Simulizi ya ujasusi: Do not shout (Usipige kelele)

DO NOT SHOUT
Sehemu ya.........30
Mtunzi: Saul David
Email: saulstewarty@gmail.com

ILIPOISHIA....
"Hapo ndipo Mahali tutakapo kutana kesho kwa ajili ya mazungumzo yetu, kesho ndio siku nitakwambia nini nataka kutoka kwako Madam Jane, karibu tujekushuhudia kwa pamoja jinsi Fiston Mayele anavyotetema" Alisema Osman Azizi kisha akakata simu.

Je, nini kitafuata?


SASA ENDELEA....
"Mpuuzi huyu" madam Jane alitukana mara tu baada ya Osman Azizi kukata simu yake.

"Anapanga nini huyu mwana haramu, kwa nini anataka tukutane uwanjani, ni lazima nitakuuwa Azizi" Madam Jane aliongea huku akionekana kukosa amani kabisa.

Haraka alipiga simu mahali na kuiweka sikioni.

"Hallo, naomba kusanya watu wote, waliopo kambini na walio nje ya kambi pia, wote akina Caren, Revo na wengine nawahitaji sasa hivi tukutane kule kwa siku zote" madam Jane alionge kisha akakata simu akapiga tena namba nyingine

"Ee Roy.. naomba nisaidie kitu kimoja, kata tiketi za watu kama ishirini hadi thelathini hivi za kuingia kesho uwanjani kwenye mechi ya yanga na Kagera Sugar pale Benjamin mkapa...we fanya hivyo maelezo mengine baadae...sawa" madam Jane alitoa agizo kisha akakata simu.
akavuta pumzi ndefu akijaribu kuituliza akili yake ambayo mpaka sasa ilikuwa imeelemewa na mambo ambayo yaliyokuwa yanamkabili.
Akatazama juu ghorofani, kwa mbali alimuona mwanae John akiwa dirishani, wakati huo John nae alikua bize na simu yake, hakujua anafanya nini.

Madam Jane aliwaza deni alilonalo kwa mwanae John, kumuweka wazi kwa kila kitu kuhusu baba yake mzazi pamoja na ule undugu uliopo kati yake na Yusto. Ilikuwa sio kazi rahisi hata kidogo, Madam Jane hakua tayari kuweka wazi kuwa Mark Moon ndiye baba mzazi wa John kwa hili hakua tayari kabisa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili ndani ya hospitali ya Mountenia.
Mark moon alionekana kuchanganyikiwa mara tu baada ya Zubeda kutaja kitu kinachoitwa code G ambayo ndio hasa ilikuwa shabaha kubwa ya Osman Azizi.

"Mark una nini lakini mbona hutulii" Zubeda alimuuliza Mark Moon baada ya kuona hali yake imebadilika ghafula.

"Zubeda, sijui hata nisemaje, hata nikikueleza huwezi kuelewa, ila jua tu nipo hatarini, Osman Azizi ni mtu hatari sana, sijui hata amefikia wapi mpaka sasa, sijui nitamdhibiti vipi, code G ndio maisha yangu Zubeda vipi kama ameshaipata bila mimi kujua" mark moon aliongea hali akipiga hatua kwenda huku na huku mbele ya kitanda alicholala Zubeda.

"Mark hebu jaribu kutulia basi, kwani nani mwingine ameingia chumbani kwako, Azizi hawezi kuipata hiyo code G unayosema, sielewi ki undani lakini jaribu kutuliza akili yako ili ufanya maamuzi sahihi" Zubeda alijaribu kumtuliza Mark Moon.

Ni kama maneno ya Zubeda yalimuamsha mark moon kutoka usingizini, hasa baada ya kusema neno chumbani, mark moon alisimama ghafula.

"Umesema chumbani ee, yes, uko sahihi, madam Jane, Azizi atakua amemtumia madam Jane kupata Code G, ooh shit, watakua wameshakutana au bado, itakua bado ningejua, lakini vipi kama.....?" Mark moon alikuwa alijiuliza na kujijibu mwenyewe, haraka alitoa simu yake akampigia Brandina.

Wakati huo Brandina alikua ndani ya chuo chake eneo la stoo jikoni, alikua akiangalia video aliyoletewa na Simigo ikonyesha matukio yaliyotokea ukumbini kwenye sherehe ya kuazimisha siku ya kuzaliwa kwa Yusto.

"Hallo bosi"
"Vipi Brandina, mmeshaanza kazi ya kumfuatilia Madam Jane"
"Aa..bosi...ee tuli..."
"Brandina please nipo kwenye matatizo makubwa, nahitaji kujua ratiba zote za hivi karibu za Madam Jane, alienda wapi alikutana na nani saa ngapi kwa ajili gani, yuko wapi sasa na anapanga nini, kama ukihitaji msaada niambie, naomba lisimamie hili kwa nguvu kubwa kuanzia sasa hivi nipe ripoti" mark moon aliongea kwa msisitizo, Brandina alielewa, akakata simu.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Brandina hakua na muda wa kupoteza haraka alijiandaa kisha akaenda kumfuata Yusto chumbani kwake kwani ndie mtu alietakiwa kuambatana nae kwenye kazi hiyo.

Brandina alifika hadi mlango wa kuingilia chumba cha Yusto, akataka kugonga lakini akasita mara baada ya kusikia sauti za watu wakiongea na kucheka ndani ya chumba hicho.

Brandina hakua na sababu ya kujiuliza mara mbili, alijua wazi kuwa Yusto yupo mle ndani na Caren.
Wivu ulimuingia kiasi, akajikuta anayakumbuka yale matukio ya msituni akiwa na Yusto lakini Sasa hakuwa na cha kufanya tayari mwenye chakula alikuwa anajipakulia na kula mwenyewe.

Brandina aliamua kuondoka na kumuacha Yusto afurahie wasaa alioupata na mpenzi wake Caren, akapanga kumtafuta baadae.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Brandina alianza kuifanya kazi aliyoagizwa na mark moon, alienda moja kwa moja hadi nyumbani kwa madam Jane, kwa bahati nzuri alifika wakati ule madam Jane anaingia kutoka Mountenia hospital akiwa pamoja na mwanae John ndani ya gari.
Waliposhuka Brandina aliweza kushuhudia lile tukio la bodaboda kuleta tiketi kutoka kwa Osmaz Azizi kwenda kwa madam Jane.

Akiwa amejificha mahali Brandina alilishuhudia tukio hilo kwa makini lakini hakujua ni nini hasa kinaendelea. Akatamani kujua zaidi ikiwa kama hatua ya kwanza ya kazi yake.

Alianza kumfuatilia yule dereva boda boda mara tu baada ya kutoka nyumbani kwa madam Jane.

Brandani akiwa na pikipiki, nyuma ya yule bodaboda alimuona akisimama mahali kisha akashuka na kwenda kwenye kibanda cha M-pesa.
Brandina alisimama mahali akiwa anachunguza nyendo za kijana huyo, alimuona akitoa pesa kama laki 4 hivi akaziweka mfukoni, hizi zilikua ni pesa alizolipwa na Osman Azizi mara baada ya kuifanya kazi ile ya kukata na kupeleka tiketi kwa Madam Jane.

Akiwa anarudi mahali alipoiacha pikipiki yake mara ghafula wakatokea vijana wanne wakamvaa yule dereva bodaboda kisha wakambeba juu juu na kuingia nae vichochoroni, lilikua ni tukio la ghafula na haraka sana ambalo halikuzua taharuki yoyote kwa watu wachache waliokuwepo eneo hilo, hakuna aliyeona.

Brandina alishuhudia yote akiwa nyuma ya mti mmoja mkubwa, hakutaka kuwaacha waende, bado kuna vitu alitamani kuvijua zaidi ili awe na taarifa kamili ya kuripoti kwa bosi wake mark moon.

Alianza kuwafuatilia vijana wale taratibu kwa nyuma hadi walipofika kwenye eneo moja la kichochoro palipojificha, wakamshusha chini yule kijana kisha wakaanza kumuhoji huku wakimpiga.
Brandina alisogea karibu yao zaidi kwa tahadhari kubwa akawa anasikiliza na kuona kila kinachoendelea.

Haukupita muda mara akaja mtu mwingine, alikuwa ni John mtoto wa madam Jane. Yeye ndiye aliyewaagiza vijana hao wamteke yule dereva bodaboda na kumuhoji ni kitu gani alileta kwa mama yake.

"Vipi ameongea" John alifika na kuuliza swali moja kwa moja.
"Ndiyo bosi ameongea" alijibu Abdullah, kijana wa John ambae ndie aliekuwa kiongozi wa wengine.

"Kasemaje?"
"Amesema yeye aliagizwa tu akakate tiketi mbili za kuingia kesho kwenye uwanja wa mkapa wakati wa mechi ya Yanga na Kagera Sugar, tiketi moja amepeleka kwa alie muagiza na nyingine ndio kamletea mama yako."

"Kaagizwa na nani?"
"Osman Azizi, yule jamaa muuza magari, unamfahamu hata ile gari yako ya mwisho ulinunua kwake"

"Sawa kuna kingine"
"Hamna bosi"

John alianza kuondoka huku akiwa bado anaonekana kutokuwa na furaha kabisa.

"Sasa bosi huyu jamaa tunamfanyaje?" aliuliza Abdullah.

"Mfungieni mpaka kesho kutwa ndio mmuachie" John alijibu kwa kifupi na kuondoka zake.

Brandina alisikia na kuona kila kilichoendelea nae aliondoka huku akipiga simu kwa mark moon akamueleza kila kitu.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Mark moon alikuwa bado yuko pale hospitali ndipo alipopokea taarifa hizo kutoka kwa Brandina, akamueleza kila kitu kuwa Madam Jane kaletewa tiketi ya kuingia uwanjani kwa mkapa na Osman Azizi siku ya kesho.

Mark moon aliipokea taarifa hizo na kutafakari kwa kina, mwisho akawa na jibu kamili.

"Hii yote ni kwa sababu ya code G, anataka kumtumia madam Jane, sijui hatua uliyofika Osman, ila ninauhakika nitakudhibiti tu" Mark Moon aliongea taratibu huku akiuma meno yake kwa hasira, hakuwa mtu wa ogomvi kabisa lakini ilionekana wazi kuwa Osman Azizi amemgusa pabaya.

"NAOMBA ITA VIJANA WOTE PAMOJA NA WALE MAJASUSI WETU NINAKAZI MUHIMU SIKU YA KESHO, PIA KATA TIKETI ZA KUWATOSHA KUINGIA KWENYE MECHI YA KESHO UWANJA WA BENJAMIN MKAPA"

Mark moon aliandika ujumbe huu kwa mtu wake wa kazi, akimtaka afanye maandalizi hayo haraka iwezekanavyo.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Caren na Yusto walikuwa hoi kitandani baada ya kufurahia penzi lao kwa zaidi ya saa moja na nusu, sasa walikuwa wamechoka mno, wakawa wanatazamana tu huku wakifanya mazungumzo ya hapa na pale wakiwa ndani ya shuka moja.

"Tumeongea sana Caren hebu twende basi kambini kwenu nikamuone mama yangu"
Alisema Yusto, ni kweli alikuwa amemkumbuka mno mama yake mlezi Zubeda.

"Aah sawa tutaenda lakini subiri kwanza bana tupumzike mi nimechoka sana, mama yuko salama yuko na Revo kule hakuna kitakacho haribika" alisema Caren na hapo akajikuta anakumbuka kuhusu maelezo aliyopewa na daktari wa saikolojia na akili yakimuhusu mpenzi wake Yusto, bosi wake madam Jane,na Zubeda mama mlezi wa Yusto.

Bado caren alikuwa na kigugumizi, hakujua wapi aanzie kumpa taarifa hizo Yusto kumweleza kuwa Madam Jane ndie mama yake mzazi.

"Yusto" Caren aliita

"Niambie mama"

"Kunakitu bado hujawahi kuniweka wazi mpenzi, kila nikitaka kukuuliza mambo yanaingiliana"

"Nini hicho Caren, hebu uliza"

"Kama nilivyokwambia mimi ni agent wa siri wa shirika fulani linalofanya kazi kwa oda maalum za kiserikali kwa siri, vipi kuhusu wewe, inakuwaje una siraha na unajua kuitumia"
Aliuliza Caren.

Yusto alibaki kimya kwa sekunde kadhaa, mwisho akageuka na kumtazama Caren usoni.

"Hunie, nitakuambia ukweli, mimi sio mwanafunzi hapa chuoni kama mnavyofikiri, mimi mlinzi tu, mlinzi wa siri pamoja na rafiki yangu Frank tunalinda usalama wa hiki chuo, tumeajiliwa moja kwa moja na mmiliki mark moon, tuna miaka miwili mpaka sasa" alieleza Yusto.

Ilikuwa ni taarifa iliyomshtua sana Caren, alijikuta akipigwa nakaubaridi ka hofu, kumbe wakati wote huo alikuwa na ukaribu na Yusto asijue kama ni mlinzi wa siri wa Mark Moon, yaani kwa tafsiri fupi alikuwa kwenye mahusiano na mpinzani wake kwani lengo kubwa la Caren kuwepo chuoni hapo ilikuwa ni kwa ajili ya kukiangusha chuo cha mark moon akiamini ni oda iliyotolewa na serikali kwa siri kupitia madam Jane, lakini haikuwa hivyo.

"Vipi mbona hivyo unaogopa?" Aliuliza Yusto baada ya kuona ni kama Caren amebadilika ghafula.

"Aah hapa niko sawa" alisema Caren,

Mara ujumbe mfupi wa maandishi ukaingia kwenye simu ndogo ya Yusto na simu ya Caren kwa pamoja.

Yusto na Caren wakatazama na kucheka, tukio hilo likionekana kuwafurahisha wote.

"Haya basi kila mtu asome meseji zake baby huenda ni taarifa muhimu" alisema Caren, akachukua simu ya Yusto na kumkabidhi kisha na yeye akachukua ya kwake, wote wakafungua zile meseji.
Yusto akawa wa kwanza kusoma.

"AISEE BOSS MARK MOON ANATUHITAJI WOTE SASA HIVI KULE UKUMBI WA MIKUTANO KUNA KAZI YA DHARULA MWAMBIE NA FRANK"

Ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa jasusi Simigo.

"CAREN, MADAM JANE ANAWAHITAJI WOTE KULE KAMBINI KUNA KAZI YA DHARULA IMEJITOKEZA" na hii ilikuwa ni meseji kutoka kwa Revocatus.
Caren na Yusto wakatazama usoni huku kila mmoja akionyesha kuwa na siri yake moyoni.

"Vipi kwema?" aliuliza Yusto
"Mmmh kwema, vipi wewe?"
"Ah fresh tu"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dakika 45 baadae tayari vikao vitatu katika sehemu tatu tofauti vilikuwa vikiendelea, na vyote vilikuwa vikilenga maandalizi ya siku ya kesho katika uwanja wa Benjamini mkapa.
Madam Jane na watu wake akiwemo Caren na Revo walikuwa wakijadili na kujipanga namna watakavyo mkabili Osman Azizi siku ya kesho kama tu mambo yatabadirika.

Osman Azizi nae na vijana wake walikuwa wakipanga mikakati jinsi ya kujilinda na kumkabili madam Jane na watu wake kama mambo yatabadilika kule uwanjani.

Na kikao cha mwisho kilikuwa cha mark moon na vijana wake wakiwemo Yusto, Frank na wale majasusi watatu yaani Brandina,Simigo na Mpili, wakawa wanapanga namna ya kumkabili Osman Azizi ambea anafuatilia kitu cha muhimu sana kutoka kwa bosi wao yaani Code G kupitia mke wa zamani wa mark moon, madam Jane.

Je, nini kitafuata?

ITAENDELEA...

USIACHE KUFUATILIA SIMULIZI YANGU MPYA
THE MODERN WAR-VITA YA KISASA.
MUHUMUHU JF

0756862047
 
Mwandishi Nimejiuliza sana kuhusu Jina lako, ni lenyewe, limepangwaau ni coincidence

Saul was compelled to place young David at the head of his army (I Samuel 18:5). Even though David then married Saul's daughter Michal and became a close friend of Saul's son Jonathan, an intense rivalry developed between the young new general and the King..

From Book of: 1 Samuel ..

ANYWAY KAZI NZURI SANA!
 
USIACHE KUFUATILIA SIMULIZI HII MPYA KUTOKA KWA SAUL DAVID...
0756862047
 
DO NOT SHOUT

Sehemu ya...................31
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Email: saulstewarty@gmail.com


ILIPOISHIA......
Dakika 45 baadae tayari vikao vitatu katika sehemu tatu tofauti vilikuwa vikiendelea, na vyote vilikuwa vikilenga maandalizi ya siku ya kesho katika uwanja wa Benjamini mkapa. Mark moon na watu wake, Osman Azizi na watu wake na madam Jane vilevile na watu wake.

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
Madam Jane na watu wake walimaliza mazungumzo yaliyokuwa yakilenga maandalizi ya siku ya kesho katika uwanja wa Benjamini mkapa, namna watavyomkabili Osman Azizi.

Wakawa wanatawanyika huku kila mmoja akiwaza namna atakavyotekeleza majukumu yake siku ya kesho.
Wakati huo Madam Jane alikuwa akiongea na baadhi wa watu wake wa karibu na muhimu kwake, mara akaja mtu mmoja akasogea na kumnong'oneza jambo.
Madam Jane alionekana kushangaa kiasi, akageuka na kumtazama Caren ambae alikuwa analizia kukusanya vitu vyake tayari kuondoka.

Caren aliinua uso wake akagonganisha macho na Madam Jane aliyekuwa akimtazama kwa macho makali.

"Vipi Madam kuna usalama kweli?" aliuliza Magdalena, mfanyakazi wa karibu wa Madam Jane baada ya kuona bosi wake ni kama amebadilika ghafula.

"Mkamateni Caren kamfungieni kule chini asubiri adhabu yake" madam Jane alitoa agizo kwa yule mtu aliyeleta taarifa, haraka akaenda pamoja na vijana wengine watano wakamkamata Caren.

Lilikuwa ni tukio la ghafula lililowashangaza watu wengi, ukizingatia Caren alikuwa ni mtu wa karibu na bosi Madam Jane hivi karibu na nimmoja kati ya watu walioaminika na kubahatika kupewa kazi kubwa yaani 'VIP order'.

Revocatus aliyekuwa mlango tayari kutoka nae pia alishangazwa na tukio hilo, ilimbidi asimame mara baada ya kumuona Caren akibebwa msobe msobe kupelekwa kwenye gereza lililokuwa vyumba vya chini vya kambi hiyo. Revocatus hakujua nini kimetokea akahisi labda ni moja kati ya mbinu za Osman Azizi ambae alitaka kuwazuia watu tegemezi wa Madam Jane ili kufanikisha jambo lake kiurahisi.

"Vipi madam, Caren kafanyaje kwani?" Magdalena aliuliza swali lingine.

"Stupid girl, huyu ndie mlisema yuko vizuri ona sasa, hajamuua Zubeda hadi leo hii, amekuwa akinidanganya. Nilikuwa MOUNTENIA hospital leo nikakutana na Mark Moon nikatuma mtu afutatilia kujua anafanya nini, hapa ndio naletewa taarifa kuwa eti kumbe Mark Moon alikuwa pale kwa ajili ya Zubeda ni mgonjwa lakini karudisha kumbukumbu zake akili yake imekaa sawa sio kichaa tena"

"Ee mungu wangu nini tena hiki, eti Zubeda amepona na yuko na Mark Moon, kivipi yani?"

"Nimechoka Magdalena nimechoka mimi jamani, huu mwaka umekuwaje kwangu, mbona mambo yananiendea kombo kila wakati, kwa nini lakini, ona sasa Zubeda na mark moon kuwa pamoja wapi na wapi, huku tena kuna Osman Azizi sijui ni kitugani kitajili hiyo kesho, Ooh shit" Madam Jane alilalamika akionekana kukata tamaa kabisa.

"Ooh please madam Jane kila kitu kitakuwa sawa, upo na timu imara usijali, hii ni changamoto ya kawaida sana, tumeshapanga mipango yote vizuri, kesho ni ama zao ama zetu kwa mkapa patachimbika, acha tumalize kwanza hili alafu tumgeukie huyo Zubeda na mark moon"
Magdalena aliongea kwa kujiamini akijaribu kumfariji madam Jane.
"Sawa Magdalena, lakini huyu binti kanikosea sana aisee hatakiwi kuishi"

"Sawa atapata anachostahili, kwanza mama na mdogo wake wanaingia kesho kutoka India"

"Ooh alafu kweli nilisahau hili, ilikuwa kama Caren akifanya kazi vizuri nimkutanishe na ndugu zake sasa kashaharibu, atakufa bila kuwaona" alisema madam Jane.

"Na hao ndugu zake wakifika tuwafanyaje sasa?"

"Wapelekeni kambi ile ya siri kule msituni wanaweza kusaidia kuwahudumia walinzi wangu, kale ka binti mpatie Kindoki kama zawadi katamfaa ananisaidia sana yule kijana." Aliongea Madam Jane akionyesha kutokuwa na hata chembe ya huruma.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili nako Mark moon alimaliza kikao na watu wake, sasa alikuwa ofisini pamoja na Yusto aliyemwita kuzungumza nae.

"Naam bosi"
"Hongera kwa kazi nzuri Yusto, nimesikia ulipigwa risasi vipi kidonda chako kinaendeaje" aliuliza Mark Moon.

"Kinaendelea vizuri bosi, niko vizuri kabisa"

"Wewe ni shabiki wa timu gani, Simba au Yanga?"

"Aaa.. mimi?"
"Ndiyo wewe"
"Mimi ni simba bosi"
"Aha ha ha, kwa hiyo kesho itakuwaje utavaa jezi ya yanga kama tulivyokubaliana, mmh?"
Aliuliza mark moon huku akitabasamu.
Yusto akapata kigugumizi kujibu hilo swali.

"Okay fine achana na hayo, Yusto nimekwita hapa nina jambo la kukwambia, aah! Kwanza kabisa ukiachilia mbali kuwa mimi ni bosi wako lakini pia mimi ni kama baba yako, nakujua vizuri sana Yusto zaidi ya unavyojijua wewe, nina mambo mengi sana nataka kuzungumza na wewe baada ya kumaliza kazi ya kesho, nina sapraizi kwako nyingi sana hivyo nimekwita hapa kukusihi kuwa hakikisha kesho unakuwa makini urudi kwangu ukiwa salama, sawa mwanangu"

"Sawa nimekuelewa bosi"

"Vizuri, napata hisia kuwa zoezi la kesho linaweza lisiwe rahisi kama mnavyozani, kuwa makini Yusto bado tunakuhitaji"

"Sawa bosi nimeelewa"
[emoji294][emoji294][emoji294]

Masaa yalienda na hatimae siku iliyokuwa ikifikiriwa na wengi ilifika.
Ilikuwa ni saa 12 jioni ikiwa limesalia lisaa limoja pekee kabla ya kuanza kwa mtanange kati ya Yanga na Kagera Sugar.

Tayari vikosi vyote vya Osman Azizi, Madam Jane na Mark moon vilikuwa ndani ya uwanja wa Benjamini mkapa wakijifanya kama mashabiki wa kawaida.

Osman Azizi na Madam Jane walikuwa wamekaa kwa pamoja eneo la watu VIP kila mmoja akiwa kimya kusubiri mchezo uanze. Naam wao walikiwa na mchezo wao maalum.

Wakati huo Mark moon yeye alikuwa ametulia nyumbani kwake akiwa ameketi nyuma ya screen mbili kubwa moja akiangalia mpira live kupitia king'amuzi cha Azam Tv na screen nyingine ikiwaonyesha moja kwa moja eneo ambalo amekaa Osman Azizi pamoja na Madam Jane.
Ilionyesha kuna mtu alikuwa na kamera ya siri iliyokuwa ikiwarekodi na kurusha moja kwa moja hadi kwa Mark Moon.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili
Caren alikuwa amefungiwa kwenye chumba kimoja kidogo tangu usiku wa jana ndani ya jengo moja ambalo lilikuwa pia ni kambi ya Madam Jane. Hakuwa amekula chochote, japo hakuhisi njaa wakati huo, mda wote alikuwa akiwaza ni namna gani atajinasua kutoka kwenye balaa ambalo lilikuwa mbele yake likimuandama, hakujua nini sababu ya yeye kukamatwa na kufungiwa lakini aliamini lazima Madam Jane atakuwa amegundua moja kati ya siri alizokuwa akizificha.

Aliwaza afanye nini lakini hakuwa na majibu, alitafuta njia ya kutoroka lakini hakuweza, kulikuwa na ulinzi imara eneo hilo akabaki ametulia ndani ya kile chumba akisubiri muujiza.

Naam ni kweli muujiza ulikuja. Caren akiwa amezama kwenye dibwi la mawazo mara alisikia sauti za watu wakilalamika kwa maumivu kisha akawa anasikia purukushani za hapa na pale.

Haraka alisimama na kwenda kushikiria nondo za chumba hicho akatamani kuona kilichokuwa kianendelea.

Kutoka na uzoefu aliokuwanao Caren aliweza kubaini kuwa watu hao wanaolalamika kwa maumivu walikuwa wakipigwa risasi na bastola iliyofungwa kifaa maalum cha kuzuia milio wa risasi usisikike (silencer).
Ni kweli sekunde chache baadae caren alimshuhudia mlinzi wa mwisho aliyekuwa jirani na chumba chake akianguka chini mara baada ya kupigwa risasi na mtu aliyekuwa anakuja taratibu huku uso wake ukiwa umezibwa na maski.

Yule mtu alifika na kufungua mlango wa chumba alichofungiwa Caren kisha akavua mask yake.

"Revocatus" Caren aliita kwa mshangao akiwa haamini baada ya kumuona Revo.

"Unafanya nini Revo,mbona..."

"Sina muda wa kujieleza Caren, nenda kamuokoe mama na mdogo wako" alisema Revocatus

"Unasemaje Revo, mama na Dokii wako india"
"Hapana wamefika leo asubihi"
"Are you serious?"
"Ndio hivyo nimekuja hapa kukutoa ukafanye hiyo kazi wako hatarini nenda haraka."

"Revo lakini mbona.....aaaaaghkooo...ooo" Caren aliongea lakini kabla hajamalizia sentensi yake alijikuta anashikwa na kichefu chefu cha ghafula akaanza kutapika.

Revocatus akawa anamtazama tu hadi alipomaliza.
"Revo hebu niambie vizuri tafadhali kwa nini umefanya hivi mama yangu yuko wapi? Kwa nini uko hapa?" Caren aliuliza hali akiwa bado na mawenge mawenge baada ya kutoka kutapika.

"Caren, kuna ngome ya siri ipo kule msituni ulipokuja kunisaidia siku ile, upande wa kulia kwa mbele kidogo utaiona, huku ndiko walikopelekwa mama na mdogo wako, ukichelewa utakuta wamefanyiwa kitu kibaya nenda sasa hivi" Revo alisisitiza kisha akampatia Caren bastola mbili.

"Inabidi ufanye hii kazi kwa nguvu zote kwa ajili ya maisha yako ya mama yako na mtoto wa Yusto aliepo tumboni mwako, pengine tunaweza tusionane tena Caren kwa heri, nisamehe kwa yote"alisema Revocatus kisha akaanza kuondoka huku akimuacha Caren akiwa kwenye mshangao mkubwa.

Revocatus alitembea hatua kadhaa akageuka na kumtazama tena Caren, wakatazamana.
Revo alikunja ngumi kisha akajipiga piga kifuani mara nne na kuibisu ngumi yake, Caren nae akafanya vivyo hivyo, hii ilikuwa ni ishara ambayo walizoea kuitumia tangu wakiwa kambini, ikiwa na maana kupeana moyo wakiwa katika mazingira magumu.
Revo alikuwa akielekea uwanja wa Benjamini mkapa, lengo lake likiwa ni moja tu kulipa kisasi kwa Osman Azizi aliyemuua baba na mdogo wake.

Caren alimuangalia hadi alipopotea kwenye upeo wa macho yake. Alitulia kwa muda huku akiyatafakari maneno ya Revo
Akajitazama tumbo na kujishika.

"It's real nina mtoto wa Yusto tumboni mwangu!!" Caren aliongea huku akitabasamu, ni kweli alikuwa na kila dalili ya kuwa mjamzito.

Haraka Caren alimsogelea mlinzi mmoja ambae amekwisha kufa, akamvua koti lake refu jeusi akalivaa yeye kisha akakusanya baadhi ya bastoli za walinzi wengine akazipachika mfukoni.
Akafungua kifundo cha nywele zake ndefu alizokuwa amezikunja, akazitawanya na kuzifanya zishuke hadi mgongoni.

"Nakuja mamangu" Alisema Caren hali akiwa amevaa sura ya kazi.
Wakati huo ilikuwa ni saa moja kamili.
Refa alipuliza kipyenga na mechi kati ya Yanga na Kagera Sugar ikaanza.

Je, nini kitatokea?

Mwisho wa haya yote unakwenda kuwa vipi?

Ungana nami katika kipande kinachofuata.

ITAENDELEA....

Malizia simulizi hii kwa tsh 500 tu
0756862047
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…