Simulizi ya kweli: Niliolewa na Jini bila kutarajia

Simulizi ya kweli: Niliolewa na Jini bila kutarajia

SEHEMU YA 06


Yule mdoli nae alikuwa mlangoni akitabasamu halafu kwa mbali nilisikia mtu akiita jina langu.
Nilizidi kuchanganyikiwa, nikaamua kupiga kelele kwa nguvu na kwa bahati muda huo sauti ilitoka.
"Mamaaaaaaaaaaaa..............."
Mama na dada walikuja mbio chumbani kwangu.
Walivyofungua mlango wangu, nilichoropoka na kukimbilia sebleni wakanifata na kuniuliza. Nilikuwa natetemeka sana.
"Kuna nini mwanangu? Kuna nini jamani??"
Mama na dada walikuwa wananishangaa, kwani jasho na machozi vilikuwa vyanitoka.
"Mdoli mama mdoli"
Niliamua kusema kilichonisumbua.
"Mdoli kafanyaje?"
"Ananitisha mama kila mahali namuona halafu anatabasamu"
"Yuko wapi sasa huyo mdoli?"
Nikaamua kuongozana nao chumbani ili nikawaonyeshe.
Kuangalia pale mlangoni hayupo, kitandani hayupo, ndipo nikatazama mezani na kumkuta ametulia kabisa kama mdoli wa kawaida.
Nikawa namuonyesha dada,
"Si umemuona yule mdoli, kafikaje pale wakati alikuwa chumbani kwako?"
Dada yangu akacheka sana hadi mama akamuuliza anachochekea.
"Kweli Sabrina ni muoga jamani loh!!"
"Sema basi unachochekea Penina?"
"Mama, yule mdoli kweli Sabrina alikuja na kumrudisha kwangu kuwa hamtaki. Me nikahisi labda kuna kitu kachukia ndomana kamrudisha yule mdoli. Kwa nimjuavyo Sabrina anapenda sana wadoli, sasa mimi nimemfanyia surplise alipokuwa amelala nikamrudisha yule mdoli na kumuweka pale mezani ili akiamka amkute na kufurahia"
Nilimshangaa sana dada, ataniwekeaje kitu ambacho nilishakikataa!
"Ila mimi simtaki huyo mdoli, jana nilishakukatalia dada."
"Penina mwanangu ulichofanya si kizuri, Sabrina mwenyewe ana maruweruwe siku hizi. Akikataa kitu usimuwekee tena, haya mtoe huyo mdoli wako."
Ikabidi dada amtoe yule mdoli, na mimi nikaendelea kuwaeleza.
"Hata hivyo wakati naenda chooni nilisikia mtu anacheka na mlangoni mwa choo ndio akatokea huyo mdoli akitabasamu"
"Maruweruwe hayo mwanangu"
"Hata hivyo niliyekuwa nacheka ni mimi, nilikuwa naongea na simu si unaju kumekucha tayari! Nilikuwa najiandaa kuoga niende kazini"
Nilishangaa sana kwani muda niliodhania mimi kuwa ni usiku wa manane kumbe ilikuwa ni alfajiri, maneno ya mama kuwa nina maruweruwe nikaona huenda yakawa ni kweli ila bado sikuwa na imani na yule mdoli.
Mchana wake wakati tumekaa na mama ikabidi aniulize,
"Hivi ni kweli ulikuwa unatishwa na yule mdoli mwanangu?"
"Ndio mama, tena amenitisha sana tu"
"Kwahiyo unaamuaje maana dadako hayupo saizi tunauwezo wa kufanya chochote"
"Itakuwa vyema kama tukimchoma moto"
"Basi sawa mwanangu"
Mama akanituma nikamchukue yule mdoli ili tumchome moto lakini nilikataa kumfata, hivyo mama akaenda kumchukua mwenyewe.
Akaniita tumchome moto, akammwagia mafuta ya taa na kumuwasha moto.
Wakati yule mdoli anaungua ikatokea harufu kama vile kuna nyama inachomwa hata mama akashangaa.
"Mbona mdoli mwenyewe ana harufu kama ya kiumbe hai?"
"Ndio uone maajabu hayo mama, mi nikisema mnaona ni maruweruwe"
"Itabidi dadako akija nimuulize alipomtoa huyo mdoli"
Wakati tunajadiliana na yule mdoli akizidi kuungua, ikanyesha mvua iliyotuondoa mahali pale kufika ndani ikakatika.
Tukarudi tena kuangalia mdoli alivyoungua, tukakuta vinaungua vitu kama vya plastiki plastiki hivi. Wala haikuonekana dalili ya mdoli, mama akasema labda mdoli alishaungua wote.
"Na hiyo plastiki inayoungua je?"
"Labda wapita njia wameweka"
Nikacheka kweli kwa makisio ya mama.
Tukarudi ndani na kukaa, mara dada akawa amerudi hata tukamshangaa jinsi alivyowahi kurudi siku hiyo.
Ikabidi mama amuulize kuwa mbona amewahi sana.
"Mbona umewahi kurudi leo?"
"Majanga mama"
Halafu akaenda chumbani kwake kuweka mkoba, kisha akarudi tena sebleni na kuniuliza.
"Kheee Sabrina umemchukua tena yule mdoli?"
Kabla sijamjibu, mama akamuuliza tena.
"Niambie Penina, majanga gani hayo?"
"Mwenzangu, (akanigeukia mimi) unakumbuka kuwa nilikwambia kuna kijana kazini kanipa zawadi ndio nikakuletea wewe yale maua na yule mdoli?"
Nikaitikia kwa kichwa huku nikiwa na hamu ya kujua kuwa huyo kijana kafanya nini, kumbe mama nae alikuwa na shauku ya kujua, akauliza haraka haraka,
"Kafanyaje?"
"Kanifata ofisini kuwa ana shida na mimi, akaniombea ruhusa kwa bosi basi nikaondoka nae. Akaniambia kitu ambacho kimenivutia sana na kufanya nifatane nae, nia yetu ilikuwa ni kuja huku nyumbani kumfata yule mdoli. Tukapanda daladala, sijui hata tumechanganyana nae vipi. Yani mi nikashuka kumbe nimemuacha kwenye gari amesinzia, namuangalia chini hayupo na gari imeondoka. Nikajaribu kupanda gari jingine hadi mwisho, nikakuta lile basi lipo kupakia abiria wengine nilipomuuliza konda akasema kuwa yule kijana alivyoshtuka akashuka njiani hata sielewi amepotelea wapi kijana wa watu jamani mweeeh! Hana namba yangu ya simu na hapa hapajui. Ndio nikaamua kurudi nyumbani tu"
"Sasa yeye alikuwa anataka nini haswaaa"
"Mama, yule mdoli kumbe alikuwa wa bosi wake, yeye hakujua. Sasa amegundua kuwa yule mdoli nyuma kwake kule kwenye zipu kuna..... (kisha akanigeukia na kusema), hebu kamlete yule mdoli Sabrina nije kumuangalia mwenyewe"
Mimi na mama tukabaki tunatazamana kwani mdoli tulishamchoma.
Dada alipoona simjibu kitu, akainuka na kwenda chumbani kwangu akapekua na kurudi.
"Umemuweka wapi yule mdoli Sabrina?"
Ikabidi mama aulize tena,
"Kwani ana nini huyo mdoli Penina?"
"Amewekwa pesa kule kwenye zipu mama, tena ni dola za kimarekani nyingi tu."
"Unasema kweli Penina?"
"Ndio mama, mmemuweka wapi sasa?"
Mama akajibu kwa unyonge,
"Tumemchoma"
Dada akawa kama vile mtu ambaye hajasikia vizuri,
"Mmemfanyaje mama?"
Ikabidi mama amueleze dada kuwa mimi na yeye tulikaa na kutafakari kuwa yule mdoli achomwe moto.
Dada alichukia sana, akaenda pale nje kuangalia kisha akarudi chumbani kwake kwa hasira.
Jioni ya leo nilikaa na mama tu sebleni kwani dada alikuwa na hasira na sisi.
Mama akaanza kuniuliza,
"Hivi na sisi tuliingiwa na nini mwanangu hadi kuchoma mdoli asiyetuhusu?"
"Ila mama, yule mdoli alikuwa ananitisha bhana"
"Tungemchunguza kwanza kabla ya kuamua kumchoma, kwakweli tulichukua maamuzi ya haraka sana"
"Ila ishatokea mama haifai kupeana lawama"
"Tumeteketeza pesa mwanangu mmh!"
Hapo nikajua tu kwa tamaa ya mama yangu lazima ashikwe uchungu juu ya hiyo pesa aliyoisikia.
Usiku sikutaka kulala chumbani kwangu, ikabidi nikalale kwa mama ingawa kulikuwa kwa masharti kwani nikilala nae hataki nishike simu kuipokea wala kujibu ujumbe wa aina yoyote ile, ilibidi nikubaliane na vyote tu.
Sam nae akaanza kunipigia simu, nilitamani kupokea ila nilimuhofia mama kuwa atachukia sana nikipokea simu, tena ukizingatia ni ya Sam kijana ambaye hampendi.
Niliiacha iite hadi kukatika sema ilikuwa ikiita kimya kimya, sikutaka kuizima kwani nilijua kuwa nikiizima nitamchukiza Sam ambaye alipiga na kupiga na kupiga bila kupokelewa.
Nikatamani kurudi chumbani kwangu ili niwe huru ila uoga ulinisumbua, nilikaa na mawazo na kupitiwa na usingizi.
Nilishtuka gafla nikiwa na kiu ile kupitiliza, kwavile mama huweka maji mezani mule chumbani kwake kwaajili ya kunywa akishtuka nami nikainuka na kumimina maji kwenye kikombe ili ninywe.
Wakati na kunywa nikahisi kama kuna mtu ameshikilia ile bilauli na kunisukumia maji yote kinywani hadi nikapaliwa, na kuanza kukohoa. Nilikohoa sana hadi mama akaamka hadi na damu zikawa zinanitoka mdomoni, mama akashangaa sana ikabidi anipatie huduma ya kwanza nayo ni kuniweka sehemu yenye hewa zaidi na kuniwashia feni inipepee.
Nilipotulia akaniuliza nini tatizo, nikamueleza mama kuwa nimepaliwa wakati wa kunywa maji na tukarudi kulala.
Nikamuomba mama asizime taa ya mule chumbani kwani kila akizima nilikuwa naona kama kuna mtu anafungua ule mlango wa mama na kuingia.
Ikabidi mama asizime ile taa na kuniona mwanae kuwa nimeanza kuchanganyikiwa, nililala nimemkumbatia mama hadi kunakucha.
Kwakweli kwangu mchana ulikuwa bora kushinda usiku kwani usiku vioja vinakuwa vingi sana.
Kulipokucha mama akaanza kunilalamikia kwa kumlaza na mwanga wakati yeye kazoea kuzima taa.
"Na leo ukalale chumbani kwako, hayo maswala ya kufanya taa ikeshe chumbani kwangu sitaki. Wewe umekuwa mtu wa maruweruwe tu siku hizi hata sijui una nini jamani? Uoga wako umetukosesha mahela toka kwa mdoli."
"Najua tu hilo la mdoli utakuwa unajilaumu siku zote ila sikuwa na la kufanya kwajinsi alivyokuwa akinitisha"
"Unamaajabu sana mwanangu, eti mdoli anatabasamu loh! Na mimi bila hata ya kufikiria mara mbili, eti tumchome mwanangu. Hii ndio haraka haraka haina baraka"
"Basi yaishe mama"
Nilibaki kujisemea kuwa laiti kama yangekuwa yanawatokea kama ambavyo yananitokea mimi labda wangeelewa.
Badae niliwasiliana na Sam ambaye alikuwa amechukizwa sana na kitendo changu cha kupotezea simu zake.
Mchana wake nilitembelewa na rafiki yangu Suzy, nilifurahi sana na kuongea nae mambo mengi kama rafiki.
Nikamueleza Suzy kuhusiana na alichonifanyia Lucy kwa Sam na jinsi Sam alivyonipa maelekezo ya ilivyokuwa.
"Kwahiyo sasa wewe umeamuaje?"
"Kwakweli nilichukizwa sana, nilitamani hata kuachana na Sam kwa usaliti wake"
"Sikia shoga yangu, usithubutu kuachana na Sam kwaajili ya Lucy. Yani Lucy ni gubegube hana mfano, kazi yake ni kuiba mabwana za watu yani hana lolote nakwambia. Usimuachie Lucy"
"Kama wao wamependana je itakuwaje?"
"Hakuna cha kupendana hapo, Lucy namjua vizuri. Usimuachie bwanako, atamuiba kweli. Unamchezea Lucy eeh! Hana masikhara yule mtoto wa pwani"
"Unanitisha sasa Suzy"
"Usiogope, unatakiwa kuwa ngangari. Pigania penzi lako, usikubali mpita njia akakuharibia safari yako."
Maneno ya Suzy yalinitia moyo kwakweli na kujikuta nikipata nguvu mpya juu ya Sam.
Jioni yake Suzy akaaga na nikaamua kumsindikiza stendi ili akapande daladala la kurudi kwao.
Tukasimama pale stendi na kuendelea na maongezi yetu huku tukingoja daladala na kulikuwa na watu wengine pale nao wakingoja usafiri.
Ikaja basi na kusimama mbele yetu, ikashusha abiria kisha Suzy akapanda basi lile na tukaagana. Kwakweli sikumuangalia hata kidogo yule abiria aliyeshuka.
Baada ya lile basi kuondoka, kuja kutahamaki nilibaki mwenyewe pale kituoni hadi nikashangaa wakati mwanzoni walikuwepo watu wengi tu, nikageuka ili nianze safari ya kurudi nyumbani.
Wakati nageuka, nikashangaa kushikwa mkono na mkaka, ule mkono wake ulikuwa na ubaridi sana uliopenya hadi moyoni mwangu, kisha akasema,
"Habari yako Sabrina"
Nilikuwa nikitetemeka, kuinua macho na kumtazama ni yule mkaka wa ndotoni.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 33



Mara gafla tukasikia dada akipiga kelele huko nje.
Tukapatwa na mashaka, na kuinuka ili twende nje
tukaangalie kuwa kuna nini. Ila kabla ya kutoka nje,
Carlos alikuwa amerudi huku amemshika dada mkono
ambapo mkono mwingine alijiziba sura. Mama
akauliza, "Kuna nini tena?"
"Kuna vitu nje vimemtisha, mwacheni akapumzike
kwanza halafu nitakuja kesho kuongea vizuri" Ikabidi
mama amshike dada mkono na kumpeleka chumbani
kwake kisha mimi na mama tukaenda chumbani kwa
mama kulala kwani na leo nikaogopa kulala chumbani
kwangu.
Nikiwa chumbani na mama, akaanza kuniuliza
maswali kuhusu Carlos.
"Unamuonaje Carlos mwanangu?"
"Kwakweli mama sina la kusema maana hata
nikisema sidhani kama utanielewa"
"Kivipi mwanangu? Nieleze tu nitaelewa"
"Nimuonavyo mimi ni kama kijana wa kwenye ndoto
zangu"
"Kivipi mwanangu? Au unatamani awe mumeo?"
"Hapana mama, simpendi name ndiomana
nimekwambia Kuwa huwezi kunielewa hata kama
nitakuelezaje"
"Haya niambie basi unaonaje anaweza kutusaidia
kweli?"
"Sijui mama, kwa kifupi simjui Carlos tofauti na
unavyofikiria"
"Sawa mwanangu kesho nitafanya kitu fulani, nadhati
kitakuwa kizuri kwetu na maisha yetu"
Halafu tukalala. Leo mambo ya ajabu hayakutokea
kabisa usiku hadi kunakucha ilikuwa shwari kabisa.
Asubuhi ya leo kama kawaida Dada alijiandaa na
kwenda kazini, akasahau yote yaliyotokea Jana yake.
Nikabaki Mimi na mama ila mama nae akajiandaa na
kutoka, akaniacha pekeyangu nyumbani nikaamua
kuangalia luninga ili kujisahaulisha baadhi ya mambo.
Nikapatwa na ugeni leo alikuwa ni dada Salome,
nikamkaribisha ndani bila ya kuhofia uchawi wake
ambao nimeambiwa.
"Asante kwa kunikaribisha mdogo wangu, Nina mengi
ya kuzungumza na wewe"
"Usijari Dada, kuwa huru tu kuniambia chochote"
"Kwanza kabisa ni kuhusu maisha yako, hivi hujioni
kuwa umebadilika?"
"Mi sijijui Dada, bora uniambie nilivyo"
"Umejibu vyema Sabrina ni kweli kabisa hujijui wewe
wala hujitambui kwa sasa, pia napenda nizungumze
nawe kuhusu yule kijana uliyekuwa nae hospitali siku
ile"
"Nani huyo? Carlos?"
"Nadhani ndio huyo huyo, yule kijana yule ni......"
Mama alikuwa karudi akiambatana na rafiki yake
mwingine, aliyeitwa mama Semeni na kukatisha
mazungumzo ya mimi na dada Salome maana mama
alimvamia Salome kwa maneno.
"Eeeh kilichokuleta na wewe?"
"Kwani vibaya mama?"
"Mara yako ya mwisho kuja hapa lini ?"
"Mwaka Jana"
"Mwaka huu umefata nini"
Dada Salome akabaki kimya.
"Haya, kama ulivyokuja naomba uondoke hivyohivyo"
Nikajaribu kumtetea,
"Lakini mama...."
"Hakuna cha lakini hapa, huyu binadamu simtaki
nyumbani kwangu"
Ikabidi dada Salome aondoke, nami nikaenda
chumbani kwangu kwani sikutaka maswali zaidi toka
kwa mama.
Baada ya muda kidogo mama akaniita, nikaamua
kutoka na kuwafata pale sebleni. "Kilichokukimbiza
ndani ni nini? Hujui kama yote haya nafanya kwaajili
yako?"
Nikabaki kimya tu huku nikimuangalia mama,
"Haya njoo ukae hapa"
Nikasogea na kukaa karibu yao ili kuwasikiliza.
"Huyu hapa mama Semeni kasema atatusaidia pia"
"Atatusaidiaje?"
"Atatupeleka kwa mtaalam"
"Mtaalam??"
Nikajua sasa mama ameanza na mambo yake ya imani za kishirikina.
"Sasa unashangaa nini?"
"Mmh mama! Huo ni ushirikina"
Mama Semeni akaongea sasa.
"Sio ushirikina Sabrina, yote haya ni katika kukusaidia
wewe na maisha yako" "Basi kama ni vya kunisaidia
mimi msinilazimishe kwanza, acheni nifikirie halafu
nitawajulisha" Mama akachukia sana,
"Huyu Sabrina kashaanza utahira wake"
"Mwache tu Mama Penina, akiwa tayari atasema
mimi nipo wakati wote nitawapeleka" Nikarudi
chumbani kwangu na kuwaacha na mazungumzo yao.
Nikawaza sana nikiwa chumbani kuwa mama ana
maana gani kutaka twende kwenye mambo ya
kishirikina ila sikupata jibu. Baada ya muda nikasikia
kuwa mama Semeni kaondoka, nikaamua kwenda
kumuuliza mama maswali yangu.
Nikamkuta ametulia kabisa akiangalia video, ila kabla
sijamuuliza alifika dada Penina akiwa ameongoza na
Carlos.
Tukashangaa kuwaona pamoja, mama akawa wa
kwanza kuuliza.
"Mmekutana wapi nyie leo?"
Dada Penina akaanza kuelezea,
"Yani huwezi amini mama jinsi Carlos alivyotusaidia
ofisini yani mpaka Salome akaondoka mwenyewe"
"Basi ndio akaja huku kutuletea mauzauza yake"
"Khee! Alikuja huku mama?"
"Ndio, nimemkuta akiongea na Sabrina.
Nimemtimuaje"
"Umefanya vizuri sana mama, huyu Sabrina ni mjinga
na hajielewi hata kidogo. Kwakweli tumshukuru sana
Carlos kwa moyo wake wa kusaidia watu"
Carlos alikuwa akitabasamu tu kufurahia sifa
alizopewa, dada Penina akaenda kupika kwa lengo
kuwa leo jioni Carlos apate kula kwetu.
Carlos aliongea kidogo na mama na kuahidi kuwa
atarudi hiyo jioni.
Kitu hiki kwa Carlos huwa kinanichanganya pia kwani
sio mtu wa kusema utakaa nae muda mrefu kuongea,
yeye akikaa kidogo tu huwa anaaga na kuondoka na
hapo hufanya nizidi kupatwa na maswali mengi zaidi
juu yake.
Tulipokuwa tunaandaa chakula cha usiku ndio muda
huohuo Carlos nae alifika tena.
"Nimekuja kutimiza ahadi yangu ya kula hapa leo"
"Bora umekuja maana kesho tungekulaumu sana"
Sikuongea neno lolote, nilikuwa kimya kabisa.
Tukaanza kula, kila mmoja na sahani yake. Wakati
nakula, Carlos alikuwa akiniangalia na kunikonyeza,
nikaishia kutabasamu tu.
Niliposhusha macho kwenye sahani yangu nikaona
kumejaa mchanga na mawe wakati kulikuwa na wali
nyama, nikasogeza sahani pembeni na kupiga kelele.
Mama akaniuliza,
"Nini wewe? Una kichaa?"
"Hapana mama, ona"
"Nione nini?"
Namuonyeshea sahani yangu,
"Si wali huu na nyama! Au ni nini?"
"Ni mchanga na mawe mama"
Mama na dada wakacheka,
"Kweli unawazimu wewe, yani wali nyama unasema
mchanga na mawe!"
"Kweli mama ni mchanga na mawe"
Carlos akainuka huku akitabasamu na kusogea
mahali nilipokuwa nimesimama, akanishika bega na
kunikalisha kwenye kitu kisha akanisogezea ile
sahani yangu ya chakula ambayo nimelalamikia kuwa
ni mchanga ili nile.
Akasogea na yeye na kula karibu yangu, nikajikuta
nikila kile chakula bila mashaka tena yani kamavile
sio mimi niliyelalamika kuwa kile chakula ni mchanga.
Tulipomaliza Carlos aliaga kuwa anaondoka, mama
hakuacha kumshukuru Carlos.
Carlos akaniangalia na kuniambia kuwa,
"Hunifikishi mlangoni Sabrina?"
Mama akadakia,
"Inuka Sabrina umsindikize mwenzio"
Nikainuka na kumfikisha mlangoni, kisha akaniambia.
"Nitakusaidia kila kitu endapo utakubali kitu kimoja tu
kutoka kwangu"
"Kitu gani hicho?"
Hakuniambia ila akaondoka na kuniacha nimesimama
pale mlangoni, kisha nikarudi ndani na kumkuta
mama na dada wakijadili kuhusu Carlos.
"Unaona mama, Carlos ndio anafaa kwa Sabrina.
Atamsaidia huyu na uchizi wake"
"Kweli kabisa maana alivyoanza pale kwenye chakula
kuwa ni mchanga sijui ingekuwaje, bora Carlos
alikuwepo"
Nikawaangalia tu na kwenda chumbani kwangu kwani
leo nilijisikia kulala kwenye chumba changu.
Nilipokuwa chumbani ile kauli ya Carlos ikanirudia
kichwani kuwa nimkubalie jambo moja tu, nikajiuliza
tena.
"Litakuwa jambo gani hilo?"
Mara nikasikia sauti kama ikininong'oneza,
"Olewa na mimi"
Nikashtuka sana na kuangalia kila mahali kuwa ni
nani anaongea, nikajijibu mwenyewe kuwa,
"Sitaki kuolewa na wewe"
Sauti ile ikasema tena,
"Lazima nikuoe Sabrina"
Uoga ukanijaa kuwa ni huyuhuyu Carlos au ni nani
maana sikujielewa kabisa.
Mara nikajiona kama nimelala halafu naota ila
nilikuwa macho kama mtu aliyepumbazika, nikaona
mbele yangu vitu vingi vya kifahari huku ile sauti
ikijirudia ndani.
"Lazima uolewe na mimi, lazima uolewe na mimi
Sabrina"
Nikajiona tena nimekuwa mwanafunzi, nimevaa sale
za shule nimesimama barabarani nikiomba lifti.
Ikaja gari na kusimama mbele yangu nikapanda,
kwenye uskani alikaa dereva, nilipomuangalia ni yule
mkaka wa ndotoni akitabasamu na kusema.
"Lazima uolewe Sabrina"
Hapo ndipo niliposhtuka kutoka kupumbazika kwangu
na kushangaa nikiwa chumbani kwangu tena
kitandani huku nimekaa bila hata ya kujielewa kwani
uoga ulikatika gafla na kujikuta nikikumbuka matukio
ya nyuma wakati nasoma.
Nakumbuka nilipenda sana kusimamisha magari ya
watu kwaajili ya lifti ila sikumbuki kama kuna siku
yoyote niliyowahi kukutana na mtu wa ajabu.
Hapohapo nikapatwa na usingizi na kulala hadi
panakucha.
Mama ndiye aliyekuja kunishtua siku ya leo.
"Khee Sabrina, umelala hadi muda huu?"
Nikaamka na kumsalimia mama,
"Leo ni siku njema mwanangu, kuna habari njema
zinakuja"
"Zipi hizo mama?"
"Sijui ila nimeoteshwa tu mwanangu"
"Sawa mama, na ziwe njema kweli"
Nikaenda kujisafisha mwili na kuendelea kufanyakazi
za ndani kama kawaida.
"Ila mama natamani kweli kwenda kuwatembelea
rafiki zangu"
"Sabrina mwanangu usitake kuniletea makubwa hapa,
hebu tulia ndani. Ngoja mambo yawe shwari utaenda,
kama umewakumbuka sana wasiliana nao kwa simu
tu"
"Hawapatikani mama, natamani sana kujua hali zao
ila siwapati"
"Usijali mwanangu, muda upo utawatembelea hadi
uchoke"
Kwakweli kukaa nyumbani kwa muda nilichoka tena
nilichoka sana
Tulipomaliza kazi na mama tulienda kupumzika sasa.
Nikaenda chumbani kwangu na kujaribu tena
kuwapigia simu rafiki zangu haswaa Sam,
nilimkumbuka sana ingawa mengi yalitokea kati yetu
ila sikuacha kumkumbuka ila hakupatikana hewani.
Rafiki zangu wote hawakupatikana hewani hadi
nikaona ni uchafu tu kuwa na simu isiyokuwa na
maana yoyote ile kwani ilikuwa ikikaa bila kupigwa
wala kutuma ujumbe, nikajisemea iwe isiwe lazima
kesho niende kumtembelea Sam.
Mawazo yalikuwa mengi sana, nikaamua kulala
ilikupunguza mawazo.
Wakati nimelala, nikawaona watu wengi sana
wamekuja nyumbani wakiwa wameambatana na yule
kaka wa ndotoni halafu mimi nilikuwa pembeni
nikishangaa.
Nikamvuta mkono dada Penina na kumuuliza.
"Kuna nini kwani?"
"Wamekuja kutoa mahari, mdogo wangu unaolewa"
Nikauliza kwa mshangao,
"Naolewa! Na nani?"
"Si yule kijana pale"
Akimuonyeshea yule kijana wa ndotoni.
Nikashangaa na kusema.
"Simtaki yule"
"Khee! Humtaki mchumba wako?"
"Sio mchumba wangu yale"
"Awe mchumba wako asiwe mchumba wako lazima
akuoe maana mahali yake ishakubaliwa"
Nikaanza kulia na kusema kuwa kuwa sitaki kuolewa,
dada akasema.
"Usilie mdogo wangu, furahia ndoa. Ndoa ni furaha"
Nikazidi kulia na kulia sana.
Kushtuka pale kitandani, mahali nilipolaza kichwa
pote palijaa machozi, hapo nikagundua kuwa nilikuwa
nalia kweli wakati naota.
Nikainuka na kukaa kitandani huku nikitafakari ile
ndoto, ila nikasikia kama kuna watu wakizungumza
sebleni nikaamua kujifuta machozi na michirizi ya
usingizi ili nikawaone kuwa ni wakina nani.
Nikatoka hadi sebleni na kuona watu kadhaa kabla
sijawatambua vizuri, mama akainuka na kuanza
kunipigia vigelegele.
Itaendelea muda sio mrefu…!!

Hadithi nzur ila inatisha
 
Hadith ni nzuri sana ila tamaa inaponza wengi
 
Hapa kuna wanawake wanatamani wangeipata hiyo nafasi ya sabrina wanawake wana roho ngumu
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
Ilikuwa kwenye mida ya saa mbili usiku wakati tumekaaa kwaajili ya chakula cha usiku.
Wakati nakula simu yangu ikaita kuangalia mpigaji ni mpenzi wangu Sam ila nikashindwa kunyanyuka kwenda kupokea kwani mama alikuwa ananiangalia sana ikabidi nibonyeze kitufye cha kimya (silence).

Mama kumbe alisikia wakati inaita akauliza,

"Nani anakupigia wakati wa kula?"

"Hakuna mtu mama, ni alarm tu"

"Unadhani sijasikia wakati inaita? Umeanza uongo eeh!!"

"Hapana mama ni Sam"

"Nilijua tu, anakupigia wakati wa kula amekununulia hiyo simu? Anaijua bei yake?"

Ikabidi nikae kimya, mama yangu alikuwa anamchukia sana Sam. Hakupenda kabisa mahusiano ya mimi na Sam ingawa tulipendana sana.

Tulipomaliza kula tulikuwa tumekaa sebleni, nikatamani kuinuka kwenda chumbani nikazungumze kidogo na Sam na kumwambia kuwa muda aliokuwa anapiga nilikuwa nakula.

Nikawa nainuka, mama akaanza kuongea kabla hata sijaanza kutembea.

"Unaenda wapi Sabrina?"

"Naenda chumbani mara moja mama"

"Kuongea na simu eeh!! Amekupa nini huyo Sam jamani? Yani unashindwa kukaa hapa kuzungumza na mama yako na chakula kitulie, wewe macho juu juu kukimbilia ndani kuongea na Sam. Amekuwa mzazi wako huyo? Sipendi hiyo tabia, haya kaa tuzungumze ya maana hapa"

Ikabidi nikae ila mawazo yangu yote yalikuwa ni kwa Sam tu hata maneno ambayo mama alizungumza sikumuelewa hata kidogo, nikaona anapiga kelele tu.

Nadhani pale aliyekuwa anamsikiliza ni dada yangu Penina tu maana ndio waliokuwa wakijibishana. Mama akaniomba simu yangu na kupigia ndugu zake, akaongea wee hadi muda wa maongezi ulipokata ndio akanirudishia. Nikabakiwa na ujumbe mfupi tu bila ya muda wa maongezi.

Mama aliponyanyuka nami nikanyanyuka kuelekea chumbani, kisha nikamtumia ujumbe mfupi Sam kuwa anipigia. Naye hakusita kunipigia ila alinipa lawama mwanzo mwisho.

"Sabrina una dharau sana, yani simu yangu hupokei. Nangoja kidogo kupiga namba inatumika yani kuna watu unawaona wanathamani sana kushinda mimi. Poa tu Sabrina"

"Jamani Sam mpenzi wangu, tafadhari nisamehe"

"Umefanya makusudi wewe, poa tu mi nalala saivi"

Halafu akakata simu, nikajisikia vibaya sana ikabidi nimtumie ujumbe wa kumuomba msamaha ila Sam hakupiga wala kujibu ujumbe wangu.

Sikuweza kumwambia Sam kama mama yangu anamchukia kwani nilijua wazi kuwa akijua tu lazima atajisikha vibaya ukizingatia kwao mama yake ananipenda sana mimi.

Asubuhi na mapema nikapata ujumbe toka kwa Sam.

"Yani wewe Sabrina una dharau sana, sijui kwavile umejua nakupenda sana. Yani umeshindwa hata kunipigia simu upooze mawazo yangu umekazana na ujumbe tu!! Najua muda wote wa maongezi umemaliza kwa watu wako ila poa tu. Mimi nitaendelea kukupenda Sabrina"

Nikaamua kuamka na kwenda kununua vocha ili nipate kuzungumza na Sam.

Ila maduka yalikuwa bado hayajafunguliwa, nikaamua kuanza kufanya kazi mbalimbali za pale nyumbani ili niwahi kumaliza na niweze kwenda kwa Sam kwani nililuwa nimemkumbuka na pia nilitaka nikamweleweshe ya jana.

Baada ya kazi nikamuaga mama kuwa naenda kumtembelea rafiki yangu Suzy, mama hakuwa na pingamizi akaniruhusu niende nami nikaenda moja kwa moja kwa Sam ila sikumkuta na mlango wake ulikuwa na kufuri.

Ikabidi niende duka la karibu kununua vocha kisha nikampigia ila hakupokea nikajua tu kisirani kimempanda.

Nikaamua kuondoka na kwenda kweli kwa kina Suzy ili badae nipate kurudi tena kumuangalia.

Nilikaa sana kwa kina Suzy ila sikumueleza Suzy jambo lolote lile kuhusu Sam, badae nikaaga na kwenda tena kwa Sam nikawa namngoja kuwa pengine ameenda kazini ila ilikuwa ni mwisho wa wiki ndiomana nilijiamini na kwenda.

Nilimngoja sana Sam bila ya kutokea, nilikata tamaa na moyo kuniuma sana kuwa kwanini Sam amenifanyia vile kwa kosa dogo kiasi kile.

Nikajaribu kuwauliza na majirani ambao walisema kuwa Sam ameondoka asubuhi sana, nikajiuliza kuwa labda ameenda kwao ila kwanini asipokee simu? Nikaona kuwa Sam ananifanyia kusudi, hisia mbaya zikanitawala kuwa Sam atakuwa kwa mwanamke mwingine tu hapo roho ikaniuma sana.

Muda ulizidi kwenda, ikabidi nirudi nyumbani.

Nilifika nyumbani kwenye mida ya saa tatu usiku, nikamkuta mama na dada wakifanya maongezi ya hapa na pale.

Nikawasalimia na kwenda kuoga kisha kula chakula.

Dada akaanza kuzungumza,
"Halafu wewe Sabrina, kupenda kwako huko kutembea usiku usiku ipo siku utakumbana na majini huko njiani"

Nikashtuka sana na kumuuliza dada,
"Majini? Una maana gani dada?"

"Usiku ni mida ya majini, yakikukumba huko usituletee balaa hapa"

"Kwani majini yakoje?"

"Ukikutana nayo lazima nywele zisisimke, halafu ni marefu sana mara nyingine huwezi ona mwisho wa urefu wao"

"Mbona unanitisha dada?"

"Sikutishi ila huo ndio ukweli, unatakiwa kuwa makini sana. Majini hayana masikhara, likikuvaa ndio limekuvaa utakula nalo, kulala nalo na kuamka nalo bila ya kutarajia"

Nikaanza kuingiwa na uoga, mama nae akaanza kuchangia hoja zake.

"Unakumbuka kule makaburini wakati wanamzika yule dada mwenye mashetani kilichotokea?"

Dada akajibu,

"Ndio nakumbuka mama, yani majini hayataki mchezo"

Ikabidi niulize tena,

"Kwani majini yanafanana na kitu gani"

"Majini yanatisha mdogo wangu usiombe ukutane nayo njiani unaweza usilale siku mbili unaweweseka tu."

"Inamaana yanaweza kutokea wakati mtu amelala?"

"Ndio, unaweza ukashangaa umelala na jini pembeni yako"

Niliogopa sana na kuwaza kwanini nimesikiliza habari za majini usiku.

Mama akaongezea kitu kingine ambacho kilifanya niende chumbani kumtafuta Sam.

"Ila leo umenifurahisha kitu kimoja, kwenda kweli kwa Suzy maana huyo Sam wako amekuwa hapa siku nzima kukungoja"

Nikagundua kuwa, wakati mimi namngoja Sam kule kwake kumbe na yeye alikuwa kwetu kuningoja ila kwanini hakutaka kupokea simu yangu.

Nikaenda zangu chumbani kwa lengo la kumpigia tena Sam simu.

Ila nikasita kwani nikaona Sam nae ananifanyia kusudi, kama kweli alikuwa kwetu kuningoja kitu gani kimemfanya asipokee simu yangu. Mara dada akaniita na kufanya yale mawazo yangu juu ya Sam yakatike.

"Vipi Sabrina ndio unataka kulala muda huu?"

"Ndio dada, nataka kulala"

"Njoo mara moja, kuna kitu nataka unisaidie huku chumbani kwangu"

Nikatoka na kufatana na dada hadi chumbani kwake.

"Kuna kitu kinanichanganya hapa kwenye computer yangu, naomba uniondolee hii picha"

Mimi nikaitazama ile picha, ilikuwa ni ya mwanaume mzuri sana. Nikamuuliza dada kuwa kwanini anataka kuifuta,

"Kwanini uifute dada? Mbona picha yenyewe ni nzuri?"

"Hata sielewi nimeidownload vipi hiyo picha hadi imekaa hapo, nitolee bhana mipicha mingine inaweza kuwa ya majini"

"Mbona unapenda sana story za majini dada?"

"Yapo na ndiomana nayaongelea, usishangae siku ukitokewa na jini"

"Basi yaishe, mi sitaki tena hizo habari nisije kushindwa kulala bure"

Nikafanya ninachojua kuifuta ile picha kisha nikamuaga dada usiku mwema na kuondoka.

Nikarudi chumbani na kuendelea kuwaza kuhusu Sam wangu. Wakati nikiwaza juu ya Sam, wazo la majini likanijia tena kichwani nikajikuta naanza kuogopa chumbani halafu ile picha ambayo dada aliniomba kuwa nimsaidie kufuta ikawa inatembea kichwani mwangu.

Niliona chumba kimekuwa kikubwa sana, nilipokaa kitandani nilihisi kama vile kuna mtu pembeni yangu nikaanza kuogopa zaidi huku nikijilaumu kuwa kwanini nimesikiliza stori za kutisha muda wa kulala. Nikachukua tena simu na kuamua kumpigia Sam ili kujiliwaza kidogo ila kabla sijapiga nikapitiwa na usingizi.

Mwanaume mzuri sana na mtanashati alikuwa mbele yangu, asili yake kama mwarabu hivi au muhindi. Alikuwa anatabasamu na kusogea taratibu kuja mahali ambako mimi nipo. Nilikuwa namwangalia kwa jicho la mshangao tu. Alipofika karibu yangu, akanivuta mkono kisha akatoa kitu cha ajabu kilichofanya nishtuke.

Itaendelea
Bado umeolewa nalo au mmeachana?
 
SEHEMU YA 22





Moja kwa moja nikajiuliza, kama mimba si ya kaka je ni ya nani? Na huyu Carlos amejuaje!
Nikamuangalia vizuri ili kumdadisi maneno yake, Carlos nae alikuwa akiniangalia kwa makini kabisa nadhani alikuwa akicheza na akili yangu. Mara akasema,
"Najua unajiuliza maswali mengi Sabrina juu ya hili swala ila ukinisikiliza kwa makini utaelewa kila kitu"
"Ndio nahitaji kujua, je kaka anajua kama ile mimba si yake?"
"Kakako hajui chochote na ndomana nimekwambia kuwa ni siri, wifi yako ameitunza kwa muda mrefu sasa na hafikirii kama kuna mtu wa kuijua siri hii"
"Wewe umejuaje sasa?"
"Nina upeo mpana tofauti na unavyofikiri Sabrina, nilirithishwa na babu yangu. Niliposalimiana na wifi yako ndipo nikaijua siri hii na nikamwambia kisiri ila yeye akapiga makelele kama mtu aliyewehuka na kuongea maneno mengi ili wewe usiniamini mimi na unione ni mtu wa ajabu ila ninachokwambia mimi ni kitu cha kweli tena ni ukweli mtupu, kama huamini kamuulize wifi yako na kama akikataa mlete kwangu nimuumbue kwani ukweli wote naujua"
Maneno ya Carlos yakafanya nifikirie sana kwani nilikuwa siamini ingawa Carlos amekuwa akiniambia mambo mengi ya kweli.
"Ila je ile mimba ni ya nani?"
"Unataka kumjua Sabrina? Na ukimjua je utachukua hatua gani?"
"Kwakweli sijui, tena sijui kabisa hatua ya kuchukua ila lazima wifi nimuulize kuhusu hilo jambo"
"Muulize tu halafu upime maneno yangu, huwa siongopi mimi hata siku moja"
Nikamuangalia sana Carlos jinsi alivyoongea kwa kujiamini kabisa tena akionekana ni mtu mwenye uhakika wa kitu anachosema.
"Basi niambie kabisa kuwa ile mimba ni ya nani?"
"Nenda ukamuulize kwanza wifi yako, akikataa ndio nikutajie mwenyewe ile mimba kuwa ni ya nani"
"Tutaonana lini sasa tena?"
"Kesho, nitakuja tena hapahapa"
Nikakubaliana na Carlos kisha kuagana na kuondoka.
Nikaamua kurudi kule kwenye kwaya ili niungane na wifi kurudi nyumbani ila sikumkuta ikabidi nifanye safari ya kwenda nyumbani nako nikakuta mlango umefungwa kwa maana kwamba wifi alikuwa bado hajarudi, ikabidi nimngoje pale nje.
Baada ya muda wifi alirudi akiwa amesindikizwa na yule mwalimu wa kwaya na kunikuta pale nje moja kwa moja wifi alianza kuongea.
"Yani Sabrina umeniudhi leo balaa, kwanini hukuniambia mapema kama utachelewa kiasi hiki? Umefanya nikungoje muda wote kuwa utarejea, kwanini lakini?"
Nikamuangalia wifi bila ya kusema chochote.
Alikuwa akiongea huku akifungua mlango, kisha tukaingia ndani na yule mwalimu akaaga na kuondoka.
Wifi hakuacha kunisema hata tulipokuwa ndani akidai kuwa nimempotezea muda wake akiningoja kule kwenye kwaya.
"Nadhani itakuwa vyema nikimwambia kaka yako kuhusu hili, umenikera sana. Au nimwambie tu kakako?"
Mara kaka alikuwa amewasili na kusikia vile ambavyo wifi alikuwa akifoka,
"Kuniambia nini tena? Kwani tatizo ni nini?"
Wifi akagelesha kwa hilo na kusema.
"Hapana bhana, nilikuwa naongea na Sabrina kuwa mtoto atakayezaliwa kama akiwa wakike basi tumuite Sabrina, yeye akawa anaogopa kuwa wewe hutokubali ndio nikamwambia kuwa au nikwambie wewe"
Maneno ya wifi yaliweza kumlainisha kaka na akakubali kuwa ndio ilivyokuwa.
"Usiogope Sabrina, wifi yako amekupenda sana ndomana anachagua jina lako"
Nikatabasamu tu ili kisieleweke chochote kwani wifi aliniokoa kwa lile maana kaka angejua kuwa kuna mahali nilienda ingekuwa shida.
Tukapika na kula ila sikuweza kumuuliza chochote wifi kwani niliogopa pa kuanzia ukizingatia kaka yupo.
Muda wa kulala nikaenda zangu chumbani na kulala.
Nilipokuwa kitandani maswali mengi sana nilijiuliza na kusema kuwa lazima nimuulize wifi kuhusu kitu nilichoambiwa na Carlos.
Mara Sam akanipigia simu, nami nikapokea na kuongea nae.
"Nasikia ulimuagiza Carlos aende kwa wakina Suzy kuwasaidia. Naomba nikuulize kitu Sabrina"
"Uliza"
"Je, huwa unaonana na Carlos huko?"
"Ndio, kwani kunatatizo?"
"Hamna tatizo nimeuliza tu, Carlos ulimpigia simu muda gani kumwambia kuwa wakina Suzy wapo khatarini?"
"Muda nilipopewa taarifa kwani nilikuwa naongea nae muda huo huo"
"Kuwa mwangalifu Sabrina sababu Carlos sio kama unavyomuona. Simjui Carlos ila namuona kama kikwazo kwenye maisha yetu"
"Kwani Carlos rafiki yako au rafiki yangu?"
"Ni rafiki yako wewe Sabrina ila mimi kama mpenzi wako nina haki ya kukwambia rafiki bora na mbaya"
"Hayo mapenzi mimi na wewe yalishaisha Sam nenda tu ukaendelee na Lucy wako"
"Ilimradi najua na kutambua kuwa hakuna chochote kinachoendelea kati yangu na Lucy basi sitaacha kukufatilia wewe Sabrina hadi mwisho wangu"
"Unajisumbua tu kwa sasa"
"Na sitaacha kujisumbua kwa mtu nimpendaye, najua umevurugwa tu kwasasa"
"Nani kavurugwa?"
"Wewe hapo umevurugwa Sabrina"
"Umevurugwa mwenyewe"
Nikakata simu kwani alikuwa akinizidishia hasira tu, ila nikatafakari sana na kuona kweli Sam ananipenda. Nikachukua simu yangu na kumtumia Sam ujumbe mfupi wa maneno.
"Asante kwa kunipenda Sam, nitakupenda daima"
Kisha nilala baada ya kutuma ujumbe huo, kwenye ndoto nikamuona Sam na Lucy wakiwa pamoja na kufurahi sana, mimi nilikuwa pembeni kuangalia jinsi wanavyofurahia mapenzi yao huku roho ikiniuma sana kutokana na wivu, kisha nikawaona ndugu wa Sam na ndugu wa Lucy wakiwa pamoja kama vile watu wanaojuana sana halafu nikamuona Sam akimvisha pete Lucy, hapo nikashtuka na kusema kwa nguvu.
"Noooooo...."
Nikaamka na kugundua kuwa ni ndoto tu, nikachukua simu yangu ili nimpigie Sam kumwambia nilivyoota.
Nikakuta ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwa Sam umeandikwa,
"Usijali mpenzi nakupenda sana Lucy wangu"
Hapo mapigo ya moyo yakaanza kunienda kwa kasi na machozi kunidondoka. Nikajiuliza nitaumia hadi lini kwaajili ya Sam? Kwanini anitese kiasi hiki halafu bado anadai kunipenda? Roho iliniuma sana, nikaghairi kumpigia tena Sam na usingizi sikupata sababu ya mawazo na machozi yaliyonitoka mfululizo hadi kunakucha sikuwa na raha yoyote.
Siku ya leo sikuwa na raha kabisa kwani nilijihisi mpweke na uchovu mwaingi huku nikitamani kumuuliza wifi kuhusu mimba yake ila sikujua ni wapi pa kuanzia kumuuliza. Nikabaki kumtazama tu kwa yote aliyokuwa akiyafanya.
Muda ulipotulia nilikaa na wifi huku tukitaniana akaanza tena kuniambia kuhusu jina la mtoo atakayezaliwa.
"Yani huyu mwanangu lazima nitamuita Sabrina"
"Hata kama wa kiume?"
"Wakike huyu, mbona unapenda kung'ang'ania jambo moja? Mimi ndio mama wa huyu mtoto na nimekwambia kuwea ni wa kiume"
"Sawa wifi, kuna swali nataka kukuuliza"
"Uliza tu, kuwa huru Sabrina"
Nikasita kidogo kwani swali langu lilikuwa na utata na sikujua wifi angelipokeaje swali lile.
"Mbona huulizi? Nipo makini hapa kukusikiliza ujue!"
Nikapumua kidogo kabla ya kuuliza swali langu. Nikaamua kutafuta njia ya kuuliza kwa urahisi nitakacho kujua.
"Wifi unadhani mtoto atakayezaliwa atafanana na nani?"
"Mmmh! Asipofanana na wewe basi atafanana na kaka yako"
"Kwanini wifi?"
"Kwanini tena?? Si kwasababu ni damu yenu"
Hapo ndipo nikabadilika na kumwambia kuwa wifi ni muongo.
"Muongo wifi"
"Mimi muongo? Uongo wangu uko wapi?"
Sasa nikapata ujasiri wa kumwambia na wifi akachukizwa sana.
"Hiyo sio damu yetu maana hiyo mimba sio ya kaka"
"Unasemaje Sabrina? Kama mimba hii sio ya kaka yako ni ya nani sasa? Wewe mtoto vipi umetumwa nini nyumba imekushinda hii eeh! Kukupenda kote Sabrina bado unanizulia maneno! Kweli binadamu wabaya"
Wifi aliongea maneno mengi bila hata ya kupumzika na akanichukia gafla.
"Sema sas, kama hii mimba si ya kaka yako ni ya nani?'
Nikabaki kutoa mimacho kwavile sikujua mimba ni ya nani.
Tangia hapo wifi hakutaka tena kuongea na mimi hata kwenye kwaya leo alienda peke yake nami nikabaki nyumbani.
Nikiwa mwenyewe nyumbani nikapigiwa simu na Carlos ambaye alihitaji kuonana na mimi, na kwa vile mimi nilitaka kuonana na yeye kwa sana nikamwambia aje pale nyumbani kwa kaka kwani wote hawapo na pia nahitaji kuzungumza nae.
Hakuchukua muda sana alikuwa ameshawasili pale kwa kaka, nikamkaribisha na kuzungumza nae.
"Wifi yangu amekataa kabisa na kunichukia"
"Nilijua hilo kabla ndiomana leo nimekuja"
"Sasa utanisaidiaje kwa hilo?"
"Wifi yako anadhani unakisia tu na huujui ukweli ndomana anakufanyia ukali ili usitambue kabisa kinachoendelea, sasa mimi nakutajia mtu aliyempa ujauzito wifi yako. Ukipata muda wa kumwambia mwambie tu halafu utaona kitakachoendelea"
"Niambie basi ile mimba ni ya nani?"
"Ile mimba ni ya kijana flani anaitwa James, mwambie wifi yako hivyo ataelewa halafu akigoma kukwambia ukweli nijulishe mimi nitakwambia kila kitu ilivyokuwa"
Kwakweli hakuna mtu aliyekuwa akinishangaza kama huyu Carlos kwani aliongea mambo mengi kwa kujiamini kisha akaniaga na kuondoka.
Nilitulia ndani nikimngoja wifi arudi huku hamu yangu ikiwa moja tu nayo ni kuujua ukweli wa mambo.
Kama kawaida wifi alirudishwa pale nyumbani na mwalimu wa kwaya kisha mwalimu huyo akaondoka,. Nilikaa na wifi ila hakunichangamkia tena halafu alionekana kuwa na hasira sana ila sikutaka kuacha kumwambia ukweli.
Nikamsogelea wifi na kumwambia,
"Hiyo mimba si ya kaka, ni mimba ya James"
Mara wifi akaanguka chini na kuanza kutapatapa kama mtu mwenye kifafa.
Itaendelea
[emoji91][emoji91][emoji95]
 
SEHEMU YA 31


Kabla sijamalizia, nikaona sura ya Carlos ikibadilika na kuwa sura ya yule kijana wa ndotoni. Nikaanza kuogopa na kupiga makelele hadi mama na Dada Penina wakatoka nje kuja kushuhudia kuwa kuna nini. Mama akauliza kwa mshangao,
"Kuna nini hapa?"
Nikiwa nimejiziba uso kwa kiganja changu nikamsikia Carlos akimjibu mama.
"Hata Mimi mwenyewe namshangaa Sabrina, sijui ana matatizo gani maana
gafla tu kaanza kupiga makelele"
Mama akasogea karibu ili anitoe mikono machoni na aweze kuona Kuwa nina tatizo gani. Sikutaka kuangalia tena, nikaamua kukimbilia ndani kwa uoga niliokuwa nao. Nikawaacha mama na dada wakiongea na Carlos pale nje.
Nilipokimbilia ndani nikaishia sebleni kwani chumbani nako niliogopa kwenda, baada ya muda kidogo mama, dada Penina na Carlos nao wakaja pale sebleni kitendo kilichofanya uoga unishike zaidi na kusema kwa nguvu,
"Jamani, huyo Carlos sio mtu"
Mama akaniuliza,
"Sasa kama sio mtu ni nani?"
"Sijui ila sio mtu"
"Umeshaanza maruweruwe yako mwanangu"
Kisha mama akamgeukia Carlos na kumwambia,
"Msamehe mwanangu, anamatatizo sana
tumehangaika nae bila jibu. Ndio anakuwaga hivyohivyo maruweruwe yakimuanza. Msamehe sana"
"Usijali mama, hata mimi naelewa kama Sabrina ana matatizo ila kila nikimuuliza anakataa. Ila mimi naweza kumsaidia na hayo matatizo yakamuondoka kabisa"
Nikaropoka hapohapo,
"Unisaidie nini wewe wakati wewe ndio tatizo"
Kisha nikakimbilia chumbani kwangu kwani uoga ulishanitoka kwa kutambua kwamba dawa ya tatizo ujue kwanza chanzo cha tatizo, nikawaacha pale sebleni wakiendelea kuongea. Moja kwa moja nikaenda kukaa kitandani kwangu, mara gafla nikasikia sauti ikipenya masikioni mwangu huku ikiita kama kwa kunong'oneza,
"Sabrina, Sabrina, Sabrina"
Ile sauti ilikuwa kama ikigongwa gongwa na mwangwi na kujirudia rudia, nikaanza kuogopa tena na kupiga makelele nadhani hata watu wa mbali waliweza kusikia ila hawakuelewa kuwa kuna nini.
Mama, dada Penina na Carlos wakaja chumbani kwangu ila sikutaka kumuona Carlos wala kuongea nae ikabidi aage na kusema.
"Kama mtahitaji msaada wangu msisite kunipigia simu. Nitakuja kuwasaidia"
Kisha akaondoka, halafu tukatoka sebleni ili tuweze kuongea vizuri.
"Kwani una matatizo gani mwanangu?"
"Sijui na hata sielewi"
"Elezea kidogo ili tupate kukusaidia"
"Hata sijui jinsi ya kuelezea mama"
"Jaribu mwanangu"
Nikataka kuwaelezea tangu mauzauza yalipoanza hadi hapa yalipofikia, ila mdomo ukawa mzito gafla, sikuweza kutamka neno lolote lile, mama akabaki kushangaa. Ikabidi dada aulize,
"Mbona kimya cha gafla?"
Nikawa nataoa machozi tu, mama akaona nitazidiwa akaamua kunipa dawa ya usingizi ili nipunguze maruweruwe, na muda huo huo nikalala kweli. Nilipoamka nilijikuta nipo chumbani kwangu, nadhani
mama alinipeleka chumbani muda nilipoanza kulala.
Ilikuwa ni usiku, nikachukua simu yangu kuangalia muda nikaona ni saa saba usiku. Nikajiuliza kama nimekula usiku wa leo na kupata jibu kuwa sijala. Mara nikasikia sauti ikiniambia.
"Usijali Sabrina, chakula nimekuwekea mezani hapo"
Nikashtuka sana na kujiuliza ni mawazo au ni kitu gani, ila nilipoangalia mezani nikaona kuna sahani na juu imefunikwa, nikaogopa.
Nikatoka chumbani kwangu na kukimbilia chumbani kwa mama ambaye alikuwa amelala, nikamtingisha ili kumwamsha na kumuuliza.
"Eti mama umeniwekea chakula mezani kwangu chumbani?"
"Ndio, nilijua ukiamka lazima utakuwa na njaa ndiomana nikakuwekea"
Nikapumua kidogo na kuona kuwa ile mwanzo
yalikuwa mawazo yananisumbua tu. Mama akaniambia tena,
"Nenda ukale tu mwanangu, usiogope"
Nikatoka chumbani kwa mama na kurudi chumbani kwangu. Nikasogea pale mezani kuona mama ameniwekea chakula gani, nikafunua sahani ya juu na kukuta ni chips kuku, nikashangaa na kujiuliza. Inamaana leo kwetu wamepika chips kuku au mama ameamua kuninunulia tu, nikajisemea kuwa nitamuuliza kesho na kuanza kula. Nilipomaliza kula, nikaenda jikoni kuchukua maji ya kunywa. Kisha nikarudi chumbani kwangu na glasi ya maji mkononi, nikashangaa kuona soda mezani na kujiuliza nani kaiweka, sauti ikaja.
"Nimeweka mimi Sabrina"
Nikaanza kuogopa na kutaka kukimbia, sauti ile ikasema tena
"Unaogopa nini sasa mbona chips zangu na kuku umekula!"
Nikahisi kuchanganyikiwa kwakweli na kutaka kupiga makelele ila ikashindikana, nikahisi kama kuna kitu kinanigusa na kujikuta nimeanguka chini na kupoteza fahamu.
Nilipozinduka ilikuwa kumekucha na nilijikuta kitandani, hapo nikaogopa pia na kukimbilia sebleni ambako nilikutana na mama.
"Nani kaniweka kitandani?"
"Khee, kwahiyo wewe uliona raha kabisa kulala pale chini!"
Nikamuangalia mama na kumuuliza tena,
"Chakula ulichoniwekea jana ni chips kuku?"
"Chips kuku? Kwa lipi haswaa? Nilikuwekea wali, maharage na mchicha kwani hujala?"
Majibu ya mama nayo aliyajua mwenyewe, hapo nikajifikiria na kuona kuwa zile chips kuku niliwekewa na lile jitu lililokuwa linaongea usiku, nikatamani hata kujitapisha lakini ilishindikana. Nikiwa nashangaa shangaa pale sebleni, mama akaenda chumbani kwangu na kutoka na sahani na chupa ya soda. Kisha akasema,
"Ona sasa, chakula nilichokuwekea hujala hata
kidogo. Bora hata usiku ule wakati unaniuliza
ungekiweka kweje friji, kitakuwa kimechacha tayari"
Huku akikinusa kile chakula, nikawa naangalia kama
mtu nisiyeelewa na kujiuliza kuwa mbona usiku
sikukiona zaidi ya zile chips kuku!
Nikamuuliza mama,
"Na hiyo chupa je?"
"Unauliza nini wakati unaona ni chupa ya soda! Au
unaona kingine mwenzetu?"
Nikatulia na kujiona kweli nina matatizo na ninahitaji
msaada wa hali ya juu saa, nikakaa kwenye kochi
pale sebleni huku nikitafakari mambo
yanavyokwenda katika maisha yangu kwani nilikuwa
sielewi hata moja nipo kama sipo.
Mchana nilitulia ndani nikiangalia video. Nikapata
ujumbe toka kwenye namba mpya ukisema.
"Una tabia mbaya sana wewe, sikutegemea kama
Sabrina utakuja kuwa na tabia kama hii"
Nikajiuliza ni tabia gani? Na nani kanitumia ule
ujumbe?
Nikajaribu kuipiga ile namba, naambiwa.
"Namba ya simu unayopiga haipo"
Basi nikazidi kuchukia kuwa kwanini iwe hivyo na
wakati amenitumia ujumbe jamani!
Mama akaja kukaa sebleni ili kuzungumza nami.
"Mwanangu una matatizo"
"Ndio nina matatizo mama"
"Unaonaje kama tukimuomba Carlos atusaidie maana
kasema kuwa anaweza kutusaidia"
"Mama, sitaki msaada wa Carlos sio mtu yule"
"Kwanini sio mtu?"
"Mtu gani, hana ndugu na wala hajulikani anapokaa!
Mimi simtaki kwakweli, sitaki kabisa anisaidie"
sana hadi tukamshangaa pale nyumbani.
Mama akamuuliza,
"Mbona mapema leo Penina?"
"Mmh! Nitakusimulia tu mama"
Akaja kwangu na kunikabidhi bahasha.
"Mzigo wako huo, kuna mtu kanipatia"
Kisha akaondoka zake, nikajiuliza ni nini na kufungua
ile bahasha.
Nikakuta kadi yenye rangi nyekundu ndani yake
imeandikwa,
"NAKUPENDA"
Ndani yake kulikuwa na pete ya dhahabu yenye jiwe
linalong'aa sana katikati nikahisi itakuwa ni almasi.
Nikajiuliza kuwa inatoka wapi maana ni vitu vya
ajabu.
Nikabeba ile bahasha na kwenda nayo chumbani kwa
dada kumuuliza kuwa kaitoa wapi.
"Dada, mbona sielewi hii bahasha! Umeitoa wapi?"
"Kwani haijaandikwa ilipotoka?"
"Haijaandikwa ndio, ila vilivyomo ndani yake sielewi"
"Ina nini kwani?"
"Kuna kadi nyekundu na pete"
"Acha masikhara Sabrina, hebu ilete tuone"
Nikampa dada, akaifungua.
"Kadi na pete viko wapi sasa? Mbona kuna barua tu!
Unajua nilipoitoa hii bahasha Sabrina?"
"Sijui"
"Nimepewa na Suzy, hebu angalia hapa ameandika
sijui mkutane wapi"
Nikashangaa na kuichukua tena, kuangalia ni kweli
ilikuwa barua. Sikutaka hata kuisoma kwani nilipatwa
na mashaka tayari.
Nikaichana na kwenda kuitupa nje, kisha nikarudi
sebleni huku nikijiuliza kuwa haya ni mambo gani. Dada akaniuliza Kuwa mbona nimeichana nikamjibu kuwa siiamini.
Muda mfupi kidogo nikapigiwa simu na Suzy.
"Bora nimekupata, maana kila nikikupigia haupatikani
ndiomana nikaandika ujumbe na kumpa dada yako ila
kaniambia umeuchana kwanini? Au ujumbe wangu
hauna maana?"
"Samahani Suzy, labda ungeniambia tu sasa hivi"
Simu yake ikakatika, nikajaribu kumpigia lakini
haikupatikana basi ikabidi niachane nayo.
Usiku ulipofika nilijikuta nikikosa hamu ya kula,
sikutamani chakula chochote kabisa hata mama na
dada walipokuwa wanakula sikujumuika nao.
"Naona umeshiba mwenzetu"
"Hapana mama, ila sijisikii kula tu"
"Kwanini wakati hata mchana hujala?"
Dada akadakia,
"Siku hizi mwanao anafanya diet, asubuhi nimeingia
chumbani kwake nimekuta soda mezani akasema
yeye hataki basi mimi nikainywa"
"Kumbe ndio ile chupa niliyoitoa asubuhi!"
Mama akanigeukia na kuniuliza,
"Kwani ulinunua muda gani soda?"
Dada akajibu,
"Aliletewa na Carlos halafu mimi nikampelekea
chumbani kwake"
"Unapendwa na Carlos mwanangu, tatizo lako
hupendeki"
Nilikuwa kimya kabisa nikiendelea kutafakari maneno
yao, kuwa snda alileta Carlos na usiku ule nikasikia
sauti ya ajabu. Huenda kweli Carlos akawa ndio lile
jitu la ndotoni.
Niliinuka pale sebleni na kwenda chumbani ili nijaribu
kulala maana ndio kazi niliyofanya, kula, kulala na
kuzunguka ndani ukizingatia bado naogopa kwenda
nje kuzurula.
Nikiwa chumbani nikapata ujumbe kwenye simu
kutoka kwa Carlos.
"Unanionea tu Sabrina, mimi sio mtu mbaya na nina
nia nzuri na wewe. Nipe nafasi nikusaidie na mambo
yako yote yataenda sawa. Ukiwa karibu na mimi
hakika utafurahia maisha. Usinitenge Sabrina, nipo
tayari kukusaidia kwa kila hali. Ukiwa na tatizo lolote
usisite kuniambia"
Nikaweka simu pembeni kwani ujumbe wake
haukuwa na maana yoyote kwangu.
Nikatulia na kuangalia mezani nikaona ile kadi
nyekundu na pete juu yake, nikashindwa kuelewa
maana hata ile barua niliichana muda ule ule sasa ile
kadi imetoka wapi tena, nikaogopa kusogelea na
kutoka nje. Nilipofika sebleni nikamvuta dada mkono
ili nae aone nilichokiona.
Nikafika nae chumbani ila ile kadi haikuwepo.
"Mbona hakuna kitu Sabrina?"
Nikatoa mimacho tu,
"Unajua wewe Sabrina una matatizo sana, kwanza
kilichokuleta kulala mapema yote hii ni nini? Twende
sebleni tukaangalie video"
Nikatoka na dada kwenda kuangalia video ila
sikuelewa chochote hadi muda ambao dada alichoka
na kwenda kulala ndipo na mimi nikainuka na kwenda
tena chumbani kwa lengo la kuchukua simu yangu
kisha niende kulala kwa mama kwani nilishapata uoga
wa kulala
chumbani kwangu.
Nikiwa chumbani, nikachukua simu ili nitoke.
Nikasikia sauti ikisema,
"Huwezi kunikimbia Sabrina"
Uoga ukanijaa na kusogelea mlango, kabla
sijaufungua ule mlango ukafunguliwa halafu akaingia
yule kijana wa ndotoni.
Itaendelea
Saf
 
SEHEMU YA 36


Nikabaki nimeduwaa tu na kukosa cha kujibu.
Nikamuangalia kwa makini Carlos na kupata jibu la
haraka kumjibu.
"Naomba unitoe kwanza eneo hili halafu hayo
mengine tutazungumza badae"
"Hakuna tatizo Sabrina, najua unanihitaji kupita
unavyofikiria"
Kisha akaniongeza hadi kwenye gari yake nikapanda,
kwavile nilikuwa nimechoka sana na usingizi kunizidia
nikajikuta nimelala.

Kuja kushtuka tayari tulikuwa tumefika nyumbani
kwetu, mama akafurahi sana kuniona huku
akimshukuru Carlos.
"Nilikwambia mama usijali nitamtafuta Sabrina hadi
nimpate, huyo hapo sasa"
"Nimefurahi sana, asante baba angu"
Tukaingia ndani na mama kisha Carlos akaenda zake.
Mama akaanza kuniuliza sasa,
"Ulikuwa wapi mwanangu?"
"Sijui mama, sijui"
"Utaniua mama yako wewe, utaniua kwa presha. Hivi
huyo Sam wako atanizalia Sabrina mwingine mimi?
Mbona unanitesa hivyo mwanangu?"
"Nisamehe mama"
"Na huo msamaha ungeombea kaburini nani
angekusikia mwanangu? Unajua utaniua wewe mtoto!
Kilichokupeleka kwa wakina Sam sijui ni kitu gani,
nadhani unaombea hata mimi nife ila ubaki na Sam
jinsi ambavyo umekosa akili wewe mtoto"
Nikakaa kimya kabisa kwani sikupenda kubishana na
mama na vilevile sikujua ni nani aliyemwambia kama
nilienda kwa wakina Sam.
Mama alipomaliza kusema yake nikaenda zangu
kuoga ili kupata nguvu kidogo, kisha nikala chakula
ambacho mama aliniandalia bila hata ya kujua kama
mwenzie nimelala maporini usiku wote wa jana.
Nilipomaliza kula, nilienda chumbani kwangu kwa
lengo la kupumzika kidogo.

Nikiwa nimetulia chumbani, nikaona mfuko wa rambo.
Nikainuka na kwenda kufungua, nikakuta viatu vizuri
sana vipo ndani yake. Nikabeba ule mfuko na kwenda
kumuuliza mama.
"Nani kaweka mfuko huu chumbani kwangu?"
"Ni mimi nimeweka, ni zawadi yako hiyo uliyoletewa
na Carlos halafu ukanidanganya kuwa unakwenda
kuifata"
"Nisamehe mama"
"Nishakwambia kuwa msamaha wako hauna maana
kwa sasa. Sema lingine tu"
Nikaviweka vile viatu chini na kuvijaribisha, kwakweli
vilikuwa vizuri na vilinipendeza sana.
Nikaanza kujaribu kuvitembelea maana vilikuwa
virefu kiasi,
"Amekupatia sana Carlos, viatu vimekupendeza sana
mwanangu"
Nikawa natabasamu huku nazunguka navyo ndani
kisha nikarudi chumbani kwangu, nikakaa kitandani ili
nivivue niweze kupumzika.
Nikavivua, mara gafla miguu ikawa kama inawaka
moto halafu inauma sana sikujua tatizo ila kuna roho
ikaniambia kuwa sababu nimevua vile viatu kwahiyo
nikavivaa tena na ile miguu ikaacha kuuma na kuwa
kama inawaka moto.
Nikajiuliza mahusiano ya kile kiatu na mguu wangu ni
nini nikakosa jibu, nikajaribu tena kuvivua nione napo
miguu ikaanza tena kupwita, nikavivaa tena na
kujiuliza nitalala na viatu miguuni leo? Ila sikuwa na
jinsi kwani nilichoka sana na kuamua kulala navyo.
Dada ndiye aliyekuja kunishtua pale kitandani.
"Sabrina, Sabrina hebu amka tuongee"
Nikaamka na kukaa, kisha nikamsalimia na
kumsikiliza.
"Ulikuwa wapi jana?"
"Sijui dada"
"Mmh Sabrina! Nasikia ulienda kwa wakina Sam
umedundwa huko hadi umekoma"
Nikawa kimya tu nikimsikiliza.
"Viatu vizuri hivyo kakununulia nani?"
"Nimevikuta humu ndani, mama kasema nimeletewa
na Carlos"
"Eeh vimekupendeza! Hadi unalala navyo duh!"
Kisha akainuka na kutoka chumbani kwangu.
Nikajitazama tena miguuni na vile viatu, nikajaribu
kuvivua hali ikawa kama ya mwanzo. Nikajiuliza ni
kwanini? Ila nikajisemea kuwa lazima Carlos anajua
sababu, nikachukua simu na kumpigia ila
hakupatikana hewani.
Nikatoka sebleni.
"Naona viatu havibanduki miguuni leo mwanangu"
Dada Penina akadakia,
"Chezea kitu kipya wewe"
Wote wakacheka, nikatamani kuwaambia
ninavyojisikia nikikivua ila mdomo ulikuwa mzito
kusema chochote kuhusu kiatu.
Nikatulia pale sebleni na kusikiliza mazungumzo ya
mama na dada ambayo yalinivutia sana, nikajisemea
kuwa badae nitamfata dada chumbani kwake ili
kumuuliza vizuri.

Usiku ulipoingia kama kawaida ya dada yangu
alikuwa yupo chumbani kwake akicheza na kompyuta
yake ya mezani, nikamfata alipo ili anijibu maswali
yangu.
"Eeh niambie mwali wa viatu vipya"
Nikacheka tu na kumwambia,
"Nimekuja kukuuliza kitu dada"
"Kitu gani hicho? Uliza tu kuwa huru"
"Ni kuhusu mazungumzo yako na mama, umesema
yule rafiki yako dada Fatuma alikuwa akisumbuliwa
na matatizo gani hadi akaachana na mchumba
wake?"
"Aah! Kumbe, alikuwa akisumbuliwa na jini mahaba
yule"
"Jini mahaba? Ndio yukoje huyo jini mahaba?"
"Kwakweli mdogo wangu sijui ila itakuwa vyema
kama hayo maswali ukienda kumuuliza Fatuma moja
kwa moja, nadhani yeye atakuwa anajua maana ndio
alikuwa nalo na likamsumbua sana"
"Ila je hilo jini lilimuachanisha vipi na mpenzi wake?"
"Nasikia lile jini likikupata huwa linataka likutawale
lenyewe tu, utashangaa gafla huna maelewano na
mpenzi wako mara unaona hakupendi mara anahisi
hakuridhishi au hakufai tena na mengineyo hadi
unafikia uamuzi wa kuachana nae"
"Sasa suluhisho ni lipi hapo?"
"Suluhisho ni kwenda kulitoa kama ukigundua unalo,
je wewe unahisi kuwa na hilo jini?"
"Sijui dada ila ninahitaji kufahamu zaidi"
"Basi nitakukutanisha na Fatuma uongee nae na
akuelezee vizuri"
"Lini sasa?"
"Hata kesho"
"Mi nataka iwe kesho dada"
Nikakubaliana na dada kuwa kesho yake atanipeleka
kwenda kukutana na Fatuma nipate kuzungumza nae.
"Nitawahi kurudi kesho halafu nitakupeleka"
"Sawa dada, utakuta nimeshajiandaa"
Akacheka kisha tukainuka na kwenda kula halafu
kulala huku nikifikiria hayo mambo ya kesho na viatu
vyangu mguuni ambavyo kuvivua sikuweza.

Nikiwa nimelala, yule mkaka wa ndotoni akanijia
kwenye ndoto kama kawaida na kusema.
"Natumaini umeifurahia zawadi yangu"
Nikashtuka na kujitazama miguuni ambako nimevaa
vile viatu kisha nikavivua kwa hasira ila maumivu
niliyoyapata sikuweza hata kusogea na kuamua
kuvivaa tena maana sikuwa na la kufanya kwakweli.
Nilipovivaa tena nikalala vizuri hadi panakucha na
kuamka huku nikifanya kazi za hapa na pale.
Mama kuniona tena na vile viatu akaanza kunitania,
"Nadhani leo utaoga navyo hivyo viatu maana
havivuliwi"
Sikujibu kitu maana hawakujua jinsi ninavyoteseka na
kile kiatu mguuni.
Nilipomaliza kazi, nikaenda kuoga.
Nilipofika bafuni nikajaribu kuvua kile kiatu ili nioge,
nikakivua na wala miguu haikuniuma ila nilipomaliza tu
kuoga ilianza kuniuma tena na kuamua nivae tena vile
viatu wakati natoka bafuni.
Nikaenda chumbani na kujiandaa ili kumngoja dada
arudi na niende nae huko kwa rafiki yake.

Dada aliporudi akapumzika kidogo kisha tukamuaga
mama na kuondoka huku vile viatu vyangu vikiwa
miguuni,
"Naona umevipenda sana hivyo viatu Sabrina"
"Ndio nimevipenda dada"
Tulipofika kwa rafiki yake na dada, tulimkuta ametulia
tu ndaki akisikiliza muziki.
Dada akaongea nae kidogo pale na kutuaga kuwa
kuna mahali anaenda mara moja akitoka huko ndio
atapitia tena hapa.
"Naona umeniletea Sabrina leo"
"Ana maswali yake huyo atakuuliza mwenyewe"
Kisha dada akaondoka na kuniacha na rafiki yake
dada Fatuma pale.
"Kuwa huru Sabrina, niulize chochote nitakujibu"
"Jana nilimsikia mama na dada wakiongelea maswala
ya jini mahaba na kusema kuwa hata wewe limewahi
kukurumbua"
"Kwahiyo unahitaji kujua kuhusu jini mahaba?"
Nikatikisa kichwa kuonyesha kwamba nahitaji kujua.
"Jini mahaba ni kiumbe mwenye tabia ya kukuingilia
kimwili bila ridhaa yako, mara nyingi huja wakati
umelala. Unakuwa unahisi kama unaota vile kuwa
unaingiliwa na mtu, ukija kushtuka mara nyingine
unajikuta umechafuka kwa mbegu za kiume, hapo
utakuwa na jini mahaba tena aliyekubuhu"
"Je mwanadamu wa kawaida anaweza kufanya
mambo kama afanyayo jini mahaba"
"Si rahisi ila akiwa mchawi anaweza maana
atakupumbaza wakati umelala kama huna kinga
thabiti dhidi ya watu wabaya"
"Unaweza kumuona jini na kuongea nae kama
binadamu wa kawaida?"
"Majini ni viumbe wa ajabu sana, kwanza wanatisha
huwezi kustahimili ukikutana nao. Halafu wananamna
nyingi za kutembea na kusafiri, anaweza kujigeuza
upepo au hata mdudu mdogo kabisa. Hata ukiwa
katika shule zenye majini utashangaa gafla upepo
mkali unapita, wanaojua watakwambia jini kapita"
"Kwahiyo huwezi ukaonana nae kabisa yani"
"Nakwambia huwezi kustahimili kumtazama jini,
kwani hujawahi kusikia watu wakisema kuwa majini
wanakwato za ng'ombe miguuni mwao, au kusikia
kuwa majini ni warefu sana hata ukikutana nao
lazima uchanganyikiwe. Si rahisi kukaa na
kuzungumza na jini mdogo wangu"
"Je wewe ukimuona jini utamjua?"
"Inategemea ila kiukweli nawaogopa majini sitaki hata
kukutana nayo nahisi nitakufa kabisa"
"Nasikia jini mahaba alifanya uachane na mpenzi
wako!"
"Ndio, unajua sifa kubwa ya jini mahaba ni wivu. Huyu
jini anawivu sana na huwa anataka akumiliki peke
yake hivyo atakufanyia visa hadi uachane na
unayempenda"
"Sasa ulifanyaje wewe ulipogundua unae?"
"Nilitafuta mtaalamu, kipindi kile nazunguka sana na
Penina tukapata mtaalamu huko mbali, yeye ndio
akatusaidia. Kwani unajihisi kuwa na jini mahaba
wewe?"
"Sielewi dada, maana nimejikuta mambo yangu
yakienda sivyo na mpenzi wangu nae nimeachana
nae. Basi nisaidie dada yangu, nipeleke kwa huyo
mtaalamu"
"Hayupo hapa kwa sasa, yupo mkoani ndio anafanyia
shughuli zake. Akirudi nitakwambia twende mdogo
wangu hata usijari"
"Sawa dada, ila ni kweli kabisa huweza kumuona
jini?"
"Wanatisha mdogo wangu, sio kama sisi tulivyo wao
ni viumbe wa ajabu."
Nilikuwa nauliza kwa makini huku moyoni mwangu
nikipima kuwa Carlos atakuwa ni mtu wa aina gani.
Dada aliporudi, tuliaga mahali pale na kurudi
nyumbani na giza lilishaingia.

Nikiwa nyumbani nikatafakari sana na kuona kuwa
yule wa ndotoni atakuwa jini mahaba tu, nikahisi
mpaka atakaporudi huyo mtaalamu wa dada Fatuma
nitakuwa nishateseka sana na kuolewa na Carlos
sikutaka maana sikumuamini na yeye, nilihisi ni
mchawi.
Nikapata wazo la kwenda kuongea na mama kuhusu
mama Semeni maana alisema yupo tayari kunipeleka.
Nikamwambia mama kuwa nipo tayari, akafurahi
sana na kumpigia mama Semeni simu muda huo huo
ambapo akasema nijiandae kesho ili twende.
"Ila mwanangu umekuwa mzungu wewe? Viatu
umezurula navyo huko na bado upo navyo ndani"
Dada akadakia tena,
"Kipya kinyemi mama"
Sikusema chochote huku nikiamini kuwa majibu ya
maswali yangu yote yatapatikana kwa huyo mtaalamu
kesho.
Nikaenda kuoga ikawa kama asubuhi, nikiwa bafuni
navivua na kuoga ila kutoka miguu inauma hadi
nivivae.
Nikazunguka vile vile na viatu hadi usiku wakati wa
kulala ila leo nililala vizuri tu wala sikupatwa na ndoto
yoyote ya kutisha hadi panakucha.

Asubuhi na mapema, mama Semeni aliwasili
nyumbani na kukuta mimi na mama tumeshajiandaa
tayari.
Safari ikaanza ya kwenda kwa huyo mtaalamu,
ilikuwa mbali kweli ila tukavumilia hadi kufika.
Ilikuwa ni kibanda cha nyasi, mama na mama Semeni
waliingia nikabaki mimi nje kwani kila nikitaka kuingia
mtaalamu ananiambia
"Vua viatu"
Vile viatu muda huu havikutaka kutoka miguuni
kabisa, kila nilipojaribu kuvua ilishindikana.
Nikamwambia yule mtaalamu,
"Havitaki kuvuka"
Yule mtaalamu akafanya dawa zake kisha akanifata
yeye mwenyewe, akainama na kushika viatu vyangu.
Mara gafla akarushwa kamavile mtu aliyepigwa na
shoti ya umeme.

Itaendelea
Ssfi
 
SEHEMU YA 42


Moja kwa moja nikajitazama kwenye vidole vyangu.
Nikakuta nimevaa pete ileile niliyovalishwa ndotoni.
Nikashtuka sana na kuwatazama watu waliopo chumbani kwangu ambao walikuwa wakipiga makofi na vigelegele, kwa haraka haraka nikaweza kumuona mama, mama Semeni, dada Penina na rafiki yake Fatuma, Lucy, Carlos na watu wengine watatu ambao sikuwafahamu.
Nikainuka pale kitandani nikiwa na hasira sana, nikaenda sebleni nao wakanifata nyuma, nikataka kutoka nje mama akanizuia huku akiniuliza,
"Unataka kwenda wapi mwanangu?"
Nikiongea kwa ukali,
"Mama huu ni udhalilishaji, huwezi kuingiza watu wote hao chumbani kwangu bila ridhaa yangu"
Mama akaongea kama kunipooza hivi,
"Ilikuwa ni surprise mwanangu"
"Surprise gani mtu nafanyiwa wakati nimelala mama? Uliona wapi bhana? Mmenikera sana"
Nikarudi nyuma na kumsogelea Carlos, kwakweli nilikuwa na hasira sana muda huu na sikumuogopa mtu yeyote wala kitu chochote. Nikamuuliza Carlos,
"Toka lini watu wanavishwa pete ya uchumba usingizini? Toka lini? Niambie upesi bhana, umenikera sana. Uchumba gani wa ndotoni"
Nikachukua kidole changu ili kuivua ile pete, nia yangu ni kumtupia nayo Carlos usoni ila ile pete haikuvuka ilikuwa imeng'ang'ania kwenye kidole changu, nikakaa chini huku machozi yakinitoka.
Dada Penina na Fatuma wakajaribu kunipooza, ila walishindwa kwamaana nilikuwa na hasira sana.
Mara gafla watu wote wakatoka pale sebleni na kuniacha mimi na Carlos tu, nadhani Carlos aliwaambia kuwa waondoke tuzungumze.
"Sasa Sabrina kilichokuchukiza ni kipi?"
"Usijifanye hujui Carlos, unajua kila kitu. Uliyoyafanya ndotoni kwangu huyajui wewe?"
"Yapi hayo Sabrina? Sijui chochote"
"Unajua, nimesema unajua tena unikome sitaki kuolewa na wewe, sitaki kuolewa na jini mimi"
Mara gafla nikasikia kicheko cha kutisha, nikaanza kuogopa na sikuwa na pa kujificha au kukimbilia pale sebleni, ikanibidi nikimbilie kwa Carlos aliyeonekana kama mtu kwangu.
Nikamsogelea nae akanikumbatia, nikajikuta nimekuwa mpole gafla na ule ukali wote wa mwanzo umepotea.
Kisha Carlos akanikalisha na kuwaita wale wa nje.
Nilikuwa kimya kabisa yani kama vile sio mimi niliyekuwa nafoka sana muda mfupi uliopita.
Carlos akaanza kutambulisha wale watu watatu ambao siwafahamu,
"Hapo kuna mama, baba na kaka yangu"
Mama alikuwa ameandaa chakula na wote wakajumuika kula kasoro mimi ambaye nilishindwa kula kabisa na kuwaacha wenyewe wale wamalize na wafurahie kitu
ambacho mimi nakichukia.
Walipomaliza kula, wakaongea mawili matatu na kuaga. Mama akauliza wanapokaa wale wazazi wa Carlos, wakamuelekeza ili na sisi tuweze kwenda.

Jioni ya leo nilikaa na kuiangalia ile pete ambapo nilitamani hata nikate kidole niweze kuitoa kwangu maana ilinikera sana ila sikuwa na la kufanya tu.
Muda wa usiku ulipofika napo sikujihisi kula na kuamua kwenda kulala hivyo hivyo.
Nikiwa nimelala, akaja yule kijana wa ndotoni na kusema
"Pole mke wangu mtarajiwa, najua una njaa na unahitaji kula. Nakuletea chakula upendacho."
Akaniletea keki na maziwa na juisi.
Nikajikuta nikila ile keki na maziwa, ila juisi nilikunywa kidogo na kuiacha.
Kisha akaniambia,
"Ulitaka kunitia aibu leo ila ni vizuri niliwahi kukudhibiti maana ungeniumbua kwa wageni wale, bora kwa mama yako na dada yako maana najua jinsi ya kuwaweka"
Nikamsikiliza tu,
"Hivi karibuni nitakuoa ila ndoa yetu haipaswi kuonwa na watu kamavile ila kuna viumbe maalum wa kushuhudia ndoa yetu"
Nikashtuka usingizini na kusema kwa nguvu,
"Viumbe gani hao?"
Sauti ikasikika,
"Ni majini wenzangu, wanaoishi baharini na mapangoni"
Nikaanza kutetemeka kwa uoga, chumbani kwangu kulikuwa na harufu ya marashi iliyotapakaa chumba kizima.
Nilipoangalia pembezoni mwa kitanda changu nikaona sahani yenye punje za keki, pakti ya maziwa na juisi iliyonywewa kidogo, hapo nikashtuka zaidi baada ya kugundua kuwa mambo yote yale ya kula na kila kitu yalifanyika chumbani kwangu, nikainuka ili nikimbie chumba. Sauti ikasikika,
"Unaenda wapi Sabrina?"
Nikazidi kutetemeka, wazo likanijia kuwa nimpigie simu Carlos, nami sikupoteza wakati nikachukua simu na kumpigia akapokea.
"Acha kunitesa Carlos"
"Nakutesaje Sabrina?"
"Unanitisha hadi naogopa kulala"
Nikamsikia Carlos akicheka sana kwenye simu hadi ile simu ikakatika, ila hali ikawa shwari mule ndani.
Sikutaka kulala tena mule ndani, nikatoka na kwenda chumbani kwa mama na kulala pembeni yake hadi kunakucha.
Mama alipoamka alishtuka na kuuliza,
"Umekuja muda gani humu?"
"Muda mrefu tu, ila mama nina ombi moja"
"Lipi hilo?"
"Naomba twende kwa wale watu ambao Carlos aliwaleta na kujifanya kuwa ni ndugu zake"
"Inamaana huwaamini?"
"Ndio siwaamini"
Basi mama akaniambia kuwa hakuna tatizo na kwavile walimuelekeza wanapoishi basi itakuwa vyema kama tukienda leo leo kabla hatujasahau zaidi hayo maelekezo.
Tuliamka na kufanya kazi za hapa na pale kisha kujiandaa kwa hiyo safari ya kuwafata hao ndugu wa Carlos.

Tuliondoka na kufika eneo ambalo tulielekezwa na wale ndugu wa Carlos, tukawapigia simu wakaja kutupokea na kutukaribisha sana.
Tulifika kwao na kuongea ya hapa na pale, nikaenda pembeni na yule ambaye alisema ni kaka wa Carlos.
"Hivi kweli Carlos ni ndugu yako?"
"Ndio ni ndugu yangu kwani vipi?"
"Ni ndugu yako kabisa?"
"Kwanini unamashaka?"
"Unajua anapoishi?"
Akasita kujibu kisha akaondoka bila ya kusema chochote.
Nikarudi tena ndani ambako kulikuwa na hao waliosema ni wazazi wake na mama.
"Samahani naomba niulize"
"Uliza tu"
"Eti nyie ni wazazi wake kabisa na Carlos?"
Mama akanikatisha,
"Ndio maswali gani hayo Sabrina?"
"Mmh mama nauliza tu"
Nikatulia tu huku nikingoja kujibiwa, yule aliyetambulishwa kama mama yake akaguna kwanza na kuanza kunijibu,
"Mmh! Sisi ni kama baba yake na mama yake mdogo"
"Kivipi? Inamaana nyie sio?"
"Hapana, sisi ni ndugu zake"
"Maana mmesema kuwa nyie ni kama, ndiomana nikapatwa na maswali hapa"
"Usijali, Carlos ni mtoto wetu sana. Tangia akiwa mdogo tulikuwa nae"
Mama nae akauliza,
"Kwani nyie ni wenyeji wa wapi?"
"Sisi ni watu wa Kigoma, Carlos amezaliwa hukohuko na kukulia hukohuko"
Kidogo nikajiridhisha ila bado sikuwa na imani nao kwa sana.
Tukaongea mengi na kuaga.

Tulipofika nyumbani tulimkuta dada Penina akiwa ndani na rafiki yake Fatuma, tuliwasalimia kisha Fatuma akaanza kuongea,
"Jamani kweli Carlos ni daktari wa ukweli mama, amenisaidia tatizo langu hata siamini"
"Kwani ulikuwa na tatizo gani?"
"Nilikuwa na tatizo la uzazi mama, yani kila hospitali waliniambia mimi ni mgumba. Kuna mganga nilienda akasema ndugu zangu wamenifunga nisizae, mwingine akasema ni lile jini mahaba lililonivaa kipindi kile ndio lilinifunga nisizae kwakweli nilikata tamaa. Siku ile tumetimuliwa kwa yule mganga mashuhuri sababu ya Sabrina niliumia sana tena sana ila Carlos kanitibia bure kabisa, dawa ile nimekunywa kwa siku moja tu nikaenda kukutana na mwenzangu kama ilivyoandikwa. Si alisema kuwa baada ya siku tatu nitapata majibu, basi leo nimechukua kipimo cha mimba na kujipima, nimekuta nina ujauzito wa siku. Kwakweli nimefurahi sana ndiomana nimekuja kuwaeleza habari hii"
Mama nae akaifurahia sana ile habari,
"Kwakweli bora nimepata mkwe daktari"
Dada Penina akadakia,
"Tena ni daktari wa madaktari"
Wakaendelea kuongea pale nami nikaenda chumbani kwangu kupumzika.
Baada ya muda kidogo nikapigiwa simu na Sam.
"Sabrina, tafadhari naomba tuonane haraka sana"
Nikakubaliana nae, kisha kisha nikatoka chumbani kwangu na kwenda kumuaga mama kuwa natoka mara moja kwani moyo wangu uliniambia kuwa kutokuaga kwangu ndio chanzo cha kutokea Sabrina wawili wawili huko njiani.
"Uwe makini Sabrina, kumbuka wewe ni mchumba wa mtu sasa"
"Usijali mama"
Nikaondoka pale nyumbani na kuelekea mahali ambako nimepanga kukutana na Sam.

Nilifika mapema kabla ya Sam kufika, nikatulia kumngoja afike na haikuchukua muda akawasili.
Akachukua mkono wangu ili kunisalimia ila akarushwa pembeni kama na umeme, akasogea na kuniuliza.
"Umeshika nini mkononi Sabrina?"
Nikamuonyesha kile kidole chenye pete.
Sam akasikitika sana na kusema,
"Umeitoa wapi?"
"Carlos kanivisha"
"Nawe ukakubali?"
"Nilikuwa nimelala Sam, alinivisha nikiwa usingizini"
Sam akazidi kusikitishwa na kile kitu.
"Sasa Sabrina umechukua hatua gani mpaka sasa?"
"Sijafanya chochote ila leo tulienda kwa ndugu wa Carlos"
"Hao ndugu sidhani kama wa kweli, kwanza niambie amekupa pete hiyo kwa misingi ipi?"
Nikaogopa kumwambia Sam kama amenipa kama mchumba wake kwani nilijua Sam atachukia tu.
"Sijui ila amenivisha tu"
"Na bado hatujachelewa Sabrina, nadhani twende leo kwa wale watu"
Nikainuka pale, Sam hakuweza kunishika hata mkono kwani alipigwa na shoti alipojaribu kunishika tena.

Safari ikaendelea ila tulipokuwa njiani nikapotezana na Sam, hata sijui nilipotezana nae vipi ila hakuonekana nikajaribu kumpigia simu hakupatikgna kwahiyo nikaamua kurudi nyumbani tu.
Kufika nyumbani nikamkuta Sam yupo nyumbani kwetu akiongea na mama,
"Huyu mwenzio ni mchumba wa mtu sasa kwahiyo usipende kumfatilia"
"Mchumba wa mtu kivipi?"
"Kwani huelewi maana ya mchumba wa mtu wewe? Ni mke mtarajiwa wa mtu"
"Ni nani huyo mumewe"
"Kumbe hujui, ni....."
Nikaingilia kati na kuleta habari za salamu kisha nikamvuta Sam,
"Umefika muda gani huku?"
"Uliponipotea nikajua lazima utarudi kwenu ndiomana nikaja huku moja kwa moja. Niambie ukweli Sabrina, au Carlos kakuvisha pete ya uchumba?"
"Hapana Sam"
"Niambie ukweli ili nijue jinsi ya kukusaidia"
"Kama ni kweli utanisaidiaje?"
"Niambie kwanza ni kweli au si kweli"
Nikiongea kwa unyonge,
"Ni kweli Sam"
"Kwanini umenificha muda wote Sabrina?"
Mara Carlos akawasili muda huo nyumbani kwetu, akatupita mimi na Sam pale nje bila ya salamu ila alimuangalia Sam kwa jicho kali sana na kuingia ndani.
Mara gafla Sam akaanza kuwashwa, alijikuna sana hadi nikamuonea huruma, akaondoka nyumbani kwetu huku anakimbia nikajaribu kumuita lakini hakugeuka nyuma kuniangalia wala nini, akapotea kabisa maana giza lilishaingia.
Nikarudi ndani kwa masononeko makubwa sana, nikawapita pale sebleni na kwenda chumbani kwangu halafu usingizi ukanipitia, kwenye ndoto nilimuona Sam tu siku ya leo, nilimuona Sam akiteseka na kuhangaika.
Nikashtuka na kusikia harufu ya marashi chumba kizima, sikutaka maajabu ingawa ni usiku sana nikainuka na kwenda kulala chumbani kwa mama.
Nikiwa nimelala tena, nikajiwa ndotoni na yule kijana wa ndotoni akasema,
"Karibia nakuja kukuchukua mke wangu, Carlos na Sam hawatahusika tena"
Nikamshangaa wakati Carlos ni yeye mwenyewe, nikaogopa sana.
Akaendelea kusema,
"Unaogopa nini sasa? Je nikikwambia kuwa muda huu upo chumbani kwako na si chumbani kwa mama yako kama unavyodhani? Na huyo uliyelala nae si mama yako bali ni mimi"
Nikashtuka tena toka usingizini na kuangalia mandhari ya chumba ilikuwa ni chumba changu na harufu ileile ya marashi. Mara gafla nikaguswa mgongoni na kuitwa jina langu.
[emoji95][emoji95]
 
SEHEMU YA 68

Tukasikia sauti ya kiume kutoka chumbani kwangu,
"Mimi ndio nimekipika"
Kila mmoja alibaki kuduwaa.
Tukaisikilizia kwa makini kuwa ni ya nani, mama akauliza kwa mshangao na uoga
"Nani amejibu?"
Ile sauti ikasikika tena
"Mimi hapa ndiyo nimejibu"
Mama akauliza tena huku akitetemeka sasa,
"Wewe ni nani?"
Tukasikia kicheko cha nguvu na kufanya tuzidi kuogopa, kisha akajibu tena
"Mimi ni jini"
Hakuna aliyepata uwezo wa kuuliza kitu chochote kile cha zaidi maana kila mmoja alikuwa akitetemeka, na ubaya zaidi hatukuweza kukimbia wala kufanya chochote kile.
Kisha tukasikia mlango wa chumbani kwangu ukifunguliwa na kufungwa bila ya kuonekana mtu yeyote yule zaidi ya hayo mauzauza tu.
Muda huo huo tukapitiwa na usingizi wa gafla sana na hakuna aliyeelewa kilichoendelea zaidi.

Nilikuwa wa kwanza kabisa kushtuka toka kwenye ule usingizi wa ajabu, ilionyesha kuwa giza limeshatanda na pale sebleni palishawashwa taa, sikutaka kujihoji zaidi kuwa nani amewasha ile taa zaidi ya kuwaamsha wenzangu ambao bado walikuwa wamelala.
Kila mmoja aliamka akiwa amechoka sana, walikazana kujinyoosha kana kwamba walilala usingizi wa maana.
Kila mmoja alikuwa akimuuliza mwenzie kuwa kuna nini? Nadhani walishasahau kasoro mimi mwenyewe ambaye nakumbuka kila kitu ambacho kimetokea.
Nikatulia pale nione kuwa watasema kitu gani ila hawakuuliza chochote zaidi ya kujishangaa kuwa wamelala sana, mama ndiye aliyeanza kuongea
"Kweli pilau imetufanya kazi, yani baada ya kula na kulala moja kwa moja mmh!"
Nikainuka na kwenda jikoni, nilipofika nikashanga kuona kuwa kuna nyama vimeokwa vizuri sana pale jikoni hadi udenda wa tamaa ukanitoka ila nikifikiria ya mchana nikaachana nayo na kurudi sebleni ambako Sam nae alikuwa akiaga kuwa anataka kuondoka ila mama na dada wakamzuia kuondoka kwa mara ya kwanza hadi nikashangaa.
Dada alikuwa anamwambia Sam,
"Leo ulale hapa hapa halafu kesho ndio uondoke Sam tafadhari sana tunakuomba"
Mama nae akamwambia Sam,
"Ingawa nilikuwa nakuhisi vibaya kwa mwanangu Sabrina ila nakuomba kwa leo ulale hapa kwanza ni usiku tayari, utaondoka kesho tu. Wewe Sam ni kama mtoto wangu tu, leo usiondoke"
Ikabidi Sam akubaliane nao na kuamua kuwa pale pale nyumbani kwa usiku wa leo, kisha mama na dada wakainuka kwenda kufanya mambo mengine halafu Sam nae akaamua kwenda kuoga maana katika misukosuko yote ile hakuoga yeye wala mimi.

Nilibaki mwenyewe pale sebleni huku nikijihoji kama niende chumbani kwangu au nibakie pale pale sebleni? Sikuwa na hamu ya kwenda kwenye chumba changu kabisa kwani hisia zangu zinanituma kuwa mauzauza yote yanaanzia chumbani kwangu.
Nikatulia pale sebleni hadi Sam alipotoka kuoga ndipo nami nikainuka na kwenda kuoga wakati huo dada Penina alitoka kabisa nje ya nyumba sijui alienda wapi.

Nilipokuwa bafuni nikawaza mambo mengi sana yanayonitokea na kujiuliza kuwa kwanini yananitokea ila sikupata jibu.
Wakati namalizia kuoga nikahisi kuwa kuna mtu nyuma yangu ananisugua, hofu ikanijaa sana ila kabla sijafanya chochote nikahisi yule mtu amenikumbatia yani niliona mikono yake mbele yangu.
Nikataka kupiga kelele, akaniziba mdomo kwa nyuma na kuniambia,
"Sabrina, kumbuka wewe bado ni mke wangu tumefunga ndoa Sabrina, ndugu zangu wote walikuwepo kushuhudia ndoa yetu au umesahau jamani mke wangu?"
Nilikuwa natetemeka mwili mzima huku nikihofia kufanywa kitu kibaya na yeye, nadhani aliyajua mawazo yangu kisha akaniambia
"Sitakufanya chochote bila ridhaa yako ndiomana mimi ni jini, nipo tofauti na binadamu wa kawaida kama ambavyo ulitaka katika maisha yako. Hakuna mwanadamu yeyote wa kiume aliyekamilika na kumuacha mtoto mzuri kama wewe akiwa mtupu mbele ya macho yake, lazima angekulazimisha tu ila mimi naridhika ukiwa hivi mbele yangu"
Moyo ulikuwa ukinienda mbio sana kupita maelezo ya kawaida na mwili wangu ulikuwa ukitetemeka muda wote ila hakulijali hilo zaidi ya kuendelea kuongea anayoyataka yeye
"Leo mchana niliwaandalia chakula kizuri sana ila nilipowaambia kuwa ni mimi nimeandaa mkaogopa, na usiku wa leo nimewaokea nyama nzuri sana najua mtaipenda"
Hapo ndipo nikagundua kuwa nyama ile ameitengeneza yeye, akanigeuza ili nitazamane nae macho kwa macho.
Kwakweli sikuweza kustahimili na kujikuta nikianguka na kupoteza fahamu.

Niliposhtuka nilikuwa nipo karibu na mama, kichwa changu kipo kwenye miguu yake.
Nikainuka na kukaa huku nikikumbuka kilichotokea, nikahisi mwili mzima ukisisimka na kutetemeka kwa uoga baada ya kukumbuka yaliyonipata kule bafuni.
Mama akanipa pole sana,
"Tumekukuta ukiwa umeanguka bafuni mwanangu, bora leo Sam yupo maana ametusaidia sana. Pole mwanangu"
"Asante mama"
Mama akaendelea kuongea,
"Tulikuozesha kwa mume asiye na maana kabisa maana tangu umeondoka hadi leo hajaja kukuulizia wala nini, tunaishia kuonana nae njiani tu huko tena wala hatusalimii kwakweli najuta kukuozesha mwanangu bila kuchunguza vizuri tabia ya anayetaka kuoa"
Kwa maneno yale ya mama nikajua anajutia sana ila akiujua ukweli kwa hakika atajutia zaidi.
Dada Penina naye alikuwepo pale pembeni akasema,
"Tena wakati naenda dukani nimekutana naye huyo Carlos akija hivi, nikajua anakuja huku"
Mimi na Sam tukashtuka sana kwani nilijua kuwa tayari tumeshamalizana na yale mambo ya Carlos wala sikujua kama atakuja tena katika maisha yetu, sikujua kama atarudi tena baada ya kumzika kwa mikono yangu mwenyewe. Nikajikuta nikiwauliza,
"Kwanini lakini?"
Mama nae akauliza,
"Kwanini kivipi?"
"Huyo Carlos mama ataacha lini kusumbua maisha yangu?"
Nikainama huku machozi yakinitoka kwani nikikumbuka kuhusu kifo cha Carlos niliumia sana, sasa kwanini huyu jini anaendelea kumsumbua huyu marehemu badala ya kumuacha apumzike kwa yote aliyopitia?
Mama alikuwa akinishangaa kuwa kwanini nalia kiasi kile, ikabidi aniulize
"Kwani vipi Sabrina?"
Nami nikaamua kumwambia mama ukweli,
"Mama, Carlos ni marehemu"
Mama na dada walishtuka sana, dada akaniuliza kwa makini
"Sijakuelewa Sabrina unasema!!"
"Carlos ni marehemu dada"
Walizidi kushangaa tu maana ni kweli hawakunielewa kabisa, kama dada Penina ndio kabisa hakunielewa ukizingatia anasema kuwa ametoka kuonana na Carlos muda mfupi uliopita kwahiyo swala la kumwambia kuwa Carlos ni marehemu hawakuelewa wala kuamini.
"Sikuelewi Sabrina hebu niambie vizuri, huyo Carlos ni marehemu kivipi?"
"Jamani muulizeni hata Sam awaeleze labda ndio mtamuelewa yeye"
Ikabidi wamuulize Sam ambapo akawajibu hivi,
"Sidhani kama ni vyema kuzungumzia habari hizo muda huu, hebu tusubiri pakuche jamani"
Dada alikuwa king'ang'anizi na kutaka kujua ukweli,
"Tuambie tu Sam ukweli, usitufiche kitu tunahitaji kujua na sisi"
Sam bado aliendelea na msimamo wake wa kutokuzungumzia chochote kwa muda huo
"Jamani usiku una mambo mengi sana, habari za kushtusha na kutisha kama hizo si vizuri kuzizungumzia kwa usiku kama huu. Tungoje pakikucha jamani"
Mama alimuelewa Sam kwa haraka sana ila bado alikuwa na maswali mengi sana dhidi ya yote yale
"Nimekuelewa sana ila bado nina maswali mengi sana ya kuhoji kuhusu hayo myasemayo maana hapo ndio pagumu kwangu."
Ikabidi tubadilishe mada kwa muda ule maana ni kweli usiku huwa na mambo sana kushinda tunavyotegemea au kutarajia.

Dada akauliza kuhusu nyama za jikoni,
"Jamani na zile nyama jikoni kaandaa nani maana zinanoga hizo balaa"
Nikamuuliza kwa mshangao,
"Inamaana umekula dada?"
"Ndio nimekula kwani kuna tatizo gani?"
Mama nae akajibu,
"Hata mimi nimekula, natumaini wewe ndio uliziandaa Sabrina kabla ya kwenda kuoga"
Niliwaangalia kwa zamu bila kuelewa wanawaza nini na akili zao zikoje maana wanakubaliana na mambo ya kijinga kama vile, niandae nyama mimi nimeitoa wapi? Kweli mama na dada bado wamevurugwa sana hawa.
Nikawajibu sasa,
"Ile nyama jikoni sijaandaa mimi ila ameandaa aliyeandaa pilau ya mchana"
Sam akashtuka sana nadhani alishaelewa kila kitu, kisha akainuka na kusema
"Jamani naomba mniruhusu niende maana sitaweza tena kukaa hapa"
Dada akamzuia Sam,
"Tafadhari Sam usiondoke"
"Hii nyumba yenu ina mauzauza sana nadhani kama yale tuliyokutana nayo Kigoma. Kwakweli sitaweza kulala hapa, bora nirudi kwetu"
Ikabidi nianze kumbembeleza Sam ili akubali kubaki na sisi, ila alikubali na kufanya niridhike na kufurahi.
Dada Penina akauliza tena,
"Kwani chakula cha mchana alipika nani?"
Nikaamua kuwajibu tena kwa kifupi
"Jamani hayo maswali yaishe, tuulizane kesho maana yasije yakatokea mengine ya kutokea tena muda huu"
Wakakubaliana na mimi, ila Sam hakuweza kula zile nyama na wala mimi sikuweza kula zile nyama.

Muda wa kulala ulipofika, tukajadiliana namna ya kulala ambapo dada akasema kuwa anaona vyema kama mimi nitaenda kulala kwa mama kisha Sam akalale chumbani kwangu chumba ambacho hata mimi mwenyewe mwenye chumba tangia nifike sijaingia ndani yake je huyo Sam ataweza kulala?
Nikaamua kupinga hilo swala kwani niliona kuwa si swala jema. Dada akauliza,
"Sasa unadhani Sam akalale wapi?"
"Bora alale hapa hapa sebleni"
"Kwani chumbani kwako kuna nini? Mwache Sam mwenyewe aamue pa kulala"
Sam nae akakubaliana na mimi kuwa bora alale pale pale sebleni na akasema kuwa hata hivyo hana usingizi kwahiyo kukaa kwake pale sebleni ni vyema sana.
Mama akaniuliza kuwa na mimi nitaenda kulala wapi maana chumbani kwangu napakataa.
"Mimi nitalala hapa sebleni au chumbani kwako mama ila sitaki kwenda kulala chumbani kwangu"
Dada akakumbusha kuhusu kile chakula cha mchana,
"Mnakumbuka kuwa hata ile mchana tulipouliza chakula kapika nani sauti ikatoka chumbani kwa Sabrina? Ndiomana Sabrina anakikataa chumba chake"
Hapo nikatambua kwamba kumbe wanakumbuka ila wanajigelesha ili wasiogope zaidi ila hatukuhoji sana zaidi ya kuangaliana tu.
Dada akaona kamavile tunambabaisha tu kwahiyo akaenda zake chumbani kwake kulala kama kawaida, pale sebleni nikabaki mimi, mama na Sam.
Nilikuwa namuhurumia Sam kulala mwenyewe pale sebleni ila kwavile mama alinitaka tukalale kwahiyo sikuwa na la kufanya zaidi ya kwenda kulala tu na kumuacha Sam pale sebleni huku nikijua wazi Sam anaogopa sema anajikaza kiume tu kulala pale.
Tulipofika chumbani haukuchukua muda mrefu usingizi ukanichukua tayari.

Niliposhtuka asubuhi nikashangaa kujikuta nimelala kwenye kibaraza nje ya nyumba, niliangalia pande zote na kujiona kweli nipo nje.
Nikainuka kwa uoga ili nikimbilie mlango wa mbele wa nyumba yetu.
Nilipofika pembezoni mwa nyumba nikamkuta dada Penina akiwa amelala hoi kwenye mchanga, ikabidi nianze kumtingisha na kumuamsha kwakweli alishtuka sana na kutoa mimacho kama mjusi kabanwa na mlango kisha akaniuliza mimi
"Mbona nimelala nje?"
"Hata mimi nimejikuta nje sielewi chochote dada"
Ikabidi ainuke tu pale chini na kujishangaa mara mbili mbili bila ya kupata jibu la maana.
Tukaingia ndani na kumkuta Sam akiwa amelala hoi pale kwenye kochi, ikanibidi nimuamshe naye alikurupuka tu huku akijiuliza mwenyewe
"Sijui hata nimelala saa ngapi?"
Dada akamjibu,
"Kheri yako wewe usiyejua umelala saa ngapi kuliko wenzio tuliojikuta tumelala nje"
"Mmelala nje!!"
"Ndio, mi nimejikuta kwenye kibaraza na dada alikuwa pembeni kwenye michanga huko"
Hapo hapo tukakumbuka kuwa mama nae yuko wapi? Ikabidi dada aende kumuangalia chumbani kwake, kisha akarudi na sura ya upole sana
"Mama hayupo chumbani kwake"
"Yuko wapi sasa?"
"Sijui"
Tukaamua kwenda kumuangalia nje kote kuwa labda na yeye amelala nje lakini hakuwepo, tukajikuta tukinyong'onyea sana na kujiuliza kuwa pengine mama nae aliamka na kwenda kututafuta maana pengine alitukosa vyumbani.
Dada akasema,
"Kama ni hivyo lazima angemuuliza Sam hapa, asingeweza kujiondokea tu kamavile mtu asiyejielewa"
Hatukuwa na la kufanya, tukaamua kurudi tu ndani.

Tulipofika sebleni tukamkva mama amekaa kwenye kochi tena huku akisikitika sana, tukamsalimia na kumuuliza kulikoni yeye kuwa vile.
"Yani hamuwezi amini, eti nimejikuta nimelala chooni jamani"
Tukampa pole sana mama na kumsimulia ya kwetu kuwa na sisi tumejikuta tumelala nje, yani kati yetu aliyesalimika ni Sam peke yake.
Mama hakutaka kupoteza muda, akataka nimueleze kuhusu Carlos kwani wakati amelala huko chooni amepatwa na ndoto mbaya sana.
Nami sikupenda yale mambo yaendelee kutendeka hivyo basi nikamwambia mama awaite wale ndugu bandia wa Carlos ili niwaeleze wote kwa pamoja kwani sikutaka kusema nusu nusu ili kuepuka yale matatizo yanayojitokeza bila sababu za msingi.
Mama akawapigia simu nao wakasema kuwa watakuja.

Mchana wa siku hiyo, wale ndugu bandia wa Carlos waliwasili nyumbani kwetu kisha tukaweka nao kikao kwenye sebule yetu.
Nikawaeleza kuwa Carlos alishakufa miaka mitano iliyopita na kufanya wote wastaajabu na kushangaa.
Yule mama bandia wa Carlos akauliza,
"Sasa yule Carlos aliyekuwa anakuja nyumbani kwetu ni nani?"
Hapo hapo ikasikika sauti,
"Ni mimi hapa"
Kisha akatoka yule jini toka chumbani kwangu na kufanya watu wote waogope.

Itaendelea kesho....!!!
Kwere
 
SEHEMU YA 75


Baada ya harusi kama kawaida wapambe wakasema
twende ufukweni kwaajili ya kupiga picha za
kupendeza na kuvutia, nikakumbuka mambo yale
yaliyowahi kunitokea nikaogopa sana kwenda
ufukweni ila wapambe walikazana na kufanya nitokwe
na machozi.
Ila kabla hatujaondoka, wifi Joy alianguka na kuanza
kutapatapa pale chini.
Nilishtushwa sana na ile hali ya wifi huku nikiwaza
kuwa labda mauzauza yamejirudia kutokana na
kwenda kule kwenye nyumba yetu tuliyohama na
kuzikuta zile pesa, hofu ikanijaa sana na kujikuta
machozi yakinikauka na kuanza kujilaumu kwa kile
ambacho nilimshawishi Sam kuwa tukifanye.
Harakati za kumbeba wifi ilikumuwaisha hospitali
zilifanyika, nilikuwa nimeduwaa tu hata sikutaka tena
kwenda ukumbini ila Sam akanilaumu sana
"Yote haya umeyataka mwenyewe Sabrina, ulijua
wazi wifi yako ni mjamzito tena mimba kubwa kabisa
ukamshawishi hadi awe msimamizi wako umeona
sasa faida ya ubishi eeh!! Ilimradi tumeshafunga ndoa basi haina shida, tufanye mengine tu"
Ni kweli nilikatazwa na wengi kuhusu hili ila mimi nikawa mbishi na kufanya yote haya yanitokee kwasababu ya ubishi, ila mama akashauri kuwa tuendelee kusherekea kwakuwa wifi alianguka kutokana na matatizo ya uzazi.
Sikuwa na raha hadi pale tulipoletewa habari kuwa wifi amejifungua salama ingawa amejifungua kabla ya miezi lakini alijifungua salama kwahiyo ilibidi akae hospitali kuangalia afya ya mtoto aliyehitajiwa uangalizi wa makini sana, watoto wa hivi mara nyingi huitwa njiti.

Baada ya wiki kadhaa aliruhusiwa kurudi nyumbani, kisha mimi na Sam tukaenda kumtembelea. Wifi alifurahi sana, mtoto wake nae alikuwa amechangamka tayari, alikuwa ni mtoto wa kike. Wifi akasema,
"Kwavile wewe Sabrina ndiye uliyefanya huyu mtoto azaliwe kabla ya siku zake basi namuita Sabrina"
Nikacheka sana na kufurahi kupata wajina, Sam akamwambia wifi kwa kumtania
"Shauri yako, atakuwa na majanga kama ya Sabrina mwenzie"
Wifi akacheka sana kuhusu alichokisema Sam na kusema
"Mmh! Atakuwa na majanga tena mmh ila yasiwe kama ya Sabrina jamani"
"Ndio hayatakuwa kama ya Sabrina ila lazima atakuwa na majanga sababu mwenye jina lake ana majanga sana"
Dada Penina nae alifika kumuona wifi Joy na kutukuta na ile mada yetu tuliyokuwa tukiizungumzia kisha akadakia na kusema
"Ila ndio atapendwa hadi na watoto wadogo maana mwenzie kapenda hadi na majini na...."
Nikamkatisha na kuguna
"Mmmh dada!!"
"Mmh kitu gani kwani uongo? Hebu nipeni Sabrina mdogo nimbebe mie"
Akamchukua mtoto na kumpakata kwa furaha na tangia hapo huyo mtoto akaitwa Sabrina mdogo.

Maisha yakaendelea huku mawazo ya ile pesa kwenye kabati yakinisumbua kwani sikuelewa kama zile pesa ni za kweli au ni pesa mauzauza, sikuelewa kama ni yule jini ameziweka au ni vipi kwahiyo nikajikuta nikiwa na mawazo muda wote na huku nikiwa na hamu ya kujua kwanini tulizikuta siku ile tuliyoenda.
Nikatamani sana kwenda kuzichukua na kuziangalia vizuri, nikajipanga kufunga safari kimya kimya kwa kuhofia kuwa Sam asijui.

Siku hiyo nikajiandaa bila hata ya kumuaga Sam na kuondoka hadi pale tulipokuwa tunaishi zamani.
Njiani nikakutana na dada Zuhura ambapo alifurahi kuniona na kuniuliza
"Unaenda wapi Sabrina?"
"Nafika kwenye nyumba yetu mara moja"
"Unaenda kufanya nini?"
Nikawaza moyoni kuwa kama nikimwambia kuhusu pesa basi lazima atataka twende wote ili tugawane, ikabidi nimwambie vitu vingine kwa kumgelesha tu. Kisha akaniuliza,
"Unadhani ni salama wewe kwenda mwenyewe?"
"Ndio dada hakuna tatizo"
"Mmh Sabrina! Ila kama utahitaji msaada usisite kunipigia simu na kunipa taarifa, sawa?"
"Sawa dada, ila kuna tatizo kwani?"
"Sijui, ila nisingependa kukushauri kwenda peke yako"
"Usijali dada, nitakuwa salama"
"Kumbuka ibada Sabrina"
Kisha akaondoka, nikaona kama anataka kuniharibia siku na mipango yangu tu kwahiyo nikashukuru kuondoka kwake kisha mimi nikaendelea na safari yangu huku moyo wangu ukiniambia kuwa nimejawa na tamaa, na kweli nimejawa na tamaa kwani yote haya ni sababu ya tamaa iliyonizunguka na ndiomana najikuta nikifanya haya ninayoyafanya, amakweli binadamu hatujakamilika kila mmoja na kasoro zake sema tu tumezidiana.

Nilipo ukaribia mlango wetu na kutaka kufungua, mkono ukasita ila nikajipa moyo na kufungua mlango ule kisha nikaurudishia na kuingia ndani ambako nilikukuta kama ambavyo tulikukuta wakati nilipokuja na Sam.
Moja kwa moja nikataka kwenda chumbani kwa mama ila roho ikasita, nikatazama mezani na kuona kitu kilichoyavuta macho yangu.
Nikasogea na kukiangalia, ilikuwa ni pete yani pete ile ile niliyoveshwa ya uchumba na yule jini.
Nikashtuka sana, nikaishika na kuiangalia vizuri nayo ilikuwa iking'aa vile vile kama ambavyo ilikuwa iking'aa mwanzoni.
Nikaichukua na kuishika mkononi kisha nikaenda chumbani kwa mama kwenye kabati moja kwa moja na kutoa ile droo nikazikuta zile pesa zikiwa vile vile, nikatabasamu kwani najua ile ni mali yangu na kufanya niwaze vitu mbali mbali kichwani kuwa ingawa nilipata mateso kumbe na faida ipo. Nikachukua zile pesa na kujaza kwenye pochi yangu kisha nikajisemea kuwa,
"Hii ni faida yangu, hizi pesa ni zangu na hii pete nitauza ili nipate pesa zaidi"
Macho yangu yakavutika kuwa nitazame upande mwingine wa kile chumba, nikaviona vile viatu vyangu vya maajabu hapo nikaogopa sasa na kutetemeka kwani vile viatu hata kumbukumbu kuwa mara ya mwisho nilivivulia wapi na ilikuwaje sikuwa nayo ila sasa ndio vipo mbele yangu, je vimetokea wapi? Nani kavileta? Maana kipindi kile Carlos alisingiziwa kuyatenda yote yale kumbe ni yule jini aliyekuwa akipitia kwa Carlos, swali kwangu je yule jini bado ananifatilia? Na kama ananifatilia ni kwa misingi gani?
Sauti ikanijia,
"Uza na hivyo uongeze idadi ya pesa zako"
Nikaogopa sana na kuamua kuinuka ili nitoke nje maana nilijua ni chumba changu tu chenye majanga kumbe hadi chumba cha mama.

Nilitoka hadi sebleni napo nikashtuka pia, kwani nilikuta lile gauni la harusi yangu na jini likiwa limewekwa kwenye kiti.
Kiukweli lile gauni lilikuwa zuri sana ila kutokana na mambo ambayo yalinitokea lile gauni lilikuwa baya machoni mwangu kama vile viatu vya maajabu ambavyo navichukia ingawa ni viatu vizuri sana tena vya gharama.
Nikaliangalia lile gauni mara mbili mbili huku nikiogopa kulisogelea, ile pete mkononi nilihisi kama inatingishika hivyo nikaamua kuirudisha mezani pale pale nilipoichukua ili niondoke nikiwa huru.
Nikakuta ujumbe mezani,
"Uliolewa na jini bila ya kutarajia ila sasa jiandae kuolewa tena na jini kwa kutarajia maana unavitu vyake bado na nia yake kwako unaijua, utaolewa na na jini kwa kutarajia sasa"
Nikatetemeka sana na kujua wazi nimejitakia mwenyewe haya mambo na sasa sina pa kukimbilia kwamaana nipo mwenyewe ingawa nishaolewa na mtu mwingine tayari.
Nikajisemea mwenyewe, ila mimi nimeshaolewa tayari!
Sauti ikasikika,
"Hata mwanzo ulishaolewa tayari ila ukafanya hila na kuolewa na mwingine hata sasa itakuwa hivyo, unanikataaje mimi wakati vitu vyangu bado unavipenda?"
Nikaangusha ule mkoba wenye hela chini na kujihisi kama naanza kuwehuka vile.
Nikatazama tena mezani, nikaona ile simu yangu ya majanga hapa ndipo nilipotambua kuwa kweli nafatiliwa tena na yule jini, nikaanza kuilaumu tamaa ya moyo wangu na kuanza kujisemea
"Mungu nisaidie"
Huku nikiwa na mawazo kwani sikuweza kusogea mbele wala kurudi nyuma, nikasimama pale pale kama mlingoti huku nikiangalia yale mauzauza ya mbele yangu.

Wakati nikishangaa yale mambo, nikahisi kushikwa bega na mtu. Hapo hapo miguu ikakosa nguvu na kujikuta nikianguka chini na kupoteza fahamu.
Akaja yule mbaba wa kutaka kunisaidia na kuniambia
"Kwanini kuiruhusu tamaa ikutawale? Kwanini utake kuharibu maisha yako kwa vitu vidogo? Una mume, una kazi pia, inakupatia kipato, ridhika na ulicho nacho. Fanya kazi kwa bidii kujiongezea kipato, hizi njia za pembeni zitakuangamiza Sabrina. Zitakuponza, kutenda kosa si kosa bali kurudia kosa, ulishayapitia yote haya kwahiyo usifanye tamaa yako kukurudisha tena ulikopita. Yote yaliyokupata mwanzo hukuyatarajia, ila hili ambalo lingekupata leo ungeritarajia sababu umejitakia mwenyewe. Tulia binti utengeneze maisha yako, haya uyatakayo sasa yatakuponza. Mshukuru yule aliyekuona ukienda mwenyewe kwenye mdomo wa mamba"
Nikashtuka huku jasho likinitoka sana, nikamuona Sam pembeni yangu na dada Zuhura akiwa pembeni na mzee mwingine ambaye sikumfahamu kwa muda huo ambapo walinisaidia na kufanya nikae vizuri huku nikiwatazama, walinipa pole kwa yote yaliyonitokea.

Nikawasimulia kila kitu nilichokikuta kwenye ile nyumba yetu, dada Zuhura akaniambia
"Nilijua wazi kama ile nyumba bado haijatengemaa ndiomana nikakukataza Sabrina, nazijua tabia za majini wanamtindo wa kumtamanisha mtu ili aingie katika vishawishi ndiomana nikakuuliza vizuri unachoenda kufanya ila wewe hukutaka kuniambia ukweli. Ile nyumba yenu mlishamkaribisha jini ndani kwamaana kwamba alishaitawala, mlichotakiwa kufanya ni kusema vitu vyake vyote ili vichomwe moto na nyumba iwe huru"
Nikakodoa macho tu kwani tamaa ndiyo imeniponza, ikabidi nimuulize Sam kuwa alijuaje kama nipo kule.
"Nilipokukosa nikaenda kwenu kukuulizia ila hukuwepo, nikapatwa na hofu kuwa umeenda pale kwenye nyumba ndiomana hujaaga kwani unajua wazi ningekukatalia, wakati nakuja nikakutana na dada hapa ambapo akaniambia ni kweli umekuja mitaa ya huku basi ndio tukaongozana kuja kukufata. Yani tunaingia tu na wewe unaanguka chini, kwakweli Sabrina wewe una mambo ya ajabu na hata hujihurumii. Ndio tumekubeba hadi kwa Shekhe hapa amekusomea hadi umeamka na kuwa katika hali ya kawaida"
Kwakweli nina majanga ila haya ya sasa yalikuwa ya kujitakia kweli.
Dada Zuhura akanishauri mambo mbali mbali pale, kisha nikarudi nae hadi kwa mama ambako akawashauri cha kufanya na nyumba yetu pia.

Baada ya wiki kadhaa, tulichoma vyote vilivyotupa mashaka hadi zile pesa kisha tukaibomoa ile nyumba na kuuza kile kiwanja, kisha kununua kiwanja kingine kama kumbukumbu ya kiwanja tulichokiuza.

Nilipata ujauzito na kujifungua mtoto wa kike, nikamuita Zuhura kama kumbukumbu ya huyu dada katika maisha yangu.
Dada yangu Penina pia alipata mchumba na kuolewa kisha akapata ujauzito na kujifungua mtoto wa kike aliyemuita Salome.
Tulifanya hivi kutokana na mambo ambayo hawa watu walitutendea ingawa tuliwanena vibaya na kuwaona ni watu wabaya ila wao bado walitupenda na kuendelea kutufundisha mambo ya Mungu.
Wifi yangu Joy nae alijifungua watoto wengine ambao walikuwa mapacha wa kiume na kuwaita mmoja Deo na wa mwisho Sam, kwahiyo akawa na watoto wanne, James, Sabrina, Deo na Sam huku Sabrina akiwa mtoto wake pekee wa kike.
Mume wangu Sam akanishauri kuandika haya niliyoyaandika.

~~~~MWISHO~~~~
Nani tunausoma kwa pamoja hii story 2024
 
Back
Top Bottom