Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

Simulizi ya kipelelezi na love story kali ndani yake; The Modern War (Vita ya Kisasa)

THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............21
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

21-(VITA BAHARINI)
ILIPOISHIA.....
Wakati huo si Bosco si Dokta Gondwe hakuna aliyekuwa akimuamini mwenzake hawakujua kuwa mzee wa kazi Jasusi Shadow alikuwa ameingia ndani ya boti hiyo naye akiwa anavitaka vimelea vya V-COBOS kama alivyoagizwa na Sultana. Tino na wale vijana wawili walienda kusubiri ndani ya ile boti ndogo, hawakujua chochote kinachoendelea..

SASA ENDELEA....
Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akiwa amemnyoshea mwenzake bastola mara walishtushwa na mtikisiko mkubwa ndani ya boti hiyo mtikisiko uliosababisha wote wawili kuanguka chini kwa pamoja. Boti iliyumba ikiwapeleka kulia na kisha kuwatupa upande wa kushoto. Walishindwa kustahimili kuendelea kushikilia siraha zao zikadondoka chini, kila mmoja akawa anajitahidi kujishikilia mahali ili asiumie kutokana na kuyumba yumba kwa boti ile wasielewe ni nini chanzo. Mara ghafula hali ikatulia kwa sekunde kadhaa kisha wakashangaa kuona boti inaanza kwenda mbele kwa kasi sana.
Mambo yakazidi kuwa mazito kwa upande wa Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akimuhisi mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa kihusika na kila kinachoendelea wakati huo hawakujua kabisa habari za kuwepo kwa Jasusi Shadow ndani ya boti hiyo.
Hapo ndipo Dokta Gondwe alipokumbuka kubonyeza saa yake kuwashtua Tino na wenzake ambao walikuwa bado wamejificha kwenye ile boti ndogo wasielewe kinachoendelea.

Bosco na Dokta Gondwe walisimama tena wakawa wanatazamana, Bado kulikuwa na mtikisiko kiasi huku boti hiyo ikizidi kukata mawimbi kuelekea kusikojulikana. Hakuna aliyejua ni wapi siraha yake imedondokea. Katikati yao kulikuwa na lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS, wote walitupa macho mbele wakaliona sanduku lile likiwa limedondoka chini, mtihani ukawa ni nani kati yao ataliwahi.

Bosco alikimbia kulifuata sanduku Dokta Gondwe naye akakimbia kumuwahi kabla hajalifikia akamvaa na kwenda naye chini wakaanguka kama magunia, sasa ikawa ni mwendo wa piga nikupige vita kali ikaibuka kati ya Bosco na Dokta Gondwe.
Wakati hali hiyo ikiendelea mara ghafula kuna moshi mweupe ulitanda ndani ya kile chumba, kwa mbali Jasusi Shadow alionekana anaingia kwa kasi akafika na kulichukua lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS kisha akatoka. Badala ya kushirikiana kumzuia Dokta Gondwe na Bosco waliendelea kupigana huku kila mmoja akiwa amemjeruhi mwenzake vibaya.
Dokta Gondwe alikuwa akivuja damu puani wakati Bosco alikuwa akivuja damu mdomoni. Waliendelea kupigana kwa kuviziana kutokana na moshi mwingi uliotanda ndani ya chumba hicho.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Baada ya kengere ya hatari kulia katika saa ya Tino na wenzake, haraka walitoka kwenye maficho yao huku Tino akiwa ndio wa kwanza.

Wote walioshuhudia ile boti kubwa ikiondoka kwa kasi kuelekea upande wa mashariki

"Shiiit!! Nini kinaendelea?" Tino aliuliza kwa kustaajabu huku akiiwasha boti haraka, akashika usukani na kukata kona akaanza kuifukuzia ile boti yake kubwa.

Kuondoka kwa boti hiyo lilikuwa ni tukio ambalo lilimshangaza sana Tino, haikuwa kwenye mpango wake kabisa, alishindwa kuelewa ni nani hasa kafanya hivyo, je ni Bosco au Dokta Gondwe?
Aliendesha boti kwa kasi kujitahidi kuifikia ile boti kubwa ambayo nayo ilikuwa kwenye mwendo wa kasi ikikata mawimbi haswa.
Spidi aliyokuwanayo Tino ilifawafanya wenzake waanze kuogoapa kwani kuna wakati boti ilikuwa ikiruka juu mita kadhaa kutoka usawa wa maji na baadae kurudi chini kishakuendelea kukata mawimbi. Ilibidi wajishikilie kwa nguvu kwenye pembe za boti hiyo.
Akiwa amebakiza umbali wa mita chache kuifikia ile boti kubwa, mara mshare wa mafuta ulianza kuyumba yumba hii ilikuwa ni ishara tosha kuwa mafuta yalikuwa yanakaribia kuisha.
Tino alipiga hesabu za haraka haraka afanye nini kwani kulikuwa na kila dalili kuwa mafuta yataisha hata kabla hajaifikia ile boti kubwa.

"Shika endesha" Tino alimwambia mmoja kati ya vijana aliokuwanao
Bila kupinga yule kijana alipishana na Tino akashika usukani.
Tino alirudi nyuma akafungua sehemu fulani ndani ya ile boti akatoa begi moja kubwa lililokuwa limejaa vifaa vya kuogerea ikiwemo pia mtungi mdogo wa gesi unaoweza kumsaidia mtu kupumua kwa dakika kadhaa akiwa ndani ya maji.
Tino alivaa vile vifaa haraka haraka, wakati anamaliza tu kuvaa tayari boti iliisha mafuta ikazima na kusimama. Tino hakutaka kujiuliza mara mbili mbili haraka alijitosa majini na kuzama alipokuja kuibuka alikuwa karibu kabisa kuifikia ile boti kubwa, akazama tena na kuogerea kwa kutumia vile vifaa alivyovaa ambavyo vilimuwezasha kwenda kwa kasi akiwa ndani ya maji alipokuja kuibuka tena kwa mara ya pili tayari alishaifikia ile boti akapanda na kuanza kusogea taratibu akipandisha ngazi.
Wale vijana wawili walibaki kwenye ile boti ndogo wakielea elea juu ya maji, hawakujua wafanye nini kwani waliachwa umbali mrefu sana. Walichofanya walichukua miko na kuanza kupiga makasia kurudi nchi kavu.

Tino alipokanyaga ngazi ya mwisho kuingia kwenye boti mara mlango uliokuwa mbele yake ulifunguliwa. Kuna mtu alikuwa akitoka kwa kasi ambaye naye alisimama ghafula mara baada ya kukutana uso kwa uso na Tino, mtu huyu alikuwa ni jasusi Shadow.

Wote wawili walikuwa wamevaa vifaa vya kufanana, isipokuwa mtungi wa gesi wa Jasusi Shadow ulikuwa ni mkubwa kuliko wa Tino lakini kila kitu walifanana.

Shadow aliweza kugundua kuwa aliyepo mbele yake ni Tino mtoto wa kwanza wa bosi Sultana lakini Tino hakuwa akimjua mtu aliyesimama mbele yake licha ya hivyo hakuweza pia kuiona sura ya mtu huyo kutokana na ile maski ya kupitisha gesi aliyovaa usoni.
Tino alimtazama Shadow kuanzia juu hadi chini na hapo ndipo akaliona lile sanduku ambalo awali alimuona nalo Dokta Gondwe. Hapo ndipo Tino akagundua kuwa mtu huyo alikuwa na lengo la kuondoka na vimelea vya V-COBOS, lilikuwa ni jambo ambalo katu asingekubali kuona linatokea mbele ya macho yake, hakuwa tayari kumruhusu aondoke na sanduku lile. Lakini Tino hakujua mtu aliyesimama mbele yake ni nani na anauwezo kiasi gani.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili mtoto wa kishua Najma ama kwa lugha ya kisasa tungemwita Pisi kali toto la mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alionekana ndani ya gari akiwa katikati ya barabara kuelekea gereza alilohifadhiwa mumewe mtarajiwa Osward.
Bado akili ya Najma haikuwa sawa kabisa, alikuwa akiwaza kuhusu majibu aliyoyapata mtandaoni baada ya kutafuta maana ya vimelea vya COBOS ambavyo alimsikia baba yake akivitaja mara nyingi wakati akiongea na simu kwa siri.
Haya ndiyo majibu ambayo Najma aliyapata mtandaoni
,,,,,,,,,,,,,COBOS virus is a virus that was secretly invented by humans 25 years ago in Mexico. This secret was leaked and the practice was strongly opposed by all countries in the world and later banned by any country or laboratory involved in the manufacture of the virus. That was the last COBOS virus to be heard, there are rumors that the virus was taken and stored by the ZMLST international laboratory in Mexico. For over 25 years now the virus has never been heard anywhere in the world.,,,,,,

(virusi vya COBOS ni virusi vilivyotengenezwa na binadamu kwa siri miaka 25 iliyopita nchini mexico. siri hii ilivuja na kitendo hicho kikapingwa vikali na nchi zote ulimwenguni baadae ikapigwa marufuku kwa nchi au maabara yoyote ulimwenguni itakayojihusisha na utengenezwaji wa virusi. Huo ndio ukawa mwisho wa virusi vya COBOS kusikia, kuna tetesi kuwa virusi hivi vilichukuliwa na kujifadhiwa na maabara ya kimataifa ya ZMLST iliyopo Mexico. Ni zaidi ya miaka 25 sasa virusi hivi havijawahi kusikika mahali popote Dunia)

Haya ni majibu ambayo yalimfanya Najma kuendelea kufuatilia ukweli wa jambo hili. Kitu kikubwa kilichomfanya Najma kuzidi kumtilia mashaka baba yake ni zile safari ambazo baba yake alikuwa akizifanya mara kwa mara kwenda nchini Mexico, hata pale alipokuwa akikosa nafasi alikuwa akimuagiza kwa siri mkwe wake mtarajiwa Osward ambaye kwa sasa yupo gerezani akisubiri hukumu ya kesi ya mauaji inayomuandama.

"Hii inawezanaje? Baba yangu anawezaje kushiriki kwenye mambo kama haya? alafu kwa nini hawa wamexico wamchague yeye, hapana hakuna ukweli wowote hapa" Najma alikuwa akijiuliza na kujijibu mwenyewe, haikuwa rahisi kukubaliana na jambo hilo.

Najma alifika karibu na lile gereza alilopo Osward, gereza ambalo ni jana tu ametoka anaumia vibaya akasaidiwa na inspekta Aron.
Najma alifika gerezani hapo kwa lengo la kuongea na Osward akitaka kumuliza juu ya safari lizokuwa akienda Mexico badala ya baba yake, alikuwa akienda kufanya nini.
Najma aliyafanya yote hayo kimya kimya bila kumueleza Inspekta Aron chochote licha ya kwamba walikuwa na ukaribu mkubwa kwa sana na alikuwa akimkumbuka sana lakini hakumpigia wala kutuma ujumbe wa maandishi.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande mwingine msituni, Inspekta Aron na Annah walianza kuzoea mazingira huku Annah kimtazama Inspekta Aron kwa jicho la tofauti, tayari mwanaume huyo alianza kuuteka moyo wake taratibu.
Wakati wote jicho la Inspekta Aron lilikuwa makini kutazama kama kuna mtu atakuja kwenye nyumba hiyo ya siri iliyojengwa na marehemu baba yake, hakuwa amemwabia Annah chochote kuhusu hisia zake zilizomwambia kuwa ni lazima kuna mtu atakuja.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mambo yalizidi kupamba moto, vita kali ilianza kati ya Tino ambaye hakutaka kumruhusu jasusi Shadow andoke na vimelea vya V-COBOS. Shadow naye hakutaka kukubali kushindwa kwa mara nyingine tena ilikuwa ni lazima ahakikishe anaondoka na sanduku hilo. Vita hiyo ilikuwa nje ya boti lakini ndani nako kulikuwa na vita kali kati ya Dokta Gondwe na Bosco kijana wa Tino. Dokta Gondwe hakutaka kumruhusu Bosco aende kwani aliamini huyu ndiye mwenye picha na video zake chafu za ngono lakini pili ni baada ya Bosco kusema kuwa anayo dawa(chupa ya kijivu) dhidi ya virusi vya V-COBOS.

Wakati haya yote yakiendela boti ilizidi kwenda kwa kasi ikikata mawimbi kuelekea kusiko julikana.

Je, nini kitafuata?

ITAENDELEA....
.Njoo WhatsApp jipatie simulizi hii yote mpaka mwisho kwa tsh 1000 tu
0756862047
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

22-(Kikosi cha Kunguru weusi)
ILIPOISHIA...
Vita kali inaibuka ndani na nje ya boti iliyokuwa ikienda kwa kasi, ni vita kati ya Tino anayemzuia Jasusi Shadow asiondoke na sanduku lenye vimelea vya V-COBOS wakati huo huo ndani ya boti hiyo mapigano makali kati ya Bosco na Wazari wa afya Dokta Gondwe yalikuwa yakiendela
Upande wa pili Najma anaanza kufuatilia na kuuchimba ukweli kuhusu vimelea vya V-COBOS.

Jez nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
Shadow alikimbia akapanda juu kabisa ya boti Tino naye akamfuata hakutaka kumpa upenyo wa kuondoka na lile sanduku. Sasa walikuwa juu kabisa ya boti hiyo iliyokua ikienda kwa kasi ikipasua mawimbi ya bahari ya hindi. Si Shadow wala si Tino wote walikuwa vizuri kwenye suala zima la mapambano ya bila kutumia siraha.
Mara punde purukushani kati ya Bosco na Waziri wa afya Dokta Gondwe ilihama kutokea ndani ya boti sasa wakahamia nje. Hapo Dokta Gondwe aliweza kumuona Tino akipigana na yule mtu aliyeondoka na sanduku lake lakini cha ajabu Dokta Gondwe hakutaka kushughulika naye yeye akaendelea kukomaa na Bosco.

"Huwezi kuondoka hapa mpaka uniambie ni wapi ilipo dawa ya virusi vya COBOS" Dokta Gondwe aliongea kwa nguvu huku akifuta damu iliyokuwa ikimtoka puani
"Unajisumbua bure Dokta hupati chochote kutoka kwangu, na nitahakikisha nasambaza picha zako chafu mtandaoni" Bosco alijibu huku akitema damu
"Siwezi kukupa hiyo nafasi kijana leo ni ama zako ama zangu" alisema Dokta Gondwe huku akikimbia na kwenda kumvaa Bosco kwa mara nyingine wakaanza tena kupigana. Wakati huo pia juu ya boti bado mpambano kati ya Tino na Jasusi Shadow ulizidi kupamba moto.

Boti iliyokuwa ikienda kwa kasi bila kuongozwa na mtu yeyote sasa ilikuwa ikielekea nchi kavu ikiwa ibakiza mita chache kugusa ardhi mara Jasusi Shadow alilishika lile sanduku kisha akalitupa ndani ya maji kitendo hicho kilimshangaza sana Tino na kwakuwa hakutaka kuvipoteza vimelea vya V-COBOS haraka alijitosa majini kulifuata sanduku lile, sekunde chache baadae Jasusi Shadow naye akajitosa majini kumfuata.

Boti ilienda kwa kasi ikatoka ndani ya maji nakupaa juu mita chache kisha ikatua nchi kavu na kupinduka upande mmoja. Dokta Gondwe na Bosco ambao walikuwa hawelewi hili wala lile wajikuta wakijipigiza vibaya kwenye kuta za boti hiyo
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dokta Gondwe aliumia vibaya mno, aliinuka kwa kujikongoja akatazama pande zote na hapo ndipo alipobaini kuwa boti ilikuwa nchi kavu kwa sasa, aliendelea kuangaza macho yake kila mahali hakumuona Bosco, hakumuona Tino wala Jasusi Shadow.

"Ameenda wapi huyu mpuuzi?" alisema Dokta Gondwe huku akishuka kutoka kwenye boti akazunguuka upande wa pili kuangalia, hakuona mtu lakini mara alisikia vishindo nyuma yake akageuka haraka kuangalia hapo ndipo alimuona Bosco kwa mbali akikimbia kuelekea msituni. Dokta Gondwe hakuwa na nguvu kabisa ya kuendelea kumfuatilia, tayari alikuwa amejeruhiwa na kuchoka karibu kile sehemu ya mwili wake, alikuwa hoi.

Dokta Gondwe aliutazama ule msitu mdogo alikokimbilia Bosco kisha akafungua simu yake akaangalia ramani ya eneo hilo, mara akatabasamu.
"Huwezi kwenda kokote kijana lazima nikupate" alisema Dokta Gondwe baada ya kubaini kuwa kule alikokwenda Bosco ilikuwa ni Rasi yaani sehemu ya ardhi iliyoingia majini, kwa maana hiyo ili Bosco atoke ilikuwa ni lazima arudi alikotoka kwani alikoenda ilikuwa ni sehemu iliyozunguukwa na maji pande zote tatu.

Dokta Gondwe alibinya simu yake akapiga namba fulani kisha akaweka simu sikioni.
"Hallo"
"Ndiyo bosi nakusikia" sauti nzito ilisikika upande wa pili
"Nahitaji msaada njoo na kikosi chote cha Kunguru weusi nakutumia ramani nilipo, nawahitaji sasa hivi"
"Sawa bosi, lakini Kamanda Tino hayupo aliondoka asubuhi sana aka...."
"Nyie njooni Tino mtamkuta huku"
Aliongea Dokta Gondwe akakata simu kisha akamtumia mtu huyo uelekeo wa mahali alipo. Baada ya hapo alituma ujumbe mfupi wa maandishi kwenda kwa Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa.

,,,,,,,,,,,,Profesa nimefanya kama ulivyonishauri lakini mambo ni mazito sana huku baharini, yaani huwezi kuamini Waziri mkubwa kama mimi nahangaika huku badala ya kukaa bungeni, hawa wamexico wananitesa sana najuta kuchua ofa yao kweli nitafika mbinguni nimechoka sana,,,,,,,,,,

Baada ya kutuma ujumbe huo Dokta Gondwe alipiga hatua akaenda kukaa pembeni ya ile boti kusubiri kikosi cha Kunguru weusi. Jambo la ajabu ni kwamba alikuwa hajali kabisa kuhusu Tino na yule mtu aliyechukua sanduku lake, akili yake yote iliielekeza kwa Bosco
[emoji294][emoji294][emoji294]

Vita ya Tino na Jasusi Shadow haikuishia kwenye ile boti, bado iliendelea hata ndani ya maji. Wakati Tino akilifuata sanduku lililokuwa linazama kwenye kina kirefu cha bahari Jasusi Shadow naye alikuwa nyuma yake akiogerea kwa kasi kumfuata. Wote walionekana ni wazoefu wa kuogerea na jambo lingine muhimu kila mmoja alikuwa na mtungi wa gesi uliomsaidia kupumua akiwa ndani ya maji.
Waliendelea kuvutana na kugeuzana wakiwa ndani ya maji kila mmoja akitaka kuwa wa kwanza kulifikia sanduku lile. Mwisho walizama mpaka chini kabisa wakagusa ardhi chini ya bahari. Jasusi Shadow alipata mwanya akafanikiwa kumbana vizuri Tino kisha akamchomolea ule mpira unaopitisha gesi kutoka kwenye mtungi akaukata kabisa, hapo Tino alijikuta anaanza kutapatapa baada ya kukosa hewa, mbaya zaidi walikuwa wamezama kwenye kina kirefu cha maji haikuwa rahisi kupata pumzi ya kutosha itakayomuwezesha kufika juu.
Jasusi Shadow alisogea hadi lilipo sanduku akalichukua kisha akaanza kuogerea kupanda juu akimfuata Tino ambaye kwa sasa alikuwa anaelekea kupoteza fahamu baada ya kukosa hewa na kunywa maji mengi.
Shadow alimfikia Tino akamshika na kuogerea naye hadi alipotokeza juu ya maji wakati huo tayari Tino alikuwa amepoteza fahamu hajitambua. Shadow alimbeba na kutoka naye hadi nchi kavu, akamlaza chini kisha akaanza kumminya tumbo kwa nguvu, Tino akawa anayatapika maji mengi aliyokunywa bila kupenda yakatokea mdomoni na puani. Shadow hakutaka kumuacha Tino afe, hilo halikuwa agizo la Sultana bosi wake ambaye pia alikuwa ni mama mzazi wa Tino, licha ya wanafamilia hao wawili kuwa na vita kali wakipigania vimelea vya V-COBOS lakini hakuna siku Sultana alimuagiza Shadow amuue Tino.

Baada ya kutoa huduma hiyo ya kwanza Shadow alimbeba Tino akaingia naye msituni hatua kadhaa kutoka usawa wa bahari akachukua kamba na kumfunga chini ya mti mmoja mkubwa. Wakati huo wote Tino alikuwa hajitambua.
Shadow alichukua lile sanduku akamtazama Tino kwa sekunde kadhaa kisha akageuka na kuondoka zake, akatokomea msituni.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili ndani ya gereza la Kanondo, gereza ambalo wafungwa walikuwa wakiishi maisha malaini sana tofauti kabisa na magereza mengine. Hapo ndipo alipokuwa ameifadhiwa kijana Osward mtoto wa kigogo mmoja maarufu kama mzee Matula, alikuwa hapo kwa zaidi ya miezi mitatu akisubiri kesi yake ya mauaji iliyokuwa bado inaendelea kuunguruma mahakamani.
Najma alifika kwa ajili ya kufanya mazungumzo nyeti na Osward ambaye alifurahi sana baada ya kumuona kwa mara nyingine tangu alipomuona siku iliyopita.
"Siamini kama umekuja kuniona tena Najma, nilipoambiwa na askari kuwa kuna mwanamke amekuja kuniona nikawa najiuliza ni nani huyo kumbe ni wewe mpenzi" Alisema Osward huku furaha yake ikionekana wazi kwa nuru iliyokuwa inang'aa usoni kwake, hakika alikuwa akimpenda sana Najma.

"Hebu kaa nina mazungumzo muhimu na wewe" Alisema Najma huku akionekana kutofurahiswa hata kidogo na maneno ya Osward.
"Sawa nimekaa, nambie mguu wako unaendeleaje?"
"Salama nilishapona"
"Kwa nini jana ukakubali kuondoka na inspekta Aron hujui kama yule ni adui yetu mkubwa na ndio sababu ya mimi kuendelea kuwa humu hadi leo?"
"Anafanya kazi yake acha kumlaumu, kama hukuua basi ukweli utajulikana tu kuwa mpole"
"Mmh mbona leo wewe ni mkali hivyo, uko sawa kweli Najma wangu?"
"Ki ukweli siko sawa, nitakuwa sawa kama utanijibu kwa uaminifu maswali yote nitakayokuuliza Osward" alisema Najma huku akikaa vizuri kwenye kiti
"Swali gani? uliza tu"
"Nataka kujua zile Safari ambazo baba alikuwa akikuagiza kwenda Mexico ulikuwa unaenda kufanya nini?" Najma aliuliza swali lililomfanya Osward ashtuke lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake
"Kwani kuna nini mbona ghafula?"
"Ghafula nini si unijibu tu"
"Aah! Ni..nimambo mambo fulani fulani tu ee...lakini sana nilikuwa naenda kusimamia biashara zake kule Mexico"
"Biashara gani? nazijua bishara zote anazofanya baba sijawahi sikia hata siku moja akasema anabiashara Mexico unanidanganya Osward"
"Ni kweli anabi..."
"Sikia acha nikurahisishie swali naona unataka kuzunguuka sana, ni hivi unaelewa nini kuhusu virusi vya COBOS?" Najma alibadilisha swali lililomfanya Osward ashtuke sana hakuweza kuficha mshtuko wake tena.
"Nambie unajua nini ku..."
"Shiii!! Shiii! Najma tulia hutakiwi kutaja hilo neno hapa" alisema Osward huku akimtaka Najma anyamaze
"Kwa nini?"
Osward aliangaza macho huku na huku kisha akamsogelea Najma na kuongea kwa sauti ya chini
"Kuwa makini na hilo neno, utajitafutia matatizo"
"Kwa nini?"
"Najma nakuomba nakuomba sana kama umeanza au unataka kufuatilia kuhusu virusi vya COBOS basi acha sasa hivi kabla hujafika mbali, hili ni suala nyeti sana, kuna watu wakubwa na wazito wako nyuma ya hii ishu Najma sitaki kupoteza mpenzi wangu naomba acha na hili suala mara moja" Osward aliongea kwa msisitizo tena kwa kumaanisha sana huku akiwa ameikukutanisha mikono yake kama mtu anayeomba toba.
Najma alibaki katika hali ya mshangao, hakuelewa ni kwa nini Osward aliongea kwa uzito kiasi kile hapo akili yake ikafunguka akaamini kuwa suala la virusi vya COBOS ni kweli lipo na nizito sana, baba yake Dokta Gondwe anahusika pia.

Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA...
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya..............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

22-(Kikosi cha Kunguru weusi)
ILIPOISHIA...
Vita kali inaibuka ndani na nje ya boti iliyokuwa ikienda kwa kasi, ni vita kati ya Tino anayemzuia Jasusi Shadow asiondoke na sanduku lenye vimelea vya V-COBOS wakati huo huo ndani ya boti hiyo mapigano makali kati ya Bosco na Wazari wa afya Dokta Gondwe yalikuwa yakiendela
Upande wa pili Najma anaanza kufuatilia na kuuchimba ukweli kuhusu vimelea vya V-COBOS.

Jez nini kitafuata?

SASA ENDELEA....
Shadow alikimbia akapanda juu kabisa ya boti Tino naye akamfuata hakutaka kumpa upenyo wa kuondoka na lile sanduku. Sasa walikuwa juu kabisa ya boti hiyo iliyokua ikienda kwa kasi ikipasua mawimbi ya bahari ya hindi. Si Shadow wala si Tino wote walikuwa vizuri kwenye suala zima la mapambano ya bila kutumia siraha.
Mara punde purukushani kati ya Bosco na Waziri wa afya Dokta Gondwe ilihama kutokea ndani ya boti sasa wakahamia nje. Hapo Dokta Gondwe aliweza kumuona Tino akipigana na yule mtu aliyeondoka na sanduku lake lakini cha ajabu Dokta Gondwe hakutaka kushughulika naye yeye akaendelea kukomaa na Bosco.

"Huwezi kuondoka hapa mpaka uniambie ni wapi ilipo dawa ya virusi vya COBOS" Dokta Gondwe aliongea kwa nguvu huku akifuta damu iliyokuwa ikimtoka puani
"Unajisumbua bure Dokta hupati chochote kutoka kwangu, na nitahakikisha nasambaza picha zako chafu mtandaoni" Bosco alijibu huku akitema damu
"Siwezi kukupa hiyo nafasi kijana leo ni ama zako ama zangu" alisema Dokta Gondwe huku akikimbia na kwenda kumvaa Bosco kwa mara nyingine wakaanza tena kupigana. Wakati huo pia juu ya boti bado mpambano kati ya Tino na Jasusi Shadow ulizidi kupamba moto.

Boti iliyokuwa ikienda kwa kasi bila kuongozwa na mtu yeyote sasa ilikuwa ikielekea nchi kavu ikiwa ibakiza mita chache kugusa ardhi mara Jasusi Shadow alilishika lile sanduku kisha akalitupa ndani ya maji kitendo hicho kilimshangaza sana Tino na kwakuwa hakutaka kuvipoteza vimelea vya V-COBOS haraka alijitosa majini kulifuata sanduku lile, sekunde chache baadae Jasusi Shadow naye akajitosa majini kumfuata.

Boti ilienda kwa kasi ikatoka ndani ya maji nakupaa juu mita chache kisha ikatua nchi kavu na kupinduka upande mmoja. Dokta Gondwe na Bosco ambao walikuwa hawelewi hili wala lile wajikuta wakijipigiza vibaya kwenye kuta za boti hiyo
[emoji294][emoji294][emoji294]
Dokta Gondwe aliumia vibaya mno, aliinuka kwa kujikongoja akatazama pande zote na hapo ndipo alipobaini kuwa boti ilikuwa nchi kavu kwa sasa, aliendelea kuangaza macho yake kila mahali hakumuona Bosco, hakumuona Tino wala Jasusi Shadow.

"Ameenda wapi huyu mpuuzi?" alisema Dokta Gondwe huku akishuka kutoka kwenye boti akazunguuka upande wa pili kuangalia, hakuona mtu lakini mara alisikia vishindo nyuma yake akageuka haraka kuangalia hapo ndipo alimuona Bosco kwa mbali akikimbia kuelekea msituni. Dokta Gondwe hakuwa na nguvu kabisa ya kuendelea kumfuatilia, tayari alikuwa amejeruhiwa na kuchoka karibu kile sehemu ya mwili wake, alikuwa hoi.

Dokta Gondwe aliutazama ule msitu mdogo alikokimbilia Bosco kisha akafungua simu yake akaangalia ramani ya eneo hilo, mara akatabasamu.
"Huwezi kwenda kokote kijana lazima nikupate" alisema Dokta Gondwe baada ya kubaini kuwa kule alikokwenda Bosco ilikuwa ni Rasi yaani sehemu ya ardhi iliyoingia majini, kwa maana hiyo ili Bosco atoke ilikuwa ni lazima arudi alikotoka kwani alikoenda ilikuwa ni sehemu iliyozunguukwa na maji pande zote tatu.

Dokta Gondwe alibinya simu yake akapiga namba fulani kisha akaweka simu sikioni.
"Hallo"
"Ndiyo bosi nakusikia" sauti nzito ilisikika upande wa pili
"Nahitaji msaada njoo na kikosi chote cha Kunguru weusi nakutumia ramani nilipo, nawahitaji sasa hivi"
"Sawa bosi, lakini Kamanda Tino hayupo aliondoka asubuhi sana aka...."
"Nyie njooni Tino mtamkuta huku"
Aliongea Dokta Gondwe akakata simu kisha akamtumia mtu huyo uelekeo wa mahali alipo. Baada ya hapo alituma ujumbe mfupi wa maandishi kwenda kwa Rais mstaafu Profesa Cosmas Kulolwa.

,,,,,,,,,,,,Profesa nimefanya kama ulivyonishauri lakini mambo ni mazito sana huku baharini, yaani huwezi kuamini Waziri mkubwa kama mimi nahangaika huku badala ya kukaa bungeni, hawa wamexico wananitesa sana najuta kuchua ofa yao kweli nitafika mbinguni nimechoka sana,,,,,,,,,,

Baada ya kutuma ujumbe huo Dokta Gondwe alipiga hatua akaenda kukaa pembeni ya ile boti kusubiri kikosi cha Kunguru weusi. Jambo la ajabu ni kwamba alikuwa hajali kabisa kuhusu Tino na yule mtu aliyechukua sanduku lake, akili yake yote iliielekeza kwa Bosco
[emoji294][emoji294][emoji294]

Vita ya Tino na Jasusi Shadow haikuishia kwenye ile boti, bado iliendelea hata ndani ya maji. Wakati Tino akilifuata sanduku lililokuwa linazama kwenye kina kirefu cha bahari Jasusi Shadow naye alikuwa nyuma yake akiogerea kwa kasi kumfuata. Wote walionekana ni wazoefu wa kuogerea na jambo lingine muhimu kila mmoja alikuwa na mtungi wa gesi uliomsaidia kupumua akiwa ndani ya maji.
Waliendelea kuvutana na kugeuzana wakiwa ndani ya maji kila mmoja akitaka kuwa wa kwanza kulifikia sanduku lile. Mwisho walizama mpaka chini kabisa wakagusa ardhi chini ya bahari. Jasusi Shadow alipata mwanya akafanikiwa kumbana vizuri Tino kisha akamchomolea ule mpira unaopitisha gesi kutoka kwenye mtungi akaukata kabisa, hapo Tino alijikuta anaanza kutapatapa baada ya kukosa hewa, mbaya zaidi walikuwa wamezama kwenye kina kirefu cha maji haikuwa rahisi kupata pumzi ya kutosha itakayomuwezesha kufika juu.
Jasusi Shadow alisogea hadi lilipo sanduku akalichukua kisha akaanza kuogerea kupanda juu akimfuata Tino ambaye kwa sasa alikuwa anaelekea kupoteza fahamu baada ya kukosa hewa na kunywa maji mengi.
Shadow alimfikia Tino akamshika na kuogerea naye hadi alipotokeza juu ya maji wakati huo tayari Tino alikuwa amepoteza fahamu hajitambua. Shadow alimbeba na kutoka naye hadi nchi kavu, akamlaza chini kisha akaanza kumminya tumbo kwa nguvu, Tino akawa anayatapika maji mengi aliyokunywa bila kupenda yakatokea mdomoni na puani. Shadow hakutaka kumuacha Tino afe, hilo halikuwa agizo la Sultana bosi wake ambaye pia alikuwa ni mama mzazi wa Tino, licha ya wanafamilia hao wawili kuwa na vita kali wakipigania vimelea vya V-COBOS lakini hakuna siku Sultana alimuagiza Shadow amuue Tino.

Baada ya kutoa huduma hiyo ya kwanza Shadow alimbeba Tino akaingia naye msituni hatua kadhaa kutoka usawa wa bahari akachukua kamba na kumfunga chini ya mti mmoja mkubwa. Wakati huo wote Tino alikuwa hajitambua.
Shadow alichukua lile sanduku akamtazama Tino kwa sekunde kadhaa kisha akageuka na kuondoka zake, akatokomea msituni.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili ndani ya gereza la Kanondo, gereza ambalo wafungwa walikuwa wakiishi maisha malaini sana tofauti kabisa na magereza mengine. Hapo ndipo alipokuwa ameifadhiwa kijana Osward mtoto wa kigogo mmoja maarufu kama mzee Matula, alikuwa hapo kwa zaidi ya miezi mitatu akisubiri kesi yake ya mauaji iliyokuwa bado inaendelea kuunguruma mahakamani.
Najma alifika kwa ajili ya kufanya mazungumzo nyeti na Osward ambaye alifurahi sana baada ya kumuona kwa mara nyingine tangu alipomuona siku iliyopita.
"Siamini kama umekuja kuniona tena Najma, nilipoambiwa na askari kuwa kuna mwanamke amekuja kuniona nikawa najiuliza ni nani huyo kumbe ni wewe mpenzi" Alisema Osward huku furaha yake ikionekana wazi kwa nuru iliyokuwa inang'aa usoni kwake, hakika alikuwa akimpenda sana Najma.

"Hebu kaa nina mazungumzo muhimu na wewe" Alisema Najma huku akionekana kutofurahiswa hata kidogo na maneno ya Osward.
"Sawa nimekaa, nambie mguu wako unaendeleaje?"
"Salama nilishapona"
"Kwa nini jana ukakubali kuondoka na inspekta Aron hujui kama yule ni adui yetu mkubwa na ndio sababu ya mimi kuendelea kuwa humu hadi leo?"
"Anafanya kazi yake acha kumlaumu, kama hukuua basi ukweli utajulikana tu kuwa mpole"
"Mmh mbona leo wewe ni mkali hivyo, uko sawa kweli Najma wangu?"
"Ki ukweli siko sawa, nitakuwa sawa kama utanijibu kwa uaminifu maswali yote nitakayokuuliza Osward" alisema Najma huku akikaa vizuri kwenye kiti
"Swali gani? uliza tu"
"Nataka kujua zile Safari ambazo baba alikuwa akikuagiza kwenda Mexico ulikuwa unaenda kufanya nini?" Najma aliuliza swali lililomfanya Osward ashtuke lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake
"Kwani kuna nini mbona ghafula?"
"Ghafula nini si unijibu tu"
"Aah! Ni..nimambo mambo fulani fulani tu ee...lakini sana nilikuwa naenda kusimamia biashara zake kule Mexico"
"Biashara gani? nazijua bishara zote anazofanya baba sijawahi sikia hata siku moja akasema anabiashara Mexico unanidanganya Osward"
"Ni kweli anabi..."
"Sikia acha nikurahisishie swali naona unataka kuzunguuka sana, ni hivi unaelewa nini kuhusu virusi vya COBOS?" Najma alibadilisha swali lililomfanya Osward ashtuke sana hakuweza kuficha mshtuko wake tena.
"Nambie unajua nini ku..."
"Shiii!! Shiii! Najma tulia hutakiwi kutaja hilo neno hapa" alisema Osward huku akimtaka Najma anyamaze
"Kwa nini?"
Osward aliangaza macho huku na huku kisha akamsogelea Najma na kuongea kwa sauti ya chini
"Kuwa makini na hilo neno, utajitafutia matatizo"
"Kwa nini?"
"Najma nakuomba nakuomba sana kama umeanza au unataka kufuatilia kuhusu virusi vya COBOS basi acha sasa hivi kabla hujafika mbali, hili ni suala nyeti sana, kuna watu wakubwa na wazito wako nyuma ya hii ishu Najma sitaki kupoteza mpenzi wangu naomba acha na hili suala mara moja" Osward aliongea kwa msisitizo tena kwa kumaanisha sana huku akiwa ameikukutanisha mikono yake kama mtu anayeomba toba.
Najma alibaki katika hali ya mshangao, hakuelewa ni kwa nini Osward aliongea kwa uzito kiasi kile hapo akili yake ikafunguka akaamini kuwa suala la virusi vya COBOS ni kweli lipo na nizito sana, baba yake Dokta Gondwe anahusika pia.

Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA...
 
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya.........23
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

23-(Najma- nautaka ukweli)

ILIPOISHIA....
Najma alibaki katika hali ya mshangao, hakuelewa ni kwa nini Osward aliongea kwa uzito kiasi kile hapo akili yake ikafunguka akaamini kuwa suala la virusi vya COBOS ni kweli lipo na nizito isivyo kawaida, baba yake Dokta Gondwe anahusika pia.

SASA ENDELEA...
"Niambie kila kitu Osward, ni nini kinaendelea? ni jambo gani ambalo baba yangu analifanya kwa siri?" aliuliza Najma
"Najma sitaki ujiingize kwenye hili tafadhali naomba nielewe"
"Nimeshajiingiza tayari na huwezi kunitoa mpaka nihakikishe naelewa kila kitu, nambie Osward ni kweli baba anavyo vimelea vya V-COBOS? anataka kuvitumia kuua watu?" Najma aliuliza maswali mfurulizo. Osward alitulia kwa muda asijue amwambie nini Najma ambaye alikuwa amemganda haswa.
"Sawa nitakwambia kitu ninachokijua lakini chonde chonde usije kufanya jambo lolote ukahatarisha maisha yako kumbuka nimekwambia huu ni mpango wa watu wakubwa sana Dunia hata baba yako hawezi kuwazuia"
"Nambie nakusikiliza"
"Sijui kiundani sana ila ninachofahamu ni kwamba virusi hivi viliingia nchini kipindi Profesa Cosmas Kulolwa akiwa madarakani kama Rais, wakati huo baba yako alikuwa Waziri wa afya kama alivyo sasa ni watu wachache sana wanaelewa uwepo wa hivi virusi nchini mpaka sasa. Mpango uliopo ni kwamba siku moja hivi virusi vitaachiwa na kuleta janga lingine Duniani kama ilivyotokea kwa huu ugonjwa wa korona" alieleza Osward

"Sasa kwa nini baba afanye hivyo? Kwa nini ahatarishe maisha yake na yetu pia?"
"Hapana sivyo kama unavyofikiria Najma, kuna tofauti kubwa kati ya hivi virusi vya COBOS na virusi vya korona. Iko hivi kirusi cha COVID-19 hatujui kama kilitengenezwa au laa lakini hiki kirusi cha COBOS kimetengenezwa na tayari kuna kinga na tiba yake hivyo kabla ya kusambaza wote ambao wako kwenye mpango huu watajikinga wao na wapendwa wao kisha ndipo mengine yafuate" Alieleza Osward

"Ooh! Mungu wangu, hii dunia ina viumbe wa aina gani jamini, hebu niambie ukweli Osward baba yangu kalazimishwa au kataka mwenyewe?"
"Sijui kwa kweli?"
"Hujui nini? Si wewe ndio huwa anakuagiza huko Mexico unashindwa vipi kujua au lenu moja ninyi ni washikirika wao si ndio? mnatakaa kuua watu kwa manufaa yenu yaani hata hamuwazi kwa nini wamevileta hivyo virusi huku badala ya kuanzia kuvisambaza huko kwao, mna uhakika hiyo dawa ni sahihi? inatibu?"
"Najma acha kuwa mfukunyuku utakufa bado mdogo nimekwambia huu ni mpango wa watu wakubwa Duniani achana nalo wewe ni nani hadi utake kuingilia?"
"Mimi ni Najma mtoto wa waziri wa afya Dokta Gondwe ambaye amezuia mpango wa wapumbavu wachache waliotaka kuleta maafa na kuua watu wasio na hatia, hivyo ndivyo historia itakavyo andikwa hata kama nitakufa sawa wewe, naondoka" Najma aliongea kwa kujiamini kisha akachukua mkoba wake na kuondoka zake.
Alitembea kinyonge kutoka nje ya gereza hilo akaingia ndani ya gari yake akajitupa kwenye kiti, kichwa kilikuwa kikimuuma sana alilibeba jambo ambalo liko nje ya uwezo wake, Najma alifunga mlango wa gari kisha akawa amejiinamia akijaribu kuyatafakari yale aliyoelezwa na Osward. Bado lilikuwa ni suala gumu lisiloingia akilini kirahisi, alimpenda na kumuamini sana baba yake Dokta Gondwe.

Sekunde chache baada ya Najma kutoka nje ya lile gereza, Osward alisimama huku akihema kwa nguvu ilikuwa ni kama amechanganyikiwa hivi. Najma alikuwa amekuja na ajenda nzito siku hiyo ajenda ambayo hakuwa ametegemea kuisikia kutoka kwake. Hofu yake kubwa ilikuwa si virusi vya COBOS bali ni usalama wa Najma. Alimpenda sana mwanamke huyo mrembo, Hulka yake ya kutaka kuingilia suala la virusi vya COBOS ilikuwa ni sawa na kujipalia makaa ya moto, ukweli alikuwa akihatarisha maisha yake.

"Hii imekaaje? Dokta Gondwe kafanya uzembe gani hadi Najma amejua kuhusu vimelea vya V-COBOS, hapana hii haiwezekani kabisa ni lazima nifanye kitu bila hivyo watamuua, watamuua Najma wangu" aliwaza Osward huku akiumiza akili yake kufikiri nini afanye
"Muda wako umeisha unatakiwa kurudi sero" alisema askari magereza mmoja aliyemsindikiza Osward wakati alipokuja kuonana na Najma
"Hapana subiri, Seleman, Seleman Selemaniiii....." Alisema Osward kisha akaanza kupiga hatua kuelekea ilipokuwa ofisi ya mkuu wa gereza, yule askari akasimama mbele yake kumzuia lakini Osward alimsukuma pembeni kisha akaendelea upiga hatua kusonga mbele hapo wakaongezeka askari wengine wawili
"Hivi wewe unamwitaje mkuu wa gereza kama bibi yako?" alihoji askari mmoja aliyeongezeka
"Nataka kuonana naye"
"Osward umeanza tena vurugu zako za kila siku, hivi unajikuta nani wewe?"
"Nina shida ya muhimu nataka kumuona Selemani" Osward liongea kwa ukali na mara hiyo mlango wa ofisi ya mkuu wa gereza ukafunguliwa, akatoka SP Seleman.
"Kuna nini mbona kelele nyingi?" SP Seleman aliuliza kwa ukali
"Ni Osward mkuu, anataka kuingia ofisini kwako kwa nguvu" alieleza askari mmoja.
SP Seleman alimtazama Osward kwa macho makali, kisha akawaonyesha ishara askari wake akarudi ofisini. Wale askari waliokuwa wakimzuia Osward walimuacha na kuondoka.
Osward aliweka sawa vifungo vya nguo yake kisha akapiga hatua kuingia ofisi ya mkuu wa gereza akafika na kukaa kwenye kiti.
"Nikimweleza baba yako mambo unayoyafanya huku unajua nini kitafuata?"
"Samahani"
"Samahani? leo unasema samahani? Haya nini shida, vurugu zote za nini?"
"Naomba simu yako nahitaji kuongea na mtu wangu" alisema Osward
"Sasa kwa nini usiwe mstaarabu ni lini umeomba simu nikakunyima, unataka kila mtu aelewe kuwa tumeshikwa masikio na baba yako" SP Selemani aliongea kwa ukali na kusimama akamtazama Osward kwa sekunde kadhaa kisha akachukua simu yake iliyokuwa mezani akampa. Haraka Osward aliingiza namba za Big' kisha akapiga, wakati huo SP Selemani alirudi kwenye kiti akakaa.

Simu ya Big' iliita upande wa pili ikiwa mikononi mwa Inspekta Aron ambaye kwa sasa alikuwa kule msituni kwenye nyumba ya siri ya marehemu baba yake.
Inspekta Aron alichukua simu ya Big' ambaye kwa sasa ni marehemu akatazama namba ya mpigaji, akachukua simu yake na kuiingiza ile namba haraka akijaribu kuzilinganisha
"Nilijua tu ni wewe SP selemani" Inspekta Aron alijisemea mwenyewe baada ya kuhakikisha namba inayopiga kuwa ni ya mkuu wa gereza la Kanondo SP Seleman alipo hifadhiwa muharifu wake Osward.

Simu iliita na mwisho ikakata, Osward akapiga tena mara ya pili ikaita kwa muda mwisho ikapokelewa. Kukawa kimya kila mtu akisubiri mwenzake azungumze kwanza
"Hallo Big'" mwisho Osward aliongea akiwa mwenye wasiwasi kidogo
"Hilo ndio jina la mtu uliyemtuma aje kuniua?" alisema Inspekta Aron, Osward alitoa macho kwa mshangao, sauti aliyoisikia ilikuwa ya mtu mwingine tofauti na aliyemtegemea
"Aron" Osward aliita
"Ndiyo ni mimi"
Alijibu Inspekta Aron na hapo Osward akanyanyua mkono wake wenye simu juu kisha akaushusha chini kwa nguvu akaibamiza simu sakafuni ikasambaratika vipande vipande.
"Nini wewe, kwa nini umevunja simu yangu?" SP Seleman aliuliza kwa mshangao huku akisimama tena kwenye kiti

"Inspekta Aron, nitakuua mwenyewe kwa mikono yangu nitakukatakata vipande vipande na kuwapa mbwa nyama yako" Osward aliongea akiwa amekunja ngumi na kuuma meno kwa hasira. Inspekta Aron alikuwa amembana kila kona, kuanzia kwenye kesi ya mauaji inayomkabili, kwa kipenzi chake Najma na sasa kwa mtu wake wa kazi Big', hali ilikuwa ni ngumu mno upande wa Osward, hata matumaini ya kushinda kesi yake yalififia ghafula.
Upande wa pili Inspekta Aron alikuwa akitabasamu baada ya kuona anazidi kumpiga bao mtuhumiwa wake
"Ukiwa na hasira utaendelea kufanya maamuzi yasiyo sahihi yatakayonifanya niendelee kukusanya ushahidi wa kutosha kukufunga Osward" Inspekta Aron aliwaza, akapiga hatua kurudi sebureni. Alipomtazama Annah aligundua kuwa amelala pale juu ya kochi. Inspekta Aron alimuinua taratibu na kumbeba akaanza kupandisha ngazi kuelekea vyumba vya juu vya nyumba hiyo iliyojengwa kwa mbao.
"Unaniepeleka wapi" Annah aliuliza kwa sauti ya kudeka akiwa bado na usingizi
"Twende ukalale chumbani"
"Mmh hii nyumba inachumbani kumbe"
"Unaichukulia poa eti?" Aliuliza Aron huku akifungua mlango wa chumba kimoja akaingia na kwenda kumlaza Annah kitandani
"Woow! Mzuri natamani hata niishi huku milele" Annah aliongea na kutabasamu, Inspekta Aron akawa kimya
"Mnh! unanisafisha kidonda saangapi?"
"Ooh! Nilisahau hata hivyo muda bado"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Dokta Gondwe alionekana akiwa amekaa na kujiinamia pembeni ya ile boti iliyoruka kutoka bahari hadi nchi kavu, alishtushwa na breki kali ya gari aina ya Noah nyeusi ambayo ilifika na kufungua breki kali mbele yake. Punde wakashuka wanaume saba wote wakiwa wamevaa makoti meusi pia walivaa maski nyeusi usoni zilizozuia sura zao kuonekana, mikononi mwao walikuwa wameshikiria bunduki aina ya SAR 21 zinazotoa miale mikali yenye rangi nyenduku
Dokta Gondwe alipowaona alitabasamu kisha akapiga hatua kuwafuata, hiki kilikuwa ni kikosi chake maarufu kama Kunguru weusi.

Je, nini kitafuata?
Tino yuko wapi?
Bosco atatoka salama?
Najma atafanya nini?
Vipi kuhusu Osward?
Nani atabaki na vimelea vya V-COBOS?
ITAENDELEA...
 
Dr. Gondwe si yupo kisiwani boti ilipokwama kwenye mchanga wa kisiwa? Hiyo Noah imefikaje hapo ndugu SIMULIZI RIWAYA ?! Nadhani ni makosa madogo ya kiuwandishi...
 
Soma vizuri simulizi hakukuwa na neno kisiwa ila Nchi kavu/ufukweni
Nakufuatilia sana, hukusema Dr. Gondwe alipogundua nyuma ya msitu alipokimbilia yule dogo kumezungukwa na maji akajifariji, akutulia na kupiga simu kuwaita vijana wake? Au niquote maneno hayo...? Any way let's enjoy the scene mkuu
 
Nakufuatilia sana, hukusema Dr. Gondwe alipogundua nyuma ya msitu alipokimbilia yule dogo kumezungukwa na maji akajifariji, akutulia na kupiga simu kuwaita vijana wake? Au niquote maneno hayo...? Any way let's enjoy the scene mkuu
Karibu endelea kufurahia SIMULIZI ZA SAUL DAVID
 
Back
Top Bottom