Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Simulizi ya Safari yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro

Mi niko vzr nnapumzi za kutosha kabisa wewe anza kabisa zoezi la kupandisha milima ya uluguru ili tukienda kilimanjaro nikufikishe kwe kilele cha kibo.

Maendeleo hayana chama


hahahhahaa haya bwana... tupande mlim tuliletee Taifa letu pesa...ili mabeberu yasije tupangia mambo ya kufanya
 
MY JOURNEY TO THE ROOF OF AFRICA

Kabla ya mwaka kuisha napenda ku share na nyie experience yangu ya kupanda mlima Kilimanjaro nitaambatanisha baadhi ya picha na video za safari yangu yote. Kama kuna watu wamewahi kupanda Mlima Kilimanjaro wanaweza ku share pia uzoefu wao.


Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails.. Kundi letu tulikua 21, Njia niliyotumia ni MARANGU.. Cost ilikua ni 560$ hii ili include kila kituu.. kuanzia usafiri Dar-Moshi Dar, chakula, hoteli.. vifaa.. fees za getini... personal guides... etc etc.. gharama zinapungua kutokana na huduma unayohitaji..

c449ae42b836bcda5f243c52a04c237b.jpg


MAANDALIZI YA SAFARI.

Baada ya ku confirm ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro. Jambo la kwanza nilifanya Medical check up.. nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni... Nikaanza mazoezi nakimbia uwanja nazunguka mara 7-10. Mazoezi ya kupandisha ngazi wanaojua jengo la UHURU HEIGHTS.. Nimepanda na kushuka hizo ngazi saana.. Pia tulikua tunafanya SEA CLIFF WALK haya yalikua matembezi kutoka Upanga hadi Sea cliff kwenda na kurudi kila jumamosi Kwa mwezi mara mbili. Kim beach kigamboni kutembea katika michanga Etc etc.

Pia nilijisajili na kitengo cha Flying Doctors Africa wako chini ya Amref.. wanatoa huduma ya helicopter kwa ajili ya ku rescue mlimani incase of emergency. Kusema ukweli nilikua muoga saana kwa sababu ya stories unazosikia so ilikua ni tahadhari maana ilikua ndio first time kupanda mlima.. & you never know nini kitatokea huko juu milimani. Fee ni 50$ kwa mtu mzima.

Nilisoma kila habari kuhusu kilimajaro na kupanda Mlima.. vifo vinavyotokea.. risk ukiwa mlimani..


KUPANDA MLIMA ULUGURU:Uluguru height ni kama 8600ft na hii ilikua ni moja ya majaribio kabla ya kupanda Mlima... Uluguru was the easiest tulienda Ijumaa.. Jumamosi tukapanda Mlima... Jumapili tukarudi Dar.. Mandhari ya Uluguru ni bomba sana...Kuna memories nyingi ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls...... Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale.. Nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikua siwezi. I wonder kwanini SUA hawarekebishi.

Tent tulizotumia kulala
181393d9af06585dd377fcf76f9b607e.jpg



Hii ndio camp kunaitwa Morning Site..tulikofikia.. humo kuna chata za watu wengi

e388057a293813c80ee7f191631c286c.jpg


The View
16bc00a84e515adb383cf530a5c579ce.jpg


3f673959c9f79e081a5f7c6109e53c62.jpg



Nitaendelea Next post.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hongera kwa udhubutu,nimefuatilia sana Uzi wako na naendelea kufuatilia,nimeona weaknesses zako pia zakupanda mlima nazifahamu.
Nilisomea hayo mambo ya wanyamapori&utalii na guides,nadhani siku zijazo naweza kukusaidia,pia kutoa ushauri kwa yeyote kuhusiana na utalii.
Mwaka2016 nipanda mlima Kilimanjaro niliamua kupanda kama pota /mgumu kwa moshi huita .kuna mambo huko mlimani na vituko.
Mimi ni mvivu wa kuandika mnisamehe.
 
hahahhahaa haya bwana... tupande mlim tuliletee Taifa letu pesa...ili mabeberu yasije tupangia mambo ya kufanya
Sio pesa tu na raha pia tunapata
Mi napenda sana utalii wa ndani tena utalii unaofikisha kileleni yaani kule juu kabisa.

Maendeleo hayana chama
 
Nakufatilia ana kwa ana. Nimepanda sana mlima since nimemaliza six. Kiingereza kilikua kinatoka kwenye meno yangu. Nikajichanganya na maguide, mmoja rasi akanichukua. Nilikua napiga sana pesa. Wazungu wakawa wanachukua namba zangu aisee, hadi leo sijawahi kwenda nje ya inchi ila itakua haikupangwa na Mungu kwa mimi kwenda nje ya nchi manake kila kitu kilikua nje nje, nikiwa kule mlimani nikapata taarifa nimepata chuo mlimani. Nikatoroka wazungu nikarudi chini(duniani) tangu siku hiyo sijawaza tena wazungu na niliposoma nawachukia wazungu hadi leo. Namshukuru Mungu maisha yangu safi na nawaona wazungu ni sawa tu na mimi kila kitu.
Ila mlima una maajabu sana. Nimepanda mara 11 nimefika kileleni mara nne ila sikuwahi hata siku moja kuacha kushangaaa kule juu, kila siku ni siku ya kushangaa achilia mbali msitu na yale mawe kuna barafu pale juuu zimejipanga kama maua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom