SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 417
- 1,285
- Thread starter
- #181
DO NOT SHOUT
(usipige kelele)
Season 2
Sehemu ya.........01
Mtunzi Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA
Mazungumzo haya yaliyoibua maswali mengi kwenye kichwa cha Yusto aliyekuwa mlangoni anawasikiliza, akawa haelewi ni nini kinaendelea.
"Caren, kwani wewe ni nani?"
Yusto alijiuliza swali ambalo hakuwa na majibu yake, lakini tayari alishaanza kuhisi kitu.
JE, NINI KITAFUATA.?
SASA ENDELEA...
Mazungumzo ya John na mama yake madam Jane yalionekana kutokuwa na manufaa yoyote kwa john, hakuwa amepata kile alichokuwa akikitafuta lakini tayari alihisi kuwa kuna jambo mama yake analificha. Alihisi kuna Siri nzito iliyokuwa imejificha kati ya mama yake na mama yake Yusto, akatamani kujua. Baada ya kutoka ndani ya ofisi ya mama yake John alipiga tena simu kwa kijana wake wa kazi Abdullah.
"Vipi anaendeleaje huyo mwenzio aliyepigwa risasi"
"Kwa sasa yupo vizuri bosi tayari tumesha muhudumia"
" Okay, sasa sikia, fuatilia hakikisha Kama kweli Yusto na mama yake wamekufa kwenye ule mripuko Kisha utanipa taarifa mimi narudi chuoni kupumzika" Alisema John
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda mfupi tu baada ya John kutoka ndani ya ofisi ya mama yake mara aliingia mtu mwingine ambaye ndiye aliekuwa amepewa kazi na madam Jane ya kufuatilia taarifa za yule mwanamke kichaa Zubeba.
"Enhe nambie imekuwaje" madam Jane alianzisha mazungumzo baada ya kusalimiana na yule mtu.
"Bosi nimemfuatia Zubeba yupo na alikua anashinda kwenye lile jalala jirani na soko la matunda Huwe.
lakini kuna taarifa nimepata kuwa kuna watu walifika wakamkamata kwa nguvu wakamuingiza ndani ya gari na kuondoka nae leo, hatujajua ni akina nani wala walipompeleka bado tunaendelea kufuatilia"
Hizi zilikua ni taarifa ambazo kwa kiasi zilimfanya madam Jane kuamini kile alichokuwa akihisi ni sahihi.
" Sitaki John ajue chochote kabla sijalipa kisasi changu kwa baba yake, naomba mtafute Zubeda popote alipo na ikibidi muueni"
"Lakini bosi yule mwanamke si ni kichaa tu, wasiwasi wako nini?"
"Vichaa wengi huwa hawapotezi kumbukumbu za mambo muhimu yaliyotokea kwenye maisha yao, nilifanya makosa kumuacha hai, tayari John ameanza kuulizia taarifa zake lolote linaweza kutokea, alafu tangu lini ukaniuliza maswali nikikupa kazi?" Madam Jane aliuliza kwa ukali kidogo
"Samahani bosi, kwa hiyo nitumie njia gani kumuua, au niwatumie vijana wako"
"Hili jambo linatakiwa kwenda kimya kimya sana kwa sababu nahisi John anaweza akawa anahusika au anafuatilia pia, nitafutie kijana mmoja makini mwenyewe uwezo mkubwa kule kambini afanye hii kazi" alisema madam Jane.
"Aah sawa bosi yupo binti mmoja makini sana anaweza kuifanya hii kazi vizuri lakini tayari yupo kwenye ile misheni ya kuchafua sifa ya chuo cha mark moon"
"Ni nani huyo?"
"Diana kwa Sasa tunamwita CAREN"
"Ooh Caren kale ka binti kazuri tuliko kachukua Burundi na mama yake tulimpeleka India kutibiwa bila shaka"
"Eeh huyo huyo, Sasa hivi yule mwanamke ni mashine ya kazi yuko vizuri sana atatusaidia"
"Lakini Mimi siamini wanawake, hebu tafuta mwingine"
"Bosi mimi pia huwa siamini wanawake lakini Caren ni mtu na nusu, anaweza sana kazi yule binti"
"Okay! muite basi Sasa hivi nionane naye"
Alisema madam Jane.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Yusto akiwa bado yuko pale mlangoni aliendelea kusikiliza mazungumzo kati ya Revocatus na yule msichana. Baada ya kumaliza mazungumzo hayo Revo alielekea moja moja kwenye chumba alichokuwepo Yusto.
Yusto baada ya kuona hivyo alikimbia na kwenda kujitupa kitandani akatulia kimya Kama vile bado hajaamka. Revocatus aliingia akamtazama kwa muda, akagundua kuwa drip ya maji ilikuwa imechomolewa, akatabasamu.
"Naona umeamka, haya inuka twende ukamuone mama yako" alisema Revo kisha akaanza kutembea kuondoka.
Yusto aliendelea kujituliza kimya lakini mwisho akafumbua macho akamtazama Revocatus ambaye tayari alishafika mlangoni, akageuka nyuma.
"oy twende basi" alisema Revo
Taratibu yusto aliinuka pale kitandani kisha akaanza kumfuata Revo huku mara kadhaa akimuangalia kwa macho ya kuibia ibia. Walianza kutembea wakiwa wamefuatana wakikatisha vyumba kadhaa ndani ya jengo hilo lililojengwa kwa muundo wa ajabu sana.
"Najua unamaswali mengi sana unatamani kuniuliza, usijali Caren atakueleza kila kitu. Muhimu kujua kwa sasa ni kwamba Mimi sio mume wa Caren kama unavyozani wala Caren hana mtoto Kama ulivyoambiwa na Sophia, kulikuwa na sababu ya sisi kufanya vile" alisema Revo kiasi cha kumfanya Yusto amtazame sana.
Mwisho waliingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na vitanda viwili ndani yake, kimoja upande wa kushoto na kingine kulia.
Upande mmoja alilala Caren na upande mwingine alilala Zubeba mama mlezi wa Yusto.
Hali ya mama yake Yusto ndio ilionekana kuwa mbaya zaidi, alikuwa amewekewa mashine maalum inayomsaidia kupumua. Yusto na Revo walifika na kusimama katikati yao.
"Mama....Caren" Yusto aliita akionyesha kuwa na wasiwasi zaidi hasa na mama yake aliekuwa anapumulia mashine.
"Usijali wote wawili watapona" alisema Revo kisha akamgeukia Yusto na kumshika begani.
"Sikiliza Yusto, Caren amejitoa sana kwa ajili yako ameweka rehani kila kitu chake kwanzia kazi hadi ndugu zake kwa ajili mapenzi yake kwako, anafanya hivyo kwa sababu anakupenda sana na kukuamini. Kama nilivyo kwambia siwezi kusema kila kitu lakini naomba nikupe onyo, ukifanya jambo lolote la kipuuzi ukahatarisha usalama wa Caren, nitakupasua mwenyewe kwa mikono yangu"
Alisema Revocatus Kisha akageuka na kuondoka, akamuacha Yusto mle ndani akiwa amesimama na kutulia kimya akiyatafakari maelezo ya Revo yaliyoonekana kuwa na maana zaidi ya moja. Akawa anawatazama Caren na mama yake kwa zamu.
Hawa walikuwa ni wanawake muhimu sana kwenye maisha yake aliwapenda pengine kuliko kitu kingine chochote.
Yusto aliendelea kusimama akiyatafakari maelezo ya Revo hali akitamani kujua zaidi ni kwa nini Caren anafanya yote yale, ni vitu gani alivyoviweka rehani kwa ajili yake? kwa nini alidanganya akijifanya mke wa mtu na mama wa mtoto? ni nini kinaendelea? Hivi ni baadhi kati ya vitu vingi ambavyo Yusto alitamani kuvijua kutoka kwa Caren.
Taratibu alisogea na kupiga magoti pembeni ya kitanda alicholala Caren.
Akawa anaitazama sura nzuri ya mwanamke huyo ambae alikuwa ni mrembo haswa. Alisahau kabisa kama walikuwa kwenye ugomvi mkubwa masaa kadhaa yaliyopita.
" Caren, siwezi kujizuia kuacha kukupenda, moyo wangu unagoma kabisa kuwa mbali na wewe, siwezi, sijui ukiamka utaniambia nini mama, naogopa. Lakini sijali hata kukiwa na sababu mia moja zakukuacha nitatafuta sababu moja tu ya kuendelea kuwa na wewe Caren wangu, nakupenda, nakupenda sana Caren"
Yusto alikuwa akiongea kwa hisia kali huku akiwa ameung'ang'ania mkono wa Caren. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda mbio, machozi yalikuwa jirani kabisa kumtoka akajikuta anashindwa kuhimili, taratibu akasimama na kuanza kuondoka.
"Yustoo"
Akiwa amefika mlango ni kama alisikia sauti imemuita, akasimama ghafula huku akijiuliza amesikia vibaya au ni kweli ameitwa.
Taratibu akageuka,
Yusto hakuamini pale alipomuona Caren akiwa amefumbua macho yake anamtazama.
Caren alikuwa amerejewa na fahamu zake tangu mda mrefu lakini aliyafumba macho yake Kama vile bado hajazinduka, maneno yote aliyozungumza Yusto aliyasikia, akajikuta anaumia na kupata faraja kwa wakati mmoja.
"Ca.. Caren" Yusto aliita,
Caren akiwa na sura ya huzuni alinyoosha mikono yake akimtaka Yusto aje kumkumbatia.
JE, NINI KITAFUTA
Nini hatima ya wawili hawa wanaopendana ?
Vipi kama madam jane atampa Caren kazi ya kumuua mama mlezi wa Yusto?
Nini kitatokea?
Harakati za John zitaishia wapi?
ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA.
Season 2 na season 3 ya mwisho zote zipo tayari njoo WhatsApp
0756862047
(usipige kelele)
Season 2
Sehemu ya.........01
Mtunzi Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA
Mazungumzo haya yaliyoibua maswali mengi kwenye kichwa cha Yusto aliyekuwa mlangoni anawasikiliza, akawa haelewi ni nini kinaendelea.
"Caren, kwani wewe ni nani?"
Yusto alijiuliza swali ambalo hakuwa na majibu yake, lakini tayari alishaanza kuhisi kitu.
JE, NINI KITAFUATA.?
SASA ENDELEA...
Mazungumzo ya John na mama yake madam Jane yalionekana kutokuwa na manufaa yoyote kwa john, hakuwa amepata kile alichokuwa akikitafuta lakini tayari alihisi kuwa kuna jambo mama yake analificha. Alihisi kuna Siri nzito iliyokuwa imejificha kati ya mama yake na mama yake Yusto, akatamani kujua. Baada ya kutoka ndani ya ofisi ya mama yake John alipiga tena simu kwa kijana wake wa kazi Abdullah.
"Vipi anaendeleaje huyo mwenzio aliyepigwa risasi"
"Kwa sasa yupo vizuri bosi tayari tumesha muhudumia"
" Okay, sasa sikia, fuatilia hakikisha Kama kweli Yusto na mama yake wamekufa kwenye ule mripuko Kisha utanipa taarifa mimi narudi chuoni kupumzika" Alisema John
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda mfupi tu baada ya John kutoka ndani ya ofisi ya mama yake mara aliingia mtu mwingine ambaye ndiye aliekuwa amepewa kazi na madam Jane ya kufuatilia taarifa za yule mwanamke kichaa Zubeba.
"Enhe nambie imekuwaje" madam Jane alianzisha mazungumzo baada ya kusalimiana na yule mtu.
"Bosi nimemfuatia Zubeba yupo na alikua anashinda kwenye lile jalala jirani na soko la matunda Huwe.
lakini kuna taarifa nimepata kuwa kuna watu walifika wakamkamata kwa nguvu wakamuingiza ndani ya gari na kuondoka nae leo, hatujajua ni akina nani wala walipompeleka bado tunaendelea kufuatilia"
Hizi zilikua ni taarifa ambazo kwa kiasi zilimfanya madam Jane kuamini kile alichokuwa akihisi ni sahihi.
" Sitaki John ajue chochote kabla sijalipa kisasi changu kwa baba yake, naomba mtafute Zubeda popote alipo na ikibidi muueni"
"Lakini bosi yule mwanamke si ni kichaa tu, wasiwasi wako nini?"
"Vichaa wengi huwa hawapotezi kumbukumbu za mambo muhimu yaliyotokea kwenye maisha yao, nilifanya makosa kumuacha hai, tayari John ameanza kuulizia taarifa zake lolote linaweza kutokea, alafu tangu lini ukaniuliza maswali nikikupa kazi?" Madam Jane aliuliza kwa ukali kidogo
"Samahani bosi, kwa hiyo nitumie njia gani kumuua, au niwatumie vijana wako"
"Hili jambo linatakiwa kwenda kimya kimya sana kwa sababu nahisi John anaweza akawa anahusika au anafuatilia pia, nitafutie kijana mmoja makini mwenyewe uwezo mkubwa kule kambini afanye hii kazi" alisema madam Jane.
"Aah sawa bosi yupo binti mmoja makini sana anaweza kuifanya hii kazi vizuri lakini tayari yupo kwenye ile misheni ya kuchafua sifa ya chuo cha mark moon"
"Ni nani huyo?"
"Diana kwa Sasa tunamwita CAREN"
"Ooh Caren kale ka binti kazuri tuliko kachukua Burundi na mama yake tulimpeleka India kutibiwa bila shaka"
"Eeh huyo huyo, Sasa hivi yule mwanamke ni mashine ya kazi yuko vizuri sana atatusaidia"
"Lakini Mimi siamini wanawake, hebu tafuta mwingine"
"Bosi mimi pia huwa siamini wanawake lakini Caren ni mtu na nusu, anaweza sana kazi yule binti"
"Okay! muite basi Sasa hivi nionane naye"
Alisema madam Jane.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Yusto akiwa bado yuko pale mlangoni aliendelea kusikiliza mazungumzo kati ya Revocatus na yule msichana. Baada ya kumaliza mazungumzo hayo Revo alielekea moja moja kwenye chumba alichokuwepo Yusto.
Yusto baada ya kuona hivyo alikimbia na kwenda kujitupa kitandani akatulia kimya Kama vile bado hajaamka. Revocatus aliingia akamtazama kwa muda, akagundua kuwa drip ya maji ilikuwa imechomolewa, akatabasamu.
"Naona umeamka, haya inuka twende ukamuone mama yako" alisema Revo kisha akaanza kutembea kuondoka.
Yusto aliendelea kujituliza kimya lakini mwisho akafumbua macho akamtazama Revocatus ambaye tayari alishafika mlangoni, akageuka nyuma.
"oy twende basi" alisema Revo
Taratibu yusto aliinuka pale kitandani kisha akaanza kumfuata Revo huku mara kadhaa akimuangalia kwa macho ya kuibia ibia. Walianza kutembea wakiwa wamefuatana wakikatisha vyumba kadhaa ndani ya jengo hilo lililojengwa kwa muundo wa ajabu sana.
"Najua unamaswali mengi sana unatamani kuniuliza, usijali Caren atakueleza kila kitu. Muhimu kujua kwa sasa ni kwamba Mimi sio mume wa Caren kama unavyozani wala Caren hana mtoto Kama ulivyoambiwa na Sophia, kulikuwa na sababu ya sisi kufanya vile" alisema Revo kiasi cha kumfanya Yusto amtazame sana.
Mwisho waliingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na vitanda viwili ndani yake, kimoja upande wa kushoto na kingine kulia.
Upande mmoja alilala Caren na upande mwingine alilala Zubeba mama mlezi wa Yusto.
Hali ya mama yake Yusto ndio ilionekana kuwa mbaya zaidi, alikuwa amewekewa mashine maalum inayomsaidia kupumua. Yusto na Revo walifika na kusimama katikati yao.
"Mama....Caren" Yusto aliita akionyesha kuwa na wasiwasi zaidi hasa na mama yake aliekuwa anapumulia mashine.
"Usijali wote wawili watapona" alisema Revo kisha akamgeukia Yusto na kumshika begani.
"Sikiliza Yusto, Caren amejitoa sana kwa ajili yako ameweka rehani kila kitu chake kwanzia kazi hadi ndugu zake kwa ajili mapenzi yake kwako, anafanya hivyo kwa sababu anakupenda sana na kukuamini. Kama nilivyo kwambia siwezi kusema kila kitu lakini naomba nikupe onyo, ukifanya jambo lolote la kipuuzi ukahatarisha usalama wa Caren, nitakupasua mwenyewe kwa mikono yangu"
Alisema Revocatus Kisha akageuka na kuondoka, akamuacha Yusto mle ndani akiwa amesimama na kutulia kimya akiyatafakari maelezo ya Revo yaliyoonekana kuwa na maana zaidi ya moja. Akawa anawatazama Caren na mama yake kwa zamu.
Hawa walikuwa ni wanawake muhimu sana kwenye maisha yake aliwapenda pengine kuliko kitu kingine chochote.
Yusto aliendelea kusimama akiyatafakari maelezo ya Revo hali akitamani kujua zaidi ni kwa nini Caren anafanya yote yale, ni vitu gani alivyoviweka rehani kwa ajili yake? kwa nini alidanganya akijifanya mke wa mtu na mama wa mtoto? ni nini kinaendelea? Hivi ni baadhi kati ya vitu vingi ambavyo Yusto alitamani kuvijua kutoka kwa Caren.
Taratibu alisogea na kupiga magoti pembeni ya kitanda alicholala Caren.
Akawa anaitazama sura nzuri ya mwanamke huyo ambae alikuwa ni mrembo haswa. Alisahau kabisa kama walikuwa kwenye ugomvi mkubwa masaa kadhaa yaliyopita.
" Caren, siwezi kujizuia kuacha kukupenda, moyo wangu unagoma kabisa kuwa mbali na wewe, siwezi, sijui ukiamka utaniambia nini mama, naogopa. Lakini sijali hata kukiwa na sababu mia moja zakukuacha nitatafuta sababu moja tu ya kuendelea kuwa na wewe Caren wangu, nakupenda, nakupenda sana Caren"
Yusto alikuwa akiongea kwa hisia kali huku akiwa ameung'ang'ania mkono wa Caren. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda mbio, machozi yalikuwa jirani kabisa kumtoka akajikuta anashindwa kuhimili, taratibu akasimama na kuanza kuondoka.
"Yustoo"
Akiwa amefika mlango ni kama alisikia sauti imemuita, akasimama ghafula huku akijiuliza amesikia vibaya au ni kweli ameitwa.
Taratibu akageuka,
Yusto hakuamini pale alipomuona Caren akiwa amefumbua macho yake anamtazama.
Caren alikuwa amerejewa na fahamu zake tangu mda mrefu lakini aliyafumba macho yake Kama vile bado hajazinduka, maneno yote aliyozungumza Yusto aliyasikia, akajikuta anaumia na kupata faraja kwa wakati mmoja.
"Ca.. Caren" Yusto aliita,
Caren akiwa na sura ya huzuni alinyoosha mikono yake akimtaka Yusto aje kumkumbatia.
JE, NINI KITAFUTA
Nini hatima ya wawili hawa wanaopendana ?
Vipi kama madam jane atampa Caren kazi ya kumuua mama mlezi wa Yusto?
Nini kitatokea?
Harakati za John zitaishia wapi?
ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII YA KUSISIMUA.
Season 2 na season 3 ya mwisho zote zipo tayari njoo WhatsApp
0756862047