Sina furaha na ajira yangu, natamani kuacha. Je, nitaachaje?

Hii kitu inawatokea sana AJIRA za tamisemi, unaomba Kaz na hujajipanga na mazingira ya Kaz.
 
Umempa ushauri mzuri sana huu, napitia njia hiyo hiyo pia baada ya shule nitaangalia nini cha kufanya. Kuacha kazi sio njia sahihi kwasababu hizi kazi wakati mwingine hazikupi pesa na maisha unayoyataka lakini unaweza zitumia kama channel ya kupata fursa zingine nzuri zaidi ndani ama nje ya nchi na ndoto zako zikatimia.
 
Jifunze kubadilisha step kuendana na beat la wimbo,maisha magumu mtaani hakikisha ukiacha una vyanzo vingine vya mapato vya kueleweka.... using'ang'anie kucheza blues wakati wimbo ulio kwenye playlist ni bolingo,mwenye masikio na asikie
 
Punguza malengo mkuu utaenjoy just imagine unalipwa laki 5 kwa mwezi halafu una malengo ya million 500 kwa kazi iyoiyo waweza kukata tamaa hasa ukiangalia life time

Punguza malengo yaendane na kipato chako na hakikisha unatimiza lengo moja moja kwa wakati baada ya muda utaona success

Pia usijipe muda mfupi kwa kila lengo let's say wataka kufanya kitu cha mil 5 nawewe waingiza lak5 kwa mwezi usijipe miezi kumi kutimiza ila jiwekee kama mwaka mzima au mwaka na nusu kutimiza icho kitu na hakikisha unatimiza.

NB: Maisha ni kuishi na kazi yako ndio maisha yenyewe iishi kazi yako ukijua ndio unaishi ivo ahsante
 
Watu wanalalamika mtaani maisha magumu ajira hawapati wewe unataka kuacha kazi.
Kama unaufahamu msoto wa kutembea na bahasha acha hiyo kazi kapambane siyo lazima kila mtu afanikiwe akiwa serikalini ila kama hukusugua kwenye mbao ndefu acha utajua hujui..
 
Kopa pesandefu Kisha ingiaa mitini ndicho nilichowafanyia halmashauri moja Huko mkoa wa rukwa
 
Haya maisha bwana kuna kina sie tunatamani tupate nafasi yyt hatuipati, kuna wengine wanasema hawana furaha kazini!!! Ama kweli Mungu ana kazi sana huko aliko!!
 
Sio koteeee kwingine wanakula maisha sana
 
Pole sana jamaa kazi za serikali jau jana sana kila mtu mjuaji plus uchawa kuchukiwa bila sababu.
Huko tamisemi ndio sehemu ilihaa miungu watu, mfanyakazi wa tamisemi huna thamani, kianzia balozi ni boss wako, mwwnyekiti wa kitongoji ni boss wako, mwenyekiti wa kijiji ni boss, mtendaji wa kijiji ni boss, mtendaji wa kata ni boss, mwalimu mkuu ni boss, diwani ni boss, mbunge ni boss, katibu afya ni boss, DMO ni boss, RMO ni boss, bado wa huko wizarani asee....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…