SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #61
THE MODERN WAR
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............21
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
21-(VITA BAHARINI)
ILIPOISHIA.....
Wakati huo si Bosco si Dokta Gondwe hakuna aliyekuwa akimuamini mwenzake hawakujua kuwa mzee wa kazi Jasusi Shadow alikuwa ameingia ndani ya boti hiyo naye akiwa anavitaka vimelea vya V-COBOS kama alivyoagizwa na Sultana. Tino na wale vijana wawili walienda kusubiri ndani ya ile boti ndogo, hawakujua chochote kinachoendelea..
SASA ENDELEA....
Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akiwa amemnyoshea mwenzake bastola mara walishtushwa na mtikisiko mkubwa ndani ya boti hiyo mtikisiko uliosababisha wote wawili kuanguka chini kwa pamoja. Boti iliyumba ikiwapeleka kulia na kisha kuwatupa upande wa kushoto. Walishindwa kustahimili kuendelea kushikilia siraha zao zikadondoka chini, kila mmoja akawa anajitahidi kujishikilia mahali ili asiumie kutokana na kuyumba yumba kwa boti ile wasielewe ni nini chanzo. Mara ghafula hali ikatulia kwa sekunde kadhaa kisha wakashangaa kuona boti inaanza kwenda mbele kwa kasi sana.
Mambo yakazidi kuwa mazito kwa upande wa Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akimuhisi mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa kihusika na kila kinachoendelea wakati huo hawakujua kabisa habari za kuwepo kwa Jasusi Shadow ndani ya boti hiyo.
Hapo ndipo Dokta Gondwe alipokumbuka kubonyeza saa yake kuwashtua Tino na wenzake ambao walikuwa bado wamejificha kwenye ile boti ndogo wasielewe kinachoendelea.
Bosco na Dokta Gondwe walisimama tena wakawa wanatazamana, Bado kulikuwa na mtikisiko kiasi huku boti hiyo ikizidi kukata mawimbi kuelekea kusikojulikana. Hakuna aliyejua ni wapi siraha yake imedondokea. Katikati yao kulikuwa na lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS, wote walitupa macho mbele wakaliona sanduku lile likiwa limedondoka chini, mtihani ukawa ni nani kati yao ataliwahi.
Bosco alikimbia kulifuata sanduku Dokta Gondwe naye akakimbia kumuwahi kabla hajalifikia akamvaa na kwenda naye chini wakaanguka kama magunia, sasa ikawa ni mwendo wa piga nikupige vita kali ikaibuka kati ya Bosco na Dokta Gondwe.
Wakati hali hiyo ikiendelea mara ghafula kuna moshi mweupe ulitanda ndani ya kile chumba, kwa mbali Jasusi Shadow alionekana anaingia kwa kasi akafika na kulichukua lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS kisha akatoka. Badala ya kushirikiana kumzuia Dokta Gondwe na Bosco waliendelea kupigana huku kila mmoja akiwa amemjeruhi mwenzake vibaya.
Dokta Gondwe alikuwa akivuja damu puani wakati Bosco alikuwa akivuja damu mdomoni. Waliendelea kupigana kwa kuviziana kutokana na moshi mwingi uliotanda ndani ya chumba hicho.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Baada ya kengere ya hatari kulia katika saa ya Tino na wenzake, haraka walitoka kwenye maficho yao huku Tino akiwa ndio wa kwanza.
Wote walioshuhudia ile boti kubwa ikiondoka kwa kasi kuelekea upande wa mashariki
"Shiiit!! Nini kinaendelea?" Tino aliuliza kwa kustaajabu huku akiiwasha boti haraka, akashika usukani na kukata kona akaanza kuifukuzia ile boti yake kubwa.
Kuondoka kwa boti hiyo lilikuwa ni tukio ambalo lilimshangaza sana Tino, haikuwa kwenye mpango wake kabisa, alishindwa kuelewa ni nani hasa kafanya hivyo, je ni Bosco au Dokta Gondwe?
Aliendesha boti kwa kasi kujitahidi kuifikia ile boti kubwa ambayo nayo ilikuwa kwenye mwendo wa kasi ikikata mawimbi haswa.
Spidi aliyokuwanayo Tino ilifawafanya wenzake waanze kuogoapa kwani kuna wakati boti ilikuwa ikiruka juu mita kadhaa kutoka usawa wa maji na baadae kurudi chini kishakuendelea kukata mawimbi. Ilibidi wajishikilie kwa nguvu kwenye pembe za boti hiyo.
Akiwa amebakiza umbali wa mita chache kuifikia ile boti kubwa, mara mshare wa mafuta ulianza kuyumba yumba hii ilikuwa ni ishara tosha kuwa mafuta yalikuwa yanakaribia kuisha.
Tino alipiga hesabu za haraka haraka afanye nini kwani kulikuwa na kila dalili kuwa mafuta yataisha hata kabla hajaifikia ile boti kubwa.
"Shika endesha" Tino alimwambia mmoja kati ya vijana aliokuwanao
Bila kupinga yule kijana alipishana na Tino akashika usukani.
Tino alirudi nyuma akafungua sehemu fulani ndani ya ile boti akatoa begi moja kubwa lililokuwa limejaa vifaa vya kuogerea ikiwemo pia mtungi mdogo wa gesi unaoweza kumsaidia mtu kupumua kwa dakika kadhaa akiwa ndani ya maji.
Tino alivaa vile vifaa haraka haraka, wakati anamaliza tu kuvaa tayari boti iliisha mafuta ikazima na kusimama. Tino hakutaka kujiuliza mara mbili mbili haraka alijitosa majini na kuzama alipokuja kuibuka alikuwa karibu kabisa kuifikia ile boti kubwa, akazama tena na kuogerea kwa kutumia vile vifaa alivyovaa ambavyo vilimuwezasha kwenda kwa kasi akiwa ndani ya maji alipokuja kuibuka tena kwa mara ya pili tayari alishaifikia ile boti akapanda na kuanza kusogea taratibu akipandisha ngazi.
Wale vijana wawili walibaki kwenye ile boti ndogo wakielea elea juu ya maji, hawakujua wafanye nini kwani waliachwa umbali mrefu sana. Walichofanya walichukua miko na kuanza kupiga makasia kurudi nchi kavu.
Tino alipokanyaga ngazi ya mwisho kuingia kwenye boti mara mlango uliokuwa mbele yake ulifunguliwa. Kuna mtu alikuwa akitoka kwa kasi ambaye naye alisimama ghafula mara baada ya kukutana uso kwa uso na Tino, mtu huyu alikuwa ni jasusi Shadow.
Wote wawili walikuwa wamevaa vifaa vya kufanana, isipokuwa mtungi wa gesi wa Jasusi Shadow ulikuwa ni mkubwa kuliko wa Tino lakini kila kitu walifanana.
Shadow aliweza kugundua kuwa aliyepo mbele yake ni Tino mtoto wa kwanza wa bosi Sultana lakini Tino hakuwa akimjua mtu aliyesimama mbele yake licha ya hivyo hakuweza pia kuiona sura ya mtu huyo kutokana na ile maski ya kupitisha gesi aliyovaa usoni.
Tino alimtazama Shadow kuanzia juu hadi chini na hapo ndipo akaliona lile sanduku ambalo awali alimuona nalo Dokta Gondwe. Hapo ndipo Tino akagundua kuwa mtu huyo alikuwa na lengo la kuondoka na vimelea vya V-COBOS, lilikuwa ni jambo ambalo katu asingekubali kuona linatokea mbele ya macho yake, hakuwa tayari kumruhusu aondoke na sanduku lile. Lakini Tino hakujua mtu aliyesimama mbele yake ni nani na anauwezo kiasi gani.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mtoto wa kishua Najma ama kwa lugha ya kisasa tungemwita Pisi kali toto la mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alionekana ndani ya gari akiwa katikati ya barabara kuelekea gereza alilohifadhiwa mumewe mtarajiwa Osward.
Bado akili ya Najma haikuwa sawa kabisa, alikuwa akiwaza kuhusu majibu aliyoyapata mtandaoni baada ya kutafuta maana ya vimelea vya COBOS ambavyo alimsikia baba yake akivitaja mara nyingi wakati akiongea na simu kwa siri.
Haya ndiyo majibu ambayo Najma aliyapata mtandaoni
,,,,,,,,,,,,,COBOS virus is a virus that was secretly invented by humans 25 years ago in Mexico. This secret was leaked and the practice was strongly opposed by all countries in the world and later banned by any country or laboratory involved in the manufacture of the virus. That was the last COBOS virus to be heard, there are rumors that the virus was taken and stored by the ZMLST international laboratory in Mexico. For over 25 years now the virus has never been heard anywhere in the world.,,,,,,
(virusi vya COBOS ni virusi vilivyotengenezwa na binadamu kwa siri miaka 25 iliyopita nchini mexico. siri hii ilivuja na kitendo hicho kikapingwa vikali na nchi zote ulimwenguni baadae ikapigwa marufuku kwa nchi au maabara yoyote ulimwenguni itakayojihusisha na utengenezwaji wa virusi. Huo ndio ukawa mwisho wa virusi vya COBOS kusikia, kuna tetesi kuwa virusi hivi vilichukuliwa na kujifadhiwa na maabara ya kimataifa ya ZMLST iliyopo Mexico. Ni zaidi ya miaka 25 sasa virusi hivi havijawahi kusikika mahali popote Dunia)
Haya ni majibu ambayo yalimfanya Najma kuendelea kufuatilia ukweli wa jambo hili. Kitu kikubwa kilichomfanya Najma kuzidi kumtilia mashaka baba yake ni zile safari ambazo baba yake alikuwa akizifanya mara kwa mara kwenda nchini Mexico, hata pale alipokuwa akikosa nafasi alikuwa akimuagiza kwa siri mkwe wake mtarajiwa Osward ambaye kwa sasa yupo gerezani akisubiri hukumu ya kesi ya mauaji inayomuandama.
"Hii inawezanaje? Baba yangu anawezaje kushiriki kwenye mambo kama haya? alafu kwa nini hawa wamexico wamchague yeye, hapana hakuna ukweli wowote hapa" Najma alikuwa akijiuliza na kujijibu mwenyewe, haikuwa rahisi kukubaliana na jambo hilo.
Najma alifika karibu na lile gereza alilopo Osward, gereza ambalo ni jana tu ametoka anaumia vibaya akasaidiwa na inspekta Aron.
Najma alifika gerezani hapo kwa lengo la kuongea na Osward akitaka kumuliza juu ya safari lizokuwa akienda Mexico badala ya baba yake, alikuwa akienda kufanya nini.
Najma aliyafanya yote hayo kimya kimya bila kumueleza Inspekta Aron chochote licha ya kwamba walikuwa na ukaribu mkubwa kwa sana na alikuwa akimkumbuka sana lakini hakumpigia wala kutuma ujumbe wa maandishi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande mwingine msituni, Inspekta Aron na Annah walianza kuzoea mazingira huku Annah kimtazama Inspekta Aron kwa jicho la tofauti, tayari mwanaume huyo alianza kuuteka moyo wake taratibu.
Wakati wote jicho la Inspekta Aron lilikuwa makini kutazama kama kuna mtu atakuja kwenye nyumba hiyo ya siri iliyojengwa na marehemu baba yake, hakuwa amemwabia Annah chochote kuhusu hisia zake zilizomwambia kuwa ni lazima kuna mtu atakuja.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mambo yalizidi kupamba moto, vita kali ilianza kati ya Tino ambaye hakutaka kumruhusu jasusi Shadow andoke na vimelea vya V-COBOS. Shadow naye hakutaka kukubali kushindwa kwa mara nyingine tena ilikuwa ni lazima ahakikishe anaondoka na sanduku hilo. Vita hiyo ilikuwa nje ya boti lakini ndani nako kulikuwa na vita kali kati ya Dokta Gondwe na Bosco kijana wa Tino. Dokta Gondwe hakutaka kumruhusu Bosco aende kwani aliamini huyu ndiye mwenye picha na video zake chafu za ngono lakini pili ni baada ya Bosco kusema kuwa anayo dawa(chupa ya kijivu) dhidi ya virusi vya V-COBOS.
Wakati haya yote yakiendela boti ilizidi kwenda kwa kasi ikikata mawimbi kuelekea kusiko julikana.
Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA....
.Njoo WhatsApp jipatie simulizi hii yote mpaka mwisho kwa tsh 1000 tu
0756862047
(Vita ya kisasa)
Sehemu ya............21
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
21-(VITA BAHARINI)
ILIPOISHIA.....
Wakati huo si Bosco si Dokta Gondwe hakuna aliyekuwa akimuamini mwenzake hawakujua kuwa mzee wa kazi Jasusi Shadow alikuwa ameingia ndani ya boti hiyo naye akiwa anavitaka vimelea vya V-COBOS kama alivyoagizwa na Sultana. Tino na wale vijana wawili walienda kusubiri ndani ya ile boti ndogo, hawakujua chochote kinachoendelea..
SASA ENDELEA....
Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akiwa amemnyoshea mwenzake bastola mara walishtushwa na mtikisiko mkubwa ndani ya boti hiyo mtikisiko uliosababisha wote wawili kuanguka chini kwa pamoja. Boti iliyumba ikiwapeleka kulia na kisha kuwatupa upande wa kushoto. Walishindwa kustahimili kuendelea kushikilia siraha zao zikadondoka chini, kila mmoja akawa anajitahidi kujishikilia mahali ili asiumie kutokana na kuyumba yumba kwa boti ile wasielewe ni nini chanzo. Mara ghafula hali ikatulia kwa sekunde kadhaa kisha wakashangaa kuona boti inaanza kwenda mbele kwa kasi sana.
Mambo yakazidi kuwa mazito kwa upande wa Bosco na Dokta Gondwe kila mmoja akimuhisi mwenzake kuwa ndiye aliyekuwa kihusika na kila kinachoendelea wakati huo hawakujua kabisa habari za kuwepo kwa Jasusi Shadow ndani ya boti hiyo.
Hapo ndipo Dokta Gondwe alipokumbuka kubonyeza saa yake kuwashtua Tino na wenzake ambao walikuwa bado wamejificha kwenye ile boti ndogo wasielewe kinachoendelea.
Bosco na Dokta Gondwe walisimama tena wakawa wanatazamana, Bado kulikuwa na mtikisiko kiasi huku boti hiyo ikizidi kukata mawimbi kuelekea kusikojulikana. Hakuna aliyejua ni wapi siraha yake imedondokea. Katikati yao kulikuwa na lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS, wote walitupa macho mbele wakaliona sanduku lile likiwa limedondoka chini, mtihani ukawa ni nani kati yao ataliwahi.
Bosco alikimbia kulifuata sanduku Dokta Gondwe naye akakimbia kumuwahi kabla hajalifikia akamvaa na kwenda naye chini wakaanguka kama magunia, sasa ikawa ni mwendo wa piga nikupige vita kali ikaibuka kati ya Bosco na Dokta Gondwe.
Wakati hali hiyo ikiendelea mara ghafula kuna moshi mweupe ulitanda ndani ya kile chumba, kwa mbali Jasusi Shadow alionekana anaingia kwa kasi akafika na kulichukua lile sanduku lenye vimelea vya V-COBOS kisha akatoka. Badala ya kushirikiana kumzuia Dokta Gondwe na Bosco waliendelea kupigana huku kila mmoja akiwa amemjeruhi mwenzake vibaya.
Dokta Gondwe alikuwa akivuja damu puani wakati Bosco alikuwa akivuja damu mdomoni. Waliendelea kupigana kwa kuviziana kutokana na moshi mwingi uliotanda ndani ya chumba hicho.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Baada ya kengere ya hatari kulia katika saa ya Tino na wenzake, haraka walitoka kwenye maficho yao huku Tino akiwa ndio wa kwanza.
Wote walioshuhudia ile boti kubwa ikiondoka kwa kasi kuelekea upande wa mashariki
"Shiiit!! Nini kinaendelea?" Tino aliuliza kwa kustaajabu huku akiiwasha boti haraka, akashika usukani na kukata kona akaanza kuifukuzia ile boti yake kubwa.
Kuondoka kwa boti hiyo lilikuwa ni tukio ambalo lilimshangaza sana Tino, haikuwa kwenye mpango wake kabisa, alishindwa kuelewa ni nani hasa kafanya hivyo, je ni Bosco au Dokta Gondwe?
Aliendesha boti kwa kasi kujitahidi kuifikia ile boti kubwa ambayo nayo ilikuwa kwenye mwendo wa kasi ikikata mawimbi haswa.
Spidi aliyokuwanayo Tino ilifawafanya wenzake waanze kuogoapa kwani kuna wakati boti ilikuwa ikiruka juu mita kadhaa kutoka usawa wa maji na baadae kurudi chini kishakuendelea kukata mawimbi. Ilibidi wajishikilie kwa nguvu kwenye pembe za boti hiyo.
Akiwa amebakiza umbali wa mita chache kuifikia ile boti kubwa, mara mshare wa mafuta ulianza kuyumba yumba hii ilikuwa ni ishara tosha kuwa mafuta yalikuwa yanakaribia kuisha.
Tino alipiga hesabu za haraka haraka afanye nini kwani kulikuwa na kila dalili kuwa mafuta yataisha hata kabla hajaifikia ile boti kubwa.
"Shika endesha" Tino alimwambia mmoja kati ya vijana aliokuwanao
Bila kupinga yule kijana alipishana na Tino akashika usukani.
Tino alirudi nyuma akafungua sehemu fulani ndani ya ile boti akatoa begi moja kubwa lililokuwa limejaa vifaa vya kuogerea ikiwemo pia mtungi mdogo wa gesi unaoweza kumsaidia mtu kupumua kwa dakika kadhaa akiwa ndani ya maji.
Tino alivaa vile vifaa haraka haraka, wakati anamaliza tu kuvaa tayari boti iliisha mafuta ikazima na kusimama. Tino hakutaka kujiuliza mara mbili mbili haraka alijitosa majini na kuzama alipokuja kuibuka alikuwa karibu kabisa kuifikia ile boti kubwa, akazama tena na kuogerea kwa kutumia vile vifaa alivyovaa ambavyo vilimuwezasha kwenda kwa kasi akiwa ndani ya maji alipokuja kuibuka tena kwa mara ya pili tayari alishaifikia ile boti akapanda na kuanza kusogea taratibu akipandisha ngazi.
Wale vijana wawili walibaki kwenye ile boti ndogo wakielea elea juu ya maji, hawakujua wafanye nini kwani waliachwa umbali mrefu sana. Walichofanya walichukua miko na kuanza kupiga makasia kurudi nchi kavu.
Tino alipokanyaga ngazi ya mwisho kuingia kwenye boti mara mlango uliokuwa mbele yake ulifunguliwa. Kuna mtu alikuwa akitoka kwa kasi ambaye naye alisimama ghafula mara baada ya kukutana uso kwa uso na Tino, mtu huyu alikuwa ni jasusi Shadow.
Wote wawili walikuwa wamevaa vifaa vya kufanana, isipokuwa mtungi wa gesi wa Jasusi Shadow ulikuwa ni mkubwa kuliko wa Tino lakini kila kitu walifanana.
Shadow aliweza kugundua kuwa aliyepo mbele yake ni Tino mtoto wa kwanza wa bosi Sultana lakini Tino hakuwa akimjua mtu aliyesimama mbele yake licha ya hivyo hakuweza pia kuiona sura ya mtu huyo kutokana na ile maski ya kupitisha gesi aliyovaa usoni.
Tino alimtazama Shadow kuanzia juu hadi chini na hapo ndipo akaliona lile sanduku ambalo awali alimuona nalo Dokta Gondwe. Hapo ndipo Tino akagundua kuwa mtu huyo alikuwa na lengo la kuondoka na vimelea vya V-COBOS, lilikuwa ni jambo ambalo katu asingekubali kuona linatokea mbele ya macho yake, hakuwa tayari kumruhusu aondoke na sanduku lile. Lakini Tino hakujua mtu aliyesimama mbele yake ni nani na anauwezo kiasi gani.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mtoto wa kishua Najma ama kwa lugha ya kisasa tungemwita Pisi kali toto la mheshimiwa Waziri wa afya Dokta Gondwe alionekana ndani ya gari akiwa katikati ya barabara kuelekea gereza alilohifadhiwa mumewe mtarajiwa Osward.
Bado akili ya Najma haikuwa sawa kabisa, alikuwa akiwaza kuhusu majibu aliyoyapata mtandaoni baada ya kutafuta maana ya vimelea vya COBOS ambavyo alimsikia baba yake akivitaja mara nyingi wakati akiongea na simu kwa siri.
Haya ndiyo majibu ambayo Najma aliyapata mtandaoni
,,,,,,,,,,,,,COBOS virus is a virus that was secretly invented by humans 25 years ago in Mexico. This secret was leaked and the practice was strongly opposed by all countries in the world and later banned by any country or laboratory involved in the manufacture of the virus. That was the last COBOS virus to be heard, there are rumors that the virus was taken and stored by the ZMLST international laboratory in Mexico. For over 25 years now the virus has never been heard anywhere in the world.,,,,,,
(virusi vya COBOS ni virusi vilivyotengenezwa na binadamu kwa siri miaka 25 iliyopita nchini mexico. siri hii ilivuja na kitendo hicho kikapingwa vikali na nchi zote ulimwenguni baadae ikapigwa marufuku kwa nchi au maabara yoyote ulimwenguni itakayojihusisha na utengenezwaji wa virusi. Huo ndio ukawa mwisho wa virusi vya COBOS kusikia, kuna tetesi kuwa virusi hivi vilichukuliwa na kujifadhiwa na maabara ya kimataifa ya ZMLST iliyopo Mexico. Ni zaidi ya miaka 25 sasa virusi hivi havijawahi kusikika mahali popote Dunia)
Haya ni majibu ambayo yalimfanya Najma kuendelea kufuatilia ukweli wa jambo hili. Kitu kikubwa kilichomfanya Najma kuzidi kumtilia mashaka baba yake ni zile safari ambazo baba yake alikuwa akizifanya mara kwa mara kwenda nchini Mexico, hata pale alipokuwa akikosa nafasi alikuwa akimuagiza kwa siri mkwe wake mtarajiwa Osward ambaye kwa sasa yupo gerezani akisubiri hukumu ya kesi ya mauaji inayomuandama.
"Hii inawezanaje? Baba yangu anawezaje kushiriki kwenye mambo kama haya? alafu kwa nini hawa wamexico wamchague yeye, hapana hakuna ukweli wowote hapa" Najma alikuwa akijiuliza na kujijibu mwenyewe, haikuwa rahisi kukubaliana na jambo hilo.
Najma alifika karibu na lile gereza alilopo Osward, gereza ambalo ni jana tu ametoka anaumia vibaya akasaidiwa na inspekta Aron.
Najma alifika gerezani hapo kwa lengo la kuongea na Osward akitaka kumuliza juu ya safari lizokuwa akienda Mexico badala ya baba yake, alikuwa akienda kufanya nini.
Najma aliyafanya yote hayo kimya kimya bila kumueleza Inspekta Aron chochote licha ya kwamba walikuwa na ukaribu mkubwa kwa sana na alikuwa akimkumbuka sana lakini hakumpigia wala kutuma ujumbe wa maandishi.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande mwingine msituni, Inspekta Aron na Annah walianza kuzoea mazingira huku Annah kimtazama Inspekta Aron kwa jicho la tofauti, tayari mwanaume huyo alianza kuuteka moyo wake taratibu.
Wakati wote jicho la Inspekta Aron lilikuwa makini kutazama kama kuna mtu atakuja kwenye nyumba hiyo ya siri iliyojengwa na marehemu baba yake, hakuwa amemwabia Annah chochote kuhusu hisia zake zilizomwambia kuwa ni lazima kuna mtu atakuja.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mambo yalizidi kupamba moto, vita kali ilianza kati ya Tino ambaye hakutaka kumruhusu jasusi Shadow andoke na vimelea vya V-COBOS. Shadow naye hakutaka kukubali kushindwa kwa mara nyingine tena ilikuwa ni lazima ahakikishe anaondoka na sanduku hilo. Vita hiyo ilikuwa nje ya boti lakini ndani nako kulikuwa na vita kali kati ya Dokta Gondwe na Bosco kijana wa Tino. Dokta Gondwe hakutaka kumruhusu Bosco aende kwani aliamini huyu ndiye mwenye picha na video zake chafu za ngono lakini pili ni baada ya Bosco kusema kuwa anayo dawa(chupa ya kijivu) dhidi ya virusi vya V-COBOS.
Wakati haya yote yakiendela boti ilizidi kwenda kwa kasi ikikata mawimbi kuelekea kusiko julikana.
Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA....
.Njoo WhatsApp jipatie simulizi hii yote mpaka mwisho kwa tsh 1000 tu
0756862047