๐ง๐๐ ๐ ๐ข๐๐๐ฅ๐ก ๐ช๐๐ฅ
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............06
Mtunzi: Saul David
Email:
saulstewarty@gmail.com
WhatsApp: 0756862047
06-(JESCA MALKIA WA NGONO)
ILIPOISHIA...05
"Bado tuna safari ndefu sana ya kwenda mimi na baba yako, bado hata sijapata nachokitaka kwake, Najma ni mapema mno kuingilia utakufa bado mbichi" Tino alijisemea mwenyewe kisha akatabasamu na kuondoka zake.
SASA ENDELEA...
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dokta Gondwe alikuwa amekaa juu ya kitanda chumbani kwake akawa anajaribu kupiga ile namba iliyomtumia picha zake chafu bila mafanikio.
"Huyu mtu kanitumia hizi picha sasa hivi inakuwaje mnasema namba haipooo...!!" Alisema Dokta Gondwe huku akiipigiza simu yake kitandani kwa nguvu.
"Baba, nini shida?" Najma aliuliza akiwa ameingia chumbani kwa baba yake bila taarifa, mkononi akiwa na kopo la dawa.
Dokta Gondwe alibaki anamtazama mwanae asijue ajibu nini, jambo lililokuwa mbele yake lilikuwa ni zito mno. Kwanza kabisa endapo akiruhusu zile picha au video zisambae mitandaoni ilikuwa ni kashfa na skendo kubwa sana ukizingatia yeye ni mtu mkubwa serikalini, Waziri wa afya. Pili mwanamke alielala naye siku hiyo alikuwa ni mke wa mtu tena mke wa kijana wake mwaminifu wa kazi zake haramu yaani Tino hii ilikuwa ni hatari kubwa, alihofu atampoteza Tino lakini pia atampoteza mke wake ambaye kwa sasa alikuwa katika mizunguuko yake nje ya nchi.
"Aibu gani hii" Dokta Gondwe aliwaza
"Haya chukua dawa zako umeze naona hata hutaki kuniambia shida ni nini umekaa kimya tu hata sikuelewi" alisema Najma akionekana kukasirika kiasi
"Sio hivyo mwanangu, hebu kaa hapa nikwambie kitu" Dokta Gondwe aliongea kwa upole akimtaka binti yake akae pembeni yake, Najma akafanya hivyo.
"Unajua nini mwanangu hebu nisikilize baba yako, ukitaka niwe salama matatizo kama haya yasinipate basi kubali kuolewa na Osward mtoto wa Mzee Matula" Dokta Gondwe aliongea kauli iliyomnyong'onyesha Najma.
"Baba una hakika hilo ndilo tatizo linalokusumbua? hakuna kitu kingine? inamaana mzee Matula anakutisha au?"
"Hilo ndio tatizo pekee mwanangu, unajua kabisa ni kiasi gani ile familia ya Mzee Matula ni muhimu kwetu, wao ndio wamenishika mkono tangu nikiwa mkuu wa mkoa mpaka sasa ni Waziri wa afya, nisipofanya kama anavyotaka nitapoteza kila kitu mwanangu, hebu fikiria uchaguzi ni mwakani tu hapa" alieleza dokta Gondwe
"Basi baba sawa nimekuelewa hata usijali, mbona nilisha kubali tangu kitambo hata leo tu naenda kumtembelea Osward kule gerezani, usiwaze baba presha yako itakutesa kama ukiwa hivyo" Najma aliongea akijaribu kumfariji baba yake akaamini suala hilo ndilo lilipelekea presha ya dokta Gondwe kupanda lakini haikuwa hivyo.
Mwisho Najma alitoka nje ya chumba cha baba yake akamuacha dokta Gondwe akihangaika tena kupiga ile namba bila mafanikio.
"Ona natuma meseji hata hazitoki, ni nani huyu unataka kucheza na akili yangu" Dokta Gondwe aliendelea kulalamika
[emoji294][emoji294][emoji294]
Ndani nyumba moja kubwa iliyojengwa kisasa, nyumba ambayo awali alikuwa akiishi mwanajeshi mstaafu Jenerali Phillipo Kasebele ambaye kwa sasa marehemu.
Katika nyumba hiyo walibaki wakiishi vijana wawili watoto wa marehemu Philipo, wote walikuwa ni wa kiume. Wa kwanza aliitwa Tino na wa pili alikuwa ni Aron.
Tino na Aron waliishi kwa pamoja kama ndugu licha ya kutofautiana sana katika shughuli wanazozifanya. Tino alikuwa ni jambazi anayefanya kazi chini ya Waziri wa afya Dokta Gondwe wakati huo Aron akiwa ni polisi kitengo cha upelelezi ambaye kwa sasa anapambana kwa udi na uvumba kuhakikisha anauangusha mtandao mzima unaofanya kazi na kaka yake Tino.
Baada ya baba yao kufariki siku chache baadae mama yao maarufu kama Madam Sultana aliugua ugonjwa wa ajabu uliomlazimu kulazwa hospitali kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita akiwa hajitambua hata kupumua kwake ilikuwa ni kwa msaada wa mashine.
Gharama za matibabu ya Madam Sultana zilikuwa ni kubwa sana, walilipa si chini ya laki sita kila iitwapo leo. Licha ya serikali kutoa mamilioni ya mchango wa matibabu kwa mama huyo kama heshima ya marehemu mumewe aliyekuwa mwanajeshi lakini bado hali ilikuwa ni tete. Tino na Aron walijikuta wakitoa pesa nyingi sana kuendesha huduma za matibabu ya mama yao pale hospitali ya Mountenia.
Tino akawa anaitumia hii kama sababu ya kuharalisha uharifu wake akidai anafanya hivyo kutafuta pesa kwa ajili ya mama yake. Licha ya Inspekta Aron kumshauri kaka yake mara kadhaa kuachana na shughuli za ujambazi lakini Tino hakuacha, akazidi kufanya mauaji na matukio mengine ya kikatili.
Mwisho uvumilivu ukamshinda Inspekta Aron aliyekula kiapo kulitumikia jeshi la polisi ipasavyo akaamua kulivalia njuga suala hili. Akaweka undugu pembeni na kuanza kutafuta namna ya kumtia hatiani kaka yake Tino. Uadui kati yao ukaongezeka licha ya kuishi ndani ya nyumba moja lakini kila mmoja akawa ni adui mkubwa wa mwenzake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Mchana majira ya saa nane Inspekta Aron alisimamisha gari yake nje ya nyumba yao, alikuwa ametoka Hospitali ya Mountenia kule alikolazwa mama yake lakini pia binti mdogo Annah ambaye alikuwa akitibiwa kwa siri.
Alishuka na kuingia ndani. Ile anakanyaga tu sebureni mara ghafula alikumbatiwa kwa nguvu na mwanamke aliyekuwa anamnyatia kwa siri kutokea nyuma yake.
"Aah shem hebu acha bwana nimeshakukataza hii michezo" Aron alilalamika akionekana kutofurahishwa na kitendo alichokifanya mwanamke huyo ambaye ni mke wa kaka yake Tino aliitwa Jesca. Ndiyo ni Jesca yule yule ambaye amemsaliti mumewe kwa kulala na mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe.
"Aah! shem nae kama nimekumis siruhusiwi kukukumbatia jamani" alisema Jesca huku akilegeza sauti na kurembua macho yake.
"Sawa lakini mazoea kama haya sio mazuri, hata kaka Tino akijua hawezi kufurahia"
"Achana na kaka yako, hapa tupo mimi na wewe"
"Vipi kuna chakula nina njaa sana" Inspekta Aron akabadilisha mada makusudi. Alishamzoea shemeji yake huyo ambaye siku zote alikuwa na vijitabia vya ajabu ajabu isingekuwa msimamo wa Aron basi angelikuwa ashapitanaye.
"Yap! nishapika muda lakini mbona huniambii kama umemkamata huyo kibaka?"
"Usimwite hivyo ni mume wako kumbuka"
"Mume gani wa mchongo, nataka tu akamatwe atuachie uhuru"
"Hapana sijamkamata, ni kweli kile kifaa ulichoweka kwenye koti lake kilitusaidia kujua hadi mahali alipo, niliomba askari wa kunisindikiza kwenda kule ila wakanichelewesha makusudi pale kituoni kuna mtu anatuzunguuka, tulifika kwa kuchelewa"
"Duh! shem jamani kwa hiyo ikawaje"
"Ndio hivyo tulikuta tayari wameshafanya mauaji yaani wamemuua baba mama na mtoto wote kwa pamoja" Aron alidanganya hakutaka kuweka wazi kuwa binti Annah yupo hai.
"Huyu mwanaume laana tupu, usijali shem nipe kifaa kingine nitamuweka tena kwenye nguo yake hadi nihakikishe unamkamata"
"Kwa sasa subiri kwanza shem" alisema Aron huku akitazama simu yake iliyoingia ujumbe mfupi wa maandishi.
"Naondoka baadae"
"Mbona ghafula, alafu vipi kuhusu kula si umesema unanjaa?"
"Baadae, kuna jambo muhimu naenda kufuatilia kule gerezani alipo yule jamaa Osward" alisema Aron, akatoka nje akaingia kwenye gari yake haraka na kuondoka kwa kasi.
Wakati Inspekta Aron anatoka, getini akakutana na gari ya kaka yake akiingia ndani. Wakati magari yao yanapishana pale getini Ndugu hawa wawili walitazamana kwa macho makali kila mmoja akionyesha chuki ya wazi wazi dhidi ya mwenzake. Mwisho wakapishana kila mtu akaenda zake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Mara tu baada ya Inspekta Aron kutoka nje na gari yake, bwana mmoja aliyekuwa amesimamisha pikipiki yake umbali wa hatua kadhaa kutoka kwenye nyumba yao alianza kumfuatilia Inspekta Aron nyuma taratibu. Mtu huyu alikuwa amevalia mavazi meusi kila sehemu kuanzia viatu,suruali,gloves,koti na mzula hata rangi ya ngozi yake pia ilikuwa ni nyeusi tii. Huyu hakuwa mwingine bali BIG' yule bwana wa miraba minne aliyetumwa na Osward wakati ule gerezani kuhakikisha anamuua Inspekta Aron. Sasa alikuwa ameianza kazi yake rasmi. Mgongoni alikuwa amebeba begi kubwa lenye rangi nyeusi pia.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Tino alishuka kwenye gari na kukanyaga ardhi nje ya nyumba yao. Akawa anatembea haraka haraka kuelekea ndani huku sura yake ikiwa imekunjamana kwa hasira.
Moyo wa mwanaume huyo ulikuwa umebaba hasira nzito dhidi ya mke wake baada tu ya kuishuhudia ile video ambayo mkewe alikuwa akimsaliti na bosi wake wa kazi mheshimiwa Dokta Gondwe.
Hakuwa amekutana wala kuwasiliana na Jesca mkewe, hii ndio ilikuwa mara yake ya kwanza tangu alipoitazama video ile chafu.
"Mumewangu kipenzi umeru...mamaaaaa!" Alisema Jesca lakini kabla hajamalizia sentensi yake kibao kizito kutoka kwa Tino kilitua kwenye paji lake la uso, kilikuwa ni kibao kizito mno kilichompeleka moja kwa moja sakafuni, damu zikawa zinamtoka puani.
"Una nini wewe mwanamke ni nini unakosa kwangu, kwa nini hata huwazi ikitokea mimi sipo nini kitakupata?" alisema Tino kisha akaingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake akatoa kifaa fulani kidogo cheusi akakitupa sakafuni mbele ya mkewe Jesca.
"Umeniwekea hiki kifaa kwenye koti ili kumsaidia shemeji yako Aron ajue nilipo si ndio? ili iweje? nikifungwa mimi wewe utaishije hapa nyumbani? mama kule hospitali nani atamlipia gharama? Jesca hivi hua hauwazi haya yote kabla ya kufanya upumbafu wako?" Tino aliongea kwa ukali, akaingia chumbani akabalisha koti kisha akatoka tena na kuondoka zake.
Wala hakugusia habari za ile video aliyoiona lakini kwa uzito wa lile kofi alilompiga mkewe ni kofi lililokuwa limebeba hasira zote zikiwa ni pamoja na zile za mke wake kumsaliti.
Akiwa ndani ya gari iliyokuwa ikienda kwa kasi kubwa, Tino alikunja kona na kufunga breki kali pembeni ya barabara. Alitulia kimya akihema kwa nguvu mapigo yake ya moyo yakimuenda mbio.
"Kwa nini? kwa nini umenifanyia hivi Jesca? kwa nini umenisaliti wewe mwanamke?" Tino aliongea kwa jazba akiugulia maumivu makali ya moyo huku akipiga piga usukani kwa mikono yote miwili, alionekana mwenye hasira isiyo na kipimo.
"Tulia Tino tulia, umebakiza hatua chache tu kuiweka Dunia nzima kwenye kiganja cha mkono wako" aliongea Tino akijaribu kujituliza mwenyewe.
Mwisho alituliza akili yake, akachukua simu akapiga namba aliyoihifadhi kwa jina la 'sniper K'
"Vipo mpo tayari....sawa jipangeni tukutane nje ya Hospitali ya Mountenia...leo tunamaliza kila kitu....ndiyo yule binti lazima afe leo...sawa njooni na vifaa vyote muhimu" Tino alimaliza mawasiliano kisha akakata simu, akapiga tena namba nyingine.
"Ee dogo Bosco, mtumie tena Dokta Gondwe kipande cha video yake ya X kama cha dakika moja hivi, mpe vitisho tena kisha upotee hewani kama kawaida..poa...poa" Baada ya mazungumzo hayo Tino akakata simu.
Je nini kitafuata?
Tino anataka kumuua Anna...
Tino anataka kuiweka Dunia kiganjani kwake...
Big anataka kumuua Inspekta Aron...
Inspekta Aron anataka kumlinda Annah...
Hali bado ni tete ndani ya MODERN WAR tukutane sehemu ya 7.
Ofa jipatie season 1 na 2 kwa tsh 1500 tu 0756862047