Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 62
Yule mama hakutuelewa kabisa tulichokuwa
tunamueleza, kisha akainuka na kuleta picha za
Carlos kuwa pengine tunamfananisha, mimi
nikaziangalia na kumjibu
"Ndio Carlos huyu huyu tunayemuongelea"
Gafla yule mama akaanza kulia tena alilia kwa
kuomboleza.
Yule mama alilia sana hadi kutufanya tuanze kuogopa kwani hatukujua analia kitu gani, mtoto wake wa kike akaja pale karibu kumbembeleza na kumuuliza kuwa kuna tatizo gani huku akituhisi kuwa sisi kuna kitu kibaya tumemfanyia mama yake.
Yule mdada nilipomuangalia vizuri ndio yule aliyenishangaa siku niliyoenda kimaajabu pia ndio yeye ambaye tulimuuliza na Sam kisha kuanza kupiga makelele ya uchawi na kuita watu watupige.
Ikabidi nijikaushe sasa na kuwa makini sana ili asije akanigundua tena na kusababisha balaa lingine.
Yule mama aliendelea kulia na kufanya yule dada atufokee kwa maswali yasiyo jibika
"Mmemfanyaje mama yangu nyie?"
"Hatujamfanya kitu"
"Kuna kitu mmemfanya, niambieni upesi sana"
Tukabaki kuangaliana tu maana hakuna tulichomfanya kwakweli ila na sisi pia tulikuwa tunamshangaa kwanini analia kiasi kile.
Yule dada nae akazidi kutukolomea, mwisho tukamweleza kuwa mama yake tulikuwa tunamuuliza kuhusu mwanae Carlos. Yule dada akaguna na kusema,
"Ndiomana ameanza kulia, basi mwacheni hadi machungu yake yatakapopungua ndipo mwendelee kuzungumza nae, maana mmemkumbusha mambo ya nyuma sana na yanayomuumiza kila siku."
Ikabidi mimi na Sam tutulie huku tukimngoja yule mama awe katika hali ya kawaida na tupate kumuuliza ya kwetu tunayotaka kuyajua.
Tukatulia kabisa huku tukimsikilizia yule mama, ambaye aliinuka na kuingia ndani huku ile albamu yenye picha za Carlos akiiacha pale pale.
Nikaichukua na kuendelea kuangalia, kulikuwa na picha nyingi sana za Carlos akiwa shule, na marafiki zake, nyingine akiwa nyumbani na kwakweli zilivutia sana kuziangalia hata nikashindwa kuelewa kuwa kwanini ananifanyia mambo ya kishetani kiasi kile na kwanini akanitambulisha familia yake ya uongo wakati alikuwa na familia nzuri tu? Na kwanini huwa anabadilika badilika na kuwa shetani? Sikuwa na jibu ila najua wazi kuwa huyu mama yake mzazi lazima atakuwa anajua kuhusu mtoto wake na kwanini amefanya yote yale sababu yeye ndio mzazi wake, kwahiyo tukatulia tukimngoja pale atakapotulia atuambie ukweli kuhusu mtoto wake.
Muda ulienda sana bila ya yule mmama kutoka ndani kwake, na sisi tulichoka kungoja pale nje maana hata njaa nayo ilianza kusumbua kwenye matumbo yetu.
Tukaamua kumuita yule dada na kumuuliza mahali pa kujipatia chakula, nikashangaa akiniangalia kwa umakini sana kisha akauliza
"Kuna mahali popote mimi na wewe tumewahi kukutana? Naona kama sura yako si ngeni machoni pangu"
Nikashtuka na kumkatalia kuwa hatujawahi kuonana itakuwa ananifananisha tu, akataka kutuelekeza pa kwenda kununulia chakula ila mama yake akatoka ndani na kumuuliza kuwa anatuelekeza wapi, naye akamjibu.
Yule mama akaturudisha wote na kusema,
"Nyie ni wageni wangu hivyo basi mtakula hapa hapa kwangu, watu wa huku hatuna roho mbaya kwahiyo karibuni"
Tukajigelesha ila hakutaka tuondoke badala yake akamuita mtoto wake mwingine ambapo akamtuma akatuletee maziwa mtindi.
Alipotuletea akatukaribisha na kutuambia kuwa tupooze njaa wakati chakula kingine kikiwa jikoni.
Kisha akakaa na kuendelea na mazungumzo na sisi huku akituuliza maswali kwa umakini sana.
Na mimi nilimuuliza huyu mama maswali kwa umakini ila kuna kipindi ilibidi niwe kimya huku nikimuangalia anavyougua kwa maumivu ya yale maswali.
Alianza kwa kuniambia,
"Hebu nielezeni kwa kifupi maana mwanzoni sikuwaelewa, umesema kuwa Carlos alikuoa?"
"Ndio Carlos alinioa"
"Mlifunga ndoa ya aina gani na mlifungia wapi?"
"Kwakweli hapo sitaweza kukueleza mama yangu maana hata mimi mwenyewe sielewi ilikuwa ni ndoa ya aina gani"
Nikamueleza pia jinsi Carlos alivyotupeleka kwa wazazi wake bandia na jinsi hao wazazi wake walivyokuja kujieleza kuwa ni bandia baada ya kuwabana sana.
Yule mama alionekana kusikitishwa sana na kusema,
"Hivi haya mambo mnayoniambia ni kweli au naota? Mbona mmeniletea uchuro jamani!"
Ikabidi nimueleze pia majina ya wale wazazi bandia wa Carlos naye akakubali kuwa ni kweli hao watu anawafahamu ila walihama miaka mingi iliyopita
"Sikia niwaambie, kinachonishangaza hapa sio hao wazazi bandia bali huyo Carlos mnayemuongelea. Nadhani hamjielewi kuwa mnamuongelea mtu wa aina gani, au mlikuwa mnamdai?"
Huku akijifuta tena machozi, ikabidi nimwambie kwa utaratibu unaotakiwa
"Hapana mama hatumdai ila hii ni kwaajili ya ukombozi wangu, Carlos amekuwa mtu wa ajabu sana kwangu, huwa anakuja na kupotea halafu mara nyingine anabadilika. Kilichonileta huku ni kuwa nahitaji kuwa huru, nahitaji niondokane na mauzauza yanayonisumbua. Tafadhali mama naomba uniambie ukweli kuhusu Carlos ila na mimi niweze kuwa huru"
Yule mama alionekana kunionea huruma pia kwa yale maelezo yangu, akaendelea kunieleza kwa mshangao sana
"Mnajua kinachonishangaza juu ya maelezo yenu ni kuwa, unamuongelea Carlos kuwa alikuoa wakati Carlos hajawahi kuoa halafu unasema kuwa huwa unaonana nae mara kwa mara halafu anakuwa mtu wa ajabu. Kwa kifupi ni kuwa, Carlos mwanangu alikufa miaka mitano iliyopita"
Kwakweli tulishtuka sana kwani hatukutegemea jibu la aina hii kabisa, nilihisi kama naota ila ndio ukweli.
Nikajikuta nikimuuliza yule mama mara mbili mbili,
"Carlos alikufa? Tena miaka mitano iliyopita?"
"Ndio, yani hata huko kaburini basi kumebaki mifupa ya mwanangu tu. Roho inaniuma sana maana mwanangu nilimpenda kupita maelezo na sitaweza kumsahau hata kesho"
Yule mama akainama akijifuta machozi kwakweli hata mimi machozi yakanitoka, nikaanza kukumbuka jinsi nilivyokutana na Carlos na jinsi alivyokuwa akinisaidia mwanzoni kabla mauzauza hayajawa makubwa sana. Kwakweli Carlos alikuwa rafiki yangu mzuri sana yani nilijihisi kama vile ndio naambiwa kuwa Carlos amekufa leo kwani sikutaka kuamini kuwa kwa kipindi chote kile nilikuwa naishi na marehemu yani nakula nae kuongea nae na kufanya nae mambo mengi, nilijikuta nikiuliza kuwa
"Kwanini alikufa?"
Yule mama alionyesha huruma sana na kuanza kutuambia historia ya mtoto wake Carlos.
"Carlos alikuwa mwanangu wa kwanza, ndiye aliyefungulia uzao wangu kwakweli nilimpenda sana na nilifanya kila kitu ili kuona kuwa mwanangu anaendelea kwani sikupenda aje aishi maisha ambayo mimi nimeishi.
Nilijua Carlos ndio atakayekuja kuikomboa familia yangu na na kuitoa katika janga la shida na umaskini ila sikujua Mungu alipanga nini, sikujua binadamu wengine wanawaza nini juu yangu.
Nilimsomesha Carlos kwa kila hali ili kutimiza ndoto yake kwani yeye alipenda kuwa daktari, na kweli alisoma chuo cha udaktari Muhimbili hadi akapata degree ya udaktari na akatimiza ndoto yake ya kuwa daktari. Mwanangu akaajiriwa na alikuwa na mshahara mzuri sana, alikuja huku kijijini kutusalimia na kuonyesha alichopata. Kwakweli tulifurahi sana na kuamua kufanya sherehe kama familia, yani huwezi amini ule usiku baada ya sherehe ndio ulikuwa usiku wa mwisho kwa Carlos (yule mama akainama na kulia kidogo kwa kwikwi, kisha akaendelea kutueleza)
Kulipokucha, Carlos hakuamka kabisa ikabidi twende kumuangalia. Nikamuona mwanangu akiwa amekauka kabisa kama mti, alikakamaa na hakuweza kupumua tena. Mwili wake wote ulikuwa wa baridi, tulimpeleka hospitali na akaonekana kuwa amekufa na hapo ukawa mwisho wa mwanangu Carlos na ndoto zake za kutusaidia. Hadi leo siwezi kusahau kifo cha mwanangu mpendwa, huwa naumia sana. Natamani awe karibu na mimi anifariji kwa maumivu haya ya moyo wangu"
Yule mama akalia sana, ikabidi mimi na Sam tuwe na kazi ya kumbembeleza. Kwakweli hata mimi mwenyewe nikaumia sana kamavile sijawahi kumchukia huyo Carlos katika maisha yangu.
Moyo wangu ukaniambia kuwa si Carlos wa kumchukia bali ni yule jini aliyekuwa akicheza ndani ya mwili wa Carlos.
Yule mama akatuambia kuwa ataenda kutuonyesha kaburi la Carlos na sisi tukakubaliana nae kwa hilo.
Nilijiangalia mara mbili mbili kama kweli mimi ni binadamu wa kawaida, yani kukaa na marehemu na kukaa na jini ni kitu cha ajabu sana kwakweli sikujiona kuwa kawaida kabisa, nikajihisi nipo tofauti na watu wengine kabisa.
Nilikaa karibu na yule mama huku akiongea kwa uchungu kuwa haelewi huyo ambaye alikuwa na mimi ni nani wakati mtoto wake alishakufa miaka ya nyuma iliyopita.
"Nashindwa kuelewa kwakweli, labda mwanangu amefanywa kuwa msukule. Roho inaniuma sana"
Tukampooza huyu mama ili asizidi kuumia maana ni kweli inauma kusikia kuwa mwanao aliyekufa miaka mingi iliyopita akionekana kwa watu wengine na kuendelea na maisha kama kawaida.
Tulimpooza pale na kujaribu kuongea mambo tofauti tofauti, ndio hapa yule mtoto wake mkubwa wa kike alipokuja tena kisha yule mama akamuelezea yote tuliyomwambia kuhusu Carlos ambapo na yeye alihudhunika sana kwa ile taarifa na kuwalaani vikali watu wachawi na kusema kuwa anawachukia sana watu wachawi.
"Kwakweli toka mwanzo nilijua tu kama kaka yangu hajafa ila amefanywa msukule, yote haya ni kuonyesha kuwa kuna mahali amewekwa ambapo sisi kama familia hatupajui. Nawachukia sana wachawi, yani yule mchawi wa juzi tungempata hakika tungemkatakata kama nyama buchani"
Mama yake akamuuliza
"Kwani juzi walikamata mchawi tena?"
"Hapana, ila ni yule dada wa kipindi kile aliyetufanyia mbwembwe za kupaa hapa ndio alikuja juzi halafu akaniita mimi, loh nilipomuona tu nilikimbilia watu ili twende tukammalize maana yule atakuwa ni mchawi wa kuzimu kabisa"
Nikahema kwa nguvu huku moyo ukinienda mbio kwani najua kwa vyovyote vile kama wakinijua ni mimi basi nipo kwenye hatari kubwa sana kwa hili.
Nikatamani kuaga na kuondoka lile eneo lakini sikufikiria kama nimeshamaliza kazi niliyopewa na yule mtu wa ajabu ili niweze kuwa huru kabisa.
Yule dada aliendelea kuzungumza huku akiniangalia kwa makini sana nadhani alikuwa anahisia kuwa ni mimi sema hakuwa na uhakika sababu ya zile nywele za bandia na miwani ukizingatia sio mtu anayenifahamu.
Muda kidogo chakula kikaletwa na tukatakiwa wote tukae kwa pamoja na kula kile chakula, walikuwa wameandaa wali kwa maharage kisha tukakaa na kuanza kula.
Wakati tunakula nikahisi kamavile kuna mtu zaidi yetu anayekula pale, kumbe mama Amina nae alihisi hicho kitu na kusema kuwa anahisi kuna kitu tofauti pale tunapokula ila yule mama alikuwa ni mwanamaombi na kuanza kukemea pale pale.
Nikahisi kichwa changu kikivurugika, nilihisi kuchanganyikiwa hadi nikaacha kula na kuanza kukimbia.
Sam akanikimbiza kwa nyuma na kunishika, hapo akafanya nishtuke na akili yangu kurudi. Sam akaniuliza kwa hasira
"Unafanya nini sasa Sabrina?"
"Sijui Sam"
"Acha mambo ya kijinga, tutaaibika hapa kumbuka tupo kwa watu"
Baada ya muda kidogo yule mama nae akanifata na kuniuliza
"Una matatizo gani binti?"
"Hapana, sina matatizo"
"Sasa mbona ulikuwa unakimbia wakati wa maombi? Au una majini wewe?"
Aliposema majini nikajikuta nikitetemeka kwa muda, kisha yule mama akanishika mkono na kunirudisha tena nyumbani kwake ila sikuwa na hamu ya kuendelea na chakula tena maana nilianza kujihisi vibaya.
Yule mama akatubembeleza tule ili tuweze kwenda kulitembelea kaburi la Carlos.
Niliwaacha waendelee kula huku mimi nikiwa na mawazo yangu yanayonisumbua.
Baada ya kumaliza kula wakaanza kujiandaa kwaajili ya kwenda kuona kaburi la Carlos, nikajipa moyo na kujitia nguvu kwani sikuwa tayari kuamini kuwa kwa muda wote niliokuwa na Carlos nilikuwa naishi na marehemu.
Walipomaliza kujiandaa, tukaanza safari ya kwenda huko makaburini.
Tulipokuwa njiani nilianza kujihisi kuwa nainuliwa juu taratibu.
Uwoga ukanijaa na kuhisi moja kwa moja kuwa watajua tena mimi mchawi.
Wakati nikihangaika ili nishushwe nikajishtukia nikitupwa chini, hakuna aliyeona nikiinuliwa ila wote waliona nilipoanguka chini kwani nilitupwa vibaya sana hadi nikahisi kiuno kinakatika halafu wigi langu nalo likanivuka kabisa.
Wote waliniangalia kwa mshangao, mara nikamsikia yule Amina akisema
"Kumbe ni wewe!"
Nikaanza kuogopa na kutetemeka sana.
Yule dada akapiga yowe la ajabu na muda huo huo watu wakajaa eneo lile.
Itaendelea kesho.
Yule mama hakutuelewa kabisa tulichokuwa
tunamueleza, kisha akainuka na kuleta picha za
Carlos kuwa pengine tunamfananisha, mimi
nikaziangalia na kumjibu
"Ndio Carlos huyu huyu tunayemuongelea"
Gafla yule mama akaanza kulia tena alilia kwa
kuomboleza.
Yule mama alilia sana hadi kutufanya tuanze kuogopa kwani hatukujua analia kitu gani, mtoto wake wa kike akaja pale karibu kumbembeleza na kumuuliza kuwa kuna tatizo gani huku akituhisi kuwa sisi kuna kitu kibaya tumemfanyia mama yake.
Yule mdada nilipomuangalia vizuri ndio yule aliyenishangaa siku niliyoenda kimaajabu pia ndio yeye ambaye tulimuuliza na Sam kisha kuanza kupiga makelele ya uchawi na kuita watu watupige.
Ikabidi nijikaushe sasa na kuwa makini sana ili asije akanigundua tena na kusababisha balaa lingine.
Yule mama aliendelea kulia na kufanya yule dada atufokee kwa maswali yasiyo jibika
"Mmemfanyaje mama yangu nyie?"
"Hatujamfanya kitu"
"Kuna kitu mmemfanya, niambieni upesi sana"
Tukabaki kuangaliana tu maana hakuna tulichomfanya kwakweli ila na sisi pia tulikuwa tunamshangaa kwanini analia kiasi kile.
Yule dada nae akazidi kutukolomea, mwisho tukamweleza kuwa mama yake tulikuwa tunamuuliza kuhusu mwanae Carlos. Yule dada akaguna na kusema,
"Ndiomana ameanza kulia, basi mwacheni hadi machungu yake yatakapopungua ndipo mwendelee kuzungumza nae, maana mmemkumbusha mambo ya nyuma sana na yanayomuumiza kila siku."
Ikabidi mimi na Sam tutulie huku tukimngoja yule mama awe katika hali ya kawaida na tupate kumuuliza ya kwetu tunayotaka kuyajua.
Tukatulia kabisa huku tukimsikilizia yule mama, ambaye aliinuka na kuingia ndani huku ile albamu yenye picha za Carlos akiiacha pale pale.
Nikaichukua na kuendelea kuangalia, kulikuwa na picha nyingi sana za Carlos akiwa shule, na marafiki zake, nyingine akiwa nyumbani na kwakweli zilivutia sana kuziangalia hata nikashindwa kuelewa kuwa kwanini ananifanyia mambo ya kishetani kiasi kile na kwanini akanitambulisha familia yake ya uongo wakati alikuwa na familia nzuri tu? Na kwanini huwa anabadilika badilika na kuwa shetani? Sikuwa na jibu ila najua wazi kuwa huyu mama yake mzazi lazima atakuwa anajua kuhusu mtoto wake na kwanini amefanya yote yale sababu yeye ndio mzazi wake, kwahiyo tukatulia tukimngoja pale atakapotulia atuambie ukweli kuhusu mtoto wake.
Muda ulienda sana bila ya yule mmama kutoka ndani kwake, na sisi tulichoka kungoja pale nje maana hata njaa nayo ilianza kusumbua kwenye matumbo yetu.
Tukaamua kumuita yule dada na kumuuliza mahali pa kujipatia chakula, nikashangaa akiniangalia kwa umakini sana kisha akauliza
"Kuna mahali popote mimi na wewe tumewahi kukutana? Naona kama sura yako si ngeni machoni pangu"
Nikashtuka na kumkatalia kuwa hatujawahi kuonana itakuwa ananifananisha tu, akataka kutuelekeza pa kwenda kununulia chakula ila mama yake akatoka ndani na kumuuliza kuwa anatuelekeza wapi, naye akamjibu.
Yule mama akaturudisha wote na kusema,
"Nyie ni wageni wangu hivyo basi mtakula hapa hapa kwangu, watu wa huku hatuna roho mbaya kwahiyo karibuni"
Tukajigelesha ila hakutaka tuondoke badala yake akamuita mtoto wake mwingine ambapo akamtuma akatuletee maziwa mtindi.
Alipotuletea akatukaribisha na kutuambia kuwa tupooze njaa wakati chakula kingine kikiwa jikoni.
Kisha akakaa na kuendelea na mazungumzo na sisi huku akituuliza maswali kwa umakini sana.
Na mimi nilimuuliza huyu mama maswali kwa umakini ila kuna kipindi ilibidi niwe kimya huku nikimuangalia anavyougua kwa maumivu ya yale maswali.
Alianza kwa kuniambia,
"Hebu nielezeni kwa kifupi maana mwanzoni sikuwaelewa, umesema kuwa Carlos alikuoa?"
"Ndio Carlos alinioa"
"Mlifunga ndoa ya aina gani na mlifungia wapi?"
"Kwakweli hapo sitaweza kukueleza mama yangu maana hata mimi mwenyewe sielewi ilikuwa ni ndoa ya aina gani"
Nikamueleza pia jinsi Carlos alivyotupeleka kwa wazazi wake bandia na jinsi hao wazazi wake walivyokuja kujieleza kuwa ni bandia baada ya kuwabana sana.
Yule mama alionekana kusikitishwa sana na kusema,
"Hivi haya mambo mnayoniambia ni kweli au naota? Mbona mmeniletea uchuro jamani!"
Ikabidi nimueleze pia majina ya wale wazazi bandia wa Carlos naye akakubali kuwa ni kweli hao watu anawafahamu ila walihama miaka mingi iliyopita
"Sikia niwaambie, kinachonishangaza hapa sio hao wazazi bandia bali huyo Carlos mnayemuongelea. Nadhani hamjielewi kuwa mnamuongelea mtu wa aina gani, au mlikuwa mnamdai?"
Huku akijifuta tena machozi, ikabidi nimwambie kwa utaratibu unaotakiwa
"Hapana mama hatumdai ila hii ni kwaajili ya ukombozi wangu, Carlos amekuwa mtu wa ajabu sana kwangu, huwa anakuja na kupotea halafu mara nyingine anabadilika. Kilichonileta huku ni kuwa nahitaji kuwa huru, nahitaji niondokane na mauzauza yanayonisumbua. Tafadhali mama naomba uniambie ukweli kuhusu Carlos ila na mimi niweze kuwa huru"
Yule mama alionekana kunionea huruma pia kwa yale maelezo yangu, akaendelea kunieleza kwa mshangao sana
"Mnajua kinachonishangaza juu ya maelezo yenu ni kuwa, unamuongelea Carlos kuwa alikuoa wakati Carlos hajawahi kuoa halafu unasema kuwa huwa unaonana nae mara kwa mara halafu anakuwa mtu wa ajabu. Kwa kifupi ni kuwa, Carlos mwanangu alikufa miaka mitano iliyopita"
Kwakweli tulishtuka sana kwani hatukutegemea jibu la aina hii kabisa, nilihisi kama naota ila ndio ukweli.
Nikajikuta nikimuuliza yule mama mara mbili mbili,
"Carlos alikufa? Tena miaka mitano iliyopita?"
"Ndio, yani hata huko kaburini basi kumebaki mifupa ya mwanangu tu. Roho inaniuma sana maana mwanangu nilimpenda kupita maelezo na sitaweza kumsahau hata kesho"
Yule mama akainama akijifuta machozi kwakweli hata mimi machozi yakanitoka, nikaanza kukumbuka jinsi nilivyokutana na Carlos na jinsi alivyokuwa akinisaidia mwanzoni kabla mauzauza hayajawa makubwa sana. Kwakweli Carlos alikuwa rafiki yangu mzuri sana yani nilijihisi kama vile ndio naambiwa kuwa Carlos amekufa leo kwani sikutaka kuamini kuwa kwa kipindi chote kile nilikuwa naishi na marehemu yani nakula nae kuongea nae na kufanya nae mambo mengi, nilijikuta nikiuliza kuwa
"Kwanini alikufa?"
Yule mama alionyesha huruma sana na kuanza kutuambia historia ya mtoto wake Carlos.
"Carlos alikuwa mwanangu wa kwanza, ndiye aliyefungulia uzao wangu kwakweli nilimpenda sana na nilifanya kila kitu ili kuona kuwa mwanangu anaendelea kwani sikupenda aje aishi maisha ambayo mimi nimeishi.
Nilijua Carlos ndio atakayekuja kuikomboa familia yangu na na kuitoa katika janga la shida na umaskini ila sikujua Mungu alipanga nini, sikujua binadamu wengine wanawaza nini juu yangu.
Nilimsomesha Carlos kwa kila hali ili kutimiza ndoto yake kwani yeye alipenda kuwa daktari, na kweli alisoma chuo cha udaktari Muhimbili hadi akapata degree ya udaktari na akatimiza ndoto yake ya kuwa daktari. Mwanangu akaajiriwa na alikuwa na mshahara mzuri sana, alikuja huku kijijini kutusalimia na kuonyesha alichopata. Kwakweli tulifurahi sana na kuamua kufanya sherehe kama familia, yani huwezi amini ule usiku baada ya sherehe ndio ulikuwa usiku wa mwisho kwa Carlos (yule mama akainama na kulia kidogo kwa kwikwi, kisha akaendelea kutueleza)
Kulipokucha, Carlos hakuamka kabisa ikabidi twende kumuangalia. Nikamuona mwanangu akiwa amekauka kabisa kama mti, alikakamaa na hakuweza kupumua tena. Mwili wake wote ulikuwa wa baridi, tulimpeleka hospitali na akaonekana kuwa amekufa na hapo ukawa mwisho wa mwanangu Carlos na ndoto zake za kutusaidia. Hadi leo siwezi kusahau kifo cha mwanangu mpendwa, huwa naumia sana. Natamani awe karibu na mimi anifariji kwa maumivu haya ya moyo wangu"
Yule mama akalia sana, ikabidi mimi na Sam tuwe na kazi ya kumbembeleza. Kwakweli hata mimi mwenyewe nikaumia sana kamavile sijawahi kumchukia huyo Carlos katika maisha yangu.
Moyo wangu ukaniambia kuwa si Carlos wa kumchukia bali ni yule jini aliyekuwa akicheza ndani ya mwili wa Carlos.
Yule mama akatuambia kuwa ataenda kutuonyesha kaburi la Carlos na sisi tukakubaliana nae kwa hilo.
Nilijiangalia mara mbili mbili kama kweli mimi ni binadamu wa kawaida, yani kukaa na marehemu na kukaa na jini ni kitu cha ajabu sana kwakweli sikujiona kuwa kawaida kabisa, nikajihisi nipo tofauti na watu wengine kabisa.
Nilikaa karibu na yule mama huku akiongea kwa uchungu kuwa haelewi huyo ambaye alikuwa na mimi ni nani wakati mtoto wake alishakufa miaka ya nyuma iliyopita.
"Nashindwa kuelewa kwakweli, labda mwanangu amefanywa kuwa msukule. Roho inaniuma sana"
Tukampooza huyu mama ili asizidi kuumia maana ni kweli inauma kusikia kuwa mwanao aliyekufa miaka mingi iliyopita akionekana kwa watu wengine na kuendelea na maisha kama kawaida.
Tulimpooza pale na kujaribu kuongea mambo tofauti tofauti, ndio hapa yule mtoto wake mkubwa wa kike alipokuja tena kisha yule mama akamuelezea yote tuliyomwambia kuhusu Carlos ambapo na yeye alihudhunika sana kwa ile taarifa na kuwalaani vikali watu wachawi na kusema kuwa anawachukia sana watu wachawi.
"Kwakweli toka mwanzo nilijua tu kama kaka yangu hajafa ila amefanywa msukule, yote haya ni kuonyesha kuwa kuna mahali amewekwa ambapo sisi kama familia hatupajui. Nawachukia sana wachawi, yani yule mchawi wa juzi tungempata hakika tungemkatakata kama nyama buchani"
Mama yake akamuuliza
"Kwani juzi walikamata mchawi tena?"
"Hapana, ila ni yule dada wa kipindi kile aliyetufanyia mbwembwe za kupaa hapa ndio alikuja juzi halafu akaniita mimi, loh nilipomuona tu nilikimbilia watu ili twende tukammalize maana yule atakuwa ni mchawi wa kuzimu kabisa"
Nikahema kwa nguvu huku moyo ukinienda mbio kwani najua kwa vyovyote vile kama wakinijua ni mimi basi nipo kwenye hatari kubwa sana kwa hili.
Nikatamani kuaga na kuondoka lile eneo lakini sikufikiria kama nimeshamaliza kazi niliyopewa na yule mtu wa ajabu ili niweze kuwa huru kabisa.
Yule dada aliendelea kuzungumza huku akiniangalia kwa makini sana nadhani alikuwa anahisia kuwa ni mimi sema hakuwa na uhakika sababu ya zile nywele za bandia na miwani ukizingatia sio mtu anayenifahamu.
Muda kidogo chakula kikaletwa na tukatakiwa wote tukae kwa pamoja na kula kile chakula, walikuwa wameandaa wali kwa maharage kisha tukakaa na kuanza kula.
Wakati tunakula nikahisi kamavile kuna mtu zaidi yetu anayekula pale, kumbe mama Amina nae alihisi hicho kitu na kusema kuwa anahisi kuna kitu tofauti pale tunapokula ila yule mama alikuwa ni mwanamaombi na kuanza kukemea pale pale.
Nikahisi kichwa changu kikivurugika, nilihisi kuchanganyikiwa hadi nikaacha kula na kuanza kukimbia.
Sam akanikimbiza kwa nyuma na kunishika, hapo akafanya nishtuke na akili yangu kurudi. Sam akaniuliza kwa hasira
"Unafanya nini sasa Sabrina?"
"Sijui Sam"
"Acha mambo ya kijinga, tutaaibika hapa kumbuka tupo kwa watu"
Baada ya muda kidogo yule mama nae akanifata na kuniuliza
"Una matatizo gani binti?"
"Hapana, sina matatizo"
"Sasa mbona ulikuwa unakimbia wakati wa maombi? Au una majini wewe?"
Aliposema majini nikajikuta nikitetemeka kwa muda, kisha yule mama akanishika mkono na kunirudisha tena nyumbani kwake ila sikuwa na hamu ya kuendelea na chakula tena maana nilianza kujihisi vibaya.
Yule mama akatubembeleza tule ili tuweze kwenda kulitembelea kaburi la Carlos.
Niliwaacha waendelee kula huku mimi nikiwa na mawazo yangu yanayonisumbua.
Baada ya kumaliza kula wakaanza kujiandaa kwaajili ya kwenda kuona kaburi la Carlos, nikajipa moyo na kujitia nguvu kwani sikuwa tayari kuamini kuwa kwa muda wote niliokuwa na Carlos nilikuwa naishi na marehemu.
Walipomaliza kujiandaa, tukaanza safari ya kwenda huko makaburini.
Tulipokuwa njiani nilianza kujihisi kuwa nainuliwa juu taratibu.
Uwoga ukanijaa na kuhisi moja kwa moja kuwa watajua tena mimi mchawi.
Wakati nikihangaika ili nishushwe nikajishtukia nikitupwa chini, hakuna aliyeona nikiinuliwa ila wote waliona nilipoanguka chini kwani nilitupwa vibaya sana hadi nikahisi kiuno kinakatika halafu wigi langu nalo likanivuka kabisa.
Wote waliniangalia kwa mshangao, mara nikamsikia yule Amina akisema
"Kumbe ni wewe!"
Nikaanza kuogopa na kutetemeka sana.
Yule dada akapiga yowe la ajabu na muda huo huo watu wakajaa eneo lile.
Itaendelea kesho.