Sharobaro la jf
JF-Expert Member
- Apr 23, 2020
- 237
- 325
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi : sharobaro la jf
CONTACT : 0765168293
SEHEMU YA KWANZA-01
"Mwizi mwizii mwiziii..", mayowe yalisikika, mayowe amabayo yalisambaa kwa kasi ya ajabu usiku ule, kitendo ambacho kilipelekea wanakijiji waliokuwa wamelala wakaamka ili kumkimbiza mwizi huyo ambaye alionekana kuwa kasi kukimbia kuokoa uhai wake. Mwizi huyo alifanikiwa kuruka vigingi mbali mbali, akakimbilia nje ya kijiji hicho akatokomea na kuwacha wanakijiji kwenye sintofahamu.
Wanakijiji hao wakajilaumu sana, kila mmoja alikuwa na hamu ya kumkata mwizi yule ili wamuadabishe. Lakini jambo hilo likawa limeenda kinyume na malengo yao. Mwizi aliwapotea.
Baada mwizi yule kuwapotea, wanakijiji waliamuwa kurudi majumbani mwao kulala. Kesho yake asubuhi palipo pambazuka mwenyekiti wa kijiji akamtaka mjumbe wake apige mbiyu kuitisha mkutano wa dharura. Dhumuni kuu la mkutano huo ni kujadili mustakabali wa matukio hayo ya wizi yaliyokuwa yakitokea mara kwa mara. Wakati mbiyu hiyo ya mgambo inalia, upande wa pili alionekana kijana Zabroni akihesabu fedha alizoiba usiku wa jana. Lakini kabla hajafikia tamati, akasikia sauti ya mama yake akimuita chumbani kwake. Hivyo alisitisha kisha akatii wito. "Naam mama nipo hapa"
"Una nini mwanangu? " Aliuliza mama Zabroni huku akigeuka kwa tabu kumtazama kijana wake. Akakohoa mara tatu mfululizo, kikohozi chepesi. Punde akaendelea kusema "Zabro mwanangu, mama yako tayari nimesha jihakikishia umauti. Huna sababu ya kuendelea kuiba mali za watu ili kuokoa maisha yangu. Tafadhali nakuomba achana na shuguli hiyo, utakufa kingali kijana mwanangu. Sasa fanya kazi za kilimo ili upate fedha za matumizi ya kawaida kwani mama yako sio waleo wala wakesho.. "
"Sikia mbiyu imelia, na hii ni kutokana na tukio lililo tokea jana. Najua fika wewe ndio muhusika, hakuna mwizi mwingine hapa kijijini. Je, unajua kwenye huo mkutano watakuwekea agenda gani? Za mwizi ni arobaini Zabroni, hebu achana na kazi hiyo haufai baba yabgu " Aliongeza kusema mama Zabroni, maneno hayo aliyaongea kwa sauti ya chini iliyojaa hofu na simanzi nzito ndani yake kitendo ambacho kilimpelekea Zabroni kudosha machozi. Lakini yote kwa yote akakubaliana na matakwa ya mama yake ili apate kumlizisha kulingana na hali tete aliyonayo, kamwe hapendi kumuona mama yake akikereka.
"Sawa mama nimekuelewa " Alijibu Zabroni kisha akarudi chumbani kwake kuendelea na zoezi lake la kuhesabu fedha alizoiba usiku wa jana kwanye duka la tajiri kijijini hapo, almaarufu kwa jina Mr. Mashaka.
"Milioni moja na nusu? Aaah pesa nyingi sana hizi, mpambanaji haogopi masikini hachoki, nitaendelea kuiba mpaka nitimize pesa ya kumsafirisha mama akatibiwe Hospitali ya kimataifa" Alijisemea Zabroni mara baada kupata idadi kamili ya pesa alizoiba siku hiyo. Furaha isiyo kifani ikawatawala moyoni mwake, upesi akazikusanya akazihifadhi kwenye mfuko mkubwa wa nailoni kisha akazifukia kwenye shimo maalumu alilokuwa amesha liandaa. Alipomaliza zoezi hilo akatoka ndani, nje akakutana na uso kwa uso na baba yake. Mzee Mwanamalindi. Mzee huyo alikuwa amelowa umande asubuhi hiyo huku uso wake ukionyesha kujaa hofu fulani. "Baba kuna tatizo?.." Zabroni akamuuliza baba yake. Lakini mzee Mwanamalindi hakujibu, aliingia ndani, moja kwa moja mpaka chumbani kwake ambapo huko alimtazama mkewe kwa macho ya huruma, akajisonya sambamba na kuketi kando yake. Akashusha pumzi ndefu na kujiuliza" Nimemkosea nini Mungu? Mbona matatizo hayakauki? Maisha haya nitaishi mpaka lini?.. " Maswali hayo aliyojiuliza mzee Mwanamalindi yaliambatana na machozi mepesi huku kinywa chake nacho kisikauke kujisonya. Kitendo hicho kikamstua mkewe. Mama Zabroni, ambapo aligeuka na kumuuliza mumewe kipi kinacho msibu.
"Loh! mke wangu nahisi kama dunia imenitenga, kila ninalo lifanya haliendi sawa kabisa mpaka muda mwingine najikuta namkufuru Mungu kwa kunileta duniani" Alisema mzee Mwanamalindi.
"Unaamaana gani?.." Akiwa na taharuki alihoji kwa mara nyingine mama Zabroni lakini kabla mumewe hajamjibu, ghafla nje ya nyumba yake ikasikika sauti ya amtu akabisha hodi.
"Subiri nikamsikilize kwanza huyu mtu, nakuja sasa hivi" Alisema mzee Mwanamalindi kisha akatii wito. Hofu na woga ulimjaa baada kufika nje kwani alimkamkuta mzee Fungafunga mdeni wake.
"Habari yako bwana Mwanamalindi" Fungafunga alimsalimu mzee mwenzake. Kwa woga na hofu mzee huyo akainamisha uso wake chini, papo hapo swali likamjia kichwani "Nitamueleza nini leo? Muda nilio muahidi kumlipa pesa zake umewadiwa?.." Alipokwisha kujiuliza swali hilo akaitikia salamu ile "Ni salama tu ingawa sio sana"
"Kwanini? Bado mkewe hali tete?.."
"Ndio bwana hata hivyo nafikiria kukopa pesa nyingine kwa mzee Malila ili niweze kumsafirisha kwenda mbali kidogo na hapa. Nimeambiwa kuna mtaalamu mmoja hivi anaweza kunisaidia "
"Sawa lakini yote kwa yote leo nataka pesa yangu, na sio ngonjera tena.." Alisema mzee Fungafunga huku akiwa amekasirika pasipo mfano.
Mwanamalindi akastuka kumuona mzee mwenzake akiwa katika hali hiyo, moyoni akajua siku hiyo mzee Fungafunga amekuja tofauti kabisa. Hivyo akajikuta hajui lipi la kufanya kwa sababu pesa ndani hakuwa nazo nawala hakujua kama usiku wa jana kijana wake kaiba pesa nyingi ambazo anaweza kulipa deni hilo na nyingine zikabaki.
"Mzee mwenzangu bado sijapata pesa yako, nimekwama tafadhali njoo kesho basi uhakika upo! Nipo chini ya miguu yako tafadhali " Alijitetea kwa mara nyingine tena mzee Mwanamalindi na wala hakuwa mzito kumpigia magoti mzee Fungafunga ili kudhihilisha kile anacho kisema. Lakini huyo katu hakutaka kuelewa propganda za mzee Mwanamalindi, akacheka kwa sarau sambamba na kuchomoa kibiriti ndani ya mfuko wa koti lake, akachomoa na sigara na kuipachika katika kinywa chake. "Sikia we masikini, ulikuja kwa mikono miwili kuomba msaada lakini malipo unasumbua kulipa. Umenizungusha mara ngapi? Au huna nia ya kuilipa?.." Akafyatua njiti akaiwasha sigara yake kisha akaendelea kusema "Mzee Mwanamalindi, hakuna asiye kuwa na matatizo. Sasa basi nakupa dakika tano tu, unipe pesa zangu la sivyo nachoma kibanda chako" Akamaliza kwa kicheko cha madaha sambamba na kupuruza moshi wa sigara mara mbili mfululizo.
Maneno hayo yalimstua mzee Mwanamalindi, kwa hofu akashusha pumzi ndefu huku akitafakari kipi cha kufanya sababu pesa hakuwa nayo muda huo, hali ya mzee Fungafunga alisimama kidete kutaka pesa zake.
"Nimekuelewa mzee mwenzangu, ngoja nikuletee" Alisema mzee Mwanamalindi na kisha kuingia ndani huku akiwa mnyonge mithili ya kifaranga kilicho nyeshewa na mvua. Moyoni mzee huyo alipania kuchukuwa uamuzi mgumu, kwani aliona dunia imemtenga. Akaingia chumbani kwa Zabroni akakata kamba aliyokuwa akitundikia nguo kijana wake kisha akajinyonga, mbali na kujiona kama dunia imemtenga, lakini pia mzee huyo aliona hana mbinu nyingine ya kujinusuru mbele ya mzee Fungafunga. Mzee asiye na masihara hata chembe pindi anapo dai chake.
Muda ulisonga mzee Fungafunga akimsubiri mzee Mwanamalindi amletee pesa yake. Baada kukatika takribani nusu saa, mzee huyo akaingiwa na imani haba. Moyoni akadhania kwamba mzee huyo kamtoroka kupitia mlango wa uwani na hivyo aliamuwa kuchoma nyumba moto ikiwa ndani yumo mzee Mwanamalindi ambaye tayari marehemu pamoja na mkewe ambaye ni mgonjwa asiye jiweza. Hali hiyo tata ilimpelekea mama huyo kushindwa kupiga mayowe kabisa, na hivyo ajali ya moto ikakatisha uhai wake.
"Jasho la mtu siku zote haliliwi" Akaanza kwa kicheko, mzee Fungafunga alisema maneno hayo kisha akaondoka mahali hapo huku nyuma akiacha moto ukitambaa kwenye nyumba kwa kasi ya ajabu. Punde baada mzee huyo kutokomea, kijana Zabroni naye alikuwa njiani akirudi nyumbani baada kutoka kijiweni kusikilizia watu wanazungumziaje wizi uliofanyika usiku wa ikiwa mwizi ni yeye mwenyewe.
Je, Zabroni atakuwa katika hali gani? KWA msiba huo??
Itaendelea
Mtunzi : sharobaro la jf
CONTACT : 0765168293
SEHEMU YA KWANZA-01
"Mwizi mwizii mwiziii..", mayowe yalisikika, mayowe amabayo yalisambaa kwa kasi ya ajabu usiku ule, kitendo ambacho kilipelekea wanakijiji waliokuwa wamelala wakaamka ili kumkimbiza mwizi huyo ambaye alionekana kuwa kasi kukimbia kuokoa uhai wake. Mwizi huyo alifanikiwa kuruka vigingi mbali mbali, akakimbilia nje ya kijiji hicho akatokomea na kuwacha wanakijiji kwenye sintofahamu.
Wanakijiji hao wakajilaumu sana, kila mmoja alikuwa na hamu ya kumkata mwizi yule ili wamuadabishe. Lakini jambo hilo likawa limeenda kinyume na malengo yao. Mwizi aliwapotea.
Baada mwizi yule kuwapotea, wanakijiji waliamuwa kurudi majumbani mwao kulala. Kesho yake asubuhi palipo pambazuka mwenyekiti wa kijiji akamtaka mjumbe wake apige mbiyu kuitisha mkutano wa dharura. Dhumuni kuu la mkutano huo ni kujadili mustakabali wa matukio hayo ya wizi yaliyokuwa yakitokea mara kwa mara. Wakati mbiyu hiyo ya mgambo inalia, upande wa pili alionekana kijana Zabroni akihesabu fedha alizoiba usiku wa jana. Lakini kabla hajafikia tamati, akasikia sauti ya mama yake akimuita chumbani kwake. Hivyo alisitisha kisha akatii wito. "Naam mama nipo hapa"
"Una nini mwanangu? " Aliuliza mama Zabroni huku akigeuka kwa tabu kumtazama kijana wake. Akakohoa mara tatu mfululizo, kikohozi chepesi. Punde akaendelea kusema "Zabro mwanangu, mama yako tayari nimesha jihakikishia umauti. Huna sababu ya kuendelea kuiba mali za watu ili kuokoa maisha yangu. Tafadhali nakuomba achana na shuguli hiyo, utakufa kingali kijana mwanangu. Sasa fanya kazi za kilimo ili upate fedha za matumizi ya kawaida kwani mama yako sio waleo wala wakesho.. "
"Sikia mbiyu imelia, na hii ni kutokana na tukio lililo tokea jana. Najua fika wewe ndio muhusika, hakuna mwizi mwingine hapa kijijini. Je, unajua kwenye huo mkutano watakuwekea agenda gani? Za mwizi ni arobaini Zabroni, hebu achana na kazi hiyo haufai baba yabgu " Aliongeza kusema mama Zabroni, maneno hayo aliyaongea kwa sauti ya chini iliyojaa hofu na simanzi nzito ndani yake kitendo ambacho kilimpelekea Zabroni kudosha machozi. Lakini yote kwa yote akakubaliana na matakwa ya mama yake ili apate kumlizisha kulingana na hali tete aliyonayo, kamwe hapendi kumuona mama yake akikereka.
"Sawa mama nimekuelewa " Alijibu Zabroni kisha akarudi chumbani kwake kuendelea na zoezi lake la kuhesabu fedha alizoiba usiku wa jana kwanye duka la tajiri kijijini hapo, almaarufu kwa jina Mr. Mashaka.
"Milioni moja na nusu? Aaah pesa nyingi sana hizi, mpambanaji haogopi masikini hachoki, nitaendelea kuiba mpaka nitimize pesa ya kumsafirisha mama akatibiwe Hospitali ya kimataifa" Alijisemea Zabroni mara baada kupata idadi kamili ya pesa alizoiba siku hiyo. Furaha isiyo kifani ikawatawala moyoni mwake, upesi akazikusanya akazihifadhi kwenye mfuko mkubwa wa nailoni kisha akazifukia kwenye shimo maalumu alilokuwa amesha liandaa. Alipomaliza zoezi hilo akatoka ndani, nje akakutana na uso kwa uso na baba yake. Mzee Mwanamalindi. Mzee huyo alikuwa amelowa umande asubuhi hiyo huku uso wake ukionyesha kujaa hofu fulani. "Baba kuna tatizo?.." Zabroni akamuuliza baba yake. Lakini mzee Mwanamalindi hakujibu, aliingia ndani, moja kwa moja mpaka chumbani kwake ambapo huko alimtazama mkewe kwa macho ya huruma, akajisonya sambamba na kuketi kando yake. Akashusha pumzi ndefu na kujiuliza" Nimemkosea nini Mungu? Mbona matatizo hayakauki? Maisha haya nitaishi mpaka lini?.. " Maswali hayo aliyojiuliza mzee Mwanamalindi yaliambatana na machozi mepesi huku kinywa chake nacho kisikauke kujisonya. Kitendo hicho kikamstua mkewe. Mama Zabroni, ambapo aligeuka na kumuuliza mumewe kipi kinacho msibu.
"Loh! mke wangu nahisi kama dunia imenitenga, kila ninalo lifanya haliendi sawa kabisa mpaka muda mwingine najikuta namkufuru Mungu kwa kunileta duniani" Alisema mzee Mwanamalindi.
"Unaamaana gani?.." Akiwa na taharuki alihoji kwa mara nyingine mama Zabroni lakini kabla mumewe hajamjibu, ghafla nje ya nyumba yake ikasikika sauti ya amtu akabisha hodi.
"Subiri nikamsikilize kwanza huyu mtu, nakuja sasa hivi" Alisema mzee Mwanamalindi kisha akatii wito. Hofu na woga ulimjaa baada kufika nje kwani alimkamkuta mzee Fungafunga mdeni wake.
"Habari yako bwana Mwanamalindi" Fungafunga alimsalimu mzee mwenzake. Kwa woga na hofu mzee huyo akainamisha uso wake chini, papo hapo swali likamjia kichwani "Nitamueleza nini leo? Muda nilio muahidi kumlipa pesa zake umewadiwa?.." Alipokwisha kujiuliza swali hilo akaitikia salamu ile "Ni salama tu ingawa sio sana"
"Kwanini? Bado mkewe hali tete?.."
"Ndio bwana hata hivyo nafikiria kukopa pesa nyingine kwa mzee Malila ili niweze kumsafirisha kwenda mbali kidogo na hapa. Nimeambiwa kuna mtaalamu mmoja hivi anaweza kunisaidia "
"Sawa lakini yote kwa yote leo nataka pesa yangu, na sio ngonjera tena.." Alisema mzee Fungafunga huku akiwa amekasirika pasipo mfano.
Mwanamalindi akastuka kumuona mzee mwenzake akiwa katika hali hiyo, moyoni akajua siku hiyo mzee Fungafunga amekuja tofauti kabisa. Hivyo akajikuta hajui lipi la kufanya kwa sababu pesa ndani hakuwa nazo nawala hakujua kama usiku wa jana kijana wake kaiba pesa nyingi ambazo anaweza kulipa deni hilo na nyingine zikabaki.
"Mzee mwenzangu bado sijapata pesa yako, nimekwama tafadhali njoo kesho basi uhakika upo! Nipo chini ya miguu yako tafadhali " Alijitetea kwa mara nyingine tena mzee Mwanamalindi na wala hakuwa mzito kumpigia magoti mzee Fungafunga ili kudhihilisha kile anacho kisema. Lakini huyo katu hakutaka kuelewa propganda za mzee Mwanamalindi, akacheka kwa sarau sambamba na kuchomoa kibiriti ndani ya mfuko wa koti lake, akachomoa na sigara na kuipachika katika kinywa chake. "Sikia we masikini, ulikuja kwa mikono miwili kuomba msaada lakini malipo unasumbua kulipa. Umenizungusha mara ngapi? Au huna nia ya kuilipa?.." Akafyatua njiti akaiwasha sigara yake kisha akaendelea kusema "Mzee Mwanamalindi, hakuna asiye kuwa na matatizo. Sasa basi nakupa dakika tano tu, unipe pesa zangu la sivyo nachoma kibanda chako" Akamaliza kwa kicheko cha madaha sambamba na kupuruza moshi wa sigara mara mbili mfululizo.
Maneno hayo yalimstua mzee Mwanamalindi, kwa hofu akashusha pumzi ndefu huku akitafakari kipi cha kufanya sababu pesa hakuwa nayo muda huo, hali ya mzee Fungafunga alisimama kidete kutaka pesa zake.
"Nimekuelewa mzee mwenzangu, ngoja nikuletee" Alisema mzee Mwanamalindi na kisha kuingia ndani huku akiwa mnyonge mithili ya kifaranga kilicho nyeshewa na mvua. Moyoni mzee huyo alipania kuchukuwa uamuzi mgumu, kwani aliona dunia imemtenga. Akaingia chumbani kwa Zabroni akakata kamba aliyokuwa akitundikia nguo kijana wake kisha akajinyonga, mbali na kujiona kama dunia imemtenga, lakini pia mzee huyo aliona hana mbinu nyingine ya kujinusuru mbele ya mzee Fungafunga. Mzee asiye na masihara hata chembe pindi anapo dai chake.
Muda ulisonga mzee Fungafunga akimsubiri mzee Mwanamalindi amletee pesa yake. Baada kukatika takribani nusu saa, mzee huyo akaingiwa na imani haba. Moyoni akadhania kwamba mzee huyo kamtoroka kupitia mlango wa uwani na hivyo aliamuwa kuchoma nyumba moto ikiwa ndani yumo mzee Mwanamalindi ambaye tayari marehemu pamoja na mkewe ambaye ni mgonjwa asiye jiweza. Hali hiyo tata ilimpelekea mama huyo kushindwa kupiga mayowe kabisa, na hivyo ajali ya moto ikakatisha uhai wake.
"Jasho la mtu siku zote haliliwi" Akaanza kwa kicheko, mzee Fungafunga alisema maneno hayo kisha akaondoka mahali hapo huku nyuma akiacha moto ukitambaa kwenye nyumba kwa kasi ya ajabu. Punde baada mzee huyo kutokomea, kijana Zabroni naye alikuwa njiani akirudi nyumbani baada kutoka kijiweni kusikilizia watu wanazungumziaje wizi uliofanyika usiku wa ikiwa mwizi ni yeye mwenyewe.
Je, Zabroni atakuwa katika hali gani? KWA msiba huo??
Itaendelea