Hali bado ni tete ndani ya MODERN WAR tukutane sehemu ya 7.

Ofa jipatie season 1 na 2 kwa tsh 1500 tu 0756862047
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(๐˜ƒ๐—ถ๐˜๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐˜€๐—ฎ๐˜€๐—ฎ)
Sehemu ya............07
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
07-(V-COBOS)
ILIPOISHIA....06
"Ee dogo Bosco, mtumie tena Dokta Gondwe kipande cha video yake ya X kama cha dakika moja hivi, mpe vitisho tena kisha upotee hewani kama kawaida..poa...poa" Baada ya mazungumzo hayo Tino akakata simu.

SASA ENDELEA....
[emoji294][emoji294][emoji294]
Aron aliendesha gari kwa mwendo wa kasi sana, dakika kumi na moja pekee zilimtosha kufika lilipo gereza la Kanondo. Hakujua kuwa tangu alipotoka nyumbani nyuma yake kuna mtu alikuwa akimfuatilia kwa lengo la kuyaondoa maisha yake.
Kanondo lilikuwa ni gereza la kawaida lenye wafungwa wachache mno, hata ulinzi wake haukuwa wa kutisha sana. Hii ni kutoka na aina ya wafungwa walikuwa wakiletwa hapo, walikuwa ni wale wenye kesi nyepesi nyepesi. Hapa ndipo walipochagua kumleta Osward mtoto wa tajiri mkubwa na maarufu nchini mzee Matula. Osward alihifadhiwa katika gereza hilo pindi anaposubiria mwenendo wa kesi yake ya mauaji iliyokuwa bado ikiunguruma mahakamani.
Inspekta Aron alipaki gari yake hatua kadhaa kutoka lilipokuwa geti kuu la kuingia ndani ya gereza hilo. Akiwa anajiandaa kushuka mara kwa mbali alimuona mwanamke mmoja mrembo sana anashuka kwenye taxi, akaanza kutembea taratibu naye akielekea kwenye geti kuu la kuingia gerezani.

Aron alimkodorea macho mwanamke huyo ambaye alikuwa na kila sifa ya kuitwa mrembo. Haikuwa mara yake ya kwanza kumuona alishakutana naye si chini ya mara tatu, alimjua vizuri ni Najma mtoto wa Waziri wa afya Mheshimiwa dokta Gondwe.

Akiwa karibu kufika lilipo gari lake, Aron alifungua mlango wa gari na kushuka taratibu, uso kwa uso akawa anatazamana na Najma.

"Ni wewe tena? sitaki maswali yako tafadhali niko bize" Najma aliwahi kuzungumza huku akijifanya mwenye haraka, tayari alishaijua nia ya Inspekta Aron kusimama mbele yake.
"Uko hapa kumtembelea Osward?"
"Yes"
"Najma hebu subiri kidogo basi tuongea"
"Inspekta Aron mbo..."
"Najma watu wanakufa, unajua leo wamekufa wangapi kwa sababu ya kitu unachokificha" Aron aliongea kwa ukali
"Nini? Mimi naficha nini Inspekta? Nilishakwambia sikuwepo wakati yale mauaji yanafanyika, sijui kama Osward aliua au laa! sijui chochote sikuona kwa nini unanilazimisha nikatoe ushahidi ambao sina uhakika nao" Najma naye alifoka.

"Lakini ulifika mapema pale Osward alipofanyia mauaji, nataka kujua angalau nini uliona Najma"
"Una uhakika gani kama nilifika? nikamate na mimi basi ukanihoji"
"Najma usipaniki tafadhali, pengine unaweza kuwa sahihi au umeamua tu kumlinda mpenzi wako Osward lakini kumbuka watu wanakufa, mashahidi wote niliowategemea kwenye kesi hii wanauwawa kikatili, wewe huwazi ni kwa nini? Najma najua unahuruma na utu pia tafadhali naomba fanya kitu ili haki itendeke" Inspekta Aron aliongea kwa hisia sana, maneno hayo kidogo yalionekana kumuingia Najma akawa kimya kwa sekunde kadhaa.

Wakati huo wote Big aliyetumwa kumuua Inspekta Aron alikuwa kwa mbali akisikiliza mazungumzo kati ya Najma na inspekta Aron.
"Huyu Inspekta kweli ni jau! Anakiherehere utadhani ameahidiwa kombe, kifo ndio adhabu pekee anayostahili huyu mbwa" Big alijisemea mwenyewe huku akivua begi lake kubwa na kuliweka juu ya tenki la mafuta la pikipiki.

Baada ya Najma kukaa kimya kwa sekunde kadhaa mwisho aliinua uso wake akamtazama tena Aron usoni.

"Ungekuwa wewe ungefanyaje? Ungekubali kushirikiana na mtu ambaye anataka kuwafunga gerezani baba na mpenzi wako? Hapana siwezi niuwie radhi Inspekta, siwezi" Najma aliongea kisha akaanza kuondoka kulielekea geti la kuingia gerezani.

"Najma.. Najma.. Najma...Na.." Inspekta Aron aliita lakini Najma aliendea kutembea kama vile hamsikii.

Inspekta Aron alibaki amesimama akijikuna kichwani, alishajaribu mara kadhaa kumshawishi Najma akubali kutoa ushahidi lakini jitihada zake siku zote ziligonga mwamba.
Aliwaza ni namna gani atafanikisha kung'oa mizizi ya mtandao wa kiharifu wa Dkt Gondwe ambao ndiyo chanzo cha kaka yake Tino kuharibikiwa.

Aron akiwa bado kwenye dwimbi la mawazo mara kuna askari magereza mmoja alifika na kuingia kwenye gari yake akakaa siti ya nyuma. Aron alishtushwa na mlio wa mlango wa gari ukifungwa ndipo akagutuka na kumchungulia mtu aliyeingia kwenye gari yake. Alimfahamu haraka naye akaingia kwenye gari.

"Enhe! nambie afande ni nini umepata? nimekuja haraka sana mara baada ya kupata ujumbe wako" Aron alianzisha mazungumzo mara tu baada ya kuingia ndani ya gari.
"Umefika tangu mda nimekuona nikashindwa kuja kwa sababu ulikuwa bize na mtoto wa Waziri, vipi umempenda au" alisema yule askari magereza
"Achana na hizo habari ndugu yangu mambo hayako kama unavyodhani nambie nimeitikia wito wako"
"Okay ni hivi, kama ulivyonambia kuwa nikusaidie kufuatilia nyendo za Osward akiwa humu gerezani"
"Mnh"
"Sasa leo tena kunakitu kimetokea, Osward aliitwa na mkuu wa gereza akapewa simu akawa anazungumza na mtu kutoka nje sikujua ni nani ila baadae kama dakika 7 hivi Osward alipata mgeni jamaa fulani hivi jeusi limejazia sana, niliwapiga picha nitakuonyesha" yule afande alianza kutoa maelezo

Wakati wakiendelea na mazungumzo hayo mara ghafula walisikia kishindo kikubwa kutoka ndani gerezani ikifuatiwa na kelele nyingi za watu.
Inspekta Aron na yule afande walitazamana kila mmoja asijue nini kimetokea, kadri muda ulivyokwenda ndivyo makelele yale yalizidi kuongezeka.

"Najma!" Inspekta Aron aliongea kwa sauti ya chini huku akishuka haraka kwenye gari akaanza kukimbia kuelekea ndani ya gereza, akili yake ilihisi moja kwa moja kuwa Najma atakuwa amepeta shida, hakujua hisia hizi zimetoka wapi ghafula, askari magereza naye akawa anamfuata nyuma.
Wote kwa pamoja walikimbia hadi lilipokuwa eneo maalum la watu kuonana na wafungwa pindi wanapowatembelea hapo ndipo kelele zilipotokea
[emoji294][emoji294][emoji294]
Punde tu baada ya Inspekta Aron kuondoka na yule askari magereza, Big alishuka kwenye pikipiki yake taratibu akanyata hadi lilipokuwa gari la Aron.
Alikuwa na kifaa furani mkononi kilichofungwa nyaya kitaalamu sana. akaangaza macho huku na huku hakuna aliyekuwa akimuona.
Taratibu aliinama chini ya uvungu wa gari la Aron akakibandika kile kifaa kisha akabonyeza vitufe fulani kwenye rimoti iliyokuwa mkononi mwake, kile kifaa kikatoa mwanga mwekundu ulioanza kuwaka na kuzima. Hili lilikuwa ni bomu la kutengenezwa kwa mkono, Big alionekana ni mbobezi wa kutengeneza aina hii ya mabomu.

"Kwisha habari yako Aron, ukiingia tu kwenye gari nakugeuza majivu" Alisema Big na hapo akaondoka kurudi ilipokuwa pikipiki yake akiwa na ile rimoti mkononi akawa anamsubiri ndege wake arudi kwenye kiota.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Kama alivyohisi Inspekta Aron ndivyo ilivyokuwa, kulikuwa na ugomvi mkubwa uliotokea kati ya Osward na wafungwa wenzie wawili waliokuja na kumvamia wakati akifanya mazungumzo na Najma.
Osward na wale wafungwa wawili walikuwa wakipigana na kurushiana viti na meza, ugomvi ulikuwa ni mkubwa mno hali iliyowafanya wafungwa waliokuwa upande wa pili kuanza kupiga yowe wakishangilia na hizi ndizo kelele alizozisikia Aron.
Askari walifika na kuzuia ugomvi huo licha ya kwamba kwa kiasi walikuwa wamechelewa lakini angalau waliweza kuwadhibiti.
Punde Inspekta Aron akaingia kwa kasi, aliangaza macho huku na huku ndani ya sekunde kumi tayari aliweza kubaini kilichokuwa kikiendelea.

"Najma" Aron aliita mara baada ya kumuona Najma akiwa amejikunyata kwenye kona moja ya ukuta huku akilia kwa maumivu, alikuwa amejeruhiwa kwenye mguu wake wa kushoto.

Inspekta Aron alikimbia kumfuata pale alipo, akafika na kuchuchumaa mbele yake.
"Vipi uko sawa Najma?"
"Mguu wangu, nimeumia mguu" Najma alilalamika, wakati huo askari wengine walifika kumtazama akiwemo mkuu wa gereza SP Seleman.
Aron alijaribu kuushika mguu wa kushoto wa Najma uliojeruhiwa. Najma akapiga kelele kutokana na maumivu makali aliyoyapata, alikuwa ameumizwa sana

"Hebu mwiteni daktari upesi" alisema SP Seleman
"Haina haja Afande acha nitamchukulia umakini usijali, unamjua huyu ni binti wa Waziri wa afya Dokta Gondwe" Aron alitoa maelekezo akiwa amegeuka kuwatazama askari magereza waliokuwa wamesimama nyuma yake.

"Aaa! Inspekta Aron uko hapa? Umefika saa ngapi mbona hujaja ofisini kwangu?" SP Seleman aliuliza kwa mshangao, alikuwa akifahamiana vizuri na inspekta Aron.
"Ndio naingia mkuu, hebu sogeeni kidogo nipite"alisema Aron huku akimnyanyua Najma akaanza kuondoka naye.

"Nitarudi mkuu ngoja nimuwahishe mtoto wa mheshimiwa hospitali"
"Umekuja na gari yako?"
"Ndiyo ipo nje kule" alijibu Aron Najma akiwa mikononi mwake.
Osward aliyekuwa ameshikiliwa na askari wawili alimtazama Aron kwa macho makali huku akilaumu ni kwa nini Big hajafanya kazi yake mpaka sasa. Hakupendezwa kabisa na kitendo cha Inspekta Aron kumbeba Najma.

Inspekta Aron alitembea taratibu akiwa makini kutoutikisa mguu wa kushoto wa Najma uliojeruhiwa. Baada ya hatua kadhaa aliinama akamtazama Najma usoni, Najma akakwepesha macho yake aliyokuwa ameyagandisha kwa muda mrefu akimtazama mwanaume huyo. Ni dakika chache tu zilikuwa zimepita walitoka kukwaruzana vikali lakini sasa anamtendea ukarimu wa hali ya juu.
Inspekta Aron aliendelea kutembea kuelekea lilipo gari lake bila kujua hatari iliyokuwa mbele yake kwani kulikuwa na bomu limetegeshwa chini ya gari hilo. Yeye aliwaza kumuwahisha Najma hospitali ya Mountenia alikomuacha Annah pia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Waziri wa afya Mheshimiwa dokta Gondwe alikuwa bado chumbani kwake aliendelea kuhangaika na ile namba iliyotumika kumtumia picha zake akiwa faragha na Jesca mke wa Tino.
Mpaka sasa tayari alikuwa ameshatumiwa picha na video nyingine fupi ikimuonyesha alivyokuwa akifurahia penzi na mke wa mtu, mheshimiwa akazidi kuchanganyikiwa.
Kitanda kilikuwa hakilaliki wala kukalika mda wote alikuwa wima anapiga hatua tano mbele tano nyuma. Aliwaza ampigie Waziri mwenzake kitengo cha mawasiliano amsaidie kufanya udukuzi lakini roho ikasita, aliogopa uchafu wake kuonekana.

Mara simu yake ikaita, haraka Dkt Gondwe akaitazama ile namba inayompigia akabaini ilikuwa ni ile ile iliyotumika kutuma zile picha zake chafu WhatsApp, haraka akapokea.

"Ndugu sema kiasi chochote unachotaka mimi nitakupatia sema chochote nitakupa tafadhali usiziweke hizo video mtandaoni nakuomba" dkt Gondwe alianza kujieleza hata kabla ya salamu.
Sauti nzito yenye mwangwi iliyojaa kitetemeshi ilisikika upande wa pili ikimjibu
"Mheshimiwa Waziri hatuhitaji pesa zako, kunakitu kingine tofauti tunakitaka kutoka kwako"
"Nini? ni nini mnataka nitafanya chochote mtakachosema"
"Vizuri sana Dokta, tunachohitaji kutoka kwako ni vimelea vya V-COBOS"
"Nini?" Dkt Gondwe aliuliza kama vile hajasikia alichoambiwa, hakuwa ametegemea kabisa kama angelisikia neno hili kutoka kwa mtu huyo mwenye sauti ya ajabu. Dkt Gondwe alibaki ameduwaa asijue ajibu nini.
Mambo yote haya alikuwa akiyaendesha kijana wake Tino ambaye kwa sasa alikuwa nje ya hospitali ya Mountenia tayari kwa kazi ya kumuua binti Annah kama alivyoagizwa lakini alikuwa anajua kila linaloendelea kwa bosi wake Dkt Gondwe, naam ni Tino mwenyewe ndiye aliyekuwa akitaka vimela vya V-COBOS
[emoji294][emoji294][emoji294]
***********
{TANGAZO:- Epuka matapeli simulizi hii imetungwa na SAUL DAVID simu 0756862047, Tafadhali usinunue kwa mtu mwingine tofauti }
******-*-

Upande wa pili tayari Tino na kikosi cha watu watano walikuwa wamefika nje ya hospitali ya kimataifa ya Mountenia tayari kwa zoezi zima la kuhakikisha wanamuua Annah binti wanayeamini ni shahidi pekee aliyesalia katika kesi ya mauaji inayomkabili Osward mkwe wa bosi wao Dokta Gondwe.
"Tino unauhakika Aron alimleta huyo binti kwenye hii hospitali?" Mmoja kati ya vijana wa Tino aliuliza swali kabla hawajashuka kwenye gari.
"Ndiyo ninao uhakika"
"Lakini mkuu hii hospitali ni kubwa sana ghorofa nne tena inavyumba kibao tutajua vipi mahali wamemficha?"
"Tutajua tu usijali"
"Kivipi Tino tuko wachache tutakagua hospitali nzima? au tuwateke wafanyakazi?"
"Acha maswali mengi, ninao mpango wa kujua ni wapi alipo Annah, wewe fuata maelekezo yangu" Tino aliongea kwa kujiamini.

Je, nini kitafuata?
Tino atafanikiwa kumuua Annah?
Vipi kuhusu Aron na Najma wanaokuja hospitalini hapo lakini gari walilopanda lina bomu chini yake?
Vimelea vya V-COBOS ni kitu gani?
Tino anajua nini kuhusu V-COBOS?
SASA TUNAENDA KUINGIA KWENYE KIINI CHA SIMULIZI YETU, USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

๐˜€๐—ฒ๐—ฎ๐˜€๐—ผ๐—ป 1&2 1500/=
0756862047
 
๐—ง๐—›๐—˜ ๐— ๐—ข๐——๐—˜๐—ฅ๐—ก ๐—ช๐—”๐—ฅ
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........08
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

08-(HOSPITALI YA MOUNTENIA)
ILIPOISHIA....07
Gari waliyopanda Inspekta Aron na Najma mtoto wa Waziri wa afya inabomu chini yake. Wakati huo pia Waziri wa afya anaambiwa alete vimelea vya V-COBOS ili video zake chafu zisisambazwe mtandaoni. Upande wa pili Tino akiwa na kikosi cha watu watano wanajiandaa kuingia hospitali ya kimataifa ya Mountenia kwa ajili ya kumuua Annah ili kufuta ushahidi
Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
[emoji294][emoji294][emoji294]
"Inspekta Aron, Inspekta Aron" Yule askari magereza alikuwa akiita wakati Aron analikaribia gari lake akiwa amembeba Najma.
Inspekta Aron alisimama na punde yule askari alifika karibu yake akasimama na kumnong'oneza kwa sauti ya chini ambayo Najma hakuweza kusikia chochote.

"Hatukumalizana, yule bwana aliyekuja hapa kuongea na Osward nilifanikiwa kumpiga picha nataka nikuonyeshe pengine zinaweza kuwa msaada"
"Ooh sawa lakini mazingira sio rafiki, hebu nitumie hizo picha WhatsApp nitaziangalia baadae" Aron alijibu kwa sauti ya chini pia. Mwisho walikubaliana, Inspekta Aron akaendelea kutembea kwa kasi kuelekea kwenye gari yake

"Usijali Najma utakuwa sawa" alisema Aron wakati akifungua mlango wa nyuma wa gari, akamsaidia Najma kuingia taratibu kisha akafungua mlango.
Wakati huo Big' alikuwa amesimama kwa mbali akiwatazama huku ile rimoti ya bomu alilolitega chini ya gari ya Inspekta Aron ikiwa mikononi mwake.

"Ooh! shit nini tena hiki, yule si Najma?" Big alijiuliza mara baada ya kumuona yule mwanamke aliyebebwa na inspekta Aron
"Yes ni Najma mwenyewe mambo gani tena haya" Big' alijijibu mwenyewe baada ya kuhakikisha yule mwanamke aliyebebwa na Inspekta Aron ni Najma.
Haikuwa rahisi tena kulilipua gari la Inspekta Aron wakati Najma akiwa ndani yake. Lengo ilikuwa ni kumuua Inspekta Aron pekee na sio Najma ambaye ni mpenzi wa aliyemuagiza kazi hiyo yaani Osward.
Wakati Inspekta Aron anaingia kwenye gari tayari kuondoka aligonganisha macho na Big' aliyekuwa amesimama kwa mbali akiwatazama, laiti kama Inspekta Aron angekubali kutazama zile picha kutoka kwa yule askari magereza wakati ule basi zingemsaidia kubaini chochote lakini kwa sasa hakumtilia maanani kabisa bwana Big' mtu hatari anayetaka kuyaondoa maisha yake. Inspekta Aron akaingia kwenye gari akaliwasha na kuanza kuondoka kwa mwendo wa taratibu sana.

"Kwanza Najma kapatwa na nini, kwanini abebwe vile na yule bwege? Nitafanyaje sasa kumuua Aron? Hapa sina jinsi itabidi nitafute nafasi nyingine, nitasubiri mpaka Najma atakaposhuka" Big aliwaza mwisho akawasha pikipiki yake na kuanza kuifuatilia gari ya Inspekta Aron kwa nyuma kama ilivyokuwa mwanzo.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Safari iliendelea kwa mwendo wa wastani kuelekea hospitali ya Mountenia huku ndiko Inspekta Aron alichagua kumpeleka Najma akafanyiwe matibabu kwani alijua atakuwa karibu pia na Annah msichana aliyetakiwa kumlinda kwa udi na uvumba, hakujua tayari Tino na kikosi chake wameshafika eneo la hospitali kwa ajili ya kumuua Annah.
Inspekta Aron na Najma waligeuka mabubu kwa muda wote waliokuwa ndani ya gari kila mtu alikuwa akimuangalia mwenzake kwa macho ya kuibia ibia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Nje ya hospitali ya kimataifa ya Mountenia majadiliano kati ya Tino na kikosi chake yalikuwa yakiendela wakiulizana ni vipi wataweza kukitambua chumba alicholazwa Annah.
"Kivipi Tino tuko wachache tutakagua hospitali nzima? au tuwateke wafanya kazi kisha tuwaulize?"
"Acha maswali mengi, ninao mpango wa kujua ni wapi alipo Annah, wewe fuata maelekezo yangu" Tino aliongea kwa kujiamini.

"Sawa basi tunakusikiliza mkuu"
"Ni kweli hatujui ni wapi Aron kamficha Annah lakini nina uhakika yupo ndani ya hii hospitali, sasa Aron mwenyewe ndiye atakayetupeleka hadi kwenye chumba alichopo Annah"
"Kivipi? tutamteka Inspekta Aron au?"
"Hapana sio hivyo nimewambia ninao mpango ninyi subirini mtaona"
Kikosi kizima kikawa kimya kusikiliza mpango ulivyo, walimuelewa sana Tino alikuwa akifanya mambo yake kwa akili sana na hii ndio sababu aliaminiwa sana na Waziri wa afya Dokta Gondwe.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili kwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe mambo yalikuwa mazito mno, bado mpaka sasa alikuwa hajazunguza chochote mara tu baada ya ile sauti kutoka kwa mtu aliyekuwa anazungumza naye kumwambia wanahitaji vimelea vya V-COBOS. Dokta Gondwe alichoka mwili na akili.

"Najua hukutegemea kusikia kitu kama hiki Dkt Gondwe kwa sababu ni moja kati ya vitu unavyoamini ni siri kubwa lakini kwa sasa huna chaguo lingine, sisi tunahitaji hivyo vimelea vya V-COBOS tunajua unaouwezo wa kutupatia kutoka maabala kuu ya serikali, kama ukishindwa basi kubali kuaibika, tutaziachia hizi video zako za ngono mtandaoni. Tunakupa muda wa kufikiria tutakutafuta tena baadae mheshimiwa" Baada ya maelezo hayo simu ikakatwa
Dokta Gondwe aliitupia simu yake kitandani, macho yake akawa ameyakaza kutazama kabati kubwa la nguo lilikuwa mbele yake, wala presha yake haikupanda kama ilivyokuwa awali.
Dokta Gondwe alijua sasa ni wakati wa mapambano tena makali sana, suala la vimelea vya V-COBOS lilikuwa ni nyeti mno tena lililo chini ya mamlaka ya watu wakubwa kutoka nchini Mexico hawa ndio walioviingiza vimelea hivi kwa siri. Uwepo wa vimelea vya V-COBOS nchini ilikuwa ni siri ya watu wachache sana, hata serikali ilikuwa hailewi chochote.
Alishindwa kuelewa mtu huyu ni nani na kajuaje kuhusu vimelea hivi. Hakujua kama kijana wake Tino ndiye aliyekuwa akichezesha mchezo wote huu, licha ya kwamba alikuwa hospitali ya Mountenia kwa sasa lakini alielewa kila kitu kinachoendelea kwa bosi wake. Tino ndiye haswa aliyekuwa akivitaka vimelea hivyo vya V-COBOS, haikujulikana kaijuaje siri hii licha ya kwamba yupo karibu na mheshimiwa Dkt Gondwe lakini bado haikuwa rahisi kwake kujua.

Dokta Gondwe alisogea hadi lilipo lile kabati akachuchumaa na kufungua droo ya chini kabisa, akapekuwa vitabu vilivyokuwa ndani ya droo hiyo, akatoa kitabu kimoja kikubwa kisha akakifunua. Katika ya kitabu hicho kulikuwa na simu ndogo aina ya Huawei. Dkt Gondwe akaichukua na kubonyeza vitufe kadhaa kisha akaiweka sikioni.

Simu iliita upande wa pili kwa mheshimiwa Profesa Cosmas Kulolwa Rais mstaafu wa awamu iliyopita
[emoji294][emoji294][emoji294]
Akiwa ndio anaingia chumba cha mazoezi Profesa Kulolwa alishituka baada ya simu yake kuita. Kilichomshtua si simu kuita hapana bali aina ya namba iliyompigia alitambua moja kwa moja kuna tatizo, Profesa Kulolwa akapokea simu.

"Nini shida?" Profesa Kulolwa aliuliza kwa sauti ya chini sana huku akiwa ametega sikio lake kwa makini
"Tuko kwenye hatari mkuu" dokta Gondwe alisikika upande wa pili akiongea kwa sauti ya chini vilevile
"Hatari ipi"
"Ni kuhusu vimelea vya V-COBOS"
"Imekuwaje tena? situlikubaliana kikao kinachofuata tukutane nao Ufaransa?"
"Hapana wala tatizo halipo kwao, tatizo tunalo sisi hapa nchini kwetu mkuu, kuna mtu kaingilia mchezo"
"Ooh! Mungu wangu, yanataka kutokea kama yale ya mwaka juzi, hebu naomba tukutane sasa hivi uko nyumbani nikufuate?"
"Hapana nyumbani si salama sana binti yangu Najma alisharudi kutoka Nairobi, tukutane ubarozini"
"Sawa"
"Sawa"
Simu zikakatwa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dakika kumi na sita zilitosha kabisa kumfikisha Inspekta Aron na Najma katika hospitali ya Mountenia. Tangu walipotoka kule Gerezani hakuna aliyekuwa amezungumza na mwenzake zaidi ya kutazamana kwa kuibiana. Hali hii pia ilimshangaza Najma mtoto wa kishua wa mheshimiwa Waziri wa afya ambaye yupo kwenye mtihani mzito wakati huu.
Najma alitamani kuwasiliana na baba yake amtaarifu kuhusu tatizo alilolipata kule gerezani wakati ameenda kumuangalia Osward lakini alisita kutokana na hali aliyonayo baba yake Dokta Gondwe, aliogopa kuifanya presha yake ipande tena.

Wakati Inspekta Aron akielekea sehemu maalum ya kuegesha magari nje ya hospitali ya Mountenia, ghafula roho yake ikafyatuka paa! kuna kitu aliona.
Ndiyo kilikuwa sio kitu cha kawaida, Inspekta Aron aliliona gari la kaka yake Tino likiwa ni moja ya magari yaliyosimama pale nje akajua moja kwa moja kaka yake Tino yupo hapo hospitali ya Mountenia.

"Mungu wangu, Annah! amekuja kumuua Annah" Inspekta Aron alisema kwa sauti ya chini lakini iliyoweza kupenya vizuri kwenye masikio ya Najma
"Vipi kuna nini? mbona hivyo? nani amekuja kuua?" Najma aliuliza maswali mfurulizo lakini Aron hakuwa na mda wa kueleza, alichomoa bastola yake kutoka kiunoni akaikoki kisha akairudisha tena ilipokuwa.

"Nakuja" alisema Aron, akafungua mlango na kutoka nje ya gari kwa kasi akaanza kuelekea lilipokuwa gari la kaka yake Tino. Alipofika akachungulia ndani ya gari akagundua hakuna mtu.

"Yupo ndani" Aron alijisemea mwenyewe na haraka akaanza kukimbia kuelekea mlango mkuu wa kuingia ndani ya hospitali hiyo kubwa ya kimataifa.
Najma aliyashuhudia yote haya akiwa ameachwa mwenyewe ndani ya gari, alishindwa kuelewa ni nini kinaendelea lakini tayari alishajua kuna kitu hakiko sawa. Alitamani kushuka ili aendelee kumfuatilia Inspekta Aron lakini hakuweza bado mguu wake ulikuwa unamuuma sana.

Inspekta Aron alikuwa akikimbia kwa kasi sana, akawa anapishana na wagonjwa pamoja na wahudumu wengine wa hospitali hiyo ambao waligeuka na kumtazama kwa mara ya pili wasijue mwanaume alikuwa kazini. Kwa kasi ile ile Aron alimaliza kupandisha ngazi za ghorofa ya kwanza sasa alikuwa anaelekea ghorofa ya pili.
Dakika nne pekee zikimtosha kufika hadi kilipo chumba cha siri alicholazwa Annah. Alifika na kuwakuta askari wake aliowaacha wakiwa wamesimama imara nje ya kile chumba.

"Anna yuko wapi?" Inspekta Aron aliuliza bila hata kusalimia, askari wake wakatazamana
"Yuko ndani mkuu" alijibu mmoja wa askari wale
Inspekta Aron alisukuma mlango na kuingia ndani kwa kasi macho yake akayatupa kitandani moja kwa moja.

JE, NINI KITAFUATA?
ANNAH YUKO SALAMA?
HIVI VIMELEA VYA V-COBOS NI KITU GANI HASA?
ITAENDELEA...

season 1 &2 Tsh 1500 tu
0756862047
 
Back
Top Bottom