Sina mzuka na mamito wangu...

Sina mzuka na mamito wangu...

wenyewe wanasema usawa unakaba na rafiki wa kweli ni baba na MAMA hao wengine wala usiwaamini kwani binadamu wa sasa wana roho saba..prof jay aliimba hivyo...pole sana

ahsante
 
Mine is deeper na mbaya zaidi najua chanzo ambacho nashindwa kukisahau na kukifuta. Post ya dDa Mkubwa King'asti imenigusa sana isipokuwa tu ni kuwa pamoja na uzee huu nilonao bado...............I think I need a big therapy

pole mpenzi
 
POLE SANA SANA EVE.....
Mtazamo wangu ni kuwa inaonekana una dharau.....inawezekana hujijui lakini kwa chochote ulichonacho huona wewe ndo wewe....Inawezekana hata marafiki zake mama yako yaani majirani wanaokuja hapo nyumbani wameshamueleza mama yako jinsi ulivyo/nae akakusoma akaona ndivyo ulivyo kujisikia....mama mzazi anawafahamu watoto wake vema sana kuliko mtu yeyote....
jaribu kukaa nae na kupiga nae story atakueleza jinsi ulivyo,inawezekana yeye anakueleza madhaifu yako wewe una comments sanaaa,una compare na wengine wakati muhusika ni wewe au hoji kutafuta sababu na kukuta mzuka unapotea na kubaki na Baba Mdogo ambaye hajui uchungu wako kama mama yako anarembaremba anapokuwa na wewe.... una ignore,hakuna mazazi anaemchukia mwanae at a Normal situations.
Mungu akubariki sana sana upokee positive nilichokueleza....

Inabidi achukue ushauri huu na aufanyie kazi
 
Hilo ni tatizo really.
Lazima uangalie umekwama wapi, unajua wamama mabinti za wakikua wanajisikia kuwa karibu nao sana sana. Me my mum tulikuwa kama friends yan tunashare kila kitu except relationship (nilikuwa msiri). Lakini nguo, mikoba, makeup yan kama ninatoka nyumbani naenda mahali lazima aniite anitazame kama kweli nimependeza au anaweza niweka nywele vizuri au aniongezee kibanio kwenye nywele. Yan sokoni shopping wote, nikikaa pembeni yake iwe shughulini au nini. Yan hadi ilifika stage baba akawa anatuonea wivu.
Rest in peace mummy...
Jitahidi nakuambia ukweli ur mum is suffering kwa hii tabia yako, unajua wanawake tunapenda kukaa na vitu rohoni na hiki ndicho mama yako anaffanya anaumia ndani kwa ndani.

Ahsante sana kwa ushauri wako....
na pole kwa kumpoteza mummy ako may her soul rest in peace.
 
Fanya pole pole jizoeshe kumnunulia zawadi kidogo kidogo, muonyeshe jinsi gani unapenda hata kwa text like mama nimekumicje yeah,
angalia hii itakuja kukuumiza sana mama yako mungu akimchukua ghafla utabaki sema ningejua duuh wakati ni huu fanya mabadiliko sasa. Amini nikumbiacho ur mummy ndio best friend wa ukweli na wa mwisho ambae anaweza sacrifice maisha yake kwa ajili yako, anayeweza kukutunzia vyote vyake, siku ikiumwa yupo radhi hata kukusafisha m...vi yako who else will do that?? Love ur mum upate baraka tele

Haya mpendwa nashukuru kwa maneno yako
najitahidi nifanye hivo...
 
Jambo hili mi linanikosesha amani,
nishajaribu mara kadhaa kujenga ukaribu bila mafanikio, kama vile kujizoesha atleast kuwa namtext nikiwa mbali
lakini haichukui hata wiki naacha na huwa nakuwa mzito sana kumpigia simu.
Huwa natamani sana watu wanaoishi na mama zao kama rafiki zao kwangu mie tofauti kabisa sio kuwa simpendi ila tu ule mzuka nae ndo sina hata nikiwa na shida siwezi kumshirikisha.
I love much my daddy bahati mbaya alishatangulia mbele za haki (R.i.p my lovely one)
Ushauri please nifanyeje nijenge ukaribu nae
Kaunga naomba uniambie kitu....
(Matusi na kejeli sitaki hili jambo linaniumiza mie kama hujisikii kushauri uache)

Nawatakieni weekend njema!!!!!

Si kosa lako, Alisema Sigmund Freud katika psychology.
Google hii kitu,
^ https://en.wikipedia.org/wiki/Electra_complex ^ na Oedipus complex - Wikipedia, the free encyclopedia
 
monaco, sometimes huwa hata sio dharau............. mwenyewe unajikuta roho inauma sana tu as to why siko karibu na my mom, but you cant help it hata ukijaribu kiasi gani. Just imagine kama kutuma sms tu inakuwa ngumu sembuse kukaa nae na kuzungumza? Mie ninaamini kabisa kuwa hili swala linahitaji saikolojia zaidi kuliko ushauri wa nadharia. Kukaa chini na kuzungumzia kwa kina nini kinasumbua. Kwa hali ilivyo siamini kabisa kuwa hajui chanzo..................... hapana. Chanzo kipo na pengine hayuko tayari kukizungumzia au hajui kama ni kitu ambacho kinawezamtenganisha na mamake. Chanzo kipo................... no matter how hard she tries to deny, but chanzo kipo na anakijua.

Ndo mawazo yake yalivo siwezi kuyabadili wala hayawezi kunibadili
najijua vizuri am a good daughter wala sijawahi kuwa na dharau mie.....
na nnachokiongea hapa si kuwa namchukia mami angu au nna ugomvi nae
wenye kunielewa wamenielewa ambao hawajaelewa wataelewa taratibu wakitaka kuelewa.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom