Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Simulizi: Kaburi la Mwanamuziki
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300
Sehemu ya 1
“Kazi yangu bila shaka kila mmoja wenu atakuwa ameifanya vizuri, nilifurahishwa na Richard, yeye aliimaliza tangu jana akaniletea Daftari lake, amefanya vizuri sana. Richard! Tafadhali njoo uchukue Daftari lako” Mwalimu wa Hesabu akasema. Richard akatoka, akaenda kuchukua Daftari lake wanafunzi wote tukimtazama, wengine wakimuonea donge, wengine wakimuona kama kiherehere huku wengine tukiwa hatujali lolote. Kisha mwalimu wa Hesabu akaendelea kusema;
“ Richard amekuwa akifanya vizuri tangu mkiwa kidato cha kwanza, sijui ninyi mnashindwaje na Richard, miaka ijayo Richard atakuja kuwa mtu muhimu sana ndani ya nchi hii. Sijui atakuwa Mchumi! Labda atakuwa Daktari bingwa! Huenda akawa Injinia mkubwa sana hapa nchini. Ati Richard unandoto ya kuwa nani hapo baadaye” Mwalimu wa Hesabu akasema, macho yake yakimtazama Richard huku akitabsamu. Richard naye kwa aibu akatabasamu huku akimtazama Mwalimu wa Hesabu, kisha akajibu;
“ Ningetamani niwe Daktari hilo lisingenishinda, masomao ya fizikia, kemia na Bilojia wote mnajua hayanishindi, labda ningesema niwe Injinia nako nisingeshindwa Mwalimu, Hesabu na Fizikia sijivunii lakini najitahidi kwa kiwango cha wanafunzi bora katika nchi hii. Hata ningesema niwe Mwanasheria, kote ninamudu, lakini yote hayo siyataki, nataka kile ambacho wengi hukitafuta, kile ambacho wengi wamekikosa ndicho ninataka kukisomea, nataka niwe mtaalamu wa mambo ya Fedha, nataka jambo lolote lihusulo Fedha lisinipite, ndoto yangu kubwa ni kuwa mtaalamu wa mambo ya fedha, ukiniita mchumi ni sawa, ukiniita mhasibu pia ni sawa, nataka nikiita fedha initii, nikiikagua inihofie, hiyo ndoto yangu kubwa Mwalimu” Richard alijibu, Darasa lote lilimsikiliza, majibu yake licha ya kuwa na matambo lakini yalionyesha kiburi cha ndani, majivuno ya akili alizojaliwa.
Mwalimu wa Hesabu alituamuru tumpongeze Richard kwa kupiga makofi, rafiki zake walipiga makofi kwa nguvu wakishangilia, wakati washindani wake wakipiga makofi ya kivivu, sisi Back benchers tulikuwa bora liende, tulikuwa tukisukuma tuu siku ziende, kwa kweli hatukuwahi kumuonea wivu yeyote kwa habari za masomo. Hata hivyo ilikuwa ni kero waalimu walipokuwa wakiingia kutufundisha, chanzo cha kero ilikuwa maneno ya baadhi ya waalimu kutudhalilisha sisi tuliokuwa hatufanyi vizuri kwenye masomo, walitukera kadiri ya uwezo wao, wenye mdomo walitumia maneno makali, wenye hasira walituchapa na kutupa adhabau kali. Mambo hayo yalinifanya nizidi kuichukia shule. Kama sio Mama yangu kunilazimisha kusoma basi ningekuwa nimeacha shule siku nyingi, huenda hata kidato cha nne nisingefika. Nilimuonea huruma mama, na hiyo huruma ndio iliyonifanya nivumilie kero za waalimu wa ile shule nikamaliza elimu ya upili.
” Natamani wote mngekuwa kama Richard au Alice, elimu ni ufunguo wa maisha, oneni wazazi wenu wanahangaika kwa umasikini kutokana na kuwa na elimu duni, ndio maana wamewaleta ninyi shuleni mpate elimu msipate shida kama wao wanavyopata lakini ninyi baadhi yenu hamuelewi lolote mkiambiwa, mnacheza na muda wenu, muda hauchezewi, mtoto mdogo unaharakia nini kwenye mapenzi, unaharakia nini mambo ya Starehe, juzi nilikutana na Kabali akitoka Bar akiwa kalewa. Kabali unajua ulinisikitisha sana” Mwalimu wa Hesabu alisema, macho yake yakimkabili Kabali aliyekaa nyuma kabisa.
“ Nisamehe mwalimu, Lakini mara mojamoja sio mbaya kushtua ubongo” Kabali akajibu.
“ Hahahahahahah!” Wote wanacheka kasoro Mwalimu aliyebaki anamtazama Kabali huku akitingisha kichwa kwa kumsikitikia.
“ Anyaway! Shauri yako. Kila mmoja aweke. Daftari la Mathematics juu ya dawati, alafu afungue mahali alipofanyia kazi niliyoitoa jana” Mwalimu wa hesabu akaagiza, jambo hilo likawa linafanyika, mimi ndio nilikuwa namalizia kuhamisha kazi ya Alice aliyoifanya kwenye Daftari langu, Mwalimu alikuwa anaanzia kusahisha madaftari ya wanafunzi waliokaa mbele, mara kwa mara nilimuona Alice akigeuka nyuma kunitazama, nami nilikuwa nikimpa ishara yakuwa namalizia. Alice akawa ananipa ishara nifanye hima, baada ya kujibu maswali matatu kati ya matano, nikaona isiwe kesi, nikamrudishia Alice Daftari yake kwa kulifaulisha kwa dawati lililofuata kwenda mbele mpaka lilipofika kwa Alice.
Sikuwa najua hesabu kusema ukweli, tangu naanza shule niliishi kwa kuibia ibia ilimradi nisiwe wa mwisho darasani, sasa yalibaki maswali mawili kati ya matano, nitayafanyaje, unajua hesabu za kidato cha nne sio za jumlisha wala kutoa, bora hata zingekuwa za Desimali ningejaribu lakini zilikuwa hesabu ngumu zenye alama nyingi, sikuwa naelewa chochote. Nikaandika andika namba za uongo uongo ilimradi kurasa za daftari langu lijae, nikajaza majibu na kuyapigia mstari kwa usafi wote labda nilifikiri mwalimu angenionea huruma hata kama nimekosea jibu basi angenipa vimaksi vya usafi katika kazi. Lakini kumbe jibu la uongo ni uongo tuu hata kama likirembwa na kupambwa.
Mwalimu akanifikia, akachukua Daftari langu, akasahihisha swali la kwanza mpaka la tatu, alipofika swali la nne, aka-stop, nikaanza kuhisi mwili ukilegea, nilihofia asijejua nimeibia kwa mtu. Akanipa alama ya kosa, swali la tano likamshtua,
“Iweje upate swali la kwanza na lapili alafu ukose swali la tano? Ati wanafunzi hiyo inawezakana?” Akauliza!
“ Haiwezekani!” Wakajibu wanafunzi wote mpaka yule jirani yangu niliyekaa naye wakati naye hana anachojua kwenye hisabati.
“ Wewe utakuwa umeibia tuu! Ndio maana nikashangaa tangu lini Gibson umekuwa na akili za kukokotoa milinganyo kama hii. Embu ona!” Mwalimu akawa anaanza kupekua daftari langu katika kurasa zingine zisizohusiana na kazi ya leo. Kiukweli nilikereka, nilihisi naenda kuumbuka.
“ Heeh! Hii nini! Gibson! Hiki ni kitu gani kwenye daftari langu la Hisabati?” Sauti ya mwalimu ikafanya darasa zima kugeuka na kutazama kilichokuwa kinaendelea, mwalimu akapita mbele akiwa kabeba daftari langu, kisha alipofika mbele kabisa ya darasa ulipo ubao, akaniita nami niende mbele. Nilipofika akaniambia nipige magoti chini. Kwa aibu uso wangu nikiukwepesha na nyuso za wanafunzi wenzangu nikawa naangalia chini nikiwa nimepiga magoti,
“ Kwa hiyo ukaona Daftari langu ndilo la kuandikia huu upuuzi wako, Gibson! Mara ngapi umekanywa na mama yako kujihusisha na Muziki? Mara ngapi! Muziki ni uhuni, hufanywa na watu wajinga, wapuuzi na wasio na haya, au unataka kukata kata mauno kama hivi! Eeh! Hivi na hivi! Ndio unataka?” Darasa zima linacheka baada ya mwalimu kukata mauno.
“ Lakini mwalimu hata muziki nao ni kazi tuu kama zilivyokazi zingine, napenda sana kuimba Mwalimu!”
“ KELELE!”
“ Unaongea utopolo gani hapa! Muziki! Muziki! Muziki! Upuuzi mtupu! Haya kwa hiyo kupenda kwako muziki ndio ukaona utumie daftari la hisabati kuandika mautopolo yako ya muziki! Hukuona masomo mengine mpaka uandikie kwenye daftari la hisabati? Unadharau HISABATI! Hahahaha! Unajua waalimu wa hisabati wapo wangapi kwenye hii nchi? Unaelewa? Hisabati ni somo lenye heshima, ambalo watu wenye akili za juu ndio hulimudu sio watu kama wewe” Mwalimu akasema, muda huu hasira zilikuwa zimeikaribia kabisa sura yake.
“ Nisamehe mwalimu!” Nikasema. Mikono yangu nikiwa nimeiweka kifuani kama ishara ya kuomba radhi.
“ Leo nitakuchapa bakora mpaka akili ikukae sawa! Haya shika chini mjinga wewe!” Sikuwa na namna nikashika chini, viboko sita vikatua katika makalio yangu, vilikuwa viboko vichungu sana vilivyoyatia maumivu makalio yangu. Nilimuona Alice akilengwa lengwa na machozi, moyoni nilijihisi kuumia sana kuuona uso wa Alice katika hali ile.
Mwalimu alimaliza kufundisha, hatimaye akatoka;
Kila baada ya Lunch ilikuwa mara nyingi waalimu hawaingii darasani. Hivyo muda huo niliutumia kufanya mazoezi ya kuimba, nilikuwa nikienda uwanjani kufanya mazoezi ya sauti, nilizipa mazoezi ala za sauti kama vile ulimi, mdomo, koo na hata Glota. Nilipanua mdomo kuhakikisha sauti yangu inatoka vizuri. Nilifanya mazoezi ya pumzi bila kuchoka kuhakikisha sauti yangu haikati pindi nikiimba sauti ya juu sana.
Kuna wakati nilikuwa nakaa kwenye vivuli ya miti sehemu tulivu, ili kupata tungo nzuri. Nilikuwa nikitunga tungo nzuri za mashairi na kuyarekodi katika kidaftari maalumu. Kivuli na upepo mwanana hutuliza akili, Huibua ubunifu na shauku ya fikra ya kutunga vitu vipya katika sanaa.
“ Labda ni kweli sina akili za masomo ya darasani, ufaulu wangu ni duni. Njia pekee iliyobaki ni kutumia kipaji changu cha kuimba, hakika nitakilinda kipaji change, nitailinda sauti yangu, nitalinda ala za sauti. Lakini Ala za sauti nzuri bila fikra thabiti zenye ubunifu hazitanisaidia kitu, nitalinda fikra zangu kwa kulinda vivuli vya miti ya dunia….” Nikawaza mwenyewe lakini mara Alice akatokea jambo ambalo lilikatisha mawazo yangu.
“ Gibson! Nimekutafuta sana! Nimezunguka uwanjani nikakukosa, nikaenda kwenye yale madarasa mapya pia sikukuona, hapo nikajua sehemu yako ya mwisho ni huku kwenye huu mti wa Mzambarau” Alice akasema.
“ Umekuwa mahiri wa kujua mizunguko yangu eeh! Haya je usingenikuta kwenye huu mti wa mzambarau ungedhani nimeenda wapi?”
“ Bila shaka ningedhani umeshaondoka kwenda nyumbani” Akajibu. Tukacheka wote sana. Alice alipenda kutembea akiwa na juisi ya kopo pamoja na Ubuyu wa rangi nyekundu. Tukala pale ubuyu tukipiga stori. Mara kimya kikafuata, nikamuona Alice akiangalia mbele kwa mbali kidogo, alikuwa kama anawaza mbali la kuhuzunisha. Alinishtua na kunipa hofu.
“ Kuna nini Alice! Unawaza nini?” Nilimuuliza. Alice akanigeukia akanitazama.
“ Mtihani wa mwisho umekaribia sana, sidhani kama mpenzi wangu umejiandaa vya kutosha! Nina wasiwasi sana juu yako Gibson” Alice akasema.
Nikamtazama bila kusema kitu, sikujua nimwambie jambo gani, Alice alikuwa ananijali licha ya kuwa nilikuwa natoka familia masikini, nikiwa naufaulu mdogo mno.
“ Mimi nafikiri ungeyaweka mambo mengine pembeni kwanza ujikite kwenye kusoma, kisha baad ya kumaliza mitihani yetu ya mwisho ndio uurudie muziki. Unaonaje Gibson?” Alice akasema.
“ Niache muziki! Alice umechanganyikiwa? Hivi unajua muziki unamaana gani kwenye maisha yangu? Alice! Uliwahi kujiuliza muziki kwangu ni nini? Labda hujawahi kufikiria jambo hili. Acha nikujuze; Muziki kwangu ni maisha, muziki kwangu ndiye mkombozi, wakati madaktari wakitumia taalamu zao kutibu watu, mimi Gibson nitautumia muziki kutibu hisia za watu zilizopondeka, wakati waalimu kama mwalimu wa hesabati wakielimisha watu ingawaje wanatunyanyasa siye tusiye na uwezo darasani, mimi Gibson nitatumia muziki kuelimisha jamii na taifa langu. Alice bado hujaelewa muziki kwangu nini? Bila shaka umeelewa! Haya bado utaniambia niuache muziki?” Nilizungumza nikimtazama Alice kwa macho yaliyojawa na usongo.
“ Lakini Gibson, sijamaanisha uache muziki moja kwa moja, nimemaanisha upumzike kipindi hiki ili tujiandae kwa pamoja kwenye mitihani yetu hii ya mwisho, kisha utaendelea na muziki wako, Gibson unajua mimi ndiye shabiki wako namba moja..”
“ Alice! Naomba tuachane na hayo, tuzungumze mambo mengine!” Baada ya Alice kuniona nimebaki kuwa na msimamo wangu, akaniacha. Niliona jinsi alivyoumia nikaona nijifanye nimekubaliana naye kishingo upande.
**************
“ Kesho ndio nitapiga hatua yangu ya kwanza katika muziki, lazima niwaonyeshe watu kuwa nina kipaji kikubwa, ikiwa ni hatua ya kwanza itanipasa niipige kwa kishindo ambacho kitatikisa vikwazo vyote vilivyombele yangu. Ngoja niendelee mazoezi” nikawaza, alafu nikachukua moja ya kidaftari nilichoandika nyimbo zangu. Nikaanza kuperuzi katika kidaftari kile.
“ Huu! Hapana! Nitaingia na huu! Utafuata huu! Alafu nitamalizia na huu!” Punde nikakatishwa na Alice aliyekuwa ameiingia akiwa na mfuko. Akanikumbatia kwa nguvu, kisha akanibusu!
“ Vipi maandalizi yanaendeleaje?” Akaniuliza, akiwa anachukua stuli, akakaa na kuweka chini mfuko aliokuja nao.
“ Kama unavyoona, nataka kesho mji mzima utikisike, nitaishangaza dunia Alice” Nikasema nikimtazama Alice,
“ Sijui kwa nini hawajatupa nafasi tuimbe walau nyimbo nne!” Nikasema lakini Alice akanikatisha.
“ Gibson mpenzi! Kesho watumbuizaji watakuwa wengi mno, zitakuwepo shule tatu kubwa za kanda hii. Wameona muda utakuwa mdogo, hata hizo nyimbo tatu mlizoambiwa mnaweza msiziimbe, Hivyo unapaswa ujiandae kwa lolote.” Alice akasema.
“ Hata wakisema niimbe moja, kesho nitawafunika wote, kesho ni siku yangu ya furaha. Alice kesho jiandae kufurahia kusikia sauti ya mpenzi wako, kesho utajivunia mimi” Nikasema.
“ Hata sasa najivunia wewe Gibson, mimi siku zote nitajivunia wewe, ila usijiamini sana Mpenzi, kujiamini ni kuzuri lakini isipitilize” Alice akasema, akanyanyuka kisha akatoa nguo kwenye ule mfuko aliokuja nao,
“ Embu vaa hizi tuone!” Akanipa suruali ya jeansi nyeusi hivi na T-shirt nyeupe yenye picha yenye Skull and bones kwa mbele, alafu nyuma yalikuwepo maandishi “ GIBSON ft ALICE”. Nikavaa. Kisha akatoa miwani nyeusi akanipa nivae, nikavaa. Hapo nikamuona Alice akitabasamu kama aliyefurahishwa na muonekano wangu mpya, alafu akatoa Viatu dizaini ya Supra akanipa nikavaa, kisha akaniambia nivae na kofia. Nikamwambia anisubiri niende chumbani kwa mama nikajiangalie kwenye kioo kikubwa. Nikamuacha!
Nilikuwa nimependeza sana, nilifanana kwa ukaribu na wanamuziki wa kimataifa wanaotumbuiza kwenye majukwaa ya kimataifa, baada ya kuridhishwa na muonekano wangu, nikarudi chumbani kwangu,
“ Sasa itabidi uende saluni ukazitengeneze nywele zako vizuri” Alice akasema, akatoa elfu mbili akanikabidhi za kunyolea. Kisha akaniambia nijaribu kutumbuiza mbele yake.
Nikashika kalamu kama maiki na kuisogeza mdomoni. Nikaachia sauti nyepesi na laini nikiupiga wimbo wa mwisho nitakaouimba kesho. Alice akajikuta anatoa machozi, nilifanikiwa kuzigusa hisia zake kikamilifu.
“ Waaaoh! Umeimba vizuri sana. Natamani kesho uimbe kama ulivyoimba leo?” Alice akasema.
“ Usijali mpenzi!Kesho utajionea mwanaume uliyenaye niwa namna gani. Nimekuahidi kuwa siku ya kesho ndio siku utakayojivunia tangu unijue” Nikasema,
Kisha tukaachana, mimi nikienda kunyoa na kuziweka nywele sawa, wakati Alice akirudi kwao. Hiyo ilikuwa saa moja ya jioni hivi.
Itaendelea
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300
Sehemu ya 1
“Kazi yangu bila shaka kila mmoja wenu atakuwa ameifanya vizuri, nilifurahishwa na Richard, yeye aliimaliza tangu jana akaniletea Daftari lake, amefanya vizuri sana. Richard! Tafadhali njoo uchukue Daftari lako” Mwalimu wa Hesabu akasema. Richard akatoka, akaenda kuchukua Daftari lake wanafunzi wote tukimtazama, wengine wakimuonea donge, wengine wakimuona kama kiherehere huku wengine tukiwa hatujali lolote. Kisha mwalimu wa Hesabu akaendelea kusema;
“ Richard amekuwa akifanya vizuri tangu mkiwa kidato cha kwanza, sijui ninyi mnashindwaje na Richard, miaka ijayo Richard atakuja kuwa mtu muhimu sana ndani ya nchi hii. Sijui atakuwa Mchumi! Labda atakuwa Daktari bingwa! Huenda akawa Injinia mkubwa sana hapa nchini. Ati Richard unandoto ya kuwa nani hapo baadaye” Mwalimu wa Hesabu akasema, macho yake yakimtazama Richard huku akitabsamu. Richard naye kwa aibu akatabasamu huku akimtazama Mwalimu wa Hesabu, kisha akajibu;
“ Ningetamani niwe Daktari hilo lisingenishinda, masomao ya fizikia, kemia na Bilojia wote mnajua hayanishindi, labda ningesema niwe Injinia nako nisingeshindwa Mwalimu, Hesabu na Fizikia sijivunii lakini najitahidi kwa kiwango cha wanafunzi bora katika nchi hii. Hata ningesema niwe Mwanasheria, kote ninamudu, lakini yote hayo siyataki, nataka kile ambacho wengi hukitafuta, kile ambacho wengi wamekikosa ndicho ninataka kukisomea, nataka niwe mtaalamu wa mambo ya Fedha, nataka jambo lolote lihusulo Fedha lisinipite, ndoto yangu kubwa ni kuwa mtaalamu wa mambo ya fedha, ukiniita mchumi ni sawa, ukiniita mhasibu pia ni sawa, nataka nikiita fedha initii, nikiikagua inihofie, hiyo ndoto yangu kubwa Mwalimu” Richard alijibu, Darasa lote lilimsikiliza, majibu yake licha ya kuwa na matambo lakini yalionyesha kiburi cha ndani, majivuno ya akili alizojaliwa.
Mwalimu wa Hesabu alituamuru tumpongeze Richard kwa kupiga makofi, rafiki zake walipiga makofi kwa nguvu wakishangilia, wakati washindani wake wakipiga makofi ya kivivu, sisi Back benchers tulikuwa bora liende, tulikuwa tukisukuma tuu siku ziende, kwa kweli hatukuwahi kumuonea wivu yeyote kwa habari za masomo. Hata hivyo ilikuwa ni kero waalimu walipokuwa wakiingia kutufundisha, chanzo cha kero ilikuwa maneno ya baadhi ya waalimu kutudhalilisha sisi tuliokuwa hatufanyi vizuri kwenye masomo, walitukera kadiri ya uwezo wao, wenye mdomo walitumia maneno makali, wenye hasira walituchapa na kutupa adhabau kali. Mambo hayo yalinifanya nizidi kuichukia shule. Kama sio Mama yangu kunilazimisha kusoma basi ningekuwa nimeacha shule siku nyingi, huenda hata kidato cha nne nisingefika. Nilimuonea huruma mama, na hiyo huruma ndio iliyonifanya nivumilie kero za waalimu wa ile shule nikamaliza elimu ya upili.
” Natamani wote mngekuwa kama Richard au Alice, elimu ni ufunguo wa maisha, oneni wazazi wenu wanahangaika kwa umasikini kutokana na kuwa na elimu duni, ndio maana wamewaleta ninyi shuleni mpate elimu msipate shida kama wao wanavyopata lakini ninyi baadhi yenu hamuelewi lolote mkiambiwa, mnacheza na muda wenu, muda hauchezewi, mtoto mdogo unaharakia nini kwenye mapenzi, unaharakia nini mambo ya Starehe, juzi nilikutana na Kabali akitoka Bar akiwa kalewa. Kabali unajua ulinisikitisha sana” Mwalimu wa Hesabu alisema, macho yake yakimkabili Kabali aliyekaa nyuma kabisa.
“ Nisamehe mwalimu, Lakini mara mojamoja sio mbaya kushtua ubongo” Kabali akajibu.
“ Hahahahahahah!” Wote wanacheka kasoro Mwalimu aliyebaki anamtazama Kabali huku akitingisha kichwa kwa kumsikitikia.
“ Anyaway! Shauri yako. Kila mmoja aweke. Daftari la Mathematics juu ya dawati, alafu afungue mahali alipofanyia kazi niliyoitoa jana” Mwalimu wa hesabu akaagiza, jambo hilo likawa linafanyika, mimi ndio nilikuwa namalizia kuhamisha kazi ya Alice aliyoifanya kwenye Daftari langu, Mwalimu alikuwa anaanzia kusahisha madaftari ya wanafunzi waliokaa mbele, mara kwa mara nilimuona Alice akigeuka nyuma kunitazama, nami nilikuwa nikimpa ishara yakuwa namalizia. Alice akawa ananipa ishara nifanye hima, baada ya kujibu maswali matatu kati ya matano, nikaona isiwe kesi, nikamrudishia Alice Daftari yake kwa kulifaulisha kwa dawati lililofuata kwenda mbele mpaka lilipofika kwa Alice.
Sikuwa najua hesabu kusema ukweli, tangu naanza shule niliishi kwa kuibia ibia ilimradi nisiwe wa mwisho darasani, sasa yalibaki maswali mawili kati ya matano, nitayafanyaje, unajua hesabu za kidato cha nne sio za jumlisha wala kutoa, bora hata zingekuwa za Desimali ningejaribu lakini zilikuwa hesabu ngumu zenye alama nyingi, sikuwa naelewa chochote. Nikaandika andika namba za uongo uongo ilimradi kurasa za daftari langu lijae, nikajaza majibu na kuyapigia mstari kwa usafi wote labda nilifikiri mwalimu angenionea huruma hata kama nimekosea jibu basi angenipa vimaksi vya usafi katika kazi. Lakini kumbe jibu la uongo ni uongo tuu hata kama likirembwa na kupambwa.
Mwalimu akanifikia, akachukua Daftari langu, akasahihisha swali la kwanza mpaka la tatu, alipofika swali la nne, aka-stop, nikaanza kuhisi mwili ukilegea, nilihofia asijejua nimeibia kwa mtu. Akanipa alama ya kosa, swali la tano likamshtua,
“Iweje upate swali la kwanza na lapili alafu ukose swali la tano? Ati wanafunzi hiyo inawezakana?” Akauliza!
“ Haiwezekani!” Wakajibu wanafunzi wote mpaka yule jirani yangu niliyekaa naye wakati naye hana anachojua kwenye hisabati.
“ Wewe utakuwa umeibia tuu! Ndio maana nikashangaa tangu lini Gibson umekuwa na akili za kukokotoa milinganyo kama hii. Embu ona!” Mwalimu akawa anaanza kupekua daftari langu katika kurasa zingine zisizohusiana na kazi ya leo. Kiukweli nilikereka, nilihisi naenda kuumbuka.
“ Heeh! Hii nini! Gibson! Hiki ni kitu gani kwenye daftari langu la Hisabati?” Sauti ya mwalimu ikafanya darasa zima kugeuka na kutazama kilichokuwa kinaendelea, mwalimu akapita mbele akiwa kabeba daftari langu, kisha alipofika mbele kabisa ya darasa ulipo ubao, akaniita nami niende mbele. Nilipofika akaniambia nipige magoti chini. Kwa aibu uso wangu nikiukwepesha na nyuso za wanafunzi wenzangu nikawa naangalia chini nikiwa nimepiga magoti,
“ Kwa hiyo ukaona Daftari langu ndilo la kuandikia huu upuuzi wako, Gibson! Mara ngapi umekanywa na mama yako kujihusisha na Muziki? Mara ngapi! Muziki ni uhuni, hufanywa na watu wajinga, wapuuzi na wasio na haya, au unataka kukata kata mauno kama hivi! Eeh! Hivi na hivi! Ndio unataka?” Darasa zima linacheka baada ya mwalimu kukata mauno.
“ Lakini mwalimu hata muziki nao ni kazi tuu kama zilivyokazi zingine, napenda sana kuimba Mwalimu!”
“ KELELE!”
“ Unaongea utopolo gani hapa! Muziki! Muziki! Muziki! Upuuzi mtupu! Haya kwa hiyo kupenda kwako muziki ndio ukaona utumie daftari la hisabati kuandika mautopolo yako ya muziki! Hukuona masomo mengine mpaka uandikie kwenye daftari la hisabati? Unadharau HISABATI! Hahahaha! Unajua waalimu wa hisabati wapo wangapi kwenye hii nchi? Unaelewa? Hisabati ni somo lenye heshima, ambalo watu wenye akili za juu ndio hulimudu sio watu kama wewe” Mwalimu akasema, muda huu hasira zilikuwa zimeikaribia kabisa sura yake.
“ Nisamehe mwalimu!” Nikasema. Mikono yangu nikiwa nimeiweka kifuani kama ishara ya kuomba radhi.
“ Leo nitakuchapa bakora mpaka akili ikukae sawa! Haya shika chini mjinga wewe!” Sikuwa na namna nikashika chini, viboko sita vikatua katika makalio yangu, vilikuwa viboko vichungu sana vilivyoyatia maumivu makalio yangu. Nilimuona Alice akilengwa lengwa na machozi, moyoni nilijihisi kuumia sana kuuona uso wa Alice katika hali ile.
Mwalimu alimaliza kufundisha, hatimaye akatoka;
Kila baada ya Lunch ilikuwa mara nyingi waalimu hawaingii darasani. Hivyo muda huo niliutumia kufanya mazoezi ya kuimba, nilikuwa nikienda uwanjani kufanya mazoezi ya sauti, nilizipa mazoezi ala za sauti kama vile ulimi, mdomo, koo na hata Glota. Nilipanua mdomo kuhakikisha sauti yangu inatoka vizuri. Nilifanya mazoezi ya pumzi bila kuchoka kuhakikisha sauti yangu haikati pindi nikiimba sauti ya juu sana.
Kuna wakati nilikuwa nakaa kwenye vivuli ya miti sehemu tulivu, ili kupata tungo nzuri. Nilikuwa nikitunga tungo nzuri za mashairi na kuyarekodi katika kidaftari maalumu. Kivuli na upepo mwanana hutuliza akili, Huibua ubunifu na shauku ya fikra ya kutunga vitu vipya katika sanaa.
“ Labda ni kweli sina akili za masomo ya darasani, ufaulu wangu ni duni. Njia pekee iliyobaki ni kutumia kipaji changu cha kuimba, hakika nitakilinda kipaji change, nitailinda sauti yangu, nitalinda ala za sauti. Lakini Ala za sauti nzuri bila fikra thabiti zenye ubunifu hazitanisaidia kitu, nitalinda fikra zangu kwa kulinda vivuli vya miti ya dunia….” Nikawaza mwenyewe lakini mara Alice akatokea jambo ambalo lilikatisha mawazo yangu.
“ Gibson! Nimekutafuta sana! Nimezunguka uwanjani nikakukosa, nikaenda kwenye yale madarasa mapya pia sikukuona, hapo nikajua sehemu yako ya mwisho ni huku kwenye huu mti wa Mzambarau” Alice akasema.
“ Umekuwa mahiri wa kujua mizunguko yangu eeh! Haya je usingenikuta kwenye huu mti wa mzambarau ungedhani nimeenda wapi?”
“ Bila shaka ningedhani umeshaondoka kwenda nyumbani” Akajibu. Tukacheka wote sana. Alice alipenda kutembea akiwa na juisi ya kopo pamoja na Ubuyu wa rangi nyekundu. Tukala pale ubuyu tukipiga stori. Mara kimya kikafuata, nikamuona Alice akiangalia mbele kwa mbali kidogo, alikuwa kama anawaza mbali la kuhuzunisha. Alinishtua na kunipa hofu.
“ Kuna nini Alice! Unawaza nini?” Nilimuuliza. Alice akanigeukia akanitazama.
“ Mtihani wa mwisho umekaribia sana, sidhani kama mpenzi wangu umejiandaa vya kutosha! Nina wasiwasi sana juu yako Gibson” Alice akasema.
Nikamtazama bila kusema kitu, sikujua nimwambie jambo gani, Alice alikuwa ananijali licha ya kuwa nilikuwa natoka familia masikini, nikiwa naufaulu mdogo mno.
“ Mimi nafikiri ungeyaweka mambo mengine pembeni kwanza ujikite kwenye kusoma, kisha baad ya kumaliza mitihani yetu ya mwisho ndio uurudie muziki. Unaonaje Gibson?” Alice akasema.
“ Niache muziki! Alice umechanganyikiwa? Hivi unajua muziki unamaana gani kwenye maisha yangu? Alice! Uliwahi kujiuliza muziki kwangu ni nini? Labda hujawahi kufikiria jambo hili. Acha nikujuze; Muziki kwangu ni maisha, muziki kwangu ndiye mkombozi, wakati madaktari wakitumia taalamu zao kutibu watu, mimi Gibson nitautumia muziki kutibu hisia za watu zilizopondeka, wakati waalimu kama mwalimu wa hesabati wakielimisha watu ingawaje wanatunyanyasa siye tusiye na uwezo darasani, mimi Gibson nitatumia muziki kuelimisha jamii na taifa langu. Alice bado hujaelewa muziki kwangu nini? Bila shaka umeelewa! Haya bado utaniambia niuache muziki?” Nilizungumza nikimtazama Alice kwa macho yaliyojawa na usongo.
“ Lakini Gibson, sijamaanisha uache muziki moja kwa moja, nimemaanisha upumzike kipindi hiki ili tujiandae kwa pamoja kwenye mitihani yetu hii ya mwisho, kisha utaendelea na muziki wako, Gibson unajua mimi ndiye shabiki wako namba moja..”
“ Alice! Naomba tuachane na hayo, tuzungumze mambo mengine!” Baada ya Alice kuniona nimebaki kuwa na msimamo wangu, akaniacha. Niliona jinsi alivyoumia nikaona nijifanye nimekubaliana naye kishingo upande.
**************
“ Kesho ndio nitapiga hatua yangu ya kwanza katika muziki, lazima niwaonyeshe watu kuwa nina kipaji kikubwa, ikiwa ni hatua ya kwanza itanipasa niipige kwa kishindo ambacho kitatikisa vikwazo vyote vilivyombele yangu. Ngoja niendelee mazoezi” nikawaza, alafu nikachukua moja ya kidaftari nilichoandika nyimbo zangu. Nikaanza kuperuzi katika kidaftari kile.
“ Huu! Hapana! Nitaingia na huu! Utafuata huu! Alafu nitamalizia na huu!” Punde nikakatishwa na Alice aliyekuwa ameiingia akiwa na mfuko. Akanikumbatia kwa nguvu, kisha akanibusu!
“ Vipi maandalizi yanaendeleaje?” Akaniuliza, akiwa anachukua stuli, akakaa na kuweka chini mfuko aliokuja nao.
“ Kama unavyoona, nataka kesho mji mzima utikisike, nitaishangaza dunia Alice” Nikasema nikimtazama Alice,
“ Sijui kwa nini hawajatupa nafasi tuimbe walau nyimbo nne!” Nikasema lakini Alice akanikatisha.
“ Gibson mpenzi! Kesho watumbuizaji watakuwa wengi mno, zitakuwepo shule tatu kubwa za kanda hii. Wameona muda utakuwa mdogo, hata hizo nyimbo tatu mlizoambiwa mnaweza msiziimbe, Hivyo unapaswa ujiandae kwa lolote.” Alice akasema.
“ Hata wakisema niimbe moja, kesho nitawafunika wote, kesho ni siku yangu ya furaha. Alice kesho jiandae kufurahia kusikia sauti ya mpenzi wako, kesho utajivunia mimi” Nikasema.
“ Hata sasa najivunia wewe Gibson, mimi siku zote nitajivunia wewe, ila usijiamini sana Mpenzi, kujiamini ni kuzuri lakini isipitilize” Alice akasema, akanyanyuka kisha akatoa nguo kwenye ule mfuko aliokuja nao,
“ Embu vaa hizi tuone!” Akanipa suruali ya jeansi nyeusi hivi na T-shirt nyeupe yenye picha yenye Skull and bones kwa mbele, alafu nyuma yalikuwepo maandishi “ GIBSON ft ALICE”. Nikavaa. Kisha akatoa miwani nyeusi akanipa nivae, nikavaa. Hapo nikamuona Alice akitabasamu kama aliyefurahishwa na muonekano wangu mpya, alafu akatoa Viatu dizaini ya Supra akanipa nikavaa, kisha akaniambia nivae na kofia. Nikamwambia anisubiri niende chumbani kwa mama nikajiangalie kwenye kioo kikubwa. Nikamuacha!
Nilikuwa nimependeza sana, nilifanana kwa ukaribu na wanamuziki wa kimataifa wanaotumbuiza kwenye majukwaa ya kimataifa, baada ya kuridhishwa na muonekano wangu, nikarudi chumbani kwangu,
“ Sasa itabidi uende saluni ukazitengeneze nywele zako vizuri” Alice akasema, akatoa elfu mbili akanikabidhi za kunyolea. Kisha akaniambia nijaribu kutumbuiza mbele yake.
Nikashika kalamu kama maiki na kuisogeza mdomoni. Nikaachia sauti nyepesi na laini nikiupiga wimbo wa mwisho nitakaouimba kesho. Alice akajikuta anatoa machozi, nilifanikiwa kuzigusa hisia zake kikamilifu.
“ Waaaoh! Umeimba vizuri sana. Natamani kesho uimbe kama ulivyoimba leo?” Alice akasema.
“ Usijali mpenzi!Kesho utajionea mwanaume uliyenaye niwa namna gani. Nimekuahidi kuwa siku ya kesho ndio siku utakayojivunia tangu unijue” Nikasema,
Kisha tukaachana, mimi nikienda kunyoa na kuziweka nywele sawa, wakati Alice akirudi kwao. Hiyo ilikuwa saa moja ya jioni hivi.
Itaendelea