Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

Do not SHOUT

Sehemu ya...........05
Mtunzi: Saul David.
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Madam Jane akawaza pia namna atakavyo endelea kulipa kisasi kwa mumewe wa zamani tajiri mark moon, tayari alishafanikiwa kwa hatua kadhaa na sasa aliwaza kuelekeza nguvu zake kwenye chuo kikubwa cha mark moon bila kujua kuwa mwanae wa kwanza Yusto yupo hai na ni mmoja kati ya watu wanaokilinda chuo hicho, na ndio huyo huyo aliemchoma kisu John.

Je, nini kitafuata....?
*****
SONGA NAYO....
Caren alionekana akiwa amekaa kitandani ndani ya chumba kimoja tulivu,
Pembeni ya kitanda alichokaa kulikuwa na kitanda kingine ambacho juu yake alikuwa amelala mama mlezi wa Yusto.

Tayari yalikua yamepita masaa kadhaa tangu Caren alipotoka kuonana na madam Jane. Kichwa chake kilikua kinauma kutokana mtihani mkubwa uliokua mbele yake.
Madam Jane alimtaka amuue mama huyo ambaye alikua ni mama wa mpenzi wake Yusto.
Caren alimuheshimu na kumpenda sana Madam Jane kwani ndiye mtu pekee alieweza kumshika mkono yeye na familia yake ndipi walipokua na hali mbaya kule nchini Burundi.
Licha ya hayo yote lakini Caren moyo wake ulikua mzito mno kutekeleza jukumu alilopewa na madam Jane, alitakiwa kuua, jambo ambalo hakuwahi kufanya Wala kuwaza kulifanya, auwe? tena sio kuua tu, bali amuuwe mama mkwe wake, hakika ulikua ni mtihani mkubwa kwake.

Wakati akizidi kutafakari hayo Mara ghafula yule mama(Zubeda) alikurupuka pale kitandani huku akipiga kelele, fahamu zilikuwa zimemrejea baada ya purukushani nzito kule bandarini. Caren alimuwahi kumzuia asianguke.

"Tulia mama utaumia hebu tulia kwanza"

"Niachenii...niachenii mnataka kuniua,
Mwanangu Yuko wapi, Yusto wangu yuko wapiiiii......Yustoooo."

Zubeda alipiga kelele huku akiliita jina la Yusto.

"Sikiliza mama hebu tulia kwanza, Yusto yupo atakuja....."

"Muongo nyinyi ni wauaji mmetumwa na janeth mje kuniua sitaki niacheniiii....."
Zubeda aliendelea kupiga kelele licha ya kwamba alikua mlemavu wa akili lakini Mambo aliyozungumza kwa kiasi yalimgusa Caren.

"Mama sikiliza, hapa uko salama sisi sio watu wabaya hakuna atakaekudhuru hapa"

"Hahahah wahuni nyie, hata Mara ya kwanza mliniambia hivo hivo mkanibeba kwenye gari lenu, madam Jane anataka kuniua tena, kila wakati huwa anashindwa amewatuma na ninyi mmeniua Mara ya kwanza nimefufuka manataka kuniua tenaa... hahahahah"

Zubeda aliongea huku akizidi kupiga kelele akimtaka Caren amuachie,
Wakati huo Revocatus aliingia ndani ya chumba hicho baada ya kuzisikia kelele za zubeda. Mkononi akiwa na bomba ndogo ya sindano yenye dawa ndani yake.

"Unamfahamu Madam Jane?" Caren aliuliza.
"Msatili muuaji yule mwanamke, namfahamu"
"Unamfahamu vipi mama?"
"Anauza matunda pale gengeni"
Alijibu zubeda kauli iliyomfanya Caren kuduwaa tena kwa mara nyingine.
Lakini mara Revocatus akadakia na kuuliza swali jingine.
"Madam Jane alikufanya nini kwani"
"Alitaka kuniuaa, Mimi na mtoto wake, tukakimbia, bado anatutafuta, tunaendeleaa kukimbiaa..."
Alisema Zubeda kauli iliyomfanya Caren na Revocatus watazamane.

Mara zubeda alikurupuka kwa Mara nyingine akitaka kumvaa Caren lakini Caren alimuwahi akamshika, hapo Revocatus akachomeka ile sindano kwenye drip ya maji aliyotundikiwa Zubeda kisha akanyunyuzia ile dawa, ndani ya sekunde chache Zubeda akatulia kimya na kulala.

"Caren japokuwa huyu mama ni kichaa lakini kunakitu nahisi hakipo sawa Kati yake na bosi wetu" Revo alizungumza kwa sauti ya kunong'ona.
"Ni kweli Revo kuna wakati haeleweki lakini nahisi kuna siri hapa ndio maana Madam Jane kaniagiza nimuue yani nachanganyikiwa mimi, hata sijui nafanyaje"

"Aisee Kama nilivyokwambia Caren, chukua mda tafakari amua cha kufanya, mimi niko nyuma yako kwa maamuzi yoyote utakayoyafanya"

"Asante Revo, sijaona tatizo kukushirikisha kwa sababu najua wewe ndio mtu pekee waweza simama upande wangu"
"Usijali Caren tuko pamoja, kwa hiyo unafanyaje"
"Nataka nijue kwanza nini kipo katikati ya mama hapa na bosi nikishajua nitajua pia nini kifuatae"

"Utajua vipi?"
" Daktari, nitatafuta Daktari wa vichaa atakuja hapa kuongea na huyu mama najua wao wanawaelewa zaidi kuliko sisi naweza pata mwanga angalau"
"Ooh wazo zuri Caren"

Alisema Revo kisha haraka wakaanza kumtafuta Daktari mtaalum wa magonjwa ya saikolojia na akili.
****

Shamla shamla za hapa na pale ziliendelea katika chuo cha MARK MOON PSP INTERNATIONAL UNIVERSITY chuo cha kisasa kinachomilikiwa na bosi Mark moon.
Hiki kilikua ni kipindi cha uchaguzi, kipindi ambacho wanafunzi huwania ngazi na nafasi mbalimbali za uongozi chuoni hapo.
Ngazi iliyokua imeteka hisia za watu wengi ni ngazi ya RAIS WA CHUO, wanafunzi wengi walikua wakisubiria kwa hamu majina mawili yatakayo pitishwa na tume ya uchaguzi chuoni hapo kuwania nafasi adhimu nafasi ya Rais wa chuo.

Naam hatimae siku ilikua imewadia majina yakatangwaza na JOHN( Master Joo) akawa ni mmoja kati ya wawili wanaowania nafasi ya Rais wa chuo.
Ambonike Mwakalebela kijana kutoka mbeya yeye ndiye alikua mgombea wa pili wa nafasi hiyo.

Hivyo ndivyo walivyokua wakitegemea wanafunzi wengi chuoni hapo John na Ambonike ilikua ni ushindani mkubwa uliovuta hisia za watu wengi.
John akiamini kabisa kwa kutumia ushawishi wa fedha zake basi hakuna kitu kingeharibika, lakini Ambonike naye akiamini kutokana na ushawishi mkubwa alionao mbele za watu.

Taarifa hizi zilisambaa kwa kasi sana chuoni hapo, watu wakawa wanasubiri kwa hamu kampeni zitakapoanza.
John akiwa tayari ametoka hospitali baada ya kujeruhiwa na Yusto Sasa alianza mikakati kuhakikisha anaichukua nafasi hiyo ya Rais wa chuo.
******

Katika chuo hicho cha mark moon ndani ya chumba kimoja cha Siri, kulikua na kikao muhimu sana cha Siri kilichokuwa kikiendelea.
Mark Moon mwenyewe ndiye aliyekua akiongoza kikao hicho, alifika chuoni hapo kwa siri akiingilia mlango wa nyuma wa chuo hicho pasipo kujulikana.

Kikao hicho kilikua mahususi kwa watu wa ulinzi na usalama wa chuo hicho na moja kati ya watu waliohudhuria alikuwepo Yusto, Frank pamoja na wale majasusi watatu yaani Brandina, Simigo na Mpili.

Ilikua ni desturi ya mark Moon kuitisha kikao cha aina hiyo mara tu kinapowadia kipindi cha uchaguzi, ukizingatia tayari chuo chake kilikua kinaandamwa na matukio ya ajabu hivyo ilimlazimu kuchukua tahadhari.

Jambo ambalo mark Moon hakujua ni kuwa tayari alikua katika vita kali dhidi na mkewe wa zamani (X-wife) madam Jane.
Mbaya zaidi mtoto wake wa kiume John ambaye hajui Kama Mark moon ni baba yake wala baba hamjui mwanae ndiye aliyekua anagombea nafasi kubwa ya Urais wa chuo chake.

Je, nini kitafuata?

Vipi kuhusu Caren na mama Yusto (Zubeda).

ITAENDELA....

0756862047(full story)
 
𝗗𝗢 𝗡𝗢𝗧 𝗦𝗛𝗢𝗨𝗧
𝘀𝗲𝗮𝘀𝗼𝗻 2
Sehemu ya............ 6
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA ...
Jambo ambalo mark Moon hakujua ni kuwa tayari alikua katika vita kali dhidi na mkewe wa zamani (X-wife) madam Jane. Mbaya zaidi mtoto wake wa kiume John ambae hajui Kama Mark moon ni baba yake wala baba hamjui mwanae ndiye aliyekua anagombea nafasi kubwa ya Urais wa chuo chake.

Je, nini kitafuata?

SONGA NAYO....
****
Kikao kilichukua mda mfupi, Mark moon pamoja na wafanyakazi wake wakapanga mikakati namna ya kuimarisha ulinzi chuoni hapo kuhakikisha hakuna jambo lolote baya linatokea katika kipindi hicho muhimu cha uchaguzi wa viongozi.
Kwa sasa hali ilikua shwari , hakukua kumetokea tukio lingine la kutishia usalama wa wanafunzi, ingawa hawakufanikiwa kumpata mhusika wa matukio hayo baada ya mtu waliekuwa wakimhisi (Caren) kuwapoteza maboya,
Lakini mark moon aliwataka Simigo na wenzake kuhakikisha wanaongeza jitihada kumpata mhusika na wasiruhusu tukio lingine tena.

Mwisho alihairisha kikao chake na kila mmoja akatakiwa kurudi kwenye nafasi yake. Brandina alikua wa kwanza kufika mlango lakini akasimama macho yake akiwa anamtazama Yusto kijana aliyekua ameuteka moyo wake vilivyo.

Ulikua umepita muda sasa tangu Brandina na Yusto walipokutana kwa mara ya mwisho hakika moyo wake ulikua umemmiss sana kijana huyo.

Mwisho aliwano Yusto na Frank wanakuja, Brandina aliachia tabasamu mwanana kiasi cha kuufanya mwanya wake mzuri uonekane.

"Mambo vipi brandina" Yusto alikua wa kwanza kumsalimia

Lakini kabla Brandina hajaitikia salamu hiyo Mara alisikia sauti ikimwita kutokea ndani ya kile chumba walichokua wakifanyia kikao.

"Abeeh" Brandina aliitika Kisha wote wakageuka kuangalia sauti ilikotokea, kwa mbali wakamuona bosi Mark Moon akimpungia mkono akimtaka asogee.
Brandina alishtuka kiasi, hakujua bosi mark moon amemuita kwa sababu gani, haikua kawaida kabisa.
Akasogea taratibu hadi pale alipokua bosi Mark moon na watu wake, Yusto na Frank wakabaki wanataza kwa mbali.

"Ndio bosi"
"Brandina, si ndio"
"Yah ndio mimi bosi"
"Tunaweza kuongozana tafadhali nina mazungumzo na wewe"
Alisema mark moon .
Mwisho Brandina na mark moon waliondoka wakiwa wameongozana, Yusto na Frank wakawa wanasindikiza kwa macho.

"Oya.. Yusto"
"Nambie"
"Ulikua wapi unajua sikuelewi ratiba zako siku hizi, unatoka tu huniagi unarudi husemi chochote, umekuwaje mshkaji wangu?" Frank aliuliza

"Aah..sio hivyo Frank unajua kuna baadhi ya vitu natakiwa kudili navyo mwenyewe sitaki nikusumbue sana kwa matatizo yangu binafsi"

"Sio kweli Yusto, umekua msiri sana siku hizi mtu wangu alafu mwanzo haukuwa hivyo, Sophia ameumia chumbani kwako kalazwa hujasema lolote, umeondoka ghafula tu ukabeba hadi na siraha yako umerudi hujasema lolote" Frank alilalamika

"Sio hivyo mtu wangu, basi nisamehe nitakwambia kila kitu, unajua John alimteka mama"
"Nini wewe? mama gani! mama kule jalalani?"
"Yah mama yangu"
"La haulaa, alimjuwaje sasa? enhe! ikawaje" Frank aliuliza kwa bashasha

"Alimteka mama Kisha akanitisha akitaka niachane na Caren"

"Atiii, kwani wewe na Caren mna nini,ni wapenzi au?"Kila kitu kilionekana kuwa kigeni kwa Frank.
Yusto alibaini kuwa ni kweli alikua amemficha rafiki yake vitu vingi mno.

"Ee sisi ni wapenzi tuliachana na tumerudiana, sa sikia unajua ilikua kidogo mimi na mama tufe alimpeleka sijui wapi huko kwenye makontena ya bandarini, kwa bahati nzuri Caren na wenzake wakatokea na kutusaidia"

"Wenzake, akina nani? Caren anawenzake gani? Alafu yule si ameolewa na anamtoto kwani hukusikia jamaangu" aliuliza Frank
Yusto akapatwa na kigugumizi kutoa maelezo mengine zaidi ilikua ni kuvunja makubaliano yake na Caren.
Hakutakiwa kumweleza mtu ile siri aliyoelezwa na Caren kuhusu uhalisia wake.

"Mbona kimya?"
"Mmh hebu subiri unajua Caren kanipigia sana wakati tupo kwenye kikao, sikupokea simu yake" alisema Yusto huku akizuga kwa kuitazama simu yake.

Ni kweli Caren alikua amempigia simu mara kadhaa baada ya kuona simu haipokelewi akamtumia sms.

"MPENZI MAMA AMEAMKA ANATAKA KUKUONA ANATUSUMBUA SANA"

Ilikuwa ni sms iliyomfanya Yusto kupatwa na ubaridi wa furaha, akajaribu kumpigia simu Caren ili ampe maelekezo zaidi kwani hakuwa akijua ile kambi ndogo ya akina Caren mahali ilipo. Kwa bahati mbaya simu ya Caren ikawa haipatikani.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Caren alionekana akiwa amesimama nje ya chumba alicholazwa zubeda mama mlezi wa Yusto.
Caren alikua akitembea anapiga hatua huku kisha anarudi tena, alionekana ni mtu mwenye mawazo sana mda huo.

Ndani ya chumba kilichokuwa mbele ya Caren alionekana Daktari wa magonjwa ya saikolojia na akili akiongea na Zubeda huku mkononi akiwa na picha kubwa na madam Jane, ya zamani na ya sasa.

Caren aliendelea kubaki pale nje huku akisubiria kwa hamu majibu kutoka kwa daktari.
Alitamani sana kujua ni uhusiano gani uliokuwepo kati ya zubeda mama mlezi wa Yusto na bosi wake madam Jane.
Aliamini lazima Daktari angekuja na majibu yatakayompa mwanga.

Hatimae dakika chache baadae daktari alitoka.

" Niambie Daktari, vipi umepata chochote?" Caren aliuliza kwa bashasha
"Aah ndio, kuna vitu vingi sana nimebaini kutoka kwa huyu mama kichaa, vipi tunaweza kuketi tukazungumza"
"Sawa twende kile chumba pale"
Alisema Caren Kisha wakaongozana na Daktari.
Wakiwa bado njiani walikutana na Revocatus.
"Revo naongea na daktari mara moja, naomba muone mama mle ndani asije kuleta vurugu tena" alisema Caren.
Revo akatikisa kichwa kukubaliana na maelezo hayo, Kisha akawa anawatazama Caren na daktari wakati wanaingia kwenye kile chumba kwa ajili ya mazungumzo.

Lakini macho ya Revocatus yalionyesha wazi kuwa naye alikua na jambo lake tena jambo la siri sana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Kwanza kabla sijaendelea Yusto ni nani?" Daktari aliuliza swali kabla ya kuanza kutoa majibu ya kile alichokipata baada ya kufanya mazungumzo na mama kichaa Zubeda.

"Ni kijana flani hivi sijui hata nikuelezaje ila amelelewa na huyo mama kabla hajaugua kichaa"

"Ooh kumbe, sio mtoto wake wa kumzaa si ndio"
"Hapana ni mama mlezi tu"

"Yes, ni Kama nilivyotegemea"
" Una maana gani Daktari"
"Aah nilichobaini ni kwamba madam Jana aliwahi kuwa mtu wa karibu na huyu mama kichaa lakini kuna Jambo lilitokea likawafanya wao kuwa maadui kiasi cha kumfanya madam Jane ajaribu kumuuwa huyu mama na mtoto wake anaemwita Yusto zaidi ya Mara moja, huyu mama anadai Yusto ni mtoto wa madam Jane yaani madam Jane ndio aliyemzaa Yusto lakini kuna Jambo lilitokea likamfanya madam Jane kutaka kuwauwa wote huyu mama na mtoto wake lakini walinusurika"

Daktari alitoa maelezo yaliyomfanya Caren abaki mdomo wazi, haikua rahisi kuamini kile alichokisikia

"Eti nini, Yusto ni mtoto wa madam Jane?"
"Ndio, nina uhakika wa asilimia 99%, binti mimi ni daktari wa vichaa naelewa vizuri Code za watu wa aina hii, Yusto ni mtoto wa madam Jane amini ninachokwambia" Daktari alisisitiza.

"Hapana haiwezekani Dr kivipi yani?"
"Binti sina sababu yoyote ya kuongea kitu ambacho sina uhakika nacho, mimi nimefanya kazi uliyoniambia"

Caren alitulia kimya baada ya kuona daktari anaongea kwa kukaanisha.
Caren akajaribu kuunganisha baadhi ya matukio, alikumbuka ni kweli Yusto alimwambia kuwa hakua akimfahamu mama wala baba yake mzazi, Zubeda alikua ni mama mlezi tu kwake.

Caren alivuta pumzi ndeefu, kisha akaitoa taratibu.

"Sawa Dr nimekuelewa, vipi kingine kipi natakiwa kujua."

"Aah hayo ndio muhimu sana labda kingine nikutoe tu hofu kuwa kichaa cha mama sio kikubwa sana, anajielewa kwa kiasi, haitochukua mda mrefu anaweza kupona na Kama mtampeleka hospitali ya vichaa itakuwa ni nzuri zaidi, huyu mama anampenda sana Yusto lakini anamchukia sana Madam Jane ni hivyo tu" alisema Dr

Baada ya maelezo hayo Caren alichukua simu yake akampigia Revocatus.
Simu ya Revocatus ilisikika ikiita mlangoni nje ya chumba walichokuwepo Caren na Daktari.
Caren akakata simu,
Revo akafungua mlango na kuingia ndani.

"kumbe ulikua hapa" aliuliza Caren huku akimtazama Revo usoni
"Aah ee...ndio.. nimekuja sio mda mama ameshalala kule"
Revo aliongea kwa kujiuma uma lakini ukweli alikua mlango tangu kitambo na alikua akifuatilia mazungumzo yote kati ya Caren na Daktari tangu mwanzo.
Ilionekana wazi kuwa Revocatus alikua anajambo lake analolifanya kwa Siri licha ya kwamba yeye na Caren waliaminiana sana.

" Amelala kivipi, umemchoma tena sindano ya usingizi"

"Yaah nimemchoma anasumbua sana kila wakati anapiga kelele Yusto, Yusto"

"Revo lakini dawa za usingizi sio nzuri kwa mama, hii ni sindano ya nne sasa unamchoma na hata siku haijaisha, daktari au wewe unasemaje"

"Ni sahihi sahihi kabisa, dawa za usingizi zinaweza kumfanya mtu akawa teja kwa kitaalam tunaita drug addiction, kichaa anatakiwa kufanyiwa vile vitu anavyovipenda Kama tu havina madhara, Kama anamtaka Yusto basi mleteeni Yusto" alisema Dr, huku Caren alitikisa kichwa kuunga mkono maelezo hayo.

" Sawa tutafanya hivyo Dr, basi Revo msindikize Daktari Kisha utapitia chuoni umlete Yusto hapa ninaimani hata yeye anatamani kumuona mama yake akiwa ameamka, nitampigia simu" alisema Caren.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dakika chache baadae Revocatus na Daktari walionekana wakiwa ndani ya gari wakitoka nje ya kambi ndogo ya akina Caren.

Kama kawaida Revocatus alikua ndiye dereva, Daktari alikua amekaa siti ya nyuma akiwa amefungwa kitambaa usoni,
Hakutakiwa kuona njia ya kufika kambini hapo.
Kwenye mapaja yake daktari alikua amepakata briefcase (begi) ndogo la pesa ikiwa ni malipo yake baada ya kufanya kazi ile ngumu ya kuzungumza na kichaa.

Kwa mwendo wa zaidi ya dakika 15, kila mmoja alikua kimya, hakuna aliyekua amefungua kinywa kuzungumza na mwenzake tangu safari ilipoanza.

"Mbona unaendesha kwa kasi sana kijana vipi?" hatimaye daktari alifungua kinywa kuzungumza
"Kijanaaa" Daktari aliita tena kwa sauti baada ya kuona Revocatus yuko kimya hamjibu chochote.
Licha ya kufanya hivyo lakini Revocatus aliendelea kuwa kimya huku akizidi kuongeza kasi ya gari yake.

Hapo Daktari akaanza kuwa na wasiwasi haraka akavua kile kitambaa alichokuwa amefungwa usoni.
Revo alifunga breki ghafula mara tu baada ya Daktari kuvua kile kitambaa.

Vumbi jingi likatimka na kupaa hewani, gari ya Revo ikiwa imesimama katikati ya daraja moja refu.

"Unajaribu ku...kufanya nini?" Daktari aliuliza huku akimtazama Revo kwa macho ya kuuliza.

Revo hakuzungumza chochote, alifungua mlango akashuka na kuzunguuka nyuma ya gari akamfungulia mlango Daktari.

"Teremka" Revo aliongea kwa sauti ya kuamrisha
"Nini?"
"Shuka kwenye gariiiii" Revo alifoka huku safari hii akichomoa bastola yake na kumnyoshea Daktari, uso wake ukiwa serious hakuonyesha hata chembe ya masihara.
"Sa.sa..wa nashuka"
Alisema Daktari kwa sauti iliyojaa kitetemeshi, huku akiteremka kwenye gari.

"Sogea nyuma"
Alisema Revo, Daktari akatii na kusogea hadi pembeni kabisa ya lile daraja

"Kwani nimekosa nini kijana, lakini si mliniita wenyewe"

"Hujui ulichokosea sio, wewe ni Daktari au mpelelezi, inakuwaje unatoa siri za mtu kwa mtu mwingine"

"Aah hapana lakini si....."
"Lakini nini, umejisahau sana dokta, Siri za madam Jane ni zake mwenyewe huwa hazitoki kirahisi hivyo, haya ruka kwenye maji ujiokoe mwenyewe"

Daktari akigeuka na kutazama nyuma yake, daraja lilikua ni refu sana lakini mbaya zaidi aliwaona mamba wakirandaranda juu ya maji, hali ilitisha mno

Daktari akageuka na kumtazama Revo huku mikono yake akiwa amenyoosha juu.
Revo akamuonyesha ishara kwa kichwa kuwa aruke huku akiwa amemnyoshea bastola.

Jasho jembamba likawa linazidi kumtoka daktari, akawa anatetemeka mwili mzima.
Mara ghafula akakimbia kwa lengo la kwenda kumvaa Revo ajiokoe mwenyewe, lakini kabla hajamfikia Revo akafyatua risasi.

Paaa!!

Daktari alihisi kitu cha moto kimepenya kifuani kwake akainama taratibu kuangalia huku damu ikimtoka mdomo.

Paaa!!

Revo akamuongeza risasi nyingine ya pili ya tatu ya nne ya tano ya sitaa, Daktari akaanguka chini.

Revo akasogea hadi pale ulipolala mwili wa daktari wakati huo simu yake ilikua ikiita.
Revo akausukuma ule mwili kwa mguu wake wa kulia, ukaanguka majini chini ya daraja huku mamba wakiupokea kwa shangwe.
Revo akapokea simu yake.

"Ndio Caren"
"Vipi umemfikisha Daktari"
"Yah hivi ndio anaingia kazini kwake"
"Asante Revo basi naomba kamchukue Yusto nimeongea naye tayari"
"Sawa dakika 7 tu nitakuwa nimefika mwambie nimkute pale nje getini"

"Powa, nisamehe bure Revo nakutumikisha kama vile nimekua bosi wako"

"Hahahah hata usijali Caren tuko pamoja"
Alisema Revo kisha akakata simu, akachungulia chini darajani akawaona wale mamba namna wanavyo ugombania vipande vya nyama ya mwili wa daktari.
Akarudi kwenye gari akaliwasha na kuondoka zake kwa kasi.

𝗜𝗧𝗔𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔𝗔𝗔...
Simulizi hii sasa itapatikana kwa wiki mara 2 tu.
Jipatie vipande 30 vilivyosalia kwa Tsh elf 1 tu
0756862047
 
𝐃𝐎 𝐍𝐎𝐓 𝐒𝐇𝐎𝐔𝐓
𝘀𝗲𝗮𝘀𝗼𝗻 2

Sehemu ya............07
Mtunzi: Saul David

ILIPOISHIA...
Revocatus mfanyakazi na rafiki wa karibu wa Caren, anafanya mauwaji ya kutisha kwa kumuuwa daktari wa magonjwa ya saikolojia na akili.
Kitendo hiki kinakua ni kinyume kabisa na makubaliano waliyoyaweka yeye na Caren hali hii inaonyesha wazi kuwa kuna vitu Revocatus alikua akivifanya kwa siri bila Caren kujua licha ya wao wawili kufanya kazi pamoja chini ya Madam Jane.
Upande wa pili,tajiri mark moon anaondoka akiwa ameongozana na jasusi Brandina kwa ajili ya kufanya nae mazungumzo.

𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔....
Tajiri Mark moon na jasusi Brandina walionekana maeneo ya ufukweni wakiwa wamesimama juu boti moja nzuri kubwa na ya kisasa.
Kulikua na upepo mtulivu uliokuwa ukipuliza taratibu eneo hilo. Mark moon na jasusi Brandina wote walikua na glasi ya kinywaji mkononi.

"Unakumbuka mara ya mwisho lini tulikua hapa?" mark moon aliuliza

"Nakumbuka bosi, kitambo sana, kipindi kile unatuagiza kupeleleza maisha ya mkeo akiwa Dubai ....ooh samahani mkeo wa zamani Madam Jane"

"Unakumbukumbu nzuri sana Brandina, wewe Simigo na Mpili mmekua watu wa muhimu sana kwangu tangu zamani, mmefanya kazi na majukumu magumu sana, natambua umuhimu wenu"

"Bosi wewe ndio unastaili shukrani zaidi, umekua mtu muhimu sana kwetu hujawahi kutuacha hata Kama ikitokea tukashindwa kufanikisha baadhi ya Mambo"

"Anyway tuyaache hayo Brandina, nimekuita hapa kwa makusudi nataka ufuatilie Jambo ambalo tulilianzisha miaka kadha iliyopita tukiwa hapa hapa, nakutoa rasmi kwenye jukumu la kulinda kile chuo changu kwanzia leo nakupa kazi nyingine"
Alisema Mark moon akanywa kidogo wine akakohoa kisha akaendelea...

"Ni kuhusu Madam Jane"
"Madam Jane?"
"Ndiyo madam Jane.."
"Kuna nini bosi?"
"Unajua nini Brandina, marehemu baba yangu aliwahi kuniambia kuwa madam Jane ameenda Dubai kukusanya nguvu na ipo siku atarudi na kutaka kunilipizia kisasi baada ya Mimi kumuacha wakati ndoa yetu ikiwa na miezi mitatu tu"
Alieleza Mark moon

"Mmh lakini si alikosea na yeye anajua alikosea sana kwa nini atake kulipa kisasi Sasa, kuna kisasi gani hapo"

"Baba alisema madam Jane anaamini sikustaili kumuacha, aibu aliyoipata ilikua ni aibu kubwa sana, habari zake zilisambaa karibu kila kona ya Dunia, ni kitu ambacho hawezi kukisahau kirahisi"

"Kwa hiyo unataka nifanye nini bosi?"

"Alipotoka Dubai akarudi Tanzania alikua kimya sana nikawambia muache kumfuatilia kabisa nikaamini alishakubali yaishe, Lakini sasa hivi biashara zangu zinaandamwa sana tena kwa kasi kubwa wewe wenyewe ni shahidi, nina maadui wengi ndio sikatai lakini madam Jane ni adui yangu pia siwezi kumbeza. Kuna baadhi ya vitu vinatokea ambavyo nahisi mtu ambaye aliwahi kunijua sana ndio anavifanya, Sasa nani mwingine zaidi ya madam Jane? huwezi jua pengine yeye ndiye chanzo cha haya yote, nataka umfuatilia hatua zake kuanzia leo sawa Brandina"

"Nimekuelewa bosi"

"Utakuwa unaripoti kila kitu kwangu, niambie unataka kushirikiana na nani kwenye hii kazi ukiacha jasusi Simigo na Mpili"

"Mmh! Yusto, nitakuwa na Yusto"

"Hahahah Kama nilivyo tegemea, wewe na Yusto mnaniini nimekuwa nawatazama sana ujue"
Alisema Mark moon, Brandina akatabasamu huku akitazama chini kwa aibu za kike.

"Haya muhimu mfanye kazi hayo mambo yenu mtajua wenyewe, huyu Yusto ni kijana mwelevu sana naomba umfundishe kufanya kazi kwa usahihi na uhakika bado sio mzoefu, naamini anaweza kuwa msaada mkubwa sana baadae"

"Sawa bosi haina shida"
"Shabaha yetu ni nani?"
"Madam Jane"
"Nani?"
"Madam Jane"
"Woow asante shujaa wangu cheers"
Alisema Mark moon Kisha wakagonganisha glasi
na Brandina....
[emoji294][emoji294][emoji294]

Madam Jane alionekana akiwa ofisini kwake amekaa akipitia pitia baadhi ya taarifa mtandaoni zinazohusiana na chuo cha mumewe wa zamani Mark moon.

"Safii hatimaye mwanagu John anakwenda kuwa Rais wa Chuo cha baba yake Kama nilivyotaka iwe, hahahahah...Mark moon safari hii mwanao uliemtelekeza hata kabla hajazaliwa atakutafuna taratibu hadi ubaki mifupa"

Alisema Madam Jane kisha akacheka kwa sauti
Mara simu yake ikaitaa akapokea..

"Ee hallo...mmemkamata huyo mtu aliemchoma mwanangu kisu....Sasa Kama bado unapiga simu ya nini.....shenzi hizo taarifa zinanisaidia nini wakati Kama huu....achana na hilo nataka huyo kijana akamatwe aletwe kwangu Mara moja........sawa......sawa...... vizuri.....nawapa dakika 45.... Enhe vipi kuhusu Caren ameshaanza kazi ya kumtafuta Zubeda.....mulize.....alafu sidhani kama atafanya kazi yule binti inabidi umuongezee nguvu maana hata kuua hajawahi....sawa...haya nasubiri"
Madam Jane alikata simu Kisha akaitupa mezani kwa hasira.

Habari za John kuchomwa kisu akiwa chuoni zikimvuruga sana, alitamani sana kuonana na huyu aliyesubutu kunyoosha mkono na kumfanyia hivyo mwanae licha ya kuambiwa kwamba jeraha halikuwa kubwa lakini hakutaka kuelewa ilikuwa ni lazima Yusto akamatwe aletwe mbele yake bila kujua kuwa Yusto alikuwa ni mtoto wake wa kumzaa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Yusto alionekana akiwa nje ya geti la chuo cha Mark moon akawa anaangaza macho huku na huku kuitafuta gari ya Revocatus Kama alivyoelekezwa na Caren. Alikua na shauku kubwa ya kwenda kumuona mama yake kwa mara nyingine.

Mara simu yake iliita akapokea,

"Beib...." Sauti laini ya Caren ilisikika ikideka upande wa pili
"Ndiyo mpenzi, "
"Mimi na mama tumekumiss vipi Revo bado hajafika"

"Nimetoka hapa nje hata simuoni...aah! naliona gari lake lile haya mpenzi nakuja sio mda"
"Okay tunakusubiri, Love you...."
"Love you more,,,," alimaliza mazungumzo na kukata simu wakati huo gari ya Revocatus ilifika na kusimama umbali wa mita kadhaa mbele yake.
Mara simu ya Yusto ikaita tena, akapokea upesi
"Brandina"
"Yes handsome wangu unaenda wapi, niko nyuma yako hapa nina habari njema kutoka kwa bosi Mark moon" alisema brandina
Haraka Yusto aligeuka nyuma kuangalia akamuona brandina akija na pikipiki moja ya bei ghali, umbo la mwili wake,sura yake, nguo alizo vaa na tabasamu alilokua nalo wakati huo vilimfanya Brandina aendane kabisa na pikipiki hiyo, hakika alivutia sana kwa kumtazama wala usingeamini Kama anafanya kazi ngumu ya ujasusi.
Kila alipokatisha aliwafanya wanaume wengi kugeuka na kumtazama Mara ya pili.

"Aah...eee..kuna nini Brandina bosi anasemaje kwani?" aliuliza Yusto huku akimtazama Revocatus kwa mbali ambaye alikua anamsubiri kwenye gari.

Yusto akajikuta yuko njia panda hakujua aende kwa Revo au amsubiri Brandina ambae alikua jirani kabisa kufika.
Akiwa anapiga hesabu za haraka haraka mara ghafula kuna mwanamke akatokea nyuma yake na kumkumbatia.

Yusto aliduwaa kwani hakuwa akimfahamu mwanamke huyo mrembo alienukia marashi ya gharama,Lilikua ni tukio la ghafula sana.
Yusto alihisi ni Kama ameguswa na kitu cha baridi tumboni akainama na kuangalia, alishtuka baada ya kugundua ilikuwa ni bastola ya yule mwanamke akiwa ameielekeza kwenye tumbo lake.

"Tulia naomba tuongozane taratiiiibu ukijitikisa tu nakumwaga utumbo wote" yule mwanamke aliongea kwa sauti laini huku akiwa amemkumbatia Yusto kwa mahaba mazito.
Haikua rahisi mtu kugundua kinachoendelea kati ya Yusto na yule mwanamke.
Mara kuna gari moja ikafika na kufungua breki Kali mbele yao, mlango ukafunguliwa haraka. Hawa walikua ni watu kutoka kwa madam Jane.

"Haya ingia kwenye hilo gari mpenzi" alisema yule mwanamke.

Yusto akiwa katika hali ya taharuki asielewe hili wale lile alimtazama Revo ambaye nae alionyesha haelewi kinachoendelea, akageuka kumtazama Brandina naye ndio kwanza alikua anapaki pikipiki yake.

Je hawa ni akina nani?
Yusto atakuwa salama?
Nini atafanya Brandina?
Vipi kuhusu Revo?

ITAENDELA....

Full story Tsh 1000 (ofa)
0756862047.
 
𝐃𝐎 𝐍𝐎𝐓 𝐒𝐇𝐎𝐔𝐓
season 2

Sehemu ya............08
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA....
Mara kuna gari moja ikafika na kufungua breki Kali mbele yao, mlango ukafunguliwa haraka. Hawa walikua ni watu kutoka kwa madam Jane.

"Haya ingia kwenye hilo gari mpenzi" alisema yule mwanamke.

Yusto akiwa amepigwa na hali ya taharuki alimtazama Revo ambae nae alionyesha haelewi kinachoendelea, akageuka kumtazama Brandina nae ndio kwanza alikua anapaki pikipiki yake.

SONGA NAYO....
Wakati Brandina anaanza kumfuata yusto pale alipokua ndipo aliposhtuka na kubaini kuwa kunatukio lililokuwa likiendelea ambalo sio la kawaida mara tu baada ya kumuona Yusto analazimishwa kuingia ndani ya lile gari.

Brandina alianza kusogea eneo lile taratibu huku akijaribu kusoma mazingira, hakuwa na uhakika na kile anacho kihisi hata hivyo ilikua ni vema pia kwake kuchukua tahadhali kabla ya kufanya chochote

Yusto hakuwa na ujanja, alijua Kama ataleta ubishi wa aina yoyote basi yule dada angempiga risasi.Aliingia ndani ya gari Kama alivyoelekezwa akakaa kwenye siti ya katika.
Mara ghafula alikabwa shingo na mtu mmoja aliekua amekaa siti ya nyuma, alimbana kwa nguvu na kumuweka kitambaa fulani chenye madawa ya kulevya puani. Yusto alijaribu kujinasua lakini haikuwezekana haukupita mda akatulia kimya akiwa tayari amepoteza fahamu.
Wakati huo tayari Brandina alishafika na kusimama nje ya mlango wa lile gari. Walipotaka kufungua Brandina akazuia.

"Unataka nini?" yule mwanamke aliemteka Yusto alihoji.
"Nyinyi akina nani, mnampeleka wapi huyu mwanafunzi?"
Brandina alijibu swali kwa swali huku akiwa bado ameshikiria mlango wa lile gari kwa nguvu.

Akiwa katika hali hiyo Mara ghafula lilichomoza teke kutoka kwa mwanaume wa miraba minne aliekuwa ndani ya gari, akamkanyaga Brandina kifuani akaanguka chini pembeni ya barabara. Bila kuchelewa dereva aliwasha gari na kuondoka kwa kasi eneo lile.

Wakati yote hayo yakiendelea Revocatus alikua pembeni akishuhudia kila kitu.
Hakuelewa ni nini kinaendelea. Simu yake ilikua ikiita kila wakati na mpigaji alikua ni Caren.
Revo aliitazama badala ya kupokea akaizima kabisa Kisha akawasha gari yake na kuanza kuifuata nyuma ile gari iliyo mbeba Yusto.
Brandina nae licha ya kupata maumivu makali baada ya kupigwa kete kali kifuani hakutaka kuendelea kupotezea muda aliinuka na kudandia pikipiki yake Kisha kwa kasi ya kubwa akawa anaelekea kule lilipo elekea lile gari.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Caren akiwa bado ndani ya kile chumba anachopatiwa matibabu mama Yusto.
Hakua ametulia kabisa mda wote alikua amesimama huku akijaribu kupiga simu kwa Yusto na Revocatus bila mafanikio. Simu ya yusto ikawa inaita tu bila kupokelewa. Alipojaribu kumpigia Revo hali ikawa ni ile ile na baadae akaacha kupatikana kabisa.

Taratibu Caren akaanza kupatwa na wasiwasi, haikua hali ya kawaida kabisa.

"Vipi hauniletei chungwa"
Zubeda (mama Yusto) akiwa pale kitandani alihoji huku akimuangalia Caren usoni.
Caren ambae alikuwa kwenye hali ya kuchanganyikiwa aligeuka na kumtazama.

"Nini"
"Chungwa, sokoni pale kaniletee chungwa"
"Kwa hiyo humtaki tena Yusto saa hizi unataka chungwa"

"Aah Yusto staki aje hapa, anaogopa sindano, kwani yule Kaka wa sindano kaenda wapi simpendiiiii"
Aliongea zubeda akiwa anamaanisha Revocatus ambae alikua akimchoma sindano za usingizi kila anapoamka.

Caren alijikuta anatabasamu, ni kweli hali ya mama Yusto haikua ya kufurahisha lakini kwa kiasi aligeuka faraja kwa Caren, akajipa matumaini huenda Revocatus na Yusto mpenzi wake watafika hivi punde.

"Enh mama nambie kwa hiyo wewe na madam Jane mlikua mnaishi wapi mwanzoni"

"Kijijini huko Mtwara masasi ndani ndani hahahaha alafu umenikumbusha madam Jane alikua anaimba kwaya bwana alikua na kikundi chake cha kwaya kanisa anaomba michango halafu anawadhurumu wenzake sasa akawa ananilazimisha nijiunge lakini mimi siwezi sauti sina ya kuimba embu sikia,,,,,
Hakuna mungu Kama wewe yawe aaah aah hakuna mungu Kama wewe yawe aaah unaweza yeyeyeye,,
Hahahaha najua eti"

Aliongea Zubeda Caren akawa anamtazama tu huku akitabasamu.
Licha ya zubeda kuwa mgonjwa wa akili lakini alikua na kumbukumbu nyingi sana alizozihifadhi kwenye kichwa chake na hii ndio sababu hasa ya madam Jane kutaka kumuua.

Mara simu ya Caren iliita haraka akaiwahi akiamini mpigaji atakua Yusto au Revocatus, lakini Mara mudi yake iliisha ghafula, baada ya kuona jina la mpigaji.

,,,,VIP,,,,

Alikua ni Madam Jane.
Caren aliitazama simu Mara mbili mbili kisha akamtazama Zubeda ambae ndiye hasa sababu ya ile simu.
Ulikua umepita mda tangu Caren alipoagizwa na madam Jane kutekeleza jukumu la kumuua Zubeda lakini hakuwa amefanya chochote hadi dakika hiyo. Hatimae Caren alipokea simu.

"Ndio bosi Caren naongea...halo...hallo....sikusikii vizuri bosi...hallo..."

Caren alikua akimsikia madam Jane kwa shida sana,
Madam Jane alionekana kuwa eneo la wazi lenye upepo mwingi pia ilisikika Kama sauti ya ndege(Helikopta)
karibu yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Baada ya mwendo wa masaa matatu hivi hatimae gari lililombeba Yusto lilikatisha na kuacha barabara kuu likafuata barabara nyingine ya vumbi iliokuwa ikikatisha katikati ya msitu.

Liliendelea kwenda kwa kasi likapandisha mlima mmoja na kuanza kutelemkia upande wa pili, huko kulikuwa na ngome nyingine kubwa yenye ulinzi mkali.
Ilikuwa ni eneo jingine ambalo lilikuwa chini ya umiliki wa madam Jane, mama mwenye pesa zake ambae alikua amejikamilisha kwa kila idara.
Huko ndiko alikokuwa akipanga na kufanya biashara zake nyingi za magendo.
Kulikua na ukuta mkubwa uliojengwa kuzunguuka ngome hiyo yenye ulinzi mkali. Revocatus alisimamisha gari yake juu ya mlima umbali mrefu kutoka ilipokua ngome hiyo akawa anaitazama kwa chini huku akijaribu kuwaza ni nini Kilikua kinaendelea, akina nani waliomteka yusto na kumleta huko na ni kwa sababu zipi. Alitamani kujua yote hayo.

Licha ya yeye pia kufanya kazi chini ya madam Jane lakini hakuwa akielewa chochote juu ya kinachoendelea wala hakuwahi kuiona wala kusikia kuhusu ngome hiyo, Kila kitu kilikua kugeni kwake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Muda mfupi baada ya gari iliyomteka Yusto kuwasili mara helkopta moja nzuri ya kisasa ilionekana angani na baadae ikatua kwenye uwanja mpana uliokuwa ndani ya ngome hiyo.

Akashuka mama mmoja alievalia kiarabu akiwa ameongozana na walinzi wawili pembeni yake, mmoja kulia mwingine kushoto.

Revocatus aliekua amejificha mlimani nyuma ya miti alijitokeza baada ya kusikia sauti ya helkopta, akachukua Darubini yake akawa anatazama watu wanaoshuka kutoka kwenye helkopta ile.

"What, bosi?, Madam Jane"
Revocatus alitahamaki baada ya kumuona madam Jane akishuka kutoka kwenye helkopta ile, hakuamini.

Akaweka Darubini yake tena machoni, ni kweli alikua ni bosi wake madam Jane mwenyewe hakua amekosea hata kidogo.

Madam jane alionekana akitembea kwa madaha huku akichukua simu yake, akapiga na kuiweka sikioni.

"Hello bosi" Caren alisikika upande wa pili wa simu ile
"Vipi Caren uandeleaje na kazi? Umempata Zubeda" aliuliza Madam Jane

"Hallo bosi..sikusikii vizuri....hallo"

Caren alisikika upande wa pili akiwa anapata tabu kumsikia madam Jane kwani bado mapanga ya helkopta yalikua yakizunguuka, istoshe kulikua na upepo mkali eneo hilo. Mwisho madam Jane akakata simu.

"Yuko wapi huyo kijana"
Madam Jane alimuuliza mmoja wa walinzi wa ngome yake.

"Wamempeleka ndani ya kile chumba"

"Mmm! safi kazi nzuri"
Alisema madam Jane huku akifungua mkoba wake akachukua miwani akaivaa Kisha taaratiibu akaanza kutembea kuelekea kwenye chumba alichoelekezwa.
Sasa ulikua ni wakati wa madam Jane kukutana na mtoto wake wa kumzaa bila kujua.

Wakati huo wote Revocatus alikua akifuatilia kila kinachoendelea kupitia Darubini yake.

"Huyu bosi sio mtu wa kawaida, tofauti kabisa na tunavyomchukulia, lakini kwa nini Yusto kaletwa huku, nini kinaendelea, au..... Hapana haiwezekani, lakini nilishamwambia Caren huenda Yusto akawa sio mtu wa kawaida ona Sasa yeye na Madam Jane uso kwa uso hii imekaaje"
Revocatus alikua akijiuliza na kujijibu mwenyewe.

Mara ghafula alishtuka baada ya pikipiki kupita kwa kasi nyuma yake, wala hakufanikiwa kuiona, ilikuwa ni tukio la kufumba na kufumbua pikipiki ilipita kama upepo.

"Ebo nini tena" Revocatus alitahamaki

ITAENDELEA....

Full story Tsh elf 1 tu
0756862047
 
Stor kali kinoma ila naona kama ndo basi tena tunaelekezwa kwenye mapidief! Sasa kazi tunayo sisi wa kwa sadala boma
 
Back
Top Bottom