Simulizi ya kusisimua- (penzi la mfungwa)

Simulizi ya kusisimua- (penzi la mfungwa)

PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0628650170

SEHEMU YA KUMI NNE-14

Baada kuguswa bega alistuka upesi akamgeukia mtu huyo aliyemgusa usiku huo wa manane. Ni Bruno. Mdogo wake marehemu Madebe,sura ya huyo kijana ilikuwa mpya kwa kwa Zabroni japo alimtazama kwa mwanga wa moto ulio tokana nyumba inayoteketea hivyo hakuweza kumtambua,zaidi alijiuliza "Huyu ni nani? Na anawezaje kunigusa bega?..", kabla hajapata jibu la hilo swali,Bruno alisema" Hujui sikujui ila kwa kumbukumbu naweza sema utanikumbuka endapo kama nitakukumbusha"
"We ni nani?..", alihoji Zabroni kwa kujiamini kabisa. Bruno alicheka sana kisha akafumbua kiganja chake,ulitokea mwanga mfano wa video. Katika mwanga huo kiganjani hapo lilionekana tukio lile la Zabroni na Madebe walipokuwa wanapigana,na mwisho wa tukio lile ilionekana ile sehemu ambayo Madebe alikuwa akimkabudhi hirizi mdogo wake huku akimtaka alipe kisasi. "Ndio mimi hapa natakiwa nifanye kile kitu kaka alicho nituma,hakika damu yake inanidai", alisema Bruno baada kumaliza kumuonyesha Zabroni ile video fupi kwenye kiganja chake. Lakini kijana Zabroni licha ya kuambiwa hayo maneno,kamwe hakuonyesha kustuka. Alicheka kisha akajibu "Nirahisi sana kunitamkia hayo maneno lakini ni vigumu kuyafanyia kazi kwa vitendo. Dogo, mimi leo ndio rasmi nimekamilisha kazi niliyofanya miezi kadhaa iliyopita. Hivyo sistahiri kuendelea kutenda dhambi zaidi,niliyo yafanya yanatosha", Kwisha kusema hayo Zabroni aliondoka zake. Bruno akamfuata,na ndipo Zabroni alipo amua kupotea kimazingara. Akaibukia kando kando ya mto,ilihali muda huo huo Buruno naye akatokea. Alistuka Zabroni baada kumuona kijana huyo anazidi kumganda wakati yeye hayupo tayari tena kufanya mauaji. "Bwana mdogo unataka nini tena kutoka kwangu?.." Zabroni alimuuliza Bruno tena kwa hasira. Bruno akajibu "Nataka kichwa chako Zabroni, sifa zako mbaya zimezagaa kila pande kwa sababu ya mauwaji yako,inakuwaje unauwa watu bila hatia? Hivyo basi kama utaweza niuwe na mimi basi lakini tofauti na hivyo utakufaa wewe ", alijibu Bruno huku akijiandaa kumrushia kombola Zabroni, ila kabla hajarusha. Zabroni akamwambia "Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini"
"Hapana huo ni ujanja wako Zabroni, sitegeki kishamba mimi", Bruno alijibu kisha akamtupia Zabroni moto wa kichawi. Moto huo ambao ulikuwa na nguvu ya ajabu ndani yake ulimpata Zablrni ukamtupa katikati ya mto ambapo muda huo huo Bruno alipaa juu huku akiwa amekunja ngumi nzito,ambayo alishuka nayo mpaka kwenye tumbo la Zabroni. Kitendo ambacho kilimzamisha chini zaidi kijana huyo mtukutu. Mamba samaki pia na wadudu wengineo waishio majini kwenye mto huo walitulia kupisha mpambano huo uliojumuisha nguvu za giza, Bruno alifanikiwa kumuadabisha Zabroni kwani kila Zabroni alipotaka kujitetea alijikuta akizidiwa ujanja na Bruno kwa kupigwa ngumi za haraka haraka zilizo changanywa na nguvu ya giza. Dakika kumi tu Zabroni hoi alisahau hata yale maneno ya kunuia ili abadilike kuwa kiumbe chochote kwa maana ngumi nzito iliyotua kichwani kwake iliweza kuyumbisha ubongo,hali iliyopelekea Zabroni huo muda kupoteza fahamu. Alipigwa sana kila mahala,Bruno alionyesha kujawa na hasira moyoni mwake. Hasira hiyo ndiyo iliyompelekea kumpiga Zabroni bila huruma kwani kila alipomkumbuka kaka yake ndivyo nguvu za kuchezea na mashavu ya Zabroni zilivyozidi kuongezeka. Mwishowe Zabroni alionekana kulegea kabisa mithiri ya kambale,hapo Bruno akajua tayari kazi imekwisha lakini ataamini vipi kama kweli kafa? Ndipo alipoamua kumvuta nchi kavu ili amuhakikishe. "Naam! Kazi imekwisha,hakuna mwamba chini ya jua zaidi ya muumba aliyekuumba. Zabroni Zabroni sasa ni wakati wako wa kwenda kulipwa yale uliyo yafanya hapa duniani", alisema Bruno baada kumkagua Zabroni kila sehemu ya mwili wake na kukuta tayari mtukutu kaaga dunia. Mara baada kusema hayo alimalizia kusema tena " Mimi ni Bruno shujaa... kwani siku zote shujaa hafi vitani bali shujaa ni yule anaye pambana na kurudi nyumbani na ushindi", Hapo alikata hirizi iliyokuwa kwenye mkono wa Zabroni kisha akawaza aondoke zake amuache Zabroni pale nchi kavu aidhaa amtupie mtoni apelekwe na maji sehemu isiyo julikana ikiwezekana awe chakula cha mamba? Kwani kwa hali ile kamwe mamba wasingemuacha salama,hirizi ambayo ingemlinda tayari ilikuwa mikononi mwake. Hivyo Zabroni atakuwa chakula cha mamba na samaki. Lakini kabla Bruno hajafanya huo uamuzi akajiuliza kwa mara nyingine tena "Tayari huyu mtu alikuwa ni tishio hapa kijijini je, hata nikipeleka habari ya kifo chake kwa wanakijiji wataniamini kweli?", alijiuliza Bruno mwishowe akaona ambebe begani moja kwa moja akaenda kumtunduki juu ya mti mkubwa kando ya barabara nyembamba ipitikayo kwa wingi na watu waendao na kurudi gulioni. Hapo ndipo Zabroni alipo tundikwa juu juu kwenye huo mti ule ambao kipindi cha nyuma aliwatundika vijusi alivyo vitoa tumboni kwa mama mjamzito. Kwisha kufanya hayo Bruno aliondoka zake na hirizi ya Zabroni. Akiwa amelowa jasho na damu aliitia hirizi ile kwenye mfuko wa koti alilokuwa amelivaa,kabla hajapotea kimazingara alizipiga hatua kadhaa kutoka pale alipo Zabroni hatua zipatazo kumi na tano kisha akasimama, akageuka kuutazama mti ule aliomtundika Zabroni akatikisa kichwa na akasema "Kufa tu hukuna namna mwanaharamu mkubwa wewe", kwisha kusema maneno hayo akachukuwa kitambaa akajifuta damu kwenye mikono yake halafu akapotea. Alipo fika kijijini alikuta nyumba tatu zimeteketea kwa moto usiku huo huo. Ndipo hapo Buruno alipokumbuka maneno ya Zabloni alipo mwambia
"Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini" Buruno alipokumbuka hayo maneno akajiongeza kwa kusema "Alaah! kumbe huyu mshenzi alimanisha nitazame juu kuangalia mwanga wa nyumba zinazo ungua? Ooh Mungu wangu" Bruno aliumia moyoni kisha akajipa moyo akisema "Sawa natumaini pindi wahanga hawa watakapo kuona ukiwa maiti basi mioyo yao itajaa tabasamu bashasha",alisema Bruno huku akiingiza mkono mfukoni aitoe hirizi ile aliyoichukua kwa Zabroni ili aitupie kwenye moto,lakini ajabu hakuikuta. Alistuka sana huku asijuwe kwamba muda ule alipotoa kitambaa kujifuta damu kiganjani aliidondosha chini. Pumzi ndefu alishusha na pindi alipotaka kurudu kuichukuwa, Mwemyekiti aliifka eneo la tukio kisha akamwambia "Hii ndio taabu ya hapa kijijini kijana wangu,hakika sitoamini siku nikimuona huyu mwanaharamu kauwawa". Hapo sasa Bruno alishindwa kumtoka Mwenyekiti ili aifuate hirizi ile kwani angeonekana hajaguswa na kitendo hicho cha nyumba kuungua. Muda huo sasa alfajiri tayari ilikuwa imeingia,umande na baridi ulimfanya Zabroni kutikisa kiuongo kimoja cha mwili wake,kumbe mtukutu alikuwa bado hajafa! U hai.

UKIWASHA MOTO KWENYE VIFUU UWE NA UWEZO WA KUUZIMA. me simo tukutane Sehemu ijayo.. mimi ni Team Zabroni aisee!
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0628650170

SEHEMU YA KUMI NNE-14

Baada kuguswa bega alistuka upesi akamgeukia mtu huyo aliyemgusa usiku huo wa manane. Ni Bruno. Mdogo wake marehemu Madebe,sura ya huyo kijana ilikuwa mpya kwa kwa Zabroni japo alimtazama kwa mwanga wa moto ulio tokana nyumba inayoteketea hivyo hakuweza kumtambua,zaidi alijiuliza "Huyu ni nani? Na anawezaje kunigusa bega?..", kabla hajapata jibu la hilo swali,Bruno alisema" Hujui sikujui ila kwa kumbukumbu naweza sema utanikumbuka endapo kama nitakukumbusha"
"We ni nani?..", alihoji Zabroni kwa kujiamini kabisa. Bruno alicheka sana kisha akafumbua kiganja chake,ulitokea mwanga mfano wa video. Katika mwanga huo kiganjani hapo lilionekana tukio lile la Zabroni na Madebe walipokuwa wanapigana,na mwisho wa tukio lile ilionekana ile sehemu ambayo Madebe alikuwa akimkabudhi hirizi mdogo wake huku akimtaka alipe kisasi. "Ndio mimi hapa natakiwa nifanye kile kitu kaka alicho nituma,hakika damu yake inanidai", alisema Bruno baada kumaliza kumuonyesha Zabroni ile video fupi kwenye kiganja chake. Lakini kijana Zabroni licha ya kuambiwa hayo maneno,kamwe hakuonyesha kustuka. Alicheka kisha akajibu "Nirahisi sana kunitamkia hayo maneno lakini ni vigumu kuyafanyia kazi kwa vitendo. Dogo, mimi leo ndio rasmi nimekamilisha kazi niliyofanya miezi kadhaa iliyopita. Hivyo sistahiri kuendelea kutenda dhambi zaidi,niliyo yafanya yanatosha", Kwisha kusema hayo Zabroni aliondoka zake. Bruno akamfuata,na ndipo Zabroni alipo amua kupotea kimazingara. Akaibukia kando kando ya mto,ilihali muda huo huo Buruno naye akatokea. Alistuka Zabroni baada kumuona kijana huyo anazidi kumganda wakati yeye hayupo tayari tena kufanya mauaji. "Bwana mdogo unataka nini tena kutoka kwangu?.." Zabroni alimuuliza Bruno tena kwa hasira. Bruno akajibu "Nataka kichwa chako Zabroni, sifa zako mbaya zimezagaa kila pande kwa sababu ya mauwaji yako,inakuwaje unauwa watu bila hatia? Hivyo basi kama utaweza niuwe na mimi basi lakini tofauti na hivyo utakufaa wewe ", alijibu Bruno huku akijiandaa kumrushia kombola Zabroni, ila kabla hajarusha. Zabroni akamwambia "Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini"
"Hapana huo ni ujanja wako Zabroni, sitegeki kishamba mimi", Bruno alijibu kisha akamtupia Zabroni moto wa kichawi. Moto huo ambao ulikuwa na nguvu ya ajabu ndani yake ulimpata Zablrni ukamtupa katikati ya mto ambapo muda huo huo Bruno alipaa juu huku akiwa amekunja ngumi nzito,ambayo alishuka nayo mpaka kwenye tumbo la Zabroni. Kitendo ambacho kilimzamisha chini zaidi kijana huyo mtukutu. Mamba samaki pia na wadudu wengineo waishio majini kwenye mto huo walitulia kupisha mpambano huo uliojumuisha nguvu za giza, Bruno alifanikiwa kumuadabisha Zabroni kwani kila Zabroni alipotaka kujitetea alijikuta akizidiwa ujanja na Bruno kwa kupigwa ngumi za haraka haraka zilizo changanywa na nguvu ya giza. Dakika kumi tu Zabroni hoi alisahau hata yale maneno ya kunuia ili abadilike kuwa kiumbe chochote kwa maana ngumi nzito iliyotua kichwani kwake iliweza kuyumbisha ubongo,hali iliyopelekea Zabroni huo muda kupoteza fahamu. Alipigwa sana kila mahala,Bruno alionyesha kujawa na hasira moyoni mwake. Hasira hiyo ndiyo iliyompelekea kumpiga Zabroni bila huruma kwani kila alipomkumbuka kaka yake ndivyo nguvu za kuchezea na mashavu ya Zabroni zilivyozidi kuongezeka. Mwishowe Zabroni alionekana kulegea kabisa mithiri ya kambale,hapo Bruno akajua tayari kazi imekwisha lakini ataamini vipi kama kweli kafa? Ndipo alipoamua kumvuta nchi kavu ili amuhakikishe. "Naam! Kazi imekwisha,hakuna mwamba chini ya jua zaidi ya muumba aliyekuumba. Zabroni Zabroni sasa ni wakati wako wa kwenda kulipwa yale uliyo yafanya hapa duniani", alisema Bruno baada kumkagua Zabroni kila sehemu ya mwili wake na kukuta tayari mtukutu kaaga dunia. Mara baada kusema hayo alimalizia kusema tena " Mimi ni Bruno shujaa... kwani siku zote shujaa hafi vitani bali shujaa ni yule anaye pambana na kurudi nyumbani na ushindi", Hapo alikata hirizi iliyokuwa kwenye mkono wa Zabroni kisha akawaza aondoke zake amuache Zabroni pale nchi kavu aidhaa amtupie mtoni apelekwe na maji sehemu isiyo julikana ikiwezekana awe chakula cha mamba? Kwani kwa hali ile kamwe mamba wasingemuacha salama,hirizi ambayo ingemlinda tayari ilikuwa mikononi mwake. Hivyo Zabroni atakuwa chakula cha mamba na samaki. Lakini kabla Bruno hajafanya huo uamuzi akajiuliza kwa mara nyingine tena "Tayari huyu mtu alikuwa ni tishio hapa kijijini je, hata nikipeleka habari ya kifo chake kwa wanakijiji wataniamini kweli?", alijiuliza Bruno mwishowe akaona ambebe begani moja kwa moja akaenda kumtunduki juu ya mti mkubwa kando ya barabara nyembamba ipitikayo kwa wingi na watu waendao na kurudi gulioni. Hapo ndipo Zabroni alipo tundikwa juu juu kwenye huo mti ule ambao kipindi cha nyuma aliwatundika vijusi alivyo vitoa tumboni kwa mama mjamzito. Kwisha kufanya hayo Bruno aliondoka zake na hirizi ya Zabroni. Akiwa amelowa jasho na damu aliitia hirizi ile kwenye mfuko wa koti alilokuwa amelivaa,kabla hajapotea kimazingara alizipiga hatua kadhaa kutoka pale alipo Zabroni hatua zipatazo kumi na tano kisha akasimama, akageuka kuutazama mti ule aliomtundika Zabroni akatikisa kichwa na akasema "Kufa tu hukuna namna mwanaharamu mkubwa wewe", kwisha kusema maneno hayo akachukuwa kitambaa akajifuta damu kwenye mikono yake halafu akapotea. Alipo fika kijijini alikuta nyumba tatu zimeteketea kwa moto usiku huo huo. Ndipo hapo Buruno alipokumbuka maneno ya Zabloni alipo mwambia
"Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini" Buruno alipokumbuka hayo maneno akajiongeza kwa kusema "Alaah! kumbe huyu mshenzi alimanisha nitazame juu kuangalia mwanga wa nyumba zinazo ungua? Ooh Mungu wangu" Bruno aliumia moyoni kisha akajipa moyo akisema "Sawa natumaini pindi wahanga hawa watakapo kuona ukiwa maiti basi mioyo yao itajaa tabasamu bashasha",alisema Bruno huku akiingiza mkono mfukoni aitoe hirizi ile aliyoichukua kwa Zabroni ili aitupie kwenye moto,lakini ajabu hakuikuta. Alistuka sana huku asijuwe kwamba muda ule alipotoa kitambaa kujifuta damu kiganjani aliidondosha chini. Pumzi ndefu alishusha na pindi alipotaka kurudu kuichukuwa, Mwemyekiti aliifka eneo la tukio kisha akamwambia "Hii ndio taabu ya hapa kijijini kijana wangu,hakika sitoamini siku nikimuona huyu mwanaharamu kauwawa". Hapo sasa Bruno alishindwa kumtoka Mwenyekiti ili aifuate hirizi ile kwani angeonekana hajaguswa na kitendo hicho cha nyumba kuungua. Muda huo sasa alfajiri tayari ilikuwa imeingia,umande na baridi ulimfanya Zabroni kutikisa kiuongo kimoja cha mwili wake,kumbe mtukutu alikuwa bado hajafa! U hai.

UKIWASHA MOTO KWENYE VIFUU UWE NA UWEZO WA KUUZIMA. me simo tukutane Sehemu ijayo.. mimi ni Team Zabroni aisee!
Makini sana mkuu kila siku huwa nakuja kuangalia mwendelezo!
Nipe ratiba ya vipande vinavyofuata ili niwe nakuja kutalii humu kwa wakati sahihi!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI TANO-15

Zabroni alitikisa mkono wake ambao ulikuwa unabembea,wakati huo chini ya ule mti aliotundikwa alikatiza kijana mmoja hivi wa makamo. Kijana huyo alikuwa katika harakati za kuwinda alfajiri hiyo mapema, hivyo akiwa chini ya mti aliotundikwa Zabroni ghafla tonya la damu lilimdondokea kichwani. Lakini alipuuzia akidhania kuwa huwenda tonya la umande ndilo lililomdondokea,ila mwishowe alistuka baada mchirizi wa damu kumdondokea kama maji. Hapo ndipo kijana huyo muwendaji alipoinua uso wake kutazama juu akamuona Zabroni akining'ia,alitaharuki. Haraka sana alitimua mbio huku akianguka mielekea mara mbili mbili wakati huo akipiga kelele akimuogopa Zabroni. Ila alipo fika mbele kidogo alisimama kisha akageuka kutazama nyuma alipotokea, mapigo ya moyo yalimuenda mbio akijiangalia yupo mikono mitupu. Sime mkuki pamoja na upanga vyote akiwa amevitupa pasipo yeye mwenywe kujielewa, yote hiyo ikiwa ni hofu ya kumuogopa Zabroni.
Kwa kutumia mkono wake wa kushoto,kijana huyo muwindaji alijigusa kichwani kisha akajitazama vidole vyake akaona damu. Akajisemea moyoni "Hii si damu? Mmh huyu jamaa atakuwa amekumbwa na nini sasa,na mbona asubuhi yote hii kanasa juu ya mti wakati sio kawaida yake?..Loh! Sio bure hapa kutakuwa kuna kitu kimetokea, Zabroni huyu ni naye mjua mimi hawezi kufa kizembe kizembe wala sio wa kujeruhiwa tu hovyo hovyo ", alijisemea muwendaji huyo huku akionekana kutaka kurudi kuchukuwa zana zake za mawindo. Lakini dhumuni hilo lilitoweka baada kukumbuka kasheshe kadhaa alizofanya Zabroni, aliamuwa kitimua mbio kuelekea kijijini kwa niaba ya kueleza kile alicho kiona. Na wakati huyo muwendaji alipokuwa akitimua mbio kwenda kutoa taarifa, upande wa pili kijijini. Alionekana Bruno akikuwa na Mwenyekiti wa kijiji pia na wazee wengineo wa kijijini hicho,walikuwa wamekaa wakiomboleza msiba mzito wa mzee Fungafunga na mkewe waliofia ndani pia na vifo vya wahanga wengine. Kiukweli yalikuwa ni majonzi ya aina yake,kila mmoja alisikitika kwa staili yake ilihari mioyoni mwao wakitamani Zabroni auwawe kwa njia yoyote kwani unyama aliokuwa akiufanya ulipitiliza kipimo hata Mungu hapendi. "Bruno,Huu ni wakati wa wewe kurudi nyumbani kwenu. Umempoteza kaka yako,chunga na wewe usije kupotea. Wazazi wenu mkawacha na viulizo,chukua mizigo yako uanze safari,haya mambo tuachie sisi",ilikuwa ni sauti ya Mwenyekiti akimwambia Bruno kwa masikitiko kabisa. Bruno naye aliposikia maneno hayo,alishusha pumzi kwanza kwa nguvu kisha akajibu. "Najua pia natambua ni namna gani mnavyopata shida,lakini mzee wangu labda nikwambie kitu. Siku zote Mungu akitaka kukupa mafanikio haji yeye kama yeye ila atapitia kwa binadamu mwenzako, lakini pia ukae ukijua hapa duniani hakuna mwamba. Bali mwamba ni Mungu pekee aliyejuu na sio sisi binadamu tulio umbwa kwa udongo na mwisho wa siku tunarudi kwenye udongo", alijibu Bruno,Mwenyekiti na wazee wengineo waliokuwepo mahala pale kila mmoja alitaharuki kusikia maneno ya kijana mdogo. Mzee mmoja alimgeukia kisha akamuuliza "Unamaana gani?.." Lakini kabla Bruno hajamjibu huyo mzee,mara ghafla yule kijana muwindaji alifika mahali hapo kwa kasi huku akihema juu juu. "We nawe vipi unawazimu?.." alihoji mzee wa pili huku akiwa amemkodolea macho. Mwenyekiti akaongezea kusema "Huyu kijana huwa namuangalia sana,kiukweli yani akili zake hazina tofauti na akili ya ndezi ama kobe. Chizi sio chizi,mwehu sio mwehu. Sijui ana akili gani huyu konono", alisema Mwenyekiti kwa hasira kali kwani huyo kijana aliwastua sana kwa kasi aliyokuja nayo,baadhi ya walitaka kukimbia wakidhania kuwa tayari mtukutu katia maguu. "Haya zungumza kilicho kufanya utoke huko mbio mbio mpaka hapa", muwendaji huyo ambae ni shuhuda,alituliza nafsi yake kwanza kabla hajaanza kuongea kile alicho kiona kule mstuni. Watu wote waliokuwepo pale kwenye maombolezo walimtazama yeye,naye alipo jihakikishia kuwa tayari yupo sawa alisema "Zabroni....",watu wote kasoro Bruno walistuka kulisikia hilo jina,Ghafla mmoja mmoja aliinuka na kisha kuondoka zake wakiogopa kwamba huwenda Zabroni yupo nyuma,ndio aliyekuwa anamkimbiza kijana huyo muwendaji aliyekuja mbio mbio. Upande wa Bruno yeye hakuwa na hofu kwa sababu aliamini kuwa tayari huyo kijana atakuwa ameona maiti ya Zabroni na hivyo atakuwa amekuja kutoa taarifa rasmi hapo kijijini kuhusu kifo cha huyo mtukutu,kitu ambacho ndicho alikuwa akikitamani na ndio maana alimtundika eneo lile la wazi ili mpita njia ama muwindaji yoyote atakae katiza eneo lile aweze kuishuhudia. Hivyo hofu ilitanda hapo,mama mmoja alisikika akiitikia kwa kusema "Heeh Zabroni? Aawapi jamani nilikuwepo nitarudi baadae", aliongea huku akiambaa na njia kutafuta mahali pa kujibanza ili kama Zabroni atafika pale yeye asiwepo. Lakini kabla hajafika mbali alisikia sauti zikisema "Mmmh jamani kweli ? "
"Aah sidhani,mzee Baluguza mtalamu. Mganga kati ya waganga kamshindwa eti leo hii ndio afe. Tena kirahisi rahisi tu? Teh teh teh..hiyo ndoto ya mchana "
"Sio bure huyu jamaa anakuwa kajambiwa na ndezi wake huko polini,anakuja kutueleza ujinga wake"
"Teh teh teh teh..Ni rahisi sana panya kubeba mimba ya paka kuliko mtu wa kawaida kumuua Zabroni, acheni kudanganyana bwana", zote hizo zilikuwa ni sauti moja ya maongezi yaliyosikika kwa fujo maeneo hayo,yote kutoka na kijana yule muwindaji kusimulia kile alicho kiona huku akisisitiza kuwa Zabroni kafa. Fujo ilisikika huku baadhi ya watu wakidiriki kumtukana,lakini baada Bruno kuona utata unazidi ndipo alipotaka kukata mzizi wa futina ili kuwaweka wanakijiji katika hali ya amani. Alifikinya kiganja chake kwa kutumia mkono wa kulia alifikanya kiganja cha mkono wa kushoto,kisha akafumbua kiganja hicho ambapo ulionekana ule mpambano aliopigana naye mpaka tamati. Hakika wanakijiji walishusha pumzi kila mmoja akimtazama Bruno kwa jicho la tatu na kumuona ni shujaa wa kukumbukwa katika hicho kijiji,yule mzee aliyemuuliza swali hapo awali alipata jibu la swali lake . Ambapo Bruno alipo mtazama,naye akamuonyeshea dole gumba kuonyesha kuwa tayari jibu analo. Furaha ilitawala sasa,hata wale walio kimbia mwanzo walirudi kuungana na wenzao kufurahia kifo cha Zabroni.
Baada ya hapo msafara wa wanakijiji ukiambatana na shujaa wao Bruno huku kiongozi akiwa Mwenyekiti,ulijikusanya ukaenda kuufuata mwili wa Zabroni ili wauchome moto. Lakini walipo fika eneo hilo hawakuuta mwili huo,walitaharuki wakamtazama Bruno ilihali Bruno naye akionekana kushindwa kujua kilicho tokea. Hofu kwa mara nyingine tena ilitanda mioyoni mwao,kila mmoja akionekana kuwa na sintofahamu kuhusu mtukutu. Na wakati wote wakiwa katika hali hiyo mara ghafla ilisikika sauti ikisema huku ikijirudia mara mbili mbili. Sauti hiyo ilisema "Mimi ndio Zabroni. Nimerudi ",sauti hiyo ikamaliza kwa kicheko kikali. Punde baada kusema hivyo ghafla....!

JE, kimetokea nini hapo?.

USIKOSE SEHEM IJAYO 16

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI NA SITA-16

Ghafla jeshi la polisi lilifika eneo la tukio,polisi hao walikuja na gari lao huku mbavuni mwao wakiwa na bunduki. Polisi mmoja aliyeonekana ndio mkuu wa msafara alitelemka kwenye gari kisha akazipiga hatua kuufuata ule umati,akiwa amekunja uso mithiri ya mtu aliyekula shubili. Polisi huyo alisema "Kuna nini mahali hapa?..", lakini wanakijiji hawakujibu,kila mmoja alionekana kukaa kimya ambapo ndipo yule mkuu wa msafara alipo muita kijana mmoja wa makamo falagha kisha kusema naye. "Kijana habari yako"
"Ni nzuri tu Afande sijui ya kwako",alijibu huyo kijana huku akionekana kujiamini kabisa,kwani hakuonyesha hofu yoyote kusimama na kamanda. Polisi alitazama kwanza upande ule waliosimama watu kabla hajaongeza nanl la pili,baadaye kidogo alirudisha uso wake kwa kijana huyo aliyekuwa naye falagha halafu akaendelea kuasema. "Naomba uniambie kuna kitu gani kimetokea hapa"
"Afande hapa bwana,tumekusanyika kuja kutazama mwili wa mtu aliyefariki usiku wa kuamkia leo. Sisi wanakijiji taarifa hiyo tumeipata asubuhi ya leo kutoka kwa mmoja ya vijana wa hapa kijijini,alitueleza kwamba kuna mtu kauliwa hapa Kwahiyo ndio maana mimi pamoja na wanakijiji wenzangu tumejumuika kuja kushuhudia. Lakini cha kustaajabisha ndugu Afande,maiti hatujaiona", alijibu kijana huyo.
"Unaweza kunitajia jina la huyo mtu aliyefariki?..", alihoji kamanda.
"Ndio, anaitwa Zabroni "
"Zabroni? ..", Afande alistuka kusikia jina hilo ni kama halikuwa jina jipya kuwahi kuisikia masikioni mwake,upesi akamuita kamanda mwenzake.
"Kamanda Pilo hebu njoo mara moja hapa",Afande huyo ambaye alifahamika kwa jina moja tu ambalo ni Pilo, alitii wito haraka sana. Alipomkalibia kiongozi wake alitoa heshima kisha akasema"Naam Afande" aliitikia.
"Pilo,chukua maelezo ya huyu kijana kisha report yake utanikabidhi tukifika ofisini", kwisha kusema hivyo kamanda huyo aliondoka zake akimuacha Pilo akimdadisi mwana kijiji kuhusu tukio nzima,lakini wakati Pilo anamdadisi kijana huyo ghafla alistuka kusikia jina la mtukutu Zabroni. Anamfahamu vizuri Zabroni, hasa hasa kipitia matukio mbali mbali aliyowahi kuyafanya huyo kijana. Wakati Pilo akifikilia matikio hayo,upande wa pili kamanda mkuu akiwa ndani ya gari aliwaza na kuwazua akajikuta kuwa jina hilo sio jipya masikioni mwake,kuthibitisha hilo akaamua kumuita kamanda mwingine aliyekuwa akizungumza na baadhi ya wanakijiji. Nahe alitii wito wa mkuu wake ambapo alipofika,kamanda alimuuliza "Je, unamfaham Zabroni ", kamanda huyo aliyeulizwa alitaharuki sana kisha akasema "Mkuu huyo mtu tema mate chini,nimeshangaa sana kutuamuru kuja kumtafuta huyu kiumbe wakati mwenzetu anatumia uchawi. Eh unona umati huu wa watu uliojikusanya hapa,walikuja kwa niaba ya kuchukua maiti yake waliamini kwamba amekufa lakini cha kushangaza hawajamkuta..", alijibu kwa hofu kamanda,wakati huo Pilo naye alikuwa amefika hapo ambapo naye alimuunga mkono kamanda mwenzake akisema kuwa maelezo aliyoyapata kutoka kwa yule kijana na ambayo amezungumza akamanda mwenzake hayana utofauti kabisa. Hapo mkuu alishusha pumzi ndefu kisha akahoji "Kwahiyo tunacheza na kifo?.."
"Kabisa "
"Ndio kamanda maisha yetu tumeyaweka rehani kabisa",walijibu hivyo hao maafande kitendo ambacho kilimkasilisha mkuu,kwa hasira akasema "Mkumbuke mliweka kiapo,sasa inakuaje mnakuwa waoga? Kwanza serikali yetu haimini masuala ya kishirikina,naomba kila mmoja afanye majukumu yake mpaka huyu mtu atiwe hatiani sawaaa?.."
"Sawa mkuuu ", walijibu wote kwa pamoja afande Pilo na mwenzake. "Haya nendeni mkuwaambie na wenzenu",aliongezea kusema hivyo kamanda kisha akawatawanya wanakijiji warudi majumbani mwao.
Bruno alionekana kuchoka maradufu,asiamini kama kweli Zabroni ni mzima. Alijiuliza ni dawa gani anayotumia kijana huyo kiasi kwamba awe moto wa kuotea mbali?. Kibaya zaidi zaidi kilicho mtia hofu kijana Bruno ni baada kufikiria kisasi gani atakacho kuja nacho huyo Zabroni ikiwa hapo awali alimueleza kuwa hayupo tayari tena kufanya unyama baada kukamilisha azma yake. "Inahitaji moyo pia na nguvu za ziada ",alijisemea Bruno huku akiwa na mwenyeketi wakitembea kurudi kijijini baada kutawanywa na jeshi la polisi. .
Usiku ulipo ingia hali ilikuwa shwari kijijini hapo,siku takribani tatu sasa zilikatika bila balaa lolote kutokea. Siku ya nne usiku,Bruno alimwambia Mwemyekiti wa kijiji ambaye pia ndio alikuwa mwenyeji wake hapo kijijini,alimwambia kuwa muda wa kurudi nyumbani kwao sasa umefika. "Mzee nimekaa sana hapa kijijini mimi pamoja na marehemu kaka yangu enzi ya uhai wake, nimeona changamoto mnazo kutana nazo kiukweli zinatisha. Kaka yangu amejaribu kupambana na huyu mtu lakini hajaweza kufua dafu,mwisho wa siku ameambulia umauti. Mimi pia nimejaribu kupambana na huyu mtu mpaka tonya la mwisho mpaka nikajua nimemmaliza,ila wapi kumbe jamaa bado yupo hai. Kiukweli huyu mtu hafai hata chembe,anatisha sana inatakiwa nguvu ya ziada kumdhibiti. Je, nguvu hii nitaipata wapi? Kwani bado inanibidi nilipe kisasi cha kifo cha kaka yangu. Nisipo fanya hivyo sitokuwa na amani ndani ya moyo wangu mpaka naingia kaburini. Sasa basi ili nilipe kisasi ni lazima nikaongeze nguvu kwenye mizimu ya ukoo wetu ili niweze kumkabili huyu mtu. Kesho narudi nyumbani mzee wangu,lazima nipambane na huyu mtu mpaka mwisho ",alisema Bruno huku akiongea kwa uchungu kutoka moyoni. Mwemyekiti alimtia moyo akimwambia kuwa hakuna mwamba chini ya jua ipo siku yake naye atakwama.
Kesho yake asubuhi mapema Bruno alianza safari ya kurudi nyumbani kwa niaba ya kuongeza makali ya kuweza kumkabili mtukutu Zabroni, lakini wakati yupo njiani,alionekana kijana Zabroni akizurula katika kijiji chakina Bruno. Na punde si punde Zabroni alijibadilisha akawa katika umbo la Bruno kisha akajongea mpaka nyumbani huku mkononi akiwa na mifuko iliyojaa vitu mbali mbali,huku mgongoni akiwa amebeba begi. Hakika watu walimshangaa sana Bruno mlowezi aliyerejea,wakati huo wengineo wakitamani kumuona na kaka yake malehemu Madebe kwani waliondoka wote katika shughuli za utafutaji maisha. Ni kiini macho na ujanja aliotumia mtukutu Zabroni ili amalize hasira zake, watu waliamini kuwa ni Bruno karejea wasijue kwamba huyo sio Bruno wanao mjua wao,bali huyo ni mtukutu Zabloni aliyechukuwa taswira ya Bruno ili afanye balaa kwa kutumia kivuli cha Bruno,mwisho wa siku msala uangukie kwa kijana huyo ambaye naye yupo njiani anarudi kuongeza dawa za kufanikisha kumkabili Zabroni. Wazazi wa Bruno walifurahi kumuona mtoto wao,Bruno alijieleza kuhusu kutokuwepo sambamba na kaka yake. Akiwa na furaha alisema "Kaka nimemuacha huko anafuatilia madeni yake,ila nafikiri kesho naye atafika "
"Aaah hakuna tatizo baba yetu, yani kama umerejea salama basi Mungu atamsaidia na yeye kurejea salama pia", akiwa na wingi wa furaha mama Bruno alimwambia kijana wake.
Kesho yake asubuhi Zabroni aliwauwa wazazi wa Bruno kisha akaondoka zake,hiyo ikiwa kama moja ya malipo ya kufatiliwa na mtoto wao aliyejikita kwenye vita isiyo muhusu. Ila atafanya nini sasa ili amuachie msala Bruno?. Hapo sasa ndipo alipomuuwa mmoja ya vijana hapo kijijini hadhalani huku baadhi ya watu wakishuhudi balaa hilo la kinyama kwani tayari ilikuwa ni asubuhi. Hivyo alivyokwisha kufanya hicho kitendo alijigamba "Mimi ndio Bruno,hakuna atakae niweza. Nimeua kwa mikono yangu ",alisema Zabroni akiwa na taswira ya Bruno kisha akatokomea zake huku akiacha maswali mengi kwa wenyeji. Habari zilizagaa upesi kila pande kuhusu hayo mauwaji, walijua dhahiri shahili Bruno ndiye aliyefanya mauwaji ilihali wakati huo huo stendi ya gari alionekana kijana Bruno mwenyewe akishuka kwenye gari baada kufika kijijini kwao alipo zaliwa,macho na hisia akitamani kuonana na wazazi wake ili wamsaidie katika kitu alicho pania kula nacho sahani moja na mtukutuku Zabroni.

USIKOSE SEHEMU IJAYO.. HII KITU INGINE Zabroni Zabroni!
kwanini PENZI LA MFUNGWA? kuwa na mimi mpaka tam

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI NA SITA-16

Ghafla jeshi la polisi lilifika eneo la tukio,polisi hao walikuja na gari lao huku mbavuni mwao wakiwa na bunduki. Polisi mmoja aliyeonekana ndio mkuu wa msafara alitelemka kwenye gari kisha akazipiga hatua kuufuata ule umati,akiwa amekunja uso mithiri ya mtu aliyekula shubili. Polisi huyo alisema "Kuna nini mahali hapa?..", lakini wanakijiji hawakujibu,kila mmoja alionekana kukaa kimya ambapo ndipo yule mkuu wa msafara alipo muita kijana mmoja wa makamo falagha kisha kusema naye. "Kijana habari yako"
"Ni nzuri tu Afande sijui ya kwako",alijibu huyo kijana huku akionekana kujiamini kabisa,kwani hakuonyesha hofu yoyote kusimama na kamanda. Polisi alitazama kwanza upande ule waliosimama watu kabla hajaongeza nanl la pili,baadaye kidogo alirudisha uso wake kwa kijana huyo aliyekuwa naye falagha halafu akaendelea kuasema. "Naomba uniambie kuna kitu gani kimetokea hapa"
"Afande hapa bwana,tumekusanyika kuja kutazama mwili wa mtu aliyefariki usiku wa kuamkia leo. Sisi wanakijiji taarifa hiyo tumeipata asubuhi ya leo kutoka kwa mmoja ya vijana wa hapa kijijini,alitueleza kwamba kuna mtu kauliwa hapa Kwahiyo ndio maana mimi pamoja na wanakijiji wenzangu tumejumuika kuja kushuhudia. Lakini cha kustaajabisha ndugu Afande,maiti hatujaiona", alijibu kijana huyo.
"Unaweza kunitajia jina la huyo mtu aliyefariki?..", alihoji kamanda.
"Ndio, anaitwa Zabroni "
"Zabroni? ..", Afande alistuka kusikia jina hilo ni kama halikuwa jina jipya kuwahi kuisikia masikioni mwake,upesi akamuita kamanda mwenzake.
"Kamanda Pilo hebu njoo mara moja hapa",Afande huyo ambaye alifahamika kwa jina moja tu ambalo ni Pilo, alitii wito haraka sana. Alipomkalibia kiongozi wake alitoa heshima kisha akasema"Naam Afande" aliitikia.
"Pilo,chukua maelezo ya huyu kijana kisha report yake utanikabidhi tukifika ofisini", kwisha kusema hivyo kamanda huyo aliondoka zake akimuacha Pilo akimdadisi mwana kijiji kuhusu tukio nzima,lakini wakati Pilo anamdadisi kijana huyo ghafla alistuka kusikia jina la mtukutu Zabroni. Anamfahamu vizuri Zabroni, hasa hasa kipitia matukio mbali mbali aliyowahi kuyafanya huyo kijana. Wakati Pilo akifikilia matikio hayo,upande wa pili kamanda mkuu akiwa ndani ya gari aliwaza na kuwazua akajikuta kuwa jina hilo sio jipya masikioni mwake,kuthibitisha hilo akaamua kumuita kamanda mwingine aliyekuwa akizungumza na baadhi ya wanakijiji. Nahe alitii wito wa mkuu wake ambapo alipofika,kamanda alimuuliza "Je, unamfaham Zabroni ", kamanda huyo aliyeulizwa alitaharuki sana kisha akasema "Mkuu huyo mtu tema mate chini,nimeshangaa sana kutuamuru kuja kumtafuta huyu kiumbe wakati mwenzetu anatumia uchawi. Eh unona umati huu wa watu uliojikusanya hapa,walikuja kwa niaba ya kuchukua maiti yake waliamini kwamba amekufa lakini cha kushangaza hawajamkuta..", alijibu kwa hofu kamanda,wakati huo Pilo naye alikuwa amefika hapo ambapo naye alimuunga mkono kamanda mwenzake akisema kuwa maelezo aliyoyapata kutoka kwa yule kijana na ambayo amezungumza akamanda mwenzake hayana utofauti kabisa. Hapo mkuu alishusha pumzi ndefu kisha akahoji "Kwahiyo tunacheza na kifo?.."
"Kabisa "
"Ndio kamanda maisha yetu tumeyaweka rehani kabisa",walijibu hivyo hao maafande kitendo ambacho kilimkasilisha mkuu,kwa hasira akasema "Mkumbuke mliweka kiapo,sasa inakuaje mnakuwa waoga? Kwanza serikali yetu haimini masuala ya kishirikina,naomba kila mmoja afanye majukumu yake mpaka huyu mtu atiwe hatiani sawaaa?.."
"Sawa mkuuu ", walijibu wote kwa pamoja afande Pilo na mwenzake. "Haya nendeni mkuwaambie na wenzenu",aliongezea kusema hivyo kamanda kisha akawatawanya wanakijiji warudi majumbani mwao.
Bruno alionekana kuchoka maradufu,asiamini kama kweli Zabroni ni mzima. Alijiuliza ni dawa gani anayotumia kijana huyo kiasi kwamba awe moto wa kuotea mbali?. Kibaya zaidi zaidi kilicho mtia hofu kijana Bruno ni baada kufikiria kisasi gani atakacho kuja nacho huyo Zabroni ikiwa hapo awali alimueleza kuwa hayupo tayari tena kufanya unyama baada kukamilisha azma yake. "Inahitaji moyo pia na nguvu za ziada ",alijisemea Bruno huku akiwa na mwenyeketi wakitembea kurudi kijijini baada kutawanywa na jeshi la polisi. .
Usiku ulipo ingia hali ilikuwa shwari kijijini hapo,siku takribani tatu sasa zilikatika bila balaa lolote kutokea. Siku ya nne usiku,Bruno alimwambia Mwemyekiti wa kijiji ambaye pia ndio alikuwa mwenyeji wake hapo kijijini,alimwambia kuwa muda wa kurudi nyumbani kwao sasa umefika. "Mzee nimekaa sana hapa kijijini mimi pamoja na marehemu kaka yangu enzi ya uhai wake, nimeona changamoto mnazo kutana nazo kiukweli zinatisha. Kaka yangu amejaribu kupambana na huyu mtu lakini hajaweza kufua dafu,mwisho wa siku ameambulia umauti. Mimi pia nimejaribu kupambana na huyu mtu mpaka tonya la mwisho mpaka nikajua nimemmaliza,ila wapi kumbe jamaa bado yupo hai. Kiukweli huyu mtu hafai hata chembe,anatisha sana inatakiwa nguvu ya ziada kumdhibiti. Je, nguvu hii nitaipata wapi? Kwani bado inanibidi nilipe kisasi cha kifo cha kaka yangu. Nisipo fanya hivyo sitokuwa na amani ndani ya moyo wangu mpaka naingia kaburini. Sasa basi ili nilipe kisasi ni lazima nikaongeze nguvu kwenye mizimu ya ukoo wetu ili niweze kumkabili huyu mtu. Kesho narudi nyumbani mzee wangu,lazima nipambane na huyu mtu mpaka mwisho ",alisema Bruno huku akiongea kwa uchungu kutoka moyoni. Mwemyekiti alimtia moyo akimwambia kuwa hakuna mwamba chini ya jua ipo siku yake naye atakwama.
Kesho yake asubuhi mapema Bruno alianza safari ya kurudi nyumbani kwa niaba ya kuongeza makali ya kuweza kumkabili mtukutu Zabroni, lakini wakati yupo njiani,alionekana kijana Zabroni akizurula katika kijiji chakina Bruno. Na punde si punde Zabroni alijibadilisha akawa katika umbo la Bruno kisha akajongea mpaka nyumbani huku mkononi akiwa na mifuko iliyojaa vitu mbali mbali,huku mgongoni akiwa amebeba begi. Hakika watu walimshangaa sana Bruno mlowezi aliyerejea,wakati huo wengineo wakitamani kumuona na kaka yake malehemu Madebe kwani waliondoka wote katika shughuli za utafutaji maisha. Ni kiini macho na ujanja aliotumia mtukutu Zabroni ili amalize hasira zake, watu waliamini kuwa ni Bruno karejea wasijue kwamba huyo sio Bruno wanao mjua wao,bali huyo ni mtukutu Zabloni aliyechukuwa taswira ya Bruno ili afanye balaa kwa kutumia kivuli cha Bruno,mwisho wa siku msala uangukie kwa kijana huyo ambaye naye yupo njiani anarudi kuongeza dawa za kufanikisha kumkabili Zabroni. Wazazi wa Bruno walifurahi kumuona mtoto wao,Bruno alijieleza kuhusu kutokuwepo sambamba na kaka yake. Akiwa na furaha alisema "Kaka nimemuacha huko anafuatilia madeni yake,ila nafikiri kesho naye atafika "
"Aaah hakuna tatizo baba yetu, yani kama umerejea salama basi Mungu atamsaidia na yeye kurejea salama pia", akiwa na wingi wa furaha mama Bruno alimwambia kijana wake.
Kesho yake asubuhi Zabroni aliwauwa wazazi wa Bruno kisha akaondoka zake,hiyo ikiwa kama moja ya malipo ya kufatiliwa na mtoto wao aliyejikita kwenye vita isiyo muhusu. Ila atafanya nini sasa ili amuachie msala Bruno?. Hapo sasa ndipo alipomuuwa mmoja ya vijana hapo kijijini hadhalani huku baadhi ya watu wakishuhudi balaa hilo la kinyama kwani tayari ilikuwa ni asubuhi. Hivyo alivyokwisha kufanya hicho kitendo alijigamba "Mimi ndio Bruno,hakuna atakae niweza. Nimeua kwa mikono yangu ",alisema Zabroni akiwa na taswira ya Bruno kisha akatokomea zake huku akiacha maswali mengi kwa wenyeji. Habari zilizagaa upesi kila pande kuhusu hayo mauwaji, walijua dhahiri shahili Bruno ndiye aliyefanya mauwaji ilihali wakati huo huo stendi ya gari alionekana kijana Bruno mwenyewe akishuka kwenye gari baada kufika kijijini kwao alipo zaliwa,macho na hisia akitamani kuonana na wazazi wake ili wamsaidie katika kitu alicho pania kula nacho sahani moja na mtukutuku Zabroni.

USIKOSE SEHEMU IJAYO.. HII KITU INGINE Zabroni Zabroni!
kwanini PENZI LA MFUNGWA? kuwa na mimi mpaka tam

Sent using Jamii Forums mobile app
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI TANO-15

Zabroni alitikisa mkono wake ambao ulikuwa unabembea,wakati huo chini ya ule mti aliotundikwa alikatiza kijana mmoja hivi wa makamo. Kijana huyo alikuwa katika harakati za kuwinda alfajiri hiyo mapema, hivyo akiwa chini ya mti aliotundikwa Zabroni ghafla tonya la damu lilimdondokea kichwani. Lakini alipuuzia akidhania kuwa huwenda tonya la umande ndilo lililomdondokea,ila mwishowe alistuka baada mchirizi wa damu kumdondokea kama maji. Hapo ndipo kijana huyo muwendaji alipoinua uso wake kutazama juu akamuona Zabroni akining'ia,alitaharuki. Haraka sana alitimua mbio huku akianguka mielekea mara mbili mbili wakati huo akipiga kelele akimuogopa Zabroni. Ila alipo fika mbele kidogo alisimama kisha akageuka kutazama nyuma alipotokea, mapigo ya moyo yalimuenda mbio akijiangalia yupo mikono mitupu. Sime mkuki pamoja na upanga vyote akiwa amevitupa pasipo yeye mwenywe kujielewa, yote hiyo ikiwa ni hofu ya kumuogopa Zabroni.
Kwa kutumia mkono wake wa kushoto,kijana huyo muwindaji alijigusa kichwani kisha akajitazama vidole vyake akaona damu. Akajisemea moyoni "Hii si damu? Mmh huyu jamaa atakuwa amekumbwa na nini sasa,na mbona asubuhi yote hii kanasa juu ya mti wakati sio kawaida yake?..Loh! Sio bure hapa kutakuwa kuna kitu kimetokea, Zabroni huyu ni naye mjua mimi hawezi kufa kizembe kizembe wala sio wa kujeruhiwa tu hovyo hovyo ", alijisemea muwendaji huyo huku akionekana kutaka kurudi kuchukuwa zana zake za mawindo. Lakini dhumuni hilo lilitoweka baada kukumbuka kasheshe kadhaa alizofanya Zabroni, aliamuwa kitimua mbio kuelekea kijijini kwa niaba ya kueleza kile alicho kiona. Na wakati huyo muwendaji alipokuwa akitimua mbio kwenda kutoa taarifa, upande wa pili kijijini. Alionekana Bruno akikuwa na Mwenyekiti wa kijiji pia na wazee wengineo wa kijijini hicho,walikuwa wamekaa wakiomboleza msiba mzito wa mzee Fungafunga na mkewe waliofia ndani pia na vifo vya wahanga wengine. Kiukweli yalikuwa ni majonzi ya aina yake,kila mmoja alisikitika kwa staili yake ilihari mioyoni mwao wakitamani Zabroni auwawe kwa njia yoyote kwani unyama aliokuwa akiufanya ulipitiliza kipimo hata Mungu hapendi. "Bruno,Huu ni wakati wa wewe kurudi nyumbani kwenu. Umempoteza kaka yako,chunga na wewe usije kupotea. Wazazi wenu mkawacha na viulizo,chukua mizigo yako uanze safari,haya mambo tuachie sisi",ilikuwa ni sauti ya Mwenyekiti akimwambia Bruno kwa masikitiko kabisa. Bruno naye aliposikia maneno hayo,alishusha pumzi kwanza kwa nguvu kisha akajibu. "Najua pia natambua ni namna gani mnavyopata shida,lakini mzee wangu labda nikwambie kitu. Siku zote Mungu akitaka kukupa mafanikio haji yeye kama yeye ila atapitia kwa binadamu mwenzako, lakini pia ukae ukijua hapa duniani hakuna mwamba. Bali mwamba ni Mungu pekee aliyejuu na sio sisi binadamu tulio umbwa kwa udongo na mwisho wa siku tunarudi kwenye udongo", alijibu Bruno,Mwenyekiti na wazee wengineo waliokuwepo mahala pale kila mmoja alitaharuki kusikia maneno ya kijana mdogo. Mzee mmoja alimgeukia kisha akamuuliza "Unamaana gani?.." Lakini kabla Bruno hajamjibu huyo mzee,mara ghafla yule kijana muwindaji alifika mahali hapo kwa kasi huku akihema juu juu. "We nawe vipi unawazimu?.." alihoji mzee wa pili huku akiwa amemkodolea macho. Mwenyekiti akaongezea kusema "Huyu kijana huwa namuangalia sana,kiukweli yani akili zake hazina tofauti na akili ya ndezi ama kobe. Chizi sio chizi,mwehu sio mwehu. Sijui ana akili gani huyu konono", alisema Mwenyekiti kwa hasira kali kwani huyo kijana aliwastua sana kwa kasi aliyokuja nayo,baadhi ya walitaka kukimbia wakidhania kuwa tayari mtukutu katia maguu. "Haya zungumza kilicho kufanya utoke huko mbio mbio mpaka hapa", muwendaji huyo ambae ni shuhuda,alituliza nafsi yake kwanza kabla hajaanza kuongea kile alicho kiona kule mstuni. Watu wote waliokuwepo pale kwenye maombolezo walimtazama yeye,naye alipo jihakikishia kuwa tayari yupo sawa alisema "Zabroni....",watu wote kasoro Bruno walistuka kulisikia hilo jina,Ghafla mmoja mmoja aliinuka na kisha kuondoka zake wakiogopa kwamba huwenda Zabroni yupo nyuma,ndio aliyekuwa anamkimbiza kijana huyo muwendaji aliyekuja mbio mbio. Upande wa Bruno yeye hakuwa na hofu kwa sababu aliamini kuwa tayari huyo kijana atakuwa ameona maiti ya Zabroni na hivyo atakuwa amekuja kutoa taarifa rasmi hapo kijijini kuhusu kifo cha huyo mtukutu,kitu ambacho ndicho alikuwa akikitamani na ndio maana alimtundika eneo lile la wazi ili mpita njia ama muwindaji yoyote atakae katiza eneo lile aweze kuishuhudia. Hivyo hofu ilitanda hapo,mama mmoja alisikika akiitikia kwa kusema "Heeh Zabroni? Aawapi jamani nilikuwepo nitarudi baadae", aliongea huku akiambaa na njia kutafuta mahali pa kujibanza ili kama Zabroni atafika pale yeye asiwepo. Lakini kabla hajafika mbali alisikia sauti zikisema "Mmmh jamani kweli ? "
"Aah sidhani,mzee Baluguza mtalamu. Mganga kati ya waganga kamshindwa eti leo hii ndio afe. Tena kirahisi rahisi tu? Teh teh teh..hiyo ndoto ya mchana "
"Sio bure huyu jamaa anakuwa kajambiwa na ndezi wake huko polini,anakuja kutueleza ujinga wake"
"Teh teh teh teh..Ni rahisi sana panya kubeba mimba ya paka kuliko mtu wa kawaida kumuua Zabroni, acheni kudanganyana bwana", zote hizo zilikuwa ni sauti moja ya maongezi yaliyosikika kwa fujo maeneo hayo,yote kutoka na kijana yule muwindaji kusimulia kile alicho kiona huku akisisitiza kuwa Zabroni kafa. Fujo ilisikika huku baadhi ya watu wakidiriki kumtukana,lakini baada Bruno kuona utata unazidi ndipo alipotaka kukata mzizi wa futina ili kuwaweka wanakijiji katika hali ya amani. Alifikinya kiganja chake kwa kutumia mkono wa kulia alifikanya kiganja cha mkono wa kushoto,kisha akafumbua kiganja hicho ambapo ulionekana ule mpambano aliopigana naye mpaka tamati. Hakika wanakijiji walishusha pumzi kila mmoja akimtazama Bruno kwa jicho la tatu na kumuona ni shujaa wa kukumbukwa katika hicho kijiji,yule mzee aliyemuuliza swali hapo awali alipata jibu la swali lake . Ambapo Bruno alipo mtazama,naye akamuonyeshea dole gumba kuonyesha kuwa tayari jibu analo. Furaha ilitawala sasa,hata wale walio kimbia mwanzo walirudi kuungana na wenzao kufurahia kifo cha Zabroni.
Baada ya hapo msafara wa wanakijiji ukiambatana na shujaa wao Bruno huku kiongozi akiwa Mwenyekiti,ulijikusanya ukaenda kuufuata mwili wa Zabroni ili wauchome moto. Lakini walipo fika eneo hilo hawakuuta mwili huo,walitaharuki wakamtazama Bruno ilihali Bruno naye akionekana kushindwa kujua kilicho tokea. Hofu kwa mara nyingine tena ilitanda mioyoni mwao,kila mmoja akionekana kuwa na sintofahamu kuhusu mtukutu. Na wakati wote wakiwa katika hali hiyo mara ghafla ilisikika sauti ikisema huku ikijirudia mara mbili mbili. Sauti hiyo ilisema "Mimi ndio Zabroni. Nimerudi ",sauti hiyo ikamaliza kwa kicheko kikali. Punde baada kusema hivyo ghafla....!

JE, kimetokea nini hapo?.

USIKOSE SEHEM IJAYO 16

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimesoma kwa mfululizo bila kusimama!
Ni bonge ya story mkuu...
Zabroni ni habari nyingine !
Mkuu naomba kufahamu ratiba za mwendelezo wa hii story Ili nisipitwe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI SABA-17

Bruno alipigwa na butwaa baada kuona watu wakimnyooshea vidole,alijiuliza kitu gani ambacho kinapelekea mpaka yeye anyooshewe vidole? Je, wameshajua kama kaka yangu kafa? Ama kuna jambo gani linalo endelea. Hatamaye alikaribia kufika nyumbani kwao,alistuka kuona umati wa watu ukiwa umejikusanya nyumbani kwao huku sauti za vilio zikisikika masikioni mwake. Bruno alishitu mara dufu, hapo sasa kijasho kikaanza kumtoka,mwili wake nao ukihisi kukosa nguvu. Upesi aliachia mazaga zaga aliyokuwa ameyabeba,mazaga ambayo yalifanana fika na yale aliyokuwa nayo Zabroni kipindi anaingia hapo kijijini kwa taswira ya Bruno. Macho ya watu walio jikusanya hapo walipomuona Bruno walikunja nyuso zao huku baadhi yao wakizungumza maneno ya kumkashifu,maneno ambayo yalisikika vema ni pale mzee mmoja wa makamo aliposikika akisema "Ama hakika damu ya mtu nzito kuliko maji,ona sasa muuwaji kajileta mwenyewe. Hebu akamatwe haraka sana iwezekavyo"
"Mmh huyu sio mtu wa kawaida jamani,tukimfuata kizembe tutajikuta tunapoteza maisha ",alidakia mtu wa pili akisema hivyo,huyo alikuwa ni kijana wapata umri miaka ishirini na mitano. Hoja yake hiyo iliungwa mkono na baadhi ya watu wengine waliokuwepo hapo wakati huo tayari Bruno alikuwa ameshafika nyumbani kwao ambapo alistaajabu kuona watu wanamkwepa,hali hiyo iliendelea kumjengea hofu moyoni mwake,na ndipo alipopasa sauti akisema "Jamani kulikoni mbona siwaelewi?.." Alihoji huku akijitazama akigeuza shingo huku na kule kutazama sehemu mbali mbali za mwili wake. Lakini hakujibiwa,hivyo aliamua kuingia ndani ambapo huko walionekana wanawake wakilia kwa uchungu ila walipo muona Bruno haraka sana walikaa kimya kisha mmoja mmoja akatoka ndani. Hakika watu walimuogopa Bruno,walijuwa ndio kafanya mauwaji kwani wakati anatoka ndani baada kuuwa alionekana na mmoja ya jirani yao huku nguo zake zikiwa zimetapakaa damu. Achilia hapo,kitendo kingine ambacho kilipelekea Bruno kuogopwa, ni pale alipomuua hadharani mmoja wa kijana kijijini hapo huku akijigamba kuwa amefanya mauaji kwa kukusudia napia hakuna mtu wa kuweza kumtia hatiani. Lakini yote hayo yaliyofanyika hakuyafanya Bruno kama watu walivyodhani,bali mtendaji alikuwa ni Zabroni ambaye alichukuwa taswira ya Bruno na kisha kuuwa ikiwa kama njia ya kumsababishia msala Buruno. Hayo yote Zabloni aliyafanya baada kuingilia ugomvi usio muhusu huku akijaribu kufanya jaribio la kumuuwa.
Bruno alikabaliana na hiyo hali watu kumuogopa,hakujali bali alijongea mpaka mahala pale ilipo lazwa miili miwili ikiwa imefunikwa vitenge. Alipo ifikia akaifunua, alistuka kuona miili ya wazazi wake ikiwa imeuwawa kikatili. Alilia sana huku akiwataja wazazi wake walio uliwa, na mwishowe alinyanyuka akatoka ndani. Nje alimuita mzee mmoja aliyemuona anabusara,mzee huyo alipoona anaitwa na Buruno aliogopa kwenda lakini wazee wenzake walipo mtaka aende alitii wito. "Habari yako mzee" alisema Bruno huku moyo wake ukiwa umefura hasira kama nyoka aliyemkosa binadam.
"Nzuri..nzuri kijana wangu ", alijibu huyo mzee akiwa na wasiwasi mfano wa mtu aliyefumaniwa ugoni.
"Hivi unawez kunitajia ama unaweza kunieleza ni nani aliyefanya hiki kitendo?.." alihoji, swali hilo lilimshangaza huyo mzee akajikuta akishindwa jibu la kumpatia kwani anafahamu fika kuwa Bruno ndio muuwaji sasa inakuwaje atake kutajiwa muuwaji?..Mzee akajiongeza kwa kukataa kwamba hamjui muuwaji. "Sawa nenda ", mzee alirudi kujichanganya na wenzake. Wakati huo huo jeshi la polisi likiambatana na mbwa watano huku likiwa na siraha mbali mbali lilifika eneo hilo la tukio,kwa niaba ya kumkata muuwaji. Bruno bado alikuwa katika hali ya kupigwa na bumbuwazi asijue kinacho endelea,lakini punde alifahamu kinacho endelea baada mama mmoja ambaye alionekana kulia kwa uchungu huku akimnyoshea kidole . Mama huyo akilia alisema "Yule pale muuwaji,kaniulia mwanangu. Hafai kabisa sitaki hata kumuona machoni mwangu",kamanda mkuu alitoa amri kuwa Bruno akamatwe. Bruno alishangaa,akajiuliza "Mimi nimekuwa muuwaji?mmmh hapana!.." baada kujiuliza hivyo ikabidi ajitetee lakini Bruno hakueleweka,alikamatwa huku wakimtaka akajieleza mbele kwa mbele. Ndani ya gari la polisi Bruno alirushwa kisha gari likatimua mbio ilihali huku nyuma wakisalia baadhi ya polisi kwa niaba ya kuzika hiyo miili iliyo uwawa kikatili. Bruno akiwa ndani ya gari hilo la polidi,alijiinamia huku akijiuliza maswali mengi kichwani mwake. Alijiuliza "Hivi ni nani muuwaji wa wazazi wangu? Na nikipi kinacho pelekea nikamatwe mimi ilihali mimi sio muuwaji?na endapo nitafungwa nitawezaje kulipa kisasi? Na iweje nifungwe kwa kosa ambalo sijafanya?..", alijiuliza Bruno huku akiwa amejiinamia . Hatimaye walifika kituo cha polisi ambapo hapo Bruno alishushwa mfano wa gunia la mkaa kwa niaba ya kuuingiza selo ili uchunguzi ufanyike kabla hajapelekwa kizimbani, lakini wakati anaingia ndani ghafla alisikia sauti ikimuita. Upesi Bruno aligeukia kule ilipo tokea sauti hiyo ajabu sana alimuona mtu aliyefananae kuanzia sura mpaka nguo alizovaa, si mwingine ni Zabroni. Hapo sasa ndipo Bruno alipofahamu fika mtandaji wa lile jambo ni Zabroni ambaye alifanya jambo lile huku akiwa katika hali yake ili kumsababishia msala yeye. Hakika Bruno akiwa na pingu mkononi aliumia sana,machungu yaliongezeka mara mbili kwani tayari Zabroni alikuwa amemuulia wazazi wake. Lakini yote yote Bruno aliingizwa ndani huku nje Zabroni naye akijinasibu kwa kusema "Mimi ndio Zabroni",kwisha kujisemea hivyo alirudi katika umbile lake la kawaida.
Kazi ikawa imemalizika sasa,wabaya wake alikuwa aneshamalizana nao. Hivyo akawa mtu wa amani wakati wote,alijichanganya na wenzake kwani mahali hapo alikuwa mgeni kwahiyo hakuna mtu hata mmoja aliyefahamu historia yake. Lakini wakati kijana Zabroni akiwa mtu wa amani wakati wote huku akiacha utukutu wake, upande wa pili kule kijijini kwao bado jeshi la polisi lilikuwa likiendelea kumuwinda kwa udi na uvumba. Na mara baada kumtafuta kwa muda mrefu bila mafanikio,hatimaye kamanda wao alipata wazo. Wazo ambalo aliwaeleza wenzake kwamba ili wamkamte Zabroni basi itawalazimu wamtumie mwanamke,kwani kufanya hivyo inaweza kupelekea kijana huyo kukamatwa bila kutoa jasho. Kwa sababu siku zote mwanaume kwa mwanamke huwa ni mzaifu sana,hivyo Mwanamke huyo atakaye teuliwa ni lazima aweke ukaribu na Zabroni wakati huo akimuuliza mambo mbali mbali kuhusu uwezo wake wa kupotea katika mazingira yoyote. Na pia asisahau kumuwekea utani kwa kumdadisi kwamba ili ujanja wake ufike tamati njia gani itatakiwa ifanyike. Kufanya hivyo inaweza kuwa rahisi sana kumkataa Zabroni pasipo kutoa jasho lakini pia mwanamke mwenyewe lazima awe mrembo,sio mwanamke awe na uso mkavu kama fenesi, pua kama nyundo. Kichogo kama kinu . Mwanamke awe mzuri kiasi kwamba akijiweka kwa Zabroni,basi mtukutu asisite kujenga naye uhusiano. Walikubaliana hilo suala wakaona linafaa, lakini ugumu kujua mahali alipokimbilia mtukutu huyo vile vile wapi watampata mrembo wa kuvutia. "Kamanda kuhusu hilo halina shaka,yupo huyu binti aliyeanza kazi wiki iliyopita Afande Veronica,huyu anafaa sana siunaona alivyokuwa mrembo? .."
"Ni kweli anafaa itabidi aje ofisini leo ili niweze kuzungumza naye hili suala ili siku yoyote aanze kazi"
"Sawa kamanda"
Siku hiyo hiyo Afande Veronica alitii wito aliambiwa jinsi hali inavyotakiwa kuwa huku akiahidiwa ZAWADI nono pia kupandishwa cheo pindi atakapo funga ukurasa wa mishe hiyo. Wakati wanafikia muafaka Veronica na mkuu wake, mara ghafla kituoni hapo alikuja raia kutoa taarifa kwamba Zabroni yupo mahali fulani anaendelea na maisha yake. Jambo la heri kiukweli kwa upande wa hao Makanda hao kwani waliona tayari mchezo unakwenda kumalizika.
"Vero,"
"Yes kamanda"
"Wewe mrembo bwana,siku mbili hizi anza kazi,hautokuwa peke yako bali na sisi tupo nyuma yako kukupa ushirikiano. Vaa nguo za kiraia anza kazi"
"Usijali kamanda,wanaume nyie wa kwetu kamwe hamruki katika suala zima la mapenzi hasa kwa mwanamke mzuri kama mimi. Nakuhakikishia hapa kanasa ",alijibu kwa masihara na kujiamini pia Afande Veronica,Afande ambaye alionekana kuvutia kila kona ya mwili. Ngozi nyororo uso mzuri mpaka mwili wake ulivutia umbo namba nane.

JE, ATAWEZA KWELI? tusubili sehemu ya 18.
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi: sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI NA NANE-18

Wahenga waliwahi sema kwamba,ukitaka kuruka?sharti uagane na nyonga. Abadani hawakukosea kusema msemo huo,bila shaka waliona mbali sana na ndio maana wakaamua kusema huo msemo ambao unatumika sana kwa mtu aliyeamua kujitosa kutenda jambo fulani. Ndivyo ilivyokuwa kwa kamanda wa kike Veronica, kamanda ambaye aliamua kujitolea kumtia Zabroni kwenye mkono wa sheria kwa kutumia mbinu ya aina yake. Ikimbukwe Zabroni kipindi cha nyuma aliwahi kufanya mauaji mbali mbali,alitia watu hasara mali zao lakini alifanya kila jambo mbaya ambalo hata mwenyezi mungu hapendi. Vitendo hivyo vilipo shamili,jeshi la polisi ndipo lilipo amua kuingilia kati ingawa bado walichemka kwa sababu Zabroni hakamatiki kwa siraha. Baada kumshindwa kwa siraha ndipo walipoona kwamba watumie njia ya mapenzi,kwani mapenzi siku zote yananguvu kuliko kitu chochote hapa duniani kwani mapenzi hayana komando. Sasa basi njia hiyo itweza kumtia mtukutu Zabroni kwenye mkono wa dola? Je, Veronica ataweza?
****
Baada ya makubaliano kufanyika, siku tatu zilikatika. Siku ya nne kamanda Veronique alianza kazi ambapo aliambiwa mahali ambapo Zabroni hupendelea kukaa katika hicho kijiji,hiyo ikawa rahisi kwake kwani alipotembelea maeneo hayo siku ya kwanza hakumkuta lakini siku ya pili alimkuta akishirikiana na wenzake katika shughuli za jamii. Baada kumuona alichomoa picha ndogo aliyokabidhiwa,aliitazama kisha akamtazama Zabroni kule alipokuwa akichakarika. Alipo jihakikishia kuwa ndiyo huyo,aliirudisha kwenye mkoba wake picha ya Zabroni kisha akarejea mjini nyumba ya wageni alipokuwa amepanga chumba. Akiwa amechoka alijilaza kitandani huku akiwa na nguo ya kulalia,kifua chake kikiwa wazi. Kiukweli kilivutia sana,chuchu zilikuwa zimesimama. Ngozi yake ikiwa nyororo pia kitovu chake kilikuwa kina shimo kidogo,tumbo lake likiwa laini kama nyama ya ulimi. Kamanda Veronique alivutia sana kizuri kisifie. Basi hapo baada kujilaza kitandani,akili yake yote aliifikiria namna ya kumkamata Zabroni. Mawazo ambayo yalimpelekea kupitiwa na usingizi ila aliamshwa na sauti ya simu ikiwa inaita,alikurupa kutoka usingizi alipo tazama jina la mtu aliyempigia akaona jina limeandikwa "Kamanda Molisy" alibonyesha kitufe cha kijani kisha akaweka sikioni alisema kwa sauti ya upole "Afande"
"Mmmh Veronique habari yako?..",ilisikika sauti ikijibu hivyo kwa mbali.
"Salama tu sijui kwenu huko"
"Kwetu salama,mbona wasikika kwa upole?..", alihoji kamanda Molisy ambaye ndio mkuu wa kikosi hicho cha kina Veronica.
"Aahmm.. nilikuwa nimelala siunajua kazi ilivyo? Lakini ondoa shaka leo nimebahatika kumuona,nina uhakika kazi itakuwa nyepesi sana", aliongea Veronica huku ikijonyoosha akizipiga hatua kwenye begi lake ili achukue taulo aingie bafuni kuoga.
"SAWA kazi njema,tutakuwa tunawasiliana. Ikitokea tatizo usisite kutupa taarifa mapema ili tuweze kulitatua", alisema Molisy.
"Sawa Afande" Veronica akakata simu kisha akaitupia kitandani,akajongea mpaka kwenye mlango wa bafuni akafungua akaenda kuoga.
Kesho yake asubuhi kabla Veronica hajaanza safari ya kwenda kijijini kuendelea na majukumu yake,alikatiza mitaa ya mji huo mdogo alikuwa amepanga chumba akatokea sokoni kufanya manunuzi mbali mbali matunda na vitu vinginevyo. Lakini wakati yupo ndani ya hilo soko, mara ghafla alimuona Zabroni akiwa na jamaa mmoja ambaye bila shaka alikuwa ni rafiki yake. Veronica alistuka, haraka sana akazipiga hatua mpaka pale alipo simama Zabroni. Alipo mkalibia alimkanyaga makusudi huku akijifanya kumpisha mtu aliyekuwa akipishana naye,kwani eneo hilo palikuwa na msongamano wa watu. Veronica alipo mkanyaga Zabroni alinyanyua mguu haraka sana kisha akasema "Jamaani pole mkaka", Zabroni aliposikia hiyo sauti nyororo alitabasamu kisha akajibu "Usijali najua ni bahati mbaya", alijibu kwa upole huku macho yake akitupia kwenye uso wa Veronica kitendo ambacho kilimfanya Veronica kuachia tabasamu pana huku aking'ata mdomo. Ghafla Zabroni alipagawa ilihali muda huo huo Veronica aliondoka zake,nyuma mkungu wake wa ndizi ukitikisika kiaina yake. Vijana walio mtazama Veronica hawakusubitu kupepesa macho,mirunzi ilisikika kutoka kwa madereva piki piki na wasukuma mikokoteni. Yote hiyo ikiwa ni shamra shamra ya kumuona Veronica akitembea huku makilio yake yakicheza,kiukweli alijaliwa ingawa sio sana.
"Daah ama kweli mjini kuna mambo Zabroni" ,alisema huyo jamaa aliyekuwa na Zabroni.
"We acha tu,tuachane na hayo. Vipi mzigo huu tutauza ama? Kwa sababu bei tuliyoikuta tofauti na tuliyo tegemea"
"Ni kweli,lakini ujue hata tusipouza ni sawa na bure tu. Hizi ni nyanya Zabroni hazichelewi kuoza, Kwahiyo kuliko tupate hasara ni bora tuuze tukagange yajayo", alisema jamaa huyo. Zabroni alijikita katika mambo ya kilimo baada kuona kumaliza kisasi chake. Hivyo siku hiyo yeye na rafiki walikuwa mji mdogo kwa niaba ya kuuza mazao yao.
Walikubalina wakawa wameuza mazao ya kwa hiyo hiyo bei waliyoikuta gulioni,na mara baada kupokea ujira wao walianza safari ya kurejea kijijini ambapo huko hukukuwa na mtu hata mmoja aliyemfahamu Zabroni. Aliishi kwa amani pasipo kuwa na shaka. Lakini kipindi wanatoka gulioni mara ghafla Zabroni akakutana tena Veronica, wote kwa pamoja waliachia tabasamu hasa Zabroni baada kukumbuka kwamba kuna muda aliyekanyagwa na huyo binti akawa amemuomba radhi. Safari hiyo Veronica alikuwa anafungua mlango wa gari teksi,kabla hajaingia ndani alimuuliza Zabroni wapi wanapo elekea,Zabroni akataja na hapo ndipo Veronica alipowataka wapande kwa madai kwamba naye anaelekea huko. Zabroni na rafiki yake walifurahi sana kupata lifti,Veronica akamwambia dereva wake afungue buti nyuma ili waweke tenga ambalo walibebea nyanya. Safari ikaanza kuelekea kijijini,wakiwa ndani ya gari walipiga zogo mpaka mwisho wa safari ya safari ya Zabroni na rafiki yake ambapo walishuka kisha wakatoa shukrani zao. Kabla hawajaondoka Veronica alimuita Zabroni ndani ya gari huku nje akibakia rafiki yake akiwa amesimama...Ndani ya gari Veronica alimwambia Zabroni "Smahani kama hutojali nilikuwa naomba kesho uje mjini tukale pamoja chakula cha mchana,usistuke nimevutiwa sana na ukarimu wako unaonekana kijana mpole,kiukweli kaa ukijua tu kwamba umenivutia sana na pia nitafurahi endapo kama utanikubalia", alisema Veronica kwa sauti nyororo huku uso wake ukionyesha haibu. Zabroni aliposikia maneno ya huyo dada,moyo wake ulistuka. Ndani ya nafsi yake akajiuliza "Bahati gani hii inanitokea? Hili ni zali la mintali siwezi kulipuuzia " kwisha kuwaza hayo alijibu "sawa nipo tayari usijali. Je, tukutane wapi?",Veronica alimuelekeza mahali pakukutana,Zabroni akawa amemuelewa ambapo alisisitiza kutokukosa.
Baada ya hapo waliagana,Veronica akaondoka zake lakini pia Zabroni naye akajua hamsini zake huku kila mmoja akijanasibu kiana yake. Mtukutu Zabroni akijigamba kwamba huwenda akawa amepata zali la mentali kwa Veronica, ilihali Veronica naye akiamini kuwa yule ndege mtutundu anakaribia kunasa kwenye tundu bovu!

JE, TAYARI KAPATIKANA PANYA WA KUMVISHA KENGERE PAKA?
 
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi: sharobaro la jf
CONTACT:0689092982

SEHEMU YA KUMI NA NANE-18

Wahenga waliwahi sema kwamba,ukitaka kuruka?sharti uagane na nyonga. Abadani hawakukosea kusema msemo huo,bila shaka waliona mbali sana na ndio maana wakaamua kusema huo msemo ambao unatumika sana kwa mtu aliyeamua kujitosa kutenda jambo fulani. Ndivyo ilivyokuwa kwa kamanda wa kike Veronica, kamanda ambaye aliamua kujitolea kumtia Zabroni kwenye mkono wa sheria kwa kutumia mbinu ya aina yake. Ikimbukwe Zabroni kipindi cha nyuma aliwahi kufanya mauaji mbali mbali,alitia watu hasara mali zao lakini alifanya kila jambo mbaya ambalo hata mwenyezi mungu hapendi. Vitendo hivyo vilipo shamili,jeshi la polisi ndipo lilipo amua kuingilia kati ingawa bado walichemka kwa sababu Zabroni hakamatiki kwa siraha. Baada kumshindwa kwa siraha ndipo walipoona kwamba watumie njia ya mapenzi,kwani mapenzi siku zote yananguvu kuliko kitu chochote hapa duniani kwani mapenzi hayana komando. Sasa basi njia hiyo itweza kumtia mtukutu Zabroni kwenye mkono wa dola? Je, Veronica ataweza?
****
Baada ya makubaliano kufanyika, siku tatu zilikatika. Siku ya nne kamanda Veronique alianza kazi ambapo aliambiwa mahali ambapo Zabroni hupendelea kukaa katika hicho kijiji,hiyo ikawa rahisi kwake kwani alipotembelea maeneo hayo siku ya kwanza hakumkuta lakini siku ya pili alimkuta akishirikiana na wenzake katika shughuli za jamii. Baada kumuona alichomoa picha ndogo aliyokabidhiwa,aliitazama kisha akamtazama Zabroni kule alipokuwa akichakarika. Alipo jihakikishia kuwa ndiyo huyo,aliirudisha kwenye mkoba wake picha ya Zabroni kisha akarejea mjini nyumba ya wageni alipokuwa amepanga chumba. Akiwa amechoka alijilaza kitandani huku akiwa na nguo ya kulalia,kifua chake kikiwa wazi. Kiukweli kilivutia sana,chuchu zilikuwa zimesimama. Ngozi yake ikiwa nyororo pia kitovu chake kilikuwa kina shimo kidogo,tumbo lake likiwa laini kama nyama ya ulimi. Kamanda Veronique alivutia sana kizuri kisifie. Basi hapo baada kujilaza kitandani,akili yake yote aliifikiria namna ya kumkamata Zabroni. Mawazo ambayo yalimpelekea kupitiwa na usingizi ila aliamshwa na sauti ya simu ikiwa inaita,alikurupa kutoka usingizi alipo tazama jina la mtu aliyempigia akaona jina limeandikwa "Kamanda Molisy" alibonyesha kitufe cha kijani kisha akaweka sikioni alisema kwa sauti ya upole "Afande"
"Mmmh Veronique habari yako?..",ilisikika sauti ikijibu hivyo kwa mbali.
"Salama tu sijui kwenu huko"
"Kwetu salama,mbona wasikika kwa upole?..", alihoji kamanda Molisy ambaye ndio mkuu wa kikosi hicho cha kina Veronica.
"Aahmm.. nilikuwa nimelala siunajua kazi ilivyo? Lakini ondoa shaka leo nimebahatika kumuona,nina uhakika kazi itakuwa nyepesi sana", aliongea Veronica huku ikijonyoosha akizipiga hatua kwenye begi lake ili achukue taulo aingie bafuni kuoga.
"SAWA kazi njema,tutakuwa tunawasiliana. Ikitokea tatizo usisite kutupa taarifa mapema ili tuweze kulitatua", alisema Molisy.
"Sawa Afande" Veronica akakata simu kisha akaitupia kitandani,akajongea mpaka kwenye mlango wa bafuni akafungua akaenda kuoga.
Kesho yake asubuhi kabla Veronica hajaanza safari ya kwenda kijijini kuendelea na majukumu yake,alikatiza mitaa ya mji huo mdogo alikuwa amepanga chumba akatokea sokoni kufanya manunuzi mbali mbali matunda na vitu vinginevyo. Lakini wakati yupo ndani ya hilo soko, mara ghafla alimuona Zabroni akiwa na jamaa mmoja ambaye bila shaka alikuwa ni rafiki yake. Veronica alistuka, haraka sana akazipiga hatua mpaka pale alipo simama Zabroni. Alipo mkalibia alimkanyaga makusudi huku akijifanya kumpisha mtu aliyekuwa akipishana naye,kwani eneo hilo palikuwa na msongamano wa watu. Veronica alipo mkanyaga Zabroni alinyanyua mguu haraka sana kisha akasema "Jamaani pole mkaka", Zabroni aliposikia hiyo sauti nyororo alitabasamu kisha akajibu "Usijali najua ni bahati mbaya", alijibu kwa upole huku macho yake akitupia kwenye uso wa Veronica kitendo ambacho kilimfanya Veronica kuachia tabasamu pana huku aking'ata mdomo. Ghafla Zabroni alipagawa ilihali muda huo huo Veronica aliondoka zake,nyuma mkungu wake wa ndizi ukitikisika kiaina yake. Vijana walio mtazama Veronica hawakusubitu kupepesa macho,mirunzi ilisikika kutoka kwa madereva piki piki na wasukuma mikokoteni. Yote hiyo ikiwa ni shamra shamra ya kumuona Veronica akitembea huku makilio yake yakicheza,kiukweli alijaliwa ingawa sio sana.
"Daah ama kweli mjini kuna mambo Zabroni" ,alisema huyo jamaa aliyekuwa na Zabroni.
"We acha tu,tuachane na hayo. Vipi mzigo huu tutauza ama? Kwa sababu bei tuliyoikuta tofauti na tuliyo tegemea"
"Ni kweli,lakini ujue hata tusipouza ni sawa na bure tu. Hizi ni nyanya Zabroni hazichelewi kuoza, Kwahiyo kuliko tupate hasara ni bora tuuze tukagange yajayo", alisema jamaa huyo. Zabroni alijikita katika mambo ya kilimo baada kuona kumaliza kisasi chake. Hivyo siku hiyo yeye na rafiki walikuwa mji mdogo kwa niaba ya kuuza mazao yao.
Walikubalina wakawa wameuza mazao ya kwa hiyo hiyo bei waliyoikuta gulioni,na mara baada kupokea ujira wao walianza safari ya kurejea kijijini ambapo huko hukukuwa na mtu hata mmoja aliyemfahamu Zabroni. Aliishi kwa amani pasipo kuwa na shaka. Lakini kipindi wanatoka gulioni mara ghafla Zabroni akakutana tena Veronica, wote kwa pamoja waliachia tabasamu hasa Zabroni baada kukumbuka kwamba kuna muda aliyekanyagwa na huyo binti akawa amemuomba radhi. Safari hiyo Veronica alikuwa anafungua mlango wa gari teksi,kabla hajaingia ndani alimuuliza Zabroni wapi wanapo elekea,Zabroni akataja na hapo ndipo Veronica alipowataka wapande kwa madai kwamba naye anaelekea huko. Zabroni na rafiki yake walifurahi sana kupata lifti,Veronica akamwambia dereva wake afungue buti nyuma ili waweke tenga ambalo walibebea nyanya. Safari ikaanza kuelekea kijijini,wakiwa ndani ya gari walipiga zogo mpaka mwisho wa safari ya safari ya Zabroni na rafiki yake ambapo walishuka kisha wakatoa shukrani zao. Kabla hawajaondoka Veronica alimuita Zabroni ndani ya gari huku nje akibakia rafiki yake akiwa amesimama...Ndani ya gari Veronica alimwambia Zabroni "Smahani kama hutojali nilikuwa naomba kesho uje mjini tukale pamoja chakula cha mchana,usistuke nimevutiwa sana na ukarimu wako unaonekana kijana mpole,kiukweli kaa ukijua tu kwamba umenivutia sana na pia nitafurahi endapo kama utanikubalia", alisema Veronica kwa sauti nyororo huku uso wake ukionyesha haibu. Zabroni aliposikia maneno ya huyo dada,moyo wake ulistuka. Ndani ya nafsi yake akajiuliza "Bahati gani hii inanitokea? Hili ni zali la mintali siwezi kulipuuzia " kwisha kuwaza hayo alijibu "sawa nipo tayari usijali. Je, tukutane wapi?",Veronica alimuelekeza mahali pakukutana,Zabroni akawa amemuelewa ambapo alisisitiza kutokukosa.
Baada ya hapo waliagana,Veronica akaondoka zake lakini pia Zabroni naye akajua hamsini zake huku kila mmoja akijanasibu kiana yake. Mtukutu Zabroni akijigamba kwamba huwenda akawa amepata zali la mentali kwa Veronica, ilihali Veronica naye akiamini kuwa yule ndege mtutundu anakaribia kunasa kwenye tundu bovu!

JE, TAYARI KAPATIKANA PANYA WA KUMVISHA KENGERE PAKA?
Asante sana mkuu kwa hii story!
Naomba kufahamu uta-post lini tena ili nije kusoma !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom