Sharobaro la jf
JF-Expert Member
- Apr 23, 2020
- 237
- 325
- Thread starter
- #61
PENZI LA MFUNGWA
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0628650170
SEHEMU YA KUMI NNE-14
Baada kuguswa bega alistuka upesi akamgeukia mtu huyo aliyemgusa usiku huo wa manane. Ni Bruno. Mdogo wake marehemu Madebe,sura ya huyo kijana ilikuwa mpya kwa kwa Zabroni japo alimtazama kwa mwanga wa moto ulio tokana nyumba inayoteketea hivyo hakuweza kumtambua,zaidi alijiuliza "Huyu ni nani? Na anawezaje kunigusa bega?..", kabla hajapata jibu la hilo swali,Bruno alisema" Hujui sikujui ila kwa kumbukumbu naweza sema utanikumbuka endapo kama nitakukumbusha"
"We ni nani?..", alihoji Zabroni kwa kujiamini kabisa. Bruno alicheka sana kisha akafumbua kiganja chake,ulitokea mwanga mfano wa video. Katika mwanga huo kiganjani hapo lilionekana tukio lile la Zabroni na Madebe walipokuwa wanapigana,na mwisho wa tukio lile ilionekana ile sehemu ambayo Madebe alikuwa akimkabudhi hirizi mdogo wake huku akimtaka alipe kisasi. "Ndio mimi hapa natakiwa nifanye kile kitu kaka alicho nituma,hakika damu yake inanidai", alisema Bruno baada kumaliza kumuonyesha Zabroni ile video fupi kwenye kiganja chake. Lakini kijana Zabroni licha ya kuambiwa hayo maneno,kamwe hakuonyesha kustuka. Alicheka kisha akajibu "Nirahisi sana kunitamkia hayo maneno lakini ni vigumu kuyafanyia kazi kwa vitendo. Dogo, mimi leo ndio rasmi nimekamilisha kazi niliyofanya miezi kadhaa iliyopita. Hivyo sistahiri kuendelea kutenda dhambi zaidi,niliyo yafanya yanatosha", Kwisha kusema hayo Zabroni aliondoka zake. Bruno akamfuata,na ndipo Zabroni alipo amua kupotea kimazingara. Akaibukia kando kando ya mto,ilihali muda huo huo Buruno naye akatokea. Alistuka Zabroni baada kumuona kijana huyo anazidi kumganda wakati yeye hayupo tayari tena kufanya mauaji. "Bwana mdogo unataka nini tena kutoka kwangu?.." Zabroni alimuuliza Bruno tena kwa hasira. Bruno akajibu "Nataka kichwa chako Zabroni, sifa zako mbaya zimezagaa kila pande kwa sababu ya mauwaji yako,inakuwaje unauwa watu bila hatia? Hivyo basi kama utaweza niuwe na mimi basi lakini tofauti na hivyo utakufaa wewe ", alijibu Bruno huku akijiandaa kumrushia kombola Zabroni, ila kabla hajarusha. Zabroni akamwambia "Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini"
"Hapana huo ni ujanja wako Zabroni, sitegeki kishamba mimi", Bruno alijibu kisha akamtupia Zabroni moto wa kichawi. Moto huo ambao ulikuwa na nguvu ya ajabu ndani yake ulimpata Zablrni ukamtupa katikati ya mto ambapo muda huo huo Bruno alipaa juu huku akiwa amekunja ngumi nzito,ambayo alishuka nayo mpaka kwenye tumbo la Zabroni. Kitendo ambacho kilimzamisha chini zaidi kijana huyo mtukutu. Mamba samaki pia na wadudu wengineo waishio majini kwenye mto huo walitulia kupisha mpambano huo uliojumuisha nguvu za giza, Bruno alifanikiwa kumuadabisha Zabroni kwani kila Zabroni alipotaka kujitetea alijikuta akizidiwa ujanja na Bruno kwa kupigwa ngumi za haraka haraka zilizo changanywa na nguvu ya giza. Dakika kumi tu Zabroni hoi alisahau hata yale maneno ya kunuia ili abadilike kuwa kiumbe chochote kwa maana ngumi nzito iliyotua kichwani kwake iliweza kuyumbisha ubongo,hali iliyopelekea Zabroni huo muda kupoteza fahamu. Alipigwa sana kila mahala,Bruno alionyesha kujawa na hasira moyoni mwake. Hasira hiyo ndiyo iliyompelekea kumpiga Zabroni bila huruma kwani kila alipomkumbuka kaka yake ndivyo nguvu za kuchezea na mashavu ya Zabroni zilivyozidi kuongezeka. Mwishowe Zabroni alionekana kulegea kabisa mithiri ya kambale,hapo Bruno akajua tayari kazi imekwisha lakini ataamini vipi kama kweli kafa? Ndipo alipoamua kumvuta nchi kavu ili amuhakikishe. "Naam! Kazi imekwisha,hakuna mwamba chini ya jua zaidi ya muumba aliyekuumba. Zabroni Zabroni sasa ni wakati wako wa kwenda kulipwa yale uliyo yafanya hapa duniani", alisema Bruno baada kumkagua Zabroni kila sehemu ya mwili wake na kukuta tayari mtukutu kaaga dunia. Mara baada kusema hayo alimalizia kusema tena " Mimi ni Bruno shujaa... kwani siku zote shujaa hafi vitani bali shujaa ni yule anaye pambana na kurudi nyumbani na ushindi", Hapo alikata hirizi iliyokuwa kwenye mkono wa Zabroni kisha akawaza aondoke zake amuache Zabroni pale nchi kavu aidhaa amtupie mtoni apelekwe na maji sehemu isiyo julikana ikiwezekana awe chakula cha mamba? Kwani kwa hali ile kamwe mamba wasingemuacha salama,hirizi ambayo ingemlinda tayari ilikuwa mikononi mwake. Hivyo Zabroni atakuwa chakula cha mamba na samaki. Lakini kabla Bruno hajafanya huo uamuzi akajiuliza kwa mara nyingine tena "Tayari huyu mtu alikuwa ni tishio hapa kijijini je, hata nikipeleka habari ya kifo chake kwa wanakijiji wataniamini kweli?", alijiuliza Bruno mwishowe akaona ambebe begani moja kwa moja akaenda kumtunduki juu ya mti mkubwa kando ya barabara nyembamba ipitikayo kwa wingi na watu waendao na kurudi gulioni. Hapo ndipo Zabroni alipo tundikwa juu juu kwenye huo mti ule ambao kipindi cha nyuma aliwatundika vijusi alivyo vitoa tumboni kwa mama mjamzito. Kwisha kufanya hayo Bruno aliondoka zake na hirizi ya Zabroni. Akiwa amelowa jasho na damu aliitia hirizi ile kwenye mfuko wa koti alilokuwa amelivaa,kabla hajapotea kimazingara alizipiga hatua kadhaa kutoka pale alipo Zabroni hatua zipatazo kumi na tano kisha akasimama, akageuka kuutazama mti ule aliomtundika Zabroni akatikisa kichwa na akasema "Kufa tu hukuna namna mwanaharamu mkubwa wewe", kwisha kusema maneno hayo akachukuwa kitambaa akajifuta damu kwenye mikono yake halafu akapotea. Alipo fika kijijini alikuta nyumba tatu zimeteketea kwa moto usiku huo huo. Ndipo hapo Buruno alipokumbuka maneno ya Zabloni alipo mwambia
"Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini" Buruno alipokumbuka hayo maneno akajiongeza kwa kusema "Alaah! kumbe huyu mshenzi alimanisha nitazame juu kuangalia mwanga wa nyumba zinazo ungua? Ooh Mungu wangu" Bruno aliumia moyoni kisha akajipa moyo akisema "Sawa natumaini pindi wahanga hawa watakapo kuona ukiwa maiti basi mioyo yao itajaa tabasamu bashasha",alisema Bruno huku akiingiza mkono mfukoni aitoe hirizi ile aliyoichukua kwa Zabroni ili aitupie kwenye moto,lakini ajabu hakuikuta. Alistuka sana huku asijuwe kwamba muda ule alipotoa kitambaa kujifuta damu kiganjani aliidondosha chini. Pumzi ndefu alishusha na pindi alipotaka kurudu kuichukuwa, Mwemyekiti aliifka eneo la tukio kisha akamwambia "Hii ndio taabu ya hapa kijijini kijana wangu,hakika sitoamini siku nikimuona huyu mwanaharamu kauwawa". Hapo sasa Bruno alishindwa kumtoka Mwenyekiti ili aifuate hirizi ile kwani angeonekana hajaguswa na kitendo hicho cha nyumba kuungua. Muda huo sasa alfajiri tayari ilikuwa imeingia,umande na baridi ulimfanya Zabroni kutikisa kiuongo kimoja cha mwili wake,kumbe mtukutu alikuwa bado hajafa! U hai.
UKIWASHA MOTO KWENYE VIFUU UWE NA UWEZO WA KUUZIMA. me simo tukutane Sehemu ijayo.. mimi ni Team Zabroni aisee!
Mtunzi:Sharobaro la jf
CONTACT:0628650170
SEHEMU YA KUMI NNE-14
Baada kuguswa bega alistuka upesi akamgeukia mtu huyo aliyemgusa usiku huo wa manane. Ni Bruno. Mdogo wake marehemu Madebe,sura ya huyo kijana ilikuwa mpya kwa kwa Zabroni japo alimtazama kwa mwanga wa moto ulio tokana nyumba inayoteketea hivyo hakuweza kumtambua,zaidi alijiuliza "Huyu ni nani? Na anawezaje kunigusa bega?..", kabla hajapata jibu la hilo swali,Bruno alisema" Hujui sikujui ila kwa kumbukumbu naweza sema utanikumbuka endapo kama nitakukumbusha"
"We ni nani?..", alihoji Zabroni kwa kujiamini kabisa. Bruno alicheka sana kisha akafumbua kiganja chake,ulitokea mwanga mfano wa video. Katika mwanga huo kiganjani hapo lilionekana tukio lile la Zabroni na Madebe walipokuwa wanapigana,na mwisho wa tukio lile ilionekana ile sehemu ambayo Madebe alikuwa akimkabudhi hirizi mdogo wake huku akimtaka alipe kisasi. "Ndio mimi hapa natakiwa nifanye kile kitu kaka alicho nituma,hakika damu yake inanidai", alisema Bruno baada kumaliza kumuonyesha Zabroni ile video fupi kwenye kiganja chake. Lakini kijana Zabroni licha ya kuambiwa hayo maneno,kamwe hakuonyesha kustuka. Alicheka kisha akajibu "Nirahisi sana kunitamkia hayo maneno lakini ni vigumu kuyafanyia kazi kwa vitendo. Dogo, mimi leo ndio rasmi nimekamilisha kazi niliyofanya miezi kadhaa iliyopita. Hivyo sistahiri kuendelea kutenda dhambi zaidi,niliyo yafanya yanatosha", Kwisha kusema hayo Zabroni aliondoka zake. Bruno akamfuata,na ndipo Zabroni alipo amua kupotea kimazingara. Akaibukia kando kando ya mto,ilihali muda huo huo Buruno naye akatokea. Alistuka Zabroni baada kumuona kijana huyo anazidi kumganda wakati yeye hayupo tayari tena kufanya mauaji. "Bwana mdogo unataka nini tena kutoka kwangu?.." Zabroni alimuuliza Bruno tena kwa hasira. Bruno akajibu "Nataka kichwa chako Zabroni, sifa zako mbaya zimezagaa kila pande kwa sababu ya mauwaji yako,inakuwaje unauwa watu bila hatia? Hivyo basi kama utaweza niuwe na mimi basi lakini tofauti na hivyo utakufaa wewe ", alijibu Bruno huku akijiandaa kumrushia kombola Zabroni, ila kabla hajarusha. Zabroni akamwambia "Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini"
"Hapana huo ni ujanja wako Zabroni, sitegeki kishamba mimi", Bruno alijibu kisha akamtupia Zabroni moto wa kichawi. Moto huo ambao ulikuwa na nguvu ya ajabu ndani yake ulimpata Zablrni ukamtupa katikati ya mto ambapo muda huo huo Bruno alipaa juu huku akiwa amekunja ngumi nzito,ambayo alishuka nayo mpaka kwenye tumbo la Zabroni. Kitendo ambacho kilimzamisha chini zaidi kijana huyo mtukutu. Mamba samaki pia na wadudu wengineo waishio majini kwenye mto huo walitulia kupisha mpambano huo uliojumuisha nguvu za giza, Bruno alifanikiwa kumuadabisha Zabroni kwani kila Zabroni alipotaka kujitetea alijikuta akizidiwa ujanja na Bruno kwa kupigwa ngumi za haraka haraka zilizo changanywa na nguvu ya giza. Dakika kumi tu Zabroni hoi alisahau hata yale maneno ya kunuia ili abadilike kuwa kiumbe chochote kwa maana ngumi nzito iliyotua kichwani kwake iliweza kuyumbisha ubongo,hali iliyopelekea Zabroni huo muda kupoteza fahamu. Alipigwa sana kila mahala,Bruno alionyesha kujawa na hasira moyoni mwake. Hasira hiyo ndiyo iliyompelekea kumpiga Zabroni bila huruma kwani kila alipomkumbuka kaka yake ndivyo nguvu za kuchezea na mashavu ya Zabroni zilivyozidi kuongezeka. Mwishowe Zabroni alionekana kulegea kabisa mithiri ya kambale,hapo Bruno akajua tayari kazi imekwisha lakini ataamini vipi kama kweli kafa? Ndipo alipoamua kumvuta nchi kavu ili amuhakikishe. "Naam! Kazi imekwisha,hakuna mwamba chini ya jua zaidi ya muumba aliyekuumba. Zabroni Zabroni sasa ni wakati wako wa kwenda kulipwa yale uliyo yafanya hapa duniani", alisema Bruno baada kumkagua Zabroni kila sehemu ya mwili wake na kukuta tayari mtukutu kaaga dunia. Mara baada kusema hayo alimalizia kusema tena " Mimi ni Bruno shujaa... kwani siku zote shujaa hafi vitani bali shujaa ni yule anaye pambana na kurudi nyumbani na ushindi", Hapo alikata hirizi iliyokuwa kwenye mkono wa Zabroni kisha akawaza aondoke zake amuache Zabroni pale nchi kavu aidhaa amtupie mtoni apelekwe na maji sehemu isiyo julikana ikiwezekana awe chakula cha mamba? Kwani kwa hali ile kamwe mamba wasingemuacha salama,hirizi ambayo ingemlinda tayari ilikuwa mikononi mwake. Hivyo Zabroni atakuwa chakula cha mamba na samaki. Lakini kabla Bruno hajafanya huo uamuzi akajiuliza kwa mara nyingine tena "Tayari huyu mtu alikuwa ni tishio hapa kijijini je, hata nikipeleka habari ya kifo chake kwa wanakijiji wataniamini kweli?", alijiuliza Bruno mwishowe akaona ambebe begani moja kwa moja akaenda kumtunduki juu ya mti mkubwa kando ya barabara nyembamba ipitikayo kwa wingi na watu waendao na kurudi gulioni. Hapo ndipo Zabroni alipo tundikwa juu juu kwenye huo mti ule ambao kipindi cha nyuma aliwatundika vijusi alivyo vitoa tumboni kwa mama mjamzito. Kwisha kufanya hayo Bruno aliondoka zake na hirizi ya Zabroni. Akiwa amelowa jasho na damu aliitia hirizi ile kwenye mfuko wa koti alilokuwa amelivaa,kabla hajapotea kimazingara alizipiga hatua kadhaa kutoka pale alipo Zabroni hatua zipatazo kumi na tano kisha akasimama, akageuka kuutazama mti ule aliomtundika Zabroni akatikisa kichwa na akasema "Kufa tu hukuna namna mwanaharamu mkubwa wewe", kwisha kusema maneno hayo akachukuwa kitambaa akajifuta damu kwenye mikono yake halafu akapotea. Alipo fika kijijini alikuta nyumba tatu zimeteketea kwa moto usiku huo huo. Ndipo hapo Buruno alipokumbuka maneno ya Zabloni alipo mwambia
"Sawa, siunataka kuniuwa? Tazama juu kuna nini" Buruno alipokumbuka hayo maneno akajiongeza kwa kusema "Alaah! kumbe huyu mshenzi alimanisha nitazame juu kuangalia mwanga wa nyumba zinazo ungua? Ooh Mungu wangu" Bruno aliumia moyoni kisha akajipa moyo akisema "Sawa natumaini pindi wahanga hawa watakapo kuona ukiwa maiti basi mioyo yao itajaa tabasamu bashasha",alisema Bruno huku akiingiza mkono mfukoni aitoe hirizi ile aliyoichukua kwa Zabroni ili aitupie kwenye moto,lakini ajabu hakuikuta. Alistuka sana huku asijuwe kwamba muda ule alipotoa kitambaa kujifuta damu kiganjani aliidondosha chini. Pumzi ndefu alishusha na pindi alipotaka kurudu kuichukuwa, Mwemyekiti aliifka eneo la tukio kisha akamwambia "Hii ndio taabu ya hapa kijijini kijana wangu,hakika sitoamini siku nikimuona huyu mwanaharamu kauwawa". Hapo sasa Bruno alishindwa kumtoka Mwenyekiti ili aifuate hirizi ile kwani angeonekana hajaguswa na kitendo hicho cha nyumba kuungua. Muda huo sasa alfajiri tayari ilikuwa imeingia,umande na baridi ulimfanya Zabroni kutikisa kiuongo kimoja cha mwili wake,kumbe mtukutu alikuwa bado hajafa! U hai.
UKIWASHA MOTO KWENYE VIFUU UWE NA UWEZO WA KUUZIMA. me simo tukutane Sehemu ijayo.. mimi ni Team Zabroni aisee!