Sina mapenzi na mama yangu

Mtafute bi mkubwa muongee,uwe huru kwake pia awe huru kwako otherwise siku akitangulia mbele ya haki kabla mambo hamjayaweka sawa, ikitokea ukapatwa na Jambo lolote baya utahisi Ni kwakuwa hukuwa vizuri na Mama yako.Hali hii itakutesa na uwezekano wa kumpata kuyamaliza hautakuwepo.Hii hali itakutesa sana.
 
Nimeishia hapo ulipokuwa unaishi na shangazi yako.

Kiujumla kilichokupata hata nami kilinipata.

Tatizo ni kuwa upendo hujengwa na mazoea wala siyo tu kwa kigezo ni Mama yako mzazi.

Hata nami ilinichukua zaidi ya miaka mi3 kukaa sawa baada ya kujilazimisha sana ila kabla ya hapo upendo wangu ulikuwa kwa Mjomba na Mke wake.

Nikachukulia kuwa hata nikimchukia hakuna mzazi aliuenileta duniani zaidi ya Mama na Baba, nikakubaliana na yote kujishusha hatimaye ninampenda na naishi naye vizuri tu.
 
Pole
Ndugu hilo ni tatizo la kisaikoljia. Kaeni na mama mumwambie muyamalize kaa kuwekana wazi na kuondoa zana potofu kwake na muwe na ukaribu angalau kwa sasa wa kumtembelea na vijizawadi mara kwa mara
 
Poleni! Tafuta njia japo uwe unamjulia hali.
 
Pole! Mjulie hali mara kwa mara, mtazoeana.
 
Halafu mawifi sijui huwa wana gubu gani na mawifi zao wa kwanza!
Sasa kilichotokea tena ni kwamba haohao mashangazi wametupindua Sisi watoto WA WiFi Yao WA Kwanza kwani mpk wamemlisha sumu Mzee kwamba dogo WA mwisho si mtoto WA Mzee Mimi pia na Mzee hakuna maelewano kbs na ndo nilikuwa kipenz chake na nilionyesha wazi sina masihara kabisa na watu wapuuzi kwny familia aisee kumbe Mzee kuwa sn upande wangu hiyo iliwauma inasemekana wakaanza uganga na uchawi kunigombanisha na Mzee na wamefanikiwa kbs sister Alishaolewa ingawa Naye kutwa nzima hao mashangaz wanaombea na kutamka ndoa haitadumu Yani vurumai Tu bt nashukuru Mungu naendelea na family yangu nilichoamua ni kuishi kama Osama hakuna kujua mawasiliano yangu wala kujua nafanya kaz wapi. Yule ma mdogo pia wivu ulimjaa kuona Mzee Yuko sn upande wangu naona ilipgwa kolabo tena kunimalza aisee. Maana Mzee alikuwa Mambo Safi na wake mashangaz njaa Kali wakaona nitakata mirija Yao ndo hivyo kwahiyo hata home Nina miaka sjakanyaga wala sina mawasiliano na Mzee tena Ila simlaumu yeye tatzo ni Dada zake Tu na na mdogo. So pale ni kama watoto WA mke wakwanza tulishaondolewa kinamna Yani pale ni kama si kwetu tena kabaki ma mdogo na watoto wake na ndugu zake Tu. Ndo maisha yalivyo Ila Niko imara kuliko Jana siyumbushwi kbs uzuri nao wananijua misimamo yangu si ya kuyumba hata Mzee ananijua. Kuna SKU shangazi mdogo wake na shangazi aliyenilea alipeleka umbea Fulani Kwa Mzee sa Mzee akapotezea ma mdogo akaja nigusia aisee nilimuwashia Moto mkali sn ni zaidi ya mara moja namuwashia Moto nadhan haya nayo yalichangia kuanza mapambano ya kunitengenisha na Mzee.
 

[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15] astaghafirullah
 
Mkuu Kwanza pole Sana kwa changamoto hyo,

Jambo la Kwanza kabisa kabla sijakushauri chochote, jifunzi kuyaweka mambo ya familia Kama Siri, maana hizi familia zinambo mazito mno, ikiwa watu watayatoa nje Ni hatari kubwa na kibaya zaidi huwa hayana solution...

Sasa Basi, naomba nami nitoe ushauri wangu,

Ni vyema kabisa ukiweza ugomvi wa kifamilia hasa wa Baba na mama usije kuuingilia au kuruhusu mtu akakuingiza kwenye ugomvi huo, iwe Ni mama au baba au ndg usiruhusu kabisa hlo Jambo, maana unaweza kuambiwa ukadhani kuwa Ni kwel kumbe wanapandkiza chuki tu Wala hakuna ukwel,

Pili, wapende wazaz wako, cjui Kama unaamini katika dini ipi, ila waombee wasaidie, wajari, tengeneza network nao bila kujal yaliyopita..

Ntakupa mfano wa aliekuwa jaji mkuu wa tz fransis nyalali, fuatilia historia yake, kifupi yy aliamua kuwasaidia wazaz wake wote bila utofauti wao, na kwake ilimpa Amani mno..

Tatu, .mkuu kwenye familia kunasili nyingi mno ambazo huwa Ni aibu na nadra kuzisema hi ni kwa kuwa husalia kuwa Siri za familia, usiruhusu mzaz wako kwa namna yoyot kumwongelea vibaya..

Nmeangalia age yako nmegundua ww ni mwanaume si mvulana, badili mtazamo wako juu ya wazaz wako, nkakuambia siku ukibadili altitude zako ukawaombea wazaza, akamwambia Mungu akufundishe namna Bora ya kuwapenda, utakuja kutoa ushuhuda hapa..

Kila raheri mkuu, Mungu akutangulie, hakuna mzazi mbaya ambae anamchukia mwanae, amka mkuu
 
Ameen kubwa sana
 
Pole sana mkuu! Maisha haya!!
 
Pole sana mkuu.. tatizo lipo kwako na kwa mama yako pia!
Inaonekana mama alichanganyikiwa na kudhoofika kisaikolojia kwa changamoto za ndoa yake hadi kufikia hatua hiyo

Labda mkipata ushauri kwa wataalumu wa afya ya saikolojia wanaweza wasaidia mkawa famili yenye upendo na umoja tena??
Au hata viongozi wa dini ..
 
Sasa wewe ni kwa mama vs shangazi, mimi ni kwa mama vs bibi mzaa baba. Nimekua na bibi na upendo wangu wote upo kwa bibi. Mama nalazimisha tu basi madogo waone nami ni ndugu yao.

Mfano naishi na mama mkoa mmoja, wilaya zimekaribiana ni kama 50 km tu, nina usafiri wangu mdogo tu wa kwenda hata kumsalikia na kurudi siku hiyo hiyo ila cha ajabu tangu nimerudi hapa mkoani mwaka 2016 nimeenda kwake mara moja tu kumsalimia tena mwaka 2019! Sijaenda tena na sioni hasa roho yangu ikinisukuma sana kwenda. Nabaki napanga nitaenda tu, nitaenda tu ila siendi. Ila kwa bibi siwezi pitisha mwezi bila kwenda, na nikienda muda mwingine nakaa hata wiki kabisa.


Tunakutana tu kwenye matukio ya kifamilia kama misiba. Kuna muda najaribu kulazimisha kusikitishwa na hili ila kiukweli hata sijisikii nikisikitika kutokea rohoni.

Nimejifunza jambo, watoto wangu nitawalea mwenyewe!
 
Mtulie tu. Na nyie watoto mnaowalea peke yenu bila baba mnawajaza roho mbaya na chuki dhidi ya baba zao. Wanakuwa hawana upendo nae kabisa, na mbaya zaidi wanamchukia. Bora hata baba hawezi kukueleza mabaya ya mama yako sana. Ila nyie wanawake wabaya mno
 
Nakukumbusha tu shangazi ako na mama ako ni mtu na wifi yake....
Fatilia zaidi mahusiano ya mawifi utagundua kitu, pole kwa yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…