SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #41
Mpooo!?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waiting for youMpooo!?
Akikujibu niambie namimi nianze kusoma, hawachelewi kusema "hata Mimi naifata mahali na Kuna majukumu mengine natakiwa kufanya" ila huyu anaonekana fresh, tushauriane Mimi na wewe tusome au tusubirie kwanza ? [emoji2][emoji2][emoji125][emoji125]Mkuu itaisha nianze kusoma? Inaonekana tamu sana, naogopa kuanza na nikakumbana na arosto
Fuatilia simulizi nazopost zote zinafika MWISHO japo ni kweli tupo ki biashara pale utakapohitaji yote kwa wakati mmoja utalazimika kuchangia, ila huku JF tutaenda mdogo mdogo mpaka MwishoAkikujibu niambie namimi nianze kusoma, hawachelewi kusema "hata Mimi naifata mahali na Kuna majukumu mengine natakiwa kufanya" ila huyu anaonekana fresh, tushauriane Mimi na wewe tusome au tusubirie kwanza ? [emoji2][emoji2][emoji125][emoji125]
Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
KESHO jionWacha nipitie na humu
Umetisha mjuba!THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..........19
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
19-( D- DAY)
ILIPOISHIA...
Inspekta Aron alisimama akiwa amepigwa na butwaa huku akihema kwa nguvu, alitazamana na Annah aliyekuwa amejikunyata ukutani kwa aibu akijaribu kujisitili.
SASA ENDELEA...
"Samahani" alisema Aron huku akitazama pembeni kwa aibu hapo Annah alisogea kitandani akachukua ile nguo pajama la wagonjwa akavaa haraka haraka
"Kwa nini umeingia ghafula hivyo, ungenikuta niko uchi sijavaa ingekuwaje" Aliuliza Annah akionekana kukasirika kiasi
"Ndio maana nimesema samahani, jiandae tunaondoka"
"Tunaenda wapi Aron?"
"Sehemu salama zaidi"
"Sehemu samala wapi?"
"Jiandae tuondoke Annah acha kuuliza maswali utajua mbele ya safari" Inspekta Aron aliongea kwa msisitizo huku akichukua simu yake, akampigia Dokta Zyunga.
Tayari Inspekta Aron alionekana kupata hofu kutokana na mfuatano wa matukio yasiyoeleweka ndani ya hospitali hiyo. Kuanzia mda ule amekutana na Tino, likafuata tukio la kuuawa kwa Big' na sasa amekutana na mtu wa ajabu ambaye hajui ni kitu gani kimemleta ndani ya hospitali hiyo.
Kwa maana hiyo kulikuwa na kila sababu za Inspekta Aron kumtoa Annah katika hospitali ya Mountenia yenye usalama mdogo.
"Hallo Dokta" aliongea Aron baada ya Dokta Zyunga kupokea simu upande wa pili
"Ndiyo Inspekta, niko mochwari huku nauhifadhi mwili wa yule bwana"
"Sawa Dokta, ukitoka huko naomba uniandalie vifaa vyote muhimu kwa ajili ya huduma ya Annah nataka nimtoe hapa hospitali"
"Mh! kwa nini mbona ghafula?"
"Aah! Hapana hakuna shida, nataka nimpeleke sehemu salama zaidi" Inspekta Aron hakutaka kuweka wazi hukusu tukio la kukutana na jasusi Shadow
"Sawa Inspekta basi nipe dakika kumi"
"Sawa"
[emoji294][emoji294][emoji294]
Ilikuwa ni katikati ya bahari ya hindi umbali wa kilometa 50 kutoka ufukweni ilionekana boti moja kubwa ya kifahari ikiwa imetia nanga huku upepo mwanana na mawimbi kiasi yakilipamba eneo hilo
Ndani ya boti hiyo wanaume wawili walioonekana kufanya maandalizi ya tukio maalum ambalo linakwenda kutokea muda mfupi ujao, hawa walikuwa ni Tino na kijana wake Bosco.
"Kila kitu kipo sawa sasa" Alisema Bosco
"Yes ni kweli lakini vipi kuhusu wewe uko tayari?" Aliuliza Tino
"Ndiyo, siwezi kukuangusha bosi"
"Najua huwezi ila unatakiwa ufanye zaidi ya uwezo wako, utakapokuwa unazungumza na Dokta Gondwe hakikisha unajiamini usionyeshe dalili zozote zitakazomfanya ahisi huenda wewe umetumwa na sio muhusika mkuu wa zile video na picha zake chafu"
"Sawa bosi nimeelewa"
"Vizuri kitu kingine cha muhimu, anaweza kuanza kukupa kauli za vitisho hata kujaribu kukuua lakini usijali mimi nitakuwa hapa kukulinda, Dokta Gondwe atakuja na mimi hapa na sio mtu mwingine hivyo usijali jiamini, nasisitiza tena jiamini"
Bosco akawa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akainua macho yake na kumtazama Tino, akauliza.
"Lakini bosi, kwa nini Dokta Gondwe amepanga kuja na vijana wake hapa wakati tulimpa sharti aje peke yake huoni kuwa lengo lake ni kuja kuua na sio kuleta virus vya COBOS?"
"Uko sahihi kuna mawili hapa, Dokta Gondwe amefanya kubeti kwanza atakuja na hivyo vimelea vya V-COBOS lakini atataka kuhakikisha kuwa video zake za ngono anazipata zote na hazipo sehemu nyingine yoyote, akihakikisha hilo basi atakuua na sio kukupa vimelea. Lakini kama utaonyesha hata kama atakuua bado video zake zitavuja basi anaweza kukupa hao vimelea ili kujilinda na mtaweka makubaliano, ndio maana nimekwambia unatakiwa kujiamini sana unapoongea na Dokta Gondwe lolote linaweza kutokea" alieleza Tino
Mwisho mipango yote ilikaa vizuri, Tino akapanda boti nyingine ndogo inayoendeshwa na mashine akarudi ufukweni akimuacha kijana wake Bosco ndani ya boti ile kubwa
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda ulizidi kusogea na sasa Tino alikuwa ufukweni pamoja na vijana wengine wawili. Tayari ile boti aliyoagiza Dokta Gondwe ilikuwa imeandaliwa sasa walikuwa wakimsuburi Dokta Gondwe wenyewe.
Muda mfupi baadae taksi moja ilisimama hatua kadhaa kutoka pale alipokuwa Tino na wenzake, akashuka mzee mmoja alievaa koti kubwa jeusi miwani na kofia pana, mkono wake wa kulia alikuwa ameshikilia sanduku dogo mfano wa begi aina ya briefcase'. Huyu hakuwa mwingine bali Mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Isaack Gondwe.
Baada ya taksi kuondoka Dokta Gondwe alianza kupiga hatua kusogea pale Tino na wenzake walipo. Kwa namna alivyokuwa amevaa usingedhani kuwa huyu ni waziri wa afya Dokta Gondwe alikuwa na muonekano wa tofauti sana haikuwa rahisi hata kwa vijana wake kumtambua kwa haraka hadi pale alipowakaribia.
Tino macho yake yote aliyaelekeza kwenye lile sanduku alilobeba Dokta Gondwe mapigo yake ya moyo yakabadikika na kuanza kwenda mbio. Kitu alichokisubiri kwa mda mrefu, kitu kilichopelekea akamuua baba yake mzazi, kitu kilichosababisha afanye kazi kwa kumtumikia Dokta Gondwe leo hii kipo karibu yake yaani vimelea vya V-COBOS.
"Vipi Tino ushaandaa kila kitu?" Aliuliza Dokta Gondwe huku akivua miwani yake
" Kila kitu kipo kama ulivyoagiza mkuu" Tino alijibu kwa unyenyekevu huku wakati wote akitazama lile sanduku mikononi mwa Dokta Gondwe
"Sawa, hii boti mbona ndogo mtajificha wapi?" Aliuliza Dokta Gondwe
"Iko vizuri bosi, kuna sehemu za kujificha kama buti hivi pendeni na katikati tutaingia humo na hatuwezi kuonekana" alieleza Tino
"Ok vizuri, kama nilivyowaeleza kuna mtu muhimu nakwenda kufanya naye maongezi huko tunapokwenda nikiwapa ile ishara yetu ya kila siku basi mtatoka na kuingia ndani ya ile boti kama nisipofanya hivyo basi mtulie humo humo msitoke" Alieleza dokta Gondwe,
"Sawa mkuu"Tino pamoja na wale vijana wawili waliitika kwa pamoja.
Sasa zilikuwa zimesalia dakika 16 kufikia ule wakati waliokubaliana kukutana baharini, Dokta Gondwe akawa anasubiri atumiwe uelekeo 'location' mahali alipo mtu ambaye wanakwenda kubadilishana virusi vya COBOS na video yake ya ngono.
Wakati wakiendelea kusubiri kwa mbali hatua kama 50 hivi kulikuwa na mlima mmoja mdogo sana usio na miti mingi. Nyuma ya mti mmoja mkubwa alionekana jasusi Shadow akiwatazama Dokta Gondwe na vijana wake kupitia Darubini. Shadow alikuwa hapo tangu kitambo akifuatilia kila kinachoendelea. Hakutaka kufanya makosa tena kama alivyowahi kufanya miaka kadhaa iliyopita akiwa na Marehemu Jenerali Phillipo Kasebele, ilikuwa ni lazima ahakikishe siku ya leo anarudi na vimelea vya V-COBOS kisha kuvikabidhi kwa Sultana. Anakumbuka miaka kadhaa aliyopita aliwahi kuagizwa kazi kama hiyo na mume wa Sultana marehemu Jenerali Phillipo Kasebele hakufanikiwa kwa asilimia zote, alifanikiwa kuiba chupa ya kijivu yenye dawa dhidi ya vimelea vya V-COBOS lakini si vimelea vyenyewe, leo kwa mara nyingine tena anakwenda kuirudia kazi hiyo akiwa chini ya Sultana.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Inspekta Aron alikuwa ndani ya gari yake pamoja na Annah binti ambaye ni shahidi pekee aliyesalia katika kesi ya mauaji inayomkabili Osward. Aron alitakiwa kumlinda Annah kwa udi na uvumba kuhakikisha anakuwa salama dhidi ya maadui ambao walikuwa wakimuwinda kila kona.
Sasa alikuwa akimuhamisha tena kwa siri kutoka hospitali ya kimataifa ya Mountenia akawa anampeleka sehemu ambayo ni yeye pekee alikuwa akijua ni wapi.
Walienda kwa muda mrefu kiasi cha kutoka nje kabisa ya mji na baadae wakafuata barabara moja ya vumbi iliyokuwa ikielekea msituni.
"Aron tunaelekea wapi mbona mbali hivi?" Annah aliuliza baada ya ukimya wa muda mrefu
"Annah ukiona hivi ujue ni wazi kuwa wewe ni mtu wa muhimu sana, si kwangu tu bali kwa watu kibao ambao wanauwawa bila hatia kila kukicha" alieleza Inspekta Aron
"Unanichanganya Aron, najua mimi ni shahidi pekee niliyebaki lakini huku tunakoenda ni wapi?"
"Ni sehemu salama usijali kuna nyumba na kila kitu utakachohitaji"
"Mmh! nyumba gani porini huku?"
"Umesahau mimi ni nani eeh! kuna nyumba ya siri huku aliijenga marehemu baba yangu, huku ndiko alikokuwa akifanya mambo mengi ya siri ya kulisaidia taifa letu baada ya kustaafu"
"Kwa hiyo wewe ulikujua vipi?"
"Aliwahi kunileta siku moja, ni sehemu ya siri mno ambayo hakuna mtu anaejua zaidi yangu na baadhi ya watu aliofanyanao kazi"
"Unataka kusema baba yako alikuamini sana"
"Sana tena sana, lakini shida alikuwa haniambii chochote kuhusu mipango yake, alidai wakati ukifika nitajua kila kitu nitaanzia pale alipoishia alinambia siku moja hatima ya hii nchi na dunia nzima itakuwa mikononi mwangu" alieleza Inspekta Aron hapo Annah akaangua kicheko tena akacheka kwa sauti sana
"Sasa mbona unacheka?"
"Hahaha umenifurahisha, hivi umejisikia ulivyoongea kweli unasemaje hatima ya Dunia iwe mikononi mwako hahah"
"Aah! usicheke, baba yangu namuamini sana kila alichokuwa akikisema kilitokea, japo alifariki ghafula lakini bado naishi kwa kuyaamini maneno yake najua ipo siku yatatimia"
"Mmh! haya bana pengine kweli, wanajeshi huwa wanamambo mengi, punguza mwendo basi spidi kali sana Aron"
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili zikiwa zimesalia dakika 5, mara simu ya Dokta Gondwe ilitoa mlio fulani haraka akaifungua na kuangalia.
"Katuma location huyu bwana" alisema Dokta Gondwe huku akitabasamu
"Tunafanyaje bosi" aliuliza mmoja wa wale vijana
"Ingieni kwenye boti jificheni, sio mbali kutoka hapa, kama dakika 5 tutakuwa tumefika alipo huyu mwanaharamu" Alisema Dokta Gondwe maneno yaliyoonekana kuuchoma moyo wa Tino moja kwa moja.
"Yaani umelala na mke wangu alafu unatuita wanaharamu" Tino aliwaza wakati huo yeye na wenzake wakiingia kwenye ile boti na kujificha
Bila kupoteza muda Dokta Gondwe akiwa na lile sanduku lake alipanda kwenye boti kisha akaiwasha taratibu akaanza safari kusogea mbele akifuata uelekeo wa ramani aliyotumiwa kwenye simu yake.
Wakati huo huo Jasusi Shadow alionekana akiteremka kwa kasi kutoka kwenye ule mlima akiwa na begi kubwa mgongoni, akafika ufukweni. Haraka alifungua begi lake akatoa mtungi wa gesi vifaa vya kuogelea na vifaa vingine vingi.
Dakika moja baadae tayari Shadow alikuwa amevaa kila kitu, mtungi wa gesi uliounganishwa moja kwa moja kwenye pua na mdomo wake pamoja na miwani maalumu ya kuogelea, alifanana kabisa na wale wazamiaji wa mamjini. Alipiga hatua kuingia ndani ya maji na baadae akazama na kupotea kabisa juu ya uso wa bahari.
ITAENDELEA...