Heaven on Earth
JF-Expert Member
- Mar 21, 2013
- 37,226
- 26,687
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA
Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.
Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..
MAANDALIZI YA SAFARI.
Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.
Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.
Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..
KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.
Tent tulizotumia kulala
Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi
The View
Nitaendelea Next post.
SAFARI YA MOSHI
Tunaingia Moshi usiku saa 2... Tunapokelewa na wenyeji.. wakarim kishenzi.. wale ma guide sijui walidhani tumetoka nchi gani hatuju kiswahili kumbe ni wabongo tu.. Nimesahau jina la hotel kiwatengu anaweza kunikumbusha. Pale hotelini kulikua na wazungu kibao.. wengi wakiwa wametoka mlimani wakipongezana dinner.. wines na kupeana vyeti... Nikawa nawatizama kwamba can I do this?? unaona watu wanachechemea miguu, sura hazitamaniki wamebabuka, hapo ni bonge la mtu wengi wako hoi.ile usiku tukafanyiwa training na rescue team ya ile kampuni.. tukapewa maelekezo yote muhim.. Asubuhi Safari ya Mlimani.
SAFARI YA MARANGU.
Alfajiri tunaamka.. Mimi pamoja na kununua vifaa vya mlimani lakini still nilikua nahitaji kodi baadhi ya vifaa kama Hiking boot, balaclava, walking stick.. sleeping bag.. na hizi ni zile zenye joooto maana huko juu tushaambiwa kuna baridi la kufa mtu.
Saa 3 asubuhi tunaanza safari ya Marangu. Si umbali mrefu. usajili getini tunamaliza saa 9. miezi ni High season kuna watu kutoka nchi mbali mbali wanakua wamekuja kupanda mlima.!kulikua na nyomi la kufa mtu. Jambo nililopenda Marangu getini kuna ramani ya njia unayotimia kufika kileleni na pia kuna picha za record za watu mbali mbali walifanikiwa kupanda mlima kwa muda mchache, kuna mmoja alipanda kwa 5hrs.. huyu najiuliza hadi leo alifanyaje fanyaje .. Masaa 5 hadi kileleni its not a joke
Marangu Getini hapo.
Fuatilia next post.. huko ndio kwenye mziki
Safari ya Mandara.
Hii ndio ilikua point yangu ya kwanza baada ya kutoka getini. Nilikua na personal porter anaitwa FREDY. Mwenyewe alinipokea bag na kijitambulisha vizuri kwangu. Ukiwa na personal guide ina maana yeye atakua na wewe bega kwa bega.. atakubebea back pack.. achana na wale guide wa group.
Tulianza kwa story akanielezea safari zake milimani.. yeye keshapanda mara 6 hadi Uhuru peak.. I was excited..mwanzo story zilikolea baadae zikakata ule uchovu.
Tunavyopanda tulikua tunakutana na makundi ya watu wanarudi na wengi walikua wanatuambia “pole pole” nadhani huu ndio msemo maarufu ukifuatiwa na “Jambo”.
Nilianza kuchoka jinsi masaa yanavyokwenda.. Nikawa kama siwezi kupumua vizuri muda mwingi Fred alikua ananisitiza kunywa maji...
Kuna muda wenzangu walikua mbele.. baada ya kupumzika nikasema hebu nikae hili kundi sitaki kubaki nyuma... Enhee bana kumbe kasi yao haiendani na mimi.. ila kutembea hata dakika 5 nyingi.. nikaona kama roho inataka kutoka mapigo ya moyo yanaenda mbio hatari roho kama yataka kuchomoka.. joto likanipanda.. Fred as usual akaniambia pumzika. Nikakaa chini vua sweta nikanywa maji.. baada ya muda ndio nikarudi hali ya kawaida.. Nilishaanza kupanick kuwa nakufa sasa. maana hapo si tulishaambiwa watu wanakufa huko sana na kila mtu unamwbia unaenda Kupanda Mlima unakuwa na doubt.. Mimi nikajua mama yangu hapa na mimi ndio bye bye
Akanishauri kuwa kila mtu ana speed yake so i should keep same speed maana tunazidi kupanda juu.. hali ya hewa ni ya mgandamizo.. Tunaingia Mandara saa 2/3 usiku. i was excited kwamba after a long walk kuna sehem tumefika tupumzike. Kitu cha kwanza ni ku register majina.. kulikua na baridi hatari mikono ilikua na ganzi hata kuandika nilishindwa waliiandikia jina nikaweka sign tu.
Tukaonyeswha dormitories nikatafuta kitanda changu cha chini..
yaani kuna bariiidi hatari nikajifunika sleeping bag nikajilaza.. nina hasira kishenzi.. ukiuliza hasira za nini sijui..
Usingizi ukanipitia baada ya muda kidogo mtu akaja kuniamsha kwa ajili ya dinner yaani nilichukia nikaona sijawahi kukutana na mtu mbaya na katili duniani kama huyo alieniamsha kula.. Na hapo tunasisitizwa kwamba ni lazima ule kama unataka kufika juu.. Kufika kileleni nataka ila kama hali ndio hii NO WAY
Nikaanza kulia ndani ya sleeping bag... lia kishenzi.. Makamasi na machozi yanatiririka tu ila nalia kimya kimya watu wasinisikie. mtu unaweza kushangaa kama ni the same person niliyekuwa nashangilia muda mchache uliopita.. Nikawa najiuliza hivi nimekuja kufanya nini huku?? Baridi lote hili tena nikale huko nje.... nikaja kuamshwa tena hapo wenzangu hawawezi kula hadi watu wote watimie.. Nimefika dinning sijataka kuongea na mtu.. wakinichekesha najilazimisha kucheka. Huo muda Akili inawaza mambo kibao.
Chakula chenyewe nakutana na vegetable soup.. macaroni.. ndio siyapendi kudadadeki.. mikate.. chai... Chakula ni kizuri ila hamu ya kula sikua nayo hata kidogo.. Duh nakula then straight in bed sisemeshani na mtu. Na mtandao ni hakuna so no whatsup. Instagram wala JF.
Hii ni asubuhi.. tunajiandaa kwenda Horombo
Huko ni njiani tu...
Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.
Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..
MAANDALIZI YA SAFARI.
Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.
Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.
Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..
KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.
Tent tulizotumia kulala
Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi
The View
Nitaendelea Next post.
SAFARI YA MOSHI
Tunaingia Moshi usiku saa 2... Tunapokelewa na wenyeji.. wakarim kishenzi.. wale ma guide sijui walidhani tumetoka nchi gani hatuju kiswahili kumbe ni wabongo tu.. Nimesahau jina la hotel kiwatengu anaweza kunikumbusha. Pale hotelini kulikua na wazungu kibao.. wengi wakiwa wametoka mlimani wakipongezana dinner.. wines na kupeana vyeti... Nikawa nawatizama kwamba can I do this?? unaona watu wanachechemea miguu, sura hazitamaniki wamebabuka, hapo ni bonge la mtu wengi wako hoi.ile usiku tukafanyiwa training na rescue team ya ile kampuni.. tukapewa maelekezo yote muhim.. Asubuhi Safari ya Mlimani.
SAFARI YA MARANGU.
Alfajiri tunaamka.. Mimi pamoja na kununua vifaa vya mlimani lakini still nilikua nahitaji kodi baadhi ya vifaa kama Hiking boot, balaclava, walking stick.. sleeping bag.. na hizi ni zile zenye joooto maana huko juu tushaambiwa kuna baridi la kufa mtu.
Saa 3 asubuhi tunaanza safari ya Marangu. Si umbali mrefu. usajili getini tunamaliza saa 9. miezi ni High season kuna watu kutoka nchi mbali mbali wanakua wamekuja kupanda mlima.!kulikua na nyomi la kufa mtu. Jambo nililopenda Marangu getini kuna ramani ya njia unayotimia kufika kileleni na pia kuna picha za record za watu mbali mbali walifanikiwa kupanda mlima kwa muda mchache, kuna mmoja alipanda kwa 5hrs.. huyu najiuliza hadi leo alifanyaje fanyaje .. Masaa 5 hadi kileleni its not a joke
Marangu Getini hapo.
Fuatilia next post.. huko ndio kwenye mziki
Safari ya Mandara.
Hii ndio ilikua point yangu ya kwanza baada ya kutoka getini. Nilikua na personal porter anaitwa FREDY. Mwenyewe alinipokea bag na kijitambulisha vizuri kwangu. Ukiwa na personal guide ina maana yeye atakua na wewe bega kwa bega.. atakubebea back pack.. achana na wale guide wa group.
Tulianza kwa story akanielezea safari zake milimani.. yeye keshapanda mara 6 hadi Uhuru peak.. I was excited..mwanzo story zilikolea baadae zikakata ule uchovu.
Tunavyopanda tulikua tunakutana na makundi ya watu wanarudi na wengi walikua wanatuambia “pole pole” nadhani huu ndio msemo maarufu ukifuatiwa na “Jambo”.
Nilianza kuchoka jinsi masaa yanavyokwenda.. Nikawa kama siwezi kupumua vizuri muda mwingi Fred alikua ananisitiza kunywa maji...
Kuna muda wenzangu walikua mbele.. baada ya kupumzika nikasema hebu nikae hili kundi sitaki kubaki nyuma... Enhee bana kumbe kasi yao haiendani na mimi.. ila kutembea hata dakika 5 nyingi.. nikaona kama roho inataka kutoka mapigo ya moyo yanaenda mbio hatari roho kama yataka kuchomoka.. joto likanipanda.. Fred as usual akaniambia pumzika. Nikakaa chini vua sweta nikanywa maji.. baada ya muda ndio nikarudi hali ya kawaida.. Nilishaanza kupanick kuwa nakufa sasa. maana hapo si tulishaambiwa watu wanakufa huko sana na kila mtu unamwbia unaenda Kupanda Mlima unakuwa na doubt.. Mimi nikajua mama yangu hapa na mimi ndio bye bye
Akanishauri kuwa kila mtu ana speed yake so i should keep same speed maana tunazidi kupanda juu.. hali ya hewa ni ya mgandamizo.. Tunaingia Mandara saa 2/3 usiku. i was excited kwamba after a long walk kuna sehem tumefika tupumzike. Kitu cha kwanza ni ku register majina.. kulikua na baridi hatari mikono ilikua na ganzi hata kuandika nilishindwa waliiandikia jina nikaweka sign tu.
Tukaonyeswha dormitories nikatafuta kitanda changu cha chini..
yaani kuna bariiidi hatari nikajifunika sleeping bag nikajilaza.. nina hasira kishenzi.. ukiuliza hasira za nini sijui..
Usingizi ukanipitia baada ya muda kidogo mtu akaja kuniamsha kwa ajili ya dinner yaani nilichukia nikaona sijawahi kukutana na mtu mbaya na katili duniani kama huyo alieniamsha kula.. Na hapo tunasisitizwa kwamba ni lazima ule kama unataka kufika juu.. Kufika kileleni nataka ila kama hali ndio hii NO WAY
Nikaanza kulia ndani ya sleeping bag... lia kishenzi.. Makamasi na machozi yanatiririka tu ila nalia kimya kimya watu wasinisikie. mtu unaweza kushangaa kama ni the same person niliyekuwa nashangilia muda mchache uliopita.. Nikawa najiuliza hivi nimekuja kufanya nini huku?? Baridi lote hili tena nikale huko nje.... nikaja kuamshwa tena hapo wenzangu hawawezi kula hadi watu wote watimie.. Nimefika dinning sijataka kuongea na mtu.. wakinichekesha najilazimisha kucheka. Huo muda Akili inawaza mambo kibao.
Chakula chenyewe nakutana na vegetable soup.. macaroni.. ndio siyapendi kudadadeki.. mikate.. chai... Chakula ni kizuri ila hamu ya kula sikua nayo hata kidogo.. Duh nakula then straight in bed sisemeshani na mtu. Na mtandao ni hakuna so no whatsup. Instagram wala JF.
Hii ni asubuhi.. tunajiandaa kwenda Horombo
Huko ni njiani tu...