Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
KABURI LA MWANAMUZIKI (EPISODE 02)
Mtunzi; Robert Heriel
whatsApp 0693322300
EPISODE 02
ILIPOISHIA
Nilikuwa nimeduwaa nikiwa namtazama akiwa anashuka kwenye ngazi polepole kwa madoido huku akitabasamu na kupiga hatua zake kwa tahadhari kwa mwendo wa catwalk, mara kwa mara alinyanyua mkono wake akizitoa nywele usoni kwa mbwembwe utadhani muigizaji mahiri wa filamu; akili haikunirejea mpaka aliponikaribia na kusimama mbele yangu kama malaika mwema na kujigeuza shaaa, nikasikia harufu ya manukato yake mazuri ajabu, kiukweli shemeji alikuwa mzuri wala sitaki kumsifia tena isijeonekana nilikuwa namtamani.
“OOH! My dear! Umevaa nini hii! Subiri nakuja” Shemeji akasema, kisha akapanda tena juu ghorofani. Hazikupita dakika nyingi akarudi akiwa na fuko lenye nguo ndani yake.
“Hizi nguo hazijavaliwa, Riadi aliletewa na Mwanamke mmoja wa kizungu ambaye kwa kweli ananiudhi sana, nahisi wanatoka naye” Shemeji akasema,
“Unamaana gani kusema hivyo?”
“Gibson, wewe sio mtoto mdogo, embu vaa tuondoke muda umekwenda” Akasema,.
*******
ENDELEA
Ndani ya Gari Shemeji alinifanyia vituko vya kila aina, mapaja yake aliyetumia ipasavyo kunifanyia emotional damage, alinitesa sana shemeji, tulifika maeneo ya mikocheni tukamuacha mtoto pale sehemu ya kuogelea tukimkabidhi kwa wahusika wa mahali pale, shemeji akaniambia; sisi twende kwa wakubwa, sio mbali kutoka hapa” na kweli haikuchukua dakika tano tulisimama eneo jingine palepale mikocheni tukaingiza gari ndani ya geti baada ya kuruhusiwa na walinzi, tuliifuata njia yenye vigae ambayo ilizungukwa na maua huku na huku, tukiwa chini ya vivuli vyenye upepo mwanana, eneo lilikuwa na kagiza kanakotokana na kivuli cha miti mingi na maua ya kuvutia yaliyokuwa eneo lile, tulipita katikati ya jengo lilokuwa mbele yetu tukatokea upande wa pili ambapo tulilakiwa na uwazi mkubwa wenye mwanga, kushoto likiwepo Bwawa kubwa la kisasa la kuogelea, tukapinda kulia kuifuata njia ambapo mbele kulikuwepo na eneo la maegesho ya magari. Baada ya kuegesha gari letu, tukashuka nikiwa nashangaa uzuri wa eneo lile, tulipotoka lile jengo kwa juu yalisomeka maandishi Turkey Resort LL. Kulikuwa pia na Mini-supermarket, mbele kabisa kwenye bwawa niliona vitanda vizuri vya kupumzika, nyuma ya vile vitanda vya kupumzikia kushoto kabisa zilikuwepo meza na viti vya dizaini ya kustaajabisha. Bado nilikuwa nikishangaa, niliona wanawake watatu, wawili wakiwa majini wakiogelea kwa raha zao, mmoja alikuwa kalala kwenye vile vitanda akiwa kava miwani nyeusi, na nguo za kuogelea ambazo kwa sehemu kubwa ziliacha sehemu za mwili wake wazi, akiwa kashikilia Glass yenye Cocktail ya rangi ya waridi.
Shemeji alinishika mkono kama vile mtu na mwenza wake, nilipotaka kupingana na jambo lake akanikazia macho, sikuwa na namna zaidi ya kumkubalia, tulioongozana mpaka kwenye ile supermarket, milango ya vioo yenye sensor ikafunguka yenyewe, tukaingia ndani, tukapokelewa na Kijana mmoja wa kituruki, tukapita moja kwa moja kwenye bidhaa, shemeji akanichagulia bukta nzuri ya kuogelea, kisha baada ya kunichagulia, tukarudi kwa yule kijana wa kituruki, tukalipia, tukatoka, akarudi kwenye gari, mimi akanielekeza niende kwenye chumba Fulani kilichokuwa karibu na maegesho ya magari ili nikabadili nguo, sikuweza kukataa,
Nilirejea nikiwa nipo kifua wazi na bukta mpya niliyonunuliwa na shemeji, ilikuwa bukta ya rangi nyeusi yenye mstari mweupe uliopita kama upinde kutoka upande wa kulia mpaka kushoto, ilikuwa imenishika vyema sana, basi nikasogea kwenye lile bwawa wale wadada wawili wakawa wananitazama kwa kujiiba iba, nikawasalimu, wakaniitikia lakini kwa kuchanganya Kiswahili na kingereza, hapo nikajua walikuwa wadada wakishua, kwani hata muonekano wao uliwatambulisha hivyo, walijaribu kunikarimu huku wakizikung’uta kila mara nywele zao zilizokuwa zimelowa maji. Sikupata muda wa kuzungumza nao sana, shemeji alikuja na kunikumbatia kwa nyuma, kisha akaniachia na kunishika mkono wa kulia, nikageuka bado nikiwa nimemshika na mkono wakulia, macho yangu yalaishutushwa, nilibaki nimetoa macho nikiukodolea mwili wa shemeji, alikuwa kavaa skirtini tamka ‘sketini’ iliyomkaa sawa, sketini ni kijivazi cha kuogelea wanachovaa wanawake ambacho huwafanya kuwa na mvuto wa kimapenzi, kwa juu huwa brazia ya kitambaa alafu chini huwa ni kisketi kifupi kilichoachia na kuyaacha mapaja mazito ya shemeji yakimeremeta. Sketini aliyokuwa amevaa ilikuwa ni rangi ya waridi na ile brazia ilikuwa ya rangi yenye mistari meusi na nyeupe. Alipendeza sana, akaninyanyua mkono wangu na kujizungusha na kufanya kile kiguo kupepea kidogo na kuzidi kuniharibu vibaya hisia zangu.
Tuliingia majini tukawa tunaogelea huku kila mara akinikumbatia, shemeji alichokuwa anakifanya ni kuwaonyesha wale wadada wengine kuwa mimi ni mtu wake, aliona jinsi walivyokuwa wakinitazama na kuna wakati nami nilikuwa najiiba kuwatazama, hii ilipelekea kunifokea kila alipokuwa akiniona, sasa tulikuwa tumeshaogelea vya kutosha, wale wadada walikuwa wamejilaza kama mamba kwenye vile vitanda wakiwa wamevaa kila mmoja miwani, tulitoka majini nikiwa nimechakazwa vibaya kihisia na Shemeji yangu, sitaki kukumbuka kwani ule ulikuwa mwanzo wa kujiingiza katika shimo refu lenye giza, ambalo lilibadilisha maisha yangu.
Tukaenda kupumzika kwenye vile vitanda tukipiga stori, kisha tulipokauka, tukaenda kwenye zile meza na viti na kuagiza chakula kwani tayari ilikuwa imetimia saa sita hivi, ile menu ilikuwa na vyakula vilivyoandikwa kwa lugha nisiyokuwa ninaielewa, kama sio picha zilizokuwemo basi nisingeelewa hata kitu kimoja katika menu ile, niliambulia kuona picha ya nyama ya ng’ombe, kuku pamoja na soseji, picha za matunda pamoja na juisi, bei zake zilinishtua sana, sikuweza kuamini kuwa kulikuwa na chakula cha elfu sabini, na juisi ya elfu thelesini na tano, nikakumbuka kauli ya Riadi kuwa pesa aliyoniachia haitanitosha, sasa nilianza kukubaliana na Riadi; kama matumizi yenyewe ndio yale basi ni kweli milioni moja kwa siku tano sio kitu. Mimi sikula vitu vingi isipokuwa nyama iliyochanganywa sijui na kitu ganai pamoja na juisi ambayo iligharimu kama laki moja na kumi, shemeji yeye alikunywa whisky Glenfiddich 15yrs ambayo iligharimu laki na ishirini yenye kiwango cha pombe asilimia arobaini. Aliagiza na nyama choma tuu zilizotengenezwa vizuri, tulimaliza kula na kuondoka wakati shemeji akiwa ameshaanza kulewa, wakati tunaingia ndani ya gari kwa bahati mbaya niliacha simu yangu kule kwenye vitanda, nikashuka kuifuata, sikuikuta pale kitandani nilipokuwa nimelala, kabla sijapawa nikasikia sauti kutoka nyuma yangu;
“Unaitafuta hii?” Nikageuka nikakutana na moja ya wale wadada waliokuwa wanaogelea bwawani akiwa amenielekezea simu huku akinitazama kwa macho ya upendo wenye Haya,
“Yes, Nashukuru sana” Nikajibu nikiipokea,
“ Usijali, naitwa Daniella” Yule mdada mrembo akasema akiwa ananitazama akiachia tabasamu jepesi la kuomba urafiki.
“ Gibson”
“ Embu nisaidie namba zako hapa” Daniella akasema akinipa simu yake niandike namba zangu, hapo nikageuka nyuma kuangalia kwenye gari kuona kama shemeji ananiona, lakini sikumuona, nikachukua ile simu nikawa naandika namba zangu;
“Unamuogopa mkeo? Akaniuliza, nikiwa naandika namba kwenye simu yake.
“sina mke mimi..” nikajibu nikimkabidhi simu yake.
“Gibson unafanya nini?” Nikamsikia Shemeji akigomba kwa nguvu akiwa kwenye gari.
“ Nakuja shem”
“ Kwa heri tutawasiliana Daniella” Nikasema kwa haraka haraka nikaondoka nikimuacha Daniella akinitazama huku akitabasamu kama mtu aliyefanikisha jambo kubwa.
Tulimpitia mtoto na safari ya kurudi nyumbani ikaanza, shemeji alikuwa amelewa kabisa, alikuwa akipiga piga makelele, huku akitaka niongeze sauti ya muziki kwenye gari, alikuwa akinengua huku akibinua makalio yake alafu kuna wakati anashindwa kujihimili anaangukia kwenye usukani, nilikuwa nikimuondoa kwani alikuwa anahatarisha usalama wetu,
“Embu zimaa! Zima muziki huo, huzikii wewe” akawa anaongea kiulevi. Nikazima, akawa ananilazimisha niimbe;
“Niimbie basi, wewe si mwanamuziki, ile nyimbo yako tamu sana, penzi lako pipi filimbi, nailamba aamu! Aamu!” Akawa anaimba huku akionyesha vile anailamba pipi filimbi huku akinishika kwenye mapaja yangu.
“ Embu acha ujinga wako bhana, huoni kuna mtoto hapa, unafanya nini sasa?” Nilimsukuma na kumchapa kibao kimoja cha adabu.
“Umenipiga sio, unajifanya kidume sio” akatulia akawa anacheua macho yakiwa legelege, mwishowe akapitiwa na usingizi.
Simu yangu ikawa inaita, sauti ambayo ilikuwa kero, ilikuwa namba ngeni kabisa, nikajua huenda atakuwa Daniella, “siwezi kupokea simu ya Daniella nikiwa na shemeji” nikawaza, ikaita mpaka ikakata, kitambo kidogo ikaita tena, sikupokea tena mpaka ikakata, bado tulikuwa njiani tukirudi nyumbani, ikaita tena, kwa kweli nilianza kukereka,
“Pokea simu hiyo” Shemeji aliropoka akiwa kalala, nikamtazama alikuwa amechoka kweli.
“ Mama yako ulimuambia akupigie leo” Shemeji akasema akigeuza uso wake kwangu bila ya kuyafumbua macho yangu, “huenda itakuwa ni mama kweli” nikawaza, kabla sijapokea simu ikakata, nikasubiri tena ili apige lakini nikaona kimya, nikaona niipigie ile namba huku nikiwa nimepunguza sauti ili shemeji asisikie upande wa pili, ile simu ikaita kisha ikapokelewa, hapo nilikuwa nimepunguza mwendo wa gari.
“Hello, ooh! Sorry, amefika mbali, tafadhali muite mama yangu, sawa” nikawa nazungumza na mtu wa kwenye simu, mama alikuwa keshaondoka lakini alikuwa hajafika mbali, mwenye duka alikuwa anamuona, dakika moja mama akapewa simu, nikaweka simu loud,
“ Shikamoo Mama!”
“Marhaba mwanangu, yaani tumeipigia simu yako mpaka tukachoka mwanangu”
“Samahani mama, nilikuwa mbali na simu” nikasema lakini shemeji akaropoka na sauti lake la ulevi “Mbali hiyo kwiyoo” nikawahi kumziba mdomo na mkono,
“Huyo ni nani mwanangu?”
“Enhee! Aah! Achana naye, hapo kuna simu gani mama?”
“ Mwanangu mimi hata najua aina za simu basi, acha nimpe mwenye duka atakuambia”
“Sawa mama” Nikajibu, nikiwa namuachia mdomo shemeji.
“Hello mkuu!” Mwenye duka akasema,
“ ndio kiongozi, hapo kuna simu gani nzuri” nikasema, akawa anataja aina ya simu na bei zake.
“ Anhaa! Hapo si una huduma za uwakala wa pesa? Basi naomba umpe Mama yangu simu nzuri ya smartphone ya laki tatu, alafu unitajie namba za uwakala nikutumie pesa yako” nikasema, shemeji akaropoka; “Mwanaume gani unamnunulia mama yako simu ya laki tatu” nikamziba mdomo tena, “embu tulia bhana, pombe zinakuendesha vibaya wewe” nikasema, nikamuona shemeji akifungua macho yake alafu akaniangalia. Akanitoa mikono yangu mdomoni;
“Hivi Gibson unafikiri mimi ni mlevi nisiyejitambua kama wewe, nimeanza kunywa hizi pombe tangu mdogo, alinifundisha Mama yangu, usidhani zinaweza kuniondolea akili” akanitazama huku akilegeza macho yake, alafu akaendelea,
“Shika simu yangu hii mtumie mama milioni moja hapo ya simu alafu umtumie pesa nyingine ya matumizi”
“Hapana shemeji, nashukuru kwa kutaka kunisaidia ila naomba unisamehe kwa kukataa msaada wako” Nikasema.
“Embu acha ushamba wewe, utakufa masikini shauri yako, hii ni bahati tuu, usione najigonga gonga kwako ukadhani siku zote nitakuwa hivi, embu lete hizo namba za wakala alizokutumia” akachukua simu yangu muda huo kuna meseji iliyokuwa imeingia, akatuma milioni mbili, yule jamaa akapiga simu,
“Boss! Wewe ndio umetuma pesa yote hii?” akaniuliza yule muuza duka kwenye simu.
“Ndio mkuu, shilingi ngapi imefika?” Nikauliza.
“Mkuu, hujui umetuma kiasi gani?”
“Mpe mama simu nzuri ya gharama alfu hiyo pesa itakayobaki mpatie” Shemeji akaropoka.
“ Kwani umetuma shilingi ngapi” Nikamuuliza shemeji.
“Milioni mbili tuu!” Akajibu, Nikapigwa na butwaa, lakini akanizuia nisiseme lolote.
“Kiongozi, mpatie simu isiyozidi milioni moja, alafu hiyo pesa nyingine mpatie”
“Haya nitampatia ya laki saba Mkuu” akajibu.
“ Sawa, mpe mama niongee naye” nikasema huku nikimtazama Shemeji,
“Ndio mama, atakupa hapo simu nzuri pamoja na milioni moja na laki tatu”
“Unasemaje Gibson?” Mama akauliza kwa kustaajabu.
“ Hiyo pesa utaanza kuikarabati nyumba pale ilipodondoka, usiwe na wasiwasi mama”
“Ubarikiwe mwanangu, kwani huko mjini unafanya shughuli gani mwanangu, hii pesa ni nyingi sana”
“Usijali mama, wewe tumia pesa za mwanao, tutawasiliana jioni” simu ikakatika.
‘ Ungemjibu shughuli uifanyayo mjini ni kumfurahisha shemeji yako, hahaha!” Shemeji akasema alafu akaachia kicheko cha kishambenga.
“Hivi kwa nini umetoa pesa yote hiyo?” Nikamuuliza.
“Mwanaume unaogopa kuhongwa na mwanamke, hahah! Unaogopa kuolewa?” shemeji akasema, wala sikumjibu nikawa naendesha gari.
“ Utachagua kuolewa na mwanaume mwenzako au kuolewa na mwanamke ambaye ni mimi, kwanza kuishi tuu kwenye nyumba ya mwanaume mwenzako huoni aibu, huko sio ndio kuolewa kwenyewe, sikiliza Gibson, wewe ni kijana mzuri nawe unastahili maisha mazuti kama aliyonayo Riadi, kuwa chini ya mwanaume mwenzako kama mke wake haipendezi, ni afadhali uwe chini yangu utapata chochote na ninaweza baadaye kukuzawadia mtoto”
“Embu tulia bhana! Mtoto yupo hapa ujue, hivi unamfundisha nini mtoto?” nikamkatisha.
“Mtoto ni wewe usiyeelewa mambo madogo, mwanangu mwenyewe anakushinda akili, si ati Junior?” akageuka siti za nyuma na kumtazama mtoto wake, Kupitia kioo cha gari kilichojuu ya mule ndani nikamuona Junior akitabasamu.
“Mimi sijaolewa na mtu, naomba tuheshimiane, kama huwezi kujiheshimu jaribu kuheshimu wengine” Nikasema,
“Hakuna cha bure Gibson, mtu yeyote mwenye akili anajua kila jambo lazima ulipie, iwe pesa au nguvu au ulipie kwa namna yoyote, hiyo ndio heshima, sijui unaposema unataka uheshimiwe unazungumzia jambo gani, ulitaka nikuambie uongo; mwanamke anaolewa sio kwa sababu ya kuwa yeye ni mwanamke isipokuwa kutokana na kutokuwa na mali, wakati mwingine kutokuwa na akili ya kutosha kumuongoza mwanaume, lakini kama mwanaume hana mali na akili pia naye ataolewa tuu. Lakini kwani lipi baya hapo, hutaki kuolewa na mwanamke mzuri kama mimi Gibson” Akasema, mwanzoni nilijua pombe zilikuwa zimemzidi lakini kumbe haikuwa hivyo, aliweza kuzitawala.
“ Mimi natafuta mali kwa jasho langu, sitaki pesa za kupewa pewa kama mtoto mdogo”
“ Hahah! Wacha weeh! Unafikiri hautazitolea jasho hizo pesa nilizompa mama yako? “ Hapo tukatazamana,
“Gibson! Unabahati sana, mimi sina huruma lakini sijui kwa nini umenigeuza kuwa kama kondoo, wewe ndio mtu wa pili baada ya Mume wangu, Riadi kumuonea huruma, nilitokea kukupenda tangu siku ya kwanza niliyokuona pale getini, ndio maana mpaka sasa hivi tupo pamoja” Akasema.
“Embu acha hizo habari, elewa wewe ni shemeji yangu, na itabaki hivyo siku zote, hakuna kitakachoendelea kati yangu na wewe, sawa” nikasema nikikatisha kwenye Geti la nyumba yetu lililokuwa linateleza polepole, tulikuwa tumefika nyumbani, tukashuka, lakini Shemeji hakuweza kushuka kutokana na pombe,
“ Shuka! Si ulisema pombe umekunywa tangu ukiwa mdogo, mbona hushuki sasa?”
“Nashuka” akashuka lakini akawa anapepesuka kidogo aanguke, nikamdaka, tukawa tunatazamana uso wangu ukiwa juu alafu wake ukiwa chini, akatabasamu, nilisikia mapigo yake ya moyo yakipiga, joto lake lilikuwa nyuzi joto za kulifanya yai la kuku lianguliwe, tukatazamana kwa kitambo mpaka niliposikia sauti ya mtoto;
“ Mama, Baba amekuja” Nilishtuka kusikia mtoto akisema hivyo, nikajinasua mikononi mwa Shemeji yangu, nikihaha kwa kuangalia huku na huku, lakini sikuweza kumuona Riadi, akili yangu ikaniambia tazama juu ya ghorofa, sikuamini niliyemuona, moyo wangu ni kama ulipigwa shoti ya umeme, nilimuona Riadi akiwa juu ghorofani amesimama akiwa ameshika kingo za ghorofa akiwa anatutazama mimi na shemeji, nilihisi kama mtu aliyefumaniwa.
ITAENDELEA
Shukrani Mkuu
Shukrani
Gibson ni mti unatoa maua Sana lakini naona hazai matunda [emoji1787][emoji1787][emoji1787] shukran Sana mkuu
[emoji1][emoji1][emoji1]
Haya maisha haya
Mkuu Leo umetusahau, Gibson mikononi mwa Riadi…Mambo ya Gibson yakianza kufunguka anakutana na Kisanga kinachomrudisha hatua mia moja nyuma
bado tuu
Mkuu shukran sana hapa naona Mambo yanogile
Unaua bendi nipo hapa hapa sioni kitu mkuuTulia hapo hapo
Kwakweli Mkuu unajua.
Unaua bendi nipo hapa hapa sioni kitu mkuu
Naomba unitag ukitaka kuendeleaChuma kipo hewani