Simulizi ya kusisimua: Kaburi la Mwanamuziki

Simulizi ya kusisimua: Kaburi la Mwanamuziki

Mkuu tutakuacha mwenyewe ujue,, maana naona huna huruma na mashabiki zako we unaona arosto zimekamata watu bado upo kimya kwanini?
 
Simulizi: Kaburi la Mwanamuziki
Mtunzi: Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

Sehemu ya 1


“Kazi yangu bila shaka kila mmoja wenu atakuwa ameifanya vizuri, nilifurahishwa na Richard, yeye aliimaliza tangu jana akaniletea Daftari lake, amefanya vizuri sana. Richard! Tafadhali njoo uchukue Daftari lako” Mwalimu wa Hesabu akasema. Richard akatoka, akaenda kuchukua Daftari lake wanafunzi wote tukimtazama, wengine wakimuonea donge, wengine wakimuona kama kiherehere huku wengine tukiwa hatujali lolote. Kisha mwalimu wa Hesabu akaendelea kusema;

“ Richard amekuwa akifanya vizuri tangu mkiwa kidato cha kwanza, sijui ninyi mnashindwaje na Richard, miaka ijayo Richard atakuja kuwa mtu muhimu sana ndani ya nchi hii. Sijui atakuwa Mchumi! Labda atakuwa Daktari bingwa! Huenda akawa Injinia mkubwa sana hapa nchini. Ati Richard unandoto ya kuwa nani hapo baadaye” Mwalimu wa Hesabu akasema, macho yake yakimtazama Richard huku akitabsamu. Richard naye kwa aibu akatabasamu huku akimtazama Mwalimu wa Hesabu, kisha akajibu;

“ Ningetamani niwe Daktari hilo lisingenishinda, masomao ya fizikia, kemia na Bilojia wote mnajua hayanishindi, labda ningesema niwe Injinia nako nisingeshindwa Mwalimu, Hesabu na Fizikia sijivunii lakini najitahidi kwa kiwango cha wanafunzi bora katika nchi hii. Hata ningesema niwe Mwanasheria, kote ninamudu, lakini yote hayo siyataki, nataka kile ambacho wengi hukitafuta, kile ambacho wengi wamekikosa ndicho ninataka kukisomea, nataka niwe mtaalamu wa mambo ya Fedha, nataka jambo lolote lihusulo Fedha lisinipite, ndoto yangu kubwa ni kuwa mtaalamu wa mambo ya fedha, ukiniita mchumi ni sawa, ukiniita mhasibu pia ni sawa, nataka nikiita fedha initii, nikiikagua inihofie, hiyo ndoto yangu kubwa Mwalimu” Richard alijibu, Darasa lote lilimsikiliza, majibu yake licha ya kuwa na matambo lakini yalionyesha kiburi cha ndani, majivuno ya akili alizojaliwa.

Mwalimu wa Hesabu alituamuru tumpongeze Richard kwa kupiga makofi, rafiki zake walipiga makofi kwa nguvu wakishangilia, wakati washindani wake wakipiga makofi ya kivivu, sisi Back benchers tulikuwa bora liende, tulikuwa tukisukuma tuu siku ziende, kwa kweli hatukuwahi kumuonea wivu yeyote kwa habari za masomo. Hata hivyo ilikuwa ni kero waalimu walipokuwa wakiingia kutufundisha, chanzo cha kero ilikuwa maneno ya baadhi ya waalimu kutudhalilisha sisi tuliokuwa hatufanyi vizuri kwenye masomo, walitukera kadiri ya uwezo wao, wenye mdomo walitumia maneno makali, wenye hasira walituchapa na kutupa adhabau kali. Mambo hayo yalinifanya nizidi kuichukia shule. Kama sio Mama yangu kunilazimisha kusoma basi ningekuwa nimeacha shule siku nyingi, huenda hata kidato cha nne nisingefika. Nilimuonea huruma mama, na hiyo huruma ndio iliyonifanya nivumilie kero za waalimu wa ile shule nikamaliza elimu ya upili.

” Natamani wote mngekuwa kama Richard au Alice, elimu ni ufunguo wa maisha, oneni wazazi wenu wanahangaika kwa umasikini kutokana na kuwa na elimu duni, ndio maana wamewaleta ninyi shuleni mpate elimu msipate shida kama wao wanavyopata lakini ninyi baadhi yenu hamuelewi lolote mkiambiwa, mnacheza na muda wenu, muda hauchezewi, mtoto mdogo unaharakia nini kwenye mapenzi, unaharakia nini mambo ya Starehe, juzi nilikutana na Kabali akitoka Bar akiwa kalewa. Kabali unajua ulinisikitisha sana” Mwalimu wa Hesabu alisema, macho yake yakimkabili Kabali aliyekaa nyuma kabisa.

Nisamehe mwalimu, Lakini mara mojamoja sio mbaya kushtua ubongo” Kabali akajibu.

Hahahahahahah!” Wote wanacheka kasoro Mwalimu aliyebaki anamtazama Kabali huku akitingisha kichwa kwa kumsikitikia.

Anyaway! Shauri yako. Kila mmoja aweke. Daftari la Mathematics juu ya dawati, alafu afungue mahali alipofanyia kazi niliyoitoa jana” Mwalimu wa hesabu akaagiza, jambo hilo likawa linafanyika, mimi ndio nilikuwa namalizia kuhamisha kazi ya Alice aliyoifanya kwenye Daftari langu, Mwalimu alikuwa anaanzia kusahisha madaftari ya wanafunzi waliokaa mbele, mara kwa mara nilimuona Alice akigeuka nyuma kunitazama, nami nilikuwa nikimpa ishara yakuwa namalizia. Alice akawa ananipa ishara nifanye hima, baada ya kujibu maswali matatu kati ya matano, nikaona isiwe kesi, nikamrudishia Alice Daftari yake kwa kulifaulisha kwa dawati lililofuata kwenda mbele mpaka lilipofika kwa Alice.

Sikuwa najua hesabu kusema ukweli, tangu naanza shule niliishi kwa kuibia ibia ilimradi nisiwe wa mwisho darasani, sasa yalibaki maswali mawili kati ya matano, nitayafanyaje, unajua hesabu za kidato cha nne sio za jumlisha wala kutoa, bora hata zingekuwa za Desimali ningejaribu lakini zilikuwa hesabu ngumu zenye alama nyingi, sikuwa naelewa chochote. Nikaandika andika namba za uongo uongo ilimradi kurasa za daftari langu lijae, nikajaza majibu na kuyapigia mstari kwa usafi wote labda nilifikiri mwalimu angenionea huruma hata kama nimekosea jibu basi angenipa vimaksi vya usafi katika kazi. Lakini kumbe jibu la uongo ni uongo tuu hata kama likirembwa na kupambwa.

Mwalimu akanifikia, akachukua Daftari langu, akasahihisha swali la kwanza mpaka la tatu, alipofika swali la nne, aka-stop, nikaanza kuhisi mwili ukilegea, nilihofia asijejua nimeibia kwa mtu. Akanipa alama ya kosa, swali la tano likamshtua,

Iweje upate swali la kwanza na lapili alafu ukose swali la tano? Ati wanafunzi hiyo inawezakana?” Akauliza!

Haiwezekani!” Wakajibu wanafunzi wote mpaka yule jirani yangu niliyekaa naye wakati naye hana anachojua kwenye hisabati.

Wewe utakuwa umeibia tuu! Ndio maana nikashangaa tangu lini Gibson umekuwa na akili za kukokotoa milinganyo kama hii. Embu ona!” Mwalimu akawa anaanza kupekua daftari langu katika kurasa zingine zisizohusiana na kazi ya leo. Kiukweli nilikereka, nilihisi naenda kuumbuka.

“ Heeh! Hii nini! Gibson! Hiki ni kitu gani kwenye daftari langu la Hisabati?” Sauti ya mwalimu ikafanya darasa zima kugeuka na kutazama kilichokuwa kinaendelea, mwalimu akapita mbele akiwa kabeba daftari langu, kisha alipofika mbele kabisa ya darasa ulipo ubao, akaniita nami niende mbele. Nilipofika akaniambia nipige magoti chini. Kwa aibu uso wangu nikiukwepesha na nyuso za wanafunzi wenzangu nikawa naangalia chini nikiwa nimepiga magoti,

“ Kwa hiyo ukaona Daftari langu ndilo la kuandikia huu upuuzi wako, Gibson! Mara ngapi umekanywa na mama yako kujihusisha na Muziki? Mara ngapi! Muziki ni uhuni, hufanywa na watu wajinga, wapuuzi na wasio na haya, au unataka kukata kata mauno kama hivi! Eeh! Hivi na hivi! Ndio unataka?” Darasa zima linacheka baada ya mwalimu kukata mauno.

Lakini mwalimu hata muziki nao ni kazi tuu kama zilivyokazi zingine, napenda sana kuimba Mwalimu!”

“ KELELE!”

“ Unaongea utopolo gani hapa! Muziki! Muziki! Muziki! Upuuzi mtupu! Haya kwa hiyo kupenda kwako muziki ndio ukaona utumie daftari la hisabati kuandika mautopolo yako ya muziki! Hukuona masomo mengine mpaka uandikie kwenye daftari la hisabati? Unadharau HISABATI! Hahahaha! Unajua waalimu wa hisabati wapo wangapi kwenye hii nchi? Unaelewa? Hisabati ni somo lenye heshima, ambalo watu wenye akili za juu ndio hulimudu sio watu kama wewe”
Mwalimu akasema, muda huu hasira zilikuwa zimeikaribia kabisa sura yake.

Nisamehe mwalimu!” Nikasema. Mikono yangu nikiwa nimeiweka kifuani kama ishara ya kuomba radhi.

Leo nitakuchapa bakora mpaka akili ikukae sawa! Haya shika chini mjinga wewe!” Sikuwa na namna nikashika chini, viboko sita vikatua katika makalio yangu, vilikuwa viboko vichungu sana vilivyoyatia maumivu makalio yangu. Nilimuona Alice akilengwa lengwa na machozi, moyoni nilijihisi kuumia sana kuuona uso wa Alice katika hali ile.

Mwalimu alimaliza kufundisha, hatimaye akatoka;

Kila baada ya Lunch ilikuwa mara nyingi waalimu hawaingii darasani. Hivyo muda huo niliutumia kufanya mazoezi ya kuimba, nilikuwa nikienda uwanjani kufanya mazoezi ya sauti, nilizipa mazoezi ala za sauti kama vile ulimi, mdomo, koo na hata Glota. Nilipanua mdomo kuhakikisha sauti yangu inatoka vizuri. Nilifanya mazoezi ya pumzi bila kuchoka kuhakikisha sauti yangu haikati pindi nikiimba sauti ya juu sana.

Kuna wakati nilikuwa nakaa kwenye vivuli ya miti sehemu tulivu, ili kupata tungo nzuri. Nilikuwa nikitunga tungo nzuri za mashairi na kuyarekodi katika kidaftari maalumu. Kivuli na upepo mwanana hutuliza akili, Huibua ubunifu na shauku ya fikra ya kutunga vitu vipya katika sanaa.

“ Labda ni kweli sina akili za masomo ya darasani, ufaulu wangu ni duni. Njia pekee iliyobaki ni kutumia kipaji changu cha kuimba, hakika nitakilinda kipaji change, nitailinda sauti yangu, nitalinda ala za sauti. Lakini Ala za sauti nzuri bila fikra thabiti zenye ubunifu hazitanisaidia kitu, nitalinda fikra zangu kwa kulinda vivuli vya miti ya dunia….” Nikawaza mwenyewe lakini mara Alice akatokea jambo ambalo lilikatisha mawazo yangu.

“ Gibson! Nimekutafuta sana! Nimezunguka uwanjani nikakukosa, nikaenda kwenye yale madarasa mapya pia sikukuona, hapo nikajua sehemu yako ya mwisho ni huku kwenye huu mti wa Mzambarau” Alice akasema.

“ Umekuwa mahiri wa kujua mizunguko yangu eeh! Haya je usingenikuta kwenye huu mti wa mzambarau ungedhani nimeenda wapi?”

“ Bila shaka ningedhani umeshaondoka kwenda nyumbani” Akajibu. Tukacheka wote sana. Alice alipenda kutembea akiwa na juisi ya kopo pamoja na Ubuyu wa rangi nyekundu. Tukala pale ubuyu tukipiga stori. Mara kimya kikafuata, nikamuona Alice akiangalia mbele kwa mbali kidogo, alikuwa kama anawaza mbali la kuhuzunisha. Alinishtua na kunipa hofu.

“ Kuna nini Alice! Unawaza nini?” Nilimuuliza. Alice akanigeukia akanitazama.

“ Mtihani wa mwisho umekaribia sana, sidhani kama mpenzi wangu umejiandaa vya kutosha! Nina wasiwasi sana juu yako Gibson” Alice akasema.

Nikamtazama bila kusema kitu, sikujua nimwambie jambo gani, Alice alikuwa ananijali licha ya kuwa nilikuwa natoka familia masikini, nikiwa naufaulu mdogo mno.

Mimi nafikiri ungeyaweka mambo mengine pembeni kwanza ujikite kwenye kusoma, kisha baad ya kumaliza mitihani yetu ya mwisho ndio uurudie muziki. Unaonaje Gibson?” Alice akasema.

Niache muziki! Alice umechanganyikiwa? Hivi unajua muziki unamaana gani kwenye maisha yangu? Alice! Uliwahi kujiuliza muziki kwangu ni nini? Labda hujawahi kufikiria jambo hili. Acha nikujuze; Muziki kwangu ni maisha, muziki kwangu ndiye mkombozi, wakati madaktari wakitumia taalamu zao kutibu watu, mimi Gibson nitautumia muziki kutibu hisia za watu zilizopondeka, wakati waalimu kama mwalimu wa hesabati wakielimisha watu ingawaje wanatunyanyasa siye tusiye na uwezo darasani, mimi Gibson nitatumia muziki kuelimisha jamii na taifa langu. Alice bado hujaelewa muziki kwangu nini? Bila shaka umeelewa! Haya bado utaniambia niuache muziki?” Nilizungumza nikimtazama Alice kwa macho yaliyojawa na usongo.

“ Lakini Gibson, sijamaanisha uache muziki moja kwa moja, nimemaanisha upumzike kipindi hiki ili tujiandae kwa pamoja kwenye mitihani yetu hii ya mwisho, kisha utaendelea na muziki wako, Gibson unajua mimi ndiye shabiki wako namba moja..”

“ Alice! Naomba tuachane na hayo, tuzungumze mambo mengine!” Baada ya Alice kuniona nimebaki kuwa na msimamo wangu, akaniacha. Niliona jinsi alivyoumia nikaona nijifanye nimekubaliana naye kishingo upande.

**************

“ Kesho ndio nitapiga hatua yangu ya kwanza katika muziki, lazima niwaonyeshe watu kuwa nina kipaji kikubwa, ikiwa ni hatua ya kwanza itanipasa niipige kwa kishindo ambacho kitatikisa vikwazo vyote vilivyombele yangu. Ngoja niendelee mazoezi” nikawaza, alafu nikachukua moja ya kidaftari nilichoandika nyimbo zangu. Nikaanza kuperuzi katika kidaftari kile.

“ Huu! Hapana! Nitaingia na huu! Utafuata huu! Alafu nitamalizia na huu!” Punde nikakatishwa na Alice aliyekuwa ameiingia akiwa na mfuko. Akanikumbatia kwa nguvu, kisha akanibusu!

“ Vipi maandalizi yanaendeleaje?” Akaniuliza, akiwa anachukua stuli, akakaa na kuweka chini mfuko aliokuja nao.

“ Kama unavyoona, nataka kesho mji mzima utikisike, nitaishangaza dunia Alice” Nikasema nikimtazama Alice,

“ Sijui kwa nini hawajatupa nafasi tuimbe walau nyimbo nne!” Nikasema lakini Alice akanikatisha.

“ Gibson mpenzi! Kesho watumbuizaji watakuwa wengi mno, zitakuwepo shule tatu kubwa za kanda hii. Wameona muda utakuwa mdogo, hata hizo nyimbo tatu mlizoambiwa mnaweza msiziimbe, Hivyo unapaswa ujiandae kwa lolote.” Alice akasema.

“ Hata wakisema niimbe moja, kesho nitawafunika wote, kesho ni siku yangu ya furaha. Alice kesho jiandae kufurahia kusikia sauti ya mpenzi wako, kesho utajivunia mimi” Nikasema.

“ Hata sasa najivunia wewe Gibson, mimi siku zote nitajivunia wewe, ila usijiamini sana Mpenzi, kujiamini ni kuzuri lakini isipitilize” Alice akasema, akanyanyuka kisha akatoa nguo kwenye ule mfuko aliokuja nao,

“ Embu vaa hizi tuone!” Akanipa suruali ya jeansi nyeusi hivi na T-shirt nyeupe yenye picha yenye Skull and bones kwa mbele, alafu nyuma yalikuwepo maandishi “ GIBSON ft ALICE”. Nikavaa. Kisha akatoa miwani nyeusi akanipa nivae, nikavaa. Hapo nikamuona Alice akitabasamu kama aliyefurahishwa na muonekano wangu mpya, alafu akatoa Viatu dizaini ya Supra akanipa nikavaa, kisha akaniambia nivae na kofia. Nikamwambia anisubiri niende chumbani kwa mama nikajiangalie kwenye kioo kikubwa. Nikamuacha!

Nilikuwa nimependeza sana, nilifanana kwa ukaribu na wanamuziki wa kimataifa wanaotumbuiza kwenye majukwaa ya kimataifa, baada ya kuridhishwa na muonekano wangu, nikarudi chumbani kwangu,

“ Sasa itabidi uende saluni ukazitengeneze nywele zako vizuri” Alice akasema, akatoa elfu mbili akanikabidhi za kunyolea. Kisha akaniambia nijaribu kutumbuiza mbele yake.

Nikashika kalamu kama maiki na kuisogeza mdomoni. Nikaachia sauti nyepesi na laini nikiupiga wimbo wa mwisho nitakaouimba kesho. Alice akajikuta anatoa machozi, nilifanikiwa kuzigusa hisia zake kikamilifu.

“ Waaaoh! Umeimba vizuri sana. Natamani kesho uimbe kama ulivyoimba leo?” Alice akasema.

“ Usijali mpenzi!Kesho utajionea mwanaume uliyenaye niwa namna gani. Nimekuahidi kuwa siku ya kesho ndio siku utakayojivunia tangu unijue” Nikasema,

Kisha tukaachana, mimi nikienda kunyoa na kuziweka nywele sawa, wakati Alice akirudi kwao. Hiyo ilikuwa saa moja ya jioni hivi.

Itaendelea
Ukipost naomba unitag[emoji3578]
 
KABURI LA MWANAMUZIKI (EPISODE 09)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

EPISODE 09

ILIPOISHIA

“ Baba yupo wapi ndugu yangu?” swali likaniponyoka.

Yule kijana akawa ananitazama kisha akamtazama hakimu,

“ Huyu ni nani, Gibson?” Hakimu akaniuliza.

“ Huyu ni mtoto wa Shahidi, alikuwa na Shahidi jana nilipoenda kule Hospitali kumuona, shahidi” Nikajibu. Hakimu akamtazama Yule kijana, kisha akasema;

“ Baba yako yupo wapi?’

“ Baba yangu! hayupo Amekufa usiku wa kuamkia leo” Yule kijana akasema, kwa kweli maneno yake yalinifanya nichanganyikiwe,

“ Nimekwisha! Nimekwisha mimi!” Nikawa napiga kelele pale mahakamani.

ENDELEA
Nilikata tamaa, tumaini langu la kuwa huru likapotea, niliyekuwa namtegemea kutoa ushahidi ili niwe huru ndiyo huyo ameshakufa. Tumaini linapokufa moyo hupoteza njia katika mapigo yake, hugeuka gari lililopoteza muelekeo na muda wowote litapinduka.

“ Basi ikiwa shahidi wako hayupo wa kuthibitisha maelezo yako, mahakama haiwezi kupokea maelezo yako na kuyachukulia kama maelezo ya ukweli, mahakama itatoa uamuzi kulingana na ushahidi uliotolewa kwa pande zote mbili, mlalamikaji na mlalamikiwa…” Hakimu anakohoa kidogo kisha akaendelea;

“ Labda kuna lolote Gibson unaweza kujitetea kwa makosa uliyofanya?”

“ Mhe. Hakimu, samahani kwa kuingilia mazungumzo yako” Yule kijana wa Mr. Kibadeni akasema. Hakimu akamtazama kwa macho ya udadisi, kisha akamruhusu aseme alichokuwa anataka kusema, hata mimi nilijawa na shauku ya kutaka kujua Kijana yule alikuwa anataka kusema nini, nilitamani aseme alikuwa akitania kuhusu kifo cha Baba yake, lakini mawazo yangu yalikuwa kama ndoto za Abunuasi.

“ Ndugu Mhe. Hakimu, siku ya jana; kijana huyu alikuja katika hospitali aliyolazwa Baba yangu, akanikuta nikiwa na Baba yangu wodini, Baba yangu akamtambulisha kwangu kama Gibson, jana ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona. Baba alinambia kuwa kijana huyu ndiye aliyemuokoa asiuawe na mtu mmoja aliyekuja hospitalini kumuua, na ndio sababu ya mzee wangu kubadilishwa wodi na kuongezewa ulinzi mkali”Yule kijana akameza mate lakini kabla hajaendelea Hakimu akauliza akiwa ameshika kalamu;

“ Wewe unaitwa nani?”

“ Oh! Sorry kumbe hata sikujitambulisha, naitwa Riadi Kibadeni, Mhe Hakimu”

“ Sawa Endelea Mr. Riadi”

“ Nashukuru sana Mhe. Hakimu, Baba yangu alinisimulia tukio zima jinsi lilivyokuwa siku aliponusurika kuuawa, kufupisha stori Baba yangu jana usiku aliniambia nimrekodi video, masikini Baba alijua atakufa” Riadi akaanza kulia.

“ Jikaze Mr. Riadi, tunajua inaumiza kumpoteza Baba, lakini itabidi ujikaze kama mwanaume utoe maelezo uliyonayo” Hakimu akasema.

“ Nilimrekodi kwa simu yangu hii, naomba niikabidhi mahakamani hapa huenda ikawa msaada kwa kijana aliyemsaidia Baba yangu asiuawe” Riadi anaondoka kizimbani anaenda kukabidhi simu. Hakimu akaipokea simu ya Riadi, kisha akamuamuru Riadi akakae, baada ya Riadi kukaa mimi bado nikiwa chini ya ulinzi mkali, nikamuona hakimu akimpa ishara mmoja wa wahudumu wa ile mahakama, yule mhudumu wa mahakama aliyevalia joho jeusi na skafu nyeupe hivi shingoni akanong’onezwa jambo Fulani, kisha akaondoka pale, bado pale ukumbini kulikuwa kimya sana, watu walitulia kuona nini kinaenda kutokea, kwa upande wangu kwa kweli nilijawa na hofu, nilikuwa na wasiwasi wa kupewa hukumu ya kifungo, katika maisha yangu sikuwahi kufikiria kama siku moja ningefungwa jela, kwenye maisha yangu niliogopa sana maeneno mawili, hospitalini hasa ICU na Jela. Nilikuwa nikiomba kimoyomoyo Ile video iliyoletwa na Riadi iweze kumshawishi Hakimu na kuniachia huru.

Punde yule mhudumu wa mahakama akarudi akiwa amebeba laptop, kisha akaenda kwa hakimu na kuiunganisha ile simu kwa waya wa USB, akabonyeza bonyeza kwenye laptop, bila shaka alikuwa akihamisha ile video kwenye Laptop, nikamuona akiunganisha laptop na waya Fulani hivi nisiojua kazi yake, alafu akasimama akalichangua lile joho mpaka alipopata nafasi ya kupitisha mkono wake kwenye mfuko wa suruali, akatoa kifaa Fulani kama rimoti, akabonyeza kuelekea juu, jambo ambalo lilifanya karibia watu wote wainue vichwa vyao juu, hapo nikaona Projector ikiwaka kitaa chekundu. Baadaye wote tukashuhudia picha ukutani upande wa kulia.

Hapo macho ya watu wote yakavutwa kuona video ya shahidi, Marehemu Kibadeni. Haikuchukua muda Hakimu akasema;

“ Tutaenda kuona na kusikiliza ushahidi wa Mr. Kibadeni ambaye ameshindwa kuhudhuria kuja kutoa ushahidi wake kwa sababu ya kukutwa na umauti, mahakama itaangalia kisha itaamua kama ushahidi huu uzingatiwe au upuuzwe, ila kwa vile mahakama ipo kwaajili ya kutoa haki, ndio maana tumeipokea ushahidi huu kama sehemu ya kumtendea haki ndugu Gibson. Tunaweza kuanza kuona”

Sijui ni kwanini mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda mbio kiasi kile, nilihisi woga sana. Punde sinema ilimuonyesha Mr. Kibadeni akiwa kwenye kitanda kilekile cha hospitalini nilipomkuta jana, akiwa kavaa kichwani kofia nyepesi ya rangi ya kijani yenye matundu madogomadogo kama chujio, akiwa katundikiwa dripu, upande wa kitanda alichokuwa amekilalia ulikuwepo mtambo mmoja wenye kioo kinachoonyesha Grafu zenye mawimbi zilizokuwa zinapanda na kushuka huku pembeni kabisa kukiwa na tarakimu za namba zenye asilimia, Mr. Kibadeni alikuwa amefunikwa shuka jeupe lenye nembo ya ile hospitali; kuanzia miguuni mpaka kiunoni karibu na kitovu, juu alikuwa amevalia shati la kijani linalofanana rangi na ile kofia aliyokuwa ameivaa. Mr. Kibadeni akajiweka sawa akijilazimisha kukaa lakini akashindwa, akatokea nyuma ya kamera Mtoto wake akaenda kumnyanyua na kumsaidia kukaa kisha akamuacha na kurudi nyuma ya kamera akimuacha Mr. Kibadeni pekeake, nikajikuta nikijiuliza nani alimuachia kamera achukue tukio lile, lakini wazo hilo lilikatishwa baada ya Mr. Kibadeni kuanza kuongea;

“ Naitwa Mr. Kibadeni, sina haja ya kujitambulisha sana ila najua Hakimu utakuwa unanifahamu” Hapo nikamtazama hakimu kwa haraka, nikamuona akiwa na uso wa kukubaliana na maneno ya Mr. Kibadeni. Hali ikanifanya nishangae.

“ Nimelazwa kwa miezi mingi sana, familia na serikali vimehangaika kuyapigania maisha yangu, kwa kweli sina chakuwalipa isipokuwa shukrani zangu, katika watu walioyapigania maisha yangu ni pamoja na huyo kijana aitwaye Gibson, hakuwa akinijua; wala mimi sikuwa namfahamu, na nadhani mpaka sasa sidhani kama ananijua, hiyo ni kawaida kwa mtu wa kawaida na kijana kama yeye kufahamu watu wa aina zetu,” Mr. Kibadeni akakohoa kidogo kisha akaendelea;

“ Usiku ule sitakuja kuusahau katika maisha yangu, nikiwa nimelala nilishtuka baada ya kuamshwa na mwanaume mmoja mrefu aliyevalia koti jeupe la kidaktari, usoni akiwa kavaa barakoa iliyoficha uso wake, mikono yake alikuwa amevaa Gloves za kitambaa yenye rangi nyeusi, mkono mmoja akiwa kashika bastola, nilijua na kuamini mtu yule alikuja kwa ajili ya kuniua hata kama asingeniambia; jinsi alivyoonekana alifanana kabisa na mtoa roho. Akanitisha, kisha akachukua kichupa cha sumu kutoka kwenye mfuko wake, akatoa na sindano akaichoma ile sumu aliyoivuta kwenye sindano na kuiingiza kwenye Dripu nililokuwa nimetundikiwa” anapumua kidogo kisha anaendelea.

“ sumu ilikuwa imeshachanganyika na maji ya Dripu, sikuwa na uwezo wa kuliondoa dripu kwani nilikuwa nimezidiwa sana, sikuweza hata kujigeuza wala kunyanyua mkono, yule Mwanaume shetani baada ya kufanya ushetani wake akaondoka, hapo nikawa nakisubiri kifo changu maana muda mfupi ujao ile sumu ingekuwa imeshaanza kuingia polepole mwilini mwangu. Lakini kwa bahati kumbe yule kijana niliyekuwa nimelazwa naye wodi moja alikuwa macho, nikashangaa ameamka upesiupesi kisha akaja kunitoa lile dripu, nilikuwa siwezi hata kuongea…” Mr. Kibadeni akaanza kukohoa mfululizo, alikohoa mpaka pale mahakamani kila mmoja wetu akawa anakunja uso kwa kuhisi maumivu anayoyapata, alikohoa zaidi na zaidi mpaka akalegea kama mlenda, nikawa naomba kimoyomoyo lolote baya lisimtokee kabla hajamaliza kueleza kila kitu, lakini nilihisi kukata tamaa nilipoona akikohoa mpaka udenda unamtoka, kwa upesi tukamuona Riadi akitokea nyuma ya kamera akiwa na chupa ya maji, akaenda akamshika Baba yake na kumpiga piga mgongoni, kisha akampa ile chupa ya maji, yule mzee akanywa, lakini alikuwa amechoka wala sio utani.

Akamuegemeza kwenye kitanda, Mr. Kibadeni alikuwa kayafumba macho yake kama siku ya kwanza niliyomkuta kule wodini, kisha akayafumbua, nilikuwa nikisali sana, niliogopa, kila muda niliyafukuza mawazo mabaya yaliyokuwa yakinijia kichwani kumhusu Mr. Kibadeni.

Mr. Kibadeni akajitahidi kusema kitu lakini akaishia kukohoa maradufu zaidi mpaka macho yakawa yanamtoka, hapo nikajua basi, ule mtambo kitandani ukaanza kulia huku kukitokea mstari mwekundu na zile tarakimu za namba zikishuka kwa kasi kutoka 205 na mpaka muda ule zikawa zinasoma 162, hisia zilizotawala pale kwenye ukumbi wa mahakama zilikuwa za msisimko. Yule muuguzi aliyenishtaki nilimuona akiwa amejawa na shauku ya kuujua ukweli. Nikamuona Mr. Kibadeni akamvuta Mwanaye, Riadi mpaka kwenye uso wake na kulisogelea sikio lake, hatukusikia alisemaje, lakini tukamuona Riadi akimpekua Baba yake kwenye mifuko ya suruali yake, tukamuona Riadi akitoa kitu kama Kadilida au memorikadi ile kubwa kutoka mfukoni mwa baba yake, alafu ghafla tukasikia mlango ukifunguliwa na punde wakajitokeza madaktari wawili waliovalia makoti ya kidaktari wakiwa na stethoscope shingoni, wakampima Mr. Kibadeni na hapohapo video ikafikia tamati.

“ Ndio Mr. Riadi, huo ndio ushahidi wa Baba yako? Mbona haujakamilika, kile ulichokitoa kwenye mfuko wa suruali yake ni kitu gani?” Hakimu akauliza akiwa anamtazama Riadi.

“ Mhe. Hakimu kama ulivyoona Baba yangu alizidiwa akiwa anatoa ushahidi wake, kwa bahati mbaya kabla hajamaliza kutoa maelezo yake akazidiwa” Riadi akasema, Hakimu akawa anaandika.

“Sasa itakuwaje kama ushahidi ndio umeishia hapa, haujakamilika?” Nikawaza.

“ Lakini kuna hii device Baba aliniambia niitoe mfukoni mwake, alinambia hii ndio ushahidi wa moja kwa moja, japo sijapata nafasi ya kuiangalia” Riadi akasema akiitoa ile device inayofanana na Memorikadi kubwa. Hakimu akaipokea kisha akamuita yule mhudumu wa Mahakama, akaichomeka ile device kwenye laptop, ghafla video ikajionyesha ingawaje ilikuwa inatingishika tingishika lakini tuliweza kuona kilichokuwa kinaendelea, video ilimuonyesha yule mwanaume mrefu alivyokuwa akimuamsha Mr. Kibadeni na matukio yote aliyoyafanya, ilinionyesha na mimi nilivyoenda kumsaidia Mr. Kibadeni, nikatoka kwenda kumuita Muuguzi kisha nikarejea nikiwa na Muuguzi, ikanionyesha ugomvi wangu na Muuguzi mpaka nilipolikanyaga lile Dripu na kulipasua. Mahakama nzima ilishangazwa na ushahidi ule, muuguzi alibaki ameduwaa asiamini kilichokuwa kimetokea. Nilishukuru sana, nilijikuta nikilia kwa uchungu mwingi, sikuamini kama wokovu ungepatikana dakika za mwisho kabisa.

Baadaye hakimu alitoa hukumu ya kuniacha huru baada ya kunikuta sina hatia.

MWISHO WA SEASON 01.

Kesho tunaendelea na season 02
Nisameheni kwa kuwaweka sana, kuna mambo yaliingiliana wakuu.
Ratiba ni kila siku saa saba mchana
 
KABURI LA MWANAMUZIKI (EPISODE 09)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300

EPISODE 09

ILIPOISHIA

“ Baba yupo wapi ndugu yangu?” swali likaniponyoka.

Yule kijana akawa ananitazama kisha akamtazama hakimu,

“ Huyu ni nani, Gibson?” Hakimu akaniuliza.

“ Huyu ni mtoto wa Shahidi, alikuwa na Shahidi jana nilipoenda kule Hospitali kumuona, shahidi” Nikajibu. Hakimu akamtazama Yule kijana, kisha akasema;

“ Baba yako yupo wapi?’

“ Baba yangu! hayupo Amekufa usiku wa kuamkia leo” Yule kijana akasema, kwa kweli maneno yake yalinifanya nichanganyikiwe,

“ Nimekwisha! Nimekwisha mimi!” Nikawa napiga kelele pale mahakamani.

ENDELEA
Nilikata tamaa, tumaini langu la kuwa huru likapotea, niliyekuwa namtegemea kutoa ushahidi ili niwe huru ndiyo huyo ameshakufa. Tumaini linapokufa moyo hupoteza njia katika mapigo yake, hugeuka gari lililopoteza muelekeo na muda wowote litapinduka.

“ Basi ikiwa shahidi wako hayupo wa kuthibitisha maelezo yako, mahakama haiwezi kupokea maelezo yako na kuyachukulia kama maelezo ya ukweli, mahakama itatoa uamuzi kulingana na ushahidi uliotolewa kwa pande zote mbili, mlalamikaji na mlalamikiwa…” Hakimu anakohoa kidogo kisha akaendelea;

“ Labda kuna lolote Gibson unaweza kujitetea kwa makosa uliyofanya?”

“ Mhe. Hakimu, samahani kwa kuingilia mazungumzo yako” Yule kijana wa Mr. Kibadeni akasema. Hakimu akamtazama kwa macho ya udadisi, kisha akamruhusu aseme alichokuwa anataka kusema, hata mimi nilijawa na shauku ya kutaka kujua Kijana yule alikuwa anataka kusema nini, nilitamani aseme alikuwa akitania kuhusu kifo cha Baba yake, lakini mawazo yangu yalikuwa kama ndoto za Abunuasi.

“ Ndugu Mhe. Hakimu, siku ya jana; kijana huyu alikuja katika hospitali aliyolazwa Baba yangu, akanikuta nikiwa na Baba yangu wodini, Baba yangu akamtambulisha kwangu kama Gibson, jana ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona. Baba alinambia kuwa kijana huyu ndiye aliyemuokoa asiuawe na mtu mmoja aliyekuja hospitalini kumuua, na ndio sababu ya mzee wangu kubadilishwa wodi na kuongezewa ulinzi mkali”Yule kijana akameza mate lakini kabla hajaendelea Hakimu akauliza akiwa ameshika kalamu;

“ Wewe unaitwa nani?”

“ Oh! Sorry kumbe hata sikujitambulisha, naitwa Riadi Kibadeni, Mhe Hakimu”

“ Sawa Endelea Mr. Riadi”

“ Nashukuru sana Mhe. Hakimu, Baba yangu alinisimulia tukio zima jinsi lilivyokuwa siku aliponusurika kuuawa, kufupisha stori Baba yangu jana usiku aliniambia nimrekodi video, masikini Baba alijua atakufa” Riadi akaanza kulia.

“ Jikaze Mr. Riadi, tunajua inaumiza kumpoteza Baba, lakini itabidi ujikaze kama mwanaume utoe maelezo uliyonayo” Hakimu akasema.

“ Nilimrekodi kwa simu yangu hii, naomba niikabidhi mahakamani hapa huenda ikawa msaada kwa kijana aliyemsaidia Baba yangu asiuawe” Riadi anaondoka kizimbani anaenda kukabidhi simu. Hakimu akaipokea simu ya Riadi, kisha akamuamuru Riadi akakae, baada ya Riadi kukaa mimi bado nikiwa chini ya ulinzi mkali, nikamuona hakimu akimpa ishara mmoja wa wahudumu wa ile mahakama, yule mhudumu wa mahakama aliyevalia joho jeusi na skafu nyeupe hivi shingoni akanong’onezwa jambo Fulani, kisha akaondoka pale, bado pale ukumbini kulikuwa kimya sana, watu walitulia kuona nini kinaenda kutokea, kwa upande wangu kwa kweli nilijawa na hofu, nilikuwa na wasiwasi wa kupewa hukumu ya kifungo, katika maisha yangu sikuwahi kufikiria kama siku moja ningefungwa jela, kwenye maisha yangu niliogopa sana maeneno mawili, hospitalini hasa ICU na Jela. Nilikuwa nikiomba kimoyomoyo Ile video iliyoletwa na Riadi iweze kumshawishi Hakimu na kuniachia huru.

Punde yule mhudumu wa mahakama akarudi akiwa amebeba laptop, kisha akaenda kwa hakimu na kuiunganisha ile simu kwa waya wa USB, akabonyeza bonyeza kwenye laptop, bila shaka alikuwa akihamisha ile video kwenye Laptop, nikamuona akiunganisha laptop na waya Fulani hivi nisiojua kazi yake, alafu akasimama akalichangua lile joho mpaka alipopata nafasi ya kupitisha mkono wake kwenye mfuko wa suruali, akatoa kifaa Fulani kama rimoti, akabonyeza kuelekea juu, jambo ambalo lilifanya karibia watu wote wainue vichwa vyao juu, hapo nikaona Projector ikiwaka kitaa chekundu. Baadaye wote tukashuhudia picha ukutani upande wa kulia.

Hapo macho ya watu wote yakavutwa kuona video ya shahidi, Marehemu Kibadeni. Haikuchukua muda Hakimu akasema;

“ Tutaenda kuona na kusikiliza ushahidi wa Mr. Kibadeni ambaye ameshindwa kuhudhuria kuja kutoa ushahidi wake kwa sababu ya kukutwa na umauti, mahakama itaangalia kisha itaamua kama ushahidi huu uzingatiwe au upuuzwe, ila kwa vile mahakama ipo kwaajili ya kutoa haki, ndio maana tumeipokea ushahidi huu kama sehemu ya kumtendea haki ndugu Gibson. Tunaweza kuanza kuona”

Sijui ni kwanini mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda mbio kiasi kile, nilihisi woga sana. Punde sinema ilimuonyesha Mr. Kibadeni akiwa kwenye kitanda kilekile cha hospitalini nilipomkuta jana, akiwa kavaa kichwani kofia nyepesi ya rangi ya kijani yenye matundu madogomadogo kama chujio, akiwa katundikiwa dripu, upande wa kitanda alichokuwa amekilalia ulikuwepo mtambo mmoja wenye kioo kinachoonyesha Grafu zenye mawimbi zilizokuwa zinapanda na kushuka huku pembeni kabisa kukiwa na tarakimu za namba zenye asilimia, Mr. Kibadeni alikuwa amefunikwa shuka jeupe lenye nembo ya ile hospitali; kuanzia miguuni mpaka kiunoni karibu na kitovu, juu alikuwa amevalia shati la kijani linalofanana rangi na ile kofia aliyokuwa ameivaa. Mr. Kibadeni akajiweka sawa akijilazimisha kukaa lakini akashindwa, akatokea nyuma ya kamera Mtoto wake akaenda kumnyanyua na kumsaidia kukaa kisha akamuacha na kurudi nyuma ya kamera akimuacha Mr. Kibadeni pekeake, nikajikuta nikijiuliza nani alimuachia kamera achukue tukio lile, lakini wazo hilo lilikatishwa baada ya Mr. Kibadeni kuanza kuongea;

“ Naitwa Mr. Kibadeni, sina haja ya kujitambulisha sana ila najua Hakimu utakuwa unanifahamu” Hapo nikamtazama hakimu kwa haraka, nikamuona akiwa na uso wa kukubaliana na maneno ya Mr. Kibadeni. Hali ikanifanya nishangae.

“ Nimelazwa kwa miezi mingi sana, familia na serikali vimehangaika kuyapigania maisha yangu, kwa kweli sina chakuwalipa isipokuwa shukrani zangu, katika watu walioyapigania maisha yangu ni pamoja na huyo kijana aitwaye Gibson, hakuwa akinijua; wala mimi sikuwa namfahamu, na nadhani mpaka sasa sidhani kama ananijua, hiyo ni kawaida kwa mtu wa kawaida na kijana kama yeye kufahamu watu wa aina zetu,” Mr. Kibadeni akakohoa kidogo kisha akaendelea;

“ Usiku ule sitakuja kuusahau katika maisha yangu, nikiwa nimelala nilishtuka baada ya kuamshwa na mwanaume mmoja mrefu aliyevalia koti jeupe la kidaktari, usoni akiwa kavaa barakoa iliyoficha uso wake, mikono yake alikuwa amevaa Gloves za kitambaa yenye rangi nyeusi, mkono mmoja akiwa kashika bastola, nilijua na kuamini mtu yule alikuja kwa ajili ya kuniua hata kama asingeniambia; jinsi alivyoonekana alifanana kabisa na mtoa roho. Akanitisha, kisha akachukua kichupa cha sumu kutoka kwenye mfuko wake, akatoa na sindano akaichoma ile sumu aliyoivuta kwenye sindano na kuiingiza kwenye Dripu nililokuwa nimetundikiwa” anapumua kidogo kisha anaendelea.

“ sumu ilikuwa imeshachanganyika na maji ya Dripu, sikuwa na uwezo wa kuliondoa dripu kwani nilikuwa nimezidiwa sana, sikuweza hata kujigeuza wala kunyanyua mkono, yule Mwanaume shetani baada ya kufanya ushetani wake akaondoka, hapo nikawa nakisubiri kifo changu maana muda mfupi ujao ile sumu ingekuwa imeshaanza kuingia polepole mwilini mwangu. Lakini kwa bahati kumbe yule kijana niliyekuwa nimelazwa naye wodi moja alikuwa macho, nikashangaa ameamka upesiupesi kisha akaja kunitoa lile dripu, nilikuwa siwezi hata kuongea…” Mr. Kibadeni akaanza kukohoa mfululizo, alikohoa mpaka pale mahakamani kila mmoja wetu akawa anakunja uso kwa kuhisi maumivu anayoyapata, alikohoa zaidi na zaidi mpaka akalegea kama mlenda, nikawa naomba kimoyomoyo lolote baya lisimtokee kabla hajamaliza kueleza kila kitu, lakini nilihisi kukata tamaa nilipoona akikohoa mpaka udenda unamtoka, kwa upesi tukamuona Riadi akitokea nyuma ya kamera akiwa na chupa ya maji, akaenda akamshika Baba yake na kumpiga piga mgongoni, kisha akampa ile chupa ya maji, yule mzee akanywa, lakini alikuwa amechoka wala sio utani.

Akamuegemeza kwenye kitanda, Mr. Kibadeni alikuwa kayafumba macho yake kama siku ya kwanza niliyomkuta kule wodini, kisha akayafumbua, nilikuwa nikisali sana, niliogopa, kila muda niliyafukuza mawazo mabaya yaliyokuwa yakinijia kichwani kumhusu Mr. Kibadeni.

Mr. Kibadeni akajitahidi kusema kitu lakini akaishia kukohoa maradufu zaidi mpaka macho yakawa yanamtoka, hapo nikajua basi, ule mtambo kitandani ukaanza kulia huku kukitokea mstari mwekundu na zile tarakimu za namba zikishuka kwa kasi kutoka 205 na mpaka muda ule zikawa zinasoma 162, hisia zilizotawala pale kwenye ukumbi wa mahakama zilikuwa za msisimko. Yule muuguzi aliyenishtaki nilimuona akiwa amejawa na shauku ya kuujua ukweli. Nikamuona Mr. Kibadeni akamvuta Mwanaye, Riadi mpaka kwenye uso wake na kulisogelea sikio lake, hatukusikia alisemaje, lakini tukamuona Riadi akimpekua Baba yake kwenye mifuko ya suruali yake, tukamuona Riadi akitoa kitu kama Kadilida au memorikadi ile kubwa kutoka mfukoni mwa baba yake, alafu ghafla tukasikia mlango ukifunguliwa na punde wakajitokeza madaktari wawili waliovalia makoti ya kidaktari wakiwa na stethoscope shingoni, wakampima Mr. Kibadeni na hapohapo video ikafikia tamati.

“ Ndio Mr. Riadi, huo ndio ushahidi wa Baba yako? Mbona haujakamilika, kile ulichokitoa kwenye mfuko wa suruali yake ni kitu gani?” Hakimu akauliza akiwa anamtazama Riadi.

“ Mhe. Hakimu kama ulivyoona Baba yangu alizidiwa akiwa anatoa ushahidi wake, kwa bahati mbaya kabla hajamaliza kutoa maelezo yake akazidiwa” Riadi akasema, Hakimu akawa anaandika.

“Sasa itakuwaje kama ushahidi ndio umeishia hapa, haujakamilika?” Nikawaza.

“ Lakini kuna hii device Baba aliniambia niitoe mfukoni mwake, alinambia hii ndio ushahidi wa moja kwa moja, japo sijapata nafasi ya kuiangalia” Riadi akasema akiitoa ile device inayofanana na Memorikadi kubwa. Hakimu akaipokea kisha akamuita yule mhudumu wa Mahakama, akaichomeka ile device kwenye laptop, ghafla video ikajionyesha ingawaje ilikuwa inatingishika tingishika lakini tuliweza kuona kilichokuwa kinaendelea, video ilimuonyesha yule mwanaume mrefu alivyokuwa akimuamsha Mr. Kibadeni na matukio yote aliyoyafanya, ilinionyesha na mimi nilivyoenda kumsaidia Mr. Kibadeni, nikatoka kwenda kumuita Muuguzi kisha nikarejea nikiwa na Muuguzi, ikanionyesha ugomvi wangu na Muuguzi mpaka nilipolikanyaga lile Dripu na kulipasua. Mahakama nzima ilishangazwa na ushahidi ule, muuguzi alibaki ameduwaa asiamini kilichokuwa kimetokea. Nilishukuru sana, nilijikuta nikilia kwa uchungu mwingi, sikuamini kama wokovu ungepatikana dakika za mwisho kabisa.

Baadaye hakimu alitoa hukumu ya kuniacha huru baada ya kunikuta sina hatia.

MWISHO WA SEASON 01.

Kesho tunaendelea na season 02
Nisameheni kwa kuwaweka sana, kuna mambo yaliingiliana wakuu.
Ratiba ni kila siku saa saba mchana

Ahsante sana, Shukran Mkuu
 
KABURI LA MWANAMUZIKI ( SEASON 2)
MTUNZI: Robert Heriel
whatsApp 0693322300

Episode 01


“Utaishi hapa kama nyumbani, jisikie amani Mr. Gibson, nashindwa ni namna gani naweza kukushukuru ndugu yangu, bila ya wewe Baba yangu angekuwa ameshakufa, lakini ulimuokoa” Riadi alisema akiwa ananikaribisha nyumbani kwake. Kauli yake ya kusema Baba yake angekuwa ameshakufa ilinishtua, nikawa nawaza; kwani bado yupo hai. Nikajikuta nikijizuia kumuuliza;

“Unamaana gani kusema angekuwa ameshakufa?”

“Aaah! Namaanisha angekufa siku ileile, angekufa kifo kibaya sana” Akasema. Tukatazamana na mwishowe nikaongeza swali jingine;

“ Kwa hiyo mazishi ya Mzee ni lini?” Nikauliza.

“ Mazishi! Gibson Achana na hayo, hilo suala lipo kifamilia zaidi, kuna mambo siwezi kuyaweka wazi kwako, wewe mwenyewe unatambua tukio lililotokea la kutaka kumuua baba yangu, unafikiri wauaji wake wameisha, mazishi yake yatakuwa siri, na sisi tuu kama wanafamilia ndio tutahusika katika mazishi” Riadi alisema akiwa anajitahidi kuelezea kwa kina ili nielewe. Nilimuelewa.

Maisha mapya katika nyumba ya Riadi yalianza, Riadi alikuwa akiishi pekeake katika jumba kubwa la kisasa lenye kila aina ya samani za kuvutia, lilikuwa jumba kubwa la ghorofa mbili, nje kulikuwa na bwawa la kuogelea na bustani za kupumzikia, upande mwingine kulikuwa na sehemu iliyotengwa kwa kuegeshea magari, ndani yake yalikuwepo magari mawili ya gharama, kwakweli sikuwahi kufikiri kuna kijana mwenye umri kama wa Riadi mwenye maisha mazuri kama yale. Yalikuwa maisha ambayo ni nadra kwa vijana waliowengi kuwa nayo, umri wa Riadi haukuwa zaidi ya miaka thelasini na mbili, akiwa hajapishana na mimi sana kiumri. Lakini maisha aliyokuwa nayo ni mara elfu elfu ukilinganisha na maisha yangu.

Baada ya siku mbili kupita tangu nifike nyumbani kwa Riadi, tayari nilianza kuzoea mazingira, nikiwa nasaidia kazi za usafi na mazingira ya nje. Riadi aliniambia kuwa angeondoka kwa siku tano kwenda mkoani kwa ajili ya mazishi ya Baba yake, basi baada ya kuniachia maagizo ya namna ya kuishi katika nyumba yake, akaniaga; aliniacha pesa ambazo alisema zitanisaidie kwenye matumizi ya pale nyumbani, kiukweli tangu kuzaliwa sikuwahi kushsika milioni moja, ile ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kushika pesa nyingi kiasi kile, tena alisisitiza atanitumia tena kwani zile aliziona hazitoshi, hapo ndipo nikajua kuwa kuna watu duniani wanapesa, wakati kuna mtu anahangaika miezi na miezi apate milioni moja, kumbe kuna mwingine anatumia hiyo milioni moja kwa siku; Sasa Riadi alinambia siku tano hiyo pesa isingeweza kunitosha hivyo akifika tuu mkoani angeweza kutuma pesa nyingine. Aliniachia simu ya smartphone ambayo ilikuwa kama simu ya pale nyumbani. Kisha akaondoka na kuniacha peke yangu.

Ingawaje ilikuwa sio nyumba yangu lakini niliona fahari ya kuwa ndani yake, sasa niliona njia yangu ya mafanikio imefunguka, kuishi katika jumba kama lile kwangu nilihesabu ni bahati kubwa, “ Kuna watu maelfu kwa maelfu tangu wamezaliwa mpaka wamekufa hawajawahi hata kuingia katika majumba ya namna hii, kwa nini nisiite hii bahati” Niliwaza.

Nikamkumbuka mama yangu kijijini, nilikumbuka makazi duni tuliyokuwa tunaishi na mama yangu kule kijijini, hapo mawazo mengi yakausonga ubongo wangu, “ Ni lazima nikukomboe mama yangu, lazima nawe siku moja uishi katika jumba zuri kama hili, Mama yangu..” Niliwaza,

“Ni muda wa miezi kadhaa karibu mwaka mzima sijawasiliana na Mama yangu, sijui anaendeleaje, bila shaka atakuwa na wasiwasi na mimi” Nilisema kwa sauti ndogo huku nikichukua ile simu na kubonyeza bonyeza namba, nikaiweka sikioni na simu ikaanza kuita.

“Hello Kaka, ndio mimi Gibson, ndio! Za siku nzuri Kaka, yaani kuna mambo yaliingiliana Kaka, eeh! Wewe acha tuu! Vipi wazima huko! Afadhali Kaka, Mama yangu anaendeleaje? Ooh! Upo karibu na nyumbani; nataka umpelekee simu nizungumze naye, sawa nasubiri” Nikakata simu baada ya kuongea na Kaka mmoja ambaye alikuwa jirani yetu, nilifurahi kusikia mama yangu hajambo, sasa nilikuwa nasubiria simu ya Kaka ambaye ameenda nyumbani kwetu kumuangalia mama yangu ili ampe simu nizungumze naye, nilikuwa na shauku kubwa ya kuongea na mama, nilimkumbuka sana. Nikiwa nipo sebuleni nikiwa natazama Muziki Luningani, punde simu ikaita, kisha ikakata, Nikaipigia; “Sawa Kaka, basi akirudi jioni unitafute nizungumze naye, sawa!” Simu ikakatika.

Mama alikuwa hayupo, alikuwa ametoka, taarifa hiyo ilinikata maini kweli. Ilipofika jioni nikampigia tena yule kaka lakini mara hii akawa hapatikani, hasira zilinipanda, nilimkasirikia lakini nikakumbuka kuwa nyumba yao pia haina umeme kama ilivyo nyumba yetu, pia hata kama ingekuwa na umeme sikuwa na uhalali wa kumkasirikia mtu ambaye hata hivyo ananisaidia tuu. “Ndio tatizo letu masikini, mtu anakusaidia lakini bado unamuona mbaya, sasa kaka anakosa gani mpaka nimkasirikie?” Nikawaza baada ya hasira kupungua.

Kesho ikafika, nikaendelea na shughuli zangu za usafi wa nyumba na mazingira ya nje, lakini wakati nafanya usafi wa bustani, kengele ya geri ikalia, hii ilimaanisha kuna mtu anabisha hodi, nikaenda getini nikapokelewa na mwanamke mmoja akiwa na mtoto wa kiume wa miaka kama minne hivi, nyuma yake kukiwa na gari zuri. Yule mwanamke alikuwa kava miwani ya yenye vioo vya rangi ya huzurungi, hereni sikioni na kilemba, mavazi yake yalifanana na mavazi ya kinaijeria ambayo yalikuwa sawa nayamtoto, yule mtoto wa kiume kichwani alivalishwa kofia inayofanana na lemba la yule mwanamke ambaye nilihisi ni mama na mwana.

“Habari yako Dada, naomba nikusaidie” Nikasema.

“ Unisaidie? Are you mad! Unaweza kunisaidia kwa lipi kijana wewe eehe! Embu fungua geti niingie” Yule mwanamke akasema kwa dharau, kwa kweli sikupendezwa kwa namna alivyokuwa akiuweka uso wake na kuupinda mdomo wake, nilitamani nimchape kibao kimoja achunge adabu yake lakini nafsi yangu ikanionya.

“Samahani Dada yangu, sikuwa na maana hiyo, nilikuwa naomba kujua wewe ni nani na unahitaji nini?” Nikasema nikiwa nimenywea, kwa kweli nilitia huruma, nilikumbuka kauli isemayo usipambane na mtu usiyemjua.

“ nimekuja kwangu, nipishe, utaingiza gari hili ndani, Mwanangu twende ndani” Yule mwanamke akasema huku akinisukuma nimpishe pale kwenye geti dogo kisha akaingia na mtoto wake, nikabaki nimeduwaa nsijue nifanye nini, nikakumbuka, nikampigia Riadi, nilishangaa Riadi akinambia yule aliyekuja ni Mke wake, alikuwa ametoka kidogo, akaniomba msamaha kwa usumbufu uliokuwa umejitokeza.

Nikaliingiza gari ndani, alafu nikaenda sebuleni ambapo nilimkuta yule mwanamke akigombezana na mtu kwenye simu ambaye baadaye nilijua alikuwa akigombana na Riadi, nikamuacha pale sebuleni kisha nikarudi zangu nje kuendelea na usafi wa bustanini. Baada ya kumaliza usafi nilirejea ndani kwa ajili ya kuandaa chai ya asubuhi, niliandaa chai ya maziwa, soseji na mayai ya kuchemsha mawili mawili. Kisha nikapanda ghorofani kumuita yule mwanamke na mtoto. Niliwakuta katika sebule ya juu ya ghorofa ya pili, alikuwa tayari keshabadili nguo na kukaa kihasara hasara akiwa ameshavua lemba kichwani, alikuwa na nywele bandia zilizomwagika mabegani.

“Vipi!” Yule mwanamke akanisemesha kwa ukali baada ya kuniona.

“Aaah! Samahani sana, nimekuja kuwaita, chai tayari”

“ Nini? Hivi wewe unaakili sawasawa! Eeeh!” Yule mwanamke akasema kisha akasimama na kunifuata akiwa amenitolea macho yake makubwa na makali.

“ Umechanganyikiwa!” Hapo akatingisha nywele zake, kisha akauweka uso wake kidada na kuung’ata mdomo wake, kisha akasema;

“ Mwenye njaa hapa ni wewe, sawa! Tena ukome kusogea eneo ambalo mimi nipo, haya futika”

Sikuwa na haja ya kusubiri arudie, nikaondoka harakaharaka huku nikimsikia mtoto wake akinicheka, nilijisikia vibaya sana, kudharaulika kusikia tuu, kila mwanadamu anataka kuheshimiwa, hakuna ambaye anapenda kudharauliwa, “hata kama mimi ni masikini isiwe sababu ya kunidharau” Niliwaza nikiwa nashuka ngazi kuelekea chini. Siku ile ikapita wala sikuonana na yule mwanamke ambaye ni mke wa Riadi.

Nilikuwa nikifanya mazoezi ya kuimba eneo la bustani kila jioni, nikiwa nina kalamu na daftari aliloninunulia Riadi, kidaftari kile nilikuwa nimeshaandika nyimbo kadhaa hivi ambazo nilitarajia siku zijazo ningezirekodi studio ili zipigwe redioni na kwenye televisheni, nikiwa nimekaa kwenye bembea pale bustanini ghafla mke wa Riadi akaja,

“ Wewe! Weewe! Hunisikii! Hivi unampigia nani kelele hapa, huoni mta mzima ulivyotulia, lisauti lako libaya kama kondoo ndio linachafua utulivu wa mtaa huu, unadhani huku ni kule uswahili kwenu! Eenhe!” Yule mwanamke akasema akiwa sasa amenikaribia, mikono yake ikiwa kiunoni, akinitazama kwa hasira zilizofichika. Mimi sikujua nimjibu jambo gani, na nisingependa kuongopa hapa, nilianza kumuogopa, ingawaje alikuwa hanipigi lakini maneno yake yalikuwa makali sana ni afadhali angenikuwa ananipiga. Silaha ya mwanamke ni mdomo wake, lakini silaha ya mwisho kubwa ya mwanamke ni mwili wake, hilo nilianza kuliona baada ya kuona kinguo alichokuwa amekuja nacho pale bustanini, alikuwa amevaa mtandio mwepesi alioufunga kidizaini, ulioshika kiuno chake chembamba na mapaja laini ambayo niliyaona Kupitia mtandio ule uliokuwa unaonyesha kwa ndani, alikuwa kava chupi aina ya bikini, juu alivalia kitopu, huku chini kabisa akiwa kava kikuku, macho yangu mara kwa mara yalikuwa yakikwepa kuziangalia shanga mbili zilizokuwa zinawakawake kwenye kiuno chake.

“ Unajifanya jeuri, lete hii” Akaninyang’anya kile kidaftari na kuanza kukipekua pekua, kisha akaanza kusoma moja ya nyimbo nilizokuwa nimeziandika kwa sauti, akijifanya anarapu;

“ Penzi lako pipi filimbi, Nitalinyonya na kulilamba,

Nitaoga kwa lako wimbi, mdomoni udenda ukinisomba,

Mzizi wa moyo wako sichimbi, mhogo wangu utausomba,

Refa keshapiga filimbi, mechi tayari nyavuni kumeshasoma,

Ooh! Mama, tingisha lako behewa, nishike zako mbili kuta,

Penzi lako my dear nalewa, nikikuchapa fimbo huwezi futa,

Unanivuta na kuning’ata kama muwa, utamu tamu kolea wauchakata….”

Anaacha kurapu alafu ananiangalia, kisha anatabasamu, nabaki namuangalia kama mtu wa maajabu hivi nisiyemuelewa,

“Hivi ndivyo washenzi mnavyodanganya watoto wa kike, sivyo, haya marapu rapu yako, haya! Haya!” Akawa anachana lile Daftari hali iliyofanya niamke na kumfuata na kunyang’anya lile daftari, lakini wakati tunanyang’anyana kwa bahati mbaya ule mtandio ukaanguka akabakiwa na bikini tuu, kiukweli nilipigwa na kitu mfano wa shoti ya umeme, kihoro kilinikaba, nikageuka upesi upande mwingine na kufumba macho yangu, Mke wa Riadi akavaa mtandio wake kisha akanipiga kichwani na vile vipande vya daftari alilokuwa amelichana, kisha akaondoka akiniacha pale nimesimama.

“Haya ni majaribu, ila yanipasa niyashinde, lazima niutawale mwili wangu, wakati mwingine kushindwa kutawala hisia za mwili ni kushindwa kujitawala, na kushindwa kujitawala ni kushindwa kuyaendesha maisha yako binafsi” Niliwaza mwenyewe nikiwa naokota zile karatasi zilizochanwa chanwa na mke wa Riadi ili kuondoa takataka pale bustanini.

Usiku uliigia, giza likachukua sehemu ya mchana, siku ya leo ilikuwa tofauti na siku zingine, Sebuleni kwenye meza ya kulia chakula, nilikuwepo mimi, Mke wa Riadi na mtoto, tukiwa tunakula chakula cha usiku. Tofauti na siku nyingine, Mke wa Riadi alikuwa kabadilika usiku huu, alikuwa mpole asiye na maneno maneno akiwa anaperuzi mtandaoni huku akila chakula, kwa kweli sikutegemea kama siku moja angethubutu kula chakula nilichokuwa nimepika, alikuwa na dharau sana yule mwanamke. Wakati Fulani alikuwa akinichungulia kwa kujiiba iba, hapo nikagundua jambo geni kabisa, Mke wa Riadi alikuwa akinionea aibu, sikujua aibu ile ilitokana na tukio la mchana au ilikuwa aibu iliyosababishwa na nini. Jambo lile hata mtoto aliliona akawa anamtazama mama yake alafu kuna muda alikuwa akinitazama mimi kwa udadisi.

“Mama mbona uko hivyo?” Mtoto akauliza akiwa anamtazama mama yake.

“ Nilikuambiaje!” Mke wa Riadi akafoka.

“Samahani Mama, uliniambia wakati wa kula sio wakati wa kuongea”

“Haya kula” Mke wa Riadi akasema bila utani. Pakawa kimya tena huku sauti ya vijiko na sahani zikiendelea kusemeshana. Tulimaliza kula, wakaondoka na kupanda ghorofani wakiniacha mimi chini,, nikatoa vyombo mezani kisha nikaenda kuoga, alafu nikarudi sebuleni kuangalia Luninga, nilijilaza kwenye sofa nikitazama muziki uliokuwa unaonyeshwa kwenye chaneli Fulani kwenye TV. Kama baada ya lisaa limoja hivi Mke wa Riadi akaja tena, muda huu alikuwa amevaa Night Dreess ya rangi ya kijibu inayong’ara ndani akiwa hajavaa nguo yoyote. Kiukweli niliona kama ananifanyia makusudi, sasa maana yake nini kuja na vinguo vya kulalia sebuleni, anataka nini sasa, nikawa nawaza, nikimuangalia kwa kijicho upembe, naye kwa makusudi akawa amesimama mahali ambapo alijua fika kabisa nitakuwa namuona, akaenda kwenye sofa na kujibwa pwaa! Kizembe zembe, alafu akakaa kiholela akiacha eneo kubwa la mapaja yake wazi, hili lilikuwa shambulio la makusudi la kunitesa kihisia, Ni kweli namheshimu sana Riadi, ni kweli kabisa amenisaidia na nipo nyumbani kwake, lakini kwa kile kilichokuwa kinaendelea kilikuwa ni kubwa zaidi ya heshima aliyonipa Riadi, wakati mwingine mtego huweza kuwa mkubwa kuliko heshima unayompa mtu.

Sio kwamba sikuyaona mapaja yake yaliyonona, rangi ya kichokozi, ma uso wake wa jinni mahaba lililodhamiria kuniteka kwa hila zake. “Gibson jizuie, huo ni mtego, jitahidi Gibson” Nilikuwa nikijiambia kimoyomoyo, sijui ni muda gani nilisahau kuwa nilikuwa naangalia muziki luningani, akili yangu ilishatekwa na Jini mbaya wa mapenzi, sasa nilikuwa kwenye miliki yake, moyo wangu ulikuwa kama askari asubiriye amri ya mkuu wake. Ghafla simu yangu ikaita ikiwa pale chini kwenye zulia, nikaichukua, zilikuwa namba za kaka jirani kule kijijini. Nilifurahia kuona akinipigia, nikakata alafu nikapiga, ikaita mara moja kisha ikapokelewa, nikaweka loud,

“Hallo Mwanangu” Ilikuwa sauti ya Mama yangu, nilifurahi sana,

“Hallo mama, shikamoo mama yangu” Nikasema.

“Marhaba Gibson, umepotelea wapi mwanangu, nilikuwa na wasiwasi mwanangu” Mama alisema kwa sauti iliyolegea sana kama mtu anayetaka kulia, nilimuelewa sana mama yangu, sauti yake ya namna hiyo ilimaanisha muda mchache ujao atalia.

“ Nisamehe Mama, nilipatwa na matatizo makubwa mama yangu, lakini kwa sasa naendelea vizuri” Nikamjibu.

“ Pole sana mwanangu, hayo ndio maisha, lazima upambane kama Mwanaume, Usikubali kushindwa kirahisi Mwanangu, lakini pia usiibe cha mtu, pia jichunge na wake za watu huko mjini” Hapo nikamtazama Mke wa Riadi ambaye naye alikuwa ananikodolea macho yake huku akiwa anakula Komamanga.

“Usijali Mama, mimi nitafuata kila ulichoniagiza mama yangu”

“Ulipatwa na nini Mwanangu?” Mama akaniuliza.

“Mamaa! Ni stori ndefu sana, siwezi kuimaliza leo, nitatafuta siku nyingine tuzungumze, kwa sasa ninachotaka kusema nimefurahi sana kujua unaendelea vizuri, kesho uende kwenye duka la simu ukachague simu nzuri nitakutumia pesa kidogo ili tuwasiliane mama yangu”

“ Gibson, unazungumzia kuninunulia simu wakati nyumba yetu ilidondoka upande wa chumba change, hapa nilipo nalala kwenye chumba chako. Kama ingefaa hiyo pesa ya kununulia simu ni bora tufanye ukarabati kwenye huu ukuta mwanangu” Mama akasema kisha akakohoa,

“Pole Mama yangu”

“Ahsante mwanangu, yaani baridi hapa inanipiga mwanangu, haya mapazia yamechakaa, tangu ulipoyaacha mpaka leo ni yaleyale, natumia vipande vya vitenge kufunika dirisha ile upepo wa baridi usiingie mwanangu” Nilimsikia mama akilia kwa sauti, nikajikuta name nikishindwa kuzuia machozi yangu.

“Mama! Mama! Usilie mama, kila kitu kitakuwa sawa Mama yangu” Nikasema,

“Sawa mwanangu nakuombea”

“Kesho ufanye nilichokuambia, simu itatusaidia kuwasiliana mimi na wewe, pia kukurushia pesa, sawa mama” Nikasema, mwishowe nikazungumza na kaka jirani na kumshukuru kwa msaada alionipa. Baada ya simu kukatika moyo wangu ulijazwa na furaha isiyokifani, nilifurahia kuongea na mama yangu.

“ Nisamehe sana Gibson” Mke wa Riadi akasema, nilishtuka kusikia akilitaja jina langu, nikakumbuka amelisikia wakati nikiongea na Mama.

“ Nikusamehe kivipi Shemeji?” Nikamuuliza.

“ Kwa yote niliyokufanyia, tangu siku ya kwanza mpaka leo jioni nilivyochana kidaftari chako. Kwa kweli sikuwa muungwana, nilifanya mambo yasiyo mazuri”

“Usijali shemeji kila jambo linasababu zake, maisha ni kujifunza” Nikasema

“ Hakika maisha ni kujifunza, name nimejifunza kwako uvumilivu na staha hata kama mtu atakukera vipi” Akasema.

“ Hata mimi umenifundisha kuomba msamaha pale ninapokuwa ninakosea, kama ulivyofanya wewe sasa hivi” Nikasema, wote tukacheka, lakini nilitamani nimuambie jambo moja, nikasita. Nilitaka kumuambia akae vizuri au akabadilishe ile nguo lakini sijui ni kwa nini nilishindwa.

Tulipiga stori nikiwa najizuia nisiangalie mapaja yake ambayo mara kwa mara alikuwa akihakikisha ninayaona na kunirembulia. Muda ulienda akaaga na kuondoka kwenda kulala, akiwa anaondoka alitembea kwa madoido huku akiyatikisa makalio yake laini, alipofika kwenye ngazi za kupanda juu ghorofani akawa anapanda kama mlimbwende huku kila akipanda ngazi tatu alizitikia nywele zake kwa madaha na kunogesha mvuto wake, akafika ngazi ya juu kabisa ili atokomee, hapo akasimama, alafu akageuka kwa upesi kunitazama, tukakutanisha macho yetu, alafu akaachia tabasamu jepesi la ulaghai kisha akainua mkono wake na kuniaga kwa ishara za kizungu, alafu akapotea kama jinni la kwenye vitabu vya Kigiriki.

Kulipambazuka, siku ya leo Shemeji alikuwa akifanya usafi wa ndani ya nyumba, nilipotaka kumzuia akanikataza, akasema yeye ni mwanamke hivyo usafi wa ndani ni jukumu lake, nikatoka kwenda nje kumwagilia maua na shughuli za nje, tulipomaliza usafi tulienda kunywa chai. Asubuhi ya leo Shemeji alikuwa na furaha zaidi kuliko siku zote.

“Kesho utaanza shule, nimekutafutia shule mwanangu” Shemeji akasema akimtamza mtoto wake.

“Shule nyingine tena mummy, Neyla naye atakuwepo” Mtoto akasema.

“ Hapana My son, Neyla atakuja siku zijazo, ukisoma vizuri naye atakuja msome wote, lakini ukiwa hautaki kwenda shule asubuhi unalialia, hatakuja kusoma na wewe”

“Sitakuwa nalia Mummy, nataka kusoma na Neyla” Mtoto alisema.

“Usijali mwanangu, maliza kula alafu leo tutatoka kwenda kuogelea” Shemeji akasema.

“ Gibson, utajiandaa tutatoka muda mfupi ujao, sawa?” Shemeji akanigeukia akinitazama kwa macho yaliyoficha hila za mapenzi.

“ Sawa! Lakini tunaenda wapi Shemeji”

“ Mmh! Gibson hujachoka tuu kukaa ndani kama mwali kwa kiluguru?”

“ Haha! Hamna shemeji, sawa nimekuelewa!” Nikajibu

“ Sawa, sisi ngoja tukajiandae, tukija uwe tayari” shemeji akasema hukua akiamka kwenye kiti na kipenzi chake kifupi kilichoacha kwa shemu kubwa mapaja yake wazi. Alikuwa akiishi maisha ya kizungu kwa kiasi kikubwa, kuna wakati nilifikiri tupo kwenye maigizo ya filamu za kisasa, lakini wala hatukuwa kwenye maigizo isipokuwa ilikuwa ni maisha halisi.

Sikuwa na mambo mengi ya kujiandaa, hivyo nilivyooga nikapaka tuu mafuta na kurudi sebuleni kuwasubiri. Shemeji alitoka akiwa amependeza mno, sikufikiria kama shemeji angefikia kiwango kile cha uzuri, alikuwa amevaa gauni la lastiki lililoushika mwili wake vizuri, likiwa limening’inia juu ya mapaja yake na kuachia mpasuo mdogo kwa mbele, lilikuwa la rangi ya kijani kibichi, shingoni alikuwa na mkufu wa silva ing’aayo, akiwa na herein zake ndogo masikioni, alivaa viatu vyenye kisigino kirefu cha wastani, mkononi akiwa na bangili ya rangi kama ya kijani mpauko, alikuwa kapendeza sana.

Nilikuwa nimeduwaa nikiwa namtazama akiwa anashuka kwenye ngazi polepole kwa madoido huku akitabasamu na kupiga hatua zake kwa tahadhari kwa mwendo wa catwalk, mara kwa mara alinyanyua mkono wake akizitoa nywele usoni kwa mbwembwe utadhani muigizaji mahiri wa filamu; akili haikunirejea mpaka aliponikaribia na kusimama mbele yangu kama malaika mwema na kujigeuza shaaa, nikasikia harufu ya manukato yake mazuri ajabu, kiukweli shemeji alikuwa mzuri wala sitaki kumsifia tena isijeonekana nilikuwa namtamani.

“OOH! My dear! Umevaa nini hii! Subiri nakuja” Shemeji akasema, kisha akapanda tena juu ghorofani. Hazikupita dakika nyingi akarudi akiwa na fuko lenye nguo ndani yake.

“Hizi nguo hazijavaliwa, Riadi aliletewa na Mwanamke mmoja wa kizungu ambaye kwa kweli ananiudhi sana, nahisi wanatoka naye” Shemeji akasema,

“Unamaana gani kusema hivyo?”

“Gibson, wewe sio mtoto mdogo, embu vaa tuondoke muda umekwenda” Akasema,

ITAENDELEA Kesho saa 7mchana
 
KABURI LA MWANAMUZIKI (EPISODE 02)
Mtunzi; Robert Heriel
whatsApp 0693322300

EPISODE 02
ILIPOISHIA

Nilikuwa nimeduwaa nikiwa namtazama akiwa anashuka kwenye ngazi polepole kwa madoido huku akitabasamu na kupiga hatua zake kwa tahadhari kwa mwendo wa catwalk, mara kwa mara alinyanyua mkono wake akizitoa nywele usoni kwa mbwembwe utadhani muigizaji mahiri wa filamu; akili haikunirejea mpaka aliponikaribia na kusimama mbele yangu kama malaika mwema na kujigeuza shaaa, nikasikia harufu ya manukato yake mazuri ajabu, kiukweli shemeji alikuwa mzuri wala sitaki kumsifia tena isijeonekana nilikuwa namtamani.

“OOH! My dear! Umevaa nini hii! Subiri nakuja” Shemeji akasema, kisha akapanda tena juu ghorofani. Hazikupita dakika nyingi akarudi akiwa na fuko lenye nguo ndani yake.

“Hizi nguo hazijavaliwa, Riadi aliletewa na Mwanamke mmoja wa kizungu ambaye kwa kweli ananiudhi sana, nahisi wanatoka naye” Shemeji akasema,

“Unamaana gani kusema hivyo?”

“Gibson, wewe sio mtoto mdogo, embu vaa tuondoke muda umekwenda” Akasema,.

*******

ENDELEA
Ndani ya Gari Shemeji alinifanyia vituko vya kila aina, mapaja yake aliyetumia ipasavyo kunifanyia emotional damage, alinitesa sana shemeji, tulifika maeneo ya mikocheni tukamuacha mtoto pale sehemu ya kuogelea tukimkabidhi kwa wahusika wa mahali pale, shemeji akaniambia; sisi twende kwa wakubwa, sio mbali kutoka hapa” na kweli haikuchukua dakika tano tulisimama eneo jingine palepale mikocheni tukaingiza gari ndani ya geti baada ya kuruhusiwa na walinzi, tuliifuata njia yenye vigae ambayo ilizungukwa na maua huku na huku, tukiwa chini ya vivuli vyenye upepo mwanana, eneo lilikuwa na kagiza kanakotokana na kivuli cha miti mingi na maua ya kuvutia yaliyokuwa eneo lile, tulipita katikati ya jengo lilokuwa mbele yetu tukatokea upande wa pili ambapo tulilakiwa na uwazi mkubwa wenye mwanga, kushoto likiwepo Bwawa kubwa la kisasa la kuogelea, tukapinda kulia kuifuata njia ambapo mbele kulikuwepo na eneo la maegesho ya magari. Baada ya kuegesha gari letu, tukashuka nikiwa nashangaa uzuri wa eneo lile, tulipotoka lile jengo kwa juu yalisomeka maandishi Turkey Resort LL. Kulikuwa pia na Mini-supermarket, mbele kabisa kwenye bwawa niliona vitanda vizuri vya kupumzika, nyuma ya vile vitanda vya kupumzikia kushoto kabisa zilikuwepo meza na viti vya dizaini ya kustaajabisha. Bado nilikuwa nikishangaa, niliona wanawake watatu, wawili wakiwa majini wakiogelea kwa raha zao, mmoja alikuwa kalala kwenye vile vitanda akiwa kava miwani nyeusi, na nguo za kuogelea ambazo kwa sehemu kubwa ziliacha sehemu za mwili wake wazi, akiwa kashikilia Glass yenye Cocktail ya rangi ya waridi.

Shemeji alinishika mkono kama vile mtu na mwenza wake, nilipotaka kupingana na jambo lake akanikazia macho, sikuwa na namna zaidi ya kumkubalia, tulioongozana mpaka kwenye ile supermarket, milango ya vioo yenye sensor ikafunguka yenyewe, tukaingia ndani, tukapokelewa na Kijana mmoja wa kituruki, tukapita moja kwa moja kwenye bidhaa, shemeji akanichagulia bukta nzuri ya kuogelea, kisha baada ya kunichagulia, tukarudi kwa yule kijana wa kituruki, tukalipia, tukatoka, akarudi kwenye gari, mimi akanielekeza niende kwenye chumba Fulani kilichokuwa karibu na maegesho ya magari ili nikabadili nguo, sikuweza kukataa,

Nilirejea nikiwa nipo kifua wazi na bukta mpya niliyonunuliwa na shemeji, ilikuwa bukta ya rangi nyeusi yenye mstari mweupe uliopita kama upinde kutoka upande wa kulia mpaka kushoto, ilikuwa imenishika vyema sana, basi nikasogea kwenye lile bwawa wale wadada wawili wakawa wananitazama kwa kujiiba iba, nikawasalimu, wakaniitikia lakini kwa kuchanganya Kiswahili na kingereza, hapo nikajua walikuwa wadada wakishua, kwani hata muonekano wao uliwatambulisha hivyo, walijaribu kunikarimu huku wakizikung’uta kila mara nywele zao zilizokuwa zimelowa maji. Sikupata muda wa kuzungumza nao sana, shemeji alikuja na kunikumbatia kwa nyuma, kisha akaniachia na kunishika mkono wa kulia, nikageuka bado nikiwa nimemshika na mkono wakulia, macho yangu yalaishutushwa, nilibaki nimetoa macho nikiukodolea mwili wa shemeji, alikuwa kavaa skirtini tamka ‘sketini’ iliyomkaa sawa, sketini ni kijivazi cha kuogelea wanachovaa wanawake ambacho huwafanya kuwa na mvuto wa kimapenzi, kwa juu huwa brazia ya kitambaa alafu chini huwa ni kisketi kifupi kilichoachia na kuyaacha mapaja mazito ya shemeji yakimeremeta. Sketini aliyokuwa amevaa ilikuwa ni rangi ya waridi na ile brazia ilikuwa ya rangi yenye mistari meusi na nyeupe. Alipendeza sana, akaninyanyua mkono wangu na kujizungusha na kufanya kile kiguo kupepea kidogo na kuzidi kuniharibu vibaya hisia zangu.

Tuliingia majini tukawa tunaogelea huku kila mara akinikumbatia, shemeji alichokuwa anakifanya ni kuwaonyesha wale wadada wengine kuwa mimi ni mtu wake, aliona jinsi walivyokuwa wakinitazama na kuna wakati nami nilikuwa najiiba kuwatazama, hii ilipelekea kunifokea kila alipokuwa akiniona, sasa tulikuwa tumeshaogelea vya kutosha, wale wadada walikuwa wamejilaza kama mamba kwenye vile vitanda wakiwa wamevaa kila mmoja miwani, tulitoka majini nikiwa nimechakazwa vibaya kihisia na Shemeji yangu, sitaki kukumbuka kwani ule ulikuwa mwanzo wa kujiingiza katika shimo refu lenye giza, ambalo lilibadilisha maisha yangu.

Tukaenda kupumzika kwenye vile vitanda tukipiga stori, kisha tulipokauka, tukaenda kwenye zile meza na viti na kuagiza chakula kwani tayari ilikuwa imetimia saa sita hivi, ile menu ilikuwa na vyakula vilivyoandikwa kwa lugha nisiyokuwa ninaielewa, kama sio picha zilizokuwemo basi nisingeelewa hata kitu kimoja katika menu ile, niliambulia kuona picha ya nyama ya ng’ombe, kuku pamoja na soseji, picha za matunda pamoja na juisi, bei zake zilinishtua sana, sikuweza kuamini kuwa kulikuwa na chakula cha elfu sabini, na juisi ya elfu thelesini na tano, nikakumbuka kauli ya Riadi kuwa pesa aliyoniachia haitanitosha, sasa nilianza kukubaliana na Riadi; kama matumizi yenyewe ndio yale basi ni kweli milioni moja kwa siku tano sio kitu. Mimi sikula vitu vingi isipokuwa nyama iliyochanganywa sijui na kitu ganai pamoja na juisi ambayo iligharimu kama laki moja na kumi, shemeji yeye alikunywa whisky Glenfiddich 15yrs ambayo iligharimu laki na ishirini yenye kiwango cha pombe asilimia arobaini. Aliagiza na nyama choma tuu zilizotengenezwa vizuri, tulimaliza kula na kuondoka wakati shemeji akiwa ameshaanza kulewa, wakati tunaingia ndani ya gari kwa bahati mbaya niliacha simu yangu kule kwenye vitanda, nikashuka kuifuata, sikuikuta pale kitandani nilipokuwa nimelala, kabla sijapawa nikasikia sauti kutoka nyuma yangu;

“Unaitafuta hii?” Nikageuka nikakutana na moja ya wale wadada waliokuwa wanaogelea bwawani akiwa amenielekezea simu huku akinitazama kwa macho ya upendo wenye Haya,

“Yes, Nashukuru sana” Nikajibu nikiipokea,

“ Usijali, naitwa Daniella” Yule mdada mrembo akasema akiwa ananitazama akiachia tabasamu jepesi la kuomba urafiki.

“ Gibson”

“ Embu nisaidie namba zako hapa” Daniella akasema akinipa simu yake niandike namba zangu, hapo nikageuka nyuma kuangalia kwenye gari kuona kama shemeji ananiona, lakini sikumuona, nikachukua ile simu nikawa naandika namba zangu;

“Unamuogopa mkeo? Akaniuliza, nikiwa naandika namba kwenye simu yake.

“sina mke mimi..” nikajibu nikimkabidhi simu yake.

“Gibson unafanya nini?” Nikamsikia Shemeji akigomba kwa nguvu akiwa kwenye gari.

“ Nakuja shem”

“ Kwa heri tutawasiliana Daniella” Nikasema kwa haraka haraka nikaondoka nikimuacha Daniella akinitazama huku akitabasamu kama mtu aliyefanikisha jambo kubwa.

Tulimpitia mtoto na safari ya kurudi nyumbani ikaanza, shemeji alikuwa amelewa kabisa, alikuwa akipiga piga makelele, huku akitaka niongeze sauti ya muziki kwenye gari, alikuwa akinengua huku akibinua makalio yake alafu kuna wakati anashindwa kujihimili anaangukia kwenye usukani, nilikuwa nikimuondoa kwani alikuwa anahatarisha usalama wetu,

“Embu zimaa! Zima muziki huo, huzikii wewe” akawa anaongea kiulevi. Nikazima, akawa ananilazimisha niimbe;

“Niimbie basi, wewe si mwanamuziki, ile nyimbo yako tamu sana, penzi lako pipi filimbi, nailamba aamu! Aamu!” Akawa anaimba huku akionyesha vile anailamba pipi filimbi huku akinishika kwenye mapaja yangu.

“ Embu acha ujinga wako bhana, huoni kuna mtoto hapa, unafanya nini sasa?” Nilimsukuma na kumchapa kibao kimoja cha adabu.

“Umenipiga sio, unajifanya kidume sio” akatulia akawa anacheua macho yakiwa legelege, mwishowe akapitiwa na usingizi.

Simu yangu ikawa inaita, sauti ambayo ilikuwa kero, ilikuwa namba ngeni kabisa, nikajua huenda atakuwa Daniella, “siwezi kupokea simu ya Daniella nikiwa na shemeji” nikawaza, ikaita mpaka ikakata, kitambo kidogo ikaita tena, sikupokea tena mpaka ikakata, bado tulikuwa njiani tukirudi nyumbani, ikaita tena, kwa kweli nilianza kukereka,

“Pokea simu hiyo” Shemeji aliropoka akiwa kalala, nikamtazama alikuwa amechoka kweli.

“ Mama yako ulimuambia akupigie leo” Shemeji akasema akigeuza uso wake kwangu bila ya kuyafumbua macho yangu, “huenda itakuwa ni mama kweli” nikawaza, kabla sijapokea simu ikakata, nikasubiri tena ili apige lakini nikaona kimya, nikaona niipigie ile namba huku nikiwa nimepunguza sauti ili shemeji asisikie upande wa pili, ile simu ikaita kisha ikapokelewa, hapo nilikuwa nimepunguza mwendo wa gari.

“Hello, ooh! Sorry, amefika mbali, tafadhali muite mama yangu, sawa” nikawa nazungumza na mtu wa kwenye simu, mama alikuwa keshaondoka lakini alikuwa hajafika mbali, mwenye duka alikuwa anamuona, dakika moja mama akapewa simu, nikaweka simu loud,

“ Shikamoo Mama!”

“Marhaba mwanangu, yaani tumeipigia simu yako mpaka tukachoka mwanangu”

“Samahani mama, nilikuwa mbali na simu” nikasema lakini shemeji akaropoka na sauti lake la ulevi “Mbali hiyo kwiyoo” nikawahi kumziba mdomo na mkono,

“Huyo ni nani mwanangu?”

“Enhee! Aah! Achana naye, hapo kuna simu gani mama?”

“ Mwanangu mimi hata najua aina za simu basi, acha nimpe mwenye duka atakuambia”

“Sawa mama” Nikajibu, nikiwa namuachia mdomo shemeji.

“Hello mkuu!” Mwenye duka akasema,

“ ndio kiongozi, hapo kuna simu gani nzuri” nikasema, akawa anataja aina ya simu na bei zake.

“ Anhaa! Hapo si una huduma za uwakala wa pesa? Basi naomba umpe Mama yangu simu nzuri ya smartphone ya laki tatu, alafu unitajie namba za uwakala nikutumie pesa yako” nikasema, shemeji akaropoka; “Mwanaume gani unamnunulia mama yako simu ya laki tatu” nikamziba mdomo tena, “embu tulia bhana, pombe zinakuendesha vibaya wewe” nikasema, nikamuona shemeji akifungua macho yake alafu akaniangalia. Akanitoa mikono yangu mdomoni;

“Hivi Gibson unafikiri mimi ni mlevi nisiyejitambua kama wewe, nimeanza kunywa hizi pombe tangu mdogo, alinifundisha Mama yangu, usidhani zinaweza kuniondolea akili” akanitazama huku akilegeza macho yake, alafu akaendelea,

“Shika simu yangu hii mtumie mama milioni moja hapo ya simu alafu umtumie pesa nyingine ya matumizi”

“Hapana shemeji, nashukuru kwa kutaka kunisaidia ila naomba unisamehe kwa kukataa msaada wako” Nikasema.

“Embu acha ushamba wewe, utakufa masikini shauri yako, hii ni bahati tuu, usione najigonga gonga kwako ukadhani siku zote nitakuwa hivi, embu lete hizo namba za wakala alizokutumia” akachukua simu yangu muda huo kuna meseji iliyokuwa imeingia, akatuma milioni mbili, yule jamaa akapiga simu,

“Boss! Wewe ndio umetuma pesa yote hii?” akaniuliza yule muuza duka kwenye simu.

“Ndio mkuu, shilingi ngapi imefika?” Nikauliza.

“Mkuu, hujui umetuma kiasi gani?”

“Mpe mama simu nzuri ya gharama alfu hiyo pesa itakayobaki mpatie” Shemeji akaropoka.

“ Kwani umetuma shilingi ngapi” Nikamuuliza shemeji.

“Milioni mbili tuu!” Akajibu, Nikapigwa na butwaa, lakini akanizuia nisiseme lolote.

“Kiongozi, mpatie simu isiyozidi milioni moja, alafu hiyo pesa nyingine mpatie”

“Haya nitampatia ya laki saba Mkuu” akajibu.

“ Sawa, mpe mama niongee naye” nikasema huku nikimtazama Shemeji,

“Ndio mama, atakupa hapo simu nzuri pamoja na milioni moja na laki tatu”

“Unasemaje Gibson?” Mama akauliza kwa kustaajabu.

“ Hiyo pesa utaanza kuikarabati nyumba pale ilipodondoka, usiwe na wasiwasi mama”

“Ubarikiwe mwanangu, kwani huko mjini unafanya shughuli gani mwanangu, hii pesa ni nyingi sana”

“Usijali mama, wewe tumia pesa za mwanao, tutawasiliana jioni” simu ikakatika.

‘ Ungemjibu shughuli uifanyayo mjini ni kumfurahisha shemeji yako, hahaha!” Shemeji akasema alafu akaachia kicheko cha kishambenga.

“Hivi kwa nini umetoa pesa yote hiyo?” Nikamuuliza.

“Mwanaume unaogopa kuhongwa na mwanamke, hahah! Unaogopa kuolewa?” shemeji akasema, wala sikumjibu nikawa naendesha gari.

“ Utachagua kuolewa na mwanaume mwenzako au kuolewa na mwanamke ambaye ni mimi, kwanza kuishi tuu kwenye nyumba ya mwanaume mwenzako huoni aibu, huko sio ndio kuolewa kwenyewe, sikiliza Gibson, wewe ni kijana mzuri nawe unastahili maisha mazuti kama aliyonayo Riadi, kuwa chini ya mwanaume mwenzako kama mke wake haipendezi, ni afadhali uwe chini yangu utapata chochote na ninaweza baadaye kukuzawadia mtoto”

“Embu tulia bhana! Mtoto yupo hapa ujue, hivi unamfundisha nini mtoto?” nikamkatisha.

“Mtoto ni wewe usiyeelewa mambo madogo, mwanangu mwenyewe anakushinda akili, si ati Junior?” akageuka siti za nyuma na kumtazama mtoto wake, Kupitia kioo cha gari kilichojuu ya mule ndani nikamuona Junior akitabasamu.

“Mimi sijaolewa na mtu, naomba tuheshimiane, kama huwezi kujiheshimu jaribu kuheshimu wengine” Nikasema,

“Hakuna cha bure Gibson, mtu yeyote mwenye akili anajua kila jambo lazima ulipie, iwe pesa au nguvu au ulipie kwa namna yoyote, hiyo ndio heshima, sijui unaposema unataka uheshimiwe unazungumzia jambo gani, ulitaka nikuambie uongo; mwanamke anaolewa sio kwa sababu ya kuwa yeye ni mwanamke isipokuwa kutokana na kutokuwa na mali, wakati mwingine kutokuwa na akili ya kutosha kumuongoza mwanaume, lakini kama mwanaume hana mali na akili pia naye ataolewa tuu. Lakini kwani lipi baya hapo, hutaki kuolewa na mwanamke mzuri kama mimi Gibson” Akasema, mwanzoni nilijua pombe zilikuwa zimemzidi lakini kumbe haikuwa hivyo, aliweza kuzitawala.

“ Mimi natafuta mali kwa jasho langu, sitaki pesa za kupewa pewa kama mtoto mdogo”

“ Hahah! Wacha weeh! Unafikiri hautazitolea jasho hizo pesa nilizompa mama yako? “ Hapo tukatazamana,

“Gibson! Unabahati sana, mimi sina huruma lakini sijui kwa nini umenigeuza kuwa kama kondoo, wewe ndio mtu wa pili baada ya Mume wangu, Riadi kumuonea huruma, nilitokea kukupenda tangu siku ya kwanza niliyokuona pale getini, ndio maana mpaka sasa hivi tupo pamoja” Akasema.

“Embu acha hizo habari, elewa wewe ni shemeji yangu, na itabaki hivyo siku zote, hakuna kitakachoendelea kati yangu na wewe, sawa” nikasema nikikatisha kwenye Geti la nyumba yetu lililokuwa linateleza polepole, tulikuwa tumefika nyumbani, tukashuka, lakini Shemeji hakuweza kushuka kutokana na pombe,

“ Shuka! Si ulisema pombe umekunywa tangu ukiwa mdogo, mbona hushuki sasa?”

“Nashuka” akashuka lakini akawa anapepesuka kidogo aanguke, nikamdaka, tukawa tunatazamana uso wangu ukiwa juu alafu wake ukiwa chini, akatabasamu, nilisikia mapigo yake ya moyo yakipiga, joto lake lilikuwa nyuzi joto za kulifanya yai la kuku lianguliwe, tukatazamana kwa kitambo mpaka niliposikia sauti ya mtoto;

“ Mama, Baba amekuja” Nilishtuka kusikia mtoto akisema hivyo, nikajinasua mikononi mwa Shemeji yangu, nikihaha kwa kuangalia huku na huku, lakini sikuweza kumuona Riadi, akili yangu ikaniambia tazama juu ya ghorofa, sikuamini niliyemuona, moyo wangu ni kama ulipigwa shoti ya umeme, nilimuona Riadi akiwa juu ghorofani amesimama akiwa ameshika kingo za ghorofa akiwa anatutazama mimi na shemeji, nilihisi kama mtu aliyefumaniwa.

ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom