Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

THE MODERN WAR
(vita ya kisasa)
Sehemu ya................15
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Ee nambie dogo umeshapata aina ya boti ninayoihitaji?....sawa..kazi nzuri...haya mkapumzike sasa tuonane asubuhi kambini...ndiyo Godwin naye ameshakamilisha kazi yake hivi ndio nimetoka kumchukua....sawa" Tino alimaliza maongezi kisha akakata simu na kuongeza mwendo wa gari yake. Upande wa pili ndani ya chumba alichokuwa Annah, damu ilionekana ikiwa imetapakaa kila kona.

SASA ENDELEA...
Usiku ule Tino na kikosi chake kinachofanya kazi chini ya Dokta Gondwe walirudi kambini kwao wakiamini mambo yote yamekwenda shwari, tayari Godwin aliwahakikishia kuwa amemtwanga Annah risasi ya kichwa kwa sasa ni marehemu, wote wakaamini hivyo.
Lakini upande wa pili ndani ya hospitali ya kimataifa ya Mountenia mambo yalikuwa ni tofauti kabisa na maelezo ya Godwin, ni kweli ndani ya chumba alichokuwa amelazwa Annah kwa mara ya kwanza kabla ya kuhamishwa kuna mwili wa mtu ulionekana ukiwa umelala sakafuni huku damu nyingi ikiwa imetepakaa kuuzunguuka mwili huo lakini haukuwa mwili wa Annah, je ni nini kilitokea?... Ilikuwa hivi.

MASAA MATATU (3) KABLA....
Wakati ule Inspekta Aron amefunika pazia la madirisha katikati chumba alicholazwa Annah hii ilimfanya Godwin(sniper G') kushindwa kuifanyia kazi yake maana hakuweza tena kuona kinachoendelea ndani ya kile chumba. Hata hivyo bunduki ile ya masafa marefu aliyoitumia Godwin ilikuwa ni bora sana kwani baada ya Inspekta Aron kufunika pazia Godwin alibadilisha lenzi ya bunduki yake akaweka lenzi nyingine ambayo ilikuwa na uwezo wa kupenya hadi ndani licha ya kwamba kulikuwa na kizuizi cha mapazia. Tofauti na lenzi nyingine lenzi hiyo haikuwa na uwezo wa kuonyesha sura ya mtu au kitu kwa uharisia wake, kila kitu/mtu kilionekana cha kijani.
Godwin aliweza kutofautisha huyu ni mtu na hiki ni kitu kutokana na umbo pamoja na mijongeo ya hapa na pale.
Kwa maana hiyo Godwin alikuwa na uwezo wa kuona kila kilichoendelea mle ndani lakini hakuweza kutofautisha kuwa huyu ni Annah huyu ni Inspekta Aron huyu ni Jada au huyu ni Dokta Zyunga hali hii ikafanya kazi yake kuwa ngumu kwani wakati huo watu walikuwa wakiingia na kutoka ndani ya chumba kile.

Kuliko kufanya kazi kwa kubahatisha Godwin aliona ni vema atulie hadi pale Annah atakapobaki peke yake mle ndani. Hakujua kuwa ile mitembeo ya hapa na pale ndani ya chumba cha Annah ilikuwa ni katika harakati za kumuhamisha, Godwin hakujua hilo badala yake akapumzika kitandani kusubiri wakati mwingine
[emoji294][emoji294][emoji294]
Ikiwa ni majira ya saa tano usiku Big' alionekana akinyata kuelekea chumba alichokuwa amelazwa Annah awali. Kwa kuwa alisikia mazungumzo ya Inspekta Aron na Inspekta Jada ambao walikubaliana kuwa Aron ndiye atakayebaki usiku huo kumilinda Annah aliamini hiyo ndio itakayokuwa nafasi ya kumuua Inspekta Aron baada ya kunusurika kwenye lile bomu. Kwa bahati mbaya Big' hakuzisikia habari za Annah kuhamishwa chumba hivyo akaamini kabisa lazima Inspekta Aron atakuwa maeneo hayo kama sio nje basi ndani ya chumba cha Annah.

Baada ya kuhakikisha nje hakuna mtu, taratibu Big' alinyata hadi mlangoni, akanyonga kitasa mlango ulikuwa wazi akafungua taratibu na kuingia huku bastola yake ikiwa mbele tayari kwa lolote.
Aliangaza macho huku na huku hakuona mtu, kilichomshtua zaidi hata yule mgonjwa aliyesikia kuwa Inspekta Aron anamlinda hakuwepo kitandani.
Big' alihisi pengine Inspekta Aron ameshtukia na kumuweka mtego, akaongea umakini. Akakagua chooni na bafuni lakini bado hakuona mtu. Kwa mara nyingine Big' akaona kabisa kuna kila dalili ya kumkosa Inspekta Aron. Aliuma meno kwa hasira huku akijipigapiga kichwani

"Kaenda wapi huyu mjingaaa" Big' alilalamika na kujitupa kitandani kwa hasira, akalala chali macho yake yakitazama paa la chumba hicho.
Akiwa bado amejilaza pale kitandani Big' aliwaza ni vipi ataweza kumpata Inspekta Aron ilikuwa ni lazima ahakikishe anamuua usiku huo hivyo ndivyo alivyomuahidi Osward.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Majira hayo hayo Godwin (sniper G') alikurupuka usingizini akachukua simu yake na kutazama saa ilikuwa ni saa sita kasoro usiku. Kulikuwa pia na ujumbe wa maandishi kutoka kwa Tino, akaufungua upesi na kuusoma.

,,,,,,,,,Vipi? Umeshamuua huyo mwanamke? Ukimaliza kazi niite upesi nije nikuchukue,,,,,,,,,
Baada ya Godwin kumaliza kuusoma ujumbe huo haraka akasogea karibu na bunduki yake ya masafa marefu, akaweka shabaha yake kuelekea chumba cha Annah kama kawaida. Bado pazia lilikuwa limefungwa lakini ile lenzi ya bunduki yake ilimuwezesha kuona kila kitu ndani.
Kulikuwa kimya kabisa wala hakuna mtu yeyote aliyemuona. Godwin akaamini kuwa wakati huo ni lazima Annah atakuwa amelala.

"Siwezi kusubiri hadi asubuhi, Tino hatanielewa kabisa" aliwaza Godwin huku akipiga mahesabu ya haraka haraka nini afanye, mwisho akapata wazo.
Godwin aliwaza apige risasi ya kwanza itakayopasua kioo na kumfanya Annah ashtuke, akijichanganya kuinuka basi hapo atapata wasaa mzuri wa kulenga shabaha na kumtwanga risasi ya kichwa.
Hivyo ndivyo alivyofanya Godwin, akafyatua risasi ya kwanza ambayo ilisafiri na kwenda kupiga kioo cha dirisha la chumba alichokuwa Annah kikapasuka, sasa akawa anasubiri matokeo kama Annah atashtuka na kuinuka pale kitandani au laa!
[emoji294][emoji294][emoji294]

Big' aliyekuwa bado amelala kitandani ndani ya chumba alichokuwepo Annah awali alishtushwa na mlio wa kioo cha dirisha kikipasuka ghafula.
Big' alitoa macho kwa mshangao na kukurupuka pale kitandani kwa kasi akasimama na kuishika bastola yake vizuri, akawa anaangaza macho huku na huku, tayari alishahisi hali ya hatari.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ni kweli kama alivyowaza Godwin ndivyo ilivyokuwa kwani sekunde chache baadae aliona mtu alikurupuka kwa kasi pale kitandani.

"Kwisha habari yako Annah" alisema Godwin huku akiweka shabaha yake vizuri na kuielekeza kwenye kichwa cha yule mtu aliyeamini kuwa ni Annah. Bahati mbaya kwake lenzi ya bunduki yake ilikuwa haiwezi kuonyesha sura ya mtu kutokana na kizuizi cha lile pazia dirishani, laiti kama angeweza kuona angegundua moja kwa moja kuwa yule ni mtu mwingine wala si Annah aliyemdhania.

Bila kupoteza muda Godwin alifyatua risasi iliyoenda moja kwa moja na kuzama kwenye kichwa cha Big' ikatokea upande wa pili. Big' alianguka chini kama gunia,akawa anarusha rusha miguu huku damu ikimtoka kwa wingi,ndani ya sekunde 30 akakata roho.

Haraka Godwin alijibu ujumbe wa Tino akamtaka aje amchukue, kisha haraka haraka akaifungua bunduki yake na kuipanga vizuri kwenye begi. Akaweka mazingira sawa kuhakikisha haachi ushahidi wowote baada ya hapo akatoka hadi nje ya Hoteli hiyo ambako alikuta tayari Tino ameshafika anamsubiri.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, aliyeuwawa hakuwa ana bali Big' rafiki kipenzi wa Osward.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Saa saba usiku Inspekta Aron alikuwa macho akizunguuka zunguuka kuangalia usalama wa kile chumba kipya alichohamia Annah kwa sasa, wala hakujua kuhusu mauji yalitokea chumba kile cha kwanza, hakuna aliyejua.
Chumba hiki kipya kilikuwa upande wa pili kutoka vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) ambako huko ndiko mama yake mzazi na Aron(Sultana) alikuwa amelezwa kwa zaidi ya miezi sita akiwa hajitambua.

Wakati inspekta Aron akizunguuka zunguuka alipata wazo akajisikia kunyoosha miguu hadi kule ICU alikolazwa mama yake akatamani kwenda kumuona, akafanya hivyo.
Alitembea taratibu huku akikumbuka mambo kadha wa kadha yaliyotokea siku hiyo, hapo akajikuta anatabasamu mara baada ya kumkumbuka Najma binti wa Waziri kuu, mwanamke aliyezoeana naye ndani ya mda mfupi sana bila kujali alikuwa na uadui mkubwa na baba mzazi wa binti huyo yaani Dokta Gondwe.
Inspekta Aron akiwa amekaribia kukifikia chumba cha mama yake mara alisikia mchakacho nyuma yake haraka akageuka kutazama lakini hakuona kitu hali ilikuwa shwari kabisa.
Ndani ya zile sekunde chache ambazo Aron aligeuka nyuma mara alionekana mtu aliyevaa mavazi meusi juu mpaka chini akitembea upesi kutokea ndani ya chumba cha mama yake Aron akafungua mlango taratibu akatoka na kuufunga kisha akapotea kama upepo.
Tukio lile lilifanyika ndani ya sekunde chache hii ilionyesha wazi kuwa mtu huyo alikuwa ni mtaalamu haswa, alitembea hata bila vishindo vya nyayo zake kusikia. Inspekta Aron alipotazama mbele tayari mtu huyo alishatoweka kitambo wala Aron hakuhisi chochote.
Inspekta Aron alisogea hadi mbele ya mlango wa chumba cha mama yake, akatazama ndani na kuhakikisha kila kitu kilikuwa sawa mama yake alikuwa amelala huku zile mashine za kumsaidia kupumua zikiendelea kufanya kazi kama kawaida. Aron aliondoka kurudi kwa Annah upesi ule mchakacho aliousikia mwanzo ulimfanya ahisi pengine kuna hatari lakini baada ya kufika alibaini hakuna hatari yoyote hali ilikuwa shwari kabisa
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dakika chache baadae ya Inspekta Aron kuondoka, yule mtu mwenye mavazi meusi alirudi tena akinyata taratibu akaingia ndani ya chumba alicholazwa mama Aron na kufungua mlango.
Alikuwa ni mwanaume mwembamba mrefu, sura yake ilikuwa ameificha kwa kufunika kitambaa cheusi na kuacha sehemu ya macho pekee, kichwani alivaa kofia nyeusi pia, kila kitu kwake kilikuwa cheusi. Alipiga hatua taratibu akasimama mbele ya kitanda cha mama Aron.
"Sultana ni mimi Shadow nimerudi" alisema yule mwanaume
Katika hali ya kushangaza mama Aron ambaye tunaamini alikuwa ni mgonjwa mahututi aliyelazwa akiwa hajitambua kwa zaidi ya miezi sita alionekana akiinuka huku akivitoa vile vifaa vya kupumulia na kuviweka pembeni, akainuka na kushusha miguu chini ya kitanda. Mama Aron alionekana ni mzima tena mzima mwenye afya tele.

"Shadow" mama Aron (sultana) aliita
"Naam Sultana" Shadow aliitika huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini kwa heshima
"Alikuwa ni nani huyo?" Aliuliza Sultana
"Alikuwa ni Inspekta Aron, mwanao"
"Aron? anafanya nini hapa hospitali usiku huu?"
"Nafikiri atakuwa anamlinda yule binti Annah niliyekwambia" alieleza Shadow
"Sasa kwa nini Dokta hajaniambia"
"Sijajua Sultana pengine na yeye hana taarifa kuwa Inspekta Aron yuko hapa" kimya kikatawala kwa sekunde kadhaa kisha Sultana akaongea.
"Enhe! nipe ripoti yangu haraka uondoke"
"Sultana, kesho ndio siku yetu ambayo pengine tunaweza kupata kitu tunachokitafuta kwa kipindi kirefu"
"Kweli? Unamaana gani shadow"
"Nimefuatilia nyendo zote za Tino, kesho ndio siku anakwenda kukabidhiana Vimelea vya V-COBOS na Waziri Dokta Gondwe"
"Hahahah!! sikutegemea kama itakuwa mapema hivi, kwani nini kimetokea?" Alisema Sultana huku akishuka kitandani, akasimama na kupiga hatua akasogea dirishani, akawa anaongea huku akitabasamu.

"Tino, Tino mwanangu hatimaye nitakwenda kuchukua vimelea vya V-COBOS kutoka kwenye mikono yako mwenyewe, huwezi kushindana na mimi wewe ni mwanangu nimewahi kuliona jua kabla yako. Najua umekuwa unatamani sana niamke ili uniulize maswali ambayo huna majibu yake kisha uniuwe kama ulivyomuua baba yako Jenerali Phillipo Kasebele. Unatumia pesa nyingi ili kuhakikisha napona na baadae nikwambie kile nachokijua kuhusu vimelea vya V-COBOS, huwezi Tino huwezi kushindana na mimi kijana wangu. Hii ni siri ambayo baba yako aliilinda kwa miaka mingi hata hao wazungu wa Dokta Gondwe kutoka Mexico hawajui chochote mpaka sasa, hahahah, mimi pekee ndiye nitakayeigeuza Dunia hii juu chini chini juu...." Sultana aliongea kwa kujiamini kisha akageuka kwa kasi kumtazama kijana wake mashuhuri, Shadow.
"Wanakutana wapi?"
"Habarini, watakuwa na boti"
"Sawa najua hakuna kitakacho kushinda hakikisha hivyo vimelea vya V-COBOS unavileta hapa sawa Shadow"
"Haina shida Sultana"
Alijibu Shadow kisha akaondoka, akimuacha Sultana ambaye alirudi na kupanda kitandani kisha akarudisha ile maski na vifaa vingine vinavyomsaidia kupumua kama awali.

JE NI NINI KILITOKEA? NI KWELI TINO ALIMUUA BABA YAKE? KWA NINI?
ILIKUAJE?
NI IPI MIPANGO YA SULTANA?
DOKTA GONDWE, RAIS MSTAAFU NA WALE WAZUNGU WATAFANYA NINI?
NINI KITATOKEA KWA ARON, OSWARD, NAJMA NA ANNAH?

TUMEMALIZA MSIMU WA KWANZA (SEASON 1) YA SIMULIZI HII KARIBU MSIMU WA PILI AMBAO TUNAKWENDA KUICHIMBA SIMULIZI HII KUJUA MBIVU NA MBICHI, NAAM HII NI MODERN WAR (vita ya kisasa).

Bila kusahau kwa wale waliolipia season 2 na 4 zipo tayari

WhatsApp 0756862047
 
Loading...
0756862047
FB_IMG_1660991488346.jpg
 
𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐍 𝐖𝐀𝐑
(vita ya kisasa)
Sehemu ya...............16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

16-(MAABARA YA ZMLST)
ILIPOISHIA (msimu wa kwanza)...
Sultana (Mama Aron) ambaye tuliamini ni mgonjwa mahututi aliyelazwa akiwa hajitambua kwa zaidi ya miezi sita mfurulizo anainuka kitandani akiwa ni mzima wa afya. Kumbe kwa kipindi chote alikuwa akiigiza kujifanya ni mgonjwa. Sultana anafanya mazungumzo na kijana wake wa siri anayemtumia siku zote anaitwa Shadow akimtaka ahakikishe anavileta vimelea vya V-COBOS mikononi mwake

Je, nini kitafuata?

TURUDI NYUMA MIAKA KUMI (10) ILIYOPITA.
MEXICO
Ndani ya nchi ya Mexico katikati ya mji maarufu wa Ciudad Juárez ndipo tunaikuta Maabara ya sayansi na teknolojia inayojulikana kwa jina la ZIVEMIC MEDICAL LABORATORY SCIENCE AND TECHNOLOGY - (ZMLST). Hii ilikuwa ni maabara kubwa na maarufu sana Duniani, kama ukitaja maabara za sayansi na teknolojia kumi bora ulimwenguni basi usinge acha kuitaja ZMLST.
ZMLST kama zilivyo maabara nyingine Duniani kote ilikuwa ikijihusisha sana na masuala ya utafiti wa magonjwa mapya yanayoibuka hasa haya ya mripuko, kuchunguza na kubaini chanzo, aina ya kimelea husika kama ni bakteria au kirusi kisha wanamaliza kwa kutengeneza kinga au dawa. Hivyo ndivyo namna maabara ya ZMLST ilivyofanya kazi.
Maabara hii ilikuwa ni kongwe kuliko maabara nyingine zote unazozifahamu lakini ukongwe wake haukuifanya ZMLST kuwa maabara bora kuliko nyingine.
Maabara nyingine kubwa zenye teknolojia ya kisasa zilikuwa zikiibuka kila iitwapo leo hali iliyopelekea ZMLST kuanza kupotea kwenye midomo ya watu, taratibu hata tenda zikaanza kupungua.
Kwa miaka mitatu mfurulizo ZMLST ikajikuta inaporomoka kwa kasi na kupoteza sifa yake kabisa, kila walipojaribu kuirudisha katika hadhi yake ya awali ilishindikana ushindani ulikuwa ni mkubwa mno.
Mwisho umaarufu wa ZMLST ukapotea na kubaki jina tu. Wanasayansi wakubwa ulimwenguni waliokuwa wakishikiriwa na maabara hii kama Dr Alain Aspeco, Prof David Baltimore, Allen Bard, Eng Timothy Berners na wengine wengi walianza kuchomoka mmoja baada ya mwingine wakihamia kampuni nyingine na baadae wakaisha wote, hali ikazidi kuwa tete
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Now it's time to use our weapon"(sasa ni wakati wa kutumia siraha yetu)
Hii ilikuwa ni kauli ya mkurugenzi mtendaji wa ZMLST Profesa Fernando Arturo ambaye pia ni mmoja kati ya waanzilishi wa ZMLST, alisema hivi akiwa amekaa kikao cha dharula na wafanyakizi waandamizi wa ZMLST. Mbele ya Profesa Fernando kulikuwa na begi dogo juu ya meza lililokuwa na muundo kama boksi hivi.
Profesa Fernando mwenye asili ya kituruki alifungua lile begi kuwaonyesha watu wake kitu kilichokuwa ndani. Wote walitazama na kushuhudia chupa mbili zilizohifadhiwa kwenye chemba mbili maalum ndani ya sanduku hilo. Chupa moja ikiwa na rangi ya kijani na nyingine ikiwa na rangi ya kijivu.

"Now it's time to show the whole world how powerful ZMLST is. We are going to spread these COBOS viruses in Africa and later around the World"( Ni muda wa kuionyesha Dunia ni jinsi gani ZMLST inanguvu, tunakwenda kusambaza hivi virusi vya COBOS Africa na baadae Dunia nzima)
Profesa Fernando aliongea kwa kumaanisha, akatulia kwa muda kisha akaendelea kuongea.

"We are the only ones who will be able to provide vaccine and cure against this deadly COBOS virus. This green bottle contains the COBOS virus and this gray bottle carries a cure/vacinne against it"( Ni sisi pekee ndio kutakaoweza kutengeneza chanjo na tiba dhidi ya kirusi hiki hatari cha COBOS. Hii chupa ya kijani imebeba virusi vya COBOS na hii chupa ya kijivu imebeba tiba/kinga yake)
Profesa Fernando alitulia tena kwa muda kuhakikisha kama maneno anayoyazungumza yanawaingia vizuri watu wake ambao wote walikuwa wakitikisa vichwa vyao wakionekana kwenda sambamba na kukubaliana na maelezo ya Profesa Fernando, akaendelea kuzungumza.
"Through this initiative we will not only make billions of money but we will also restore the dignity and status of our laboratory that was lost for many years. The important thing right now is to choose one country in Africa that will be our starting point. We will persuade some key leaders to join our initiative" (kupitia mpango huu si tu kutengeneza mabilioni ya pesa bali tutarudisha heshima na hadhi ya maabara yetu iliyopotea kwa miaka mingi. Kitu muhimu kwa sasa ni kuchagua nchi moja huko Africa ambayo itakuwa kama sehemu yetu ya kuanzia. Tutawashawishi baadhi ya viongozi muhimu waingie kwenye mpango wetu)
Alieleza Profesa Fernando.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa miezi michache baadae kila kitu kikawa kimekamilika Nchi husika Africa ikapatikana na baadhi ya viongozi muhimu wakaingizwa moja kwa moja kwenye mpango huu huku wakipewa kiwango kikubwa cha pesa na kuhakikishiwa usalama wao na ndugu zao kwani tiba na kinga ya virusi vya COBOS ilikuwepo.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Timu ya wazungu wanne(4) kutoka Mexico iliwasili nchini wakijifanya watalii ambao walipata mualiko rasmi hadi ikulu kwa Rais wa awamu hiyo Profesa Cosmas Kulolwa ambaye alikuwa ni mmoja kati ya viongozi waliopo kwenye mpango wa kuingizwa kwa virusi vya COBOS nchini. Viongozi wengine wa nchi walioshiriki alikuwepo Waziri wa afya Mheshimiwa dokta Isaack Gondwe, Mkemia mkuu wa serikali bwana Andiwelo Katabi, Mkuu wa masheji Jenerali Gwamaka Antony ambaye aliteuliwa na Rais wa awamu hiyo mara baada ya Marehemu Jenerali Phillipo Kasebele kustaafu (baba wa Tino na Aron).

Vimelea vya Virus-COBOS(V-COBOS) vikawa vimewasili rasmi nchini, kilichobaki ikawa inasubiriwa siku ambayo imepangwa kuviachia rasmi na kusababisha mripuko wa ugonjwa hatari ambao utasambaa kwa kasi na kuitikisa Dunia nzima.
ZMLST wakiwa katikati ya mpango huu hatari mara ukaibuka ugonjwa mwingine ukianzia China, ugonjwa huu ulikuwa ni mpya unaosababishwa na kirusi cha COVID-19 uliitwa KORONA. Hii ikawafanya ZMLST wasitishe zoezi la kukiachia kirusi cha COBOS mpaka pale maambukizi ya COVID-19 yatakapopungua au kuisha kabisa.
Zile chupa mbili yaani chupa ya kijani iliyobeba kimelea cha V-COBOS na ile ya kijani iliyobeba tiba na kinga ya V-COBOS zikahifadhiwa katika maabara kuu ya serikali kwa siri, na hii ikawa ni siri ya watu wachache.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati mambo haya yakiendela Jenerali Phillipo Kasebele ambaye ni baba wa Inspekta Aron na Tino lakini pia mume wa Sultana alikuwa ni mmoja wa watu waliotakiwa kuwa kwenye mpango huu, lakini alikataa kata kata kuwa mshirika wao akisimamia kanuni misingi na kiapo alichokula kwa ajili ya Nchi yake na hii ndiyo sababu iliyomfanya Rais Cosmas Kulolwa kumtaka Jenerali Phillipo astaafu kwa lazima kabla ya muda wake kufika. Ikawa hivyo Jenerali Phillipo akastaafu na punde Rais akamteua mkuu wa majeshi mwingine Jenerali Gwamaka Antony.

Baada ya Jenerali Phillipo kustaafu hakutaka kuishia hapo na kuuacha mpango huo hatari wa kusambazwa kwa virusi vya COBOS kuendelea, alijipanga kuhakikisha anazuia taratibu zao zote.
Jenerali Phillipo alikuwa na kijana wake mashuhuri jasusi kutoka Kenya aliitwa Shadow.
Shadow alikuwa ni jasusi kweli kweli katika kazi zote alizokuwa akizifanya hakuwahi kushindwa hata mara moja.
Hakuna aliyewahi kuiona sura yake wala hakujulikana ni wapi anaishi hata Jenerali Phillipo wenyewe hakujua. Wakati wote shadow alikuwa anavaa mavazi meusi juu mpaka chini kuficha sura yake.
Kazi ya kwanza aliyopewa na Jenerali Phillipo ilikuwa ni kuiba vimelea vya V-COBOS kutoka maabara kuu ya serikali kazi iliyokuwa ngumu kwa Shadow pengine kuliko kazi nyingine zote alizowahi kuzifanya.
Siku zote Shadow aliamini 'kujaribu ukashindwa ni bora zaidi kuliko kushindwa kujaribu' hivyo aliifanya kazi hiyo na mwisho akafanikiwa kuiba chupa ya kijivu iliyokuwa na tiba dhidi ya V-COBOS lakini hakufanikiwa kuiba ile chupa ya kijani yenye virusi vya COBOS.

Ingawa haikuwa lengo la Jenerali Phillipo lakini kupata chupa ile ya kijivu ilikuwa ni hatua kubwa sana iliyowarudisha nyuma ZMLST ambao walikuja juu wakimtaka Rais Profesa Cosmas Kulolwa afanye kila analoliweza kuhakikisha chupa hiyo inarudi hali iliyoleta mkanganyiko mkubwa. Hadi anatoka madarakani Profesa Cosmas Kulolwa hakufanikiwa kujua ni wapi na ni nani aliyeiba chupa ile ya kijivu.
Mbaya zaidi ZMLST hawakuwa na uwezo wa kutengeneza tiba wala kinga nyingine ya virusi vya V-COBOS. Hii ilikuwa ni hazina yao iliyotuzwa kwa muda mrefu, hakuna aliyejua fomula ya kutengeneza au kuharibu V-COBOS na ili kufanikiwa ilihitaji utafiti mwingine ambao ungewachukua miaka zaidi ya kumi. Hii ndiyo sababu wakawa wanashinikiza iwe mvua iwe jua lazima chupa ile ya kijivu ipatikane.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Baada ya miaka mitatu kupita baadae wakaja kugundua kuwa Jenerali Phillipo Kasebele ndiye aliyehusika kuiba chupa ile ya kijani. Kukawa na vita kali baina ya mwanajeshi huyu mstaafu na viongozi wa serikali waliokuwa wakiijua siri.
Ilikuwa ni ngumu kwao kumshambulia moja kwa moja Jenerali Phillipo kwani waliogopa siri hii kujulikana hivyo wakawa wanawindana kimya kimya na mzee huyo ambaye kwa miaka hiyo mitatu alijipanga kikamilifu kuilinda chupa ile ya kijivu akishirikiana na mkewe Sultana.
Baada ya kuona wanashindwa kupambana naye wakaamua kutumia njia mbadala.

Siku moja Waziri wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe alifanikiwa kumlaghai Tino mtoto wa kwanza wa Jenerali Phillipo ambaye alishawishika kwa pesa kidogo akakubali kumsaliti baba yake. Tino hakuelezwa chochote kuhusu vimelea vya V-COBOS lakini kwa mikono yake alimuua baba yake bila mtu yeyote kujua hivyo ndivyo alivyokubaliana na Dokta Gondwe, kuanzia siku hiyo akawa ni kibaraka wake.
Licha ya kwamba Dokta Gondwe hakuweka wazi sababu za kumtaka Tino amuue baba yake mzazi lakini tayari Tino alikuwa anajua mchezo mzima kuhusu vimelea vya V-COBOS. Kuna wakati alikuwa akimsikia Baba na mama yake wakizungumzia suala hili nyeti kwa siri hivyo hata kabla ya kuungana na Dokta Gondwe tayari Tino alikuwa anajua karibu kila kitu kuhusu vimelea vya V-COBOS na hii ndio sababu alikubali kirahisi sana kumuua baba yake, kumbe naye alikuwa na mipango yake kichwani. Aliingia tamaa ya kuzitaka chupa zote mbili, ile ya kijani kutoka kwa Dokta Gondwe ile ya kijivu kutoka kwa mama yake.

Baada ya Jenerali Phillipo Kasebele kufariki siri ilipo chupa ya kijani ilibaki kwa mkewe Sultana pamoja na yule jasusi Shadow.
Sultana alielewa kila kitu kuhusu mwanae Tino kuwa ameshagundua siri ya vimelea vya V-COBOS na ndiye aliyemuua mume wake. Alijua wazi ipo siku Tino atambana na kutaka chupa ya kijivu pengine anaweza hata kujaribu mumuua kama alivyofanya kwa mumewe. Ili kujiepusha na hilo Sultana alitumia akili kubwa akatengeneza mpango kwa kujifanya mgonjwa akalazwa hospitali ya Mountenia kwa kipindi kirefu huku akifanya mambo yake kimya kimya.
Sultana naye alikuwa kinyume na matakwa ya marehemu mumewe aliyetaka kuzuia mpango huu hatari wa virusi vya COBOS. Baada ya kufariki Sultana aliingiwa na tamaa akatamani kuzipata chupa zote mbili ile ya kijani na hii ya kijivu aliyoachiwa na mumewe hivyo kipindi chote alichokuwa akijifanya mgonjwa alimtumia jasusi Shadow kufuatilia nyendo za Tino ili aweze kupata chupa ile ya kijani kutoka maabara kuu ya serikali.
Tamaa aliyokuwa nayo Sultana ndio hiyo hiyo aliyokuwa nayo mtoto wake. Tino alikuwa akizitaka chupa zote mbili ile ya kijani yenye vimelea vya V-COBOS na hii ndio sababu akajiweka karibu na Waziri wa afya Dokta Gondwe akiamini atamtumia kama njia ya kuvipata vimelea hivyo. Lakini pia Tino aliendelea kusimamia matibabu ya mama yake kwa nguvu zote huku akitumia pesa nyingi sana akiamini mama yake ndiye anaejua ilipo chupa ile ya kijivu hivyo lazima ahakikishe anapona.
HIVYO NDIVYO ILIVYOKUWA.
[emoji294][emoji294][emoji294]

SASA TURUDI KWENYE STORI YETU...
Usiku wa saa nane hali iliendelea kuwa tulivu ndani ya hospitali ya Mountenia. Inspekta Aron alikuwa amekaa nje ya chumba kipya alichohamia Annah kwa sasa, wakati huo mama yake (Sultana) alikuwa katika hospitali hiyo hiyo ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi ICU akiyatafakari maelezo ya Shadow aliyemwambia kuwa kesho ndio siku ambayo Dokta Gondwe atakabidhi vimelea vya V-COBOS kwa Tino. Sultana akajikuta anatabasamu akiamini lengo lake linakwenda kutimia. Atamvamia Tino kirahisi na kumnyang'anya vimelea vya V-COBOS. Ilikuwa ni kama vile anamtegea mwanae, alisubiri aanze kisha yeye amalizie. Huu ndio ulikuwa mpango mzima wa Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Usiku huo pia ulikuwa ni mrefu kwa Tino ambaye alitamani masaa yaende kwa kasi ifike ule wakati ambao Dokta Gondwe aliahidi kutoa vimelea vya V-COBOS kutoka maabara kuu ya serikali kuvileta kwake. Tayari alishapanga kila kitu na kijana wake Bosco ambaye ndiye ataekuwa kwenye boti badala yake. Licha ya kwamba kulikuwa na kila dalili kuonyesha Dokta Gondwe anampango mwingine tofauti lakini Tino aliamini kupitia zile picha na video za ngono za Dokta Gondwe zitampa nafasi ya kuendelea kumthibiti.

"Acha ajichanganye na kuleta janja janja atajua hajui" aliwaza Tino
[emoji294][emoji294][emoji294]
Hali ilikuwa hivyo hata kwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe, hakuwa amepata hata chembe ya usingizi usiku huo bado alikuwa akiwaza kama mpango alioshauriwa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa utafanya kazi au laa!.

JE NINI KITAFUATA?
SASA TUMEELEWA KWA KINA KUHUSU VIMELEA HIVI VYA V-COBOS KUTOKA MEXICO...
JE NI NINI HATIMA YA MCHEZO HUU HATARI?
ITAENDELEA....
 
𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐃𝐄𝐑𝐍 𝐖𝐀𝐑
(vita ya kisasa)
Sehemu ya...............16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

16-(MAABARA YA ZMLST)
ILIPOISHIA (msimu wa kwanza)...
Sultana (Mama Aron) ambaye tuliamini ni mgonjwa mahututi aliyelazwa akiwa hajitambua kwa zaidi ya miezi sita mfurulizo anainuka kitandani akiwa ni mzima wa afya. Kumbe kwa kipindi chote alikuwa akiigiza kujifanya ni mgonjwa. Sultana anafanya mazungumzo na kijana wake wa siri anayemtumia siku zote anaitwa Shadow akimtaka ahakikishe anavileta vimelea vya V-COBOS mikononi mwake

Je, nini kitafuata?

TURUDI NYUMA MIAKA KUMI (10) ILIYOPITA.
MEXICO
Ndani ya nchi ya Mexico katikati ya mji maarufu wa Ciudad Juárez ndipo tunaikuta Maabara ya sayansi na teknolojia inayojulikana kwa jina la ZIVEMIC MEDICAL LABORATORY SCIENCE AND TECHNOLOGY - (ZMLST). Hii ilikuwa ni maabara kubwa na maarufu sana Duniani, kama ukitaja maabara za sayansi na teknolojia kumi bora ulimwenguni basi usinge acha kuitaja ZMLST.
ZMLST kama zilivyo maabara nyingine Duniani kote ilikuwa ikijihusisha sana na masuala ya utafiti wa magonjwa mapya yanayoibuka hasa haya ya mripuko, kuchunguza na kubaini chanzo, aina ya kimelea husika kama ni bakteria au kirusi kisha wanamaliza kwa kutengeneza kinga au dawa. Hivyo ndivyo namna maabara ya ZMLST ilivyofanya kazi.
Maabara hii ilikuwa ni kongwe kuliko maabara nyingine zote unazozifahamu lakini ukongwe wake haukuifanya ZMLST kuwa maabara bora kuliko nyingine.
Maabara nyingine kubwa zenye teknolojia ya kisasa zilikuwa zikiibuka kila iitwapo leo hali iliyopelekea ZMLST kuanza kupotea kwenye midomo ya watu, taratibu hata tenda zikaanza kupungua.
Kwa miaka mitatu mfurulizo ZMLST ikajikuta inaporomoka kwa kasi na kupoteza sifa yake kabisa, kila walipojaribu kuirudisha katika hadhi yake ya awali ilishindikana ushindani ulikuwa ni mkubwa mno.
Mwisho umaarufu wa ZMLST ukapotea na kubaki jina tu. Wanasayansi wakubwa ulimwenguni waliokuwa wakishikiriwa na maabara hii kama Dr Alain Aspeco, Prof David Baltimore, Allen Bard, Eng Timothy Berners na wengine wengi walianza kuchomoka mmoja baada ya mwingine wakihamia kampuni nyingine na baadae wakaisha wote, hali ikazidi kuwa tete
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Now it's time to use our weapon"(sasa ni wakati wa kutumia siraha yetu)
Hii ilikuwa ni kauli ya mkurugenzi mtendaji wa ZMLST Profesa Fernando Arturo ambaye pia ni mmoja kati ya waanzilishi wa ZMLST, alisema hivi akiwa amekaa kikao cha dharula na wafanyakizi waandamizi wa ZMLST. Mbele ya Profesa Fernando kulikuwa na begi dogo juu ya meza lililokuwa na muundo kama boksi hivi.
Profesa Fernando mwenye asili ya kituruki alifungua lile begi kuwaonyesha watu wake kitu kilichokuwa ndani. Wote walitazama na kushuhudia chupa mbili zilizohifadhiwa kwenye chemba mbili maalum ndani ya sanduku hilo. Chupa moja ikiwa na rangi ya kijani na nyingine ikiwa na rangi ya kijivu.

"Now it's time to show the whole world how powerful ZMLST is. We are going to spread these COBOS viruses in Africa and later around the World"( Ni muda wa kuionyesha Dunia ni jinsi gani ZMLST inanguvu, tunakwenda kusambaza hivi virusi vya COBOS Africa na baadae Dunia nzima)
Profesa Fernando aliongea kwa kumaanisha, akatulia kwa muda kisha akaendelea kuongea.

"We are the only ones who will be able to provide vaccine and cure against this deadly COBOS virus. This green bottle contains the COBOS virus and this gray bottle carries a cure/vacinne against it"( Ni sisi pekee ndio kutakaoweza kutengeneza chanjo na tiba dhidi ya kirusi hiki hatari cha COBOS. Hii chupa ya kijani imebeba virusi vya COBOS na hii chupa ya kijivu imebeba tiba/kinga yake)
Profesa Fernando alitulia tena kwa muda kuhakikisha kama maneno anayoyazungumza yanawaingia vizuri watu wake ambao wote walikuwa wakitikisa vichwa vyao wakionekana kwenda sambamba na kukubaliana na maelezo ya Profesa Fernando, akaendelea kuzungumza.
"Through this initiative we will not only make billions of money but we will also restore the dignity and status of our laboratory that was lost for many years. The important thing right now is to choose one country in Africa that will be our starting point. We will persuade some key leaders to join our initiative" (kupitia mpango huu si tu kutengeneza mabilioni ya pesa bali tutarudisha heshima na hadhi ya maabara yetu iliyopotea kwa miaka mingi. Kitu muhimu kwa sasa ni kuchagua nchi moja huko Africa ambayo itakuwa kama sehemu yetu ya kuanzia. Tutawashawishi baadhi ya viongozi muhimu waingie kwenye mpango wetu)
Alieleza Profesa Fernando.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa miezi michache baadae kila kitu kikawa kimekamilika Nchi husika Africa ikapatikana na baadhi ya viongozi muhimu wakaingizwa moja kwa moja kwenye mpango huu huku wakipewa kiwango kikubwa cha pesa na kuhakikishiwa usalama wao na ndugu zao kwani tiba na kinga ya virusi vya COBOS ilikuwepo.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Timu ya wazungu wanne(4) kutoka Mexico iliwasili nchini wakijifanya watalii ambao walipata mualiko rasmi hadi ikulu kwa Rais wa awamu hiyo Profesa Cosmas Kulolwa ambaye alikuwa ni mmoja kati ya viongozi waliopo kwenye mpango wa kuingizwa kwa virusi vya COBOS nchini. Viongozi wengine wa nchi walioshiriki alikuwepo Waziri wa afya Mheshimiwa dokta Isaack Gondwe, Mkemia mkuu wa serikali bwana Andiwelo Katabi, Mkuu wa masheji Jenerali Gwamaka Antony ambaye aliteuliwa na Rais wa awamu hiyo mara baada ya Marehemu Jenerali Phillipo Kasebele kustaafu (baba wa Tino na Aron).

Vimelea vya Virus-COBOS(V-COBOS) vikawa vimewasili rasmi nchini, kilichobaki ikawa inasubiriwa siku ambayo imepangwa kuviachia rasmi na kusababisha mripuko wa ugonjwa hatari ambao utasambaa kwa kasi na kuitikisa Dunia nzima.
ZMLST wakiwa katikati ya mpango huu hatari mara ukaibuka ugonjwa mwingine ukianzia China, ugonjwa huu ulikuwa ni mpya unaosababishwa na kirusi cha COVID-19 uliitwa KORONA. Hii ikawafanya ZMLST wasitishe zoezi la kukiachia kirusi cha COBOS mpaka pale maambukizi ya COVID-19 yatakapopungua au kuisha kabisa.
Zile chupa mbili yaani chupa ya kijani iliyobeba kimelea cha V-COBOS na ile ya kijani iliyobeba tiba na kinga ya V-COBOS zikahifadhiwa katika maabara kuu ya serikali kwa siri, na hii ikawa ni siri ya watu wachache.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati mambo haya yakiendela Jenerali Phillipo Kasebele ambaye ni baba wa Inspekta Aron na Tino lakini pia mume wa Sultana alikuwa ni mmoja wa watu waliotakiwa kuwa kwenye mpango huu, lakini alikataa kata kata kuwa mshirika wao akisimamia kanuni misingi na kiapo alichokula kwa ajili ya Nchi yake na hii ndiyo sababu iliyomfanya Rais Cosmas Kulolwa kumtaka Jenerali Phillipo astaafu kwa lazima kabla ya muda wake kufika. Ikawa hivyo Jenerali Phillipo akastaafu na punde Rais akamteua mkuu wa majeshi mwingine Jenerali Gwamaka Antony.

Baada ya Jenerali Phillipo kustaafu hakutaka kuishia hapo na kuuacha mpango huo hatari wa kusambazwa kwa virusi vya COBOS kuendelea, alijipanga kuhakikisha anazuia taratibu zao zote.
Jenerali Phillipo alikuwa na kijana wake mashuhuri jasusi kutoka Kenya aliitwa Shadow.
Shadow alikuwa ni jasusi kweli kweli katika kazi zote alizokuwa akizifanya hakuwahi kushindwa hata mara moja.
Hakuna aliyewahi kuiona sura yake wala hakujulikana ni wapi anaishi hata Jenerali Phillipo wenyewe hakujua. Wakati wote shadow alikuwa anavaa mavazi meusi juu mpaka chini kuficha sura yake.
Kazi ya kwanza aliyopewa na Jenerali Phillipo ilikuwa ni kuiba vimelea vya V-COBOS kutoka maabara kuu ya serikali kazi iliyokuwa ngumu kwa Shadow pengine kuliko kazi nyingine zote alizowahi kuzifanya.
Siku zote Shadow aliamini 'kujaribu ukashindwa ni bora zaidi kuliko kushindwa kujaribu' hivyo aliifanya kazi hiyo na mwisho akafanikiwa kuiba chupa ya kijivu iliyokuwa na tiba dhidi ya V-COBOS lakini hakufanikiwa kuiba ile chupa ya kijani yenye virusi vya COBOS.

Ingawa haikuwa lengo la Jenerali Phillipo lakini kupata chupa ile ya kijivu ilikuwa ni hatua kubwa sana iliyowarudisha nyuma ZMLST ambao walikuja juu wakimtaka Rais Profesa Cosmas Kulolwa afanye kila analoliweza kuhakikisha chupa hiyo inarudi hali iliyoleta mkanganyiko mkubwa. Hadi anatoka madarakani Profesa Cosmas Kulolwa hakufanikiwa kujua ni wapi na ni nani aliyeiba chupa ile ya kijivu.
Mbaya zaidi ZMLST hawakuwa na uwezo wa kutengeneza tiba wala kinga nyingine ya virusi vya V-COBOS. Hii ilikuwa ni hazina yao iliyotuzwa kwa muda mrefu, hakuna aliyejua fomula ya kutengeneza au kuharibu V-COBOS na ili kufanikiwa ilihitaji utafiti mwingine ambao ungewachukua miaka zaidi ya kumi. Hii ndiyo sababu wakawa wanashinikiza iwe mvua iwe jua lazima chupa ile ya kijivu ipatikane.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Baada ya miaka mitatu kupita baadae wakaja kugundua kuwa Jenerali Phillipo Kasebele ndiye aliyehusika kuiba chupa ile ya kijani. Kukawa na vita kali baina ya mwanajeshi huyu mstaafu na viongozi wa serikali waliokuwa wakiijua siri.
Ilikuwa ni ngumu kwao kumshambulia moja kwa moja Jenerali Phillipo kwani waliogopa siri hii kujulikana hivyo wakawa wanawindana kimya kimya na mzee huyo ambaye kwa miaka hiyo mitatu alijipanga kikamilifu kuilinda chupa ile ya kijivu akishirikiana na mkewe Sultana.
Baada ya kuona wanashindwa kupambana naye wakaamua kutumia njia mbadala.

Siku moja Waziri wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe alifanikiwa kumlaghai Tino mtoto wa kwanza wa Jenerali Phillipo ambaye alishawishika kwa pesa kidogo akakubali kumsaliti baba yake. Tino hakuelezwa chochote kuhusu vimelea vya V-COBOS lakini kwa mikono yake alimuua baba yake bila mtu yeyote kujua hivyo ndivyo alivyokubaliana na Dokta Gondwe, kuanzia siku hiyo akawa ni kibaraka wake.
Licha ya kwamba Dokta Gondwe hakuweka wazi sababu za kumtaka Tino amuue baba yake mzazi lakini tayari Tino alikuwa anajua mchezo mzima kuhusu vimelea vya V-COBOS. Kuna wakati alikuwa akimsikia Baba na mama yake wakizungumzia suala hili nyeti kwa siri hivyo hata kabla ya kuungana na Dokta Gondwe tayari Tino alikuwa anajua karibu kila kitu kuhusu vimelea vya V-COBOS na hii ndio sababu alikubali kirahisi sana kumuua baba yake, kumbe naye alikuwa na mipango yake kichwani. Aliingia tamaa ya kuzitaka chupa zote mbili, ile ya kijani kutoka kwa Dokta Gondwe ile ya kijivu kutoka kwa mama yake.

Baada ya Jenerali Phillipo Kasebele kufariki siri ilipo chupa ya kijani ilibaki kwa mkewe Sultana pamoja na yule jasusi Shadow.
Sultana alielewa kila kitu kuhusu mwanae Tino kuwa ameshagundua siri ya vimelea vya V-COBOS na ndiye aliyemuua mume wake. Alijua wazi ipo siku Tino atambana na kutaka chupa ya kijivu pengine anaweza hata kujaribu mumuua kama alivyofanya kwa mumewe. Ili kujiepusha na hilo Sultana alitumia akili kubwa akatengeneza mpango kwa kujifanya mgonjwa akalazwa hospitali ya Mountenia kwa kipindi kirefu huku akifanya mambo yake kimya kimya.
Sultana naye alikuwa kinyume na matakwa ya marehemu mumewe aliyetaka kuzuia mpango huu hatari wa virusi vya COBOS. Baada ya kufariki Sultana aliingiwa na tamaa akatamani kuzipata chupa zote mbili ile ya kijani na hii ya kijivu aliyoachiwa na mumewe hivyo kipindi chote alichokuwa akijifanya mgonjwa alimtumia jasusi Shadow kufuatilia nyendo za Tino ili aweze kupata chupa ile ya kijani kutoka maabara kuu ya serikali.
Tamaa aliyokuwa nayo Sultana ndio hiyo hiyo aliyokuwa nayo mtoto wake. Tino alikuwa akizitaka chupa zote mbili ile ya kijani yenye vimelea vya V-COBOS na hii ndio sababu akajiweka karibu na Waziri wa afya Dokta Gondwe akiamini atamtumia kama njia ya kuvipata vimelea hivyo. Lakini pia Tino aliendelea kusimamia matibabu ya mama yake kwa nguvu zote huku akitumia pesa nyingi sana akiamini mama yake ndiye anaejua ilipo chupa ile ya kijivu hivyo lazima ahakikishe anapona.
HIVYO NDIVYO ILIVYOKUWA.
[emoji294][emoji294][emoji294]

SASA TURUDI KWENYE STORI YETU...
Usiku wa saa nane hali iliendelea kuwa tulivu ndani ya hospitali ya Mountenia. Inspekta Aron alikuwa amekaa nje ya chumba kipya alichohamia Annah kwa sasa, wakati huo mama yake (Sultana) alikuwa katika hospitali hiyo hiyo ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi ICU akiyatafakari maelezo ya Shadow aliyemwambia kuwa kesho ndio siku ambayo Dokta Gondwe atakabidhi vimelea vya V-COBOS kwa Tino. Sultana akajikuta anatabasamu akiamini lengo lake linakwenda kutimia. Atamvamia Tino kirahisi na kumnyang'anya vimelea vya V-COBOS. Ilikuwa ni kama vile anamtegea mwanae, alisubiri aanze kisha yeye amalizie. Huu ndio ulikuwa mpango mzima wa Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Usiku huo pia ulikuwa ni mrefu kwa Tino ambaye alitamani masaa yaende kwa kasi ifike ule wakati ambao Dokta Gondwe aliahidi kutoa vimelea vya V-COBOS kutoka maabara kuu ya serikali kuvileta kwake. Tayari alishapanga kila kitu na kijana wake Bosco ambaye ndiye ataekuwa kwenye boti badala yake. Licha ya kwamba kulikuwa na kila dalili kuonyesha Dokta Gondwe anampango mwingine tofauti lakini Tino aliamini kupitia zile picha na video za ngono za Dokta Gondwe zitampa nafasi ya kuendelea kumthibiti.

"Acha ajichanganye na kuleta janja janja atajua hajui" aliwaza Tino
[emoji294][emoji294][emoji294]
Hali ilikuwa hivyo hata kwa mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe, hakuwa amepata hata chembe ya usingizi usiku huo bado alikuwa akiwaza kama mpango alioshauriwa na Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa utafanya kazi au laa!.

JE NINI KITAFUATA?
SASA TUMEELEWA KWA KINA KUHUSU VIMELEA HIVI VYA V-COBOS KUTOKA MEXICO...
JE NI NINI HATIMA YA MCHEZO HUU HATARI?
ITAENDELEA....

0756862047
 
Mkuu itaisha nianze kusoma? Inaonekana tamu sana, naogopa kuanza na nikakumbana na arosto
Akikujibu niambie namimi nianze kusoma, hawachelewi kusema "hata Mimi naifata mahali na Kuna majukumu mengine natakiwa kufanya" ila huyu anaonekana fresh, tushauriane Mimi na wewe tusome au tusubirie kwanza ? [emoji2][emoji2][emoji125][emoji125]

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Akikujibu niambie namimi nianze kusoma, hawachelewi kusema "hata Mimi naifata mahali na Kuna majukumu mengine natakiwa kufanya" ila huyu anaonekana fresh, tushauriane Mimi na wewe tusome au tusubirie kwanza ? [emoji2][emoji2][emoji125][emoji125]

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
Fuatilia simulizi nazopost zote zinafika MWISHO japo ni kweli tupo ki biashara pale utakapohitaji yote kwa wakati mmoja utalazimika kuchangia, ila huku JF tutaenda mdogo mdogo mpaka Mwisho
 
THE MODERN WAR
(vita ya kisasa)
Sehemu ya.............17
Mtunzi: saul david
WhatsApp: 0756862047

17-(USIKU WA CHATTING)
ILIPOISHIA...16
Sehemu iliyopita tulifanikiwa kujua chimbuko la virusi vya COBOS namna vilivyotoka Mexico mpaka vikaingia nchini. Namna marehemu Jenerali Phillipo Kasebele alivyopambana na baadae kuuwawa kikatili na mtoto wake wa kumzaa, Tino.
Simulizi yetu iliishia wakati Godwin amemuua Big' akidhani kuwa ni Annah asijue Annah alihamishiwa chumba kingine tofauti na sasa yuko chini ya uangalizi mkali wa Inspekta Aron mwenyewe.
Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
Ikiwa ni majira ya saa 8 usiku Inspekta Aron alikuwa amekaa kwenye moja ya viti vilivyokuwa nje ya chumba alicholazwa Annah ndani ya hospitali ya Mountenia. Alikuwa amechoka sana huku usingizi ukionekana kumuelemea lakini hakutaka kukubali kuyafumba macho yake hata sekunde moja. Kumlinda Annah ilikuwa ni kipaombele chake cha kwanza siku hiyo.
Akiwa anahangaika kupambana na usingizi huo kumbe kwa muda mrefu Annah alikuwa ameinuka kutoka kitandani akawa amesimama nyuma ya mlango wa kioo akimtazama Inspekta Aron namna alivyokuwa akihangaika pale nje kwa ajili yake.

Annah aliitumia nafasi hiyo kumkagua Inspekta Aron kwa muda mrefu sana, akajikuta anawaza mengi kumuhusu kaka huyo ambaye hakujua kama kuna mtu amesimama kwa muda mrefu anamtazama.

"Amechoka, anapambana kwa ajili ya usalama wangu, ameyaokoa maisha yangu na sasa yupo hapa ananilinda dhidi ya maadui" aliwaza Annah, mawazo yake yakampeleka mbali sana akakumbuka siku moja aliwahi kuambiwa maneno fulani na marehemu mama yake

"Mwanangu wewe bado ni msichana mdogo, usiyapaparikie mapenzi utaharibikiwa mapema. Unatakiwa utulie uchague mwanaume ambaye ni sahihi kwako, siku moja mimi na baba yako hatutokuwepo kila kitu tunachokifanya kwako sasa hivi kama kukupenda, kukujali na kukulinda atatakiwa kufanya huyo mwanaume ambaye utamchagua hivyo kuwa makini"
Sauti hii ya mama yake ilijirudia kichwani kwa Annah

"Mmeondoka mapema mama mmeondoka hata kabla sijamjua mtu atakayeyafanya hayo yote kwa ajili yangu" Alisema Annah machozi yakimlenga kwa mara nyingine.
Mara alishtuka kumuona Inspekta Aron liyekuwa ameanza kusinzia pale kwenye kiti alikurupuka ghafula baada ya kutaka kudondoka.

Inspekta Aron alifikicha macho yake yaliyojaa usingizi kisha akatazama huku na huku kuhakikisha usalama na hapo ndipo macho yake yalipogongana na macho ya Annah aliyekuwa kwenye mlango wa chumba chake anamtazama

Walitazamana kwa sekunde kadhaa kisha Annah akatazama pembeni kwa aibu za kike kike huku akitabasamu. Inspekta Aron naye alipata aibu kiasi baada ya kubaini kumbe alikuwa anasinzia mbele ya mrembo huyo.

"Wewe" Inspekta Aron aliita kwa sauti ya chini wakati huo Annah alikuwa akifungua mlango akatoka na kutembea taratibu hadi pale alipokuwa Inspekta Aron.
"Nambie afande"
"Mbona hujalala"
"Sijapata usingizi, nilitaka kutoka nje nitembee tembee kupunguza mawazo ndio nikakuona hapa"
"Aah! wewe mwanamke utembee uende wapi sasa usiku huu?"
"Kwani ni saa ngapi?" aliuliza annah huku akikaa kwenye kiti pembeni ya Inspekta Aron
"Ni saa tisa kasoro usiku"
"Mda hata hauendi jamani, sasa na wewe kwa nini haujalala?"
"Mimi nipo hapa, nakulinda"
"Ahahah unanilinda au unasinzia?" Alisema Annah, kwa mara ya kwanza Inspekta Aron akaliona tabasamu la mwanamke huyo aliyekuwa na huzuni kwa muda mrefu

"Angalau amecheka, mh! ni mrembo kumbe"Aliwaza Inspekta Aron
"Umesema?" Aliuliza Annah
"Nini kwani nimeongea?"
"Ndio kwamba nimesikia vibaya"
"Huenda, mbona mimi sijasema kitu" Alisema Inspekta Aron huku akimtazama Annah usoni wakatazamana tena kisha wakatabasamu kwa pamoja, lakini mara lile tabasamu likapotea ghafula kwenye uso wa Annah.

"Nini! Unawaza nini?" Aliuliza Aron
"Hamna niko sawa.. Aron, unaitwa Aron si ndio?"
"Yeah Aron Phillipo Kasebele"
Alijibu Aron kisha kukawa kimya tena, baadae Annah akavunja ukimya, akawa anazungumza kwa uchungu...
"Najaribu kuwaza tu ni jinsi gani maisha yangu yamebadilika ghafula, kweli hakuna aijuae kesho yake, ni siku chache tu nilikuwa naishi kwa furaha mimi na wazazi wangu wote wawili lakini kila kitu kikabadilika ghafula tangu siku ile ya Birthday yangu. Najuta kwa nini nilitaka tufanye ile part kwenye ule mgahawa, mwisho tukajikuta tunashuhudia mauaji ya kutisha. Yule Osward aliua mtu mbele ya macho yetu bila huruma akakimbia, baadae akaanza kuua watu walioshuhudia tukio lile mmoja baada ya mwingine, licha ya kukamatwa lakini bado watu wake wakaendelea kuua ili tu kufuta ushahidi, na hatimaye zamu yetu ikafika, wakamuua baba wakamuua na mama pia, mimi nikanusurika na sasa najua wananisaka kwa udi na uvumba kuhakikisha nakufa,najua ndio maana uko hapa Inspekta Aron, maisha yangu yamebadilika nimekuwa kama.....aaah jamani" Annah aliongea kwa uchungu akashindwa kumalizia sentensi yake, akaanza kulia kwa uchungu sana.

Inspekta Aron alijikuta anaanza umpya kumbembeleza Annah anyamaze, hakika maisha ya binti huyo yalikuwa ya kuumiza sana.
"Usijali Annah hiyo yote ni mipango ya mungu, kila kitu kitakuwa sawa hakuna baya litakalokukuta HAKUNA MTU ATAKAYEKUGUSA KABLA HAJANIGUSA MIMI" Aron aliongea kwa kumaanisha, maneno hayo yalikuwa ni faraja kubwa kwa Annah, akajikuta anamkumbatia Inspekta Aron kwa nguvu.

Walikumbatiana kwa zaidi ya dakika mbili, hapo Inspekta Aron akamtoa Annah taratibu huku akimpiga piga mgongoni

"Usiniachiee.." Alisema Annah kwa sauti iliyojaa mchoko. Inspekta Aron akamlaza kwenye kifua chake huku akiuzunguusha mkono wake nyuma ya mgongo wa Annah, akamshika vizuri.
Haukupita mda Annah akawa amepitiwa na usingizi akalala. Taratibu Inspekta Aron akamlaza kwenye miguu yake kisha akachukua shuka alilokujanalo akamfunika.

Inspekta Aron aliinamisha uso wake akawa anamtazama Annah kwa macho yenye huruma na upendo mwingi. Akawa anashikashika nywele ndefu za binti huyo na wakati mwingine akiugusa uso wake, alikuwa ni mrembo haswa.

Hapo Inspekta Aron aliikumbuka simu yake, akachukua kutoka mfukoni kisha akatazama saa, ilikuwa ni saa kumi kasoro usiku.
Inspekta Aron alifungua uwanja wa meseji kwenye simu yake akakuta kuna jumbe 14 ambazao hazijasomwa na zote kutoka kwa Najma mtoto wa Waziri Dokta Gondwe. Aron alifungua pia upande wa mtandao wa WhatsApp huko akakuta ametumiwa picha na yule rafiki yake ambaye ni askari magereza, zilikuwa ni picha zikimuonyesha Big na Osward wakati ule wakifanya mazungumzo pale gerezani.
Inspekta Aron alizitazama picha zile kwa makini kisha akausogeza karibu uso wa Big', alihisi ni kama mtu huyo alimuona mahali lakini hakukumbuka ni wapi, ni kweli Inspekta Aron alimuona Big' kwa mbali wakati ule akiwa amembeba Najma na kumuingiza kwenye gari lakini kwa bahati mbaya akawa hakumbuki.

***********
{TANGAZO:- Epuka matapeli simulizi hii imetungwa na SAUL DAVID simu 0756862047, Tafadhali usinunue kwa mtu mwingine tofauti }
******-*-
Inspekta Aron aliamua kuachana na picha hizo akiamini kabisa mchoko aliokuwanao ndio sababu hasa ya kumfanya asahau ni wapi alimuona Big' ambaye kwa sasa tunajua ni marehemu mwili wake ukiwa kwenye chumba ambacho Annah alikuwa amelazwa awali.
Inspekta Aron alirudi kwenye uwanja wa meseji akafungua na kuaanza kusoma zile jumbe 14 kutoka kwa Najma moja baada ya mwingine.

,,, Habari za mida,,,,,
,,,,,,Mambo,,,,,,,
,,,,,,Aron umelala?,,,,,,
,,,,,,Sorry naweza kupiga simu,,,,,,
,,,,,,,Aron Dokta wangu mguu umeanza kuuma sasa nafanyaje, nitumie dawa ipi kati ya hizi?,,,,,,
,,,,,,,Aron mwenzio naumia,,,,,,
,,,,,Sijapata usingizi hadi sasa,,,,,
,,,,,Hlw,,,,,,
,,,,,,,Aron,,,,,,
,,,,,,,Ee jaman huyo mkeo si akuache kidogo,,,,,,
,,,,,,Aron naumwa serious,,,,,,
,,,,,Hlw hadi sasa saa 7 sijapata usingizi Aron mguu unauma sana,,,,,
,,,,,,We mwanaume,,,,,,
,,,,,,,Mmh,,,,,,,

Inspekta Aron alijikuta anatabasamu mara baada ya kumalizia kuzisoma meseji hizo kutoka kwa pisi kali mtoto wa Waziri wa afya Dokta Gondwe.

,,,,,,,,,Pole, samahan nilikua bize kidogo si unajua hizi kazi zetu nitakupigia asubuh pumzika,,,,,,
Aron alijibu huku akimtazama Annah ambaye alikuwa akijigeuza kwenye miguu yake, akagundua shingo ilikuwa imeanza kukuuama baada ya kulala kwa muda mrefu kwenye miguu yake. Aron akaweka simu pembeni akavua koti lake kisha akamuinua Annah taratibu akaweka lile koti juu ya miguu yake kisha akamlaza tena.
Alipoichukua simu yake akakutana meseji mbili zilizoingia mfurulizo kutoka kwa Najma.

,,,,Eeh pole mwaya,,,,,,,
,,,,,Mguu unauma sana Aron au nimeumia sana?,,,,,,

"Duh hajalala huyu mwanamke" Alisema Inspekta Aron na hapo akajikuta anaanza kuchati na Najma. Ikawa ni mwendo wa meseji mfurulizo kila mmoja akionekana kufurahia kuchat na mwenzake. Wakati huo wote Annah alikuwa amelala kwenye miguu ya Inspekta Aron.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Hatimaye kukapambazuka ikafika asubuhi ya siku ambayo ilikuwa ikisubiwa kwa hamu, siku ambayo hakuna aliyejua itaisha vipi si Dokta Gondwe si Tino si Sultana wala si Shadow ilikuwa ni siku yenye kitendawili kizito ni nani atabaki na vimelea vya V-COBOS.

ITAENDELEA....
 
USIACHE KUFUATILIA SIMULIZI ZANGU ZINAZOENDELEA HUKU JAMII FORAM

1. DO NOT SHOUT - usipige kelele
2. THE MODERN WAR- Vita ya kisasa
3. STAY WITH ME- baki na mimi
4. KARANI
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.............18
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
18-(Jasusi Shadow na Arone)
ILIPOISHIA....17
Hatimaye kukapambazuka ikafika asubuhi ya siku ambayo ilikuwa ikisubiwa kwa hamu, siku ambayo hakuna aliyejua itaisha vipi si Dokta Gondwe si Tino si Sultana wala si Shadow ilikuwa ni siku yenye kitendawili kizito ni nani atabaki na vimelea vya V-COBOS

SASA ENDELEA....
Ikiwa ni majira ya saa 12 alfajiri Inspekta Aron alimuinua Annah aliyekuwa amelala miguuni pake akambeba na kumuingiza chumbani kwake, akamlaza taratibu kitandani.
Inspekta Aron alisimama kwa sekunde kadhaa akimuangalia Annah ambaye alionekana bado amelala. Aron alitabasamu akamfunika vizuri kisha akaanza kuondoka.

"Unaenda wapi Aron" mara ilisikika sauti yenye uchovu mwingi kutoka kwa Annah, Inspekta Aron akashtuka na kugeuka
"Nilijua umelala?"
"Hamna niko macho usiku wote hata sijalala"
"Mmh!!"
"Ndiyo, sikuwahi kuwaza kama maaskari nao huwa wanachati kwa muda mwingi kama wewe leo, usiku kucha wewe na simu huo usingizi mimi ningepata wapi?" alisema Annah huku akifumbua macho yake kumtazama Inspekta Aron ambaye alitazama pembeni kwa aibu

"Aheheh unataka kusema mimi ndio nimesababisha usipate usingizi?"
"Ndio hivyo hata ungekuwa wewe ungelala?"
"Hahah haya bana samahani alikuwa ni mtu muhimu ndio maana" alijibu Aron huku akijichekesha
"Hata mimi naona alikuwa ni muhimu kweli kweli" Alisema Annah kauli iliyokuwa na wivu ndani yake.
"Ingia bafuni basi uoge nimwite daktari aje akuangalie kidonda" Alisema Aron wakati huo simu yake ikawa inaita mpigaji alikuwa ni Dokta Zyunga, akapokea.

"Inspekta Aron uko wapi?"
"Niko huku kwa Annah, vipi kuna shida Dokta?" Aliuliza Aron akihisi kuna jambo haliko sawa kutokana na namna Dokta Zyunga alivyozungumza
"Ndio hebu njoo mara moja"
"Nije wapi?"
"Huku juu chumba alichokuwa Annah mwanzoni"
"Sawa" Aron alikata simu kisha akatoka upesi bila hata kumuaga Annah.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dakika mbili baadae Aron alifika mahali alipoitwa. Ndani alimkuta Dokta Zyunga na nesi mmoja wamesimama mbele yao kukiwa na mwili wa mtu umelala sakafuni huku damu nyingi ikiwa imetapakaa kuuzunguuka mwili huo

"Nini kinaendelea Dokta Zyunga?" Aliuliza Aron
"Mauaji?"
"Ni nani huyu amekufa, Oh! My God hii ni Risasi kutoka bunduki ya masafa marefu" alisema Aron mara baada ya kuliona jeraha la marehemu. Inspekta Aron akageuka na kutazama dirishani, kioo kilikuwa kimepasuka upande mmoja na upande mwingine kulikuwa na tundu risasi ilipopita
Inspekta Aron aliendelea kukagua kila mahali kwa macho yenye uzoefu wa kipelelezi hazikupita dakika tano tayari akawa anamajibu ya kila kitu.

"Nesi hebu tupishe mara moja tuzungumze, hakikisha hii pia inakuwa ni siri usimwambie mtu" Alisema Dokta Zyunga, yule nesi akatikisa kichwa kukubaliana na maelezo hayo kisha akatoka na kuwaacha Inspekta Aron na Dokta Zyunga ambao walianza kujadili tukio lile.

"Inspekta Aron mbona sielewi, nawaza hawa watakuwa ni watu wanaomtafuta Annah lakini kivipi huyu ameuwawa hapa?" Aliuliza Dokta Zyunga
"Namjua huyu mtu"
"Unamjua!! Kivipi? ni nani?"
"Alikuwa akinifuatilia mimi, ametumwa na Osward yule kijana mwenye kesi ya mauaji aliyepo gerezani mtoto wa mzee Matula" Alisema Aron huku akitoa simu yake akafungua na kumuonyesha Dokta Zyunga zile picha za Big' alizotumiwa na rafiki yake askari magereza.

"Hapo alikuwa akifanya mazungumzo na Osward akamtuma aje kuniua, alikuwa akinifuatilia tangu jana nilipotoka kule gerezani, wakati naingia kwenye gari nilimuona lakini sikumtilia maanani" alieleza Inspekta Aron kumbukumbu zake zikionekana kukaa sawa sasa

"Mmh! sasa nani kamuua na kwa nini?"
"Watu wanaotaka kumuua Annah ndio wamefanya haya mauaji, mdunguaji alikuwa ndani ya hiyo hoteli jirani hapo mbele, hakuweza kumuona muhusika anayempiga risasi kwa sababu ya haya mapazia hivyo wanaamini wamemuua Annah" Inspekta Aron alieleza akionyesha ni namna gani amebobea kwenye kazi yake ya upelelezi, alilielezea tukio zima kwa uharisia wake kama vile alikuwepo.

"Kwa hiyo tunafanyaje"
"Kila kitu kiendelee kuwa siri Dokta Zyunga hadi siku ya mahakamani itakapofika, kwa kuwa wanaamini wamemuua Annah basi na mimi nitawaaminisha hivyo ili waache kabisa kitufuatilia"
"Sawa vipi kuhusu huu mwili"
"Kautunze mochwari, Dokta Zyunga swali gani hilo unauliza? wewe ni mtu mkubwa hapa hospitalini unaogopa watakuhoji"
"Aah hapana ilaa...."
"Nini, au humwamini huyu nesi wako?"
"Hapana! hapana! huyu nesi hana shida, basi sawa nitafanya hivyo Inspekta ila kuwa makini hili swala ni zito, una maadui wengi sana Inspekta, narudia tena kuwa makini kwa kila hatua unayopiga"
"Usijali, kuwa makini pia mimi nikiwa hatarini hata watu wangu wanaonizunguuka wanakuwa hatari" Alieleza Inspekta Aron huku akiinama na kukagua mifuko ya nguo alizovaa Big' akakuta simu, akaichukua
"baadae narudi kwa Annah" alisema Inspekta Aron akapiga hatua na kuondoka.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Sasa ni wakati wa kucheza kikubwa kaka Tino" Aliwaza Inspekta Aron akiwa anaingia ndani ya lifti, wakati huo akapishana na mtu mwingine akishuka kutoka kwenye lifti hiyo hiyo.
Walipopishana Inspekta Aron akageuka kumtazama tena mtu huyo. Alikuwa mwanaume aliyevaa mavazi meusi juu mpaka chini pia kichwani alivaa kofia aina ya kapero aliyoishusha chini kufunika sura yake, alitembea akiwa ameinama kiasi cha kumfanya Inspekta Aron asiione kabisa sura ya mwanaume huyo, hakuwa mwingine bali Shadow jasusi anayefanya kazi chini ya mama yake yaani Sultana.

"Hello kaka habari" Inspekta Aron alimsalimia, Shadow akavunga kama vile hajasikia akaendela kutembea
"Oi brother hebu simama kwanza..." Aron aliongea kwa mara ya pili tena kwa sauti kubwa zaidi ya mwanzo hapo Shadow akasimama lakini hakugeuka
Inspekta Aron alikuwa ni mtu makini sana zile sekunde chache alizopishana na Shadow zilitosha kuwasha taa nyekundu kwenye akili yake akajua moja kwa moja mtu aliyepishana naye hakuwa mtu wa kawaida.
Kwa bahati mbaya hakujua ile hatari aliyoinusa kwa mtu huyo ilikuwa ni mara mbili yake, Shadow alikuwa ni moto wa kuotea mbali, hata marehemu baba yake alikuwa akimpigia saluti.
Baada ya Shadow kusimama Inspekta Aron alihairisha kuingia kwenye lifti akaanza kupiga hatua taratibu kumsogelea
"Samahani ndugu mimi ni asifa wa polisi niko hapa kwa kazi maalumu tafadhali naweza kukutambua wewe ni nani" Aron aliongea kwa upole akiwa amebakiza hatua kadhaa kumfikia Shadow.

Shadow alitulia kimya bila kuzungumza chochote hakugeuka wala nini. Shadow alikuwa ni mtu mwenye maisha yenye misingi ya ajabu sana hakuwa akiruhusu mtu yeyote aione sura yake hata marehemu Jenerali Phillipo Kasebele hakuwahi kuiona sura yake licha ya kufanya kazi pamoja kwa zaidi ya miaka 10. Kitendo cha Inspekta Aron kutaka kumtambua lilikuwa ni jambo ambalo hawezi kukubali litokee, haraka alikili yake ilifanya kazi upesi akapata jibu nini cha kufanya

Inspekta Aron aliyekuwa anazidi kusogea karibu na Shadow alisita ghafula baada ya kuhisi mtu huyo alikuwa anataka kufanya jambo akachukua tahadhali
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili nyumbani kwa wazari wa afya Mheshimiwa Dokta Isaack Gondwe aliamka asubuhi na mapema tofauti na ilivyokuwa kawaida yake, akajiandaa vizuri kisha akatoke nje ya nyumba yake, ratiba yake ya kwanza ilikuwa ni kwenda maabara kuu ya serikali vilipo hifadhiwa virusi vya COBOS

"Shikamoo Baba mbona mapema leo wapi?" Aliuliza Najma aliyekuwa akimwagilia maua nje ya nyumba yao
"Marhaba binti yangu, mguu wako unaendeleaje?"
"Safi ila usiku umeuma sana ila kwa sasa afadhali kidogo"
"Sawa leo nawahi ofisini nina kazi muhimu sana, baadae mwanangu" Dokta Gondwe aliongea kwa kifupi kisha akaingia kwenye gari lake, walinzi wakafuata na safari ikaanza

Najma alilisindikiza kwa macho gari la baba yake hadi lilipotoweka kwenye upeo wa macho yake. Najma alikumbuka yale maongezi nyeti aliyoyasikia usiku wakati baba yake akiongea kwenye simu na mtu ambaye hakumtambua, alihisi maongezi yale yalikuwa ni moja kati ya sababu ya baba yake kuamka mapema leo.
Baada ya kumaliza shughuli ya kumwagilia maua Najma alioga akapata kifungua kinywa kisha akakaa sebureni akiwa na kompyuta yake ndogo, akaifungua na kuwasha mtandao kisha akaandika maneno yafuatayo kwenye tovuti ya Google...

what's the V-COBOS...(nini maana ya V-COBOS)

Hili lilikuwa ni neno ambalo Najma alilisikia mara nyingi sana wakati ule baba yake anaongea na simu, sasa rasmi Najma akaanza kufuatilia nyendo za baba yake mzazi hasa baada ya Inspekta Aron kumwambia kuwa baba yake si mtu mzuri kama anavyofikiri hivyo Najma akawaza kulithibitisha hilo mwenyewe. Kwanza kabisa akataka kufuatilia kujua maana ya vimelea vya V-COBOS ambavyo baba yake alikuwa akivitaja mara nyingi wakati wa mazungumzo yale usiku
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Aron aliendelea kusogea karibu na Shadow lakini mara alisita ghafula baada ya kuhisi Shadow anataka kufanya jambo ikabidi achukue tahadhari
Haraka Inspekta Aron alizunguusha mkono wake wa kuume nyuma ya kiuno chake akachomoa bastola akaikoki na kumnyoshea Shadow kichwani. Alifanya hivyo ndani ya sekunde chache tu kiasi cha kumfanya Shadow ahairishe kufanya kile alichokusudia kufanya.

"Tulia hivyo hivyo, weka mikono kichawani alafu geuka nyuma taratibu" Inspekta Aron alitoa amri
Shadow hakuwa mbishi, akatii kile alichoambiwa, akageuka nyuma taratibu lakini akiwa bado ameficha sura yake kwa kuinama chini.
"Inua uso wako juu tafadhali" alisema Inspekta Aron huku akichukua tahadhali zote muhimu, tayari nafsi yake ilimwambia aliyesimama mbele yake hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo na huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe.
Shadow alitulia kwa sekunde kadha kisha taratibu akawa anainua uso wake. Inspekta Aron alitoa macho kwa shauku kubwa ya kutaka kuitambua sura ya mwanaume huyo ambaye mapaka sasa alifanikiwa kuona kidevu, mdomo na pua yake tu.
Ghafula Shadow alifungua mdomo na kutema kitu fulani kidogo mfano wa sindano kilichoenda kwa kasi na kutua kwenye shingo ya Inspekta Aron.
Lilikuwa ni tukio la kufumba na kufumbua baada ya kufanya hivyo Shadow aligeuka na kuanza kuondoka, Inspekta Aron alipojaribu kuzungumza alishindwa alipojaribu kupiga hatua kumfuata alishindwa, kifua kilimbana ghafula na kujikuta anakosa pumzi, akaanza kupumua juu juu na bastola yake ikidondoka chini. Aliinama huku akiwa ameshikilia kifua chake na kuhema kwa taabu sana. Aron alidumu katika hali hiyo kwa zaidi ya dakika mbili baadae akaanza kupata nafuu.

Inspekta Aron alipeleka mkono wake shingoni akachomoa ile sindano ndogo iliyotoka kwenye mdomo wa Shadow. Kilikuwa kijisindano kidogo sana kilichomchubua Inspekta Aron shingoni wala hata damu haikutoka.

"Baba!" Inspekta Aron alijikuta analiita jina la baba yake wakati anaitazama ile sindano. Haikuwa mara yake ya kwanza kuiona aina ile ya siraha aliwahi kuiona pia kwa marehemu baba yake Jenerali Phillipo Kasebele. Inspekta Aron alijikuta akiyakumbuka maneno aliyowahi kuambiwa na marehemu baba yake siku anaiona siraha hiyo ya ajabu.

"Mwanangu Aron nitakufundisha namna ya kuirusha hii sindano kwa kuipuliza, ni siraha nzuri sana inaweza kukusaidia ukiwa kwenye shida. Hakuna mwingine anaeijua zaidi yangu, nililetewa na kijana wangu mmoja ni jasusi yupo kenya" Haya yalikuwa ni maneno ya marehemu baba yake ambaye alifariki hata kabla hajamfundisha matumizi ya siraha hiyo. Kwa mujibu wa maelezo ya baba yake alisema hakuna mwingine anaejua kuhusu siraha hiyo zaidi yake na huyo Jasusi kutoka kenya, hali hii ikamfanya Inspekta Aron kujiuliza maswali

"Au huyu bwana atakuwa ni huyo Jasusi wa baba kutoka kenya? Kafuata nini huku? Hapana sio yeye" Inspekta Aron alijiuliza na kujijibu mwenyewe na hapo akajikuta anamkumbuka Annah, alihofu huenda bado ni watu wanaotaka kumuua binti huyo, mbaya zaidi yule bwana alitokea sakafu ya chini ya hospitali hiyo kule kilipo chumba cha Annah.

Inspekta Aron alianza kukimbia akiteremka kwenye ngazi kwa kasi, wala hakukumbuka tena kupanda lifti. Kadri alivyokuwa akisogea ndivyo hofu yake ikazidi kuongezeka, imani yake ilimwambia huenda yule bwana akawa amemfanyia kitu kibaya Annah kama sio kumuua kabisa.
Akiwa kwenye kasi ile ile Inspekta Aron alifika na kunyonga kitasa cha mlango akaingia moja kwa moja ndani ya chumba cha Annah.

"Mamaa..." Annah aliyekuwa anajiandaa kwenda kuoga alipiga kelele kwa hofu iliyochanganyikana na mshangao mara baada ya Inspekta Aron kuingia ghafula bila kupiga hodi, mbaya zaidi Annah alikuwa amevua nguo zake zote akiwa amesalia na nguo za ndani pake yake.
Haraka alichukua taulo dogo lililokuwa kitandani akajifunika upande wa mbele kuanzia kwenye matiti hadi katikati ya mapaja yake sehemu kubwa ya mwili wake ikawa wazi.
Inspekta Aron alisimama akiwa amepigwa na butwaa huku akihema kwa nguvu, alitazamana na Annah aliyekuwa amejikunyata ukutani kwa aibu akijaribu kujisitili.

Je, nini KITAFUATA?
Aron ataweza kugundua lolote kuhusu jasusi Shadow aliyewahi kufanya kazi na marehemu baba yake?
Vipi kuhusu NAJMA aliyeanza kufuatilia kuhusu vimelea vya V-COBOS?
Ni nani ataibuka mshindi ndani ya bahari ya Hindi Ni Shadow au Tino? Ni Dokta Gondwe au Sultana?
ITAENDELEA....
Kupata simulizi hii yote njoo WhatsApp 0756862047
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........19
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

19-( D- DAY)
ILIPOISHIA...
Inspekta Aron alisimama akiwa amepigwa na butwaa huku akihema kwa nguvu, alitazamana na Annah aliyekuwa amejikunyata ukutani kwa aibu akijaribu kujisitili.

SASA ENDELEA...
"Samahani" alisema Aron huku akitazama pembeni kwa aibu hapo Annah alisogea kitandani akachukua ile nguo pajama la wagonjwa akavaa haraka haraka

"Kwa nini umeingia ghafula hivyo, ungenikuta niko uchi sijavaa ingekuwaje" Aliuliza Annah akionekana kukasirika kiasi
"Ndio maana nimesema samahani, jiandae tunaondoka"
"Tunaenda wapi Aron?"
"Sehemu salama zaidi"
"Sehemu samala wapi?"
"Jiandae tuondoke Annah acha kuuliza maswali utajua mbele ya safari" Inspekta Aron aliongea kwa msisitizo huku akichukua simu yake, akampigia Dokta Zyunga.
Tayari Inspekta Aron alionekana kupata hofu kutokana na mfuatano wa matukio yasiyoeleweka ndani ya hospitali hiyo. Kuanzia mda ule amekutana na Tino, likafuata tukio la kuuawa kwa Big' na sasa amekutana na mtu wa ajabu ambaye hajui ni kitu gani kimemleta ndani ya hospitali hiyo.
Kwa maana hiyo kulikuwa na kila sababu za Inspekta Aron kumtoa Annah katika hospitali ya Mountenia yenye usalama mdogo.

"Hallo Dokta" aliongea Aron baada ya Dokta Zyunga kupokea simu upande wa pili
"Ndiyo Inspekta, niko mochwari huku nauhifadhi mwili wa yule bwana"
"Sawa Dokta, ukitoka huko naomba uniandalie vifaa vyote muhimu kwa ajili ya huduma ya Annah nataka nimtoe hapa hospitali"
"Mh! kwa nini mbona ghafula?"
"Aah! Hapana hakuna shida, nataka nimpeleke sehemu salama zaidi" Inspekta Aron hakutaka kuweka wazi hukusu tukio la kukutana na jasusi Shadow
"Sawa Inspekta basi nipe dakika kumi"
"Sawa"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ilikuwa ni katikati ya bahari ya hindi umbali wa kilometa 50 kutoka ufukweni ilionekana boti moja kubwa ya kifahari ikiwa imetia nanga huku upepo mwanana na mawimbi kiasi yakilipamba eneo hilo

Ndani ya boti hiyo wanaume wawili walioonekana kufanya maandalizi ya tukio maalum ambalo linakwenda kutokea muda mfupi ujao, hawa walikuwa ni Tino na kijana wake Bosco.

"Kila kitu kipo sawa sasa" Alisema Bosco
"Yes ni kweli lakini vipi kuhusu wewe uko tayari?" Aliuliza Tino
"Ndiyo, siwezi kukuangusha bosi"
"Najua huwezi ila unatakiwa ufanye zaidi ya uwezo wako, utakapokuwa unazungumza na Dokta Gondwe hakikisha unajiamini usionyeshe dalili zozote zitakazomfanya ahisi huenda wewe umetumwa na sio muhusika mkuu wa zile video na picha zake chafu"
"Sawa bosi nimeelewa"
"Vizuri kitu kingine cha muhimu, anaweza kuanza kukupa kauli za vitisho hata kujaribu kukuua lakini usijali mimi nitakuwa hapa kukulinda, Dokta Gondwe atakuja na mimi hapa na sio mtu mwingine hivyo usijali jiamini, nasisitiza tena jiamini"

Bosco akawa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akainua macho yake na kumtazama Tino, akauliza.

"Lakini bosi, kwa nini Dokta Gondwe amepanga kuja na vijana wake hapa wakati tulimpa sharti aje peke yake huoni kuwa lengo lake ni kuja kuua na sio kuleta virus vya COBOS?"
"Uko sahihi kuna mawili hapa, Dokta Gondwe amefanya kubeti kwanza atakuja na hivyo vimelea vya V-COBOS lakini atataka kuhakikisha kuwa video zake za ngono anazipata zote na hazipo sehemu nyingine yoyote, akihakikisha hilo basi atakuua na sio kukupa vimelea. Lakini kama utaonyesha hata kama atakuua bado video zake zitavuja basi anaweza kukupa hao vimelea ili kujilinda na mtaweka makubaliano, ndio maana nimekwambia unatakiwa kujiamini sana unapoongea na Dokta Gondwe lolote linaweza kutokea" alieleza Tino

Mwisho mipango yote ilikaa vizuri, Tino akapanda boti nyingine ndogo inayoendeshwa na mashine akarudi ufukweni akimuacha kijana wake Bosco ndani ya boti ile kubwa
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda ulizidi kusogea na sasa Tino alikuwa ufukweni pamoja na vijana wengine wawili. Tayari ile boti aliyoagiza Dokta Gondwe ilikuwa imeandaliwa sasa walikuwa wakimsuburi Dokta Gondwe wenyewe.

Muda mfupi baadae taksi moja ilisimama hatua kadhaa kutoka pale alipokuwa Tino na wenzake, akashuka mzee mmoja alievaa koti kubwa jeusi miwani na kofia pana, mkono wake wa kulia alikuwa ameshikilia sanduku dogo mfano wa begi aina ya briefcase'. Huyu hakuwa mwingine bali Mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Isaack Gondwe.

Baada ya taksi kuondoka Dokta Gondwe alianza kupiga hatua kusogea pale Tino na wenzake walipo. Kwa namna alivyokuwa amevaa usingedhani kuwa huyu ni waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwa na muonekano wa tofauti sana haikuwa rahisi hata kwa vijana wake kumtambua kwa haraka hadi pale alipowakaribia.

Tino macho yake yote aliyaelekeza kwenye lile sanduku alilobeba Dokta Gondwe mapigo yake ya moyo yakabadikika na kuanza kwenda mbio. Kitu alichokisubiri kwa mda mrefu, kitu kilichopelekea akamuua baba yake mzazi, kitu kilichosababisha afanye kazi kwa kumtumikia Dokta Gondwe leo hii kipo karibu yake yaani vimelea vya V-COBOS.

"Vipi Tino ushaandaa kila kitu?" Aliuliza Dokta Gondwe huku akivua miwani yake
" Kila kitu kipo kama ulivyoagiza mkuu" Tino alijibu kwa unyenyekevu huku wakati wote akitazama lile sanduku mikononi mwa Dokta Gondwe

"Sawa, hii boti mbona ndogo mtajificha wapi?" Aliuliza Dokta Gondwe
"Iko vizuri bosi, kuna sehemu za kujificha kama buti hivi pendeni na katikati tutaingia humo na hatuwezi kuonekana" alieleza Tino
"Ok vizuri, kama nilivyowaeleza kuna mtu muhimu nakwenda kufanya naye maongezi huko tunapokwenda nikiwapa ile ishara yetu ya kila siku basi mtatoka na kuingia ndani ya ile boti kama nisipofanya hivyo basi mtulie humo humo msitoke" Alieleza dokta Gondwe,
"Sawa mkuu"Tino pamoja na wale vijana wawili waliitika kwa pamoja.

Sasa zilikuwa zimesalia dakika 16 kufikia ule wakati waliokubaliana kukutana baharini, Dokta Gondwe akawa anasubiri atumiwe uelekeo 'location' mahali alipo mtu ambaye wanakwenda kubadilishana virusi vya COBOS na video yake ya ngono.

Wakati wakiendelea kusubiri kwa mbali hatua kama 50 hivi kulikuwa na mlima mmoja mdogo sana usio na miti mingi. Nyuma ya mti mmoja mkubwa alionekana jasusi Shadow akiwatazama Dokta Gondwe na vijana wake kupitia Darubini. Shadow alikuwa hapo tangu kitambo akifuatilia kila kinachoendelea. Hakutaka kufanya makosa tena kama alivyowahi kufanya miaka kadhaa iliyopita akiwa na Marehemu Jenerali Phillipo Kasebele, ilikuwa ni lazima ahakikishe siku ya leo anarudi na vimelea vya V-COBOS kisha kuvikabidhi kwa Sultana. Anakumbuka miaka kadhaa aliyopita aliwahi kuagizwa kazi kama hiyo na mume wa Sultana marehemu Jenerali Phillipo Kasebele hakufanikiwa kwa asilimia zote, alifanikiwa kuiba chupa ya kijivu yenye dawa dhidi ya vimelea vya V-COBOS lakini si vimelea vyenyewe, leo kwa mara nyingine tena anakwenda kuirudia kazi hiyo akiwa chini ya Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Aron alikuwa ndani ya gari yake pamoja na Annah binti ambaye ni shahidi pekee aliyesalia katika kesi ya mauaji inayomkabili Osward. Aron alitakiwa kumlinda Annah kwa udi na uvumba kuhakikisha anakuwa salama dhidi ya maadui ambao walikuwa wakimuwinda kila kona.
Sasa alikuwa akimuhamisha tena kwa siri kutoka hospitali ya kimataifa ya Mountenia akawa anampeleka sehemu ambayo ni yeye pekee alikuwa akijua ni wapi.
Walienda kwa muda mrefu kiasi cha kutoka nje kabisa ya mji na baadae wakafuata barabara moja ya vumbi iliyokuwa ikielekea msituni.

"Aron tunaelekea wapi mbona mbali hivi?" Annah aliuliza baada ya ukimya wa muda mrefu
"Annah ukiona hivi ujue ni wazi kuwa wewe ni mtu wa muhimu sana, si kwangu tu bali kwa watu kibao ambao wanauwawa bila hatia kila kukicha" alieleza Inspekta Aron
"Unanichanganya Aron, najua mimi ni shahidi pekee niliyebaki lakini huku tunakoenda ni wapi?"
"Ni sehemu salama usijali kuna nyumba na kila kitu utakachohitaji"
"Mmh! nyumba gani porini huku?"
"Umesahau mimi ni nani eeh! kuna nyumba ya siri huku aliijenga marehemu baba yangu, huku ndiko alikokuwa akifanya mambo mengi ya siri ya kulisaidia taifa letu baada ya kustaafu"
"Kwa hiyo wewe ulikujua vipi?"
"Aliwahi kunileta siku moja, ni sehemu ya siri mno ambayo hakuna mtu anaejua zaidi yangu na baadhi ya watu aliofanyanao kazi"
"Unataka kusema baba yako alikuamini sana"
"Sana tena sana, lakini shida alikuwa haniambii chochote kuhusu mipango yake, alidai wakati ukifika nitajua kila kitu nitaanzia pale alipoishia alinambia siku moja hatima ya hii nchi na dunia nzima itakuwa mikononi mwangu" alieleza Inspekta Aron hapo Annah akaangua kicheko tena akacheka kwa sauti sana

"Sasa mbona unacheka?"
"Hahaha umenifurahisha, hivi umejisikia ulivyoongea kweli unasemaje hatima ya Dunia iwe mikononi mwako hahah"
"Aah! usicheke, baba yangu namuamini sana kila alichokuwa akikisema kilitokea, japo alifariki ghafula lakini bado naishi kwa kuyaamini maneno yake najua ipo siku yatatimia"
"Mmh! haya bana pengine kweli, wanajeshi huwa wanamambo mengi, punguza mwendo basi spidi kali sana Aron"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili zikiwa zimesalia dakika 5, mara simu ya Dokta Gondwe ilitoa mlio fulani haraka akaifungua na kuangalia.
"Katuma location huyu bwana" alisema Dokta Gondwe huku akitabasamu
"Tunafanyaje bosi" aliuliza mmoja wa wale vijana
"Ingieni kwenye boti jificheni, sio mbali kutoka hapa, kama dakika 5 tutakuwa tumefika alipo huyu mwanaharamu" Alisema Dokta Gondwe maneno yaliyoonekana kuuchoma moyo wa Tino moja kwa moja.

"Yaani umelala na mke wangu alafu unatuita wanaharamu" Tino aliwaza wakati huo yeye na wenzake wakiingia kwenye ile boti na kujificha
Bila kupoteza muda Dokta Gondwe akiwa na lile sanduku lake alipanda kwenye boti kisha akaiwasha taratibu akaanza safari kusogea mbele akifuata uelekeo wa ramani aliyotumiwa kwenye simu yake.

Wakati huo huo Jasusi Shadow alionekana akiteremka kwa kasi kutoka kwenye ule mlima akiwa na begi kubwa mgongoni, akafika ufukweni. Haraka alifungua begi lake akatoa mtungi wa gesi vifaa vya kuogelea na vifaa vingine vingi.
Dakika moja baadae tayari Shadow alikuwa amevaa kila kitu, mtungi wa gesi uliounganishwa moja kwa moja kwenye pua na mdomo wake pamoja na miwani maalumu ya kuogelea, alifanana kabisa na wale wazamiaji wa mamjini. Alipiga hatua kuingia ndani ya maji na baadae akazama na kupotea kabisa juu ya uso wa bahari.
ITAENDELEA...
 
USIACHE KUFUATILIA SIMULIZI ZANGU ZINAZOENDELEA HUKU JAMII FORAM

1. DO NOT SHOUT - usipige kelele
2. THE MODERN WAR- Vita ya kisasa
3. STAY WITH ME- baki na mimi
4. KARANI
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........19
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

19-( D- DAY)
ILIPOISHIA...
Inspekta Aron alisimama akiwa amepigwa na butwaa huku akihema kwa nguvu, alitazamana na Annah aliyekuwa amejikunyata ukutani kwa aibu akijaribu kujisitili.

SASA ENDELEA...
"Samahani" alisema Aron huku akitazama pembeni kwa aibu hapo Annah alisogea kitandani akachukua ile nguo pajama la wagonjwa akavaa haraka haraka

"Kwa nini umeingia ghafula hivyo, ungenikuta niko uchi sijavaa ingekuwaje" Aliuliza Annah akionekana kukasirika kiasi
"Ndio maana nimesema samahani, jiandae tunaondoka"
"Tunaenda wapi Aron?"
"Sehemu salama zaidi"
"Sehemu samala wapi?"
"Jiandae tuondoke Annah acha kuuliza maswali utajua mbele ya safari" Inspekta Aron aliongea kwa msisitizo huku akichukua simu yake, akampigia Dokta Zyunga.
Tayari Inspekta Aron alionekana kupata hofu kutokana na mfuatano wa matukio yasiyoeleweka ndani ya hospitali hiyo. Kuanzia mda ule amekutana na Tino, likafuata tukio la kuuawa kwa Big' na sasa amekutana na mtu wa ajabu ambaye hajui ni kitu gani kimemleta ndani ya hospitali hiyo.
Kwa maana hiyo kulikuwa na kila sababu za Inspekta Aron kumtoa Annah katika hospitali ya Mountenia yenye usalama mdogo.

"Hallo Dokta" aliongea Aron baada ya Dokta Zyunga kupokea simu upande wa pili
"Ndiyo Inspekta, niko mochwari huku nauhifadhi mwili wa yule bwana"
"Sawa Dokta, ukitoka huko naomba uniandalie vifaa vyote muhimu kwa ajili ya huduma ya Annah nataka nimtoe hapa hospitali"
"Mh! kwa nini mbona ghafula?"
"Aah! Hapana hakuna shida, nataka nimpeleke sehemu salama zaidi" Inspekta Aron hakutaka kuweka wazi hukusu tukio la kukutana na jasusi Shadow
"Sawa Inspekta basi nipe dakika kumi"
"Sawa"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ilikuwa ni katikati ya bahari ya hindi umbali wa kilometa 50 kutoka ufukweni ilionekana boti moja kubwa ya kifahari ikiwa imetia nanga huku upepo mwanana na mawimbi kiasi yakilipamba eneo hilo

Ndani ya boti hiyo wanaume wawili walioonekana kufanya maandalizi ya tukio maalum ambalo linakwenda kutokea muda mfupi ujao, hawa walikuwa ni Tino na kijana wake Bosco.

"Kila kitu kipo sawa sasa" Alisema Bosco
"Yes ni kweli lakini vipi kuhusu wewe uko tayari?" Aliuliza Tino
"Ndiyo, siwezi kukuangusha bosi"
"Najua huwezi ila unatakiwa ufanye zaidi ya uwezo wako, utakapokuwa unazungumza na Dokta Gondwe hakikisha unajiamini usionyeshe dalili zozote zitakazomfanya ahisi huenda wewe umetumwa na sio muhusika mkuu wa zile video na picha zake chafu"
"Sawa bosi nimeelewa"
"Vizuri kitu kingine cha muhimu, anaweza kuanza kukupa kauli za vitisho hata kujaribu kukuua lakini usijali mimi nitakuwa hapa kukulinda, Dokta Gondwe atakuja na mimi hapa na sio mtu mwingine hivyo usijali jiamini, nasisitiza tena jiamini"

Bosco akawa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akainua macho yake na kumtazama Tino, akauliza.

"Lakini bosi, kwa nini Dokta Gondwe amepanga kuja na vijana wake hapa wakati tulimpa sharti aje peke yake huoni kuwa lengo lake ni kuja kuua na sio kuleta virus vya COBOS?"
"Uko sahihi kuna mawili hapa, Dokta Gondwe amefanya kubeti kwanza atakuja na hivyo vimelea vya V-COBOS lakini atataka kuhakikisha kuwa video zake za ngono anazipata zote na hazipo sehemu nyingine yoyote, akihakikisha hilo basi atakuua na sio kukupa vimelea. Lakini kama utaonyesha hata kama atakuua bado video zake zitavuja basi anaweza kukupa hao vimelea ili kujilinda na mtaweka makubaliano, ndio maana nimekwambia unatakiwa kujiamini sana unapoongea na Dokta Gondwe lolote linaweza kutokea" alieleza Tino

Mwisho mipango yote ilikaa vizuri, Tino akapanda boti nyingine ndogo inayoendeshwa na mashine akarudi ufukweni akimuacha kijana wake Bosco ndani ya boti ile kubwa
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda ulizidi kusogea na sasa Tino alikuwa ufukweni pamoja na vijana wengine wawili. Tayari ile boti aliyoagiza Dokta Gondwe ilikuwa imeandaliwa sasa walikuwa wakimsuburi Dokta Gondwe wenyewe.

Muda mfupi baadae taksi moja ilisimama hatua kadhaa kutoka pale alipokuwa Tino na wenzake, akashuka mzee mmoja alievaa koti kubwa jeusi miwani na kofia pana, mkono wake wa kulia alikuwa ameshikilia sanduku dogo mfano wa begi aina ya briefcase'. Huyu hakuwa mwingine bali Mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Isaack Gondwe.

Baada ya taksi kuondoka Dokta Gondwe alianza kupiga hatua kusogea pale Tino na wenzake walipo. Kwa namna alivyokuwa amevaa usingedhani kuwa huyu ni waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwa na muonekano wa tofauti sana haikuwa rahisi hata kwa vijana wake kumtambua kwa haraka hadi pale alipowakaribia.

Tino macho yake yote aliyaelekeza kwenye lile sanduku alilobeba Dokta Gondwe mapigo yake ya moyo yakabadikika na kuanza kwenda mbio. Kitu alichokisubiri kwa mda mrefu, kitu kilichopelekea akamuua baba yake mzazi, kitu kilichosababisha afanye kazi kwa kumtumikia Dokta Gondwe leo hii kipo karibu yake yaani vimelea vya V-COBOS.

"Vipi Tino ushaandaa kila kitu?" Aliuliza Dokta Gondwe huku akivua miwani yake
" Kila kitu kipo kama ulivyoagiza mkuu" Tino alijibu kwa unyenyekevu huku wakati wote akitazama lile sanduku mikononi mwa Dokta Gondwe

"Sawa, hii boti mbona ndogo mtajificha wapi?" Aliuliza Dokta Gondwe
"Iko vizuri bosi, kuna sehemu za kujificha kama buti hivi pendeni na katikati tutaingia humo na hatuwezi kuonekana" alieleza Tino
"Ok vizuri, kama nilivyowaeleza kuna mtu muhimu nakwenda kufanya naye maongezi huko tunapokwenda nikiwapa ile ishara yetu ya kila siku basi mtatoka na kuingia ndani ya ile boti kama nisipofanya hivyo basi mtulie humo humo msitoke" Alieleza dokta Gondwe,
"Sawa mkuu"Tino pamoja na wale vijana wawili waliitika kwa pamoja.

Sasa zilikuwa zimesalia dakika 16 kufikia ule wakati waliokubaliana kukutana baharini, Dokta Gondwe akawa anasubiri atumiwe uelekeo 'location' mahali alipo mtu ambaye wanakwenda kubadilishana virusi vya COBOS na video yake ya ngono.

Wakati wakiendelea kusubiri kwa mbali hatua kama 50 hivi kulikuwa na mlima mmoja mdogo sana usio na miti mingi. Nyuma ya mti mmoja mkubwa alionekana jasusi Shadow akiwatazama Dokta Gondwe na vijana wake kupitia Darubini. Shadow alikuwa hapo tangu kitambo akifuatilia kila kinachoendelea. Hakutaka kufanya makosa tena kama alivyowahi kufanya miaka kadhaa iliyopita akiwa na Marehemu Jenerali Phillipo Kasebele, ilikuwa ni lazima ahakikishe siku ya leo anarudi na vimelea vya V-COBOS kisha kuvikabidhi kwa Sultana. Anakumbuka miaka kadhaa aliyopita aliwahi kuagizwa kazi kama hiyo na mume wa Sultana marehemu Jenerali Phillipo Kasebele hakufanikiwa kwa asilimia zote, alifanikiwa kuiba chupa ya kijivu yenye dawa dhidi ya vimelea vya V-COBOS lakini si vimelea vyenyewe, leo kwa mara nyingine tena anakwenda kuirudia kazi hiyo akiwa chini ya Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Inspekta Aron alikuwa ndani ya gari yake pamoja na Annah binti ambaye ni shahidi pekee aliyesalia katika kesi ya mauaji inayomkabili Osward. Aron alitakiwa kumlinda Annah kwa udi na uvumba kuhakikisha anakuwa salama dhidi ya maadui ambao walikuwa wakimuwinda kila kona.
Sasa alikuwa akimuhamisha tena kwa siri kutoka hospitali ya kimataifa ya Mountenia akawa anampeleka sehemu ambayo ni yeye pekee alikuwa akijua ni wapi.
Walienda kwa muda mrefu kiasi cha kutoka nje kabisa ya mji na baadae wakafuata barabara moja ya vumbi iliyokuwa ikielekea msituni.

"Aron tunaelekea wapi mbona mbali hivi?" Annah aliuliza baada ya ukimya wa muda mrefu
"Annah ukiona hivi ujue ni wazi kuwa wewe ni mtu wa muhimu sana, si kwangu tu bali kwa watu kibao ambao wanauwawa bila hatia kila kukicha" alieleza Inspekta Aron
"Unanichanganya Aron, najua mimi ni shahidi pekee niliyebaki lakini huku tunakoenda ni wapi?"
"Ni sehemu salama usijali kuna nyumba na kila kitu utakachohitaji"
"Mmh! nyumba gani porini huku?"
"Umesahau mimi ni nani eeh! kuna nyumba ya siri huku aliijenga marehemu baba yangu, huku ndiko alikokuwa akifanya mambo mengi ya siri ya kulisaidia taifa letu baada ya kustaafu"
"Kwa hiyo wewe ulikujua vipi?"
"Aliwahi kunileta siku moja, ni sehemu ya siri mno ambayo hakuna mtu anaejua zaidi yangu na baadhi ya watu aliofanyanao kazi"
"Unataka kusema baba yako alikuamini sana"
"Sana tena sana, lakini shida alikuwa haniambii chochote kuhusu mipango yake, alidai wakati ukifika nitajua kila kitu nitaanzia pale alipoishia alinambia siku moja hatima ya hii nchi na dunia nzima itakuwa mikononi mwangu" alieleza Inspekta Aron hapo Annah akaangua kicheko tena akacheka kwa sauti sana

"Sasa mbona unacheka?"
"Hahaha umenifurahisha, hivi umejisikia ulivyoongea kweli unasemaje hatima ya Dunia iwe mikononi mwako hahah"
"Aah! usicheke, baba yangu namuamini sana kila alichokuwa akikisema kilitokea, japo alifariki ghafula lakini bado naishi kwa kuyaamini maneno yake najua ipo siku yatatimia"
"Mmh! haya bana pengine kweli, wanajeshi huwa wanamambo mengi, punguza mwendo basi spidi kali sana Aron"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili zikiwa zimesalia dakika 5, mara simu ya Dokta Gondwe ilitoa mlio fulani haraka akaifungua na kuangalia.
"Katuma location huyu bwana" alisema Dokta Gondwe huku akitabasamu
"Tunafanyaje bosi" aliuliza mmoja wa wale vijana
"Ingieni kwenye boti jificheni, sio mbali kutoka hapa, kama dakika 5 tutakuwa tumefika alipo huyu mwanaharamu" Alisema Dokta Gondwe maneno yaliyoonekana kuuchoma moyo wa Tino moja kwa moja.

"Yaani umelala na mke wangu alafu unatuita wanaharamu" Tino aliwaza wakati huo yeye na wenzake wakiingia kwenye ile boti na kujificha
Bila kupoteza muda Dokta Gondwe akiwa na lile sanduku lake alipanda kwenye boti kisha akaiwasha taratibu akaanza safari kusogea mbele akifuata uelekeo wa ramani aliyotumiwa kwenye simu yake.

Wakati huo huo Jasusi Shadow alionekana akiteremka kwa kasi kutoka kwenye ule mlima akiwa na begi kubwa mgongoni, akafika ufukweni. Haraka alifungua begi lake akatoa mtungi wa gesi vifaa vya kuogelea na vifaa vingine vingi.
Dakika moja baadae tayari Shadow alikuwa amevaa kila kitu, mtungi wa gesi uliounganishwa moja kwa moja kwenye pua na mdomo wake pamoja na miwani maalumu ya kuogelea, alifanana kabisa na wale wazamiaji wa mamjini. Alipiga hatua kuingia ndani ya maji na baadae akazama na kupotea kabisa juu ya uso wa bahari.
ITAENDELEA...
Umetisha mjuba!

Ngoja niweke kambi na hapa.
 
THE MODERN WAR
(vita ya kisasa)
Sehemu ya..............20
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

20-(Kuilinda au kuiteketeza Dunia)
ILIPOISHIA...
Inspekta Aron anaamua kumuhamisha Annah kutoka hospitali ya kimataifa ya Mountenia kwenda msituni katika nyumba ambayo yalikuwa ni makazi ya siri ya baba yake Jenerali Phillipo enzi za uhai wake. Upande wa pili Dokta Gondwe yuko kwenye boti tayari kwenda kufanya mapatano na mtu anayeamini anazo video na picha zake za ngono, wakati huo pia Jasusi Shadow anawafuatilia kwa siri.

Nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
"Aah! usicheke, baba yangu namuamini sana kila alichokuwa akikisema kilitokea, japo alifariki ghafula lakini bado naishi kwa kuyaamini maneno yake najua ipo siku yatatimia" Inspekta Aron aliongea tena kwa msisitizo ilibidi Annah ajilazimishe kukubaliana na kauli hiyo japo haikumuingia akilini kabisa

"Eti hatima ya Dunia nzima iwe mikononi mwako mbona ajabu sana hii" aliwaza Annah, wakati huo Inspekta Aron alinyonga usukani akakata kona upande wa kushoto wa barabara ile ya vumbi akaenda kwa mwenda wa taratibu kisha akasimamisha gari yake katika kichaka kimoja kikubwa

"Shuka tumefika" Alisema Inspekta Aron
"Mmh!!" Annah aliguna hali akiangaza macho huku na huku kuangalia mazingira ya eneo hilo, ilikuwa ni katikati ya msitu mnene
Walishuka na kuliacha gari wakaanza kutembea kwa miguu Aron akiwa ndiye kiongozi. Baada ya mwendo kama wa dakika kumi hivi hatimaye mbele yao waliliona jengo moja lenye muonekana chakavu kwa nje lakini ndani kulikuwa na kila kitu cha kumuwezesha mtu kuishi huko hata mwaka mzima.

Asilimia kubwa ya nyumba hii ilijengwa kwa miti ya mbao, ilikuwa na muundo kama ghorofa moja hivi yaani juu na chini. Kabla ya kuingia ndani Aron alikagua mazingira ya nje kujiridhisha na usalama wa eneo hilo baadae akaingia ndani akafanya hivyo hivyo. Wakati akifanya ukaguzi huo Inspekta Aron aligundua kitu cha tofauti

"Kuna mtu anaishi hapa, atakuwa ni nani huyo?" Inspekta Aron alijiuliza wakati akiendelea kuchunguza mazingira ya nyumba hiyo mwisho alirudi sebureni akamkuta Annah amajilaza kwenye kochi

"Mara ya mwisho kuja hapa ilikuwa ni lini afande?" Aliuliza Annah
"Tangu mwaka jana"
"Kwa hiyo hakuna mwingine anaejua kuhusu uwepo wa hii nyumba zaidi yako"
"Ndiyo ni mimi tu" Aron alidanganya akiuficha ukweli kuwa kuna kila dalili zinazoonyesha kuna mtu huwa anakuja au anaishi ndani ya nyumba hiyo, swali likabaki kichwani mwake, ni nani?
"Kwa hiyo Aron tutaishi huku hadi siku ya mahakamani ifike si ndiyo? au utakuwa unaondoka na kuniacha mwenyewe?" Aliuliza Annah swali ambalo lilikuwa ni muhimu sana kwa Aron, awali aliamini mazingira hayo yangemuweka Annah salama zaidi dhidi ya watu wanaotaka kumuua, aliamini ataweza kwenda kazini akamuacha Annah lakini kwa bahati mbaya bado aliona nyumba hiyo haiko salama pia

"Mbona hujibu?" Annah aliuliza huku akimtazama Inspekta Aron usoni
"Ah..ee tutaishi huku wote, siwezi kukuacha mwenyewe unakumbuka nilikuahidi nitakuwa na wewe kila wakati kukulinda" Alisema Aron maneno yaliyopenya moja kwa moja kwenye moyo wa Annah akajikuta anatabasamu na kumtazama Inspekta Aron kwa macho maregevu, taratibu Annah akaanza kujikuta anampenda Inspekta Aron.
[emoji294][emoji294][emoji294]
BAHARI YA HINDI...
Baada ya mwendo wa dakika tano ndani ya maji hatimaye Dokta Gondwe alifika akasimamisha boti yake pembeni ya boti nyingine kubwa iliyokuwa imetia nanga katikati ya bahari. Kwa mujibu wa ramani aliyotumiwa hapo ndipo alipokuwa mtu anaetegemea kukutana naye.

Akiwa na lile sanduku Dokta Gondwe alishuka, akakanyaga ngazi za ile boti kubwa akaanza kupiga hatua taratibu hadi alipoufikia mlango fulani uliokuwa wazi akaingia ndani. Chumba cha kwanza kilikuwa kitupu lakini mbele yake kulikuwa mlango mwingine tena ulio wazi pia Dokta Gondwe akasonga mbele na kuzidi kuingia ndani ya vyumba vya boti hiyo yenye muundo wa kisasa.
Huku nyuma ndani ya ile boti ndogo aliyokujanayo Dokta Gondwe aliwaacha Tino na vijana wake wengine wawili wakiwa wamejificha kusubiri maelezo ya bosi wao. Katika mikono yao ya kushoto wote walivaa saa ambayo ni maalumu kwa ajili ya kutoa mlio wa kengere ya hatari mara tu Dokta Gondwe atakapo bonyeza kitufe kwenye saa yake ambayo imeunganishawa kitaalamu na saa hizo walizovaa vijana wake.

Baada ya kuvuka vyumba kadhaa hatimae Dokta Gondwe alifika kwenye chumba cha mwisho ambacho kilikuwa na meza nyembamba na ndefu sana, upande mmoja wa meza hiyo alimuona mtu aliyepigilia suti nadhifu yenye rangi ya ugoro akiwa amesimama na kumpa mgongo huku mikono yake ikiwa mfukoni, huyu hakuwa mwingine bali Bosco kijana aliyeaminiwa na kusimama badala ya Tino.

"Karibu kiti" Alisema Bosco huku akigeuka taratibu akavuta kiti na kukaa upande moja wa meza ile ndefu. Akiwa na tahadhali kubwa Dokta Gondwe naye alivuta kiti kilichokuwa upande wa pili wa meza ile akakaa.

"Sikuwa nategema kama nitakutana na kijana mdogo kama wewe" Dokta Gondwe aliongea kwa kujiamini
"Sidhani kama tuna mda wa kutosha hadi kupata nafasi ya kuzungumzia mambo ya umri, tuna robo saa tu kila kitu kiwe kimekwisha" Bosco aliongea kwa kujiamini vile vile
"Sawa, nimekuletea virusi vya COBOS kama ulivyotaka hivi hapa" Dokta Gondwe aliongea na kuliweka lile sanduku juu ya meza, akatulia kwa muda kisha akaendelea kuongea

"Kabla sijakukabidhi vimelea hivi nataka kujua kwanza utavifanyia nini?"
"Sijapanga bado" alijibu Bosco
"Unamaana gani?"
"Maana yangu ni hii kuna mawili, pengine nikailinda Dunia au nikaiteketeza Dunia"
"Una maana gani kusema utailinda au kuiteketeza Dunia?"
"Kuilinda Dunia maana yake nitavisambaratisha hivo virusi vipotee kabisa visiwepo tena Duniani, na kuiteketeza Dunia maana yake nitasambaza hivi virusi Duniani kote na watu wataumwa na kufa kama ilivyokuwa kwa virusi vya Corona" Bosco aliendelea kuongea kwa kujiamini sana.
"Kwa nini ufanye hivyo, huoni kama utaua watu wengi wasio na hatia wakiwemo ndugu na jamaa zako tena ndani ya nchi yako mwenyewe"
"Hayo maswali mimi ndio natakiwa kukuuliza wewe na viongozi wenzako mliokubali kuviingiza vimelea hivi nchini, je unaweza kunijibu mlikuwa mnawaza nini?" Aliuliza Bosco huku akimtazama dokta Gondwe usoni ambaye alibaki kimya
"Hahah jibu ni jepesi tu Dokta Gondwe, mlijiamini kwa sababu mlijua dawa ipo mtakunywa na kupona lakini wengine watakufa, basi mimi sina tofauti na ninyi kwa kuwa ninayo dawa dhidi ya virusi vya COBOS basi nitafanya chochote nachotaka" Bosco aliongea kwa kujiamini sana yaani ilikuwa ni zaidi ya vile aliivyotaka Tino.
Kauli hiyo ilimfanya Dokta Gondwe ameze fundo kubwa la mate, kusikia kuwa mtu aliyepo mbele yake anayo dawa dhidi ya virusi vya COBOS, dawa iliyoibiwa miaka michache iliyopita ilikuwa ni habari nyingine mpya kwake.
Hii ilikuwa ni moja kati ya mbinu waliyopanga kuitumia Bosco na Tino ili kumteka kiakili mheshimiwa Waziri Dokta Gondwe lakini ukweli ulikuwa ni kwamba wanaojua dawa ya virusi vya COBOS ilipo ni jasusi Shadow na Sultana pekee na hii ndiyo sababu Tino alikuwa akipigania uhai wa mama yake Sultana kwa udi na uvumba kuhakikisha anapona.

"Nikikupa hivi vimelea vya V-COBOS vipi kuhusu usalama wa picha na video zangu chafu?"
"Nitazifuta"
"Utazifuta, hivyo tu? mimi nitaaminije kama umezifuta?"
"Nitakupa video orijino kutoka kwenye kamera iliyokurekodi, najua unaelewa hata kama nitabaki na kopi itakuwa haina nguvu sana kama video orijino"
"Hayo ni mambo ya wataalamu wa kompyuta TI mimi najulia wapi alafu kwanini...." Alisema Dokta Gondwe lakini kabla hajamalizia kauli yake mara walisikia sauti ya kioo cha dirisha kikipasuliwa kutoka chumba jirani ikifuatiwa na kishindo

Bosco na Dokta Gondwe walitazamana kwa macho ya kuulizana kila mmoja akionyesha kusikia sauti hiyo lakini haelewi kinachoendelea mbaya zaidi watu hao wawili walikuwa hawaaminiani kabisa kila mmoja alikuwa anawaza mwenzake anaweza kumsaliti mda wowote.

Baada ya kutazamana kwa muda ghafula kila mmoja akachukua bastola yake na kumnyoshea mwenzake, ilikuwa ni kitendo cha haraka haraka kila mmoja akawa amemuwahi mwenzake kwa kumnyoshea bastola. Bosco aliitoa bastola yake chini ya meza usawa wa eneo alipokuwa amekaa, wakati Dokta Gondwe aliitoka kwenye mfuko wa juu wa koti lake

Sasa kila mmoja akawa anatazamana na mdomo wa bastola ya mwenzake

"Unataka kufanya nini mheshimiwa Waziri?" Aliuliza Bosco
"Nikuulize wewe unampango gani wa siri?"
"Sina mpango wowote"
"Hiyo sauti imetoka wapi na ni ya nani, uliniambia tutakuwa wawili tu?"
"Nikulize wewe umekuja na nani?"
"Niko mwenyewe, hii sauti imetoka ndani humu humu acha kujitoa ufahamu unaelewa kinachoendelea kijana" Dokta Gondwe aliongea huku akiishikilia bastola yake saawia.
Wakati huo si Bosco si Dokta Gondwe hakuna aliyekuwa akimuamini mwenzake hawakujua kuwa mzee wa kazi Jasusi Shadow alikuwa ameingia ndani ya boti hiyo naye akiwa anavitaka vimelea vya V-COBOS kama alivyoagizwa na Sultana. Tino na wale vijana wawili walienda kusubiri ndani ya ile boti ndogo, hawakujua chochote kinachoendelea..
Je, nani ataibuka mshindi kuondoka na sanduku?
Ni nani ambaye anaishi kwenye ile nyumba msituni walipo Annah na inspekta Aron kwa sasa?.
Vipi kuhusu Annah kuanza kumpenda Inspekta Aron?
Vipi kuhusu Najma?

ITAENDELEA...

Full 1500 tu
0756862047
 
Back
Top Bottom