Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Heaven on Earth

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2013
Posts
37,226
Reaction score
26,687
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA

Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.


Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..

c449ae42b836bcda5f243c52a04c237b.jpg


MAANDALIZI YA SAFARI.

Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.

Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.

Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..


KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.

Tent tulizotumia kulala
181393d9af06585dd377fcf76f9b607e.jpg



Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi

e388057a293813c80ee7f191631c286c.jpg


The View
16bc00a84e515adb383cf530a5c579ce.jpg


3f673959c9f79e081a5f7c6109e53c62.jpg



Nitaendelea Next post.

SAFARI YA MOSHI

Tunaingia Moshi usiku saa 2... Tunapokelewa na wenyeji.. wakarim kishenzi.. wale ma guide sijui walidhani tumetoka nchi gani hatuju kiswahili kumbe ni wabongo tu.. Nimesahau jina la hotel kiwatengu anaweza kunikumbusha. Pale hotelini kulikua na wazungu kibao.. wengi wakiwa wametoka mlimani wakipongezana dinner.. wines na kupeana vyeti... Nikawa nawatizama kwamba can I do this?? unaona watu wanachechemea miguu, sura hazitamaniki wamebabuka, hapo ni bonge la mtu wengi wako hoi.ile usiku tukafanyiwa training na rescue team ya ile kampuni.. tukapewa maelekezo yote muhim.. Asubuhi Safari ya Mlimani.


SAFARI YA MARANGU.

Alfajiri tunaamka.. Mimi pamoja na kununua vifaa vya mlimani lakini still nilikua nahitaji kodi baadhi ya vifaa kama Hiking boot, balaclava, walking stick.. sleeping bag.. na hizi ni zile zenye joooto maana huko juu tushaambiwa kuna baridi la kufa mtu.

Saa 3 asubuhi tunaanza safari ya Marangu. Si umbali mrefu. usajili getini tunamaliza saa 9. miezi ni High season kuna watu kutoka nchi mbali mbali wanakua wamekuja kupanda mlima.!kulikua na nyomi la kufa mtu. Jambo nililopenda Marangu getini kuna ramani ya njia unayotimia kufika kileleni na pia kuna picha za record za watu mbali mbali walifanikiwa kupanda mlima kwa muda mchache, kuna mmoja alipanda kwa 5hrs.. huyu najiuliza hadi leo alifanyaje fanyaje .. Masaa 5 hadi kileleni its not a joke

Marangu Getini hapo.

3e60d5fda7033b8ca1a8b1013a96d1f3.jpg
96e92c82d02ef15bdf21e69ee621c59f.jpg


Fuatilia next post.. huko ndio kwenye mziki



Safari ya Mandara.

f75e778e28a5a00dfe275f01fe7babc5.jpg


Hii ndio ilikua point yangu ya kwanza baada ya kutoka getini. Nilikua na personal porter anaitwa FREDY. Mwenyewe alinipokea bag na kijitambulisha vizuri kwangu. Ukiwa na personal guide ina maana yeye atakua na wewe bega kwa bega.. atakubebea back pack.. achana na wale guide wa group.

Tulianza kwa story akanielezea safari zake milimani.. yeye keshapanda mara 6 hadi Uhuru peak.. I was excited..mwanzo story zilikolea baadae zikakata ule uchovu.
Tunavyopanda tulikua tunakutana na makundi ya watu wanarudi na wengi walikua wanatuambia “pole pole” nadhani huu ndio msemo maarufu ukifuatiwa na “Jambo”.
Nilianza kuchoka jinsi masaa yanavyokwenda.. Nikawa kama siwezi kupumua vizuri muda mwingi Fred alikua ananisitiza kunywa maji...

Kuna muda wenzangu walikua mbele.. baada ya kupumzika nikasema hebu nikae hili kundi sitaki kubaki nyuma... Enhee bana kumbe kasi yao haiendani na mimi.. ila kutembea hata dakika 5 nyingi.. nikaona kama roho inataka kutoka mapigo ya moyo yanaenda mbio hatari roho kama yataka kuchomoka.. joto likanipanda.. Fred as usual akaniambia pumzika. Nikakaa chini vua sweta nikanywa maji.. baada ya muda ndio nikarudi hali ya kawaida.. Nilishaanza kupanick kuwa nakufa sasa. maana hapo si tulishaambiwa watu wanakufa huko sana na kila mtu unamwbia unaenda Kupanda Mlima unakuwa na doubt.. Mimi nikajua mama yangu hapa na mimi ndio bye bye

Akanishauri kuwa kila mtu ana speed yake so i should keep same speed maana tunazidi kupanda juu.. hali ya hewa ni ya mgandamizo.. Tunaingia Mandara saa 2/3 usiku. i was excited kwamba after a long walk kuna sehem tumefika tupumzike. Kitu cha kwanza ni ku register majina.. kulikua na baridi hatari mikono ilikua na ganzi hata kuandika nilishindwa waliiandikia jina nikaweka sign tu.


Tukaonyeswha dormitories nikatafuta kitanda changu cha chini..

c282b3eeccab55a3f072cfe19f3a018c.jpg


yaani kuna bariiidi hatari nikajifunika sleeping bag nikajilaza.. nina hasira kishenzi.. ukiuliza hasira za nini sijui..
Usingizi ukanipitia baada ya muda kidogo mtu akaja kuniamsha kwa ajili ya dinner yaani nilichukia nikaona sijawahi kukutana na mtu mbaya na katili duniani kama huyo alieniamsha kula.. Na hapo tunasisitizwa kwamba ni lazima ule kama unataka kufika juu.. Kufika kileleni nataka ila kama hali ndio hii NO WAY

Nikaanza kulia ndani ya sleeping bag... lia kishenzi.. Makamasi na machozi yanatiririka tu ila nalia kimya kimya watu wasinisikie. mtu unaweza kushangaa kama ni the same person niliyekuwa nashangilia muda mchache uliopita.. Nikawa najiuliza hivi nimekuja kufanya nini huku?? Baridi lote hili tena nikale huko nje.... nikaja kuamshwa tena hapo wenzangu hawawezi kula hadi watu wote watimie.. Nimefika dinning sijataka kuongea na mtu.. wakinichekesha najilazimisha kucheka. Huo muda Akili inawaza mambo kibao.

Chakula chenyewe nakutana na vegetable soup.. macaroni.. ndio siyapendi kudadadeki.. mikate.. chai... Chakula ni kizuri ila hamu ya kula sikua nayo hata kidogo.. Duh nakula then straight in bed sisemeshani na mtu. Na mtandao ni hakuna so no whatsup. Instagram wala JF.

Hii ni asubuhi.. tunajiandaa kwenda Horombo

57e4798f9e4bd7a8400770fcc660ae35.jpg


Huko ni njiani tu...
 
HOROMBO.

5b9b773c85ba173c3a61848751efa146.jpg


Katika vituo vyote sehem niliyoipenda zaidi kukaa ni horombo. Ilituchukua masaa karibu 9/10 kufika HOROMBO. Ni sehem iliyo changamka.. kama kijiji fulani hivi..katika safari yetu Kuna vituo vya kupumzika.. Na pia kuna sehem huko huko barabarani ni stop kwa ajili ya Lunch... Kuna upepo na baridi sana yaani kuliko kukaa nje mtu unaenda chooni upepo usikupige. Vyoo ni Safi na vimejengwa vizuri.

nakumbuka nikiwa nakaribia kibao cha Horombo I was excited kwamba nimefika after a long walk, nikaanza kutembea haraka huku nashangilia na kupiga mayowe, haikuchukua hata sekunde kadhaa hali yangu ikabadilika I couldn’t walk, mapigo ya moyo hayakua sawa kutembea nikashindwa, kihere here chote kikaishia hapo.. ikabidi nipumzike chini na waanze kuniangalia hali yangu. baada ya dakika kadhaa hali yangu ilivyokua sawa ndio nikafika hapo. Yaani usicheze na mambo ya altitude..

Complication..

Ilipofika usiku nikaanza kujisikia vibaya... Yaani sijielewi elewi hali yangu sio nzuri, nikaenda kupima oxygen na vitu vingine wakanambia niko safi tu laba uoga na mawazo. Na kweli I was scared. Nikaingia kulala mapema nikashtuka kama saa 7 USIKU, MAPIGO YANGU ya moyo yanapiga kwa kasi ya ajabu, siwezi kuhema vizuri, nikiangalia pembeni naona kama kila mtu kalala, nikalaani kitendo cha kushtuka mida hiyo nikihesabu muda naona hadi kukuche its like forever. Na nikawa naogopa pia kulala usingizi what if hivi ninavyoshindwa ku breathe ndio nipitilize moja kwa moja.

Sim hazitoki... hakuna mtandao..The only thing nilifanya ni kusikiza music tu mpaka kunakucha. Nimesikiza album za Maher Zain hapoo wee.. Asubuhi tunavyohadithiana kumbe kila mtu anasema I couldn’t sleep last night..





Sent from my iPhone using JamiiForums

View ya Horombo jioni utaona mlima unaonekana kwambalii
eb09577086d34256d89f5ed7753968ab.jpg



Kuelekea Horombo.. Mvua ilikua inayesha muda huo.. ndio maana full kujifunika
ed299501727a66b26ceeb7f8e45f97c8.jpg



Hawa porters.. Imagine hii ndio maisha yao ya kila siku.. wadada tuwe na huruma [emoji23]
43ddc7a5d575fb3e0232efa1b502b968.jpg


Picha ya kwanza baada ya kuweza kutembea na kufika kibaoni[emoji23][emoji23]

a214bb2f38fc77b729224f8bfe21cefd.jpg


Baada ya kupata joto..

b390627c55eb4e7f9398dc5f64a1d03d.jpg


Lunch point hiyo sehem kuna upepo hatari. Mr Peter huyo rasta yeye kazi yake ilikua kuhakikisha tunapata msosi. He is a very nice guy.. anajua kazi yake.. Sijapata kuona aisee

5896567e1c96d7c4065684ffdcb8a586.jpg
18a0cabeec5b7293383222e9e4b6f093.jpg


SAFARI YA ZEBRA ROCKS - ACCLIMATIZATION DAY

078fa31d626341b788a6ee01e95ef626.jpg


Hapa tunakaa one day kwa ajili ya Acclimatization. Sijui kiswahili wanasemaje. Ukipita njia ya Marangu lazima uwe na siku moja ya kukaa hapo ili kuzoea hali ya hewa ya mlimani.. hii pia wanasema inaongeza chance ya kufika summit

Asubuhi nikawa fresh sio kama yule mtu nilikua naumwa usiku. Tangu tuanze safari hii ndio siku naingia kuoga.. Kuna baridi saana yaani maji yanatoka katika bomba ila yanaganda na kuwa barafu.. ila niliona bora kuoga. Kama huogi unajisafisha na wet wipes ama wet towels na kubadili nguo tu.


NAKUMBUKA ilikua birthday wa mmoja wa crew yetu wale ma guide walifanya suprise ya cake, wakaimba nyimbo zao fresh saana, mimi mwenyewe nikawa mmoja wa waimbaji baada ya breakfast mood ikawa zero kabisaa, nikaenda kuongea na guide mkuu akanambia nisiwe na wasi wasi I will be okay. machozi yakaanza kunilenga lenga Mim nikaona kama hanitendei haki ataniambiaje niko sawa wakati mimi namwambia naumwa.

DIAMOX:Hizi ni dawa tulishauriwa kununua zinasaidia kama mtu ukipata altitude sickness na mimi kwa vile nilivyokua najisikia nikazinywa kwa mara ya kwanza.

I was so emotional and sensitive..nikapanda juu tunakolaa nikaanza kulia, ila nalia sitak mtu ajue kama nalia.. Ilivyoanza safari ya Zebra Rock nikawa wa mwisho kabisa kutoka hapo niko na FRED.. Mtu akiniongelesha ndio nahisi nipaze sauti nilieee .. Nilitembea kidogo then nikakaa katika jiwe nikaanza kulia.. Fred na porter mwingine wamesimama pembeni yangu kimya wananiacha tu nilie..

Tulienda Zebra rocks na kurudi Horombo. Ni kama 4500m kufika. Kufika kule nikawa poa kabisa kama sio yule niliekua nalia huko chini.. nikajumuika na watu na pia nikapanga mawe kule. Ukitembea Zebra Rocks pembezoni watu wamepanga Mawe na hawashauri kupangua hayo mawe if you want unaweza kupanga ya kwako.

One thing nili notice watu wengi tulikua tunapata emotional break down bila sababu ya msingi.. sio mimi tu nilililia kuwa wengine pia.. na kila mtu alikua na namna alivyo i handle.




Sent from my iPhone using JamiiForums

a4aca4a91708c93f92530680389d139a.jpg


Nikiwa na Fred.. He is such a nice guy sijapata kuona.. Mtu mwema sana

0dc38baa36bc40e3bbc503a1fb7491ba.jpg


Kunaitwa Zebra Rocks kutokana na hiyo mistari kama pundamilia..

7e13c1fdf131cd175b50a39fd98ae600.jpg


Hiko kilima hapo nyuma ni Mawenzi

8a56c6b733c81c0c50bb931585493815.jpg


Okay

8ee8ab5002b515215590686241ab9737.jpg



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
SAFARI YA KIBO.

5a39fad92fe0b860539a404fb8f9f622.jpg


Siku iliyofata ilikua ni tunaodoka Horombo kwenda Kibo... Nilikua mzima kabisa.. Kila asubuhi na jioni tulikua tunafanyiwa check up. Nilikua salama. Safari ya Horombo hadi Kibo ilikua ndefuuu saaana.Sikumbuki masaa mangapi tulitumia.

Nilikua niko na Fred pia.. He was so helpful.. Njiani tulikua tunapishana wengine wanakwenda wengine wanarudi.. Wazungu ndio wengi sana.. huko utaambiwa wish you luck.. Pole pole.. Pia nilikua naulizia hali ya huko wanatuambia its very windy & Cold.. Wengine anakwambia point aliyofika.. Hii yote tulikua tunadadisi ili kujua ninachoenda kukabiliana nacho huko mbeleni. Nilikua natembea pole pole.. ila pia speed ya mtu automatically inapungua tu.

Kulikua na upepo saana. Ilivyofika mchana tulikua tunahitajika kula sehem ya kula ilikua ni kwenye Mapango ya mawe.. hiyo ndio sehem atleast mnaweza kukaa mkala chakula na upepo ukapiga kidogoo.. Upepo unavuma haswaa. Jua lilikua linawaka saana tu ila upepo ndio hatari.

Kuelekea Kibo kuna point ambayo ndio mwisho maji yanapopatikana. Huko mbele ni kama jangwani hakuna maji. Kwahiyo hata porters ilikua inawalazim kubeba maj kutoka hiyo sehem hadi Kibo camp. Dum la lita 20 ya maji ndio mtu anabeba. Ni kazi nzito saaana.Mimi tu nilikua na ka back pack ila hoi ila yeye ndio maisha yake ya kila siku hayo. Kubebelea maji kupeleka Camp.

HABARI YA KIFO..

Tukiwa bado masaa machache kufika camp kuna mtu akawa kabebwa katika stretcher anashushwa chini.. huku filimbi inapuliza.. wote tukasogea pembeni kupisha. Alikua ni mwanaume mtu mzima mzungu.. kalala chali huku Mke/partenr wake alikua akilia saana nakumbuka maneno niliyoyasikia hadi leo “Ooh my God..Nitafanya nini mimi.. Nitaeleza nini katika familia yetu Maisha yangu bila yeye yatakua ya namna gani” nimefanya kunukuu kiswahili

Analia kishenzi.. Mwili wote ukapata ganzi.. I was schocked.. nikasimama huku nimepigwa na butwaa..Tulivyofika camp tuliambiwa kuwa alifika summit vizuri alivyorudi akalala kabla hajaendelea na safari ya kurudi Horombo so mauti ilimkuta usingizini. Imagine unapanda mlima salama then mauti yanakufika baadae..

Huo muda wakati wanashuka na stetcher akili yangu inawaza kuwa huyu mtu aliyelala anashushwa chini akiwa maiti naweza kuwa mimi.. naweza kuwa mimi ndio nashushwa chini kama maiti.. nakuja kupanda Mlima then nafia huku.. hivi niendelee ama nirudi tu nilikotoka I cant risk my life kama hivi.. Nadhani kila mtu alikua anafikiri yake na kilichotuumiza ni namna yule mama alivyokua analia.. Lilikua tukio la kusikitisha Saana.

Watu wanaweza kuogopa ukisikia hivyoo.. Kama ana mpango wa kwenda akaahitosha lol.. Safari ikaendelea hadi Kibo.. Kibo ni camp kuko busy saana.. Jamani kuna upepo saaana pale Camp.. Ila ukiingia bwenini kuna joto.. Nilikua nawawazia wale wanaolala katika tent nje.. Mimi tu nilikua ndani ila nilikua nasikia hivyo hao wa nje je? Vyoo pia si safi maybe kutokana na kutokua na maji..

Mtu mmoja katika kikundi chetu anapata shida kufika Kibo.. Alifika njiani nae akashindwa kutembea hali yake ikawa mbaya.. Alibebwa juu juu hadi maana alishindwa kutembea kabisa... Na yeye ndio tulikua na wasi wasi nae saana kama angefika akiwa haumwi.

Tuna masaa machache ya kupumzika kabla ya kuanza kupanda Mlima. Saa 6 usiku ndio Safari itaanza

Naenda kuleeee kileleni [emoji4]


1e4b57f88fbaa7f5071f6234d5e45cb9.jpg


Huyu mtoto ana miaka 10 alitokea SA.. wakiwa na Trek4Mandela.. Sijui alifika summit

1659e050ed47d9aae8fcd9741fa10165.jpg


Hii ndio sehem ya mwisho maji kupatikana

fb4082a14402e62a0786908a5e18d88e.jpg


Angalia hao porters

c347751072ae8b7ac44d5b216c81dae0.jpg


e7a1be1ead060058f678e2ab411d2978.jpg


Huyu baba kapanda Mlima mara 18 na siku zote alifika kileleni
cf04cf91cf6d364bffcf48953a4f356a.jpg


Hiko kitanda cha pembeni juu kabisa ndio nililala hapo.. Chini kulikua na mdada mzungu anatapika kishenzi..

4fe4ba885b7b3b2101e99f1c0d788559.jpg


Mandhari ya KIBO

f812dcd0ea12517e859d013166f0921d.jpg


Sehem ya kupumzika

438448f24dab6db9fc860a0d5c9a7ad8.jpg


Kulikua na baridi nje.. Hiko choo nilienda kuingia ndani.. Ushawahi kuona unakaa chooni na unaona ndio sehem nzuri kabisaa kuliko nje

f706f46ae3d08f281b5a3431cf16fe1b.jpg



SUMMIT NIGHT.


KUELEKEA GILMAN'S POINT

824dbcf3bbf8f2526bbd3ae7b07acce4.jpg




Mlima Kilimanjaro haupandwi mchana wala asubuhi ni mnapanda usiku.. yaani ile Mid night ndio safari ya kupanda inaanza. Mimi nakumbuka tulihimizwa kula haraka na kwenda kulala mapema. By Saa 5 sharp tunaamshwa... yaani nilijiona hata sijalala hata kidogo then muda huo.

Hapa unashauriwa kupanda Mlima na clean clothes kuanzia chupi hadi socks.. sijajua ni kwanini. Wakati naamka yule mzungu alielala chini ya kitanda changu wao ndio walikua wanaondoka. So naamka kivivu naanza kubadili nguo kuna baridi so nilikua naona kama mateso fulani cos inabidi nichojoe nguo zooote. Sim yangu ilikua full charged na nilikua na power bank maana nilitaka kupiga as many pictures as possible.

Katika group yetu mtu mmoja anashindwa kupanda Mlima.. Yeye aliishia Kibo hata alivyopimwa ikaonekana oxygen kwake itakua shida so bora abaki.. Na huko juu ndio kuna mgandamizo mkubwa wa hewa. Nikamuonea huruma. Huyu ni yule aliebebwa pia hadi kufika Kibo maana alishindwa kutembea.

Saa 7 kamili ndio tunaanza safari...Hii ni kosa kubwa tulifanya la kuchelewa kuondoka nadhani tulikua group kubwa la watu wengi kuchelea kutoka. lazima uwe na head tochi hio inakusaidia kuona usiku cos kuna mawe saana.. Chupa ya hot water..tulipangwa katika msururu mmoja.. Tukasisitizwa kutembea katika line bila kuachana wala kutoka katika mstari.. Wale ma Guide ndio walikua pembeni. Tukapiga sala ya pamoja pale then safari ikaanza.

Taratibu ule mstari ukaanza kuachia.. wengine wakaanza kubaki nyuma.. wengine katikati.. wengine mbele.. Mimi hapo mwanzo nilikua fresh.. yaani mambo mswano naona Uhuru ile inafikika fasta tu... Wale porters wanaimba nyimbo za kutuhamasisha kupanda Mlima.. Yaani wale jamaa wanafanya kazi kubwa saana. Mimi ile hali niliyokua nayo hata kunyanyua mdomo nilikua siwezi..

Kwa mbali unaziona tochi tu kwa juu yako.. I’m like I wish mimi ndio ningekua kule juu ama yatokee maajabu nipae hadi kule juu lakini ilikua haiwezekani ni lazima upande wewe mwenyewe.. Njia ya kuelekea Gilmans ni zig zag yaani mnakua mnazunguka na hii inachangia pia kuchoka na kutumia muda mwingiiii... kuna mawe mengi na makubwa pia so walikua wanasisitiza kuwa makini.

Nikaanza kuchoka.. Speed yangu ikawa ndoogo.. Nahema kwa shida kama mbwa alietoka kukimbia mbio ndefu halafu vile anakua anatoa ulimi wake nje kuhema ndio nilikua mimi... Muda mwingine ilinibidi kufungua mdomo ili kuweza kutoa na kuingiza hewa. There is very thin layer huko juu.... Mtu mwingine hali yake inabadilika inabidi arudishwe chini haraka sana. Na kunakua na team kazi yao ni kurudisha watu.. Akaanza kulia hataki kurudi.. She is like I came all the way then nirudie hapa SIRUDI.. nyie niacheni niendeelee.... wakifanya vipimo vyao wanaona hii ngoma ikipanda zaidi ya hapo ni atarudishwa akiwa mahututi ama kifo.. walitumuia Muda kum convince ndio akakubali. Wale ma Guide pia hawataki kuchukua risk za namna hiyo..Uruhusu mtu aende juu then akafie huko..... Kwenye 21 tukabaki 19

Nilikua sizungumzi na mtu ni macho tu ndio yanaongea. Yaani ukinitizama usoni unaweza kujua hata nini kinaendelea katika mind yangu... nikawa nawashangaa hata wale wengine wanapata wapi nguvu za kuimba... Tunatembea then kidogo mnasimama kupumzika.. Nilikua nakasirika tukipumzika kidogo hao tunaambiwa tunyanyuke tuendelee na safari. Kwasababu Mimi katika group ya watu 8 let say nakuwa mwishoni wenyewe wako mbeleni so wakati wao washapumzika mimi ndio nafika...Muda wa kupumzika unakua hautoshi.

Nilikua na usingizi wa kufa mtu yaani pamoja na lile baridi nilikua nikifumba macho huku tunatembea naona kabisa usingizii huo unanipitia... Guides walitusisitiza tujitahidi tusifumbe macho.. The thing is unaweza kupitiwa na usingizi then ikawa moja kwa moja. Kwa mara ya kwanza katika maisha niliona usiku ni mrefu... yaani hakukuchi kufike asubuhi

Kuna muda nikasimama nikaangalia chini nilikotoka naona Taa zinamulika yaani unaona kabisa mjini.. Nikaanza kujiuliza hivi mimi why did I come here?? Ili iweje?? Sasa hivi si ningekua nimelala sehem nzuri badala yake niko mlimani huku.. ningekua nakula vizuri badala yake nimekuja huku. Nikaanza kumuonea wivu yule tulimuacha KIBO. Nikaona si bora ningebakia zangu kibo nipumzike.. nilale weeee. Nikaona yeye kubaki was the best decision ever.


Kwenda Gilmans sio mchezo jamani.. na mnatembea usiku kwa usiku kuanzia saa 7.. ngoma ikagonga saa 10 mtu unatembea tu na haujui unafika saa ngapi..unaambiwa in one hour utakua Gilmans.. lisaa linapita hufiki..Naanza kukata tamaa... Nguvu ya ku Give up ikawa inakuja..Nikaona to hell with all these.. Ngoja tu nipoteze pambano nirudi zangu Kibo.. Then upande mwingine nafikiria hivi mimi I came all the way nije kukata tamaa hapa what if ni kipande kichache kimebakia then nitakua nimefika..

Asubuhi kunakucha na kupambazuka hatujafika Gilmas.. Fred mwanzoni nilikua nae lakini baadae kuna mtu katika group akawa hali yake sio nzuro ikabidi nimuache nae ili aje nae juu taratibu..

Kisa cha Bangi

Tukiwa njian tunaenda kuna hao wazungu tulikua nao sambamba.. Kuna sehem wakafika katika mawe makubwa kupumzika wakawa wanavuta sasa kaka mmoja (Alex nimpe hilo jina) tulikua nae group yetu wakamwambia you wanna try.. It helps a-lot.. Alex kihere here akajoin bila kujua hao wazungu ni wazoefu wa hizo mambo.... sisi hao tukaendelea mdogo mdogo.. Baada ya muda tukawaona hao wanakuja na wapo mwendo mkali kidogo zaidi ya wakwetu.. Na Alex alikua nao so akatuacha sisi akawajoin hao wazungu..

Nakumbuka kimoyo moyo nikasema ningejua ningejaribu hata puff moja mbona jamaa yetu kawa na nguvu.. So wakatupita.. Muda si muda nikashangaa Alex anarudishwa chini mzobe mzobe kabebelewa hali imekua tete hajiwezi.. Tukashtuka labda tushampoteza huko tukaambiwa he is okay ila he cant breathe well wanamrudisha huko chini akatafutiwa stretcher likamshusha. Baadae alivyokuka kutuhadithia nilicheka sana kumbe wenzake ni wazoefu wa zile mambo anasema alichungulia mlango wa kifo

Mida ya saa mbili kasoro nadhani ndio naingia Gilmas.. Sisi tumefika Gilmans kuna group nyingine walikua washafika Uhuru peak wanarudi chini.. Tulichelewa sana kufika Sikuamini aisee Nikawa naona kama muujiza fulani.. Tulivyofika tu wakatuwahi na maji moto. Jua liko vizuri ila the thing is baridi unaisikia hadi katika mifupa.

Nikiwa Gilmans

29ebfa60118c2c475ae9132664cd7062.jpg



Japo sim yangu ilikua full charge ukiwa juu ikazima kabisa kwamba battery empty. the last picture I took with my phone


40c7062c34b9a820756b5e9342e2d9c6.jpg



Tulikua tunatembea namna hiyo

10d184e1216887a442a07b5e2fe05ea5.jpg



Hapa ukiwa maeneo umya Juu Gilmas ukiangalia tulikotoka kule chini

4c00e27f62e7db0468d8e1ff7db5dc6d.jpg



3c45e6688ea9cb7a5b206c08aed9e104.jpg
 
STELLA POINT.
e43ceb86210e16086d81156551c61482.jpg


Nilivyofika Gilmans nilipata some sort ya relief.. Na kwa mimi nafikiria Gilmans was the hardest part. Watu wengi huwa wanaishia hapo anakosa nguvu ya kuendelea mbele. Wote katika group yetu tulipumzika then tukaanza safari ya kuelekea Stelle.

Njiani kulikua na barafu saana.. The wind is blowing hatari.. tulikua tunatembea juu ya barafu.. Problem nyingine ni kwamba tulikua hatuwezi kuonana kutokana na ukungu..Mtu yuko hatua tatu mbele ila huwezi kumuona kwasababu kuna ukungu wa kufa mtu. To be honest ilikua inatisha..

Shida inakuja kuwa hewa inakua ndogo saana. Nikaanza kuona hali tete kabla hatujafika...baada ya Masaa kadhaa tukafika Stella... Pale Kibaoni tukapiga picha haraka ili tuendelee mbele.

f88521fdd08c07bd253e06eb7726140c.jpg




Sim yangu haikuweza kuwaka.. We only took group photos

8539d6d4096127f29fe7bbc33369ec6e.jpg



UHURU PEAK.

Baada ya pale tukaanza kuitafuta Uhuru..Ambayo ni kama 30mints.. hizi dakika kuzitamka hapa unaona chache ila ukiwa kule juu ni kama mwaka...Yaani hali ya hewa ilikua mbaya saana. Nilikua nime sha give up nimechoka na nilikua sijielewi yaani natembea tu.. Sielewi kitu. Nilipata Hallucination..

Kuna baba mmoja mwanzoni niliwaambia kuwa yeye kapanda mara 18 ila alisema katika kipindi choote alichopanda hakuwahi kukutana na hali tuliyokutana nayo sisi kule juu. Storm inayopiga ni ya hatari..... Upepo unapiga mnakimbilia katika jiwe kubwa ili atleast upepo upungue kidogo ndio tuendelee mbele. Jamani nilikua kama naiona jehanam. It was life and death experience kule juu. Upepo ukivuma ukija hivi uso wote unafunikwa na barafu... Nilikuja kuambiwa baadae kuwa storm tuliyokutana nayo huko juu haijawahi kutokea for decades

Tukaanza kupotezana hapo.. Guide mkuu akasisitiza hali ni mbaya turudi tusiendelee mbele..kiongozi wetu anasema haiwezekani.. Mimi nilikua sielewi kitu siwezi kuongea nawatizama tu.... hata haya mengine nilikuja kuhadithiwa Yeye alikua anasisitiza hakuna mtu anarudi.... Yaani hapo hadi ulitokea ugomvi kati yetu na guide mkuu anaetuongoza. Storm ni ya hatari inapuliza mpaka unasikia jiwe kubwa linatikisika hapo nawaza hili jiwe si linaweza kubiringita hapa then litudondokee ndio iwe bye bye

I reached Uhuru Peak.. kufika summit was one of the best experiences of my life. The summit view was absolutely stunning and I don’t think any words could really give a justice... Unapaswa ushuhudie mwenyewe mtu asikuhadithie. Yaani nilisahau hata ile dhoruba tuliyokutana nayo...

Niliona mazoezi na jitihada zangu zimezaa matunda mwisho wa siku, I felt a sense of achievement kwa kutimiza kile ambacho nilijiwekea kwamba i want to STAND ON THE ROOF OF AFRICA. Nakumbuka nililia saana.... Nikiwa summit na pia wakati wa kurudi ni machozi ya furaha na relief. Mind you sisi hatukuchuka hata dakika pale juu tuligeuza muda ule ule kutokana na hali ya hewa.

4d30f6deb3d8dd89ae4b96c4086403f6.jpg


Group yetu wote hatukufanikiwa kukigusa kibao wala kupiga picha katika kile kibao.. Hii ni kutokana na barafu nyingi. Wote tulikubaliana as long as tumefika Peak hiyo inatosha... It was sad thing kutokupiga picha pale lakini pia ukifikiri ulikotoka na pale tulipofika unaona IT was okay

Nikipokea certificate yangu

daa9cf6211f80256f29dd4d894cd559b.jpg


Ukumbusho wa cheti.

f351a28485629dae51e0af9feaf946f6.jpg


Next post ya mwisho nitamalizia kushuka.
 
SAFARI YA KUSHUKA MLIMA..

71e42ea7ef4312fde77d882c8c3243de.jpg


Kule juu hatukuchukua muda tulianza kurudi kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya.. Nilikua nimechoka saaaaana. Tukatembea weee hadi tukafika Gilmans. Uzuri wa kushuka ni unaenda straight hakuna mambo ya kusema upite zig zag mle mle katika njia unapita tu.

Nilivyofika Gilmans nikaanza kushindwa kutembea miguu ikagoma kabisa..nikitembea dakika moja nyingi naishiwa nguvu nasimama au nakaa. Huo muda Fred alikua ameshashuka chini kwani yule mwenzetu niliemuacha nae aliishia Stella so alimrudisha chini. This time nikawa ma guide mmoja mtu mzima anaitwa Moses no comment on him but... Nikamkumbukaje Fred hapa angekua ananibembeleza [emoji23]

Nikaanza kulia.. kushuka ni rahisi ila mimi nilikua nimeishiwa nguvu. Kuna muda nilikua nakuangali kule juu najiuliza hivi mimi niliwezaje kupanda juu halafu hapo najisemea hata unipe bilion moja hunirudishi huko juu mimi...

mzee Moses ananisisitiza nijitahidi nishuke ananiambia Kibo ni pale tunafika sasa hivi wewe jitahidi..Na kweli naona vibanda vilee najipa moyo mwenyewe nanyamaza then naendelea kutembea.. Nikitembea kidogo nachoka nakaa tena naanza kulia. It was a mixed feeling... halafu pia nilikua nimeikumbuka familia yangu.... Tukipishana na watu wananipa pole kama zote.... Nikaishiwa nguvu siwezi kutembea mwenyewe so akawa ananishikilia ndio naweza kutembea.... Tumeshikizana wee Kufika sehem I couldn’t walk at all yaani hata kusimama mwenyewe nikawa siwezi... Hata nikijaribu vipi nashindwa.... ilikuja stretcher kunibeba na kunirudisha Kibo.

Wakati tunaelekea Kibo nilishangaa porters wengi wanapanda kuelekea mlimani. Nikawa najiuliza hawa jua lote hili ndio wanaenda kupanda Mlima nikauliza akanambia wanaenda kupokea watu wanaotoka mlimani. Wengine ndio hao wanarudi na hali kama ya kwangu.

Ukifika Kibo yaani wanakuhudumia vizuri hapo.. Nikapewa chai.. mara soup ya moto.. Tukaambiwa tupumzike kidogo tukiamka tunaanza safari ya Horombo. Ngoma hailali. Nikamuwazia yule mzungu aliefariki.. Nikasema silali wala nini nitakaa macho hadi hiyo time ya kurudi Horombo.. Nisije kufia usingizini. Ila Chezea usingizi na uchovu nilikuja kushtuka naamshwa nikale.. I wish niweke picha moja niliyopigwa wakati nimelala... I was half dead.. chakaram.

ku pack vitu was a headache.. Na ilitupasa tufanye haraka maana hizo domitories kuna wageni wengine walikua wamefika so inabidi waingie.. Saa 8/9 tunaaza safari ya kurudi Horombo.. Usingizi ulinisaidia sana huku nilikua poa njiani tunapiga story kwa saaana na wala sikua na uchovu mkubwa sana.. Rohoni kwangu najisikia safiii. Horombo nawahi kufika mapema kushinda hata wale wengine..Kuna baadhi ya watu walienda kuoga mimi sikuoga wala nini.. Nilisema hadi nifike mjini.. I want hot shower nikae hata lisaa bafuni.

Horombo tunalala then kesho asubuhi inaanza safari ya kurudi Marangu getini. Kabla hatujaondoka hapo Horombo tuliimbiwa nyimbo nadhani kama ni utamaduni fulani.. Nili enjoy saana zile nyimbo.. tukacheza pale.. Mimi na wenzangu 3 tulirudi Marangu getini na ambulance. Asubuhi ile Guide kama kuna mtu katika watu wake hayuko vizuri kuna gari linakuwepo for emergency kuwarudisha getini.. So wengine wanatangulia kwa miguu sisi tunabakia kusubiri gari...

Katika Ambulance kuna waarabu fulani ambao niliwakumbuka vizuri wakati wa kupanda kuanzia Mandara tulikua wote benet.. nao wanarudi kwa ambulance na mchina mmoja. Wale waarabu wa 4 they told us kwamba only 1 of them was able to reach the peak.. huyo mwanaume wale wadada hawakufika.... Mmoja wao alikua anatapika saana... alikua analalamika kuumwa... walituambia wametokea UAE.. Kurudi na gari was another experience..

Ile asubuh tulipoamka Horombo ndio tulianza kushangaana sura zetu [emoji23][emoji23] ni pua zimebabuka... ngozi haiko sawa.. ukimuangalia mwenzako unaweza kujiona wewe una afadhali na mwenzako nae akikuangalia anajiona yeye ana afadhali.. Sisi ndio tunakua wa kwanza kufika tunasubiria wenzetu waliokuja.

Final Goodbye na Porters

Tunapata wasaa wa kuagana na crew ya Origin pale Marangu getini maana baada ya hapo tulikua tunaenda hotelini na wengi wao wasingeweza kuja kule.. It was very sad. Its only few days we stayed in Kili but the bond we had shared with those people was so strong... Watu walilia saana...

Tip tulichangishana tangu mwanzo elfu 75 each.. na mwanzo tulipanga kila mtu achangie laki wengine wakaona laki nyingi tufanye 75... Maana tayari tulishalipia fedha.... ila baada ya kupanda mlima na kuona kazi wale watu wamefanya we all thought kwama 75 haikua pesa.. It was nothing compared na service walitotupatia kule juu. Ile pesa waligawana katika group. Sisi hatukutaka kila mtu ampe tip mtu mkononi kivyake.. maana kuna mtu wa jikoni yeye humuoni unashangaa tu chakula mezani.. kuna mtu anaebeba bag yako humuoni ila muda wote ukifika point fulani unaletewa bag liko salama. So kuna wengine hatu interact nao ila tunapata service yao. Wao wenyewe walijua waligawana vipi ile pesa.

Nilichukua mawasiliano na Fred.. Alinambia hataweza kuja hotelini.. na mpaka kesho kutwa huwa tunawasiliana ingawa most of the time anakua hapatikaniki yuko mlimani.. Nilimpatia tip yake personal tofauti na ile ya group na pia vifaa vingi nilivyonunua kwa ajili ya kupanda mlima nilimuachia.. Alishukuru sana. Pia alinambia ataenda kusomea mambo ya u guide kuna chuo huko.. Kwasababu yeye ni porter na ili uwe guide inabidi upate cheti... So kitu ambacho nimepanga ni kumsaidia part ndogo ya ada.. Mimi sio tajiri maisha yangu ya kuunga unga but what he did kwangu ni wema na utu wa hali ya juu. He was extremely caring. Very understanding.... Maybe that is the only way I can repay him.. Mara kibao huwa namwambia yeye ni mtu poa saana.

Tunarudi Hotelini.. Hiyo ndio siku kulikula misosi tunayopendelea.. It was a celebration evening.. Hiyo siku nilitumia karibu saa nzima kuoga.. maji ya motoooo... I was so relieved... Jioni tukagawiwa certificates wenye kunywa bia ndio walizinywa hapo na pia nilipata nafasi ya kuonana na kiwatengu kwa mara ya kwanza na nitumie nafasi hii kumshukuru kwa ushauri wake na moyo wa kunisaidia mpaka nikafanikisha safari yangu Kilimanjaro.

Wengi wetu tulipata na ganzi katika mikono siku zile za mwanzoni lakini baadae iliishia taratibu.

We came back to DSM safely with a lot of great memories. Climbing Mt Kilimanjaro to the peak is something that I will hold close into my heart. My trip was very eventful and joyous, I met new people who were very generous and down to earth like Fred.. they took care of me as if I were their own child/sister, I came across various obstacles, I strived for the best and most importantly I achieved my goal. It’s unreal how we became so attached with guides/porters in such a short period of time. I journeyed through pain, laughter, suffering, dirtiness and Mr Peters famous porridge and soup.(ambayo ilikua huwezi kukwepa kunywa)

I had the greatest moments and created incredible memories which will remain in my mind and heart forever. As they say nothing comes easy and it’s true, It wasn’t easy at all but I did it... One thing I learned is to appreciate everything this life offers.

I thank God for protecting me all the time, My Mother for her support.. My group mate who not only made the trip funny but also easy,.....Mr Emmanuel & Origin Team for for this wonderful journey[emoji92]

My family & Friends made this for Us..

80a1aea0e82016378de52fa15f5dd06e.jpg


The Team behind our success

28135f6fadaf143b68a13658755970bf.jpg


Going back to Horombo

8c6fd52e073b6e6758d8a5cbbf46ecb0.jpg


Last picture @ Kibo

bd15f5493f3ad6121c40f423cd68be42.jpg


I bought so many things pale Marangu Getini ikiwemo hii T shirt na i dedicate kwa wote ambao wanasema hawawezi kupanda Mlima

6ea49fb4301c3a3c19cbfaa139eae9f8.jpg





THE END
 
Hongera mrembo, nina binamu yangu ameshapanda Kilimanjaro mara 2 kama si 3 ila anasema haina uzoefu unaweza kupanda mara nyingi na bado ukapata emergency ukadanji au ikabidi ushuke mlima na safari iishie hapo.

Huwa nawataniaga wafanyakazi wenzangu jamani tuchukue likizo ya pamoja twendeni tukapande Mlima Kilimanjaro... wanaishia kuniambia kama umechoka kula pizza tuache sie tupakatie pakacha zetu. Basi huwa nacheekaa.


Binafsi napenda sana kutembea na nilishapanda milima ya kawaida ya vijijini ikiwa ni njia ya kuelekea ninakofikia. Najiona namudu ila sijajipanga kupanda mlima wowote japo natamani.

Naishiaga kwenda Mbuga za wanyama nalala hoteli basi.

Hongera sana mamii.
 
86339179-5152-4B83-AF08-0597A410EBF9.jpeg
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA

Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.


Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..

c449ae42b836bcda5f243c52a04c237b.jpg


MAANDALIZI YA SAFARI.

Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.

Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.

Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..


KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.

Tent tulizotumia kulala
181393d9af06585dd377fcf76f9b607e.jpg



Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi

e388057a293813c80ee7f191631c286c.jpg


The View
16bc00a84e515adb383cf530a5c579ce.jpg


3f673959c9f79e081a5f7c6109e53c62.jpg



Nitaendelea Next post.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nimepanda huo mlima zaidi ya mara tano (5) wengi wa wanaobabuka ngozi zao zinakuwa zimeathirika kwa namna moja ama nyingine, mfano wanaojichuna ngozi n.k
.
KINAPA hawashauri mwendo wa haraka hapa ndipo tulipokuwa tunakosana nataka niende haraka nikitembe taratibu nitachoka, ilifikia wakati nikagombana na tour guides sijawahi kurudi tena.
.
Mwanamke atembee taratibu na kila Stopping center tupumzike huu ujinga ulinishinda, mara mia Mt Margarita Uganda fanya unachoweza.
 
yaan ulikuja had kwenye shamba langu knabisa la [emoji526][emoji526][emoji526].....na kweli mandhari ya huko ni mazuri sana sana...karibu tena morogoro mamy[emoji4]
Money anza mazoezi kabisa mwakani panapo majaaliwa twende wote tukapande mlima tena nihakikishe nakufikisha kileleni ili usije ukaleta lawama hapa kua nimekupandisha mlima lkn sijakufikisha kileleni.

Sent from my GT-P5200 using Tapatalk
 
Back
Top Bottom