Simulizi ya kusisimua- (penzi la mfungwa)

Simulizi ya kusisimua- (penzi la mfungwa)

umeirudia
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi : Sharobaro la jf
CONTACT : 0765168293

SEHEMU YA NANE-08

Moto ule uliokuwa unawaka kwenye nyumba ya mzee Ngurumo uliwastua sana wanakijiji,pia hata mzee Baluguza naye alionyesha kustuka ingawa sio rahisi kutumbua endapo kama ukimtazama usoni kwa pupa. Ngurumo alitaharuki baada kuona nyumba inaungua, alipasa mayowe huku akijing'atua eneo alilokuwa amekaa akitaka kwenda walau kuokoa baadhi ya vitu vilivyokuwemo ndani,lakini kabla hajaondoka,Mwenyekiti alimshika mkono akamvuta karibu yake kisha akasema "Hata ukiondoka hutaweza kuokoa kitu chochote mzee mwenzangu, kwahiyo nakusihi hebu punguza jazba ili leo tumtambue kirusi wa kijiji hiki" alisema Mwenyekiti akimwambia mzee Ngurumo ambaye muda huo alikuwa akilia kilio cha mtu mzima. Mke wake alisimama akilia machozi mithili ya mke aliyefiwa na mumewe,mwanamke huyo akamkumbatia mumewe huku akiangua kilio. Kitendo hicho kilitia simanzi mkutanoni hapo,baadhi ya wakina mama na wakina baba wenye hekima walijaribu kuwatuliza wazee hao,nao kila mmoja alitulia kwa muda wake ingawa mioyoni mwao wakiwa wamefura hasira zisizo na mfano.
Utulivu ulipo tawala,mzee Baluguza akaanza kufanya mambo yake akiwa na nia ya kumuweka hadharani kirusi huyo wa kijiji,kwenye mti mnene kiasi alibandika kitambaa cheupe huku akiimba nyimbo zake za asiri. Alipo maliza aliwaambia wanakijiji wawe makini kukitazama hicho kitambaa umakini na utulivu ukaongezeka kwa wanakijiji hao ilihali kijana Zabroni naye akiwa hajui chochote ila aliamini kuwa huyo mzee hawezi kitu chochote juu yake. Na wakati akijiaminisha hayo ndani ya nafsi yake,Ghafla kwenye kile kitambaa cheupe alionekana Zabroni akiwa anafanya kile kitendo kwenye Nyumba ya mzee Ngurumo. Wanakijiji walitaharuki kila mmoja alionekana kushungaa, ilihari Zabroni naye alijikuta akijishangaa na kujiuliza maswali mengi kichwani mwake juu ya kile kilicho kuwa kikiendelea kwenye kitambaa kile cheupe. Aliingiwa na hofu pasipo kuchelewa alisimama akaanza kunuia maneno yake ili apate kupotea maeneo hayo lakini kabla hajatamka chochote,kundi la wanakijij likaanza kumvagaa na kisha kumpiga. Zabroni alichezea kipigo cha mbwa mwizi ila baadaye kidogo alifanikiwa kupotea katikati ya umati wa watu,ajabu aliwaachia nguo zake tu. Kitendo hicho kiliwastua wanakijiji,hapo sasa kila mmoja akajawa na hofu huku maswali yaliyokosa majibu yakitawala akili mwao. Ni kitendo ambacho kilimshangaza sana mzee Baluguza, alijiuliza uwezo gani alio nao kijana huyo, Na baada kumaliza shughuli hiyo aliona hakuna haja ya kuendelea kukaa kijijini hapo kwani kwa maono yake aliona kamwe hatoweza kufua DAFU kumkabili Zabroni, ili kulinda uhai wake aliamua kufunga safari usiku wa manane kurudi kijijini kwao. "Nayapenda maisha yangu", alijisemea mzee Baluguza ndani ya nafsi yake huku akiandaa vilago vyake. Hatimaye kila kitu kilikaa sawa, na sasa alianza safari wakati anatoka nyumbani hapo kwa Mwenyekiti alipokuwa amefikia,punde si punde Zabroni alitua maeneo hayo. Akiwa na lengo moja tu ambalo ni kutekeleza ahadi yake aliyojiwekea. Pasipo kupoteza muda Zabroni alichukuwa kamba yake akaitambalika kisha akachoma moto. Moto ambao ulianza kutembea pole pole kuelekea kwenye nyumba wakati huo yeye tayari ameshapotea eneo hilo,nia kuu ya kijana Zabroni kuwahi kuchoma moto nyumba ya Mwenyekiti ni kumuuwa mzee Baluguza ili apate kufanya kazi yake kwa uhuru zaidi bila kubuguziwa na mtu yoyote, aliona kama mzee huyo anataka kuharibu mkakati wake.
"Kufa tu hakuna namna mwanaharamu mkubwa wewe", aliongea Zabroni na hata asijue kuwa tayari amechelewa kwani mzee Baluguza alishafungasha vilango vyake na kuondoka zake. Ule moto uliendelea kutembea kwenye kamba ile kwa kasi ya ajabu ila kabla haujanasa kwenye nyasi za nyumba,zilisikika kelele za mbwa wakibweka kwa nguvu kiasi kwamba mkewe Mwenyekikiti ilimfanya aamke na kisha kumwamsha mumewe ili atoke nje akatazame ni nini kinacho endelea huko. Kumbe wakati Zabroni anaondoka nyumbani hapo kwa Mwenyekiti alijibadilisha akawa katika umbo la kutisha liliacha harufu mbaya ambayo iliwafanya mbwa kubweka kuashiria nje kuna kitu cha hatari, Mwenyekiti akamsikiliza mkewe haraka sana akatoka nje ambapo alizunguka nyuma ya nyumba akakuta moto tayari umeshika nyumba. "MOto moto motoooo" alilalama Mwenyekiti usiku ule wa manane, mkewe akiwa ndani akastuka alipotaka kukimbia akajikuta anazima kibatali kilichokuwa kinawaka. Hapo sasa aliukosa mlango wa kutokea kwamaana ndani palikuwa na giza nene,upande wa pili napo Mwenyekiti alikuwa akihaha japo kuuzima kwa mchanga lakini alipoona moto unazidi kukolea alirudi hima upande ulipo mlango ili amuamshe mzee Baluguza pia amtoe ndani mke wake,lakini kabla hajafanya jambo lolote,moto ulifunika nyumba nzima kwani muda ule kulikuwa na upepo mkali uliofanya moto kutambaa kwa kasi zaidi. Mwenyekiti akajikuta anashindwa afanye nini, alibaki amesimama huku mikono akiwa ameweka kichwani pia akilia kilio cha mtu mzima akilitaja jina la mkewe aliyepoteza maisha kwa ajari hiyo ya moto. Baada ya lisaalimoja mwanakijiji mmoja mmoja alijitokeza kwa Mwenyekiti kuja kushuhudia kitu gani kimetokea,walimkuta Mwenyekiti wao akiwa mnyonge asijue cha kuwaambia. Hakika walichoka sana kila moja aliona hakuna haja ya kuendelea kuishi katika hicho kijiji cha mauaji ya kinyama,na hivyo baadhi za familia zilianza kufanya mikakati ya kukikimbia kijiji hicho. Alfajiri mapema mbiyu ililia kwa mara nyingine,mbiyu hiyo ilitangaza maafa yalitokea kwa Mwenyekiti huku mtoa taarifa aliwajuza wanakijiji kuwa Mwenyekiti kafiwa na mke wake usiku wa jana,alienda mbali zaidi na kusema si mke wake bali na mzee Baluguza. Hapo wanakijiji walizidi kuchanganyikiwa kwa taarifa ile "Mmh sio bure huyu mtu atakuwa anakisasi na kijiji hiki ", alisema mzee mmoja mlemavu akiwa ndani ya nyumba yake ya matete asubuhi hiyo baada kusikia hiyo taarifa. Na wakati mpiga mbiyu anaendelea kutangaza taarifa hapo kijiji,mara ghafla akafika eneo lile walilo fanyia mkutano siku iliyopita. Punde alistua mpiga mbiyu huyo baada kuona damu chini ya mti huo ambao waliutumia kumwona mtukutu Zabroni akichoma nyumba ya mzee Ngurumo. Mpiga mbiyu akajiuliza "Damu hii kakamatwa nguruwe pori ama?..", akiwa na wasi wasi alijiuliza hilo swali,tonya la damu likamdondokea kutoka juu ya mti huo. Aliinua uso wake kutazama juu akauona mwili wa mzee Baluguza ukiwa unaning'inia huku damu zikivujia kwenye shingo. Alichinjwa kikatiri mtaalamu Baluguza. Mpiga mbiyu alistuka,mwili ulimsisimka huku akitetemeka kwa hofu, muda huo huo ilisikika sauti ikijirudia mara mbili mbili, ilikuwa sauti ya Zabroni Sauti ya ilisema "Zabroni! Zabroni " sauti hiyo ilimaliza kwa kicheko kizito.

USIKOSE MUENDELEZO

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi : Sharobaro la Jf
CONTACT : 0765168293

SEHEMU YA KUMI-10

Zabroni alipotea baada kufanya unyama ule,alimuacha mama mjamzito tumbo lake likibubujika damu baada kutolewa vijusi vilivyokuwemo kwenye tumbo hilo,ulikuwa ni unyama ulio pitiliza kipimo kiasi kwamba binadamu mwenye roho nyepesi hawezi kufanya hicho kitendo.
Upande wa pili yule jamaa alipo maliza mikakati yake alianza safari kumfuata mkewe huku moyoni akiwa na hofu kwani mapigo ya moyo wake kuna muda yalikuwa yakimuenda mbio pia wasiwasi nao ukimtawala kila mara,alijiuliza maswali kuhusu hali hiyo ambayo ningeni kabisa kuwahi kumtokea. Lakini jamaa huyo alipiga moyo konde kisha akaanza safari,kabla hajakimaliza kijiji ghafla akasikia mzee mmoja akimshuhudia mzee mwenzake kitu alichokiona huko porini. Mzee huyo alisema "Ama hakika tunako elekea sasa hii dunia imefika mwisho"
"Kwanini tena mzee mwenzangu? .."
"Dah huwezi amini nimekuta mama mmoja pori lile la miti mingi kapasuliwa tumbo,vile vitoto sasa vimetundikwa juu kama mishikaki " alijibu huyo mzee huku akifatia na sikitiko.
"Lahaulla..Mungu tutazame waja wako sisi mmmmh ", alisikika mzee msimuliwa akisema maneno hayo kwa sikitiko, na wakati wanasemazana hayo, kijana yule mwenye mke aliyetumbuliwa tumbo alistuka bila kupoteza muda alitimua mbio kuelekea huko ili akatazame kama ni mkewe ndio kafanyiwa hicho kitendo. Alipofika alimkuta ni mkewe kauliwa kikatili, hakika alilia sana hasa hasa alipovitazama vijusi vile vilivyo ning'inizwa juu kwenye mti kama mshikaki. Hali hiyo ilimpelekea kudata, uchungu wa kufiwa na mkewe aliyempenda kwa dhati ulimfanya kuwa kichaa. Dhambi na dumu nzito ikazidi kutanda juu ya kijana Zabroni,alifanya hayo akiamini kwamba analipa kisasi juu ya kifo cha wazazi wake. Habari ya hayo mauaji ilisambaa kila kona,na kila aliyeipata alihuzunika huku baadhi yao wakijiuliza ni roho gani aliyonayo muuwaji huyo?. Majibu alikosa,na baadhi ya watu kutoka vijiji vya jirani walitamani japo kwa dakika sifuri wamtie machoni mtukutu huyo. Na mara baada ya kufanya mauaji hayo,alitulia kwa takribani wiki mbili. Wanakijiji walipata ahueni wakiamini kuwa huwenda Zabro kauliwa kutoka na dhambi zake,lakini imani hiyo punde ilitoweka baada kuchomwa nyumba nyingine usiku wa manane. Na hapo ndipo hofu ilipo rudia kutanda kunako mioyo yao. Kwa kuamini hilo,mzee Fungafunga ambaye ndio chanzo hasa ya matatizo hayo aliingiwa na hofu aliamini kuwa muda wowote naye zamu yake itafika. Na wakati huyo mzee akiamini hilo jambo kutendeka muda wowote, upande wa pili kijiji jirani. Kijiji ambacho kilionekana kuchangamka kulingana na mishe mishe zake,lilionekna kundi la vijana wakicheza kamali. Kamali hiyo kimuonekano ilikuwa ya mazingaombwe. Unapewa lingi ndogo unailipia pesa kisha unaambiwa uchague mahala pakuirusha kwenye mazaga zaga waliyosambaza. Palikuwa na pesa zaidi ya ile unayoliyolipia lingi, vile vile palikuwa na juisi soda na mazaga zaga mengine ambayo ukiirushe ile lingi iwezekanike kuvivaa. Mchezo huo uliandelea kwa vijana wa pale,wengi walikosa kiasi kwamba baadhi yao iliwapelekea kununua lingi nyingi wakiamini kuwa huwenda wakafanikiwa. Lakini mambo bado yaliendelea kuwa vile vile bado waliangukia pua,wenye moyo mwepesi waliondoka zao huku wenye roho ngumu wakizidi kukomaa. Na wakati kamali hiyo inaendelea,ghafla walionekana vijana wawili wakiwa na mabegi yao mgongoni. Vijana hao wa makamo walionekana ni wageni katika hicho kijiji,kwani nyuso zao zahili shahili zilionyesha. Walipokuwa katika pitapita yao waliuona mchezo ule wa kamali uliokuwa unaendelea. Kijana mmoja ambaye aliitwa Madebe alimshika bega mwenzake kisha akasema "Bruno,pesa imetuishia. Kiukweli iliyobaki haitoshi halafu istoshe bado tunasafari ndefu. Vipi tufanyeje?..",alisema Madebe huku akikodolea macho upande ule uliojaa watu wacheza kamali pamoja na watazamaji.
"Doh ni kweli kaka,lakini unadhani tutafanyaje sasa"
"Hivi ile hirizi ipo humo kwenye begi?.." alihoji Madebe.
"Ndio ipo" alijibu Bruno.
"Sawa hebu nipe tusogee pale Kwenye kamali,unajua huu mchezo wanatia kiini macho,kwahiyo kwa kuwa wao wanafanya ujinga acha na sisi tufanye upumbavu", alisema Madebe. Bruno akaangua kicheko huku akifungua zipu ili ampe kaka yake hirizi. Alipo mkabidhi, Madebe aliivaa kisha akasogea eneo lile, alilipia lingi. Safari ya kwanza aliirusha kwenye pesa,akawfanikiwa. Akarudia kurusha kwenye pesa lingi ya pili,nayo vile vile akifanikiwa. Hapo sasa taita akaona Madebe anawaumbua,upesi alimuita kando kisha akasema "Ndugu naomba tusihalibiane kazi,nina familia inanitegemea sawa. Kwahiyo naomba upotee hapa mara moja kabla hatujahalibiana siku" Taita kiongozi wa kamali ile aliongea kwa sauti ya kunong'ona huku uso wake akiwa ameukunja. Madebe alipo ambiwa maneno hayo hakutaka kubishana naye,alimuita mdogo wake kisha wakaondoka zao wakati huo nyuma yao wakimuacha Taita anawasindikiza kwa macho.
Madebe na Brruno tayari walikuwa na pesa ya kuanzia huko wanako elekea, walikwenda kwenye mgahawa kula chakula kabla hawajaendelea na safari ya kuelekea kijiji kilw kinacho endelea maafa kwa niaba ya kutafuta vibarua ikiwa kama njia ya utafutaji wa pesa. Walanguzi. Wawili hao walipokuwa mgahawani, ghafla akaingia Zabroni . Hakutaka kuongea na mtu zaidi aliketi kisha akaagiza chakula akala, alipomaliza akaondoka zake bila kulipa. Hiyo ndio ilikuwa tabia yake sasa baada kujiona ni tishio kila pande. Ni tabia ambayo iliwakera mama ntilie wa kijiji kile lakini kutokana sifa mbaya na yakutisha aliyokuwa nayo Zabroni,mama ntilie hao walimuogopa sana kwa maana hiyo hata pesa ya chakula walikuwa hawamdai. Ila siku hiyo ilikuwa siku tofauti kidogo kwa mama ntilie huyo,alisikika akisema kwa jazba "Mijitu mingine bwana. Akha yanakera sio siri "
"Kwanini mama?..",alihoji Madebe baada kusikia mama huyo akilalama.
"Yani we acha tu,huyu jamaa hafai hata kidogo. Anachoma nyumba za watu anauwa bila hatia yani sijui anaroho gani huyu mtu. Ubabe na yeye na na ubabe sijui kwanini serikali inaendelea kumuangalia. ", Madebe na Bruno walistuka kusikia habari hiyo, ni habari ambayo iliwacha midomo wazi Kiukweli.
"Kwahiyo unataka kusema kashindikanika?..", kwa taharuki Bruno aliuliza.
"Kabisa hawezekaniki,anatumia dawa"
"Daah poleni sana", alimaliza kwa kusema hivyo Madebe kisha wakalipia chakula walicho kula wakaendelea na safari yao. Walitumia saa moja na nusu kufika,walipofika walipigwa na butwaa baada kukuta nyumba zikiwa majivu huku nyinginezo zikisalia kuta. Vilio kila kona kijijini hapo,Madebe akamgeukia Bruno kisha akasema "Hii hali inatisha sana, na bila shaka huyu ndio yule mshenzi tuliye ambiwa na mama ntilie..."
"Kweli kabisa kaka, je tuchukue hatua gani sasa maana hii hali yatisha ujue" alijibu Bruno huku akiangaza kila kona ya kijiji.
"Daah! Nafikiri ni kupambana naye tu hakuna namna"
"Je, tutampataje?.." ,Madebe aliingiza mkono mfukoni akatoa kitambaa cheusi chenye fundo akafungua fundo ambalo lilikuwa na unga mweusi. Unga huo aliupakaza kwenye kiganja kisha akasema "Tazama kiganjani kwangu ", Bruno akatazama alimuona Zabroni akiwa kwenye makaburi mawili,makaburi ya mama na baba yake. "Umeona? Huyu jamaa hapa ndio makazi yake. Sasa mdogo wangu lazima tule nage sahani moja..tuombe kwanza kibali cha kuishi kijijini hapa kisha tufanye kazi yetu kwa utulivu", aliongea Madebe,kijana aliyetunikiwa miradhi ya ndagu kutoka kwa marehemu babu yake.

JE MADEBE ATAWEZA KUFUA DAFU?
Usikose maendeleo, nani atamfunga paka kengere?
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0765168293

SEHEMU YA KUMI NA MOJA-11

Madebe pamoja na Bruno walizipiga hatua kuelekea kwenye nyumba moja kijijini hapo wakiwa na lengo la kumuulizia Mwenyekiti wa kijiji,kwenye mji huo waliwakuta watoto. Watoto hao walionekana wanyonge sana hasa kutokana na mambo maovu yaliyokuwa yanaendelea hapo kijijini huku wao wakishuhudi kwa macho yao,hali hiyo ya unyonge kwa watoto iliwauma sana Madebe na Bruno lakini iliwapasa kupiga moyo konde wakawauliza watoto hao wapi walipo wazazi wao. Mtoto mmoja mkubwa kuliko wote alijibu "Mama na baba hawapo wameenda shamba", alijibu mtoto huyo huku akionekana kuwa na hofu,nao hao vijana baada kupata jibu hilo kutoka kwa mtoto huyo waliendelea na safari yao,ilihali macho yao yakionekana kutazama kila pande ya kijiji kutazama jinsi kijiji kilivyo chakaa majivu yaliyotokana na nyumbaa kuungua.
Hatimaye walifika kwenye nyumba ya pili,hapo waliwakuta wenye nyumba. Madebe alijitambulisha pia alimtambulisha na mdogo wake kisha wakasema nia na dhumuni ya kufika kijijini hapo,nia yao ni kusaka maisha kwa njia ya kilimo. Vile vile walisema kuwa ni vema kabla ya kuanza kazi waonane kwanza na Mwenyekiti wa kijiji ili pindi yatakapo tokea matatizo basi wajue ni jinsi gani ya kuweza kusaidiana. Baba mwenye nyumba hiyo aliwaelekeza mahali ilipo nyumba ya Mwenyekiti wa kijiji,Madebe na Bruno wakaelekea huko ambapo walimkuta Mwenyekiti akijenga nyumba yake ndogo baada kubwa aliyokuwa akiishi hapo wali kuungua na moto.
"Hodi hapa ", alisema Madebe,mwenyekiti alipo sikia sauti hiyo alisitisha zoezi lake la kuparata udongo pembeni kisha akageukia kule ilipotokea sauti. Aliwaona vijana wawili. Vijana hao walikuwa wageni kabisa machoni mwake. Hivyo kimoyo moyo alijisemea "Ugeni huu", wakati anasema hayo tayari hao vijana walikuwa wameshajongea Karibu yake kabisa.
"Shikamoo mzee"
"Shikamoo babu" Madebe na Bruno walimsalimia Mwenyekiti. "Malahabaa hamjambo? Karibuni sana", alijibu Mwenyekiti huku akiwasogezea benchi ili wapate kukaa. Walikaa kisha utambulisho ukafuatia,Madebe alijitambulisha pia akamtambulisha na Bruno. Na mwisho wa yote Madebe alieleza lengo kuu lililowafanya waje hapo kijijini,na katika malengo hayo hawakuweza kusema kama wanamikakati ya kulikomesha tatizo sugu linalo kikumba kijiji hicho.
"Karibuni sana vijana,kweli siku zote ujana ndio nafasi pekee ya kujijenga kiuchumi ili uzeeni usipate shida. Hakika nyinyi ni mfano wa kuigwa, lakini je mtapaweza hapa?..", alihoji Mwenyekiti, Madebe na Bruno walitazamana kisha Bruno akajibu "Siku zote mtaka cha uvunguni sharti ainame. Kwahiyo sisi tuatapewaza tu kama nyinyi wazee mnapaweza sembuse sisi? Tena vijana wanye nguvu zetu?.." Madebe naye alidakia akasema "Kwani ni sababu ipi ambayo inakutia hofu kuwa sisi hatukiwezi kijiji hiki? .." Mwemyekiti hakujibu zaidi alishusha pumzi kwanza kisha akajibu "Zabroni! Zabroni, kijana mtukutu ambaye tangu nizaliwe sijawahi kumuona kijana kama huyu. Hana hata chembe ya huruma,tangu wazee wake wauliwe kwa kuchomwa moto wakiwa ndani ya nyumba basi amekuwa muuaji,katili yani doh",alidondosha machozi Mwemyekiti huku akisimulia jinsi mtukutu Zabroni anavyofanya mambo ambayo binadamu wa kawaida hawezi kufanya,jambo kuu ambalo lilimuuma Mwenyekiti wakati anasimulia hayo ni kuhusu kifo cha mkewe pia na kifo cha mzee Baluguza.
"Pole sana mzee wetu lakini kuhusu hilo wewe usijali sisi tutavumilia istoshe tuna malengo na maisha yetu,mpambanaji hachoki mzee wetu" alisema Buruno.
Walipata nafasi ya kulaza mbavu zao,kesho yake asubuhi Mwenyekiti aliambatana na vijana hao mpaka nyumbani kwa muhindi,ambaye ndio tajiri wa kijiji. Hapo mwenyekiti aliamini lazima jamaa huyo atakuwa na shida na vibarua kwani ni mara chache sana shambani kwake kukaukiwa vibarua lakini kutokana na mambo yaliyokuwa yanajili kijijini hapo ikafikia hatua vibarua wakaadimika. Vibarua walipata, hekari mbili walikabidhiwa za kupalilia zao la muhogo huku hifadhi yani mahali pa kulala ikiwa ni kwa Mwenyekiti.
Kesho yake asubuhi walianza kazi,walifanya kazi huku mioyoni mwao wakiwa na lengo lao lile lile ambalo ni kumshikisha adabu mtukutu Zabroni, na lengo lao hilo waliliweka siri yao wawil pasipo kumwambia mtu yoyote.
Siku zilisonga wakiendelea kufanya vibarua, walisaidiana na Mwenyekiti kujenga nyumba kwa mapema zaid wakawa sasa wanalala ndani kwa amani kwani kipindi hicho Zabroni alikuwa ametuliza makeke yake. Miezi takribani miwili sasa ilikatika,hali ikiwa shwari kijijini hapo. Hakika ilikuwa ni jambo la furaha sana kwa wanakijiji, na hapo ndipo uvumi ulipoa anza kuzagaa kila kona ya kijiji pamoja na vijiji jirani wakivumisha kwamba Zabroni kauliwa,wengine wakisema katiwa uchizi huku wengine wakidiriki kuvumisha ya kwamba kijana huyo mtukutu kafungwa jela. Ila baadae uvumi huo ulikuja kuonekana si chochote si lolote baada usiku mmoja kuungua nyumba. Lakini pia usiku huo huo jeshi la polisi lilivamia kijiji hicho wakimtafuta Zabroni pasipo kujua kuwa kijana huyo anatumia dawa hakamatiki kirahisi. Jeshi hilo lilikesha likifanya dolia, kesho yake asubuhi ndipo lilipogundua kwamba kijana huyo wanayemtafuta ni mtu hatari sana. Polisi hao waliamini hilo jambo baada kuona nyumba nyingi zimeunguzwa kuachilia mbali hiyo iliyounguzwa usiku wa jana huku wao wakiwa humo humo kijijini. Hivyo waliendelea na kazi yao wakizunguka huku na kule huku wakishirikiana na mwanakijiji mmoja ambaye alijitolea kuwatembeza polisi hao akiwapeleka maeneo ambayo Zabroni hupenda kukaa. Walitembea kila sehemu lakini hadi jua linazama kamwe hawakuweza kumuona,ila kesho yake asubuhi hivyo hivyo harakati ziliendelea. Kama ilivyo ada walizulura kila kona kuanzia asubuhi mpaka jua la saa saba mchana,bado hawakuweza kumuona. Jioni ilipofika,polisi hao wakiwa tayari wamekata tamaa walirudi sasa kwenye gari yao ili wakapumzike. Ghafla mwanakijiji walio kuwa nae alimuona Zabroni akiwa juu ya tanuru akipangua matofali,mwanakijiji huyo alistuka akasimama kisha akasema kwa sauti ya chini. "Haya sasa mtu mwenye yuleee", alisema huku akinyoosha kidole chake kuelekea kule alipo Zabroni ambaye alionekana kuwa bize kupangua matofali kwenye tanuru la mzee Maguso,mzee ambaye anamkubali sana katika maisha yake. Kwa maana hiyo baadhi ya shughuli mbali mbali alikuwa akimsaidia,lakini pia kilichokuwa kikimfanya Zabroni ampende huyo mzee ni pale alipokuwa akimtia moyo na ujasiri katika mambo yake ya kulipa kisasi.
Jeshi hilo baada kumuona mtuhumiwa,hawakutaka kuamini mapema. Hivyo walichukuwa picha waliyokuwa nayo wakaitazama kisha wakamtazama na Zabroni kule alipo,ingawa alikuwa ameinamisha uso wake lakini kuna baadhi ya vitu walivitazama wakaamini kuwa ni yeye. Hapo ndipo waliposogea mpaka kwenye tanuru,kwa amri wakamtaka Zabroni ashuke kutoka juu ya tanuru. Zabroni aligoma alisema "Sishuki,kwani nyinyi akina nani? Na mnataka nini?.." majibu ya Zabroni yaliwastua polisi hao,mmoja akasema kwa sauti kali "Alo kwahiyo unapingana na serikali? Shuka haraka sana ..", alisema polisi huyo huku akimnyooshea bastora Zabroni. Lakini bado Zabro alionyesha kutostuka,kwa ujasiri alijibu "Sishuki mkitaka fanyeni jambo lolote,siogopi. Kwani serikali ndio nini? Achanani na mimi bwana", Zabroni alipokwisha kujibu hivyo aliendelea na kazi yake ya kupangua matofali wakati huo polisi nao wakizikoki bastora zao ili wamshuti kwa kigezo cha kukaidi matakwa yake,punde si punde polisi hao walifyatua risasi kama njugu lakini cha ajabu zilipomkuta Zabroni alicheka huku damu zikibubujika mwilini mwake kisha akapotea pale kwenye tanuru zikabaki nguo na vumbi huku mwenye mtukutu akiwa ameshayeyuka. Polisi hoi kila mmoja alikimbia anapo pajua yeye,ilimradi wafike kwenye gari lao. Lakini pia cha ajabu walipofika kwenye gari lao walimkuta mzee wa makamo akiwa na mkongojo wake kando kando ya gari hilo .

NANI HUYO?
Je Madebe atamuweza Zabro?
Na je,ni nani atamfunga paka kengere.
Na ni kwanini hii ni PENZI LA MFUNGWA?
Tukutane sehem ijayo!
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0765168293

SEHEMU YA KUMI NA MBILI-12

Jeshi lile la polisi walitaharuki kumuona yule mzee,ghafla waliingiwa na hofu huku kila mmoja akisita kulisogelea gari. Wakati huo upande wa pili alionekana polisi mwingine akija hea hea kwa kasi ya ajabu,alipolifikia gari alifungua mlango kisha akaliwasha. Kabla hajaondoka aliwatazama wenzake kisha akasema kwa sauti kuu "Mnashangaa nini? Hebu pandeni juu tuondoke ebo ", alisema hivyo huyo kamanda huku akivutia resi kiasi kwamba ilifanya gari hilo ya polisi kutoa mlio mkali. Makamanda nao baada kuambiwa kuwa wapande gari waondoke,walimtazama kwanza yule mzee waliomkuta pembeni ya gari lao kisha haraka sana walidandia ambapo kamanda yule aliyeshikiria usukani akaliendesha gari kulikimbia balaa la Zabroni. Baaada kutoweka, ghafla yule mzee aligeuka kutoka katika hali hiyo akawa mwenye Zabroni.
"Ahahahah", Zabroni aliangua kicheko kisha akasema "Mimi ni Zabroni", sauti hiyo ilijirudia mara mbili mbili.
Upesi akanuia maneno yake ili apate kupopetea maeneo hayo. Lakini kabla hajapotea, mara ghafla kijana Madebe alitokea akamshika bega kisha akamuuliza "Kwanini unauwa raia hovyo? Wanamakosa gani?.." Zabroni aliposikia sauti hiyo iliyoambatana na kuguswa kwake bega,aligeuka akamtazama mtu aliyemshika kisha akahoji "Hii ngoma ya kikabila hupaswi mrusi ama mzungu kutii maguu, kwani wewe unaniuliza kama nani labda" alihoji Zabroni huku akiwa amekunja uso wake. "Mimi Madebe, mtetezi wa wanyonge" alijibu Madebe.
"Ala! Kwahiyo umeamua kujitolea kwa ajili ya watu wa kijiji hiki?.." Zabroni alirudia kumuuliza Madebe,lakini Madebe hakujibu. Zaidi alinyoosha mkono wa kulia juu,punde si punde kwenye kiganja cha mkono ulitokea upanga. Panga ambalo lilimelemeta sana huku likionyesha makali yasiyo na mfano. Zabroni alistuka haraka sana alipotea akaibukia sehemu nyingine tofauti na ile ya awali,hapo sasa naye aliinyoosha mkono juu ila abadani hakikutokea kitu chochote. Hofu ilimjaa akajiuliza "Nifanye nini sasa ili nimkabili huyu mtu anaye taka kuharibu mipango yangu? ", wakati anajiuliza swali hilo,Madebe alitokea mbele yake akiwa na panga lake. alimtazama Zabroni kisha akasema"Wewe si mwanaume? Mbona sasa unanikimbia?", aliongea kwa kujiamini kijana Madebe huku akimsogelea Zabroni ilihari Zabroni naye akirudi nyuma. Mwishowe Zabroni aliamua kujibadilisha akawa katika umbile la nyoka aina ya cobra,hapo sasa ndipo ugomvi ulipo anza. Madebe alijitahidi kurusha panga lake kwa umahiri ili akate kichwa cha huyo nyoka, pia Zabroni naye ambaye yupo katika umbile la nyoka alifanya juu chini ili amgonge Madebe amtie sumu kali aliyokuwa nayo. Na alipoona hilo zoezi linakuwa ngumu,ndipo aliporusha mate lakini nayo hayakuthubutu kufua dafu kwa Madebe. Hakika ilikuwa vurugu maeneo hayo,ndege na wadudu mwitu walitulia kuona ugomvi huo wa aina yake.
Na wakati hayo yanajili kati ya Zabroni na Madebe,upande wa pili mzee Fungafunga alipata taarifa kuwa dada yake anamtaka Tina aende Dar es salam kuishi naye kwa maana kamkumbuka sana. Hivyo nafasi hiyo mzee Fungafunga aliitumia kama moja ya kuyatenganisha mahusiano ya mwanaye na kijana Zabroni. Alisubiri baadaye muda wa chakula cha usiku aseme na binti yake kuhusu taarifa hiyo ilihari moyoni akijisemea kwamba "Iwe isiwe lazima ataenda tu,sitaki mimi nipate mkwe katili kama huyu" alijisemea mzee Fungafunga huku kwingineko ugomvi ulikuwa bado unaendelea ila mwishowe Zabroni alipotea akaibukia juu kabisa ya kile cha mlima. Alisimama huko wakati huo akihema kwa nguvu ya ajabu akionekana kuchoshwa na balaa la mtukutuku mwenzie ambaye si mwingine ni Madebe. Hofu sasa ilianza kumtanda Zabroni, alijiuliza "Ni dawa gani anatumia huyu mtu?..", kabla hajapata jibu ,Madebe akatokea kwa mara nyingine tena. Safari hiyo alikuwa na sime mkononi yenye chata ya fuvu. Madebe akasema "Zabroni ulipo lala wewe ndipo tulipo amkia,nafikiri umefika wakati wako wa mwisho. Damu nyingi umemwaga lakini leo hii zitamwagika zako" alisema Madebe huku macho yake yakionekana kutisha yalifanana na macho ya nyoka,hali ambayo ilizidi kumtisha Zabroni. Aliogopa sana ila hakuwa na budi kupiga moyo konde ili amalizane na Madebe. Mvua ikaanza kunyesha,radi pamoja na ngurumo mbali mbali zililindima angani. Wakati huo huo Madebe akarusha sime yake,kabla haijamkuta mlengwa ambaye ni Zabroni. Zabro alilala,sime ikapita juu kisha papo hapo akajiugeuza akawa katika hali yake ile ile ya nyoka. Hakuwa na njia nyingine kwani kwa kasi aliyokuwa anatumia Madebe, ilimbidi Zabroni kutumia njia hiyo. Kweli juhudi yake hiyo iliweza kuzaa matunda,kwani alifanikiwa kumgonga Madebe mguuni baada Madebe kuzubaa kwa sekunde kadhaa. Madebe alianguka chini lakini pia kabla Zabroni hajafanya jambo lingine lolote juu yake,ghafla ile sime aliyoirusha ilirejea mkononi mwake ambapo bila kuchelewa aliitupa kwa Zabroni ambaye yupo katika umbile la nyoka,nayo ilimpata ubavuni hali ambayo ilimfanya arudi kwenye hali ya kawaida ambapo napo hakupoteza muda alipotea kisha Madebe naye akatoweka.
Kijijini alionekana Madebe akichechea huku mguu ukiwa umevimba,nyoka aliyemgonga alikuwa na sumu kali mno. Na kipindi Madebe akiwa na hali hiyo,ndani Mwenyekiti alimuuliza Bruno "Wapi alipo elekea kaka yako?.." Bruno hakujibu chochote,zaidi aliishia kujisonya kwani hakufahamu ndugu yake alipo elekea..aliondoka bila hata kumuaga. Ila wakati Mwenyekiti na Bruno wakiwa na sintofahamu,ghafla nje walimuona Madebe akija huku akkchechema mara ananguka na kuinuka. Bruno alistuka hima akamkimbilia,alipo mfikia alimnyanyua huku akimuuliza kilicho msibu. Lakini Madebe hakuweza kujibu chochote,hali yake tayari ilikuwa mbaya sana,sumu imeshapanda kwenye moyo. Bruno alizidi kuchanganyikiwa alirudia kumuuliza kaka yake "Kaka nini kimekusibu?..", lakini Madebe hakujibu,zaidi alijifungua hirizi yake akamkabidhi mdogo wake kisha akasema kwa taabu sana "Zabroni.. Za..broni. mdogo wangu lipa kisasi li..pa ki sa..sasiiii", kwisha kusema hivyo Madebe akaaga dunia. Kiukweli Bruno alilia sana kwa uchungu wa kumpoteza kaka yake. Aliamini aliyefanya kitendo hicho ni Zabroni. Wakati huo upande wa pili,Zabroni alikuwa kwenye Makaburi ya wazazi wake huku akijitazama kidonda chake alicho jeruhiwa na sime. Zabroni aliwaza na kuwazua akaona kabisa siku zake za kuishi zina hesabika hivyo hana budi kumaliza mchezo kwa kumuadabisha mlengwa mkuu ambaye ni mzee Fungafunga ili kisasi chake kiweze kutimia. Wakati anawaza hayo Zabroni, kwingineko Tina alipoambiwa kuwa anatikiwa kwenda Dar es salam kwa shangazi yake,aliona hawezi kwenda bila kukwichi na mpenzi wake wakuitwa Zabroni ilihari Zabroni naye dawa alizo nazo hatakiwi kufanya mapenzi. Na endapo atafanya basi zitapotea mwili mwake.

USIKO SEHEM IJAYO. Kitumbua hicho Dadeki.
nani wa KUMFUNGA PAKA KENGERE?
Bonge moja ya story haichoshi kusoma!!
Mwendelezo lini mkuu??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la Jf
CONTACT:0765168293

SEHEMU YA KUMI NA MBILI-12

Jeshi lile la polisi walitaharuki kumuona yule mzee,ghafla waliingiwa na hofu huku kila mmoja akisita kulisogelea gari. Wakati huo upande wa pili alionekana polisi mwingine akija hea hea kwa kasi ya ajabu,alipolifikia gari alifungua mlango kisha akaliwasha. Kabla hajaondoka aliwatazama wenzake kisha akasema kwa sauti kuu "Mnashangaa nini? Hebu pandeni juu tuondoke ebo ", alisema hivyo huyo kamanda huku akivutia resi kiasi kwamba ilifanya gari hilo ya polisi kutoa mlio mkali. Makamanda nao baada kuambiwa kuwa wapande gari waondoke,walimtazama kwanza yule mzee waliomkuta pembeni ya gari lao kisha haraka sana walidandia ambapo kamanda yule aliyeshikiria usukani akaliendesha gari kulikimbia balaa la Zabroni. Baaada kutoweka, ghafla yule mzee aligeuka kutoka katika hali hiyo akawa mwenye Zabroni.
"Ahahahah", Zabroni aliangua kicheko kisha akasema "Mimi ni Zabroni", sauti hiyo ilijirudia mara mbili mbili.
Upesi akanuia maneno yake ili apate kupopetea maeneo hayo. Lakini kabla hajapotea, mara ghafla kijana Madebe alitokea akamshika bega kisha akamuuliza "Kwanini unauwa raia hovyo? Wanamakosa gani?.." Zabroni aliposikia sauti hiyo iliyoambatana na kuguswa kwake bega,aligeuka akamtazama mtu aliyemshika kisha akahoji "Hii ngoma ya kikabila hupaswi mrusi ama mzungu kutii maguu, kwani wewe unaniuliza kama nani labda" alihoji Zabroni huku akiwa amekunja uso wake. "Mimi Madebe, mtetezi wa wanyonge" alijibu Madebe.
"Ala! Kwahiyo umeamua kujitolea kwa ajili ya watu wa kijiji hiki?.." Zabroni alirudia kumuuliza Madebe,lakini Madebe hakujibu. Zaidi alinyoosha mkono wa kulia juu,punde si punde kwenye kiganja cha mkono ulitokea upanga. Panga ambalo lilimelemeta sana huku likionyesha makali yasiyo na mfano. Zabroni alistuka haraka sana alipotea akaibukia sehemu nyingine tofauti na ile ya awali,hapo sasa naye aliinyoosha mkono juu ila abadani hakikutokea kitu chochote. Hofu ilimjaa akajiuliza "Nifanye nini sasa ili nimkabili huyu mtu anaye taka kuharibu mipango yangu? ", wakati anajiuliza swali hilo,Madebe alitokea mbele yake akiwa na panga lake. alimtazama Zabroni kisha akasema"Wewe si mwanaume? Mbona sasa unanikimbia?", aliongea kwa kujiamini kijana Madebe huku akimsogelea Zabroni ilihari Zabroni naye akirudi nyuma. Mwishowe Zabroni aliamua kujibadilisha akawa katika umbile la nyoka aina ya cobra,hapo sasa ndipo ugomvi ulipo anza. Madebe alijitahidi kurusha panga lake kwa umahiri ili akate kichwa cha huyo nyoka, pia Zabroni naye ambaye yupo katika umbile la nyoka alifanya juu chini ili amgonge Madebe amtie sumu kali aliyokuwa nayo. Na alipoona hilo zoezi linakuwa ngumu,ndipo aliporusha mate lakini nayo hayakuthubutu kufua dafu kwa Madebe. Hakika ilikuwa vurugu maeneo hayo,ndege na wadudu mwitu walitulia kuona ugomvi huo wa aina yake.
Na wakati hayo yanajili kati ya Zabroni na Madebe,upande wa pili mzee Fungafunga alipata taarifa kuwa dada yake anamtaka Tina aende Dar es salam kuishi naye kwa maana kamkumbuka sana. Hivyo nafasi hiyo mzee Fungafunga aliitumia kama moja ya kuyatenganisha mahusiano ya mwanaye na kijana Zabroni. Alisubiri baadaye muda wa chakula cha usiku aseme na binti yake kuhusu taarifa hiyo ilihari moyoni akijisemea kwamba "Iwe isiwe lazima ataenda tu,sitaki mimi nipate mkwe katili kama huyu" alijisemea mzee Fungafunga huku kwingineko ugomvi ulikuwa bado unaendelea ila mwishowe Zabroni alipotea akaibukia juu kabisa ya kile cha mlima. Alisimama huko wakati huo akihema kwa nguvu ya ajabu akionekana kuchoshwa na balaa la mtukutuku mwenzie ambaye si mwingine ni Madebe. Hofu sasa ilianza kumtanda Zabroni, alijiuliza "Ni dawa gani anatumia huyu mtu?..", kabla hajapata jibu ,Madebe akatokea kwa mara nyingine tena. Safari hiyo alikuwa na sime mkononi yenye chata ya fuvu. Madebe akasema "Zabroni ulipo lala wewe ndipo tulipo amkia,nafikiri umefika wakati wako wa mwisho. Damu nyingi umemwaga lakini leo hii zitamwagika zako" alisema Madebe huku macho yake yakionekana kutisha yalifanana na macho ya nyoka,hali ambayo ilizidi kumtisha Zabroni. Aliogopa sana ila hakuwa na budi kupiga moyo konde ili amalizane na Madebe. Mvua ikaanza kunyesha,radi pamoja na ngurumo mbali mbali zililindima angani. Wakati huo huo Madebe akarusha sime yake,kabla haijamkuta mlengwa ambaye ni Zabroni. Zabro alilala,sime ikapita juu kisha papo hapo akajiugeuza akawa katika hali yake ile ile ya nyoka. Hakuwa na njia nyingine kwani kwa kasi aliyokuwa anatumia Madebe, ilimbidi Zabroni kutumia njia hiyo. Kweli juhudi yake hiyo iliweza kuzaa matunda,kwani alifanikiwa kumgonga Madebe mguuni baada Madebe kuzubaa kwa sekunde kadhaa. Madebe alianguka chini lakini pia kabla Zabroni hajafanya jambo lingine lolote juu yake,ghafla ile sime aliyoirusha ilirejea mkononi mwake ambapo bila kuchelewa aliitupa kwa Zabroni ambaye yupo katika umbile la nyoka,nayo ilimpata ubavuni hali ambayo ilimfanya arudi kwenye hali ya kawaida ambapo napo hakupoteza muda alipotea kisha Madebe naye akatoweka.
Kijijini alionekana Madebe akichechea huku mguu ukiwa umevimba,nyoka aliyemgonga alikuwa na sumu kali mno. Na kipindi Madebe akiwa na hali hiyo,ndani Mwenyekiti alimuuliza Bruno "Wapi alipo elekea kaka yako?.." Bruno hakujibu chochote,zaidi aliishia kujisonya kwani hakufahamu ndugu yake alipo elekea..aliondoka bila hata kumuaga. Ila wakati Mwenyekiti na Bruno wakiwa na sintofahamu,ghafla nje walimuona Madebe akija huku akkchechema mara ananguka na kuinuka. Bruno alistuka hima akamkimbilia,alipo mfikia alimnyanyua huku akimuuliza kilicho msibu. Lakini Madebe hakuweza kujibu chochote,hali yake tayari ilikuwa mbaya sana,sumu imeshapanda kwenye moyo. Bruno alizidi kuchanganyikiwa alirudia kumuuliza kaka yake "Kaka nini kimekusibu?..", lakini Madebe hakujibu,zaidi alijifungua hirizi yake akamkabidhi mdogo wake kisha akasema kwa taabu sana "Zabroni.. Za..broni. mdogo wangu lipa kisasi li..pa ki sa..sasiiii", kwisha kusema hivyo Madebe akaaga dunia. Kiukweli Bruno alilia sana kwa uchungu wa kumpoteza kaka yake. Aliamini aliyefanya kitendo hicho ni Zabroni. Wakati huo upande wa pili,Zabroni alikuwa kwenye Makaburi ya wazazi wake huku akijitazama kidonda chake alicho jeruhiwa na sime. Zabroni aliwaza na kuwazua akaona kabisa siku zake za kuishi zina hesabika hivyo hana budi kumaliza mchezo kwa kumuadabisha mlengwa mkuu ambaye ni mzee Fungafunga ili kisasi chake kiweze kutimia. Wakati anawaza hayo Zabroni, kwingineko Tina alipoambiwa kuwa anatikiwa kwenda Dar es salam kwa shangazi yake,aliona hawezi kwenda bila kukwichi na mpenzi wake wakuitwa Zabroni ilihari Zabroni naye dawa alizo nazo hatakiwi kufanya mapenzi. Na endapo atafanya basi zitapotea mwili mwake.

USIKO SEHEM IJAYO. Kitumbua hicho Dadeki.
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0765168293

SEHEMU YA KUMI NA MBILI-12

Jeshi lile la polisi walitaharuki kumuona yule mzee,ghafla waliingiwa na hofu huku kila mmoja akisita kulisogelea gari. Wakati huo upande wa pili alionekana polisi mwingine akija hea hea kwa kasi ya ajabu,alipolifikia gari alifungua mlango kisha akaliwasha. Kabla hajaondoka aliwatazama wenzake kisha akasema kwa sauti kuu "Mnashangaa nini? Hebu pandeni juu tuondoke ebo ", alisema hivyo huyo kamanda huku akivutia resi kiasi kwamba ilifanya gari hilo ya polisi kutoa mlio mkali. Makamanda nao baada kuambiwa kuwa wapande gari waondoke,walimtazama kwanza yule mzee waliomkuta pembeni ya gari lao kisha haraka sana walidandia ambapo kamanda yule aliyeshikiria usukani akaliendesha gari kulikimbia balaa la Zabroni. Baaada kutoweka, ghafla yule mzee aligeuka kutoka katika hali hiyo akawa mwenye Zabroni.
"Ahahahah", Zabroni aliangua kicheko kisha akasema "Mimi ni Zabroni", sauti hiyo ilijirudia mara mbili mbili.
Upesi akanuia maneno yake ili apate kupopetea maeneo hayo. Lakini kabla hajapotea, mara ghafla kijana Madebe alitokea akamshika bega kisha akamuuliza "Kwanini unauwa raia hovyo? Wanamakosa gani?.." Zabroni aliposikia sauti hiyo iliyoambatana na kuguswa kwake bega,aligeuka akamtazama mtu aliyemshika kisha akahoji "Hii ngoma ya kikabila hupaswi mrusi ama mzungu kutii maguu, kwani wewe unaniuliza kama nani labda" alihoji Zabroni huku akiwa amekunja uso wake. "Mimi Madebe, mtetezi wa wanyonge" alijibu Madebe.
"Ala! Kwahiyo umeamua kujitolea kwa ajili ya watu wa kijiji hiki?.." Zabroni alirudia kumuuliza Madebe,lakini Madebe hakujibu. Zaidi alinyoosha mkono wa kulia juu,punde si punde kwenye kiganja cha mkono ulitokea upanga. Panga ambalo lilimelemeta sana huku likionyesha makali yasiyo na mfano. Zabroni alistuka haraka sana alipotea akaibukia sehemu nyingine tofauti na ile ya awali,hapo sasa naye aliinyoosha mkono juu ila abadani hakikutokea kitu chochote. Hofu ilimjaa akajiuliza "Nifanye nini sasa ili nimkabili huyu mtu anaye taka kuharibu mipango yangu? ", wakati anajiuliza swali hilo,Madebe alitokea mbele yake akiwa na panga lake. alimtazama Zabroni kisha akasema"Wewe si mwanaume? Mbona sasa unanikimbia?", aliongea kwa kujiamini kijana Madebe huku akimsogelea Zabroni ilihari Zabroni naye akirudi nyuma. Mwishowe Zabroni aliamua kujibadilisha akawa katika umbile la nyoka aina ya cobra,hapo sasa ndipo ugomvi ulipo anza. Madebe alijitahidi kurusha panga lake kwa umahiri ili akate kichwa cha huyo nyoka, pia Zabroni naye ambaye yupo katika umbile la nyoka alifanya juu chini ili amgonge Madebe amtie sumu kali aliyokuwa nayo. Na alipoona hilo zoezi linakuwa ngumu,ndipo aliporusha mate lakini nayo hayakuthubutu kufua dafu kwa Madebe. Hakika ilikuwa vurugu maeneo hayo,ndege na wadudu mwitu walitulia kuona ugomvi huo wa aina yake.

Na wakati hayo yanajili kati ya Zabroni na Madebe,upande wa pili mzee Fungafunga alipata taarifa kuwa dada yake anamtaka Tina aende Dar es salam kuishi naye kwa maana kamkumbuka sana. Hivyo nafasi hiyo mzee Fungafunga aliitumia kama moja ya kuyatenganisha mahusiano ya mwanaye na kijana Zabroni. Alisubiri baadaye muda wa chakula cha usiku aseme na binti yake kuhusu taarifa hiyo ilihari moyoni akijisemea kwamba "Iwe isiwe lazima ataenda tu,sitaki mimi nipate mkwe katili kama huyu" alijisemea mzee Fungafunga huku kwingineko ugomvi ulikuwa bado unaendelea ila mwishowe Zabroni alipotea akaibukia juu kabisa ya kile cha mlima. Alisimama huko wakati huo akihema kwa nguvu ya ajabu akionekana kuchoshwa na balaa la mtukutuku mwenzie ambaye si mwingine ni Madebe. Hofu sasa ilianza kumtanda Zabroni, alijiuliza "Ni dawa gani anatumia huyu mtu?..", kabla hajapata jibu ,Madebe akatokea kwa mara nyingine tena. Safari hiyo alikuwa na sime mkononi yenye chata ya fuvu. Madebe akasema "Zabroni ulipo lala wewe ndipo tulipo amkia,nafikiri umefika wakati wako wa mwisho. Damu nyingi umemwaga lakini leo hii zitamwagika zako" alisema Madebe huku macho yake yakionekana kutisha yalifanana na macho ya nyoka,hali ambayo ilizidi kumtisha Zabroni. Aliogopa sana ila hakuwa na budi kupiga moyo konde ili amalizane na Madebe. Mvua ikaanza kunyesha,radi pamoja na ngurumo mbali mbali zililindima angani. Wakati huo huo Madebe akarusha sime yake,kabla haijamkuta mlengwa ambaye ni Zabroni. Zabro alilala,sime ikapita juu kisha papo hapo akajiugeuza akawa katika hali yake ile ile ya nyoka. Hakuwa na njia nyingine kwani kwa kasi aliyokuwa anatumia Madebe, ilimbidi Zabroni kutumia njia hiyo. Kweli juhudi yake hiyo iliweza kuzaa matunda,kwani alifanikiwa kumgonga Madebe mguuni baada Madebe kuzubaa kwa sekunde kadhaa. Madebe alianguka chini lakini pia kabla Zabroni hajafanya jambo lingine lolote juu yake,ghafla ile sime aliyoirusha ilirejea mkononi mwake ambapo bila kuchelewa aliitupa kwa Zabroni ambaye yupo katika umbile la nyoka,nayo ilimpata ubavuni hali ambayo ilimfanya arudi kwenye hali ya kawaida ambapo napo hakupoteza muda alipotea kisha Madebe naye akatoweka.

Kijijini alionekana Madebe akichechea huku mguu ukiwa umevimba,nyoka aliyemgonga alikuwa na sumu kali mno. Na kipindi Madebe akiwa na hali hiyo,ndani Mwenyekiti alimuuliza Bruno "Wapi alipo elekea kaka yako?.." Bruno hakujibu chochote,zaidi aliishia kujisonya kwani hakufahamu ndugu yake alipo elekea..aliondoka bila hata kumuaga. Ila wakati Mwenyekiti na Bruno wakiwa na sintofahamu,ghafla nje walimuona Madebe akija huku akkchechema mara ananguka na kuinuka. Bruno alistuka hima akamkimbilia,alipo mfikia alimnyanyua huku akimuuliza kilicho msibu. Lakini Madebe hakuweza kujibu chochote,hali yake tayari ilikuwa mbaya sana,sumu imeshapanda kwenye moyo. Bruno alizidi kuchanganyikiwa alirudia kumuuliza kaka yake "Kaka nini kimekusibu?..", lakini Madebe hakujibu,zaidi alijifungua hirizi yake akamkabidhi mdogo wake kisha akasema kwa taabu sana "Zabroni.. Za..broni. mdogo wangu lipa kisasi li..pa ki sa..sasiiii", kwisha kusema hivyo Madebe akaaga dunia. Kiukweli Bruno alilia sana kwa uchungu wa kumpoteza kaka yake. Aliamini aliyefanya kitendo hicho ni Zabroni. Wakati huo upande wa pili,Zabroni alikuwa kwenye Makaburi ya wazazi wake huku akijitazama kidonda chake alicho jeruhiwa na sime. Zabroni aliwaza na kuwazua akaona kabisa siku zake za kuishi zina hesabika hivyo hana budi kumaliza mchezo kwa kumuadabisha mlengwa mkuu ambaye ni mzee Fungafunga ili kisasi chake kiweze kutimia. Wakati anawaza hayo Zabroni, kwingineko Tina alipoambiwa kuwa anatikiwa kwenda Dar es salam kwa shangazi yake,aliona hawezi kwenda bila kukwichi na mpenzi wake wakuitwa Zabroni ilihari Zabroni naye dawa alizo nazo hatakiwi kufanya mapenzi. Na endapo atafanya basi zitapotea mwili mwake.

USIKO SEHEM IJAYO. Kitumbua hicho Dadeki.
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0765168923

SEHEMU YA KUMI NA TATU-13

Siku tatu sasa zilikatika tangu Madebe afariki dunia,siku iliyofuata ambayo ni siku ya nne ndio siku ambayo Tina alipanga akutane na Zabroni ili wafanye mapenzi. Hivyo siku hiyo asubuhi Tina alidamka akaelekea mahali anapoishi Zabroni, alikuta majivu tu huku nyumba ikiwa imeteketezwa na moto. Tina alistuka sana baada kukuta hali ile,alitazama kulia na kushoto wakati huo akijiuliza ni wapi anapoishi Zabroni? Na kabla hajapata jibu mara ghafla alisikia sauti ikimuita,alistuka kisha akatazama kule ilipo tokea sauti akamuona kijana Zabroni akiwa chini ya mti mdogo huku pembeni yakionekana makaburi. Tina alizidi kushangaa kiasi kwamba alionyesha uso wa hofu ila Zabroni akawa amemuondoa hofu yake kwa kumwambia "Njoo mpenzi wangu usiniogope,haya ndiyo maisha yangu kwa sasa"
"Kwanini lakini umeamua kuishi huku?ujue tabia yako mimi sijaipenda" alisema Tina huku akizipiga hatua kumsogelea mpenzi wake. Alipo mfikia alikaa kando kando yake halafu akaongeza kusema "Hivi Zabro unajisikiaje kukaa kwenye mazingira haya? Sehemu nyingine zooote hujaziona mpaka uje kukaa eneo hili?.." Zabroni akajibu "Tina,kama nilivyokwisha kusema hapo awali kwamba haya ndio maisha yangu. Nimeamua kuja kukaa huku na wazee wangu ili nipate amani ya moyo wangu kwahiyo naomba usiwaze wala kuumiza kichwa kwa suala hili" alisema Zabroni tena kwa msisitizo.
"Zabro,.."
"Naam "
"Unanipenda kweli?.."
"Ndio tena nakupenda"
"Sawa asante,ila leo kuna jambo naomba nikuulize"
"Jambo gani?.."
"Naomba uniambie kwanini unauwa hovyo, unawarudisha wanakijiji nyuma kwa kuchoma nyumba na malighafi zao kwanini lakini.. tazama mpaka baba kaniambia niachane na wewe kutokana na tabia zako eti hawezi kuwa na mkwe mwenye roho mbaya. Kwahiyo Zabro mpenzi hatakama hutaweza kuniambia sababu ila basi achana na unyama huu tafadhali.." yote hayo alikuwa akiyasema Tina akijaribu kumshawishi Zabroni aachane na matendo anayo yafanya,lakini mara baada Zabroni kusikia maneno hayo ya Tina. Ghafla alipandwa na hasira,alimtazama Tina mara mbili mbili kisha akayatazama makaburi ya wazazi wake. Akasema tena huku akiwa na hasira kiasi kwamba mdomo wake ulionekana kutetemeka "Abadani Tina huwezi kunibadilisha tabia mimi,lengo nililo liweka moyoni mwangu huwezi kulipangua. Tena kawaambie washauri wako waniache ,pia vile vile waambie dawa ya moto ni moto" kwisha kusema hayo Zabroni alisimama kisha akaondoka zake,Tina naye alisimama akaanza kumfuata huku akiomba msamaha pia akiomba japo dakika moja ili aseme nae jambo. Zabroni alizidi kutembea huku akikazana lakini aliposikia msamaha wa Tina,hatimaye alisimama kisha akamgeuki halafu akahoji kwa hasira "Unasemaje?.." Tina alijishusha akawa mnyonge kisha akasema huku akilia "Zabroni, samahani kama nimekukera. Pia nashukuru kwa kunipa nafasi ya kunisikiliza. Mpenzi mimi naenda Dar es salam siku yoyote. Hivyo naumia sana kukuacha mwenyewe mpenzi wangu,lakini pia nilikuwa nina ombi moja" hapo Tina alisita kidogo ambapo ndipo Zabroni naye alipo pata nafasi ya kumuuliza huku akimtazama usoni "Kitu gani?.."
"Unajua siku..siku siku nyingi mimi na wewe hatujafanya mapenzi,kwahiyo naomba tukumbushie basi hata kwa nusu saa. Ikiwa kama njia pia ya kukuaga, hakika nitafurahi sana nikiondoka huku nikiwa nimefanya mapenzi na wewe kwani nitajiona mwepesi sana" Tina aliongea huku akichezea chezea vidole vyake, uso wake nao ukiona haya. Zabroni kijana mtutuku anayelipa kisasi huku tegemezi lake kuu ikiwa ni dawa,dawa ambayo sharti yake kuu hutakiwi kufanya mapenzi. Aliwaza sana,ukweli anampenda sana Tina istoshe anauchupa usio wa kawaida ila tatizo ni hapo tu. Je, atafanya mapenzi? Ilihali tayari anaadui nyuma anamnyemelea. Lakini pia kabla Zabroni hajatoa jibu juu ya ombi la mpenzi wake,alikumbuka kuwa mlengwa mkuu bado hajamalizana naye ambaye ni mzee Fungafunga baba yake Tina. Mtihani kwa Zabroni ila mwishowe alimpa jibu moja tu Tina "Nenda tutakatana jioni kwa sasa sina hamu yoyote,siunajua mapenzi hisia?.."Tina alitabasamu baada kusikia maneno ya Zabroni kisha akamwambia "Sawa lakini umenisamehe?.." Zabloni akajibu "Ndio "
"Mmh basi cheka kama kweli umenisamehe", Tina alitania Zabroni akacheka kama Tina alivyotaka huku ikiwa moyoni analake jambo,muda huo huo waliagana Tina alienda nyumbani kwao huku akiamini kuwa jioni atakuwa na mchezo dhidi ya Zabroni. Hakika furaha isiyo kifani ilimjaa moyoni ilihari upande wa pili Zabroni alijisemea kwamba hatoweza kufanya mapenzi mpaka pale atakapo kamilisha zaezi lake la kulipa kisasi. Tina alipo fika nyumbani,baba yake alianza kumfokea. Alimuuliza wapi alipokwenda,lakini binti huyo alikosa majibu ya kumpa baba yake ambaye ni mzee Fungafunga. Hivyo kitendo hicho kilimfanya mzee huyo kuhisi kuwa huwenda mwanaye katoka kwa Zabroni jambo ambalo halipendi katika maisha yake. Kwa hasira alimuamuru mkewe amuhimze binti yake wajiandae ili waanze safari ya kwenda mjini ili kesho yake iwe safari ya moja kwa moja Dar es salam. Upesi maandalizi yalifanyika,maandalizi ambayo waliyafanya huku Tina akilia kwani aliona anondoka bila kurudia kuhonja penzi la mtukutuku Zabroni. Alijiuliza ni lini tena itatokea hiyo nafasi? Kwa maana hakuwa na imani kama Zabroni ataishi miaka mingi kutokana na mambo anayo yafanya. Safari ilianza kati ya Tina na mama yake huku mzee Fungafunga akimsisitiza mkewe awahi mapema kwani hali sio shwari kwenye kijiji. Wakati mama Tina na mwanaye wakiwa njiani,Zabroni aliwaona. Alijua dhahiri Tina atakuwa anasafiri kama alivyomwambia hapo awali, Zabroni alifurahi sana kwani alijua tayaru kapata nafasi ya kukamilisha malengo yake. "Bado muhusika" alijisemea Zabroni kisha akatoweka eneo lile alilokuwa amekaa muda wote.
Usiku ulipoingia, aliamka tayari kwa niaba ya kwenda kukamilisha jambo lake. Siku hiyo mzee Fungafunga na mkewe walilala ndani wakiamini kwamba huwenda siku hiyo mtukutuku Zabroni asitembeze moto. Mke na mume walilala tena kwa furaha huku mzee Fungafunga akijisemea moyoni "Hapa moyo wangu umetulia sasa, kumtoa mwanangu kijijini hapa ni jambo la heri. Sasa ngoja nione huyu mwana haramu atachukuwa hatua gani,siwezi kuwa na mkwe mwenye roho mbaya kama huyu",kwisha kujisemea hayo Fungafunga alijivutia shuka tayaru kwa kuanza kuutafuta usingizi. Na punde si punde usingizi ulimpitia yeye pamoja na mkewe,walilala fo fo fo ilihari muda huo wazee hao wakiwa kwenye dimbwi la ndoto,Zabroni naye alitua nje ya nyumba. Alifyatu njiti akawasha sigara yake aina ya ngaja kisha moto uliosalia kwenye njiti akatupia juu kwenye nyumba. Sekunde dakika moto ulisikika huku mzee Fungafunga na mke wakiwa ndani,walistuka kutoka usingizini huku tayari moto ukiwa mkali kiasi kwamba walishindwa kujiokoa. "Ahahahaha hahahahah", Zabloni alicheka sana baada kufanya kitendo kile,katika akili yake aliamini kuwa tayari shughuli imekamilika. Lakini wakati akiwa katika imani hiyo mara ghafla aliguswa bega!

NANI HUYO?. Usikose sehem ijayo.
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0765168923

SEHEMU YA KUMI NA TATU-13

Siku tatu sasa zilikatika tangu Madebe afariki dunia,siku iliyofuata ambayo ni siku ya nne ndio siku ambayo Tina alipanga akutane na Zabroni ili wafanye mapenzi. Hivyo siku hiyo asubuhi Tina alidamka akaelekea mahali anapoishi Zabroni, alikuta majivu tu huku nyumba ikiwa imeteketezwa na moto. Tina alistuka sana baada kukuta hali ile,alitazama kulia na kushoto wakati huo akijiuliza ni wapi anapoishi Zabroni? Na kabla hajapata jibu mara ghafla alisikia sauti ikimuita,alistuka kisha akatazama kule ilipo tokea sauti akamuona kijana Zabroni akiwa chini ya mti mdogo huku pembeni yakionekana makaburi. Tina alizidi kushangaa kiasi kwamba alionyesha uso wa hofu ila Zabroni akawa amemuondoa hofu yake kwa kumwambia "Njoo mpenzi wangu usiniogope,haya ndiyo maisha yangu kwa sasa"
"Kwanini lakini umeamua kuishi huku?ujue tabia yako mimi sijaipenda" alisema Tina huku akizipiga hatua kumsogelea mpenzi wake. Alipo mfikia alikaa kando kando yake halafu akaongeza kusema "Hivi Zabro unajisikiaje kukaa kwenye mazingira haya? Sehemu nyingine zooote hujaziona mpaka uje kukaa eneo hili?.." Zabroni akajibu "Tina,kama nilivyokwisha kusema hapo awali kwamba haya ndio maisha yangu. Nimeamua kuja kukaa huku na wazee wangu ili nipate amani ya moyo wangu kwahiyo naomba usiwaze wala kuumiza kichwa kwa suala hili" alisema Zabroni tena kwa msisitizo.
"Zabro,.."
"Naam "
"Unanipenda kweli?.."
"Ndio tena nakupenda"
"Sawa asante,ila leo kuna jambo naomba nikuulize"
"Jambo gani?.."
"Naomba uniambie kwanini unauwa hovyo, unawarudisha wanakijiji nyuma kwa kuchoma nyumba na malighafi zao kwanini lakini.. tazama mpaka baba kaniambia niachane na wewe kutokana na tabia zako eti hawezi kuwa na mkwe mwenye roho mbaya. Kwahiyo Zabro mpenzi hatakama hutaweza kuniambia sababu ila basi achana na unyama huu tafadhali.." yote hayo alikuwa akiyasema Tina akijaribu kumshawishi Zabroni aachane na matendo anayo yafanya,lakini mara baada Zabroni kusikia maneno hayo ya Tina. Ghafla alipandwa na hasira,alimtazama Tina mara mbili mbili kisha akayatazama makaburi ya wazazi wake. Akasema tena huku akiwa na hasira kiasi kwamba mdomo wake ulionekana kutetemeka "Abadani Tina huwezi kunibadilisha tabia mimi,lengo nililo liweka moyoni mwangu huwezi kulipangua. Tena kawaambie washauri wako waniache ,pia vile vile waambie dawa ya moto ni moto" kwisha kusema hayo Zabroni alisimama kisha akaondoka zake,Tina naye alisimama akaanza kumfuata huku akiomba msamaha pia akiomba japo dakika moja ili aseme nae jambo. Zabroni alizidi kutembea huku akikazana lakini aliposikia msamaha wa Tina,hatimaye alisimama kisha akamgeuki halafu akahoji kwa hasira "Unasemaje?.." Tina alijishusha akawa mnyonge kisha akasema huku akilia "Zabroni, samahani kama nimekukera. Pia nashukuru kwa kunipa nafasi ya kunisikiliza. Mpenzi mimi naenda Dar es salam siku yoyote. Hivyo naumia sana kukuacha mwenyewe mpenzi wangu,lakini pia nilikuwa nina ombi moja" hapo Tina alisita kidogo ambapo ndipo Zabroni naye alipo pata nafasi ya kumuuliza huku akimtazama usoni "Kitu gani?.."
"Unajua siku..siku siku nyingi mimi na wewe hatujafanya mapenzi,kwahiyo naomba tukumbushie basi hata kwa nusu saa. Ikiwa kama njia pia ya kukuaga, hakika nitafurahi sana nikiondoka huku nikiwa nimefanya mapenzi na wewe kwani nitajiona mwepesi sana" Tina aliongea huku akichezea chezea vidole vyake, uso wake nao ukiona haya. Zabroni kijana mtutuku anayelipa kisasi huku tegemezi lake kuu ikiwa ni dawa,dawa ambayo sharti yake kuu hutakiwi kufanya mapenzi. Aliwaza sana,ukweli anampenda sana Tina istoshe anauchupa usio wa kawaida ila tatizo ni hapo tu. Je, atafanya mapenzi? Ilihali tayari anaadui nyuma anamnyemelea. Lakini pia kabla Zabroni hajatoa jibu juu ya ombi la mpenzi wake,alikumbuka kuwa mlengwa mkuu bado hajamalizana naye ambaye ni mzee Fungafunga baba yake Tina. Mtihani kwa Zabroni ila mwishowe alimpa jibu moja tu Tina "Nenda tutakatana jioni kwa sasa sina hamu yoyote,siunajua mapenzi hisia?.."Tina alitabasamu baada kusikia maneno ya Zabroni kisha akamwambia "Sawa lakini umenisamehe?.." Zabloni akajibu "Ndio "
"Mmh basi cheka kama kweli umenisamehe", Tina alitania Zabroni akacheka kama Tina alivyotaka huku ikiwa moyoni analake jambo,muda huo huo waliagana Tina alienda nyumbani kwao huku akiamini kuwa jioni atakuwa na mchezo dhidi ya Zabroni. Hakika furaha isiyo kifani ilimjaa moyoni ilihari upande wa pili Zabroni alijisemea kwamba hatoweza kufanya mapenzi mpaka pale atakapo kamilisha zaezi lake la kulipa kisasi. Tina alipo fika nyumbani,baba yake alianza kumfokea. Alimuuliza wapi alipokwenda,lakini binti huyo alikosa majibu ya kumpa baba yake ambaye ni mzee Fungafunga. Hivyo kitendo hicho kilimfanya mzee huyo kuhisi kuwa huwenda mwanaye katoka kwa Zabroni jambo ambalo halipendi katika maisha yake. Kwa hasira alimuamuru mkewe amuhimze binti yake wajiandae ili waanze safari ya kwenda mjini ili kesho yake iwe safari ya moja kwa moja Dar es salam. Upesi maandalizi yalifanyika,maandalizi ambayo waliyafanya huku Tina akilia kwani aliona anondoka bila kurudia kuhonja penzi la mtukutuku Zabroni. Alijiuliza ni lini tena itatokea hiyo nafasi? Kwa maana hakuwa na imani kama Zabroni ataishi miaka mingi kutokana na mambo anayo yafanya. Safari ilianza kati ya Tina na mama yake huku mzee Fungafunga akimsisitiza mkewe awahi mapema kwani hali sio shwari kwenye kijiji. Wakati mama Tina na mwanaye wakiwa njiani,Zabroni aliwaona. Alijua dhahiri Tina atakuwa anasafiri kama alivyomwambia hapo awali, Zabroni alifurahi sana kwani alijua tayaru kapata nafasi ya kukamilisha malengo yake. "Bado muhusika" alijisemea Zabroni kisha akatoweka eneo lile alilokuwa amekaa muda wote.
Usiku ulipoingia, aliamka tayari kwa niaba ya kwenda kukamilisha jambo lake. Siku hiyo mzee Fungafunga na mkewe walilala ndani wakiamini kwamba huwenda siku hiyo mtukutuku Zabroni asitembeze moto. Mke na mume walilala tena kwa furaha huku mzee Fungafunga akijisemea moyoni "Hapa moyo wangu umetulia sasa, kumtoa mwanangu kijijini hapa ni jambo la heri. Sasa ngoja nione huyu mwana haramu atachukuwa hatua gani,siwezi kuwa na mkwe mwenye roho mbaya kama huyu",kwisha kujisemea hayo Fungafunga alijivutia shuka tayaru kwa kuanza kuutafuta usingizi. Na punde si punde usingizi ulimpitia yeye pamoja na mkewe,walilala fo fo fo ilihari muda huo wazee hao wakiwa kwenye dimbwi la ndoto,Zabroni naye alitua nje ya nyumba. Alifyatu njiti akawasha sigara yake aina ya ngaja kisha moto uliosalia kwenye njiti akatupia juu kwenye nyumba. Sekunde dakika moto ulisikika huku mzee Fungafunga na mke wakiwa ndani,walistuka kutoka usingizini huku tayari moto ukiwa mkali kiasi kwamba walishindwa kujiokoa. "Ahahahaha hahahahah", Zabloni alicheka sana baada kufanya kitendo kile,katika akili yake aliamini kuwa tayari shughuli imekamilika. Lakini wakati akiwa katika imani hiyo mara ghafla aliguswa bega!

NANI HUYO?. Usikose sehem ijayo.
Mwendelezo lini mkuu??
Mana hii ni bonge ya story!
Salute kwako mtunzi!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom